Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
|
|
- Estella Stone
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1 Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo ya Ushirika - Septemba 2006
2
3 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo ya Ushirika - Septemba 2006
4
5 YALIYOMO Dibaji ii Sera ya Maendeleo ya Ushirika Ushirika ni nini? Kwa nini tunahitaji sera ya ushirika? Serikali imedhamiria kukuza aina gani ya ushirika?...2 Ushirika na Maendeleo Muundo wa ushirika Nani watakaoongoza vyama vya Ushirika? Elimu na Mafunzo ya Ushirika Asasi za kiushirika za Fedha Wajibu wa Serikali Sheria ya Vyama vya Ushirika 2003 na Kanuni za Vyama vya Ushirika Ni aina gani ya vyama vitakavyosajiliwa?...8 Chama cha msingi kitaanzishwaje? Vyama vya Ushirika vya Msingi Haki na Wajibu wa Mwanachama Dhima za Wanachama Usimamiaji wa Vyama vya Ushirika Kazi za Vyama Vilivyosajiliwa Shirikisho la Vyama vya UshirikaTanzania Taarifa zaidi na anwani muhimu USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA i
6 DIBAJI Vyama vya Ushirika vimekuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya Tanzania kwa miaka 75. Ni kweli kwamba vimepata mafanikio mengi na matatizo, katika kipindi chote hicho hakuna taasisi nyingine yoyote zaidi ya Ushirika iliyowaunganisha pamoja watu wengi katika azma na lengo linalofanana.. Baada ya Azimio la Arusha, vyama vya ushirika vilipewa kipaumbele katika kujenga moyo wa kujitegemea. Hata hivyo, kufuatia kuanzishwa kwa mfumo wa soko huru, vyama vya ushirika vimejitahidi kushindana na sekta binafsi na vingi havikuweza kuwapa wanachama wake huduma wanazozihitaji. Serikali imelishughulikia tatizo hili kwa kutunga Sera ya Maendeleo ya Ushirika (2002) ili kuvisaidia vyama vya ushirika kurudisha tena umuhimu wake katika maisha ya watu kiuchumi na kijamii. Sera inaeleza jinsi serikali inavyopanga kuwezesha maendeleo ya eneo maalum la uchumi kama vile kilimo, elimu au ushirika. Wakati ambapo sera zinatueleza mipango ya serikali ilivyo, sheria zinahitajika kuwezesha mipango hiyo kutekelezeka. Sheria zinaeleza jinsi ambavyo vyama kama vile vya ushirika vinavyopaswa kutenda katika njia ya kidemokrasia na ya kibiashara. Sheria: Zinataja haki na wajibu wa taasisi na watu binafsi. Zinaeleza mfumo wa utekelezaji wa maagizo. Zinaongoza mahakama katika kutekelezaji wake. Kwa hiyo, sheria zinawapa wadau haki na majukumu. Sera zinatoa tu mwongozo wa jinsi gani wadau wanavyoweza kuhusishwa. Kijitabu hiki kinaeleza hoja kuu za Sera ya Maendeleo ya Ushirika 1 na Sheria 2 na Kanuni 3 ambazo zimetungwa ili kuifanya sera hiyo itumike. Kimebuniwa kuzisaidia jumuiya kufanya maamuzi kuhusu maendeleo ya ushirika wao wenyewe. Aidha, kitawezesha jamii kuzungumza na wawakilishi wao waliowachagua kuhusu jinsi ambavyo serikali inapaswa kuzifanya sheria katika siku zijazo zitakazowasaidia kuwa na ushirika unaofanya kazi vizuri kwa wale wanaoamua kuwa wanachama. Wadau ni kina nani? Ni wale wote wenye nafasi katika sera, ikiwa ni pamoja na wale ambao: wanaathiriwa na sera wanatekeleza sera wanatoa fedha ili kusaidia sera 1 Sera ya Maendeleo ya Ushirika ya Sheria ya Vyama vya Ushirika Kanuni za Chama cha Ushirika 2004 ii USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
7 SERA YA MAENDELEO YA USHIRIKA Ushirika ni nini? Ushirika ni muungano wa watu ambao wanafanya kazi pamoja kwa hiari ili kufanikisha mahitaji yao ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kupitia shughuli ya biashara inayomilikiwa kwa pamoja na kudhibitiwa kidemokrasia. Ushirika unazingatia maadili ya kujisaidia mwenyewe, jukumu binafsi, demokrasia, usawa na mshikamano. Wanachama wa ushirika wanaamini katika uaminifu, uwazi, uwajibikaji kwa jamii na kuwajali wengine. Kwa nini tunahitaji sera ya ushirika? Serikali na wadau wameamua kuunda sera na sheria mpya kwa ajili ya maendeleo ya ushirika kwa sababu: Vyama vingi vya ushirika havijafanikiwa katika uchumi wa soko huru. Matokeo yake vimeshindwa kutoa huduma za pembejeo, mikopo na masoko ya mazao kwa wanachama. Serikali inauona ushirika kuwa ni muhimu katika kufanikisha malengo ya maendeleo. Wachuuzi binafsi hawajaziba pengo lililoachwa na kuanguka kwa ushirika. Kwa hiyo, watu wanapaswa kuungana ili kutoa huduma kwa ajili ya jumuiya zao. Watu wanaofanya kazi pamoja wanaweza kutatua matatizo ambayo hayawezi kutatuliwa na mtu mmoja mmoja. Sera na Sheria za awali hazikushughulikia ipasavyo baadhi ya masuala ambayo ni muhimu kwa ushirika unaofanya kazi katika soko huru kama vile nafasi ya mwanawake katika Ushirika, kutunza mazingira na wajibu walionao wadau mbalimbali katika maendeleo ya ushirika. USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 1
