Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

Size: px
Start display at page:

Download "Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi"

Transcription

1

2

3 Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP ) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini pia changamoto zake kwa wote walioshiriki katika kufanikisha programu hiyo ya UNDAP ya kila mwaka. Timu ya Umoja wa Mataifa Nchini (UNCT), katika muktadha wa Mpango wa maboresho wa Kufanya Kazi Pamoja (DaO), ilionyesha bayana ushirika wake na Serikali ya Tanzania, upande wa Bara na ule wa Zanzibar, na kuthibitisha dhamira yake katika kuhakikisha kuwa utekelezaji wa UNDAP unawanufaisha Watanzania wote. Serikali ya Tanzania, kwa upande wake, iliendelea kushirikiana na UNCT ili kuhakikisha kunakuwa na ufanisi na tija katika utekelezaji wa Mpango kwa kutoa miongozo na michango kama inavyopaswa kufanywa na washirika katika utekelezaji. Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi wa Serikali na Umoja wa Mataifa, ninafurahi kuleta mbele yenu Ripoti ya Mwaka ya nne ya utekelezaji wa UNDAP. Mafanikio ya UNDAP ( ) ni sehemu ya wigo mpana wa michakato ya kitaifa inayochangia katika utengenezaji misingi wezeshi kwa ajili ya utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu, ambayo yanalenga katika kutomwacha yeyote nyuma, hasa katika kukabiliana na ukosefu wa usawa, ubaguzi, kutenga na aina nyingine ya ukandamizaji unaozuia uwezekano wa wanaume, wanawake na watoto wa Tanzania kukua kiuchumi, kijamii na kisiasa. Zaidi ya hayo, matokeo yaliyopatikana yanashabihiana na vipaumbele vya Serikali yakiwemo malengo ya kiutu. Wakati ambapo utekelezaji wa MKUKUTA II, FYDP I na MKUZA II unakaribia mwisho, serikali inatoa shukrani zake za dhati na msaada endelevu katika uandaaji wa Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano wa pili wa Serikali ya Tanzania na Mkakati wa Kuendeleza MKUZA II wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Lililo muhimu, mafanikio yaliyopatikana pamoja na tafiti huru mbili, Tathmini ya UNDAP na Uchambuzi wa Hali ya Tanzania vilitoa mang amuzi muhimu katika uandaaji wa UNDAP II ikishirikisha wadau wote muhimu. Kwa upande wa mafanikio ya kifedha, ripoti inaonyesha kwamba Vikosi Kazi vya UNDAP I saba kati ya kumi vilifikia zaidi ya asilimia 90 ya viwango vya utekelezaji katika kipindi cha mwaka wakati ambapo taarifa za awali za matumizi kwa miaka minne ya mwanzo ya UNDAP ilikuwa katika wastani wa asilimia 73 kwa kulinganisha na bajeti ya UNDAP ya miaka mitano. Kutokana na viashiria chanya hivyo katika matumizi ya Mwaka wa IV, matarajio ni kupata karibu asilimia 100 ya viwango vya mafanikio ya kifedha kwa kipindi cha mwaka Hiyo inatoa viashirio vya mafanikio kwa matokeo yanayotarajiwa kutokana na UNDAP I. Licha ya matokeo yaliyotajwa hapo juu, bado kuna changamoto. Miongoni mwa nyinginezo, kuna kupungua kwa rasilimali za msingi na uhamishaji wa fedha usiozingatia muda kwa washirika/mawakala wanaoshiriki katika utekelezaji. Tutaendelea kushirikiana ili kushughulikia changamoto hizi ili kuleta ufanisi na kuwa na utekelezaji wa programu katika muda uliopangwa. Mwaka ujao utashuhudia mafanikio mapya hasa kwa sababu ndio mwanzo wa utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ya dunia, wakati ambapo sisi hapa Tanzania tutakuwa tukizindua mipango mipya ya maendeleo. Mwisho, niwahakikishie wadau wote, wakiwemo UNCT na Marafiki wa Umoja wa Mataifa kwamba Serikali ya Tanzania itaendelea kuunga mkono jitihada za Mpango wa Kufanya Kazi Pamoja kwa ajili ya kuwa na programu zenye ufanisi, tija na endelevu na inarudia ahadi yake kuwa itaendelea kutoa uongozi kwa mageuzi ya Umoja wa Mataifa, wakati huohuo ikiimarisha mchango wake kupitia sekta na idara zake katika ngazi za kitaifa na mahalia. Dkt. Servacius Likwelile Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Dar es Salaam UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 1

4 2 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 UN Tanzania/Andrew Njoroge

5 YALIYOMO DIBAJI KUTOKA KWA MWENYEKITI WA KAMATI YA UONGOZI YA PAMOJA (JSC) 1 MUHTASARI YAKINIFU 4 Utangulizi 4 Matokeo muhimu yaliyopatikana hadi sasa kwa msaada wa Umoja wa Mataifa UTANGULIZI Muundo wa ripoti MUKTADHA WA NCHI MPANGO WA UNDAP : MATOKEO YALIYOKWISHA PATIKANA Ukuaji uchumi na utawala wa uchumi Mazingira Elimu Afya & lishe VVU/Ukimwi Kinga ya jamii WASH Utawala Wakimbizi Dharura Masuala mtambuka ya kuzingatia Kuwasiliana kama kitu kimoja Kuendesha mipango kama kitu kimoja MUUNDO-DHANA WA BAJETI YA PAMOJA Upatikanaji wa fedha VIKWAZO NA CHANGAMOTO: HATUA TULIZOCHUKUA HITIMISHO 97 Kiambatisho CHA i: vifupisho NA MAJINA KWA ufupi 99 UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 3

6 MUHTASARI YAKINIFU Utangulizi Mnamo mwaka 2007, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania URT ilionyesha dhamira juu ya nia yake kuwa moja kati ya nchi nane za mradi wa majaribio wa maboresho wa Umoja wa Mataifa ujulikanao kama Mpango wa Kufanya Kazi Pamoja (DaO). Kufuatia hatua hiyo Umoja wa Mataifa nchini Tanzania ulipewa jukumu la kubuni na kuendesha majaribio ya namna ya kuweka mipango, kutekeleza na kutoa taarifa kama kitu Kimoja miongoni wa mashirika yake ili kukuza mshikamano, ufanisi na tija katika maeneo makuu manne: Programu Moja, Kiongozi Mmoja, Bajeti Moja na Ofisi Moja (kuoanisha taratibu za utendaji kazi). Katika hatua za baadaye, Sauti Moja (mawasiliano ya pamoja) iliongezwa kama moja ya kipengele katika ngazi ya nchi, ambapo kilipata uthibitisho rasmi katika Kongamano la Nne la Viongozi wa Ngazi ya Juu kati ya Serikali Kadhaa kuhusu Dao, kule Montevideo mwaka Kutokana na maarifa yaliyopatikana katika awamu ya kwanza ya maboresho ( ), Timu ya Nchi ya Umoja wa Mataifa (UNCT) ilianzisha Programu moja ya Umoja wa Mataifa nchini kwa ajili ya shughuli za mashirika yote ya Umoja wa Mataifa kwa duru zinazofuatia za uandaaji programu: Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP) kwa kipindi cha Mpango huo Mmoja kwa ajili ya Tanzania unaunga mkono ufikiwaji wa vipaumbele vya kitaifa vya maendeleo na vilevile kupiga hatua katika kuelekea katika Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) na upatikanaji wa haki za binadamu za kimataifa nchini. Mafanikio Muhimu Yaliyopatikana Hadi Sasa kwa Msaada wa Umoja wa Mataifa Mpango wa UNDAP unaelezwa vizuri na michango mikuu mitatu katika maendeleo ya taifa, katika kutafuta kufikia lengo la muda mrefu la kusimika haki za binadamu nchini Tanzania. Haya ni: Kupunguza umaskini wa kipato kupitia ukuaji uchumi unaolenga watu maskini na kuimarisha uwezo wa kujinusuru Kuongeza ubora wa maisha na kufikia maisha bora kwa kila mmoja, wakiwemo wale walio hatarini zaidi Kujenga msingi imara na motomoto wa utawala bora ili kuwezesha ukuaji na hali bora ya maisha jumuishi Katika miaka minne tangu utekelezaji uanze, mashirika 24 ya Umoja wa Mataifa yanayofanya kazi nchini Tanzania yenye ukaazi na yasiyo na ukaazi yameshirikiana katika jitihada mbalimbali chini ya mada kuu tatu hizi. Yameshirikiana na washirika wa kitaifa kupiga hatua ili kufikia Matokeo ya UNDAP yaliyokubaliwa, yakiwemo yale yanayolenga ajenda ya mwenendo wa Umoja wa Mataifa na mageuzi ya DaO. Matini iliyo hapa chini inaangazia matokeo muhimu kutokana na uchukuaji hatua huu, huku taarifa zaidi zikiwa katika ripoti kuu. Programu Moja: Kupunguza umaskini wa kipato kupitia ukuaji uchumi unaolenga watu maskini na kuimarisha uwezo wa kujinusuru Katika mada hii ya kwanza, mashirika mbalimbali ya Umoja wa Mataifa yanaweka rasilimali zao pamoja ili kuhamasisha ukuaji katika sekta zote muhimu ambazo zinajumuisha na kuwanufaisha watu maskini na walio hatarini zaidi katika jamii ya Watanzania, huku ikijenga uwezo wa kujinusuru dhidi ya mabaa ya asili na yanayotokana na binadamu. Uangaziaji ni pamoja na: Kuanzisha mazingira wezeshi kwa sera za maendeleo ya kiuchumi, mikakati na jitihada zinazowalenga maskini Maofisa kutoka Wizara ya Kazi na Ajira (MoLE) na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) walijengewa uwezo ili kuchambua kwa usahihi viashiria vikuu vya soko la ajira: ajira, ukosefu wa ajira, na ajira chini ya kiwango, n.k. kwa ajili ya Tafiti Kamilifu ya Nguvukazi ya Msaada zaidi wa kiufundi na kifedha uliotolewa ili kufanya uchambuzi wa kina kuhusu masuala ya jinsia, kuwezesha uingizwaji katika mkondo mkuu masuala ya usawa wa jinsia na kuondoa viashiria vya ubaguzi katika Tafiti Kamilifu ya Nguvukazi ya / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

7 Kama ishara ya kufikiwa kwa uendelevu, Kitengo cha Upelelezi katika Sekta ya Viwanda chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara (MIT) ilitoa mihtasari mitatu ya kiufundi ya sera za sekta ya uzalishaji mali viwandani ili kutathmini hali ya utendaji wa sekta nzima, na hasa sekta ya viwanda vya mazao ya kilimo. Hizi zitatumika kama michango katika Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo unaofuatia, kwa kuweka mkazo katika maendeleo ya viwanda, na kwa mapitio ya Mkakati wa Maendeleo ya Viwanda Fungamanishi. Sera na Sheria zilizofanyiwa maboresho za Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (ST&I) zimetayarishwa na wadau muhimu wamekwishapewa taarifa. ST&I itaingizwa katika mkondo mkuu katika miundo-dhana ya sera ya maendeleo ya taifa na ubunifu. Mpango-Kazi wa Ajira ya Vijana Zanzibar ( ) ulikamilishwa na kusambazwa tayari kwa utekelezaji. Sekta muhimu tayari zimeanza utekelezaji, huku mafunzo yakitolewa katika biashara ya viwanda na TEHAMA. Mfumo wa Taifa wa Uchambuzi wa Data za Ushirika (National Cooperative Data Analysis System (CODAS)) mfumo wa data unaoendeshwa kwa kompyuta ili kukusanya na kuchambua data za ushirika na mienendo ya ukuaji ulikamilishwa na unaoendeshwa na zana ya kimtandao. Taarifa zinazopatikana zinaangazia utungaji na utekelezaji sera. Kituo cha Taarifa za Biashara kimekwishaanzishwa katika Umoja wa Biashara, Viwanda na Kilimo (ZNCCIA) ili kutoa huduma kama taarifa za biashara (mfano bei za soko, teknolojia iliyopo, sheria na kanuni, n.k.), mafunzo ya TEHAMA na uanzishwaji wa programu za msambazaji katika sekta binafsi. Huduma hizi hupanua msingi wa maarifa na seti za ujuzi zilizopo na kampuni pamoja na biashara za kifamilia zenye matarajio ili zikuze uzalishaji wao. Kupata uwezo wa taifa kujinusuru dhidi ya majanga ya asili na yanayosababishwa na binadamu Rasimu ya Sera ya Taifa ya Mazingira ilianzishwa kama matokeo ya mashauriano kati ya wadau. Mchakato wa mashauriano pia uliwezesha uingizwaji wa kiungo kikuu cha Mazingira ya Umaskini katika mchakato wa kupitia Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo. Miundo ya Kitaifa ya Utafutaji Fedha kwa ajili ya Mabadiliko ya Tabia ya Nchi ilianzishwa Bara na Zanzibar. Miundo hii inajumuisha miundo-dhana ya kisheria, kifedha na utekelezaji. Itakapoanza kazi, hii itaisaidia nchi kupata fedha katika ngazi ya kitaifa na kimataifa kwa ajili ya mabadiliko ya tabia nchi ikiwemo Green Climate Fund, fedha za pande mbalimbali pamoja na miongoni mwa washirika. Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira (VPO-DoE), Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais (VPO), NEMC, Wizara ya Fedha na baadhi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa zilijengewa uwezo ili kuingiza udhibiti wa mabadiliko ya tabia nchi katika mipango na mikakati ya maendeleo ya wilaya 37. Miundo-dhana ya kitaasisi kwa ajili ya udhibiti wa mabadiliko ya tabia nchi nchini vilevile iliimarishwa kupitia uanzishwaji na uendeshaji wa Kamati ya Uongozi ya Taifa ya Mabadiliko ya Tabia ya Nchi na Kamati ya Kiufundi ya Taifa ya Mabadiliko ya Tabia ya Nchi. Kituo cha Mafunzo cha Mkoa cha Msingi kilianzishwa na kuzinduliwa na Rais wa Zanzibar. Hivi sasa wanawake wanapata mafunzo ya teknolojia za nishati ya jua katika kituo hicho na watafanya kazi ya kuunganisha mifumo ya umeme jua katika kaya katika vijiji vyao ambavyo vingi havina umeme. Vilevile watakuwa na wajibu wa kufanya matengenezo na marekebisho kila baada ya miaka mitano. Zaidi ya hayo, kituo kinatoa mafunzo ya nyongeza kwa wanawake kuhusu kuwa mafundi wa umeme wanawake kutoka Bara na Visiwani kuhusu teknolojia za nishati ya jua na LED. Kupandisha hadhi ya Mbuga ya Taifa Saadani hadi kuwa Hifadhi ya Biosphere ni jambo lililowezeshwa, huku mchakato shirikishi ukizingatiwa. Programu ilikuza maarifa na ujuzi kuhusu hifadhi ya mifumo ya viumbehai, bio-anuwai na menejimenti endelevu ya rasilimali za asili miongoni mwa mamlaka kuu zinazohusika, kama vile Baraza la Taifa la Menejimenti ya Mazingira (NEMC) na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, na jamii ya mahali panapohusika. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 5

8 Miongozo ya Uendeshaji ya Kitaifa na Muundo-dhana wa Usimamizi na Tathmini ilisambazwa ili kuwa na utayari wa kukabili dharura wenye ufanisi na ulioshikamana. Hii inakamilishwa na jukwaa la ngazi ya mikoa la Kukabili Majanga ambalo huwaleta pamoja wadau mbalimbali ili kuweka uratibu na ushirikiano bora zaidi. Kwa kipindi cha mavuno cha 2014/2015, Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) ilinunua takribani Metriki Tani 30,000 za mahindi kutoka katika vyama 165 vya wakulima kwa bei ya soko. Kwa hiyo, NFRA iliongeza akiba yake ya chakula cha dharura kwa ajili ya maeneo ambayo yangekumbwa na njaa huku ikibadili mkakati wake wa kununua ili kunufaisha wakulima wadogo kupitia vyama vyao, kwa kuzingatia modeli ya Umoja wa Mataifa ya Kununua ili Kuleta Maendeleo. Kwa upande wa mahitaji, kuanzishwa kwa miundo ya Ulengaji na Usambazaji Inayosimamiwa na Jamii (CMTD) katika wilaya zilizochaguliwa zenye uhaba wa chakula imehakikisha kuwa makundi ya watu wasio na usalama kabisa wa chakula na walio hatarini zaidi wanafikiwa kwa urahisi zaidi wakati wa dharura. Programu Moja: Kuongeza ubora wa maisha na kufikia maisha bora kwa kila mmoja, wakiwemo wale walio hatarini zaidi Eneo la pili la kipaumbele linafafanua jitihada mbalimbali zinazolenga kuhakikisha kuwa kunakuwepo na maisha bora kwa kila mmoja, huku shabaha mahususi ikiwa kwa watu walio katika hatari zaidi katika jamii ya Watanzania. Hiyo inabeba uanzishwaji wa mifumo ya kijamii ya kusaidiana, hatua za kujikinga dhidi ya uonevu, ukatili au kupuuzwa, na vilevile kusimamia upatikanaji wa taifa lenye siha na lililoelimika na ambalo linaweza kuchangia katika kuleta maendeleo endelevu na jumuishi. Vidokezo ni pamoja na: Kujenga mfumo wa kinga ya jamii unaohusisha sekta nyingi kwa ajili ya mahitaji ya watu walio hatarini zaidi Tamko la Azimio la Arusha kuhusu Kinga ya jamii nchini Tanzania lapitishwa. Serikali ya Tanzania imesisitiza kuwa Tamko halina budi kutumika kama Mwongozo katika Kuchukua Hatua ili kuhamasisha kinga ya jamii na kupambana na ukosefu wa usawa, ubaguzi, kutenga na aina nyingine ya vikwazo vinavyozuia uwezekano wa Watanzania wanaume, wanawake na watoto kujiendeleza. Misingi yake mikuu imeingizwa katika Muundodhana wa Taifa wa Kinga ya Jamii (NSPF). Tamko hilo linajumuisha nia za dhati maalumu kutoa taarifa ya matokeo kuhusu kada ya chini, ili iwe kichocheo cha kuimarisha ajenda ya Umoja wa Mataifa ya usawa. Kanuni mbili za nyongeza zilianzishwa ili kuoanisha manufaa ya pensheni kuendesha Mfuko wa Fidia wa Wafanyakazi na kuongoza na kulinda ajira ya Wasio Raia nchini Tanzania. Mfuko huo wa awali unaendeleza utaratibu wa siku zote wa fidia na kutoa huduma ya tiba na gharama za marekebisho ili kuzuia hatari za mahali pa kazi. Hii ya pili, kuendana na haki ya kufanya kazi, inaunganisha pengo kati ya haki za watu wasio raia kama inayoelekezwa na viwango vya kimataifa vya masuala ya kazi na hali halisi ilivyo sasa Mfumo wa kinga ya mtoto ulienezwa katika wilaya nyingine tano upande wa Bara na moja kule Zanzibar, na kufanya jumla ya wilaya 19 zinazosaidiwa na Umoja wa Mataifa katika kuanzisha mifumo ya kinga ya mtoto. Programu inaendelea kuhakikisha mfumo unafanya kazi kuanzia ngazi ya wilaya hadi ya kijiji, ikiwemo kuimarisha njia za ukataji rufaa na kujenga uwezo kwa watoa huduma, kuimarisha uratibu ili kuzuia na kutoa majibu kwa visa mafunzo, na kuishirikisha jamii kuzuia ukatili dhidi ya watoto. Kinga ya Mtoto iliingizwa katika mtaala wa Chuo cha Ustawi wa Jamii (ISW) na Chuo Kikuu cha Serikali cha Zanzibar (SUZA), kwa hiyo kutoa hakikisho kwamba wafanyakazi wa ustawi wa jamii wanaomaliza mafunzo yao wanakuwa na stadi za kinadharia na vitendo kuendana na Sheria ya Mtoto ya 2009 na Sheria ya Mtoto ya Zanzibar ya 2011 na kanuni na miongozo inayoendana nazo. ISW hivi sasa inafanya kazi kupitia Chama cha Vyuo vya Ustawi wa Jamii nchini Tanzania ili kusaidia taasisi 11 zenye programu ya Ustawi wa Jamii ili kuingiza kinga ya mtoto katika mitalaa yao 6 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

9 Walimu 4,162 walipewa mafunzo kuhusu mtalaa mpya wa taifa wa KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu) na kuwanufaisha wanafunzi 90,300 wa shule za msingi katika shule 2,081 kwenye wilaya 21 zilizolengwa kwa msaada katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe. UN Tanzania/Andrew Njoroge UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 7

10 Mpango Kazi wa Gharama wa Taifa (NCPA-II) wa pili kwa MVCs ( ) ulizinduliwa, na kuwezesha upatikanaji wa huduma za msingi za jamii zikiwemo kinga dhidi ya ukatili, uonevu na kutengwa, na kuongeza ubora, upatikanaji na ufikiwaji wa huduma kwa lengo kubwa la kuzuia na kubaini mapema hatari za MVC. Wizara zinazohusika (zikiwemo TAMISEMI na Wizara ya Fedha) zinaendeleza makusudio maalumu ili kuongeza kiasi cha fedha kwa ajili ya utekelezaji wa NCPA-II katika sekta zote zinazostahili. Takribani asilimia 60 ya Mamlaka za Serikali za Mitaa zinaakisi mikakati ya NCPA katika MTEFs zao, huku kukiwa na mchango wa fedha kiasi cha kuridhisha kutoka kwenye vyanzo vyao zenyewe. Kuhamasisha Upatikanaji wa Huduma za Afya za Kutosha kwa Wote Mpango Ulioboreshwa wa Afya ya Uzazi, wakinamama, Watoto Wachanga na Watoto (RMNCH), ingawa huu awali ulianzishwa kwa kulenga mikoa ya magharibi na Kanda ya Ziwa ambayo ina viashiria vichache vya afya ya mama na mtoto, hivi sasa umesambazwa katika mikoa yote, kwa msaada wa UNFPA, UNICEF na WHO. Hatua kuu za uingiliaji kati zilizopendekezwa zimeingizwa katika Mipango ya Afya ya Baraza Kamili (CCHP) ili kuimarisha ubora wa utoaji huduma wa RMNCH. Ubora wa CHPs uliimarishwa zaidi kwa msaada uliotolewa na Timu za Mikoa na Wilaya kutumia Zana ya Mpango Wakilishi (Plan Rep Tool) katika michakato yao ya kuweka mipango. Sera ya Taifa ya Chakula na Lishe ilipitiwa upya na Mpango elekezi kuandaliwa kwa ajili ya maandalizi ya Mpango Kazi wa Lishe wa Taifa Unaohusisha Sekta Nyingi wa 2016/ /21. Kuanzishwa kwa Muundo-dhana wa Programu ya Jamii ya Afya ya Wafanyakazi (kwa ushirikiano wa mashirika mbalimbali na msaada kutoka UNFPA, UNICEF, WHO) na ukamilishaji wa mpango mkakati wa kitaifa wa kuendesha Programu ya Afya katika Jamii (CBHP) iliyounganisha na miongozo ya sera. Kwa pamoja, hizi zitapanua ufikiwaji wa huduma za afya maeneo ya vijijini. Mikoa mitatu imepokea msaada wa Umoja wa Mataifa ili kutekeleza mpango uliotajwa hapo awali, kwa mrengo wa kuhusisha RHMTs, CHMTs na wadau wengine. Hizi zimesababisha uanzishaji wa CHPs ambazo zitaingizwa katika CCHPs ya 2015/2016. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (MoHSW) imeanzisha Mpango Mkakati wa Uuguzi na Ukunga ( ), lengo likiwa ni kuimarisha utoaji mafunzo na huduma zenye ubora zaidi. Jambo hili limeimarishwa na uundwaji wa Miongozo ya Sera kwa Watoa Mafunzo ya Hospitali na Miongozo ya Kitaalamu ya Stadi za Maabara. Tathmini ya muda wa kati kuhusu utekekelezaji wa Mpango Mkakati wa Taifa wa Zanzibar kuhusu VVU/ UKIMWI (ZNSP II) ulikamilishwa na Mpango wa Uendeshaji na Gharama Zake ili kuongoza ushughulikiaji VVU/UKIMWI kwa kipindi kilichobaki ulianzishwa. Data kutoka majukumu hayo mawili zilichangia katika kutumia kwa mafanikio GFATM iliyotajwa hapo awali. Kifurushi cha hatua za kuchukua juu ya VVU kwa ajili ya KPs kilianzishwa na ZACP kwa kuzingatia miongozo ya kimataifa. Matokeo ya Tafiti ya Ufuatiliaji Unganifu wa Tabia na Kibiolojia (IBBS) iliyosambazwa hivi karibuni huko Zanzibar ( ) yaliingizwa katika vifurushi na watoa huduma za afya na watekelezaji wa KP walipata mafunzo kuhusu namna ya kuzitumia. Jitihada za kufika uwandani zimesababisha kuongezeka kwa huduma za VVU zinazotolewa na KPs huko Zanzibar kutoka 1,108 hadi 3,833. Suhula za WASH (vyoo, upatikanaji wa maji na kunawa mikono) zimejengwa katika shule 47 upande wa Bara na Zanzibar. Hii imewapa zaidi ya wanafunzi 59,000 ( wasichana 30,690 na wavulana 28,310) fursa ya kupata huduma hizi zinazoweka mazingira yao ya kusomea kuwa salama na yenye kinga. Suhula hizo zinaendana na mahitaji ya miongozo ya Kitaifa ya WASH Mashuleni, na kujenga vyoo tofauti kwa wavulana na wasichana ili kuleta faragha na kutoa huduma zinazostahili kwa wasichana wanaovunja ungo na watoto wenye ulemavu. Wajumbe wa kamati za uendeshaji shule, viongozi wa kijamii, wazazi na wajumbe wengine wamehamasishwa, kupewa maelekezo na mafunzo kuhusu uendeshaji wa mpango wa WASH mashuleni, uwekaji mipango, na utengenezaji bajeti ikiwemo kuanzishwa kwa mifuko itakayosaidia usimamizi makini na uendelevu wa suhula zilizokwishakamilika. 8 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

11 Rasimu ya mwisho ya Mkakati Endelevu wa Kitaifa kuhusu usambazaji maji vijijini ulianzishwa. Mwongozo wa muundo-dhana uliandaliwa kupitia jitihada za ushirikiano wa wadau katika sekta, uchambuzi wa hali za sasa, kubaini changamoto zinazoathiri uendelevu ikiwemo mazingira wezeshi/yasiyo wezeshi (sera, uwezo, taasisi, fedha, sheria na ufundi) ili kushughulikia vikwazo na kuimarisha utoaji wa huduma ya maji vijijini. Mkakati unajumuisha miongozo kuhusu matumizi ya zana usimamizi zilizoanzishwa kwa msaada wa DPs, hasa Ubainishaji wa Eneo lenye Maji GIS ambayo huwezesha ukusanyaji data na uchambuzi, utengenezaji ripoti na usambazaji. Ushahidi utawezesha utoaji uamuzi kwa usawa na weledi katika kuweka mipango, kubuni na kuelekeza rasilimali kwa wale wanaozihitaji zaidi. Kutoa Elimu Bora kwa Wote Sera Mpya ya Elimu na Mafunzo (ETP) ilizinduliwa, ikitoa mwongozo wa kuwepo kwa mwaka mmoja wa masomo ya awali wa lazima ili kuleta matokeo bora katika kujifunza, huku mzunguko wa elimu ya msingi ukipanuliwa. ETP inatoa mwongozo kwa maendeleo ya sekta ya elimu katika kiwango cha kati hadi muda mrefu. Rasimu ya Sera ya Taifa ya Matunzo ya mtoto, Ukuaji na Maendeleo (NCCGDP) ilikamilishwa ili kukuza uratibu wa sekta nyingi kwa lengo la kuratibu maendeleo ya mtoto (ikiwemo ECD) kwa watoto wa umri kati ya Mwaka , mpango wa mlo mmoja kwa siku ulitekelezwa kwa shule 640 katika wilaya 16 katika maeneo yanayokumbwa na ukame na kutokuwa na chakula cha kutosha na wanakoishi wafugaji katika mikoa ya Dodoma, Singida, Arusha na Manyara, na kuwafikia wanafunzi 370,000. Bidhaa za chakula zilinunuliwa kila ilipowezekana kupitia programu ya Kununua kwa Maendeleo (P4P) ambayo huwezesha ununuzi wa moja kwa moja wa mahindi na mbaazi kutoka kwa wakulima wadogo katika vyama vya wakulima vilivyosajiliwa au kupitia NFRA. Manufaa ya kuonekana ya programu hiyo ni pamoja na kuongezeka kwa kipato na uwezo wa jamii kuchangia fedha taslimu, chakula au bidhaa zisizo chakula kwa mpango wa chakula shuleni na nyingine za maendeleo ya jamii. Walimu 4,162 walipewa mafunzo kuhusu mtalaa mpya wa taifa wa KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu) na kuwanufaisha wanafunzi 90,300 wa shule za msingi katika shule 2,081 kwenye wilaya 21 zilizolengwa kwa msaada katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe. Umoja wa Mataifa pia imetoa msaada katika kuongeza ubora wa msaada wa elimu na saikolojia-jamii katika shule 28 wa mahitaji maalumu zilizoanzishwa ili kutoa mazingira salama ya kujifunzia na kuishi kwa watoto wenye ulemavu wa ngozi (albino). Programu ya masomo kwa njia ya posta (CELMA) ilianzishwa katika wilaya nane, huku mafunzo ya mwelekeo na awali yakitolewa kwa walimu wakuu wa shule zote za msingi. Baadhi ya moduli hususan Utunzaji Vifaa, Mipango, Mitalaa, Uongozi na Menejimenti zilianzishwa kuandaa mwongozo wa Matokeo Makubwa (BRN) kwa walimu wakuu nchini kote. Moduli za CELMA pia zimetumika pamoja na moduli za BRN ili kutoa mafunzo kwa walimu wakuu 10,601 na Waratibu Kata wa Elimu 2,588 katika mikoa 17 ya Tanzania Bara. Programu Moja: Kujenga msingi imara na motomoto wa utawala bora ili kuwezesha ukuaji na hali bora ya maisha jumuishi Mada ya mwisho katika programu inasaidia uanzishwaji wa mazingira bora wezeshi ili kuleta ukuaji unaolenga maskini kwa lengo la kuwa na maisha bora. Chini ya ufafanuzi mpana wa utawala bora, Umoja wa Mataifa na washirika wake wanawasaidia watu mmojammoja na taasisi ili kutimiza wajibu wao wa kisiasa na kiserikali, uikiwemo wajibu wa kimataifa chini ya ajenda ya utendaji wa kawaida, na vilevile kuziwezesha jamii kushiriki katika majadiliano ya kidemokrasi na amani. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 9

12 Vidokezo ni pamoja na: Kuziwezesha taasisi kutimiza kwa ufanisi zaidi kazi zao za uchaguzi na siasa Katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwa serikali ya Muungano na ule wa Zanzibar, mamlaka zenye dhamana ya kusimamia uchaguzi zilitekeleza mapendekezo kutoka kwa waangalizi wa uchaguzi mkuu wa Haya yalijumuisha uanzishwaji wa zana mpya za mawasiliano/uwazi zikiwemo tovuti na mikakati ya mawasiliano. Zaidi ya hayo, kuingiza taarifa mpya katika daftari la kudumu la mpiga kura na kurekebisha mfumo wa utunzaji data ambavyo vyote vilifanyika kwa mafanikio Zanzibar na uandikishaji wapiga kura kukamilika kwa msaada wa kiufundi na vifaa. Mkakati wa Mabadiliko katika Sekta ya Sheria wa Zanzibar ( ) ulipitishwa na kuchukuliwa na Baraza la Mawaziri na, kufuatia msaada wa ushauri, Sera ya Msaada wa Sheria ilikamilishwa. Hizi ziliweka msingi kwa uanzishwaji taasisi ya muundo wa msaada wa sheria na maendeleo yanayoendeleza muundo-dhana wa utungaji sheria ya msaada wa sheria kamili ili kuleta huduma za utoaji haki na sheria kwa wanajamii walio hatarini zaidi. Kikosi Kazi cha Uingizaji Masuala ya Jinsia katika Sera Pana (GMWG-MP) kama muundo muhimu wa Serikali ya Muungano kwa ajili ya uratibu wa masuala ya jinsia katika ngazi ya sera kimeimarishwa. Kikisimamiwa na wenyeviti wenza kutoka serikalini na Umoja wa Mataifa, Kikosi Kazi sasa kinashughulisha wadau wengi zaidi (Wizara katika Sekta, Vyama vya Kiraia na academia), ili kujenga uwezo wa MCDGC, na hufanya kazi kama mfumo hai wa uwajibikaji kupitia GEWE. Kama matokeo ya ushirikiano, zana kuu za sera za kuendeleza GEWE nchini Tanzania zimeandaliwa, zikiwemo miongozo kwa kuingiza masuala ya jinsia katika mkakati wa BRN, ripoti ya kitaifa ya Beijing Baada ya Miaka 20 ambayo inaweka kumbukumbu ya maendeleo na changamoto zilizopo hadi sasa na Wasifu wa Nchi kuhusu Jinsia. Hiyo ya mwisho inaleta pamoja data zilizo katika makundi madogomadogo na uchambuzi makini wa masuala ya jinsia kwa kufuata sekta, hii ikiwa ni mara ya kwanza, kuimarisha uwajibikaji wa taifa kutimiza ahadi zake za kikanda na kiulimwengu, yakiwemo mahitimisho yaliyokubaliwa ya CSW na Tamko la Beijing na Jukwaa la Uchukuaji Hatua. Mabadiliko ya mfumo mzima katika namna Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs) zinavyofanya kazi yalifikiwa kwa kwezesha wafanyakazi upande wa ufundi kuhakikisha kwamba miradi ya uwekezaji inaakisiwa katika mfumo ya ngazi ya mikoa katika kuweka mipango na kuandaa bajeti. Msaada wa kiufundi kwa miradi mitatu ya maendeleo ya kiuchumi ambayo ni vituo vikuu vya mabasi na soko la kisasa katika halmashauri za Moshi na Mji wa Kibaha imevutia takribani dola za Marekani milioni 24 kutoka katika taasisi za fedha za hapa nchini Tanzania. Programu ya Harakati za Utafutaji Fedha Mahalia kwa Tanzania (LFI-T) pamoja na TAMISEMI inabaini na kuanzisha miradi ya ngazi ya chini hadi kati ya miundombinu ili kunufaisha jamii za mahalia, kuwezesha wanawake, kutengeneza nafasi za ajira na shughuli za kuingiza kipato. Kwa namna ya pekee, njia za uwekezaji katika miradi na zana za utafutaji fedha za miradi tayari zimeanzishwa. Ni muhimu kujenga urafiki na washirika wa maendeleo ili kupata rasilimali zaidi kwa ajili ya prorgamu na kuanzisha njia imara zaidi za utoaji mikopo kwa ajili ya miradi iliyochaguliwa. Utafutaji fedha mahalia nchini Tanzania sasa inatumiwa kama modeli ulimwenguni, huku nchi ikiwa mwenyeji wa Ofisi ya Dunia kwa ajili ya Mpango wa Kutafuta Fedha Mahalia. Kusaidia utimizaji wa wajibu wa mikataba ya kimataifa na kuendeleza zaidi uhamasihaji wa haki za binadamu nchini Mpango Kazi wa Kitaifa kuhusu Haki za Binadamu (NHRAP) umepitishwa kwa ajili ya utekelezaji kote nchini na kuingizwa kama sehemu ya Mafunzo kwa Wakufunzi katika Elimu ya Haki za Binadamu katika taasisi za elimu. Washirika wameandaa mikakati yao wenyewe ili kutoa elimu ya haki za binadamu katika taasisi zao. CHRAGG imepewa msaada zaidi ili kuchambua kwa ufanisi zaidi na kutoa data kuhusu matokeo yanayopimika na kwa hiyo kuimarisha majukumu yake katika kutekeleza Mpango Kazi wa NHRAP. 10 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

13 Kama sehemu ya kuadhimisha Siku ya KImataifa ya Wanawake, wanawake na wanaume 1,000 waliandamana katika mitaa ya Morogoro ili kuadhimisha mafanikio ya Tanzania na walitoa wito kwa hatua zaidi katika kuleta usawa wa jinsia na haki za wanawake. Photo: UN Women/ Stephanie Raison UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 11

14 Miradi mitatu ya redio za jamii huko Unguja na tatu upande wa Bara ilianzishwa na kuongeza idadi ya wasikilizaji hadi raia 634, Jumla ya redio za jamii 28 zimesaidiwa kote katika mzunguko wa Mpango wa UNDAP, zikiwafikia jumla ya watu milioni 16, zikiwafundisha kuhusu haki zao kupokea taarifa za maendeleo na kushiriki katika mijadala ya kidemokrasia. Kuimarishwa kwa jitihada za utetezi na mawasiliano kuhusu GEWE kulizinduliwa na IAGG kwa ushirikiano baina ya mashirika ikiwa ni pamoja na kusherehekea Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Siku 16 za Uanaharakati dhidi ya Ukatili wa Kijinsia (GBV). Kama sehemu ya kuadhimisha Siku ya KImataifa ya Wanawake, wanawake na wanaume 1,000 waliandamana katika mitaa ya Morogoro ili kuadhimisha mafanikio ya Tanzania na walitoa wito kwa hatua zaidi katika kuleta usawa wa jinsia na haki za wanawake. Kwa mwitikio, Rais alithibitisha ahadi ya serikali ya kushughulikia kukosekana kwa usawa ambao wanawake wameendelea kukabiliana nao nchini Tanzania. Kuandaa mifumo rafiki na ya haki ya makimbilio na makazi mapya kwa kuzingatia viwango vya kimataifa Msaada wa tiba wa kisaikolojia na kijamii kwa wahanga wa vitendo vya SGBV. Mapitio ya miundo-dhana ya kuzuia na kuitikia yalifanyika na Mfumo wa Menejimenti Taarifa za GBV (GBVIMS) kuanzishwa ili kuwezesha kukabili mienendo na wasifu wa manusura na wakosaji, ili kuimarisha programu za uzuiaji na uchukuaji hatua. Kiasi kikubwa cha rasilimali kimeelekezwa katika kuhakikisha kunakuwepo na malazi ya kutosha, salama na yanayokalika, mfumo bora zaidi wa maji ili kupunguza migogoro katika maeneo ya kuchotea maji na kupunguza utegemezi katika kuni kwa kuanzisha majiko yenye ufanisi zaidi na kugawa taa za nishati ya jua kwa kaya ili ziwe na chanzo cha mwanga. Jumla ya taa 13,527 za nishati ya jua ziligawiwa kwa kaya za wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo na asilimia 19 ya idadi ya watu walinufaika kutokana na majiko yenye ufanisi (Save80). Zaidi ya watoto wakimbizi kutoka Kongo 1500 wamepewa huduma mbadala za matibabu zikiwemo rufaa kwa mahitaji ya msingi ya huduma za afya na msaada wa kisaikolojia-kijamii. Taasisi za Nafasi 3 Rafiki kwa Mtoto zimetoa kinga, fursa ya kujifunza na maeneo ya kuchezea kwa watoto wakimbizi zaidi ya 15,000. Watoto wakimbizi kutoka Burundi waliokuwa peke yao walibainishwa, kufuatiliwa historia yao na kupewa utaratibu mwingine wa matunzo ikiwa ni pamoja na kuwapa msaada wa kisakiolojiakijamii, kinga na rufaa kwa ajili ya huduma za afya. Lengo la mwaka la kuwapa makazi wakimbizi kutoka Kongo 4,520 huko Nyarugusu lilitimizwa na hata kuvukwa kwa asilimia 16. Kukamilika kwa uhakiki wa watu kuliongeza ubora wa usajli data, na kwa hiyo kusaidia kuleta ufanisi zaidi katika kushughulikia kesi. Watu wenye mahitaji rasmi walipewa kipaumbele katika kupewa makazi mapya, wakiwemo manusura wa vitendo vya ukatili, wanawake na wasichana walio hatarini, wagonjwa mahututi na wa magonjwa ya muda mrefu na watu wenye ualbino. Ilipofika Juni 30, Tanzania ilikuwa tayari imefikia asilimia 51.3 ya lengo la mwaka kuhusu rufaa za wakimbizi 2,577 la kupeleka mbele maombi katika nchi mpya za ukaazi wa wakimbizi. Hili likiwa ongezeko kubwa katika kuandaa utoaji makazi katika taifa lingine lilikuwa katika mwaka 2015, ambapo jumla ya wakimbizi 826 waliondoka kwenye nchi za nyingine (USA, Canada na Australia) ili kupata makazi mapya ya ukimbizi. Mkakati Kamili wa Menejimenti ya Uhamiaji (Comprehensive Migration Management Strategy (COMMIST)) ulianzishwa, na kutoa kipaumbele kwa utungwaji wa sheria kuhusu hadhi ya wahamiaji wasio wa kawaida nchini na kuwezesha usajili kwa teknolojia ya biometriki ya wakimbizi hao wasio wa kawaida. Hadi sasa, wahamiaji 22,282 walijitokeza kuandikishwa mkoani Kigoma, mkoa uliochaguliwa kwa ajili ya majaribio. Wahamiaji waliosajiliwa walikabidhiwa kadi za kuwapa kinga kwamba ukaaji wao nchini ulikuwa hauna shida na ambayo itadumu kwa miaka minne kabla ya hadhi yao kuangaliwa upya na wahamiaji wangeweza kuomba vibali vya ukaazi au kuomba kusaidiwa kurejea makwao kwa hiyari. Raia wa Tanzania pia wanaweza kuomba uthibitisho wa uraia wao katika mchakato huu. Kuanzishwa na kupanuliwa kwa usajili wa kibiometriki unapangwa kwa ajili ya wahamiaji wasio wa kawaida kote nchini katika miaka mitano ijayo. 12 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

