KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

Size: px
Start display at page:

Download "KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA"

Transcription

1 KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

2 KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa vituo vya radio vya barani Afrika, maarifa, nyenzo na stadi za kuwashirikisha vijana kwenye uandaaji wa vipindi vya radio katika ngazi ya chini Lengo lake ni kuboresha stadi za utangazaji na uandaaji wa vipindi vya radio kwa vijana kushiriki kikamilifu na kuwapa mwongozo utakaochochea ubunifu ili waweze kufanya kazi yenye tija Mwongozo huu utawasaidia kuanzisha kipindi cha radio kinachoendana na vijana ambacho kinaweza kuboreshwa kuendana na uwezo wa kituo chako cha radio na mahitaji ya wasikilizaji wa jamii yako Inapaza sauti za vijana barani Afrika

3 Kuunganisha Vizazi Mwongozo kutoka Afrika Kwa Waandaaji wa Vipindi vya Redio Wanaofanyakazi na Watoto na Vijana

4 Imechapishwa mwaka 2013 na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni 7, place de Fontenoy, 75352, Paris 07 SP, UNESCO 2013 Haki zote zimehifadhiwa ISBN Nyadhifa zilizotumika na mambo yaliyowasilishwa kwenye chapisho hili hayahusiani kwa namna yoyote na msimamo wa UNESCOkuhusiana na hadhi ya kisheria ya nchi, jimbo, jiji au eneo lolote au mamlaka yake, au kuhusiana na ukomo wa mipaka yake. Maoni yaliyomo kwenye chapisho hili na yale ya wahariri wake, sio maoni ya UNESCO na hayahusiani na asasi hii Ukurasa wa mbele umesanifiwa na: CLD/UNESCO Kurasa za ndani zimesanifiwa na: Meghan Adams Mukobeko Usanifu kwa ajili ya kuchapisha umefanywa na: CLD/UNESCO Imechapishwa na UNESCO, Ufaransa

5 DIBAJI Watoto na vijana ni zaidi ya theluthi moja ya watu wote duniani na idadi yao inaweza kubwa zaidi miaka ijayo. Kwenye nchi zinazoendelea, vijana ni karibu asilimia 70 ya watu wote. Vijana ambao hawana ajira na elimu inakadiriwa kuwa asilimia 10 ya vijana ikijumuisha na wale walioacha shule. Radio inaendelea kutoa fursa kubwa za mawasiliano kwa vijana na watoto. Kwanini radio ambayo, ni maarufu zaidi, imesambaa na njia yenye kuwafikia watu wengi, mara nyingi imeshindwa kuwakilisha sauti za vijana? Labda watangazaji wanaongea kwenye vipaza sauti kwa niaba ya vijana kuliko kuwaacha wajiongelee wenyewe, au kwa sababu kundi hili halichukuliwi kama soko kitu ambacho kinapunguza uwezo wa radio kuonyesha utofauti. Mwongozo huu unatoa fursa kwa watangazaji wa radio ndani na nje ya Afrika kuanza kutumia mbinu jumuishi na shirikishi ili kujumuisha uwepo na uwakilishi wa vijana kwenye utangazaji. Afrika kusini mwa Sahara, radio inaweza kuingia kwenye maisha ya vijana kama mshauri, rafiki, mtoa taarifa, mwalimu na stadi, ikitoa fursa kwa vijana wa kike na kiume walio kwenye shinikizo kutokana na hali za kijamii na kiuchumi ambazo mara nyingi zinavuruga elimu yao. Kiwango cha juu cha kusoma na kuandika kwa watoto wenye miaka minane na tisa kwenye maeneo ya vijijini barani Afrika kimechangiwa na kufikiwa kwa kiasi kikubwa na radio za kijamii. Vijana wa kiume wenye umri wa kupata watoto ni sehemu muhimu ya hadhira ya vyombo vya habari kote Afrika Kusini mwa Sahara. Ili kipindi chao cha mpito kutoka utotoni kuelekea ukubwani kiwe cha mafanikio, inategemea uwezo wao kutawala shughuli zao za kujiingizia kipato kwa kutumia kiwango kidogo cha maarifa walichonacho. Uwezo wao kushirikiana na wengine uvumilivu, maarifa na uzoefu wao kupitia radio inaweza kuwa na mchango mkubwa kwa maendeleo wa jamii husika na kwa usalama wa vizazi vijavyo. Juhudi za jumuiya ya kimataifa yamepelekea kuanzishwa kwa vyombo vya kimataifa vya kuwasaidia watoto na utangazaji. Mkataba wa Afrika kuhusu Utangazaji unaowahusu watoto ni moja ya juhudi za kupongezwa ambazo zinastahili kupewa kipaumbele na watangazaji katika ngazi ya kitaifa na chini kabisa kote barani Afrika. Mikataba mingine ni Changamoto za Oslo (Oslo Challenge) na Ilani ya Dunia kuhusu Utangazaji (World Manifesto on Radio), ambayo ina hoja za nguvu kuhusu mipango jumuishi. Siku hizi, teknolojia inatoa fursa zaidi kwa vijana kutoa maoni yao kuhusu masuala ya kijamii, ambayo yataathiri maisha yao kama watu wazima. Uwezo wao wa kurekodi na kutengeneza vipindi vyenye maudhui ya eneo husika ambavyo vinashughulikia mahitaji ya wenzao, umekuwa juu sana kuliko mwanzo. Runinga imebadilika kutoka rangi nyeupe na nyeusi na katuni hadi vipindi vya elimu vya watoto na vijana ambavyo ni 3D na vyenye mwingiliano, radio pia inaweza kuwa na vipindi vya muziki vinavyojirudia rudia kuendana na ratiba za vijana na kuongezeka kwa vipindi shirikishi vya radio vilivyoandaliwa kwa ajili ya vijana na vile vilivyoandaliwa na vijana wenyewe. Ukiwa umefadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (Sida), mwongozo huu ni marejeo ya msingi kwa waandaaji wa vipindi vya radio ambao wanapenda kufanya kazi na watoto na vijana katika namna ambayo ina heshima, inayoweza kusimamiwa na yenye tija. Umeandaliwa kwa ushirikiano na Children s Radio Foundation (CFR) ili kuongeza kiwango cha ushiriki wa vijana hususani wa kike, kwenye uandaaji wa vipindi vya radio kwenye vituo vya radio 32 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Kenya, Lesotho, Namibia, Afrika Kusina, Tanzania na Zambia. Watangazaji wa radio popote walipo wanatakiwa kubadilisha desturi za vituo vya ili kutumia fursa ya mwongozo huu kwa kuanzisha vipindi vya radio vya vijana, kuongeza maudhui tofauti na yenye ubora kwa vijana na kuyajumuisha kwenye utangazaji wa radio wa kisasa. Janis Karklins UNESCO Mkurugenzi Mkuu Msaidizi Idara ya Mawasiliano na Habari

6 YALIYOMO SEHEMU YA KWANZA: JINSI YA KUANZA UTANGULIZI KWANINI RADIO YA VIJANA? JINSI YA KUTUMIA MWONGOZO HUU SEHEMU YA PILI KANUNI ZA MSINGI SURA YA 1: KUWASHIRIKISHA VIJANA SURA YA 2: KUFANYA KAZI NA VIJANA KUWA MSHAURI SURA YA 3: MAADILI NA IDHINI SEHEMU YA TATU KUJUA KIWANGO CHA UWEZO NA KUPANGA NGAZI YA 1: RADIO KWA AJILI YA VIJANA NGAZI YA 2: RADIO PAMOJA NA VIJANA NGAZI YA 3: RADIO YA VIJANA NGAZI YA 4: KUWAFIKIA VIJANA SEHEMU YA NNE MAREJEO MUHIMU NA VIAMBATISHO 46 5