8 Serikali imedhamiria kukuza aina gani ya ushirika? Serikali inataka ushirika nchini Tanzania ufanye kazi kwa mujibu wa maadili yanayotumika katika nchi nyingi. Maadili hayo yanaitwa Kanuni za Kimataifa za Vyama vya Ushirika: Kanuni Uanachama wa Hiari na ulio wazi Wanachama na Udhibiti wa kidemokrasia Ushiriki wa wanachama katika shughuli za kiuchumi Uhuru na kujitegemea Maana Ushirika uko wazi kwa watu wote walio tayari kukubali majukumu ya uanachama bila ya aina yoyote ya ubaguzi. Wanachama wote wana haki sawa ya kupiga kura (mwanachama mmoja, kura moja). Wanachama wanachangia kwa usawa na kwa kidemokrasia wanadhibiti mtaji wa ushirika wao. Wanachama wanaweza kugawa ziada kwa moja au yote ya madhumuni yafuatayo: kuwekeza katika ushirika wao au kuwanufaisha wanachama kwa uwiano wa hisa zao katika ushirika. Vyama vya Ushirika ni vyombo huru na vinavyojitegemea chini ya uongozi na usimamizi wa wanachama. Endapo ushirika utafanya makubaliano na asasi nyingine, ikiwa ni pamoja na serikali, au kutafuta fedha nje ya ushirika, unafanya hivyo endapo tu wanachama wote wameamua kidemokrasia kuwa hivyo ndivyo wanavyotaka. Pia makubaliano yoyote lazima yahakikishe kuwa ushirika unabakia kuwa huru. Sheria na sheria ndogo za vyama vyote vya ushirika zifuate Kanuni za Kimataifa. Elimu, mafunzo na taarifa Ushirika unatoa elimu na mafunzo kwa wanachama wake na wafanyakazi ili waweze kusaidia maendeleo ya ushirika wao. naujulisha umma mzima kuhusu faida za ushirika. 2 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
9 Ushirika miongoni mwa Vyama vya Ushirika Ushirika kuijali Jamii Ushirika unaimarisha vyama vyote vya ushirika kwa kushirikiana kupitia mitandao ya wananchi, taifa, kanda na ya kimataifa. Ushirika unafanya kazi kwa ajili ya maendeleo ya uchumi, jamii na utamaduni wa wanachama wake na jumuiya nzima. Pia unajali kutunza mazingira na vizazi vijavyo. Ushirika na Maendeleo Kwa miaka michache serikali ya Tanzania imekuwa ikitekeleza Mkakati wa Kupunguza Umaskini. Mchakato huu unatambua umuhimu wa asasi zinazowaunganisha pamoja watu maskini, kama ushirika. Kama sehemu ya programu ya kupunguza umaskini, serikali inataka kuwahamasisha watu kuunda ushirika ili kuboresha matarajio yao ya kiuchumi. Kuwahimiza watu kuunda Serikali ingependa kuona ushirika unapanuka aina tofauti za vyama vya katika sekta mbalimbali, kama vile fedha, ushirika, Serikali inaweza nyumba, viwanda, madini, mifugo, uvuvi, kutoa ushauri kwa watu ni ufugaji nyuki na usafirishaji. Ili watu wengi namna gani kila chama cha iwezekanavyo waweze kuhusishwa katika ushirika kinavyoweza chama cha ushirika, serikali: kuleta manufaa. Itahakikisha kwamba wanawake wanahamasishwa kuwa wanachama kamili wa ushirika. Itasaidia vikundi vyenye biashara ndogo ndogo vinavyohusisha vijana, wanawake, wahitimu wa vyuo wasio na ajira na walemavu kujiunga kwenye ushirika. Muundo wa Ushirika Katika kipindi kilichopita zimekuwepo na ngazi nyingi za ushirika nchini ikiwa ni pamoja na vyama vya msingi, vyama vikuu, vyama vikuu kilele na Shirikisho la Vyama vya Ushirika. Kwa nyakati tofauti vyama vikuu vimepoteza mawasiliano na vyama vyao vya msingi na vikaanza biashara ambazo hazikuhusiani na zile zilizokuwa zikifanywa na vyama vya msingi. Mpango uliopo sasa ni kukifanya chama cha msingi kuwa ngazi muhimu na ya msingi ya ushirika na kuhakikisha kuwa vyote vinajitegemea na vinadumu. Ushirika wa ngazi ya juu unawajibika kutoa ushauri na kujenga uwezo wa vyama vya msingi kibiashara. USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 3
10 Aidha ushirika wa juu una jukumu la kuwa mwakilishi makini wa vyama vya msingi ngazi ya Taifa na Kimataifa katika kutetea haki, kutafuta masoko n.t. Kwa sasa Serikali ina mipango ifuatayo 4 : Kuhamasisha sekta mbalimbali za kiuchumi kuunda ushirika. Ushirika unapaswa Kusaidia vikundi vya biashara ndogo ndogo kuendeshwa kama biashara kusajiliwa katika ushirika. endapo utataka kudumu Kuhamasisha uanzishaji wa asasi za kifedha katika soko huria katika vyama vya Ushirika vya msingi. Kuwezesha vyama vya ushirika kujijengea uwezo wake wa fedha. Kusaidia vyama vya ushirika kupata mikopo kutoka benki. Kutoa udhamini kwa baadhi ya mikopo kutoka kwenye mabenki kwenda vyama vya ushirika. Kuhamasisha vyama vya msingi kuwa na biashara ya pamoja na vyama vingine vya msingi ili kuongeza ufanisi. Pia serikali kuendelea kutoa ushauri kuhusu baadhi ya vyama vya ushirika kuungana kila itakapoona inafaa. Serikali inatambua kuwa ushawishi mkubwa wa kisiasa katika kuendesha ushirika hapo zamani mara nyingi ulisababisha uendeshaji mbaya wa ushirika Nani watakaoongoza vyama vya Ushirika? Siku zilizopita vyama vingi vya msingi vilikuwa vikiongozwa vibaya kwa sababu: Baadhi ya viongozi walikuwa wakishika madaraka kwa muda mrefu sana. Hapakuwa na sheria za kuwabana viongozi kuwa watendaji wazuri na kufanya kazi kwa maslahi ya wanachama. Wanasiasa wameingilia mara kwa mara katika masuala ya vyama vya Ushirika. Kumbukumbu sahihi na taarifa za utendaji havikuwekwa na hesabu zilizokaguliwa hazikuwasilishwa katika Mkutano Mkuu wa Mwaka. Viongozi wamekuwa wakitoa maamuzi bila ya kuwahusisha wanachama katika Mkutano Mkuu wa Mwaka. Ili kuboresha hali hii serikali inataka kuhakikisha kuwa viongozi wa vyama vya Ushirika: Wanazo sifa za kufanya kazi za uongozi Watiifu kwa wanachama wa chama cha Ushirika Wanawajibika kwa wanachama wao kupitia uwasilishaji kwa bodi na mikutano mikuu ya mwaka wa taarifa za ukaguzi wa hesabu, makisio, mipango ya shughuli na taarifa za utendaji 4 Kupitia mabadiliko ya ushirika na mpango wa kufanya ushirika uwe wa kisasa (CRMP), mpango wa miaka kumi, ambao ulianza Januari USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
