JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Similar documents
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

HOTUBA YA WAZIRI WA AFYA MHESHIMIWA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Maoni ya Wananchi juu ya Huduma za VVU na UKIMWI Nchini Tanzania

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

ORDER NO BACKGROUND

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MHESHIMIWA MHANDISI DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA WIZARA YA KILIMO KWA

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

DIRA DHIMA. Kuendeleza, kuwezesha, kudhibiti na kusimamia matumizi endelevu ya Rasilimali za Nishati na Madini kwa manufaa ya Watanzania.

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

Deputy Minister for Finance

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI

HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT

HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

Kutetea Haki za Binadamu

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

Draft 03 MWENGE KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO MWENGE

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

Human Rights Are Universal And Yet...

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI

UTANGULIZI. 1. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako. 2. Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie fursa hii kuungana na

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

Makala ya Mshiriki wa Mafunzo

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

Govt increases vetting threshold of contracts

Transcription:

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA TANZANIA BARA 2004 Imetayarishwa na: Idara ya Tiba Afya Makao Makuu P.O. Box 9083, DAR ES SALAAM June 2005

Yaliyomo Ukurasa Vifupisho 4 Utanguli 5 1.1 Ripotiya Huduma za Aya Makao Makuu 2004/2005 6 1.2 Dira/Mwelekeo (Vision ya Wizara) 6 1.3 Majukumu ya Wizara ya Afya 6 1.4 Azma (Mission) ya Wizara ya Afya 6 1.5 Malengo ya Wizara ya Afya 6 1.6 Maeneo yaliyopewa Kipaumbele 2004/2005 7 1.7 Muhtasari wa kazi zilizopangwa kutekelezwa na Wizara ya Afya 2004/2005 8 2.0 Utekelezaji wa Majukumu Afya Makao Makuu 2004/2005 9 2.1 Mipango ya Maendeleo 9 2.2 Sera na Mipango 10 2.2.1 Mabadiliko katika Sekta ya Afya 10 2.2.2 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya 11 2..2.3 Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya 13 2.3. Huduma za Kinga 14 2.3.1 Udhibiti wa wa Magonjwa ya Kuambukiza 14 2.3.2 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria 15 2.3.3 Mpango wa Taifa wa Kifua Kikuu na Ukoma 16 2.3.4 Mpango wa Taifa wa Kuzuia Upofu na Kudhibti Ugonjwa wa Usubi 18 2.3.5 Huduma ya Elimu ya Afya kwa Umma 19 2.3.6 Huduma ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto 19 2.3.7 Mkakati wa Kutibu Magonjwa ya Watoto kwa Uwiano 20 2.3.8 Mpango wa Taifa wa Chanjo 21 2.3.9 Huduma ya Afya Shuleni 21 2.3.10 Afya ya Mazingira 21 2.3.11 Huduma za Afya Mipakani 22 2.3.12 Afya katika Sehemu za Kazi 23 2.3.13 Huduma za Afya Wilayani (District Health Services) 23 2.3.14 UKIMWI 24 2.3.15 Mradi wa Uimarishaji wa Huduma Muhimu za Afya 25 2.4 Huduma za Tiba 26 2.4.1 Huduma za Uchunguzi wa Magonjwa 26 2.4.2 Huduma za Tiba Asili 27 2.4.3 Hudma za Afya ya Kinywa 28 2.4.4 Huduma za Afya ya Akili na Vita Dhidi ya Dawa za Kulevya 28 2.4.5 Huduma za hospitali za Mshirika ya Kujitolea na Watu Binafsi 29 2.4.6 Huduma ya Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba 29 2.4.7 Huduma za Kuzuia Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto 30 2.4.8 Huduma ya Matibabu ya Nje ya Nchi 30 2.5 Hudma ya Utawala na Utawala na Utumishi 31 2.5.1 Idara ya Utawala 31 2.6 Huduma ya Mafunzo ya Watumishi 32 2.7 Ofisi ya Mganga Mkuu Kiongozi 34 2.7.1 Huduma za Dharura na Maafa 34 2.7.2 Ukaguzi wa Huduma za Afya 35 2.7.3 Huduma za Uuguzi na Ukunga 35 2.8 Uhasibu na Fedha 36 2.8.1 Ukusanyaji wa Mapato 36 2.8.2 Matumizi ya Fedha za kawaida 37 2.8.3 Matumizi ya Fedha za Miradi ya Maendeleo 37 3.0 Taasisi na Mamlaka zilizo chini ya Wizara ya Afya 39 3.1 Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) 39 3.2 Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali 40 3.3 Mamlaka ya Chakula na Dawa 42 3.4 Taasisi yataifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu 43 3.5 Matatizo na changamoto 45 3.6 Maeneo yaliyopewa kipaumbele mwaka 2005/2006 46 4.0 Ripoti ya huduma za Afya Mikoa 48 4.1 Utangulizi 48 4.2 Mchanganuo wa Watu katika 48 4.3 Mchanganuo wa hali ya Vifo vya Watoto na Mama wajawazito katika Mikoa 48 4.4 Mchanganuo wa Maeneo ya kiutawala katika Mikoa 50 4.5a Uwiano wa Wataalam wa Afya na Idadi ya Watu 50 4.5b Uwiano wa Wataalam wa Afya ya Kinywa (Dental) na Idadi ya Watu 53 4.6 Idadi ya Vituo vya kutolea Tiba na Umiliki wake 53 4.7 Idadi ya vitanda vya kulaza wagonjwa kwa kufuata miliki ya Vituo vya kutolea tiba 56 2

