JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
|
|
- Gwendolyn Evans
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1 horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY MUKHTASARI
2
3 Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya FY Ushirikiano kwa ajili ya Maendeleo ya Pamoja na Ustawi MUKHTASARI Juni 2014
4 FY Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
5 Utangulizi Safari ya Kenya ya maendeleo kwa wote Kenya ina nafasi ya kuwa mojawapo ya mataifa yaliyostawi barani Afrika. Hii ni kwa sababu taifa hili linajivunia sekta ya kibinafsi iliyoimarika, idadi kubwa ya vijana na kuandaa uchaguzi mkuu uliopita kwa amani; maswala yanayoipatia fursa nzuri ya kupata maendeleo kwa jamii zote katika miaka ijayo. Hata hivyo, viwango vya umaskini vingali juu huku watu wanne kati ya kumi wakiwa maskini licha ya kwamba asilimia 10 ya matajiri nchini wanamiliki asilimia 40 ya jumla ya pato la taifa. Je, ni nini kinaweza kufanywa kumaliza umaskini na kupata maendeleo kwa kila mmoja ifikiapo mwaka 2030? Na je mashirika ya Benki ya Dunia (WBG) yanayojumuisha IFC, MIGA na Chama cha maendeleo ya Kimataifa IDA yanaweza kusaidia vipi katika azma ya Kenya kujiendeleza katika miaka ijayo? Maswali haya ndiyo msingi wa Mkakati wa kitaifa wa Maendeleo kwa ushirikiano na WBG, (CPS). Mkakati huu umetayarishwa kwa ushirikiano wa karibu na serikali ya Kenya, serikali za county, sekta ya kibinafsi, mashirika ya umma, na mashirika ya kimataifa yanayohusika na maendeleo. Ripoti hii inaangazia haja ya mipangilio ya kudumu itakayopelekea kustawisha uchumi kwa haraka na kutilia maanani sekta zinazowaathiri watu wanaoishi katika umaskini. Sekta ya umma inaweza kuongoza katika kubuni nafasi mpya za ajira huku serikali ikiboresha mazingira ya kufanyia biashara ili mashirika yaweze kuimarisha biashara zao. Hata hivyo, ustawi bora ni lazima ujumuishe maswala yote muhimu ili kila mmoja afurahie maisha bora. Wakenya wengi wanapitia hali ngumu ya maisha kutokana na kwamba walizaliwa katika maeneo fulani au hali za familia zao na wala sio kwa sababu ya juhudi zao au talanta zao; jambo ambalo haliwezi kukubalika.ustawi wa jumla utaboresha huduma Ushirikiano kwa ajili ya Maendeleo ya Pamoja na Ustawi i
6 za afya, kuhakikisha kwamba vijana wanaweza kufanya kazi, kuimarisha kilimo haswa katika jamii zenye mapato ya chini, kulinda jamii maskini dhidi ya majanga na athari za mabadiliko ya anga na kuboresha hali ya maisha katika miji mikuu. Ustawi bora pia ni lazima uweze kuwajibikiwa. Katiba mpya ya mwaka 2010 ni hatua kubwa kwani inaweka masharti ya usawa wa kijinsia na inatoa nguvu zaidi kwa mashirika ya kupambana na ufisadi. Vile vile inatoa mwongozo wa ugatuzi kwa kiwango kikubwa ambacho hakijaonekana kwingineko. Hizi zote ni changamoto kubwa. Azimio letu ni kutoa dola bilioni 4 au zaidi kwa miradi na rasilmali mpya katika miaka ijayo, ili kusaidia taifa hili kuafikia agenda yake ya maendeleo thabiti yanayojumuisha kila sekta na kufikia kila mwananchi na ambayo yanaweza kuwajibikiwa. Benki ya Dunia inajivunia uhusiano mwema kati yake na Kenya na inatazamia ushirikiano mzuri wa washirika wa kitaifa na kimataifa katika sekta za umma na kibinafsi. Kwa ushirikiano, Kenya ina fursa ya kuafikia uwezo wake wa kuinua maisha ya mamilioni ya familia kutoka kwa umaskini na kustawisha uchumi wake kufikia viwango vya kisasa. Diariétou Gaye Mkurugenzi anayesimamia Kenya, Benki ya dunia, bara la Africa Cheikh, Oumar Seydi Mkurugenzi wa IFC, Mashariki na kusini mwa Africa ii FY Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
