Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi
|
|
- Berenice Sanders
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1
2 Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau wote katika jamii. Madhumuni ya Elimu kwa ujumla ni kuifanya dunia kuwa mahali pazuri pa kuishi watu wa kizazi cha leo na vizazi vijavyo. Inakusudiwa kuwapa watu maarifa na ujuzi watakaoutumia vizazi na vizazi ili kuwasaidia kupata njia mpya na bora zaidi ya kutatua matatizo yao ya kiafya, kiuchumi, kijamii na mengine yanayohusu mazingira wanayoishi. Elimu lazima imkomboe binadamu kiakili na kimwili, imuwezeshe binadamu kujikwamua na kumpa binadamu uwezo wa kupambana na matatizo au changamoto zinazomkabili katika maisha. Inapaswa kuipa jamii utambuzi au ujuzi kuwa wao ni nani, wanatoka wapi, wanakwenda wapi, na wajipange vipi ili wafike huko wanakotaka kwenda. Malengo ya msingi ya elimu ni kumkomboa binadamu. Kumkomboa maana yake ni kumweka huru, na kumweka huru kutoka hali au jambo fulani (Nyerere 1974). Inamaanisha kuwa kuna vikwazo ambavyo lazima avishinde. Tanzania mara tulipopata uhuru mwaka 1961 tulisema kuwa tuna maadui watatu: ujinga, maradhi na umaskini. Maadui hawa bado tunao hadi leo; ni vikwazo ambavyo tunaweza kuvishinda tukipata elimu, na hasa tukipata Elimukombozi. 2.0 Elimukombozi ni nini? Mwalimu Nyerere alifafanua Elimukombozi kuwa ni aina ya elimu inayomkomboa Mwafrika kutoka mawazo ya utumwa/kitumwa na ukoloni na kumfanya ajihisi kuwa binadamu sawa na binadamu wengine, mwenye haki na wajibu wa kibinadamu. Elimu inayomkomboa kutoka tabia za kukubali mazingira yanayomnyanyasa na kupunguza utu wake na hadhi yake kana kwamba hayabadilishiki na hana uwezo juu ya mazingira hayo. Pia lazima imkomboe kutoka minyororo ya ujinga wa teknolojia ili aweze kutumia vifaa vya kujiweka sawa ili kujiendeleza yeye na binadamu wenzake (Nyerere 1974). (Tafsiri yangu) Dhana hii ya elimukombozi hapa imetumika kumaanisha elimu inayomwezesha binadamu kujitambua, kujikomboa na kushiriki katika kuikomboa jamii yake. Katika muktadha wa Afrika na Tanzania ni elimu inayomtoa Mwafrika kutoka mawazo ya 1 Martha Qorro ni Mhadhiri Mwandamizi katika Idara ya Lugha za Kigeni na Isimu, Chuo kikuu cha Dar es salaam. Anapatikana kwa barua pepe mqorro@yahoo.co.uk 1
3 kitumwa tuliyopandikiziwa na elimu tuliyoirithi kutoka kwa wakoloni na ambayo mengi tumeyaendeleza hata baada ya Afrika yote kuwa na uhuru wa bendera. 3.0 Elimu tuliyorithi kwa wakoloni na athari zake Elimu yetu hivi sasa haina sifa tulizotaja za Elimukombozi. Elimu ya sasa ni elimu tuliyoirithi kutoka kwa wakoloni. Sote tumeathirika kwa kiasi kikubwa na elimu hii. Malengo yake yalikuwa kutubadili/kutugeuza (Buchert 1994) ili tuwe watumishi wema, watiifu, wasiouliza maswali, wavumilivu, wenye bidii ya kazi na wenye kukubali hali yo yote ya maisha, hata iwe ngumu kiasi gani. Ni elimu inayojenga uwoga na utiifu usiohoji hata masuala ya msingi; inayojenga upole unaorahisisha kutawaliwa kwa maslahi ya wengine. Elimu ya kikoloni pia imetugeuza na kutufanya tudharau mambo yetu na kujidharau au kukosa kujiamini. Elimu hii imetugeuza kuwa watumwa kiasi kwamba sasa, miaka zaidi ya 45 tunaiendesha wenyewe kama ilivyokusudiwa na mkoloni. Kwa maneno mengine, tunajigeuza kuwa watumwa wa ukoloni sisi wenyewe kwa manufaa ya nchi tajiri na gharama ya kujigeuza kuwa watumwa tunailipa sisi. Mbaya zaidi, hatuamini kwamba hicho ndicho tunachokifanya. Elimu pia imetufanya kuthamini kipato kuliko huduma tunazotoa kwa jamii zetu; tukidai kuwa thamani yetu katika soko ni juu zaidi kuliko mshahara tunaolipwa Tanzania. Mwalimu Nyerere (1974) alisema binadamu pekee wenye thamani katika soko ni watumwa. Yaani bila kujitambua tunasema kwamba elimu hii tuliyopata imetugeuza kuwa bidhaa za kuuzwa sokoni kama pamba, katani au kahawa Katika mustakabali wa utandawazi na soko huria, elimu tuliyoipata na tunayoendelea kutoa haitusaidii kama jamii, kwa kuwa haitukomboi katika utumwa bali inatuweka tayari kuwa watumishi