KUPWA NA KUJAA KWA BAHARI. (TIDES AND TIME)

Similar documents
Information for assessors (do not distribute this page to participants):

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Deutsche Welle, Learning by Ear 2009 Seite 1 People Who Make A Difference Liberia: Anita Varney Health Facilitator, Fishtown/Liberia

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

Human Rights Are Universal And Yet...

TIST HABARI MOTO MOTO

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

PDF created with pdffactory trial version

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza

Lesson 11 Weather and Seasons Hewa Majira

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI NA VITUNGUU TWAUMU (SWAUMU)

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya

TIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO

Kiu Cha umtafuta Mungu

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

UNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (

K. M a r k s, F. E n g e l s

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

Bustani 10,000 Katika Afrika. Alberto Prina

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

April 14, 2016 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 52

United Pentecostal Church June 2017

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

Mutugi Kamundi. Jemma Kahn. Kiswahili. Demane na pacha wake. Author - South African Folktale

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

Oktoba-Desemba

UMRI WA MAKAMO NA KUKOMA KWA HEDHI

International Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

Ni kwa nini mkulima awe maskini?

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12

walozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w

Ndugu na dada zangu wapendwa,

2

LBE 2009 Migration Episode 3: Living without documents

KUTAMBUA SIKU YA KO NA UJUMBE WAKE

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo

ORDER NO BACKGROUND

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College

Agano Lililofunikwa Kwa Damu

Upande 1.0 Bajeti yako

Roho Mtakatifu Ni Nini?

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

Jumuiya ya Waislamu Waahmadiyya Tanzania

2 Usimamizi wa Rutuba ya Udongo Tanzania Organic Agriculture Movement

maombi, kabla tu hatujalifungua Neno hili la Kiungu.

Kifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1

Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q

AMMA KWA AFRIKA RATIBA/ITIKADI. Ratiba Maalum ya Kutibu Magonjwa Maambukizi na Hususan Fikra Zinazoleta Pooza Mwili na Akili

KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS

Early Grade Reading Assessment for Kenya

Cambridge International Examinations Cambridge Ordinary Level

UFUPISHO WA 35. Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji mazao: Clive James Chair, ISAAA Board of Directors

MAANA HALISI IMAAN ( I )

UFAHAMU NAME INDEX SCHOOLDATE UFAHAMU

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

JAZANDA YA NJOZI KATIKA BAADHI YA MASHAIRI YA EUPHRASE KEZILAHABI (ONEIRIC IMAGES IN EUPHRASE KEZILAHABI S SELECTED POEMS) 1

2 LILE NENO LILILONENWA

YEHOVA-YIRE 1. 2 Baba yetu wa Mbinguni, tunakikaribia Kiti Chako cha. 3 Tunakushukuru kwa kutuzuru jana jioni. Tunaomba

WEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23

Kuwa na Ukimwi ni kama vile kutakiwa kuendelea kuuzima moto unaoniunguza bila kukoma.

Uzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania

The International year of light 2015 The Open University animation Swahili translation

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Transcription:

KUPWA NA KUJAA KWA BAHARI. (TIDES AND TIME) Ili kuona athari ya mwezi kwa ratiba za kujaa na kupwa kwa bahari na jinsi mawimbi ya bahari yanavyohusika na mwezi mwandamo, nilichukua hatua zifuatazo: Kwanza nilinunua kijitabu cha ratiba za mawimbi kwa bandari za Tanzania kwa mwaka 2006, ambacho hutolewa na kuuzwa na mamlaka ya bandari Tanzania Tanzania Ports Authority (TPA) kwa thamani ya Tsh. 5,000. Nilipoona ningehitaji vya miaka ya nyuma, nikafanya mawasiliano zaidi na wahusika na kupata vyengine vya miaka ya 1999, 2001, na 2004. Tayari kwa sasa (2008) ninavyoandika, nimeshanunua vitabu hivyo kwa mwaka 2007 na 2008 kwa thamani hiyo hiyo. Nilisafiri hadi Mombasa. Baada ya kuunganishwa kwa huyu na yule bila mafanikio, hatimae nilifanikiwa kupata kijitabu hicho kwa njia ya kutoa fotokopi kutoka maktaba ya chuo cha Bandari Bandari College. Kitabu hicho kwa bandari ya Kilindini kwa mwaka 2000 kina ratiba za mawimbi kwa bandari za Tanzania mwaka huo pia. Kijitabu hicho cha mamlaka ya bandari Kenya Kenya Ports Authority, mkutubi alisisitiza ndicho cha mwisho kupokea. Mamlaka zote mbili za bandari kila wanapochapisha hutoa shukrani kwa kuruhusiwa kunakili takwimu kwa "Institute of Oceanographic Science, Proudman Oceanographic Laboratory, Bidston Observatory, Birkenhead, Merseyside L 43 7RA, England". Pamoja na vitabu vya ratiba za mawimbi ya bahari, nilinunua takwimu kwa jina la DATA SALES kutoka idara ya hali ya hewa Tanzania Tanzania Meteorological Agency (TMA), tawi la Tanga kwa risiti na 11476503 ya tarehe 19/12/2006. Kwa njia hiyo afisa aliyehusika aliahidi kunipa ushirikiano zaidi. Mnamo mwezi June 2008 nilitumia muda mwingi kupekua mitandao mbali mbali ya masuala ya bahari.hatimaye bwana Todd Ehret wa National Oceanographic Services ( NOAA) wenye makao makuu nchini Marekani ndiye aliyekubali kunitumia takwimu nyingi, za bandari mbali mbali nililzochagua kati ya zile walizonazo.ameniandikia invoice ili nilipe kiasi kidogo.nasikitika mpaka sasa nimeshindwa kumlipa kutokana na kutokukamilika taratibu za credit card. Kama tutakavyoona mbele, nimefanya mahojiano na watu kadhaa ambao niliona wengenipatia taarifa muhimu kuhusiana na bahari, hata hivyo kwa upande wa takwimu (data), kila zitakapotajwa huko mbele, zinazohusiana na mwezi na mawimbi ya bahari, itakuwa ni kutoka Tanzania Ports Authority (THA), Kenya Ports Authorithy (KHA), Tanzania Meteorological Agency (TMA) na National Oceanographic Services( NOAA). 1

UHUSIANO WA MAJI KUPWA NA MAJI KUJAA KWA SHUGULI ZA BAHARI. Angalia jadweli ya sura za mwezi Jo (uk.19) bandari ya Kilindini Mombasa, mwaka 2000 tarehe maalum Nov. 27. Muhimu zaidi ni kuwa siku hiyo ilikuwa ni tarehe mosi Ramadhani mwaka 1421(H) kulingana na kitabu cha kumbukumbu (Diary) cha Ansaar Sunna. Siku hiyo maji yaliendelea kujaa katika kiwango cha hali ya juu, na yalitoka ( kupwa ) kwa kiwango cha chini pia. Maji yalijaa mpaka 3.62m saa kumi na moja kasoro dakika 14 alfajiri (04 46). Yalitoka mpaka 0.19m saa tano barabara asubuhi (11 00). Yalijaa tena mpaka 3.01m saa 11 na dakika 11 jioni (17 11) na kupwa tena mpaka 0.48m mnamo saa tano kasoro dakika 4 usiku (22 56). Kupwa na kujaa kwa bahari daima huwa kunapishana kwa wastani wa masaa 6.Katika kipindi hicho pwani zinakuwa na moja kati ya matukio mawili hayo;ama kujaa kwa bahari au kupwa kwa bahari. Tarehe za mwezi mwandamo maji yanapojaa sana na kutoka sana, uvuvi wa samaki unakuwa kwa mabamvua mawili. Siku hizo ambapo maji hutoka sana inakuwa ni kama sherehe kwa wavuvi wa miguu. Hawa ni wale ambao hutumia fursa za maji kutoka kufika mpaka kwenye mito ya bahari ambako kikawaida huwa hakufikiki. Wavuvi wa miguu wanatumia zana kama konzo na matando ya aina mbali mbali. Kwa kule kwetu siku hizo ni maarufu kuwaona akinamama na watoto wengi wakiwa wako katikati ya bahari wakivua kwa mtindo unaojulikana kama kurambaza. Uvuvi huo ni pamoja na uokotaji vitu kama korong'onjo, kuchokoa pweza, kuchimbua panga na kukamata mafukulile. Uvuvi mwengine maarufu maji yanapotoka hivyo, ni kushika ngisi, duvi, kuokota kombe na majongoo ya pwani Pwani za Tumbe na Msuka kaskazini ya Pemba kwa mfano, maji yanapokupwa, ambako wenyewe pia hukuita maji mauka, inakuwa ni kama jangwa kubwa. Isingekuwa maji kujaa baadae, basi uwanja wa ndege wa kimataifa ungefaa kujengwa hapo, ingekuwa kuna tatizo la eneo la kujengwa viwanda vidogo vidogo, majangwa hayo yangefaa vilevile. Watoto siku hizi wanajazana baharini kukimbizana huku na kule. Enzi zetu tulifaidi mazingira hayo sisi waswahili peke yetu, kwani hakukuwa na watalii wala maeneo tuliyozuiwa tusiyafike Siku za tarehe hizi ni maarufu pia kwa ajali za aina mbali mbali za bahari. Kwanza ni kukatwa na aina ya kitoweo kinachoitwa panga. Nashindwa kumwita samaki kwani ni kitu king'aracho chenye umbile la pembe tatu, pembe moja iliyochongoka zaidi huwa imezama kwenye mchanga na mbili zenye makali kama wembe au panga zimeelekea juu. Wavuvi wengi wa aina hii huwa maguu peku peku; wanapozikanyaga panga hizi ndio maana hukatwa vibaya sana na damu nyingi huwatoka. Vitu vyengine wanavyovikanyaga na kudhurika ni samaki anayeitwa bocho na wengine humwita nungunungu. Tofauti na panga, bocho si rahisi kumwona kwenye maji madogo hayo. Miba yake ina sumu kali sana. Bila tiba ya haraka muathirika anaweza kupoteza maisha. Wavuvi wa aina hii ambao mara nyingi ni watoto na akinamama wasio na uzoefu wa bahari, au zaidi tuseme ni wanafunzi wa bahari,sherehe ya kufika mbali baharini 2

