Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,
|
|
- Sophie Ross
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1 HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, KWENYE SHEREHE YA KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA, TAREHE 08 JUNI 2008, MSIMBAZI CENTRE, DAR ES SALAAM Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam; Mhashamu Askofu Mkuu Joseph Chennoth, Balozi wa Vatican, Tanzania; Wahashamu Maaskofu; Waheshimiwa Mapadri; Waheshimiwa Watawa; Viongozi wa Kanisa na Waumini; Wageni Waalikwa; Mabibi na Mabwana. TUMSIFU YESU KRISTU!! Naungana nanyi nyote kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kukusanyika hapa leo katika sherehe hii ya Kuadhimisha Miaka 50 ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania. Hii ni siku ya furaha na siku njema iliyopangwa na Mungu kushuhudia uwepo wa Baraza hili tangu lianzishwe rasmi mapema mwaka Maandiko ya Mtunga Zaburi yanasema: Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA. Tutaishangilia na kufurahia (Zaburi 118:24). Aidha, nitumie nafasi hii kutambua wageni wote mliotoka nje na ndani ya Tanzania. Nasema: For our visitors from abroad, KARIBUNI SANA TANZANIA. You are welcome to Tanzania and feel at home!!
2 Wahashamu Maaskofu, nianze kwa kutoa salaam kutoka kwa Rais, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye awali alitarajia angeshiriki nanyi siku ya leo, lakini kutokana na majukumu mengine ya Kitaifa baada ya kumalizika kwa mkutano mkubwa wa Leon Sullivan, haikuwezekana kuwa nasi leo. Anawasalimu na anawapongeza kwa kutimiza miaka 50 ya Baraza hili. Aidha, anawatakia wote kheri na baraka katika majukumu yenu ya kuwaongoza wana kondoo wa Mungu katika nchi yetu. Nami nitumie fursa hii kuungana na Mheshimiwa Rais, kuwapongeza kwa kazi kubwa mliyoifanya katika kipindi chote cha uhai wa Baraza hili. Nawapongeza kwa majukumu mazito ambayo Baraza limetekeleza. Hongereni Sana! Wahashamu Maaskofu, moja ya majukumu muhimu yaliyotekelezwa na Baraza hili ni kuliweka Kanisa katika hali ya Umoja na Mshikamano. Wote tunatambua na tunakubali kuwa viongozi wa dini, ni moja ya nguzo muhimu katika kujenga mshikamano wa Kitaifa. Historia inaonyesha kwamba, wakati harakati za kupigania Uhuru zilianza miaka ya 1950, tayari viongozi wa dini ukiwemo Umoja wa Maaskofu Tanzania, walikuwa wamekwishaanza kujenga misingi ya muungano mapema tangu mwaka Huu ni uthibitisho kuwa harakati za kujenga Umoja zilianza zamani. Harakati hizo za upande wa siasa zilikwenda sambamba na harakati za upande wa Kidini kwa pamoja zikachangia kuwaleta wananchi kwa pamoja na hivyo kujenga umoja wa kitaifa. Wahashamu Maaskofu na Wageni Waalikwa, tunapoangalia mwanzo wa Umoja huu wa Maaskofu, tunabaini kwamba malengo yake hakika yaliangalia maendeleo ya mwananchi. Tumebaini hili katika jina la kwanza kabisa ambalo umoja huu ulijisajili Serikalini. kumbukumbu zinaonyesha kwamba, mwaka 1958, chombo hiki cha Maaskofu kilisajiliwa Serikalini kwa jina la Tanganyika Catholic Welfare Organization. Neno linalogusa maslahi ya jamii ndilo lililokuwa kiini cha umoja huu. Welfare! Jamii imejionea yenyewe kwamba hata baada ya jina kubadilika mwaka 1965 na kuwa Tanzania Episcopal Conference au Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, bado moyo na ile dhamira ya tangu mwanzo ya kumhudumia mwananchi imedumu. Mafanikio Wahashamu Maaskofu, katika kipindi hiki cha miaka 50, Baraza la Maaskofu Katoliki, limepata mafanikio mengi katika nyanja ya kiuchungaji na katika maendeleo ya jamii. Ninaelewa tangu mwanzo Baraza hili limekuwa kinara wa Maendeleo Fungamano ya Binadamu (Human Integral Development). Hili linathibitishwa na ukweli kwamba, idara za
