Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
|
|
- Edwina Bridges
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1 Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba S
2 Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh Rajani 2 Elimu inayotolewa ni lazima ijenge mambo matatu kwa kila mwananchi, akili ya kuuliza, uwezo wa kujifunza kutoka kwa wengine - na kuyakataa au kuyakubali kutokana na mahitaji yake - na uwezo wa kujiamini kama raia huru na sawa katika jamii, anayethamini wengine na kuthaminiwa kwa anayofanya na siyo kwa anachopata Julius Nyerere, Elimu ya Kujitegemea. Utangulizi Hali ya elimu ikoje miaka arobaini baada ya uhuru? Sasa hivi tuna Mpango wa Maendeleo Elimu ya Msingi (MMEM), ambao ni habari nzuri sana. Baada ya miongo miwili ya kuanguka na kusahauliwa, hatimaye kuna kitu kinatokea. Kipindi cha miaka ya 1970 Tanzania ilipiga hatua za kuridhisha katika kupanua elimu kwa wote (UPE). Mwaka 1980 uandikishaji ulikaribia asilimia 100. Lengo la kila mmoja kupata elimu ya bure lilikuwa linaonekana wazi. Mwalimu Nyerere alifahamika duniani kote kwa nia yake ya kuwapatia watu wake elimu, ambayo ingewakomboa kutokana na umaskini. Lakini hali hii ilibadilika ghafla kuanzia mwanzoni mwa miaka ya Matatizo ya uchumi yaliyotokana na vita vya Uganda, kushuka kwa bei za bidhaa kutokana na bei ya mafuta kupanda, usimamizi mbaya wa uchumi wa ndani na kuvunjika kwa mahusiano na taasisi za fedha za kimataifa uliikosesha Serikali mapato na kupoteza mwelekeo wake. Nguzo kuu za sera ya Ujamaa, kama utoaji wa elimu bure, uliathirika kutokana na mpango wa kuchangia gharama Kufika mwaka 2000, idadi ya watoto walioandikishwa iliporomoka hadi asilimia 77. Utafiti ulionyesha takriban zaidi ya nusu ya watoto wote walikuwa hawamalizi shule ya msingi, ambapo waliotoka familia fukara ndiyo wengi. Ubora wa elimu ambao haukuwa wa kuridhisha tangu awali ulizidi kushuka kufikia moja ya viwango cha chini duniani. Jitihada za kurekebisha hali ya elimu zilizaa mrundiko wa taarifa zilizoandikwa na wataalam kuelezea hali halisi. Lakini elimu iliendelea kuporomoka. Ndio maana MMEM, iliyozinduliwa mwishoni mwa mwaka 2001, na kuanza utekelezaji rasmi 2002, imeleta mabadiliko na matumaini mapya. Kati ya sera muhimu za nchi yetu katika muongo huu, ada zote za shule za msingi na michango ya lazima ilifutwa kuhakikisha hakuna mtoto anayeachwa kutokana na kukosa uwezo wa kulipia. Matokeo yake yalionekana mara moja. Mwaka 2002, Uandikishaji darasa la kwanza ulipanda watoto kufikia milioni 1.6, kutoka milioni 1.1 mwaka uliotangulia. Idadi ya uandikishaji ilipanda kwa asilimia 100 kwa kipindi cha mwaka mmoja. Zaidi ya madarasa 16,000 yalijengwa kwa msaada wa ruzuku za maendeleo na nguvu za wananchi. Takriban walimu wapya 7,000 waliajiriwa. Mageuzi haya yalishirikisha Serikali, wafadhili na Mashirika ya hiari yalionekana kuanza kunyooka. MMEM ni jaribio la kufurahia. Serikali inastahili pongezi za dhati kwa hilo. 1 Nakala halisi ya mada hii iliwasilishwa katika baraza la wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dar es Salaam, Mei, 2003 Mada hii ya Uchambuzi ulichapishwa kwa mara ya kwanza na HakiElimu katika lugha ya Kiingereza mwaka Rakesh Rajani ni Mkurugenzi Mtendaji wa HakiElimu 1
3 Wakati tunaiangalia elimu miaka 40 baada ya uhuru, tunahitaji kurudi nyuma na kutafakari kwa kina. Ina maana gani miaka 40 baada ya uhuru, kufikia kiwango ambacho tulishakifikia miaka 20 iliyopita, katika miaka ya 1980? Na nini katika elimu tunachosherehekea? Kwamba majina ya watoto yako kwenye orodha na pengine wanasoma katika shule zenye kuta za matofali, zege na mapaa ya mabati? Hakuna shaka yote haya ni muhimu. Lakini inaonyesha nini pale ambapo haya tu ndiyo tunaweza kujivunia miaka 40 baada ya uhuru? Insha hii ina sehemu tatu. Katika sehemu ya kwanza nitaonyesha hali ya elimu ya msingi ilivyo sasa na kutaja mambo yanayokera hata baada ya kuanzishwa kwa MMEM. Sehemu ya pili nitageukia maandiko ya Mwalimu Nyerere juu ya elimu, na kuyatumia kama kioo kuonyesha hali halisi ilivyo. Na katika hatua ya tatu, ya hitimisho, nitapendekeza ili kupata miundo endelevu katika elimu mambo ambayo bado hatuna kwa sasa, mfumo mwingine kabisa wa mtazamo wa siasa na kijamii na siyo tu mabadiliko ya kitaalam na kiufundi na kisera lakini vuguvugu la wananchi makini