Kumb.Na.KSS/. Tarehe:.. Ndugu:.. SHULE YA SEKONDARI KIBAHA S.L.P 30053, KIBAHA SIMU NA. 023-2402143 e-mail Kibaha Secondary@kec.or.tz www.kec.or.tz TAARIFA YA KUCHAGULIWA KUINGIA KIDATO CHA TANO 2018 Ninayo furaha kukufahamisha kuwa umechaguliwa kuingia kidato cha V mwaka wa masomo wa 2017 Unatakiwa kufika hapa shuleni tarehe 17/07/2018. Nafasi yako atapewa mtu mwingine kama hutafika shuleni baada ya 30/07/2018. Shule iko Kilometa 40 kutoka Dar es Salaam karibu na Kiwanda cha TANCHIN zamani TAMCO Scania kilicho upande wa kulia mwa barabara inayoelekea Morogoro). Fuata barabara iliyo kushoto ukitokea Dar es Salaam hadi Tumbi Hospitali kilipo kituo cha mabasi nje ya Geti dogo la Hospitali. Uliza njia ya kuelekea shule ya Sekondari Kibaha. Yafuatayo ni maelezo na maagizo ambayo unashauriwa kuyatumia kabla hujafika hapa shuleni. 1. MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA: (i) Fika shuleni ukiwa na cheti cha kuzaliwa. (ii) Fika na Fomu ya kupimwa ikiwa imejazwa kikamilifu na Daktari wa serikali. (iii) Fika na result slip ya kidato cha nne. (iv) Lete File/Jalada la kutunzia mitihani yako. (v) Fika shuleni ukiwa na kadi ya BIMA ya afya. 2.SARE YA SHULE: (i) Anatakiwa awe na suruali mbili (DARK-BLUE) na mashati mawili (MEUPE) yenye mikono mifupi yenye nembo ya shule, tai na fulana (T-shirt) ya Shule. Pia mwanafunzi anatakiwa awe na nguo rasmi za kushindia(shamba wear). Hivi vinapatikana shuleni. (ii) Viatu jozi moja au zaidi visivyochongoka wala kuinuka mbele. Hivi viwe vya ngozi rangi nyeusi (vyenye gidamu) vya kufungwa kwa kamba. Ndala hazitaruhusiwa kuvaliwa pamoja na sare ya shule. (iii) Soksi fupi jozi mbili za rangi nyeusi na zisizo na mapambo yoyote. (iv) Aje na mkanda mweusi wa ngozi wa suruali wenye buckle ndogo. (v) Bukta au kaptura kwa ajili ya michezo na kazi za mikono. (vi) Raba za michezo jozi moja (01) (vii) Aje na sweta (dark-blue) yenye shingo ya herufi V (viii) Aje na nguo za michezo. (track suit na bukta mbili za rangi ya Blue) TANBIHI: Nguo utakazopewa baada ya kulipia zinatosha,hivyo usije na nguo za nyumbani. 3.MAHITAJI MENGINE: (i) Kila mwanafunzi awe na Sahani, Bakuli, Kikombe, Kijiko kwa ajili ya chakula. (ii) Lete Shuka tatu za Bluu, mto na Foronya mbili, pamoja na Chandarua. (ukipenda unaweza kuleta blanketi moja ingawa hali ya hewa ya Kibaha ni ya joto. Vile vile ulete taulo moja ya kuogea na vifaa vingine vya usafi wa binafsi. (iii) (iv) (v) Ndoo 2 kwa ajili ya kutunzia maji ya kunywa na kuogea. Fika shuleni ukiwa na kwanja kwa ajili ya matumizi ya shule. Fika shuleni ukiwa na Mfagio laini 1, Mfagio Mgumu (hardbroom) 1, na Mpira Page 1 of 8