wema, watiifu, wasiouliza maswali, na wavumilivu wa mataifa tajiri. Elimu yetu imekuwa mradi wa mataifa tajiri wa kuendeleza ukoloni wao hata baada ya uhuru wa kisiasa. Haijatuandaa kutafuta suluhu au kujiuliza namna ya kujikwamua. Tunakuwa tumebaki kulalamika na kukosa matumaini. Hata viongozi, maprofesa, madaktari wasomi wa falsafa tunalalamika; tumechanganyikiwa, hatujui tulipokosea na tunaamua kuukataa ukweli tunaoujua! Naamini kabisa kuwa haya ni matokeo/matunda ya elimu tuliyorithi na tunayoendelea kutoa katika taifa letu na hata bara zima la Afrika. Elimu tuliyopata imetuandaa kuulimbukia utandawazi (na mengine yote watakayosema nchi tajiri) bila kutambua kuwa ni mwendelezo wa ukoloni. Hatutambui kuwa elimu tuliyopata imetulea tuamini kuwa hivi ndivyo inavyopaswa kuwa; ndiyo maana tukakubali na tukayaendeleza hadi leo. Ni muhimu tujiulize kama tunapenda kuendelea na hali hii ya utumwa wa kujitumikisha wenyewe kwa manufaa ya mataifa tajiri huku tukilipa gharama za kujigeuza watumwa, au tujikomboe na tuondokane na utumwa huu. Njia mojawapo ya kujikomboa ni kurudi katika misingi ya Elimukombozi kama alivyoainisha Baba wa Taifa Mwalimu J. K. Nyerere. Tukitambua kuwa haitatusaidia hata kama tukijitahidi kujidharau na kuamini kwamba tukikataa mambo yetu, tutakuwa kama wazungu, kamwe hatutakuwa, na hatatuweza kujibadilisha. Tutabaki Waafrika kama tulivyo. Ni heri tujikubali na tuanze kujithamini na kujiheshimu kama binadamu wengine. Tuondokane na utumwa huu kwa maana hata hao tunaotaka kufanana nao hawatutaki na kwa kweli hawataturuhusu tuwe 2
4 kama wao hata tungejaribu vipi. La msingi ni kwamba hatuhitaji kuiga kila kitu kiasi cha kujidhalilisha. Tukilitambua hilo, tutakuwa katika hatua ya kuanza kujikomboa. 4.0 Elimukombozi kuwa njia ya kujikwamua. Kazi ya kujikomboa, hasa tunapoamini kwamba hatuna tatizo la utumwa wa kifikra ni changamoto kubwa. Kazi kubwa ya kwanza ni kuwafanya watu wajitambue kuwa sisi sote tu waathirika wa elimu ya kikoloni. Tunahitaji kushirikiana na wadau wa sekta na maeneo mbali mbali ya jamii yetu tueleweshane kwamba tunahitaji Elimukombozi. Ukisoma makala ya wataalamu katika sekta mbali mbali (Kaduma 2003, Simba 2003, Lazaro na Mdoe 2003, Likwelile 2003) utaona kwamba baadhi wanakubali kuwa tuna mawazo ya utegemezi, ambayo nayatafsiri kuwa ni dalili za utumwa. Tunapoulizana wapi tuanzie ili kuondokana na wale adui watatu: ujinga, maradhi na umaskini tulioainisha mara baada ya uhuru, wengi huwa wanajibu kwamba tuanze na kuboresha uchumi wa nchi. Yaani tuuondoe umaskini kwanza, halafu ndiyo yafuatie ujinga na maradhi. Kwa maoni yangu, naamini ni muhimu kuanza kwenye elimu kwa kuwa ndiyo inayotupa ufahamu, uelewa na dira ya kuwa: sisi ni nani, tunatoka wapi, tunataka kwenda wapi na tunahitji kufanya nini ili tufike huko tunakotaka kwenda. Kama alivyosema Ngugi wa Thiongo, kuwa wasomi wa Afrika tuna jukumu la kuunganisha kichwa na kiwiliwili cha Bara letu Afrika, baada ya wakoloni kuvitenganisha. Kichwa ikiwa ni viongozi na wasomi na kiwiliwili ni jamii ya watu wa Afrika. Kwa hiyo, jambo la uelewa wa pamoja kama jamii katika suala la kujitambua naliona ni la muhimu sana na la msingi. Kwanza, jambo la kuelewana na kukubaliana na kuweka mwelekeo halina gharama kubwa zaidi ya rasilimali watu, ambayo tunayo kwa uwingi. Pili, bila kuwa na uelewa, makubaliano na ushiriki wa wadau wengi, umaskini na maradhi ni vigumu kupambana navyo. Kwa hiyo, elimu itakayotoa ujinga, itatupa mwanga wa kuyafanya hayo mengine kwa manufaa ya jamii. Tatu, tusipoanza na hili la kuondoa ujinga, (na kujikwamua kwenye utumwa) ni rahisi tukadanganywa na wajanja kwa manufaa yao binafsi au ya jamii zao. Wengi watahoji: tutaanzaje na elimu wakati tuko maskini? Hoja yao ni kwamba tukiboresha uchumi, ndiyo utakaotumika kuboresha elimu na kuondoa ujinga. Sikubaliani na hoja hii kwa sababu kabla hatujajikomboa kifikra na kiakili (kupitia elimu, hasa elimukombozi) siyo rahisi kukuza uchumi kwa manufaa ya jamii zetu. Tuanze katika elimu na