Forum:MyElimu Home for Students to Share Knowledge Thread: Dunia Uwanja Wa Fujo
|
|
- Blaise Fitzgerald
- 6 years ago
- Views:
Transcription
1 Forum:MyElimu Home for Students to Share Knowledge Thread: Dunia Uwanja Wa Fujo MwlMaeda - June 10, 2017, 9:19 am Dunia uwanja wa fujo ni riwaya iliyoandikwa na Euphrase Kezilahabi mwaka wa Ni riwaya ambayo inasawiri maisha ya wanadamu hususani waishio Afrika Mashariki, hasa hasa katika nchi ya Tanzania. â œdunia uwanja wa fujoâ inaelezea jinsi maisha yaliyopo duniani ni sawasawa na fujo, kwani kila mtu anayekuja duniani huleta fujo zake na baadaye kutoweka. Mwandishi anaelezea kwamba kila mtu anafanya fujo zake na kusababisha matatizo mbalimbali katika jamii yake kama vile mauaji, ukabila, umalaya, uchawi, ubakaji, ulevi wa kupindukia n.k. Hivyo basi mwandishi anaamini kwamba katika dunia kila mtu anakuja na fujo zake na kutoweka. Kwa mfano, mhusika Tumaini katika riwaya hii ameleta fujo zake kama vile umalaya, mauaji na mengine mengi na baadaye kutoweka. Mbinu za kifani katika riwaya hii Fani za kijadi ndizo zilizosababisha riwaya izalike. "Dunia ni uwanja wa fujoâ ni mojawapo ya riwaya zilizotokana na fani ya kijadi ambayo ni sira. Sira ni fani ya kijadi ambayo hujumuisha wasifu na tawasifu, yaani habari za maisha ya watu; kwa mfano mwandishi E. Kezilahabi katika riwaya yake hii amejaribu kumuonyesha mhusika Tumaini maisha aliyokuwa akiishi. Mfano uk. 11, â œalibatizwa, alikuwa mtoto wa mwalimu Kapingaâ â â. Vile vile Tumaini alikuwa mlevi, malaya, mfano uk. 73 â œmwenyewe kaingiaaaa, tajiri wetuuuâ. Hivyo basi riwaya hii inasadifu kuwa ni mojawapo ya riwaya za fani za kijadi ambayo hujumuisha wasifu wa mhusika Tumaini toka mwanzo hadi mwisho wa maisha yake. Muundo Muundo ni namna visa na matukio hufuatana kwa mtiririko. Hivyo tunaweza kusema pia muundo ni mfuatano wa masimulizi katika kazi ya fasihi. Katika riwaya hii mwandishi ametumia muundo wa rejea pamoja na changamano. Katika muundo wa rejea mwandishi anaanza kwa kuonyesha maisha ya Dennis pale alipowapokea wageni akina Tumaini na pia kurejelea kwa kuonyesha maisha ya Dennis pale tangu utoto wake (uk.66). Pia mwandishi ametumia muundo changamano au rukia ambapo visa vinakuwa vinarukiana: hii inajidhihirisha sehemu ya kwanza ambapo anatuonyesha nyumbani kwa Kasala ambaye anaishi kijijini Bugolola; kisa hakijaisha tunaona pia kisa cha Tumaini (uk.11) ambapo mwandishi anaonyesha alivyozaliwa na kubatizwa. Mwandishi pia ameigawa kazi yake katika sehemu kuu tatu na kila sehemu ameipa namba ili kusadifu yaliyomo katika kazi yake ya riwaya. Katika sehemu ya kwanza E. Kezilahabi amewachora wahusika kwa kuonyesha adha na matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii ya Bugolola, kwa mfano ushirikina, umalaya na ulevi: mambo hayo yote ameyaonyesha katika namba 1, 2, 3, 4, 5. Pia katika sehemu ya pili tunamuona Tumaini akiwashawishi akina John na Anastasia kwenda nao mjini Dar es Salaam, lakini inakomea Shinyanga baada ya kukutana na dada ya Dennis, kitu kilichompelekea Tumaini na wenziwe kuanza maisha mapya mjini Shinyanga. Lakini katika maisha hayo Tumaini na John wanakuwa wenye kupenda pombe na ansa, kitu kilichopelekea kufilisika kwa Tumaini. Sehemu ya tatu inaonyesha baada ya Tumaini kuamua kufanya kazi alivyopata mafanikio makubwa, lakini mafanikio hayo yanaingia doa baada ya serikali kuingiza mfumo wa ujamaa, kitu kilichopelekea mali zote za Tumaini. Mwisho kabisa tunamuona akichukua jukumu la kumuua mkuu wa wilaya ya Shinyanga ambaye ndiye alikuwa msimamizi mkuu wa shughuli za ujamaa; kitendo hicho kinapelekea hukumu ya kifo kwa Tumaini (namba 12, 13, 14).
2 Msuko Mbunda Msokile (1992:206) anasema kuwa msuko ni mtiririko au mfuatano wa matukio yanayosimuliwa kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Hali hii huandamana na uchaguzi au mpangilio na ufundi wa kusimulia matukio yaliyoungwa vyema katika kazi ya sanaa ya kubuni itumiayo lugha. Lakini si tofauti na ule ufafanuzi huu si tofauti na ule unaofafanua muundo, kwani nao ni mtiririko wa matukio jinsi jinsi yanavyopangwa kiufundi kutoka mwanzo wa simulizi hadi mwisho. Pesa za urithi alizoachiwa Tuamini pamoja na malezi mabaya kutoka kwa wazazi wake ndio zinakuwa usababishi wa utonvu wa nidhamu wa Tumaini katika kijiji chao cha Bugolola, mambo hayo ya uonvu wa nidhamu ni kama vile;- mlevi, Malaya, kutofanya kazi, pia alitumia ovyo mali alizoachiwa. Mfano katika (uk.15) â œtunamuona mama yake Tumaini akimkabithi Tumaini funguo ya kufungua sanduku la marehemu baba yake ammbalo lilikuwa limebeba urithi wake. Tumaini baada ya kupewa pesa za urithi hapa ndio tunaona mshitikizo kwani kwani pesa za urihi zilimsababisha kuamua kuacha shule na kuanza kuzitumia pea hizo ovyo kama vile ukahaba umalaya, ulevi, na mengineyo. (Uk. 16, 17). Pia katika riwaya hii msuko unaendea kuonekana pale ambapo Tumaini, John, na Anastazia walipofika Mwanza na kufanya maamuzi ya kuelekea Daes saalam baada ya kuona eneo la Mwanza haitawafaa kwa kuanza maisha mapya kwani palikuwa karibu mno na kijini kwao, sababu nyingine ilikuwa Akina Tumaini hawahuondoka kijijini kwao kwa wema. Safari yao ya kuelekea Dar es saalam inafikia kikomo pale ambapo walipofika Shinyanga na kukutana na Dennis ambaye aliwasihi wasitishe safali yao ili aambatane nao wakapajue kwake na kumpasha habari juu ya mambo yaliyokuwa yakiendelea kijijini kwao Mugele (uk.55-72). Hali ya kuahilisha safari ya kuelekea Shinyanga ilisababisha akina Tumaini kuanza maisha mapya mjini Shinyanga na kwa vile Tumaini alikuwa na pesa nyingi za urithi alianza maisha ya anasa hali hiyo ilipelekea kuishiwa Tumaini kipato na kumpelekea Tumaini kutafuta kazi ya ulinzi ambayo alisaidiwa na Dennis katika kuipata ajija hiyo(uk.114). Lakini pindi alipoanza kazi hiyo alijikuta akichukiawa na watu mbalimbali kutokana na kazi yake ya kuchunguza watu sili zao na kuzilipotisha serikarini. Kzi hiyo ilisababisha hata baadhi ya watu kumkimbia Tumaini mahali alipotia mguu wake. Mfano pindi alipofika baa wateteja walikunjwa haraka haraka na kukimbia hali hiyo ilisababisha