huwafanya wajisahau. Kikawaida majangwa hayo huwa yanahadaa sana. Wenyeji huhusisha ubabaifu huo na chunusi. Tukiwa madarasani siku hizi tuliweza kuona kwa mbali, vivuli vya wenzetu waliotoroka vipindi skuli siku hiyo,vivuli hivyo vikikimbizana huku na kule jangwani. Sehemu ile ile baadae au siku nyengine tuliona ngalawa zikienda na kurudi kuuza samaki wao,au kutoka safari za mbali nje ya kisiwa cha Pemba. Ni njia ya bahari maarufuu kwa wakazi na wavuvi wa Kojani na Shumba mjini. Kama tunavyoijua bahari, hali ya kutoka maji kiasi hicho si ya kudumu. Baada ya muda mfupi maji huanza kufuata mito yake na kujaa. Wavuvi hawa wasiokuwa na hadhari hujikuta wamezungukwa na bahari ambayo huwa inajaa kwa kasi siku hiyo. Katika hali hiyo wanaookoka ni wale wanaouja kuogelea vizuri, watakaoweza kukimbia kufuata sehemu ambayo maji hayajafunga kikamilifu. Ujuzi wa kuogolea nao sehemu nyengine huwa hausaidii, kwani kasi ya maji huwa kama kwamba yanasukumwa na kujisonga kwa kasi.eneo la Funguni mjini Pangani, ambapo mto Pangani unaingia baharini ni mfano huo.wageni wengi wamepoteza maisha hapo. Fungu la Pangani lipo mita chache tu kutoka juu lakini maji yanayojaa hutokea kaskazini na kupitia mchirizi mdogo katikati ya fukwe na fungu na kumwagika kwa kasi mtoni na kuitibua bahari yote yanapoangukia(angalia sehemu ya chini kushoto katika picha).hapo mjuzi wa kuogelea hukosa nguvu za kuishinda nguvu ya maji kukatisha masafa mafupi tu ili afike juu.ni hatari hata kwa anayejaribu kuokoa bila vyombo maalum vya kuelea na kuzamia.rasi hii ndipo sheikh Khalifa alipotutajia kuwa shujaa wa kupigania uhuru wa Tanzania;Abushiri bin Salim alinyongwa kwa kunin ginizwa kwenye nguzo na wajerumani karne ya 19.Yeye tarehe 14/11/2008 tulipohojiana naye alikuwa na miaka 83 naye alipewa habari hizo na marehemu baba yake. 3

Kikundi cha watoto wa familia moja kimewahi kupotea kwenye mazingira haya kule kwetu Tumbe. Ikitokea hivyo hali ya huzuni huwa kubwa, hasa unapoyakumbuka mayowe ya vijana hao waliotaharuki. Wengine walijaribu kuwaita wenzao muda wa kuondoka ulipokaribia "Hamadi! Hamadi!" upesi turudini maji yajaa. "Wengine wakaita "Bijaa! Bijaa!.maji yajaa. Lakini kutokana na ukubwa wa jangwa wala hawakusikizana.wao na ndugu zao walizama na kukokotwa na mito ya bahari inayosukumia Mombasa na Somalia, kwani hawakuonekana tena. Maji yanapotoka kiasi hicho, mwanzo wa mwezi na katikati yake huwa yanawacha wazi vile vile mafungu katikati ya bahari na miamba.sehemu hizi ni hatari kwa vyombo vya kusafiria na vya mizigo. Ramani za bahari huwa zinayaonesha maeneo hayo na manahodha hata kwenye giza huwa wanayakwepa Kwa wavuvi wazoefu maeneo haya, hasa mafungu ni maeneo muhimu kwa shughuli zao, kwanza ni kama maeneo ya mapumziko ya muda katikati ya bahari. Pili maeneo haya ni machumo muhimu kwa samaki wakubwa ambao wavuvi huwa wanawatafuta. Mfano ni jangwa la Kipwachashi katikati ya bahari baina ya Pemba na Tanga na karibu na Pemba zaidi. Hapo wavuvi wa madau na ngarawa. maji yanapotoka huegesha vyombo vyao. Maji yanapojaa huwasubiri samaki wakubwa ambao hufika hapo kwenda kula kombe na mwani. Vyambo hivyo viwili eneo hilo vipo kwa wingi, kutokana na kusukumwa na mawimbi ya bahari. Kwa wasafiri baina ya Zanzibar na Dar-es salaam watakumbuka eneo kama hilo maeneo yanayoitwa Magogoni.Mara nyingi sehemu hiyo samaki aina ya Pomboo (Dolphin),huonekana huku ndege angani ambao kwetu tunawaita chakwe, wakipiga mbizi za mara kwa mara. Hii ni dalili ya mkusanyiko wa samaki wengine chini wanaokwenda kufuata maslahi mbalimbali hapo. Hata wavuvi wa vyombo vidogo karibu na fukwe siku za maji kujaa sana kazi zao zinapata unafuu mkubwa. Hii ni kwa sababu samaki wengi maji yanapojaa, ama husukumwa kuja karibu na fukwe au huyafuata maji kutoka mikondoni kwa sababu zao nyengine. Badala ya wavuvi kuwafuata mikondoni kwa gharama na tabu, samaki wenyewe wanakwenda huko huko waliko wavuvi. Katika Surat AnNahl (16)aya ya 14; Allah (s.w) anasema: {Yeye ndiye aliyeifanya bahari ikutumikieni ili kutokana na humo mpate kula nyama laini, na mtoe humo mapambo mnayoyavaa na unaona marikebu zikikata maji humo ili mtafute fadhila zake, na mpate kushukuru} Katika Surat Ttuur (52) aya za 1-5 Mwenyezi Mungu kaviapia Mlima,Kitabu,Nyumba inayozuriwa daima na Mbingu.Katika aya ya 6 ameiapia bahari iliyojaa; والبحر المسجور (Na kwa bahari zilizojazwa (maji Kwenye sura ya 42:32 Allah subhaanahu wataala amesema vyombo viendavyo baharini ni moja ya ishara zake. Kumbuka tarehe 12 Disemba 2006 ambayo, ilikuwa moja ya siku ya maji mafu. Asubuhi mapema nilimpigia simu baba yangu aliyekuwepo Wete. Akiwa ni mtaalamu wa bahari nilitaka anihakikishie baadhi ya hali zilizohusiana na siku hiyo. Akaniambia siku za maji 4

