Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda

Size: px
Start display at page:

Download "Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda"

Transcription

1 WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya Utambulisho ya P Mradi Mkopaji/Wakopaji SERIKALI YA TANZANIA Wakala wa utekelezaji Wizara ya Nishati na Madini 754/33 Barabara ya Samora S.L.P Dar es Salaam, Tanzania Simu: (255 22) Nukushi: (255 22) Wizara ya Fedha na Uchumi S.L.P Dar es Salaam, Tanzania Daraja la Mazingira [ ] A [X] B [ ] C [ ] FI [ ] TBD (kuamuliwa) Tarehe ya Kuandaliwa PID Aprili 16, 2009 Makisio ya Tarehe ya Aprili 16, 2009 Kuidhinishwa Tathmini Makisio ya Tarehe ya Juni 9, 2009 Kuidhinishwa na Bodi Nchi ya Mradi na Historia ya Sekta Nchi ya Tanzania inashika nafasi ya 162 kati ya nchi 177 katika ripoti ya hali ya maendeleo ya watu iliyotolewa na UNDP mwaka Uchunguzi wa hivi karibuni juu ya bajeti za kifamilia umeonyesha mafanikio katika kutokomeza umaskini nchini Tanzania. Upatikanaji wa mahitaji muhimu, ubora wa makazi, na baadhi ya viashiria vya maendeleo ya kijamii, kama vile elimu, imeboreka sana, kuashiria kwamba uchumi unakua kwa kasi ya kuridhisha, na matumizi ya taifa pia yameongezeka katika kipindi cha miezi sita iliyopita. Kwa wastani, hali ya utofauti wa kipato baina ya wananchi haikuwa kubwa sana. Hata hivyo, vipimo vingine muhimu vya umaskini, kama vile umaskini wa kipato, vimeonyesha mafanikio madogo kama siyo kuongezeka. 1 Hali hii pia imeonekana katika viashiria vingine vya kijamii, kama vile upatikanaji wa chakula bora na maji safi na salama ya kunywa. Kuanzia mwaka 2001 hadi 2007, umaskini wa kipato umepungua kidogo Tanzania bara. Umaskini wa mtu mmoja mmoja na hali ya umaskini kwa ujumla ilipungua, na uwiano wa utokomezaji wa umaskini wa mtu mmoja mmoja umekuwa sawa mijini na vijijini. Ingawa, inasemekana kuwa umaskini umepungua kidogo kuliko ilivyoainishwa katika malengo ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA), au malengo yanayoainishwa katika Mpango wa Maendeleo ya Milenia. Umaskini katika Tanzania bara umepungua kwa asilimia 2.2, yaani kutoka asilimia 35.7 kwa mwaka hadi kufikia asilimia 33.5 mwaka Hii inamaanisha kuwa kuna ongezeko la watu maskini ikiwa suala la ongezeko la watu katika miaka hiyo litazingatiwa. 1 Hali hii imejirudia katika tafiti nyingi, jambo ambalo halionyeshi uwiano na ubora wa makazi au upatikanaji wa mahitaji muhimu au huduma muhimu za kijamii.

2 Katika miaka ya karibuni, Tanzania imeshuhudia ukuaji endelevu wa uchumi na kuongezeka kwa pato la taifa kwa takriban asilimia 7.4 kwa mwaka Matatizo ya ndani kama vile mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya shilingi kunaathiri uchumi. Shilingi iliendelea kushuka thamani kila siku kiasi cha kupita malengo ya MKUKUTA ya asilimia 4 tangu mwaka 2004, na ikashuka zaidi mwaka 2007 na 2008 ambapo mtikisiko wa kiuchumi na kushuka kwa thamani ya bidhaa za nje kuliongeza kiwango cha kushuka kwa shilingi. Hii ilisababisha kufikia kiwango cha kati ya asilimia katika robo ya mwisho ya mwaka Ongezeko lilikuwa kubwa zaidi katika robo ya mwisho ya mwaka 2008, na ingawa mtikisiko wa uchumi ulisababisha kushuka kwa bei ya mafuta na vyakula katika soko la dunia bado shilingi iliendelea kushuka thamani. Hali ya Tanzania katika mtazamo wa kimataifa kwa sasa ni nzuri. Ongezeko la uuzaji wa dhahabu na bidhaa nyinginezo na kushuka kwa bei ya mafuta kutaisaidia Tanzania kupiga hatua. Hata hivyo, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita urari wa malipo umezidi kuwa dhaifu. Upungufu katika akaunti ya hundi umezidi kiwango cha msaada kutoka nje ya nchi, hivyo kufanya urari wa malipo kutegemea fedha kutoka vyanzo binafsi vya nje ya nchi, hususan uwekezaji kutoka nje (FDI). Msukosuko wa sasa wa kiuchumi duniani unaweza ukasababisha uchumi wa nchi ukaathirika kwa kiasi kikubwa hasa ikiwa itatokea kupungua kwa kiwango cha uwekezaji kutoka nje ya nchi pamoja na kushuka kwa mapato yatokanayo na utalii. Sekta ya fedha Tanzania haihusiani moja kwa moja na mambo yaliyosababisha mtikisiko wa uchumi na hivyo benki zake hazijaathirika. Sekta ya fedha nchini Tanzania haihusiani moja kwa moja na rasilimali zilizosababisha mtikisiko wa uchumi, na hivyo mabenki yake hayakuathirika. Ingawaje tishio katika mfumo wa kibenki si kubwa sana, benki kadhaa zilizoathirika na mtikisiko wa kiuchumi duniani zina matawi nchini. Uchumi wa Tanzania haujaathiriwa na mtikisiko huu hadi sasa, lakini athari za mtikisiko wa kiuchumi ulioikumba dunia katika mwaka wa fedha umeongeza gharama ya matumizi ya nchi hususan kutokana na manunuzi ya nje. Njia kuu za kukabiliana na hali hii zinaweza kuwa kwa kupitia utalii, uwekezaji kutoka nje ya nchi, na mtiririko wa fedha za kigeni (na hasa kupitia madini na utalii), uuzaji mdogo wa bidhaa nje ya nchi, bei ndogo za mazao, na kupungua kwa misaada toka nje. Takwimu zinaonyesha kuwa pato ghafi la taifa (GDP) lilikuwa kwa asilimia 6.5 kwa mwaka Katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, sekta ya madini nchini Tanzania imepata mafanikio makubwa katika uvumbuzi wa madini na shughuli yenyewe ya uchimbaji. Baadhi ya maendeleo yanayoonekana wazi ni ubinafsishaji wa migodi sita mikubwa ya dhahabu ya Nzega, Geita, Bulyanhulu, North Mara, Buhemba, na Tulawaka. Katika kipindi hiki pia, zaidi ya migodi 15 tarajiwa ya dhahabu, nikeli, na yuranimu imeendelezwa na kufikia hatua mbalimbali za uvumbuzi. Hii imesababisha ongezeko la uzalishaji wa dhahabu toka chini ya tani moja kwa mwaka kwa mwaka 1998 na kufikia karibu tani 50 kwa mwaka 2008 na hivyo kuifanya Tanzania kuwa ya tatu Afrika kwa uzalishaji wa dhahabu na kuifanya sekta ya madini nchini kuwa sekta ya pili kwa kuchangia ukuaji uchumi ikitanguliwa na sekta ya utalii. Zaidi ya ongezeko la uzalishaji wa madini, mchango wake katika pato la taifa na la serikali umeendelea kuwa mdogo. Udogo wa mchango wa madini katika pato la taifa ulifikia wastani wa asilimia 3 kwa miaka ya huku mchango wake katika pato la serikali ukiwa ni asilimia 1.5. Hata hivyo, mauzo ya madini nje ya nchi yamefikia asilimia 48 ya mauzo makubwa, na hadi kufikia asilimia 24 ya mauzo yote. Aidha, jumla ya mapato ya fedha za kigeni katika sekta ya madini kwa miaka 10 iliyopita imezidi dola za Kimarekani bilioni 2.5 na imeajiri takribani asilimia 1 ya wafanyakazi wote. Mambo yaliyosababisha ukuaji wa haraka wa sekta ya madini Tanzania yanajumuisha mazingira mazuri ya kijiolojia; utulivu wa kisiasa; kuongezeka kwa bei ya dhahabu katika soko la dunia (kutoka dola za kimarekani 287 kwa wakia kwa mwaka 1998 hadi dola za kimarekani 687 kwa wakia kwa mwaka 2008, ikiwa ni ongezeko kubwa na la kihistoria katika kipindi hicho), uchimbaji

