MIONGOZO MIWILI KUPAA NA KUTUNGULIWA KWA AZIMIO LA ARUSHA

Size: px
Start display at page:

Download "MIONGOZO MIWILI KUPAA NA KUTUNGULIWA KWA AZIMIO LA ARUSHA"

Transcription

1

2 KIGODA CHA TAALUMA CHA MWALIMU NYERERE MIONGOZO MIWILI KUPAA NA KUTUNGULIWA KWA AZIMIO LA ARUSHA Yamekusanywa na kuhaririwa na: Bashiru Ally Saida Yahya-Othman Issa Shivji CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere katika Umajumui wa Afrika S. L. P , Dar es Salaam, Tanzania Simu: Barua pepe: Tovuti: nyererechair.udsm.ac.tz Kitabu hiki kimechapishwa kwa ufadhili wa Shirika la HakiElimu katika maadhimisho ya Tamasha la Tano la Kitaaluma la Julius Nyerere, Aprili 10-12, 2013, lililoandaliwa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere katika Umajumui wa Afrika, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

3 KIGODA CHA TAALUMA CHA MWALIMU NYERERE CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere katika Umajumui wa Afrika S. L. P , Dar es Salaam, Tanzania Simu: Barua pepe: Tovuti: nyererechair.udsm.ac.tz Kitabu hiki kimechapishwa kwa ufadhili wa Shirika la HakiElimu katika maadhimisho ya Tamasha la Tano la Kitaaluma la Julius Nyerere, Aprili 10-12, 2013, lililoandaliwa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere katika Umajumui wa Afrika, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ISBN

4 YALIYOMO Dibaji 4 Utangulizi: Ujio na uzito wa Miongozo Miwili 11 Kingunge Ngombale Mwiru Sura ya Kwanza 23 Azimio la Arusha la 1967 Sura ya Pili 43 Mwongozo wa TANU wa 1971 Sura ya Tatu 55 Mwongozo wa CCM wa 1981 Sura ya Nne 116 Maamuzi ya Zanzibar ya 1991 Sura ya Tano 132 Miongozo Miwili ya Chama na tabaka lililopindua Ujamaa Issa Shivji MIONGOZO MIWILI 3

5 DIBAJI Kitabu hiki kimeandaliwa na Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere kwa ajili ya kuweka kumbukumbu ya matukio muhimu katika historia ya nchi yetu tangu Uhuru. Kuna nyaraka nne katika kitabu hiki: Azimio la Arusha la 1967, Mwongozo wa 1971, Mwongozo wa 1981 na Maamuzi ya Zanzibar ya 1991, ambayo ni hotuba ya Mzee Ali Hassan Mwinyi. Kwa nini tumechagua nyaraka hizo na sio nyengine? Kwa sababu kila nyaraka ina muhula wa kihistoria wa kuhadithia. Muongo mmoja kati ya 1971 na 1981 ni kipindi cha uzalendo wa hali ya juu, uzalendo wa mrengo wa kushoto, uliozaliwa na itikadi ya Umajumui wa Afrika (Pan-Africanism). Kipindi hiki kilipewa jina rasmi la kipindi cha Ujamaa na Kujitegemea. Mwongozo wa 1981 ni waraka wa kipekee ambayo inafanya uchambuzi wa miaka 14 ya Azimio kwa mtazamo wa kitabaka, ambao, lazima tukiri, haukuwa mtazamo wa Chama wala Mwalimu. Muongo wa 1981 mpaka 1991 ni kipindi cha mpito kutoka muhula wa kizalendo na kuingia muhula wa uliberali mambo-leo. Maamuzi ya Zanzibar ya 1991 (kwa msamiati wa kisiasa huitwa Azimio la Zanzibar ), ni hotuba ya Rais wa Awamu ya Pili, inayoelezea na kuhalalisha mtazamo, mwelekeo, itikadi na sera za uliberali mambo-leo. Baada ya kuchagua nyaraka hizi, tukamuomba Mzee Kingunge Ngombale Mwiru, kutuandikia Utangulizi wa Miongozo Miwili. Mzee Ngombale anajulikana kwa sifa yake ambayo anaistahili - ya kuzungumzia itikadi na nadharia ya Chama kwa ufasaha, na kwa undani; ni kingunge hasa wa itikadi ya Chama. Yeye amekuwa mwanaitikadi (ideologue) wa Chama kwa miongo kama minne hivi. Umahiri wake wa kiitikadi unadhihirishwa vema na ukweli usiopingika kwamba amekuwa msemaji mkuu wa itikadi ya Chama katika awamu zote za utawala wa kisiasa nchini kuanzia awamu ya Mwalimu, ambayo ilikuwa awamu ya kizalendo; kupitia awamu ya Mzee Ali Hassan Mwinyi ambayo ilikuwa awamu ya mpito kuelekea kwenye uliberali mambo-leo; ikifuatiwa na awamu ya Mheshemiwa Benjamin William Mkapa, ambayo ilikuwa awamu ya kuiimarisha bila vikwazo misingi mikuu ya uliberali mambo-leo, au kwa msamiati wake 4 MIONGOZO MIWILI

6 mwenyewe, utandawazi; kufikia kipindi cha kwanza cha Mheshemiwa Jakaya Mrisho Kikwete ambaye amefuata nyayo za Mzee Mkapa na kwa mara ya kwanza utawala wake umeanza kuonja joto kali la uchumi wa ubepari wa kimataifa. Ili tuweze kuelewa kwa ufasaha na kwa kina, hasa chimbuko la Miongozo Miwili na umuhimi wake wa kihistoria, tumeweka makala ya mwanazuoni Issa Shivji, iliyoandikwa kwa mara ya kwanza mnamo 2009, inayochambua Miongozo hii kwa mtazamo wa kitabaka. Azimio la Arusha, 1967 Miaka sita tu baada ya Uhuru wetu mnamo 1961, chama tawala, TANU, ambacho kwa asili na hulka yake tunaweza tukakiita chama cha ukombozi, kilitangaza Azimio la Arusha (ang. Sura ya Kwanza). Azimio lilikuwa ni dalili ya kutambua kwamba uhuru wa nchi na watu wake haukamiliki kutokana na kupata wimbo na bendera ya kitaifa au mawaziri na viongozi wazawa. Uhuru wa kinchi kilichotawaliwa na wakoloni ni hatua ya kwanza, ya awali kabisa, katika mchakato wa ukombozi. Ukombozi katika jamii kama yetu una pembe tatu. Kwanza kuna uhuru wa nchi, kwa maana kwamba, huwezi ukawa huru katika nchi ambayo inatawaliwa kimabavu na nchi ya nje. Pili, kuna uhuru wa watu au jamii katika nchi. Unaweza ukawa na nchi huru bila ya watu kuwa huru, kwa maana kwamba hawana uwezo wa kujiamulia mambo yao wenyewe. Ingawa nchi yao ni huru, lakini bado wanajikuta kwamba kuna kundi au tabaka dogo la watu wanaowatawala na kufanya maamuzi kwa niaba yao au kwa ajili ya waliowengi. Katika hali yetu halisi, tabaka-tawala la ndani linakuwa bado chini ya himaya ya ubeberu na kwa hiyo watawala hao wanakuwa vibaraka wa matabakatawala ya kibeberu. Na hali hii inasababisha, sio tu tabaka-tawala la ndani kuwa tegemezi, lakini hata nchi yenyewe inakuwa tegemezi kwa sababu inakosa uongozi unaojitegemea na kufanya maamuzi kwa manufaa na maslahi ya watu wake. Pembe ya tatu ya ukombozi ni ukombozi wa wavujajasho kutoka makucha ya unyonyaji na ukandamizaji. Na ukombozi wa kijamii-tabaka (social MIONGOZO MIWILI 5

7 emancipation) hauwezi kupatikana bila kufanya mapinduzi ya mfumo wenyewe wa uzalishaji na utawala; kwa sababu unyonyaji na ukandamizaji havitokani na nia, dhamira au lengo la mtu binafsi. Hakuna mtu anayezaliwa akiwa mnyonyaji. Tabaka la wanyonyaji linatokana na nafasi yao katika mfumo wa uzalishaji. Ukiwa bepari, bila kujali usamaria mwema wako, lazima utakuwa mnyonyaji. Ndivyo ulivyo mfumo wa kibepari. Azimio la Arusha lilizungumzia pembe zote tatu za ukombozi. Mosi, lilitambua kwamba uhuru wa nchi hautakuwa na maana wala hautakuwa salama kama tukiendelea kuwa tegemezi, yaani, kutegemea misaada, mikopo na uwekezaji kutoka nje. Kwa sababu mikopo haitapatikana ya kutosha na hiyo kidogo itakayopatikana itaambatana na masharti yatakayoididimiza nchi zaidi. Isitoshe, hata kama tungepata misaada, mikopo na uwekezaji kwa ajili ya maendeleo, vitahatarisha uhuru wetu. Kujitawala ni kujitegemea. Kujitawala kwa kweli hakuwezekani ikiwa Taifa moja linategemea misaada na mikopo ya Taifa jingine kwa maendeleo yake. (ang. Sura ya kwanza, uk) Ukweli huu unajidhihirisha wazi tukiangalia mwenendo wetu wa kama miongo miwili iliyopita. Tumekuwa tegemezi sana kiasi kwamba leo hii hatuna uhakika kwamba tunajitawala au tunatawaliwa na wawekezaji na wafadhili wa nje, yaani, nchi za kibeberu. Pili, Azimio liliainisha matabaka-nyonyaji na matabaka-nyonywaji - mabepari na makabaila kwa upande mmoja na wakulima na wafanyakazi kwa upande mwingine. Nchi yenye Ujamaa kamili ni nchi ya wafanyakazi: haina ubepari wala ukabaila. (ang. Sura ya kwanza, uk.25) Hata hivyo, mkakati wa Azimio wa kujikomboa kutokana na unyonyaji ulikuwa ni kutaifisha njia kuu za uchumi kwa maana ya serikali kumiliki na kudhibiti viwanda vikubwa, migodi, mabenki, taasisi nyingine za fedha, na biashara za nje na ndani. Ni ukweli usiopingika kwamba Azimio lilitambua kwa dhati kuwa haitoshi serikali kumiliki njia za uchumi kama serikali yenyewe sio ya kidemokrasia, kwa maana ya kudhibitiwa na kuwajibika kwa wananchi. Hata hivyo, kama tutakavyobainisha hivi punde, katika suala la demokrasia Azimio halikufanikiwa, pamoja na kuwa na nia njema ya kukomboa wanyonge. Wanyonge hujikomboa wao wenyewe kupitia vyombo vyao na huendeleza mapambano ya kitabaka 6 MIONGOZO MIWILI

8 kwa ustadi na kwa kutumia mikakati yao wenyewe. Mapinduzi kamwe sio fadhila ya wakubwa au wasamaria wema. Mwongozo wa 1971 Baada ya miaka minne tu ya Azimio, TANU ikapitisha nyaraka nyingine ya kihistoria, Mwongozo wa TANU (ang. Sura ya Pili). Msimamo wa Mwongozo ulikuwa wa kimapinduzi zaidi kuliko ule wa Azimio. Mzee Ngombale, katika Utangulizi wake wa kitabu hiki anaeleza kwa ufasaha chimbuko la Mwongozo wa 1971 na maudhui yake. Aidha anasisitiza ibara muhimu za Mwongozo kuhusu ulinzi wa Taifa dhidi ya ukoloni wa Kireno na Kikaburu ambao waliendelea kukalia nchi za Afrika ya kusini. Kwa msimamo thabiti wa Mwalimu, vita vya ukombozi katika nchi za Msumbiji, Angola na Afrika ya kusini, viliungwa mkono na Tanzania kwa hali na mali. Kwa hivyo, Tanzania yenyewe ilikuwa katika hatari ya kuvamiwa au kushambuliwa. Ili kujilinda dhidi ya uwezekano huo, ndipo Mwongozo wa 1971 ukaweka sera ya kuwa na Jeshi la Wananchi, kwa maana ya mgambo. Kama anavyoeleza Mzee Ngombale, wananchi, hasa wafanyakazi viwandani, walishawishika sana na wakajitolea kujiunga na mgambo. Ni sahihi kabisa kwa Mzee Ngombale kusisitiza kwamba sera hii ilifanikiwa kiasi kwamba wakati nchi yetu ilipovamiwa na nduli Iddi Amin Dada, dikteta wa Uganda, askari wa mgambo walipigana kwa ustadi na ujasiri. Mchango wao kamwe hauwezi kusahaulika. Lakini, kwa mtazamo wa kitabaka, nafasi mahsusi na ya kihistoria ya Mwongozo inatokana na ibara yake ya 15. Ibara hii ambayo ilishutumu tabaka chipukizi wakati huo la warasimu viwandani na serikalini ilikuja kuwa panga na ngao ya tabaka la wafanyakazi kuibua na kuendeleza mapambano yao dhidi ya tabaka la vibwenyeye wa kirasimu. Katika historia ya mapambano ya tabaka la wafanyakazi nchini mwetu, hakuna kipindi kilichokuwa na msisimko mkubwa kama hiki ( ). Kwa sababu ambazo haziko wazi, Mzee Ngombale, ingawa anagusia ibara ya 15 katika Utangulizi wake, hakuchambua kwa undani umuhimu wa kipekee wa ibara hii katika mapambano ya kitabaka. Hata hivyo, MIONGOZO MIWILI 7

9 wasomaji wanaweza wakaangalia makala ya uchambuzi ya Shivji (ang. Sura ya Tano) kuhusu mapambano hayo. Mapambano hayo, hatimaye, yalidhoofishwa na kukosa nguvu na uhalali kwa tamko la Mwenyekiti wa Chama, naye sio mwingine isipokuwa Mwalimu. Katika hotuba yake ya Mei Mosi mwaka 1974 Mwalimu alihoji: Mnapogoma mnamgomea nani? akiwa na maana kwamba kwa kuwa viwanda na mashirika yalikuwa mali ya umma, wakiwemo wafanyakazi wenyewe, basi walikuwa wanajigomea wenyewe! Jibu la swali la Mwalimu kwamba wafanyakazi walikuwa wanamgomea nani lilipatikana katika uchambuzi wa Mwongozo wa Mwongozo wa 1981 Mchakato wa kuandaa Mwongozo wa 1981, kama ulivyoelezwa na Mzee Ngombale, ni wa kipekee na ni tofauti na taratibu za Chama zilizozoeleka. Kwanza, tuuelewe muktadha wa mchakato wenyewe. Kipindi cha mwisho cha utawala wa Mwalimu, , kilikuwa kigumu kupita kiasi kutokana na sababu mbalimbali. Hapa sio mahali pake kuangalia kwa undani sababu hizo isipokuwa kusisitiza tu kwamba ilikuwa katika hali hii ndipo Mzee Ngombale mwenyewe alipoonyesha dhamira yake ya kupendekeza kwamba Chama hakina budi kuzungumzia hali hii. Kwa hivyo, mchakato wa Mwongozo haukuanzia katika sekretariati ya Chama wala Kamati Kuu. Badala yake, ulianza kutokana na pendekezo lililotolewa na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama (NEC), yaani Mzee Ngombale mwenyewe. Pili katika kikao hikihiki cha NEC, kamati ya kuandaa Programu, ikiwa ni pamoja na kufanya uchambuzi kosoa, ilichaguliwa. Na kinyume na taratibu zilizozoeleka za Chama, aliyewasilisha Programu katika Mkutano Mkuu alikuwa Mzee Ngombale na sio Mwenyekiti, yaani Mwalimu mwenyewe. Kwa mujibu wa Mzee Ngombale, Mwalimu alipendekeza kwamba nyaraka iitwe Mwongozo badala ya programu kwa sababu wanachama walikuwa hawajazoea msamiati wa Programu. Katika Utangulizi wake, mwandishi anaweka mkazo katika ibara za Mwongozo wa 1981 zinazozungumzia suala la demokrasia katika Chama na muundo wa Chama. Pia anatuarifu kwamba vyombo vya Chama vilizungumzia Mwongozo. Kwa kadri ninavyokumbuka mimi, 8 MIONGOZO MIWILI

10 Mwongozo wa 1981 haukuwa gumzo la wananchi katika ujumla wao kama ulivyokuwa ule wa Kwa kiasi kikubwa, Mwongozo wa 1981 ama ulisahaulika au ulisahaulishwa. Hakuna kumbukumbu zozote zinazoonyesha kwamba Mwongozo wa 1981 ulipigiwa debe au kufanyiwa kampeni au kuzungumziwa mitaani na matawini. Wazee wengi wa chama waliokuwepo wakati ule, ukiwauliza juu ya Mwongozo wa 1981, wanakuwa ama wanachanganya mambo au wanajifanya hawaukumbuki. Hatuna ushahidi wa moja kwa moja, lakini ushahidi wa mazingira na hali halisi unatulazimisha kujenga hoja kwamba Mwongozo wa 1981 haukuwa utashi wa viongozi wakuu wa CCM. Mwongozo wa 1981 unatahadharisha kwamba tayari kulikuwa na watu/wanachama ambao walikuwa wananung unika na kusema kichinichini kwamba Ujamaa ulishindwa na kulikuwa na haja ya kubadili mtazamo na mwelekeo wa nchi. Mwongozo ulisema kwa ufasaha kwamba chini ya mwavuli wa Azimio na sekta ya umma lilijengeka tabaka la vibwanyenye wa kirasimu (bureaucratic bourgeoisie) ambalo lilikuwa linahujumu Ujamaa. Kwa mara ya kwanza katika nyaraka ya Chama, mapambano ya kitabaka yalizungumziwa waziwazi bila kutafuna maneno. Makala ya Shivji (ang. Sura ya Tano) inajaribu kufanya uchambuzi wa ibara muhimu za Mwongozo wa Hitimisho la makala hiyo ni kwamba tabaka linaloshutumiwa katika Mwongozo kuhusiana na hujuma dhidi ya Ujamaa ndilo likawa kinara wa kubeba mtazamo, itikadi na sera za uliberali mambo-leo. Bila shaka, kama kawaida ya nchi zetu ambamo matabaka-tawala ya ndani ni dhaifu, tabaka hili liliungwa mkono na taasisi za kifedha za kimataifa na nchi za kibeberu wakiwemo eti wafadhili. Kinadharia na kiitikadi, wasomi wa Chuo Kikuu, hususan wachumi waliosoma Marekani, ndio wakawa wasemaji wakuu wa sera za uliberali. Hatimaye, Mwalimu akang atuka kwa hiari yake, na labda pia kwa kutambua kwamba sera zake hazingefua dafu tena, na viongozi wa awamu ya pili ndio wakakumbatia, hatua kwa hatua, sera za ulegezaji wa masharti ya biashara, uwekezaji na ubinafsishaji. Sura ya Nne inaashiria kuzikwa kwa Azimio na mambo yote yalosimamiwa MIONGOZO MIWILI 9

11 na Azimio. Bila shaka, Mzee Ruksa bado anajitangaza kuwa muumini wa Azimio. Kwake yeye, maamuzi ya Zanzibar yalipitishwa ili kupanua tafsiri ya Azimio na sio kulizika. Kila zama ina Mwongozo wake, anasema Mzee Mwinyi katika hotuba yake, na mwongozo wa zama ya uliberali mamboleo ni Azimio la Zanzibar! Naam. Hitimisho Sio nia yangu kuendelea kuchambua historia yetu ya miongo miwili tangu Maamuzi ya Zanzibar. Ni juu ya vijana-wanazuoni wetu kuchambua hali halisi na hasa zama zetu hizi za misukosuko na zahma za kisiasa na kiuchumi. Jukumu mojawapo la Kigoda ni kuibua mijadala juu ya masuala muhimu na magumu ambayo watawala hupenda kuyakwepa au kuyazika. Nia yetu ya kuchapisha upya toleo hili la nyaraka muhimu katika historia yetu ni kuwakumbusha vijana-wanazuoni kwamba huwezi ukaelewa kwa undani na ufasaha hali iliyopo bila kuelewa na kuchambua hali iliyotangulia na iliyozaa hali ya leo. Shukrani Kwa mara nyingine tena ningependa kuishukuru taasisi ya HakiElimu na hasa Mkurugenzi Mtendaji wake Bi. Elizabeth Missokia kwa kuwezesha uchapishaji wa kitabu hiki. Ninapenda pia kumshukuru Mzee Ngombale kwa kutuandikia Utangulizi. Namshukuru kwa namna ya kipekee mchoraji mashuhuri wa katuni, Masudi Kipanya kwa kutuchorea katuni murua. Mwisho, bila ya ushupavu, ukereketwa na uchapakazi wa wanakigoda, hasa Mwalimu Bashiru Ally, Profesa Saida Yahya-Othman na Walter Rodney Luanda, tusingeweza kukamilisha kitabu hiki. Asanteni sana na kila la heri. Issa Shivji Profesa wa Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Aprili MIONGOZO MIWILI

12 UTANGULIZI UJIO NA UZITO WA MIONGOZO MIWILI Kingunge Ngombale Mwiru Mwongozo wa TANU wa 1971 Mwongozo wa TANU wa 1971 ni mwendelezo wa moyo wa Azimio la Arusha. Waandazi wa Mwongozo huu ni watu waliojazwa hisia kali za uzalendo zilizotamka: tumeonewa kiasi cha kutosha, tumenyonywa kiasi cha kutosha, tumenyanyaswa kiasi cha kutosha. Unyonge wetu ndio uliotufanya tuonewe, tunyonywe na kupuuzwa. Sasa tunataka kufanya mapinduzi, ili tusionewe tena, tusinyonywe tena na tusipuuzwe tena! Katika moyo ule ule wa Azimio la Arusha, Mwongozo wa TANU wa 1971 unapalilia ari ya mapambano ya Waafrika dhidi ya Ukoloni, Ukoloni- Mamboleo na Ubeberu na dhidi ya Waafrika wanaotumia madaraka kufifisha Uhuru na kudhalilisha utu wa wananchi. Ujio wa Mwongozo Mwongozo wa TANU wa 1971 ulitolewa na kutangazwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya TANU ya dharura mwanzoni mwa mwezi wa Februari, Dar es Salaam. Mwezi wa Januari mwaka 1971 Jeshi la Uganda chini ya Iddi Amin Dada, liliangusha serikali ya Rais Milton Obote na kutwaa madaraka. Kufika Agosti kitendo cha uchokozi kisicho cha kawaida kikosi cha Jeshi la Iddi Amin kilikivamia kikosi cha doria cha polisi wa Tanzania mpakani Mutukula na kumteka nyara Kamanda wa Polisi wa Mkoa (RPC) na kumtoroshea Uganda. Kitendo hiki cha uhasama kutoka kwa nchi jirani kilihitaji kupatiwa jibu la haraka na la kimkakati. Ndipo nilipoitwa Ofisini kwa Makamu MIONGOZO MIWILI 11

13 wa Pili wa Rais, Ndugu Rashid Mfaume Kawawa, ambaye nilimkuta na Meja Hashim Mbita (wakati ule Katibu Mtendaji Mkuu wa TANU). Ndugu Kawawa alinieleza kwa kifupi kuwa Mwalimu alimwagiza aniarifu kuwa ameamua mimi niongoze timu ya viongozi wa vijana kadhaa wa TYL kwenda Mkoa wa Ziwa Magharibi kufanya kazi ya kuhamasisha wananchi kisiasa na kiulinzi na usalama ili waweze kukabiliana ipasavyo na chokochoko zozote zile kutoka nchi jirani. Pamoja na kukubali jukumu nililopewa na kuahidi kuanza maandalizi mara moja, nilitoa rai kwa Makamu wa Pili wa Rais kwamba kwa kuwa tishio kwa usalama wa nchi kutoka Uganda ni sehemu tu ya tishio kwa taifa maana kuna tishio kubwa zaidi kwenye Ukanda wa Kusini la majeshi ya Wareno na uhasama wa Wareno na uhasama wa dola za Afrika ya Kusini na Rhodesia, ingekuwa busara kuitisha kikao cha NEC kutafakari juu ya ulinzi na usalama wa Taifa. Ndugu Kawawa alikubaliana na pendekezo langu na palepale aliondoka akifuatana na Ndugu Hashim Mbita, kwenda kuonana na Mwalimu Ikulu. Walirejea baada ya nusu saa na kunitaarifu kuwa Mwalimu amekubali pendekezo nililolitoa na tayari ameagiza NEC iitishwe kwa dharura. Kikao cha NEC kilipoketi wiki moja baadaye mimi nilipata fursa ya kufungua dimba la mjadala baada ya hotuba fupi ya ufunguzi ya Mwenyekiti. Pamoja na kuchangia mawazo kuhusu mapambano ya ukombozi wa Afrika na suala muhimu wakati ule la kuunga mkono vyama halisi vya ukombozi wa nchi za Afrika, nilitumia muda kujenga hoja ili NEC iikubali dhana ya msingi ya ulinzi na usalama wa Umma ambapo wananchi wenyewe ndio wanaokabidhiwa jukumu la ulinzi na usalama wao. Wananchi wote wanahusika na ulinzi na usalama wao kwa njia ya ulinzi wa mgambo na majeshi ni sehemu ya mstari wa mbele wa ulinzi na usalama huo wa Umma. Utekelezaji wa Mwongozo wa TANU na mafanikio yake Kupitishwa na kutangazwa kwa Mwongozo wa TANU wa 1971 kulipokewa kwa shangwe kubwa sana hasa Dar es Salaam. Matawi mengi ya chama 12 MIONGOZO MIWILI

14 wakati huo jijini Dar es Salaam yalianzisha utaratibu wa wanachama wote kukutana baada ya kazi ili kuzijadili ibara moja moja za Mwongozo. Matawi mengine yalianzisha madarasa ya itikadi ili kujadili Mwongozo. Maelfu ya wafanyakazi wa jijini Dar es Salaam walijiunga na mafunzo ya ulinzi wa mgambo kuitikia wito wa Mwongozo wa TANU. Wakati wa mafunzo ya mgambo muda kidogo ulitengwa kujadili ibara za Mwongozo. Makada waliohamasisha wakazi kujiunga na ulinzi wa mgambo walijenga hoja za uzalendo. Basi msimamo na lugha iliyotawala miongoni mwa wanamgambo ilikuwa ya kizalendo na kuihami nchi. Wanazuoni wa historia watakuja kufanya tathmini na kutoa kauli lakini sisi wenye busara za kawaida tu tunaweza kutamka bila kukosea kwamba uamuzi wa NEC ya TANU ya Februari 1971 kukubali sera ya ulinzi wa mgambo na kuagiza itekelezwe ulikuwa mwafaka na ulisaidia sana kuyafanya matokea ya vita ya Kagera kuwa yalivyokuwa. Hali ilivyo hivi sasa ni kwamba tunahitaji kuifanyia uchambuzi na tafakuri ya kina hali ya sasa ya ulinzi wa mgambo tukizingatia hoja za ibara za 21, 22 na 23 za Mwongozo wa 1971 zilizotufikisha kwenye uamuzi wa kuwa na sera ya ulinzi wa mgambo nchini. Katika kuhitimisha sehemu hii napenda kusisistiza kuwa suala la sera ya ulinzi na usalama wa Umma ambalo ndilo linaloibeba sera ndogo sahihi ya ulinzi wa mgambo ndio uamuzi mkuu wa Mwongozo wa TANU wa Dhana na nadharia ya ukombozi wa Mwafrika na hasa kama ilivyochambuliwa katika ibara ya 28 ya Mwongozo wa 1971 ina umuhimu wa kipekee hasa kwa viongozi na watafutao madaraka ya kisiasa nchini kwetu. Ibara ya 28 inatuambia kuwa kwa watu waliotokana na mifumo kandamizi kama Utumwa, Ukoloni, Ukabaila au/na Ubepari, maendeleo ni ukombozi. Na ukombozi unaainishwa kama kitendo kinachowaongezea watu uhuru wa kuamua mambo yao wenyewe na kutawala maisha yao wenyewe. Mwongozo katika ibara hii ya 28 unaendelea kusema kwetu sisi maendeleo yenye maana ni yale yanayotuondolea kuonewa, kunyonywa, MIONGOZO MIWILI 13

15 kunyanyaswa na mawazo ya kufungwa, na kutuongezea uhuru na utu wetu. Mwongozo unalileta suala la maendeleo ya watu kwa kutamka: Kwa hiyo katika kufikiria maendeleo ya Taifa letu na katika kupanga mipango ya maendeleo wakati wote mkazo mkubwa uwekwe kwenye maendeleo ya WATU na sio ya vitu. [W]atu wenyewe lazima washiriki katika kufikiria, kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo yao. Mwongozo wa 1981 Mwongozo wa CCM wa 1981, kama ulivyokuwa mwongozo wa TANU wa 1971, ulikuwa ni mwendelezo wa fikra na matarajio ya Ujamaa na Kujitegemea uliotangazwa na Azimio la Arusha. Mwongozo huu ni matokeo ya mila iliyokuwa imejengwa ndani ya Chama ya kutumia vikao vikuu vyake, hususan NEC, kujadili na kuchambua masuala mazito ya nchi, ya siasa, uchumi na jamii, na kuyatolea maelekezo ya kisera, kiufafanuzi na kiutekelezaji. Wakati Mwongozo wa TANU wa 1971 ulijielekeza kwenye mapambano dhidi ya Ukoloni, Ukoloni-Mamboleo na Ubeberu ili kufanikisha Ukombozi wa Afrika na wa Mwafrika na kuweka mkakati wa ulinzi na usalama wa umma ili nchi iwe na uwezo wa kukabiliana na uvamizi wowote kutoka kwa ubeberu au na vibaraka vyake, Mwongozo wa CCM wa 1981 umejikita katika kufanya uchambuzi kosoa wa kina na mpana juu ya hali ya kisiasa na kiuchumi iliyokuwepo nchini, hali ya maendeleo ya demokrasia nchini na ndani ya chama, n.k., na kutoa mapendekezo ya kuimarisha na kupanua demokrasia katika Chama na nchi. Ujio wa Mwongozo Mambo matatu yaliwezesha kikao kiamue kujadili yaliyomo katika Mwongozo huu. La kwanza ni kuwa hali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ilikuwa ngumu wakati ule na hivyo kuhitaji kuzungumzwa. Pili ni ujasiri na umahiri wa mmoja wa wajumbe wa NEC ambaye kwa unyenyekevu kabisa alitoa ombi la kusema jambo kabla shughuli kuanza. Aliporuhusiwa na kiti 14 MIONGOZO MIWILI

16 alisema kama hivi: Ndugu mwenyekiti na ndugu wajumbe naamini wote mnafahamu hali yetu ya sasa ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Hali ni ngumu. Ingefaa tutumie muda wa kikao hiki kutafakari na kufanya uchambuzi wa kina juu ya hali ya sasa ya kisiasa, kiuchumi na kijamii ili tupate mikakati ya kukipa chama chetu na serikali zake nguvu na msukumo mpya na uwezo zaidi wa kuwahudumia wananchi. Naomba kikao chetu kijadili hali ya nchi na ya chama chetu. Sababu ya tatu ni usikivu aliokuwa nao Mwalimu Nyerere kwa mambo yaliyohusu watu na yanayoihusu nchi. Na katika hili, mara mjumbe alipomaliza kusema na kukaa Mwalimu alinena naona hili ni jambo jema, wakati umefika wa kuzungumzia hali yetu. Mnaonaje wajumbe? Wajumbe wote wakaunga mkono. Mjadala ulianza mara baada ya kikao kupitisha kumbukumbu za mkutano uliotangulia pamoja na yatokanayo yake. Mimi niliyetoa hoja ya kuomba mjadala huo maalum ufanyike nilipewa nafasi ya kuanzisha mazungumzo. Wajumbe wengi wa kikao hicho walishiriki kwa kuchangia mawazo katika mjadala ulioendelea kwa siku mbili. Jioni ya siku ya pili, Mwenyekiti alipendekeza majina ya wajumbe wa Kamati. Kutokana na pendekezo la msemaji wa kwanza kwamba NEC iunde Kamati itakayoandaa Programu ya Chama yenye kuainisha majukumu makuu (Central Tasks) katika kipindi ambacho kingeamuliwa pamoja na mpangilio wa vipaumbele katika maeneo mbali mbali ya kiuchumi na kijamii bila kusahau maendeleo ya chama chenywe, kamati ikaitwa kamati ya Programu ya Chama. Wajumbe wa kamati walikubaliana kumchagua Ndugu Peter Siyovelwa (marehemu) kuwa Mwenyekiti wake na Kingunge Ngombale Mwiru kuwa Katibu/Rapporteur. Wajumbe wengine walikuwa Ndugu Peter Kisumo, Moses Nnauye (Marehemu), Getrude Mongella, Maalim Seif Shariff Hamad, Isaac Sepetu, Pius Msekwa na Joseph Sinde Warioba (hawa wawili wa mwisho walichaguliwa baadae). Wajumbe wa Kamati ya Programu ya Chama walipiga kambi mjini Dodoma ili kufanya kazi waliyopewa. Kwanza wajumbe walijadili mapendekezo ya MIONGOZO MIWILI 15

17 sura ya Programu na dondoo za kila SEHEMU yake na kukubaliana nayo. Baada ya hapo, kwenye kila hatua, wajumbe walipokea na kujadili kwa kina rasimu ya maudhui ambayo Katibu wa Kamati aliwasilisha. Rasimu mpya juu ya sehemu iliyojadiliwa iliandaliwa kwa msingi wa mwelekeo wa michango ya wajumbe na uzito wa hoja. Rasimu za kwanza ya Programu ya Chama iliwasilishwa kwenye NEC ya Mwezi Septemba Mjadala wa NEC ulikuwa wa kusisimua kulingana na mawazo chanya na changamfu yaliyobebwa na Programu hiyo. Ilibainika waziwazi kuwa maudhui ya Programu yatahitaji marekebisho makubwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano na baadhi ya sheria. Kwa hivyo, NEC iliona vyema kuwateua wajumbe wapya wawili wa Kamati ya Programu, Ndugu Pius Msekwa na Ndugu Joseph Sinde Warioba. Kamati iliagizwa kwenda kuandaa rasimu ya mwisho kwa ajili ya NEC ya Desemba NEC ilikutana Mwezi Desemba 1981 ili kupitisha Programu hiyo. Mambo mawili yalitokea. Kwanza Mwalimu alishauri kuwa Programu ya chama tuiite Mwongozo wa chama wa 1981; neno Programu ni jipya lingeweza kuwatatanisha watu bure. Na pili kutokana na pendekezo la Mwenyekiti iliamuliwa kuwa Mwongozo wa CCM wa 1981 upitishwe na kutangazwa na Mkutano Mkuu wa dharura ambao ungefanyika Tarehe 19 Januari, 1982, Dar es Salaam. Mkutano Mkuu ulifanyika kama ilivyopangwa. Baada ya kuufungua mkutano na kuwakaribisha wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa Mwenyekiti, Mwalimu Nyerere, alimwomba Katibu wa Kamati, Ndugu Kingunge Ngombale Mwiru, awasilishe Mwongozo wa CCM wa Mwaka 1981 kwa niaba ya Halmashauri Kuu ya Taifa. Mkutano Mkuu ulipokea Mwongozo wa Mwongozo wa 1981: maudhui na utekelezaji MWONGOZO wa CCM wa 1981 uliandaliwa ili kukiwezesha Chama cha Mapinduzi kuikabili hali ngumu ya kiuchumi na kijamii ya wakati ule. 16 MIONGOZO MIWILI

18 Lakini ni muhimu ikumbukwe kuwa matarajio ya wananchi yaliyoibuliwa na kutangazwa kwa Azimio la Arusha na Siasa ya TANU ya Ujamaa na Kujitegemea yalichangia katika kuwasukuma Wajumbe wa NEC watoe mawazo yaliyomo katika MWONGOZO huo. Ndiyo maana sehemu kubwa ya maudhui ya MWONGOZO wa 1981 ni uchambuzi kosoa wa utekelezaji wa Azimio la Arusha. Waandazi wa MWONGOZO walikuwa na hisia kwamba sera za Chama na hasa Azimio la Arusha, lilikuwa sahihi lakini mafanikio katika utekelezaji wake ili yakidhi matarajio ya wananchi, yangehitaji Chama kiwe madhubuti zaidi katika fikra, muundo na utekelezaji na serikali sawia. Ili kufikia lengo hilo, walitumia methodolojia ya kufanya uchambuzi wa kujikosoa kama Chama. Sehemu hii ya pili ya MWONGOZO ina umuhimu mkubwa sana. Kwa upande mmoja inaonyesha upungufu wa Chama katika maeneo mbalimbali na hatua za kurekebisha ili kukiimarisha na kwa upande mwingine inatoa mchango wa mawazo ambao ni mwongozo katika nadharia ya ujenzi wa Chama. Katika kila kipengele kilichoorodheshwa kwenye sehemu hii ya pili kuna mchango mahsusi wa kukifanya Chama kiwe madhubuti na chenye ufanisi. Tuchukue kipengele cha pili (2) katika Sehemu ya Pili ya MWONGOZO inayosema Wana-CCM ndio askari wa mstari wa mbele wa mapambano Historia yetu inatuonyesha jinsi wanatanu waliopigania uhuru wetu walivyokuwa na hamasa za kuupinga ukoloni na kukataa kutawaliwa. Wito wa TANU na ASP uliwafanya washikamane kwa kauli na vitendo. Tanzania Bara haikuchelewa kunyakuwa uhuru wake. Tangu tupate Uhuru na Mapinduzi ya Zanzibar hadi sasa pumzi ya wanachama wetu ya kusukuma mapambano na kujenga jamii mpya imepungua hasa kwa kuachia ubinafsi uwe na nafasi kubwa katika siasa na jamii kwa ujumla. Kwa wana CCM sasa kuwa askari wa mstari wa mbele wa mapambano yetu kutahitajika mageuzi ya msingi. Lakini hili bado linawezekana. Wasomi wa falsafa wanasema nadharia ni mwanga muhimu kwa wanaohusika na kutekeleza mambo, kutenda. Nadharia ni mwanga MIONGOZO MIWILI 17

19 unaoangaza ili wanaohusika na kutenda waangaziwe. Ndiyo maana kuna vipengele juu ya umuhimu wa nadharia sahihi ya Chama na Mshikamano wa nadharia na vitendo. Uchambuzi huu umefanywa kwanza ili kuwaonyesha wanaodharau nadharia kuwa wanakosea na pili kusisitiza kuwa viongozi/ makada wasioandaliwa vizuri katika nadharia wana hatari ya kufanya kazi ya Chama kwa kubahatisha. Viongozi na makada wanatakiwa wawe watu wanaojiamini, wenye uhakika na wanayoyaeleza, wenye uwezo wa kujenga hoja na kutumia nguvu ya hoja siyo hoja ya nguvu, kuwaelimisha, kuwashauri na kuwavuta watu upande wa Chama. Suala la chombo na maudhui yake Mwaka 1981 ulikuwa mwaka wa kumi na nne (14) tangu Azimio la Arusha. Utekelezaji wa Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ya TANU ulikuwa umefikia kiwango kikubwa nchini. Sekta ya Umma iliyoundwa katika kipindi hicho ilikuwa kubwa na anuai. Viwanda vya Umma na Mashirika mbalimbali ya Umma ndiyo yaliyokuwa yakiongoza. Sekta hii ya Umma ya uchumi ilikuwa inaajiri wafanyakazi wengi na kutarajiwa kuzalisha mali na kutoa huduma kwa ufanisi. Mwongozo pamoja na mambo mengine unajadili upungufu uliojitokeza ndani ya sekta ya umma na kuhoji kama hali hiyo haianzishi mgongano na makusudio ya kuundwa kwa sekta ya umma ambayo ndiyo ya ujamaa. Itakumbukwa pia kuwa katika MWONGOZO wa TANU wa 1971 kuna Ibara ya 15 ambayo inahoji viongozi wa kazi wenye tabia ya unyapara, wasioheshimu watu, wakaripiaji n.k. katika sehemu za kazi. Hapa pana suala kubwa kwa watu wanaoamini katika ujamaa na wale wanaoamini katika uhuru na utu, na kuwa maendeleo yenye maana ni maendeleo ya watu. Haitoshi katika nchi kuunda vyombo vya ujamaa kama viwanda, mabenki, mashirika ya umma ya huduma n.k.; lazima ndani ya vyombo hivyo kujenga uhusiano wa kijamaa yaani ule unaoheshimu misingi ya usawa, haki, ushirikiano, mshikamano, kuchapa kazi na uaminifu. Je, demokrasia ina nafasi ipi? Na nidhamu nayo? MWONGOZO wa CCM wa 1981 katika kufanya uchambuzi kosoa ulilenga kubainisha mapungufu katika maeneo ya uchumi, siasa 18 MIONGOZO MIWILI

