TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

Similar documents
Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

Maoni ya Wananchi juu ya Huduma za VVU na UKIMWI Nchini Tanzania

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT

Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

Kutetea Haki za Binadamu

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

Draft 03 MWENGE KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO MWENGE

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

Human Rights Are Universal And Yet...

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

Makala ya Mshiriki wa Mafunzo

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

Govt increases vetting threshold of contracts

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Deputy Minister for Finance

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

ORDER NO BACKGROUND

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...

Kuwa na Ukimwi ni kama vile kutakiwa kuendelea kuuzima moto unaoniunguza bila kukoma.

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Kuwafikia waliotengwa

The Government is committed to improve marine transport and has a number

ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

Transcription:

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam Simu +255 22 2666355/7 Nukushi +255 22 2668015 Barua-pepe: info@sikika.or.tz, Tovuti www.sikika.or.tz Sikika 2010

Shukrani Sikika ni shirika lisilo la kiserikali linalotekeleza shughuli mbalimbali zenye lengo la kuchochea upatikanaji wa huduma za afya zenye uwiano, ubora unaokubalika, zilizo nafuu na endelevu. Moja ya kazi za shirika ni kutafsiri kwa lugha rahisi na ya kueleweka kwa wananchi wote nyaraka mbalimbali zikiwemo sera, miongozo, mipango na sheria mbalimbali katika utoaji wa huduma za afya. Ni kutokana na ukweli kwamba nyaraka hizi huwa katika lugha za kigeni ama za kitaalamu kwa mwananchi wa kawaida kuelewa. Hali hii inarudisha nyuma nguvu ya wananchi katika kufuatilia utekelezaji wa mipango, sera, sheria na miongozo hiyo. Sikika imeandaa kijitabu hiki ili kumpatia fursa mwananchi wa kawaida kujua, kufuatilia na kushiriki katika kutekeleza mpango wa serikali wa kuboresha na kusogeza huduma bora za afya ya msingi kwa kila mwananchi. Pia kijitabu hiki kitawasaidia watendaji wote wanaohusika na utekelezaji wa mpango huu, kuelewa kwa urahisi majukumu yao kutokana na urahisi wa kijitabu hiki pamoja na sababu nyingine ambazo zitawafanya kushindwa kupata na kusoma mpango mama. Kukamilika kwa kijitabu hiki kulihitaji juhudi na jitihada za wadau mbalimbali. Sikika inatambua mchango mkubwa wa ndugu Geofrey Chambua kwa ushauri, uchambuzi na kuboresha mantiki ya kijitabu hiki pamoja na ndugu Nathan Mpangala kwa kukisanifu kijitabu hiki kwa michoro ya kuvutia (katuni). Kwa namna ya pekee, Sikika inawashukuru wafanyakazi pamoja na vijana wake wa kujitolea kwa mchango wao mkubwa wa mawazo, maoni na kukipitia kwa ujumla wake kijitabu hiki. Ingawa si rahisi kumshukuru mtu mmoja mmoja kwa ushiriki wake, Sikika inatambua thamani ya mchango wa wale wote walioshiriki kwa namna moja ama nyingine katika kukamilisha kijitabu hiki. Irenei Kiria MKURUGENZI MTENDAJI Sikika i

Tafsiri Ya Maneno ya Msingi CCHP CHF HSR HSSP MMAM MKUKUTA NACP Mpango Kabambe wa Afya wa Halmashauri (Comprehensive Council Health Plan) Community Health Fund (Mfuko wa Afya ya Jamii) Health Sector Reforms - Mabadiliko katika Sekta ya Afya. Health Sector Strategic Plan - Mpango Mkakati wa Sekta ya Afya Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Tanzania National AIDS Control Program - Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI NHIF National Health Insurance Fund (Bima ya Afya ) PPP SAFE TAMISEMI TDHS UKIMWI VVU WHO YAV Public Private Partnership (Ushirikiano baina ya Serikali na Sekta Binafsi) Sugery for in-turned eyelids, Antibiotics for active disease, Face washing to prevent infection and Environment changes Mkakati wa kutokomeza ugonjwa wa macho (vikope) Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tanzania Demographic Health Survey Utafiti wa Takwimu za Afya Tanzania Upungufu wa Kinga Mwilini Virusi Vya UKIMWI World Health Organisation (Shirika la Afya Duniani) Youth Action Volunteers ii

YALIYOMO Shukrani Tafsiri ya Maneno ya msingi 1.0 VIFUNGU VYA AWALI 1 1.1 Utangulizi 1 1.2 Hali Halisi ya Huduma za Afya Tanzania 1 1.3 Hali ya Huduma za Afya ya Msingi Nchini Tanzania 1 2.0 SERA, MIPANGO NA MIKAKATI MBALIMBALI KATIKA KUBORESHA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA YA MSINGI NCHINI TANZANIA 3 2.1 Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 3 2.2 Malengo ya Maendeleo ya Milenia 3 2.3 Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA) 3 2.4 Sera ya Afya, 2007 4 2.5 Mpango Mkakati wa Sekta ya Afya - HSSPIII 4 2.6 Mpango wa Maboresho katika Utumishi wa Umma 4 2.7 Mabadiliko katika Sekta ya Afya - HSR 5 2.8 Waraka wa Sera ya Kuboresha Muundo wa Serikali za Mitaa. 5 3.0 MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 6 3.1 Maelezo ya Mpango 6 3. 2 Malengo ya Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi 6 3.2.1 Lengo kuu la MMAM 6 3.2.2 Malengo mahususi 6 4.0 MAENEO MAKUU YALIYOAINISHWA KATIKA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI 8 4.1 Rasilimali Watu Katika Sekta ya Afya 8 4.2 Utoaji Huduma za Afya Katika Ngazi ya Wilaya 9 4.3 Huduma za Afya kwa Mama Wajawazito na Watoto. 10 i ii iii