wenye biashara zao kumchukia Tumaini na ikafikia hatua ya kumtafutia Tumaini wajambazi wa kumuadabisha Tumaini. Baada ya Tumaini kutafutiwa majambazi na kuwa ameadabishwa hali hiyo inatumika kama usababishi wa Tumaini kuichukia kazi yake na kuamua kutafuta kazi nyingine ya kujiajili yeye mwenyewe, kazi yenyewe ilikuwa ni kazi ya ukulima japo alianza kama mkulima mdogo lakini baadae akajikuta akipata maendeleo makubwa katika kazi yake mfano alinunua shamba kubwa na alitumia Trekta katika shuguli zake za kilimo. lakini ngombe wa maskini hazai serikali ikapitisha mfumo wa ujamaa ambapo ilidai hakuna umiliki binafsi na mali zote ni za ni za umma hali hiyo ilisababisha kumuingiza tumaini matatani kwa hakukubaliana na hali hiyo na kupelekea kufanya tukio la mauaji ambapo alimuua mkuu wa wilaya ambaye ndiye alikuwa ni kiongozi wa ujamaa (uk.114), Kitendo hicho kilitumika kama usababishi kwa Tumaini kuwekwa chini ulinzi wa polisi na hatimaye kuhukumiwa kunyongwa (Uk.131). Mtindo Mtindo ni jinsi msanii anavyotumia ufundi, umahiri na hisia zake katika kutenda au kueleza jambo fulani. katika riyawa hii kuna mitindo mbalimbali ambayo mwandishi ameitumia ni kama vile; VIPENGELE VYA MTINDO VILIVYOTUMIKA KATIKA RIWAYA HII; Monolojia [Masimulizi] kwa kiasi kikubwa mwandishi ametumia lugha ya masimulizi katika kuelezea visa/matukio, sifa na tabia za wahusika katika kuikamilisha kazi yake. MTINDO WA BARUA Mwandishi pia ametumia mtindo wa barua, m kwa mfano katika uk.68 mwandishi ametumia mtindo wa barua tunaona Vera akimwandikia Denis barua, pia uk.105 mwandishi ametumia mtindo huu wa barua, Tunamuona Tumaini akimuandikia Joku barua vilevile katika uk.110 â œtunamuona Denis akipokea barua kutoka kwa Veraâ, uk.123 â œbibi Kimalio alimuandikia barua denisâ. HOTUBA Mwandishi katika kazi yake hii ya riwaya ya â œdunia ni uwanja wa fujoâ ametumia mtindo wa hotuba. Kwa mfano katika uk. ( ) mtindo wa hotuba umetumika na hotuba
3 ilikuwa ya kusisitiza Azimio la Arusha ambalo lililenga hatua ya siasa ya ujamaa nakujitegemea ambayo ilitaka watu wote wamiliki mali na uchumi kwa pamoja bila kujali mwenye nacho na asiye ncho. NYIMBO Ni mtindo mmoja wapo aliotumia mwandishi aliotumia mwandishi wa riwa hii. Kwa mfano uk.10 mwandishi ametumia wimbo ulioimbwa na mpiga zeze. â œwanaume Bugolola Mchana hawajambo Usiku hawana tendoâ Mwandishi pia ametumia wimbo kwa mtindo wa shairi katika kazi yake hii kwa mfano katika uk.13 tunona Tumaini akiandika shairi ambalo lilisomwa na mwalimu darasani kama ifuatavyo. â œyeh, Nitaoa msichana Msichana mwenye shingo Shingo shingo kama la mbuni..â Mwandishi ametumia wimbo wa maungunzo, mwandishi katika mtindo wa mazungumzo ametumia nafsi zote tatu yaani nafsi ya nafsi ya kwanza, nafsi ya pili, nafsi ya tatu katika kazi yake yake hii ya Dunia uwanja wa fujoâ kwa mfano. - Uk. 13 tuaona nafsi ya kwanza umoja â œnitaoa msichanaâ na - uk.27 tunaona nafsi ya kwanza wingi. â œhata sisi,â pia - Pia nafsi ya pili katika riwaya hii imetumika kwa mfano uk.36 â œâ wewe kasala Pia nafsi ya tatu katika riwaya hii tunaona katika uk.35 â œâ.yeye alisema kwa machozi MATUMIZI YA LUGHA Lugha ni muhimu katika kazi ya fasihi. Posipo lugha hakuna riwaya. Mwandishi wa riwaya hii â œdunia ni uwanja wa fujoâ ametumia lugha sanifu iliyosheheni taswira, mkoto, misemo, methali, tamathali za semi, nahau, lugha za kigeni, na mbinu zingine, za kisanaa kama ifuatavyo:- Lugha sanifu ni moja wapo ya ambayo mwandishi ametumia toka mwanzo hadi mwisho. Lugha iliyotumika ni Kiswahili sanifu. Pia mwandishi ametumia lugha isiyo sanifu kwa kiasi kidogo. Kwa mfano katika uk. 5, Mwandishi anasema â œâ. Batoto bamenisosondogorasondogola na chichwa, bengine bamenikorokorakorokora na kuchaâ. Uk. 30 â œâ. Vizuri walilia kwa sauti za kutisha, yuhuu. Huba, huba, huba. Wotha,wothaâ LUGHA YA KIGENI Imetumiwa na E. Kezilahabi katika riwaya yake hii. Lugha ya kigeni aliyotumia ni Kiingereza kwa mfano:- - â œafricans royal barâ (uk. 62). - â œsnow capâ (uk.62) - â œyou are too optimistic about life and you are too pessimisticâ (uk.65, 66). - â œwelcome backâ (uk.88). - â œsecurity (uk.89 na 90). MCHANGANYO NDIMI Ni matumizi ya lugha ambayo mwandishi ametumia katika riwaya hii. Mchanganyo ndimu ni ile hali mtu kuongea kwa kutumia lugha zaidi ya mbili. - Mfano. (Uk. 41) â œmimi â naturalistâ. LUGHA ZA MATUSI Ni Mbinu nyingine ilizotumiwa na mwandishi katika riwaya hii ni lugha za matusi kwa mfano. - â œwashenzini ninyiâ.(uk.12). - â œkumbe bado washenziâ (uk.50). - â œyule mshenzi amekwendaâ (uk.93) - â œnimemfukuza mbwa tumaini (uk.109). - â œkwanza wewe bwege. (uk.121). -â œâ. Alidakia na kusema unyokonyoko (uk.122). TAMATHALI ZA SEMI Ni maneno yanayotumiwa yanayotumiwa na wasanii Ili kutia nguvu katika kazi hiyo. Hivyo tamathali za semi zinazotumika katika riwaya hii ni pamoja na : TASHIBIHA/MSHABAHA Ni maneno ambayo hutumia kulinganisha kitu na kitu na kitu kingine kwa kutumia maneno kama vile â œmithili, sawa, kamaâ mfano:- - â œmiaka ni kama kunguniâ (uk.6). - â œbaba yako atakuwa mkali kama sambaâ (uk.6). - â œmapenzi ni kama mpunga mototo wanguâ (uk.14). - â œlakini mimi ninaumwa ninaumwa kama panya.â (uk.17). - â œsi tutakufa kama mbwaâ. (uk.19). - â œkukaa kama watakatifuâ. (uk.19.) - â œaliyekunyata nyumbani kwake kwa uoga kama panya aliyesikia mlio wa pakaâ. (uk.130). SITIARI Ni tamathali za semi ambazo ulinganisha vitu vizuri kwa kutumia viunganishi au linganishi.mfano â œniâ :- - â œwatoto wote yatima ni watoto wanguâ. (uk.15). - â œhuyo ni
