JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
|
|
- Ada Britney Butler
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012
2 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho Utangulizi Umuhimu wa Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo Katika Taifa Letu Hali ya Sekta Miongozo ya Kuendeleza Sekta Fursa za Kuendeleza Sekta Mafanikio yaliyopatikana Katika Sekta Hitimisho
3 iii. Upatikanaji mitaji Wizara kupitia Mfuko wa Wafanyabiashara Wananchi (NEDF) unaoendeshwa na SIDO imeweza kutoa huduma ya mikopo ya zaidi ya shilingi bilioni 21 kwa kwenye zaidi ya miradi midogo 46,000 na kuwezesha kupatikana kwa ajira zaidi ya 160,000. iv. Fursa za Masoko Wajasiriamali wadogo 228 wanaozalisha bidhaa na huduma mbalimbali wameweza kuunganishwa na makampuni makubwa na ya kati. Aidha, zaidi ya wajasiriamali wadogo 1500 waliwezeshwa kushiriki maonesho ya biashara katika kipindi cha mwaka 2011/ Juhudi hizi zimesaidia jasiriamali ndogo kuzalisha bidhaa bora na kuweza kuhimili ushindani wa soko nchini na hata baadhi za bidhaa kupenya katika masoko ya nje ya Tanzania. v. Elimu kwa ujasiriamali wadogo 14 Wizara kwa kushirikiana na SIDO katika kipindi cha mwaka 2011/ 2012 pekee imeweza kutoa mafunzo ya ujuzi ya usindikaji nafaka na matunda kwa wajasiriamali 1,764, usindikaji wa mafuta ya alizeti, utengenezaji sabuni, mishumaa, chaki, utengenezaji wa mizinga ya kisasa na usindikaji wa asali kwa wajasiriamali 2,054 kupitia kozi 143. Aidha, wajasiriamali 63 walipata mafunzo ya usindikaji wa ngozi na bidhaa zake. Mafunzo hayo yamewawezesha wajasiriamali kufanya kazi kwa kujiamini na kuweza kuzalisha bidhaa bora zenye kukubalika na soko la ndani na nje ya nchi. Hali kadhalika, wajasiriamali 10,964 walipata mafunzo ya huduma za kuendeleza ujasiriamali, wajasiriamali 16,138 walipata huduma za ushauri na ugani. 7.0 Hitimisho Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo ni sehemu kubwa ya Sekta Binafsi hapa nchini. Sekta hii inabeba ahadi ya kulikomboa taifa letu kiuchumi na kijamii na kuliwezesha taifa letu kufikia Dira yake ya Maendeleo ya mwaka Hivyo, Wizara inatoa rai kwa wadau wote wa Sekta hii wakiwemo Washirika wa Maendeleo kushirikiana katika kuiendeleza sekta hii muhimu ili iweze kuwa shindani na yenye kujenga msingi wa maendeleo ya sekta zingine. Orodha ya Vifupisho CAMARTEC Centre for Agricultural Mechanization and Rural Technology CTI Confederation of Tanzania Industries CoET College of Engineering and Technology CHC Consolidated Holding Corporation EPZ Export Processing Zone EPZA Export Processing Zone Authority GDP Gross Domestic Product JICA Japan International Cooperation Agency LAT Leather Association of Tanzania NBS National Bureau of Stastistics NDC National Development Corporation PSRC Parastatal Sector Reform Commission SEZ Special Economic Zone SME Small and Medium Enterprise SIDO Small Industries Development Organization TCCIA Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture TEMDO Tanzania Engineering and Manufacturing Design Organisation TILT Tanzania Institute of Leather Technology TIRDO Tanzania Industrial Research and Development Organisation TFDA Tanzania Food and Drug Association TANTRADE Tanzania Development Authority TAHA Tanzania Horticulture Association TGF Tanzania Gatsby Foundation TRA Tanzania Revenue Authority UNDP United Nations Development Programme UNIDO United Nations Industrial Development Organisation 3
4 1.0 Utangulizi Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo (Small and Medium Enterpises - SMEs) ni mtambuka ambayo inagusa shughuli zote za kiuchumi kutegemeana na ukubwa wa shughuli husika. Baadhi ya shughuli za kiuchumi katika sekta hiyo ni kama uvuvi, uwindaji, dukawala, migahawa, maduka ya dawa, uchimbaji madini, ufugaji nyuki, usindikaji, viwanda, karakana, mawasiliano, utengenezaji vipuri, kliniki, shule, uchezaji ngoma, usafirishaji, ushauri nasaha na utafiti. Ili kuweza kufahamu kama shughuli fulani ya kiuchumi ni ya sekta Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo kuna vigezo vinavyotumika ambavyo nchi