15 Mpango wa Kufanya Kazi Pamoja: Kuweka Progamu yenye Ufanisi, Tija na Iliyo Endelevu Nguzo zilizobakia chini ya DaO zinapanua wigo wa upande wa ubora katika kutekeleza programu, kushughulikia masuala ya ufanisi, tija kuhusu gharama na kufaa kwake. Vidokezo ni pamoja na: Kuwasiliana kwa Sauti Moja Chini ya mwamvuli wa Kuwasiliana kwa Sauti Moja, Umoja wa Maofisa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa umeandaa nyenzo kadhaa za mawasiliano zinazolenga kutoa matokeo, na ambazo zimetumika kama zana muhimu za utetezi. Hizi ni pamoja na: Kitita cha Matokeo ya UNDAP chenye habari za wakati huo kwa Kiingereza na Kiswahili. Wadau 5,000 wamepokea vitita hivi, wakiwemo washirika wa Serikali na Maendeleo, vyama vya kiraia na wasomi, kupitia usambazaji, wakati wa maonyesho au kupitia tovuti ya Umoja wa Mataifa Tanzania. Nakala za jarida la Sauti kutoka Uwandani (Voices from the Field) zimesambazwa kwa wadau wa kitaifa na kupatikana kupitia meza za maonyesho, tovuti ya Umoja wa Mataifa Tanzania na vyombo vya habari vya nchini. Tovuti ya Umoja wa Mataifa Tanzania iliyoundwa upya ambayo inaendelea kutoa fursa ya nyaraka muhimu na taarifa mpya kuhusiana na matukio/matokeo mapya katika usanifu kurasa ulio rahisi kutumia. Tovuti inakamilishwa na majukwaa ya mitandao ya kijamii (kwa mfano: Twitter, Facebook na Youtube) vyote vikieneza nembo ya DaO kwa umma. Jarida la kila baada ya miezi miwili. Hili huangazia habari za mafanikio makubwa ya mchango wa Umoja wa Mataifa Tanzania katika maendeleo ya taifa na vipaumbele vya kiutu. Usambazaji wake umepanuliwa hadi kwa wasio watumishi wa Umoja wa Mataifa na wafadhili, bali pia Serikali, vyombo vya habari na vijana, huku usomaji wake ukiongezeka hadi 5,000 katika mwaka Umoja wa Mataifa Tanzania pia imetumia matukio mbalimbali kupanua kufahamika kwa kazi zake, hasa ujumbe muhimu chini ya ajenda yake ya utendaji kazi na SDGs. Siku za Umoja wa Mataifa kama vile Siku ya Kimataifa ya Wanawake, Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, Siku ya Kujenga Uelewa Kuhusu Ualbino, Siku ya Kimataifa ya Vijana, Siku ya Umoja wa Mataifa, Siku ya haki za Binadamu na Siku ya UKIMWI Duniani ziliadhimishwa huku kampeni kupitia vyombo vya habari ikifanywa. Vilevile, Maonyesho ya Saba Saba 2015, ambayo ni miongoni mwa maonyesho makubwa Afrika Mashariki, ilitumika kama jukwaa la kuonyeshea mafanikio makubwa ya Umoja wa Mataifa. Zaidi ya watu 5,000 walitembelea banda la Umoja wa Mataifa, miongoni mwao ni Rais Jakaya Kikwete, mawaziri na wanadiplomasia. Uwezeshaji wa ushirika kati ya vituo vya redio mahalia na serikali umefanywa, na hivyo kuchangia katika kuboresha programu zinazohusu masuala muhimu yanayoishughulisha Umoja wa Mataifa. Kwa mfano, Ofisi ya Waziri Mkuu (Maafa), Mamlaka ya Hali ya hewa na Wizara ya Kilimo zilihimizwa kutumia redio za mahalia ili kuhamasisha utayari wa kukabiliana na majanga; MCDGC imeandaa mipango ya majaribio ili kupanua ushirikiano na vituo vya redio mahalia ili kuhamasisha matumizi ya Dawati la Jinsia, n.k. Mikakati imewekwa ili kukuza ushirikiano na LGAs kuhakikisha kwamba ni taarifa sahihi na zinazofaa kiutamaduni ndizo zinazorushwa ili kuwafikia wanawake na wanaume katika jamii zilizo pembezoni. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 13

16 Mfumo wa kinga ya mtoto ulienezwa katika wilaya nyingine tano upande wa Bara na moja kule Zanzibar, na kufanya jumla ya wilaya 19 zinazosaidiwa na Umoja wa Mataifa katika kuanzisha mifumo ya kinga ya mtoto. Programu inaendelea kuhakikisha mfumo unafanya kazi kuanzia ngazi ya wilaya hadi ya kijiji. UN Tanzania/Andrew Njoroge 14 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

17 Kufanya Kazi kama Kitu Kimoja Timu ya Manunuzi ya Pamoja ya Tanzania (TOPT) inaendelea kupiga hatua katika jitihada zake za kuleta pamoja na kuongeza matumizi ya ununuzi wa pamoja ndani ya Umoja wa Mataifa Tanzania. Idadi ya Nyaraka za Manunuzi (LTAs) za kawaida zimeongezeka hadi 66, huku LTA maalumu kwa shirika la Umoja wa Mataifa zikiendelea kutumiwa na mashirika mengine dada. LTA za kawaida ni pamoja na utoaji huduma za jumla kama vile utumiaji benki moja, huduma za ulinzi na usafi katika ofisi za Umoja wa Mataifa, menejimenti ya usafiri na upigaji chapa. Matumizi ya mashirka bado yako juu, huku LTAs zikitumiwa katika asilimia 45 ya oda zote za manunuzi. Mafanikio makubwa wakati wa kipindi cha mpango kazi kwa mwaka 2014/15 ilikuwa ni maandalizi ya warsha kwa ajili ya watoa huduma, ambayo ilihudhuriwa na watoa huduma 70, ambapo walielimishwa kuhusu kanuni za manunuzi za Umoja wa Mataifa, namna ya kufanya biashara na Umoja wa Mataifa na kanuni za Global Compact. Vilevile ilitoa fursa ya kupata mrejesho kuhusu namna Umoja wa Mataifa inavyotazamwa kama mnunuzi. Mapendekezo yanayohusiana na ufanyaji malipo kwa muda na urahisishaji mchakato wa tenda yanafanyiwa kazi. Katika miezi ya hivi karibuni, msingi wa mtandao usiotumia waya kupitia miundombinu ya Mkonga wa Mawasiliano umebadilishwa. Suala hili limepunguza gharama za uendeshaji zinazohusiana na kupungua kwa thamani ya vifaa visivyounganishwa kwa waya, matengenezo ya minara na huduma za uunganishaji. Miundombinu mipya ya msingi wa Mkonga wa Mawasiliano vilevile umeondoa kusuasua kwa mtandao, na hivyo kuongeza kasi ya mawasiliano ya intaneti kwa watumiaji. Manufaa mengine ya muhimu ni kuongezeka kwa stadi ya mapatano katika soko, ambapo kuongezeka mara dufu kwa kasi na uwezo wa intaneti tangu kuanzishwa kwa mradi bila gharama za ziada. Mashirika yote yanayoshiriki yanaunganishwa kwa huduma ya intaneti ya kasi ya Mbps 14 ambayo inatumiwa kwa pamoja kulingana na idadi ya watumiaji kwa kila shirika, huku kukiwa na uwezekano wa kuongeza kadiri ya mahitaji katika kiwango cha juu cha kiasi kisichotumika. Muundo-dhana wa Bajeti ya Pamoja Mpango wa UNDAP unajumuisha muundo-dhana wa bajeti moja unaojumuisha rasilimali za msingi na zisizo za msingi za mashirika na Mfuko Mmoja. Utekelezaji wa Programu ya Ushirikiano, ikiwemo ajenda ya mabadiliko, hutegemea uhamasishaji wenye mafanikio wa rasilimali zote tatu za fedha. Kila Kikosi Kazi kinatakiwa kutoa taarifa kuhusu matumizi na kama sehemu ya Mapitio ya Kila Mwaka ya Mipango Kazi ya Mwaka (AWPs) Takwimu hizi ni za muda. Data bado haijathibitishwa na makao makuu ya mashirika. Takwimu rasmi zitapatikana tu katika robo ya pili ya mwaka Data kuhusu ahadi, akiba na matumizi ya Mfuko Mmoja zitatolewa katika ripoti ya fedha itakayochapishwa mnamo tarehe 31 Mei 2016 kuhusu Multi- Partner Trust Fund Office Gateway Hii ni kwa kuzingatia mahitaji ya utoaji ripoti za Mfuko Mmoja wa Umoja wa Mataifa kama ilivyofafanuliwa katika Randama ya Makubaliano (MOU). Kwa mujibu wa utoaji taarifa chini ya Mapitio ya Mwaka, Vikosi Kazi vilipata kiwango cha asilimia 92 ya matumizi, ikionyesha kuwa ufikiwaji malengo uliongezeka wakati ambapo UNDAP inaingia katika mwaka wake wa mwisho wa utekelezaji. Vikosi Kazi Saba vilifikia zaidi ya asilimia 90 ya kiwango cha malengo katika mwaka wakati ambapo taarifa za awali za matumzi kwa miaka minne ya kwanza ya UNDAP ilikuwa wastani wa asilimia 73 dhidi ya bajeti ya miaka mitano ya UNDAP. Takwimu hii ni kubwa kuliko asilimia 52 iliyoonyeshwa mwaka jana, ingawa kulikuwa na kuongezeka kwa jumla kwa bajeti nzima. Kufuatia matokeo haya chanya katika mwaka wa IV wa matumizi, karibu asilimia 100 ya kiwango cha utoaji huduma kinatarajiwa katika mwaka UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 15

18 Vikwazo na Changamoto: Mwitikio Wetu Changamoto kadhaa zimeathiri ufanisi na tija katika utoaji huduma kwa matokeo yaliyopangwa chini ya UNDAP. Hapa chini kuna orodha ya maendeleo katika hatua za kurekebisha zilizochukuliwa ili kushughulikia masuala haya. Kiwango cha chini cha utoaji fedha kupitia mfumo wa Mhazini Mkuu wa Serikali mara nyingi unatajwa kama changamoto katika utekelezaji majukumu kwa wakati. Kwa hiyo, UNCT itaendelea kufanya kazi na Wizara ya Fedha ili kubaini na kutafuta suluhisho kwa vikwazo hivi vikubwa, ikiwemo kupitia upya mfumo na michakato ya utumaji fedha kupitia mfumo wa mhazini mkuu. Sambamba na hilo, Umoja wa Mataifa itaendelea kuisaidia Wizara ya Fedha kujenga uwezo wa Wadau Wanaotekeleza mipango ili kuhakikisha kuwa MTEFs zinaakisiwa sawasawa katika makisio ya bajeti, yanaingizwa inavyopaswa katika vitabu vya bajeti na uelekezwaji wa namba za ruhusua zinapatikana kwa ajili ya uhamishaji fedha kwa wakati kutoka Hazina. Katika miezi 12 iliyopita, UNCT imepanua sana shughuli zake za Mawasiliano na Huduma za Nje kupitia seti fungamani za miradi ambayo inatoa ujumbe mmoja kuhusu taratibu na amali za Umoja wa Mataifa na vilevile matokeo yaliyopatikana. Kufahamika kwa Umoja wa Mataifa kumeongezeka, kwa hiyo imepanua nafasi ya Umoja wa Mataifa katika muktadha wa maendeleo ya nchi, na kuvutia uwekezaji mpya ili kupata ahadi chini ya UNDAP. Kwa kuendelea, Umoja wa Mataifa itaendelea kubuni njia za kufafanua vizuri na kuongeza thamani iliyoletwa na Umoja wa Mataifa kupitia DaO, kwa kusaidiana na programu maalumu na vilevile kanuni pana za utengenezaji programu. Tunapoingia kipindi cha baada ya 2015, Umoja wa Mataifa itahakikisha kwamba mfumo wake ni wa kufaa kadiri ya malengo, inaweza kujibu kadiri ya mahitaji yanayoibuka ya ajenda ya mabadiliko ya SDGs katika ngazi za ulimwengu na nchi. Hii itakuwa na maana ya kufunga mkanda katika kulenga njia za mfumo wa Umoja wa Mataifa ulioshikamana ambao kwao taathira chanya ya ujuzi uliowekwa pamoja wa mashirika ya Umoja wa Mataifa unaweza kutumiwa kikamilifu. Hii itafikiwa kwa msaada wa Serikali na Washirika wa Maendeleo, kwa kuendana na vipaumbele na mipango kamili ya maendeleo ya taifa na kupitia utekelezaji wa uelekezaji miundo ambayo inapunguza urudufuji wa michakto na ulengaji matokeo. Hitimisho Katika mwaka kabla ya mwaka wa kukamilisha kipindi cha utekelezaji UNDAP kumekuwa na ongezeko la utoaji huduma, kwa rasilimali zilizowekwa pamoja na zaidi ya mashirika 20 ya Umoja wa Mataifa ya ukaazi na yasiyo ya ukaazi kupata mafanikio makubwa katika kuleta maendeleo ya kitaifa na kusimika haki za binadamu nchini Tanzania. Kwa kasi hii ya utoaji huduma na kwa msaada unaoendelea kutolewa kwa utekelezaji wetu na washirika wa maendeleo, tutaongeza jitihada zetu kupanua taathiria yetu na kupanua mshikamano katika mfumo mzima ili kuhakikisha kunakuwa na mafanikio kama ilivyokubaliwa katika Matokeo ya UNDAP ya Juni, / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

19 Tunapoingia kipindi cha baada ya 2015, Umoja wa Mataifa itahakikisha kwamba mfumo wake ni wa kufaa kadiri ya malengo, inaweza kujibu kadiri ya mahitaji yanayoibuka ya ajenda ya mabadiliko ya SDGs katika ngazi za ulimwengu na nchi. Photo: UN Tanzania /Andrew Njoroge UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 17

20 Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge 18 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

21 1.0 UTANGULIZI Katika kufanyia kazi mapendekezo yaliyotolewa na Mkutano wa Viongozi Wakuu kuhusu Mfungamano wa Mfumo Mzima wa Umoja wa Mataifa kwamba mfumo wa Umoja wa Mataifa hauna budi Kufanya Kazi Pamoja (DaO) katika ngazi ya nchi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (URT) ilionyesha dhamira juu ya nia yake kuwa moja kati ya nchi nane za mradi wa majaribio katika mageuzi hayo mwaka Kufuatia hatua hiyo Umoja wa Mataifa nchini Tanzania ulipewa jukumu la kubuni na kuendesha majaribio ya namna ya kuweka mipango, kutekeleza na kutoa taarifa kama kitu Kimoja ili kukuza mshikamano, ufanisi na tija katika maeneo makuu manne: Programu Moja, Kiongozi Mmoja, Bajeti Moja na Ofisi Moja (ambayo ilipewa jina jipya chini ya Taratibu za Viwango vya Uendeshaji wa DaO kama Uendeshaji kama Kitu Kimoja). Katika hatua ya baadaye, Sauti Moja (ambayo ilipewa jina jipya chini ya Taratibu za Viwango vya Uendeshaji wa DaO kama Uendeshaji kama Mawasiliano ya Pamoja) iliongezwa kama moja ya kipengele katika ngazi ya nchi, ambapo kilipata uthibitisho rasmi katika Kongamano la Nne la Viongozi wa Ngazi ya Juu kati ya Serikali Kadhaa kuhusu Mpango wa Kufanya Kazi Pamoja, kule Montevideo mwaka Kati ya 2008 na 2011, Umoja wa Mataifa Tanzania ilianzisha Programu za Pamoja tisa chini ya mwamvuli wa Programu Moja na Programu za Pamoja mbili zinazohusiana na Ofisi Moja na Sauti Moja. Hizi ziliweka mazingira ya ushirikiano katika mashirika 14 ya Umoja wa Mataifa yaliyokuwa yakishiriki, kuunda njia yenye mshikamano na inayoshughulika katika maeneo yote yanayoyagusa kwa pamoja. Kutokana na uzoefu huu, UNCT ilianzisha Programu moja wa Nchi iliyo shikamani kwa ajili ya shughuli za mashirika yote ya Umoja wa Mataifa (yenye ukaazi na yasiyo na ukaazi) kwa kipindi kilichofuatia cha programu: Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP ). Mpango huu Mmoja kwa Tanzania unasaidia ufikiwaji wa Malengo ya Maendeleo Yaliyokubaliwa Kimataifa, Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) na upatikanaji wa haki za binadamu nchini, ikiwemo haki ya msaada wa kiutu kwa wakimbizi. UNDAP inakuza umiliki wa kitaifa na uwajibikaji wa Umoja wa Mataifa kwa kueleza bayana mchango halisi wa Umoja wa Mataifa katika vipaumbele vya taifa kama vilivyofafanuliwa katika mikakati ya taifa ya kupunguza umaskini, MKUKUTA II (Bara) & MKUZA II (Zanzibar). Mpango huo unaendana kabisa na mzunguko wa mipango ya fedha ya ST, ambapo kila Mpango Kazi wa Mwaka (AWP) huanza kutoka Julai 1 hadi Juni 30. Maeneo ya programu yanayosaidiwa na UNDAP yamewekwa kwenye Kielelezo cha 1. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 19

22 Kielelezo cha I: Maeneo ya Ushirikiano ya Mpango wa UNDAP Mpango wa UNDAP unatekelezwa kitaifa na kusimamiwa na Kamati ya Uongozi ya Pamoja ya Serikali ya Tanzania na Umoja wa Mataifa (JSC), ambayo ina wenyeviti wenza wawili, yaani Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa. Wajumbe kutoka wizara kuu na zinazohusika (wakiwemo wa kutoka Zanzibar) huingia kwenye JSC, huku uwakilishi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Kiti cha Marafiki wa Umoja wa Mataifa kama Mwakilishi wa Jamii ya Wafadhili wakiingia kwa kupokezana. Kwa kufuata utaratibu maalumu Mpango wa UNDAP huingiza kwa mpangilio kanuni tano za uendeshaji programu za Umoja wa Mataifa Njia Inayozingatia Haki za Binadamu (HRBA), Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji Wanawake (GEWE), Uendelevu wa Mazingira, Kuendeleza Uwezo na Menejimenti Inayotokana na Matokeo kwa pamoja kuingiza maarifa uwekaji mipango ya programu na utekelezaji. Masuala mtambuka yanayofaa ya kuzuia migogoro, kupunguza hatari ya majanga, usalama wa chakula, wenyeji, kujitolea, VVU na UKIMWI, ajira na kazi zenye hadhi yote pia yanazingatiwa na kuingizwa pale panapostahili. Mpango una Jedwali la Matokeo ya Programu (muundo-dhana wa Matokeo na Vilishi vya Kipekee, Vinavyopimika, Vinavyofikiwa, Vilivyo Halisia na Vyenye Muda maalumu ukiongeza na Vitendo Vikuu) huku likikamilishwa na Jedwali la Usimamizi na Tathmini (M&E) ambalo lina viashiria, misingi, malengo ya mwaka na njia ya kuthibitisha. Mpango wa UNDAP unatekelezwa kwa seti ya AWPs zinazoendana na Jedwali la Matokeo, ili kuendeleza mshikamano wa Umoja wa Mataifa na kwa hiyo kuimarisha ufanisi, tija na kupunguza gharama za uhamishaji fedha. Haya yanaandaliwa kwa mashauriano kati ya wadau, huku likipata kibali cha mwisho kutoka kwa JSC. Matokeo motomoto yanayotokana na mfumo wa usimamizi (kwa kutumia jukwaa la mtandaoni synisys.com/undaprms), huwezesha mapitio ya kila baada ya miaka miwili juu ya hali ya utekelezaji na kufaa kwa mikakati na malengo pamoja na kurandanisha upya pale panapostahili ili kushughulikia kwa ufanisi kwa hali halisi zinazobadilika katika programu. 20 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

23 Zaidi ya hayo, Jedwali la DaO hufafanua malengo mkakati yanayotakiwa na hatua za mchakato wa mageuzi. Hizi zinabeba kazi za ndani zilizobuniwa kuimarisha vigezo vya ubora katika utekelezaji wa programu, kushughulikia masuala ya kufaa na ufanisi kadiri yanavyohusiana na Kiongozi Mmoja, Kuendesha Mambo kama KituKimoja (hapo kabla Ofisi Moja), Kuwasiliana kama Kitu Kimoja (hapo kabla Sauti Moja) na kanuni za msingi za uandaaji programu. Chini ya uwekaji mipango katika UNDAP na mfumo wa ufuatiliaji matokeo, vipengele hivi vinafanyiwa tathmini kali kama ilivyo kwa programu zenyewe. 1.1 Muundo wa ripoti Ripoti ya Mwaka ya Mpango wa UNDAP inaendeleza Ripoti za Mwaka zilizotangulia wakati wa mzunguko wa uendeshaji programu. Inatoa muhtasari wa matokeo yaliyopatikana hadi sasa, na pia changamoto za kila siku na hatua ya kurekebisha ili kupeleka matokeo mbele. Ripoti inaundwa na data zilizo katika ripoti za maendeleo na taarifa za fedha zilizotolewa na kila moja ya Vikosi Kazi 18 vya UNDAP, chini ya Mapitio ya Mwaka Ripoti inaanza na muhtasari mfupi wa mienendo mikuu ya maendeleo nchini Tanzania. Taarifa kuu ya ripoti (Sehemu ya Tatu) inaangazia mafanikio makuu, baadhi ya mifano ya ushirikiano wa mashirika na nyakati za uingizaji kanuni za Haki za Binadamu na GEWE katika Programu, Uendeshaji, Masuala Mtambuka, na Mawasiliano ya Vikosi Kazi. Sehemu hiyo inafuatiwa na data za viasharia kuhusu utoaji fedha, hadi sasa na hasa Sehemu ya Nne inaeleza changamoto kuu zilizojitokeza, pamoja na hatua za kusahihisha zinazotarajiwa kutumika. Ripoti inahitimisha kwa maelezo ya jumla kuhusu utekelezaji wa Mpango hadi wakati huu, kurudia ahadi yetu ya kuendeleza mshikamano, ufanisi na tija ya Umoja wa Mataifa Tanzania tunapojiandaa kwa ajenda ya baada ya mwaka 2015 na UNDAP Taarifa kuhusu utekelezaji upande wa fedha bado ni za muda na kiasi kilichothibitishwa kilikuwa bado hakijapatikana hadi wakati wa kuandaa ripoti hii. Data iliyothibitishwa inatolewa tu na makao makuu ya shirika kwa kufuata kalenda ya mwaka. Taarifa mpya za kiasi kilichothibitiswha pamoja na uchambuzi kuhusiana na Mfuko Mmoja wa Umoja wa Mataifa vinapatikana kwa usomaji kila ifikapo tarehe 31 Mei ya kila mwaka, inaendelea hadi Desemba, katika tovuti ya Ofisi ya Mfuko wa Hisani wa Washirika UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 21

24 Photo: UN/Julie 22 / UNDAP Pudlowski RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

25 2.0 MUKTADHA WA NCHI Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Muungano kati ya Bara na visiwa vyenye mamlaka kiasi fulani vya Zanzibar. Amani na utulivu vimedumishwa tangu uhuru katika ukanda wenye machafuko mengi. Tangu kumalizika rasmi kwa mfumo wa utawala wa chama kimoja miaka ya mwanzoni ya 1990, Tanzania imekuwa ikipiga hatua kuelekea utawala wenye ufanisi wa kidemokrasi huku chaguzi za vyama vingi zikifanyika kwa wakati uliopangwa sambamba na mabadiliko kadhaa ya kisheria na kisera yanayoakisi nia ya dhati ya malengo ya utawala wa sheria nchini. Tanzania imepitia ukuaji wenye utulivu, ikiwa na wastani wa kiwango cha asilimia 7 cha ukuaji kwa muongo uliopita huku makadirio katika mwaka 2015 yakiwa ni asilimia 7.2. Uchumi unaonyesha ishara za mageuzi ya hatua kwa hatua. Uwekezaji katika sekta ya madini, kuongezeka kwa kasi ya matumizi katika miundombinu, mawasiliano ya simu, huduma za fedha, utalii na ujenzi vyote hivi vimekuwa vichocheo vikuu vya ukuaji. Mchango wa sekta ya kilimo katika Pato Ghafi la Taifa (GDP) hatimaye umeshuka kutoka asilimia 29 mwaka 2006 hadi asilimia 23 mwaka 2014, wakati ambapo mchango wa sekta ya viwanda umekua kutoka asilimia 20 hadi asilimia 22.2 katika kipindi hichohicho, huku sekta ya huduma ikichangia zaidi ya asilimia 45 ya GDP mwaka Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwa na maendeleo makubwa katika kudumisha uhai wa mtoto (idadi ya vifo vya watoto chini ya miaka mitano ya 66.5 kwa kila uzazi hai 1,000, vifo vya watoto wachanga kwa kiwango cha watoto 46.2 kwa kila uzazi hai wa watoto 1,000 (Sensa ya Watu na Makazi, 2012) na uandikishwaji katika shule za msingi (asilimia 89.7%, Takwimu za Elimu ya Msingi nchini Tanzania, 2013). Kuenea kwa VVU pia kumepungua, hivi sasa uko katika asilimia 5.1 ya idadi ya watu wazima. Licha ya hali nzuri inayoonekana katika uchumi, bado kuna vitendawili kuhusiana na kufasiri ukuaji huu katika kupunguza umaskini miongoni mwa walio wengi. Mwaka 2014, Tanzania ilishika nafasi ya 159 kati ya nchi 187 katika Faharasa ya Maendeleo ya Watu, ikipata alama ya Kiwango cha umaskini kilipungua kidogo tu kutoka asilimia 33.3 mwaka 2007 hadi asilimia 28.4 mwaka 2012, huku kukiwa na tofauti kubwa ambazo zimegoma kubadilika kati ya mkoa na mkoa na kati ya mijini na vijijini. Idadi ya vifo vya akina mama bado iko juu (432 kwa uzazi hai 100,000) na utapiamlo bado ni tatizo sugu huku kudumaa kukiwa juu katika asilimia 34.7 (Tafiti ya Lishe Kitaifa Nchini Tanzania 2014). Kiwango cha ufikiwaji huduma bora za maji kiko katika asilimia 57.3 na huduma zilizoongezewa ubora za kufanyia usafi maeneo ya vijijini ni asilimia 15. Ubora wa elimu bado unakabiliwa na changamoto kubwa: ni asilimia 30.7 tu ya wanafunzi ndio walifaulu mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi mwaka Tofauti kati ya jinsia ni kubwa, ambapo wasichana na wanawake wakiwa na hadhi ya chini ya kiuchumi, wakikabiliwa na hatari zaidi na wako nyuma katika kupata huduma. Asilimia 72 ya wanawake wanajua kusoma na kuandika ikilinganishwa na asilimia 82 ya wanaume (Utafiti wa Demografia & Afya, 2010). Wasichana wana uwezekano wa zaidi ya mara mbili kufanyiwa vitendo vya ukatili wa kingono kuliko wavulana (Utafiti wa Ukatili Dhidi ya Watoto nchini Tanzania, 2009). Vilevile, wanawake na wasichana wana viwango vya juu zaidi vya kupata VVU kuliko wanaume (Asilimia 6.2 ikilinganishwa na asilimia 3.8, Utafiti wa Viashiria vya VVU & Malaria, 2012). UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 23

26 Kwa muda mrefu, Tanzania imekuwa kimbilio la wakimbizi wanaotafuta hifadhi kutoka nchi jirani zenye mapigano, hasa katika miaka ya 1990 ambapo ilipokea mamia elfu ya wakimbizi kutoka Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. 24 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 Photo: UN Tanzania /Andrew Njoroge

27 Viwango na ukali wa majanga ya hivi karibuni kama vile mafuriko ya kule Kilosa na Kinondoni, ukame kule Longido na Micheweni na kurejea kwa milipuko ya kipindupindu upande wa Bara na Zanzibar vinathibitisha kwamba taifa linapitia ongezeko la ukali, kujirudiarudia, taathira na hatari ya majanga, kwa kiasi Fulani yakitokana na mabadiliko ya tabia nchi. Fahara ya Hatari Duniani ya mwaka 2014 (World Risk Index (WRI)) inaiweka Tanzania katika kundi la hatari ya kiwango cha juu, ikiangukia katika nafasi ya 55 kati ya nchi 177 mwaka 2014 (mpangilio unaanza na nchi zenye hatari zaidi hadi zile zilizo salama zaidi). Makundi ya watu yanayoathirika zaidi wakati wa mafuriko ni watoto, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu kwa sababu ya kushindwa kujinusuru kwa kutoka haraka maeneo ya hatari wakati wa uokoaji. Kwa muda mrefu, Tanzania imekuwa kimbilio la wakimbizi wanaotafuta hifadhi kutoka nchi jirani zenye mapigano, hasa katika miaka ya 1990 ambapo ilipokea mamia elfu ya wakimbizi kutoka Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Hadi mwaka huu, mchakato wa kuwarejesha makwao, na vilevile kutoa uraia kwa baadhi ya jamii za wakimbizi wa muda mrefu ulikuwa umewapunguza wakimbizi na kuwabakiza kiasi cha wakimbizi 64,000. Hata hivyo, kuibuka kwa machafuko mapya nchini Burundi hivi karibuni kulileta mmiminiko wa wakimbizi nchini na idadi iliitikisa tena Tanzania ilipowapokea zaidi ya 140,000. Changamoto za kuleta ukuaji jumuishi ambao una athari chanya kwa Watanzania walio wengi yanabainishwa na kuelezwa katika nyaraka zinazofuatia za MKUKUTA na MKUZA II. Katika ngazi ya kitaifa, Mpango wa pili wa Maendeleo ya Taifa wa Miaka Mitano (FYDP II), ambao utekelezaji wake utaanza tarehe 1 Julai, 2016, vipaumbele va ukuaji wa uchumi ulio jumuishi huku pia ukihamasisha maisha bora ya jamii na utawala bora kwa raia wote. Vivyo hivyo, mkakati utakaofuatia MKUZA II kwa Zanzibar umebainisha mada zifuatazo na maendeleo zaidi: ukuaji uchumi ulio jumuishi na endelevu; uendelezaji wa mtaji watu; huduma bora kwa wote; uendelevu wa mazingira; na utawala bora. Umoja wa Mataifa utaendelea kutoa msaada katika maeneo yote haya ili kuwezesha kuimarika kwa ubora wa maisha ya Watanzania wote katika sekta zote, hasa wale walio katika hatari zaidi na makundi ya watu ambao ni vigumu kuwafikia. UNDAP / 25 RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 25

28 26 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge

29 3.0 MPANGO WA UNDAP : MATOKEO YALIYOKWISHA PATIKANA 3.1 UKUAJI WA UCHUMI NA UTAWALA WA UCHUMI Taasisi kuu za kitaifa zianzishe / ziimarishe sera na mikakati yenye ushahidi ya maendeleo ya kiuchumi yanayowalenga maskini Matokeo haya yanaweka msingi wa ushahidi kwa ajili ya muundo-dhana wa sera ya ukuaji uchumi wenye kulenga maskini nchini Tanzania na unaopanua uwezekano wa kuwepo kwa kazi zenye hadhi. Umoja wa Mataifa inashirikiana na washirika katika sekta muhimu nyingi ili kuzalisha na kutumia data sahihi kwa ajili ya programu bora, wakati ikihakikisha kanuni za msingi kama vile jinsia na uendelevu wa mazingira zinazingatiwa. Hadi sasa kuna matokeo mengi yaliyokwishapatikana, yakiwemo: Kama ishara ya kufikiwa kwa uendelevu, Kitengo cha Upelelezi wa Mambo ya Viwanda cha Wizara ya Viwanda na Biashara (MIT) kiliandaa mihtasari mitatu ya sera ya sekta ya ufundi wa viwanda vya uzalishaji ili kutathmini hali ya utendaji wa sekta nzima na hasa viwanda vya kilimo. Mihutasari hiyo itatumiwa kama sehemu ya miongozo katika Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo unaofuatia, kwa kuweka mkazo kwenye maendeleo ya viwanda, na kwa mapitio ya Mkakati Fungamani wa Maendeleo ya Viwanda. Sera ya Taifa ya Biashara, Sera ya Mali za Kiakili (Ubunifu) na Mkakati wa Viwanda vya Nguo na Vitambaa ilipitiwa kwa kuzingatia jinsia, kuweka msingi wa ushahidi kwa ajili ya mapendekezo kwenda MIT. Utafiti wa kubaini taratibu bora za mahalia pamoja na fursa za kutafuta fedha kutoka sekta binafsi kwa kuweka mkazo kwenye GEWE kuhusiana na Umaskini na Mazingira ulikamilika. Uchambuzi utatumika kusaidia utekelezaji wa jitihada zinazokazia sana jinsia kwa lengo la kupanua taratibu bora zilizopangwa. Rasimu ya Sera ya Taifa ya Mazingira iliandaliwa kama matokeo ya mashauriano na wadau. Michakato ya mashauriano pia iliwezesha uingizwaji wa kiungo cha Umaskini na Mazingira katika mchakato wa mapitio ya Mpango wa Miaka Mitano wa Maendeleo. Sera na Sheria ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (ST&I) iliyopitiwa imeandaliwa na wadau wamehusishwa. ST&I itaunganishwa katika miundo-dhana ya sera za maendeleo ya taifa na ubunifu. Mpango Kazi wa Ajira ya Vijana Zanzibar ( ) ulikamilishwa na kusambazwa kwa ajili ya utekelezaji. Sekta muhimu zimeanza utekelezaji, huku mafunzo yakitolewa katika biashara ya kilimo na TEHAMA. Kituo cha Kulea Teknolojia na Biashara (ZTBI) kilianzishwa katika Taasisi ya Karume ya Sayansi na Teknolojia (KIST) mapema mwaka 2015 na MESWYWC kwa kulenga kilimo, TEHAMA na Utalii. Kituo cha ZTBI kimewekewa zana muhimu za miundombinu ya TEHAMA kama vile mfumo wa kuhifadhi data na timu ya menejimenti yenye uwezo wa kusaidia kukuza mawazo ya biashara ya vijana. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 27

30 Uwezo wa taasisi mbili za kusaidia viwanda, TIRDO na TEMDO, umepanuliwa katika uchambuzi makini wa chakula na usanifu wa software ili kuhakikisha kunakuweko na huduma bora kwa Biashara Ndogo na za Kati (SMEs) za kusindika vyakula. Kuimarisha maeneo makuu ya maendeleo ya jinsia katika Wizara ya Viwanda na Biashara kumeleta matokeo katika kuhusika kwa uandaaji wa miongozo kwa ajili ya kuanzisha madawati ya jinsia mipakani na vilevile mchango wake kwa uendelezaji wa masuala ya jinsia katika bajeti ya mwaka ya Wizara. Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs), taasisi za kusaidia kilimo na wakulima wadogo ili kuongeza uzalishaji wa kilimo, kupata masoko na kuleta usalama wa chakula Umoja wa Mataifa inaelekeza msaada wake katika sekta ya kilimo chini ya Matokeo haya katika vipengele vikuu vitatu: kubadilishana maarifa bora katika uzalishaji wa kilimo na utunzaji chakula; kuimarisha masoko; kusaidia vyama vya wakulima ili kutoa huduma bora na nafuu na bidhaa bora kwa wanachama wao. Vidokezo katika maendeleo ya hivi karibuni kabisa ni pamoja na: Mfumo wa Taifa wa Kuchambua Data za Ushirika (CODAS) mfumo wa kompyuta wa data wa kukusanya na kuchambua data za ushirika kuhusiana na hali na mienendo ya ukuaji ulikamilishwa na kutengenezwa kuwa kiendesha programu ya kompyuta. Taarifa zilizozalishwa huangazia utungaji sera na utekelezaji. Wajumbe na wafanyakazi wa vyama vya ushirika vya mambo ya fedha wakiwakilisha wajumbe 20,000 na vyama vya ushirika vya fedha 51 kutoka katika mikoa 8 walijengewa uwezo katika usimamizi wa fedha, uhamasishaji rasilimali/akiba na usimamizi wa mikopo. Vyama vya ushirika vilivyoshiriki kwa hiyo vimewezeshwa kuongeza ubora wa huduma za fedha vinazotoa kwa wanachama wao, kuendesha miradi yao ya mikopo kwa ufanisi na kuhamasisha usimamizi bora wa rasilimali zao. Kuanzisha vyama vya ushirika kulihamasishwa miongoni mwa vijana pia mipango kazi inayolenga ajira za vijana ilikubaliwa katika Wizara, Idara na Wakala 4 na LGAs 22 na Vyama vya Vijana katika mikoa 8. Kuunga mkono mnyororo wa viongeza thamani, vyama vya ushirika vya akina mama vya ufugaji ng ombe wa maziwa katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro kulisaidia kufanya manunuzi ya vifaa vya kusindika na kufungasha ambavyo kwa sehemu vinajiendesha vyenyewe na kuwanufaisha zaidi ya wanachama wa vyama vya ushirika wafugaji 300 na kuleta ongezeko kubwa katika kukusanya na kuchakata maziwa yaliyopatikana. Vyama vitano vya wakulima katika mikoa ya Dodoma na Singida wakisaidiwa kupitia mradi wa Kununua ili Kuleta Maendeleo, waliunda vikundi 12 vya akina mama vyenye wanachama 241. Vikundi vilipewa mashine zinazojiendesha na kuokoa nguvukazi na hivyo kuwawezesha wengi kupata fursa ya kusimamia vizuri mapato kutokana na uendeshaji huo katika jamii zao. Zaidi ya vyama 100 vya Wakulima vilitoa wastani wa Tani za Metriki 20,000 za mahindi kwenda katika Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) katika msimu wa masoko wa 2014/2015. Wakulima wadogo 5,000 katika mikoa 7 walitia saini mikataba na kuuza mahindi katika kampuni binafsi za usagishaji, baada ya kupata mafunzo kuhusu namna ya kusimamia mazao baada ya mavuno, utunzaji na kujenga uelewa juu ya mikataba. Kitabu cha Uendeshaji cha NFRA kilitolewa ili kueleza Viwango muhimu vya Hatua za Uendeshaji na wajibu wa NFRA kwa hadhira ya nje, na wafanyakazi walilipiwa gharama ili kushiriki katika mafunzo ya kimataifa kuhusu kozi za Uwekaji Mipango katika ngazi ya utawala na usimamizi wa Bajeti. Tani Metriki 34,000 za mahindi ziliuzwa kutoka NFRA kwenda Umoja wa Mataifa ili kukidhi mahitaji ya kiutu ya chakula katika nchi jirani zenye migogoro. 28 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

31 Wizara, Idara na Wakala; Mamlaka za Serikali za Mitaa na Wadau Wasio wa Kiserikali wanaohusika waimarishe miundo na sera zinazohamasisha sekta za biashara na biashara ndogo na za kati zinazofaa na zinazolenga maskini Lengo hili linahimiza uwekezaji mkubwa zaidi na maendeleo ya uchumi wa mahalia katika sekta kuu za uzalishaji na ubunifu, kwa kushirikiana na sekta binafsi. Matokeo kadhaa yamekwishapatikana katika miezi 12 iliyopita: Maghala 30 yalifanyiwa matengenezo na biashara ilianza chini ya Mpango wa Masoko kwa Kutumia Ghala la Pamoja (COWABAMA). Mpango huo humuunganisha mkulima mdogo na vyanzo vya mahitaji ya bidhaa zake na hivyo kuimarisha uwezo wake wa kupatana bei kupitia mauzo ya mzigo mkubwa kwa msimu. Makundi 25 yasiyo rasmi ya akina mama yenye wajumbe zaidi ya 400 katika mkondo wa usafirishaji Tanzania walisaidiwa kurasimisha na kuanzisha Vyama Vya Ushirika vya Akiba na Mikopo (SACCOS), huku wakipewa mafunzo ya usimamizi wa fedha. Uunganishwaji na fedha za mzunguko ( Kupunguza Unyonge katika Mkondo wa Usafiri wa Kusini mwa Afrika ) ulianzishwa kwa hiyo kuwezesha upatikanaji wa huduma za fedha kwa watu zaidi ya 800 kwa mkopo wenye thamani ya dola za Marekani 200,000 (sawa na shilingi milioni 440) zilizotolewa katika uwekezaji kwenye fursa za kujipatia riziki. Ujumuishwaji pamoja wa vyama vya ushirika zaidi ya 20 vya wafugaji wa ng ombe wa maziwa Kilimanjaro uliwezeshwa, na kuwaleta pamoja wakulima/wazalishaji zaidi ya 3,000 ili kusindika, kufungasha na kuuza bidhaa kwa pamoja, kwa hiyo kuwaongezea uwezo wa kupatana bei na kuwaletea kipato zaidi na fursa ya kupata mahitaji, masoko na huduma nyingine. Maeneo mawili ya kuchinjia katika wilaya za Iringa na Mbeya yalipatiwa vifaa, kujengwa vizuri zaidi na mafunzo ya usimamizi yalitolewa. Kujenga upya maeneo hayo kumesaidia kuweka mazingira safi na kwa hiyo kuwasaidia walaji kupata nyama yenye ubora zaidi. Klasta ya kusindika korosho yenye makundi matatu ya wasindika korosho imeanzishwa na sasa inafanya kazi kutokea katika eneo la viwanda la SIDO baada ya eneo hilo kufanyiwa marekebisho na wao kupatiwa vifaa. Kituo cha Biashara kimezinduliwa katika Chama cha Wenye Biashara, Viwanda na Kilimo wa Zanzibar (ZNCCIA) ili kutoa huduma kama vile taarifa za biashara (kwa mfano bei za masoko, teknolojia inayopatikana na sheria), mafunzo ya TEHAMA na programu ya uendelezaji watoa huduma kwa sekta binafsi. Huduma hizi zimepanua msingi wa ujuzi na stadi za makampuni yaliyopo na yanayotarajiwa kuanzishwa pia biashara za kaya ili kuongeza uzalishaji, na pia kuiwezesha ZNCCIA kupata picha nzuri zaidi miongoni mwa sekta binafsi kama mtoa huduma. Huduma hizi ni za bure ili kuhakikisha kunakuwepo na uendelevu wa kifedha. Utaratibu wa mtu mwenye uzoefu kumfundisha asiye na uzoefu hasa kuhusiana na masuala ya kuingiza wanachama na kuhakikisha wanadumu ulitolewa kwa maofisa watendaji na wafanyakazi wa sekretariet katika ofisi tisa za mikoa za Vyama vya Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo. Zaidi ya wafanyabiashara 300 wapya waliandikishwa na/au kuhuisha uanachama wao. Vihifadhia data vya ofisi za mikoa yote tisa vilihuishwa na kuongezewa taarifa mpya ili kuwezesha usanifu wa njia za uchukuaji hatua za kulenga, usambazaji taarifa wenye tija na kujenga mitandao ya uhusiano miongoni mwa wafanyabiashara wadogo, wa kati na nyinginezo. Mikutano mitatu ya mijadala ya biashara iliandaliwa, kupitia mikutano hiyo, zaidi ya wajasiriamali 240 walipata maarifa kuhusu haki za mali za ubunifu, ushindani katika biashara, usajili wa biashara, viwango vya ubora na njia za kupata mikopo. Matokeo yake, zaidi ya wajasiriamali zaidi ya 40 wameandaa ukaguzi wa mali za kiubunifu, watano waana usajili katika IPs na watatu walisajili biashara kupitia njia ya mtandao na kwa hiyo kuokoa fedha za uendeshaji na kuhamasika kurasimisha biashara. Tanzania Global Compact Local Network ilianzishwa, ikihamasisha wafanyabiashara kuzingatia, kuunga mkono na kupitisha (ndani ya maeneo yao wanayoweza kuleta ushawishi) seti kuu ya amali katika maeneo ya haki za binadamu, viwango vya kazi, mazingira na upigaji vita rushwa. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 29