7 MUKHTASARI 1Kenya ni miongoni mwa mataifa yaliyo na nafasi bora zaidi ya kustawi barani Afrika. Kenya inajivunia idadi kubwa ya vijana, sekta ya kibinafsi inayoimarika, na msingi wa mabadiliko kutokana na katiba mpya. Aidha inajivunia kuandaa uchaguzi mkuu uliopita kwa amani na inaongoza kiuchumi na kimaendeleo katika Afrika Mashariki. Hata hivyo viwango vya umaskini nchini viko juu huku takwimu zikionyesha kwamba angalau watu wanne kati ya kumi ni maskini hohe hahe huku asilimia 10 ya matarjiri wakimiliki asilimia 40 ya pato la kitaifa. Malalamishi kuhusu uongozi yamekithiri na japo uchumi umeripotiwa kukua, unatatizwa na viwango vya chini vya uwekezaji na mapato duni kutoka kwa viwanda na mashirika. Ukuaji kiuchumi bado haujafikia viwango vinavyohitajika kubadilisha maisha ya mwananchi. Matarajio ya kujiendeleza: Uchunguzi wa kina wa hali ya taifa na agenda ya maendeleo 2Mpangilio huu unatokana na uchunguzi wa kina wa ushahidi kutambua changamoto na nafasi za Kenya katika kuafikia malengo mawili muhimu. Kulingana na takwimu, viwango vya Ushirikiano kwa ajili ya Maendeleo ya Pamoja na Ustawi iii
8 umaskini vilishuka kutoka asilimia 47 mwaka 2005 hadi asilimia 39 mwaka Viashiria muhimu vya maisha vimeimarika japo bado hakuna usawa kati ya watu wa tabaka tofauti. Nafasi za kujiendeleza kwa wanawake ni duni ikilinganishwa na wanaume haswa wale wanaoishi maeneo ya mashambani yasiyo na maendeleo huku pia swala la ukabila likiathiri maendeleo ya jamii. Kwa mtazamo, kumaliza umaskini hohe hahe ifikiapo mwaka 2030 kutamaanisha kupunguza viwango vya umaskini kwa silimia 2 kila mwaka. Hili litawezekana tu ikiwa uchumi wa taifa unatua mara mbili ya ilivyo sasa na pia ikiwa tofauti ya mapato kati ya matajiri na maskini itapungua kwa asilimia 50. Ili kuanzisha maendeleo ya kudumu, ni sharti Kenya kuangazia changamoto za uwekezaji duni na uzalishaji wa viwango vya chini katika viwanda. Ukuaji wa haraka unahitaji mabadilikoo katika sera za matumizi ya pesa za umma kuimarisha miundo msingi. Aidha mazingira ya kufanya biashara yanastahili kuboreshwa ili kuimarisha sekta ya kibinafsi na kuthibiti ushuru unaotozwa wafanyibiashara. Maono: Kipaumbele cha serikali na mikakati ya kipindi cha (Medium Term Plan) 3Kenya inalenga kuwa taifa linalotambulika kote ulimwenguni kwa ukuaji wa kiuchumi na hali nzuri ya maisha kwa wananchi wake. Mpango wa Vision 2030, umeundwa kwa misingi ya uchumi, jamii na siasa na unajumuisha maazimio ya serikali iliyopita na iliyoko mamlakani sasa. Msingi wa kiuchumi unaazimia kuimarisha sekta muhimu zikiwemo kilimo na huduma za fedha kupelekea ukuaji wa uchumi kwa silimia 10 kila mwaka. Msingi wa kijamii unalenga kuimarisha hali ya maisha ya wananchi kupitia kwa elimu, huduma za afya na makaazi bora haswa kwa wanawake, vijana na jamii zilizotengwa. Nao msingi wa kisiasa unaangazia hali ya baadaye ya taifa hili kwa kuboresha utekelezaji wa sheria, na kutilia mkazo iv FY Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
9 uwazi katika uongozi. Hii inaungwa mkono na mpango wa kipindi cha mwaka (second Medium-Term Plan (MTP2, ), ambao agenda yake inalingana na lengo la Benki ya dunia la kuangamiza umaskini kote duniani. Hali hii pamoja na mchango wa washika dau unaofuatia mazungumzo ya kina inatoa mwanzo mzuri kwa mkakati wa ushirikiano huu. (CPS) Changamoto na nafasi za maendeleo 4Changamoto kuu na ya msingi ni kuafikia ukuaji ulioimarika na kwa haraka angalau katika muongo mmoja. Nafasi iliyopo ni kutumia rasilmali za umma na za kibinafsi kupitia ushirikianao mathubuti wa sekta za umma na kibinafsi ambao kwa sasa haujakuzwa ipasavyo. Juhudi mpya zinastahili kutiliwa maanani kuthibiti mishahara ya wafanyikazi wa umma ili kuimarisha mfumo wa kifedha kwa ujumla. Pia, kuna haja ya mipangilio mahsusi kuimarisha mazingira ya kufanya biashara sawa na kushughulikia maswala yaliyoangaziwa na ukaguzi uliofanywa na Benki ya Dunia. Mabadiliko haya yatawezekana tu kukiwepo na takwimu halali na zinazotolewa kwa muda unaofaa kusaidia katika uundaji wa sera na ukaguzi wa miradi. 