5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

Size: px
Start display at page:

Download "5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:"

Transcription

1 HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban siku ya 81 tangu Bunge lako Tukufu lilipoanza Mkutano wa Kumi na Mbili, tarehe 10 Juni 2008 hapa Dodoma. Ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuongoza, kutusimamia, kutulinda na kutuweka salama hadi siku ya leo, tarehe 29 Agosti 2008 tunapohitimisha Mkutano huu wa Kumi na Mbili wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 2. Mheshimiwa Spika, ni dhahiri muda tuliokaa hapa Dodoma ni kipindi kirefu kwa maisha ya binadamu. Mambo mengi yametokea. Msomi wa siku nyingi Bwana Terry Flanagan aliandika: A lot of Water has passed under the Bridge. Nakubaliana naye kwamba ni kweli maji mengi yamepita chini ya daraja. Yapo matukio ambayo yametokea katika kipindi hicho yakiwepo ya furaha na mengine ya huzuni. Nitumie nafasi hii ya mwanzo kabisa kukupongeza wewe Mheshimiwa Spika kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola kwa kipindi hiki hadi mwaka 2009 utakapofanyika Mkutano wa 55 wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola Mjini Arusha, Tanzania. Kuchaguliwa kwako, ni heshima kwako binafsi, kwa Bunge letu na kwa Taifa kwa ujumla, na ni uthibitisho wa Tanzania kukubalika Kimataifa. Nakupongeza Sana. 3. ` `Niungane nanyi tena Waheshimiwa Wabunge, pamoja na Watanzania wote kutoa pole kwa kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Tarime, Mheshimiwa Chacha Zakayo Wangwe ambaye alifariki dunia kwa ajali ya gari wakati akisafiri kutoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam. Vilevile, nampa pole Mheshimiwa Severina Mwijage, Mbunge wa Viti Maalum CUF, kwa kufiwa na binti yake, mjukuu wake pamoja na dereva wake katika ajali ya gari mwezi Julai Nitumie fursa hii pia kutoa salaam za pole kwa Wabunge wenzetu na Watanzania wote waliopata majeraha, kwa kupoteza ndugu, jamaa, marafiki na mali kutokana na ajali, maradhi na sababu nyingine mbalimbali. Ni dhahiri kuwa, kwa wenzetu waliopoteza maisha tuliwahitaji sana katika maisha yetu na ujenzi wa Taifa kwa ujumla, lakini Mwenyezi Mungu amekubali watutangulie mbele ya haki. Tunamuomba Mwenyezi Mungu aziweke Roho za marehemu wote mahala pema peponi. Amina. 4. Mheshimiwa Spika, kwa huzuni kubwa na kwa niaba ya Watanzania wote, napenda kuungana na wananchi na jirani zetu wa Zambia katika wakati huu mgumu wa kumpoteza Rais wao, Hayati Dkt. Levy Patrick Mwanawasa ambaye alifariki dunia tarehe 19 Agosti 2008, mjini Paris, Ufaransa. Marehemu atakumbukwa sana kwa uhodari wake katika kusimamia uchumi, kujenga Demokrasia na Utawala Bora katika nchi yake. Kama Mwenyekiti wa Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika, atakumbukwa kwa juhudi zake zisizo na kikomo katika kujaribu kumaliza migogoro ya kisiasa katika Bara la Afrika. Nawapa Pole sana Jirani na Ndugu zetu wa Zambia. Tunamuomba Mwenyezi Mungu aiweke Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi. Amina. 5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

2 i) Muswada wa Sheria ya Ukaguzi wa Hesabu za Umma wa Mwaka 2008 [The Public Audit Bill, 2008]; ii) Muswada wa Sheria Mpya ya Utawala wa Bunge wa Mwaka 2008 [The National Assembly (Administration) Bill, 2008]. iii) Muswada wa Sheria ya Kuidhinisha Matumizi ya Serikali wa Mwaka 2008 [Appropriation Bill, 2008]; na iv) Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2008 [Finance Bill, 2008]. 6. Vilevile, Miswada ifuatayo ilisomwa kwa mara ya kwanza: (i) Muswada wa Sheria ya Wanyamapori wa Mwaka 2008 [The Wildlife Bill, 2008] ; (ii) Muswada wa Sheria ya Ustawi wa Wanyama wa Mwaka 2008 [The Animal Welfare Bill, 2008] ; (iii) Muswada wa Sheria ya Kurekebisha Sheria ya Bodi ya Usajili wa Makandarasi wa Mwaka 2008 [The Contractors Registration (Amendment) Bill, 2008]; na (iv) Muswada wa Vyama vya Siasa (Marekebisho) wa Mwaka 2008 [The political Parties (amendment) Bill, 2008]; Katika Mkutano huu Bunge lako Tukufu pia lilipitisha Azimio la Bunge la Kuridhia Kufuta na Kusamehe Madai ya Kodi pamoja na Riba na Hasara itokanayo na Upotevu wa Fedha na Vifaa vya Serikali na Maduhuli yaliyoshindikana kukusanywa kwa kipindi kinachoanzia Mwaka wa Fedha 1990/1991 hadi tarehe 30 Juni, Nitumie nafasi hii kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa kazi nzuri mliyoifanya katika kujadili na hatimaye kupitisha Miswada na Maazimio yote yaliyowasilishwa mbele ya Bunge lako Tukufu katika kipindi cha Mkutano huu. Vilevile, nitumie nafasi hii kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa kupokea Taarifa ya Kamati ya kuishauri Serikali kuhusu Usimamizi wa Sekta ya Madini, Taarifa ya Utekelezaji wa Azimio la Bunge linalohusu Uuzwaji wa Nyumba za Serikali na Taarifa ya Serikali kuhusu Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge juu ya Mkataba baina ya TANESCO na Richmond Development Company LLC niliyoiwasilisha kama Bunge lako Tukufu lilivyoelekeza. 7. Mheshimiwa Spika, katika Mkutano huu, Waheshimiwa Wabunge walipata nafasi ya kuuliza Maswali 500 ya Msingi pamoja na mengine mengi ya nyongeza. Nitumie fursa hii kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge kwa Maswali yao mazuri ambayo yameisaidia Serikali kutoa ufafanuzi wa Shughuli za Maendeleo kwa ajili ya Taifa letu. Vilevile, nawapongeza Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri ambao walijibu kwa ufasaha Maswali yote yaliyoulizwa na Waheshimiwa Wabunge. Pamoja na mambo mengine, changamoto iliyoko mbele yetu ni kuwahimiza Wataalam wetu kuendelea kupata majibu mafupi na sahihi kwa wakati, na yenye kulenga katika kutumia muda wa Maswali kikamilifu na kwa ufanisi zaidi. Kwa kufanya hivyo, Bunge letu Tukufu litaweza kujibu Maswali mengi zaidi na hivyo kuwapatia Wananchi picha