32 Taasisi zinazostahiki kujenga uwezo wa taifa katika kuhamasisha ushirikiano wa kikanda na biashara ya kimataifa Uwezo wa kujihusisha katika biashara ya kikanda na kimataifa unajengwa chini ya Lengo hili, katika ngazi ya uchumi wa mahalia na ule mpana. Uingiliaji kati huhamasisha mwingiliano unaofaa kati ya sheria, huduma na viwango vya biashara ili kuleta na ushindani katika ushirikiano katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, sambamba na ushirikiano katika kubadilishana maarifa kuhusu kufaa na matumizi ya wazalishaji wadogo. Mafanikio hadi sasa ni pamoja na: Ulianzishwa utaratibu wa uandaaji nyaraka kuhusiana na leseni katika mfumo wa Kanuni za kielektroniki nchini Tanzania unaosimamiwa na Kituo cha Uwekezaji (TIC). Kwa kila leseni, mfumo wa Kanuni za kieletroniki unatoa taarifa juu ya hatua, matokeo, mahitaji na uhalali wa kisheria, gharama, taasisi/watu wanaohusika na namna ya kupata msaada wakati wa shida. Mfumo unatoa fursa kwa wizara zinazohusika kutathmini hatua ili kubaini uwezekano wa kurahisisha. Wafanyakazi 33 wa Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogovidogo (SIDO) na wawili wa TanTrade walifundishwa na kupewa ujuzi kuhusu Usimamizi wa Taarifa za Biashara. Kutokana na jitihada hiyo, washiriki wamekwishaandaa Wasifu wa Kiufundi wa Uchumi, wakitumia yaliyomo kwenye mtandao ili kuandaa rasimu, mapendekezo ya kibiashara/masoko kwa SMEs na kuanzisha viunganisho na masoko ya kimataifa. SIDO hivi sasa inawasaidia wazalishaji wa mafuta ya alizeti kuhusiana na masoko ya nje ya nchi kwa kutumia zana za TEHAMA. Ushirikiano wa SIDO na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake wa Tanzania umeanzisha majukwa katika vituo kumi vya mipakani vya Tanzania. Hivi hutoa fursa rasmi kwa wafanyabiashara wanawake ili kukutana na watumishi wa serikali kuanzisha mitandao na kwa hiyo kupata taarifa na mafunzo. Majukwaa hayo hivi sasa yametambuliwa rasmi na Serikali huku Wenyeviti wake sita wakiwa pia wajumbe wa Kamati ya pamoja ya Mipaka, kwa hiyo kuwezesha utetezi wenye ufanisi wa wanawake wafanyabiashara. Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge 30 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

33 Mafunzo ya awali kuhusu sheria zinazoongoza biashara ya mipakani yamewajengea uwezo wanawake ili kutumia maeneo rasmi ya kuvuka mipaka, huku fursa za kiuchumi zikiongezeka kwa zaidi ya wanawake 1,000. Biashara 26 nyingine zimerasimishwa na idadi ya wanawake wenye bidhaa zilizopewa vibali na Shirika la Viwango la Tanzania (TBS) ikiongezeka kutoka asilimia 14 hadi 31, yote yakiwa ni baada ya mafunzo kuhusu mahitaji ya biashara ya kimataifa (yakiwemo ya Mali za Ubunifu, utunzaji nyaraka na mikataba ya biashara) kutolewa. Kuhusishwa kwa maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania katika mafunzo kumepunguza mivutano na wanawake wafanyabiashara wa mipakani, jambo lililofanya kupungua kwa bidhaa zilizoshikiliwa na mamlaka utaratibu ambao hapo kabla uliwafedhehesha sana wanawake walioshikiliwa na maofisa hao. Mwongozo uliorahisishwa kwa ajili ya wasafirisha biadhaa nje ya nchi wadogo na wa kati uliandaliwa. Mwongozo huo unawapa maarifa wasafirishaji hao wa Tanzania kuhusu mahitaji, taratibu na sheria na kwa hiyo kuongeza uwezo wao wa kuyafikia masoko ya kikanda na kimataifa. Tume ya Haki katika Ushindani (The Fair Competition Commission (FCC)) ilijengewa uwezo ili kukuza maarifa ya menejimenti, mawasiliano ya ndani na michakato ya biashara ili kukabiliana na bidhaa bandia. Ili kuleta ufanisi zaidi, vyombo vya habari vilipewa mafunzo kuhusu namna ya kutangaza juu ya bidhaa bandia sambamba na utoaji wa matangazo ya redio na televisheni ili kukuza uelewa wa jamii juu ya bidhaa feki na madhara yake katika uchumi na afya ya watumiaji. Wizara, Idara na Wakala zinazohusika kwa pamoja na Wadau Wasio wa Kiserikali wakuze ujuzi na programu za ujasiriamali ili kuimarisha uzalishaji wa nguvukazi na kutengeneza nafasi zaidi za ajira Lengo hili kwa namna ya pekee linawahusu wanawake na vijana ili kutoa msaada wa kiujasiriamali na kuleta matumaini zaidi ya ajira. Mafanikio makubwa yaliyopatikana karibuni ni pamoja na: Maofisa wa Wizara ya Kazi na Ajira na Shirika la Viwango walijengewa uwezo wa kuchambua kwa usahihi viashiria vikuu vya soko la ajira: ajira, ukosefu wa ajira, uduni wa ajira n.k. kwa ajili ya Utafiti Kamili wa Hali ya Ajira wa Msaada zaidi wa kiufundi na kifedha ulitolewa ili kufanya uchambuzi wa kina kuhusu masuala ya jinsia, kuwezesha uingizwaji katika mkondo mkuu wa usawa wa jinsia na masuala ya kutokuwepo kwa ubaguzi katika ripoti ya Utafiti Kamili wa Hali ya Ajira ya JEDWALI TOFAUTI KUHAMASISHA AJIRA YA VIJANA Mkutano wa siku mbili kuhusu ajira ya vijana kwa ajili ya Wakuu wa Mikoa (RCs) iliandaliwa na MoLE kwa ufadhili wa Umoja wa Mataifa ili kutoa jukwaa kwa watoa uamuzi kubaini suluhisho kwa tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana nchini Tanzania. Mkutano huo ulikwa na wajumbe 226 wakiwemo wawakilishi kutoka katika Wizara zinazohusika na taasisi nyingine za serikali, wakuu wa mikoa, wafanyakazi na vyama vya waajiri, sekta binafsi, na washirika wa maendeleo. Uzoefu, mafunzo yaliyopatikana, taratibu nzuri na mapendekezo yaliwekwa mezani na mikoa, sekta binafsi na vijana wenyewe na vilevile uzoefu wa dunia kuhusu uhamasishaji ajira ya vijana. Matokeo yake, Wakuu wa Mikoa walitia saini tamko la pamoja kuonyesha dhamira yao ya kuingiza suala la ajira ya vijana katika mipango ya mikoa na wilaya na kuhakikisha kwamba rasilimali za lazima zielekezwe katika kuhamasisha ajira ya vijana. Wakuu wa mikoa pia waliahidi kupelekea ripoti za kila robo mwaka katika MoLE, kuhusu utekelezaji wa mipango kazi hiyo iliyokubaliwa. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 31

34 JEDWALI TOFAUTI: KUHUISHA SEKTA YA VIUNGO YA ZANZIBAR Mzee Mussa alizoea kuuza pilipili kandokando mwa barabara kwa wapiti njia na watalii mmoja mmoja katika ncha ya kaskazini magharibi mwa Unguja, ambacho ndio kisiwa kikuu cha Zanzibar. Viungo vyake hivyo karibu vitapatikana kwa wingi katika hoteli kubwak katika mkoa wote na atajipatia fedha zaidi. Tofauti ikiwa ni: taswira ya biashara. Shirika la Biashara la Serikali ya Zanzibar linapanga kuzindua tangazo moja la kwanza kabisa la viungo vinavyopatikana visiwani humo, Zanzibar Exotic Originals, ambavyo vitafungashwa na kupewa sura ya nje iliyosanifiwa vizuri na ITC. Kwa kuanzia, viungo hivyo vitatangazwa kwa watalii wanaofika visiwani humo, kisha Tanzania Bara na hatimaye kusafirishwa hadi nchi jirani na masoko mengine zaidi. Kwa kuweka sura ya kibiashara katika bidhaa hizi, tunaona faida yake ya kweli, alisema Nasor Mazrui, Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko wa Zanzibar. Viungo vyenye nembo ya Zanzibar vimefungashwa katika namna ya kuwavutia wageni. Watalii wanaokuja visiwani wanapenda kununua bidhaa za mahalia za ubora wa juu, na tangazo hili moja la bidhaa linakidhi mahitaji hayo, alisema Julian Raphael, Katibu Mkuu wa Wizara. Kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo maofisa wa serikali, wakulima na sekta ya hoteli, ITC imesaidia kuweka mkakati na kutangaza sura ya visiwa na bidhaa zake za viungo (karafuu na vinginevyo vikiwemo, iliki na pilipili). Msaada wa ITC ulijumuishia: mafunzo kwa wazalishaji ili kuandaa na kuhifadhi viungo katika chupa; kuanzisha na kutoa mipango ya biashara kwa kampuni za nyumbani; kuendeleza na kutoa Mwongozo Kamili kuhusu Picha ya Biashara na Usanifu wa Picha ya Biashara; kusanifu lebo za bidhaa na kutafuta chupa na lebo zinazofaa na teknolojia ya kupiga chapa; kuanzisha wavuti kwa ajili ya uhamasishaji na utafutaji masoko kwa njia za kidijitali; kuandaa vipeperushi na vigusaji kwa ajili ya utangazaji maendeo ya uwanja wa ndege, n.k. 32 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

35 Mipango Kazi ilianzishwa ili kuhakikisha uingizwaji kamilifu wa viwango vya ajira vya kitaifa na kimataifa na pia mifano mizuri ya utendaji kuhusiana na utoaji wa huduma za ajira na Wizara ya Kazi na Ajira (MoLE), Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA), vyama vya wafanyakazi na waajiri baada ya mafunzo yanayostahili. TaESA ilijengewa uwezo wa kuanzisha Kituo Kimoja cha Taarifa kwa ajili ya kutoa huduma zenye ufanisi na tija kuhusu ajira kwa watafuta kazi, huku kukiwa na mipango ya kuanzisha vituo vingine Mwanza na Arusha. Hadi sasa, zaidi ya vijana wanawake na wanaume 317 wamenufaika na huduma za kituo hicho. Uanzishwaji wa muundo-dhana wa taifa wa uanagenzi kwa upande wa Bara ulianzishwa, kusanifiwa ili kueleza miundo ya utawala kwa programu za uanagenzi nchini Tanzania. Mara utakapokamilika na kuanza kazi, muundo-dhana utatoa mwongozo kwa waendelezaji na watoaji wote wa uanagenzi. Pia utaweka msingi ambao Serikali inaweza kuutumia kuanzisha na kutekeleza vifurushi vya motisha, sheria zinazosaidia na kuhakikisha kuanzishwa kwa programu za uanagenzi zenye ubora. Programu ya kwanza kabisa ya uanagenzi katika tasnia ya hoteli ilizinduliwa na Serikali, huku ikilenga kupokea wanagenzi wa mwanzo 100. Muundo-dhana wa Taifa wa Uanagenzi ulikamilishwa, jambo lililofungua njia ya kuingizwa kwa uanagenzi katika mtaala wa elimu unatumika mashuleni. Huu umekamilishwa na mafunzo kazini kwa walimu na wakufunzi mahiri wa elimu ya ujasiriamali katika Vituo na Vyuo 74 vya Ualimu. Hifadhi data ya vikundi vya kibiashara vya wanawake, pamoja na shughuli zao za uzalishaji mali tayari imeandaliwa kupitia utafiti wa ukusanyaji taarifa za mahalia upande wa Zanzibar. Ufuatiliaji utajumuisha ujenzi wa uwezo katika utetezi na upatikanaji wa taarifa za masoko katika sekta za kipaumbele ili kuimarisha fursa na manufaa ya kiuchumi. Wanawake wa vijijini 1,099 kutoka katika makundi rika ya kusaidiana mkoani Kilimanjaro walipata mikopo ipatayo 2,364 kwa ajili ya shughuli za kujiingizia kipato, ambayo ilitokana na uwekaji wao akiba. Matokeo yake, wanawake 464 wamepanua shughuli zao na/au kuanzisha biashara 628 huku wanawake 972 wakitoa taarifa za kukua kwa kipato chao na kuongeza ubora na wingi wa chakula kinacholiwa katika kaya zao, wakimudu kulipia huduma za afya na ada za shule na kuwapatia mahitaji watoto wanaoanza shule. Wanawake 187 walipata msaada wa kisheria kupitia huduma za nasaha za kisheria, upatanisho na kupeleka mashauri mahakamani, na wanawake 1,079 zaidi walifikiwa na watoa huduma wa serikali wenye mafunzo na huduma za kisheria. Baada ya mafunzo ya masoko na ziara za mabadilishano zilizoandaliwa na KWIECO, jumla ya wanawake 536 mkoani Kilimanjaro wamepata masoko yanayofaa kwa bidhaa zao. 3.2 MAZINGIRA Wizara, Idara na Wakala pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa zinazohusika ziingize masuala ya kuendana na kukabili mabadiliko ya tabia ya nchi katika mikakati na mipango yao Katika eneo hili la kwanza la matokeo, uwezo unajengwa ili kuunda, kuchukua na kutekeleza mikakati ya kuendana na mabadiliko ya tabia nchi katika ngazi za mahalia na kitaifa. Matokeo maalum ni pamoja na: Mkakati wa Mabadiliko ya Tabia Nchi wa Zanzibar ulikamilishwa na kuzinduliwa na Rais wa Zanzibar wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mazingira (WED) mwezi Juni, Uendelezaji wa Mpango Kazi uliokubaliwa kwa ajili ya utekelezaji wa Mkakati pia umekwishaanzishwa. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 33

36 Wakati wa maadhimisho ya WED, jitihada za kujenga uelewa ukiwalenga watu binafsi na taasisi uliweka mkazo katika wajibu wa wote kuhusiana na matumizi endelevu ya rasilimali, kwa kutambua kasi kubwa ya kuongezeka idadi ya watu. Mada iliyobeba ujumbe huu wa utetezi ilikuwa: watu bilioni 7, Sayari Moja, Tumia kwa Uangalifu. Ujumbe wa utetezi ulisambazwa nchi nzima kupitia vyombo vya habari na mikutano ya hadhara, ambapo inakadiriwa kuwa ujumbe uliwafikia walau asilimia 80 ya watu nchini. Miundo ya Kitaifa ya Utafutaji Fedha kwa ajili ya Mabadiliko ya Tabia Nchi ilianzishwa kwa upande wa bara na Zanzibar. Miundombinu itashughulikia masuala ya kisheria, kifedha, na miundo-dhana ya utekelezaji. Mara itakapoanza kazi, hii itaisaidia nchi kupata na kufuatilia fedha zinazotolewa nchini na kimataifa kwa ajili ya mabadiliko ya tabia ya nchi, ikiwepo Mfuko wa Tabia ya Nchi ya Kijani (Green Climate Fund), mifumo ya fedha ya pande nyingi na ile ya ushirikiano baina ya pande mbili. Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira (VPO-DoE), Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais (1st VPO), Baraza la Taifa la Mazingira (NEMC), Wizara ya Fedha (MoF) na Mamlaka za Serikali za Mitaa zilizochaguliwa zilijengewa uwezo ili kuelekeza usimamizi wa mabadiliko ya tabia ya nchi katika mipango na mikakati ya maendeleo ya wilaya 37. Miundo-dhana ya kitaasisi kwa ajili ya usimamizi wa mabadiliko ya tabia ya nchi nchini vilevile uliimarishwa kuptia kuundwa na uendeshaji wa Kamati ya Uongozi ya Taifa ya Mabadiliko ya Tabia ya Nchi na Kamati ya Taifa ya Ufundi ya Mabadiliko ya Tabia ya Nchi. Utafiti wa kubadili nishati Zanzibar ulifanyiwa majaribio kama sehemu ya uhamasishaji mpana wa teknolojia za nishati mbadala zilizo rafiki. Hii ilihusisha usambazaji wa majiko ya gesi ya ethano katika kaya 130 na nishati inayozalishwa na mabaki katika kiwanda cha Sukari cha Zanzibar. Matokeo ya awali ni ya kutia moya, huku jamii zikitaka uzalishaji uongezwe. Vituo mbalimbali vidogovidogo vya uzalishaji umeme wa maji vilianzishwa, vikiwemo vya uwezo wa Kilowati500 kule Wilaya ya Mbinga, hivi sasa kikitoa umeme unaotosha katika kaya 120 na biashara ndogondogo zipatazo 20. Kituo cha Mafunzo cha Mkoa cha Walalahoi (The Barefoot Regional Training Centre) kilianzishwa na kuzinduliwa rasmi na Rais wa Zanzibar. Hivi sasa kuna wanawake wanaojifunza teknolojia ya nishati ya jua katika kituo hicho na watakwenda kufunga taa hizo za nishati ya jua katika nyumba za kaya za vijini kwao, vijiji visivyofikiwa na umeme. Vilevile wanakuwa na wajibu wa kufanya matengenezo na kurekebisha walau kwa miaka mitano. Zaidi ya hayo, kituo kinatoa mafunzo ya mwanzo kwa wahandisi wanawake wa nishati ya jua kutoka Bara na Zanzibar kuhusu teknolojia za umeme jua na LED. Vituo vya hali ya hewa vinavyojiendesha 16 na vifaa vya kupimia hali ya hewa vilinunuliwa kwa ajili ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania na Mabonde ya Mto Pangani na Mto Ruvuma. Vifaa vitaongeza ubora za ukusanyaji, uchambuzi na usambazaji wa taarifa za hali ya hewa nchini kwa ajili ya kuwaongoza wakulima na mamlaka zinazosimamia rasilimali za maji. Maeneo 33 katika mikoa ambayo hukumbwa na baa la njaa yalisaidiwa kwa ushirikiano na Mamlala za Serikali za Mitaa ili kuandaa mali zifuatazo kujenga/kurekebisha malamba yenye uwezo kuanziaha lita za ujazo 40,000/ 100,000m3, miti 12,000, kujenga/kurekebisha mifereji miwili ya umwagiliaji, kusafisha mashamba ya ekari 1,000 kwa uzalishaji wa maembe, alizeti na ufuta. Mikutano ya Jamii ya Ulengaji na Usambaji wa Kulenga (CMTD) ilitoa miongozo kwa jamii kuhusu ulengaji wanufaikaji, na pia usimamizi wa mali za chakula na kilimo zilizopatikana. 34 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

37 Wizara, Idara na Wakala pamoja na Mamlaka za Serikali za Mitaa zinazohusika ziimarishe usimamizi wa sheria na kanuni za mazingira ili kulinda mifumo ya ikolojia, uanuwai na usimamizi endelevu wa rasilimali za asili Mashirika ya Umoja wa Mataifa chini ya Lengo hili yanashirikiana ili kusaidia watendaji ndani ya nchi na mahalia kusimamia kwa ufanisi zaidi rasilimali za mazingira na za asili. Mafanikio yaliyokwishapatikana hadi sasa ni pamoja na: Azimio la Arusha lililopitishwa wakati wa mkutano wa kikanda ili kukabili uhalifu dhidi ya wanyama pori. Azimio linatoa wito wa kuchukuliwa hatua kamilifu ili kuimarisha ushirikiano baina ya nchi moja na nyingine. Utafiti kamili ulifadhiliwa, ukionyesha tathmini ya utekelezaji na uoanishaji wa sera, na vilevile uwezo wa taasisi mama wa kusimamia rasilimali za asili. Matokeo ya utafiti (ambayo yanapendekeza ugawaji wa kutosha wa bajeti ili kuleta uelekezwaji wenye ufanisi wa kanuni za Usimamizi Endelevu wa Ardhi, ukiwekewa mkazo na msukumo wa dhati wa kisiasa) vyote vimepelekwa katika Ofisi ya Makamu wa rais ili kuingizwa katika mapitio ya Sera ya Mazingira. Mkakati na Mpango Kazi wa Taifa wa Bioanuwai (NBSAP) ulipitiwa upya, ukitumiwa kuanzisha mfumo wa wazi wa uratibu. Huo wa mwisho unahamasisha matumizi yenye kuzingatia uhifadhi na uendelevu wa bioanuwai na pia kutunza bidhaa na huduma zinazotokana na mfumo wa ikolojia. Kupandishwa hadhi kwa Mbuga ya Saadani ili kuwa Hifadhi ya Biosfia kuliwezeshwa, ambapo mchakato shirikishi ulizingatiwa. Programu hiyo iliimarisha maarifa na ujuzi kwa ajili ya uhifadhi wa mifumo ya kiikolojia, bioanuwai na usimamizi endelevu wa rasilimali za miongoni mwa wadau wakuu, kama vile NEMC na 1st VPO, na pia jamii za mahalia. Taarifa kuhusu Mifumo ya Kiikolojia iliyo katika Mhamo kwenda Uchumi wa Kijani na Wajibu wa REDD+ katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilizinduliwa, huku matokeo ya taarifa hiyo yakitumika kutoa miongozo ya menejimenti ya rasilimali kwa ufanisi. Utafiti wa pili uliopewa kichwa cha habari Mazingatio ya Jinsia katika Shughuli za Miradi ya Kusimamia Uendelevu wa Ardhi katika Nyanda za Juu Mkoani Kilimanjaro: Mambo ya Kujifunza na Mtazamo wa Baadae umesambazwa kwa wadau wanaotekeleza, kuhakikisha ushirikishwaji mkubwa wa wanaume na wanawake katika shughuli za miradi kwa ajili ya kipato zaidi. Jamii zilizo katika Hifadhi ya Biosfia ya Usambara Mashariki ilipewa vifaa pamoja na ujuzi na maarifa ya kijasiriamali, mazingra na bioanuwai. Biashara mbili mpya za kijani zimeanzishwa hivi karibuni, huku kukiwa na nyongeza ya wakulima 199 waliopewa mafunzo ili kuchukua njia ya uendeshaji kibiashara kwa kuleta mtawanyiko zaidi katika uchumi mahalia. Kaya zinazoongozwa na wanawake na zilizo katika hatari ya kukumbwa na njaa zilipewa kipaumbele kwa ajili ya kusaidia kujikimu kimaisha. Programu ya kuchukua sampuli za kimazingira kuhusiana na uchimbaji madini ya urani zilianzishwa na Tume ya Nishati ya Atomiki ya Tanzania. Wajumbe walijengewa uwezo wa kuongeza ubora wa kanuni kuhusiana na umma kuwa maeneo yenye mionzi ya kiredio. 3.3 ELIMU Wizara, Idara na Wakala (MDAs) zinazohusika ziendeshe sera ya taifa kuhusu Makuzi ya Mtoto Tangu Umri Mdogo (IECD) Katika eneo hili la matokeo, Makuzi Kamili ya Mtoto katika Umri Mdogo (Integrated Early Childhood Development (IECD)) yanahamasishwa kama msingi muhimu wa kuleta matokeo bora katika elimu. Umoja wa Mataifa imesaidia miradi kadhaa ili kuendeleza mihimili mikuu ya Maendeleo ya Mtoto katika Umri Mdogo na kujenga ushawishi kuhusiana na sera ya taifa. Matokeo ya hivi karibuni ni pamoja na: UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 35

38 Uzinduzi wa Sera Mpya ya Elimu na Mafunzo (ETP), wito wa kuanzishwa kwa mwaka mmoja wa lazima wa elimu ya awali ili kuimarisha matokeo ya kujifunza ndani ya mzunguko uliopanuliwa wa elimu ya msingi. Sera ya ETP inaongoza maendeleo ya sekta ya elimu katika malengo ya kati na ya muda mrefu. Mpango wa Muda Mfupi wa Utendaji kwa ajili ya Elimu ya Awali 2015/2016 ulitungwa, ukitangulia uanzishwaji wa mkakati wa utekelezaji sekta hiyo ya upili. Rasimu ya Sera ya Taifa ya Matunzo ya Mtoto, Ukuaji na Maendeleo (NCCGDP) ilikamilishwa ili kuimarisha uratibu unaohusisha sekta nyingi katika maendeleo ya mtoto (ikiwemo ECD) kwa watoto wenye umri kati ya miaka Rasimu ya awali ya Sera ya Mtoto ya Zanzibar ilianzishwa, ambapo inajumuishia kipengele cha Makuzi ya Mtoto katika Umri Mdogo (ECD). Tathmini ya mkabala wa ECD katika Madrassa katika shule za awali za umma ilikamilishwa na kutumiwa kuangazia mipango katika sekta ndogo ya mipango ya ECD huko Zanzibar wakati wa mkutano mkuu wa taifa juu ya ECD. Uchambuzi na utambuzi wa Taratibu za Matunzo ya Uzazi na Familia ulizinduliwa ili kuangazia uanzishwaji wa Mkakati wa Taifa wa Uzazi. Mamlaka sita za serikali za mitaa huko Mbeya, Iringa na Njombe na mitandao mitatu ya ECD kimkoa ilishiriki kupanga, kuratibu na kutekeleza usaili mzima wa ECD. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imeweka mfumo wa chakula shuleni, ikiweka mkazo katika maeneo yenye upungufu wa chakula Eneo hili la Matokeo linalenga katika utoaji wa chakula shuleni kwa watoto hasa katika maeneo ambayo yana shida kubwa ya chakula Tanzania Bara. Mkakati unalenga kutoa motisha kwa wazazi ili wawapeleke watoto wao shuleni, kupunguza njaa na kuimarisha afya na lishe ya mtoto. Mwaka , mlo mmoja kwa siku ulitolewa kwa shule 640 katika wilaya 16 katika maeneo yenye ukame wa kudumu na yasiyo na uhakika wa chakula na maeneo ya wafugaji ya mikoa ya Dodoma, Singida, Arusha na Manyara, na kuwafikia wanafunzi 370,000 wa shule ya msingi. Bidhaa za chakula zilipatikana nchini kadiri ilivyowezekana kupitia programu ya Kununua kwa ajili ya Maendeleo (P4P) ambayo iliwezesha manunuzi ya moja kwa moja kutoka kwa wakulima wadogo waliosajiliwa au kupitia NFRA. Manufaa ya kuonekana ya programu hiyo ni pamoja na kuongezeka kwa kipato na kuimarisha uwezo wa jamii kuchangia fedha taslimu, chakula na bidhaa zisizo za chakula kwa utoaji chakula shuleni na miradi mingine ya maendeleo katika jamii inayohusika. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (MoEVT) inaimarisha ubora wa programu ya mafunzo ya walimu kwa Elimu ya Msingi katika masomo yanayopewa kipaumbele Mkakati mkuu wa kutekeleza Lengo hili ni Programu ya Elimu na Mafunzo ya Walimu Kazini (INSET) katika mazingira ya shule kwa walimu wa shule za msingi. Ni njia ya kuendeleza ujuzi wa kipedagojia na kuhamasiaha ufundishaji shirikishi ili kutoa elimu bora. Matokeo yake hadi sasa ni pamoja na: Wanafunzi 90,300 wa msingi katika shule 255 zilizoteuliwa katika wilaya za Mbeya, Iringa na Njombe wamenufaika kutokana na njia zilizoimarishwa za kuweka mkazo kwa mwanafunzi kufuatia ushiriki wa walimu 2,260 katika programu ya INSET ilipofika / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

39 Walimu 4,162 walifundishwa kuhusu mkakati mpya wa taifa wa KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu). Mtaala uliwanufaisha wanafunzi 90,300 katika shule ya msingi katika shule zote 2,081 kwenye wilaya 21 zilizolengwa katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe. Walimu wa elimu ya awali kutoka shule 168 zilizolengwa na watoa matunzo 88 katika ECD katika wilaya zilizolengwa walipata mafunzo ili kuongeza ubora wa elimu ya awali, kujenga utayari wa shule na uwezo wa wanafunzi wa mapema wa stadi za kusoma na kuhesabu. Programu ya elimu ya awali kupitia INSET kwa Zanzibar ilisanifiwa na kupitishwa na serikali, huku walioandikishwa wakipangwa kwa mwaka wa fedha wa 2015/2016. Kukamilika kwa tathmini ya ubora wa shule katika Elimu na WASH kwa kutumia Gredi ya Usomaji wa Mapema na Gredi ya Kuhesabu ya Mapema, kuimarisha msingi wa maarifa kuhusiana na ubora wa ufundishaji na kujifuza katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe. Kupitia Viwango vya Umahiri wa Walimu Tanzania katika TEHAMA ulikamilishwa na Wizara ya Elimu na wakufunzi wa Sayansi na Hisabati kutoka Vyuo vya Ualimu vya Monduli, Morogoro na Tabora waliofundishwa juu ya Jukwaa la Kujifunzia la Mtandaoni (MOODLE). Jitihada zote mbili ni sehamu ya programu kwa kuunganisha pengo la ubora wa elimu Tanzania. Photo: UN/Julie Pudlowski UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 37

40 Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge / / UNDAP UNDP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

41 Kuimarisha uwezo wa MDA kuongeza ufikiwaji kwa usawa elimu na mafunzo ya ufundi yenye ubora na yaliyo sahihi (TVET) Ili kuunga mkono ufundishaji wenye viwango wa Sayansi katika Shule za Sekondari na Taasisi za Elimu ya Juu, katika Lengo hili shule za sekondari 180 za kufanyia majaribio katika mikoa 9 upande wa Bara zilipokea vifurushi vya vifaa vya sayansi na mafunzo ili kufanikisha ufundishaji wa Biolojia, Kemia na Fizikia. Vifaa hivi vilibuniwa ili kupunguza tofauti kati ya shule zenye maabara zenye vifaa vya kutosha na zile zisizo na vifaa au ambazo hata maabara hazina. Tathmini ya mwisho ya majaribio ilionyesha kuwa matumizi ya vifurushi hivyo vya vifaa vilileta mabadiliko, kwa maana ya kuongeza udadisi wa wanafunzi na shauku katika masomo kutokana na kufundishwa kwa vitendo huku wakishiriki katika majaribio. Ripoti ilipendekeza jitihada hii ipanuliwe, jambo ambalo huenda litatazamwa upya katika ETP mpya. MoEVT ipanue fursa za utoaji elimu mbadala ili kutumia mitindo isiyotumia sana walimu, inayolenga watoto wasio shuleni na watu wazima wasiojua kusoma na kuandika Umoja wa Mataifa imekuwa ikihamasisha kupanuliwa kwa fursa za ujifunzaji mbadala kwa kupitia Programu ya majaribio Kamili Baada ya Elimu ya Msingi (IPPE) katika wilaya nane katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe na Shinyanga. Jitihada inawalenga hasa watoto wa shule na akina mama vijana, kutoa fursa ya pili ya kujifunza ili kuwapa washiriki stadi za maisha na kujitafutia riziki na hivyo kupanua uwezekano wao wa kuajiriwa. Hadi sasa, matokeo yaliyopatikana ni: Kuanzishwa kwa vituo 40, huku zaidi ya mafundi mchundo na walimu 240 wa mahalia wakiwa wamepewa mafunzo ili kusaidia IPPE na wanafunzi 2,441 walijiandikisha katika vyuo mbalimbali vya ufundi kama vile ufundi seremala, umakenika, ufundi umeme, uhaziri na ujenzi wa nyumba na masomo ya shule za sekondari, hivyo kuvuka lengo lililowekwa la wanafunzi 2,115 hadi mwisho wa Mahafali ya vijana 220 waliotokana na IPPE kwa uandikishaji uliopangwa wa fursa ya Mafunzo kwa Njia ya Posta (ODL) inayotolewa na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima. Kuandaa na kusambaza nakala 20,000 za makabrasha ya kujifunzia kwa wanafunzi chini ya IPPE katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe kutakakofanywa na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima ikihusisha stadi za jumla za kielimu na kabla ya mafunzo ya ufundi. MOEVT yatekeleza mikakati ya elimu jumuishi Kama sehemu ya msaada wa Umoja wa Mataifa katika elimu jumuishi, ufikiwaji, kuwaweka shuleni, na ushiriki wa wasichana waliovunja ungo ambao wako katika hatari ya kuacha masomo kwa sababu ya ujauzito na ndoa za mapema mkazo zaidi uliwekwa katika wilaya sita zilizolengwa. Hatua za uingiliaji kati zinawahusu si wasichana peke yao bali wavulana, walimu, menejimenti ya shule, wazazi na hata jamii pia. Kwa wanafunzi, maeneo salama yaliandaliwa na miradi midogo ya shuleni, ikiwemo ujuzi wa ujasiriamali vilianzishwa. Zaidi, moduli kamili ya masuala ya jinsi ilianzishwa kwa lengo la muda mrefu la kupunguza mimba za mapema. Zaidi ya hayo, walimu, walimu wakuu na wakaguzi kutoka katika shule zilizolengwa walishiriki katika Pedagojia Inayozingaita Suala la Jinsia ili kuhamasisha uingizwaji wa mitazamo na njia za ufundishaji zinayozingatia jinsia katika shughuli za kila siku. Kwa wazazi na jamii, harakati za kuelimisha jamii zimefanyika katika wilaa za Shinyanga Vijijini na Kahama, ambapo nyongeza ya shule 20 imefanyika ili kuwa sehemu ya programu. Zaidi ya hayo, viongozi wa jamii wapatao 200 kutoka wilaya za Ngorongoro, Kahama na Muheza wameshirikishwa ili kusaidia katika juhudi za kuwabakiza wasichana katika mfumo wa elimu, jambo lililosaidia uanzishwaji wa mipango ya kazi za jamii ili kukabili vikwazo katika safari yao ya elimu. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 39

42 Vilevile, Wizara ya Elimu imepata msaada katika ngazi za kitaifa, wilaya na shule ili kuhamasisha usawa wa jinsia katika elimu. Kwa namna ya pekee, Kitabu cha Mwongozo na Ushauri kiliandaliwa na kuingizwa katika vifurushi vya kufundishia ili kuwawezesha walimu kushughulikia vema zaidi visa vigumu zaidi kama vile unyanyasaji wa kimwili na kijinsia shuleni. Mapitio ya Kanuni ya Mwenendo ya Walimu na Maadili ya Kazi ya Walimu yaliwezeshwa, huku lengo likiwa ni kupunguza vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya wasichana na wavulana katika shule za msingi. Zaidi ya hayo, Umoja wa Mataifa iliendelea kutoa msaada kwa vilabu rika vya uwezeshaji wasichana na wavulana (TUSEME) kwa kuongezwa shule 90 katika mwaka , kufikiwa shule za msingi 335 katika wilaya 7 (Mbeya Vijijini, Njombe, Makete, Mbarali, Iringa, Temeke na Mufindi). Vilevile, Umoja wa Mataifa imetoa msaada ili kukuza ubora wa msaada wa kielimu na kisaikolojia katika shule 28 za watoto wenye mahitaji maalumu zilizoanzishwa ili kutoa mazingira salama ya kujifunza na kuishi kwa watoto wenye ualbino. Kwa msisitizo katika hili, Umoja wa Mataifa ilishiriki katika mapitio ya Jukwa la Haki za Mtoto wa Kiafrika ili kutazama hali za watoto wenye ualbino miongoni mwa haki za watoto. Hatimaye, kwa ajili ya Lengo hili, utafiti unaopima kiasi ambacho EMIS hukusanya data za watoto wenye ulemavu tayari umeanzishwa. Ufuatiliaji utawezesha uwekaji mipango yenye ufanisi na utekelezaji wa hatua lengefu za utekelezaji ili kusaidia aina hii ya elimu jumuishi. MDAs zinazohusika zifanye uwekaji mipango, usimamizi na uhakikishaji wa ubora kwa kutumia ushahidi katika ngazi za kitaifa, wilaya na shule Umoja wa Mataifa huchukua njia kamili ya kusaidia uwekaji mipango na menejimenti katika sekta ya elimu inayozingatia ushahidi ili kujenga uwezo katika ngazi zote za utoaji huduma. Mafanikio hadi sasa ni pamoja na: Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Ukaguzi (The Inspectorate Management Information System (IMIS)) na Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Elimu ya Msingi (the Basic Education Management Information system (BEMIS)) imehuishwa na kuingizwa katika mfumo wa shuleni kwa ajili ya kufuatilia matokeo ya elimu (SISTER). Katika mwaka , mfumo wa kuwezesha mitandao katika mawasiliano ya simu za mkononi, ambao unaunganisha mifumo ya uendeshaji data za BEMIS na IMIS, ili kuingiza sensa ya mwaka na vilevile taarifa zinazohuishwa mara kwa mara (mwezi/miezi mitatu) ilianzishwa na kupewa uhalali. Wataalamu wa Teknolojia ya Habari kutoka Wizara ya Elimu na TAMISEMI walipewa mafunzo juu ya matumizi ya vitengeneza mfumo wa uendeshaji simu za mkononi (StatEduc 3) ili kuhakikisha kuwepo kwa mfumo endelevu unaomilikiwa kitaifa na katika ngazi ya shule na ambao unaendeshwa na kufanyiwa matengenezo na mafundi kutoka wizara zinazohusika na sekta ya elimu. Mafunzo juu ya IMIS/BEMIS yalitolewa kwa Waratibu wa Elimu katika Kata (WECs), wakaguzi wa shule, na wakaguzi wakuu wa shule katika ngazi ya wilaya katika wilaya 12, kuwezesha kupatikana kwa data za sensa shuleni zinazofikiwa na zisizofikiwa na mtandao kwa ajili ya sensa ya shule iliyounganishwa na mfumo wa hakikisho la ubora. Progamu ya elimu ya wazi na kwa njia ya masafa (CELMA) ilianzishwa katika wilaya nane, huku mwelekeo na mafunzo ya awali yakitolewa kwa walimu wakuu wa shule zote za msingi. Baadhi ya moduli hasa Usimamizi wa Mali, Uwekaji Mipango, Mtaala, Uongozi na Menejimenti zilitumiwa kuandaa mwongozo wa mpango wa kitaifa wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now (BRN)) kwa ajili ya walimu wakuu katika taifa. Moduli za CELMA pia zimetumika kwa pamoja na moduli nyingine za BRN ili kutoa mafunzo kwa walimu wakuu 10,601 na Waratibu wa Elimu Kata 2,588 katika mikoa 17 ya Tanzania Bara. 40 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

43 Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge Maofisa muhimu 1,359 wa wilaya, kata na vijiji katika wilaya 6 (wakiwemo maofisa elimu wilaya, maofisa mipango, wakaguzi wa shule, madiwani, waratibu elimu kata, wenyeviti wa vijiji, maofisa watendaji wa vijiji, wajumbe wa kamati za shule n.k.) walipewa mafunzo juu ya utafutaji rasilimali kwa ajili ya Mpango wa Maendeleo wa Shule Nzima ambapo utekelezaji wake kwa sasa uko katika kiwango cha asilimia 75. Uchambuzi wa Sekta ya Elimu umeanzishwa ili kuleta matokeo ya uandaaji wa programu ya maendeleo ya sekta ya elimu inayofuatia. Msaada pia umetolewa kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kupitia upya muundo wa sasa wa diolojia katika elimu. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 41

44 3.4 AFYA & LISHE MDAs na LGAs zinazohusika zianzishe, kutekeleza na kusimamia sera, mipango na bajeti ili kuleta utoaji huduma za afya zenye ufanisi Lengo hili linalenga kuendeleza zaidi uwezo wa Wizara ya Afya na Mamlaka za Serikali za Mitaa kutekeleza, kusimamia na kutathmini Mpango Mmoja kwa huduma za Afya kwa Mama, Watoto Wachanga na Watoto kama njia ya kupata maendeleo ya Tanzania katika kufikia shabaha zake katika Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs). Hadi sasa kuna matokeo yaliyokwishapatikana: Ingawa hapo awali Mpango Kamambe wa Afya ya Uzazi, Akina Mama, Watoto Wachanga na Watoto (RMNCH) ulianzishwa ili kulenga mikoa ya Magharibi na Kanda ya Ziwa kama maeneo yenye viashiria hafifu vya afya ya mama na mtoto, tayari umeenezwa katika mikoa yote 26 kwa msaada wa UNFPA, UNICEF na WHO. Mapendekezo muhimu ya hatua za kuchukua tayari yameingizwa katika Mipango Kamili ya Afya ya Halmashauri (CCHP) ili kuongeza ubora wa utoaji huduma chini ya RMNCH. Ubora wa CHPs uliimarishwa zaidi kwa msaada uliotolewa na Timu za Mikoa na Wilaya ili kutumia Zana ya Mpango Wakilishi katika michakato yao ya uwekaji mipango. Tathamini ya Dharura ya Uzazi na Watoto Wachanga ilifanyika katika mikoa 11 katika mikoa ya Magharibi na Kanda ya Ziwa. Matokeo yatasaidia kuangazia kiwango cha ubora na uwekaji mipango kwa ajili ya kuchukua hatua kuendana na Mpango Kamambe wa Afya na BRN. Ziara za awali za uwandani zinaonyesha kuimarika kwa kiasi kikubwa kwa ubora wa huduma na kuwa hilo linawezekana panapokuwa na usimamizi wa karibu karibu wa kiufundi na mwongozo unaotolewa na wenye uzoefu. Mwongozo II wa uliandaliwa ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa uchukuaji hatua ili kukomesha vifo vinavyoweza kuzuilika vya mama, watoto wachanga na watoto na kuhakikisha upatikanaji wa afya ya ngono na uzazi. Kuongezeka kwa ahadi na msaada kwa utekelezaji wa hatua za RMNCH kumeonekana katika ngazi za taifa, mikoa na mahalia. Vituo vya afya vilivyochaguliwa katika mikoa saba upande wa Bara na kote Pemba na Unguja kwa upande wa Zanzibar vimepandishwa hadhi ili kutoa huduma za RMNCAH kupitia utoaji vifaa tiba na msaada ili kuimarisha mfumo wa utoaji rufaa. Maarifa na ujuzi wa watoa huduma uliimarishwa kupitia utoaji miongozo, mafunzo kuhusu vifurushi vya MNCAH vikiwemo matunzo ya watoto wachanga, kushtua ili aliyezimia apate fahamu, mafunzo kwa njia ya masafa, Menejimenti Fungamanishi ya Magonjwa ya Utotoni (IMCI) na Uzazi wa Mpango. Miongozo ya kitaifa kuhusu Ufuatiliaji na Uchukuaji Hatua kwa Kipindi (kwa majuma) cha Kabla au Baada ya Uzazi na Vifo (MPDSR) iliongezewa maarifa mapya ambapo mikoa na wilaya (zikiwemo za Zanzibar), zilisaidiwa ili kukuza uwezo wao katika kufanya mapitio ya vifo vya kipindi cha kabla ya uzazi au kujifungua, ufuatiliaji na uchukuaji hatua kupitia mikutano ya mapitio ya kila robo mwaka. Ubora wa matunzo wakati wa kujifungua umeimarika kupitia kubaini vikwazo vinavyosababisha vifo au almanusura na uandaaji wa mipangokazi ya kushughulikia vyanzo vya vifo. Upande wa Zanziabr, tathmini ilifanyika ili kubaini vikwazo kwa utoaji huduma ili kuongeza uwezekano wa watoto wachanga kunusurika. UNICEF na UNFPA, kwa msaada wa Kanada, wanatekeleza programu ( ) ili kushughulikia upungufu na ukosefu wa uwezo uliobainika hapo kabla. Watu 150,000, wakiwemo wanawake wajawazito wanaokadiriwa kuwa 7,500 na watoto chini ya umri wa miaka mitano 30,000, wamepata matunzo bora zaidi ya afya katika Kituo cha Afya ya Msingi cha Kivunge katika Wilaya ya Kaskazini, unguja kufuatia ujenzi wa tawi jipya la MNCH na kuanzishwa kwa huduma rafiki kwa mteja za MNCH. 42 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