na wenye mwamko nchini kote, ambao watahakikisha tunayo elimu ifaayo. Mambo mawili inapasa niyaseme: Kwanza, makala hii iliandikwa kwa ajili ya kongamano la Chuo Kikuu, lakini nitazungumzia kuhusu elimu ya msingi. Zipo sababu nyingi za kufanya hivi. Mojawapo ni kuwa Chuo Kikuu, wakiwemo maprofesa na wanachuo, wanatakiwa kujishughulisha zaidi katika harakati za elimu ya msingi. Ukiachia washauri wachache, mchango wa Chuo Kikuu, katika mabadiliko yanayofanyika haupo kabisa. Nini utakuwa mchango wa Chuo Kikuu kama hakijishirikishi katika swala kubwa la kisera lililoko mbele ya jamii leo hii? Pili, pengine ningetakiwa kuzungumzia kuhusu elimu za sekondari. Sitafanya hivyo, lakini budi sote tuelewe tatizo moja. Sasa hivi Tanzania ni asilimia 7-8 tu ya watu wote ambao wanapata elimu ya sekondari. Hiki ni kiwango cha chini sana duniani, ambako takwimu zinapatikana. Uganda wametupita mara mbili na Kenya mara nne. Hii ni fedheha kwa taifa, baada ya miaka 40 ya uhuru, hii ni kashfa. Swala ni kwamba tuko wapi, mkiwemo ninyi wa Chuo Kikuu, tunafanya nini? 1. Hali ya Elimu ya Msingi Tanzania 1.1 Upatikanaji wa Elimu MMEM inaleta mabadiliko nchini kote, lakini muhimu kuelewa kuwa tunaishi katika nchi yenye tofauti kubwa. Katiba yetu inasisitiza usawa wetu, lakini kipimo chochote cha elimu kinaonyesha kuwa nafasi aliyonayo mtoto wa kijijini sehemu za ndanindani ya Tanzania ni tofauti kabisa na ile ya mtoto aliyepo Upanga mjini Dar es Salaam. Tofauti kati ya wilaya ni kubwa zaidi. Kwa mfano mwaka 2000 wakati watoto waliandikishwa kwa takriban asilimia 94 Kibaha na asilimia 87 Ilala, Lindi vijijini ilikuwa asilimia 28 na asilimia 37 Ngorongoro. Kati ya mwaka 1995 na 2000, uwiano wa idadi ya watoto walioandikishwa ilikuwa asilimia 15 zaidi kwa mijini ikilinganishwa na vijijini. Cha kushangaza zaidi ni tofauti iliyopo ndani ya wilaya kati ya kata na kata. Takwimu zake hazichapishwi na mifumo au taasisi za taifa na ni vigumu kuzipata. Lakini utafiti wa hali halisi ya shule kuanzia 1999 na 2000 unaonyesha tofauti kubwa. Temeke kwa mfano, katika kata za Somangila na Kurasini, zilikuwa na viwango vya uwiano kati ya asilima 80-90, wakati Tandika ilikuwa na asilimia 27 na Mjimwema asilimia 15 tu. (Ni dhihaka ya namna gani kwa mtoto kuishi Mjimwema wakati matajiri wanafaidi fukwe za kusini). Hizi takwimu ni za muda mfupi 2
4 kidogo na inawezekana MMEM imeleta mabadiliko. Je, tunajua kama kweli tofauti kubwa hizi na athari zake katika jamii zinapunguzwa? Wakati tukisherehekea watoto wanakwenda shule, haki inadai tuangalie wale walioachwa nyuma. Ni akina nani hawa? Sera ya MMEM, ambayo inapingana na ushauri wa kiufundi, ni kuandikisha kwanza watoto wa miaka saba darasa la kwanza na kama nafasi ipo, kuwachukua wa miaka minane na zaidi. Taarifa zinaeleza zaidi ya watoto milioni moja wenye umri zaidi ya miaka 9 hadi 13 hawapati elimu ya msingi leo. Wengi wa watoto hawa inawezekana wanatoka katika familia zilizoathirika na VVU/UKIMWI, ambao wamelazimika kukatiza masomo yao kuangalia familia zao. Watoto waliopo nje ya shule wametakiwa wajiandikishe majina yao katika Mpango wa Elimu ya Msingi kwa Waliokosa (MEMKWA) na wasubiri elimu isiyo rasmi. Hata hivyo zoezi la ukaguzi la Serikali limeonyesha jambo hili kama mchezo mtupu. Wazazi wameandikisha watoto wenye umri wa miaka kwa mpango wa MEMKWA. Lakini halmashuri za wilaya zote, ukiachilia zile za majaribio [3] na Temeke, hazijaanzisha vituo vyovyote vya MEMKWA (Wizara ya Elimu na Utamaduni 2002:77). Naelewa kuwa hivi karibuni kazi hiyo imefanywa kwa ajili ya elimu isiyo rasmi, lakini huko chini watoto hawa bado wanasubiri, miaka 40 baada ya uhuru inaendelea. Kwa wale walio walemavu ndiyo watazidi kusubiri. Makadirio ya Shirika la Afya la Kimataifa (WHO) yanaonyesha inakisiwa ipo idadi ya watoto wenye ulemavu na taahira milioni 1.6 nchini Tanzania. Huko nyuma, mwaka 1974, Mwalimu Nyerere aliongea kwa uchungu kuhusu kukomesha ubaguzi dhidi ya watoto wenye ulemavu kwenye elimu. Lakini mwaka 2003 MMEM haina nafasi kwa watoto wenye ulemavu na hakuna kinachofanyiwa kazi kurekebisha hali hiyo. Madarasa 16,000 yaliyojengwa mwaka jana hayakuzingatia watoto walemavu. Mipango ya kuongeza walimu na vitabu havizingatii matatizo ya walemavu. Miaka 40 baada ya uhuru, bajeti yetu pia haina fungu lao la kutosha. Akiongelea kuhusu mageuzi ya elimu mwezi Aprili 2003, mwakilishi wa Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) alisema, kwetu, uhuru bado hatuna. 