wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.
|
|
- Phoebe Cox
- 6 years ago
- Views:
Transcription
1 HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWENYE IBADA YA KUWEKWA WAKFU NA KUINGIZWA KAZINI ASKOFU MARTIN FATAELI SHAO WA DAYOSISI YA KASKAZINI YA KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA, KANISA KUU, MOSHI, 09 MEI 2004 Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Baba Askofu Dkt. Samson Mushemba; Askofu Mpya wa Dayosisi ya Kaskazini ya KKKT, Baba Askofu Martin Fataeli Shao; Maaskofu Wengine Wote; Wachungaji, Viongozi wa Kanisa na Waumini; Wageni Waalikwa; Mabibi na Mabwana: Bwana Asifiwe! Naungana nanyi kumshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kutuweka sote hai hadi siku hii ya leo aliyoipanga yeye mwenyewe ya kubadilishana uongozi wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania kwa heshima na taadhima. Ibada imekwenda vizuri sana. Nawapongeza walioiandaa na kuiendesha. Nawashukuru waumini wote walioniombea nilipolazwa hospitalini Uswisi mpaka ikampendeza Mwenyezi Mungu kunusuru maisha yangu. Na kwa yote haya sifa, heshima na utukufu ni kwa Bwana Mungu wetu, kwani: Kwa njia ya rehema za Mungu wetu, Ambazo kwazo mwangaza utokao juu umetufikia, Kuwaangazia wakaao katika giza na uvuli wa mauti, Na kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani. (Luk. 1:78-79) Ndugu Wana-Dayosisi ya Kaskazini: Katika siku hii muhimu, nakuja kwenu na salamu za shukrani na upendo. Ninawashukuruni sana kwa kunialika kwenye ibada hii, na ninashukuru sana kwa mapokezi mema, ya upendo, mliyonipa mimi na Mama Mkapa, na ujumbe wangu wote. Kwa niaba yao wote, nasema ahsanteni sana.
2 Kwa niaba yao pia nakupongezeni sana Wana-Dayosisi hii kwa kupata kiongozi mpya, aliyepatikana kwa ridhaa yenu, mliyeridhika naye, kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya Dayosisi. Kule nje kwenye uwanja wa siasa, baada tu ya uchaguzi, utasikia kesi chungu nzima zinafunguliwa kupinga matokeo, na pengine hata kupakana matope tu. Kwenu mambo ni shwari kabisa. Aliyechaguliwa amechaguliwa, na wengine wote wanakiri hivyo na kuonyesha utii wao kwa kiongozi wao mpya. Laiti mngekuja kutupiga msasa kwenye siasa, ili huko nje nako kuwe na chaguzi za kiungwana kama hizi!! Naungana pia na waliozungumza kabla yangu kukupongeza sana Baba Askofu Martin Fataeli Shao kwa kustahiki heshima hii kubwa, na kuonekana mwenye uwezo wa kiroho na kimwili kubeba mzigo wa kuchunga kondoo wa Bwana. Kwa niaba ya Mama Mkapa, na familia yangu yote; na kwa niaba ya Serikali, nakupongeza sana na kuungana na wote wanaokuombea kwa Mwenyezi Mungu akupe busara, uvumilivu, na afya ya kubeba mzigo mzito huu. Baba Askofu, Natumia maneno mzigo mzito kwa makusudi. Biblia inawaita viongozi wa kanisa wa ngazi yako kuwa ni wachungaji wa kondoo. Na wewe ndivyo utakavyokuwa. Ukirudi nyuma kwenye historia, wachungaji kondoo walikuwa na maisha magumu. Wale tunaowasoma kwenye Kitabu cha Mwanzo waliishi maisha ya shida, kwenye joto sana misimu fulani na baridi sana misimu mingine. Walipambana na ukame na uhaba wa malisho, na walipigana na wanyama wakali waliokuwa wanavizia kondoo. Hayo ndiyo maisha unayoyaanza leo, Baba Askofu Shao. Yakobo alikuwa mchungaji mwema, japo kazi hiyo aliifanya kama mahari ya kuolea katika nyumba ya Labani. Ninyi viongozi wa dini mnayajua mazingira yaliyomfanya Labani amfanyie fujo Yakobo wakati wakiachana mwisho wa mkataba wake. Lakini, napenda ninukuu maneno ya Yakobo kwa Labani. Alisema ifuatavyo, akielezea rekodi yake ya uchungaji katika nyumba ya Labani: Miaka hii ishirini nimekaa kwako; kondoo zako wala mbuzi zako wake hawakuharibu mimba wala waume katika wanyama wako sikuwala. Kilichoraruliwa na hayawani sikukuletea, mimi mwenyewe nimetwaa hasara yake, wewe umekidai katika mkono wangu, ikiwa kilichukuliwa mchana, au ikiwa kilichukuliwa usiku. Hii ilikuwa hali yangu; mchana jua likanipata, na baridi usiku, usingizi ukanitoka machoni mwangu. Miaka hii ishirini nimekaa nyumbani mwako; nilikutumikia miaka kumi na minne kwa binti zako wawili, na miaka sita kwa wanyama wako, nawe umebadili mshahara wangu mara