3 mkubwa; na mageuzi makubwa ya kiuchumi yaliyofanywa tangu katikati ya miaka ya 1990 ambayo yalileta mageuzi katika sekta ya madini toka katika kuwa chini ya umiliki wa serikali hadi kuwa chini ya wawekezaji binafsi. Mageuzi haya yalijumuisha utungaji wa sera mpya za madini mwaka 1997 ukifuatiwa na utungaji wa sheria za madini ambazo ni shindani kimataifa. Maendeleo katika sekta ya madini yanaleta changamoto na kutoa fursa kwa Tanzania. Tanzania ina uwezo wa kuzalisha vyuma vya thamani kubwa na ya kati, vyuma vya besi, vyuma vya ferasi, na madini ya viwandani ili kukidhi mahitaji yake ya ndani na mahitaji ya nje ya nchi; aidha, inaweza kuzalisha kiasi kikubwa cha mawe ya thamani ya rangi (ikiwa ni pamoja na almasi na tanzanaiti) na madini ya thamani ya kati kwa ajili ya kuingiza fedha za kigeni. Uchimbaji wa madini Tanzania unajibainisha kwa uchimbaji mkubwa ambao unatumia mashine kubwa kubwa za uchimbaji na uchimbaji mdogo (ambao hufanyika hasa vijijini) ambao unajumuisha wajasiriamali wa ndani na wachimbaji wadogowadogo. Uchimbaji mdogo unatumia zana duni na unafanywa kwa jinsi duni pia. Sifa kubwa ya uchimbaji mdogo ni ukosefu wa mbinu bora za udhibiti na usimamizi; kutokujali usalama wa wachimbaji na mazingira; na ukosefu wa miundo mbinu bora. Sekta ya madini ndiyo kipaumbele cha ukuzaji wa uchumi na kupunguza umaskini katika MKUKUTA. Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali za Madini (SMMRP) umeanzishwa ili kuisaidia serikali kukabiliana na changamoto hizi na kujinufaisha na fursa zilizopo katika sekta hii. Mradi wa SMMRP unajengwa katika msingi imara wa uchambuzi, kufuatana na mradi wa msaada wa kiutendaji katika maendeleo ya sekta ya madini unaosaidiwa na IDA, ulioanzishwa katikati ya mwaka Kazi ya uchambuzi na shughuli zilizopo katika mradi huu zilisaidia kuvutia uwekezaji katika uvumbuzi wa madini na uendelezaji wa shughuli za uchimbaji kupitia uboreshaji wa muundo wa sekta ya madini, ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa taasisi na mashirika yanayosimamia sekta ya madini. Hata hivyo, maendeleo ya haraka ya sekta ya madini, hususan uchimbaji mdogo, unategemea kwa kiasi kikubwa uwezo wa kitaasisi wa serikali. Taasisi zilizopo zinakosa mbinu, utaalamu, na mfumo wa kitaasisi unaohitajika kusimamia na kusaidia sekta ya madini iwe inayojiendesha kibiashara. Wakati Tanzania imefanikiwa kuvutia wawekezaji, serikali na jamii kuzunguka migodi zimeendelea kutoridhishwa na kiwango cha mchango wa sekta ya madini katika ukuaji wa uchumi. Ukosoaji umehusu uwezo mdogo wa kitaasisi kuiendeleza sekta hii, na hasa katika kuhakiki gharama za uwekezaji, gharama za utunzaji wa mazingira, na kuingiza viwango bora vya usalama na afya za wafanyakazi; usimamizi mbovu wa kodi ya usafirishaji wa madini kwenda nje ya nchi; kasi ndogo ya kuleta mageuzi na mbinu za kisasa za uchimbaji kwa wachimbaji wa kati na wadogo; na ushirikishwaji duni wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa. Mengi kati ya mambo haya yameelezwa siku za hivi karibuni katika utafiti wa kina wa sekta ya madini Tanzania uliofanywa na Baraza la Kimataifa la Madini na Vyuma (ICMM). 2 Masuala haya yalisababisha kuundwa kwa Kamati ya Kupitia Sera ya Madini (Ripoti ya Kipokola) mwaka 2004; hii ilifuatiwa na Tume ya Rais ya Sekta ya Madini mwaka 2008 (Ripoti ya Bomani). Mapitio haya ya kina juu ya sekta ya madini yalikusudia kubainisha maeneo yanayostahili kuboreshwa katika sekta ya madini ili kuinua ukuaji wa uchumi. Mapendekezo haya kutoka katika ripoti za Kipokola na Bomani yalitoa mwongozo wa mchakato wa mageuzi ya sera za serikali zilizopo. Ripoti zote mbili zilisisitiza haja ya kujenga uwezo wa taasisi na mashirika ya serikali yanayosimamia sekta ya madini ili (a) kuwezesha maendeleo endelevu ya kuwa na sekta ya kisasa ya madini na inayojiendesha kibiashara, ambayo itanufaisha nchi; (b) kuanzisha usimamizi wa kisasa na wa uwazi na muundo mpya wa usimamizi wa sekta ya madini; (c) kuendeleza maendeleo 2 Making Mining Count in Tanzania, Resource Endowment Initiative, ICMM, UNCTAD, na Benki ya Dunia, Octoba 2006.

4 ya sekta ya madini yaliyopatikana tangu mwishoni mwa miaka ya 1990; na (d) kuendeleza taarifa za msingi za kijiolojia ili kuvutia uwekezaji katika sekta ya madini. Kutokana na kuporomoka kwa uchumi kwa siku za hivi karibuni na mtikisiko wa uchumi, ni muhimu kwa nchi ya Tanzania kuendelea kuwa kivutio katika uwekezaji wa sekta ya madini na kujiandaa kwa mafanikio. Masuala yahusuyo sekta ya madini, ikiwa ni pamoja na kiwango cha mapato yatokanayo na sekta ya madini na yanayopatikana kwa serikali (kupitia ushuru, kodi na kadhalika), pia yaliifanya serikali kujikita kwenye utekelezaji wa mpango wa uwazi katika uchimbaji (EITI) kwenye sekta ya madini (na gesi) kwa ujumla, hasa mwishoni mwa mwaka Serikali (kwa msaada wa Serikali ya Norway na Benki ya dunia) ulizindua EITI katika warsha ya wadau iliyofanyika Disemba mwaka Warsha hii ilifuatiwa na warsha nyingine ya wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na wawakilishi wa mashirika ya kijamii na, wachimbaji wadogowadogo iliyofanyika mwishoni mwa mwezi Januari 2009 na kutoa muswada wa mpangokazi wa EITI. Mwezi Februari 2009, Tanzania ilikubaliwa na bodi ya kimataifa ya EITI kuwa katika orodha ya nchi zinazoomba kuwa na EITI. Uundwaji wa kikosi kazi cha EITI cha Tanzania kinachoundwa na wadau mbalimbali uko katika hatua za mwisho. Kwa kiasi kufani, utekelezaji wa EITI nchini Tanzania utawezeshwa na SMMRP, pamoja na vyanzo vingine ambavyo serikali itavipata (m.f., mfuko wa mashirika mbalimbali ya misaada ya EITI, na misaada inayotokana na makubaliano baina ya nchi na nchi). Muundo wa Kisheria Sekta ya madini nchini Tanzania inasimamiwa na serikali kuu. Sheria mama zinazosimamia sekta ya madini ni Sheria ya Madini ya mwaka 1998, Sheria ya Milipuko ya mwaka 1963, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004, na Sheria ya Kodi ya Mapato ya mwaka Sheria ya Kodi ya Mapato inaenda sambamba na Sheria ya Uwekezaji ya Tanzania, iliyoweka muundo unaosimamia sekta ya madini na mambo yanayoangaliwa ili kujua faida na mtaji, na pia kufuata mchakato wa usuluhishi wa kimataifa. Mambo yaliyomo katika muundo wa Tanzania ni pamoja na kodi ya mapato, ushuru, kodi ya zuio, na viwango vya ushuru wa forodha. Inajumuisha pia msamaha wa kodi ambao unajumuisha uwezekano wa miradi mkubwa ya uchimbaji wa madini kuingia makubaliano ya kimaendeleo na serikali ili kuzuia ongezeko la kodi kama lilivyokuwa wakati wa kusainiwa kwa mkataba. Kulingana na Sheria ya Madini, madini yaliyopo ardhini ni mali ya serikali ya Tanzania. Hakimiliki ya kutafuta na kuchimba madini inatolewa kwa leseni maalumu chini ya Sheria ya Madini, na leseni hizi zinatolewa kwa kuangalia aliyeomba kwanza, isipokuwa pale ambapo leseni hizi zitakuwa zimetangazwa kwa njia ya tenda. Mfumo wa sheria wa Tanzania, miongozo, sheria za kesi, na sheria za forodha vimeigwa toka kwa mfumo wa sheria wa Uingereza. Sheria za Uingereza hutumika pale ambapo hakuna sheria za miongozo, na pia hutumika pale ambapo sheria za biashara zimekwisha tumika kwa kipindi kirefu. Kwa ujumla, sheria za forodha zinatumika katika mambo ya umiliki wa ardhi wa kurithi, na katika maswala ya ndoa. Muundo wa kitaasisi Msimamizi mkuu wa sekta ya madini ni Wizara ya Nishati na Madini (MEM). Kamishna wa madini huteuliwa na rais ili kusimamia na kudhibiti utekelezaji wa sheria ya madini. Waziri na Kamishna ni mamlaka zinazotambuliwa kisheria zinazoweza kufanya kazi kwa pamoja au kwa kujitegemea chini ya sheria ya madini. Mkaguzi wa madini anasimamia sekta kulingana na matakwa ya sheria ya madini. Masuala ya sayansi ya jiolojia yanasimamiwa na Taasisi ya Uchunguzi wa Jiolojia (GST), ambayo ni shirika muhimu lililo chini ya MEM.

