MAFUNDISHO YA UMISHENI

Similar documents
Information for assessors (do not distribute this page to participants):

GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI

MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI

"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.

WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT

Kifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1

WEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu?

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia. Ellis Forsman. Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1

UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA

walozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w

Agano Lililofunikwa Kwa Damu

Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College

NGUVU. Utangulizi. Yesu alisema,

Kifo Na Mbingu (Death And Heaven)

BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE

Mzabibu Na Matawi. (The Vine And The Branches) Ellis P. Forsman. Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) 1

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

United Pentecostal Church June 2017

Maisha Ya Mkristo Ni Nini?

UTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha

B. Wanafunzi watapata ufahamu mkubwa wa kitabu hiki, na jinsi kinavyofundisha kuhusu kanisa.

Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally

JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?

FORWARD BY DANIEL SZMIOT

Tazama Yuaja. Kuhusu Toleo Hili. Umuhimu wa Mafundisho ya Biblia. Nguvu katika neno la Mungu.

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu

Roho Mtakatifu Ni Nini?

Patanishwa, Hesabiwa Haki, Takaswa

Silaha Za Shetani. Ellis Forsman. Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1

IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level

Kiu Cha umtafuta Mungu

Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia

Kufunga Milango - Uponyaji Kutokana na Athari za Giza

VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI

RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO

Kiumbe Kipya Katika Kristo

Uongozi Siri Na Larry Chkoreff. Version 1.2 Desemba 2010

KITABU CHA KUONGOZA FAMILIA

MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA

MASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO

Makasisi. Waingia Uislamu

Maisha Yaliyojaa Maombi

Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani?

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa.

Rahisi. Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Kitabu cha mwanafunzi. Rahisi

MWONGOZO WA NAMNA YA KUHAMASISHA MAOMBI YA MCHANA NA USIKU YA SIKU 10.

Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu

Kanuni. Muhimu za Kujifunza Biblia. Mchungaji Drue Freeman. Dan Hawkins & Joseph Brown. General Editors.

WAKOLOSAI MTAALA. B. Maoni: Tunapendekeza uwe na fafanuzi (commentary) yoyote yenye kushikilia mafundisho ya awali (conservative) katika Wakolosai.

Na Itafunika Wingi Wa Dhambi

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi. Iliyoendelea sana

Watumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1

YEHOVA-YIRE 1. 2 Baba yetu wa Mbinguni, tunakikaribia Kiti Chako cha. 3 Tunakushukuru kwa kutuzuru jana jioni. Tunaomba

UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI

Mwongozo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Early Grade Reading Assessment for Kenya

Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu (Watch Out for Wolves)

MSAMAHA NA UPATANISHO

KWA NINI SISI SI MADHEHEBU?

MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA

JE! MUNGU ANAMPA MWANAMKE HAKI YA KUTOA MIMBA IWAPO NI MHANGA WA UBAKAJI?

Iliyoendelea sana. Kitengo cha 2. Kitabu cha mwanafunzi Iliyoendelea sana

Rahisi. Kitabu cha mwanafunzi. Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Rahisi

Human Rights Are Universal And Yet...

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (

KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU?

MELKISEDECK LEON SHINE. katoliki.ackyshine.com

Aina Tatu Za Ibada. Ellis Forsman. Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 1

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Uponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14).

Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E)

Oktoba-Desemba

UZAO WA NYOKA. 2 Basi, usiku huu, tuna malimbuko tu ya utukufu huo mkuu. 3 Kwa uchaji tunasimama kwa imani yetu katika Uwepo

ONYO LA MWISHO KWA DUNIA

Hakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn

maombi, kabla tu hatujalifungua Neno hili la Kiungu.

# 18 Uponyaji Kutokana na Kukataliwa

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

United Pentecostal Church April Kushangilia Kwa Sala

Tumaini Kwa Afrika. Thomas Schirrmacher. Hoja 66. Dibaji na Prof. Mchungaji Dk. Thomas K. Johnson. Thomas Schirrmacher Tumaini Kwa Afrika TASCM RVB

Sura ya 7 Kielelezo: Tumepatanishwa na Mungu na Wanadamu

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

UNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW

Transcription:

MAFUNDISHO YA UMISHENI UINJILISTI NA UANAFUNZI Muhtasari: Elekeza kwa mada ilioko hapa chini nayo itakuelekeza kwa mada hiyo. I. Lengo la Sehemu Hii II. Uhusiano kati ya Uinjilisti na Uanafunzi III. Kwa nini Tufanya Uinjilisti na Kuwafanya Wanafunzi? IV. Ni Nani Anafaa Kufanya Uinjilisti? V. Tuzo la Kufanya Uinjilisti VI. Ni Nani Anayelengwa? VII. Tunafaa Kufanya Uinjilisti Wapi? VIII. Jinsi ya kufanya Uinjilisti A. Mpango Mkuu B. Uinjilisti wa Kibinafsi C. Uinjilisti wa Uhusiano D. Mahubiri ya Uinjilisti E. Uinjilisti Uliojaa F. Uinjilisti Uliolowa G. Uinjilisti wa Kusudi H. Kushinda Vizuizi IX. Uanafunzi A. Hatua za Uanafunzi B. Kuongezeka kwa Kiroho C. Uanafunzi wa Viongozi na Wafuasi D. Mtalaa na Shauri Zinazohusika X. Mahitaji ya Mwanafunzi Haki ya Kunakili 2008 Shirika la Mafunzo ya Umisheni. Haki Imehifadhiwa. 1

UINJILISTI NA UANAFUNZI I. Lengo la Sehemu Hii Unapomaliza sehemu hii unatakiwa kuwa: Unaweza kufafanua maneno haya mkristo mpya, mwanafunzi na uanafunzi. Unajua uhusiano kati ya uinjilisti na uanafunzi. Umeelewa msingi wa kibiblia wa kuwafanya wanafunzi Umejua tuzo na mateso yanayohusika na kuwafanya wanafunzi Kujua wale mnaotarajia kuitikia ushahidi wetu vyema. Anza kuomba ya kwamba Mungu atakuonyeshe ni wapi anataka uwe na wanafunzi Elewa mpango mkuu wa uinjilisti Unajua utaratibu wa uinjilisti wa kibinafsi Unaelewa ni nini akronimi FIRE inawakilisha Eleza maswali mawili ya elimu ya mlipuko wa uinjilisti Andika ushuhuda wako mwenyewe Eleza sheria nne za kiroho Kariri maandiko kutoka kwa barabara ya Warumi Unaweza kumuongoza mtu kwa Mungu ukitumia Yohana 3 Eleza njia tano za kukua kiroho kama zilivyo katika kifaa cha uinjilisti cha evangecube Kujua Kifungu kinachoeleza juu ya Kuongea ukweli kwa upendo. Itikia kipingamizi ambacho mtu anahitaji kupitia ili kupata wokovu Eleza kwa nini ukristo ni uhusiano Jua ni kwa nini wingi hauwezi kuwa kweli Jua umuhimu wa uhusiano kwa uinjilisti Jua maana ya uinjilisti wa jumla na uinjilisti wa kuloa Jua utaratibu wa uanafunzi Unaweza kueleza kuzidisha kwa kiroho Taja kanuni tatu ambazo Paulo alionyesha kwa mfano katika kuwafanya wanafunzi. Jua mawazo matano ya utendaji kutoka kwa Waylon B. Moore ya kuwafundisha wanafunzi. Kuza muhtasari mfupi wa mtalaa wa urefu wa miezi sita wa kufunza wanafunzi. 2

