KITABU CHA KUONGOZA FAMILIA

Similar documents
Information for assessors (do not distribute this page to participants):

GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Agano Lililofunikwa Kwa Damu

UTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.

"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.

United Pentecostal Church June 2017

WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

Maisha Yaliyojaa Maombi

Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

MAFUNDISHO YA UMISHENI

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

WEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

B. Wanafunzi watapata ufahamu mkubwa wa kitabu hiki, na jinsi kinavyofundisha kuhusu kanisa.

BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa.

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI

Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia. Ellis Forsman. Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1

Uponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14).

MELKISEDECK LEON SHINE. katoliki.ackyshine.com

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT

UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA

# 18 Uponyaji Kutokana na Kukataliwa

Mwongozo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

walozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w

NGUVU. Utangulizi. Yesu alisema,

Kiu Cha umtafuta Mungu

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Kanuni. Muhimu za Kujifunza Biblia. Mchungaji Drue Freeman. Dan Hawkins & Joseph Brown. General Editors.

Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu

Kijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

WAKOLOSAI MTAALA. B. Maoni: Tunapendekeza uwe na fafanuzi (commentary) yoyote yenye kushikilia mafundisho ya awali (conservative) katika Wakolosai.

Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally

IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE

Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia

United Pentecostal Church April Kushangilia Kwa Sala

PDF created with pdffactory trial version

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?

Uponyaji wa Vitu na Mahali

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia

Human Rights Are Universal And Yet...

MWONGOZO WA NAMNA YA KUHAMASISHA MAOMBI YA MCHANA NA USIKU YA SIKU 10.

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI

FORWARD BY DANIEL SZMIOT

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza

UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza

Uongozi Siri Na Larry Chkoreff. Version 1.2 Desemba 2010

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu?

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees

Kufunga Milango - Uponyaji Kutokana na Athari za Giza

Sura ya 7 Kielelezo: Tumepatanishwa na Mungu na Wanadamu

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Silaha Za Shetani. Ellis Forsman. Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Maisha Ya Mkristo Ni Nini?

MSAMAHA NA UPATANISHO

Tazama Yuaja. Kuhusu Toleo Hili. Umuhimu wa Mafundisho ya Biblia. Nguvu katika neno la Mungu.

Kifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1

RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO

Patanishwa, Hesabiwa Haki, Takaswa

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Shabaha ya Mazungumzo haya

Mzabibu Na Matawi. (The Vine And The Branches) Ellis P. Forsman. Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) 1

Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu (Watch Out for Wolves)

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo. Zanzibar, 7-10 Februari 2006

MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara

IBADA NA UMOJA WA KANISA Na Mchg. Dkt. Msafiri Mbilu

Watumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1

Hakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn

Waandishi: wa Toleo la 5. Scholastica Jullu Athanasia A. Soka Safina Hassan Mary Njau. Toleo la 5: 2008 ISBN

MUHTASARI WA SEMINA YA TAASISI YA BIBLIA NA UTUMISHI MOROGORO TAREHE 18/11/2014

Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Roho Mtakatifu Ni Nini?

Kifo Na Mbingu (Death And Heaven)

Transcription:

KITABU CHA KUONGOZA FAMILIA

KITABU CHA KUONGOZA FAMILIA Kimechapishwa na Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu la Siku za Mwisho Mjini Salt Lake, Utah

1992, 1999, 2001, 2006 na Intellectual Reserve, Inc. Haki zote zimehifadhiwa Kimechapishwa Marekani Kiingereza kimeidhinishwa: 2/06 Tafsri imeidhinishwa: 2/06 Tafsri ya Family Guidebook Swahili

Yaliyomo Familia: Tangazo Kwa Ulimwengu: iv Mpangilio na Madhumuni ya Familia 1 Kufundisha Injili Nyumbani 4 Kutimiza Wajibu wa Familia. 12 Mafundisho ya Uongozi. 15 Kuandaa Ibada ya Maombi Nyumbani (Kwa familia zilizo kwenye maeneoyaliyotengwa) 16 Maagizo na Baraka za Ukuhani 18 Kupokea Vifaa vya Kanisa na Kupata habari kuhusu Historia ya Familia 26

Familia: Tangazo Kwa Ulimwengu Mnamo1995, Urais wa Kwanza na Jamii ya Wale Mitume Kumi na Wawili Walitoa tamko hili, Familia: Tangazo kwa Ulimwengu. Tangazo hili linadhihirisha ukweli wa mafundisho na matendo ambayo manabii wamenena mara kwa mara katika historia yote ya Kanisa. Limo na kanuni muhimu yanayoleta furaha na ukuaji wema kwa kila familia. Wanafamilia wanapaswa kusoma hilo tangazo kwa kutii mafundisho yake. Sisi, Urais wa Kwanza na Jamii ya wale Mitume kumi na wawili wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa siku za mwisho, kwa heshima tunatangaza kwamba ndoa kati ya mwanamume na mwanamke imetakaswa na Mungu na kwamba familia ndiyo kiini katika mpango wa Muumba wa watoto Wake kuishi maisha ya milele. Wandamu wote wa kiume kwa wa kike wameumbwa kwa mfano wa Mungu. Kila mmoja wetu ni mpendwa mwana na binti wa kiroho wa wazazi wa mbinguni, na, kwa hivyo, kila mmoja wetu yuko na hali takatifu na majaliwa. Ujinsia ni hali muhimu ya maisha ya mtu kabla ya kuzaliwa, maishani mwake duniani, na kutambulika kwake na dhamira yake mbinguni milele. Katika maisha kabla ya kuzaliwa, wana na mabinti wa kiroho wa Mungu walitambua na kumwabudu Mungu kama Baba yao wa Milele na wakalikubali mpangowake ambayo kwayo watoto Wake wangepata mwili na kupokea ujuzi wa kidunia ili waweze kuendelea kwa ukamilifu na hatimaye kupata maisha yake tukufu kama mrithi wa uzima wa milele. iv Mpango takatifu wa furaha unawezesha uhusiano wa kifamilia kuendelea baada ya kifo. Ibada takatifu na maangano yanayopatikana katika hekalu takatifu yanawezesha watu kurudi kwenye uwepo wa Mungu na kwa familia kuungana pamoja milele. Sheria ya kwanza ambayo Mungu alimpa Adamu na Hawa ilihusika na uwezo wao wa kuwa wazazi kama mume na mke. Tunatangaza kwamba sheria za Mungu kwa watoto Wake kuzaana na kujaza dunia bado inadumu. Tunatangaza zaidi kwamba Mungu ameamuru kwamba uwezo takatifu wa uzazi unafaa kutumika tu kati ya mwanamke na mwanamume waliooana kisheria kama mume na mke. Tunatangaza kwamba jinsi ambavyo maisha ya dunia yameumbwa yametakaswa vilivyo. Tunathibitisha utakatifu wa maisha na umuhimu wake katika mpango wa Mungu wa milele. Mume na mke wanajukumu la kipekee la kupendana na kujaliana wao wenyewe na watoto wao. Wana ndio urithi wa Bwana (Zaburi 127:3) Wazazi wana jukumu takatifu la

kukuza watoto wao katika upendo na utakatifu, kuwatimizia mahitaji yao ya kimwili na kiroho, kuwafunza kupendana na kutumikiana, kutii sheria za Mungu na kutii sheria za nchi. Waume na wake akina mama na akina baba watapasishwa mbele ya Mungu kwa utendaji wa jukumu hizi. Familia imetawazwa na Mungu. Ndoa kati ya mwanaume na mwanamke ni muhimu katika mpango Wake wa milele. Watoto wanahaki ya kuzaliwa ndani ya kifungo cha ndoa, na kukuzwa na baba na mama wanaotii nadhiri za ndoa kwa uaminifu kamili. Furaha ndani ya maisha ya familia hupatikana kwa urahisi ukijengwa kwa mafundisho ya Bwana Yesu Kristo. Ndoa na familia bora yanajengwa na kuimarishwa juu ya kanuni za imani, maombi, toba, usamehe, heshima, upendo,huruma, kazi, na maburudisho yafaayo. Katika mpango tukufu, akina baba wanapaswa kuongoza familia zao kwa upendo na utakatifu. Na wanajukumu la kupeana mahitaji ya maisha na kinga kwa familia zao. Akina mama wanajukumu la kuwakuza watoto wao. Katika majukumu haya takatifu, akina baba na akina mama wanajukumu la kusaidiana kama kitu kimoja. Ulemavu, kifo, au hali ingine itasababisha mtu kujiandaa vilivyo. Jamii ya familia inapaswa kutoa msaada inapohitajika. Tunaonya wale watakao vunja maagano ya usafi, wanaodhulumu wapendwa wao au watoto, au wanaokataa kutimiza majukumu ya familia, kwamba siku moja watapasishwa mbele ya Mungu. Kwa kuongezea, tunaonya kwamba utengano wa familia utawaletea watu, jamii, na mataifa maangamizi yaliyotajwa na manabii wa zamani na wa sasa. Tunawaalika wanainchi wenye jukumu na maafisa wa serikali kote kuendeleza ushauri huu uliyowekwa kwa ajili ya kuboresha na kuimarisha familia kama msingi muhimu wa jamii. (Ensign, Nov. 1995, 102). v

