UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)
|
|
- Corey Cameron
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1 Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii
2 MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni mbinu zinazonuiwa kuyakidhi mahitaji yao ya kila siku na ya kimazingira. Kuna kazi chache ambazo zimechapishwa za kuelezea kinagaubaga hizo mbinu bunifu na vile zilianzishwa,vile ziliathiri wakaaji wa sehemu mbali mbali na vile zimekuwa zikibadilika pindi wakati unapotita. Wachache wamejitokeza kuelezea wazi wazi juu ya miradi yao, na hata wale ambao wamefanya hivyo ni wakuu wa vijiji ambao wamefanya kuelezea kufaulu kwao. Mradi huu wa Equator Katika unadhamiria kujaza hili pengo kama njia moja ya kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake. Masimulizi juu ya huu mradi ni baadhi tu ya mingi ambayo imefaulu na kushinda tuzo za Equator baada ya kukaguliwa na kutathiminiwa katika kitengo cha makundi ya kijamii yanayo hifadhi mazingira na kuinua maisha ya wanafijiji. Miradi hii inakusudiwa kuwa mifano ya kuiwa na kuwatia shime kuzungumzia ilivyofaulu ili kuhamasisha ulimwengu juu ya uhifadhi wa mazingira. Bonyeza katika ramani ya miradi ya Equator ili upate kupata habari zaidi Wahariri Mhariri Mkuu : Muhariri Meneja : Wahariri Waliochangia : Joseph Corcoran Oliver Hughes Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Erin Lewis, Whitney Wilding Wahandishi Waliochangia Edayatu Abieodun Lamptey, Erin Atwell, Toni Blackman, Jonathan Clay, Joseph Corcoran, Larissa Currado, Sarah Gordon, Oliver Hughes, Wen-Juan Jiang, Sonal Kanabar, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Rachael Lader, Patrick Lee, Erin Lewis, Jona Liebl, Mengning Ma, Mary McGraw, Gabriele Orlandi, Juliana Quaresma, Peter Schecter, Martin Sommerschuh, Whitney Wilding, Luna Wu Uchoraji Oliver Hughes, Dearbhla Keegan, Matthew Konsa, Amy Korngiebel, Kimberly Koserowski, Erin Lewis, John Mulqueen, Lorena de la Parra, Brandon Payne, Mariajosé Satizábal G. Shukrani Equator ingependa kuwashukuru wanachama wa Honey Care Africa na haswa mwongozo mchango wa Madison Ayer. Picha zote ni za Honey Care Africa, ramani ni za CIA World Factbook na Wikipedia. Masimulizi juu ya mradi huu yalitafsiriwa kwa Kiswahili na Dr. Ken Ramani. Nukuu Ziada United Nations Development Programme Honey Care Africa, Kenya. Equator Initiative Case Study Series. New York, NY.
3 UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya MAELEZO KUHUSU MRADI HUU Honey Care Africa ni mradi wa kijamii ambao unajishughulisha na mbinu za kuinua mapato ya wakulima wa mashinani nchini Kenya kwa njia ya ufugaji nyuki. Huku mradi huu ukizingatia utamaduni wa ufugaji nyuki nchini kama njia moja ya kuzalisha chakula na pia kujitafutia riziki, washikadau wana lengo la kuimarisha kiwango cha mapato miongoni mwa familia masikini kama njia moja ya kupambana na uwindaji haramu, ukataji miti kwa ajili ya mbao na uchomaji makaa. Kupitia kwa njia ya kuuza mizinga maalumu ya nyuki, mpango huu umeimarisha njia za kuisambaza kwa wakulima kwa kukubali kununua asali yao kwa bei wastani na hivyo kusaidia wafugaji kununua kwa wingi mizinga hii ya kipekee na kuimarisha na kupanua uzalishaji asali. Asali hiyo utengenezwa na kupakiwa kwa hali ya juu ya usafi na kuuzwa chini ya anwani: Honey Care Africa na Beekeepers Delight. Kiwango kikubwa cha faida inayotokana na bishara hii inagaiwa jamii 15,000 ambazo zinashiriki ufugaji wa nyuki kwa sasa. YALIYOMO MUHTASARI ULISHINDA TUZO YA EQUATOR: Mwaka 2002 ULIANZISHWA: Mwaka 2000 ENEO: Mikoa saba kati ya minane nchini Kenya WANAOFAIDIKA: Watu katika kaya 15,000 MAZINGIRA: Manufaa ya mchavusho Historia na Mandhari 4 Majukumu Makuu na Ubunifu 5 Matokeo ya Kimazingira 6 Matokeo ya Kijamii 6 Matokeo ya Kisera 6 Jinsi ya Kudumisha Mradi Huu 7 Maono 7 Wahisani 8 3