huwa zinakubaliana kulingana na mazingira halisi ya kiuchumi na kijamii. Vigezo ambavyo hutumika na nchi nyingi ni pamoja na idadi ya ajira, kiwango cha mtaji kinachowekezwa katika shughuli na mapato yatokanayo na mauzo ya bidhaa. Kwa Tanzania, vigezo vya kuitambulisha sekta hii vilivyokubalika vimeainishwa vyema katika Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo ya Mwaka 2003 ambavyo ni idadi ya ajira pamoja na kiwango cha uwekezaji katika shughuli. Kulingana na Sera hiyo, sekta hii hutambulika kama ifutavyo: 4 Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo Sana (Micro Enterprises) ambazo huajiri watu wasiozidi 4 na kuwa na mtaji wa uwekezaji (mashine) wa chini ya Shilingi milioni 5 za kitanzania. Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo (Small Enterprises) ambazo huajiri kuanzia watu 5 na 49 na kuwa na mtaji uwekezaji (mashine) wa kati ya Shilingi milioni 5 hadi milioni 200 za kitanzania. Viwanda vya Kati na Biashara za Kati (Medium Enterprises) ambazo huajiri kati ya watu 50 na 99 na kuwa na mtaji wa uwekezaji (mashine) wa kati ya Shilingi milioni 200 na milioni 800 za kitanzania. Kwa kutambua umuhimu wa maendeleo ya teknolojia, tafsiri ya sekta inalichukulia suala la ajira kwa tahadhari. Endapo ajira katika shughuli inayoendeshwa itakuwa kwenye vigezo tajwa hapo juu, lakini mtaji ukawa nje ya vigezo hivyo, shughuli husika haihesabiki kama ni ya sekta hii. Kwa mfano, kama kiwanda kimeajiri watu 20 tu na mtaji wake ni Shs. Billioni moja kiwanda hiki kitahesabika ni kikubwa na kama kuna fursa maalum katika sekta kiwanda kama hicho hakitahusika. Baadhi ya zana za kilimo zinazozalishwa katika karakana za SIDO pamoja na CAMARTEC 6.0 Mafanikio Yaliyopatikana Katika Sekta Katika harakati ya kutekeleza Mikakati ya Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo na kuwawezesha wajasiriamali wadogo kutumia fursa zilizopo, sekta imeweza kupata mafanikio kadhaa. i. Ufanisi katika mlolongo wa thamani Programu ya Muunganisho wa Ujasiriamali Vijijini (MUVI) imewezesha uanzishwaji na uimarishaji wa vyama/vikundi 319 vya wazalishaji na wakulima vyenye wanachama 15,482. Aidha, program hii imewezesha kuimarisha mifumo ya usambazaji wa mbegu bora na pembejeo katika mikoa ya mradi. ii. Taarifa za Sekta Ili kuwezesha wadau wa sekta kupanga mipango endelevu ya kuendeleza sekta, na kuongeza kasi ya upatikanaji na usambazaji wa taarifa zinazohusiana na sekta, Wizara imekamilisha utafiti wa sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo nchini (SME Baseline Survey). 13
5 2.0 Umuhimu wa Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo katika Taifa Letu Mjasiriamali mdogo akitumia fursa ya maonesho kuuza bidhaa zake katika moja ya Maonyesho ya wajasiriamali katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam v. Fursa za Mitaji Wizara kupitia SIDO imekuwa ikitoa mitaji kwa wajasiriamali wadogo katika mikoa yote yenye ofisi. Mikopo hii ni pamoja na ile ya Mfuko wa Wafanyabiashara Wananchi (National Entrepreneurship Development Fund (NEDF) na wakati mwingine baadhi ya Washirika wa Maendeleo huitumia SIDO kufikisha mikopo yao kwa walengwa wao. vi. Teknolojia na Ubunifu Wizara inaratibu utafutaji, uzalishwaji kwa wingi na kusambazwa kwa teknolojia na zana za kilimo zinazoleta tija kwa wajasiriamali wadogo ikiwa ni pamoja na kuhamasisha wajasiriamali wadogo kujenga misingi ya ubunifu. Kupitia karakana za SIDO na Kituo cha Zana za Kilimo na Ufundi Vijijini (CAMARTEC) zana nyingi za kurahisisha uzalishaji wa bidhaa na usindikaji wa mazao ya kilimo zimeweza kupatikana. 