Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College

Size: px
Start display at page:

Download "Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College"

Transcription

1 Theolojia 1 Ujumla Mike Taylor Semester Munguishi Bible College

2 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 i THEOLOJIA Utangulizi! 1 1. Kumfahamu Mungu katika Injili! Mawazo Makuu Maana ya Theolojia Umuhimu wa Kusoma Theolojia Vyanzo au Vifaa vya Kusoma Theolojia Tunamfahamu Mungu katika Injili Kwa hiyo: Muhtasari: Kazi ya Nyumbani 7 2. Mungu Utatu! Mawazo Makuu Maana ya Utatu Ushuhuda wa Biblia Makosa Imani Umuhimu Kwa hiyo Muhtasari: Mungu Mwenyezi! Mawazo Makuu mwenye uweza; mwema na mwenye hekima Mungu Mwenyezi (II)! Majina ya Mungu Lugha ya Binadamu inayotumika kwa Mungu Utawala Mkuu wa Mungu Maswali? Kazi 35 Insha #2: Maelezo ya Mambo Machache! UFUNUO! Ufunuo wa Kiujumla Ufunuo Maalumu Ufahamu wa Mungu nje ya Ufunuo Uumbaji Mungu anatawala kwa kuumba! Mwanzo Mungu Utatu aliumba Kuangalia Uumbaji sehemu zingine za Biblia Kulinganisha Uumbaji wa Kibiblia na hadithi za utamaduni 56

3 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 1 UTANGULIZI Karibu! Somo hili ni somo la Theolojia. Lengo ni kufahamu Biblia inasemaje juu ya Mungu hasa lakini mambo mengi pia. Mipango ya somo la Theolojia ni kufanya hiki kwa miaka mitatu ya kozi ya Hati: MWAKA WA KWANZA: MWAKA WA PILI: THEOLOJIA - KWA UJUMLA THEOLOJIA YA KINA: MAFUNDISHO YA MUNGU; UTATU; UUMBAJI; UFUNUO; UANADAMU; DHAMBI; HUKUMU. MWAKA WA TATU: THEOLOJIA YA KINA: MAFUNDISHO YA WOKOVU; YESU NAFSI NA KAZI YAKE; ROHO MTAKATIFU; KANISA; SIKU ZA MWISHO; N.K. PIA CONTEXTUALIZATION (KUWIAINISHA KWA MAZINGIRA) NA MAELEKEO YA THEOLOJIA YA SIKU HIZI. Yaani, katika mwaka wa kwanza tutaangalia kila jambo la theolojia kwa kifupi na kama juujuu; na katika mwaka wa pili na tatu tutarudia yote polepola na kuingia kwa kina zaidi. Theolojia inahusu kumjua Mungu na sisi wenyewe kama tunavyohusu naye. Biblia ni chanzo chetu cha theolojia, bali maisha yetu ni mahali pa kuishi theolojia yetu. Theolojia yetu kamwe isibaki katika karatasi ya vitabu vyetu, bali kuchoma mioyo, mapenzi na akili zetu. Mipango Kwa muhula huu tunalenga hivi Kugusa na kuona mambo yote ya mafundisho ya Biblia kwa ujumla kuelewa na kuweza kueleza Injili kuelewa na kuweza kueleza mambo makuu ya theolojia kutafakari namna ya kufanya theolojia. kuona upendo wa Kristo katika Biblia nzima jinsi ulivyo upana, na urefu, na kimo, na kina. Makadirio Ili tufika malengo haya, makaradio ya muhula huu yatakuwa:

4 2 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR % mahudhurio, kazi ya nyumbani na kusoma 10% Insha # 1: Maelezo ya Injili 20% Insha # 2: Maelezo ya Mambo machache 35% Insha #3: Kauli ya imani 25% Mtihani wa Mwisho wa Muhula Ratiba ya Semesta Juma Tarehe Mada Aug 12-Aug 19-Aug 26-Aug 2-Sep 9-Sep 16-Sep 23-Sep 30-Sep 8-Aug Kufahamu Mungu 15-Aug Mungu - Utatu 22-Aug Mungu - Tabia na Sifa Zake 29-Aug Ufunuo 5-Sep Uumbaji 12-Sep Ubinadamu 19-Sep Dhambi na Hukumu 26-Sep Kazi ya Mungu kuokoa A.K. 3-Oct Kazi ya Mungu kuokoa Kumtuma Mwana 7-Oct 10-Oct Mitihani 14-Oct 17-Oct Likizo Oct 28-Oct 4-Nov 11-Nov 18-Nov 25-Nov 2-Dec 24-Oct Yesu - Kazi na Nafsi 31-Oct Mafundisho ya Neema 7-Nov Roho Mtakatifu 14-Nov Kanisa 21-Nov Maisha ya Kikristo 28-Nov Misheni 5-Dec Siku za Mwisho 17 9-Dec 12-Dec Mithani

5 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA KUMFAHAMU MUNGU KATIKA INJILI 1.1. MAWAZO MAKUU Theolojia inamhusu kumfahamu Mungu Theolojia ni muhimu kwa maisha yetu ya kikristo na kihuduma - kujenga juu ya mwamba; kuwa ni msingi wa upendo na moyo wa huduma. Biblia ni chanzo cha Theolojia Tunafahamu Mungu aliyetupenda sisi kwanza katika kujitoa nafsi yake kwa ajili yetu. Alitutafuta kama kondoo mpotovu, na hivyo Injili ni mwanzo na moyo wa Theolojia. Umuhimu zaidi ni kujulikana na Mungu MAANA YA THEOLOJIA Theolojia inamhusu kumfahamu Mungu. Kamusi inasema theolojia (au theologia) maana yake ni: utafiti kuhusu Mungu jinsi alivyo na imani inayohusika naye. Neno theolojia inatoka na maneno mawili ya kiyunani, theos = Mungu logos = neno, somo, mafundisho. Kamusi ya Kiswahil inasema theolojia maana yake ni: Wafuasi wa Yesu wanajali theolojia si kwa sababu ni somo la kusomea pekee yake, kama ni jiografia au hisabiti. Tunataka kujifunza zaidi na zaidi kuhusu Mungu na dunia ambayo aliiumba pamoja na sisi kwa sababu tunataka kumfahamu Mungu. Tunasoma theolojia kwa sababu ya upendo na imani. Mtu moja alisema theolojia ni imani inayotafuta kuelewa. Yaani, tunaamini, na kwa sababu hiyo tunataka kuelewa zaidi na zaidi. Au kwa upande wa upendo tunaweza kusema theolojia ni sehemu ya upendo. Kwa sababu tunampenda Mungu ndiyo tunataka kumfahamu zaidi na zaidi; kuboresha uhusiano wetu naye na ili tupate kumpenda zaidi. Lakini pia, kama kitu ambacho tunakipenda (kwa rafiki yangu ni.) tunataka kutazama na kujifunza na kuangalia kwa sababu ya upendo ule tu. Bali Biblia inasema tunampenda Mungu kwa sababu kutupenda sisi kwanza (1 Yn 4:19) ni hivyo theolojia ni kumwelewa yeye aliyetutafuta kutuokoa. Kufahamu Mungu wetu kwa kufikiri, kutafakari na kujifunza mawazo yake kama alivyotufunulia.

6 4 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 Kweli, theolojia ni yale yote tunayofikiri kuhusu Mungu, ibada, maisha, maadili na kumfuata Yesu Kristo; theolojia ni ufahamu wa Mungu na yote yahusika naye (vyote!). Theolojia inatupa miwani ya kuona dunia kweli na hasa kutuona sisi kwa kweli. Lakini hasa ni kumfahamu Mungu na tunafanya ili tupate kumfahamu. John 17:3 Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma UMUHIMU WA KUSOMA THEOLOJIA Ikiwa si wazi tayari sababu za kusoma theolojia, tunaweza kufikiri zaidi. Ni rahisi kwa mtu kusema, k.m., theolojia haina faida; uhai wa ukristo ni katika miujiza na nguvu za Roho, katika nyimbo na katika. Au mwingina labda asema, mtu ni mkristo wa kweli na wa rahisi; kuvisoma vitabu vingi ni sawa kwa wengine, lakini kwa mimi nini uhusiano wangu na Mungu; sina hitaji kwa theolojia. Pia tunaweza kushtakiwa kama tunachafua maji yaliyo wazi/safi. Kuna waislamu, kwa mfano, wanaweza kusema kwamba tumeharibu mafundisho ya Uungu kwa kusoma soma na kuumba mafundisho ya utatu. Afadhali, angeweza kusema, kusikia na kutii tu - bila kuhoji. Je, ungesema nini kwa watu kama hao? Hata Biblia nyenyewe inatoa onyo juu ya kusoma soma bila hekima Mhu. 12:12 Tena, zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo; hakuna mwisho wo wote wa kutunga vitabu vingi; na kusoma sana huuchosha mwili. Tunaweza kusema ni katika uteteaji wa kusoma sana Biblia na vitabu vingine ili tupate kufahamu zaidi na zaidi Mungu wetu na maisha yetu mbele zake? Hebu soma na tafakari vifungu hivi vifuatavyo. Vinasema nini kuhusu thamani ya kusoma na kujifunza theolojia?

7 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA Timotheo 4: Wafilipi 1: Mathayo 7: VYANZO AU VIFAA VYA KUSOMA THEOLOJIA Tunaenda wapi kupata ufahamu wetu wa Mungu? Kwa kifupi Mungu. Tunaenda kwa neno lake ambalo ni ufunuo wake. Katika Biblia Mungu alijifunua kwa ajili yetu. Alinena kwa manabii katika AK na katika siku hizi za mwisho alinena kwa Mwana (Ebr 1:1-2). AJ ni ushuhuda wa Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ulioandikwa na mitume wake kwa Roho Mtakatifu. Biblia ni Neno la Mungu lililo kweli, hai na bila makosa. Pia ni neno lake la dhahiri, na la wazi. Ingawa inawezekana kwa Mungu kusema na mtu fulani nje la Biblia, neno hili siyo wazi na hatuwezi kutumia katika fikira zetu za theolojia. Tutafikiria zaidi ufunuo baada ya wiki kadhaa. Neno la Mungu ndipo ni mahali pa kufahamu Mungu, kuhusiana naye na kupata theolojia.