4.8 Watumishi wa Sekta ya Afya na Sehemu za Kazi 58 4.9a Magari na Pikipiki 58 4.9b Hadubini 59 4.9c Mashine za X-ray 59 4.9d Vifaa vya Utakasaji 60 4.9e Vifaa vya Tiba ya Meno 60 4.10 Magonjwa yanayotolewa Taarifa 61 4.11 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa wa Nje 64 4.12 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa Waliolazwa 66 4.13 Taarifa ya Huduma Maalum 68 4.14 Aina za X-ray zilizopigwa 69 4.15 Huduma za Maabara 69 4.16 Matokeo ya Vipimo vya Maabara 70 4.17 Huduma za kliniki ya Meno 70 4.18 Mahudhurio ya kliniki kwa Mama Wajawazito 71 4.19 Mama wajawazito kujifungua 71 4.20 Huduma kwa Mama waliojifungua 72 4.21 Matatizo ya akinamama wakati wa kujifungua 72 4.22 Sababu za Vifo vya Mama wajawazito 73 4.23a Taarifa ya watoto waliozaliwa mmojammoja 74 4.23b Taarifa ya Watoto waliozaliwa zaidi ya mmoja 74 4.24 Idadi ya watoto chini ya mwaka mmoja waliopata chanjo 75 4.25 Chanjo ya TT2+ kwa akinamama wajawazito 77 4.26 Wateja wa uzazi wa mpango wanaoendelea na Huduma 77 4.27 Watoto waliopata matone ya Vitamin A 78 4.28 Kiwango cha Watoto wenye Utapiamlo Mkali 80 4.29 Kiwango cha Kaya zenye vyoo vinavyokubalika na maji toka vyanzo salama 80 4.30 Mapato na vyanzo vyake 81 4.31 Fedha zilizotumika 82 5.0 Ripoti ya Hospitali za Rufaa 84 5.1 Utangulizi 84 5.2 Ripoti ya huduma zilizotolewa 88 5.2.1 Mahudhurio ya Nje 88 5.2.2 Wagonjwa waliolazwa 89 5.2.3 Magonjwa yaliyojitokeza kwa mahudhurio ya nje 89 5.2.4 Magonjwa Kumi yaliyoongoza kwa Mahudhurio ya Nje 90 5.2.5 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa wa Ndani 91 5.2.6 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa waliolazwa Idara ya Internal Medicine 92 5.2.7 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa waliolazwa Wodi ya Upasuaji 92 5.2.8 Huduma za Upasuaji 92 5.2.9 Magonjwa ya Akinamama (Ggynaecology) 94 5.2.10 Sababu za kulazwa Mama wajawazito 94 5.2.11 Kujifungua Mama Wajawazito 95 5.2.12 Aina ya kujifungua Mama Wajawazito 95 5.2.13 Matokeo ya kujifungua Mama Wajawazito 96 5.2.14 Sababu ya Vifo vya Mama Wajawazito 96 5.2.15 Sababu za kulazwa na vifo wodi za watoto 97 5.2.16 Sababu ya Vifo vya watoto wa umri chini ya mwaka mmoja 97 5.2.17 Magonjwa ya Macho kwa waliolazwa 98 5.2.18 Magonjwa ya Akili kwa waliolazwa 98 5.2.19 Magonjwa ya Kinywa 99 5.2.20 Idara ya Vipimo vya Maabara 99 5.2.21 Takwamu za Damu Salama 100 5.2.22 Takwimu za X-ray zilizopigwa 101 5.2.23 Takwimu za kipimo cha Ultrasound 101 5.2.24 Takwimu za kipimo cha CT Scan 102 5.2.25 Takwimu za Watumishi 103 5.2.26 Takwimu za Madaktari Bingwa 103 5.2.27 Taarifa ya Fedha za Kuendesha Huduma 104 5.3 Mafanikio na Matatizo katika Hospitali za Rufaa 105 6.0 Ripoti za Hospitali za Huduma Maalum 107 6.1 Hospitali ya Kibongoto 107 6.2 Taasisi ya Tiba ya Magonjwa ya Mifupa MOI 107 6.3 Hospitali ya Mirembe na Taasisi ya Mirembe 108 6.4 Taasisi ya Saratani Ocean Road 109 7.0 Ushirikiano na Nchi za Nje 110 8.0 Shukrani 111 3