(vi) (vii) (viii) (ix) (x) (xi) (xii) wa kupigia deki 1 (Rubber squeezer), na Fagio la Chelewa lenye mkono. Dawa ya kusafishia choo Lita tano (AINA YA CARELINE). Toilet Paper kumi (10) au zaidi kwa matumizi binafsi. Godoro moja lenye Futi 2½ kwa 6 kwa matumizi binafsi(yanapatikana Maduka yaliyo jirani na shule) Truncker kwa ajili ya kuhifadhia vitu. Nguo za kushindia zinapatikana shuleni. (Suruali Mbili na Tshirt mbili zenye Nembo). Hairuhusiwi kuja na nguo za nyumbani Uniform zinapatikana shuleni (Suruali mbili na Tshirt mbili na mashati mawili yenye Nembo). Unatakiwa ulete Mathematical set (Mkebe wa vifaa vya Mahesabu) moja. (xiii) Kwa upande wa masomo unatakiwa kuleta daftari kubwa (counter books 4 Quire) zisizopungua 10. kwa muhula za kutosha kuandikia katika masomo yako yote (xiv) Shule yetu inafanya majaribio mengi. Leta ream mbili za karatasi za Photocopy Upeleke Ofisi ya Taaluma. (xv) (xvi) (xvii) (xviii) (xix) (xx) Alete scientific calculator kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita Kwa watakaosoma Biology A-Level waje na Dissecting Kit ambayo wataitunza wenyewe. Fika shuleni na Jembe na mpini wake kwa ajili ya bustani ya shule. Jitahidi mnunulie mwanao vitabu vifuatavyo kwa ajili ya rejea:- 1. Physics advanced Level by Chand 2. Chemistry advanced level by Chand 3. Understanding Biology advanced level. 4. Principle of Biology form V VI. 5. Modern ABC Physics volume 1 and 2. 6. Modern ABC Biology volume 1 and 2 7. Business accounting 2 by Frank wood 11 edition 8. Advanced mathematics by Chand. Mfungulie mwanao akaunti kwa ajili ya kutunza fedha za matumizi. Mwanafunzi akabidhi stampu na bahasha kwa ajili ya kutuma fomu ya maendeleo ya kitaaluma kwa muhula. 4. FEDHA ZA MUHIMU KULIPWA a) Za kulipia benki Akaunti namba 21201100007 Kibaha secondary school subvention account nmb bank (i) Shilingi 70,000/= kwa ajili ya Ada kwa mwaka au shilingi 35,000 kwa muhula. (ii) Shilingi 15,000/= kwa ajili ya tahadhali (Caution money) (hazitarejeshwa) (iii) Shilingi 10,000/= kwa ajili ya gharama za Uanachama na matumizi ya Maktaba kwa mwaka. (iv) Shilingi 10,000/= kwa ajili ya Fomu ya kujiunga na shule. (v) Shilingi 65,000 kwa ajili ya samani za Shule. TANBIHI: Malipo yalipwe kupitia benki ya NMB na Stakabadhi ya malipo iletwe shuleni Na iandikwe jina la Mwanafunzi na kidato chake kwenye pay in slip ya Benki na si jina la mzazi. b) Za kuleta taslimu shuleni (vi) Shilingi 150,000 kwa ajili ya nguo za sare na nguo za kushindia(suluari 4,mashati 2,T shirts 3 na tai 1). (vii) Shilingi 8,000/= kwa ajili ya Kitambulisho cha shule na usajili. (viii) Shilingi 20,000/= kwa ajili ya maboresho ya Taaluma. (viii) Shilingi 10,000/= kwa ajili ya usafi wa nywele/ndevu kwa muhula. (x) Shilingi 50,000 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa uzio wa shule (makubaliano vikao vya wazazi). Page 2 of 8
5. MAELEKEZO MENGINE MUHIMU: (i) Unapofika shuleni uripoti kwa mwalimu wa zamu ukiwa na Pay in Slips za Benki ambazo utazionyesha kwa msarifu msaidizi na yeye atakupatia risiti kwa malipo uliyolipia benki. Mwanafunzi hatapokelewa shuleni ikiwa hatakamilisha malipo ya Ada na michango mingine. (ii) Unatakiwa uwe na nauli ya kurudia nyumbani wakati wa likizo. Haturuhusu mwanafunzi kubaki shuleni wakati wa likizo. (iii) Pasi inaruhusiwa shuleni na ni lazima ijulishwe kwa mwalimu mlezi wa nyumba. (iv) Utakapofika hapa shuleni utasomewa sheria za shule na utaratibu mzima wa shule hii na utalazimika kuufuata. Ukikosa, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yako. (v) Mwanafunzi