3 mwanzo kabisa zilizoanzishwa katika Baraza la Maaskofu, zilikuwa zile zinazojishughulisha na mambo ya kijamii. Ziko idara za elimu, afya, maendeleo ya jamii (Caritas) na mawasiliano. Hizi ni idara zilizoanzishwa muda mrefu tangu mwaka Elimu Wahashamu Maaskofu na Wageni Waalikwa, madhehebu ya dini yamekuwa mstari wa mbele katika kuendeleza huduma za jamii nchini. Kwa mfano, katika upande wa elimu, Kanisa Katoliki limetoa mchango mkubwa katika sekta ya elimu. Nakumbuka historia ya sekondari chache, kama vile Marian College ambayo kwa sasa ni Sekondari ya Kilakala au St. Francis ambayo sasa ni Sekondari ya Pugu. Hii ilijengwa mwaka Kuna Kurasini ambayo sasa ni Makao Makuu ya Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC) ilijengwa mwaka Ninazo taarifa kwamba Maaskofu Tanzania, mmoja mmoja na katika ujumla wao, sasa hivi wanamiliki shule 150 za sekondari, vyuo takriban 200 vya mafunzo stadi, Vyuo viwili vya walimu, Chuo Kikuu cha St. Augustine chenye vyuo vikuu vishiriki vitatu. Aidha, nimepata taarifa kwamba, mwaka huu wahitimu kutoka katika vyuo vikuu vya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania watakuwa zaidi ya 5,000. Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kwa mfano, nalo limechangia sana katika elimu. Kwa sasa lina shule za awali 469, shule za msingi maalumu kwa walemavu 10, shule za sekondari 61, vyuo vya elimu na ufundi 35, Chuo Kikuu na Vyuo Vikuu vishiriki sita. Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) limechangia kwa kuwa na shule za chekechea 500, shule za msingi tatu (3), shule za sekondari 27, Chuo cha Ualimu cha Al-Haramain na Chuo Kikuu cha Morogoro cha Kiislam kimoja. Haya ni maendeleo na mafanikio makubwa yanayowagusa wananchi moja kwa moja. Asanteni Sana. Afya Wahashamu Maaskofu, katika upande wa huduma za afya, historia inaonyesha kwamba mwaka 1961, Maaskofu mmoja mmoja na katika ujumla wao walikuwa wanamiliki Hospitali 23, Zahanati 74, Kliniki 64, Vituo 7 vya Wakoma na Vyuo 5 vya Wauguzi. Leo hii ziko Hospitali 44, Zahanati 328 na Vituo 52 vya Afya. KKKT wanazo Hospitali 138, Vituo vya Afya 13, Vituo vya Wauguzi sita (6), Vituo vya Watoto Yatima 11 na Kituo cha Wazee kimoja (1). Baraza Kuu la Waislam Tanzania limejenga Vituo vya Afya 12, Vituo vya kulelea Watoto Yatima sita (6) na Mradi wa Kitengo cha UKIMWI ambao uko makao makuu ya BAKWATA. Kwa kupitia vyombo hivi vya afya ambavyo vimesambaa Tanzania nzima, Baraza la Maaskofu linachangia asilimia 20 ya huduma za afya katika nchi yetu!! Tunawashukuru sana kwa mchango wenu! Vilevile, tunatambua mchango wa Baraza hili kwa kupitia vyombo vyake kama vile Caritas Tanzania vinavyofanya kazi kwa kusaidia wananchi wanaoathirika na majanga mbalimbali kama vile njaa, mafuriko, ukame, n.k. Kwa upande wa KKKT wanasaidia majanga mbalimbali kupitia Tanzania Commission for Refugees Services (TCRS), na Action by Churches Together (ACT), n.k. Mafanikio yote haya yamewezekana kwa vile madhehebu ya dini yakiongozwa na
