HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001
|
|
- Octavia Harrington
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa unapokopa. Lakini kabla sijafanya hivyo napenda niwashukurukuni nyote kwa kupokea vizuri na kuunga mkono uteuzi wangu wa Makamu wa Rais, Dkt. Ali Mohamed Shein, baada ya msiba mkubwa uliotupata. Nimepokea barua nyingi - kutoka hata kwa wananchi wa kawaida - wakipongeza uteuzi huo, ulioungwa mkono na karibu Waheshimiwa Wabunge wote. Siwezi kumjibu kila mmoja aliyeniandikia, maana ni wengi sana. Naomba wote waliotuma rambirambi kwa kifo cha Dkt. Omar Ali Juma, na wote waliotuma pongezi kwa uteuzi wa Dkt. Ali Mohamed Shein, wapokee kupitia hotuba hii shukrani zangu za dhati kabisa. Tuzidi kumwombea marehemu wetu kwa Mwenyezi Mungu; na kuendelea kutoa ubani wetu kwa mjane na familia yake kama ilivyo desturi yetu. Kifo cha Dkt. Omar Ali Juma, na uteuzi wa Dkt. Ali Mohamed Shein, ni mambo yaliyoonyesha wazi ni sifa zipi Watanzania wanazitarajia kwa viongozi wao. Usomi ni mojawapo, lakini hasa ni tabia ya mhusika. Miongoni mwa sifa hizo, Ni utu wake na uadilifu wake; Ni upendo wake na heshima yake kwa watu wote, bila ubaguzi wowote; Ni kupenda kazi na kutumikia wananchi, badala ya kupenda kutumikiwa na kutukuzwa; Ni kuweka mbele maslahi ya taifa na Watanzania, badala ya maslahi binafsi au maslahi ya vikundi; Ni unyenyekevu, badala ya kupenda makuu; na Ni kutoa matumaini kwa wananchi kuwa ile misingi ya taifa lao, kama vile haki, usawa, fursa sawa na matumaini kwa wote, amani, umoja, upendo, mshikamano na Muungano wetu, kwamba misingi hiyo itakuwa salama mikononi mwa kiongozi anayehusika. Mimi nina uhakika kuwa maombolezo yenu, na ushiriki wenu wa kupigiwa mfano katika maziko ya mpendwa wetu Dkt. Omar Ali Juma; na faraja yenu kwa uteuzi wa aliyechukua nafasi yake, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, ambao wote wana sifa
2 nilizoziorodhesha, ni uthibitisho wenu kuwa hizi ndizo sifa mzitakazo kwa viongozi wenu. Hivyo, ni wajibu wetu viongozi tuliopo kuiga sifa hizo kama kweli tunataka kustahiki kuendelea kuwaongozeni. Majuzi, tarehe 18 Julai, nilizindua mgodi mkubwa wa dhahabu wa tatu kujengwa nchini katika miaka minne iliyopita, na wenye kina kirefu zaidi kuliko yote. Mgodi ule wa Bulyanhulu, kama ile miwili iliyotangulia, ni wa kisasa, sawa kabisa, na pengine kuzidi, iliyopo katika nchi zilizoendelea na tajiri. Lakini mgodi wa aina hiyo, na uchimbaji wenye ufanisi kiasi cha kuleta faida wakati bei ya dhahabu imeshuka duniani, unahitaji teknolojia ya kisasa kabisa, menejimenti ya kisasa na mtaji mkubwa sana. Kwa mgodi wa Bulyanhulu, gharama yake ilikuwa dola za kimarekani 280 milioni, sawa na shilingi zetu 224 bilioni, kiasi kinachokaribia nusu ya mapato yetu ya fedha za kigeni kwa mwaka yatokanayo na mauzo ya bidhaa nje ya nchi yetu. Kwa taarifa yenu tu, katika miaka 5 iliyopita, wawekezaji wakubwa kwenye sekta ya madini wametumia zaidi ya dola za kimarekani bilioni moja, sawa na zaidi ya Sh.800 bilioni, katika kutafuta, kuchimba na kujenga migodi ya madini katika nchi yetu. Kiasi hicho cha zaidi ya sh. 800 bn ni karibu sawa na mapato yetu yote ya ndani kwa mwaka. Ni dhahiri basi kuwa sisi wenyewe, kama taifa, hatuna uwezo wa kuchimba madini haya peke yetu, na hatutakuwa nao kwa miaka ya karibuni. Kwa hivyo, ningependa leo tutafakari pamoja inakuwaje kampuni binafsi kama hizi zinaweza kuwa na uwezo mkubwa wa mitaji kiasi hiki. Mojawapo ya vyanzo vya uwezo wa fedha wa kampuni hizi ni hisa za wamiliki wa kampuni. Hawa wanaweza kuwa watu kutoka pembe zote za dunia, ambao kupitia soko la hisa na mitaji huwekeza akiba zao kwa kununua hisa. Kampuni ya Barrick Gold, inayomiliki Kampuni ya Dhahabu ya Kahama, makao