7 SEHEMU YA KWANZA JINSI YA KUANZA UTANGULIZI KWANINI RADIO YA VIJANA? JINSI YA KUTUMIA MUONGOZO HUU 6

8 Sehemu ya kwanza Jinsi ya kuanza Utangulizi UTANGULIZI Kupitia mafunzo ya utangazaji, nimejifunza kuwa mtangazaji mzuri, jinsi ya kuwauliza watu maswali ambayo yananipatia majibu mazuri na pia kutafuta habari nzuri ambazo zinaongeza ufahamu wangu kuhusu mambo mbalimbali. Nafikiri kipindi chetu cha radio kitabadilisha hali ya mambo; kipindi kitaigusa jamii, kitapanua fikrazao kuhusu mambo mbalimbali, kitawapa matumaini na kuwabadilisha kuwa na hali bora na hatimaye kuibadilisha Tanzania nzima Fadhili (16), mwandishi wa habari kijana, Radio Pambazuko, Ifakara, Tanzania Kwa zaidi ya miaka miwili, Radio Pambazuko imekuwa ikishirikiana na kikundi cha vijana 15 kama Fadhili kipindi cha radio cha vijana kinachotoka kila wiki. Kipindi hicho kinachorushwa moja kwa moja kinahusu haki za watoto na kujadili masuala kama ajira, udhalilishaji na elimu ya watoto. Hata hivyo, kinahusisha pia masuala ya kawaida kama muziki na michezo, na kinasimulia hadithi za kutia moyo za watu waliofanikiwa. Kipindi kinatoa nafasi ambapo vijana kutoka eneo husika kutoamaoni yao na kuzungumza kwa uhuru masuala ambayo ni muhimu kwao. Kinaifanya jamii kuzungumza na kufikiri na kuwaweka vijana katika nafasi ya kushawishi ufanyaji wa maamuzi ambayo yanawaathiri Kwa bahati mbaya Radio Pambazuko inabaki kuwa ya kipekee kwa radio zinazorusha matangazo yake barani Afrika. Radio ina uwezo wa kuboresha kwa kiwango kikubwa hali za maisha ya vijana, lakini katika sehemu nyingi, haitumiwi kikamilifu. Radio inawafikia zaidi ya asilimia 95 ya watu wote duniani na vituo kadhaa vya radio barani Afrika kila kimoja kina zaidi ya wasikilizaji milioni moja. Afrika kusini mwa Sahara, idadi ya vituo vya radio za kijamii imeongezeka maradufu katika miaka ya karibuni. Kwa mfano Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ina zaidi ya vituo 250 vya radio za kijamii mwaka 2006 kulinganisha na 10 tu mwaka Moja ya faida ya radio za jamii ni kwamba zinawafikia watu wa aina tofauti na kuelezea mambo mbalimbali ya maisha yao. Iwekuwatangazia jamii za wafugaji wanaohamahama maeneo ya vijijini nchini Kenya, wachimbaji wa shaba nchini Zambia, wafanyabiashara wa sokoni nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo au wanafunzi wa sekondari ya sekond ari ya juu nchini Afrika Kusini, radio ya jamii mara nyingi inaoengea lugha inayodharauliwa na vyombo vikubwa vya habari na inawapatia habarimuhimu hadhira ambayo ni ngumu kuifikia. Watoto na vijana ni sehemu kubwa ya hadhira hii. Lakini sauti za vijana hazisikiki mara kwa mara na hazitambuliki ingawa karibu nchi zote duniani zimeridhia Azimio la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu na Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Mtoto (UNCRC) na sheria nyingine zinazohimiza ushiriki wa watoto. Hata hivyo, kama wafanyakazi kwenye vyombo vya habari, ni wajibu wenu kuhakikisha watoto na vijana wanaonekana, wanatumia na kutengeneza vipindi vya radio vya vijana wakati ushiriki kwenye miradi yenu ukizingatia sheria za kimataifa na kitaifa zinazohusiana na watoto 7

9 Sehemu ya kwanza Jinsi ya kuanza Utangulizi MKATABA WA UMOJA WA MATAIFA WA HAKI ZA MTOTO UNCRC inatoa mwongozo wa kile serikali na watu binafsi wanapaswa kufanya ili kuhimiza na kulinda haki za msingi za watoto wote Ibara ya 1 inaelezea maana ya neno mtoto kuwa ni mtu aliye chini ya miaka 18 Ulipitishwa kwa kauli moja na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 1989, toka hapo umeridhiwa na serikali zote duniani isipokuwa Somalia na Marekani. Zinaporidhia Mkataba serikali zinajifunga kuhakikisha watoto wanakuwa katika mazingira mazuri na salama, huku wakipata elimu bora na huduma bora za afya na hali nzuri za maisha Ibara za mkataba ambavyo ni mahususi kuhusiana na ushiriki wa watoto na vijana ni kama ifuatavyo: IBARA YA 2: BILA UBAGUZI Mkataba huu unawahusu watoto wote, bila kujali rangi, dini au uwezo, wanachofikiri au kusema, aina ya familia wanayotoka. Haijalishi watoto wanaishi wapi, wanaongea lugha gani, wazazi wao wanafanya kazi gani, kama ni wavulana au wasichana, ni wa utamaduni gani, kama wana ulemavu au kama ni matajiri au maskini. Kusiwe na mtoto anayetendewa vibaya kwa sababu yoyote ile. IBARA YA 12 IBARA YA 13 MAONI YA MTOTO Mtoto ana haki ya kuelezea maoni yake na yafanyiwe kazi kwa kuzingatia masuala au mchakato unaomuathiri mtoto UHURU WA KUJIELEZA Watoto wana uhuru wa kupata na kutengeneza habari zao wenyewe na kutoa maoni yao, bila kuathiri haki za wengine IBARA YA 14 UHURU WA KUFIKIRI, DHAMIRi NA KUABUDU Mtoto ana haki ya kufikiri, kujitambua na kuabudu, kutokana na mwongozo sahihi wa wazazi na sheria za nchi IBARA YA 15 UHURU WA KUJIUNGA NA CHAMA Mtoto ana haki ya kukutana na watu wengine na kujiunga au kuunda vyama, bila kuathiri haki za wengine IBARA YA 16 KINGA YA MAISHA BINAFSI Watoto wana haki ya kulindwa dhidi ya kuingiliwa katika miasha yao binafsi, ya kifamilia, nyumbani na mawasiliano na dhidi ya kauli / vitendo vinavyoshusha hadhi IBARA YA 17 KUPATA TAARIFA SAHIHI Vyombo vya habari vina wajibu wa kusambaza habari kwa watoto ambazo ni za kijamii, kimaadili, zenye kuelimisha na zenye manufaaya kiutamaduni kwao na ambazo zinaheshimu utamaduni wao. Serikali ihimize machapisho/habari zenye manufaa kwa watoto na kuwalinda dhidi ya machapisho/habari zenye athari kwao. UNCRC inatoa viwango ambavyo kwavyo juhudi za kila nchi kuboresha hali za watoto zinaweza kupimwa. Kila baada ya miakamitano serikali zinatakiwa kutoa taarifa ya maendeleo yaliyofikiwa kwa Kamati ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Mtoto Kamati hukutana na wawakilishi wa serikali na kusikiliza maoni ya asasi zisizo za kiserikali (NGOs) kabla ya kutoa mapendekezo yake kuhusu hatua ambazo kila nchi inabidi kuchukua ili kutimiza wajibu wake. Hata hivyo katika sehemu nyingi za dunia haki ya watoto na vijana kushiriki (Kifungu cha 17 cha UNCRC) haiheshimiwi au inakiukwa. Mara nyingi hii inatokana na kutoelewa nini cha kufanya ili kuwashirikisha vijana kwenye vituo vya radio vya kijamii na jinsi radio inavyoweza kutumika kuchochea mazungumzo, ushiriki na kuwa raia bora (Muhtasari wa CRC uliotolewa kama kiambatisho 1) 8

10 Sehemu ya kwanza Jinsi ya kuanza Kwanini Radio ya Vijana? KWANINI RADIO YA VIJANA? Radio ya vijana inaweza kuwa katika miundo mbalimbali. Hakuna mkakati ulio sahihi au usio sahihi kwa kuwa yote ina uhusiano wa moja kwa moja na idadi ya wafanyakazi na rasilimali zilizopo na mali na matatizo ya vituo vya radio. Kwa hakika, miongoni mwa vituo vya radio vinavyofanya kazi barani Afrika, vina rasilimali chache na msaada mdogo wa kitaasisi. Matokeo yake kiwango cha ushiriki wa vijana kinatofautiana sana. Wakati mwingine vijana wanahojiwa kwenye vipindi maalum kwa watu wazima, na ushahidi mwingine wa vijana unajumuishwa kwenye vipindi vya watu wazima na mara chache vijana wanaandaa na kuongoza vipindi wao wenyewe. Hata hivyo, vituo kadhaa vya radio za kijamii vina vipindi vinavyochochea maendeleo ya watoto wadogo. Mara nyingi vina mtangazaji mtu mzima anayewafundisha wasikilizaji watoto nyimbo, anayesoma hadithi za watoto au kujenga stadi za lugha. Wakati mwingine kikundi cha watoto kinaalikwa studio ili kushiriki kwenye kipindi. Wakati vipindi hivi vinakidhi mahitaji ya jamii yao, tatizo ni kwamba muda si mrefu watoto wanaviona vimepitwa na wakati, na kama vijana, wanalazimika kusikiliza vipindi vya watu wazima. Matokeo yake, kuna haja ya kuziba pengo hilo, kuwasikiliza na kuwapa sauti vijana walio kati ya miaka 10 na 18. Hiki ni kipindi muhimu sana kwa maisha ya kijana ambapo mabadiliko mengi hutokea, maamuzi hufanywa na malengo ya maisha ya kiutu uzima huwekwa. Vijana ni zaidi ya nusu ya watu wote barani Afrika, na kitu cha muhimu ni kwamba fursa yao kama washirika na hadhira muhimu inaendelezwa na haidharauliwi. Majadiliani kwenye jamii na kujenga uwezo ni mamba ya muda mrefu ya kuzingatia kwenye vipindi vya vijana, ambavyo vinaweza kuongeza usikivu wa vituo vya radio. MAJADILIANO KWENYE JAMII Majadiliano ni hali ya kubadilishana kati ya pande mbili yaani kituo cha radio na jamii. Inahusisha kushirikishana taarifa, kutoa fursa sahihi ya kusikiliza maoni ya hadhira na kuyafanyia kazi. Mchakato huu unawaleta pamoja vijana ili kujadili masuala mbalimbali ambayo wanayapenda na ni muhimu kwao, kuanzia burudani hadi vipindi vinavyozungumzia mambo ya msingi, maigizo, ucheshi, midahalo na vipindi vya maswali na majibu. Zingatia tofauti za mahitaji kati ya wavulana na wasichana-fanyia kazi mahitaji yao kwa namna tofauti kama ni lazima. Vipindi vya radio vilivyoandaliwa vizuri vimeweza kujadili mambo ya msingi kama shinikizo la kundi rika au uonevu shuleni. Ngazi hiyo ya ushirikishaji inaviweka vituo vya radio katika nafasi muhimu kwenye masuala ya kijamii. Kwenye vipindi, watangazaji vijana wanazungumzia masuala wanayoyapa kipaumbele, wasikilizaji wanapenda vipindi vya vijana na wanapenda kusikiliza zaidi, hivyo tumeongeza muda ili kuwapa wasikilizaji kile wanachotaka. Wanapenda pia kusikia watoto wakielezea uzoefu wao John Liveti, mtangazaji, Radio Tumaini, Dar es Salaam, Tanzania Kila Jumamosi wote tunakusanyika kuizunguka radio ili kusikiliza kipindi, wote, kama jamii. Watu wanashangaa kwamba tupo radioni na tunaweza kufanya wenyewe kama watoto Mwajuma (14), mwandishi wa habari kijana, Radio Tumaini, Dar es Salaam, Tanzania KUJENGA UWEZO Kujenga uwezo mara nyingi kunachukuliwa kwa maana sawa na mafunzo. Ingawa, neno hilo lina maana pana zaidi na ni muhimu kwa maendeleo endevu ya kituo cha radio na ushirikiano wake na vijana. Kutoa stadi za msingi za uandaaji wa vipindi, ushauri, nafasi, vifaa na ukarabati ni baadhi ya mambo muhimu Kwa kuwekeza kwa vijana, ninapanda mbegu kwenye bustani yangu Paul Obakeng Mahlate, Meneja wa kituo, Aganang FM, Potchefstroom, Afrika Kusini 9

