Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

Similar documents
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Ufundishaji wa lugha nyingine

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue?

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo. Zanzibar, 7-10 Februari 2006

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

Shabaha ya Mazungumzo haya

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

Human Rights Are Universal And Yet...

Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Evaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

Mipango ya miradi katika udugu

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

Kutetea Haki za Binadamu

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

UHUSIANO WA MIKAKATI YA UFUNDISHAJI WA FASIHI YA WATOTO YA KISWAHILI NA UMILISI WA KUSOMA KATIKA SHULE ZA MSINGI, KASARANI, KAUNTI YA NAIROBI, KENYA

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

Kuwafikia waliotengwa

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

ORDER NO BACKGROUND

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

Makala ya Mshiriki wa Mafunzo

KISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA

Mwongozo wa Mwezeshaji

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO. Training and Research Support Centre

Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

HALIYA VITABUVYA WATOTOKATIKA TANZANIA

Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo

Transcription:

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna ya kuifafanua upya na kuhamasisha elimu bora kwa wote. Utafutaji wa Elimu bora nchini Tanzania una historia ndefu. Tukirudi nyuma hadi mwaka 1922, ubora na uhalisia wa Elimu nchini Tanzania uliwekwa wazi katika taarifa ya Tume ya Stokes (Stokes Commission Report). Baadaye, mnamo mwaka 1967, Rais Julius Nyerere alielezea dhana ya ubora katika sera yake ya Elimu ya Kujitegemea. Hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete alisisitiza suala la Elimu bora katika hotuba yake ya kuzindua Bunge mnamo tarehe 30 December 2005. Taarifa za vyombo vya habari kutoka nchini kote zinaonesha kuwa suala la ubora wa elimu linawashughulisha sana wazazi, wanafunzi na walimu. Taarifa hizi zinaonesha kuwa suala la ubora wa Elimu ni endelevu miongoni mwa viongozi wa kisiasa na raia pia. Hata hivyo, wakati kila mtu anakubaliana kuwa ubora ulale katika kiini cha Elimu, kuna makubaliano kidogo kuhusu tabia za ubora. Mtu aliyeelimika ni nani? Nini kinatokea katika darasa lenye mafanikio? Shule nzuri ina muonekano upi? Dhana ya ubora ichukuliwe vipi? HakiElimu imeng ang ana na maswali haya tangu ilipoanzishwa na waraka huu unatafuta kutoa jibu la awali. Tunaamini kwamba ubora wa elimu unaeleweka zaidi siyo kwa kutaja zana za kufindishia (kama idadi ya madarasa na madawati), bali kwa kutaja matokeo au ujuzi wa mwanafunzi - ujuzi na vipaji ambavyo wanafunzi wanavijenga wanapokua katika mchakato wa Elimu. Tunatoa mwongozo wa namna ya kufikiria uwezo wa wanafunzi kutokana na tafiti nyingi kuhusu elimu na uzoefu wa wanaopanga mipango ya Elimu katika nchi nyingi. Ikiwa ujuzi wa wanafunzi ndilo jambo kuu katika kujifunza, basi jambo hili ndilo linahitajika kufanywa kiini cha mfumo wa elimu. Mambo mengine yote kama vile mafunzo ya waalimu, mitaala na mitihani- yanapaswa kutengenezwa kwa ajili ya kufikia lengo kuu ambalo ni kukuza uwezo wa mwanafunzi. Kufundisha watoto vizuri ni changamoto tata na nzito, na utata huo unaweza kutulemea na kutuondoa kwa urahisi katika kufikia lengo kuu la elimu. Chapisho hili limeandaliwa ili kuamsha majadiliano ya wazi na kujenga maafikiano juu ya malengo makuu ya elimu ili sisi wote wazazi, wanafunzi, walimu, wanajamii, viongozi wa serikali na wananchi wote wanaoguswa tuweze kulenga katika malengo hayo na kuunganisha jitihada, hata tunapokabiliana na masuala mbalimbali yahusuyo elimu. 2.Kufafanua Upya Ubora: Kuvuka Mipaka ya PEDP na SEDP Suala la ubora ni la muhimu sana kwa sasa katika wakati ambapo mabadiliko makubwa yanafanyika katika elimu ya msingi na sekondari nchini Tanzania. Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya msingi (MMEM) ulioanzishwa mwaka 2001 na Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES) wa mwaka 2004 ilielezea msukumo mkubwa kuhusu ubora wa elimu na 1 Kazi hii imeandikwa na Rakesh Rajani na Linda Scholl na Gervas Zombwe. Ruth Carlitz, Kajubi Mukanga, Newton Kyando na Suleman Sumra wamechangia katika hatua mbalimbali za kazi. Waandishi wote na wachangiaji walikuwa wafanyakazi, washauri au waliojitolea kufanya kazi na Hakielimu 2006 na 2007. Kazi hii imenufaika na mapitio ya maandiko mbalimbali, maandiko yaliyopitiwa yameorodheshwa mwishoni mwa kazi hii kama Marejeo. 1