4 Historia na Mandhari Mradi wa Honey Care Africa ulianzishwa mnamo mwaka 2000 kama shirika la kijamii ili kuimarisha na kukuza ufugaji wa nyuki miongoni mwa jamii mbali mbali mashariki mwa Afrika. Shirika hili hufanya kazi na wakulima wadogo miongoni mwa jamii za mashinani nchini Kenya kwa kuwapa misaada ya kifedha, mafunzo na ushauri ili kuwapa nguvu na uwezo wa kujiinua kutokana na umasikini unaowakumba. Kwa kuziwezesha familia kufuga nyuki na kuuza asali kwa mapato ya juu, mpangilio huu umesaidia Wakenya wengi wa mashambani kugundua mbinu zaidi za kujipatia riziki. Ufugaji nyuki: raslimali ambayo imesahaulika Mwanzoni, ufugaji wa nyuki ulichukuliwa kama njia ya kujipatia riziki kwa watu wanaoishi sehemu kame za Kenya. Hii dhana ilitokana na maamuzi ya wakazi wa maeneo haya kulingana na hali ya mazingira, utamaduni, na mienendo ya kijamii. Dhana hizi zimekuwa zikinawiri kufuatia misukumo mbali mbali inayotokana na Serikali pamoja na mipangilio mbali mbali ya Kimsingi, wale wanaoishi katika sehemu zenye mvua nyingi, udongo wenye rutuba, na hali ya hewa baridi walijisghulisha na kilimo cha mimea na mazao ya kuuza, huku wale wanaoishi katika sehemu kame na sizizo na rutuba waliamua kufuga wanyama na kuhamahama kutoka sehemu moja hadi nyingine wakiwatafutia maji na malisho. Wengine katika sehemu kame walijishughulisha na ukuzaji wa mimea ambayo inahimili kiangazi huku wakifuga nyuki kama njia mbadala ya kuzalisha chakula. Baada ya uhuru wa Kenya, serikali na mashirika yalihimiza watu kuendelea na mtindo huo huo wa ufugaji katika sehemu kame huku sehemu zenye mvua zikihimizwa kukuza mimea kwa ajili ya chakula na mapato ya kifedha. Mashirika ya kimataifa yalionekana yakisisitiza mpangilio wa zamani badala ya kuhimiza watu walioishi katika sehemu zenye mvua kushiriki katika mbinu mbadala kama vile ufugaji nyuki kwa ajili ya asali. Kwa hiyo, ufugaji nyuki na usalishaji asali ulinasibishwa na sehemu kame kama vile Ukambani. Ni wazi kwamba sehemu ambazo zina uwezo wa kuzalisha asali ncini Kenya hazijahusishwa wala kutumika ipasavyo. Hali hii imekuwa mbaya kwa sababu mbinu za kisasa za ufugaji nyuki hazijakumbatiwa na wakazi wa maeneo yanayoshughulikia ufugaji. Pia kunahitajika elimu kwa wafugaji ambayo itawawezesha kutumia mbinu mpya za ufugaji. Kwa sasa, wafugaji wengi nchini Kenya wanatumia mbinu za zamani ambapo mizinga ya zamani na mbinu za kuvuna asali kwa kutumia moshi zinatumika badala ya ile ya kisasa. Mashirika mbali mbali yameshindwa kuhimiza mbinu za kisasa za kuzalisha asali, jambo linaloashiria kwamba utafiti katika sekta hii ni wa hali ya chini sana. Mpangilio wa kufaidi wote Mradi wa Honey Care Africa ulianzishwa na wafanyibishara watatu ambao ni Wakenya ili kuziba pengo hili la kushirikiana kati ya jamii na wafadhili wa kimataifa na mashirika ya kibinafsi.wakulima hupewa mikopo midogo kununua mizinga ya kisasa na ya hali ya juu inayotengenezwa na Honey Care. Baadaye wakulima hao hupewa mafunzo bora kuhusu ufugaji wa nyuki na uzalishaji wa asali wa hali ya juu. Mradi huu pia huwatafutia wafugaji nyuki soko ya asali kwa bei inayofaa. Honey Care huchukua asali kutoka kwa wafugaji na kuwalipa wakulima papo hapo, huitengeneza na kuipakia na kuitafutia soko kwa kuiuza katika maduka ya jumla nchini huku wakipata faida kidogo. Asali hiyo ambayo inauzwa kwa anwani mbili za Honey Care Africa na Beekeeper s Delight imejulikana kote eneo la Afrika Mashariki na imekubalika katika masoko ya eneo hilo. Kufikia sasa, mradi huu wa Honey Care umewafaa takriban watu 75,000 katika sehemu zenye umasikini mkubwa nchini Kenya. Mazingira pia yametunzwa kupitia kwa njia ya kutunza miti ili kufuga nyuki. Mfano wa kimataifa ulitia fora Biashara hii imefanikiwa kwa kupata msukumo kutoka kwa mashirika ya kibinafsi na wafadhili ambao wameungana na wenyeji kuleta maendeleo na kuhifadhi mazingira. Muungano huo umetambuliwa kwa manufaa yake nchini Kenya na mataifa mengine kote ulimwenguni. Muungano huo umepata sifa na hata kutuzwa na mashirika kama vile Benki ya Dunia na Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP). Mnamo 2004, mpango Honey Care ulipeleka huduma zake nchini Tanzania, ikitumia mkopo kutoka kwa Kampuni ya Mikopo ya Kimataifa (AFC). Mipango ya shirika hili ni pamoja na kutafuta soko katika sehemu za mabanda katika miji mbali mbali. Mabadiliko ya hali ya anga na matokeo yake kwa kilimo ni janga kuu kwa kwa wakulima wadogo eneo la Afrika Mashariki ni janga kuu kwa vile linahusu maisha ya binadamu. Jamii zimeenzi ufugaji nyuki kama njia moja ya kujitarazaki. Madison Ayer, CEO, Honey Care Africa 4