UINJILISTI NA UANAFUNZI II. Uhusiano kati ya uinjilisti na uanafunzi Uinjilisti ni kutangaza Habari njema za Yesu Kristo kwa waliopotea. Waliopotea ni wale watu wasiomwamini Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi. Wako kama kondoo waliopotea, ambao mchungaji mwema huwatafuta na kuwaleta kwa usalama. (Mathayo 18:12). Lengo la uinjilisti ni kupata waumini wapya. Muumini mpya ni yule anayemwamini Kristo; amebadilishwa kutoka kwa kutoamini na kuwa muumini. Mwanafunzi ni muumini anayefuata maagizo ya msingi ya imani ya kikristo. Neno mwanafunzi lina maana ya mwanafunzi, mtu anayejifunza kwa kufuata. Elimu hiyo ni zaidi ya elimu ya kichwa pia ni elimu-ya moyo. Mwanafunzi wa kweli hajui tu kuhusu Kristo, bali hufuata mafunzo ya Kristo. Katika Theologia ya kikristo, uanafunzi ni njia ya kufundisha watu kuwa wanafunzi waliokomaa. Uanafunzi ni zaidi ya kugawana ujumbe inahusika na kuendeleza watu kumpenda na kumtii Mungu. Uinjilisti na uanafunzi umeunganishwa pamoja. Uinjilisti huleta waumini wapya, nao waumini wapya hufunzwa kuwa wanafunzi. Wanafunzi hueneza injili ili kupata waumini wapya ambao wanafunzwa kuwa wanafunzi. Kwa hivyo uinjilisti huleta wanafunzi nao wanafunzi hueneza injili mpaka injili ienee duniani kote. Ikiwezekana, uanafunzi unafaa kufuata uinjilisti. Uinjilisti huleta watu kuzaliwa kiroho mara ya pili (tazama Yohana 3:3), kwa hivyo waumini wapya ni watoto wa kiroho. Waumini wapya wanahitaji uanafunzi ili wakomae. Sio vyema kupata mtoto wa kimwili alafu umuache. Vile vile, sio vyema kupata mtoto wa kiroho alafu umuache. Waumini wapya ni lazima wafunzwe na wakristo wengine. Tazama uhusiano ulioko kati ya uinjilisti na uanafunzi na umisheni. Misheni za kikristo zinahusika na kueneza injili kwa tamaduni. Kwa hivyo mmisheni anaeneza injili kwa kundi la watu au tamaduni mbali na lile lake. Uinjilisti na uanafunzi ni njia ambazo hutumika kukamilisha kazi ya umisheni. Uinjilisti na uanafunzi pia hufanyika katika tamaduni ya mtu mwenyewe, kwa hivyo sio uinjilisti wote na uanafunzi wote uko katika kiwango cha umisheni. 3

UINJILISTI NA UANAFUNZI III. Kwa nini Tufanye uinjilisti na Kuwafanya kuwa Wanafunzi? Fikiria msingi wa kibibilia wa uinjilisti na uanafunzi. A. Kristo aliiamrisha Katika kila moja ya zile Injili nne na Matendo ya Mitume, Yesu aliwaamuru wafuasi wake kuwafanya watu kuwa wanafunzi. Tume kuu inapatikana kwa maandiko yafuatayo: 18 Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. 19 Basi, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; 20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi sikuzote, hata ukamilifu wa dahari. (Mathayo 28:18-20). 15 Akawaambia, Enedeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. 16 Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. (Marko 16:15, 16). 46 Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; 47 na kwamba mataifa yote yatahubiriwa kwa jina lake kwa habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. (Luka 24:46-48). 21 Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. 22 naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu. 23 Wo wote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wo wote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa. (Yohana 20:21-23). 8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi. 9 Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao. (Matendo 1:8, 9). Umuhimu wa Tume Kuu unasisitizwa kwa kujitokeza kama sehemu ya maagizo ya Kristo kwa wanafunzi wake katika Injili zote nne. Na katika Matendo ya Mitume, Tume Kuu ndio maneno ya mwisho ya Kristo kabla ya kupaa. B. Kuokoa wenye dhambi. Kristo ametuamuru tufanye uinjilisti and uanafunzi ili wenye dhambi waweze kuokolewa kutoka jehanamu. Jehanamu ni mahali pa mateso (Tazama Luka 16:19-31). Kristo alisema mwogope Mungu, mwenye uwezo wa kumtupa mwenye dhambi jehanamu. 4 Nami nawaambia ninyi rafiki zangu, msiwaogope hao wauao mwili, kisha baada ya hayo hawana wawezalo kutenda zaidi. 5 Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumuua mtu ana uwezo wa kumtupa katika Jehanamu; naam, nawaambia. Mwogopeni huyo. (Luka 12:4, 5). 4

Mbali na Kristo, watu wamelaaniwa kwa kufa na kwenda jehanamu (Tazama Yahana 3:16-18; Ufunuo 20:15). Wale ambao hawajaokoka maishani mwao hapa duniani watatenganishwa na Mungu milele. Maandiko yanasema kila mtu anaishi mara moja duniani, kisha anahukumiwa. 27 Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu; 28 kadhalika Kristo naye, akiisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi; atatokea mara ya pili, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu. (Waebrania 9:27, 28). Yesu alikufa msalabani, kulipa deni la dhambi, ndipo wenye dhambi waokolewe kutoka jehanamu. Alisema alikuja kutafuta na kuokoa waliopotea (Tazama Luka 19:10). Anataka watu wawe na furaha ya kuishi na Mungu milele. Furaha hiyo imeelezwa katika maandiko yafuatayo. 3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. 4 Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwepo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwepo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita. (Ufunuo 21:3, 4). Kristo alikufa kuokoa wenye dhambi kutoka jehanamu, na anatarajia wafuasi wake watangaze hizi habari njema na kuwaonya kuhusu hatari za jehanamu. Kama hatutatii Tume Kuu, tutawajibika kwa roho zilizopotea na kuelekea jehanamu. Mungu alimpa Ezekieli wajibu wa kuhubiri toba. 8 Nimwambiapo mtu mbaya, Ewe mtu mbaya, hakika utakufa, nawe husemi neno la kumwonya mtu huyo, aiache njia yake, mtu mbaya huyo atakufa katika [a] uovu wake, lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako. 9 Walakini ukimwonya mtu mbaya kwa sababu ya njia yake, kusudi aiache; wala yeye asiiache; atakufa huyo katika uovu wake, lakini wewe umejiokoa roho yako. (Ezekieli 33:8, 9). [a] Ezekieli 33:8 au hapo ndani Kama Ezekieli alivyo wajibika kwa kuhubiri toba, Mungu anataka wafuasi wake kuwafanya watu kuwa wanfunzi. Mtume Paulo alitambua haya, na akasema kwamba nyeye yumaasumu kwa damu ya watu wote kwa sababu alitangaza neno la Mungu (tazama Matendo 20:26, 27). Wenye dhambi wanapookoka, Mungu hutukuzwa. Mungu ni mshindi katika dhambi na mauti. Wale waliompinga Mungu hutubu na kumuabudu Mungu. C. Kupanua ufalme Kristo aliamuru kwamba wafuasi wake wafanye uinjilisti na kuwafanya watu kuwa wanafunzi ili kupanua ufalme wa Mungu.Katika sabato yake ya kwanza duniani, alikaribisha ufalme. Kristo atakaporudi, ataanzisha amri yake juu ya ufalme. Tazama Ufalme wa Mungu katika sehemu ya mafunzo ya, Theologia. 5

Kanisa linafaa kupanua Ufalme wa Mungu kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Kanisa litakapomaliza tume hii, Kristo atarudi. Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja. (Mathayo 24:14). Ufalme wa Mungu unapopanuka, Mungu anaabudiwa na watu wa mataifa yote. Kwa hivyo upanuzi wa Ufalme unampa Mungu utukufu (tazama Ufunuo 5:9, 10, 13). Kupanua Ufalme kunatoa maisha matimilifu kwa wale wanao mkubali Kristo (tazama Yohana 10:10). Kristo anatoa usalama wa milele, upendo, mwongozo na tumaini. Watu wanapompokea Kristo, maisha yao hubadilishwa. Walevi wanapojikabidhi kwa Kristo huachana na pombe. Wenye mazoea ya kujamiiana wanaojikabidhi kwa Kristo huaachana na uovu wa kujamiiana. Watu walafi wanaojikabidhi kwa Kristo hugawana mali yao na wengine. Wale ambao ni maskini wa kiroho hujikabidhi kwa Kristo na wanajipata matajiri wa kiroho. 6