5Kuna haja kubwa ya kutilia mkazo kuimarishwa kwa hali ya maisha ya wananchi. Ukuaji unafaa kujumuisha watu wote ili kila mmoja ashuhudie, na kufurahia maendeleo. Inasikitisha kwamba, Kenya ni miongoni mwa mataifa ya bara Afrika ambapo vifo vingi zaidi vya watoto wachanga huripotiwa. Kwa kila watoto laki moja wanaozaliwa, 488 huaga dunia. Aidha wananchi wengi hawana chakula cha kutosha, wanakosa maji safi, hawawezi kufikia huduma za afya na hawana makao mazuri. Asilimia 21 ya vijana hawana ajira,mara mbili zaidi ya watu wazima. Kuna umuhimu kuwapa vijana elimu ya kisasa na nafasi za kazi ili kutambua na kukuza talanta zao. Ushirikiano kwa ajili ya Maendeleo ya Pamoja na Ustawi v
10 Miji mikuu isiwe tu ya kutengeneza nafasi za ajira bali pia inafaa kutoa huduma muhimu za kimsingi kwa wakaazi wake. Kwa kuwa Kenya ni taifa la watu wa tabaka mbali mbali, ni bora kufanya juhudi kushirikisha kikamilifu watu waliotengwa na wasiojiweza katika jamii katika mipango yote ya maendeleo ya taifa. Ili kuamliza umaskini, ni sharti maendeleo yaanzie mashinani ambako kuna idadi kubwa ya watu maskini wanaolengwa katika miradi ya kuangamiza umaskini. Uwekejazi unafaa kuelekezwa mashinani ili kuboresha kilimo na kuweka mikakati ya kuwazuia wananchi kutumbukia katika umaskini. Aidha mikakati hii inafaa kuvutia wawekezaji wa kibinafsi, kuinua viwango vya elimu na kuboresha huduma za afya mashinani. 6Mabadiliko katika taasisi za uongozi na usimamizi wa rasilmali yamepelekea ugatuzi ambapo baadhi ya shughuli za serikali sawa na asilimia 30 ya pato la taifa zipelekwa katika uongozi wa serikali za kaunti 47. Mabadiliko haya bila shaka ni ya kihistoria haswa ikizingatiwa kwamba ni mataifa machahe tu ambayo yamejaribu kufuata mfumo huu wa uongozi. Changamoto iliyoko mbele ni kutimiza malengo ya ugatuzi kwa kushirikisha wananchi, kuboresha huduma za serikali, na kuweka miundo msingi bora ya serikali mashinani. Miundo misingi hii itaimarisha uhusiano kati ya serikali kuu na serikali za county na kuwezesha rasilmali kutumika kikamilifu kuunda sera zitakazotumika kuleta mabadiliko ya kudumu mashinani. 7Nafasi hizi zote zinaweza kutumika kikamilifu ikiwa kutawekwa mikakati ya kuboresha uongozi na kupunguza ufisadi. Ili kuafikia maazimio haya muhimu, benki ya dunia itasisitiza umuhimu wa kumaliza ufisadi na kutii sheria kwa wananchi wa tabaka zote huku ikiweka matarajio yanayoweza kuafikia maendeleo hatua kwa hatua. Kuna nafasi ya kuboresha usimamizi wa fedha za umma, kuimarisha vi FY Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
11 uongozi, kuhimiza uwazi katika shughuli za serikali na kudumisha mipango itakayolinda mikakati hii. Mpangilio huu wa kuimarisha taasisi utasaidia kulinda hadhi ya rasilmali za Benki ya dunia na pia rasilmali za Kenya ambazo huchangia asilimia 90 ya matumizi ya pesa za umma. Mikakati muhimu ya utumizi bora wa rasilmali za WBG 8Ushirikiano huu unalenga Kusaidia Kenya kukabiliana na changamoto hizi. Aidha ushirikiano huu unatokana na uhusiano bora wa miaka mingi na unatoa mpangilio wa jinsi rasilmali za Benki ya Dunia IFC na MIGA zitatumika kikamilifu kusaidia taifa hili kuafikia lengo lake la kustawi na kueneza maendeleo kwa wananchi wake wote. Benki ya dunia itatumia