Mpangilio na Madhumuni ya Familia Mpangilio Katika Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu la Siku za Mwisho Familia ni takatifu na ndiyo chombo muhimu zaidi kwa jamii wakati huu na milele. Mungu amejenga familia kwa kuleta furaha kwa watoto Wake, kuwaruhusu kujifunza kanuni njema katika hali bora, na kuwatayarisha kupata uzima wa milele. Nyumbani ndio mahali bora pa kufundisha, kusoma, na kufuata kanuni za injili. Ndio mahali ambapo watu hujifunza kuandaa chakula, mavazi, nyumba, na mahitaji mengine. Baba na mama, kama kitu kimoja, wanapaswa kusaidia kila mwanafamilia ku: Tafuta ukweli na kukuza imani katika Mungu. Tubu dhambi, kubatizwa kwa uondoleo la dhambi, kuwa mshiriki wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu la Siku za Mwisho, na kupokee Roho Mtakatifu. Heshimu sheria za Mungu, soma maandiko kwa uangalifu, sali 1

kibinafsi kila siku, na kutumikia wengine. Shirikisha injili na wengine. Pata endaomenti na kuolewa hekaluni kwa mpenzi anayestahili kwa umilele, weka hali yenye furaha katika nyumba yenu, na kuimarisha familia kwa upendo na kujitolea. Tafuta habari kuhusu vizazi waliofariki na uwafanyie ibada za hekalu. Peana lisho linalo hitajika kwa afya ya kiroho, maburudisho, kimwili, na hisia. Baba huongoza familia na ana jukumu la kufundisha watoto na kuwapa mahitaji yao. Baba anayestahili kanisani ana nafasi ya kupokea ukuhani, ambao ndio uwezo na mamlaka ya kufanya kazi katika jina la Mungu. Kwa uwezo huu na mamlaka, baba huwa kiongozi wa ukuhani wa familia. Anaongoza familia yake katika kuwatayarisha kurudi kwenye uwepo wa Baba yetu wa Mbinguni. Mkewe ndiye mwenzi wa maana kwake, mshirika, na mshauri. Mume na mke wanapaswa kushauriana pamoja katika mambo yote yanayohusika na familia nyumbani. Baba anapaswa kupea mahitaji ya kiroho kwa familia yake.anapaswa kuona kwamba wamefundishwa injili ya Yesu Kristo na inampasa kufanya lolote awezalo kuwatia moyo na kuwasaidia kutii sheria za Bwana. Baba aliye na ukuhani anaweza kubariki wanafamilia wake na kuwapa mahitaji yao ya kiroho. Kwa mamlaka ya ukuhani aliyonao na kwa ruhusa kutoka kwa kiongozi wake wa ukuhani, baba anaweza: 1. Kuwapa jina na kubariki watoto. 2. Kubatiza watoto (na watu wengine) 3. Kuthibitisha watoto washiriki wengine wa Kanisa na kuwawekelea mikono ili wapate Roho Mtakatifu. 4. Kupeana Ukuhani kwa vijana wake(na wengine) na kuwatawaza kwenye maafisi za ukuhani. 5. Kubariki na kupeana sakramenti. 6. Kuweka wakf makaburi. Bila kupata ruhusa kutoka kwa kiongozi wake wa ukuhani, baba aliye na Ukuhani wa Melkizedeki anaweza 2

kuibariki mafuta na kuwabariki wanafamilia wake na wengine wakiwa wagonjwa kwa kuwatolea maombi maalum wakati mwingine kunapo kuwa na mahitaji. (Ona kurasa 18 25 kwenye kitabu hiki cha maongozi kwa mafundisho kuhusu jinsi ya kutenda ibada na baraka za ukuhani) Baba anastahili kuhakikisha kwamba familia yake inahusika kikamilifu katika majukumu matatu ya kimsingi: 1. Kujitayarisha kibinafsi na kifamilia kiroho na kimaisha. 2. Kushirikisha injili. 3. Kujihusisha katika historia ya familia na ibada za hekalu kwa waliohai na waliokufa. Mama ni mshirika sawa na mshauri kwa mume wake. Anamsaidia kufundisha watoto wao amri za Mungu. Kama hakuna baba nyumbani, mama huongoza familia. Baba na mama ni lazima wawe katika dhamira moja. Lengo lao lapaswa kuwa la kuwatayarisha wanafamilia wote kurudi kwa Baba wetu wa Mbinguni. Wanapswa kuungana wanapo jaribu kutimiza lengo hili. Bwana ameunda Kanisa ili kuwasaidia akina baba na mama kuwafunza na kulinda familia zao. Watoto wanapoingia katika familia, wazazi wanafaa kuwapenda, kuwafunza ukweli wa injili, na kuwa mifano ya maisha takatifu. Watoto wanafaa kujifunza na kutii sheria za Mungu. Wanapaswa kuheshimu wazazi wao. Nguvu ya Kanisa inategemea familia na watu binafsi kuishi injili ya Yesu Kristo. Jinsi ambavyo familia hufurahia baraka za injili hutegemea zaidi namna baba na mama wanavyo elewa vyema na kutekeleza majukumu yao ya kimsingi kama wazazi. Kanisa halina nia ya kupeana mpangilio au majukumu ya kanisa kwa akina baba na akina mama ambayo yatawalemea au kuwashusha moyo au kuwafanya kupuuza wajibu wao muhimu. Madhumuni Kwa sababu Baba wetu wa Mbinguni anatupenda, Anataka sisi tuinuliwe jinsi Alivyo.Ili kutusaidia, Ametupatia mpango wa kufuata kulingana na amri takatifu za kweli. Wale watakao jifunza kuhusu mpango huo na kuufuata kikamilifu wataweza siku moja kukua kama Baba wetu wa Mbinguni na kufurahia jinsi ya maisha Anayoishi. Sehemu ya Mpango huu ilikuwa ni sisi kuondoka mbinguni na kuja duniani. Hapa tunapokea mwili, tunajifunza kupitia matukio, na kujithibitisha kustahili kuishi tena katika uwepo wa Mungu. Tunajithibitisha kwa kuchagua kibinafsi kutii amri Zake. (Ona Abrahamu 3:23 25; 2 Nefi 2:27). Baba wetu wa mbinguni ametuweka katika familia, ili kutusaidia kujitayarisha kuishi pamoja Naye. Kupitia kwa ibada takatifu na maagano, familia zetu zinaweza kuungana milele. 3