3 halisi kuhusu maendeleo ya Nchi yetu na kutatua kero zao kwa kasi zaidi. 8. Mheshimiwa Spika, katika Mkutano huu, pia Bunge lako Tukufu lilipokea Kauli Nne (4) za Serikali zilizotoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kutoka Serikalini. Nawapongeza Waheshimiwa Mawaziri waliotoa Kauli za Serikali kwa ufafanuzi mzuri na Waheshimiwa Wabunge waliowasilisha Hoja Binafsi ili kupata ufafanuzi na ufahamu zaidi wa masuala mbalimbali. MASWALI KWA WAZIRI MKUU 9. Mheshimiwa Spika, kipindi cha kila Alhamisi cha Maswali ya Papo kwa Papo kwa Waziri Mkuu ambacho kilianza mwezi Aprili 2008, katika Mkutano wa Kumi na Moja kimeleta msisimko wa kipekee. Kwa upande mmoja, Wabunge wamepata fursa nyingine ya kuuliza Maswali ya Kisera na kupata majibu ya moja kwa moja kutoka kwa Waziri Mkuu. Kwa upande mwingine, Serikali imetumia Maswali ya kipindi hicho kujua hisia za Wabunge ambao ndio Wawakilishi wa Wananchi. Tumeweza kujua ni maeneo gani makubwa ambayo Serikali inahitaji kuweka mkazo katika utendaji kazi wake wa kila siku. 10. Mheshimiwa Spika, tangu kuanzishwa kwa kipindi hicho, Waheshimiwa Wabunge wameuliza jumla ya Maswali 85 ya Msingi na Maswali 31 ya Nyongeza. Ili kubaini maeneo yenye kuhitaji mkazo, Ofisi ya Waziri Mkuu imefanya tathmini na uchambuzi wa Maswali yote yaliyoulizwa na kuyaweka kwenye makundi matatu ya MKUKUTA. Makundi hayo ni Ukuaji wa Uchumi na Kupunguza Umaskini wa Kipato, Huduma za Jamii, na Utawala Bora. Katika uchambuzi huo, imeonekana kuwa kati ya maswali yote yaliyoulizwa, Maswali 40 yanahusu Ukuaji Uchumi na Kupunguza Umaskini wa Kipato, Maswali 17 Huduma za Jamii na Maswali 53 Utawala Bora. Vilevile, kuna Maswali 6 yaliyoulizwa na Waheshimiwa Wabunge ambayo hayaangukii moja kwa moja katika makundi haya matatu ya MKUKUTA. Maswali haya ni yale yanayohusu masuala ya Kimataifa ambayo pia ni muhimu kwa ustawi wa Nchi yetu. Takwimu hizi zinaonyesha kwamba eneo la Utawala Bora lina maswali mengi kulinganisha na makundi mengine. Kwetu sisi Serikalini, hii ni changamoto kubwa na ni ujumbe kwamba kunahitajika jitihada za ziada kuimarisha Taasisi zetu za Utawala Bora. Sote tunatambua umuhimu wa Utawala Bora katika kuweka mazingira mazuri ya Ukuaji Uchumi na Ufanisi katika utoaji wa huduma kwa Wananchi. 11. Ni ukweli usiopingika kwamba, Taasisi zenye misingi mizuri ya Utawala Bora, zinazojenga mazingira ya Utawala Bora unaozingatia Sheria, Taasisi zinazohakikisha kwamba mali za watu zinakuwa na usalama, Taasisi zinazodhibiti Rushwa ili isiathiri utendaji kazi ni misingi muhimu ya Ukuaji Uchumi. Hivyo, nawahakikishia Waheshimiwa Wabunge na Wananchi wote kwamba, Serikali imechukua wingi wa Maswali katika eneo la Utawala Bora kama ujumbe wa eneo linalohitaji kuwekewa mkazo zaidi katika ngazi zote za utendaji wa Serikali. Vilevile, Serikali itaendelea kuweka mkazo katika Kukuza Uchumi ambao ndio msingi wa kuongeza Mapato yatakayoiwezesha kutoa huduma bora za jamii na kuimarisha Taasisi za Utawala Bora. Nichukue tena fursa hii kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa Maswali yenu. Changamoto iliyo mbele yetu ni kutumia fursa hii ya Maswali ya Papo kwa Papo kujikita katika Masuala ya Sera zaidi kama Kanuni zetu zinavyoelekeza. Kwa kufanya hivyo tutaweza kuboresha zaidi muda huu

4 adimu ambao tumejipangia kukubaliana. 12. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilipata bahati ya kutembelewa na Wananchi wengi kutoka sehemu mbalimbali Nchini, ikiwa ni pamoja na Viongozi wa Serikali na Vyama vya Siasa, Viongozi wa Dini, Waheshimiwa Madiwani na kadhalika. Vilevile, katika Mkutano huu, wapo Wageni kutoka nje ya Nchi ambao walitembelea Bunge hili wakiwemo Wageni kutoka Mabunge ya Denmark, Kenya, Msumbiji, Namibia na kutoka Jimbo la Gauteng Afrika Kusini. Walikuwepo pia Wageni kutoka Chama cha Mabunge ya Nchi za Jumuiya ya Madola-CPA, Uingereza, akiwemo Dkt. William Shija, Katibu Mkuu wa Chama hicho. Tulitembelewa na kuhutubiwa hapa Bungeni na Dkt. Asha-Rose Migiro, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, New York na mwisho Rais wa Jamhuri ya Visiwa vya Comoro, Mheshimiwa Ahmed Mohamed Sambi, ambaye pia alihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano. Tunawashukuru Wageni wote waliotutembelea, kuongea nasi na hata wale waliokuja kujionea jinsi tunavyoendesha shughuli zetu hapa Bungeni. 13. Mheshimiwa Spika, kutembelewa na Wageni hawa ni ishara tosha kwamba Bunge lako Tukufu, lina uhusiano mzuri na Wananchi pamoja na Mabunge mengine Duniani. Nina imani Wageni wetu wamejifunza mengi mazuri ya Bunge hili, nasi tumepata uzoefu wa yale wanayofanya katika Mabunge yao kule walikotoka. 14. Mheshimiwa Spika, kwa moyo wa dhati kabisa na kwa niaba ya Watanzania wote, napenda kumpongeza Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kwanza, kwa uamuzi wake wa kuja kulihutubia Bunge na Pili, kwa Hotuba yake nzuri sana aliyoitoa ndani ya Bunge hili tarehe 21 Agosti Kama alivyosema mwenyewe Mheshimiwa Rais na kama ilivyodhihirishwa na Hotuba yenyewe, Watanzania kwa ujumla wamepata Mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Nne kwa kutambua na kuelewa Serikali yao imetoka wapi, iko wapi na inaelekea wapi. 15. Wengi wetu tunaamini kwamba siku zote Sala ni Chakula cha Roho. Vivyo hivyo, sichelei kusema kwamba Hotuba ya Mheshimiwa Rais imekuwa Chakula cha Amani, Utulivu na Mshikamano uliodumu katika Nchi yetu kwa muda mrefu. Hotuba hii hakika imekuwa chakula cha kutupa nguvu ya kusukuma kwa Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya utekelezaji wa Mipango mbalimbali ya Maendeleo ya Taifa ikiwemo, Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya Mwaka 2005, MKUKUTA, Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025, na Malengo ya Maendeleo ya Milenia ya Umoja wa Mataifa. 16. Mheshimiwa Spika, vilevile tunampongeza Mheshimiwa Rais kwa uamuzi wake wa kuelekeza kwenye Sekta ya Kilimo fedha za EPA. Uamuzi wake ni wa Kijasiri, Kishujaa na unastahili kupongezwa na Watanzania wote. Mheshimiwa Rais Hongera Sana kwa uamuzi huu wa Kihistoria. Wakati tukifurahia uamuzi huu, Viongozi na Wananchi wote tunao wajibu mzito na changamoto kubwa ya kuhakikisha kwamba Wakopaji wa fedha hizo zitakazoelekezwa katika shughuli za Kilimo watazielekeza na kuzitumia kwa kuwekeza, kuinua na kuendeleza Sekta ya Kilimo. Taratibu za kuziingiza fedha hizo katika Bajeti ya Mwaka 2008/2009 zitazingatiwaa kama Sheria na Kanuni za Matumizi ya Fedha zinavyotaka. 17. Mheshimiwa Spika, Mkutano huu ulikuwa mahsusi kwa ajili ya kuwasilisha, kujadili na

5 hatimaye kupitisha Bajeti ya Serikali pamoja na Makadirio ya Fedha kwa Wizara, Mikoa na Taasisi mbalimbali kwa mwaka 2008/2009. Waheshimiwa Wabunge wote mtakubaliana nami kwamba, Hoja zote zilijadiliwa na Waheshimiwa Wabunge kwa umahiri mkubwa. Vilevile, naamini mtaungana na mimi kukubali kwamba mjadala ulikuwa wenye msisimko na wakati mwingine wenye hisia kali. Mkutano huu wa Kumi na Mbili utakumbukwa sana hasa kwa mjadala mkali wakati wa kujadili Wizara ya Katiba na Sheria; na Ofisi ya Makamu wa Rais, (Muungano). Mimi ninaamini kabisa kwamba, Waheshimiwa Wabunge waliochangia kwa hisia zao walikuwa na hoja ambazo zililenga katika kujenga Nchi yetu. Mwanafalsafa Karl Max alisema kwamba Jamii isiyokuwa na msukumo wa mawazo haiwezi kuendelea. Kwa hiyo, mambo tunayojadiliana kwa mtizamo tofauti ni dalili njema ya kujaribu kutafuta mwelekeo wa kufikia mwafaka mzuri wa Hoja. Na pengine tukubali kwamba kusikiliza mawazo ya wengine hata kama ni tofauti na unavyowaza ni ustaarabu wa kutosha na kuna wakati tutafika na kukubaliana kwa kiasi kikubwa. Kwa misingi hiyo, ninaamini kabisa kwamba majadiliano haya yanayoonekana yenye hisia kali yatakuwa ni kichocheo na changamoto kwetu kurekebisha yale ambayo yataonekana ni busara kuyarekebisha kwa maslahi ya Taifa letu. 18. Napenda nitumie nafasi hii tena kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote waliochangia Mijadala kwa Maandishi na kwa Kauli wakati wa Kupitisha Makadirio ya Mipango na Matumizi ya Fedha ya Wizara mbalimbali. Michango yenu ni chachu katika kuongeza kasi ya kuwatafutia Wananchi wetu Maisha Bora pamoja na kuipa Serikali changamoto ya kuboresha utendaji na Mipango yake. Ni matumaini yangu kwamba tutaendelea kuhimiza yale yote yaliyopendekezwa na ushauri uliotolewa kutimiza malengo tuliyojiwekea. Tuendelee na juhudi hizo, kwani zinatoa mchango mkubwa katika kusukuma Maendeleo ya Wananchi wetu na Taifa kwa jumla. 19. Mheshimiwa Spika, Bajeti ya Mwaka huu wa Fedha 2008/2009, imelenga kukusanya Mapato ya ndani Shilingi Trilioni 4.7. Hili ni ongezeko la asilimia 31 ikilinganishwa na Makusanyo ya Mapato katika mwaka 2007/2008. Ili kufikia lengo hili, hatua kadhaa zitachukuliwa ikiwa ni pamoja na: (i) Kupanua wigo wa Mapato ya Serikali kwa kusajili Walipa Kodi wapya na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji katika Sekta zote za Uchumi; (ii) Kuimarisha usimamizi wa ukusanyaji wa Ushuru na Kodi katika Forodha pamoja na kuziba mianya ya ukwepaji kodi; (iii) Kusimamia utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Tatu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, kwa nia ya kuongeza uwajibikaji miongoni mwa Walipa Kodi na Watoza Kodi kadhalika; (iv) Kurekebisha Sera na Sheria zinazotoa misamaha ya kodi kwa Sekta ya Madini. Serikali inatafakari na kuainisha marekebisho ya Sheria mbalimbali ambayo yatahitajika yafanywe ili kupunguza misamaha ya kodi na kuokoa mapato ya Serikali; na (v) Kuendelea kutoa Elimu ya Biashara na namna ya ukokotoaji kodi kwa Wafanyabiashara. 20. Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kueleza matumaini yetu na ya Wananchi kwa ujumla kwamba wote wanaohusika kwa namna moja au nyingine na katika ngazi zote katika ukusanyaji wa Mapato, watatimiza wajibu wao ili fedha zinazokusudiwa zikusanywe. Hii itatuwezesha