mafu ni mwezi (tarehe) 8,9 katika bamvua la uvuvi la mwanzo na mwezi 21,23 bamvua la pili. Baadae nikampigia simu kaka yangu ambaye ni afisa katika kampuni la kilimo cha mwani, na ambaye anazitembelea pwani zote za Pemba na Tanga mara kwa mara. Tarehe hii na zote zilizobaki za mwezi disemba nilikuwa nikizunguka pwani kadhaa za Tanga kuangalia iwapo bado uelewa wetu wa hali za bahari uliendelea kama tulivyozoea.kwa tarehe hii nikakuta madau mengi yametiwa nanga. Magulio ya Dipusii eneo la Chumbageni na Sahare yalikuwa na harakati chache za wavuvi nyakati za asubuhi, baadae ikawa kimya kabisa nyakati za mchana na jioni. Siku hizi kwa wavuvi wadogo, ambao hawana vyombo vya kuwafuata samaki mikondoni, huwa ni siku za mapumziko. Mapumziko haya huwa yanaanzia kwa samaki wenyewe. Wavuvi wanasema samaki walio wengi wakitupiwa chambo siku za maji mafu huwa hawana hamu ya kukila; hivyo huwa hawakamatiki kirahisi.tabia hii ya samaki inafanana na ya wanyama wengine wa pori mfano simba na wa kufugwa kama paka,ambao hupendelea kula kile wanachokipata kwa kukimbizana nacho. Hii ni tabia ya tahadhari ya kiafya. Maji yanapojaa na kutoka,samaki huwa katika harakati nyingi za kwenda huku na kule kupingana na msukumo wa bahari,ikiwa ni dalili ya afya zao. Wale wanaokula wenzao hupata uhakika kwamba chakula chao ni kizima. Na hata hudanganyika hivyo kwa vyambo wanavyotupiwa na wavuvi. Samaki aina ya Kenengwa siku hizi za maji mafu hawapendi kula lakini ni muda wao wa kufurahi na kucheza maji madogo chini ya mikandaa, pengine kwa kujua wavuvi wako mapumzikoni. Wakulima wa mwani, siku za maji mafu ni siku za rutuba na kumea kwa mwani wao. Hii ni kwa vile mwani unapata utulivu mkubwa kutokana na mawimbi ya maji kupwa na maji kujaa. Vilevile katika hatua za mwisho kabla ya mavuno mwani unakuwa umesalimika na harakati za wavuvi wa maji madogo. Kilimo cha mwani ni kilimo cha wiki mbili mbili, yaani baina ya mabamvua mawili kwa kila mwezi.mbegu za mwani hufungwa kwenye kamba maalum zinazoshikiliwa na vijiti vinavyokitwa chini ya bahari. Wakulima hupanda mbegu zao kwenye vikataa vidogo vidogo muda wa maji yanapowawezesha kupanda bila tabu ya kuzamia baharini. Kishamba hicho kinaendelea kufunikwa na maji zaidi kila siku, na kufikia kikomo baada ya wiki mbili ambao huwa ni muda wa mavuno. Shamba dogo la mwani linaweza kutoa tani kadhaa za mwani baada ya kuvunwa.mwani hukaushawa tayari kwa kuuzwa. Aya zenye kuitaja bahari kwa jumla kaika Qur'an ni pamoja na 14:32, 20:77, 24:40,31, 27, na 55:24.Mawinbi ya bahari yametajwa kwenye aya za 10:22, 11:42, 24:40, 31:42 na kadhalika. MAWIMBI MAKUU 5

Fursa ya maji mafu, ambayo huwa yametulia inatumiwa sana na vijana wanaojifundisha kuogelea na watu wengine wanaopenda michezo ya baharini. Tarehe ile 12 Disemba nilipata taarifa ya kijana mmoja kuzama kwenye moja ya klabu ya kuogelea maeneo ya Raskazone, ambapo vijana hutumia maeneo hayo kwa malipo. Nilipofika kufuatilia nikakuta ukimya tu. Nilipokuwa chuoni UCEZ, nilijikumbusha enzi za utoto wetu. Kwa kutiwa moyo na mkusanyiko wa madau ya wavuvi wa Chukwani,nikajikuta nimeogelea na kufika mbali.safari ya kurudi ikawa ya woga wa kiutuuzima;kwamba ningedonolewa na samaki wakubwa kwa chini ambako kikawaida ni giza kabisa.nikalazimika kupumzika kwenye moja ya madau hayo nikiangalia masafa mpaka ufukweni na kuwaza kina kikubwa cha maji mbele yangu, wakati huo wenzangu wakinisubiri na kunihimiza kurudi Chuoni. Wakazi wa ukanda wa pwani, wamezoea kuona maji ya bahari yakijaa na kupungua katika nyakati maalum.uelewa wa nyakati hizi ni moja ya utamaduni wa watu wa pwani. Kwa wavuvi wa bahari, kupwa na kujaa ni matukio muhimu zaidi, kwa sababu nyakati za kuvua samaki, na hata upatikanaji wa samaki ni vitu vyenye uhusiano mkubwa na matukio hayo. Kupwa na kujaa kwa bahari kunayafanya maisha ya kando kando ya bahari yawe na ladha tofauti na maisha ya bara. Bahari inapojaa, kimaumbile huwa inatisha na inabidi iwe hivyo, kwani bahari hukokozoa vitu vingi vilivyopwelewa kutoka mikondoni na kuvileta ufukweni.unaweza kuona chochote cha kukusisimua hai au kilicho mfu.sijapata kuona ukimya na kusikia sauti za huzuni na mandhari ya kutisha kuliko vile inavyokuwa wakati maji yamejaa pomoni, ukawa uko peke yako nyakati za giza,chini ya vivuli vya miti iliyo kando kando ya bahari.binadamu maeneo kama haya huwa yuko karibu zaidi na kutokewa na majini kuliko watu. Mabadiliko haya ya bahari ni matokeo ya mwendo wa mwezi angani kuizunguka dunia. Mwezi unapopita angani, bahari chini yake huvutwa juu na kufanya wimbi kubwa ambalo linasogea mashariki siku baada ya siku.kwa kadiri mwezi unavyopitiwa na dunia inavyojizungusha uwelekeo wa mashariki ndivyo tunavyopata maji kupwa na maji kujaa (tides). Mvutano hasa ni baina ya dunia na mwezi. Lakini kwa vile maji yapo juu ya dunia na ni tepetepe, ndio maana yanavutika kirahisi.wimbi linalopelekea ukomo wa maji kujaa katika siku husika, haliwi ni moja tu. Hii ni kwa vile athari ya kuvutika kwa maji kutokana na nguvu ya mwezi huongezeka hatua kwa hatua jinsi mwezi unavyosogea kwa dunia kujizungusha. Kwa maana nyengine mawimbi huongezeka kila dunia, mtu sehemu alipo inavyoukaribia mwezi. Mara mwezi unapopita kuelekea magharibi kwa siku husika;ambayo ni athari ya mzunguko wa dunia,kwa maana dunia inapoupita mwezi kuelekea mashariki, na maji nayo hurudi bahari kuu na fukwe kuwa nyeupe bila maji. Yaani maji yamekupwa. 6

PICHA AO Kama tulivyoona kabla, kwamba mwezi huizunguka dunia, kwa kasi ya takriban dakika hamsini kila masaa 24, kuelekea mashariki ya dunia. Na muda wa kujaa maji nao huongezeka kwa takriban saa moja kila siku.unaweza kusema pia muda wa kujaa maji huchelewa kwa muda huo.iwapo jana ilikuwa saa 9 mchana,leo itakuwa ni saa 9.50.Tuangalie kidogo asili ya nyongeza ya wastani wa dakika 50 kwa siku. Mwezi huwa unakwenda kuizunguka dunia kwa kasi ya kukatisha nyuzi za latitude 12.20 kila siku, kuelekea upande ule ule dunia inakojizungushia wa mashariki kwa kasi ya 3600 kwa siku.hii ina maana kuwa sehemu yoyote juu ya dunia yenye kujizungusha ni lazima itembee 3600 +12.20 =372.20 ili iweze kuufikia mwezi ulipo kutoka ulipokuwa jana yake.kila 10 latitudo ni dakia 4 hivyo 150 ni sawa na saa 1 (60min). Nyongeza ya 12.20 ni sawa na (12.20/150) 60 min= 48.8min,muda ambao ni wastani wa dakika 50.Ingezingatiwa athari hii ya mwezi pekee, basi nyongeza ya dakika 50 kila siku ingekuwa bila mabadiliko. Pindi bahari inayoelekeana na mwezi inapokuwa imejaa na bahari iliyo upande wa pili wa dunia nayo pia hujaa. Hii ni kwa vile mwezi huwa unaivuta dunia yote, lakini huwa inavuta zaidi upande ulioelekezana nao kuliko upande wa pili. Maji yanayomiminika ni kwa kushindwa kuufuata mwezi na kushindikana kukokotwa na dunia.hili ni matokeo ya kanuni kadhaa.maji hayo hujikusanya na kufanya wimbi jengine la kujaa upande huo wa pili ambalo ni dogo kuliko hili la upande uliko mwezi. Angalia wimbi mmiminiko(wkmm) kwenye picha A0 hapo juu.wimbi hili ni rangi ya bluu iliyovimba kwa juu sehemu (i) ya picha AO.Upande wa dunia unaoelekeana na mwezi hutupatia wimbi kuu mburuziko (WKM B). Kwa bahari, kinachotokea hasa upande wa pili,ni kuwa dunia inavutwa kuelekea uliko mwezi (Mm) pamoja na maji yake.sehemu ya maji yanamiminika na kubaki nyuma.moja ya 7

kanuni za kuuelezea mmiminiko huu ni kanuni ya nguvu inayoshikilia kitu kikizunguka katika duara (centripetal force). Kumbuka nguvu ya mwezi ndiyo muhimu zaidi inayoathiri maji (m) katika mchoro hapo chini.mwezi kwa hivyo unachangiana na dunia katika kuyavuta maji (m). Pande mbili za dunia zilizo usawa mmoja na mwezi zinapokuwa na maji kujaa, pande mbili nyengine zilizo kinyume na usawa huo (900E,900W), nazo huwa na maji kupwa.angalia tena kulia na kushoto ya Dunia (DE) kwenye sehemu ya (i) ya Picha AO. Kwa kila siku moja dunia inapokamilisha mzunguko kwenye mhimili wake tunapata nyakati mbili mbili za kujaa na kupwa kwa bahari.kiuhalisia ni kuwa dunia inapitisha kila eneo lake chini ya mwezi katika muda wa masaa 24 na dakika 50.Katika muda huo,masaa 23 na dakika 56 ni za mzunguko wa dunia kwenye mhimili wake.dakika 54 zilizobaki kwa hesabu hii ni nyongeza kutokana na mzunguko wa mwezi kuizunguka dunia katika uwelekeo ule ule wa magharibi kwenda mashariki.1 Ukigawanya muda huo utaona kuwa robo ya masaa 24 na dakika 50 ni masaa 6 na dakika 13.Kwa maeneo ya ikweta ina maana kuwa baada ya masaa 6 na dakika 13 kila eneo lililokuwa na maji kupwa litakuwa limesogea na kufika eneo la maji kujaa na kila eneo la maji kujaa limefikia maji kupwa. Huku dunia ikijizungusha kama tulivyoona kabla,wimbi kuu mburuziko (WKMB) huwa linaendelea kupanda na kushuka katika mwendo maalum kiasi kuwa linafika eneo lilipokuwa jana yake kwa kuchelewa kwa wastani wa dakika 50 mbele. 8