5 Maswala ya mazingira ni wajibu wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), ambalo pia linafanya kazi na kitengo cha MEM kinachosimamia maswala ya mazingira katika sekta ya madini. Changamoto za Sekta Changamoto kubwa zinazoikabili sekta ya madini ni pamoja na: Matarajio makubwa ya kufaidika na madini kwa Serikali ya Tanzania na jamii zinazozunguka migodi kutokana na uwekezaji mkubwa na mapato yanayotokana na sekta ya madini; Kuharibika kwa mazingira ya uwekezaji kutokana na maoni ya wananchi na wito wa maafisa wa serikali wa kubadilisha sera ili kuinufaisha zaidi Serikali; Ukosefu wa miundombinu ya barabara, reli na umeme migodi mingi haijaunganishwa na gridi ya taifa ya umeme na hivyo hutegemea umeme wao wenyewe unaozalishwa kwa kutumia jenereta za dizeli ambazo hutumia gharama kubwa; Kuendeleza ushindani wa Tanzania kama mahali pazuri pa uwekezaji katika sekta ya madini katika mazingira ya mtikisiko wa uchumi unaoikabili dunia; Ukosefu wa fedha kwa taasisi za serikali zinazosimamia sekta ya madini; Ukosefu wa uwezo wa kusimamia sekta ya madini ipasavyo maombi ya leseni ya uchimbaji madini huchukua zaidi ya miezi 12 kushughulikiwa, MEM inakosa rasilimali za kuendeshea ukaguzi wa migodi kuona kama wachimbaji wametimizwa matakwa ya leseni zao, mahitaji ya kiafya, usalama na mazingira; Kukosekana kwa uzalishaji mbadala wa madini toka kwenye dhahabu na mawe ya thamani kwenda kwenye vyuma vya besi na madini mengineyo; na Ushirikishwaji duni wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa. Malengo Kufuatana na Dira ya Serikali, Malengo ya Maendeleo ya Mradi (PDO) ni: Kuimarisha uwezo wa Serikali ya Tanzania kusimamia sekta ya madini ili kudhibiti athari za kijamii na kiuchumi za uchimbaji mkubwa na mdogo nchini Tanzania na kuhimiza wawekezaji wa ndani na nje katika sekta ya madini. PDO ina vipengele vitatu: (i) athari za kijamii na kiuchumi; (ii) Uwezo wa serikali; na (iii) uwekezaji. Uwekezaji katika sekta ya madini una historia ndefu sana na, kutokana na hali ya sasa ya mtikisiko wa uchumi duniani unaoathiri sekta ya madini, viashiria hapa chini vinaonyesha yale ambayo serikali na timu ya mradi inaamini yanaweza kupatikana na kuonekana katika kipindi chote cha mradi. Hata hivyo, izingatiwe kuwa faida kubwa ya uwekezaji wowote mpya katika sekta ya madini inatarajiwa kuonekana baada ya kufungwa kwa mradi, kama ilivyokuwa kwa Mradi wa awali wa Msaada wa Kiutendaji Katika Sekta ya Madini. Hata hivyo, shughuli za kuboresha usimamizi wa hati za madini na kazi za kukagua madini zinatarajiwa kusababisha ongezeko la ada za leseni na ukusanyaji wa kodi kwa takribani asilimia 5 katika muda wa mradi. Uwekezaji mpya

6 katika sekta ya madini utadhibitiwa, lakini unatarajiwa kuendelea baada ya mradi kwisha kwa kiwango cha dola za kimarekani milioni 250 kwa mgodi. Kiashiria kikuu kilichochaguliwa katika kupima uwekezaji katika sekta ya nafasi ya Tanzania katika nchi zenye mazingira mazuri ya uwekezaji katika uchimbaji wa madini ili kuisaidia kufanya vizuri katika uwekezaji wa kimataifa pale hali ya uchumi duniani itakapotengamaa. Vilevile, huku uzalishaji wa wachimbaji wa kati na wadogo unatarajiwa kuongezeka kutokana na msaada wa kiutendaji, mambo mengine yatakuwa na athari hasi kwa kipato cha kaya. Kwa hiyo, kiwango cha kipato na kiwango cha uzalishaji kitadhibitiwa. Viashiria vya msingi vya kivitendo ambavyo vitatathmini mafanikio ya mradi ni: (i) Athari za Kijamii na Kiuchumi: Asilimia ya ongezeko la viwango vya kipato cha kaya kwa jamii za wachimbaji wa kati na wadogo zilizoteuliwa (ASM). Asilimia ya wananchi toka katika jamii zinazoshiriki ambao wanaona kwamba mawazo yao yamezingatiwa katika mchakato wa maendeleo. (ii) Uwezo: Muda wa kushughulikia leseni za madini (miezi) na idadi ya leseni zenye matatizo; Machapisho ya kila mwaka ya mapato yanayotokana na sekta ya madini. (iii) Uwekezaji: Uboreshaji wa nafasi ya Tanzania katika viwango vya nchi kama mahali pazuri pa kuwekeza katika sekta ya madini kama ilivyothibitishwa na uchunguzi huru wa uwekezaji (Taasisi ya Fraser); Ongezeko la asilimia ya mapato yatokanayo na madini. Maelezo ya Ushiriki wa Benki ya Dunia Madini ni sekta muhimu katika ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini. MKUKUTA unatoa wito wa kuboresha sera na sheria pamoja na kuendeleza na kuhimiza uwepo wa mazingira mazuri kwa uwekezaji katika sekta ya madini. Mpango wa Pamoja wa Kusaidia Nchi unabainisha kuwa Benki ya Dunia ina msaada wa utaalamu wa kiutendaji katika kuisaidia sekta ya madini Tanzania. Mradi wa awali wa Msaada wa Kiutendaji wa Maendeleo ya Sekta ya Madini uliokuwa ukisaidiwa na Benki ya Dunia ulikuwa na ufanisi katika kuweka misingi ya awamu ya awali ya ukuaji wa sekta, na Benki ya Dunia imeendeleza mazungumzo na Tanzania juu ya sekta hii tangu kufungwa kwa mradi huu. Kutokana na msaada wa utaalamu wa kiutendaji wa Benki ya Dunia katika sekta ya madini na mafanikio ya mradi wa awali, serikali iliomba msaada mwingine wa Benki ya Dunia katika sekta ya madini ili kuendeleza mafanikio yaliyopatikana na kuzisaidia taasisi zinazohusika kuboresha usimamizi, ufanisi, na mchango wa sekta hii katika maendeleo ya taifa. Ifahamike kuwa serikali haijaomba msaada wa Benki ya Dunia katika mageuzi yake ya sera ya madini na mageuzi ya mfumo wa sheria ya madini. Badala yake, serikali imeomba msaada wa Benki ya Dunia ulenge kutoa mikopo kwa wachimbaji wa kati na wadogo, kuhimiza uwazi katika sera/sheria/muundo wa usimamizi, rasilimali watu na kujenga uwezo wa kitaasisi, na kuboresha taarifa za kijiolojia. Benki ya Dunia ina uzoefu mkubwa katika sekta ya madini na inaweza kutumia mafunzo iliyopata kupitia miradi kama hii katika nchi mbalimbali na za jirani kama vile Msumbiji, Uganda, na Zambia. Benki ya Dunia ipo katika nafasi ya kipekee ya kutoa msaada unaoweza kusaidia shughuli

7 nzima ya uchimbaji (pia unajulikana kama mkabala wa EITI++ ). SMMRP utatosheleza moja kwa moja mahusiano ya 1, 2, 3, na ya 5 ya mkufu wa fedha (angalia kielelezo cha 1), unaoitwa upatikanaji wa rasilimali (m.f., kupitia uimarishaji hakimiliki za madini), kusimamia uchimbaji (m.f., kupitia kuongeza uwezo wa wakaguzi wa shughuli za uchimbaji), ukusanyaji wa kodi na ushuru (m.f., kupitia uimarishaji wa ukaguzi wa mara kwa mara), na matumizi endelevu na yenye ufanisi ya mapato (m.f., kupitia chunguzi za awali juu ya upangaji wa bajeti na mipango katika jamii za wachimbaji madini); mradi pia utatosheleza mahusiano ya 4 juu ya ugawaji wa mapato. Kwa kuwa mapato ya madini Tanzania yanakusanywa kama mapato ya jumla (ambapo dola za kimarekani 200,000 tu ndizo hurejeshwa kwenye jamii zinazozunguka migodi mikubwa), mahusiano ya 4 yanatoshelezwa chini ya shughuli za mitaji mikubwa za Benki ya Dunia, inayojumuisha uhusiano wa usimamizi wa matumizi ya umma. Tanzania ina mfumo wa usimamizi wa matumizi ya umma uliogawanyika sana, ambao una fedha zilizokusanywa pamoja na kugawanywa katika wilaya na mikoa. Baadhi ya fedha chache zinazohusiana na madini zilizolipwa moja kwa moja kwa serikali za mitaa zitashughulikiwa na kitengo kidogo cha mradi cha maendeleo ya kiuchumi ya vijiji. Kielelezo cha 1. Mkufu wa Fedha za Uchimbaji Madini (EITI++) EITI Vipengele vya Mradi Award of Regulation Implementation Contracts and Collection Revenue of Sustainable and Monitoring of Taxes Management Development Licenses Link 1 of Operations and Royalties and Allocation Policies and Link 2 Link 3 Link 4 Link 5 Projects Link 1 Link 2 Link 3 Link 4 Link 5 Mradi unajumuisha vipengele vinne: (a) Kuboresha manufaa ya sekta ya madini kwa Tanzania: kuboresha wachimbaji wa kati na wadogo (ASM), mipango ya maendeleo ya nchi, na kuboresha utendaji kazi; (b) Kuimarisha usimamizi na uwazi katika sekta ya madini; (c) Kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya madini; na (d) Kuboresha ushirikiano, usimamizi, udhibiti na tathmini ya mradi. Kipengele A. Kuboresha Manufaa ya Sekta ya Madini kwa Tanzania: Kuboresha Wachimbaji wa Kati na Wadogo, Mipango ya Maendeleo ya Nchi na Kuendeleza Utendaji kazi Lengo kuu la kipengele hiki ni kuboresha manufaa yatokanayo na madini kwa Tanzania kama nchi, na kwa wananchi wake kwa kutekeleza mkakati wa ASM wa maendeleo ya kitaifa, kuongeza ushirikishwaji wa sekta ya madini katika uchumi wa nchi, na utendaji kazi unaohitajika katika sekta ya madini. Manufaa haya yataelekezwa kwa wachimbaji wa kati na wadogo, jamii zinazoishi kuzunguka migodi, na wachimbaji wazalendo kupitia MEM. A.1 Utafiti wa Msingi. Kipengele hiki kidogo kitatoa taarifa za msingi zinazohusu vipengele vingine na ambazo zitasaidia katika usimamizi na utathmini. Kitasaidia tafiti za awali katika: (a) kutathmini, kubainisha shughuli za wachimbaji wa kati na wadogo, na kukusanya na kutafsiri takwimu katika ombwe la takwimu la ASM; (b) kuchunguza athari na manufaa kwa kijamii na kwa kiuchumi za migodi mikubwa ya Geita, Bulyanhulu na Mirerani TanzaniteOne; (c) kutathmini