12 Ni dhahili kuwa Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo ina nafasi ya kipekee katika taifa letu. Hata hivyo, ni vigumu kupata maneno halisi ya kueleza umuhimu wa Sekta hii katika taifa na jumuia ya kitanzania. Ili kuyatendea haki maelezo ya umuhimu huo, inahitaji muda mrefu na kurasa nyingi katika kitabu. Katika makala hii tutaeleza kwa kifupi umuhimu wa sekta katika Tanzania tukigusia zaidi masuala ya uchumi na kijamii. Kwanza kabisa, sekta hii ina mchango mkubwa katika ajira kwa watanzania. Katika kuajiri, sekta hii haibagui makundi yoyote ya kijamii kushiriki katika shuguli za kiuchumi na hivyo hutoa fursa kwa wananchi wa makundi mbalimbali ya kijamii hususan wanawake na vijana ambao wengi wao hawabahatiki kupata fursa za ajira rasmi katika sekta mbalimbali kutokana na sababu nyingi zikiwemo viwango hafifu vya elimu na ujuzi. Vilevile, sekta hii imekuwa ni kimbilio kubwa la kundi la vijana wengi wanaomaliza masomo katika vyuo mbalimbali hapa nchini. Na hivyo kuleta matumaini makubwa ya kuiboresha sekta hii kwa kutumia ujuzi na nyenzo wanazozipata wakiwa masomoni. Hivi sasa sekta inasemekana kuwa mwajiri namba mbili kwa watanzania baada ya kilimo na inaajiri watanzania zaidi ya millioni tano. Pili, ushiriki wa Watanzania wengi katika shughuli za kiuchumi kumeiwezesha sekta kuchangia kwa kiasi kikubwa katika pato la Taifa. Baada ya utafiti wa kina imebainika kuwa, hivi sasa sekta inachangia asilimia 27 katika pato la Taifa. Sekta hii pia imekuwa ni kichocheo cha ukuaji wa uchumi katika maeneo ya vijijijni na imechangia sana katika kukuza vipato vya wananchi wengi. Kwa mantiki hiyo, Sekta ina nafasi muhimu na kubwa katika harakati za kuondoa umaskini na hata kusaidia katika kupunguza wimbi la uhamiaji wa watu toka vijijini kwenda mjini. Tatu, sekta hii ni chimbuko la maendeleo ya ujasiriamali na sekta binafsi ya nchi yetu kwa vile inatoa mwanya mkubwa kwa watanzania kujifunza kuendesha shughuli za biashara na uzalishaji. Hii hasa imewezekana kwa kuzingatia ukweli kuwa uingiaji katika sekta hii unakuwa ni rahisi kwa kuwa wakati mwingine huhitaji mtaji mdogo na teknolojia rahisi. Mwisho, Sekta hii ni kiungo mahiri kwa sekta ya kilimo na maliasili. Kwa hivi sasa kuna wajasiriamali wengi wanaojihusisha na uongezaji thamani wa mazao ya kilimo 5
6 na maliasili. Aidha shughuli hii hufanyika kwa kutumia teknolojia rahisi na yenye gharama nafuu ambazo zinatengenezwa na baadhi ya wajasiriamali wadogo hapa nchini. Hii, imewezesha wajasiriamali kuanzisha viwanda vidogo vya usindikaji mazao ya kilimo na kuwezesha kupunguza upotevu wa mazao baada ya mavuno (Post harvest losses). Hapa chini ni baadhi tu ya bidhaa za wajasiriamali wadogo vilivyotokana na mafunzo hayo. Baadhi ya bidhaa zinapatikana katika maduka makubwa (supermarkets). 3.0 Hali Ya Sekta Kama ilivyotangulia kuelezwa hapo awali, Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo inahusisha shughuli za sekta zote za kiuchumi. Takriban, katika kila shughuli za kiuchumi, sekta hii inachukua nafasi kubwa. Hata hivyo shughuli nyingi za sekta hii ziko katika sekta isiyo rasmi. Kwa ujumla picha ya mgawanyo wa sekta hii unasimama kama inavyoonekana katika mchoro hapa chini: Mgawanyo wa SMEs Tasnia za Kati 6 Tasnia Ndogo Sana Zisizo Rasmi Tasnia Ndogo Tasnia Ndogo Kabisa Rasmi Kutokana na takwimu zilizopo, kuna jumla ya wajasiriamali wadogo milion 2.7 ambao wanamiliki jasiriamali milioni 3.2. Katika mgawanyo wa kijinsia, takwimu zinaonyesha kuwa washiriki wengi wa sekta hii ni wanawake kwa asilimia 54.3 na asilimia 45.7 Baadhi ya bidhaa zilizosindikwa na wajasiriamali wadogo kutokana na malighafi zinazopatikana nchini iv. Fursa za Masoko Wizara kwa kushirikiana na SIDO imekuwa ikiendesha maonesho ya biashara ya Kikanda. Maonesho haya hufanyika kila Kanda ya Tanzania mara moja kwa mwaka na hii huwarahisishia Wajasiriamali wadogo wengi kushiriki katika katika kila maonesho. Mgawanyo wa Kanda hizi ulizingatia ukaribu wa mikoa na hujumuisha Kanda sita ambazo ni: Kaskazini ijumuishayo mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara; Ziwa ijumuishayo mikoa ya Mwanza, Kagera, Mara na Shinyanga; Kati ijumuishayo Mikoa ya Kigoma, Tabora, Singida na Dodoma; Pwani ijumuishayo mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro na Pwani; Kusini ijumuishayo mikoa ya Ruvuma, Lindi na Mtwara; na Nyanda za Juu Kusini ijumuishayo mikoa ya Iringa, Rukwa na Mbeya. Aidha, Wizara inashirikiana na SIDO kuwaunganisha wajasiriamali wadogo na wafanyabiashara wakubwa ili wauze bidhaa zao. 11