4 ninyi viongozi kwa kuwashirikisha waumini wenu mlikuwa na nia thabiti ya kumkomboa Mtanzania kutoka katika adui ujinga, maradhi na umaskini. Tunajua pia kuwa, nia njema pekee bila raslimali watu na fedha, isingeweza kufanya hayo yote. Tunatambua kwa dhati mchango mkubwa wa Serikali ya Vatican na Makanisa mengine ulimwenguni. Tunawashukuru wote waliowaunga mkono Maaskofu wetu Tanzania katika nia yao njema ya kumkomboa Mtanzania. Thank you very much The Vatican for your assistance to the Government of Tanzania! Changamoto Wahashamu Maaskofu, tunazo changamoto kubwa bado zinazoikabili nchi yetu katika nyanja za elimu, afya, maji, watoto yatima, watoto wenye ulemavu, suala zima la janga la UKIMWI na suala la ushirikina. Changamoto hizi zinatupa vigezo vya kupima juhudi na uwezo wetu kama viongozi wa serikali na viongozi wa dini katika kuhudumia jamii. Ninachotaka kusema ni kwamba, tuna kazi kubwa katika kuilea Jamii katika kukabiliana na changamoto hizi. Sisi kama Serikali tunaweza kurekebisha mambo ya kimwili. Lakini ninyi kama wachungaji wa Kondoo wa BWANA, mnayo nafasi ya kubeba mzigo mkubwa wa wanakondoo Kiroho. Waumini wenye shida kama ya ulemavu na UKIMWI watahitaji upendo, uvumilivu na moyo wa kuwasaidia. Wanahitaji walindwe katika mazingira magumu yanayowakabili kwa sasa. Aidha, tunahitaji kuwaelekeza juu ya ufumbuzi wa shida zinazowakabili huku tukiwasihi wasikate tamaa kwa maana shida hazikuumbwa kwa ajili yao tu, bali binadamu yoyote. Uko msemo wa watu wa kale usemao: I wept because I had no shoes until I saw a man who had no feet ikimaanisha: Nililia sana kwa sababu sikuwa na viatu lakini nilikoma kulia nilipokutana na mtu ambaye hana mguu. Hivyo tunawakumbusha kuwa kutokana na udhaifu wetu kama binadamu wataweza kuwa wanasononeka kwa kukosa viatu wakati kuna wasio na miguu kabisa na hawajakata tamaa ya kuishi. Aidha, ni rahisi kuyakuza matatizo yaliyopo yakaonekana makubwa sana tukasahau Baraka ambayo Mungu wetu Mkuu ametupatia. Nasisitiza kuwa katika kazi ya kuwaongoza waumini wa kanisa au wananchi, jukumu kubwa ni kuwasaidia kupata ufumbuzi wa matatizo yao. Mauaji ya Maalbino
5 Wahashamu Maaskofu, Taifa letu kwa siku za hivi karibuni limekumbwa na tatizo la imani za kishirikina na kichawi. Napenda nichukue nafasi hii kulisema hili kwa uchungu na masikitiko makubwa sana. Sote kwa pamoja, Serikali, Madhehebu ya Dini na wananchi kwa ujumla, tumeshuhudia mauaji ya kutisha ya watu wasiokuwa na hatia kwa ajili ya imani za kujipatia utajiri wa haraka. Tumeshuhudia ndugu zetu Maalbino wakiuawa eti kwa sababu ya imani za kichawi kuwa viungo vyao vinaleta utajiri. Haya ni mawazo potofu. Haya ni mawazo ya kishetani. Hawa ni wauaji. Naomba Kanisa na madhehebu mengine ya dini na Watanzania wote wenye mapenzi mema waisaidie Serikali kulaani unyama huo, kulaani vitendo hivi vya kinyama na kusaidia wahusika waweze kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria kujibu makosa ya mauaji. Wanaofanya vitendo hivi vya kinyama, tunaishi nao, tunawafahamu, tunakula nao, tunacheka nao, tunasali nao na wakati mwingine kushirikiana nao. Kwa niaba ya Serikali, naomba tuwafichue waovu hawa. Kwa viongozi wote wa madhehebu mbalimbali ya dini na ninyi mliopo hapa na hasa, Maaskofu na Mapadre tusaidieni kukemea na hatimaye kutokomeza uovu huo. Kuendelea kwa maovu haya ni mmomonyoko mkubwa wa maadili na utu katika jamii na hasa Kanisa. Suala hili la mauaji ya watu wasiokuwa na hatia ni changamoto ambayo sote inabidi kupigana nayo kwa kutumia