11 Wanachaguliwa kidemokrasia na wanachama Hawana maslahi ya nje ambayo yatakiathiri chama cha Ushirika. Ili kufanya hivyo, sera iliyopo inaainisha kwamba serikali ina mpango wa: Wafanyakazi lazima wawe na ujuzi unaofaa ili kuhakikisha ushirika una faida kwa wanachama. Kuunda kamati imara za usimamizi katika vyama vya Ushirika. Kuweka ukomo wa muda wa uongozi katika Vyama vya Ushirika Kuanzisha kanuni za maadili ili kuwafanya viongozi wawajibike kwa wanachama na kwa kamati. Pia serikali itahakikisha kuwa wafanyakazi ambao wanaajiriwa wanafanyakazi kwa uadilifu, uaminifu na uwajibikaji kwa wanachama. Kwa sababu hii, serikali itahamasisha ushirika kuwavutia wafanyakazi wenye sifa kwa kuweka mazingira mazuri ya kazi. Elimu na Mafunzo ya Ushirika Serikali inaamini kuwa ni muhimu kuwaelimisha watu katika maadili ya ushirika. Wakati soko huru lilipoanzishwa, mafunzo yasiyotosheleza yalitolewa kwa ushirika kuhusu namna ya kujiendesha katika mazingira mapya. Matokeo yake biashara ya Ushirika imeshuka kwa zaidi ya asilimia 50 Ushirika unashughulikia kiasi kidogo cha biashara ya wananchi ikilinganisha na hapo awali. USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 5
12 Sera inasisitiza kusisitiza umuhimu wa ukuzaji wa elimu ya ushirika, ambayo italenga: Kuwa na viongozi wa ushirika walioelimika na wanaowajibika ambao wanaweza kudumisha maadili ya ushirika na kuendesha shughuli za biashara kwa ufanisi. Kuboresha usimamizi, biashara na ujuzi wa ujasiriamali wa wafanyakazi wa ushirika na wajumbe wa kamati. Kuhakikisha kuwa wanaushirika wanaarifiwa na kufahamu hali halisi ya shughuli za uchumi wa ushirika, kazi na majukumu yao na manufaa yanayotokana na uanachama wao katika ushirika. Kuuarifu umma kwa ujumla kuhusu hali halisi ya ushirika. Kuingizwa kwa Elimu ya Ushirika kwenye Mitaala na mfumo wa Elimu. Kuhakikisha kuwa ngazi zote za uongozi wa kiutawala wana hamasishwa kuhusu maadili na umuhimu wa ushirika. Asasi za Fedha za Ushirika Baada ya kuanzishwa kwa soko huru, Serikali ilipunguza kusaidia Vyama vya Ushirika moja kwa moja. Kwa kuwa ushirika haukuweza tena kupata fedha kutoka benki, ina maana ilikuwa vigumu kutoa huduma zinazofaa kwa wanachama. Wachuuzi binafsi waliweza kuchukua nafasi na kujinufaisha na hali hiyo, lakini matokeo yake yamekuwa ni huduma duni kwa wazalishaji wadogo. Serikali inazichukulia asasi za fedha za ushirika kama mbadala muhimu kwa mfumo wa uendeshaji benki kibiashara. Sababu ni kwamba ushirika unaweza kuhamasisha kuweka akiba na uangalifu katika kutumia fedha. Pia mikopo inaweza kutolewa kwa 6 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
13 wanachama kwa masharti nafuu kuliko ile itolewayo na benki za biashara. Asasi za kiushirika za fedha ni muhimu kwa sababu benki za biashara zinavichukulia vyama vya Ushirika kuwa havikopesheki. Mikopo inapaswa kupatikana kwa urahisi kwa wanachama wa SACCOs katika vipindi muhimu vya mwaka. Hivyo, Serikali inataka kuhamasisha uundaji wa asasi za fedha za ushirika kama vile: Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) Serikali inatambua kuwa kasi ya ukuaji wa SACCOS imekuwa ndogo, hususan katika maeneo ya vijijini. SACCOS nyingi zimeanzishwa mijini na maeneo ya kazi. Matokeo yake wanachama wa vyama vya msingi vijijini wameshindwa kupata mikopo. Mfumo wa zamani wa Serikali kujihusisha katika mambo yote ya uhai wa ushirika ulikuwa na gharama kubwa kwa nchi. Ili kuboresha hali hiyo, serikali inahamasisha uanzishaji wa SACCOS katika maeneo ya vijijini. Ushauri utatolewa katika ngazi ya chini kuhusu kuanzisha SACCOS na msaada wa kitaalamu pia utapatikana kwa SACCOS zote zilizopo ili ziweze kuboresha huduma zao na kuwa endelevu. Benki za Ushirika Uanzishaji wa benki za ushirika utakuwa ni sehemu muhimu ya uanzishaji wa asasi za fedha za ushirika zilizo imara. Serikali imeazimia kuhamasisha na kusaidia uanzishaji wa benki za Ushirika ili baadaye kuwa na benki ya Ushirika ya kitaifa iliyo imara. Katika ngazi ya Wilaya Ofisa Ushirika wa Wilaya atamuwakilisha Mrajis. Jukumu la Serikali Siku za nyuma serikali ilikuwa na jukumu kubwa katika ushirika. Ilijihusisha kwa kiasi kikubwa katika kutoa pembejeo, fedha na mafunzo. Kwa siku zijazo Serikali itawajibika katika uandaaji tu wa mazingira mazuri ya ushirika kustawi. Mihimili mikuu ya kukua itakuwa wanachama na menejimenti ya ushirika wenyewe. Lengo ni kuwezesha vyama vya ushirika kujenga uwezo wa kujitegemea kidemokrasia na kujimudu kiuchumi. USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 7