4 baba yakoâ (uk.12). - â œujamaa ni mzuriâ. (uk.112). Takriri ni tamathali za semi ambayo neon hujirudiarudia kwa lengo la kusisitiza jambo Fulani. Takriri ni matumizi ya lugha ambayo msanii ametumia katika riwaya hii, mfano wa takriri:- - â œmauti, mautiâ. (uk.17). - â œhe! Hee! Hee!â (uk.18) - â œkasala, kasala, ngoja nije!â (uk.22) - â œyuhu! Yuhu!â (uk.27) - â œhaa! Haa! Haa! (uk.42) - â œmsiue, msiue!â (uk.44) TASHIHISI Ni tamathali za semi ambazo vitu ambavyo si viumbe hai hupewa hadhi ya kutenda kama binadamu. Mfano:- - â œmwezi uliona nyota ziliona hata jua liliona.â (uk.12) - â œtumaini alisikia sauti kama ya ndege akiimba kwa huzuni.â (uk.19) - â œkila jiwe walilokalia liliwaambia â œsamahani umekalia bega languâ. (uk.32) TANAKALI SAUTI Ni tamathali ya semi ambayo uigaji wa sauti za asili. Mfano Katika riwaya hii tanakari sauti alizotumia msanii ni kama ifuatavyo:- â œboooouuu! (uk.130) TAFSIDA Ni tamathali za semi ambazo kwazo matumizi zake ni za adabu. Mfano : â œkazi kutembeza kengele zako kwenye mabaa.â Uk â œtumaini alikuwa akishika mahali pabayaâ. Uk.53. METHALI Usemi wa kisanii wa kimapokea unaofikiriwa na jamii kuwa kweli na unaotumiwa kufumbia au kutolea mifano na huwa unabeba maana pana kuliko maneno yenyewe yanayotumiwa. Kwa mfano:- - â œwema wa mtu hujulikana siku ya mazishi yake.â (Uk.13) - â œugonjwa haufichwi. Afichae ugonjwa ndio hufa.â (Uk.29) - â œkweli wajinga ndio waalimu wa kuwafunza welevu. (uk.78) - â œukishikwa shikamana.â (Uk.102) MISEMO Ni mafungu ya maneno yanayotumiwa na jamii ya watu wa lugha hiyo kwa namna maalumu ili kutoa mafunzo, maadili na kuihadharisha jamii. Misemo ni maneno ambayo jamii huyatumia kutokana na uzoefu katika maisha. Kwa mfano: - â œponda mali kifo chaja.â (Uk.10) - â œulimwengu hauna mwema.â (Uk.103) - â œmapenzi yao sasa yalikuwa yamekwisha pata kovuâ. (Uk.108) - â œnilitaka uniondoe kwenye mdomo wa samba.â (Uk.24) NAHAU Haya ni mafungu ya maneno yenye maana maalumu ambayo haitokani na maneno ya kawaida yaliyopo kwenye maneno hayo. Nahau za lugha yoyote hutumiwa zaidi na jamii yenye asili ya lugha hiyo. Kwa mfano:- - â œamezunguka mbuyu - amekula rushwaâ. (uk.25 - â œunamvika kilemba cha ukokoâ. (Uk.71) Tanakali sauti - â œbooouuu!â MJALIZO Katika tamathali hii sentensi huwa ni mfuatano tu wa maneno yasiyo na viungo vyovyote. Mfano:- - â œwenye mashoka! wenye mikuki na miundu! Wenye pinde na wenye mapanga walianza kulifyeka lile chakaâ. (Uk.27) WAHUSIKA Wahusika ni watu au viumbe waliokusudiwa wawakilishe tabia za watu katika kazi za fasihi. Wahusika wa fasihi ni wa aina kuu tatu,wahusika kazi ya fasihi wanaweza kuwa wahusika wakuu, wahusika wadigo, na ewahusika wajenzi.wahusika huonyesha dhana mbili muhimu katika maisha ya watu yaani wema na mabaya pia wahusika humaanisha tabia maalumu iliyokusudiwa na jamii. Katika riwaya ya â œdunia uwanja Fujoâ wahusika wake ni mhusika mkuu, whusika wadogo, na wahusika wajenzi kama alivyoainisha Catherine Ndugo (1991) na Wangali Mwai(1991).ika riwaya hii mwandishi ametumia wahusika wa aina tatu kwa kutumia kigezo cha Catherine na Wangeri Mwai(1991) Kama wahusika wakuu, wadogo, na wajenzi kama ifuatavyo:- MHUSIKA MKUU Mhusika mkuu; huyu ni yule anejitokeza kila mara katika kazi za fasihi tangu mwanzo hadi mwisho. Maudhui ya kazi ya fasihi huwa yanamzungukia na hata kutolewa na mhusika mkuu zaidi ya wahusika wengine. TUMAINI Huyu Ndio mhusika mkuu katika riwaya hii kwani maudhui na dhamira zimejengwa juu yake. Pia tunaona wahusika wajenzi akina John, Anastazia, Dc, na mgeni kutoka Dar es saalam dhamira wanazozitenda zinamgusia mhusika mkuu ambaye ni Tumaini. Jina Tumaini ni jina ambalo
5 amepewa na mzazi wake mzee Kapinga ambaye alikuwa mwalimu. Jina Tumaini linasadifu matumaini ya wazazi wake, pia alikuwa ni mototo pekee wa kiume katika familia ya mwalimu Kapinga pia walikuwa na matumaini pindi atakapomaliza shule ndio atakuwa msaada wao katika familia na pindi watakapokuwa wazeeka.mambo hayo yanapatikana katika (uk.11). inasema â œâ Naam Tumaini alikuwa motto wa watu hawa. Tumaini kama jina lenyewe lionyeshavyo alikukuwa peke yake katika tumbo la mama yakeâ..â WASIFU WA TUMAINI - Alikuwa ni motto wa Kapinga. (uk.9) - Alikuwa Malaya (uk.8, 24) - Alikuwa mlevi (uk.94) - Mchapa kazi (uk. 114) - Mtumia Pesa vibaya (uk. 55) - Alikuwa muuaji. (uk.128) - Alikuwa na mapenzi ya dhati kwa mkewe (uk.128) Alikuwa na matusi (uk. 12) WAHUSIKA WADOGO WADOGO Hawa ni wahusika ambao hawajitokezi mara kwa mara katika kazi ya fasihi ndio ambao husimamia dhamira ndogo ndogo Katika riwaya hii ya â œdunia uwanja wa fujoâ wahusika wadogo wadogo waliojitokeza ni kama ifuatavyo:- 1. KAPINGA. SIFA ZA KAPINGA - Baba yake na Tumini. (uk.9) - Alikuwa mwalimu. (uk.9) - Alikuwa na malezi mabaya kwa mwanae. (uk.12) - Alikuwa ni Mume wa miango. (uk.9) - Alikuwa ni mbinafsi. (uk.15) - Alikuwa hapendi kushilikiana katika jamii. (uk. 12). 2. KASALA SIFA ZA KASALA - Ni mwanakijiji wa Bugolola. (uk. 1). - Mtoto wa Mugala. (uk. 2). - Baba yake na Misana. (uk. 2). - Mume wake na Mugele. (uk. 2). - Mtu mwema. (uk. 4). - Kiasi Fulani alikuwa ni mvivu.(uk.6) 3. MUNGERE SIFA ZA MUNGERE;- - Mke wa Kasala (uk.2). - Mama yake na Misana (uk.2). - Mwanakijiji wa Bugolola (uk.2). - Mtu mwema na mchapa kazi. (uk. 4). 4. MISANA. SIFA MISANA;- - Mtoto wa Kasala (uk.2). - Alikuwa mtundu. (uk.3). - Mtoto wa Mungere (uk.2). - Mdogo wao na akina Dennis, Leonila, Aulelia. (Uk.5). 5. MUGALA - mwananchi wa Bugolola. Uk.3 - Mchawi. Uk.3 na 7. - Ni mama yake na Kasala. uk.2 - Ni mjane uk.4. - Mtu mwenye hasila uk.22 - Alikuwa na malezi mabaya kwa wajukuu zake uk LEONILA - Alikuwa dada yake Dennis na Misana. - Alikuwa ni motto wa Kasala Mungere. - Alikuwa ni mpenzi wa Tumaini uk. 8 na BENADETA - Mke wa pili wa Dennis uk Mtu mwenye chuki uk Alikuwa na dharau na mwenye matusi. uk CHRISTINA - Alikuwa kahaba. Uk.96 - Alikuwa mlevi uk.94 - Alikuwa mlagai uk.95 - Hana mapenzi ya dhati uk.96 - Alikuwa anapenda sana pesa. Uk MAKOROBOI - Alikuwa jambazi uk.96 - Alikuwa mkatil na mwenye kisasi uk.96 - Anapenda pesa. Uk.96 WAHUSIKA WAJENZI Ni wahusika ambao maudhui yao na dhamira wanazozitenda zinamsaidia mhusika mkuu katika dhamira azitendazo. Mara nyingi wahusika wajenzi wanakazi ya kunjenga au kumsaidia mhusika mkuu katika dhamira zake. Katika riwaya hii wahusika wajenzi ni kama ifuatavyo: 1. JOHN JOHN Ni mhusika mjenzi kwani dhamira alizobeba na nafasi alizotumiwa na mwandishi ni kwa lengo la kumjenga mhusika mkuu tumaini. Pia tunaona John na Tumaini walikuwa na mahusiano na ushirikiano tangu wakiwa kijijini Bugolola mpaka waliposafiri kuelekea mjini Shinyanga. -Alikuwa mlevi uk.62 -Alikuwa Malaya uk.62 na 66. -Alikuwa mvivu uk. -Ana mapenzi ya dhati uk ANASTAZIA Anastazia pia huyu ni mhusika mjenzi kwani alikubali kuambatana na Tumaini kijijini kwenda Mwanza halafu mjini Arusha. Pia uhusiano wao ulidumu na kupelekea kuoana na Tumaini. WASIFU WA ANASTAZIA NI KAMA IFUATAVYO:- - Alikuwa na mapenzi ya dhati. Uk.57, 97, & Alikuwa mke wa Tumaini. Uk Mtu mwenye huruma uk.99 - Mtu mvumilivu. Uk DENNIS Ni mmoja wapo wa wahusika wajenzi kwani ndio anaemjenga mhusika Tumaini kwa