45 Ushiriki motomoto na msaada wa kiufundi uliotolewa kwa ajili ya uundwaji wa Mpango Mkakati wa IV wa Sekta ya Afya (HSSP), Mpango wa II wa RMNCAH Moja na vilevile Maabara ya Afya ya Matokeo Makubwa Sasa (BRN), na kusababisha utoaji kipaumbele cha MNCH na ubora wa matunzo. Hili Lengo vilevile linaunga mkono upanuaji wa uchukuaji hatua wenye kusukumwa na ushahidi kwa magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza. Kwa mfano: Kiwango cha utoaji chanjo ya kinga kimeendelea kuwa zaidi ya asilimia 90 kwa DPT 3 na karibu kiwango kama hicho kwa chanjo nyingine, kupitia utekelezaji wa mkakati wa Kumfikia Kila Mtoto. Ufuatiliaji na utekelezaji ulioimarishwa wa kampeni fungamani ya surua rubella iliyofanyika katika mikoa ililenga watoto wenye umri chini ya miaka 15 milioni 21 ambapo mafanikio yalikuwa asilimia 95. Programu mapitio ya utoaji kinga Immunization ilifanyika, matokeo yalitumika kutengeneza Mpango Mkakati wa Kutengeneza Chanjo ya Kinga kwa miaka mitano ijayo. Mpango wa Utambuzi wa Mapema wa Wimbi la Malaria huko Zanzibar (MEEDS)ulianza kufanya kazi katika vituo vyote vya afya na mpango wa kusambaza katika vituo binafsi inaendelea. Umoja wa Mataifa itafanya kazi na washirika ili kutumia data zilizopatikana kuandaa utayari na mwongozo wa mwitikio wa mlipuko wa malaria. Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 43

46 Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge Hospitali za ngazi ya juu na zile za wilaya upande wa Zanzibar endapo kutakuwa na ongezeko la ubora wa EMOC, watoto wachanga, watoto na huduma za baada ya uzazi Likiwa linahusiana na eneo lililopita la matokeo, Lengo hili linalenga upatikanaji na mahitaji ya huduma za EmOC bora, Watoto Wachanga na Baada ya Uzazi upande wa Zanzibar. Kwa msaada wa mashirika ya Umoja wa Mataifa, mafanikio yafuatayo yamepatikana: Miongozo iliandaliwa na mielekeo kuwekwa kwa ajili ya Uwekaji Madaraja 10 Magonjwa kwa Utaratibu wa Kimataifa (ICD) na usimamizi wa utokeaji na kudumu kwa viwango vya vifo vya akina mama kutoakan ana uzazi. Uwezo na ubora wa matunzo kwa huduma za MNCH uliimarishwa, kupitia mafunzo na ufuatiliaji wa watoa huduma za afya kote katika huduma za afya za IMCI, uzazi na watoto wachanga pamoja na usimamizi wa kila robo mwaka unaofanywa na timu za MNCH za wilaya na mikoa. Ubora wa matunzo katika suhula zilizochaguliwa uliimarishwa kupitia utoaji wa vifaa tiba kama vile mabakuli ya kuchemshia, vifaa vya hewa ya oksijeni na vifaa vya upasuaji. 44 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

47 Uwezo wa watoa huduma 183 uliimarishwa kwa utoaji huduma za uzazi wa mpango zikiwemo Usafishaji wa Mji wa Mimba Baada ya Kujifungua (PPIUD), matunzo ya baada ya uzazi na usimamizi saidizi kwa Wasambazaji Walio katika Jamii. Ujuzi wa watoa huduma za afya waliochaguliwa uliboreshwa katika ukusanyaji data na utoaji taarifa kupitia miongozo na mielekeo mipya ya RMNCH kuhusu matumizi ya zana hizo. Suhula zote ziliwekewa rejesta mpya za RMNCH kwa ajili ya ukusanyaji data. Ili kuongeza huduma za Afya ya Ngono iliyo Rafiki kwa Vijana (SRH), vijana wa kike na kiume walifikiwa kwa taarifa na huduma kuhusu matumizi ya dawa za kulevya, mimba za utotoni, ngono salama na Magonjwa Yanayoambukizwa kwa Njia ya Ngono (STIs). Watoa huduma pia walishiriki kutoa Huduma Zilizo Rafiki kwa Vijana (kupitia mafunzo na utoaji wa dawa na vifaa tiba), na watoa elimu rika wa kike na kiume walipewa mafunzo juu ya SRH/GBV/VVU kwa kutumia miongozo ya watoa elimu walio katika rika linalohusika. Zaidi ya hayo, ziara za kubadilishana zilihamasishwa katika kliniki zote ili kubadilishana uzoefu bora na kutoa ithibati kwa YFS na kutambua zana zilizotengenezwa. MDAs na LGAs zinazohusika ziingize suala la lishe katika sera, mipango na bajeti ili kuimarisha mpangilio wa kitaasisi katika kutoa huduma Hatua za kuchukuliwa katika Lengo hili zinafanya kazi katika ngazi mbili. Upande wa utawala, jitihada zipangiliwe katika namna inayohakikisha mpangilio sahihi wa taasisi za kitaifa ili kutoa kipaumbele kwa sera, mipango na bajeti za lishe. Mafanikio yaliyoonekena katika kipindi kinachoripotiwa ni pamoja na: Mapitio ya Sera ya Taifa ya Chakula na Lishe na Mwongozo uliandaliwa kwa ajili ya kuandaa Mpango Kazi wa Lishe wa Kitaifa Unaohusisha Sekta Nyingi wa 2016/ /21 Mapitio ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Lishe wa 2011/ /16; upungufu ulioonekana umeonyesha njia kwa ngazi zote za kutoa uamuzi katika sekta mbalimbali Mifumo ya taarifa za lishe iliimarishwa, huku Tafiti za Taifa za Lishe za kila baada ya miaka miwili na kuanzishwa kwa kadi za kuweka kumbukumbu za masuala ya lishe katika sekta mbalimbali ili kufuatilia viashiria vya lishe katika ngazi ya mkoa katika kila robo mwaka Utaratibu huu wa kawaida wa taarifa za lishe na mfumo wa ufuatiliaji viliimarishwa ili kutoa maendeleo ya kila mara kupitia mapitio na kuingizwa kwa viashiria vya lishe katika DHIS/HMIS na mifumo ya ufuatiliaji. Katika ngazi ya mikoa, ile mikoa na wilaya za kupewa kipaumbele zimesaidia kupanua huduma muhimu za lishe. Matokeo kutoka katika maeneo haya yaliyolengwa ni pamoja na: Utoaji wa tiba kwa Utapiamlo sugui miongoni mwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, ambapo kulikuwa na ongezeko kutoka chini ya asilimia 5 hadi zaidi ya asilimia 30. Utoaji wa nyongeza ya Vitamini A na dawa za minyoo uliongezeka hadi asilimia 61 kutoka asilimia 50 mwaka 2010 na kufika asilimia 72 na 71 mwaka Matumizi ya chumvi yenye madini joto kule Zanzibar yaliongezeka kutoka asilimia 70 hadi asilimia 77. Takribani watoto 900 na wakina Mama Wajawazito au Wanaonyonyesha (PLW) ambao walikuwa na Utapiamlo sugu Kiasi walitibiwa kwa mafanikio, huku viashiria vya utendaji vikiwa ndani ya viwango vilivyopendekezwa. Programu ya kuzuia kudumaa iliendelea, ikitoa vyakula vyenye viinilishe maalumu (SNF) kwa takribani watoto 30,000 chini ya miaka 2 na akina mama wajawazito na wanaonyonyesha katika wilaya zilizosaidiwa na Umoja wa Mataifa. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 45

48 Huduma za jamii zinazohamasisha utaratibu wa kutoa lishe ya kutosha kwa Watoto Wachanga na Watoto Wakubwa kidogo miongoni mwa PLW uliongezeka kutoka asilimia 0 hadi asilimia 10. Programu ya taifa ya mafunzo kazini ilisaidiwa na asilimia 87 ya maofisa lishe wa wilaya na asilimia 60 ya maofisa lishe wa mikoa walionufaika na kuimarishwa kwa ujuzi na maarifa. Hii imesababisha kuanzishwa kwa kamati za uongozi juu ya masuala ya lishe katika ngazi za wilaya na mikoa ili kuimarisha uratibu na kuonyesha ongezeko katika matumizi ya wilaya katika masuala ya lishe kutoka shilingi za Tanzania milioni 65 mwaka 2011/12 hadi shilingi za Tanzania milioni 128 katika mwaka 2014/15. Uwezo wa watoa huduma za kusimamia na kushughulikia utapiamlo uliongezeka kupitia utoaji wa vifaa vya upimaji, mafunzo Kamili juu ya Kukabili Utapiamlo Mkali, viinilishe vidogo na usimamizi. Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge 46 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

49 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, LGAs na Shehia zinaimarisha mikakati ya miundo na mawasiliano ili kuhamasisha tabia zinazojali lishe Chini ya Lengo hili, programu inalenga afya ya jamii, kama eneo la kipaumbele la kuimarisha afya na lishe katika taifa. Matokeo yaliyopatikana hadi sasa ni: Kuanzishwa kwa Muundo-dhana wa Programu ya Wafanyakazi wa Afya ya Jamii (kwa msaada wa ushirikiano wa mashirika ya UNFPA, UNICEF, WHO) na kukamilishw akwa mpango mkakati wa kitaifa wa kuendesha sera mwongozo ya Programu ya Afya katika Jamii (CBHP). Kwa pamoja, hii itasaidia kupanuliwa kwa huduma za afya katika maeneo ya vijijini. Mikoa mitatu imepokea msaada wa Umoja wa Mataifa katika utekelezaji wa mipango hiyo, huku mafunzo elekezi yakihusisha RHMTs, CHMTs na wadau wengine. Haya yamesababisha kuanzishwa kwa CHPs ambayo itaingizwa katika CCHPs ya 2015/2016 CCHPs. Kwa kutumia Muundo-dhana wa Programu ya Wafanyakazi wa Afya ya Jamii, programu inayojikita katika jamii ya RMNCH imetekelezwa katika mikoa mitatu na kuhusisha vijiji 235. Hii itasaidia kuongeza ubora wa hali ya afya ya wale wanaoishi maeneo ya vijijini kupitia mawasiliano ya mabadiliko ya tabia kwa kulenga kuhamasisha afya na kuwahimiza wanawake na watoto kutumia huduma za afya. Serikali ilisaidia kuanzisha, kupitia Kikosi Kazi cha Watoa Huduma za Afya ya Jamii na Kundi la Wafanyakazi wa Masuala ya Ufundi katika Afya, kada yenye pande tatu ya watumishi wa afya ikijumuisha Watumishi Afya ya Jamii Wasaidizi (SWA) na Madaktari Wasaidizi (MA). Mtalaa wa Watumiji wa Afya ya Jamii umeandaliwa tayari na unahakikisha kuwepo kwa viwango, na ubora wa afya inayotolewa. (CHW ni miongoni mwa vigezo muhimu vya mtiririko wa kazi wa MNCH chini ya BRN). Mwongozo wa Taifa na Mkakati wa Taifa kwa ajili ya Kuhamasisha Afya (NGHP na NSHP ilibuniwa na kutekelezwa katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe, ili kujenga uwezo wa halmashauri za wilaya sita katika kuweka mipango na kuandaa bajeti, na vilevile kwa utekelezaji na usimamizi wa mipango ya kuhamasisha afya. Halmashauri hizi sita zimeandaa mipango ya kuhamasisha afya iliyoingizwa katika CCHPs zao za 2015/2016. Kamati za Ulinzi wa Afya katika Sheia 38 (SHCCs) katika Wilaya ya Kaskazini A zilianzishwa, huku kukiwa na utoaji elimu ya umma na shuleni na mikutano ya afya ikiratibiwa. Kipindi cha afya cha kila wiki katika redio kinachoitwa Kijana na afya ya uzazi kimeanzishwa na kurushwa na Kahama FM na hutoa kwa jamii elimu ya kinga na kuhamasisha masuala ya elimu. Vikundi 13 vya wasikilizaji katika ngazi ya vitongoji vilianzishwa ili kuwezesha programu hiyo ya redio, kwa msaada wa wanajamii na wataalamu wa afya. Wizara ya Afya na Mamlaka za Serikali za Mitaa wazalishe data bora na kwa wakati ili kuandaa ushahidi unaohitajika katika kuweka mipango na utoaji uamuzi Tafiti na jitihada mbalimbali zinasaidiwa chini ya eneo hili la matokeo ili kuhakikisha kwamba kunakuwa na utungaji sera na uwekaji mipango unatokana na ushahidi katika sekta ya afya ili kuwa na ulengaji wenye ufanisi kwa wale wanaohitaji zaidi. Hadi sasa hizi ni pamoja na: Tathmini kamili ya hali ya Usajili wa Kiraia na Takwimu Muhimu (CRVS) ilifanyika na mpango wa uwekezaji (CRVS ya kimkakati) uliundwa kwa ajili ya kushughulikia masuala haya yaliyobainishwa kubeba muundodhana wa sera na sheria, usajili wa vizazi na vifo na kubaini vyanzo vya vifo na takwimu muhimu. Mpango huo utahakikisha kwamba vizazi na vifo vyote vinasajiliwa katika namna ya kufaa na kuchangia ufuatiliaji wa taarifa za vifo, hasa miongoni mwa wakina mama na watoto. Maofisa wa programu katika ngazi za taifa na wilaya waliwezeshwa ili kufanya uchambuzi wa data za HMIS/DHIS ili kufuatilia maendeleo kwa kupima dhidi ya kadi ya matokeo ya wilaya na taifa ya RMNCH (na kuchukua hatua ya kurekebisha mambo, inapokuwa lazima). UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 47

50 Msaada wa kiufundi ulitolewa kwa Utafiti wa Demografia na Afya nchini Tanzania (TDHS) na Tathmini ya Utoaji Huduma nchini Tanzania (TSPA). Ukusanyaji data utasaidia ufuatiliaji wa matokeo kuelekea MDGs hasa kuhusiana na MNCH na Malaria na ubora wa utoaji huduma za RMNCH. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na Mamlaka za Serikali za Mitaa zitayarishe Watumishi kwa ajili ya mipango na sera za afya Lengo hili linakusudiwa kuwa na Watumishi wenye ubora ili kutoa huduma zilizoboreshwa kwa upande wa Bara na Zanzibar, kwa msaada wa uandaaji, utekelezaji na usimamizi wa sera, na vilevile kuendeleza ujuzi na kutumia watumishi wa afya. Katika kipindi cha kutolea taarifa, mafanikio yafuatayo yameripotiwa: Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ilianzisha Mpango Mkati wa Manesi na Wakunga ( ), ukilenga kuimarisha ubora wa mafunzo na utoaji huduma. Hili limekamilishwa na utungaji wa Miongozo ya Sera kwa Wakufunzi wa Masuala ya tiba na Miongozo ya Njia za Stadi za Maabara. Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wakunga (5 Mei) huku yakihudhuriwa na viongozi wa ngazi za juu kutoka Serikali, walioongozwa na Mh. Waziri Mkuu. Kusambazwa kwa mapana na marefu kwa taarifa kulichangia sana kuonekana na watu kuelewa suala la wakunga na wajibu wao katika kuokoa maisha ya mama, na kwa kupokelewa na kutumiwa zaidi kwa huduma zao. Uwezo wa taasisi za elimu zilizochaguliwa na maeneo ya kufanyia mafunzo kwa vitendo kwa MNCH kuliimarishwa kupitia ununuzi wa vitu vya kujifunzia, maabara za mafunzo na vifaa vya EmONC. Watumishi wa afya kutoka Hospitali za Wilaya za Newala na Nachingwea walisaidia katika kushiriki katika programu za mafunzo za miezi mitatu kuhusu CEmONC na Utumiaji Dawa za Kufa Ganzi na Usingizi kama sehemu ya kubadilisha modeli ya mhamo kutoka EmONC. Watumishi wa afya kutoka MOH wamefuzu katika programu ya miaka miwili ya Watumishi wa Afya Wasaidizi, na kusaidia kuongeza upatikanaji wa HRH ili kusaidia utoaji wa huduma za MNCH. Huduma iliyounganishwa na yenye ufanisi ya taifa ya usambazaji na mfumo wa menejimenti kwa ajili ya usambazaji vifaa tiba unafanya kazi Lengo hili linashughulikia upungufu katika Sekta ya Afya kwa maana ya upatikanaji wa idadi, manunuzi, uhifadhi na usambazaji wa bidhaa za dawa. Inahamasisha uwekaji kanuni na matumizi yenye hekima ya vifaa tiba na teknolojia ili kuongeza ukubwa na kuhakikisha kufikiwa kwa ubora. Matokeo makubwa hadi sasa ni pamoja na: Watumishi wa afya wapewe mafunzo katika Mfumo wa Taarifa na menejimenti ya kielektroniki ya lijistiki (elmis), ambao yanatolewa katika wilaya zote. elmis imewezesha ufuatiliaji wa akiba ya dawa na uchukuliwaji wa hatua stahiki pale upungufu unapojitokeza. Mpango Kazi wa Viwanda vya Kuzalisha Dawa Tanzania (TPMPA) wa ulianzishwa, ukisaidia mpango mkakati kwa ajili ya kupanua utengenezaji na utoaji huduma za dawa nchini.msaada uliendelea kutolewa ili kuimarisha uwezo wa utaratibu wa kuhifadhi dawa kwenye majokofu katika ngazi za wilaya na taasisi, huku kukiwa na jumla ya majokofu 400 ya MK 401, majokofu 735 ya RCW50EG, vihifadhi baridi 202 vya RCW25, vibebeo 900 vya chanjo na magari yenye uwezo wa kubeba tani nne yenye majokofu yalinunuliwa. Sera ya Dawa ya Zanzibar ilifanyiwa mapitio na mafunzo yaliandaliwa kwa wanaoandika dawa na kuuza dawa Unguja na Pemba. 48 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

51 Watumishi wa Bodi ya Chakula na Dawa ya Zanzibar waliwezeshwa kushiriki katika mafunzo ya mwezi mmoja katika ofisi za Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) juu ya matumizi ya vifaa vya maabara, kujenga uwezo wao na kuchambua dawa na kwa upande mwingine kupanua ubora wa dawa kule Zanzibar. Sambamba na hilo, TFDA ilijengewa uwezo ili kuendesha ufuatiliaji wa kimasoko wa dawa muhimu zilizoorodheshwa chini ya Bidhaa za Kuokoa Uhai za Umoja wa Mataifa. Ili kuongeza udhibiti zaidi wa dawa nchini, vituo vya kupimia vya TFDA viliwezeshwa kuendana na mahitaji ya SOPs na viwango vya ubora. Taarifa za ubashiri na uwekaji idadi zilihuishwa kwa bidaa zinazookoa uhai 12. Amoxicillin DT, copacekd ORS/ Zinc, dawa za kuzuia mimba baada ya tendo na kondomu za kike ziliongezwa katika orodha iliyothibitishwa ya ADDO ili kuhakikisha upatikanaji mpana zaidi. Msaada uliendelea kutolewa ili kuimarisha uwezo wa utaratibu wa kuhifadhi dawa kwenye majokofu katika ngazi za wilaya na taasisi, huku kukiwa na jumla ya majokofu 400 ya MK 401, majokofu 735 ya RCW50EG, vihifadhi baridi 202 vya RCW25, vibebeo 900 vya chanjo na magari yenye uwezo wa kubeba tani nne yenye majokofu yalinunuliwa. Mafundi walipewa mafunzo ili kuunganisha na kufanya matengenezo ya majokofu yanayotumia umeme jua (SDDs) kujiendesha, kama sehemu ya jitihada pana zaidi ili kufikia usambazaji wa zaidi ya asilimia 95 ya chanjo ya Surua ya Rubela. Majokofu 15 ya SDDs hivi sasa yamefungwa katika wilaya nne. 3.5 VVU/UKIMWI Vyama vya Kiraia na mitandao ya Watu Wanaoishi na VVU waratibu kwa ufanisi na kushiriki katika majukwaa ya kutoa uamuzi Chini ya Lengo hili, ujuzi na uwezo wa uendeshaji Vyama vya Kiraia, vikiwemo vikundi vya PLHIV na Makundi Muhimu ya Watu (KPs), wanawezeshwa kuhakikisha uratibu bora zaidi na pia ushiriki wao wenye tija na mchango katika jitihada za Taifa za kushughulikia VVU. Taratibu za uchukuaji hatua hadi sasa zilijumuisha: Tathmini ya Kamati ya Taifa ya Uongozi ya Vyama vya Kiraia (NSC) na kukamilika kwa uandaaji wa Mpango Mkakati wa kwa ushiriki wa wadau wote kuhakikisha uhamasishaji wenye tija wa mitandao na vyama vya kiraia ili kutoa utetezi wa utoaji huduma bora zaidi kuhusu masuala ya VVU. Ripoti ya rekodi ya vyama vya kiraia vinavyoshirikiana na Jamii Muhimu ya Watu katika mikoa 10 ambayo ina mzigo mkubwa wa VVU upande wa Bara iliandaliwa, kuwezesha kushirikishana taarifa na kuboresha utoaji huduma. Vyama ya Imani FBOs (kupitia Jukwaa la Watu wa Imani zote Tanzania) vilijengewa uwezo wa kuandaa na kutekeleza uchukuaji hatua kutokana na ushahidi, ikiwemo kukabili masuala ya unyanyapaa na ubaguzi, VVU na SRH. Kubadilisha maarifa kuliwezeshwa, kama vile ziara za mafunzo nchini India ambapo vyama vya kiraia vilianzisha mtandao wa mafunzo na wenzao wa Asia wanaofanya kazi na KPs ili kubadilishana mambo mazuri yatokanayo. Msaada kwa vyama vya kiraia unachangia katika kutoa uamuzi kuhusiana na vipaumbele vya nchi kwa Mfuko wa Dunia wa Kupambana na VVU/UKIWI, Kifua Kikuu na Malaria (GFATM). UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 49

52 Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) na Tume ya Ukimwi Zanzibar (ZAC) kutoa mwongozo wenye ufanisi katika jitihada za Taifa kushughulikia VVU/UKIMWI kwa kutumia ushahidi kwa mujibu wa viwango vilivyokubaliwa vya Haki za Binadamu Tume mbili za UKIMWI zimejengewa uwezo ili kuongoza utayarishaji, uchambuzi na matumizi ya taarifa za kimkakati ili kutoa uamuzi kwa kutumia ushahidi. Zaidi ya hayo, licha ya kuunganisha kanuni za haki za binadamu na usawa wa jinsia, kuna haja ya kuimarisha uelewa wa mienendo ya janga la VVU na uanzishwaji wa programu na sera kamambe za VVU. Ushirikiano mkubwa zaidi kati ya TACAIDS, NACP, ZAC na washirika wa maendeleo umesababisha kupatikana kwa mafanikio haya: Matini za Dhana ya Mfuko wa Dunia wa Pamoja wa Kifua Kikuu/VVU kwa Tanzania Bara na Zanzibar ziliandaliwa na kuthibitishwa. Uanzishwaji, ukiwemo, wa mikutano ya hiyari ya wadau wa kitaifa kama sehemu ya ushiriki katika mchakato wa majadiliano ya kitaifa. Tathmini ya katikati ya muhula wa utekelezaji Mpango Mkakati wa Taifa wa VVU/UKIMWI wa Zanzibar ulikamilishwa na Mpango wa Gharama za Uendeshaji ili kuongoza utoaji majibu wa VVU/UKIMWI kwa kipindi kilichobaki uliandaliwa. Data kutoka katika majukumu hayo mawili ulichangia katika utumiaji kwa mafanikio wa GFATM. Mpango wa Kusimamia na Kutathamini Sekta ya Afya ya taifa juu ya VVU/UKIMWI ulifanyiwa mapitio. Muundo-dhana huu unaendana na DHIS II ambayo hivi sasa inatumiwa katika wilaya na mikoa kutoa taarifa za viashiria vinavyohusiana na afya na VVU (ukiachilia mbali ART). Mpango Mkakati wa Taifa kuhusu Usugu wa Dawa za VVU (HIVDR) uliandaliwa, kwa kujumuisha vipengele vyote nane vilivyopendekezwa na WHO vya usimamizi. Tafiti juu ya usugu wa dawa za VVU na ufuatiliaji wa ufanisi wa dawa za kupunguza makali ya VVU (ARV) zilianzishwa, kutekelezwa na data kutumiwa na Wizara ya Afya kuimarisha programu ya ART ili kuleta ufanisi kwa kuimarisha usalama wa mgonjwa, kukuza kudumu kwa tiba na matokeo kutokana na kupata usimamizi sahihi wa matokeo mabaya ya ARV na usalama wa dawa. Kwa kuoanisha na Muundo-Dhana Mkakati wa Kitaifa wa Sekta Nyingi kuhusu VVU na UKIMWI (NMSF III), Mpango Mkakati wa Sekta ya Afya juu ya VVU (HSHSP III) pamoja na shauku ya UNAIDS ya hamu ya kupata , mikoa 10 yenye tatizo hilo zaidi kusaidia uanzishwaji wa mipango mikakati ya VVU katika mikoa kuwa kipaumbele maalumu. Hizi zitatumiwa kuongoza na kusimamia utekelezaji katika ngazi ya mikoa. Tovuti ya ZAC iliundwa upya na kuwekewa taarifa mpya huku kukiwa na msisitizo kuwa matengenezo ya mara kwa mara yafanyike. Tovuti inatoa taarifa muhimu kuhusu hatua zinazochukuliwa kukabili VVU katika visiwa hivyo, kama vile jitihada za kila mkoa, AZISE zinazotoa huduma na taratibu zinazofaa. Tafiti zilizofanyika ni pamoja na: utafiti kuhusu kuenea kwa VVU na Magonjwa yanayoambukizwa kwa Ngono, maarifa yanayohusiana na afya, mitazamo na vitendo miongoni mwa wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao; utafiti kuhusu masuala na mienendo ya kijamii-kiutamaduni ya ngono kinyume na maumbile inayofanywa na wanaume na wanawake; mapitio ya programu ya VVU/UKIMWI katika mazingira ya gerezani nchini Tanzania na vilevile mapitio ya sheria kuhusu VVU na UKIMWI katika mazingira ya magereza. Uchambuzi wa hali halisi ya Mabalehe Wanaoishi na VVU (ALHIV) na huduma zilizopo zinazofanywa na Serikali ya Tanzania katika kutambua mahitaji maalumu na mienendo ya jumla yanayozidi kuongezeka ya maadili kuhusiana na UKIMWI miongoni mwa mabalehe sambamba na uchambuzi wa kina kuhusu hali ya Mabalehe kwa kutumia data kutoka THMIS 2012, VAC 2009 na TDHS Tathmini ya uwezo wa utambuzi wa mtawanyiko na uendeshaji ya vyama vya kiraia vinavyoshughulika na VVU na SRH miongoni mwa vijana iliendeshwa ili kusaidia jitihada za baadaye za kujenga uwezo. 50 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

53 Tathmini ya Mazingira ya Kisheria kuhusu VVU nchini Tanzania ilifanyika, ili kupima athari yake katika hatua zinazochukuliwa kitaifa. Tathmini ya matumizi ya huduma za SRH iliyofanywa na PWIDs, SW na MSM mjini Zanzibar ilikamilishwa. Ripoti itaangazia maendeleo ya kizazi cha pili cha Mkakati wa kitaifa wa mpango wa VVU kwa upande wa Zanzibar. Zingatia: Masuala ya haki za watu na jinsia (hasa yanayohusu wanawake na wasichana) yamezingatiwa kikamilifu katika nyaraka mbalimbali za msingi (Muundo-Dhana wa III wa Mkakati wa Sekta Mbalimbali Kitaifa, Mpango Mkakati wa III wa Sekta ya Afya kuhusu VVU) kuhusiana na hatua zinazochukuliwa kitaifa. Zaidi ya hayo, tafiti hizi zinajazia ukusanyaji taarifa wa mara kwa mara wa data zinazostahili katika ngazi ya mikoa; walau zaidi ya asilimia 65 ya wilaya zote zinatoa taarifa kwa Mfumo wa Ufuatiliaji Matokeo Tanzania katika VVU na UKIMWI na Mfumo wa Taarifa wa Usimamizi wa Afya. Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge MDAs, LGA na NSAs zinazohusika ziongeze jitihada ya kuingiza programu za VVU/UKIMWI mahali pa kazi (WPP) Eneo hili la matokeo linapanua mjadala kuhusu jitihada za taifa kupambana na VVU/UKIMWI ili kuhusisha pia sekta binafsi na vyama vya kijamii na vilevile wizara, idara na wakala mbalimbali za serikali ili kuwa na mkabala wenye ufanisi na kuhusisha sekta nyingi zaidi. Kuna sera na programu nyingi zilizoanzishwa, ambapo mafanikio yafuatayo tayari yamepatikana: Chama cha Waajiri Tanzania na Shirikisho ya Biashara la Kudhibiti UKIMWI Zanzibar yameandaa mipango mikakati ya miaka mitano kulingana na ZNSP II na NMSF III. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 51

54 Uwezo wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) kushughulikia kampeni ya Upimaji na Nasaha kwa Hiyari (VCT) mahali pa kazi (Voluntary Counselling and Testing imeongezwa nguvu kupitia mafunzo kwa Waratibu/Watoa Elimu-rika Mahala Pa Kazi katika biashara ya mbao na vilevile mashamba makubwa ya kahawa ya Iringa na Mbeya. Utafiti juu ya kufahamika, ukubwa wa janga na athari ya unyanyapaa na ubaguzi kutokana na VVU katika sekta za umma na binafsi nchini Tanzania ulionyesha kuendelea kuwepo kwa vitendo vinavyokiuka sheria mahali pa kazi, na athari mbaya kwa mfanyakazi anayeishi na VVU anayetafuta huduma za afya. Mapendekezo ya kushughulikia changamoto kama hizi ni pamoja na uhaba wa vifurushi vya taarifa za VVU na UKIMWI na huduma mahali pa kazi, usambazaji wa muhtasari wa sheria, sera, mikakati na miongozo kazini na utatuzi wa mashauri ya kisheria kuhusiana na upimaji ili kuweka mifano hai ya kuchukua. Mpango Kazi wenye muda maalumu hatimaye umeandaliwa na ATE sambamba na utoaji elimu kwa wafanyakazi 18,320 (Wanaume 10,576 na Wanawake 7,744) ili kupata huduma bora za VCT, ambapo rufaa kwa asilimia 100 kwa wale wanaokutwa wakiwa na VVU ni za uhakika ili wapate huduma za matunzo na tiba. Wawakilishi wa utawala na wafanyakai kutoka makampuni 18 waliandaa sera na mipango kazi ya VVU kwa ajili ya utekelezaji baada ya mafunzo. Katika kipindi hiki kinachoripotiwa, programu za VVU zimezinduliwa katika sekta binafsi na za umma tano (uzalishaji viwandani, kilimo, utalii, na elimu). Kila moja ilichukua kanuni kumi za Kanuni ya Mwenendo ya ILO na Mapendekezo 200 kuhusu VVU na UKIMWI katika Ulimwengu wa Kazi. Wanawake na wasichana, wanaojishushulisha katika sekta isiyo rasmi pale Chalinze katika Ukanda wa Usafirishaji wa Tanzania-Zambia wamejiunga katika vikundi 26, huku wakipewa mafunzo ya SRH na kupata fursa za kujitafutia riziki, vyote vikihusianishwa na kanuni za kazi zenye hadhi. Dola za Marekani 140,000 (sawa na shilingi za Tanzania milioni 300) zilitolewa kama mkopo nafuu kwa wanawake, wanaume na wasichana walioonekana kuwa hatarini zaidi kupatwa na maambukizi ya VVU kutokana na ugumu wa kiuchumi na kwa hiyo kujihusisha na tabia hatarishi. Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge 52 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

55 MDAs, LGAs na NSAs zilizochaguliwa kutekeleza programu zinazotokana na msingi wa ushahidi kuhusu kinga ya VVU Lengo hili linashughulikia moja ya Sifuri za dunia ambazo Serikali ya Tanzania imeahidi kutekeleza, yaani kuwepo na uambukizi sifuri wa VVU. Umoja wa Mataifa uliotoa mfumo wa msaada kwa washirika muhimu wa MDA, LGA na CSO, ili kuhakikisha uoanishaji programu ya kuzuia maambukizi ya VVU kwa NMSF. Matokeo makubwa ni pamoja na: Mapitio ya miongozo ya mipango-kazi na VVU katika tiba ili kuoanisha hatua za kuchukua katika vipaumbele vya ulimwengu kuhusu upanuzi wa tiba ya matumizi ya dawa za kupunguza makali ya VVU, kushughulikia Kifua Kikuu/VVU, KPs na hatua za kukabili VVU miongoni mwa watoto. Jitihada za nchi zilipata msukumo kutokana na msaada wa kukuza na kupanua Tiba ya Kutahiri Wanaume kwa Hiyari (VMMC). Mijadala kuhusu sera na uanzishaji majaribio wa njia iliyopendwa sana ya VMMC isiyohusisha upasuaji iliwezeshwa, huku matokeo yakisambazwa na kutolewa kama ilivyopangwa. Viashiria vya ulimwengu kwa ajili ya kupima mwitikio wa sekta ya elimu katika janga la UKIMWI uliingizwa katika hifadhi data ya Elimu ya MIS. Hii itawezesha kubadilishana data na kutoa ripoti katika ngazi za mahalia na ulimwengu kupitia hifadhi data za taifa (ghala) katika Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI. Kupitia uteuzi wa Mshauri wa Kiufundi wa Masuala ya Balehe pale TACAIDS, hatua sahihi za kufaa kwa ajili ya vijana katika umri wa balehe zilisambazwa na uwezo wa taifa na mikoa wa wafanyakazi wa TACAIDS kuimarishwa kwa ajili ya uandaaji programu inayotokana na ushahidi kamili kuhusu masuala ya vijana wa umri wa balehe. Kupitia mafunzo, ziara za kila mara za usimamizi wa kiufundi, kutoa miongozo na kufundisha kwa vitendo kutoka katika Timu za Mikoa za Kujenga Uwezo na Waratibu wa mikoa wa TACAIDS, uwezo wa kamati za UKIMWI katika sekta mbalimbali za Halmashauri, Kata na Vijiji ziliimarishwa ili kutekeleza, kusimamia na kutoa taarifa kuhusu ushahidi juu ya hatua zinazochukuliwa dhidi ya VVU katika mikoa inayolengwa. Miongozo ya Taifa kwa mabadiliko ya tabia ya mawasiliano kwa vijana ilipewa uhalisia na kupitishwa na TACAIDS. Mashirika yanayowahudumia vijana, Waratibu wa UKIMWI kutoka mikoa ya Njombe, Mbeya na Dar es Salaam wamepewa miongozo kuhusu matumizi yake. Kifurushi kitatumika kama waraka wa mwongozo kuongeza utumiaji huduma za kinga dhidi ya VVU/SRH/Mtoto na kuhimiza tabia salama ya kujikinga. Programu ya kutoa elimu ya afya inayoongozwa na wanarika watu wazima na mifumo ya rufaa katika masuala ya afya ya mtoa-huduma na mwanarika ilitekelezwa na Chuo Kikuu cha Dodoma na Chuo Kikuu cha Mt. Agustion cha Tanzania. Inakadiriwa kuwa programu hiyo iliwafikia zaidi ya wanafunzi 10,000 katika vyuo vikuu hivyo viwili hadi sasa. Zaidi ya vilabu 350 vya uwezeshaji vya wanarika mashuleni vilianzishwa katika shule za msingi katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe. Vilabu hivi vinahamasisha ushiriki wa watoto, hasa wasichana, katika kubaini na kushughulikia masuala yanayohusiana na VVU katika shule, familia na jamii. Walimu wakuu, walezi na walimu washauri, waratibu elimu katika kata na maofisa elimu kutoka wilaya zinazolengwa na Umoja wa Mataifa walipata mafunzo juu ya moduli za stadi za maisha, miongozo na huduma za ushauri. Maarifa yaliyopatikana yamewajengea uwezo walimu kuwasaidia wanafunzi na kuweka mazingira salama ya kujifunzia. Redio Shuga programu ya vipindi 12 vya redio kwa ajili ya vijana ilitangazwa kitaifa na kupitia vituo vya redio jamii 10, kuhamasisha upimaji VVU na ushauri (HTC), matumizi ya ya kondomu kila wakati miongoni mwa vijana wanaoshiriki ngono na tabia salama za ngono kwa vijana, ambapo iliwafikia zaidi ya vijana Watanzania milioni 4. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 53

56 Jumla ya wasichana waliovunja ungo 8,524 walipata maarifa na stadi za SRH/VVU/kuzuia ukatili na wasichana 1,543 walipata huduma za HTC/SRH na kinga ya mtoto. Wasichana pia walipata mafunzo ya kujipatia riziki na waliwezeshwa kujihusisha na shughuli za kujipatia kipato ambapo baadhi ya wasichana walipata mtaji wa kuanzia/vifaa kama vile vyerehani ili kuanza kujikusanyia mali. Wanachama 13,782 wa jamii na viongozi wa mahalia walipewa mafunzo juu ya haki za wasichana, huku wazazi wapatao 1,149 wakipewa mafunzo kuhusu mawasiliano na vijana walio katika umri wa balehe kuhusu masuala ya SRH/ukatili, ambapo kesi 85 za VAC ziliripotiwa katika mikoa iliyolengwa ya Iringa, Mbeya na Njombe. MDAs, LGAs na NSAs zilizochaguliwa zitoe huduma bora zaidi ya matunzo na tiba ya VVU/UKIMWI Eneo hili la matokeo linashughulikia vipengele muhimu vinavyoweka msingi wa ahadi muhimu ya pili ya Serikali ya Tanzania: kufuta kabisa vifo vinavyotokana na UKIMWI, yaani vifo sifuri kwa sababu ya UKIMWI. Katika Lengo hili, washirika wa Umoja wa Mataifa wanatekeleza jitihada mbalimbali kuanzia matunzo na tiba kwa watu wazima na watoto, hadi kuondoa athari mbaya za VVU kwa mtu mmojammoja na familia ambao wameambukizwa na kuathiriwa na VVU. Ndani ya mwaka: Miongozo ya taifa juu ya matunzo na tiba ya VVU ilipitiwa upya ili kuingiza mapendekezo yaliyokusanywa mwaka 2013 kupitia Mwongozo wa WHO kuhusu VVU/UKIMWI. Mpango wa kupanua tiba ya watoto katika ngazi ya mikoa hususan kuhusu VVU ilianzishwa, kwa kuendana na mapendekezo kutokana na tathmini ya vikwazo vinavyoathiri uingizwaji wa mapema wa kubaini magonjwa kwa watoto wachanga (EID), kubaini watoto wenye VVU, mwanzo wa ART na vilevile uhifadhi, matunzo ya jumla na msaada. Usimamizi wa kiwango cha ART kwa mgonjwa uliimarishwa kupitia kuanzishwa kwa kituo cha teknolojia ya matunzo ya upimaji, na vilevile kuimarishwa kwa uwezo wa watoa huduma kwa ajili ya usimamizi wa tiba katika ART. Miongozo ya Taifa kwa ajili ya Huduma Zinazotolewa katika Jamii zinazohusiana na VVU na UKIMWI iliundwa upya ili kushughulikia kinga ya VVU, matunzo na tiba katika ngazi ya familia na kuhamasisha uhusiano mkubwa zaidi kati ya huduma za hospitalini na katika jamii. Kuimarishwa na kupanuliwa kwa utoaji wa shughuli zinazohusiana za Kifua Kikuu/VVU ambazo zimesababisha kuongezeka kwa watu walioambukizwa Kifua Kikuu/VVU katika huduma za matunzo na tiba ya VVU/AIDS. Kuanzishwa kwa Vilabu vya Vijana wa Balehe kwa vijana wa umri wa balehe wanaoishi na VVU katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe na Dar es Salaam. Hii ilikuja na matokeo ya kuimarisha kwa huduma za VVU na ART kupitia ujumuishwaji wa kisaikolojia, SRH na elimu ya stadi za maisha. Katika mwaka huu hakukuwa na taarifa za kupungua kwa akiba ya bidhaa za uzazi wa mpango, zikiwemo kondomu. MDAs, LGAs na Wadau Wasio wa Kiserikali kutekeleza kwa ufanisi Mpango Kazi wa Taifa wenye gharama (NCPA) kwa ajili ya MVC Vilevile, kilichokuwa muhimu kwa ajili ya kupunguza makali ya maambukizo ya VVU kwa mtu mmojammoja na familia ni kutokana na athari za VVU miongoni mwa Watoto Wengi Walio katika Hatari (MVC) na familia zao, katika ngazi ya sera na jamii. 54 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