Kufundisha injili Nyumbani Kufundisha Watoto kwa Ufadhili na Upendo Bwana Ameamuru wazazi kufundisha watoto wao injili. Amesema: Na tena, kama wazazi wanao watoto Sayuni, au katika kigingi chake, chochote ambacho kimeundwa, ambao hawawafundishi wao kuelewa mafundisho ya toba, imani katika Kristo Mwana wa Mungu aliye hai, na wa ubatizo na kipawa cha Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono wafikapo miaka minane, dhambi zao zitakuwa juu ya vichwa vya wazazi. Kwani hii itakuwa sheria kwa wakazi wa Sayuni, au katika kila kigingi chake kilichoundwa. Watoto wao watabatizwa kwa uondoleo la dhambi wakiwa na miaka minane, na kupokea kuwekwa kwa mikono. Na pia wawafundishe watoto wao kuomba na kusimama wima mbele za Bwana (M&M 68:25 28) Wazazi wanapaswa kufundisha kwa ufadhili, wakikumbuka ushauri wa Mtume Paulo lea[watoto wao] katika adabu na maonyo ya Bwana (Waefeso 6:4) Masomo ya Familia ya Maandiko Matakatifu Tunaweza kuwa kama Baba wetu wa Mbinguni na kufurahia aina ya maisha ambayo Anaishi tu kwa kutii 4

sheria ambazo baraka zake hutoka (Ona M&M 130:20-21). Kabla (hatujaishi kwa) ya kutii sheria hizo, lazima tujue ni sheria aina gain. Haiwezekani kwa mwanadamu kuokolewa katika ujinga (M&M 131:6). Yesu Kristo ndiye kiongozi na Mtoa sheria wetu. Anajua njia na sheria ambazo tunapaswa kutii, na Amealika kila mmoja wetu kumfuata. Alisema, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi (Yohana 14:6) Vitabu vinne ambavyo Kanisa imekubali kama maandiko matakatifu ni Biblia, Kitabu cha Mormoni, Mafundisho na Maagano, na Lulu ya Thamani Kuu. Vinaeleza sheria za injili na kanuni ambayo kwayo tunaweza kupima fikira yote, matendo, na mafundisho. Vinatusaidia kujifunza kuhusu maisha na mafundisho ya Yesu Kristo na kupeana mifano ya watu waliokuwa na imani kwa Mungu na kutii amri Zake. Yesu ametufundisha kutafuta na kuya soma maandiko matakatifu (ona Yohana 5:39; 3 Nefi 23:1; M&M 88:118). Inawapasa Familia kuyasoma maandiko matakatifu pamoja kila mara kuwawezesha kujifunza na kufuata mafundisho za Bwana. Wazazi wanafaa kuleta pamoja wanafamilia wao wakati wote kila siku kusoma na kujadili maandiko. Kila mwana familia anayeweza kusoma anafaa kupewa nafasi kusoma kutoka kwa maandiko matakatifu. Mwana familia anaweza kujitolea kuomba kabla ya kusoma maandiko na kuomba Baba wa Mbinguni kubariki kila mmoja aweze kuelewa kitakachosomwa na kupokea ushuhuda. Au familia wanaweza kuwa na maombi yao baada ya somo la maandiko. Bila shaka, familia wanaposoma na kutafakari maandiko, watatamani kuwa zaidi kama Mwokozi na watapokea furaha nyingi na amani maishani mwao. Maombi ya kibinafsi na ya kifamilia Kila mmoja wetu lazima ajifunze kuongea na Baba wetu wa mbinguni kupitia maombi. Anatupenda na anataka tuongee Naye. Anataka tumshukuru juu ya baraka zetu na kuomba kwake usaidizi na uongozi. Atatusaidia tunapoomba. Mara nyingi maombi hutolewa kwa kuinamisha vichwa vyetu na kufunga macho yetu wakati tumepiga magoti, tumekaa, au kusimama. Tunapaswa kukumbuka kanuni nne muhimu wakati tunapoomba: 1. Tunaanzisha maombi yetu kwa kuongea na Baba wetu wa Mbinguni: Baba wetu wa Mbnguni... 5

2. Tunamshukuru Baba wetu wa Mbinguni kwa vitu Atupeavyo: Tunakushukuru... 3. Tuna mwomba usaidizi Wake: Tunakuomba... 4. Tunafunga maombi yetu katika jina la Mwokozi: Katika jina la Yesu Kristo, amina. Maombi yetu sio lazima yafuate hatua hizi zote nne, lakini kuziweka akilini itatusaidia kujifunza kuomba. Ni lazima kila mara tuanzishe na kufunga maombi yetu kwa hatua ya kwanza na ya mwisho lakini kile tunachosema katikati itategemea na kile tunachofikiria ni muhimu. Mara nyingine tunaweza kutumia muda wetu mwingi wa maombi kwa kumshukuru Baba wetu wa Mbinguni. Na mara nyingine tunaweza kutumia muda wetu mwingi wa maombi tukiomba usaidizi Wake. Maombi ya kibinafsi Kila mtu anapaswa kuomba kibinafsi angalau kila asubuhi na jioni. Wazazi wanapaswa kufunza watoto wao kuomba kibinafsi mara tu baada ya kuanza kuongea. Wazazi wanaweza kufundisha watoto jinsi ya kuomba kwa kupiga magoti pamoja nao na kuwafanya kurudia sentesi moja kila wakati. Kwa haraka watoto wataweza kupeana maombi yao ya kibinafsi. Maombi ya Familia Kila familia lazima wawe na maombi ya kila siku. Familia nzima hupiga magoti pamoja, na kiongozi wa familia hutoa maombi ama huuliza mwanafamilia kuomba. Lazima kila mmoja apate nafasi ya kuomba kila mara. Watoto wadogo wanaweza kupewa nafasi yao na kusaidiwa na wazazi wao. Wakati wa maombi ya familia ni nafasi bora ya kuwafundisha watoto jinsi ya kuomba na pia kuwafundisha kanuni kama imani 6

katika Mungu, unyenyekevu, na upendo. Maombi Maalum Wazazi wanapaswa kufundisha watoto wao kwamba Mungu yuko tayari kusikia maombi yao. Kwa kuongezea kwenye maombi yao ya kibinafsi na ya kifamilia, wanaweza kuomba kwa wakati wowote wanapohitaji usaidizi maalum au wanapotaka kudhihirisha shukrani zao. na mama walio na watoto, wazazi wenye watoto walio pekee, wazazi wasio na watoto nyumbani, wale hawajaoa katika vikundi vya mkutano wa jioni, na wale wanaoishi pekee yao ama na wenzao kwenye vyumba. Kila mtu haijalishi hali yake, atabarikiwa kwa kuwa na mkutano wa jioni wa familia. Kanisa halijapangia shughuli zozote kila Jumatatu jioni ili wanafamilia waweze kuwa pamoja katika mkutano wa jioni wa familia. Kubariki chakula Wazazi wanapaswa kuhakikisha kwamba wanafamilia wanajifunza kumshukuru Mungu kwa chakula chao na kumwomba kuibariki kabla hawajaila. Kila mtu, pamoja na watoto wadogo, wanapaswa kuchukua mkondo wa kupeana maombi. Kupeana maombi kwa baraka za chakula husaidia wazazi na watoto kujifunza kuwa wenye shukrani kwa Baba wetu wa Mbinguni. Mkutano wa Jioni wa Familia Kila mtu anapaswa kuwa na Mkutano wa jioni wa Familia, baadhi yao mume na mke waliooana majuzi, akina baba Urais wa Kwanza ulisema: Tunawaahidi baraka kuu kama mtafuata ushauri wa Bwana na kuwa na mkutano wa familia jioni kila mara. Tunaomba kila mara kwamba wazazi Kanisani watakubali wajibu wao wa kufundisha na kuwa mfano kwa watoto wao kwa kutii kanuni za injili. Bwana Awabariki ili muwe watendaji katika jukumu hili muhimu ( Message from the First Presidency, Family Home Evening Resource Book [1983], iv). Kama Mzee wa familia yake, baba huongoza kwenye mkutano wa jioni wa familia. Kama baba amekosekana, mama huongoza. Wazazi wataongoza 7