Tarehe Mpishano wa muda Wimbi Muda 1.00 Jul-04 Kujaa am Kupw 7.13 Jul-04 a am 6hrs 13min 1.25 Jul-04 Kujaa pm 6hrs 12min Kupw 7.38 Jul-04 a pm 6hrs 13min 1.50 Jul-05 Kujaa am 6hrs 12min Jadweli Jk Ukanda wa Afrika Mashariki unapokuwa na maji kujaa mchana, maeneo ya upande wa pili ambayo yanaangukia katikati ya bahari ya pacific baina ya bara la Austraslia na Amerika nayo huwa katika hali kama hii. Afrika Mashariki ikipata wimbi mburuziko, maeneo hayo hupata wimbi mmiminiko na kinyume chake. Inapokuwa Indonesia (1200E) ipo chini ya mwezi sasa, huwa inapata wimbi kuu mburuziko (WKMB).Venezuela (600W) nyakati hizo huwa inapata wimbi kuu mmiminiko (WKMM).Baada ya masaa 12 na dakika 25 pwani hizo zinakuwa zimebadilishana mawimbi.katika muda wa siku nzima wimbi kuu husogea masafa ya wakati juu ya dunia yasiyofikia hata saa 1,yaani dakika hizo 50. Tumetaja kwa ufupi mambo muhimu yanayopelekea mawimbi ya bahari kutokea.hata hivyo suala zima lina mambo mengi yanayohusiana nalo,baadhi ya hayo ni muinuko wa ardhi bahari ilipo,umbile la fukwe na ukali wa chumvi. Kwa ujumla ziko aina tatu za mawimbi nazo ni : (1.) Semi diurnal tides,(2.)diurnal tides na (3.) Mixed tides.pwani za Afrika mashariki na maeneo ya ikweta yanahusika zaidi na aina ya 3.Hii ni aina ambayo mawimbi ya maji kupwa na maji kujaa huwa mawili mawili kwa siku yanayokuwa kwa ujazo tofauti kila moja.. 1. Inategemea na namna mahesabu yanavyopigwa,hatimaye 51 min hutajwa kama wastani 9

Kwenye visiwa vidogo kama Unguja na Pemba, maji hujaa mashariki na magharibi kwa wakati mmoja kwa vile mvuto wa mwezi huvienea visiwa hivyo sawa kwa sawa pande zote. Wanaokuwa Uroa (mashariki) kisiwani Unguja na Shangani (magharibi), watagundua bahari inakuwa na tabia sawa katika mawimbi yake kwa wakati maalum,ukiondoa athari za mabadiliko ya hali ya hewa. Nguvu ya mvutano ya jua ( Sun's gravity), nayo ina athari kwa maji na hali ya bahari. Athari yake si kubwa kuliko ile ya mwezi kwa vile jua liko mbali zaidi kuliko ulipo mwezi. Wakati mwezi unapokuwa mchanga (mwezi mwandamo) na unapokuwa mpevu (mbalamwezi au mwezi mdande), Jua, mwezi na dunia kwa kiwango kikubwa zinakuwa zimejipanga usawa mmoja (Angalia tena sehemu (i) Picha A0 juu). Nguvu ya uvutano ya jua (Js) huwa inachangiana na nguvu ya uvutano ya mwezi (Mm). Nguvu mbili hizo, moja dhaifu;ya jua na nyengine madhubuti; ya mwezi, hufanya mawimbi ya bahari kujaa, yawe makubwa zaidi kuliko siku nyengine. Kimatumizi ya kibaharia hali hii huitwa Spring tides (SP). Mwezi unapokuwa unaonekana nusu yake kamili, unakuwa ama uko robo ya mzunguko wake au robo tatu ya safari yake kuizunguka dunia. Katika hali hii nguvu ya mvuto ya jua huwa inapingana na ile ya mwezi. Moja huwa inavuta kusini/kaskazini na nyengine mashariki/magharibi ya anga la dunia. Kupwa na kujaa kwa bahari huwa ni kwa viwango 10

vidogo vidogo vya mawimbi (Angalia sehemu (ii) ya picha Ao juu). Kibaharia mawimbi hayo huitwa Neap tides (NP). Watu wa pwani (waswahili) wanayaita mawimbi haya Maji mafu. Mzee SAIDI wa Kigamboni Ratiba ya bahari ni sehemu muhimu ya maisha ya wakazi wa pwani na utamaduni wao. Na ndiyo inayotofautisha na yale maisha ya wakazi wa bara. Kwa wakazi wa maeneo haya mwezi una maana ya ziada kuliko unavyojulikana na wakazi wa bara Maelezo yalilyotangulia mpaka hapa,pamoja na kwamba ni kwa ufupi lakini yamelionesha kuwa suala la maji kupwa na maji kujaa ni suala gumu kueleweka na kwamba linaambatana na na vipengele kadhaa vya kielimu na kitafiti.kwa upande wetu na madhumuni ya lengo letu hapa, tunakusudia kutoa mwangaza tu wa jinsi mtu yeyote mwenye shauku ya mambo haya na mwenye matumizi nayo aweze kufuatilia angalau kwa uchache wa makisio. Uchache wa makisio,kwa mfano, ni mgawanyo wa nyakati wa waswahili;maji ya asubuhi,maji ya mchana,maji ya jioni na maji ya usiku.ni matamko mepesi ambayo hayazingatii usahihi wa wakati, lakini ni elimu kubwa ya bahari.hivyo mtu yeyote akiweza kujua mgawanyo huo, kwa matumizi yetu atakuwa amejiongezea elimu kwa upande wa bahari. Kwa ujumla hali za bahari huwa zinabadilika kulingana na mabadiliko ya mwezi, na huwa zinajirudia kila baada ya wiki mbili.. Kupwa na kujaa kwa bahari kama tulivyogusia kabla, kunategemeana na namna fukwe za bahari zilivyochongeka. Katika baadhi ya fukwe, bahari hujaa kwa futi chache tu, wakati baadhi ya maeneo yenye ghuba,babari hujaa kwa kiwango kikubwa kabisa. Hii ni kwa vile badala ya maji kujaa kwa kutawanyika, hujikusanya na kujaza eneo jembamba. Namna maji yanavyojaa eneo la Chwaka kisiwani Unguja ni tofauti na yanavyojaa kwenye mto wa bahari wa Vitongoji kisiwani Pemba.Sehemu ambapo maji hujaa zaidi duniani hadi kufikia urefu wa ghorofa kadhaa ni ghuba ya Fundy nchini Canada. Manahodha wa meli na wavuvi kikawaida hutia nanga vyombo vyao kulingana na ratiba za kupwa na kujaa kwa bahari.wavuvi wa madema na uzio wa maji madogo huwa wanajua muda halisi wa kwenda kutegua mitego yao hiyo. Wavuvi wa madau na ngarawa kwa kujua makisio ya ratiba za maji kujaa huwa wanatia nanga vyombo vyao eneo ambapo wanajua wakirudi kwa ajili ya kwenda tena kuvua, watakuta chombo chao bado kinaelea tayari kwa safari. Wakazi wa maeneo ya pwani yanayotenganishwa na fukwe na mito, bila kuwa na uelewa angalau mdogo wa ratiba za maji kujaa na maji kupwa,hujikuta wakikwama kuendelea na safari zao, na kupata usumbufu mkubwa. Moja ya usumbufu huo ni kulazimika kutafuta njia ndefu ya kuvuka eneo ambalo nyakati nyengine hupitika kwa miguu. Vyenginevyo hulazimika kuvunja safari kabisa au kuchukua uamuzi wa kuogelea. Mara nyingi hali hii ya kuamua kuogelea husababisha ajali za kuzama kwa wakazi wa pwani, pale wanapokata tamaa kufuata njia ndefu, ilhali mfano magharibi imeingia, au kwa sababu maalum hataki kufuata njia hiyo ndefu.hata kwa wajuzi wa kuogelea hutokea kuzidiwa nguvu na maji yanayoanza kupwa kurudi mikondoni. Hivyo ndivyo ilivyokuwa eneo la Kigamboni jijini Dar es Salaam kabla ya kuchimbwa kwa ajili ya kujengwa bandari. 11