8 6 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 Lakini hatusomi peke yetu. Tunasoma katika jamii. Tunasoma na kutafakari kwa pamoja, watu wa Mungu wa sasa hivi pamoja na wao waliotutangulia. Wote ni zawadi ya Mungu kwetu na tunasoma theolojia pamoja nao. Hivyo historia ya kanisa pamoja na maandiko ya wengine hasa watheolojia wakuu ni muhimu kwa ajili yetu. Pia tunatumia akili zetu, uzoefu wetu na mapokeo yetu. Zote zinatusaidia kufikilia ufahamu wa kweli. Lakini lile ambalo linatawala vyote ni Kristo kupitia neno lake. Ni neno ambalo lina mamlaka. Hivyo tukipata kupingana kati ya akili au uzoefu au mapokeo na neno la Mungu ni neno la Mungu (kwa kadiri ya uwezo wetu kulielewa) ambalo ni kweli (k.m. Mk 7:8). Neno la Mungu ni chanzo na bwana wa theolojia TUNAMFAHAMU MUNGU KATIKA INJILI. Biblia inasema wanadamu ni watumwa wa dhambi na wanaishi katika giza. Inasema fikira zetu zimepofishwa na Shetani (2 Kor 4:4), na kwamba tumebadili kweli ya Mungu kuwa uongo (Rum 1:25). Alipokuja kwake, hawakumtambua (Yn 1:10-11); badala yake, wakamwua (1 Kor 2:8). Yaani, kiasili hatuwezi kufahamu Mungu. Lakini kama yule mchungaji aliyetafuta kondoo aliyepotea (Luka 15:3-7); ndivyo ilivyo na sisi, Mungu alitutafuta, akaingia gizani ili afungue macho yetu tupate kuona ukweli na kumfahamu Yesu Kristo na kumwamini yeye. Hiyo ndiyo Injili ya Bwana wetu - alitupenda sisi kwanza. Alipokuja kuokoa Biblia inasema wale watu waliona mwana mkuu (Mat 4:16). Katika kuokolewa ndipo tunapata kufahamu na kuelewa kweli. Yesu alionyesha ukweli huo katika huduma yake kwa kuponya vipofu (k.m. Yoh 9). Kwa hiyo tunamfahamu Mungu katika Injili. Alikuja kututafuta. Kwa Roho Mtakatifu anatujia, akituhuisha, kutuonyesha Yesu, kutuwezesha kumwamini na kupewa uzima wa milele. Na hiyo Injili ni chanzo cha ufahamu lakini pia ni moyo wa ufahamu wetu wa Mungu kwa sababu ni njia tunamkaribia yeye na pia ni utukufu wake mkuu katika kuwaokoa wenye dhambi kwa kujitoa nafsi yake. Kama inavyosema katika waraka wa Yohana, 1Yn 3:16 Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; Kwa hiyo mwanzo wetu na hata mwisho wetu ni kumfahamu Mungu kama anatujia katika mwana wake Yesu Kristo na katika kutuokoa. Injili ndipo chanzo cha kufahamu Mungu. Kwa mtazamo huu tunaweza kuona theolojia ni kitu cha neema. Tunafahamu Mungu kwa zawadi yake ya kujifunulia kwetu. Alituonyesha jinsi alivyo na hasa upendo wake mkuu. Inatukumbusha pia kwamba kuwa na umuhimu zaidi ya

9 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 7 ufahamu wetu wa Mungu ni ufahamu wake wa kwetu. Yaani ni muhimu zaidi kwamba yeye Mungu ananijua mimi, kuliko mimi kumfahamu yeye. 1 Kor 8:3 Lakini mtu akimpenda Mungu, huyo amejulikana naye Gal. 4:9 Bali sasa mkiisha kumjua Mungu, au zaidi kujulikana na Mungu Luke 10:20 Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni KWA HIYO: Je, unafahamu Mungu? Umesikia Injili? Unajua Mungu jinsi alivyotukaribia katika Yesu Kristo kwa Roho Mtakatifu? Unajulikana naye Mungu? Je, umepata uzima wa milele kwa imani? Kama theolojia ni imani kutafuta kuelewa, afadhali tuanze na imani MUHTASARI: Andika mawazo makuu ya leo KAZI YA NYUMBANI Injili ni nini? Andika maelezo mafupi ya Injili kwa mtu ambaye hajui Mungu. Soma mistari hii: Marko 1:1-14; Rum 1:1-6; Kol 1:21-23; 2 Tim 2:8; 1 Pet 1:17-23; Isa 52:13-53:12; Yon 4:1-2; Luka 18:9-14; 1 Thes 1:8-10; Rum 5:1-11

10

11 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA MUNGU UTATU 2.1. MAWAZO MAKUU Mungu ni Mmoja hakuna mwingine Mungu ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu Baba siyo Mwana siyo Roho Mtakatifu Baba ni Mungu, Mwana ni Mungu, Roho ni Mungu (tangu awali) Hakuna miungu mitatu ila ni mmoja 2.2. MAANA YA UTATU Jambo la pekee kabisa katika ukristo ni kwamba tunaamini katika Utatu. Utatu ni yale mafundisho yanayosema kwamba Mungu ni mmoja na pia Mungu ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Kamusi ya Theolojia inasema kwamba maana ya utatu ni: asili moja ya Mungu ni umoja wa nafsi tatu na kwamba Mungu anafunuliwa kuwa nafsi tatu tofauti: Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. asili = jinsi kitu kilivyo; ama kwa mwili au kwa sifa/tabia au kwa desturi au nyingine. K.m. Asili ya Simba ni kuwinda Punda Milia; au asili ya Mti ni mbao. nafsi = utu; msingi/uwezo wa au mahali pa kuhusiana na mwingine. Ni mimi au wewe - kile kitu kinachokufanya wewe kuwa wewe na siyo mwingine. Angalia katika Kamusi ya Theolojia kwa maana ya theolojia na andika hapo chini (Jaribu Don Fleming, Kamusi ya Biblia).

12 10 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR USHUHUDA WA BIBLIA Agano Jipya Hasa Jambo la Utatu linafundishwa katika Agano Jipya. Ila si kufundishwa moja kwa moja kama sisi tunavyojaribu kufanya. Linafundishwa kupitia kauli yake katika kuhubiri Kristo na kumshuhudia yeye na kazi yake kuokoa. Hivyo hatuoni sentensi kama nilivyoandika juu mungu baba ni mungu, na siyo mwana au nyingine, bali tunaona Yesu kuitwa Mungu na pia Mwana, tunamwona kumwomba Baba yake na kusikia sauti yake na kuendelea. Kwa kuzingatia mambo hayo na kwa ushuhuda wa maandiko matakatifu yote ndiyo tutaweza kuona Mungu ni Utatu. Linafunuliwa katika AJ kwa sababu ni katika Mungu mwana kutwaa utu wetu tunapata kuona Mungu jinsi alivyo kweli. Hii siyo kusema kwamba hayupo kwa AK - yupo. Si kwamba alianza kuwa Utatu wakati alipozaliwa Yesu. Lakini hakufunua ya kwamba ni namna alivyo. Katika AK tunaona Mungu kuwa ni Mungu kweli, lakini katika AJ na kwa nafsi ya Yesu Kristo tunapata picha ya Mungu wa ndani. Kwa hiyo hatuna sababu kuangalia angalia kwa utatu katika AK ingawa tunaamini Mungu alikuwa Mungu Baba, Mwana na RM tangu awali. Mat. 11:27 Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia Mungu ni Umoja wa Nafsi Tatu Yesu anafunua Mungu kuwa ni uhusiano wa upendo kamili wa nafsi tatu - Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Kwa hiyo ni mkamalifu kabisa ndani yake na ndiye ni Upendo. Fikiri mistari hii: Mark 14:36 Yohana 17 (hasa m ) 1 Kor 2:10-13 Yn 3:35 Yn 16:13 Ni umoja wa kweli na hakuna utenganisho. Ingawa kuna kutofautiana kwa nafsi upendo wao ni kamili na hivyo umoja ni kamili. Katika umoja huu ndio ni ukweli wa kuwa Mungu ni Mmoja na twasema Mungu ni asili moja katika nafsi tatu. Kwa sababu tunaona Asili ya Mungu ni Umoja wa Nafsi Tatu inatuambia kwamba msingi wa uanadamu wetu ni uhusiano wa upendo. Ndivyo maana kwa sehemu ya kuumbwa katika mfano wake - ni kuumbwa kwa ajili ya uhusiano wa upendo.

13 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA Mungu Baba ni Mungu Katika AJ kwa mara nyingi neno Mungu maana yake ni Mungu Baba. Si mara zote na ni lazima kusoma kwa akili, bali kawaida ni hivyo. Mara nyingine maana yake ni Mungu Utatu bila kutaja nafsi zao na hii ndiyo namna ilivyotumika zaidi katika Agano la Kale. Mara kadhaa Mungu Baba anaitwa na Yesu kuwa Baba (Yn 10:30) au kwa wengine kuwa Baba wa Yesu Kristo (2 Kor 1:3). Hivyo tunaona nafsi yake ni Baba. Kwa ushuhuda wa AJ inaonekana kuna uhusiano wa Baba kwa Mwana ulio kweli kati ya Mungu Baba na Mungu Mwana. Katika Mungu Baba tunapata picha ya ubaba mkamilifu (km. Luka 11:11-13; Ebr 12:5-11) na katika Mungu Mwana tunapata picha ya uana kamili (taz. Rum 8). Hivyo tunaona ingawa Mungu Mwana ni Mungu kamili bila upungufu ni mwana wa Baba na anamtii na kumpenda kama ni Baba. Mwishoni mwa mambo yote Mungu mwana atakabidhi vyote kwa Baba (1 Kor 15:23-28). Katika maombi tunafundishwa na Yesu kumwomba kama yeye kwa Baba yake, kwa sababu Baba yake ndiye Baba yetu katika Kristo. Wana theologia wanasema Baba ni kama chanzo cha vitu vyote na anafanya kwa kupitia Mwana na Roho. Hivyo, utukufu wote mwishoni ni kwa Baba Fil 2:9-11 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba. (taz. pia Efe 1:3-14 hasa m. 3-4) lakini utukufu wake ni katika upendo na tunaona namna anavyotoa kwa Mwana ili mwana aheshimiwe kama Baba mwenyewe. Yn 5:20 Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizo atamwonyesha, ili ninyi mpate kustaajabu. 21 Maana kama Baba awafufuavyo wafu na kuwahuisha, vivyo hivyo na Mwana awahuisha wale awatakao. 22 Tena Baba hamhukumu mtu ye yote, bali amempa Mwana hukumu yote; 23 ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba aliyempeleka

14 12 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR Mungu Mwana ni Mungu Katika Injili aliposhuka kutuokoa tunamwona Mwana wa Mungu na tunamwona kuwa ni Mungu. Nafsi ya pili ya Mungu (Mwana) alishuka na kutwaa utu wa binadamu ili awaokoe (Ebr 2). Biblia ni wazi na hakuna mashaka kwamba Yesu Kristo wa Nazarethi ndiye Mungu aliyeshuka duniani. Fikiria mistari hii: Yoh 1:1-3, 18 Mat 11:27 Tit 2:13 Yoh 20:26-29 Kol 1:15-20 FIl 2:5-11 Ebr 1 Mk 2:1-12 Ufu 1:17 Haitangazi kwamba Yesu ni Mungu tu, ila pia Biblia inaonyesha kwamba Yesu anafanya matendo ambayo ni Mungu tu anayeweza kufanya au anayo mamlaka ya kufanya. Kwa mfano, Alisamehe dhambi kama Mungu (Marko 2) Alikubali kuabudiwa kama Mungu (Yn 9:38; Ufu 19:10) Alikubali kuaminiwa kama Mungu (Yn 14:1) Alikubali kuombwa kama Mungu (Mdo 7:59-60; taz. pia Lk 23:46) Aliahidi kujibu maombi yao (Yn 14:13-14) Alituma Roho Mtakatifu (Yn 20:22) Aliokoa (ambayo ni Mungu tu aliyeweza - Zab 49; 146:3-6) Neno lake linatimia (Lk 24:6-8) Ni mhukumu (Yn 5:21) Anatoa uhai na kufufua wafu (Yn 5:21; taz. Yn 11) Ana uzima nafsini mwake (Yn 5:26) Anaumba (Yn 1:1-3; Kol 1:15-17; Ebr 1). Pia Yesu mwenyewe anadai kuwa na uhusiano wa ndani na Baba hata athubutu kusema na sisi. Mara moja kwa kumwita Mungu kuwa Baba yake wayahudi walijaribu kumwua kwa kufuru (Yn 8). Bali ingawa alikuwa katika mazingira haya alisema, Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake (Yn 14:23).