6 kiasi kikubwa akiwa mjini Shinyanga. Pia TUMAINI ALIKUWA NA SIFA ZIFUATAZO -Ni mtu mwenye mapenzi ya dhati. Uk.59 -Alikuwa ni mototo wa Kasala. Uk 3 - Alikuwa ni mtumishi wa serikalini MAUDHUI katika kazi ya fasihi ni jumla ya mawazo yote yanayozungumzwa pamoja na mtazamo wa mwandishi juu ya mawazo hayo. Maudhui hujumuisha mawazo pamoja na mafunzo mbalimbali yaliyomsukuma msanii hadi akatunga na kusanii kazi fulani ya kifasihi. Vipengele vya maudhui ni pamoja na dhamira, migogoro, falsafa ujumbe na msimamo. Katika riwaya hii Dunia uwanja wa fujo mwandishi amejitahidi kwa kiasi kikubwa kuonyesha maudhi mbalimbali katika kazi yake kupitia vipengel;e mbalimbali kama vile Dhamira, migogoro, ujumbe, falsafa, mtazamo itikadi hii yote ni kwa lengo kuu la la kuelimisha jamii kuhusu mambo mbalimbali yanayotukia katika jamii hiyo. Dhamira; hili ni wazo kuu au mawazo mbalimbali yanayojitokeza katika kazi ya fasihi. Senkoro anataadharisha maana hii isichanganywe na maudhui kwani dhamira ni sehemu tu ya maudhui na aghalabu dhamira kuu ndio hujenga kiini cha kazi ya fasihi. Dhamira zimegawanyika katika makundi mawili, kuna dhamira kuu na dhamira ndogondogo. Dhamira kuu ni wazo kuu linalojitokeza katika kazi ya fasihi, dhamira kuu katika riwaya hii ni matatizo na mikinzano ya kijamii, kiuchumi, na kisiasa, sasa tuangalie ni kwa jinsi gani mwandishi ameijadili dhamira hii; Matatizo na mikinzano ya kijamii, kiuchumi, na kisiasa, Katika riwaya hii â œdunia uwanja wa fujoâ kwa kiasi kikubwa riwaya hii imejikita katika dhamira hii ambapo ameonyesha matatizo na mikinzano kiuchumi na kijamii ambayo jamii ya kitanzania iliyoandikiwa hukabiliwa nayo. Ili kuijenga dhamira hii mwandishi amewatumia wahusika kama vile Tumaini, John,Anastazia, Kapinga, Dennis ili kuiunda dhamira yake kuu katika riwaya hii. Tukianza na Tumaini mwandishi amemuonyesha kuwa ni mhusika ambaye anapinga sera za kijamaa ya siasa ya ujamaa iliyoanzishwa na serikari nchi nzima hali hiyo inaleta ukinzani kwa tabaka lenye mali kwani hawakuwa tayari kuachia mali zao kwa umma. Hali hii inadhihilisha pale Tumaini alipoamua kupingana na hali hiyo ya kunyanganywa mali zake na kupelekea kumuua mkuu wa wilaya, ambaye alikuwa ndio kiongozi mkuu katika mkoa Shinyanga katika shughuli za kusimamia sera hiyo ya ujamaa'.(uk.127) Hali hiyo ni mfano tosha kudhihilisha kuwa dhamira kuu katika riwaya hii ni'matatizo na mikinzano ya kijamii, kiuchumi, na kisiasa. Dhamira ndogo ndogo.haya ni mawazo yanayojitokeza ili kujenga dhamira kuu. Dhamira ndogondogo zinazojitokeza katika riwaya hii ni; MAPENZI NA NDOA. Mwandishi E. Kezilahabi amejadili suala la mapenzi na ndoa katika pande mbili tofauti, kwanza ameonesha mapenzi ya dhati na mapenzi ya ulaghai lakini pia ameonesha ndoa za dhati na ndoa za ulaghai. tukianza na mapenzi ya dhati, mapenzi ya dhati yanajitokeza kwa: a) MAPENZI YA DHATI KWA TUMAINI NA MKEWE ANASTAZIA Mwandishi ameonesha mapenzi ya dhati aliyokuwa nayo Tumaini kwa mke wake, Mwandishi anathibisha hili pale anapoamua kutoroka na Anstazia na kuelekea mjini Shinyanga ambako walianza maisha mapya pia tunaona jinsi gani wawili hawa walivyojaliana hata katika kipindi cha matatizo. Mfano Anastazia alionyesha mapenzi ya kweli pale alipompelekea Tumaini chakula na kumfaliji kuwa atapona, pindi Tumaini alipopigwa na akina makoloboi. Uk.97 Mapenzi ya dhati aliyokuwa nayo kwa mke wake pia yanajidhihirisha pindi mke wake huyo alipokubali kuishi na Tumaini japo alikuwa ni mhuni na mlevi pia ha baada ya Tumaini kupigwa na kualibiwa sura Anastazia alindelea kuafiki kuishi na na Mumewe Tumini, hii ni kwa kuwa alikuwa akimpenda. Mwandishi anathibitisha hili katika. [Uk 64] 2. Ulevi. Mwandishi E, Kezilahabi hakuwa nyuma kujadili suala la ulevi na athari zake kwa binadamu na jamii kwa ujumla, katika riwaya yake hii amemtumia muhusika Tumaini pamoja na John kuelezea dhamira hii. Tukianza na Tumaini, mwandishi anamwonesha Tumaini akianza tabia ya ulevi wa
7 pombe kali baada ya kufiwa na wazazi wake kijijini Bugololola hata alipoamia mkoani Shinyanga aliendelea na tabia hiyo ya ulevi wa pombe, Mwandishi hakuishia hapo tu bali ameonesha na athari za tabia hiyo ya ulevi kama vile kupelekea kufilisika kwa tumaini kama mwandishi anavyothibitisha (Uk 94 &95) 3. MALEZI KWA WATOTO. Hii ni dhamira nyingine inayojitokeza katika riwaya hii, Mwandishi amemtumia muhusika Tumaini kuilezea dhamira hii, tunamwona Tumaini akipata malezi mabaya kutoka kwa wazazi wake kitu kilichopelekea kuyahalibu maisha ya Tumaini na kumfanya aache shule, awe mlevi, pamija na mengine mengi. Mfano Siku moja Tumaini alimchoma mlezi wake jichoni. Yule kijana alimpiga Tumaini kidogo, Tumaini alikimbia kwenda kushtaki kwa mama yake. â œmama Mpishi amenipiga!â Kwa nini umempiga mtoto wangu!â Mugaya alifoka.â Hali hii inaeleza jinsi Tumaini alivyo lelewa vibaya na kudekezwa na wazazi wake; uk 11 USHIRIKINA NA UCHAWI Ni hali ya kuamini nguvu za giza, ni jambo ambalo lina sababisha jamii nyingi kugawanyika na kukosa amani. Kwani mwandishi anadhihirisha hili anaposema; â œvizuu walilia kwa sauti ya kutisha : yuhu!yuu! huba!â uk. 30. â œtena alikuwa akilala ndani ya nyumba yako! Ndio maana mama yako alikuwa mchawiâ uk. 36. Suala la ushirikina katika jamii inayotuzunguka ni janga ambalo kila siku linahatarisha maisha ya watu hususani wazee wenye macho mekundu wako hatiani kupoteza maisha yao katika baadhi ya maeneo mfano mkoa wa Shinyanga na Simiu,hivyo dhamira hii haijapitwa na wakati. UNAFIKI. Hii ni dhamira pia inayojitokeza katika riwaya hii, katika kuijadili dhamira hii Mwandishi amemtumia mke wa Dennis kama mtu mnafiki kwani alijifanya anampenda mmewe kumbe alikuwa na uhusia mwamume mwingine ambaye ni John rafiki y yake na Dennis. Mwandishi anadhihilisha hali hiyo akionyesha katika kitabu chake kwamba; â œheshima yangu imekwishapotea John ukiniacha hivihivi nitaona aibu sana!