8 uwezo wa kitaasisi ili kupata takwimu za migodi na uwezo wa migodi hiyo kwa ajili ya utunzaji wa takwimu, na (d) kuandaa mkakati na muundo wa usimamizi na utathmini wa mradi. A.2 Huduma za Ushauri za ASM. Kipengele hiki kidogo kitaimarisha uwezo wa kiusimamizi ili kutoa huduma za ushauri kupitia ofisi za madini za kanda na za mikoa (ZMO na RMO), ambazo kwa sasa hazijawezeshwa kufanya kazi hizi kwa ufanisi. Kwa sasa MEM inaboresha uwezo wake ili kutekeleza ipasavyo mkakati wa uendelezaji wa wachimbaji wadogo. Lengo ni kuwezesha ofisi za kanda na za mikoa kujenga imani kwa jamii za wachimbaji, kutoa huduma za ushauri, na kubainisha kwa njia sahihi mikabala mbalimbali ya kimkakati na kiutendaji ili kuhimiza uchimbaji rasmi na unaowajibika. Hii itawezesha ofisi za kanda na za mikoa kushughulikia maswala yanayohusiana na madini kama vile uchimbaji wa madini na teknolojia inayotumika, usimamizi wa fedha, mazingira, na usalama wa afya, ushirikishaji wa jamii zinazozunguka migodi, mafunzo ya elimu ya jinsia, usimamizi, na uhalalishaji wa shughuli za wachimbaji wadogo. Ofisi hizi pia zitashirikiana na wachimbaji, kupitia utoaji wa elimu, mawasiliano ya mara kwa mara, na mbinu nyinginezo, kushughulikia matatizo makubwa ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi wa Albino ambayo yanasababishwa na imani kwamba kuua Albino kutawafanya wachimbaji kupata madini wanayoyatafuta. MEM itashirikiana zaidi na wachimbaji wa kati na wadogo kwa kuwapa msaada wa kiutendaji ili kuwahimiza kurasimisha shughuli zao. Jamii za ASM zitakazokuwa zinapata ushauri zinatarajiwa kuboresha maisha yao kwa kuongeza uzalishaji na kupunguza athari hasi kwa jamii na kwa mazingira. Mradi utasaidia juhudi za MEM kugawanya rasilimali za madini ili (a) Kuimarisha idara ya wachimbaji wadogo ya wizara ya nishati na madini makao makuu; (b) Kuboresha uwezo wa kutoa ushauri katika ofisi za kanda na za mikoa; (c)kuboresha uwezo wa taasisi zinazotoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo kama vile Mamlaka ya Utendaji Stadi (VETA), na Shirika la Viwanda Vidogo ili kutoa kozi fupi kwa wachimbaji wadogo; (d) Kuanzisha vituo vya wachimbaji wadogo kwa ajili ya kupata ushauri na kuwa kama kituo cha mafunzo ambapo vitini vya mafunzo, vitini vya maelekezo ya uchimbaji mdogo vitakuwa vinapatikana; na pia vituo hivi vitatoa mafunzo. Baadhi ya vituo hivyo ni Itumbi Chunya (dhahabu), Mpanda (dhahabu), Mazizi Morogoro (dhahabu), Londoni Manyoni (dhahabu), Rwamagaza-Geita (dhahabu), Katente-Bukombe (dhahabu), Mirerani-Simanjiro (tanzanaiti), na Masuguru-Mbinga (sapphire). Tathmini ya athari za kimazingira na kijamii itafanyika katika maeneo yaliyobainishwa kabla ya uteuzi, na jukumu la serikali litakuwa kuwezesha mafunzo, huku umiliki na maswala ya utendaji kazi yatasalia mikononi mwa mmiliki wa mgodi husika; (e) Kuboresha uwezo wa ofisi za kanda na za mikoa kutoa ushauri kwa kuwapa mafunzo maafisa watakaokuwa wanatoa ushauri na kuwapatia vitini vya kufanyia kazi na vifaa vya kivitendo vinavyohamishika ili kuwajengea uwezo zaidi, kuwawezesha kusafiri, na kuwajibika haraka pale inapotokea dharura migodini; (f) Kuandaa vitini vya kufanyia kazi vitakavyokuwa vinatumiwa na wote pamoja na miiko ya kuzingatia katika uchimbaji mdogo, na hasa kuhusu uchimbaji wenyewe, usalama na afya za wachimbaji, jiolojia na uandaaji wa madini kwa kila aina ya madini na katika maswala mtambuka kama vile VVU/UKIMWI, mazingira (ikiwemo madhara ya zebaki inayotolewa migodini), ujasiriamali, uwajibikaji wa kijamii, na (g) Kuhimiza mipango madhubuti ya makampuni makubwa ya uchimbaji wa madini kutoa mafunzo na ushauri kwa wachimbaji wadogo wa Geita, Mererani, Kahama, na Kabanga ili kuwapa uzoefu wa matatizo waliyokumbana nayo na mikakati ya kusuluhisha migogoro baina ya ASM na wachimbaji wakubwa. A.3 Programu Zilizokusudiwa Kuendeleza Madini Maalumu ya Viwandani na ongezeko la Thamani la Mawe ya Thamani. MKUKUTA unabainisha uhamasishaji wa ongezeko la thamani ya madini kama mojawapo ya kipaumbele cha kupambana na umaskini Tanzania. Mwaka 2003, MEM ilianzisha kituo cha mawe ya thamani na uchongaji Arusha kwa lengo la kutoa mafunzo kwa wajasiriamali juu ya jinsi ya mambo yanayoweza kuongeza thamani ya mawe yao ya thamani na

9 mawe mengine ya mapambo. Nusu ya kituo tayari imekamilika, hususan hasa katika ukarabati wa majengo, utoaji wa mafunzo, na zana za kufanyia kazi. Lengo la MEM ni kukiboresha kituo hiki hadi kufikia hadhi ya taasisi ya kimataifa ya mawe ya thamani ambayo itaendesha mafunzo, itazalisha, na kuhamasisha mazao ya mawe ya thamani na mawe mengine ya mapambo. Kipengele hiki kidogo kitasaidia kutoa msaada wa kiutendaji kwa wajasiriamali wazalendo ili kuendeleza uzalishaji na uuzaji wa madini ya viwandani, na kusaidia kupandisha thamani ya mawe ya thamani kubwa na ya kati, pamoja na uanzishaji wa kituo cha pamoja cha uzalishaji wa bidhaa hizi. Kituo hiki kitakuwa kama kituo cha viwanda, mafunzo, na mauzo kikiwa na lengo la kuendeleza sekta ya shindani ya viwanda vidogo vinavyojishughulisha na uchongaji wa mawe na utengenezaji wa vito vya dhahabu. Utoaji wa mafunzo na misaada utawawezesha Watanzania kufanya kazi bila utegemezi katika shughuli zinazoinua thamani ya mawe na kuwa wawekezaji katika sekta hii. Msaada utatolewa pia katika mipango ya kuwa na biashara sawa katika bidhaa za ASM. Kipengele hiki kidogo kitasaidia (a) Kuboresha Kituo cha Uchongaji wa Mawe cha Arusha; (b) kuanzisha sehemu ya vito na programu ya mafunzo katika kituo cha uchongaji wa mawe Arusha; (c) kuwajengea uwezo wajasiriamali kuzalisha na kuuza hapahapa nchini madini fulani ya viwandani; na (d) kuwezesha mkakati wa biashara sawa. A.4 Msaada wa kifedha kwa Wachimbaji Wadogo na Shughuli na Zinazosaidia Kupandisha Thamani ya Madini. Wachimbaji wadogo na wa kati wapo katika kundi la wajasiriamali wadogo na wa kati. Kundi hili linakabiliwa na matatizo makubwa, hususan upatikanaji wa mitaji na mikopo. Ukosefu wa fedha za mitaji na za kugharimia shughuli za uchimbaji unasababisha viwango duni katika machimbo na ushiriki mdogo wa wachimbaji wadogo katika mikakati mingine, kama vile mkakati wa kupata mafunzo na ushauri. Ukosefu wa mbinu bora za ujasiriamali unabainishwa kuwa mojawapo ya mambo yanayosababisha kukosa mitaji kutoka kwa taasisi za kifedha nchini Tanzania. Kipengele hiki kidogo kinalenga kumwezesha mfanyabiashara mmojammoja kupata mbinu za kifedha ili kuweza kujiajiri, kupata mafunzo na msaada wa kupata masoko na ushauri wa kuchagua na kununua zana za uchimbaji zinazofaa, na pia kuzisaidia jamii katika miradi yao ya uwekezaji iliyoteuliwa kuwa na miundo mbinu bora, utayarishaji wa madini, na biashara za kuwapatia wachimbaji bidhaa na huduma muhimu. Kwa kushirikiana na Vyama vya Uchimbaji Madini vya Mikoa (REMA) na wadau wengine, Programu itahamasisha: (a) utoaji wa mafunzo ya ujasiriamali kwa wachimbaji wadogo; (b) kuboresha na kusaidia miradi ya ukopeshaji na upatikanaji wa zana za uchimbaji katika vituo vya wachimbaji wadogo; na (c) uendelezaji wa programu ya utoaji wa msaada wa kifedha kwa njia ya mikopo midogo ili kuwasaidia wachimbaji na vyama vya wachimbaji vya maeneo husika katika programu zinazohusu mambo kama vile uboreshaji wa mazingira, miradi midogo mbadala ya uzalishaji mali, uboreshaji wa afya na usalama wa wachimbaji migodini, na matumizi ya teknolojia katika maeneo ya wachimbaji wadogo. Programu itatathmini mapendekezo ya miradi yao katika hali ya ushindani na kuhitaji miradi yote iliyopendekezwa kufuata mbinu bora za kusaidia jamii na kuhifadhi mazingira. Mikopo midogomidogo itatolewa kwa awamu mbili, awamu ya pili ikitegemea mafanikio ya awamu ya kwanza. A.5 Ushirikishwaji wa Sekta ya Madini katika Uchumi wa Taifa. Moja ya changamoto zinazoikabili sekta ya madini ni ushirikishwaji mdogo wa sekta ya madini katika uchumi wa taifa. Kipengele hiki kidogo kinalenga kuimarisha ushirikishwaji wa wachimbaji wakubwa na wadogo katika uchumi wa serikali za vijiji za maeneo yao na pia katika mamlaka za mikoa husika (LGRA) kwa kusaidia uandaaji wa mipango mikakati ya maendeleo ya uchumi wa vijiji na mikoa husika