15 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 13 Hivyo tunaona mambo matatu juu ya Yesu na Uungu wake. AJ linafundisha kwamba Yesu ni Mungu kamili na kabisa bila upungufu Yesu ni pamoja na Baba na Roho (ni kwa Mungu Yn 1:1, 2) Baba na Mwana ni mmoja - na huu upendo wa kukaa ndani ya mwingine ndiyo ni umoja wao (Ni Mungu Yn 1:1; Yn 17:21 Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako ) Mungu Roho ni Mungu Roho Mtakatifu ni Mungu kabisa na kamili, kuhusiana na Mungu Baba na Mungu mwana milele na milele katika upendo. Anaitwa Roho wa Mungu (Mat 3:16) Roho wa Baba ya wanafunzi wa Yesu (Mat 10:20) Roho wa yule aliyemfufua Yesu (Rum 8:11) Roho wa Mwana (Gal 4:6) Roho wa Kristo (Rum 8:9) Roho wa Kweli (Jn 14:17) Roho wa Kufanya wana (Rum 8:15) Roho ya Uhai (Ufu 11:11) Roho ya Neema (Ebr 10:29) Roho ya Hekima na Ufunuo (Efe 1:17) Roho ya Utukufu (1 Pet 4:14). Pia anaitwa Msaidizi mwingine - yaani, mwingine baada ya Yesu: Yn 14:16-17, 25, 15:26-27, 16:7-15. Anania alimwambia uongo RM hivyo alimwambia uongo Mungu (Mdo 5:3-4). Pia, mara kadhaa AJ likitumia nukuu ya Mungu katika AK linasema limesemwa na RM (km. Mdo 28:25-27, Ebr 3:7-9). Ni wa milele (Ebr 9:14) na wa utawala wote (Yn 3:8). RM anatoka kwa Baba. Yaana hakuumbwa au kuzaliwa au kuhulukiwa. Hivyo pia siyo sawasawa na Mungu kabisa. Ni mwingine aliyetendewa kama ni mwingine na Baba na Mwana. Alitumwa na wote Baba na Mwana. Ni namna ambayo Baba na Mwana wanatengeneza nyumba yao ndani yetu. Ni namna ambayo sisi tunafahamu ukweli, kuamini, kufanywa watoto na kuvumulia. Ni yeye anayeamini nani anafanya nini kanisani (1 Kor 12:4-7,11). RM anafanya kile Mungu anachofanya. Anatoa uhai (Yn 3:5-6), anafufua (Rum 8:11), anasema kama alivyosikia na anatukuza Mwana na Baba. Anawezesha imani (1 Kor 12:3), anatakasa (Gal 5:16-18) na kuzaa tunda la haki (Gal 5:22-23).

16 14 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 Kwa wengine jambo gumu siyo kwamba RM ni Mungu au siyo, bali kama ni nafsi kama Baba na Mwana. Bali Biblia inatoa ushuhuda wa yeye RM kuongea: Mdo 13:2. Pia ana uelewa, mapenzi na nguvu. Anaamua ni nani atakayepokea karama kanisani. Anafanya vitu vingine ambayo ni nafsi tu anayeweza kufanya, kama kufaraji, kusaidai, kutia moyo na kuonga. Pia tunaweza kumwambia uongo (Mdo 5:3), kumhuzunisha (Efe 4:30), na kumkufuru (Mark 3:29) Ni tofauti lakini kwa pamoja Hatuna budi kusema Mungu Baba ni tofauti na Mungu Mwana na Roho Mtakatifu. Hiyo nii kwa sababu ya ushuhuda wa Maandiko Matakatifu hasa Yohana 1:1-3; 14:16-17, 25, 15:26-27, 16:7-15, 17:1-26 n.k.. Mitume wanatofautisha kati yao bila kuwatenga. Na hivyo tunapaswa kuona kuna nafsi tatu hapa wanaohusiana kwa upendo tangu milele lakini kwa sababu ya upendo huu huu wa kamili tangu awali ni Mungu mmoja na asili yake ni umoja wa nafsi tatu. Tunaweza kusema Baba, Mwana na Roho Mtakatifu wanashiriki katika asili moja Huu umoja wa Nafsi Tatu ndiye Mungu Mmoja: Hakuna mwingine. Ushuhuda wa Biblia nzima ni kwamba Mungu ni Mmoja na hakuna mwingine. Tunapata katika picha za uumbaji - kuna mmoja tu aliyefanya. Lakini kwa wazi tunaweza kuona katika mistari hii: Kumb. 6:4-5 Isaya 45 1 Korintho 8:4-6 Mungu ni Baba na Mwana na Roho Mtakatifu wanaohusiana kwa upendo tangu milele mpaka milele. Wanatukuziana na kupendana kamili na hivyo tunaona ni Mungu moja hasa washiriki katika jina mmoja kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu (Mat 28:19). Wanafanya kazi kwa pamoja (taz. Gal 4:6 au 2 Thes 2:13-14). Hivyo tunaona neema ya Mungu kwetu, na neema yenyewe. 2 Kor 13:12 Neema ya Bwana Yesu Kristo, na pendo la Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote

17 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA MAKOSA Katika historia ya kanisa tumejifunza katika makosa ya wale waliotutangulia. Hakuna jambo zaidi ya utatu ambalo tunaweza kuona namna tulivyokosa zamani na hadi siku hizi. Makosa hayo yatafundisha katika Historia ya Kanisa na kwa mwaka wa pili wa theolojia. Lakini kwa kifupi tunaweza kuangalia. Kuna wengine wanaosisitiza Mungu mmoja na kuharibu nafsi tatu. Mfano moja ni modalism (umodali?). Hii inasema Mungu alikuwa Baba, halafu alikuwa mwana halafu alikuwa Roho - na siyo nafsi tatu wakato wote tangu milele. Kuna wengine wanaosisitiza nafsi tatu na kuharibu umoja. Wanalofundisha kweli ni miungu mitatu na inakataliwa kwa nguvu katika Biblia. Kuna wengine wanaotaka kukiri Yesu ni kitu maalumu, bali kumtofautisha na Baba ambaye ni Mungu kabisa. Mfano moja ni waariani (Arius) wanaosema Yesu ni mungu mdogo. Ingawa ni ngumu tunapaswa kuamini na kukiri kwamba Mungu Baba ni Mungu, Mungu Mwana ni Mungu na Mungu Roho ni Mungu - ni nafsi tatu wanaotofautiana kati yao bali pia ni wenye umoja bila upungufu na hivyo wanashiriki asili moja - ni Mungu Mmoja na hakuna mwingine IMANI Tunasaidiwa sana na wenzetu waliotutangulia kwa sababu walijadiliana mambo haya kwa hekima na akili na upendo. Walitunga kauli za imani yetu - Imani ya Mitume, Imani ya Nikea na Imani ya Athanasio ili jambo la Utatu lifundishwe wazi kabisa. Soma Kauli za Imani zile tatu (angalia kitabu cha Sala) na andika maswali na mawazo yako kuhusu mafundisho yao juu ya Mungu Utatu. Pia kuna Sharti la Kwanza la Sharti 39 za Dini 1. Juu ya Kuuamini Utatu Utakatifu (Of Faith In The Holy Trinity) MUNGU aliye hai na wa kweli, na wa milele, ni mmoja tu, naye hana mwili, wala viungo, hageuki; mwenye enzi, na hekima, na wema usio na ukomo; Mhuluku na Mhifadhi wa vyote vinavyoonekana navyo visivyoonekana. Na katika umoja wa Uungu huo mna Nafsi tatu zenye asili, na uwezo, na umilele mmoja; Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu.

18 16 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014

19 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA UMUHIMU Tunaweza kuwa na wasiwasi kuhusu mafundisho hayo. Kwa nini Mungu siyo rahisi? Tumewahi kupingwa na wengine wanaosema mafundisho hayo ni kuchafua yaliyo wazi na safi. Kwa nini ni muhimu kujua na kuamini katika Utatu. Fikiria mambo hayo: Ni kweli na namna Mungu alivyo - hivyo ni utukufu wake. Katika Yesu kuwa ni Mungu tuna ufunuo wa kweli wa Mungu Katika Yesu kuwa ni Mungu anaweza kulipa deni zetu zote na hivyo kutuokoa Utatu unaonyesha upendo wa Mungu katika kujitoa kwa ajili yetu Utatu unaonyesha upendo wa Mungu ndani yake - Baba kwa Mwana n.k., Utatu unathibitisha ukamilifu wa Mungu; hana haja kwa uumbaji. Pia tuna utatu kufunuliwa katika Injili kwa sababu Mungu Baba alituma Mungu Mwana kutwaa utu wetu, kufa na kufufuka kwa ajili ya wokovu wetu na pamoja Mungu Baba na Mwana wanatuma Roho Mtakatifu kutuhuisha, kuanzisha imani ndani yetu na kwa Roho wanakaa ndani yetu KWA HIYO Tunapaswa kutafakari na kuamini na kuabudu Mungu huyu aliyejifunuliwa kuwa Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Siyo jambo la kusadiki tu. bali kufurahia katika utukufu na wema wake. Je, unapenda na kuamini Mungu Baba, Mwana na Roho Mtakatifu kuwa ni mmoja na Mungu wetu? Vivyo hivyo unasadiki na kumawabudu Mungu Mwana na Mungu Roho kuwa Mungu pamoja na Baba? Je, unaweza kuelewa kwa nini Mungu Utatu ni msingi wa wokovu wetu? 2.8. MUHTASARI: Mungu wetu jinsi alivyo ni Mungu Baba, Mungu Mwana na Mungu Roho Mtakatifu. Mungu Baba ni Mungu. Mungu Mwana ni Mungu na Mungu Roho ni Mungu. Baba siyo Mwana siyo Roho. Katika uhusiano wao wa upendo kamili ndio kuna umoja bila upungufu na hivyo kuna Mungu Moja tangu milele mpaka Milele na hakuna mwingine: huyu Mungu, Yahweh, ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.

20

21 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA MUNGU MWENYEZI 3.1. MAWAZO MAKUU Mungu ni tofauti na wanadamu Mungu ni Mwenye uweza hutawala mambo yote Mungu ni Mwema anachofanya ni chema sana Mungu ni Mwenye Hekima anajua namna ya kufanikia Jina la Bwana linaonyesha tabia yake Matendo ya Mungu yanaonyesha tabia yake 3.2. MWENYE UWEZA; MWEMA NA MWENYE HEKIMA Swali tunalotaka kujaribu kujibu leo ni hili: Mungu ni nani? Tumekwishaona kwamba Mungu ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Bali tunaweza kusema nini zaidi kuhusu Mungu? Kwa kifupi tunaweza kusema Mungu ni mwenye uweza; mwema na mwenye hekima. Lakini, kwanza tuone kwamba Mungu ni tofauti na mwandamu Tofauti na Mwanadamu Kwanza kabisa ni muhimu kutambua kwamba Mungu ni tofauti sana na mwanadamu. Mungu ni mtakatifu. Maana ya Utakatifu kimsingi ni utofauti na utenganisho. Mungu ni tofauti pia ametengwa na wanadamu. Watu wengi wanafikiri Mungu ni kama sisi, mkubwa tu. Bali siyo. Mungu ni tofauti kabisa, na ingawa tumeumbwa kwa mfano wake na kwa sehemu tunafanana naye, hatuwezi kusahau kwamba yeye ni Mungu na sisi ni viumbe. Njia chache ambazo Mungu ni tofauti ni hizi: hategemei kitu kwa uwepo wake ni wa milele ana uweza wote ana ufahamu wote yupo kila mahali ni roho haonekani Fikiria mistari hii:

22 20 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR Mwenye Uweza Mungu anatawala kila kitu. Hakuna kinachotokea bila utawala wake. Anapanga na kufanya mambo yote ya historia ili alete wanadamu kukombolewa na Kristo kwa ajili ya utukufu wake wote. Mungu ni huru kabisa. Hawezi kuzuiliwa na chochote isipokuwa tabia yake mwenyewe. Siyo giza wala nguvu wala wanadamu wala malaika inayoweza kumzuia. Ni huru katika wakati, nafasi, uwezo na ufahamu. Wakati Anatawala wakati. Aliuumba wakati na anatawala juu yake. Au kwa lugha nyingine ni wa milele; hana mwanzo wala mwisho. Haathiriwi na kupita kwa wakati. Anajua kamili wakati uliopita, wakati ulio sasa na wakati ujao. Zab 102:25-27 (taz. Ebr 1:10-12) Hapo mwanzo uliutia msingi wa nchi, Na mbingu ni kazi ya mikono yako. Hizi zitaharibika, bali Wewe utadumu Naam, hizi zitachakaa kama nguo; Na kama mavazi utazibadilisha, Nazo zitabadilika. Lakini Wewe U Yeye yule; Na miaka yako haitakoma. Nafasi [mwenye kupatikana/kuwa kila mahali] Anatawala nafasti. Aliumba nafasi na kila kilichomo. Ni Roho na hakuna mahali ambapo hayupo. Uwepo wake upo kila mahali. Zab 139:7-12 Niende wapi nijiepushe na roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako? Kama ningepanda mbinguni, Wewe uko; Ningefanya kuzimu kitanda changu, Wewe uko. Ningezitwaa mbawa za asubuhi, Na kukaa pande za mwisho za bahari; Huko nako mkono wako utaniongoza, Na mkono wako wa kuume utanishika. Kama nikisema, Hakika giza litanifunika, Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku; Giza nalo halikufichi kitu, Bali usiku huangaza kama mchana; Giza na mwanga kwako ni sawasawa. Uwezo Hakuna kinachoweza kupigania na Mungu, wala kumzuia wala kumshinda. Anatawala vyote kwa mapenzi yake. Yuko huru kufanya yoyote anayochagua,

