Kuwafikia waliotengwa

Size: px
Start display at page:

Download "Kuwafikia waliotengwa"

Transcription

1 Kuwafikia waliotengwa

2 Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO

3 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Ripoti hii ni chapisho huru lililoanzishwa na Shirika la UNESCO kwa niaba ya Jamii ya Kimataifa. Inatokana na juhudi za ushirikiano kati ya wanachama wa jopo la kuandaa ripoti hii pamoja na watu wengine wengi, wakala mbalimbali, taasisi na serikali mbalimbali. Vyeo pamoja na ujumbe uliowasilishwa katika toleo hili haviwakilishi, kwa vyovyote vile, maoni ya shirika la UNESCO kuhusu hali ya kisheria ya nchi, himaya, jiji, maeneo na mifumo ya tawala zake, au kuhusu uwekaji wa mipaka yazo. Jopo la Kimataifa linalosimamia mradi wa Elimu kwa Wote (EFA) ndilo lenye jukumu la kuchuja na kuwasilisha hoja na maoni yote katika muhtasari huu. Maoni haya hayafungamanishwi na wajibu wa shirika la UNESCO. Wajibu wa kijumla kuhusu maoni na misimamo iliyojitokeza katika ripoti hii ni kwa Mkurugenzi wake. Jopo la Wachunguzi wa Kimataifa wa mradi wa Elimu Kwa Wote Mkurugenzi Kevin Watkins Samer Al-Samarrai, Nicole Bella, Marc Philip Boua Liebnitz, Mariela Buonomo, Stuart Cameron, Alison Clayson, Diederick de Jongh, Anna Haas, Julia Heiss, François Leclercq, Anaïs Loizillon, Leila Loupis, Patrick Montjourides, Karen Moore, Claudine Mukizwa, Paula Razquin, Pauline Rose, Sophie Schlondorff, Suhad Varin. Kwa habari zaidi kuhusu Ripoti, Tafadhali wasiliana na: Mkurugenzi, Jopo la wachunguzi wa Kimataifa ya wa mradi wa Elimu kwa Wote (EFA) c/o UNESCO 7, place de Fontenoy, Paris 07 SP, France efareport@unesco.org Tel.: Fax: Ripoti za awali za Usimamizi wa Mradi wa Elimu kwa Wote Overcoming inequality: why governance matters Education for All by 2015 Will we make it? Strong foundations Early childhood care and education Literacy for life Education for All The quality imperative 2003/4. Gender and Education for All The leap to equality Education for All Is the world on track? Imechapishwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni , Place de Fontenoy, Paris 07 SP, France Usanii wa Kurasa: Sylvaine Baeyens Muundo: Sylvaine Baeyens Imechapishwa na UNESCO Chapisho la kwanza 2010 UNESCO 2010 Imetafsiriwa na kuchapishwa mjini Nairobi ED-2010/WS/2

4 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 3 Dibaji Toleo hili la Ripoti ya Usimamizi Wa Mradi wa Kimataifa wa Elimu kwa Wote(EFA) 2010, kwa anwani Kuwafikia Waliotengwa, limeandaliwa katika wakati wa mashaka mengi ulimwenguni. Tungali tunajizatiti kukabiliana na poromoko la kiuchumi na kibiashara ulimwenguni, sio tu katika sekta ya benki, lakini katika nyanja zote za maendeleo ya kibinadamu ikiwemo elimu. Hivyo basi, tunajipata katika njia panda; tuendelee na shughuli zetu kama kawaida na kuhatarisha maendeleo kwa kurudisha nyuma hatua zote tulizopiga kimaendeleo katika mwongo uliopita, au tuchukulie hali hii kama fursa nyingine ya kujenga mifumo ya kudumu itakayowezesha ushiriki wa wote na kukomesha aina zote za ubaguzi. Faida iliyopatikana tangu kuanzishwa kwa mradi huu wa Elimu kwa Wote (EFA) na Malengo ya Maendeleo ya Milenia mwaka 2000 haziwezi kupuuziliwa kamwe. Hatua kubwa zimepigwa katika malengo ya kufikia elimu ya msingi kwa wote, kuongezeka kwa idadi ya wanafunzi waojiunga na shule za sekondari na vyuo mbalimbali, na katika nchi nyingi, uimarishaji wa usawa wa kijinsia umeafikiwa. Kwa upana zaidi, juhudi za kupambana na njaa na umaskini zimeimarishwa, pamoja na kupunguza viwango vya vifo vya watoto wanaozaliwa na vya kina mama wazazi. Mfumko wa kiuchumi ulimwenguni unaweza kuibadilisha hali hii kabisa. Katika toleo hili la, Kuwafikia Waliotengwa, inadhihirika kwamba, upungufu wa mapato ya serikali na ongezeko la ukosefu wa kazi vinaathiri nyanja zote za maendeleo ya kibinadamu. Bajeti za Serikali zimepunguzwa zaidi kiasi cha kuathiri ufadhili wa elimu. Nazo familia maskini zinajipata katika hali hiyo hiyo ya kukabiliana na changamoto zizo hizo za kiuchumi. Takwimu za awali zinaonyesha kuwa katika hali kama hii, watoto aghalabu huwa wa kwanza kuathirika, ambapo elimu yao hukomeshwa. Ili kukabiliana na tatizo hili, mataifa yanahitaji kubuni mbinu za dharura za kuwalinda maskini na wasiojiweza katika jamii. Lazima pia Mataifa yatwae fursa na mbinu zitakazoyawezesha kujenga jamii itakayokuwa na usawa ili wote waweze kufaidika na kujiendeleza. Zaidi ya kuweka msingi bora wa maisha ya baadaye kwa kufundisha kusoma na kuandika, shule pia hutekeleza majukumu muhimu sana ya kukuza uvumilivu, amani na uelewano miongoni mwa watu, na kwa njia hii kupigana na aina zote za ubaguzi. Kwa sababu hii, elimu haina budi kupewa kipaumbele. Ni shuleni tu ambapo jamii za mashambani zinaweza kujifundisha kusoma na kuandika lugha zao, ambapo tofauti za kijamii zinaweza kuvumiliwa na watoto kuepushwa na hali ngumu zinazosababishwa na mizozo inayowakosesha makazi. Ripoti ya mwaka huu Global Monitoring Report inaeleza kuwa bado safari ni ndefu. Takriban watoto milioni 72 wangali wanakosa haki yao ya kupata elimu kwa sababu za kijamii au kimaeneo. Mamilioni ya vijana huacha shule kabla ya kumudu mbinu za kuwawezesha kupata kazi yenye ajira. Mtu mmoja kati ya watu sita hunyimwa haki ya kujifunza kusoma na kuandika. Ripoti ya mwaka wa 2010 ni kama mwito wa kutenda. Ni lazima tuwafikie waliotengwa. Mfumo wa elimu jumlishi tu ndio uwezao kusanya ujuzi unaohitajika katika kujenga jamii zenye ujuzi za karne ya ishirini na moja. Jamii ya kimataifa ina jukumu muhimu la kutoa mwongozo katika kuunga mkono juhudi za mataifa za kuendeleza na kupanua mifumo ya elimu katika mataifa yao. Hatupaswi kuzitenga nchi hizi katika wakati wao wa uhitaji mkuu. Kwa sasa, ni lazima ahadi za kuyasaidia mataifa maskini kujikomboa zifasiliwe kifedha ili kufaidi serikali zao. Ni kusudio langu kuwa Shirika la UNESCO litaendelea kuwania ongezeko la uwekezaji katika elimu. Kama wakala, iliyo katika mstari wa mbele katika kupigania Elimu kwa Wote, tuna wajibu mahsusi wa kuwapa moyo na kusaidia waliokabiliwa na hali ngumu kutokana na poromoko hili. Ikisalia miaka mitano tu ya kuzitimiza ahadi za pamoja, tunajipata katika njia panda na ni lazima kuamua kwa pamoja mkondo utakaowezesha watoto, vijana na watu wazima kutimiza haki zao za kupata elimu. Irina Bokova

5 4 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Hoja muhimu katika Ripoti ya Elimu kwa Wote 2010 Miaka kumi imepita tangu jamii ya kimataifa ipitishe na kukubali malengo sita ya Elimu Kwa Wote mjini Dakar mwaka wa 2000.Tangu wakati huo, kumekuwa na takwimu mseto. Mambo mengi yakiwa yametimizwa katika mwongo uliopita, nchi maskini zaidi ulimwenguni hazijafaulu kufikia malengo ya mwaka wa Kutoweza kuwafikia waliotengwa kumewanyima watu wengi haki ya kupata elimu. Huku athari za mfumko wa hali za kiuchumi ulimwenguni zikizidi kuumiza, kuna hatari kuwa kasi ya maendeleo iliyoshuhudiwa katika miaka iliyopita inaweza kukwama au hata kufifia kabisa. Hali hii inahatarisha elimu. Kuna haja ya mataifa kubuni mbinu jumuishi zitakazohusisha mikakati bora ya kuwalinda wengi walio hatarini na kupambana na ukosefu wa usawa katika jamii. Upunguzaji wa athari za mfumko wa kiuchumi katika elimu Jamii ya kimataifa inahitaji kutambua hatari inayokumba elimu kutokana na hali mbaya za kiuchumi na mfumko wa bei za vyakula ulimwenguni... Viarifa vinavyoangazia maendeleo ya kibinadamu vinaonyesha uzorotaji. Inakadiriwa kuwa takriban watu milioni 125 zaidi watakabiliwa na tatizo la utapiamlo katika mwaka wa 2009 na wengine milioni 90 watakabiliwa na umaskini katika mwaka wa Huku umaskini na ukosefu wa ajira ukiongezeka na msaada ukiendelea kudorora, familia maskini zinalazimika kupunguza gharama ya elimu na ikiwalazimu, hata kuwaondoa wanao shuleni. Bajeti za nchi maskini zimepunguzwa sana. Mataifa ya Afrika- Kusini mwa jangwa la Sahara yanakabiliwa na uwezekano wa kupoteza karibu Dola bilioni 4.6 kila mwaka katika ufadhili wa elimu katika miaka ya 2009 na Kiwango hiki ni sawa na upungufu wa 10% ya gharama ya kila mwanafunzi.... ili kuibuka na njia bora ya kukabili hali hii: Misaada ikadiriwe na idumishwe ili iweze kufidia hasara inayoletwa na ukosefu wa fedha, igharamie miradi muhimu kwa jamii na iendeleze elimu. Kongomano la wafadhili liandaliwe katika mwaka wa 2010 kwa lengo la kuziba mwanya wa kifedha unaokumba ufadhili wa mradi wa Elimu Kwa Wote. Kufikia malengo ya Elimu kwa Wote Hatua kadha zimepigwa... Idadi ya watoto wasiohudhuria shule imepunguka kwa milioni 33 kote ulimwenguni tangu Nchi za Asia Kusini na Magharibi zilipunguza idadi ya watoto ambao walikuwa hawaendi shule kwa zaidi ya nusu-upungufu wa milioni 21. Baadhi ya nchi zimepiga hatua ambazo si za kawaida. Benin ilianzia kama taifa mojawapo ya mataifa yalikuwa na viwango vya chini zaidi ulimwenguni vya usajili shuleni mnamo mwaka wa 1999 lakini sasa inaweza kuwa miongoni mwa mataifa yanayoelekea kufikia lengo la Elimu ya Msingi kwa Wote kufikia mwaka wa Idadi ya wasichana ambao walikuwa hawaendi shule imepunguka kutoka 58% hadi 54%, na mwanya wa kijinsia liliokuwepo katika shule za msingi unaendelea kupungua katika nchi nyingi. Baina ya mwaka wa na , viwango vya kujua kusoma na kuandika miongoni mwa watu wazima viliongezeka kwa 10%, kufikia kiwango cha sasa cha 84%. Idadi ya wanawake wanaojua kusoma na kuandika imeongezeka kwa kasi zaidi kuliko ile ya wanaume....lakini bado kuna mengi ya kutimizwa: Utapiamlo unaathiri karibu watoto wachanga milioni 175 kila mwaka na hii ina madhara kwa kiafya na kielimu. Kulikuwa na watoto milioni 72 wasioenda shule kufikia mwaka wa Tukiendelea hivi bila kufanya juhudi za ziada, tutaishia kuwa na watoto milioni 56 ambao hawatakuwa shule kufikia mwaka wa Takriban 54% ya watoto ambao hawaendi shule ni wasichana. Barani Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara, karibu wasichana milioni 12 huenda wasijiunge na Shule kabisa. Nchini Yemen, 80% ya wasichana ambao hawaendi shule huenda wasiwahi kujiunga na shule, asilani wakilinganishwa na wavulana 36% katika hali iyo hiyo. Kujua kusoma na kuandika hubakia kuwa mojawapo ya malengo ya elimu yaliyopuuzwa zaidi, huku kukiwa na watu wazima milioni 759 wasiojua kusoma wala kuandika. Thuluthi mbili ya hawa wakiwa wanawake.

6 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 5 Mamilioni ya watoto wanaondoka shuleni bila kujipatia ujuzi wa kimsingi wa kusoma na kuandika. Katika baadhi ya mataifa barani Afrika-Kusini mwa Sahara, vijana waliohudhuria shule kwa miaka mitano walikuwa na uwezekano wa hadi 40% wa kuwa hawawezi kusoma wala kuandika. Nchini Dominican Republic, Ecuador na Guatemala, chini ya nusu ya wanafunzi waliofika katika darasa la nne ndio walikuwa na zaidi ya ujuzi wa kimsingi wa kufahamu kusoma. Karibu walimu wapya milioni 1.9 wanafaa kuajiriwa ili kuweza kutimiza lengo la kuwa na elimu ya msingi kufikia mwaka Kuwafikia waliotengwa Serikali zinashindwa kukabiliana na vianzo vikuu vya kutengwa katika elimu. Takwimu mpya zinazohusu kutengwa na kunyimwa elimu zinaonyesha viwango vipya vya kuachwa nje katika mataifa themanini... Katika mataifa ishirini na mawili, 30% au zaidi ya vijana walipata chini ya miaka minne ya elimu shuleni, na idadi hii inaongezeka na kufikia 50% au zaidi katika mataifa kumi na moja barani Afrika Kusini mwa janga la Sahara. Katika mataifa ishirini na sita, 20% ya vijana huhudhuria shule kwa muda wa chini ya miaka miwili na katika mataifa mengine, yakiwa ni pamoja na Burkina Faso na Somalia, idadi ni 50% au zaidi. Hali za ukosefu wa usawa huchangia ongezeko la hatari ya kuachwa nyuma. Nchini Uturuki, 43% ya wasichana wazungumzao Kikurdi na watokao katika familia maskini huwa wanapata chini ya miaka miwili shuleni, huku kiwango cha wastani cha taifa zima kikiwa ni 6%. Nchini Nigeria, 97% ya wasichana wazungumzao Kihausa waliweza kupata elimu ya chini ya miaka miwili. Kukosa kukabiliana na utabaka, shutuma za kila aina na ubaguzi unaohusishwa na utajiri, jinsia, ukabila, lugha, mazingira na ulemavu ndivyo vinavyolemaza maendeleo ya kupatikana kwa Elimu Kwa Wote....na katika kuanzisha mifumo husishi ya elimu kuna haja ya: Kuongeza uwezo wa kufikia elimu na kuboresha uwezo wa kuimudu gharama kwa makundi yaliyotengwa kwa kufutilia mbali karo, kuleta shule karibu na jamii zilizotengwa na kuanzisha miradi ya kutoa fursa-ya-pili. Kuimarisha mazingira ya kufundishia kwa kuwatuma walimu waliofuzu kote nchini na kutoa msaada wa kifedha na kimasomo kwa shule ambazo zimepungukiwa, na kutoa elimu ya tamaduni mseto na uwililugha. Kupanua upatikanaji wa haki na nafasi za kujiendeleza kwa kutekeleza sheria dhidi ya ubaguzi, kuanzisha miradi ya kuilinda jamii na kusambaza upya mapato ya serikali kwa umma. Kubuni mifumo mbalimbali ya kukusanya takwimu na kutambua makundi yaliyotengwa na kusimamia maendeleo yao. Kugharamia Elimu kwa Wote Rekodi ya msaada kwa elimu hairidhishi Kwa jumla, msaada umekuwa ukiongezeka, ingawa US$50, nyongeza iliyoahidiwa mwaka wa 2005 haijatimizwa. Bara la Afrika linakadiriwa kukabiliwa na upungufu mkubwa zaidi, wa takriban Dola bilioni18 za Marekani. Msaada kwa elimu umekuwa ukiongezeka, lakini ahadi kutimizwa kumekwama kwa muda sasa. Ahadi za msaada kwa elimu ya msingi zilishuka kwa 22% na kufikia Dola bilioni 4.3 za Marekani kufikia mwaka Msaada wa elimu hauwafikii wanaouhitaji zaidi. Baadhi ya wafadhili huendelea kutotilia maanani elimu ya msingi. Mataifa yaliyoathiriwa na mizozo hayapokei msaada wa kutosha, na hili linahujumu matumaini ya kujinusuru. Elimu hukosa mfumo wenye wahusika wengi wa kuharakisha maendeleo, ikiathirika na uhaba wa ufadhili na ukosefu wa ufadhili kutoka kwa sekta za kibinafsi....lazima serikali zote fadhili na fadhiliwa ziongeze raslimali inayotengewa elimu na kuboresha usimamizi wa misaada: Nchi zilizo na mapato haba zinaweza kutoa Dola milioni 7 za Marekani zaidi kwa mwaka- au 0.7% Ya mapato ya kitaifa (GDP). Hata baada ya jitihada hizi bado mapengo ya kifedha yatabakia bila kujazwa. Ripoti hii inakadiria upungufu au pengo la kifedha katika kutimiza malengo ya Elimu Kwa Wote katika mataifa yenye mapato haba kuwa Dola bilioni 16 za Marekani kila mwaka. Wafadhili wanafaa kuimarisha juhudi za kutekeleza ajenda ya Paris iliyohusu matumizi bora ya misaada na kutathmini usawazishaji wa usaidizi wao katika viwango tofauti vya elimu. Wafadhili pia wanafaa kuongezea misaada kwa nchi zilizoathiriwa na mizozo, na kutafuta njia bunifu za kutoa usadizi wa muda mrefu itakayosimamiwa ipasavyo. Mfumo wa kimataifa ushirikishao wahusika wengi kwa mahitaji ya elimu unahitaji kuimarishwa kupitia kwa mabadiliko muhimu ya mradi wa Kuharakisha Elimu Kwa Wote. Umoja wa Mataifa unafaa kuandaa kongamano la dharura la kutoa ahadi za misaada kwa mwaka wa 2010 ili kuhamasisha kuhusu upatikanaji wa fedha zaidi zinazohitajika na pia kutimiza ahadi za maafikiano ya Dakar.

7 6 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Mfumko wa kiuchumi: Madhara kwa dunia Mazingira ya kufanikisha malengo ya Elimu kwa Wote yamedidimia maradufu. Ukuaji wa chini wa kiuchumi una madhara makubwa zaidi katika ufadhili wa elimu katika nchi maskini zaidi. Nchi hizi zinahitaji kwa dharura ongezeko la misaada ili kufidia hasara za mapato, kustawisha matumizi ya kijamii na kukuza ustawi. Hatua zinazochukuliwa na jamii ya kimataifa katika kukabiliana na majanga ya kifedha, kwa kiasi kikubwa, zimekosa kuangazia mahitaji muhimu ya ustawi wa kibinadamu. Mapengo katika ufadhili wa Elimu kwa Wote yanafaa kuwekwa chini ya mpango wa kimataifa wa kufufua ustawi wa kibinadamu. Sura ya 1 Elimu hatarini: athari Toleo hili la Ripoti ya Uchunguzi wa kimaaifa kuhusu Elimu kwa Wote linajiri wakati mgumu zaidi kiuchumi ulimwenguni, tangu poromoko kuu la kiuchumi. Mifumo mingi ya elimu katika nchi nyingi maskini zaidi ulimwenguni, kwa sasa, inakabiliwa na athari za mgogoro wa kifedha uliotokana na mifumo ya kiuchumi ya mataifa yaliyoendelea. Kunayo hatari isiyoepukika kuwa, baada ya mwongo wa hatua za kutia moyo, maendeleo ya kufikia malengo ya elimu yatajikokota au hata kurudi nyuma kutokana na umaskini unaozidi kuongezeka, kupungua kwa ukuaji wa uchumi na kuongezeka kwa mizigo ya bajeti za serikali. Jamii ya kimataifa inahitaji kuingilia kati haraka iwezekanavyo ili kuzuia hatari hiyo. Ni rahisi kukosa kutambua kilicho hatarini kwa sasa. Hatimaye, uchumi wa ulimwengu utafufuka kutoka kwa mfumko mkuu kote duniani, lakini mgogoro huo utakuwa umepoteza kizazi kizima cha watoto katika nchi zilizo maskini zaidi, ambao nafasi zao maishani zitakuwa zimeharibiwa kwa kukosa kulinda haki zao za kielimu. XINHUA/Gamma/Eyedea Presse Hatari maradufu: bei za vyakula na mgogoro wa kiuchumi Kuzorota kwa uchumi kulifuata kupanda kwa bei za vyakula katika nyanja za kimataifa baina ya mwaka Athari za ongezeko la bei za vyakula ulimwenguni na mfumko wa kifedha zimedororesha zaidi juhudi za kiuchumi katika kufikia malengo yote ya maendeleo ya 2015, ikiwa ni pamoja na malengo ya Elimu kwa Wote. Bei ghali za vyakula ziliwaacha wengine milioni 175 katika hali ya utapiamlo baina ya mwaka wa 2007 na Kufikia 2010, mporomoko wa kiuchumi utakuwa umewasukuma wengine milioni 90 katika umaskini uliokithiri. Kuna zaidi ya watu bilioni moja wanaoteseka na njaa kote ulimwenguni.

8 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 7 Jeroen Oerlemans/PANOS Watoto wapiga foleni kupokea chakula nchini Pakistan: kupanda kwa bei kumeathiri zaidi maskini za mgogoro wa kiuchumi Utapia mlo ulioenea sana na matumaini yaliyodorora ya kupunguza umaskini uliokithiri una athari kuu kwa elimu. Huku ukosefu wa kazi ukiongezeka na pesa zinazotumwa kutoka ng ambo kuzidi kudidimia, familia nyingi maskini na zisizo na uwezo zinalazimika kupunguza gharama ya kuelimisha au kuwaondoa watoto shuleni kabisa. Nchini Bangladesh, kwa mfano, takriban thuluthi ya familia maskini, kulingana na ripoti ya utafiti fulani zililazimika kupunguza ugharamiaji wa elimu ili kukabiliana na bei ya vyakula inayozidi kuongezeka. Njaa haitishi maisha tu, bali pia inazorotesha uwezo wa ubongo kukua na pia kuathiri mustakabali wa uwezo wa mtoto katika kujifunza mambo. Mgogoro wa kiuchumi wa Asia Mashariki wa mwaka wa 1997 ulileta madhara makuu kwa afya na elimu ya watoto. Tunaweza kujifunza kutokana na mafunzo haya. Kudorora kwa matumaini ya kukua kwa uchumi kuna athari kubwa kwa ugharamiaji elimu na hata malengo mengine ya jumla ya maendeleo ya kimataifa. Huku mataifa matajiri yakionyesha ishara za kufufuka kiuchumi, ukuaji wa mataifa yanayoendelea ni wa kujikokota na kupunguka kwa maduhuli ya serikali.hili ndilo baadaye huathiri bajeti za kitaifa na mgao wa fedha za kugharamia elimu. Makadirio ya ukuaji wa uchumi yanaonyesha kuwa Bara la Afrika Kusini mwa Sahara linakabiliwa na uwezekano wa kupoteza US$4.6 bilioni kila mwaka ya jumla ya pesa zote zinazopatikana za kugharamia elimu katika mwaka wa (Jedwali1). Hii ni maradufu kiwango cha msaada unaotolewa kwa elimu ya msingi katika eneo hilo. Gharama kwa kila mwanafunzi wa shule ya msingi ingepunguka kwa 10% mwaka wa 2010 iwapo makadirio ya kabla ya kuzorota kwa uchumi yangetimizwa. Upungufu huu unaweza kufasiriwa kwa kupunguza malipo kwa walimu, kupunguza gharama ya kujenga madarasa na kuendesha miradi ambayo inawafikia wale wametengwa zaidi. Jedwali 1: Kugharamia elimu katika bara la Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara kunaweza kuathiriwa na kujikokota kwa ukuaji wa uchumi. Kisawia cha PPP 2006 Dola $ mabilioni Asili: Tazama Mchoro 1.3 katika EFA Global Monitoring Report 2010 Makadirio ya kabla ya mgogoro wa kiuchumi Ugharamiaji wa Shule ya msingi Jumla ya gharama ya elimu Utapiamlo uliokithiri kote na kudidimia kwa matumaini ya kupunguza umaskini mkubwa vina athari mbaya kwa elimu.