â uk72. Tukigeukia katika uhalisia, tabia hii ya unafiki imeshamiri katika jamii zetu, unaweza ukawa na rafiki au ndugu ambaye akawa mnafiki kwako. Jamii inatakiwa kuondokana na tabia hii kwa haifai kabisa. NAFASI YA MWANAMKE. Katika riwaya hii mwanamke amechorwa katika pande mbili, amechorwa katika upande hasi lakini pia mwanamke amechorwa katika upande chanya, upande hasi mwanamke amechorwa kama kiumbe duni na dhaifu wakati katika upande chanya amechorwa kama mtu jasiri, mchapa kazi, mwenye upendo. n.k. Sasa hebu tuangalie nafasi ya mwanamke katika jamii kama alivyochorwa katika riwaya hii tukianza na upande hasi; Katika riwaya hii mwanamke amechorwa kama kiumbe duni, dhaifu, katika nafasi mwanamke amechorwa kama; A) CHOMBO CHA STAREHE. Mwandishi amemchora mwanamke kama chombo cha starehe anayeweza kutumiwa kuwastarehesha wanaume ili mradi kufurahisha nafsi zao, hili linathibitishwa na Mwandishi katika riwaya hii akimtumia muhusika Christina kama chombo cha starehe, ambaye alionekana kujirahisishwa kwa wanaume ili mladi apate fedha. Mfano;uk 95 & 96. â œsijaona mwanaume mwoga kama wewe! Kristina alisema. Tumaini alilala kitandani. Kristina alizima taaâ uk.96 Hata katika jamii yetu inayotuzunguka wanawake kwa kujijua au kutojua wamekuwa wakifanywa kama chombo cha starehe kuwastarehesha wanaume, jamii inatakiwa kubadilika na kuondokana na dhana hii kwani mwanamke pia anastahiri heshima katika jamii. B) MTU ASIYE NA MAAMUZI KATIKA JAMII Mwandishi amemchora mwanamke kama mtu asiye na maamuzi katika jamii yake, kwa mfano anamtumia muhusika ambaye alikuwa nini mama yake Tumaini kushindwa kufanya maamuzi juu mali alizoziacha kama urithi wa Tumaini japo hakupenda kumuachia mtoto wao fedha nyingi(alijua zitamuangamiza mwanae) lakini alishindwa kubatilisha kutokana na maamuzi yaliyoachwa na
8 mumewe.mfano anaonyesha; â œni vizuri zaidi mtoto kurithi vitu kama hivyo, licha ya hekima na kumrithisha mototo pesa ni ni kunvisha taji la uovu.â Baba yako alikataa kabisa; na kwa kuwa nilishindwa mawazo ya baba yako alipokuwa bado mzima, siwezi sasa kugeuza tamshi lake.â uk15 Hata katika jamii yetu, inawachukulia wanawake kama watu wasio na maamuzi katika familia na pindi inapotokea kufiwa na waume zao huwa wanapata shida na manyanyaso kutoka kwa ndugu wa mwanaume kama vile kufukuzwa kwenye nyumba, kunyang'anywa watoto na mali nyingine alizoshirikiana kuzichuma na mumewe. jamii inatakiwa kumpa nafasi mwanamke na itambue kuwa ana haki sawa kama mwanaume. MWANAMKE AMECHORWA KAMA MSALITI. Hii ni nafasi nyingine ambayo mwandishi amemchora mwanamke, kwa mfano tunaona mke wa Dennis kama mtu mnafiki kwani alijifanya anampenda mmewe kumbe alikuwa na uhusia mwamume mwingine ambaye ni John rafiki y yake na Dennis. Mwandishi anadhihilisha hali hiyo akionyesha katika kitabu chake kwamba; â œheshima yangu imekwishapotea John ukiniacha hivihivi nitaona aibu sana!â uk72. Migogoro ni mivutano na misuguano mbalimbali katika kazi za fasihi. Migogoro inaweza kuwa kati ya wahusika, familia zao, matabaka yao, au hata katika nyadhifa mbalimbali. Vilevile migogoro yaweza kuwa ya kiuchumi, kijamii, mogogoro ya nafsi, na migogoro ya kisiasa ambayo hujitokeza katika mitazamo tofauti kulingana na mtiririko wa visa na matukio yanavyopangwa na mwandishi. Kwa kuanza Mgogoro wa nafsi tunamuona Tumaini akipatwa mgogo nafsi pindi alipofiwa na wazazi wake na baadae kug unduli kuwa walikuwa wamechuliwa ka vizuu na bibi ake na Leonila pia mgogoro nafsi wa pili ni pale ambapo leonila ankataliwa kuolewa na Tumaini anajikuta akiingia katika lindi la mgogoro nafsi. Pia Leonila anjikuta akiingia katika mgogo wa nafsi pindi pindi wazazi wake walipomwandalia mazingila ya kuolewa na tembo uk.15 &39 Mgogoro kati ya mtu na mtu; Hapa tunaona mgogoro kati ya Anastazia pamoja na wazazi wake, Dennis na John, Dennis na Benadeta, Tumaini na Serikali,Kasala na mama yake.mfano. uk.22,23,&128. -â œkumtunza mzee ni mzigo lakini inabibi uuchukue kwa fulahaâ uk.23 -â œbaba nihurumie! Lakini Kasala aliendelea kumpiga. Bibi wameniua kwa sababu yako!â uk.22. UJUMBE/MAFUNZO Ujumbe; mwandishi anapoandika kazi yake huwa na ujumbe ambao hutaka uifikie jamii aliyoikusudia. Ujumbe katika kazi fasihi ni mafunzo mbalimbali ambayo hupatikana baada ya kusoma kazi ya fasihi. Katika kazi ya fasihi dhamira kuu hubeba ujumbe wa msingi na dhamira ndogondogo hubeba ujumbe ambao husaidia kuujenga au kuupa uzito zaidi ujumbe wa msingi. Baadhi ya ujumbe unaopatikana katika riwaya hii ni pamoja na;- Kikulacho kinguoni mwako, Huu ni ujumbe ama funzo tunalolipata baada ya kusoma riwaya hii, ujumbe huu tunaupata kupitia muhusika mama Resi pindi kwani alijifanya anampenda mmewe kumbe alikuwa na uhusia mwamume mwingine ambaye ni John rafiki yyake na Dennis.uk.72 Majuto ni mjukuu, Ujumbe huu unajitokeza pia katika riwaya hii, mwandishi anamtumia muhusika Tumaini pale alipoendekeza starehe zilimsababisha aingie kwenye mtego wa majambazi wa kupigwa na kuhalibiwa sura yake. uk.98 Elimu ni ufunguo wa maisha, Mwandishi anatupa ujumbe mwingine kuwa, ili mtu aweze kufanikiwa hana budi kushikiria na kuizingatia elimu kwani elimu ni ufunguo wa maisha, ujumbe huu katika riwaya hii unajitokeza kwa muhusika Dennis ambaye alipata kazi nzuri sababu alikuwa amekwenda shule na kupata elimu ya kutosha. â œnyumba ya Dennis ilikuwa ni kubwa sana. Ilikuwa na vyumba saba bila kuhesabu jiko lililokuwa mumo humo ndaniâ uk.60 Mpende akupendaye asiyekupenda achana nae, katika riwaya hii anaipa ujumbe jamii yake kuwa penda pale unapopendwa na si kumng'ang'ania tu mtu kwa kuwa moyo wako unataka tu kuwa naye, ujumbe huu tunaupata kupitia kwa muhusika Denni alipogundua kuwa mke wake alikuwa na mapenzi ya uongo aliamua kuachana nae.