kutenga fedha za kutosha kusaidia mfumo wa elimu unaozidi kupanuka. Lakini ni dira gani ya ubora inayooneshwa katika mabadiliko hayo? Je, dira hiyo itawekwa katika vitendo? Je dira hiyo italeta hali ya kuwepo kwa maendeleo endelevu na demokrasia katika maisha ya watu na nchi yetu kwa ujumla? Je, itawezesha wananchi kukabiliana vilivyo na changamoto mpya na kuweza kuendelea katika ulimwengu huu unaobadilika kwa kasi kubwa? Mipango ya MMEM na MMES inategemewa kuchangia katika kufikiwa kwa Malengo ya Maendeleo Milenia (MDGs) na Mfumo wa Elimu kwa Wote (EFA) kwa nchi zinazoendelea. Nyaraka hizi elekezi zinaonyesha wazi umuhimu wa elimu katika kuondoa umaskini, kukuza matarajio ya kiuchumi ya watu na nchi kwa ujumla, na kusaidia upatikanaji wa haki za msingi za binadamu. Mipango hii yote inatoa wito wa kuongeza upatikanaji elimu na kuongeza ubora wa elimu. Hata hivyo katika utekelezaji, nchi nyingi zinazoendelea zimelenga zaidi katika lengo la kwanza la kuongeza uandikishwaji shuleni na mara nyingi zimekuwa zikichanganya mafanikio katika lengo hili na kuongezeka kwa ubora wa elimu. Kwa maneno mengine, ubora wa elimu unapojadiliwa, marejeo ya awali hufanywa kuhusu wingi wa zana kama vile majengo mengi, walimu wengi, uandikishwaji kwa wingi na vitabu vingi. Uwepo wa zana hizi huchukuliwa kama alama ya Elimu bora. Hatukubaliani na mtazamo huu: Tunakubali kwamba mipango ya MMEM na MMES imeleta mafanikio muhimu. Mapitio na taarifa nyingi zimeonyesha kwamba mipango hii imefanikiwa kuongeza uandikishwaji, ujenzi wa madarasa na shule mpya, kutoa vitabu vipya na waalimu, na kuongeza misaada ya kifedha mashuleni. Mabadiliko haya yameleta msisimko wa furaha nchini. Pamoja na hayo, swali la msingi ni je, mabadiliko haya yanawawezesha wanafunzi kufanikiwa katika jamii zao? Pamoja na umuhimu mkubwa wa zana za kufundishia, hazituoneshi ni nini kinachozalishwa. Hatufahamu kama mamilioni ya watoto wanaohudhuria shule siku zote wanajifunza na kupata ujuzi utakaowawezesha kufanikiwa ulimwenguni kupata kazi, kutengeneza ajira, kutatua matatizo na kusaidia jamii zao kusonga mbele. Ndiyo maana watafiti wa masuala ya elimu wanalenga kutafiti matokeo ya kusoma. Wanatoa hoja kwamba mfumo wa Elimu unatakiwa kulenga katika kutengeneza: watu wenye stadi tofauti ( zikiwemo: ujuzi, maarifa na mtazamo wa kiufahamu na usio wa kiufahamu) muhimu katika kuleta maisha yenye kutosheleza na maendeleo katika jamii zao (Prichett, 2004, 1). Kwa kutumia fasili hii ya ubora, mapitio mengi ya hivi karibuni yanayochunguza maendeleo ya Mfumo wa elimu yanayofanywa katika nchi nyingi zinazoendelea yamegundua kwamba wakati nchi nyingi kama Tanzania zimepata mafaniko makubwa katika kuongeza upatikanaji wa Elimu, matokeo ya mafanikio hayo yanabaki kuwa duni: Kuhitimu elimu ya msingi au ya juu zaidi hakumaanishi kuwa mhitimu anao ujuzi na upeo unaohitajika. Hata hivyo shuhuda zilizopo zinaonyesha kwamba karibu katika nchi zote zinazoendelea viwango vya Mafanikio yapatikanayo kwa kusoma bado ni duni sana (Pritchett, 2004, 11). Je, Ubora na wingi vinaweza kuongezwa kwa pamoja? Rais Mkapa na Kikwete wamekuwa wakieleza kwa nyakati tofauti kwamba haiwezekani kuongeza upatikanaji wa elimu na ubora kwa wakati mmoja, wakimaanisha kuwa mtu ajenge madarasa na kuandikisha wanafunzi kwanza na kushughulikia ubora wa elimu baadaye. Lakini utaratibu huu unamaanisha nini katika kusoma? Je, ni kweli kuwa ubora utakuja baadaye? Kikundi cha Taathmini ya ndani ya Benki ya Dunia (IEG) kimegundua kwamba: 2

Matokeo mazuri ya kujifunza yanaweza kudhoofishwa na upanuzi wa haraka wa mfumo wa elimu. Nchi zilizoendelea haraka ambazo zimefuata utaratibu upanuzi wa haraka haraka wa upatikanaji wa Elimu za msingi zimekua haraka kiasi kwamba zimekuwa zikishindwa kutoa huduma za msingi za kielimu. Mara nyingi nchi zinakuwa na ashki ya kupanua upatikanaji wa Elimu kwanza na kushughulikia matokeo yake baadaye, lakini utendaji mzuri ni kupanua upatikanaji elimu na matokeo mazuri ya kusoma kwa pamoja (IEG REACH, 2006). Dhana zinazojitokeza kutoka taarifa hizi ipo wazi. Ushahidi unaonyesha utaratibu unaosema wingi kwanza na kisha ubora, unakubaliwa kwa kiwango kidogo sana. Juhudi za kielimu ni lazima zilengwe katika kuunda stadi bora zaidi zipatikanazo kwa kusoma na maatokeo mazuri kwa wanafunzi kwanza. Tofauti na mitazamo ya awali kwamba idadi ya miaka ya kusoma au kukamilisha Elimu ya msingi au sekondari ndiyo kitu cha msingi, uchambuzi umeonesha kwamba ubora unaofasiliwa kwa maana ya uwezo na ujuzi ndiyo unaleta tofauti: Kwa sasa, vipimo vya ubora wa programu vilivyopo maranyingi vinategemea vipimo tofauti vya kupima zana ambavyo kwa bahati mbaya havihusiani moja kwa moja na usomaji kwa mwanafunzi tumefikia hitimisho kwamba ubora wa Elimu hasa katika kuchambua sera za nchi zinazoendelea ndiyo jambo kubwa Kuna ushahidi kwamba ujuzi wa kiufahamu wa watu zaidi ya kuhitimu shule unahusishwa sana na mafanikio ya mtu binafsi, mgawanyo wa mapato na kukua kwa uchumi (Hanushek, 2007, 77, 1, abstarct) Ujuzi na uwezo wa kiufahamu unaojadiliwa hapo juu haupimwi na mtihani wa kumaliza Elimu ya msingi, ambao kuboreka kwa matokeo yake hivi karibuni kunachukuliwa kama ishara ya kuongezaka kwa ubora wa elimu. Ni makosa kuchukulia matokeo mazuri ya mitihani ya maswali ya kuchagua kama kipimo halali cha ubora wa elimu. Mtihani wa kumaliza elimu ya msingi unapima uwezo wa kufikiri kwa kiwango cha chini mno kama vile uwezo wa kukariri 2, badala ya kupima ufahamu, ubunifu na uwezo wa kuchambua mambo, utatuzi wa matatatizo, na uwezo wa kufanya taathmini. Ujuzi huu ni tathmini ya kipimo kizuri zaidi cha ubora kwa kuwa unaashiria uelewa mpana na wa kina na uwezo wa kutumia taarifa zenye manufaa. Kwa vile majaribio kama mitihani wa kuhitimu darasa la saba haikuundwa kwa ajili ya kupima uwezo wa uelewa wa mwanafunzi, haifai kuwa kipimo cha ubora wa elimu. Kwa sababu hiyo, haishangazi kuona kwamba wahitimu wengi wanaofaulu mitihani hiyo wanashindwa kukabiliana na changamoto za maisha na wanakuwa na maandalizi madogo ya kuendelea na masomo. Hoja ya kimataifa ya kutaka kuieleza elimu kwa kuzingatia matokeo na si zana za kufundishia inazidi kusisitizwa nchini Tanzania pia. Mtandao wa Elimu Tanzania (TENMET) umekuwa ukikazia msimamo huu wakati wa kukusanya mapitio ya kutathimini sekta ya elimu kila mwaka. Tahariri za magazeti na waajiri pia wametoa wito wa kuzingatiwa zaidi kwa ujuzi na uwezo kuliko kujifunza kwa kukariri tu. Katika kiwango cha jamii wazazi wengi wameonyesha kusikitishwa na kushindwa kwa elimu waliyonayo watoto wao kuwapa njia ya kujihakikishia maisha. Mjadala huu unaonyesha tunahitaji kuwa na dira imara ya Elimu bora Tanzania. Tunahitaji kuzingatia kwa makini mabadiliko gani ya Elimu yatahitajika ili kukuza maendeleo yake. Bila kuwa na ufasaha katika maono na mwelekeo, juhudi zetu zinaweza kushindwa kutufikisha 2 Kwa mjadala zaidi kuhusu yaliyomo katika mipango ya mtihani wa kuhitimu darasa la saba na kwa maelezo zaidi juu ya zinazowezekana kuwa sababu za kuongezeka kwa matokeo mazuri ya PSLE angalia zaidi ripoti tatu za Sumra na wenzake zinazopatikana (HakiElimu na TENMET), Dar es- salaam 3