au kuchagua mwana familia kuendesha mkutano wa jioni wa familia. Wanafundisha somo au kukabidhi mafundisho kwa watoto walio na umri wa kutosha kuweza kufunza. Kila mmoja aliye na umri wa kutosha anapaswa kuwa na nafasi ya kushiriki. Watoto wadogo wanaweza kusaidia kwa njia kama kuongoza nyimbo, kunukuu maandiko, kujibu maswali, kubeba picha, kupeana viburudisho, na kuomba. Mpangilio uliowekwa kwa mkutano wa jioni wa familia ni kama yafuatayo: Wimbo wa kufungua (na familia) Maombi ya kufungua (na mwanafamilia) Shairi au masomo la maandiko matakatifu (na mwanafamilia) Mafundisho (na baba, mama, au mototo mkubwa) Shughuli (Ikiongozwa na mwanafamilia na wanafamilia wote wakiwa wanashiriki) Wimbo wa kufunga (na familia) Maombi ya kufunga (na mwanafamilia) Viburudisho Familia inaweza kufanya mkutano wa jioni wa familia kwa njia nyingine nyingi. Shughuli yo yote ambayo inaleta familia pamoja, inayo imarisha upendo kati yao, Inayosaidia kuwaleta karibu na Baba wa Mbinguni, na kuwahimiza kuishi kitakatifu, huwa ni mkutano wa jioni wa familia. Mifano ya shughuli kama hizo ni pamoja na kusoma maandiko matakatifu, kujadili injili, kushirikisha ushuhuda, kufanya kazi ya huduma, kuimba pamoja, kuenda kukulia mashambani, kucheza mchezo wa familia, na kusafiri kwa miguu. Mikutano zote za jioni za familia lazima ziwe na maombi. Masomo ya mkutano wa jioni wa familia yanaweza kuhusiana na maandiko matakatifu; maneno ya manabii wa siku za mwisho, haswa ujumbe wa mkutano mkuu; na matukio ya kibinafsi na ushuhuda. Masomo mengi yanafaa yataje kuzaliwa, kuishi, mafundisho, na Upatanisho wa Mwokozi. Kanuni za injili, Misingi za injili, Kweli katika Imani, Kwa Uthabiti wa Vijana, na magazeti za Kanisa huwa na nakala na habari ingine inayohusu masomo mengi ambayo yanaweza kutumika katika masomo ya mkutano wa jioni wa familia. Vichwa vifuatavyo vinaweza kusaidia katika majadiliano yenu: Mpango wa wokovu Maisha na mafundisho ya Yesu Toba Maombi Kufunga Neno la Hekima Kanuni ya Bwana ya uadilifu Maana ya sakramenti Fungu la kumi Shukrani 8

Uaminifu Uchaji kwa Mungu na heshima kwa maumbile Yake. Kujitayarisha kwa ubatizo, agizo la ukuhani, au ndoa. Kujitayarisha kwenda hekaluni Kusoma maandiko matakatifu Kuweka takatifu siku ya Sabato Kusamehe wengine Kupokea na kushirikisha ushuhuda Kushiriki injili na wengine Kukusanya historia za familia Kuelewa na kukubali kifo Kusuluhisha matatizo za familia Kusimamia mambo ya fedha ya familia Kugawana kazi ya nyumbani ya familia Kufurahia na kusherekehe muziki Sikukuu na Matukio Maalum Sikukuu na Matukio maalum, kama vile Sikukuu ya kuzaliwa kwa Kristo; Pasaka; ukumbusho wa urejesho wa ukuhani; kwenda misheni kwa mwanafamilia; au kuzaliwa, ubatizo, kutawaza kwa mwanafamilia, zote zinaweza kuwa nafasi bora zaidi kwa kufundisha ukweli wa injili. Fungu la kumi na Zaka Bwana ameamuru watu Wake kuishi sheria ya fungu la kumi na kustahili baraka zilizo ahidiwa (ona Malaki 3:8 11). Wakati bora kwa wazazi kufundisha sheria ya fungu la kumi na zaka ni wakati wanapolipa wenyewe. Watoto wanavutiwa na kile wanaona wazazi wao wanafanya. Watoto wanaopokea pesa wanapaswa kulipa fungu la kumi. Kila mtoto anaweza kuwa na mahali tatu tofauti pa kuwekea pesa: moja pa fungu la kumi, moja pa misheni, na moja pa pesa ya matumizi. Kila wakati watoto wanapopokea pesa, wanapaswa kujifunza kuweka asili mia kumi kwenye benki ya fungu la kumi kwanza, halafu pesa zingine katika benki ya misheni, na yaliyo bakia kwenye benki ya pesa za matumizi. Wakati watoto wanalipa fungu la kumi, wazazi wanapaswa kuwafundisha kujaza kwenye kijikaratasi cha fungu la kumi, kuiweka kwenye bahasha pamoja na pesa, na kupeana au kutuma bahasha hiyo kwa mwanachama wa Uaskofu au urais wa tawi. Familia zinazoishi kwenye sehemu zilizotengwa wanapaswa kupeana fungu lao la kumi kwa kiongozi wao wa ukuhani. 9

Mazungumzo Wakati wa kula Wakati wa kula unaweza kuwa muda mzuri wa kuongea kuhusu injili. Watoto wadogo wanapenda kuuliza na kujibu maswali za injili. Ikiwa hawajui majibu, baba au mama anaweza kupeana majibu mafupi na kufundisha injili. Sio wakati wote wa kula lazima uwe ni majadiliano ya injili, lakini majadiliano kama hayo mara mbili au tatu kwa wiki yanaweza kusaidia familia kujifundisha injili. Hadithi wakati wa kulala Kwa sababu watoto wengi wanapenda kusikiliza hadithi kabla ya kulala, huu ni wakati bora wa kufundisha injili kwa kusema au kusoma hadithi kutoka kwa maandiko matakatifu, machapisho ya Kanisa, au matukio ya kibinafsi. Hadithi kuhusu uaminifu, kushirikiana, na wema yanafundisha kanuni muhimu za injili. Kufanya kazi Pamoja Nafasi nyingi za kufundisha injili huja wakati familia wanafanya kazi pamoja nyumbani. Wanaposafisha nyumba au kufanya kazi uwanjani au shambani, kwa mfano, wazazi wanafaa kuwa macho ili kupata nafasi za kuwazungumzia injili. Mtoto atauliza maswali kila mara. Wazazi wanafaa kuchukua wakati na kuwapa majibu rahisi. Misemo kama Wewe ni mfanyikazi mzuri. Nina hakika Baba wa Mbinguni anapendezwa nawe au Tazama mawingu mazuri ambayo Baba wa Mbinguni ametengeneza yanaweza kuwapa watoto hisia za shukrani kwa Baba wetu wa Mbinguni na uhakikisho kwamba Yeye yuko. Mabaraza za Familia Wazazi wanaweza kuleta pamoja wanafamilia katika baraza la familia. Familia zinaweza kutumia mabaraza haya kujadili malengo ya familia, kusuluhisha matatizo ya familia, kujadili mambo ya kifedha, kufanya mipango, kuunga na kuimarisha kila mmoja wao, kupeana ushuhuda, na kuombeana. Baraza linaweza kufanywa wakati wowote inapohitajika. Wazazi wanaweza kufanya baraza la familia kila jumapili au pamoja na mkutano wa jioni wa familia. Heshima kwa maono na hisia za wengine ni muhimu kwa ufanisi wa mabaraza za familia. 10

Mahojiano ya Faragha Wazazi wengi hugundua kwamba mahojiano ya faragha ya kila mara na kila mtoto huwasaidia kuwa na uhusiano mzuri na watoto wao, inawahimiza, na kuwafundisha injili. Mahojiano kama hayo yanaweza kuwa yenye kupangwa au yasiopangwa na inaweza kufanyika kila mara. Mzazi anapaswa kudhihirisha upendo na uthabiti kwa mtoto, na mtoto anapaswa kuwa na nafasi ya kudhihirisha hisia zake kuhusu jambo lolote, shida, au matukio. Mzazi lazima asikie kwa makini na kuchukua matatizo na siri mtoto za kwa makini. Mzazi na mtoto wanaweza kuomba pamoja. Matatizo yanayo tambulika kwenye mahojiano ambayo yanahusisha wanafamilia wengine yanaweza kukabiliwa kwenye mkutano ujao wa jioni wa familia. Shughuli za Familia Wazazi wanapaswa kupanga kila mara wakati wa kuifanya familia nzima kufanya vitu pamoja. Matembezi, kufanya kambi, mradi wa familia, kazi za uwanjani na nyumbani, kuogelea, kutali kwa miguu, na sinema za kufaa na tamasha mengine ni machache ya shughuli ambazo familia wanaweza kufurahia pamoja. Familia ambayo inafurahia shughuli kwa pamoja itahisi upendo mkubwa na amani. Watoto wataweza kuwa huru kuwasikiliza wazazi wao na kufuata mashauri yao wanapojihisia kuwa karibu nao. Wazazi wataweza kufundisha injili vyema zaidi. 11