Mji wa Dar es salaam ulianzishwa na mtawala wa Zanzibar mwenye asili ya Oman;sultan.seyyid Majid,ambapo aliufanya moja ya makao yake kutokana na uzuri wa bandari yake.wajerumani katika mwaka 1891 walipokuwa watawala wa Tanganyika walihamisha shughuli kubwa za kibandari kutoka Bagamoyo kuja Dar es salaam na kupageuza makao yao ya kiutawala kwa Afrika mashariki.shughuli kubwa za upanuzi wa bandari zilifanyika mara baada ya vita vya pili vya dunia 1945;wakati wa utawala wa Uiengereza. Mwaka 2006 nilipokwenda kutembelea ndugu maeneo hayo ya Kigamboni nilioneshwa mzee mmoja;wenyeji wanamfahamu kwa jina la mzee Saidi.Mzee huyu alikisiwa kuzidi miaka mia moja(100).katika uzee huo alikuwa bado akijiweza na kujiendesha kwa kuwajengea watu majengo ya miti na kuwakandikia. Enzi za utoto na ujana wake anasimulia kuwa walikuwa wakivuka eneo hilo kuja mjini (Mzizima) kwa miguu siku maji yanapotoka.kwa sasa eneo hilo ni lazima uvuke kwa vivuko maalum vinavyosimamiwa na serikali.eneo hili ni pale panapoitwa sasa maarufu Feri, ambapo ni mdomo wa kuingilia bandari ya Dar es salaam. Katikati ya mwaka 2008 nilifika maeneo ya bandari kwa mara nyengine eneo la Kurasini sehemu inayoitwa Malawi cargo, lango kuu no.5. Kupitia hapo unafika mpaka kwenye ghala kuu la kutolea mizigo inayofungashwa na wenzake kujaza kontena,yaani isiyofikia ujazo wa kontena kamili. Muda wa swala ukifika tulikuwa tukienda mpaka mwisho wa njia kwenye kijiji cha asili cha wavuvi.eneo hilo lilikuwa ni mtaa mkubwa uliokuwa na msikiti wake uliojengwa kwa tufali za saruji. Wakati wa kutia udhu na baada ya swala nilikuwa nikipata fursa kuangalia chini ya kilima kwenye mikandaa ambapo uliweza kuwaona wenyeji katika harakati mbali mbali kandoni mwa mto wa bahari.ng ambo ya pili juu ya kilima ilikuwa ni mandhari nzuri ya vichaka na miti mikubwa kama vile mikorosho na miembe.palifanana sana na maeneo mengine ya kando kando ya bahari na mito ya bahari niliyowahi kufika.eneo hili ni magharibi kabisa ya Kigamboni.Nilikisia haya ni moja ya maeneo mzee Saidi aliyo akicheza na wenzake ama kuvuka wakielekea Kurasini na Shimo la udongo enzi za utoto wao.yawezekana pia ndipo walipokuwa wakijifundishia kuogelea na kuvua samaki aina ya kamba ambao hupendelea mito ya aina hii. Tarehe 6 Julai 2009 nilifika tena eneo hili kusubiri kutoa mzigo.muda wa swala ulipofika nikaelekea tena eneo lile,lakini kabla kufika nikaona mabadiliko yaliyonisikitisha.hatimae nikarudishwa kwa maelezo ya wauzaji vyakula maarufu kwa jina la mama ntilie, ambao wala hawana maeneo ya kudumu zaidi ya magunia wanayojizibia mvua na jua pembezoni mwa barabara.wakanifahamisha kuwa mji ule wote umevunjwa na msikiti(misikti) yake haipo tena. Nikasimama kidogo kuangaza huku na kule,nikaweza kuona ujenzi mkubwa ukiendelea eneo lililokuwa bonde na mikandaa.hata hivyo bado mandhari ya miti ng ambo ya pili ilikuwa bado inaonekana.mzee Saidi naye nikaulizia na kuelezwa kuwa bado yu hai, lakini najua penye uhai na uzima mwaka 2010 hakutokuwa na nafasi tena ya kuona mandhari ya ng ambo ya magharibi ya Kigamboni kutokana na ujenzi utakaokuwa umekamilika wa wawekezaji. Masikitiko zaidi ni jinsi wanadamu wanavyozidi kupenda mali na kumsahau Mola aliyeumba hizo mali na wao wenyewe.maeneo asilia ya wenyeji waislamu yanauzwa kwa watu wanaoitwa wawekezaji ambao wengi wao ni makafiri.hawana hata heshima ya 12

kusema wenyeji wakihama angalau misikiti yao ibaki na kutumika na mamia ya watu wanaoshinda maeneo hayo kwa shughuli mbali mbali na wale wanaofika kutoa mizigo yao. MISIMU NA NYAKATI Tarehe 11 Disemba 2006, wakati wa asubuhi saa 12 maeneo ya Tanga mjini, mwezi ulikuwa unakamilisha robo ya safari yake kuizunguka dunia siku hiyo. Kwa sura yake ulikuwa uko nusu ya ukubwa wa duara lake. Muda huo, mwezi ulikuwa uko kushoto kidogo utosini, angani. Maji kujaa Tanga ilikuwa ni saa mbili kamili (08:00) tofauti ya dakika 7 na Dar-es-Salaam yalikojaa saa mbili kasoro dakika saba (07:53) kwa ukubwa wa 2.86m. Maji yalipojaa ni wazi mwezi utakuwa ulikuwa umesogea kushoto zaidi utosini mwangaliaji akiwa ameelekea kaskazini, kwa vile dunia ilikuwa inaendelea kujizungusha kuelekea mashariki. Jua kuchomoza Tanga siku hiyo, ilikuwa ni saa kumi na mbili na dakika saba (06:07). Jua kutokana na kasi ya dunia kujizungusha lilipanda haraka kuukaribia mwezi. Ilipofikia kikomo cha kujaa; saa 2, jua halikuwa limeufikia mwezi. Bado mwezi ulikuwa kushoto utosini na jua kulia utosini. Kupishana kwao, mimi mwangaliaji nikiwa ndio kigezo chao ilikuwa kwa makisio ya kipembe cha nyuzi sitini (600). Siku ya pili yake tarehe 12, saa 12 asubuhi tena,mwezi ulikuwa sawa na utosi angani. Jua lilikuwa bado kuchomoza. Mpishano wa eneo lilipokuwa jua na mwezi, mwangaliaji akiwa ndiye kigezo (base) ni nyuzi tisini (900). Mwezi ulikuwa unayavuta maji upande wake na jua upande tofauti. Kwenye jadweli za mawimbi siku hiyo ndiyo iliyoonesha ya maji mafu halisi (NP). Maji kujaa kulichelewa mpaka saa mbili dakika 44 kwa Dar-es-salaam na saa mbili dakika 51 kwa Tanga.Tofauti za muda wa kujaa maji ni sawa na nyongeza ya muda kutokana na kasi ya mwendo wa mwezi. Namna nyengine ya kulibagua wimbi la maji mafu kwa ulinganisho na siku za jirani ni kwa kutoa ujazo wa mawimbi mawili ya kujaa yanayofuatana. Utapata jawabu yenye kiwango cha chini kulinganisha na siku za jirani yake. Kituo cha Zanzibar tarehe 12, kulikuwa na mawimbi mawili ya maji kupwa ya 1.35m na 1.16m nyakati za saa 0238 na 1506.Pia mawimbi mawili ya maji kujaa 2.85m na 2.83m, nyakati za saa 0849 na 2136.Ukitoa ujazo wa maji kujaa 2.85m 2.83m jawabu ni 0.02m ni kiwango cha chini pekee kwa siku za jirani. Wakati huo saa mbili na dakika 51 kwa Tanga ambapo maji yalijaa katika ujazo finyu wa maji mafu, bado usawa wa mwezi na jua vilipokuwa angani, mwangaliaji akiwa ndiye kigezo, bado vilikaribiana lakini vilipishana kwa nyuzi takribani 90. angani.hapa mwezi na jua kila moja ulikuwa ukiyavuta maji kwa usawa tofauti kama ilivyo sehemu (ii) picha Ao. Muda wa kujaa ulichelewa mpaka saa mbili na dakika 51, nyongeza ya muda sawa na nyongeza ya mwendo wa mwezi kuizunguka dunia.vile vile maji yalijaa bila kusubiri jua kuufikia mwezi.kwa maana nyengine ni kuwa muda huo ndipo ambapo mzunguko wa dunia kwenye mhimili wake uliyakaribisha maumbile hayo mawili (jua na mwezi) yenye athari kwa maji ya bahari. 13