UINJILISTI NA UANAFUNZI IV. Nani Anafaa kufanya Uinjilisti? Ni nani ana jukumu la kufaya uinjilisti? Wamisheni? Wachungaji? Waalimu? Kulingana na maandiko, wakristo wote wanafaa kufanya uinjilisti. Yesu alitoa Tume Kuu kwa mitume wake kumi na mmoja na wanafunzi wengine wachache. Ni dhahiri kuwa kundi hili dogo la wafuasi halingeweza kutangaza Injili hadi mwisho wa dunia na kuwafanya wanafunzi wa mataifa yote. Sasa Tume Kuu ni yako na mimi na waaminio wote. Mtu anaweza kusema, Lakini si ni kazi ya wainjilisti kueneza Injilil? Ndio, ni jukumu la Wainjilisti kueneza Injili. Wako na kipawa cha uinjilisti. Sasa wanafaa kushawishi mioyo kwa Kristo. Lakini sio wainjilisti peke yao wanafaa kuwafanya watu kuwa wanafunzi. Kila mkristo ambaye anaweza kushahidi ameamrishwa kumshahidi Kristo. Ni sehemu ndogo tu ya kanisa iliyo na kipawa cha uinjilisti, lakini kila mkristo mwenye uwezo wa kufikiria na kuongea anaweza kushuhudia Kristo ni Bwana. Ni kupitia kwa mashahidi walioongezeka kwa mamilioni ya wakristo ambao wataeneza injili kwa kila kundi la watu wa duniani kwa haraka. Wakristo wanatumika kila siku kama mashahidi katika jimii zao, kwa marafiki, na kwa wafanyikazi wenzao. Kila muumini ni kasisi, na kasisi huongoza watu kumuabudu Mungu. 9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wamiliki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu. (1 Petro 2:9). Tunafanya kazi kama mabalozi wa Kristo kwa wasio amini (tazama 2 Wakorintho 5:20). 7

UINJILISTI NA UANAFUNZI V. Tuzo la Kufanya Uinjilisti Ni mazoea ya mwanadamu kuuliza, Ni tuzo gain nitapata nikifanya uinjilisti? Mtume Petro aliuliza atapata tuzo gani kwa kumfuata Kristo. Yesu akajibu:... Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, [a] au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele. (Mathayo 19:29). a. Mathayo 19:29 Muswada zaidi mama au mke Kuna ridhaa kuu kwa kuwaongoza watu kwa Kristo. Tuzo kuu zaidi ambayo mtu anaweza kutoa ni kuongoza mtu apokee uzima wa milele. Kwa hivyo kazi ya uinjilisti ni kuridhisha. Pia, wakristo wanaposafiri nchi mbalimbali na kuwaongoza watu kwa Kristo, watu hao huwakaribisha wainjilisti nyumbani kwao. Kwa hivyo wale wametoka manyumbani hukaribishwa nyumba mia zaidi. Walio wacha jamii hubarikiwa na upendo wa jamii mia zaidi. Na wanaoacha nyumba zao kwa ajili la Kristo wana nyumba ya milele mbinguni. Mara kunapokuwa na tuzo kuu kwa kuwaongoza watu kwa Kristo, muinjilisti anaweza kupatwa na mateso na taabu (tazama Yohana 15:18-21). Lakini walioitwa kwa ajili ya Mungu, Bwana huleta uzuri kutokana na mabaya unayopitia (tazama Warumi 8:28). Mitume walifanya uinjilisti na kuwafanya watu kuwa wanafunzi, kwa hivyo viongozi wa Kiyahudi waliamrisha kuchapwa kwa mitume. Alafu Wayahudi wakaamrisha mitume wasiongee kwa jina la Yesu. Angalia itiko la mitume. 41 Nao wakatoka katika ile baraza, wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuaibishwa kwa ajili ya jina hilo. 42 Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo. [a] (Matendo 5:41,42) [a] Matendo 5:42 Au Masiha Mitume walifurahia mateso yao kwa ajili ya Kristo! Kutangaza Injili sio rahisi, lakini kunafuraha kwa kazi kama hiyo. 8

UINJILISTI NA UANAFUNZI VI. Ni Nani Anayelengwa Je, tushiriki injili na watu gain? Lazima tuwe tayari kuwafanya watu wote kuwa wanafunzi. Yesu aliwafunza wanafunzi wake kuwa mashahidi vijijini mwao,nchini mwao, na mwisho wa dunia (Matendo 1:8). Alisema wafanyeni wanafunzi wa mataifa yote (Mathayo 28:19). Lakini sio wote wataitikia ushahidi wetu kwa usawa. Kwa hivyo tunafaa kutazamia kushiriki injili na wale wanao uwezo wa kumkubali Kristo. Kupitia kwa maombi, tunakubali Roho Mtakatifu kutuongoza kwa matumaini mema ya kufanya uinjilisti.ndani ya tamaduni zetu, tunaweza kuongozwa kushuhudia jamii, marafiki, majirani, wafanyikazi wenzetu, ama watu wengine tulio na uhusiano. Tunapata watu hawa wanakubaliana nasi vyema. Mtu mzee anafaa kwa kuongea na wazee wengine. Binti anafaa kwa kuongea na mabinti wengine. Mara nyingi, watu wa ukoo wetu waweza hutuitikia vyema zaidi kuliko watu wa koo zingine.tunawapenda watu wa kila umri, jinsia, na ukoo, na tunataka kushirikiana na watu wote. Lakini pia tunataka kuliona kanisa likikua haraka iwezekanavyo. Kwa hivyo tunawatafuta wale walio tayari kukubaliana na Habari Njema. Kama wamisheni katika makundi ya watu wengine, tunafuata Roho na kuona ni watu gani wanaitikia Injili. Tunaweza kuongozwa kulenga kufanya uinjilisti kati ya kundi la watu ambao wanaitikia sana. Yesu aliwatuma wanafunzi kufanya uinjilisti na akawaambia kama watu wa mjini hawataitika vizuri enendeni mahali pengine (tazama Luka 10:10, 11). Katika njia hiyo hiyo, mkifanya uinjilisti kwa njia nzuri, watu wa mahali fulani wasimkubali Kristo kama Bwana, enendeni mahali pengine. Mtume Paulo alifanya uinjilisti kwanza kwa watu ambao hawakuwa wameisikia injili ya Yesu Kristo (tazama Warumi 15:20-21). Tunajitahidi kufanya vivyo hivyo. 9

UINJILISTI NA UANAFUNZI VII. Tunafaa kuinjili wapi? Kama mmishonari, Bwana nakuongoza wapi ili uweze kufanya uinjilisti na kuwafanya wanafunzi? Unapojiandaa kwenda kwa uwanja wa umisheni, omba tene na tena kwamba Mungu akuongoze mahali unapofaa kwenda. Kwa mwoozo wa maombi, angalia kwa mtandao hapo chini. Kituo cha wamisheni huko America hutoa mtandao huu ambao hutambua makundi ya watu ambao waweza kufanyia uinjilisti. http://www.joshuaproject.net/index.php Dunia ya utendaji katika mtandao ufuatao unaomba maombi kwa mataifa mbalimbali ya dunia. http://www.24-7prayer.com/ow/?skin=247 Kwa mawazo zaidi kuhusu mahali pa kufanya uinjilisti, ongea na watu wa sehemu ya kutuma wamisheni. A. Anapoongoza Roho Mtakatifu. Roho alimuongoza mtume Paulo na wenzake kuepuka mahali Fulani na kuelekea Makedonia kwa kazi ya umisheni(tazama Matendo 16:6-10). Roho Mtakatifu alimuonya Paulo juu ya hatari, lakini akamshurutisha kwenda kama shaidiyerusalemi (tazama Matendo 20:22-24). Pia Roho anaweza kukuongoza kumisheni mahali sawa. B. Palipo na watu. Kwa jumla ni vyema zaidi - lakini sio sawa wakati wote kufanya uinjilisti katika miji na mijini badala ya mashambani. Watu wa miji na mijini hueneza injili nchini. Na watu mjini huwa kama mashahidi kwa wale waliotoka mashambani wanapokuja mjini kufanya biashara. Tambua kwamba Yesu aliwatuma wanafunzi kufanya uinjilisti mijini (tazama Luka 10:1). Paulo alienda mahali panapo watu wengi kufanya uinjilistii. Tazama Hila ya wamisheni Enenda mahali Mungu anataka uende katika sehemu ya Missiology. 10