5 Majukumu Makuu na Ubunifu Majukumu manne makuu ya Honey Care ni pamoja na utengenezaji wa mizinga ya nyuki ya hali ya juu aina ya Langstroth ambayo husambaza katika jamii za mashambani, kutoa mafunzo ya ufugaji nyuki kwa wenyeji na mawaidha ya kimsingi kuhusu ufugaji huo, kununua asali inayovunwa na wafugaji kwa bei bora na kutengeneza na kuuza asali hiyo. La muhimu katika njia hii yote ni kuiboresha asali, kuinua hali ya maisha kwa familia husika na kuwaelimisha umuhimu wa kuhifadhi na kuendeleza mazingira. Kwa vile ufugaji nyuki haukuwa jambo geni kwa wenyeji, vifaa vya ufugaji kwa mazao ya hali ya juu, ujuzi na elimu pamoja na soko ya asali hazikuwapo kwa wingi mnamo mwaka Katika hali hii, Honey Care huwapa wafugaji mbinu za kufuga nyuki, jinsi ya kuhakikisha kwamba asali inayotengenezwa ni ya hali ya juu, kutafuta soko na mafunzo kuhusu matumizi ya pesa na jinsi ya kupata mapato makubwa. Mtindo mpya wa kuzalisha asali ya hali ya juu kupitia kwa mpango wa pamoja unaodhamiria kuhifadhi mazingira na wanaowaletea wenyeji mapato umefanikiwa kwa vile kulikuwa na misingi ya ufugaji wa nyuki katika jamii za Kenya. Mbinu za kitamaduni zilitumia mizinga ambayo iliundwa kutokana na miti au vyungu au mizinga duni. Kwa kawaida, kuvuna asali kulisababisha vifo vya nyuki wengi na kuacha moshi kwa asali. Mradi wa Honey Care ulianza kutengeneza mizinga ya kisasa ya Langstroth, ambayo inaweza kubomolewa na kuondoa asali kwa utaratibu bila ya kutawanya nyuki. Njia hii pia huchukua muda mfupi sana kuvuna asali kwa wiki ikiwa ni kati ya dakika 5 na 10. Kwa kuwahakikishia wafugaji soko, Honey Care imewapa motisha ili washiriki kwa wingi katika njia hii mpya ya uzalishaji mali. Ushirikiano Mafanikio ya mradi huu wa Honey Care yametokana na ushirikiano mkuu na mashirika mbali mbali huku lengo kuu likiwa ni kuwanufaisha Wakenya milioni 25 masikini ambao wanaishi mashinani. Hadi leo, mpango huu umeshirikisha makundi mbali mbali katika wilaya za Kitui na Taita Taveta huku yakipata msaada kutoka kwa Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Denmark (DANIDA) na Wizara ya Ufugaji na Uvuvi ya serikali ya Kenya. Mashirika mengine ambayo yanasaidia mradi huu ni kama Aga Khan Foundation kupitia kwa mpango wa Coastal Rural Support Programme ulioko wilaya ya Kwale; mpango wa kufuga nyuki na kuhifadhi mazingira katika msitu wa Kakamega kupitia kwa Community Action for Rural Development (CARD); na mipango minine mingi katika hifadhi ya wanyama pori ya Mlima Kenya na mpango wa kuhifadhi misitu uliogharamiwa na shirika la Global Environment (GEF). Pia kunao mpango wa kukopesha mizinga ya nyuki katika mikoa ya Nyanza, Magharibi, Rift Valley kupitia kwa K-Rep Development Agency (KDA), Africa Now, na IFC. Mradi wa Honey Care pia hushirikiana na makundi madogo madogo, makundi ya wanawake na yale ya vijana ili kutoa huduma zao kwa wale wanaozihitaji. Kufikia sasa, zaidi ya 15,000 watu wameingia katika ufugaji nyuki. Idadi hii inasimamia karibu watu 75,000 ambao hutegemea ufugaji nyuki. 5
6 Matokeo MATOKEO YA KIMAZINGIRA Ufugaji wa nyuki una manufaa mengi kwa mazingira. Miradi ya Honey Care kila mara hulenga kupunguza visa vya uharibifu wa mazingira. Mpango huu umefanikiwa kupunguza visa hivi na kuimarisha mzingira bora kupitia maafisa wa mashinani. Ukataji miti umekomeshwa Mpango huu wa Honey Care hutoa fedha za matumizi kwa jamii husika ili wasijishughulishe na visa vy uharibifu wa mazingira kwa njia ya kukata miti kwa ajili ya kuchoma makaa. Mafunzo kuhusu ufugaji nyuki husisitiza umuhimu wa mazingira bora. Kupitia kwa mpango wao wa Bees for Trees yaani nyuki kwa miti, mradi huu unmetoa mizinga na vifaa vingine kwa wafugaji kwa makubaliano ya kutunza misitu na kupanda mingine ambapo mizinga hiyo itahifadhiwa. Manufaa ya mchavusho kwa kilimo na mazingira Ni dhahiri kuwa nyuki husaidia kwa kiasi kikubwa katika mchavusho (pollination) wa mazingira. Faida zinazotokana na mchavusho huonekana katika mazao ya vyakula na mimea mingine. Mnamo 2005, makadirio ya manufaa ya mchavusho kutokana na wadudu hasa nyuki ulimwenguni yalikuwa karibu dola za Amerika billioni 208. Hii ilikuwa karibu asilimia 9.5 ya vyakula vyote vilivyozalishwa ulimwenguni wakati huo. Ubora wa vyakula vinavyozalishwa kwa njia ya mchavusho wa wadudu ni mara nne zaidi ya vile vinavyozalishwa bila mchavusho (Gallai N. et al., 2009). Katika utafiti uliofanyika nchini Kenya, faida zinazotokana na uchavusho ni asilimia 40 kutokana na mauzo ya mazao hayo (Kasina et al., 2009). Faida hii inatokana na mazao ya kila mara ya kiwango na hali ya juu. Mimea kama malenge haiwezi kuzaa matunda bila mchavusho. Mradi wa Honey Care umejaribu kukusanya habari kuhusu umuhimu wa ufugaji nyuki kupitia kwa maafisa wake walio mashinani. Kufikia sasa zaidi ya mizinga 30,000 imenasa nyuki wenye asili ya Kenya ambao ndio wanalengwa na mpango huu Honey