MTIHANI WA PAMOJA WA WEZOJE

Similar documents
Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS

(Hati ya kuhitimu kisomo cha sekondari Kenya (K.C.S.E)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q

TATHMINI YA PAMOJA SHULE ZA UPILI ZA JIMBO LA MACHAKOS.

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

MTIHANI WA MWIGO WA WILAYA YA NANDI KASKAZINI 2013

Early Grade Reading Assessment for Kenya

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Human Rights Are Universal And Yet...

MARUDIO K.C.S.E KNEC KISWAHILI KARATASI 102/2 MASWALI NA USAHIHISHO

KISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA SUBUKIA

TRANS-NZOIA COUNTY KCSE REVISION MOCK EXAMS 2015

KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

Kutetea Haki za Binadamu

NAFASI YA MUZIKI ULIOPENDWA KATIKA FASIID YA KISWAHILI PAMELA M. Y NGUGI. Inkisiri. M a kala. AAP 64 (2000): Swahili Forum VII

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

UFAHAMU NAME INDEX SCHOOLDATE UFAHAMU

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

TASFIDA KAMA MKAKATI WA UPOLE: UWIANO WA TASFIDA ZA KISWAHILI NA EKEGUSII

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

Evaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya

Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Ufundishaji wa lugha nyingine

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

ATHARI ZA KIMOFOFONOLOJIA ZA KIOLUSUBA KATIKA MATUMIZI YA KISWAHILI SANIFU KAMA LUGHA YA PILI

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI KITABU CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

KUCHUNGUZA UJINSIA NA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA METHALI ZA WAKURYA

Deutsche Welle, Learning by Ear 2009 Seite 1 People Who Make A Difference Liberia: Anita Varney Health Facilitator, Fishtown/Liberia

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza

MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

1. UFAHAMU: (Alama 15)

KUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA

Shabaha ya Mazungumzo haya

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA III VI

Kiu Cha umtafuta Mungu

Na Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Hakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

NAFASI YA MWANAMKE: JINSI INAVYOTETEWA KATIKA NYIMBO ZA TAARAB ZA ZANZIBAR ELIZABETH KANGOGO YEGO C50/68796/2011 IDARA YA ISIMU NA LUGHA

ATHARI ZA KIISIMU ZA LAHAJA YA KIMAKUNDUCHI KATIKAKISWAHILI SANIFU KINACHOTUMIKA SHULENI MAKUNDUCHI ZANZIBAR

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

Tanzania, sasa kondoo anayesubiri kuchinjwa

UJAGINA WA MWANAMKE KATIKA PANGO

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

Transcription:

Jina... Nambari yako.. Shule.. Tarehe... Sahihi ya Mtahiniwa.... 102/2 KISWAHILI Karatasi ya 2 Kidato cha 4 LUGHA ( Ufahamu, Muhtasari, Matumizi ya lugha na Isimu jamii) Aprili 2013 Muda: Saa 2 1 / 2 MTIHANI WA PAMOJA WA WEZOJE - 2013 (Hati ya Kuhitimu Kisomo cha Sekondari) Kiswahili Karatasi ya 2 MAAGIZO Andika jina lako na namba yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu. Weka sahihi na tarehe ya mtihani katika nafasi zilizoachwa. Jibu maswali yote. Andika majibu yako katika nafasi zilizoachwa katika kijitabu hiki cha maswali MATUMIZI YA MTAHINI Swali Upeo Alama 1 15 2 15 3 40 4 10 JUMLA 80 WEZOJE Kidato cha 4 Muhula wa 1 2013 1 Kiswahili P2