4.4 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (NACP) 12 4.5 Malaria 13 4.6 Kifua Kikuu na Ukoma 14 4.7 Uimarishaji Afya na Elimu kwa Umma 15 4.8 Lishe Bora 16 4.9 Ushirikiano baina ya Serikali na Sekta Binafsi (PPP) 16 4.10 Tiba Asilia na Tiba Mbadala 17 4.11 Magonjwa Yasiyoambukiza 18 4.12 Magonjwa Yanayosahaulika 19 4.13 Afya Mazingira 20 4.14 Uraghabishi na Uhamasishaji 21 4.15 Mfumo wa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi 21 4.15.1 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii 21 4.15.2 TAMISEMI 22 4.14.3 Ngazi ya Mikoa 22 4.15.4 Ngazi ya Halmashauri 23 4.15.5 Ngazi ya Kata na Vijiji 23 4.15.6 Bodi ya Huduma ya Afya ya Halmashauri 23 4.15.7 Kamati ya Afya ya Kituo 24 4.16 Rasilimali Fedha katika Sekta ya Afya 24 4.17 Tathmini na Usimamizi wa Utekelezaji wa Mpango 25 5.0 HITIMISHO 25 iv

1.0 VIFUNGU VYA AWALI 1.1 UTANGULIZI Maradhi ni mojawapo ya maadui watatu ukiacha ujinga na umasikini ambao serikali imekuwa ikipigana nayo tangu Tanzania ipate uhuru wake mwaka 1961. Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM) ni mojawapo ya mikakati ya serikali ya kutokomeza adui maradhi. Chimbuko la mpango huu ni Sera ya Afya ya mwaka 1990 iliyorejewa mwaka 2007 inayoelekeza kuongeza kasi ya kusogeza huduma bora za afya ya msingi kwa kila mwananchi ili kuboresha hali ya ustawi wa maisha na kukuza uchumi wa kipato. Ongezeko la watu na nia ya serikali ya kurudisha madaraka katika ngazi ya serikali za mitaa pia ni sababu zingine za kuanzishwa kwa mpango huu. 1.2 HALI HALISI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA Tanzania inakabiliwa na ongezeko kubwa la maradhi. Malaria imekuwa ni miongoni mwa magonjwa yanayosababisha vifo vya watanzania wengi hususani wakina mama wajawazito na watoto wenye umri chini ya miaka mitano ikifuatiwa na UKIMWI na kifua kikuu. Magonjwa haya matatu yamekuwa ni kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya huduma za afya nchini pamoja na kusababisha kupungua kwa wastani wa umri wa kuishi wa Mtanzania hadi kufikia miaka 51. Kwa mujibu wa takwimu za afya za TDHS (2004-2005), watoto 112 kati ya 1000 wenye umri chini ya miaka 5 hufariki dunia kila mwaka. Pia akina mama 578 kati ya 100,000 hufariki dunia kwa mwaka kutokana na matatizo mbalimbali wakati wa kujifungua. Hii ni wastani wa akina mama 24 wanaofariki kwa siku au mwanamke mmoja kila baada ya saa moja. Takwimu hizi zinalenga katika kuonesha changamoto kubwa zinazoikabili serikali katika kukabiliana na utoaji wa huduma za afya ya msingi hapa nchini. 1.3 Hali ya Huduma za Afya ya Msingi Nchini Tanzania Huduma za afya ya msingi zipo katika mfumo wa Piramidi ambao huundwa na huduma kutoka katika ngazi ya zahanati, vituo vya afya na hospitali za wilaya. Kwa sasa Tanzania ina jumla ya zahanati 4679, vituo vya afya 481 pamoja na hospitali 219. Zahanati na vituo vya afya ambavyo ndizo nguzo kuu za huduma za afya ya msingi hutoa huduma za awali kwa watanzania kati ya elfu kumi (10,000) kwa Zahanati na elfu hamsini (50,000) kwa kituo cha afya. Hata hivyo kasi ya ongezeko la idadi ya watu, upungufu wa watumishi wenye sifa, upungufu wa nyenzo, madawa, umbali wa vituo vya kutolea huduma, ubovu wa barabara pamoja na tatizo la usafiri wenye uhakika ni changamoto kubwa zinazokabili utoaji wa huduma za afya ya msingi hapa nchini. 1

2

2.0 SERA, MIPANGO NA MIKAKATI MBALIMBALI KATIKA KUBORESHA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA YA MSINGI NCHINI TANZANIA Serikali imeandaa misingi ya kisera na kuweka mazingira mazuri ya utekelezaji ili kuboresha huduma za afya nchini. Misingi hii ambayo ni chimbuko la MMAM ni ya kitaifa na kimataifa kama ilivyoainishwa hapo chini. 2.1 Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 Lengo kuu la Dira hii ni kuboresha maisha ya mtanzania kwa kuboresha afya ya msingi, afya ya uzazi, kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto, kuongeza umri wa kuishi, upatikanaji wa maji safi na salama kwa wote, uhakika wa chakula cha kutosha na salama, kufikia lengo la usawa wa kijinsia katika ngazi mbalimbali za maamuzi ya kiafya na kuhamasisha ushiriki wa wananchi katika mipango ya utoaji wa huduma za afya. 2.2 Malengo ya Maendeleo ya Milenia Kama ilivyo kwa dira ya maendeleo ya taifa 2025, malengo ya Milenia pia yanalenga kupunguza robo tatu ya vifo vya watoto chini ya miaka 5, kuboresha afya ya mama wajawazito kwa kupunguza vifo vinavyotokana na uzazi pamoja na kupiga vita UKIMWI, malaria na magonjwa mengine 2.3 Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania (MKUKUTA) Mkakati huu mbali na malengo mengine, pia unalenga kuboresha maisha na ustawi wa jamii ya Watanzania kwa kuitaka wizara ya afya na ustawi wa jamii kutumia kiasi kikubwa cha bajeti yake kwa ajili ya chanjo dhidi ya magonjwa kwa watoto chini ya miaka mitatu, afya ya uzazi, kuzuia malaria, Virusi vya UKIMWI, Kifua kikuu na Ukoma. 3