57 Ili kufikia lengo hili, Mpango Kazi wenye Gharama wa pili wa Taifa (NCPA-II) kwa ajili ya MVCs ( ) ulizinduliwa, huku ukiwezesha ufikiwaji wa huduma za jamii za msingi ikiwemo kutoa kinga dhidi ya ukatili, unyanyasaji na kupuuzwa, na kuimarisha ubora, upatikanaji na ufikiwaji wa huduma huku lengo likiwekwa zaidi katika kuzuia na utambuzi wa mapema wa hatari za MVC. Wizara zinazohusika (ikiwemo TAMISEMI na Wizara ya Fedha) zinapeleka mbele ahadi maalum ili kuongeza utoaji fedha kwa utekelezaji wa NCPA-II katika sekta zote zinazostahili. Takribani asilimia 60 ya LGAs zinaangazia mikakati ya NCPA katika Mipango yao ya Muda wa Kati na Mrefu (MTEFs), huku kukiwa na mchango wa kutosha wa fedha kutoka katika vyanzo vyao wenyewe. Miongozo ya uwekaji mipango na bajeti kwa kinga ya mtoto (kama kipengele cha huduma ya MVC katika NCPA ya II) kimeanzishwa na Wizara ya Fedha kwa msaada wa Umoja wa Mataifa tayari unaenezwa katika Sekretariati za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs). Zaidi ya hayo, Kinga ya Mtoto imeingizwa katika muundo-dhana wa Usimamizi na Tathmini ya NCPA-II, kwa upitishwaji wa mfumo wa menejimenti ya taarifa ya kinga maalum ya mtoto (CPMIS). Jitihada zinafanyika ili kueneza viunganishi kati ya CPMIS na Mfumo wa Usimamizi Matokeo Tanzania kwa ajili ya VVU/UKIMWI (TOMSHA chini ya TACAIDS), Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Tanzania (TASAF) mfumo wa Usimamizi na Tathmini na hifadhi data ya MVC (chini ya DSW). Jambo hili litawezesha uhamishaji data na utoaji taarifa kuhusu mwitikio wa sekta mbalimbali kupitia ngazi ya kuu (TACAIDS). Kama matokeo ya jitihada zinazoendelea za utetezi na msaada wa kiufundi unaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa na wadau wengine wanaotekeleza maendeleo, TASAF itapitisha uhamishaji fedha wa nyongeza kwa sharti la mahudhurio katika shule za sekondari. TASAF imekubali kuingiza moduli ya vijana walio katika umri wa balehe katika tathmini ya athari zake, kupima athari za uhamishaji fedha taslimu katika tabia hatarishi za ngono na afya bora. Kwa kutumia ushahidi wa ulimwengu, uhamishaji fedha huu unaweza kupunguza hatari ya VVU kwa vijana walio katika umri wa balehe. MDAs na CSOs ziyafikie Makundi Muhimu ya watu ili kutumia huduma sahihi na rafiki za VVU/UKIMWI Kipengele muhimu cha kinga dhidi ya VVU ili kuunga mkono Watu Muhimu (KPs) ambao wako katika hatari zaidi ya kupata maambukizo ya VVU (wakiwemo makahaba, watu wanaotumia dawa za kulevya kwa kujidunga sindano, wale walio katika mazingira ya gerezani na MSM ili kufikiwa na huduma lengefu za jamii na afya, zenye ubora, sizizo zenye kunyanyapaa ama kuwabagua kijamii na kiafya. Pasipo kuzingatia haya, wale walio na VVU katika eneo linalohusika wataendeleza kuambukiza wengine. Hatua mbalimbali zimechukuliwa ili kuchukua mashaka ya KP katika ngazi ya sera na uandaaji programu, kama vile: Miongozo kamili ya taifa katika sekta ya afya na hatua za kuchukua dhidi ya VVU kwa KPs zimekamilika na kusambazwa sambamba na machapisho mengine yanayooanisha menejimenti na mikabala ili kukidhi mahitaji ya KPs katika sekta ya afya. Nyenzo za kukamilishia za Usimamizi na Tathamini tayari zimekwishatayarishwa. Masuala ya KP yaliingizwa katika Mpango Mkakati wa II wa Taifa wa Zanzibar (ZNSP-II ) na Mpango wa Uendeshaji wa ZNSP II ili kutoa mwitikio bora zaidi. Kifurushi cha hatua za kuchukua juu ya VVU kwa KPs kiliandaliwa na ZACP kwa uzingatia miongozo ya kimataifa. Matokeo Jumuishi ya Utafiti wa Ufuatiliaji Kitabia na Kibiolojia wa Zanzibar ( ) yaliyosambazwa hivi karibuni yaliingizwa katika vifurushi vya watoa matunzo ya afya na watekelezaji wa KPs waliopewa mafunzo juu ya matumizi yake. Jitihada za kufika uwandani zilisababisha kuongezeka kwa huduma za VVU zilizotolewa na KPs huko Zanzibar kutoka 1,108 hadi 3,833. Kituo cha afya cha umma kilicho rafiki kwa vijana kilianzishwa Rahaleo, Unguja, maalumu kikilenga KPs vijana wenye huduma za kinga ya SRH na VVU & STI. Kituo kingine rafiki cha afya kule Miembeni kilifanyiwa matengenezo na kuwekewa simu ya bure kwa ajili ya SRH na VVU/UKIMWI. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 55

58 Vilabu kumi vya watoto vilivyoko katika visiwa vya Unguja na Pemba vilifufuliwa, ambapo hutoa huduma za msaada wa kisaikolojia, vipindi vya tiba na stadi za maisha, vikisaidia watoto 523 (wavulana 248 na wasichana 275) walioambukizwa au kuathiriwa na VVU. Zanzibar ilitengeneza vizuri zaidi mwongozo wa elimu ya stadi za maisha ulioandaliwa kwa msaada wa UNFPA na UNICEF. Huu unatumika kama mwongozo kwa mafunzo kwa vijana walio nje ya mfumo wa shule ili kuwapa elimu ya stadi za maisha. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, ZAC na CSOs ziwahimize PLHIV, MVC na makundi mengine ya walioathirika ili kutumia zaidi huduma za VVU/UKIMWI Mwisho kabisa, kwa programu ya Umoja wa Mataifa ya VVU/UKIMWI nchini Tanzania, Lengo hili linashughulikia ahadi ya tatu ya Serikali ya Tanzania, yaani, Kuondoa Kabisa Unyanyapaa na Ubaguzi, ambapo ahadi hiyo kwa ujumla inachangia kuweka mazingira yanayowezesha (au kutowezesha) PLHIV na wale walioathiriwa na VVU. Vipengele muhimu vya haki za msingi za binadamu, kama vile haki ya kupata huduma za afya, kwa kawaida havionekani sana katika namna huduma zinavyotolewa. Eneo hili la matokeo, kwa hiyo, huwawezesha washirika muhimu wa serikali na wasio wa kiserikali kuhakikisha kwamba kila mmoja mwenye kuhitahi huduma kuhusiana na VVU anazipata kwa ufanisi, pasipo kufanyiwa unyanyapaa au ubaguzi. Jitihada zinawalenga watoa huduma na washirika muhimu katika jamii kama vile viongozi dini, walimu, na viongozi wengine wa kijamii kuhamasisha matumizi ya huduma zilizopo za SRH PLHIV, KPs na vijana. Matokeo yaliyokwishapatikana hadi sasa ni pamoja na: Uandaaji na utekelezaji wa tathmini ya Faharasa ya Unyanyapaa VVU upande wa Bara ili kuboresha uelewa wa unyanyapaa na ubaguzi wa kila siku ambao watu wanaoishi na VVU wanakumbana nao. Utungaji na usambazaji wa machapisho ya Mawasiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabia kwa kulenga KPs ili kuhamasisha madai ya huduma za VVU. KPs wapatao 4,590 (karibu sawa na asilimia 50) walifikiwa na taarifa na huduma, ambapo KPs 4,020 walipimwa na wale waliokutwa wameambukizwa walipewa huduma za VVU. Ongezeko la watu kutumia huduma za VVU na KPs kule Zanzibar lilikuwa kutoka 3,833 hadi 4,226 kufuatia kupanuliwa kwa huduma za uwandani. Tathmini ya maonyesho ya Sanaa katika kutoa elimu juu ya masuala ya Ukatili kwa Misingi ya Kijinsia katika ngazi ya jamii ilikamilishwa. Matokeo yanaonyesha kwamba njia ya hadithi za masimulizi ilikuwa na ufanisi zaidi katika kupanua uelewa na kuhamasisha mabadiliko chanya ya tabia miongoni mwa vijana wa Zanzibar. Matokeo haya yataongoza uanzishwaji wa Mpango Mkakati wa Taifa wa Zanzibar wa kizazi cha pili. Uwezo ulioimarishwa wa waelimisha rika 130 kutoka sekta tofauti ili kuendesha utetezi wa haki za binadamu, jinsia, ikiwemo namna ya kushughulikia mahitaji ya wasiojiweza miongoni mwa makundi muhimu imesababisha mabadiliko chanya ya tabia miongoni mwa wanajumuiya wa Zanzibar. Chama cha Waandishi wa Habari Wanaopambana na UKIMWI Tanzania kiliwezeshwa ili kuandika kwa ufanisi zaidi na kwa hiyo kupunguza unyanyapaa miongoni mwa watu wanaoishi na VVU na makundi muhimu ya watu. Kwa kushirikiana na Msaada wa Kuhamasisha Masuala ya Afya Tanzania, waelimisha rika katika mikoa 19 walijengewa uwezo ili kutoa elimu zaidi kuhusu saratani ya kizazi na kuongeza matumizi ya huduma zinazolenga kupunguza Saratani ya Kizazi kwa wanawake wanaoishi na VVU nchini Tanzania. Hii ni moja ya michango ya Umoja wa Mataifa kwa ushirika wa Utepe wa Zambarau, Utepe Mwekundu (Pink Ribbon Red Ribbon (PRRR)). 56 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

59 3.6 KINGA YA JAMII Serikali ya Tanzania inaratibu mwitikio wa sekta mbalimbali kuhusu kinga ya jamii ili kutatua mahitaji ya makundi ya watu wenye hali ngumu ya uchumi na yasiyo salama Lengo hili linaweka msingi wa kuanzisha na kuendesha sera shikamani, muundo-dhana wa sheria na kanuni kuhusu kinga ya jamii, kupanua kinga ya msingi kwa wote. Matokeo hadi sasa ni pamoja na: Kupitishwa kwa Tamko la Arusha Kuhusu Kinga ya Jamii nchini Tanzania. Serikali imedhamiria kwamba Tamko hilo litumike kama Mwongozo wa Uchukuaji hatua za kuhamasisha kinga ya jamii na kukabili ukosefu wa usawa, ubaguzi, kutenga na aina nyingine za kunyima haki, yaani yote yale yanayozuia uwezekano wa wanaume, wanawake na watoto Watanzania kukua. Vipengele vyake muhimu vimeingizwa katika Muundodhana wa Kinga ya Jamii Kitaifa (NSPF). Tamko pia linajumuisha ahadi maalumu za kutolea taarifa matokeo kwa ajili ya kundi la watu la chini, na hivyo kutumika kama vihamasisho kwa ajenda ya usawa ya Umoja wa Mataifa. Uchambuzi wa fursa ya masuala ya fedha kuhusu kinga ya jamii iliyofanywa kwa msaada wa Wizara ya Fedha na Ofisi ya Waziri Mkuu hivi sasa imekuwa sehemu ya mkakati wa fedha wa NSPF. Utetezi umefanikiwa kujumuisha katika TASAF uhamishaji nyongeza ya fedha kiasi Fulani kwa ajili ya shule za sekondari ili kuhamasisha uandikishaji na mahudhurio. Msaada ulisaidia kupima athari za uhamishaji fedha taslimu zinazohusu vijana katika umri wa balehe chini ya TASAF, kwa kukazia katika tabia hatarishi za ngono na ustawi. Msaada wa nyongeza wa Ufuatiliaji na Tathmini ukiwezeshwa na uteuzi wa Umoja wa Mataifa kuingia katika Kamati ya Taifa ya Kiufundi ya kutathmini TASAF III. Mkakati wa utafutaji fedha za afya ambao huchangia katika upatikanaji afya kwa wote, kupitia mabadiliko ya Mfuko wa Taifa wa sasa wa Bima ya Afya. Ikikamilishwa na usanifu wa Mpango wa Bima ya ya Afya ya Taifa huko Zanzibar. Kanuni mbili za nyongeza zilitayarishwa ili kuleta uwiano wa mafao ya pensheni uendeshaji wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi pamoja na kusimamia na kulinda ajira za Wasio Raia nchini Tanzania. Huo wa kwanza unaendeleza fidia iliyozoeleka miaka yote na kushughulikia gharama za tiba na marekebisho kwa ajili ya kuzuia hatari mahali pa kazi. Huo wa pili, unaendana na haki ya kufanya kazi, unaziba pengo kati ya haki za wasio raia kama zinavyoonyeshwa kwenye viwango vya kimataifa vya kazi na hali halisi ya sasa. Umoja wa Mataifa ikishirikiana na Umoja wa Ulaya umeelekeza kwamba Msaada Jumla wa Bajeti (dola za Marekani milioni 240, ) ulenge kusaidia maskini kupitia ujumuishwaji wa viashiria vya kinga ya jamii katika muundo-dhana wake wa tathmini ya utendaji. Kikosi Kazi cha Hifadhi ya Jamii ya Taifa kikiongozwa na Wizara ya Fedha kilifufuliwa (Umoja wa Mataifa ni mwenyekiti mwenza) na kuanza kukutana mara kwa mara, baada ya kupita muda mrefu bila chochote kuendelea. Kitasaidia katika mfumo wa uratibu wa kinga ya jamii katika ngazi ya sekta. Wizara, Idara na Wakala za serikali ziingize Kinga ya Mtoto (CP) katika programu zao za kitaifa Uendeshaji na usimamizi wa Mpango Kazi wa Taifa kwa Watoto Walio Hatarini Zaidi (NCPA MVC II) na Mpango Kazi wa Taifa wa Kuzuia na Kuchukua Hatua dhidi ya Vitendo vya Ukatili kwa Watoto (NPA VAC) na pia Mpango Kazi wa Taifa wa Kupambana na Vitendo vya Ukatili dhidi ya Watoto Zanzibar (ZNPA VAC) katika ngazi ya taifa na mikoa inalengwa kusaidiwa chini ya Lengo hili. Matokeo ni pamoja na: UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 57

60 Njia za kufuatilia maendeleo na matokeo katika NCPA MVC II ziliimarishwa kupitia uoanishaji wa zana za ukusanyaji na uchambuzi wa data. Hatua za kuchukuliwa ili kumlinda mtoto zitasimamiwa hata katika wilaya hizo ambazo hivi sasa zinanufaika kutoka katika jitihada ya kuimarisha mifumo ya CP. Serikali na washirika katika utekelezaji wameimarisha uwezo wa kutoa usimamizi na kufuatilia kwa ufanisi mipango miwili ya taifa kupitia mikutano ya mara kwa mara na kubadilishana njia zenye kuleta matokeo bora katika Kikosi Kazi Kinachohusisha Sekta Nyingi (MSTF) (ambacho pia kilifanya mapitio yake ya kwanza ya mwaka juu ya NPA VAC), mikutano ya Kamati ya Ushauri ya Taifa kuhusu Kinga ya Mtoto na Kundi la Washirika Watekelezaji (IPG). Upande wa Zanzibar, Kamati ya Kitaifa ya Viongozi Wakuu ya Kinga ya Mtoto, Kamati za Ufundi za Kinga ya Mtoto za Unguja na Pemba, Kamati ya Sekta Nyingi Kushughulikia VAC na Kikosi Kazi cha Haki za Mtoto zimekutana mara mbili kwa mwaka na kuimarisha uratibu wa uchukuaji hatua za kinga ya mtoto kwa ajili ya mwitikio bora zaidi. Kwa msaada wa Umoja wa Mataifa, Ofisi ya Waziri Mkuu inatoa uongozi wa ngazi ya juu, pamoja na TAMISEMI, DSW na MCDGC, ili kuunganisha mifumo mbalimbali ya uratibu watoto kuwa mfumo mmoja kamili wa uratibu kuanzia ngazi ya taifa hadi ya kijiji. Hii itaongeza ufanisi, uwazi, na uunganishaji kiprogramu na matumizi ya rasilimali kwa usimamizi na utoaji ripoti juu ya programu za watoto katika ngazi za taifa na mikoa. Kongamano la kwanza kabisa la taifa la Watoto Walio Hatarini Zaidi lilifanyika mwezi Februari, 2015, ili kufanya mapitio ya maendeleo na changamoto katika utekelezaji wa NCPA MVC II na NPA VAC. Msisitizo zaidi ulikuwa katika kupanua zaidi mfumo wa kinga ya mtoto kitaifa ulioainishwa vema zaidi kisheria, na hivi sasa unafanya kazi katika wilaya 36. Mipango iliwasilishwa ili kupanua mifumo hiyo katika wilaya zote ndani ya miaka mitano ijayo. Photo: UN Tanzania / Zoe Glorious 58 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

61 Miongozo ya taifa kuhusu Kuanzishwa na Kuimarishwa kwa Mifumo ya Kinga ya Mtoto ilianzishwa chini ya DSW na kutekelezwa katika zaidi ya Mamlaka za Mitaa 30. Miongozo inakamilishwa na Miongozo iliyoanzishwa ya Uwekaji Bajeti ya Kinga ya Mtoto ili kusaidia wizara zote za serikali zinazostahili ili kugharimia majukumu yao ya kinga ya mtoto. Mfumo wa kinga ya mtoto ulienezwa katika wilaya tano zaidi upande wa Bara na wilaya moja upande wa Zanzibar, na kufikisha jumla ya wilaya 19 zinazosaidiwa na Umoja wa Mataifa katika kuanzisha mifumo ya kinga ya mtoto. Msaada unaendelea kuhakikisha mfumo unafanya kazi katika ngazi ya kijiji, ikiwemo njia za rufaa na uwezo wa watoa huduma, kuimarisha uratibu na kuzuia na kujibu kesi, na kujishughulisha na jamii ili kuzuia ukatili dhidi ya watoto. Watoa uamuzi na jamii wanaelewa masuala yanayohusu vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto zikiwemo huduma zilizopo za kinga Katika kufikia Lengo hili, Umoja wa Mataifa imehamasisha mkakati wa mawasiliano wa sekta na ngazi mbalimbali ili kushughulikia vitendo vya ukatili dhidi ya watoto. Hii imewatia moyo wadau wa kila aina, kwa mfano: Maofisa Maendeleo ya Jamii na wawezeshaji kutoka katika ngazi za taifa, wilaya na kata wamejengewa uwezo ili kuwezesha mijadala na wazazi na walezi, kupembua namna malezi ya wazazi yanavyoendeshwa, masuala muhimu ya familia na hatua za kuleta nidhamu zisizohusu vitendo vya ukatili. Kule Zanzibar, wawezeshaji wa ngazi ya taifa wametoa mafunzo kwa Maofisa wa Ustawi wa Jamii na Maofisa wa Akina Mama na Watoto kama wawezeshaji wa jamii, ambao sasa wanashirikiana na wazazi/ walezi wa watoto wenye umri kati ya miaka 7-13 ili kupembua taratibu za malezi ya wazazi na kubuni njia za jamii kuchukua hatua ili kuwalinda watoto. Majukwaa saba ya Muunganiko wa Imani Tofauti yenye lengo la kuzuia Ukatili dhidi ya Watoto katika Mamlaka za Mitaa yameanzishwa na kuwafikia viongozi wa dini 150 katika jamii. Majukwaa haya yanatumika kujenga uelewa juu ya masuala ya kinga ya mtoto na kuimarisha mshikamano wa kijamii miongoni mwa wanajamii wenye imani tofauti. Mwongozo wa Imani unaounganisha amali za dini kuhusu haki za mtoto umeandaliwa ili kuongoza ujumbe wa Asasi za Kidini kupitia ushirikiano wa imani tofauti. Zaidi ya hayo, kule Zanzibar, Asasi za Kidini na mitandao ya wanaume imetengeneza mwongozo wa Kupinga Vitendo vya Ukatili kwa Msingi wa Jinsia (GBV) ya Waislamu na Wakristo ili kuwaongoza walimu wa madrasa, Maimamu, na wahubiri katika mafundisho yao. Vipindi 40 vya mchezo wa redio wa Mshike Mshike kuhusu GBV vilitayarishwa na kurushwa na Shirika la Utangazaji Zanzibar Radio (ZBC), Redio Zenji FM, Redio ya Jamii ya Mtegani and Redio ya Jamii ya Micheweni na kuwafikia walau wasikilizaji 200,000 upande wa Zanzibar na Mkoa wa Pwani. Redio za Jamii za Mtegani, Tumbatu, na Micheweni ziliwezesha kuandaliwa na kurushwa kwa programu mpya 96 za SRH/ GBV. Programu hizi ziliongeza utoaji elimu katika ngazi ya jamii na hii imejidhihirisha baada ya kupungua kwa uvumilivu wa Vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (VAWC) na kuongezeka kwa matukio ya utoaji taarifa katika madawati ya jinsia katika vituo vya polisi na kituo kimoja (Unguja) kutoka matukio 850 mwaka 2012 hadi 2,239 mwaka 2015 (MESWYWC, 2015). Programu ya redio ya Walinde Watoto, ambayo ndio njia kuu ya kueneza kampeni ya kitaifa ya elimu kuhusu VAC, bado inaendelea kurushwa kupitia TBC Taifa na ZBC, na kupitia vituo vya jamii 17 kote nchini Tanzania na kuwafikia kiasi cha asilimia 60 ya wasikilizaji wote wa redio. Hadi sasa, progamu 39 za redio kuhusu kinga ya mtoto zimeandaliwa na kurushwa. Vituo vya redio vimeanzisha vikundi vya usikilizaji ambavyo hufungulia programu hizo na kuhamasisha wanajamii kuwalinda watoto. Vikundi vya mitandaoni hasa kupitia Twitter na Whatsapp navyo pia vimeanzishwa. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 59

62 Kule Mwanza, Mbeya na Zanzibar, waandishi wa habari wamewezeshwa ili kuandika habari kwa kuzingatia maadili kuhusu usafirishaji, uhamiaji na wakimbizi. Vituo vya redio vya jamii mkoani Mwanza (Afya Radio na Sengerema FM) na Arusha (Triple A na ORS FM Simanjiro) navyo pia vilitumiwa kutoa ujumbe unaopinga usafirishaji. Matokeo ya mapema yanaonyesha kuna ongezeko la matukio ya usafirishaji watoto. Kwa upande wa Zanzibar, kampeni ya miaka miwili ya kushughulikia vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ilizinduliwa na Rais mwezi Desemba, Jitihada imeisukuma Serikali ya Zanzibar kuanzisha mpango kazi wa miaka mitano na mkakati maalumu wa kushughulikia vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Serikali ya Tanzania yashughulikia upungufu wa kipaumbele katika sheria, mikakati na miongozo ya kulinda watoto na wanawake dhidi ya unyanyasaji, ukatili na unyonyaji Maeneo muhimu kwa maana ya upungufu wa kisheria na kikanuni yameshugulikiwa chini ya Lengo hili kuhusiana na wahanga wa biashara ya usafirishaji binadamu na watoto, hasa walio chini ya uangalizi. Matokeo hadi sasa ni pamoja na: Kupitishwa (na kutangazwa katika gazeti la serikali) kwa Kanuni za Kinga ya Mtoto za Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AGO). Upande wa Zanzibar, Kanuni za Mahakama za Watoto zilianzishwa na Kanuni za Matunzo na Kinga zilifanyiwa mapitio makubwa huku Miongozo ya Maelezo ikitungwa kwa kila moja ya hizo. Kanuni za Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Binadamu ya mwaka 2008 ilichapishwa rasmi kwenye gazeti la serikali Mpango Kazi wa Taifa wa Kupinga Biashara ya Usafirishaji Binadamu wa kupitishwa. Machapisho hayo mawili yatazinduliwa Agosti 21, Mkakati wa Usajili Watoto Chini ya Miaka 5 ulishuhudia ongezeko la usajili wa watoto wa kundi hilo ambao pia walipewa vyeti kutoka 150,000 (asilimia 36) hadi 202,807 (asilimia 48.12) mkoani Mbeya ambako mfumo ulipelekwa katika ngazi ya mkoa na ambako ulianza kufanya kazi. Kufuatia mafanikio hayo, uzinduzi kule Mwanza mwezi Mei, 2015, ulishuhudia ongezeko la usajili na utoaji vyeti kwa watoto chini ya miaka 5 kutoka 101,000 (asilimia 20.2), hadi 171,881 (asilimia 34.3). Mpango Mkakati wa Usajili wa Kiraia wa Miaka Mitano na gharama zake na Mifumo Muhimu ya Takwimu (CRVS) iliandaliwa rasimu na kuthibitiswa kufuatia mashauriano na wadau. Mpango unatoa mfumo wa usajili nchini Tanzania ulio rahisi, uliopelekwa ngazi ya chini na uraia mmoja (ukiwemo wa kuzaliwa). Kwa upande wa Zanzibar, Chama cha Maimamu kilianzisha programu ya utoaji elimu kuhusu kuzuia na kuchukua hatua dhidi ya GBV wakilenga takribani Maimamu 100 na walimu wa Madrasa. Miundo ya mahalia na kitaifa (Shehia na kamati zenye wajumbe kutoka wizara mbalimbali za GBV) zimeimarishwa ili kuzuia vizuri zaidi na kutoa majibu kwa GBV, matokeo yake ni kuongezeka kwa utoaji taarifa juu ya matukio ya GBV kutoka 924 kwa 2012/13 hadi 2,268 kwa 2014/15. Upande wa Zanzibar, Kamati za Shehia za kupambana na GBV huko Unguja na Pemba na wafanayakazi wa mahakama, wakiwemo mahakimu na waendesha mashtaka, waliwezeshwa ili kuendesha mashauri maalumu mahakamani kuhusiana na SGBV. Makundi ya Kiimani ya FBOs (ZIADA na JUMAZA) na Mitandao ya Wanaume ya kuzuia GBV na kuongeza uelewa iliimarika kupitia mafunzo na utoaji miongozo. Viongozi wa asili/machifu wakiwakilisha koo 13 kule Tarime, Mkoa wa Mara, walitoa tamko la kupinga ukeketaji (FGM) baada ya kampeni, mafunzo ya sekta mbalimbali na kuhamasisha mila mbadala na ajenda ya kukomesha FGM. 60 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

63 Wavulana 207 wa umri kati ya miaka 5-17 walilindwa dhidi ya njia ya kutahiri wanaume za kizamani na kutahiriwa kwa njia ya kisasa. Wavulana pia walishiriki katika mafunzo kuhusu jinsia, haki za binadamu na masuala ya GBV na walipewa huduma za VCT kuhusu VVU/UKIMWI. Redio za jamii (Micheweni, Tumbatu na Makunduchi-Mtegani) ziliwezeshwa ili kuandaa programu za SRH/GBV/haki za binadamu na taarifa za habari, huku kukiwa na ushahidi wa kuongezeka kwa ubora wa utangazaji. Kampeni mbili za taifa dhidi ya Ndoa za Watoto upande wa Bara na kupinga GBV upande wa Zanzibar zilizinduliwa. Hiyo ya pili ilipangwa kimkakati ili iendane na utayarishaji rasimu ya Katiba Mpya ya Tanzania, ambapo kulikuwa na mafanikio katika kujumuisha tafsiri ya mtoto kama mtu mwenye umri chini ya miaka 18. Dawati la ziada la Jinsia na Watoto lilianzishwa katika Kituo Cha Polisi ya Sitakishari huku kikiwa na vifaa vinavyohitajika ili kuwasaidia wahanga na manusura wa GBV na unyanyasaji watoto ili wapate haki na huduma nyingine muhimu. Mwongozo wa kushughulikia ukatili wa majumbani na kuimarisha ukusanyaji data kuhusu vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake tayari umeandaliwa mjini Zanzibar. Hii imekamilishwa na uanzishwaji wa Mpango wa Kuzuia na Kuchukua Hatua Uliooanishwa katika Sekta Mbalimbali kuhusu GBV/VAC ili kuongoza jitihada za kushughulikia GBV/VAC. Photo: UN / Julie Pudlowski UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 61

64 Wizara, Idara na Wakala za Serikali, Mamlaka za Serikali za Mitaa, vyombo vya kusimamia sheria na vyama vya kiraia vilivyochaguliwa vipate stadi zilizoboreshwa za kiufundi na kushughulikia kesi za unyanyasaji/ vitendo vya ukatili/ na unyonyaji dhidi ya watoto Lengo hili linazingatia mkakati wa kujenga uwezo katika sekta mbalimbali ili kuimarisha stadi na maarifa yanayohusiana na kuzuia na kuchukua hatua kukabili unyanyasaji watoto, vitendo vya ukatili na unyonyaji dhidi yao (ikiwemo biashara ya usafirishaji watu). Mafanikio ni pamoja na: Wajumbe wa Timu Mama na Wawezeshaji wa Kitaifa kwa upande wa Bara na kule Zanzibar walipatiwa Miongozo ya Mafunzo Juu ya Kinga ya Mtoto; kila mmoja ikitoa mafunzo kwa Timu za Kinga ya Mtoto za Wilaya (CPT) na Kamati za Watoto Walio Hatarini Zaidi (MVCC) ambao wameshirikisha maarifa yao na wajumbe wa CPT katika Kata. Uwezo wa kuzuia na kuchukua hatua katika kesi za kinga ya mtoto tangia hapo umeongezeka ili kukidhi mahitaji ya kinga ya jamii. Maofisa Ustawi wa Jamii kama watu wa kwanza kuwauliza jambo katika kila mkoa upande wa Bara, wakipata mafunzo kuhusu matunzo na amri za usimamizi na matumizi ya miongozo rasmi ya kinga ya mtoto. Maofisa hivi sasa wako katika nafasi ya kutoa msaada wa kiufundi wa siku hadi simu na usimamizi kwa wafanyakazi wengine wa mstari wa mbele katika ngazi ya wilaya. Kwa Zanzibar, jitihada za usajili na upangaji majukumu ya Maofisa wa Ustawi wa Jamii hivi sasa wana maana kwamba wilaya zote zina maeneo yaliyotengwa kwa ajili yao kulenga ili kusimamia vema masuala ya kinga ya mtoto. Kinga ya Mtoto iliingizwa katika mitalaa ya Chuo cha Ustawi wa Jamii (ISW) na Chuo Kikuu cha Umma cha Zanzibar (SUZA), jambo lililohakikisha Wafanyakazi wa Ustawi wa Ja,mii waliofuzu kwa stadi za nadharia na vitendo kwa kuendana na Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 na Sheria ya Watoto Zanzibar ya mwaka 2011 na kanuni na miongozo inayoendana nazo. ISW hivi sasa inafanya kazi kupitia Chama cha Vyuo vya Ustawi wa Jamii nchini Tanzania ili kuunga mkono taasisi 11 zenye programu za Ustawi wa Jamii ili kuingiza kinga ya mtoto katika mitaala yao. Nakala 500 za Kiingereza na 350 za Kiswahili za Kitabu cha Mwongozo cha Watoa Huduma kwa Wahanga wa Biashara Haramu ya Usafirishaji watu zilisambazwa kwa wadau mbalimbali (serikali, vyombo vya habari, vyama vya kiraia na wanajamii) katika mikoa zaidi ya 15. Ikitumiwa kama chapisho lililo rejea kuu ya kuwasiliana na mamlaka zinazohusika au kufanya rejea kwa msaada, Mwongozo huo unaendelea kutumika kama rejea muhimu ya kuwasiliana na mamlaka husika au namna ya kupata msaada, Miongozo ya watoa mafunzo kwa vyama vya kiraia kuhusu utekelezaji wa Sheria ya Kupinga Usafirishaji Haramu wa Binadamu nchini Tanzania na Sheria ya Polisi ya Tanzania ya Kupinga Usafirishaji Haramu wa Watu tayari zimetafsiriwa katika Kiswahili, kupigwa chapa na kusambazwa kwa wadau wanaohusika. Wawezeshaji kutoka Jeshi la Polisi na Vyama vya Kiraia wanatumia miongozo ili kutoa mafunzo kwa wafanyakazi wao kuhusu kuzuia, kinga, msaada, uendeshaji mashtaka kuhusiana na biashara haramu ya binadamu katika eneo la usafirishaji wa biashara haramu. 62 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

65 Photo: UN Tanzania / Zoe Glorious Photo: UN Tanzania Zoe Glorious UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 63

66 Watoa huduma wa mahalia wawe na mwitiko wa kufaa kwa wanawake na watoto walio wahanga wa unyanyasaji, ukatili na unyonyaji katika maeneo yaliyochaguliwa Katika eneo hili la matokeo, Umoja wa Mataifa inaimarisha uwezo wa uendeshaji na utendaji wa watoa huduma wa mahalia ili kutoa huduma za kipekee kwa idadi kubwa zaidi ya wanawake na watoto walio wahanga wa unyanyasaji, vitendo vya ukatili na unyonyaji. Matokeo chini ya UNDAP ni pamoja na: Vituo vitabu vilitoa malazi, matunzo ya kitabibu na kisaikolojia, msaada wa kielemu na mafunzo ya ufundi kwa watoto wahanga wa biashara haramu ya usafirishaji watu, kusaidia zaidi ya wahanga 50 katika miezi 12 iliyopita. Manusura walipata mafunzo kuhusu ushonaji, uzalishaji chakula na bidhaa za mikono ili kupunguza uwezekano wao wa kusafirishwa tena kwa njia haramu baada ya kuunganishwa na familia zao. Jumla ya manusura 36 tayari wameunganishwa na familia zao na watatu wameajiriwa katika uzalishaji chakula. Wahanga 22 kutoka nchi za kigeni wa biashara haramu ya usafirishaji walisaidiwa na kurejeshwa kwenye nchi zao. Utaratibu wa Watoto kupiga simu za dharura, wakipewa fursa ya kupiga pasipo kutozwa malipo na chini ya menejimenti ya C-SEMA. Kati ya Julai 2014 na Juni, 2015, Kituo cha Mawasiliano kilipokea simu halisi 1,109 huku 455 kati ya hizo zikitoa taarifa moja kwa moja kuhusu visa vya kinga ya mtoto, hasa ukatili wa kimwili, kutelekezwa, ajira ya watoto, unajisi na watoto waliopotea. Jitihada za kuboresha huduma za Kituo cha Mawasiliano ni pamoja na kuchukua hatua ili kufungamanisha na kuimarika kwa michakato ya rufaa kwa ajili ya uchukuaji hatua za kufaa kwa wakati mwafaka kwa Maofisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya. Kituo cha Mawasiliano kwa Msaada wa Mtoto kilizinduliwa Zanzibar, ambapo C-Sema na Kitengo cha Kinga ya Mtoto cha zmeswywc zinashirikiana katika utekelezaji wake. Kwa upande wa Zanzibar, Kamati za Shehia ya kupamabana na GBV upande wa Unguja na Pemba zikielekezwa kwenye mrengo wa masuala ya haki za binadamu wa mtazamo wa kuzuia GBV na uchukuaji hatua kuikabili, kusaidia na kuimarisha rekodi na kutumia matukio ili kuandaa mwitikio bora zaidi katika siku za usoni. Wizara, Idara, wakala kutumia na kutoa ripoti kuhusu data hizo zilizovunjwa vunjwa kuhusu ukatili / unyanyasaji / kusafirisha wanawake na watoto kwa mujibu wa muda maalumu uliopangwa Mfumo wa Taarifa wa Menejimenti ya Kinga ya Mtoto (CPMIS) bado ni mfumo mkuu wa kufikia mafanikio ya Lengo hili la mwisho chini ya programu ya Kinga ya Jamii. Mfumo tayari umekwishaanzishwa ili kukusanya data zinazohusiana na unyanyasaji, ukatili na unyonyaji wa wanawake na watoto, ikiwemo wakati wa biashara haramu ya watu. Mfumo wa Usimamizi wa Kesi katika Ngazi za Wilaya (DCMS), kama moduli katika CPMIS daima unaziwezesha mamlaka za mitaa kupata data katika kesi zote zilizoshughulikiwa na CPTs. Inaonyesha kwamba wakati wa kipindi cha kutoa taarifa ya Mpango wa UNDAP, jumla ya watoto 2,910 (wasichana 1,756 na wavulana 1,194) wamepata huduma za Kinga ya Mtoto. 64 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

67 Ukiendana na mpango wa Usimamizi na Tathamini wa NCPA MVC II, Daftari jipya la usajili limeanzishwa ili kuwezesha data kuhusu kinga ya mtoto kupatikana kupitia Mfumo wa Taarifa wa Afya wa Wilaya. Zana hii imetengenezwa ili wilaya zote zitekeleze NCPA MVC II kwa Kamati za MVC; hii ina maana kwamba data kuhusu kinga ya mtoto itapatikana karibu katika asilimia 80 ya wilaya zote nchini Tanzania. Zile wilaya zinazotekeleza mfumo wa CP zimebadilishana uzoefu kuhusiana na ubadilishanaji na matumizi ya data katika mchakato wa kutoa uamuzi. Hii imesaidia kila moja kufanya tafsiri bora zaidi na kutoa kipaumbele kwa masuala muhimu kutoka katika data, kusaidia uendelezaji wa hatua za kila mwaka za Kinga ya Mtoto kama ilivyoonyeshwa katika MTEFs katika mwaka 2015/2016. Makao Makuu ya Polisi imeanzisha Daftari la Usajili linalotumiwa na Madawati ya Jinsia na Watoto upande wa Bara na Zanzibar na kuhifadhi kumbukumbu zinazohusiana na: watoto wahanga wa vitendo vya ukatili, unyanyasaji, kutelekezwa na kunyonywa; watoto walio katika mgogoro na sheria; watu wazima walio wahanga wa GBV. Pamoja na Kituo cha Mawasiliano kwa Msaada wa Mtoto (tazama Lengo la sita juu) na Ubao wa Usajili Vizazi wa RITA (Lengo la nne), mifumo hii inatoa data pana zilizomeng enywa kuhusu huduma zinazotolewa na mamlaka zinazohusika kwa malengo ya kutoa ushahidi wa ubora wa hali ya juu kwa ajili ya uwekaji vipaumbele kimkakati, mipango na menejimenti kwa ajili ya kutoa huduma za kinga. JEDWALI TOFAUTI: MPANGO WA PAMOJA WA KUSAIDIA MITANDAO YA KIJAMII ILIYO SALAMA NA YENYE TIJA Programu ya pamoja (JP) ya miaka miwili inayohusisha mashirika manne UNICEF, UNDP, UNFPA na ILO imeanzishwa ili kuisaidia TASAF katika kupanua Mitandao ya Kijamii iliyo Salama na yenye Tija (PSSN). Programu inaziba pengo kati ya uchukuaji hatua kisera na ngazi ya jamii kwa kutoa msaada kwa ngazi pana, za kati na chini. Katika ngazi pana, JP itaimarisha uratibu wa mwingiliano wa sekta na kushughulikia masuala ya upande wa utoaji kwa kusaidia ukamilishaji na uendeshaji wa Muundo-dhana wa Hifadhi (Kinga) ya Jamii (NSPF). Katika ngazi ya kati, JP itaimarisha tija na ufanisi wa PSSN kwa kuimaisha utekelezaji wa programu na mifumo ya utoaji, wakati ambapo ngazi ya chini itachangia kukusanya mtaji-watu na hali bora ya wanufaikaji kwa kuimarisha utafutaji riziki endelevu na mifumo ya kujinusuru kwa PSSN. Upanuzi wa programu ya PSSN katika ngazi ya chini utakuwa na maana kwamba kaya 920,000 zinazoishi chini ya kizio cha umaskini zitawezeshwa kuboresha ulaji wao wa chakula chenye viini-lishe, kupata huduma muhimu za afya kwa akina mama wajawazito na watoto wenye umri chini ya miaka mitano, kuongeza uandikishaji na mahudhurio shuleni kwa watoto wa umri wa kusoma, na kuboresha njia zao za kujipatia riziki. Katika Kijiji cha Chasimba, Wilaya ya Bagamoyo, wanufaikaji tayari walinufaika na uhamishaji fedha wenye masharti ili kupata mahitaji ya msingi ya lishe katika ngazi ya kaya na mahitaji ya shule kwa watoto wao. Utoaji chakula shuleni umesaidiakuongezeka kwa viwango vya mahudhurio na kuimarisha utendaji wa kitaaluma kwa kwenda mbele. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 65

68 3.7 WASH (MAJI, USAFI, AFYA) Wizara, Idara na Wakala za Serikali zinazohusika zitoe mwitiko ulioratibiwa na kuoanishwa vema ili kupanua utoaji huduma bora na rafiki kwa mtoto na msichana na huduma ya WASH kupatikana katika mazingira ya shule Katika eneo hili la matokeo, Umoja wa Mataifa inasaidia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kutekeleza upanuzi ulioratibiwa wa WASH kote nchini Tanzania. Maendeleo hadi sasa ni pamoja na: Uratibu wenye ufanisi, uoanishaji wa njia na kuendana na miongozo ya kitaifa iliyopitishwa inayowezeshwa na mikutano vya kila robo mwaka ya vikosi kazi vinavyohusisha Wizara ya Elimu na washirika. Hizi zinakamilishwa katika ngazi ya wilaya na waratibu wa WASH ambao hutathmini suhula za WASH na kusimamia hatua za usimamizi kwa kutumia kasha-zana na miongozo ya taifa. Kufuatia upitishaji wa serikali wa njia Inayofaa kwa Shule nchini Tanzania (inayolenga kuleta mabadiliko ya kitabia miongoni mwa watoto wanaohudhuria shule na kuimarisha afya kupitia shughuli kama vile kunawa mikono kwa sabuni), zaidi ya shule 40+ zimebainishwa kushiriki katika mradi wa majaribio, zikisaidiwa na timu ya wataalamu 30 inayojumuisha washiriki wenye mafunzo katika ngazi ya taifa na mkoa kutoka katika serikali na vyama vya kiraia. Njia inaongozwa na kanuni kuu tatu wepesi, uwezekano wa kupanuliwa, na uendelevu ili kuendeleza haki za maji, usafi na mazingira salama shuleni. Vifurushi-dhana 3 na 5 vya miongozo ya Mpango wa Taifa wa WASH imepitiwa na kuimarishwa kufuatia maoni kutoka uwandani. Mipango ya kuchapishwa matoleo mapya inaendelea kwa ajili ya upanuzi wa programu ya WASH shuleni. Timu za watalaamu wa WASH kutoka katika wilaya 18 za nyongeza katika mikoa ya Mbeya, Iringa, Njombe na Dar es Salaam tayari zimesaidiwa kufahamu mazingira na kupewa mafunzo kuhusu matumizi ya miongozo ya WASH mashuleni, huku mafunzo kama hayo yakianzishwa katika ngazi za kata na shule katika wilaya sita zilizosaidiwa hapo mwanzo za Mbarali, Mbeya, Mufindi, Iringa, Makete, na Njombe. Jitihada zinahakikisha kwamba taasisi zinazostahili zina uwezo wa kutosha kupanga, kutekeleza, kuratibu na kufanya utetezi wa huduma bora na endelevu za WASH mashuleni, na pia kuhamasisha upatikanaji wa suhula salama na rafiki kwa mtoto. Suhula za WASH (vyoo, maji na mahali pa kunawia mikono) zimejengwa katika shule 47 upande wa Bara na Zanzibar. Hatua hii imewapa zaidi ya wanafunzi 59,000 (takribani wasichana 30,690 na wavulana 28,310) kupata huduma salama na kuwa katika mazingira ya kujifunzia yanayowalinda. Suhula hizo zinaendana na mahitaji ya miongozo ya kitaifa ya WASH, ikiweka vyumba tofauti vya msalani kwa wavulana na wasichana ili kuweka faragha ya kutosha hasa kwa wasichana walio katika umri wa kuvunja ungo na watoto wenye ulemavu. Wajumbe wa kamati za uendeshaji shule, viongozi wa kijamii, wazazi na wanajamii wengine walihamasishwa, kuelekezwa na kupewa mafunzo juu ya programu ya WASH mashuleni hasa utawala wake, uwekaji mipango, utayarishaji na utekelezaji bajeti pamoja na kuanzishwa kwa mifuko ya fedha ili kuhakikisha menejimenti sahihi na uendelevu wa suhula zilizokamilishwa. Serikali ya Tanzania / Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zinatekeleza mwitikio wa kitaifa ulioratibiwa, kupanuliwa, na kuboreshwa wa usafi na afya ya mwili (S&H) Hatua za kuchukua katika Lengo hili zinaimarisha miundo ya kitaasisi na uwezo, ikiwemo rasilimali a utekelezaji, katika sekta ya kati ya usafi na afya ya mwili. Hii inajumuisha vitendo katika ngazi ya kaya vya kutibu maji na kuyahifadhi kwa namna salama na mikakati ya kuhamasisha afya. Kwa mfano: 66 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

