Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds, clips) / Narrators Intro/Outro male around 30 english Narrator female around 30 english Pascal Monson male about 50 french Céline Allah female 20 french Pronunciation (German): [Ju-liE~ Adaïeh] (E~ = in, please ask a french native speaker) [Pas-kal MM~sM~] (M~ = on, please ask a french native speaker) [Celin Ala] 1
Intro: Hujambo na karibu katika sehemu ya tano kwenye mfululizo wa vipindi hivi vya Noa Bongo Jenga maisha yako kuhusu Haki za Binadamu. Haki za Binadamu ni kwa wote..ingawa " Uhuru wa binadamu ni haki ya kuzaliwa, na lazima kuwepo na usawa katika kudumisha hadhi na haki kwa wote, na hii ndio nguzo muhimu katika azimio hili la Umoja wa Mataifa, kwamba kila binadamu, ana uhuru na uwezo wa kutumia azimio hili kudai haki na uhuru kama inavyobainishwa kwenye azimio hilo. Haki hizi zimeangaziwa katika kifungu nambari 1 na 2 ambavyo ni msingi wa azimio hili. Kifungu nambari 26, kinaeleza kwamba kila binadamu ana haki ya kupata elimu bora. Hii ni mongoni mwa haki ambazo haziheshimiwi hasa miongoni mwa mataifa mengi barani Afrika. Je, nini kinaweza kufanya kuhakikisha haki ya elimu inaimarishwa na kudumishwa kwa wote? Julien Adayé [Ju-liE~ Adaïeh] amesafiri hadi nchini Côte D'Ivoire kuchunguza zaidi suala hili. 1. Narrator Kila mmoja ana haki ya kupata elimu bora. Kifungu nambari 26 katika azimio hili la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, kinasema kuwa kila mmoja ana haki ya kupata elimu ya msingi. Lakini tatizo kubwa ni kwamba haki ya elimu bora haidumishwi au mara nyingi inapuuzwa katika mataifa mengi ulimwenguni, kwasababu ya kukosa ufahamu au ukosefu wa fedha. Na matokeo yake, idadi kubwa ya watu hawawezi kusoma na kuandika. Mfano nchini Côte D Ivoire, asilimia 51 ya idadi ya watu waliotimu miaka 15 na zaidi nchini humo hawajui kusoma na 2
kuandika. Watoto wengi wanakosa kwenda shule na kisha kujutia baadaye. Hali hii imemtokea Céline Allah [Celin Ala], msichana wa miaka 20 hivi: 2. O-Ton ALLAH CELINE (French) Nilizaliwa katika kambi moja huko msituni. Babangu aliniambia kuwa si lazima wasichana waende shule kwasababu ni rahisi kupata mume na kuolewa. Wakati huo tayari mamangu alikuwa ametengana na babangu. Ninahuzunika sana ninapowaona wasichana wengine wakienda shule. Mara nyingi unashindwa kujieleza kwa marafiki zako. Na hili ndilo jambo linalonitia machungu zaidi. 3. Narrator Céline hayuko peke yake. Takwimu zinaonyesha kuwa elimu ya msichana imepuuzwa zaidi kuliko ile ya mvulana. Jumla ya asilimia 40 ya wavulana nchini Côte D Ivoire, hawawezi kusoma na kuandika. Yapo mashirika mengi nchini humo ambayo yamejitolea kuhakikisha kuwa kiwango cha kutojua kusoma na kuandika, kinashuka nchini Cote D Ívoire. Shirika la ABC limekuwa likiendesha shughuli zake nchini humo kwa muda mrefu sana, na makao yake makuu yapo katikati mwa mji wa Cocody mashariki mwa mji mkuu Abidjan. Hapa tunakutana na Pascal Monson [Pas-kal Mo~so~], mshirikishi wa shirika la ABC na anatuelezea kuhusu taaluma yake: 4. O-Ton MONSON PASCAL Nimefanya kazi katika sekta hii ya elimu tangu mwaka wa 1983, nikiwa mfanyakazi serikalini. Nimefanya kazi hii kwa zaidi ya miaka 8 kabla ya serikali kunipeleka kufundisha shule ya msingi, ambako nilifunza kwa muda wa miaka miwili kisha kuhamishwa hadi shule ya sekondari jijini. 3