1.2 Ubora wa Elimu Mpaka sasa tunazungumzia tarakimu tu za nani yupo shule na nani hayupo. Pengine jambo la kutilia maanani zaidi ni ubora wa elimu. Ripoti iliyochapishwa hivi karibuni inaeleza vizuri kuwa: ongezeko kubwa la watoto kuandikishwa linaonekana katika miaka ya karibuni. Lakini viwango vya kuandikisha pekee havitoshi. Tunategemea watoto wanapoandikishwa kuendelea kusoma katika mazingira yanayofaa na kufanya vizuri katika mitihani yao na kuendelea na sekondari mpaka pale uwekezaji wa kutosha utakapofanyika kuhakikisha ubora wa elimu ya msingi unakuwepo, wanafunzi na wazazi wanaweza kukatishwa tamaa na mpango wa elimu na kusababisha kupoteza mafanikio yote yaliyopatikana (URT 2003:ukurasa 23-24) Inakubalika wazi kwamba wanafunzi wana vitabu vichache pamoja na vifaa vingine vya kujifunzia. MMEM ina fungu la kununulia vitu hivi, lakini taarifa kutoka jumuiya zinaonyesha kuwa shule nyingi bado hazijapokea vitabu na vifaa vingine kwa kiwango cha kuridhisha. Vitabu vichache vilivyopo vinashikiliwa na walimu kwa kisingizio cha kuvilinda visiharibiwe au kupotezwa na wanafunzi! Ubunifu mkubwa wa MMEM ni kutoa dola 10 (takriban shilingi 10,000/-) kwa kila mwanafunzi kwa mwaka kama ruzuku ya uendeshaji. Kifungu ambacho ni kidogo sana ukilinganisha na hali halisi na mahitaji. Hata hivyo, ni afadhali kuliko shule zilivyokuwa zinapata miongo kadhaa nyuma. Taarifa za mwaka 2002 hata hivyo zinaonyesha shule nyingi zimepokea 3
5 dola 2 (au shilingi 2,000) tu kwa kila mwanafunzi. Hizi ni kwa ajili ya kuongeza ufanisi, mitihani, karatasi, kalamu, chaki na rangi nyeusi ya kupaka ubaoni, na gharama zote nyingine isipokuwa mishahara ya walimu, kupandishwa daraja na ujenzi wa madarasa mapya. Gharama zote hizi kutoka shilingi 2000 tu! Fedha ambayo inatosha kununulia sahani moja ya mlo mitaani au kikombe cha kahawa katika hoteli ya Royal Palm. Miaka 40 baada ya uhuru. Walimu ndio kiini cha shule yoyote nzuri. Lakini hali zao bado zina mashaka. Wengi wao hawafundishwi na kuandaliwa ipasavyo kufanya jukumu nyeti sana nchini mwetu. Hivi sasa ni nusu yao tu wenye vyeti vinavyostahili (ingawa siyo wakati wote cheti ni dalili ya uwezo). Mgawanyo wao katika maeneo ya kazi pia hauna uwiano. Ingawa asilimia 59 ya walimu mijini walikuwa wana vyeti mwaka 2000, kule vijijini ambako ndiko watu wengi wanaishi, asilimia 45 tu ndiyo walikuwa na vyeti. Uwiano wa wanafunzi kwa walimu nao ulikuwa unapishana kwa mwaka huo huo, kutoka chini ya kiwango 30:1 Bukoba mjini na Morogoro mjini hadi 70:1 Meatu na zaidi ya 80:1 Mafia. Ripoti za vyombo vya habari mara nyingi zinazungumzia mrundikano wa wanafunzi na upungufu wa walimu, katika shule nyingi hivi sasa. Miezi michache nyuma tulisoma juu ya shule ambayo watoto huenda likizo, siku mwalimu pekee aliyepo akiugua. Katika gazeti la Nipashe toleo la Julai 13, 2002 tumesoma mwalimu mmoja anafundisha darasa la kwanza hadi la tano mjini Arusha. Picha za wanafunzi waliojazana darasani na wanaofundishwa na mwalimu mmoja ni za kawaida. Katika hali kama hizi ualimu inakuwa kama kazi ya kuzuia fujo, huku fimbo zikitembea, badala ya kuwa kazi ya maingiliano na kujifunza. Mashirika kama Kuleana na UNICEF yametoa tahadhari ya vitendo visivyokubalika kisheria vya kuendelea na viboko mashuleni, lakini hakuna ushahidi hali hii inapungua. Idadi kubwa ya wanafunzi darasani inaweza kuwa ni kichocheo cha vitendo vya adhabu za viboko. Viwango vya vipimo vya mitihani ya taifa vimeongezeka kwa mwaka Hili ni jambo la kutia moyo. Lakini hadithi ni kuwa kwa kila wanafunzi wanne wanaofanya mtihani wa taifa watatu wanashindwa kufaulu (takriban moja ya tatu hadi nusu yao huwa wameacha shule kabla ya hatua hii), hata kama alama za kufaulu ni za chini mno. Nimekutana na wanafunzi wa darasa la saba ambao hawawezi kuandika hata aya moja yenye kueleweka, achilia mbali kufikiri kwa umakinifu na ubunifu. Katika sehemu nyingi tofauti za jinsia kwenye mitihani ziko wazi ambapo karibu nusu ya wanafunzi wa kike wanakuwa nyuma ya wanaume kimaendeleo darasani. Jambo lililomsababisha mwenzangu mmoja kusema kuwa, mfumo wa elimu yetu umefanikiwa kutoa wanafunzi wanaoshindwa. Miaka 40 baada ya uhuru. 