14 SHERIA YA VYAMA VYA USHIRIKA Na. 20 YA 2003 NA KANUNI ZA VYAMA VYA USHIRIKA ZA 2004 Sheria na kanuni hizi zinaelezea jinsi ushirika unavyopaswa kuanzishwa na kuendeshwa nchini Tanzania. Zinakusudia kutekeleza kwa vitendo sera ambayo tumekuwa tunaizungumzia hapo juu.. Sheria ya Vyama vya Ushirika inaeleza kwamba ushirika unapaswa kuanzishwa na kuendeshwa kwa mujibu wa Kanuni za Kimataifa za vyama vya Ushirika zilizotajwa mwanzoni mwa kijitabu hiki.( Ukurasa wa 2-3) Serikali na Waziri mwenye dhamana ya Ushirika wana wajibu wa kuunda sheria ambazo zinahamasisha uanzishwaji wa ushirika nchini. Aidha Rais kumteua Mrajis wa Vyama Vya Ushirika ambaye ndiye Afisa msimamizi wa utekelezaji wa Sheria na Kanuni zake. Kazi za Mrajis ni pamoja na: Kusajili, kuendeleza, kukagua na kuvishauri vyama vya ushirika. Kumshauri Waziri wakati vyama vya ushirika vinapohitaji msaada. Kuhamasisha uanzishaji wa vyama vya ushirika mbali mbali katika maeneo yote ya uchumi. Kwa sasa sera ya Serikali ni kuhamasisha ukuaji wa kujitegemea wa ushirika kwa kuwapa watu taarifa na ushauri ambao ni rahisi kuufuata na ambao unapatikana kwa urahisi. Kadri ushirika utakavyokua na kukomaa ndivyo ambavyo Mrajis wa Vyama Vya Ushirika atakamilisha majukumu yake (ya mafunzo, ushauri n.k.) kwa vyama vyenyewe, na kubakia na majukumu ya lazima ya usajili za usimamizi wa Sheria. Ni aina gani ya vyama vinavyoweza kusajiliwa? Kwa sababu serikali imepania kuhamasisha uanzishwaji wa ushirika katika sekta zote za uchumi, Mrajis anaweza kusajili ushirika katika maeneo kama vile: Kilimo, mifugo, uvuvi au ufugaji nyuki Uchimbaji madini Akiba na kukopa, Biashara ya jumla au rejareja miongoni mwa wanachama Viwanda Ushirika wa Nyumba unaojishughulisha na ujenzi, majengo na programu za nyumba kwa wanachama wao Ushirika wa ujuzi maalum n.k. 8 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
15 Chama cha msingi kitaanzishwaje? Chama cha msingi kinaweza kuanzishwa na: Watu 50 au zaidi kama ni chama cha kilimo Watu 20 au zaidi kama ni ushirika wa kuweka na kukopa Watu 10 au zaidi kama kinahusisha watu wenye ujuzi maalumu Watu 10 au zaidi kwa aina nyingine za Vyama vya ushirika Nani anaweza kuwa mwanachama? Umri wake haupungui miaka kumi na nane na mwenye akili timamu Yuko katika shughuli inayohusu chama cha msingi Ana mahitaji yanayofanana na ya wanachama wengine Anaweza kulipa ada na kununua hisa Hata hivyo Kijana mwenye umri Chama cha Ushirika cha Mwanzo ni asasi ya uchumi au kijamii inayoanzishwa kwa hiari na watu binafsi wenye maslahi sawa na kufanya kazi pamoja kama chama. usiopungua miaka 15 anaweza kuwa mwanachama na haki zote za kuwa kiongozi katika chama cha Ushirika cha shule. USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 9
16 Vyama vya Ushirika vya awali, na jinsi ya kuanzisha Chama cha Ushirika kama huna wanachama wa kutosha Serikali itavitambua na kuvilea vikundi vya watu wenye muelekeo wa Ushirika hatimaye viwe vyama vya Ushirika kamili. Ili kuanzisha Ushirika lazima pawe na angalau watu watano. Ili kuweza kutambuliwa, kikundi kinatakiwa kwanza kuandika barua kwa Ofisa Ushirika wa Wilaya kuelezea nia yake na hivyo kuomba kutambuliwa. Mwombe msaada Ofisa Ushirika wa Wilaya wakati wa kukamilisha kazi hizo. Uandikishwaji wa chama utakuwaje? Wanachama wa Ushirika wa awali wapange kukutana chini ya uenyekiti wa afisa Ushirika wa wilaya ili kuchagua Bodi ya uundaji yenye Mwenyekiti na Katibu. Bodi ya uundaji itabidi ikamilishe majukumu yafuatayo: Kuamua ni aina gani ya chama kitakachoundwa Kutayarisha sheria ndogo za chama; Kutathmini kiwango cha shughuli cha wanachama waanzilishi Kutabiri chama kitakuwa na wanachama wangapi wa siku zijazo na viwango vya shughuli ambazo chama kitafanya Upembuzi yakinifu utajumuisha taarifa kuhusu idadi ya wanachama muhimu ambao chama kinaweza kuwa nao na viwango vyao vya biashara. Pia utazungumzia uwezo wa uongozi wa chama ili kuhakikisha chama kinapata faida na kuendeshwa kwa maslahi ya wanachama wote. 10 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
17 Kuandaa taarifa ya upembuzi yakinifu Kuandaa orodha ya wanachama waanzilishi na kurekodi mtaji wa hisa zao na michango Kuandaa orodha ya wanachama wanaotarajiwa na kurekodi mtaji wa hisa na michango wanayoweza kutoa Kuandaa mfumo mzuri wa utunzaji wa hesabu na nyaraka mbalimbali. Kuteua mwakilishi mfawidhi wa kuwakilisha kikundi katika mambo yote ya kiraia USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 11