6 kutekeleza kikamilifu mipango mbalimbali iliyopangwa katika Bajeti hii. 21. Kuhusu matumizi, napenda kusisitiza kuwa Serikali itaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha usimamizi na udhibiti wa matumizi ya fedha za Umma. Aidha, tutaimarisha uwezo wa ufuatiliaji wa utekelezaji wa kazi mbalimbali za Serikali zilizopangwa ikiwemo Miradi ya Maendeleo ili kuhakikisha kuwepo kwa nidhamu katika utekelezaji wa Bajeti ya Serikali. Napenda kuzipongeza Kamati zote za Kudumu za Bunge lako Tukufu zinazohusika na masuala ya matumizi ya mali na fedha za Umma. Tunathamini mchango wao na ushauri wao kila mara umekuwa changamoto kwetu ya kuongeza ufanisi zaidi. Bei ya Mafuta 22. Mheshimiwa Spika, kasi ya upandaji wa Bei ya Mafuta katika Soko la Dunia inaendelea kuyumbisha uchumi wa Nchi zote Duniani na hasa zile masikini sana kama yetu. Kinachosikitisha zaidi ni kwamba, upo uwezekano mkubwa kuwa Bei hizi za mafuta zikaendelea kupanda tena katika siku za usoni. Hata hivyo, katika siku za karibuni tumepata faraja baada ya kuona bei zikishuka badala ya kupanda. Sababu mojawapo ya ongezeko la Bei hizi ni Umoja wa Nchi zinazozalisha mafuta kwa wingi (OPEC) kutumia mwanya wa kupanda kwa Bei za Mafuta kuongeza matumizi yao ya Kibajeti na hivyo kutotaka kushusha viwango vya matumizi hayo. Vilevile, Benki Kuu za Nchi hizi za OPEC zimelazimika kujiwekea fedha nyingi za tahadhari ili kujikinga na mabadiliko yoyote mabaya ya kiuchumi yanayoweza kutokea siku za usoni na kuathiri Uchumi wa Nchi zao. Nchi hizi pia zimeamua kutumia fursa hii ya mapato yatokanayo na Mafuta ili kuwekeza zaidi kwa ajili ya maendeleo ya vizazi vijavyo. Hii ni kwa sababu upo wasiwasi kuwa miaka ijayo rasilimali hii inaweza kwisha au Bei kushuka kutokana na mabadiliko makubwa ya Teknolojia ambayo yanaelekea kutumia nishati mbadala. Kwa vyovyote vile, Bei hizi kubwa zinaziwezesha Nchi hizi kujiweka vizuri hasa ikizingatiwa kwamba wana uwezo wa kukaa pamoja na kupanga Bei. 23. Pamoja na kwamba kuna mwelekeo wa kushuka kwa Bei za mafuta, bado kushuka huko kunaweza kusitusaidie sana katika kipindi cha muda mrefu kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya Mafuta Duniani kunakosababishwa na ukuaji mkubwa wa uchumi hasa kwa Nchi za China na India. Kwa Nchi zinazozalisha Mafuta, kupanda kwa Bei za Mafuta ni mavuno ya kwelikweli ambayo hawana budi kuyatumia ili kufanikisha mipango yao ya sasa na kwa vizazi vijavyo. Lakini kwa Nchi maskini kulazimika kulipia matumizi makubwa ya Nchi hizo ni mzigo mkubwa ambao utaathiri uchumi kwa kiasi kikubwa sana. 24. Mheshimiwa Spika, tafsiri ya upandaji huu wa Bei za Mafuta na kutokuwepo utayari wa Nchi za OPEC kushusha Bei hizo ni kwamba tutalazimika kutumia fedha zetu za kigeni zaidi ili kuendelea kutumia mafuta ambayo ni muhimu katika kuendesha uchumi wetu. Kwa vile mafuta yanatumika kwa usafirishaji na uzalishaji, gharama za usafiri na usafirishaji wa bidhaa nyingi zitaendelea kupanda. Pili, tutahitaji fedha nyingi zaidi za kigeni kuagiza mafuta kwa ajili ya Viwanda na Usafirishaji. 25. Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji itaendelea kuhakikisha kwamba Bei za Mafuta hapa Nchini hazipandishwi kiholela ili kumlinda mlaji asiathirike sana. Kwa kuwa hatuna uwezo wa kudhibiti upandaji Bei katika Soko la Dunia, tunaangalia yale tunayoweza

7 kuyafanya ndani ya Nchi yetu ikiwa ni pamoja na kukamilisha Kanuni zitakazotumiwa na Waagizaji Mafuta, ikiwemo TPDC ili waweze kuanza kuingiza mafuta kwa wingi na kwa bei nafuu inayotokana na ushindani wa Waagizaji Mafuta. Wizara ya Nishati na Madini ikishirikiana na EWURA ifuatilie kwa karibu mwenendo wa Bei za Mafuta katika Soko la Dunia ili kuhakikisha kwamba Wafanyabiashara hawatumii mwanya huu kuwaumiza Wananchi. Vilevile, kadri matumizi ya Gesi katika Viwanda na vyombo vya usafiri yatakayokuwa yanaongezeka tutapunguza uagizaji wa mafuta kutoka nje. Serikali yetu inaelekeza nguvu katika utafiti wa Gesi zaidi ili itumike kama nishati mbadala. KILIMO 26. Mheshimiwa Spika, Tanzania tukifananishwa na Nchi nyingine tumebarikiwa kuwa na ardhi kubwa yenye rutuba nzuri, maji ya kutosha (Maziwa na Mito) pamoja na hali ya hewa nzuri ya kutuwezesha kuleta mabadiliko makubwa katika Sekta ya Kilimo. Kuanzia mwaka jana, 2007 kumekuwepo na upungufu mkubwa wa Chakula pamoja na kuendelea kupanda kwa bei za chakula Duniani kote. Hali hii inaweza kuwa ni neema kwa Wakulima kama tutatumia fursa hiyo vizuri. Kama Nchi za OPEC zinavyonufaika kutokana na ongezeko la Bei ya Mafuta, na sisi tunaweza kufaidika vya kutosha na ongezeko la Bei ya Vyakula kama tutajipanga vizuri. Watanzania tunayo fursa kubwa ya kuleta Mapinduzi ya Kilimo, lakini Mapinduzi haya hayawezi kuja bila ya kuwa na mabadiliko makubwa ya namna tunavyowekeza rasilimali zetu na mtizamo wetu kwenye Sekta ya Kilimo. 27. Mheshimiwa Spika, tunalo eneo la Hekta Milioni 44 linalofaa kwa Kilimo, lakini eneo linalolimwa ni Hekta Milioni 10.8, sawa na asilimia 24 tu. Vilevile, tunazo takriban Hekta Milioni 30 zinazofaa kwa Kilimo cha Umwagiliaji, lakini ni jumla ya Hekta 29,000, sawa na asilimia 0.1 tu zinazotumika. Takwimu hizi zinadhihirisha kwamba tunahitaji kubadilisha mwelekeo wa matumizi ya maeneo yanayofaa kwa Kilimo ili tuweze kuyatumia kikamilifu. Ili kuweza kuongeza eneo la Kilimo, ni wakati muafaka wa kuanza Kilimo cha Mashamba makubwa yanayotumia Teknolojia ya Kisasa, yaani Kilimo cha Kibiashara (Commercial Farming). Mimi ninaamini wapo watu wanaoweza kujitosa katika Kilimo hicho cha Biashara hapa Nchini. Tatizo ni woga wa kuanza. Mimi nasema Tusiogope! Tuanze sasa. 28. Mheshimiwa Spika, ninaelewa kwamba chini ya Programu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo ASDP kupitia Mpango wa Kilimo wa Wilaya - DADPS, Wananchi wanaweza kupata Matrekta makubwa na madogo, Majembe ya kukokotwa na Ng ombe na Maksai. Ziko Pikipiki na Baiskeli kwa Maafisa Ugani. Vilevile, uko Mpango wa kuwajengea nyumba Maafisa Kilimo wa Tarafa, n.k. Kinachotakiwa ni kuwashirikisha Wananchi ili miradi hiyo iibuliwe na Wananchi wenyewe na kupitishwa na Wilaya. Nilijaribu kupata Taarifa jinsi Wananchi wanavyoshirikishwa katika kuibua miradi yao kwa maendeleo yao nikabaini kwamba hili halijafanyika. Hivi najiuliza tatizo ni nini? Inaelekea Halmashauri hazijawahamasisha Wananchi kufanya hivyo chini ya DADPS, hivyo hawajui. Naziagiza Halmashauri zote kuchukua jukumu la kuwahamasisha Wananchi kushiriki katika kuibua miradi ya Kilimo inayolenga katika Kilimo cha Kibiashara. 29. Mheshimiwa Spika, katika Karne hii ya mabadiliko ya Hali ya Hewa na Mazingira kwa ujumla, Kilimo kinatakiwa kubadilishwa na kwenda na wakati kulingana na mabadiliko hayo na kuwa na Kilimo cha Kisasa na cha Kibiashara kinachoangalia mwelekeo wa mahitaji ya Soko na