11 Sehemu ya kwanza Jinsi ya kuanza Jinsi ya kutumia mwongozo huu KWANINI RADIO YA VIJANA? Kujifunza kutafiti, kufanya mahojiano na kutangaza vinaongeza hali ya kujiamini kwa vijana na kunajenga stadi za mawasiliano nakufikiri kwa kina. Uzoefu wa kutangaza radioni hugeuka kuwa stadi muhimu inayotumika katika nyanja mbalimbali za maisha, kutoka darasani hadi kazini kwa siku za baadaye. Kipindi cha radio kimenisaidia kujenga hali ya kujiamini kwa kiwango kikubwa, hususani shuleni. Siku za nyuma, kama aliongea na kufafanua jambo darasani na sikuweza kuelewa, tungenyamaza kimya bila kusema kitu, lakini sasa kwa kuwa sehemu ya kipindi hiki cha radio, siogopi kuuliza maswali hadi nielewe. Cecilia (10), mwandishi wa habari kijana, Radio Sauti, Moshi, Tanzania 10

12 Sehemu ya kwanza Jinsi ya kuanza Jinsi ya kutumia mwongozo huu JINSI YA KUTUMIA MWONGOZO HUU JE, UNGEPENDA Kufanya sauti i za vijana zisikike zaid? Kuwashirikisha vijana kwenye kipindi chako? Kupata vidokezo na ushauri jinsi ya kufanya kazi na vijana? BASI MWONGOZO HUU WA VIJANA NA RADIO UPO KWA AJILI YAKO. Umeandaliwa kuwasaidia waandaaji na mameneja wa vipindi wanaofanya kazi na vijana na kuhimiza mbinu zinazowalenga vijana zinazotokana na mafunzo kutoka kwa wafanyakazi wa radio za jamii wenye uzoefu na vijana barani Afrika. Inahimiza mbinu zinazotumia teknolojia ya chini na bila uhariri kwa kutumia mada ambazo zinaonyesha vipindi ambavyo tayari vimerekodiwa tayari kwa kurushwa radioni Lengo la msingi ni kuvisaidia vituo vya radio kuanzisha na kuendeleza ushiriki wa vijana pamoja na kuwapa taarifa na kuimarisha vipindi kwa ujumla. Kanuni, motisha na baadhi ya vifaa vya msingi vya kurekodia ni muhimu. Maudhui ya mwongozo huu yanawasilishwa kielektroniki ambapo unaweza kuyapata na kuyatumia kwenye mtandao au kuyapakua kwa muda wa PDF. Unapotumia nakala ya kwenye mtandao, bonyeza kwenye viunganishi sahihi ili kupata marejeo zaidi na makala za kusikiliza. Sehemu mbili za kwanza za mwongozo zinakuwezesha kujua mahitaji ya msingi ambayo unapaswa uyatimize na uyatilie mkazo kwenye shughuli zako za radio ili kuwashirikisha vijana kikamilifu. Miongozo maalum inayofuata hatua kwa hatua yenye lengo la kuonyesha mbinu sahihi kwa ajili ya kufanya kazi na vijana na kuweka viwango ambavyo vinaweza kutumika kukidhi mahitaji yako, inatolewa katika Sehemu ya 3. Orodha ya marejeo muhimu na ya ziada yanapatikana Sehemu ya 4. Vidokezo na mifano kwenye mwongozo huu itakusaidia kufanya kazi na vijana wanaotaka kutengeneza vipindi vya radio ambavyo vyenye utajiri wa maudhui, ujuzi na endelevu ambavyo vinaonyesha hali halisi ya jamii yao. Ongeza idadi ya masikio yanayosikiliza na sauti zinazoongea! Ni jambo lenye faida kubwa kutumia muda kwa ajili ya vijana na radio, lakini usidharau moyo wa kijitolea. Ni vizuri kama kazi yako inajadiliwa na inaungwa mkono na mkuu wako na hivyo kupewa majukumu yanayotambulika ili kuyafanyia kazi kikamilifu. Zingatia: Wasiliana na mamlaka za eneo lako ili kuhakikisha kwamba fomu ya idhini ya mfano iliyowekwa kwenye mwongozo huu (Kiambatisho 4) inakidhi mahitaji ya kisheria ya nchi yako. 11

13 Sehemu ya kwanza Jinsi ya kuanza Jinsi ya kutumia mwongozo huu 1. NGAZI YA USHIRIKISHAJI Mwongozo huu umepangwa katika ngazi nne za ushirikishaji wa vijana kulingana na Ngazi ya ushiriki ya Roger Hart, mwongozo umeandaliwa na kutumika kupima ushiriki wa watoto. Ngazi hizi zinafafanuliwa vizuri kwenye Sehemu ya 3 ya mwongozo huu na zimeorodheshwa kwa muhtasari hapa chini. Zinaweza kutumika kuonyesha uwezo wa kituo cha radio kuwashirikisha vijana kwenye vipindi, kupanga kikamilifu na kusimamia kazi stahiki. Stadi muhimu, shughuli zenye uhusiano na mfano wa vipindi vya radio vinavyoonyeshwa katika kila ngazi vinaendelea kwa kufuatana, hivyo inabidi ujue kuwa, kama unaamua watoto waendeshe mdahalo wa moja kwa moja radioni kama inavyoelezewa kwenye Ngazi ya 3, radio yako lazima iwe tayari ina stadi za msingi zinazoelezewa katika Ngazi ya 1. KIWANGO CHA USHIRIKISHAJI NGAZI YA 1: RADIO KWA AJILI YA VIJANA Katika ngazi hii ya mwanzo wafanyakazi wa radio wanaandaa vipindi vinavyohusu mada za vijana. Vijana wanashirikishwa katika maandalizi ya mwanzo na baada ya kutangazwa kwa kipindi. Usimamizi /ushauri: Hauhitajiki NGAZI YA 2: RADIO PAMOJA NA VIJANA Wafanyakazi wa radio bado wanaandaa vipindi lakini sasa wanajumuisha mawazo ya vijana. Wanashirikishwa zaidi kwenye maandalizi na baada ya kutangazwa kwa kipindi na wanaombwa watoe maoni yao au kuwahoji vijana wengine na watu wazima ili kupata maoni yao. Halafu rekodi hizi zinajumuishwa kwenye vipindi vya watu wazima. Usimamizi /ushauri: Ni muhimu NGAZI YA 3: RADIO YA VIJANA Kikundi kinaandaa vipindi ambavyo vitawasaidia wafanyakazi wa kituo cha radio. Wanahusika kwenye maandalizi na utangazaji Usimamizi / ushauri: Ni muhimu (lakini unaweza kupungua kadri kikundi kinavyoweza kujitegemea) NGAZI YA 4: KUWAFIKIA VIJANA ZAIDI Vijana kwa msaada wa wafanyakazi wa radio, waandae matukio ya kijamii kuhusiana na vipindi vyao na kukutana na vyombo vingine vya habari ili kupata uzoefu wa kazi zao. Hii itakipa kituo cha radio na kipindi chake cha vijana matokeo makubwa na kuongeza usikivu wake na kuongeza ufahamu wao wa mambo yanayowagusa vijana. Usimamizi / ushauri: Ni muhimu (lakini unaweza kupungua zaidi kadri kikundi kinavyoweza kujitegemea) 12

