KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.
|
|
- Gregory Sutton
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1
2
3 KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana na thamani ya mfumo wa haki za binadamu. Malengo ya AFRODAD ni pamoja na yafuatayo: 1. Kuongeza ufanisi na usimamizi wenye tija na matumizi ya rasilimali ya serikali za Afrika; 2. Kupata/kuleta mabadiliko katika dhana ya kimataifa ya kijamii na kiuchumi na mpangilio wa kidunia wa kisiasa kwenye mchakato wa maendeleo unaotambulisha mahitaji na matakwa ya watu wengi duniani; 3. Kuwezesha mazungumzo kati ya vyama vya kiraia na serikali kwenye masuala yanayohusiana na Madeni na maendeleo Afrika au sehemu nyingine.
4 MKATABA WA KUKOPA Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika Toleo Lililorekebishwa Hatimiliki 2013 AFRODAD Haki zote zimehifadhiwa ISBN EAN
5 YALIYOMO DIBAJI 6 1. UZINGATIAJI WA BUSARA NA DESTURI ZA UKOPAJI NA USIMIMIAJI WA MADENI YA UMMA 8 2. UWEPO WA SHERIA NA KANUNI ZINAZOTABIRIKA MIUNDO NA WAJIBU ZINAZORATIBIKA NA MADHUBUTI UWEPO WA OFISI HURU YA USIMAMIZI WA MADENI USHIRIKI WA UMMA, UJUMUISHWAJI NA KUWEKA TAARIFA HADHARANI KUHESHIMU UBINADAMU NA HAKI ZA WATU ZA KIIKOLOJIA KUHESHIMIANA NA USAWA KATIKA UBIA NA WAKOPESHAJI NA WAFADHILI WA KIMATAIFA 25 MAREJEO NA USOMAJI WA ZIADA 27
6 MKATABA WA KUKOPA DIBAJI Nchi za Kusini mwa jangwa la Sahara zinakabiliwa na changamoto kubwa katika michakato ya kuingia mikataba ya madeni na usimamizi wa madeni ya umma. Changamoto hizo zinatokana na vyanzo vya fedha za maendeleo, michakato ya kuidhinisha mikopo, hali na masharti ya mikopo, uchumi mkuu na sera za udhibiti, uwezo wa kitaasisi kwa ujumla, na uwezo wa nchi kukopesheka. Majeraha ya Migogoro ya madeni ya miaka ya 1970, 1980 na 1990 yanatokana na udhaifu wa michakato ya uingiaji wa mikataba ya mikopo na usimamizi wa madeni ya umma. Migogoro hii ya madeni ilichangia kwa kiasi kikubwa matatizo ya kiuchumi na kijamii katika nchi za Kusini mwa jangwa la Sahara kwa kuathiri uimara wa uchumi na uwezo wa kukopesheka kimataifa. Madeni ya muda mrefu yalidumaza uwekezaji, ukuaji wa uchumi na biashara. Kulipia madeni kuliyasonga matumizi ya serikali katika elimu, afya na mahitaji mengine ya kijamii katika nchi nyingi zilizokuwa zinadaiwa. 6
7 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika Mkataba huu wa Kukopa una Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha. Unataka kutoa mwongozo na kujulisha ukopaji huru kwa lengo la kuchangia uboreshaji wa utawala dhaifu wa sasa, michakato ya kitaasisi na kisheria ya mikataba ya mikopo na usimamizi wa deni la umma. Kwahiyo, AFRODAD inazihimiza nchi zote zinazokopa hasa zile zilizopo Kusini mwa jangwa la Sahara kufuata kanuni na miongozo, ili kuhakikisha ufanisi na utumiaji wenye tija wa rasilimali madeni na vifaa, kuzuia kujirudia kwa migogoro ya madeni na kuzifanya serikali kuwajibika kwa wananchi wao. Mkataba huu una kanuni na miongozo saba pana zifuatazo: 1. Uzingatiaji wa busara na desturi za ukopaji na usimimiaji wa madeni ya umma 2. Uwepo wa sheria na kanuni zinazotabirika 3. Miundo na wajibu zinazoratibika na madhubuti 4. Uwepo wa ofisi huru ya usimamizi wa madeni 5. Ushiriki wa umma, ujumuishwaji na kuweka taarifa hadharani 6. Kuheshimu ubinadamu na haki za watu za kiikolojia 7. Kuheshimiana na usawa katika ubia na wakopeshaji na wafadhili wa kimataifa 7
8 MKATABA WA KUKOPA 1 UZINGATIAJI WA BUSARA NA DESTURI ZA UKOPAJI NA USIMIMIAJI WA MADENI YA UMMA 1.1 Msaada wa Kisiasa: Serikali za Kitaifa zinahitaji kutumia busara na kuupatia msaada umuhimu wa kisiasa ukopaji na usimamizi wa madeni ya umma ili kuhakikisha uendelevu wa madeni. 1.2 Mazingira Imara ya Kiuchumi: Serikali za Kitaifa lazima: Zihakikishe kuwa mkakati wa madeni ya Umma unaendana na sera kuu ya uchumi kwa kuhakikisha kwamba kiwango cha ukuaji wa thamani ya sasa ya deni jipya linalotolewa ni sawa au ni pungufu ya kiwango cha ukuaji wa mauzo ya nje ya nchi, kwa ajili ya uendelevu wa deni la nje Angalia kama mkopo mpya wa mradi unaendana na sera ya maendeleo ya uchumi kwa ujumla kabla ya kuidhinishwa. 8