3 kumi. Kama Mungu wa baba yangu, Mungu wa Ibrahimu na Hofu ya Isaka, hangalikuwa pamoja nami, hakika sasa ungalinifukuza mikono mitupu. Mateso yangu na kazi za mikono yangu Mungu ameziona, akakukemea usiku huu. (Mwanzo 31:38 42) Ndugu Wana-Dayosisi, Hayo ndiyo maisha ya mchungaji bora wa kondoo. Maaskofu wanaitwa wachungaji wa kondoo wa Bwana. Wanabeba mengi. Wanavumilia mengi. La muhimu kwao si uhodari tu wa uongozi, bali pia moyo wa upole, uvumilivu, na kuwa tayari kufanya kazi katika mazingira magumu, na kuwalinda kiroho na kimwili wale waliokabidhiwa kwao kuwaongoza. Maneno ya Yakobo akiagana na Labani ni maneno yanayofaa kusemwa na kiongozi yoyote wa Kanisa aliyefanya na kumaliza vizuri kazi yake. Ndugu Viongozi wa Kanisa: Taifa letu halina dini rasmi. Na hivyo Serikali haiko madarakani kupendelea dini au madhehebu yoyote ya dini. Lakini Serikali inatambua na kuheshimu uhuru wa imani ya dini wa kila raia; na inachukulia kwa uzito mkubwa wajibu wake kuhakikisha kila raia anayo haki na uhuru wa kuamini na kuabudu apendavyo ili mradi havunji sheria, na haingilii uhuru wa raia mwingine naye kuamini na kuabudu apendavyo. Nasema hivyo kwa sababu inaonekana wapo watu ambao wanataka Katiba ya Nchi yetu ilinde haki yao peke yao ya kuabudu. Unajua, mambo ya imani ni magumu sana, na nyeti sana. Maana, kila muumini anaamini kwa dhati kabisa kuwa aaminivyo na aabuduvyo yeye ndivyo sahihi, na ndivyo Mwenyezi Mungu atakavyo na alivyoagiza. Katika hali hiyo, njia pekee ya kuhakikisha amani na usalama katika jamii ni kutoa ruhusa kwa kila mtu kuamini na kuabudu apendavyo, lakini bila kudhihaki, kudharau, kutukana, kubeza au kupuuza imani na ibada za wengine. Naomba sana kila Mtanzania azingatie kanuni na wajibu huo wa kuheshimu imani na ibada za wenzake. Tusiwe wabinafsi. Tusigombane. Tusidharauliane. Maana hakuna binadamu yeyote mwenye ufunguo wa mbinguni. Kwa hiyo hayuko mwanadamu ambaye ataamua nani mwenye haki ya kuingia mbinguni na nani mkosaji wa kwenda kuzimu. Sasa kwa nini tusivumiliane, na tukamwachia Mwenyezi Mungu mwenyewe aamue nani kati yetu mwenye haki na nani mkosaji? Lipo tatizo la msingi katika mambo ya imani za dini. Kwa kadri mtu anavyojihisi amemkaribia Mwenyezi Mungu, au ameokoka, ndivyo anavyokuwa hatarini kutumbukia kwenye mtego wa kushawishika kuwaona wengine kuwa ni wakosefu, waliopotea,
4 wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine. Kazi hiyo tumwachie Mwenyezi Mungu. Ndugu Viongozi wa Kanisa, Kama ilivyo kawaida yangu, nipatapo fursa kama hizi, napenda kutambua, kwa shukrani, mchango wa mashirika ya dini katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika nchi yetu. Leo pia napenda nitoe shukrani zangu za dhati kwa mchango wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania kwenye ujenzi na uendeshaji wa huduma za jamii. Na kwa njia ya pekee nampongeza na kumshukuru Baba Askofu, Dkt. Erasto Kweka, ambaye katika miaka yake yote ya uongozi wa Dayosisi hii amekuwa mkereketwa mkubwa, kwa imani na kwa vitendo, wa maendeleo kwa jumla, lakini hasa maendeleo ya elimu, afya na maji. Kwa niaba ya Serikali, nakushukuru sana Baba Askofu Dkt. Erasto Kweka, kwa mchango wako mkubwa, na ushirikiano wako. Kwa pamoja tumefanya kazi kubwa kwa maendeleo na ustawi wa wananchi katika Dayosisi yako na kwingine. Unayo haki kuyaonea fahari mafanikio hayo. Napenda kumhakikishia Askofu mpya, Baba Askofu Martin Fataeli Shao, kiwango hicho hicho cha ushirikiano tulichokupa wewe, ili kwa pamoja tudumishe na kuendeleza kazi nzuri ya Kanisa kwa maendeleo