10 kwa kuwashirikisha wachimbaji, makampuni ya uchimbaji, na jamii husika katika michakato ya mipango hiyo. Mradi utasaidia utafiti wa awali ili kupima utekelezaji wa kipengele hiki katika wilaya za Geita, Kahama, Tarime na Biharamulo. Mikakati iliyofanikiwa itahamishiwa katika wilaya zingine ili kuwezesha uchumi wa vijiji na mikoa kunufaika na uwekezaji wa madini katika maeneo yao kama kichocheo cha maendeleo ya mkoa mzima, ikiwa ni pamoja na uboreshaji wa miundo mbinu, upatikanaji wa fursa za maendeleo, uhamishaji wa ujuzi, na uchumi mbadala. Kipengele hiki kidogo kitasaidia LGRA zilizoteuliwa (a) kuingiza shughuli za uchimbaji katika mipango mikakati yao katika ngazi ya wilaya kwa kuendeleza kwa namna fulani mipango mikakati ya maendeleo ya uchumi ya maeneo husika, kwa kushirikiana na makampuni ya uchimbaji, wafanyabiashara, jamii, na mashirika ya kijamii ya maeneo husika (b) kuingiza shughuli za wachimbaji wadogo na wa kati katika muundo wa utawala wa wilaya na (c) kuendeleza mbinu ya kuiwezesha jamii katika maeneo yaliyoteuliwa kuwekeza katika utoaji wa huduma na bidhaa migodini. A.6. Uendelezaji wa Rasilimali Watu kwa Ajili ya Migodi. Mipango ya kuendeleza wa ujuzi wa kiutendaji na mafunzo katika migodi hapa Tanzania ipo katika hatua za awali. Lengo la kipengele hiki kidogo ni kuwezesha uanzishwaji wa muundo wa mpango wa uendelezaji wa ujuzi, utoaji wa mafunzo, uthibitishaji wa mafunzo, na kudhibiti viwango vya mafunzo ili kuongeza tija na usalama wa afya za wachimbaji migodini. Pia, kipengele hiki kidogo kitanufaisha nchi kwa kuongeza fursa kwa Watanzania kuajiriwa katika nafasi za juu katika sekta ya madini na kujenga uwezo kwa manufaa ya baadaye. Vilevile, kipengele hiki kidogo kitaisaidia MEM katika (a) kutathmini mahitaji ya uendelezaji wa rasilimali watu katika sekta ya madini; na (b) kuanzisha na kuwezesha muundo wa kusimamia mipango ya mafunzo, ujuzi, na ujifunzaji katika sekta ya madini. Kipengele B. Kuboresha Usimamizi na Uwazi Migodini B.1 Mageuzi ya Kisheria na Uwazi. Kipengele hiki kidogo kitaegemea tafiti na uzoefu wa awali na hivyo kusaidia mapitio yanayoendelea na marekebisho ya mfumo wa kisheria, kiutawala, na mifumo ya udhibiti ya sekta ya madini Tanzania. Kipengele hiki kidogo kitasaidia shughuli zifuatazo (a) kuimarisha kitengo cha huduma za kisheria za MEM; (b) kusaidia mapitio ya Sera ya Madini, Sheria ya Madini, na sheria nyingine zinazohusiana nazo, lengo likiwa ni kuziboresha; (c) kuanzisha mfumo wa kisheria na wa kiudhibiti wa shughuli za kupandisha thamani na ukataji wa madini; (d) kuibua uelewa wa wananchi juu ya Sera ya Madini na muundo wa kisheria na wa kiutawala; na (e) kusaidia shughuli zinazohusiana na utekelezaji wa EITI. B.2 Ujengaji wa Uwezo wa Kitaasisi. Muundo wa MEM umepitia mabadiliko muhimu kutokana na matokeo ya tathmini ya taasisi hii kati ya mwaka 2001 na Ingawa kumekuwa na mabadiliko, MEM imeendelea kukabiliana na changamoto mbalimbali ambazo zimeleta haja ya kupitia upya kazi zake na muundo wa jumla wa taasisi hii ili kuboresha ufanisi. Kipengele hiki kidogo kitasaidia uchambuzi wa kitaasisi ili kubainisha haja ya kujenga uwezo na kuimarisha mahusiano na ushirikiano na taasisi nyingine za serikali ambazo zinasimamia sekta ya madini. Mradi umeshabainisha haja ya kuimarisha shughuli za ukaguzi wa hesabu na ukaguzi mwingine unaofanywa na MEM ikiwa ni pamoja na mapitio ya tathmini ya athari ya mazingira na usimamizi wa matakwa ya sheria za uchimbaji, usimamizi wa afya na usalama wa wachimbaji, na ukaguzi wa teknolojia kama unawiana na matakwa ya leseni na sheria. Kipengele hiki kidogo kinajumuisha shughuli zifuatazo: (a) mapitio ya kazi za MEM; (b) uimarishaji wa ukaguzi wa

11 migodi; (c) uimarishaji wa kitengo cha ukaguzi wa madini; (d) utoaji wa mafunzo kwa wafanyakazi wa MEM; na (e) uboreshaji wa zana na vifaa vya ofisi za kanda na za mikoa. B.3. Uboreshaji wa Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Kada ya Madini. Kipengele hiki kidogo hiki kitajenga uwezo juu ya mfumo wa usimamizi wa taarifa mpya za kada ya madini (MCIMS) ambao ulianzishwa kwa msaada wa Mfuko wa Maendeleo wa Norway. MCIMS ilijengwa kuzunguka takwimubezi ya Dar es Salaam ikiwa na mtandao mpana unaounganisha ofisi 20 za MEM za mikoa. Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 2007, MCIMS imeshindwa kutoa mafunzo ya kutosha kwa watawala na wachimbaji, imekosa vifaa vya kutosha katika ofisi zake za mikoa, ilikabiliwa na matatizo makubwa ya kiutendaji ulioathiri takwimu, na imeshindwa kushughulikia ipasavyo maombi ya leseni za wachimbaji wadogo. Hadi sasa, karibu maombi 10, 0000 ya leseni tangu mwaka 2007, bado hayajashughulikiwa. Kipengele hiki kidogo kinalenga kusaidia jitihada za MEM kuimarisha MCIMS kwa kuboresha vifaa vyake vya utendaji kazi, rasilimali watu, na kwa kuanzisha mbinu bora ya kuuendeleza mfumo wake. Kipengele hiki kidogo kitasaidia (a) kutathmini mahitaji ya kada ya madini, ikiwa ni pamoja na mikakati, vifaa na mafunzo; (b) maboresho ya mfumo; (c) mafunzo ya wafanyakazi juu ya utendaji kazi wa MCIMS; (d) kuboresha masjala kuu na masjala ndogondogo za ofisi za kanda na za mikoa; (e) uthibitisho wa migodi ya wachimbaji wadogo kama leseni zao zinavyoonyesha ili kuwezesha uingizwaji kamili wa sekta ndogo ya wachimbaji wadogo katika MCIMS; na (f) uimarishaji wa MCIMS na kuondoa vikwazo vilivyopo katika maombi ya leseni za uchimbaji. B.4. Usimamizi wa Mazingira na Jamii. Kwa kutambua unyeti wa shughuli za uchimbaji na athari za kimazingira zinazoambatana nazo, MEM imeanzisha kitengo kinachosimamia mazingira, yaani (EMU). Tangu kuanzishwa, EMU imekuwa ikishirikiana na NEMC kuhakikisha kwamba athari za kijamii na kimazingira za uchimbaji wa madini nchini zinapunguzwa. Lengo la kipengele hiki kidogo ni kusaidia jitihada za kushughulikia maswala ya kijamii na kimazingira ya migodi na kubainisha matokeo ya uchunguzi na mapendekezo yao na ya SESA yahusuyo shughuli za uchimbaji mdogo. Utafiti wa mwaka 2004 wa UNIDO pia umebainisha jinsi zebaki ilivyojichanganya na migodi ya wachimbaji wadogo na wa kati na hivyo kuibua tatizo kubwa la kiafya. Uchambuzi wa hali ya umaskini na athari za mazingira (PSIA) utafanyika pia ili kuisaidia serikali kufanya maamuzi sahihi ya kisera. Shughuli zinazowezeshwa na kipengele hiki kidogo zinajumuisha (a) kuimarisha EMU (mafunzo na zana) ili iweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo; (b) kufanya tathmini bora ya athari kwa mazingira na kwa jamii (SESA); (c) kufanya PSIA; (d) kuanzisha mtandao wa ombwe la taarifa za mazingira zihusuzo kada ya madini na mfumo wa jiolojia na madini (MIS); (e) kuandaa na kuboresha miongozo ya mazingira na ya kijamii na miiko ya kuzingatia (itakayoelemea kwenye matokeo ya SESA) juu ya masuala kama kufunga migodi, uchimbaji mdogo na athari ya zebaki, masuala ya jinsia, malalamiko ya jamii zizungukazo migodi na jinsi ya kuyatatua kwa kutumia mbinu zinazokubalika kimataifa; (f) mipango ya kuibua mwamko wa kimazingira na kijamii katika maeneo ya wachimbaji wadogo na wakubwa; (g) kuendeleza muundo wa kusimamia migodi iliyotelekezwa; na (h) kuimarisha uwezo wa kusimamia mazingira makao makuu MEM, katika RMO, ZMO, na LGRA kupitia mafunzo na msaada wa kiutendaji, na kwa kuboresha mazingira ya kazi. Kipengele C. Kuhamasisha Uwekezaji katika Sekta ya Madini C.1. Kuimarisha Miundombinu ya Kijiolojia. Kipengele hiki kidogo kinajengwa juu ya kazi iliyofanywa chini ya Mradi wa Maendeleo ya Sekta ya Madini uliodhaminiwa kwa pamoja baina ya Mfuko wa Maendeleo wa Norway na serikali ya Tanzania kati ya mwaka 2006 na 2007.