Kutimiza Wajibu w Familia Lengo la Kanisa la Bwana ni kusaidia watu wote kuja kwa Kristo. Familia zinaweza kusaidia kutimiza lengo hili ikiwa wana: 1. Jipatia mahitaji yao ya kiroho na kimwili na kusaidia kutimiza mahitaji ya wengine. 2. Shiriki injili na wengine. 3. Hakikisha kwamba wanafamilia wanapokea ibada za hekalu na kusaidia katika kuwapa wazazi wao waliokufa baraka hizi. Mahitaji ya Kiroho na ya Kimwili Mahitaji ya Kiroho Katika Sehemu zilizotangulia za kitabu hiki cha mwongozo, kichwa 12 Kufundisha Injili Nyumbani, ziko na habari juu ya jinsi familia wanaweza kujipa mahitaji ya kiroho. Mahitaji ya Kimwili Familia wanapaswa kijitegemea wenyewe ili waweze kujipatia mahitaji yao ya kimwili na kuwasaidia wengine. Ili kuweza kujitegemea, wanafamilia lazima wakubali kufanya kazi. Maana ya kazi ni juhudi ya kimwili, kiakili, au ya kiroho. Ndiyo chanzo cha matendo mema, furaha, heshima, na utajiri. Wazazi lazima wajaribu kujitegemea wenyewe na wanapaswa kuwafundisha watoto wao vivyo hivyo. Ukiwa mwenye kujitegemea, utaweza kusaidia wengine wenye mahitaji.

Akina Baba wana jukumu la kuwapa familia zao ulinzi na mahitaji za maisha. Akina mama wana jukumu muhimu la kuwakuza watoto wao. Wazazi huhakikisha kwamba familia wanayo nyumba safi, chakula cha kutosha, mavazi, matibabu na uangalifu wa meno, nafasi za masomo, maelezo katika kusimamia rasilmali za kifedha, na ikiwezekana, mafunzo jinsi ya kukuza vingi vya vyakula vyao. Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao jinsi ya kupika vyakula vyao wenyewe na jinsi ya kuvitunza kwa matumizi ya baadaye. Wazazi lazima waweze kufanya kazi kwa bidii ili kutosheleze mahitaji haya ya kimwili Na hamtakubali watoto wenu kupatwa na njaa, au kukaa uchi (Mosia 4:14). Wazazi lazima wajipange na kujitayarisha kutoa mahitaji ya familia wakati wa ugonjwa, majanga, ukosefu wa kazi, au matatizo mengine. Kama baba hawezi kupeana mahitaji ya kimwili ya familia yake na kama wanafamilia wengine hawawezi kusaidia, anaweza kutafuta usaidizi kutoka kwa viongozi wa ukuhani. Watoto wanaweza kusaidia kwa kutoa mahitaji ya kimwili ya familia zao kwa kuwasaidia wazazi wao kwa kazi, kusoma vyema shuleni, kutunza mavazi na vitu vingine vyao, kujiweka wenyewe na nyumba yao safi na iliyopangwa, na kuhifadhi afya bora. Wanafamilia lazima waongeze uwezo wao wa kusoma, kuandika, na kufanya mahesabu ya kimsingi na lazima wachukue kila nafasi kupata elimu na kuongeza ujuzi. Ni lazima waheshimu Neno la Hekima na kukula chakula yenye afya. Iwezekanapo, familia lazima iweke akiba ya mwaka mmoja, au kadiri wawezavyo, ya vitu muhimu vinavyohitajika kuedeleza maisha. Wanafamilia lazima waepuke na madeni yasiyohitajika, waweke akiba kwa wakati ujao, watimize mahitaji yao yote, na kuzitumia rasilmali kwa hekima, na kuzuia hasara. Wazazi lazima wafundishe watoto wao kugawana na wengine. Karibu kila mtu anaweza kupeana kitu, haijalishi kiasi walicho nacho. Njia moja ya kuwasaidia walio na mahitaji ni kwa kufunga kwa kula kila mwezi na kutoa zaka la kufunga, ambayo inatumika kwa kuwalisha wenye njaa, kuwapa makao wasiokuwa nao, kuwavalisha waliouchi, na kuwasaidia walioathiriwa. Tunaonyesha upendo wetu kwa Bwana tunapowasaidia wengine. Alisema, Kadiri mlivyomtedea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitedea mimi (Mathayo 25:40). Ushiriki wa Injili 13

Bwana, kupitia kwa Manabii Wake wa siku za mwisho, amefundisha kwamba kila mshirika wa Kanisa ana jukumu la kushiriki injili na wengine. Ni wajibu wa kila mtu ambaye ameonywa amwonye jirani yake. (Ona M&M 88:81) Alma, nabii katika Kitabu cha Mormoni, alielezea kwamba wakati tunapobatizwa lazima tukubali kusimama kama mashahidi wa Mungu nyakati zote na katika vitu vyote, na katika mahali popote mlipo (Mosia 18:9). Wanafamilia wanapaswa kufanya kila wawezavyo kuwasaidia jamaa zao, marafiki, na majirani kujifunza kuhusu injili ya Yesu Kristo na baraka itakayoleta maishani mwao. Katika kushiriki injili, wazazi na watoto wanaweza kuimarisha ushuhuda wao wenyewe na kuleta baraka za injili kwa wengine. Familia zinaweza: Kuwa mfano mwema kwa kutii sheria zote (ona Mathayo 5:16). Kuwa na shukrani kwa uanachama wao Kanisani (ona Warumi 1:16) na kuwajulisha wengine kwamba wao ni washiriki. Kuwauliza marafiki kama wangetaka kujua mengi kuhusu Kanisa. Kuuliza Bwana kuwasaidia kuchagua familia au mtu ambaye yuko tayari kusikiliza injili. Kufahamisha familia au mtu binafsi kwa Kanisa kwa njia tofauti, kama kuwaalika kwenye mkutano wa jioni wa familia au kwenye mkutano au shughuli za Kanisa, kuwapa vitabu vya Kanisa au vijitabu kusoma, au kuzungumza nao kuhusu baraka za injili. Kualika familia au mtu binafsi nyumbani mwao kufundishwa na wamissionari. Wazazi wana jukumu la kujitayarisha na kuwatayarisha watoto wao kutumikia umisheni wa muda wote. Ili kuwatayarisha watoto, haswa vijana, wazazi wanapaswa kufundisha injili nyumbani, soma maandiko matakatifu na kuwa na maombi kibinafsi na kifamilia, na kuzungumza kila mara kuhusu majukumu na baraka za kushiriki injili. Wanaweza kuwafundisha watoto wao jinsi ya kuweka pesa kwa ajili ya misheni, kufanya kazi kwa bidii, kujitegemea wenyewe, na kuwapenda na kuwatumikia watu wengine. Ibada ya Hekalu kwa waliohai na waliokufa Hekaluni, washiriki wa Kanisa hupokea ibada tukufu na kufanya maagano 14