silaha zote kama vile sala, maombi na sheria. Amani na Utulivu Tanzania Wahashamu Maaskofu, madhehebu yote ya dini yanaiombea nchi yetu amani na utulivu. Aidha, huwaombea viongozi wake wawe na afya njema na kubwa zaidi upendo, busara na hekima katika kuwaongoza wananchi. Tunawashukuru sana. Uko ukweli kwamba, nchi nyingi duniani zenye mafanikio ya uchumi imara ni kwa sababu ya kujiwekea misingi bora ya amani na utulivu. Aidha, uchumi imara ni matokeo ya juhudi za wananchi walizowekeza katika uzalishaji kutokana na uhakika wa uongozi imara na sera nzuri za uwekezaji. Kwa maana hiyo, kama tunataka uchumi imara ni lazima tuilinde nchi yetu idumu katika hali ya amani na utulivu wakati wote. Hata Vitabu Vitakatifu vinasema: Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote (Waeb. 12:14) Maadili Mema Wahashamu Maaskofu, Serikali inakabiliwa na changamoto ya kujenga maadili mema miongoni mwa watumishi wake, kwani yamekuwa yakiporomoka siku hadi siku. Moja ya changamoto hizo ni suala la rushwa. Rushwa ni tatizo ambalo wananchi wanakumbana nalo katika nyanja mbalimbali hususan katika utoaji wa huduma za jamii na uchumi na pia katika utendaji kazi wa Serikali. Rushwa ina athari kubwa kiuchumi, kisiasa na kijamii. Athari zitokanazo na vitendo vya rushwa ni nyingi na ipo mifano mingi. Kwa mfano, rushwa huathiri utekelezaji wa majukumu ya Serikali; hukwamisha utoaji wa haki na husababisha kuongezeka kwa maovu katika jamii. Aidha, rushwa husababisha wananchi kukosa imani na Serikali yao; wananchi hukosa huduma muhimu za kijamii na kusababisha kutolewa kwa huduma duni. Hizi ni baadhi tu ya athari nyingi zinazotokana na rushwa. Kutokana na athari hizi, ni dhahiri kwamba tunao
6 wajibu mkubwa katika kupambana na rushwa kwa nguvu zote. Katika kupambana na rushwa inabidi kufanya yafuatayo: (i) Kufuata sheria na taratibu kwa kuepuka njia za mkato kupata huduma ili kuepuka mianya ya rushwa; (ii) Kusimamia na kutathmini mipango ya maendeleo na kufuatilia fedha za miradi zinazotolewa na Serikali ili kuthibiti ubadhirifu wa fedha hizo; (iii) (iv) Kuwaelimisha Wananchi kutotoa wala kupokea rushwa; Kutowaonea aibu viongozi au watumishi wa umma wanaoomba na kupokea rushwa; (v) Kutoa ushirikiano kwa vyombo vya dola, kama TAKUKURU mara wanapotakiwa kutoa ushahidi. Kama wananchi wote watashirikiana kutekeleza hayo yote, ni dhahiri upo uwezekano wa kushinda vita dhidi ya rushwa. Tunaendelea kuchukua hatua za dhati kupambana na kuzuia rushwa. Mtakuwa mashahidi kwamba Serikali haipo kimya tu. Mapambano ya rushwa sio jambo la kufanya mara moja na kulimaliza, bali ni mchakato ambao unahitaji ushirikiano wa hali ya juu. Lakini jitihada zetu zinaonekana. ndio maana tumeshuhudia siku za hivi karibuni nchi mbalimbali na mashirika ya kimataifa yakisifu jitihada zetu katika mapambano haya. Ninyi Viongozi wa Dini mnayo nafasi kubwa ya kusaidia mapambano haya. Wahashamu Maaskofu, tunatambua kuwa kazi ya kupambana na rushwa sio ya Serikali peke yake. Aidha, baadhi ya wananchi wanaotoa na kupokea rushwa ni waumini wenu. Kushiriki katika rushwa ni matokeo ya ukosefu wa maadili mema. Hivyo, ninyi kama viongozi wa dini, mnayo nafasi nzuri ya kuijenga jamii katika maadili yanayokubalika ikiwemo kukataaa kushiriki katika kutoa na kupokea rushwa. Katika Methali 5:13 na 19, Mtume Paulo ameandika maneno ya Yesu akiwaambia Wanafunzi wake kwamba: Ninyi ni nuru ya Ulimwengu