9 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika Kuhakikisha kuwa mkopo ni kwa ajili ya sekta zilizo kipaumbele na lazima kuimarisha uwezo wa sekta ya Umma hasa katika usimamizi wa uwekezaji wa umma ili kuongeza thamani ya fedha kwenye miradi inayofadhiliwa na mkopo Kuhakikisha uthabiti wa uchumi mkuu, uendelevu wa fedha, viwango vya chini vya riba, na usimamiaji wa viwango vya athari za ukopeshaji taasisi huru. 1.3 Vifungu vya Katiba: Serikali lazima zianzishe mifumo sahihi na yenye nguvu kisheria na miundo itakayowajibika kuratibu na kusimamia madeni ya Umma. 1.4 Ridhaa ya Umma na Uwazi: Serikali lazima zichukue hatua za Kisheria kuhakikisha kwamba ukopaji wote wa Umma na usimamizi wa madeni unapata idhini ya Bunge na Umma kwa ujumla. 1.5 Kujenga Uwezo: Serikali ni lazima zihakikishe kuwa nchi zao zina uwezo wa kina, endelevu na wa muda mrefu wa kusimamia madeni. Hii ni pamoja na: 9
10 MKATABA WA KUKOPA Kuwa na fungu la zana za usimamizi wa madeni: Kumbukumbu sahihi na rekodi za kisasa za madeni yote na madeni yote ya nje yaliyohakikiwa wazi wazi, ratiba ya majukumu ya malipo ya madeni ikiwa ni pamoja na masuala ya dharura; uwezo wa kukadiria athari za maamuzi ya kukopa ya taasisi nyingi za ndani kwenye wasifu mzima wa deni la nchi; bajeti ya Taifa na uwiano wa malipo Kuhakikisha kwamba wafanyakazi wote wa Umma wanaoshughulika na kuingia mikataba ya mikopo na usimamizi wa deni la Umma wanalenga katika ufanisi wa kazi na majukumu yao: Hakikisha mafunzo zaidi kwa walioshika ofisi zinazohusika kwenye mikataba ya mikopo na usimamizi wa deni la Umma wakaguzi wa hesabu, wahasibu, wachumi na wanasheria Hakikisha kwamba wafanyakazi wenye uzoefu na motisha wanabakia na kupatiwa msaada wa miundombinu muhimu, teknolojia na rasilimali fedha Hamasisha ushirikishaji wa wataalamu wa nje ili kujenga ujuzi wa rasilimali watu waliopo inavyotakiwa au hitajika Hamasisha kaguzi za pamoja na Taasisi nyingine kubwa za Ukaguzi zilizoendelea. 10
11 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika 2 UWEPO WA SHERIA NA KANUNI ZINAZOTABIRIKA 2.1 Mfumo wa Sheria: Mikataba yote ya mikopo ya Umma na sheria na kanuni za usimamizi wa madeni lazima zifungamane na vifungu vya katiba na sehemu nyingine halisi za sheria zinazofafanua jinsi gani mikopo ya Umma ipatikane, itumike na kulipwa Mfumo wa Sheria lazima pia utoe muda maalum ambamo maombi ya mkopo yatafanyika na kuidhinishwa ili kuepuka kupunguza kasi ya michakato ya uidhinishaji ili kuhakikisha utekelezaji kwa wakati na ufuatiliaji wenye ufanisi Mikataba mipya ya mikopo itakuwa ndani ya muktadha wa mkakati mzima wa deni la serikali na kulingana na programu/mipango ya maendeleo ya Taifa. Mipango ya kukopa ya serikali inabidi kuendana na uendelezaji wa muda mrefu wa deni. 2.2 Mamlaka ya Kukopa: Mfumo wa Kisheria lazima uweke wazi ni nani mwenye mamlaka ya kukopa kwa niaba ya serikali. 11
12 MKATABA WA KUKOPA Kuna haja ya kuwa na miongozo iliyowazi ya kisheria/kikatiba kuhusu majukumu na uwajibikaji kati ya wakala wa serikali wanaohusika kwenye usimamizi wa madeni, hasa kwa upande wa Wizara ya Fedha, Benki Kuu na wakala tofauti au yeyote wa usimamizi wa madeni na majukumu ya wafanyakazi yaliyoainishwa vizuri ikiwa ni pamoja na sera bayana za udhibiti na ufuatiliaji na mipangilio ya utoaji taarifa. 2.3Kiwango cha juu cha Kukopa: Inabidi ziwepo sheria, kanuni na sera ambazo zitaainisha mipaka ya ukopaji wa madeni ya Umma ya nje. Hii lazima ilandane na uchambuzi endelevu wa deni la nchi. 2.4 Idhini ya Kukopa: Muhimili wa kutunga sheria wa serikali Bunge litaidhinisha mikopo kabla mikataba haijasainiwa. Hii itawezesha na kuhakikisha kwamba mchakato wa mkataba wa mkopo ilifanyika kulingana na miongozo na sheria zilizowekwa, na inaweza kulipwa katika bajeti ya Taifa. 2.5 Mchakato wa Kuidhinisha: Sera ya Kukopa ambayo inaainisha taratibu za kuidhinisha, muundo wa kamati ya majadiliano na maandalizi ya majadiliano lazima zianzishwe. 12