14 Sehemu ya kwanza Jinsi ya kuanza Jinsi ya kutumia mwongozo huu 2. HATUA ZA UTENGENEZAJI WA KIPINDI Hatua za utengenezaji wa kipindi zimeandaliwa ili kukusaidia kuona na kutambua hatua mbalimbali za utengenezaji ili kuamua wapi na jinsi ya kuwashirikisha vijana na kwa kiasi gani. Zitumie ili kujua kiwango cha ushirikishaji wa vijana ambacho kizuri kwa ajili yako. MAADALIZI YA AWALI UTENGENEZAJI UTANGAZAJI MREJESHO 3. KUELEWA ALAMA MALENGO VIDOKEZO Introduction to help you understand why this is important. Stadi/sanduku la vidokezo SAUTI MAZOEZI YA KUJIFUNZIA Quote from youth and mentors that relates to this section / chapter. Mada za vitendo REJEA MAREJEO Ngazi, inarejesha sura iliyotangulia marejeo / viunganishi / mifano ya makala za kusikiliza MIFANO Mifano ya hali halisi ili kukusaidia kuelewa 13

15 SEHEMU YA PILI KANUNI ZA MSINGI SURA YA 1: KUWASHIRIKISHA VIJANA SURA YA 2: KUFANYA KAZI NA VIJANA KUWA MSHAURI SURA YA 3: MAADILI NA IDHINI 14

16 Sehemu ya Pili Kanuni za Msingi Sura ya 1 Kuwashirikisha vijana SURA YA 1: KUWASHIRIKISHA VIJANA Kuna namnna nyingi za kuwashirikisha vijana katika radio yako. Katika hatua ya mwanzo kabisa unaweza kuliita jopo la vijana kutoa mrejesho wa wiki kuhusu kipindi cha vijana na kuonyesha mitazamo ya vijana kwenye vipindi vya mazungumzo au unaweza kwenda mbali zaidi na kukialika kikundi cha vijana waandae kipindi chao wenyewe. Inabidi ujue kiwango cha ushirikishaji wa vijana ambacho ni stahiki na endelevu kwa ajili ya kituo chako cha radio ya kijamii. NGAZI YA USHIRIKISHAJI WA VIJANA Bila kijali kiwango cha ushirikishaji, tunashauri kuwe na ushirikishaji wa mara kwa mara na wa kina ambao utawasaidia vijana kujifunza na kuchochea mchakato wa uandaaji wa kipindi. Dhamira ya dhati itakuwa ni mchango mkubwa kutoka kwa vijana. Katika ngazi ya Hart ya ushirikishaji wa vijana, ngazi tatu za kwanza udhibiti, mapambo na kuigiza kama kuna usawa zinajulikana kama ngazi zisizo shirikishi ambapo vijana wanatumiwa na watu wazima kwa malengo yao. Ili kuepuka hili, inabadi ushauriane na vijana katika kikundi chako katika kila ngazi ya mchakato na kuhakikisha kwamba wanaelewa vizuri jinsi michango yao itavyotumika. Ni wajibu wako kuwa mwangalifu ili kikundi kisijiingize au kuwaingiza wengine katika hatari kutokana na maudhui wanayorekodi na kutangaza. SURA YA 3: MAADILI NA IDHINI Hii ni pamoja na kuhakikisha kwamba wao na vipindi vyao havitumiki kwa malengo ya kisiasa na kiuchumi, kwa mfano kuunga mkono kampeni za kisiasa au kutangaza bidhaa. Hakikisha kwamba malengo na madhumuni yako yanafafanuliwa vizuri kwa uongozi wa kituo chako cha radio, vijana na wazazi na walezi wao kabla kuanza mradi. Kuunga mkono kwao ni jambo muhimu kwa mafanikio ya mradi. Ni wajibu wako kisheria na kimaadili kuhakikisha kwamba haki za vijana zinalindwa na hazikiukwi. Usichukulie hili kama jambo gumu bali lenye faida kwa kila mmoja. Zingatia kwamba vijana hawachukuliwi kwa ajili ya kufanya kazi bali kushiriki kwenye kipindi cha radio, hii itachangia kuonyesha uhalisia wake na kutumia fursa za maendeleo binafsi. Shirika la Kazi Duniani (ILO) linaelezea maana ya ajira za watoto kama: Kazi yoyote ambayo kiakili, kimwili, kijamii au kimaadili ni hatari na mbaya kwa watoto na inavuruga masomo yao au kuwazuia wasiende shule Child Labor: A textbook for university students, International Labor Organization, 2004 Lakini ILO inaunga mkono shughuli ambapo watoto au vijana wanashiriki kwenye shughuli zinazochochea ukuaji, za kujitolea au kazi ambazo haziaathiri afya zao na ukuaji wao au kuvuruga masomo yao na hii inafafanuliwa kupitia: mpango wa mwongozo ulioandaliwa ili kurahisisha uchaguzi wa kazi au aina ya mafunzo ambayo yanachukuliwa kama chanya (Article 6 (C), ILO Minimum Age Convention, 1973, (N 138)) Inabidi uhakikishe kwamba vijana wanashirikishwa kama wachangiaji wa mara kwa mara, wanakuja kutoa maoni yao na kujenga uwezo wao. Hakikisha kwamba hili linafahamika kwa utawala wa kituo chako cha radio, vijana washiriki na wazazi au walezi wao. Masaa matano kwa wiki ni kiwango cha juu ambacho vijana wanaruhusiwa kufanya kazi katika kituo cha radio ili kuandaa kipindi chao cha radio cha kila wiki. Hii inajumuisha: Kipindi cha masaa mawili cha mkutano wa maandalizi ili kuchanganua mada Kipindi cha masaa mawili ambapo waandishi vijana wanaingia mitaani ili kurekodi makala zao Saa moja kwa ajili ya kutangaza kipindi moja kwa moja radioni 15

17 Sehemu ya Pili Kanuni za Msingi Sura ya 1 Kuwashirikisha vijana Kuna njia nyingi za kufanya mradi uweze kusimamiwa na vijana. Kwa mfani unaweza kuunda vikundi viwili ambavyo vinaweza kubadilishana kila wiki, ambapo kila kikundi kiwe kinakuja kwenye kituo cha radio kila wiki ya pili. Kwa vijana kutoa mrejesho kuhusu kipindi au kuchangia mara kwa mara kama wahojiwa, muda unaotumiwa kwa wiki kwenye kituo cha radio usizidi masaa matano KUCHAGUA WASHIRIKI Kuwa na washiriki sahihi ni jambo la muhimu kwa mafanikio ya kipindi chochote cha vijana, hususani wanaposhirikishwa katika namna ambayo ni endelevu. Iwe unachagua kikundi wewe mwenyewe au kwa msaada asasi mshirika, hakikisha kuwa huharakishi mchakato wa uchaguzi. Kikundi ambacho hatimaye utakichagua kitakuwa msingi wa kipndi chako cha radio cha vijana. Kutokuchukua muda wa kutosha na tahadhari kumechangia kuanguka kwa miradi mingi ya radio za vijana. Usisahau kuweka usawa kwenye idadi ya washiriki wa kike na kiume. Pia jiandae kwa kuwa sio washiriki wote watashiriki kwa usawa au wataendelea, heshimu sababu zao. 1. KUTAFUTA WASHIRIKA SAHIHI Kama unaamua kufanya kazi kwa ushirikiano na asasi nyingine, ni muhimu kwa asasi hiyo kuelewa vizuri na kuunga mkono mradi wako na malengo yake. Unaweza kushirikiana na shule ya sekondari iliyo karibu na kituo chako cha radio. Omba kufanya mkutano na mkuu au mwalimu maarufu wa shule na elezea dira yako, vijana wangapi unapenda kuwashirikisha na jinsi itakavyowasaidia wao na shule yao. Ulizia kuhusu vijana wanaopenda uandishi wa habari na kuongea mbele za watu au labda walio kwenye klabu ya midahalo au uandishi wa habari ya shule. Sisitiza kwamba kushiriki kwenye mradi wako hakutaingiliana na masomo ya washiriki. Vinginevyo unaweza kushirikiana na asasi ya kijamii ambayo inafanya kazi na vijana katika sekta mahususi kama (VVU na Ukimwi, mabadiliko ya tabia nchi, vijana walio katika mazingira hatarishi) Asasi mshirika mara kwa mara itasaidia kwenye masuala ya miundo mbinu kama kupata usafiri au sehemu ya kukutana na kutoa mwongozo muhimu kuhusu kufanya kazi na vijana. Toka mwanzo washirikishe wazazi wa washiriki. Waalike kwenye mkutano wa kwanza na waambie kwamba utapokea maswali yao na mrejesho kutoka kwao katika hatua yoyote. Mara tu mradi unapoanza na kuendelea, wape CD ya vipindi vilivyorekodiwa na watoto wao (au namna nyingine ya kusikiliza) mara kwa mara. 2. FIKIRIA KUHUSU MIUNDO MBINU UKUBWA WA KIKUNDI Kiwango unachotaka cha ushirikishaji wa vijana na rasilimali za kituo chako miundombinu wafanyakazi na teknolojia itasaidia kujua ukubwa wa kikundi. Kama unataka vijana wasiwe wachangiaji wa mara kwa mara, itakuwa rahisi kufanya kazi na kundi kubwa la hadi watu 20. kama unataka watangaze wenyewe vipindi vyao mara kwa mara, kikundi cha watu 10 ni rahisi kukisimamia. Tangu wakati ambapo kikundi kinaanza kushirikishwa kwenye mchakato wa uandaaji wa kipindi, utahitaji mshauri kwa kila kikundi cha vijana watano. SURA YA 2: KUFANYA KAZI NA VIJANA KUWA MSHAURI MAHALI NA VIFAA Utahitaji kuwa na chumba kiknachofaa chenye viti na choo kilicho karibu. Hakikisha vyoo vinakidhi hitaji la kujistiri kwa wanawake na hakikisha kuna nafasi nyingine ambayo unayoweza kuhitaji. Toa vifaa vya kuandikia kama penseli na madaftari, nyaraka na machapisho ya marejeo. Orodha ya vifaa unavyoweza kuhitaji kwa ajili ya kuandaa semina inapatikana kwenye Kiambatisho 2 ORODHA YA VIFAA MUHIMU KWA AJILI KUFANYIA SEMINA NA VIJANA 16