23 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 21 isipokuwa vile vinavyo kinyume ya tabia yake. Kwa mfano, hawezi kusema uongo (Ebr 6). Kwa Mungu yote yawezekana (Mk 14:36). Ayubu kinaoyesha kwamba Shetani anahitaji kwenda Mungu kwa ruhusa kabla ya kumtesa Ayubu (Ayu 1-2). Uwezo wa Mungu unaonekana hasa katika uumbaji, kushinda miungu ya Misri, kuingiza watu wake katika nchi ya ahadi, kumweka Daudi kuwa mfalme, kutoa watku wake kutoka Babeli (baada ya kuwatuma kule kwanza) na katika kumtuma Yesu Kristo. Yer 32:17 hapana neno lililo gumu usiloliweza Isa 40:21-32 Ufahamu Hakuna ambacho Mungu hakukifahamu. Anajua vyote hata siri za miyo yetu. Hakuna ambayo ni ngumu sana kumshinda, wala kuwa ndogo sana kwamba hajali. Yuko huru kujua kila kitu na kila mtu. 1 Yn 3:20 naye anajua yote Ebr 4:13 Mat 10:30 Zab 139:1-6; (kuwepo kila mahali na kujua kila kitu ni pande mbili za kitu kimoja) Hivyo katika kuona kuwa Mungu ni mwenye uweza tunaona ni huru kabisa, Mungu wetu yuko mbinguni, Alitakalo lote amelitenda (Zab 115:3). Ni mtawala wa mambo yote. Isa 45:6b-7 Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine. Mimi naiumba nuru, na kulihuluku giza; mimi nafanya suluhu, na kuhuluku ubaya; Mimi ni Bwana, niyatendaye hayo yote. Katika Biblia tunaona utawala huu hasa katika kifo cha Yesu Kristo. Yesu alikufa kwa ajili ya utimilifu wa mipango ya Mungu, lakini pia kwa sababu watu waovu walitaka kumwua. Mungu hutawala mambo yote kwa ajili ya wema. Akiwa mwenye uwezo wote tunaweza kumtegemea kabisa. Bila uwezo wa kufanya, hatutaweza kujua atatuokoa na kujibu maombi yetu. Hata hatutaweza kujua anaweza kusikia maombi. Hivyo na kuwepo kila mahali na kila wakati na kufahamu mambo yote. Inatutia moyo - Mungu wetu ni mwenye enzi na yuko kwa upande wetu. Mat 28:16-20

24 22 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari. Maswali? Soma Kutoka 34:5-8. Orodhesha kila sifa ya Mungu inayotajwa na jina lake. Pembeni kila sifa andika maana yake kwa lugha yake mwenyewe, au kwa kutafuta maana katika kamusi ya kiswahili. Halafu fikiria mfano katika Biblia ambao tunaona sifa hii ya Mungu. Nitafanya mfano moja Sifa Maana Mfano mwingi wa huruma kujaa na upendo wa namna ya kumsaidia mwenye haja Mwa 29:31; 30:22-23; Kumb 24:19; Luka 10:30-37; Mat 9:36

25 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 23

26

27 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA Mwema Luka 18:9 Yesu akamwambia, Mbona unaniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, naye ndiye Mungu. Mungu ni mwema. Vyote anavyofanya ni vyema na kwa nia njema na matokeo yao ni mema. Kwa historia ya wanadamu tunaona kuanzia uumbaji (ni njema..ni chema sana). Lakini tunaona kupitia maisha yetu na mpaka siku ya mwisho tutaona Mungu ni mwema (1 Pet 2:12). Wema ni nini? Wema ni vyote vinavyokaa na lengo zuri na safi na takatifu. Tunaposema vitu ambavyo Mungu alivyoviumba ni vyema, maana yetu ni kwamba vinakaa na kusudi la Mungu kwa ajili yao na kuakisi hata kidogo wema wake. Kwa kusema Mungu ni mwema ni kusema Mungu amejaa vyote vilivyo vyema na vya urembo, vinavyopendezwa, vinavyofaa na kusaidia, vinavyo vitakatifu na safi. Wema wa Mungu ni utukufu wake katika ufadhili, ukarimu na upendo. Ni cha kwenda nje, kwa sababu Mungu ni kwa ajili ya wengine katika asili yake. Mara zote anatenda kwa ajili ya wengine - hasa uumbaji wake. Vyote alivyofanya na atakavyofanya katika uumbaji ni maonyesho ya wema wake. Wema wake ni tabia yake ya utakatifu na haki. Ni ukweli na uaminifu. Chochote anachofanya ni chema na hakuna uovu naye. Mifano ya wema wake: Neh 9:25 Wakaitwaa miji yenye boma, na nchi yenye neema, wakazitamalaki nyumba zilizojaa vitu vyema, birika zilizochimbwa, mizabibu, na mizeituni, na miti mingi yenye matunda; hivyo wakala, wakashiba, wakanenepa, wakajifurahisha katika wema wako mwingi. Mdo 14:17 Lakini hakujiacha pasipo ushuhuda, kwa kuwa alitenda mema, akiwapeni mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha. Mungu ni chanzo cha wema. Hakuna anayeweza kufanya wema bila msaada wa Mungu. 3 Yn 11 Mpenzi, usiuige ubaya, bali uige wema. Yeye atendaye mema ni wa Mungu, bali yeye atendaye mabaya hakumwona Mungu. Historia ya uhusiano kati ya Mungu na Israeli inaonyesha wema wake. Aliahidia, kukomboa, kujitoa, kuhukumu, kuokoa na kuvumulia (km. Ezek 16, Neh 9). Msalaba ni ishara tupu ya wema wake, tukimwona Mungu kufanya kutoka upendo wake kwa viumbe vyake na pia kwa kadiri ya haki yake. Hata kupitia maovu ya watu Mungu

28 26 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 anafanya wema (km. Mwa 50:20, Mdo 2:23-24), na anafanya kwa ajili ya wema wetu (Rum 8:28ff). Hapa inatusaidia kuangalia pia sifa hizi za Mungu: uaminifu, upendo, rehema, huruma, neema, utakatifu, mwenye haki. Uaminifu Ebr 13:8 Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele Uaminifu ni tabia ya Mungu kutobadilika na kutimiza neno lake. Tuna uhakika ya kwamba yeye aliyekuwapo jana na yupo leo ndiye atakayekuwa kesho. Mungu ni Mungu wa Baba zenu ni yule yule, kwa sababu habadiliki kama mtu na ni mwaminifu. Num. 23:19 Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza? Kumb 7: Kor 1:18-22 Upendo Rom. 5:8 Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Upendo ni kutenda kwa ajili ya wema wa mwingine. Kwa mfano, mtu anaweza kumsindikiza mgonjwa hospitalini kwa ajili ya kumtunza. Mungu ni upendo, lakini pia ni wingi wa upendo. Katika historia yake na Israeli tunaona wingi huu wa upendo kwa kuendelea kuwafanyia wema, lakini pia, kwa kukataa kuacha kuwatendea wema. Ezra 9:7-9 1 Yn 4:8-10. Tunapenda kumwiga Mungu na kumtii. Tunapenda kwa sababu yeye aliwahi kutupenda sisi (1 Yn 4:19) Kuna maneno matatu ambayo yanaeleweka kuwa upendo katika hali fulani. Ni huruma, rehema na neema. Hakuna tofauti sana kati ya maneno hayo, bali tunaweza kufikiria namna hizi zifuatazo. Huruma Matt. 11:28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa

29 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 27 moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; 30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi. Huruma ni kuonyesha upendo kwa mtu mwenye haja. Akiwa mgonjwa, au maskini au menye hitaji mwingine, kumwonyesha upendo ni huruma. Mfano mmoja ni yule Msamaria aliyemhurumia mgonjwa katika mithali ya Yesu (Luka 10:30-37). Taz. pia: Amu 2:18; 1 Fal 3:26; 2 Nya. 30:9; Mat 14:14, 15:32, 20:34, Je - tukisema Mungu anakuona kwa huruma, inasema nini juu ya hali yako? Rehema Zab 51:1 Ee Mungu, unirehemu, Sawasawa na fadhili zako. Kiasi cha wingi wa rehema zako, Uyafute makosa yangu. Rehema ni kutokumpa mtu kama anavyostahili katika hali ya kuhukumu au kuadhibiwa. Kwa mfano, mwanafunzi anaweza kuja darasani na hajafanya insha. Anastahili sifuri, bali kumrehemu ni kumpa muda wa ziada au kumwachie asiadhibiwe. Kuna mifano mingi ya rehema za Mungu katika Biblia. Kuna Yona na Waninawi, kuna Lutu katika Sodoma na Gomorra, na kuna Wanaisraeli wakati wa kutengeneza sanamu ile ya ndama wakati wa Aruni. Rehema ni sehemu ya upendo. Yaani ni kwa hiari ya yeye anayetoa, na siyo kudaiwa. Mungu anarehemu anayerehemu tu - kwa maamuzi yake mwenyewe (Rum 9:15). Rehema zake ni wokovu wetu na chanzo cha maadili yetu (Rum 12:1-2). Taz. pia Luke 18:9-14 Je, tukisema Mungu anakurehemu, inasema nini juu ya hali yako? Neema Eph. 2:8-10 Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; 9 wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. 10 Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo. Neema ni kumpa mtu kitu ambacho hakistahili. Kwa mfano, mwanafunzi anastahili sifuri lakini mwalimu anampa 100%. Neema ni namna ya kutoa zawadi kwa ukarimu, bure, bila malipo. Inasisitiza kwa sababu yule aliyepokea hastahili kabisa. Hakuna ustahili naye kabisa.

30 28 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 Neema siyo uwezo Mungu anayoitia ndani kumwezesha mtu kumtii. Mungu anafanya hivyo, na anafanya kwa neema yake, lakini neema siyo kitu ni namna ya kutoa zawadi. Ni upendo. Rum 4:1-8 Maneno hayo matatu yanatusaidia kuelewa wokovu. Tunastahili hukumu, bali Mungu anaturehemu, akiacha kutuadhibu. Tu wanyonge, mateka na kudhulimiwa na dhambi, kifo na kufuata ulimwengu, bali Mungu alituonea kwa huruma, kuondoa mizigo yetu na kutukomboa na nyororo zetu. Hatustahili kuingia wala kurithi ufalme wa Mungu, hatuwezi kujipatia haki, kutimiza sheria, bali Mungu anatupa wokovu kuwa ni zawadi - neema - kutusamehe na kutuhesabia imani yetu kuwa ni haki hatuwezi kustahili sisi wenyene. Utakatifu Kut 33:20 Huwezi kuniona uso wangu, maana mwanadamu hataniona akaishi Sehemu nyingine ys wema wake Mungu ni utakatifu wake. Ni mtakatifu halisi na kabisa. Utakatifu ni kuwa tofauti na pia kuwa safi kimaadili. Mungu ni mtakatifu na kila anachogusa kinafanywa kuwa kitakatifu. Anapotuita anatufanya kuwa watakatifu ili tufanye kazi yake. Kwa viumbe utakatifu ni kutengwa na Mungu kwa kusudi maalumu, pamoja na kuandaliwa (kuoshwa/kusafishwa) naye kufaa kwa kusudi hii. Law 10:1-3 Isa 6:1-6 Mungu ametengwa na uovu na dhambi; anachukia dhambi. Ni safi sana hata hawezi kutazama uovu. Kama mwovu akifika katika uwepo wa Mungu Mtakatifu, mwovu ataangamiza. Tumeitwa kuwa watakatifu kwa sababu Mungu ni mtakatifu. Yaani kujitenga na uovu wa dunia hii na kusafishwa na kuishi maisha safi. Mwenye Haki Prov. 17:15 Yeye asemaye kwamba asiye haki ana haki; naye asemaye kwamba mwenye haki hana haki; Hao wote wawili ni chukizo kwa Bwana. Sehemu ya mwisho ya wema wake Mungu ambayo nataka kuangalia juu yake leo ni mwenye haki. Haki ni kukaa vizuri na bila upungufu na kiwango cha kisheria au kimaadili. Hasa ni neno la kisheria na kwa Mungu linasema kwamba kwa sheria yake Mungu anakidhi kila neno.