tubadilishe mitazamo ya kutawaliwa na kutumikia wengine. Tuwe binadamu huru, sawa na binadamu wengine; kama tulivyopambana tukapata uhuru wa kisiasa (bendera) vivyo hivyo tuanze kutafuta uhuru wa kifikra, kimtazamo na kimawazo kwa kuanzia kwenye elimu na kuifanya elimu yetu iwe Elimukombozi. Ili kuwa na Elimukombozi tunahitaji kuchukua hatua kadhaa; baadhi ya hizo hatua ni kama ifuatavyo: Elimu ilenge katika kuwaandaa wasomi kuwa wadadisi, wanaouliza maswali na kutafuta majibu ya matatizo yanayoikabili jamii. Wawe na uwezo wa kufikiri, kuchambua, kutafakari na kutumia taaluma walizojifunza shuleni na vyuoni kutatua matatizo ya jamii. Mitaala na mbinu za kufundishia ziendane na malengo ya elimu. Kufanya mitaala iwe na malengo ya kujikomboa Elimu iwe sehemu ya jamii, na kamwe isijaribu kuwatenganisha wasomi na jamii zao ili kuwa na mawasiliano ya karibu kufanikisha maendeleo. Wasomi wapewe 3
5 changamoto ya kuandaa makala katika lugha rahisi kwa ajili ya jamii zao. Kwa kuwa ni kujidhalilisha na wala hatunufaiki kukataa utambulisho wetu kama Waafrika, bora tuikubali hali hiyo na kuanza kujithamini. Tutumie wataalamu wetu kuandika vitabu kwa ajili ya shule zetu, ili tusiwe wategemezi kwa baadhi ya vitabu ambavyo siyo lazima kuagiza kutoka nje. Tuanzishe tafiti zinazolenga kuendeleza jamii zetu katika maeneo ya sera na mipango. Ili elimukombozi iweze kufanikiwa, inahitaji lugha inayoeleweka kwa walimu na wanafunzi; jambo ambalo tutalijadili katika sehemu inayofuata. 5.0 Suala la Elimukombozi, lugha na upashanaji habari. Katika sehemu hii tutajadili na kuonyesha jinsi gani Elimukombozi inavyotegemea lugha. Hapa kuna suala la lugha katika nyanja mbili: ya kwanza, ni lugha ya kufundishia shuleni na vyuoni. Pili, ni lugha inayotumika na kueleweka zaidi katika jamii. Uelewa wa lugha uko katika ngazi tofauti. Ingawa ngazi hizo zinaweza kuwa nyingi, na ni za hali ya mfululizo, katika makala hii nitaainisha ngazi tatu tu kama ifuatavyo: 5.1 Ngazi ya uelewa wa lugha na uwezo wa mzungumzaji kutumia lugha hiyo 1. Uelewa mdogo sana: Uwezo wa lugha ya kuombea maji. Akilazimika kutumia kujifunzia lugha katika ngazi hii mzungumzaji inabidi akariri karibu kila kitu kwa kuwa ana uelewa mdogo. Huchukua muda mrefu kuelewa mambo madogo kwa kuwa lugha ni kikwazo. Haoni uhusiano kati ya maisha yake na mambo yale anayofundishwa au anayoelezwa shuleni. Masomo humchosha na mawazo huhama darasani/kutoka eneo la mazungumzo. 2. Uelewa wa kati: Uwezo wa kumpa mtu maelekezo ya namna ya kufika sehemu fulani. Uelewa wa juu juu wa mambo yanayozungumzwa au kufundishwa kwa lugha hiyo. Tabia ya kukariri bado inaendelea, ingawa imepungua kwa kiasi kikubwa. Uwezo wa kuandika sentensi fupi fupi sahihi na kuuliza maswali rahisi. Kuna uwezekano mkubwa wa kutoelewa, au kuelewa vibaya maana iliyokusudiwa. Lugha bado ni kikwazo katika kutoa ushiriki wakati wa kufundishwa au katika mazungumzo ya kawaida. 3. Uelewa wa hali ya juu: Uwezo wa kufikiri, kutafakari, kujadili, kuchambua na kuchanganua masuala na dhana mbali mbali yanayozungumzwa au kufundishwa kwa lugha husika. Mzungumzaji anakuwa na uwezo mkubwa wa kutumia lugha kama nyenzo ya kuvumbua mambo mapya; ana uhuru wa kutumia lugha husika na yote atakayoelezwa katika kujikomboa kimawazo. Lugha siyo kikwazo katika kuelewa, kupambana na changamoto za maisha. Hahitaji kukariri; bali hutumia uelewa wake katika kujibu maswali au kutoa maelezo juu ya yale anayoyaelewa. Ni katika 4