makuu yake yapo nchini Kanada. Lakini pamoja na soko la mitaji la Toronto, Kanada, hisa zake zinauzwa pia kwenye masoko ya mitaji yaliyopo London, Uingereza; New York, Marekani; Paris, Ufaransa; na kwingineko. Kwa kufanya hivyo, wanakusanya akiba za watu kwa kuwauzia hisa, na kisha kutumia fedha hizo kununulia teknolojia, kuwekeza, kufanya ajira ya wafanya kazi wa bidii na maarifa, na kupata faida kubwa iwezekanavyo ili wanahisa wawe na uhakika kuwa amana zao ziko salama na thamani yake inaongezeka; na zaidi sana kwamba watalipwa gawio kutokana na faida itakayopatikana. Wale wanaotumia akiba yao kununua hisa wanavutiwa na rekodi ya kampuni inayohusika, na wanajiridhisha kuwa kampuni hiyo ina uhakika wa kulinda thamani ya hisa wanazonunua, na kwa kuzitumia vizuri, kwa kuwekeza katika miradi mizuri, watazalisha faida, thamani ya hisa zao iongezeke, na pia wapate gawio. Ili kuwekeza katika miradi mikubwa sana kampuni hizi hutegemea zaidi ya hisa. Kampuni za namna hiyo pia hukopa fedha kutoka katika benki na taasisi nyingine za fedha kama vile mifuko ya akiba ya wafanyakazi. Fedha hizo wanazokopa toka benki na mifuko mbalimbali, nazo ni akiba za watu wengine kutoka pembe mbalimbali za dunia, ambao
3 matumaini yao ni kuwa akiba yao itakuwa salama, na kwamba benki itazitumia kukopesha wengine, kwa riba nzuri, na hivyo kuhakikisha kuwa siku wakiwa na shida, au wakistaafu kazi, watakuta fedha zao ziko salama, na zimepata faida kubwa iwezekanavyo. Huu ndio mfumo na utaratibu unaohimili sehemu kubwa ya uchumi endelevu wa nchi, na dunia nzima, na kuleta maendeleo. Watu hufanya kazi, wakapata faida au kulipwa mishahara, wakaweka akiba benki au kununua hisa, ambapo hisa na akiba hizo hufanywa chanzo cha mitaji ya kuwekeza katika uzalishaji na huduma mbalimbali, zitakazotoa ajira, tija na ziada, na zitakazohakikisha hisa na akiba hizo ni salama, na zinakua. Hivyo, mfumo wa fedha na uchumi duniani hutegemea mambo yafuatayo: Kwanza, lazima watu wafanye kazi kwa bidii na maarifa, waongeze tija, wapate faida, na wawe tayari kuweka akiba au kununua hisa. Pili, lazima ziwepo kampuni zenye uwezo wa uzalishaji na kutoa huduma kwa faida na hivyo kuvutia watu kununua hisa, au benki kuwa tayari kuzikopesha kwa kuamini hisa na mikopo hiyo itakuwa salama, na thamani yake itaongezeka. Tatu, mfumo unahitaji sana, na unahimiliwa, na mazingira ya kuaminiana. Anayenunua hisa lazima aiamini kampuni anaponunua hisa. Mweka akiba lazima aiamini benki anakoweka akiba yake. Benki lazima iiamini kampuni inayoikopesha, kwamba kweli itazalisha kwa faida, na italipa mkopo kwa wakati kulingana na mkataba wa kukopa. Udanganyifu, na kutolipa mikopo, ni adui wakubwa wa mfumo huu. Benki inapofanya kazi ipasavyo, mfumo huo una uwezo wa kukusanya amana na akiba kutoka kila pembe ya dunia na kuzileta kama mitaji zikajenga migodi ya dhahabu Tanzania na kwingineko, pamoja na uwekezaji mwingine wa aina mbalimbali. Tumeingia karne mpya; lazima tuende na wakati. Tunayo mengi ya kujifunza katika mfumo huu. Ni mfumo unaofuta mipaka na kudharau ubinafsi, uchoyo, na uvivu wa fikra na ubunifu. Lazima tuwe taifa la wachapa kazi, kwa bidii na maarifa, na tuwe wazalishaji wa faida na ziada, kisha tuziwekeze kama akiba au tununue hisa. Baada ya kufungua mgodi wa dhahabu Bulyanhulu, siku ya pili yake nilifungua tawi la Benki ya Ushirika na Maendeleo Vijijini (CRDB) mjini Kahama. Nafarijika sana kwamba Benki hii ni kielelezo kizuri na jibu sahihi ya hoja na changamoto ninayoelezea katika mazungumzo yangu nanyi leo hii. Benki ya Ushirika na Maendeleo Vijijini ina wanahisa zaidi ya 10,000 waliotapakaa kila pembe ya nchi yetu. Amana za Benki hii ambazo ni akiba za Watanzania wa kawaida zimekua kwa asilimia 45 kati ya mwaka 1997 na Benki hii imetoa mikopo inayofikia sh.42 bilioni, ikiwa ya wastani wa sh.20 milioni, na mkopo wa chini kabisa ukiwa wa sh.500,000/= tu. Kwa kutambua kuwa kuwekeza kwenye mikopo ya uzalishaji ndio kichocheo kikubwa cha kukuza uchumi, na kwa ubunifu mkubwa, Benki hii imewalenga wenye shughuli ndogondogo, shughuli ambazo ni pamoja na kilimo, ufugaji mdogo mdogo, wafanyabiashara