UINJILISTI NA UANAFUNZI VIII. Jinsi ya Kufanya Uinjilisti A. Mpango mkuu. Mpango wote wa uinjilisti ni kufanya mafunzo ya uinjilisti, mtegemee Roho Mtakatifu, enenda ukashuhudie, na mwachie Mungu matokeo. 1. Lazima viongozi wafunze watu kufanya Uinjilisti. Wamisheni na wachungaji wanafaa kuwashawishi mkutano wao kufanya uinjilisti. Viongozi huto mfano kwa kwa kufanya uinjilisti. Mtu aliandika, Uinjilisti hushikwa sana kuliko kufunzwa. Kwa maneno mengine, wanafunzi hushikilia uinjilisti kwa kwenda kuinjili na mashahidi wenye uzoefu. Ni vizuri kusoma msingi wa uinjilisti darasani, lakini ujuzi mwingi wa uinjilisti unasomwa kutokana na mazoezi. Shahidi wenye mazoea akiinjili pamoja na mwanafunzi mwenye mazoea kidogo, mwanafunzi hujiusisha kwa kushaidi anapojisikia yuko tayari. Mwanafunzi huyo atasoma zaidi katika kila nyumba atakayotembelea. Mahali pengi uinjilisti wa nyumba kwa nyumba huleta waumini wengi. Mahali pengine aina zengine za uinjilisti hafaa zaidi. Makanisa yenye huduma za nguvu na vipindi vya uanafunzi ndio hukua. Kama kanisa halina watu wa kutosha kusaidia katika kazi ya kanisa na mtumishi, kanisa hilo laweza kuwa dhaifu kwa uinjilisti. Kwa hivyo mchungaji anafaa kuwatembelea washiriki sana. 2. Omba. Kama huduma zingine zote, kazi inaanzwa kwa maombi. Omba kabla ya kwenda, unapofanya uinjilisti, na baada ya kuinjili. Mtume Paulo alisema tujivike silaha zote za Mungu kukumbana na maadui wa kiroho. Sehemu kuu ya hiyo silaha ni maombi. 12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama, bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 18 Kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote. 19 pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya injili, 20 ambayo kwa ajili yake mimi ni mjumbe katika minyororo, hata nipate ujasiri katika hiyo kunena jinsi inipasavyo kunena. (Waefeso 6:12,18-20). Moja wapo ya mahitaji ya uinjilisti ni wafanyikazi walio tayari. Mavuno ni mengi lakini wavunaji ni wachache. Kabla Yesu kuwatuma wanafunzi sabini na mbili wakafanye uinjilisti, aliwaambia wamuulize Bwana wa mavuno awatume wafanyikazi (tazama Luka 10:2). 11

3. Tegemea Nguvu za Roho Mtakatifu. Kama tunamwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na Mkombozi, tumempokea Roho Mtakatifu. Kwa hivyo tunamtegemea Roho kututangulia na kutuandalia nafasi ya kueneza injili. Tunamtegemea Roho Mtakatifu kuonyesha wenye dhambi hatia zao, na kuwaongoza kwa ukweli wa Yesu Kristo (tazama Yohana 16:7-11). Njia moja ya Roho kuwaongoza watu kwa Kristo ni kufanya miujiza kama kuponya. Ninajua kundi la wakristo linalo muhubiri Kristo kwa waislamu. Kulingana na imani ya waislamu Kristo alikuwa nabii. Maandiko ya Waislamu--Koran inafunza Waislamu kusoma Injili zilizo katika Bibilia. Bibilia inafunza kwamba Yesu aliwaponya watu wengi kimiujiza. Kwa hivyo kundi hili la Wakristo linaenda kwa waislamu na kuomba kwa jina la Yesu wagonjwa wao wapone. Wagonjwa wanapopona, baadhi ya Waislamu wanamwamini Kristo. Waislamu wameona nguvu za Kristo zikifanya kazi kupitia kwa Roho Mtakatifu. Yesu alihubiri kwa nguvu. 37 Jambo lile ninyi mmelijua, lililoenea katika Uyahudi wote likianzia Galilaya, baada ya ubatizo aliouhubiri Yohana-- 38 habari za Yesu wa Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na nguvu, naye akazunguka huko na huko, akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na ibilisi, kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye. (Matendo 10:37-38). Mtume Paulo alieneza Injili kwa nguvu za Roho Mtakatifu. 4 Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu, 5 ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu. (1 Wakorintho 2:4, 5). Nimesikia watu wakiponywa kimiujiza kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Lakini sio wote wanaponywa kimwili. Sio kusudi la Mungu watu wote wapone ili waendelee kuishi milele katika dunia hii. Kwa hivyo tunaomba uponyaji kwa jina la Yesu kulingana na mpango wa Mungu. 4. Pelekea Watu Kanisa. Uinjilisti si kuleta watu kwa kanisa. Bali uinjilisti ni kuwapelekea watu kanisa. Uinjilisti unahusisha kupeleka Injili, kupata waumini wapya. Watu wanapoamini, hutaka kukutana na Wakristo wengine wa kanisa. 5. Mwachie Mungu Matokeo. Tunaomba na kufanya uinjilisti kwa nguvu za Roho Mtakatifu. Tunafuatisha uinjilisti na uanafunzi. Kisha tunamwachia Mungu matokeo. Hatuwezi kuokoa waliopotea. Tunaweza kutoa Habari Njema, na kumtegemea Mungu kuwaokoa wenye dhambi. 12

B. Uinjilisti wa Kibinafsi Uinjilisti wa watu wengi hufanyika kwa watu wengi, lakini uinjilisti wa kibinafsi huhusisha kusemezana kuhusu Injili na mtu mmoja ama kundi dogo la watu. Wakristo wanapokuwa kwa kusudi la kufanya uinjilisti wanatakiwa kwenda wawili wawili (tazama Luka 10:1). Wanaume wawili wanaweza kwenda pamoja, au wanawake wawili au bwana na bibi. Kwenda wawili kufanya uinjilisti kwa watu usiowajua kuna usalama zaidi. Kwa kawaida haipendekezwi, mwanamume mmoja na mwanamke mmoja kwenda pamoja kuinjili. Wakristo wanafaa kuepuka kuonekana na utovu wa nidhamu. Zaidi na uinjilisti uliopangwa, uinjilisti wa binafsi unaweza fanyika kila siku, kama Tume Kuu ilivyo katika Mathayo 28:19 inasema, Enendeni mkawafanye wanafunzi. Lakini neno la kigiriki lilifafanua enendeni inamaana tunafaa kutengeneza wanafunzi tunapoenda. Tumuombe Mungu atufungue akili ili tumshuhudie yeyote tutakaye kutana naye. Ili tuweze kufanya uinjiliti tunapofanya kazi za kila siku, tunafaa kujua jinsi ya kuwasiliana mambo ya kiroho. Ifuatayo ni mifano: Kama ni siku nzuri na unaongea na mtu unaweza kusema, Mungu ametupa siku njema ili tufurahie, si ni kweli? Mtu akilalamika kwa ugonjwa wake, unaweza kusema, pole kwa ugonjwa, utapona. Yesu amewaponya wengi. Kama mtu anahofu, unaweza kusema, Wengi wetu huhofia mambo, lakini nimepata njia ya kutoa wasiwasi wangu. Namwambia Yesu atoe wasiwasi wangu, na ananisaidia. Tushiriki pamoja maandiko yanayo fafanua hayo (soma maandiko kama Luka 12:22-31). Kama msikilizaji anaitikia vizuri endelea kumueleza zaidi. Ni vyema kuendelea pole pole unapoeneza Injili. Mwinjilisti huongea na kumruhusu msikilizaji kujibu. Alafu mwinjilisti anaongea tena, kumjibu. Mtu alilinganisha uinjilisti na kulisha vindege mbugani. Kijana mdogo alichukua mkate mzima na kuwatupia vindege, kuwaogofya walipeperuka. Alafu kuna mzee aliuokota mkate ule na kumwambia kijana yule wakae naye kwenye fomu ya mbuga. Mzee alimenyua vipande vidogo vidogo na kuvirusha chini. Kindege kiliruka chini nakuanza kula mkate ule. Mzee alirusha vipande vyengine zaidi na vindege zaidi wakaja wakala. Baada ya dakika chache vindege wengi sana walikuwa wakila. Jinsi hiyo hiyo tunaweza kupeana ukweli wa kiroho kidogo kwa mtu na kuona kama mtu huyo ana haja ya kusikia zaidi. Akronomi FIRE ni kifaa muhimu cha kukumbuka unapoanza mazungumzo na kuendelea na kuinjili. FIRE ina maana. 13