Care. Hatua hii inalenga kupunguza uwezekano wa athari za kuleta nyuki kutoka nchi zingine. Miongoni mwa jamaa wanaofuga nyuki, 3,500 huishi katika maeneo kame na hivyo kurahisisha kazi ya ufugaji nyuki chini ya mradi huu kutokana na ujuzi walio nao wenyeji. Kwa vile wakulima sasa wana njia mbadala ya kupata riziki, ukataji miti kwa ajili ya kuchoma makaa umepungua kiasi kikubwa. Mizinga 5,000 inapatikana katika msitu wa kilomita tatu, mbuga za wanyama pori au sehemu tambarare ambapo wanahitajika kufugwa kwa njia ya kawaida. Kwa upande wa mimea, kumekuwa na uimarishaji kilimo kwa kati ya asilimia 15 na 30, huku mazao yakiongezeka kwa zaidi ya asilimia 100. MATOKEO YA KIJAMII Mradi wa Honey Care kwa sasa unashirikiana na mikoa saba kati ya mikoa minane nchini Kenya na limeendeleza huduma zake kwa nchi jirani za Malawi, Tanzania, na Sudan Kusini. Nchini Kenya, wafugaji waliopata huduma hizi ni karibu 75,000, wote wakiwa ni wenyeji ambao wanaishi mashinani. Waliofaidika kutokana na mradi huu mnamo mwaka wa 2010 ni 32,250 ambao asilimia 43 ni wanawake. Mapato ya kila familia ambayo inashiriki mpango huu wa Honey Care ni dola za Amerika 250. Mapato haya hutokana na asali ambayo huuzwa katika soko mbali mbali na mapato yanayotokana na mavuno ya vyakula mbabi mbali yaliyoongezeka kutokana na mchavusho. Utafiti unaonyesha kuwa wakulima hutumia asilimia 33 ya mapato yao kutoka kwa asali kwa chakula na dawa, asilimia 25 kwa mbolea na mbegu, asilimia 18 kwa ada za elimu, asilimia 10 kwa nyumba na makao, na asilimia 5 biashara mbali mbali. MATOKEO YA KISERA Mradi wa Honey Care hujishughilisha na watu wa mashinani hata kama kwenye baadhi ya mipango umeshirikiana na Serikali ya Kenya. Kundi hili limenasibishwa na maendeleo ya kijamii na shirika la kukadiria ubora wa bidhaa nchini (Kenya Bureau of Standards). Kwa hiyo, kundi hili limetuzwa Kenya Quality Award katika kiwango cha bishara ndogo na za wastani mnamo mwaka wa Shirika hili lilikuwa mojawapo ya mashirika anzilishi ya Kenya Honey Council mnamo Linawakilisha wahisani wakuu katika ufugaji nyuki nchini Kenya. Liliundwa kama shirika kuu la kuwezesha washikadau kukuza na kuendeleza malengo yao. Malengo mengine makuu ni pamoja na kukuza na kupanua ufugaji nyuki nchini Kenya, kuelimisha wananchi kuhusu manufaa ya asali na nyuki kwa jumla na kuhakikisha kwamba bidhaa zinazotokana na ufugaji nyuki ni za hali ya juu kwa kutoa mafunzo yanayohitajika, kwa wakulima na hata wanaotumia bidhaa hizo. Maazimio yao pia ni kujadiliana na Serikali ya Kenya ili kuibua sheria zinazostahili katika sekta hii. Pia, hujadiliana na serikali za mataifa mengine kutoa mwongozo bora wa biashara ya bidhaa zinazotoka nchini Kenya. Shirika hili la Honey Care lingali likiunda muungano wa mashirika ya kibinafsi na serikali ili kukuza ufugaji nyuki wa kiasi kikubwa nchini Kenya. Mpango huo unaendelea kutumika katika maeneo mbali mbali nchini hasa maeneo ambayo yanafuga nyuki ambapo wakulima hupata mikopo inayojulikana kama Asali Loan kwa usaidizi wa wahisani kama vile Benki ya Equity. Kutoa mafunzo kwa maafisa wasaidizi mashinani kpitia kwa wizara ya Ufugaji na kituo cha ufugaji wa nyuki. 6
7 Jinsi ya Kudumisha Mradi Huu JINSI YA KUDUMISHA MRADI HUU Kwa miaka saba ambayo shirika la Honey Care limedumu, limekuwa shirika la manufaa kwa wengi. Mpango wa Honey Care unajikita katika misingi ya kuhimiza mbinu za uzalishaji mali ambazo zinahifadhi mazingira ambayo inaweza kudumu.mpango huu unahakikisha kwamba kila mmoja wa washiriki anatoa mchango wake wa kimawazo. Kila mshiriki hufaidika kwa kushiriki kikamilifu. Wafuga nyuki mashinani huona manufaa ya uzalishaji asali ya hali ya juu, na manufaa mengine yanayotokana na shughuli zingine za kilimo mbali na ufugaji nyuki. Mradi huu wa Honey Care hupata faida kutokana na ujuzi wao wanaoutumia wakati unahitajika. Asali iliyosafishwa huleta faida kubwa kwa washiriki wote katika uzalishaji na usafishaji wa asali na wale wanaouza bidhaa hizo. Mashirika wafadhili ambao hushirikiana na Honey Care katika ufugaji wa nyuki hufaidika kutokana na maendeleo haya ya kila wakati. Watu wengine pia hunufaika kutokana na ufugaji wa nyuki kwa njia ya mazingira bora. Shirika la Honey Care huchukua jukumu la uongozi katika mashirika mbali mbali katika biashara hii. Washiriki wengine husaidia katika kuwainua washiriki kifedha kwa njia ya mikopo kwa wakulima ili kuanzisha mbinu hizi mpya za ufugaji wa nyuki. Hata kama