tunakokwenda hivyo inawezekana rasilimali na nguvu zikawa zinatumika kwa ajili ya mambo yasiyo ya muhimu katika kuleta matokeo mazuri. Katika vipengele vifuatavyo, tutajadili ni kwa namna gani ubora unaweza kuwa kiini cha elimu kwa kubakia tu kulenga katika kuboresha uwezo wa wanafunzi na kupangilia muundo wa elimu kwa ajili ya kulifikia lengo hilo. 3. Vipawa vya Wanafunzi Tumejadili hapo awali kwamba kitu cha muhimu zaidi ni wanafunzi walio katika hatua zote za elimu kuweza kufanya vizuri ulimwenguni. Ndio maana dira ya Elimu nchini Tanzania inatakiwa kusisitiza kuendeleza uwezo wa wanafunzi. Wanafunzi wanatoka katika mazingira mbalimbali na wana njia tofauti za kujifunza; hata hivyo, wanafunzi wote wanao uwezo wa kujifunza. Walimu wengi sasa wanakubali kwamba kuna namna nyingi za kuwa mwerevu na kwamba werevu unaweza kuja kwa kufunzwa na kutegemezwa. Watoto wengi wanajifunza vizuri kama mbinu bora na shirikishi za kufundishia zitatumika. Mbinu kama hizi zinawawezesha wanafunzi kufikiri kwa kiwango cha juu na kuwaongezea mbinu shirikishi zinazochagiza au kuamsha ari ya kujifunza kwao kwa kuwapatia changamoto na kazi muhimu zinazotakiwa kushughulikiwa kwa kushirikiana na zinazowapa ujuzi na mtazamo tofauti. Kwa kufanya hivi, wanafunzi wanapata werevu. Matokeo yake, katika waraka huu tunasisitiza kwamba mifumo ya elimu inahitaji kuwa jumuishi kwa wanafunzi wote (ikiwa ni pamoja na wanafunzi wenye ulemavu wa mwili, maendeleo duni na wenye uwezo mdogo wa kuelewa), na kwamba ni Juhudi na si Vipaji, inayotawala uwezo wa mwanafunzi kujifunza na kwamba walimu wanaweza kupangilia madarasa yao na kusaidia kufikia lengo hili (Institute for Learning, 2007). Kimsingi, maarifa na ujuzi ambao wanafunzi wanahitaji kujifunza vimegawanywa katika masomo ya: kiswahili, kiingereza, hisabati, sayansi, historia n.k. Mafunzo katika masomo haya yanatakiwa kutolewa na waalimu, kuchukuliwa na wanafunzi na kunukuliwa katika mitihani. Hata hivyo, tunagundua kwamba zaidi ya maarifa na ukweli wa masomo haya, wanafunzi wanahitaji kupata ujuzi wa taaluma mbalimbali na nafasi ya kuzitumia katika mazingira tofauti. Uwezo wa wanafunzi unaweza kujengwa pale waalimu wanapowahamasisha wanafunzi kufikiri kwa kina kuhusu mambo mbalimbali, kuzielewa dhana tofauti na kutumia taarifa mbalimbali, mitazamo na utambuzi wa vitu na matatizo wanayopambana nayo katika maisha ya kila siku. Mtazamo wetu uweke msisitizo katika uwezo wa kufikiri badala ya maarifa ya somo fulani pekee. Katika ulimwengu huu unaobadilika kwa kasi, maarifa ya somo mahsusi hupitwa na wakati au kutohusika tena kwani watu wanakua wakijishughulisha na changamoto mpya. Uwezo mkubwa wa kuelewa mambo mbalimbali na kupambana na changamoto mpya na kufahamu jinsi ya kupata maarifa mahsusi ya matatizo yanayoibukia ni ya thamani zaidi kuliko maarifa kidogo ya somo moja la darasani. Je, ujuzi na vipawa hivi ni vipi? Je, vipawa vipi ni vya muhimu zaidi? Wanafunzi wanahitaji kujiamini na kujituma ili kuwa wajuzi zaidi ya masomo mbalimbali. Wanahitaji kuweza kutatua matatizo kwa usanisi, kuchambua na kutathmini taarifa, na kutumia mitazamo waliyojifunza eneo moja katika eneo jingine. Wanahitaji kuelewa na kuwajibika kwa mahitaji ya jamii zao na ulimwengu wanaoishi kwa ujumla. Vipawa hivi haviwezi kukuzwa kama wanafunzi watanukuu maneno na kanuni za vitabuni na kuzikariri. Wanafunzi lazima wapewe nafasi ya kijishughulisha na wenzao ili kuelewa taarifa na kuzitumia taarifa hizo maishani mwao. 4

