Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele. Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? UKURASA WA 12 NYIMBO: 97, 101. Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana

Size: px
Start display at page:

Download "Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele. Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? UKURASA WA 12 NYIMBO: 97, 101. Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana"

Transcription

1 JANUARI 15, MAKALA ZA FUNZO MACHI 3-9 Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele UKURASA WA 7 NYIMBO: 106, 46 MACHI Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? UKURASA WA 12 NYIMBO: 97, 101 MACHI Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana UKURASA WA 17 NYIMBO: 41, 89 MACHI Kumtumikia Yehova Kabla Siku Zenye Msiba Hazijaja UKURASA WA 22 NYIMBO: 54, 17 MACHI 31 APRILI 6 Ufalme Wako na Uje Lakini Utakuja Lini? UKURASA WA 27 NYIMBO: 108, 30

2 MAKALA ZA FUNZO UKRAINIA JALADA: Kuwahubiria wanafunzi wa chuo kikuu katika jiji la Lviv wanaotoka nchi nyingine IDADI YA WATU 45,561,000 WAHUBIRI 150,887 Kuna makutaniko 1,737 na vikundi 373 vya lugha 15, kutia ndani Kihungaria, Kiromania, Lugha ya Ishara ya Urusi, na Kiukrania PIA KATIKA TOLEO HILI ˇ Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele Makala hii itathibitisha kwamba Yehova amekuwa Mfalme sikuzote na itaonyesha jinsi ambavyo ametumia mamlaka yake juu ya viumbe wake mbinguni na duniani. Makala hii pia itatuchochea kuiga mifano ya watu wa kale walioamua kumwabudu Yehova, Mfalme wa umilele. ˇ Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? Makala hii itatusaidia kuthamini zaidi mambo yaliyotimizwa na Ufalme wa Kimasihi katika miaka 100 ya kwanza ya utawala wake. Itamtia moyo kila mmoja wetu kuwa raia mshikamanifu wa Ufalme, na itatusaidia kutafakari kuhusu maana kamili ya andiko letu la mwaka wa ˇ ˇ Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana Kumtumikia Yehova Kabla Siku Zenye Msiba Hazijaja Nitayatumiaje maisha yangu? Hilo ni swali muhimu kwa yeyote aliyejiweka wakfu kwa Yehova. Katika makala hizi, tutazungumzia kanuni zinazoweza kuwaongoza vijana Wakristo kumtumikia Mungu kikamili, na nafasi ambazo Wakristo waliozeeka wanazo za kupanua huduma yao. 3 Walijitoa Wenyewe kwa Hiari Afrika Magharibi 32 Uamuzi Niliofanya Utotoni ˇ Ufalme Wako na Uje Lakini Utakuja Lini? Leo, watu wengi wanakengeushwa na hali za ulimwengu au kwa kufuatia mapendezi yao wenyewe. Makala hii inazungumzia mambo matatu yanayowasaidia Wakristo kuwa na hakika kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utakomesha mfumo huu mwovu January 15, 2014 Vol. 135, No. 2 Semimonthly SWAHILI Gazeti hili haliuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu ya Biblia ya ulimwenguni pote inayotegemezwa kwa michango ya hiari. Isipokuwa iwe imeonyeshwa vingine, Maandiko yamenukuliwa kutoka katika Biblia Takatifu Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. The Watchtower (ISSN ) is published semimonthly by Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.; L. Weaver, Jr., President; G. F. Simonis, Secretary-Treasurer; 25 Columbia Heights, Brooklyn, NY , and by Watch Tower Bible and Tract Society of South Africa NPC, 1 Robert Broom Drive East, Rangeview, Krugersdorp, Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Printed in South Africa.

3 WALIJITOA WENYEWE KWA HIARI Afrika Magharibi PASCAL, aliyelelewa katika kijiji cha watu maskini nchini Cote ˆ d Ivoire, alitamani sana kuishi maisha bora. Akiwa mwanandondi asiye na uzoefu, alijiuliza hivi: Nitafanya nini ili niwe mashuhuri na kuwa tajiri? Alipokuwa na umri wa miaka 20 hivi, aliamua kuhamia Ulaya ili atimize mradi wake. Lakini alitaka kuingia Ulaya kwa njia isiyo halali kwa sababu hakuwa na hati za kusafiri. Katika mwaka wa 1998, akiwa na umri wa miaka 27, Pascal alianza safari yake. Alivuka mpaka na kuingia nchini Ghana, akasafiri hadi Togo na kuingia Benin, na hatimaye akafika kwenye mji wa Birni Nkonni huko Niger. Sehemu iliyobaki ya safari yake ilikuwa hatari zaidi. Ili kufika upande wa kaskazini, angehitaji kusafiri kwa lori na kuvuka Jangwa la Sahara. Kisha, angehitaji kusafiri kwa mashua hadi Ulaya kupitia bahari ya Mediterania. Huo ndio uliokuwa mpango Pascal anayetumika nchini Niger wake, lakini mambo mawili yalimzuia kuondoka nchini Niger. Kwanza, pesa zake ziliisha. Pili, alikutana na No e, painia aliyeanza kumfundisha Biblia. Mambo aliyojifunza yalimgusa moyo sana na kumfanya abadili maoni yake kuhusu maisha. Alianza kufuatilia miradi ya kiroho badala ya miradi ya kimwili. Pascal alibatizwa mnamo Desemba Ili kumshukuru Yehova, alianza kutumikia akiwa painia mwaka wa 2001 nchini Niger, katika mji alikojifunzia kweli. Anahisije kuhusu utumishi wake? Anasema hivi kwa uchangamfu: Sasa nina maisha bora kabisa! KUISHI MAISHA BORA BARANI AFRIKA Kama Pascal, wengi wametambua kwamba kufuatilia miradi ya kiroho huleta uradhi zaidi maishani. Ili kufikia miradi hiyo, wengine wamehamia Afrika kutoka Ulaya ili kutumika katika maeneo yenye uhitaji mkubwa zaidi wa wahubiri wa Ufalme. Kwa kweli, Mashahidi 65 hivi kutoka Ulaya walio na umri wa kati ya miaka 17 na 70 wamehamia maeneo yenye uhitaji mkubwa wa wahubiri huko Afrika Magharibi katika nchi ya Benin, Burkina Faso, Niger, na Togo. Ni nini kilichowachochea kufanya uamuzi huo mzito, na matokeo yamekuwa nini? Anne-Rakel kutoka Denmark anasimulia hivi: Wazazi wangu walikuwa wamishonari nchini Senegal. Kila mara walisimulia kwa msisimuko kuhusu maisha ya umishonari hivi kwamba nikatamani kuwa na maisha kama hayo. Miaka 15 hivi iliyopita, Anne-Rakel alipokuwa na umri wa miaka 20 hivi alihamia Togo anakotumikia katika kutaniko la lugha ya ishara. Kufanya hivyo kumewachocheaje wengine? Anasema hivi: Baadaye ndugu na dada yangu mdogo walijiunga nami nchini Togo. Ofisi ya tawi ya Benin husimamia kazi katika nchi hizo nne zinazotumia lugha ya Kifaransa. 3

4 Aurele, ndugu aliyeoa mwenye umri wa miaka 70 kutoka Ufaransa anasema hivi: Nilipostaafu miaka mitano iliyopita, nilihitaji kuamua ama kuishi maisha matulivu nchini Ufaransa nikisubiri Paradiso au kupanua huduma yangu. Aurele aliamua kupanua huduma yake. Miaka mitatu hivi iliyopita, yeye na mke wake, Albert- Fayette, walihamia Benin. Aurele anasema hivi: Kujitolea kumtumikia Yehova katika eneo hili ndio uamuzi bora zaidi tuliowahi kufanya. Anaongezea hivi huku akitabasamu: Sehemu fulani za pwani tunazohubiri zinanikumbusha kuhusu Paradiso. Clodomir na mke wake, Lysiane, walihamia Benin kutoka Ufaransa miaka 16 iliyopita. Mwanzoni, walitamani sana kurudi Ufaransa ili kuona familia na marafiki wao, na walikuwa na wasiwasi kwamba hawangeweza kuishi Benin. Hata hivyo, hawakuwa na sababu ya kuwa na wasiwasi. Walipata shangwe nyingi. Clodomir anasema hivi: Kwa miaka 16, tumekuwa na pendeleo la kumsaidia angalau mtu mmoja kila mwaka kukubali kweli. S ebastien na Johanna, wenzi wa ndoa kutoka Ufaransa walihamia Benin mwaka wa S ebastien anasema hivi: Kuna mengi sana ya kufanya kutanikoni. Ni kama tunazoezwa mambo mengi sana ya kitheokrasi kwa muda mfupi! Watu wanaitikiaje katika huduma? Johanna anasema hivi: Watu wana kiu ya kujifunza kweli. Hata tunapokuwa katika shughuli zetu za kibinafsi, watu hutusimamisha njiani na kuuliza maswali ya Biblia na kuchukua machapisho yetu. Kuhama kumeisaidiaje ndoa yao? S ebastien anasema hivi: Kumeimarisha ndoa yetu. Ninafurahia sana kuhubiri siku nzima na mke wangu. Eric na mke wake, Katy, wanafanya upainia katika eneo lenye watu wachache kaskazini mwa Benin. Walipoishi Ufaransa miaka kumi hivi iliyopita, walianza kusoma makala kuhusu kutumikia katika maeneo yenye uhitaji mkubwa zaidi na kuzungumza na watumishi wa wakati wote. Hilo liliwachochea kuhamia nchi nyingine katika mwaka wa Walitiwa moyo sana walipoona ongezeko. Eric anasema hivi: Miaka miwili iliyopita, kikundi chetu katika mji wa Tangui eta kilikuwa na wahubiri 9; sasa wamefika 30. Watu 50 hadi 80 huhudhuria mikutano siku ya Jumapili. Ni shangwe iliyoje kuona ongezeko hilo kubwa! TAMBUA NA USHINDE CHANGAMOTO Baadhi ya ndugu na dada waliohamia maeneo yenye uhitaji mkubwa zaidi wa wahubiri walikabili changamoto gani? Benjamin, mwenye umri wa miaka 33, ni Jinsi ya Kuwazoeza Wengine Pascal, painia na mzee wa kutaniko kutoka Ufaransa, ametumika nchini Benin kwa miaka zaidi ya 12. Anasema hivi: Ni baraka kuona ndugu na dada wakifanya maendeleo ya kiroho. Amewasaidiaje baadhi yao kufanya maendeleo? Ninatumia mbinu tofauti kumzoeza kila mmoja wao. Nilijifunza kutoka kwa ndugu wenyeji jinsi ya kuwafikia na kuwasalimu watu katika huduma. Wengine walijifunza nini kutoka kwangu? Kuandika mambo fulani kuhusu wanaopendezwa. Mitaa mingi haina majina, na nyumba hazina nambari. Wahubiri fulani hawakuwa wakiandika chochote na hivyo hawakuwarudia watu wote waliopendezwa. Niliwaonyesha jinsi kuandika mambo machache tu kuhusu tunaowahubiria kunavyotusaidia kukumbuka watu wanaopendezwa na mahali wanapoishi na hivyo kutuchochea kuwarudia. Huku, watu hujifunza mambo kwa kusikiliza. Wanajifunza lugha kadhaa bila kutumia kitabu cha lugha, lakini wengi wao hawajui kusoma vizuri. Niliwazoeza ndugu kadhaa vijana kusoma kwa sauti. Kadiri walivyofanya maendeleo, ndivyo walivyofurahia zaidi kusoma. Kisha niliwaonyesha jinsi ya kufanya utafiti. Walifanya maendeleo baada ya muda mfupi na kuwekwa rasmi kuwa watumishi wa huduma.

5 (1) Albert-Fayette na Aurele (2) Anne-Rakel (3) Lysiane na Clodomir wakiwa na baadhi ya watu waliowasaidia kujifunza kweli (4) Marie-Th er ese ` (5) Benjamin kaka ya Anne-Rakel. Alipokuwa nchini Denmark mwaka wa 2000, alikutana na mmishonari aliyetumika nchini Togo. Benjamin anakumbuka hivi: Nilipomwambia mmishonari huyo kwamba nilitaka kuwa painia, alisema: Unaweza kuwa painia nchini Togo. Benjamin alifikiria jambo hilo. Anasema: Wakati huo, sikuwa nimefikisha umri wa miaka 20, lakini dada zangu wawili tayari walikuwa wakitumika nchini Togo. Basi, ilikuwa rahisi zaidi kwangu kuhamia huko. Kwa hiyo, akahama. Hata hivyo, alikabili changamoto fulani. Benjamin anasema hivi: Sikujua neno hata moja la Kifaransa. Hali ilikuwa ngumu miezi sita ya kwanza kwa sababu sikuweza kuwasiliana na watu. Hata hivyo, baadaye alifanya maendeleo. Benjamin sasa anafanya kazi katika Betheli ya Benin, akisaidia katika idara ya kompyuta na kusafirisha machapisho. Eric na Katy, waliotajwa mwanzoni walitumika katika eneo la lugha ya kigeni nchini Ufaransa kabla ya kuhamia Benin. Afrika Magharibi ilitofautianaje na Ufaransa? Katy anasema: Haikuwa rahisi kupata nyumba nzuri. Kwa miezi kadhaa, tuliishi katika nyumba isiyokuwa na umeme wala maji ya bomba. Eric anaongezea hivi: Majirani walipiga muziki kwa sauti ya juu hadi usiku wa manane. Unahitaji subira na kuwa tayari kuishi katika mazingira ya aina hiyo. Wote wanakiri hivi: Shangwe ya kutumikia katika eneo lisilohubiriwa kwa ukawaida haiwezi kamwe kulinganishwa na matatizo yoyote yale. Michel na Marie-Agnes, ` wenzi wa ndoa wenye umri wa miaka karibu 60 kutoka Ufaransa walihamia Benin miaka mitano hivi iliyopita. Mwanzoni walikuwa na 4 5 wasiwasi. Michel anasema hivi: Baadhi ya watu walisema ni kana kwamba tuliketi kwenye toroli iliyosukumwa na mwanasarakasi juu ya kamba! Hatukuogopa kwa sababu tulijua kwamba Yehova ndiye aliyekuwa akisukuma toroli hiyo. Kwa hiyo, tulihama kwa sababu ya Yehova na kwa ajili yake. JINSI YA KUJITAYARISHA Wale walio na uzoefu wa kuhubiri maeneo yenye uhitaji mkubwa zaidi wanasema kwamba ni muhimu sana kujitayarisha kwa njia zifuatazo: Panga mapema. Jifunze kuishi chini ya hali mbalimbali. Usinunue vitu ambavyo hujapanga kuvinunua. Mtegemee Yehova. Luka 14: S ebastien, aliyetajwa mwanzoni anasema hivi: Kabla ya kuhama, mimi na Johanna tuliweka pesa akibani kwa miaka miwili. Hatukutumia pesa nyingi kwa ajili ya burudani wala hatukununua vitu tusivyohitaji. Wanafanya kazi barani Ulaya kwa miezi michache kila mwaka ili waweze kuendelea na upainia nchini Benin kwa miezi inayosalia. JANUARI 15,

6 Marie-Th er ese ` ni kati ya dada waseja 20 hivi kutoka nchi nyingine wanaotumikia katika maeneo yenye uhitaji mkubwa wa wahubiri huko Afrika Magharibi. Alikuwa dereva wa basi nchini Ufaransa; hata hivyo, katika mwaka wa 2006 alichukua likizo ya mwaka mmoja ili afanye upainia nchini Niger. Baada ya muda mfupi, aligundua kwamba hayo ndiyo maisha aliyotamani sana. Marie-Th er ese ` anasema: Baada ya kurudi Ufaransa, nilimwomba mwajiri wangu abadili ratiba yangu ya kazi, akakubali kuibadili. Kwa sasa, kuanzia Mei hadi Agosti, ninafanya kazi ya kuendesha basi nchini Ufaransa, kisha kuanzia Septemba hadi Aprili ninafanya upainia nchini Niger. Wale wanaoutafuta kwanza Ufalme wanaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atawaandalia vitu vingine vyote vya lazima. (Mt. 6:33) Kwa mfano: Fikiria kisa cha Saphira, dada mseja kutoka Ufaransa mwenye umri wa miaka karibu 30 anayefanya upainia nchini Benin. Alirudi Ufaransa mwaka wa 2011 kufanya kazi ili aweze kujitegemeza kwa mwaka mwingine (mwaka wake wa sita) barani Afrika. Saphira anasema hivi: Siku yangu ya mwisho kazini ilikuwa Ijumaa, lakini bado nilihitaji kufanya kazi siku kumi zaidi ili nipate pesa za kutosha kunitegemeza kwa mwaka mzima. Nilipaswa kuondoka Ufaransa baada ya majuma mawili tu. Nikasali kwa Yehova kuhusu hali yangu. Baada ya muda mfupi, kampuni inayowaajiri watu ilinipigia simu na kuniuliza ikiwa ningependa kumshikia mtu fulani kazi kwa majuma mawili. Siku ya Jumatatu, Saphira alienda kuzoezwa na mfanyakazi aliyepaswa kumshikia kazi kwa majuma hayo mawili. Anasema: Nilishangaa nilipojua kwamba ni dada Mkristo aliyehitaji likizo ya siku kumi ili ahudhurie Shule ya Utumishi wa Painia. Mwajiri wake alimwambia kwamba hangempa likizo ikiwa hawangepata mtu wa kufanya kazi yake. Dada huyo alimsihi sana Yehova amsaidie, kama nilivyokuwa nimefanya. CHANZO CHA URADHI WA KWELI Baadhi ya ndugu na dada wamehamia Afrika Magharibi na kuishi huko kwa miaka mingi. Wengine wametumika huko kwa miaka michache na kurudi katika nchi zao. Hata hivyo, bado wahubiri hao waliotumika katika maeneo yenye uhitaji mkubwa zaidi wananufaika na mambo waliyojifunza walipotumika katika maeneo hayo. Walijifunza kwamba kumtumikia Yehova huleta uradhi wa kweli maishani (6) Johanna na S ebastien (7) Katy na Eric (8) Marie-Agnes ` na Michel (9) Saphira 6