VIFUPISHO ADB ADDO ARVs BADEA BF CCHP CHSB CDC CEDHA CHF CLP CUAMM DANIDA DDH DFID DOTS EEG EOP EPI EU HFGC GAVI GTZ ICU IDRC IMCI ITI JICA KCMC KfW MDRTB MDT MKUKUTA MOI MoU MSF MTUHA MUHUMA NACTE NEPHI NIMR OC OPD ORCI OREC OPET PHCI PMTCT DOTS PPM RHMT SAFI SAREC SDC SIDA SP STI SWAP TAMISEMI TALGWU TFDA TFNC TIKA TUGHE UKIMWI UNHCR UNDP UNFPA UNICEF USAID VAs VCT VVF WB WHO ZBTC African Development Bank Accredited Drug Dispensing Outlets Anti Retro Viral Drugs Bangue Arabe pour Development Economique en Afrique Basket Funds Comprehensive Council Health Plans Council Health Services Board Centre for Disease Control and Prevention Centre for Education in Health Development Arusha Community Health Fund (Mfuko wa Afya ya Jamii) Central Pathology Laboratory International College for Health Cooperation in Developing Countries Danish International Development Agency Designated District Hospital United Kingdom Department for International Development Directly Observed Treatment Short Course Electro Encephalogram Emergency Operational Plan Expanded Programme of Immunization European Union Health Facility Governing Committee Globed Fund for Vaccine Initiative Gesellschaft fuer Technische Zusammenarbeit Intensive Care Unit International Development Research Centre of Canada Integrated Management of Childhood Illnesses International Trachoma Initiate Japan International Cooperation Agency Kilimanjaro Christian Medical Centre German Bank for Development Multi Drug Resistant TB Multi Drugs Therapy Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania Muhimbili Orthopedic Institute Memorandum of Understanding Medicine Sans Frontieres Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya Mradi wa Uimarishaji wa Huduma za Afya National Council for Technical Education National Essential Package of Health Interventions Institute for Medical Research Other Charges Out Patient Department Ocean Road Cancer Institute Organization of Petroleum Producing Countries Overseas Related Export Trade Primary Health Care Institute Prevention of Mother to Child Transmission Directly Observed Treatment Short Course Planned Preventive Maintenance Regional Health Management Team Sawazisha Kope, Anza Matibabu Mapema, Fanya Usafi wa Uso na Mwili Imarisha Mazingira Swedish Agency for Research Cooperation in Leading Countries Swiss Agency for Development and Cooperation Swedish International Development Authority Sulphurdoxine Pyrimethemine Sexually Transmitted Infections Sector Wide Approach Programme Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa Tanzania Local Government Workers Union Tanzania Food and Drug Authority Tanzania Food and Nutrition Centre Tiba kwa Kadi Tanzania Union for Government Health Employees Ukosefu wa Kinga Mwilini United Nations High Commission for Refugees United Nations Development Programme United Nations Fund for Population Activities United Nations Children Fund United States Agency for International Development Voluntary Agencies Voluntary Councelling and Testing Vesicle Vaganal Fistula World Bank Word Health Organization Zonal Blood Transfusion Centres 4