jaribio maalum kuchagua jinsi ya kugawa rasilmali ili kuongezea uwezekano wa kupata matokeo bora zaidi. Mpangilio wa jaribio hili utakuwa katika viwango vinne; a) kufuatilia na kuthibitisha maono ambayo yatapelekea mabadiliko ya kudumu kukabiliana na umaskini na kuanzisha maendeleo. (b) Kukagua kikamilifu uwezo wa Benki ya Dunia na kuzingatia nafasi yake bora katika kuleta mabadiliko muhimu kupitia kwa ushirikiano (c) Kusisitiza umuhimu wa mwananchi kumiliki miradi na d) kuchunguza na kutilia maanani uwezo wa mteja (Mwananchi) kulingana na mpangilio wa miradi yenyewe. Jaribio hili hutumika kwa muundo wa kuwiana kutambua majukumu matatu yanashirikishwa, kutambua maswala muhimu katika kila jukumu na kulinganisha uhusiano kati ya mipangilio, ushauri na ukaguzi. 9Jukumu la kwanza la ushirikiano nikuimarisha ushindani na maendeleo. Uti wa mgongo wa maendeleo ya kudumu ni kuboresha miundo msingi, kuboresha mazingira ya kufanyia biashara na kukabiliana na shinikizo kutokana na mabadiliko ya kila Ushirikiano kwa ajili ya Maendeleo ya Pamoja na Ustawi vii
12 mara. Sera za benki ya dunia zitasaidia viongozi kutoa mpangilio maalum wa utenda kazi na uthibiti wa sekta ya kawi. Ufadhili wa IDA utaelekezwa kwa uwekezaji wa miradi ya umma nazo IFC na MIGA zitasaidia kuvutia rasilmali za sekta ya kibinafsi. Kwa mapana, Benki ya dunia itaongeza mara dufu mchango wake kwa ushirikiano wa sekta ya umma na kibinafsi haswa huduma za maji na uchukuzi zinazoonyesha matumaini ya kukua kwa kipindi kilichoko. Katika uchukuzi, IDA itaelekeza ufadhili wake kwa barabara za vijijini na zile zinazounganisha kaunti tofauti ili kurahisisha usafiri na kuwezesha wananci kufikia nafasi zaidi za uwekezaji. Aidha, ushindani utaimarishwa kwa kuboresha mazingira ya kufanyia biashara, kutoa nafasi zaidi za uwekezaji katika kila sekta kulingana na maeneo na kuendeleza huduma za fedha na soko la hisa. Benki ya Dunia pia itaunga mkono juhudi za serikali za kuimarisha sekta mpya za mafuta na gesi. Ufadhili wa IFC na Benki ya Dunia utatumika kutengeneza nafasi za ajira katika sekta ya kibinafsi na kuboresha hali ya maisha katika miji mikuu ambako hali ya umaskini limekuwa donda ndugu. Jukumu letu la pili katika ushirikiano huu ni kuwalinda 10waliotengwa na wanaokabiliwa na hatari katika jamii na kuwasaidia wafikie malengo yao, jambo ambalo ni muhimu katika maendeleo. Uhifadhi wa maadili na hadhi ya jamii pia utaangaziwa huku Benki ya Dunia ikiendelea kushikilia nafasi muhimu katika kuafikia haya. Afya pia ni muhimu sana; katika sekta hii, juhudi za pamoja za IDA NA IFC, pamoja na ufadhili wa kimataifa na washirika wengine, zitaimarishwa. Njia nyingine muhimu ya kuwasaidia wasiojiweza ni kulenga kilimo. Kutokana na kwamba kilimo husaidia moja kwa moja familia za mashambani ambako idadi kubwa ya wakenya wanaishi. Mipango ya IFC ya kuwekeza katika miundo msingi, kuongeza dhamana katika bidhaa za kilimo, pamoja na mashirika ya kifedha, viii FY Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
13 pia husadia lengo hili. Kuongezeka kwa idadi ya vijana kunachangia kuleta fursa na pia changa moto katika juhudi za WBG kusaidia katika elimu, kubuni ajira na kutoa mafunzo. Kuwasaidia wasiojiweza ambao pia wanaathirika kutokana na mabadiliko ya kila mara ya hali anga, pia kutakuwa katika mipango yetu ya usaidizi. Pamoja na kwamba shughuli za kijinsia za WBG zitaimarishwa, ikiwemo elimu ya wasichana, biashara, na kusaidia makundi ya wanawake wa mashambani. Jukumu la tatu katika kazi hii, litakuwa kuangazia usawa na 11kuona kwamba mradi huu unakuwa thabiti na wa kutegemewa. Hili ni jukumu la muda mrefu ambalo