7 Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele Kwa Mfalme wa umilele... kuwe na heshima na utukufu milele. 1 TIM. 1:17. MFALME SOBHUZA WA PILI wa Swaziland alitawala kwa miaka 61 hivi. Hakuna mfalme mwingine yeyote katika siku zetu aliyewahi kutawala kwa kipindi kirefu hivyo. Hata ingawa tunavutiwa na urefu wa utawala wa Mfalme Sobhuza, kuna mfalme asiyeweza kufa. Kwa kweli, Biblia inasema kwamba yeye ni Mfalme wa umilele. (1 Tim. 1:17) Mtunga-zaburi mmoja alitaja jina la huyo Mwenye Enzi Kuu kwa kusema hivi: Yehova ni Mfalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele. Zab. 10:16. 2 Hakuna mwanadamu yeyote anayeweza kutawala kwa umilele kama Mungu. Hata hivyo, tunavutiwa hasa na njia ya Yehova ya kutawala. Mfalme aliyetawala taifa la kale la Israeli kwa miaka 40 alimsifu Mungu hivi: Yehova ni mwenye rehema na mwenye neema, si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa fadhili zenye upendo. Yehova amekifanya imara kiti chake cha ufalme mbinguni; nao ufalme wake mwenyewe umetawala juu ya kila kitu. (Zab. 103:8, 19) Yehova si Mfalme wetu tu bali pia ni Baba yetu wa mbinguni mwenye upendo. Hilo linatokeza maswali haya mawili: Yehova ni Baba katika njia gani? Yehova ametumiaje mamlaka yake akiwa Mfalme tangu uasi ulipotokea katika Edeni? Majibu ya maswali hayo yatatuchochea UNGEJIBUJE? Kwa nini tunavutiwa na njia ya Yehova ya kutawala? Yehova ameendeleaje kuonyesha kwamba anaipenda familia yake ya wanadamu? Ni nini kinachokuchochea kumwabudu Mfalme wa umilele? 1, 2. (a) Ni nani aliye Mfalme wa umilele, na kwa nini anastahili cheo hicho? (Tazama picha kwenye ukurasa huu.) (b) Kwa nini tunavutiwa na utawala wa Yehova? JANUARI 15,

8 kumkaribia zaidi Yehova na kumwabudu kwa moyo wetu wote. MFALME WA UMILELE AANZISHA FAMILIA YA ULIMWENGUNI POTE 3 Bila shaka, Yehova alifurahi sana alipomuumba Mwana wake mzaliwa-pekee! Mungu hakumtendea mzaliwa wake wa kwanza kana kwamba ni mtu wa hali ya chini. Badala yake, alimpenda kama Mwana na kushiriki naye shangwe ya kuumba viumbe wengine wakamilifu. (Kol. 1:15-17) Viumbe hao walitia ndani makumi ya maelfu ya malaika. Malaika hao wanaomtumikia Mungu kwa shangwe wanaitwa wahudumu wake, wanaofanya mapenzi yake, naye anawaheshimu kwa kuwaita wana. Wao ni sehemu ya familia ya Yehova ya ulimwenguni pote. Zab. 103:20-22; Ayu. 38:7. 4 Baada tu ya kuumba mbingu na dunia, Yehova alipanua familia yake ya ulimwenguni pote. Baada ya kuifanya dunia kuwa makao maridadi yanayodumu, Yehova alifikia upeo wa kazi zake duniani kwa kumuumba mwanadamu wa kwanza, Adamu, kwa mfano Wake mwenyewe. (Mwa. 1:26-28) Akiwa Muumba, Yehova alikuwa na haki ya kutarajia Adamu amtii. Akiwa Baba, Yehova alitoa maagizo yake yote kwa upendo na fadhili. Maagizo hayo hayakuwanyima uhuru isivyo lazima. Soma Mwanzo 2: Tofauti na wafalme wengi wanadamu, Yehova hufurahia kuwakabidhi raia wake mapendeleo akiwaona kuwa washiriki wa familia yake wanaotegemeka. Kwa mfano, alimpa Adamu mamlaka ya kutawala viumbe wengine na mgawo wenye kufurahisha usio rahisi wa kuwapa wanyama maji- 3. Ni nani aliyekuwa mshiriki wa kwanza wa familia ya Yehova ya ulimwenguni pote? Ni nani wengine walioumbwa wakiwa wana wa Mungu? 4. Wanadamu walikujaje kuwa sehemu ya familia ya Mungu ya ulimwenguni pote? 5. Mungu alifanya mpango gani ili dunia ijae watoto wake wa kibinadamu? na. (Mwa. 1:26; 2:19, 20) Mungu hakuumba mamilioni ya wanadamu wakamilifu ili kuijaza dunia. Badala yake, aliamua kumuumba Hawa, mwanamke mkamilifu ili awe kikamilisho cha Adamu. (Mwa. 2:21, 22) Kisha, akawapa wenzi hao pendeleo la kuzaa watoto na kuijaza dunia. Chini ya hali nzuri kabisa, wanadamu wangepanua mipaka ya Paradiso hatua kwa hatua ili ienee duniani pote. Wakiwa sehemu ya familia ya Yehova ya ulimwenguni pote, wangemwabudu milele kama malaika wanavyofanya mbinguni. Hilo lilikuwa tumaini zuri ajabu! Kwa kweli, Yehova aliwaonyesha upendo kama wa baba. WANA WAASI WAKATAA UTAWALA WA MUNGU 6 Inasikitisha kwamba Adamu na Hawa hawakumkubali Yehova kuwa Mwenye Enzi Kuu wao. Badala yake, walichagua kumfuata Shetani, mwana wa roho aliyemwasi Mungu. (Mwa. 3:1-6) Kuishi bila utawala wa Mungu kuliwaletea wao na watoto wao huzuni, kuteseka, na kifo. (Mwa. 3: 16-19; Rom. 5:12) Mungu hakuwa tena na raia waliomtii duniani. Je, hilo lilimaanisha kwamba alipoteza mamlaka yake juu ya dunia na wanadamu akiwa Mwenye Enzi Kuu? La hasha! Alitumia mamlaka yake kumfukuza Adamu na Hawa kutoka katika bustani ya Edeni, na ili kuwazuia wasirudi, aliweka makerubi kuilinda njia ya kuingia kwenye bustani. (Mwa. 3:23, 24) Wakati huohuo, Mungu alionyesha upendo wake akiwa Baba kwa kuahidi kwamba bado angetimiza kusudi lake la kuwa na familia ya ulimwenguni pote ya malaika na wanadamu waaminifu. Aliahidi kutokeza mzao atakayemwangamiza Shetani na kuondoa madhara ya dhambi ya Adamu. Soma Mwanzo 3: (a) Uasi ulianzaje katika familia ya Mungu? (b) Tunajuaje kwamba Yehova hakupoteza mamlaka yake baada ya uasi kutokea? 8 MNARA WA MLINZI

9 7 Katika karne zilizofuata, kuna watu waliochagua kuwa washikamanifu kwa Yehova, kama vile Abeli na Enoko. Hata hivyo, wanadamu wengi walimkataa Yehova aliyekuwa Mfalme na Baba yao. Kufikia siku za Noa, dunia ilikuwa imejaa jeuri. (Mwa. 6: 11) Je, hilo lilimaanisha kwamba Yehova alipoteza mamlaka yake juu ya dunia? Historia inaonyesha nini? 8 Fikiria simulizi linalomhusu Noa. Yehova alimpa maagizo hususa ya kujenga safina kubwa sana ambayo ingemwokoa Noa na familia yake. Pia, Mungu alionyesha kwamba anaipenda sana familia yake yote ya wanadamu alipomwagiza Noa awe mhubiri wa uadilifu. (2 Pet. 2:5) Bila shaka, Noa aliwasihi pia watu watubu na aliwaonya kuhusu uharibifu uliokuwa karibu, lakini hawakumsikiliza. Kwa miaka mingi, Noa na familia yake waliishi katika ulimwengu uliojaa jeuri na wenye maadili mapotovu sana. Akiwa Baba anayejali, Yehova aliwalinda na kuwabariki wanadamu hao wanane waliokuwa washikamanifu. Yehova alitumia mamlaka yake kuwahukumu wanadamu waasi na malaika waovu kwa kuleta Gharika juu ya dunia yote. Bila shaka, Yehova hakupoteza kamwe mamlaka yake. Mwa. 7: UTAWALA WA YEHOVA BAADA YA GHARIKA 9 Noa na familia yake walipotoka ndani ya safina na kupumua hewa safi katika dunia iliyosafishwa, bila shaka walimshukuru sana Yehova kutoka moyoni kwa kuwatunza na kuwalinda. Mara moja, Noa alijenga madhabahu na kumwabudu Yehova kwa kumtolea dhabihu. Mungu alimbariki Noa na familia yake na kuwaagiza wazae, wawe wengi na kuijaza dunia. (Mwa. 8:20 9:1) 7, 8. (a) Hali zilikuwa mbaya kadiri gani kufikia siku za Noa? (b) Yehova alichukua hatua gani ili kuisafisha dunia na kuilinda familia ya wanadamu? 9. Ni fursa gani ambayo Yehova aliwapa wanadamu baada ya Gharika? Kwa mara nyingine tena, wanadamu walikuwa na fursa ya kuungana katika ibada na kuijaza dunia. 10 Hata hivyo, Gharika haikuondoa hali ya kutokamilika, na wanadamu walihitaji kuendelea kupambana na uvutano usioonekana wa Shetani na malaika wengine waasi. Baada ya muda mfupi, uasi ulitokea dhidi ya utawala wa Yehova wenye upendo. Kwa mfano, Nimrodi, mwana wa mjukuu wa Noa, aliupinga vikali utawala wa Yehova. Nimrodi anaitwa mwindaji mwenye nguvu kwa kumpinga Yehova. Alijenga majiji makubwa kama vile Babeli, na kujiweka mwenyewe kuwa mfalme katika nchi ya Shinari. (Mwa. 10:8-12) Akiwa Mfalme wa umilele, Mungu alichukua hatua gani ya kumkomesha mfalme huyo mwasi na jitihada zake za kuzuia kusudi la Mungu la kuijaza dunia? Mungu alivuruga lugha yao, na kuwafanya wafuasi wa Nimrodi wasioelewana watawanyike juu ya uso wote wa dunia. Waliendelea kufuata ibada yao ya uwongo na mifumo ya wanadamu ya kutawala. Mwa. 11: Hata ingawa wengi waliabudu miungu ya uwongo baada ya Gharika, wanadamu fulani waaminifu waliendelea kumheshimu Yehova. Kwa mfano, Abrahamu alimtii Yehova kwa kuacha maisha ya starehe katika jiji la Uru na kuishi katika mahema kwa miaka mingi. (Mwa. 11:31; Ebr. 11: 8, 9) Abrahamu aliyekuwa akihama-hama, alizungukwa mara nyingi na wafalme walioishi katika majiji yaliyozingirwa na kuta. Hata hivyo, Yehova alimlinda Abrahamu na familia yake. Mtunga-zaburi alisema hivi kuhusu jinsi Yehova alivyowalinda akiwa Baba yao: [Mungu] hakuruhusu binadamu 10. (a) Uasi dhidi ya Yehova ulitokea wapi na wakati gani baada ya Gharika? (b) Yehova alichukua hatua gani ili kuhakikisha kwamba kusudi lake linatimia? 11. Yehova alionyeshaje ushikamanifu kwa Abrahamu rafiki yake? JANUARI 15,

10 Sikuzote Yehova ametumia mamlaka yake akiwa Mfalme (Tazama fungu la 6, 8, 10, 12, 17) Bustani ya Edeni Gharika ya siku za Noa 2370 K.W.K. Mnara wa Babeli Baada ya 2269 K.W.K. Bahari Nyekundu 1513 K.W.K. Yesu afufuliwa 33 W.K. yeyote awapunje, bali aliwakaripia wafalme kwa sababu yao. (Zab. 105:13, 14) Yehova alionyesha ushikamanifu kwa Abrahamu rafiki yake kwa kumwahidi hivi: Wafalme watatoka ndani yako. Mwa. 17:6; Yak. 2: Mungu alimwahidi pia Isaka, mwana wa Abrahamu, na Yakobo mjukuu wake, kwamba angewabariki na wazao wao wangekuwa wafalme. (Mwa. 26:3-5; 35:11) Hata hivyo, kabla ya wazao wa Yakobo kutokeza wafalme, walikuwa watumwa huko Misri. Je, hilo lilimaanisha kwamba Yehova hangetimiza ahadi yake au alikuwa amepoteza mamlaka yake juu ya dunia akiwa Mwenye Enzi Kuu? Hapana! Kwa wakati unaofaa, Yehova alimwonyesha Farao aliyekuwa mkaidi kwamba Yeye ni Mungu mwenye nguvu na Mwenye Enzi Kuu. Waisraeli waliokuwa utumwani walimtegemea Yehova, naye akawakomboa kwa njia ya pekee sana kwa kuwapitisha katikati ya Bahari Nyekundu. Bila shaka, Yehova bado alikuwa Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote, naakiwababaanayejali,alitumianguvu 12. Yehova alitumiaje mamlaka yake juu ya Misri? Na hilo lilikuwa na matokeo gani kwa watu wake? zake nyingi kuwalinda watu wake. Soma Kutoka 14:13, 14. YEHOVAAWAMFALMEWAISRAELI 13 Baada tu ya kukombolewa kimuujiza kutoka Misri, Waisraeli walimsifu Yehova kwa kumwimbia wimbo wa ushindi. Wimbo huo ulio katika Kutoka sura ya 15, unatia ndani maneno haya yaliyo katika mstari wa 18: Yehova atatawala akiwa mfalme mpaka wakati usio na kipimo, naam, milele. Kwa kweli, Yehova alikuwa Mfalme wa taifa hilo jipya. (Kum. 33:5) Hata hivyo, Waisraeli hawakuridhika kutawaliwa na Yehova, Mfalme wao asiyeonekana. Miaka 400 hivi baada ya kuondoka Misri, walimwomba Mungu awachagulie mfalme mwanadamu ili wawe kama jirani zao wapagani. (1 Sam. 8:5) Hata hivyo, bado Yehova alikuwa Mfalme na alionyesha hivyo waziwazi wakati wa utawala wa Daudi, mfalme wa pili wa Israeli. 14 Daudi alilileta sanduku takatifu la agano Yerusalemu. Wakati huo wa shangwe, Walawi waliimba wimbo wa sifa uliokuwa 13, 14. (a) Waisraeli walitangaza nini kuhusu ufalme wa Yehova walipoimba? (b) Mungu alimwahidi nini Daudi kuhusu ufalme wake? 10 MNARA WA MLINZI

11 na maneno ya pekee yaliyo katika 1 Mambo ya Nyakati 16:31: Semeni kati ya mataifa: Yehova amekuwa Mfalme! Huenda mtu akajiuliza hivi: Kwa kuwa Yehova ni Mfalme wa umilele, inawezekanaje kwamba alikuwa Mfalme wakati huo? Yehova huwa Mfalme anapotumia mamlaka yake au anapomweka mtu ili amwakilishe kwa kipindi fulani au ashughulikie hali fulani hususa. Ni muhimu sana kuelewa jambo hilo. Kabla Daudi hajafa, Yehova alimwahidi kwamba ufalme wake haungekuwa na mwisho. Alisema hivi: Nitainua uzao wako baada yako, ambao utatoka ndani ya viuno vyako; nami kwa kweli nitaufanya imara ufalme wake. (2 Sam. 7:12, 13) Hatimaye, uzao huo wa Daudi ulitokea zaidi ya miaka 1,000 baadaye. Mzao huyo alikuwa nani, na angekuwa Mfalme wakati gani? YEHOVA AMWEKA RASMI MFALME MPYA 15 Katika mwaka wa 29 W.K., Yohana Mbatizaji alianza kuhubiri kwamba ufalme wa mbinguni umekaribia. (Mt. 3:2) Yohana alipombatiza Yesu, Yehova alimtia mafuta Yesu kuwa Masihi aliyeahidiwa na Mfalme ambaye angetawala katika Ufalme wa Mungu. Akiwa Baba, Yehova alionyesha kwamba anampenda Yesu aliposema hivi: Huyu ni Mwanangu, mpendwa, ambaye nimemkubali. Mt. 3: Katika huduma yake yote, Yesu alimtukuza Baba yake. (Yoh. 17:4) Alifanya hivyo kwa kuhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu. (Luka 4:43) Hata aliwafundisha wafuasi wake wasali Ufalme huo uje. (Mt. 6:10) Yesu aliwaambia hivi watu waliompinga kwa sababu alikuwa Mfalme Aliyechaguliwa: Ufalme wa Mungu umo katikati yenu. (Luka 17:21) Baadaye, jioni ya mwisho kabla ya kifo chake, Yesu alifanya agano kwa ajili ya ufalme pamoja na wafuasi 15, 16. Yesu alitiwa mafuta wakati gani ili awe Mfalme? Yesu alipokuwa duniani alifanya mipango gani kwa ajili ya utawala wake? wake. Hivyo, akawapa baadhi ya wanafunzi wake waaminifu tumaini la kuwa wafalme pamoja naye katika Ufalme wa Mungu. Soma Luka 22: Yesu angeanza wakati gani kutawala akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu? Hangeanza kutawala mara moja. Siku iliyofuata wakati wa mchana, Yesu aliuawa na wafuasi wake wakatawanyika. (Yoh. 16:32) Hata hivyo, sawa na ilivyokuwa zamani, Yehova hakupoteza mamlaka yake. Mungu alimfufua Mwana wake siku ya tatu, na katika siku ya Pentekoste ya 33 W.K., Yesu alianzisha ufalme wa kiroho juu ya kutaniko la Kikristo la ndugu zake watiwa-mafuta. (Kol. 1: 13) Hata hivyo, Yesu alihitaji kusubiri ili apewe mamlaka kamili ya kifalme juu ya dunia akiwa uzao ulioahidiwa. Yehova alimwambia hivi Mwana wake: Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako. Zab. 110:1. MWABUDU MFALME WA UMILELE 18 Kwa maelfu ya miaka, utawala wa Yehova ulipingwa mbinguni na duniani. Yehova hakupoteza kamwe mamlaka yake akiwa Mwenye Enzi Kuu; aliendelea kutawala. Akiwa Baba mwenye upendo, aliwalinda na kuwatunza raia wake washikamanifu kama vile Noa, Abrahamu, na Daudi. Je, hilo halituchochei kujinyenyekeza kwa Mfalme wetu na kumkaribia zaidi? 19 Lakini huenda tukauliza: Yehova amekuwaje Mfalme leo? Tutaonyeshaje kwamba sisi ni raia washikamanifu wa Ufalme wa Yehova ili wakati ujao tuwe watoto wakamilifu katika familia yake ya ulimwenguni pote? Tunaposali Ufalme wa Mungu uje, tunamaanisha nini? Maswali hayo yatajibiwa katika makala inayofuata. 17. Yesu alianzaje kutumia kwa kadiri fulani mamlaka yake ya kifalme katika karne ya kwanza, lakini alihitaji kusubiri nini? 18, 19. Tunachochewa kufanya nini? Tutajifunza nini katika makala inayofuata? JANUARI 15,