Utangulizi Katika kipindi cha mwaka 2004/05, Huduma za Afya nchini ziliendelea kuimarika. Malengo yaliyowekwa katika kipindi hicho yalitekelezwa kwa ufanisi na vipaumbele vya Wizara pia vilifikiwa. Pamoja na mafanikio yaliyofikiwa katika kipindi hicho kulikuwa na tatizo la takwimu kutokamilika katika Sekta ya Afya. Kwa ujumla wake bado limeendelea kujitokeza katika uandikaji wa taarifa za mwaka za hospitali za Rufaa na Mikoa. Kutokana na hali hiyo bado ipo haja ya kuzingatia umakini katika kupata takwimu sahihi za utendaji kwani ndizo zitakazosaidia kutoa takwimu sahihi ya hali ya magonjwa na hali halisi ya Huduma za Afya Nchini. Matatizo yaliyojitokeza katika taarifa zetu za utendaji za mwaka yanatoa changamoto kwetu sisi watendaji tujipange upya katika kutekeleza majukumu yetu katika Sekta ya Afya. Aidha, takwimu zimeonyesha kushuka kwa viashiria vingi vya hali ya Afya katika taarifa za mwaka za Mikoa na Hospitali za Rufaa. Iwapo hapatakuwa na juhudi za kutosha za kurekebisha hali hiyo ni wazi kwamba hali ya Huduma ya Afya itazidi kushuka na hivyo kuathiri afya za wananchi. Kutokana na hali hiyo zinahitajika jitihada za kutosha za kujifunza kwa Mikoa/Hospitali iliyofanya vizuri ili kasoro zilizojitokeza ziweze kurekebishwa. Changamoto la tatizo la UKIMWI linataka kujipanga upya ili kutekeleza wajibu wetu katika kutoa huduma za afya kwa Watanzania. 5