18 Sehemu ya Pili Kanuni za Msingi Sura ya 1 Kuwashirikisha vijana USAFIRI Kuwashirikisha vijana wa mijini na vijijini ni wazo zuri lakini kuchagua washiriki wanaoishi umbali wa kilomita kadhaa ambao hawana usafiri ili kufika kwenye kituo cha radio, hatimaye unaweza kukosa wa mtu kufanya kipindi. Usafiri unaweza kuwa ghali sana na hiyo itawafanya vijana wanaoishi maeneo ya mbali kutoshiriki kikamilifu. Uzoefu unaonyesha kwamba njia bora ya kufanya ushiriki wa vijana kuwa endelevu ni kuchagua wale wanaoishi au wanaosoma karibu na kituo cha radio. 3. WASHIRIKISHE VIJANA KUHUSU MRADI WAKO Kama kusipokuwa na mchango wa vijana, inabidi ushauriane na kuawashirikisha vijana kwenye kupangilia mradi. Kuna uwezekano wataleta mawazo mapya kwenye mradi, lakini ushirikishaji katika hatua za mwanzo kwa kiasi kikubwa utawapa hali ya kujiona wamiliki. Huko Khayelitsha, kitongoji kilicho nje ya Cape Town, Afrika Kusini, Children s Radio Foundation inafanya kazi kwenye kliniki ya vijana wanaoishi na VVU ambao wanaandaa na kutangaza vipindi kwenye kituo cha radio kilicho kwenye eneo hilo. Washauri walifikiria kwamba kipindi kiwe na makala zilizorekodiwa kwenye eneo hilo zinazohusiana moja kwa moja na VVU na Ukimwi, kama kupima na unyanyapaa. Kwenye mkutano wa kwanza, vijana walielezea kwamba walitaka kutengeneza kipindi cha majadiliano ya moja kwa moja kwa njia ya simu na ushauri rika. Kwa kujua vionjo na tabia za vijana wa Khayelitsha, walishiriki walijua kwamba muundo huu ungefanya kazi vizuri, ambapo washauri walikuwa hawajui chochote kuhusu hilo. Kwa kuwa washauri walishaurina na vijana, kipindi kilipewa muundo mpya wenye kuvutia. 4. USIFANYE MAAMUZI YA HARAKA Vijana ambao wana aibu au wasio waongeaji wanaweza kuwa washiriki wazuri. Usiweke mkazo kwa vijana wachangamfu tu kwenye jamii husika. Utashangaa kuona nani ataibuka kiongozi kwenye kikundi. Anza kila mkutano kwa michezo ya kikundi na kujumuisha nyimbo na kucheza, ni njia nzuri ya kuvunja ukimya na kuwafanya vijana kujuana na kufanya kazi kwa ufanisi kama kikundi. MIFANO YA MICHEZO YA KUVUNJA UKIMYA NA KUTIA NGUVU: KIAMBATISHO CHA 3 Fafanua moja kwa moja kwenye mkutano wako wa kwanza kwamba kuwa radioni hakumaanishi kuwa DJ. Radio inahitaji pia watafiti, watangazaji na waandaaji wa vipindi. Orodhesha kazi na maandalizi yanayopaswa kufanywa na kikundi cha watu ili mtu mmoja aweze kutangaza kipindi. Ni muhimu kwamba kikundi hicho kijue nini kinachohitajika kwenye mradi na kiwe tayari kwa kazi kitakachofanya. 5. UWE NA MCHAKATO WA UCHAGUZI ULIO WAZI Iwe unawaambia waandike utungaji au waje kwa ajili ya mahojiano, vijana lazima wajue na waelewe ngazi za mchakato wa uchaguzi na mambo yanayohitajika 6. ZINGATIA TOFAUTI ZA UMRI Kama wanakikundi wote wana umri sawa, itabadilisha hali ya kikundi. Itaathiri pia mahitaji ya washiriki na jukumu lako kama mshauri. Zingatia tofauti za ukuaji, hususani kwenye vikundi vyenye mchanganyiko wa rika tofauti. Wakati mwingine ni vizuri kuwa na vijana wa umri tofauti kwenye kundi moja lakini inaweza kuwa tatizo kwenye baadhi ya miradi 7. HAKIKISHA KUNA USAWA WA KIJINSIA Mara nyingi wavulana wanakuwa watu wenye kujiamini na wazungumzaji zaidi kuliko wasichana hivyo ni kazi yako kuhakikisha wasichana wana nafasi sawa ya kushiriki. Hii ni kuanzia mwanzo wa mchakato wa uchaguzi hadi kwenye semina na utangazaji. 17

19 Sehemu ya Pili Kanuni za Msingi Sura ya 1 Kuwashirikisha vijana 8. KAMWE USIWALIPE VIJANA ILI WASHIRIKI Weka wazi toka mwanzo kuwa huu ni mradi wa kujitolea na hakuna mtu atakayelipwa. Hata hivyo unaweza kuwapa vinywaji baridi na vitafunwa kabla au baada ya semina. Kama baadhi ya vijana au wazazi wao watauliza vijana watapata nini kutoka kwenye mradi huu, unaweza kujibu Stadi muhimu za maisha na sauti na maoni yako kusikika radioni. Washiriki watajifunza kufanya utafiti, kufanya mahojiano na kutangaza. Hii itaimarisha hali yao ya kujiamini. Shauriana na wazazi na walezi unapoandaa ratiba na kumbuka kwamba, wewe kama mshauri wao, inabidi uendane na ratiba ya vijana, na si vinginevyo. Mara zote shule ipewe kipaumbele na hii inaweza kuzuia au kuathiri ushiriki wao wakati wa mitihani. 18

20 Sehemu ya Pili Kanuni za Msingi Sura ya 2 Kufanya kazi na vijana Kuwa mshauri SURA YA 2: KUFANYA KAZI NA VIJANA KUWA MSHAURI JUKUMU LA MSHAURI Sababu ya kuitwa mshauri ni kwa sababu utakuwa unawaongoza vijana kadri wanavyopata stadi fulani. Wewe sio mwalimu na sio mkufunzi-uko hapo kwa ajili ya kuwasaidia kujieleza na kukuza stadi zao ili kuwa watangazaji vijana. Iwe unashauriana na vijana kuhusu mada wanazozipenda au unawaongoza wanapoandaa kipindi chenye maudhui yao wenyewe, mambo yafuatayo ni ya kuzingatia MAMBO YA MUHIMU KWA AJILI YA USHAURI 1. ANDAA MAZINGIRA YA UAMINIFU NA USALAMA Toka mwanzo onyesha kwamba unavutiwa na kila mmoja. Kwa namna hiyo, kila mmoja kwenye kikundi atajiona anatambuliwa na kutiwa moyo kujieleza kwa uwazi na uaminifu. Fafanua kwamba kila wanachosema kwenye vikao vyako kitakuwa siri, kwa mfano, unaweza kusema hakuna atakayemwambia mtu aliye nje ya kikundi kilichosemwa kwenye vikao. Fafanua kwamba hilo linakuhusu wewe pia. Onyesha umuhimu wa usiri kwa kutumia mfano wa kijana aliyetoa siri kwa rafiki yake ambaye naye alimsimulia kila mtu shuleni. Wanaulize wana kikundi wangejisikiaje kama mmoja wa rafiki zao angevunja uaminifu wao kama hivyo. Elezea tofauti kati ya faragha na usiri kwa kufafanua kwamba faragha inahusu mambo yote ya maisha ya mtu wakati usiri unahusiana na kile kinachosemwa na mtu. Faragha ambayo ni haki ya msingi ya watoto iliyotajwa kwenye kifungu cha 16 cha Mkataba wa Haki za Mtoto na usiri ni misingi ya uhusiano wenye uaminifu kati ya mshauri na vijana. 2. UWE NA HESHIMA Tumia mwonekano wako na sauti yako kuonyesha heshima kwa vijana. Usijiweke kama kiongozi kwa kusimama mbele ya chumba kila wakati, huku ukiwaonyeshea vijana na kuwapa amri. 3. USIWE POA SANA Wachukulie vijana kwa heshima na upendo, lakini kumbuka wewe sio rafiki yao 4. HESHIMU TOFAUTI ZAO Historia yako na imani yako inaweza isiwe sawa na zile za vijana. Wanaweza kuwa wanatoka katika familia, tamaduni, jinsia na imani tofauti. Mara zote zikubali na kuziheshimu tofauti na kuhimiza mazungumzo. Wasichana na wavulana wana vitu maalum wanavyovipenda na wanaweza kutofautiana kimtazamo. Mambo tofauti wanayoyapenda lazima yaheshimiwe na yasibezwe. 19