9 â œdennis alipofika nyumbani alipiga kerere nimemfukuza mbwa,tumainiâ uk.109 MSIMAMO Msimamo; katika kazi ya fasihi, mawazo, mafunzo na falsafa ya msanii hubainisha msimamo wake kuhusu masuala mbalimbali ya kijamii. Msimamo ni ile hali ya mwandishi kuamua kufuata na kushikilia jambo fulani. Jambo hili huweza kukataliwa na wengi lakini akalishikilia tu. Msimamo ndio huweza kuwatofautisha wasanii wawili au zaidi wanaoandika kuhusu mazingira yanayofanana. Hivyo basi mwandishi anamsimamo kwamba mambo yote yanayotendeka katika ulingu huu ni sasawa na fujo tupu, kwani hata kama utajitahidi vipi kupambana na shida za ulimwengu huu matatizo yataendelea kukukabili mpaka umauti utakapokufikia. Jina na jalada la kitabu, Tukianza na jina la kitabu, jina la kitabu ni â œdunia uwanja wa fujoâ linasadifu yale yaliyomo ndani ya kitabu kwani tangu mwanzo wa riwaya hii kuna matukio au fujo mbalimbali ambazo zimejitokeza fujo hizo ni kama vile umalaya, ulevi, uchawi pamoja na mengineyo mengi. Mfano suala la uchawi lidhihilika pale katika uk.36 unasema â œtena alikuwa akilala ndani ya nyumba yako! Ndio maana mama yako alikuwa mchawiâ uk. 36. FALSAFA YA MWANDISHI. Kulingana na Mbunda Msokile yeye anasema kuwa Falsafa ni wazo ambalo mtu anaamimini lina ukweli Fulani unaotawala maisha yake pamoja na maisha ya jamii. Hivyo basi katika riwaya hii anaamini kuwa katika riwaya yake ya â œdunia ni uwanja wa fujoâ Kwamba maisha hayana raha wala maana isipokuwa dunia ni uwanja wa fuzo. KUFAULU KWA MWANDISHI Mwandishi wa riwaya hii amefaru kwa kiasi kikubwa kuibua dhamira dhamira mbalimbali katika jamii. Kwani dhamira hizo zimeonekana kuwa ni kikingamizi kikubwa cha katika maendeleo ya jamii. Mfano suala la uchawi na ushilikina, malezi mabaya, ukale na usasa. Pia mwandishi amefaulu katika suala zima la lugha kwani ametumia lugha lahisi na inayoeleweka kwa msomaji yeyote hata kama si msomi mkubwa.
Information for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationHati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako
More informationMbinu za Ujenzi wa Wahusika na Usawiri wa Sifa Zao: Uhakiki wa Riwaya ya Dunia Uwanja Wa Fujo ya E. Kezilahabi
38 MULIKA NA. 34 Mbinu za Ujenzi wa Wahusika na Usawiri wa Sifa Zao: Uhakiki wa Riwaya ya Dunia Uwanja Wa Fujo ya E. Kezilahabi Leonard Flavian Ilomo Ikisiri Kipengele cha wahusika ni muhimu katika kuunda
More informationUsimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya
Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013
www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper
More informationHati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI/AGOSTI 2011 MUDA: 2 ½ Kiswahili Fasihi Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E) MAAGIZO Jibu maswali manne pekee Swali la kwanza ni lazima Maswali
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level
UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level * 899145 4 672* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2010 Additional Materials: Answer Booklet/Paper READ
More informationMTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya
Jina Nambari.. Shule... 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI / AGOSTI. 2007 MUDA: SAA 2 ½ MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya 102/3 KISWAHILI FASIHI
More informationTheolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College
Theolojia 1 Ujumla Mike Taylor Semester 1 2014-2015 Munguishi Bible College MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 i THEOLOJIA Utangulizi! 1 1. Kumfahamu Mungu katika Injili! 3 1.1. Mawazo Makuu 3 1.2. Maana ya
More informationMwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza
Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)
More informationKUCHUNGUZA UJINSIA NA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA METHALI ZA WAKURYA
i KUCHUNGUZA UJINSIA NA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA METHALI ZA WAKURYA TIMANYWA FELICIAN TASINIFU INAYOWAKILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SEHEMU YA SHARTI PEKEE LA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (M.A. KISWAHILI)
More informationUtumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted
More informationSANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI KITABU CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO
KISWAHILI SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI KITABU CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO KITABU CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO YALIYOMO UTANGULIZI v MPANGILIO WA MASOMO YA KISWAHILI: KIDATO CHA TANO 1 FUNZO: Fasihi (Ukurasa
More informationusudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-
Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More information"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.
KUJA KWA KRIST0 MARA YA PILI "ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28. Mara nyingi sana kuja kwa Kristo mara ya pili huangaliwa tu kama fundisho la dini. Ni
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationKiu Cha umtafuta Mungu
ZAIDI YA NAKALA MILLION 3 ZIMECHAPISHWA KATIKA LUGHA 59 KOTE DUNIANI K Kiu Cha umtafuta Mungu Huduma ya Daktari Richard A. Bennett ilianza katika mabaraza ya miji. Akiwa mwanafunzi chuoni, alikumbana na
More informationMUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.
MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO. MUHTASARI WA UTANGULIZI WA THIOLOGIA YA USHIRIKA WA NAFSI TATU ZA UUNGU. GRACE COMMUNION INTERNATIONAL LIVING AND SHARING THE GOSPEL MUNGU ANADHIHIRISHWA NA
More informationMACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI
This booklet on Becoming a Parent was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at. MACHAGUO
More information# 18 Uponyaji Kutokana na Kukataliwa
119 Uponyaji Kutokana na Kukataliwa Kukataliwa ni mojawapo ya mitindo ya Shetani ya ukandamizaji. Kukataliwa kunaweza kumzuia mwenye dhambi kumjia Mungu ili apate wokovu na kumzuia Mkristo kuufikia uwezo
More informationNordic Journal of African Studies 23(4): (2014)
Nordic Journal of African Studies 23(4): 292 306 (2014) Fani za Fasihi Zinazoibua Fantasia Katika Hadithi za Watoto za Nyambura Mpesha Janice Mwikali MUTUA Egerton University, Kenya & Chai FURAHA Egerton
More informationN09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q
N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q 88092387 SWAHILI B HIGHER LEVEL PAPER 1 SOUAHÉLI B NIVEAU SUPÉRIEUR ÉPREUVE 1 SUAHILI B NIVEL SUPERIOR PRUEBA 1 Tuesday 3 November 2009 (morning) Mardi 3 novembre 2009 (matin)
More informationUfunguo wa Kutaalamika Haraka
0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11
More informationUJAGINA WA MWANAMKE KATIKA PANGO
UJAGINA WA MWANAMKE KATIKA PANGO NA MUNIU GEORGE GITHUCI C50/65581/2011 TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA KISWAHILI NOVEMBER
More informationMutugi Kamundi. Jemma Kahn. Kiswahili. Demane na pacha wake. Author - South African Folktale
You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way: Demane na pacha wake Author - South African Folktale Adaptation -
More informationJifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti
Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu
More informationAdhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu
Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu Nabii Musa alipotoka mlima Sinai kupewa amri kumi za Mungu zilizoko kwenye kitabu cha Kutoka 20:1 17, Mungu alimpa na sharia zingine ambazo lengo lake
More informationJHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI
JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika
More informationSANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO
KISWAHILI 5 SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO YALIYOMO YALIYOMO UTANGULIZI iii iv SURA YA KWANZA : FASIHI. 1 SURA YA PILI : TAMATHALI
More informationKUCHUNGUZA MCHOMOZO KATIKA FASIHI YA KISWAHILI: UTAFITI LINGANISHI WA USHAIRI KATIKA DIWANI YA USTADHI ANDANENGA
KUCHUNGUZA MCHOMOZO KATIKA FASIHI YA KISWAHILI: UTAFITI LINGANISHI WA USHAIRI KATIKA DIWANI YA USTADHI ANDANENGA AUGUSTINO TENDWA TASNIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SHARTI PEKEE LA KUTUNUKIWA
More informationFANI KATIKA NYIMBO TEULE ZA ANASTACIA MUKABWA MBURU JAMES MUNGAI TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA
FANI KATIKA NYIMBO TEULE ZA ANASTACIA MUKABWA MBURU JAMES MUNGAI TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI (M.A.) KATIKA IDARA YA KISWAHILI CHUO KIKUU CHA NAIROBI 2014
More informationUshindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT
Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT 1 Ushindi Ndani ya Kristo Na W. W. Prescott Mfasiri: M. Mwamalumbili Victory in Christ - Kiswahili 2 Yaliyomo Alinipenda Mimi Aliishi kwa ajili Yangu Mimi Alikufa
More informationHaja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (
Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Haja Ya Dini Haja Ya Dini Author(s): Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi [3] Publisher(s): Bilal Muslim Mission of Tanzania [4] Katika kijitabu
More informationKUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA
KUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA BIBIANA MASSAWE AMBROSE TASINIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SHARTI PEKEE LA KUTUNUKIWA DIGRII
More informationPDF created with pdffactory trial version
المملكة العربية السعودية وزارة التعليم العالي الجامعة الا سلامية بالمدينة المنورة عمادة البحث العلمي قسم الترجمة تعريف موجز بالا سلام بل( لغة السواحلية) ١ بسم االله الرحمن الرحیم MAELEZO KWA UFUPI KUHUSU
More informationTora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA
SOMO LA KWANZA UTANGULIZI KWA TORA For videos, study guides and other resources, visit Third Millennium Ministries at thirdmill.org. 2014 nathird Millennium Ministries Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu
More informationUFASIHI SIMULIZI KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: Mifano kutoka Adili na Nduguze na Wasifu wa Siti Binti Saad. Khatib Khamis Saleh
UFASIHI SIMULIZI KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: Mifano kutoka Adili na Nduguze na Wasifu wa Siti Binti Saad Khatib Khamis Saleh Tasinifu ya Uzamili Katika Kiswahili Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Septemba,
More informationJAZANDA YA NJOZI KATIKA BAADHI YA MASHAIRI YA EUPHRASE KEZILAHABI (ONEIRIC IMAGES IN EUPHRASE KEZILAHABI S SELECTED POEMS) 1
SWAHILI FORUM 11 (2004): 69-73 JAZANDA YA NJOZI KATIKA BAADHI YA MASHAIRI YA EUPHRASE KEZILAHABI (ONEIRIC IMAGES IN EUPHRASE KEZILAHABI S SELECTED POEMS) 1 GRAZIELLA ACQUAVIVA This article is based upon
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationK. M a r k s, F. E n g e l s
W a (any a kazi wa nchi zote, unganeni! K. M a r k s, F. E n g e l s Maelezo ya chama cha kikomunist Idara ya Maendcleo Moscow Tafsiri hii ya "Maelezo ya Chama cha Kikomunist" inatokana na maandishi
More informationCHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA KISWAHILI MAMLAKA NA ITIKADI KATIKA NYIMBO TEULE ZA TAARAB
CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA KISWAHILI MAMLAKA NA ITIKADI KATIKA NYIMBO TEULE ZA TAARAB TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA CHUO KIKUU CHA NAIROBI NOVEMBA
More informationNAFASI YA MUZIKI ULIOPENDWA KATIKA FASIID YA KISWAHILI PAMELA M. Y NGUGI. Inkisiri. M a kala. AAP 64 (2000): Swahili Forum VII
AAP 64 (2000): Swahili Forum VII 145-152 NAFASI YA MUZIKI ULIOPENDWA KATIKA FASIID YA KISWAHILI PAMELA M. Y NGUGI Inkisiri Nyimbo, kama tanzu ya fasihi yeyote ile zina majukumu mbalimbali ambayo hutekeleza
More informationNa Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4
;II. -~ ~.! ~ l Na Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4 ~n.~ SURA YA KWANZA SHERIA YA ARDHI 1 UTANGULIZI Sura hii itaiangalia ARDHI na umuhimu wake katika maisha ya binadamu. Ardhi ni rasilimali
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationKiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika
Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to
More informationHakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn
TAFSIRI YA BIBLIA Mwandishi Jonathan M. Menn B.A., University of Wisconsin-Madison, 1974 J.D., Cornell Law School, 1977 M.Div., Trinity Evangelical Divinity School, 2007 Equipping Church Leaders-East Africa
More informationNdugu na dada zangu wapendwa,
UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2014 Na Rais Thomas S. Monson Upendo Asili ya Injili Hakika hatuwezi kumpenda Mungu kama hatuwapendi wasafiri wenzetu katika safari hii ya maisha duniani. ninafurahia mawazo
More informationNAFASI YA MWANAMKE: JINSI INAVYOTETEWA KATIKA NYIMBO ZA TAARAB ZA ZANZIBAR ELIZABETH KANGOGO YEGO C50/68796/2011 IDARA YA ISIMU NA LUGHA
NAFASI YA MWANAMKE: JINSI INAVYOTETEWA KATIKA NYIMBO ZA TAARAB ZA ZANZIBAR ELIZABETH KANGOGO YEGO C50/68796/2011 IDARA YA ISIMU NA LUGHA CHUO KIKUU CHA NAIROBI TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI
More informationTufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue?
Tufundishane! Let s teach each other! This newsletter is published by The Foundation for Tomorrow and is meant to be a venue for teachers and schools to share and learn from each other s best practices.
More informationUJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI
Toleo 14 BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI Hazina ya maelezo kutoka
More informationMafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally
Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo Na Andrew Connally 1 YALIYOMO Milango ya Kitabu: Ukurasa: 1. Mungu-Kuwako kwake na hali yake 03 2. Huyo Kristo-Nafsi yake na kazi yake 12 3. Maandiko Matakatifu ni yenye
More informationDeutsche Welle, Learning by Ear 2009 Seite 1 People Who Make A Difference Liberia: Anita Varney Health Facilitator, Fishtown/Liberia
Deutsche Welle, Learning by Ear 2009 Seite 1 Title: Anita Varney Health Facilitator, Fishtown/Liberia Author: Stefanie Duckstein, HA Afrika/ Nahost Editor: Christine Harjes Translator: Tony Dunham Sound
More information(Hati ya kuhitimu kisomo cha sekondari Kenya (K.C.S.E)
JINA. NAMBARI YAKO SHULE...TAREHE.. SAHIHI.. 102/2 KISWAHILI KARATASI YA 2 UFAHAMU, UFUPISHO, MATUMIZI YA LUGHA NA ISIMU JAMII MUDA: SAA 2 ½ (Hati ya kuhitimu kisomo cha sekondari Kenya (K.C.S.E) MAAGIZO
More informationMITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012
MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012 TASNIFU HII IMEWASILISHWA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI
More informationUFAHAMU NAME INDEX SCHOOLDATE UFAHAMU
NAME INDEX SCHOOLDATE 1. 1995 1. UFAHAMU UFAHAMU Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali Ama kweli maisha ya vijana wa kisasa yanatofautiana na kuhitilafiana pakubwa na yale ya wazee wao. Sio katika
More informationUponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14).