2.4 Sera ya Afya, 2007 Dira ya Sera ya Afya ni kuwa na jamii yenye afya ambayo itachangia kikamilifu katika maendeleo binafsi na ya taifa kwa ujumla. Pia sera hii inakusudia kutoa huduma muhimu za afya zenye uwiano wa kijiografia, viwango vya ubora unaokubalika, gharama nafuu na zilizo endelevu. 2.5 Mpango Mkakati wa Sekta ya Afya - HSSPIII Mpango huu unajumuisha uboreshaji wa huduma za afya katika ngazi za wilaya, mkoa, na taifa ikijumuisha hospitali za rufaa za kanda na maalum. MMAM inalenga kuboresha huduma za afya katika ngazi ya wilaya kama moja ya malengo ya HSSP III. 2.6 Mpango wa Maboresho katika Utumishi wa Umma Mpango huu una lengo la kuboresha utumishi wa umma ili uwe na mpango endelevu wa kuboresha huduma za jamii kwa kuzingatia uwezo na ufanisi wa wataalamu waliobobea katika fani hizo. Hili ni moja ya lengo muhimu la MMAM. 4

2.7 Mabadiliko katika Sekta ya Afya - HSR Huu ni mkakati wa Serikali wenye lengo la kuimarisha utoaji wa huduma za afya na zinazokidhi mahitaji kwa jamii. Mabadiliko haya yameainisha mikakati tisa muhimu ambayo ni; Utoaji wa huduma katika ngazi ya wilaya Mabadiliko katika Huduma za Hospitali Majukumu ya Wizara ya afya na Ustawi wa Jamii Uboreshaji na maendeleo ya rasilimali watu katika sekta ya afya Mfumo wa usambazaji huduma Rasilimali fedha Ushirikiano baina ya sekta binafsi na serikali Uratibu wa Ushirikiano na Wahisani Udhibiti UKIMWI. 2.8 Waraka wa Sera ya Kuboresha Muundo wa Serikali za Mitaa. Maboresho haya ni pamoja na kuweka mgawanyo wa madaraka kwa kuunda mfumo wa serikali za mitaa zenye uhuru wa kujiamulia mambo yake na mipango yake ya maendeleo kuanzia ngazi ya jamii. 5

3.0 MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 3.1 Maelezo ya Mpango Tangu uhuru, serikali imekuwa ikitilia mkazo suala la upatikanaji wa huduma bora za afya kwa kila mwananchi hususani kwa wanaoishi katika maeneo ya pembezoni, ingawa azma hii imekuwa ikigonga mwamba kutokana na vikwazo mbalimbali. Moja ya vikwazo hivi ni kutokuwepo kwa uwiano wa vituo vya huduma hususani katika maeneo ya vijijini, umbali kati ya vituo vya huduma na makazi ya wananchi, ubovu wa miundombinu, upungufu wa wataalamu wa afya na vifaa. Kutokana na vikwazo hivi, serikali kupitia mpango huu inadhamiria kusogeza na kuboresha huduma za afya katika ngazi ya Halmashauri ambapo wananchi wateweza kupata huduma kwa urahisi. 3. 2 Malengo ya Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi 3.2.1 Lengo kuu la MMAM Kuboresha huduma za afya ya msingi ifikapo mwaka 2017. 3.2.2 Malengo mahususi Kukarabati na kuanzisha vituo vya huduma za afya katika ngazi zote ili kuleta usawa na kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya, Kuanzisha taasisi za mafunzo ya afya ili kuhakikisha upatikanaji wa watumishi wa kutosha, wenye sifa na ujuzi, Kuwajengea uwezo wafanyakazi, kupandisha daraja na kuendeleza watumishi wa afya walioko kazini ili kukabiliana na mahitaji na changamoto katika kutoa huduma za afya, Kuboresha mfumo wa taarifa na kumbukumbu za watumishi wa afya, Kuhakikisha uwepo wa vifaa, dawa na mahitaji mengine katika vituo vya huduma yanayokidhi viwango na ubora wa huduma za afya, Kuimarisha ufanisi katika mfumo wa rufaa kwa wagonjwa na ikiwezekana kuwa na kliniki zinazotembea (za magari) ili kuwafika wananchi katika maeneo yao na hivyo kupunguza rufaa zisizo za ulazima Kuongeza bajeti ya sekta ya afya kwa lengo la kufikia Azimio la Abuja la asilimia 15. 6