13 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika 3 MIUNDO NA WAJIBU ZINAZORATIBIKA NA MADHUBUTI 3.1 Muundo wa Taasisi, Uratibu na Mawasiliano: Serikali zitaanzisha Ofisi ya Usimamizi wa Madeni ya Taifa (OUMT) kuhakisha uratibu na mawasiliano mazuri kati ya wadau mbalimbali kwenye kuingia mikataba ya mikopo na taratibu za usimamizi wa madeni. 3.2 Wizara ya Fedha: Wizara husika (mf. Wizara ya Fedha) itawasilisha mahitaji ya serikali kukopa kwa ajili ya idhini bungeni ili kupitishwa kama inavyotakiwa kwa mujibu wa sheria na kanuni za nchi Wizara ya Fedha: Itasimamia fedha za nchi ili kuhakikisha kuwa uwajibikaji kamili unafanyika kwa Bunge na kwamba udhibiti wake wa fedha unaimarishwa Wizara husika: Wizara husika zita: Toa taarifa za mara kwa mara za maendeleo ya programu zote zinazofadhiliwa na mikopo ya nje/ miradi kwa Wizara ya Fedha. 13
14 MKATABA WA KUKOPA Shiriki katika majadiliano na mashauriano yote ya mikataba yote ya mkopo kwa ajili ya miradi na programu chini ya mamlaka yao Tekeleza, fuatilia na tathmini miradi na programu zote kwenye mamlaka yao kwa kushirikiana kwa karibu na wafadhili, Wizara ya Fedha, asasi za kiraia na walengwa. 3.3 Uangalizi wa Bunge: Bunge litasimamia jukumu muhimu la kuhakikisha uwajibkaji katika kuingia mikataba na michakato ya usimamizi wa madeni Bunge madhubuti na linalowajibika hukabiliana na athari za ukopaji uliokithiri kwa kushinikiza mifumo ya uwajibikaji wa serikali na uchunguzi wa kisheria, na kuishinikiza serikali kuboresha utendaji wa kifedha na kibajeti Mwanasheria Mkuu: Mwanasheria Mkuu wa Serikali atatoa ushauri wa kisheria wakati mchakato wa mkataba wa mkopo ili kuhakikisha kwamba unaenda sambamba na sheria za nchi. 3.4 Ukopaji wa Makampuni ya Umma: Serikali lazima ianzishe utaratibu na vigezo kwa ajili ya kutoa dhamana kwa makampuni ya Umma. Hii ni muhimu kwasababu endapo makampuni ya Umma yatashindwa kulipa riba na gharama za madeni, serikali itatakiwa kulipa. 14
15 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika 3.5 Jukumu la Benki Kuu: Benki Kuu itapaswa kufanya kazi kama mshauri wa kifedha wa serikali kwenye masuala ya mikataba ya mikopo na kusimamia madeni Sheria ya nchi inatakiwa ionyeshe wazi madaraka ya Benki Kuu, uhusiano wake na Wizara ya Fedha, uhuru wake, uwajibikaji wake kwa Bunge na Taifa, tahadhari lazima ichukuliwe ili kuepuka udhalimu/matumizi mabaya ya madaraka kama hayo Benki Kuu inatakiwa kudumisha mfumo salama na madhubuti wa malipo na ulipaji Benki Kuu itapaswa kupata maelezo yote ya mali fedha za serikali na taasisis zake kutoka kwenye taasisi za fedha na kuziwasilisha kwenye Ofisi ya Madeni na Wizara ya Fedha Benki Kuu itapaswa kuwezesha ulipaji wa madeni kwa kufuata ushauri wa Ofisi ya Usimamizi wa Madeni. 3.6 Mkaguzi Mkuu wa Hesabu: Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa hesabu itawajibika kukagua taarifa za madeni ya umma zilizowekwa wazi kwenye taarifa za fedha za serikali au nyaraka nyingine ambazo kiasi cha deni la Umma limeonyeshwa na kuhakikisha kuwa kiasi kimeonyeshwa/wakilishwa katika misingi sahihi. 15
16 MKATABA WA KUKOPA Mkaguzi Mkuu wa Hesabu lazima awezeshwe vizuri na aripoti kwa wakati kuhusu akaunti ya umma ya nchi Mkaguzi Mkuu wa Hesabu atafanya uchambuzi huru na kuhakikisha kwamba taarifa zinawekwa bayana kwa umma na bodi muhimu au makundi ili kuwezesha usimamizi wa madeni ulioboreshwa na uelewa wa athari za kujifunga kifedha za sasa na za baadaye. Mkaguzi Mkuu wa Hesabu lazima afanye kaguzi kuhakikisha ufuatiliaji wa vigezo vya biashara za kifedha vilivyowekwa kwenye usimamizi wa madeni. 3.7 Mhasibu Mkuu: Ofisi ya Mhasibu Mkuu itatoa miongozo na taratibu kwa ajili ya usimamizi wa fedha za umma. Ofisi ya Mhasibu Mkuu inapaswa kuweka mfumo wa jumla wa udhibiti na utumiaji wa rasilimali za umma. 3.8 Taasisi za Fedha za Kimataifa/wakopeshaji: Taasisi za fedha za Kimataifa kwa kutumia Miongozo ya Usimamiaji wa Madeni ya Umma ya Kundi la IMF/ Benki ya Dunia lazima ziwezeshe ushauri wa kitaalamu kwa nchi, mara kwa mara kusisitiza haja ya madeni endelevu na kuwezesha utekelezaji wenye ufanisi wa mipango ya uchumi. 16
17 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika Uwezo wa ufadhili wa ndani: Taasisi za Fedha za Kimataifa zisaidie katika kujenga na kuimarisha uwezo wa ndani wa kufanya tafiti ambazo zitaarifu mchakato wa kutengeneza sera. 17