20 na jamii ili kutoa mapendekezo chanya ya kukijenga Chama na dola. Watu wenye fikra za kimaendeleo tayari wakati ule walikuwa wanaona haja ya kuleta mabadiliko makubwa ndani ya Chama ili kupanua demokrasia na kuimarisha uongozi na utendaji. Kwa hiyo, MWONGOZO ulisisitiza umuhimu wa kuwapata viongozi wa Chama kwa njia ya uchaguzi badala ya uteuzi kwa lengo la kuunganisha uongozi wa chama (Halmashauri Kuu za kila ngazi) na utendaji katika Chama. MWONGOZO ulielekeza kuanzishwa kwa Sekretarieti za Halmashauri Kuu za kila ngazi ambazo zingeongozwa na makatibu wa Halmashauri Kuu hizo. Sekretarieti za Halmashauri Kuu ya Chama katika kila ngazi zilikusudiwa ziwe timu za uongozi wa pamoja katika ngazi husika na chemchem za fikra za chama, wakati kila mmoja ni kiongozi na msimamizi mahiri wa shughuli za Chama katika idara yake. MWONGOZO katika kusisitiza umuhimu wa kupanua demokrasia ndani ya Chama umetilia mkazo uwakilishi wa wanawake na vijana kutokana na uzito wa makundi haya katika jamii. Waandazi wa MWONGOZO wa CCM wa 1981 hawakusita kujielekeza kwenye suala la demokrasia katika dola. Ndiyo maana MWONGOZO uliona umuhimu wa kuimarisha uwakilishi wa wafanyakazi, wakulima, vijana na wanawake Bungeni. Aidha, ulisisitiza umuhimu wa uchaguzi kama kigezo cha msingi cha demokrasia ya kijamaa na hivyo uchaguzi uwe ndiyo njia kuu ya kuwapata wabunge na wawakilishi wengine katika dola. MWONGOZO vile vile ulihimiza haja ya kupanua demokrasia kwa kusisitiza umuhimu wa kuimarisha madaraka ya umma hadi kwenye ngazi ya vijiji na ushirikishwaji wa wananchi katika shughuli za maendeleo yao. Mapokezi na utekelezaji MWONGOZO wa CCM wa 1981 ulipata mapokezi makubwa ndani ya Chama na katika jamii nzima nchini. Kitendo cha kuitishwa Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM wa dharura ili kuupokea na kuupitisha MIONGOZO MIWILI 19

21 MWONGOZO huo kilifanya ujumbe wa MWONGOZO ufike kwenye pembe zote za nchi kwa ufanisi mkubwa. Jinsi masuala muhimu ya Chama na ya Nchi yalivyochambuliwa kwa ufasaha na umahiri ilifanya MWONGOZO kuwa gumzo la mabarazani na vijiweni na mada za kujadiliwa kwenye vyuo vya Chama, madarasa ya itikadi na mijadala miongoni mwa wasomi. Kwenye NEC ya Septemba 1981 ambapo Kamati ya Programu iliwasilisha rasimu ya kwanza ya MWONGOZO wajumbe wawili wapya wa kamati waliteuliwa, Ndg. Pius Msekwa na Ndg. Joseph Sinde Warioba, ili kuiongezea Kamati uzoefu wa masuala ya kiufundi ya Chama na Dola kama vile masuala ya Katiba. Kwa upande wa Chama, utekelezaji wa maelekezo ya MWONGOZO ulijikita kwenye mambo makubwa matatu. La kwanza, ni kufanya marekebisho ya Katiba ili kimsingi viongozi wote katika Chama wapatikane kwa kuchaguliwa na katika ngazi zote. La pili, mpangilio wa vikao na majukumu yake uliwekwa wazi zaidi. Mikutano mikuu ni vikao vya kutoa sera na maamuzi elekezi na kuchagua wajumbe walio wengi wa Halmashauri Kuu; Halmashauri Kuu za kila ngazi kuwa vyombo vya kusimamia na kuongoza utekelezaji wa katiba, sera na maamuzi katika ngazi zao na Kamati za Siasa kwa kila ngazi kusimamia utekelezaji wa Chama wa siku hadi siku. La tatu, ili kuunganisha uongozi (Halmashauri Kuu) na utendaji katika Chama ziliundwa Sekretarieti za Halmashauri Kuu kwa kila ngazi. Katika ngazi ya Taifa wajumbe wa Sekretarieti wanachaguliwa na NEC kutoka miongoni mwa wajumbe wa NEC yenyewe na inaongozwa na Katibu Mkuu wa Chama. Katika ngazi zilizobaki makatibu katika kila ngazi ndio wanaoongoza Sekretarieti za ngazi zao. La nne, marekebisho ya katiba yaliweka nafasi maalum kwa uwakilishi wa wanawake na vijana katika NEC na vikao vingine kama MWONGOZO ulivyosisitiza. Kwa upande wa dola maelekezo mengi ya MWONGOZO yalizingatiwa katika maeneo mbalimbali. Hapa tutayataja yale ambayo yaliingizwa katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 kwa marekebisho ya mwaka La kwanza ni lile la kulifanya suala la haki za binadamu, kuwa ni sehemu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania badala 20 MIONGOZO MIWILI

22 ya kuwa sehemu ya Dibaji tu ya Katiba hiyo. Pili ni hatua ya kuimarisha na kupanua demokrasia nchini kupitia uchaguzi ulio huru na wa haki wa uwakilishi wa wananchi katika ngazi za Ubunge na Serikali za Mitaa. Jambo la tatu linahusu madaraka ya umma. Mwongozo ulisisitiza juu ya madaraka ya umma kuanzia vijijini hadi wilayani na mijini. Kutokana na mwelekeo huo wa MWONGOZO marekebisho ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano yaliyofanywa mwaka 1984 yalipanua dhana finyu ya Serikali za Mitaa katika mtazamo nyumbufu wa madaraka ya umma na kusisitiza juu ya haki ya wananchi kwa serikali zao katika maeneo yao. Changamoto zinazohitaji tafakuri Unapoisoma miongozo hii miwili, wa TANU wa 1971 na wa CCM wa 1981, huwezi kukosa kubaini kuwa fikra, nadharia na tafakuri kubwa zilitumika katika utunzi wake. Haya ni matokeo ya viongozi wa chama wanapokaa pamoja na kufikiri pamoja. Hii ni aina mojawapo ya uhai wa chama iliyo muhimu sana kwa uhai wa jumla wa chama cha siasa. Je, mila hii iliyokuwa imejengeka huko nyuma CCM yetu ya sasa inaiendeleza? Je Vyama vingine vya siasa nchini vinajaribu kujenga tabia ya viongozi wake kuketi pamoja na kufikiri pamoja na kuchambua pamoja hali ya nchi yetu na namna vitakavyozikabili changamoto mbalimbali? Huu umaskini wetu wa sasa wa falsafa unaotuathiri vibaya unatokana na nini? Mwongozo wa TANU wa 1971, katika ibara zake za 21, 22 na 23 ulijenga msingi wa sera ya ulinzi na usalama wa umma, sera iliyozaa ulinzi wa mgambo. Maandalizi sahihi ya wanamgambo, yaani kuhamasishwa kwa mbinu ya uzalendo, uandikishaji na mafunzo makini ya kijeshi chini ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania ndiyo yaliyowezesha wanamgambo kushiriki bega kwa bega na wapiganaji wengine katika Jeshi la Tanzania lilolishinda na kulitokomeza Jeshi la Nduli Iddi Amin wa Uganda. Miaka 33 imekwishapita tangu vita vya Kagera viishe. Vita hivyo vya kujihami dhidi ya uvamizi uliofanywa na majeshi ya Iddi MIONGOZO MIWILI 21

23 Amini wa Uganda dhidi ya nchi yetu vilidhihirisha ubora wa sera mkakati ya ulinzi wa usalama wa umma. Wakati huu ambapo tumejumuika kumuenzi Mwalimu Nyerere miaka 91 tangu azaliwe, ni jambo linalopendeza kujipa muda wa kutathmini sera nzito alizozianzisha na ambazo zimetoa mchango mkubwa kwa taifa kama ile ya ulinzi na usalama wa umma iliyozaa ulinzi wa mgambo. Ni vizuri kupitia mazingira ya wakati huo, misingi ya kuanzishwa kwake, taratibu zilizotumika na matokeo/tija iliyopatika nchini. Je, hali ya ulinzi wa mgambo ya sasa inakidhi matarajio ya sera za ulinzi na usalama wa umma kama ilivyoasisiwa katika mwongozo wa TANU wa 1971? Mjadala wowote wa maana kuhusu Mwongozo wa TANU wa 1971 haukamiliki pasi na mjadala kuhusu ibara za 28. Kwa watu ambao vizazi vyao vilivyotangulia viliishi katika mifumo kandamizi ya utumwa, ukoloni, ukabaila na ubepari, dhana kwamba maendeleo ni Ukombozi yenyewe inasaidia kutukomboa kifikra. Ibara hii inatoa muhtasari sahihi wa ujumbe wake inaposema kwetu sisi maendeleo ya maana ni yale yanayotuondolea kuonewa, kunyonywa, kunyanyaswa na mawazo ya kufungwa, na kutuongezea uhuru na utu wetu. Na katika hitimisho ibara hii imesema kwa hiyo katika kufikiria maendeleo ya taifa letu, na katika kupanga mipango ya maendeleo, wakati wote lazima mkazo mkubwa utiliwe kwenye maendeleo ya WATU na siyo ya vitu. Ili maendeleo haya yaweze kuwa ya watu, watu wenyewe lazima washiriki katika kufikiria, kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo yao. Mwongozo wa TANU wa 1971 ulitufikisha hapo katika nadharia. Je, sisi wasomi na wanasiasa wa leo hatuna la kuchangia? 22 MIONGOZO MIWILI

24 SURA YA KWANZA AZIMIO LA ARUSHA Ujamaa na Kujitegemea (Lilipitishwa na Halmashauri Kuu ya TANU, mwezi Januari 1967, na kuthibitishwa na Mkutano Mkuu wa TANU) (Lilitolewa rasmi tarehe 5 Februari 1967) SEHEMU YA KWANZA IMANI YA TANU Siasa ya TANU ni kujenga nchi ya Ujamaa. Misingi ya Ujamaa imetajwa katika Katiba ya TANU, nayo ni hii: Kwa kuwa TANU inaamini: (a) Kwamba binadamu wote ni sawa; (b) Kwamba kila mtu anastahili heshima; (c) Kwamba kila raia ni sehemu ya Taifa na anayo haki ya kushiriki sawa na wengine katika Serikali tangu ya Mitaa, ya Mikoa hadi Serikali Kuu; (d) Kwamba kila raia anayo haki ya uhuru wa kutoa mawazo yake, wa kwenda anakotaka, wa kuamini dini anayotaka na wa kukutana na watu mradi havunji Sheria; (e) Kwamba kila mtu anayo haki ya kupata kutoka katika jamii hifadhi ya maisha yake na ya mali yake aliyonayo kwa mujibu wa Sheria; (f) Kwamba kila mtu anayo haki ya kupata malipo ya haki kutokana na kazi yake; (g) Kwamba raia wote kwa pamoja wanamiliki utajiri wa asili wa nchi hii ukiwa kama dhamana kwa vizazi vyao; (h) Kwamba ili kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi unakwenda sawa Serikali lazima iwe na mamlaka kamili juu ya njia muhimu za kuukuza uchumi; na MIONGOZO MIWILI 23

25 (i) Kwamba ni wajibu wa Serikali, ambayo ni watu wenyewe, kuingilia kati kwa vitendo maisha ya uchumi ya Taifa ili kuhakikisha usitawi wa raia wote na kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine au kikundi kimoja kunyonya kikundi kingine na kuzuia limbikizo la utajiri kufikia kiasi ambacho hakipatani na siasa ya watu wote kuwa sawa. MADHUMUNI YA TANU Kwa hiyo basi, makusudi na madhumuni ya TANU yatakuwa kama hivi yafuatavyo: (a) Kuudumisha uhuru wa nchi yetu na raia wake; (b) Kuweka heshima ya mwanadamu kwa kufuata barabara kanuni za Tangazo la Ulimwengu la Haki za Binadamu; (c) Kuhakikisha kwamba nchi yetu inatawaliwa na Serikali ya watu ya kidemokrasia na ya kisoshalist; (d) Kushirikiana na vyama vyote vya siasa katika Afrika vinavyopigania uhuru wa bara lote la Afrika; (e) Kuona kwamba Serikali inatumia mali yote ya nchi yetu kwa kuondoshea umaskini; ujinga na maradhi; (f) Kuona kwamba Serikali inasaidia kwa vitendo kuunda na kudumisha vyama vya ushirika; (g) Kuona kwamba kila iwezekanapo Serikali inashiriki hasa katika maendeleo ya uchumi wa nchi yetu; (h) Kuona kwamba Serikali inatoa nafasi zilizo sawa kwa wote, wake kwa waume, bila kujali rangi, kabila, dini au hali; (i) Kuona kwamba Serikali inaondoa kila namna ya dhuluma, vitisho, ubaguzi, rushwa na upotofu; (j) Kuona kwamba Serikali ya nchi yetu inasimamia barabara njia kuu za kuzalisha mali na inafuata siasa ambayo itarahisisha njia ya kumiliki kwa jumla mali za nchi yetu; (k) Kuona kwamba Serikali inashirikiana na dola nyingine katika Afrika katika kuleta Umoja wa Afrika. (l) Kuona kwamba Serikali inajitahidi kuleta amani na salama ulimwenguni kwa njia ya Chama cha Umoja wa Mataifa. 24 MIONGOZO MIWILI

26 (a) Hakuna Unyonyaji SEHEMU YA PILI SIASA YA UJAMAA Nchi yenye Ujamaa kamili ni nchi ya wafanyakazi: haina ubepari wala ukabaila. Haina tabaka mbili za watu: tabaka ya chini ya watu wanaoishi kwa kufanya kazi, na tabaka ya juu ya watu wanaoishi kwa kufanyiwa kazi. Katika nchi ya Ujamaa kamili mtu hamnyonyi mtu, bali kila awezaye kufanya kazi hufanya kazi, na kila mfanyakazi hupata pato la haki kwa kazi aifanyayo na wala mapato ya wafanyakazi mbalimbali hayapitani mno. Katika nchi ya Ujamaa kamili watu peke yao ambao huishi kwa jasho la wenzao, na ni haki yao kuishi kwa jasho la wenzao, ni watoto wadogo, wazee wasiojiweza, vilema na wale ambao, kwa muda, Jumuia imeshindwa kuwapatia kazi yoyote ya kujipatia riziki kwa nguvu zao wenyewe. Nchi yetu ni nchi ya Wakulima na Wafanyakazi, lakini si nchi ya Ujamaa kamili. Ina misingi ya ubepari na ukabaila na vishawishi vyake. Misingi hii ya ubepari na ukabaila yaweza ikapanuka na kuenea. (b) Njia Kuu za Uchumi ni Chini ya Wakulima na Wafanyakazi Namna ya pekee ya kujenga na kudumisha ujamaa ni kuthibitisha kuwa njia kuu zote za uchumi wa nchi yetu zinatawaliwa na kumilikiwa na Wakulima na Wafanyakazi wenyewe kwa kutumia vyombo vya Serikali yao na Vyama vyao vya Ushirika. Pia ni lazima kuthibitisha kuwa Chama kinachotawala ni Chama cha wakulima na wafanyakazi. Njia kuu za Uchumi ni: kama vile ardhi, misitu, madini, maji, mafuta na nguvu za umeme; njia za habari, njia za usafirishaji; mabenki, na bima; biashara na nchi za kigeni na biashara za jumla; viwanda vya chuma, mashini, silaha, magari, simenti, mbolea; nguo, na kiwanda chochote kikubwa ambacho kinategemewa na sehemu kubwa ya watu katika kupata riziki zao au kinachotegemewa na viwanda vingine; mashamba MIONGOZO MIWILI 25

27 makubwa na hasa yale yanayotoa mazao ya lazima katika viwanda vikubwa. Baadhi ya njia hizi na nyingine zisizotajwa hapa hivi sasa zinamilikiwa au kutawaliwa na Serikali ya Wananchi. (c) Kuna Demokrasi Nchi haiwi ya Ujamaa kwa sababu tu njia zake kuu au zote za uchumi hutawaliwa na humilikiwa na Serikali. Sharti Serikali iwe inachaguliwa na kuongozwa na Wakulima na Wafanyakazi wenyewe. Serikali ya Makaburu wa Rhodesia au Afrika ya Kusini ikitawala au kumiliki njia zote za uchumi, hiyo itakuwa ni njia ya kukomaza Udhalimu siyo njia ya kuleta Ujamaa. Hakuna Ujamaa wa kweli pasipo na Demokrasi ya kweli. (d) Ujamaa ni Imani Lakini Ujamaa hauwezi kujijenga wenyewe. Kwani Ujamaa ni imani. Hauna budi kujengwa na watu wanaoamini na kufuata kanuni zake. Mwana-TANU wa kweli ni Mjamaa, na Wajamaa wenzie, yaani waamini wenzie katika imani hii ya kisiasa na uchumi ni wote wale wanaopigania haki za wakulima na wafanyakazi katika Afrika na popote duniani. Wajibu wa kwanza wa mwana-tanu na hasa kiongozi wa TANU, ni kutii kanuni hizi za ujamaa hasa katika maisha yake mwenyewe. Na hasa mwana- TANU kiongozi hataishi kwa jasho la mtu mwingine au kufanya jambo lolote ambalo ni la kibepari au kikabaila. Utimizaji wa shabaha hizo na nyinginezo zinazofuatana na siasa ya ujamaa unategemea sana viongozi kwa sababu ujamaa ni imani na ni vigumu kwa viongozi kujenga siasa ya ujamaa ikiwa hawaikubali imani hiyo. SEHEMU YA TATU SIASA YA KUJITEGEMEA Tunapigana Vita TANU ina vita vya kulitoa Taifa letu katika hali ya unyonge na kulitia katika hali ya nguvu; vita vya kuwafanya wananchi wa Tanzania (na 26 MIONGOZO MIWILI

28 wananchi wa Afrika) watoke katika hali ya dhiki na kuwa katika hali ya neema. Tumeonewa kiasi cha kutosha, tumenyonywa kiasi cha kutosha, na tumepuuzwa kiasi cha kutosha. Unyonge wetu ndio uliotufanya tuonewe, tunyonywe, na kupuuzwa. Sasa tunataka mapinduzi; mapinduzi ya kuondoa unyonge ili tusionewe tena, tusinyonywe tena na wala tusipuuzwe tena. Mnyonge Hapigani kwa Fedha Lakini ni dhahiri kwamba tumefanya makosa katika kuchagua silaha; kwani silaha tuliyochagua ni fedha. Tunataka kuondoa unyonge wetu kwa kutumia silaha ya wenye nguvu, silaha ambayo sisi wenyewe hatuna. Katika mazungumzo yetu, mawazo yetu, na vitendo vyetu ni kama tumekata shauri kwamba bila fedha mapinduzi yetu hayawezekani. Ni kama tumesema, Fedha ndiyo msingi wa maendeleo. Bila fedha hakuna maendeleo! Hii ndiyo imani yetu ya sasa. Viongozi wa TANU mawazo yao ni kwenye fedha. Viongozi wa Serikali, wanasiasa na watumishi, mawazo yao na matumaini yao ni kwenye fedha. Viongozi wa wananchi na wananchi wenyewe katika TANU, NUTA, Bunge, UWT, Vyama vya Ushirika, TAPA na makundi mengine ya wananchi, mawazo yao na maombi yao na matumaini yao ni FEDHA. Ni kama wote tumekubaliana na tunasema kwa sauti moja, Tukipata fedha tutaendelea, bila fedha hatutaendelea! Mpango wetu wa maendeleo ya miaka mitano shabaha zake kwa kifupi ni shibe zaidi, elimu zaidi na afya zaidi. Na silaha yetu tuliyotilia mkazo sana ni fedha. Ni kama tumesema, Katika miaka mitano ifuatayo tunakusudia kujiongezea shibe, elimu na afya, na ili kutimiza shabaha hizo tunatumia 250,000,000. Kama tumetaja na tunapotaja vyombo vingine vya kututimizia shabaha hizo tunavitaja kama nyongeza tu; lakini chombo kikubwa katika akili zetu, silaha kubwa katika mawazo yetu, ni FEDHA. Mheshimiwa Mbunge anaposema kuwa wananchi wa sehemu yake wana shida ya maji, je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa shida hiyo? Jibu analotaka ni kwamba: Serikali inao mpango wa kuwapa maji wananchi wa sehemu hiyo KWA FEDHA. MIONGOZO MIWILI 27

29 Mbunge mwingine anaposema kuwa sehemu yake haina barabara au shule au hospitali au vyote, je, Serikali ina mpango gani? Naye pia jibu ambalo angependa kupewa ni kuwa Serikali inao mpango safi kabisa wa kutengeneza barabara au kujenga shule au hospitali au vyote kwa wananchi wa sehemu ya Mbunge Mheshimiwa huyo kwa FEDHA. Kiongozi wa NUTA anapoikumbusha Serikali kuwa mishahara ya chini kwa wafanyakazi wengi bado ni midogo mno na nyumba wanazolala si nzuri, je, Serikali inao mpango gani? Jibu apendalo kusikia ni kuwa Serikali inao mpango maalum wa kuongeza mishahara na kujenga majumba bora KWA FEDHA. Kiongozi wa TAPA anaposema kuwa wanazo shule nyingi sana ambazo hazipati msaada wa Serikali, je, Serikali ina mpango gani wa kuzisaidia shule hizo, jibu analopenda kusikia ni kuwa Serikali iko tayari kabisa kesho asubuhi kuzipa shule hizo msaada unaotakiwa wa FEDHA! Kiongozi wa Chama cha Ushirika akitaja shida yoyote ya mkulima jibu apendalo kusikia ni kuwa Serikali itaondoa shida hizo za mkulima kwa FEDHA. Mradi kila shida inayolikabili Taifa letu wananchi tunawaza Fedha, Fedha, Fedha! Mwaka hata mwaka kila Wizara na kila Waziri hufanya makadirio yake ya matumizi yaani fedha wanazohitaji mwaka huo kwa kazi za kawaida na mipango ya maendeleo. Waziri mmoja tu na Wizara moja tu hushughulika pia kufanya makadirio ya mapato. Ni Waziri wa Fedha. Kila Wizara ina mipango mizuri sana ya maendeleo. Wizara zinapoleta makadirio yao ya matumizi huwa zinaamini kwamba fedha zipo ila mkorofi ni Waziri wa Fedha na Wizara yake. Na kila mwaka lazima Waziri wa Fedha na Wizara yake awaambie Mawaziri wenzake na Wizara zao kwamba hakuna fedha. Na kila mwaka Wizara zote huinung unikia Wizara ya Fedha kwa kupunguza Makadirio yao ya matumizi. Kadhalika Wabunge na Viongozi wengine wanapodai Serikali itimize mipango mbalimbali huwa nao wakiamini kwamba fedha zipo ila mkorofi ni Serikali. Lakini kukataa huku kwa Wizara, na Wabunge na Viongozi wengine hakuwezi kuondoa ukweli; nao ni kwamba Serikali haina fedha. 28 MIONGOZO MIWILI

30 Na kusema kuwa Serikali haina fedha maana yake ni nini? Maana yake ni kuwa Wananchi wa Tanzania hawana fedha. Kiasi walichonacho hutozwa kodi, na kodi hiyo ndiyo inayoendesha shughuli za Serikali hivi sasa na maendeleo mengine ya nchi. Tunapotaka Serikali ifanye shughuli zaidi za maendeleo kwa fedha tunataka Serikali itumie fedha zaidi. Na kama Serikali haina fedha zaidi tunataka izipate, yaani iongeze kodi. Ukidai Serikali itumie fedha zaidi unataka izipate; na njia ya kuzipata ni kodi. Kudai Serikali itumie fedha nyingi zaidi bila kukubali kodi zaidi ni kudai Serikali ifanye miujiza; ni sawa na kudai maziwa zaidi bila kutaka ng ombe akamuliwe tena. Lakini kukataa huku kukiri kwamba tunapodai Serikali itumie fedha zaidi nia yetu ni kutaka Serikali iongeze kodi kunaonyesha kuwa tunatambua ugumu wa kuongeza kodi. Tunatambua kuwa ng ombe hana maziwa zaidi; kwamba hata kama ng ombe mwenyewe angependa ayanywe maziwa hayo au yanywewe na ndama wake au yauzwe yamfae yeye na jamaa yake; utashi huo hauwezi kuondoa ukweli kwamba hana maziwa zaidi. Fedha kutoka Nje ya Tanzania, je? Njia moja tunayotumia kujaribu kuepukana na lazima hii ya kukiri kodi zaidi ikiwa twataka fedha zaidi ni kutilia sana mkazo fedha za kutoka nje ya Tanzania. Fedha hizi za kutoka nje ni za aina tatu:- (a) Zawadi: Yaani Serikali ya nje iipe Serikali yetu fedha za bure tu kama sadaka kwa ajili ya mpango fulani wa maendeleo. Wakati mwingine shirika lolote la nje liipe Serikali yetu au Shirika jingine katika nchi yetu msaada fulani kwa ajili ya maendeleo. (b) Mkopo: Sehemu kubwa ya fedha tunazotazamia kupata kutoka nchi za kigeni si zawadi au sadaka, bali ni mkopo. Serikali ya nje au Shirika la nje, kama vile Benki, hukopesha Serikali yetu fedha fulani kwa ajili ya kazi zetu za maendeleo. Mkopo huu huwa una masharti yake ya kulipa, kama vile muda wa kulipa, na kima cha faida. (c) Raslimali ya Kibiashara: Aina ya tatu ambayo pia ni kubwa kuliko ya kwanza, ni ile ya fedha za watu au makampuni yanayotaka kuja katika nchi yetu kuanzisha shughuli mbalimbali za uchumi kwa manufaa yao wenyewe. Na sharti kubwa walitakalo jamaa MIONGOZO MIWILI 29

31 hawa wenye fedha zao ni kwamba shughuli yenyewe iwe ni ya faida kwao na pia kwamba Serikali iwaruhusu kuondoa faida hiyo Tanzania na kuipeleka kwao. Hupenda pia kwa jumla Serikali iwe na siasa wanayokubaliana nayo au ambayo haihatarishi uchumi wao. Hizo ndizo njia tatu kubwa za kupata fedha kutoka nje ya nchi yetu. Kuna mazungumzo mengi ajabu juu ya jambo hili la kupata fedha kutoka nchi za kigeni. Serikali yetu na viongozi wetu wa makundi mbalimbali hawaachi kufikiria njia za kupata fedha kutoka nje. Na tukizipata au japo tukipata ahadi tu ya kuzipata mara magazeti yetu, au radio zetu na viongozi wetu hutangaza jambo hilo ili kila mtu ajue kuwa neema imekuja au iko njiani inakuja! Tukipata msaada hutangaza; tukipata mkopo hutangaza; tukipata kiwanda kipya hutangaza; tukiahidiwa msaada, mkopo au kiwanda kipya hutangaza. Japo tukianza mazungumzo tu na nchi au shirika la kigeni juu ya msaada, mkopo au kiwanda, mara hutangaza japo hatuna hakika ya matokeo ya mazungumzo hayo. Na kisa? Ni kuwajulisha wananchi kwamba, tunaanza mazungumzo ya neema! TUSITEGEMEE FEDHA KULETA MAENDELEO Ni jambo la kijinga kuchagua fedha kuwa ndiyo chombo chetu kikubwa cha maendeleo na hali tunajua kuwa nchi yetu ni maskini. Ni ujinga vilevile, kwa kweli ni ujinga zaidi, tukidhani kuwa tunaweza kuondoa hali hii ya unyonge wetu kwa kutegemea fedha za kutoka nje badala ya fedha zetu wenyewe. Ni ujinga kwa sababu mbili. Kwanza, hatuwezi kuzipata. Ni kweli kwamba zipo nchi ambazo zaweza na zapenda kutusaidia. Lakini hakuna nchi moja duniani ambayo iko tayari kutupa misaada au mikopo au kuja kujenga viwanda katika nchi yetu kwa kiasi cha kuiwezesha nchi yetu kutimiza shabaha zake zote za maendeleo. Nchi zenye dhiki ni nyingi sana duniani. Na hata kama nchi zote zenye neema zingekubali kuzisaidia nchi zenye dhiki, bado ingekuwa msaada huo hautoshi. Lakini nchi zenye neema hazitakubali. Hata katika 30 MIONGOZO MIWILI

32 nchi ileile, matajiri huwa hawatoi fedha zao kwa hiari ili zisaidie Serikali kuondoa dhiki. Njia ya kuzipata fedha za matajiri ili zisaidie umma ni kuwatoza kodi wakipenda wasipende. Hata hivyo huwa hazitoshi. Ndiyo maana japo tungewakamua vipi wanananchi na wakazi wa Tanzania, matajiri na maskini, hatuwezi kupata fedha za kutosha kutimiza mipango yetu ya maendeleo. Wala duniani hakuna Serikali ambayo yaweza kuyatoza kodi mataifa yenye neema, yakipenda yasipende, ili kusaidia mataifa yenye dhiki. Hata hizo zisingelitosha. Hakuna Serikali ya Dunia nzima. Fedha ambazo nchi zenye neema hutoa huwa kwa wema wao, au hiari yao au kwa manufaa yao wenyewe. Haiwezekani basi, tupate fedha za kutosha kwa njia hiyo. MISAADA NA MIKOPO VITAHATARISHA UHURU WETU Pili, japo kama tungeweza kuzipata; hivyo ndivyo tunavyotaka kweli? Kujitawala ni kujitegemea. Kujitawala kwa kweli hakuwezekani ikiwa Taifa moja linategemea misaada na mikopo ya Taifa jingine kwa maendeleo yake. Hata kama pangetokea Taifa au mataifa ambayo yako tayari kutupa fedha zote tunazohitaji kuendesha mipango yetu ya maendeleo isingekuwa sawa kwa nchi yetu kuipokea misaada hiyo bila kujiuliza matokeo yake yatakuwa nini kwa Uhuru wetu na uzima wetu. Msaada ambao ni kama chombo cha kuongeza juhudi, au nyenzo ya juhudi, ni msaada ambao una manufaa. Lakini msaada unaoweza ukawa sumu ya juhudi si msaada wa kupokea bila kujiuliza maswali. Kadhalika mikopo. Kweli mkopo ni bora kuliko misaada ya bure. Mkopo nia yake ni kuongeza jitihada au kuifanya jitihada itoe matunda mengi zaidi. Sharti moja la mkopo huwa ni kuonyesha jinsi utavyoweza kuulipa. Maana yake ni kwamba sharti uonyeshe kuwa unakusudia kuufanyia kazi itakayoleta manufaa ya kukuwezesha kuulipa. Lakini hata mikopo ina kikomo. Sharti upime uwezo wa kulipa. Tunapokopa MIONGOZO MIWILI 31

33 fedha kutoka nje mlipaji ni Mtanzania. Na kama tulivyokwishasema Watanzania ni watu maskini. Kuwabebesha watu maskini mikopo ambayo inawazidi kimo si kuwasaidia bali ni kuwaumiza. Na hasa inapokuwa, mikopo hiyo ambayo wanatakiwa walipe, haikuwafaidia wao, bali ilifaidia watu wachache tu. Na Viwanda vya wenye raslimali zao je? Ni kweli tunavitaka. Hata tumepitisha katika Bunge sheria ya kulinda raslimali ya wageni wanaoanzisha mipango mbalimbali ya uchumi katika nchi yetu. Nia yetu na matumaini yetu ni kuwafanya waone kuwa Tanzania ni nchi inayofaa kuingiza raslimali zao. Kwani raslimali yao itakuwa salama italeta faida. Na faida hiyo wenyewe wataweza kuiondoa bila vipingamizi. Tunayo matumaini ya kupata fedha za maendeleo mbalimbali kwa njia hii. Lakini hatuwezi kupata za kutosha. Lakini hata kama tungeweza kuwaridhisha kabisa Wageni hao na Makampuni hayo mpaka yakubali kuanzisha mipango yote ya uchumi tunayohitaji katika nchi yetu, hivyo ndivyo tunavyotaka kweli? Kama tungeweza kushawishi wenye raslimali wa kutosha kutoka Amerika, na Ulaya kuja kwetu na kuanzisha Viwanda vyote, na mipango mingine yote ya uchumi tunayohitaji katika nchi hii, hivi kweli tungekubali bila kujiuliza maswali? Tungekubali kweli kuacha uchumi wetu wote uwe mikononi mwa wageni kwa ajili ya kupata faida na kuipeleka katika nchi zao? Hata kama wasingedai kuhamisha faida na kupeleka makwao, bali faida yote watakayopata wataitumia hapa hapa Tanzania kwa maendeleo zaidi. Hivi kweli tungekubali jambo hili bila kujiuliza hasara zake kwa Taifa letu? Huu Ujamaa tunaosema kuwa ndiyo shabaha yetu tungeujengaje? Twawezaje kutegemea nchi za nje na Kampuni za nje kwa misaada na mikopo na raslimali kwa maendeleo yetu bila kuhatarisha uhuru wetu? Waingereza wana methali isemayo Amlipaye mwimbaji ndiye huchagua wimbo. Tutawezaje kutegemea nchi za kigeni na Makampuni ya kigeni kwa sehemu kubwa ya maendeleo yetu bila kuzipa nchi hizo na makampuni hayo sehemu kubwa ya uhuru wetu wa kutenda tupendavyo? Ukweli wenyewe ni kwamba hatuwezi. Tukariri basi. Tumefanya makosa kuchagua fedha, kitu ambacho hatuna, kiwe ndicho chombo kikubwa cha mipango yetu ya maendeleo. Tunafanya 32 MIONGOZO MIWILI

34 makosa kudhani kuwa tutapata fedha kutoka nchi za kigeni. Kwanza, kwa sababu kwa kweli hatuwezi kupata fedha za kutosha kwa maendeleo yetu. Na pili, hata kama tungeweza, huko kutegemea wengine kungehatarisha uhuru wetu na siasa nyingine za nchi yetu. TUMEKAZANIA MNO VIWANDA Kwa sababu ya kutilia mkazo fedha tumefanya kosa kubwa la pili. Tumekazania mno viwanda. Kama vile tulivyosema Bila Fedha hakuna maendeleo, ni kama twasema pia Viwanda ndiyo maendeleo. Bila viwanda hakuna maendeleo. Hii ni kweli siku tutakapokuwa na fedha nyingi, tutaweza kusema kwamba tumeendelea. Tutaweza kusema, Tulipoanza mipango yetu tulikuwa hatuna fedha za kutosha na upungufu huu wa fedha ulitupunguzia nguvu za kuendesha maendeleo yetu haraka zaidi. Lakini leo tumeendelea na tunazo fedha za kutosha. Na hivyo ndivyo itakavyotupasa kusema, Tumeendelea, kwa hiyo, tunazo fedha za kutosha. Yaani fedha zetu zitakuwa zimeletwa na maendeleo. Kadhalika siku tutakapokuwa na viwanda tuna haki ya kusema kuwa tumeendelea. Maendeleo yatakuwa yametuwezesha kupata viwanda. Kosa tunalofanya ni kudhani kwamba maendeleo yetu yataanza kwa viwanda. Ni kosa maana hatuna uwezo wa kuanzisha viwanda vingi vya kisasa katika nchi yetu. Hatuna fedha zinazohitajiwa na hatuna ufundi unaohitajiwa. Haitoshi kusema kuwa tutakopa fedha na kuazima mafundi kutoka nje kuja kuanzisha viwanda hivyo. Kosa hili jibu lake ni lilelile kwamba hatuwezi kupata fedha za kutosha na kuazima mafundi wa kutosha kutuanzishia viwanda hivyo tunavyotaka. Na pia kwamba hata kama tungeweza kupata msaada huo kuutegemea huko kunaweza kukapotosha siasa yetu ya Ujamaa. Siasa ya kualika msululu wa mabepari kuja kuhodhi viwanda katika nchi yetu ingefanikiwa kutupatia viwanda vyote tunavyotaka, basi ingefanikiwa pia kuzuia maendeleo ya Ujamaa. Ila labda tuwe tunaamini kwamba bila kujenga ubepari kwanza hatuwezi kujenga Ujamaa. MIONGOZO MIWILI 33

35 TUMJALI ZAIDI MKULIMA VIJIJINI Vilevile mkazo wa fedha na wa viwanda unatufanya tukazanie zaidi maendeleo ya mijini. Tunatambua kuwa hatuwezi kupata fedha za kutosha kuleta maendeleo katika kila kijiji na ambayo yatamfaa kila mwananchi. Tunajua pia kuwa hatuwezi kujenga kiwanda katika kila kijiji ili kisaidie kuleta maendeleo ya fedha na viwanda katika kila kijiji; jambo ambalo tunajua kuwa haliwezekani. Kwa ajili hiyo, basi, fedha zetu huzitumia zaidi katika miji na viwanda vyetu pia hujengwa katika miji. Na zaidi ya fedha hizi huwa ni mikopo. Japo zijenge shule, hospitali, majumba au viwanda ni fedha za mikopo. Hatimaye lazima zilipwe. Lakini ni dhahiri kwamba haziwezi kulipwa kwa fedha zinazotokana na maendeleo ya mijini au maendeleo ya viwanda. Hazina budi zilipwe kwa fedha tunazopata kutokana na vitu tunavyouza katika nchi za nje. Kutokana na viwanda vyetu hatuuzi na kwa muda mrefu sana hatutauza vitu vingi katika nchi za nje. Viwanda vyetu zaidi ni vya kutusaidia kupata vitu hapa hapa ambavyo mpaka sasa tunaviagiza kutoka nchi za nje. Itapita miaka mingi kabla ya kuweza kuuza katika nchi za nje vitu vinavyotokana na viwanda vyetu. Kwa hiyo ni dhahiri kwamba fedha tutakazotumia kulipa madeni haya ya mikopo ya fedha kwa maendeleo na viwanda mijini hazitatoka mijini na wala hazitatokana na viwanda. Zitatoka wapi, basi? Zitatoka vijijini na zitatokana na KILIMO. Maana ya ukweli huu ni nini? Ni kwamba wale wanaofaidi maendeleo yanayotokana na fedha tunazokopa sio kwa kweli watakaozilipa. Fedha zitatumika zaidi katika miji lakini walipaji watakuwa zaidi ni wakulima. Jambo hili linafaa kukumbukwa sana, maana kuna njia nyingi za kunyonyana. Tusisahau hata kidogo kwamba wakaaji wa mijini wanaweza wakawa wanyonyaji wa jasho la wakulima wa vijijini. Hospitali zetu kubwa zote ziko katika miji. Zinafaidia sehemu ndogo sana ya wananchi wa Tanzania. Lakini kama tumezijenga kwa fedha za mkopo walipaji wa mkopo ni wakulima, yaani wale ambao hawafaidiwi sana na hospitali hizo. Mabarabara ya lami yako katika miji, kwa faida ya wakaaji wa mijini na hasa wenye magari. Kama mabarabaraba hayo 34 MIONGOZO MIWILI

36 tumeyajenga kwa fedha za mikopo walipaji ni wakulima; na fedha zilizonunua magari yenyewe zilitokana na mazao ya wakulima. Taa za umeme, maji ya mabomba, mahoteli na maendeleo mengine yote ya kisasa yako zaidi katika miji. Karibu yote yametokana na fedha za mikopo na karibu yote hayana faida kubwa kwa mkulima, lakini yatalipwa kwa fedha zitakazotokana na jasho la mkulima. Tusisahau jambo hili. Japo tunapotaja unyonyaji hufikiria mabepari, tusisahau kuwa bahari ina samaki wengi. Nao hutafunana. Mkubwa hutafuna mdogo na mdogo naye humtafuna mdogo zaidi. Katika nchi yetu twaweza kugawa wananchi kwa njia mbili. Mabepari na Makabaila upande mmoja; na wafanyakazi na wakulima upande mwingine. Pia twaweza tukawagawa wakaaji wa mijini upande mmoja, na wakulima wa vijijini upande mwingine. Tusipoangalia tutakuja kugundua kuwa wakaaji wa mijini nao ni wanyonyaji wa wakulima. WANANCHI NA KILIMO Maendeleo ya nchi huletwa na watu, hayaletwi na fedha. Fedha ni matokeo siyo msingi wa maendeleo. Ili tuendelee twahitaji vitu vinne: (i) Watu; (ii) Ardhi; (iii) Siasa safi na (iv) Uongozi bora. Nchi yetu ina zaidi ya watu milioni kumi 1* na eneo la eka 362,000. MAENDELEO YATALETWA NA KILIMO Sehemu kubwa ya eneo hili ni yenye rutuba na mvua ya kutosha. Nchi yetu inaweza kutoa mazao ya aina mbalimbali ambayo tunayahitaji kwa chakula na kwa fedha. Mazao ya chakula (na fedha kama tukiyatoa kwa wingi) ni kama vile mahindi, mchele, ngano, maharage, karanga n.k. Mazao ya fedha ni kama vile mkonge, pamba, kahawa, tumbaku, pareto, chai n.k. 1 * Hesabu ya watu ya mwaka 1967 ilionesha kuwa watanzania ni zaidi ya milioni kumi na mbili. MIONGOZO MIWILI 35

37 Pia nchi yetu ni nzuri sana kwa ufugaji wa ng ombe, mbuzi, kondoo, kuku n.k. Pia twaweza kuvua samaki katika maziwa, bahari na mito. Wakulima wetu wako katika sehemu ambazo zaweza kutoa mazao haya, kama si yote walau mawili matatu au hata zaidi. Kila mkulima wetu aweza akaongeza mazao haya ili ajipatie chakula kingi zaidi au fedha nyingi zaidi. Na kwa sababu nia kubwa ya maendeleo ni kupata chakula zaidi na fedha zaidi kwa ajili ya kujipatia mahitaji yetu mengine, ndiyo kusema kuwa jitihada ya kuongeza mazao ni jitihada, na kwa kweli ndiyo jitihada peke yake, ambayo italeta maendeleo, yaani chakula zaidi na fedha zaidi kwa kila mwananchi. MASHARTI YA MAENDELEO (a) Juhudi Kila mwananchi anataka maendeleo, lakini si kila mwananchi anaelewa na kukubali masharti ya maendeleo. Sharti moja kubwa ni JUHUDI. Twendeni vijijini tuzungumze na wananchi kuona kama inawezekana au haiwezekani wananchi kuongeza juhudi. Kwa mfano, katika miji, mfanyakazi wa mshahara hufanya kazi kwa saa saba na nusu au nane kutwa kwa muda wa siku sita au sita na nusu kwa juma. Tuseme saa 45 kwa juma, kuondoa majuma mawili au matatu ya livu, katika mwaka mzima. Ndiyo kusema mfanyakazi wa mjini hufanya kazi ya saa 45 kwa juma kwa majuma 48 au 50 kwa mwaka. Katika nchi kama yetu muda huu ni mdogo kwa kweli. Nchi nyingi hata zilizoendelea kutuzidi hufanya kazi kwa muda mrefu zaidi kuliko saa 45 kwa juma. Si jambo la kawaida nchi changa kuanza na muda mfupi kama huo. Jambo la kawaida ni kuanza na muda mrefu zaidi na kuupunguza kila nchi inavyozidi kuendelea. Sisi kwa kuanza na muda mfupi huu na tunapodai muda mfupi zaidi kwa kweli tunaiga nchi zilizoendelea. Na kuiga huku kunaweza kukaleta majuto. Lakini hata hivyo wafanyakazi wa mishahara hufanya kazi ya saa 45 kwa juma; livu yao kwa mwaka haizidi majuma manne. 36 MIONGOZO MIWILI