7

4.0 MAENEO MAKUU YALIYOAINISHWA KATIKA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI Ili malengo ya MMAM ya kuhakikisha kuwa kila mwananchi anafikiwa na huduma za afya ya msingi karibu na eneo analoishi yatimie, yafuatayo ni maeneo muhimu ya utekelezaji yaliyoainishwa katika mpango huu. Rasilimali watu katika sekta ya afya Utoaji huduma za afya katika ngazi ya wilaya Huduma za afya kwa mama wajawazito na watoto Malaria Janga la UKIMWI Kifua kikuu na ukoma Magonjwa yasiyoambukiza Afya Mazingira Uimarishaji wa Afya na Elimu kwa Umma Lishe bora Tiba za asili Magonjwa yanayosahaulika Ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi Uraghabishi na uhamasishaji Mfumo wa utekelezaji wa Mpango Rasilimali fedha katika sekta ya afya Ufuatiliaji na tathimini Maeneo haya yameonekana kuwa na changamoto nyingi ambazo zinahitaji kufanyiwa kazi ili mpaka kufikia mwaka 2017 lengo la MMAM la kuboresha na kusogeza huduma za afya ya msingi kwa watanzania wote liwe limetimia. 4.1 Rasilimali Watu Katika Sekta ya Afya Miongoni mwa changamoto kubwa inayoikabili sekta ya afya ni pamoja na upungufu wa watumishi kwa takribani asilimia 67.9 ambayo ni sawa na watumishi 31,808 katika kada zote. Hii inachangiwa kwa kiasi kikubwa na kasi ya ongezeko la idadi ya watu pamoja na milipuko ya magonjwa mbalimbali. Zaidi ya yote, hata wale wahudumu wachache waliopo hulazimika kuacha kazi na kutafuta ajira katika sekta zingine. 8

Malengo ya MMAM Kusomesha watumishi na wakufunzi wengi zaidi pamoja na kuajiri na kujengea uwezo wafanyakazi wanaokubali kufanya kazi katika maeneo yaliyoko pembezoni. Mikakati Kuwaongezea watumishi motisha na kuwapatia mahitaji yanayoendana na hadhi yao ili kuongeza tija na ufanisi katika kuboresha huduma za afya nchini. Kuhakikisha upatikanaji wa vitendea kazi na dawa za kutosha kwa wahudumu ili kuwapa motisha na moyo wa kuendelea kufanya kazi. 4.2 Utoaji Huduma za Afya Katika Ngazi ya Wilaya Utoaji wa huduma za afya katika ngazi ya wilaya unakabiliwa na changamoto zifuatazo; Upungufu wa vifaa muhimu kwa ajili ya utoaji wa huduma za afya kama vile samani, vifaa vya usafiri na mawasiliano, dawa muhimu, maji, vifaa vya kuhifadhi taka, mfumo duni wa rufaa na usimamizi katika uendeshaji wa vituo vya huduma za afya. Uhaba wa watumishi wenye sifa na ujuzi katika kutoa huduma za afya. Umbali baina ya vituo vya huduma na maeneo ya wananchi pamoja na misululu mirefu ya wagonjwa kwenye vituo huduma. Ufinyu wa bajeti kwa ajili ya kuendeshea huduma na kuboresha miundombinu. 9

Malengo ya MMAM Kukarabati, kujenga na kuboresha zahanati, vituo vya afya na hospitali za wilaya pamoja na kuzipatia vifaa vya kutosha kama vile samani, vifaa vya usafiri na mawasiliano, kliniki zinazohamishika, dawa muhimu (hususani za Kifua kikuu na Ukoma). Mikakati Kuimarisha mfumo wa rufaa kwa wagonjwa na kuongeza uwezo wa uongozi kitaaluma. Kuimarisha taasisi za utoaji mafunzo ya afya kwa kuzipatia vifaa na dhana za kufundishia, ili kuongeza usaili wa wanafunzi wa fani mbalimbali za masuala ya afya kwa lengo la kuongeza wataalamu wa afya. Kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya kuendeshea huduma za afya za wilaya. 4.3 Huduma za Afya kwa Mama Wajawazito na Watoto. Ingawa inakadiriwa kuwa asilimia themanini (80%) ya watanzania wote hupata huduma za afya chini ya umbali wa kilometa 5, lakini vifo vya akina mama wajawazito, watoto na watoto wachanga vimekuwa vikiongezeka. Akina mama 578 kati ya 100,000 hufariki dunia kutokana na matatizo ya uzazi. Vifo hivi husababishwa na; Upungufu wa wataalamu na mabingwa wa huduma ya mama wajawazito na watoto wachanga. Ni asilimia arobaini na sita tu (46%) ya kina mama wanaojifungua chini ya uangalizi wa wataalam waliobobea katika vituo vya huduma nchini. Wahudumu hao wachache waliopo, huelemewa na idadi kubwa ya wagonjwa wanaowahudumia, Umaskini, Umbali kati ya vituo vya huduma na makazi ya wananchi, Ubovu wa miundombinu, Lugha chafu pamoja na manyanyaso kutoka kwa watoa huduma hasa wakunga, Upungufu wa vitendea kazi kama vile; dawa, magari ya kubebea wagonjwa, vyumba vya upasuaji, vyumba vya kulaza wagonjwa, akiba za damu salama na kiliniki za kuhamishika ambazo zingetumika kuokoa maisha ya akina mama na watoto wengi endapo vingepatikana kwa wakati na kulingana na mahitaji, Ukosefu wa huduma rafiki za uzazi kwa vijana. Hii husababisha matatizo na vifo vingi vitokanavyo na uzazi kwa vijana wenye umri mdogo (chini ya miaka 19). 10