7 Baadhi ya Wajasiriamali waliopata fursa za kuhudhuria mafunzo ya uendeshaji biashara na ujasiriamali yaliyotolewa na SIDO mjini Dodoma iii. Uhamasishaji wa uzalishaji na utengenezaji wa bidhaa mpya Katika harakati za kuhamasisha wajasiriamali kutengeneza bidhaa mpya, SIDO imekuwa ikitoa huduma ya mafunzo maalum katika usindikaji wa mazao ya kilimo. Mafunzo haya yamefanikiwa na kuwawezesha wajasiriamali wengi kuingia katika huduma za usindikaji wa vyakula. wakiwa ni wanaume. Hata hivyo shughuli nyingi za sekta hii zimejikita katika kununua na kuuza yaani biashara ambayo inawakilisha asilimia 55 wakati jasiriamali za huduma ni asilimia 30. Wajasirimali wachache hujihusisha na uzalishaji ambazo zinafikia asilimia 13.6 na nyinginezo zinachukua asilimia 1 kama inavyofafanuliwa katika jedwali Namba 1. Kama ilivyokwishaelezwa hapo awali pia, sekta hii imeajiri takribani Watanzania milioni 5.2 wengi wao wakiwa wamiliki wa moja kwa moja wa hizo jasiriamali kama inavyofafanuliwa na jedwali Namba 2. Jedwali Namba1: Mgawanyo wa Jasiriamali Kisekta Idadi ya Waajiriwa Biashara Huduma Uzalishaji Nyinginezo Mwajiriwa 1-4 1,710, , ,426 14,830 Waajiriwa 5 au zaidi 40,012 21,639 23,965 2,534 Jedwali Namba 2: Mgawanyo wa Jasiriamali Kijinsia Idadi ya Waajiriwa Wanaume Wanawake Mwajiriwa 1 833,279 1,259,817 Waajiriwa , ,295 Waajiriwa 5 au zaidi 75,287 12,263 Wananchi wanaojishughulisha na sekta hii wamegawanyika katika makundi ya umri tofauti kama inavyoonekana katika jedwali Namba 3. Jedwali Namba 3: Mgawanyo wa Umri wa Wajasriamali Tanzania Umri Wanawake% Wanaume% Chini ya Miaka Miaka Miaka Miaka Zaidi ya Miaka Sekta hii inaendeshwa na Watanzania wa viwango na kada mbalimbali za elimu. Taarifa zilizopo zinaonyeshwa kuwa wengi wa wajasiriamali hao wana elimu ya msingi na wachache sana wana elimu ya chuo kikuu na ya ufundi. Watafiti wengi wa sekta 10 7
8 hii wanadai kuwa elimu ya waendesha miradi ina mahusiano ya moja kwa moja na ukuaji wa biashara zao pamoja na urasimishaji wa biashara. Kama madai haya ni ya kweli, inawezekana yanachangia ukubwa wa sekta isiyo rasmi na umiliki mkubwa wa sekta hii kuwa chini ya mtu mmoja. Kwa ujumla viwango vya elimu vya waendesha sekta vimeainishwa katika Jedwali Namba 4. Jedwali Namaba 4: Viwango vya elimu wamiliki wa shughuli za sekta Kiwango cha Elimu Wasiosoma kabisa Elimu ya Msingi bila kuhitimu Waliohitimu Elimu ya Msingi Elimu ya Sekondari bila kuhitimu Waliohitimu Elimu ya Sekondari Elimu ya Ufundi Chuo Kikuu 4.0 Miongozo ya kuendeleza Sekta 8 Asilimia Kimsingi, Wizara ya Viwanda na Biashara na tafsiri ya Taifa ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo inahusika na sekta rasmi. Lakini kwa hali halisi, imekuwa ni vigumu kuachana na sekta isiyo rasmi kwa kuwa ni kubwa mno na yenye ufanisi mdogo. Ili kuweza kuboresha utendaji wa sekta isiyo rasmi, Wizara imekuwa na mikakati endelevu ya kuboresha mazingira ya biashara ili kuwezesha sekta isiyo rasmi kuwa rasmi. Shughuli za maendeleo ya sekta hii zinaongozwa na Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo ya Mwaka 2003, ambayo mikakati ya utekelezaji wake imejikita katika kuboresha mifumo ya sheria na taratibu; kuimarisha miundombinu na maeneo ya kufanyia kazi; Kuimarisha ujasiriamali na masoko ya huduma za uendelezaji wa biashara; kuboresha fursa za upatikanaji wa fedha kwa sekta; kuimarisha uwezo wa wadau katika kutekeleza program za sera hiyo; kuimarisha viwanda vijijini; masuala mtambuka hasa mazingira; jinsia ; makundi maalum na kukabiliana na maambukizi na usambazaji wa virusi vya ukimwi. Utekelezaji wa Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo unazingatia mipango mikuu ya kitaifa ikiwemo Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025, Mkakati wa Kupunguza Umaskini (MKUKUTA I &II), Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2010, Mpango wa taifa wa maendeleo wa miaka mitano na Azma ya KILIMO KWANZA hasa nguzo namba 7 inayokazia masuala ya upatikanaji wa zana na pembejeo za kuboresha kilimo na uongezaji thamani wa mazao ya kilimo. 