31 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 29 Mungu ni mwenye haki. Kila wakati anatenda kwa kadiri ya tabia zake za haki na sheria yake. Kwa historia ya Israeli na mataifa tunaona haki yake kwa sababu anaadhabu wenye hatia na kuwatoa huru wenye haki. Mungu hawezi kuacha uovu bila kuadhibu kwa sababu ni mwenye haki, lakini pia hataadhibu kamwe mtu asiye na hatia. Kila mara anatenda lililo haki. Neh 9:26-27 Kwa hiyo swali kuu la waraka wa Warumi ni hili Mungu anawezaje kusamehe dhambi na kubaki mwenye haki? Jibu linapatikana katika kuona Yesu kuwa mbadala kwa ajili ya wenye dhambi. Rum 3: Mwenye Hekima Mungu ni mwenye hekima. Hekima ni kujua lililo bora na namna ya kutekeleza. Ni kuchagua nakufanya kwa kadiri ya makusudi mazuri. Mungu ana ufahamu wote, na pia anajua namna ya kufika mipango yake na kuitekeleza. Kwetu chanzo cha hekima ni kumcha Bwana - kwa sababu ndiye mwenye hekima na yote anayofanya ni kwa hekima. Mifano ya hekima ya Mungu ni uumbaji, namna alivyotawala na kusaidia akina Ibrahimu, namna alivyookoa Israeli kutoka Misri kwa mapigo na kutuma mnyonge Musa, na hasa katika maisha (mapema) ya Sulemani na mafundisho yake. 2 Nya 2:12 Praise be to the LORD, the God of Israel, who made heaven and earth! He has given King David a wise son, endowed with intelligence and discernment, who will build a temple for the LORD and a palace for himself. Bali zaidi ni namna atakavyochukua kwa ajili yake watu kutoka kila taifa na kukaa nao, wakiwa wamasamehewa na kutakaswa, wakiwa wamefanywa watoto wake na kufanana na mwanae kihusiano na kimaadili na kitabia. Msalaba na wokovu wa wenye dhambi wa mataifa yote ndio mfano mkuu wa hekima yake anajua namna ya kufanya na anatekeleza. Tunaona hekima hii ni kubwa sana, kushinda hekima ya wanadamu kwa kiasi kubwa sana, ya kwamba inaonekana hata upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya Mungu. Hiyo si kusema Mungu ana upumbavu, bali hekima yake ni kubwa sana, ya kwamba hata ndogo sana yake ni zaidi sana hekima ya wanadamu, na pia alilofanya msalabani katika hekima inaonekana kwetu kuwa ni upumbavu. 1 Kor 1:18-31.

32 30 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 Katika lugha yake mwenyewe andika maana na mfano wa maneno yafuatayo: 1. Wema 2. Uaminifu 3. Upendo 4. Huruma 5. Rehema 6. Neema 7. Utakatifu 8. Haki 9. Hekima

33 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA MUNGU MWENYEZI (II) 4.1. MAJINA YA MUNGU Kuna majina kadhaa kwa ajili ya Mungu kupitia Biblia. Tumeshaona mmoja, Yahweh, jina ambalo kwa hilo anajifunua kwa Musa. Yesu anatufundisha kumwita Mungu, Baba, na kubatiza watu kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Pia anarejewa katika Biblia kuwa ni Mungu na Bwana au Muumba. Kuna mengine pia. Siyo muhimu sana, na hatuwezi kusema nyingi juu yao, kwa sababu ya lugha, bali ni nzuri kugusa hata mara moja kwa sababu yamo katika Biblia. Mungu Aliye juu sana (El Elion) Maana yake ni Mungu aliyeinuliwa juu vyote au kutukuzwa au kuwa na mamlaka zaidi yote. Au kwa lugha nyingine Mungu wa Miungu, au Mungu mzuri sana mno. Hata wengine wakidai wanao miungu yao, Mungu aliye juu sana ni Mungu wa miungu hawa. Mwa 14:19-22 Mungu Mwenyezi (El Shaddai) Maana yake ni Mungu anayetoa au kutunza au kubariki. Zamani wengine walisema ni kuangamiza, bali siyo sana. Kwa mfano, Mungu anaitwa El Shaddai au Mungu mwenyezi katika Mwanzo 17, ambapo anaahidi mtoto na nchi ya wingi kwa Ibrahimu. Njia yoyote inatangaza wema wake na uweza wake na hekima yake. Mwa 17:1-8 Bwana wa Majeshi [Yahweh Zavot] Hili linatumika sana na Manabii na halipatikiani katika vitabu vya kwanza bali ni wakati wa wafalme na baada ya hapo. Ni jina la cheo cha ufalme kwa Mungu. Labda Israeli walikuwa na mfalme, bali kuna mfalme mkuu wa pekee moja tu. Pia maana yake ni kivita - Majeshi ni Majeshi. Majeshi yake Mungu yaweza kuwa ni malaika au labda ni watu, bali yeye ni kiongozi na ana majeshi makuu na mengi. Ni jina lake la kifalme. Zab 59: LUGHA YA BINADAMU INAYOTUMIKA KWA MUNGU

34 32 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 Mara nyingi katika Biblia waandishi huweza kutumia tabia za bindamu ili waeleze Mungu. Kwa mfano, wanasweza kusema Mungu alikomboa Israeli kwa mkono ulionyoshwa (k.m. Kut 6:6). Wanapotumia lugha hii ni lugha ya kusaidia katika maelezo na siyo kufundisha kwamba Mungu anazo tabia hizi au viungo hivi. Ni lugha ya picha. Mungu, bila shaka, ni Roho; yaani hana mwili. Tunatumia kila siku sisi kwa sisi lugha ya namna hii. Kwa mfano, naweza kusema mikono ya miti yanayumbayumba au mti ule unasimama juu. Si kwamba nasema mti ni mtu mwenye mkono au mikono yake ni ya kwetu au kwamba kama mtu unaweza kusimama. Waandishi hutumia lugha hii kusaidia kuelewa na kuongeza uzito wa yale wanayotaka kusema. Mifano mingine: Isa 51:9 Amka, amka, jivike nguvu, Ee mkono wa Bwana; Amka kama katika siku zile za kale, Katika vizazi vile vya zamani. Zab 34:15 Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao. Kwa mistari hiyo tunaona mkono, macho na masikio lakini pia maneno ya kitenzi kama amka na huelekea. Tunaweza kuelewa maana yake si kufundisha Mungu ana masikio, bali anajua kila kitu. Kwa lugha ya kiingereza lugha hii inaitwa anthropomophism. Swali gumu linakuja tukianza kufikiria juu ya mambo mengine na siyo viungo tu. Mambo kama viungo ni ya binadamu tu, bali je, juu ya fikira, hisia, hekima, kuamua na kupenda? Pia, tukiumbwa kwa mfano wake, je hatuwezi kutegemea kwamba Mungu atafanana nasi hata kidogo? Ndiyo tunaweza. Na ingawa Mungu hana mwili na hafanani nasi kimwili, sisi tukiumbwa kwa mfano wake tunafanana naye kwa mambo mengi - hasa katika uwezo wetu wa kuhusiana na tabia zile za kuwezesha mtu kuhusiana na mwingine. Hivyo, Mungu anapenda kweli, ana hekima kweli, anaamua kweli, anahisi kweli na tunafanana naye katika mambo pasipo mwili. ** Lakini Mungu ni halisi na sisi ni mfano wake. Kwa hiyo, sisi tunamwiga yeye, na yeye hatuigi sisi. Tunapenda kwa sababu alitupenda sisi kwanza UTAWALA MKUU WA MUNGU Mojawapo ya matatizo ambayo watu wanaweza kusumbuliwa nayo kuhusu Mungu ni mipaka ya utawala wake. Hasa wanaona uovu na kusema Mungu aliye mwema hawezi kukubali uovu. Kwa hiyo, kuna mpaka kwa utawala wake. Au mwingine labda atasema kwamba kwa wanadamu kuwa na hiari kweli, Mungu hawezi kutawala juu ya mioyo yao. Jibu la Biblia kwa maswali hayo ni nini?

35 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA Mungu ni Mtawala Bila shaka Biblia inafundisha kwamba Mungu ni mtawala mkuu na hakuna mwingine. Hakuna mipaka kwa utawala wake. Anatawlaa kila kitu na kila tukio kwa ajili ya kutimiza mapenzi yake mema. Mungu ni mtawala mkuu bila upungufu, bali upungufu wake haizuii wala kupunguza wajibu wa wanadamu. 1 Fikiri mistari hii yafuatayo: Kumb. 32:39 1 Sam 2:6-10 Zab 115:2-3 Zab 135:5-6 Mith 16:4, 9, 33 Isa 45:5-7 Dan 4:34-35 Rum 9:6-26 Efe 1:11 Kwa njia ambayo hatuwezi kuelewa, Mungu ni mtawala hata katika wakati mwovu pasipo kuwa mwovu wala kuathiriwa na uovu yeye mwenyewe, kama ni wazi kwa mistari yafuatayo: Kut. 21:13 Ruth 1:13 Isa 45:6-7 Omb. 3:32-33, Sam 24:1; 1 Fal 22:21ff Wanadamu wana wajibu halisi Wanadamu wameumbwa kuwa na kubeba wajibu. Wanaweza kuchagua, kuamua, kuamini, kuitikia, kutii au kutokutii, na kwa maamuzi yao kuna umuhimu wa kimaadili au ki-wema. Lakini katika Biblia wajibu wa kibinadamu kamwe hauzuii wala kupunguza utawala mkuu wa Mungu, wala haukufanya Mungu kutegemea kitu wala mtu kwa njia yoyote. Mara nyingi katika Biblia wanadamu wanaitwa kutii, kuamua, kuamini na wanahukumiwa wakikosa kufanya. Mungu mwenyewe anasihi watu kutubu: Isa 30:18, 65:2 1 Nimesaidiwa sana kwa sehemu hii na sehemu ya kitabu kilichoandikwa na Don Carson, kinachoitwa kwa kiingereza A Call to Spiritual Reformation.