12 Andiko letu la mwaka wa 2014 ni: Ufalme wako na uje. Mathayo 6:10 Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? Matendo yako ni makuu na ya ajabu, Yehova Mungu,... Mfalme wa umilele. UFU. 15:3. JE, UNAWEZA KUJIBU? Yehova alikuwaje Mfalme mwaka wa 1914? Ni baadhi ya mambo gani yaliyotimizwa na Ufalme mwanzoni? Yesu ametumiaje Ufalme wa Kimasihi kuwasafisha, kuwafundisha, na kuwapanga raia washikamanifu wa Mungu walio duniani? Sala yetu ya Ufalme wako na uje itajibiwa kikamili wakati gani, na hilo litamaanisha nini? ALIPOKUWA mlimani karibu na Kapernaumu wakati wa majira ya kuchipua ya mwaka wa 31 W.K., Yesu Kristo aliwafundisha wafuasi wake kusali hivi: Ufalme wako na uje. (Mt. 6:10) Watu wengi leo wana shaka ikiwa Ufalme huo utakuja. Hata hivyo, tuna hakika kwamba sala zetu za kutoka moyoni za kuomba Ufalme wa Mungu uje zitajibiwa. 2 Yehova atatumia Ufalme huo kuunganisha familia yake ya mbinguni na duniani. Kusudi hilo la Mungu litatimia. (Isa. 55:10, 11) Kwa kweli, Yehova tayari amekuwa Mfalme katika siku zetu! Mambo yenye kusisimua yaliyotukia katika miaka 100 iliyopita yanathibitisha hilo. Mungu anatenda mambo makuu na ya ajabu kwa ajili ya mamilioni ya raia wake washikamanifu. (Zek. 14:9; Ufu. 15:3) Hata hivyo, kuna tofauti kati ya Yehova kuwa Mfalme na kuja kwa Ufalme wa Mungu ambao Yesu alitufundisha kusali kuuhusu. Matukio hayo yanatofautianaje na yanatuhusuje? MFALME ALIYEWEKWA RASMI NA YEHOVA ACHUKUA HATUA 3 Mwishoni mwa karne ya 19, unabii huu wa Danieli ulioandikwa miaka 2,500 iliyopita ulianza kueleweka: Katika siku za wa- 1, 2. Ufalme wa Mungu utatimiza nini? Kwa nini tunaweza kuwa na hakika kwamba Ufalme huo utakuja? 3. (a) Yesu aliwekwa rasmi kuwa Mfalme wakati gani na wapi? (b) Unaweza kuthibitishaje kwamba Ufalme ulianza kutawala katika mwaka wa 1914? (Tazama maelezo ya chini.) 12 MNARA WA MLINZI

13 falme hao, Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. (Dan. 2:44) Kwa makumi ya miaka Wanafunzi wa Biblia waliendelea kusema kwamba mwaka wa 1914 ungekuwa wa muhimu. Watu wengi walitarajia hali nzuri. Mwandishi mmoja anasema hivi: Ulimwengu wa mwaka wa 1914 ulikuwa na tumaini na matarajio mengi mazuri. Hata hivyo, unabii wa Biblia ulitimia baada ya Vita vya Kwanza vya Ulimwengu kuanza mwaka huo. Kutokea kwa njaa, matetemeko ya nchi, tauni, na kutimia kwa unabii mwingine wa Biblia kulionyesha wazi kwamba Yesu Kristo alianza kutawala mbinguni akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu katika mwaka wa Alipomweka rasmi Mwana wake kuwa Mfalme wa Kimasihi, Yehova alianza kuwa Mfalme kwa njia mpya! 4 Mfalme mpya aliyewekwa rasmi na Mungu alianza kwa kupigana vita na Shetani, Adui mkuu wa Baba yake. Yesu na malaika zake waliwatupa Ibilisi na roho wake waovu kutoka mbinguni. Hilo lilileta shangwe kubwa mbinguni lakini msiba ambao haukuwa umewahi kutokea duniani. (Soma Ufunuo 12:7-9, 12.) Kisha, Mfalme akawaelekezea fikira raia wake walio duniani ili awasafishe, awafundishe, na kuwapanga kufanya mapenzi ya Mungu. Acheni tuone jinsi walivyotuwekea mfano mzuri kwa kutii utawala wa Ufalme katika mambo hayo matatu. MFALME WA KIMASIHI AWASAFISHA RAIA WAKE WASHIKAMANIFU 5 Baada ya Yesu kusafisha mbingu kwa kuondoa uvutano wote wenye kudhuru wa Tazama kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? ukurasa wa Mfalme mpya aliyewekwa rasmi alichukua hatua gani mara moja? Kisha aliwaelekezea nani fikira? 5. Ni kazi gani ya kutakasa iliyofanywa kati ya mwaka wa 1914 na mwanzoni mwa 1919? Shetani na roho waovu, Yehova alimwagiza Mfalme huyo akague na kuwasafisha kiroho wafuasi wake duniani. Nabii Malaki alisema kwamba walitakaswa kiroho. (Mal. 3:1-3) Historia inaonyesha kwamba jambo hilo lilitokea kati ya mwaka wa 1914 na mwanzoni mwa Ili tuwe sehemu ya familia ya ulimwenguni pote ya Yehova ni lazima tuwe safi, au watakatifu. (1 Pet. 1:15, 16) Ni lazima tuepuke kuchafuliwa kwa njia yoyote ile na dini ya uwongo au siasa za ulimwengu huu. 6 Kisha, Yesu alitumia mamlaka yake ya kifalme kumweka rasmi mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Mtumwa huyo angeandaa kwa ukawaida chakula cha kiroho cha kutosha kilicho bora kwa ajili ya wote walio sehemu ya kundi moja lililo chini ya uangalizi wa Yesu. (Mt. 24:45-47; Yoh. 10:16) Kuanzia mwaka wa 1919, kikundi kidogo cha ndugu watiwa-mafuta kimetimiza kwa ushikamanifu jukumu hilo zito la kulisha watumishi wa nyumbani. Chakula kingi cha kiroho kinachoandaliwa na kikundi hicho hutusaidia kukua katika imani. Kinaimarisha azimio letu la kuendelea kuwa safi kiroho, kiadili, kiakili, na kimwili. Pia, chakula hicho cha kiroho kinatufundisha na kutuwezesha kuwa na ustadi wa kushiriki kikamili katikakazi muhimu zaidi ya kuhubiri. Je, unatumia kikamili maandalizi hayo? MFALME AWAFUNDISHA RAIA WAKE KUHUBIRI ULIMWENGUNI POTE 7 Yesu alisema hivi alipoanza huduma yake duniani: Ni lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu kwenye majiji mengine pia, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo. (Luka 4:43) Kwa miaka mitatu Tazama Mnara wa Mlinzi, Julai 15, 2013, ukurasa wa 22-23, fungu la Chakula cha kiroho huandaliwa jinsi gani? Kwa nini chakula hicho ni muhimu? 7. Yesu alianzisha kazi gani muhimu alipokuwa duniani? Kazi hiyo ingeendelea kwa muda gani? JANUARI 15,

14 USAFISHAJI 1914 hadi 1919 Yesu akagua na kuwasafisha kiroho wafuasi wake duniani. Mwaka wa 1919, Yesu amweka rasmi mtumwa mwaminifu na mwenye busara 1919 Mkurugenzi wa utumishi awekwa rasmi 1927 Kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba Jumapili yapangwa 1938 Watumishi waanza kuwekwa rasmi kitheokrasi 1943 Shule ya Gileadi na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi 1972 Usimamizi wa kutaniko wawekwa chini ya baraza la wazee Idadi ya Wahubiri Ulimwenguni Pote: 6,000 17, , , na nusu, kazi hiyo ilikuwa muhimu sana maishani mwa Yesu. Aliwaagiza hivi wanafunzi wake: Mnapoenda, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. (Mt. 10:7) Baada ya kufufuliwa, Yesu alitabiri kwamba wafuasi wake wangeeneza ujumbe huo mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia. (Mdo. 1:8) Aliahidi kwamba angeitegemeza kazi hiyo muhimu sana mpaka mwisho. Mt. 28:19, Kufikia mwaka wa 1919, habari njema ya ufalme ilikuwa muhimu hata zaidi. (Mt. 24:14) Mfalme alikuwa anatawala mbinguni, na tayari alikuwa amekusanya duniani kikundi kidogo cha raia waliotakaswa. Raia hao walitii kwa haraka agizo hili la Yesu: Hubiri duniani pote habari njema ya Ufalme wa Mungu unaotawala! (Mdo. 10:42) Kwa mfano, mnamo Septemba 1922, wahubiri 20,000 hivi wa Ufalme walihudhuria kusanyiko la kimataifa huko Cedar Point, Ohio, nchini Marekani. Hebu wazia jinsi walivyosisimka Ndugu Rutherford alipotoa hotuba yenye kichwa Ufalme, na kisha akatangaza hivi: Tazameni, Mfalme anatawala! Ninyi ndio mawakili wa kumtangaza. Kwa hiyo, mtangazeni, mtangazeni, mtangazeni, Mfalme na ufalme wake. Wajumbe elfu mbili waliitikia mwito huo kwa kushiriki katika Siku ya pekee ya Utumishi. Walihubiri kufikia umbali wa kilomita 72 kutoka 8. Mfalme aliwachocheaje raia wake duniani kutenda? katika eneo la kusanyiko. Mjumbe mmoja aliyechochewa na himizo hilo alisema hivi: Siwezi kamwe kusahau mwito huo wa kutangaza Ufalme na bidii ya umati uliokusanyika! Wahudhuriaji wengi walikuwa na maoni kama yake. 9 Kufikia mwaka wa 1922, kulikuwa na watangazaji wa Ufalme zaidi ya 17,000 wenye bidii katika nchi 58 duniani pote. Hata hivyo, walihitaji kuzoezwa. Katika karne ya kwanza, Mfalme Aliyechaguliwa aliwaeleza waziwazi wanafunzi wake ujumbe wa kuhubiri, eneo la kuhubiri, na jinsi ya kuhubiri. (Mt. 10:5-7; Luka 9:1-6; 10:1-11) Vivyo hivyo leo, Yesu anahakikisha kwamba wote wanaoshiriki katika kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme wanapewa maagizo na vifaa wanavyohitaji ili wahubiri kwa ustadi. (2 Tim. 3:17) Kupitia Kutaniko la Kikristo, Yesu anawazoeza raia wake kwa ajili ya huduma. Anatumia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ili kuwazoeza raia wake. Shule hiyo inafanywa katika makutaniko zaidi ya 111,000 ulimwenguni pote. Kupitia shule hiyo, wahubiri zaidi ya milioni saba wamezoezwa kikamili kuhubiri na kufundisha kwa njia inayovutia watu wa namna zote. Soma 1 Wakorintho 9: Zaidi ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, shule nyingine za Biblia zimea- 9, 10. (a) Ni mipango gani ambayo imefanywa ili kuwazoeza watangazaji wa Ufalme? (b) Wewe binafsi umefaidikaje na mazoezi hayo? 14 MNARA WA MLINZI

15 1976 Baraza Linaloongoza lapangwa katika halmashauri sita 6,035,564 7,224,930 Tengenezo 1977 Shule ya Utumishi wa Painia 2,175, Shule ya Mazoezi ya Kihuduma 1999 Shule ya Waangalizi Wanaosafiri 2011 Shule ya Biblia ya WenziwaNdoa Wakristo Elimu 1,384, nzishwa ili kuzoeza wazee wa kutaniko, mapainia,nduguwaseja,wenziwandoa Wakristo, washiriki wa Halmashauri za Tawi na wake zao, waangalizi wanaosafiri na wake zao, na wamishonari. Wanafunzi wa darasa moja la Shule ya Biblia ya Wenzi wa Ndoa Wakristo walisema hivi kwa uthamini kuhusu shule hiyo: Mazoezi ya pekee tuliyopokea yametusaidia kumpenda zaidi Yehova na kutuzoeza kikamili kuwasaidia wengine. 11 Adui yetu Shetani anapinga jitihada hizo kubwa za kuhubiri na kufundisha kuhusu Ufalme. Anajaribu kukomesha kazi hiyo kwa kuwashambulia wahubiri wa Ufalme na ujumbe wao. Anafanya hivyo kwa njia ya moja kwa moja au kwa hila. Hata hivyo, jitihada za adui huyo hazitafanikiwa. Yehova amemweka Mwana wake juu zaidi kuliko kila serikali na mamlaka na nguvu na utawala. (Efe. 1:20-22) Akiwa Mfalme, Yesu anatumia mamlaka yake kulinda na kuwaongoza wafuasi wake ili kuhakikisha kwamba mapenzi ya Baba yake yanatimizwa. Habari njema inahubiriwa na mamilioni ya watu wenye mioyo minyoofu wana- Tazama Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 2012, ukurasa wa13-17,chiniyakichwa ShulezaKitheokrasiZinathibitishaUpendowaYehova. Gazeti la MnarawaMlinzila Desemba 1, 1998, ukurasa wa 19-22, linaonyesha ushindi wa kisheria tuliopata katika nchi kadhaa. 11. Wahubiri wa Ufalme wamewezaje kuendelea na kazi ya kuhubiri licha ya upinzani? fundishwa njia za Yehova. Tuna pendeleo kubwa la kushiriki katika kazi hiyo muhimu sana. MFALME AWAPANGA RAIA WAKE KWA AJILI YA UTENDAJI ZAIDI 12 Tangu Ufalme ulipoanza kutawala mwaka wa 1914, Mfalme ameboresha utaratibu wa kitengenezo unaofuatwa na watumishi wa Mungu ili kutimiza mapenzi ya Baba yake. (Soma Isaya 60:17.) Mwaka wa1919,mkurugenziwautumishialiwekwa rasmi katika kila kutaniko ili kuongoza katika kazi ya kuhubiri. Kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba kila Jumapili ilianzishwa mwaka wa Wahubiri wa Ufalme walichochewa kuhubiri kwa bidii zaidi mwaka wa 1931 walipoanza kutumia jina la Kimaandiko, Mashahidi wa Yehova. (Isa. 43:10-12) Mwaka wa 1938, waangalizi katika makutaniko walianza kuwekwa rasmi kitheokrasi badala ya kuchaguliwa kidemokrasia. Mnamo 1972, usimamizi wa kutaniko uliwekwa chini ya baraza la wazee badala ya mwangalizi mmoja wa kutaniko. Wanaume wote waliostahili walihimizwa wafanye maendeleo ili washiriki katika kazi ya kulichunga kundi la Mungu lililo chini ya uangalizi wao. (1 Pet. 5:2) Mwaka wa 1976, Baraza Linaloongoza lilipangwa katika halmashauri sita ili kusimamia kazi ya Ufalme 12. Ni baadhi ya marekebisho gani yaliyofanywa katika tengenezo tangu Ufalme ulipoanza kutawala? JANUARI 15,