4 wadogo, wamiliki wa viwanda vidogovidogo, na akina mama na baba ntilie, au lishe kama wanavyoitwa siku hizi. Na la kuridhisha zaidi ni kwamba imepunguza riba inayotoza wakopaji kwa wastani wa asilimia mbili (2%). Imefanya yote hayo bila kupoteza dira mbele ya wateja wake kuwa: Kuwekeza na kukopesha ni kupata faida. Naipongeza na kuishukuru sana Benki ya Ushirika na Maendeleo Vijijini (CRDB). Lazima taasisi za fedha zijenge uwezo wa kukusanya akiba za wananchi, kuzihifadhi, na kuongeza thamani yake kwa kukopesha kwa uangalifu, na kuhakikisha mkopaji analipa kwa wakati. Hivyo mwekaji akiba akipata dharura akute fedha zake, au akistaafu kazi apate fedha zake na faida ya kuridhisha. Lazima wakopaji binafsi, au makampuni yanayokopa, wakope tu kwa ajili ya miradi iliyochambuliwa na kufanyiwa upembuzi yakinifu ili kuthibitisha kuwa kweli itafanikiwa na kuleta faida kwa wakati uliotarajiwa, na mikopo kurejeshwa. Si sahihi hata kidogo kwa benki kukopesha akiba za wateja wao kwa miradi ya mwito tu wa kusadikika, au ya Pwagu na Pwaguzi. Kwa bahati mbaya, sifa yetu Watanzania katika jambo hili si nzuri hata kidogo. Tusipende kuwa taifa la warushaji, wanaogeuza mkopo kuwa msaada au sadaka. Tabia hizo ndizo zilizoua Benki ya Nyumba ya Taifa, na kuzifanya taabani benki zetu nyingine. Mambo hayo sasa lazima yakome. Benki tulizo nazo sasa haziwezi kutukopesha kama tutaendelea na tabia ya kutorejesha mikopo kwa wakati. Kila nipatapo nafasi nawataka wenye benki wapunguze riba ya mikopo yao. Wameanza; lakini bado hawajaridhika na rekodi yetu ya kurejesha mikopo, na wanasema hiyo ni sababu mojawapo ya riba ya mikopo kuendelea kuwa kubwa. Ninaamini kuwa iwapo rekodi yetu ya kuweka akiba na kurejesha mikopo kwa wakati itakuwa bora zaidi, mikopo ya masharti na riba nafuu itatolewa kwa wingi zaidi, taifa litasonga mbele, na mazingira yatawawezesheni nyinyi wananchi kupiga vita vizuri zaidi dhidi ya umaskini. Hivyo, namalizia kwa kuwatanabahisha kuwa mfumo na kanuni zilizowezesha kampuni ya Barrick Gold kutoka Kanada na kuja kuchimba dhahabu hapa kwa gharama kubwa ambayo sisi hatuiwezi, ndio mfumo na kanuni hizo hizo ambazo tukikubali kuongozwa nazo nasi tutaendelea kwa haraka, na hatimaye tutaweza kuvuna maliasili yetu, hata kuchimba madini yetu, wenyewe, au kwa ubia. Masharti yako wazi. Tuongeze bidii ya kazi na kuzalisha faida. Tuweke akiba zaidi na kununua hisa. Nimewahi kusema, na leo ninarudia. Wengi wetu si matajiri; lakini kuweka akiba ni utamaduni zaidi kuliko utajiri; na akiba nyingi huzaa utajiri wa mitaji mikubwa. Tusitumie kwanza, na kuweka akiba kinachobaki. Hakitabaki kitu, maana mahitaji yetu ni mengi. Badala yake tujenge tabia na utamaduni wa kutumia kile kinachobaki baada ya kuweka akiba. Pili, tufute aibu hii ya kufanya biashara au uwekezaji kwa ujanja ujanja tu, na udanganyifu. Tuachane na malalamiko yasiyofanyiwa kwanza upembuzi yakinifu. Tuanzishe miradi baada ya uchambuzi wa kina kuonyesha kweli faida itapatikana. Na ninaziomba benki zetu, hasa zile zinazojali wateja wadogo, ziwe na idara maalumu za kuwasaidia wanaotaka kukopa wafanye kwanza uchambuzi na upembuzi yakinifu wa miradi, na wawasimamie kwa karibu katika kila hatua ya utekelezaji, ili miradi iendeshwe kitaalam, faida ipatikane, na mikopo irejeshwe kwa wakati. Mikopo ni mkusanyo wa akiba ya wengi.