Family (Jamii). Anza kwa kuuliza, je una jamii? Watu wengi hupenda kuongelea juu ya jamii zao sana sana watoto na wajukuu wao. Lakini si vizuri kulazimisha mtu kuongea kuhusu talaka ama mambo mengine ya kijamii kama hataki. Baada ya kuongea kuhusu jamii zao uanweza kuongea kuhusu yako kwa ufupi. Interests.(Upendeleo) Uliza, Unafanya nini wakati wa ziada? Jua nyumba ama mazingira ya mtu huyo. Mtu huyu anaonekana kuwa na jambo alipendalo? Zungumzia kitu kinacho mfurahisha mtu huyo. Religion.(Dini) Uliza, Dini yako ni gani? Ama, Ushafikiria kuhusu mambo ya kiroho? Evangelism.(Uinjilisti) Kama msikilizaji si Mkristo, unaweza kupata nafasi ya jadiliana kuhusu injili. Unaweza fanya uamuzi kutokana na majibu ya msikilizaji. 1. Mlipuko wa Uinjilisti. Kama hauna uhakika kama mtu ni mkristo, unaweza kutaka kuuliza maswali mawili. Dkt. James Kennedy anatoa maswali haya kama baadhi ya njia ya Mlipuko wa Uinjilisti. Mswali ni kama yafuatayo. 1. Unajua kwa uhakika kwamba utaenda kuwa na Mungu mbinguni? Kutategemea jinsi mtu huyo atajibu, utataka kuuliza swali la 2. 2. Kama Mungu atakuuliza, Kwa nini nikuingize Mbinguni Kwangu? Utasema nini? Maswali haya na njia za uinjilisti zinazoambatana zinapatikana kwa kabila tano. Bonyeza katika Unajua? kwa kiunganishi kifuatacho: http://www.eeinternational.org/ Kijitabu ya mlipuko wa uinjilisti kinapatikana kwa mtandao ufuatao: http://www.menorah.org/eetract.html Maswali hayo mawili yanakusaidia kujua kama msikilizaji ni Mkristo anayeelewa Thiologia ya Kikristo. Na wanakupa nafasi ya kueneza injili. 2. Ushuhuda wa kibinafsi. Badala ya kwenda kwa maandiko msikilizaji anapojibu maswali yale ya awali, unaweza kumtolea ushuhuda wako mwenyewe. Kama msikilizaji hana uhakika wa kuwa na Mungu atakapokufa, unaweza sema, naweza kukuelezea vile nilipata uhakika kuwa nitaenda mbinguni nitakapo kufa? Kwa kawaida msikilizaji atakuruhusu umtolee ushuhuda wako. Ushuhuda wako unafaa kufuata mtindo huu. a) Maisha yangu yalikuwaje kabla niwe Mkristo. 14

b) Jinsi nilikuwa Mkristo. c) Vile maisha yangu yamebadilika kutokana na kumwamini Yesu kama Bwana na Mwokozi. d) Vile unaweza kuwa Mkristo. Ili kuwa na mpangilio ninashauri huwe umeandika ushuhuda wako. Andika ushuhuda ambao unaweza kutoa kwa kadika tatu. Pia kuza masimulizi ya ushuda wako unaoweza kutoa kwa dakika tano au sita. Kama una mengi ya kusema unaweza kuza masimulizi ya urefu ya ushuhuda wako. Simulizi la urefu unaweza kulitumia kwa makundi ya watu waliojiandaa kusikiliza. Fanya mazoezi kwa kuwatolea Wakristo wengine ushuhuda wako, na uulize maoni ili kuinua matoleo yako. Katika uinjilisti, ni muhimu kupeana ujumbe muhimu, epuka kumsinya msikilizaji kwa ujumbe usiofaa. Ushuhuda ulioandika ni wako wa kutumia, kwa sababu utatoa ushuhuda wako kwa kuongea. Wakati mwingine ni vizuri kuandika ushuhuda wako ili iweze kuwapa wale ambao wanaoongea lugha tofauti. Unaweza kutafsiri katika lugha zao mapema. Mwisho wa ushuhuda wako, unaweza kumuuliza msikilizaji kama angependa kupata uhakika wa uzima wa milele na Mungu. Akisema, Ndio, unaweza kumwongoza katika maandiko ya mpango wa wokovu. Kuna maandiko mengi yanaweza kutumika. Kijitabu cha mlipuko wa uinjilisti kinapatikana hapo juu. 3. Sheria nne za Kiroho. Kijitabu kingine ni Sheria nne za Kiroho, kinapatikana kwa mtandao katika kabila nyingi. http://www.greatcom.org/laws/languages.html Bonyeza kwa kabila unayoielewa ili uone kijitabu cha Sheria Nne za Kiroho. Pia bonyeza kwa zaidi ili utazame filamu ya Yesu. Filamu hii inatoa hadithi ya Yesu kwa kabila zaidi ya 800. Unaweza taka kupata nakala ya filamu ya Yesu kabla ya kwena katika umisheni. Muhtasari wa amri nne za kiroho ni ufuatao. 1. Mungu anakupenda na anampango mzuri kwa maisha yako. (tazama Yohana 3:16; Yohana 10:10). 2. Binadamu ni mwenye dhambi na ametenganishwa na Mungu. Kwa hivyo hawezi kujua na kuutambua upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yake. (tazama Warumi 3:23; 6:23 ). 3. Yesu Kristo ndiye toleo la pekee la Mungu kwa dhambi ya mwanadamu. Kupitia kwake unaweza kujua na kutambua upendo na mpango wa Mungu kwa maisha yako. (tazama Warumi 5:8; 1 Wakorintho 15:3-6; Yohana 14:6 ). 15

4. Lazima tumkubali Yesu Kristo kama Mwokozi na Bwana; alafu tutajua na kutambua upendo na mpango wa Mungu maishani mwetu. (tazama Yohana 1:12; Waefeso 2:8,9; Yohana 3:1-8; Ufunuo 3:20 ). Kijitabu cha Sheria Nne za Kiroho kinafafanua kuwa kumkubali Yesu inamaanisha kumkubali ayakabidhi maisha yako kumkubali Yesu aketi kwenye kiti cha enzi na kuyachunga maisha yako, mbali na mtu kijikabidhi maisha yake. Kama msikilizaji yuko tayari, mwinjilisti atamuongoza kwa maombi ya kumpokea Kristo. Maombi yaliyopendekezwa kutoka kwa kijitabu cha Sheria Nne za Kiroho ni: "Bwana Yesu, Nakuhitaji. Asante kwa kukufa msalabani kwa ajili ya dhamdi zangu. Ninafungua mlango wa maisha yangu na kukupokea wewe kama Mwokozi na Bwana. Asante kwa kunisameha dhambi na kunipa uzima wa milele. Chukua madaraka ya kiti cha enzi cha maisha yangu. Nifanye mtu mwenye unataka niwe." Amri nne za kiroho zinaonyesha misingi ilivyoonyeshwa katika vijitabu tofauti vikionyesha mpango wa wokovu. 4. Barabara ya Warumi kwa Wokovu. Njia nyengine ya kuonyesha mpango wa wokovu ni barabara ya Warumi. Kijitabu hiki kina kabila nyingi tofauti katika mtandao ufuatao. http://www.gotquestions.org/romans-road-salvation.html Muhtasari wa Barabara ya Warumi kwa wokovu ukitumia maandiko kutoka kwa Biblia Takatifu. Warumi 3:23. Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu. Warumi 6:23. Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. Warumi 5:8. Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Warumi 10:9,10,13. 9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. 10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.... 13kwa kuwa, Kila atakayeliita Jina la Bwana ataokoka." Njia rahisi ya kukumbuka mistari ya Barabara ya Warumi iliopo ni kukariri kumbukumbu ya kwanza: Warumi 3:23. Fanya mlango wa 3 maradufu na unapata Warumi 6:23. Kariri kumbukumbu: Warumi 5:8. Fanya maradufu malango huo na unapata Warumi 10. Hii inakukumbusha kukumbuka Warumi 10:9,10,13. Jua 16