2. Kufikiri na Nyerere: Tunaelekea Upande Sahihi? Mjadala hapo juu unadhihirisha baadhi ya changamoto muhimu kuhusu elimu ya msingi ambazo MMEM itahitaji kuzikabili. Mabadiliko huchukua muda. Ukubwa wa tatizo ulivyo haitegemewi mafaniko kupatikana mara moja. Lakini swali muhimu ni hili: tupo katika mwelekeo sahihi? Baadhi ya mapungufu, kama haki za watoto wenye ulemavu, zimetajwa hapo awali. Yapo maswali mengine ya msingi. Nini kusudio la elimu? Nini maana ya mtoto aliyeelimika? Tunachotaka kutoka elimu ya darasa la saba ni nini? Nini dira yetu kuhusu jukumu la elimu na raia aliyeelimika katika jamii? Tunatumia muda mfupi sana kufikiria mambo haya, lakini yana maana kubwa kwa mustakabali wa nchi yetu. Kama mnavyoelewa Mwalimu Nyerere aliwaza, aliandika na kuongelea mengi juu ya elimu. HakiElimu na washirika wetu tumechapisha kitabu juu ya maandiko yake kuhusu elimu (Lema, et al 2003). Kwa hiyo, kwa nini tusifikiri pamoja na Mwalimu Nyerere, kuyatafakari mabadiliko na kujaribu kujibu swali. Je, tunaelekea upande sahihi? 4
6 Hapa nataka kufanya jambo moja rahisi sana. Nitamnukuu Mwalimu Nyerere kwa mapana katika nyanja tano za elimu. Mimi nitatoa mawazo yangu kwa uchache, na kuacha fikra zake ziongee. Nia yangu kwako, wewe, utafakari na kuamua. 2.1 Kusudio la Elimu Kwa Mwalimu Nyerere elimu na jamii viliingiliana sana. Kwa Tanzania huru, elimu ilikuwa ijenge mtazamo fulani na jamii mpya. Katika mada yake kubwa, mwaka 1967, juu ya Elimu ya Kujitegemea, Nyerere anasema: Hii ina maana mfumo wa elimu Tanzania lazima usisitize juhudi za pamoja, siyo maendeleo ya mtu mmoja mmoja, lazima usisitize misingi ya usawa na wajibu wa kutoa huduma ambao unaendana na kipaji maalum, iwe kwenye ufundi seremala, ufugaji au katika kutafuta elimu. Na haswa, elimu yetu ni lazima ipingane na mawazo ya kiburi cha usomi, kwani hii inapelekea kwa waliosoma kuwadharau wale ambao vipaji vyao siyo vya kisomi au wasio na uwezo wowote lakini ni binadamu wa kawaida. Dharau kama hii haina nafasi katika jamii ya raia walio sawa. Aliendelea kuongeza:. raia huru wa Tanzania wataamua maswala yanayohusu jamii wenyewe; hakuna na wala hakutakuwepo msahafu wa siasa utakaotoa majibu yote kuhusu matatizo ya jamii, siasa au uchumi yatakayolikabili taifa letu huko mbele...watu walio huru tu na wanaotambua thamani yao na usawa wao ndiyo watakaojenga jamii huru. 2.2 Walimu na Ualimu MMEM ina vifungu kwa ajili ya mafunzo ya walimu na kujiendeleza. Mafunzo kabla ya kazi yanapaswa kuwa ya mwaka mmoja wa masomo na wa pili wa kufanyia mazoezi ya kazi shuleni. Mkazo pia utapewa kwenye kukomaza ujuzi walimu waliokuwepo. Mambo yote haya bado kuanzishwa kikamilifu na kufanyiwa kazi. Katika hotuba yake Nguvu ya Walimu aliyotoa Chuo cha Walimu Morogoro, mwaka 1966, Mwalimu alisema yafuatayo; Taifa letu taifa lolote ni kubwa, ni zuri na mahali pazuri pa kuishi na kuendelea kama raia wake watalifanya liwe hivyo. Uongozi wake unaweza kuwa mzuri, mbaya au usiojali lakini kama watu wake wameamka na wanajitambua haitachukua muda mrefu kuwakilisha mtazamo wa jamii. Na ukweli ni kuwa ni walimu, kuliko kundi lolote jingine ndio wanaoamua mtazamo huu, na kubadili mawazo na matumaini ya taifa. Cha muhimu zaidi ni jinsi walimu wanavyofundisha kwa hili sina maana mbinu za kupeana taarifa tu, ingawa hizi zina uwezo wa kuongeza au kudumaza uwezo wa mtoto kujifunza ujuzi. Nina maana zaidi ya hiyo. Mwalimu anapokuja darasani amechoka au kuonekana amechoka, amekata tamaa na hana hamu yoyote ya kazi, iwapo mwalimu ataona kwamba kila kazi yenye kuhitaji nguvu ifanywe na watoto wakati yeye akiangalia tu, au iwapo mwalimu ataona kila mwanafunzi ni kero, mzembe, kwa hali hiyo watoto watajenga mawazo kuwa kazi ni kitendo cha kuepukwa, na kuwa mafunzo ni kitu cha mpito tu, na kwamba namna ya kutumia madaraka ni kuwafanya watu wengine wakutumikie 5