na Mungu. Wanashiriki pia katika kazi ya ibada kwa mababu zao waliokufa. Ikiwezekana, baba na mama wanapaswa kupokea cheti cha kuingia hekalu kutoka kwa viongozi wa ukuhani na kuenda hekaluni kupokea ibada zao wenyewe. Kama hawawezi kuenda hekaluni, wanapaswa kuishi kustahili hiyo cheti. Familia zina jukumu la kuhakikisha kwamba ibada za hekalu zinafanyiwa mababu wao waliokufa kabla ya kuzipokea. Washiriki wa Kanisa waliopokea ibada zao lazima warudi hekaluni mara kwa mara kadiri wakati, uwezo, na nafasi hekaluni inawawezesha kuwayafanyia ibada mababu zao. Akina baba na mama lazima wakusanye kumbukumbu zilizoandikwa za matukio muhimu maishani mwao na katika maisha ya watoto wao, pamoja na vyeti vya baraka, ubatizo, maagizo, ndoa, na vifo; mabarua muhimu; picha; matangazo muhimu; na vitu kama hivyo. Wanapaswa kukusanya historia zao wenyewe za kibinafsi na kuhimiza kila mwanafamilia kuweka historia yake mwenyewe. Wanapaswa kuwasaidia watoto wao kuanzisha historia zao za kibinafsi. Familia zinapaswa kukusanya habari kuhusu mababu zao na kuiweka kwenye historia za familia. Wanapaswa kuanza hii kwa kukusanya habari juu ya vizazi vinne vya kwanza. Mafundisho ya Uongozi Chini ya uongozi wa viongozi wa kigingi, misheni, au wilaya, viongozi wa ukuhani na wasaidizi wa vitengo wanapaswa kuwafundisha wazazi kuelewa na kutenda jukumu tatu za kifamilia (ona kurasa 12 15). Viongozi wanapaswa kuwafundisha akina baba na mama jinsi ya kuongoza familia zao. Kama familia wanaishi kwenye eneo iliyojitengwa, viongozi wa kigingi, misheni, au wilaya wanapaswa kuhakikisha kwamba wazazi wanajifunza na kutimiza majukumu yao. 15

Kuandaa Ibada ya Maombi Nyumbani (Kwa familia zilizo kwenye maeneo Yaliyotengwa) Baadhi ya familia wanaoishi kwenye maeneo yaliyotengwa na hawawezi kufika kwenye mikutano za mtaa au tawi. Ruhusa kutoka kwa rais wa kigingi, misheni, au wilaya itawezesha familia kama hizo kufanya ibada za maombi ya Jumapili nyumbani mwao. Kwenye maeneo yasiyokuwa na mipangilio ya Kanisa, familia zinahitaji ruhusa kutoka kwa Rais wa Eneo. Baba au kiongozi mwingine wa ukuhani anaweza kutayarisha na kubariki sakramenti kama anastahili, kama ni kuhani katika ukuhani wa Haruni au anao Ukuhani wa Melkizedeki, na anayo ruhusa kutoka kwa viongozi wake wa ukuhani. Mwenye ukuhani yeyote anaweza kupeana sakramenti. Maelezo kwa upeanaji wa sakramenti yako katika kurasa 21 23 wa kitabu hiki cha maongozi. 16 Ibada ya Jumapili inapaswa kuendashwa kwa njia rahisi, takatifu, na yenye heshima. Inaweza kujumulisha yafuatayo: 1. Wimbo wa kufungua 2. Mombi ya kufungua 3. Kubariki na Kupeana sakramenti 4. Moja au zaidi ya mambo yafuatayo: Somo moja au mbili (ya maongezi mafupi) au ushuhuda. Kusoma na kujadilia juu ya Maandiko matakatifu kama familia Mafundisho na mwanafamilia 5. Wimbo wa kufunga 6. Maombi ya kufunga

Katika kupanga ibada ya Jumapili, wazazi wanapaswa kutamani na kufuata maongozi ya Roho wa Bwana. Watu kwenye Kitabu cha Mormoni walipeana mifano ya huduma aina hii: Na mikutano yao iliendeshwa na kanisa kulingana na njia ambayo Roho aliwaongoza, na kwa uwezo wa Roho Mtakatifu; kwani vile uwezo wa Roho Mtakatifu ulivyowaongoza kuhubiri, au kuhimiza, au kuomba, hata hivyo ndivyo ilivyofanywa (Moroni 6:9). Familia inapaswa kutumia maandiko matakatifu kama mwongozo wao wake wa msingi. Pia Kwa kuongezea, wanaweza kutumia ujumbe wa mkutano mkuu, Misingi ya za Injili injili, Kanuni za Injili injili, Imara Katika Imani Ukweli kwa Imani, Kwa Uthabiti wa Vijana, vijitabu vya umisionari, nakala za Kanisa, na machapisho mengine ya Kanisa na mitazamo ya video. Kama hakuna yeyote katika familia aliye na ukuhani ufaao, baba au mama anaweza kuwakusanya wanafamilia pamoja kuimba nyimbo, kusoma maandiko matakatifu, kuomba, na kukua karibu pamoja na kwa Baba wa Mbinguni. Kiongozi wa familia anapaswa kupanga mara kwa mara, nafasi za familia kupokea sakramenti. Wazazi wanapaswa kuwa na shughuli za wiki, kama matembezi mbali na nyumbani, matembezi ya kula mshambani, maonyesho bora ya sinema, kuwatembelea jamii, michezo, mipangilio ya muziki, na kuogelea. Familia wanapaswa kutoa fungu la kumi, zaka za kufunga, na matoleo mengine kwa kiongozi wao wa ukuhani. Familia hawatoi ripoti yoyote iliyoandikwa kwa Kanisa, lakini kiongozi wao wa ukuhani humhoji baba kila mara, na kumuuliza kuripoti juu ya familia. Palipo na haja, viongozi wanaweza kufanya mahojiano haya kwenye simu. 17

Ibada na Baraka za Ukuhani Ibada za Maagizo ya Ukuhani ni vitendo takatifu vinavyopewa na Bwana na kutendwa kwa mamlaka ya ukuhani. Baraka za Ukuhani zinapewa kwa mamlaka ya ukuhani kwa uponyaji, faraja na kutia moyo. Ndugu wanaotenda ibada na kutoa baraka wanapaswa kujitayarisha kwa kuishi kulingana na kanuni za injili na kwa kujitahidi kuongozwa na Roho Mtakatifu. Wanapaswa kufanya kila ibada na kutoa baraka katika njia ya heshima na kuambatana na mahitaji yafuatayo; ibada inapaswa: 1. Kufanywa katika jina la Yesu Kristo 2. Kufanywa kwa mamlaka ya ukuhani. 3. Kufanywa na mipangilio muhimu, kama vile kutumia maneno kamili au kutumia mafuta yaliyotakaswa. 4. Kuruhusiwa na kiongozi aliyechaguliwa aliye na vifunguo vinavyostahili, ikihitajika. Ibada zinazohitaji ruhusa ya kiongozi wa ukuhani ni kuwapa watoto majina na kuwabariki, kufanya ubatizo na uthibitisho, kupeana ukuhani na kuagizwa kwa afisi ya ukuhani, kubariki na kupeana sakramenti, na kuweka wakfu makaburi. Wakati ndugu kadha wanaposhiriki kwenye agizo au kubariki, kila mmoja huweka mkono wake wa kushoto kwenye bega la ndugu aliye upande wa kushoto. Tabia ya kualika kikundi kikubwa ya wenye ukuhani haifai. 18

Ibaada na baraka yaliyoelezwa kwenye sehemu hii yatawasaidia akina baba kutumika kama wazee wenye heshima kwenye familia zao. Kuwataja na kuwabariki Watoto 1. Humwita Baba wa Mbinguni 2. Husema kwamba baraka linapeanwa kwa mamlaka ya Ukuhani wa Melkizedeki. 3. Humpa mtoto jina 4. Husema baraka za Ukuhani jinsi Roho anavyoelekeza. 5. Hufunga katika jina la Yesu Kristo. Ubatizo Kila muumini wa Kanisa la Kristo mwenye watoto anapaswa kuwaleta kwa Wazee, mbele ya Kanisa, ambao wataweka mikono juu yao katika jina la Yesu Kristo, na kuwabariki katika jina la lake (D&C 20:70). Kulingana na ufunuo huu, wanaume wanaostahili walio na Ukuhani wa Melkizedeki wanaweza kushiriki katika kuwataja na kuwabariki watoto. Agizo la kuwataja na kuwabariki watoto linahitaji ruhusa kutoka kwa mamlaka ya usimamizi. Wakati wa kubariki mtoto, wanaume waliyo na Ukuhani wa Melkizedeki hukusanyika kwenye mviringo na kumbeba mtoto mikononi mwao. Wakati wa kubariki mtoto mkubwa, ndugu wataweka mikono yao kwa urahisi juu ya kichwa cha mtoto. Mtu anayepeana baraka: Chini ya uongozi wa mamlaka wa usimamizi, kuhani anayestahili au mtu aliye na Ukuhani wa Melkizedaki anaweza kufanya ubatizo. Ili kufanya hivyo, yeye: 1. Husimama ndani ya maji pamoja na mtu anayebatizwa. 2. Kwa mkono wake wa kushoto, yeye hushikilia kifundo cha kiume cha mtu anaye batizwa kwa njia iliyo rahisi na ya ulinzi; mtu anaye batizwa hushikilia kifundo cha kushoto cha yule anayembatiza kwa mkono wake wa kushoto. 3. Huinua mkono wake wa kulia kwa mraba 19