12 Kipengele hiki kidogo kitaisaidia GST (a) kukamilisha utafiti mkubwa wa jinsi mfumo wa hewa unavyoathirika na shughuli za kijiolojia na kuweka mazingira ya ufuatiliaji katika maeneo yaliyoteuliwa, ikiwa ni pamoja na wilaya za Chunya, Dodoma, Kiomboi, Kondoa, Manyoni, Babati, Handeni, Kilindi, Mvomero, Bahi, na Chamwino; (b) kupata na kuboresha taarifa za kijiolojia kutokana na uainishaji wa kijiolojia na tafiti za kijiofiziolojia na kijiokemia, na kuchapisha ramani na taarifa husika, na hasa kwa maeneo teule ya wilaya za Kiomboi, Mbulu, Hanang, Babati, Singida, Kondoa, Kiteto, Handeni, Kilindi, Manyoni, Dodoma, Kongwa, Mpwapwa, Iringa, Ludewa, Kilolo, Mufindi, Njombe, Bagamoyo, Mvomero, Kilosa, Mbarali, Kyela, Chunya, Bahi, Chamwino, Songea, Mbinga, na Namtumbo; (c) kukokotoa, kuweka katika takwimu, na kuboresha MIS iliyopo; (d) kutoa mafunzo kwa watumishi na kuboresha maabara kwa viwango vya kimataifa; (e) kuboresha na kutunza maktaba ya ramani za kijiolojia na makavazi ya miamba na vyanzo vya madini; na (f) kutengeneza takwimu na taarifa ya kijiosayansi (ikiwa ni pamoja na ramani za kimetologeniki) ili ziweze kupatikana kirahisi kwa wawekezaji na wadau muhimu na pia kwa mamlaka zinazohusika na mipango ya miundombinu. C.2. Majukumu ya Baadaye ya Shirika la Taifa Madini (STAMICO). Kipengele hiki kidogo kitagharimia utathmini wa STAMICO, kampuni ya migodi inayomilikiwa na serikali, kwa kuchunguza uwezo wake wa sasa na mipango ya kujiendesha yenyewe, kama sharti la shughuli zake za baadaye pamoja na sekta binafsi ili kutoa fursa kwa wachimbaji wakubwa na wadogo. C.3. Taarifa na uhamasishaji wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini. Kipengele hiki kidogo kinalenga kuhamasisha uimarishaji wa rasilimali ya madini, uendelezaji wa takwimu na mawasiliano. Itaweka mtandao baina ya GST na Mfumo wa takwimu wa masjala ya Hakimiliki za Madini na kusaidia juhudi za MEM katika (a) kuimarisha uchumi wa madini na kitengo cha biashara kinachojishughulisha, takwimu na uhamasishaji; (b) kukiwezesha kitengo cha taarifa, elimu na mawasiliano ili kuleta picha nzuri ya sekta ya madini katika jamii; (c) kuboresha kitengo cha usimamizi wa mfumo wa taarifa; (d) kuboresha upatikanaji wa takwimu, uandaaji na usambazaji wa takwimu za sekta hii na kuhamasisha vifaa; na (e) kuboresha mawasiliano katika sekta ya madini kwa kutekeleza mkakati wa mawasiliano na uhamasishaji, ikiwa ni pamoja na kutoa mbinu bora ya elimu kwa umma juu ya sekta ya madini taarifa (m.f., masuala yahusuyo mauaji ya maalbino). Kipengele D. Usimamizi na Ushirikishwaji wa Mradi Timu ya mradi itakayojumuisha watumishi wa MEM na ambayo pia itagharimiwa na MEM itahusika na utekelezaji wa mradi. Vilevile, kamati ya Uongozi ya Mradi (PSC) na Kamati ya Utendaji ya Mradi (PTC) zitaanzishwa. Wataalamu wa ziada wataajiriwa kwa muda ili kuisaidia na kuipa mafunzo timu ya mradi. Kipengele hiki kidogo kitagharimia uendeshaji wa mradi, ikiwa ni pamoja na (a) Uendeshaji wa mradi; (b) manunuzi; (c) udhibiti na tathmini; na (d) tafiti za nje za mradi ili kutathmini utendaji kazi wa jumla wa mradi, hususan utekelezaji wa malengo yake, mafanikio na matatizo, na hatua za kuchukua. Ugharimiaji Chanzo: Dola za kimarekani (kwa Mamilioni) Mkopaji 5.0 Shirika la Maendeleo la Kimataifa 50.0 Jumla 55.0

13 Mipangilio ya Utekelezaji Mpango wa ngazi tatu wa usimamizi na uratibu wa mradi ulipendekezwa. Katika utendaji kazi zake za kila siku, MEM imepewa shughuli za uratibu wa mradi, utoaji wa msaada wa kiutendaji na mafunzo, kazi za manunuzi na usimamizi wa fedha na uangalizi na utathmini wa maendeleo ya utekelezaji wa mradi. Kwa sababu hiyo, timu ya mradi imewekwa wizarani ili kufanya shughuli za kila siku za usimamizi wa mradi, ikiwa ni pamoja na kufanya manunuzi, utoaji wa fedha, usimamizi wa fedha, na uangalizi na utathmini wa mradi. Timu ya mradi inayoundwa na wafanyakazi wanaolipwa mshahara na wizara ambao watajitolea kwa dhati katika mradi na watawajibika kwa kamishna wa madini wizarani. Timu ya mradi itaongezewa nguvu na wataalamu wa ziada ambao wataajiriwa kwa muda maalumu na kwa shughuli maalumu zinazohusiana na utoaji wa mikopo midogo, uendelezaji wa rasilimali watu, uangalizi na utathmini wa mradi. Majukumu ya jumla ya kusimamia na kuratibu mipangilio ya kitaasisi na ya kiutendaji yatakuwa chini ya kamati ya uongozi ya mradi (PSC). PSC itaongozwa na Katibu Mkuu wa Kudumu wa MEM, na itajumuisha pia kamishna wa madini wa MEM; afisa mkuu wa utawala wa GST; Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa MEM; Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa MEM; Msarifu Mkuu wa MEM; Mkurugenzi wa Mazingira toka ofisi ya Makamu wa Rais; na Mkurugenzi wa Serikali za Mitaa toka Ofisi ya Waziri Mkuu. Malengo ya PSC ni kuhakiki uratibu na ushirikiano baina ya taasisi husika na washirika wa nje na kutoa mwongozo wa ngazi ya juu kwa MEM katika maamuzi muhimu yanayohusiana na (i) Mradi na shughuli nyingine katika sekta ya madini zinazogharimiwa na wahisani, pamoja na (ii) jinsi mageuzi katika sekta ya madini yanavyoweza kuchangia katika maendeleo ya uchumi wa nchi kwa mapana yake. Taasisi ya kati itakayokuwa na jukumu la kutoa ushauri wa kiutendaji itaanzishwa ili kuwa kama kiunganishi kati ya PSC na timu ya mradi. Kamati ya utendaji ya mradi (PTC) itaundwa na mratibu wa mradi; mratibu wa mradi toka GST; wakuu wa idara wa MEM zinazohusika na mazingira, huduma za kisheria, mahusiano ya umma, manunuzi, na teknolojia ya mawasiliano; na wakuu wa idara katika kitengo cha madini wanaohusika na wachimbaji wadogo, uhamasishaji, ukaguzi wa migodi, na hakimiliki za madini. PTC itawajibika katika usimamizi wa shughuli za mradi zinazohusiana na majukumu yao. Kuwezesha usimamizi na utekelezaji wa mradi, Mwongozo wa utendaji kazi wa mradi utajumuisha maelezo ya kina juu ya (a) mbinu za utendaji kazi na mahusiano ya ngazi hizi; (b) kiwango cha mamlaka iliyonayo kila ngazi; (c) mpangilio wake, majukumu yake, kazi; na (d) mahusiano baina ya ngazi hizi na baina yao na timu ya usimamizi ya mradi. Mwongozo wa utendaji kazi, ambao utapaswa kupitiwa kwanza na kuidhinishwa na Benki ya Dunia, utaandaliwa. Uendelevu Vigezo vya msingi vya uendelevu wa mradi unajumuisha udhati wa serikali katika kuendeleza utekelezaji agenda yake ya mageuzi katika sekta ya madini, na katika kushughulikia kero za wananchi juu ya kutokunufaika kwao kutokana na uwekezaji wa madini. Sekta ya madini inabakia kuwa kipaumbele kikubwa katika maendeleo na uboreshaji wa hali za kiuchumi na kijamii Tanzania. Kuboresha usimamizi wa sekta ya madini kutayafanya manufaa haya yawe dhahiri na kuifanya Tanzania kuendelea kuwa kivutio kikubwa cha wawekezaji wapya katika sekta ya madini. Katika kipindi kirefu, uwekezaji katika sekta ya madini unatarajiwa kutoa mapato endelevu ambayo yatatumika kuendeleza sekta hii (m.f., kada ya madini) kwa usimamizi bora wa sekta ya madini. Mafunzo kwa wakufunzi miongoni mwa ASM katika vituo vya maonyesho kutasaidia utoaji wa ushauri na mafunzo endelevu ya ASM.