Siku moja nilipokuwa nikifundisha, nilikutana na mwanafunzi ambaye hakujua kusoma wala kuandika. Baada ya kujiunga na shule alitokwa na machozi ya furaha siku alipopata cheti kwa kufuzu mtihani wake wa mwisho. Na hii ilinipa msukumo wa kuendelea kuwasaidia watu kujua kusoma na kuandika, ili waweze kuwa watu wa kutegemewa katika jamii. 5. Narrator Kujua kusoma na kuandika, ni ufunguo wa maisha bora, kwani inatoa fursa kwa mtu kuendeleza taaluma unayopenda maishani na kuwa mtu wa kuheshimiwa katika jamii. Mfano kusoma barua na ujumbe mfupi wa simu ya mkononi, kwa wengi huwa ni kiyama. Licha ya matatizo yanayomkumba Celine anafahamu vyema teknolojia ya kisasa ya mawasiliano. Kama wasichana wengine wa rika lake, ana simu ya mkononi ingawa hajui kusoma wala kuandika. Je, huwa anaitumia vipi hasa anapopokea ujumbe kwenye simu yake? 6. O-Ton ALLAH CELINE (French) Siwezi kusoma wala kuandika ujumbe mimi husaidiwa na rafiki zangu. Ni jambo linalonisikitisha sana hasa wanaponisomea ujumbe kwenye simu yangu kutoka kwa mpenzi wangu, lakini nitafanyaje! Ilinibidi nimweleza mchumba wangu kwamba siwezi kusoma na kuandika. Na siku hizi yeye hunipigia simu tu. 7. Narrator Watu ambao hawawezi kusoma na kuandika hawataki kuonekana ni washamba. Wanataka kuwa na simu ya mkononi kama Céline, na kisha baadaye kujifunza pole pole namna ya kukitumia kifaa hicho. Mfano 4
msichana huyu amevumbua mbinu ya kuhifadhi nambari za simu za watu ana kuwapa watu namba yake. 8. O-Ton ALLAH CELINE (French) Huwa naandika nambari hizi kwa karatasi au kadi ndogo zenye maelezo. Na ninazo nyingi kwenye mkoba wangu, huwa nazipeana kwa watu wanaponiuliza nambari zanhu za simu. Na kisha huwa nawapa simu yangu ili waweze kuandika nambari zao pia. 9. Narrator Shirika hili la ABC linadhamiria kuwapa elimu watu wasiojua kusoma na kuandika, ili kukabiliana na changamoto hizi. Ingawa halina darasa hata moja, limeweka mikakati ya kufanikisha azma hii. Anasema Pascal Monson [Pas-kal Mo~so~]. 10. O-Ton MONSON PASCAL (FRENCH) Tuko na wanafunzi 50, ambao wamejiunga na elimu ya watu wazima. Tunatoa huduma zetu kwa awamu tatu. awamu ya kwanza kuanzia saa nne hadi saa sita, ya pili saa tisa hadi kumi na moja jioni na ya mwisho saa kumi na mbili hadi saa mbili usiku. Masomo haya yamegawanywa katika vitengo vitatu, kitengo cha elimu ya msingi, kwa watu wasiojua kabisa kusoma na kuandika, kisha kitengo cha pili cha kundi la wanaoelewa kidogo kidogo yaani kuanzia mwaka mmoja hadi miaka miwili na kitengo cha tatu wale ambao wamejua kusoma na kuandikamwaka mmoja hadi miwili. 11. Narrator Mfumo huu wa elimu unaambatana na ule wa kitaifa nchini Cote D Ivoire ambapo wanafunzi wanaojiunga na masomo kwa mara ya kwanza 5
wanajifunza jinsi ya kusoma herufi na nambari, na kisha kuanza kusoma kuandika na kuhesabu. 12. ATMO : Literacy classes 13. Narrator Wanapokamilisha masomo hupewa vyeti vya kuhitimu elimu ya msingi. Mafunzo yanayotolewa na shirika la ABC humgharimu mtu kiasi cha faranga 2000 kila mwezi, kiasi sawa na shilingi elfu sita hivi. Kiwango hiki bado ni cha gharama ya juu sana hasa ikizingatiwa pato la mtu wa kawaida la faranga 500 kwa siku yaani chini ya shilingi elfu mbili nchini Cote D Ivoire. Kwa hivyo, si familia nyingi zinaweza kumudu gharama hii. Hata hivyo, lakini ili kuweza kuwasaidia watu wengi zaidi wanaotaka kujiunga na masomo, mashirika yasiyo ya kiserikali yameimarisha juhudi za kutafuta ufadhili kutoka nje. Wakati wa sherehe za kuadhimisha siku ya kujua kusoma na kuandika, wizara ya elimu nchini humo ilitangaza mipango ya kupunguza kiwango cha kutojua kusoma na kuandika kutoka asilimia 51 hadi asilimia 35 ifikapo mwaka 2020, na kwamba itashirikiana na mashirka mengine kutimiza lengo hili. Tayari mashirika yasiyo ya kiserikali yameimarisha juhudi za kuwahamasisha watu kuhusu umuhimu wa kujua kusoma na kuandika na hapa tena ni Pascal Monson [Pas-kal Mo~so~] : 14. O-Ton MONSON PASCAL (FRENCH) Hivi majuzi serikali ilitangaza kwamba kiwango cha kutojua kusoma na kuandika kimefikia asilimia 51- kiwango hiki kiko juu sana. Hii nikumaanisha kwamba nusu ya idadi ya watu nchini humu hawajui kusoma na kuandika. Na ndio sababu hivi majuzi serikali iliyaalika 6