Malengo ya MMAM Kupunguza vifo vya akina mama wajawazito kutoka 578 hadi kufikia 175 kwa kila vizazi hai 100,000. Kupunguza vifo vya watoto chini ya miaka 5 kutoka 112 hadi 45 kwa kila watoto 1,000 wanao zaliwa hai Kuongeza idadi ya wanawake wajawazito wanaohudumiwa na wahudumu wa afya wenye ujuzi, uzoefu na utalaamu wa kutosha kutoka asilimia arobaini na sita (46%) hadi kufikia asilimia themanini na nane (88%). Mikakati. Kuhakikisha uwepo wa vifaa kama vile redio za masafa, magari ya kubebea wagonjwa, kujenga na kuongeza vyumba vya upasuaji, wodi za kulaza wagonjwa na idadi ya kliniki. Kuongeza idadi ya wanafunzi wanaodahiliwa katika vyuo vya mafunzo ya afya na pia kuwapatia mafunzo ya ziada watumishi wa afya ili kuongeza uwezo wao kitaaluma pamoja na kuajiri kwa mikataba madaktari bingwa wa akinamama na watoto. 11

4.4 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI (NACP) Moja ya changamoto kubwa inayoikumba serikali, jamii, kaya na watu binafsi ni janga la UKIMWI. Mbali na kusababisha vifo vingi, UKIMWI umeathiri nguvu kazi ya taifa pamoja na kuongeza mzigo wa gharama za kuwahudumia waathirika wa VVU. Kutokana na changamoto hizi MMAM inalenga kuongeza nguvu zaidi kwa NACP ili kuweza kuwafikia wananchi wengi zaidi katika kutoa huduma za matibabu pamoja na za kijamii, ikiwa ni pamoja na kutoa dawa za kurefusha maisha kwa waathirika wa VVU, vifaa vya maabara na huduma za kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto Malengo ya MMAM Kutibu na kutunza watu waishio na VVU kutoka idadi ya watu 440,000 kwa mwaka 2008 hadi kufikia idadi ya watu 800,000 kwa mwaka 2017 Kuongeza huduma za kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto katika vituo vyote vinavyotoa huduma za mama na mtoto Mikakati Kuzuia kuenea zaidi kwa virusi vya UKIMWI Kutoa mafunzo kwa watoa huduma za afya katika hospitali za wilaya, vituo vya afya na zahanati ya jinsi ya kuwahudumia waathirika wa UKIMWI pamoja na kutoa dawa na vifaa tiba vya kutosha ili waweze kuwahudumia wagonjwa wengi zaidi Kuwawezesha wananchi kwa kuwapa miongozo ili kutoa huduma kwa wagonjwa wa majumbani 12

4.5 Malaria Kila mwaka kati ya watu milioni kumi na saba hadi ishirini (17-20) wanaugua malaria, na kati yao, watu laki moja (100,000) hufariki dunia. Wagonjwa wengi wanaougua malaria ni akina mama wajawazito na watoto. Umaskini husababisha baadhi ya wajawazito kushindwa kumudu gharama za vyandarua vyenye dawa ili kujikinga na mbu waenezao malaria. Takribani asilimia thelathini na sita (36%) ya vifo vya watoto chini ya umri wa miaka mitano (5), vinatokana na malaria. Kutokuwepo kwa uelewa wa kutosha kwa wananchi juu ya mazalia ya mbu pamoja na upungufu wa wataalam, dawa na vifaa tiba, ni moja ya sababu za kuenea kwa ugonjwa huu. Malengo ya MMAM Kupunguza makali ya malaria kwa asilimia 80% ifikapo mwaka 2017 Mikakati Kusambaza na kugawa bure vyandarua vyenye dawa kwa akina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano, Kutoa elimu kwa jamii ya jinsi ya kujikinga na malaria Kupulizia dawa majumbani na sehemu za mazalia ya mbu ili kudhibiti ugonjwa huo. 13

4.6 Kifua Kikuu na Ukoma Kifua Kikuu na Ukoma ni moja ya magonjwa yanayoendelea kuwatesa watanzania walio wengi. Kwa mwaka 2004, zaidi ya watanzania 64,000 waliugua Kifua kikuu na watanzania 4500 (sawa na watu 1.4 kwa kila watu 10,000) waliugua ukoma. Takwimu hii imevuka viwango vilivyowekwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) ya kila watu 10,000, mtu mmoja huugua ukoma. Kifua kikuu huathiri kwa kiasi kikubwa watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI, pamoja na watu wanaoishi katika mazingira magumu. Kadhalika asilimia kumi (10%) ya watu wenye ukoma wana ulemavu wa kudumu. Magonjwa haya yamekuwa ni changamoto kubwa katika jamii kutokana na uchache wa wahudumu wa afya, ufinyu wa bajeti, upungufu wa dawa na vifaa pamoja na kutokuwepo kwa uelewa wa jamii kuhusiana na maambukizi, kinga na tiba ya magonjwa haya. Hali hii inasababisha vifo, kuongezeka kwa unyanyapaa na matatizo ya kisaikolojia kwa wagonjwa. Malengo ya MMAM Kupunguza idadi ya watu wanaougua au kufa kwa ugonjwa wa kifua kikuu kwa asilimia hamsini (50%) hadi kufikia 2017, Kupunguza ugonjwa wa ukoma kutoka kiwango cha watu 1.4 wanaougua mpaka kufikia kiwango cha chini ya mtu mmoja kati ya watu 10,000 mpaka kufikia 2017 Mikakati. Kuongeza watumishi wa afya wenye utaalam, Kuimarisha bajeti na kuhakikisha upatikanaji wa dawa na vifaa ili kuwezesha uchunguzi, kuzuia na kutibu kifua kikuu na ukoma kwa wagonjwa hususani kwa watu wenye virusi vya UKIMWI na wanaoishi katika mazingira magumu. Kuendesha kampeni nchi nzima za kuwajengea wananchi uwezo wa jinsi ya kujikinga, kugundua na kutibu kifua kikuu na ukoma mapema. Mkakati huu utajumuisha pia mbinu ya ufuatiliaji na kutoa takwimu na taarifa sahihi za kifua kikuu na UKIMWI kwa wadau mbalimbali kwa ajili ya kuchukua hatua madhubuti. 14