4. Hutaja majina kamili ya yule mtu na kusema, Kwa mamlaka niliyopewa na Yesu Kristo, Ninakubatiza katika jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Amina (M&M 20:73) 5. Ndipo anayebatizwa atashikilia mapua yake kwa mkono wa kulia kwa urahisi; yule anayefanya ubatizo ataweka mkono wake wa kulia juu kwenye mgongo wa yule anayebatizwa na kumzamisha kabisa katika maji, pamoja na mavazi yake. 6. Kumwinua aliyebatizwa kutoka kwa maji. Makuhani wawili au wanaume walio na Ukuhani wa Melkizedeki hushuhudia kila ubatizo ili kuhakikisha limefanyika vilivyo. Ubatizo lazima urudiwe kama maneno hayajasemwa jinsi yalivyopeanwa katika Mafundisho na Maagano 20:73 au kama sehemu ya nguo ya anayebatizwa haikuzamishwa yote. Mtu anaye batizwa na yule anayebatiza lazima wavae mavazi meupe yasiyo penyeka wakati ziko baridi. Uthibitisho Waongofu walio na miaka tisa au zaidi na wale walio na miaka nane na amabao wazazi wao sio washiriki wanathibitishwa kwenye mkutano wa sacrament (ona M&M 20:41). Watoto wa miaka minane wanaweza kuthibitishwa punde tu baada ya ubatizo kwenye eneo la ubatizo kama angalau mzazi mmoja ni mshiriki wa Kanisa na wazazi wote wamepeana idhini kwa ubatizo na uthibitisho. Chini ya maelekezo ya askofu au rais wa tawi, mwanaume mmoja au zaidi aliye na Ukuhani wa Melkizedeki anaweza kufanya agizo hili. Wanaweka mikono yao kwa upole juu ya kichwa cha mtu. Yule anayefanya agizo: 1. Atasema majina kamili ya mbatizwa. 2. Atasema kwamba agizo linafanywa kwa mamlaka ya Ukuhani wa Melkizedeki. 3. Atamthibitisha mbatizwa kama mshiriki wa Kanisa la Yesu Kristo la watakatifu wa siku za mwisho. 4. Atampea karama la Roho Mtakatifu kwa kusema, Pokea Roho Mtakatifu. 5. Atatoa baraka ya ukuhani jinsi Roho anavyoelekeza. 6. Atafunga katika jina la Yesu Kristo. 20

Kupeana Ukuhani na kuagiza kwa Afisi za Ukuhani. Askofu au rais wa tawi husimamia upeanaji wa Ukuhani wa Haruni na maagizo kwa maafisi za shemasi, mwalimu, na kuhani. Kabla mtu hajaagizwa kwa afisi katika Ukuhani wa Haruni, lazima ahojiwe na askofu au rais wa tawi na apatikane anastahili. Pia, lazima athibitishwe kwenye mkutano wa sakramenti. Kwa idhini ya askofu au rais wa tawi, kuhani anaweza kupeana Ukuhani wa Haruni kwa mtu mwingine na kumwagiza kwenye afisi ya Ukuhani wa Haruni. Rais wa kigingi au misheni husimamia upeanaji wa Ukuhani wa Melkizedeki na uagizo kwenye maafisi za mzee na kuhani mkuu Ili kupeana ukuhani au kuagiza mtu kwenye afisi ya ukuhani. Mtu mmoja au zaidi aliye na ukuhani unaofaa na aliye idhinishwa na mamlaka ya usimamizi huweka mikono yao kwa urahisi juu ya kichwa cha mtu huyo. Yule anayefanya agizo: 1. Anaita mtu kwa majina yake kamili. 2. Anasema mamlaka(ukuhani wa Haruni au Melkizedeki) ambayo kwayo agizo linafanywa. 3. Anapasisha Ukuhani wa Haruni au wa Melikizedeki, ila tu kama limepeanwa mbeleni. 4. Anamwagiza kwa afisi katika Ukuhani wa Haruni au wa Melkizedeki na kumkabidhi haki, uwezo, na mamlaka ya afisi hio. 5. Anapeana baraka ya ukuhani jinsi Roho anavyoelekeza. 6. Anafunga katika jina la Yesu Kristo. Sakramenti Sakramenti ni agizo takatifu sana. Kupokea sakramenti hutupatia nafasi ya kukumbuka maisha, mafundisho, na Upatanisho wa Yesu Kristo. Ni wakati wa kuweka upya maagano uliyoweka na Bwana wakati wa ubatizo. (ona Mosiah 18:8 10). Waalimu na makuhani wanaweza kutayarisha sakramenti; makuhani wanaweza kuibariki; na mashemasi, waalimu, na makuhani kuipeana. 21

Ndugu waliyo na Ukuhani wa Melkizedeki wanaweza kutayarisha, kubariki, na kupeana sakramenti lakini kwa kawaida watafanya hivyo tu wakati kuna ndugu wachache wenye Ukuhani wa Haruni. Kama mtu ametenda makosa mabaya, hapaswi kutayarisha, kubariki, au kupeana sakramenti hadi atakapo tubu na kusuluhisha jambo hilo na askofu wake au rais wa tawi. Wale wanaotayarisha, kubariki, au kupeana sakramenti kwa wengine wanafanya agizo hilo kwa niaba ya Bwana. Kila mtu aliye na ukuhani anapaswa kutekeleza kazi hii kwa hali ya utaratibu, na utukufu. Anapaswa kuwa mnadhifu, msafi, na mwenye mavazi mema. Sura ya kibinafsi inapaswa kuonyesha utakatifu wa agizo. Wandugu wanao tayarisha sakramenti wanapaswa kufanya hivyo kabla mkutano halijaanza. Wanaweka mkate ambao haujakatwa kwenye sinia na kuweka sinia za vikombe vya sakramenti vilivyo na maji safi kwenye meza ya sakramenti. Wanafunika mkate na maji kwa kitambaa cheupe kilicho safi. Wakati wa wimbo wa sakramenti, wale kwenye meza la sakramenti wanaondoa kitamba kutoka kwenye sinia za mikate na kukata mikate kwa vipande vidogo vidogo. Baada ya wimbo, mtu anaye bariki mkate anapiga magoti na kutoa maombi ya sakramenti kwa mkate. Halafu ndugu wanapitisha mkate kwa walioko kwa njia iliyo taratibu na takatifu. Wasimamizi wenye mamlaka mkutanoni hupokea sakramenti kwanza. Wakati kila mtu amepata nafasi ya kupokea mkate, wanaoupitisha wanarudisha sinia zao kwenye meza ya sakramenti. Wale wanaobariki sakramenti hufunika sinia tena mara tu mkate umepeanwa. Wale kwenye meza ya sakramenti huondoa kitamba kwenye sinia za maji. Yule anayebariki maji hupiga magoti na kutoa maombi ya sakramenti kwa maji. Halafu ndugu wanapitisha maji kwa walioko. Sinia hurudishwa kwenye meza ya sakramenti na kufunikwa tena. Ndugu wanao bariki na kupeana sakramenti hukalia viti vyao pamoja na waumini. Sakramenti ni ya waumini wa Kanisa, pamoja na watoto. Yule anayeongoza mkutano hafai kutangaza kwamba itagawiwa washiriki pekee; wale wasio washiriki hawafai kuzuiliwa kuipokea. Maombi ya sakramenti yanapaswa kusemwa kwa njia dhahiri, barabara na ya heshima. Kama mtu anayebariki sakramenti anafanya makosa katika maneno na hajirekebishi, askofu au rais wa tawi humwambia arudie ombi na kulitoa itakikanavyo. Ombi kwa mkate linafuata Ee Mungu, Baba wa Milele, tunakuomba katika jina la Mwanao, Yesu Kristo, ubariki na utakase mkate huu kwa roho za wale wote watakaoula, ili waweze kuula kwa ukumbusho wa mwili wa Mwanao, na wakushuhudie, 22