8 Ushindani wa Uzalishaji wa Kimataifa. Jambo hili ni muhimu, hasa tukizingatia kuimarishwa kwa Soko la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na Afrika kwa ujumla. 30. Kilimo hapa Nchini bado hakijawa Kilimo chenye Tija kutokana na kuendeleza Kilimo cha Kujikimu (Subsistance Farming), badala ya Kilimo cha Biashara. Hii ndiyo sababu kubwa ya Wakulima wengi kuendelea kuwa maskini. Kilimo chetu bado kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na Uwekezaji Mdogo, Vishamba Vidogo Vidogo, Matumizi ya Teknolojia Duni, Uhaba wa Miundombinu, na Uhaba wa Masoko ya Mazao tunayolima. Vilevile, Kilimo chetu kinategemea zaidi Mvua kuliko Umwagiliaji Maji; Wakulima wengi kulima bila kutekeleza Kanuni za Kilimo Bora; na tatizo la upatikanaji mdogo wa Pembejeo za Kilimo, kama madawa, mbolea na mbegu bora. Kwa mfano, takwimu zinaonyesha kuwa mwaka 2007/2008, tumelima Hekta Milioni 2.88 za Mahindi kati ya Hekta Milioni 44.0 za Ardhi inayofaa kwa Kilimo na kuvuna Tani Milioni 3.6 kwa wastani wa Tani 1.2 kwa Hekta. Hata kwa eneo hilo hilo la Hekta Milioni 2.88 kwa Kilimo cha Mahindi kama tungetumia Teknolojia Sahihi na Zana Bora za Kilimo, tungezalisha wastani wa Tani 5 kwa Hekta na tungeweza kupata Mahindi tani Milioni 14.4 na kuongeza Usalama wa Chakula Nchini. Tunahitaji kuboresha Kilimo chetu ili kuongeza uzalishaji kwa Hekta, hivyo kuongeza kipato. 31. Mheshimiwa Spika, kutokana na upungufu wa Chakula na Upandaji wa bei za Vyakula Nchini, ambao umesababishwa na Teknolojia duni zinazotumika, ikiwa ni pamoja na uduni wa matumizi ya Zana za Kilimo, inabidi sasa tuongeze uzalishaji wa Chakula kwa kutumia Teknolojia ya Matrekta Madogo aina ya Power Tillers. Trekta la Power Tiller, linafanya kazi baada ya mtu kulisukuma na linaweza kufanya kazi zote ambazo zinafanywa na matrekta makubwa. Matrekta haya husukumwa na mtu wakati wa kulima, na gharama zake ni kidogo sana na linabana matumizi ya mafuta. 32. Mheshimiwa Spika, takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa Trekta hizi ndogo za kusukumwa Power Tillers, hutumia Lita 2 za mafuta kwa kulima ekari moja, ikilinganishwa na Lita 8 kwa ekari kwa kutumia trekta kubwa. Kwa Dar es Salaam, Trekta hizi zinauzwa kati ya Shilingi Milioni 4.0 na Milioni 8.4 kwa mfano, Trekta la Kichina Shilingi Milioni 4.25, Trekta la Kijapani Kubota Shilingi Milioni 6.1. Bei hizi ni pamoja na vifaa vyake mbalimbali, kama vile Jembe, Haro, Tela, Gurudumu za Mpira na Gurudumu za Chuma. CHANGAMOTO KWA HALMASHAURI 33. Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa iliyopo ni kwa Halmashauri za Wilaya kuwawezesha Wakulima kupata pembejeo kwa urahisi. Kwa mfano, kama bei ya Power Tiller moja ni takriban Shilingi Milioni 6.1 pamoja na zana zake muhimu, na kama Halmashauri itatenga hata Shilingi Milioni 50 tu kwa mwaka, itaweza kuanza kununua na kusambaza zana hizi kwa Vikundi vya Wakulima au Mkulima mmoja mmoja. Trekta hizi ni nzuri na zitatusaidia sana katika kuongeza uzalishaji wa mazao, hasa kwa Wakulima wadogo wenye mashamba kati ya ekari 5 hadi 20. Uongozi wa Halmashauri uhamasishe Wakulima katika kuendeleza matumizi ya Matrekta haya katika maeneo yao. Vilevile, Halmashauri ziwawezeshe Wakulima kuyanunua au kukopeshwa Matrekta haya ili kuongeza uzalishaji. Hii ni pamoja na kuhamasisha uundaji wa Vikundi Vidogo Vidogo, ambavyo vinaweza kukopeshwa na vikaanzisha Vituo vya Kukodisha Matrekta ili kurahisisha Kilimo cha Mazao ya Chakula na Biashara. Kwa kuanzia nimeziagiza

9 kila Halmashauri kuweka kwenye Ajenda zake wazo hili na nimezitaka kunipatia taarifa kuhusu maamuzi yao na hatua wanazozichukua kueneza zana hizi. Hili ni jambo linalowezekana kwa kutumia Bajeti zetu. 34. Vilevile, ili kuwapa Wakulima huduma za Ugani, Halmashauri ziwawezeshe Mabwana na Mabibi Kilimo na Mifugo kuwafikia Wakulima. Kwa mfano, bei ya pikipiki moja ni takriban Shilingi Milioni 3. Kwa bei hizo, hivi kweli Halmashauri zetu haziwezi kutenga fedha kwenye Bajeti zao kununua pikipiki kwa Mabwana na Mabibi Shamba. Nitapenda vilevile kupata taarifa jinsi kila Halmashauri Nchini ilivyoweka mikakati katika kutekeleza jambo hili. Wakuu wa Mikoa watoe taarifa za Halmashauri zao ifikapo tarehe 30 Septemba Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutoa mafunzo juu ya matumizi ya Zana Bora za Kilimo ili kuongeza uelewa wa Wakulima wa zana mpya. Zana zitakazohusika ni pamoja na Matrekta Madogo ya Mikono na vifungashi vyake, mashine za kupandikiza mpunga, majembe ya palizi yanayokokotwa na Wanyamakazi na mashine ndogo za kusindika muhogo, korosho na mtama. Serikali pia itafanya tathmini ya kina juu ya mahitaji ya mashine na Zana mbalimbali za Kilimo kulingana na uwezo na mahitaji Nchini na kuanzisha mfumo wa ukusanyaji, utunzaji na usambazaji wa takwimu za Zana za Kilimo ili kurahisisha uandaaji wa Mipango ya Maendeleo. Mwongozo wa kutumia Zana za Kilimo kibiashara utaandaliwa na Wizara itaendelea kutoa ushauri wa kiufundi na utaalam katika Halmashauri za Wilaya ili kuongeza ufanisi wa matumizi ya Zana za Kilimo na hivyo kuongeza uzalishaji na tija katika Kilimo. 36. Mheshimiwa Spika, Mwandishi, Mshairi na Mchekeshaji wa Uingereza Bwana Paul Chatfield aliandika: Kilimo ndicho Mkemia Bora kuliko wote, hugeuza Ardhi, na hata Mbolea, kuwa Dhahabu, humlipa na kumzawadia Mkulima afya bora. Nakubaliana na Mwandishi huyu kwamba tunaweza kubadili Ardhi yetu kuwa Dhahabu kama tukizingatia Kilimo Bora kwa kutumia Zana Bora za Kilimo na Pembejeo nyingine kwa usahihi. Nichukue fursa hii kwa mara nyingine tena kumpongeza sana Mheshimiwa Rais kwa uamuzi wake wa kuongeza fedha za Akaunti ya EPA kwa ajili ya Kilimo. Nina imani kuongezeka kwa fedha hizi kutatia hamasa Kilimo na uzalishaji kuongezeka kwa kiasi kikubwa. Nisisitize tena hizi siyo fedha za Warsha za Kilimo kwa Watendaji Maofisini, ni fedha za kununulia Pembejeo na ihakikishwe kwamba yule anayestahili kupata, anapata na kutumia. MASOMO YA HISABATI 37. Mheshimiwa Spika, katika Hotuba yangu ya kufunga Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge lako Tukufu niliyoitoa tarehe 25 Aprili 2008, nilizungumzia kwa kirefu kuhusu maboresho ya Sekta ya Elimu, hususan umuhimu wa Masomo ya Hisabati na Sayansi. Pamoja na kuongezeka kwa kiwango cha ufaulu kwa Wanafunzi, nilitoa tahadhari ya kukosa Wana-Sayansi ambao ni Watu muhimu sana katika maendeleo ya Taifa letu kwenye Karne hii na nyingine zijazo. Nililinganisha ufaulu wa Masomo ya Sayansi na Sanaa katika Shule za Msingi na Sekondari ambako ilithibitika kwamba ufaulu wa Masomo ya Sayansi katika Shule hizi kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2003 hadi 2007 ulikuwa umeshuka sana.