38 Yafaa kujiuliza wananchi wakulima hasa wanaume, hufanya kazi kwa saa ngapi kwa juma na miezi mingapi kwa mwaka. Ni wengi mno ambao hawatimizi hata nusu ya wastani wa mfanyakazi wa mshahara. Ukweli wenyewe ni kwamba vijijini kina mama hufanya sana kazi. Pengine hutimiza saa 12 au 14 kutwa. Hawana Jumapili, na hawana livu. Kina mama wa vijijini hufanya kazi zaidi kuliko mtu mwingine yeyote katika Tanzania. Lakini kina baba wa vijijini (na baadhi ya kina mama wa mijini) nusu ya maisha yao ni livu. Nguvu hizi za mamilioni ya kina baba vijijini na maelfu ya kina mama wa mijini ambazo hivi sasa hazifanyi kazi yoyote ila kupiga soga, kucheza ngoma na kunywa pombe, ni hazina kubwa yenye manufaa zaidi kwa maendeeo ya nchi yetu kuliko hazina za mataifa matajiri. Tutafanya jambo la faida kubwa kwa nchi yetu kama tukienda vijijini na kuwaambia wananchi kwamba wanayo hazina hii na kwamba ni wajibu wao kuitumia kwa faida yao wenyewe na faida ya Taifa letu. (b) Maarifa Sharti la pili la maendeleo ni MAARIFA. Juhudi bila maarifa haiwezi kutoa matunda bora kama juhudi na maarifa. Kutumia jembe kubwa badala ya jembe dogo, kutumia jembe la kuvutwa na ng ombe badala ya jembe la mkono, kutumia mbolea badala ya ardhi tupu, kunyunyizia dawa ili kuua wadudu, kujua ni zao gani lifaalo kupandwa na zao gani lisilofaa, kuchagua mbegu vizuri kabla ya kuzipanda, kujua wakati mzuri wa kupanda, wakati wa kupalilia n.k., ni maarifa yanayowezesha juhudi kutoa mazao mengi zaidi. Fedha na wakati tunaotumia kuwapa wakulima maarifa haya ni fedha na wakati uletao faida kubwa zaidi kwa nchi yetu kuliko fedha na wakati mwingi tunaotumia katika mambo mengi tunayoyaita maendeleo. Jambo hili kwa kweli tunalifahamu. Katika mpango wetu wa miaka mitano, mipango inayoendelea vizuri na hata kuzidi makisio ni ile inayotegemea juhudi ya wananchi wenyewe. Pamba, kahawa, korosho, tumbaku, pareto ni mazao yaliyoongezeka kwa haraka sana katika muda wa miaka mitatu iliyopita. Lakini ni mazao ambayo yameongezeka kwa sababu ya juhudi na uongozi wa wananchi, siyo kwa sababu ya fedha. MIONGOZO MIWILI 37

39 Kadhalika wananchi kwa juhudi zao wenyewe na maelekezo au msaada kidogo wametimiza mipango mingi sana ya maendeleo huko vijijini. Wamejenga shule, dispensari, majumba ya maendeleo, wamechimba visima, mifereji ya maji, mabwawa, mabarabara, wamejenga mabirika ya kukoshea mifugo na kujiletea wenyewe maendeleo ya aina mbalimbali. Kama wangengoja fedha wasingeyapata maendeleo hayo. JUHUDI NI SHINA LA MAENDELEO Mipango inayotegemea fedha inakwenda vizuri lakini kuna mingi ambayo imesimama na yumkini mingine haitatimizwa kwa sababu ya upungufu wa fedha. Lakini kelele zetu bado ni kelele za fedha. Juhudi yetu ya kutafuta fedha inazidi kuongezeka! Sio kwamba tuipunguze, bali, badala ya safari nyingi, ndefu na zenye gharama kubwa za kwenda katika miji mikuu ya mataifa ya kigeni kwenda kutafuta fedha za maendeleo yetu, itafaa kufunga safari kwenda vijijini kuwafahamisha na kuwaongoza wananchi katika kujiletea maendeleo kwa juhudi yao wenyewe. Ndiyo njia ya kweli ya kuleta maendeleo kwa kila mtu. Hii maana yake si kwamba tangu sasa hatutajali fedha, wala hatutajenga viwanda au kufanya mipango yoyote ya maendeleo inayohitaji fedha. Wala siyo kusema kuwa tangu sasa hatutapokea wala kutafuta fedha kutoka nchi za nje kwa ajili ya maendeleo yetu. LA, SIVYO. Tutaendelea kutumia fedha; na mwaka hata mwaka tutatumia fedha nyingi zaidi kwa maendeleo yetu ya aina mbalimbali kuzidi mwaka uliopita. Kwani hiyo itakuwa ni dalili moja ya maendeleo yetu. Lakini hii ni kusema kwamba tangu sasa tutajua nini ni shina na nini ni tunda la maendeleo yetu. Katika vitu viwili hivyo FEDHA na WATU, ni dhahiri kwamba watu na JUHUDI yao ndiyo shina la maendeleo, fedha ni moja ya matunda ya juhudi hiyo. Tangu sasa tutasimama wima na kutembea kwa miguu yetu badala ya kupinduka na kuwa miguu juu vichwa chini. Viwanda vitakuja, na fedha zitakuja, lakini msingi wake ni WANANCHI na JUHUDI yao na hasa katika KILIMO. Hii ndiyo maana ya kujitegemea. Kwa hiyo basi, mkazo wetu na uwe: 38 MIONGOZO MIWILI

40 (a) Ardhi na Kilimo. (b) Wananchi. (c) Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, na (d) Uongozi bora. (a) Ardhi Kwa kuwa uchumi wa Tanzania unategemea na utaendelea kutegemea kilimo na mifugo, Watanzania wanaweza kuyaendesha maisha yao barabara bila ya kutegemea misaada kutoka nje kwa matumizi bora ya ardhi hiyo. Ardhi ni ufunguo wa maisha ya binadamu kwa hiyo Watanzania wote waitumie ardhi kama ni raslimali yao kwa maendeleo ya baadaye. Kwa kuwa Ardhi ni mali ya Taifa, Serikali ni lazima iangalie kuwa ardhi inatumiwa kwa faida ya Taifa zima na wala isitumiwe kwa faida ya mtu binafsi au kwa watu wachache tu. Ni wajibu wa TANU kuona kuwa nchi yetu inalima chakula cha kutosha na kutoa mazao ambayo yataleta fedha nchini kwa kuuzwa katika nchi za ng ambo. Ni wajibu wa Serikali na Vyama vya Ushirika kuona kuwa wananchi wanapatiwa vyombo, mafunzo ya uongozi unaohitajika katika kilimo na ufugaji wa kisasa. (b) Watu Kuiwezesha siasa ya kujitegemea itekelezwe vizuri, wananchi ni budi wajengwe moyo na shauku ya kujitegemea. Wajitegemee katika kuwa na chakula cha kutosha, mavazi ya kufaa na mahali pazuri pa malazi. Katika nchi yetu kazi iwe ni kitu cha kujivunia. Bali uvivu, ulevi na uzururaji uwe ni jambo la aibu kwa kila mwananchi. Katika upande wa ulinzi wa Taifa, wananchi wawe macho na vibaraka waliomo nchini ambao wanaweza kutumiwa na maadui wa nje wenye nia mbaya ya kuliangamiza Taifa hili na wawe tayari kulilinda Taifa inapolazimika kufanya hivyo. (c) Siasa Safi Msingi wa siasa ya kujitegemea lazima uambatane na siasa ya Ujamaa ya TANU. Ili kuzuia unyonyaji ni lazima kila mtu afanye kazi na aishi kwa MIONGOZO MIWILI 39

41 jasho lake yeye mwenyewe. Na ili kuleta usawa wa kugawana mapato ya nchi ni lazima kila mtu atimize wajibu wake kwa kufanya kazi kwa bidii zake zote. Asiweko mtu wa kwenda kwa ndugu yake na kukaa kwa muda mrefu bila kufanya kazi kwa sababu atakuwa anamnyonya yule ndugu yake. Vilevile mtu yeyote asiruhusiwe kuzurura zurura hovyo mijini au vijijini bila kufanya kazi ya kumwezesha kujitegemea mwenyewe bila kuwanyonya ndugu zake. TANU inaamini kuwa kila anayelipenda Taifa lake ni budi aweze kulitumikia kwa kujitolea nafsi yake na kushirikiana na wananchi wenzake kwa kuijenga nchi kwa manufaa ya watu wote. Ili kudumisha Uhuru wa nchi yetu na raia zake barabara ni budi kujitegemea kwa kila hali bila kwenda kuomba misaada nchi zingine. Kujitegemea kwa mtu mmoja ni kujitegemea kwa nyumba kumi. Kujitegemea kwa nyumba zote kumi za balozi ni kujitegemea kwa tawi zima. Kujitegemea kwa matawi ni kujitegemea kwa Wilaya ambayo ni kujitegemea kwa Mkoa. Kujitegemea kwa Mikoa yote ni kujitegemea kwa Taifa lote ambalo ndilo lengo letu. (d) Uongozi Bora TANU inatambua umuhimu wa kuwa na Uongozi Bora. Tatizo lililopo ni ukosefu wa mipango maalum ya kuwafundisha Viongozi na kwa hiyo Ofisi Kuu ya TANU ni budi itengeneze utaratibu maalum kuhusu mafundisho ya Viongozi tangu wa Taifa zima hadi Mabalozi ili waielewe siasa yetu na mipango ya uchumi. Viongozi ni lazima wawe mfano mzuri kwa wananchi kwa maisha yao na vitendo vyao pia. SEHEMU YA NNE UANACHAMA Tangu Chama kilipoanzishwa, tumethamini sana kuwa na wanachama wengi iwezekanavyo. Hii ilifaa wakati wa kupigania vita vya kumng oa mkoloni. Hivyo ndivyo ilivyobidi TANU kufanya kwa wakati huo. Lakini sasa Halmashauri Kuu inaona kuwa wakati umefika wa kutilia mkazo kwenye imani ya Chama chetu na siasa yake ya Ujamaa. 40 MIONGOZO MIWILI

42 Kifungu cha Katiba ya TANU kinachohusu uingizaji wa mtu kwenye Chama kifuatwe na ikiwa inaonekana kuwa mtu haelekei kuwa anakubali imani, madhumuni na sheria na amri za Chama, basi asikubaliwe kuingia. Na hasa isisahauliwe kuwa TANU ni Chama cha wakulima na wafanyakazi. SEHEMU YA TANO AZIMIO LA ARUSHA Kwa hiyo basi, Halmashauri Kuu ya Taifa iliyokutana katika Community Centre ya Arusha kuanzia tarehe 26/1/67 mpaka 29/1/67, inaazimia ifuatavyo: A. Viongozi 1. Kiongozi wa TANU au wa Serikali sharti awe mkulima au mfanyakazi na asishiriki katika jambo lolote la kibepari au kikabaila. 2. Asiwe na hisa katika makampuni yoyote. 3. Asiwe mkurugenzi katika kampuni ya kikabaila au kibepari. 4. Asiwe na mishahara miwili au zaidi 5. Asiwe na nyumba ya kupangisha. 6. Viongozi tunaofikiria hapa ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Mawaziri, Wabunge, Wakuu wa Vyama vilivyoshirikishwa na TANU, Wakuu wa Mashirika ya Kiserikali, Viongozi kutokana na kifungu chochote cha Katiba ya TANU, Madiwani, na Watumishi wa Serikali wenye vyeo vya kati na vya juu. (Kwa mujibu wa kifungu hiki kiongozi ni mtu au mtu na mkewe au mke na mumewe). B. Serikali na Vyombo Vingine 1. Inaipongeza Serikali kwa hatua zote ilizokwishachukua mpaka hivi sasa katika kutimiza siasa ya Ujamaa. 2. Inaihimiza Serikali, bila kungojea Tume ya Ujamaa, ichukue MIONGOZO MIWILI 41

43 hatua zaidi za kutimiza siasa yetu ya Ujamaa kama ilivyoelezwa katika Tamko la TANU juu ya Ujamaa. 3. Inahimiza Serikali kutengeneza mipango yake kwa kutegemea uwezo wa nchi hii kuiendesha mipango hiyo na wala isitegemee mno mikopo na misaada ya nchi za ng ambo kama ilivyofanya katika mpango wa maendeleo ya miaka mitano. Halmashauri Kuu ya Taifa inaazimia mpango huo urekebishwe ili ulingane na siasa ya kujitegemea. 4. Serikali ione kuwa mapato ya wafanyakazi nje ya Serikali hayapitani mno na yale ya wafanyakazi Serikalini. 5. Serikali itilie mkazo sana njia za kuinua maisha ya wakulima. 6. Inahimiza NUTA, Vyama vya Ushirika, TAPA, UWT, TYL, mashirika yote ya Serikali, kuchukua hatua ili kutekeleza siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. C. Uanachama Wanachama wafundishwe kwa ukamilifu imani ya TANU ili waielewe, na wakumbushwe wakati wote umuhimu wa kuishika imani hiyo. 42 MIONGOZO MIWILI

44 SURA YA PILI MWONGOZO WA TANU WA 1971 TUMECHOKA KUCHEZEWA 1. Mabeberu wathubutu Kujifanya mbwa-mwitu, Au kujifanya mwewe, Kwa kuachia wenyewe Tudhaniwe tu makoo Ya kuku au kondoo. 2. Lakini watu ni watu, Watu si mang ondi katu: Beberu angajigamba, Angaruka, angatamba, Ni mtu, hana mabawa: Naye hufa, hana dawa. 3. Sasa linalia tena La mgambo, linanena: Beberu, leo ni leo! Tulipozima koleo, Mlidhani ndiyo mwisho, Mkazidisha vitisho! 4. Linalia la mgambo, Lisikike hadi ng ambo: Tumechoka kuonewa! Tumechoka kuchezewa! Tunasema: sasa basi Ubeberu na uasi! 5. Kwani sasa kimefika, Kizazi cha Afrika; Kizazi kipya thabiti, Sumu yao wasaliti; Mabeberu watajuta Hapo kitapowakuta. 6. Si kizazi cha vivuli, Na wala sio cha nduli Si kizazi cha watwana: Ni kizazi cha vijana Madhubuti, Wajamaa, Waso ila, waso waa. 7. Kimefika pasi shaka Kiyashike madaraka; Wanaojidai ubwana Watalia kama wana; Watatetema kwa homa, Na kutubu: Tumekoma! 8. Vijana wa Afrika, Siku yenu imefika! Siku yenu ndiyo leo, Siku ya kufunga teo: Tumechoka kuonewa! Tumechoka kuchezewa! 9. Shime, Onyesheni njia, Vijana wa Tanzania: Wapigeni wanyonyao, Pamwe na vijibwa vyao; Mabeberu makaburu, Wapigeni kwa uhuru. 10. Wamezidi kutughasi Kwa kudhani ndiyo basi: Semeni: leo ni leo, Twali tukisuka teo! Kimbieni, tumefika: Iacheni Afrika! MIONGOZO MIWILI 43

45 MWONGOZO WA CHAMA JUU YA KULINDA, KUIMARISHA NA KUENDELEZA MAPINDUZI YA TANZANIA NA YA AFRIKA Tumeonewa kiasi cha kutosha, tumenyonywa kiasi cha kutosha, tumepuuzwa kiasa cha kutosha. Unyonge wetu ndio uliotufanya tuonewe tunyonywe na kupuuzwa. Sasa tunataka kufanya mapinduzi... UTANGULIZI (Azimio la Arusha) 1. Bara letu la Afrika leo ni kiwanja cha mapambano makali ya ukombozi. Mapambano hayo ni kati ya wale ambao kwa karne nyingi wamekuwa wakinyonya utajiri wa Afrika, na kuwatumia wananchi wa bara hili kama vyombo vyao, kama watumwa wao, na wananchi wa Afrika ambao, baada ya kutambua hali ya unyonge na kunyonywa, wameamua kuingia katika mapambano ya kujikomboa. Mapambano haya ni magumu na ya muda mrefu. Wakati mwingine huwa ya kimya kimya, mara yalipuke kama baruti; wakati mwingine mafanikio huenda kwa wananchi, halafu punde si punde mafanikio yakawaponyoka wananchi. Hiyo ndiyo historia ya Afrika mpaka mwaka 1960, ambapo nchi nyingi za Afrika zilipata uhuru wao wa bendera. Tangu mwaka huo mpaka leo Serikali nyingi za Afrika zimeangushwa kwa nguvu, na Serikali mpya kuundwa. Hivi juzi mabadiliko ya ghafla na ya mabavu yametokea Uganda, ambako Kibaraka Amini na kikundi cha wanajeshi wenzake waasi wameiasi Serikali ya Kimapinduzi ya U.P.C inayoongozwa na Raisi Obote. Wanajeshi walio wengi hawakubaliani na maasi hayo, na wengi wao, hasa maafisa wakubwa wameuawa na vibaraka hao. Ni dhahiri kuwa wanaofurahia maasi ya vibaraka hawa ni wale waliokuwa wakipinga siasa ya U.P.C ya kuleta Umoja na Ujamaa, na kuondoa ukabila na Unyonyaji. Ndiyo maana Chama chetu kina wajibu wa kuifafanua shabaha kuu ya mapinduzi yetu na ya Afrika, na kuwatambua maadui wa mapinduzi haya, ili kutayarisha mipango 44 MIONGOZO MIWILI

46 na mbinu zitakazotuwezesha kulinda, kuimarisha na kuendeleza mapinduzi yetu. 2. Mapinduzi ni mabadiliko ya haraka katika jamii, mabadiliko ambayo yanawanyang anya wachache madaraka ambayo walikuwa wakiyatumia kwa manufaa yao (na ya wanyonyaji wa nje), na kuyaweka madaraka hayo mikononi mwa wengi ili kuendeleza maslahi yao. Kinyume cha mapinduzi ni kupinga mapinduzi, yaani mabadiliko ya haraka yanayo wanyang anya madaraka wananchi walio wengi, na kuwapa wachache, kwa madhumuni ya kuzuia maendeleo ya Umma. 3. Shabaha kuu ya mapinduzi ya Afrika ni kumkomboa Mwafrika. Ukombozi huu haudondoki kama mvua, bali hupatikana kwa kupambana na unyonyaji, ukoloni, na ubeberu. Wala ukombozi huu hauletwi na wataalam maalum. Wataalam wa ukombozi huu ni sisi wenyewe tunaonyanyaswa, tunaonyonywa, na tunaoonewa. Hakuna taifa lolote ulimwenguni lenye utaalam wa kufundisha Waafrika jinsi ya kujikomboa. Wajibu wa kujikomboa ni wetu, na utaalam wa mbinu za mapambano ya kujikomboa tutaupata katika mapambano yenyewe. 4. Kadhalika, hali ilivyo hivi sasa katika Afrika ni kwanba hakujawa na wananchi wa nchi yoyote ya Afrika ambao wamekwisha fikia kiwango cha ukombozi halisi. Afrika bado ni Bara la watu waliomo katika unyonge wa kuonewa na kunyanyaswa, ndiyo kusema kwamba Vyama vya Siasa vya kimapinduzi katika nchi nyingi za Afrika zinazojitawala, kama vile TANU, bado vingali ni Vyama vya Ukombozi. 5. Mapinduzi ya Afrika ambayo lengo lake ni ukombozi kamili wa Mwafrika yanapingana na siasa za unyonyaji za Ukoloni-Mamboleo na Ubeberu na kuhakikisha kwamba utajiri wa Afrika unatumika kwa maslahi ya nchi za kibepari za Ulaya na Marekani, badala ya kuwanufaisha Waafrika wenyewe. Kwa hiyo kushiriki katika mapinduzi ya Afrika ni kushiriki katika mapambano ya kupinga Ukoloni na Ubeberu. MIONGOZO MIWILI 45

47 6. Nchi za kibeberu ambazo zimekuwa zikinyonya na kukandamiza Afrika kwa karne nyingi ni nchi za Ulaya Magharibi, hasa Uingereza, Ufaransa, Ureno, Ubelgiji na Hispania. Nichi za kibeberu ndiyo hasa zinazokabiliana na wananchi wa Afrika katika suala la ukombozi wa Mwafrika. Majaribio mbali mbali yanayofanywa kuvuruga maendeleo ya mapinduzi ya Afrika hasa kutokana na hila za mabeberu wa Ulaya kutaka kuhifadhi na kuendeleza mirija yao ya zamani. 7. Kwa Tanzania lazima ieleweke kwamba maadui tunaokabiliana nao ana kwa ana ni ubeberu wa Kiingereza, ukoloni wa Kireno, na ubaguzi wa rangi wa makaburu wa Afrika ya Kusini na Rhodesia. Kwa sababu za historia, za jiografia na za siasa, mabeberu hawa watakuwa tayari kutushambulia pindi wapatapo nafasi. 8. Mashambulio yaliyofanywa na mabeberu wa Kireno kuivamia Jamhuri ya Guinea ni funzo kubwa sana kwetu. Sababu ya kwanza ya Guinea kuvamiwa na mabeberu wa Kireno ni siasa yake ya usawa na kupinga unyonyaji; na sababu ya pili ni msimamo wake thabiti wa kuunga mkono wapigania ukombozi wa Guinea Bissau na wa Afrika. Kwa sababu hizo hizo mabeberu hawa wanaweza siku moja wakathubutu kuishambulia Tanzania. Lakini Guinea inatufundisha vile vile kuwa wananchi na majeshi yao wakisimama imara pamoja, hakuna mtu atakayeweza kuwanayang anya uhuru wao. 9. Funzo tulilojifunza Uganda ni la usaliti na la kupinga mapinduzi. Yaani, badala ya kuivamia nchi ili kuiangusha Serikali ya kimapinduzi, mabeberu hupendelea sana kuwatumia vibaraka wananchi kuiangusha Serikali halali, ili kuunda Serikali ya wanyapara, itakayowaruhusu mabeberu hao, wakishirikiana na vibwanyenye vienyeji, kunyonya mali ya Taifa. Wananchi inawapasa kuelewa, kutokana na tukio la Uganda na hata la Guinea kwamba ingawa ubeberu bado una nguvu, uwezo wake wa kuangusha Serikali ya Kimapinduzi unategemea sana uwezekano wa kuwapata wapinga mapinduzi wa ndani wa kuwasaidia kuyasaliti mapinduzi. 46 MIONGOZO MIWILI

48 10. Watanzania tunathamini sana uhuru wa Taifa letu, maana hapo ndipo unapoanzia ukombozi wetu, na mategemeo ya mapambano ya ukombozi wa wananchi wengi wa Afrika. Kwa sabau hii tunawajibu wa kuchukua hatua zote muhimu zitakazotuwezesha kuulinda uhuru wetu, ili tuweze kuendeleza mapinduzi yetu, na kuifanya nchi yetu kuwa mfano imara wa mapinduzi ya Afrika. Chama SIASA 11. Wajibu wa kuongoza Umma na vyombo vyake mbali mbali katika juhudi ya kulinda uhuru, ili mapinduzi ya ukombozi wa Mwafrika yaendelee, ni wa Chama. Wajibu wa Chama cha Kijamaa ni kuongoza shughuli zote za Umma. Serikali, Mashirika, Vyama vya Umma, n.k, ni vyombo vya kutekelezea siasa ya Chama. Historia yetu fupi ya uhuru inaonyesha matatizo yanayoweza kutokea wakati Chama hakiongozi vyombo vyake. Sasa wakati umefika wa chama kushika barabara hatamu na kuongoza shughuli zote za Umma. 12. Kuongoza kwanza maana yake ni kutoa lengo la Taifa. Hili linaeleweka, na Chama kimekwisha timiza wajibu huo. Lengo letu ni kujenga Ujamaa Tanzania. Chama kimekwisha toa miongozo juu ya Ujamaa vijijini, Elimu ya Kujitegemea n.k. Lakini, ili lengo la Taifa liweze kufikiwa, lazima chama kitoe siasa na miongozo kuhusu mipango mbali mbali ya shughuli za umma. Uko umuhimu wa kufafanua siasa ya Chama juu ya nyumba, afya, kazi, siasa ya fedha, mikopo n.k. 13. Lakini kutoa lengo la siasa hakutoshi kudhihirisha uongozi madhubuti wa Chama. Maana nyingine ya kuongoza ni kuwaandaa watu. Ndiyo kusema Chama ndicho kinachoamua umbile la Serikali, mashirika mbali mbali, majeshi, n.k. Pamoja na umbile la Serikali, Chama kitoe mwongozo juu ya utaratibu wa kutenda kazi, na namna ya kufikia uamuzi. Ukweli ni kwamba siyo tu kuwa tumerithi muundo wa Serikali ya kikoloni, bali hata tabia za kikoloni MIONGOZO MIWILI 47

49 za utaratibu wa uongozi tumezifanya zetu. Kwa mfano, Serikalini, viwandani, na katika Mashirika ya Umma, tumerithi tabia ya utawala wa mtu mmoja, na wengine ni watu wa kupokea amri. Matokeo ya watu kutokushirikishwa katika mipango ya kazi ni kuwafanya watu wakione chombo cha Umma kana kwamba si chombo chao, na wafanya kazi kuwa na tabia ya wakodiwa. Chama kina wajibu wa kuchukua hatua za kudhihirisha uongozi wake katika jambo hili. 14. Pamoja na kuwaandaa watu, kuongoza ni kusimamia utekelezaji wa siasa ya chama. Lazima zitafutwe njia za kuhakikisha kwamba Chama kinasimamia, kwa vitendo shughuli na mwendo wa vyombo vyake vya utekelezaji. Kadhalika, kuongoza ni kuweza kupima matokeo ya utekelezaji. Ni wajibu wa Chama kuhakikisha kwamba kinapima matokeo ya utekelizaji wa siasa unaofanywa na vyombo vyake. Hii ndiyo njia ya pekee ya kuweza kuwa na hakika kwamba maofisini, viwandani, katika majeshi, vijijini, n.k. wananchi wenyewe wanashiriki katika kutafuta njia za kutatua matatizo yao. 15. Pamoja na suala la watu kushiriki katika kutatua matatizo yao kuna swala la tabia ya viongozi kazini na katika maisha yao ya kila siku. Lazima iwepo jitihada ya kujenga usawa kati ya viongozi na waongozwa. Iwe ni mwiko kwa kiongozi wa Tanzania kuwa mwenye majivuno, ubadhirifu, dharau au uonevu. Kiongozi wa Tanzania awe mtu anayeheshimu watu, asiwe mpenda makuu; siyo mnyapara, mkaripiaji na mwamrishaji watu. Kiongozi awe mfano wa ushujaa, upiganiaji haki na usawa. Kadhalika Chama kina wajibu wa kukomesha maonevu yanayofanywa na baadhi ya vyombo vyake kwa wananchi, maana vitendo hivi haviendelezi Siasa ya Ujamaa. Hivyo ni vitendo vinavyokifanya Chama na Serikali vifarakane na watu. 16. Kuna tabia hivi sasa ya baadhi ya viongozi kutotimiza masharti hayo, na kupuuza na kukwepa kiujanja masharti na nia ya masharti ya Uongozi. Wakati umefika wa Chama kuwa na utaratibu wa kusimamia mwenendo na tabia za viongozi. 48 MIONGOZO MIWILI

50 Siasa ya Nchi za Nje 17. Siasa yetu ya nchi za nje ni siasa ya kutofungamana na upande wo wote. Tuko tayari kushirikiana kirafiki na nchi yoyote yenye nia njema kwetu bila kujali kama hiyo ni ya mashariki au ya magharibi. Jambo la pili muhimu katika siasa yetu ya nje ni kuimarisha uhusiano, ushirikiano na kuunga mkono vyama halisi vya Ukombozi wa Afrika. Tumesema hapo mwanzoni kwamba sisi wenyewe bado tuko kwenye hatua za Chama cha Ukombozi. Hivi sasa katika Afrika Vyama vya Ukombozi ndivyo vilivyo katika mstari wa mbele wa mapambano ya kupinga Ukoloni na Ubeberu, Tukiimarisha kushirikiana kwetu, tukielewa kuwa vita vyao ni vita vyetu, tutaongeza sana nguvu zetu za kuleta ukombozi wa Afrika nzima. Chama kichukue hatua zinazofaa za kujenga uhusiano huo wa kimapinduzi na Vyama vya Ukombozi vya Afrika, vya Asia na vya Marekani Kusini. Vile vile ni wajibu wetu kujenga uhusiano wa kidugu na wa kimapinduzi na raia wa Amerika wanaopigania haki na usawa wa binadamu. 18. Aidha, tunao wajibu wa kuimarisha kushirikiana na kuungana mkono na nchi za kimapinduzi za Afrika, maana sote tumo katika jahazi moja, na safari yetu ni moja. Tukiungana na kushirikiana, maadui zetu hawataweza kutumaliza mmoja mmoja kama ilivyo tabia yao. 19. Kwenye Umoja wa Mataifa katika Mashirika mengine ya kimataifa kuna haja ya kutilia mkazo kushirikiana na nchi zote za kirafiki, za Kijamaa na za Kimapinduzi za Afrika, Asia na Marekani ya Kusini. Uganda na Jumuiya ya Afrika ya Mashariki 20. Tunatambua umuhimu na manufaa yaliyopo, kisiasa na kiuchumi, katika umoja na ushirikiano uliopo kati ya nchi za Afrika ya Mashariki. Hivyo, hali ya hivi sasa iliyoletwa na vibaraka wa Uganda kwa kuvamia serikali halali ya Chama cha U.P.C. inatuletea wasiwasi mkubwa katika ushirikiano na katika kuendesha shughuli za Jumuiya. Hali hii ikiendelea inaweza kufanya maendeleo na mafanikio ya Jumuiya hii kuwa magumu sana, na pia ushirikiano MIONGOZO MIWILI 49

51 wa nchi za Afrika Mashariki huenda ukawa wa shida sana na dhaifu. Chama kinaunga mkono msimamo wa Serikali ya Tanzania juu ya Uganda na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Ingawa swala la ukombozi wa Uganda ni la wananchi wa Uganda, ni wajibu wa wananchi wa Tanzania kuunga mkono ndugu zetu wa Uganda katika juhudi zao za kujikomboa. ULINZI NA USALAMA Katika upande wa ulinzi wa Taifa, wananchi wawe macho na vibaraka waliomo nchini ambao wanaweza kutumiwa na maadui wa nje wenye nia mbaya ya kuliangamiza Taifa inapolazimika kufanya hivyo. (Azimio la Arusha) 21. Msingi wa Maendeleo yote ya Watanzania ni Watanzania wenyewe: kila Mtanzania; na hasa kila mzalendo, na kila mjamaa. Msingi wa Maendeleo ya Ulinzi na Usalama wa Tanzania ni Watanzania wenyewe: kila Mtanzania; na hasa kila mzalendo, na kila mjamaa. 22. Kama Chama chetu kingalilazimika kupigana Vita vya Ukombozi, kila mwana-tanu angalilazimika kuwa askari, ama ndani ya jeshi, au popote alipo: Mwana-TANU angalikuwa ni Mwanajeshi, na Mwanajeshi angalikuwa ni Mwana-TANU. Siyo Chama chetu tu ambacho kingalikuwa ni Chama cha Ukombozi; bali Jeshi letu pia lingalikuwa ni jeshi la Ukombozi-ngumi na ngao ya Chama cha Ukombozi. 23. Chama chetu hakikulazimika kupigana Vita ya Ukombozi. Kilikuwa Chama cha Ukombozi bila Jeshi la Ukombozi. Likini tangu mwaka 1964 tumekuwa tukiunda Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Kama vile Chama cha TANU kilivyo bado ni Chama cha Ukombozi; basi Jeshi la Wananchi wa Tanzania pia ni Jeshi la Ukombozi wa Wananchi wa Tanzania. Uhusiano wa TANU na Jeshi la Wananchi ni lazima uwe 50 MIONGOZO MIWILI

52 ni uhusiano baina ya Chama cha Wananchi na Jeshi la Wananchi. Ni juu ya TANU kuhakikisha kuwa Jeshi la Wananchi ni Jeshi la Ukombozi na Ulinzi wa Wananchi. Ni kazi ya TANU pia kuona kuwa kazi kubwa ya Jeshi wakati wa amani ni kuwawezesha wananchi kulinda uhuru wao na siasa yao ya Ujamaa na Kujitegemea. 24. Halmashauri Kuu ya Taifa inatilia mkazo juu ya utekelezaji wa Azimio la Arusha, na hasa kuzidisha mwamko wa Siasa, ili kila Mwananchi aweze kufahamu mazingira ya Taifa letu, na umuhimu wa kulinda usalama na maisha ya wananchi: Siasa yetu, Uhuru wetu, Uchumi wetu na Utamaduni wetu. 25. Kutokana na mwamko wa Siasa, wananchi wafahamishwe maadui wa Taifa letu, na hila wanazotumia kupiga vita siasa yetu, Uhuru wetu, Uchumi wetu na Utamaduni wetu. Papo hapo, ili wananchi waweze kumkabili adui huyo, lazima wafahamishwe nguvu za adui huyo katika fani zote, kama vile majeshi yao, biashara zao, maisha yao na tabia zao, na jinsi zinavyogongana na hali zetu. 26. Ili waweze kuwakabili maadui hao, wananchi hawana budi kufahamu kwamba wao wenyewe ndio ngao ya Taifa. Hii maana yake ni kwamba shughuli za Ulinzi na Usalama ziwekwe mikononi mwa watu wenyewe. Hatuna uwezo wa kuunda majeshi makubwa makubwa ya kudumu kulinda nchi yetu yote. Majeshi yetu lazima yawe majeshi ya Umma, na yatumike kwa kuwafunza wananchi wenyewe jinsi ya kujilinda katika sehemu wanazoishi, na kuwa na uwezo wa kutoa habari zinazohusu usalama wa Taifa letu. Kwa hiyo ni lazima kuanzisha mafunzo ya malisha kwa nchi nzima. Hawa malisha, kwa sababu wataenea nchini, ndio watakaokuwa na wajibu wa kulinda mipaka ya nchi kavu na pwani, hali kadhalika anga, na kuwafichua majasusi na maadui kwa kushirikiana na majeshi yetu ya kawaida. Chama Kuongoza Majeshi 27. Uandikishaji wa malisha na wa majeshi yote lazima uwe wa uangalifu sana, na usimamiwe na Chama. Ushirikiano wa majeshi na malisha, na MIONGOZO MIWILI 51

53 mafunzo ya Elimu ya Siasa kwa wote, iwe ni kazi muhimu ya Chama. Chama basi kiunde Kamati ndogo ya Kamati kuu, ishughulikie Ulinzi na Usalama. UCHUMI NA MAENDELEO Maendeleo ya nchi huletwa na watu Maendeleo ya Watu (Azimio la Arusha) 28. Kwa watu ambao walikuwa watumwa, au ambao walikuwa wakionewa, wakinyonywa, na kunyanyaswa kwa sababu ya Ukoloni, Ukabaila au Ubepari, maendeleo maana yake ni ukombozi. Kitendo chochote kinachowapa uwezo zaidi wa kuamua mambo yao wenyewe, ni kitendo cha maendeleo, japo kama hakiwaongezei afya wala shibe. Kitendo chochote kanachowapunguzia uwezo wao wa kuamua mambo yao wenyewe na kutawala maisha yao wenyewe, si kitendo cha maendeleo, ni kitendo cha kuwarudisha nyuma, japo kama kitendo chenyewe kinawaongezea afya na shibe kidogo. Kwetu sisi maendeleo ya maana ni yale yanayotuondolea kuonewa, kunyonywa, kunyanyaswa na mawazo ya kufungwa, na kutuongezea uhuru na utu wetu. Kwa hiyo katika kufikiria maendeleo ya Taifa letu, na katika kupanga mipango ya maendeleo, wakati wote mkazo mkubwa utiliwe kwenye maendeleo ya WATU na siyo ya vitu. Ili maendeleo hayo yawe ya watu, watu wenyewe lazima washiriki katika kufikiria, kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo yao. Chama chetu kazi yake si kuhimiza wananchi kutekeleza mipango iliyoamuliwa na wataalam na viongozi wachache. Chama chetu kazi yake ni kuona kuwa viongozi na wataalam wanatekeleza mipango ya maendeleo kama ilivyoamuliwa na wananchi wenyewe. Uamuzi huu wa wananchi unapokuwa unahitaji ujuzi ambao walio nao ni viongozi na wataalam, ni wajibu wa viongozi na wataalamu hao kufikisha ujuzi huo kwa wananchi ili waweze kujifanyia uamuzi wao; lakini 52 MIONGOZO MIWILI

54 si haki kwa viongozi na wataalam kujinyakulia wajibu wa kuamua kila jambo badala ya wananchi wenyewe, ati kwa sababu wao ndio wenye ujuzi. 29. Ili wananchi wawe na ari ya kulinda nchi yao, lazima Serikali ya TANU kwanza itilie nguvu sana hali ya Uchumi wa wananchi. Mtindo wa Uchumi tuliorithi kwa wakoloni, ambao umewatupa wananchi wengi nje ya uchumi, lazima ubadilishwe bila kukawia, na kuanzisha mipango ya kuongeza matumizi na kutumbukiza rasilimali katika Wilaya zote. Kwa mfano, Mpango wa Fedha za Maendeleo Mikoani umeonyesha kusaidia kuamsha shughuli za kiuchumi na kuleta manufaa ya wazi wazi kwa wananchi, na itafaa mpango huo utiliwe mkazo kwa kuongeza fedha hizo na kufanya matumizi hayo yawe ya mwanzo katika makisio ya fedha za Serikali. Chama kitilie mkazo kushirikisha watu katika kazi mbali mbali za kujenga Taifa. Akiba 30. Pia ni wajibu wa Chama kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kujiwekea Akiba katika vyombo vya Umma, kama vile Benki ya Akiba na Benki ya Biashara badala ya kuweka ovyo ovyo tu. Uchumi wa Kitaifa 31. Katika kuimarisha Maendeleo ya watu, hivi sasa ipo haja kubwa ya kujenga na kustawisha uchumi wa ndani ya Taifa letu. Ingawa jambo hili limegusiwa katika Mpango wa Pili wa Miaka Mitano, halikutiliwa mkazo katika utekelezaji, na matokeo yake hayajaonekana. Kadhalika, vitu ambavyo vinatengenezwa nchini mwetu lazima vilindwe na mashindano yasiyo ya lazima kutoka nchi za nje. Biashara ya Nje 32. Juu ya Biashara yetu na nchi za nje ni lazima kuepuka utumiaji wa akiba yetu ya fedha za Kigeni kwa kununua vitu visivyosaidia Uchumi wetu. Serikali na Mashirika yake vionyeshe mfano katika MIONGOZO MIWILI 53

55 jambo hilo. Vikao vinavyoagiza vitu toka nje lazima vipewe mwongozo unaolingana na Siasa yetu ya Ujamaa na Kujitegemea, na ihakikishwe kwamba vinafuata. Ni wajibu wa kila Mwanachi, na hasa Kiongozi kukumbuka kwamba upungufu wa fedha za Kigeni unadhoofisha uchumi wetu na kuhatarisha uhuru wetu. Mashirika ya Umma 33. Hali, tabia na shughuli za mashirika ya Umma lazima kutupiwa macho na kuhakikisha kuwa zinasaidia kupeleka mbele Siasa yetu ya Ujamaa na Kujitegemea. Shughuli za mashirika hayo lazima ziwe za kuridhisha na sio za kuleta manung uniko. Chama kihakikishe kwamba mashirika hayo hayatumii fedha kwa fujo na katika mambo yasiyonufaisha Uchumi wa Nchi kwa jumla. Ziada 34. Serikali isimamie na kuongoza matumizi ya fedha zote za ziada zinazopatikana kutokana na shughuli za Uchumi za Mashirika ya Umma 35. Tumeonewa kiasi cha kutosha, tumenyonywa kiasi cha kutosha, na tumepuuzwa kiasi cha kutosha. Unyonge wetu ndio uliotufanya tuonewe, tunyonywe na kupuuzwa. Sasa tunataka mapinduzi; mapinduzi ya kuondoa unyonge ili tusionewe tena, tusinyonywe tena na wala tusipuuzwe tena. 54 MIONGOZO MIWILI

56 SURA YA TATU MWONGOZO WA CCM WA 1981 YALIYOMO DIBAJI SEHEMU YA KWANZA UTANGULIZI SEHEMU YA PILI UCHAMBUZI WA KUJIKOSOA KAMA CHAMA SEHEMU YA TATU KUJENGA MSINGI WA UCHUMI WA KIJAMAA WA TAIFA LINALOJITEGEMEA SEHEMU YA NNE CHAMA NA MAPINDUZI YETU MIONGOZO MIWILI 55