9 8 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Mataifa tajiri yametoa msaada kidogo tu kwa mataifa maskini zaidi ulimwenguni na kwa wananchi wasiojiweza Kupanua hazina ya serikali- Kipaumbele cha Elimu kwa Wote Mataifa matajiri yameweza kupata hazina kubwa ya kusaidia ufufuzi wa nchi kiuchumi na kulinda matumizi ya pesa za umma. Yamewekeza pakubwa katika miradi iliyolenga kurejesha ukuaji wa uchumi, kuwalinda wananchi wasiojiweza na kuitunza miundombinu muhimu ya kijamii. Elimu imepewa kipaumbele kwa mfano, Sheria ya Amerika ya Kujifufua na Kujikarabati (ARRA) hutenga takriban Dola bilioni 130 kugharamia masuala yanayohusiana na elimu. Mataifa mengi yaliyo maskini zaidi hukosa rasilimali za kukabiliana na hatari hizi. Kwa wengi, kuongezeka kwa misaada ndiyo njia ya pekee ya kuongeza hazina ya serikali na kupunguza mizigo katika bajeti kwa muda mfupi. Ni muhimu sana kwa msaada huu kufikishwa kabla ya mzigo wa kiuchumi kugeuka hatari ya kudumu kwa maendeleo. Hatari ya moja kwa moja ni kuwa bila msaada, serikali hazitaweza kutekeleza mipango ya kifedha inayohusiana na malengo ya elimu ya msingi. Upungufu huu wa kuingilia kati umefichika katika mfumo wa kimazingaombwe wa kuripoti: aghalabu, kinachoitwa msaada wa ziada huwa kwa kweli ni ufadhili ule ule ila tu huwa umewasilishwa kwa njia tofauti. Takriban Dola baina ya bilioni 2 hadi bilioni 3 huwa zimetolewa kila mwaka kama msaada wa ziada au mpya kwa mataifa yaliyo na mapato kidogo kwa jumla, hasa kupitia Shirika La Fedha Ulimwenguni (IMF). Hii inaweza kulinganishwa na upungufu wa msaada wa Dola bilioni 80 kwa mwaka ikilinganishwa na makadirio ya kabla ya mgogoro katika bara la Afrika Kusini mwa Sahara katika mwa wa 2009 na Hasara za viwango kama hivi huwa bila shaka zina athari kubwa zaidi katika ufadhili wa elimu na kwa jumla kufikia Malengo ya Maendeleo ya milenia kwa jumla. Mgogoro wa kiuchumi ulimwenguni umetukumbusha kuwa kutegemeana kiuchumi baina ya mataifa kuna sura ya kibinadamu. Watoto katika mataifa yaliyo maskini zaidi ndio huathirika zaidi na kuporomoka kwa mifumo ya benki za Kimagharibi kwa kuachana na fursa ya kupata elimu ambayo ingeweza kumwinua kutoka katika umaskini. Itiko la Kimataifa: kukosekana kwa mkabala wa kibinadamu Hadi wa leo, itiko la kimataifa lifaalo kwa mgogoro huu limekosekana. Serikali za mataifa tajiri na makongamano ya mara kwa mara ya mataifa ya G20 na G8 yamepiga hatua kubwa kiuchumi kustawisha mifumo ya kiuchumi, kufungua masoko ya mikopo na kuinua hali ya kifedha ulimwenguni kwa jumla. Licha ya hayo, juhudi hizi zote zimefaulu kutoa msaada mdogo tu kwa mataifa maskini zaidi ulimwenguni na kwa wananchi wasio na uwezo. Kuepuka madhara: mvulana anafanyia kazi ya shuleni nyumbani mjini Freetown, Sierra Leone Matokeo kama hayo hayakubaliki na yanaweza kutilia nguvu utaratibu wa kimataifa uliojengeka katika matabaka ambayo tayari yana tofauti kubwa sana. Matendo yanahitajika katika viwango vingi. Zifuatazo ndizo hatua zinazohitaji kupatiwa kipaumbele kwa dharura: Kuitisha mkutano wa hali ya juu kuhusu ufadhili wa Elimu Kwa Wote katika mwa wa 2010 ili kujadiliana mikakati itakayowezesha fedha kupatikana. Kuupa umbele, msaada unaotabirika na unaodumishwa ili kukumbana na ukosefu wa mapato ya serikali katika mwaka wa ili kuzisaidia nchi zinazoendelea ziweze kulinda na kuimarisha hazina yao ya mapato ya kutumia kwa umma. Kuhakikisha kuwa kuna usimamizi ufaao na wa kisasa wa bajeti za serikali, uhudhuriaji shule na idadi ya wanaoacha zimesimamiwa na UNESCO pamoja na wizara za elimu ya kitaifa na fedha. Kuhakikisha kuwa msaada wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) umetolewa kwa misingi ya mahitaji yaliyopo sambamba na uafikiaji wa malengo ya Elimu kwa Wote hasa kuhusiana na gharama za kuwaajiri walimu, mafunzo na mishahara. Kuongeza msaada kwa mataifa yaliyo maskini zaidi kupitia kwa hazina ya Benki ya Dunia ya Muungano wa Maendeleo ya Kimataifa ikishirikiana na ziada za wafadhili waliojitolea kusaidia. Aubrey Wade/PANOS Kulipa kipaumbele suala la kulinda jamii kwa kuwatumia pesa, mipango ya chakula na msaada uliopangiwa, ili kulinda familia zisizo na uwezo kutokana na gutuko la kiuchumi na kuwasaidia kuhakikisha watoto wao wanaenda shule.

10 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 9 Kutafuta elimu Uchina mashambani: watoto kutoka makabila madogo hutembea masafa marefu. Patrick Le Floch/Explorer/Eyedea Illustration Sura ya 2 Mafanikio katika malengo sita ya EFA Sura hii inafuatilia mafanikio katika kufikia malengo ya Elimu kwa Wote yaliyowekwa chini ya Mfumo wa Dakar, kukiwa na miaka mitano pekee kabla ya tarehe iliyotengwa ya kuyatimiza. Takwimu za 2007, ambazo ndizo za zaidi hivi punde, zinaonyesha maendeleo mazuri ulimwenguni, huku mataifa mengi maskini yakiwa yamefanikiwa katika nyanja nyingi. Hata hivyo, mafanikio katika kuyafikia malengo ya Dakar yanajikokota sana, na ni vigumu kuyafikia kufikia mwaka wa Tatizo ni kushindwa kwa serikali nyingi kuzipa nafasi jamii zilizotengwa. Hali hii itapelekea kukosa kutimizwa kwa ahadi za Dakar miongoni mwa jamii ya kimataifa. Sura hii pia inatoa uhakiki wa kina na wa hivi karibuni kuhusu haja ya utoaji fedha za kusaidia kutimizwa kwa EFA. Hakiki unaonyesha kwamba mapengo katika ufadhili yamekosa kukadiriwa vyema, na kwamba serikali za mataifa yanayoendelea na watoaji ufadhili, wote watahitajika kuchukua hatua za haraka kuziba mapengo haya. Malezi ya utotoni na elimu Lengo 1: Kupanua na kuimarisha utoaji wa malezi bora ya utotoni na elimu, hasa kwa watoto wanaokabiliwa na hatari nyingi na wasiojiweza. Malezi wanayopata watoto katika miaka yao ya kwanza huathiri sana maisha yao yote. Malezi bora ya utotoni na elimu (ECCE) yatawapa watoto nafasi bora ya kujikwamua kutoka kwa umaskini na kutojiweza. Licha ya haya, kila mwaka, mamilioni ya watoto hujiunga na shule wakikabiliana na ulemavu unaotokana na utapiamlo, ukosefu wa afya bora na umaskini. Kukosekana kwa usawa katika miradi mingi inayotolewa kabla ya mtoto kujiunga na shule kumebaki kuwa mzigo mkuu katika mataifa tajiri na maskini. Jumbe Kuu Utapiamlo, ambao huathiri watoto wachanga milioni 178 kila mwaka, ni dharura ya kiafya na kielimu. Kuimarishwa kwa upatikanaji wa elimu ya afya kwa mama na mtoto kuna umuhimu mkubwa kwa elimu pamoja na afya ya umma. Kuondolewa kwa ada zinazotozwa watu kunafaa kupewa kipaumbele. Serikali zinafaa kukabiliana na ukosefu wa usawa katika kufikia malezi ya utotoni, hasa ule unaohusiana na mapato na elimu ya wazazi. Utapiamlo na ukosefu wa afya bora: dharura nyamavu katika elimu Kujikokota kwa ukuaji katika tumbo la mama, kudumaa kwa ukuaji utotoni na anemia huathiri na hurudisha nyuma uwezo wa mtoto wa kujifunza. Utapiamlo na kudumaa huweza kusababisha athari za kudumu, pamoja na uwezo wa chini wa kiutambuzi na kutopata alama bora. Lishe ya watoto na vifo vya utotoni vinachora taswira mbaya ya jinsi watoto wanavyoendelea kote duniani kwa sasa. Kila mwaka, mamilioni ya watoto hujiunga na shule wakibeba ulemavu unaotokana na utapiamlo, ukosefu wa afya bora na umaskini.

11 1 0 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Alfredo Caliz/PANOS elimu huwa na uwezekano mkubwa wa kupanga uzazi, na pia kutafuta huduma bora za afya. Katika Kusini na Magharibi mwa Asia, ni 10% pekee ya wanawake wenye elimu ya shule za upili waliozaa bila huduma za mkunga aliyehitimu, ikilinganishwa na karibu nusu ya wanawake wasio na elimu. (Mchoro 2) Kukabiliana na utapiamlo: mtoto mchanga nchini Ethiopia apimwa uzito Sera zinazowezesha mafanikio ya haraka katika utoaji huduma afya za uzazi, lishe kwa mtoto na uwezo wa kuishi zimo, hata katika baadhi ya mataifa maskini zaidi duniani. Kuwepo kwa uhusiano kati ya ajenda za elimu na afya kuna umuhimu mkubwa. Sera nyingine ni pamoja na kuimarishwa kwa huduma za afya ya mama na mtoto, miradi ya utoaji misaada ya afya, huduma za afya bila malipo, kufanya lishe bora kuwa nguzo katika kukabiliana na umaskini na kuanzisha miradi mikubwa inayolinda, jamii kwa mfano kuimarisha lishe ya watoto. Ili kufanikisha kupatikana kwa mipango kama hiyo, mataifa yanafaa kubuni mifumo ya kufanikisha upatikanaji wa huduma za afya, kama njia ya kuishirikisha na mikakati mingine inayolenga makundi yasiyojiweza. Elimu ni moja ya viuasumu vya hatari za kina mama na afya ya watoto 1. Kudumaa ama kimo kidogo kwa umri kusababishwa na ukosefu wa lishe bora kwa muda mrefu na maambukizi ya mara kwa mara, hutokea hasa kabla ya miaka 2, nayo madhara yake hayarekebiki Ingawa kumekuwa na mafanikio kadha katika kufikia Malengo ya Milenia ya kupunguza vifo vya watoto na utapiamlo, bado kuna upungufu. Kulikuwa na vifo milioni 9.3 vya watoto mwaka wa Utapiamlo huhusika moja kwa moja na vifo viwili kati ya vitatu vya watoto chini ya umri wa miaka mitano.mmoja katika watoto watatu wenye umri huo jumla ya watoto milioni 178 huugua sana au kwa kiasi fulani kutokana na kudumaa kwa ukuaji utotoni. Viwango vya juu zaidi vya uvizaji vinapatikana Afrika ya Kati na Mashariki, na katika Asia Kusini. Zaidi ya nusu ya watoto milioni 19 wanaozaliwa na uzito wa chini hupatikana Asia Kusini na hukabiliwa na hatari kubwa ya kufa wakiwa watoto. Afya ya uzazi, ukosefu wa lishe bora, kutopatikana kwa wakunga waliohitimu kuzalisha na kukosa kupewa kipaumbele kwa afya ya mama na mtoto katika sera za kitaifa ni chanzo kuu cha vifo vya watoto. Takriban wanawake nusu milioni hufa kila mwaka kutokana na matatizo yanayohusiana na mimba na uzazi, na watoto milioni 4 wanaozaliwa kila mwaka hufa katika mwezi wao wa kwanza. Kando na gharama za maisha zilizotajwa hapa juu, kukosekana kwa afya bora ya mama na mtoto ambako husababisha takwimu hizi za kutisha kunaweza kuathiri uwezo wa watoto wanapokua na kuwafunga katika changamoto za kielimu baadaye. Umaskini, mazingira ya jamii asili au makabila yenye watu wachache, na viwango vya chini vya elimu ya uzazi hupunguza upatikanaji wa afya bora. Katika Asia Kusini, kuwa maskini hupunguza uwezekano wa kupata mkunga kwa mara tano. Nchini Guatemala, wanawake kutoka jamii zisizo asili huwa na uwezekano mara mbili wakilinganishwa na wanawake wa jamii asili wa kuzaa katika kituo cha afya na chini ya usimamizi wa mkunga aliyehitimu. Elimu ni moja ya viuasumu vya hatari kwa kina mama na kwa afya ya watoto. Wanawake wenye viwango vya juu vya Mipango ya elimu ya chekechea: rekodi mseto Ushiriki katika elimu ya chekechea umekuwa ukiongezeka kwa kasi tangu kuanzishwa kwa malengo ya Elimu kwa Wote mwaka wa Watoto milioni 140 walijumuishwa katika mipango ya elimu ya chekechea kote duniani mwaka wa 2007, hili likiwa ongezeko kutoka milioni 113 mwaka wa Uwiano wa watoto kujiunga katika shule (GER) ulipanda kutoka 33% hadi 41% katika kipindi hicho huku ongezeko kubwa zaidi likishuhudiwa Afrika Kusini mwa Sahara, na Kusini na Magharibi mwa Asia licha ya idadi ndogo. Kuangazia zaidi ya takwimu za maeneo, kunaonyesha tofauti kubwa miongoni mwa mataifa. Katika mataifa ambayo takwimu zake zinapatikana, mataifa kumi na saba katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara yana GER za chini ya 10%. Ingawa mataifa ya Kiarabu yana utajiri zaidi, mataifa kumi na manne kati ya kumi na tisa yaliyoangaziwa yana GER za chini ya 50%. Misri na Saudi Arabia zina viwango vya chini kuliko baadhi ya mataifa Mchoro 2: Kina mama waliosoma hupata huduma bora za kabla ya kujifungua % ya watoto chini ya umri wa miaka 3 wanaozaliwa bila ya huduma za kabla ya kuzaliwa Kusini na Magharibi mwa Asia Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara Asili: Tazama Mchoro 2.3 katika EFA Global Monitoring Report Bila elimu Msingi Ya upili au juu

12 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 1 1 maskini sana, yakiwemo Nepal na Jamhuri ya muungano ya Tanzania. Mataifa ya Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara yameongeza viwango vya watoto kujiunga na shule mara tatu kushinda mataifa ya Uarabuni, huku mengine kama Burundi, Liberia na Senegal, yalikiongeza GER kwa 20% tangu Ingawa GER katika mataifa yanayoendelea ziko juu, kufikika na muda shuleni huwa na tofauti kubwa miongoni mwa mataifa. Mataifa ya Scandinavia yana viwango vya juu vya ujumuishaji kote nchini katika elimu ya watoto wenye umri wa chini ya miaka 3, huku mataifa mengine ya OECD yakishirikisha umri wa miaka 4 hadi 6. Mataifa mengi ya Ulaya hutoa elimu ya chekechea bila malipo kwa muda wa miaka miwili. Nchini Amerika, baadhi ya majimbo husimamia kabisa elimu ya watoto wa miaka 4, ingawa mengine hayana mfumo wowote wa elimu ya chekechea. Kufikia wasio na uwezo na waliotengwa Ushahidi kote duniani unaonyesha kwamba viwango vya juu vya afya ya utotoni vina umuhimu mkubwa kwa watoto, hasa wanaotoka katika jamii zisizojiweza. Lakini wale wanaofaa kunufaika zaidi kutokana na malezi ya utotoni mara nyingi hutengwa. Watoto wanaozaliwa na kulelewa kwenye umaskini au wale ambao kina mama zao hawana elimu yoyote, wana uwezekano mdogo sana wa kushiriki katika mipango ya elimu ya chekechea. Kuzaliwa katika familia maskini zaidi nchini Zambia hupunguza uwezekano wa kufikia malezi ya utotoni kwa alama 12, ikilinganishwa na mtoto kutoka familia tajiri zaidi, na alama hii huongezeka hadi 25 nchini Uganda na 28 nchini Misri. Umbali kimasafa na kutoweza kumudu karo ni vikwazo vingine vinavyokumba jamii zisizojiweza. Mataifa tajiri pia yamewania kutimiza malengo ya usawa. Kuna ushahidi mkubwa kutoka kwa Muungano wa Ulaya na Amerika kwamba familia zenye mapato ya chini na wahamiaji hukosa kufikia huduma bora ya malezi ya utotoni. Baadhi ya mataifa yametoa kipaumbele kwa upanuzi wa mipango yake ya watoto, hasa katika kufikia makundi yasiyojiweza. Chile imeanzisha mkakati wa kitaifa wa ustawi wa watoto kiafya na kielimu. Inalenga kuwafikia watoto wote walio chini ya umri wa miaka 5, kwa kuangazia sana wale kutoka familia maskini zaidi ambazo ni 40%. Nchini New Zealand, juhudi zimefanywa za kuimarisha elimu ya chekechea inayopewa watoto wa jamii asili ya Maori. Katika miaka mitano iliyomalizika, mwaka wa 2007, idadi ya watoaji elimu kwa jamii ya Maori iliongezeka mara tatu na sehemu ya watoto wa Maori waliojiunga na shule za msingi, na ambao walihudhuria masomo ya chekechea iliongezeka kutoka 86% hadi 91%. Serikali zinafaa kutambua manufaa yanayoweza kupatikana kutoka kwa uwekezaji katika malezi ya watoto. Uwekezaji wa umma unafaa kulenga kupunguza tofauti za usawa, kwa kuangazia makundi yaliyotengwa na kutoa huduma za hali ya juu zinazofikiwa hata na watu maskini. Elimu ya msingi kwa wote Lengo 2: Kuhakikisha kwamba kufikia mwaka 2015, watoto wote, hasa wasichana, watoto wanaoishi katika hali ngumu na wale kutoka makabila madogo, wanafikia na kumaliza, elimu ya msingi ya lazima bila malipo na ya hali ya juu. Mwongo uliopita umeshuhudia mafanikio makubwa katika kuhakikisha elimu ya msingi kwa wote. Baadhi ya mataifa maskini zaidi duniani yameongeza pakubwa idadi ya watoto wanaojiunga na shule, yamepunguza pengo la jinsia na kupanua nafasi kwa makundi yanayotengwa. Licha ya haya, mamilioni ya watoto bado hawamo shuleni na mamilioni wengine huacha shule kabla ya kukamilisha masomo ya msingi. Lengo la 2015 la kuhakikisha kila mtoto anajiunga na shule na kumaliza mkondo wote wa elimu ya msingi linaweza kutimizwa, lakini litahitaji serikali zichukue hatua shupavu katika miaka miwili ijayo, hasa katika hali ya sasa ya kiuchumi. Jumbe Kuu Kumekuwa na mafanikio ya kutia moyo katika baadhi ya mataifa, huku idadi ya watoto wanaoacha shule ikishuka kwa milioni 33 kote duniani tangu Huku idadi hii ikishuka, bado kuna watoto milioni 72 ambao hawamo shuleni. Watoto milioni 56 hawatakuwa shuleni kufikia mwaka wa Ingawa kumekuwa na mafanikio katika kufikia usawa wa jinsia miongoni mwa watoto wanaojiunga na shule, vikwazo vya jinsia bado vimekita mizizi. Kuwafikisha watoto shuleni ni moja tu ya changamoto nyingi: mamilioni ya watoto hujiunga na shule wakiwa wamechelewa, huacha shule mapema na huwa hawamalizi mkondo wote wa elimu. Vijana ambao hawamo shuleni hukosa kuangaziwa: kuna watoto milioni 71 wenye umri wa chini wa shule za upili ambao hawamo shuleni. Idadi ya watoto wasio shuleni inapungua, lakini si kwa kasi inayohitajika Mwongo wa kwanza wa karne ya 21 umeshuhudia kupungua kwa idadi ya watoto wasio shuleni na kuongezeka kwa wanaomaliza shule za msingi. Hata hivyo, kuna idadi kubwa ya watoto waliofikisha umri wa kwenda shule ambao bado hawamo shuleni wanakadiriwa kuwa milioni 72 na ni lawama kuu kwa serikali za kitaifa na jamii ya kimataifa kwa jumla (Sanduku 1). Takriban 44% ya watoto wenye umri wa kwenda shule katika mataifa yanayoendelea huenda wasijiunge na shule kamwe na watakabiliwa na dhuluma kubwa kielimu. Bado kuna watoto 72 milioni wasioenda shule

13 1 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Sanduku 1: Watoto wasioenda shule: darubini ya ulimwengu Darubini ya mwaka 2007 ya watoto kwenye shule za msingi na ambao hawamo shuleni inaashiria mafanikio, lakini bado kuna upungufu mkubwa Mafanikio mema tangu 1999 Idadi ya wasiohudhuria shule duniani ilishuka kwa milioni 33 kutoka mwaka wa 1999 hadi milioni 72 mwaka (mchoro 3). Mchoro 3: Idadi ya watoto wasio shuleni inapungua lakini kwa mwendo wa kinyonga Watoto wasio shuleni (milioni) milioni milioni Asili: Tazama mchoro 2.7 katika EFA Global Monitoring Report Pande zingine za ulimwengu Amerika Kusini na Caribbean Mataifa ya Kiarabu Asia Mashariki na Pacific Asia Kusini na Magharibi Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara Idadi ya wasichana wasio shuleni imeshuka kutoka 58% hadi 54% Mataifa ya Asia Kusini na Magharibi yalipunguza kwa zaidi ya nusu, idadi ya watoto wasio shuleni kwa milioni 21 na kupunguza idadi ya wasichana wasio shuleni. Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara imepunguza idadi yake ya watoto wasio shuleni kwa karibu milioni 13 au 28%. Lakini ulimwengu bado umo nje ya mkondo Lengo la 2015 litakosa kutimizwa. Ikiwa ulimwengu utaendelea katika kasi sawa na ya sasa, kutakuwa na takriban watoto milioni 56 wasiokuwa shuleni mwaka Mwendo umepungua kasi. Thuluthi mbili ya jumla ya upungufu wa idadi ya wasiokuwa shuleni ilishuhudiwa kati ya mwaka wa 2002 na 2004 ambapo idadi ilishuka kwa milioni 22. Katika miaka mitatu iliyofuata upungufu ulikuwa wa chini ya milioni 8. Mafanikio makuu yametokea Asia Kusini na Magharibi. India ilishuhudia upungufu wa watoto milioni 15 ambao hawakuwa shuleni kati ya mwaka 2001 na Pengo katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara bado ni kubwa. Robo ya watoto wenye umri wa kwenda shule katika eneo hilo hawakuwa shuleni mwaka wa Nusu ya mataifa ishirini yenye zaidi ya watoto 500,000 wasio shuleni yamo Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara. Mizozo nayo ni kizuizi kikuu cha watoto kuhudhuria shule. Makadirio mema zaidi yanadokeza kwamba zaidi ya watoto milioni 2 wasio shuleni, licha ya kufikisha umri wa kwenda shule, wamo katika mataifa yaliyoathiriwa na mizozo 35% ya jumla ya idadi yote duniani. Idadi ya watoto wasio shuleni huenda imekadiriwa kwa kiasi cha chini. Ushahidi wa utafiti wa familia unaonyesha kwamba huenda takwimu rasmi hukadiria viwango vya wasio shuleni kwa hadi 30%. 1. Idadi hii haifai kulinganishwa na makadirio katika ripoti ya 2009 Education for All Global Monitoring Report, ambayo yaliangazia kundi ndogo la mataifa. Idadi ya watoto wasio shuleni huenda imekadiriwa kwa chini, kukiwa na uwezekano wa kupunguzwa kwa asilimia 30 duniani Kutambua ni nani asiyehudhuria shule kuna umuhimu mkubwa katika kubuni sera za umma, sawa na kuelewa ni watoto gani wanaoanza shule wakiwa wamechelewa, ni gani wanaoacha shule na ni wepi wasiofika shuleni kamwe. Wasichana, na watoto kutoka jamii maskini na zinazoishi mashambani, wote hukabiliwa na hatari kubwa ya kutoweza kuhudhuria shule. Makundi haya matatu huingiliana na pamoja na sababu nyingine - kama vile lugha, ukabila na ulemavu kubuni vikwazo vinavyowazuia watoto kujiunga na shule na kukaa huko. Wasichana wadogo walichukua 54% ya watoto wasiokuwa shuleni duniani mwaka Sehemu ya wasichana wasiokuwa shuleni iko juu zaidi katika Mataifa ya Kiarabu, Asia ya Kati, ya Kusini na ya Magharibi. Usajili shuleni wa watoto waliofikisha umri huo unaongezeka kwa upole sana Mengi ya mataifa yanayoendelea, ambayo mwongo ulipoanza yalikuwa mbali sana na kufikia malengo ya kujiunga na shule za msingi kwa wote, yamepiga hatua kuu. Tangu 1999, mataifa ya Asia Kusini na Magharibi, na Afrika Kusini mwa Sahara yameongeza idadi ya wanaojiunga na shule kwa mara tatu na tano, ya viwango vya miaka ya 1990, na kufikisha 86% na 73% mtawalia. Mafanikio hayo ni ushahidi kwamba malengo ya Dakar yanaweza kutimizwa. Mataifa yaliyoendelea na mataifa yaliyo katika mpito yamo karibu sana kutimiza lengo la elimu ya msingi kwa wote. Mafanikio kwa jumla katika kutimiza elimu ya msingi kwa wote inaficha hali zisizoeleweka kwa urahisi za mataifa. Mataifa yana ustawi tofauti, baadhi hayasongi kamwe, mengine yanarudi nyuma. Baadhi ya mataifa maskini zaidi duniani yamepiga hatua kubwa mbele. Benin ilianza mwaka 1999 ikiwa na viwango vya chini zaidi vya wanaojiunga na shule duniani lakini kwa sasa imo mbioni kutimiza malengo ya elimu ya msingi kwa wote mwaka 2015 (Sanduku 2). Mataifa mengine yaliyokuwa na viwango vya chini vya wanaojiunga na shule na idadi kubwa ya wanaoacha shule