18 MKATABA WA KUKOPA 4 UWEPO WA OFISI HURU YA USIMAMIZI WA MADENI 4.1 Mfumo wa Usimamizi wa Madeni: Kwa madhumuni ya kuwa na mfumo mzuri wa uratibu wa mikataba ya mikopo na usimamizi wa madeni serikali inabidi ianzishe Ofisi ya Usimamizi wa Madeni. Shughuli za Usimamizi wa Madeni lazima ziwekwe chini ya Ofisi moja ya Usimamizi wa Madeni yenye majukumu ya nyuma, kati na ya mbele ya kiofisi. Wakati ofisi ya mbele itashughulika na sera za madeni, sera za kukopa, taratibu na mbinu za kujadiliana, uelewa wa kitaaluma, ofisi ya kati itajikita kwenye kitengo cha uchambuzi/upembuzi na athari, umuhimu wa mkopo uliopendekezwa wakati ofisi ya nyuma itajishughulisha na utunzaji wa takwimu, ukuaji wa mikopo, uthibitishaji wa taarifa za madeni, misaada na masharti. 4.2 Uratibu wa Madeni yote: Ofisi ya Usimamizi wa Madeni inaiwezesha nchi kuunganisha, kupanga na kuimarisha shughuli zote za usimamizi wa madeni kwenye chombo kimoja maalumu kilicho huru. Hii inaruhusu mpangilio mzuri wa udhibiti na inaondoa mwingiliano na kujirudia kunakohusiana na ushirikishwaji wa mawakala wengi, na ambapo usambaaji wa habari ni dhaifu na unaratibiwa vibaya. 18
19 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika 4.3 Mfumo wa Taarifa za Usimamizi wa Madeni: Shughuli na jukumu la Ofisi ya Usimamizi wa Madeni vinapaswa kuwa vimeandikwa vizuri na kuwekwa kwenye nyaraka, ikiwa na kitabu cha muongozo, ikiwa ni pamoja na program muhimu za usimamizi za komputa. 4.4 Uwepo wa huduma za Kitaalamu: Ofisi huru ya Usimamizi wa madeni ya umma (DMOs) itoe faida za kipekee za kiutawala na utumishi na ubadilikaji ambao sio wa kawaida kwa ofisi/vitengo vya usimamizi wa madeni ambavyo vimeingizwa kwenye wizara za fedha na/benki Kuu. 4.5 Aina ya Ofisi ya Usimamizi wa Madeni: Jukumu la Ofisi ya Madeni linategemeana na shughuli zake za usimamizi wa madeni, kama majukumu inayopangiwa na sheria na taratibu, kwenye mkakati inayochagua kuufuata na kwenye njia ilizowekewa kuyafikia malengo yake. Ili kuhakikisha kwamba michakato ya usimamizi wa madeni, kama vile ulipaji wa madeni inafanyika kwa ufanisi zaidi; wajibu na majukumu lazima yawe wazi na taarifa za madeni lazima ziwe zimeimarishwa. 19
20 MKATABA WA KUKOPA 5 USHIRIKI WA UMMA, UJUMUISHWAJI NA KUWEKA TAARIFA HADHARANI 5.1 Umiliki na Uwajibikaji: Umiliki wa Kitaifa ni muhimu kwa mafanikio ya miradi yote ya maendeleo inayofadhiliwa kwa mikopo na ruzuku. Watu, ambao wanapaswa kuwa walengwa wa mwisho wa mikopo iliyochukuliwa kwa jina lao, lazima wawe na haki ya kushiriki katika mchakato wa kufanya maamuzi ya yanayohusu kukopa kwa umma. Hili lifanyike kupitia uwakilishi wa bunge, ushiriki wa raia wa moja kwa moja au ushiriki wa raia kupitia asasi za kiraia au uwakilishaji. Asasi za kiraia, hasa waangalizi na makundi yenye maslahi, yanapaswa kutambuliwa kama njia za kuimarisha umiliki wa fedha za umma na uwajibikaji. 5.2 Uwazi na ushirikishaji wa wananchi kikamilifu: Mchakato wa mkataba wa mkopo lazima uwe wa uwazi na shirikishi, ukiwashirikisha wananchi na jamii zinazoathirika kwa kuwapa taarifa na muda wa kutosha kujadili uchukuaji wa mkopo, ikiwa ni pamoja na kusudi na masharti ya mkopo kwa mujibu wa katiba ya nchi. 20
21 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika 5.3 Kutambuliwa asasi za Kiraia Kisheria na Kitaasisi: Serikali zilizokubaliana na Mkataba huu zianzishe mabaraza na taratibu ambazo wananchi kwa kupitia hayo mabaraza na hizo taratibu wanaweza kujadili na kushawishi mapendekezo ya sera za kiuchumi kuimarisha umiliki wa umma wa mikakati ya uchumi na madeni. Sheria za serikali lazima zionyeshe wazi kwamba hii asasi ya kiraia ita: Kuwa na jukumu la kushauri katika mchakato wa mkataba wa mkopo na usimamizi wa madeni ikifanya kama wataalamu ikifanya kazi kwa karibu na wanaoongoza majadiliano na serikali kwa kushawishi maamuzi ya kisera, kwa kutoa ushauri wa kisheria, kitaalamu au kiufundi Fanya tafiti na uhamasishaji wakati wa kutengeneza mapendekezo ya mradi/programu na kwenye hatua za majadiliano ya makubaliano ya mkopo Fuatilia miradi na mipango ya maendeleo, ikiwa ni pamoja na namna inavyofadhiliwa. Hii inaruhusu asasi za kiraia kufuatilia matokeo ya miradi na programu zinazofadhiliwa na mikopo, pamoja na fedha zilizotolewa kama matokeo ya mipango ya msamaha wa madeni. 21