kumbukumbu za maandiko haya manne na unaweza kutumia kumuongoza mtu kwa wokovu. Baada ya kuzungumzia Warumi 10:13 na msikilizaji, muulize kama angependa kuomba nawe ili aupate uzima wa milele na Kristo. Akikubali, Unaweza kuamua arudie maombi yako mstari baada ya mwengine. Sema maombi kwa kufanya sentensi fupi na rahisi. Barabara ya Warumi inahusisha maandiko fulani yanayoonyesha matokeo ya wokovu Ukiwa na amani na Mungu na usalama wa muamini (tazama Warumi 5:1; 8:1, 38, 39). 5. Kuzaliwa Kupya Yohana 3. Njia ninayopenda kutumia kuwaongoza watu kwa Kristo ni kutumia maandiko ya Yohana 3. Mlango huu unatueleza, kuwa ili mtu aweze kuingia mbinguni ni lazima azaliwe tena. Jambo la kwanza ni kupata kumjua mtu, na kwa kutumia njia ya akronimi FIRE. Naweza kutolea ushuhuda wangu. Nieleze kwamba nimepata uhakika kuwa nikifa nitaenda kuwa na Mungu. Ndipo naweza kuuliza, Ungependa kupata uhakika wa maisha ya milele leo? Mtu akikubali nitafungua Bibilia yangu katika kitabu cha Yohana 3. Ninaeleza, Yohana 3 inasema, kiongozi wa dini aitwae Nicodemus alimwendea Yesu na kusema kwamba kwa sababu ya miujiza Yesu aliyotenda, lazima iwe Mungu yuko naye. Yesu akamjibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu (Yohana 3:3). Baadaye nifafanue mazungumzo kati ya Yesu na Nicodemus. Inawezekanaje? Nicodemus aliuliza. mtu hawezi kuzaliwa mara ya pili kimwili. Yesu akajibu, Ili kupokea uzima wa milele, lazima uzaliwe kiroho. Angazia haya: unajua upepo ni wa kweli, kwa sababu unauhisi. Unaona majani ya mti yakipepea kunapokuwa na upepo. Lakini haujui unatoka na unaenda wapi. Kwa njia hiyo hiyo, unapopoke Roho Mtakatifu wa Mungu, unajua ni wa kweli. (Utatambua mwongozo wake. Roho atakufunza ukweli wa kiroho, akifungua akili yako kwa ukweli unaofunzwa katika Bibilia.) Alafu nisome vifungu vifuatavyo. 16 "Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe pekee, [a] ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. 17Maana Mungu hakumtuma mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. 18Amwaminiye yeye hahukumiwi, asiyeamini 17

amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la mwana pekee wa Mungu. [b] a. John 3:16 Au mwanawe pekee b. John 3:18 Au mwana pekee wa Mungu Maandiko yanafunza kwamba hapo mwanzo, mwanamume na mwanamke wa kwanza walikuwa na ushirika na Mungu. Bwana akaeleza kuwa wasipomtii, watapoteza ushirika ule na kufa. Mwanamume na mwanamke wa kwanza hawakutii wakafanya dhambi basi wakafa. Tangu wakati huo, kila mwandamu ameridhi tabia ya kutomtii Mungu. zote tunafanya dhambi na tunakufa kimwili. Hatuna chochote cha kumtolea Mungu kwa ajili ya dhambi zetu, ila maisha yetu. Lakini Mungu anatupenda sana hata akamtoa mwanawe wa pekee afe kwa ajili yetu. Yesu hakuwa na dhambi, alitoa maisha yake yasio na dhambi kwa ajili ya dhambi zetu. Yesu alisulubiwa msalabani miaka 2,000 iliyopita. Siku ya tatu, alifufuka. Yuko na Mungu sasa, Babake. Ukimuamini Yesu, utaupata uzima wa milele leo, ili utakapokufa roho yako itaenda kuwa na Mungu. Ungependa kupata uzima wa milele sasa hivi? Msikilizaji akikubali, nitasema, Ninaenda kuomba, na ninakuuliza urudie kila sentesi nyuma yangu. Mungu Baba, nimetenda dhambi. Nisamehe dhambi zangu. Ninaamini Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi zangu. Ninaamini alifufuliwa kutoka kaburini. Nipe uzima wa milele leo. Nimemkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi wangu. Kwa jina la Yesu nimeomba. Amina. Biblia inafundisha kuwa ili tuokoke, tunafaa kuwa tayari kumkiri Kristo mbele ya watu (tazama Mathayo 10:32, 33). Ningependa Muumini mpya kudhibitisha kuwa anamuamini Kristo. Niniweza kumuuliza hili, Kama unaamini maneno uliyoyasema, nisalimie. Alafu muumini huyo ananisalimia, kuonyesha anamuamini Kristo. Hii ni ishara kukiri kwa imani kwa kila mtu kati yetu kuwa anamaanisha aliyochosema. Na hii itakuwa kumbusho kubwa kwa muumini huu mpya. Baadaye nitamwelezea muumini huu mambo kadhaa. Tunapookoka, tunakuwa watoto kwa kiroho. Mungu anataka tukue kwa imani. Tunapoendelea kukua, tunajifunza ukweli wa kiroho na kutambua furaha ya kumjua Mungu. Kuna mambo matano tunafaa kufanya ili tuweze kukua katika imani. a. Mpende Mungu na jirani yako kama unavyojipenda. Hizi ni amri mbili kuu za Mungu. b. Soma Biblia. Anza kwa kusoma Injili ya Yohana. (Nimuonyeshe muumini huyu mpya mpya mahali Injili ya Yohana inapatikana katika Biblia. Kama muumini huyu mpyahana Biblia, nitafute namna ya yeye kusoma kwa kumpa maandiko fulani kama vile kumwalika kanisani. Kama muumini huyu mpya hasomi, nilielezee kanisa ili lifunze maandiko hayo.) 18

c. Omba kila siku kwa jina la Yesu. d. Kutaneni kila wiki pamoja na Wakristo wengine wanao funza Biblia. e. Ambia wengine kuhusu wokovu ndani ya Yesu. (Hizi ni njia tano za kukua katika imani kama ilivyo kwenye sinema ya evangecube hapo chini.) Nitajaribu kufuatilia Mkristo huyo ama nihakikishe mtu kutoka kwa kanisa anamfuatilia. Ni vizuri kama mtu atamtembelea baada ya siku, ama baada ya wiki. Kama ilivyo elezwa awali, hatuwaachi watoto wa kiroho peke yao, na hatutaki kuwaacha peke yao. Mkristo mpya ana mengi ya kufikiria. Anaweza kuwa na maswali kutokana na maandiko aliyosomewa. Pengine maandiko muhimu yaliachwa nje wakati wa mazungumzo. Anahitaji kukumbushwa maandiko yanayomhakikishia wokovu. Anapokendelea kukua atatambua Roho Mtakatifu akimuongoza na kumpa uhakika. Pia anahitaji msaada kutoka kwa wakristo wengine. Pia anahitaji kutiwa moyo wa kukutana na wakristo wengine kwa ibada na masomo ya Biblia. Kama hawezi kuja kanisani, mtu kutoka kanisani anafaa awe akukutana naye mara kwa mara kwa ajili ya uanafunzi. 6. Kifaa cha Unjilisti (Evangecube). Njia ya uinjilisti ukitumia kifaa kiitwacho evangecube imeoneshwa katika mtandao ufuatao. Ninasisitiza utazame sinema hii kwa kwenda kwa mstari uliopo na kubonyeza anza hapa. http://www.letusteachkids.com/magic/evangecube.htm Evangecube ni kifaa muhimu cha kushiriki Injili katika tamaduni na kabila zengine. Inaonyesha njia ya wokovu kwa kutumia picha. Inashikilia mawazo ya watu sana sana ya watoto. Ni kifaa muhimu cha kumwongozo Mwinjiliti katika kazi yake. 7. Ujumbe zaidi wa Uinjilisti wa Kibinafsi. Mtandao ufuatao unatoa vifaa vya kufundishia uinjilisti wa kibinafsi, na video za ushahidi Amerika. 8. Kipingamizi kwa Injili. http://www.mercystreet.com/university/index.html Unapokuwa ukitoa mpango wa wokovu, wasikilisazi waweza kutoa pingamizi kadhaa. Wakati mwingine msikilizaji huwa anataka kupata ukweli, na atataka jibu. Wakati mwingine anataka kuchepua mazungumzo kwa sababu hana haja na kumjua Yesu. Wasikilizaji mara nyingine, hutaka kutuchepua kutoka kwa mpango wa wokovu kwa sababu hawataki kukubali ni wenye dhambi na kubadili maisha yao. Tunafaa kuwa na uwezo wa kukabiliana na vipingamizi, na kurudi kueneza Injili. Kuwa na elimu nzuri ya 19

