Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Similar documents
JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MOJA. Kikao cha Hamsini na Tatu Tarehe 19 Juni, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi)

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,

Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Human Rights Are Universal And Yet...

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

3 FEBRUARI, 2015 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA NANE. Kikao cha Saba - Tarehe 3 Februari, 2015

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE. Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Saba Tarehe 13 Aprili, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE. Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

MWONGOZO WA USHIRIKISHWAJI KATIKA KUPANGA MATUMIZI YA ARDHI WORLD BANK

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Kuwafikia waliotengwa

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

TIST HABARI MOTO MOTO

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA

ORODHA YA WAJUMBE WA BARAZA LA WAWAKILISHI SPIKA MHE. PANDU AMEIR KIFICHO. Shughuli za Serikali/Jimbo la Mwanakwerekwe.

UFUPISHO WA 35. Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji mazao: Clive James Chair, ISAAA Board of Directors

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

Kutetea Haki za Binadamu

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA MBILI. Kikao cha Tatu Tarehe 6 Septemba, (Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

MIONGOZO MIWILI KUPAA NA KUTUNGULIWA KWA AZIMIO LA ARUSHA

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA KUMI NA TISA. Kikao cha Pili - Tarehe 14 Aprili, 2010

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document)

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI

TANGA CEMENT PLC ANNUAL REPORT TAARIFA YA MWAKA.

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document)

13 APRILI, 2012 BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Nne Tarehe 13 Aprili, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA ISHIRINI KIKAO CHA KUMI NA MBILI TAREHE 22 JUNI, 2005

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017

Transcription:

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA, KATIKA UKUMBI WA KIMATAIFA WA MIKUTANO WA MWL. NYERERE, TAREHE 7 8, FEBRUARI, 2017, DAR ES SALAAM Mhe. Roeland Vande, Balozi wa EU Nchini Tanzania; Mama Bella Bird, Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia anayewakilisha Tanzania, Malawi, Burundi na Somalia; Dkt. Gero Carto, Mwakilishi wa Benki ya Dunia kutoka Roma; Wawakilishi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa; Viongozi Waandamizi wa Serikali mliopo katika Ukumbi huu; Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu; Mtakwimu Mkuu, Ofisi ya Mtakwimu Mkuu Zanzibar; Wataalam wote wa Takwimu kutoka Ndani na Nje ya Tanzania; Waandishi wa Habari; Wageni Waalikwa; Mabibi na Mabwana. Awali ya yote napenda nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuijalia nchi yetu amani. Amani, utulivu na umoja wetu ndiyo tunu kubwa ambayo inatupatia fursa ya kuwa wenyeji wa mikutano ya kimataifa kama mkutano huu wa leo ambao ni mahsusi kwa ajili ya kujadili matumizi bora ya takwimu zinazohusu mwenendo wa umasikini katika bara letu la Afrika. Ninawapongeza kwa dhati waandaaji wa mkutano huu kwa kuchagua mada muhimu sana kwa ajili ya kujenga ustawi na maendeleo endelevu ya wananchi wetu katika bara la Afrika. Nasema hivi kwa sababu kazi ya kuondoa umasikini ndiyo ajenda mama katika nchi zetu ili kujenga Afrika tunayoitamani, yaani Afrika yenye neema kama ilivyobainshwa katika Ajenda ya 2063 (Agenda 2063: The Africa we want). Umuhimu wa Mkutano huu ndiyo umenifanya nisafiri kutoka Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano. Kwa niaba ya Serikali Tanzania, napenda kuwakaribisheni nyote kwenye Mkutano huu wa Kimataifa wa siku mbili ambao nimeambiwa una washiriki takriban 150 kutoka ndani na nje ya Nchi. KARIBUNI SANA TANZANIA na karibuni katika Jiji la Dar es Salaam (The Harbour of Peace). Nimeelezwa kuwa lengo kuu la Mkutano huu ni kuwakutanisha wataalam mbali mbali kutoka pande zote za dunia chini ya uratibu wa Benki ya Dunia kujadili: (i) matumizi ya taarifa za ufuatiliaji wa hali ya umaskini katika Sera za Nchi ikiwemo Tanzania; na (ii) njia bora zaidi ya kupima hali ya umaskini ili iendane na dhana nzima ya viashiria 1