69 Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge Kipengele kilichotengwa maalumu kwa ajili ya Usafi na Afya ya Mwili kimeingizwa katika Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji Awamu ya II ( WSDP II) kufuatia jitihada za utetezi kupitia mfumo wa majadiliano katika sekta. Programu ya WSDP II ilizinduliwa na serikali mwezi Septemba, 2014 kwa ongezeko la dola za Marekani 150,000,000 kwa miaka mitano ijayo. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (MoHSW) na Wizara ya Maji (MoW) zilijengewa uwezo wa kuendeleza na kutekeleza Mpango wa Maji Salama unaoendana na mabadiliko ya tabia ya nchi. Mameneja wa Mamlaka za Maji za Wilaya, kutokana na hayo, wataendeleo kuwezeshwa ili kutathmini na kulinda mitandao ya usambazaji maji dhidi ya athari za mabadiliko ya tabia ya nchi na kuhakikisha utoaji wa huduma za maji salama kwa jamii. Chini ya programu ya Kampeni ya Taifa ya Usafi, Timu za Maji na Usafi za Wilaya (DWSTs) zikifanya kazi kwa mujibu wa kanuni za Usafi Kamili Unaosimamiwa na Jamii (CLTS) zimewezeshwa ili kupunguza kujisaidia ovyo mahali pa wazi kupitia ujenzi wa suhula za vyoo vyenye kujali usafi na vya gharama nafuu. Ili kupanua matumizi ya suhula bora, wasanii wa mahalia na wajasiriamali katika ngazi ya kijiji wamepewa mafunzo juu ya ujenzi wa vyoo na kuweka bidhaa na huduma muhimu. Siku ya Dunia ya Kunawa Mikono, Siku ya Vyoo Duniani, Wiki ya Taifa ya Usafi na Wiki ya Kimataifa ya Maji ziliadhimishwa, huku matukio yakiandaliwa nchi nzima ili kuhamasisha tabia za usafi. Kuhamasisha vyombo vya habari vya mtandaoni, kusambaza taarifa kwa vyombo vya habari na kufanya maonyesho kuliwezesha zaidi ya raia milioni tatu kufikiwa na ujumbe wa usafi na afya. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 67

70 Serikali ya Tanzania / Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zipitishe hatua zinazotokana na ushahidi ili kuimarisha utoaji uamuzi; usawa na ujumuishwaji katika mpango wa WASH wa wanawake, watoto na makundi ya watu walio hatarini Lengo hili linawezesha kuanzishwa na matumizi yenye ufanisi ya mifumo ya usimamizi ya taifa ili kutoa taarifa bora kuhusu programu ya WASH. Inahusisha msaada wa kiufundi na kifedha ili kuboresha MIS katika usambazaji maji na ushiriki wa makundi ya watu walio hatarini ili kushawishi mjadala wa taifa kuhusu sera kuhusiana na usawa na uendelevu wa upatikanaji wa maji. Hadi sasa: Rasimu ya mwisho ya Mkakati Endelevu wa Taifa kwa ajili ya usambazaji maji vijijini imeshaandaliwa. Muundo-dhana unaoongoza, uliandaliwa kupitia jitihada za ushirikiano na wadau katika sekta, unachambua hali ya sasa, unabaini changamoto zinazoathiri uendelevu ikiwemo mazingira wezeshi/yasiyowezesha (sera, uwezo, taasisi, fedha, sheria, ufundi) ili kushughulikia vikwazo na kusaidia utoaji huduma ya maji vijijini. Mkakati unajumuisha matumizi ya zana za usimamizi sekta, zilizoandaliwa kwa msaada wa DPs, hasa Utambuaji wa Vituo vya Maji wa GIS ambao huwezesha ukusanyaji na uchambuzi data, kutoa taarifa ya uandaaji na usambazaji. Ushahidi utawezesha utoaji uamuzi kwa usawa na kwa kutumia ushahidi katika kuweka mipango, kubuni na kuelekeza rasilimali kule ambako kuna mahitaji zaidi. Hatua zilizochukuliwa katika wilaya za Njombe na Mufindi zimefanywa kuwa mradi wa majaribio ili kupata mafunzo ya kuangazia sera ya taifa na miongozo ya uendeshaji kwa mipangilio iliyoimarishwa ya kitaasisi katika kusimamia miradi ya maji vijijini na kufufuliwa kwa miradi ya maji iliyokufa katika wilaya chini ya mkakati wa Taifa wa Huduma Endelevu ya Usambazaji Maji Vijijini. Vikundi 25 vya Usambazji Maji Vinavyomilikiwa na Jamii vimewezeshwa kuunda na kusajili, huku vikipata mafunzo ili kuimarisha uwezo wao wa kuendesha na kusimamia miradi ya maji, kuhakikisha uwajibikaji na umiliki wa wanajamii wenyewe. Matengenezo ya miradi 10 ya usambazaji maji katika wilaya za Mufindi na Njombe yamekamilika, kufufua vituo vya maji 63 vinavyohudumia jumla ya watu 19,320. Upanuzi wa mtandao wa usambazaji mabomba katika jamii zisizohudumiwa tayari umetekelezwa katika vijiji vinne vya Pemba, na kuwezesha zaidi ya watu 2,000 kupata huduma ya maji salama na ya uhakika na hivyo kupunguza mzigo kwa akina mama na watoto. Miradi ya majaribio ya ZAWA na WASH jijini Dar es Salaam imeboresha uendelevu wa huduma zao Lengo hili la ushirika ili kusaidia uendelevu mpana zaidi wa huduma za usambazaji maji safi, ikiwemo Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka ya Dar es Salaam (DAWASA) na watoa huduma katika Ziwa Viktoria. Kuhusiana na hiyo ya mwanzo, ZAWA imepanua mradi wa Usimamizi wa Mahitaji ya Maji na hivyo kupunguza maji yasiyotozwa gharama, upotevu wa maji kwa sababu ya kuvuja na matumizi yasiyoidhinishwa. Hatua hivi sasa zinachukuliwa ili kutumia maarifa yaliyopatikana na kuenezwa kote Zanzibar, huku jamii zikinufaika kutokana na kupungua kwa gharama za maji na kupatikana kwa wingi zaidi kwa maji yaliyotibiwa (yaliyowekewa dawa). Vilevile, upande wa Zanzibar, miradi nane ya uvunaji maji ya mvua imejengwa katika shule, zahanati na misikiti. Umoja wa Mataifa imesaidia uendelezwaji wa mkakati wa kuvuna maji ya mvua na kutekeleza mwongozo wa kuingiza katika sekta ya maji mabadiliko ya sera na kujazia jitihada za taifa zinazohamasisha kuvuna maji ya mvua kama chanzo cha nyongeza. Matumizi ya maji ya mvua hupunguza mzigo wa vyanzo vya maji ya ardhini huko visiwani, kwani viko katika hatari kubwa kwa sababu utaratibu huo unaweza kusababisha maji ya bahari kujipenyeza na kuchanganyika. 68 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

71 Kwa Dar es Salaam, miradi ya jamii iliyounganishwa na jitihada za WASH ikitegemea tathmini ya mahitaji ya jamii katika makazi yasiyo rasmi inaendelea na inawanufaisha watu 21,500, ambapo miongoni mwao 11,200 ni watoto. Mradi wa majaribio wa uzalishaji gesi-hai (biogas) pia imeanzishwa kwa kujenga kituo cha uzalishaji katika Shule ya Sekondari Manzese iliyoko Tandale huku kikiwa na uwezo wa mita za ujazo 200. Hiki kitasaidia kuboresha mifumo ya usafi kwa kutoa nishati kwa ajili ya kupikia na umeme. Mara mradi wa majaribio utakapofanikiwa, modeli ya kituo cha gesi-hai itachukuliwa tayari kwa usambazaji katika shule nyingine. Chini ya Programu ya Maji na Usafi katika Ziwa Viktoria Awamu ya II, mamlaka tatu za udhibiti zilishiriki katika jitihada za kujenga uwezo ili kuboresha uendeshaji na matengenezo ya vituo vya kutibu maji. Jitihada hizi zimehusisha uandaaji wa mipango kazi, uwekaji gharama za maji, menejimenti ya maji taka na kinyesi, yote kwa lengo la kuleta ufanisi, usawa, tija na uendelevu katika kutoa huduma kwa jamii. MDAs na LGAs zinazohusika ziimarishe uratibu na kuingiza IWRM katika mipango yao ya sekta na kuimarisha sera, mikakati na uwezo wao kuhusu mazingira na afya, ili kufanya tathmini ya athari kwa mazingira na afya Uendelevu wa mazingira unazingatiwa katika Lengo hili, kama kanuni kuu ya Umoja wa Mataifa katika uendeshaji programu. Hii imetafsiriwa katika jitihada mbalimbali zikiwemo: Msaada ili kuendesha Tathmini ya Athari kwa Afya na Mazingira kunakofanywa na timu za wilaya za zmoh. Maarifa na ujuzi uliopatikana pia umewezesha utambuzi wa uhusiano wa afya na mazingira na matumizi yao katika kulinda na kuhamasisha afya ya jamii. Utekelezaji wa mitazamo ya Tamko la Libreville kuhusu Afya na Mazingira nchini, suala lililosababisha kuanzishwa kwa mipango ya taifa kwa hatua za pamoja za kushughulikia viungo vya afya na mazingira na upungufu katika kutoa huduma. Zana za mawasiliano (machapisho ya IEC) zilianzishwa, kuelezea mabadiliko ya tabia ya nchi kuhusu afya na hususan kuhusu WASH na kutetea uanzishwaji wa mipango/mikakati ya kujinusuru dhidi ya mabadiliko ya tabia ya nchi, kulinda vyanzo vya maji na pia usafi na suhula za afya. Kutokana na jitihada hizo, miongozo ya mipango ya kujinusuru dhidi ya mabadiliko ya tabia ya nchi kwa upande wa maji iliandaliwa ili kuwezesha uanzishwaji wa Mipango ya Maji Salama ya Mamlaka za Miji na Vijiji za Maji. Hii itaimarisha usimamizi na kushughulikia hatari za maji katika mfumo wa usambazaji maji ambazo zingeweza kusababishwa na mabadiliko ya tabia ya nchi na majanga mengine. Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 69

72 3.8 UTAWALA Wizara, Idara na Wakala zinazohusika ziendeleze mikakati ya kitaifa iliyo muhimu ili kuleta utawala bora Katika Lengo hili, mihimili mitatu ya utawala bora inalengwa ili kupewa nguvu: yaani, mabadiliko ya kisheria, kupiga vita rushwa na Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji Wanawake (GEWE). Matokeo yaliyopatikana ni pamoja na: Mkakati wa Marekebisho ya Sekta ya Sheria Zanzibar wa ulithibitishwa na kupitishwa na Baraza la Mawaziri na, kufuatia msaada wa ushauri, Sera ya Msaada wa Sheria ilikamilishwa. Hizi zinaweka msingi kwa mfumo wa msaada wa kisheria kupata sura ya kitaasisi na uandaaji unaoendelea wa muundo-dhana kamili wa sheria ya kusimamia msaada wa kisheria ili kuimarisha upatikanaji wa haki na huduma za kisheria kwa wanyonge katika jamii. Tume ya Marekebisho ya Sheria iliyofufuliwa (LRC) ilisaidiwa kupitia manunuzi ya vifaa muhimu. Tathamini ya uwezo na mahitaji ya mafunzo pia ilifanyika ili kubaini stadi wanazohitaji wafanyakai katika taasisi za sekta ya sheria huko Zanzibar, ambapo mfululizo wa mafunzo ulitolewa. Kauli ya kuunga mkono na kujenga mwafaka kuhusu vipaumbele muhimu vya maendeleo na haki za binadamu kwa uandaaji wa miundo-dhana ya baada ya 2015, kwa hiyo, inatarajiwa. Upungufu wa uwezo miongoni mwa wafanyakazi walio katika taasisi za sekta ya sheria huko Zanzibar ulishughulikiwa baada ya kufanyika tathmini ya mahitaji. Wafanyakazi viungo hivi sasa wanaonyesha uwezo bora zaidi katika menejimenti ya kupanga miradi, kuandaa taarifa, kuendesha usimamizi na tathmini, maandalizi ya sera na uchambuzi na hivyo kuchangia katika kuimarisha kwa ubora na ufanisi katika kutoa huduma za kisheria. Mashauriano, yakiwemo mikutano ya kuthibitisha wadau wa umma, kuwezesha ukamilishaji wa mipango mipya ya kupiga vita rushwa ambayo inazitaka sekta za umma na makampuni 100 katika sekta binafsi kuweka ahadi ya kufufua mapambano dhidi ya rushwa. Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge 70 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

73 Dhana ya kudai ngono kama rushwa ilipitishwa katika kazi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) na moduli ya kudai ngono kama rushwa iliingizwa katika mafunzo ya wasimamia sheria na mahakimu. Mamlaka ya Zanzibar ya Kupiga Vita Rushwa na Makosa ya Kiuchumi ilianzishwa sambamba na maandalizi ya mkakati wa kupiga vita rushwa huko Zanzibar. Msaada endelevu ili kuwa na Mamlaka yenye ufanisi umetolewa kwa maana ya mafunzo, msaada wa kiufundi na utoaji wa vifaa. Kujitathmini kwa UNCAC kulikofanywa na Tanzania kulitoa mchango muhimu kwa kazi za siku za usoni kuhusiana na kupiga vita rushwa. Mapendekezo kutokana na kujitathmini kutatekelezwa kwa msaada wa Umoja wa Mataifa kama ilivyokubaliwa na serikali kupitia TAKUKURU. Awamu ya pili ya kujitathmini itafanyika mwaka 2016 na itaendeshwa na Umoja wa Mataifa. Taasisi ya Utafiti Masuala ya Uchumi na Jamii na Idara ya Uchumi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ziliwezeshwa ili kuchambua hali ya haki za kiuchumi na kijamii (ESR) nchini Tanzania na kutoa Ripoti zenye ubora wa hali ya juu za Maendeleo ya watu, na kwa hiyo kuwezesha ujenzi bora wa hoja za yaliyomo katika sera na utawala wa ESR nchini, ili kuingizwa katika muundo-dhana wa maendeleo baada ya Kikosi Kazi cha Uingizwaji Masuala ya Jinsi kwa Sera Pana (GMWG-MP) kama mfumo muhimu wa serikali ya Muungano kwa uratibu wa masuala ya jinsia katika ngazi ya sera kimeimarishwa. Kikiendeshwa na wenyeviti wenza mmoja wa serikali na mwingine wa Umoja wa Mataifa, Kikosi Kazi sasa kinahusisha kundi kubwa zaidi la wadau (Wizara katika Sekta hii, Vyama vya Kiraia na wasomi), ili kujenga uwezo wa kiuongozi kwa MCDGC, na hutenda kazi kama mfumo hai wa uwajibikaji katika GEWE. Kama matokeo ya ushirikiano, zana muhimu za sera za kuendeleza GEWE chini Tanzania zimeandaliwa, ikiwemo miongozo ya uingizwaji jinsia katika mpango wa BRN, ripoti ya Beijing baada ya miaka 20 ambayo inaweka taarifa za maendeo na changamoto zilizopo hadi sasa na Wasifu wa Nchi kuhusu masuala ya Jinsia. Hiyo ya mwisho inaleta pamoja data zilizonyumbulishwa pamoja na uchambuzi makini wa jinsia kwa sekta kwa mara ya kwanza, kuimarisha uwajibikaji wa kitaifa kwa ahadi za kikanda na ulimwengu, ikiwemo mahitimisho yaliyokubaliwa ya CSW na Tamko la Beijing na Jukwaa la Kuchukua Hatua. Mfumo wa uratibu jinsia katika ngazi ya sera umeanzishwa Zanzibara kwa mara ya kwanza. Kikiongozwa na MSWYWCD, Kikosi Kazi cha Kiufundi cha Kuingiza Jinsia kinasaidia mazungumzo ya ngazi ya juu kuhusu sera. Hii tayari inainua wasifu wa masuala yanayohusiana na GEWE na ubaguzi mkali dhidi ya wanawake katika jamii za Zanzibar. Mikutano ya Wabunge wanawake kwa upande wa Bara na Zanzibar wameanzisha mpango mkakati wa miaka mitano ili kuongoza utekelezaji na kuimarisha usawa wa jinsia na haki za wanawake Bungeni. Zaidi ya hayo, kila upande umefanyia mapitio ya katiba yake ili kuhamasisha uwakilishi mkubwa zaidi katika mchakato wa kutoa uamuzi ili kuimarisha uungwaji mkono kutoka katika vyama vyote vya kisiasa. Uwezo wa wabunge wanawake katika kushawishi bajeti zinazozingatia masuala ya wanawake, masuala ya utawala, programu za jinsia zilizoimarisha na uingizwaji taratibu za za kufaa wakati wa ziara katika Bunge la Rwanda. Vipindi vya kufanya kazi kwa wabunge wanawake kuhusu uandaaji bajeti unaozingatia masuala ya jinsia katika sekta za elimu, afya, maji ambapo vilimwezesha kila mmoja kuelewa upungufu katika masuala ya jinsia kwenye bajeti, ambapo masuala 55 ya jinsia katika bajeti yaliibuliwa katika vipindi vya bunge kupitia michango ya maandishi na kwa kuzungumza. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 71

74 Serikali ya Tanzania iweke usimamizi na uratibu misaada kwa ufanisi zaidi Katika Lengo hili, UN inatoa msaada muhimu wa kiufundi na uratibu ili kusaidia kuimarishwa kwa ushirikiano wa maendeleo na menejimenti ya fedha za umma. Kwa namna ya pekee: Mkakati wa Serikali ushirikiano wa maendeleo wa miaka mingi Muundo-dhana wa Ushirikiano wa Maendeleo (DCF) umewasilishwa kwa viongozi waandamizi wa Wizara ya Fedha kwa mapitio ya mwisho. DCF inahamasisha matumizi makubwa zaidi ya mikondo mingi ya maendeleo (kuhama kutoka utegemezi uliozoeleka wa msaada kuelekea kwenye ushirikiano zaidi na sekta binafsi, vyama vya kiraia, na wahisasni wasio DAC kupitia ushirikiano wa Nchi za Kusini. Serikali ya Tanzania na Washirika wa Maendeleo (DPs) wanataraji kufanya kazi pamoja kupitia mpango kazi wa kuendesha DCF na kwa pamoja kupitia upya Miundo ya Majadiliano pale mkakati mpya wa maendeleo ya taifa utakapokuwa umekwishaanzishwa. Mfumo ulioimarishwa wa usimamizi wa misaada umewezesha michakato ya serikali ya kupanga mipango ya muda wa kati na mrefu, maandalizi ya miongozo ya bajeti na pia bajeti, huku utayarishaji ripoti na usambazaji wa data zinazostahiki ukiwa umeongezwa. Ripoti ya ODA 2012/13 ilichapishwa mwezi Septemba 2014 na Wizara ya Fedha ya Muungano huku rasimu ya kwanza ya ODA ya Zanzibar ikitarajiwa mwishoni mwa mwaka Ripoti ya hivi karibuni kabisa kuhusu Matumizi ya Umma na Uwajikaji katika Masuala ya Fedha (PEFA 2013) inaonyesha kwamba AMP imeimarisha kwa kiasi kikubwa utoaji ripoti kwa wahisani kuhusu utoaji wa misaada kwa programu/miradi na GBS ili kuimarisha maisha ya watu maskini kupitia maandalizi mazuri ya bajeti na utekelezaji. Mkutano wa Mwaka wa Mapitio ya Matumizi ya Umma (PER) Wiki ya Sera kuhusu Umaskini ya kila mwaka chini ya uangalizi wa Wizara ya Fedha ilianzisha mada muhimu kuhusu kufungulia ukuaji wa kitaifa na kuongoza jitihada za kupunguza umaskini kwa wadau wa aina mbalimbali. Ushahidi uliokusanywa kutoka katika tafiti za kuisaidia Serikali kufanya uamuzi. Kwa mfano, Sheria Mpya ya VAT, inajumuisha mapendekezo kadhaa kutoka kwenye utafiti wa msamaa wa kodi. Jitihada za uratibu wa Washirika wa Maendeleo kwanza ulianzishwa kupitia Sekretariati ya DPG inayosaidiwa na UN, ikiwemo vipindi maalumu kuhusu kutafuta fedha kwa ajili ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) na kuingiza michango ya Washirika wa Maendeleo katika Wiki ya Sera kuhusu Umaskini ili kuhakikisha kunakuwepo na majadiliano yenye tija na yaliyoshikamana katika kuanzishwa kwa hatua za kuchukua kuhusiana na vipaumbele vya taifa. Photo: UN Tanzania/Zoe Glorious 72 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

75 MDAs na LGAs ziwe na uwezo mkubwa zaidi wa kupanga, kuweka bajeti, kusimamia na kuandaa ripoti Ili kufikia Lengo hili, UN ilijenga uwezo wa taasisi muhimu katika ngazi ya kitaifa, kama vile Tume ya Mipango, na vilevile zile za Mamlaka za Serikali za Mitaa zilizoteuliwa ili kuendesha uchambuzi wa sera kwa msingi wa ushahidi, miongozo na zana, kwa ajili ya menejimenti na masuala ya fedha yaliyoboreshwa huku kukiwa na mkazo kuhusu masuala ya wanawake na watoto. Maendeleo yaliyofikiwa wakati wa kuandaa ripoti ni pamoja na: Mabadiliko katika mfumo mzima katika namna LGAs zinavyofanya kazi yalifikiwa na kuwawezesha wafanyakazi katika kitengo cha ufundi ili kuhakikisha kwamba miradi ya uwekezaji inaakisiwa katika mifumo ya mikoa kwa kupanga na kuweka bajeti. Msaada wa kiufundi kwa miradi mitatu ya maendeleo ya kiuchumi ambayo ni kituo kikuu cha mabasi na soko la kisasa katika halmashauri za miji ya Moshi na Kibaha imevutia takribani dola za Marekani milioni 24 kutoka katika taasisi za fedha za mahali nchini Tanzania. Programu ya Utafutaji Fedha za Mahalia nchini Tanzania (LFI-T) pamoja na Ofisi ya Rais-TAMISEMI inabaini na kuendeleza miundombinu ya miradi midogo na ya ukubwa wa kati ili kuzinufaisha jamii za wenyeji, uwezeshaji wanawake, utengenezaji nafasi za ajira na shughuli za kuingiza kipato. Kwa namna ya pekee, njia za uwekezaji katika miradi na vifurushi vya zana vya miradi ya fedha vimeandaliwa. Ushirikiano na washirika wa maendeleo kama vile Shirika la Msaada wa Maendeleo la Swideni (SIDA), Shirikla la Msaada wa Maendleo la Denimaki (DANIDA) na Shirika la Msaada wa Maendeleo la Ufaranza (AFD) umeanzishwa ili kupata rasilimali zaidi kwa ajili ya programu na kuanzisha suhula za kuimarisha masuala ya fedha kwa ajili ya miradi iliyoteuliwa. Mpango wa utafutaji fedha nchini Tanzania hivi sasa unatumika kama modeli ya ulimwengu, ambapo nchi imekuwa mwenyeji wa Ofisi ya Ulimwengu kwa ajili ya Programu ya Utafutaji Fedha za Miradi Mahalia. Kuboreshwa kwa uwezo wa kitaasisi na majukumu ya sekretariati ya baraza la mawaziri wa muungano na kitengo cha kuratibu maboresho na hivyo kujweka uwiano sawia wa sera za kitaifa, maboresho na mifumo ya tathmini. Mwongozo wa kufanya tahmini na usimamizi pamoja na kuanzishwa kwa program ya mafunzo na watumishi kupata mafunzo ya uchambuzi wa sera na kufanya tathmini... Ofisi ya Rais wa Zanzibar na Baraza la Mawaziri nao pia walipangwa upya ili kuboresha menejimenti, uratibu na mawasiliano ya umma. Kuingiza utaratibu wa kisasa kulisaidia kutofautisha kazi za huduma za kisiasa na jamii na wajibu wa kuoansiha ofisi na taratibu za utawala bora na uwajibikaji. Kituo cha Nyaraka za Sera kilianzishwa katika Sekretariati ya Baraza la Mawaziri, na hivyo kuimarisha upatikanaji wa taarifa kwa ajili ya uratibu wa sera na utekelezaji. Ripoti ya Kila Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA (MAIR 2013) na Ripoti ya MDGs ya 2014 iliandaliwa, kufuatia mifumo ya uendeshaji wa usimamizi na utoaji ripoti. Ubora wao wa juu unaonyesha uwezo ulioimarishwa wa Kitengo cha Kuondoa Umaskini (MoF) kusimamia maendeleo kuelekea katika malengo ya maendeleo. Ofisi ya Rais wa Zanzibar na Baraza la Mawaziri zilipangwa upya ili kuleta uratibu na mawasiliano bora zaidi, jambo lililoimarisha uwezo kwa ajili ya mapitio na uchambuzi wa sera zilizopelekwa katika Baraza la Mawaziri ili kupitishwa. Mipango mikakati mipya inayozingatia jinsia iliandaliwa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ili kujenga hoja bora zaidi kuhusu majukumu na wajibu wa wateule katika ofisi, ikiwemo upungufu wa uwezo na vilevile matokeo ya maendeleo yanayobashiriwa kwa wenye haki ili kufikiwa katika miaka mitatu ijayo. Rasimu ya Mwongozo wa Uendeshaji wa Kuandaa Bajeti Inayozingatia Jinsia (GRB) iliandaliwa ili kuongoza uingizwaji masuala ya jinsia katika bajeti za serikali, kuwezesha upanuaji wa GRB katika Wizara, Idara na Wakala zote za Serikali. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 73

76 Serikali ya Tanzania ikazanie kutimiza wajibu wake kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa Kuna sura mbalimbali zenye kuhusiana katika uchukuaji hatua chini ya Lengo hili, mkazo ni kuhakikisha Serikali ya Tanzania inatimiza wajibu wake katika kutoa taarifa na kutekeleza mikataba muhimu na Kufanya Mapitio ya Kila Baada ya Muda ya Ulimwengu (UPR). Serikali iliwasilisha ripoti yake mbele ya Kamati ya CRC mwezi Januari, 2015, ambayo iliongoza kamati katika kuandaa mahitimisho waliyoona. Pia, mwaka 2014, Umoja wa Mataifa ilisaidia wajumbe 80 wa Jukwaa la Haki za Mtoto Tanzania kuandaa na kuwasilisha Ripoti Mbadala mbele ya CRC kule Geneva. Hii iliongeza taarifa muhimu kuhusu hali ya utekelezaji haki za mtoto, uchambuzi wa masuala muhimu, na mapendekezo yenye mashiko ya kuongeza ubora wa hali ya watoto nchini Tanzania. Mpango Kazi wa Taifa wa Haki za Binadamu (NHRAP) umepitishwa tayari kwa utekelezaji kitaifa na kuanzishwa kama sehemu ya Mafunzo kwa Wakufunzi wa Elimu ya Haki za Binadamu katika taasisi za elimu. Washiriki wametoa mikakati yao ili kueneza elimu ya haki za binadamu katika taasisi wanazofanyia kazi. CHRAGG imesaidiwa ili kuchambua kwa ufanisi zaidi na kuzalisha data katika matokeo yanayopimika na kwa hiyo kuimarisha wajibu wake katika kusimamia utekelezaji wa NHRAP. Mfumo wa Utoaji Haki wa Serikali ya Tanzania utoe kinga bora zaidi kwa haki za wanawake na watoto katika mikataba/maeneo ya migogoro na sheeria na iweze kushughulikia mahitaji yao kiukamilifu zaidi Lengo hili lina shabaha ya kuhakikisha kunakuwa na Mfumo kamilifu wa Haki ya Mtoto na Mahakama ya Mtoto kama inavyoelekezwa katika Sheria ya Mtoto na viwango vya kimataifa, muundo-dhana wenye ufanisi na wenye kuzingatia masuala ya jinsia ili kukabili GBV, pamoja na uwezo wa lazima ndani ya Mahakama, Vyombo vya Kusimamia Sheria (LEA), ustawi wa jamii na vipengele vingine vinavyohusika katika utekelezaji kwa ufanisi wa hatua zinazongatia wanawake na watoto hasa kuhusu haki zao. Maendeleo yamefanyika kuhusu pande mbalimbali, kama vile: Mafanikio katika kuanzisha madawati ya Jinsia na watoto katika vituo 14 vya polisi. Kizio cha mwaka 2013 cha kesi za GBV/unyanyasaji watoto 4441 zilizotolewa taarifa imeonekana kuongezeka kwa asilimia 160 hadi kesi 11,650 (tazama sehemu ya Kinga ya Jamii kuhusu matokeo yanayohusika). Haki ya msaada wa kisheria iliendelezwa kwa watoto 306 hivi sasa wanaoendelea kushikiliwa katika magereza ya watu wazima na katika makazi ya watoto watukutu, na watoto 181 (asilimia 100) ya watoto katika Mahakama ya Watoto na katika mahakama tatu za wilaya jijini Dar es Salaam. Katika mzigo huo wa kesi, kesi 89 zilifutwa na watoto 27 waliachiwa kwa dhamana. Hii ilisababisha kesi kusikilizwa katika muda uliokusudiwa, utoaji haki katika hukumu, na kupunguza muda ambao watoto waliutumia wakiwa katika mahabusu. Watetezi wa Watoto waliwasaidia watoto 152 katika vituo vitatu vya polisi, jambo lililowezesha watoto wasioambatana na watu wazima kupata msaada wakiwa katika kituo cha polisi. Upande wa Temeke, watoto wengine 35 waliingizwa katika Programu ya Marekebisho ya Jamii kati ya Julai na Desemba, 2014 na hivyo kuongeza idadi hadi 144 ya watoto walionufaika kutokana na programu hiyo tangu kuanzishwa kwake. Programu kama hizo (marekebisho ya jamii na utoaji msaada wa sheria kwa watoto walio na mgogoro wa kisheria) zimenakiliwa na kutumika katika mkoa wa Mbeya, na hivyo kuwapa watoto fursa ya kupata haki na kuunguza urefu wa muda wanaotumia wakiwa vizuizini. Jamii zilizochaguliwa zishiriki katika majadiliano ya kidemokrasi na amani Lengo hili linahusisha hatua za kulenga vyombo vya habari vya jamii kama jukwaa la msingi kwa majadiliano ya jamii kuhusu masuala ya Amani na demokrasia, ambapo lilikuwa muhimu sana katika kipindi cha kuelekea katika 74 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

77 Uchaguzi Mkuu wa Kwa lengo hili katika : Miradi mitatu mipya ya redio za jamii kule Unguja na tatu upande wa Bara ilianzishwa, kupanua ufikiwaji wa watu wapatao 634,744. Jumla ya Redio za Jamii 28 zimesaidiwa katika mzunguko wa Mpango wa UNDAP, ambapo watu milioni 16 wamefikiwa, huku haki zao za kupata taarifa za maendeleo na kushiriki katika mijadala ya demokrasia zikitetewa. Mtandao wa Wanahabari Vijana (YRN), jitihada inayotoa mafunzo kwa watoto kuhusu utetezi wa haki za watoto katika redio na televisheni, umepanuliwa na kuingiza wilaya mbilil mpya (Kahama na Ilemela). Programu hiyo inawapa watoto fursa ya kutoa maoni yao na kushiriki kikamilifu katika majadiliano ya demokrasia na amani. Wizara ya Mambo ya Ndani (Naibu Waziri) alishiriki katika mkutano wa kikanda wa AU-SADC-UNDP mwezi Septemba ili kuhamasisha uanzishwaji wa miundombinu ya kitaifa ya amani. Wizara sasa inaongoza jitihada za Tanzania, kwa kuungwa mkono na Umoja wa Mataifa, kwa kuanzishwa kwa mtandao wa vyama vya kiraia (makundi ya kiimani, AZISE, wasomi, n.k.) na kukamilishwa kwa miundombinu iliyopo ya kitaifa ya amani. Taasisi muhimu zitekeleze kwa ufanisi majukumu yao ya uchaguzi na kisiasa Lengo la mwisho chini ya Kikosi Kazi hiki linawapa Wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kushughulikia kikamilifu uwakilishi, shughuli za kutunga sheria na majukumu yao ya kuisimamia serikali. Matokeo yaliyopatikana katika eneo hili ni pamoja na: Miongozo Mipya ya Usikilizaji wa Hadhara iliandaliwa na Kikosi Kazi cha Bunge ili kuimarisha fursa ya wananchi kupata taarifa na kuwawezesha kushiriki katika kutoa uamuzi. Msaada wa Umoja wa Mataifa uliwezesha Bunge kuchapisha taarifa na ripoti kutoka katika mikutano miwili ya kibunge ya kikanda (SADC) ambayo Bunge la Muungano lilikuwa wenyeji mwezi Septemba na Oktoba, kwa hiyo kuimarisha uelewa wa raia kuhusu kazi zao na masuala ya kikanda. Ofisi ya Bajeti katika Bunge ilianzishwa na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar. Hii itarahisisha kunyumbulisha taarifa za bajeti ambazo huwa ni vigumu kwa wabunge kuzielewa, na kuwezesha uchambuzi makini wa bajeti na menejimenti na fedha kwa kutumia data zilizo mezani. Upungufu wa utungaji sheria kuhusu jinsia katika Sheria ya Vyama vya Siasa, Sheria ya Uchaguzi na Sheria ya Gharama za Uchaguzi ulibainishwa kufuatia mapitio ya Jukwaa la Wanawake Kutoka Vyama Vyote Tanzania (TWCP) kwa lengo la kusimamia mabadiliko ya sheria yajayo. Mapendekezo ya mwisho yalitumwa NEC na ZEC, Msajili wa Vyama vya Siasa na wadau wengine. Wanawake wabunge walizindua Mkakati Kamambe wa Mawasiliano kuhusu Ushiriki wa Wanawake katika Michakato ya Kisiasa na Kidemokrasia ambayo inashughulikia uhamasishaji na uwezeshaji wanawake kugombea nafasi mbalimbali za kisiasa na kushiriki katika michakato ya kidemokrasia katika ngazi zote. Hii imeimarisha uelewa wa jamii na maarifa kuhusu majukumu muhimu ya wanawake katika utawala wa siasa na demokrasia hasa kupitishwa kwa nafasi za uongozi katika ngazi mbalimbali. Katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu 2015 kwa upande wa Muungano na ule wa Zanzibar, tume za uchaguzi zilitekeleza mapendekezo kutoka kwa watazamaji wa ndani na wa kimataifa wa Uchaguzi Mkuu wa Hii ilikuwa pamoja na kuanzishwa kwa zana mpya za mawasiliano/uwazi kama vile tovuti na mikakati ya mawasiliano. Zaidi ya hayo, kuboresha taarifa katika daftari la kudumu la wapiga kura na kuimarisha mfumo wa utunzaji data yote yalitekelezwa kwa mafanikio kwa Zanzibar na usajili wa wapiga kura ulikamilika kwa kutoa msaada wa kiufundi na vifaa. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 75

78 Photo: UN Tanzania 3.9 WAKIMBIZI Wakimbizi wapate huduma za msingi na kinga kama inavyoelekezwa na taratibu na viwango vya kimataifa Kikosi Kazi cha Programu ya Wakimbizi, ambacho kinahusisha mashirika ya UNHCR, IOM, UNICEF, WFP na UNFPA kinaendelea kuzingatia viwango vya kimataifa vya kinga na utoaji wa msaada wa vitu ikiwemo: WASH, Kinga ya Mtoto, Ukatili kwa Msingi wa Jinsia, Elimu, Makazi, Afya na Lishe kwa wakimbizi na wanaotafuta hifadhi. Wakati wa kipindi cha Mpango Kazi wa Mwaka, kwa kushirikiana na washirika mbalimbali wa utekelezaji, huduma zilitolewa kwa zaidi ya wakimbizi 149,000 katika Kambi ya Nyarugusu, wakiwemo Warundi waliowasili hivi karibuni (57.8%), Wakongo (42.1%) na mataifa mengine. Msaada muhimu ulijumuisha: Utoaji wa huduma za msingi zisizo na malipo za afya huku msisitizo ukiwa katika huduma ya kinga dhidi ya magonjwa makuu ya kuambukiza na majanga, kama vile malaria, kipindupindu, surua na homa ya uti wa mgongo. Kiwango cha kukamilisha kutoa chanjo kwa watoto walio chini ya miaka mitano ni asilimia 96, matokeo yanayoonyesha kuongezeka kwa kupokelewa kwa kinga dhidi ya milipuko. Kudhibit mapema kwa janga la kipindupindu mwezi Mei 2015, ilitokana na kufufua kwa kikosi kazi cha mashirika tofauti: jitihada za kuhamasisha usafi ziliimarishwa kwa kutumia watu wanaojitolea katika jamii kutoka jamii za wakimbizi, utoaji dawa ili kutibu kipindupindu na kutoa vifaa vya kuhifadhia maji kwa walioathirika na kipindupindu. Jumla ya wagonjwa 3,504 walitibiwa huku 18 wakipoteza maisha, ambapo wastani wa vifo ulikuwa asilimia 0.5, kiasi ambacho ni chini ya viwango vya Afya ya Umma cha asilimia 1. Karibu kiasi cha tani metriki 16,080 za aina mbalimbali za vyakula ziligawiwa kwa wakimbizi, na hivyo kutoa hakikisho la walau kiwango cha chini cha chakula kila siku cha kipimo cha 2,100 kcal na kwa hiyo walipata mahitaji yao ya lishe. Takribani makundi ya wanyonge 7,000, kama vile watoto chini ya miaka miwili na PLW walinufaika kutokana na nyongeza ya viinilishe katika mlo kupitia programu ya kutoa vyakula vya nyongeza kwa wote ili kuzuia utapitamlo. Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI pia walipokea msaada wa lishe ili kuzuia kuporomoka kwa hadhi yao ya lishe. Utafiti wa Upanuzi wa Lishe yenye Viwango (SENS) ulifanywa Desemba, 2014, ambapo ulionyesha kwamba Utapiamlo Mkali wa Wengi (GAM) na Utapiamlo Mkali Sana (SAM) (asilimia 1.4 na asilimia 0.0) vyote vimo ndani ya viwango vilivyokubalika vya Shirika la Afya Duniani (WHO). Tiba ya utapiamlo mkali zilianzishwa upya na hivyo kuchangia kupunguza idadi ya vifo kwa zaidi ya asilimia 0.5 kwa watoto waliolazwa hospitalini kwa sababu ya utapiamlo. Kwa kulinganisha na hali ya lishe ya mwaka 2012, utafiti ulionyesha kupungua kwa viwango vya upungufu wa damu miongoni mwa watoto wenye umri kati ya miezi 6 na 59 kutoka asilimia 38 hadi asilimia / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

79 Elimu, ambapo jumla ya kiwango cha kuandikisha iko katika asilimia 98 katika shule 12 za msingi na asilimia 97 ya uandikishaji katika programu za Maendeleo ya Mapema ya Utotoni. Msaada wa kutosha ulitolewa ili kuimarisha mazingira ya kujifunzia shuleni, ambapo jumla ya madarasa mapya 80 yalijengwa na 166 kufanyiwa marekebisho, ambapo madawati 4,954 kugawiwa, na vyoo 64 kufanyiwa matengenezo. Kulikuwa na uhakika wa elimu bora kwa watoto wakimbizi Wakongo wapatao 24,000 kupitia utoaji vifaa ya kujifunzia na elimu. Msaada wa tiba na saikolojia-jamii kwa wahanga wa vitendo vya ukatili wa ngono kwa msingi wa jinsia SGBV. Mapitio ya miundo-dhana ya kinga na hatua za kuchukua yalifanyika ambapo Mfumo wa Menejimenti ya Taarifa za GBV (GBVIMS) ulianzishwa ili kuwezesha ufuatiliaji mienendo na tabia za manusura na watesi, ili kuimarisha programu ya kuzuia na kuchukua hatua stahiki. Kiasi kikubwa cha rasilimali kilitolewa ili kuhakikisha malazi ya kutosha, salama na uhakika yanapatikana, mfumo wa maji uliimarishwa ili kupunguza migogoro katika vituo vya usambazaji maji, na kupunguzwa kwa utegemezi katika kuni kwa kuanzishwa majiko yanayotumia kuni kidogo na usambazaji wa taa zinazotumia umeme wa jua kwa kaya ili kuangaza usiku. Jjumla ya taa zinazotumia umeme wa jua 13,527 ziligawiwa kwa kaya za wakimbizi kutoka Kongo na asilimia 19 ya idadi ya watu walinufaika kutokana na majiko yanayotumia kuni kidogo (Save80). Zaidi ya watoto wakimbizi kutoka Kongoa 1500 walipatiwa matunzo mbadala yakiwemo kupewa rufaa kwa mahitaji ya msingi ya afya na msaada wa kisaikolojia. Makazi Maalumu Rafiki kwa Mtoto zilitoa kinga, mazingira ya kujifunzia na michezo kwa watoto wakimbizi wapatao 15,000. Watoto wakimbizi Warundi waliokuwa peke yao na wasiambatana na watu wazima walibainishwa, kufuatiliwa na kupewa huduma maalumu zikiwemo kuwapa msaada wa kisaikolojia, kinga na rufaa kwa huduma za afya. Usajili na Utunzaji Taarifa. Kukamilishwa kwa utafiti wa kina wa kuhakiki idadi ya watu ulitoa picha ya kuaminika na kamili ya kambi na hivyo kuwezesha uwekaji mipango na utekelezaji wa programu za kinga na msaada na pia kubaini njia za kulenga za uchukuaji hatua za kudumu ili kupata ufumbuzi. Kila kaya ya wakimbizi yenye waraka wa familia (uthibitisho wa Usajili na kadi ya mgawo), watu wenye mahitaji maalumu walibainishwa. Hadi kufika Julai, 2015, jumla ya wakimbizi wapya kutoka Burundi walisajiliwa kwa mfumo wa kisasa wa kibiometriki. Photo: UN Tanzania UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 77