4.7 Uimarishaji Afya na Elimu kwa Umma Uimarishaji Afya na elimu kwa Umma ni njia muhimu ya kuwashirikisha wananchi katika shughuli za kuboresha huduma za afya pamoja na kujikinga na baadhi ya magonjwa. Njia hii pia itasaidia kushirikisha wadau wote katika kufanikisha na kutimiza malengo ya MMAM. Lengo ya MMAM Kuijengea uwezo jamii ili iweze kushirikia katika kutunza afya zao wenyewe Mikakati Kuchochea uwelewa wa jamii na wadau wengine ili waweze kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa MMAM 15

4.8 Lishe Bora Ingawa tatizo la utapia mlo limepungua nchini kutoka asilimia 44% hadi 38% kati ya mwaka 1999 na 2004, bado kuna changamoto ya jamii kutokuchukua hatua za kuimarisha lishe bora. Hii inatokana na uhaba wa wataalam wa kuratibu shughuli za lishe bora katika ngazi ya jamii na wilaya. Malengo ya MMAM Kujenga uelewa na uwezo wa kushugulikia masuala ya lishe bora katika ngazi ya jamii na Wilaya Mikakati Kusomesha na kuajiri wataalamu wa kuratibu masuala ya lishe bora. 4.9 Ushirikiano baina ya Serikali na Sekta Binafsi (PPP) Mara tu baada ya Uhuru, huduma zote za afya zilikuwa zikitolewa bure na serikali. Kutokana na ongezeko la magonjwa na ufinyu wa rasilimali, serikali ilianzisha mfumo wa kushirikisha watu binafsi katika kutoa huduma za afya nchini. Kwa sasa asilimia arobaini (40%) ya vituo vyote vya huduma za afya nchini, vinamilikiwa na watu binafsi. Changamoto kubwa kwa sasa ni kuwa zaidi ya asilimia 90% ya vituo binafsi vipo mijini na kuacha asilimia kubwa ya watanzania takribani 80% inayoishi vijijini kukosa huduma muhimu za afya. 16

Malengo ya MMAM Kuimarisha na kukuza ushiriki wa sekta binafsi katika kutekeleza Mpango wa Maendeleo ya afya ya msingi nchini kote Mikakati Kuandaa na kufanyia marekebisho miongozo mbalimbali kwa ajili ya kufuatilia huduma za afya ambazo zinatolewa na watu binafsi ili zilingane na zile zinazotolewa katika vituo vya umma Serikali na sekta binafsi zitashirikiana kutoa huduma za afya kwa jamii kwa kuzingatia sera na miongozo ya utoaji wa huduma hiyo nchini. 4.10 Tiba Asilia na Tiba Mbadala Ingawa Tiba asilia na tiba mbadala zimekuwa zikitumiwa na watanzania wengi, takribani asilimia 53-60% ya wakina mama hujifungulia kwa wakunga wa jadi; huduma hizi zimekuwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutokuwepo kwa elimu ya kutosha ya utaalamu wao, kutokutambuliwa kisheria kwa watoa huduma asilia, uhaba wa vifaa maalum iwapo dharura inatokea, kukosekana kwa taarifa na kumbukumbu za matibabu yao, kutokuwepo kwa mfumo wa ufuatiliaji na tathmini wa huduma zao, imani za kishirikina na ukosefu wa tafiti za kina. 17

Malengo ya MMAM Kuhakikisha kwamba, wananchi wanapata tiba asilia na tiba mbadala zenye kuzingatia ubora wa hali ya juu, na ambazo zimethibitishwa kwa kuzingatia utafiti uliokamilika bila kuathiri maslahi ya upande wowote. Kurasimisha watoa huduma asilia pamoja na kuhakiki, kusajili na kuthibitisha rasmi dawa asilia Mikakati Kuanzisha na kufungua vituo rasmi vya huduma asilia Kufanya tafiti kwa taasisi zote zinazojishughulisha na utoaji wa dawa asilia na tiba mbadala ili kupatiwa hati miliki na serikali. Kuandaa mpango maalum kwa watoa huduma za asili kufanya ufuatiliaji wa wagonjwa wao, kutayarisha na kutoa taarifa kwa serikali juu ya maendeleo ya tiba zao 4.11 Magonjwa Yasiyoambukiza Tanzania inakabiliwa na changamoto ya ongezeko la magonjwa yasiyoambukiza kama vile, kisukari, magonjwa ya moyo, saratani, utapia mlo, magonjwa ya akili na waathirika wa mihadarati. Hata hivyo, idadi ya watumishi wenye sifa na ujuzi wa kushughulikia magonjwa haya haiendani na wingi wa mahitaji. Pia wananchi wengi hawana uelewa kuhusu jinsi ya kuchunguza, kugundua na kujikinga na magonjwa haya Malengo ya MMAM Kuboresha huduma ya kinga na udhibiti wa magonjwa yasiyoambukiza katika ngazi ya msingi kabisa ya utoaji huduma za afya Mikakati Kutoa mafunzo ya awali kwa watoa huduma za afya kuhusiana na jinsi ya kugundua, kutibu na kuhudumia watu wenye magonjwa haya Kuwashirikisha wananchi na wadau wengine katika kuzuia na kujikinga na magonjwa haya. 18