6 hatua hii ya uelewa ndiyo wanafunzi wanapoweza kushiriki Elimukombozi. Tafiti nyingi (Mlama na Matteru 1978, Criper and Dodd 1984, Roy-Campbell and Qorro 1987, Rubagumya, Jones and Mwansoko 1998, Qorro 1999, Mwinsheikhe 2003, Puja 2003, Brock Utne 2004, Vuzo 2005) zimeonyesha kuwa wanafunzi wengi katika shule za sekondari na vyuo nchini Tanzania wana uwezo wa hatua ya kwanza au ya pili ya uelewa wa lugha inayotumika kufundishia. Kwa kung ang ania kutumia lugha wasiyoelewa, tunawafundisha wanafunzi hawa kushindwa! Wengi wa wanafunzi hawa wanajifunza kutodadisi, kutofikiri, kutouliza maswali, kunakili na kukariri, kuwa waoga, kutojiamini, kukubali kila hali, na kukata tamaa kwa kauli ya yote maisha. Kwa maana nyingine wanafunzi walio wengi katika shule na vyuo vya Tanzania hawapati elimu iliyokusudiwa, achilia mbali Elimukombozi, kwa kuwa uelewa wao wa lugha inayotumika kufundishia ni mdogo. Kwa hiyo, badala ya elimu yetu kutokomeza ujinga, inapalilia ujinga! Ni vema tukajiuliza, hali hii ya kuandaa vijana wasioweza kuelewa, kujadili, kufikiri, kuchambua na kuchanganua masuala na dhana mbali mbali zinazofundishwa ni kwa maslahi ya nani? Ni wazi kwamba tunahitaji Elimukombozi; na kwamba ili kufanikisha Elimukombozi shuleni na vyuoni, ni lazima wanafunzi watumie lugha ambayo wao na walimu wao wana uelewa wa hali ya juu. Jitihada za Serikali kubadili elimu mara baada ya uhuru hazijaendelezwa. Mwalimu Nyerere (1968) alisema kwamba, elimu inayotolewa haina budi kumchochea mtu kuwa na mambo matatu yafuatayo: akili zenye udadisi wa mambo, uwezo wa kujifunza kutokana na yale yanayofanywa na wengine, kujiamini kama mtu huru na aliye sawa na wengine katika jamii, mtu anayethamini na pia kuthaminiwa na wenzake kwa sababu ya matendo yake na siyo kwa kile alichonacho. Katika hali ambayo wanafunzi wana uelewa mdogo wa lugha, wanafunzi wa kike huathirika zaidi kwa kuwa mara nyingi huona aibu kuuliza, au kujibu maswali kwa kuogopa kuchekwa pindi watakapokosea lugha. Matumizi ya lugha wasiyoielewa vizuri huwafanya wanafunzi wengi, hasa wasichana, kuwa wanyonge, na kwa muda mwingi hunakili maadiko ya mwalimu (mengine yakiwa na makosa) kwa kadri watakavyoweza kuyasoma. Maandiko hayo kwa sehemu kubwa wengi hawayaelewi. Badala ya kujifunza masuala ya msingi, wanafunzi wanaishia kukariri maneno kwa lugha wasiyoelewa na muda mwingi unapotea na ari ya kusoma inapungua. Elimu hii ya kunakili na kukariri haiwapi uwezo wa kujikomboa bali huenda kinyume na makusudio. Badala yake huwafundisha kuwa: wavumilivu, wasikivu, na watii/watekeleza amri bila maswali. Yaani kuwa watumishi wazuri au watwana. Hapa lugha inatumika kama kikwazo cha kuzuia wengi wasipate uelewa uliokusudiwa. Haya yalikuwa malengo ya elimu ya kikoloni; lakini kwa kujua au bila kujua tumekuwa tukiiendeleza hadi leo, miaka zaidi ya 45 baada ya Uhuru. Brock-Utne (1997) anapendekeza kwamba, ili kuleta mabadiliko kwenye mfumo wa elimu Afrika, hatuna budi kuwakomboa Waafrika kifikra; na kwamba hali hiyo itawezekana iwapo Waafrika watachukua mamlaka juu ya taratibu zinazotumika kuendesha elimu yao. Anasisitiza kwamba kuna haja ya kutunga upya vitabu vya kiada vinavyotumiwa na wanafunzi shuleni ili viwe na mafunzo ya Kiafrika katika lugha za Kiafrika wanazoelewa wanafunzi hawa ili kuwaandaa wasomi kuwa wadadisi, wanaouliza maswali na kutafuta majibu ya matatizo yanayoikabili jamii. 5
7 Wawe na uwezo wa kufikiri, kuchambua, kutafakari na kutumia taaluma walizojifunza shuleni na vyuoni kutatua matatizo ya jamii katika lugha zao. Obaro (1997) naye anakubaliana na Brock-Utne kwamba Waafrika sharti watambue umuhimu wa kubadili elimu wanayoitoa ya nchi za Magharibi ili badala yake watoe kwa watoto wao elimu ya Kiafrika. Tunahitaji kuwa na vitabu na vifaa vya kufundishia vinavyoendana kwa karibu na mahitaji na pia hali halisi ya jamii ya Kiafrika. 5.2 Elimukombozi na hali ya upashanaji habari katika jamii Kwa kuwa lengo la elimu (MOEC 1995) ni kuwaandaa vijana kuwa sehemu ya jamii, ni vema maandalizi hayo yakafanywa katika lugha kuu ya jamii. Matumizi ya lugha moja katika elimu na jamii inaimarisha mahusiano kati ya jamii na shule au vyuo. Ili kuifanikisha Elimukombozi ifikie jamii kubwa zaidi nje ya shule na vyuo ni muhimu kutumia lugha ambayo sehemu kubwa ya jamii inaelewa. Katika hali tuliyorithi, ambapo elimu hutolewa kwa lugha ngeni katika jamii, upashanaji habari wa yale yanayotolewa katika elimu kuenea kwa jamii kubwa ni mgumu. Kwa mfano, hivi sasa maandiko mengi ya tafiti na taaluma mbali mbali katika bara la Afrika yako katika