14 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 1 3 Idadi kubwa na ukosefu wa vifaa: darasa nchini Malawi Louise Gubb/Corbis kwa mfano Nigeria yana mwelekeo bora, lakini kwa kasi ya konokono. Mataifa thelathini yanayoendea, ambayo takwimu zinapatikana, yalishuhudia kusimama au kushuka kwa viwango vya waliojiunga na shule kati ya mwaka 1999 na Sanduku 2: Benin: Mkondo mzuri ila kukabili utengwaji kupewe kipaumbele Benin imekuwa miongoni mwa mataifa yanayosonga kwa kasi sana katika usajili wa watoto shuleni huku uwiano wa jumla ukiongezeka kutoka 50% mwaka wa 1999 hadi 80% mwaka Pengo kati ya jinisia pia limepungua, kutoka kwa wasichana 67 dhidi ya wavulana 100 waliokuwa shuleni mwaka wa 1999 hadi wasichana 83 mwaka wa Kwa mwelekeo huu, Benin inaweza kutimiza malengo ya (UPE) kufikia mwaka wa Kudumisha mtindo huu kutakuwa vigumu, hata hivyo. Ufanisi wa haraka umeleta changamoto za sera kama kuongeza viwango vya wanaomaliza shule, kupunguza tofauti kimaeneo na kukabiliana na umaskini. Serikali tayari imejitolea sana kwenye bajeti. Ili kuhakikisha Benin inafika hatua ya mwisho ya elimu ya msingi kwa wote, misaada kutoka kwa jamii ya kimataifa inahitajika kupiga jeki ufadhili wa kitaifa. Mengi ya mataifa haya yanaathiriwa au yanajikwamua kutoka kwa mizozo kama vile Liberia au Himaya za Utawala wa Palestina. Usawa wa jinsia: mafanikio yapo lakini kibarua kingalipo Kupanuliwa kwa elimu ya msingi kumeenda bega kwa bega na mafanikio katika kupunguza pengo kati ya jinsia, ingawa kuna tofauti kubwa kati na ndani ya manaeneo. Katika mataifa yaliyoanza na viwango vya chini vya waliojiunga na shule mwaka wa 1999, kama vile Burkina Faso, Ethiopia na Yemen, hatua za kufikia usawa wa jinsia kutoka kiwango cha chini sana zimesaidia kuongeza viwango vya wanaojiunga na shule. Hata hivyo, mataifa 28 yana wasichana chini ya 90 kwa wavulana 100 walio shuleni; 18 ya mataifa haya yamo Afrika Kusini mwa Sahara. Kuna pengo kubwa pia kati ya jinsia katika Mataifa ya Kiarabu, Asia Kusini na Magharibi: nchini Afghanistan kuna wasichana 63 kwa wavulana 100 walio shuleni. Huku yakiwa na baadhi ya mapengo makubwa zaidi ya kijinsia duniani, mataifa kadha ya Afrika Magharibi yamekumbatia sera zinazolenga kuimarisha usawa katika mkakati shirikishi wa kufanikisha elimu ya msingi kwa wote. Nguzo kuu za sera hizi ni kubadilisha mtazamo wa jamii kwa nafasi ya wasichana na wanawake katika jamii, kutoa vishawishi vya kifedha kwa wanaowapeleka wasichana shule, kutoa maji na huduma za usafi katika shule, kuwaajiri walimu wa kike na kuongeza idadi ya walimu wanaotumwa maeneo ya mashambani, na uhamasishaji wa walimu kuhusu jinsia. Katika maeneo ya mashambani yaliyo mbali zaidi na miji, ambapo umbali wa shule huwa hofu kuu ya wazazi kwa usalama wa wasichana wao, serikali zinajaribu kuleta madarasa karibu na jamii, kwa kujenga shule za muda. Kuwapeleka wasichana shuleni huhitaji juhudi za pamoja na viongozi wa kisiasa kubadili mtazamo na tamaduni za kazi na utekelezaji majukumu nyumbani. Kuwadumisha shuleni wanapobaleghe huibua changamoto nyingine hasa katika mataifa ambayo ndoa za mapema hufanyika, na dhuluma dhidi ya wasichana huoana na umaskini na ukabila. Mataifa kama vile Bangladesh na Cambodia yamethibitisha kwamba vishawishi vya kifedha vinaweza kuongeza uwezekano wa wasichana kujiunga na vidato vya chini vya shule za upili na kuongeza hitaji la elimu ya msingi. Kinyume ni kuwa, katika mataifa kadha yanayoendelea, idadi ya wasichana wanaojiunga na shule huwa ya juu kuliko ya wavulana. Baadhi ya hali hizi husababishwa na mahitaji mengi ya ajira za wavulana. Kwa mfano, katika familia maskini zinazoishi katika nyanda za juu nchini Lesotho, aghalabu hutegemea wavulana kuchunga ng ombe, jambo linalochangia wao kuacha shule baada ya darasa la tatu. Kuwapeleka wasichana shuleni huhitaji juhudi za pamoja na viongozi wa kisiasa kubadili mtazamo na tamaduni za kazi na utekelezaji majukumu nyumbani.

15 1 4 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Takriban vijana milioni 71 hawakuwa shuleni mwaka wa 2007, sawa na mmoja katika vijana watano katika rika hilo Mkondo wa mwisho: Baadhi ya mataifa yenye viwango vya juu vya wanajiunga na shule yanakabiliwa na matatizo Baadhi ya mataifa hayafanyi vyema kama yalivyotarajiwa ikizingatiwa utajiri wayo. Nchini Ufilipino, idadi ya watoto wasiokuwa shuleni wenye umri wa miaka 6 hadi 11 ilifika milioni 1 mwaka wa 2007, 100,000 zaidi ya mwaka wa Viwango vya uwiano vya waliojiunga na shule nchini Uturuki vimesalia 90% tangu kuanza kwa mwongo huu. Mataifa yote mawili yanakabiliwa na changamoto mzito za baadhi ya makundi kuwekwa pembezoni. Nchini Ufilipino, utengwaji umehusishwa sana na umaskini na eneo: Eneo Linalojitawala la Kiislamu la Mindanao, ambalo hutatizwa sana na umaskini na mizozo limebaki nyuma. Nchini Uturuki, dhuluma zimewalemea watoto kutoka jamii maskini, na wasichana walio mashambani hasa mashariki mwa nchi hiyo. Katika mataifa haya mawili, sera za sasa hazikomeshi dhuluma za jadi. Kutoka kusajiliwa mpaka kuhitimu na baadaye: safari ngumu, isiyoweza kupimika Kwa mamilioni ya watoto wanaojiunga na shule za msingi, safari katika mfumo wa elimu mara nyingi hucheleweshwa, huwa yenye hatari nyingi na ya muda mfupi. Katika nusu ya mataifa katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, na Asia Kusini na Magharibi, mmoja kati ya watoto watatu wanaojiunga na shule za msingi huacha shule kabla ya kumaliza. Katika maeneo yote mawili, wengi huwa hawapiti kihunzi cha kwanza. Mwaka 2006, 13% ya wanafunzi katika Asia Kusini na Magharibi na 9% Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara waliacha shule kabla ya kumaliza darasa la kwanza. Nchini Nicaragua, 67% ya watoto waliofikisha umri rasmi wa kujiunga na shule walijiunga mwaka wa 2006, lakini ni robo tu kati yao waliomaliza shule (Mchoro 4). Vifaa vya sasa vya kuchunguza havitoi njia fungamani ya kukadiria mambo matatu muhimu katika kuafikia elimu ya msingi kwa wote: kujiunga na shule katika muda unaofaa, kuendelea vyema na mfumo shuleni na kumaliza shule. Ripoti inaeleza haja ya kuwa na mbinu shirikishi ya kutambua viwango halisi vya kumaliza shule. Vijana walioacha shule Kulenga watoto wenye umri wa kuhudhria shule za msingi ambao hawamo shuleni kumekosesha umakinifu katika tatizo lililo kuu.watoto wengi waliofikisha umri wa kuhudhuria vidato vya shule za upili pia hawamo shuleni, kwa sababu hawakumaliza masomo ya msingi au walipotea katika kiwango cha mpito. Takriban vijana milioni 71 hawakuwa shuleni katika mwaka wa 2007, sawa na mmoja katika vijana watano katika rika hilo. Tatizo hili ni kubwa sana Afrika Kusini mwa Sahara, huku 38% ya vijana wakiwa hawamo shuleni na wengine 28% Kusini na Magharibi mwa Asia. Sawa na shule za msingi, wasichana waliobalehe wana uwezekano mkubwa wa kuacha shule wakilinganishwa na wavulana. Duniani, 54% ya vijana ambao hawakuwa shuleni mwaka wa 2007 walikuwa wasichana. Shughuli ya mpito kutoka shule za msingi hadi ngazi ya chini ya shule za upili huwa ngumu kwa watoto wengi. Vikwazo katika kiwango cha msingi huzidisha makali katika shule za upili kwa mfano gharama, umbali wa shule, mahitaji ya kufanya kazi na hasa kwa wasichana waliolazimishwa katika vikwazo vya kijamii, kitamaduni na kiuchumi. Nchini Mauritania na Senegal, umbali wa wastani wa safari ya kwenda katika shule ya upili iliyo karibu ni wa dakika themanini katika maeneo ya mashambani; nchini Senegal, ni mara 25 mbali kuliko shule ya msingi iliyo karibu. Umbali unaweza kuzidisha athari za umaskini, huku familia maskini zikishindwa kugharamia nauli au nafasi katika shule za mabweni. Mpito kuingia vidato vya shule za upili sasa ndio unaoangaziwa katika ajenda ya Elimu kwa Wote katika mataifa mengi. Huku watoto wengi wakijiunga na kuendelea na masomo ya msingi, mahitaji ya nafasi katika shule za upili yanaongezeka. Hata hivyo muhimu kwa serikali na wafadhili kujiepusha na mabadiliko yasiyokomaa ya sera. Huku mamilioni ya watoto wakiwa bado hawapati elimu ya msingi, na ulimwengu ukikosa kutimiza malengo ya mwaka 2015, kuongeza shule za upili hakufai kuathiri uimarishaji wa viwango vya elimu ya msingi. Mchoro 4. Safari ngumu ya kupata elimu ya msingi: mfano wa Nicaragua Umri wa kujiunga na shule ya msingi (100%) Kiwango cha kujiunga na darasa la kwanza (67%) 67 Kundi linalojiunga katika umri unaofaa Kuendelea hadi darasa la 5 (47 ya kundi lililojiunga) Nchini Nicaragua, viwango vya kujiunga na darasa la kwanza vilikuwa asilimia 67 mwaka Viwango vya kufikisha darasa la 5 vilikuwa 47% na vya kumaliza masomo ya msingi asilimia 40. Viwango hivi vinatuwezesha kukadiria matumaini ya kundi la wanafunzi wenye umri wa miaka 6 (umri wa kujiunga na shule ya msingi) kumaliza mkondo huo wa miaka sita. Ikiwa viwango vya kurudia darasa na kuacha shule havitabadilika, kati ya wanafunzi 100 wenye umri wa miaka 6, 67 watajiunga na darasa la kwanza katika umri unaofaa. Kati ya hawa, 32 watasoma hadi darasa la 5, na 27 watafuzu kutoka darasa la mwisho. 32 Wanaosalia hadi darasa la 5 katika kundi hilo (32 %) Kiwango cha kukamilisha elimu ya msingi (40% ya kundi lililojiunga) 27 Kiwango cha kumaliza (27%) Asili: Tazama Mchoro 2.22 katika EFA Global Monitoring Report 2010

16 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 1 5 Ujuzi wa vijana na watu wazima kupanua nafasi Lengo 3: Kuhakikisha kwamba mahitaji ya vijana wote na watu wazima yanatimizwa kwa kuwezesha kufikika kwa miradi ya mafunzo na ujuzi wa kusajidia maishani Katika uchumi wa dunia unaoongozwa na maarifa, mafunzo na ujuzi hutekeleza jukumu muhimu katika kuleta matumaini ya ukuaji wa kiuchumi, ufanisi wa pamoja na kupunguza umaskini. Licha ya haya, tangu 2000 lengo la tatu la EFA limekosa kuangaziwa. Jumbe Kuu Idadi inayoongezeka ya vijana wasio na ajira ni changamoto inayozidi kukua ulimwenguni. Serikali, vyama vya wafanyakazi na waajiri wote wanafaa kufanikisha elimu ya taaluma ambayo itawapa vijana ujuzi wanaohitaji ili kufanikiwa kazini. Ili ujuzi uwe wa kufaa na kupelekea shughuli laini ya mpito kutoka shule hadi kazini, mipango ya mafunzo ya taaluma sharti iambatane na mahitaji ya wafanyakazi sokoni. Serikali zinapaswa kutilia nguvu elimu ya msingi na kuhakikisha vijana wanafika shule za upili ili kujenga msingi bora wa ufanisi wa mipango ya mafunzo ya kitaalamu. Serikali katika mataifa yenye mapato ya chini zinapaswa kuangazia zaidi sekta isiyo rasmi na kutoa fursa ya pili. Mfumko wa kiuchumi duniani ulisukuma juu utoaji mafunzo kwenye ajenda za kisiasa. Ukosefu wa kazi miongoni mwa vijana unaongezeka kutoka viwango ambavyo bado vilikuwa juu: viwango vilivyokadiriwa vya mwaka 2009 ni kati ya 14% na 15%, ikilinganishwa na 12% mwaka Serikali kote duniani kwa sasa zinakabiliwa na changamoto la kutoa usaidizi kwa wasiojiweza huku ikiwapa watu ujuzi wanaohitaji ili kupata kazi tena. Nafasi ya mafunzo ya kitaalamu katika elimu ya upili na vyuo Ushiriki katika mafunzo ya kiufundi na kitaalamu umeongezeka sambamba na kupanuka kwa elimu ya upili. Mataifa yaliyoendelea yako karibu kufikia elimu ya upili kwa wote, na pia wanaojiunga na vyuo wameongezeka, huku viwango vya kujiunga na vyuo vikifikia 67% mwaka Maeneo maskini yanajaribu kuyafikia ingawa kwa kasi tofauti. Viwango vya kujiunga na shule za upili viko tofauti kutoka 34% Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara hadi 65% katika Mataifa ya Kiarabu na 90% Amerika Kusini. Kiwango cha kujiunga na vyuo ni 6% pekee Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, kikilinganishwa na 22% katika Mataifa ya Kiarabu na 35% Amerika Kusini. Katika mataifa yaliyoendelea, takriban 16% ya waliojiunga na shule za upili walisomea ufundi na utaalamu mwaka wa 2007, ikilinganishwa na 9% katika mataifa yanayoendelea. Viwango vya kujiunga na shule za upili vilikuwa vya chini zaidi Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara (6%) na Asia Kusini na Magharibi (2%). Tofauti kubwa zilikuwepo baina ya mataifa katika maeneo tajiri na maskini. Wanafunzi wa kike mara nyingi huwa wachache katika elimu ya ufundi na utaalamu. Katika nchi za Asia Kusini na Magharibi na Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, wasichana walijumuisha 44% ya wanafunzi katika shule za upili mwaka wa 2007, lakini 27% na 39% pekee mtawalia walijiunga na vyuo vya ufundi. Katika tisa kati ya mataifa kumi na moja ya Kiarabu yaliyoangaziwa, wasichana walijumuisha chini ya 40% ya waliosomea taaluma. Tofauti za kijinsia hazifikii kikomo kwa kujiunga na vyuo pekee. Mara nyingi, wasichana wanaojiunga na vyuo hufunzwa taaluma zinazojulikana kuwa za malipo duni. Nia njema, matokeo mabaya: matatizo katika mataifa yanayoendelea Katika mataifa mengi yanayoendelea, elimu ya ufundi na taaluma imeathiriwa sana na mchanganyiko wa ukosefu wa fedha, muundo duni, mtazamo mbaya wa wazazi na uhusiano dhaifu kati yake na masoko yanayotoa ajira. Hali katika maeneo mbalimbali hutofautiana sana. Katika Mashariki ya Kati, eneo linalojulikana sana kwa viwango vya juu vya ukosefu wa ajira kwa vijana takriban 20% ya vijana hawana kazi serikali zimetambua mafunzo ya ufundi na utaalamu na kuyapa kipaumbele. Hata hivyo elimu ya kitaalamu huathiriwa na mambo kama vile uratibu duni wa serikali, raslimali haba zinazotengwa kwenye bajeti, ukosefu wa walimu waliohitimu, mtaala usio na uhusiano na ujuzi unaotakikana na waajiri na ukosefu wa viwango maalum. Hata hivyo, kuna mataifa yaliyojitenga. Nchini Misri, ushirikiano bunifu umeleta pamoja serikali, wafanyabiashara na wafadhili. Morocco imekumbatia mageuzi makuu ya usimamizi yanayolenga kuimarisha viwango, manufaa na usawa. Hata hivyo, rekodi kwa jumla ni duni. Katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, serikali zinakabiliwa na mojawapo ya changamoto kuu zaidi katika kufanyia mageuzi mifumo ya elimu ya kiufundi na kitaaluma. Matatizo kama vile gharama ya juu, ukosefu wa uwekezaji wa kutosha, mishahara duni na ukosefu wa watu waliohitimu huuma sana. Wanafunzi huingizwa katika mifumo ya kitaaluma mapema sana na wanaofuzu bado hukosa ajira. Zaidi ya hayo, utafiti nchini Burkina Faso, Ghana na Jamhuri ya Tanzania umeonyesha kwamba makundi yaliyowekwa pembezoni huenda yasifaidike Mfumko wa kiuchumi duniani ulisukuma juu utoaji mafunzo na ujuzi katika ajenda za kisiasa

17 1 6 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Miradi ya Jóvennes imefanikiwa sana katika kuwafikia waliotengwa, na kuleta uhusiano kati ya ajira na utoaji mafunzo kutokana na mipango ya utoaji mafunzo ya kiufundi na kitaalamu.mikakati yenye manufaa, hata hivyo, inaibuka katika mataifa kama vile Cameroon, Ethiopia na Rwanda. Sawa na katika maeneo mengine, serikali za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara sharti zitafute uwiano kati ya elimu ya kawaida, ya kiufundi na ya kitaaluma. Lengo kuu linafaa kuwa kuongeza idadi ya wanaojiunga, kudumisha na kumaliza elimu ya msingi na hatimaye kujiunga na shule za upili. Elimu ya taaluma inaweza kutekeleza jukumu muhimu, hata hivyo, katika kutoa fursa ya pili kwa vijana waliotengwa. Kuwapa vijana fursa ya pili Ili kukabiliana vilivyo na kutengwa kwa baadhi ya makundi, mipango ya elimu ya ufundi na taaluma inafaa kutazama zaidi ya shule na elimu rasmi. Sharti pia itoe fursa ya pili kwa mamilioni ya vijana katika mataifa tajiri na maskini ambao walinyimwa fursa ya elimu katika miaka yao ya kwanza maishani. Udadisi kote duniani umeonyesha kwamba utoaji wa mipango ya fursa ya pili unaweza kuleta tofauti kubwa. Mbinu shirikishi zinazotoa mafunzo kama sehemu ya fungu kubwa la ujuzi na usaidizi zina uwezekano mkubwa wa kufanikiwa. Mipango ya Jovennes katika mataifa kama vile Argentina, Chile, Peru na Uruguay imefanikiwa sana katika kuwafikia waliowekwa pembezoni, na kuleta uhusiano kati ya ajira na utoaji mafunzo. Ingawa hili linaashiria yale yanayowezekana, elimu ya fursa ya pili imesahauliwa na wengi, na mara nyingi hukosa kujumuishwa katika mfumo wa elimu, na hupokea usimamizi kiasi kutoka kwa serikali. Mipango inayoleta matokeo Ufanisi wa mipango ya elimu ya ufundi na taaluma huwa tofauti sana na hutegemea mambo yaliyo nje ya sekta ya elimu. Baadhi ya mafunzo muhimu yanayofaa kuzingatiwa ni haja ya: Kuimarisha uhusiano kati ya elimu na masoko ya kazi. Kutambua kwamba mafanikio ya zamani si hakikisho la ufanisi siku za usoni, na kwamba serikali sharti zibadilishe na kubuni upya mipango ya mafunzo ya taaluma kuambatana na mabadiliko ya hali. Kuepuka kutenganisha elimu ya taaluma na elimu ya kawaida kwa kuweka njia thabiti katika mifumo ya mafunzo ya taaluma hasa mapema maishani. Katika jamii ya sasa yenye msingi wake katika maarifa, yale unayojua yana umuhimu mdogo kuliko yale unayoweza kujifunza. Kubuni mifumo ya uhitimu wa kitaifa inayoongozwa na uwezo kwa kuhusisha sekta ya kibinafsi, ambayo itawezesha utoaji mafunzo kwa kuhamisha alama kwa ufundi na elimu kwa jumla. Kufungamanisha mipango ya mafunzo ya taaluma na mikakati ya kitaifa ya ujuzi, na kuilainisha kulingana na mahitaji ya sekta zinazohitaji ukuaji wa juu. Hakuna serikali inayoweza kupuuza jukumu la ujuzi na mafunzo katika kusaidia ukuaji wa uchumi, kukabiliana na umaskini na kukabiliana na kutengwa kwa baadhi ya jamii. Serikali na jamii ya kitaifa zinapaswa kutayarisha, kwa dharura vigezo muhimu vya kupima maendeleo na sera za kufanikisha usawa. Misaada kwa familia maskini inaweza kusaidia kurejesha watoto wanaofanyishwa kazi shuleni, nchini Ufilipino Marconi Navales