Kulingana na mapitio ya maandishi yaliyofanywa sehemu mbalimbali ulimwenguni na makadirio yake kwa muktadha wa Tanzania, tunapendekeza kupanga vipawa katika sehemu kuu nne. sehemu hizi zinaunda wazo la kujifunza linalomlenga mwanafunzi. Ingawa tumepanga vipawa vya wanafunzi katika sehemu tofauti nne na kuvijadili vyote tofauti, bado vinategemeana kwa kiasi kikubwa. Kujifunza kila mmoja wa mipangilio hii ya vipawa kunategemea na kuimarisha maendeleo ya vipawa vingine. Sehemu hizi nne za vipawa ni za muhimu ndani na nje ya masomo na vinaruhusu wanafunzi kuvitumia na kuvifanyia majaribio kwa kazi na mazingira mbalimbali. VIPAWA VYA MWANAFUNZI Kujua kusoma na kuhesabu Ajue kusoma, kuelewa, kuandika, na kutamka. Aweze kutatua matatizo ya kihesabu Maendeleo binafsi mwenye kujiamini awe tayari kwa lolote mwenye msimsmo thabiti Ujuzi wa kiufahamu mchunguzi na mdadisi mbunifu na mfikiriaji mtatuzi muwasilianaji Maadili mwenye kujali na msaidiaji muwazi mwenye ushirikiano Sasa tujadili mipangilio yote ya vipawa kwa zamu. 3.1 Kujua kusoma na kuhesabu Awe na hamasa ya kujua kusoma kuandika na kuongea Mwenye hamasa na mpenzi wa kutatua maswali ya kimahesabu Anayekua na hamasa ya kupenda kujishughulisha na aina mbalimbali za maandishi. mwenye ufasaha na mapenzi ya kufanya mawasiliano kwa kuongea na kuandika mwenye kuwa na uelewa wa dhana za kihesabu na mahusiano mwenye kutawala habari za kimahesabu na kuzitumia kutatua matatizo ya kila siku Kusoma, kuandika na hesabu ni vitu muhimu sana katika elimu yoyote. Katika jitihada za kielimu watoto wote wanahitaji kupata motisha na ufasaha kusoma taarifa zilizoandikwa, kutunga na kukokotoa maswali ya kihesabu. Hata hivyo, kusoma si uwezo tu wa kutambua herufi, maneno na sentensi, bali zaidi ni uwezo wa kuelewa kinachosomwa, kujifunza na kutumia taarifa na ujuzi wanaoupata. Uwezo huu tunauita Ufahamu au Uelewa. Kuandika na kuongea hakuhusishi kuweka maneno katika karatasi au kuongea bila lengo maalum. Ujuzi huu unahusisha namna mtu anavyowasiliana na wengine mawazo tata kwa ufasaha, ustadi na kwa ufupi. Hali kadhalika hesabu za msingi haziwajengi wanafunzi kuwa tu na uwezo wa kiufundi wa kutawala namba katika muktadha wa kufikirika bali pia kuelewa kutumia dhana za kihesabu na kufikiri juu ya matatizo ya kimahesabu ambayo watu au vikundi wanakabiliana nayo maishani. Wakati shule zimelenga kuwaendeleza watoto katika ujuzi wao wa awali uwezo wa kiufundi na kiutaratibu wa kutumia maneno na tarakimu zinaweka msisitizo mdogo katika kuendeleza ujuzi wao kwa ajili ya maisha yao ya baadaye. Shule zinaweza kufanya kusoma, kuandika na kuongea kuwa muhimu na zenye matumizi kwa wanafunzi kwa kuhamasisha matumizi ya ufahamu huu 5

katika maisha ya kila siku ya wanafunzi. Kujua kusoma, kuandika na kuhesabu kunahusiana kwa karibu na aina zifuatazo za vipawa vya mwanafunzi. Ujuzi vya kiufahamu: 3.2 Ujuzi wa kiufahamu Mchunguzi na mdadisi Mbunifu na mwenye fikra Mtatuzi Muwasilianaji mwenye kutamani kujua mwenye kuuliza maswali mwenye kutafuta maelezo mwenye kufurahia kufanya majaribio anatoa mawazo mapya anazalisha uwezekano na mibadala tofauti mwenye mawazo mapana anaelezea matatizo anakusanya, kuchambua na kuunganisha taarifa anatekeleza masuluhisho anatathmini matokeo Mwenye kutumia maarifa aliyojifunza kutoka eneo moja katika kukabiliana na changamoto katika eneo jingine. anayesikiliza na kuchunguza kwa umakini hutumia lugha fasaha kufafanua masuala huelezea anachokifahamu katika njia mbalimbali kwa ufasaha Uwezo wa kiufahamu unahusisha kukua kwa maarifa na uwezo wa kisomi kuanzia umri wa awali wa kusoma. Kikubwa zaidi ya kukua kwa ujuzi huu, ni hali ya upembuzi na udadisi. Upembuzi huwaongoza watoto kujifunza zaidi juu ya somo kwa kuwa wanamotisha, wanajihusisha zaidi na wanajiongezea uelewa na maarifa mapya. Watoto wanaposaidiwa na kuhamasishwa kuwa wachunguzi, baada ya muda fulani wanaunda hali ya udadisi ambayo huwafanya wakaanza kuuliza maswali kama vipi? kwa nini? na vipi kama? na wanaanza kugundua wapi watapata taarifa zinazotosheleza uchunguzi wao. Pia watafanya majaribio kwa namna nyingi na matokeo ya majaribio hayo yataleta maswali mapya. Ubunifu na kufikiri kunahusishwa na kukua kwa hali ya udadisi na ubunifu. Kama kufikiri na kubuni kutakuzwa, wanafunzi wanaunda njia mpya za kuelewa mambo, wanakua wavumbuzi na wanatumia akili zao kuzalisha mawazo na kufikiria uwezekano mpya. Wanapanua mipaka na kutumia akili zao kupata mawazo na kuunda mibadala. Vipawa vyote hivi ni muhimu kwa jamii yeyote inayotaka kukua na kusonga mbele. Kwa kawaida, watoto wengi huwa na sifa nyingi za kiufahamu kati ya hizo hapo juu tangu wanapokuwa na umri mdogo sana. Ni wachunguzi kuhusu mazingira yao na ulimwengu wanamoishi na wanashauku ya kujifunza. Michezo yao imejaa ubunifu na majaribio. Kwa bahati mbaya watoto wanapoingia shule vipawa hivi havilelewi na havichochewi. Hakika watoto wengi wanajifunza kuvikandamiza vipawa hivi kwa kuwa wanatarajia kujifunza wanachofundishwa. Kuendeleza uchunguzi, udadisi na ubunifu kunahusisha kuwashughulisha watoto katika kujifunza kwa vitendo Kukua kwa uwezo wa kutatua matatizo kunaenda pamoja na ujuzi uliotajwa hapo juu ambao ni wa muhimu sana katika maisha ya watu binafsi na jamii. Katika darasa ambapo uwezo wa kutatua matatizo unasisitizwa, watoto wanajifunza kutambua matatizo na kutafuta mawazo mbadala, wanajifunza kukusanya, kuunganisha na kuchambua taarifa zitakazosaidia kupata mtazamo mpya juu ya tatizo. Wanajifunza pia kutekeleza ufumbuzi wa tatizo na kisha kutathmini matokeo ya juhudi zao. Hatimaye, wanaweza kuchukua walichojifunza katika mchakato huo, kutohoa na kutumia maarifa yao katika changamoto za madarasa mengine. 6