Nuru yenu na iangaze mbele za watu wapate kuyaona matendo mema, wamtukuze Baba yenu aliye Mbinguni. Tuungane na Mtume Paulo kwa tafsiri ya kuwatambua kuwa ninyi mmetumwa kueneza maadili ya kujenga watu kiroho.wito wangu kwenu nawaomba muisaidie Serikali katika mapambano dhidi ya rushwa.mnalo kundi kubwa la waumini wanaowategemea. Tutumie fursa ya kuwa na kundi hili la waumini kuwapelekea habari njema za kiroho ili wawe na utamaduni wa kuwa na matendo mema kwa kutumia imani zao. Tuwakumbushe kuwa na matumaini ya maisha yenye maadili mema ya kiroho. Tuwajengee imani njema inayoambatana na matendo mema. Tukishirikiana Serikali na viongozi wa dini katika hili la maadili mema, tutajenga Taifa lenye watu waadilifu na hivyo kupunguza kero nyingi zinazoikabili jamii ya Watanzania.
7 Yuko mkulima mmoja ambaye alikuwa analima kwa jembe la kukokotwa na ng ombe wawili. Ng ombe mmoja mkubwa, lakini mzee na mwingine mdogo, lakini mwenye nguvu. Kila wakati jembe likikwama, mkulima yule anampiga yule ng ombe mzee anamwacha yule mdogo ambaye ndiye alikuwa anasababisha jembe kukwama kwa kujaribu kujinasua kwenye konga za jembe kila mara. Mpita njia akawa ameona kilichokuwa kinatendeka. Akamuuliza yule mkulima; Vipi bwana, mbona unamchapa huyo ng ombe mzee tu wakati anayesababisha jembe kukwama ni huyo mdogo? Mkulima yule akajibu: Aah! Nimempiga huyu mzee kwa sababu ndiye anayemfundisha huyu mdogo tabia mbaya!! Wahashamu Maaskofu, tumepewa dhamana kama viongozi kuwafundisha waumini wetu tabia nzuri zenye maadili mema. Tutumie nafasi hiyo vizuri. Ni kweli hatutapigwa mijeledi kama mkulima yule alivyokuwa anampiga ng ombe mzee, lakini tunaweza tukalaumiwa na wenzetu kwamba tulipewa jukumu la kuwaongoza, lakini hatujawaongoza vizuri. Vilevile, tusisahau kuwa tabia mbaya za vijana wetu kwa njia moja au nyingine zinatuathiri kama wazazi, au wanajamii. Tutumie nafasi ya uongozi wetu kuwafundisha vizuri waumini wetu na Wananchi wetu kwa ujumla kuhusu Maadili Mema. Wahashamu Maaskofu, hatuwezi kutenganisha dini na maendeleo ya watu. Hivyo, hatuwezi kutenganisha dini na umaskini. Lakini kwa kiasi fulani umaskini unaletwa na watu kutofanya kazi kwa bidii na maarifa, kutojituma na kutokuwa wabunifu. Tunahitaji kufanya kazi kwa bidii na maarifa ili kupata maisha bora. Hakuna njia fupi na rahisi ya maisha bora. Natoa wito kwa viongozi wote nchini kuwaelimisha waumini na wananchi wao juu ya kufanya kazi kwa bidii. Mtusaidie kuwahimiza wajibidishe katika kazi zao kwa kutengeneza maisha yao yawe bora zaidi na hatimaye kuondokana na umaskini. Mwisho Wahashamu Maaskofu, kwa kumalizia, napenda nichukue fursa hii tena kulipongeza Kanisa Katoliki kwa ujumla kwa kuwa na ushirikiano mzuri na Serikali. Ushirikiano huu ni wa kihistoria. Naupongeza uongozi wa Kanisa kwa uamuzi wa kuwekeza katika maeneo ya huduma za jamii zikiwemo shule, vyuo, zahanati, n.k. Serikali itaendelea kushirikiana na Kanisa Katoliki, dini na madhehebu mengine katika kuwahudumia Watanzania. Lengo ni kutimiza kauli mbiu yetu ya Maisha Bora kwa kila Mtanzania. Wahashamu Maaskofu, tumeshiriki kwa sala na ibada tangu tuanze maadhimisho haya. Tumeshuhudia mafanikio ambayo Kanisa limepata kwa nusu karne tangu Baraza hili lianzishwe. Tunamuomba Mungu azidi kulibariki Kanisa hili na viongozi wake wawe na afya njema, nguvu, hekima na busara ili waendelee kuwaongoza kondoo wake kwenye malisho mema.