5 Wewe uliyekopa kutorejesha mkopo ni sawa na kuiba akiba ya watu wengine. Ni aibu, na inavunja hali ya kuaminiana ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa kisasa. Ipo methali isemayo, Mwezi hauwezi kuandama mpaka uliotangulia umeondoka. Nasi hatuwezi kupata maisha mapya, ya kisasa, wakati bado tunang ang ania tabia, hulka na mienendo ya kufanya kazi kizamani. Tukiwa wabunifu zaidi, tukijituma zaidi, na tukifanya mambo yetu kisasa, tutapata maisha bora ya kisasa. Mimi nina hakika tukiamua tunaweza, na tutafanikiwa. Mungu Ibariki Afrika. Mungu Ibariki Tanzania. Ahsanteni kwa kunisikiliza. You might need to download Realplayer in order to view and listen the President's speeach Speeach... HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa unapokopa. Lakini kabla sijafanya hivyo napenda niwashukurukuni nyote kwa kupokea vizuri na kuunga mkono uteuzi wangu wa Makamu wa Rais, Dkt. Ali Mohamed Shein, baada ya msiba mkubwa uliotupata. Nimepokea barua nyingi - kutoka hata kwa wananchi wa kawaida - wakipongeza uteuzi huo, ulioungwa mkono na karibu Waheshimiwa Wabunge wote. Siwezi kumjibu kila mmoja aliyeniandikia, maana ni wengi sana. Naomba wote waliotuma rambirambi kwa kifo cha Dkt. Omar Ali Juma, na wote waliotuma pongezi kwa uteuzi wa Dkt. Ali Mohamed Shein, wapokee kupitia hotuba hii shukrani zangu za dhati kabisa. Tuzidi kumwombea marehemu wetu kwa Mwenyezi Mungu; na kuendelea kutoa ubani wetu kwa mjane na familia yake kama ilivyo desturi yetu. Kifo cha Dkt. Omar Ali Juma, na uteuzi wa Dkt. Ali Mohamed Shein, ni mambo yaliyoonyesha wazi ni sifa zipi Watanzania wanazitarajia kwa viongozi wao. Usomi ni mojawapo, lakini hasa ni tabia ya mhusika. Miongoni mwa sifa hizo,
6 Ni utu wake na uadilifu wake; Ni upendo wake na heshima yake kwa watu wote, bila ubaguzi wowote; Ni kupenda kazi na kutumikia wananchi, badala ya kupenda kutumikiwa na kutukuzwa; Ni kuweka mbele maslahi ya taifa na Watanzania, badala ya maslahi binafsi au maslahi ya vikundi; Ni unyenyekevu, badala ya kupenda makuu; na Ni kutoa matumaini kwa wananchi kuwa ile misingi ya taifa lao, kama vile haki, usawa, fursa sawa na matumaini kwa wote, amani, umoja, upendo, mshikamano na Muungano wetu, kwamba misingi hiyo itakuwa salama mikononi mwa kiongozi anayehusika. Mimi nina uhakika kuwa maombolezo yenu, na ushiriki wenu wa kupigiwa mfano katika maziko ya mpendwa wetu Dkt. Omar Ali Juma; na faraja yenu kwa uteuzi wa aliyechukua nafasi yake, Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, ambao wote wana sifa nilizoziorodhesha, ni uthibitisho wenu kuwa hizi ndizo sifa mzitakazo kwa viongozi wenu. Hivyo, ni wajibu wetu viongozi tuliopo kuiga sifa hizo kama kweli tunataka kustahiki kuendelea kuwaongozeni. Majuzi, tarehe 18 Julai, nilizindua mgodi mkubwa wa dhahabu wa tatu kujengwa nchini katika miaka minne iliyopita, na wenye kina kirefu zaidi kuliko yote. Mgodi ule wa Bulyanhulu, kama ile miwili iliyotangulia, ni wa kisasa, sawa kabisa, na pengine kuzidi, iliyopo katika nchi zilizoendelea na tajiri. Lakini mgodi wa aina hiyo, na uchimbaji wenye ufanisi kiasi cha kuleta faida wakati bei ya dhahabu imeshuka duniani, unahitaji teknolojia ya kisasa kabisa, menejimenti ya kisasa na mtaji mkubwa sana. Kwa mgodi wa Bulyanhulu, gharama yake ilikuwa dola za kimarekani 280 milioni, sawa na shilingi zetu 224 bilioni, kiasi kinachokaribia nusu ya mapato yetu ya fedha za kigeni kwa mwaka yatokanayo na mauzo ya bidhaa nje ya nchi yetu. Kwa taarifa yenu tu, katika miaka 5 iliyopita, wawekezaji wakubwa kwenye sekta ya madini wametumia zaidi ya dola za kimarekani bilioni moja, sawa na zaidi ya Sh.800 bilioni, katika kutafuta, kuchimba na kujenga migodi ya madini katika nchi yetu. Kiasi hicho cha zaidi ya sh. 800 bn ni karibu sawa na mapato yetu yote ya ndani kwa mwaka. Ni dhahiri basi kuwa sisi wenyewe, kama taifa, hatuna uwezo wa kuchimba madini haya peke yetu, na hatutakuwa nao kwa miaka ya karibuni. Kwa hivyo, ningependa leo tutafakari pamoja inakuwaje kampuni binafsi kama hizi zinaweza kuwa na uwezo mkubwa wa mitaji kiasi hiki.