41 Uponyaji Wa Laana Ijapokuwa baraka ni kinyume cha laana, kuna mambo yanayofanana katika vitu hivyo. Ni maneno yaliyotajwa, yaliyoamriwa, au kuandikwa katika Biblia kwa nguvu na mamlakao ya kiroh kwa
More informationMUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI
MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Mwanzo 1:1 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi. Wakolosai
More informationShabaha ya Mazungumzo haya
Karibu Katika Mazungumzo Kuhusu Mchakato wa Uhamasishaji Maendeleo ya Kanisa na Jamii CCMP/UMOJA Shabaha ya Mazungumzo haya Kuwafahamisha viongozi wa makanisa kuhusu Mchakato wa CCMP ambao umekuwa ukitumika
More informationTAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA
TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0
More informationWanawake katika Uislamu
Wanawake katika Uislamu Ukilinganisha na Wanawake katika Mafundisho ya Kiyahudi-Kikristo: Hadithi za kubuni na uhakika DR. SHERIF ABDEL AZIM Ph.D. - QUEENS UNIVERSITY, KINGSTON, ONTARIO, CANADA Yaliyomo
More informationTASFIDA KAMA MKAKATI WA UPOLE: UWIANO WA TASFIDA ZA KISWAHILI NA EKEGUSII
TASFIDA KAMA MKAKATI WA UPOLE: UWIANO WA TASFIDA ZA KISWAHILI NA EKEGUSII NA FLORAH N. OMOSA C50/84117/2012 TASNIFU HII IMETOLEWA KWA MADHUMUNI YA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJIYA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA
More informationPronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:
More informationMwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo
Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu Nyenzo ya Mafunzo Vi Agroforestry Vi Agroforestry ni shirika la ushirikiano la maendeleo la Sweden, linalopambana dhidi ya umasikini na
More informationKUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA
KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa
More informationMARUDIO K.C.S.E KNEC KISWAHILI KARATASI 102/2 MASWALI NA USAHIHISHO
102 1B KISWAHILI KARATASI 1B OCT/ NOV 1995 2 ½ HOURS Jibu maswali yote MARUDIO K.C.S.E KNEC 1995 2010 KISWAHILI KARATASI 102/2 MASWALI NA USAHIHISHO 1. UFAHAMU Soma Makala yatuatayo kisha ujibu maswali
More informationwasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWENYE IBADA YA KUWEKWA WAKFU NA KUINGIZWA KAZINI ASKOFU MARTIN FATAELI SHAO WA DAYOSISI YA KASKAZINI YA KANISA LA
More informationElimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi
Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau
More informationKufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007
Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna
More informationRoho Mtakatifu Ni Nini?
Roho Mtakatifu Ni Nini? kwa ajili ya mkutano. Mkutano huu utakuwa tofauti, kidogo na ile ya kawaida tunayokuwa nayo hapa. Kwa kawaida, kila wakati tunapokuja pamoja hapa, ni mkutano kwa wa kwa ajili ya
More informationV\ FANI KATIKA USHAIRI WA HASSAN MWALIMU MBEGA: UHAKIKI WA UPISHO WA UMALENGA NA DAFINA YA UMALENGA DONALD OMWOYO OSIEMO
gftgff AROGAHA COLLECTION MADA: V\ FANI KATIKA USHAIRI WA HASSAN MWALIMU MBEGA: UHAKIKI WA UPISHO WA UMALENGA NA DAFINA YA UMALENGA NA: DONALD OMWOYO OSIEMO TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI
More informationKISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA
KISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA Maagizo (a) Andika jina lako na namba yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu. (b) Tia sahihi yako na tarehe ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu. (c) Jibu maswali
More informationUsimulizi katika Utenzi wa Swifa ya Nguvumali
73 Rosemary N. Burundi, Mwenda Mukuthuria na Enock S. Matundura Ikisiri Makala haya yanachunguza usimulizi katika Utenzi wa Swifa ya Nguvumali uliotungwa na Hassan bin Ismail. Yanachunguza jinsi fani ya
More informationKutetea Haki za Binadamu
Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and
More informationMATATIZO YA MWANAMKE KATIKA KIDAGAA KIMEMWOZEA NA NYUSO ZA MWANAMKE. MONICA C RUTO
MATATIZO YA MWANAMKE KATIKA KIDAGAA KIMEMWOZEA NA NYUSO ZA MWANAMKE. NA MONICA C RUTO TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA CHUO KIKUU CHA NAIROBI. 2015
More informationElimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi
Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Gervas Zombwe 1 1. Utangulizi Katika mazingira ya kawaida kabisa ndani ya jamii yetu, Imezoeleka kusikia au kuona watu wakioanisha dhana ya elimu
More informationMADA MATUMIZI YA TAKRIRI NA SITIARI KATIKA UTENZI WA RASI LGHULI JUSTUS MAUNDU NDUMBU C50/65902/2011 CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA ISIMU NA LUGHA
MADA MATUMIZI YA TAKRIRI NA SITIARI KATIKA UTENZI WA RASI LGHULI NA JUSTUS MAUNDU NDUMBU C50/65902/2011 CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA ISIMU NA LUGHA TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI
More informationUTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha
UTARATIBU WA KANISA Tumemaliza hivi punde ule mkutano mkubwa wa siku, tano usiku kwenye Maskani, ambapo, kwa neema ya Mungu na kwa msaada Wake, nimejaribu sana, kwa Maandiko, kuliweka Kanisa la Bwana Yesu
More informationMukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika
Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika (A Summary Of Arguments For And Against Individual Communion Cups) Na J D Logan Communion Cups) 1 Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi
More informationUpekee wa Utenzi wa Swifa ya Nguvumali: Utenzi wa Mpito, Mseto wa Imani za Jadi Na Usasa MWENDA MUKUTHURIA Egerton University, Kenya
Nordic Journal of African Studies 16(3): 298 319 (2007) Upekee wa Utenzi wa Swifa ya Nguvumali: Utenzi wa Mpito, Mseto wa Imani za Jadi Na Usasa MWENDA MUKUTHURIA Egerton University, Kenya ABSTRACT Nguvumali
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More informationKUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini
More informationWaandishi: wa Toleo la 5. Scholastica Jullu Athanasia A. Soka Safina Hassan Mary Njau. Toleo la 5: 2008 ISBN
KIONGOZI CHA SHERIA Hakimiliki 2008 Kimetolewa na: Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) Waandishi: wa Toleo la 5 Scholastica Jullu Athanasia A. Soka Safina Hassan Mary Njau Toleo la 5: 2008 ISBN
More informationSautiElimu. Sauti Yako Isikike
SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian
More informationHatari, Haki za Usalama katika Bahari 03
Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03 AEG swahili Bahari ya Aegean Brosha ya maelezo hii ni kwa watu wanaofikiria kuvuka bahari ya Aegean kati ya Ugiriki na Uturuki.Kuvuka kihramu ni uhalifu katika
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More informationElimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...
Elimu Bora, lakini... Shukrani za dhati kwa wote waliotusaidia katika kutayarisha kijitabu hiki: Nsa Kaisi, Mshauri wa Rais, kwa mchango wake mkubwa wa mawazo Wafanyakazi wote wa HakiElimu 2003-2004 Many
More informationCONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC)
CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, SIGOR CONSTITUENCY, AT KIBICHBICH D.O. S OFFICE 2 ON Monday 1 st July 2002 CONSTITUENCY PUBLIC HEARING SIGOR
More informationJE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?
JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? JOE CREWS 1 JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? Na Joe Crews (Hotuba Na. 16 ya Mambo ya Kweli Yanayoshangaza) Mfasiri: M. Mwamalumbili Is It Possible To
More informationMhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, KWENYE SHEREHE YA KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA, TAREHE 08 JUNI 2008, MSIMBAZI CENTRE, DAR ES SALAAM Mhashamu
More informationRISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO
RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO 1 RISALA FUPI copyright Hidaya Creativity, publishing Department. P.O. BOX 44799, 00100, GPO, NAIROBI-KENYA. Haki
More informationLUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI
LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI SIKOMBE YIZUKANJI YORADI TASNIFU YA KISWAHILI KWA MINAJILI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (MA. KISWAHILI) KITIVO CHA SANAA
More informationYaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!
Yaliyomo Kuhusu kitabu hiki Kuhusu kitabu hiki.........................................................1 Unapojisikia vibaya.........................................................2 Unapoanza kuwa mzima
More informationKimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:
Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200
More informationMAKALA: USHAIRI WA KISWAHILI KATIKA NJIA PANDA: KUTUMIA AU KUTOTUMIA METHALI
MAKALA: USHAIRI WA KISWAHILI KATIKA NJIA PANDA: KUTUMIA AU KUTOTUMIA METHALI Na Joseph Nyehita Maitaria Mwanafunzi wa Ph.D Idara ya Kiswahili na Lugha za Kiafrika Chuo Kikuu cha Kenyatta Ikisiri Makala
More informationMisamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?
Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.
More informationKUCHUNGUZA UFASIHI SIMULIZI UNAOJITOKEZA NDANI YA HADITHI ZA KUSADIKIKA NA ADILI NA NDUGUZE
KUCHUNGUZA UFASIHI SIMULIZI UNAOJITOKEZA NDANI YA HADITHI ZA KUSADIKIKA NA ADILI NA NDUGUZE MUHAMMED ALI SALIM TASINIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SEHEMU YA MASHARTI YA KUTUNIKIWA SHAHADA YA
More information