14 Katika ngazi ya kitaifa, mradi utasaidia kuboresha uwezo wa serikali kusimamia ipasavyo sekta ya madini, kuhakikisha kwamba uwezo wa mapato ya Tanzania yatokanayo na madini (na hasa dhahabu) yanaenda hazina, na kusaidia katika ukuaji wa uchumi na kupandisha thamani ya madini Tanzania. Mradi unatarajiwa kuimarisha uwezo wa Tanzania kushughulikia athari za shughuli za uchimbaji wa madini katika mazingira na jamii kupitia muundo wa sera na mamlaka husika na kufanikisha uwezo wa kitaasisi na rasilimali watu katika utekelezaji wa sera na usimamizi huo. Katika ngazi ya jamii, mafanikio endelevu ya mradi yatashadidiwa mabadiliko chanya yaliyotokana na kuzishirikisha jamii za wachimbaji katika michakato muhimu ya kufanya maamuzi. Na hasa, wanatarajiwa kuona athari zake katika maendeleo ya uchumi wa nchi, na kuboreka kwa mahusiano ya kiuchumi na kijamii migodini. Kwa kusaidia juhudi za wachimbaji wadogo na wa kati katika kuboresha mbinu zao, mradi unatarajiwa kuboresha usimamizi wa rasilimali ya madini kwa maisha endelevu. Ni muhimu kuzingatia kwamba shughuli za uchimbaji kwa kawaida zinafanyika vijijini na katika maeneo ambayo umaskini una athari sana. Mambo ya Kujifunza Toka Katika Miradi ya Awali Kwa ujumla, fundisho kubwa lililopatikana katika miradi ya kimataifa na shughuli za ujengaji wa uwezo kwa usimamizi endelevu wa sekta ya madini katika maeneo mbalimbali ni pamoja na; (a) haja ya kuanzisha mradi utakaolenga mahsusi sekta hii na maboresho yatakayobainisha wazi idara na majukumu ya wizara na mashirika mbalimbali yanayohusika katika sekta hii; (b) ushirikishwaji wa walengwa katika maandalizi ya mradi, usimamizi, utekelezaji na uratibu; (c) vitengo endelevu vya mradi vilivyojengwa katika msingi wa ushirikiano; na (d) nia ya dhati katika kutekeleza malengo ya mradi. Katika ngazi ya sera, uzoefu wa utekelezaji wa mradi umeonyesha kwamba umiliki wa serikali ni muhimu kwa matokeo bora ya miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia. Benki ya Dunia imeendeleza mjadala hai na mamlaka za serikali kwa miaka kadhaa, ambao umeonyesha nia hiyo ya dhati katika umiliki wa miradi. Maandalizi ya mradi yalihusisha mawasiliano na Wizara ya Fedha na Uchumi. Mamlaka ya Mapato, na Serikali za Mitaa, ili kuhakikisha kwamba unaenda sambamba na malengo ya maendeleo ya serikali. Mradi umejengwa katika msingi uliowekwa na Mradi wa Msaada wa Kiutendaji katika Sekta ya Madini, uliokamilika kwa mafanikio mwaka Mafunzo yaliyopatikana katika mradi wa awali yamebainika katika uundaji wa utendaji kazi wake, ikiwa ni pamoja na (a) Nia ya dhati ya serikali katika mageuzi ya kitaasisi; (b) Mbinu shirikishi na zinazotekelezwa kwa awamu katika kuendeleza sekta ya madini; (c) ushirikishwaji wa wadau mbalimbali na kutaka ridhaa ya wadau wote katika malengo na matokeo ya uendelezaji wa sekta ya madini; (d) mikakati na mipango ya maendeleo ya mikoa, kwa kuzingatia hali ya shughuli za kiuchumi zinazotokana na uchimbaji wa madini ambayo kimsingi hayarudi tena ardhini; (e) uboreshaji na usimamizi wa taarifa na mfumo wa takwimu za sekta ya madini; (f) uhusianishaji wa karibu wa programu kwa ajili ya kujenga uwezo wa kitaasisi pamoja na shughuli maalumu za mradi zinazopaswa kutekelezwa na taasisi na mashirika yaliyo chini ya mradi huu; (g) mkabala unaozingatia gharama na mantiki katika usimamizi wa mradi katika hali ya ushirikiano baina ya serikali na Benki ya Dunia. Mradi unazingatia umuhimu wa kujiingiza katika mbinu shirikishi katika mageuzi ya kisekta kwa kuzihusisha shughuli zitakazochangia katika vipengele vikuu vya mikakati ya serikali, kama vile, huduma za ushauri kwa ASM, kuboresha mfumo wa usimamizi wa taarifa za kada ya madini, kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya madini, na kuimarisha mahusiano baina ya sekta ya madini na uchumi.

15 Mradi unajumuisha hatua thabiti ili kuwasaidia wachimbaji wadogo na wa kati wanaowajibika zinazoonyesha mbinu bora za kimataifa zilizopatikana katika ushirikishwaji wa Benki ya Dunia katika kusaidia sekretarieti za jamii na wachimbaji wadogo na wa kati (CASM). Uzoefu wa CASM umeonyesha masuala ya wachimbaji wadogo yanapaswa kushughulikiwa kwa njia sahihi zitakazojenga hali ya kuaminiana na wachimbaji wadogo na wa kati, na uboreshaji wa mazingira na jamii yataendana na urasimishaji na matokeo bora. Mafunzo yaliyopatikana toka katika mradi wa kimataifa wa UNEP wa programu ya shughuli za uteketezaji wa zebaki Tanzania yameingizwa katika mradi huu. Ushirikishwaji wa jamii na mashirika ya kijamii katika miradi ya sekta ya madini unaweza kuleta ufanisi katika maendeleo. SMMRP inajumuisha ushirikishwaji wa moja kwa moja wa jamii na mashirika ya kijamii katika kipengele cha maendeleo ya uchumi wa nchi kwa ushiriki katika mchakato wa mipango mikakati katika ngazi za chini. Shughuli za wachimbaji wadogo na wa kati zinaelekezwa katika migodi ya jamii nzima. Kipengele cha mazingira na jamii kinajumuisha ushirikishwaji wa mashirika ya kijamii katika PSIA na SESA pamoja na kushirikishwa katika kanuni, miongozo na programu za mwamko wa kimazingira na kijamii. Kipengele hiki kidogo cha taarifa na uhamasishaji katika sekta ya madini kinajumuisha ushirikishwaji wa mashirika ya kijamii na vyombo vya habari katika uhamasishaji. Aidha, Tanzania inatekeleza EITI, ikiwa ni pamoja na kuwa na uwakilishi wa mashirika ya kijamii katika kikosi kazi cha wadau wa EITI. Sera za Usimamizi (ikiwa ni pamoja na ushirikishwaji wa jamii) Mradi unatarajiwa kuwa na faida kwa jamii na mazingira kwa kuboresha usimamizi wa mazingira na jamii katika sekta ya madini, kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya kisasa na kuhimiza uwezo wa usimamizi wa mazingira na jamii katika Wizara ya Nishati na Madini (MEM). Kama msaada wa kiutendaji, shughuli nyingi hazina utekelezaji wa wazi na kujielekeza katika uboreshaji wa sera na udhibiti. Hata hivyo, shughuli dhahiri za mradi hususan za idara za maonyesho ambazo zitahamasisha matumizi endelevu ya teknolojia katika uchimbaji mdogo, ukarabati wa majengo ya vituo vya uchongaji wa mawe ya thamani, programu ya mikopo midogomidogo, utafiti wa jinsi shughuli za uchimbaji zinavyochafua jiofizikia ya hewa, na utafiti wa jiofizikia kwa ujumla unaweza kupunguza athari kwa mazingira na jamii (kama vile athari za kelele, vumbi, maji taka toka migodini, uchafuzi wa maji, na athari kwa afya na usalama wafanyakazi migodini). Uboreshaji wa muundo wa sera na udhibiti katika mradi huu unaweza kuongeza kiwango cha biashara ya madini, shughuli za ASM, na kupunguza athari kwa mazingira na jamii. Matokeo yake, mradi utasaidia OP 4.01 juu ya tathmini ya mazingira na OP 4.12 juu ya uhamishwaji wa hiari, na umewekwa katika kundi B la EA. Kuhakikisha kutimia kwa OP 4.01 maeneo halisi zitakapokuwepo shughuli za miradi zinazoshughulikia wachimbaji wadogo na wa kati yatabainishwa tu katika kipindi cha utekelezaji wa mradi ambapo muundo wa usimamizi wa mazingira na jamii (ESMF) uliandaliwa. ESMF unatoa mbinu za kuhakikisha athari za msingi kwa mazingira na jamii zinapunguzwa katika kipindi cha utekelezaji wa mradi na hatua mahsusi za kukabiliana nazo zinabainishwa. Katika upunguzaji huu, maeneo mahsusi ya kufanya tathmini ya mazingira au kuanzisha mipango ya usimamizi wa jamii yataanzishwa, hatua kwa hatua, kulingana na sera ya taifa ya mazingira ya 1997, tathmini ya athari za kimazingira na kanuni za ukaguzi 2005, na sera za mazingira na kijamii za Benki ya Dunia. ESMF inabainisha mbinu za kushughulikia migogoro inayoibuka. Uandaaji wa ESMF unajumuisha ushirikishwaji wa wadau katika ngazi ya chini na ya kitaifa, ikishirikisha mashirika/wizara za serikali, makampuni ya madini, sekta binafsi, wachimbaji wadogo na wa kati, mashirika yasiyo ya kiserikali, na jamii zinazoishi kuzunguka migodi. Ziara za migodini pia zilifanywa katika maeneo maalumu ya SMMRP yaliyokusudiwa. Kazi ya kupitia