1.0 RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA MAKAO MAKUU 2004/2005 1.1 Utangulizi Kwa mwaka 2004/2005 huduma za afya nchini ziliendelea kutolewa kwa kuzingatia sera, miongozo, mipango na mikakati mbalimbali iliyowekwa na Wizara ya Afya. Kazi zilizopangwa kufanyika katika kipind hiki zililenga dira, malengo na majukumu yaliyopewa kipaumbele. Vyote hivi ni mwendelezo wa utekelezaji wa mipango na mikakati iliyowekwa katika mwaka 2003/2004. 1.2 Dira/Mwelekeo (Vision) ya Wizara Dira ya Wizara ya Afya ni Kutoa huduma za afya zenye ubora wa hali ya juu zinazofaa na zinazofikiwa na kutumiwa na wananchi wote kulingana na mahitaji yao kupitia mfumo wa afya ulio imara na endelevu. 1.3 Majukumu ya Wizara Ili kuiwezesha Wizara kufikia dira yake inatakiwa kutekeleza majukumu yafuatayo:- Kusimamia Sera na kutayarisha miongozo ya Afya ya huduma za Kinga na Tiba Kudhibiti kemikali na kuendesha uchunguzi wa kisayansi wa sababu za vifo Kusimamia na kudhibiti ubora wa dawa, vifaa tiba, vipodozi na vyakula Kuendeleza huduma za Tiba ya Asili Kusimamia Mpango wa Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto Ukaguzi wa huduma za afya Kuandaa na kusimamia programu za mafunzo ya wataalamu wa afya na kuwaendeleza kitaaluma watumishi wa sekta ya afya Kuinua kiwango cha ushirikiano kati ya Wizara, mashirika ya umma na dini, sekta binafsi, idara na miradi mbalimbali ya afya katika kuongeza na kuimarisha ubora wa huduma za afya Kutafuta rasilimali na vyanzo vya kutosha vya fedha na kuhakikisha matumizi bora ya watumishi wa afya, fedha na vifaa Kuongoza na kusimamia wakala za Serikali, taasisi na mashirika ya umma yaliyo chini ya Wizara ya Afya Kushirikiana na jumuia za kimataifa katika kuimarisha huduma za Afya. 1.4 Azma (Mission) ya Wizara ya Afya Azma ya Wizara ya Afya ni kutoa huduma za afya kulingana na mahitaji, kusimamia sera na kutayarisha miongozo sahihi inayowezesha upatikanaji wa wataalamu wa afya wenye ari na hamasa ili kuboresha afya hasa ya wale walio katika hatari ya kuugua zaidi. 1.5 Malengo ya Wizara ya Afya Kupunguza magonjwa na idadi ya vifo kwa makundi yanayoathirika zaidi hasa watoto wachanga, na walio chini ya miaka mitano, chipukizi ambao hawajafikisha umri wa kwenda shule na walio shuleni, vijana, watu wenye ulemavu, wazee na wanawake walio katika umri wa uzazi na kuongeza umri wa kuishi 6

Kuhakikisha kuwa huduma muhimu na za msingi za afya zinasaidiwa na kusimamiwa kwa utaratibu sahihi wa huduma za rufaa, utafiti, takwimu zenye mgawanyo wa kijinsia na kuwahusisha kikamilifu wananchi Kufanya tathmini na kudhibiti usalama na ubora wa vyakula, dawa, kemikali na vipodozi ili kulinda afya ya wananchi wote na mazingira kwa ujumla Kuzuia na kudhibiti magonjwa yanayoambukiza na yasiyoambukiza yakiwemo Malaria, Kifua Kikuu, Utapiamlo na yale mengine yanaohusiana na afya ya mazingira, afya kazini, matumizi ya kemikali Kupanga mafunzo ya watumishi na kujitosheleza kwa wataalam wa afya wenye uwezo na ujuzi katika kada mbali mbali kwa kuzingatia uwiano wa kijinsia katika kutoa huduma za afya katika ngazi zote Kuainisha mahitaji na kukarabati miundo mbinu ya afya kwa kuzingatia huduma zinazotolewa kwa watu wenye ulemavu na kuweka mfumo wa matengenezo ya majengo ya afya, mitambo na vifaa Kufanya mapitio, kutayarisha, kuhamasisha, kueneza, kufuatilia na kutathmini sera ya afya, mipango na bajeti, miongozo, sheria za afya za viwango mbali mbali vya huduma, kanuni na taratibu zinazohakikisha huduma za afya zinatolewa kwa ubora unaotakiwa Kuweka mazingira mazuri ya kazi na vitendea kazi kwa ajili ya kutoa huduma bora na muhimu za kiutendaji na utawala zenye kuzingatia jinsia. 1.6 Maeneo yaliyopewa kipaumbele 2004/2005 Maeneo yaliyopewa kipaumbele ni yale yaliyolenga katika kupunguza umasikini, magonjwa na vifo kwa wananchi wote, kuongeza umri wa kuishi na ubora wa maisha. Maeneo hayo yaliainishwa kama yafuatayo:- Kuzipatia hospitali, vituo vya afya na zahanati dawa muhimu na vifaa vya hospitali Kuimarisha huduma za hospitali za rufaa kwa kuzipatia vifaa vya hospitali, vifaa vya uchunguzi na dawa za maabara. Vifaa hivi huwawezesha waganga kugundua tatizo mapema na kutoa tiba sahihi Udhibiti na uzuiaji wa Malaria Kutoa mafunzo ya kitaalamu ya watarajali (pre-service) ya wataalam wa afya na ya kujiendeleza kwa kada zote za afya Kuimarisha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto, kwa kusambaza dawa za uzazi wa mpango, vifaa vya uzazi na kutoa mafunzo kwa waganga na wauguzi jinsi ya kutambua, kuainisha na kutoa tiba sahihi kwa magonjwa ya watoto kwa kupitia mpango wa uwiano wa kutibu magonjwa ya watoto (IMCI) Kuimarisha huduma za chanjo kwa kununua dawa za chanjo, vifaa na vipuli kwa ajili ya mnyororo baridi Udhibiti na uzuiaji wa kuenea kwa Kifua Kikuu na Ukoma Kuboresha hali ya elimu ya lishe nchini Kuimarisha afya na usafi wa mazingira nchini kote Kuzipatia fedha hospitali Teule (DDH) na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) ili kuongeza uwezo wa kutoa huduma kwa wananchi katika sehemu zisizo na vituo vya afya vya Serikali Kutekeleza majukumu ya sekta ya afya katika kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI Kutumia matokeo ya utafiti yanayotolewa na taasisi mbalimbali za utafiti katika kutoa mapendekezo ya sera, miongozo na mipango mbali mbali ya afya Kutoa mchango wa Serikali katika miradi yote inayopewa fedha na wahisani mbali mbali 7