mashirika yasiyo ya kiserikali kwenye warsha iliyokusudiwa kupigana na vita dhidi ya kutojua kusoma na kuandika. Tulihudhuria warsha hiyo na wizara ilionyesha moyo na kuahidi kuendelea kushirikiana na mashirika yasiyo ya kiserikali katika kupambana na vita hivi nchini Cote D Ivoire. 15. Narrator Matamshi haya ya Pascal Monson [Pas-kal Mo~so~] yanawiana na yale ya wizara ya elimu nchini humo. HUshirikiana katika kuhakikisha haki ya kujua kusoma na kuandika inatekelezwa. lakini mpango huu utaweza kufaya kazi vipi? 16. O-Ton MONSON PASCAL (FRENCH) Mfano iwapo shirika lisilo la kiserikali linataka kusaidia katika kuimarisha kiwango cha elimu, serikali huwa inasaidia kwa kufungua milango ya taasisi zake hasa katika sehemu ambazo miradi hiyo inatekelezwa, mfano katika shule za umma. Katika sehemu hizi Wizara ya Elimu inashirikiana kwa karibu na mashirika haya, kwa msaada unaohitajika 17. Narrator Pia wizara hutoa misada ya kifedha ili kufadhili elimu ya watu wazima mbali na kutoa kandarasi kwa mashirika haya. 18. O-Ton MONSON PASCAL (FRENCH) Pia shule nyingi za kibinafsi huwa tayari kusaidia katika kuimarisha elimu ya watu wazima nchini Côte d Ivoire. Kunapotokea kandarasi kubwa, wizara hiyo ya elimu huyaalika mashirika yasiyo ya kiserikali ili yaweze kutekeleza kandarasi hiyo na kulipwa faida kidogo. Pia, kuna kitengo maalum katika wizara hiyo kilichobuniwa kushughulikia elimu ya watu wazima nchini humo Côte D Ivoire. Kitengo hiki hushirikiana na mashirika yasiyo ya serikali kupunguza kiwango hiki ya kutojua kusoma 7
na kuandika. Ama kwa hakika kifungu nambari 26 kwenye azimio la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu kinazingatiwa hapa nchini. 19. Narrator Céline pia anataka kuona kifungu hiki Cha 26 kinazingatiwa kikamilifu sio tu nchini Côte D Ivoire bali kote Barani Afrika. Pia mama huyu ana hamu sana ya kuendelea na elimu ya watu wazima lakini hawezi kugharamia masomo hayo na pia kupata muda wa kufanya kazi zake. Lengo kubwa ni kutoa hamasa kwa wazazi kutilia mkazo elimu ya watoto wao, kwani hangependa kuwaona watoto wengine katika hali hii. 20. O-Ton ALLAH CELINE Mtu ambaye hajui kusoma na kuandika ni kama kipofu. Huwa si rahisi kufahamu mambo maishani. Na mimi nisingependa kuona watoto wengine wakipata shida kama mimi. Ni mrembo ndio, lakini siwezi kujieleza, jambo linalonisikitisha sana. Nawahimiza wazazi kuwapeleka watoto wao shuleni. 21. Narrator Kwa kufanya hivyo, kunawapa nafasi nzuri ya kuwa na maisha bora. Kifungu cha 26 kwenye azimio hili kinasema kuwa, Elimu inafaa kudumishwa kwa wote kwa lengo la kustawisha maendeleo ya binadamu na kwa kuheshimu na kuzingatia misingi ya uhuru na haki za binadamu Outro Iwapo serikali ina nia njema na kwa ushirikiano wa mashirika yasiyo ya kiserikali, kila mmoja anaweza kupata elimu bora. Na kwa ripoti hii iliyotayarishwa na Julien Adayé, ndipo tunapokamilisha sehemu ya tano ya mfululizo wa vipindi vya Noa Bongo, Jenga maisha yako kuhusu haki za binadamu. Asante kwa kutusikiliza na endapo ungetaka 8
kukisikiliza tena kipindi hiki, tembelea mtandao wetu wa dw.de / lbe. Hadi wakati mwengine tutakapokutana tena kwa makala nyingine, kwaheri kwa sasa! 9