1. UFAHAMU (Alama 15) Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali Haki za Watoto na Wanawake Makamishina wa Tume za Haki za Binadamu, waandalizi, waalikwa, watoto, mabibi na mabwana. Kwa muda mrefu kumekuwa na tofauti katika uhusiano baina ya wanajamii. Tofauti hizi zimesababisha wanawake na watoto kudunishwa. Udunishaji unachukua mwelekeo mbaya zaidi kama watoto ni wa kike. Kupuuzwa kwa wanawake na watoto kuna historia ndefu. Jambo hili limepata usugu kutokana na imani hasi zilizoota akilini mwa wanaume na hata wanawake. Rasilimali na majukumu yamegawanywa kwa misingi inayowatabakisha wanajamii kuanzia wanaume, wanawake halafu chini kabisa watoto. Katika jamii nyingi, wanawake na watoto wa kike hawarithi chochote ingawa ndio wenye mchango mkubwa katika uzalishaji mali. Aidha mchango wao kuhusu masuala muhimu nyumbani na katika jamii hupuuzwa hata kama wamesoma kuliko waume na akina baba zao. Inasikitisha kuwa wanawake na watoto hawana sauti kuhusu uamuzi nyumbani. Wao hulazimishwa kutenda wanavyoamriwa na wanaume. Kwa mfano, si ajabu mwanamke kulazimishwa kupika pombe na watoto kusukumizwa kwenda kununua sigara. Yote haya ni kinyume cha matarajio ya Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu. Ili kuzuia tabia ya ujuaji wanaume wengi hupiga marufuku redio, simu, magazeti na televisheni kwa wanawake na watoto. Amri hii hutekelezwa vikali ili wahusika wasijifunze tabia ya kukaidi amri za wazee. Pengine hii ndiyo sababu katika jamii fulani, neno mzee lina maana moja tu, ya wanaume waliokomaa kiumri wala si wanawake. Hii si kweli Haki za binadamu ni msingi wa utu. Bila haki hizo mwanadamu hawezi kutumia vipawa na uwezo wake wa kiakili na kihisia kikamilifu. Udunishaji wa wanawake na watoto unapingana na ukweli huu. Imani potofu zinazoendeleza uovu huu zimejikita akilini na katika utamaduni, zinahitaji kuondolewa. Nafurahi kuwa mmeibua mikakati thabiti ya kulipiga vita tatizo hili. Kwa kweli, sherehe kama hizi ni muhimu sana katika kuwafumbua macho wadau kuhusu haki za wanawake na watoto. Naamini hotuba zilizotolewa hapa zitakuwa mbegu zitakazochipua mabadiliko katika fikra na matendo ya watu. Yafaa watu wakubali kuwa mke na watoto ni wenza na wadau katika safari ndefu ya maisha. Nimeona mabango, maigizo, ngoma na michoro ya waume kwa wake, wazee kwa watoto na wavulana kwa wasichana kuhusu mada hii. Ujumbe umewasilishwa wazi. Ni moyo uliofumwa kwa chuma tu ambao hauwezi kuathiriwa na jumbe kuhusu nafasi ya wanawake kurithi na kusikilizwa. Lakini vita vya panga haviamuliwi kwa fimbo. Kilichobaki sasa ni kufanya utafiti wa kukusanya data kuhusu mielekeo na itikadi zinazopingana na lengo letu. Kutokana na matokeo, mikakati iwekwe ili kuvunja nguvu, desturi zinazochochea taasubi za kiume. Mabibi na mabwana, yapasa juhudi zifanywe za kusambaza habari kuhusu umuhimu wa kuheshimu na kujali binadamu wote na mchango wao. Aidha hatuna budi kuhakikisha nafasi sawa kwa kila mtu kutoa maoni na kusikizwa. Litakuwa jambo la kusikitisha kama jamii itasahau mchango wa wanawake na watoto katika kuzalisha na kulinda mali. Twahitaji kuondoa uoga kutoka kwa akina mama wasiotaka mabadiliko. Sekta zote za umma lazima zijitahidi kutekeleza haya. WEZOJE Kidato cha 4 Muhula wa 1 2013 2 Kiswahili P2