10 38. Vilevile, tarehe 26 Julai 2008, nilipata fursa ya kuwatunukia zawadi Wanafunzi wa Darasa la Saba wa Mkoa wa Dodoma na Walimu ambao walifanya vizuri zaidi kwenye Mtihani Maalum wa kupima uwezo wao wa Somo la Hisabati. Katika hafla hiyo, Wanafunzi 20 walipewa zawadi na Benki ya CRDB kwa kufanya vizuri. Kati ya Wanafunzi 20, Wasichana walikuwa 10 na Wavulana ni 10. Aidha, ilibainika kwamba Washindi wawili wa mwanzo ni Wasichana. Nawapongeza sana Wanafunzi wote 20 na hasa Wasichana Wawili walioshika namba moja na mbili kwa kuonyesha mfano wa kufanya vizuri katika Hisabati. Hii inadhihirisha kuwa kufanya vizuri inawezekana kwa kila Mwanafunzi. 39. Mheshimiwa Spika, natoa changamoto kwa Halmashauri zote na Mikoa yote Tanzania kuiga mfano huu wa Dodoma wa kuwapima na kuwashindanisha Wanafunzi kwenye Somo la Hisabati na Sayansi. Itakuwa vizuri pia kuwatambua Walimu wa Hisabati na Sayansi ambao Wanafunzi wao watafanya vizuri katika kuwashindanisha. Tuwabainishe na wote wapewe zawadi kama walivyofanya katika Mkoa wa Dodoma. Nayaomba Makampuni mbalimbali na Watu binafsi kujitokeza katika kutoa zawadi kama walivyofanya wenzao wa CRDB kwa Mkoa wa Dodoma. Lengo liwe ni kuwaongezea ari na juhudi Walimu katika kufundisha Masomo ya Hisabati na Sayansi na Wanafunzi kupenda na kuongeza juhudi katika Masomo haya na kuwapa motisha Wanafunzi wanaofanya vizuri. HALI YA KUFUNDISHA NA KUJIFUNZA HISABATI NCHINI ILIVYO SASA 40. Mheshimiwa Spika, kwa kuwa nilizungumzia kwa kina kuhusu Masomo ya Hisabati na Sayansi katika Mkutano wa Kumi na Moja, leo napenda nitumie muda kidogo kuelezea kuhusu hali ya ufundishaji na ufaulu wa Somo la Hisabati peke yake hapa Nchini. Imedhihirishwa kwamba Somo la Hisabati ndilo Somo ambalo ufaulu wake ni wa kiwango cha chini sana kuliko Masomo mengine yote. Taarifa za Ukaguzi wa Shule zinaonyesha kwamba, hali ni mbaya zaidi katika Shule za Msingi. Kwa mfano, mwaka 2001, katika Mtihani wa kumaliza Darasa la Saba, asilimia 62 ya Watahiniwa katika Wilaya ya Morogoro Vijijini walipata Sifuri katika Mtihani wa Hisabati. Hali hii inamaanisha asilimia 62 ya Wanafunzi wa Darasa la Saba katika Wilaya hii walimaliza shule bila kujua Hisabati rahisi za kujumlisha, kutoa, kuzidisha na kugawanya. Katika Mtihani wa Kidato cha Nne, mwaka 2007, matokeo yanaonyesha kwamba asilimia 69 ya Watahiniwa Walishindwa katika Mtihani wa Hisabati. Katika zama hizi za Sayansi na Teknolojia hali kama hii inatisha na haiwezi kuruhusiwa kuendelea kutokea. 41. Mheshimiwa Spika, sababu nyingi zimetolewa kuhusu kushindwa kwa Wanafunzi katika Masomo, hususan Hisabati. Baadhi ya sababu hizo ni pamoja na zifuatazo: i) Msingi Mbaya kuanzia Elimu ya Awali: Imekuwa ni kawaida watoto kuwekewa msisitizo katika Somo la Kiingereza katika Elimu ya Awali. Hali hii imesababisha Wanafunzi wengi kukifahamu Kiingereza kwa sababu ya msingi mzuri, imara na bora. Inasikitisha hali sivyo ilivyo katika ufundishaji wa Hisabati. Wakati sasa umefika wa kuanza kuweka msisitizo katika ufundishaji wa Hisabati kuanzia Elimu ya Awali. Wanafunzi wajengewe msingi mzuri ili wapende na kujua umuhimu wa Hisabati; ii) Upungufu wa Walimu: Shule nyingi hazina Walimu wa Hisabati; iii) Woga wa Somo la Hisabati: Wanafunzi wengi wamekuwa waoga kwa jinsi Hisabati zilivyo.

11 Wako wanaojiandaa kabisa kujihami na wengine wanachukia kabisa kusoma Somo la Hisabati; iv) Uhaba wa Vitabu na Vifaa vingine vya Kufundishia: Kwa hali hiyo, Walimu wanakuwa ndio Waandikaji Wakuu kwa kutumia Ubao na Chaki. Aidha, Wanafunzi hawawezi kupata nafasi ya kujisomea wala kufanya mazoezi ya kutosha; v) Ukosefu wa Motisha: Walimu na Wanafunzi wanakosa motisha ya kufanya Somo la Hisabati. Baadhi ya Walimu wamekata tamaa katika ufundishaji wa Somo la Hisabati; vi) Kushindwa kuanza kufundisha mapema Somo la Hisabati Ziada Additional Mathematics kuanzia Kidato cha Kwanza: Pamoja na kwamba utaratibu huu ulikwishaanza takriban miaka miwili iliyopita, baadhi ya Shule hazijaanza kufundisha Somo hilo; na vii) Ukosefu wa Walimu wenye uwezo wa Kufundisha Somo la Hisabati: Baadhi ya Walimu hawajawahi kuhudhuria Mafunzo Maalumu ya Somo la Hisabati. Wapo Walimu waliosoma Uhasibu ambao ndio wanaoutumiwa kufundisha Hisabati. Inakuwa vigumu kwa Mwalimu huyu aliyesoma Uhasibu kuweza kufundisha Hisabati katika Vidato vya juu zaidi, k.m. Kidato cha Tatu na cha Nne. Aidha, kuna baadhi ya Walimu ambao hawakufaulu vizuri Hesabu au hawafahamu vizuri Hesabu. Haya ni baadhi tu ya matatizo yaliyobainishwa ambayo yamesababisha kushuka kwa ufaulu wa Somo la Hisabati. Lakini Mwandishi mmoja wa Vitabu, Bwana Henri Marie Beyle akielezea hisia zake kuhusu Somo la Hisabati alisema: I used to love Mathematics for its own sake, and still I do, because it allows for no hypocrisy and no vagueness.. Anachosema Bwana Henri ni kwamba kwa Somo la Hisabati halina unafiki wala utata. Ni somo la wazi ambalo ni dhahiri. Unaposema: mbili zidisha mbili ni nne na sio vinginevyo. Kwa maana hiyo, ni muhimu tuchukue hatua za maksudi kuliendeleza. HATUA ZINAZOCHUKULIWA 42. Mheshimiwa Spika, pamoja na sababu zilizoorodheshwa hapo juu, zipo hatua za maksudi ambazo zimeanza kuchukuliwa. Baadhi ya hatua hizo ni: i) Kuundwa kwa Chama imara cha Somo la Hisabati Nchini, kinachojulikana kama Chama cha Hisabati Tanzania (CHAHITA) ambacho kimekuwa mstari wa mbele kukuza na kuendeleza Somo la Hisabati Nchini. Chama hiki kimekuwa kikiwaunganisha Walimu wa Hisabati Nchini kwa kufanya Warsha mbalimbali na kuandaa Mikutano ya Mwaka yenye lengo la kubadilishana uzoefu na mbinu za kufundisha somo hilo muhimu. Wito wangu kwa Walimu wote wa Hisabati Nchini ni kujiunga na Chama hiki ili kuweka mawazo yao pamoja ya jinsi ya kuendeleza Somo hili la Hisabati; ii) Kuinua na kukuza Rasilimali Watu, hususan wale ambao tayari wana Elimu ya Hisabati kwa kuwapatia mafunzo zaidi ya mbinu mbalimbali za Hisabati. Kupanua upeo na uwezo wao wa kujua Hisabati ili waendane na mahitaji ya maendeleo ya sasa. Wale ambao wamekuwa wakijenga tabia ya kupenda Hisabati wamepata maendeleo na kurahisisha kazi zao; iii) Kujenga dhana ya kujiamini kwa Watu wanaojua Hisabati na kujenga falsafa ya mambo