18 Sheria ndogo? Kila kikundi chenye mwelekeo wa Ushirika na chama cha Ushirika kinapaswa kuwa na masharti ili kuhakikisha kuwa vinaongozwa katika njia ambayo inawanufaisha wanachama wote kwa usawa. Masharti haya yanajulikana kama sheria ndogo. Aina mbalimbali za vyama zinaweza kutunga sheria ndogo ndogo za aina mbalimbali. Kwa mfano, chama cha ushirika wa Akiba na Mikopo (SACCOS) kitakuwa na sheria ndogo tofauti na za chama cha ushirika wa kilimo. Inaweza kuwa muhimu kupata msaada kutoka kwa Afisa Ushirika wa Wilaya au mtu mwingine mwenye sifa husika wakati wa kutengeneza sheria hizo ndogo. Kuna idadi ya sheria ndogo ambazo zinapaswa kutungwa na aina zote za vyama. Sheria hizo ndogondogo zitafafanua: Jina la chama na mahali pa kufanyia shughuli zake. Lengo la chama. Madhumuni ya kuomba fedha kwa ajili ya chama na jinsi fedha zitakavyotunzwa, kutumiwa au kuwekezwa. Kanuni za uanachama ikiwa ni pamoja na masharti ya kuingia, hisa na ada ya kuingilia. Kanuni kuhusu malipo, kama yapo, iwapo mwanachama atafukuzwa au kuacha. Hisa zitahamishiwa kwa nani endapo mwanachama atafariki. Kiwango cha madeni ya mwanachama katika kikundi na jinsi kitakavyoamuliwa. Jinsi mikutano mikuu itakavyoendeshwa na nini kitakachoamuliwa katika mikutano hiyo. Kanuni kuhusu kazi za wajumbe wa Bodi, jinsi watakavyochaguliwa, watakaa madarakani kwa muda gani na wataondolewaje kama itabidi kufanya hivyo. Kanuni kuhusu kazi za wajumbe wa Bodi, jinsi watakavyochaguliwa, watakaa katika nafasi hizo kwa muda gani na wataondolewaje kama itabidi kufanya hivyo. Kumwidhinisha ofisa kutia saini nyaraka kwa niaba ya chama. Vyama vya aina tofauti vitakuwa na masharti mengine tofauti. Kwa mfano, chama cha ushirika wa Akiba na Mikopo kitahitaji masharti ya ziada kuhusu viwango vya riba, masharti ya mikopo, dhamana ya mikopo na kanuni za kushindwa kulipa deni. Chama cha ushirika wa biashara kitahitaji sera ya kupanga bei kuongezea katika kanuni zilizopo. 12 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
19 Faini: Ni muhimu kutambua kwamba vyama vinaweza kuunda masharti ambayo yanaweza kumtoza faini mwanachama endapo atakiuka kanuni za chama. Faini hizo zitakuwa kama faini za kisheria kwa mujibu wa Sheria ya Ushirika na zinaweza kulipwa mahakamani kama ni lazima. Pindi wanachama wa kikundi chenye muelekeo wanapotaka kuwa chama cha ushirika cha awali watakamilisha taratibu zote za uanzishwaji wa chama, wanapaswa kutuma maombi kwa Mrajis au mwakilishi wake. Wawakilishi wa Mrajis ngazi ya mkoa (Mrajis Msaidizi) na ngazi ya Wilaya (Afisa Ushirika wa Wilaya). Ni kitu gani kinachohitajika kwa ajili ya Maombi ya usajili? Nakala iliyothibitishwa ya azimio lililopitishwa katika mkutano wa kwanza wa kikundi na Afisa Ushirika wa Wilaya Nakala nne za masharti za chama zilizopendekezwa Nakala nne za taarifa ya upembuzi yakinifu Hati nyingine zozote zitakazoombwa na Mrajis Ada ya Usajili Mrajis au Afisa Ushirika wa Wilaya pia wanaweza kuomba barua kutoka kwa watu wanaokusudia kujiunga, taarifa zaidi kuhusu kuwepo kwa mtaji au taarifa zaidi kuhusu uwezo wa chama kinachotarajiwa kusimamia biashara yake vizuri. Kama maombi yatakubaliwa Mrajis atatoa barua ya utambuzi. Barua hiyo inakiruhusu kikundi kufanya shughuli kwa miaka miwili kama chama kilichopo katika majaribio mpaka kitakapotimiza masharti yanayotakiwa ili kuwa chama kamili cha ushirika. Kama chama hakikutimiza masharti baada ya miaka miwili, kwa mfano hakikupata wanachama wa kutosha, basi barua hiyo itabatilishwa. Endapo Mrajis atakataa kusajili chama, wanachama wana haki ya kukata rufaa kupinga uamuzi huo kwa Waziri wa Ushirika na Masoko ndani ya siku 60. Uamuzi wa Waziri ni wa mwisho. USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 13
20 Haki na Wajibu wa Wanachama Wanachama wote wa vyama vya ushirika mara wanapolipa kiingilio, hisa, na malipo mengine wanakuwa na haki zifuatazo: Majina na saini zao kuingizwa katika Daftari la Wanachama Kupiga kura na kupigiwa kura. Kila mwanachama ana kura moja bila ya kujali idadi ya hisa anazomiliki Kupewa hati za hisa mara tu wanapolipia hisa zao Kushiriki katika nafasi za uongozi Kuitisha mikutano kwa mujibu wa sheria ndogo Kuteua mrithi-kufuatana na masharti ya chama. Kupata taarifa kuhusu masuala yote ya chama na kuweza kukagua nyaraka za chama Kuarifiwa kuhusu masuala yote ya chama na kuweza kukagua nyaraka za chama Kupata kipato kutokana na shughuli za biashara ya chama Kushiriki katika kuandaa sheria ndogo za chama Kujitoa katika uanachama Kufanya uchunguzi katika masuala ya chama Kushiriki katika kuandaa na kurekebisha masharti ya chama Kukata rufaa Kwa vyama vya Akiba na Mikopo,mwanachama ana haki ya kulipa kwa kuzingatia mwanachama ana Akiba na amana za kutosha Tahadhari Ili kuhakikisha kuwa hakuna mwanachama hata mmoja anayekuwa na udhibiti mkubwa katika chama, ni kinyume cha sheria kwa mwanachama mmoja kumiliki zaidi ya moja ya tano ya hisa za chama. Kwa sababu kama hizo, ni kinyume cha sheria kwa kampuni iliyosajiliwa kuwa mwanachama wa chama cha ushirika mpaka Mrajis aandike barua inayoidhimisha kuwa kampuni hiyo itakuwa na manufaa kwa chama. Pia ni kinyume cha sheria kwa mtu kuwa mwanachama wa vyama viwili vinavyojihusisha na aina moja ya shughuli (katika eneo moja) kwa kuwa hali hiyo italeta mgongano wa kimaslahi. Wanachama wana Wajibu ufuatao: Kufuata masharti na taratibu za chama. Kulipia hisa zao, stahili na madeni mengine yoyote wanayodaiwa na chama Kushiriki katika shughuli za chama Kuhudhuria mikutano ya chama na kufuata maamuzi yaliyotolewa 14 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