8 Baba Askofu na Rais wa Baraza, Wahashamu Maaskofu, Wageni Waalikwa, Mabibi na Mabwana, Nawashukuru sana kwa kunishirikisha katika sherehe hii. Nawatakia nyote baraka tele za Mwenyezi Mungu. Mungu atubariki sote, Mungu alibariki Kanisa na waumini wake na Mungu Aibariki Tanzania!!
wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWENYE IBADA YA KUWEKWA WAKFU NA KUINGIZWA KAZINI ASKOFU MARTIN FATAELI SHAO WA DAYOSISI YA KASKAZINI YA KANISA LA
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationInformation for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More information5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationJAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationAzimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]
This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More informationAgano Lililofunikwa Kwa Damu
Agano Lililofunikwa Kwa Damu na Ellis Forsman Agano Lililofunikwa Kwa Damu (The Blood-Sealed Covenant) 1 Agano Lililofunikwa Kwa Damu na Ellis Forsman Oktoba 14, 2012 Agano Lililofunikwa Kwa Damu (The
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013
www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper
More informationUnited Pentecostal Church June 2017
Kwa Nini Tusali? Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa "Chagua" Ladies Prayer International kwa Facebook United Pentecostal Church June 2017 Tuko na wafuasi Facebook katika Marekani, Hong Kong, Philippines,
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationPronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:
More informationPDF created with pdffactory trial version
المملكة العربية السعودية وزارة التعليم العالي الجامعة الا سلامية بالمدينة المنورة عمادة البحث العلمي قسم الترجمة تعريف موجز بالا سلام بل( لغة السواحلية) ١ بسم االله الرحمن الرحیم MAELEZO KWA UFUPI KUHUSU
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationShabaha ya Mazungumzo haya
Karibu Katika Mazungumzo Kuhusu Mchakato wa Uhamasishaji Maendeleo ya Kanisa na Jamii CCMP/UMOJA Shabaha ya Mazungumzo haya Kuwafahamisha viongozi wa makanisa kuhusu Mchakato wa CCMP ambao umekuwa ukitumika
More informationTheolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College
Theolojia 1 Ujumla Mike Taylor Semester 1 2014-2015 Munguishi Bible College MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 i THEOLOJIA Utangulizi! 1 1. Kumfahamu Mungu katika Injili! 3 1.1. Mawazo Makuu 3 1.2. Maana ya
More informationMALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU
MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa
More informationHaja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (
Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Haja Ya Dini Haja Ya Dini Author(s): Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi [3] Publisher(s): Bilal Muslim Mission of Tanzania [4] Katika kijitabu
More informationMAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA
MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA
More informationSonga kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa
Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More informationKITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO
KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa
More informationRipoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationEllen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar
Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ukristo leo unadhihirisha waumini karibu bilioni mbili katika maelfu ya madhehebu tofauti na tofauti na madhehebu. Kati ya hizi, zaidi ya 500 madhehebu
More informationDibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi
Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini
More informationElimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi
Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau
More informationMUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.
MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO. MUHTASARI WA UTANGULIZI WA THIOLOGIA YA USHIRIKA WA NAFSI TATU ZA UUNGU. GRACE COMMUNION INTERNATIONAL LIVING AND SHARING THE GOSPEL MUNGU ANADHIHIRISHWA NA
More informationBUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, 2017 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA:
More informationMAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI
MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha
More informationMukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika
Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika (A Summary Of Arguments For And Against Individual Communion Cups) Na J D Logan Communion Cups) 1 Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi
More informationTAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA
TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0
More informationusudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-
Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa
More information"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.