16 ulimwenguni pote. Kwa kufaa, Mfalme aliyewekwa rasmi na Yehova ameendelea kuwapanga raia wa Ufalme kitheokrasi, yaani, kulingana na utawala wa Mungu. 13 Fikiria mambo ambayo Mfalme wa Kimasihi ametimiza katika miaka 100 ya kwanza ya utawala wake. Amewasafisha watu kwa ajili ya jina la Yehova. Ameongoza kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme katika nchi 239 na kuwafundisha mamilioni ya watu njia za Yehova. Amewakusanya raia zaidi ya milioni saba walio washikamanifu, na kila mmoja wao amejitoa kwa hiari kufanya mapenzi ya Baba yake. (Zab. 110:3) Kwa kweli, Yehova anatimiza kazi kubwa na za ajabu kupitia Ufalme wa Kimasihi. Tunatazamia matukio yenye kusisimua hata zaidi wakati ujao! BARAKA ZITAKAZOLETWA NA UFALME WA KIMASIHI 14 Ingawa Yehova alimvisha taji Mwana wake Yesu Kristo kuwa Mfalme wa Kimasihi mwaka wa 1914, sala ya Ufalme wako na uje haikujibiwa kikamili. (Mt. 6:10) Biblia ilitabiri kwamba Yesu angeenda akitiisha katikati ya adui zake. (Zab. 110:2) Hata hivyo, bado Ufalme wa Mungu unapingwa na serikali za kibinadamu zinazoongozwa na Shetani. Tunaposali Ufalme wa Mungu uje, tunamwomba Mungu atumie Mfalme wa Kimasihi na watawala wenzake kukomesha utawala wa wanadamu na kuondoa adui za Ufalme walio duniani. Hilo litatimiza maneno ya Danieli 2:44 kwamba Ufalme wa Mungu utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote. Utaondoa serikali zinazopinga Ufalme huo. (Ufu. 6:1, 2; 13:1-18; 19:11-21) Hilo litatukia hivi karibuni. Miaka 100 imepita 13. Umenufaikaje na mambo ambayo yametimizwa na utawala wa Ufalme katika muda wa miaka 100? 14. (a) Tunamwomba Mungu nini tunaposali: Ufalme wako na uje? (b) Andiko letu la mwaka wa 2014 ni andiko gani, na kwa nini linafaa? tangu Ufalme wa Mungu ulipoanza kutawala mbinguni. Na inafaa kwamba andiko letu la mwaka wa 2014 ni Mathayo 6:10 linalosema hivi: Ufalme wako na uje! 15 Baada ya Mfalme wa Kimasihi kuangamiza adui za Mungu, atamtupa Shetani na roho wake waovu ndani ya abiso kwa miaka elfu moja. (Ufu. 20:1-3) Baada ya uvutano mwovu wa Shetani kuondolewa, Ufalme utaanza kuwasaidia watu kunufaika na faida za dhabihu ya fidia ya Yesu, nao utaondoa kabisa madhara ya dhambi ya Adamu. Mfalme huyo atafufua mamilioni ya wafu na kupanga programu kubwa ya elimu ili wafundishwe kumhusu Yehova. (Ufu. 20:12, 13) Dunia nzima itakuwa paradiso kama bustani ya Edeni. Wanadamu wote waaminifu watakuwa wakamilifu. 16 Mwishoni mwa Utawala wa Miaka Elfu Moja wa Kristo, Ufalme wa Kimasihi utakuwa umetimiza kusudi lake. Kisha Yesu atamkabidhi Baba yake Ufalme. (Soma 1 Wakorintho 15:24-28.) Hakutakuwa tena na uhitaji wa kuwa na mpatanishi kati ya Yehova na watoto wake walio duniani. Wana wote wa Mungu walio mbinguni na watoto wake walio duniani wataungana na Baba yao wa mbinguni na kuwa washiriki wa familia yake ya ulimwenguni pote. 17 Matukio yenye kusisimua katika miaka 100 ya utawala wa Ufalme yanatuhakikishia kwamba Yehova hajapoteza mamlaka yake na atatimiza kusudi lake kwa ajili ya dunia. Acheni tuendelee kuwa raia wake washikamanifu na kumtangaza Mfalme na Ufalme wake. Tunafanya hivyo tukiwa na uhakika kabisa kwamba hivi karibuni Yehova atajibu sala hii tunayotoa kwa bidii: Ufalme wako na uje! 15, 16. (a) Ni mambo gani yenye kusisimua yatakayotukia wakati wa Utawala wa Miaka Elfu Moja? (b) Mwishowe Yesu, yule Mfalme wa Kimasihi, atafanya nini? Hilo litamaanisha nini kuhusiana na kutimizwa kwa kusudi la Yehova? 17. Umeazimia kufanya nini kuhusu Ufalme? 16 MNARA WA MLINZI

17 Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana Enyi vijana, nanyi mabikira,... mlisifu jina la Yehova. ZAB. 148:12, 13. TUNAISHI katika nyakati muhimu sana. Sasa, kuliko wakati mwingine wowote, mamilioni ya watu kutoka katika mataifa yote wanajiunga na ibada ya kweli. (Ufu. 7:9, 10) Vijana wengi wanapata mambo yaliyoonwa yenye kusisimua wanapowasaidia wengine kuelewa kweli za Biblia zinazookoa uhai. (Ufu. 22:17) Baadhi ya vijana wanawasaidia watu kuwa na maisha bora zaidi kwa kujifunza nao Biblia. Wengine wanahubiri habari njema kwa bidii katika maeneo ya lugha za kigeni. (Zab. 110:3; Isa. 52:7) Utafanya nini ili ushiriki kikamili zaidi katika kazi inayofanywa na watu wa Yehova? 2 Ukiwa kijana, unaweza kufanya maamuzi yatakayokuwezesha kupata mapendeleo mazuri ya kumtumikia Mungu baadaye. Kwa mfano, ni wazi kwamba Timotheo aliyetoka Listra alifanya maamuzi ya hekima yaliyomwezesha kupata mgawo wa kuwa mmishonari akiwa tineja au akiwa na umri wa miaka 20 hivi. (Mdo. 16:1-3) Inaonekana kwamba baada ya miezi michache tu, upinzani mkali ulimlazimisha mtume Paulo kuliacha kutaniko jipya la Thesalonike, hivyo akamkabidhi JE, UNAWEZA KUELEZA? Vijana wanaweza kufanya nini sasa ili wafurahie mapendeleo mazuri ya kumtumikia Yehova baadaye? Baadhi ya vijana wametumiaje miaka yao ya ujana? Ni kanuni gani za Biblia zinazoweza kukusaidia kufanya maamuzi bora zaidi maishani? 1. Vijana wengi Wakristo wanafurahia mambo gani mazuri? 2. Mfano wa Timotheo unaonyeshaje kwamba Yehova yuko tayari kuwakabidhi vijana majukumu? (Tazama picha kwenye ukurasa huu.) JANUARI 15,

18 kijana Timotheo mgawo wa kurudi Thesalonike ili kuwaimarisha akina ndugu. (Mdo. 17:5-15; 1 The. 3:1, 2, 6) Hebu wazia jinsi Timotheo alivyohisi alipopewa mgawo huo! UAMUZI MUHIMU ZAIDI UNAOWEZA KUFANYA 3 Wakati wa ujana ndio wakati wa kufanya maamuzi muhimu. Lakini, uamuzi wa kumtumikia Yehova ni uamuzi muhimu zaidi kuliko maamuzi mengine yote. Ni wakati gani mzuri wa kufanya uamuzi huo? Yehova anasema hivi: Mkumbuke... Muumba wako Mkuu katika siku za ujana wako. (Mhu. 12:1) Njia pekee inayokubalika ya kumkumbuka Yehova ni kumtumikia kikamili. (Kum. 10:12) Uamuzi wako wa kumtumikia Mungu kwa moyo wako wote ndio uamuzi muhimu zaidi maishani. Utakuwezesha kuwa na maisha mazuri ya wakati ujao. Zab. 71:5. 4 Bila shaka, uamuzi wako wa kumtumikia Yehova si uamuzi pekee unaohusu wakati wako ujao. Kwa mfano, huenda pia ukahitaji kuamua ikiwa utafunga ndoa, utakayefunga naye ndoa, na kuchagua kazi ya kimwili. Hayo ni maamuzi muhimu, lakini ni hekima kuamua kwanza ikiwa unataka kumtumikia Yehova kikamili iwezekanavyo. (Kum. 30:19, 20) Kwa nini? Kwa sababu maamuzi hayo yanahusiana. Uamuzi wako kuhusu ndoa na kazi ya kimwili utaathiri jinsi utakavyomtumikia Mungu. (Linganisha na Luka 14: ) Vivyo hivyo, tamaa yako ya kumtumikia Mungu itakuongoza unapofanya uamuzi kuhusu ndoa na kazi ya kimwili. Basi, fanya maamuzi muhimu kwanza. Flp. 1: Ni uamuzi gani muhimu zaidi unaoweza kufanya maishani, na unaweza kuufanya wakati gani? 4. Ni maamuzi gani mengine muhimu yatakayoathiri jinsi utakavyomtumikia Yehova? UTAFANYA NINI UKIWA KIJANA? 5 Baada ya kuamua kumtumikia Mungu, unaweza kufikiria kwa uzito anachotaka ufanye na kuamua jinsi utakavyomtumikia. Ndugu mmoja Mjapani aliandika hivi: Nilipokuwa na umri wa miaka 14, nilihubiri na mzee wa kutaniko aliyegundua kwamba sikufurahia huduma. Akaniambia hivi kwa upole: Yuichiro, nenda nyumbani. Keti na ufikirie kwa makini mambo ambayo Yehova amekufanyia. Nilifanya hivyo. Kwa kweli, niliendelea kufikiria na kusali kwa siku kadhaa. Mtazamo wangu ulibadilika hatua kwa hatua. Baada ya muda, nilianza kufurahia kumtumikia Yehova. Nilifurahia kusoma masimulizi kuhusu wamishonari, nikaanza kufikiria jinsi ninavyoweza kumtumikia Mungu kikamili zaidi. 6 Yuichiro anaendelea kusema hivi: Niliamua kufanya maamuzi ambayo yangeniwezesha kumtumikia Yehova katika nchi nyingine. Kwa mfano, niliamua kujifunza Kiingereza. Nilipomaliza shule, niliamua kufanya kazi ya muda ya kufundisha Kiingereza ili niweze kufanya upainia. Nilipokuwa na umri wa miaka 20, nilianza kujifunza Kimongolia na nilitembelea kikundi cha wahubiri Wamongolia. Miaka miwili baadaye, katika mwaka wa 2007, nilitembelea nchi ya Mongolia. Nilipoenda kuhubiri na baadhi ya mapainia na kuona kwamba watu wengi walitaka sana kujifunza kweli, nilitamani kuhamia nchini humo ili kuwasaidia. Nilirudi Japani ili kufanya mipango ya kuhama. Nimekuwa nikifanya upainia nchini Mongolia tangu mwezi wa Aprili, mwaka wa Maisha ni magumu katika nchi hii. Lakini watu wanakubali habari njema, na ninawasaidia kumkaribia Yehova. Ninahisi kwamba nilichagua njia bora zaidi ya maisha. 5, 6. Simulia jambo linaloonyesha kwamba kufanya maamuzi mazuri huleta baraka. (Tazama pia makalayenye kichwa Uamuzi Niliofanya Utotoni, katika toleo hili.) 18 MNARA WA MLINZI

19 7 Ni lazima kila Shahidi wa Yehova aamue mwenyewe jinsi atakavyotumia maisha yake. (Yos. 24:15) Hatuwezi kukuambia uoe au kuolewa, hatuwezi kukuchagulia mwenzi wa ndoa au kazi ya kimwili. Je, utachagua kazi inayohitaji mazoezi ya muda mfupi? Baadhi yenu vijana Wakristo mnaishi katika vijiji maskini; wengine wanaishi katika majiji yenye utajiri. Ulimwenguni pote, mna nyutu mbalimbali, uwezo, uzoefu, imani, na mapendezi tofautitofauti. Huenda maisha yenu yanatofautiana kama maisha ya vijana Waebrania yalivyotofautiana na maisha ya Musa aliyekuwa pia kijana katika taifa la kale la Misri. Alikuwa na maisha mazuri sana katika makao ya mfalme, lakini Waebrania wengine walikuwa watumwa. (Kut. 1:13, 14; Mdo. 7:21, 22) Waliishi katika nyakati muhimu sana kama ninyi. (Kut. 19:4-6) Kila mmoja wao alihitaji kuamua jinsi ambavyo angetumia maisha yake. Musa alifanya uamuzi unaofaa. Soma Waebrania 11: Yehova hukupa mashauri yanayoweza kukusaidia kufanya maamuzi ya hekima ukiwa kijana. Anafanya hivyo kwa kukupa kanuni unazoweza kutumia kulingana na hali zako. (Zab. 32:8) Isitoshe, wazazi wako Wakristo na wazee wa kutaniko wanaweza kukusaidia kuelewa jinsi unavyoweza kutumia kanuni hizo. (Met. 1:8, 9) Acheni tuchunguze kanuni tatu za msingi za Biblia zinazoweza kukusaidia kufanya maamuzi ya hekima yatakayokuwezesha kuwa na maisha mazuri wakati ujao. KANUNI TATU ZA BIBLIA ZA KUKUONGOZA 9 Tafuta kwanza Ufalme wa Mungu na 7. Ni lazima tujifanyie maamuzi gani, na Musa alituwekea mfano gani? 8. Vijana watapata wapi msaada wanapofanya maamuzi maishani? 9. (a) Yehova anatuheshimu jinsi gani kwa kutupatia uhuru wa kuchagua? (b) Unapata nafasi gani ukiutafuta kwanza Ufalme? uadilifu wake. (Soma Mathayo 6:19-21, 24-26, ) Yehova anatuheshimu kwa kutupatia uhuru wa kuchagua. Hasemi utumie miaka mingapi ya ujana wako kuhubiri kuhusu Ufalme. Lakini Yesu alitupatia kanuni muhimu ya kuutafuta kwanza Ufalme. Jinsi unavyotumia kanuni hiyo ndivyo utakavyopata nafasi za kuonyesha kwamba unampenda Mungu, unawajali jirani zako, na unathamini tumaini la uzima wa milele. Unapotafakari kuhusu ndoa na kazi ya kimwili, chunguza ikiwa maamuzi yako yatakufanya uhangaikie mahitaji ya kimwili au yataonyesha kwamba unatafuta kwa bidii Ufalme wa Mungu na uadilifu wake. 10 Pata furaha kwa kuwatumikia wengine. (Soma Matendo 20:20, 21, 24, 35.) Yesu alitufundisha kwa fadhili kanuni hiyo muhimu maishani. Alikuwa mtu mwenye furaha sana kwa sababu alifanya mapenzi ya Baba yake badala ya mapenzi yake mwenyewe. Yesu alifurahia kuwaona watu wapole wakikubali habari njema. (Luka 10:21; Yoh. 4:34) Labda tayari umepata furaha kwa sababu ya kuwasaidia wengine. Ukitumia kanuni alizofundisha Yesu kufanya maamuzi muhimu maishani, bila shaka utapata furaha na kumfurahisha Yehova. Met. 27: Kumtumikia Yehova hutuletea furaha nyingi hata zaidi. (Met. 16:20) Inaonekana kwamba Baruku, mwandishi wa Yeremia, alisahau jambo hilo. Pindi fulani, alipoteza furaha yake katika utumishi wa Yehova. Yehova alimwambia hivi: Unaendelea kujitafutia makuu. Usiendelee kuyatafuta. Kwa maana, tazama, ninaleta msiba juu ya wote wenye mwili,... nami nitakupa wewe nafsi yako kuwa nyara katika mahali pote utakapoenda. (Yer. 45:3, 5) Unafikiri Baruku angepataje furaha? Je, angepata 10. Kwa nini Yesu alikuwa mwenye furaha? Ni maamuzi gani yatakayokuletea furaha? 11. Kwa nini Baruku alipoteza shangwe yake, na Yehova alimpa shauri gani? JANUARI 15,

20 furaha kwa kutafuta makuu au kwa kuokoka uharibifu wa Yerusalemu akiwa mtumishi mwaminifu wa Mungu? Yak. 1: Ndugu anayeitwa Ramiro alipata furaha kwa kuwatumikia wengine. Anasema hivi: Ninatoka katika familia maskini inayoishi katika kijiji kimoja kwenye Milima ya Andes. Kwa hiyo, ndugu yangu mkubwa alipojitolea kunilipia masomo ya chuo kikuu, ilikuwa nafasi kubwa ya kutajirika. Lakini baada tu ya kubatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova, painia mmoja alinialika ili nihubiri naye katika mji fulani mdogo. Nikiwa huko nilijifunza kunyoa nywele, kisha nikafungua kinyozi ili nipate riziki. Watu walithamini sana tulipojitolea kuwafundisha Maandiko. Baadaye, nilijiunga na kutaniko jipya la lugha ya wenyeji wa eneo hilo. Nimekuwa mtumishi wa wakati wote kwa miaka kumi sasa. Hakuna kazi nyingine yoyote inayoweza kunile- 12. Ni uamuzi gani uliomletea Ramiro furaha maishani? tea shangwe ninayopata kwa kuwafundisha watu habari njema katika lugha yao. 13 Furahia kumtumikia Yehova ukiwa kijana. (Soma Mhubiri 12:1.) Usiwe na maoni ya kwamba ni lazima kwanza upate kazi nzuri ili uweze kumtumikia Yehova. Wakati wa ujana ndio wakati mzuri wa kuanza kumtumikia Yehova kikamili. Vijana wengi hawana majukumu mengi ya kifamilia, wana afya nzuri na nguvu za kutimiza migawo migumu. Ungependa kumfanyia nini Yehova ukiwa kijana? Labda una mradi wa kuwa painia. Huenda ungependa kujitolea kuhubiri katika eneo la lugha ya kigeni. Au huenda ukatambua njia mbalimbali za kutumika kikamili zaidi kutanikoni. Ili utimize mradi wowote ulio nao wa kumtumikia Mungu, unahitaji kujiruzuku. Utahitaji kujifunza kazi ya kimwili kwa muda gani? Utachagua kazi gani? 13. Kwa nini wakati wa ujana ndio wakati mzuri wa kumtumikia Yehova kikamili? Ramiro amefurahia kumtumikia Yehova tangu ujanani (Tazama fungu la 12)