18 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 1 7 Kujua kusoma na kuandika kwa watu wazima Lengo 4. Kuafikia ongezeko la 50% katika viwango vya elimu ya watu wazima kufikia mwaka wa 2015, hasa kwa wanawake, na pia usawa katika kupata elimu ya kimsingi na ya ziada kwa watu wote wazima. Jumbe Kuu Licha ya mafanikio thabiti, takriban watu wazima milioni 759 hawajui kusoma na kuandika. Thuluthi mbili kati yao ni wanawake. Huku usawa wa kijinsia ukiimarika, wanawake na vikundi vingine visivyobahatika katika jamii wanazidi kunyimwa haki zao za kujua kusoma na kuandika. Kuendelea na elimu nchini Lebanon: kusoma huimarisha bila kubagua umri REUTERS/Zohra Bensemra Juhudi mwafaka za kuimarisha mafanikio haya zisipofanywa, takriban watu wazima milioni 710 watakuwa hawajui kusoma wala kuandika ifikapo mwaka wa Juhudi za haraka za kufikia ufanisi zinaweza kupatikana iwapo sera nzuri na mikakati itawekwa. Watu wanapomaliza shule bila kupata elimu bora ya kimsingi, na kufanya Hisabati, wao hukumbana na shida za kijamii na kiuchumi katika maisha yao yote. Licha ya hayo, jamii kwa ujumla hupoteza uwezo wa kujiendeleza na kujikuza. Aidha ufanisi kwa wote, na ushiriki katika siasa hukosekana. Moja kati ya changamoto kuu za karne ya 21 ni kupiga vita kutojua kusoma na kuandika. Ripoti ya ustawi baada ya mkutano wa Dakar Hivi leo, takriban watu milioni 759 hawajui kusoma wala kuandika; hii ikiwa ni karibu 16% ya idadi ya watu watatu wazima duniani, takribani thuluthi mbili kati yao wakiwa wanawake. Hali hii ya kutojua kusoma na kuandika imejikita katika idadi ndogo ya nchi zilizo na idadi kubwa ya watu (Mchoro wa 5). Zaidi ya nusu ya watu wazima wasiojua kusoma wala kuandika hupatikana katika nchi nne tu; Bangladesh, Uchina, India na Pakistan. Katika Asia Kusini na Magharibi pamoja na nchi za Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara, mmoja kati ya watu watatu wazima hawajui kusoma wala kuandika. Katika nchi nne zilizoko barani Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara, yaani Burkina Faso, Guinea, Mali na Niger, idadi yao imefika 70%. Tofauti za kijinsia ndizo chanzo kikuu cha kutojua kusoma na kuandika miongoni mwa watu wazima katika sehemu hizi tatu. Nchini Afghanistan, kwa mfano, 57% ya wanaume wazima walikuwa hawajui kusoma na kuandika katika mwaka wa Mataifa tajiri pia yana idadi fulani ya watu wasiojua kusoma wala kuandika. Kwa mfano, nchini Uingereza watu milioni 1.7 (5% ni wale walio kati ya miaka 16-65) wana uwezo wa kusoma na kuandika ulio chini ya ujuzi wa mwanafunzi wa miaka 7 kwa kuzingatia mitihani ya kitaifa na mitaala, huku wengine milioni 5.1 wakiwa na ujuzi ulio chini ya ujuzi wa mwanafunzi wa miaka 11. Kufahamu kusoma na kuandika miongoni mwa watu wazima kumekuwa kukiimarika. Hali hii imefaulishwa na kuimarishwa kwa shule na mikakati ya kusoma na kuandika. Katika miaka ya na idadi ya watu wazima ambao hawakujua kusoma na kuandika ilipungua kwa13% huku kiwango cha wanaojua kusoma na kuandika kikiongezeka kwa 10%, na kufikia 84% hivi sasa. Kuimarika huku kulishuhudiwa, hasa mashariki mwa Asia na Pacific, huku Uchina na Asia zikionyesha ufanisi wa hali ya juu zaidi. Nchini India, nchi iliyokuwa na idadi kubwa zaidi ya wasiojua kusoma na kuandika, ujuzi huu uliimarika kutoka nusu ya idadi ya watu wazima kufikia zaidi ya thuluthi mbili. Nchini Burkina Faso na Chad, nchi ambazo zilikuwa na idadi kubwa zaidi duniani ya wasiojua kusoma na kuandika, idadi ya wanaojua kusoma na kuandika iliongezeka maradufu nchini Burkina Faso, huku ikikaribia kuongezeka kwa mara tatu nchini Chad. Hata hivyo, kulingana na mielekeo hii, takriban watu wazima milioni 710, hii ikiwa ni13% ya watu wazima duniani, bado watakosa ufahamu wa kimsingi wa kujua kusoma na kuandika ifikapo mwaka Usawa wa kijinsia unaimarika lakini vizuizi fulani bado vingalipo Kuimarika kwa kusoma na kuandika kumesababisha kupungua kwa ubaguzi wa kijinsia. Usawa wa kijinsia unaimarika katika mataifa yote, isipokuwa 8 kati ya 79 yaliyokuwa na rekodi bora za kurejelewa. Nchini Bangladesh, Burkina Faso, Burundi, Malawi, Nepal na Yemen kujua kusoma na kuandika miongoni mwa wanawake kuliimarika marudufu au hata mara tatu. Ongezeko hili ni maradufu ya Nigeria 17 Misri 14 Brazil 13 Indonesia 10 Morocco Hivi leo, takriban watu milioni 759 hawajui kusoma wala kuandika Mchoro 5: Elimu ya watu wazima imekithiri katika kundi dogo la nchi zenye idadi kubwa Uchina Bangladesh Pakistan Ethiopia India Nchi zilizosalia Watu wazima (miaka 15 na zaidi) wasiojua kusoma na kuandika, katika mamilioni Asili: Tazama Mchoro 2.29 katika EFA Global Monitoring Report 2010

19 1 8 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Tangu mwaka wa 2003, mpango wa Brazil wa kuimarisha kusoma na kuandika umetoa mafunzo ya kielimu kwa karibu wanafunzi milioni 8 walio na umri wa zaidi ya miaka Kikao cha tatu cha kimataifa kwa masomo ya Sayansi na Hisabati (TIMSS 2007) ongezeko la wanaume. Kati ya miaka ya na idadi ya wanawake wazima waliojua kusoma na kuandika iliongezeka kwa 14% ikilinganishwa na 7% kwa wanaume. Kwa hakika, wanawake wanajizatiti katika nyanja hii, ingawaje katika mataifa mengi wanaanzia mbali sana. Dhuluma wanazopitia wanawake, sio chanzo tu cha ukosefu wa usawa miongoni mwa mataifa. Kutojua kusoma na kuandika miongoni mwa watu wazima hujikita katika umaskini, maeneo ya kijiografia, elimu ya wazazi, kabila, lugha na ulemavu. Kwa mfano, nchini Guatemala, 60% ya watu wazima wanaoishi katika uchochole, hawajui kusoma wala kuandika ikilinganishwa na 17% ya walio matajiri. Makabila madogomadogo na ya kiasili, aghalabu huwa na idadi ndogo ya wanaojua kusoma na kuandika. Nchini Vietnam, wanaojua kusoma na kuandika ni 94% miongoni mwa kabila la Kinh, kabila la walio wengi zaidi, huku makabila mengine ya walio wachache yakiwa na 72%. Idadi ya wasiojua kusoma na kuandika inaonekana kuongezeka katika maeneo maskini, maeneo ya mashambani na katika vitongoji duni. Kubadilisha mkondo: kufanya mwongo wa kusoma na kuandika kutambulika Ufanisi wa kijumla wa kufikia kujua kusoma na kuandika kama lengo lililoafikiwa huko Dakar umekuwa wa kuvunja moyo. Kupiga vita ujinga hakujapewa kipaumbele na nyanja za kisiasa. Aidha, ahadi za kifedha hazijatimizwa na juhudi za kujumuisha mikakati ya kuimarisha kujua kusoma na kuandika katika mpango mpana wa kupunguza umasikini hazijaimarishwa. Hata hivyo, kuna matumaini. Mataifa kadha yaliyo na idadi kubwa ya wasiojua kusoma na kuandika yanazidi kuwekeza katika mikakati ya kitaifa ya kuimarisha elimu. Tangu mwaka wa 2003, mpango wa Brazil wa kuimarisha kusoma na kuandika (Programa Brazil Alfabetizado) umetoa mafunzo ya kielimu kwa karibu wanafunzi milioni 8 walio na umri wa zaidi ya miaka 15. Nchini India, mikakati ya elimu kitaifa (National literacy mission) inapanuliwa kwa makadirio ya Dola bilioni 21. Mafunzo ya kimsingi na mafunzo ya ziada yanaendelezwa na mradi huu kwa lengo la kuondoa ujinga. Pia, mikakati ya kufundisha kwa lugha za kiasili inawekwa. Katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, vituo vya mafunzo vya kijamii vimeanzishwa na shirika la kiserikali la kufanikisha elimu kwa watu wazima (literacy movement organization). Watu milioni 3.1 wasiojua kusoma na kuandika walijiunga navyo kati ya mwaka wa 2000 na 2006 kwa elimu ya kimsingi. Mengi yanahitaji kufanywa ili kuimarisha hatua za kupata elimu. Mataifa duniani kote yanahitaji kujitolea kisiasa na kuyapa kipaumbele masuala ya elimu katika kujenga taifa. Ujinga ni gharama kubwa sana kwa jamii na uchumi wa nchi na kuwekeza katika elimu kutafaidi nchi pakubwa. Ubora wa elimu Lengo 6: Kuimarisha nyanja zote za elimu na kuhakikisha ubora kwa yote ili matokeo bora yaafikiwe, hasa katika kusoma na kuandika, hesabu na katika ujuzi muhimu maishani. Jumbe Kuu Ubora wa shule hutofautiana sana miongoni mwa mataifa huku viwango vya mafunzo vikiwa vya chini sana katika mataifa mengi maskini. Ukosefu wa usawa katika mafunzo umeenea sana katika mataifa yenye mapato ya chini na kuzua umuhimu wa kuwa na sera za kuhakikisha wote wanapata nafasi sawa. Kupata ujuzi wa kusoma katika shule za msingi ni muhimu katika kupata ufanisi shuleni na katika maisha ya baadaye. Kuhakikisha kuwa walimu wamehitimu na wana motisha ya kufundisha ni muhimu kwa ufundishaji bora. Zaidi ya walimu milioni 1.9 watahitaji kuajiriwa ili kuhakikisha kuwa Elimu kwa Wote (EFA) inaafikiwa kufikia mwaka wa Mamilioni ya watoto hufuzu kutoka shuleni kila mwaka bila ya kupata ujuzi mwafaka wa kusoma na kuhesabu. Wabuni-sera, walimu na wazazi wanahitaji kuchunguza zaidi kiini cha elimu: wahakikishe kuwa wanafunzi wanapata ujuzi utakaowafaa katika siku za usoni. Pengo katika elimu: kutoka kimataifa hadi kitaifa Utafiti wa kimataifa kuhusu mafunzo unaangazia changamoto mbili katika nyanja hii: mwanya mkubwa ulimwenguni kimafunzo na viwango vya chini vya mafunzo/elimu katika mataifa mengi maskini. Utafiti wa hivi karibuni kuhusu somo la Hisabati na Sayansi (TIMSS) 2 unaonyesha ukosefu wa usawa ulimwenguni. Alama ya wastani (Average test score) katika mtihani wa Hisabati kwa mwanafunzi wa darasa la nane katika jamhuri ya Korea, ambayo ni nchi inayofanya vizuri sana, zilipiku za wanafunzi nchini Ghana, iliyokuwa ya mwisho kimataifa, maradufu. Kwa maneno mengine, wanafunzi walio na ujuzi wa wastani nchini Ghana, Indonesia au Morocco wako katika kiwango sawa, au chini ya wanafunzi 10% wa mwisho katika mataifa yanayofanya vizuri kimasomo. Katika darasa la 4 katika shule za msingi, takriban wanafunzi wote nchini Japan walikuwa na ujuzi wa wastani katika somo la Hisabati, ilhali nchini Yemen hakuna hata mwanafunzi mmoja aliyepata alama zaidi ya kiwango hicho. Mataifa maskini hayajawakilishwa sana na tathmini za kimataifa; lakini hakuna ushahidi unaoonyesha tatizo hili kuwa sugu. Utafiti wa kimaeneo uliofanywa na SACMEQ katika eneo Afrika Kusini mwa Sahara unaonyesha kuwa zaidi ya nusu ya wanafunzi wa darasa la sita katika shule za msingi walifeli kupata viwango vya kimsingi vya kuhesabu. Nchini Pakistan mashambani, utafiti wa hivi punde unaonyesha kuwa thuluthi mbili ya wanafunzi wa darasa la tatu waliweza kufanya hesabu rahisi za kuondoa.

20 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 1 9 Chretien Eric/Gamma/Eyedea Presse Eneo la HIndu Kush nchini Pakistan; fanani wa kiasili anasisimua hadhira yake Nchini India mashambani 28% tu ya wanafunzi wa darasa la tatu waliweza kufanya hesabu ngumu kiasi za kuondoa, huku thuluthi moja wakijua kusoma saa. Tofauti za elimu kati ya mataifa Ni haki ya kila binadamu kupata elimu hasa shuleni bila kuzingatia mapato ya wazazi wake, jinsia, kabila au ukoo. Hata hivyo, katika mataifa mengi, tofauti kubwa hudhihirika katika masomo. Tofauti hizi husababishwa na aina za shule ambazo wanafunzi huhudhuria au familia wanazotoka. Tofauti baina ya shule huchangia pakubwa kupanua mwanya katika mifumo ya elimu. Katika mataifa mengi yanayostawi, mifumo ya elimu hudhihirisha tofauti katika idadi ya wanafunzi darasani, upatikanaji wa vitabu na vifaa vya kufundishia, ubora wa walimu na viwango vya mijengo ya shule. Kuimarishwa kwa viwango vya shule na kupunguzwa kwa tofauti baina ya shule kutasaidia kupunguza tofauti za usawa katika matokeo ya wanafunzi katika mtihani. Katika miaka ya kati ya 1999, nchi ya Brazil ilianzisha mradi wa FUNDEF kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanagharamiwa kwa usawa, kielimu, nchini kote. Matokeo ya mwanzo yalionyesha kuwa mgao huu ulipunguza tofauti za kimasomo. Tofauti za kielimu shuleni huchangiwa na mambo mengi. Mapato ya wazazi na elimu yao, lugha ya nyumbani, na mambo mengine yanaathiri elimu ya mwanafunzi. Nchini Pakistan, watoto kutoka familia tajiri walifanya vizuri katika mtihani ikilinganishwa na waliotoka katika familia maskini. Nchini Peru, wanafunzi walioweza kuongea Kihispania walifanya vizuri katika mtihani wa Hisabati ikilinganishwa na wanafunzi walioongea lugha za kiasili. Katika mataifa yenye usawa wa kielimu, ufanisi masomoni hauathiriwi sana na maskani ya mwanafunzi. Palipo na uhusiano mkubwa kati ya utendaji wa mwanafunzi na maskani yao, au tofauti kubwa za kinyumbani zinapodhihirika miongoni mwa wanafunzi, ni vigumu sana kwa usawa wa kielimu kuleta mabadiliko ya kutajika. Mipango mahsusi ya kuimarisha masomo miongoni mwa watoto wasiofanya vizuri shuleni itafaa zaidi. Katika mataifa mengi, wavulana wengi hujiunga na shule zaidi kuliko wasichana. Hata hivyo, wasichana hushindana sawa na wavulana au hata kuwapiku. Palipo na tofauti za kiufanisi shuleni. Kwa kawaida huwa kidogo, wasichana hufanya vizuri katika masomo ya lugha huku wavulana wakifanya vizuri katika Sayansi na hisabati. Iwapo Elimu kwa Wote (EFA) itaafikiwa, ni muhimu kuondoa mapengo yote yaliyosalia. Ufundishaji wa kusoma katika shule za msingi Ni muhimu sana kuwafunza watoto kusoma katika shule za msingi. Watoto wanaotatizika katika kusoma na kufahamu katika madarasa ya chini huenda wakapata matatizo zaidi shuleni katika miaka ya baadaye. Matokeo ya utafiti uliofanywa katika nchi maskini yanatisha. Kwa mfano, nchini Uhabeshi, mnamo mwaka wa 2008, utafiti ulionyesha kuwa katika wilaya ya Woliso 36% ya wanafunzi hawangeza kusoma hata neno moja katika lugha yao ya kiasili ya Afa Oromo. Kuchunguza ujuzi wa kusoma katika shule za msingi husaidia kuwatambua wanafunzi walio na matatizo na kuwasaidia mapema. Ushahidi wa mataifa kadha unaonyesha kuwa sera nzuri huweza kuwasaidia wanafunzi kubadilika. Huko Uttar Pradesh, nchini India, shughuli inayoendeshwa na shirika moja lisilo la kiserikali (NGO) hutumia mafunzo ya ziada (remedial reading camps) kwa usaidizi wa walimu waliojitolea kuboresha ujuzi wa kusoma katika miaka ya awali shuleni. Nchini Pakistan mashambani, utafiti wa hivi punde unaonyesha kuwa thuluthi mbili za wanafunzi wa darasa la tatu waliweza kufanya hesabu rahisi za kuondoa

21 2 0 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Watoto wanaotatizika katika kusoma na kufahamu katika madarasa ya chini huenda wakapata matatizo zaidi shuleni katika miaka ya baadaye Kuimarisha masomo shuleni Hali duni ya mazingira huchangia kutofanya vizuri shuleni. Ili kuimarisha masomo, ni sharti mazingira yaimarishwe pia. Hali kama vile za madarasa yasiyokuwa na madirisha au nafasi za kupitisha hewa safi, mapaa yanayovuja, hali duni ya afya na ukosefu wa vifaa ni vikwazo vya elimu bora katika shule nyingi. Utafiti wa hivi karibuni nchini Nigeria ulionyesha kuwa 80% ya madarasa katika eneo la Unugu na 50% huko Kuduna, ama hayakuwa na ubao au uliokuwepo ulikuwa hauandikiki. Utafiti unaeleza kuwa iwapo wanafunzi wataweza kuhudhuria shule kwa muda mwingi kwa mwaka, uwezo wa kukamilisha silabasi na kutimiza malengo ya elimu utaimarika. Katika mifumo ya elimu iliyofaulu, 80% ya muda ambao wanafunzi wanakuwa shuleni hutumiwa darasani, hali ambayo shule nyingi katika mataifa yanayostawi yameshindwa kuafiki. Nchini Uhabeshi na Guatemala, kwa mfano, utafiti wa hivi punde unaonyesha mahudhurio ya darasa yakiwa thuluthi moja ya muda wote waliokuwa shuleni kwa muhula mmoja. Hali hii inaweza kuboreshwa na usimamizi bora, kuwapa walimu motisha na kwa kutoa usaidifi zaidi kwa wanafunzi wanaojitahidi kuhudhuria shule za kutoka jamii zisizojiweza. Wajibu mkuu wa walimu Walimu ndio rasilimali muhimu zaidi katika sekta ya elimu. Katika mataifa mengi, upungufu wa walimu ni kikwazo katika kuafikia malengo ya Elimu kwa Wote (EFA), hasa miongoni mwa jamii zilizotengwa. Tangu mwaka wa 1999, kumekuwa na wanafunzi wengi sana wanaojiunga na shule za msingi, hali ambayo inaenda sambamba na ongezeko la usajili wa walimu. Mataifa mengi katika Afrika- Kusini mwa Sahara yamejizatiti na kuzidisha idadi ya walimu kwa maradufu, hivyo kuimarisha uwiano wa mwalimu kwa mwanafunzi. Licha ya ufanisi katika mwongo uliopita, uhaba wa walimu umekuwa changamoto kuu. Katika masomo ya msingi, mataifa 26 yamezidisha uwiano uliokubaliwa wa kimataifa mwaka 2007 wa idadi ya wanafunzi kwa mwalimu (yaani 40:1). Tisho lingine ni idadi ya wanafunzi kwa mwalimu aliyehitimu. Kwa mfano, katika mataifa ya Madagaska, Msumbiji, Sierra Leone na Togo, uwiano wa wanafunzi kwa mwalimu ni wa juu zaidi, yaani 80:1. Uwiano kati ya mwalimu na wanafunzi kitaifa unatofautiana pakubwa kwa kuwa wengi wa walimu waliohitimu ni wa kike na wako mijini. Nchini Uganda na Zambia, mgao wa walimu wa kike katika shule za mijini ulikuwa 60%, ikilinganishwa na 15% na 35% katika sehemu za mashambani. Makadirio ya walimu watakaohitajika katika mwaka wa 2015 Idadi ya walimu watakaoajiriwa katika siku za usoni itategemea zaidi eneo husika. Ripoti ya mwaka huu inakadiria kuwa walimu zaidi, milioni 10.3, watahitajika kote ulimwenguni iwapo malengo ya Elimu kwa Wote yataafikiwa kufikia mwaka Kati ya hawa, walimu milioni 8.4 watahitajika kuchukua nafasi za wanaotarajiwa kustaafu au kuacha kazi kabla ya mwaka Mbali na hayo, nafasi nyingine za walimu, milioni 1.9, zitabuniwa. Thuluthi mbili ya nafasi hizi mpya, yaani karibu nafasi milioni 1.2, zitabuniwa katika eneo la Afrika- Kusini mwa Sahara. Katika mataifa mengi maskini ulimwenguni, tatizo si idadi ndogo ya walimu tu, lakini pia ukosefu wa motisha miongoni mwa walimu, pamoja na mafunzo duni wanayopata. Walimu wengi hulazimika kutafuta pato la ziada ili kufidia mishahara yao. Serikali na wafadhili wanafaa kuhakikisha kuwa mishahara ya walimu, pamoja na masharti yao ya kazi yanaoana na kujitolea kwao kazini ili walimu wapate motisha na kuwapa wanafunzi elimu bora. Kielelezo cha Maendeleo cha Elimu kwa Wote Ingawa kila lengo kati ya malengo sita ya Elimu kwa Wote (EFA) yanajisimamia, ahadi za serikali za mwaka 2000 zilikusudia kuendeleza nyanja zote. Katika Kielelezo cha maendeleo ya Elimu kwa Wote (EDI) malengo yote kwa jumla yamewakilishwa yakiwemo malengo manne ya EFA, yaani: (Elimu ya Msingi kwa Wote) UPE, kujua kusoma na kuandika kwa watu wazima, usawa wa kijinsia na elimu bora. Katika ripoti hii, iliwezekana kutathmini EDI ya mataifa 128 yaliyokuwa na takwimu zao za malengo haya kufikia mwaka Kati ya mataifa 128 yaliyohusika: Mataifa 62, sita zaidi ya yaliyokuwa mwaka 2006, yalikuwa ama yamefikia malengo manne ya elimu au yakikaribia kufikia yakiwa na EDI ya na zaidi. Kwa kuongezea kwa mataifa yaliyoendelea ya Marekani Kaskazini na Uropa, orodha hii inajumlisha pia mataifa kutoka maeneo yote ulimwenguni isipokuwa ya Afrika- Kusini mwa jangwa la Sahara. Mataifa 36, mengi yakiwa ya Latin Amerika na Caribbean (16), eneo la Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara (8) na eneo la Arabia (6) yanakaribia kuafikia malengo ya Elimu kwa Wote zikiwa na EDI za viwango vya kati ya 0.80 na Hata hivyo, mengi ya mataifa haya yana ripoti mseto; mahudhurio ya shule yakionyesha kuimarika, elimu kwa watu wazima na viwango vya masomo vinabaki kuwa vya chini.