KUJA KWA KRIST0 MARA YA PILI "ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28. Mara nyingi sana kuja kwa Kristo mara ya pili huangaliwa tu kama fundisho la dini. Ni
More informationRIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI
International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR
ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini
More informationMwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo
More informationKufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007
Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna
More informationMheshimiwa Spika, Mheshimiwa Spika,
HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KATIKA WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, WASANII NA MICHEZO, MHESHIMIWA JOSEPH OSMUND MBILINYI (MB), KUHUSU BAJETI YA WIZARA HIYO KWA MWAKA WA FEDHA
More informationKANISA NA UAMSHO Na Mchg. Dkt. Faith Lugazia
1 KANISA NA UAMSHO Na Mchg. Dkt. Faith Lugazia Awali ya yote namshukuru Mungu wa Utatu aliyenitia nguvu na kuniwezesha kusimama mbele yenu wajoli wenzangu. Pili ninaishukuru Halmashauri Kuu ya Kanisa la
More informationKutetea Haki za Binadamu
Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and
More informationWIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
More informationWEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23
Toleo X Toleo 23 WEWE NI NANI? (Habari ifuatayo ni hadithi ya mambo ambayo yamenakiliwa katika Matendo 19:10-20 SUV). Paulo mtume wa Yesu Kristo alihubiri katika mji wa Efeso kwa miaka miwili. Katika muda
More informationTumaini Kwa Afrika. Thomas Schirrmacher. Hoja 66. Dibaji na Prof. Mchungaji Dk. Thomas K. Johnson. Thomas Schirrmacher Tumaini Kwa Afrika TASCM RVB
Tunawezaje kudhihirisha msingi wa Kibiblia wa tumaini letu na kulithibitisha kwa Wakristo na kwa wasioamini walioshirikishwa? Tunawezaje kutamka matumaini yetu kwa Wabunge, kwa wafanya biashara au kwa
More informationMpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari
More informationElimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi
Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Gervas Zombwe 1 1. Utangulizi Katika mazingira ya kawaida kabisa ndani ya jamii yetu, Imezoeleka kusikia au kuona watu wakioanisha dhana ya elimu
More informationLUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI
LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI SIKOMBE YIZUKANJI YORADI TASNIFU YA KISWAHILI KWA MINAJILI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (MA. KISWAHILI) KITIVO CHA SANAA
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationHii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA TISA. Kikao cha Pili - Tarehe 14 Aprili, 2010
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA TISA Kikao cha Pili - Tarehe 14 Aprili, 2010 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel
More informationUshindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT
Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT 1 Ushindi Ndani ya Kristo Na W. W. Prescott Mfasiri: M. Mwamalumbili Victory in Christ - Kiswahili 2 Yaliyomo Alinipenda Mimi Aliishi kwa ajili Yangu Mimi Alikufa
More informationBUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE. Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma
More informationMipango ya miradi katika udugu
Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi
More informationJuni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia
34567 APRILI 15, 2013 Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia UKURASAWA 3 NYIMBO ZA KUTUMIWA: 114, 113 Juni 10-16 Jinufaishe na Uwanufaishe Wengine kwa KutumiaNenolaMungu UKURASAWA 18 NYIMBO ZA KUTUMIWA:
More informationMaisha Yaliyojaa Maombi
(A Prayer-Filled Life) na Terry Warford (A Prayer-Filled Life) 1 (A Prayer-Filled Life) na Terry Warford Nov 5, 2011 (A Prayer-Filled Life) 2 Sura ya nne nay a tano ya kitabu cha Ufunuo ni vifungu vinavyovutia.