12 kwa mpangilio wenye mantiki (Logic Thinking) kwa kuwapatia mazoezi ya mara kwa mara; na iv) Kuwekeza katika Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia msingi wake ni ujuzi na uwezo katika Somo la Hisabati. Kwa maneno mengine ni vigumu kukawa na Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia bila kutegemea Hisabati. 43. Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba Somo la Hisabati linaonekana kuwa gumu, mwenendo wa sasa wa Wanafunzi wengi kushindwa katika Mitihani ya Somo hili ni suala ambalo linahitaji hatua za haraka ili kuinua ubora na kiwango cha ufaulu wa Somo hili. Hivyo, pamoja na hatua zilizotajwa hapo juu zinazochukuliwa hivi sasa, hatua zifuatazo pia zitachukuliwa: i) Kufundisha Walimu wengi zaidi wa Hisabati wenye mbinu mpya na za kisasa za ufundishaji wa Somo la Hisabati; ii) Kuandaa vifaa vya kufundishia ambavyo vinaendana na mabadiliko yanayotokea ya Somo la Hisabati ili Somo hili liweze kuvutia; iii) Kutunga na kuwa na vitabu vya kutosha vya Somo la Hisabati Mashuleni na vyenye mifano halisi inayozingatia Mazingira ya Nchi yetu; iv) Kubadilisha mbinu za ufundishaji kutoka katika mbinu za mhadhara (lectures) kwenda katika mbinu shirikishi (participatory oriented teaching); v) Kuboresha mbinu za kupima uwezo wa Mwalimu akiwa Darasani na uwezo wa Mwanafunzi kuelewa; vi) Kuwekeza zaidi katika Somo la Hisabati kwa kutenga Bajeti ya kutosha katika Somo hili; vii) Kuimarisha Ukaguzi wa Somo la Hisabati ili kubaini mapungufu mapema na kuyaondoa; na viii) Kuanzisha Somo la Additional Mathematics kuanzia Kidato cha Kwanza kila Shule ya Sekondari. 44. Mheshimiwa Spika, upo ukweli kwamba Somo la Hisabati ni Somo linalojenga dhana ya kujiamini na kujenga falsafa ya mambo kwa mpangilio wenye mantiki. Hii inanikumbusha kisa cha Mwalimu mmoja ambaye alitoa zoezi la Hisabati Darasani, akawa anamwuliza Mwanafunzi wake kama ifuatavyo: Kama nikikupatia Panya wawili na wawili tena na wengine wawili, Panya wangapi utakuwa nao? Mwanafunzi yule akajibu: Saba! Mwalimu akasema: Hapana, hebu sikiliza vizuri swali langu. Kama nikikupatia Panya wawili na wawili tena na wengine wawili, Panya wangapi utakuwa nao?

13 Mwanafunzi yule akajibu: Saba! Mwalimu akasema: Aah! Hebu niulize kwa njia nyingine. Kama nikikupatia Maembe mawili na mawili tena, na mengine mawili, utakuwa na Maembe mangapi? Mwanafunzi yule akajibu: Sita! Mwalimu akasema: Safi sana. Sasa nirejee kwenye swali langu. Kama nikikupatia Panya wawili na wawili tena na wengine wawili, Panya wangapi utakuwa nao? Mwanafunzi akajibu: Saba! Mwalimu kwa hasira akamwambia Mwanafunzi yule: Inakuwaje kwa akili zako timamu unasema mafungu matatu ya Panya wawili wawili ni Saba? Mwanafunzi akajibu tena kwa upole : Kwa vile tayari ninaye Panya mmoja nyumbani!! Mfano huu unaonyesha umuhimu wa Mwalimu wa Hisabati kutumia muda mrefu kwa Mwanafunzi mmoja mmoja ili somo hilo lieleweke vizuri pamoja na mpangilio mzuri wa kuuliza kile unachotaka na Mwanafunzi kukielewa. Ninachotaka kusisitiza hapa ni kwamba, Somo la Hisabati ni muhimu sana kwa kujenga uwezo wa awali wa Mwanafunzi. Napenda kurudia wito wangu kwa Mashirika, Taasisi na Watu Binafsi kutoa motisha kwa Wanafunzi, Walimu na Shule ili kukuza Vipaji vya Somo la Hisabati. Ninaamini tukiamua tunaweza. Tulifanya vizuri kuwatambua na kuwaenzi wenye Vipaji katika Mchezo wa Mpira wa Miguu hapa Bungeni, tufanye hivyo hivyo pia kwa wenye Vipaji kwa masomo ya Hisabati ili kuendeleza fani hii. Tuwaenzi Wanafunzi na Tuwaenzi Walimu wao. 45. Mheshimiwa Spika, ziko taarifa kwamba mambo mengi yanayozungumzwa kuhusu Somo la Hisabati hayajaungwa mkono na utafiti wa uhakika kubaini chanzo cha Wanafunzi kushindwa vibaya katika Somo hili. Nimeambiwa kwamba Chama cha Hisabati Tanzania (Mathematics Association of Tanzania) wamependekeza kufanya utafiti wa uhakika wa kubaini chanzo cha Wanafunzi kushindwa vibaya. Nitumie nafasi hii pia kuiagiza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kufuatilia kwa karibu pamoja na mambo mengine mapendekezo yatakayotolewa na CHAHITA na Taasisi zingine zilizopo kama vile, Idara ya Hisabati ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ili kubainisha matatizo na nini kifanyike. 46. Mheshimiwa Spika, leo nimeongelea sana kuhusu Somo la Hisabati. Hata hivyo, ziko changamoto nyingi zinazoikabili Sekta ya Elimu kwa ujumla. Changamoto kubwa ni kuinua kiwango cha Ubora wa Elimu kinachotolewa, kuboresha utoaji wa Elimu, utekelezaji wa lengo la Pili na la tatu la Malengo ya Maendeleo ya Milenia ya Umoja wa Mataifa Kuhusu Elimu; na Utekelezaji wa Malengo tuliyojiwekea kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka Katika Ilani ya CCM kwa mfano, tumejiwekea Malengo ya kujenga angalau Shule moja ya Sekondari katika kila Kata. Vilevile, tumejiwekea Malengo ya kuboresha mazingira ya Shule, ikiwemo upatikanaji wa Vifaa na Ujenzi wa Maabara na kukabiliana na upungufu wa