lugha za Kigeni: Kiingereza, Kifaransa, Kireno au Kiarabu. Ni vigumu, na wakati mwingine haiwezekani kabisa kwa maandiko haya kusomwa na wanajamii. Iwapo lugha ya elimu ni ile ile inayotumiwa na watu wengi katika jamii, kama ilivyo katika nchi za Ulaya na Asia, basi ujuzi na maarifa yanayopatikana katika elimu yangewafikia watu wengi katika jamii. Hali hii ingelipunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la upashanaji habari, na lingenufaisha watu wengi zaidi kuliko ilivyo sasa. Kubadili lugha ya kufundishia ni hatua muhimu ya msingi katika kuboresha elimu; lakini peke yake haitoshi. Tunahitaji kubadilisha mtazamo wetu wa sasa kuwa chanya kuhusu uwezo wetu wa kutoa elimu yenye manufaa kwetu sisi. Tunahitaji kuyapitia upya malengo yetu ya elimu ili yaendane na Elimukombozi. Ili kuukabili utandawazi ni muhimu tuwe na uelewa wa kina wa mambo mbali mbali na tujifunze lugha kadhaa za kimataifa. Tushiriki katika utandawazi tukiwa binadamu wenye wajibu na haki kama binadamu wengine. 6.0 Hitimisho na Mapendekezo Katika makala hii tumejadili hali halisi ya elimu inayotolewa katika jamii yetu. Ingawa msisitizo umekuwa kuwawezesha watoto/vijana wengi kadri iwezekanavyo kwenda shule, bado kuna umuhimu wa kutizama mbali zaidi na kujua nini kinachofanyika ndani ya darasa. Tumeona kwamba elimu tuliyorithi kwa wakoloni ya kuandaa watumishi na jamii ya watu wa kutawaliwa kirahisi bado tunaiendeleza. Lugha ya kufundishia kwa sehemu kubwa inatumiwa kama kikwazo cha kuzuia wengi wasipate uelewa uliokusudiwa. Ingawa tulidhamiria (Nyerere 1974) kuwa malengo ya msingi ya elimu ni kumkomboa binadamu, hali halisi inaonyesha kwamba yanayofanyika ni kinyume kabisa na ukombozi. Elimu yetu, miaka 45 baada ya uhuru, bado inaendeleza malengo yale yale ya wakoloni. Kwa maoni yangu, njia pekee ya haraka na uhakika ni kuangalia upya elimu yetu ili tuweze kujikomboa kifikra. Elimukombozi ni njia muafaka na ya lazima iwapo tutapenda kujikomboa. Changamoto iliyopo mbele yetu ni namna ya kuelezea dhana hii na kuifanya 6
8 ikubalike miongoni mwa jamii hasa kwa wafanyamaamuzi. Ni vizuri tukatambua kuwa hii ni kazi ngumu, kwa maana mizizi ya upotofu wa elimu tuliyorithi kwa wakoloni na kasumba za kujidharau na kuhusudu vya wengine imejikita sana miongoni mwetu. Sisi tuliopo hapa, tukishirikiana na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) pamoja na asasi zingine za kijamii tuna wajibu. Wajibu wa kuwa kichocheo cha mabadiliko. Tukumbuke kwamba, popote palipo na kukandamizwa, kuonewa, kunyimwa haki kwa aina yo yote; wanawake mara nyingi huathirika zaidi. Hata hivyo, pamoja na kuathirika zaidi, wanawake huwa ndiyo wenye uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko katika jamii. Tushirikiane wake kwa waume, tujikomboe na tulete mabadiliko chanya katika jamii zetu na kwa ulimwengu mzima. Tujihadhari tusije tukatumia mbinu zile zile walizotumia wakoloni za kutugawa makundi zikaturudisha tulipoondokea. Tuwe na upendo, amani na mshikamano. Tutafanikiwa! 7
9 Marejeo Brock-Utne, B. (1997). Decolonizing the African Mind, in Education in Africa Report No. 8. Institute of Educational Research, University of Oslo, Norway Buchert, L. (1994). Education in the Development of Tanzania , James Currey, London/Mkuki na Nyota, Dar es Salaam. Kaduma, I. (2003). Vita dhidi ya umaskini: Hali kuzidi kuwa ngumu, katika chapisho Kwanini Tanzania ni Maskini Miaka 40 Baada Ya Uhuru? Jumuiya ya wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Lazaro, E. A. na Ntengua Mdoe (2003). Sekta ya Kilimo Uti wa mgongo au vunja mgongo, katika chapisho Kwanini Tanzania ni Maskini Miaka 40 Baada Ya Uhuru? Jumuiya ya wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Likwelile, S. B. (2003). Mikakati ya Kupunguza Umaskini Tanzania: Mbinu za kuufuta, mambo ya kujifunza na changamoto za baadaye, katika chapisho Kwanini Tanzania ni Maskini Miaka 40 Baada Ya Uhuru? Jumuiya ya wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. MEOC, (1995). Education and