wakulima hupata faida na kujitegemea, kuna wakati fulani ambapo wanahitaji pesa za kuwasaidia kuinua zaidi bishara yao. Mashirika wafadhili walio na ofisi katika maeneo mbali mbali pia husaidia. Honey Care kuwafikia wakulima wa mashinanii, na hivyo kupunguza gharama ya kupeleka huduma kwao. MAONO Honey Care inaendelea kuungana na wahisani wengine kwa madhumuni ya kueneza habari na kuhimiza Wakenya kwamba ufugaji nyuki ni njia muhimu ya kujipatia riziki. Kuanzisha biashara hiyo huwa ni vigumu wakati mwingine kwa sababu ya ukosefu wa fedha kwa wakulima wengi wa mashambani. Shirika lenyewe linahitaji fedha za kuwahamazisha wakulima kuhusu mbinu mpya za ufugaji, kuyakusanya makundi ambayo yanahusika katika ufugaji nyuki, kuwapa mafunzo, vifaa na maafisa wa kuwaelekeza jinsi ya kutumia vifaa hivyo. Shirika hili pia linajishughulisa na mafunzo ya mbinu za kuvuna asali mahali ambapo inapokelewa na malipo. Honey Care pamoja na washirika wa serikali, mashirika ya kiserikali hutoa fedha za kuanzisha biashara hii. Ufugaji nyuki ni bisahara ambayo inapanuka kwa kasi baada ya misingi bora kuwekwa. Hii ni kwa sababu kuna wafanyakazi katika sekta hii, ardhi ndogo inayohitajika na kuwepo nyuki ambao hawanunuliwi.wahisani wa kibinafsi huchangia kwa kuwasaidia wakulima kupanua biashara yao. Shirika la Honey Care limeshiriki katika miradi mbali mbali ya ufugaji nyuki nchini Kenya, Tanzania, Malawi na Sudan Kusini. Miradi yake mikubwa, hata hivyo imo nchini Kenya. Honey Care Africa Tanzania, ilianzishwa 2005, na imekua hata kiwango cha shirika kubwa zaidi la kuzalisha na kuuza asali katika nchi zingine. Biashara hii nchini Kenya na Tanzania imeendelezwa sambamba, kila moja ikishughulikia changamoto zake kivyake. Lakini kwa sasa nchi hizo zinafanya bishara hii kwa ukuruba mkuu zikiwa na lengo la kuunganisha miradi yao ili kuunda ushirikiano wa kusambaza bidhaa zao katika eneo lote 7
8 la Afrika Mashariki. Huku Kenya na Tanzania zikiwa nchi anzilishi za mradi huu, kuna mipango ya kujumuisha mataifa mengine ya Afrika Mashariki ili kuanzisha umoja wa ufugaji nyuki eneo zima. Changamoto kuu ambayo inatarajiwa katika muungano mkuu wa aina hiyo ni jinsi ya kuwashrikisha wahusika wote katika eneo hilo pana. Sheria za ufugaji nyuki hutofautiana kutoka nchi moja hadi nyingine; pia kuna njia mbali mbali ambazo jamii tofauti zinalichukulia suala kama hilo. Washirika tofauti pia wana tofauti zao wenyewe kwa jinsi ambavyo yanatoa misaada na pia malengo yao makuu ambayo yanaambatahnishwa na ufadhili wao. Hata hivyo, kudumu kwa ufugaji nyuki kama njia moja ya uzalishajia mali utategemea pakubwa washiriki kutoka upande wa serikali na wafadhili ili kuweka misingi inayohitajika kwa wakulima kufuga nyuki. Mashirika ya kibinafsi yanahitajika kutoa misaada itakayowawezesha wakulima kupanua biashara yao. WAHISANI Wahisani wa Serikali na Mashirika ya Kiserikali Wizara ya Ufugaji (Kenya) Kituo cha Kufuga Nyuki (Kenya) Wizara na Viwanda (Kenya) Wizara ya Misitu na Wanyamapori (Kenya) Wizara ya Misitu na Ufugaji Nyuki (Tanzania) Mashirika ya Maendeleo DANIDA / Serikali ya Kenya Swiss Contact & Swiss Development Corporation Belgian Technical Cooperation (BTC)/Wizara ya Mazingira na Mali Asili DFID, Dorcas Aid and Mama Mzungu Foundation UNDP (GEF) EU, DFID, Soros Foundation & World Bank (SME) U.S. Ambassador s Fund Ubalozi wa Uingereza Ubalozi wa Ujerumani Ubalozi wa Finland Swedish International Development Agency (SIDA) Mashirika yasiyo ya Kiserikali Aga Khan Foundation Community Action for Rural Development (CARD) German Agro Action World Vision Action Africa Help International (AAHI) Wildlife Society for Protection of Animals (WSPA) Biodiversity Conservation Programme (BCP) Rotary Club of Stroud (UK) and Rotary Club of Hurlingham Farm Africa Africa Now Sekta ya Kibinafsi Kakuzi Ltd. Business Alliance Against Chronic Hunger (BAACH) Equity Bank Bidco 8