Ningependa kuwakumbusha kuwa kanuni za ubalozi haziniruhusu kuingilia masuala ya ndani ya nchi hii. Hata hivyo, nalazimika kushauri jambo moja. Nashauri ibuniwe Wizara ya Maendeleo ya Wanawake, Vijana na Watoto. Wizara hii itakuwa na jukumu la kuondoa vikwazo dhidi ya wanyonge. Kubuni wizara tu hakutasaidia. Wakereketwa washawishi mabadiliko katika sheria kuhusu wanawake na watoto hasa wajane na mayatima. Wanaharakati nao yapasa wahakikishe kuwa sheria hizo zinaheshimiwa. Shirika langu liko tayari kutoa msaada wa kifedha na kitaaluma kwa sababu hii. Mambo haya yasikomee hapa. Mrudi mlikotoka na mbuni vikundi vya kufuatilia mapendekezo yaliyotolewa. Ni muhimu kusambaza mliyojifunza hapa ili mambo hayo yapenye katika kila nyumba. Asanteni. a) Tambua na kuthibitisha anayehutubia washika dau. (Alama 2) b) Eleza mielekeo hasi inayosababisha wanawake na wanaume hudunishwa. (Alama 4) c) Kwa kuzingatia suala ibuka la haki, orodhesha haki zozote tatu ambazo wanaume na watoto wananyimwa. (Alama 3) d) Vita vya panzi haviamuliwi kwa fimbo Fafanua. (Alama 2) e) Taja mchango wa mwandishi wa hotuba hii katika kuirekebisha hali hii ya kudumisha wanawake na watoto. (Alama 2) f) Eleza maana ya i) Kukaidi amri (Alama 1) ii) Moyo uliofumwa kwa chuma (Alama 1) WEZOJE Kidato cha 4 Muhula wa 1 2013 3 Kiswahili P2

2. UFUPISHO (Alama 15) Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali ya ufupisho. Sawa na jinsi binadamu alivyokuwa na idadi kuenea kutoka usuli wake, ndivyo lugha ya Kiswahili ilivyoenea. Haitishwi na matatizo mengi bali inasambaa kwingi kila uchao. Kiswahili kimesambaa sio tu katika nchi za Afrika Mashariki bali bara nzima na ulimwengu kwa jumla. Lugha hii imepata hadhi na kuwa mojawapo ya lugha kumi na mbili za dunia. Vivyo hivyo imetwikwa majukumu katika ngazi ya kitaifa na kimataifa pia. Kwanza watu wa makabila mbalimbali huwasiliana kwa Kiswahili. Ikawa kwamba kanisani na hata vituo vya magari utawasikia watu wazungumza Kiswahili. Hali hii imedidimiza ule uhasama wa kikabila na kuleta utangamano baina ya makabila. Katika mikutano na makongamano ya kimataifa, Kiswahili hutumika sana kwa jinsi hii, ushirikiano wa kimataifa huimarishwa. Si ajabu kuwasikia Waasia, Waamerika na Waafrika wakiwasiliana kwa Kiswahili. Wao hujihisi wamoja kwa sababu ya kutumia lugha moja ya Kiswahili. Jumuiya ya Afrika Mashariki ilifanya Kiswahili lugha rasmi. Washirika husisitiza mawasiliano kwa lugha hiyo, hali kadhalika, Umoja wa Afrika uliiga sera hiyo ya kutumia Kiswhaili kama lugha rasmi. Ilikuwa fahari kubwa kuwasikia viongozi kama vile Rais Fredrick Chiluba akihutubia mkutano kwa Kiswahili. Umoja huo umeandaa mikutano ya kujadili mizozo mbalimbali barani humu ambapo lugha ya Kiswahili imekuwa ikitumika katika mikutano hii. Tukirejelea hali nchini, mikutano ya viongozi imeongozwa kwa lugha ya Kiswahili. Rais wa nchi huhutubia wananchi kwa Kiswahili. Mawaziri na viongozi hufuata mtungo huo huo kueleza sera za serikali kwa wananchi. Hivyo, Kiswahili hutumiwa kupatanisha serikali na wananchi wake. Katika kufunza Kiswahili, utamaduni na maarifa ya Waafrika hupitishwa kutoka kizazi hadi kingine. Mathalani, methali husheheni mengi kuhusu mila na destruri za jamii mbalimbali. Nyimbo, ngano na misemo vivyo hivyo. Mwafrika amepata fursa ya kutoa mchango wake katika ustaarabu wa wanadamu kupitia lugh hii. Wanaisimu wapenzi wa Kiswahili wamejitahidi kukisanifisha Kiswahili kadri ulimwengu inavyokua kukitumia na kukionea fahari katika nyanja tunazoshiriki. Maswali a) Fupisha aya mbili za kwanza kwa maneno kati ya 25-35 (Alama 5) Matayarisho Nakala Safi WEZOJE Kidato cha 4 Muhula wa 1 2013 4 Kiswahili P2