21 KUTUMIA KANUNI ZA BIBLIA KUFANYA MAAMUZI YA HEKIMA 14 Kanuni tatu za Biblia ambazo tumezungumzia zinaweza kukusaidia kuchagua kazi ya kimwili. Bila shaka, washauri wa shule wanajua fursa za kazi zinazopatikana katika eneo lenu. Au huenda ukapata habari hizo kutoka kwa shirika la serikali nchini mwenu au katika eneo unalotaka kuhamia. Unaweza kupata habari muhimu kutoka vyanzo mbalimbali, hata hivyo, unapaswa kujihadhari. Watu wasiompenda Yehova watajaribu kukuchochea kuupenda ulimwenguni. (1 Yoh. 2:15-17) Moyo wako unaweza kukudanganya kwa urahisi ukikazia fikira fursa zinazopatikana ulimwenguni. Soma Methali 14:15; Yer. 17:9. 15 Baada ya kupata habari kuhusu kazi unazoweza kufanya, unahitaji mashauri ya hekima. (Met. 1:5) Ni nani anayeweza kukusaidia kuchanganua kazi hizo ukitumia kanuni za Biblia? Wasikilize watu wanaompenda Yehova, wanaokupenda, wanaokuelewa,na wanaojua hali zako vizuri. Watakusaidia kuchanganua uwezo wako na nia yako. Huenda wakasema mambo yatakayokusaidia kufikiria upya miradi yako. Umebarikiwa sana ikiwa una wazazi wanaompenda Yehova. Pia, wazee wa kutaniko lenu ni wanaume wanaostahili kiroho wanaoweza kukuongoza. Unaweza pia kuzungumza na mapainia na waangalizi wanaosafiri. Kwa nini walichagua utumishi wa wakati wote? Walianzaje kufanya upainia? Wanapataje riziki? Huduma inawaridhisha jinsi gani? Met. 15: Wale wanaokujua vizuri kabisa wanaweza kukushauri kwa utambuzi. Kwa mfano, namna gani ikiwa unataka kuacha elimu yako ya sekondari ili uanze upainia kwa 14. Mtu anapaswa kujihadhari kuhusu nini anapofikiria jinsi atakavyotumia maisha yake? 15, 16. Ni nani wanaoweza kukupa mashauri bora kuhusu kazi? sababu hupendi kusoma kwa bidii. Mtu anayekupenda anaweza kutambua nia yako na kukusaidia kuelewa kwamba unaweza kujifunza sifa ya ustahimilivu unayohitaji sana ili kumtumikia Yehova kikamili. Zab. 141:5; Met. 6: Kila mtu anayemtumikia Yehova anakabili hatari za kiroho, yaani, mambo yanayoweza kumfanya ajitenge na Yehova. (1 Kor. 15:33; Kol. 2:8) Lakini kuna kazi zinazoweza kuhatarisha zaidi hali ya kiroho ya mtu kuliko kazi nyingine. Je, imani imevunjika ya baadhi ya Wakristo katika eneo lenu baada ya kuchagua kazi ya aina fulani? (1 Tim. 1:19) Bila shaka, litakuwa jambo la hekima kuepuka kufanya maamuzi yanayohatarisha uhusiano wako na Mungu. Met. 22:3. FURAHIA MAISHA UKIWA KIJANA MKRISTO 18 Ikiwa unatamani kumtumikia Yehova, tumia nafasi unazopata za kumtumikia Mungu ukiwa kijana. Fanya maamuzi yatakayokuwezesha kufurahia kumtumikia Yehova katika nyakati hizi zenye kusisimua. Zab. 148:12, Unapaswa kufanya nini ikiwa huna tamaa ya kumtumikia Yehova? Endelea kujitahidi kuimarisha imani yako. Baada ya mtume Paulo kueleza jinsi alivyojitahidi kuishi maisha yanayompendeza Mungu, aliandika hivi: Mkiwa na mwelekeo wa akili ulio tofauti na huo kwa jambo lolote, Mungu atawafunulia ninyi mtazamo huo ulio hapo juu. Kwa vyovyote, kwa kadiri ambavyo tumefanya maendeleo, na tuendelee kutembea kwa utaratibu katika kawaida hiyohiyo. (Flp. 3:15, 16) Endelea kufikiria upendo wa Mungu na mashauri yake ya hekima. Yehova anaweza kukusaidia kufanya maamuzi ya hekima ukiwa kijana kuliko mtu mwingine yeyote. 17. Tunapaswa kuepuka kufanya maamuzi gani? 18, 19. Kijana anapaswa kufanya nini ikiwa hana tamaa ya kumtumikia Yehova? JANUARI 15,

22 Kumtumikia Yehova Kabla Siku Zenye Msiba Hazijaja Mkumbuke... Muumba wako Mkuu. MHU. 12:1. JE, UNAWEZA KUELEZA? Wakristo wenye uzoefu wanaweza kuwasaidiaje vijana? Ni mifano gani ya Biblia inayoonyesha kwamba Wakristo wenye umri mkubwa leo wanaweza kunufaika wakitumikia katika eneo lenye uhitaji mkubwa zaidi? Baadhi ya Wakristo wenye umri mkubwa wameanza kumtumikia Mungu kwa njia gani mpya? MFALME SULEMANI aliongozwa na roho ya Mungu kuwaandikia vijana maneno haya: Mkumbuke... Muumba wako Mkuu katika siku za ujana wako, kabla siku zenye msiba hazijaja. Siku zenye msiba ni siku gani? Sulemani alitumia maneno ya kishairi kufafanua matatizoyanayowakumba waliozeeka, kama vile,kutetemeka mikono, kuyumbayumba miguu, kung oka meno, kupungua kwa uwezo wa kuona na kusikia, kuota mvi, na mwili kuinama. Hivyo, hatupaswi kungoja mpaka tunapozeeka ndipo tuanze kumtumikia Yehova. Soma Mhubiri 12: Wakristo wengi wenye umri wa miaka zaidi ya 50 bado wana nguvu nyingi. Labda wana mvi, lakini inaelekea kwamba hawana matatizo ya afya aliyotaja Sulemani. Je, Wakristo hao wenye umri mkubwa wanaweza kunufaika na shauri hili lililoongozwa na roho ambalo Sulemani aliwaandikia vijana: Mkumbuke... Muumba wako Mkuu? Shauri hilo linamaanisha nini? 1, 2. (a) Sulemani aliongozwa na roho ya Mungu kuwaandikia vijana shauri gani? (b) Kwa nini Wakristo wenye umri wa miaka zaidi ya 50 wanaweza pia kunufaika na shauri hilo la Sulemani? 22 MNARA WA MLINZI

23 3 Hata ikiwa tumemtumikia Yehova kwa miaka mingi, ni vizuri kutafakari mara kwa mara na kwa uthamini kuhusu ukuu wa Muumba wetu. Bila shaka, uhai ni zawadi ya pekee sana. Wanadamu hawawezi kuelewa uumbaji kwa ukamili. Yehova ameumba vitu vingi sana vya aina mbalimbali vinavyotuwezesha kufurahia maisha. Tunapotafakari kuhusu uumbaji wa Yehova, tunachochewa kuthamini zaidi upendo, hekima, na nguvu zake. (Zab. 143:5) Hata hivyo, kumkumbuka Muumba wetu Mkuu kunatia ndani pia kutafakari kuhusu wajibu wetu kumwelekea. Bila shaka tunapotafakari, tunachochewa kumshukuru Muumba wetu kwa kumtumikia kikamili iwezekanavyo maadamu tuko hai. Mhu. 12:13. NAFASI ZA PEKEE ZA KUMTUMIKIA MUNGU UNAPOZEEKA 4 Ikiwa una uzoefu wa miaka mingi maishani, jiulize swali hili muhimu: Nitayatumiaje maisha yangu sasa nikiwa bado nina nguvu? Ukiwa Mkristo mwenye uzoefu, una nafasi za kutumika ambazo wengine hawana. Unaweza kuwafundisha vijana yale uliyojifunza kutoka kwa Yehova. Unaweza kuwaimarisha wengine kwa kuwasimulia mambo uliyofurahia katika utumishi wa Mungu. Mfalme Daudi alisali ili apate nafasi za kufanya hivyo. Aliandika hivi: Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu... Na mpaka wakati wa uzee na wa kuwa na kichwa chenye mvi, Ee Mungu, usiniache. Mpaka nikitangazie kizazi habari za mkono wako, habari za nguvu zako, kwa wale wote watakaokuja. Zab. 71:17, Unaweza kuwafundishaje wengine he- 3. Kumkumbuka Muumba wetu Mkuu kunatia ndani nini? 4. Wakristo wenye uzoefu mwingi wanaweza kujiuliza swali gani, na kwa nini? 5. Wakristo wenye umri mkubwawanaweza kuwafundishaje wengine mambo waliyojifunza? kima uliyopata maishani? Je, unaweza kuwaalika vijana wanaomtumikia Mungu ili wafurahie ushirika wenye kujenga nyumbani mwako? Je, unaweza kuwaalika ili wahubiri pamoja nawe na kuona shangwe unayopata unapomtumikia Yehova? Elihu aliyeishi zamani alisema hivi: Siku zinapaswa kusema, na wingi wa miaka ndio unaopaswa kujulisha hekima. (Ayu. 32:7) Mtume Paulo aliwashauri wanawake Wakristo wenye uzoefu wawahimize wengine kwa maneno na matendo. Aliandika hivi: Wanawake wenye umri mkubwa wawe... walimu wa yaliyo mema. Tito 2:3. FIKIRIA JINSI UNAVYOWEZA KUWASAIDIA WENGINE 6 Ikiwa wewe ni Mkristo mwenye uzoefu, unaweza kufanya mengi ili kuwasaidia wengine. Hebu fikiria mambo unayoelewa sasa ambayo hukujua miaka 30 au 40 iliyopita. Unaweza kutumia kwa ustadi kanuni za Biblia maishani. Bila shaka, unaweza kufundisha kweli ya Biblia kwa njia inayogusa moyo. Ikiwa wewe ni mzee wa kutaniko, unajua jinsi ya kuwasaidia akina ndugu wanaojikwaa katika kosa. (Gal. 6:1) Huenda umejifunza kusimamia utendaji wa kutaniko, idara za makusanyiko, au ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Labda unajua jinsi ya kuwahimiza madaktari kutumia mbinu za matibabu zisizohusisha damu. Hata ikiwa umejifunza kweli hivi karibuni, una uzoefu wenye thamani maishani. Kwa mfano, ikiwa umelea watoto, umepata hekima nyingi yenye manufaa. Wakristo wenye umri mkubwa wanaweza kuwatia moyo sana watu wa Yehova kwa kuwafundisha, kuwaongoza, na kuwaimarisha akina ndugu na dada. Soma Ayubu 12: Kwa nini Wakristo wenye uzoefu wa miaka mingi hawapaswi kufikiri kwamba hawawezi kuwasaidia wengine? JANUARI 15,

24 7 Unaweza kutumiaje uwezo wako kwa ukamili zaidi? Labda unaweza kuwaonyesha vijana jinsi ya kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia. Ikiwa wewe ni dada, je, unaweza kuwafundisha akina mama vijana kuwa na usawaziko wanaposhughulikia mambo ya kiroho na kuwatunza watoto wao? Ikiwa wewe ni ndugu, je, unaweza kuwafundisha ndugu vijana kutoa hotuba kwa shauku na kuhubiri habari njema kwa ustadi zaidi? Je, unaweza kuwaonyesha jinsi unavyowatembelea na kuwatia moyo kiroho ndugu na dada waliozeeka? Hata ikiwa sasa huna nguvu za kimwili, una nafasi nzuri sana za kuwazoeza vijana. Neno la Mungu linasema hivi: Uzuri wa vijana ni nguvu zao, na utukufu wa wazee ni kichwa chao chenye mvi. Met. 20:29. KUTUMIKIA KATIKA ENEO LENYE UHITAJI MKUBWA ZAIDI 8 Mtume Paulo alimtumikia Mungu kikamili zaidi hata alipozeeka. Alipowekwa huru kutoka gerezani huko Roma karibu mwaka wa 61 W.K., tayari alikuwa ametumika kwa miaka mingi akiwa mmishonari na alivumilia majaribu mengi. Hivyo, angeamua kubaki Roma ili ahubiri huko. (2 Kor. 11:23-27) Bila shaka, akina ndugu katika jiji hilo kubwa wangethamini sana msaada wake. Lakini Paulo aliona kwamba maeneo mengine yalikuwa na uhitaji mkubwa zaidi. Aliendelea na kazi yake ya umishonari akiwa na Timotheo na Tito. Walienda Efeso, kisha Krete, na huenda walifika Makedonia. (1 Tim. 1:3; Tito 1:5) Hatujui ikiwa Paulo alifika Hispania, lakini alikusudia kwenda huko. Rom. 15:24, Huenda mtume Petro alikuwa na umri 7. Wakristo wenye umri mkubwawanaweza kuwazoeza vijana kwa njia gani muhimu? 8. Mtume Paulo alifanya nini hata alipozeeka? 9. Huenda Petro alihamia eneo lenye uhitaji mkubwa zaidi wakati gani? (Tazama picha kwenye ukurasa wa 22.) wa miaka zaidi ya 50 alipohamia eneo lenye uhitaji mkubwa zaidi. Tunajuaje? Ikiwa umri wake ulikuwa sawa na wa Yesu au ulizidi kidogo, basi huenda alikuwa na umri wa miaka 50 hivi alipokutana na mitume wengine huko Yerusalemu mwaka wa 49 W.K. (Mdo. 15:7) Muda fulani baada ya mkutano huo, Petro alienda kuishi Babiloni ili awahubirie Wayahudi wengi walioishi katika eneo hilo. (Gal. 2:9) Alikuwa akiishi huko alipoandika barua yake ya kwanza iliyoongozwa na roho, karibu mwaka wa 62 W.K. (1 Pet. 5:13) Si rahisi kuhamia nchi ya kigeni, hata hivyo Petro hakuruhusu umri wake mkubwa umzuie kupata shangwe ya kumtumikia Yehova kikamili. 10 Leo, Wakristo wengi wenye umri wa miaka zaidi ya 50 hupata fursa za kumtumikia Yehova hali zao zinapobadilika. Baadhi yao wamehamia maeneo yenye uhitaji mkubwa zaidi. Kwa mfano, Robert aliandika hivi: Mimi na mke wangu tulikuwa na umri wa miaka 55 hivi tulipotambua fursa tulizokuwa nazo za kumtumikia Yehova. Mwana wetu alihama nyumbani, hatukuwa tena na wazazi waliozeeka waliohitaji kutunzwa, na tulikuwa tumeachiwa urithi. Nilitambua kwamba ikiwa tungeuza nyumba yetu, tungepata pesa za kutosha kulipia mkopo wa nyumba hiyo na za kutumia hadi wakati ambapo ningepata marupurupu ya kustaafu. Tulipata habari kwamba nchini Bolivia watu wengi wanakubali kujifunza Biblia na gharama za maisha ziko chini. Hivyo tukaamua kuhamia huko. Haikuwa rahisi kuzoea maisha yetu mapya. Maisha yalikuwa tofauti kabisa na yale tuliyozoea huko Amerika Kaskazini. Hata hivyo, jitihada zetu zilithawabishwa. 11 Robert anaendelea kusema: Sasa tuna mengi ya kufanya katika kutaniko. 10, 11. Simulia kuhusu ndugu aliyehama ili kutumikia katika eneo lenye uhitaji mkubwa zaidi. 24 MNARA WA MLINZI

25 Baadhi ya watu tuliojifunza nao Biblia wamebatizwa. Tulijifunza na familia mojamaskini inayoishi katika kijiji kilicho mbali. Hata hivyo, kila juma familia hiyo hujitahidi sana kuhudhuria mikutano mjini. Hebu wazia shangwe nyingi tunayopatatunapoonafamilia hiyo ikifanya maendeleo na mwana wao mkubwa akifanya upainia! UHITAJI KATIKA MAENEO YA LUGHA ZA KIGENI 12 Ndugu na dada wenye umri mkubwa wanaweza kuyasaidia sana makutaniko na vikundi vya lugha za kigeni kupitia mfano wao mzuri. Wanaweza pia kufurahia kuhubiri maeneo kama hayo. Kwa mfano, Brian kutoka Uingereza aliandika hivi: Mimi na mke wangu hatukuwa na mengi ya kufanya nilipostaafu nikiwa na umri wa miaka 65. Watoto wetu walihama nyumbani, na haikuwa rahisi kupata na kuongoza mafunzo ya Biblia. Hata hivyo, nilikutana na kijana fulani Mchina aliyekuwa akifanya utafiti 12, 13. Mkristo mmoja alianzaje kumtumikia Yehova katika njia mpya baada ya kustaafu? kwenye chuo kikuu katika eneo hilo. Alihudhuria mikutano nilipomwalika, kisha nikaanza kujifunza naye Biblia. Baada ya majuma machache, alikuja na mfanyakazi mwenzake Mchina. Majuma mawili baadaye, alikuja na Wachina wengine wawili. 13 Mchina wa tano aliyekuwa pia mtafiti alipoomba kujifunza Biblia, nilifikiria hivi: Ingawa nina umri wa miaka 65, siwezi kustaafu kumtumikia Yehova. Hivyo, nikamuuliza mke wangu aliye na umri wa miaka 63 ikiwa angependa kujifunza Kichina. Tulijifunza Kichina miaka kumi iliyopita kwa kusikiliza kanda zilizorekodiwa. Kuhubiri katika eneo la lugha ya kigeni kulitufanya tuhisi tukiwa vijana. Kufikia sasa, tumejifunza Biblia na Wachina 112! Wengi wao wamehudhuria mikutano. Mmoja wao hutumika pamoja nasi akiwa painia. FURAHIA KUMTUMIKIA YEHOVA KADIRI UWEZAVYO 14 Ingawa Wakristo wenye umri wa miaka zaidi 50wana fursa bora za kumtumikia 14. Wakristo wenye umri mkubwa hawapaswi kusahau nini? Mfano wa Paulo unawatiaje moyo? Unaweza kupanua huduma yako hata ikiwa umezeeka (Tazama fungu la 12 na 13)