9 MAREJELEO YA ZIADA Jiwa, F Honey Care Africa s tripartite model: an innovative approach to sustainable beekeeping in Kenya. XXXVIII Congress APIMON- DIA, Ljubljana, Slovenia. Gallai N, Salles JM, Settele J, Vaissière BE, Economic valuation of the vulnerability of world agriculture confronted to pollinator decline. Ecological Economics (68), Kasina M., J. Mburu, M. Kraemer and K. Holm-Müller Economic benefit of crop pollination by bees: A case of Kakamega small-holder farming in western Kenya. Journal of Economic Entomology, 102 (2): Masimulizi kuhusu miradi mingine, bonyeza hapa: Equator Initiative Environment and Energy Group United Nations Development Programme (UNDP) 304 East 45th Street, 6th Floor New York, NY Tel: Mradi wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa ndio unaoendesha miradi ya maendeleo ya Umoja wa Mataifa kote ulimwenguni kwa kutoa mwito wa mageuzi na kuelekeza mataifa kwa maarifa, na malighafi ili kusaidia watu kujiimarisha kimaisha. Mradi huu wa Equator huleta pamoja Umoja wa Mataifa, serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, wafanyibiashara na makundi ya mashinani ili kutambua na kuimaliza maendeleo himili kwa watu na jamii kwa jumla Haki Zote ni za Mradi wa Equator
JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
More informationMAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI
MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha
More informationTANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko
TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationInformation for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationMKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationMwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI
David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition
More informationBustani 10,000 Katika Afrika. Alberto Prina
Bustani 10,000 Katika Afrika Alberto Prina K i j i t a b u Timu ya wahariri: Abderrahmane Amajou, Typhaine Briand, Roba Bulga Jilo, Davide Dotta, Emanuele Dughera, Michela Lenta, Velia Lucidi, Irene Marocco,
More informationKilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira
Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kiongozi hiki kimeandaliwa kikiwa ni sehemu ya mradi wa
More informationUhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI
Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI b Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI 1 Mwongozo wa Uzalishaji
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationNGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA
NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.
More informationJifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti
Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationNGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017
TAARIFA Agosti 2017 NGUO MPYA ZA UKOLONI Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika Jumuiya ya Jamii ya 2007: Wajumbe wanaadhamana Nairobi dhidi ya EPAs. SwissInfo Tangu mwaka
More informationUtumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted
More informationUFUPISHO WA 35. Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji mazao: Clive James Chair, ISAAA Board of Directors
I S A A A Huduma ya kinimataifa ya upataji na utumizi wa kiteknolojia ya kuboresha kilimo MUHTASARI WA KIUTEKELEZAJI UFUPISHO WA 35 Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji
More informationProgramu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi
Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini
More informationPronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationDibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi
Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini
More informationTIST HABARI MOTO MOTO
TIST HABARI MOTO MOTO Tel. +255784-537720/+255717-062960/+255782-250947, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@tist.org May 2010 Cash Payments for Trees Clean Air Action has developed a way to pay the groups
More informationUNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI
UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationMwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More informationRipoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013
W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa
More informationKuwafikia waliotengwa
Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E 2 0 1 0 Ripoti
More informationKiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika
Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR
ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationKufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi
PAN AFRICAN PARLIAMENT PARLEMENT PANAFRICAIN البرلمان PAN- PARLAMENTO األفريقي AFRICANO Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi Julai 21 22, 2011 Bunge la
More informationKIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized!. viromen-alsc:a.. Environmental & Social MRADI WA UMEME WA GESI YA * Assessment & Management
More informationUzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania
Uzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wapilipili Tanzania Wildlife Division, Tanzania Wildlife
More informationMwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira
Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Moduli ya kwanza Uhamasishaji Jamii juu ya Afya ya Mazingira Kimechapishwa kutokana na Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Jeff Conant na Pam Fadem i COBIHESA
More informationMpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari
More informationTIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees
TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST
More informationUpatikanaji wa Silaha Ndogo ndogo na Hisia za Usalama nchini Kenya: Ukadiriaji
Ripoti Maalum Upatikanaji wa Silaha Ndogo ndogo na Hisia za Usalama nchini Kenya: Ukadiriaji Manasseh Wepundi, Eliud Nthiga, Eliud Kabuu, Ryan Murray, na Anna Alvazzi del Frate Ripoti Maalum Juni 2012
More informationMaswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA
Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA TWN Third World Network 1. WEMA ni nini? Mahindi yanayotumia maji kwa ufanisi yajulikanayo kwa kingereza kama Water Efficient Maize for Africa (WEMA) ni mpango
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationmuhtasari 37 brief 37 Kiwango cha kiutandawazi cha mazao ya kibiashara ya kibayoteki/ugeuzi jeni: 2007 Clive James Bordi ya wakurugenzi wa ISAAA
i s a a a Huduma ya Kimataifa ya Upataji na Utumizi wa Tekinolojia ya Kuboresha Kilimo muhtasari 37 brief 37 Kiwango cha kiutandawazi cha mazao ya kibiashara ya kibayoteki/ugeuzi jeni: 2007 Na Clive James
More informationMradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda
WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More informationSera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji
Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na
More informationMuhtasari wa taarifa ya warsha ya wataalamu juu ya mfumo wa habari kwa njia ya ramani (PGIS), Morogoro, Juni 30 - Julai 1, 2014
Muhtasari wa taarifa ya warsha ya wataalamu juu ya mfumo wa habari kwa njia ya ramani (PGIS), Morogoro, Juni 30 - Julai 1, 2014 Wandishi (Jina la kwanza kiherufi): Edmund Githoro, Simon Fraval, Joanne
More informationRipoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya
More informationSummaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili
Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili 1. 2-Muhtasari wa Ukurasa wa Ripoti ya Miaka minne ya Bodi Kuu ya Kanisa & Jamii............................... 2 2. Kamati ya Kawaida ya Malipo ya
More informationMALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU
MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationMwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo
Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu Nyenzo ya Mafunzo Vi Agroforestry Vi Agroforestry ni shirika la ushirikiano la maendeleo la Sweden, linalopambana dhidi ya umasikini na
More informationMWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK
Kudumisha uhusiano kati ya jamii, ufugaji na wanyamapori MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK Kudumisha uhusiano kati ya jamii, ufugaji na wanyamapori MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI
More information2 Usimamizi wa Rutuba ya Udongo Tanzania Organic Agriculture Movement
Mwongozo wa Mafunzo ya Kilimo-Hai Afrika Mwongozo kwa Wakufunzi 2 Usimamizi wa Rutuba ya Udongo Tanzania Organic Agriculture Movement CHAPISHO YALIYOMO Mchapishaji: FiBL, Research Institute of Organic
More informationUtangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu
Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu BLOOD PRESSURE UK Shinikizo la damu ndicho chanzo kikubwa cha ulemavu na vifo vya mapema kule Uingereza, kupitia kiharusi, mshtuko wa moyo na maradhi ya moyo.
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationIn the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment
In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationUSIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI
USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03
More informationNi kwa nini mkulima awe maskini?