Training Policy, Adult Education Press, Dar es Salaam Nyerere, J. K. (1967). Elimu ya Kujitegemea, hotuba kuhusu Waraka wa Sera, ya Marchi 1967, Dar es Salaam. Nyerere, J. K. (1968). Education for Self-Reliance, in Freedom and Socialism, Uhuru na Ujamaa, Oxford University Press, Oxford. Nyerere, J. K. (1974). Education for Liberation, a speech at Dag Hammarskjold Seminar on 20 th May, 1974, Dar es Salaam Simba, I. (2002). Sababu za kushindwa na Namna ya kujikwamua, makala katika chapisho Kwanini Tanzania ni Maskini Miaka 40 Baada Ya Uhuru? Jumuiya ya Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 8
10
Shabaha ya Mazungumzo haya
Karibu Katika Mazungumzo Kuhusu Mchakato wa Uhamasishaji Maendeleo ya Kanisa na Jamii CCMP/UMOJA Shabaha ya Mazungumzo haya Kuwafahamisha viongozi wa makanisa kuhusu Mchakato wa CCMP ambao umekuwa ukitumika
More informationKufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007
Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013
www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper
More informationInformation for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationUtumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationLUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI
LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI SIKOMBE YIZUKANJI YORADI TASNIFU YA KISWAHILI KWA MINAJILI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (MA. KISWAHILI) KITIVO CHA SANAA
More informationElimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi
Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Gervas Zombwe 1 1. Utangulizi Katika mazingira ya kawaida kabisa ndani ya jamii yetu, Imezoeleka kusikia au kuona watu wakioanisha dhana ya elimu
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationKiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika
Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationWIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationUfundishaji wa lugha nyingine
CHUO CHA ELIMU CHA KIMATAIFA OFISI YA ELIMU YA KIMATAIFA Ufundishaji wa lugha nyingine Na Elizabeth B. Bernhardt ELIMU MAZOEA KITABU NA. 20 1 Chuo cha Elimu cha Kimataifa (The International Academy of
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationUfunguo wa Kutaalamika Haraka
0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11
More informationJHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI
JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationSautiElimu. Sauti Yako Isikike
SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian
More informationMITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012
MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012 TASNIFU HII IMEWASILISHWA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI
More informationHati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako
More informationMpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari
More informationTAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA
TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0
More informationMazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo. Zanzibar, 7-10 Februari 2006
Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Imechapishwa na: The Atlas Alliance Schweigaardsgt 12 SLP 9218 Grønland 0134 Oslo, Norway Simu: +47
More informationMwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza
Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)
More informationUfanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania
Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Desemba 2014 1 Shukurani Ripoti hii iliandikwa na Dk. Mkumbo. Ushauri wa kitaalamu ulitolewa na Elizabeth Missokia na Godfrey
More informationElimu-Jumuishi Kwa Vitendo
Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo Taarifa ya Warsha Kuhusu Elimu-Jumuishi Iliyofanyika Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Kujifunza hakuna mwisho. Kazi ya vikundi imenipa fursa ya kujieleza bila kuhofia kuwa ningekosea.