vilivyoanishwa katika utekelezaji wa Malengo Endelevu ya Maendeleo ya mwaka 2030. Wote mnafahamu kuwa kuna Malengo 17 ambayo tuliyaridhia kimataifa mwaka 2015 na katika hayo, lengo la Kwanza ni Kuondoa Kabisa Umaskini wa Mahitaji ya Msingi na Chakula ifikapo mwaka 2030. Nitumie nafasi hii kusema wazi kuwa tafsiri ya umaskini na namna ya kuupima umasikini hasa katika Nchi zinazoendelea imeendelea kuwa changamoto hususan kwa sisi Mawaziri wenye dhamana ya kusimamia sera za uchumi katika Nchi zaafrika Kusini mwa Jangwa Sahara. Kwa mfano, hivi karibuni kule Bungeni Dodoma, nilitumia takwimu za umasikini kimkoa (basic needs poverty line by region) na lengo langu lilikuwa ni kubainisha mikoa ambayo ni masikini zaidi hapa nchini. Katika mjadala uliofuata baadhi ya wabunge hawakukubaliana kama takwimu hizo kweli zinaakisi hali halisi ya kiwango cha umasikini katika mikoa yao ikilinganishwa na mikoa mingine. Aidha baadhi ya wabunge waliitaka Serikali kuja na programu maalum kupiga vita umasikini katika mikoa hiyo masikini zaidi. Naomba nitumie nafasi hii kutoa wito kwa Benki ya Dunia na ninyi mabingwa wa takwimu mnaoshiriki katika mkutano huu kuangalia upya moduli mbali mbali zinazotumika katika kupima hali ya umaskini katika Nchi zetu hizi ili kutuwezesha kubuni mikakati ya uhakika ya kupambana na umasikini katika nchi zetu. Wageni Waalikwa Mabibi na Mabwana Sote tunafahamu kuwa lengo kuu la Serikali yoyote duniani ni kuhakikisha kwamba, Wananchi wake wanaishi maisha bora zaidi na yenye neema na kipato cha kumudu gharama za mahitaji ya msingi (chakula, mavazi, makazi, elimu, afya, maji, umeme, usafiri, mawasiliano n.k). Kwa upande wa Serikali ya Awamu ya Tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sisi tumedhamiria kuinua kipato cha Wananchi wetu maskini kwa kuweka nguvu zaidi katika sekta ya Viwanda, hasa viwanda vidogo na vya kati ambavyo vinatumia malighafi zinazozalishwa hapa nchini na hasahasa kutokana na kilimo cha mazao, mifugo, uvuvi na madini mbalimbali. Sisi tunaamini kuwa viwanda vinavyoongeza thamani ya kila tunachozalisha ndivyo vitatupatia ajira za kutosha na hususan kwa vijana ambao ni zaidi ya asilimia 50 ya watu wote Nchini. Ni wazi kuwa utekelezaji wa azma hii ya Serikali itahitaji takwimu bora ili kuweza kufuatilia kama kweli mkakati huu unazaa matunda yaliyokusudiwa kwa maana ya kupunguza kwa kiwango kikubwa hali ya umasikini hapa nchini. Napenda nitumie fursa hii kusisitiza kuwa umaskini wa kipato na chakula ni changamoto kwa dunia nzima na hasa kwa nchi za bara la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na kuwa juhudi za ziada zinahitajika ili kukabiliana na changamoto hii. Kwa mujibu wa Takwimu za Benki ya Dunia za mwaka 2013 asilimia 10.7 ya watu wote duniani (7.1 Bilioni) walikuwa wakiishi chini ya dola 1.90 kwa siku ikilinganishwa na asilimia 12.4 mwaka 2012. Hata hivyo, pamoja na takwimu hizi za kuendelea kushuka kwa kasi ndogo ya umaskini duniani, mafanikio haya hayajaonekana wazi kwa baadhi ya Nchi zinazoendelea na hususan kwa Nchi zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara ikiwemo Tanzania hususan kutokana na ukweli kuwa 2