57 DIBAJI Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama, katika Mkutano wake uliofanyika mjini Dar es Salaam kuanzia tarehe 23 Novemba, 1981 hadi tarehe 7 Desemba, 1981 ilipitisha MWONGOZO WA CHAMA CHA MAPINDUZI wa Halmashauri Kuu ya Taifa ilifikia uamuzi huu baada ya kuzingatia na kuchambua hali halisi ilivyo hivi sasa nchini katika masuala ya siasa, uchumi na maendeleo ya jamii, na kuona kuwa kuna haja sasa ya kutoa msukumo mpya wa ujenzi wa Ujamaa, pamoja na utekelezaji sahihi wa maamuzi mengine mbalimbali yaliyokwisha kutolewa. Shabaha ya Mwongozo wa 1981 ni kufafanua kwa upana zaidi nadharia ya Chama juu ya masuala muhimu na ya msingi ya Siasa yetu katika fani mbalimbali, pamoja na kutoa maelekezo yaliyo wazi zaidi kuhusu mbinu sahihi za utekelezaji wa siasa hiyo. Katika kipindi kilichofuatia kutangazwa kwa Azimio la Arusha, Chama kilitoa maandishi muhimu kadhaa yanayochambua na kufafanua fani mbalimbali za Siasa yetu ya Ujamaa na Kujitegemea, pamoja na kuelekeza njia sahihi za utekelezaji wa siasa hiyo. MWONGOZO WA TANU wa mwaka 1971 ni miongoni mwa matamko hayo muhimu ya kipindi hicho. Mwongozo huo wa TANU unabaki na nafasi yake maalum katika historia ya mapambano ya Chama katika kusukuma mapinduzi ya Tanzania na Afrika kwa jumla katika kipindi hicho. 56 MIONGOZO MIWILI

58 SEHEMU YA KWANZA Utangulizi 1. Historia ya Watanzania kwa vile ni sehemu tu ya historia kubwa zaidi ya Waafrika kwa jumla lazima wakati wote ichambuliwe na kueleweka katika mazingira ya umoja wa Afrika na watu wake. Waafrika wamepitia vipindi na karne za fanaka na maendeleo ya jamii na pia vipindi na karne za misukosuko mikubwa na hata unyonge kitaifa. 2. Historia ya Waafrika ina mifano ya dola zilizofikia hatua kubwa ya maendeleo, ustaarabu na fanaka katika sehemu mbalimbali za bara hili na kwa nyakati mbalimbali. Maandishi, magofu, zana na mabaki ya vifaa vya aina mbalimbali vinavyogunduliwa sasa na wataalamu katika sehemu mbalimbali za Afrika vinathibitisha ustaarabu wa wakati huo katika fani za kilimo, ujenzi, vita, biashara na siasa. 3. Historia ya bara hili pia ina kumbukumbu za vipindi vya misukosuko ya kuingia kwa mataifa ya kigeni. Kuna kipindi Waasia walipoingia Afrika kwa madhumuni ya kujinufaisha na biashara walizoendesha humu Afrika. Mojawapo ya biashara haramu walizoanzisha ni biashara ya watumwa ambayo ilienea hata hapa Tanzania. Biashara ya Watumwa katika Afrika iliendeshwa pia na mataifa ya Ulaya. Inakisiwa kuwa Waafrika wapatao milioni mia moja walihusika na biashara hii ya utumwa. Kumbukumbu za kipindi hiki ambacho watu walisakwa, walikamatwa na kuuzwa bado zingali hai miongoni mwa Watanzania. 4. Kipindi kilichofuatia ni cha wakoloni wa mataifa ya Ulaya waliowanyang anya Waafrika ardhi yao, kuigawa na halafu wakawatawala. Wakati huu Watanzania walitumikishwa na wakoloni. Mazao na matunda ya jasho lao yalichukuliwa kupelekwa nchi za wakoloni kujenga uchumi wao. 5. Watanzania, kama ilivyokuwa kwa Waafrika wengine kote barani Afrika, hawakukiri uvamizi, utumwa wala kutawaliwa bali MIONGOZO MIWILI 57

59 walisimama imara kupambana na maadui kwa vita na mbinu nyingine. 6. Ni vigumu hapa kueleza kwa undani mifano yote ya mapambano ya Watanzania dhidi ya uvamizi wa kikoloni. Hata hivyo ni muhimu kutaja mifano michache ambayo ni vielelezo vya ushujaa, moyo wa uzalendo na jeuri ya kukataa kutawaliwa: vita vya Wasambaa chini ya Kimweri, vita vya Wahehe vikiongozwa na Mkwawa, vita vya Maji Maji vikiongozwa na Kinjeketile, Mputa na Kibasila. Wakati huo huo Waafrika wa Zanzibar walipambana kuupinga uvamizi uliofanywa na Waarabu ambao baadaye walishirikiana na ukoloni wa Waingereza. Watanzania wakati huo hawakufanikiwa kuwang oa wakoloni. 7. Kushindwa kwa Waafrika katika mapambano hayo kunaelezeka. Kwanza ni kwa sababu Waafrika hawakuwa na umoja, walikuwa wamegawanyika katika makabila ambayo yaliishi kwa kutiliana mashaka, kushambuliana na kudharauliana. Wavamizi waliuelewa mfarakano huu na walitumia laghai za aina mbalimbali ili kuwagawa zaidi na kuwashinda mmoja mmoja. Pili zana za vita za Waafrika wakati huo zilikuwa hafifu ukilinganisha na silaha bora zaidi za wavamizi. Na Tatu ni kuwa sababu ya kwanza na ya pili zilifanya upeo wao wa kuandaa malengo na mbinu za vita uwe mfinyu sana na ambao ulitegemea zaidi ushupavu na ushujaa kuliko kuchambua uhusiano wa nguvu kati yao na adui na kutambua nguvu na udhaifu wao na nguvu na udhaifu wa adui ili kuvitumia vipengele hivyo kwa maslahi yao. 8. Miaka iliyofuatia Vita vya Maji Maji ilikuwa ya misukosuko na matatizo makubwa kwa wananchi. Pamoja na unyonge wa watu waliopoteza maelfu ya ndugu zao, miaka hiyo ilikuwa na janga la njaa na magonjwa ya kuambukiza, hasa ndui. 9. Wakati huo huo maelefu ya watu walilazimishwa kuutumikia ukoloni kwenye ujenzi wa Reli ya Kati na ya Tanga na kazi nyingine za harubu ambako walikumbana na ukatili wa Wajerumani usioelezeka. Katika Vita Vikuu Vya Kwanza Vya Dunia wananchi 58 MIONGOZO MIWILI

60 walilazimishwa kushirikiana na wakoloni wa Kijerumani au wa Kiingereza kutetea ukoloni na kwa mara nyingine tena wengi walipoteza maisha yao katika vita visivyokuwa vyao. 10. Lakini, pamoja na hayo vuguvugu la kisiasa liliongezeka. Haikupita miaka mingi baada ya Vita Vikuu vya Kwanza ishara za kwanza zilijitokeza Bara na Visiwani. Mwaka 1929 Waafrika walianzisha African Association kwa Bara ambayo mwaka 1948 ikajiita Tanganyika African Association na 1934 walianzisha African Association Visiwani, vyote vikiwa vyama vilivyojishughulisha na ustawi wa jamii pamoja na utetezi wa maslahi fulani fulani ya Waafrika. 11. Mwisho wa Vita Vikuu vya Pili ulifuatiwa na vuguvugu la mwamko wa kisiasa ulioongezeka kutokana na hali ya ukoloni nchini kuwakera na kuwabana mno wananchi pamoja na vuguvugu la askari waliorudi toka mpakani. 12. Wakati huo huo, kuongezeka kwa idadi ya wafanyakazi bandarini na Serikalini na siasa ya ubaguzi wa rangi na ya mishahara iliyoendeshwa na watawala wa Kiingereza kuliwatia wafanyakazi dukuduku la kutaka kuungana na kupigania haki zao. Mgomo mkubwa wa kwanza wa makuli wa Dar es Salaam na pia Zanzibar uliowatikisa wakoloni ulitokea kunako mwaka Hali ilikuwa inajiandaa kwa uwezekano wa kuanzishwa vyama halisi vya kisiasa nchini. A. KUZALIWA KWA TANU NA ASP 13. Historia ya sasa ya mapambano ya ukombozi katika Tanzania ni historia ya vyama vya kisiasa vya TANU na ASP. Tanganyika African Association na African Association na Shirazi Association kwa Zanzibar vilianzisha vuguvugu la siasa na kuandaa mazingira ya kuviwezesha vyama kamili vya kisiasa kujitokeza. Vuguvugu la vyama vya wafanyakazi nalo liliongezea joto joto la kisiasa nchini. Wakati huo huo nchi nyingine kama Ghana ya Kwame Nkrumah MIONGOZO MIWILI 59

61 na Kenya ya Jomo Kenyatta, zilikwisha anza kuunda vyama vya kuongoza mapambano ya uhuru, na vuguvugu lake liliongezea mwamko wa uhuru wa Watanzania. 14. Hivyo, TANU (7.7.54) na ASP (5.2.57) viliundwa na kujipa majukumu ya mashujaa wa Maji Maji na wengineo walioshindwa huko nyuma na kujibunia malengo, mbinu na zana mpya kwa madhumuni yale yale ya kuung oa ukoloni wa Kiingereza nchini Tanzania Bara na usultani na uwakala wa Kiingereza Visiwani Zanzibar. Mapambano yalikuwa makali na magumu Tanzania Bara na Visiwani. 15. TANU, chini ya uongozi wa Mwalimu Julius K. Nyerere, ilifaulu kuwaunganisha Watanganyika kwa jumla katika hali ngumu ya ukabila, hila, vitisho na mbinu za Serikali ya Kiingereza. TANU iliyafikisha mapambano ya uhuru hadi kwenye uwanja wa kimataifa na Umoja wa Mataifa ambako hila za ukoloni wa Kiingereza zilifichuliwa na kushindwa. Vyama kadhaa vilivyozushwa ili kuwagawa Waafrika na kuchelewesha uhuru vyote vilishindwa. Uingereza ilibidi ikiri nguvu na sauti ya TANU na tarehe 9 Desemba, 1961 Tanganyika ilijinyakulia uhuru wake, miaka saba tu baada ya kuundwa kwa Chama hicho. 16. Afro-Shirazi Party, chini ya uongozi wa Sheikh Abeid Amaan Karume, kilikua mwaka hadi mwaka na kuvishinda vyama vingine vyote vya upinzani. Lakini dola ya Sultani kwa kushirikiana na ukoloni wa Uingereza walikinyang anya Chama cha Afro-Shirazi ushindi wake wa halali katika Uchaguzi Mkuu mara nne mfululizo. Ndipo tarehe Chama Cha Afro-Shirazi kikafanya mapinduzi halali ya silaha yaliyoitokomeza Serikali haramu ya Sultani mwezi mmoja baada ya Sultani na vibaraka wake wa Nationalist Party kukabidhiwa uhuru wa bandia na Waingereza. 17. Vyama vya TANU na ASP vilijenga historia ya kushirikiana na kuungana mkono tangu kuundwa kwao. Kwa hiyo, mara baada ya mapinduzi ya Zanzibar, Serikali ya TANU iliyatambua mapinduzi hayo na kuyaunga mkono kwa vitendo. Miezi mitatu baada ya mapinduzi ya Zanzibar ushirikiano na udugu wa jadi wa wananchi wa Tanganyika na wa Zanzibar uliimarishwa kwa kitendo cha 60 MIONGOZO MIWILI

62 kimapinduzi cha kuunganisha nchi mbili hizi katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao sasa unaitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. B. MAPAMBANO YA KULINDA UHURU NA KUJENGA JAMII MPYA 18. Serikali ya Mapinduzi ya ASP haikuchelewa kuchukua hatua za kuimarisha ushindi iliyoupata dhidi ya usultani. Hatua muhimu katika fani za siasa, uchumi na ustawi wa jamii zilichukuliwa kama msingi wa kwanza katika kazi ngumu ya kuijenga jamii mpya ya haki na usawa. Ardhi ilitaifishwa na hodhi kubwa za makabaila wa kiarabu waligawiwa umma wa wananchi wasiokuwa na ardhi. Wakati huo huo mabenki na biashara ya nje zilitaifishwa na vyombo vya umma kuundwa. 19. Serikali ya TANU haikuchelewa kuchukua hatua za dhati za kujiimarisha ili kuikabili kazi kubwa ya kulinda uhuru na kuanza ujenzi wa uchumi na wa jamii mpya inayojitawala katika hali ya matazamio makubwa ya wananchi kwamba uhuru utawaletea mabadiliko ya haraka katika hali ya maisha yao. Miaka mitano ya kwanza iliyofuatia uhuru ilikuwa kipindi kigumu kwa TANU na Serikali yake changa. TANU yenyewe ilibidi iondokane na hali ya kuwa Chama cha kupigania uhuru na kuwa Chama cha kulinda uhuru na kujenga Taifa linalojitawala. Wakati huo huo Chama kiliwajibika kuiongoza Serikali na wananchi kwa jumla katika jitihada ya kutafuta falsafa ya jamii itakayolingana na matazamio ya wananchi na inayoweza kuwaletea maendeleo halisi nchini. 20. Ilidhihirika katika miaka hiyo ya mwanzo ya uhuru wa Tanganyika kuwa mgongano ulianza kujengeka kati ya matazamio ya wananchi kwa jumla kwamba uhuru ungaliwaletea mabadiliko katika hali ya maisha yao na kwa haraka, na uwezo mdogo wa Serikali wa kukidhi haja za wananchi kulingana na matazamio yao. Mabadiliko makubwa ya mapato na hali ya maisha yaliyoonekana kwa wachache, viongozi na maafisa wa Chama na serikali MIONGOZO MIWILI 61

63 waliokabidhiwa madaraka yaliyokuwa yanashikwa na wakoloni zamani, pamoja na vitendo vya baadhi ya viongozi na maafisa hawa vya kuanza kutumia nafasi zao kujitajirisha, viliimarisha mgongano huo. Tafsiri ya hali hii ilijitokeza wazi wazi wakati umma ulianza kuwaita wale walioonekana wanafaidika kwa vyeo vya uhuru Naizesheni wakati wananchi waliobaki kuitwa Baba kabwela. 21. Pamoja na misuguano hii ya kijamii, uongozi wa Chama ulianza kuwa na wasi wasi na maendeleo ya kiuchumi yaliyopatikana tangu uhuru. Maongozi ya uchumi wakati huo yalikuwa kwamba msingi wa maendeleo ya nchi ni rasilimali toka ng ambo. Ilianza kudhihirika kuwa utekelezaji wa msimamo huo kiuchumi haukuwa na matokeo yaliyotarajiwa. 22. Katika hali hiyo ambapo Chama kilianza kuona kuwa Serikali yake inashindwa kutosheleza matazamio ya wananchi kwa jumla na badala yake kukabiliwa na ongezeko la misuguano ya kijamii mijini na vijijini, na ambapo kilianza kuingiwa na mashaka na kutoridhika na matokeo ya utekelezaji wa mipango ya uchumi wa taifa uliotegemea rasilimali toka ng ambo kuwa ndiyo msingi wa maendeleo, Chama kiliwajibika kujiuliza maswali juu ya usahihi wa siasa ambayo kimeifuata na kuitekeleza tangu nchi ijipatie uhuru. Siasa ya uchumi ya kipindi hiki ilikuwa na sura mbili: kujenga nchi kwa msingi wa ubebari na kwa kutegemea rasilimali toka ng ambo. Funzo tulilopata kama Chama ni kuwa siasa hiyo ya uchumi ilikuwa imeshidwa kwa maana mbili: Kwanza ni kuwa badala ya kusaidia kuimarisha umoja wa Taifa ulioanza kujengwa wakati wa kupigania uhuru ilizalisha migongano ya kijamii na kuanza kukifarakanisha Chama na umma. Pili, Siasa hiyo ya uchumi wa kibepari unaotegemea rasilimali toka ng ambo kama msingi wa maendeleo hayo pia ilishindwa maana utekelezaji wake hakuleta vuguvugu la maendeleo ya kiuchumi yaliyotegemewa na wala hakukuwa na mtiririko wa rasilimali za kutosha toka ng ambo kuingia nchini. 62 MIONGOZO MIWILI

64 C. AZIMIO LA ARUSHA 23. Tangu nyakati za kupigania uhuru Chama kiliweza wakati wote kuelewa na kutambua mwenendo wa hali ya mapambano nchini na duniani kwa jumla na kuchukua hatua sahihi kwa wakati unaofaa ili kuimarisha na kuendeleza mapambano ya wananchi. Kuna maamuzi kadhaa katika historia ya Chama chetu, ambayo ni pamoja na uamuzi wa kuunganisha nchi za Tanganyika na Zanzibar yanayoonyesha kinaganaga uwezo huo wa Chama kukua na nyakati. 24. Kielelezo kimoja kikubwa cha uwezo wa Chama kukua na nyakati na kuelewa mahitaji halisi ya maendeleo ya mapinduzi ya umma ni Azimio la Arusha juu ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Kwa uamuzi huo, misingi mipya na ya kimapinduzi ya kulijenga na kulilinda Taifa iliwekwa hadharani. Kutaifishwa kwa mabenki, biashara ya nje na mashamba makubwa ya mabepari, kuundwa kwa mashirika ya umma na kuanzishwa kwa viwanda vya umma ni baadhi tu ya mambo yaliyodhihirisha nia ya Chama ya kuunda mfumo mpya wa uchumi utakaofanana na jamii ya kijamaa inayodhamiriwa kujengwa. 25. Hatua za kujenga Ujamaa zilizochukuliwa hadi sasa zimejenga msingi unaotia moyo na ni mafanikio ya kujivunia. Njia muhimu za uchumi kama benki, viwanda, biashara ya nje na ya ndani, mashamba makubwa, reli na posta zinamilikiwa na umma, tofauti ya mishahra kati ya iliyokuwa chini kabisa na iliyokuwa juu kabisa serikalini wakati wa kupata uhuru ilikuwa ya uwiano wa 1:7 na sasa ni ya uwiano wa 1:4. Pamoja na hali ya uchumi wetu kitaifa kuwa ya matatizo, tumefaulu kutoa elimu bure toka msingi hadi Chuo Kikuu na elimu kwa watoto wote wa kiwango cha msingi; wakati huo huo tunatoa matibabu bure toka vijijini hadi mijini; wananchi wana nafasi ya kushiriki katika mambo yanayowahusu, wafanyakazi wana mabaraza yao, wakulima vijijini wana Serikali zao zinazoendesha shughuli zao wakati mpango wa demokrasia ya Chama kimoja unawapa nafasi wananchi kuchagua wabunge wao. Yote haya na mengine ni vielelezo vya mafanikio ya Siasa ya Ujamaa. Aidha, uwezo tuliouonyesha kwa kukabiliana na shida kubwa ya njaa mwaka 1974/75 bila Watanzania MIONGOZO MIWILI 63

65 kupoteza maisha yao na pia ushindi wetu dhidi ya majeshi ya uvamizi ya Iddi Amin ambao umepatikana kutokana na mshikamano sahihi wa Chama, Serikali, wananchi na wapiganaji, yote haya ni mafanikio ya ujamaa. 26. Tungeweza kuendelea kukariri mafanikio yaliyopatikana nchini kutokana na utekelezaji wa siaisa ya Chama ya Ujamaa na Kujitegemea. Lakini jambo la kuzingatia ni kuwa hatua tulizozichukua katika kutekeleza Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ni za awali tu na kwamba kubwa zaidi tulilofanikiwa ni kujichorea barabara tunayodhamiria kufuata katika kulijenga Taifa letu la watu sawa na huru ambalo lengo lake ni maendeleo kwa wote. SEHEMU YA PILI UCHAMBUZI WA KUJIKOSOA KAMA CHAMA (1) Upungufu katika kusimamia uchumi 27. Halmashari Kuu ya Chama ya Taifa katika kikao chake cha tarehe 15 hadi 17 Mei, 1981 ilizingatia hali ya uchumi na jamii inayolikabili Taifa na kufanya uchambuzi ili kubainisha kiini cha matatizo haya. Uchambuzi uliofanywa ulidhihirisha mambo makubwa matatu. Kwanza, ni kwamba matatizo ya kiuchumi yanayoikabili nchi yetu si ya kipekee kwa Tanzania bali ni matatizo yaliyozikumba nchi zote, zisizoendelea na hata zile zilizoendelea, zilizoamua kujenga ujamaa na zile zilizoamua kujenga ubebari. 28. Jambo la pili lililodhihirika ni kuwa baadhi ya sababu za matatizo yetu ya kiuchumi ziko nje ya uwezo wetu. Mfumo wa biashara ya kimataifa ulivyo unazikandamiza na kuzinyonya nchi changa kama Tanzania. Kwa mujibu wa mfumo huu wa biashara ya kimataifa nchi za viwanda zinajipangia bei za bidhaa za viwanda vyao na kutuuzia sisi na wakati huo huo nchi hizo hupanga wao bei za mazao ya kilimo tunayozalisha sisi na kuwauzia. Vile vile Tanzania haina kauli na bei za mafuta tunayoyaagiza toka ng ambo. 64 MIONGOZO MIWILI

66 29. Sasa, bei za mafuta na bei za bidhaa za viwanda vya nchi zilizoendelea zimepanda sana katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Tanzania sasa inawajibika kutumia asilimia sitini ya mapato yake yote ya fedha za kigeni kununulia mafuta ambapo mwaka 1972 ilitumia asilimia kumi ya fedha za kigeni kununua kiasi hicho hicho cha mafuta. Wakati huo huo, kwa kutumia mbinu za kupandisha bei za bidhaa zao za viwanda na kushusha bei za mazao ya nchi changa, nchi zilizoendelea zimefaulu kuupunguza kabisa uwezo wetu wa kununua bidhaa za viwanda vyao zinazohitajika sana na nchi changa. Kwa mfano, miaka kumi iliyopita Tanzania iliweza kununua trekta moja toka ng ambo kwa thamani ya tani tano za chai iliyouzwa ng ambo. Leo Tanzania inahitaji tani kumi na saba za chai ili kununua trekta la aina ile ile. Hali hii lazima iwe na matokeo mabaya kwa uchumi wa Taifa letu. 30. Nchi yetu pia imepatwa na matatizo ya ndani ambayo pia tusingekuwa na uwezo wa kuyazuia na yote yameathiri hali yetu ya uchumi. Matatizo hayo ni pamoja na vita vya kujihami tulivyolazimika kupigana dhidi ya majeshi ya uvamizi wa Iddi Amin, mafuriko makubwa ya 1978/79 na hali ya ukame katika baadhi ya mikoa. 31. Jambo la tatu lililodhihirika vile vile ni kwamba sisi wenyewe kama taifa hatukutumia kwa kiasi cha kutosha nguvu za Chama, Serikali na za wananchi katika kutatua matatizo ya uchumi ambayo ufumbuzi wake tuna uwezo nao. 32. Jambo la kwanza linahusu kilimo kwa jumla. Pamoja na kuwa bei za mazao yetu tuyauzayo ng ambo imekuwa ikishuka, mapato ya fedha za kigeni kwa Taifa kutokana na mazao yanategemea pia kiasi taifa linachozalisha na kuuza. Taifa linalozalisha kidogo litauza kidogo na kupata fedha chache za kigeni. Likizalisha mazao kwa wingi na kuuza litapata fedha za kigeni zaidi. Lakini, utoaji wa karibu mazao yetu yote ya biashara umepungua ukilinganisha na miaka ya nyuma. Ni dhahiri kuwa hata kama tumekuwa na matatizo ya mafuriko na ya ukame hapa na pale, kushindwa kwetu kuongeza utoaji MIONGOZO MIWILI 65

67 wa mazao ya biashara na chakula kunatokana pia na kushindwa kwetu kuwaongoza wananchi kwa maandalizi thabiti, mipango na msukumo katika kilimo. 33. Pili kuna suala la utengenezaji mali wa kijamaa. Laiti kama Chama kingeongoza, kusimamia, kuhimiza na kusaidia utekelezaji wa Ujamaa Vijijini vizuri tangu Azimio la Arusha hadi sasa, tungeweza kuwa na sekta kubwa ya ujamaa katika kilimo vijijini ambavyo ingetuwezesha kutoa ziada ya mazao ya chakula na biashara kuliko ilivyo sasa. Kama wastani wa ekari za ujamaa wa kila kijiji nchini ungekuwa angalau ekari mia kwa kila kijiji wakati huu basi sekta ya Ujamaa vijijini katika kilimo ingekuwa na ekari zipatazo laki sita. Ekari laki sita za ujamaa zingeweza kuongeza ziada ya mazao yanayotolewa na Taifa kwa kiasi kikubwa. 34. Na tatu ni kuwa jitihada zetu za kuunda na kupanua sekta ya umma haikuambatana na jitihada ya kutosha ya kuelimisha, kuwaandaa na kuwajenga wafanyakazi na viongozi wa kazi katika misingi ya kufanya kazi kwa nidhamu na ari, misingi ya uzalendo na ya uaminifu kwa umma. Hali hii imeathiri utengenezaji mali na utoaji huduma wa sekta hii. Viwanda vingi nchini havitoi mali kwa kadri ya uwezo vilio nao na pia mali nyingi ya umma hupotea kutokana na vitendo vya wizi, uzembe na ubadhirifu. Upungufu wetu katika kujenga maadili ya kijamaa miongoni mwa wafanyakazi na wakuu wa kazi ni moja ya sababu zilizofanya viwanda na mashirika yaliyo mengi nchini yasitoe mchango wa kutosha katika kuujenga uchumi wa taifa. 35. Lakini maadui wa ujamaa wa nje na wa ndani wanaeneza kuwa matatizo yetu yanatokana na Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Maadui hawa wa ujamaa wanajua kuwa wayasemayo si kweli, lakini kwao wao kukashifu ujamaa ni sehemu muhimu ya mbinu zao za vita vya ghiliba dhidi ya Ujamaa. Kwani ukweli unaojitokeza wazi wazi ni kuwa baadhi ya matatizo yetu ya uchumi yanatokana na kutotekeleza kwa dhati Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea vijijini na katika sekta ya umma tuliyoianzisha. Zaidi ya hivyo, 66 MIONGOZO MIWILI

68 wakati mwingine katika miaka kumi na minne tangu Azimio la Arusha, Chama, Serikali na vyombo vyake vimetumika kukuza sekta ya kibepari nchini katika viwanda, biashara, usafirishaji, ujenzi na kadhalika na ubepari huo uliopanuka katika kipindi hiki umeimarisha vitendo vya kuivuruga na kuidhoofisha sekta yetu ya Umma. 36. Aidha, kuna matatizo ya kijamii kama vile kuongezeka kwa rushwa, hujuma za kiuchumi, wizi, ujambazi na uharibifu wa mali ya umma, mambo ambayo yanatupunguzia nguvu zetu za kiuchumi na kudhoofisha dhamira ya umma ya kujenga ujamaa. Haya yote yamo katika uwezo wa Chama, Serikali na wananchi kuyapiga vita na kuyashinda. 37. Hivyo, katika kufanya uchambuzi wa kujikosoa, Halmashauri Kuu ya Chama ya Taifa ya Mei, 1981 ilikiri kuwa pamoja na kwamba Chama chetu, tangu TANU na ASP hadi sasa Chama Cha Mapinduzi, kimepata mafanikio na ushindi wa kihistoria katika nyanja mbalimbali za mapambano, ni muhimu kukubali pia kwamba kimeonyesha upungufu usiokatalika, kama chombo kikuu cha uongozi wa Taifa na hasa chombo cha uongozi wa harakati za kujenga Ujamaa na Kujitegemea nchini. Kukiri upungufu huu si kitendo cha kujidhoofisha bali ni kitendo cha kujiamini na kujiimarisha. (2) Wana CCM ndiyo askari wa mstari wa mbele wa mapambano ya kujenga Ujamaa 38. Uchambuzi wa kujikosoa umedhihirisha kuwa kwa miaka mingi Chama hakikuthamini ipasavyo uanachama na kuitambua nafasi ya wanachama katika harakati za ujenzi wa ujamaa na wa Taifa kwa jumla. Chama cha kijamaa kama CCM ni chombo cha kuongoza mapambano ya ujamaa nchini. Ni kweli kuwa ujamaa kimsingi ni siasa ya Wakulima na Wafanyakazi na kwamba utajengwa na wafanyakazi katika umoja wao wa kitabaka. Lakini ni kweli pia kwamba bila ya wapiganiaji ujamaa wa mstari wa mbele, bila ya kikosi cha askari wa mstari wa mbele wa harakati za ujamaa, lengo MIONGOZO MIWILI 67

69 la kujenga ujamaa haliwezi kufikiwa. Kikosi hicho cha wapiganiaji ujamaa wa mstari wa mbele ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi. 39. Vyama vyetu asilia, ASP na TANU, vilifaulu kuwawezesha wanachama wake kuwa kikosi thabiti cha mstari wa mbele cha kupigania uhuru. Wanachama hao kwa jumla walijitolea mhanga kwa ajili ya mapambano ya uhuru wa nchi yao, mapambano yao waliyaweka kabla ya maslahi yao binafsi na mengine yoyote. Tutakuwa tunajidanganya tukisema kuwa wanachama wote wa Chama cha Mapinduzi na pia wanachama wote wa TANU na ASP katika miaka kadhaa kabla ya kuundwa kwa CCM, walikuwa kikosi kinachotimiza sifa hizo kwa upande wa lengo la kujenga Ujamaa. Mapambano ya uhuru yalikuwa ya wenyewe, wanatanu na wana ASP wa enzi hizo, na kuwa wananchi waliobaki walielimishwa, walihamasishwa na walishirikishwa katika mapambano ambayo chimbuko la vuguvugu lake lilikuwa msimamo na vitendo vya wanachama. Katika maana hiyo, mapambano ya kujenga Ujamaa Tanzania lazima yawe na wenyewe. 40. Hali hii haikuzuka siku moja bali ni matokeo ya msimamo na vitendo vya miaka mingi. Ilianza tangu baada ya uhuru, wakati viongozi wa ngazi ya taifa, Mkoa na Wilaya hawakuipa uzito kwa vitendo nafasi ya mwanachama katika mapambano yetu. Karibu viongozi wote tulishughulika na mikutano ya hadhara, mikutano ya wananchi kwa jumla bila ya kujali kukutana na wanachama. Viongozi wengine wa Chama tulilemazwa na umangi meza na wengine hata kufikiri wangeimarisha utekelezaji wa shughuli za Chama kwa njia ya vyombo vya habari tu. Ingewezekana kwa viongozi kuhakikisha kuwa kila baada ya mikutano ya hadhara ya wananchi wote, ambayo pia ina umuhimu wake, wanakutana na wanachama wenzi wao ili kuulizia juu ya hali ya Chama mahali hapo na pia kuonyesha kuwa uanachama ulikuwa na maana na uzito maalum ambao viongozi wanautambua. Lakini hatukufanya hivyo na matokeo yake ni kwamba fikra zilijengeka kuwa uananchi ulikuwa unatosha kabisa. 68 MIONGOZO MIWILI

70 41. Kwa wanachama walio wengi wa CCM kutokuwa kikosi cha mstari wa mbele cha kupigania ujamaa na kutojiona kuwa ndiyo wenye mapambano ya kujenga ujamaa kumetokana pia na ukweli kuwa Chama hakikuwa na mpango wa kuwajenga na kuwaandaa wanachama kwa madhumuni hayo. Mwamko wa kitaifa na wa kizalendo ulikuwa rahisi kumpata Mwafrika wa Tanzania wakati wa ukoloni maana adui, ambaye ni mtawala wa kigeni, alikuwa anaonekana wazi wazi na hivyo suala la fedheha ya kutawaliwa ilikuwa rahisi kulieleza na rahisi pia kueleweka na kumkera mtu. Uadui wa mfumo wa kibepari ni mgumu zaidi kuuelezea mpaka ueleweke na kumtia mtu mori ya kuuchukia na kuukataa. Ubepari au unyonyaji si suala la rangi ya mtu na hivi sasa baadhi ya wanyonyaji nchini ni Waafrika wenzetu. Kwa hiyo, wanachama wa Chama cha kujenga ujamaa wanahitaji zaidi maandalizi ili waelewe uzito wa mapambano na kupata mbinu za kuongoza mapambano ya umma kwa vitendo. Viongozi wanahitaji maandalizi ya hali ya juu zaidi. 42. Hali hii ambapo wanachama na viongozi kwa jumla waliachiwa wajitetee wenyewe (na wengine wametimiza wajibu wao kwa sifa) iliimarisha hali iliyozungumziwa hapo awali kwamba uanachama na uananchi ulikuwa sawa tu na hivyo suala la nani amwongoze nani lilijitokeza: maana kama kuongoza ni kuonyesha njia basi haikuweza kuwa dhahiri wakati wote kuhusu nani aijuaye njia, ni mwanachama wa CCM au wananchi kwa ujumla, ni viongozi wa CCM au wanachama. 43. Vyuo vya chama ambavyo ndivyo ingebidi viwe mahala pa kuandaa wanachama hasa viongozi wa Chama vimeendelea kuwa vyuo vya Elimu ya Siasa kwa jumla. Ni kweli kuwa Chama chochote cha kijamaa halisi lazima kiwe na mipango thabiti ya kutoa elimu ya siasa ili kuwahamasisha wananchi kwa jumla na hasa makundi ya taasisi mbalimbali kama vyuo, shule, majeshi, vijana, wafanyakazi, wakuu wa kazi na kadhalika. Lengo la elimu ya siasa kwa taasisi hizi ni kuinua mwamko wao wa siasa na kuwapa wahusika mwelekeo wa kisiasa kwa kulingana na shughuli zao katika nchi. Lakini wanachama wanahitaji mafunzo ya siasa ya Chama ili kuongeza MIONGOZO MIWILI 69

71 upeo wao wa kuielewa siasa ya ujamaa, mafunzo ya mbinu za kushiriki na kuongoza umma mahali walipo katika harakati za kujenga ujamaa na mafunzo ya kuwapa uwezo wa kueneza na kutetea siasa ya Chama. Mafunzo haya hutolewa na vyuo vya Chama kwa utaratibu na malengo yaliyo wazi. (3) Umuhimu wa nadharia sahihi ya Ujamaa 44. Pamoja na upungufu wetu kama Chama kuhusu nafasi ya uanachama na wanachama katika mapambano yetu ya kujenga ujamaa kuna suala linalohusu umuhimu wa nadharia sahihi ya Chama. Chama ni muungano wa watu wanaokubaliana juu ya lengo katika jamii na namna ya kulifikia. Kinachowaunganisha ni fikra zao, itikadi yao, inayohusu jinsi gani shughuli za jamii nchini ziendeshwe na kwa maslahi ya nani. Ni muhimu kusisitiza kuwa kinachowaunganisha wanachama ni itikadi, fikra na falsafa yao ya siasa. 45. Lakini masuala ya falsafa, itikadi na fikra ni masuala ya nadharia. Hivyo suala la nadharia ya Chama ni suala la msingi kabisa kwa uhai wa Chama, kwa maendeleo ya mapambano ya Chama, kwa malengo na mbinu za mapambano hayo na kwa umoja, nguvu na usahihi wa vitendo vya Chama na vya wanachama. 46. Chama chetu ni miongoni mwa vyama vichache katika Afrika ambavyo vimefaulu kubuni nadharia ya ujamaa iliyo sahihi, wazi na ya kiwango cha juu. Nadharia hiyo ya Chama inajidhihirisha yenyewe katika Katiba, Azimio la Arusha, Mwongozo na maandishi mengine muhimu ya Chama. Nadharia hii ya siasa yetu ya Ujamaa na Kujitegemea imetujengea msingi wa uelewano, umoja na ushirikiano wa aina mpya katika ujenzi wa taifa na kutufanya tueleweke na wengi kimataifa, jambo ambalo limetupa sifa na heshima duniani kote. 47. Tumetamka hapo awali katika kujikosoa kuwa siku za nyuma tumeonyesha upungufu kwa kutokuwa na mipango thabiti ya kuwaandaa wanachama na hasa viongozi. Upungufu huu umekuwa na matokeo kwa upande wa nadharia. Pamoja na nadharia fasaha 70 MIONGOZO MIWILI

72 iliyomo katika maandishi makuu ya Chama, pamoja na jitihada na uwezo wa Mwenyekiti wa Chama Mwalimu J. K. Nyerere, wa kufafanua na kuendeleza nadharia ya Chama, viongozi wengi tumetosheka na kiwango kisichoridhisha cha nadharia. Wengine tumediriki hata kuipiga vita nadharia na kupuuza umuhimu wa kujifunza siasa na nadharia ya Chama, kuinua uwezo wetu wa uchambuzi wa masuala mbalimbali ili kuweza kutetea na kueneza siasa ya Chama kwa hoja, uchambuzi na ufafanuzi ulio wazi na sahihi. 48. Ni muhimu kusisitiza kuwa pamoja na maandishi ya Chama yaliyo sahihi na ya kimapinduzi, pamoja na upeo na uwezo mkubwa alionao Mwenyekiti, Mwalimu J. K. Nyerere, wa kutafakari na kuchambua masuala mbalimbali kwa kina na ufasaha au wa kiongozi mwingine yeyote, lakini kwa kuwa Chama ni wanachama na viongozi wote kwa pamoja katika mshikamano wao wa nadharia na vitendo, basi ni hatari kwa maendeleo ya Chama na ya siasa yake ya ujamaa kuiachia hali ambapo kiwango cha kuielewa nadharia ya Chama kinahitilafiana mno kati ya wana CCM na hata kati ya viongozi wa ngazi moja ya uongozi. 49. Chama chetu kinaongoza mapambano ya Watanzania katika mazingira ya kimataifa yaliyo magumu na yenye sura nyingi katika siasa, uchumi na jamii. Kuweza kuliongoza Taifa katika mazingira haya magumu, Chama kinahitaji kuwa na uwezo wa juu wa kuyaelewa mazingira hayo ambayo hayawezi kueleweka bila ya uchambuzi wa kina na nyenzo za kufanyia uchambuzi huo. Uchambuzi huu lazima ukiwezesha Chama kufichua mvutano wa maslahi uliopo baina ya mataifa kufichua uhusiano halisi wa nguvu kati ya ubeberu na ubepari wa dunia kwa upande mmoja na nguvu za ujamaa kwa vuguvugu la ukombozi wa taifa kwa upande mwingine, na kufichua uhusiano halisi uliopo kati ya mataifa ya viwanda na mataifa yasiyo ya viwanda. Uchambuzi wa aina hiyo ndio utakaokiwezesha Chama kuliongoza Taifa kwa usalama kimataifa na kwa maslahi yetu. 50. Wakati huo huo hali ya ndani ya Tanzania imebadilika sana. Uchumi wa taifa, huduma na jamii yenyewe yote imekuwa na kupanuka. MIONGOZO MIWILI 71

73 Kuielewa vema jamii ya Tanzania ya leo kunataka uchambuzi wa hali ya juu pia. Uchambuzi huu ukiwezeshe Chama kuielewa migongano ya maslahi ya tabaka ambayo imejitokeza nchini. M i g o n g a n o hii ina mizizi yake katika mgongano wa msingi kati ya ujamaa na ubepari, kati ya maslahi ya wakulima na wafanyakazi kwa upande mmoja, na ya ubinafsi ubwanyenye na ubepari ambao umekuwa ukijengeka tangu Azimio la Arusha kwa upande mwingine. Kwa hiyo, ili Chama kiweze kuendelea kuongoza mapambano ya kujenga ujamaa ni muhimu kuwa na uwezo wa kufanya uchambuzi sahihi wa hali ya jamii yetu. 51. Jambo linalosisitizwa hapa ni kuwa kwa Chama Cha Mapinduzi kuongoza ipasavyo siasa ya ndani na ya nje ya nchi yetu ni muhimu kwa viongozi wa ngazi zote na pia wanachama kuwa na uwezo wa hali inayoridhisha ya nadharia kama silaha katika kutekeleza jukumu hilo. Hivyo, ni jambo la umuhimu wa kwanza kwa viongozi na wanachama kujiendeleza katika nadharia ya siasa ya Chama. Kwa kiongozi au mwanachama wa CCM kupuuza, kudharau au kukataa kujiendeleza katika nadharia kwa visingizio vyovyote ni msimamo wa uhasama dhidi ya maendeleo ya Chama. 52. Ujenzi wa ujamaa si lelemama bali ni mapambano, mapambano ya kudumu dhidi ya ubepari na unyonyaji, dhidi ya wapinga maendeleo na wababaishaji wa kisiasa, dhidi ya wahujumu uchumi, majambazi, wezi, wazururaji na wazembe. Msimamo sahihi wa mapambano unaotokana na nadharia sahihi ya ujamaa ungelituepusha na maamuzi na vitendo ambavyo vimerahisisha kuoteshwa kwa mizizi ya ubepari, kinyume cha msimao wa mapambano dhidi ya ubepari. Leo ubepari una vishawishi vingi zaidi nchini kuliko ulivyokuwa kabla ya Azimio la Arusha kwa sababu pamoja na kwamba sasa tuna sekta kubwa ya umma lakini kutokana na udhaifu wa kutopambana nao, ubepari umefaulu kujipanua na kujipenyeza hata ndani ya sekta yenyewe ya Umma. Na ndiyo maana ubepari sasa unathubutu kujitokeza hadharani kuukashifu ujamaa, kubabaisha baadhi ya viongozi na kututaka tubadilishe siasa yetu. 72 MIONGOZO MIWILI