Kufanya ukarabati wa majengo ya afya yaliyo katika hali mbaya na vifaa vya tiba na kuweka utaratibu wa kufanya matengenezo ya kinga (Planned Preventive Maintainance PPM) Kufanya uchunguzi wa vyakula, dawa na kemikali, kutoa ushauri wa kitaalam na kutambua vyanzo vya vifo kwa kufanya uchunguzi wa kisayansi Kusimamia na kudhibiti kemikali za viwandani na majumbani, utakaotekelezwa na Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali. 1.7 Muhtasari wa kazi zilizopangwa kutekelezwa na Wizara ya Afya 2004/2005 Katika kipindi hiki kazi zilizopangwa kutekelezwa na Wizara ya Afya kwa kutumia fedha za matumizi ya kawaida na miradi ya maendeleo, imefuata vipaumbele vilivyoanishwa hapo juu. Kazi hizo ni kama zifuatavyo:- Kutoa dawa na vifaa vya hospitali kwa zahanati, vituo vya afya na hospitali katika ngazi zote ili kuiwezesha Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kutoa huduma muhimu za afya kwa wananchi Kutoa ruzuku kwa hospitali za mashirika ya dini Kusimamia, kufuatilia na kutathmini huduma za afya zitolewazo na Serikali za Mitaa, Mikoa, hospitali za Rufaa na Taifa Kuimarisha huduma za chanjo, kuendeleza ubadilishaji wa mfumo wa uendeshaji wa majokofu ya chanjo kutoka matumizi ya mafuta ya taa kwenda katika matumizi ya gesi. Shughuli za chanjo zitaendelea kuimarishwa kote nchini Kutekeleza mpango wa ukarabati na matengenezo ya hospitali za Mikoa na za Rufaa. Karakana Kuu za Kanda za vifaa na za ukarabati zitatumika kusaidia hospitali za Mikoa na Serikali za Mitaa kuanzisha uhakikimali na kuweka viwango kamili vya vifaa vya kutolea huduma za afya vinavyotumiwa na vituo vinavyotoa huduma za afya Kufuatilia na kusimamia ubora na usalama wa chakula, dawa na vipodozi utakaotekelezwa na Mamlaka ya Taifa ya Chakula na Dawa (TFDA) kwa kutoa huduma za ukaguzi, usajili wa uzalishaji, majaribio na uchunguzi wa kimaabara wa sampuli ili kuhakikisha kuwa wazalishaji, wasafirishaji nje, waagizaji, wasambazaji na wauzaji wanazingatia ubora, viwango, taratibu na matendo ya utunzaji yanayokubalika Kuzuia magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza hasa Malaria, UKIMWI, Kifua Kikuu na Utapiamlo. Hatua zitakazochukuliwa zitajumuisha uimarishaji na kuinua elimu ya afya na usimamizi wa kemikali Kuweka kipaumbele katika utekelezaji wa mkakati mpya wa sekta ya afya wa kupambana na UKIMWI kwa kuhakikisha mpango huu unatekelezwa na kila idara umeingizwa katika mpango wa afya wa mwaka wa kila Halmashauri ya Wilaya. Kutoa huduma za tiba kwa wagonjwa wa UKIMWI na magonjwa yanayoambatana nayo, kutoa ushauri nasaha na kupunguza unyanyapaa kwa walioathirika Kutoa mafunzo kwa wataalamu mbalimbali wa afya juu ya tiba sahihi ya Malaria katika Wilaya zote nchini, uhamasishaji juu ya utumiaji wa vyandarua vyenye viuatilifu, utafiti wa usugu wa vimelea vya Malaria na tiba mseto Kuhakikisha usalama wa damu, kuzuia maambukizi ya UKIMWI kwa mtoto toka kwa mama, kuhamasisha uzuiaji wa kuenea kwa UKIMWI kupitia ngono, uaminifu kwa mpenzi mmoja na matumizi ya kondom Kuchukua hatua ambazo zitaongeza upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI kwa kushirikiana na wahisani na mifuko mbali mbali kama vile Global Fund, The Bill and Melinda Gates Foundation, Clinton Foundation na President G. W. Bush Initiatives 8