wetu haruhusiwi kuendelea na masomo ya muhula kama hajakamilisha malipo yote. Itabidi arudi nyumbani kwa gharama za mzazi/mlezi wake ili kufuata michango hiyo. (vi) Mwanafunzi haruhusiwi kumiliki Simu, Laptop na Ipod shuleni. Akipatikana na vitu hivyo atasimamishwa masomo au kufukuzwa shule na simu itaharibiwa. (vii) Endapo mwanafunzi/mzazi/mlezi atakuwa na dharura awasiliane kwa kutumia simu ya shule. (viii) Mzazi anaruhusiwa kuja kumsalimia mtoto wake kila jumapili ya mwisho wa mwezi kwa miezi ya Februari,Aprili,Augasti na Oktoba tu. 6.MAKOSA YANAYOWEZA KUSABABISHA KUFUKUZWA SHULENI. (i) Kumiliki simu ya mkononi na laini shuleni. (ii) Wizi,uasherati,ubakaji na ushoga. (iii) Ulevi,uvutaji bangi na matumizi ya madawa ya kulevya. (iv) Makosa ya jinai. (v) Kupigana au kupiga (vi) Kuharibu kwa makusudi mali ya umma (vii) Kudharau Bendera ya Taifa. (viii) Kuoa (ix) Kugoma,kuchochea na kuongoza au kuvuruga amani na usalama. (x) Kukataa adhabu kwa makusudi. 7. KIKAO CHA WAZAZI Shule ina utaratibu wa vikao vya wazazi ambavyo hufanyika kila mwaka. Lengo kuu la vikao hivyo ni kupanga na kusimamia mipango mbalimbali ya kuboresha taaluma, nidhamu na miundombimu ya shule. Mwaka huu kikao kitafanyika tarehe 25.8.2018 kuanzia saa tatu kamili. Unatakiwa usikose kuhudhuria 8.HITIMISHO Mwisho natumia fursa hii kwa niaba ya walimu, wafanyakazi na wanafunzi wote wa shule hii kukukaribisha hapa shuleni na naamini utatumia vizuri nafasi hii uliyopewa na Taifa ya kukuongezea elimu yako. Karibu sana. Nakala kwa: Maafisa Elimu (M) Ambilikile, C.M, Mkuu wa Shule, SHULE YA SEKONDARI KIBAHA. SIMU YA MKONONI: 0752 453639/0717 054360 MIKOA YOTE YA TANZANIA BARA Taarifa kwa wanafunzi Page 3 of 8
Anuani...... Tarehe:... Mkuu wa Shule, Shule ya Sekondari Kibaha, S.L.P. 30053, KIBAHA YAH: BARUA YA KUKUBALI KUJIUNGA NA SHULE HII Aksante kwa barua yako Kumb.Na.. ya tarehe (a) (b) (c) (d) (e) Nakubali/sikubali nafasi niliyopewa ya Kidato cha Tano kwa mwaka. Niko tayari/siko tayari kufuata sheria, maagizo na masharti yote ya Kibaha Sekondari Nitahudhuria/Sitahudhuria masomo yote ninayotakiwa kusoma hapa shuleni Nikishindwa kuhudhuria bila sababu ya msingi nifukuzwe shule. Nitaleta/Sitaleta (i) (ii) (iii) (iv) (v) Uthibitisho wa Uraia/Cheti cha kuzaliwa (Affidavit hairuhusiwi) Vitu vinavyohitajika kwa matumizi yangu Cheti cha Afya Fomu ya kuandikisha na habari zangu za mzazi/mlezi wangu. Result slip ya kidato cha nne. Aksante....... JINA NA SAHIHI YA MWANAFUNZI JINA NA SAHIHI Page 4 of 8
FOMU YA KUANDIKISHA SHULENI NA HABARI ZA WAZAZI WA MWANAFUNZI SEHEMU A: (HABARI ZA MWANAFUNZI): 1. Jina kamili (Kama kwenye mtihani) 2. Tarehe ya kuzaliwa Dini..Dhehebu 3. Mahali na Wilaya ulipozaliwa. 4. Shule ulipomaliza Kidato cha IV.., Mwaka uliomaliza 5. Kidato unachokuja kuingia hapa shule ya Sekondari ya Kibaha 6. Namba yako ya mtihani Kidato cha nne ilikuwa 7. Michezo unayopendelea: TANBIHI: Hairuhusiwi kubadili dini ukiwa shuleni au kushawishi wanafunzi wengine kubadili dini. 1 2 3 JINA LA MCHEZO MAHALI/SHULE MWAKA 8. Kazi yeyote ya uongozi uliyowahi kufanya kama vile kiongozi wa michezo, kwaya, ngoma, kiranja, maktaba n.k. MADARAKA AU UONGOZSHULE/MAHALI MWAKA 9. Mambo unayopendelea kufanya nje ya masomo (kama vile michezo, mpira, bustani, ushonaji viatu, nguo, michezo ya kuigiza). kuimba 1.2. 