Jarida la kilimo endelevu Afrika Mashariki Ni kwa nini mkulima awe maskini? Swali hili limekuwa likijirudia mara kwa mara. Kwa watu walio wengi hata wakulima wenyewe, wana majibu mengi sana ambayo wamekuwa
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA
More informationJHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI
JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More informationRIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI
International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More informationHUDUMA ZA AFYA KWA WOTE
SAUTIZETU HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE 01 SAUTIZETU HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE SAUTI ZETU Huduma za Afya kwa wote THE OPEN SOCIETY INITIATIVE FOR EASTERN AFRICA (OSIEA) (JAMII WAZI YA MPANGO WA AFRIKA MASHARIKI)
More informationUnyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa
Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda
More informationWaangalizi wa Maendeleo Endelevu
Waangalizi wa Maendeleo Endelevu Vol.1 Issue 4 June - December 2013 Mpango wa Ushauri na Mafunzo Wahamasisha Kujifunza Miongoni mwa jamii katika Eneo Ujenzi wa mabwawa ya maji chini ya mradi wa LVEMPII
More informationMipango ya miradi katika udugu
Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi
More informationTaarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania
Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3
More informationKimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:
Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200
More informationMWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI
MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI
More informationAzimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]
This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationMwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health
Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health Wasiojua kusoma na kuandika katika karne ya 21 hawatakuwa wale wasiojua kusoma na kuandika lakini wale ambao hawawezi kujifunza, kutojifunza na kujifunza
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationIn the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment
In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationKAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA
KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI
More informationMWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18
MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2
More informationNilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania
Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TAARIFA YA MAFANIKIO CHINI YA UONGOZI WA MHE. SOSPETER MUHONGO (MB) KATIKA SEKTA NDOGO YA UMEME Disemba, 014 A. MAFANIKIO 1. Kuongezeka kwa uzalishaji
More informationTIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO
TIST HABARI MOTO MOTO Tel. 026-2322246 P.O.BOX 53 MPWAPWA E-Mail tist@twiga.com 01 October 2000 Y2K PREPARATIONS Holes and Seedlings made ready for the year 2000 programme By Gayo Mhila The process of
More informationSonga kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa
Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided
More informationTAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014
TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...
More informationMAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA
MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA
More information3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,
HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, MHESHIMIWA JOHN POMBE MAGUFULI, (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2007/08 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationUwepo, Athari na Udhibiti wa Sumu-Suvu Kwenye Vyakula vya
Uwepo, Athari na Udhibiti wa Sumu-Suvu Kwenye Vyakula vya Kuku Tanzania Dr Flora KAJUNA Livestock Training Agency (LITA)-Morogoro Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Utangulizi Sumu-kuvu ni nini? Sumu kuvu
More informationKUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA
KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA Toleo la kwanza 2012 Mwandishi: USAID DELIVER PROJECT Wachangiaji: Gary Steele, John Snow, Inc. and Judith
More informationKUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.
KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana
More information5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa
More information