litahusisha sana ugatuzi. Mpango wa benki ya dunia wa kuwapa watu wengi uwezo na mpango wa AAA, itachangia shughuli kadhaa za IDA kusaidia kaunti na mashirika ya kitaifa katika juhudi zake za kuona kwamba ugatuzi unafaulu. Ikiwa WBG itaulizwa isaidie, basi itaanzisha na kusimamia hazina ambayo itatumiwa na wafadhili kuweka pesa za msaada ambazo wanaolengwa watazifikia kwa urahisi. Mpango wa uwekezaji wa IDA utasaidia mbinu za kubuni sera ambazo zinategemea hali ilivyo, kutumia fedha za umma na mageuzi katika kusimamia fedha za umma. Ustawi wa maendeleo ya Kenya utategemea uthabiti wa ushirikiano wakanda hii na mataifa jirani; na mpango wa uwekezaji wa WBG utafanywa wa mataifa, ikiwemo sekta za kawi na uchukuzi. Kibinafsi na kijumla, kufaulu kwa maendeleo ya kudumu 12kunaweza tu kupatikana ikiwa kuna ushirikiano kupitia mfumo utakaohakikisha utawala bora, swala ambalo limekuwa vigumu kuafikiwa hapo mbeleni. Mpango wa usaidizi wa WBG, pia hutoa mafunzo yanayolenga kuimarisha taasisi simamizi, ikiwa ni pamoja na mafunzo kuhusu usimamizi bora wa fedha za umma na zaidi Ushirikiano kwa ajili ya Maendeleo ya Pamoja na Ustawi ix
14 uwazi katika taasisi na hasa uwazi kwa upande wa wanaotafuta huduma, na hivyo ni muhimu pia kutumia mikutano iliyo wazi ya kijamii kwa manufaa ya pande zote. Benki itaendelea kuchunguza manufaa ya mikakati inayowekwa kusimamia miradi ambayo tayari ipo, na kuimarisha zaidi mikakati iliyofaulu, ikiwa ni pamoja na kupata usaidizi kutoka kwa kitengo cha WBG cha INT kuhusu namna ya kulinda miradi na usaidizi kwa mashirika ya kutegemewa kama vile tume ya maadili na kupambana na ufisadi, EACC. WBG itatumia mbinu za kuchunguza ufisadi katika mradi wake wa kukopesha pesa kwa kubadilisha sehemu zinazolengwa na kupunguza pesa ikiwa kutazuka maswala ya kutiliwa shaka ambayo yanatishia mipango ya IDA na IFC katika matumizi yake ya fedha. Kutekeleza kwa ajili ya matokeo Mkakati huu unahusisha kulenga matokeo katika ushirikiano 13 huu, hasa shughuli maalum, na mkakati wenyewe unafaa kuwa tayari kuangazia hali mpya na habari kama vile kuhusu takwimu zinazoongezwa kuhusu umaskini. Matokeo yanayolengwa yamedhihirika katika mtindo wa sekta mbali mbali, kuashiria kutegemeana kwa huduma kote katika mkakati huo. Juhudi za pamoja na benki kusimamia matokeo katika mpango huo kote nchini, zinategemea mifumo ya taifa na uwezo wa kupima na kuchunguza hatua zinazopigwa. Ushirikiano katika benki na pia na washirika wengine utalenga maswala Fulani kama vile hali ya biashara, sekta ya fedha, ushirikiano wa sekta za umma na kibinafsi, kawi, na kilimo. Majaribio ya kuchagua tayari yanailazimu WBG kupanua baadhi ya shughuli zake kama vile kusaidia miji midogo, kusaidia maendeleo mashambani, pamoja na ugatuzi na kuhakikisha benki inashiriki katika mambo mengine kama vile barabara kuu, usimamizi wa mali asili, na mabadiliko ya kisheria. Utaratibu huu hubadilika, na uchunguzi pia utaendelea kubadikila. x FY Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
15 WBG inaweza kuwa ikitoa zaidi ya dola billion 1 kila mwaka kwa 14Kenya kwa muda wote wa ushirikiano huu. Usimamizi bora wa mradi huu utaendelea kuwa muhimu katika kuhakikisha matokeo mazuri pamoja na mbinu bora za kushughulikia hali mbali mbali za benki, mipango ya uwekezaji ya IFC, na MIGA. IFC inalenga kupanuliwa kwa mradi huu pengine hata kufikia dola million 785 kufikia kati ya mradi huu (FY14), ikiwa hali itaruhusu. Kwa sasa MIGA inatumia jumla ya dola million 255 hapa Kenya, na haja ya wawekezaji wa kimataifa kuwekeza katika sekta za miundo msingi, kawi, na kilimo biashara, inatoa fursa ya upanuzi