22 MKATABA WA KUKOPA Hamasisha umma na ongeza ufahamu juu ya masuala ya mikopo, ruzuku na masuala ya fedha za maendeleo. 5.4 Utoaji wa taarifa kwa umma: Sheria ya Serikali ya Fedha za Umma na uwajibikaji ieleze bayana kuwa taarifa za matumizi ya fedha za mikopo ziwekwe wazi kwa umma, hasa makundi ya kiraia, yenye nia ya kufuatilia mikopo na ruzuku za serikali. Mkataba wa mkopo uwekwe wazi kwa umma na usambazwe kwa wadau mbalimbali kwa kutumia njia sahihi za mawasiliano na zinazopatikana chini. Hii inaweza kuwa kupitia kwa wabunge, matangazo kwa njia ya tovuti, vyombo vya habari vya taifa, radio na/au televisheni. 5.5 Lugha: Mkataba upatikane kwa lugha kuu za Taifa (ikiwa ni pamoja na lugha za jumuiya zilizoathirika). Matoleo yote mawili toleo kuu na lililotafsiriwa yawe na uhalali sawa mahakamani. 22
23 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika 6 KUHESHIMU BINADAMU NA HAKI ZA WATU ZA KIIKOLOJIA 6.1 Haki ya Umma ya Maendeleo endelevu: Sambamba na mkataba wa Afrika Haki za Binadamu serikali zihakikishe kuwa wananchi wanayo haki ya kupata kikamilifu haki yao ya maendeleo endelevu kutoka kwenye rasilimali madeni. Haki ya maendeleo na uchumi zisitengwe na haki za kijamii, kisiasa na kitamaduni. 6.2 Kukabili madhara ya Kukopa: Serikali ihakikishe kwamba madhara ya kukopa na athari zozote za utekelezaji wa miradi ya maendeleo vinapunguzwa mpaka kiwango cha chini kwa watu wa kawaida hasa makundi maalumu kama vile wanawake na watoto. Miradi inayofadhiliwa kwa madeni lazima isikiuke haki za binadamu na wala isichangie ukiukwaji wa haki za binadamu. Haki hizi zimebainishwa kwenye Mikataba na makubaliano yanayotambulika kimataifa ya Haki za Binadamu ambayo wakopaji au wakopeshaji wamesaini. 23
24 MKATABA WA KUKOPA 6.3 Uhamishaji: Miradi mikubwa ya maendeleo kwa hali yoyote ile lazima iepuke kuwa chanzo cha uhamishaji wa wazawa, masikini wa vijijini na wale wa kwenye makazi duni mijini kwenye ardhi yao, chanzo cha kipato na jamii. Iwapo miradi ya maendeleo kwa sababu yoyote itasababisha uhamishaji wa watu kutoka kwenye makazi yao fidia stahili itatolewa kwa jamii zilizoathiriwa. 6.4 Uharibifu wa Mazingira: Ukopaji wowote wa Umma ni lazima usikubali miradi inayokiuka viwango vya chini vinavyokubalika kimataifa vya utunzaji/ulinzi wa jamii, kazi na mazingira. 24
25 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika 7 KUHESHIMIANA NA USAWA KATIKA UBIA NA WAKOPESHAJI NA WAFADHILI WA KIMATAIFA 7.1 Kuheshimiana: Serikali zitahakikisha kuwa uingiaji wa mikataba ya mikopo na masuala ya usimamizi wa madeni na wakopeshaji yanafanyika kwa kuheshimiana na utu. Kanuni za msingi za Ufanisi wa Msaada kwenye Azimio la Paris ya mwaka 2005, Ajenda ya Accra ya mwaka 2008 na Ushirikiano wa Busan kwa Ushirikiano Madhubuti wa Maendeleo ya mwaka 2011 lazima zitumike kuhakikisha usawa katika ushirikiano kati ya wafadhili na mataifa yanayokopa. 7.2 Kukataa Masharti: Nchi wanachama wa Mkataba huu lazima wakatae utumiaji wa masharti wa wafadhili na taasisi za fedha za kimataifa wanapokopa fedha. Hii huwasababishia kuwajibika kwa wakopeshaji na sio kwa wananchi wao. 25
26 MKATABA WA KUKOPA 7.3 Kuheshimu na Kuwezesha Taasisi za ndani: Wafadhili na Wakopeshaji wote wanapaswa kuvipatia vyombo vya uangalizi vya serikali na mabunge msaada wa kifedha na kitaalamu kuviwezesha kushiriki kikamilifu katika kujadili na kufuatilia mikopo ya nje. 7.4 Usuluhishi wa Haki na Uwazi: Mkataba wa mkopo lazima uwe na kifungu kwa ajili ya utaratibu wa usuluhishi huru na wazi iwapo kutakuwa na ugumu katika ulipaji au mgogoro (kwa ombi la mkopaji au mkopeshaji). Kutakuwa na usubirishaji wa ulipaji wa deni wakati majadiliano yakiendelea. Mkopaji asifunguliwe kesi mahakamani wakati majadiliano yanaendelea. Wakopaji na Wakopeshaji lazima wakubaliane na uamuzi wa msuluhishi huru na kuna haki ya kukata rufaa. 26