22 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 2 1 Pengo la ufadhili wa Elimu kwa Wote Ufadhili wa malengo ya Elimu kwa Wote katika mataifa yaliyo na pato dogo utahitaji ongezeko kubwa. Mataifa hayo pia yanaweza kutia juhudi za kujitafutia fedha. Hata hivyo, ukosefu wa ongezeko la fedha za kufadhili mradi wa elimu ya msingi, mafanikio yake hayatawezekana kwa sababu ya pengo hili kubwa la kifedha. Ripoti hii inaeleza kwa kina gharama zinazohusiana na malengo msingi ya Elimu kwa Wote. Kwa kurejelea mataifa maskini 46, uchunguzi huu unahusisha makadirio ya kuimarisha ratiba ya masomo ya chekechea, elimu ya msingi kwa wote na elimu kwa watu wazima. Tofauti na makadirio ya awali, ripoti hii imekadiria jinsi ya kufikia jamii zilizotengwa. Kadirio la aina hii ni muhimu kwa sababu litagharimu zaidi kuwafikia watoto waliotengwa katika jamii kwa sababu ya umaskini, kabila, lugha, jinsia na pia makazi yasiyofikika. Baadhi ya yaliyoafikiwa na kupendekezwa ni pamoja na: Mataifa yanayoendelea na yenye pato dogo yaweze kutenga Dola bilioni 7 kila mwaka au 0.7% ya pato la kitaifa (GDP). Ili kutekeleza haya, itayabidi kuimarisha raslimali za kitaifa na kusawazisha bajeti zao. Pengo la takriban Dola bilioni 16 kwa kila mwaka litabaki katika ufadhili wa mradi wa Elimu kwa Wote (EFA) hata kama hazina ya taifa itaimarishwa. Hii ni 1.5% ya pato la kitaifa (GDP) la mataifa yaliyohusishwa. Kwa pengo hili, eneo la Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara linawakilisha takriban thuluthi mbili, yaani Dola bilioni 11. Dola bilioni 3.7 zitahitajika kugharamia upanuzi wa elimu ya shule za msingi ili kufikia jamii zote zilizotengwa. Misaada ya sasa ya takribani Dola bilioni 2.7 ya kugharamia elimu ya msingi katika mataifa maskini 46, haitoshi. Itabidi iongezwe kwa mara sita ili kufikia karibu Dola bilioni 16 (mchoro 6). Kongamano la dharura la kuchanga fedha za msaada litahitaji kuandaliwa katika mwaka wa 2010 ili kuchochea hali ya kuchanga fedha za kutimiza makubaliano ya Dakar. Mchoro 6: Msaada kwa elimu ya msingi utahitaji kuzidishwa mara sita kuziba pengo la ufadhili la Dola bilioni 16 Kisawia cha 2007 Dola $ mabilioni Dola billioni 16 Dola billioni 2.7 Jumla ya pengo la ufadhili Msaada wa sasa kwa elimu ya msingi Asili: Tazama mchoro 2.49 katika EFA Global Monitoring Report 2010 Katika mataifa 30, mataifa 17 yakiwa ya Afrika Kusini mwa Sahara yana EDI ya kiwango cha chini, (chini ya 0.80) Mataifa mengine katika kategoria hii na yaliyo na idadi kubwa ya watu ni pamoja na Bangladesh, India na Pakistan. Nchi za Uhabeshi, Mali na Niger zinaripotiwa kuwa na viwango vya chini sana vya EDI (chini ya 0.6). Nchi nyingi ambazo zimetimiza malengo ya EFA kwa viwango vya chini zinakabiliwa na changamoto nyingi: mahudhurio ya shule ni ya chini, hali ya elimu ni duni, viwango vya kujua kusoma na kuandika kwa watu wazima ni vya chini na tofauti za kijinsia zinabainika. Ilikuwa rahisi kuchanganua mabadiliko katika viwango vya EDI vya mataifa 43 kati ya miaka Viwango vya EDI viliongezeka katika nchi 30 kati ya hizi, baadhi yazo kama vile Uhabeshi, Mozambique, Nepal na Zambia zikiandikisha faida kuu ambazo zilirekodi ongezeko la EDI la 12%. Ongezeko la usajili wa wanafunzi katika shule za msingi ndilo lililochangia kuboreka kwa EDI tangu mwaka 1999; ambapo ongezeko la wastani la usajili katika shule za msingi liliimarika kwa 8.7%. Hata hivyo, si nchi zote ambazo zimekuwa na maendeleo mazuri; viwango vya EDI vinapungua katika mataifa 13 yakiwemo mataifa ya Dominika na Fiji. Misaada ya sasa ya kugharamia elimu ya msingi itabidi iongezwe kwa mara sita ili kuziba pengo la ufadhili la Dola bilioni 16

23 2 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Serikali nyingi zinakosa kuchukua hatua madhubuti katika kukabiliana na kutengwa katika elimu, hali inayodumaza maendeleo ya mpango wa Elimu kwa Wote Umaskini na ukosefu wa usawa wa kijinsia huzidisha hatari nyingine mbali na kuzuia fursa za mamilioni ya watoto kupata elimu Sera za elimu jumlishi zinafaa kushughulikia uwezo wa kufikia na ule wa kumudu pamoja na mazingira ya elimu kwa makundi maskini katika mfumo wa kupunguza umaskini Takwimu tofauti zinaweza kusaidia katika kutambua makundi yaliyotengwa ili kusaidia katika kuchunguza hatua za kufanikisha usawa Sura ya 3 Kuwafikia waliotengwa Kuondoa utengwaji katika elimu kunafaa kuwa sera yenye kupewa uzito zaidi na kila serikali. Takriban kila serikali huidhinisha sera ya kuwepo nafasi sawa kwa wote katika elimu. Serikali hizi zinatambua kwamba kuweka vikwazo katika kupatikana kwa elimu kunahujumu haki za binadamu mbali na kuendeleza hali ya ukosefu wa usawa katika jamii pamoja na kurudisha nyuma ustawi wa kiuchumi. Katika mkakati wa Framework for Action ulioafikiwa huko Dakar, serikali mbalimbali ziliapa kutambua kwa uwazi, kulenga na kuchukua hatua madhubuti katika kukabiliana na matakwa na hali za jamii maskini zaidi na zile zilizotengwa zaidi, ama zile zenye kukabiliwa na matatizo ya mara kwa mara. Serikali nyingi, hata hivyo, zimekosa kuwajibikia kiapo hiki. Kukosa kutatua tofauti za kimuundo na zile za mamlaka hasa kuhusiana na mali, jinsia, tabaka, kabila/lugha, ulemavu na mengine, kunahujumu juhudi za kuhakikisha kuwa kuna Elimu kwa Wote na badala yake kuchangia mgawanyiko mkubwa wa kutengwa katika jamii. Kuepuka kutengwa kwa jamii katika elimu inafaa kuwa sera yenye kupewa uzito zaidi na kila serikali. Elimu inapaswa kupewa kipaumbele. Sura hii inatoa mbinu mpya na mwafaka za kutambua na kuchunguza utengwaji katika elimu, inachanganua sababu kuu za kutowashirikisha baadhi ya watu na makundi na pia kudokeza mikakati na sera tekelezi za kustawisha elimu ambayo itawajumuisha wote katika mtazamo mpana wa kupunguza umaskini na kushirikisha jamii. Kupima utengwaji katika elimu Kupima kiwango cha utengwaji katika elimu kwa kawaida ni vigumu. Mara nyingi takwimu za kitaifa hazina maelezo ya kutosha kuyawezesha makundi yaliyotengwa kutambulika. Serikali nyingi vilevile hazitilii maanani zaidi kupatikana kwa takwimu bora kuhusu baadhi ya makundi yanayokumbwa na ugumu huu kama vile watoto wanaofanyishwa kazi, walemavu na wale wanaoishi katika mitaa ya mabanda sawa na wanaoishi mashambani. Ripoti ya mwaka huu inajumuisha mbinu mpya ya kuchukua takwimu, Kunyima haki na kudhalilisha katika elimu Deprication and Marginalization in Education, ambayo inaainisha kiwango cha utengwaji katika nchi mbalimbali na katika miundo ya jamii zilizotengwa kwa jumla (Sanduku 3). Licha ya hatua iliyopigwa mwongo uliopita, uwazi katika kunyima haki za elimu unasalia katika viwango vya juu. Kuwa na miaka chini ya minne katika elimu katika mizani yoyote ya kimataifa ni ishara ya ubaya zaidi wa hali. Mbinu ya DME inatambua hii kama chanzo cha ukosefu wa elimu, huku miaka chini ya miwili shuleni ikiwa ithibati ya kukithiri kwa hali hii. (Mchoro 7). Matokeo kutoka mataifa 63, mengi yayo yenye mapato ya chini yanaonyesha kuwa: Umaskini wa elimu. Katika nchi 22, 30% ama zaidi ya wale wenye umri wa kati ya miaka 17 na 22 wana miaka chini ya 4 ya elimu. Kiwango hicho hata hivyo kinazidi hadi 50% ama zaidi katika nchi 11 katika Africa kusini mwa jangwa la Sahara. Kukithiri kwa umaskini katika elimu. Katika nchi 26, 20% ama zaidi ya wale walio kati ya umri wa miaka 17 na 22 wana chini ya miaka miwili katika masomo huku katika

24 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 2 3 Abbie Trayler-Smith/PANOS Kuunga mkono huleta badiliko: wasichana wengi nchini Yemen sasa wanaenda shule baadhi ya nchi zikiwemo Burkina Faso na Somalia zikiwa na asilimia hamsini ama zaidi. Makadirio haya yanadhihirisha upeo wa ukosefu wa usawa unaohusishwa na mali na jinsia. Nchini Ufilipino, viwango vya umaskini katika elimu miongoni mwa jamii maskini ni mara nne zaidi ya kiwango cha kitaifa. Katika nchi nyingine, viwango vya juu vya utengwaji hasa miongoni mwa wanawake maskini huchangia kwa kiasi kikubwa umaskini katika elimu. Idadi isiyozidi nusu ya wasichana kutoka jamii maskini walio kati ya umri wa miaka 17 na 22 nchini Misri ndio waliowahi kupata elimu, japo kwa miaka isiyozidi minne ilhali nchini Morocco kiwango hicho ni asilimia 88. Ukosefu wa usawa wa kijamii vilevile inachangia pakubwa katika tofauti hizi kati ya nchi na majirani zake. Huku jumla ya pato la nyumbani likilinganishwa na lile la Vietnam, kiwango cha umaskini katika elimu nchini Pakistan ni mara tatu zaidi, na huashiria tofauti zinazohusishwa na mali, jinsia na eneo. Vipengele vinavyosababisha kutengwa havijiendelezi kivyao. Mali na jinsia hushirikiana na kabila/ lugha, eneo na tofauti kati ya miji na mashambani katika kuweka tofauti hizi. Takwimu za DME zinazohusu vijana zinasaidia kutambua makundi yanayokabiliwa vikali na vikwazo maalum katika nafasi za elimu na kudokeza kiwango cha tofauti hizo kitaifa. Sanduku 3: Chombo kipya cha kukadiria utengwaji Ripoti hii ya uchunguzi wa kimataifa imeibuka na takwimu za kimataifa ambazo zinalenga kudhalilishwa katika elimu ambayo serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na watafiti wanaweza kutumia. Takwimu hizo kuhusu kunyima haki na kudhalilisha katika elimu zinatumia takwimu nyingine za kitaifa na kibinafsi kutoka mataifa 80 ambayo kati yayo, takriban nusu yana mapato ya chini na kubaini kuwa: Umaskini wa elimu: Vijana kati ya umri wa miaka 17 na 22 ambao wana chini ya miaka minne katika masomo huenda wakakosa maarifa ya kimsingi katika kusoma na kuhesabu. Ukosefu zaidi wa elimu: Vijana walio na elimu ya chini ya miaka miwili wana hatari ya kukabiliwa na vikwazo katika sehemu nyingi katika maisha yao ikiwemo afya na ukosefu wa ajira. 20% wa chini: Hawa ni wale waliohudhuria masomo kwa miaka michache zaidi katika jamii husika. Takwimu hizi zinapatikana kwenye tovuti katika Uchunguzi baina ya nchi mbalimbali unabainisha mifumo tata ya udhalimu huu. Makundi fulani ya kijamii yanakabiliwa na udhalimu kote duniani, mfano bora ukiwa jamii ya wafugaji wa kuhamahama Afrika kusini mwa jangwa la Sahara. Katika nchi ya Uganda ambayo imekuwa ikipiga hatua madhubuti katika kuafiki elimu ya msingi kwa wote, wafugaji wa jamii ya

25 2 4 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Mchoro 7: Kukadiria viwango vya elimu katika baadhi ya nchi Idadi ya kadiri ya miaka chini ya sita katika elimu Idadi ya kadiri ya miaka kati ya 6 na 8 katika elimu Idadi ya kadiri ya miaka zaidi ya 8 katika elimu Burkina Faso, 2003 Chad, 2004 Ethiopia, 2005 Senegal, 2005 Morocco, 2003 Guatemala, 1999 Pakistan, 2006 Nepal, 2006 Bangladesh, 2004 Yemen, 2005 Nigeria, 2003 India, 2005 Congo, 2005 Kenya, 2003 Egypt, 2005 Viet Nam, 2002 Turkey, 2003 Philippines, Mgao wa watu walio na chini ya miaka 4 na chini ya miaka 2 katika elimu Ukosefu zaidi wa elimu Asili: Tazama mchoro 3.1 katika EFA Global Monitoring Report 2010 Ukosefu wa elimu Muda unaotumika shuleni ni upande mmoja wa utengaji huu. Aidha, ipo mianya katika ufanisi wa kielimu ambao unahusishwa na hali za kijamii na kiuchumi. Watoto kutoka jamii tajiri katika nchi za Brazil na Mexico hupata kati ya 25% na 30% juu zaidi katika mitihani ya Hisabati kwa jumla, hii ikiwa ni zaidi ya wanayopata watoto kutoka jamii maskini. Utengwaji katika nchi tajiri Kutengwa katika elimu kunaathiri mataifa yote. Ingawa mafanikio ya kawaida kwa kadiri huwa ya juu katika mataifa yaliyostawi, kudorora zaidi kwa hali hizo vilevile kunasikitisha. Katika jumuiya ya Ulaya, 15% ya vijana wa kati ya miaka 18 na 24 huwacha masomo baada ya kuhitimu katika shule za upili, idadi inayofika 30% nchini Uhispania. Ushahidi kutoka Marekani unadokeza uchochezi mkuu wa mali na rangi. Wamarekani wenye asili ya Kiafrika wanakabiliwa na hatari ya kutojiunga na shule mara mbili zaidi ya wale weupe huku vijana kutoka jamii maskini wakikabiliwa na hatari hiyo mara tatu zaidi ya wale kutoka jamii tajiri. Uchunguzi wa masomo katika kiwango cha kimataifa unabainisha kiwango cha kutengwa huku kitaifa. Katika mizani ya TIMSS katika Hisabati, Marekani inaorodheshwa ya tisa kati ya nchi 48 lakini shule za Marekani zilizo na viwango vya juu vya umaskini zinaorodheshwa katika nafasi ya 13 chini ya shule nyingine. Wale walio kwenye asilimia 10 wa nyuma nchini Marekani hawajafikia kiwango cha Thailand na Tunisia. Nchini Guatemala, mahudhurio ya shule ni kutoka miaka 6.7 kwa wazungumzaji wa Kihispania hadi 1.8 kwa wale wanaozungumza Q eqchi Karamajong wanakadiriwa kuhudhuria masomo kwa kipindi kisichozidi mwaka mmoja. Mataifa mengine mengi vilevile yanaandikisha tofauti kubwa zinazohusishwa na lugha. Huko Guatemala, makadirio ya waliohudhuria masomo ni miaka 6.7 kwa wazungumzaji wa Kihispania na 1.8 kwa wale wanaozungumza Q eqchi. Takwimu hizo za DME zinaangazia zaidi ya udhalimu halisi ili kutambua baadhi ya mienendo ya wale wanaoachwa nyuma. Matokeo yanadokeza nguvu ya mshawasha wa hali za kijamii ambazo kwazo watoto hawawezi kuepuka katika nafasi zao za maisha. Hali hizi pia zinavuta nadhari katika viwango visivyokubalika vya kutokuwepo usawa: Kuzaliwa katika jamii maskini kunazidisha hatari ya kuwa katika kundi la nchi zilizoko asilimia 20 nyuma katika ustawi kama vile India, Ufilipino na Viet Nam. Tofauti za kieneo zinamaanisha kwamba kuishi katika maeneo kama mashambani mwa nyanda za juu za Misri, Kaskazini mwa Cameroon ama Mashariki mwa Uturuki kunazidisha maradufu hatari ya kufika katika asilimia 20 za chini zaidi. Jinsia, umaskini, lugha na tamaduni mara nyingi hujumlika kuzidisha kwa kiasi kikubwa hatari ya kuachwa nyuma zaidi. Nchini Uturuki, 43% ya wasichana kutoka jamii maskini wanaozungumza Kikurdi walipata elimu kwa miaka isiyozidi miwili huku kiwango hicho kikiwa 6% kitaifa. Nchini Nigeria, 97% ya wasichana kutoka jamii maskini wanaozungumza Kihausa vilevile wana miaka chini ya miwili katika elimu. (Mchoro 8). Kupima utengwaji hakufai kutazamiwa kuwa mwisho bali kama njia za kuibua sera na kuingilia kati swala hilo ili kuleta uwajibikaji zaidi na kuifanya Elimu kwa Wote kuwa yenye manufaa. Serikali zinafaa kuanza kwa kuweka malengo ya kuziba mianya kati ya makundi yaliyotengwa na jamii kwa jumla. Kuchunguza mafanikio katika malengo haya kwa kusambaza takwimu huenda kukasaidia kustawisha sera zinazolengwa mbali na kuzidisha uwezekano wa kutambulika kwa waliotengwa. Kuachwa nyuma Udhalimu wa kutabirika, unaokithiri na kuzidi ni taswira ya hali ambazo watoto huzaliwa, na mazingira ambayo wanakulia na kustawi. Ripoti hii inachunguza hatua ambayo kwayo hali hizi zinawafungia watoto nje ya elimu. Umaskini na ajira ya watoto Umaskini ni mojawapo ya vyanzo vikuu vya ukosefu wa elimu. Kimataifa, kuna watu bilioni 1.4 ambao wanaishi chini ya Dola 1.25 za Marekani kwa siku. Kwa familia hizi, gharama ya elimu inashindaniwa na ile ya mahitaji ya kimsingi kama vile matibabu na chakula. Hali ya wazazi kutomudu gharama ya elimu ni mojawapo ya sababu kuu zinazowafanya watoto kutohudhuria masomo, hata katika nchi ambazo zimefutilia mbali karo za shule, kwa sababu bei za sare za shule, vitabu na kalamu zinatatiza hali hii. Viwango vya juu vya umaskini vinadhibiti uwezo wa jamii kustahimili shinikizo za mapigo ya kiuchumi.

26 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 2 5 Mchoro 8: Mti wa tofauti za kielimu : Kupima utengwaji nchini Uturuki na Nigeria 14 Uturuki Nigeria 14 Ukraine Wavulana Wasichana Ukraine Wavulana Wasichana Makadirio ya miaka katika elimu Miaka nane ya elimu Cuba Bolivia Indonesia Honduras Matajiri zaidi 20% Mjini Mashambani Mjini Cameroon Mashambani Maskini zaidi Bangladesh 20% Wasichana maskini wa mashambani wa miaka 5 Kurdish Wavulana tajiri mashambani wa miaka 9.6 Wavulana tajiri mjini wa miaka 9.6 Wavulana maskini wa miaka 8.7 Wavulana maskini wa Kikurdi wa miaka 6.1 Nigeria miaka 6.7 ya elimu Cuba Bolivia Indonesia Honduras Cameroon Bangladesh Maskini zaidi 20% Mashambani Mjini Mjini Wavualana tajiri mashambani wa miaka10.6 Wavulana tajiri mjini wa miaka 9.8 Wavulana maskini wa mjini wa miaka Makadirio ya miaka katika elimu 2 Chad Ukosefu wa elimu Wasichana maskini wa kikurdi wa miaka 3 Chad Maskini zaidi 20% Mashambani Wasichana maskini mashambani wa miaka Ukosefu zaidi wa elimu Somalia 0 Asili: Tazama Mchoro 2.3 katika EFA Global Monitoring Report Somalia Hausa mashambani Wasichana maskini wa Kihausawa mashambani wa miaka Jamii maskini zaidi aghalabu huona ugumu kukinga elimu ya wanao kutokana na hasara wanazopata katika mtaji na vitegauchumi, inayosababishwa na ukame, mafuriko, magonjwa ama msukosuko wa kiuchumi. Wasichana huwa wa kwanza kupokea madhara hayo. Nchini Pakistan na Uganda, ukame umesababisha kuondolewa kwa wasichana wengi shuleni, ikilinganishwa na wavulana. Ajira ya watoto ni chanzo kingine cha umaskini kinachoathiri zaidi elimu. Kulingana na makadirio ya hivi punde, wapo watoto wapatao milioni 116 walio kati ya miaka 5 na 14 kote ulimwenguni ambao wanafanya kazi. Huku watoto wengi wakijikaza kumudu kazi na masomo, ushahidi kutoka Latin America unaonyesha kwamba hali hii ina madhara mabaya zaidi katika matokeo ya masomo na kwamba kwa watoto wengi, muda mrefu wanaofanya kazi unawazuia kabisa kusoma. Tofauti za kijinsia mara nyingi huashiria kushirikishwa kwa mtoto msichana katika kazi za nyumbani. Katika jamhuri ya kidemokrasi ya watu wa Lao, wasichana wadogo hutumia mara mbili zaidi ya muda wao katika kutekeleza majukumu ya nyumbani wakilinganishwa na wavulana. Matatizo ya kimakundi Katika nchi nyingi, watoto kutoka kabila lenye idadi ndogo ya watu, kundi la kiasili ama wa tabaka la chini huenda shuleni tayari wakiwa na matumaini ya chini ya kufanikiwa, hivyo kuwafanya kuhudhuria masomo kwa miaka michache na kupelekea wao kuibuka na alama za chini. Unyanyapaa vilevile ni chanzo kikuu cha kutengwa. Kutoka kwa jamii ya Aboriginal nchini Australia hadi ile ya milimani nchini Cambodia, kukosa kutoa mafunzo kwa lugha asili ni njia mojawapo ya udhalili na ubaguzi wa kijamii. Mara nyingi hayo, uzoefu ambao watoto hupata shuleni hudhibiti na kuendeleza utengwaji huu. Mfumo wa viwango vya kijamii Kusini mwa Asia huwadhalilisha watoto wengi (Sanduku 4). Mfano mmoja mkuu ni kutoka India, ambapo watafiti walibaini kwamba watoto kutoka jamii maskini walikuwa na matokeo ya chini katika elimu wakati hali zao za kiuchumi ziliwekwa wazi ikilinganishwa na wakati hali hizo zilibanwa. Matokeo ya utafiti huu yanadhihirisha athari za unyanyapaa kwa imani ya mtu binafsi na kwa uwezo wa mtu wa kujifunza na jinsi watoto katika hali hizi wanavyohudumiwa katika mazingira ya shuleni. Hali ya wazazi ya kutomudu gharama ya elimu ni mojawapo ya sababu kuu zinazowafanya watoto kukosa kuhudhuria masomo

27 2 6 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Watu ambao hawazungumzi lugha rasmi ya taifa fulani aghalabu hudhalilishwa katika elimu na hali nyingine. Watoto wapatao milioni 221 huzungumza lugha tofauti wakiwa nyumbani kinyume na ile wanayotumia wakiwa shuleni. Kwa uyakinifu zaidi, sababu kuu ambayo huwafanya watoto kutoka jamii zilizotengwa kutofanya vyema katika masomo ni kuwa wanafundishwa katika lugha ambayo wanang ang ana kufahamu. Changamoto za kutatua dhuluma zinazohusiana na lugha linazipa serikali mbalimbali na jamii nyingi. Utafiti unaonyesha kwamba katika uchanga wao, watoto wanasoma vyema zaidi wanapofunzwa kwa lugha zao za nyumbani huku lugha nyingine zikishirikishwa muda baada ya muda. Wazazi na watoto, hata hivyo, hutazamia masomo katika lugha rasmi ya kitaifa kama njia bora ya kupata ajira katika siku za usoni pamoja na kuimarisha hali za maisha. Nchi nyingi, hata hivyo, zinatafuta mbinu mwafaka ya kusawazisha mifumo ya lugha katika elimu. Ami Vitale/PANOS Sanduku 4: Kuishi na unyanyapaa: wawindaji wa panya kutoka Uttar Pradesh Matatizo mara mbili: Wasichana kutoka jamii maskini nchini India hukabiliwa na vizingiti vikubwa zaidi Wanafunzi kutoka jamii tajiri hutusimanga kuwa tunanuka, msichana mmoja alisema.mwingine aliongeza, Dhihaka tunazopata zinatuzuia kuja shuleni na kukaa na wanafunzi kutoka jamii zinazojiweza. Wasichana hawa kutoka kjiji cha Khalispur, karibu na jiji la Varanasi, ni wa jamii ya Musahar ama wawindaji wa panya ya mashariki mwa Uttar Pradesh, India. Khalispur ina shule ya msingi inayofadhiliwa na serikali. Licha ya kuwa na haki ya kupata malipo, chakula cha mchana na sare za shule, ni wasichana wachache wa Musahar wanahudhuria masomo. Kwa wasichana hawa, shuleni ni mahali ambapo wanatengwa kijamii. Njia mbalimbali za ubaguzi zinadhibiti tofauti za kiviwango darasani. Tunalazimishwa kuketi sakafuni, msichana mmoja alisema. Madawati na viti darasani ni za wale wenye kujiweza. Kulingana na viongozi wa Musahar, sera za serikali zimeimarika isipokuwa hulka za kijamii: Wanaruhusu watoto wetu shuleni na sasa tuna haki kisheria, lakini walimu na wanafunzi kutoka jamii zenye uwezo wangali kikwazo kwa juhudi hizi. Watoto wetu basi hawathubutu kuhudhuria masomo. Ufichuzi huu wa Musahar ni tone tu katika bahari lenye matatizo mengi. Serikali nyingi zimepiga marufuku dhuluma za namna yoyote, lakini hulka za kijamii hazijavutia hisia kuu kutoka kwa wanasiasa na hivyo kutatiza mafanikio ya mabadiliko mapana ya kijamii. Uwingi wa lugha husababisha changamoto, lakini katika nyanja kama za kuwaajiri walimu, kuunda mtaala wa elimu na vifaa vya kufunzia na kutoa sera kuhusu elimu ya lugha hukosa kutekelezwa kikamilifu. Nchini Peru, ni 10% pekee ya watoto wa kiasili ambao huhudhuria shule zinazowaleta pamoja watoto kutoka tamaduni mbalimbali na mafunzo ya lugha mbalimbali. Mahali na hali za maisha Watoto wanaoishi katika mitaa ya mabanda, mashambani ama maeneo yanayokumbwa na majanga ni miongoni mwa wale maskini zaidi na walio katika hatari zaidi. Katika uhalisia, ndio walio na uwezo mkubwa wa kunufaika na elimu lakini wanaishi katika maeneo yenye uhaba mkubwa wa huduma za kimsingi. Katika makadirio, mmoja kati ya watu watatu wanaoishi mijini katika nchi zinazostawi. Jumla ya watu milioni 900 wanaishi katika mitaa ya mabanda. Mitaa hii ni vito vya ukosefu wa elimu hasa kutokana na umaskini, lakini pia kwa sababu serikali nyingi katika nchi hizi vilevile, zimekosa kutambua haki za wakazi wa mitaa hii za kupata huduma za kimsingi. Mjini Dhaka, nchini Bangladesh, watu wapatao milioni 4 wanaishi katika mitaa ya mabanda. Watoto wengi katika mitaa hii, aidha hawahudhurii masomo ama wanahudhuria, lakini kwa kutegemea msaada wa mashirika yasiyo ya kiserikali. Hali za maisha na mahali pa kuishi huwa viashiria vikuu vya dhuluma za kijamii katika elimu. Watoto wanaoishi mashambani hukabiliwa na hatari za kutengwa katika elimu, hasa wakiwa watoto wasichana kutoka jamii maskini. Watoto hawa hutembea masafa marefu kufika shuleni, wakati mwingine katika mazingira magumu. Jamii za wafugaji wa kuhamahama zina idadi kubwa ya viwango vya chini vya elimu kutokana na kutokuwepo miundombinu ya elimu kwa jamii hiyo kila wanakohamia, pamoja na kuwa ratiba za shule hazizingatii maslahi ya jamii hii.