7 Kama mwalimu atajipendekeza kwa viongozi wanaomtembelea, na kumwona mkulima maskini kama takataka, watoto watakuwa wakielewa kuwa hiyo ndiyo tabia inayofaa katika maendeleo ya taifa letu. Haitasaidia chochote nini mwalimu anafundisha katika somo la uraia au mahala penginepo, watajifunza kutokana na vitendo vyake. Lakini mtu anayeheshimu watu wote, anayejadili msimamo wake kwa ufasaha, bila ya jazba kwa utulivu na kila mtu bila ya kujali madaraja yao, mwalimu kama huyo anajenga moyo wa usawa, wa urafiki na kuheshimiana. Na anafundisha kwa mfano jambo ambalo ndio la maana zaidi lililopo. 2.3 Ushiriki wa Wanafunzi na Uraia Vipi kuhusu wanafunzi? MMEM ina kiambatanisho juu ya Uimarishaji wa Kitaasisi ambao unazungumzia juu ya demokrasia ya utawala wa shule, kushirikisha wanafunzi kufanya maamuzi, ikiwemo wao kuwa wajumbe kamili wa kamati za shule. Uhusiano kati ya ushiriki wa wanafunzi na demokrasia unaonekana kama jambo geni, lakini Nyerere aliongelea katika Elimu ya Kujitegemea : Wanafunzi wapewe nafasi ya kufanya maamuzi kadiri inavyowezekana ingawa mwanzoni makosa mengi yatafanyika, na hata hivyo itakuwa makosa kuwaachia fursa yote wanafunzi wadogo tangu mwanzoni. Lakini ingawa mwongozo ni lazima utolewe na uongozi wa shule, na nidhamu kusisitizwa, wanafunzi ni budi washiriki kwenye maamuzi na kujifunza kutokana na makosa yao. Na katika mkutano wa Wakuu wa Shule za Sekondari, Dar es Salaam, Desemba 1967, alisema: Mafanikio ya sehemu kubwa ya jaribio letu kujenga jamii ya kidemokrasia ni mkusanyiko wa mjadala huru kufuatiwa na utendaji wa maamuzi ya pamoja; kama watoto watazoea haya shuleni watakuwa wanajifunza majukumu ya uraia katika jamii huru. 2.4 Mitihani Mitihani ya kumaliza shule ndiyo kigezo kinachotumika leo, kupima uwezo na maendeleo katika elimu ya msingi. Kwenye mada yake ya mwaka 1967 juu ya Elimu ya Kujitegemea Mwalimu Nyerere alikuwa na haya ya kusema: shule zetu za msingi na sekondari ni lazima ziwatayarishe vijana wetu kukabiliana na hali halisi na mahitaji ya Tanzania; kufanya hivyo kunahitaji mabadiliko ya kimapinduzi, siyo tu katika mfumo wa elimu lakini pia katika tabia zilizojengeka katika jumuiya. Kikubwa inahitaji mitihani ishushwe daraja machoni mwa Serikali na jamii...kimsingi inapima uwezo wa mtu kujifunza mambo na kuyaelezea anapotakiwa kwa wakati fulani. Mara nyingi haifanikiwi kupima uwezo wa mtu kuchambua na kufikiri zaidi, haipimi tabia na utayari wa kutumikia. Mitaala na mihtasari yetu iliyopo ni kwa ajili ya mitihani tu - mara chache hii inakuwa tofauti na hivyo. Mwalimu anayewasaidia wanafunzi mara nyingi anaangalia mitihani ya nyuma na kuamua ni maswali yapi yatatolewa tena na kukazania kufundisha maeneo hayo, akijua hiyo ndiyo njia ya kuhakikisha anawapa nafasi nzuri wanafunzi ya kufaulu kwenda sekondari au chuo kikuu 6
8 Tunachotakiwa kufanya sasa ni kufikiria aina gani ya elimu tunayohitaji kutoa, na tukishafikiri hivyo tufikirie aina ya mitihani inayofaa kumalizia mfumo upi wa masomo. Ndipo ubuniwe mtihani kwa ajili ya elimu iliyotolewa. 2.5 Elimu ya Watu Wazima na Demokrasia Inakubalika kuwa mipango ya elimu ya watu wazima imeanguka nchini kote. Bado wako watu wazima wengi wasio na elimu ya msingi. Kutokana na uchunguzi wa hivi karibuni wa Matumizi ya Kaya (URT 2002) takriban asilimia 40 ya wanawake vijijini hawana uwezo wa kusoma wala kuandika, miaka 40 baada ya uhuru. Miaka iliyopita, 1976, Mwalimu Nyerere alikuwa na haya ya kusema: Jambo moja lisiloepukika ni kwamba lazima rasilimali zitengwe kwa ajili ya elimu ya watu wazima. Bila ya hivyo haitafanyika! Kupo kusisitiza katika wakati wa matatizo ya uchumi jambo ambalo kwa nchi maskini ni la kila mara kwa serikali kubana pesa kwa ajili ya elimu ya watu wazima. Na kuna tabia, pia wakati wa ukosefu wa wataalam, kuamua kuwa elimu ya watu wazima isubiri. Ipewe kipaumbele kipi, pengine ni moja ya maamuzi makubwa ya kisiasa, ambayo serikali inaweza kufanya. Kama elimu ya watu wazima itatekelezwa, tena kikamilifu, ni nguvu kubwa ya watu walio huru na ambao watasisitiza kuamua maisha yao ya baadae. Elimu inaamsha udadisi na kuchokoza maswali changamoto kuhusu mambo ya kale na kufanyika kwa mazoea. Kijiji cha Ujamaa kilichoelimika kwa mfano, hakiwezi kukubali au kuvumilia ubadhilifu wa wahasibu wake au umangi meza wa viongozi wake. Taifa la watu waliosoma litahoji vitendo vya wawakilishi wao akiwemo Rais. 3. Hitimisho Leo nimeshirikiana nanyi mambo mawili. Nimeelezea hali ya elimu ya msingi Tanzania na kuwakaribisha kutafakari pamoja na Mwalimu Nyerere. Nina imani baadhi yenu mtaamua kujishughulisha kubadilisha hali ilivyo. Nasema haya kwa sababu naamini mchango wenu ni muhimu. Maswali ambayo Mwalimu Nyerere anauliza yanahitaji mjadala na jamii kushiriki. Wataalam na warasimu wanalo jukumu la kufanya, ingawa sidhani kama peke yao, wanaweza