ukuaji wa uchumi wa nchi zetu unatoka zaidi kwenye sekta zinazoajiri wananchi wachache tena nyingi zikiwa zimejikita mijini sambamba na kasi kubwa ya ongezeko la idadi ya watu. Takwimu hizo zinaonesha kuwa, umaskini bado ni changamoto kwa watu wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara ukilinganisha na maeneo mengine ya dunia. Katika kipindi cha mwaka 2013 umaskini katika eneo hili ulipungua kwa asilimia 4 hivyo watu milioni 389 walikuwa bado wanaishi kwa kipato cha chini ya dola 1.90 kwa siku. Hii ina maana kuwa zaidi ya nusu ya watu maskini duniani walikuwa wanaishi Kusini mwa Jangwa la Sahara (chini ya dola 1.90 kwa siku). Taarifa hizi zinaonesha kuwa, wengi wa watu hawa maskini duniani wanaishi maeneo ya vijijini na hawana elimu ya kutosha, na zaidi wamejiajiri katika sekta ya kilimo ambapo zaidi ya nusu ni watoto wenye umri chini ya miaka 18. Ni dhahiri kuwa upimaji wa hali ya umaskini kwa kutumia kigezo cha Dola za Kimarekani 1.90 kwa siku kina changamoto zake baina ya Nchi na Nchi. Dkt. Blandina ameeleza baadhi ya changamoto na mimi naziunga mkono. Kuna baadhi ya vigezo vinavyotumika vingi havieleweki kwa wananchi wetu. Miasamiati mingi inayotumika kama Gini Coefficient wananchi wetu hawaelewi. Hivi kwa nchi kama Tanzania yenye ardhi ya kutosha ambayo kila Mwananchi anamiliki kipande cha ardhi na ambacho anaweza kukitumia kwa lengo la kustawisha kaya na kupunguza umaskini Je, kwanini tusihuishe kigezo cha US$1.90 kwa siku kisihuishwe kuzingatia umiliki wa ardhi? Kadhalika, naamini umiliki wa vifaa kama vile gari, nyumba, na vitu vingine vyenye thamani kubwa katika ngazi ya kaya navyo vinaweza kutumika kuhuisha vigezo vya umaskini. Hili ninawaachia nyinyi watalaam kutafakari kwa kina namna bora zaidi ya kupima umasikini katika mazingira ya nchi zetu. Utafiti wa mwisho wa Mapato na Matumizi ya Kaya uliofanyika Tanzania mwaka 2011/12 na ambao ulitupatia takwimu rasmi za hali ya umaskini hapa Nchini ulionesha kwamba, asilimia 28.2 ya Wananchi wote walikuwa na umaskini wa mahitaji ya msingi na chakula. Kiwango hiki cha umaskini kilipungua kutoka asilimia 38.6 mwaka 1990. Nimeelezwa utafiti mwingine unaandaliwa mwaka 2017/18 kwa kushirikiana na Benki ya Dunia. Nitapenda kuona utafiti unajibu maswali yangu niliyoyauliza hapo juu na baadhi ya wenzangu. Nina imani kubwa kuwa tukitumia tafsiri pana zaidi za umasikini kama nilizozitaja hapo juu ni dhahiri tutaona mabadiliko makubwa katika umaskini wa mahitaji ya msingi yakiwemo ya chakula. Ninasema hivi kwa sababu Serikali ya Awamu ya Tano, na kama zilivyokuwa kwa awamu zilizotangulia imejipanga kuendelea na juhudi za kukuza uchumi na kuondoa umaskini. Serikali itaendelea kuweka mazingira mazuri yatakayowezesha Wananchi 3