Maandiko na sehemu za kupata Maandiko hayo katika Biblia ndiyo njia ya kujibu vipingamizi. Ni muhimu kukariri Maandiko muhimu. Alafu omba ili Roho Mtakatifu akuongoze kujibu maswali ya watu. Ongea ukweli kwa upendo (tazama Waefeso 4:15). Alex Strauch anatufunza kuwapenda wale tunaowashahidia. Tazama dondoo kutoka mtandao ufuatao. http://www.bible.org/page.php?page_id=2765 Mwinjilisti Bob Smith anasema, Asili mia tisaini ya uinjilisti hufanyika kupitia kwa upendo. Uinjilisti unahusisha kuwapenda watu, kutaka kuwafikia, kuwa rafiki na wazi nao, na kuwatumikia. Hatufai kushindana tunaposhuhudia kutoa ishara ya kwamba tuna majibu yote. Tusiwe wa kuchukiza na wenye maringo, tukiwawala kila mazungumzo. Tujifunze kutulia kuwapa watu Injili na kumwachia Roho Mtakatifu afungulie nguvu zake. Kama Roho Mtakatifu hatafanya kazi kwa roho ya mtu, kubishana kwetu hakutasaidia. Jibu maswali vyema kulingana na uwezo wako, na kama hauna jibu mwambie unayezungumza naye utatafuta jibu hilo. 1 Paulo anasema, Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu (Wakolosai. 4:6). Unapojua unafaa kuwa na neema na kukolea munyu, basi hauhofii na kufikiria, Nafaa kuwahimiza mbinguni, niwaonyeshe niko sawa. Nafaa kuwaonyesha mimi ni mwenye imani kamili na sio mmoja wa madhehebu. Ni jambo la kushangaza kutaka kuwa wa neema na mshindi. Haufai kutilia maanani wakati asiyeamini anajibizana na kukuita majina. Unaweza kujibu kwa upole, Ninakuelewa, lakini nataka ujue dhambi zangu zimesamehewa. Nina tumaini jipya kwa sababu ninajua maisha ya Mungu mapya yamo ndani yangu. 2 Na msimamo huo wa upendo, wacha tutazame jinsi ya kujibu vipingamizi. a. Kazi Nzuri. Watu wengi hutaka kufanya kazi nzuri ili wampendeze Mungu. Kila dini ya duniani isipokuwa ya Kikristo huhimiza kazi nzuri ili uweze kuingia mbinguni ama kufikia kiwango cha juu cha kiroho. Ukristo ni ya kipekee. Ukristo unasema ya kwamba Kristo ameshafanya kazi hiyo nzuri. Kristo alikufa kutuokoa kwa mauti ya dhambi. Ili tuweze tuokolewe, tunafaa kumwamini Yesu. Tukiwa na imani hii ya Kibibilia, tunatubu dhambi zetu (kuachana na dhambi zetu) na kufuata mafunzo ya Yesu. Tumeokolewa kwa neema ya Mungu kupitia kwa imani ili tufanye kazi nzuri. 8 Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; 9wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. 10Maana tu kazi yake, tuliumbwa katika 20

Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo. (Waefeso 2:8-10 ) Mtu akifikiria kwamba kazi zake nzuri zitampeleka mbinguni, Ninasema, Mungu ni mkamilifu na anatarajia kila atakaye ingia Ufalme wake asiwe na dhambi. Lakini sote tu wenye dhambi. Hakuna aliye mkamilifu. Kujaribu kuwa mkamilifu ni kama kujaribu kuogelea ili kuvuka bahari. Wakati mmoja sote hukosea. Ni Kristo peke yake aliyeishi maisha kamilifu yasiyo na dhambi. Kwa kumuamini Kristo, tumeokoka. Na tunapompenda Kristo, tunataka kufanya kazi nzuri. Ukriso ni zaidi ya uhusiano kuliko dini. Dini hutoa sheria za kufuata ili uwe mtakatifu. Ukristo ni kuhusu uhusiano wa imani na Mungu kupitia kwa Mwanawe. Kristo ndiye Mwana wa pekee wa Mungu. Yeye huwa bora zaidi kwetu. Lakini waaminifu ni panga watoto wa Mungu (tazama Yohana 1:12; Warumi 8:14-16). Kristo ni ndugu yetu mkubwa, na sisi tu wana wa kuunganishwa wa uzima wa milele na Kristo (tazama Warumi 8:17). Tu wana wa Mungu kupitia kwa imani, kwa hivyo kazi nzuri hazitufanyi tuwe zaidi ya watoto ama kidogo ya mtoto. Ninaieleza hivi, Mtoto amezaliwa na baba. Kama huyo mtoto hafanyi matendo mema, mtoto huyo hukoma kuwa wake? Mtoto huyo bado ni wake. Mtoto akifanya matendo mema, mtoto huyo huwa wake kwa njia zaidi? Hapana, mtoto ni wake bila kutazama matendo mema. Lakini kama mtoto anapenda babaye, mtoto hutaka kufanya matendo ya kumfurahisha babaye. Ukristo uhusiano kati ya Mungu na wanawe. Mtu anapomuamini Kristo, mtu huyo hupangwa katika jamii ya Mungu. Kupangwa huku ni zaidi ya kupangwa kwa kisheria. Kupanga kwa mtoto kwa jamii ya Mungu, mtoto huzaliwa upya amezaliwa upya kiroho. Hata kama hatuwezi kulipia wokovu, lazima tuungame dhambi zetu. Tunaungama kwa kuacha maisha yetu ya dhambi. Tunapokuwa katika mwili, tutafanya dhambi, lakini tutakomaa ili tufanye dhambi kwa nadra. Maneno matatu yanayofanya muhtasari wa kurudi kwa Yesu ni kuungama, kuamini, na kukiri. Tunatubu dhambi, kuamini kwa kujitolea kwa Yesu, na kukiri Yesu ni Bwana. b. Njia Zingine za Wokovu. Mtu anaweza kuamini kwa wingi akisema kuna dini nyingi na njia nyingini za wokovu. Ninaeleza kuwa Yesu alisema yeye ndiye njia ya pekee ya wokovu. Yesu akamwambia, Mimimndimi njia, na kweli, na uzima: mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi (Yohana 14:6). Nieleze kwamba Yesu alikuwa Mungu kwa mwili (tazama Yohana 5:18; 10:30; Wakolosai. 1:15-20; 2:9). Hakuna dini nyingine inayosema inamwanzilishi anayesema ni Mungu. Kama Mungu ni ambaye anasema kuwa, ni Bwana na ukristo ni njia moja ya wokovu. Kama Kristo sio yeye anayesema kuwa, ni muongo ama mwenda wazimu na ukristo sio njia ya wokovu. Lakini hakuna kiwanja cha katikati; Ukristo na dini zengine za dunia hazikubaliani kwa hivyo haziwezi kuelekeza kwa wokovu. Mwandishi wa Kikristo, C. S. Lewis, alitoa malalamishi kwa Yesu ni Bwana, muongo ama wazimu. 21

C. Uinjilisti wa uhusiano Uinjilisti wa uhusiano ni kushiriki Injili na watu munaohusiana nao. Mara nyingi watu huja kwa Kristo kupitia kwa marafiki au jamii. Huko Amerika, habari ya historia inapendekeza kwamba zaidi ya asili mia sabini na tano ya watu wanaokuja kwa Kristo hushawishwa na marafiki na jamii. 3 Bibilia inapeana mifano ya uinjilisti wa uhusiano. Yohana mbatizaji aliwatambulisha wanafunzi wake wawili kwa Yesu, na kila mmoja wao akamjulisha ndunguye ama rafikiye kwa Yesu (tazama Yohana 1:35-51). Kiongozi wa ukristo Uturuki, nchi iliyojawa na Waislamu, anaelezea umuhimu wa uinjilisti wa uhusiano katika tamaduni ile. Tazama mtandao ufuatao. http://www.foursquarechurch.org/articles/141,1.html Kwa sababu ya shinikizo ya ushirikiano iliyoko ya waislamu kuwakataa wakristo, Mwislamu atahitaji kuwa na uhusiano wa kuaminika na Mkristo kabla ya kuikubali Injili. Tazama mtandao ufuatao kwa mafunzo ya uinjilisti wa uhusiano. http://ourworld.compuserve.com/homepages/dcarlton121/index.htm Mtandao ufuatao unatoa ushauri wa kutengeneza orodha ya wale wasio wakristo unaowajua, kwa kuwa na uhusiano na watu kama hao na kuwakaribisha kuja kwa wokovu kwa Kristo. http://www.kristenonline.com/download/book/relationship%20evangelism.pdf Tunaweza kutumia akili yetu ya uinjilisti wa uhusiano kuwashuhudia marafiki na jamii. Tunafaa kuombea zamu za kushuhudia. Kwa sababu tuna uhusiano na marafiki na jamii tayari, tunaweza kushiriki ushuhuda na mipango ya wokovu wakati unaofaa. Ama tunaweza kwenda kwa maombi pamoja na rafiki. Kazi ya utangulizi ya kuwa na uhusiano imeshafanyika. D. Mahubiri ya Uinjilisti. Kuhubiri ni njia bora ya kupata waumini wapya. Siku ile kanisa la kwanza lilianza, Petro alihubiri na watu 3,000 wakawa wakristo (Matendo 2:41). Karne zilizo pita, wahubiri wamewaleta watu wengi kwa ukristo. Katika karne ya ishirini, Mwinjilisti Billy Graham aliwaongoza wengi kumpokea Yesu ulimwengu wote. Katika 22