zaidi wa mradi wa MIGA. Mipango ya kila mwaka ya benki hii itategemea mpango wa IDA 17 ambao hutumia dola million 600 kila mwaka. Hali hii itaimarisha mpango wa IDA nchini Kenya wa dola billion 4.3 kufikia kati ya mradi ( FY14), kufadhili miradi 23 ya kitaifa kwa gharama ya dola bilioni 3.5) na miradi 7 ya maeneo ambayo Kenya ni mwanachana (kwa gharama ya dola 0.8B). Ni muhimu kuendelea kupiga hatua hasa katika uwekezaji wa IDA, na pia katika juhudi za IFC, kwa kuangazia miradi mikubwa na matumizi mazuri ya fedha za ziada. Kudhibiti uwezekano wa hatari Hali yoyote ya ukosefu wa uthabiti katika mradi wowote ambao 15sio wa fedha nyingi, inaweza kuwa hatari sana kwa juhudi za kupigana na umaskini. Mkakati wa kusaidia, bila shaka unahusisha mipango ya muda mrefu ya kuimarisha ushindani na mauzo ya nje, pamoja na mikakati ya kuweka akiba, na kuweza kufikia fedha za kimataifa ili kuweka kukabiliana na hatari hiyo. Majanga na hatari nyingine yoyote; inayotokana na mabadiliko ya ulimwengu na kusababishwa na binadamu, vinaweza kutokea japo wakati wake ama ukubwa wake haviwezi kujulikan; benki na washirika wakewatatafuta mbinu za kusaidia kukabiliana na hatari hiyo katika siku za baadaye. Ushirikiano kwa ajili ya Maendeleo ya Pamoja na Ustawi xi
16 Hatari nyingine inaweza kuhusisha mabadiliko ya ghafla ya kisiasa, mwelekeo wa kisera na mwelekeo wa wizara katika sekta muhimu, mabadiliko ya haja ya kufadhili kwa upande wa wafadhili ama kukosa kuona maana ya mpango unaofadhiliwa kwa upande wa wafadhili wa IFC na MIGA. Haya yote, yatahitaji kujipanga tena ili kuzuia mabadiliko hayo kuathiri mipango inayofadhiliwa na WBG. Hatimaye, hatari zinazoambata na kuendesha mpango wenyewe ni pamoja na usimamizi mbaya na ufisadi, hata katika kaunti ambako utawala mpya unapanua shughuli zale. Hatua ambazo zinaweza kuokoa hali ni (a) kufanya mabadiliko ambayo yatahakikisha usimamizi bora wa ushirikiano huu na pia kushiriki ugatuzi, (b) ushirikiano mwema kati ya INT, benki na mamlaka husika ili kuwekwe mikakati ya kuzuia na madai yanapozuka, yanashughulikiwa haraka na hatua zinachukuliwa; na (c) mawasiliano mazuri na washirika dau, ikiwa ni pamoja na bodi. xii FY Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
17 Raha tupate na ustawi ~ Wimbo wa Taifa Picha: Benki ya Dunia
18 VIDOKEZO
19
20 The World Bank Delta Center Menengai Road, Upperhill PO Box Nairobi, Kenya Tel: Fax: Website: JOIN THE CONVERSATION! Cover image: Original Images Design/Layout: Robert Waiharo
UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)
Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationKuwafikia waliotengwa
Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E 2 0 1 0 Ripoti
More informationMAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI
MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationRipoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya
More informationDibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi
Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationMKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA
More informationMALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU
MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa
More informationTANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko
TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,
More informationMradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda
WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya
More informationAzimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]
This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR
ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini
More informationKiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika
Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to
More informationInformation for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More informationMAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA
MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationRipoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013
W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa
More informationMwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3
More informationTaarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania
Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3
More informationNGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA
NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.
More informationKUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.
KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana
More informationMWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18
MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationMpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari
More informationUNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI
UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump
More informationKutetea Haki za Binadamu
Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationKufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi
PAN AFRICAN PARLIAMENT PARLEMENT PANAFRICAIN البرلمان PAN- PARLAMENTO األفريقي AFRICANO Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi Julai 21 22, 2011 Bunge la
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationKAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA
KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationTAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA
TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA
More informationPronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:
More information5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban
More informationUnyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa
Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI
More informationSonga kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa
Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More informationHUDUMA ZA AFYA KWA WOTE
SAUTIZETU HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE 01 SAUTIZETU HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE SAUTI ZETU Huduma za Afya kwa wote THE OPEN SOCIETY INITIATIVE FOR EASTERN AFRICA (OSIEA) (JAMII WAZI YA MPANGO WA AFRIKA MASHARIKI)
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationUtumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted
More informationProgramu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi
Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini
More informationUpatikanaji wa Silaha Ndogo ndogo na Hisia za Usalama nchini Kenya: Ukadiriaji
Ripoti Maalum Upatikanaji wa Silaha Ndogo ndogo na Hisia za Usalama nchini Kenya: Ukadiriaji Manasseh Wepundi, Eliud Nthiga, Eliud Kabuu, Ryan Murray, na Anna Alvazzi del Frate Ripoti Maalum Juni 2012
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationSera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji
Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na
More informationKimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:
Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200
More informationTAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014
TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...
More informationRIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI
International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa
More informationJifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti
Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MHESHIMIWA SOPHIA M. SIMBA (MB.), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2013/14 DODOMA Mei,
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More informationWIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
More informationNGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017
TAARIFA Agosti 2017 NGUO MPYA ZA UKOLONI Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika Jumuiya ya Jamii ya 2007: Wajumbe wanaadhamana Nairobi dhidi ya EPAs. SwissInfo Tangu mwaka
More informationMwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI
David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition
More informationUtangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu
Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu BLOOD PRESSURE UK Shinikizo la damu ndicho chanzo kikubwa cha ulemavu na vifo vya mapema kule Uingereza, kupitia kiharusi, mshtuko wa moyo na maradhi ya moyo.
More informationKIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized!. viromen-alsc:a.. Environmental & Social MRADI WA UMEME WA GESI YA * Assessment & Management
More informationMipango ya miradi katika udugu
Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA BARA 2004 Imetayarishwa na: Idara ya Tiba Afya Makao Makuu P.O. Box 9083, DAR ES SALAAM June 2005 Yaliyomo Ukurasa Vifupisho
More informationRIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
More informationShabaha ya Mazungumzo haya
Karibu Katika Mazungumzo Kuhusu Mchakato wa Uhamasishaji Maendeleo ya Kanisa na Jamii CCMP/UMOJA Shabaha ya Mazungumzo haya Kuwafahamisha viongozi wa makanisa kuhusu Mchakato wa CCMP ambao umekuwa ukitumika
More informationUzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania
Uzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wapilipili Tanzania Wildlife Division, Tanzania Wildlife
More informationSummaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili
Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili 1. 2-Muhtasari wa Ukurasa wa Ripoti ya Miaka minne ya Bodi Kuu ya Kanisa & Jamii............................... 2 2. Kamati ya Kawaida ya Malipo ya
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013
www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper
More informationUSIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI
USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03
More informationKuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia
Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa
More informationIn the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment
In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationKufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007
Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna
More informationUFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI
JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MFUMO WA RUZUKU YA MAENDELEO YA MTAJI WA SERIKALI ZA MITAA (LDCDG) UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI Kijitabu cha Mshiriki
More informationIn the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment
In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities
More informationHAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII
HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY
More informationNilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania
Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza
More information3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,
HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, MHESHIMIWA JOHN POMBE MAGUFULI, (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA MWAKA WA FEDHA 2007/08 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationDraft 03 MWENGE KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO MWENGE
MWENGE KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO MWENGE MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO WA MAENDELEO YA KANISA 2013-2017 i YALIYOMO 1. UTANGULIZI... 1 1.1 Lengo kuu... 1 1.2 Historia kwa ufupi... 1 1.3 Malengo ya
More informationAfya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia
Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Shukrani Ripoti
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TAARIFA YA MAFANIKIO CHINI YA UONGOZI WA MHE. SOSPETER MUHONGO (MB) KATIKA SEKTA NDOGO YA UMEME Disemba, 014 A. MAFANIKIO 1. Kuongezeka kwa uzalishaji
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA
More informationUhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI
Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI b Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI 1 Mwongozo wa Uzalishaji
More informationTANGA CEMENT PLC ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA.
TANGA CEMENT PLC 2016 ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA www.simbacement.co.tz ANNUAL REPORT 2016 ANNUAL REPORT2016 TAARIFA YA MWAKA 2016 TAARIFA YA MWAKA 2016 02 ANNUAL REPORT 2016 Chairperson s Statement
More informationMaswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA
Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA TWN Third World Network 1. WEMA ni nini? Mahindi yanayotumia maji kwa ufanisi yajulikanayo kwa kingereza kama Water Efficient Maize for Africa (WEMA) ni mpango
More informationKilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira
Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kiongozi hiki kimeandaliwa kikiwa ni sehemu ya mradi wa
More information