14 Walimu. Ni dhahiri kwamba, changamoto hizi ni kubwa na zinahitaji kiasi kikubwa cha fedha ili kukabiliana nazo. 47. Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto hizo katika Sekta ya Elimu, ndio maana mwaka 2001, Bunge lako Tukufu lilipitisha Sheria ya Bunge Na. 8 iliyoanzisha Mfuko wa Elimu hapa Nchini. Madhumuni yakiwa ni kuongezea nguvu zaidi juu ya zile za Serikali katika kugharamia Sekta ya Elimu katika kuinua kiwango cha Ubora wa Elimu. Vilevile, tunayo Mamlaka ya Elimu Tanzania ambayo imeanzishwa Sambamba na Sheria hii ili kusimamia upatikanaji wa Mapato na Shughuli za Mfuko huu. Jukumu kubwa la Mamlaka hii ni kuelimisha na kuhamasisha Wadau wa Elimu wakiwemo ninyi Waheshimiwa Wabunge na Umma kwa jumla juu ya umuhimu wa kuchangia Maendeleo ya Elimu Nchini, hususan kupitia Mfuko wa Elimu. Pamoja na kuwa na Mfuko wa Elimu kwa Nchi nzima, napenda kuziagiza kila Halmashauri katika ngazi ya Wilaya na kila Mkoa kuwahamasisha Wananchi kuanzisha Mifuko ya Elimu kwa ajili ya Maendeleo ya Elimu katika Wilaya na Mikoa. Kwa kufanya hivyo, tutaweza kuboresha kiwango cha Elimu kilichopo sasa kwa kasi zaidi bila ya kusubiri Serikali kufanya kila kinachohitajika. 48. Mheshimiwa Spika, tarehe 19 Agosti, 2008 nilipata nafasi ya kufungua Warsha ya Uendeshaji na Usimamizi wa Mifuko ya Elimu iliyofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa hapa Dodoma. Bila shaka yapo mengi mazuri tuliyojifunza katika Warsha ile, hususan kutoka kwa wenzetu wa Ghana na Nigeria ambao walialikwa kutoa Mada kuhusu uzoefu wao katika Uendeshaji na Usimamizi wa Mifuko ya Elimu. Naitaka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kusambaza Azimio lililokubalika kwenye Warsha hiyo pamoja na uzoefu uliopatikana kwa Mikoa na Wilaya zote ili kuipa ufahamu wa Mifuko hiyo hapa Nchini. Azimio hilo liandaliwe kwa lugha nyepesi ambayo itaeleweka na Wadau wa ngazi zote. Utekelezaji wa Mpango wa Afya ya Msingi (MMAM) 49. Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na TAMISEMI, imeandaa Mpango wa Maendeleo wa Afya ya Msingi (MMAM) wa mwaka 2007/2008. Mpango huu una lengo la kusogeza huduma za afya karibu na Wananchi. Mpango huu utatekelezwa katika Awamu Mbili za miaka mitano mitano. Katika Awamu ya Kwanza kipaumbele kimewekwa kwenye upatikanaji wa Watumishi watakaotoa huduma katika vituo vilivyopo ambavyo havina Wataalam. Vituo hivyo vinajumuisha Zahanati 652 zilizojengwa na Wananchi kwa msaada wa TASAF. 50. Mheshimiwa Spika, tangu Mpango huu kuanza kutekelezwa mwaka wa fedha 2007/2008, mafanikio yaliyopatikana ni katika maeneo yafuatayo: i) Watumishi na Ajira: Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii katika mwaka 2007/2008, iliajiri jumla ya Watumishi 200 wa Kada mbalimbali kwa ajili ya Hospitali za Rufaa za Kibong oto, Mbeya na Mirembe. Vilevile, Serikali ilitoa kibali cha Ajira kwa Wataalam 6,437 wa Kada za Afya katika Halmashauri, Sekretarieti za Mikoa na Wizara mbalimbali. Kutokana na kutokuwepo kwa Wataalam wa kutosha katika Soko la Ajira Serikali iliwapangia vituo Wataalam 4,812 tu. Wataalamu 3,645 kati ya hao walipangiwa kutoa huduma katika Vituo na Zahanati mbalimbali zikiwemo 253 kati ya 652 zilizojengwa na Halmashauri kwa kushirikiana na Wananchi na

15 TASAF. Zahanati hizo tayari zimefunguliwa na zinafanya kazi. ii) Mafunzo ya Watumishi wa Afya: Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii imeweza kuvifanyia ukarabati na kubadilisha matumizi ya Vyuo mbalimbali. Mpango huu wa ukarabati na upanuzi wa Vyuo utaendelea mwaka hadi mwaka kadri fedha zitakavyopatikana ili kuongeza idadi ya Wanafunzi wanaodahiliwa na kufikia lengo la Watumishi wanaohitajika. Vilevile, Serikali imebadili matumizi ya Vyuo 16 (Vyuo 10 vya Uuguzi na 6 vya Sayansi Shiriki) vilivyokuwa vya mafunzo ya kujiendeleza kuwa vya Wataalam wa Afya. Hii imewezesha Wizara kudahili jumla ya Wanafunzi Watarajali 827 katika Vyuo hivyo. Kati ya hao 519 ni wa Vyuo vya Uuguzi. Chuo cha Uuguzi Mirembe kimeongezewa Programu ya Stashahada kwa Wanafunzi, Wataalam wa Afya watarajiwa. Vyuo vya Sayansi Shiriki 6 vilidahili jumla ya Wanafunzi 308. Utekelezaji wa Mpango wa Afya ya Msingi unaendelea na inatarajiwa utapata kasi zaidi. 51. Mheshimiwa Spika, kabla ya kuhitimisha hoja yangu, napenda kusisitiza maeneo machache yafuatayo:- Moja: Tunayo changamoto ya kupanda kwa Bei ya Mafuta ambayo inaathiri uchumi wetu kwa kupanda kwa bei za bidhaa muhimu. Tusitumie kupanda kwa bei ya Mafuta kuwa kisingizio cha kuwaumiza Wananchi hata pale ambapo hapastahili kupandisha bei za bidhaa. Vyombo vinavyohusika vifuatilie kwa karibu mwelekeo wa Bei ya Mafuta na bei za bidhaa kuhakikisha kwamba Wafanyabiashara hawatumii mwanya huu kuwaumiza Wananchi; Pili: Bado ipo nafasi ya kutumia Kilimo katika kubadili maisha ya Mtanzania. Viongozi wote wakiwemo Waheshimiwa Wabunge tuonyeshe mifano katika kuendeleza Sekta ya Kilimo. Tuwahimize Wananchi waongeze juhudi, tuwape moyo na kuwahamasisha kutumia Zana Bora za Kilimo ili kuongeza tija. Maisha Bora yanapatikana kama tukitumia utaalam kwenye Kilimo; Tatu: Suala la Watoto wetu kupenda kusoma Somo la Hisabati linahitaji msukumo wa pekee. Tuliseme, tuliongee, na tulizungumze bila kuchoka kuanzia Majumbani, Chekechea na kuendelea. Tuwape moyo Watoto wetu wajue umuhimu wa kusoma na kufanya vizuri katika Somo la Hisabati; na Nne: Tuwahimize Wananchi wapende kuanzisha na kuchangia katika Mifuko ya Elimu kwenye maeneo yetu. Tunayo mifano kwamba katika ngazi ya Familia tunaweza kuchangia vizuri sana katika kufanya Sherehe mbalimbali. Tutumie dhamira hiyo hiyo kuchangia Mifuko ya Elimu kuwasomesha Watoto wetu. Tubadilike kifikra. Tujiunge na jamii zenye kupenda maendeleo ya Elimu. Tunaweza! Kilichobaki ni kuamua na tufanye hivyo sasa! Hitimisho 52. Mheshimiwa Spika, mwisho nikushukuru wewe mwenyewe Mheshimiwa Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wa Bunge kwa kutuongoza vizuri, kwa busara na kwa kuzingatia Kanuni za Bunge wakati wote wa Mkutano huu. Tumejifunza mengi kuhusu Taratibu na Kanuni za Bunge. Mmetuvumilia, mmetuongoza na tumekubaliana. Ninawashukuru tena Waheshimiwa Wabunge