21 Sehemu ya Pili Kanuni za Msingi Sura ya 2 Kufanya kazi na vijana Kuwa mshauri 5. KUWA MTU WA MSAADA Wakati mwingine wana kikundi watakuelezea mambo au matatizo usiyoyategemea kama kifo cha mzazi au mambo yanayowatatiza. Sikiliza na uwe mtu wa msaada lakini kumbuka kuwa kikao hicho cha kikundi sio wakati wa kutoa majibu au unasihi na kwamba wewe sio mnasihi, tatibu wa akili au mtu wa ustawi wa jamii. Zungumzia suala hilo kwa faragha na mhimize mtu huyo aomba msaada au mwelekeze kwa mtu mwenye taaluma anayeweza kusaidia 6. USIMLAZIMISHE MTU YEYOTE KUSHIRIKI Zingatia ukweli kwamba baadhi ya vijana wana aibu kuliko wengine. Kama mtu hapendi kushiriki kwenye kitendo, kamwe usimlazimishe. Usimweke kijana kwenye shinikizo. Badala yake fikiria namna nyingine za kuwafanya washiriki, kama kwa kuwaambia wakionyeshe kikundi zoezi la kuchangamsha mwili. Kiambatisho cha 3 kinaonyesha mazoezi ya kuchangamsha mwili. KUFANYA KAZI NA VIJANA Kufanya kazi na vijana hakumaanishi kuwaambia jinsi ya kufanya kitu fulani. Bali ni kuwasaidia kutafuta namna ya kufanya wao wenyewe. VIDOKEZO VYA JINSI YA KUFANYA KAZI NA VIJANA 1. Jibu maswali yote lakini usitoe maelezo zaidi ya kile ulichoulizwa 2. Mara zote kubali kama kuna kitu hujui 3. Sikiliza. Ongea pale inapohitajika 4. Himiza kazi za kikundi na hakikisha maamuzi yanafanywa kwa pamoja 5. Changanya vikundi ili marafiki wasiwe kila mara wanafanya kazi pamoja 6. Waache vijana waongoze kadri iwezekanavyo 7. Kila mara toa mrejesho chanya 8. Hakikisha kikundi kinajifunza kwa kutenda 9. Mara zote watambulishe wana kikundi wapya na washirikishe kwenye mambo yanayoendelea. Hii inahusu hata wageni watu wazima 10. Tengeneza sheria na waache vijana watengeneze sheria zao za ndani ili kutoa mwongozo wa kipi kinachokubalikana kipi hakikubaliki NGAZI YA 1: RADIO KWA AJILI YA VIJANA Kamwe usitumie nguvu au matusi. Kama kijana anasumbua wakati wa kipindi rejea sheria za ndani na kiambie kikundi kiamue hatua ya kuchukua kutokana na tabia yake 20

22 Sehemu ya Pili Kanuni za Msingi Sura ya 3 Maadili na Idhini SURA YA 3: MAADILI NA IDHINI MAADILI: KUFANYA KAZI NA VIJANA Kama mshauri unapaswa ujue haki za vijana kwa kuwa zinaathiri jinsi utakavyofanya kazi nao. Kwa maneno mengine, haki zao zitakuwa mwongozo wa taratibu zako. Kama mshauri, utaweza kushirikishana na vijana mapenzi yako kwa radio na kuchochea maisha yao na kuwasaidia kujieleza kikamilifu kuhusu mada ambazo ni muhimu kwao. Unaweza kufanya kazi kwenye jamii ambayo haitoa fursa sawa kwa wasichana na wavulana. Kama mshauri una jukumu muhimu la kuhakikisha kuna haki sawa na kuonyesha fursa na namna mpya zenye faida kwa vijana kutoa maoni yao. KANUNI ZA MAADILI ZA MSHAURI Kuwa makini na mambo ambayo yanaweza kuwa hatari kwa vijana kimwili au kihisia na yadhibiti Wakati Brandon mwenye miaka 13 na Keith kutoka Manenberg, Afrika Kusini, waliamua kufanya mahojiano na mhalifu maarufu na mtumiaji wa madawa ya kulevya katika kitongoji chao, kuhusiana na matumizi ya madawa ya kulevya, mshauri wao ilibidi awe mwangalifu Walikubaliana kwamba wale vijana wangefanya mahojiano wenyewe lakini alipitia maswali pamoja nao ili kuhakikisha kwamba sio ya kuudhi. Halafu waliwasindikiza vijana pamoja na mkuu wa kituo cha eneo hili anayemjua vizuri mhojiwa. Walipofika nyumbani kwake, waliutambulisha mradi wa radio na vijana walitaka kumhoji kuhusiana na maudhui ya kipindi cha matumizi ya madawa ya kulevya. Walipitia kwa pamoja naye masuala ya idhini na kutotajwa jina. Vijana walifanya mahojiano yao, wakiamini kuwa watu wazima watatu waliokuwepo wangeingilia kati kama mambo yangeenda ndivyo sivyo. Mahojiano yalirushwa hewani na mhojiwa aliridhishwa na matokeo yake. KWA UJUMLA NI MAKOSA: Kutumia muda mwingi peke yako na vijana wakiwa mbali na wenzao Kumpeleka kijana mahali mtakapokuwa wawili tu wewe na yeye A MENTOR MUST NEVER: Kumweka kijana katika hatari kwa ajili ya kurekodi kipindi Kumpiga au kumshambulia kimwili kijana Kuwa na mahusiano ya kimwili au kimapenzi na kijana Kuwa na mahusiano na kijana ambayo yanachukuliwa kama ya kinyonyaji, yasiyofaa au kudhalilisha Kutenda kwa namna ya kudhalilisha au kumweka mtoto katika hatari ya kudhalilishwa Kuwalipa vijana au kuwapa upendeleo kwa ajili ya kufanya kazi MSHAURI LAZIMA AEPUKE VITENDO AMBAVYO VINAWEZA KUONEKANA KAMA VIOVU AU VYA KUDHALILISHA, KWA MFANO, KAMWE: Usitumie lugha, kutoa mapendekezo, kufanya ishara au kutoa ushauri usiofaa, kuudhi au kudhalilisha Usiwe na tabia ambayo sio sahihi kimwili au inayodhalilisha kijinsia Usiwaruhusu vijana kukaa hadi usiku wa manane kwe chumba cha watu wazima Usiwafanyishe kazi vijana kwenye kituo cha radio kwa zaidi ya masaa matano kwa wiki Kama utaandaa michezo kwa ajili ya kufungua kipindi, zingatia kuna miiko fulani kuhusu kugusa kati ya wavulana na wasichana. Katika baadhi ya mazingira, hutakiwi kufanya michezo ambayo inahusisha ukaribu kama huo. Kama ni hivyo watenganishe vijana kulingana na jinsia kama utafanya michezo inayohusisha kugusana. Usisahau mila hizo zinakuhusu wewe na washiriki. Sio vizuri kwa mshauri wa kiume kumgusa mshiriki wa kike, hata kama ni sehemu isiyo na shida ya nyuma Je, unataka kushauriana na vijana? A Toolkit of Good Practice, Save The Children,

23 Sehemu ya Pili Kanuni za Msingi Sura ya 3 Maadili na Idhini MAADILI: KUWAHOJI VIJANA Maadili ni kitu muhimu sana unapowahoji vijana walio chini ya miaka 18. Hakikisha kwamba unawalinda na haukiuki haki zao kwa kujifunza na kuzielewa kanuni za kimaadili na kuziimarisha kwa vitendo. Unapowahoji vijana wanaweza kukushirikisha taarifa muhimu au kukuelezea matatizo wanayokumbana nayo. Unaweza kuwahoji vijana ambao wamekuwa wakinyanyapaliwa kwa sababu ya rangi ya ngozi zao, jinsia au dini yao. Unaweza kukutana na vijana ambao wanafanya kazi au waathirika wa udhalilishaji. Wasichana kutokana kwenye mazingira magumu wako kwenye hatari zaidi ya haki zao kukiukwa kuliko makundi mengine. Kufuata kanuni za kimaadili kutakusaidia kuhakikisha unaweka uwiano mzuri kati ya haki ya vijana kushiriki na haki yao ya kulindwa. MAMBO MUHIMU ILI KUWA MSHAURI MZURI Wakati unafanya utafiti wako, hakikisha una taarifa za kutosha kuhusu hadhi ya kisheria na kijamii ya vijana unaowahoji. Hususani kama wanatoka kwenye kundi au jamii maalum au ya wachache (vijana wenye ulemavu, vijana wanaofanya kazi, vijana wahalifu) Hakikisha vijana unawaowahoji wanaelewa maana ya sauti zao zinazorekodiwa kurushwa hewani na watoe idhini kwa maandishi IDHINI: KUWAHOJI VIJANA 3. Hakikisha wazazi au walezi wa vijana wanajua kwamba wanafanya mahojiano. Wafafanulie madhumuni ya mahojiano na matumizi yanayokusudiwa 4. Kwa mfano masimulizi nyeti (udhalilishaji, ubaguzi), wahimize vijana watumie majina bandia 5. Katika mazingira mengine yoyote, waambie vijana watumie majina yao ya kwanza na kusiwe na taarifa nyingine binafsi (jina la ukoo, anwani, jina la shule). Tofauti na runinga na magazeti, radio ni chombo cha habari kipofu, lakini sauti zinatambulika hivyo fikiria kama unaweza kubadilisha sauti Waelezee kwamba hawapaswi kuwataja watu wengine kwenye vipindi. Unapomtaja mtu kwenye habari, tumia majina ya jumla (rafiki, ndugu, mwalimu, n.k) Mara zote toa muktadha sahihi kwa ajili ya habari za vijana na hakikisha kwamba wanasimulia habari mambo halisi yaliyowatokea. Kama una shaka, ipitie habari pamoja na ndugu au mwalimu lakini hakikisha lakini hakikisha uhakiki unafanyika bila ya kuwaweka vijana kwenye hatari. Hakikisha maswali yako hayakiuki haki ya vijana ya faragha, yanazingatia hali zao binafsi na yasiyoendeleza dhana potofu Kamwe usimpe kijana upendeleo wowote kwa ajili ya kujibu maswali Kamwe usimlipe kijana ili kuhojiwa 11. Hakikisha kwamba mwongozo wa kuwahoji vijana unapatikana katika lugha ya kienyeji kwa wafanyakazi wa radio na washirikishe wengine 12. Upitie na uboreshe mwongozi wako kila baada ya muda fulani, kwa mfano, mwanzo wa awamu mpya. International Federation of Journalists Guidelines and Principles for Reporting on Issues Involving Children 22