Katika mivutano hii kunapatikana athari za aina mbili; ile ya mwelekeo wa wimbi kwa kutokana na nguvu za uvutano wa dunia na mwezi moja kwa moja na mburuziko wa uwelekeo unaobadili nyakati za kujaa na kupwa kunakotokana na jua na mchanganyiko wa vitu kadhaa vyenye kuathiri. Katika elimu ya fizikia tunajua kuwa nguvu mbili za ukubwa tofauti, zinapovuta kitu kimoja kuelekea pande 2 tofauti, ni kawaida hicho kinachovutwa hukokoteka (huburuzika) uwelekeo tofauti na hizo nguvu mbili. Ile nguvu kubwa kati ya hizo itakuwa na athari zaidi kwa usawa wa kuburuzika hicho kinachovutwa kwa kubadili uwelekeo wa resultant force.katika mchoro hapo chini mstari mrefu unaoelekea kulia ndio mwelekeo wa halisi kutokana na nguvu mbili zenye uwelekeo na nguvu tofauti. Kwa upande mwengine Kanuni ya uvutano ya Newton inatupa sababu ya kwanini wimbi huundika kwa uvutano huo.ni kwa vile kila kimoja kati ya mwezi,dunia na jua kina nguvu yake inayovutania na mwenzake. Newton's Universal Law of Gravitation states that any two objects exert a gravitational force of attraction on each other. The direction of the force is along the line joing the objects (See Fig below). The magnitude of the force is proportional to the product of the gravitational masses of the objects, and inversely proportional to the square of the distance between them. Gravitational Force Between Two Masses Ndivyo inavyokuwa kwa wimbi kuu linalopelekea maji kujaa katika siku na muda husika. Mwezi na jua angani vinaonekana kupishana kwa nyuzi fulani na maji kujaa uwelekeo tofauti na mielekeo yao. Kwa matumizi ya mjadala huu katika makala haya, wimbi la aina hii lenye kutokana na athari ya moja kwa moja ya mivutano ya jua na mwezi tumeliita wimbi mburuziko. Kinyume cha wimbi hili kama tulivyoona kabla ni wimbi mmiminiko; 14

linalotokea upande wa pili wa dunia ulio kinyume na upande mwezi ulipo angani, Rudia kuangalia tena kielelezo cha Picha A0. Kwa tarehe 11 December, 2006 muda huo, wa saa 2 asubuhi ungechora msatari wa makisio popote ulipo Tanga, kuunganisha mashariki na magharibi, basi ungegundua kuwa jua lilikuwa kusini mashariki mwa mstari huo. Ungeendelea kufanya hivyo miezi mitatu baadae na zaidi ya hapo, utakuta mabadiliko ya vituo vya mwezi na jua juu ya uso wa dunia. Kwa upande wa vituo vya jua ni kutokana na sehemu dunia ilipo katika njia yake ya kulizunguka jua. Kwa vile daima iko kwenye mwegamo wa 23 1/2 na mhimili wake, inapelekea jua kuipiga dunia katika hali zinazoelezewa kama Solstice na Equinox, na mielekeo mingine baina ya hali hizo. Ama kwa upande wa mwezi, vituo vyake juu ya uso wa dunia hubadilika kwa uwazi kila siku kutokana na mzunguko wake kuizunguka dunia.iwapo utajaalia kama ilivyozoeleka, kuwa dunia imegawanywa vyumba vyumba na mistari ya makisio ya Longitudo na latitudo. Basi kila baada ya muda, na hasa baada ya masaa 24 mwezi unakuwa umeingia chumba kingine. Katika safari yake ya daima, dunia kulizunguka jua tarehe 22 December, na 21 Juni, inasababisaha misimu ya winter na "Summer".Ncha moja ya dunia ikiwa Summer nyengine inakuwa Winter. Kwa tarehe 22 Septemba na 21 Machi inasababisha misimu ya Autum na spring. Misimu hii inakuwa wazi zaidi kwa wakazi wa kaskazini ya dunia. Kwa Spring na Autum jua hupiga miale yake takriban sawa kusini na kaskazini ya dunia. Kwa wakazi wa Ikweta, jua huchomoza Mashariki barabara. Kwa misimu ya Summer na Winter jua hupiga ama kuenea kaskazini zaidi (Summer solstice for North) au kupiga kusini zaidi (Southern Summer). Upande mmoja ukiwa Summer mwengine unakuwa winter. Misimu hii kwa watu wa ikweta jua huonekana kuchomoza kwenye vipembe vya kaskazini au kusini. Kama tulivyorudia kufafanua kabla. Makka nchini Saudi Arabia, ni mji wa kiibada kwa waislamu. Mji wa Makka na nchi za Afrika Mashariki zimepangiwa na wagawaji wa nyakati tangu zamani kuwa ziwe kwenye zoni moja. Hii ni kwa kufuata vigezo vyao kadhaa ili kurahisisha mipango mbalimbali ya kidunia. Hata hivyo Makka ipo karibu zaidi na mstari wa latitudo wa tropic of Cancer, eneo la lat 210 43 ' N. long 400E; maeneo ya kati ya kaskazini ya dunia. Nchi za Afrika Mashariki zipo maeneo ya Ikweta katikati ya uso wa dunia. Misimu ya kiangazi (summer) na majira ya baridi (winter). Makka na Tanzania kwa mfano, zinatofautiana kwa nyakati za sala kwa viwango vidogo pamoja na kuwa ziko zoni moja. Ibada ya sala za faridha imewekewa nyakati maalum (Qur'an 4:103) ambazo katika hadithi ya Mtume صلى ال عليه و سلم iliyosimuliwa na Abdallah Ibn Amr, nyakati hizo zinafafanuliwa na viwango vya muwangaza unavyokuwa kila wakati. Hivyo juu ya kuwa Makka; Saudia na Tanzania zimepangwa zoni moja, lakini daima nyakati zao za sala zinapishana hata ikiwa ni kwa dakika chache; kwani daima muwangaza wa jua utakuwa 15

ukiwafikia katika ukali na vipembe tofauti kulingana na vituo vya dunia na mielekeo yake kulizunguka jua. Zifuatazo ni nyakati za sala kwa tarehe tofauti za Disemba 2006. msimu wa Hija 1427 na January 2007 kwa ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki na miji ya Saudi Arabia. MJI TAREHE MADIN A UNGUJA 20-12-2006 MAAWI YO MACHWE O ADHUH UR ALASI R MAGHRI BI ISHA ALFAJI R 12:19 3:18 5:18 7:08 5:35 20-12 -2006 12:23 3:43 6:33 7:53 4:54 JEDDAH 24-12 2006 12:22 3:26 5:48 7:18 5:34 TANGA 24 12 2006 12:25 3:45 6:33 7:55 4:56 MAKKA 21 12-2006 TANGA 21 12-2006 MAKKA 20 12 2006 06:11 TANGA 20 12 2006 07:00 5:20 18:33 12:24 3:44 6:34 7:54 4:55 12:32 3:40 6:02 7:32 5:39 12:37 3.57 6:46 8:06 5:09 Jadweli Jn Kumbuka kuwa kuanzia tarehe 22, December, jua linakuwa linapiga kwa ukali zaidi kusini ya dunia. Linawahi kuchomoza na kuchelewa kutua. Mchana unaweza kuitwa ni mrefu kuliko usiku wake. Sala ya alfajiri inawahi na Magahrib kuchelewa kidogo ukilinganisha ma miji ya Saudi Arabia. Kuanzia tarehe 21 Juni, inakuwa ni kinyume ya hivyo. Angalia kwenye jadweli Jn hapo juu, miji ya Madina na Unguja. Tarehe 20/12/2006 sala ya Magharib kwa Madina ilikuwa mapema saa 11 na dakika 18 jioni (5.18) ambapo kwa Unguja na nchi za jirani ilichelewa mpaka saa 12 na dakika 33 yaani (6:33) Alfajiri; Madina tarehe hiyo ilikuwa saa 11 na dakika 35; (5:35), kwa Tanga ni sa 10 na dakika 54 alfajiri (4:54). Angalia pia miji ya Jeddah na Tanga tarehe 24/12/2006. Makka tarehe 20/1/2007 jua lilichomoza saa 1 kamili (7:00), wakati Tanga tarehe 21/12/2006 lilichomoza saa 12 na dakika 11, (06:11) yaani kwa vile jua liko kusini zaidi,tanga linawahi na Makka kuchelewa kidogo. Kwa nyakati za sala ya adhuhuri ambayo huanza mara jua linapopinduka mpaka kivuli cha mtu kinapokuwa sawa na kimo chake, ndio muda pekee unaokaribiana zaidi. Mzunguko wa mwezi kuizunguka dunia kwa kiwango kikubwa hauathiriwi na misimu inayosababishwa na dunia kulizunguka jua. Hata hivyo kutokana na aina ya duara dunia na mwezi zinazozungukia ni wazi kuwa mwezi na jua vitakuwa vinapishana kwa viwango tofauti tofauti. Kwa vile mwezi na jua vina athari kwa bahari. Hivyo ni wazi pia kuwa mawimbi ya bahari yataathiriwa na misimu inayotokana na mzunguko wa dunia. Ndio maana ukubwa wa maji kujaa na maji kupwa unabadilika kidogo kidogo muda baada ya muda kadiri mwaka unavyosogea. 16