80 Vifaa vya Msingi vya Msaada/Vifaa Visivyo Chakula (NFIs): Kwa mara ya kwanza katika miaka mitano iliyopita ugawaji wa jumla wa NFIs ulifanyika katika Kambi ya Nyarugusu ambapo vikombe vya bati 37,106; ndoo 6,635; vyandarua 38,000; matandiko ya plastiki 24,596; seti ya vifaa vya jikoni 14,613; mablanketi 14, 613 na madumu ya maji 15,963 (zikiwemo nguo) viligawiwa kwa wakimbizi wa Wakongo. Zaidi ya hayo, wanawake na wasichana 20,845 wa zaidi ya miaka 10 waligawiwa vifaa vya kujisitiri. Hadi kufika mwezi Juni, 2015, jumla ya wanawake 20,845 walio katika umri wa kuzaa waligawiwa chupi, sabuni na kanga kama sehemu ya vifaa vya kujisitiri; zaidi ya hayo, kuna ugawaji wa kila mwezi wa sabuni kwa jamii nzima ya Kambi ya Nyarugusu. Operesheni hiyo iliimarisha jitihada za kuwawezesha wanawake katika kutoa uamuzi kupitia mke katika kaya kuwa Wawakilishi Wakuu wa Kaya. Lengo la kufanya hivyo lilikuwa kuhakikisha msaada uliotolewa kwa kaya uliwafikia wanufaikaji waliokusudiwa, tofauti na miaka iliyopita ambapo kulikuwa na taarifa za matumizi mabaya yaliyofanywa na wenza wanaume. Wakimbizi wapya kutoka Burundi nao pia waligawiwa vifaa vya msingi vya msaada. Ufumbuzi wa kudumu kwa wakimbizi walio kambini upatikane Ufumbuzi wa kudumu kwa wakimbizi unachukua sura tatu za pekee: kuhamishiwa katika nchi ya tatu; kufanywa kuwa sehemu ya jamii ya wenyeji; kurejeshwa kwao kwa hiyari. Lengo la mwaka la kuwapatia makazi mapya wakimbizi Wakongo 4,520 katika Kambi ya Nyarugusu ilifanikiwa na kupitwa kwa asilimia 16. Kukamilishwa kwa uthibitisho wa watu kulisaidia kuimarika kwa ubora wa data za usajili, ambao hatimaye uliongoza katika kuwa na michakato yenye ufanisi ya kesi. Watu wenye mahitaji maalumu walipewa kipaumbele katika utaratibu wa kupewa makazi mapya, wakiwemo manusura wa vitendo vya ukatili, wanawake na wasichana walio hatarini, wagonjwa walio katika hali mbaya na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino). Hadi kufika Juni 30, Tanzania ilikuwa imekwishafikia lengo la asilimia 51.3 kwa sehemu yake katika mwaka 2015 ili kutoa rufaa kwa wakimbiz 2,577 kwa ajili ya maombi yao ya kuhamishiwa katika nchi ya tatu. Kulikuwa na ongezeko kubwa mwaka 2015 la uhamaji, ambapo jumla ya waliondoka kwenda kwenye nchi ya tatu ya makazi yao (Marekani, Kanada na Australia). Katika kipindi cha kutolea taarifa, hali Mashariki mwa Kongo iliendelea kukosa utulivu ambapo ripoti za mapigano na mauaji ya hapa na pale yaliendelea. Uhamishaji kwa hiyari kurudi makwao kwa hiyo halikuwa jambo lililowezekana kwa zaidi ya wakimbizi Wakongo 60,000 wanaokaa katika Kambi ya Nyarugusu. Wakimbizi waliopewa uraia wafurahie haki zao kamili kama raia wa Tanzania na jamii na LGAs zinazowapokea zijengewe uwezo ili kuwapokea Mwezi Septemba, 2014, Serikali ya Tanzania iliwapa uraia waliokuwa wakimbizi kutoka Burundi wapatao 162,156. Hawa waliingia Tanzania mwaka Rais alitoa maelekezo kwa mamlaka zinazohusika kushughulikia utoaji wa vyeti vya uraia kwa raia hawa 162,156 wapya wa Tanzania waliokuwa wakiishi katika Makazi ya Zamani ambapo walipewa uhuru wa kuchagua kuishi au katika maeneo yao ya sasa au kuhamia mahali pengine nchini na kufurahia haki zao kama raia. Hadi kufika Aprili, 2015, jumla ya vyeti vya uraia 149, 630 vilikwishatolewa. Roundi ya pili imepangwa kwa mwezi Septamba, 2015, ndani nan je ya maeneo ya Makazi ya Wakimbizi. Kama sehemu ya programu ya uingizwaji katika jamii, uchambuzi wa hali halisi katika mikoa yenye Makazi hayo ulifanyika. Matokeo yameweka muundo-dhana kwa uanzishwaji wa mwongozo mkakati mpya wa kupokelewa mahalia (SPLI) kwa raia wapya. Kwa sasa, Umoja wa Mataifa imetekeleza miradi kadhaa ya maendeleo ya kijamii-kiuchumi ya jamii yenye lengo la kusaidia usalama wa watu na ili kusaidia kuishi kwa amani katika Makazi ya Zamani ya Katumba, Mishamo na Ulyankulu na jamii za jirani. Jitihada hizi zinashughulikia Afya, Elimu, Maji na usalama dhidi ya vitendo vya ukatili na unyonyaji. Vituo vitatu vya polisi na nyumba za wafanyakazi zinaendelea kujengwa, shule saba zenye mifumo ya maji zinafanyiwa ukarabati, wadi mbili za wazazi na idadi ya nyumba kadhaa kwa watumishi wa afya zinafanyiwa marekebisho na kuwekewa vifaa. 78 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

81 Mifumo ya utoaji hifadhi na uhamiaji iimarishwe kwa kuendana na taratibu na viwango vya kimataifa Msaada unaendelea kwa uanzishwaji na uendeshaji wa sheria na sera za kitaifa nchini Tanzania zinazoendana na sheria na mikataba ya kimataifa kuhusiana na masuala ya hifadhi na uhamiaji. Matokeo makubwa yaliyopatikana hadi sasa ni pamoja na: Idadi ya vikao kwa ajili ya Kamati ya Taifa ya Mtu Mwenye Sifa (NEC) iliongezeka hadi sita, kwa hiyo kupanua upatikanaji wa ruhusa ya hifadhi na kupunguza ucheleweshwaji wa michakato ya kesi. Mipango Mkakati ya Kikanda kuhusu utawala na kinga ya wakimbizi na wanaoomba hifadhi katika mikoa ya Kigoma na Kagera iliandaliwa rasimu, kufuatia mafunzo ya maofisa Waandamizi wa Serikali iliyofadhiliwa na IOM na UNHCR, pamoja na ushiriki katika semina za kikanda na kimataifa kuhusiana na haki za wakimbizi na wahamiaji. Maofisa wasimamizi wa sheria na waandishi wa habari 319 walipata maarifa maalumu kuhusu usimamizi wa masuala ya kibinadamu mipakana na vilevile haki na mahitaji ya wahamiaji nchini Tanzania. Mkakati wa Menejimenti Kamili ya Uhamiaji (COMMIST) ulianzishwa, ukitoa vipaumbele kwa utungaji kanuni za hadhi ya wahamiaji wasio wa kawaida nchini na kuwezesha usajili wa kibiometriki wa wahamiaji hawa wasio wa kawaida. Hadi sasa, wahamiaji 22,282 walijitokeza kujisajili mkoani Kigoma, ambao ulichaguliwa kwa ajili ya majaribio. Wahamiaji waliosajiliwa walipewa kadi za kinga ambazo ziliwapa uhalali wa kuishi nchini kwa miaka isiyozidi minne kabla hadhi yao haijatathminiwa na wao kuweza kuomba vibali vya kuishi nchini au kuomba kusaidiwa kurudi kwa hiyari yao katika nchi zao za asili. Raia wa Tanzania pia wanaweza kuomba uthibitisho wa uraia wao katika mchakato huu. Kupanuliwa na kuenezwa kwa usajili wa kibiometriki kunapangwa kwa ajili ya wahamiaji wasio wa kawaida kote nchini katika miaka mitano ijayo DHARURA Idara za Kukabili Maafa zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (PMO) na Ofisi ya Waziri Kiongozi (CMO) kwa ufanisi ziendeshe Utayari na Hatua za Kuchukua ili kukabili Dharura (EPR) huku kukiwa na mkazo katika maeneo yenye uwezekano wa kupata maafa Lengo hili linahamasisha uratibu wa hatua zinazochukuliwa kukabili maafa, kuweka muundo-dhana wa uendeshaji na miundo ya mazungumzo ambayo huhusisha sekta na mashirika mbalimbali, kwa kulenga wilaya na shehia zilizo hatarini zaidi. Matokeo makubwa yaliyopatikana hadi sasa ni: Miongozo ya Taifa ya Uendeshaji na Muundo-dhana wa Usimamizi na Tathmini ilisambazwa ili kuwa na mwitikio ulioshikamana na wenye ufanisi wa utayari wa dharura. Hii inakamilishwa na jukwaa la ngazi ya mikoa la Maafa RERR ambalo huleta pamoja wadau mbalimbali kwa uratibu na ushirikiano bora zaidi. Hatua mbalimbali za kujenga uwezo ili kusaidia Idara ya Kusimamia Maafa (DMD) katika Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais (VPO) kule Zanzibar, kama vile marekebisho ya ghala kule Pemba, manunuzi ya mahitaji yaliyowekwa tayari kwa dharura na vilevile mafunzo katika wilaya tano zenye kukumbwa na maafa ya mara kwa mara tayari kwa utekelezaji wenye ufanisi wa EPRPs kufuatia mazoezi ya utayari yaliyowahusisna wataalamu wa mipango wa wilaya wapatao Upande wa Bara, EPRPs za wilaya tatu za nyongeza zilianzishwa katika Mkoa wa Mtwara, kwa ushiriki wa wawakilishi kutoka LGAs, AZISE na FBOs, makundi ya wanawake na vijana kwa tathmini inayofuatia ya hatari na viwango vya kukosa uwezo wa kukabili maafa. Vilevile, kwa upande wa Bara, kamati za kusimamia maafa kutoka katika wilaya 15 zilichangia katika utekelezaji wa EPRP, na kuwezesha kupatikana kwa mafunzo na kuimarika kwa utekelezaji. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 79

82 Tathmini ya hatari, udhaifu na uwezo ilifanywa katika wilaya za Kilosa na Mvomero na hivyo kusaidia mabadiliko ya tabia ya jamii kwa kuepuka vitendo vya hatari vinavyosababisha mafuriko. Jamii zipate taarifa za kuaminika kuhusu dharura ili zichukue hatua mapema Katika kutambua umuhimu wa mifumo ya utoaji tahadhari mapema na ufanisi wa mawasiliano katika nyakati za dharura, Umoja wa Mataifa inatoa rasilimali za kuwezesha upashanaji habari makini katika ngazi za kitaifa na wilaya. Msaada huo unajumuisha sekta na wadau mbalimbali, kwa mfano: Ili kukabili madhara ya mabadiliko ya tabia nchi, maofisa ugani na wakulima katika Muundo-dhana wa Ulimwengu kwa ajili ya Huduma za Tabia Nchi (GFCS) katika wilaya za majaribio za Longido na Kiteto zimeelekezwa kuhusu matumizi ya ubashiri wa hali ya hewa ya msimu kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa ya Tanzania kwa ajili ya kuweka mipango ya shughuli za kilimo kwa mujibu wa mvua inayotarajiwa. Makundi ya Mashamba Darasa na wawezeshaji katika maeneo yote yanayolima pamba katika mikoa ya ukanda wa kati na kaskazini magharibi mwa Tanzania waliwezeshwa ili kutumia teknolojia za Uzalishaji Fungamani na Menejimenti ya Kudhibiti Wadudu Waharibifu (IPPM) katika mashamba yao ya pamba, ambapo ni njia za kubana matumizi kwa upande wa gharama, ni endelevu na rafiki kwa mazingira wakati wa kudhibiti wadudu waharibifu wa mazao. Njia kama hizo zilitumiwa kwa ajili ya usimamizi endelevu wa ugonjwa wa migomba unaoitwa Banana Xanthomonas Wilt (BXW). Wanavijiji walipewa mafunzo juu ya udhibiti wenye ufanisi, ambapo nakala 4,000 za machapisho yanayofundisha namna ya kubaini BXW na namna ya kuushughulikia yaliandaliwa na kusambazwa kote mkoani Kagera na jumla ya wanachama 318 wa kikosi kazi cha kukabili BXW na viongozi wa jamii walipewa mafunzo. Mafunzo ya kutoa elimu kwa walimu katika wilaya tano za Zanzibar ili kuhamasisha hifadhi ya mazingira na uingizwaji wa mada zinazohusiana na dharura katika mtalaa wa shule yalitolewa. Vipindi vya uelekezaji jamii katika Shehia 60 za Pemba na Unguja vimesaidia katika kuboresha usimamizi wa mifumo ya maji taka, usafi wa jumla na kuimarisha sheria ndogondogo ili kulinda mimea kama sehemu ya kudhibiti kipindupindu, mafuriko na ukame. MDAs, LGAs, na NSAs zinazohusika ziwe tayari, ziwe na uwezo wa kutosha wa kisekta na kutoa mwitikio ulioratibiwa vizuri wa ndani katika nyakati za dharura Uratibu wa kitaifa wa mifumo ya Afya, Lishe, WASH na Elimu iimarishwe ili kukuza uwezo wa mwitikio chini ya Lengo hili. Matokeo ni pamoja na: Wadau wa WASH ya Zanzibar wawezeshe mikutano ya mara kwa mara ya uratibu kwa ajili ya watendaji wa WASH na Lishe, kuimarisha utambuzi na kubadilishana taarifa kuhusu hali ya mambo kabla ya bidhaa za mwitikio wa dharura. Takribani watu 1,400 walitawanyika kufuatia mafuriko katika Mkoa wa Morogoro ambapo walipatiwa suhula za WASH, kama vile maji salama yaliyoletwa kwa magari na baadaye kufungwa kwa matenki ya ujazo wa mita 20, kujengwa kwa vyoo takribani 100 vyenye kutumiwa kwa mujibu wa jinsi, mabafu na suhula za kunawia mikono pamoja na vyombo vya kuhifadhia maji majumbani na vidonge vya kutibu maji. Kuhamasisha usafi binafsi ni jambo lingine lililofanyika huku kukiwa na ufuatiliaji wa mara kwa mara wa hali ya WASH utaratibu ambao ulipunguza milipuko ya magonjwa yanayoenezwa kwa maji. Watu maalumu katika ngazi ya Mkoa na Wilaya ya WASH kutoka katika Wizara ya Afya na TAMISEMI katika mikoa miwili iliyo hatarini zaidi walipewa mafunzo ili kukabili tathmini ya haraka na shughuli za mwitikio katika matukio ya dharura, kwa kutumia zana za viwango maalumu. 80 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

83 Matayarisho ya Elimu katika Dharura (EiE) na mazoezi kuhusu utayari na mwitikio vilifanyika katika asilimia 50 ya shule zilizoteuliwa katika mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe ili kujenga utayari wa kujinusuru wa watoto hasa dhidi ya vitisho vya kila kawaida. Watu katika ngazi ya mkoa na Wizara ya Afya wanaoshughulika na EiE walijengewa uwezo ili kuleta uratibu bora zaidi katika sekta na kutoa mwitikio wa kufaa kwa homa za virusi na za kutoka damu ikiwemo Ebola. PMO/DMD itoe upatikanaji wa chakula cha msaada wakati wa dharura kwa kaya ambazo hazina usalama wa chakula katika nyakati za dharura Kuimarishwa kwa uwezo wa kilojistiki na mifumo ya usambazaji ya mahalia kwa ajili ya msaada wa chakula cha ziada ndio mkakati mkuu kwa ajili ya matumizi ya Lengo hili la mwisho. Matokeo ya utafiti wa uwezekano yametumika kuangazia uanzishwaji wa muundo-dhana kwa ajili ya kuanzisha na kuendesha Akiba ya Hifadhi ya Nafaka ya Zanzibar, kuhakikisha akiba ya kutosha ya chakula kwa ajili ya nyakati za upungufu katika kaya. Utafiti kamili wa mnyororo wa usambazaji mchele kule Zanzibar, ukiwemo uchambuzi wa masoko ili kubaini hatari zilizopo na zinazoweza kutokea katika ngazi zote, ulikamilishwa mwezi Juni 2015 ambapo mapendekezo yalitumika kuongoza uanzishaji wa mipango kazi kwa ajili ya huduma endelevu ya Akiba la Nafaka. Kwa msimu wa mavuno wa 2014/2015, NFRA ilinunua takribani tani metriki 30,000 za mahindi kutoka kwa vyama 165 vya wakulima kwa bei nzuri ya soko. Kwa hiyo, NFRA iliongeza akiba yake ya dharura kwa ajili ya makundi ya watu wasio na usalama wa chakula ambapo pia ilibadili mkakati wake wa manunuzi ili kunufaisha vyama vya wakulima wadogo, kwa mujibu wa modeli ya Kununua kwa Maendeleo. Kwa upande wa mahitaji, kuanzishwa kwa mifumo ya Ulengaji na Usambazaji Inayosimamiwa na Jamii (CMTD) katika wilaya zilizochaguliwa zenye upungufu wa chakula ili kuhakikisha kwamba makundi ya watu yaliyo katika hatari kubwa ya kukosa chakula yanalengwa ipasavyo nyakati za dharura MASUALA MTAMBUKA YA KUZINGATIA Uwekaji mipango, ufuatiliaji, tathmini na utoaji taarifa wa Timu ya Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa ujikite katika matokeo na ushahidi Kikosi Kazi cha Mipango, Usimamizi na Tathmini (PMEWG) kimepewa jukumu la kutimiza Lengo hili, kikiihudumia Timu ya Umoja wa Mataifa Nchini na vikosi kazi vingine vya Mpango wa UNDAP vilivyopo, kikishirikiana na kila kimojawapo ili kuhakikisha kwamba michakato ya Uwekaji Mipango, Usimamizi, Tathmini na uandaaji taarifa vinajikita katika ushahidi na matokeo. Katika miezi 12 iliyopita, licha ya msaada unaoelekezwa katika michakato ya ndani chini ya Mpango wa UNDAP wa I, Kikosi Kazi kilifanya kazi kubwa katika kuandaaa Mpango wa UNDAP II. Mchakato huo ulisanifiwa katika namna iliyohakikisha unatumia ushahidi na ni jumuishi. Uwekaji vipaumbele wa kimkakati wa Programu ya Umoja wa Mataifa ya Ushirikiano ( ) ulitumia data kwa kuzingatia mahitaji ya nchi na uwezekano wa Umoja wa Mataifa kutekeleza majukumu yake, huku kukiwa na mkazo mahususi katika makundi ya watu yaliyo hatarini zaidi na yanayofikika kwa taabu. Mchakato ulikuwa shirikishi, na ulitoa fursa kwa Serikali, Vyama vya Kiraia, Vyombo vya Habari, Washirika wa Maendeleo, Sekta Binafsi na Umma kwa Ujumla kuchangia. Zaidi ya hayo, uandaaji na zao lenyewe viliongozwa na kanuni za programu muhimu za Umoja wa Mataifa, yaani: Mtazamo wa Haki za Binadamu; Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji Wanawake; Uendelevu wa Mazingira; Utamaduni na Maendeleo; Kujenga Uwezo; Menejimenti inayotumia Matokeo. Hapa chini kuna orodha ya vipengele vikuu vilivyofikiwa: UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 81

84 Mwongozo wa Mpango wa UNDAP II ulipitishwa na kamait ya Uongozi ya Pamoja mwezi septemba, 2014 baada ya kufanyiwa mapitio na UNCMT na UNDG ngazi ya kanda. Mafunzo ya Menejimenti Iliyojikita katika Matokeo (RBM) kwa washirika wa Umoja wa Mataifa na Serikali kupitia warsha tatu sehemu ya kifurushi kamili kuhusu kanuni za uendeshaji programu za Umoja wa Mataifa ili kuhakikisha wadau waliandaliwa vya kutosha kuchangia katika utekelezaji wa programu ya Mpango wa UNDAP II (tazama hapa chini). Tafiti muhimu za kusaidia uwajibikaji wa UNCT ili kuleta matokeo yaliyokubaliwa na kusaidia uchukuaji mafunzo katika mzunguko unaofuatia wa programu, ikiwemo: a) Tathmini ya Mpango wa UNDAP I pamoja na Kikosi Kazi kinachohudumia kama Kundi la Tathmini ya Menejimenti kwa kushirikiana na wawakilishi wa Serikali ya Tanzania. (Kabla ya kuanza kazi, mapitio ya kina ya majedwali Usimamizi na Tathmini ya Mpango wa UNDAP I yakihuisha takribani viashiria 50 yalifanyika kwa ushirikiano na wafanyakazi wa shirika kama sehemu ya zoezi la utayari wa kutathminiwa). b) Uchambuzi wa Hali ya Tanzania ambao ulifafanuliwa na changamoto za vipaumbele vya maendeleo, vikiwemo upungufu wa uwezo na fursa zilizo katika Umoja wa Mataifa. c) Utafiti wa Mitazamo wa Wadau ambao ulikusanya namna programu za Umoja wa Mataifa zilivyoitikiwa, maeneo ya vipaumbele kwa hatua za siku zijazo na masuala yanayopendekezwa zaidi na njia za kupokea taarifa, kulenga Serikali, Vyama vya Kiraia, Washirika wa Maendeleo, Vyombo vya Habari na Umma kwa Ujumla. d) Majedwali ya Matokeo na Usimamizi na Tathmini kuhusu Mpango wa UNDAP II pamoja na majadiliano ya Kikosi Kazi, uendeshaji na vikundi vya kiufundi vya mawasiliano (ilihusisha zaidi wa wafanyakazi 130, katika kipindi cha zaidi ya miezi mitatu) ili kukamilisha Malengo na Michango pamoja na viashiria na shabaha kwa mujibu wa kanuni za RBM. Huku kukiwa na hakikisho la Mpango wa UNDAP ulionyooka na wenye kulenga matokeo MAHIRI zaidi ambayo yanaendana vizuri na vipaumbele vya taifa na mifumo ya data na pia Malengo ya Maendeleo Endelevu. UNCT inaimarisha uingizwaji wa masuala ya jinsia na uwezeshaji wanawake katika utekelezaji wa programu mbalimbali na kampeni za utetezi Kundi la Jinsia la Mashirika Mbalimbali (IAGG) liimarishe programu za utoaji huduma na jitihada za utetezi kupitia uingizwaji wa Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji wanawake (GEWE). Katika mwaka , Kundi la Jinsia (IAGG) liliweka mkazo katika kutoa msaada wa kiprogramu kwa Timu ya Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa Nchini (UNCT) na wadau wa kitaifa ili kuleta mwingiliano wenye tija wa masuala ya GEWE katika matokeo yanayopangwa na mifumo ya usimamizi kwa programu ifuatayo ya ushirikiano, Mpango wa UNDAP Semina za maelekezo zilitolewa kwa wafanyakazi na washirika, upande wa Bara na ule wa Zanzibar kama sehemu ya maandalizi kuelekea kwenye mchakato wa mashauriano (kwa kushirikiana na makundi mengine mtambuka), ili kuwezesha uingizwaji wa mikakati inayozingatia jinsia katika mada kuu mbalimbali kuanzia zinazohusu ukuaji uchumi hadi maendeleo, elimu na lishe. Licha ya hayo, matokeo pekee yakihamasisha usawa wa jinsia kuhusiana na wanawake na ushiriki wa Mpango wa UNDAP II ulianzishwa na pia maeneo muhimu yaliyoshughulikia vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Kundi la Jinsia IAGG litaendelea kutoa msaada kwa makundi mbalimbali yanapojiandaa kutunga mipango-kazi yao kwa mwaka wa kwanza wa utekelezaji Mpango wa UNDAP II. Wajumbe wa IAGG, kama sehemu ya Kundi Pana la Jinsia la Washirika wa Maendeleo, wameendelea kusaidia Kikosi Kazi cha Uingizaji Masuala ya Jinsia katika Sera Pana (GMWG-MP), jukwa la juu kabisa la sera kuhusu masuala ya jinsia chini ya muundo wa majadiliano na kiungo muhimu cha uratibu na mjadala wa kimkakati wa sera kuhusu GEWE. Kwa sababu hiyo, Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa unatumia miongozo ya uingizaji 82 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

85 jinsia, Wasifu wa Jinsia wa Nchi ya Tanzania umeandaliwa ili kuongoza sera na programu za baadaye na viashiria vya mwitikio wa jinsia vimechaguliwa kwa usimamizi wa baadae wa mipango ya maendeleo ya taifa (Tazama Kikosi Kazi cha Utawala wa taarifa zaidi kuhisiana na hili). Zaidi ya hayo, IAGG imeshirikiana na Serikali ili kusaidia maandalizi ya Miaka zaidi ya Ishirini baada ya Beijing na uingizwaji wa malengo ya SDGs katika jamii mahalia, huku kukiwa na mkazo katika ufikiwaji wa ahadi za GEWE chini ya sheria ya kimataifa. Jitihada zilizoimarika zaidi za utetezi na mawasiliano kuhusu GEWE zilizinduliwa na IAGG ambapo ushirikiano katika mashirika-shirikishi yakiwemo maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake na Siku 16 za Uanaharakati dhidi ya Vitendo vya Ukatili kwa Misingi ya Jinsia. Kama sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Kimatiafa ya Wanawake, zaidi ya wanawake na wanaume 1,000 waliandamana katika mitaa mbalimbali ya Tanzania ili kuadhimisha mafanikio ya Tanzania na kutoa wito zaidi wa kuchukua hatua katika kuleta usawa kwenye jinsia na kutetea haki za wanawake. Kama mwitikio wake, Rais alirudia ahadi ya serikali ya kutatua tatizo la ukosefu wa usawa ambao wanawake nchini Tanzania wanaendelea kukabiliana nao. UNCT ihamasishe kwa ufanisi zaidi Haki za Binadamu kupitia utetezi, uendeshaji programu na menejimenti yenye kulenga kuleta matokeo Kikosi Kazi cha Haki za Binadamu (HRWG) kinasaidia Timu ya Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa (UNCT) kuingiza masuala ya Haki za Binadamu katika programu na kampeni zake, na wakati huohuo kikihamasisha kwa ufanisi kuhamasisha haki za binadamu katika muktadha wa taifa kupitia jitihada za utetezi. Matokeo ya jitihada hizi za kuchukua hatua zinaweza kuonekana kupitia Vyombo vya Mikataba vya Umoja wa Mataifa kama vile Kamati ya Haki za Mtoto, kazi iliyofanywa juu CEDAW na utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Haki za Binadamu (NHRAP), na hasa katika kufanyia majaribio mifumo inayohusika ya usimamizi na kuandaa ripoti. Undani zaidi unaweza kupatikana kwenye sura juu ya Kikosi Kazi cha Utawala cha jitihada hizi. Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 83

86 Katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, HRWG kimefanya jitihada kadhaa ili kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya haki za binadamu ambayo yanaleta maana katika muktadha wa taifa, yakiwemo: Kutengeneza na kutangazwa kwa dakika moja kwa Tangazo la Utumishi wa Umma (PSA) ambalo lilitayarisha dhana na kutoa mifano ya haki za binadamu kupitia moja ya vipindi vinavyopendwa sana na watoto katika vituo vya televisheni UBONGO Kids huku kikivutia watazamaji kutoka kote katika Afrika Mashariki. Utangazaji wa mchezo wa redio wenye sehemu mbili ambao unaangazia aina zinazofahamika vema za ubaguzi unaotokea nchini Tanzania, hii ni pamoja na ule unatokana na jinsia au kutokana na ulemavu na hali fulani kwa watu wanaoishi na ualbino. Kuandaliwa kwa michoro ya vichekesho inayoeleza Tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Wenyeji kwa maelezo mepesi kueleweka. Kutengeneza michoro hiyo ya vichekesho katika Kiswahili ambapo inaelezea kwa ufupi taratibu katika mahakama za watoto. Zaidi ya hayo, wajumbe wa HRWG walishiriki katika mchakato wa Mapitio ya Kila Baada ya Muda wa Pamoja, kusaidia utekelezaji, usimamizi na tathmini ya mapendekezo 107 yaliyopitishwa katika mzunguko wa kwanza wakati ambapo nafasi ikiandaliwa pia kwa ajili ya mazungumzo kuhusu mapendekezo yaliyokataliwa na Serikali ya Tanzania. Kuhusiana na hilo la pili, CHRAGG imejengewa uwezo wa kuandaa uelewa dhana na uwezo madhubuti zaidi wa utetezi ili kutambua Haki za Makundi ya Wenyeji na kwa ajili ya Wizara, Idara na Wakala za Serikali ili kuelewa vema zaidi dhana muhimu na maana ya Tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Wenyeji. Vilevile kumekuwa na ongezeko la jitihada za utetezi zinazohusiana na Watu wenye Ualbino, kupambana na FGM na Ndoa za Utotoni. Kwa namna ya pekee, ofisi zinazohusika za Umoja wa Mataifa zimetumika kuleta maelewano na umoja katika kuondoa ubaguzi na kuzuia mashambulizi dhidi ya watu wenye ualbino kupitia matukio muhimu kama vile Siku ya Kimataifa ya Amani ili kukuza uelewa. Hizi zimesaidia kubadili mitazamo na kuongeza kasi katika uendeshaji mashtaka kwa hiyo kuvunja utamaduni wa kuruhusu vitendo viovu vinavyohusiana na mauaji na mashambulizi dhidi ya Watu Wenye Ualbino. Katika miezi 12 iliyopita, kumekuwepo na kupungua kwa mashambulizi kutoka wastani wa tukio moja kila baada ya siku 45 hadi tukio moja kila baada ya siku 120. Zaidi ya hayo, uchunguzi maalumu wa Ofisi ya Mwendesha Mashtaka ili kupeleleza vikwazo na changamoto katika utoaji haki kuhusiana na makosa dhidi ya Watu wenye Ualbino ulifanywa, na hivyo kuongeza hatua zaidi zilizochukuliwa na Serikali ya Tanzania kuimarisha uendeshaji mashtaka kuhusiana na ubaguzi huo. Kuanza kwa kampeni za kitaifa dhidi ya FGM na ndoa za utotoni kulikofanywa na Bi Graca Machel kulisaidia kuongeza uelewa na ahadi ya Serikali ya Tanzania na viongozi wa mahalia kwa umma katika Kanda ya Ziwa kuzuia vitendo vya FGM. Utaratibu mbadala wa unyago na jando uliandaliwa, ambapo zaidi ya wasichana 650 na wavulana 220 walishiriki, wakisaidiwa na wazazi na viongozi wa kimila. Walau ngariba wawili waliokuwa wakishiriki kuendesha vitendo vya FGM waligoma kushiriki katika utaratibu huo wa kimila muda ulipofika na walipewa kinga na msaada na viongozi wa mahalia kufuatia hatua zilizochukuliwa na wanachama wa HRWG. (Kazi ya nyongeza iliyofanywa na Kikosi Kazi cha Kinga ya Jamii). Kama ilivyoelezwa hapo juu, kwa kushirikiana na PMEWG na IAGG, Kikosi Kazi cha HRWG pia kiliandaa mafunzo ya awali ili kuhakikisha kwamba masuala ya Haki za Binadamu yaliingizwa katika matokeo yote yaliyopangwa na mifumo ya usimamizi ya Mpango wa UNDAP wa Warsha hizo za siku moja zilitoa uelewa mpana zaidi kuhusu dhana muhimu na matumizi yake katika mchakato wa uandaaji programu kwa wafanyakazi na washirika kwa upande wa Bara na Zanzibar. 84 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

87 JEDWALI TOFAUTI: ZANZIBAR YAKATAA KABISA VITENDO VYA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO MSWYWCD ilizindua Kampeni ya Uvumilivu Sifuri (Kukataa Kabisa) kwa Vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Wasichana mwezi Desemba, Wizara pia iliandaa mpango-dira wa kushughulikia vitendo vya ukatili majumbani na kuimarisha ukusanyaji taarifa kuhusu Vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na kusababisha mapendekezo ya mapitio ya mipango ya GBV na VAC na kuandaliwa kwa Mpango Oanishi na Kamili wa Kuzuia na Kutatua GBV/VAC. Mikakati na shughuli katika maeneo manne ya kimkakati yalihusisha kinga, mwitikio, sheria na sera pamoja na Usimamizi na Tathmini. Inatarajiwa kwamba NPA mpya kuhusu VAW na VAW vitakuwa tayari hadi Desemba, Watu wapatao 2000 kutoka Zanzibar waliunga mkono Kampeni ya Kukataa Kabisa yenye lengo la Kukomesha Vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto iliyozinduliwa na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mh. Dkt. Ali Mohamed Shein, wakati wa Siku 16 za Kupinga Vitendo vya Ukatili kwa Msingi wa Kijinsia. Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, Bw. Alvaro Rodriguez, aliipongeza Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhusu uzinduzi huo, hasa wa MSWYWCD ambao wanaongoza Kampeni na uchukuaji hatua ambao utaendeshwa kwa miaka miwili kwa kushirikiana na Umoja Mataifa (Umoja wa Mataifa Wanawake, UNICEF, UNFPA) na wadau wengine. Akizungumza katika tukio hilo, Bw. Rodriguez alisema: Sisi sote tutoe ahadi ya kuungana ili kukomesha vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Ahadi ya kukataa kabisa vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ni ahadi ya maendeleo ustawi na furaha ya kweli kwa watu wa Zanzibar. Funguka! Chukua Hatua Kukomesha Vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto Zanzibar! 3.12 KUWASILIANA KAMA TIMU MOJA Timu ya Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa iendeshe mikakati ya utetezi na mawasiliano iliyo shikamani na yenye ufanisi Wataalamu wa mawasiliano kutoka katika mashirika mbalimbali washirikiane katika shughuli mbalimbali zinazohusu utetezi na mawasiliano, kwa shughuli za ndani na za nje, ili kuendeleza uendeshaji programu za maendeleo na za kiutu nchini Tanzania. Chini ya mwamvuli wa Kuwasiliana kama Kitu Kimoja, Kundi la Mawasiliano la Umoja wa Mataifa limeandaa machapisho kadhaa ya mawasiliano yanayolenga matokeo, ambayo pia yametumika kama njia zenye ufanisi za utetezi. Hizi ni pamoja na: Kitita cha Matokeo ya UNDAP chenye taarifa za hivi karibuni kwa Kiingereza na Kiswahil. Wadau 5,000 wamepata vitita, wakiwemo Serikali na Washirika wa Maendeleo, vyama vya kiraia na wasomi, kupitia usambazaji wa moja kwa moja, nyakati za maonyesho au kutoka katika tovuti ya Umoja wa Mataifa Tanzania. Majarida ya Voices from the Field (Sauti kutoka Uwandani) yalisambazwa kwa wadau wa kitaifa na kupatikana kupitia meza za maonyesho, tovuti ya Umoja wa Mataifa Tanzania na mitandao ya kijamii. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 85

88 Tovuti ya Umoja wa Mataifa Tanzania iliyoandaliwa upya, ambayo inaendelea kutoa nyaraka na taarifa mpya kuhusu matukio/matokeo katika usanifu ulio rafiki kwa msomaji/mtumiaji. Tovuti inajaziwa na majukwaa ya mitandao ya kijamii (kama vile Twitter, Facebook na Youtube) ambayo yote yanasaidia kutangaza Mpango wa Kufanya Kazi Pamoja (DaO) miongoni mwa jamii. Jarida la kila baada ya miezi miwili la Umoja. Jarida hili huangazia habari za mafanikio ya Umoja wa Mataifa Tanzania katika kutoa mchango kwa vipaumbele vya maendeleo na masuala ya kiutu katika Taifa. Usambazaji umepanuliwa na kuhusisha si tu wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa na wafadhili, bali pia Serikali, vyombo vya habari na vijana na kuongeza usomaji hadi walau watu 5,000 mwaka 2015 kila linapotoka. Umoja wa Mataifa Tanzania pia imetumia matukio mbalimbali kukuza uelewa wa kazi yake, hasa ujumbe muhimu chini ya ajenda ya utaratibu wa kawaida na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs). Sherehe za Umoja wa Mataifa kama vile Siku ya Kimataifa ya Umoja wa Mataifa, Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, Siku ya Kukuza Uelewa Kuhusu Ualbino, Siku ya Kimataifa ya Vijana, Siku ya Umoja wa Mataifa, Siku ya Haki za Binadamu na Siku ya Kukuza Uelewa kuhusu UKIMWI zote zilisherehekewa kwa kufanya kampeni za kulenga. Vilevile, Maonyesho ya Saba Saba ya 2015, ambayo ni miongoni mwa maonyesho makubwa kabisa Afrika Mashariki, yalitumika kama jukwaa la kuonyesha mafanikio muhimu ya Umoja wa Mataifa. Zaidi ya watu 5,000 walitembelea banda la Umoja wa Mataifa, akiwemo Rais Jakaya Kikwete, mawaziri na wanadiplomasia. Shughuli za kufikia watu waliko pia zilikuwa sehemu muhimu ya kipengele cha Kuwasiliana kama Kitu Kimoja nchini Tanzania. Katika miezi 12 iliyopita, zaidi ya wanafunzi 1,000 na vijana walio nje ya mfumo wa elimu walifikiwa na programu ya ufikiaji katika masuala ya elimu na mafunzo ya ujasiriamali. Vijana 130 zaidi walishiriki jukwaa la Modeli ya Umoja wa Mataifa Kitaifa lililofanyika Arusha chini ya mada Vijana Wajadili Baada ya 2015: Wakati wa Uchukuaji Hatua wa Pamoja. Jukwaa liliwahusisha vijana katika ajenda ya maendeleo ya baada ya mwaka 2015, ambapo maazimio yao yalipelekewa kwenye tume ya mipango ya Serikali ili yajumuishwe kwenye ripoti ya taifa. Ushirikiano kati ya vituo vya redio vya mahalia na serikali uliwezeshwa, jambo lililochangia katika kuimarishwa kwa uendeshaji programu katika masaual muhimu yanayoihusu Umoja wa Mataifa. Kwa mfano, DMD-PMO, TMA na MAFSC zilihimizwa kutumia vituo vya redio za jamii kwa ajili ya utayari na mwitikio dhidi ya maafa; Wizara ya Afya imeshirikiana kwa mafanikio katika kampeni za kutoa chanjo ya kinga; MCDGC imeandaa majaribio ya mipango ili kupanua ushirika na vituo vya redio vya jamii ili kuhamasisha matumizi ya Dawati la Jinsia, mathalani. Mikakati imeandaliwa ili kuongeza ushirikiano na Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs) ili kuhakikisha kwamba taarifa sahihi, zinazoenddana na utamadauni zinawafikia wanawake na wanaume katika jamii za pembezoni. Kama sehemu ya msaada wa programu ya ndani, UNCG imetayarisha Mihtasari ya Sera ya kila robo mwaka ya Mpango wa DaO. Hii inatumika na wafanyakazi kama rejea za haraka kuhusu maandalizi muhimu ya Mageuzi ya Umoja wa Mataifa, na hivyo kuimarisha uelewa wao na hamasa kwa mchakato wa Mpango wa DaO. Kwa kuongezea, mafunzo ya vyombo vya habari kwa wazungumzaji wa Umoja wa Mataifa yalitolewa ili kutoa mwanga juu ya namna waandishi wa habari wanavyofikiri na kufanya kazi, kumpa kila mmoja ujasiri wa kushirikiana na vyombo vya habari wakati wa mahojiano kama fursa ya kuhamasisha malengo ya Umoja wa Mataifa na kuleta matokeo bora KUFANYA KAZI KAMA KITU KIMOJA UNCT kuimarisha miundo ya menejimenti ya manunuzi ya pamoja na kusaidia mifumo ya manunuzi ya taifa Chini ya Lengo hili, miundo ya menejimenti ya manunuzi ya pamoja ianzishwe ili kusaidia programu zenye ufanisi za utekelezaji, kimsingi kuanzia matumizi ya Mikataba ya Huduma za Muda Mrefu (LTAs) ya pamoja. Makubaliana ya namna hiyo ya kimkataba inapunguza idadi ya michakato ya manunuzi na kwa hiyo kupunguza gharama. 86 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

89 Zaidi ya hayo, uwezo wa kupatana bei wa Umoja wa Mataifa unaimarishwa kupitia Manunuzi ya Pamoja badala ya kila shirika kufanya manunuzi yake. Timu ya Manunuzi ya Pamoja ya Tanzania (TOPT) inaendelea kupiga hatua katika jitihada za kuoanisha na kuongeza matumizi ya manunuzi ya pamoja katika mfumo wa Umoja wa Mataifa Tanzania. Idadi ya LTAs za pamoja imeongezeka hadi 66, huku kukiwa na LTAs maalumu kwa shirika ambazo pia zinaweza kutumiwa na mashrika mengine. LTAs za pamoja zinajumuisha zile za huduma za jumla kama vile benki, ulinzi na usafi katika ofisi za Umoja wa Mataifa, huduma za mipango ya usafiri na upigaji chapa. Hata hivyo matumizi ya mashirika bado yako juu, ambapo LTAs zikitumika kwa asilima 45 tu ya manunuzi yote. Mafanikio makubwa katika kipindi cha mpango kazi (AWP) cha 2014/15 kilikuwa nia mipangilio ya warsha za watoa huduma, zilizohudhuriwa na zaidi ya watoa huduma 70, ambapo walielimishwa kuhusu kanuni za manunuzi za Umoja wa Mataifa, jinsi ya kufanya biashara na Umoja wa Mataifa na kanuni za Fungasho la Pamoja. Hii imetoa fursa ya kupokea mrejesho kuhusu namna Umoja wa Mataifa inavyotazamwa kama mnunuzi. Mapendekezo, yanayohusiana na muda wa utoaji malipo na urahisi wa michakato ya zabuni, hivi sasa unafanyiwa mapitio mapya. Hifadhi ya taarifa ya watoa huduma 313 kwa bidhaa na watoa huduma wadogo 276 imekwishaanzishwa, kufuatia utafiti kamili wa hali ya soko. Hifadhi hii ya taarifa inasaidia mashirika ya Umoja wa Mataifa kupata taarifa za mtoa huduma wakati wa mchakato wa utangazaji zabuni, na kwa hiyo kuongeza uwezekano wa kupata bei shindani na zenye ubora kulingana na huduma itakayotolewa. Michakato ya Rasilimali-Watu ya nchini ionishwe, iwe yenye tija na itoa majibu kwa mahitaji ya programu Umoja wa Mataifa ifuatilie njia inayooana vema na michakato muhimu ya uajiri na menejimenti ya rasilimali watu ili kuhakikisha upatikanaji wa kikosi kazi mahiri na chenye ari kwa ajili ya ufanisi, ubora wa uendeshaji programu kwa matokeo bora. Mafanikio kadhaa yamepatikana wakati wa kipindi cha Mpango wa UNDAP. Haya ni pamoja na: Uanzishwaji na matumizi ya utaratibu wa pamoja wa utoaji matangazo ya nafasi za kazi kwa mashirika mengine ili kuleta mshikamano katika uwekaji nyaraka wa nje na kwa uwezekano wa kutumia tovuti tofauti za mashirika. Mafunzo kuhusu usawa wa jinsia na uingizwaji katika mchakato wa uajiri kwa wafanyakazi wa idara ya rasilimali watu, kama sehemu ya ahadi ya fursa sawa mahala pa kazi. Usambazaji wa mwongozo wa utendaji kazi kwa wafanyakazi ili kuwawezesha wageni kuendana na utendaji kazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania na kurahisisha kushirikiana na wengine katika timu walizojiunga nazo. Uingizwaji wa Malengo ya Utendaji Kazi wa Mpango wa DaO katika zaidi ya asilimia 50 ya wasifu za wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa (kwa msingi wa kujitolea), kuhimiza kujituma na tathmini sahihi ya wafanyakazi katika mchakato wa ushirikiano wa mashirika. Kuanzishwa kwa Mpango wa Uokoaji wa wakati wa Maafa kwa Huduma za Pamoja za Umoja wa Mataifa, ambapo hifadhi kwa ajili ya mifumo muhimu tayari imeanzishwa. UNCT ioanishe michakato ya msingi ya menejimenti ya fedha na kushugulikia upungufu katika uwezo Eneo hili la matokeo linakazia uanzishwaji na uendeshaji wa michakato iliyooanishwa ili kuleta ufanisi katika utoaji fedha, ukaguzi wa mahesabu na kuthibitisha ubora, na kwa sababu hiyo kukuza uwazi na uwajibikaji wa wadau muhimu. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 87