5.0 Fursa za kuendeleza Sekta Kufuatia utekelezaji wa mikakati ya Sera ya Maendeleo ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo, Wizara kwa kushirikiana na wadau wa sekta imewezesha sekta kuwa na fursa za aina nyingi zinazowasaidia wajasiriamali wadogo kuendeleza shughuli zao. Fursa hizi zinajumuisha program na huduma mbalimbali zitolewazo na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo SIDO pamoja na wadau wengine. Baadhi ya program na huduma hizo ni hizi zifuatazo: i. Programu ya Muunganisho wa Ujasiriamali Vijijini (MUVI) Programu hii imejikita katika kuongeza ufanisi wa thamani ya mazao ya kilimo ikitumia njia ya mlolongo wa thamani (value chain). Bidhaa zinazohusika ni mazao ya alizeti, mihogo, mifugo, matunda na nyanya katika Wilaya 19 za mikoa sita ambayo ni: Mkoa wa Iringa: Iringa Vijijini, Kilolo na Njombe; Mkoa wa Manyara: Simanjiro, Hanang na Babati; Mkoa wa Pwani: Bagamoyo, Rufiji na Mkuranga; Mkoa wa Ruvuma: Songea Vijijini, Namtumbo na Mbinga; Mkoa wa Mwanza: Sengerema, Kwimba na Ukerewe ; na Mkoa wa Tanga: Muheza, Korogwe, Kilindi na Handeni. ii. Huduma za Kuendeleza Biashara Wizara kupitia SIDO imekuwa ikitoa huduma za kuendeleza na kuendesha biashara ikiwa ni pamoja na mafunzo, ushauri na huduma za ugani. Aidha, SIDO imekuwa ikiwawezesha wajasiriamali wadogo kupata vifungashio vya bidhaa zao. 9
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationTANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko
TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,
More informationNGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA
NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TAARIFA YA MAFANIKIO CHINI YA UONGOZI WA MHE. SOSPETER MUHONGO (MB) KATIKA SEKTA NDOGO YA UMEME Disemba, 014 A. MAFANIKIO 1. Kuongezeka kwa uzalishaji
More informationMradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda
WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More informationJAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
More informationTaarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania
Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationRipoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationUKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)
Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni
More informationDibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi
Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationMWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18
MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More information3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,
HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, MHESHIMIWA JOHN POMBE MAGUFULI, (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2007/08 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationMKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/14 DODOMA Mei,
More informationMALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU
MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA
HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA MWAKA 2018/2019 YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 HALI
More informationATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR
ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini
More informationIn the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment
In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for
More informationUtumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationUTANGULIZI. 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na
HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA, MHESHIMIWA STEPHEN MASATO WASIRA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA KWA MWAKA 2008/2009 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationProgramu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi
Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationKAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA
KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI
More informationMwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo
More informationNGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017