Kwa maana hiyo mwezi katika sura yake ileile;mfano (30%,50%,80%) ya ujazo wake,huwa unaleta mabadiliko madogo madogo ya nyakati za maji kupwa na maji kujaa, siku baada ya siku katika miezi tofauti ya mwaka. Hata hivyo kwa mtumiaji wa bahari wa mara kwa mara na mgeni kabisa wa bahari, sura za mwezi mwandamo J0 inampa makisio mazuri ya kudumu ya hali ya bahari kwa kila siku. Tumeona kuwa mpishano wa maji kupwa na maji kujaa ni masaa 6.13,maji kujaa mpaka kujaa au kupwa mpaka kupwa ni masaa 12.25.Kila baada ya masaa 24 muda wa kujaa au kupwa husogea wastani wa dakika 50.Hii kwa kweli ni athari ya mwezi kama ungekuwa pekee. Kwa kutumia takwimu za bandari kadhaa maeneo ya ikweta ambayo huwa yanapata zaidi aina ya mawimbi ya Mixed tides;kusogea wimbi kuu baada ya masaa 24 utagundua sio lazima iwe dakika 50.Mara nyengine huwahi kabla ya wakati huo na mara nyengine huchelewa zaidi.hii ni kutokana na mambo kadhaa, zaidi ikiwa ni athari ya jua. RATIBA ZA BAHARI NA SURA ZA MWEZI ATHARI YA JUA KWA MAWIMBI YA BAHARI (Priming and Lagging of Tides) Tumetaja mara nyingi kuhusu athari kubwa ya mwezi kwa mawimbi ya bahari,hata hivyo jua nalo lina athari ya kipekee na ya kuzingatiwa kwa nyakati za mawimbi hayo. Jua liko masafa ambayo ni mara 370 zaidi kuliko ulipo mwezi.hata hivyo jua hilo hilo ni kubwa mara 370 kuliko mwezi.kushabihiana kwa vitu viwili hivi tungetaraji kuwa athari ya jua kwa mawimbi ya bahari kuwe ni sawa na athari ya mwezi.hivyo sivyo ilivyo,kwani athari ya mwezi ni kubwa zaidi,hata hivyo jua nalo lina athari ya kutosha kubadili nyakati na ukubwa wa mawimbi. Athari ya mwezi na jua pamoja kungetupa wimbi ambalo ni rahisi kupimika kama ingekuwa njia za jua na mwezi angani ni duara moja kwa moja,pia kama vyote viko usawa (plane) moja na kama mhimili wa dunia ungekuwa uko 900 na huo usawa (plane) wa dunia na mwezi pamoja.kwa sababu hivyo sivyo ilivyo, vipimo vya mawimbi vinahitaji kuzingatia vigezo vya ziada ili kuweza kuyapima. SURA ZA MWEZI MWANDAMO (JO) NA RATIBA ZA MAWIMBI MWEZI SHAABAN/RAMADHAN 1421 (H) SAWA NA NOV/DEC.2000(AD).BANDARI YA KILINDINI MOMBASA; LAT 40 03 S,LONG. 39038 E 17

Kasi halisi ya mwezi kuizunguka dunia ni 12.20/hr.Hii ndiyo inayosababisha kusogea kwa wimbi kuu kwa dakika 50-51 baina ya jana na leo iwapo mwezi pekee ndiwo wenye athari 18

kwa mawimbi. Kasi ya mwezi kuizunguka dunia ni wastani wa siku 28.Kasi ya kiinimacho ya mwezi kuizunguka dunia ni 28.980/hr kutokana na dunia nayo kujizungusha upande huo huo nwezi unaoizungukia dunia (W E).Kutokana na hali hiyo ndiyo maana kunakuwa na kuchelewa kwa muda wa kufika wimbi kuu baina ya jana na leo,kinyume na matarajio ya dakika 51. Kwa upande mwengine tunakumbuka kuwa jua liko masafa ya maili 93,000,000 kutoka ilipo dunia na kwamba mwangaza unasafiri kwa kasi ya maili 186,000 kwa sekunde, hivyo kutoka kwenye jua, muangaza huchukua dakika 8.33 kuifikia dunia.unaweza kusema pia kuwa jua lipo masafa ya mwangaza ya 8 light minutes kutoka duniani. Jua kutoka duniani linachukua upana wa 30 arc minutes ya mzingo wa anga.dunia inajizungusha kwa kasi ya kukatiza 150 long. kwa kila saa 1 (360/24) au 10 kwa kila dakika 4 (15/60).Vile vile tunaweza kusema dunia inakatiza 15 arc minutes kwa saa,na ni sawa na kusema 15 arc minutes kwa dakika,kwa sababu 10 ya upana ni sawa na 60 minutes,vile vile 1hr ya muda ni sawa na 60 minutes.hivyo 150/hr = 15 60min/1 60min. Muda wa wastani wa dakika 8 muangaza inaochukua kuifikia dunia,jua linakuwa limebadili eneo ukilitazama kutoka duniani na kuwa (15/60min)arc min 8min =2arc min.yaani dunia inapokuwa imejizungusha 15 0 katika saa 1, jua linakuwa limesogea angani mara mbili ya lilipokuwa awali.kwa hivyo ili dunia isipotezane masafa na jua itabidi kila saa moja ijizungushe mara mbili,na kwa siku nzima iwe mizunguko 2 ya dunia; 2 360=7200 =24 30arc minutes.kinyume cha hivyo dunia kwa masafa ilipo sasa, ingebidi iwe mara mbili ya ukubwa wake au ibadili eneo kwa kulisogelea jua kwa nusu ya masafa baina yao. Ikiwa dunia ilikute wimbi kuu litokanalo na jua peke yake ililoanza nalo katika muda maalum, ingepaswa ijizungushe mara mbili ili kulifikia.lakini hali sivyo ilivyo.dunia kwa maumbile yalivyo inahusika na mawimbi yote mawili;yatokanayo na mwezi na jua,na zaidi na mawimbi yatokanayo na mwezi.kutokana na hali hiyo ndiyo maana kunakuwa na ama kuharakishika au kuchelewa kwa muda wa kufika mawimbi kinyume na matarajio ya dakika 50/51 kila siku kama ingekuwa ni mwezi peke yake. Hali hii ndiyo inayoitwa priming and lagging of tides. Wimbi linaharakishika (priming) pindi mwezi unapokuwa baina ya mwandamo na robo ya mzunguko wake (new and first quarter),na pia unapokuwa baina ya mwezi mdande (mwezi mpevu) na robo ya mwisho (full moon and third quarter).wimbi kuu huwa linatokea kabla mwezi haujavuka utosi wa anga (meridian). Dunia inajizungusha kwenye mhimili wake kutoka magharibi kwenda mashariki;ni clockwise direction au kushoto kwenda kuliandivyo inavyoonekana ukiwa masafa makubwa juu ya dunia na ukaiangalia dunia kutokea maeneo ya tropic na equator.ukweli huo unajulikana ukiwa juu ya ardhi ya dunia yenyewe, kwa kuangalia mabadiliko ya nafasi ya vitu vilivyo mbali sana angani kama vile nyota na sayari. Unaposimama juu ya ncha ya kaskazini ya dunia (North pole) au ukawa uko ndani ya chombo juu angani na ukaingalia dunia maeneo hayo ya N.pole unaona hali ni kinyume nyume.mchoro wa priming hapo chini umechorwa kwa mtazamo huu.hivyo mwezi (Moon) unaonekana kuizunguka dunia katika anticlockwise direction au kulia kwenda kushoto. Mwezi(Moon) unaonekana upo baina ya mwandamo (NewMoon) na 1st quarter.wimbi kuu (High water tide) limeharakishika na kutokea kabla dunia haijajizungusha na kufikia 19