27 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika Marejeo na Usomaji na Ziada 1. AFRODAD (2007) The Loan Contraction Process in Africa: Making Loans Work for the Poor: The Case of DRC, Study Report 2. AFRODAD (2007) The Loan Contraction Process in Africa: Making Loans Work for the Poor: The Case of Malawi, Study Report 3. AFRODAD (2007) The Loan Contraction Process in Africa: Making Loans Work for the Poor: The Case of Tanzania, Study Report 4. AFRODAD (2007) The Loan Contraction Process in Africa: Making Loans Work for the Poor: The Case of Mozambique, Study Report 5. Borresen P and Pascal E.C (2001); Role and organization of a debt office, Proceedings of the second inter-regional debt management conference, United Nations Conference on Trade and Development, pp Chadambuka. Z.T. (2009) A Critical Review of the Legal Framework of the Public Loan Contraction and Debt Management System in Zimbabwe. ZIMCODD, Harare. 7. Mutasa, C. (2007) Operationalizing debt sustainability in UNCTAD (2007) Proceedings of the Fifth Inter-regional Debt Management Conference, UN, Geneva. 27
28 MKATABA WA KUKOPA 8. De Renzio, P and Krafchik, W. (2007) Lessons from the field: The impact of Civil Society Budget Analysis and Advocacy in Six Countries, A Practitioners Guide, International Budget Project, Washington D.C. International Budget Project. 9. Fyson, S (2009) Sending in the Consultants: development agencies, the private sector and the reform of public finance in low-income countries, International Journal of Public Policy, Vol.4 n. ½. 10. Krafchik, W (2003) What role can Civil Society and Parliament Play in Strengthening the External Auditing Function? International Budget Project, Washington D.C. International Budget Project. 11. Maruping. A.M. (2003) Public Debt Sustainability and the development of domestic markets in UNCTAD (2003) Proceedings of the Fifth Inter-regional Debt Management Conference and WADMO conference, UN, Geneva. 12. MEFMI (2004) Towards an Effective national debt management strategy in Tanzania, Workshop on Debt Management, Dar es Salaam, United Republic of Tanzania. 13. MEFMI (2005) MEFMI, Public Debt Management Procedures Manual vol 1. Sable Press (PVT) Ltd, Harare. 14. Meja, V. (2008) The Public Loan Contraction Process-A key to Debt Management and Economic Governance, AFRODAD. Harare. 15. Overseas Development Institute (2007) Reforming public financial management when the politics aren t right: A proposal, Opinion Paper 89, London. 28
29 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika 16. UNCTAD (2007) Proceedings of the Fifth Inter-regional Debt Management Conference, UN, Geneva. 17. UNCTAD (2003) Proceedings of the Fifth Inter-regional Debt Management Conference and WADMO conference, UN, Geneva. 18. United Republic of Tanzania (2004) Governments Loans, Guarantees and Grants Act, 1974 and Amendments UNITAR (2002) Institutional Framework for Public Sector Borrowing, UNITAR Training Programmes in the Legal Aspects and Financial Management, Document No.17. Geneva. 29
30 MKATABA WA KUKOPA KWA TAARIFA ZAIDI WASILIANA NA African Forum and Network on Debt and Development (AFRODAD) 31 Atkinson Drive, Hillside S.L.P. CY1517, Causeway Harare, Zimbabwe Simu: /6 Nukushi: Tovuti: Barua pepe: afrodad@afrodad.co.zw 30
31 Kanuni na Miongozo ya Ukopaji huru wa fedha kwa nchi za Afrika 31
32 African Forum and Network on Debt and Development 31 Atkinson Drive, Hillside S.L.P. CY1517, Causeway Harare, Zimbabwe Simu: /6 Nukushi: Tovuti:
Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationMKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More informationMWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18
MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2
More informationAzimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]
This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationKuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia
Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa
More informationSonga kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa
Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided
More informationMpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari
More informationMwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationJAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
More informationMAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI
MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha
More informationUFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI
JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MFUMO WA RUZUKU YA MAENDELEO YA MTAJI WA SERIKALI ZA MITAA (LDCDG) UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI Kijitabu cha Mshiriki
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationMradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda
WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya
More informationRipoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya
More informationDibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi
Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini
More informationTAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA
TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0
More informationKutetea Haki za Binadamu
Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and
More informationJifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti
Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu
More informationNGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA
NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.
More informationInformation for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA
More informationRIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationMALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU
MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationRIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI
International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa
More informationTANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI
MFUMO WA TATHMINI WA TAARIFA (IRM): TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI 2014 2016 Ngunga Greyson Tepani Mtafiti wa IRM Taarifa ya Mwishoni mwa Utekelezaji 2014-2016 First End-of-Term Report INDEPENDENT
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationTANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko
TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,
More informationProgramu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi
Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini
More informationIn the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment
In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for
More informationHAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII
HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY
More informationORDER NO BACKGROUND
In the matter of an Application by the DAR ES SALAAM URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (DAWASA) For a Tariff Adjustment, Submitted on January 8 th, 2008 (TR-W-08-001) ORDER NO. 08-001 1.0 BACKGROUND
More informationKufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi
PAN AFRICAN PARLIAMENT PARLEMENT PANAFRICAIN البرلمان PAN- PARLAMENTO األفريقي AFRICANO Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi Julai 21 22, 2011 Bunge la
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationMwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI
David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition
More informationKIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized!. viromen-alsc:a.. Environmental & Social MRADI WA UMEME WA GESI YA * Assessment & Management
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA
More informationMAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA
MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA
More informationUNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI
UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump
More informationGovt increases vetting threshold of contracts
> ISSN: 1821-6021 Vol IX - No. 19 May 10, Free with Daily News every Tuesday DID YOU KNOW? NEWS IN Numbers?