24 Sehemu ya Pili Kanuni za Msingi Sura ya 3 Maadili na Idhini IDHINI: KUFANYA KAZI NA VIJANA Maana ya idhini ni kibali au makubaliano ambayo yamefikiwa katika ya kituo cha radio, vijana na wazazi au walezi ili washiriki wafanye kazi kwenye radio kwa usalama na kujiamini. Inamaanisha kuelewa kikamilifu, hususani kwa vijana wanaoshiriki kwenye mradi wako Mwanzoni mwa mradi, vijana wote lazima waelewe idhini. Fomu zako za idhini lazima ziandikwe kwa lugha ambayo vijana wanaielewa. Epuka kutumia misamiati kama "haki miliki au hati miliki. Unaweza kusoma kila mstari wa idhini pamoja na vijana na kuwauliza kama kuna kitu ambacho hawakielewi. MFANO WA FOMU YA IDHINI: KIAMBATISHO 4 Lazima upate ruhusa na uungaji mkono wa wazazi, walezi na asasi washirika. Ni muhimu kwao kukuelewa na kujua kile utakachokuwa unafanya. Hii itakulinda na kukusaidia kuungwa mkono kwenye mradi wako. Kila fomu ya idhini ya mshiriki inabidi isainiwe pia na wazazi au walezi wake. Kumbuka kwamba vijana wanaweza kubadilisha mawazo hata kama mwanzo walikupa idhini ya kusikiliza na kutangaza vipindi walivyorekodi. Itabidi ujiandae kupambana na mazingira magumu ambapo wazazi wanaweza kukataa kutoa idhini. Kumbuka ni muhimu kuwashirikisha wazazi wakati wa mashauriano yako na jamii ili kuepuka vikwazo IDHINI: KUWAHOJI VIJANA Idhini iko pande mbili. Kama waandishi wa habari vijana wanavyoombwa idhini yao, kila wanaowahoji au kuzungumza nao lazima washauriane nao na kuomba idhini yao. Ni muhimu sana kufafanua kikamilifu sababu ya kutangaza radioni kipindi kilichorekodiwa na kukishirikisha na jamii. Usisite kuelezea kwamba matangazo ya radio ni kurusha hewani taarifa kwa wasikilizaji wengi. Mara wanapokuwa wameelewa, inabid upate idhini ya mdomo ya waandaji wote wa vipindi vya radio na washiriki. Tumia hadithi ili kikundi kielewe umuhimu wa idhini, kwa mfano, hadithi ya msichana aliyeadhibiwa shuleni, kwa kusimulia hadithi huku akitaja jina la mwalimu. Waulize vijana unaofanya kazi nao kingetokea nini kama hadithi hiyo ingerushwa hewani na kituo cha radio cha jamii na hivyo kila mtu kwenye jamii angesikia mwanafunzi akimkosoa mwalimu wake. Je, angepata madhara gani? Je, mwalimu angepata madhara gani? Je, mwanafunzi angekuwa tayari kukubali madhara hayo? Vijana inabidi waelewe kwamba ingawa vipindi vinarekodiwa mbali na macho ya watu, vinaishi mara tu vinaporushwa hewani na kuwa na matokeo yasiyopendeza Vijana watakaohojiwa inabidi kwanza watoe idhini ya mdomo Hakikisha wewe na waandishi wa habari vijana wanawaambia wahojiwa maana ya mahojiano na kwamba yanaweza kutangazwa radioni Kama mhojiwa ana miaka chini ya 18, anayehoji inabidi atumie jina la kwanza tu na kamwe asitumie jina la ukoo au eneo analoishi radioni. Wahimize vijana wanaohojiwa kufanya hivyo hivyo Habari, jina langu ni... na ningependa kuwauliza maswali machache kwa ajili ya kipindi kitakachorushwa hewani kwenye kituo chetu cha radio. Sawa? Andika majina kamili, umri na mawasiliano ya wanaohojiwa. Fafanua kwamba taarifa hizo hazitarushwa hewani bali ni kwa ajili ya kuwajulisha kama michango yao imerushwa hewani. Pia hakikisha kwamba wanajua jinsi ya kuwasiliana na wewe iwapo wanabadilisha mawazo na hawataki michango yao kurushwa hewani 23

25 KABLA HUJAJIINGIZA KATIKA ULIMWENGU WA RADIO YA VIJANA, HAKIKISHA UNAKUMBUKA: 1. Umuhimu wa kuchagua kwa usahihi kikundi chako cha washiriki au vijana na kuwashirikisha toka mwanzo na mara kwa mara 2. Wajibu wako kama mshauri na inajumuisha kazi na majukumu yapi 3. Kwamba kila mmoja anayeshiriki atimize majukumu yake binafsi na idhini ya kila mmoja ni muhimu sana KUWEKA VIZURI MALENGO NA MWONGOZO KUTARAHISISHA KIPINDI CHA MPITO KUTOKA KUPANGA MRADI WA RADIO YA VIJANA HADI KUIANZISHA 24

26 SEHEMU YA TATU KUJUA KIWANGO CHA UWEZO NA KUPANGA NGAZI YA 1: RADIO KWA AJILI YA VIJANA NGAZI YA 2: RADIO PAMOJA NA VIJANA NGAZI YA 3: RADIO YA VIJANA NGAZI YA 4: KUWAFIKIA VIJANA The levels will help you to assess your radio station s capacity and include young people s involvement in your planning at a manageable degree. The necessary skills, linked activities and model radio formats presented in each level advance progressively, so be aware that if you decide to have young people hosting a live audio debate as described in Level 3, your radio station will need to have met the foundation skills described in Level 1. 25

27 Sehemu ya Tatu Kujua Kiwango cha Uwezo na Kupanga Ngazi ya 1: Radio kwa Ajili ya Vijana NGAZI YA 1: RADIO KWA AJILI VIJANA Ngazi hii itakusaidia: Kutangaza mahojiano na vijana kwenye kituo cha radio ya jamii Kujumuisha zaidi maudhui ya vijana kwenye kipindi cha watoto Kuboresha ubora wa kipindi chako cha sasa kwenye radio ya vijana Kumbuka kuwa vijana ni sehemu muhimu ya jamii na kwamba kama mfanyakazi wa chombo cha habari ni jukumu lako kuwawakilisha kwa usahihi na kwa heshima SURA YA 3: MAADILI NA IDHINI TARATIBU (SAA 1) Weka taratibu ambazo zitafanyiwa kazi na wafanyakazi wenzako ambao wanafanyakazi na vijana au wapo kwenye mradi wa vijana A Resource Kit for Journalists, Media Monitoring - Africa Codes of Practice (p19 to 24) 1. MAANDALIZI YA UTENGENEZAJI WA VIPINDI: VIKUNDI VYA MAJADILIANO Washirikishe vijana kwenye awamu ya maandalizi ya vipindi kwa ajili na kuhusu vijana kutoa maoni yao na kugundua mambo wanayoyapenda Zingatia mambo tofauti yanayopendwa na wasichana na wavulana na yaheshimu. Umuhimu wa hili ni kugundua mambo ya kuyaingiza kwenye kipindi na kujenga imani ya washiriki 1.1 KUANDAA KIKUNDI CHA MAJADILIANO NA VIJANA (SAA 1) 1. Watambue vijana kwenye jamii au eneo lako ambao wanapenda uandishi wa habari na wakaribishe wahudhurie majadiliano ya kikundi. Tumia ushirikiano ulio nao na shule na asasi za vijana 2. Usiwaite vijana wengi. Kumi ni idadi ya kutosha 3. Hakikisha kuna usawa kati ya wasichana na wavulana na kwamba umri wa washiriki unafaa kwa aina ya vipindi vya radio unavyoviandaa 4. Pitisha karatasi ya mahudhurio mwanzoni mwa kipindi ili kila mtu aandike mawasiliano yake 5. Endesha kipindi kwenye chumba au eneo ambalo linafikika kwa urahisi na vijana wote 6. Andaa mazingira rafiki na jumuishi. Ni vizuri kupanga viti kwa duara 7. Kama inawezekana, tumia manila, karatasi na kalamu za kuandikia ubaoni au ubao ili kuandika kila kitu kinachosemwa na vijana ili wafanye marejeo kwa kuona na kurekodi 8. Kama unaweza andaa vinywaji na vitafunwa kwa ajili ya vijana kujifurahisha baada ya kipindi 9. Waruhusu vijana watembelee kituo chako cha radio baada ya majadiliano ya kikundi 10. Fanya kipindi kwa saa moja 26