26 Yehova katika njia mpya, si wote wanaoweza kufanya hivyo. Baadhi yao ni wagonjwa, na wengine wanawatunza wazazi waliozeeka au wanawatunza watoto wao. Usisahau kwamba Yehova anathamini utumishi wako. Hivyo, badala ya kuvunjika moyo kwa sababu huwezi kutimiza mengi, furahia yale unayoweza kufanya. Mfikirie mtume Paulo. Kwa miaka mingi alikuwa katika kifungo cha nyumbani, hivyo hangeendelea na safari zake za umishonari. Hata hivyo, watu walipomtembelea, aliwafafanulia Maandiko na kuwaimarisha katika imani. Mdo. 28:16, 30, Yehova huthamini pia utumishi wa Wakristo wenye umri mkubwa. Yehova huthamini Wakristo wenye umri mkubwa wanapojitahidi kumsifu hata ingawa Sulemani alisema kwamba si rahisi kumtumikia Yehova katika siku zenye msiba, matatizo ya kiafya yanapokuwa mengi. (Luka 21:2-4) Makutaniko yanathamini mfano wa ndugu na dada waaminifu ambao wamemtumikia Mungu kwa muda mrefu. 16 Biblia inasema kwamba mjane aliyeitwa Ana aliendelea kumtumikia Yehova kwa uaminifu hata alipokuwa amezeeka. Alikuwa na umri wa miaka 84 Yesu alipozaliwa. Inawezekana kwamba alikufa bila kupata pendeleo la kuwa mfuasi wa Yesu, kutiwa mafuta kwa roho takatifu, au kuhubiri habari njema ya Ufalme. Hata hivyo, Ana alifurahia kumtumikia Yehova kadiri alivyoweza. Alikuwa hakosi kamwe kuwa katika hekalu, akitoa utumishi mtakatifu usiku na mchana. (Luka 2:36, 37) Kuhani alipokuwa akifukiza uvumba hekaluni kila asubuhi na jioni, Ana alijiunga na umati uliokusanyika katika ua na kusali kimyakimya kwa nusu saa hivi. Alipomwona Yesu, 15. Kwa nini Wakristo waliozeeka wanathaminiwa sana? 16. Inaelekea Ana aliyekuwa amezeeka hakupata mapendeleo gani, lakini alifanya nini ili kumwabudu Mungu? aliyekuwa mtoto mchanga, alianza kusema juu ya mtoto huyo kwa wale wote waliokuwa wakiungojea ukombozi wa Yerusalemu. Luka 2: Leo, tunapaswa kuwa tayari kuwasaidia Wakristo waliozeeka au wagonjwa. Baadhi yao wangependa sana kuhudhuria mikutano au makusanyiko kwa ukawaida lakini hawawezi. Kwa upendo, makutaniko fulani hufanya mipango ili waliozeeka wasikilize mikutano kupitia simu. Huenda makutaniko mengine yasiweze kufanya hivyo. Hata hivyo, Wakristo ambao hawawezi kuhudhuria mikutano wanaweza kutegemeza ibada ya kweli. Kwa mfano, wanaweza kusali kwa ajili ya kutaniko la Kikristo. Soma Zaburi 92: 13, Huenda Wakristo waliozeeka wasitambue jinsi wanavyowatia moyo sana wengine. Kwa mfano, ingawa Ana alienda hekaluni kwa uaminifu kwa miaka mingi, labda hakujua kwamba mfano wake ungewatia moyo wengine kwa karne nyingi. Upendo wa Ana kumwelekea Yehova uliandikwa katika Maandiko. Bila shaka, waabudu wenzako hawatasahau kamwe upendo wako kumwelekea Mungu. Ndiyo sababu Neno la Mungu linasema hivi: Kichwa chenye mvi ni taji la uzuri kinapopatikana katika njia ya uadilifu! Met. 16: Yale tunayotimiza katika utumishi wa Yehova hutofautiana kwa sababu sote tuna uwezo na hali mbalimbali. Hata hivyo, wale walio na nguvu wanapaswa kuazimia kutii maneno haya yaliyoongozwa na roho ya Mungu: Mkumbuke... Muumba wako Mkuu... kabla siku zenye msiba hazijaja. Mhu. 12: Tunaweza kuwasaidiaje Wakristo waliozeeka na walio wagonjwa kushiriki katika ibada ya kweli? 18, 19. (a) Kwa nini huenda Wakristo waliozeeka wasitambue jinsi wanavyowatia moyo sana wengine? (b) Ni nani anayeweza kufuata shauri hili: Mkumbuke... Muumba wako Mkuu? 26 MNARA WA MLINZI

27 Ufalme Wako na Uje Lakini Utakuja Lini? Mnapoona mambo yote hayo, jueni kwamba yuko karibu milangoni. MT. 24:33. HUENDA umegundua kwamba mara nyingi watu walioshuhudia tukio fulani hukumbuka mambo tofauti-tofauti. Vivyo hivyo, huenda mtu asikumbuke maneno hususa aliyoambiwa na daktari aliyempima. Watu wengine husahau mahali walipoweka miwani au funguo zao licha ya kwamba hazijapotea. Watafiti wanasema kwamba huenda hali hizo zote zinasababishwa na upofu wa aina fulani unaomfanya mtu asione kitu au asahau jambo kwa sababu ya shughuli nyingi. Inasemekana kwamba wakati mwingine ubongo wetu hufanya kazi kwa njia hiyo. 2 Watu wengi leo ni kama vipofu inapohusu matukio ya ulimwengu. Huenda wakakubali kwamba ulimwengu umebadilika kwa kiasi kikubwa tangu mwaka wa 1914, lakini hawaoni maana halisi ya matukio hayo. Tukiwa wanafunzi wa Biblia, tunajua kwamba kwa njia fulani Ufalme wa Mungu ulikuja katika mwaka wa 1914 Yesu alipowekwa kuwa Mfalme mbinguni. Lakini tunajua kwamba sala hii inahusisha mengi zaidi: Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni. (Mt. 6:10) Ni wazi kwamba hilo linatia UNGEJIBUJE? Tangu mwaka wa 1914, hali za ulimwengu zimetimizaje unabii wa Biblia? Kwa nini uovu unazidi kuwa mbaya ulimwenguni? Unahisije unapozingatia kwamba mwisho uko karibu? 1, 2. (a) Ni nini kinachoweza kuathiri jinsi tunavyoona mambo? (b) Tuna uhakika gani kuhusu Ufalme wa Mungu? JANUARI 15,

28 ndani kuondolewa kwa mfumo mwovu uliopo. Mfumo huu mwovu utakapoondolewa, mapenzi ya Mungu yatatendeka duniani kama ilivyo mbinguni. 3 Kwa kuwa tunajifunza Neno la Mungu kwa ukawaida, tunaweza kuona unabii ukitimia leo. Mtazamo wetu ni tofauti kabisa na wa watu wengine. Wanahangaikia sana maisha yao hivi kwamba wanapuuza uthibitisho ulio wazi wa kwamba Kristo amekuwa akitawala tangu mwaka wa 1914, na hivi karibuni, ataleta hukumu ya Mungu. Hata hivyo, ikiwa umekuwa ukimtumikia Mungu kwa miaka mingi, jiulize hivi: Je, bado ninatambua umuhimu wa nyakati tunamoishi kama nilivyofanya miaka mingi iliyopita? Hata kama umekuwa Shahidi hivi karibuni, unakazia fikira mambo gani? Kwa vyovyote vile, acheni tuchunguze sababu tatu muhimu zinazotuthibitishia kwamba Mfalme aliyetiwa mafuta na Mungu atachukua hatua zaidi hivi karibuni ili kuhakikisha kwamba kusudi la Mungu linatimizwa kikamili duniani. WAPANDA-FARASI WAMETOKEA 4 Mwaka wa 1914, Yesu Kristo, aliyepanda farasi mweupe, alipewa taji lake la kifalme mbinguni. Mara moja alienda kukamilisha ushindi wake dhidi ya mfumo mwovu wa Shetani. (Soma Ufunuo 6:1, 2.) Unabii ulio katika Ufunuo sura ya 6 ulitabiri kwamba baada ya Ufalme wa Mungu kuanza kutawala, hali za ulimwengu zingezidi kuwa mbaya. Kungekuwa na vita, upungufu wa chakula, magonjwa ya kuambukiza, na mambo mengine yanayosababisha kifo. Hali hizo zinafanani- 3. Tofauti na wengine, kujifunza Neno la Mungu kumetusaidiaje? 4, 5. (a) Yesu amekuwa akifanya nini tangu mwaka wa 1914? (Tazama picha kwenye ukurasa wa 27.) (b) Wale wapanda-farasi watatu wanafananisha nini, na unabii huo umetimizwaje? shwa na wapanda-farasi watatu wanaomfuata Yesu Kristo kwa ukaribu. Ufu. 6: Kama ilivyotabiriwa, amani iliondolewa duniani licha ya kwamba mataifa mengi yaliahidi kushirikiana katika kudumisha amani. Matukio ya hivi karibuni yanathibitisha kwamba Vita vya Kwanza vya Ulimwengu vilikuwa mwanzo tu wa vita vingi ambavyo vingesababisha uharibifu mkubwa ulimwenguni. Licha ya kwamba kumekuwa na maendeleo makubwaya kiuchumi na ya kisayansi tangu mwaka wa 1914, bado upungufu wa chakula unahatarisha uhai wa watu ulimwenguni. Ni wazi kwamba magonjwa ya kuambukiza ya kila aina, misiba ya asili, na mapigo mengine yenye kufisha yanaendelea kuua mamilioni ya watu kila mwaka. Mambo hayo yanatokea mara nyingi zaidi na kuua watu wengi zaidi kuliko wakati mwingine wowote katika historia yote ya wanadamu. Je, unajua hilo linamaanisha nini? 6 Watu wengi walivurugika wakati Vita vya Kwanza vya ulimwengu vilipotokea na pia homa ya Kihispania. Lakini Wakristo watiwa-mafuta walikuwa wakitazamia sana kwamba mwaka wa 1914 ungekuwa mwisho wa Nyakati za Mataifa, au nyakati zilizowekwa za mataifa. (Luka 21:24) Hawakujua kwa hakika unabii huo ungetimizwaje. Hata hivyo, walijua kwamba mwaka wa 1914 ungekuwa mwaka wa mabadiliko muhimu sana katika utawala wa Mungu. Baada tu ya kutambua utimizo wa unabii huo wa Biblia, waliwatangazia wengine kwa ujasiri kwamba utawala wa Mungu umeanza. Waliteswa vikali kwa sababu ya bidii yao ya kutangaza Ufalme. Unabii wa Biblia ulitimia pia walipoteswa katika mataifa mengi. Katika miaka mingi iliyofuata, maadui wa Ufalme walianza kutu- 6. Ni nani waliotambua utimizo wa unabii wa Biblia, nao walifanya nini? 28 MNARA WA MLINZI

29 nga matatizo kwa njia ya amri. Walianza pia kuwatendea kwa jeuri, kuwafunga magerezani, kuwanyonga, kuwapiga risasi, au kuwakata vichwa ndugu zetu. Zab. 94:20; Ufu. 12:15. 7 Kuna mambo mengi yanayothibitisha kwamba tayari Ufalme wa Mungu unatawala mbinguni. Basi, kwa nini watu wengi hawatambui jambo hilo? Kwa nini hawaoni kwamba matukio ya ulimwengu yanatimiza unabii hususa wa Biblia, jambo ambalo watu wa Mungu wamekuwa wakitangaza kwa miaka mingi? Je, inawezekana kwamba watu wengi wanapuuza maana ya mambo wanayoona? (2 Kor. 5:7) Je, kujishughulisha sana na mambo ya kimwili kumewapofusha wasione mambo ambayo Mungu anafanya? (Mt. 24:37-39) Je, wengine wao wamekengeushwa na mawazo na malengo ya ulimwengu wa Shetani? (2 Kor. 4:4) Mtu anahitaji imani na utambuzi wa kiroho ili aone mambo ambayo Ufalme wa Mungu unatimiza. Tunafurahi kama nini kwamba sisi si vipofu tusiweze kuona mambo hayo! 7. Kwa nini watu wengi hawatambui maana ya matukio ya ulimwengu? UOVU UNAKUWA MBAYA HATA ZAIDI 8 Kuna sababu ya pili inayotuonyesha kwamba Ufalme wa Mungu utaanza kuitawala dunia hivi karibuni: Uovu katika jamii ya wanadamu unakuwa mbaya hata zaidi. Hali zilizotabiriwa katika 2 Timotheo 3: 1-5 zilionekana wazi katika karne iliyopita. Hali zinazotajwa katika andiko hilo zinaongezeka na kuwa mbaya zaidi duniani pote. Je, si kweli kwamba unabii huo unaendelea kutimia? Acheni tuchunguze mambo machache yanayothibitisha jambo hilo. Soma 2 Timotheo 3:1, Linganisha mambo yaliyoonekana kuwa mabaya katika miaka ya 1940 na 1950 na yale yanayofanywa leo katika burudani, michezo, maeneo ya kazi, na katika mitindo ya mavazi. Leo, maadili mapotovu na jeuri inayopita kiasi ni mambo ya kawaida. Watu hushindana ili waonekane kuwa wakali zaidi, wenye maadili mapotovu zaidi, au wakatili zaidi. Vipindi vya televisheni ambavyo havikufaa katika miaka ya 1950, sasa vinaonwa kuwa (a) Andiko la 2 Timotheo 3:1-5 limetimizwaje? (b) Kwa nini tunaweza kusema kwamba uovu unakuwa mbaya hata zaidi? Hali za ulimwenguni zinazidi kuwa mbaya kwa sababu ya wale wapanda-farasi (Tazama fungu la 4 na 5)

30 vinafaa kutazamwa na familia. Na watu wanaofanya ngono na watu wa jinsia yao ni maarufu sana katikaburudani na inapohusu mitindo ya mavazi. Nao huwachochea wengine hadharani wawaige. Tunathamini sana kwamba tunajua maoni ya Mungu kuhusu mambo hayo. Soma Yuda 14, Mkristo anaweza pia kulinganisha uasi wa vijana katika miaka ya 1950 na mambo yanayotendeka leo. Wakati huo, wazazi waliogopa kwamba watoto wao wangevuta sigara, kunywa pombe, au kucheza dansi kwa njia isiyofaa. Siku hizi, ni jambo la kawaida kusikia habari zenye kushtua, kama vile, Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 15 awafyatulia risasi wanadarasa wenzake, akiua 2 na kujeruhi 13. Vijana walevi wamuua kikatili msichana mwenye umri wa miaka tisa, nao wampiga baba na binamu yake. Inasemekana kwamba asilimia 50 ya visa vya uhalifu katika nchi moja ya Asia, vilifanywa na vijana katika kipindi cha miaka kumi iliyopita. Je, si kweli kwamba mambo yamezidi kuwa mabaya hata zaidi? 11 Mtume Petro hakukosea aliposema hivi: Katika siku za mwisho watakuja wadhihaki na dhihaka zao, wakiendelea kulingana na tamaa zao wenyewe na kusema: Huku kuwapo kwake kulikoahidiwa kuko wapi? Kwani, tangu siku mababu zetu walipolala katika kifo, mambo yote yanaendelea sawasawa kama tangu mwanzo wa uumbaji. (2 Pet. 3:3, 4) Kwa nini baadhi ya watu wana mtazamo huo? Inaonekana kwamba watu wanapozoea jambo fulani, wanakuwa na mwelekeo wa kulipuuza. Huenda tusishtuke kuona maadili ya watu kwa ujumla yakizorota hatua kwa hatua, lakini tunaweza kushtuka tukiona tabia ya rafiki yetu ikibadilika kwa ghafla. Hata hivyo, kuzorota hatua kwa hatua kwa maadili ni jambo hatari. 11. Kwa nini watu wengi hawatambui kwamba hali zinazidi kuwa mbaya? 12 Mtume Paulo alituonya kwamba katika siku za mwisho, hali zingekuwa ngumu kushughulika nazo. (2 Tim. 3:1) Lakini hakusema kwamba hatuwezi kamwe kushughulika nazo, basi ni lazima tupambane nazo. Kwa msaada wa Yehova, roho yake, na kutaniko la Kikristo, tunaweza kushinda woga au hali yoyote inayotuvunja moyo. Tunaweza kuendelea kuwa waaminifu. Mungu atatupatia nguvu zinazopita zile za kawaida. 2 Kor. 4: Kumbuka kwamba kabla ya kutaja unabii kuhusu siku za mwisho, Paulo alisema hivi: Ujue jambo hili. Maneno hayo yanatuhakikishia kwamba mambo aliyosema yangetimia. Bila shaka, watu wasiomwogopa Mungu wataendelea kutoka ubaya mpaka ubaya zaidi hadi Yehova atakapowaangamiza. Wanahistoria wanasema kwamba mataifa na jamii fulani zimeangamia baada ya maadili kuzorota kabisa. Leo, maadili ya wanadamu ulimwenguni yamepotoka kuliko wakati mwingine wowote katika historia. Huenda watu wengi wakapuuza maana ya matukio hayo yaliyoanza mwaka wa 1914, lakini yanapaswa kututhibitishia kwamba hivi karibuni Ufalme wa Mungu utakomesha kabisa uovu. KIZAZI HIKI HAKITAPITILIA MBALI 14 Sababu ya tatu inayotuhakikishia kwamba mwisho uko karibu sana ni historia ya watu wa Mungu. Kwa mfano, kabla ya Ufalme wa Mungu kuanza kutawala mbinguni, kikundi cha watiwa-mafuta waaminifu kilikuwa kikimtumikia Mungu kwa bidii. Watiwa-mafuta hao walifanya nini mambo fulani waliyotarajia yalipokosa kutimia katika 12, 13. (a) Kwa nini matukio ya ulimwengu hayapaswi kutuvunja moyo? (b) Tutakabiliana na hali za leo zilizo ngumu kushughulika nazo tukitambua nini? Ni sababu gani ya tatu inayotusadikishia kwamba Ufalme wa Mungu utakuja hivi karibuni? 30 MNARA WA MLINZI