b) Eleza majukumu ya Kiswahili. (maneno 40-50) (Alama 8) Matayarisho Nakala safi 3. MATUMIZI YA LUGHA (Alama 40) a) Taja irabu za sifa zifuatazo. (Alama 2) i) Kati / mbele mtandozo ii) Kati / nyuma mviringo b) Tunga sentensi mbili kuonyesha matumizi ya ritifaa. ( ) (Alama 2) c) Bainisha ngeli za nomino zifuatazo. (Alama 2) i) Bati ii) Mpira d) Andika kwa wingi. (Alama 2) Chumbani mna chatu sita e) Ainisha. (Alama 2) Panya atafutwaye ameingia shimoni. f) Yakinisha sentesi ifuatayo. (Alama 2) Mama hakutuchapa hakutupa chakula wala maji. WEZOJE Kidato cha 4 Muhula wa 1 2013 5 Kiswahili P2

g) Eleza matumizi ya ka na hu katika sentensi zifuatazo. (Alama 2) i) Nilienda kanisani nikamkuta, nikamwamkua, nikamwomba msamaha. ii) Baba hufika nyumbani usiku wa manane. h) Andika katika usemi halisi. (Alama 2) Waziri alisema kuwa wangepata tiba ya bure kama bunge lingepitisha mswada huo. i) Tofautisha sentensi zifuatazo kimaana. (Alama 2) i) Basi la shule ya upili ya Sokomoko limeibwa. ii) Basi la shule ya upili ya Sokomoko limeibiwa. j) Tumia mzizi o-te katika sentensi kama: (Alama 2) i) Kivumishi ii) Kiwakilishi k) Andika sentensi ifuatayo kulingana na maagizo. (Alama 2) i) Hali timilifu ii) Mazoea l) Sahihisha. (Alama 2) Vitabu hizi ambazo zimesahihishwa ni za wanafunzi. m) Bainisha shamirisho katika sentensi ifuatayo. (Alama 3) Aliwaletea wachezaji zawadi kwa rukwama. WEZOJE Kidato cha 4 Muhula wa 1 2013 6 Kiswahili P2

n) Changanua sentensi ifuatayo kwa kutumia jedwali. (Alama 4) Wanafunzi walisoma taratibu huku walimu wakiwaelekeza vizuri. o) Andika kwa ukubwa. (Alama 3) Mtoto yule amemwaga kikombe cha maziwa. p) Neno kijana linaweza kutumiwa kama kivumishi au nomino, tunga sentensi kudhihirisha:- i) Kivumishi ii) Nomino q) Eleza matumizi ya viambishi vilivyopigiwa mstari. (Alama 3) i) Aliyemcheka ii) Uishipo iii) Chezeni r) Tunga sentensi ukitumia fa katika kauli ya kutendesha. (Alama 2) s) Toa kisawe cha; (Alama 1) Ugali WEZOJE Kidato cha 4 Muhula wa 1 2013 7 Kiswahili P2

4. ISIMUJAMII (Alama 10)... Kastoma kuna strong tea, githeri... i) Hii ni sajili gani. (Alama 1) ii) Andika neno muafaka la Kiswahili kwa msamiati ufuatao. (Alama 3) Kastoma Strong tea Githeri iii) Eleza sababu mbili zinazomfanya msomaji kutumia msamiati huu. (Alama 2) iv) Eleza sifa nne za sajili hii. (Alama 4) WEZOJE Kidato cha 4 Muhula wa 1 2013 8 Kiswahili P2