74 53. Upungufu wa nadharia ya ujamaa unaweza kuathiri maslahi ya Chama kwa namna nyingine. Chama cha kijamaa kama CCM ni chombo cha uongozi, si chombo cha amri na utawala wa mabavu. Kinaongoza kwa kuelimisha, kuelewesha, kushauri, kushawishi, kushirikisha na kuelekeza na nguvu yake kubwa inatokana na kukubalika kwake na umma, mshikamano wa wanachama wake na fikra sahihi za siasa yake inayolingana na maslahi ya Umma, mshikamano wa wanachama wake na fikra sahihi za siasa yake inayolingana na maslahi ya Umma. Ili kutimiza jukumu lake la uongozi kinahitaji nguvu ya hoja siyo hoja ya nguvu. Hivyo, kiwango cha juu cha nadharia kinahitajika kwa viongozi wa ngazi zote na hata wanachama ili kuwaelimisha na kuwashawishi wasio wanachama, kuitetea siasa dhidi ya hujuma za maadui, kufafanua masuala mbalimbali na kujibu hoja za wanachama au wananchi kwa jumla. Kufanya ufafanuzi usioridhisha, kujibu hoja halali kwa juu juu au kuwaita waulizao maswali wapinzani wa Chama kama ifanyikavyo wakati mwingine hakujengi bali hudhoofisha Chama. (4) Mshikamano wa nadharia na vitendo 54. Katika kufanya uchambuzi wa kujikosoa katika Chama ni muhimu kuzingatia suala la uhusiano uliopo, mshikamano uliopo, kati ya nadharia na vitendo. Nadharia ina kazi ya kuangaza na kuongoza vitendo. Lakini kwa kuwa lengo la ujamaa ni kuibadili dunia, kujenga misingi mipya ya uchumi, kuleta mfumo mpya wa jamii basi vitendo vya kijamaa ndicho kipimo cha ujamaa kwa Chama na ujamaa kwa Wanachama. 55. Suala hili la mshikamano wa nadharia na vitendo, la kutenda mapinduzi, linatusaidia kuelewa kwa undani mwenendo wa ujenzi wa ujamaa kama linavyohusu uamuzi wa kutaifisha na kazi ya kukibadili kilichotaifishwa kiwe chombo cha ujamaa. Kazi ya kuunda vyombo vya umma kama mabenki, viwanda, mashirika ya biashara, mashamba ya Taifa ni kazi ya kujenga ujamaa. Lakini kazi nyingine muhimu ya kijamaa ni kuhakikisha kuwa ujamaa unajengwa ndani ya vyombo hivyo. Tatizo letu katika siku za MIONGOZO MIWILI 73

75 nyuma ni kuwa hatukutilia mkazo umuhimu wa kujenga ujamaa ndani ya vyombo vya umma na hii imerahisisha fikra na tamaa za kibepari kuzagaa katika vyombo hivi na mwisho kutekwa nyara ili vihudumie ubepari na ubinafsi. 56. Upungufu wa kuuelewa vilivyo uhusiano wa nadharia na vitendo katika harakati za ujamaa unaweza kusababisha pia msimamo usio sahihi wa kutenganisha jukumu la uongozi na utendaji au kazi. Uongozi si kazi ingawa zipo kazi za uongozi. Hivyo, wajumbe wa vikao vya Chama ni lazima wawe au na kazi zao za kawaida kama za ajira au kilimo ama wawe na kazi za uongozi katika Chama, Serikali au Mashirika ya Umma. Vinginevyo kutakuwa na watu katika Chama ambao si wakulima wala si wafanyakazi na huu ndio mwanzo wa kujenga kundi la wababaishaji wa kisiasa, jambo ambalo ni hatari sana kwa harakati za ujamaa. Tabia ya kutenganisha uongozi na utendaji imeathiri maendeleo ya Chama kwa msukumo, usimamizi na utekelezaji maana kati ya uamuzi na utendaji kumekuwa hakuna kiungo. 57. Tatizo hili la kutenganisha uongozi na utendaji linaweza pia kukizorotesha Chama kwa kukifanya kisahau kuwa chenyewe vile vile ni mtendaji na kwamba kitapimwa kwa vitendo vyake kama Chama. Katika maana hiyo Halmashauri Kuu ya CCM ya Tawi ipimwe na vikao vya juu kwa utekelezaji wake wa Siasa ya Chama; kama wanachama wake wako mstari wa mbele kwa ujamaa, kama wanashiriki katika shughuli za kujitolea, kama ni wafanyakazi hodari, kama kijiji chao kina maendeleo ya kijamaa na kadhalika. Vivyo hivyo kwa kamati ya utendaji ya Wilaya, Mkoa na Taifa. Kwa hiyo, pamoja na kushughulikia uongozi wa serikali, Jumuiya na vyombo vingine, Chama kina kazi ya kujijenga chenyewe ili kujipa uwezo wa kutosha wa kuongoza Umma na vyombo vyake, ili kutekeleza majukumu yake ambayo ndiyo sababu ya kuwepo kwake. (5) Kujikosoa na kukosoana ni silaha ya Mapinduzi 58. Kuna mambo mawili tuliyojifunza ambayo ni muhimu pia kuyazingatia. La kwanza linahusu suala la kukosoa, kujikosoa 74 MIONGOZO MIWILI

76 na kukosoana kama njia ya kukijenga na kukiimarisha Chama na wanachama. Ni kweli kuwa katika TUJISAHIHISHE Mwalimu anasisitiza jambo hili na kwamba Katiba ya CCM inatamka waziwazi juu ya umuhimu wake. Lakini ni kweli pia kuwa hatujaijenga tabia hii ipasavyo. Mara nyingi tumependelea kuteteana, kufichiana makosa na hata kutafuta visingizio visivyo na msingi. Neno kuleana, kwetu sisi (ingawa kuna malezi mema na mabaya) limechukua nafasi ya kukosoana. Wanachama wenye upungufu husaidiwa kama wanakosolewa ili wajirekebishe. Lakini hatua za nidhamu wakati mwingine zimechukuliwa bila ya mhusika kuelezwa wazi wazi upungufu wake ili ajirekebishe na pia wananchi wameachiwa wabuni wenyewe sababu. 59. Suala la kukosoa, kujikosoa na kukosoana lina sura kadhaa. Kwanza linataka wanachama na viongozi kuwa tayari kusema kweli katika vitendo vyao na kukubali kuambizana ukweli. Pili, linataka wanachama na hasa viongozi wawe tayari kukosolewa bila kuhamaki na inapobidi kukubali kujirekebisha. Tatu ni kuwa Chama chenyewe katika vikao vyake vya ngazi mbalimbali kuwa na utaratibu wa kujikosoa. 60. Sura hii ya tatu ni muhimu sana kwa mafanikio ya utekelezaji wa siasa ya Chama. Kuongoza ni kutoa maamuzi yanayohusu utekelezaji wa siasa. Kujikosoa kama Chama ni kuwa na utaratibu wa kuyarudia maamuzi ya nyuma, kuona jinsi yalivyotekelezwa na kupima matokeo ya utekelezaji huo kwa kuzingatia nia ya Chama katika kutoa uamuzi huo. Kama makosa yamefanyika katika utekelezaji basi ni muhimu kutafuta sababu za makosa hayo na kuchukua hatua za haraka za kuyarekebisha. Makosa pia yanaweza kutokana na uamuzi wenyewe kutokuwa sahihi. Katika hali hiyo, itabidi uchambuzi ufanywe ili kubainisha kiini cha upungufu wa uamuzi huo na kuchukua hatua za kurekebisha mambo. Kama kuna mafanikio basi ni nafasi kwa Chama kuzingatia mbinu zilizotumika kwa manufaa ya utekelezaji wa baadaye. Hivyo utaratibu wa kujikosoa kwa Chama ukitekelezwa kwa dhati ni shule kubwa ya ujenzi wa Ujamaa. MIONGOZO MIWILI 75

77 61. Ni dhahiri kuwa mapinduzi yetu yangekuwa yamepiga hatua kubwa zaidi kuliko ilivyo sasa kama tungezingatia utaratibu huu wa harakati za kujenga Ujamaa. Mfano mmoja unatosha kuelezea ukweli wa mambo. Msimamo wa Chama juu ya UJAMAA VIJIJINI uliopitishwa na Mkutano Mkuu wa Chama, Mwanza, mwezi Oktoba, Tangu wakati huo wananchi wameitikia mwito huo kwa njia na mafanikio mbalimbali. Lakini hadi sasa, miaka kumi na minne baadaye, hakuna kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kilichokaa na kupima maendeleo ya Ujamaa vijijini, kubainisha kilichofanya kuwa mpaka sasa sekta ya ujamaa vijijini ikawa bado finyu na kutafuta malengo na mbinu mpya za kuleta msukumo wa ujenzi wa ujamaa vijijni. Ni dhahiri kuwa Chama kingalifanya hivyo kila mwaka na baada ya kila miaka mitano, kiwango cha ujamaa vijijini na nchini kingelikuwa cha juu kuliko kilivyo sasa na kwamba Chama kingalikuwa na hazina kubwa zaidi ya mbinu za kuongoza harakati za ujamaa. Na kwa kuwa ujamaa vijijini kwanza kabisa ni utengenezaji mali, basi maendeleo ya vijijini hii leo yangekuwa yamepiga hatua kubwa na kwamba huenda matatizo ya sasa ya upungufu wa ziada ya mazao nchini yangelikuwa yamepatiwa ufumbuzi wake. 62. Msimamo wa kujikosoa ni msimamo wa kimapinduzi. Unazingatia upungufu wa binadamu na papo hapo kutambua uwezo wa binadamu wa kufanya vizuri na zaidi mradi tu anajipa nafasi ya kujifunza, kujirekebisha na kujaribu tena na tena. Kwa Chama cha kijamaa kama Chama cha Mapinduzi hakuna kinachoweza kuchukua nafasi ya kujikosoa. (6) Umuhimu wa kuzungumzia jinsi ya kutekeleza 63. Jambo la pili tulilojifunza katika kujikosoa na ambalo linahitaji kuzingatiwa linahusu methodolojia ya kuunganisha uamuzi wetu na utekelezaji. Tumekuwa na tabia ya kuzungumzia suala na kufanya uamuzi. Baada ya hapo tunaachia utekelezaji ufanyike kwa kutegemea hisia, uwezo na msimamo wa wanaohusika. Kwa kawaida, suala la kuzungumzia namna ya kutekeleza, kuzungumzia mipango 76 MIONGOZO MIWILI

78 na mbinu za utekelezaji, hatukuwa na tabia ya kulishughulikia hasa kitaifa. Huu ni upungufu katika Chama maana namna ya kutekeleza uamuzi, mipango na mbinu za utekelezaji ni sehemu muhimu ya harakati za kutafsiri fikra (uamuzi) katika vitendo na ndiyo njia iliyo wazi ya kuhakikisha mafanikio ya utekelezaji. 64. Tabia ya kutozungumzia namna ya kutekeleza mipango na mbinu za utekelezaji husababisha matatizo katika Chama. Tatizo lililo dhahiri ni kuwa viongozi mmoja mmoja au vikao vya mikoa, wilaya na vijiji vinaachiwa vibuni njia za utekelezaji kwa kutegemea aonavyo kiongozi mhusika au kikao kihusika. Pale ambapo kiongozi mhusika ana msimamo thabiti wa chama au wajumbe wa kikao ni watu makini na wenye uwezo na busara, utekelezaji unaweza kufanyika vizuri. Lakini kuna pia sehemu nyingine katika nchi yetu na kwa vipindi mbalimbali ambako viongozi wamelazimisha utekelezaji kinyume cha matazamio ya Chama na wananchi na mara nyingine hata kusababisha usumbufu usio wa lazima kwa wananchi. Ufafanuzi wa namna ya kutenda na mbinu za utekelezaji unajenga nidhamu katika utekelezaji, unarahisisha usimamizi wa shughuli za Chama katika ngazi zote na unajenga na unawezesha kutumika kwa utaratibu wa kujikosoa na kukosoana. Zaidi ya hayo, unaimarisha umoja na nguvu za Chama kama chombo cha kutenda, yaani kuongoza mapinduzi ya kujenga Ujamaa Tanzania. 65. Mwongozo mpaka hapa umegusia historia ya mapambano ya taifa letu katika vipindi mbalimbali, umechambua mafanikio makubwa tuliyoyapata katika kutekeleza siasa ya Chama ya Ujamaa na Kujitegemea na kumalizia kwa kufanya uchambuzi wa kujikosoa katika Chama ili kwa kuzielewa nguvu na upungufu wa Chama chetu tuweze kujizatiti kwa kuikabili kazi kubwa iliyo mbele yetu. 66. Historia ya nchi yetu tangu kuzaliwa kwa TANU na ASP ni historia ya mapambano makali dhidi ya ukoloni na ubeberu na tumefanikiwa kupata ushindi mwaka hadi mwaka. Hali yetu ya uchumi na ya jamii ni ngumu kuliko ambavyo imewahi kuwa tangu tupate uhuru. Huko nyuma tulishinda katika mapambano yetu kutokana na umoja wetu MIONGOZO MIWILI 77

79 wa kitaifa, usahihi wa siasa yetu na uongozi bora wa Chama. Leo na katika siku za usoni tutahitaji umoja imara zaidi, siasa sahihi na uongozi bora wa chama. Lakini katika kipindi hiki ambapo ubepari na ubeberu wa dunia umejitokeza hadharani kwa kampeni na njama za kuhujumu ujamaa na kutaka kulibana Taifa, wakati ambapo vibepari na vibwanyenye vya humu nchini vimeonyesha dhahiri uhasama wao dhidi ya maslahi ya wakulima na wafanyakazi, umoja wa sasa lazima usimame juu ya misingi iliyo wazi na sahihi, misingi ya ujamaa; kwa hiyo ni umoja wa wakulima na wafanyakazi na wale wote wanaounga mkono kwa vitendao ujenzi wa ujamaa nchini. SEHEMU YA TATU KUJENGA MSINGI WA UCHUMI WA UJAMAA WA TAIFA LINALOJITEGEMEA 67. Lengo kuu la mapinduzi ya Tanzania ni kujenga nchi ya ujamaa ambamo unyonyaji wa mtu na mtu utakuwa umetokomezwa, ambamo uchumi wa taifa utakuwa unamilikiwa na kudhibitiwa na umma wa wakulima na wafanyakazi washirika na ambamo uhusiano wa watu katika jamii utakuwa ni wa udugu na kushirikiana kwa maendeleo ya wote na ambamo kazi imepewa hadhi ya kuwa wajibu wa kila mtu. 68. Uamuzi wa kujenga ujamaa Tanzania ni uamuzi wa kimsingi na kihistoria na haubadiliki. Chama kilijua tangu mwanzo kuwa kujenga ujamaa hakungekuwa mteremko bali ni mapambano magumu dhidi ya ubepari na unyonge wa humu humu ndani na dhidi ya njama za ubeberu wa dunia. Na isitoshe, Chama kilijua tangu mwanzo kuwa kujenga ujamaa ni pia mapambano dhidi yetu wenyewe katika ubinafsi na upungufu wetu wa aina mbalimbali. Harakati za miaka kumi na minne tangu Azimio la Arusha zimetuthibitishia ukweli huu. 69. Mapambano ya kutekeleza siasa ya Ujamaa ya Chama katika miaka kumi na minne tangu Azimio la Arusha yametuwezesha kufanya mabadiliko ya kimsingi katika uchumi wa nchi yetu. Kabla ya Azimio 78 MIONGOZO MIWILI

80 la Arusha uchumi wetu ulikuwa na mfumo wa kikoloni mamboleo kwani benki, bima, biashara ya nje yote yalikuwa matawi tu ya makampuni ya kibepari ya ulaya na marekani wakati mazao ya kilimo cha biashara yaliwekewa lengo la kutumikia viwanda vya kibepari vya nchi za ng ambo. 70. Kutaifishwa kwa benki, bima na kampuni za biashara za nje za kibepari na kuanzishwa kwa mashirika ya biashara ya ndani na ya nje katika kutekeleza Azimio la Arusha kumeleta marekebisho ya kimapinduzi ya mfumo wa uchumi. Hatua thabiti zimechukuliwa pia za kuanzisha na kupanua viwanda vinavyotumia bidhaa asili za kilimo chetu kama ngozi, pamba, katani, korosho, tumbaku, pareto, miwa na kadhalika. Kwa upande wa kilimo hatua za mwanzo zimechukuliwa kukielekeza kwenye mfumo wa kijamaa: sehemu kubwa ya mashamba ya kibepari, hasa ya mkonge ilitaifishwa, mashamba makubwa kadhaa ya Taifa ya kilimo na ya ufugaji yameanzishwa wakati sekta ya ujamaa katika baadhi ya vijiji imeanza kushamiri. Tanzania Visiwani, Serikali ya Mapinduzi ilitaifisha ardhi, benki, nyumba na kuanzisha mashirika ya biashara ya nje na ya ndani na kuanzisha viwanda vinavyotumia miwa na mbata. Hatua zote hizi zilizochukuliwa zimetujengea msingi wa uchumi wenye mwelekeo wa nchi ya ujamaa. Mafanikio haya yamewezekana kutokana na kazi, ujasiri na kujitolea mhanga kwa wakulima na wafanyakazi chini ya uongozi wa Chama. 71. Lakini, pamoja na mafanikio haya, nchi yetu hivi sasa imekumbwa na hali mbaya ya uchumi kama vile hali hiyo ilivyozikumba nchi zote duniani, zilizoendelea na zisizoendelea, nchi kubwa na ndogo, za kibepari na za kijamaa. Hali hii lazima tuikabili kwa kujipa kazi mbili ambazo zitakwenda sambamba. Kazi moja ni kutekeleza malengo ya muda mrefu ya kujenga msingi wa uchumi wa kijamaa wa Taifa linalojitegemea. Na kazi ya pili ni kuchukua hatua thabiti kuanzia sasa za kujihami kiuchumi ili kuhakikisha kuwa hali ya uchumi wetu haiendelei kudidimia na kuathiri hata msingi tuliokwisha ujenga. MIONGOZO MIWILI 79

81 72. Ni muhimu kutamka hapa kuwa siasa ya uchumi ya Chama cha Mapinduzi ina lengo la kutosheleza mahitaji ya wananchi ya chakula na kulipa Taifa uwezo wa kujitegemea katika mahitaji ya maendeleo ya sasa na ya baadaye. MWELEKEO WA MAENDELEO YA UCHUMI NA JAMII YA MUDA MREFU 73. Chama Cha Mapinduzi kiimekwishatoa mwelekeo wa maendeleo ya uchumi na jamii kwa miaka ishirini ijayo. MWONGOZO wa Chama unayazingatia na kuyafanya maelekezo hayo ndiyo msingi wa mwelekeo wake wa uchumi na wa jamii kwa kipindi hicho. 74. Kwa hiyo, Mwongozo wa Chama hautayakariri yaliyomo katika mwelekeo wa miaka ishirini isipokuwa kusisitiza juu ya masuala yanayohitaji mkazo maalum pia ni kutoa mwelekeo mpya pale ambapo pana umuhimu wa kutazamwa upya na hapakushughulikiwa na mwelekeo wa maendeleo ya miaka ishirini. 75. Mambo makubwa mawili yanastahili kutajwa katika kiwango hiki. La kwanza linahusu kilimo. Kwa kuwa kilimo ndio msingi wa maendeleo yetu ya sasa na ya miaka mingi ijayo, ni muhimu kwa Chama kulitilia mkazo suala hili kwa kufanya ufafanuzi wa nafasi ya kilimo katika maendeleo ya uchumi wa taifa na njia inayohitajika kuhudumia maendeleo hayo. Hivyo, suala la kilimo na hasa kilimo cha kijamaa linapewa nafasi kubwa katika mwongozo huu. 76. Jambo la pili linahusu mfumo wa upangaji wetu wa maendeleo. Kwa kuzingatia kwamba maendeleo ya kijamaa ni maendeleo yaliyopangwa, Chama katika kipindi kinachoanza sasa kitalitazama kwa undani zaidi suala la upangaji wetu wa mipango ya maendeleo kwa madhumuni ya kuimarisha na kukaza usimamizi wa utekelezaji. Chama kitaona kama Tume ya Mipango katika sura yake ya sasa kinatimiza makusudio ya Chama. Wakati huo huo Tume ya Bei itafanyiwa uchambuzi ili ipatiwe nafasi yake ya kuwa chombo cha upangaji wa uchumi badala ya kuwa chombo cha biashara kama 80 MIONGOZO MIWILI

82 ilivyo sasa. Sifa moja kubwa ya uchumi wa kijamaa ni kuwa ni uchumi wa mpango tofauti na uchumi wa kibepari ambao ni uchumi wa soko. Uchumi wetu kwa sasa ni mchanganyiko: kwa sehemu fulani unapangwa na kwa sehemu kubwa unategemea mvutano wa soko. Chama kitalitazama suala hili kwa undani zaidi ili kuelekeza zaidi uchumi wetu kwenye mfumo wa uchumi wa mpango kuliko ilivyo sasa. Nafasi ya Tume ya Mipango na Bunge katika kupanga na kusimamia utekelezaji wa mipango itatazamwa upya. Aidha, matumizi ya fedha za kigeni yataingizwa katika mfumo wa upangaji mipango. 77. Kwa kuwa uchumi wa kijamaa ni uchumi wa mipango, basi tutahitaji watu wenye taaluma ya kupanga katika taifa. Mikoa, Wilaya na Vijiji na kwa viwango mbalimbali vya utaalamu. Hivyo Serikali itawajibika kuwaandaa mapema iwezekanavyo wataalam wa mipango kwa wingi. Wakati huo huo ihakikishwe kuwa upangaji wa kinchi unapewa uzito sawa na upangaji wa kimradi ambao ndio unaoeleweka zaidi na wataalam wetu. A. MAPINDUZI KATIKA KILIMO NDIYO KAZI YA UMUHIMU WA KWANZA 78. Msingi wa uchumi wa nchi yetu ni kilimo. Asilimia themanini na tano ya Watanzania wanaishi kwa kilimo; biashara yetu na nchi za kigeni inategemea zaidi mazao tunayoyatoa katika kilimo; viwanda vichache tulivyonavyo nchini vinategemea mazao ya kilimo; uwezekano wa kutoa ziada itakayowezesha nchi kugharimia mapinduzi ya viwanda (kugharimia viwanda vya madawa) upo katika sekta ya Kilimo. 79. Katika hali hii, uongozi na usimamizi thabiti na makini wa Chama cha Mapinduzi uelekezwe zaidi katika sekta hii ya uchumi wa Taifa. Kazi iliyo mbele yetu ni kuleta mapinduzi katika kilimo. Kwa kuwa asilimia themanini na tano ya Watanzania ni wakulima wa vijijini, basi mkazo wa mapinduzi katika kilimo lazima uwe kilimo cha vijijini wakati mashamba ya Taifa pia yanashughulikiwa. MIONGOZO MIWILI 81

83 80. Mapinduzi ya kilimo vijijini katika nchi yetu ni kilimo cha kijamaa na cha kisasa ambacho kina sifa zifuatazo: Kwanza ni kilimo cha mashamba makubwa ya kijamaa ya vijiji, pili ni kilimo kinachotumia pembejeo, zana za utaalamu na tatu ni kilimo kinachotekelezwa kwa utaratibu bora wa kazi unaoleta ufanisi. 81. Sifa moja ya kilimo cha kisasa duniani kote ni kuwa ni kilimo cha mashamba makubwa. Tofauti iliyopo ya mashamba hayo ni katika umilikaji. Katika nchi za kibepari mashamba hayo makubwa ni mali ya mabepari, wakati katika nchi za kijamaa mashamba hayo makubwa ni mali ya Taifa au ni mali ya ushirika wa wanavijiji. Hali hiyo imeanza kujitokeza pia katika kilimo cha kisasa nchini Tanzania. 82. Mantiki iliyokisukuma kilimo cha kibepari cha kisasa kiwe cha mashamba makubwa ni ile ile iliyokisukuma kilimo cha kijamaa cha kisasa kiwe cha mashamba makubwa. Kilimo cha kisasa ni kilimo cha zana, na ukishavuka kilimo cha plau za maksai na kuingia katika matrekta na mashine nyingine za kupandia na kuvunia, basi ni hasara kubwa kuzitumia zana hizo katika vishamba vidogo vidogo vya ekari kadhaa tu. Ufanisi wa hali ya juu unapatikana wakati zana hizo zinatumika katika maeneo makubwa. Wakati huo huo ni kuwa zana hizi za kisasa ni aghali na haiwezekani kwa kila mkulima mwenye ekari chache kupata uwezo wa kuzinunua hata katika nchi za kibepari. Hivyo, katika nchi za kibepari ni wakulima wakubwa tu ndio wenye uwezo wa kumiliki zana hizi na katika mashindano hayo, wakulima wadogo wamelazimika kutoa nafasi kwa wakulima wakubwa. Katika nchi za kijamaa uwezekano wa kumiliki zana hizi ni kwa kupitia Serikali (Mashamba ya Taifa) na ushirika wa wakulima vijijini. 83. Uwezekano wa kuanzishwa kwa mashamba makubwa ya ujamaa vijijini ni mkubwa katika Tanzania maana mafanikio yaliyopatikana mpaka sasa katika vijiji vilivyotekeleza ujamaa vijijini yameufungua macho umma wa Wakulima vijijini. Wakati huo huo maeneo ya kuanzisha na kupanua mashamba ya ujamaa hayana matatizo katika 82 MIONGOZO MIWILI

84 sehemu kubwa ya vijiji vyetu nchini mradi tu kuna nia, mipango na uongozi thabiti. 84. Wakulima vijijini wamepiga hatua za mwanzo katika kutekeleza maagizo ya Siasa ni Kilimo kwa upande wa masharti ya kilimo bora cha mazao ya chakula na mazao ya biashara. Pembejeo za viwanda na samadi zimeanza kutumika pia. Katika siku za usoni Chama kitawajibika kufanya mambo mawili kuendelea kuwaelimisha wakulima juu ya umuhimu wa kutimiza masharti ya kilimo bora na kuhakikisha kuwa serikali inakuwa na mipango thabiti ya upatikanaji wa pembejeo na kwa bei nafuu kwa wakulima. Matumizi ya samadi lazima yahimizwe kwa mkazo zaidi. 85. Suala la zana za kisasa ni gumu zaidi. Hivi sasa sehemu kubwa ya kilimo vijijini inalimwa kwa jembe la mkono. Kuna maeneo yenye mifugo mingi ambako kazi ya kilimo inaendeshwa pia na plau za kuvutwa na maksai. Yapo pia matrekta katika baadhi ya vijiji. Lengo la Chama katika miaka ijayo ni kumtoa mkulima kutoka kwenye hali yake ya sasa ya kutegemea jembe la mkono na kumfikisha kwenye kutumia zana za kisasa. Kazi hiyo, pamoja na ya kuhakikisha kuwa matumizi ya mikokoteni yanaenea vijijini kote lazima itekelezwe kwa nguvu zote. 86. Wakati huo huo Chama kihakikishe kuwa serikali inaagiza matrekta toka ng ambo kwa kuzingatia uwezo na uzito unaolingana na umuhimu wa kilimo kwa maendeleo ya Taifa letu. Kupanga ni kuchagua. Hivyo, kama kwa mfano, ni kuchagua kati ya magari madogo na matrekta, basi uzito uwe kwenye matrekta. Lakini, kwa kuzingatia hali halisi ya uchumi wetu (upungufu wa fedha za kigeni na kwamba hatuna viwanda vyetu vya chuma na vya matrekta), itachukua muda wa miaka mingi kabla ya kilimo cha trekta kuwa ndicho kilimo cha vijiji vyetu. Kwa sasa mbinu ya kutufikisha huko siyo kungoja matrekta bali ni kutumia majembe ya mkono na plau za maksai katika kilimo cha kijamaa na cha binafsi vijijini ili kuongeza ziada ya mazao kitaifa ambayo ndiyo ufunguo wa kulipatia Taifa uwezo wa matrekta zaidi na kukuza uwezo wetu wa kuanzisha viwanda mama na vinginevyo. MIONGOZO MIWILI 83

85 87. Sifa ya tatu ya mapinduzi ya kijamaa katika kilimo vijijini ni utaratibu wa kazi wenye ufanisi. Shughuli za kijamaa vijijini huko nyuma zimezoroteshwa pia kutokana na vijiji kutokuwa na utaratibu mzuri wa kazi. Mara nyingi kazi za ujamaa zimefanywa holela, bila kujali ufanisi wa kuridhisha. Chama kitawajibika kuhakikisha kuwa unabuniwa utaratibu wa kupanga na kugawa kazi kwa mfumo ambao utajenga nidhamu, kurahisisha utekelezaji wa majukumu, kubainisha mchango wa kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi kuendeleza hisia za ushirikiano na kuongeza ufanisi. 88. Lakini mapinduzi katika kilimo nchini lazima pia yaambatane na mapinduzi ya msimamo wa serikali na vyombo vyake kuhusu nafasi ya kilimo katika mapambano ya ujenzi wa taifa. Katika siku za usoni, Chama kitahakikisha kuwa serikali na vyombo vyake, kwa vitendo, vinautekeleza wajibu wake wa kuhudumia na kusukuma maendeleo ya kilimo, kilimo cha kijamaa kikipewa nafasi ya kwanza. 89. Mapinduzi katika msimamo ni pamoja na kuupiga vita umangi meza na mila na tabia zinazopingana na mahitaji ya kilimo cha kisasa na pia kubuni njia bora zaidi za kuandaa wataalamu watakaohitajika sana vijijini kama zile zilizotuwezesha kutekeleza Azimio la Musoma kuhusu Elimu ya msingi kwa wote. Kwa kuwa kilimo cha kijamaa ni kilimo cha mashamba makubwa, basi ihakikishwe kuwa mafunzo ya kilimo yanazingatia pia suala la menejimenti ya mashamba makubwa. B. HATUA NYINGINE ZA UMUHIMU WA KWANZA KATIKA UCHUMI 90. Pamoja na maelekezo ya maendeleo ya miaka ishirini yaliyokwishapitishwa na Chama, masuala yafuatayo yanahitaji kusisitizwa: (1) Kilimo cha umwagiliaji maji Kilimo hiki kimepewa umuhimu wake katika mwelekeo wa muda mrefu. Kwa kuelewa kuwa pamoja na miradi mikubwa ya kitaifa ya 84 MIONGOZO MIWILI

86 umwagiliaji, miradi midogo midogo ya vijijini ndiyo ambayo inaweza kutoa matunda ya haraka, hatua za dhati zichukuliwe za kuandaa wataalam wa fani hiyo kwa wingi nchini na ng ambo na pia kutafuta uwezekano wa kuanzisha kiwanda cha zana za umwagiliaji maji. Wakati huo huo Chama kijizatiti barabara ili kuimudu kazi ya kuwashirikisha wananchi, maana utekelezji wa miradi ya umwagiliaji vijijini utategemea zaidi jasho la wananchi wenyewe kuliko matumizi ya zana za kisasa. (2) Kilimo cha matunda na mboga Kilimo hiki hadi sasa hakijatiliwa mkazo nchini. Licha ya mahitaji ya chakula bora yanavyozidi kuongezeka, matunda na mboga yanaweza kuwa mazao muhimu ya biashara ya nje kwa nchi yetu. Nchi nyingi za Afrika ambazo hazina mazingira bora zaidi ya haya ya nchi yetu hujipatia fedha nyingi za kigeni kutokana na matunda na mboga. Chama kihakikishe kuwa m i r a d i ya Taifa na ya vijiji ya kilimo cha matunda na mboga inaanzishwa kwa madhumuni ya kuwapatia wananchi matunda na mboga za kutosha nchini kote na ziada ya kuuza ng ambo. Katika lengo maalum la kuwapatia wafanyakazi wa mijini matunda na mboga kwa wingi, vijiji vilivyo karibu na miji mikubwa visaidiwe kuanzisha miradi mikubwa ya vijiji ya mazao haya. (3) Uendelezaji wa mifugo na ufugaji Tanzania ina utajiri mkubwa wa mifugo hasa ng ombe, mbuzi na kondoo. Inakisiwa kuwa idadi ya ng ombe peke yake waliomo nchini ni zaidi ya milioni kumi. Lakini hali ya mifugo yenyewe ni duni maana wafugaji walio wengi bado wanathamini zaidi wingi wa mifugo badala ya ubora wa mifugo. Misingi ya ufugaji wa kisasa haijafikishwa ipasavyo kwa wananchi na aina bora za mifugo kwa ajili ya maziwa na nyama hazijaenezwa nchini. Katika hali hii kazi kubwa ya Chama katika fani ya mifugo itakuwa kuhakikisha kuwa Serikali inaandaa sera ya kuendeleza mifugo nchini na kuhakikisha kuwa wafugaji wanaelimishwa na wanatekeleza misingi ya ufugaji wa kisasa na kuchukua hatua za dhati za kueneza mbegu bora za ng ombe wa maziwa na wa nyama. MIONGOZO MIWILI 85

87 Chama kitaongoza jitihada za kuanzisha na kupanua ufugaji wa kijamaa vijijini kwa njia ya ranchi za ng ombe bora wa maziwa na ranchi za vijijini za kunenepesha mifugo. Katika hali hiyo, suala la mipango ya matumizi bora ya ardhi vijijini linakuwa la umuhimu wa kwanza. Jingine la kulikabili ni suala la uhaba wa nyama, maziwa na mayai na bei za juu mno za mazao hayo nchini. Ili kulipatia ufumbuzi tatizo hili, Chama kitawajibika kuhakikisha kuwa serikali inaingiza katika mipango yake miradi mikubwa ya ufugaji wa kuku, nguruwe na ng ombe karibu na miji mikubwa. Aidha, Chama na Serikali visaidie vijiji vinavyozunguka miji kuanzisha miradi ya ufugaji hasa wa kuku, nguruwe, sungura na ng ombe wa maziwa. Wakati huo huo, jitihada za kueneza mifugo katika maeneo yasiyo nayo ya kutosha itabidi isimamiwe na Taifa. Pamoja na kwamba wafugaji wengi wa Tanzania wana mifugo mingi, bado wengi wao hawaitumii wala kuiona mifugo kama chombo cha kuwaletea maendeleo na maisha bora zaidi. Hivyo, suala la kutumia mifugo ili kuinua hali halisi ya maisha ya wafugaji na ya vijiji vyao lazima liwe mkabala maalum wa Chama kuanzia sasa. (4) Viwanda Jambo la kusisitiza linahusu hali ya utengenezaji mali katika viwanda vilivyopo nchini hivi sasa ambapo vilivyo vingi havitengenezi mali kwa kadiri ya uwezo vilivyo nao. Chama itabidi kijihusishe na matatizo ya viwanda hivi na kuhakikisha kuwa vinapata misaada yote ili viweze kutengneza mali kwa kadiri ya uwezo wake. Licha ya matatizo ya vipuri na utaalam, viwanda hivi vinakabiliwa pia na matatizo ya kisiasa kama vile upungufu wa mwamko wa siasa na utovu wa nidhamu. Viwanda vingi tulivyonavyo nchini hutoa makapi ambayo yangeweza kutumika kwa utengenezaji wa bidhaa nyingine, lakini jitihada hiyo haijafanywa. Viwanda kama vya sukari, mafuta, mbolea, nyama na vya nguo ni miongoni mwa viwanda vya aina hiyo. Kuanzia sasa Serikali itawajibika kuandaa mipango ya kuyatumia makapi yatokanayo na viwanda vya aina hiyo ili kutengeneza bidhaa zinazoweza kutengenezwa. 86 MIONGOZO MIWILI

88 Chama pia kitatilia mkazo utekelezaji wa Agizo la Viwanda Vidogo Vidogo mijini na vijijini. Chama kitahakikisha kuwa kila Mkoa unaandaa mpango wa muda mrefu wa utekelezaji wa Agizo hili la viwanda vidogo. (5) Mwamko wa Siasa wa wafanyakazi Mwamko wa siasa una uwezo mkubwa wa kuongeza ufanisi wa kazi kwa kuwatia wafanyakazi ari na makini zaidi katika kazi. Hali ya sasa viwandani na ofisini inaonyesha upungufu wa mwamko wa siasa. Hisia za kimapinduzi za kuthamini kazi na wajibu, moyo wa uaminifu na wa kujitolea muhanga, tabia ya kuthamini mali ya umma, yote haya yamepoteza nguvu zake. Ni jukumu la Chama kutia pumzi mpya wakati wote katika viwanda, Serikalini na katika Mashirika ya Umma itakayoleta vuguvugu la kimapinduzi miongoni mwa wafanyakazi kwa kuuinua mwamko wao wa siasa, mwamko wa uvumbuzi, ili waongeze juhudi ya kazi wakitambua kuwa sehemu zao za kazi ndio uwanja wao wa mapambano ya kujenga ujamaa na hivyo washiriki kwa dhati katika harakati hizo. (6) Wizi wa mali ya umma, hujuma katika uchumi, magendo na ujambazi Kumekuwa na ongezeko kubwa la uhalifu wa aina mbalimbali nchini tangu tupate uhuru. Uhalifu wenye kutia wasiwasi maalum ni uhalifu katika uchumi. Wizi wa mali ya umma umeanza kuwa jambo la kawaida. Kumekuwa na matukio ya baadhi ya maafisa kuhusika na kuidhinisha mikataba na kampuni za nchi za nje bila kujali maslahi ya Taifa. Wakati huo huo vipusa, dhahabu na mali mbalimbali za taifa zinatoroshwa nje ya nchi kwa magendo na kusabisha hasara kubwa kwa Taifa. Ujambazi wa kutumia silaha nao umetumika ili kunyang anya mali na kutisha wananchi. Chama kitahakikisha kuwa serikali inachukua hatua kali za kupambana na vitendo hivi vinavyodhoofisha uchumi wa Taifa. Iko haja pia kwa sasa ya kubuni sheria maalum zitakazoelekezwa kwenye vita dhidi ya uhalifu katika uchumi unaozidi kuongezeka. MIONGOZO MIWILI 87

89 (7) Uharibifu wa vyombo vya kazi na wa mali ya umma Imezuka tabia ya aibu nchini ambayo imekuwa ikiongezeka ya vitendo vya kuharibu na kuvitumia vibaya vyombo muhimu vya kazi na mali ya umma kwa jumla. Magari, matrekta zana nyingine muhimu za Chama, Serikali na Mashirika ya Umma mara nyingi hayadumu muda mrefu kama ambavyo ingetazamiwa kutokana na matumizi mabaya. Nchi inapatishwa hasara kubwa ya fedha za kigeni itokanayo na ajali za malori, mabasi, magari madogo n.k. zinazosababishwa na uzembe na ulevi. Kuna tabia ya baadhi ya abiria kuharibu mabehewa ya treni ambayo kesho watahitaji kuyatumia mabehewa hayo hayo tena. Tunalo tatizo vile vile la tabia ya kuchafua na kuharibu nyumba za serikali na za mashirika za kuishi inayofanywa na baadhi ya wapangaji wenyewe. Wakati mwingine majengo ya ofisi za Chama, Serikali na Mashirika ya Umma hayahifadhiwi na kuhudumiwa ipasavyo. Tabia ambayo baadhi ya mifano yake imetolewa hapo juu ni ishara kuwa kuna mushkeli wa msimamo katika jamii. Chama kuanzia sasa kitalifanyia uchunguzi suala hili ili kukielewa chanzo chake na kulipatia ufumbuzi wa kudumu. C. MAENDELEO YA JAMII 91. Katika kipindi kinachoanzia sasa Chama kitatilia mkazo suala la ujenzi wa tabia na maadili ya kijamaa nchini. Pamoja na jitihada iliyofanywa ya kutoa elimu na kuunda vyombo vya umma, jamii yetu bado inazo mila, tabia na maadili yaliyo kinyume na maadili ambayo yanafanana na misingi ya siasa ya ujamaa tunayosukudia kuijenga. 92. Watu wameanza kuthamini zaidi vitu kuliko utu na tamaa ya kujipatia mali bila ya kuitokea jasho inaenea, matukio ya wizi wa mali ya umma yameongezeka. Lakini lililo baya zaidi ni kuwa mwizi wa aina hiyo anapogunduliwa, baadhi ya wananchi badala ya kumfichua au kulaani kitendo chake, humsifu na kumhusudu. Wakati mwingine mvivu na mtegaji kazini hutetewa hata na vyombo 88 MIONGOZO MIWILI

90 vya Chama vyenyewe. Wakati huo huo, bado kuna mabaki ya tabia ya kupuuza elimu ya shule kwa watoto na badala yake kuna wazazi wanaopendelea watoto wao wachunge mifugo au hata kuolewa badala ya kuendelea na shule. 93. Jitihada ya Chama za kujenga tabia na maadili ya kijamaa itaelekezwa kwenye taasisi muhimu za nchi kama shule na vyuo, majeshi na sehemu za kazi. Lakini Chama kitahakikisha pia kuwa maisha ya hadhara ya jamii yetu yanasaidia kujenga misingi ya tabia na maadili ya Taifa linalojenga ujamaa na la kimaendeleo kwa ujumla. Hivyo, Chama kitapiga vita tabia ya baadhi ya wananchi na hasa wakiwa viongozi inayokwaza na kupotosha umma. Jamii lazima iwe shule ya kwanza ya maadili ya kijamaa. (1) Maendeleo ya jamii (a) Uchumi wa fedha ni mpya katika nchi yetu na ndiyo maana tabia ya kutumia fedha kwa mipango haijaenea. Chama kitaendelea kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kutumia fedha kwa mipango, kuweka akiba benki na kupiga vita tabia ya ufujaji mali na matumizi ya fahari. (b) Uzururaji wa aina mbalimbali umeongezeka nchini. Kwa kuzingatia kushindwa kwa hatua za pupa zilizotumika katika siku za nyuma, Chama kitalitafakari kwa undani zaidi suala la mipango na mbinu za kupambana na uzururaji kwa kutia maanani kuwa ufumbuzi wa kudumu utategemea maendeleo ya ujenzi wa ujamaa vijijini pamoja na mipango thabiti ya kuwashirikisha wakazi wa mijini katika ushirika wa viwanda vidogo. Vijiji ambavyo vimepiga hatua za ujamaa vimekwishaanza kulitatua tatizo la uzururaji na vimeanza kuwa na mipango ya kuwatunza vikongwe na walemavu. (c) Utaratibu wa bima na pensheni hauwezi kuwa wa wafanyakazi pekee. Katika siku za usoni Chama kitahakikisha kuwa unaanzishwa utaratibu wa bima na pensheni kwa wakulima washirika kwa kutegemea maendeleo yao. MIONGOZO MIWILI 89