31 mwaka wa 1914? Wengi wao walidumisha utimilifu na kuendelea kumtumikia Yehova licha ya majaribu na mateso. Baadhi ya watiwamafuta hao wamekufa wakiwa waaminifu. 15 Yesu alitabiri hivi kuhusu umalizio wa mfumo huu wa mambo: Kizazi hiki hakitapitilia mbali kamwe mpaka mambo yote hayo yatukie. (Soma Mathayo 24:33-35.) Tunaelewa kwamba Yesu aliposema kizazi hiki, alikuwa akirejelea vikundi viwili vya Wakristo watiwa-mafuta. Kikundi cha kwanza kilikuwapo mwaka wa 1914, nacho kilitambua waziwazi ishara ya kuwapo kwa Kristo mwaka huo. Washiriki wa kikundi hicho walikuwa hai katika mwaka wa 1914 na walitiwa mafuta kwa roho na kuwa wana wa Mungu katika mwaka huo au kabla ya mwaka huo. Rom. 8: Kikundi cha pili cha kizazi hiki kinatia ndani watiwa-mafuta walioishi wakati mmoja na watiwa-mafuta wa kikundi cha kwanza. Washiriki wa kikundi cha pili hawakuwa hai tu wakati huo bali pia walitiwa-mafuta kwa roho takatifu kikundi cha kwanza kilipokuwa duniani. Hivyo, si kila mtiwa-mafuta aliye hai leo ni sehemu ya kizazi hiki, alichozungumzia Yesu. Leo, wale walio katika kikundi hiki cha pili wamesonga kwa umri. Hata hivyo, maneno ya Yesu katika Mathayo 24:34 yanatuhakikishia kwamba kizazi hiki hakitapitilia mbali kamwe kabla ya kuona mwanzo wa dhiki kuu. Hilo linapaswa kutusadikishia hata zaidi kwamba ni muda mfupi tu uliobaki kabla ya Mfalme wa Ufalme wa Mungu kuwaharibu waovu na kuleta ulimwengu mpya wenye uadilifu. 2 Pet. 3:13. KRISTO ATAKAMILISHA USHINDI WAKE HIVI KARIBUNI 17 Tunaweza kufikia mkataa gani kutokana na sababu hizo tatu tulizochungu- 17. Tunafikia mkataa gani kutokana na sababu tatu tulizochunguza? za? Kwa kweli, hatujui siku wala saa hususa, kama Yesu alivyosema. (Mt. 24:36; 25:13) Lakini Paulo alisema kwamba tunaweza na tunajua majira. (Soma Waroma 13:11.) Tunaishi katika majira hayo, yaani, siku za mwisho. Tukikazia kabisa uangalifu unabii wa Biblia na mambo ambayo Yehova Mungu na Yesu Kristo wanatimiza, bila shaka tutaona uthibitisho ulio wazi unaoonyesha kwamba tunakaribia mwisho kabisa wa mfumo huu wa mambo. 18 Watu wanaokataa kutambua mamlaka kubwa aliyopewa Yesu Kristo, yule Mpandaji wa farasi mweupe anayeshinda, hivi karibuni watalazimika kukubali kosa lao. Hawataponyoka kamwe. Wakati huo, wengi watapaaza sauti hivi kwa hofu: Ni nani anayeweza kusimama? (Ufu. 6:15-17) Hata hivyo, sura inayofuata katika kitabu cha Ufunuo inajibu swali hilo. Bila shaka, siku hiyo watiwa-mafuta na wale wenye tumaini la kuishi milele duniani watasimama wakiwa na kibali cha Mungu. Kisha, umati mkubwa wa kondoo hao wengine utaokoka dhiki kuu. Ufu. 7: 9, Tukiendelea kukazia uangalifu unabii wa Biblia unaotimia katika nyakati hizi muhimu, hatutakengeushwa na mawazo na malengo ya ulimwengu wa Shetani; wala hatutakuwa vipofu tusielewe maana halisi ya matukio ya ulimwengu. Hivi karibuni, Kristo atakamilisha ushindi wake dhidi ya watu wasiomwogopa Mungu kwa kupigana vita vya mwisho kwa uadilifu. (Ufu. 19: 11, 19-21) Hebu wazia maisha mazuri kabisa tunayoahidiwa katikabiblia! Ufu. 20: 1-3, 6; 21:3, Itakuwaje kwa wale wanaokataa kutambua Ufalme wa Mungu? 19. Kwa kuwa unatambua, kukubali, na kutenda kupatana na uthibitisho wa kwamba mwisho utakuja hivi karibuni, unatazamia nini? JANUARI 15,

32 Nilipokuwa mvulana Uamuzi Niliofanya Utotoni Mwaka wa 1985, nilipokuwa na umri wa miaka kumi, watoto fulani kutoka Kambodia walijiunga na shule yetu huko Columbus, Ohio, Marekani. Mmoja kati ya wavulana hao alijua maneno machache ya Kiingereza. Kwa kutumia picha, alinisimulia mambo mengi yenye kutisha kuhusu mateso, mauaji, na jinsi walivyokimbia hali hiyo. Nililia usiku kila mara nilipokumbuka watoto hao. Nilitaka kuwaambia kuhusu tumaini la Paradiso na la ufufuo, hata hivyo hawakujua Kiingereza. Ingawa nilikuwa mvulana tu, niliamua kujifunza Kikambodia ili niwahubirie wanashule wenzangu kumhusu Yehova. Uamuzi huo ulikuwa na matokeo mazuri sana maishani mwangu. Haikuwa rahisi kujifunza Kikambodia. Mara mbili, niliamua kuacha kujifunza lugha hiyo, lakini Yehova alinitia moyo kupitia wazazi wangu. Baada ya muda, walimu na wanafunzi wenzangu walianza kunihimiza nifuatilie elimu ya juu ili nipate kazi nzuri ya kimwili. Kwa kuwa nilitaka kufikia mradi wangu wa kuwa painia, nilichagua masomo ya sekondari ambayo yangenisaidia kupata kazi ya muda. Kwa kawaida nilihubiri na mapainia kila siku nilipotoka darasani. Nilijitolea pia kuwafundisha wanafunzi fulani Kiingereza, na kufanya hivyo kulinisaidia sana baadaye. Nilipokuwa na umriwa miaka 16, niliambiwa kwamba kuna kikundi cha lugha ya Kikambodia huko Long Beach, California, Marekani. Nilienda huko na kujifunza kusoma Kikambodia. Baada tu ya kuhitimu shule nikawa painia na kuendelea kuwahubiria Wakambodia walioishi karibu nasi. Nilipofikisha umri wa miaka 18, nilianza kufikiria kuhamia Kambodia. Ingawa eneo hilo lilikuwa hatari, nilijua kwamba ni wachache tu kati ya watu milioni kumi nchini Kambodia waliokuwa wamesikia habari njema ya Ufalme. Wakati huo, kulikuwa na kutaniko moja tu lenye wahubiri 13 katika nchi nzima. Nilipokuwa na umri wa miaka 19, nilitembelea Kambodia kwa mara ya kwanza. Miaka miwili baadaye, niliamua kuhamia huko. Nilifanya kazi ya muda nikiwa mtafsiri na mwalimu wa Kiingereza huku nikiendelea na huduma. Baadaye, nilipata mke aliyekuwa na miradi kama yangu maishani. Tumefurahia kuwasaidia Wakambodia wengi kujiweka wakfu kwa Mungu. Yehova amenipa maombi ya moyo wangu. (Zab. 37:4) Hakuna kazi nyingine yoyote inayoridhisha sana kama kazi ya kufanya wanafunzi. Katika muda wa miaka 16 ambayo nimeishi Kambodia, kile kikundi kidogo cha watumishi 13 wa Yehova kimeongezeka na sasa kuna makutaniko 12 na vikundi 4 vilivyo mashambani! Limesimuliwa na Jason Blackwell. s Unaweza n o kupakua gazeti hili na machapisho mengine bila malipo kwenye p Unaweza pia kusoma Biblia ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya kwenye Intaneti Tembelea au utumie alama hii kufungua gazeti w14 01/15-SW

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia

Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia 34567 APRILI 15, 2013 Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia UKURASAWA 3 NYIMBO ZA KUTUMIWA: 114, 113 Juni 10-16 Jinufaishe na Uwanufaishe Wengine kwa KutumiaNenolaMungu UKURASAWA 18 NYIMBO ZA KUTUMIWA:

More information

"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.

ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu. Waebrania 9:28. KUJA KWA KRIST0 MARA YA PILI "ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28. Mara nyingi sana kuja kwa Kristo mara ya pili huangaliwa tu kama fundisho la dini. Ni

More information

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) 102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako

More information

MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI

MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Mwanzo 1:1 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi. Wakolosai

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper

More information

Agano Lililofunikwa Kwa Damu

Agano Lililofunikwa Kwa Damu Agano Lililofunikwa Kwa Damu na Ellis Forsman Agano Lililofunikwa Kwa Damu (The Blood-Sealed Covenant) 1 Agano Lililofunikwa Kwa Damu na Ellis Forsman Oktoba 14, 2012 Agano Lililofunikwa Kwa Damu (The

More information

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT 1 Ushindi Ndani ya Kristo Na W. W. Prescott Mfasiri: M. Mwamalumbili Victory in Christ - Kiswahili 2 Yaliyomo Alinipenda Mimi Aliishi kwa ajili Yangu Mimi Alikufa

More information

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke- Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited

More information

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ukristo leo unadhihirisha waumini karibu bilioni mbili katika maelfu ya madhehebu tofauti na tofauti na madhehebu. Kati ya hizi, zaidi ya 500 madhehebu

More information

UNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW

UNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW Kama unataka kujifunza zaidi njia ya Mkristo wa kweli anavyopaswa kuishi, basi ni lazima ujifunze Biblia. Ili kukusaidia; Kanise la Christadelphian Bible Mission limechapisha kijitabu kuhusu mafunzo ya

More information

United Pentecostal Church June 2017

United Pentecostal Church June 2017 Kwa Nini Tusali? Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa "Chagua" Ladies Prayer International kwa Facebook United Pentecostal Church June 2017 Tuko na wafuasi Facebook katika Marekani, Hong Kong, Philippines,

More information

GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI

GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI Utambulisho Grace Communion International ni muungano wa washiriki kutoka pembe mbali mbali za dunia hasa nchi zenye washiriki kwa sasa ni 100. Wito wetu ni

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited

More information

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu Nabii Musa alipotoka mlima Sinai kupewa amri kumi za Mungu zilizoko kwenye kitabu cha Kutoka 20:1 17, Mungu alimpa na sharia zingine ambazo lengo lake

More information

Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College

Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College Theolojia 1 Ujumla Mike Taylor Semester 1 2014-2015 Munguishi Bible College MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 i THEOLOJIA Utangulizi! 1 1. Kumfahamu Mungu katika Injili! 3 1.1. Mawazo Makuu 3 1.2. Maana ya

More information

B. Wanafunzi watapata ufahamu mkubwa wa kitabu hiki, na jinsi kinavyofundisha kuhusu kanisa.

B. Wanafunzi watapata ufahamu mkubwa wa kitabu hiki, na jinsi kinavyofundisha kuhusu kanisa. Waefeso Mtaala I. Habari kwa Ujumla A. Mkufunzi: Don Walker na kutafsiriwa na Chris Mwakabanje B. Kila darasa ni takribani dakika 38. II. Maelezo na Kusudi A. Mafunzo haya ni uchambuzi wa kina katika Waefeso,

More information

walozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w

walozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w MAMLAKA Tunamshukuru Bwana kwa vile alivyo na yale aliyoyatenda. Tukiweza tu kumfikiria hata tukiwa na mahitaji mbalimbali, yeye atatutimizia. Tusiwatazame watu, tusijitazame sisi wenyewe, tumtazame Mungu

More information

WEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23

WEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23 Toleo X Toleo 23 WEWE NI NANI? (Habari ifuatayo ni hadithi ya mambo ambayo yamenakiliwa katika Matendo 19:10-20 SUV). Paulo mtume wa Yesu Kristo alihubiri katika mji wa Efeso kwa miaka miwili. Katika muda

More information

Kanuni. Muhimu za Kujifunza Biblia. Mchungaji Drue Freeman. Dan Hawkins & Joseph Brown. General Editors.

Kanuni. Muhimu za Kujifunza Biblia. Mchungaji Drue Freeman. Dan Hawkins & Joseph Brown.   General Editors. Kanuni Muhimu za Kujifunza Biblia na Mchungaji Drue Freeman General Editors Dan Hawkins & Joseph Brown a publication of www.villageministries.org Kanuni Muhimu za Kujifunza Biblia 2013 na Village Ministries

More information

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO. MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO. MUHTASARI WA UTANGULIZI WA THIOLOGIA YA USHIRIKA WA NAFSI TATU ZA UUNGU. GRACE COMMUNION INTERNATIONAL LIVING AND SHARING THE GOSPEL MUNGU ANADHIHIRISHWA NA

More information

Human Rights Are Universal And Yet...

Human Rights Are Universal And Yet... Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,

More information

Roho Mtakatifu Ni Nini?

Roho Mtakatifu Ni Nini? Roho Mtakatifu Ni Nini? kwa ajili ya mkutano. Mkutano huu utakuwa tofauti, kidogo na ile ya kawaida tunayokuwa nayo hapa. Kwa kawaida, kila wakati tunapokuja pamoja hapa, ni mkutano kwa wa kwa ajili ya

More information

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka 0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level * 899145 4 672* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2010 Additional Materials: Answer Booklet/Paper READ

More information

Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally

Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo Na Andrew Connally 1 YALIYOMO Milango ya Kitabu: Ukurasa: 1. Mungu-Kuwako kwake na hali yake 03 2. Huyo Kristo-Nafsi yake na kazi yake 12 3. Maandiko Matakatifu ni yenye

More information

BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE

BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE Toleo 10 BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE UBATIZO WA MUUMINI Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa

More information

WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen

WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen 1 Index latest update 26. feb. 2008 WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen Wafunaji wa nafsi ABC Mark 16:15-20 Huduma/uiinjilisti Wakristo wachache sana wameitikia mwito wa

More information

Mutugi Kamundi. Jemma Kahn. Kiswahili. Demane na pacha wake. Author - South African Folktale

Mutugi Kamundi. Jemma Kahn. Kiswahili. Demane na pacha wake. Author - South African Folktale You are free to download, copy, translate or adapt this story and use the illustrations as long as you attribute in the following way: Demane na pacha wake Author - South African Folktale Adaptation -

More information

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Ndugu na dada zangu wapendwa, UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2013 Utiifu Huleta Baraka Elimu ya ukweli na majibu ya maswali makuu huja kwetu tunapokuwa watiifu kwa amri za Mungu. Ndugu na dada zangu wapendwa, nina shukrani jinsi gani

More information

Kifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1

Kifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1 Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Na Ellis P. Forsman Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1 Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Na Ellis P. Forsman Oktoba 11, 2011 Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 2 Kifo

More information

Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu?

Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu? Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu? (Attitude Towards Christ Do you Honor Him?) Na Ellis P. Forsman (4-Attitude Towards Christ - Do you Honor Him) 1 Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu? (Attitude Towards

More information

Maisha Ya Mkristo Ni Nini?

Maisha Ya Mkristo Ni Nini? Maisha Ya Mkristo Ni Nini? na Ellis P. Forsman Maisha Ya Mkristo Ni Nini? (What Is The Christian Life?) 1 Maisha Ya Mkristo Ni Nini? na Ellis P. Forsman Oktoba 17, 2011 Maisha Ya Mkristo Ni Nini? (What

More information

WAKOLOSAI MTAALA. B. Maoni: Tunapendekeza uwe na fafanuzi (commentary) yoyote yenye kushikilia mafundisho ya awali (conservative) katika Wakolosai.

WAKOLOSAI MTAALA. B. Maoni: Tunapendekeza uwe na fafanuzi (commentary) yoyote yenye kushikilia mafundisho ya awali (conservative) katika Wakolosai. WAKOLOSAI MTAALA I. MAELEZO KWA UJUMLA. A. Mwalimu: Don Walker B. Mkalimani: Chris Mwakabanje C. Kila darasa linachukua takribani dakika 38. II. III. MAELEZO NA MALENGO. A. Kujifunza kwa kina Waraka kwa

More information

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika (A Summary Of Arguments For And Against Individual Communion Cups) Na J D Logan Communion Cups) 1 Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi

More information

Kiu Cha umtafuta Mungu

Kiu Cha umtafuta Mungu ZAIDI YA NAKALA MILLION 3 ZIMECHAPISHWA KATIKA LUGHA 59 KOTE DUNIANI K Kiu Cha umtafuta Mungu Huduma ya Daktari Richard A. Bennett ilianza katika mabaraza ya miji. Akiwa mwanafunzi chuoni, alikumbana na

More information

Tazama Yuaja. Kuhusu Toleo Hili. Umuhimu wa Mafundisho ya Biblia. Nguvu katika neno la Mungu.