Kwa kuwa changamoto nyingi hutatuliwa kwa juhudi za ushirikiano, wanafunzi wanahitaji kujifunza kushirikiana na wenzao katika kutatua matatizo yao. Katika muktadha huu, uwezo wa kuwasiliana ni wa muhimu. Wakipewa nafasi ya kutatua matatizo kwa pamoja, watoto wanajifunza kuwasikiliza wenzao kwa makini na kueleza mitazamo yao kwa ufasaha na uhakika. Wanajifunza kubainisha mawazo yao na kudhihirisha uelewa wao kwa kusema au kuandika. Elimu ya kukuza uwezo wa kiufahamu inahitaji mazingira ya kiutendaji zaidi na shirikishi ya kujifunzia. Hii inamaanisha watoto wanatakiwa kufanya kitu kingine zaidi ya kujaza madaftari yao, au kujibu maswali ya mwalimu. Wanafunzi ni lazima wajisikie huru kuuliza maswali, kufanya majaribio na kutumia mawazo yao. Wanahitaji kuwa na kazi ngumu za kufanya na kukamilisha, za binafsi au katika makundi madogo na wenzao. Wanahitaji kushirikiana na kufanyakazi kama kutafiti miradi pamoja, kukamilisha majaribio, uwasilishaji na uandishi wa kibunifu. Wanafunzi hukua zaidi kimasomo wanapopewa nafasi kuwasilisha uelewa wao wa mambo au somo, na pia nafasi ya kusikiliza na kuwajibu wenzao. Uwezo huu huimarika wanafunzi wanapopewa nafasi ya kuuweka katika vitendo. Ingawa tunafikiri kuwa wanafunzi wakubwa tu ndio wanaweza kufanyakazi katika daraja hili, hata watoto wadogo wa shule za msingi na awali wanaweza kujengewa ujuzi huu kwa kuanzia. Kadri watu wanavyokua (na kama mazingira ya kujifunzia yanashawishi) uwezo huu unaweza kujikita na kurekebishwa mwaka baada ya mwaka. 3.3 Maendeleo binafsi Kujiamini Awe tayari kwa lolote Asiyekoma anajivunia thamani yake mwenye kuamini katika uwezo wake wa kujifunza na kukua mfikiriaji na mtendaji huru na mwenye uwezo wa kuwa na mawazo binafsi mwenye kuhangaikia ubora wake anatafuta changamoto na kushughulikia majukumu anafanya majaribio ya kazi na masuluhisho anajifunza kutokana na makosa mwenye kuvumilia malengo na kazi zenye changamoto kubwa mwenye kutoa maaoni yenye msaada katika mijadala mwenye kutengeneze njia za kukamilisha kazi Uwezo wa kiutendaji wa kusoma, kuandika na hesabu pamoja na uwezo wa kiufahamu vinaweza kukua na kutumiwa kama wanafunzi watakua na kujiamini na watastawisha vipaji binafsi. Kwa sababu hii mifumo ya elimu inahitaji kuzingatia kujenga maendeleo binafsi ya kila mwanafunzi. Wanafunzi wanaojiamini wenyewe na kuamini uwezo wao watakua tayari kujihusisha na wengine na mazingira yao pia. Hawataogopa kupambana na changamoto mpya, kujaribu na kukosea, kufikiri kwa namna tofauti na kujaribu njia mpya za kuunda vitu. Matokeo haya ni muhimu ili kukuza akili na kufanya watu wachangamke ulimwenguni. Yanaweza pia kuongeza hali ya uharaka na kutamani kufanya mambo yawe mazuri, ikiwa ni pamoja na kuhangaikia kuwa mtu bora na ubora katika kila kinachofanywa. Ikilinganishwa na hali ya kukaa tu bila vitendo, hali hii inamwezesha pia kutimiza majukumu binafsi na ya kiulimwengu. Ni muhimu kueleza pia kuwa kutengeneza mazingira saidizi na salama ya kusoma ni muhimu sana katika kuhamasisha maendeleo binafsi. Wanafunzi hawawezi kusikika au kuwa na uthubutu pale ambapo vitendo vyao havipewi kipaumbele au vinaadhibiwa, na pale ambapo kusoma kunachukuliwa katika mazingira ya uoga na mgandamizo. Kwa kufikiri kwetu, nidhamu ni muhimu katika kuunda hali ya usalama, lakini pia ni lazima iwe nidhamu iliyo chanya. Ni lazima pia ifahamike kuwa kufanya makosa kunaweza kuwa kuzuri na kwenye kutia moyo wanafunzi kufanya majaribio na kuwa na mtazamo sahihi katika kusoma. Adhabu za kimwili na mbinu 7