wakaleta mabadiliko makubwa tunayohitaji. Kwa msaada wa wafadhili na mashirika ya hiari, Serikali inapiga hatua za maana juu ya MMEM. Lakini inatakiwa ninyi pamoja na watu wa kawaida, nchini kote, kuuliza maswali juu ya madhumuni, maana na namna ya elimu. Inahitaji raia waliochangamka, wanafunzi, wazazi, walimu na wengine kuelewa na kuhoji sera, kujadili mapungufu kati ya sera na utendaji na kuchukua maamuzi yatakayoboresha shule. Inahitaji taarifa za uhakika kuhusu mazuri na mabaya yanayofanyika. Inahitaji vuguvugu la kijamii lenye mwamko wa dira, wa lengo na mkakati. Mabadiliko ya elimu yanahitaji aina hii ya utendaji wa kidemokrasia kwa sababu ndiyo tumaini kubwa la kuiweka serikali yetu macho na matarajio ya watu. Nimalizie na nukuu moja ya mwisho ya Nyerere, ambae alielewa thamani ya msukumo wa jamii. Katika kutayarisha kitabu cha Nyerere kuhusu Elimu, makala ya mwanzo kabisa tuliyogundua ilikuwa hotuba yake ya 1954 kwenye Baraza la Kutunga Sheria, ambayo aliongelea juu ya ari 7
9 kubwa ya elimu. Nyerere alilaumu serikali ya kikoloni juu ya hatua zilizochukuliwa za mageuzi ya elimu, huku gavana akikasirishwa na wazalendo aliowaita wakorofi kwa hoja zao. Katika hotuba yake, Mwalimu Nyerere alisema: Serikali ndiyo inayoweza kutambua kuwa mtu ni mkorofi au ana haki ya kuikosoa serikali Natarajia watu nchini hawatachukulia onyo la Gavana dhidi ya wakorofi nchini kumaanisha kuwa hakuna ukosoaji dhidi ya serikali za mitaa au serikali kuu utakaovumiliwa, kwa sababu naona itakapofika hapo, mheshimiwa, watu wengi wataondolewa fursa ya pekee ya ama kutoa mawazo kwa mamlaka kuhusu jinsi ya kuendesha mambo au kupendekeza tu wanayofikiria hata kama yanaonekana ni ya upuuzi kiasi gani kwa wengine. Marejeo Lema, E; Mbilinyi, M na Rajani, R (2003) Nyerere kuhusu Elimu, HakiElimu na E & D Ltd. Ministry of Education and Culture (2002), Taarifa ya Tathmini ya MMEM Julai 2002 United Republic of Tanzania URT (2001), Primary Education Development Plan (PEDP), Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Elimu (ESDP) United Republic of Tanzania URT (2002), Household Budget Survey United Republic of Tanzania URT (2003), Poverty and Human Development report, Mkuki na Nyota Publisher United Republic of Tanzania URT and UNICEF (2001), Situation Analysis of Children in Tanzania 8
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari
More informationInformation for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013
www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper
More informationKufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007
Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationNilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania
Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza
More informationSautiElimu. Sauti Yako Isikike
SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationElimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi
Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau
More informationJAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationUfanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania
Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Desemba 2014 1 Shukurani Ripoti hii iliandikwa na Dk. Mkumbo. Ushauri wa kitaalamu ulitolewa na Elizabeth Missokia na Godfrey
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationElimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...
Elimu Bora, lakini... Shukrani za dhati kwa wote waliotusaidia katika kutayarisha kijitabu hiki: Nsa Kaisi, Mshauri wa Rais, kwa mchango wake mkubwa wa mawazo Wafanyakazi wote wa HakiElimu 2003-2004 Many
More informationWIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationUtumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More informationIn the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment
In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationElimu-Jumuishi Kwa Vitendo
Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo Taarifa ya Warsha Kuhusu Elimu-Jumuishi Iliyofanyika Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Kujifunza hakuna mwisho. Kazi ya vikundi imenipa fursa ya kujieleza bila kuhofia kuwa ningekosea.
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA
More informationHati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationTufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue?