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA
More informationMALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU
MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa
More informationKENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS
KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS ALLIANCE BOYS HIGH SCHOOL KISWAHILI KARATASI YA 2 SCHOOLS NET KENYA Osiligi House, Opposite KCB, Ground Floor Off Magadi
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationPronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:
More informationKUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA
KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationKimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:
Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More informationRipoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013
W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationAzimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]
This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationRipoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya
More informationJAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
More informationUsimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya
Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma
More informationTheolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College
Theolojia 1 Ujumla Mike Taylor Semester 1 2014-2015 Munguishi Bible College MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 i THEOLOJIA Utangulizi! 1 1. Kumfahamu Mungu katika Injili! 3 1.1. Mawazo Makuu 3 1.2. Maana ya
More informationTufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue?
Tufundishane! Let s teach each other! This newsletter is published by The Foundation for Tomorrow and is meant to be a venue for teachers and schools to share and learn from each other s best practices.
More informationSera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji
Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationMwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo
Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu Nyenzo ya Mafunzo Vi Agroforestry Vi Agroforestry ni shirika la ushirikiano la maendeleo la Sweden, linalopambana dhidi ya umasikini na
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More informationUnited Pentecostal Church June 2017
Kwa Nini Tusali? Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa "Chagua" Ladies Prayer International kwa Facebook United Pentecostal Church June 2017 Tuko na wafuasi Facebook katika Marekani, Hong Kong, Philippines,
More informationUKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)
Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni
More informationMwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira
Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Moduli ya kwanza Uhamasishaji Jamii juu ya Afya ya Mazingira Kimechapishwa kutokana na Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Jeff Conant na Pam Fadem i COBIHESA
More informationusudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-
Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa
More informationNGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017
TAARIFA Agosti 2017 NGUO MPYA ZA UKOLONI Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika Jumuiya ya Jamii ya 2007: Wajumbe wanaadhamana Nairobi dhidi ya EPAs. SwissInfo Tangu mwaka
More informationMATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza
1 Matumizi bora ya Facebook kwa Biashara MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA Kwa Wanaoanza For IT Services & Web Solutions Web: Email: info@dudumizi.com Phone: 0768816728 2 Matumizi bora ya Facebook kwa
More informationKAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA
KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI
More informationKISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA
KISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA Maagizo (a) Andika jina lako na namba yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu. (b) Tia sahihi yako na tarehe ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu. (c) Jibu maswali
More informationEllen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar
Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ukristo leo unadhihirisha waumini karibu bilioni mbili katika maelfu ya madhehebu tofauti na tofauti na madhehebu. Kati ya hizi, zaidi ya 500 madhehebu
More informationUHUSIANO WA MIKAKATI YA UFUNDISHAJI WA FASIHI YA WATOTO YA KISWAHILI NA UMILISI WA KUSOMA KATIKA SHULE ZA MSINGI, KASARANI, KAUNTI YA NAIROBI, KENYA
UHUSIANO WA MIKAKATI YA UFUNDISHAJI WA FASIHI YA WATOTO YA KISWAHILI NA UMILISI WA KUSOMA KATIKA SHULE ZA MSINGI, KASARANI, KAUNTI YA NAIROBI, KENYA NA SELINA RHOBI CHACHA E55/23475/11 TASNIFU HII IMEWASILISHWA
More informationMwongozo wa Familia wa Kujifunza
Shule za umma za kata ya Fayette 1 Mwongozo wa Familia wa Kujifunza Muhtasari wa yale watoto wanastahili kufahamu na kuweza kufanya na njia za familia kuongeza masomo nyumbani. Tunaamini familia ni wenzetu.