nyingine za kudhalilisha wanafunzi hazina nafasi katika kusoma kwa kuwa zinajenga woga, kulazimisha ubabe na zinashusha utu wa mtu. Badala yake, mbinu za kinidhamu zinasosisitiza kuwepo kwa tabia chanya ndizo senye kufaa zaidi. 3.4 Maadili Kujali na kusaidia Mwenye Upeo Mwenye ushirikiano anahisi matatizo ya wengine na ana tabia ya kusaidia wengine anathamini umuhimu wa kila mtu kwa jamii anaheshimu haki za wengine Anasikiliza kwa makini na kwa heshima. anajali mitazamo, mahitaji, na tamaduni za wengine anathamini tofauti binafsi za watu katika imani na maadili anatoa mchango mkubwa kwa jamii anafanya kazi kiujenzi kutatua matatizo na mawazo yanayokinzana Sehemu ya nne ya vipawa inatambua kwamba kila mwanafunzi anahitaji kujifunza kushirikiana na wengine kwa namna inayoheshimu haki za binadamu, yenye usawa na tahadhari. Kufanya hivyo kunahitaji japo sifa tatu za muhimu; Kwanza watu wanahitaji kujifunza kuwajali na kuwasoma wengine. Hii inahusisha kukubali tofauti zilizopo. Pili, hii inamaanisha kukua kwa uwezo wa kupokea mawazo ya wengine, na hali inayostawisha kujifunza kwa makini na mahusiano yenye heshima, kukubali kwa mawazo tofauti, na uwazi wa kupambana na kufikiria kibinafsi. Hii inahusisha uelewa wa tamaduni na mifumo tofauti ya kimaisha, na kupendezwa na maadili ya jamii huru inayoweza kuchukuliana na tofauti hizi. Tatu, kulenga katika maadili kunawawezesha wanafunzi kujua namna ya kufanya kazi pamoja na wengine, kupambana na mafarakano na kufanya kazi yenye mafanikio kwa mawazo tofauti na kufikia maafikiano. Inafundisha wanafunzi kutafuta njia zitakazo waunganisha watu kufikia malengo na kufanya kazi kwa mafanikio ya jamii. Kukua kwa vipaji vya kimaadili huenda ndio muhimu zaidi leo katika ulimwengu wa utandawazi ambapo mgongano kati ya mawazo tofauti na mifarakano baina ya watu ni ya kawaida. Uwezo wa kulinda haki na hali nzuri ya kila mtu, hasa wale walio rahisi kudhurika na waliotengwa kihistoria, unakuwa na umuhimu wa pekee katika kuwezesha wanafunzi kuhamasisha haki. 4. Kuupa Mwelekeo mpya Mfumo wa Shule Inasemekana kuwa kila mfumo umeundwa sawa na matokeo unayoyaleta. Mfumo wa elimu wa sasa umeundwa kwa ajili kuzalisha idadi kubwa ya wanafunzi waliosoma kwa miaka mingi na vyeti vingi lakini wenye ujuzi mdogo. Baada ya mabadiliko ya hivi karibuni, mfumo wa kielimu nchini Tanzania unaweza kuelezwa kuwa una sifa ya kusomesha sana lakini kujifunza kudogo. Kwa upande mwingine, kama tunataka kubadili matokeo ya wanafunzi kusoma, tunahitaji kuunda mfumo unaoleta matokeo hayo. Mbinu ya vipawa vya wanafunzi inatoa nafasi kuunda upya mfumo wa Elimu ili kupata mafunzo ya kweli na kukuza vipawa halisi. Ili kuhamasisha kukua kwa vipaji, badala ya kuongeza uandikishwaji na kuongezeka kwa kiwango cha kufaulu mitihani, kunahitajika mabadiliko ya jumla ya mtazamo, sera, mipango na taasisi. Mifumo ya elimu, kujumuisha mitaala, ufundishaji na ukaguzi, inatakiwa kulenga zaidi katika kukuza vipaji vya wanafunzi. Kubadili madhumuni ya elimu hakutafanikiwa kama vipengele vyote muhimu vitabaki kama vilivyokuwa awali. Hivyo kubadilika kwa falsafa, muundo, na sera za kielimu za sasa ni muhimu. Jedwali hili hapa chini linaonesha vipengele vikuu vinavyotakiwa kushughulikiwa: 8

Tathmini ya Ubora Sera Walimu na Ufundishaji Vipawa vya Wanafunzi Ukaguzi Uwezo wa mwanafunzi unatakiwa kuwa ndicho kiini cha jitihada za kielimu, na mambo mengine yote yapangwe kwa ajili ya kufikia lengo hili. Hili litaleta mfumo na mpangilio wenye motisha zaidi tofauti na awali. Kwanza, kama alivyosisitiza Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere mara nyingi, kipimo kikuu cha kufanikiwa katika elimu kitahitajika kuwekwa bayana. Kuwa na falsafa ya wazi ya Elimu inayotambulika, mitaala na mafunzo ya kufundishia. Hakutakuwa na maana kama mitihani imepima kitu kingine na imetumika kama alama ya mafanikio na maendeleo yaliyopatikana kutoka hatua moja hadi nyingine katika elimu. Badala ya kutegemea utaratibu mmoja wa kupima uwezo wa mwanafunzi (kama mtihani wa darasa saba), ambao haupimi ujuzi na uwezo halisi wanaohitaji wanafunzi, tunahitaji mfumo wa elimu endelevu ambao utatathmini uwezo wa wasomi kwa namna mbalimbali kulingana na muda. Upimaji huu unatakiwa kuchunguza kukua kwa maeneo hayo manne na vipaji vingine. Upimaji wa mwendelezo na kipindi maalumu ni chombo muhimu katika elimu kwa kuwa unahamasisha mwendelezo wa mzunguko wa kusoma na unamwendeleza mwalimu na mwanafunzi. Nyongeza ya hapo, mfumo wa elimu wenye kujenga hautegemei majaribio ya kawaida pekee, bali hufanywa kwa njia nyingi. Waalimu wanaweza kukagua uwezo wa wanafunzi wao kwa kutumia njia ya maswali, kwa kuwataka wanafunzi kutumia maarifa yao na ujuzi kukamilisha kazi mahsusi ambazo zimekuwa lengo la mafunzo waliyopata karibuni, au kwa kuangalia wanafunzi wanavyofanya kazi na wenzao katika vikundi vidogo. Wakati mwingine, kumbukumbu za maendeleo ya mwanafunzi zinazoonesha viwango mablimbali vya mafanikio ya mwanafunzi vinaweza kutengenezwa. Kwa hiyo alama za hatua ya mwisho ya elimu zitakua sehemu ya ukaguzi wa siku nyingi na mfululizo wa maendeleo ya mwanafunzi (na mtihani wa mwisho ukichangia si zaidi ya 25%). Ukaguzi huu unapaswa kuelezea ubora zaidi na kuwa ndicho kipimo kinachofaa ya kujifunzia. Pili, Elimu ya Ufundishaji na njia za kufundishia vinahitaji kupewa mwelekeo mpya ili kuhamasisha kujifunza kwa vitendo na ushirikishwaji ambako kunamlenga zaidi mwanafunzi badala ya mwalimu. Hii itahitaji mabadiliko kutoka desturi ya sasa ya kufundisha ya chaki na kuongea, ambapo mwalimu anafundisha au anaandika ubaoni na wanafunzi wananakili. Badala yake, wanafunzi watatakiwa kushiriki kwa vitendo katika somo husika, kuuliza maswali, na kujifunza kwa vitendo. Lengo zima litakua kukuza hali ya udadisi, kufanya majaribio, kujaribu na 9