16 wote kwa michango yenu ya dhati kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi yetu. Niwashukuru Watumishi na Wataalam wote wa Serikali waliosaidia kujibu Maswali na Hoja mbalimbali za Waheshimiwa Wabunge zilizojitokeza hapa wakati wa Mkutano huu. Aidha, nawashukuru Waandishi na Vyombo vya Habari kwa kuwapatia Wananchi habari kuhusu Majadiliano yaliyokuwa yanaendelea hapa Bungeni. 53. Kwa namna ya pekee niruhusu niwashukuru Madereva wote wa Viongozi, Madereva wa Waheshimiwa Wabunge, Madereva wote wa Watendaji Wakuu wa Serikali na Taasisi mbalimbali za Serikali na Binafsi ambao katika kipindi chote cha Mkutano huu wamehusika kuwaendesha Viongozi wote wakiwemo Waheshimiwa Wabunge pamoja na Wataalam kutoka sehemu mbalimbali Nchini kufika hapa Dodoma kuhudhuria Mkutano huu wa Kumi na Mbili. Wamefanya kazi nzuri. Nawasihi waendelee kuwa Makini katika kazi yao hii muhimu. Nasi tunawahakikishia kwamba tunathamini mchango wao katika maendeleo ya Nchi yetu. Mwisho kabisa namshukuru Kaimu Katibu wa Bunge Dkt. Thomas Kashililah na Watumishi wote wa Ofisi ya Bunge kwa huduma nzuri zilizowezesha kukamilisha shughuli zilizopangwa katika Mkutano huu bila matatizo. 54. Mheshimiwa Spika, kazi kubwa ambayo bado iko mbele yetu hususan baada ya kukaa Bungeni kwa kipindi chote hiki ni kwenda kushirikiana na Wananchi katika kutekeleza yote tuliyoyapitisha kwenye Mkutano huu. Bwana Albert Einstein Mwanafizikia aliandika: The World is a dangerous place. Not because of the People who are evil; but because of the People who don t do anything about it. Nchi yetu ni nzuri na ina Amani tele. Tukitimiza wajibu wetu sote nina hakika tutafanikiwa katika azma yetu ya kujiletea maisha bora. Twendeni tukawajibike. Twendeni tukafanye kazi. Twendeni tukatumie rasilimali zilizopo katika Nchi yetu kuinua uchumi wetu. Tutumie fedha tulizoziidhinisha hapa kwa uangalifu na nidhamu kubwa. Tumekuwa hapa kwa siku 81 tukijadili na kuidhinisha Bajeti za kila Wizara. Kazi iliyofanyika ya kuidhinisha fedha hizi ni kubwa. Itakuwa haina maana kama tutaacha fedha hizo zilizoidhinishwa zitumike bila mpangilio! Wananchi wetu hawatatuelewa. Umaskini utaisha na maisha bora yatapatikana kama tutatumia vizuri rasilimali zilizopo kwa maendeleo yetu. Sote tushirikiane kila mmoja kwa nafasi yake kutimiza wajibu kwa ajili ya Maendeleo ya Taifa letu. 55. Mheshimiwa Spika, nitumie muda huu kumwomba Mwenyezi Mungu awatangulie, awalinde na awaongoze katika safari ya kurejea nyumbani na Majimboni mwenu. 56. Mheshimiwa Spika, Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani unatarajiwa kuanza mwanzoni mwa Mwezi Septemba Napenda niwatakie Waislamu wote Mfungo mwema na wenye mafanikio ili kila atakayeamua kufanya Ibada hiyo aifanye kikamilifu na kama inavyoagizwa katika Kitabu cha Quran Tukufu. 57. Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo napenda kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu sasa liahirishwe hadi tarehe 28 Oktoba 2008, Siku ya Jumanne, Saa 3:00 Asubuhi litakapokutana katika Ukumbi huu hapa Dodoma. 58. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited

More information

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano. HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,

More information

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari

More information

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

More information

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,

More information

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria; HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited

More information

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na. JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3

More information

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2

More information

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for

More information

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper

More information

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania

More information

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya

More information

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA

More information

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.

More information

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya

More information

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities

More information

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika

More information

UTANGULIZI. 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na

UTANGULIZI. 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA, MHESHIMIWA STEPHEN MASATO WASIRA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA KWA MWAKA 2008/2009 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

More information

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi 3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi

More information

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI

More information

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA

More information

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza

More information

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA

More information

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA MWAKA 2018/2019 YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 HALI

More information

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh

More information

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA

More information

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3

More information

Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,

Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo, HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, KWENYE SHEREHE YA KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA, TAREHE 08 JUNI 2008, MSIMBAZI CENTRE, DAR ES SALAAM Mhashamu

More information

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA

More information

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi

More information

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017

More information

Human Rights Are Universal And Yet...

Human Rights Are Universal And Yet... Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,

More information

ORDER NO BACKGROUND

ORDER NO BACKGROUND In the matter of an Application by the DAR ES SALAAM URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (DAWASA) For a Tariff Adjustment, Submitted on January 8 th, 2008 (TR-W-08-001) ORDER NO. 08-001 1.0 BACKGROUND

More information

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini

More information

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, 2017 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA:

More information

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni

More information

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini

More information

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna

More information

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Desemba 2014 1 Shukurani Ripoti hii iliandikwa na Dk. Mkumbo. Ushauri wa kitaalamu ulitolewa na Elizabeth Missokia na Godfrey

More information

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TAARIFA YA MAFANIKIO CHINI YA UONGOZI WA MHE. SOSPETER MUHONGO (MB) KATIKA SEKTA NDOGO YA UMEME Disemba, 014 A. MAFANIKIO 1. Kuongezeka kwa uzalishaji

More information

13 APRILI, 2012 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Nne Tarehe 13 Aprili, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

13 APRILI, 2012 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Nne Tarehe 13 Aprili, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA Kikao cha Nne Tarehe 13 Aprili, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Mwenyekiti (Mhe. Jenista J. Mhagama) Alisoma Dua MWENYEKITI: Waheshimiwa

More information

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Ishirini na Mbili Tarehe 6 Julai, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/14 DODOMA Mei,

More information

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya

More information

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa

More information

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha

More information

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE. Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE. Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006 (Ulianza Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta)

More information

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA. Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi)

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA. Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU

More information

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika, HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, MHESHIMIWA JOHN POMBE MAGUFULI, (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2007/08 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau

More information

BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE. Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE. Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma

More information

3 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA NANE. Kikao cha Saba - Tarehe 3 Februari, 2015

3 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA NANE. Kikao cha Saba - Tarehe 3 Februari, 2015 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Saba - Tarehe 3 Februari, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA

More information

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

SautiElimu. Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA, ENG. DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB.) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA, ENG. DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB.) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA, ENG. DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB.) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO MIFUGO NA UVUVI KWA MWAKA 2017/2018 YALIYOMO

More information

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA PILI. Kikao cha Nne - Tarehe 29 Januari, (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA PILI. Kikao cha Nne - Tarehe 29 Januari, (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA PILI Kikao cha Nne - Tarehe 29 Januari, 2016 (Kikao Kilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alikalia Kiti HATI ZA KUWASILISHA

More information

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT

HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT. HUSSEIN ALI MWINYI (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2015/16 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika,

More information

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI

More information

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA TISA. Kikao cha Pili - Tarehe 14 Aprili, 2010

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA TISA. Kikao cha Pili - Tarehe 14 Aprili, 2010 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Pili - Tarehe 14 Aprili, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel

More information

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA

More information

Ufundishaji wa lugha nyingine

Ufundishaji wa lugha nyingine CHUO CHA ELIMU CHA KIMATAIFA OFISI YA ELIMU YA KIMATAIFA Ufundishaji wa lugha nyingine Na Elizabeth B. Bernhardt ELIMU MAZOEA KITABU NA. 20 1 Chuo cha Elimu cha Kimataifa (The International Academy of

More information

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to

More information

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu

More information

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA

More information

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi

More information

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Saba Tarehe 13 Aprili, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Saba Tarehe 13 Aprili, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA Kikao cha Saba Tarehe 13 Aprili, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge naomba

More information

TIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO

TIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO TIST HABARI MOTO MOTO Tel. 026-2322246 P.O.BOX 53 MPWAPWA E-Mail tist@twiga.com 01 October 2000 Y2K PREPARATIONS Holes and Seedlings made ready for the year 2000 programme By Gayo Mhila The process of

More information

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03

More information

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa

More information

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue?

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue? Tufundishane! Let s teach each other! This newsletter is published by The Foundation for Tomorrow and is meant to be a venue for teachers and schools to share and learn from each other s best practices.

More information

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini

More information

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa

More information

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu

More information

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document)

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Tatu - Tarehe 14 Julai, 2003 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Naibu

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA

HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA ANNA MARGARETH ABDALLAH, MBUNGE, KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2004/2005 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba sasa Bunge likubali

More information

DIRA DHIMA. Kuendeleza, kuwezesha, kudhibiti na kusimamia matumizi endelevu ya Rasilimali za Nishati na Madini kwa manufaa ya Watanzania.

DIRA DHIMA. Kuendeleza, kuwezesha, kudhibiti na kusimamia matumizi endelevu ya Rasilimali za Nishati na Madini kwa manufaa ya Watanzania. DIRA Kuwa Taasisi yenye ufanisi na inayojali tija ili kuhakikisha kuwa Rasilimali za Nishati na Madini zinachangia ipasavyo katika maendeleo ya nchi kijamii na kiuchumi. DHIMA Kuendeleza, kuwezesha, kudhibiti

More information

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...

More information

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted

More information

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017 TAARIFA Agosti 2017 NGUO MPYA ZA UKOLONI Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika Jumuiya ya Jamii ya 2007: Wajumbe wanaadhamana Nairobi dhidi ya EPAs. SwissInfo Tangu mwaka

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA BARA 2004 Imetayarishwa na: Idara ya Tiba Afya Makao Makuu P.O. Box 9083, DAR ES SALAAM June 2005 Yaliyomo Ukurasa Vifupisho

More information

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI SIKOMBE YIZUKANJI YORADI TASNIFU YA KISWAHILI KWA MINAJILI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (MA. KISWAHILI) KITIVO CHA SANAA

More information

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST

More information

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Thelathini na Nne - Tarehe 27 Julai, 2004 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika

More information

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini... Elimu Bora, lakini... Shukrani za dhati kwa wote waliotusaidia katika kutayarisha kijitabu hiki: Nsa Kaisi, Mshauri wa Rais, kwa mchango wake mkubwa wa mawazo Wafanyakazi wote wa HakiElimu 2003-2004 Many

More information