7 Mojawapo ya vyanzo vya uwezo wa fedha wa kampuni hizi ni hisa za wamiliki wa kampuni. Hawa wanaweza kuwa watu kutoka pembe zote za dunia, ambao kupitia soko la hisa na mitaji huwekeza akiba zao kwa kununua hisa. Kampuni ya Barrick Gold, inayomiliki Kampuni ya Dhahabu ya Kahama, makao makuu yake yapo nchini Kanada. Lakini pamoja na soko la mitaji la Toronto, Kanada, hisa zake zinauzwa pia kwenye masoko ya mitaji yaliyopo London, Uingereza; New York, Marekani; Paris, Ufaransa; na kwingineko. Kwa kufanya hivyo, wanakusanya akiba za watu kwa kuwauzia hisa, na kisha kutumia fedha hizo kununulia teknolojia, kuwekeza, kufanya ajira ya wafanya kazi wa bidii na maarifa, na kupata faida kubwa iwezekanavyo ili wanahisa wawe na uhakika kuwa amana zao ziko salama na thamani yake inaongezeka; na zaidi sana kwamba watalipwa gawio kutokana na faida itakayopatikana. Wale wanaotumia akiba yao kununua hisa wanavutiwa na rekodi ya kampuni inayohusika, na wanajiridhisha kuwa kampuni hiyo ina uhakika wa kulinda thamani ya hisa wanazonunua, na kwa kuzitumia vizuri, kwa kuwekeza katika miradi mizuri, watazalisha faida, thamani ya hisa zao iongezeke, na pia wapate gawio. Ili kuwekeza katika miradi mikubwa sana kampuni hizi hutegemea zaidi ya hisa. Kampuni za namna hiyo pia hukopa fedha kutoka katika benki na taasisi nyingine za fedha kama vile mifuko ya akiba ya wafanyakazi. Fedha hizo wanazokopa toka benki na mifuko mbalimbali, nazo ni akiba za watu wengine kutoka pembe mbalimbali za dunia, ambao matumaini yao ni kuwa akiba yao itakuwa salama, na kwamba benki itazitumia kukopesha wengine, kwa riba nzuri, na hivyo kuhakikisha kuwa siku wakiwa na shida, au wakistaafu kazi, watakuta fedha zao ziko salama, na zimepata faida kubwa iwezekanavyo. Huu ndio mfumo na utaratibu unaohimili sehemu kubwa ya uchumi endelevu wa nchi, na dunia nzima, na kuleta maendeleo. Watu hufanya kazi, wakapata faida au kulipwa mishahara, wakaweka akiba benki au kununua hisa, ambapo hisa na akiba hizo hufanywa chanzo cha mitaji ya kuwekeza katika uzalishaji na huduma mbalimbali, zitakazotoa ajira, tija na ziada, na zitakazohakikisha hisa na akiba hizo ni salama, na zinakua. Hivyo, mfumo wa fedha na uchumi duniani hutegemea mambo yafuatayo: Kwanza, lazima watu wafanye kazi kwa bidii na maarifa, waongeze tija, wapate faida, na wawe tayari kuweka akiba au kununua hisa. Pili, lazima ziwepo kampuni zenye uwezo wa uzalishaji na kutoa huduma kwa faida na hivyo kuvutia watu kununua hisa, au benki kuwa tayari kuzikopesha kwa kuamini hisa na mikopo hiyo itakuwa salama, na thamani yake itaongezeka. Tatu, mfumo unahitaji sana, na unahimiliwa, na mazingira ya kuaminiana. Anayenunua hisa lazima aiamini kampuni anaponunua hisa. Mweka akiba lazima aiamini benki anakoweka akiba yake. Benki lazima iiamini kampuni inayoikopesha, kwamba kweli itazalisha kwa faida, na italipa mkopo kwa wakati kulingana na mkataba wa kukopa. Udanganyifu, na kutolipa mikopo, ni adui wakubwa wa mfumo huu. Benki inapofanya kazi ipasavyo, mfumo huo una uwezo wa kukusanya amana na akiba kutoka kila pembe ya dunia na kuzileta kama mitaji zikajenga migodi ya dhahabu Tanzania na kwingineko, pamoja na uwekezaji mwingine wa aina mbalimbali.
8 Tumeingia karne mpya; lazima tuende na wakati. Tunayo mengi ya kujifunza katika mfumo huu. Ni mfumo unaofuta mipaka na kudharau ubinafsi, uchoyo, na uvivu wa fikra na ubunifu. Lazima tuwe taifa la wachapa kazi, kwa bidii na maarifa, na tuwe wazalishaji wa faida na ziada, kisha tuziwekeze kama akiba au tununue hisa. Baada ya kufungua mgodi wa dhahabu Bulyanhulu, siku ya pili yake nilifungua tawi la Benki ya Ushirika na Maendeleo Vijijini (CRDB) mjini Kahama. Nafarijika sana kwamba Benki hii ni kielelezo kizuri na jibu sahihi ya hoja na changamoto ninayoelezea katika mazungumzo yangu nanyi leo hii. Benki ya Ushirika na Maendeleo Vijijini ina wanahisa zaidi ya 10,000 waliotapakaa kila pembe ya nchi yetu. Amana za Benki hii ambazo ni akiba za Watanzania wa kawaida zimekua kwa asilimia 45 kati ya mwaka 1997 na Benki hii imetoa mikopo inayofikia sh.42 bilioni, ikiwa ya wastani wa sh.20 milioni, na mkopo wa chini kabisa ukiwa wa sh.500,000/= tu. Kwa kutambua kuwa kuwekeza kwenye mikopo ya uzalishaji