36 34 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 Omb. 3:31-36 Ezek 18:30-32, 33:11 Mdo 17:30 Joshua anawaita waisraeli kumtumikia Bwana - Josh 24:14-15 kama Musa aliyemtangulia aliwaita kuchagua uzima - Kumb. 30:19. Injili inawaita wanadamu kuamini na kukiri Yesu ni Bwana (Rum 10:9-11), ingawa sura iliyotangulia imesema Mungu atachagua ni nani atakayerehemu (Rum 9:18). Kwa hiyo, tunaweza kuamua kweli kweli kwa hiari yetu. Ingawa tutajifunza pia siku nyingine ya kwamba hiari ya wanadamu siyo hiari, tu watumwa wa dhambi na tamaa za mwili. Uhuru si uwezo kabisa. Kwa mfano, sina uhuru wa kuruka kama ndege, wala kubali chini ya bahari kwa siku nyingi. Bali Mungu anatukubali kufanya kwa kadiri ya tamaa zetu. Na hivyo tuna wajibu kwa matendo na maamuzi yetu, na tutahukumiwa, bila shaka. Hivi vyote haivpunguzi utawala mkuu wa Mungu anayetawala vyote Zote zaenda pamoja Kwa hiyo, kwa imani, lazima tushike zote pamoja. Mungu ni mtawala bila upungufu, na sisi ni wenye wajibu. Wajibu wetu ni kweli na hauzuii utawala wa Mungu juu ya maamuzi yetu. Utawala wa Mungu ni kweli na hauzuii wajibu wetu kufanya wema. Fikiria na mwenzako mistari hii na namna inavyofundisha zote mbili ya kwamba wanadamu ni wenye wajibu na Mungu ni mwenye mtawala wote. Mwanzo 50:19-20 Yoh 6:37-40 Fil 2:12-13 Mdo 19:9-10 Mdo 4:23-30 Katika mambo hayo tunapaswa kukumbuka mambo machache. 1. Mungu ni mwema, hafanyi uovu, na anachofanya mambo yote ni mema. 2. Hatujui kila kusudi la Mungu wala kila tokeo la jambo fulani (Kumb 29:29) 3. Mungu anatawala juu ya wema na juu ya uovu tofauti. Anapaswa kusifiwa kwa wema wote, lakini hawezi kulaumiwa kwa uovu wowote Wokovu Hata wokovu wetu ni kwa mapenzi ya Mungu. Wote watakaookolewa wameteuliwa naye tangu mwanzoni, lakini pia wana wajibu kuamini. Efe 1:1-14 na Rum 9, na Yoh 10 hasa zinafundisha jambo hili.

37 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 35 Ukweli huu hutia motisha kwa ajili ya kufanya uinjilisti. Nina uhakika kwamba neno la Mungu litafanya kazi yake. Nikihubiri najua Mungu ana watu wake na wataamini kwa sababu ya neema na uchaguzi wake. Mdo 13:48 Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini Sala Pia utawala wa Mungu hutia motisha wa kuomba. Hata hivyo sala ni ushuhuda wa kwamba Mungu ni mtawala na tuna wajibu. Kwa mfano, kama Mungu hatawali mambo yote, mbona unaomba. Au mwingine, kama hatuna wajibu na Mungu hasikii maombi yetu, mbona unaomba. Bali Mungu kwa neema yake anatusikia na anachagua kwa neema kutumia maombi yetu kutimiza makusudi yake ya milele. Kwa mfano, mtu fulani aliokoka. Aliamini kwa sababu alichaguliwa na Mungu tangu milele kufananishwa na mwanae. Lakini pia, aliokoka kwa sababu anaamini, alisikia Injili na kuelewa na kushawishiwa na maisha mema ya wakristo. Lakini pia, aliokoka kwa sababu ya maombi ya watu wa Mungu ambayo Mungu alichagua kwa neema kujibu. Hivyo - kwa sababu Mungu ni mtawala na tuombe! 4.4. MASWALI? 4.5. KAZI Katika Don Fleming, Kamusi ya Biblia, soma wakala: Amri ya Mungu ya Kabla Mamlaka, Nguvu Maongozi ya Mungu

38 36 THEOLOJIA 1 MIKE TAYLOR 2014 INSHA #2: MAELEZO YA MAMBO MACHACHE Kazi: Chagua ama mada ya Utatu au mada ya Mungu Mwenyezi na andika maelezo ya mambo makuu juu ya mada hii. Changamoto: Lakini naomba uandike katika mmojawapo ya aina mbili hizi: Ama andika maelezo yako kwa ajili ya kufundisha watoto wa shule ya jumapili, Au andika maelezo yako katika wimbo wa kuimba (km. tenzi 6) Tarehe ya kukusanyika: 31/10/2014 Kumbuka kutumia Biblia!

39 MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA UFUNUO Ufunuo ni mafundisho ya namna tunavyoweza kujua Mungu. Ni Ufunuo kwa sababu hatuwezi kumfahamu nje yeye kusema nasi. Tutaongea mwisho wa sura hii juu ya majaribio ya kumfahamu Mungu nje ya ufunuo. Lakini tuanze na Ufunuo. Kuna aina mbili ya ufunuo. Kuna ufunuo wa kiujumla, na ufunuo maalumu. Maana yao tofauti hasa ni kwa nani na kwa vipi Mungu alisema. Kwa rahisi Ufunuo wa kiujumla ni kwa watu wote, mahali pote, nyakati zote bila kutenga au kusisitiza. Ufunuo maalumu ni kwa akina fulani ya watu, mahali fulani na wakati fulani. Ni kama upendo wa Mungu. Huonyesha upendo kwa wote kwa kuwatumia mvua (Rum 5:45), lakini ana upendo maalumu kwa wale aliowachagua kwa kuwaokoa UFUNUO WA KIUJUMLA. Sehemu kuu za Biblia zinazofundisha juu ya ufunuo wa namna hii ni: Zab 19:1-6 Mdo 14:14-17 Mdo 17:22-31 Rum 1:18-32 Ebu Jaza chati hii: Kifungu Mungu anajifunua kwa vipi? Mungu anasema na nani? Nini kinajulikana juu ya Mungu?

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.

ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu. Waebrania 9:28. KUJA KWA KRIST0 MARA YA PILI "ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28. Mara nyingi sana kuja kwa Kristo mara ya pili huangaliwa tu kama fundisho la dini. Ni

More information

MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI

MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Mwanzo 1:1 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi. Wakolosai

More information

GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI

GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI Utambulisho Grace Communion International ni muungano wa washiriki kutoka pembe mbali mbali za dunia hasa nchi zenye washiriki kwa sasa ni 100. Wito wetu ni

More information

Agano Lililofunikwa Kwa Damu

Agano Lililofunikwa Kwa Damu Agano Lililofunikwa Kwa Damu na Ellis Forsman Agano Lililofunikwa Kwa Damu (The Blood-Sealed Covenant) 1 Agano Lililofunikwa Kwa Damu na Ellis Forsman Oktoba 14, 2012 Agano Lililofunikwa Kwa Damu (The

More information

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT 1 Ushindi Ndani ya Kristo Na W. W. Prescott Mfasiri: M. Mwamalumbili Victory in Christ - Kiswahili 2 Yaliyomo Alinipenda Mimi Aliishi kwa ajili Yangu Mimi Alikufa

More information

B. Wanafunzi watapata ufahamu mkubwa wa kitabu hiki, na jinsi kinavyofundisha kuhusu kanisa.

B. Wanafunzi watapata ufahamu mkubwa wa kitabu hiki, na jinsi kinavyofundisha kuhusu kanisa. Waefeso Mtaala I. Habari kwa Ujumla A. Mkufunzi: Don Walker na kutafsiriwa na Chris Mwakabanje B. Kila darasa ni takribani dakika 38. II. Maelezo na Kusudi A. Mafunzo haya ni uchambuzi wa kina katika Waefeso,

More information

Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally

Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo Na Andrew Connally 1 YALIYOMO Milango ya Kitabu: Ukurasa: 1. Mungu-Kuwako kwake na hali yake 03 2. Huyo Kristo-Nafsi yake na kazi yake 12 3. Maandiko Matakatifu ni yenye

More information

Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu

Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu 134 Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu Picha tuliyonayo kuhusu Mungu ni mojawapo ya kizuizi kikubwa cha kupata uponyaji wetu. Mara nyingi huwa hatujui vizuri kwamba Mungu anatupenda kwa hivyo angependa

More information

JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?

JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? JOE CREWS 1 JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? Na Joe Crews (Hotuba Na. 16 ya Mambo ya Kweli Yanayoshangaza) Mfasiri: M. Mwamalumbili Is It Possible To

More information

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO. MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO. MUHTASARI WA UTANGULIZI WA THIOLOGIA YA USHIRIKA WA NAFSI TATU ZA UUNGU. GRACE COMMUNION INTERNATIONAL LIVING AND SHARING THE GOSPEL MUNGU ANADHIHIRISHWA NA

More information

WAKOLOSAI MTAALA. B. Maoni: Tunapendekeza uwe na fafanuzi (commentary) yoyote yenye kushikilia mafundisho ya awali (conservative) katika Wakolosai.

WAKOLOSAI MTAALA. B. Maoni: Tunapendekeza uwe na fafanuzi (commentary) yoyote yenye kushikilia mafundisho ya awali (conservative) katika Wakolosai. WAKOLOSAI MTAALA I. MAELEZO KWA UJUMLA. A. Mwalimu: Don Walker B. Mkalimani: Chris Mwakabanje C. Kila darasa linachukua takribani dakika 38. II. III. MAELEZO NA MALENGO. A. Kujifunza kwa kina Waraka kwa

More information

Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu?

Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu? Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu? (Attitude Towards Christ Do you Honor Him?) Na Ellis P. Forsman (4-Attitude Towards Christ - Do you Honor Him) 1 Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu? (Attitude Towards

More information

Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia. Ellis Forsman. Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1

Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia. Ellis Forsman. Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1 Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia na Ellis Forsman Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1 Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia na Ellis Forsman Oktoba 8, 2011 Inavyodaiwa

More information

WEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23

WEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23 Toleo X Toleo 23 WEWE NI NANI? (Habari ifuatayo ni hadithi ya mambo ambayo yamenakiliwa katika Matendo 19:10-20 SUV). Paulo mtume wa Yesu Kristo alihubiri katika mji wa Efeso kwa miaka miwili. Katika muda

More information

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika (A Summary Of Arguments For And Against Individual Communion Cups) Na J D Logan Communion Cups) 1 Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi

More information

United Pentecostal Church June 2017

United Pentecostal Church June 2017 Kwa Nini Tusali? Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa "Chagua" Ladies Prayer International kwa Facebook United Pentecostal Church June 2017 Tuko na wafuasi Facebook katika Marekani, Hong Kong, Philippines,

More information

walozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w

walozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w MAMLAKA Tunamshukuru Bwana kwa vile alivyo na yale aliyoyatenda. Tukiweza tu kumfikiria hata tukiwa na mahitaji mbalimbali, yeye atatutimizia. Tusiwatazame watu, tusijitazame sisi wenyewe, tumtazame Mungu

More information

WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen

WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen 1 Index latest update 26. feb. 2008 WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen Wafunaji wa nafsi ABC Mark 16:15-20 Huduma/uiinjilisti Wakristo wachache sana wameitikia mwito wa

More information

UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA

UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA Dynamic Churches International Simeon Oyui P. O. Box 798-00515 Bukubura, Nairobi, Kenya EAST AFRICA Email: ncc_africa@yahoo.com Dynamic Churches International 164 Stonegate

More information

Kifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1

Kifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1 Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Na Ellis P. Forsman Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1 Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Na Ellis P. Forsman Oktoba 11, 2011 Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 2 Kifo

More information

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke- Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa

More information

Kanuni. Muhimu za Kujifunza Biblia. Mchungaji Drue Freeman. Dan Hawkins & Joseph Brown. General Editors.

Kanuni. Muhimu za Kujifunza Biblia. Mchungaji Drue Freeman. Dan Hawkins & Joseph Brown.   General Editors. Kanuni Muhimu za Kujifunza Biblia na Mchungaji Drue Freeman General Editors Dan Hawkins & Joseph Brown a publication of www.villageministries.org Kanuni Muhimu za Kujifunza Biblia 2013 na Village Ministries

More information

Maisha Yaliyojaa Maombi

Maisha Yaliyojaa Maombi (A Prayer-Filled Life) na Terry Warford (A Prayer-Filled Life) 1 (A Prayer-Filled Life) na Terry Warford Nov 5, 2011 (A Prayer-Filled Life) 2 Sura ya nne nay a tano ya kitabu cha Ufunuo ni vifungu vinavyovutia.

More information

MSAMAHA NA UPATANISHO

MSAMAHA NA UPATANISHO Hakimiliki 2007-2017 na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa. MSAMAHA NA UPATANISHO na Jonathan M. Menn B.A., Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, 1974 J.D., Cornell Law School, 1977 M.Div., Trinity Evangelical

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper

More information

IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE

IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE IMANI NA MATENDO IMANI NA MATENDO Hotuba na Makala za Ellen G. White Masomo kutoka katika Hotuba zake Kumi na Tisa zilizotolewa Nzima au kwa Sehemu kuanzia mwaka 1881

More information

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) 102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako

More information

Roho Mtakatifu Ni Nini?