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationMwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania Msingi wa Programu zote za Uimarishaji Ubora Toleo la 1 kwa Lugha ya Kiswahili
More informationTAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014
TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...
More informationAfya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia
Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Shukrani Ripoti
More informationSera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji
Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationUSIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI
USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03
More informationDeputy Minister for Finance
ISSN: 1821-6021 Vol XI - No - 34 DID YOU KNOW? A procuring entity is?s required to use suppliers pliers?pliers?pliers?pliers among those awarded ed?ed?ed?ed framework agreements by GPSA for procurement?ents
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationMWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI
MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality
More informationKAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA
KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationHuduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig
KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1
More informationIn the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment
In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationAfya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia
Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Shukrani Ripoti
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationAZAKI PIGA KURA UCHAGUZI MKUU TANZANIA OKTOBA. #TanzaniaTuitakayo OKTOBA 2015 ILANI YA UCHAGUZI YA AZAKI TANZANIA.
ILANI YA UCHAGUZI YA AZAKI TANZANIA AZAKI. #TanzaniaTuitakay PIGA KURA UCHAGUZI MKUU TANZANIA OKTOBA 2015 Tvuti: http://www.thrd.r.tz/ Barua pepe: thrddefenders@gmail.cm Sanduku la Psta: 105926 Mahali:
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3
More informationATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR
ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More information3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,
HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, MHESHIMIWA JOHN POMBE MAGUFULI, (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2007/08 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationMipango ya miradi katika udugu
Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi
More informationWIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
More informationHISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU 9 DESEMBA 2011.
Saint Augustine University of Tanzania From the SelectedWorks of Daudi Mwita Nyamaka Mr. Winter December 9, 2011 HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More informationWaandishi: wa Toleo la 5. Scholastica Jullu Athanasia A. Soka Safina Hassan Mary Njau. Toleo la 5: 2008 ISBN
KIONGOZI CHA SHERIA Hakimiliki 2008 Kimetolewa na: Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) Waandishi: wa Toleo la 5 Scholastica Jullu Athanasia A. Soka Safina Hassan Mary Njau Toleo la 5: 2008 ISBN
More informationUKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)
Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni
More informationUnyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa
Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda
More informationKimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:
Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200
More informationTaarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania
Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3
More informationUzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania
Uzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wapilipili Tanzania Wildlife Division, Tanzania Wildlife
More informationKUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA
KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA
More informationRipoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013
W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationKilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira
Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kiongozi hiki kimeandaliwa kikiwa ni sehemu ya mradi wa
More informationKITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO
KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa
More informationNa Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4
;II. -~ ~.! ~ l Na Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4 ~n.~ SURA YA KWANZA SHERIA YA ARDHI 1 UTANGULIZI Sura hii itaiangalia ARDHI na umuhimu wake katika maisha ya binadamu. Ardhi ni rasilimali
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/14 DODOMA Mei,
More informationInternational Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi
International Labour Office Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi 1 Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2007 Kimechapwa mara ya kwanza 2007 Machapisho ya Ofisi ya Shirika la
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO
ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO Mradi wa Kuondoa Madini ya Risasi Katika Rangi Barani Afrika 2015 ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO 2015 SHUKRANI Tunachukua
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA BARA 2004 Imetayarishwa na: Idara ya Tiba Afya Makao Makuu P.O. Box 9083, DAR ES SALAAM June 2005 Yaliyomo Ukurasa Vifupisho
More informationKuwafikia waliotengwa
Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E 2 0 1 0 Ripoti
More informationKIJARIDA JUU YA HAKI ZA RAIA KATIKA MFUMO JINAI
KIJARIDA JUU YA HAKI ZA RAIA KATIKA MFUMO JINAI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY (LSF) 1 KIMEANDALIWA NA Chama Cha Wanasheria Tanzania
More informationThe Government is committed to improve marine transport and has a number
ISSN: 1821-6021 Vol X - No - 52 Tuesday December 26, 2017 Free with Daily News every Tuesday Govt set to meet promises on DID YOU KNOW?? The law requires a procuring procurement of marine vessels entity
More informationSummaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili
Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili 1. 2-Muhtasari wa Ukurasa wa Ripoti ya Miaka minne ya Bodi Kuu ya Kanisa & Jamii............................... 2 2. Kamati ya Kawaida ya Malipo ya
More informationMwongozo wa Mwezeshaji
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Ushauri Nasaha na Upimaji wa VVU kwa Hiari Mwongozo wa Mwezeshaji Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Machi 2010 Kimetafsiriwa kutoka lugha
More information