kukuza uchumi na kupunguza umaskini katika kaya zao. Juhudi kubwa inayofanyika ni kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa Nchi yenye uchumi wa kati unaotegemea zaidi viwanda ifikapo mwaka 2025. ; Kabla sijahitimisha maelezo yangu nitoe rai yangu kwenu kama ifuatavyo: Kwanza; kama mnavyofahamu uchumi wa Nchi ya Tanzania umeendelea kukua kwa wastani wa asilimia 7.0 kwa zaidi ya muongo mmoja na nusu sasa na kupunguza umasikini wa kipato hadi asilimia 28.2. Nina imani kuwa fursa zinazotokana na ukuaji huu wa uchumi huu ndizo zimetufikisha hapa tuliko na niwaombe tuendelee kutumia fursa zinazopatikana katika nchi zetu zinatumika ki-ukweli katika kuleta Maendeleo tunayotaka kuyaona. Pili; Viongozi tuliopewa dhamana ya kusimamia uchumi wa Nchi zetu na kuinua kipato cha Wananchi maskini tuendelee na dhana nzima ya kutumia takwimu bora ambazo ndizo macho na masikio ya Serikali yoyote ile duniani. Sisi Mawaziri wa Fedha na Uchumi katika Kikao cha Nane cha Umoja wa Afrika kilichofanyika Machi mwaka 2015 wote kwa pamoja tuliazimia kutumia takwimu rasmi katika kupanga mipango endelevu ya maendeleo ya Bara la Afrika na tulienda mbali zaidi kuwa kila bajeti ya Taifa ni lazima tutenge asilimia 0.15 ya bajeti yote kwa ajili ya kukusanya, kuchambua na kusambaza takwimu katika kupanga mipango ya maendeleo. Ninawaomba wenzangu kuwa tulitekeleze azimio hili. Tatu; napenda nitumie fursa hii kuwaomba watalaam mlioko hapa kutoka Nchi mbali mbali kuhakikisha kuwa mnatumia vigezo vya ndani ya Nchi (country specific definitions) na vya kimataifa kwa lengo la kutoa taswira nzima ya hali ya umaskini katika Nchi na mwendelee kuelimsha matumizi ya takwimu bora katika kupanga maendeleo ya Wananchi wa Afrika na dunia kwa ujumla. Hili ni jukumu lenu mlioko hapa kuhakikisha mnafuatilia Mipango-mikakati ya kuelimisha umma kuhusu matumizi ya takwimu bora na za wakati. Ninapoelekea kumalizia hotuba hii ya ufunguzi napenda kuishukuru Benki ya Dunia kwa kuleta Mkutano huu wa Kimataifa Nchini Tanzania na Balozi wa EU hapa Nchini kwa kuendelea kuisadia Tasnia ya Takwimu kupitia Mpango Kabambe wa Kitaifa wa Kuboresha na Kuimarisha Takwimu Tanzania. Serikali kwa upande wake inaahidi kuendelea kusaidia taasisi zetu za takwimu bara na Zanzibar na taasisi za mafunzo ya takwimu kuziwzesha zifanye kazi yake ipasavyo. Mwisho, napenda kuwaambia wageni wetu kuwa sisi Watanzania ni watu wakarimu. Ni watu wa Taifa lenye amani na mshikamano. Dar es Salaam tulipo hivi sasa ni salama kabisa. Aidha nchi yetu ina vivutio vingi vya utalii tena vya kipekee na maarufu ulimwenguni ikijumuisha mbuga za wanyama kama vile Serengeti, Ngorongoro, Mikumi, Manyara, Selous, Katavi na makazi asili ya sokwe mtu (chimpanzees) ya 4

Gombe magharibi mwa Tanzania. Aidha tuna Mlima Kilimanjaro - dari la Afrika (Africa's roof top), fukwe mwanana bahari ya Hindi (pristine beaches along the Indian Ocean) na visiwa vya Unguja na Pemba vinavyounda Zanzibar maarufu kama spicy islands n.k. Nitumie nafasi hii kuwashawishi mtumie fursa ya hii adhimu ya uwepo wenu hapa Tanzania kabla ya kurudi majumbani kwenu mtembelee vivutio hivi. Ninawahakikishia kuwa mtavifurahia na hamtasahau mtakayoyaona maishani mwenu. Naamini baada ya hapo wote mtageuka kuwa mabalozi wa kutangaza utalii wa Tanzania ambao umeendelea kuchangia vizuri katika kukuza uchumi wa Tanzania na kupunguza umaskini. Baada ya maneno haya naomba niseme kuwa Mkutano wa Kimataifa wa Kujadili Matumizi ya Takwimu za Umaskini na namna Bora ya Kupima Hali ya Umaskini Afrika, sasa umefunguliwa. ASANTENI KWA KUNISIKILIZA 5