Roho Mtakatifu Ni Nini? Roho Mtakatifu Ni Nini? kwa ajili ya mkutano. Mkutano huu utakuwa tofauti, kidogo na ile ya kawaida tunayokuwa nayo hapa. Kwa kawaida, kila wakati tunapokuja pamoja hapa, ni mkutano kwa wa kwa ajili ya

More information

Watumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1

Watumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1 Watumishi Wa Kristo na Ellis P. Forsman Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1 Watumishi Wa Kristo na Ellis P. Forsman Oktoba 14, 2011 Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 2 Sisi ni watumishi Watumishi

More information

NGUVU. Utangulizi. Yesu alisema,

NGUVU. Utangulizi. Yesu alisema, NGUVU Utangulizi Kwas miaka mingi nimemtafuta Bwana ili aachilie mazingira mazuri ya uwepo wake, nguvu na utukufu wake kudhihirika. Tumeona na kujua matokeo ya yale Bwana ametufunulia. Ikiwa unatafuta

More information

Aina Tatu Za Ibada. Ellis Forsman. Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 1

Aina Tatu Za Ibada. Ellis Forsman. Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 1 Aina Tatu Za Ibada na Ellis Forsman Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 1 Aina Tatu Za Ibada na Ellis Forsman Octoba 15, 2011 Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 2 Aina Tatu Za Ibada Yoh.

More information

Tazama Yuaja. Kuhusu Toleo Hili. Umuhimu wa Mafundisho ya Biblia. Nguvu katika neno la Mungu.

Tazama Yuaja. Kuhusu Toleo Hili. Umuhimu wa Mafundisho ya Biblia. Nguvu katika neno la Mungu. Tazama Yuaja Kuhusu Toleo Hili. Kuna makanisa mengi duniani yanayo dai kuwa yanafundisha ukweli. Yote pia yana mafundisho tofauti yaliyo mafundisho na desturi ya watu. Muungano wa makanisa na uwongozi

More information

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka 0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11

More information

Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu

Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu na Ellis P. Forsman God) 1 Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu na Ellis P. Forsman Oktoba 7, 2011 God) 2 Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu Mat. 6:24-34 Yesu alitoa maelezo haya

More information

BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE

BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE Toleo 10 BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE UBATIZO WA MUUMINI Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa

More information

Mzabibu Na Matawi. (The Vine And The Branches) Ellis P. Forsman. Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) 1

Mzabibu Na Matawi. (The Vine And The Branches) Ellis P. Forsman. Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) 1 Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) na Ellis P. Forsman Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) 1 Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) na Ellis P. Forsman Oktoba 15, 2011 Mzabibu

More information

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ukristo leo unadhihirisha waumini karibu bilioni mbili katika maelfu ya madhehebu tofauti na tofauti na madhehebu. Kati ya hizi, zaidi ya 500 madhehebu

More information

Kiu Cha umtafuta Mungu

Kiu Cha umtafuta Mungu ZAIDI YA NAKALA MILLION 3 ZIMECHAPISHWA KATIKA LUGHA 59 KOTE DUNIANI K Kiu Cha umtafuta Mungu Huduma ya Daktari Richard A. Bennett ilianza katika mabaraza ya miji. Akiwa mwanafunzi chuoni, alikumbana na

More information

Maisha Ya Mkristo Ni Nini?

Maisha Ya Mkristo Ni Nini? Maisha Ya Mkristo Ni Nini? na Ellis P. Forsman Maisha Ya Mkristo Ni Nini? (What Is The Christian Life?) 1 Maisha Ya Mkristo Ni Nini? na Ellis P. Forsman Oktoba 17, 2011 Maisha Ya Mkristo Ni Nini? (What

More information

Tumaini Kwa Afrika. Thomas Schirrmacher. Hoja 66. Dibaji na Prof. Mchungaji Dk. Thomas K. Johnson. Thomas Schirrmacher Tumaini Kwa Afrika TASCM RVB

Tumaini Kwa Afrika. Thomas Schirrmacher. Hoja 66. Dibaji na Prof. Mchungaji Dk. Thomas K. Johnson. Thomas Schirrmacher Tumaini Kwa Afrika TASCM RVB Tunawezaje kudhihirisha msingi wa Kibiblia wa tumaini letu na kulithibitisha kwa Wakristo na kwa wasioamini walioshirikishwa? Tunawezaje kutamka matumaini yetu kwa Wabunge, kwa wafanya biashara au kwa

More information

Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu (Watch Out for Wolves)

Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu (Watch Out for Wolves) Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu (Watch Out for Wolves) Na Ellis P. Forsman Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu (Watch Out for Wolves) 1 Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu Na Ellis P. Forsman Oktoba 7, 2011 Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu

More information

UTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha

UTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha UTARATIBU WA KANISA Tumemaliza hivi punde ule mkutano mkubwa wa siku, tano usiku kwenye Maskani, ambapo, kwa neema ya Mungu na kwa msaada Wake, nimejaribu sana, kwa Maandiko, kuliweka Kanisa la Bwana Yesu

More information

Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani?

Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani? Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani? na Ellis P. Forsman Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani? (Why Did Jesus Die On The Cross?) 1 Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani? na Ellis P. Forsman Oktoba 17, 2011 Kwa Nini Yesu

More information

RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO

RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO 1 RISALA FUPI copyright Hidaya Creativity, publishing Department. P.O. BOX 44799, 00100, GPO, NAIROBI-KENYA. Haki

More information

Kifo Na Mbingu (Death And Heaven)

Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Na Ellis P. Forsman The Rapture And Millennialism 1 Kifo Na Mbingu Na Ellis P. Forsman Octoba 11, 2011 The Rapture And Millennialism 2 Kifo Na Mbingu Heb. 9:27 Ili kufika

More information

MELKISEDECK LEON SHINE. katoliki.ackyshine.com

MELKISEDECK LEON SHINE. katoliki.ackyshine.com katoliki.ackyshine.com SALA ZA ASUBUHI Kwa jina la Baba.. Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,Mwana na Roho. Nilinde tena siku hii,niache dhambi nikutii.naomba sana

More information

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu Nabii Musa alipotoka mlima Sinai kupewa amri kumi za Mungu zilizoko kwenye kitabu cha Kutoka 20:1 17, Mungu alimpa na sharia zingine ambazo lengo lake

More information

PDF created with pdffactory trial version

PDF created with pdffactory trial version المملكة العربية السعودية وزارة التعليم العالي الجامعة الا سلامية بالمدينة المنورة عمادة البحث العلمي قسم الترجمة تعريف موجز بالا سلام بل( لغة السواحلية) ١ بسم االله الرحمن الرحیم MAELEZO KWA UFUPI KUHUSU

More information

Rahisi. Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Kitabu cha mwanafunzi. Rahisi

Rahisi. Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Kitabu cha mwanafunzi. Rahisi Rahisi kitengo cha 2 Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu Rahisi Rahisi Kitabu cha mwanafunzi Kuwa bingwa.wewe na Mimi lazima tujifunze kuishi kwa tunda la Roho Mtakatifu, na kupigana dhidi ya

More information

Patanishwa, Hesabiwa Haki, Takaswa

Patanishwa, Hesabiwa Haki, Takaswa Patanishwa, Hesabiwa Haki, Takaswa na Ellis P. Forsman Patanishwa, Hesabiwa Haki, Takaswa (Reconciled-Justified-Sanctified) 1 Patanishwa, Hesabiwa Haki, Takaswa na Ellis P. Forsman Oktoba 14, 2011 Patanishwa,

More information

Silaha Za Shetani. Ellis Forsman. Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1

Silaha Za Shetani. Ellis Forsman. Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1 Silaha Za Shetani na Ellis Forsman Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1 Silaha Za Shetani na Ellis Forsman Oktoba 15, 2012 Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 2 Silaha Za Shetani 2 Kor. 2:11

More information

UNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW

UNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW Kama unataka kujifunza zaidi njia ya Mkristo wa kweli anavyopaswa kuishi, basi ni lazima ujifunze Biblia. Ili kukusaidia; Kanise la Christadelphian Bible Mission limechapisha kijitabu kuhusu mafunzo ya

More information

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org ( Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Haja Ya Dini Haja Ya Dini Author(s): Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi [3] Publisher(s): Bilal Muslim Mission of Tanzania [4] Katika kijitabu

More information

Sura ya 7 Kielelezo: Tumepatanishwa na Mungu na Wanadamu

Sura ya 7 Kielelezo: Tumepatanishwa na Mungu na Wanadamu Sura ya 7 Kielelezo: Tumepatanishwa na Mungu na Wanadamu 61 62 Ufafanuzi wa Jumla Sura ya 7 Tumepatanishwa na Mungu na Wanadamu Kielelezo cha 7 ni picha ionekanayo ambayo inaonyesha Wakristo wakiishi Huduma

More information

UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI

UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI Toleo 14 BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI Hazina ya maelezo kutoka

More information

VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI

VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI Asante, Ndugu Neville, Bwana akubariki. Bila shaka ni, majaliwa kuwa hapa usiku wa leo. Nina furaha sana ya kwamba Mungu alituruhusu

More information

FORWARD BY DANIEL SZMIOT

FORWARD BY DANIEL SZMIOT FORWARD BY DANIEL SZMIOT 2017 marks the 40th anniversary of the start of Lighthouse Ministry. As in all wars, soldiers continue to fight the battle for the body, mind, will, and emotions. We as Christian

More information

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Ndugu na dada zangu wapendwa, UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2014 Na Rais Thomas S. Monson Upendo Asili ya Injili Hakika hatuwezi kumpenda Mungu kama hatuwapendi wasafiri wenzetu katika safari hii ya maisha duniani. ninafurahia mawazo

More information

MAFUNDISHO YA UMISHENI

MAFUNDISHO YA UMISHENI MAFUNDISHO YA UMISHENI UINJILISTI NA UANAFUNZI Muhtasari: Elekeza kwa mada ilioko hapa chini nayo itakuelekeza kwa mada hiyo. I. Lengo la Sehemu Hii II. Uhusiano kati ya Uinjilisti na Uanafunzi III. Kwa

More information

KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU?

KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU? KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU?, Asante, Ndugu Neville, na habari za jioni, marafiki. Nimerudi tena. Sikupata ila masaa manne asubuhi ya leo. Hiyo ni aibu. Na baada ya

More information

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA SOMO LA KWANZA UTANGULIZI KWA TORA For videos, study guides and other resources, visit Third Millennium Ministries at thirdmill.org. 2014 nathird Millennium Ministries Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu

More information

Uongozi Siri Na Larry Chkoreff. Version 1.2 Desemba 2010

Uongozi Siri Na Larry Chkoreff. Version 1.2 Desemba 2010 Uongozi Siri Na Larry Chkoreff Version 1.2 Desemba 2010 Kimetafsiriwa na kuchapishwa na: Cistern Materials Translation & Publishing Center, Nairobi, Kenya Barua pepe: info@cisternmaterialscenter.com www.cisternmaterialscenter.com

More information

KWA NINI SISI SI MADHEHEBU?