4.12 Magonjwa Yanayosahaulika Magonjwa yanayosahaulika hujumuisha usubi, matende, minyoo, kichocho na magonjwa ya macho (vikope). Inakadiriwa kuwa takribani watanzania milioni mbili wapo katika hatari ya kuugua ugonjwa wa usubi. Minyoo na kichocho huwapata zaidi wanafunzi wa shule za msingi. Malengo ya MMAM Kupunguza wingi wa magonjwa haya na ikiwezekana kuyatokomeza kabisa mpaka ifikapo mwaka 2017 Mikakati Kutekeleza mkakati wa (SAFE) wa kutokomeza ugonjwa wa vikope kwa; kufanya upasuaji kwa wagonjwa wenye matatizo makubwa, kutoa dawa kwa ajili ya kutibu na kuzuia maambukizi yasienee, kampeni ya usafi wa mtu binafsi (hasa uso) pamoja na mazingira ili kuzuia maambukizi. Kuendeleza programu za afya mashuleni ili kutokomeza magonjwa ya minyoo na kichocho kwa wanafunzi Kuendeleza programu za kuzuia kusambaa kwa Ugonjwa wa matende 19

4.13 Afya Mazingira Afya mazingira inajumuisha usafi wa mazingira, matumizi sahihi ya vyoo, utunzaji sahihi wa taka, upatikanaji wa chakula na maji safi na salama pamoja na usafi wa mtu binafsi. Uharibifu wa mazingira husababisha kuenea kwa magonjwa. Tanzania inakabiliwa na tatizo la uchafuzi wa mazingira na hivyo kusababisha kuenea kwa magonjwa ya milipuko. Ni asilimia 52.8 tu ya watanzania wote hutumia vyoo salama, kati yao ni asilimia 36.7 tu ya shule zote zinatumia vyoo salama. Changamoto ya uchafuzi wa mazingira hutokana na upungufu wa maafisa mazingira katika ngazi ya wilaya na tarafa, kutokuwepo kwa sheria na kanuni madhubuti za usafi wa mazingira pamoja na jamii kutofuata kanuni na sheria za usafi. Malengo ya MMAM Kuboresha afya mazingira kuanzia ngazi ya kaya Mikakati Kuwajengea uwezo Maafisa mazingira katika ngazi za wilaya na kata wa jinsi ya kuhifadhi mazingira Kuelimisha na kuishirikisha jamii katika kufuata kanuni na taratibu za usafi katika kutunza afya ya mazingira yao. 20

4.14 Uraghabishi na Uhamasishaji Ni mfumo wa mawasiliano unaolenga kubadilisha tabia katika jamii ili kufikia malengo yaliyowekwa. Malengo ya MMAM Kuchochea uwelewa wa wadau ili waweze kushiriki kikamilifu katika kufanikisha malengo ya MMAM. Mikakati Kuongeza uwelewa wa jamii ili waweze kushiriki katika utekelezaji wa MMAM. 4.15 Mfumo wa utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi Kwa kuwa utekelezaji wa mpango huu unahusisha ngazi mbalimbali kuanzia ngazi ya kitaifa mpaka ngazi ya vijiji/mitaa, mfumo madhubuti wa mgawanyo wa majukumu, utekelezaji, utoaji wa mrejesho na taarifa kwa ajili ya kutathmini maendeleo ya mpango kwa wadau unahitajika. Ufuatao ni mfumo wa utekelezaji wa majukumu na wajibu wa wadau wakuu katika utekelezaji wa MMAM 4.15.1 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Wizara hii ni kiungo kikuu cha uratibu wa mpango huu ikishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Majukumu ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Kuandaa miongozo, sera na mikakati kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huu. Kutafuta na kukusanya rasilimali kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa MMAM Kuzisaidia na kuziwezesha sekretarieti za mikoa ili ziweze kuzijengea uwezo mamlaka za Serikali za mitaa katika kutekeleza mpango huu Kufuatilia, kutathmini na huhakiki utekelezaji wa mpango huu, ikisaidiana na wadau wengine. Kupitia kikosi kazi chake, wizara ina Wajibu wa kuandaa mipango kazi, kufuatilia ukarabati na ujenzi wa vituo vya huduma pamoja na mchakato wa ununuzi na ugavi. 21

4.15.2 TAMISEMI Majukumu ya TAMISEMI Kusimamia utoaji wa huduma za afya katika ngazi za hospitali, vituo vya afya, zahanati na ngazi ya vijiji/kaya. Kuhakikisha kuwa mamlaka za Serikali za Mitaa zinaandaa mipango na bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa MMAM Kutenga na kugawa rasilimali kwa sekretarieti za mikoa na serikali za mitaa kwa ajili ya utekelezaji wa MMAM Kusimamia utekelezaji wa MMAM katika ngazi ya Serikali za mitaa 4.15.3 Ngazi ya Mikoa Majukumu ya Sekretarieti ya mkoa kupitia Timu ya Uendeshaji Huduma za Afya ya Mkoa Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa Serikali za mitaa ili kuhakikisha utekelezaji wa MMAM Kuhakikisha kuwa MMAM inajumuishwa katika bajeti na Mpango Kabambe wa afya wa Halmashauri - CCHP Kusimamia na kuweka mazingira mazuri ya kuhakikisha utekelezaji wa MMAM. 22