28 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 2 7 Mamilioni ya watoto waliotengwa zaidi duniani wanaishi katika nchi zinazokabiliwa na mizozo. Watoto wapatao milioni 14 walio kati ya umri wa miaka 5 na 17 kote duniani wamelazimika kupiga kambi kama wakimbizi kutokana na mizozo, na hivyo kuwakosesha vifaa vya kimsingi vya elimu. Nchini Pakistan, hesabu ya wakimbizi iliyofanywa mwaka wa 2005 ilibaini kuwa yapata watoto wakimbizi milioni moja kutoka nchini Afghanistan walikuwa hawahudhurii tena masomo. Kufurushwa kwa watu kutoka makwao pia kunaweza kusababisha matatizo makubwa katika elimu kwa kufurikisha mifumo ya elimu katika maeneo wanakohamia waliofurushwa. Nchini Ufilipino, mzozo unaoendelea umetatiza pakubwa masomo ya watoto na kuliacha eneo zima la Mindanao, lenye idadi kubwa ya Waislamu, kubaki nyuma katika elimu. Hali ambayo ni ngumu kukadiria ikilinganishwa na madhara ya kuhudhuria masomo ni uchungu unaotokana na vita. Vita vya aina hiyo katika mwaka wa 2008 na 2009 viliathiri pakubwa mfumo wa elimu katika ukanda wa Gaza. Katika ripoti iliyoandaliwa Bunge la pamoja la Umoja wa Mataifa, ushahidi kutoka pande zote na ambao unawalenga raia ulitolewa. Vitendo vya wanajeshi wa Israeli vilisababisha vifo vya wanafunzi 164 na walimu 12 na kuharibu kabisa shule 280 zikiwemo zile za chekechea. Katika eneo hilo 69% ya watoto waliobaleghe wanakabiliana na uchungu wa taswira hiyo ya vita, wengi wao sasa wamerejea shuleni wakiwa wangali na madhara ya mshtuko kwa waliyokumbana nayo. Ulemavu Duniani kote, kuna watoto walemavu wapatao milioni 150, wanne kwa watano katika idadi hiyo wakiwa katika nchi zinazostawi. Mamilioni zaidi wanaishi na wazazi ama jamaa walemavu pia. Zaidi ya madhara waliyonayo ya kiafya, ulemavu wa kimwili na kiakili watotot hawa hukumbwa na unyanyapaa ambao kamwe hupelekea wao kutengwa katika jamii na hata shuleni. Nchini Bulgaria na Romania, jumla ya idadi ya wale wanaojiunga na shule kati ya watoto wenye umri wa miaka 7 hadi 15 ilikuwa zaidi ya 90% katika mwaka wa 2002, 58% wakiwa ni watoto walemavu. Mwelekeo wa vizuizi vinavyohusishwa na ulemavu unatofautiana. Watoto wenye matatizo ambayo yanaathiri uwezo wao wa kuwasiliana, na matatizo mengi kwa ujumla huwa hasa na nafasi ndogo kabisa ya kupata elimu, hasa katika nchi maskini. Nchini Burkina Faso, watoto viziwi ama bubu, wale wenye akili taahira ama vipofu mara nyingi hawasajiliwi shuleni kinyume na wale wenye ulemavu wa kimwili. Ukimwi na Virusi vya HIV Takriban watu milioni 33 walikuwa wanaishi na virusi vya Ukimwi mnamo mwaka wa 2007, wakiwemo watoto milioni mbili walio chini ya miaka 15. Ukimwi huhatarisha maisha, huwafanya watoto kutohudhuria masomo na kutatiza elimu. Vilevile, unachangia pakubwa katika matatizo yanayotokana na umaskini na ubaguzi wa kijamii kama vile: shinikizo la kiuchumi, uyatima, unyanyapaa, ubaguzi katika taasisi mbalimbali na tofauti kubwa za kijinsia katika elimu. Uchunguzi fulani uliofanywa nchini Thailand ulibaini kuwa wale wanaoishi na virusi vya Ukimwi walinyimwa nafasi katika shule, kinyume cha sheria za nchi hiyo. Walimu walielezea wasiwasi wao kwamba baadhi ya wazazi wangetofautiana na usajili wa wanafunzi wanaoishi na virusi hivyo. Serikali nyingi, hata hivyo, zimekosa kushughulikia kwa dharura masuala yanayohusiana na Ukimwi katika elimu, ikiwemo changamoto ya kupambana na dhana potofu na jinsi ya kuepuka unyanyapaa. Kusawazisha nafasi Kutoa nafasi za elimu yenye thamani kwa watoto waliotengwa huwa ngumu lakini kuna uwezekano wa kupiga hatua kama kungekuwa na uwajibikaji kisiasa. Uelewa wa mbinu za kijamii zinazochangia utengwaji wa watoto hao katika hali mbalimbali sawa na kuwajibikia tofauti za kijamii, usawa katika nafasi na haki za kimsingi, zote, ni sehemu za mikakati ya kudumu. Shule zinaweza kuleta mabadiliko makubwa katika maisha ya wanafunzi waliotengwa. Pia zinaweza kufifisha vizuizi walivyopata katika utotoni mwao. Chakula, mavazi, afya na malezi ya mtoto pamoja na elimu ni mchakato bora wa kukabili utengwaji. Ulemavu wa kimwili na kiakili husababisha unyanyapaa ambao kamwe hupelekea wao kutengwa katika jamii na hata shuleni Mifumo ya elimu na hali katika darasa huweza kuchangia katika kukabiliana na ubaguzi, unyanyapaa na kupuuzwa kwa wanafunzi katika taasisi za elimu, jamii na hata nyumbani. Hali hizi huwa na madhara mabaya, lakini kutokana na ukosefu wa mahala maalum, upungufu wa walimu waliohitimu na vifaa vya kufundishia, na mienendo ya kibaguzi darasani huweza kudidimiza nafasi. Handicap International Shule ya pekee nchini Nicaragua inawajali wote

29 2 8 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Kupatiwa malipo kwa makundi yaliyotengwa zaidi kunaweza kufanya masomo kumudika kwao pamoja na kuwashawishi watoto kusalia shuleni Mchoro 9: Pembe tatu jumuishi ya elimu Kufikia na kumudu kupunguza gharama za moja kwa moja na zile zisizo za moja kwa moja kutoa vishawishi vinavyolengwa vya kifedha kuwekeza katika miundombinu ya shule kujenga madarasa karibu na wanafunzi kuunga mkono vifungu vya sheria muafaka kushirikisha na kuchunguza sheria zisizo za serikali Ripoti hii inatoa sera tatu kuu zinazoweza kuangamiza utengwaji. Sera hizi zinaweza kuchukuliwa kama pembe tatu katika elimu: ufikiaji na kumudika, mazingira ya masomo na haki kupate fursa (Mchoro 9). Kupanua ufikiaji na kuimarisha kumudika kwa elimu kwa makundi tengwa Katika nchi nyingi zilizo katika hatari ya kukosa kufikia lengo la kutoa elimu ya msingi, uimarishaji wa fursa katika elimu mara nyingi humaanisha kupunguza vikwazo vya gharama na kupeleka shule hizi karibu na wanafunzi waliotengwa. Kufutilia mbali karo pia ni muhimu katika kuwafikia maskini zaidi, lakini hilo pekee halitoshi. Serikali zinahitajika pia kupunguza gharama zisizo za moja kwa moja kama za sare, vitabu vya kiada na malipo mengine. Nchini Vietnam, ambapo gharama ya elimu inatajwa kama chanzo cha wanafunzi kuacha shule, vitabu vya kiada na madaftari yamekuwa yakitolewa kwa watoto kutoka jamii zilizo na idadi ndogo ya watu. Kupatiwa malipo kwa makundi yaliyotengwa zaidi kunaweza kufanya masomo kumudika kwao pamoja na kuwashawishi watoto kusalia shuleni katika kiwango cha msingi na hata sekondari. Nchini Bangladesh na Cambodia, hatua hizi zimechangia pakubwa kupunguza mianya ya kijinsia pamoja na kuimarisha kipindi cha wale wanaojiunga na shule za sekondari. Masafa kati ya watoto na madarasa yanasalia kuwa kizingiti kikuu katika upatikanaji wa Elimu kwa Wote. Upungufu wa madarasa huongeza masafa ya kufika shuleni. Nchi nyingi maskini katika Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara hazina madarasa ya kutosha: kuna upungufu wa madarasa milioni 1.7. Nchi hizi bila shaka zitahitaji kuongeza idadi ya madarasa kwa mara mbili zaidi ili kufikia malengo ya Elimu kwa Wote kufikia mwaka wa Mazingira ya masomo usawa katika ugavi wa walimu kuwaajiri na kuwapa mafunzo walimu kutoka makundi yaliyotengwa kutoa msaada wa ziada kwa shule zisizojiweza kubuni mtaala unaofaa kutoa elimu kuhusu lugha na tamaduni mbalimbali Haki na fursa kustawisha mikakati ya kupunguza umaskini kukabili kudorora kwa hali ya mtoto akiwa mdogo kutekeleza sheria zinazopinga ubaguzi kutoa ulinzi wa kijamii kuweka usawa katika matumizi ya pesa za umma Kupeleka shule karibu na jamii zilizotengwa ni muhimu zaidi hasa katika kusawazisha tofauti za kijinsia na kuwawezesha watoto walemavu kufika shuleni. Mipango ya kujenga darasa inayolenga maeneo ya mashambani inaweza kupunguza umbali wa shule na kuimarisha mahudhurio ya masomo kama inavyodhihirika nchini Ethiopia. Nchi nyingi zimestawisha mifumo ya kutoa elimu ijulikanayo kama satellite school ambapo shule zinajumlishwa kwa kuletwa pamoja; ile yenye vifaa vya kutosha na zile ndogondogo. Mfumo kama huo unaojulikana kama núcleo nchini Bolivia umechangia pakubwa kuzidisha upatikanaji wa elimu kati ya watoto maskini kutoka maeneo ya nyanda za juu. Mbinu muafaka zaidi za kutoa elimu huenda zikafanikisha upatikanaji wa elimu kwa baadhi ya watoto waliotengwa zaidi duniani. (Sanduku 5). Watoto na vijana wengi waliotengwa kamwe hawahudhurii masomo ama huacha shule mapema. Kutoa mpango utakaowawezesha kurudi shuleni ni mkakati muhimu katika kuwaepusha vijana na madhara ya umaskini. Fursa nyingi za pili kama hizo huendeshwa na mashirika yasiyo ya kiserikali. Yanaweza kuzidisha upatikanaji wa elimu kwa watoto na vijana katika maeneo yenye hali ngumu za maisha, kuanzia jamii ya wafugaji na watoto wanaorandaranda mitaani nchini Bangladesh hadi wale kutoka maeneo maskini nchini Ghana. Mradi huo wa 'shule kwa maisha' unatoa kozi maridhawa za elimu kwa watoto kati ya miaka 8 na 14 ili kuwaandaa kurejea tena katika shule za msingi na umefanikiwa kuwafikia watoto wapatao 85,000 katika mwongo uliopita. Serikali zinahitaji kushirikisha mashirika kama hayo katika mipango ya kitaifa huku ikichunguza ubora wa elimu inayotolewa nayo. Mazingira ya masomo Kuwarudisha watoto waliotengwa shuleni ni hatua moja tu. Kuhakikisha kuwa watoto hawa wanapata elimu bora kunazua changamoto kuu za kisera. Kuhakikisha kwamba walimu wamepata mafunzo pamoja na kuwa na vifaa mwafaka vya kuwawezesha kutoa elimu bora pamoja na kwamba wanazingatia maslahi ya watoto wenye matatizo ni swala muhimu zaidi katika mkakati wowote wa kukomesha utengwaji. Kuwaajiri walimu kutoka katika makundi yaliyotengwa huenda kukaleta mitazamo tofauti, kukakomesha ubaguzi na kuhakikisha kwamba watoto wanaweza kusoma katika lugha yao asili. Nchini Cambodia, jamii zilizotengwa hupewa umuhimu katika mafunzo ya ualimu. Kupata idadi ya walimu wa kutosha katika maeneo yenye ugumu wa maisha huhitaji usawazishaji wa ajira na kulenga kusaidia shule zinazoanguka. Nchini Gambia na Mozambique, tuzo ama marupurupu maalum hupatiwa walimu wanaofanya kazi katika maeneo ya mashambani. Walimu wanahitaji mafunzo ili kuwawezesha kufundisha bila matatizo katika madarasa yenye watoto kutoka asili mbalimbali. Hii ni changamoto kwa mielekeo yao kuhusiana na waliotengwa. Mfano bora wa mipango hiyo ni katika eneo la Amazonian, Peru, ambapo wataalam wa kiasili na wa kigeni hushirikiana kutoa mafunzo kwa walimu wa lugha mbalimbali na kuwazoesha na tamaduni za kiasili.

30 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 2 9 Kutoa elimu ya lugha na tamaduni mbalimbali ni muhimu zaidi katika kuwafikia watoto kutoka jamii zilizotengwa kikabila na kilugha. Mifano mingi ya mipango kutoka Afrika kusini mwa jangwa la sahara inaashiria kwamba ufundishaji kwa lugha ya kiasili ya mtoto hutoa matokeo mazuri. Shule zinazofunza lugha tofauti nchini Burkina Faso, zimezidisha mafanikio katika masomo huku zikipunguza idadi ya wanafunzi wanaoacha shule nchini Mali. Mabadiliko katika elimu katika baadhi ya nchi za Latin America yamependekeza kutekelezwa kwa elimu ya lugha tamaduni tofauti ili kutatua masuala ya lugha na tamaduni. Nchini Bolivia, utangazaji wa tamaduni na lugha mbalimbali umeanzishwa kwa lugha tatu kuu ambazo zilitumika na 11% ya shule zote za msingi mwaka wa Vitabu vya kiada vilibadilishwa pia ili kuitilia uzito zaidi historia ya taifa hilo na jukumu la raia asili wa nchi hiyo. Elimu ya tamaduni mbalimbali ina jukumu kubwa sio tu katika kuwafikia waliotengwa bali pia kutoa mtaala kwa wanafunzi wote ambao utaheshimu tamaduni mbalimbali, ukomeshe dhuluma, utoe hamasisho kuhusu tofauti za kijamii na kuibua mjadala. Kuhakikisha kwamba watoto walemavu wananufaika na fursa za elimu katika mazingira jumuishi kunahitaji mabadiliko katika mwelekeo wa serikali sawa na uwekezaji katika mafunzo ya walimu, uboreshaji wa miundombinu na utoaji wa vifaa vya elimu. Kongamano la mwaka wa 2008 kuhusu haki za walemavu linaainisha ajenda pana ya utoaji wa huduma na ni muhimu kwa kila serikali kuziunga mkono. Baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali yanatoa mitazamo muhimu. Katika jamhuri ya kidemokrasi Lao mtandao wa zaidi ya shule 500 unatoa nafasi kwa watoto wenye mahitaji maalum kupata mafunzo katika mazingira shirikishi. Sanduku 5: Kuwafikia wafugaji Kaskazini mwa Kenya Taswira hii imekuwa ikibadilika kufuatia kuibuka kwa mashirika ya kijamii yanayotetea jamii hizi pamoja na kundi kuu la wafugaji bungeni, hatua ambayo imepelekea kutambulika kwa makundi ambayo awali yalitengwa zaidi nchini humo. Kubuniwa kwa wizara ya ustawi wa eneo la Kaskazini mwa Kenya na maeneo kame katika afisi ya rais ni hatua mojawapo muhimu zaidi kuwahi kuchukuliwa na serikali kwa lengo la kushughulikia changamoto katika eneo hilo kwa utekelezi zaidi. Sheria ya kutetea elimu ya jamii ya wafugaji ilibuniwa mnamo mwaka wa Ubunifu huo ulijumuisha kushirikishwa kwa maarifa ya kiasili katika mtaala, kutoa ruzuku kwa shule tanga, kuanzisha shule zinazowapa chakula watoto katika jamii hiyo, kukarabati mfumo rasmi ili kuafiki hali ya wafugaji, kuwaajiri walimu hasa wa kike kutoka jamii hiyo kupitia usawa wa uwakilishi wa kijinsia na kutumia redio na rununu kufikia hadhira zaidi. Changamoto kuu inasalia kwa wizara kutekeleza jukumu lake pana na kwa serikali kuzidisha ufadhili. Haki na fursa Matarajio ya kuwepo kwa usawa katika elimu hutegemea hali ya watoto baada ya shule, na mikakati ya kijamii na kiuchumi ambayo inaendeleza utengwaji. Haki, sheria na hamasisho za kisiasa Mifumo ya sheria inaweza kutoa nafasi nzuri ya kukabiliana na ubaguzi. Makongamano ya kimataifa na asasi za kutetea haki za binadamu huweka kanuni na kubuni mfumo wa taasisi wa kuendeleza haki za kijamii, kiuchumi na kisiasa. Sheria na katiba za nchi hufasiri kanuni hizi katika misingi ya haki. Katika hali nyingine, njia mbadala ya kuhakikisha sheria inazingatiwa imekuwa shinikizo kuu la mabadiliko. Hukumu kubwa zaidi katika haki za kijamii nchini Marekani ni ile iliyotolewa mnamo mwaka wa 1954 na bodi ya elimu ya Brown v. Board, ambayo ilibatilisha sheria zilizowatenga watoto wa rangi mbalimbali kusoma katika shule moja. Kanuni zilizotumiwa kwenye kesi hii zilitumiwa kupinga ubaguzi katika maeneo mengine, na ilikuwa hatua kubwa kwa Waamerika weusi katika kupigania usawa wa uraia pamoja na kisiasa. Watoto wasiozidi asilimia 40 walisajiliwa katika shule mnamo mwaka wa 2007 katika mkoa wa Kaskazini Mashariki nchini Kenya, miaka minne baada ya serikali kufutilia mbali karo za shule. Hali ya maisha ya jamii ya wafugaji wa kuhamahama na hatari inayoikabili jamii hizo ina maana kuwa kufutilia mbali karo pekee hakutoshi kuwawezesha watoto wao kwenda shuleni. Makundi mengine yaliyotengwa kama Roma huko Ulaya, yamefanikiwa pia kupinga uhalali wa sera zinazosababisha ubaguzi wa kitaasisi. Nchini India, uwajibikaji wa kikatiba kufanikisha Elimu kwa Wote bila malipo umekuwa ukitiliwa maanani tangu mwaka wa 1950, lakini ni hivi karibuni tu ambapo umekuwa jukumu la kisheria ambalo linatekelezwa kupitia kwa mahakama. Kulindwa kisheria huenda kukaleta ufanisi zaidi iwapo kutaungwa mkono na hamasisho za kisiasa hasa wanaotengwa. Nchini New Zealand, vuguvugu la lugha ya jamii ya ko-hanga reo limetoa mtazamo wake wa kuwatetea watoto wa jamii ya Ma-ori katika maswala ya kijamii, kisiasa na kitamaduni mbali na kuchangia katika upanuzi wa nafasi za elimu kwa watoto wao pamoja na kuweka mfumo wa elimu unaojumuisha tamaduni mbalimbali. Ulinzi wa kijamii: ubadilishaji wa pesa taslimu na zaidi Ulinzi wa kijamii ni silaha muhimu kwa jamii katika kupunguza madhara yanayotokana na umaskini. Mipango ikiwemo ubadilishaji wa pesa taslimu, usalama kikazi na kuboresha lishe. Mipango ya ulinzi wa kijamii huko Latin America ina rekodi nzuri katika Kutoa elimu ya uwili - lugha na tamaduni mbalimbali ni muhimu zaidi katika kuwafikia watoto kutoka jamii zilizotengwa kikabila na kilugha

31 3 0 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Nchini New Zealand, vuguvugu la lugha ya jamii ya kōhanga reo limetoa mtazamo wake wa kuwatetea watoto wa jamii ya Māori kuimarisha hali ya kuhudhuria masomo na kufanya vizuri darasani. Kwa mfano, mpango wa kijamii wa Red de Protección nchini Nicaragua ambao ulilenga watoto ambao hawakuwahi kumaliza masomo katika shule za msingi uliimarisha usajili wa watoto waliojiunga tena na shule kwa 13% huku watoto kutoka jamii maskini zaidi wakinufaika zaidi. Nchi maskini zaidi vilevile zimepata mafunzo kutokana na mipango ya ulinzi wa kijamii. Baadhi ya nchi hizo zimeandikisha matokeo bora katika elimu. Mpango wa Productive Safety Net Programme nchini Ethiopia umeziwezesha jamii maskini kuzidisha matumizi ya mtaji wao katika elimu na afya na kuhakikisha kuwa watoto wanasalia shuleni katika majira ya kiangazi. Kuongezwa kwa uwekezaji unaolenga ulinzi wa kijamii na serikali pamoja na wafadhili kuna uwezekano wa kuendeleza usawa na kuzidisha maendeleo kwa nia ya kuafiki malengo ya kufanikisha Elimu kwa Wote. Kutoa bajeti inayolenga waliotengwa Kuwafikia waliotengwa zaidi aghalabu hugharimu zaidi ikilinganishwa na gharama za maeneo tajiri. Jukumu la serikali ni kubwa zaidi katika kuelekeza raslimali za kifedha katika maeneo hayo na jamii zenye uhitaji mkubwa. Nchi nyingi zimeweka mikakati ya kusambaza upya pesa za umma kama vile kuanzisha raslimali mpya, kuupa umuhimu usawa katika ugavi ama kulenga ustawi wa kieneo. Mpango wa FUNDEB nchini Brazil ni mfano bora wa jaribio la kupunguza viwango vya ugavi wa pesa unaotekelezwa na serikali katika elimu. Hii imenufaisha zaidi maeneo maskini, japo tofauti kubwa katika ufadhili huo zingalipo. Kutengwa kielimu hudumishwa na mielekeo ya umma pamoja na hatua za kijamii ambazo zinayanyanyapaza makundi maskini na kudhibiti nafasi zao. Hiyo ndiyo sababu ripoti hii inatilia mkazo umuhimu wa serikali zote kuweka mikakati bora ya kukomesha utengwaji kwa mapana zaidi ili kupunguza umaskini na kuleta usawa wa kijamii. Kusonga mbele: jamii ya wafugaji zinahitaji suluhisho zinazoweza kubadilika Giacomo Pirozzi/PANOS

32 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 3 1 REUTERS/Ahmad Masood Sura ya 4 Mizozo na kufurushwa katika makazi huathiri zaidi elimu, Afghanistan Swala la Msaada: kukosa kutimiza ahadi Huku nchi nyingi maskini zikikabiliwa na shinikizo za bajeti kutokana na poromoko la uchumi duniani, ongezeko la msaada wa kimataifa ni muhimu zaidi katika kufikia malengo ya ustawi wa binadamu. Jumla ya viwango vya msaada vinaongezeka lakini ipo hatari kwamba wafadhili watakosa kutimiza ahadi zao za mwaka wa Utoaji msaada wa elimu ya msingi unaongezeka lakini ahadi hazitimizwi, hali ambayo inaibua wasiwasi kuhusu utoaji wa misaada hiyo katika siku za baadaye. Baadhi ya wafadhili wakiwemo wanachama wa (G8) wanakosa kutimiza ahadi zao katika kutoa msaada. Njia za kutoa msaada zimeimarishwa, lakini hatua za kufikia malengo yaliyoafikiwa ni tofauti. Nchi nyingi zinazokabiliwa na mizozo hupokea msaada usiotosha kukidhi matakwa katika elimu.