ndio kichocheo kikubwa cha kukuza uchumi, na kwa ubunifu mkubwa, Benki hii imewalenga wenye shughuli ndogondogo, shughuli ambazo ni pamoja na kilimo, ufugaji mdogo mdogo, wafanyabiashara wadogo, wamiliki wa viwanda vidogovidogo, na akina mama na baba ntilie, au lishe kama wanavyoitwa siku hizi. Na la kuridhisha zaidi ni kwamba imepunguza riba inayotoza wakopaji kwa wastani wa asilimia mbili (2%). Imefanya yote hayo bila kupoteza dira mbele ya wateja wake kuwa: Kuwekeza na kukopesha ni kupata faida. Naipongeza na kuishukuru sana Benki ya Ushirika na Maendeleo Vijijini (CRDB). Lazima taasisi za fedha zijenge uwezo wa kukusanya akiba za wananchi, kuzihifadhi, na kuongeza thamani yake kwa kukopesha kwa uangalifu, na kuhakikisha mkopaji analipa kwa wakati. Hivyo mwekaji akiba akipata dharura akute fedha zake, au akistaafu kazi apate fedha zake na faida ya kuridhisha. Lazima wakopaji binafsi, au makampuni yanayokopa, wakope tu kwa ajili ya miradi iliyochambuliwa na kufanyiwa upembuzi yakinifu ili kuthibitisha kuwa kweli itafanikiwa na kuleta faida kwa wakati uliotarajiwa, na mikopo kurejeshwa. Si sahihi hata kidogo kwa benki kukopesha akiba za wateja wao kwa miradi ya mwito tu wa kusadikika, au ya Pwagu na Pwaguzi. Kwa bahati mbaya, sifa yetu Watanzania katika jambo hili si nzuri hata kidogo. Tusipende kuwa taifa la warushaji, wanaogeuza mkopo kuwa msaada au sadaka. Tabia hizo ndizo zilizoua Benki ya Nyumba ya Taifa, na kuzifanya taabani benki zetu nyingine. Mambo hayo sasa lazima yakome. Benki tulizo nazo sasa haziwezi kutukopesha kama tutaendelea na tabia ya kutorejesha mikopo kwa wakati. Kila nipatapo nafasi nawataka wenye benki wapunguze riba ya mikopo yao. Wameanza; lakini bado hawajaridhika na rekodi yetu ya kurejesha mikopo, na wanasema hiyo ni sababu mojawapo ya riba ya mikopo kuendelea kuwa kubwa. Ninaamini kuwa iwapo rekodi yetu ya kuweka akiba na kurejesha mikopo kwa wakati itakuwa bora zaidi, mikopo ya masharti na riba nafuu itatolewa kwa wingi zaidi, taifa litasonga mbele, na mazingira yatawawezesheni nyinyi wananchi kupiga vita vizuri zaidi dhidi ya umaskini.
9 Hivyo, namalizia kwa kuwatanabahisha kuwa mfumo na kanuni zilizowezesha kampuni ya Barrick Gold kutoka Kanada na kuja kuchimba dhahabu hapa kwa gharama kubwa ambayo sisi hatuiwezi, ndio mfumo na kanuni hizo hizo ambazo tukikubali kuongozwa nazo nasi tutaendelea kwa haraka, na hatimaye tutaweza kuvuna maliasili yetu, hata kuchimba madini yetu, wenyewe, au kwa ubia. Masharti yako wazi. Tuongeze bidii ya kazi na kuzalisha faida. Tuweke akiba zaidi na kununua hisa. Nimewahi kusema, na leo ninarudia. Wengi wetu si matajiri; lakini kuweka akiba ni utamaduni zaidi kuliko utajiri; na akiba nyingi huzaa utajiri wa mitaji mikubwa. Tusitumie kwanza, na kuweka akiba kinachobaki. Hakitabaki kitu, maana mahitaji yetu ni mengi. Badala yake tujenge tabia na utamaduni wa kutumia kile kinachobaki baada ya kuweka akiba. Pili, tufute aibu hii ya kufanya biashara au uwekezaji kwa ujanja ujanja tu, na udanganyifu. Tuachane na malalamiko yasiyofanyiwa kwanza upembuzi yakinifu. Tuanzishe miradi baada ya uchambuzi wa kina kuonyesha kweli faida itapatikana. Na ninaziomba benki zetu, hasa zile zinazojali wateja wadogo, ziwe na idara maalumu za kuwasaidia wanaotaka kukopa wafanye kwanza uchambuzi na upembuzi yakinifu wa miradi, na wawasimamie kwa karibu katika kila hatua ya utekelezaji, ili miradi iendeshwe kitaalam, faida ipatikane, na mikopo irejeshwe kwa wakati. Mikopo ni mkusanyo wa akiba ya wengi. Wewe uliyekopa kutorejesha mkopo ni sawa na kuiba akiba ya watu wengine. Ni aibu, na inavunja hali ya kuaminiana ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa kisasa. Ipo methali isemayo, Mwezi hauwezi kuandama mpaka uliotangulia umeondoka. Nasi hatuwezi kupata maisha mapya, ya kisasa, wakati bado tunang ang ania tabia, hulka na mienendo ya kufanya kazi kizamani. Tukiwa wabunifu zaidi, tukijituma zaidi, na tukifanya mambo yetu kisasa, tutapata maisha bora ya kisasa. Mimi nina hakika tukiamua tunaweza, na tutafanikiwa. Mungu Ibariki Afrika. Mungu Ibariki Tanzania. Ahsanteni kwa kunisikiliza. You might need to download Realplayer in order to view and listen the President's speeach Speeach...