KWA NINI SISI SI MADHEHEBU? KWA NINI SISI SI MADHEHEBU? Nimejaliwa kurudi mimbarani tena baada ya kama,, nadhani, karibu kutokuwepo kwa muda wa miezi mitatu. Kindi wamekuwa na wakati mgumu, na mimi pia. Loo, nimeburudika, hata hivyo,

More information

MASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO

MASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO MASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO Sasa, kama ye yote ana swali lo lote wanalotaka kulileta,, basi, hebu yasogezeni tu juu hapa, acha mtoto fulani ayalete au vyo vyote mtakavyo. Au, labda, tukimaliza

More information

Na Itafunika Wingi Wa Dhambi

Na Itafunika Wingi Wa Dhambi Na Itafunika Wingi Wa Dhambi na Ellis Forsman Na Itafunika Wingi Wa Dhambi (And Shall Hide A Multitude Of Sins) 1 Na Itafunika Wingi Wa Dhambi na Ellis Forsman Oktoba 10, 2011 Na Itafunika Wingi Wa Dhambi

More information

H. M. Baagil, M. D. WAMY Studies on Islam

H. M. Baagil, M. D. WAMY Studies on Islam Mazungumzo ya Mwislamu na Mkristo H. M. Baagil, M. D. WAMY Studies on Islam 1 YALIYOMO Muhtasari wa Mtunzi... 4 Utangulizi... 6 MAZUNGUMZO... 8 Biblia Takatifu... Error! Bookmark not defined. Imani ya

More information

YEHOVA-YIRE 1. 2 Baba yetu wa Mbinguni, tunakikaribia Kiti Chako cha. 3 Tunakushukuru kwa kutuzuru jana jioni. Tunaomba

YEHOVA-YIRE 1. 2 Baba yetu wa Mbinguni, tunakikaribia Kiti Chako cha. 3 Tunakushukuru kwa kutuzuru jana jioni. Tunaomba YEHOVA-YIRE 1 Na tuendelee kusimama tu kwa muda kidogo wakati, tumeinamisha vichwa vyetu kwa maombi. Tunapoinamisha vichwa vyetu, sijui ni wangapi usiku huu wangetaka kukumbukwa katika maombi, una jambo

More information

Hakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn

Hakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn TAFSIRI YA BIBLIA Mwandishi Jonathan M. Menn B.A., University of Wisconsin-Madison, 1974 J.D., Cornell Law School, 1977 M.Div., Trinity Evangelical Divinity School, 2007 Equipping Church Leaders-East Africa

More information

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya Jina Nambari.. Shule... 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI / AGOSTI. 2007 MUDA: SAA 2 ½ MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya 102/3 KISWAHILI FASIHI

More information

wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.

wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine. HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWENYE IBADA YA KUWEKWA WAKFU NA KUINGIZWA KAZINI ASKOFU MARTIN FATAELI SHAO WA DAYOSISI YA KASKAZINI YA KANISA LA

More information

Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia

Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia 34567 APRILI 15, 2013 Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia UKURASAWA 3 NYIMBO ZA KUTUMIWA: 114, 113 Juni 10-16 Jinufaishe na Uwanufaishe Wengine kwa KutumiaNenolaMungu UKURASAWA 18 NYIMBO ZA KUTUMIWA:

More information

ONYO LA MWISHO KWA DUNIA

ONYO LA MWISHO KWA DUNIA ONYO LA MWISHO KWA DUNIA Mpango wa Ulimwengu Mpya Unakuja!. Viongozi wa Ulimwengu. Jinsi ya kuukwepa usiwe wanautaka mhanga. Unaungwa mkono na. Kuanguka kwake ghafula wengi na kwa ukamilifu. Ulitabiriwa

More information

Kiumbe Kipya Katika Kristo

Kiumbe Kipya Katika Kristo Kiumbe Kipya Katika Kristo na Ellis P. Forsman Kiumbe Kipya Katika Kristo (The New Creature In Christ) 1 Kiumbe Kipya Katika Kristo na Ellis P. Forsman Oktoba 15, 2011 Kiumbe Kipya Katika Kristo (The New

More information

maombi, kabla tu hatujalifungua Neno hili la Kiungu.

maombi, kabla tu hatujalifungua Neno hili la Kiungu. ALAMA YA MNYAMA Sasa, kesho usiku Daima tunaonyesha jambo moja,, Bwana Yesu Kristo, ni hivyo tu, na lo lote ambalo ni mapenzi Yake ya Kiungu kwetu kufanya. Lakini kama ni mapenzi Yake ya Kiungu kesho usiku,

More information

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Ndugu na dada zangu wapendwa, UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2013 Utiifu Huleta Baraka Elimu ya ukweli na majibu ya maswali makuu huja kwetu tunapokuwa watiifu kwa amri za Mungu. Ndugu na dada zangu wapendwa, nina shukrani jinsi gani

More information

MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA

MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA 133 134 MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA Ni heri nione mahubiri kuliko kusikia moja siku yeyote ile. Ni heri mtu atembee nami kuliko kunionyesha njia. Jicho ni mwanafunzi mzuri na mwenye hamu kuliko sikio. Mausia

More information

MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara

MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara 1 MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara 1. UTANGULIZI Miaka 500 ya matengenezo ya Kanisa inatufanya tuangalie nyuma na kuona jinsi Mungu alivyotumia wanadamu

More information

UZAO WA NYOKA. 2 Basi, usiku huu, tuna malimbuko tu ya utukufu huo mkuu. 3 Kwa uchaji tunasimama kwa imani yetu katika Uwepo

UZAO WA NYOKA. 2 Basi, usiku huu, tuna malimbuko tu ya utukufu huo mkuu. 3 Kwa uchaji tunasimama kwa imani yetu katika Uwepo UZAO WA NYOKA Mungu, Mungu aliye mkuu na mwenye nguvu, Yeye, aliyefanya mambo yote kwa nguvu za Roho Wake; na amemleta Yesu Kristo, Mwanawe wa pekee, aliyejitolea akafa kwa ajili yetu wenye dhambi, Mwenye

More information

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Ndugu na dada zangu wapendwa, UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, NOVEMBA 2011 Na Rais Thomas S. Monson Simama Pahali Patakatifu Mawasiliano na Baba yetu aliye Mbinguni pamoja na maombi yetu Kwake na maongozi Yake kwetu ni muhimu ili tuweze

More information

JE! MUNGU ANAMPA MWANAMKE HAKI YA KUTOA MIMBA IWAPO NI MHANGA WA UBAKAJI?

JE! MUNGU ANAMPA MWANAMKE HAKI YA KUTOA MIMBA IWAPO NI MHANGA WA UBAKAJI? Jarida la Dunia Yerusalemu Mpya Mchungaji Tony Alamo Makanisa Ulimwenguni Kote Taifa la Kikristo la Alamo Mchungaji Tony na Susan Alamo, Okestra, na kwaya katika kipindi chao cha kimataifa cha televisheni.

More information

Oktoba-Desemba

Oktoba-Desemba Oktoba-Desemba 2014 1 Habari za Unabii wa Biblia 8 13 24 Katika toleo hili: 25 28 33 3 MwanaFiladelfia wa Karne ya 21 ni nani? Je, Yesu alifundisha kwamba kungekuwepo na tofauti kubwa baina ya Wakristo

More information

Uponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14).

Uponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14). 41 Uponyaji Wa Laana Ijapokuwa baraka ni kinyume cha laana, kuna mambo yanayofanana katika vitu hivyo. Ni maneno yaliyotajwa, yaliyoamriwa, au kuandikwa katika Biblia kwa nguvu na mamlakao ya kiroh kwa

More information

KUTAMBUA SIKU YA KO NA UJUMBE WAKE

KUTAMBUA SIKU YA KO NA UJUMBE WAKE KUTAMBUA SIKU YA KO NA UJUMBE WAKE Habari za asubuhi, wapendwa. Hebu na tuendelee, kusimama kwa muda kidogo tu. Mungu mpendwa, sisi, tulio kwenye wakati wa mahangaiko na kakara za maisha, tumetulia kwa

More information

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma

More information

United Pentecostal Church April Kushangilia Kwa Sala

United Pentecostal Church April Kushangilia Kwa Sala Kushangilia Kwa Sala Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa Kushangilia Kwa Sala Na Wanda Fielder United Pentecostal Church April 2017 Kuwa alimfufua katika kanisa tangu kuzaliwa, daima aliamini Neno la

More information

Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele. Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? UKURASA WA 12 NYIMBO: 97, 101. Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana

Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele. Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? UKURASA WA 12 NYIMBO: 97, 101. Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana JANUARI 15, 2014 34567 MAKALA ZA FUNZO MACHI 3-9 Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele UKURASA WA 7 NYIMBO: 106, 46 MACHI 10-16 Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? UKURASA WA 12 NYIMBO: 97, 101 MACHI

More information

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa.

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa mabingwa itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa. Mkuu Inahitaji dhabihu. Unahitaji kujisukuma hadi mwisho wako. Lakini nakupa ahadi hii,

More information

MWONGOZO WA NAMNA YA KUHAMASISHA MAOMBI YA MCHANA NA USIKU YA SIKU 10.

MWONGOZO WA NAMNA YA KUHAMASISHA MAOMBI YA MCHANA NA USIKU YA SIKU 10. 6-15 Mei 2005. MWONGOZO WA NAMNA YA KUHAMASISHA MAOMBI YA MCHANA NA USIKU YA SIKU 10. Kujenga kifuniko cha maombi juu ya mabara yote ya ulimwengu. Kufurikisha Jamii zetu kwa Maombi. Anzisha vituo vitakavyofukuta

More information

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi kitengo cha 2 Iliyoendelea sana Iliyoendelea sana Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu Iliyoendelea sana Kitabu cha mwanafunzi Kuwa bingwa.wewe na Mimi lazima tujifunze kuishi kwa tunda la Roho

More information

Rahisi. Kitabu cha mwanafunzi. Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Rahisi

Rahisi. Kitabu cha mwanafunzi. Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Rahisi kitengo cha 3 Rahisi Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu Rahisi Rahisi Kitabu cha mwanafunzi Kuwa bingwa.wewe na mimi lazima tujifunze kuishi kwa tunda la Roho Mtakatifu, na kupigana na dhambi

More information

Iliyoendelea sana. Kitengo cha 2. Kitabu cha mwanafunzi Iliyoendelea sana

Iliyoendelea sana. Kitengo cha 2. Kitabu cha mwanafunzi Iliyoendelea sana Iliyoendelea sana Kitengo cha 2 Kitabu cha mwanafunzi Iliyoendelea sana Mungu hutumia neno lake kuongea nasi kila wiki. Je, Mungu anakuambia nini el día de Leo? 1 Suala la spishi zinazotishiwa #01 Oo.

More information

Human Rights Are Universal And Yet...

Human Rights Are Universal And Yet... Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,

More information

Kwa Kongamano Kuu 2016

Kwa Kongamano Kuu 2016 The Upper Room za Kwa Kongamano Kuu 2016 Selected from The Upper Room Disciplines with Invited Writers SIKU 60 ZA SALA Kwa Kongamano Kuu 2016 2016 na Upper Room Books. Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu

More information

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi. Iliyoendelea sana

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi. Iliyoendelea sana kitengo cha 3 Iliyoendelea sana Iliyoendelea sana Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu Iliyoendelea sana Kitabu cha mwanafunzi Kuwa bingwa.wewe na mimi lazima tujifunze kuishi kwa tunda la Roho

More information

LALA. Terry Warford. LALA (Sleep - Terry Warford) 1

LALA. Terry Warford. LALA (Sleep - Terry Warford) 1 LALA na Terry Warford LALA (Sleep - Terry Warford) 1 LALA na Terry Warford Novemba 6, 2011 LALA (Sleep - Terry Warford) 2 LALA Kulala ni sehemu muhimu katika maisha yetu ya kila siku, tukiipa akili zetu

More information

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau

More information

Makasisi. Waingia Uislamu

Makasisi. Waingia Uislamu 1 Makasisi Waingia Uislamu 2 KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU MAKASISI WAINGIA UISLAMU Yaliyomo 1. KASISI YUSUFU ESTES ALIYEKUWA MFANYABIASHARA WA KIKRISTO & MUHUBIRI (USA)...

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level * 899145 4 672* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2010 Additional Materials: Answer Booklet/Paper READ

More information

IBADA NA UMOJA WA KANISA Na Mchg. Dkt. Msafiri Mbilu

IBADA NA UMOJA WA KANISA Na Mchg. Dkt. Msafiri Mbilu 1 IBADA NA UMOJA WA KANISA Na Mchg. Dkt. Msafiri Mbilu SOMO LA I Kama kuna nyakati katika Historia ya Kanisa ambazo tunapaswa kuangalia kwa undani juu ya IBADA NA UMOJA WA KANISA, ni sasa. Sababu kubwa

More information