33 3 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Msaada wa kielimu nchini Mozambique umesaidia kupunguza idadi ya watoto wasioenda shule kwa nusu milioni Mchoro 10: Afrika inakabiliwa na upungufu mkubwa katika jumla ya msaada Jumla ya ODA, zilizotolewa mwaka 2004 kwa Dola mabilioni Msaada wa kimataifa ni sehemu muhimu katika kufanikisha swala la Elimu Kwa Wote. Katika mwaka wa 2000, mataifa tajiri yaliapa kwamba hakuna nchi ambayo imejitolea kufikia malengo ya kutoa elimu kwa wote itakosa kufanikisha malengo hayo kutokana na ukosefu wa kifedha. Msukosuko wa uchumi wa dunia umechangia pakubwa umuhimu wa kujitolea huko. Ukuaji dhaifu wa kiuchumi na ongezeko la shinikizo katika bajeti za serikali linatishia kurudisha nyuma ufanisi uliopatikana kwa ugumu katika mwongo uliopita. Kukabili tishio hilo kutahitaji sio tu kuzidisha utoaji wa msaada bali pia kuimarisha ubora wa misaada hiyo. Baadhi ya wachunguzi wanaoshuku uwazi katika misaada hii wamekuwa wakitoa mwito wa kutiliwa masharti ama kusitishwa kwa misaada hii. Ushahidi wao hata hivyo hauoani na matakwa hayo. Msaada wa kielimu nchini Mozambique, kwa mfano, umesaidia kuimarisha kusajili kwa wanafunzi katika shule za msingi kutoka asilimia 52 mwishoni mwa miaka ya tisini hadi asilimia 76 mwaka wa 2007 huku idadi ya watoto wanaokosa kwenda shule ikipungua kwa nusu milioni. Nchini Afghanistan, msaada unawanufaisha mamilioni ya watoto hasa wasichana kuhudhuria masomo kwa mara ya kwanza. Msaada wa kimataifa hauwezi kuchukua mahala pa sera madhubuti za kitaifa lakini unaweza kusaidia kuondoa vikwazo dhidi ya elimu ambavyo vimesababishwa na umaskini, jinsia na vyanzo vingine vya kutengwa. Rekodi kuhusu uwasilishaji Kiwango cha msaada wa kimataifa katika elimu kinategemea pakubwa kiasi cha hazina ya msaada huo duniani. Habari njema ni kwamba, jumla ya msaada wa Jumla ya ODA Lengo la jumla la ODA Jumla ya ODA Jumla ya ODA kwa Afrika Makadirio ya ongezeko la jumla la ODA Asili: Tazama Mchoro 4.1 katika EFA Global Monitoring Report 2010 Jumla ya ODA kwa Afrika Lengo la Afrika 2010 Makadirio ya ongezeko la ODA kwa Afrika Lengo la dunia 2010: upungufu wa dola bilioni 20 Lengo la Afrika 2010: upungufu wa dola bilioni 18 kiustawi ulipanda zaidi mnamo mwaka wa 2008 huku msaada ukiongezeka kwa takriban asilimia 10 kutoka mwaka uliotangulia na kufikia dola bilioni 101 za Marekani (kinyume na bei za mwaka 2004). Mgao wa msaada huo katika jumla ya pato la taifa (GNI) kwa mataifa tajiri vilevile ulipanda hadi asilimia Hata hivyo, wafadhili hawana nia ya kutimiza viapo walivyotoa katika msururu wa mikutano ya kimataifa mnamo mwaka wa 2005, ukiwemo kongamano kwa jina Gleneagles la mataifa ya G8, wa kuongeza jumla ya msaada hadi dola bilioni 130 za Marekani kufikia mwaka wa Katika mkondo wa sasa, huenda kukawa na pengo la dunia kati ya kima cha msaada kilichopangiwa kutumika na msaada halisi wa takriban dola bilioni 20 za Marekani ambao unatumika katika mwaka wa 2010, dola bilioni 18 ikitengewa bara la Afrika. (Mchoro 10). Wafadhili wana takwimu mbalimbali dhidi ya utendakazi wa vituo mbalimbali vya kimataifa. Wanachama wa jumuiya ya ulaya wanawajibika kwa pamoja kufanikisha msaada kwa mataifa yanayolengwa katika mgao huo wa asilimia 0.56 kufikia mwaka wa 2010 na asilimia 0.70 kufikia mwaka wa 2015(Mchoro 11). Huku Ujerumani na Uhispania zikiwa zimeongeza msaada wao kwa nchi hizo, taifa la Italy limeandikisha ongezeko, Marekani kutoandikisha badiliko lolote huku Japan ikiandikisha upungufu. Nchi tano zilizidi kiwango zilizowekewa na Umoja wa Mataifa cha asilimia 0.7, huku Uswizi ikiwekeza kiasi cha asilimia moja. Matarajio ya kutimiza malengo ya msaada ya mwaka wa 2010 yamedidimia hata zaidi kufuatia poromoko la uchumi wa dunia. Mipango ya nchi nyingi wafadhili ingali kufafanuliwa ingawa mafunzo kutoka majanga ya hapo awali yanatoa kila sababu ya kuwa na hofu. Ireland ambayo imepata pigo kubwa la poromoko hili itakata bajeti yake kwa moja juu ya tano, ingawa viapo vimetolewa kurejesha upungufu huo wakati uchumi utakapoimarika. Ni muhimu hatua kuchukuliwa ili kulinda utoaji wa msaada. Kusitisha msaada wakati ambapo jamii nyingi maskini zinakabiliwa na msukosuko wa kiuchumi kunaweza kuharibu uwekezaji wa awali katika ustawi wa binadamu na hivyo kuangamiza malengo ya mwaka Mifumo ya hivi karibuni Utoaji wa msaada wa elimu ya kawaida na ile ya msingi umekuwa ukikua hatua kwa hatua. Kwa jumla, msaada uliotolewa kwa sekta ya elimu ulifika dola bilioni 10.8 za Marekani mwaka wa 2007, hii ikiwa mara mbili zaidi ya idadi iliyotolewa mwaka wa Malipo ya msaada kwa elimu ya msingi yalikuwa kwa upole, kutoka dola bilioni 2.1 za Marekani mnamo mwaka wa 2002 hadi dola bilioni 4.1 mwaka wa Ongezeko hili linatokana na ongezeko la jumla la msaada, sio kwa kuwa malipo hayo yalipewa umuhimu mkubwa. Katika miaka ya , elimu ilichangia kadiri ya asilimia 12 ya jumla ya ahadi za msaada, kiasi sawa na kilichokuwa katika miaka ya Taswira ya ahadi za msaada inakinzana vikali na ile ya utoaji. Kwa jumla, viwango vya ahadi havisongi ingawa hali hiyo haitabiriki. (Mchoro 12). Mnamo mwaka wa 2007, ahadi zilizotolewa katika elimu zilifikia dola bilioni 12.1,

34 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 3 3 Mchoro 11: Karibu wahisani wote hawatimizi ahadi za msaada wa 2010 Mchoro 12: Baada ya kuimarika mwanzoni mwa mwongo, ahadi za kielimu zinadumaa Italia Ugiriki Marekani Japan Austria New Zealand Uhispania Australia Canada Ujerumani Uingereza Ufini Irelandi Ubelgiji Uswizi Ufaransa Ureno Uholanzi Uswidi Luxembourg Denmaki Norwe Jumla ya DAC Mataifa ya DAC-EU ODA kama % ya GNI Asili: Tazama Mchoro 4.2 katika EFA Global Monitoring Report (ongezeko) 2008 (upungufu) lengo 2010 yamkini viwango sawa na vile vya mwaka wa Elimu ya msingi inasalia kuwa eneo lenye kutia wasiwasi. Huku ahadi za elimu zikiimarika kwa 58% miaka kadha baada ya mkataba wa Dakar mnamo mwaka wa 2000, kipindi tangu mwaka wa 2004 kimeshuhudia kukwama kulikochangiwa na mdidimio mkubwa. Katika uhalisia, dola bilioni 4.3 za Marekani zilizoripotiwa mwaka wa 2007 ziliwakilisha upungufu wa 22% ama kiasi cha dola milioni 1.2 kutoka kiwango chake cha mwaka wa Kupunguka kwa ahadi hizo kwa elimu ya msingi kulizidi ile ya elimu katika jumla. Huku tofauti katika ahadi za wahisani kila mwaka ukikosa kuepukwa, mikondo ya hivi karibuni inadokeza matatizo ya mifumo. Tatizo moja ni kwamba jumla ya utoaji wa msaada katika elimu hujumuisha kikundi kidogo cha wafadhili. Wafadhili watano wakubwa wa elimu, Ufaransa, Ujerumani, Muungano wa Ustawi wa Kimataifa unaosimamiwa na benki ya dunia, Netherlands na Uingereza walichangia kiasi chini ya 60% ya jumla ya ahadi za msaada wa elimu. Athari ya idadi ya ndogo ni kwamba hatua ya mfadhili mmoja ama wafadhili wawili inaweza kusababisha upungufu mkubwa katika viwango vya jumla vya msaada. Wasiwasi mwingine ni kusawazishwa kwa msaada unaotolewa kati ya viwango tofauti vya elimu. Mnamo mwaka wa 2000, wafadhili waliahidi kuongeza umuhimu wanaoipa elimu ya msingi lakini ahadi hiyo haijaleta Kisawia cha 2007 Dola $ mabilioni Jumla ya msaada wa elimu Jumla ya msaada wa elimu ya msingi mabadiliko katika mgao wa raslimali. Elimu ya msingi ilichangia mbili kwa tano ya jumla ya hazina ya msaada wa elimu katika miaka ya , kadiri kiasi sawa na mwaka wa Nchi zenye mapato ya chini zinaendelea kupokea chini ya nusu ya jumla ya msaada wa elimu kwa kadiri, huku yapata 60% ya msaada huo ukitengewa elimu ya msingi. Wafadhili wa kibinafsi hutofautiana pakubwa katika ahadi kwa viwango tofauti vya elimu. Wawili kati ya wafadhili sita wakuu wa elimu: Netherlands na Marekani hutoa zaidi ya 60% ya msaada kwa elimu ya msingi. Wengine watatu: Ufaransa, Ujerumani na Japan hutoa zaidi ya 55% kwa elimu inayozidi ile ya msingi. Nchini Ufaransa na Ujerumani, kiwango kikubwa cha bajeti ya elimu hutengewa taasisi zao za elimu ambazo huwasajili wanafunzi wa kigeni. Wafadhili wengine kama Uhispania, wanaelekeza msaada mwingi katika elimu ya msingi. Vyanzo vipya na muhimu vya msaada vinaibuka, huku baadhi yavyo vikitazamiwa kuwa huenda vikaipiga jeki pakubwa elimu. Wafadhili wasioegemea kamati ya usaidizi ya OECD kama vile Uchina na Saudi Arabia, wametoa michango katika elimu katika miaka ya hivi karibuni. Msaada kutoka sekta ya kibinafsi vilevile umeongezeka. Mifumo bunifu ya kifedha kama vile ile ambayo tayari imestawishwa katika sekta nyingine inaweza kuhamasishwa zaidi kujaza pengo la ufadhili wa elimu (Sanduku 6). Kuifanya misaada kufaa zaidi Ni vigumu kupima thamani ya msaada ikilinganishwa na kiwango. Mkataba wa mwaka 2005 kuhusu ufaafu wa msaada ulioafikiwa mjini Paris uliweka jaribio la wafadhili na wapokezi wa msaada kutafuta mbinu za kutoa misaada kwa njia bora zaidi, lakini hatua zilizopigwa katika malengo ya mkataba huo zimechanganywa. Italazimu juhudi kuzidishwa katika kipindi cha miaka mitatu ijayo ikiwa malengo hayo yataafikiwa Asili: Tazama mchoro 4.7 katika EFA Global Monitoring Report Ahadi ya Dola bilioni 4.3 za Marekani kwa elimu ya msingi zilizotolewa mwaka 2007 ziliwakilisha upungufu wa asilimia 22

35 3 4 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Mifumo bunifu ya ufadhili inafaa kuhamasishwa ili kuziba pengo la ufadhili wa elimu Sanduku 6: FIFA na Kombe la Dunia zasaidia kufikia malengo ya EFA Mchuano wa kuwania kombe la dunia wa mpira wa kandanda mwaka wa 2010 unazidi kuwa kigezo kikubwa kwa hatua za kimataifa katika kuendeleza kampeni za Elimu Kwa Wote. Shirika la The Global Campaign for Education linafanya kazi kwa pamoja na Shirikisho la Soka Ulimwenguni (FIFA) kutoa hamasisho kwa matatizo ya elimu yanayokabili Afrika Kusini mwa la jangwa la Sahara. Ubunifu katika ufadhili huenda ukaendelea kuinufaisha elimu hata baada ya kombe la dunia. Makubaliano kati ya vilabu vikuu vya jumuiya ya ulaya na FIFA kuweka ada ndogo ya asilimia 0.4% ya Mustakabali Bora (Better Future) kwa udhamini wa baadaye na mapato yatokanayo ya mauzo ya vyombo vya habari huenda yakachangia kiasi cha dola milioni 50 za Marekani kila mwaka. Hii itawawezesha watoto laki tano zaidi kutoka nchi maskini zaidi duniani kujiunga tena na shule kutokana na msaada zaidi. Uwezo wa kutabiri msaada Bila kupata msaada uliotabiriwa kwa wakati ufaao, serikali zinazopokea misaada hiyo hujipata hutatizika kuratibu mipango ya muda mfupi ya kifedha na kuitekeleza. Mnamo mwaka wa 2007, ni asilimia 63 pekee ya msaada iliyofika kwa wakati ufaao. Kwa baadhi ya nchi, kiwango hiki kilikuwa cha chini mno. Nchini Yemen, thuluthi moja tu ya msaada uliopangiwa ilitolewa katika mwaka wa 2007 na dola milioni 151 pekee za Marekani kati ya ile 477 ambayo Benin ilipaswa kupatiwa ndiyo iliwasilishwa. Matatizo yanayotokana na utabiri wa msaada sio majukumu ya pekee kwa wafadhili. Kwa kawaida, matatizo hutokea pande zote za ubia wa msaada kutokana na mipango duni ya wapokezi na ukosefu wa uwajibikaji mpana wa wafadhili. Utafiti uliofanywa katika Jamhuri ya muungano ya Tanzania ulibainisha kwamba utoaji wa msaada kwa kiwango cha chini katika mpango wa kitaifa wa elimu ya msingi ulihusishwa na kuchelewa kuidhinishwa kwa mipango ya kazi na viwango duni vya ripoti za uhasibu, sawa na ripoti za mahitaji zisizo za kweli kuhusu ufadhili. Mifumo ya usimamizi wa misaada ya nchi Wafadhili wameweka lengo madhubuti la kutoa asilimia 80 ya msaada kupitia kwa mifumo ya umma, ya nchi zinazopokea msaada huo kufikia mwaka wa Mafanikio ya lengo hili yamekuwa ya chini: mwaka wa % pekee ya msaada ulitolewa kupitia kwa mifumo hii. Hii ilitokana na udhaifu wa mifumo hiyo na hali yao ya kutoweza kusimamia misaada mikubwa. Lakini hata palipo na mfumo dhabiti, wafadhili wakati mwingine, huchelewa kuzidisha kiasi cha msaada unaotolewa kupitia kwayo. Zaidi, ubora wa mfumo wa usimamizi wa pesa za umma katika nchi yoyote ile husalia kuwa kigezo hafifu cha kutumiwa na wafadhili. Bangladesh ina mfumo hafifu zaidi ya Mozambique, Rwanda ama Zambia, ingawa ina mgao wa juu wa msaada kwa sababu ya mifumo ya uropoti wa kitaifa. Matokeo kama hayo huibua maswali kuhusu ufanifu wa vishawishi vya mabadiliko ambavyo huwekwa na jamii ya wafadhili. Kusawazisha msaada na kushirikisha shughuli Ushirikiano bora wa msaada unamaanisha wafadhili kufanya kazi pamoja ili kusawazisha shughuli pamoja na mipango ya serikali zinazopewa misaada. Kiashiria cha mafanikio katika sehemu hii ni mgao wa msaada kutegemea mipango. Katika miaka ya , elimu ya msingi ilipata 54% ikilinganishwa na 31% katika miaka ya Mozambique na Zambia zimekuwa zikilengwa zaidi katika ufadhili wa elimu huku wafadhili wakifanya kazi pamoja kupitia kwa mifumo ya kitaifa na mikakati ya ujumla ya kuripoti. Kukumbatia lugha mbili, Peru UNESCO/Ernesto Benavides

36 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 3 5 Crispin Hughes/PANOS Wafadhili daima hutambua umuhimu wa kujenga upya mifumo ya kijamii na kiuchumi katika hali za kivita na zile za baada ya vita. Hata hivyo, mafanikio katika taratibu za sera zinazooanisha msaada wa muda mrefu wa ustawi zimekuwa zikipunguzwa. Kutekeleza mikakati ya dharura Ili kutimiza changamoto zilizoangaziwa huko Dakar kufikia mwaka wa 2015, ulimwengu unahitaji mkakati bora wa ufadhili ili kutoa raslimali muhimu kwa kustawisha mifumo ya elimu. Mkakati huo wa dharura wa Fast Track Initiative (FTI) ulizinduliwa mnamo mwaka wa 2002, ukitazamiwa kuwa kichocheo cha maendeleo ya elimu kwa wote. Hata hivyo, mpangilio wake umekosa kuzaa matunda. Badiliko kuu la FTI litakuwa mkakati huu ni muhimu zaidi ili kufikia malengo ya elimu kwa wote. Masomo yanaendeshwa chini ya mti, Uganda: kuweka elimu katika mahitaji ya jamii Msaada kwa nchi zinazokabiliwa na mizozo Ni muhimu kuongezwa kwa msaada wa elimu katika nchi maskini na ambazo zinakabiliwa na mizozo ya kivita. Ingawa msaada unaopewa nchi hizi unazidi kuongezeka, msaada huo hautoshelezi mahitaji ya yanayohitajika. Nchi 20 maskini ambazo zinakumbwa na mzozo wa kivita zinachangia kiasi cha mtoto mmoja kwa watatu ambao hawaendi shuleni, lakini katika mwaka wa ni chini ya kiasi cha moja kwa tano ya jumla ya msaada wa elimu ya msingi ulitolewa kwa nchi hizi maskini huku zaidi ya nusu ya msaada huo ukiziendea nchi tatu pekee: Afghanistan, Ethiopia na Pakistan. Kutoka kwa msaada wa kibinadamu hadi wa ustawi: upungufu uliopo Katika nchi nyingi zinazokabiliwa na mizozo ya kivita, matumizi ya pesa katika maswala ya usalama na msaada wa kibinadamu yanapewa umuhimu na mataifa wafadhili, huku mipango ya muda kuhusu ustawi kwa jumla na hasa wa elimu ikikosa kuangaziwa zaidi. Makadirio yanakisia kwamba katika mwaka wa 2008, elimu ilichangia asilimia mbili ya jumla ya msaada wa kibinadamu, hii ikiwa sawa na dola milioni 237 za Marekani. Katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, kiasi cha dola milioni 5 za Marekani ambacho ni asilimia moja ya msaada wa kibinadamu kilitumika kufadhili elimu katika mwaka wa 2007, huu ukiwa ni upungufu wa dola milioni 27 ambacho ndicho kiasi cha chini zaidi kilichohitajika kitaifa kufadhili sekta ya elimu. Tatizo hapa si kwamba jamii ya kimataifa inawekeza zaidi katika usalama na kupunguza baa la njaa bali kiasi kidogo zaidi kinawekezwa katika idara nyingine ambazo hazina umuhimu zaidi katika ujenzi mpya baada ya vita. Jumbe Kuu Ulimwengu unahitaji mpangilio bora na wa kimataifa ili kuzidisha mafanikio katika kutimiza malengo ya elimu kufikia mwaka wa Ingawa pamekuwa na baadhi ya mafanikio muhimu, mkakati wa dharura umefeli kuhamasisha na kufanikisha ufadhili katika kiwango kinachohitajika. Sheria mpya za usimamizi zinahitajika ili kuziangazia nchi zinazostawi pamoja na kuweka uwazi katika maamuzi. Hatua zaidi zinafaa kuchukuliwa ili kufadhili nchi zinazokabiliwa na mizozo. Mabadiliko muhimu katika mikakati ya dharura iliyopo kwa sasa ni bora, na mipango ya afya duniani inaweza kutoa mafunzo muhimu. Mpango wa mkakati wa dharura Wakati wa kubuniwa kwake, lengo la mkakati wa dharura(fti) lilikuwa kuthibiti mpango wa kitaifa wa elimu ili kupata ushirikishi zaidi wa wafadhili pamoja na kuzidisha msaada wa kimataifa. Mkakati huo ulitazamiwa kupata raslimali kupitia kwa mpango wa kuidhinisha huku idhini yake ikitoa fursa ya ufadhili zaidi. Vilevile, mkakati huo ulikuwa chanzo cha ufadhili kivyake kupitia kwa hazina fasilishi (Catalytic fund). Matokeo yamekuwa ya kusikitisha. Wakati wa utathmini kwa kulinganisha na pengo la kifedha, mkakati wa FTI umekosa kupata raslimali kulingana na mahitaji. Mabadiliko ya kimsingi yanahitajika. Usimamizi wa FTI unahusisha washiriki wengi na pia hatua tatanishi. Ingawa juhudi zimefanywa kubadilisha haya, matatizo manne yanasalia: Wafadhili daima hutambua umuhimu wa kujenga upya mifumo ya kijamii na kiuchumi katika hali za kivita na zile za baada ya vita

37 3 6 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Nchi zinazoendelea zina usemi mdogo katika maamuzi ya FTI Kukithiri kwa wafadhili na ukosefu wa wakaguzi huru, na baraza linalofahamu taratibu za benki ya dunia; Ukosefu wa mamlaka kwa nchi zinazostawi katika kufanya maamuzi; Viwango tofauti vya kufanya maamuzi kati ya makundi ya wafadhili wa ndani na benki ya dunia ambayo inaweza kuwa na msimamo tofauti au ikose kutegemewa; Uongozi dhaifu ambao unahusishwa na ukosefu wa kuungwa mkono kisiasa katika mashirika muhimu na nchi wafadhili. Utoaji wa fedha: chache zaidi na za kutobashiriwa Kuna ushahidi mdogo zaidi kwamba kuidhinishwa kwa mkakati wa dharura kunapelekea ongezeko la kuungwa mkono kati ya jamii ya wafadhili wa ndani na nje. Utoaji fedha kupitia kwa hazina fasilishi pia umekuwa wa kuvunja moyo. Mpango huo ambao ulizinduliwa mnamo mwaka wa 2003 kama njia ya moja kwa moja ya kufadhili elimu umekumbwa na matatizo ya ukosefu wa uhamasisho wa raslimali, viwango duni vya kusambazwa kwa raslimali na misingi dhaifu ya wafadhili. Kati ya dola bilioni 1.2 za Marekani ambazo zilipokelewa na mpango huo kufikia mwezi Machi 2009, ni dola milioni 491 pekee ambazo zilikuwa zimetolewa huku nusu ya kiasi hiki ikiendea nchi tatu: Kenya, Madagascar na Rwanda. Mgao wa Senegal mnamo mwaka wa 2007 ulikuwa bado kutolewa kufikia mwezi Aprili Miaka miwili baada ya kutengwa kwa pesa hizo, Mozambique ilipata dola milioni 29 kati ya zile milioni 79 zilizotolewa. Kufuatwa kwa sheria nyingi kali mnamo mwaka wa 2007 kulirudisha nyuma maradufu utoaji wa pesa hizo ingawa pamekuwepo dalili za kuimarika hapo mwaka uliopita. (Mchoro 13) Nchi zinazokabiliwa na vita hazijapata ufadhili mzuri kutoka kwa mkakati huu wa dharura ingawa zimepitia hatua za kuidhinishwa. Miezi mitatu baada ya mkakati huo kuidhinisha mpango wa elimu ya kitaifa nchini Sierra Leone, nchi hiyo ilipewa idhini ya kupata ufadhili wa dola milioni 13.9 za Marekani kupitia kwa mkakati huo wa dharura. Mwezi Aprili 2009, miaka miwili baada ya uamuzi wa mgao huo, nchi hiyo ilikuwa bado inasubiri mgao wake wa kwanza. Mpango wa Liberia uliidhinishwa vilevile lakini ombi lake la msaada kutoka hazina fasilishi lilikataliwa. Mafunzo kutoka kwa mashirika ya kufadhili afya duniani Mwongo uliopita ulishuhudia ustawi mkubwa wa mikakati ya dunia katika ufadhili wa kiafya, hali ambayo imekuza uungwaji mkono kisiasa kwa kulipa swala la afya umuhimu katika ajenda za ustawi wa kimataifa. Mifano maarufu ni pamoja na mpango wa kutoa ufadhili wa kukabiliana na Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria na ule wa GAVI Alliance (awali ukijulikana kama Global Alliance for Vaccination and Immunization), ambayo imekuwa na mafanikio makubwa katika sekta ya afya. Mpango wa Hazina ya Dunia umetoa dawa za kupunguza makali ya virusi vinavyosababisha Ukimwi kwa watu wapatao milioni mbili, mbali na kutibu watu milioni 4.6 wanaougua Kifua Mchoro 13: Kuchelewa zaidi kati ya kutenga na kutolewa msaada kutoka Hazina Fasilishi Ethiopia Guinea Mongolia * Sierra Leone Mozambique Cambodia Benin Mauritania Mali Yemen * Nicaragua * Ghana * Rwanda Kyrgyzstan Cameroon Lesotho Tajikistan Djibouti Rep. Moldova Kenya Madagascar Januari 2003 Januari 2004 Januari 2005 Januari 2006 Januari 2007 Januari 2008 Januari 2009 badiliko katika sheria za uchelewa kati ya kutenga na muafaka wa ufadhili, Trust Fund katika miezi * ufadhili wa mwaka wa tatu Asili: Tazama mchoro 4.19 katika EFA Global Monitoring Report 2010 kuchelewa kati ya muafaka wa msaada na utoaji wa kwanza, katika miezi