21 Kuteua warithi wao Kulinda na kutetea mali ya chama Ukomo wa uanachama Mtu anaweza kukoma kuwa mwanachama wa chama endapo: Ataacha kumiliki hisa au kutoa michango iliyowekwa katika masharti ya chama. Atahama na kwenda mbali na eneo la chama Atafukuzwa au kusimamishwa baada ya kufanya kosa Kutunza na kulinda sifa na heshima ya chama Kifo Wanachama wote lazima wafahamu kuhusu biashara ya chama. Kushindwa kushiriki katika shughuli za kiuchumi za chama kufuatana na masharti ya chama Kurukwa akili Kuacha uanachama kwa hiari. Atakuwa hashiriki katika shughuli za chama. Dhima za wanachama Wanachama wanaweza kubeba dhamana ya madeni ya chama katika moja ya njia mbili: Dhima kwa hisa Hiki ni kiwango cha kawaida cha dhima na kinamaanisha kuwa mwanachama anawajibika kulingana na uwiano wa hisa zake za chama. USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 15
22 Dhima kwa dhamana Kama masharti ya chama yanaruhusu, mwanachama anaweza kukubali kuwajibika kwa kiasi kikubwa kuliko hisa yake. Hii inajulikana kama dhima kwa dhamana. Usimamizi wa Vyama vya Ushirika Mikutano Mikuu Udhibiti wa jumla wa chama cha ushirika unafanywa na wanachama katika mikutano mikuu. Mikutano Mikuu inapaswa kufanywa angalau mara moja kwa mwaka. Masuala yote ya chama yanaweza kujadiliwa, yakiwemo; Uchaguzi, kusimamishwa au kuondolewa kwa Bodi Kuteua Mkaguzi wa Hesabu Kuzingatia na kuridhia hesabu zilizokaguliwa Kuamua kuhusu mgao wa ziada Kuamua kiasi cha posho itakayotolewa kwa wa wajumbe wa Bodi na maofisa wasiolipwa mishahara Kuzingatia bajeti na mipango ya kazi Kuzingatia marekebisho ya masharti ya chama Kuamua kuhusu ununuzi au uuzaji wa mali za chama Kubadili wajumbe wa Bodi mara kwa mara kunahakikisha kuwa hakuna mtu au kikundi kinachoweza kuwa na mamlaka zaidi katika chama. Angalizo Ili kutoa maamuzi katika mkutano lazima pawepo na angalau nusu ya wanachama, au wanachama 100, wowote walio wachache. Wanachama wote lazima wapewe notisi ya wiki tatu ya tarehe, mahali na muda wa mkutano. Bodi Kila chama cha ushirika ni lazima kichague Bodi ya wajumbe wasiopungua watano na wasiozidi tisa Ili kuhakikisha kuwa hakuna mwanachama au kikundi cha wanachama wanaojaribu kuwa na sauti zaidi katika kuendesha chama, hakuna mjumbe wa Bodi atakayeshika nafasi ya ujumbe kwa zaidi ya miaka tisa mfululizo Kwa kuongeza, Mrajis au mwakilishi wake, Ofisa Ushirika wa Wilaya, anapaswa kwanza kuwapima Viongozi na watendaji wote kabla ya kuwaajiri. Katika miaka ya kwanza ya chama, theluthi moja ya Wajumbe wa Bodi wanapaswa kubadilishwa kila baada ya miaka mitatu ili kuendana na sheria 16 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
23 Hakuna mwanachama atakayechaguliwa kwenye Bodi kama anamiliki, anasimamia au ana ushawishi katika biashara inayofanana na shughuli za chama Kila mwaka, kila mjumbe wa Bodi lazima ajaze fomu akitaja mali na biashara alizonazo, anazosimamia na lazima wakabidhi fomu hizo kwa Mrajis. Bodi inawajibika kuhakikisha kuwepo kwa uongozi mzuri wa chama kwa mujibu wa masharti ya chama. Ili kusaidia katika kazi hiyo Bodi inaweza kuajiri watu wanaofaa kusimamia uendeshaji wa kila siku wa chama. Kwa mujibu wa sheria, hakuna mtu atakayeajiriwa na ushirika kama hana elimu na ujuzi wa kufanya kazi iliyotangazwa. Kwa mfano, ni kinyume cha sheria kuwaajiri wafanyakazi kwa misingi ya uhusiano wao na mjumbe wa Bodi, rangi yao, kabila au utajiri wao. Pia ni kinyume cha sheria kwa mtu kutoa malipo ili kushawishi uamuzi wa kuajiriwa. Aidha, kila mfanyakazi wa chama cha msingi anapaswa kudhaminiwa na mdhamini. Mdhamini atawajibika endapo mfanyakazi atahusika na upoteaji au kushindwa kulipa deni. Mikutano Mikuu Maalumu Kama theluthi moja au zaidi ya wanachama wanataka kujadili jambo maalumu wanaweza kuitisha Mkutano Mkuu Maalum. Ili kufanya hivyo, wanachama husika wanapaswa kuandika barua inayoelezea dhamira yao na ni lazima watume nakala ya barua hiyo kwa Mrajis. Inatakiwa watoe notisi ya siku saba. Mrajis (au Afisa aliyemteua), ana mamlaka ya kuitisha Mkutano Mkuu Maalumu wa chama kama anaona ni lazima. Hii inaweza kutokea kufuatilia ukaguzi wa mambo ya chama. Katika mkutano huo Mrajis au Afisa aliyemteua ana mamlaka ya kuisimamisha Bodi iliyopo na kuweka Bodi ya muda kama itaonekana kuna ulazima wa kufanya hivyo. Anaweza pia kutoa amri ya kukivunja chama. USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 17