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi

More information

Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo

Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo Mazoezi ya wenye umri wa miaka 11-14 Hivi Ndivyo Nilivyo kwa wenye umri wa miaka 11-14 Kuhusu Hivi Ndivyo Nilivyo Ikiwa

More information

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi 3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi

More information

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)] This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)

More information

Ufundishaji wa lugha nyingine

Ufundishaji wa lugha nyingine CHUO CHA ELIMU CHA KIMATAIFA OFISI YA ELIMU YA KIMATAIFA Ufundishaji wa lugha nyingine Na Elizabeth B. Bernhardt ELIMU MAZOEA KITABU NA. 20 1 Chuo cha Elimu cha Kimataifa (The International Academy of

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper

More information

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery

More information

Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo. Zanzibar, 7-10 Februari 2006

Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo. Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Imechapishwa na: The Atlas Alliance Schweigaardsgt 12 SLP 9218 Grønland 0134 Oslo, Norway Simu: +47

More information

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza 1 Matumizi bora ya Facebook kwa Biashara MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA Kwa Wanaoanza For IT Services & Web Solutions Web: Email: info@dudumizi.com Phone: 0768816728 2 Matumizi bora ya Facebook kwa

More information

Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO. Training and Research Support Centre

Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO. Training and Research Support Centre Shangazi Stella Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO Training and Research Support Centre Zimbabwe Shangazi Stella Kiongozi cha Mwezeshaji

More information

Human Rights Are Universal And Yet...

Human Rights Are Universal And Yet... Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,

More information

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017

More information

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza Shule za umma za kata ya Fayette 1 Mwongozo wa Familia wa Kujifunza Muhtasari wa yale watoto wanastahili kufahamu na kuweza kufanya na njia za familia kuongeza masomo nyumbani. Tunaamini familia ni wenzetu.

More information

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

More information

Kutetea Haki za Binadamu

Kutetea Haki za Binadamu Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and

More information

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA

More information

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika

More information

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji! Yaliyomo Kuhusu kitabu hiki Kuhusu kitabu hiki.........................................................1 Unapojisikia vibaya.........................................................2 Unapoanza kuwa mzima

More information

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0

More information

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi

More information

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA

More information

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya

More information

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya

More information

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika

More information

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted

More information

Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health

Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health Wasiojua kusoma na kuandika katika karne ya 21 hawatakuwa wale wasiojua kusoma na kuandika lakini wale ambao hawawezi kujifunza, kutojifunza na kujifunza

More information

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna

More information

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh

More information

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau

More information

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana

More information

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda

More information

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu BLOOD PRESSURE UK Shinikizo la damu ndicho chanzo kikubwa cha ulemavu na vifo vya mapema kule Uingereza, kupitia kiharusi, mshtuko wa moyo na maradhi ya moyo.

More information

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya

More information

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

SautiElimu. Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian

More information

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) 102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako

More information

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)

More information

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA

More information

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa

More information

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu

More information

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu: Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200

More information

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.

More information

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini... Elimu Bora, lakini... Shukrani za dhati kwa wote waliotusaidia katika kutayarisha kijitabu hiki: Nsa Kaisi, Mshauri wa Rais, kwa mchango wake mkubwa wa mawazo Wafanyakazi wote wa HakiElimu 2003-2004 Many

More information

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1

More information

International Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi

International Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi International Labour Office Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi 1 Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2007 Kimechapwa mara ya kwanza 2007 Machapisho ya Ofisi ya Shirika la

More information

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari

More information

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini

More information

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Desemba 2014 1 Shukurani Ripoti hii iliandikwa na Dk. Mkumbo. Ushauri wa kitaalamu ulitolewa na Elizabeth Missokia na Godfrey

More information

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA

More information

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI

More information

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo

More information

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI

More information

Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo

Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu Nyenzo ya Mafunzo Vi Agroforestry Vi Agroforestry ni shirika la ushirikiano la maendeleo la Sweden, linalopambana dhidi ya umasikini na

More information

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited

More information

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa

More information

Mwongozo wa Mwezeshaji

Mwongozo wa Mwezeshaji JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Ushauri Nasaha na Upimaji wa VVU kwa Hiari Mwongozo wa Mwezeshaji Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Machi 2010 Kimetafsiriwa kutoka lugha

More information

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided

More information

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,

More information

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni

More information

Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo

Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo Taarifa ya Warsha Kuhusu Elimu-Jumuishi Iliyofanyika Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Kujifunza hakuna mwisho. Kazi ya vikundi imenipa fursa ya kujieleza bila kuhofia kuwa ningekosea.

More information

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST

More information

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality

More information

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue?

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue? Tufundishane! Let s teach each other! This newsletter is published by The Foundation for Tomorrow and is meant to be a venue for teachers and schools to share and learn from each other s best practices.

More information

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza

More information

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Shukrani Ripoti

More information

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya

More information

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa

More information

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na. JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3

More information

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia : Maelekezo ya kutumia Kupatwa kamili kwa jua Jumatatu, 21 Agosti 2017 Agreement v1.4 Mar 2014 2014-2017 Eclipse2017.org, Eclipse2017.org, inc. inc. TERMS AND CONDITIONS FOR USE OF SOLAR VIEWER Please

More information

Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi

Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Gervas Zombwe 1 1. Utangulizi Katika mazingira ya kawaida kabisa ndani ya jamii yetu, Imezoeleka kusikia au kuona watu wakioanisha dhana ya elimu

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA

More information

Makala ya Mshiriki wa Mafunzo

Makala ya Mshiriki wa Mafunzo JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Ushauri Nasaha na Upimaji wa VVU kwa Hiari Makala ya Mshiriki wa Mafunzo Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Machi 2010 Kimetafsiriwa kutoka

More information

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini

More information

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MFUMO WA RUZUKU YA MAENDELEO YA MTAJI WA SERIKALI ZA MITAA (LDCDG) UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI Kijitabu cha Mshiriki

More information

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini

More information

MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012

MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012 MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012 TASNIFU HII IMEWASILISHWA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI

More information

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI This booklet on Becoming a Parent was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at. MACHAGUO

More information

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY

More information

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Shukrani Ripoti

More information

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012

More information

Namba ya moduli 3 Kuangalia sanaa

Namba ya moduli 3 Kuangalia sanaa Rasilimali za Msingi Mafunzo Ya Jamii Na Sanaa Namba ya moduli 3 Kuangalia sanaa Sehemu ya 1 Kuchunguza Kazi za Sanaa zionekanazo Sehemu ya 2 Kuandaa Shughuli za Sanaa kwa Vitendo- Sehemu ya 3 Kutumia

More information

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAISI-TAMISEMI HALMASHAURI YA WILAYA BUMBULI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAISI-TAMISEMI HALMASHAURI YA WILAYA BUMBULI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAISI-TAMISEMI HALMASHAURI YA WILAYA BUMBULI NAMBA ZA SIMU: Mkuu Wa Shule: 0784524029 / 0766805826. Makamu Mkuu Wa Shule: 0714356735 / 0767356735. SHULE YA SEKONDARI

More information

Mipango ya miradi katika udugu

Mipango ya miradi katika udugu Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi

More information

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma

More information

Early Grade Reading Assessment for Kenya

Early Grade Reading Assessment for Kenya EDDATA II Early Grade Reading Assessment for Kenya Baseline Instruments: Kiswahili and English EdData II Technical and Managerial Assistance, Task Number 4 Contract Number EHC-E-01-04-00004-00 Strategic

More information

KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA

KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA Toleo la kwanza 2012 Mwandishi: USAID DELIVER PROJECT Wachangiaji: Gary Steele, John Snow, Inc. and Judith

More information

Shabaha ya Mazungumzo haya

Shabaha ya Mazungumzo haya Karibu Katika Mazungumzo Kuhusu Mchakato wa Uhamasishaji Maendeleo ya Kanisa na Jamii CCMP/UMOJA Shabaha ya Mazungumzo haya Kuwafahamisha viongozi wa makanisa kuhusu Mchakato wa CCMP ambao umekuwa ukitumika

More information

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka 0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11

More information

Kuwafikia waliotengwa

Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E 2 0 1 0 Ripoti

More information

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03

More information

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q 88092387 SWAHILI B HIGHER LEVEL PAPER 1 SOUAHÉLI B NIVEAU SUPÉRIEUR ÉPREUVE 1 SUAHILI B NIVEL SUPERIOR PRUEBA 1 Tuesday 3 November 2009 (morning) Mardi 3 novembre 2009 (matin)

More information

Bustani 10,000 Katika Afrika. Alberto Prina

Bustani 10,000 Katika Afrika. Alberto Prina Bustani 10,000 Katika Afrika Alberto Prina K i j i t a b u Timu ya wahariri: Abderrahmane Amajou, Typhaine Briand, Roba Bulga Jilo, Davide Dotta, Emanuele Dughera, Michela Lenta, Velia Lucidi, Irene Marocco,

More information

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI SIKOMBE YIZUKANJI YORADI TASNIFU YA KISWAHILI KWA MINAJILI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (MA. KISWAHILI) KITIVO CHA SANAA

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA

More information