TAARIFA Agosti 2017 NGUO MPYA ZA UKOLONI Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika Jumuiya ya Jamii ya 2007: Wajumbe wanaadhamana Nairobi dhidi ya EPAs. SwissInfo Tangu mwaka
More informationHAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII
HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationWIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
More informationUhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI
Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI b Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI 1 Mwongozo wa Uzalishaji
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA, ENG. DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB.) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA
HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA, ENG. DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB.) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO MIFUGO NA UVUVI KWA MWAKA 2017/2018 YALIYOMO
More informationNilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania
Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza
More informationMpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More informationInformation for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationMAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA
MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA
More informationMaswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA
Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA TWN Third World Network 1. WEMA ni nini? Mahindi yanayotumia maji kwa ufanisi yajulikanayo kwa kingereza kama Water Efficient Maize for Africa (WEMA) ni mpango
More information5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban
More informationMAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI
MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha
More informationMwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI
David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition
More informationTANGA CEMENT PLC ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA.
TANGA CEMENT PLC 2016 ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA www.simbacement.co.tz ANNUAL REPORT 2016 ANNUAL REPORT2016 TAARIFA YA MWAKA 2016 TAARIFA YA MWAKA 2016 02 ANNUAL REPORT 2016 Chairperson s Statement
More informationIn the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment
In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationSonga kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa
Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA
HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA ANNA MARGARETH ABDALLAH, MBUNGE, KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2004/2005 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba sasa Bunge likubali
More informationDIRA DHIMA. Kuendeleza, kuwezesha, kudhibiti na kusimamia matumizi endelevu ya Rasilimali za Nishati na Madini kwa manufaa ya Watanzania.
DIRA Kuwa Taasisi yenye ufanisi na inayojali tija ili kuhakikisha kuwa Rasilimali za Nishati na Madini zinachangia ipasavyo katika maendeleo ya nchi kijamii na kiuchumi. DHIMA Kuendeleza, kuwezesha, kudhibiti
More informationRipoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013
W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa
More informationBUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE. Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa
More informationHuduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig
KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1
More informationUfanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania
Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Desemba 2014 1 Shukurani Ripoti hii iliandikwa na Dk. Mkumbo. Ushauri wa kitaalamu ulitolewa na Elizabeth Missokia na Godfrey
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA
More information28 JUNI, 2018 MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA. Kikao cha Hamsini na Tisa Tarehe 28 Juni, (Mkutano Ulianza Saa 3.