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited

More information

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3

More information

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.

More information

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.

More information

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na. JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3

More information

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya

More information

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya

More information

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana

More information

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam

More information

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited

More information

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

More information

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi 3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TAARIFA YA MAFANIKIO CHINI YA UONGOZI WA MHE. SOSPETER MUHONGO (MB) KATIKA SEKTA NDOGO YA UMEME Disemba, 014 A. MAFANIKIO 1. Kuongezeka kwa uzalishaji

More information

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA

More information

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya

More information

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini

More information

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria; HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri

More information

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for

More information

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA

More information

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa

More information

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA

More information

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini

More information

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA

More information

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided

More information

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA

More information

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI

More information

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano. HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,

More information

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017

More information

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012

More information

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa

More information

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika, HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, MHESHIMIWA JOHN POMBE MAGUFULI, (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2007/08 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

More information

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI

More information

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu

More information

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi

More information

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MFUMO WA RUZUKU YA MAENDELEO YA MTAJI WA SERIKALI ZA MITAA (LDCDG) UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI Kijitabu cha Mshiriki

More information

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha

More information

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo

More information

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized!. viromen-alsc:a.. Environmental & Social MRADI WA UMEME WA GESI YA * Assessment & Management

More information

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump

More information

Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania

Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania Msingi wa Programu zote za Uimarishaji Ubora Toleo la 1 kwa Lugha ya Kiswahili

More information

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI

More information

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA BARA 2004 Imetayarishwa na: Idara ya Tiba Afya Makao Makuu P.O. Box 9083, DAR ES SALAAM June 2005 Yaliyomo Ukurasa Vifupisho

More information

DIRA DHIMA. Kuendeleza, kuwezesha, kudhibiti na kusimamia matumizi endelevu ya Rasilimali za Nishati na Madini kwa manufaa ya Watanzania.

DIRA DHIMA. Kuendeleza, kuwezesha, kudhibiti na kusimamia matumizi endelevu ya Rasilimali za Nishati na Madini kwa manufaa ya Watanzania. DIRA Kuwa Taasisi yenye ufanisi na inayojali tija ili kuhakikisha kuwa Rasilimali za Nishati na Madini zinachangia ipasavyo katika maendeleo ya nchi kijamii na kiuchumi. DHIMA Kuendeleza, kuwezesha, kudhibiti

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA

More information

ORDER NO BACKGROUND

ORDER NO BACKGROUND In the matter of an Application by the DAR ES SALAAM URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (DAWASA) For a Tariff Adjustment, Submitted on January 8 th, 2008 (TR-W-08-001) ORDER NO. 08-001 1.0 BACKGROUND

More information

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI MFUMO WA TATHMINI WA TAARIFA (IRM): TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI 2014 2016 Ngunga Greyson Tepani Mtafiti wa IRM Taarifa ya Mwishoni mwa Utekelezaji 2014-2016 First End-of-Term Report INDEPENDENT

More information

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...

More information

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/14 DODOMA Mei,

More information

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi PAN AFRICAN PARLIAMENT PARLEMENT PANAFRICAIN البرلمان PAN- PARLAMENTO األفريقي AFRICANO Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi Julai 21 22, 2011 Bunge la

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA MWAKA 2018/2019 YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 HALI

More information

TANGA CEMENT PLC ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA.

TANGA CEMENT PLC ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA. TANGA CEMENT PLC 2016 ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA www.simbacement.co.tz ANNUAL REPORT 2016 ANNUAL REPORT2016 TAARIFA YA MWAKA 2016 TAARIFA YA MWAKA 2016 02 ANNUAL REPORT 2016 Chairperson s Statement

More information

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1

More information

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition

More information

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania

More information

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu

More information

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa

More information

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA

More information

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa

More information

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery

More information

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)] This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)

More information

Govt increases vetting threshold of contracts

Govt increases vetting threshold of contracts > ISSN: 1821-6021 Vol IX - No. 19 May 10, Free with Daily News every Tuesday DID YOU KNOW? NEWS IN Numbers?

More information

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality

More information

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo: HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban

More information

Kutetea Haki za Binadamu

Kutetea Haki za Binadamu Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and

More information

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza

More information

Deputy Minister for Finance

Deputy Minister for Finance ISSN: 1821-6021 Vol XI - No - 34 DID YOU KNOW? A procuring entity is?s required to use suppliers pliers?pliers?pliers?pliers among those awarded ed?ed?ed?ed framework agreements by GPSA for procurement?ents

More information

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA, ENG. DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB.) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA, ENG. DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB.) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI MHESHIMIWA, ENG. DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB.) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO MIFUGO NA UVUVI KWA MWAKA 2017/2018 YALIYOMO

More information

Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI

Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI b Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI 1 Mwongozo wa Uzalishaji

More information

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA TWN Third World Network 1. WEMA ni nini? Mahindi yanayotumia maji kwa ufanisi yajulikanayo kwa kingereza kama Water Efficient Maize for Africa (WEMA) ni mpango

More information

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini

More information

MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK

MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK Kudumisha uhusiano kati ya jamii, ufugaji na wanyamapori MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK Kudumisha uhusiano kati ya jamii, ufugaji na wanyamapori MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI

More information

Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira

Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kiongozi hiki kimeandaliwa kikiwa ni sehemu ya mradi wa

More information

Muhtasari wa taarifa ya warsha ya wataalamu juu ya mfumo wa habari kwa njia ya ramani (PGIS), Morogoro, Juni 30 - Julai 1, 2014

Muhtasari wa taarifa ya warsha ya wataalamu juu ya mfumo wa habari kwa njia ya ramani (PGIS), Morogoro, Juni 30 - Julai 1, 2014 Muhtasari wa taarifa ya warsha ya wataalamu juu ya mfumo wa habari kwa njia ya ramani (PGIS), Morogoro, Juni 30 - Julai 1, 2014 Wandishi (Jina la kwanza kiherufi): Edmund Githoro, Simon Fraval, Joanne

More information

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY

More information

Mipango ya miradi katika udugu

Mipango ya miradi katika udugu Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi

More information

The Government is committed to improve marine transport and has a number

The Government is committed to improve marine transport and has a number ISSN: 1821-6021 Vol X - No - 52 Tuesday December 26, 2017 Free with Daily News every Tuesday Govt set to meet promises on DID YOU KNOW?? The law requires a procuring procurement of marine vessels entity

More information

UTANGULIZI. 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na

UTANGULIZI. 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA, MHESHIMIWA STEPHEN MASATO WASIRA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA KWA MWAKA 2008/2009 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA

HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA ANNA MARGARETH ABDALLAH, MBUNGE, KUHUSU MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2004/2005 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba sasa Bunge likubali

More information

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017 TAARIFA Agosti 2017 NGUO MPYA ZA UKOLONI Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika Jumuiya ya Jamii ya 2007: Wajumbe wanaadhamana Nairobi dhidi ya EPAs. SwissInfo Tangu mwaka

More information

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0

More information

ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO

ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO Mradi wa Kuondoa Madini ya Risasi Katika Rangi Barani Afrika 2015 ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO 2015 SHUKRANI Tunachukua

More information

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na

More information

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa

More information

4. Kanuni za Petroli (Ushiriki wa Watanzania) za mwaka 2017 zilianza kutumika rasmi tarehe 5 Novermba Shughuli za Petroli za kwanza ni

4. Kanuni za Petroli (Ushiriki wa Watanzania) za mwaka 2017 zilianza kutumika rasmi tarehe 5 Novermba Shughuli za Petroli za kwanza ni MWONGOZO WA JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA KUWEKWA KWENYE KANZIDATA YA WATANZANIA WENYE UWEZO WA KUUZA BIDHAA AU KUTOA HUDUMA (LSSP) KWENYE SHUGHULI ZA MAFUTA NA GESI ASILIA NCHINI Utangulizi 1. Mamlaka

More information

Kuwafikia waliotengwa

Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E 2 0 1 0 Ripoti

More information