utosi wa anga (meridian);ambapo mstari (AB) wenye kuonesha eneo la mawimbi makuu ungekuwa umenyooka sawa na mstari (CD) unaopelekea muangaliaji kuuona mwezi juu ya utosi wake.ukiuuona mwezi hapo (AB CD) inakuwa umesimama juu ya longitude ambayo ni great circle. Kuharakishika huku kwa wimbi kuu kunatokea tena mwezi unapokuwa uko baina ya mwezi mpevu (Full moon) na 3rd Quarter.Angalia mchoro wa Priming, ambapo wakati dunia inajizungusha kutokea kulia kwenda kushoto kutokea juu ya N.pole,wimbi kuu kwenye AB linatokea kabla dunia haijajizungusha na kufikia utosi wa anga na mwezi (AB CD). Angalia mchoro wa Sura za mwezi na ratiba za mawimbi Jo. Siku ya Jumatatu (Mon) Ramadhani mosi; tarehe 27 Nov.(Kwa matumizi ya maelezo ya sehemu hii siku hii tunaiita hivyo kama ilivyokubalika wakati huo).wimbi kuu siku hiyo lilikuwa la 3.62m lilitokea saa 0446.Siku ya mwezi pili Ramadhani wimbi kuu lilikuwa 3.54m saa 0513.Tofauti ya muda kati ya mwezi mosi na mwezi pili ni 0513hr-0446hr ambayo ni 27min.Nyakati zinazofuatia ni 0541,0611,0644,0721.0804,0905, na 1035. Ukiendelea kutoa muda wa kufika wimbi kuu baina ya jana na leo utapata tofauti zifuatazo 28min,30min,33min,37min,43min,59min na 90min. Siku ya maji mafu (NP) mwezi 9 Ramadhani ndipo lilipokawia zaidi na kuiwacha jana yake kwa saa moja na nusu nzima. Mwezi kwa mwezi huo wa Ramadhani 1421H,ulivuka mwezi mpevu (full moon) kuanza 3rd quarter ya mzunguko wake siku ya Jumanne mwezi 16 Ramadhani.Wimbi kuu la 3.10m lilitokea saa1703.siku ya mwezi 17 hakukua na ongezeko la ukubwa wa wimbi lakini 20

lilichelewa kufika mpaka saa 1744.Tofauti ya muda ya leo na jana yake ni dakika 41 (41min). Ukiendelea kulifuatilia wimbi kuu mpaka kufikia siku ya maji mafu;mwezi 23 Ramadhani,utapata tofauti za muda zifuatazo 43min,48min,54min,63min,74min na 79min. Kuchelewa kwa wimbi (lagging) kunatokea wakati mwezi unapokuwa uko baina ya robo ya mwanzo (1st quarter) na mwezi mpevu (full moon).vile vile wakati unapokuwa upo baina ya robo ya mwiso (3rd quarter ) na kuandama (New moon).mawimbi makuu katika vipindi hivyo huwa yanatokea baada ya mwezi kuvuka utosi wa anga (meridian). Ukiangalia mchoro wa Lagging hapo juu,utaona kuwa mstari AB unaoonesha maeneo yanayopaswa kutokea mawimbi makuu umeshavuka mstari CD ambao unaashiria maeneo ya utosi wa anga. Turudi kwenye jadweli ya sura za mwezi mwandamo (JO) siku ya mwezi 10 Ramadhani;Wed 06 Dec.Siku hiyo mwezi ulikuwa umeshavuka robo ya mwanzo katika mzunguko wake.wimbi kuu lilikuwa ni 2.35m muda wa saa 1212hr.Siku ya pili yake mwezi 11 Ramadhani,wimbi kuu lilikuwa ni 2.49m muda wa saa 1319 hr. Siku ya mwezi 11 lipo wimbi kuu jengine la 2.73m saa 0100 ambalo ni kubwa kuliko hili la 2.35m,lakini hili silo wimbi kuu tunalofuatana nalo.hili ni wimbi kuu mmiminiko (WKMM) ilhali sisi tunafuatana na WKMB.Tofauti ya muda wa kufika wimbi kuu baina ya mwezi 10 na mwezi 11 Ramadhani ni 1319hr-1212hr sawa na 67min.Ukiendelea kulifuatilia wimbi kuu mburuziko (WKMB) utapata tofauti za muda wa kufika kama ifuatavyo:54min,46min,42min,41min,41min. 21

Mwezi 23 Ramadhani wimbi kuu lilikuwa ni 2.76m saa 2345hr.Mwezi 24 wimbi kuu halikuleta mabadiliko yoyote katika ukubwa wake na muda wa kufika.hii inatokea mara nyingi mwezi unapovuka kutoka maji mafu. Mwezi 25 Ramadhani wimbi kuu lilikuwa ni 2.91 saa 0058.Siku iliyofuata wimbi kuu ni 3.09m saa 0157.Kutokea jana yake muda wa kufika ni 59m.Mpaka kufikia mwezi 29 muda wa kufika wimbi kuu ni kama ifuatavyo 50min,39min,25min. Vipindi vya wimbi kuharakishika tofauti ya muda huwa unaongezeka kila siku.kwa upande mwengine vipindi vya wimbi kuchelewa muda huwa unapungua kila siku.ukiangalia vipindi vya kuharakishika wimbi kuu huwa linapungua ukubwa (uzito) kila siku.kinyume chake vipindi vya kuchelewa huwa linaongezeka uzito kila siku.hali hizo zinaendana na kanuni za mwendo za Newton,ambapo iwapo hakuna mabadiliko ya ziada kwa vitu vinavyotegemeana juu ya nguvu ya mwendo wa kitu,basi kila uzito unapoongezeka kasi inapungua na kila uzito unapopungua kasi na hatimae muda vinaongezeka (a=f/m).a ni kasi,f ni nguvu na m ni uzito. Newtons Second law of motion: The acceleration of a particle is directly proportional to the resultant external force acting on the particle and is inversely proportional to the mass of the particle (F=ma) Kwa ufupi ni kuwa katika robo ya mwanzo na ya tatu ya mzunguko wa mwezi mawimbi huwa yanaharakishika kufika kabla mwezi kukatiza utosini.tofauti ya muda baina ya jana na leo huwa inaongezeka kila siku na wimbi huwa linapungua kidogo kidogo.katika robo ya pili na ya mwisho mawimbi makuu huwa yanachelewa kufika mpaka mwezi unapokuwa umeshakatisha utosini.tofauti ya muda huwa inapungua na wimbi huwa linaongezeka ukubwa kila siku. JADWELI YA WAVUVI NA WACHUUZI 22

Watu wengi;wakazi wa maeneo ya pwani, hupendelea kuteremka wenyewe baharini kununua kitoweo ili wapate kwa bei rahisi.kwa wengi kazi hii sio rahisi,kwani bila kujua ratiba ya kurudi kwa wavuvi na muda wachuuzi wanapokusanyika mnadani,uamuzi wa kuteremka baharini huwa ni kuongeza gharama badala ya kupunguza.kwa sababu unaweza ukateremka baharini muda ambao wavuvi wameshafika makwao na minada kufungwa. Kwa kweli wavuvi na wachuuzi walio wengi ni wazoefu wa ratiba za bahari,hivyo jadweli tutakayojaribu kuitayarisha inawafaa zaidi washtiri wa vitoweo na itawasaidia wanaopendelea kuanza kuingia kwenye shughuli za kutafuta riziki kwa njia za bahari. Kwa matumizi ya maelezo ya sehemu hii,nyakati kama tulivyotangulia,tunafuata nyakati za zoni kwa mzunguko wa masaa 24 yanayoanzia saa sita usiku.hivyo saa 0100 (EUR.TIME)-nyakati za kizungu ni saa 7 usiku (SWAH.TIME)-nyakati za waswahili,na saa 2300 ni saa 5 usiku. EUR.TIME SWAH.TIME 0100 0200 0300 0400 0500 0600 0700 0800 0900 1000 1100 1200 07.00 08.00 09.00 10.00 11.00 12.00 01.00 02.00 03.00 04.00 05.00 06.00 USIKU USIKU USIKU ALFAJIRI ALFAJIRI ASUBUHI ASUBUHI ASUBUHI ASUBUHI ASUBUHI ASUBUHI MCHANA EUR.TIME SWAH.TIME 1300 1400 1500 1600 1700 1800 1900 2000 2100 2200 2300 2400 07.00 08.00 09.00 10.00 11.00 12.00 01.00 02.00 03.00 04.00 05.00 06.00 MCHANA MCHANA MCHANA JIONI JIONI JIONI MAGHRIB USIKU USIKU USIKU USIKU USIKU Kwenye jadweli ya sura za mwezi mwandamo (Jo) uk 18,upana wa 3cm uliokozeshewa na kwenda chini kimarefu ni dunia (Earth).Mshale mdogo juu uliopinda unaonesha upande dunia inakojizungushia kwenye mhimili wake-magharibi kwenda mashariki;west(w) to East(E) mtazamaji akiwa ameelekea kaskazini ya dunia. Kulia;sehemu iliyokoza sana weusi ni mwezi mchanga.juu ya mchoro huo mshale mwengine mdogo unaonesha njia ya mwezi kuizunguka dunia ambayo ni mwelekeo mmoja na wa dunia kujizungusha (magharibi kwenda mashariki). Siku ya Jumatatu (Mon.) ilikuwa ni tarehe 27 Nov-2006.Siku hii ilikuwa ni mwezi 1 Ramadhani (RMDN) mwaka 1421-H.Sura ya mwezi siku hiyo ni mwembamba kuliko tarehe zote zinazofuatia.siku ya pili yake;jumanne (TUE) ilikuwa ni mwezi pili Ramadhani.Ukilinganisha na tarehe mosi;mwezi unakuwa umeongezeka kidogo.kuongezeka huku kunaitwa waxing 23