4.15.4 Ngazi ya Halmashauri Majukumu yake: Kusimamia kazi, kuajiri wafanyakazi, kutoa ushauri wa kitaalam kwa vituo vya Afya na zahanati na kutoa taarifa na ripoti za utekelezaji wa MMAM. Kutoa elimu kwa jamii na kuhakikisha kuwa wananchi wanahusika katika utekelezaji wa MMAM pamoja na kuhakikisha kuwa MMAM inajumuishwa katika Mpango kabambe wa Afya wa Halmashuri - CCHP. 4.15.5 Ngazi ya Kata na Vijiji Majukumu ya Kamati ya Maendeleo ya Kata na Serikali ya Kijiji ni: Kutoa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya Afya na zahanati Kusimamia na kuhamasisha jamii kuchangia fedha na nguvu kazi kwa ajili ya utekelezaji wa MMAM. Hii itasaidia kuwafanya wananchi kuwa wamiliki na wasimamizi huduma za afya. Kutoa taarifa za maendeleo ya MMAM Kuweka mazingira mazuri ya kuwezesha utekelezaji wa MMAM na utendaji wa watoa huduma za afya katika vituo vya huduma. 4.15.6 Bodi ya Huduma za Afya ya Halmashauri Majukumu yake: Kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya, Bodi za afya zinawajibu wa kutafuta na kusimamia matumizi ya rasilimali ili kutekeleza malengo ya MMAM. 23

4.15.7 Kamati ya Afya ya Kituo Majukumu yake: Kukusanya rasilimali kwa ajili ya utekelezaji wa MMAM, Kuhamasisha jamii kuchangia fedha na nguvu kazi kwa ajili ya utekelezaji wa MMAM, Kutoa taarifa kwa jamii juu ya maendeleo ya utekelezaji wa MMAM, Kuweka na kuhakikisha mazingira mazuri ya kufanyia kazi kwa watoa huduma za afya. 4.16 Rasilimali Fedha katika Sekta ya Afya Kuna aina mbili za vyanzo vya mapato ya kuendeshea huduma za afya katika vituo vya huduma vya umma. Vyanzo hivyo ni fedha kutoka katika bajeti kuu ya serikali pamoja na michango ya nchi wahisani na fedha zitokanazo na uchangiaji wa gharama za huduma za afya na miradi mbalimbali ya Halmashauri husika. Mpaka sasa bajeti ya sekta ya afya kutoka serikali kuu ni asilimia 11% pungufu ya makubaliano ya maazimio ya Abuja ya kutenga kiasi cha asilimia 15% ya bajeti ya serikali katika sekta ya afya. Kutokana na upungufu huu wa rasilimali fedha katika sekta ya afya, serikali ilianzisha mfumo wa jamii ili kuchangia gharama pamoja na Bima ya Afya ambayo ni - NHIF na CHF. Malengo ya MMAM Kutafuta vyanzo vingine vya fedha ili kutekeleza Mpango. Kutenga fedha za kutosha ili kufanikisha utekelezaji wa MMAM kwa Serikali, wadau wa maendeleo, mashirika yasiyo ya kiserikari na asasi za kiraia. Mikakati Kutafuta vyanzo vingine vya fedha ndani na nje ya nchi. Kuviwezesha vyanzo vya mapato vilivyopo NIHF,CHF na Uchangiaji ili kuhakikisha utekelezaji wa MMAM 24

4.17 Tathmini na Usimamizi wa Utekelezaji wa Mpango Usimamizi na tathmini ya maendeleo ya Mpango vinalenga katika kuhakikisha kwamba malengo ya mpango yanatekelezwa kama ilivyopangwa na kwa muda muafaka Malengo ya MMAM Kufanya tathmini ya utekelezaji wa maendeleo ya Mpango kulingana na malengo yaliyowekwa. Mikakati Kuweka mfumo imara na endelevu wa kusimamia utekelezaji wa Mpango katika ngazi zote za utekelezaji Kuongeza nguvu na uwezo wa Wizara ya afya na Ustawi wa Jamii, TAMISEMI, sekretatrieti za mikoa na Halmashauri katika kusimamia utekelezaji wa shughuli za Mpango. 5.0 HITIMISHO Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM), unategemewa kutekelezwa kwa kipindi cha miaka kumi kuanzia mwaka 2007 hadi 2017. Matumaini ya serikali ni kwamba baada ya kipindi hiki MMAM itakua imesaidia kwa kiasi kikubwa kusogeza huduma za afya kwa wananchi na hivyo kuboresha hali ya maisha na ustawi wao, kama mojawapo ya malengo ya MKUKUTA na Dira ya Maendeleo 2025. Sikika inaipongeza serikali kwa kuona umuhimu wa kuboresha huduma za afya kwa wananchi na hatimaye kutoa mpango huu ili kufikia azma hii. Ni matumaini yetu kuwa kila mmoja wetu atatimiza majukumu yake kulingana na nafasi yake kama ulivyoainisha Mpango na hivyo kutimiza lengo la kusogeza huduma za afya karibu na maeneo ya wananchi wote mpaka kufikia mwaka 2017. 25

Kwa maelezo zaidi, maoni na ushauri, Tafadhali Tuandikie kupitia Anuani hii. Sikika, S.L.P 12183, Dar es Salaam. Au tuma ujumbe mfupi wa maneno kupitia +255 688 493 882...... 26

Kwa maelezo zaidi, maoni na ushauri, Tafadhali Tuandikie kupitia Anuani hii. Sikika, S.L.P 12183, Dar es Salaam. Au tuma ujumbe mfupi wa maneno kupitia +255 688 493 882...... 27

Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam Simu +255 22 2666355/7 Nukushi +255 22 2668015 Barua-pepe: info@sikika.or.tz, Tovuti www.sikika.or.tz Sikika 2010