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationInformation for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationTaarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania
Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania Benki Kuu ya Tanzania Septemba 2016 YALIYOMO 1.0 HALI YA UCHUMI WA TANZANIA... 3 1.1 UKUAJI WA UCHUMI... 3 1.2 MATAZAMIO YA UKUAJI WA UCHUMI MWAKA 2016... 4 1.3
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationTANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko
TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,
More informationJifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti
Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationIn the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment
In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA MUSTAFA HAIDI MKULO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationMwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013
www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper
More informationNGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017
TAARIFA Agosti 2017 NGUO MPYA ZA UKOLONI Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika Jumuiya ya Jamii ya 2007: Wajumbe wanaadhamana Nairobi dhidi ya EPAs. SwissInfo Tangu mwaka
More informationApril 14, 2016 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 52
MOMBASA COUNTY ASSEMBLY HANSARD REPORT Thursday, 14 th April, 2016 The House met at 2.48pm. (Hon. Deputy Speaker (Mr. Mswabah Rashid) in the Chair) PRAYERS Hon. Deputy Speaker (Mr. Mswabah Rashid): Kindly
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2018/19 1 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationNGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA
NGUZO KUMI ZA KWANZA (MFUMO WA UTEKELEZAJI) NGUZO YA 1 DIRA YA TAIFA YA KWANZA 1.1 Kupitisha Dira ya KWANZA SHUGHULI MAJUKUMU MUDA MHUSIKA MKUU 1. AZIMIO LA KWANZA 2. mpango wa utekelezaji wa KWANZA 3.
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationTIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO
TIST HABARI MOTO MOTO Tel. 026-2322246 P.O.BOX 53 MPWAPWA E-Mail tist@twiga.com 01 October 2000 Y2K PREPARATIONS Holes and Seedlings made ready for the year 2000 programme By Gayo Mhila The process of
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More information5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationJAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
More informationMAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI
MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha
More informationHuduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig
KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1
More informationMKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA
More informationPronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationKUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.
KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana
More informationTANGA CEMENT PLC ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA.
TANGA CEMENT PLC 2016 ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA www.simbacement.co.tz ANNUAL REPORT 2016 ANNUAL REPORT2016 TAARIFA YA MWAKA 2016 TAARIFA YA MWAKA 2016 02 ANNUAL REPORT 2016 Chairperson s Statement
More informationMhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, KWENYE SHEREHE YA KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA, TAREHE 08 JUNI 2008, MSIMBAZI CENTRE, DAR ES SALAAM Mhashamu
More informationTIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees
TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST
More informationUtumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted
More informationHii ni Nakala ya Mtandao (Online Document)
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MBILI Kikao cha Ishirini na Tatu - Tarehe 14 Julai, 2003 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) DUA Naibu
More informationusudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-
Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa
More informationUpande 1.0 Bajeti yako
Upande 1.0 Bajeti yako Bajeti (Budget) ni muhustari wa njisi wewe (na familia yako) mnavyopata na kutumia pesa. Inaunganisha pesa zinazoingia nyumbani kwako (Kipato/ income) na zile unazotumia (matumizi/expenses).
More informationKiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika
Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationMWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18
MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18 WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO NOVEMBA, 2016 ISBN 978-9987 - 829-02 - 9 ii YALIYOMO 1.0 UTANGULIZI... 1 2.0 MABORESHO YA MFUMO WA KIBAJETI... 2
More informationMarch 14, 2018 PARLIAMENTARY DEBATES 1 NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL REPORT. Wednesday, 14 th March The House met at 9.30 a.m.
March 14, 2018 PARLIAMENTARY DEBATES 1 NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL REPORT Wednesday, 14 th March 2018 The House met at 9.30 a.m. [The Temporary Deputy Speaker (Hon. (Ms.) Mbalu) in the Chair] PRAYERS QUORUM
More informationEllen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar
Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ukristo leo unadhihirisha waumini karibu bilioni mbili katika maelfu ya madhehebu tofauti na tofauti na madhehebu. Kati ya hizi, zaidi ya 500 madhehebu
More informationRipoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013
W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa
More informationHati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako
More informationMaswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA
Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA TWN Third World Network 1. WEMA ni nini? Mahindi yanayotumia maji kwa ufanisi yajulikanayo kwa kingereza kama Water Efficient Maize for Africa (WEMA) ni mpango
More informationTAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA
TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA
More informationSautiElimu. Sauti Yako Isikike
SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian
More informationMAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA
MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA KUHUSU JINSI YA KUINGIZA MASUALA YA USAWA WA JINSIA KATIKA RASIMU YA PILI YA KATIBA YA TANZANIA KWA NINI MISINGI YA USAWA
More informationJHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI
JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika
More informationKufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi
PAN AFRICAN PARLIAMENT PARLEMENT PANAFRICAIN البرلمان PAN- PARLAMENTO األفريقي AFRICANO Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi Julai 21 22, 2011 Bunge la
More informationwasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWENYE IBADA YA KUWEKWA WAKFU NA KUINGIZWA KAZINI ASKOFU MARTIN FATAELI SHAO WA DAYOSISI YA KASKAZINI YA KANISA LA
More informationUKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)
Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni
More information28 JUNI, 2018 MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA. Kikao cha Hamsini na Tisa Tarehe 28 Juni, (Mkutano Ulianza Saa 3.