90 Katika kipindi kinachohusu taarifa hii, mpango wa ukaguzi hesabu wa HACT wa 2014 uliandaliwa na hesabu za ukaguzi zilikamilika kwa mafanikio. Jumla ya ukaguzi hesabu wa pamoja 42 ulifanyika kwa upande wa Bara na Zanzibar wenye thamani ya dola za Marekani milioni 24 (sawa na shilingi za Tanzania bilioni 50). Kwa sababu hiyo, mpango wa hakikisho la pamoja ulikubaliwa ili kushughulikiahatari zilizobainishwa. Matumizi ya tathmini za pamoja kwa miradi midogomidogo imesaidia kuokoa gharama yenye thamani ya dola za Marekeani 46,000 (sawa na shilingi za Tanzania milioni 95) katika kipindi cha mpango kazi wa 2014/15. Hatua zilichukuliwa kuhusiana na mapendekezo ya mapitio ya hivi karibuni kuhusu vikwazo vya sasa katika uhamishaji fedha kupitia mfumo wa Hazina Kuu ambapo sasa uko katika matayarisho, yote yanafanyika kwa ushirikiano na Wizara ya Fedha. Hizi zitapunguza muda unaotumika kugawa fedha na hivyo kuimarisha viwango vya utoaji huduma vya programu. UNCT kuanzisha suluhu za TEHAMA zenye gharama nafuu ili kusaidia uendeshaji wa programu Kikosi Kazi cha TEHAMA cha Mashirika Mbalimbali kianzishe na kuendesha zana za kompyuta zinazotumika katika Umoja wa Mataifa nzima ili kusaidia programu na uendeshaji wa kazi za menejimenti. Mafanikio makubwa yaliyopatikana katika miezi ya hivi karibuni ni hasa kuweka kiungo kikuu cha mtandao usiotumia waya kupitia miundombinu ya mtandao wa Nyaya za Kioptiki. Hii imesaidia kupunguza gharama za uendeshaji hasa kwa kupungua thamani ya vifaa visivyotumia nyaya, marekebisho ya minara na huduma za wapagazi. Miundombinu ya kiungo hicho kikuu cha Nyaya za Kioptiki pia kimeondoa uzubaifu wa mtandao, kwa hiyo kimeongeza kasi ya intaneti kwa watumiaji. Manufaa mengine ni pamoja na kuimarisha uwezo wa kupatana bei katika soko, huku kiwango cha uwezo wa intaneti kikiongezeka maradufu tangu kuanzishwa kwa mradi huu pasipo kuingia gharama ya ziada. Mashirika yote yanayoshiriki pia yameunganishwa kwa huduma ya intaneti inayosimamiwa pamoja yenye kasi ya 14Mbps kwa kuzingatia idadi ya mashirika, huku uwezekano wa kuongeza kasi kuhusu mahitaji kwa kuzingatia mgao wa juu wa vifurushi visivyotumiwa. KATIKA JEDWALI TOFAUTI MAFUNZO KWA MTANDAO (E-LEARNING) ILI KUENEZA KANUNI ZA GLOBAL COMPACT Umoja wa Mataifa Tanzania imepata fedha kupitia ubunifu wa suhula ya UNDOCO ili kuanzisha programu ya mafunzo kwa njia ya mtandao kuhusu kanuni za global impact utakaotolewa kwa wauzaji wadogowadogo mwaka Jitihada hiyo inakamiilsha shughuli za kiprogramu za UN Tanzania kuhusu haki za binadamu, kwa kuimarisha maarifa ya wauzaji wadogowadogo wa mahalia kuhusu kanuni kuu mahali pa kazi katika manunuzi, menejimenti ya rasilimali watu na matumizi ya rasilimali. Umoja wa Mataifa inaweza kufanya majadiliano ya mikataba ambayo inaingiza vipengele fulani na kusimamia namna watoa huduma wanavyozingaita kanuni zilizokubaliwa kupitia ukaguzi wa hiyari. Kwa kuchagua watoa huduma ambao wana rekodi nzuri katika masuala ya haki za binadamu na kwa kutoa taarifa stahiki kuhusu umuhimu wa kanuni kama hizo, Umoja wa Mataifa inaweza kuwa na ushawishi chanya katika haki za binadamu nchini Tanzania. 88 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/ /

91 Photo: UN Women / Stephanie Raison UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 89

92 90 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 Photo: UN Women/ Stephanie Raison

93 4.0 MUUNDO-DHANA WA BAJETI YA PAMOJA Mpango wa UNDAP wa unajumuisha muundo-dhana wa bajeti ya pamoja unaoundwa na rasilimali za msingi za shirika, rasilimali zisizo za msingi za shirika na Mfuko Mmoja. Utekelezaji wa Programu ya Ushirikiano, ikiwemo ajenda ya mabadiliko, hutegemea mafanikio katika kuhamasisha vyanzo vyote vitatu vya fedha. Rasilimali za msingi zinatolewa na nchi wanachama kwa msingi wa hiyari kwa ajili ya kazi za msingi (na baadhi za kiprogramu) za shirika. Hizi hutolewa na makao makuu ya ofisi za nchi. Ni mashirika machache tu ya Umoja wa Mataifa yanayoweza kupata fedha za msingi. Rasilimali zisizo za msingi zinaundwa na fedha za ziada kwa kazi za kiprogramu (na baadhi za msingi) za mashirika. Hizi zinapatiwa fedha kutokana na jitihada za uhamasishaji za ngazi ya makao makuu, kanda na nchi. Mashirika yote ya Umoja wa Mataifa yanatumia njia za fedha sizizo za msingi. Mfuko wa Pamoja wa Fedha wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania ulianzishwa mwaka 2007 chini ya ajenda ya mageuzi ya Umoja wa Mataifa ya DaO, ili kutoa fedha za kazi za kiprogramu na uendeshaji katika ngazi ya nchi. Unasimamiwa na Ofisi ya Mfuko wa Wadhamini wa Washirika Wengi (MPTF) wa New York na unafadhiliwa kupitia michango ya Washirika wa Maendeleo makao makuu kupitia miundo kama vile Mfuko wa Pamoja wa Kuleta Matokeo na vilevile katika ngazi ya nchi kupitia makubaliano ya pande mbili. Karibu vyombo vyote vya Umoja wa Mataifa vinachangia katika Mpango wa UNDAP wa nchini Tanzania kwa kupata kutoka katika Mfuko Mmoja. Ugawaji unafanyika kwa msingi wa kila mwaka na JSC kwa kuzingatia sifa zilizokubaliwa na vigezo vya utendaji, kama inavyofafanuliwa katika MoU ya Mfumo Mmoja wa Umoja wa Mataifa na Hadidu za Rejea. Muundo-dhana wa Bajeti ya Pamoja unatoa fursa ya uwazi zaidi. Kupitia Mfumo wa Usimamizi Matokeo ya UNDAP kupitia mtandao (RMS) ( washirika wanaweza kupata taarifa za ndani za AWPs, ripoti za kila baada ya miaka miwili na taarifa mpya kuhusu maendeleo yaliyopatikana hadi wakati huo kwa programu na uendeshaji. Zaidi ya hayo, kupitia Ofisi ya LANGO la MPTF ( factsheet/fund/tz100) washirika wanaweza kupata data za wakati huohuo zinazohusiana na michango ya wahisani, bajeti za programu na uhamishaji kwa mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayoshiriki chini ya Mfuko wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa. Timu ya Nchi ya Umoja wa Mataifa inatumia kanuni za Ushirikishaji Uhamasishaji wa Rasilimali ili kuhakikisha kuwepo kwa uwazi, njia fungamani katika ushiriki. Hii inahitaji mashirika kutoa taarifa Zmpya katika RMS kuhusiana na fedha zilizohamasishwa ili kuwezesha tathmini ya kila baada ya muda ya pengo la fedha na uwekaji vipaumbele kadiri ya mahitaji na mazingira. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 91

94 Kama waungaji mkono wa mchakato wa Umoja wa Mataifa Moja nchini Tanzania, Marafiki wa Umoja wa Mataifa huwa kama chombo kisicho rasmi cha Washirika wa Maendeleo ambacho hukutana na wawakilishi wa Umoja wa Mataifa ili kujadili masuala ya pamoja. Mratibu Mkazi huongoza ushiriki wa Umoja wa Mataifa katika ngazi ya Wakuu vya Ubalozi, ambapo hutumia majukwaa hayo kueleza matokeo yaliyopatikana na kupata uungwaji mkono wa jitihada za Umoja wa Mataifa zinazoendelea. Ofisi ya Mratibu Mkazi hushugulikia katika ngazi ya kiufundi, kuwafahamisha wajumbe maendeleo yaliyopo sasa katika ngazi ya dunia kuhusu mpango wa DaO, kutoa taarifa mpya kuhusu maendeleo ya msingi ya Umoja wa Mataifa katika ngazi ya nchi kama vile hatua zilizopigwa katika kuunda UNDAP na mchakato wa utekelezaji na kuwaalika wajumbe wa UNCT kuonyesha maeneo fulani ya uendeshaji programu zao. Kielelezo cha II: Mpango wa UNDAP Muundo-dhana wa Bajeti ya Pamoja (taarifa mpya ni za Oktoba, 2015) 4.1 UTOAJI HUDUMA ZA FEDHA Kama ilivyoelezwa katika utangulizi, takwimu zilizotolewa katika sehemu hii ni za mpito. Data bado hazijapata kibali cha makao makuu ya mashirika yanayohusika. Takwimu zilizoruhusiwa zitapatikana tu mwishoni mwa robo ya pili ya mwaka Data kuhusu ahadi, akiba na matumizi ya Mfuko Mmoja yataelezwa kwa kina katika ripoti ya fedha itakayochapishwa Mei 31, 2016 katika Lango la Mfuko wa Wadhamini wa Washirika Wengi mptf.undp.org/factsheet/fund/tz100. Hii ni kwa kuendana na masharti ya utoaji ripoti za Mfuko wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa kama ilivyoelezwa katika Makubaliano ya Makataba (MoU). Kwa mujibu wa utoaji taarifa chini ya Mapitio ya Kila Mwaka, Vikosi Kazi vilipata wastani wa asilimia 92 kwa miezi 12 iliyopita. Hili ni ongezeko la asilimia 2 kulinganisha na takwimu za mwaka uliopita, kuonyesha mkazo wa viwango vya kufikia malengo kadiri UNDAP inavyoingia katika mwaka wake wa mwisho wa utekelezaji. Kielelezo cha III kinaonyesha viwango vya matumizi ya fedha dhidi ya fedha zilizotengwa kwa Julai 1, 2014 Juni 30, 2015, kwa kila Kikosi Kazi cha Programu na jitihada za pamoja chini ya DaO (Mawasiliano, PME, Manunuzi, Rasilimali Watu, TEHAMA, HACT/Fedha, Usawa wa Jinsia na Haki za Binadamu). Vikosi Kazi vya Programu Saba vilifikia asilimia 90 ya matoke au kuzidi, huku akiba ya ndani katika Vikosi Kazi vya Uendeshaji ikisababisha alama za chini katika Maboresho ya makundi ya DaO. 92 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

95 Kielelezo cha III: AWP Fedha Zilizotengwa kwa Bajeti na Matumizi ya Mpito Kielelezo cha IV kinaonyesha bajeti ya jumla ya UNDAP iliyofanyiwa marekebisho mwishoni mwa Mwaka IV ili kufananisha na mabadiliko ya vipaumbele vya programu na matarajio ya upataji fedha sambamba na matumizi limbikizo kwa kila Kikosi Kazi cha Programu na jitihada za Maboresho ya DaO. Matumizi ya mpito kwa miaka minne ya mwanzo ya UNDAP uko katika wastani wa asilimia 73 dhidi ya bajeti ya miaka mitano ya UNDAP. Kiwango hiki kiko juu sana kuliko asilimia 52 iliyoonyeshwa mwaka jana, licha ya ongezeko la bajeti nzima. Hii inaendana na makisio kwamba viwango vya utoaji huduma za fedha vitaendelea kukua kadiri UNDAP inapoelekea ukingoni, kama ilivyoonyeshwa na takibu za bajeti ya AWP. Kielelezo cha IV: Bajeti Iliyopangwa na Matumizi ya Mpito ya UNDAP Hadi Sasa UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 93

96 Photo: UN Tanzania/Andrew Njoroge 94 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

97 5.0 VIKWAZO NA CHANGAMOTO: MWITIKIO WETU Changamoto kadhaa zimeathiri ufikiwaji kwa ufanisi na namna ya kufaa wa malengo yaliyopangwa chini ya Mpango wa UNDAP. Hapa chini pana orodha ya maendeleo ya hatua za usahihishaji zilizotekelezwa ili kushughulikia masuala hayo ya kutia mashaka. Vikwazo maalumu kwa kila sekta vilishughulikiwa kupitia Vikosi Kazi chini ya mpango ulionyumbulishwa katika Mwaka wa AWPs. Maendeleo ya utaratibu huu hupimwa kila mara, huku tathmini rasmi ikifanyika wakati wa Mapitio ya Katikati ya Mwaka ya AWPs kipindi cha Desemba-Januari. Menejimenti Iliyoimarishwa na Matumizi ya Mfumo wa Hazina ya Serikali Kasi ndogo ya utoaji fedha kupitia mfumo wa Mfuko wa Hazina wa Serikali bado ni miongoni mwa changamoto kubwa katika utekelezaji wa mipango kwa wakati. UNCT imejitahidi kuweka katika mfumo wa mtandao makisio ya uhuilishaji fedha katika Jukwaa la Usimamizi wa Msaada kwa mujibu wa ratiba ya Serikali, hata hivyo, taarifa hizi mara nyingi haziakisiwi kwa utaratibu ule ule katika vitabu vya bajeti vya Serikali na hivyo kuzorotesha ufanisi wa upelekaji fedha kwa washirika. UNCT itaendelea kushirikiana na Wizara ya Fedha ili kubaini suluhu kwa vikwazo vikubwa ikiwemo kufanya mapitio makubwa ya mfumo na michakato ya upelekeaji fedha kupitia mfumo wa hazina. Sambamba na hilo, Umoja wa Mataifa itaisaidia Wizara ya Fedha kujenga uwezo wa Washirika Watekelezaji wanaohusika ili kuhakikisha kuwa MTEFs zinaakisiwa katika makadirio ya bajeti, yanaingizwa katika vitabu vya bajeti na utoaji wa namba za utambuzi za bajeti zipatikane ili kuwezesha upelekaji fedha kwa wakati kutoka hazina. Kuhamasisha Ajenda ya Kanuni Kuu na Matokeo Zaidi ya miezi 12 iliyopita, UNCT imepanua kwa kiasi kikubwa sana shughuli zake za Mawasiliano na Uwandani kupitia seti iliyounganishwa ya mipango ambayo inatoa utumaji ujumbe kamili kuhusiana na kanuni na amali za Umoja wa Mataifa na pia kupata matokeo. Matokeo yake, taarifa za Umoja wa Mataifa zimeenea zaidi, na kwa hiyo kuongeza uzito wa nafasi ya Umoja wa Mataifa katika muktadha wa maendeleo ya nchi, na kuvutia vyanzo vipya vya fedha ili kutekeleza ahadi zilizotolewa chini ya UNDAP. Fursa ya kuleta majadiliano miongoni mwa wanaohusika kutoka nyanja mbalimbali zimefuatiliwa, zikiwemo mwingiliano wa kina zaidi na vyama vya kiraia na kushirikisha ushirika na wadau waliozoeleka na wapya. Katika miaka ijayo, Umoja wa Mataifa itaendelea kutafuta njia zenye ubunifu ili kutoa ufafanuzi bora zaidi na kuongeza thamani kupitia Mpango wa Kufanya Kazi Pamoja wa Umoja wa Mataifa, kwa kusaidia malengo ya programu maalumu na pia kauni pana zaidi ya uendeshaji programu. Kurejea Ahadi ya Kuleta Maboresho katika Makao Makuu na Ngazi ya Nchi Tunapoingia kipindi cha baada ya mwaka 2015, Umoja wa Mataifa utahakikisha kwamba mfumo unaendana na lengo, utaweza kuitikia vema zaidi mahitaji ya ajenda za kimageuzi za SDGs katika ngazi za ulimwengu nan chi. Hii itakuwa na maana ya mkazo madhubuti zaidi wa uunganishaji wa njia za mfumo wa Umoja wa Mataifa ambazo kwazo taathira chanya ya kuunganisha ujuzi miongoni mwa mashirika ya Umoja wa Mataifa unaweza kufikiwa. Umoja wa Mataifa Tanzania itahitajika kuimarisha jitihada za ushirikiano katika programu zake zote, uendeshaji shughuli na mawasiliano. Hii itafikiwa kupitia msaada wa Serikali na Washirika wa Maendeleo kwa uoanishaji kamili wa vipaumbele na mipango ya maendeleo na kupitia utekelezaji wa mifumo iliyounganishwa ambayo inapunguza urudifishaji wa michakato na uwekaji mkazo katika kuleta mabadiliko chanya kwa Watanzania wote. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 95

98 Photo: UN Tanzania/ Zoe Glorious 96 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

99 6.0 HITIMISHO Mwaka mmoja kabla ya kumalizika kwa mpango wa UNDAP wa umeshuhudia kasi ya utoaji huduma ikiongezeka, kukiwa na rasilimali za pamoja za zaidi ya mashirika 20 ya Umoja wa Mataifa yenye ukaazi na yasiyo na ukaazi yakipata matokeo makubwa katika kutafuta maendeleo ya kitaifa na kusaidia upatikanaji wa haki za binadamu nchini Tanzania. Sura zilizotangulia zimeangazia michango mikubwa iliyopatikana katika maeneo ya mada kuu tatu, yaani: Kupunguza umaskini wa kipato kupitia ukuaji wa uchumi unaowalenga maskini na kuimarisha uwezo wa kujinusuru Kukuza ubora wa maisha na kufikia hali bora kijamii kwa wote, wakiwemo walio hatarini zaidi Kuandaa msingi wa utawala bora ulio motomoto ili kuweza kujumuisha ukuaji na hali bora ya kijamii Kwa kiwango cha sasa na kwa mwendelezo wa uungaji mkono wa washirika wetu katika utekelezaji na maendeleo, tutaongeza juhudi zetu ili kupanua taathira yetu na kuimarisha mfumo mzima wa mshikamano ili kuhakikisha ufikiwaji wa Malengo yaliyokubaliwa ya Mpango wa UNDAP ifikapo Juni Katika siku zijazo, Umoja wa Mataifa Tanzania itaendelea kuandaa ajenda ya baada ya Programu itakayorithi Mpango wa UNDAP I tayari imepitishwa na Serikali, kufuatia mchakato unaotokana na ushahidi na ulio jumuishi wa uwekaji vipaumbele ambavyo vilitumia data kulingana na mahitaji ya nchi na uwezo wa Umoja wa Mataifa kutekeleza, huku mkazo ukiwa kwa watu walio dhaifu zaidi na wasiofikiwa kwa urahisi. Mchakato ulikuwa shirikishi, huku fursa za Serikali, Vyama vya Kiraia, Vyombo vya Habari, Washirika wa Maendeleo, Sekta Binafsi na Umma Wote kwa Ujumla ili kuchangia. Zaidi ya hayo, uandaaji na bidhaa yaliyongozwa na kanuni za utengenezaji programu za msingi za Umoja wa Mataifa, yaani: Njia Zinazotokana; Kujenga Uwezo na Haki za Binadamu; Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji Wanawake; Uendelevu wa Mazingira; Utamaduni na Maendeleo; Menejimenti Inayotokana na Matokeo. Mpango wa UNDAP wa II utaendeleza au kujenga juu ya mifumo mingi, miundo na michakato ambayo imewezesha kupiga hatua kuelekea katika maendeleo endelevu nchini katika uhai wa Mpango wa UNDAP wa I. Mpango huo mpya unaangazia mwendelezo wa nia ya kuwa na umiliki wa dhati na uongozi wa wadau wa kitaifa, msisitizo kuhusu amali za pamoja, miiko na viwango katika mfumo wa Umoja wa Mataifa na mwendelezo wa dhamira ya kupata matokeo ambao utaleta tofauti iliyo chanya kwa watu wa Tanzania. Mpango utaendelea kufuata njia kuu ya asili na iliyoshikamana katika kuendesha programu na njia iliyo bayana zaidi ya sekta mbalimbali katika kuchukua hatua, huku mkazo ukiimarishwa zaidi kuhusu ajenda za masuala ya kawaida na msisitizo zaidi juu ya mshikamano wa sera na matumizi ya data. Tunapoingia katika mwaka wa mwisho wa utekelezaji wa Mpango wa UNDAP I, baadhi ya mafunzo yanayoibuka kutoka katika michakato ya mashauriano kwa uandaaji wa UNDAP II (ikiwa ni pamoja na Tathmini ya UNDAP) yanaingizwa kwa makusudi mazima katika programu zetu. Kwa hiyo, mwaka nao unaelekea kuwa wenye mafanikio kwa maana ya kupata mabadiliko chanya yanayoonekana kwa Watanzania wote, hasa walio hatarini zaidi na wale walio pembezoni. UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 97

100 Photo: UN Tanzania/ Zoe Glorious 98 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

101 KIAMBATANISHI CHA I: VIFUPISHO VYA MAJINA AMP ART AWP BCC BOS BRN CBOs CHRAGG CMO CMO CMTD CPT CRVS CSO DaO DCF DHIS DPG DRR DSW EAC ECD EiE EMOC emtct EPRP EPRPs FAO FSN GBV GDP GEWE GoT HACT HRBA IADG IAEA IAGG ICT IECD IGCD ILO IMCI INSET IOM IP IPPE ITC JAST JP JSC LGAs Aid Management Platform (Jukwaa la Menejimenti ya Msaada) Anti-Retroviral Therapies (Tiba za Dawa za Kupunguza Makali ya VVU) Annual Work Plan (Mpango Kazi wa Mwaka) Behaviour Change Communication (Mawasiliano Juu ya Mabadiliko ya Tabia) Business Operations Strategy (Mikakati ya Uendeshaji Biashara) Big Results Now (Matokeo Makubwa Sasa) Community-Based Organizations (Asasi za Kijamii) Commission for Human Rights and Good Governance (Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora) Chief Minister s Office (Zanzibar) (Ofisi ya Waziri Kiongozi wa Zanzibar) DMD Chief Minister s Office Disaster Management Department (Ofisi ya Waziri Kiongozi wa Zanzibar Idara ya Kudhibiti Maafa) Community Managed Targeting and Distribution (Ulengaji na Usambazaji Unaosimamiwa na Jamii) Child Protection Teams (Timu za Kinga ya Mtoto) Civil Registration and Vital Statistics systems (Mifumo ya Usajili Jamii na Takwimu Muhimu) Civil Society Organization (Asasi za Kiraia) Delivering as One (Mpango wa Kufanya Kazi Pamoja) Development Cooperation Framework (Muundo-dhana wa Ushirikiano katika Maendeleo) District Health Information System (Mfumo wa Taarifa za Afya katika Wilaya) Development Partners Group (Kundi la Washirika wa Maendeleo) Disaster Risk Reduction (Kupunguza Hatari ya Maafa) Department of Social Welfare (Idara ya Ustawi wa Jamii) East African Community (Jumuiya ya Afrika Mashariki) Early Childhood Development (Makuzi ya Awali ya Mtoto) Emergency in Education (Dharura katika Elimu) Emergency Obstetrics Care (Matunzo Wakati wa Dharura ya Uzazi) Elimination of HIV Transmission from Mother to Child (Kukomesha Maambukizo ya VVU kutoka kwa Mama kwenda kw Mtoto) Emergency Preparedness and Response Plans (Utayari dhidi ya Dharura na Mipango ya Mwitikio) Emergency Preparedness Response Plans (Utayari dhidi ya Dharura na Mipango ya Mwitikio) Food and Agriculture Organization of the United Nations (Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo) Food Security and Nutrition (Usalama wa Chakula na Lishe) Gender Based Violence (Vitendo vya Ukatili kwa Msingi wa Jinsia) Gross Domestic Product (Pato Ghafi) Gender Equality and Women s Empowerment (Usawa wa Jinsi na Uwezeshaji Wanawake) Government of the United Republic of Tanzania (Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) Harmonized Approach to Cash Transfers (Njia Zilizoanishwa za Uhamishaji Fedha) Human Rights-Based Approach (Njia Zinazolenga Haki za Binadamu) Internationally Agreed Development Goals (Malengo ya Maendeleo Yaliyokubaliwa Kimataifa) International Atomic Energy Agency (Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomi) Inter Agency Gender Group (Kundi la Jinsia katika Mashirika ya UN) Information and Communication Technology (Teknolija ya Habari na Mawasiliano) Integrated Early Childhood Development (Makuzi ya Mapema Mtoto Yaliyo Kamili) Interest Group on Culture and Development (Makundi ya Maslahi katika Utamaduni na Maendeleo) International Labour Organisation (Shirika la Kazi Duniani) Integrated Management of Childhood Illnesses (Udhibiti Kamili wa Magonjwa ya Utotoni) In-Service Education and Training (Elimu na Mafunzo Kazini) International Organization for Migration (Shirika la Kimataifa la Uhamiaji) Implementing Partner (Mshirika Mtekelezaji) Integrated Post Primary Education (Elimu Kamili ya Baada ya Shule ya Msingi) International Trade Centre (Kituo cha Kimataifa cha Biashara) Joint Assistance Strategy for Tanzania (Mkakati wa Pamoja wa Msaada kwa Tanzania) Joint Programme( Programu ya pamoja) Government and UN Joint Steering Committee (Kamati ya Pamoja ya Uongozi ya Serikali na UN) Local Government Authorities (Mamlaka za Serikali za Mitaa) UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 99

102 LMIS LTA M&E MARPs MDAs MDGs MIS MIT MKUKUTA MKUZA MLEYD MNCH MoEVT MoF MoHA MoHSW MoLDF MOLE MoNRT MoTTI MoU MPDSR MPTF MSD MSWYWCD MTEF MUCHALI MVC NBS NCD NCPA NGO NMSF NOG NPA NRA NSPF ODA OHCHR OMT One UN Fund PE PLHIV PLW PMO PMO-DMD PMO-RALG PMTCT POPC PRSP PSSN PUN QCPR RBM RC RCH Labour Market Information System (Mifumo ya Taarifa za Soko la Ajira) Long Term Agreement (Mkataba wa Muda Mrefu) Monitoring and Evaluation (Usimamizi na Tathmini) Most at Risk Persons (Watu Walio Hatarini Zaidi) Ministries, Departments and Agencies (Wizaa, Idara na Wakala wa Serikali) Millennium Development Goals (Malengo ya Maendeleo ya Milenia) Management Information Systems (Mifumo ya Usimamizi Taarifa) Ministry of Industry and Trade (Wizara ya Biashara na Viwanda) Kiswahili acronym of the National Strategy for Growth and Reduction of Poverty (Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania) Kiswahili acronym of the Zanzibar Poverty Reduction Plan (Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Zanzibar) Ministry of Labour, Employment and Youth Development (Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana) Maternal, Newborn and Child Health (Afya ya Akina Mama, Watoto Wachanga na Watoto) Ministry of Education and Vocational Training (Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi) Ministry of Finance (Wizra ya Fedha) Ministry of Home Affairs (Wizara ya Mambo ya Ndani) Ministry of Health and Social Welfare (Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii) Ministry of Livestock Development and Fisheries (Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi) Ministry of Labour and Employment (Wizara ya Kazi na Ajira) Ministry of Natural Resources and Tourism (Wizara ya Maliasili na Utalii) Ministry of Trade, Tourism and Industry (Wizara ya Biashara, Utalii na Viwanda) Memorandum of Understanding (Mkataba wa Makubaliano) Maternal and Perinatal Death Surveillance and Response (Ufuatiliaji wa Vifo vya Akina Mama na Kabla ya Kuzaa) Multi-Partner Trust Fund (Mfumo wa Wadhamini wa Sekta Mbalimbali) Medical Stores Department (Shirika la Dawa na Vifaa Tiba la Serikali ya Tanzania) Ministry of Social Welfare, Youth, Women, and Children Development (Zanzibar) (Wizara ya Maendeleo ya Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake, na Watoto) Medium Term Expenditure Framework (Muundo-dhana wa Matumizi ya Muda wa Kati) Food Security and Nutrition Information (Swahili Acronym) (Taarifa za Usalama wa Chakula na Lishe) Most Vulnerable Children (Watoto Walio Hatarini Zaidi) National Bureau of Statistics (Taasisi ya Taifa ya Takwimu) Non-Communicable Diseases (Magonjwa Yasiyo ya Kuambukiza) National Costed Plan of Action for Most Vulnerable Children (Mpango Kazi wa Taifa wa Watoto Walio Hatarini Zaidi) Non-Governmental organization (Asasi Isiyo ya Kiserikali) National Multi-sectoral Strategic Framework (Muundo-dhana wa Mkakati wa Kitaifa wa Sekta Mbalimbali) National Operational Guidelines (Miongozo ya Uendeshaji ya Taifa) National Plan of Action (Mpango Kazi wa Taifa) Non-resident Agency (Shirika Lisilo la Ukaazi) National Social Protection Framework (Muundo-dhana wa Taifa wa Kinga ya Jamii) Overseas Development Assistance (Msaada wa Maendeleo ya Nje) Office of the High Commissioner for Human Rights (Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu) Operational Management Team (Timu ya Uendeshaji Menejimenti) One United Nations Fund for the United Republic of Tanzania (Mfuko wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) Peer Educators (Waelimisha Rika) People Living with HIV (Watu Wanaoishi na VVU) Pregnant and Lactating Women (Akina Mama Wajawazito na Wanaonyonyesha) Prime Minister s Office (Ofisi ya Waziri Mkuu) Prime Minister s Office - Disaster Management Department (Ofisi ya Waziri Mkuu Idara ya Kukabiliana na Maafa) Prime Minister s Office - Regional Administration and Local Government (Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa) Prevention of Mother-to-Child Transmission of HIV (Kuzuia Maambukizi ya VVU kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto) President s Office Planning Commission (Ofisi ya Rais-Mipango) Poverty Reduction Strategy Paper (Waraka wa Makakati wa Kupunguza Umaskini) Productive Social Safety Net (Mtandao wa Usalama wa Jamii) Participating UN Organisation (Shirika la UN Linaloshiriki) Quadrennial Comprehensive Policy Review (Mapitio Kamili ya Sera) Results Based Management (Menejimenti Inayolenga Matokeo) United Nations Resident Coordinator (Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa) Reproductive and Child Health (Afya ya Uzazi na Mtoto) 100 / UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015

103 RCO REDD RGoZ RMNCAH RMS SAGCOT SAM SGBV Shehias SMEs SOP SRH SSRA STEM UN UN Women UNA UNAIDS UNCDF UNCG UNCMT UNCT UNCTAD UNDAF UNDAP UNDG UNDOCO UNDP UNEP UNESCO UNFPA UN-HABITAT UNHCR UNIC UNICEF UNIDO UNODC UNV UPR VCT VPO WASH WEC WFP WG WHO WPP YUNA ZAC ZAWA zmoh zmolpeec ZNSP ZSPP United Nations Resident Coordinator s Office (Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa) Reducing Emissions from Deforestation and Forest Degradation Revolutionary Government of Zanzibar (Serikali ya Mapinduzi Zanzibar) Reproductive Maternal New Born Child and Adolescent Health (Afya ya Akina Mama, Uzazi, Watoto Wachanga, Watoto na Vijana Mabalehe) Results Monitoring System (Mfumo wa Usimamizi Matokeo) Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania (Ukanda wa Ukuzaji Kilimo wa Kusini mwa Tanzania) Severe Acute Malnutrition (Utapiamlo Mkali Kupitiliza) Sexual and Gender Based Violence (Vitendo vya Ukatili kwa Msingi wa Ngono na Jinsia) Zanzibar Local Government Authorities (Mamlaka ya Serikali za Mitaa Zanzibar) Small and Medium-sized Enterprises (Biashara za Viwango vya Chini na Kati) Standard Operational Procedures (Viwango vya Taratibu za Uendeshaji) Sexual and Reproductive Health (Afya ya Ngono na Uzazi) Social Security Regulatory Authority (Mamlaka ya Kudhibiti Mifuko ya Hifadhi ya Jamii) Science, Technology, Engineering and Mathematics (Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hisabati) United Nations (Umoja wa Mataifa) United Nations Entity for Gender Equality and the Empowerment of Women (Shirika la Umoja wa Mataifa Kuhusu Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji Wanawake) United Nations Association (Chama cha Umoja wa Mataifa) United Nations Programme on HIV/AIDS (Programu ya VVU/UKIMWI ya Umoja wa Mataifa) United Nations Capital Development Fund (Mfuko wa Maendeleo ya Mtaji wa Umoja wa Mataifa) United Nations Communication Group (Kundi la Maofisa Mawasiliano la Umoja wa Mataifa) United Nations Country Management Team (Timu ya Nchi ya Menejimenti ya Umoja wa Mataifa) United Nations Country Team (Timu ya Nchi ya Umoja wa Mataifa) United Nations Conference on Trade and Development (Shirika la Umoja wa Mataifa la Biashara na Maendeleo) United Nations Development Assistance Framework (Shirika la Umoja wa Mataifa la Muundo-dhana wa Msaada wa Maendeleo) UN Development Assistance Plan (Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa) United Nations Development Group (Kundi la Maendeleo la Umoja wa Mataifa) United Nations Development Operations Coordination Office (Orisi ya Uratibu Uendeshaji Shughuli za Maendeleo ya Umoja wa Mataifa) United Nations Development Programme (Shirika la Umoja wa Mataifa la Programu ya Maendeleo) United Nations Environment Programme (Programu ya Mazingira ya Umoja wa Mataifa) United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization (Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni) United Nations Population Fund (Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu) United Nations Human Settlements Programme (Shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi ya Watu) United Nations High Commissioner for Refugees (Shirika la Umoja wa Mataifa la Kushughulikia Wakimbizi) United Nations Information Centre (Kituo cha Taarifa cha Umoja wa Mataifa) United Nations Children s Fund (Mfuko wa Maendeleo ya Watoto wa Umoja wa Mataifa) United Nations Industrial Development Organization (Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda) United Nations Office on Drugs and Crime (Shirika la Umoja wa Mataifa la Dawa za Kulevya na Jinai) United Nations Volunteers (Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanaojitolea) Universal Periodic Review Voluntary Counselling and Testing (Nasaha na Upimaji wa Hiyari VVU) Vice President s Office (Ofisi ya Makamu wa Rais) Water Sanitation and Hygiene (Maji, Usafi na Usafi wa Mwili) Ward Education Coordinators (Waratibu Kata wa Elimu) World Food Programme (Shirika la Mpango wa Chakula Duniani) Working Group (Kikosi Kazi) World Health Organization (Shirika la Afya Duniani) Workplace Programmes (Programu za Mahali pa Kazi) Youth of United Nations Association (Shirika la Umoja wa Mataifa la Vijana) Zanzibar Aids Commission (Tume ya UKIMWI ya Zanzibar) Zanzibar Water Authority (Mamlaka ya Maji ya Mji wa Zanzibar) Zanzibar Ministry of Health (Wizara ya Afya ya Zanzibar) Ministry of Labour, Peoples Economic Empowerment and Cooperatives (Wizara ya Kazi, Uwezeshaji Watu Kiuchumi na Ushirika ya Zanzibar) Zanzibar National HIV/AIDS Strategic Plan (Mpango Mkakati wa Kitaifa dhidi ya VVU/UKIMWI Zanzibar) Zanzibar Social Protection Policy (Sera ya Kinga ya Jamii ya Zanzibar) UNDAP RIPOTI YA MWAKA 2014/2015 / 101

104

105 Office of The UN Resident Coordinator P.O. Box 9182 Dar Es Salaam Fax: Website: Facebook:

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited

More information

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya

More information

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2

More information

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya

More information

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.

More information

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari

More information

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa

More information

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA

More information

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na. JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3

More information

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi 3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi

More information

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA

More information

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited

More information

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017

More information

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika

More information

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)] This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)

More information

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi

More information

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for

More information

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA

More information

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria; HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi

More information

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

More information

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha

More information

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya

More information

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided

More information

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza

More information

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/14 DODOMA Mei,

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA

More information

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA

More information

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,

More information

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini

More information

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3

More information

Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania

Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania Msingi wa Programu zote za Uimarishaji Ubora Toleo la 1 kwa Lugha ya Kiswahili

More information

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities

More information

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI

More information

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano. HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,

More information

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa

More information

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TAARIFA YA MAFANIKIO CHINI YA UONGOZI WA MHE. SOSPETER MUHONGO (MB) KATIKA SEKTA NDOGO YA UMEME Disemba, 014 A. MAFANIKIO 1. Kuongezeka kwa uzalishaji

More information

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

More information

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni

More information

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Shukrani Ripoti

More information

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA

More information

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa

More information

Kutetea Haki za Binadamu

Kutetea Haki za Binadamu Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and

More information

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery

More information

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi PAN AFRICAN PARLIAMENT PARLEMENT PANAFRICAIN البرلمان PAN- PARLAMENTO األفريقي AFRICANO Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi Julai 21 22, 2011 Bunge la

More information

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0

More information

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012

More information

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition

More information

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1

More information

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na

More information

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Shukrani Ripoti

More information

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MFUMO WA RUZUKU YA MAENDELEO YA MTAJI WA SERIKALI ZA MITAA (LDCDG) UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI Kijitabu cha Mshiriki

More information

Kuwafikia waliotengwa

Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E 2 0 1 0 Ripoti

More information

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Desemba 2014 1 Shukurani Ripoti hii iliandikwa na Dk. Mkumbo. Ushauri wa kitaalamu ulitolewa na Elizabeth Missokia na Godfrey

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA BARA 2004 Imetayarishwa na: Idara ya Tiba Afya Makao Makuu P.O. Box 9083, DAR ES SALAAM June 2005 Yaliyomo Ukurasa Vifupisho

More information

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania

More information

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI

More information

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu

More information

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika, HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, MHESHIMIWA JOHN POMBE MAGUFULI, (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2007/08 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI MFUMO WA TATHMINI WA TAARIFA (IRM): TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI 2014 2016 Ngunga Greyson Tepani Mtafiti wa IRM Taarifa ya Mwishoni mwa Utekelezaji 2014-2016 First End-of-Term Report INDEPENDENT

More information

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya

More information

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa

More information

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh

More information

Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili

Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili 1. 2-Muhtasari wa Ukurasa wa Ripoti ya Miaka minne ya Bodi Kuu ya Kanisa & Jamii............................... 2 2. Kamati ya Kawaida ya Malipo ya

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

More information

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY

More information

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu: Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200

More information

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized!. viromen-alsc:a.. Environmental & Social MRADI WA UMEME WA GESI YA * Assessment & Management

More information

ORDER NO BACKGROUND

ORDER NO BACKGROUND In the matter of an Application by the DAR ES SALAAM URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (DAWASA) For a Tariff Adjustment, Submitted on January 8 th, 2008 (TR-W-08-001) ORDER NO. 08-001 1.0 BACKGROUND

More information

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo: HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban

More information

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted

More information

Human Rights Are Universal And Yet...

Human Rights Are Universal And Yet... Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,

More information

Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health

Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health Wasiojua kusoma na kuandika katika karne ya 21 hawatakuwa wale wasiojua kusoma na kuandika lakini wale ambao hawawezi kujifunza, kutojifunza na kujifunza

More information

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality

More information

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa

More information

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini

More information

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda

More information

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA

More information

Deputy Minister for Finance

Deputy Minister for Finance ISSN: 1821-6021 Vol XI - No - 34 DID YOU KNOW? A procuring entity is?s required to use suppliers pliers?pliers?pliers?pliers among those awarded ed?ed?ed?ed framework agreements by GPSA for procurement?ents

More information

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna

More information

HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE

HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE SAUTIZETU HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE 01 SAUTIZETU HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE SAUTI ZETU Huduma za Afya kwa wote THE OPEN SOCIETY INITIATIVE FOR EASTERN AFRICA (OSIEA) (JAMII WAZI YA MPANGO WA AFRIKA MASHARIKI)

More information

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12 Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:

More information

Ripoti hii ni kwa heshima ya wale wanaharakati wengi wa Tanzania ambao ndio binafsi wanaopitia hali iliyoangaziwa, na vilevile wale walioyapoteza

Ripoti hii ni kwa heshima ya wale wanaharakati wengi wa Tanzania ambao ndio binafsi wanaopitia hali iliyoangaziwa, na vilevile wale walioyapoteza Utafiti wa mazingira ya haki za jamii za Wafanyakazi wa Ngono na LGBTI nchini Tanzania 2015 2016 Ripoti hii ni kwa heshima ya wale wanaharakati wengi wa Tanzania ambao ndio binafsi wanaopitia hali iliyoangaziwa,

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA MWAKA 2018/2019 YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 HALI

More information

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA TWN Third World Network 1. WEMA ni nini? Mahindi yanayotumia maji kwa ufanisi yajulikanayo kwa kingereza kama Water Efficient Maize for Africa (WEMA) ni mpango

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA

HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA ANNA MARGARETH ABDALLAH, MBUNGE, KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2004/2005 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba sasa Bunge likubali

More information