kutatua matatizo, katika mchakato ambao wanafunzi wanajenga maarifa badala ya kuyapokea kama yalivyo kutoka kwa mwalimu. Kuwezesha kujifunza kwa vitendo kunahitaji kulenga zaidi katika ubora wa nguvu kazi (hasa waalimu), kuliko sasa ambapo majengo na rasilimali nyingine zinazoonekana zinapatiwa kipaumbele zaidi. Ili kuwawezesha waalimu kufikia hatua hii, mitaala na mafunzo ya kitaalamu vitahitaji kusaidia mafunzo kwa vitendo na shiriki zaidi. Kwa kuwa walimu wengi wamefundishwa kwa njia ya chaki na kuongea, wanahitaji mafunzo ya ziada kabla ya kuanza kufundisha, pamoja na nafasi za kujiendeleza. Ili kufikia lengo hili, mbinu na masomo ya vyuo vya ualimu na vituo vya waalimu vinahitaji mabadiliko. Zaidi ya hayo, mfumo wa matumizi ya motisha (za kifedha na zisizo za kifedha, ikiwa ni pamoja na ukaguzi), unahitaji kusisitizwa ili waalimu wanaotumia njia bora watambuliwe na kuzawadiwa. Kushirikisha Chama wa Waalimu Tanzania (TTU), ambacho kina dira ya kuboresha hali za maisha ya waalimu na viwango vya ubora wa elimu ni muhimu katika kufikia lengo hili. Mwisho, waalimu wanahitaji kuwa na umahiri katika masomo husika wanayotakiwa kufundisha. Hapa pia taratibu zinatakiwa kusisitiza uwezo wa kufikiri zaidi ili wanafunzi waweze kuelewa dhana nzima ya somo husika kuliko kuelewa yale tu yanayofundishwa na mwalimu. Kwa sababu hii somo husika na ufundishaji wake vinahusiana sana,na havitengani. Kwa mtazamo huu, suala la lugha ya kufundishia haliwezi kuachwa pembeni. Nchini Tanzania, elimu ya msingi hufundishwa kwa lugha ya Kiswahili na ile ya sekondari inafundishwa kwa lugha ya Kiingereza, japo wengi wa wanafunzi hawana uwezo mkubwa katika matumizi yake. Matokeo yake wanafunzi wengi wanajikuta wakilazimika kujifunza masomo tofauti kwa kutumia lugha wasiyoielewa. Ushahidi wa kisayansi upo wazi: wanafunzi wanajifunza vizuri zaidi kwa kutumia lugha ya mama au lugha nyingine wanayoimudu vizuri. Hata hivyo, sera ya serikali na mtazamo mpana wa jamii unaonekana kulinganisha Kiingereza na maendeleo na mafanikio. Elimu bora Tanzania haiwezi kupatikana bila kuzingatia suala la lugha ya kufundishia. Tatu, lengo hili linahitaji kuwa kiini cha muundo wa sera. Kwa sasa, nyaraka za muhimu zinachukulia ubora wa elimu kama kufaulu, lakini hazitoi ufafanuzi wa kina wa dhana hiyo. Zaidi ya hayo, viashirio vya mafanikio vya kisiasa na kitaalamu vinapendelea vipimo duni vyenye kuzingatia idadi. Mfumo wa elimu unaotoa kipaumbele kwa ujenzi wa uwezo wa wanafunzi unahitaji kupewa mwongozo mpya katika sera na malengo yake. Bajeti zitahitaji kuhusishwa na kupewa kipaumbele katika malengo ya sera hizi. Jambo la muhimu zaidi ni kwamba hizi siyo changamoto za kidhana na kiufundi tu. Suala la uundaji wa sera na utekelezaji wake ni mambo ya kisiasa na kijamii, hivyo mabadiliko haya yatatakiwa kufanywa kwa namna itakayotoa kipaumbele zaidi kwa mawasiliano na jamii na midahalo ya wazi na mashauriano na wadau. Uongozi imara na wenye msukumo na tamko la dira unatakiwa kuwasilishwa na Rais na viongozi wengine, na kuunda nafasi kubwa ya kushirikishwa kwa wananchi pamoja na wanafunzi wadogo na wakubwa na walimu.jumuiya ya kiraia na vyombo vya habari huru vina wajibu wa muhimu katika kuundeleza mfumo huu. Mabadiliko ya mfumo wa elimu kutoka katika vigezo vya kuzingatia wingi na kulenga zaidi katika ubora linaweza kuwa suala rahisi kuzungumzia lakini gumu kulitekeleza. Mabadiliko yatachukua muda. Hata hivyo, ingawa ni vigumu, Tanzania haipaswi kuendelea kufuata njia inayofuatwa sasa ikiwa inataka kupata maendeleo na demokrasia ya kweli. Kukiwa na dira ya wazi na malengo, uongozi imara, Tanzania inaweza kufuata mfumo unaowawezesha watu wake kustawi na kujihakikishia manufaa yao katika jamii. Waraka huu utakuwa umefanya kazi yake kama utachangia katika mdahalo wa kitaifa juu ya jinsi gani hili linaweza kufanyika. 10