Ee Mungu Baba wa Milele, kwamba wanataka kujivika juu yao jina la Mwanao, na kushika amri zake ambazo amewapa, ili daima wawe na Roho yake. Amina (M&M 20:77 na Moroni 4). Ombi kwa maji linafuata: Ee, Mungu, Baba wa Milele, tunakuomba katika jina la Mwanao, Yesu Kristo, ubariki na utakase [maji] haya kwa roho za wale wote watakaoyanywa, ili waweze kufanya hivyo kwa ukumbusho wa damu ya Mwanao, ambayo ilimwagwa kwa ajili yao; kwamba washuhudie kwako, Ee Mungu, Baba wa Milele, kwamba daima wamkumbuke, ili Roho wake apate kuwa pamoja nao. Amina (M&M 20:79 na Moroni 5). Sakramenti inapaswa kuondolewa mezani haraka iwezekanavyo baada ya mkutano. Mkate wowote unaobakia unaweza kutumiwa kama chakula. Kubariki na kupeana sakramenti kunahitaji idhini kutoka kwa msimamizi aliye na mamlaka. Kutakasa Mafuta Mtu mmoja aliye na Ukuhani wa Melkizedeki hutakasa mafuta halisi ya mzeituni kwa matumizi yake takatifu ya kuwabariki wagonjwa au wale walio na msiba Yule anayetakasa mafuta: 1. Hushika chupa kilicho wazi cha mafuta ya mzeituni. 2. Anamwita Baba wetu wa Mbinguni. 3. Anasema kwamba anatenda kwa mamlaka ya Ukuhani wa Melkizedeki. 4. Anatakasa mafuta (sio chupa) na kuyatenga kwa kazi ya kuwabariki wagonjwa na wale walio na msiba 5. Anafunga katika jina la Yesu Kristo. Kuwahudumia Wagonjwa Ni wanaume tu walio na Ukuhani wa Melkizedeki wanaoweza kuhudumia wagonjwa au wenye msiba Kwa kawaida, wawili au zaidi huhudumu pamoja, lakini mmoja anaweza kuifanya peke yake. Kama mafuta yaliyotakaswa hayapatikani, mtu aliye na Ukuhani wa Melkizedeki anaweza kupeana baraka kwa mamlaka ya ukuhani. Baba aliye na Ukuhani wa Melkizedeki anafaa kuhudumia wanafamilia wake wagonjwa. Anaweza kumwuliza mtu mwingine aliye na Ukuhani wa Melkizedeki kumsaidia. 23

Kuhudumia wagonjwa kuna sehemu mbili: (1) kupaka kwa mafuta na (2) kufunganisha upako. Kupaka kwa mafuta Mtu mmoja aliye na Ukuhani wa Melkizedeki humpaka mtu mgonjwa. Ili kufanya hivyo, yeye: 1. Huweka tone la mafuta yaliyotakaswa kwenye kichwa cha mtu huyo. 2. Huweka mikono yake kwa upole kwenye kichwa cha mtu huyo na kumwita kwa majina yake kamili. 3. Husema kwamba anampaka mtu yule kwa mamlaka ya Ukuhani wa Melkizedeki. 4. Husema kwamba anampaka kwa mafuta yaliyowekwa wakfu kwa kuwapaka na kuwabariki wagojwa na wale walio na msiba 5. Hufunga katika jina la Yesu Kristo. Kufunganisha Mpako Kwa kawaida, mtu mmoja au zaidi walio na Ukuhani wa Melkizedeki huweka mikono yao kwa upole kwenye kichwa cha mtu mgonjwa. Mmoja wa watu wale hufunganisha upako. Ili kufanya hivyo, yeye: 1. Humwita mtu kwa majina yake kamili. 2. Husema kwamba anafunganisha upako kwa mamlaka ya Ukuhani wa Melkizedeki. 3. Hupeana baraka jinsi Roho anavyoelekeza. 4. Hufunga katika jina la Yesu Kristo. Baraka za Baba na Baraka Zingine za Ufariji na Ushauri Baraka za Baba na baraka zingine za ukuhani zinapewa ili kupeana mwongozo na faraja jinsi Roho anavyoelekeza. Baba aliye na Ukuhani wa Melkizedeki anaweza kupeana baraka za baba kwa watoto wake. Baraka kama hizo zinaweza kuwa muhimu haswa wakati watoto wanapoondoka nyumbani, kwenda sehemu kama shule au kwenda misheni, au wanapoanza ajira, kuolewa, kuungana na huduma za kijeshi, au wanapokumbana na matatizo ya kibinafsi. Baraka hizi zinaweza kuwa za uthabiti mkubwa kwa familia. Familia inaweza kuandika baraka ya baba kwa kumbukumbu ya familia, lakini haihifadhiwi katika kumbukumbu za Kanisa. Wazazi wanapaswa kuhimiza watoto wao kutafuta baraka za baba yao wakati wa mahitaji. Wanaume wanaostahili walio na Ukuhani wa Melkizedeki pia 24

wanaweza kupeana baraka za ufariji na ushauri kwa wake zao, wanafamilia wa kando, na wengine wanao uliza. Ili kupeana baraka ya baba au baraka zingine za ufariji na ushauri, mtu aliye na Ukuhani wa Melkizedeki, awe peke yake au na mmoja au zaidi wa wanaume walio na ukuhani wa Melkizedeki, huweka mikono yake kwa upole kwenye kichwa cha yule anayepokea baraka. Mafuta hayahitajiki kwa baraka kama hizo. Yule anayepeana baraka: 1. Humwita mtu huyo kwa majina yake kamili. 2. Husema kwamba anapeana baraka kwa mamlaka ya Ukuhani wa Melkizedeki. 3. Hupeana baraka jinsi Roho anavyoelekeza. 4. Hufunga katika jina la Yesu Kristo. Kuweka wakfu Makaburi Mtu anayeweka wakfu kaburi lazima awe na Ukuhani wa Melkizedeki na lazima aidhinishwe na afisa wa ukuhani anayeongoza ibada. Ili kuweka wakfu kaburi, yeye: 1. Humwita Baba wa Mbinguni. 2. Husema kwamba analiweka wakfu kaburi kwa mamlaka ya Ukuhani wa Melikizedeki. 3. Huiweka wakfu na kuitenga sehemu ya mazishi kama sehemu ya mapumziko kwa mwili wa marehemu. 4. Panapofaa, huomba kwamba sehemu hiyo itakuwa takatifu na ya kulindwa hadi siku ya Ufufuko 5. Humwomba Bwana kufariji familia na husema maneno mengine jinsi Roho anavyoelekeza. 6. Hufunga katika jina la Yesu Kristo. Kama familia inapenda, mtu (haswa mtu aliye na Ukuhani wa Melkizedeki) anaweza kupeana maombi ya kando ya kaburi badala ya maombi ya kuweka wakfu. 25

Kupata Vifaa vya Kanisa na Kutafuta habari kuhusu Historia ya Familia. Viongozi wa kawaida na washiriki wengine wanaweza kupata vifaa vya Kanisa, vikiwemo maandiko matakatifu, vitabu vya masomo, nakala za kanisa, mavazi, na nguo za hekalu, kutoka kwa Kituo chao cha mgawo ama huduma, kutoka kwa Kituo cha Mgawo cha Salt Lake Salt Lake Distribution Center, (Kituo cha mgawo cha Salt Lake) au kupitia kwa mtandao rasmi wa Kanisa, unaopatikana kwenye www.lds.org. Habari kuhusu historia ya familia inapatikana kwenye Mtandao wa Kanisa wa historia ya familia, ambao unapatikana kwenye www.familysearch.org. 26

SWAHILI 4 02311 80743 7 31180 743