91 (d) Hali ya vijiji vingi ingali duni kwa ustawi wa jamii na utamaduni. Chama kitalishughulikia suala la kuleta mapinduzi ya mazingira vijijini katika fani hiyo. (e) Kuhusu walemavu, Chama kitahimiza serikali kuchukua hatua za kuimarisha na kuvipanua vifaa muhimu kwa walemavu kama baiskeli, viatu, magongo, na kadhalika. (2) Elimu Chama kuanzia sasa kitajihusisha zaidi na shughuli za elimu nchini hasa kwa upande wa maandalizi ya waalimu na maendeleo yao na ya shule na vyuo maana waalimu wana mchango mkubwa wa kutoa katika kumjenga Mtanzania mpya. Katika lengo hilo, Chama kitafanya tathmini ya mafanikio tuliyoyapata katika kuielewa na kuitekeleza falsafa ya Chama ya Elimu ya Kujitegemea. Aidha, Chama kitalitazama upya Agizo la Musoma katika vipengele vyake vyote. Kwa sasa imedhihirika kuwa utekelezaji wa Azimio hilo kuhusu utaratibu wa kuingia Chuo Kikuu unahitaji mabadiliko ya msingi. Pamoja na mafanikio tuliyoyapata katika Elimu ya Watu Wazima Chama kitaendelea kuhimiza wananchi na hasa wanaccm na viongozi kujiendeleza kwa elimu kwa kadiri ya uwezo wao na kujenga tabia ya kusoma kama sehemu ya maisha yao. (3) Afya Kazi moja muhimu ambayo ni ya Chama katika miaka ijayo ni kuhimiza kuenezwa kwa elimu ya kinga ya maradhi pamoja na kuongoza mapambano dhidi ya tabia na mila zisizo nadhifu. Hali ya afya ya wananchi wengi vijijini inaathiriwa na tabia na mila ambazo zinapingana na maendeleo ya jamii kama vile tabia ya kutotumia vitanda, tabia ya kuishi katika nyumba moja na mifugo, tabia ya kutotumia vyoo, tabia ya kunywa maji yasiyochemshwa, miiko mbalimbali, na kadhalika. Wakati huo huo Chama kitatilia mkazo suala la usafi wa mazingira mijini na vijijini pamoja na umuhimu wa kuwepo kwa vyoo vya umma mijini. 90 MIONGOZO MIWILI

92 (4) Ujenzi wa nyumba Mahitaji ya ujenzi wa nyumba za kuishi mijini na wa majengo ya ofisi na viwanda nchini yanazidi kuwa makubwa. Kazi moja ya Chama ni kuona kama kuna umuhimu wa kuingiza teknolojia mpya ya ujenzi nchini itakayosaidia kutoa msukumo wa shughuli za ujenzi wa nyumba za kuishi na za kazi. Kuna ukweli kuwa upungufu wa vifaa vya ujenzi umechelewesha maendeleo ya ujenzi nchini. Lakini huenda ikadhirika pia kuwa mashirika ya Msajili wa Majumba na Shirika la Nyumba yatahitaji pia teknolojia bora zaidi ili kuweza kutatua matatizo ya nyumba za wafanyakazi mijini. Sera ya nyumba itashughulikiwa pia katika kipindi kinachoanza sasa. (5) Nishati Suala la nishati ni la msingi kwa maendeleo ya Taifa letu. Pamoja na kuendelea kutafuta mafuta, Chama kitahakikisha kuwa serikali inazidisha mipango thabiti itakayoliwezesha Taifa kuanza kutumia nguvu za maji, makaa, upepo na jua. Pamoja na miradi mikubwa ya nguvu za maji kuna haja ya kutia maanani miradi midogo midogo ya nguvu za maji. Suala la kuni itabidi lipewe umuhimu mkubwa kwa kuwa na mipango kamambe ya kupanda miti vijijini na miradi ya Mikoa na Taifa. Chama kiihimize Serikali kuendelea na kutafuta mbinu za kutumia makaa ya mawe tuliyonayo kusukuma uchumi wetu. Umuhimu wa suala la nishati utahitaji sera maalum. (6) Msimamo juu ya kuendeleza sayansi na teknolojia Mpango wa miaka Ishirini unatoa mwelekeo wa maendeleo ya sayansi na teknolojia, kwani sayansi na teknolojia ni msingi muhimu kwa maendeleo ya kisasa. Chama kijihusishe zaidi na mipango ya kuwapata wanasayansi na wanateknolojia wenye uwezo wa viwango mbalimbali vya utaalamu na msimamo sahihi wa siasa. Wakati huo huo, Chama kishughulikie ustawi wa wataalamu na mabingwa tulionao hivi sasa nchini ili kuhakikisha kuwa wanaishi katika mazingira yanayowawezesha kutoa mchango wao kwa ukamilifu katika ujenzi wa Taifa letu. Kutokana na kukosa msimamo sahihi wa kuwashughulikia wataalamu wetu kumewafanya baadhi ya MIONGOZO MIWILI 91

93 wataalam kubabaika na Serikali kupoteza mabingwa katika fani za uganga, uhandisi, urubani wa ndege na kadhalika. Maendeleo ya uchumi wetu hasa kwa upande wa viwanda na nishati utahitaji mafundi wa viwango mbalimbali kwa wingi sana. Chama kihakikishe kuwa serikali inakuwa na mipango thabiti ya namna ya kuwapata mafundi hawa na kwamba inatumia nafasi zinazoweza kupatikana kuwaandaa hapa nchini na ng ambo. 94. Chama kitakuwa na utaratibu wa kuandaa mikutano na wataalamu wa fani mbalimbali ili kubadilishana mawazo juu ya mbinu za kusukuma mbele mapinduzi katika sayansi na teknolojia nchini. D. ULINZI NA USALAMA Msingi wa maendeleo ya Ulinzi na Usalama wa Tanzania ni Watanzania wenyewe, kila Mtanzania, na hasa kila mzalendo na kila mjamaa. (Mwongozo wa TANU, 1971) 95. Kazi kubwa ya Chama ni kuhakikisha kuwa uhuru wa taifa, mipaka ya nchi na matunda ya uhuru na ya ujamaa ya wakulima na wafanyakazi yanalindwa na kuhifadhiwa. Majeshi yetu yote kwa pamoja ndicho chombo kikuu cha kutekeleza siasa ya Chama ya ulinzi na usalama. Lakini chimbuko la majeshi ni Umma wa wakulima na wafanyakazi ambao pia wanashiriki katika ulinzi na usalama wa nchi yao kwa kupitia ulinzi wa mgambo na kwa kuwa macho katika sehemu zao za kazi na za kuishi viwandani na maofisini, vijijini na mijini. 96. Chama kitaendelea kuimarisha kazi ya kuyaelimisha majeshi na wananchi kwa jumla juu ya maumbile ya mapambano yetu na kufanya uchambuzi wa kutambulisha maadui wa taifa na wa siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ambao ni ubepari na ubeberu wa dunia na vibaraka wao wa humu nchini. 97. Kazi ya Chama ni kuhakikisha kuwa majeshi yetu yanakuwa tayari kwa mapigano wakati wote. Ili kufikia lengo hilo, Chama 92 MIONGOZO MIWILI

94 kitahakikisha kuwa wanajeshi wanakuwa na mwamko wa hali ya juu wa kizalendo na wa kijamaa na wanajengeka katika misingi ya nidhamu ya kujituma ya jeshi la kijamaa. Chama kitahakikisha pia kuwa maendeleo ya teknolojia na uimarishaji wa michepuo jeshini yanapewa umuhimu wa kwanza. Ni muhimu kwa Chama kuyasaidia majeshi yetu katika jitihada zao za kupambana na tabia iliyoanza kujitokeza hapa na pale majeshini ya kutothamini mali ya jeshi, ubadhirifu na tabia ya kutojali kwa jumla. Vitendo hivi ni kinyume cha mila za kijeshi na maadili ya jeshi lolote na hasa jeshi la kijamaa amayo majeshi yetu, chini ya uongozi wa Chama, yatatilia mkazo wakati wote. 98. Ushindi wetu wa vita dhidi ya majeshi ya uvamizi ya fashist Idd Amin umetudhihirishia usahihi wa siasa ya Chama ya Ulinzi na Usalama, kutuonyesha ushujaa na uzalendo wa wanajeshi wetu na uwezo mkubwa walionao makamanda wetu wa kuongoza mapigano. Kazi ya Chama sasa ni kufanya majumuisho ya ujuzi mkubwa tulioupata kwa manufaa ya harakati za ulinzi na usalama wa Taifa kwa siku za usoni. Miongoni mwa mambo yanayohitaji uchambuzi na ufafanuzi wa Chama ni uhusiano wa majeshi, nafasi ya ulinzi wa mgambo katika mfumo wa ulinzi na usalama wa Taifa wakati wa amani na vita, muundo wa ulinzi na usalama kwa uongozi na utendaji yaani uhusiano wa wizara na majeshi, nafasi ya wanawake katika majeshi yetu na kazi za Chama katika majeshi. 99. Chama kitahakikisha kuwa jeshi la Polisi linapata misaada yote toka Serikalini ili kuliimarisha. Jeshi la Polisi linahitaji kupewa uwezo zaidi wa mafunzo ya hali ya juu ya mbinu za kupambana na majambazi na wahalifu wenye ujuzi mkubwa pamoja na kupewa uwezo wa zana muhimu za kazi Chama pia kina kazi ya kuchambua tena na kwa makini nafasi ya Jeshi la Kujenga Taifa katika kusukuma mapinduzi ya ulinzi na ya uchumi wa Taifa. Pamoja na kwamba madhumuni ya awali ya J.K.T. bado hayajakiukwa na wakati, Chama kitazame namna ya kulipa J.K.T. na J.K.U. uwezo wa kuwa chombo cha kukabili kazi za ujenzi MIONGOZO MIWILI 93

95 wa barabara, majengo, mabwawa n.k. kwa hali ya juu zaidi, kuukuza uwezo wao wa kutoa chakula na mifugo kwa ajili ya Taifa na pia kuwezesha J.K.T. na J.K.U. kuwa mahali pa kutoa mafunzo ya muda mfupi ya wataalamu wengi wa kada ya chini ya ufugaji, kilimo na ufundi toka Vijijini Jambo moja tulilojifunza kutokana na vita dhidi ya uvamizi ni umuhimu wa viwanda vinavyohudumia majeshi. Chama kitahimiza Serikali kulipa uzito maalum suala la kukuza na kupanua viwanda vya majeshi kwa madhumuni ya kuyapatia majeshi na ulinzi wa mgambo vifaa muhimu wanavyohitaji. E. MSUKUMO WA UJENZI WA UJAMAA 102. Imedhihirika katika kipindi cha miaka kumi na minne tangu Azimio la Arusha kuwa serikali na vyombo vyake na hata baadhi ya viongozi wamehusika katika kuupa nguvu na kuukuza ubepari nchini. Katika kipindi kinachoanzia sasa, Chama kitakuwa macho na kitahakikisha kuwa uwezo wa Serikali na vyombo vyake, uwezo wa Chama, unatumika kuimarisha na kuendeleza Ujamaa Katika lengo hili, dhamira ya Chama ya kujenga ujamaa ijidhihirishe kwa kuhakikisha kuwa: (a) Benki zinaelekeza nguvu za fedha za Taifa kwenye kujenga ujamaa kwa kuvipa umuhimu wa kwanza vijiji, vyama halisi vya ushirika na mashirika ya umma. (b) Kampuni za umma za ujenzi zilizopo zinapewa uwezo wa kumudu kazi zaidi na kwamba kampuni mpya za umma za ujenzi zinaundwa ili kuikabili kazi ya ujenzi nchini inayoongezeka mwaka hadi mwaka. Ihakikishwe pia kuwa Serikali na mashirika ya umma hayawapi kazi za ujenzi makontrakta wa kibepari isipokuwa wakati hakuna uwezekano mwingine. Fedha za Serikali na mashirika ya umma zimesaidia sana kuupa nguvu ubepari katika sekta hii. (c) Utaratibu wa sasa wa serikali na vyombo vyake kutumia 94 MIONGOZO MIWILI

96 mawakala wa biashara za nje na biashara za ndani ya nchi ukomeshwe. Utaratibu huu pia umesaidia kujenga ubepari nchini. (d) Kamati za kugawa matrekta na magari nchini zinatoa umuhimu wa kwanza kwa mashirika na makampuni ya umma, vijiji na vikundi vya ushirika halisi. (e) Mipango thabiti inafanywa na serikali ya kuhakikisha kuwa mtindo wa sasa wa watu binafsi kupewa zabuni za kulisha makundi ya umma kama majeshi, shule na vyuo unakomeshwa hatua kwa hatua. Kwa hatua ya kwanza, vyakula vinavyoshughulikiwa na mashirika ya umma kama sembe, mchele, maharage na sukari vipatikane moja kwa moja toka huko. (f) Usafirishaji unaofanywa na vyombo vya umma uimarishwe na kupanuliwa na kwamba ugawaji wa malori na mabasi ufanywe kwa lengo la kukuza ujamaa katika sekta hii. (g) Kila Mkoa unaandaa mpango wa muda mrefu unaoonyesha malengo ya ukuaji wa sekta ya ujamaa katika kilimo, ufugaji, viwanda na viwanda vidogo, biashara na usafirishaji. Mpango huo uhakikishe kuwa kila kijiji kinakuwa na malengo yanayoonyesha ukuaji wa shughuli za kijamaa, mkazo ukiwa katika kukuza uzalishaji mali. Kutokana na mipango yake, Serikali iandae mpango unaoonyesha mwelekeo wa ukuaji wa sekta ya ujamaa nchini. (h) Utekelezaji wa Siasa ya ujamaa unatilia mkazo suala la Kujitegemea maana Ujamaa unaojengwa kwa misingi ya kutegemea ni ujamaa batili. Chama kitaichambua falsafa inayoongoza upangaji wetu wa mipango ili kuhakikisha kuwa mipango ijayo ya maendeleo inaonyesha waziwazi mwelekeo wa kujitegemea katika mpango. Serikali ihakikishe pia kuwa uwezo wetu wa kujitegemea katika vipuri mbalimbali unakuzwa kwa kutumia uwezo uliopo nchini. MIONGOZO MIWILI 95

97 SEHEMU YA NNE CHAMA NA MAPINDUZI YETU Chama tunachokiunda tunataka kiwe chombo madhubuti katika muundo wake na hasa katika fikra zake na vitendo vyake vya kimapinduzi vya kufutilia mbali aina zote za unyonyaji nchini, na kupambana na jaribio lolote lile la mtu kumwonea mtu, au shirika au chombo cha nchi kuonea au kudhalilisha wananchi, kudhoofisha uchumi au kuzorotesha maendeleo ya Taifa. (Katiba ya CCM) 104. Chama chetu, Chama cha Mapinduzi, ni Chama chenye historia ya kipekee katika Afrika. Historia yake ni ya mafanikio na ushindi katika fani mbalimbali za utekelezaji wa malengo ya siasa yake. Wanazuoni watakapokuja andika historia ya Chama chetu wataweza kuyachambua kwa kina na mapana mafanikio hayo yasiyo na kifani Chama cha Mapinduzi ni Chama cha kijamaa. Kazi kubwa ya CCM ya sasa ni kuziunganisha nguvu zote za kijamaa na za kimaendeleo nchini na kuziongoza katika mapambano ya kujenga ujamaa Tanzania na kujenga ushirikiano wa kimapinduzi wa wajamaa na wapenda maendeleo wote katika Afrika na Dunia katika mapambano dhidi ya ukoloni, ukoloni mambo leo, ubepari na ubeberu Chama cha Mapinduzi ni chombo kikuu na cha pekee cha uongozi wa taifa letu. Kuongoza ni kuonyesha njia. Kwa hiyo, Chama chetu ni mwanga unaotumulikia njia katika hali ngumu ya mapambano ya wakulima na wafanyakazi kuelekea kwenye ujamaa. Uhalali wa uongozi wa Chama chetu una misingi ya kihistoria ingawa historia peke yake haitoshi kuelezea uhalali wa Chama cha Mapinduzi kwa sasa kuongoza Taifa. TANU na ASP vilijijengea uhalali machoni mwa wananchi kwa kuwadhihirishia kuwa vinastahili kuongoza kutokana na usahihi wa siasa na mbinu zao katika mapambano 96 MIONGOZO MIWILI

98 dhidi ya ukoloni, kwa vitendo vya kujitoa mhanga vya wanachama na viongozi wa vyama hivyo na kwa kudhihirisha kwa vitendo kuwa ndio watetezi halisi wa maslahi ya wananchi. Hatua za kimapinduzi zilizochukuliwa Zanzibar baada ya Mapinduzi Januari 12, 1964, na hatua za kimapinduzi zilizofuatia kutangazwa kwa Azimio la Arusha Februari 5, 1967 zilijenga uhalali mpya wa ASP na TANU katika misingi ya Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea Pamoja na uhalali wa kihistoria, ambao ni uhalali wa kurithi, Chama cha Mapinduzi chenyewe lazima kijijengee uhalali wake katika hali ya mapambano ya sasa kwa kudhihirisha kwa vitendo kuwa ndicho mtetezi wa kuaminika wa maslahi ya wakulima na wafanyakazi nchini. Kwa kuwa kukubalika na kuaminika kwa ASP na TANU kulijengwa kwa vitendo vya kimapinduzi vya uamininifu na ukweli kwa umma na kwa kujitolea mhanga kwa wanachama na viongozi wa TANU na ASP wakati huo, vivyo hivyo, uhalali wa uongozi wa CCM na kukubalika na kuaminiwa kwake na umma kutategemea vitendo vya kimapinduzi vya uaminifu na ukweli kwa umma vya wanachama na hasa viongozi wa CCM katika harakati za kila siku za kujenga ujamaa viwandani, ofisini, vijijini na mijini. Hii ndiyo njia ya pekee ya kukifanya Chama kiwe ndani ya umma na kiwe mwakilishi wa kweli na halali wa matumaini yao ya haki. A. CHAMA NA SERIKALI 108. Serikali ndicho chombo kikuu cha utekelezaji wa siasa ya Chama. Chama kinaiongoza Serikali na vyombo vyake kwanza kabisa kwa kutoa shabaha na malengo, siasa (sera), maelekezo na maagizo ya mara kwa mara ambayo Serikali huyatafsiri katika mipango ya utekelezaji na sheria. Hii ina maana kuwa Chama ndicho kinachowajibika kuzungumzia na kuamua juu ya masuala mazito na makubwa ya nchi kabla hayajaelekezwa Serikalini kwa uchambuzi na utekelezaji Serikali kwa maumbile yake ni chombo cha madaraka ya mabavu. Serikali ni sheria, ni majeshi, ni mahakama na ni jela. Kwa hiyo, MIONGOZO MIWILI 97

99 hata katika hali yetu ya demokrasia na ujamaa, wakati wote ni muhimu kwa Chama na umma kuwa na hakika na anayekabidhiwa madaraka haya ya Serikali maana yakiangukia mikononi mwa mpinga mapinduzi madaraka hayo yanaweza kutumiwa dhidi ya maslahi ya umma wenyewe. Hivyo, Chama kuongoza maana yake ni kuhakikisha pia kuwa madaraka muhimu ya Serikali na ya mashirika ya umma wanakabidhiwa watu ambao pamoja na uwezo wao wa kitaalamu ni wenye msimamo wa kizalendo na waaminifu kwa Chama na kwa wakulima na wafanyakazi wa Tanzania Kuhusu suala hili, Chama cha Mapinduzi kina kazi mbele yake ya kujumlisha tuliyojifunza tangu tupate uhuru na hasa baada ya Azimio la Arusha juu ya hatari zinazoweza kutokea kwa siasa ya Chama na kwa taifa wakati madaraka muhimu ya Chama, Serikali au Mashirika ya Umma wanakabidhiwa watu ambao kisiasa ni chui katika ngozi ya kondoo Serikali na Mashirika ya Umma vile vile ni vyombo vya kutoa huduma kwa wananchi. Katika nafasi yake ya uongozi, Chama kina wajibu wa kuhakikisha kuwa utoaji wa huduma kwa umma hausababishi manung uniko. Kuongoza katika hali hii maana yake ni kuwaelimisha na kuwasaidia watendaji katika siasa ili kuinua na kuimarisha ari na uwezo wao wa kutoa huduma. Wakati huo huo kuongoza ni kuwaelimisha na kuwaelekeza wananchi juu ya maamuzi halali ya serikali na umuhimu wa kuyatekeleza kwa maendeleo yao na ya taifa na pia wakati wote kuhakikisha kuwa wananchi hawafichwi au kudanganywa juu ya hali halisi na matatizo ya kweli ya nchi yao Aidha katika nafasi yake ya kiongozi wa serikali na vyombo vyake, Chama kina wajibu wa kuhakikisha kuwa muundo, taratibu na utendaji kazi wa serikali na wa mashirika ni wenye kutekeleza siasa ya Chama kama ilivyokusudiwa na kuleta ufanisi. Hapa ni muhimu kusisitiza kuwa Chama kiongoze mapambano dhidi ya umangi meza na tabia zozote zionazozorotesha kazi na utoaji wa 98 MIONGOZO MIWILI

100 huduma bora kwa umma. Chama kione pia kuwa mifumo iliyopo Serikalini na katika Mashirika ya Umma inamwezesha mfanyakazi kushiriki katika uongozi wa kazi mahali alipo na kwamba kwa kushirikiana na wenzake anapata nafasi anayostahili ya kulijenga na kulitumikia Taifa lake. Chama na mfumo wa siasa na jamii 113. Chama cha Mapinduzi ni muungano wa Wakulima na Wafanyakazi wa mstari wa mbele kaika mapambano ya kujenga Ujamaa Tanzania. Mfumo wetu wa kisiasa na kijamii unajengwa kwa mujibu wa msingi na mahitaji ya nchi inayojenga ujamaa. Lengo ni kujenga mfumo wa demokrasia ya kijamaa ambamo wakulima, wafanyakazi, washirika na watu wote wanaoishi kwa jasho lao sio tu kuwa watashirikiana na kuwa na kauli ya mwisho katika mambo ya siasa na ya jamii ya nchi yao bali wakati huo huo watamiliki na kudhibiti uchumi wa Taifa kwa kupitia Serikali, Mashirika ya umma, Vijiji vya ujamaa na vyama vya ushirika. Demokrasi ya Chama kimoja ya sasa ni hatua inayotuelekeza kwenye lengo hilo Hivyo ni muhimu kwa Chama katika kipindi kinachoanza sasa kuonyesha njia itakayolielekeza Taifa kwenye kiwango cha juu zaidi cha demokrasi ya wakulima na wafanyakazi washiriki kila hali inapohitaji ifanyike hivyo. Katika maana hiyo, ni muhimu kwa Chama kuutazama tena mfumo wa demokrasi yetu ya Chama kimoja kwa lengo la kuuimarisha Kwanza kuna suala la mgawanyo wa madaraka ya nchi kati ya Chama, Rais wa Jamhuri ya Muungano na Bunge na kati ya Chama, Rais wa Zanzibar na Baraza la Wawakilishi. Sasa ni miaka ishirini tangu Tanzania bara ipate uhuru na miaka 18 tangu Mapinduzi ya Zanzibar. Huu ni wakati unaofaa kutazama upya mfumo wa madaraka wa nchi yetu ili kuchukua hatua za kuimarisha uongozi wa pamoja kwa kutoa madaraka zaidi kwa Bunge ambalo pamoja na Rais ndio wawakilishi wa taifa. Kulipa Bunge madaraka zaidi ya kusimamia utekelezaji wa Serikali ni kuimarisha madaraka ya Umma. MIONGOZO MIWILI 99

101 116. Jambo la pili ni kuwa Bunge lenyewe linahitaji kufanyiwa uchambuzi kwa madhumuni ya kuimarisha uwakilishaji wa maslahi ya wakulima na wafanyakazi. Chama kitatumia kipindi kinachoanza sasa kutafakari juu ya njia bora zaidi zitakazohakikisha kuwa wakulima, wafanyakazi, washirika, vijana na wanawake wote wanawakilishwa kulingana na nia ya Chama ya kuendeleza mapinduzi yetu ambayo yanahitaji Bunge linalowakilisha maslahi halisi ya Wakulima na Wafanyakazi na kwa kutia maanani nafasi ya wanawake na vijana katika Taifa letu Jambo la tatu linahusu wabunge wa kuchaguliwa na wa kuteuliwa. Bunge letu katika sura yake ya sasa lina asilimia kubwa ya wateuliwa. Chama kitalitafakari suala hili ili kuona kuwa ubunge wa kuchaguliwa unapata nafasi kubwa zaidi kuliko ilivyo sasa ikieleweka kuwa uchaguzi wa wawakilishi ni sehemu muhimu ya demokrasi ya kijamaa Wakati huo huo, Chama kitafanya uchambuzi ili kupata njia za kuimarisha madaraka ya umma tangu vijijini hadi Taifa kwa jumla. Chama kitayarudia maamuzi yake ya nyuma kuhusu suala hili tangu tupate uhuru hadi sasa ili kujipa msingi wa kubuni utaratibu wa kujenga madaraka ya umma yatakayotuelekeza kwenye demokrasia ya kijamaa, katika jitihada hii, Chama kitaepuka jaribio la kurudisha mifumo ya tawala za kizamani, badala yake Chama kitajifunza toka mifumo ya zamani na hata ya nchi nyingine ili kubuni mfumo mpya utakaolingana na mahitaji ya maendeleo ya kidemokrasi na ya ujamaa ya Tanzania ya leo na ya kesho. Hivyo, Chama kitayashughulikia masuala ya madaraka ya miji, wilaya na vijiji pamoja na suala la vyama vya ushirika katika msimamo huo Kwa hiyo, Chama pia kina wajibu wa kuhakikisha kuwa wananchi katika fani zote za maisha wanashiriki kwa ukamilifu katika ujenzi wa taifa lao. Katika nchi yetu wakulima na wafanyakazi ndio msingi wa mfumo wa jamii yetu na siasa ya ujamaa ya Chama ni siasa ya tabaka hili. Hivyo harakati za kujenga ujamaa ni harakati 100 MIONGOZO MIWILI

102 za kuwaendeleza wakulima na wafanyakazi. Pamoja na hayo, Chama kinatambua nafasi maalum ya wanawake na vijana katika mapambano yetu. Lengo hili linaweza kufikiwa kwa kupitia Jumuia ya wafanyakazi, Jumuia ya vijana, Jumuia ya wanawake na Jumuia ya Washirika. Suala la Jumuiya ni suala ambalo Chama kinahitaji kulifanyia uchambuzi zaidi ili kufafanua waziwazi uhusiano wake na Chama na nafasi yao halisi katika harakati za ujenzi wa Taifa Pamoja na suala la Jumuia za Wananchi kuna umuhimu kwa Chama kuunda mazingira nchini yatakayowawezesha wakulima na wafanyakazi kushiriki kwa ukamilifu zaidi katika mapambano ya kisiasa na ya kiitikadi. Miaka iliyofuata Azimio la Arusha na baadaye mwongozo wa TANU ilikuwa kipindi cha vuguvugu la kimapinduzi lililowawezesha vijana, wakulima na wafanyakazi nchini kushiriki katika kuijadili siasa ya Chama na kujiendeleza kinadharia na kiitikadi. Utekelezaji wa Mwongozo wa Chama cha mapinduzi unahitaji vuguvugu la namna yake. Hakuna msukumo wa kweli wa ujenzi wa ujamaa unaowezekana bila ya msukumo unaolingana na mijadala juu ya nadharia na itikadi ya ujamaa. Chama kitaunda mazingira nchini yatakayouwezesha umma kushiriki kwa nadharia na kwa vitendo katika utekelezaji wa maelekezo ya mwongozo wa Chama Tabia moja ya mapinduzi iliyoanza kujengeka wakati wa vuguvugu la Azimio la Arusha na Mwongozo wa TANU na imefifia sasa ni ile ya wafanyakazi na vijana wa vyuoni na shule za Sekondari kujenga uhusiano wa kidugu na ushirikiano na vijiji vilivyo karibu nao. Maelfu ya wafanyakazi na vijana walifanya kazi za kujitolea wakati wa mwisho wa juma kudhihirisha mshikamano wa wakulima na wafanyakazi, na vijana katika kujenga ujamaa Utaratibu wa kazi za kujitolea kwa wanachama wa Chama Cha Kijamaa, kwa wafanyakazi na vijana wana mapinduzi, ni jambo muhimu kwa maendeleo yao ya kisiasa na kiitikadi na kwa maendeleo ya Ujamaa. Katika jitihada zake za kushirikisha umma katika ujenzi wa Taifa, Chama cha mapinduzi kitawajibika kufufua MIONGOZO MIWILI 101

103 na kuendeleza tabia itakayowawezesha wana CCM, wafanyakazi na vijana kujitokeza kwa wingi katika kazi za kujitolea na kujenga ushirikiano kwa vitendo kwa vijana, wanajeshi, wakulima na wafanyakazi vijijini. Chama na siasa ya nchi za nje 123. Siasa ya nchi za nje ya Chama cha Mapinduzi inaongozwa na misingi ya Uhuru wa Taifa wa kujiamulia mambo yake bila kuingiliwa na yeyote; kushirikiana na vyama na nchi za kimaendeleo na za kijamaa katika kuimarisha mapambano dhidi ya nguvu za ukoloni, ukoloni mamboleo, ubepari, ubeberu na ubaguzi wa rangi katika Afrika na kote duniani; kuunga mkono ukombozi wa Afrika na Umoja wa Afrika; na kushirikiana na mataifa mengine katika umoja wa nchi huru za Afrika, katika nchi zisizofungamana na upande wowote na katika Umoja wa Mataifa katika jitihada za kulinda na kudumisha amani na usalama duniani Kwa kuwa chimbuko la siasa yetu ya nje ni ya ndani ya ujamaa na kujitegemea tunayoijenga, basi kazi moja kubwa ya Chama na Serikali katika suala hili ni kuielezea siasa yetu na kutetea misingi ya haki, usawa na uhuru katika mikutano ya kimataifa na kulijengea Taifa uhusiano wa kidugu na ushirikiano na mataifa ya kimaendeleo na ya kimapinduzi na yale yote ambayo yanataka ushirikiano nasi katika misingi ya kuheshimiana, kutoingiliana katika mambo ya ndani na ya kuzingatia maslahi ya pande zote mbili Chama chetu, tangu wakati wa ASP na TANU kiliwajenga wanachama wake na wananchi kwa jumla katika hisia za kimapinduzi za kujishirikisha na mapambano ya ukombozi wa nchi nyingine za Afrika na za dunia. Lakini pamoja na historia hiyo ya Chama na wananchi kushiriki kwa vitendo katika kuongoza siasa yetu ya nchi za nje, kumekuwa na vipindi ambapo shughuli za nchi za nje Chama kiliachia Serikali pekee Kuanzia sasa Chama kitahakikisha kuwa uhusiano wetu na nchi za kigeni unakuwa sehemu muhimu ya shughuli zake. 102 MIONGOZO MIWILI

104 Katika lengo hilo Chama kitaendeleza na kujenga uhusiano maalum na vyama halisi vya ukombozi, vya kijamaa na vya kimaendeleo vya Afrika na kote duniani ili kubadilishana uzoefu na kuimarisha mapambano dhidi ya ubeberu wa dunia. B. CHAMA KUJIZATITI ILI KUONGOZA MAPINDUZI Lakini Ujamaa hauwezi kujijenga wenyewe. Kwani Ujamaa ni Imani. Hauna budi kujengwa na watu wanaoamini na kufuata kanuni zake. Mwana- TANU wa kweli ni mjamaa, na wajamaa wenziwe yaani waamini wenziwe katika imani hii ya kisiasa na kiuchumi ni wote wale wanaopigania haki za wakulima na wafanyakazi katika Afrika na popote duniani. Azimio la Arusha 127. Kazi kubwa ya Chama Cha Mapinduzi kwa mujibu wa Mwongozo huu ni kuchukua hatua za kujizatiti, kujijenga na kujiimarisha ili kujipa uwezo unaolingana na uzito wa mapambano yaliyo mbele yetu ya kujenga ujamaa katika kipindi ambapo ubepari na ubeberu wa dunia na vibwanyenye na wapinga Ujamaa wa humuhumu nchini wanazidisha kujenga vitimbi vya uhasama dhidi ya siasa yetu ya Ujamaa na Kujitegemea Kujizatiti kwa mapambano ya kujenga ujamaa kwanza kabisa ni kuwa na hakika na wapiganaji wa mstari wa mbele wa mapambano hayo ambao ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi. Kwa hiyo, hatua ya kwanza ya Chama kujizatiti kwa mapambano ni kuwawezesha wanachama wa CCM kifikra na vitendo, mmoja mmoja na katika umoja wao, kutimiza wajibu wao wa kimapinduzi. (1) Kazi ya kuwajengea na kuwaimarisha wanachama: (a) Maandalizi: Vuguvugu la mijadala ya kichama katika Mashina, Matawi na Nchini kote. MIONGOZO MIWILI 103

105 129. Chuo Kikuu cha Wanamapinduzi duniani kote ni kushiriki kwa vitendo katika harakati za kimapinduzi pale walipo. Chuo cha kuwajenga Wana CCM katika msimamo wa kimapinduzi ni kwa Wana CCM kushiriki kwa vitendo katika harakati za kusukuma mbele ujenzi wa ujamaa pale walipo, kama ni kijijini, kiwandani, ofisini, jeshini, chuoni au katika kata ya mjini wanakoishi. Kushiriki kwa vitendo katika mapinduzi ni pamoja na vitendo vya kujiendeleza au kujinoa katika nadharia ya mapinduzi Kwa hiyo, hatua ya kwanza kuelekea kwenye lengo litakalomwezesha mwana CCM kushiriki katika harakati za mapinduzi pale alipo ni kwa Chama kuanzisha mashina na matawi nchini kote. Mikutano hii ya wana CCM tu iitishwe kujadili maendeleo ya Chama katika sehemu zao; wanachama wakosoane na kujikosoa kuhusu vitendo vyao kama wanachama ili kuona kama vinafanana na mahitaji ya mapinduzi. Mikutano hii pia izungumzie hali ya uchumi ilivyo nchini na kuchambua hatua za kujihami zinazotarajiwa kuchukuliwa na Taifa na katika sehemu zao Viongozi na maafisa wa Chama wa ngazi zote wawajibike kushiriki katika mijadala hii kama wanachama wengine. Mijadala hii iwe na lengo la kumwezesha kila mwanachama na kila Tawi kudhihirisha walivyojitahidi kutekeleza majukumu yake katika Chama, wapi mwanachama (tawi) alipoonyesha udhaifu na kutafuta njia za kutimiza majukumu vizuri zaidi Vuguvugu hili la mikutano ya wanachama liende sambamba na mijadala ya hadhara ya wananchi wote vijijini, katika sehemu za kazi na mijini. Mikoa ipange mipango itakayowawezesha viongozi wa Chama wa ngazi zote kwenda vijijini, viwandani, majeshini, vyuoni na mijini kuelezea kwa kinaganaga hali ya uchumi wetu na hatua za kujihami kiuchumi ambazo lazima zichukuliwe. Kushiriki huku kutawapa nafasi ya kujifunza na kuielewa zaidi hali ya nchi. Wakati huo huo magazeti na redio vitumike na Chama kuendeleza na kuelekeza mijadala hii. 104 MIONGOZO MIWILI

106 133. Mijadala hii ya wanachama na ya wananchi kwa jumla itasaidia kuinua mwamko wa kisiasa wa wananchi, kuwaelimisha zaidi juu ya matatizo ya nchi yetu na kuwaongezea ari ya kudhamiria kushiriki kwa ukamilifu zaidi katika harakati za kujihami kiuchumi na kisiasa. Mijadala hii katika Matawi, ikiendeshwa kwa makini na kwa utaratibu mzuri, itawezesha wanachama wa kweli kufahamiana na wanachama wa bandia kufichuliwa. Hii itahusu pia viongozi kueleweka katika msimamo Katika hali hii, hatua inayofuata ni kwa kila Tawi la Chama kuchukua hatua ya kuwajadili wanachama wake mmoja mmoja ili kuamua kama bado wanastahili kuendelea na uanachama au la. Kwa kuwa wazembe, wazururaji, wezi na majambazi watakuwa wamefichuliwa katika vikao hivi, kwa kuwa wapinga ujamaa kiitikadi na kwa vitendo watakuwa pia wamefichuliwa, basi hii ndiyo nafasi ya kukitakasa Chama. Matawi yapendekeze kwenye vikao vya juu hatua za kuwachukulia wanachama watakaodhihirika kuwa hawatimizi masharti na wajibu wa wanachama. Azimio la Arusha linasisitiza juu ya ubora wa wanachama badala ya wingi wa wanachama. Vuvuvugu hili la mijadala ya wanachama wenyewe tu litasaidia kuunda hali itakayowezesha kupiga hatua za mwanzo za kuelekea kwenye lengo hilo la Azimio la Arusha Kazi hii ya Chama ya kuongoza mijadala ya kujikosoa na kukosoana iendelee hadi itakapofikia kipindi cha mikutano mikuu ya mwaka wa tano tangu CCM kuzaliwa. Kipindi hiki ni kirefu cha kutosha kwa mashina na matawi ya Chama kufanya vikao kadhaa vya wanachama wote ili kuwezesha kuelewana na kupimana kwa makini. Kipindi hiki ni kizuri pia kupimana kwa sababu ni kipindi ambapo Chama kitaongoza mapambano ya utekelezaji wa hatua za kujihami kiuchumi nchini kote. Na wakati huo huo hiki ni kipindi cha kuanzisha msukumo mpya wa ujenzi wa ujamaa nchini Ni dhahiri kuwa katika hali hii ya vuguvugu la mapinduzi la utekelezji wa siasa ya Chama, wanachama matawini watapata nafasi nzuri ya kufahamiana na kuelewana kwa vitendo. Wana MIONGOZO MIWILI 105

107 CCM halisi watajitokeza kwa vitendo katika utendaji wao wa kila siku kazini na wanakoishi. Wana CCM wa vijijini watadhihirisha uanachama wao kwa kuwa katika mstari wa mbele katika kutekeleza majukumu ya Ujamaa ya kijiji na katika kushiriki kwa dhati katika kazi za kujitolea kwa jumla kama ujenzi wa shule, zahanati, barabara za kijiji, shamba la kijiji, kushiriki katika elimu ya watu wazima, ulinzi wa kijiji na kadhalika Wana CCM wafanyakazi, watadhihirisha uanachama wao kwa vitendo kwa kufanya kazi kwa makini na kwa nidhamu, kwa kushirikiana na wafanyakazi wenzao kuhakikisha kuwa malengo ya kazi yaliyowekwa yanatimizwa, kwa kupambana bila woga na vitendo vyo vyote vile vya uvivu na uzembe kazini, vya kuzorotesha kazi au vya kuhujumu uchumi. (b) Mafunzo ya Siasa ya Chama 138. Chama kinapanga na kuendesha mafunzo ya siasa yake ikiwa na malengo makubwa matatu: Mafunzo ya Siasa ya Chama yanatolewa kwa wananchi kwa jumla kwa lengo la kuieneza siasa hiyo ili ieleweke na kukubalika na wakati huo ili kupiga vita upotoshaji na uzushi juu ya siasa ya ujamaa unaoenezwa na maadui wa ujamaa kwa nia ya kukifanya Chama kifarakane na Umma. Nia wakati wote ni kuelimisha umma na kuufanya uwe karibu zaidi na Chama ili ushiriki katika kutekeleza maelekezo na mwito wake kwa ari na hiari Lengo la pili la mafunzo ya siasa ya Chama ni kuhakikisha kuwa wananchi katika taasisi maalum za wananchi: wanafunzi, wanajeshi, wafanyakazi, vijana, wanawake, wanautamaduni, viongozi wa kazi, waandishi wa habari n.k. wanahamasishwa ili kuinua mwamko wao wa kisiasa, na kuwapa wahusika mwelekeo wa siasa kulingana na jinsi Chama kinavyoiona nafasi yao katika ujenzi wa taifa kwa sasa na kwa baadaye Lengo la tatu la mafunzo ya siasa ya Chama ni kuhakikisha kuwa wanachama na viongozi wanaimarika katika itikadi ya ujamaa na 106 MIONGOZO MIWILI