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tisa Tarehe 28 Juni, 2013 (Mkutano Ulianza Saa 3.00 Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma Dua HATI ZILIZOWASILISHWA
More informationATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR
ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini
More informationUfunguo wa Kutaalamika Haraka
0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationK. M a r k s, F. E n g e l s
W a (any a kazi wa nchi zote, unganeni! K. M a r k s, F. E n g e l s Maelezo ya chama cha kikomunist Idara ya Maendcleo Moscow Tafsiri hii ya "Maelezo ya Chama cha Kikomunist" inatokana na maandishi
More informationKimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:
Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200
More informationBUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA. Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi)
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, 2018 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationBUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE. Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, 2012 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Anne S. Makinda) Alisoma
More informationBUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, 2017 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua NAIBU SPIKA:
More informationMALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU
MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU NA WAJIBU WA Serikali za Mitaa Kimetayarishwa na Kikundi Kazi cha Serikali za Mitaa cha Policy Forum Kimehaririwa
More informationDeputy Minister for Finance
ISSN: 1821-6021 Vol XI - No - 34 DID YOU KNOW? A procuring entity is?s required to use suppliers pliers?pliers?pliers?pliers among those awarded ed?ed?ed?ed framework agreements by GPSA for procurement?ents
More informationORDER NO BACKGROUND
In the matter of an Application by the DAR ES SALAAM URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (DAWASA) For a Tariff Adjustment, Submitted on January 8 th, 2008 (TR-W-08-001) ORDER NO. 08-001 1.0 BACKGROUND
More informationMradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda
WARAKA WA TAARIFA YA MRADI (PID) HATUA YA TATHMINI TAARIFA NA..: AB4376 Jina la Mradi Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda AFRIKA Sekta Madini na Uchimbaji mwingine (100%) Namba ya
More informationUhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI
Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI b Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI 1 Mwongozo wa Uzalishaji
More informationHii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE. Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006 (Ulianza Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta)
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More informationRIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA TAIFA YA UKAGUZI RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KUHUSU UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA KWA MWAKA WA FEDHA 2009/2010 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
More informationMWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI
MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality
More information2
2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 CKRC VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, KALOLENI CONSTITUTENCY, HELD AT MARIAKANI SECONDARY
More informationHii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA SITA Kikao cha Ishirini na Mbili Tarehe 6 Julai, 2009 (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika
More informationUnited Pentecostal Church June 2017
Kwa Nini Tusali? Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa "Chagua" Ladies Prayer International kwa Facebook United Pentecostal Church June 2017 Tuko na wafuasi Facebook katika Marekani, Hong Kong, Philippines,
More informationProgramu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi
Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania Modeli wa Ukodishaji Mradi Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini
More informationUSIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI
USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03
More informationMukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika
Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika (A Summary Of Arguments For And Against Individual Communion Cups) Na J D Logan Communion Cups) 1 Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi
More informationHAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII
HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII SHERIA KATIKA LUGHA RAHISI KIMETOLEWA NA CHAMA CHA WANASHERIA TANZANIA BARA (TANGANYIKA LAW SOCIETY) KWA UFADHILI WA TAASISI YA LEGAL SERVICE FACILITY
More informationRipoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07
Mwongozo wa Lugha Rahisi wa Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07 Mwongozo huu Umeandaliwa na Hakikazi Catalyst kwa niaba ya Wizara ya Fedha na Uchumi. Desemba 2007 Dibaji Ripoti ya Mwaka ya
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More informationNa Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4
;II. -~ ~.! ~ l Na Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4 ~n.~ SURA YA KWANZA SHERIA YA ARDHI 1 UTANGULIZI Sura hii itaiangalia ARDHI na umuhimu wake katika maisha ya binadamu. Ardhi ni rasilimali
More informationORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI SPIKA MHE. PANDU AMEIR KIFICHO. Rais.
ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI SPIKA MHE. PANDU AMEIR KIFICHO 1.Mhe. Kamal Basha Pandu 2.Mhe. Ali Mzee Ali 3.Mhe. Shamsi Vuai Nahodha Naibu Spika/Jimbo la Rahaleo. Mwenyekiti wa Baraza/Uteuzi
More informationMwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI
David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition
More informationUshindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT
Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT 1 Ushindi Ndani ya Kristo Na W. W. Prescott Mfasiri: M. Mwamalumbili Victory in Christ - Kiswahili 2 Yaliyomo Alinipenda Mimi Aliishi kwa ajili Yangu Mimi Alikufa
More informationBUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Saba Tarehe 13 Aprili, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A
BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA Kikao cha Saba Tarehe 13 Aprili, 2017 (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Job Y. Ndugai) Alisoma Dua SPIKA: Waheshimiwa Wabunge naomba
More informationKuwa na Ukimwi ni kama vile kutakiwa kuendelea kuuzima moto unaoniunguza bila kukoma.
This booklet on HIV/AIDS was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at VIRUSI VYA
More informationElimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi
Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Gervas Zombwe 1 1. Utangulizi Katika mazingira ya kawaida kabisa ndani ya jamii yetu, Imezoeleka kusikia au kuona watu wakioanisha dhana ya elimu
More informationUsimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya
Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationKilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira
Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira Kiongozi hiki kimeandaliwa kikiwa ni sehemu ya mradi wa
More information