na ustawi wa wananchi. Baba Askofu: Tunashirikiana vizuri kwenye mambo mengi. Lakini napenda kujenga hoja ya kushirikiana pia katika kubadilishana mawazo. Ni jambo la kusikitisha kuwa yapo matatizo mengi duniani ambayo chanzo chake ni kukosekana kwa mawasiliano na majadiliano baina ya watu au taasisi mbalimbali. Binadamu tumeumbwa tofauti, tukakulia katika mazingira tofauti, tukaelimika tofauti, na tukapewa majukumu tofauti hapa duniani. Haiwezekani tukawa na uelewa au uzoefu sawa wa kila jambo, au tukawa na mtazamo mmoja. Mimi ninaamini kuwa, ukiacha kando yale mambo ya kiroho, kwenye mengine yote yaliyobaki hakuna sababu ya kutokuwa na mawasiliano, mashauriano, na kubadilishana mawazo baina ya Serikali na viongozi wa dini katika ngazi mbalimbali. Hapo ndipo kila upande utauelewa vizuri upande mwingine, na hasa kuelewa chanzo cha tofauti za mtazamo na mikakati. Maelewano ni mwanzo mzuri wa ushirikiano na kuheshimiana, hata pale ambapo hatukubaliani kwa kila jambo. Inawezekana, na wala si ajabu, yakatokea mambo ya kiserikali yasiyowapendeza viongozi wa dini. Pengine kwa sababu za kweli, za msingi; lakini pia pengine kwa kutoelewa undani wa jambo lenyewe na mazingira
5 yake. Inawezekana pia wakati mwingine yakawepo mambo ya kidini yasiyowapendeza viongozi wa Serikali. Pengine kwa sababu za kweli, za msingi; lakini pia pengine kwa kutoelewa undani wa jambo lenyewe na mazingira yake. Katika hali hiyo, ushauri wangu ni kuwa uwepo utaratibu na tabia kwa viongozi wa dini na wale wa Serikali kujadiliana zaidi, badala ya kusemana zaidi. Mimi nina uhakika kuwa Mwenyezi Mungu, ambaye serikali zipo madarakani kwa ridhaa yake, atapendezwa zaidi akiona viongozi wa dini na viongozi wa Serikali wakiwa wabia wa kweli katika kuwahudumia viumbe wake. Hakuna raia wa kawaida, wa dini yoyote au dhehebu lolote la dini, ambaye atafaidika kwa magomvi kati ya Serikali na viongozi wa dini. Ndugu Viongozi wa Kanisa: Tanzania tumepiga hatua kubwa, kuliko Waafrika wenzetu wengine, katika kujenga hisia za utaifa na kuziweka mbele, badala ya kutanguliza hisia za udini, ukabila na umajimbo. Lakini hata kwetu Watanzania, bado unasikia minong ono ya udini, ukabila na umajimbo. Minong ono hiyo inasikika kwenye siasa, hasa tunapoelekea kwenye uchaguzi; na nimesikia, kwa mshangao, kuwa hata kwenye dini ipo minong ono ya ukabila na umajimbo. Nashukuru sana kuwa, kwa ujumla, viongozi wa dini wameungana na Serikali kuonya na kukemea mwelekeo wa kutaka kurejesha mambo ya udini, ukabila na umajimbo katika nchi yetu. Viongozi wa dini wanaheshimika sana kwenye jamii. Kwa hakika Serikali inawaheshimu sana. Viongozi wa dini kwa ujumla ni wasomi na waelewa wa mambo. Kwa heshima wanayopewa, na uelewa tunaoamini wanao, viongozi wa dini wana ushawishi mkubwa katika jamii. Naomba sana waelekeze ushawishi wao kwa yaliyo mema kwa taifa letu; na usiwe ushawishi wa maneno tu, bali pia ushawishi kwa mfano wa vitendo vyao wao wenyewe. Mtakubaliana nami kuwa yaliyo mema kwa taifa letu ni maendeleo, ni umoja, ni utaifa, ni upendo na ni mshikamano. Na kama hayo ndiyo malengo yetu sisi sote, kwenye dini na kwenye siasa, lazima tutumie majukwaa yote, ya dini na siasa, kuhubiri na kushawishi uimarishaji wa taifa letu kwa kukataa mambo yanayodhoofisha umoja wetu, kama vile udini, ukabila na umajimbo, na kuhimiza yale tu yaliyo mema kama vile maendeleo, umoja, utaifa, upendo na mshikamano. Ushawishi wetu kwenye siasa kama kwenye dini uwe wa sisi wenyewe kwanza kuamini, kisha kunena na hatimaye kutenda. Kauli zetu na vitendo vyetu viwe na mwelekeo mmoja, na mfano kwa wengine. Nikiwa Mkristo mwenzenu, sisahau maneno ya hekima yaliyo katika Waraka wa Yakobo kwa Watu Wote:
6 Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je, ile imani yaweza kumwokoa? Ikiwa ndugu mwanamume au mwanamke yu uchi na kupungukiwa na riziki, na mtu wa kwenu akamwambia, Enendeni zenu kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini asiwape mahitaji ya mwili, yafaa nini? Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake. (Yak. 2:14 17) Ndugu Wananchi: Hali ni hiyo hiyo kwenye mambo ya kidunia. Kwenye majukwaa ya kisiasa, na yale ya kidini, tunaweza kuhubiri sana umoja wa kitaifa; tunaweza kulaani udini, ukabila na umajimbo. Ni muhimu kufanya hivyo, lakini peke yake haitoshi. Lazima kauli hizo zithibitishwe kwa vitendo. Tunaelekea kwenye Uchaguzi Mkuu mwakani. Na uchaguzi unaweza kuimarisha umoja na utaifa wetu. Lakini ukitekwa nyara na wanaohubiri jambo moja, na kutenda jambo jingine, uchaguzi huo unaweza kuathiri sana umoja na utaifa wetu. Nawasihi sana wanasiasa, na viongozi wa dini: Twende kwenye kipindi cha uchaguzi tukitetea imani yetu ya umoja na utaifa, kwa kauli, lakini hasa hasa kwa vitendo. Kisitokee chama cha siasa, na asitokee mgombea kwenye uchaguzi, kukita kampeni zao kwenye kabila fulani, dini fulani au kanda fulani. Vilevile zisitokee kama ilivyokuwa kwenye baadhi ya chaguzi zilizopita Jumuiya za dini kutumia heshima yao kubwa, na ushawishi wao mkubwa, kuwachagulia wafuasi wao wagombea wanaostahili kuungwa mkono, au chama cha kukipigia kura. Katiba ya Nchi ndiyo imani yetu kitaifa. Kila mtu akiulizwa atasema anaamini binadamu wote ni sawa, kwamba wanastahili heshima, kwamba wana uhuru kwenye mambo ya imani za dini, na mvuto wa kisiasa. Lakini imani hiyo imekufa nafsini mwake kama haijidhihirishi kwa vitendo. Naomba sana twende kwenye Uchaguzi Mkuu mwakani tukiwa tumeamua kutekeleza imani zetu za usawa, umoja, utaifa, mshikamano na uhuru wa kuamua, kwa vitendo. Ndugu Viongozi wa Kanisa: Namalizia kwa kukupongeza tena Baba Askofu, Dkt. Erasto Kweka, kwa kuhitimisha uongozi wako wa Dayosisi hii na kwa ushirikiano wako. Nakushukuru kwa kunialika mimi na Mama Mkapa kushuhudia unapohitimisha kazi yako kubwa, ya kuongoza Dayosisi hii kwa miaka mingi, na kuikabidhi salama kwa awamu nyingine ya uongozi, ikiwa imepiga hatua kubwa ya maendeleo ya kiroho na kimwili tangu ulipokabidhiwa kuiongoza. Nakupongeza sana,
7 na ninakushukuru sana. Pongezi hizi tunazitoa pia kwa Mama Askofu Kweka ambaye nina uhakika amekuwa nguzo yako katika miaka yote hii ya uongozi wako wa Dayosisi hii. Kwa pamoja tunawatakieni mapumziko mema, furaha, afya njema, maisha marefu na baraka tele za Bwana. Nakupongeza sana Baba Askofu Martin Shao kwa heshima hii, na madaraka haya makubwa, uliyopewa. Nampongeza pia Mama Askofu Shao ambaye nina uhakika atakuwa nguzo yako katika uongozi wako. Kwa upande wa Serikali tunakuhakikishia ushirikiano mkubwa sana katika kazi zako. Baba Askofu: Nimeuelezea wadhifa uliopewa leo kuwa mzigo mzito. Nami pia, kwa muda wa miaka 8 na nusu sasa, katika medani nyingine, nimebeba mzigo mzito kama huo. Katika kutekeleza jukumu la mzigo huo, mara kwa mara nimefarijiwa na maneno ya Utenzi wa Roho yafuatayo: HYMN We fish in vain who fish alone And think ourselves the harvest s lord, For we but catch what you have sown In seas we neither make nor own, And have no claim to work s reward. The sea and all their fish are yours, And we your servants at the oar; Then let us work while night endures Until the rising sun assures That you await us on the shore. Twasumbuka bure tuvuao peke yetu Kujidhania sisi ndio bwana wa mavuno, Maana hatuvuni ila ulichopanda wewe Katika bahari tusizoziumba wala kuzimiliki, Na wala hatustahili malipo kwa kazi hizo. Bahari na samaki vyote ni vyako,
8 Tulichoshika watumishi wako ni makasia; Tufanye kazi basi usiku ungalipo Hadi pambazuko litufariji Kuwa wewe watungoja pwani. Baba Askofu Shao: Namwomba Mwenyezi Mungu azidi kukubariki na kukuongoza, wewe na Mama Askofu Shao, na kukupeni hekima na busara. Ahsanteni kwa kunisikiliza. Bwana Asifiwe!
Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, KWENYE SHEREHE YA KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA, TAREHE 08 JUNI 2008, MSIMBAZI CENTRE, DAR ES SALAAM Mhashamu
More informationInformation for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013
www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper
More informationAdhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu
Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu Nabii Musa alipotoka mlima Sinai kupewa amri kumi za Mungu zilizoko kwenye kitabu cha Kutoka 20:1 17, Mungu alimpa na sharia zingine ambazo lengo lake
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationUfunguo wa Kutaalamika Haraka
0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11
More informationusudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-
Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa
More informationUshindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT
Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT 1 Ushindi Ndani ya Kristo Na W. W. Prescott Mfasiri: M. Mwamalumbili Victory in Christ - Kiswahili 2 Yaliyomo Alinipenda Mimi Aliishi kwa ajili Yangu Mimi Alikufa
More informationWatumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1
Watumishi Wa Kristo na Ellis P. Forsman Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1 Watumishi Wa Kristo na Ellis P. Forsman Oktoba 14, 2011 Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 2 Sisi ni watumishi Watumishi
More informationEllen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar
Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ukristo leo unadhihirisha waumini karibu bilioni mbili katika maelfu ya madhehebu tofauti na tofauti na madhehebu. Kati ya hizi, zaidi ya 500 madhehebu
More informationPDF created with pdffactory trial version
المملكة العربية السعودية وزارة التعليم العالي الجامعة الا سلامية بالمدينة المنورة عمادة البحث العلمي قسم الترجمة تعريف موجز بالا سلام بل( لغة السواحلية) ١ بسم االله الرحمن الرحیم MAELEZO KWA UFUPI KUHUSU
More informationKuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu
134 Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu Picha tuliyonayo kuhusu Mungu ni mojawapo ya kizuizi kikubwa cha kupata uponyaji wetu. Mara nyingi huwa hatujui vizuri kwamba Mungu anatupenda kwa hivyo angependa
More informationTheolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College
Theolojia 1 Ujumla Mike Taylor Semester 1 2014-2015 Munguishi Bible College MIKE TAYLOR 2014 THEOLOJIA 1 i THEOLOJIA Utangulizi! 1 1. Kumfahamu Mungu katika Injili! 3 1.1. Mawazo Makuu 3 1.2. Maana ya
More informationApril 14, 2016 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 52
MOMBASA COUNTY ASSEMBLY HANSARD REPORT Thursday, 14 th April, 2016 The House met at 2.48pm. (Hon. Deputy Speaker (Mr. Mswabah Rashid) in the Chair) PRAYERS Hon. Deputy Speaker (Mr. Mswabah Rashid): Kindly
More informationWEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23
Toleo X Toleo 23 WEWE NI NANI? (Habari ifuatayo ni hadithi ya mambo ambayo yamenakiliwa katika Matendo 19:10-20 SUV). Paulo mtume wa Yesu Kristo alihubiri katika mji wa Efeso kwa miaka miwili. Katika muda
More informationShabaha ya Mazungumzo haya
Karibu Katika Mazungumzo Kuhusu Mchakato wa Uhamasishaji Maendeleo ya Kanisa na Jamii CCMP/UMOJA Shabaha ya Mazungumzo haya Kuwafahamisha viongozi wa makanisa kuhusu Mchakato wa CCMP ambao umekuwa ukitumika
More information"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.
KUJA KWA KRIST0 MARA YA PILI "ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28. Mara nyingi sana kuja kwa Kristo mara ya pili huangaliwa tu kama fundisho la dini. Ni
More informationUnited Pentecostal Church June 2017
Kwa Nini Tusali? Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa "Chagua" Ladies Prayer International kwa Facebook United Pentecostal Church June 2017 Tuko na wafuasi Facebook katika Marekani, Hong Kong, Philippines,
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More informationRoho Mtakatifu Ni Nini?
Roho Mtakatifu Ni Nini? kwa ajili ya mkutano. Mkutano huu utakuwa tofauti, kidogo na ile ya kawaida tunayokuwa nayo hapa. Kwa kawaida, kila wakati tunapokuja pamoja hapa, ni mkutano kwa wa kwa ajili ya
More informationKimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:
Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P. 21425,Dar es Salaam. Simu: +255 713 607 207 edkissuu@gmail.com Katuni zimechorwa na: Adam Lutta Babatau Inc. Box 13565 Dar es salaam, Simu:+255 713 474200
More informationMELKISEDECK LEON SHINE. katoliki.ackyshine.com
katoliki.ackyshine.com SALA ZA ASUBUHI Kwa jina la Baba.. Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,Mwana na Roho. Nilinde tena siku hii,niache dhambi nikutii.naomba sana
More informationMSAMAHA NA UPATANISHO
Hakimiliki 2007-2017 na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa. MSAMAHA NA UPATANISHO na Jonathan M. Menn B.A., Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, 1974 J.D., Cornell Law School, 1977 M.Div., Trinity Evangelical
More informationNia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu?
Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu? (Attitude Towards Christ Do you Honor Him?) Na Ellis P. Forsman (4-Attitude Towards Christ - Do you Honor Him) 1 Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu? (Attitude Towards
More informationHaja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (
Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Haja Ya Dini Haja Ya Dini Author(s): Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi [3] Publisher(s): Bilal Muslim Mission of Tanzania [4] Katika kijitabu
More informationMUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI
MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. Mwanzo 1:1 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi. Wakolosai
More informationAgano Lililofunikwa Kwa Damu
Agano Lililofunikwa Kwa Damu na Ellis Forsman Agano Lililofunikwa Kwa Damu (The Blood-Sealed Covenant) 1 Agano Lililofunikwa Kwa Damu na Ellis Forsman Oktoba 14, 2012 Agano Lililofunikwa Kwa Damu (The
More informationKWA NINI SISI SI MADHEHEBU?
KWA NINI SISI SI MADHEHEBU? Nimejaliwa kurudi mimbarani tena baada ya kama,, nadhani, karibu kutokuwepo kwa muda wa miezi mitatu. Kindi wamekuwa na wakati mgumu, na mimi pia. Loo, nimeburudika, hata hivyo,
More informationTAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA
TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0
More informationHati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako
More informationUTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha
UTARATIBU WA KANISA Tumemaliza hivi punde ule mkutano mkubwa wa siku, tano usiku kwenye Maskani, ambapo, kwa neema ya Mungu na kwa msaada Wake, nimejaribu sana, kwa Maandiko, kuliweka Kanisa la Bwana Yesu
More informationIBADA NA UMOJA WA KANISA Na Mchg. Dkt. Msafiri Mbilu
1 IBADA NA UMOJA WA KANISA Na Mchg. Dkt. Msafiri Mbilu SOMO LA I Kama kuna nyakati katika Historia ya Kanisa ambazo tunapaswa kuangalia kwa undani juu ya IBADA NA UMOJA WA KANISA, ni sasa. Sababu kubwa
More informationJE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?
JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? JOE CREWS 1 JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI? Na Joe Crews (Hotuba Na. 16 ya Mambo ya Kweli Yanayoshangaza) Mfasiri: M. Mwamalumbili Is It Possible To
More informationORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI SPIKA MHE. PANDU AMEIR KIFICHO. Rais.
ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI SPIKA MHE. PANDU AMEIR KIFICHO 1.Mhe. Kamal Basha Pandu 2.Mhe. Ali Mzee Ali 3.Mhe. Shamsi Vuai Nahodha Naibu Spika/Jimbo la Rahaleo. Mwenyekiti wa Baraza/Uteuzi
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationKifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1
Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Na Ellis P. Forsman Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1 Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Na Ellis P. Forsman Oktoba 11, 2011 Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 2 Kifo
More informationNGUVU. Utangulizi. Yesu alisema,
NGUVU Utangulizi Kwas miaka mingi nimemtafuta Bwana ili aachilie mazingira mazuri ya uwepo wake, nguvu na utukufu wake kudhihirika. Tumeona na kujua matokeo ya yale Bwana ametufunulia. Ikiwa unatafuta
More informationwalozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w
MAMLAKA Tunamshukuru Bwana kwa vile alivyo na yale aliyoyatenda. Tukiweza tu kumfikiria hata tukiwa na mahitaji mbalimbali, yeye atatutimizia. Tusiwatazame watu, tusijitazame sisi wenyewe, tumtazame Mungu
More informationKifo Na Mbingu (Death And Heaven)
Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) Na Ellis P. Forsman The Rapture And Millennialism 1 Kifo Na Mbingu Na Ellis P. Forsman Octoba 11, 2011 The Rapture And Millennialism 2 Kifo Na Mbingu Heb. 9:27 Ili kufika
More informationUongozi Siri Na Larry Chkoreff. Version 1.2 Desemba 2010
Uongozi Siri Na Larry Chkoreff Version 1.2 Desemba 2010 Kimetafsiriwa na kuchapishwa na: Cistern Materials Translation & Publishing Center, Nairobi, Kenya Barua pepe: info@cisternmaterialscenter.com www.cisternmaterialscenter.com
More informationInavyodaiwa na wanaochanganya Biblia. Ellis Forsman. Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1
Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia na Ellis Forsman Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1 Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia na Ellis Forsman Oktoba 8, 2011 Inavyodaiwa
More informationNdugu na dada zangu wapendwa,
UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2014 Na Rais Thomas S. Monson Upendo Asili ya Injili Hakika hatuwezi kumpenda Mungu kama hatuwapendi wasafiri wenzetu katika safari hii ya maisha duniani. ninafurahia mawazo
More informationMACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI
This booklet on Becoming a Parent was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at. MACHAGUO
More informationMaisha Yaliyojaa Maombi
(A Prayer-Filled Life) na Terry Warford (A Prayer-Filled Life) 1 (A Prayer-Filled Life) na Terry Warford Nov 5, 2011 (A Prayer-Filled Life) 2 Sura ya nne nay a tano ya kitabu cha Ufunuo ni vifungu vinavyovutia.
More informationTora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA
SOMO LA KWANZA UTANGULIZI KWA TORA For videos, study guides and other resources, visit Third Millennium Ministries at thirdmill.org. 2014 nathird Millennium Ministries Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu
More informationKAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU?
KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU?, Asante, Ndugu Neville, na habari za jioni, marafiki. Nimerudi tena. Sikupata ila masaa manne asubuhi ya leo. Hiyo ni aibu. Na baada ya
More informationMaisha Ya Mkristo Ni Nini?
Maisha Ya Mkristo Ni Nini? na Ellis P. Forsman Maisha Ya Mkristo Ni Nini? (What Is The Christian Life?) 1 Maisha Ya Mkristo Ni Nini? na Ellis P. Forsman Oktoba 17, 2011 Maisha Ya Mkristo Ni Nini? (What
More informationMUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.
MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO. MUHTASARI WA UTANGULIZI WA THIOLOGIA YA USHIRIKA WA NAFSI TATU ZA UUNGU. GRACE COMMUNION INTERNATIONAL LIVING AND SHARING THE GOSPEL MUNGU ANADHIHIRISHWA NA
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationKiu Cha umtafuta Mungu
ZAIDI YA NAKALA MILLION 3 ZIMECHAPISHWA KATIKA LUGHA 59 KOTE DUNIANI K Kiu Cha umtafuta Mungu Huduma ya Daktari Richard A. Bennett ilianza katika mabaraza ya miji. Akiwa mwanafunzi chuoni, alikumbana na
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationMakasisi. Waingia Uislamu
1 Makasisi Waingia Uislamu 2 KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU MAKASISI WAINGIA UISLAMU Yaliyomo 1. KASISI YUSUFU ESTES ALIYEKUWA MFANYABIASHARA WA KIKRISTO & MUHUBIRI (USA)...