108 kujitegemea; kuwapanua wanachama na viongozi upeo wao wa kuyaelewa masuala mbalimbali; kuwapa methodolojia na mantiki ya kutafakari na kufanya uchambuzi wa msuala; kuwazatiti kwa hoja na mbinu zitakazowasaidia katika harakati za kuongoza utekelezaji wa siasa ya ujamaa pia kueneza na kutetea siasa ya Chama Mafunzo ya aina zote tatu ni muhimu kwa maendeleo ya mapinduzi yetu. Mafunzo ya aina ya tatu, yaani mafunzo ya wanachama na viongozi, ndiyo yatakayowezesha kufanikiwa kwa mafunzo ya aina ya kwanza na ya pili. Katika miaka ya usoni, Chama kitaendelea kuendesha mafunzo ya siasa ya Chama kwa mipango na msukumo mkubwa zaidi kwa kuzingatia kuwa mapambano ya kisiasa na kiitikadi ni sehemu muhimu ya mapambano ya kujenga ujamaa na kuzifichua na kuzishinda mbinu za adui Hivyo, Chama kitachukua hatua za kuimarisha na kupanua mipango ya mafunzo ya wanachama na viongozi. Wanachama walio wengi itabidi wapate mafunzo yao ya nadharia matawini kwao. Mafunzo hayo yatakayoendeshwa kwa msingi wa semina yatasimamiwa na mikoa na wilaya zenyewe. Wanachama watakaojitokeza, kwa msimamo na uwezo, yaani wanachama wenye sifa za kada, pamoja na viongozi wa matawi, wilaya, mikoa na Taifa wataingia katika mpango maalum wa kupata mafunzo katika vyuo vya Chama vya ngazi zinazolingana na mahitji yao. Utaratibu katika vyuo vya Chama wa mafunzo ya kada na viongozi wa Chama utahitaji maandalizi ya makini na ya hali ya juu Chuo cha Chama ni mahala anapopelekwa mwanachama aliyejitokeza katika Chama, yaani kada wa Chama au kiongozi wa Chama, kwa madhumuni ya kumwandaa kwa kazi kubwa zaidi za Chama. Chama ndicho kinachomwandaa mwanachama mwenye msimamo wa sifa za kada wa Chama au kinaamua kumpeleka chuoni apate upeo mkubwa zaidi wa kukitumikia Chama. Mwanachama huyu anaweza akawa afisa wa serikali, mfanyakazi wa chama au mkulima. La msingi ni kuwa anateuliwa na Chama MIONGOZO MIWILI 107

109 kutokana na sifa zake katika Chama na kwa madhumuni ya Chama ya kuendeleza kazi zake za kuongoza Taifa kama Chama Wakati huo huo Chama kitaimarisha mafunzo ya siasa ya Chama ya aina ya pili kwa ajili ya taasisi kama majeshi, shule na vyuo, wafanyakazi, vijana pamoja na wataalamu na Wakuu wa kazi wa viwango na taasisi mbalimbali. Kwa utaratibu, mafunzo ya aina hii huendeshwa kwenye taasisi zenyewe na kusimamiwa na Chama Mafunzo haya ya siasa ya Chama yatatumika pia kuwatambua wale wenye sifa za kada wa Chama. Wale watakaobainika kuwa wana mwelekeo huo basi wataingizwa katika utaratibu wa kupatiwa mafunzo zaidi katika vyuo vya Chama. Hii ina maana kuwa maafisa wa serikali na mashirika yake hata wafanyakazi katika sekta ya kibepari walio wana CCM wakijitokeza katika mafunzo ya Chama ya taasisi zao kwa kuwa wana sifa za kada wa Chama watafanyiwa mpango ili inapotokea nafasi wajiunge na vyuo vya Chama. (2) Kuimarisha muundo, demokrasi na utendaji wa Chama 146. Vyama hujipa muundo unaowesesha shughuli zake kutekelezwa kwa nidhamu na ufanisi. Kwa madhumuni hayo vyama hujipa vikao vya aina tatu hivi katika kila kiwango: Kikao cha aina ya Mkutano Mkuu ambacho ni cha wajumbe wengi na ndicho kikao kinachotoa mwelekeo na kupanga siasa na mambo makubwa ya kutekelezwa katika kipindi kirefu kifuatacho. Vikao vya aina hii hukutana baada ya kipindi kirefu kupita. Kikao cha aina ya pili ni kipana na kina wajumbe wengi na ndicho kinachoongoza na kusimamia utekelezaji na maamuzi ya mkutano mkuu. Mwisho huwa kuna chombo kidogo cha wajumbe wachache ambao huunda Kamati ya Utendaji ya kikao kikubwa cha aina ya pili Sasa, utaratibu wa zamani wa TANU na wa ASP ulikuwa na mfumo wa aina hii. Na uzoefu tulioupata hadi sasa unadhihirisha ubora wa mfumo wa aina hii maana unaunganisha mahitaji ya demokrasi pana ya vikao vya aina ya kwanza na ya pili na wakati huo huo unarahisisha utendaji kwa kuwa na kamati ya utendaji 108 MIONGOZO MIWILI

110 ya Wajumbe wachache watakaokabidhiwa majukumu ya utendaji siasa wa kila siku. Chama kitachukua hatua za kurekebisha muundo wake wa sasa ili kulifikia lengo hili katika ngazi zote za Chama Imedhihirika pia kuwa kuna umuhimu kwa sasa wa kuimarisha demokrasi ya Chama katika kiwango cha Taifa na baadaye katika viwango vya chini yake. Hali ilivyo kikatiba hivi sasa ni kuwa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ni mchanganyiko wa wanaochaguliwa na wanaoteuliwa. Wakati umefika wa kuimarisha demokrasi ya Chama kwa kurekebisha Katiba ili wajumbe wote wa Halmashauri Kuu ya Taifa watokane na uchaguzi wa Chama Hatua nyingine inayohitaji kuchukuliwa ili kuimarisha Chama inahusu kuunganisha uongozi wa Chama yaani wa Halmashauri Kuu ya Taifa na utendaji kazi wa Ofisi yake yaani Makao Makuu ya Chama. Mfumo wa hivi sasa una hitilafu inayoathiri kazi za Chama. Kwa mujibu wa mfumo huu viongozi kazi yao ni kuamua katika vikao na halafu kuna watendaji ambao ni maafisa waajiriwa wa Chama wa kutekeleza maamuzi hayo. Chama kitaurekebisha utaratibu huu (pamoja na mfumo wa sasa wa Kamati za Kamati Kuu) kwa kuweka utendaji kazi za Halmashauri Kuu ya Taifa chini ya makatibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa yenyewe. Kazi muhimu za Halmashauri Kuu ya Taifa ni pamoja na Elimu, Uenezi na Itikadi ya Siasa, Uchumi na Mipango, Organaizesheni, Ulinzi na Usalama, Uhusiano na Nchi za Nje na Nidhamu na Udhibiti. Utaratibu huu utahusu Mikoa, Wilaya na Matawi kwa hatua zitakazoamuliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa. (3) Kuimarisha uongozi wa Chama katika sehemu za kazi 150. Kuanzia sasa Chama kitahakikisha kuwa serikali inachukua hatua za kuuwezesha utaratibu wa malengo ya utoaji mali kutumika katika viwanda na mashirika yake na kuinua uwezo wa utoaji huduma wa vyombo vyake. Wakati huo huo Chama kitahakikisha kuwa wakuu wa kazi wanasaidia kisiasa ili wawe na msimamo wa kizalendo utakaoimarisha uwezo wao wa kitaalamu. MIONGOZO MIWILI 109

111 151. Hata hivyo, kazi kubwa ya Chama katika sehemu ya kazi itafanywa na tawi la Chama la mahali pa kazi panapohusika. Kazi ya Chama katika Taifa, Mkoa na Wilaya ni kuunda hali itakayoliwezesha Tawi la Chama kutekeleza wajibu wake wa uongozi. Ili kuhakikisha kuwa Chama katika sehemu ya kazi kinashika nafasi yake ya uongozi kuna masuala kadhaa ya kutia maanani La kwanza ni kuwa suala la umuhimu wa kwanza kwa Chama katika mahali pa kazi katika mazingira ya nchi inayojenga ujamaa ni kuleta mafanikio ya utekelezaji wa kazi. Hivyo, jitihada ya Chama katika sehemu ya kazi ni kuhakikisha kuwa wanachama na viongozi wa chama wanakuwa katika msitari wa mbele katika kutimiza wajibu wao wa kazi na kuona kuwa malengo yaliyowekwa yanafikiwa. Ni mwiko kwa mwanachama wa CCM au kiongozi kuwa miongoni mwa wategaji, wavivu na wazoroteshaji kazi Jambo la pili ni kuwa vyama vya kijamaa halisi haviongozi kwa mabavu bali kwa kuelimisha, kushawishi, kuelekeza na kwa chama chenyewe kuonyesha njia kwa vitendo. Kwa hiyo, kazi ya Chama katika sehemu za kazi itakuwa kuwajenga wana CCM kujua namna ya kuwashirikisha wafanyakazi wenzao katika kutekeleza malengo na wajibu wa kazi kutokana na mfano wao wenyewe wa kutekeleza wajibu kwa makini na kwa ari na uwezo wao wa kushawishi, kushauri na kuwashirikisha wafanyakazi Jambo la tatu la kuzingatia kuhusu suala la uongozi wa Chama katika sehemu za kazi ni kuwa ujuzi ni madaraka. Watu wana tabia ya kumsikiliza anayejua zaidi kuliko wao juu ya suala fulani. Sasa, mahali pa kazi ni mahali penye ujuzi wa aina mbalimbali. Atakayejitokeza kuwa anajua zaidi katika fani fulani wenzake humheshimu, humtegemea na kumsikiliza. Chama kitahakikisha kuwa katika siku za usoni wanachama wa CCM wanajiendeleza katika fani zao za kazi ili kuwa miongoni mwa wanaotegemewa na kusikilizwa na wafanyakazi wenzao katika fani zao za kazi Jambo la nne linahusu matatizo ya kila siku ya wafanyakazi. Kiongozi, pamoja na sifa nyingine, ni mtu mwenye kuyaelewa 110 MIONGOZO MIWILI

112 matatizo ya watu na anayejua vile vile kuyaelezea na kuyajengea hoja. Chama kitahakikisha kuwa wanachama wa CCM wanaaminiwa na wafanyakazi wenzao kwa kuwa wanayaelewa matatizo yao na wana uwezo wa kuyaelezea kwa ufasaha na kushirikiana nao katika kutafuta jawabu. Ili kufikia hapo Wana CCM watawajibika kujiendeleza katika nadharia ya Chama na elimu kwa jumla Suala linarudia pale pale tulipoanzia. Kwa Chama cha Mapinduzi kuongoza mapinduzi katika sehemu za kazi, kazi ya msingi ni kuwaandaa wanachama na viongozi wa matawini kwa mafunzo thabiti ya siasa ya Chama; ni kwa Chama kuhakikisha kuwa katika kila sehemu ya kazi viongozi wa Chama waliopo na wanachama kwa jumla wanapata miongoni mwao kada wa Chama wenye uwezo wa juu wa uchambuzi na mbinu watakaosaidiana nao katika mawimbi ya harakati. Hii ndiyo kazi kubwa ya Chama katika siku zijazo. K.m. katika jitihada za kuimarisha uongozi wa chama katika majeshi, miradi muhimu ya Taifa na taasisi, Chama kinaweza kuteua kamisaa wa siasa na kumpeleka katika sehemu hiyo. Kazi yake ni kusaidiana na uongozi uliopo kuimarisha utekelezaji wa majukumu, kuendeleza nidhamu na kwa kusaidiana na Chama katika sehemu hizi, kuuinua mwamko wa siasa na wa uzalendo wa wapiganaji, wafanyakazi au wanafunzi na kuwaongezea ari katika utekelezaji wao. Matawi na Mashina ya kazini na mijini kuimarishwa 157. Ili Chama kitimize wajibu wake wa kuongoza katika sehemu za kazi tegemeo lake kubwa ni wanachama. Lakini wanachama pia wanategemea muundo wa mashina na matawi uliopo. Hivi sasa kuna matawi ambayo wanachama wao ni wengi mno kwamba uwezekano wao wa kufahamiana na kushirikiana ni mfinyu mno. Katika siku zijazo Chama kitahakikisha kuwa katika sehemu za kazi suala la kuwaunganisha wanachama katika mashina linatiliwa MIONGOZO MIWILI 111

113 mkazo zaidi. Wakati huo huo utatazamwa uwezekano wa kuunda matawi zaidi ya moja katika sehemu za kazi zenye wanachama wa CCM wengi mno Aidha, Chama kitalishughulikia suala la matawi ya Chama ya Kata za Mijini. Katika hali ya sasa matawi mengi ya kata za mjini ni makubwa kiasi kwamba wanachama hawawezi kujihusisha kwa ukamilifu katika matawi yao. (4) Kuimarisha Chama kwa kuimarisha uongozi 159. Kiongozi wa Chama cha Mapinduzi kwanza kabisa lazima awe na msimamo wa kijamaa. Itikadi yake ya ujamaa, vitendo na tabia yake vijidhihirishe kwa wanaowaongoza, wanachama na wananchi, kuwa ni vya kijamaa. Imani ya kiongozi inaambukiza na kuimarisha imani ya anaowaongoza. Lakini kiongozi anayegunduliwa na anaowaongoza kuwa ni mnafiki kwa msimamo ni adui mkubwa kwa Chama maana anawavunja moyo wanachama, anawavuruga wananchi na kuunda hali itakayowafanya wananchi wasiwe na imani na viongozi wengine na Chama. Hivyo suala la viongozi wa Chama kuwa na msimamo sahihi kwa itikadi na katika maisha ya kila siku ni jambo lenye umuhimu wa kwanza kwa Chama cha Mapinduzi Lakini pia msimamo thabiti wa ujamaa wa kiongozi uambatane na uwezo wa kuongoza. Tumetamka hapo juu katika Mwongozo huu kuwa Chama cha Mapinduzi hakiongozi kwa mabavu bali kwa kuelimisha, kuelekeza, kushauri, kushawishi na kushirikiasha. Hii ina maana kuwa kiongozi wa Chama hana budi awe na uwezo wa kushauri na kuelimisha, kushawishi na kushirikisha, kwa jumla awe na uwezo wa kuieneza na kuitetea siasa ya Chama na kuwaunganisha wanachama na wananchi katika harakati za kujenga ujamaa nchini na kwa kiwango cha uongozi wake Kutokana na hayo, Chama kuanzia sasa kitalipa uzito suala la msimamo na uwezo wa viongozi wake. Ndiyo kusema kwamba 112 MIONGOZO MIWILI

114 katika siku za usoni uchambuzi wa viongozi waliopo na waombao nafasi za uongozi utasisitiza juu ya msimamo wao kwa itikadi na kwa vitendo pamoja na uwezo wao wa kumudu uongozi huo Chama kitatumia njia mbali mbali za mafunzo ili kuwasaidia viongozi wenye nia njema kuimarisha msimamo wao kiitikadi. Chama pia kitakuwa na utaratibu wa kuwasaidia viongozi wenye msimamo sahihi lakini uwezo mdogo wa kuongoza kupata nafasi ya kuendeleza uwezo wao. Lakini Chama kitahakikisha kuwa viongozi ambao msimamo wao kwa itikadi na kwa vitendo ni kinyume cha misingi ya ujamaa hawapewi nafasi ya kukihujumu Chama kutoka ndani ya Chama. Wakati huohuo Chama kitahakikisha pia kuwa suala la uwezo linakuwa sehemu muhimu ya uchaguzi au uteuzi wa viongozi wa Chama cha Mapinduzi. (5) Maandalizi ya waombaji unachama 163. Chama kitaendelea kupokea wanachama wapya isipokuwa kwamba kuanzia sasa suala la wanachama litekeleze kwa vitendo agizo la Azimio la Arusha kuhusu ubora wa wanachama badala ya wingi wao. Wakati huo huo, jitihada zitafanywa ili kuhakikisha kuwa idadi ya wanachama wanawake, wakulima, wafanyakazi na vijana inafanana na nafasi yao halisi katika jamii yetu. Mafunzo kwa waombaji uanachama 164. Mwelekeo na mkazo wa mafunzo ya wanachama wapya yatafanyiwa mabadiliko ya kimsingi. Mwanachama wa CCM kwa mujibu wa Mwongozo huu atapimwa kwa vitendo vyake vya kutekeleza siasa ya Chama katika maisha yake ya kila siku. Vivyo hivyo, mtu anayeomba kuwa mwanachama wa CCM itabidi apewe kipindi cha majaribio ambapo atapimwa kuhusu kufaa kwake kuingia katka Chama kwanza kabisa kwa vitendo vyake vya kutekeleza siasa ya Chama. Aidha, atawajibika kuhusika na shina na tawi ambalo ndilo litakalompangia majukumu ya kichama ya kuyatekeleza na ndiko atakakokuwa akijadiliwa hatua kwa hatua MIONGOZO MIWILI 113

115 na uamuzi kufanywa kuhusu kuingizwa au kutoingizwa katika Chama wakati utakapofika. (6) Kuimarisha Chama kifedha 165. Pamoja na kuimarisha usimamizi wa Fedha za Chama, Chama kitachukua hatua thabiti za kujiimarisha kwa kujiongezea mapato. Mambo matatu yanakusudiwa kufanywa: - Jambo la kwanza ni kuwa Chama kitaimarisha udhibiti wa fedha zake. Jambo la pili ni kuwa kitawataka wanachama na viongozi wa CCM kutoa mchango wa hiari wa kuimarisha Chama kwa kiwango cha asilimia itakayoamuliwa ya mshahara wa kila mwezi kwa kila kiongozi na mwanachama. Utaratibu wa aina hiyo utabuniwa kwa ajili ya wanachama wakulima na wanaojiajiri wenyewe. Hatua ya tatu ni Chama kutafuta njia nyingine za kudumu za kukiwezesha kuongeza mapato yake. (7) Kuimarisha Jumuia za Wananchi 166. Jumuia za wananchi zina umuhimu mkubwa sana kwa Chama katika malengo na mbinu zake za mapambano. Pamoja na kuwa vyombo vinavyowaunganisha wananchi wenye hali inayofanana katika shughuli zao za kazi za kila siku au wananchi wanaofanana kwa maumbile ili kuendeleza maslahi yao, Jumuia za wananchi pia ni mikondo inayokiwezesha Chama kuufikia umma wa wananchi kwa fikra, msimamo, maelekezo na miito mbalimbali Katika hali hii Jumuia za wananchi zinaweza kuwa vyombo muhimu vya mapambano ya Chama na kuwa nguvu zake za akiba. Katika kipindi kinachoanzia sasa, Chama kitajitahidi kuzijenga jumuia kwa kushirikiana nazo ili ziweze kuwa nguvu thabiti za mapinduzi ya kujenga ujamaa. Papo hapo, Chama kitahakikisha kuwa Jumuia za wananchi zinapata msaada utakaoziwezesha kushirikiana na Chama bila ya kupoteza uwezo wao wa kuziendesha shughuli zao wenyewe bila ya kuingiliwa. 114 MIONGOZO MIWILI

116 168. Kwa sasa, wakati Chama kinaanzisha vuguvugu la mapinduzi la mijadala ya kujikosoa na kukosoana kwenye Chama katika matawi yake, Jumuiya zichukue nafasi hii kushiriki kwa ukamilifu katika harakati hizi. Chama kitawataka wana CCM wote kuwa katika mstari wa mbele katika vuguvugu la kuleta mwamko wa siasa katika Jumuia zao. Ni wajibu wa kila mwanachama wa jumuiya hizo kujiunga na Jumuiya zinazomhusu kueneza siasa ya Chama miongoni mwa wanachama wa Jumuiya hizo na kuwashawishi wananchi wengine kujiunga na Jumuiya. MWISHO MIONGOZO MIWILI 115

117 SURA YA NNE MAAMUZI YA ZANZIBAR, 1991 (Hotuba ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Ali Hassan Mwinyi wakati akizungumza na wazee wa chama, viongozi wa taifa, mashirika ya umma na watu binafsi juu ya ufafanuzi wa maamuzi ya Halmashauri Kuu ya Taifa katika kikao chake cha Zanzibar: Diamond Jubilee Dar es Salaam, tarehe 25/2/1991) Ndugu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Mkoa wa Dar es Salaam, Ndugu Katibu Mkuu, Ndugu Mwenyekiti wa Wazee wa Dar es Salaam, Ndugu Viongozi wa Chama na Serikali na Ndugu zetu waalikwa, Kabla ya yote, labda niseme kwamba kwa kuwa tumo katika mwezi wa pili tokea kuanza kwa mwaka mpya, nami sijapata nafasi ya kukutana nanyi wazee, ni vyema nitumie nafasi hii kwanza kukutakieni heri ya mwaka mpya, na baraka zote za mwaka (Makofi). Ninakuombeeni uzima, nguvu, baraka na mafanikio. Pili, tuna kawaida katika nchi yetu, kwamba kila linapotokea jambo muhimu katika Taifa, tunatafuta nafasi ya kukutana nanyi na kukuelezeni. Hivyo, leo napenda kuzungumza nanyi wazee wa Dar es Salaam na, kupitia kwenu, iwe ninazungumza na Wazee wenzenu wa Tanzania nzima. Kwa hiyo, hayo nitakayokuambieni nyinyi, ninawaambia pia Wazee wa Taifa letu wote kwa jumla. Hivi karibuni Halmashauri Kuu ya Taifa ilifanya kikao chake cha kawaida Zanzibar, ambacho kilijadili mambo mbalimbali. Kikao hicho kilimalizika kwa kutoa maamuzi maalum. Maamuzi hayo yana uzito mkubwa. Inaelekea baadhi yetu, pamoja na Vyombo vyetu vya Habari, hatukuyaelewa vizuri maamuzi hayo. Kwanza, nataka nivivue lawama Vyombo vyetu vya Habari. Maana hatukuwa nao huko. Kwa hivyo walitangaza vile walivyoelewa. Kwa sababu hiyo nimeona ni vyema 116 MIONGOZO MIWILI

118 kuzungumza nanyi ili kusahihisha matangazo ya vyombo vyetu. Nimeona ni vyema kutumia nafasi hii kutoa ufafanuzi. LAZIMA TWENDE NA WAKATI Inaelekea kuna hofu kwamba Azimio la Arusha linageuzwa. Kwa hiyo, tokea mwanzo, kabla ya kusema lolote, nataka tuelewane kwamba siasa yetu bado ni ile ile ya Ujamaa na Kujitegemea. (Makofi). Haikugeuka wala hatutazamii kuigeuza. Kwa hali yoyote sisi Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi hatutaigeuza Siasa hii. (Makofi). Kule Zanzibar tulizungumza mambo mengi, miongoni mwao, ni kutoa tafsiri ya baadhi ya vipengele vya Azimio ili vifanane na wakati tulionao. Azimio la Arusha, kama tunavyojua, limetangazwa mwaka Hii leo tuko katika mwaka Imepita miaka mingi, zaidi ya 20 tokea kutangazwa kwa Azimio la Arusha. Na katika kipindi cha miaka 20 yametokea mabadiliko mengi duniani na pia katika hali ya maisha yetu. Hali yetu ya sasa, hasa ya kiuchumi, siyo ile ile ya mwaka Ndio maana mishahara ya wafanyakazi ingawa imeongezeka sana lakini bado haikidhi mahitaji yao - haiwatoshi hata wale wanaopokea mishahara mikubwa miongoni mwetu. Isitoshe, wakati wa Azimio idadi ya Watanzania ilikuwa ndogo. Sasa hivi idadi yetu imeongezeka zaidi ya mara mbili. Kwa sababu ya wingi wetu mahitaji yetu nayo yemeongezeka sana, wakati mapato yetu yamekuwa yakipungua wakati wote. Kwa hivyo ni dhahiri kwamba jamii ya Tanzania lazima itie maanani mabadiliko haya na ijiandae kwenda na wakati. Kama hatukwenda na wakati, kazi yetu itakuwa ni kufukuzia wakati - jambo ambalo hatulimudu. Tabia ya wakati ni kama ile ya bahari. Bahari inakupwa na kujaa mpaka ukingoni mwa maji. Baadaye maji huopwa polepole, mpaka kufika wakati ikawa maji yote yamekwishaondoka ufukoni. Samaki werevu huondoka nayo hayo maji, yaani yakijaa huja nayo, yakitoka hutoka nayo, vinginevyo hupwelewa. Samaki watakaozembea kufuata maji watajikuta wamechelewa wanatapatapa juu ya mchanga wakati maji hayo hayapo. Hiyo ndiyo maana ya kupwelewa (Makofi). Hapa Afrika, kwa mfano, imeanzishwa mipango mbalimbali ya MIONGOZO MIWILI 117

119 ushirikiano wa uchumi. Mipango hiyo ni pamoja na Ushirikiano wa Nchi za Kusini mwa Afrika (SADCC) na Eneo la Soko Nafuu (PTA). Afrika pia imeazimia kuunda Jumuiya ya Uchumi. Nchi zinazoendelea nazo zimedhamiria kuzidisha ushirikiano miongoni mwao. Nchi yetu lazima ifanye mabadiliko ili iweze kushiriki kwa ukamilifu katika shughuli zote hizo zinazosaidia maendeleo yetu. KILA ZAMA NA MWONGOZO WAKE Ndugu Wazee, Msahafu wa Waislam unasema LIKULLI AJALIN KITABU Mwingereza mmoja kaitafsiri aya hiyo hivi: TO EVERY AGE ITS BOOK yaani Kila zama ina Kitabu (Mwongozo) chake. Na sisi Wana-CCM tunakubali kuwa kila Zama zinahitaji kuwa na Mwongozo wake. Azimio la Arusha ni Mwongozo wetu wa msingi. Ni dira inayoongoza mwelekeo wa jamii yetu. Lakini tafsiri zake zinabidi zirekebishwe kila inapohitajika ili zisipitwe na wakati. Miongozo ina tabia moja: inakuja ili kufafanua, kuelekeza au kukemea hali mbaya inayojitokeza. Mojawapo ya malengo ya maamuzi ya Zanzibar ni kutoa tafsiri sahihi ili kupunguza kebehi inayofanywa dhidi ya siasa yetu ya Ujamaa na Kujitegemea na pia kwenda na wakati. Mwaka 1967 lilitangazwa Azimio la Arusha. Mwaka 1971 ulifuatiwa na tamko la Iringa la Siasa ni Kilimo. Tamko hili lilikuwa ni mbinu na msisitizo wa Siasa yetu ya Kujitegemea. Lilipanua tafsiri ya Azimio la Arusha. Katika mwaka 1981 ilionekana kuna haja ya kutolewa mwongozo mwingine kulingana na wakati ule ambao nao ni upanuzi wa tafsiri ya Azimio. Ulitangazwa ili kukidhi haja ya wakati ule. Aidha, kabla ya hapo, katika mwaka 1974, Chama kilipitisha Agizo la Musoma kuhusu Elimu ya Kujitegemea ambalo madhumuni yake yalikuwa kutazama upya suala la uingizaji wanafunzi Chuo Kikuu na kupanua Elimu ya Msingi ili kutoa fursa kwa watoto wote wenye umri wa kwenda shule kufanya hivyo. Maandiko yote hayo hayakupingana na Azimio la Arusha ila yakiongeza mwangaza kwa mambo ambayo yalihitaji yafanane na wakati wake. Na lazima iwe hivyo, kwani bila ya kwenda na wakati tungechekesha. 118 MIONGOZO MIWILI

120 Kwa mfano wakati wa Azimio la Arusha, mtakumbuka kuwa tafsiri ya neno Kiongozi ni pamoja na yule mwenye mshahra uliofikia shilingi 1,066/= kwa mwezi. Tungeng ang ania tafsiri hii tu, basi leo pasingekuwapo wafuasi. Wafanyakazi wote wangetafsirika kuwa ni viongozi wa CCM. Kwani ukiacha wakulima, wafanyakazi wote sasa kwa tafasiri ya 1967 ni viongozi tena maradufu. Maana kima cha chini sasa ni Sh.2,500/=, ambazo ni zaidi ya mara mbili ya Sh.1,066/=. Ndiyo maana tukasema jamii yetu italazimika kufanya marekebisho kila inapokuwa lazima kufuatana na wakati. Tutafanya hivyo bila ya kuachana na misingi ya siasa yetu. Kwa hivyo, tulichokifanya kule Zanzibar ni kupanua tafsiri za Azimio ili ilingane na wakati tulionao. Kufanya hivyo si kuua Azimio bali ni kuliimarisha. CHIMBUKO LA AZIMIO LA ARUSHA Historia ya Azimio la Arusha tunaijua sote. TANU ilipigania kwa maneno mpaka nchi ikapata UHURU wake. Tanganyika ilipopata Uhuru na tukaanza kujitawala ishara potofu zilianza kuchomoza. Baadhi ya viongozi walianza kuutumia uongozi wao kama mradi wa kujineemesha. Kwa kutumia nyadhifa zao, wakikopa fedha benki na kuanza kujijengea mashamba - si ya miti - bali ya majumba; si nyumba za kuishi tu bali majumba mengi ya kupangisha. Tabia hiyo ilizusha manung uniko ya watu. Jamii ilianza kugawanyika makundi mawili; manaizi na makabwela. Kitendo hicho ndio chimbuko la kutangazwa kwa Azimio la Arusha. Azimio lilikuja kutoa mwongozo wa maadili ya wanachama na viongozi wa TANU. Kwa hivyo nia ya Azimio la Arusha, miongoni mwa mambo mengine, ilikuwa ni kuwazuia viongozi kutumia uongozi wao kujitajirisha. Hilo ndilo lililokuwa tatizo la hatari miongoni mwa matatizo wakati ule. Azimio lilikuja kuokoa jahazi - kukemea tabia potofu. MIONGOZO MIWILI 119

121 TATIZO LA SASA NI UCHUMI TEGEMEZI Mtu anaweza kuuliza je sasa kuna tatizo gani? Tatizo letu katika miaka ya tisini na kuendelea ni lile la uchumi tegemezi. Tatizo letu sasa ni kwamba uchumi wetu ni duni mno. Wakati idadi yetu inaongezeka, mapato ya Taifa, hasa ya fedha za kigeni, hayaongezeki. Wakati wa Uhuru idadi yetu ilikuwa ni watu milioni tisa. Lakini leo, tuko milioni tisa na tisa tena na nusu ya tisa. Lakini mapato yetu ya pesa za kigeni yapo pale pale, $ milioni 400. Wakati Azimio la Arusha lilitutaka tujitegemee, hali halisi ni kuwa tumekuwa wategemezi wakubwa. Maana Taifa letu hivi sasa, kwa pato lake lenyewe la fedha za ndani, linaweza kujitegemea kwa kipindi cha miezi saba tu katika mwaka. Tunategemea watu wengine, kwa njia ya ruzuku na mikopo, kumalizia miezi mitano inayosalia katika mwaka. Hii ni hatari. Lazima tuendelee kubuni mbinu za kuondokana na hali hiyo. MBINU ZA KUJITEGEMEA Ilani ya Uchaguzi inasema hivi: Makusudi ya Chama katika kipindi cha miaka mitano ijayo ni kwa Taifa kukusanya nguvu zote za wananchi kwa kusaidiana na Serikali zao (Mbili), na kuzitumia katika kila eneo la maendeleo ili kutoa msukumo mpya wa utekelezaji wa siasa ya Ujamaa na Kujitegmea. Hivyo, Chama na Serikali zake zinawajibika kuwarahisishia wananchi wao kujitegemea kwa chakula, kujitegemea kwa mavazi na kujitegemea kwa malazi. Ili kutimiza lengo hilo Taifa lazima liwawezeshe wananchi wake kuzalisha mazao ya biashara na chakula kwa wingi. Pia ni wajibu wa Chama na Serikali kuandaa mbinu za kuwasaidia wananchi kujijengea nyumba zao za kuishi ili ziwasitiri wanapostaafu au kuwa wazee. Je wananchi wakituuliza: hivi ni mbinu gani mlizofanya kumshirikisha kila mmoja wetu kutumia nguvu zake zote katika kuzalisha kama Ilani inavyosema? Tungejibu nini? Lakini sasa kila mwananchi, pamoja na mwana CCM, hataweza kutoa kisingizio kwa kusema:- 120 MIONGOZO MIWILI

122 Mimi sikuweza kutumia nguvu zangu zote katika kufanya kazi ya kuzalisha kwa sababu nimezuiwa na Azimio la Arusha. MWANACHAMA KUCHANGIA UCHUMI KIKAMILIFU Azimio la Arusha lipo. Narudia tena kusema kuwa wanaohusika na tafsiri hii ni wanachama. Sisemi Viongozi, bali wanachama wa CCM. Tunataka kumpa Mwanchama wa CCM, kama mwanachama mwingine yeyote, uhuru zaidi wa kuzalisha ili kuchangia kadiri ya uwezo wake katika pato lake yeye mwenyewe na pato la Taifa kwa jumla. Ili tujitoe, kitaifa, kwenye shimo la utegemezi tulimo hivi sasa, mbinu bora ni kutoa uhuru kwa kila mwananchi wa kila Kaya, wa kila Kata, wa kila Tarafa, wa kila Wilaya na wa kila Mkoa kutumia nguvu zake zote katika kuzalisha. Matokeo ya hatua hii ni kumwezesha kila mtu katika Kaya, Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa kujitegemea. Tukifika hapo ndipo Taifa litapokuwa limeondokana na hali ya sasa ya uchumi tegemezi. KUPANGISHA NYUMBA Jambo la kupangisha nyumba nalitaja tu, kwani si lazima kwa sababu si jipya; hata hivyo ni vyema nalo litajwe. Mwenyekiti Mstaafu alilisemea jambo hili mahali pengi sana, tena alianza zamani kulisemea, sijui. Kwa mfano, hivi karibuni alilitaja tena katika hotuba yake ya kuadhimisha miaka ishirini ya Azimio aliposema hivi: Masharti hayo yanamkataza kiongozi wetu kuishi kikabaila kwa mbinu za kupangisha majumba. Lakini sharti hili halimkatazi mtu mwenye vyumba vya ziada katika nyumba yake anamoishi kuvipangisha kwa watu wengine kwa kodi nafuu, Hili ni jambo la kawaida kabisa katika nyumba zetu za Waswahili na upangishaji huu mimi MIONGOZO MIWILI 121

123 nimekuwa nikiutetea tangu zamani. Utaratibu huu unawasaidia sana watu wenye mapato madogo, wanafunzi, au wafanyakazi ambao bado hawajaoa au kuolewa kupata vyumba vya kupanga kwa kodi nafuu. Ni kweli kwamba huko nyuma tumekuwa wakali mno katika kutafsiri msharti haya. Azimio la Arusha linachokataa ni unyonyaji. Hivyo maskini ya Mungu mwenye kijumba chake cha mbavu za mbwa akimwona maskini mwenziwe anapata taabu, hana pakukaa, asimpangishe? Je akimpangisha atakuwa anamnyonya? Au anamstiri? Kwa hiyo tangu zamani kustiriana ni ruhusa (Makofi). Hatukuishia hapo kule Zanzibar, tulikwenda zaidi, tulisema pia kwamba wapo viongozi miongoni mwetu ambao baadhi yao wamefanya kazi za Chama au za Serikali kwa miaka 30 au zaidi. Lakini hawana nyumba; ukifika wakati wao wa kustaafu viongozi hao huwa wanababaika kwa kutojua wataishi wapi. Ndipo wanapoanza kutafuta mbinu - ndiyo maana siku hizi utakuta misururu mirefu katika Ofisi ya Vyeti vya kuzaliwa. Watu wanakwenda kubadilisha tarehe zao za kuzaliwa, kujifanya bado wangali vijana ili wachelewe kustaafu. (Makofi). Sisi tunaamini kwamba baada ya kipindi kirefu cha utumishi, mtu aweze kuwa na nyumba ili, hata akiwa kipofu angalau aweze kupapasa kuta zake na kusema: Hii ni nyumba yangu niliyoipata kwa jasho langu la kazi ya miaka 30. Tunataka awe na kitu. Lakini, Ndugu Wazee, bahati nzuri wanachama wa CCM, kama wananchi wengine, wanaruhusiwa kukopa. Wanaweza kukopa kwenye benki zetu wakajenga nyumba za kukaa. Sasa jamani tukisema kwamba hata mtu aliyekopa asiipangishe nyumba hiyo atalipia nini huo mkopo? Vinginevyo tutakuwa tunamfanyia mzaha mtu huyo. Maana atachukua mkopo, ajenge nyumba, kisha ashindwe kulipa huo mkopo. Waliomkopesha wataikamata hiyo nyumba na kuiuza ili kurudisha fedha yao. Katika hali hiyo mwana-ccm gani atakayekuwa na nyumba 122 MIONGOZO MIWILI

124 iwapo mwisho wake ni kuchukuliwa na kile chombo kilichomkopesha? Kwa hivyo nasema mtu kama huyu ana dharura; ana dharura ya deni. Amejenga nyumba kwa nia ya kukaa mwenyewe lakini ana deni la mkopo. Kama anaweza kukaa nyumbani mwake, akae. Lakini pia awe na ruhusa ya kupangisha nyumba yake, akitaka, ili imsaidie kulipa mkopo. Anapostaafu awe anayo nyumba ya kumstiri uzeeni. Kitendo hicho kisimpotezee uanachama wake wa CCM. Kwa hivyo Ndugu Wanachama, huko ndiko kwenda na wakati, vinginevyo tutapwelewa. Mtu kama huyu aruhusiwe kupangisha nyumba yake, iwe nusu ya nyumba, ama robo ya nyumba au yote (makofi). BIASHARA YA KUPANGISHA MAJUMBA BADO NI MWIKO Lakini kikao cha Zanzibar hakikutengua miiko ya kiongozi wala ya mwanachama wa CCM. Bado ni mwiko kwao kuwa na biashara ya kupangisha majumba. Kwa mfano, kama kuna mwanachama anayeomba mkopo, akipata anajenga nyumba, halafu anaikodisha, akipata fedha za kodi anajenga nyingine mpya, ambayo nayo anaikodisha na kuendelea kujenga nyingine. Huyo ni mfanyabiashara. Kazi yake ni kujenga na kupangisha majumba. Kikao cha Zanzibar hakikusudii mwanachama wa aina hii. Huyu siye (Makofi). Vile vile, Mwanachama wa CCM, hata akiwa kiongozi katika mazingira maalum, aruhusiwe kukodisha nyumba yake, ikiwa haihitaji kuikaa wakati ule. Inawezekana haihitaji kuishi katika nyumba yake kwa kuwa kapata uhamisho. Mfano, mtu kahamishiwa Iringa kwa kazi wakati nyumba yake iko Dar es Salaam. Je ikae bure watu waitumie bure tu kweli? (Makofi). Ni mwanachama wa aina hii ndiyo tulisema huko Zanzibar kuwa aruhusiwe kupangisha nusu ya nyumba ama robo ya nyumba au yote, maadam mtu huyo anapo pengine pa kukaa. Lakini tunasisitiza kuwa bado si ruhusa kwa mwana CCM wala kiongozi wa CCM kuendesha biashara ya kupangisha majumba. MIONGOZO MIWILI 123

125 HISA KATIKA MAKAMPUNI YA UMMA, KUPUNGUZA UKWASI! La pili lililoamuliwa huko Zanzibar ni kuwaruhusu wanachama wa CCM, kwa kufuatana na hali ya wakati ulivyo, sasa aruhusiwe kuwa na hisa katika kampuni ya Umma. Hii leo tunayo Mashirika ya Umma zaidi ya 400, lakini mengine yao hayana fedha za kuendeshea kazi zao. Mfano kuna mwananchi mmoja alikwenda kwenye kiwanda cha Umma kutaka huduma ya kusafishiwa ngozi zake. Alipofika hapo alikuta pamelala paka ; yaani palikuwa kimya, hapakuwa na kazi yoyote inayofanyika. Kumbe kile kiwanda kilikuwa kimefungwa kwa kukosekana fedha za kukiendeshea... umeme ulikatwa na wafanyakazi walipewa likizo. Meneja alimfahamisha huyo mteja kuwa kiwanda kimefungwa kwa sababu ya deni la maji na umeme pamoja na pesa za mishahara ya wafanyakazi. Huyo mteja alikubali kulipa arubuni (advance) ya milioni saba ili kukikwamua kiwanda. Wiki ya pili yake kiwanda kilianza kufanya kazi zake za kuzalisha kama kawaida. Kisa cha kiwanda hicho kusimama kazi ni kukosa fedha za kuendeshea. Kiswahili cha siku hizi huitwa ukwasi. Kwa hiyo kazi ilisimama. Katika hali kama hii, tumeona ni vyema kuwaruhusu wananchi wote pamoja na wakulima, na wafanyakazi wa shirika lenyewe wakiwemo wanachama wa CCM kununua hisa chache kwa kila atakaetaka. UBIA WA UMMA NA DOLA KATIKA SHIRIKA Narudia, watakaoruhusiwa kununua hisa ni wananchi wowote watakaopenda pamoja na wakulima wa pamba, korosho, kahawa, tumbaku na wafanyakazi wa hilo shirika lenyewe. Kwa njia hiyo, Shirika hilo sasa litapata sura mpya, litakuwa ni la ubia kati ya Serikali, wafanyakazi na wananchi. Fedha tunazozizungumzia hivi sasa, za kulipia taa na mahitaji mengine zingetokana na ununuzi wa hisa ili uzalishaji uendelee. Katika hali kama hiyo kiwanda kitakuwa ni mali ya umma kweli. Maana kuna tofauti ya Shirika la Dola na Shirika la Umma kwa maana ya wananchi wenyewe. 124 MIONGOZO MIWILI