24 Kazi za Vyama Vilivyosajiliwa Kuweka Kumbukumbu Vyama vyote vya ushirika vinapaswa kuweka kumbukumbu ambazo zinaweza kukaguliwa na wanachama na Mrajis au mwakilishi wake. Kumbukumbu hizo ni pamoja na: Orodha ya wanachama na hisa zao Maelezo ya hesabu za biashara zinazohitajika kwa wanachama zinazoonyeshwa kwa umma. Hesabu zilizoidhinishwa na Mkaguzi wa Hesabu aliyechaguliwa na Mkutano Mkuu na kuidhinishwa na Mrajis Nakala ya Sheria ya Ushirika 2003, Kanuni za Vyama vya Ushirika 2004 na masharti ya chama chenyewe Marekibisho ya Masharti ya Chama Marekebissho ya masharti ya chama ambayo yameidhinishwa na mkutano mkuu yanapaswa kupelekwa kwa Mrajis kwa ajili ya kuidhinishwa. Hilo linafanyika ili Msajili aweze kuhakikisha kuwa mabadiliko hayo ni kwa mujibu wa sheria. Taarifa ya Hesabu Kila chama cha ushirika kinapaswa kutunza taarifa sahihi za hesabu. Mkaguzi wa Hesabu aliyesajiliwa anapaswa kukagua hesabu hizo angalau mara moja kwa mwaka. Hesabu hizo zinapaswa kuidhinishwa na Mrajis na wanachama katika Mkutano Mkuu wao na baadaye kutumwa kwa Mrajis. Kama chama kitashindwa kutayarisha hesabu katika miezi mitatu ya mwisho ya mwaka wake wa fedha, Mrajis atakuwa na uhuru wa kuondoa Bodi ya Uongozi iliyopo madarakani na kuweka nyingine. Wajumbe wa Bodi wanaoondolewa kwa jinsi hiyo, hawawezi kuchaguliwa tena kwenye Bodi kwa miaka sita.. Endapo Mrajis anaona ni muhimu, anaweza kukagua akaunti za chama zilizopo benki au mahali popote na anaweza kutoa amri ya kukielekeza chama kuchukua hatua ya kurekebisha kasoro zozote zitakazoonekana. Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC) TFC ni nini? Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC) ni asasi mama ya ushirika kitaifa ambayo inakuza, kuhudumia na kuratibu maendeleo na ustawi wa vyama vyote vya ushirika Tanzania bara. TFC ni asasi isiyo ya Kiserikali inayojitegemea na isiyo ya kisiasa inayomilikiwa na wanachama na kusimamiwa kwa mtazamo wa kanuni na maadili ya ushirika yanayotambuliwa kimataifa. Ni mwanachama wa Muungano wa 18 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
25 Vyama vya Ushirika Duniani (ICA) na linashirikiana na mashirika mengine kadhaa ya kitaifa na kimataifa yenye muelekeo unaofanana. TFC lilisajiliwa tarehe 8 Desemba 1994 (Namba ya usajili 5503). Wanachama wa TFC ni nani? Wanachama wake wa sasa ni: Vyama vikuu vilele vya ushirika vinavyosimamia mazao ya pamba na tumbaku; Vyama vikuu maalum vinavosimamia Ushirika wa viwanda na Akiba na Mikopo nchini TICU na SCCULT 5 ; na Vyama vikuu vya Ushirika wa mazao vitano ambavyo ni Karagwe District Cooperative Union (KDCU), Kagera Cooperative Union (KCU), Tandahimba-Newala Cooperative Union (TANECU), Mtwara-Masasi Cooperative Union (MAMCU) na Kilimanjaro Native Cooperative Union (KNCU). Uanachama wa Shirikisho ni wazi kwa Vyama vyote vya Ushirika kuanzia ngazi ya Msingi mpaka Ngazi ya Vyama vikuu vilele ili mradi chama hicho si mwana chama wa chama kingine ngazi ya kati. Mfumo mzima wa TFC unafanyiwa rejea ili kubaini maeneo muafaka ya kufanyia maboresho kwa manufaa na maendeleo ya wanachama. Uanachama wa jumla wa TFC unajumuisha Vyama vya msingi 5,700 vyenye wanachama binafsi zaidi ya 700,000. Maarubu ya TFC Shirikisho litajitahidi kuwa asasi mama ya ushirika ya taifa yenye uhai ambapo aina zote za ushirika zitaunganishwa katika kuvutia na kuhamisha maadili ya ujasiriamali na utawala bora. Madhumuni yake ni kuimarisha uendelevu wa ushirika ili wanachama wafaidike moja kwa moja kutokana na kupambana kwao dhidi ya umaskini kupitia ushirikishwaji kiuchumi katika ujenzi wa uchumi. 5 TICU Tanzania Industrial Cooperative Union Ltd; and SCCULT Savings and Credit Cooperative Union League of Tanzania. USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA 19
26 Malengo ya TFC Malengo yake ni kujenga msingi imara wa ushirika kwa: Kuwezesha na kuratibu uanzishwaji, maendeleo na ukuaji wa ushirika endelevu na wa kidemokrasia; Kufanya utafiti na kutoa huduma za ushauri kwa vyama vya ushirika wanachama katika maeneo ya masoko, biashara, fedha, bidhaa na huduma mpya; Kukusanya takwimu na taarifa kuhusu hali ya ushirika, masoko na bei na kuvisambaza kwa wanachama; Kuanzisha elimu shirikishi ya ushirika na programu za mafunzo miongoni mwa wanachama wake; na Kutangaza na kuhamasisha kuhusu aina zote za shughuli za ushirika nchini. Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi: SHIRIKISHO LA VYAMA VYA USHIRIKA TANZANIA Ghorofa ya 9, Ushirika Building, Barabara ya Lumumba, S.L.P 2567, Dar es Salaam. Simu: 255 (0) Faksi: 255 (0) Baruapepe: ushirika@ushirika.co.tz 20 USHIRIKA NA MAENDELEO TANZANIA
27
28 SHIRIKISHO LA VYAMA VYA USHIRIKA TANZANIA LINGEPENDA KUPATA MAONI YAKO KUHUSU KIJITABU HIKI. TAFADHALI ANDIKA KWA: Katibu Mtendaji, Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania, Ghorofa ya 9, Jengo la Ushirika Mtaa wa Lumumba S.L.P Dar es Salaam Simu: 255 (0) Nukushi: 255 (0) Barua pepe: ushirika@ushirika.co.tz Tovuti: TAARIFA ZAIDI Kwa taarifa zaidi kuhusu sheria, kanuni na taratibu zinazoongoza vyama vya ushirika kuna nyaraka kuu tatu za kusoma: Sheria ya Vyama vya Ushirika Na. 20 ya 2003 Kanuni za Vyama vya Ushirika 2004 Sera ya Maendeleo ya Ushirika 2002 Inawezekana kupata nyaraka hizi kutoka kwa: Ofisa Ushirika wa Wilaya wako; - Mrajis Msaidizi wa Mkoa wako; - Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (anwani ya hapo juu); au Mrajis wa Vyama Vya Ushirika, Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, S.L.P. 201, Dodoma.
Information for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More informationKUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.
KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationMpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari
More informationAzimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]
This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)
More informationSonga kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa
Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided
More informationNGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA
NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.
More informationJifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti
Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu
More informationUzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania
Uzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wapilipili Tanzania Wildlife Division, Tanzania Wildlife
More informationMWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18
MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2
More informationKimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:
Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationJAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
More informationMAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI
MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha
More informationMKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationMWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI
MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationRIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI
International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3
More informationHuduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig
KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1
More informationRipoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya
More informationKAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA
KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationTANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko
TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,
More informationTAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA
TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationMALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU
MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa
More informationIn the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment
In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationHAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII
HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY
More informationProgramu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi
Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini
More informationUNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI
UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationKutetea Haki za Binadamu
Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and
More informationRIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
More informationIn the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment
In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationKITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO
KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More informationDibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi
Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA
More informationKuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia
Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationJHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI
JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika
More informationUKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)
Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni
More informationMradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda
WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya
More informationTAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014
TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...
More informationTIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees
TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More informationWaandishi: wa Toleo la 5. Scholastica Jullu Athanasia A. Soka Safina Hassan Mary Njau. Toleo la 5: 2008 ISBN
KIONGOZI CHA SHERIA Hakimiliki 2008 Kimetolewa na: Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) Waandishi: wa Toleo la 5 Scholastica Jullu Athanasia A. Soka Safina Hassan Mary Njau Toleo la 5: 2008 ISBN
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationSera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji
Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na
More informationUFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI
JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MFUMO WA RUZUKU YA MAENDELEO YA MTAJI WA SERIKALI ZA MITAA (LDCDG) UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI Kijitabu cha Mshiriki
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationMAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA
MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA
More informationORDER NO BACKGROUND
In the matter of an Application by the DAR ES SALAAM URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (DAWASA) For a Tariff Adjustment, Submitted on January 8 th, 2008 (TR-W-08-001) ORDER NO. 08-001 1.0 BACKGROUND
More informationNa Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4
;II. -~ ~.! ~ l Na Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4 ~n.~ SURA YA KWANZA SHERIA YA ARDHI 1 UTANGULIZI Sura hii itaiangalia ARDHI na umuhimu wake katika maisha ya binadamu. Ardhi ni rasilimali
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationWIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013
www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper
More informationElimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...
Elimu Bora, lakini... Shukrani za dhati kwa wote waliotusaidia katika kutayarisha kijitabu hiki: Nsa Kaisi, Mshauri wa Rais, kwa mchango wake mkubwa wa mawazo Wafanyakazi wote wa HakiElimu 2003-2004 Many
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More information4. Kanuni za Petroli (Ushiriki wa Watanzania) za mwaka 2017 zilianza kutumika rasmi tarehe 5 Novermba Shughuli za Petroli za kwanza ni
MWONGOZO WA JINSI YA KUWASILISHA MAOMBI YA KUWEKWA KWENYE KANZIDATA YA WATANZANIA WENYE UWEZO WA KUUZA BIDHAA AU KUTOA HUDUMA (LSSP) KWENYE SHUGHULI ZA MAFUTA NA GESI ASILIA NCHINI Utangulizi 1. Mamlaka
More informationMwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI
David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition
More informationUhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI
Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI b Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI 1 Mwongozo wa Uzalishaji
More informationTaarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania
Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationHISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU 9 DESEMBA 2011.
Saint Augustine University of Tanzania From the SelectedWorks of Daudi Mwita Nyamaka Mr. Winter December 9, 2011 HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU
More informationKijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia
IDARA YA KUFIKIA HUDUMA ZA AFYA VERMONT Kijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia GreenMountainCare MIASHA YENYE AFYA BORA ZAIDI Jedwali la Yaliyomo Jedwali la Yaliyomo... 2 Karibu kwenye Programu ya
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationTANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI
MFUMO WA TATHMINI WA TAARIFA (IRM): TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI 2014 2016 Ngunga Greyson Tepani Mtafiti wa IRM Taarifa ya Mwishoni mwa Utekelezaji 2014-2016 First End-of-Term Report INDEPENDENT
More informationDeputy Minister for Finance
ISSN: 1821-6021 Vol XI - No - 34 DID YOU KNOW? A procuring entity is?s required to use suppliers pliers?pliers?pliers?pliers among those awarded ed?ed?ed?ed framework agreements by GPSA for procurement?ents
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA
More informationSautiElimu. Sauti Yako Isikike
SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian
More informationUtumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More information3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,
HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, MHESHIMIWA JOHN POMBE MAGUFULI, (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2007/08 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationKIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized!. viromen-alsc:a.. Environmental & Social MRADI WA UMEME WA GESI YA * Assessment & Management
More informationUfundishaji wa lugha nyingine
CHUO CHA ELIMU CHA KIMATAIFA OFISI YA ELIMU YA KIMATAIFA Ufundishaji wa lugha nyingine Na Elizabeth B. Bernhardt ELIMU MAZOEA KITABU NA. 20 1 Chuo cha Elimu cha Kimataifa (The International Academy of
More informationUpande 1.0 Bajeti yako
Upande 1.0 Bajeti yako Bajeti (Budget) ni muhustari wa njisi wewe (na familia yako) mnavyopata na kutumia pesa. Inaunganisha pesa zinazoingia nyumbani kwako (Kipato/ income) na zile unazotumia (matumizi/expenses).
More informationMipango ya miradi katika udugu
Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi
More informationMATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza
1 Matumizi bora ya Facebook kwa Biashara MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA Kwa Wanaoanza For IT Services & Web Solutions Web: Email: info@dudumizi.com Phone: 0768816728 2 Matumizi bora ya Facebook kwa
More informationUnyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa
Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda
More informationKUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA
KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa
More information5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban
More informationTIST HABARI MOTO MOTO
TIST HABARI MOTO MOTO Tel. +255784-537720/+255717-062960/+255782-250947, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@tist.org May 2010 Cash Payments for Trees Clean Air Action has developed a way to pay the groups
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/14 DODOMA Mei,
More informationNilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania
Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza
More informationDraft 03 MWENGE KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO MWENGE
MWENGE KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO MWENGE MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO WA MAENDELEO YA KANISA 2013-2017 i YALIYOMO 1. UTANGULIZI... 1 1.1 Lengo kuu... 1 1.2 Historia kwa ufupi... 1 1.3 Malengo ya
More information