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tisa Tarehe 28 Juni, 2013 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA
More informationThe Government is committed to improve marine transport and has a number
ISSN: 1821-6021 Vol X - No - 52 Tuesday December 26, 2017 Free with Daily News every Tuesday Govt set to meet promises on DID YOU KNOW?? The law requires a procuring procurement of marine vessels entity
More informationKuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia
Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa
More informationKUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.
KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana
More informationSera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji
Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA BARA 2004 Imetayarishwa na: Idara ya Tiba Afya Makao Makuu P.O. Box 9083, DAR ES SALAAM June 2005 Yaliyomo Ukurasa Vifupisho
More informationBUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA. Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi)
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU
More informationHii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA ISHIRINI KIKAO CHA KUMI NA MBILI TAREHE 22 JUNI, 2005
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA ISHIRINI KIKAO CHA KUMI NA MBILI TAREHE 22 JUNI, 2005 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Spika ( Mhe. Pius
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationUNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI
UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump
More informationBustani 10,000 Katika Afrika. Alberto Prina
Bustani 10,000 Katika Afrika Alberto Prina K i j i t a b u Timu ya wahariri: Abderrahmane Amajou, Typhaine Briand, Roba Bulga Jilo, Davide Dotta, Emanuele Dughera, Michela Lenta, Velia Lucidi, Irene Marocco,
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationAzimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]
This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)
More informationTAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014
TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...
More informationJifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti
Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA
More informationTIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO
TIST HABARI MOTO MOTO Tel. 026-2322246 P.O.BOX 53 MPWAPWA E-Mail tist@twiga.com 01 October 2000 Y2K PREPARATIONS Holes and Seedlings made ready for the year 2000 programme By Gayo Mhila The process of
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationUnyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa
Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda
More informationUFUPISHO WA 35. Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji mazao: Clive James Chair, ISAAA Board of Directors
I S A A A Huduma ya kinimataifa ya upataji na utumizi wa kiteknolojia ya kuboresha kilimo MUHTASARI WA KIUTEKELEZAJI UFUPISHO WA 35 Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji
More informationKiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika
Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to
More informationUSIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI
USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03
More informationMuhtasari wa taarifa ya warsha ya wataalamu juu ya mfumo wa habari kwa njia ya ramani (PGIS), Morogoro, Juni 30 - Julai 1, 2014
Muhtasari wa taarifa ya warsha ya wataalamu juu ya mfumo wa habari kwa njia ya ramani (PGIS), Morogoro, Juni 30 - Julai 1, 2014 Wandishi (Jina la kwanza kiherufi): Edmund Githoro, Simon Fraval, Joanne
More informationSautiElimu. Sauti Yako Isikike
SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian
More information3 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA NANE. Kikao cha Saba - Tarehe 3 Februari, 2015
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Saba - Tarehe 3 Februari, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA
More informationRipoti hii ni kwa heshima ya wale wanaharakati wengi wa Tanzania ambao ndio binafsi wanaopitia hali iliyoangaziwa, na vilevile wale walioyapoteza
Utafiti wa mazingira ya haki za jamii za Wafanyakazi wa Ngono na LGBTI nchini Tanzania 2015 2016 Ripoti hii ni kwa heshima ya wale wanaharakati wengi wa Tanzania ambao ndio binafsi wanaopitia hali iliyoangaziwa,
More informationKilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira
Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kiongozi hiki kimeandaliwa kikiwa ni sehemu ya mradi wa
More informationUFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI
JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MFUMO WA RUZUKU YA MAENDELEO YA MTAJI WA SERIKALI ZA MITAA (LDCDG) UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI Kijitabu cha Mshiriki
More informationMWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK
Kudumisha uhusiano kati ya jamii, ufugaji na wanyamapori MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK Kudumisha uhusiano kati ya jamii, ufugaji na wanyamapori MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI
More information