More informationK. M a r k s, F. E n g e l s
W a (any a kazi wa nchi zote, unganeni! K. M a r k s, F. E n g e l s Maelezo ya chama cha kikomunist Idara ya Maendcleo Moscow Tafsiri hii ya "Maelezo ya Chama cha Kikomunist" inatokana na maandishi
More informationTASFIDA KAMA MKAKATI WA UPOLE: UWIANO WA TASFIDA ZA KISWAHILI NA EKEGUSII
TASFIDA KAMA MKAKATI WA UPOLE: UWIANO WA TASFIDA ZA KISWAHILI NA EKEGUSII NA FLORAH N. OMOSA C50/84117/2012 TASNIFU HII IMETOLEWA KWA MADHUMUNI YA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJIYA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA
More informationTora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA
SOMO LA KWANZA UTANGULIZI KWA TORA For videos, study guides and other resources, visit Third Millennium Ministries at thirdmill.org. 2014 nathird Millennium Ministries Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu
More informationVijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO. Training and Research Support Centre
Shangazi Stella Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO Training and Research Support Centre Zimbabwe Shangazi Stella Kiongozi cha Mwezeshaji
More informationElimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...
Elimu Bora, lakini... Shukrani za dhati kwa wote waliotusaidia katika kutayarisha kijitabu hiki: Nsa Kaisi, Mshauri wa Rais, kwa mchango wake mkubwa wa mawazo Wafanyakazi wote wa HakiElimu 2003-2004 Many
More informationKilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira
Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kiongozi hiki kimeandaliwa kikiwa ni sehemu ya mradi wa
More informationMakala ya Mshiriki wa Mafunzo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Ushauri Nasaha na Upimaji wa VVU kwa Hiari Makala ya Mshiriki wa Mafunzo Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Machi 2010 Kimetafsiriwa kutoka
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationTANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko
TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationHati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI/AGOSTI 2011 MUDA: 2 ½ Kiswahili Fasihi Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E) MAAGIZO Jibu maswali manne pekee Swali la kwanza ni lazima Maswali
More informationHakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn
TAFSIRI YA BIBLIA Mwandishi Jonathan M. Menn B.A., University of Wisconsin-Madison, 1974 J.D., Cornell Law School, 1977 M.Div., Trinity Evangelical Divinity School, 2007 Equipping Church Leaders-East Africa
More informationEvaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya
Evaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya Oduori T. Wamubi Prof. Simala, K. Inyani Profesa Mshiriki Masinde Muliro University of Science and Technology Prof.
More informationTIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees
TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST
More informationJifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti
Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu
More informationMwongozo wa Mwezeshaji
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Ushauri Nasaha na Upimaji wa VVU kwa Hiari Mwongozo wa Mwezeshaji Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Machi 2010 Kimetafsiriwa kutoka lugha
More informationMUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.
MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO. MUHTASARI WA UTANGULIZI WA THIOLOGIA YA USHIRIKA WA NAFSI TATU ZA UUNGU. GRACE COMMUNION INTERNATIONAL LIVING AND SHARING THE GOSPEL MUNGU ANADHIHIRISHWA NA
More informationMTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya
Jina Nambari.. Shule... 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI / AGOSTI. 2007 MUDA: SAA 2 ½ MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya 102/3 KISWAHILI FASIHI
More informationMAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI
MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha
More information5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban
More informationHaja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (
Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Haja Ya Dini Haja Ya Dini Author(s): Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi [3] Publisher(s): Bilal Muslim Mission of Tanzania [4] Katika kijitabu
More informationKUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA
KUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA BIBIANA MASSAWE AMBROSE TASINIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SHARTI PEKEE LA KUTUNUKIWA DIGRII
More informationATHARI ZA KIISIMU ZA LAHAJA YA KIMAKUNDUCHI KATIKAKISWAHILI SANIFU KINACHOTUMIKA SHULENI MAKUNDUCHI ZANZIBAR
ATHARI ZA KIISIMU ZA LAHAJA YA KIMAKUNDUCHI KATIKAKISWAHILI SANIFU KINACHOTUMIKA SHULENI MAKUNDUCHI ZANZIBAR SALEH ABDELSALAM MOHAMMED SALEH TASINIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUKAMILISHA MASHARTI YA
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa
More informationMwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo
More informationMAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA
MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More informationATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR
ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini
More informationJE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?
JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? JOE CREWS 1 JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? Na Joe Crews (Hotuba Na. 16 ya Mambo ya Kweli Yanayoshangaza) Mfasiri: M. Mwamalumbili Is It Possible To
More informationNilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania
Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania Kwa toleo neno la waraka huu, tafadhali email:crd@hrw.org FEBRUARI 2017 ISBN: 978-1-6231-34464 Nilikua na Ndoto ya Kumaliza
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationKutetea Haki za Binadamu
Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and
More informationKuwafikia waliotengwa
Kuwafikia waliotengwa Kuwafikia waliotengwa Muhtasari Chapisho la UNESCO 2 M U H T A S A R I R I P O T I Y A U S I M A M I Z I W A K I M A T A I F A W A M R A D I W A E L I M U K W A W O T E 2 0 1 0 Ripoti
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3
More informationMwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health
Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health Wasiojua kusoma na kuandika katika karne ya 21 hawatakuwa wale wasiojua kusoma na kuandika lakini wale ambao hawawezi kujifunza, kutojifunza na kujifunza
More information