makanisani yaliyoko duniani kote, siku hizi wachungaji huhubiri na kuwabatiza mamilioni. Ili kupata waumini wapya kupitia kwa mahubiri, mahubiri yanafaa kuwa ya kiinjilisti. Wachungaji hawahubiri mahubiri ya kiinjilisti saa zote. Uinjilisti ni kwa wale wasio na imani kwa Kristo. Wachungaji wanaweza kuchagua wakati wa kuhubiri mahubiri ya uinjilisti ama ya uanafunzi. Mahubiri ya uinjilisti yamekusudiwa kuwaleta watu kwa uamuzi wa kumpokea Kristo kama Bwana na Mwokozi. Kwa hivyo kifungu cha Biblia kinachochaguliwa chatakiwa kuwa kinafaa kwa uinjilisti. Vifungu vingi kutoka vitabu vya Injili na Matendo, kwa mfano vyaweza kuhimiza watu kuja kwa Kristo. Mahubiri ya kiinjilisti yanafaa kushugulikia mahitaji ya washiriki. Mara nyingi, Mwinjilisti Billy Graham, alidhihirisha matatizo ya dunia yaliyoripotiwa kwa vichwa vya magazeti, na akatoa habari njema ya kwamba Yesu anaweza kutatua shida hizo. Yesu anaweza kushinda upweke, uhalifu, uhusiano uliovunjika, pasipo tumaini, na shida zingine. Mahubiri ya uinjilisti hufungwa kwa maombi ya kuwakaribisha watu kumpokea Yesu kama Bwana na Mwokozi. Uamuzi unafaa ufanywe papo hapo. Maandiko yanafunza kuwa leo ndio siku ya wokovu (tazama 2 Wakorintho 6:2). Udanganyifu mmoja wa Shetani ni kuwafanya watu wafikirie kwamba hakuna haraka ya kuwa Mkristo. Watu wengi wanaweza kupuuza maamzi ya kumpokea Kristo na mioyo yao iwe baridi wanapoendelea kuzeeka. Leo yaweza kuwa siku ya mwisho ambayo watu wengine wanayo ya kumpokea Kristo. Wanapokataa mwaliko, wanaweza wasiwe na nafasi kama hiyo tena. Wanaweza kufa. Wanaweza wasikubali uinjilisti kwa siku zijazo. Mhubiri anafaa kuwaonya watu kufikiria ufupi wa wakati. E. Uinjilisti wa Watu Wengi. Mbali na uinjilisti wa kibinafsi, uinjilisti wa watu wengi hutegea watu wengi kwa mikutano ya pahali wazi. Uinjilisti wa namna hii hufana kama matayarisho yamefanywa vizuri. Kunaweza hitajika pesa za kupata mahali pa mikutano na kutangaza. Mtandao ufuatao una sehemu za uinjilisti za watu wengi. Bonyeza kwenye Kituo cha kupokea mafundisho chagua mafundisho ya Uinjilisti. http://www.amesbible.org/virtualcampus.html Kuhubiri Barabarani Kuhubiri mahali wazi hapahitaji malipo wala matayarisho. Mbinu hii ya kuhubiri hufana sana mahali pengine. 23

F. Uinjilisti Uliojaa Watu. Uinjilisti uliojaa watu unatafuta kueneza Injili kwa kila mtu katika sehemu hiyo au nchini. Mtandao ufuatao unapendekeza vifaa tofauti vya uinjilisti uliojaa watu. http://www.ad2000.org/gcowe95/satevang.html Vifaa vilivyopendekezwa kwa uinjilisti ulojaa kabisa katika mtandao wa hapo juu ni: Kueneza kwa Redio and Televisheni. Kusambaza fasihi ya Kibibilia na Kikristo. Wainjilisti wa kuzungukazunguka, Wanenaji maalum, na uinjilisti wa kundi. Kampeni za pamoja za uinjilisti wa kibinafsi Uinjilisti wa filamu ukitumia filamu ya Yesu Kuwepo kwa Mafunzo ya Viongozi. Uinjilisti wa watu wengi unafuata amri ya kuhubiria viumbe vyote (tazama Marko 16:15). Na inafuata kanuni ya kupanda kwa wingi ili uvune kwa wingi (tazama 2 Wakorintho 9:6). G. Uinjilisti wa Kusudi. Njia zozote za uinjilisti zinazo tumika, lazima ziwe za kusudi hivyo ni, lazima tukuze mipango ya kufanya uinjilisti. Kama uinjilisti wa kibinafsi unafanyiwa mazoezi, basi inaweza kuhusisha mtindo wa kila siku wa kutafuta nafasi ya kushiriki habari za Yesu. Hivyo basi kanisa linapaswa kutenga wakati wa kuenenda na kushiriki kuhusu Yesu. Uinjilisti wa undugu unahusisha kuwafikiria watu wasiomjua Kristo, na kupanga njia za kushiriki nao kuhusu Kristo. Uinjilisti wa watu wengi unahitaji mipango malum. H. Kushinda Vizuizi 1. Uoga. 24 Moja wapo ya vizuizi vya uinjilisti ni uoga. Watu wanaogopa kufanya uinjilisti kwa sababu hawataki kukataliwa. Hawataki kuonekana wajinga. Ama katika nchi zengine, wanaogopa kushutumiwa na wenye mamlaka ama tamaduni zilizo karibu nao.

Maandiko yanawafunza Wakristo watarajie kukataliwa (tazama Yohana 15:20; Mathayo 24:9). Linalo onekana kama ujinga kwa mwanadamu wa kawaida ni hekima kwa Mungu (tazama 1 Wakorintho. 2:14). Kwa hivyo tunafaa kutii tume kuu. Tunapotii, tunapata uhuru wa kufanya uinjilisti. Akiwa jela, Mtume Paulo aliuliza kanisa la Efeso limuombee ili aweze kutangaza Injili bila uoga (tazama Waefeso 6:19, 20). Tunafaa tuombe, ili kila mmoja wetu awe na uhuru wa kushiriki ujumbe wa yesu Kristo bila woga. 2. Vipaumbele Vingine. Usipoupa uinjilisti kipaumbele, mambo mengine yatachukua wakati wetu. Makanisa yana mwelekeo wa kutazamia mahitaji yao wenyewe na kukuwa mahala pa mazungumzo. Washiriki wa kanisa wana mahitaji mengi, na wanaweza kusahau kwa haraka kwamba kuna ulimwengu unakufa karibu nao. Kanisa la pale likisahau ulimwengu unaokufa, kanisa la pale litakufaa. 1Alex Strauch: http://www.bible.org/page.php?page_id=2765 2Alex Strauch: http://www.bible.org/page.php?page_id=2765 3ChurchGrowth: http://www.cmfhq.org/training/relational%20evangelism/ relational_evangelism.htm 25

UINJILISTI NA UANAFUNZI IX. Uanafunzi Mwanafunzi ni msomi ama mwanafunzi 4 Tume Kuu inatufunza jinsi ya kuwafanya watu kuwa wanafunzi. Katika Theologia ya Kikristo, hatua ya kuwafanya wanafunzi inaaitwa uanafunzi. Maandiko yanafunza wanafunzi kukomaa. Mtume Paulo aliaandika kwamba watu kanisani wanafaa kufanya kazi pamoja kuleta wanafunzi kwa ukomavu. Wanafunzi wanakomaa kwa kuwa kama Kristo. 11 Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa wanabii, na wengine kuwa wainjilisti, na wengine kuwa wachungaji na waalimu, 12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe, 13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo. 14 Ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu. 15 Lakini tuishike kweli na katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo. 16 Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo. (Waefeso 4:11-16) Ni kazi ya kanisa lote kuwafanya watu kuwa wanafunzi. Wengine kanisani hutilia mkazo uinjilisti, wengine kufunza, wengine kazi zingine. Kwa kufanya kazi pamoja, washiriki wanaleta wanafunzi kwa ukomavu. Na makanisa na vyama vya umisheni vinaanzisha makanisa mapya, wakiwafanya watu zaidi kuwa wanafunzi. A. Jinsi ya Uanafunzi. 26