Marejeo Boissiere, M. (2004). Determinants of primary education outcomes in developing countries. Washington DC: World Bank. Calgary Board of Education. (1998). Quality Learning. Work in Progress. Calgary, Canada. Chickering, A.W., & Gamson, Z.F. (May 2007). Seven principles for good practice in undergraduate education. Retrieved August 22, 2007, from http://honolulu.hawaii.edu/intranet/committees/facdevcom/guidebk/teachtip/7princip.htm. Filmer, D., Hasan, A, & Prtichett, L. (2006). A millennium learning goal: Measuring real progress in education. Working Paper Number 97. Washington DC: Center for Global Development. Freire, P. (1970). Pedagogy of the Oppressed, Continuum, USA. HakiElimu. (2005). Three years of PEDP implementation: Key findings from official reviews. Dar es Salaam, November 2005. HakiElimu. (2007a). Five years (2002-2006) of PEDP implementation: Key findings from official reviews. Dar es Salaam, TZ. HakiElimu. (2007b). Two years of SEDP implementation (2004-2006): Key findings from government reviews. Dar es Salaam, TZ. Hanushek, E.A. & Woessman, L. (January 2007). The role of school improvement in economic development. NBER Working Paper No. 12832. Cambridge MA: National Bureau of Economic Research. Highland Council Education, Culture and Sport Service. (2007). Learning and teaching should be inclusive and enjoyable: What makes a good teacher? Highland Learning and Teaching Toolkit. Retrieved August 22, 2007, from http://www.highlandschools-virtualib.org.uk/ltt/inclusive_enjoyable/teacher.html Independent Evaluation Group. (2006a). From schooling access to learning outcomes: An unfinished agenda. An evaluation of World Bank support to primary education. Washington DC: World Bank Group. Independent Evaluation Group. (2006b). The unfinished agenda in primary education. Washington DC: World Bank Group. Retrieved August 22, 2007, from http://worldbank.org/ieg Institute for Learning. (2007). Principles of learning. University of Pittsburgh: Learning Research and Development Center. Retrieved August 22, 2007, from http://ifl.lrdc.pitt.edu/ifl/index.php/section=pol. International Baccalaureate Organization. (March 2006). The IB learner profile. United Kingdom. Retrieved August 22, 2007, from http://www.ibo.org/programmes/documents/learner_profile_en.pdf Kikwete, J.K. (2005). Speech by the President of the United Republic of Tanzania, His Excellency Jakaya Mrisho Kikwete, on inaugurating the fourth phase parliament of the United Republic of Tanzania, Parliament Buildings, Dodoma, 30 December 2005. Retrieved August 22, 2007, from http://www.parliament.go.tz/bunge/docs/pspeech_en.pdf Krumme, G. (2005). Major categories in the taxonomy of educational objectives (Bloom 1956). Retrieved August 22, 2007, from http://faculty.washington.edu/krumme/guides/bloom1.html Low Eng Guan, J. Helping your pupils to develop their thinking skills in the English language primary school. Kuala Lumpur: Ministry of Education. Retrieved August 22, 2007 from http://www.ppk.kpm.my/html/program/masteryguide/asri1.html Naker, D. (2007). What is a good school? Imagining beyond the limits of today to create a better tomorrow. Kampala, Uganda: Raising Voices. National Center for Fair and Open Testing. (1999). The value of formative assessment. Fair Test Examiner, Winter 1999. Retrieved August 22, 2007, from http://www.fairtest.org/examarts/winter99/k-forma3.html??? not correctly copied, please check! 11

Nyerere, J.K. (1967). Education for Self-Reliance. in Nyerere on Education, Lema, E; Mbilinyi, M. and Rajani, R (editors, 2004), Dar es Salaam: HakiElimu.. Pritchett, Lant. (June 2004). Towards a new consensus for addressing the global challenge of the lack of education. Washington DC: Center for Global Development. Puhl, C. (1997). Develop, not judge: Continuous assessment in the ESL classroom. English Teaching Forum, Vol 35 No 2. Minneapolis, MN: Search Institute, 2005. Retrieved August 22, 2007, from http://www.search-institute.org/research/40assetsec.pdf. Queensland Studies Authority. (2007). Early years curriculum guidelines: Learning statement overviews for curriculum decision making. Retrieved August 22, 2007, from http://www.qsa.qld.edu.au/early/curriculum_guidelines/part4_learning_statement.html. Connecticut State Board of Education. (1998). Connecticut s common core of learning. State of Connecticut, USA. Stokes, A.P. (1922). Education in Africa, a study of West, South and Equatorial Africa. NY: Phelps-Stokes Fund, and the African Education Commission. Retrieved August 22, 2007, from http://www.archive.org/details/educationinafric00afriuoft. TENMET (2006), Strengthening Basic Education in Tanzania, submission to the Annual Education Review, Dar es Salaam. United Nations Educational, Scientific, and Cultural Organization. Education For All. Retrieved August 22, 2007, from http://portal.unesco.org/education/en/ev.phpurl_id=47044&url_do=do_topic&url_section=201.html??? Not correctly copied, please check! United Nations. Millennium Development Goals. Retrieved August 22, 2007 from http://www.un.org/millenniumgoals/goals.html URT (2001). Education Sector Development Programme: Primary Education Development Plan (2002 2006), Basic Education Development Committee (BEDC), Ministry of Education and Culture. URT (2002a). PEDP Implementation Stocktaking Report, MOEC, 28 th May 2002. URT (2002b). PEDP National Monitoring Report 2001 2002, PO-RALG. URT (2003a). Joint Review of the PEDP, MOEC and PO-RALG, November 2003. URT (2003b) 2002 Population and Housing Census: Volume II: Age and Sex Distribution. Dar es Salaam: Central Census Office, President s Office Planning and Privatization URT (2004a). Secondary Education Development Plan (2004-2009). Ministry of Education and Culture. URT (2004b). PEDP National Monitoring Report July 2002 March 2004, PO-RALG URT (2004c). Joint Review of the PEDP, MOEC and PO-RALG, October 2004. URT (2004d). Basic Statistics in Education 1995 2004: National Data, MOEC July 2004. URT (2006a). Secondary Education Development Plan, Annual Performance Report, July 2005-June 2006. Ministry of Education and Vocational Training. URT (2006b). Basic Education Statistics in Tanzania (BEST): 2002-2006, MoEVT June 2006. URT (2006c). PEDP Progress Report July 2005-June 2006, MoEVT and PMO-RALG, October 2006. 12