Tufundishane! Let s teach each other! This newsletter is published by The Foundation for Tomorrow and is meant to be a venue for teachers and schools to share and learn from each other s best practices.
More information5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban
More informationTAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA
TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0
More informationDibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi
Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini
More informationUfundishaji wa lugha nyingine
CHUO CHA ELIMU CHA KIMATAIFA OFISI YA ELIMU YA KIMATAIFA Ufundishaji wa lugha nyingine Na Elizabeth B. Bernhardt ELIMU MAZOEA KITABU NA. 20 1 Chuo cha Elimu cha Kimataifa (The International Academy of
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3
More informationLUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI
LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI SIKOMBE YIZUKANJI YORADI TASNIFU YA KISWAHILI KWA MINAJILI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (MA. KISWAHILI) KITIVO CHA SANAA
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More informationKAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA
KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI
More informationMazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo. Zanzibar, 7-10 Februari 2006
Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Imechapishwa na: The Atlas Alliance Schweigaardsgt 12 SLP 9218 Grønland 0134 Oslo, Norway Simu: +47
More informationATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR
ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini
More informationKuwafikia waliotengwa
Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E 2 0 1 0 Ripoti
More informationEllen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar
Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ukristo leo unadhihirisha waumini karibu bilioni mbili katika maelfu ya madhehebu tofauti na tofauti na madhehebu. Kati ya hizi, zaidi ya 500 madhehebu
More informationElimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi
Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Gervas Zombwe 1 1. Utangulizi Katika mazingira ya kawaida kabisa ndani ya jamii yetu, Imezoeleka kusikia au kuona watu wakioanisha dhana ya elimu
More informationMAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA
MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA
More informationusudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-
Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa
More informationRipoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya
More informationMIONGOZO MIWILI KUPAA NA KUTUNGULIWA KWA AZIMIO LA ARUSHA
KIGODA CHA TAALUMA CHA MWALIMU NYERERE MIONGOZO MIWILI KUPAA NA KUTUNGULIWA KWA AZIMIO LA ARUSHA Yamekusanywa na kuhaririwa na: Bashiru Ally Saida Yahya-Othman Issa Shivji CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
More informationJHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI
JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More informationUfunguo wa Kutaalamika Haraka
0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11
More informationRipoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013
W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa
More informationKITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO
KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa
More informationKiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika
Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to
More informationProgramu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi
Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini
More informationRIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI
International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa
More informationMKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA
More informationUtangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu
Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu BLOOD PRESSURE UK Shinikizo la damu ndicho chanzo kikubwa cha ulemavu na vifo vya mapema kule Uingereza, kupitia kiharusi, mshtuko wa moyo na maradhi ya moyo.
More informationMwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo
Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu Nyenzo ya Mafunzo Vi Agroforestry Vi Agroforestry ni shirika la ushirikiano la maendeleo la Sweden, linalopambana dhidi ya umasikini na
More informationPronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:
More informationMACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI
This booklet on Becoming a Parent was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at. MACHAGUO
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationMhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, KWENYE SHEREHE YA KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA, TAREHE 08 JUNI 2008, MSIMBAZI CENTRE, DAR ES SALAAM Mhashamu
More informationSummaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili
Summaries of GC Reports 2012, Vol. 2, Sec. 1, Swahili 1. 2-Muhtasari wa Ukurasa wa Ripoti ya Miaka minne ya Bodi Kuu ya Kanisa & Jamii............................... 2 2. Kamati ya Kawaida ya Malipo ya
More informationUnyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa
Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda
More informationEarly Grade Reading Assessment for Kenya
EDDATA II Early Grade Reading Assessment for Kenya Baseline Instruments: Kiswahili and English EdData II Technical and Managerial Assistance, Task Number 4 Contract Number EHC-E-01-04-00004-00 Strategic
More informationORDER NO BACKGROUND
In the matter of an Application by the DAR ES SALAAM URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (DAWASA) For a Tariff Adjustment, Submitted on January 8 th, 2008 (TR-W-08-001) ORDER NO. 08-001 1.0 BACKGROUND
More informationMwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza
Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)
More informationVijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO. Training and Research Support Centre
Shangazi Stella Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO Training and Research Support Centre Zimbabwe Shangazi Stella Kiongozi cha Mwezeshaji
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA
More informationKimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:
Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200
More informationAzimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]
This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)
More informationTaarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania
Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3
More informationUFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI
JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa MFUMO WA RUZUKU YA MAENDELEO YA MTAJI WA SERIKALI ZA MITAA (LDCDG) UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI Kijitabu cha Mshiriki
More informationMTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya
Jina Nambari.. Shule... 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI / AGOSTI. 2007 MUDA: SAA 2 ½ MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya 102/3 KISWAHILI FASIHI
More informationKuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo
Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo Mazoezi ya wenye umri wa miaka 11-14 Hivi Ndivyo Nilivyo kwa wenye umri wa miaka 11-14 Kuhusu Hivi Ndivyo Nilivyo Ikiwa
More informationTora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA
SOMO LA KWANZA UTANGULIZI KWA TORA For videos, study guides and other resources, visit Third Millennium Ministries at thirdmill.org. 2014 nathird Millennium Ministries Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu
More informationKuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia
Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa
More informationMKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI
More informationMwongozo wa Familia wa Kujifunza
Shule za umma za kata ya Fayette 1 Mwongozo wa Familia wa Kujifunza Muhtasari wa yale watoto wanastahili kufahamu na kuweza kufanya na njia za familia kuongeza masomo nyumbani. Tunaamini familia ni wenzetu.
More informationMwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health
Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health Wasiojua kusoma na kuandika katika karne ya 21 hawatakuwa wale wasiojua kusoma na kuandika lakini wale ambao hawawezi kujifunza, kutojifunza na kujifunza
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationMATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza
1 Matumizi bora ya Facebook kwa Biashara MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA Kwa Wanaoanza For IT Services & Web Solutions Web: Email: info@dudumizi.com Phone: 0768816728 2 Matumizi bora ya Facebook kwa
More informationKUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA
KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa
More informationMwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo
More informationTIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees
TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST
More informationIn the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment
In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities
More informationHAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII
HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY
More informationHISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU 9 DESEMBA 2011.
Saint Augustine University of Tanzania From the SelectedWorks of Daudi Mwita Nyamaka Mr. Winter December 9, 2011 HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU
More informationNGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017
TAARIFA Agosti 2017 NGUO MPYA ZA UKOLONI Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika Jumuiya ya Jamii ya 2007: Wajumbe wanaadhamana Nairobi dhidi ya EPAs. SwissInfo Tangu mwaka
More informationK. M a r k s, F. E n g e l s
W a (any a kazi wa nchi zote, unganeni! K. M a r k s, F. E n g e l s Maelezo ya chama cha kikomunist Idara ya Maendcleo Moscow Tafsiri hii ya "Maelezo ya Chama cha Kikomunist" inatokana na maandishi
More informationMradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda
WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationSonga kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa
Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided
More informationYaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!
Yaliyomo Kuhusu kitabu hiki Kuhusu kitabu hiki.........................................................1 Unapojisikia vibaya.........................................................2 Unapoanza kuwa mzima
More informationMALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU
MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa
More information