More informationUfunguo wa Kutaalamika Haraka
0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11
More informationSautiElimu. Sauti Yako Isikike
SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian
More informationKiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika
Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to
More informationSummaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili
Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili 1. 2-Muhtasari wa Ukurasa wa Ripoti ya Miaka minne ya Bodi Kuu ya Kanisa & Jamii............................... 2 2. Kamati ya Kawaida ya Malipo ya
More informationHati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/14 DODOMA Mei,
More informationNdugu na dada zangu wapendwa,
UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2014 Na Rais Thomas S. Monson Upendo Asili ya Injili Hakika hatuwezi kumpenda Mungu kama hatuwapendi wasafiri wenzetu katika safari hii ya maisha duniani. ninafurahia mawazo
More informationVol. 113, Namba 1, 2013 ISSN
GAZETI LA KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA TOLEO LA 1, 2013 Bei Sh. 600 Yaliyomo Kanisa kuadhimisha jubili Walutheri wafika milioni 6 NKM Huduma za Jamii aajiriwa Jukumu letu kutunza uumbaji Kanisa
More informationMIONGOZO MIWILI KUPAA NA KUTUNGULIWA KWA AZIMIO LA ARUSHA
KIGODA CHA TAALUMA CHA MWALIMU NYERERE MIONGOZO MIWILI KUPAA NA KUTUNGULIWA KWA AZIMIO LA ARUSHA Yamekusanywa na kuhaririwa na: Bashiru Ally Saida Yahya-Othman Issa Shivji CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationWAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen
1 Index latest update 26. feb. 2008 WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen Wafunaji wa nafsi ABC Mark 16:15-20 Huduma/uiinjilisti Wakristo wachache sana wameitikia mwito wa
More informationKAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA
KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI
More informationMwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza
Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)
More informationUTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha
UTARATIBU WA KANISA Tumemaliza hivi punde ule mkutano mkubwa wa siku, tano usiku kwenye Maskani, ambapo, kwa neema ya Mungu na kwa msaada Wake, nimejaribu sana, kwa Maandiko, kuliweka Kanisa la Bwana Yesu
More informationNilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania
Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza
More informationGRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI
GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI Utambulisho Grace Communion International ni muungano wa washiriki kutoka pembe mbali mbali za dunia hasa nchi zenye washiriki kwa sasa ni 100. Wito wetu ni
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationKocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa.
Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa mabingwa itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa. Mkuu Inahitaji dhabihu. Unahitaji kujisukuma hadi mwisho wako. Lakini nakupa ahadi hii,
More informationHISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU 9 DESEMBA 2011.
Saint Augustine University of Tanzania From the SelectedWorks of Daudi Mwita Nyamaka Mr. Winter December 9, 2011 HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU
More informationMACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI
This booklet on Becoming a Parent was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at. MACHAGUO
More information3 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA NANE. Kikao cha Saba - Tarehe 3 Februari, 2015
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA NANE Kikao cha Saba - Tarehe 3 Februari, 2015 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA
More informationBUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA. Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi)
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU
More informationWatumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1
Watumishi Wa Kristo na Ellis P. Forsman Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1 Watumishi Wa Kristo na Ellis P. Forsman Oktoba 14, 2011 Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 2 Sisi ni watumishi Watumishi
More informationMKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA
More informationKuwafikia waliotengwa
Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E 2 0 1 0 Ripoti
More informationApril 14, 2016 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 52
MOMBASA COUNTY ASSEMBLY HANSARD REPORT Thursday, 14 th April, 2016 The House met at 2.48pm. (Hon. Deputy Speaker (Mr. Mswabah Rashid) in the Chair) PRAYERS Hon. Deputy Speaker (Mr. Mswabah Rashid): Kindly
More informationMaisha Ya Mkristo Ni Nini?
Maisha Ya Mkristo Ni Nini? na Ellis P. Forsman Maisha Ya Mkristo Ni Nini? (What Is The Christian Life?) 1 Maisha Ya Mkristo Ni Nini? na Ellis P. Forsman Oktoba 17, 2011 Maisha Ya Mkristo Ni Nini? (What
More informationwalozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w
MAMLAKA Tunamshukuru Bwana kwa vile alivyo na yale aliyoyatenda. Tukiweza tu kumfikiria hata tukiwa na mahitaji mbalimbali, yeye atatutimizia. Tusiwatazame watu, tusijitazame sisi wenyewe, tumtazame Mungu
More informationMIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara
1 MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara 1. UTANGULIZI Miaka 500 ya matengenezo ya Kanisa inatufanya tuangalie nyuma na kuona jinsi Mungu alivyotumia wanadamu
More information