Tazama Yuaja. Kuhusu Toleo Hili. Umuhimu wa Mafundisho ya Biblia. Nguvu katika neno la Mungu. Tazama Yuaja Kuhusu Toleo Hili. Kuna makanisa mengi duniani yanayo dai kuwa yanafundisha ukweli. Yote pia yana mafundisho tofauti yaliyo mafundisho na desturi ya watu. Muungano wa makanisa na uwongozi

More information

Aina Tatu Za Ibada. Ellis Forsman. Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 1

Aina Tatu Za Ibada. Ellis Forsman. Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 1 Aina Tatu Za Ibada na Ellis Forsman Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 1 Aina Tatu Za Ibada na Ellis Forsman Octoba 15, 2011 Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 2 Aina Tatu Za Ibada Yoh.

More information

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Ndugu na dada zangu wapendwa, UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2014 Na Rais Thomas S. Monson Upendo Asili ya Injili Hakika hatuwezi kumpenda Mungu kama hatuwapendi wasafiri wenzetu katika safari hii ya maisha duniani. ninafurahia mawazo

More information

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA SOMO LA KWANZA UTANGULIZI KWA TORA For videos, study guides and other resources, visit Third Millennium Ministries at thirdmill.org. 2014 nathird Millennium Ministries Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu

More information

JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?

JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? JOE CREWS 1 JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? Na Joe Crews (Hotuba Na. 16 ya Mambo ya Kweli Yanayoshangaza) Mfasiri: M. Mwamalumbili Is It Possible To

More information

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA

More information

MWONGOZO WA NAMNA YA KUHAMASISHA MAOMBI YA MCHANA NA USIKU YA SIKU 10.

MWONGOZO WA NAMNA YA KUHAMASISHA MAOMBI YA MCHANA NA USIKU YA SIKU 10. 6-15 Mei 2005. MWONGOZO WA NAMNA YA KUHAMASISHA MAOMBI YA MCHANA NA USIKU YA SIKU 10. Kujenga kifuniko cha maombi juu ya mabara yote ya ulimwengu. Kufurikisha Jamii zetu kwa Maombi. Anzisha vituo vitakavyofukuta

More information

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03 Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03 AEG swahili Bahari ya Aegean Brosha ya maelezo hii ni kwa watu wanaofikiria kuvuka bahari ya Aegean kati ya Ugiriki na Uturuki.Kuvuka kihramu ni uhalifu katika

More information

Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia. Ellis Forsman. Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1

Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia. Ellis Forsman. Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1 Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia na Ellis Forsman Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1 Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia na Ellis Forsman Oktoba 8, 2011 Inavyodaiwa

More information

UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA

UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA Dynamic Churches International Simeon Oyui P. O. Box 798-00515 Bukubura, Nairobi, Kenya EAST AFRICA Email: ncc_africa@yahoo.com Dynamic Churches International 164 Stonegate

More information

Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu

Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu 134 Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu Picha tuliyonayo kuhusu Mungu ni mojawapo ya kizuizi kikubwa cha kupata uponyaji wetu. Mara nyingi huwa hatujui vizuri kwamba Mungu anatupenda kwa hivyo angependa

More information

Watumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1

Watumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1 Watumishi Wa Kristo na Ellis P. Forsman Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1 Watumishi Wa Kristo na Ellis P. Forsman Oktoba 14, 2011 Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 2 Sisi ni watumishi Watumishi

More information

United Pentecostal Church April Kushangilia Kwa Sala

United Pentecostal Church April Kushangilia Kwa Sala Kushangilia Kwa Sala Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa Kushangilia Kwa Sala Na Wanda Fielder United Pentecostal Church April 2017 Kuwa alimfufua katika kanisa tangu kuzaliwa, daima aliamini Neno la

More information

NGUVU. Utangulizi. Yesu alisema,

NGUVU. Utangulizi. Yesu alisema, NGUVU Utangulizi Kwas miaka mingi nimemtafuta Bwana ili aachilie mazingira mazuri ya uwepo wake, nguvu na utukufu wake kudhihirika. Tumeona na kujua matokeo ya yale Bwana ametufunulia. Ikiwa unatafuta

More information

Kifo Na Mbingu (Death And Heaven)

Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Na Ellis P. Forsman The Rapture And Millennialism 1 Kifo Na Mbingu Na Ellis P. Forsman Octoba 11, 2011 The Rapture And Millennialism 2 Kifo Na Mbingu Heb. 9:27 Ili kufika

More information

UTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha

UTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha UTARATIBU WA KANISA Tumemaliza hivi punde ule mkutano mkubwa wa siku, tano usiku kwenye Maskani, ambapo, kwa neema ya Mungu na kwa msaada Wake, nimejaribu sana, kwa Maandiko, kuliweka Kanisa la Bwana Yesu

More information

IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE

IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE IMANI NA MATENDO IMANI NA MATENDO Hotuba na Makala za Ellen G. White Masomo kutoka katika Hotuba zake Kumi na Tisa zilizotolewa Nzima au kwa Sehemu kuanzia mwaka 1881

More information

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Ndugu na dada zangu wapendwa, UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, NOVEMBA 2011 Na Rais Thomas S. Monson Simama Pahali Patakatifu Mawasiliano na Baba yetu aliye Mbinguni pamoja na maombi yetu Kwake na maongozi Yake kwetu ni muhimu ili tuweze

More information

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA

More information

KITABU CHA KUONGOZA FAMILIA

KITABU CHA KUONGOZA FAMILIA KITABU CHA KUONGOZA FAMILIA KITABU CHA KUONGOZA FAMILIA Kimechapishwa na Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu la Siku za Mwisho Mjini Salt Lake, Utah 1992, 1999, 2001, 2006 na Intellectual Reserve, Inc.

More information

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya Jina Nambari.. Shule... 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI / AGOSTI. 2007 MUDA: SAA 2 ½ MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya 102/3 KISWAHILI FASIHI

More information

Maisha Yaliyojaa Maombi

Maisha Yaliyojaa Maombi (A Prayer-Filled Life) na Terry Warford (A Prayer-Filled Life) 1 (A Prayer-Filled Life) na Terry Warford Nov 5, 2011 (A Prayer-Filled Life) 2 Sura ya nne nay a tano ya kitabu cha Ufunuo ni vifungu vinavyovutia.

More information

K. M a r k s, F. E n g e l s

K. M a r k s, F. E n g e l s W a (any a kazi wa nchi zote, unganeni! K. M a r k s, F. E n g e l s Maelezo ya chama cha kikomunist Idara ya Maendcleo Moscow Tafsiri hii ya "Maelezo ya Chama cha Kikomunist" inatokana na maandishi

More information

MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA

MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA 133 134 MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA Ni heri nione mahubiri kuliko kusikia moja siku yeyote ile. Ni heri mtu atembee nami kuliko kunionyesha njia. Jicho ni mwanafunzi mzuri na mwenye hamu kuliko sikio. Mausia

More information

VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI

VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI Asante, Ndugu Neville, Bwana akubariki. Bila shaka ni, majaliwa kuwa hapa usiku wa leo. Nina furaha sana ya kwamba Mungu alituruhusu

More information

RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO

RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO 1 RISALA FUPI copyright Hidaya Creativity, publishing Department. P.O. BOX 44799, 00100, GPO, NAIROBI-KENYA. Haki

More information

UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI

UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI Toleo 14 BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI Hazina ya maelezo kutoka

More information

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI This booklet on Becoming a Parent was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at. MACHAGUO

More information

Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu

Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu na Ellis P. Forsman God) 1 Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu na Ellis P. Forsman Oktoba 7, 2011 God) 2 Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu Mat. 6:24-34 Yesu alitoa maelezo haya

More information

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST

More information

MASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO

MASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO MASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO Sasa, kama ye yote ana swali lo lote wanalotaka kulileta,, basi, hebu yasogezeni tu juu hapa, acha mtoto fulani ayalete au vyo vyote mtakavyo. Au, labda, tukimaliza

More information

Makasisi. Waingia Uislamu

Makasisi. Waingia Uislamu 1 Makasisi Waingia Uislamu 2 KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU MAKASISI WAINGIA UISLAMU Yaliyomo 1. KASISI YUSUFU ESTES ALIYEKUWA MFANYABIASHARA WA KIKRISTO & MUHUBIRI (USA)...

More information

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji! Yaliyomo Kuhusu kitabu hiki Kuhusu kitabu hiki.........................................................1 Unapojisikia vibaya.........................................................2 Unapoanza kuwa mzima

More information

Uongozi Siri Na Larry Chkoreff. Version 1.2 Desemba 2010

Uongozi Siri Na Larry Chkoreff. Version 1.2 Desemba 2010 Uongozi Siri Na Larry Chkoreff Version 1.2 Desemba 2010 Kimetafsiriwa na kuchapishwa na: Cistern Materials Translation & Publishing Center, Nairobi, Kenya Barua pepe: info@cisternmaterialscenter.com www.cisternmaterialscenter.com

More information

FORWARD BY DANIEL SZMIOT

FORWARD BY DANIEL SZMIOT FORWARD BY DANIEL SZMIOT 2017 marks the 40th anniversary of the start of Lighthouse Ministry. As in all wars, soldiers continue to fight the battle for the body, mind, will, and emotions. We as Christian

More information

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu

More information

Kwa Kongamano Kuu 2016

Kwa Kongamano Kuu 2016 The Upper Room za Kwa Kongamano Kuu 2016 Selected from The Upper Room Disciplines with Invited Writers SIKU 60 ZA SALA Kwa Kongamano Kuu 2016 2016 na Upper Room Books. Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu

More information

Uponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14).

Uponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14). 41 Uponyaji Wa Laana Ijapokuwa baraka ni kinyume cha laana, kuna mambo yanayofanana katika vitu hivyo. Ni maneno yaliyotajwa, yaliyoamriwa, au kuandikwa katika Biblia kwa nguvu na mamlakao ya kiroh kwa

More information

UNABII WA HABARI ZA BIBLIA

UNABII WA HABARI ZA BIBLIA CCOGAFRICA.ORG Aprili-Juni 2017 UNABII WA HABARI ZA BIBLIA African Conference 2017 in Nairobi Kenya Kutoka kwa Mhariri: Kongamano la Afrika 2017.Kanisa la Mungu Linaloendelea Makabila 12 ya Waisraeli wako

More information

MAFUNDISHO YA UMISHENI

MAFUNDISHO YA UMISHENI MAFUNDISHO YA UMISHENI UINJILISTI NA UANAFUNZI Muhtasari: Elekeza kwa mada ilioko hapa chini nayo itakuelekeza kwa mada hiyo. I. Lengo la Sehemu Hii II. Uhusiano kati ya Uinjilisti na Uanafunzi III. Kwa

More information

wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.

wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine. HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWENYE IBADA YA KUWEKWA WAKFU NA KUINGIZWA KAZINI ASKOFU MARTIN FATAELI SHAO WA DAYOSISI YA KASKAZINI YA KANISA LA

More information

ONYO LA MWISHO KWA DUNIA

ONYO LA MWISHO KWA DUNIA ONYO LA MWISHO KWA DUNIA Mpango wa Ulimwengu Mpya Unakuja!. Viongozi wa Ulimwengu. Jinsi ya kuukwepa usiwe wanautaka mhanga. Unaungwa mkono na. Kuanguka kwake ghafula wengi na kwa ukamilifu. Ulitabiriwa

More information

JE! MUNGU ANAMPA MWANAMKE HAKI YA KUTOA MIMBA IWAPO NI MHANGA WA UBAKAJI?

JE! MUNGU ANAMPA MWANAMKE HAKI YA KUTOA MIMBA IWAPO NI MHANGA WA UBAKAJI? Jarida la Dunia Yerusalemu Mpya Mchungaji Tony Alamo Makanisa Ulimwenguni Kote Taifa la Kikristo la Alamo Mchungaji Tony na Susan Alamo, Okestra, na kwaya katika kipindi chao cha kimataifa cha televisheni.

More information

MSAMAHA NA UPATANISHO

MSAMAHA NA UPATANISHO Hakimiliki 2007-2017 na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa. MSAMAHA NA UPATANISHO na Jonathan M. Menn B.A., Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, 1974 J.D., Cornell Law School, 1977 M.Div., Trinity Evangelical

More information

KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU?

KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU? KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU?, Asante, Ndugu Neville, na habari za jioni, marafiki. Nimerudi tena. Sikupata ila masaa manne asubuhi ya leo. Hiyo ni aibu. Na baada ya

More information

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh

More information

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org ( Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Haja Ya Dini Haja Ya Dini Author(s): Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi [3] Publisher(s): Bilal Muslim Mission of Tanzania [4] Katika kijitabu

More information

Silaha Za Shetani. Ellis Forsman. Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1

Silaha Za Shetani. Ellis Forsman. Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1 Silaha Za Shetani na Ellis Forsman Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1 Silaha Za Shetani na Ellis Forsman Oktoba 15, 2012 Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 2 Silaha Za Shetani 2 Kor. 2:11

More information

maombi, kabla tu hatujalifungua Neno hili la Kiungu.

maombi, kabla tu hatujalifungua Neno hili la Kiungu. ALAMA YA MNYAMA Sasa, kesho usiku Daima tunaonyesha jambo moja,, Bwana Yesu Kristo, ni hivyo tu, na lo lote ambalo ni mapenzi Yake ya Kiungu kwetu kufanya. Lakini kama ni mapenzi Yake ya Kiungu kesho usiku,

More information

H. M. Baagil, M. D. WAMY Studies on Islam

H. M. Baagil, M. D. WAMY Studies on Islam Mazungumzo ya Mwislamu na Mkristo H. M. Baagil, M. D. WAMY Studies on Islam 1 YALIYOMO Muhtasari wa Mtunzi... 4 Utangulizi... 6 MAZUNGUMZO... 8 Biblia Takatifu... Error! Bookmark not defined. Imani ya

More information

MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara

MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara 1 MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara 1. UTANGULIZI Miaka 500 ya matengenezo ya Kanisa inatufanya tuangalie nyuma na kuona jinsi Mungu alivyotumia wanadamu

More information

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to

More information

Tumaini Kwa Afrika. Thomas Schirrmacher. Hoja 66. Dibaji na Prof. Mchungaji Dk. Thomas K. Johnson. Thomas Schirrmacher Tumaini Kwa Afrika TASCM RVB

Tumaini Kwa Afrika. Thomas Schirrmacher. Hoja 66. Dibaji na Prof. Mchungaji Dk. Thomas K. Johnson. Thomas Schirrmacher Tumaini Kwa Afrika TASCM RVB Tunawezaje kudhihirisha msingi wa Kibiblia wa tumaini letu na kulithibitisha kwa Wakristo na kwa wasioamini walioshirikishwa? Tunawezaje kutamka matumaini yetu kwa Wabunge, kwa wafanya biashara au kwa

More information

Oktoba-Desemba

Oktoba-Desemba Oktoba-Desemba 2014 1 Habari za Unabii wa Biblia 8 13 24 Katika toleo hili: 25 28 33 3 MwanaFiladelfia wa Karne ya 21 ni nani? Je, Yesu alifundisha kwamba kungekuwepo na tofauti kubwa baina ya Wakristo

More information

MELKISEDECK LEON SHINE. katoliki.ackyshine.com

MELKISEDECK LEON SHINE. katoliki.ackyshine.com katoliki.ackyshine.com SALA ZA ASUBUHI Kwa jina la Baba.. Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,Mwana na Roho. Nilinde tena siku hii,niache dhambi nikutii.naomba sana

More information

TIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO

TIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO TIST HABARI MOTO MOTO Tel. 026-2322246 P.O.BOX 53 MPWAPWA E-Mail tist@twiga.com 01 October 2000 Y2K PREPARATIONS Holes and Seedlings made ready for the year 2000 programme By Gayo Mhila The process of

More information

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa.

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa mabingwa itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa. Mkuu Inahitaji dhabihu. Unahitaji kujisukuma hadi mwisho wako. Lakini nakupa ahadi hii,

More information

KUTAMBUA SIKU YA KO NA UJUMBE WAKE

KUTAMBUA SIKU YA KO NA UJUMBE WAKE KUTAMBUA SIKU YA KO NA UJUMBE WAKE Habari za asubuhi, wapendwa. Hebu na tuendelee, kusimama kwa muda kidogo tu. Mungu mpendwa, sisi, tulio kwenye wakati wa mahangaiko na kakara za maisha, tumetulia kwa

More information

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi. Iliyoendelea sana

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi. Iliyoendelea sana kitengo cha 3 Iliyoendelea sana Iliyoendelea sana Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu Iliyoendelea sana Kitabu cha mwanafunzi Kuwa bingwa.wewe na mimi lazima tujifunze kuishi kwa tunda la Roho

More information

Kiumbe Kipya Katika Kristo

Kiumbe Kipya Katika Kristo Kiumbe Kipya Katika Kristo na Ellis P. Forsman Kiumbe Kipya Katika Kristo (The New Creature In Christ) 1 Kiumbe Kipya Katika Kristo na Ellis P. Forsman Oktoba 15, 2011 Kiumbe Kipya Katika Kristo (The New

More information

Jumuiya ya Waislamu Waahmadiyya Tanzania

Jumuiya ya Waislamu Waahmadiyya Tanzania na Hadhrat Mirza Ghulam Ahmad wa Qadian Masihi Mauʻudi na Imam Mahdi as Jumuiya ya Waislamu Waahmadiyya Tanzania HOTUBA YA SIALKOT Tafsiri ya Kiswahili ya: Lecture Sialkot (Urdu) Imeelezwa na: Hadhrat

More information

PDF created with pdffactory trial version

PDF created with pdffactory trial version المملكة العربية السعودية وزارة التعليم العالي الجامعة الا سلامية بالمدينة المنورة عمادة البحث العلمي قسم الترجمة تعريف موجز بالا سلام بل( لغة السواحلية) ١ بسم االله الرحمن الرحیم MAELEZO KWA UFUPI KUHUSU

More information

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted

More information