3.. 10. Ndugu wa karibu wa mwanafunzi (wa kiume/wa kike) k.m. Mjomba, mama, shangazi, kaka, dada kufuatana na umri wao wa kuzaliwa. 1. 2. 3. 4. 5. 6. 7. 8. JINA LA NDUGU KAZI ANAYOFANYA UHUSIANO NA MWANAFUNZI KIWANGO CHA ELIMU ANUANI NAMBA YA SIMU Nathibitisha kwamba habari zilizotolewa hapo juu ni kweli. Naahidi kuwa na tabia nzuri, mchapa kazi na mwenye bidii ya masomo. Tarehe:.. Sahihi ya Mwanafunzi Page 5 of 8
SEHEMU B: (HABARI ZA MZAZI/MLEZI): 1. Jina kamili 2. Kazi yake. 3. Mahali anapoishi... Anwani ya nyumbani Kijiji.Kata Tarafa Wilaya.Mkoa 4. (a) Anuani ya Mahali pa kazi ya mzazi/mlezi. (b) Nambari ya simu.. 5. Dini ya mzazi.. Madhehebu. 6. Anuani kamili ya nyumbani ambako mtoto atakuwa anakwenda siku za likizo. 7. Anwani ya kazini (ikiwa inatofautiana na hiyo hapo juu na kila mara inapobadilika tunaomba utuarifu rasmi kwa barua kupitia Mkuu wa Kata, Tarafa au wa Kijiji chako) 8. Nathibitisha kwamba habari zilizotolewa hapo juu ni za kweli. 9. Naahidi kushirikiana na walimu kuhakikisha kwamba kijana wangu anakuwa na tabia nzuri, mchapa kazi na mwenye bidii ya masomo. Tarehe..Sahihi ya Mzazi/Mlezi Page 6 of 8
MINISTRY OF EDUCATION AND VOCATIONAL TRAINING KIBAHA SECONDARY SCHOOL P.O BOX 30053, KIBAHA SPECIAL REQUEST FOR MEDICAL EXAMINATION The Medical Officer.From Headmaster,(GOVERNMENT M.O) Kibaha Secondary School, Date: Name of Student... Date Term.. Year.. I shall be very grateful if you will kindly examine the above named student and give us a report regarding his fitness to undertake studies well in our school. A: PRELIMINARY INFORMATION: MEDICAL HISTORY NO DISEASE YES NO DISEASE YES NO DISEASE YES NO 1. Tuberculosis 7 Kidney/ trouble 13 Operation 19 2. Asthma 8 Diabetes 14 Eye disorder 20 3 Pneumonia 9 Neverous breakdown 15 V.D 21 4 Heart 10 Ear/Noise/Throat 16 Disabled 22 trouble trouble 5 Recurrent 11 Skin disorder/ 17 indigestion disease 6 Jaundice 12 Anaemia 18 B: VITAL STATISTICS Age.. Height Weight.. Blood group Blood pressure. Pulse rate.. Systolic Diastolic. C: MEDICAL EXAMINATION: REMARKS/TREATMENT EAR RT. LT. VISION RT. EYE LT. EYE THROAT CHEST EXAMINATION ABDOMINAL EXAM. LIVER SPLEEN OTHER COMMENTS M.S. SYSTEM UPPER LIMBS LOWER LIMBS SKIN ANY OTHER FINDING Page 7 of 8
D: LABORATORY EXAMINATIONS/INVESTIGATION: (1) STOOL: - Ova..Leucocytes (2) URINALYSIS: PROTEIN GLUCOSE SEDMENT: - OVA Leucocytes (3) Hb. (4) B/S. (5) VDRL (6) WBC Total Differential: N L M E B.. (7) X-ray Chest (If necessary). (8) ANYOTHERINVESTIGATION MEDICAL CERTIFICATE: We request the medical officer to complete the following: I have examined the above named student and considered that he is physically fit/unfit for most activities taken at the school as my findings indicated above. Date: Station..Dr s Name: Signature Thank you in advance. Ambilikile C,M, Headmaster, KIBAHA SECONDARY SCHOOL. Page 8 of 8