38 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 3 7 Fursa nzuri: watoto kutoka vitongoji duni wakiwa nje na ndani ya darasa, Bangladesh UNESCO/Samer Al-Samarrai Kikuu na kuokoa takriban maisha ya watu milioni 3.5. Kufikia mwisho wa mwaka wa 2008, mpango huo ulikuwa umetoa dola bilioni 7. Nao mpango wa GAVI umeepusha vifo vinavyokadiriwa kuwa milioni 3.4. Mingi kati ya msimamo na shughuli za ubia wa mipango ya afya duniani inaafiki kwa FTI. Wamefuzu katika kuzidisha raslimali za msaada na kudhibiti viwango vya juu vya ufadhili, mbali na kutafuta fedha kwingine hasa kutoka wakfu wa philanthropic. Mipangilio katika usimamizi imechangia ufanisi wao. Taasisi ya hazina ya dunia ni shirika huru na usioingiliwa kati na shirika ama mfadhili yeyote. Serikali za nchi zinazostawi pamoja na mashirika ya kijamii huchukua msimamo dhabiti na kupelekea mipango kutekelezwa na kamati za kitaifa chini ya mifumo yenye uwazi katika kufanya kimaamuzi. Licha ya kuwepo kwa tofauti kati ya afya na elimu, yapo mafunzo muhimu ambayo yanapatikana kutokana na mkakati wa dharura. Kulenga mabadiliko katika mpango wa elimu duniani Kutekelezwa kwa mabadiliko katika FTI kunaweza kuleta mafanikio makubwa katika kufikia malengo ya Dakar. Ripoti hii inapendekeza njia kadha za kuendeleza ufanisi wa kimataifa katika elimu: Rejelea kanuni za awali: mpango utakaofaa katika ufanisi wa kimataifa unafaa kutilia maanani njia za kuziba mapengo ya ufadhili katika mpango wa elimu kwa wote kwa kuunga mkono na mipango shirikishi ya kitaifa Zindua FTI kama wakfu huru na yenye baraza huru na thabiti mbali na benki ya dunia, mbali na kuifanyia marekebisho mipangilio ya uongozi ili kuthibiti sauti za serikali na mashirika ya kijamii katika nchi zinazostawi Kupangilia upya mifumo kwa uwazi na kupunguza kukithiri kwa wafadhili katika maamuzi ya kifedha Weka msingi salama wa kifedha ambao unaweza kutabiriwa kwa kuandaa makongamano ya mara kwa mara ya ahadi. Shughulikia matakwa maalumu ya nchi zinazokumbwa na vita kwa kufadhili mipango ya muda mfupi ya kujikwamua pamoja na ile ya muda mrefu kwa pamoja katika FTI. Marekebisho katika FTI yatahitaji hatua tekelezi itakayooana na uongozi wa kisiasa na mtazamo mpya. Changamoto kuu ni kwa watetezi wa elimu kati ya serikali za nchi zinazostawi, wafadhili na mashirika ya kijamii kuewza kufanya kazi pamoja ili kuleta mabadiliko haya. Mingi ya misimamo na desturi za ubia wa mipango ya afya duniani zinaafiki mikakati ya FTI

39 3 8 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Sura ya 5 Kukabili changamoto za Elimu kwa Wote Malengo ya Elimu kwa Wote hayatafikiwa katika nchi nyingi ikiwa serikali hazitaelekeza rasilimali na makini kwa wale wanaoachwa nyuma Ikiwa imesalia miaka mitano kabla ya kufikia mwaka wa 2015 uliolengwa, malengo ya Elimu kwa Wote yako katika njia panda. Nyingi kati ya nchi maskini zaidi duniani zimesalia nyuma katika malengo yaliyoafikiwa huko Dakar. Huenda, hata hivyo, zikasukumwa nje zaidi kwa kuwa matarajio yao ya kujikwamua kutoka kwa poromoko la uchumi wa dunia yamesalia ndoto. Ipo hatari kubwa kwamba hatua hizi zitakwama na kwamba katika baadhi ya nchi, mafanikio yaliyoafikiwa kwa shida tangu mwaka wa 2000 huenda yakatoweka. Iwapo dunia inataka kufikia mafanikio makuu katika malengo ya Dakar, serikali, wafadhili na jamii ya kimataifa sharti zionyeshe uwajibikaji mkubwa wa kisiasa. Warsha ya malengo ya maendeleo ya milenia ya mwaka wa 2010 inatoa fursa ya kuweka mkondo mpya. Huku serikali zikitazamia mwaka wa 2015, ni jambo la muhimu kukumbuka utengwaji katika kila aina ya ajenda ya Elimu kwa Wote. Malengo ya Elimu kwa Wote hayatafikiwa katika nchi nyingi ikiwa serikali zitaelekeza raslimali na manani yao kwa wale wanaoachwa nyuma kutokana na tofauti za umaskini, jinsia, kabila na dhuluma nyinginezo. Ripoti hii inatambua matatizo yanayohitaji kushughulikiwa pamoja na baadhi ya mafunzo muhimu ya sera. Mpango wenye hatua kumi za kuepuka utengwaji katika elimu hutokana na mafunzo haya: 1. Kuweka malengo yenye usawa kwa malengo yote ya Elimu kwa Wote Serikali hazifai tu kukadiria malengo ya kiwango cha kitaifa bali pia kulenga yale yenye usawa ambayo yanaangazia jamii iliyotengwa. Haya yanaweza kuchukuliwa kama njia za kupunguza tofauti za umaskini, jinsia, kabila na eneo. 2. Kustawisha mifumo ya kutafuta takwimu kwa kulenga takwimu zilizotawanyika ili kutambua makundi yaliyotengwa na kuchunguza maendeleo yao Kuchunguza na kupima kunafaa kutazamiwa kama kitengo muhimu cha mikakati inayokusudiwa kutambua wale wanaoachwa nyuma ili kuweka sera za kuwasaidia. Ufanisi katika utafutaji na uhifadhi wa takwimu unahitajika pia ili kutathmini hatua zilizopigwa katika malengo ya kudumisha usawa. Takwimu za udhalimu na utengaji, ambazo zimetolewa mahususi kwa ripoti hii, zinaweza kutumiwa kama sehemu ya nyenzo za kuthibiti na kuangazia usawa. Serikali zinahitaji kuwekeza zaidi katika njia za kuchukua takwimu za kitaifa ili kuwezesha uelewekaji wa muktadha wa utengwaji. Takwimu kama hizo zinaweza pia kutumika kushughulikia pengo la usawa kwa kupeleka raslimali kwa shule na maeneo yaliyo nyuma kimaendeleo. 3. Kutambua vichocheo vya utengwaji wa makundi fulani Madhara ya jumla ya kutengwa ni kuwanyima fursa watoto kutokana na sababu ambazo hawawezi kudhibiti na ambazo zinatofautiana pakubwa. Matatizo yanayowakabili wakazi wa mitaa ya mabanda si sawa na yale yanayowakabili wale maskini walio mashambani. Ingawa umaskini ni chanzo kikuu cha kutengwa katika elimu ulimwenguni, dhuluma zinazohusiana nao ambazo zinawakumba wasichana wadogo, makabila madogo ama watoto walemavu zinaendelezwa na itikadi za kijamii ambazo zinahujumu imani ya mtu binafsi na kudunisha thamani ya elimu. Kuelewa sababu kama hizi ni muhimu kwa kuwa hatua zitakazopelekea ufanisi katika kutatua utengwaji ni sharti zilenge sababu fulani kuu ambazo huenda zikakosa kutiliwa maanani katika hali ya ujumla. 4. Kuidhinisha wa sera jumuishi itakayotatua vyanzo vya dhuluma katika elimu na zaidi Serikali zinahitaji kuangazia usawa kama sera kuu ya kitaifa pamoja na kuelezea manufaa ya kiuchumi na kijamii yanayotokana na usawa huo katika elimu. Pembe tatu jumuishi za elimu ambayo ilibuniwa mahususi kwa ripoti hii inataja maeneo matatu makuu ya kuleta mabadiliko: Serikali zinafaa kuimarisha uwezo wa kumudu na kufikia elimu hii kwa kufutilia mbali karo za namna yoyote, kuwapa usaidizi muafaka waliotengwa, kupunguza hatua kati ya shule na jamii na kuweka hatua bainifu za kutoa elimu ikiwemo shule tanga kwa jamii ya wafugaji na kuzidisha viwango vya mafunzo katika maeneo ya mashambani.

40 R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E M U H T A S A R I 3 9 Francçois Perri Kwa hali yoyote: Kwenda shule kwa mashua, Mali Kuthibiti mazingira ya masomo kwa kuwaajiri walimu kwa usawa zaidi pamoja na kuweka mfumo wa elimu unaolenga kabila na tamaduni tofauti mbali na kuelekeza msaada wa kifedha na kielimu kwa shule katika maeneo kame na yenye idadi kubwa ya watoto waliotengwa kunaweza pia kufanya mabadiliko. Kupanua haki na nafasi za elimu kwa kutekeleza sheria dhidi ya ubaguzi, kutoa ulinzi wa kijamii na kutoa upya fedha za umma. Kila moja kati ya masuala haya linahitaji kushirikishwa katika mfumo wote wa elimu uliounganishwa na mikakati pana ya kupunguza umaskini na kudumisha umoja wa jamii. 5. Kuzidisha utoaji rasilimali ili kudhibiti matumizi ya pesa za umma Nchi zinazostawi na zenye mapato ya chini zina uwezo wa kuongeza matumizi yao katika elimu ya msingi kwa 0.7% ya jumla ya pato la nyumbani ama Dola bilioni saba za Marekani. Aidha, shinikizo zinazoibuka katika bajeti kutokana na ukuaji mdogo wa uchumi wa dunia zimefanya kuwepo ongezeko la bima katika usawa. Serikali zinahitaji kuweka taratibu za ufadhili ambazo zinayapa umuhimu mahitaji, kuhakikisha kwamba maeneo na makundi maskini zaidi ya kijamii yanalengwa katika ufadhili. 6. Kutimiza ahadi za ufadhili pamoja na kuitisha kongamano la Elimu kwa Wote Hatua zinazoendelezwa katika kufikia malengo ya Elimu kwa Wote zinahitaji wafadhili kutimiza ahadi zao za ufadhili wa elimu ya msingi ambazo walitoa mwaka wa 2005 na kuzidisha wajibu wao katika elimu. Changamoto ni kuu zaidi ya ilivyodhaniwa awali, licha ya kuongezeka kwa ahadi za serikali. Kwa kuzingatia mahitaji zaidi ya kifedha ili kuwafikia waliotengwa, pengo lililopo duniani ni takriban Dola bilioni 16 za Marekani, huku barani Afrika Kusini mwa jangwa la Sahara likichangia thuluthi mbili za pengo hilo. Katika nchi 46 zenye mapato ya chini ambazo zimeangaziwa katika utafiti huu, viwango vya msaada wa elimu ya msingi vitahitaji kuongezwa kutoka Dola bilioni 2.7 hadi Dola bilioni 16 kila mwaka. Mfumko wa uchumi wa dunia umezidisha haja ya kuchukuliwa hatua za dharura na jamii ya kimataifa katika kutoa msaada. Katika nchi nyingi maskini, ukuaji mdogo wa uchumi, umepelekea shinikizo kubwa za kiuchumi. Kuna hatari kwamba shinikizo hizi zitasababisha viwango vya chini vya bajeti katika elimu au hata kupunguzwa kwa bajeti. Huku mwaka wa 2015 unaolengwa katika ufanisi wa Elimu kwa Wote ukikaribia, ni muhimu kwa wafadhili kuchukua hatua za dharura kuziba pengo la kifedha. Kongamano la kuangazia ahadi katika mpango wa Elimu kwa Wote linafaa kuitishwa katika mwaka wa 2010 kama mojawapo ya mikakati ya kimataifa katika kufikia malengo ya ustawi wa milenia. Nchi zinazostawi na zenye mapato ya chini zina uwezo wa kuongeza pesa za matumizi katika elimu ya msingi kwa 0.7% ya jumla ya pato la nyumbani ama Dola bilioni saba za Marekani

41 4 0 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E Juhudi za mashirika yasiyo ya kiserikali ambazo zimefaulu kuwafikia waliotengwa zinafaa kujumuishwa katika mifumo ya elimu 7. Kuthibiti misaada, kuangazia zaidi nchi zilizokabiliwa na mizozo Wafadhili wanahitaji kuthibiti juhudi za kutekeleza mkataba wa Paris kuhusu manufaa ya msaada. Ingawa pamekuwepo mafanikio, msaada mara nyingi hufungamana na gharama ya juu ya kibiashara inayotokana na ushirikishi duni, kukosa kutumia mifumo ya kitaifa na kupendelea kufanya kazi kwa miradi. Kuongezwa kwa msaada kunastahili kwenda sawa na mabadiliko katika malengo ili kuleta usaidizi wa maana katika elimu ya msingi katika nchi zenye mapato ya chini. Licha ya kupigwa hatua tangu kutolewa ahadi za Dakar, mataifa fadhili yanafaa kuchunguza upya makadirio ya msaada yanaotoa kwa viwango mbalimbali vya elimu. Inawalazimu pia kuongeza kiwango cha msaada kwa nchi zinazokumbwa na mizozo 8. Kuthibiti ufundi wa kimataifa wa msaada kwa elimu Msaada wa kimataifa wa elimu unahitaji mfumo thabiti wa mpango wa kimataifa, ambao utazidisha hamasisho la rasilimali za kifedha na kuweka elimu katika ajenda ya ustawi wa kimataifa. Katika mpangilio wa sasa, mkakati wa dharura kwa Elimu kwa Wote, unahitaji marekebisho muhimu. Mfumo huo, aidha unafaa kuundwa upya kama shirika huru lisilohusika na benki ya dunia huku nchi UNESCO/Ernesto Benavides Elimu kwa Wote: Shule inayofunza lugha na tamaduni tofauti kwa watoto wakiasili, Peru zinazostawi zikipewa jukumu la kujisimamia katika viwango vyote. Marekebisho ya FTI yanafaa kuzingatia mafunzo kutoka kwa mashirika yanayofadhili afya duniani na mengine. Mifumo hii imewezesha uhamasisho wa ufadhili mpya na wa ziada, imestawisha misingi pana ya ufadhili, imezihusisha sekta za kibinafsi, imetoa fursa kwa mifumo mipya ya ufadhili na kuchochea uungwaji mkono kisiasa. Lengo la Elimu kwa Wote linafaa kuwekwa katika kiwango sawa mbali na wafadhili kuhamasisha utoaji wa Dola bilioni 1.2 ambazo zinahitajika kufanikisha mahitaji hayo kupitia hazina fasilishi. Ufanisi katika elimu kati ya mataifa utahitaji mabadiliko makuu ya kitaasisi. Aidha, kundi ambalo linashughulikia Elimu kwa Wote katika kiwango cha juu linafaa kulenga ustawi wa utaratibu wenye kuangazia matokeo pamoja na kuwa na ajenda angavu na ufuatilizi madhubuti. 9. Kuweka pamoja mapendekezo ya mashirika yasiyo ya serikali katika mifumo ya elimu Mashirika yasiyo ya kiserikali yamekuwa katika mstari wa mbele katika juhudi za kutoa fursa za elimu kwa makundi yaliyotengwa. Mengi ya mashirika hayo yanatoa elimu katika vitongoji duni na maeneo ya mashambani. Pia, yanafanya kazi moja kwa moja na watoto walioajiriwa, wale kutoka jamii ya wafugaji na walemavu ili kuwapa fursa ya pili ya kufanikisha ndoto zao katika elimu. Juhudi za mashirika haya ambazo zimezaa matunda miongoni mwa waliotengwa zinafaa kujumuishwa katika mifumo ya elimu. 10. Kupanua haki za waliotengwa kupitia hamasisho za kisiasa na kijamii Kukabili utengwaji kunahusu kubadilisha sera na mahusiano ya kisiasa. Sheria madhubuti zinaweza kusaidia katika kupanua haki za makundi yenye mahitaji ili kuyawezesha kupata huduma na raslimali. Sheria aidha zinaweza kuweka vikwazo dhidi ya ubaguzi na usawa katika utoaji wa nafasi. Hata hivyo, sheria zina makali zaidi zinapoambatana na hamasisho za kisiasa na kijamii. Kutoka kwa vuguvugu la kutetea haki za binadamu nchini Marekani hadi lile la watu wa kawaida huko Latin America, mashirika ya kijamii yametekeleza wajibu mkubwa katika kuunda miungano na kushinikiza kutekelezwa kwa matakwa ya wakulima, hali ambayo imepelekea mabadiliko makuu. Katika kiwango cha kimataifa, mashirika ya kutetea haki za binadamu huhakikisha kwamba vilio vya waliotengwa vinasikika katika warsha baina ya mashirika ya serikali. Mashirika hayo yanaweza pia kuchunguza uwajibikaji wa serikali na wafadhili kwa muafaka wa Dakar kwa lengo la kufanikisha Elimu kwa Wote. Shirika la Kampeni za ulimwengu kwa elimu, muungano wa mashirika yasiyo ya kiserikali, miungano ya walimu na mashirika mengine ya kijamii, huchukua jukumu kubwa zaidi katika swala hili.

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya

More information

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya

More information

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari

More information

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa

More information

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA

More information

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza

More information

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi

More information

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni

More information

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini

More information

Human Rights Are Universal And Yet...

Human Rights Are Universal And Yet... Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,

More information

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12 Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:

More information

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam

More information

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi 3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi

More information

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa

More information

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.

More information

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha

More information

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted

More information

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na. JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi

More information

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,

More information

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano. HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,

More information

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to

More information

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika

More information

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI

More information

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA

More information

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania

More information

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh

More information

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Desemba 2014 1 Shukurani Ripoti hii iliandikwa na Dk. Mkumbo. Ushauri wa kitaalamu ulitolewa na Elizabeth Missokia na Godfrey

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited

More information

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0

More information

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu

More information

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini

More information

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery

More information

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)] This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)

More information

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu BLOOD PRESSURE UK Shinikizo la damu ndicho chanzo kikubwa cha ulemavu na vifo vya mapema kule Uingereza, kupitia kiharusi, mshtuko wa moyo na maradhi ya moyo.

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper

More information

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017

More information

Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili

Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili 1. 2-Muhtasari wa Ukurasa wa Ripoti ya Miaka minne ya Bodi Kuu ya Kanisa & Jamii............................... 2 2. Kamati ya Kawaida ya Malipo ya

More information

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump

More information

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA

More information

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA

More information

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA

More information

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

More information

Kutetea Haki za Binadamu

Kutetea Haki za Binadamu Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI

More information

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya

More information

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI

More information

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012

More information

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna

More information

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau

More information

HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE

HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE SAUTIZETU HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE 01 SAUTIZETU HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE SAUTI ZETU Huduma za Afya kwa wote THE OPEN SOCIETY INITIATIVE FOR EASTERN AFRICA (OSIEA) (JAMII WAZI YA MPANGO WA AFRIKA MASHARIKI)

More information

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini

More information

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2

More information

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

More information

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na

More information

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria; HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri

More information

International Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi

International Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi International Labour Office Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi 1 Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2007 Kimechapwa mara ya kwanza 2007 Machapisho ya Ofisi ya Shirika la

More information

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

SautiElimu. Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian

More information

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo: HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban

More information

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.

More information

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized!. viromen-alsc:a.. Environmental & Social MRADI WA UMEME WA GESI YA * Assessment & Management

More information

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya

More information

UFUPISHO WA 35. Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji mazao: Clive James Chair, ISAAA Board of Directors

UFUPISHO WA 35. Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji mazao: Clive James Chair, ISAAA Board of Directors I S A A A Huduma ya kinimataifa ya upataji na utumizi wa kiteknolojia ya kuboresha kilimo MUHTASARI WA KIUTEKELEZAJI UFUPISHO WA 35 Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji

More information

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017 TAARIFA Agosti 2017 NGUO MPYA ZA UKOLONI Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika Jumuiya ya Jamii ya 2007: Wajumbe wanaadhamana Nairobi dhidi ya EPAs. SwissInfo Tangu mwaka

More information

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana

More information

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa

More information

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi PAN AFRICAN PARLIAMENT PARLEMENT PANAFRICAIN البرلمان PAN- PARLAMENTO األفريقي AFRICANO Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi Julai 21 22, 2011 Bunge la

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/14 DODOMA Mei,

More information

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI SIKOMBE YIZUKANJI YORADI TASNIFU YA KISWAHILI KWA MINAJILI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (MA. KISWAHILI) KITIVO CHA SANAA

More information

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for

More information

Upatikanaji wa Silaha Ndogo ndogo na Hisia za Usalama nchini Kenya: Ukadiriaji

Upatikanaji wa Silaha Ndogo ndogo na Hisia za Usalama nchini Kenya: Ukadiriaji Ripoti Maalum Upatikanaji wa Silaha Ndogo ndogo na Hisia za Usalama nchini Kenya: Ukadiriaji Manasseh Wepundi, Eliud Nthiga, Eliud Kabuu, Ryan Murray, na Anna Alvazzi del Frate Ripoti Maalum Juni 2012

More information

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo

More information

ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO

ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO Mradi wa Kuondoa Madini ya Risasi Katika Rangi Barani Afrika 2015 ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO 2015 SHUKRANI Tunachukua

More information

Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo

Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu Nyenzo ya Mafunzo Vi Agroforestry Vi Agroforestry ni shirika la ushirikiano la maendeleo la Sweden, linalopambana dhidi ya umasikini na

More information

Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo

Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo Taarifa ya Warsha Kuhusu Elimu-Jumuishi Iliyofanyika Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Kujifunza hakuna mwisho. Kazi ya vikundi imenipa fursa ya kujieleza bila kuhofia kuwa ningekosea.

More information

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition

More information

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided

More information

KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA

KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA Toleo la kwanza 2012 Mwandishi: USAID DELIVER PROJECT Wachangiaji: Gary Steele, John Snow, Inc. and Judith

More information

Mipango ya miradi katika udugu

Mipango ya miradi katika udugu Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi

More information

muhtasari 37 brief 37 Kiwango cha kiutandawazi cha mazao ya kibiashara ya kibayoteki/ugeuzi jeni: 2007 Clive James Bordi ya wakurugenzi wa ISAAA

muhtasari 37 brief 37 Kiwango cha kiutandawazi cha mazao ya kibiashara ya kibayoteki/ugeuzi jeni: 2007 Clive James Bordi ya wakurugenzi wa ISAAA i s a a a Huduma ya Kimataifa ya Upataji na Utumizi wa Tekinolojia ya Kuboresha Kilimo muhtasari 37 brief 37 Kiwango cha kiutandawazi cha mazao ya kibiashara ya kibayoteki/ugeuzi jeni: 2007 Na Clive James

More information

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue?

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue? Tufundishane! Let s teach each other! This newsletter is published by The Foundation for Tomorrow and is meant to be a venue for teachers and schools to share and learn from each other s best practices.

More information

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA TWN Third World Network 1. WEMA ni nini? Mahindi yanayotumia maji kwa ufanisi yajulikanayo kwa kingereza kama Water Efficient Maize for Africa (WEMA) ni mpango

More information

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY

More information

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika

More information

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA BARA 2004 Imetayarishwa na: Idara ya Tiba Afya Makao Makuu P.O. Box 9083, DAR ES SALAAM June 2005 Yaliyomo Ukurasa Vifupisho

More information

Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira

Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Moduli ya kwanza Uhamasishaji Jamii juu ya Afya ya Mazingira Kimechapishwa kutokana na Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Jeff Conant na Pam Fadem i COBIHESA

More information

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa

More information

Ripoti hii ni kwa heshima ya wale wanaharakati wengi wa Tanzania ambao ndio binafsi wanaopitia hali iliyoangaziwa, na vilevile wale walioyapoteza

Ripoti hii ni kwa heshima ya wale wanaharakati wengi wa Tanzania ambao ndio binafsi wanaopitia hali iliyoangaziwa, na vilevile wale walioyapoteza Utafiti wa mazingira ya haki za jamii za Wafanyakazi wa Ngono na LGBTI nchini Tanzania 2015 2016 Ripoti hii ni kwa heshima ya wale wanaharakati wengi wa Tanzania ambao ndio binafsi wanaopitia hali iliyoangaziwa,

More information

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI This booklet on Becoming a Parent was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at. MACHAGUO

More information