More informationKutetea Haki za Binadamu
Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and
More informationNa Itafunika Wingi Wa Dhambi
Na Itafunika Wingi Wa Dhambi na Ellis Forsman Na Itafunika Wingi Wa Dhambi (And Shall Hide A Multitude Of Sins) 1 Na Itafunika Wingi Wa Dhambi na Ellis Forsman Oktoba 10, 2011 Na Itafunika Wingi Wa Dhambi
More informationRISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO
RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO 1 RISALA FUPI copyright Hidaya Creativity, publishing Department. P.O. BOX 44799, 00100, GPO, NAIROBI-KENYA. Haki
More informationYEHOVA-YIRE 1. 2 Baba yetu wa Mbinguni, tunakikaribia Kiti Chako cha. 3 Tunakushukuru kwa kutuzuru jana jioni. Tunaomba
YEHOVA-YIRE 1 Na tuendelee kusimama tu kwa muda kidogo wakati, tumeinamisha vichwa vyetu kwa maombi. Tunapoinamisha vichwa vyetu, sijui ni wangapi usiku huu wangetaka kukumbukwa katika maombi, una jambo
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationLALA. Terry Warford. LALA (Sleep - Terry Warford) 1
LALA na Terry Warford LALA (Sleep - Terry Warford) 1 LALA na Terry Warford Novemba 6, 2011 LALA (Sleep - Terry Warford) 2 LALA Kulala ni sehemu muhimu katika maisha yetu ya kila siku, tukiipa akili zetu
More informationGRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI
GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI Utambulisho Grace Communion International ni muungano wa washiriki kutoka pembe mbali mbali za dunia hasa nchi zenye washiriki kwa sasa ni 100. Wito wetu ni
More informationUsimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya
Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma
More informationMukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika
Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika (A Summary Of Arguments For And Against Individual Communion Cups) Na J D Logan Communion Cups) 1 Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi
More informationKANISA NA UAMSHO Na Mchg. Dkt. Faith Lugazia
1 KANISA NA UAMSHO Na Mchg. Dkt. Faith Lugazia Awali ya yote namshukuru Mungu wa Utatu aliyenitia nguvu na kuniwezesha kusimama mbele yenu wajoli wenzangu. Pili ninaishukuru Halmashauri Kuu ya Kanisa la
More informationWAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen
1 Index latest update 26. feb. 2008 WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen Wafunaji wa nafsi ABC Mark 16:15-20 Huduma/uiinjilisti Wakristo wachache sana wameitikia mwito wa
More informationKitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake
Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationMIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara
1 MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara 1. UTANGULIZI Miaka 500 ya matengenezo ya Kanisa inatufanya tuangalie nyuma na kuona jinsi Mungu alivyotumia wanadamu
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationB. Wanafunzi watapata ufahamu mkubwa wa kitabu hiki, na jinsi kinavyofundisha kuhusu kanisa.
Waefeso Mtaala I. Habari kwa Ujumla A. Mkufunzi: Don Walker na kutafsiriwa na Chris Mwakabanje B. Kila darasa ni takribani dakika 38. II. Maelezo na Kusudi A. Mafunzo haya ni uchambuzi wa kina katika Waefeso,
More informationAzimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]
This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)
More informationNdugu na dada zangu wapendwa,
UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2013 Utiifu Huleta Baraka Elimu ya ukweli na majibu ya maswali makuu huja kwetu tunapokuwa watiifu kwa amri za Mungu. Ndugu na dada zangu wapendwa, nina shukrani jinsi gani
More informationWAKOLOSAI MTAALA. B. Maoni: Tunapendekeza uwe na fafanuzi (commentary) yoyote yenye kushikilia mafundisho ya awali (conservative) katika Wakolosai.
WAKOLOSAI MTAALA I. MAELEZO KWA UJUMLA. A. Mwalimu: Don Walker B. Mkalimani: Chris Mwakabanje C. Kila darasa linachukua takribani dakika 38. II. III. MAELEZO NA MALENGO. A. Kujifunza kwa kina Waraka kwa
More informationMwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza
Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)
More informationMASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO
MASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO Sasa, kama ye yote ana swali lo lote wanalotaka kulileta,, basi, hebu yasogezeni tu juu hapa, acha mtoto fulani ayalete au vyo vyote mtakavyo. Au, labda, tukimaliza
More information2
2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 CKRC VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, KALOLENI CONSTITUTENCY, HELD AT MARIAKANI SECONDARY
More informationNdugu na dada zangu wapendwa,
UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, NOVEMBA 2011 Na Rais Thomas S. Monson Simama Pahali Patakatifu Mawasiliano na Baba yetu aliye Mbinguni pamoja na maombi yetu Kwake na maongozi Yake kwetu ni muhimu ili tuweze
More informationKwa Nini Yesu Alikufa Msalabani?
Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani? na Ellis P. Forsman Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani? (Why Did Jesus Die On The Cross?) 1 Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani? na Ellis P. Forsman Oktoba 17, 2011 Kwa Nini Yesu
More informationTumaini Kwa Afrika. Thomas Schirrmacher. Hoja 66. Dibaji na Prof. Mchungaji Dk. Thomas K. Johnson. Thomas Schirrmacher Tumaini Kwa Afrika TASCM RVB
Tunawezaje kudhihirisha msingi wa Kibiblia wa tumaini letu na kulithibitisha kwa Wakristo na kwa wasioamini walioshirikishwa? Tunawezaje kutamka matumaini yetu kwa Wabunge, kwa wafanya biashara au kwa
More informationUNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW
Kama unataka kujifunza zaidi njia ya Mkristo wa kweli anavyopaswa kuishi, basi ni lazima ujifunze Biblia. Ili kukusaidia; Kanise la Christadelphian Bible Mission limechapisha kijitabu kuhusu mafunzo ya
More informationMzabibu Na Matawi. (The Vine And The Branches) Ellis P. Forsman. Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) 1
Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) na Ellis P. Forsman Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) 1 Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) na Ellis P. Forsman Oktoba 15, 2011 Mzabibu
More informationMwongozo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato
Mwongozo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato 1 Mafungu yote yaliyonukuliwa kwa ruhusa kutoka katika Biblia ya Kiswahili Union Version 1952 (Ilishahihishwa 1989) ISBN 978 Haki miliki 2013 Haki zote zimeifadhiwa
More informationJHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI
JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika
More informationmaombi, kabla tu hatujalifungua Neno hili la Kiungu.
ALAMA YA MNYAMA Sasa, kesho usiku Daima tunaonyesha jambo moja,, Bwana Yesu Kristo, ni hivyo tu, na lo lote ambalo ni mapenzi Yake ya Kiungu kwetu kufanya. Lakini kama ni mapenzi Yake ya Kiungu kesho usiku,
More informationMafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally
Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo Na Andrew Connally 1 YALIYOMO Milango ya Kitabu: Ukurasa: 1. Mungu-Kuwako kwake na hali yake 03 2. Huyo Kristo-Nafsi yake na kazi yake 12 3. Maandiko Matakatifu ni yenye
More informationOktoba-Desemba
Oktoba-Desemba 2014 1 Habari za Unabii wa Biblia 8 13 24 Katika toleo hili: 25 28 33 3 MwanaFiladelfia wa Karne ya 21 ni nani? Je, Yesu alifundisha kwamba kungekuwepo na tofauti kubwa baina ya Wakristo
More informationVITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI
VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI Asante, Ndugu Neville, Bwana akubariki. Bila shaka ni, majaliwa kuwa hapa usiku wa leo. Nina furaha sana ya kwamba Mungu alituruhusu
More informationCONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC)
CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, SIGOR CONSTITUENCY, AT KIBICHBICH D.O. S OFFICE 2 ON Monday 1 st July 2002 CONSTITUENCY PUBLIC HEARING SIGOR
More information2
2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 38 39 40 41 42 43 44 45 46 47 48 49 50 51 52 53 54 55 56 57 58 59 60 61 62 63 64 65 66 67 68 69 70 71
More informationONYO LA MWISHO KWA DUNIA
ONYO LA MWISHO KWA DUNIA Mpango wa Ulimwengu Mpya Unakuja!. Viongozi wa Ulimwengu. Jinsi ya kuukwepa usiwe wanautaka mhanga. Unaungwa mkono na. Kuanguka kwake ghafula wengi na kwa ukamilifu. Ulitabiriwa
More informationUZAO WA NYOKA. 2 Basi, usiku huu, tuna malimbuko tu ya utukufu huo mkuu. 3 Kwa uchaji tunasimama kwa imani yetu katika Uwepo
UZAO WA NYOKA Mungu, Mungu aliye mkuu na mwenye nguvu, Yeye, aliyefanya mambo yote kwa nguvu za Roho Wake; na amemleta Yesu Kristo, Mwanawe wa pekee, aliyejitolea akafa kwa ajili yetu wenye dhambi, Mwenye
More informationMAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA
133 134 MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA Ni heri nione mahubiri kuliko kusikia moja siku yeyote ile. Ni heri mtu atembee nami kuliko kunionyesha njia. Jicho ni mwanafunzi mzuri na mwenye hamu kuliko sikio. Mausia
More informationUponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14).
41 Uponyaji Wa Laana Ijapokuwa baraka ni kinyume cha laana, kuna mambo yanayofanana katika vitu hivyo. Ni maneno yaliyotajwa, yaliyoamriwa, au kuandikwa katika Biblia kwa nguvu na mamlakao ya kiroh kwa
More informationCONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC)
CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) Verbatim Report Of CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, GANZE CONSTITUENCY, HELD AT GODOMA SECONDARY SCHOOL 2 ON Friday, 3 rd May 2002 VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY
More informationSilaha Za Shetani. Ellis Forsman. Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1
Silaha Za Shetani na Ellis Forsman Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1 Silaha Za Shetani na Ellis Forsman Oktoba 15, 2012 Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 2 Silaha Za Shetani 2 Kor. 2:11
More informationIMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE
IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE IMANI NA MATENDO IMANI NA MATENDO Hotuba na Makala za Ellen G. White Masomo kutoka katika Hotuba zake Kumi na Tisa zilizotolewa Nzima au kwa Sehemu kuanzia mwaka 1881
More informationHISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU 9 DESEMBA 2011.
Saint Augustine University of Tanzania From the SelectedWorks of Daudi Mwita Nyamaka Mr. Winter December 9, 2011 HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU
More informationCONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC)
2 3 CONSTITUTION OF KENYA REVIEW COMMISSION (CKRC) 4 VERBATIM REPORT OF 5 6 CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, ORGANISED GROUPS EMBAKASI CONSTITUENCY, HELD AT DANDORA KINYAGO SHOOL (GITARI MARIGU) ON 28 TH
More information