126 Endapo shirika la umma litataka kuwashirikisha wananchi na wafanyakazi wake kwa kulichangia ili kuondoa tatizo la Ukwasi, jambo hilo liwe ni halali, na Mwana CCM naye aruhusiwe kuwa miongoni mwao. (Makofi)..Kilichofanywa na maamuzi ya Zanzibar ni kumruhusu mwanachama wa CCM naye kushiriki kikamilifu katika sera ya Taifa ya uwekezaji wa rasilimali nchini. Katika sera ya uwekezaji rasilimali tunaruhusu ubia katika uchumi wetu. Ubia huo unaweza kuwa baina ya watu wa ndani ya nchi peke yao, au kati ya wawekezaji wa nje na wa ndani. Baada ya kuikubali misingi hiyo hatuoni kwa nini tusianzie kwa kuwaruhusu wananchi, wakulima na wafanyakazi kuwa na hisa katika Mashirika wanayofanyia kazi (Makofi). WAFANYAKAZI KUSIMAMIA UWAJIBIKAJI Nia nyingine ya kufanya hivyo inatokana na kutambua kuwa wafanyakazi wenye hisa katika kiwanda watakuwa wasimamizi wakereketwa wa uwajibikaji katika viwanda hivyo. Watakereketwa zaidi pakiwa na ubadhirifu au kutowajibika. Hivi leo baadhi ya mashirika ya Umma ni mashirika ya umma kwa jina tu. Watu wanayaibia wakidai wanachukua chao. Pengine wanashindana kufanya hivyo ili wasipunjwe. Baadhi ya mashirika ya Umma yanahujumiwa kana kwamba hayana wenyewe. Baada ya maamuzi ya Zanzibar kuanza kutekelezwa, Mashirika hayo yatakuwa na wenyewe. MWONGOZO WA 1981 KUHUSU UWAJIBIKAJI Maamuzi ya Zanzibar si mapya. Mwongozo wa chama wa 1981 umetoa ilani juu ya kupungua kwa uwajibikaji katika Mashirika ya Umma, jambo ambalo hivi sasa tunalitafutia ufumbuzi. Mwongozo wa 1981 unasema hivi: Imezuka tabia ya aibu nchini ambayo imekuwa ikiongezeka ya vitendo vya kuharibu na kuvitumia vibaya vyombo muhimu vya kazi na mali ya umma kwa jumla. Magari, matrekta, zana nyingine muhimu za chama, serikali, mashirika ya umma MIONGOZO MIWILI 125

127 mara nyingi hayadumu muda mrefu kama ambavyo ingetazamiwa kutokana na matumzi mabaya. Lakini ikiwa watu pale pale wenyewe wana hisa katika kampuni au shirika - mfano TANESCO [au] kuwa Mkurugenzi katika kampuni ya Kibepari. Napenda suala hili lieleweke vizuri ili kujibu fikra zilizojengeka kuwa uamuzi huo umevunja Azimio la Arusha. Kwanza inafaa tufafanue maana ya Mkurugenzi. Tafsiri ya Mkurugenzi inayojulikana sana ni ile ya mjumbe wa bodi ya wenye hisa katika Kampuni fulani. Kwa hiyo wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi katika Kampuni ya Kibepari huwa ni miongoni mwa wale wenye hisa zao katika kampuni inayohusika. Watu hao huchaguliwa na wenzao wenye hisa kama wa kuongoza shughuli za Kampuni yao kwa faida ya pamoja. Mkurugenzi wa aina hii hawezi kuwa mwanachama wa CCM. Lakini kuna Mkurugenzi wa aina nyingine ambaye ni tofauti kabisa na Mkurugenzi mwenye mali. Mkurugenzi huyu ni yule ambaye ameajiriwa tu na wenye mali yao, kutokana na sifa zake za utaalam, kuendesha kampuni. Mtu huyu huwa ni mwajiri tu, anayefanya kazi. Huyu ni mtumishi tu kama watumishi wengine, hana chake katika kampuni inayohusika. Anachotegemea ni mshahara wake na marupurupu mengine kama yapo. Huyu ndiye Mkurugenzi anayeruhusiwa kuwa mwanachama wa CCM. Azimio la Arusha bado liko pale pale kwa wale wakurugenzi wa aina ya kwanza. Wao Azimio linawabana, hawawezi kuwa wanachama wa CCM. Lakini huyu wa aina ya pili aliyeajiriwa tu, akija kuomba uwanachama tunamkubali. Azimio la Arusha kamwe halijamkataa mfanyakazi mwenziwao kwa koa la kutumikia Kampuni ya Kibepari, hivyo ndivyo tulivyoamua Zanzibar. MWANA-CCM KUWA NA HISA KATIKA KAMPUNI YA KIBEPARI Jambo jingine ambalo halikueleweka vizuri na linahitaji ufafanuzi ni lile la kumruhusu mwanachama wa CCM kuwa na hisa katika kampuni ya Kibepari. Hili nalo tumeliruhusu huko Zanzibar, lakini sharti iwe katika mazingira maalum. 126 MIONGOZO MIWILI

128 Ni vyema kukumbushana kuwa yapo makampuni ya kibepari ambayo tumekuwa nayo hata kabla ya Azimio la Arusha. Kampuni hizo zimekuwa zikikidhi kiasi fulani cha ajira ya Watanzania, pamoja na Wanachama wa CCM. Ili jambo hili lieleweke vizuri, nitatoa mfano tu wa Kampuni ya mtu binafsi. Mwenye Kampuni ya binafsi anaweza kabisa akaamua kwa hiari yake kuuza baadhi ya hisa kwa wafanyakazi wake ili kuwapa motisha ya kazi. Tajiri yeyote akiamua kufanya hivyo, Chama na Serikali vitamwona kuwa amechukua hatua ya kimaendeleo. Kitendo chake hicho ni halali. Kwa sababu itakuwa ameuzimua ubepari kwa kuifanya kampuni yake ni ya ubia kati yake na wananchi aliowaajiri. Kwa kweli kampuni hiyo itakuwa kama chama cha ushirika. Katika hali hiyo, hata Mwanachama wa CCM anaruhusiwa kupokea/ kununua hisa alingane na wafanyakazi wenzie. Ni mazingira maalum ya namna hii tu ndiyo yanayoruhusu Mwanachama wa CCM, kama mfanyakazi mwingine, kuchukua hisa katika Kampuni anayofanyia kazi. Atakapostaafu ataweza kuendelea kupokea faida ya hisa yake au kuiuza. MISHAHARA MIWILI KWA MWANA-CCM Kuhusu mishahara miwili, Azimio la Arusha linasema hivi: Kwamba kila mtu anayo haki ya kupata malipo ya haki kutokana na kazi yake. Kufuatana na ukweli huo, anayefanya kazi mbili za halali anastahiki kupata malipo ya kazi ya pili. Tuchukue mfano wa Profesa ambaye mchana kutwa anasomesha Chuo Kikuu. Baada ya saa za kazi anaweza kuamua kufanya kazi ya akili, kwa mfano kutoa ushauri au kuandika mradi kwa aliyemwomba huduma hiyo. Mwanachama huyo atastahiki kupata malipo ya kazi hiyo. Hili si geni, katika sherehe za kuadhimisha miaka 20 ya Azimio la Arusha, baba wa taifa alisema hivi: MIONGOZO MIWILI 127

129 Lile sharti la kutopokea mishahara miwili kwa kweli ni sharti la tahadhari tu. Ni vigumu sana kufanya kazi mbili za kuajiriwa na zote mbili ukazifanya vizuri. Huwezi kuwatumikia mabwana wawili! Lakini sharti hili halimkatazi kiongozi wetu kujiongezea pato kwa kutumia muda wake wa kupumzika kwa kufanya shughuli nyingine: kama kulima au kufuga, ikiwa yeye si mkulima au mfugaji, kuandika, kufanya kazi ya useremala, au kufanya shughuli nyingine yoyote kwa mikono yake au kwa ajili zake. Jambo la msingi ni kwamba lazima twende na wakati. Mwaka 1967 lilipotungwa Azimio la Arusha ilikuwa hakuna haja ya kuwa na mishahra au malipo ya kazi zaidi ya moja kwa sababu wakati ule mshahara mmoja ulikuwa unatosha kukidhi mahitaji yote muhimu. Kwa mfano, mimi, mwenyewe, mshahara wangu wakati ule ulikuwa shilingi 2,200/= kwa mwezi. Mshahara huo, hasa kwa Zanzibar, ulikuwa ukinitosha kukidhi mahitaji yangu yote ya lazima. Wazee wangu watakumbuka kwamba wakati ule kule kitunguu, pilipili na bizari - vyote hivyo kwa senti tano tu. Ilikuwa inawezekana pia kununua samaki mkubwa kiasi kwa senti ishirini mpaka 50 tu; au kununua kuni za kuweza kupikia mlo mzima kwa senti kumi tu. Siku hizo iliwezekana mnunuzi kujaziwa mafuta ya kupikia au samli kikombe kizima kwa senti ishirini au sitini tu. Halikadhalika kwa senti ishirini tu mtu aliweza kununua matunda, kama vile fungu la ndizi mbivu au machungwa au papai. Kwa ufupi, kwa mahitaji ya siku nzima, tangu asubuhi hadi jioni, iliwezekana mtu kutumia pesa kidogo sana. Katika hali hiyo, kulikuwa hakuna ulazima wa kufanya kazi ya pili. Afanyae kazi zaidi ya moja huonekana ni mlafi au ana tamaa. Kwa mshahara huo huo niliweza kudunduliza pesa na mwishowe kununua gari mpya kabisa. Gari hilo lilinigharimu pesa nyingi kwa wakati huo - shilingi 13,000/=!! Wakati huo bei ya mafuta nayo ilikuwa shilingi tatu tu kwa galoni zima. Katika mazingira ya aina hii mshahara mmoja ulimudu kukidhi mahitaji ya wafanyakazi wengi ukiacha walevi. 128 MIONGOZO MIWILI

130 HALI IMEBADILIKA Lakini leo mambo yamebadilika. Gharama ya maisha imepanda sana. Serikali yenyewe imeungama waziwazi kuwa haina uwezo wa kumlipa mfanyakazi wake mshahara unaomwezesha kumudu gharama za maisha. Kutokana na hali hiyo, wafanyakazi wengi, wanashindwa kukidhi mahitaji yao muhimu. Ndio maana Chama na Serikali yake vimekuwa vikiwahimiza wafanyakazi kufanya shughuli nyingine za halali, baada ya saa za kazi, ili kujiongezea mapato. Mfano wa kazi hizo ni kama vile: kutibu, kuandika vitabu, kuandika mradi, kutoa ushauri wa kitaalamu, kufundisha, overtime, useremala, ufundi bomba, ufundi umeme, ufundi cherahani, kilimo, ufugaji, kuziba mipira ya magari, kuteka maji ya kuuza, kupiga matofali, kutengeneza baiskeli na kadhalika. KOFIA MBILI MSHAHARA MMOJA Lakini lazima tuelewane kuwa hii mishahara miwili tunayozungumzia haimhusu kiongozi mwenye kofia mbili. Kwa mfano, Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya, ambao vile vile ni Katibu wa Chama wa Mkoa au Wilaya, hawaruhusiwi kupokea mishahara miwili. Hawa watalipwa mshahara mmoja tu, maana hii kazi ya pili ni sehemu tu ya ile ya kwanza. Lakini wanaruhusiwa kufanya kazi za ziada kama vile kilimo, ufugaji na kadhalika, baada ya saa za kazi, kama walivyoruhusiwa wafanyakazi wengine. Hapa nitapenda kusisitiza kuwa wale watu wanaoeneza maneno ya kejeli kuwa ati Maamuzi ya Zanzibar ni mbinu tu za wakubwa kujinufaisha wenyewe, ijulikane kuwa si kweli. Kazi zilizoorodheshwa hapa si za wakubwa bali ni kazi zinazoweza kufanywa na kila mtu kufuatana na ujuzi alionao na mazingira ya mahali anapofanyika kazi. MWANA-CCM MKULIMA NA MFUGAJI Watanzania wengi ni wakulima, wakulima ndio wengi zaidi. Mkulima kwa maana pana ni pamoja na mfugaji. Katika siku za nyuma, baadhi ya wanachama waliwahi kutiwa msukosuko kwa kuwa na mashamba makubwa au kufuga kuku 500. Lakini baadaye Chama kilijisahihisha kama inavyosema Programu ya Chama: MIONGOZO MIWILI 129

131 Chama Cha Mapinduzi ni Chama kinachokua (haikudumaa). Kinakaa katika nadharia na falsafa yake, (ili kwenda na wakati). Hii ndio ilivyokifanya Chama kijisahihishe kila kinapokosea. Kwa hiyo kama siku moja tulimtia mwenzetu msukosuko kwa kuwa na shamba kubwa, mbuzi 18 au kuku 500, sasa Chama kimekua katika falsafa yake. Falsafa ya sasa inatia maanani hali halisi ya wakati wa sasa. Ndio maana kule Zanzibar tukaruhusu kiongozi awe na shamba lisilozidi hekta 20, hasa kama shamba hilo limo katika eneo la kijiji. Kuhusu ufugaji, kuna baadhi ya wenzetu katika makabila ya Tanzania ambao kwao ni utamaduni wao kuwa na ng ombe wengi. Mfano mzuri ni wenzetu wa makabila ya Wamasai, Wasukuma na Wagogo. Je, mwenye utamaduni wa kumiliki ng ombe wengi akataliwe katika Chama kwa sababu ya kumiliki ng ombe wengi? Tunasema hapana. Akiomba uanachama wa CCM akubaliwe. Chama Cha Mapinduzi hakimkatai tajiri aliyepata utajiri wake kwa njia ya halali na kulipa kodi ya Serikali analipa. Anayekataliwa na CCM ni yule aliyepata utajiri kwa wizi, kwa rushwa, dhuluma na kwa njia nyingine za haramu. Huko Zanzibar tulifikiria labda tuweke kiwango maalum cha mifugo, kama vile iwe mwisho ng ombe 200 peke yake. Lakini tulijiuliza kama ng ombe mmoja akizaa na jumla kufikai 201, je huyo ndama amnyonge shingo? Hiyo ndio hali halisi iliyotufanya tukubaliane kuwa mfugaji yeyote anaetaka kuwa mwanachama bila ya kujali idadi ya mifugo yake. Mwenye mshahara mkubwa, vile vile hata wa malaki, maadam ni mshahara wa kazi halali, naye pia aruhusiwe kuwa mwanachama wa CCM. MAFUNZO YA MIEZI MITATU Ili kukiimarisha zaidi Chama, tumewaruhusu wananchi kuwa wanachama wa CCM bila ya kuhudhuria yale mafunzo ya miezi mitatu. 130 MIONGOZO MIWILI

132 BIASHARA NDOGO NDOGO Huko Unguja hatukuishia hapo. Tuliamua kuwa Mwanachama wa CCM wa kawaida naye pia aruhusiwe kuwa na biashara ndogo ndogo ili kumwongezea kipato. Biashara hizo, ambazo sharti zifanywe baada ya saa za kazi, ni pamoja na uvuvi, kuwa na gari ndogo au pick-up ya kukodisha kwa kuchukulia abiria au mizigo, kushona, kusindika matunda, mafuta na mashine ya kukoboa au kusaga unga. Mwanachama mwenye mashine ya kusaga unga hanyonyi bali anatoa huduma kwa jirani zake kijijini. Chama na Serikali vimo mbioni kuhimiza na kutafuta teknolojia ya kumrahisishia kazi Mtanzania, hasa wanawake. Ni vyema kukaribisha teknolojia ya kuwasaidia wanawake waondokane na kufanya kazi ngumu ngumu zinazoweza kuwapotezea wakati na kuathiri afya zao, kama vile kutwanga au kusaga nafaka, kubeba mizigo ya kuni, maji na mtoto mgongoni. Si vyema kwa jamii yetu kuingia katika karne ya ishirini na moja katika hali hiyo. Ndio maana kule Zanzibar tuliamua kuruhusu biashara ndogo ndogo kuendeshwa na mwanachama wa CCM kwa manufaa yao na ya jamii. Ndugu Wazee, haya kwa muhtasari ndio yaliyoamuliwa Zanzibar. Haya kamwe hayabomoi Azimio la Arusha, badala yake yanaliimarisha. Azimio la Arusha ni msingi wa siasa yatu ya Ujamaa na Kujitegemea. Ili tuweze kujitegemea lazima tuandae mbinu na mikakati ya kuzalisha mali, huduma na chakula. Hili ndio lengo la maamuzi ya Zanzibar. Mshairi mmoja amesema:- Kutaraji uongofu bila kupitia njia zake ni kama kulitaka jahazi kutembea nchi kavu. Ndugu Wazee Ahsanteni sana. (Makofi) MIONGOZO MIWILI 131

133 SURA YA TANO Miongozo Miwili ya Chama na Tabaka Lililopindua Ujamaa* Issa Shivji Mwongozo wa TANU, 1971 Chama cha TANU kilichopigania uhuru wa Tanganyika chini ya uongozi wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ndicho kilichoasisi Azimio la Arusha mwaka wa Azimio liliweka mtazamo na sera za Ujamaa na Kujitegemea. Wakati ule nyaraka mbalimbali ziliandaliwa na kuandikwa ili kutoa miongozo katika kutekeleza Azimio la Arusha. Waraka muhimu mmojawapo ni Mwongozo wa TANU wa Mwongozo huo una umuhimu wa kipekee katika historia ya siasa za Tanzania. Mambo muhimu matatu yamezungumziwa katika Mwongozo huo. Mosi ni kutambua kwamba ubeberu unaendelea kunyanyasa na kunyonya Waafrika hata baada ya ukoloni kupitia sura yake mpya ya ukolonimamboleo. Kutokana na ukweli huo, Vyama vya Siasa vya kimapinduzi katika nchi nyingi za Afrika zinazojitawala, kama vile TANU, bado vingali ni Vyama vya Ukombozi. Pili ni umuhimu na ulazima wa kuunda jeshi la mgambo ambalo litalinda uhuru wa nchi dhidi ya maadui. Chimbuko la uamuzi huo linajulikana. Tanzania ilikuwa mstari wa mbele kusaidia ukombozi wa nchi za Afrika ambazo bado zilikuwa chini ya ukoloni. Wapigania uhuru ambao walikuwa wanasaidiwa na Tanzania moja kwa moja walikuwa wale wa Afrika ya Kusini, Namibia, wakati ule ikiitwa South West Afrika, na Msumbiji ambayo ilikuwa chini ya ukoloni katili wa Wareno. Huko Afrika ya Magharibi, nchi mojawapo ambayo ilifanana sana na Tanzania katika sera zake na hasa katika kusaidia wapigania uhuru ilikuwa Guinea-Conakry chini ya uongozi wa Sekou Toure. Wapigania * Makala hii yalichapishwa mara ya kwanza katika jarida la Chemchemi, toleo na. 2, Oktoba, Imesahishishwa kwa ajili ya kitabu hiki. 132 MIONGOZO MIWILI

134 uhuru wa Guinea-Bissau na Cape Verde, ambazo zilikuwa nchi moja wakati huo, chini ya uongozi shupavu wa Amilcar Cabral, walisaidiwa na Sekou Toure. Kutokana na nafasi ya Guinea-Conakry katika vita vya ukombozi, majeshi ya Wareno yalivamia Guinea-Conakry. Hata hivyo hawakufanikiwa kwa sababu Guinea-Conakry iliweza kuwashinda, hasa kutokana na jinsi wanamgambo walivyopigana kwa ujasiri na ushupavu. Isitoshe, karibu na nyumbani, Rais Obote wa Uganda alipinduliwa na jeshi lake chini ya Idi Amin Dada akisaidiwa na Uingereza na Israeli. Hii ilitokea baada ya Obote kutangaza kasiasa ka kijamaa na pia kuunga mkono nchi zilizokuwa mstari wa mbele katika ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika ambazo bado zilikuwa zinatawaliwa na wakoloni na makaburu. Mambo haya yote mawili ni wazi yalikuwa tishio kwa Tanzania. Tanzania pia ilikuwa na wasiwasi wa kuvamiwa na jeshi la Wareno. Ndio maana chama na serikali waliamua kuwa na jeshi la wanamgambo. Jambo hili ni la kwanza linalozungumziwa katika Mwongozo wa Tanu wa Pia, Tanzania ilikuwa haipendwi na mabeberu kutokana na siasa zake za kijamaa. Pamoja na mambo haya, sifa moja ya Mwongozo ni uchambuzi wake wa radikali wa hali halisi ambao unaufanya Mwongozo kuwa nyaraka ya kimapinduzi zaidi kuliko zote zingine zilizoandikwa wakati wa enzi za Azimio la Arusha. Mfano mmoja tu unatosha kudhihirisha hili. Mapinduzi ni mabadiliko ya haraka katika jamii, mabadiliko ambayo yanawanyang anya wachache madaraka ambayo walikuwa wakiyatumia kwa manufaa yao (na ya wanyonyaji wa nje), na kuyaweka madaraka hayo mikononi mwa wengi ili kuendeleza maslahi yao. Katika hili, Chama chini ya uongozi wa Mwalimu, kwa mara ya kwanza, umeweka wazi maadui wa Mapinduzi ya kijamaa, wakiwa vibaraka wa ndani wakiungwa mkono na wanyonyaji wa nje kwa maana ya mabepari wa kimataifa kutoka nchi za kibeberu. *** MIONGOZO MIWILI 133

135 Lakini zaidi ya yote jambo ambalo lilifanya Mwongozo uwe na historia ya kipekee ni ibara ya 15 ya Mwongozo. Ibara hii inasema: Lazima iwepo jitihada ya kujenga hali ya usawa kati ya viongozi na wanaowaongoza. Iwe ni mwiko kwa kiongozi wa Tanzania kuwa mwenye majivuno, ubadhirifu, dharau na uonevu. Kiongozi wa Tanzania awe ni mtu anayeheshimu watu, asiwe ni mpenda makuu, sio mnyapara, mkaripiaji na muamrishaji watu. Ibara hii ikawa kauli mbiu na itikadi ya tabaka la wafanyakazi dhidi ya menejimenti yao viwandani. Takribani miaka minne kufuatia kutangazwa kwa Mwongozo, kuliibuka vuguvugu la wafanyakazi ambalo lilikuwa halijawahi kutokea katika historia ya nchi. Katika kipindi kifupi cha miaka mitatu tu ( ), kulikuwa na migomo zaidi ya 30, ambayo ilihusisha wafanyakazi takriban 23,000 na siku za kazi zilizopotea ni takriban 64,000. Kwa kasi kubwa sana wafanyakazi walijifunza mikakati na mbinu za mapambano ya kitabaka. Walianza na migomo ya kawaida kwa maana ya kuweka chini zana za kazi. Kutokana na kulaumiwa kwamba wafanyakazi walikuwa hawajali maslahi ya taifa, wafanyakazi wakabadili mbinu zao katika awamu ya pili. Badala ya kugoma, wakaanza kuwafungia nje wanyapara na wamiliki wa viwanda wakati wakiendelea na uzalishaji. Lakini kama unaweza kuzalisha bila menejimenti, kwa nini ukubali menejimenti? Kwa hivyo, mapambano yakakoma na wafanyakazi wakaanza kutwaa viwanda. Hapo ndipo, watawala wa kisiasa na kiuchumi wakashtuka. Viongozi wa chama na serikali wakaanza kuwashutumu wafanyakazi wazi wazi kwa kusema kwamba ingawa chama kilikuwa na sera ya kutaifisha viwanda hii haikuwa na maana kwamba wafanyakazi wenyewe waanze mtindo huo. Utaifishaji lazima ufuate taratibu na ustaarabu! Katika hotuba ya Mei Mosi (ya mwaka wa 1974) yenye kichwa cha habari Ukigoma unamgomea nani? Mwalimu aliwashutumu wafanyakazi, jambo 134 MIONGOZO MIWILI

136 ambalo mara moja lilivunja nguvu za wafanyakazi. Hotuba ya Mei Mosi ikawa mwongozo wa menejimenti au warasimu, nao walifurahia sana. Kwa kweli, vuguvugu la wafanyakazi lilikuwa mapambano ya kitabaka dhidi ya tabaka la warasimu. Katika makala yangu ( The Silent Class Struggle au Mapambano Baridi ya Kitabaka) iliyochapishwa na jarida la kimapinduzi la wanafunzi wanamapinduzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Cheche, nilifanya uchambuzi na nikaliita tabaka hili jipya mabepari wa kirasimu (bureaucratic bourgeoisie). Baada ya mwaka mmoja nikaandika makala ya pili ambayo hatimaye ilichapishwa kama kitabu, kwa jina la Class Struggles in Tanzania (Mapambano ya Kitabaka Nchini Tanzania). Wakati ule watu wachache sana waliweza kukubaliana na uchambuzi wangu na viongozi walibeza kwamba Tanzania ni nchi ya wakulima na wafanyakazi na hakuna matabaka. Kwa kiasi fulani, kulikuwa na ukweli humu kwa sababu matabaka bado yalikuwa katika uchanga wake, yalikuwa hayajakomaa hasa kutokana na sera mbalimbali za Mwalimu za kuzuia viongozi na warasimu wasijilimbikizie mali (kwa mfano kwa kupitia katika Miiko ya Uongozi). Kwa hivyo, nguvu ya tabaka la wafanyakazi ikavunjika na hatimaye kwa sheria ya 1975, wafanyakazi wakawekwa chini ya chama cha NUTA (National Union of Tanganyika Workers) ambacho kwa vyovyote vile kilikuwa chini ya himaya ya chama tawala. Kwa upande mwingine, sera ya Chama juu ya vijiji vya ujamaa pia ikatekwa na wenye jazba na wapiga debe katika Chama. Mtazamo wa Ujamaa Vijijini ambao ulisisitiza kwamba vijiji vya ujamaa viwe chaguo la hiari la wakulima wenyewe ukageuzwa. Sera ukawa vijiji vya maendeleo na wanakijiji wakalazimshwa, mara nyingine chini ya ulinzi na mabavu ya FFU (Field Force Unit) kuhamia katika vijiji vya maendeleo. Jambo hili lilifanya wakulima waanze kupoteza imani na Chama. Kwa ufupi basi, matabaka ya wafanyakazi na wakulima wakafarakanishwa na kutenganishwa na Chama, na kwa kiasi fulani Mwalimu mwenyewe. Kwa upande mwinigine, kuvunjika kwa nguvu za wavujajasho, kukasafisha njia kwa warasimu na wamangimeza wa Chama na Serikali, kuendelea kujilimbikizia madaraka (na hata mali angalau kwa kificho) na kujijenga MIONGOZO MIWILI 135

137 kama tabaka jipya la vibepari chini ya himaya ya ubeberu. Hawa ndio hatimaye wakaja kuainishwa kwa ufasaha kama wapingamapinduzi katika Mwongozo wa Mwongozo wa CCM, 1981 Kipindi cha mwisho cha Mwalimu Nyerere ( ) kilikuwa kigumu kuliko vyote katika utawala wake. Hali ya uchumi ilidorora kutokana na sababu mbalimbali za ndani na nje, pamoja na vita vya Uganda, ambavyo viliigharimu nchi sana; kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kupanda kwa bei za petroli. Mnamo 1981, Chama tawala, wakati huo CCM, kilifanya tathmini ya miaka 14 ya Azimio la Arusha na kiliainisha hali halisi ya siasa, jamii na uchumi. Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Chama kufanya uchambuzi wa kina bila ya kujali maslahi yake ya muda mfupi. Kwa maoni yangu, hoja ambayo ni nzito katika uchambuzi huo ni kwamba chini ya mwavuli wa Azimio la Arusha na sekta ya umma, hususan mashirika ya umma, lilijengeka tabaka jipya la mabepari. Mwongozo unasema: Kwani ukweli unaojitokeza wazi wazi ni kuwa baadhi ya matatizo yetu ya uchumi yanatokana na kutotekeleza kwa dhati siasa ya Ujamaa na Kujitegemea vijijini na katika sekta ya umma tuliyoianzisha. Zaidi ya hivyo, wakati mwingine katika miaka kumi na minne tangu Azimio la Arusha, Chama, Serikali, na vyombo vyake vilitumika kukuza sekta ya kibepari nchini katika viwanda, biashara, usafirishaji, ujenzi na kadhalika na ubepari huo uliopanuka katika kipindi hiki umeimarisha vitendo vya kuivuruga na kuidhoofisha sekta yetu ya Umaa (ib. 35). Sehemu nyingine, Mwongozo unaendelea kueleza kwa ufasaha mkubwa kwamba: 136 MIONGOZO MIWILI

138 Leo ubepari una vishawishi vingi zaidi nchini kuliko ulivyokuwa kabla ya Azimio la Arusha kwa sababu pamoja na kwamba sasa tuna sekta kubwa ya umma lakini kutokana na udhaifu wa kutopambana nao, ubepari umefaulu kujipanua na kujipenyeza hata ndani ya sekta yenyewe ya umma. Na ndio maana ubepari sasa unathubutu kujitokeza hadharani kuukashifu Ujamaa, kubabaisha baadhi ya viongozi na kututaka tubadilishe siasa yetu (ib. 52). Kwa hakika matamko haya yalikuwa ni kukiri wazi wazi kwamba sera za Ujamaa zilikuwa zimehujumiwa na viongozi wenyewe waliopewa jukumu la kuongoza ujenzi wa Ujamaa kutokana na maslahi yao ya kitabaka ya kibepari. Hapa tunashuhudia kwa mara ya kwanza, Chama kikikiri kwamba kuna mapambano au harakati za kitabaka dhana ambayo kila mara Chama, na hasa Mwalimu mwenyewe, alikuwa anaikanusha. Kinadharia na kiitikadi Mwalimu hakukubaliana kabisa na dhana ya mapambano ya kitabaka. Hata hivyo ibara ya 50 ya Mwongozo inaenda mbali zaidi kwa kueleza kwamba: Kuielewa vema jamii ya Tanzania ya leo kunataka uchambuzi wa hali ya juu pia. Uchambuzi huu ukiwezeshe Chama kuielewa migongano ya maslahi ya tabaka ambayo imejitokeza nchini. Migongano hii ina mizizi katika mgongano wa msingi kati ya Ujamaa na ubepari, kati ya maslahi ya wakulima na wafanyakazi kwa upande mmoja, na ya ubinafsi, ubwanyenye na ubepari ambao umekuwa ukijengeka tangu Azimio la Arusha kwa upande mwingine. Uchambuzi huo ni wazi na umefanywa kwa ufasaha na kisayansi. Swali muhimu kwa wasomi, wanazuoni na wakereketwa wa Usoshalisti ni: Je, Chama kilifanikiwa katika mapambano haya na kurudisha nchi kwenye Ujamaa? Au tabaka hili liliojengeka lilishinda mapambano na MIONGOZO MIWILI 137

139 ndilo injini inayosukuma gurudumu la mageuzi ya kisiasa na kiuchumi kuelekea kwenye uliberali mamboleo, ambao ni mfumo wa kibepari? Je, tabaka hilo la mabepari warasimu ndilo hasa chimbuko la mfumo huo wa ubepari uchwara, ukiungwa mkono na ubeberu, na ambao ndio unatutawala leo? Je, si kweli kwamba, katika awamu hasa ya tatu tabaka hili la mabepari warasimu ndilo lililokuwa mstari wa mbele kutetea ubepari wakimnukuu kwa furaha Deng Tsio-Ping, kiongozi wa China, aliyepindua ujamaa nchini China? Katika mahojiano yake na mwandishi wa habari Jonathan Power wa jarida la Prospect (na. 112, Julai 2005), Rais mstaafu Benjamin Mkapa alikiri kwamba yeye alikuwa anamheshimu Deng Tsio-Ping. Alipoulizwa na Jonathan Power kwamba je, Nyerere akifufuka angesemaje, Mkapa akamjibu: Angesema kwamba mimi nimegawia mengi yaliyokuwa katika sekta ya umma. Na angefadhaishwa na ukweli kwamba mimi nimefanikiwa kujenga tabaka la mabepari matajiri. Sina hakika kama Rais Mkapa alifanikiwa kujenga tabaka la mabepari matajiri au alijenga tabaka la vibepari uchwara tu. Ni suala la kutafiti. Haikuwa nia yangu kuangalia suala hili kwa undani bali ni kudokeza tu kwamba kama tunataka kuelewa vema na kisayansi hali halisi ya nchi na jamii yetu ya leo hatuna budi kufanya uchambuzi wa kitabaka katika mfumo wa ubepari uchwara chini ya utawala wa kibeberu, hususan, tabaka lililoongoza mageuzi. Na hoja yangu ni kwamba Mwongozo wa CCM wa 1981 unatuweka mahali pazuri pa kuanzia. Kazi kwetu! Ni jukumu la wasomi na wanazuoni kuchambua jamii yao, kuonyesha jamii sura yake halisi na kuainisha mielekeo ya maendeleo na mielekeo ya wapingamendeleo. Kama Mwongozo wa 1981 unasema : mapinduzi sio lelemama. Mapinduzi yanahitaji wakereketwa wa kijamii ambao msimamo wao kwa upande wa wavujajasho hautetereki: Ujenzi wa ujamaa si lelemama bali ni mapambano, mapambano ya kudumu dhidi ya ubepari na unyonyaji, dhidi ya wapinga maendeleo na wababaishaji wa kisiasa, dhidi ya wahujumu uchumi, majambazi, 138 MIONGOZO MIWILI

140 wezi, wazururaji na wazembe. Msimamo sahihi wa mapambano unaotokana na nadharia sahihi ya ujamaa ungelituepusha na maamuzi na vitendo ambavyo vimerahisisha kuoteshwa kwa mizizi ya ubepari, kinyume cha msimamo wa mapambano dhidi ya ubepari. Leo ubepari, una vishawishi vingi zaidi nchini kuliko ulivyokuwa kabla ya Azimio la Arusha kwa sababu pamoja na kwamba sasa tuna sekta kubwa ya umma lakini kutokana na udhaifu wa kutopambana nao, ubepari umefaulu kujipanua na kujipenyeza hata ndani ya sekta yenyewe ya Umma. Na ndiyo maana ubepari sasa unathubutu kujitokeza hadharani kuukashifu ujamaa, kubabaisha baadhi ya viongozi na kututaka tubadilishe siasa yetu. (ibara ya 52) Ukweli uliojitokeza tangu uchambuzi huo wa Mwongozo wa 1981, ni kwamba ubepari ukisimamiwa na vibepari uchwara wa ndani na nchi za kibeberu (ambao siku hizi wanaitwa eti wabia wetu wa maedeleo) ukashinda katika mapambano. Chini ya visingizio mbalimbali, pamoja na fikra hafifu ya kwenda na wakati, Azimio likapinduliwa na uliberali mambo-leo ukashinda. MIONGOZO MIWILI 139

141 Marejeo Mapolu, Henry. (mh.), (1976), Workers and Management, Dar es Salaam, Tanzania Publishing House. Mapolu, Henry na Issa Shivji. (1984), Vuguvugu la Wafanyakazi Nchini Tanzania, Kampala, Urban Rural Mission. Mihyo, P. (1975), The Struggle for Workers Control in Tanzania, Review of African Political Economy, No.4. Shivji, Issa G. (1976), Class Struggles in Tanzania, Dar es Salaam, London & New York, Tanzania Publishing House, Heinemaan and Monthly Review. Shivji, Issa G., (1970), Tanzania : The Silent Class Struggle (Cheche 1970) na kuchapishwa tena katika Issa G. Shivji (mh.) na wengine : The Silent Class Struggle, (1972), Tanzania Publishing House. 140 MIONGOZO MIWILI

142

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited

More information

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited

More information

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)] This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)

More information

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania

More information

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari

More information

HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU 9 DESEMBA 2011.

HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU 9 DESEMBA 2011. Saint Augustine University of Tanzania From the SelectedWorks of Daudi Mwita Nyamaka Mr. Winter December 9, 2011 HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU

More information

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo

More information

Kutetea Haki za Binadamu

Kutetea Haki za Binadamu Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and

More information

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria; HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri

More information

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh

More information

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu: Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200

More information

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika

More information

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA

More information

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano. HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,

More information

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau

More information

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Songa kwenye kilele cha upeo Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa United Republic of Tanzania Photos provided

More information

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya

More information

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012

More information

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA

More information

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017

More information

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA

More information

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi 3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi

More information

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha

More information

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) 102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi

More information

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality

More information

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0

More information

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA

More information

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2

More information

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI

More information

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa

More information

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.

More information

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi

More information

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni

More information

K. M a r k s, F. E n g e l s

K. M a r k s, F. E n g e l s W a (any a kazi wa nchi zote, unganeni! K. M a r k s, F. E n g e l s Maelezo ya chama cha kikomunist Idara ya Maendcleo Moscow Tafsiri hii ya "Maelezo ya Chama cha Kikomunist" inatokana na maandishi

More information

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted

More information

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana

More information

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya

More information

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to

More information

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia HakiElimu & Policy Forum KUUELEWA MCHAKATO.indd a 1/20/10 11:00:56 AM KUUELEWA MCHAKATO.indd b 1/20/10 11:00:57 AM Kuuelewa Mchakato wa

More information

Human Rights Are Universal And Yet...

Human Rights Are Universal And Yet... Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) Dar es Salaam Oktoba 2007 YALIYOMO ORODHA YA VIFUPISHO DIBAJI SHUKRANI MUHTASARI RASMI SURA

More information

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( ) JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI (2008 2012) TOLEO LA PILI Dar es Salaam, Oktoba, 2007 i ii JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI

More information

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA

More information

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa

More information

Je! imezingatia maslahi ya mkulima mdogo?

Je! imezingatia maslahi ya mkulima mdogo? Toleo NO. 044 Januari Machi 2014 Bei Shs. 500/= ISSN 0856-5937 Rasimu ya katiba mpya: Je! imezingatia maslahi ya mkulima mdogo? Yaliyomo Uk. 9 Uk. 11 Uk. 13 MVIWATA yapata wawakilishi wawili ndani ya Bunge

More information

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for

More information

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya

More information

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...

More information

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Spika,

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Spika, HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI KATIKA WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, WASANII NA MICHEZO, MHESHIMIWA JOSEPH OSMUND MBILINYI (MB), KUHUSU BAJETI YA WIZARA HIYO KWA MWAKA WA FEDHA

More information

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya

More information

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

SautiElimu. Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA

More information

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika

More information

Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,

Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo, HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, KWENYE SHEREHE YA KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA, TAREHE 08 JUNI 2008, MSIMBAZI CENTRE, DAR ES SALAAM Mhashamu

More information

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini

More information

Mwongozo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato

Mwongozo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato Mwongozo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato 1 Mafungu yote yaliyonukuliwa kwa ruhusa kutoka katika Biblia ya Kiswahili Union Version 1952 (Ilishahihishwa 1989) ISBN 978 Haki miliki 2013 Haki zote zimeifadhiwa

More information

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3

More information

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu

More information

Shabaha ya Mazungumzo haya

Shabaha ya Mazungumzo haya Karibu Katika Mazungumzo Kuhusu Mchakato wa Uhamasishaji Maendeleo ya Kanisa na Jamii CCMP/UMOJA Shabaha ya Mazungumzo haya Kuwafahamisha viongozi wa makanisa kuhusu Mchakato wa CCMP ambao umekuwa ukitumika

More information

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI MFUMO WA TATHMINI WA TAARIFA (IRM): TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI 2014 2016 Ngunga Greyson Tepani Mtafiti wa IRM Taarifa ya Mwishoni mwa Utekelezaji 2014-2016 First End-of-Term Report INDEPENDENT

More information

April 14, 2016 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 52

April 14, 2016 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 52 MOMBASA COUNTY ASSEMBLY HANSARD REPORT Thursday, 14 th April, 2016 The House met at 2.48pm. (Hon. Deputy Speaker (Mr. Mswabah Rashid) in the Chair) PRAYERS Hon. Deputy Speaker (Mr. Mswabah Rashid): Kindly

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT

HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT. HUSSEIN ALI MWINYI (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA KWA MWAKA 2015/16 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika,

More information

wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.

wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine. HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWENYE IBADA YA KUWEKWA WAKFU NA KUINGIZWA KAZINI ASKOFU MARTIN FATAELI SHAO WA DAYOSISI YA KASKAZINI YA KANISA LA

More information

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo: HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban

More information

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini

More information

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke- Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa

More information

Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira

Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kiongozi hiki kimeandaliwa kikiwa ni sehemu ya mradi wa

More information

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam

More information

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika (A Summary Of Arguments For And Against Individual Communion Cups) Na J D Logan Communion Cups) 1 Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi

More information

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition

More information

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level * 899145 4 672* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2010 Additional Materials: Answer Booklet/Paper READ

More information

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa

More information

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa

More information

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda

More information

United Pentecostal Church June 2017

United Pentecostal Church June 2017 Kwa Nini Tusali? Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa "Chagua" Ladies Prayer International kwa Facebook United Pentecostal Church June 2017 Tuko na wafuasi Facebook katika Marekani, Hong Kong, Philippines,

More information

BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE. Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE. Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na. JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3

More information

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE. Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE. Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006 Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006 (Ulianza Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta)

More information

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ukristo leo unadhihirisha waumini karibu bilioni mbili katika maelfu ya madhehebu tofauti na tofauti na madhehebu. Kati ya hizi, zaidi ya 500 madhehebu

More information

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu

More information

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump

More information

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)

More information

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma

More information

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi PAN AFRICAN PARLIAMENT PARLEMENT PANAFRICAIN البرلمان PAN- PARLAMENTO األفريقي AFRICANO Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi Julai 21 22, 2011 Bunge la

More information

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa

More information

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized!. viromen-alsc:a.. Environmental & Social MRADI WA UMEME WA GESI YA * Assessment & Management

More information

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya Jina Nambari.. Shule... 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI / AGOSTI. 2007 MUDA: SAA 2 ½ MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya 102/3 KISWAHILI FASIHI

More information

KATIKA UCHAGUZI MKUU HUU TUSIRUHUSU MAFISADI WALICHEZEE TAIFA

KATIKA UCHAGUZI MKUU HUU TUSIRUHUSU MAFISADI WALICHEZEE TAIFA KATIKA UCHAGUZI MKUU HUU TUSIRUHUSU MAFISADI WALICHEZEE TAIFA Edward Lowasa ni balaa kwa Taifa! Democratic Party (DP) inatarajia kufikisha Mahakamani chama cha CCM pamoja na wanachama wake sita, Edward

More information

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY

More information

KUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA

KUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA KUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA BIBIANA MASSAWE AMBROSE TASINIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SHARTI PEKEE LA KUTUNUKIWA DIGRII

More information