Kutekeleza mikakati ya pamoja ya kudhibiti maambukizi ya Kifua Kikuu na UKIMWI, kutoa dawa za Kifua Kikuu na Ukoma katika vituo vyote vya matibabu. Kufanya utafiti wa kitaifa wa Kifua Kikuu na kampeni za kutokomeza Ukoma Kuendelea kutoa kipaumbele kwa magonjwa mengine kwa kutekeleza mipango na kazi zinazolenga utoaji wa huduma muhimu za afya kwa jamii, huduma za afya ngazi ya Wilaya na katika hospitali za Mikoa na Rufaa Kuimarisha mipango ya mafunzo ya wataalamu na kuboresha mafunzo katika vyuo vyake ili kuhakikisha elimu inayotolewa na vyuo hivyo inakuwa bora zaidi. Kuweka mkazo zaidi katika mafunzo ya kujiendeleza ili kuwaongezea ujuzi na utaalamu wafanyakazi wa afya katika ngazi zote. Kuandaa mipango ya mafunzo endelevu ya wafanyakazi ambayo itatengenezwa kulingana na mahitaji ya kazi Kukarabati majengo na vifaa vya kutolea huduma za afya na kukamilisha uchunguzi utakaosaidia uandaaji wa mpango wa maendeleo wa miaka 10 wa huduma za hospitali Kukamilisha mapitio ya Sera ya Taifa ya Afya kwa kujumuisha maoni yaliyotolewa na wadau wengine wa afya Kuwasilisha muswada wa sheria ya Afya ya Jamii katika Wizara ya Sheria na Mambo ya Katiba ili ukamilishwe na uwasilishwe bungeni Kuimarisha ushirikiano na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Kutoa mafunzo ya huduma za dharura kwa wazazi kwa kufundisha waalimu 12 wa kitaifa na 80 kutoka Mikoani. 2.0 UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU AFYA MAKAO MAKUU 2004/2005 2.1 Mipango ya Maendeleo Mwaka 2004/05 Wizara ya Afya ilitengewa kiasi cha shilingi 91,215,753,600/= kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Kati ya kiasi hicho, jumla ya shilingi 3,552,448,200/= zilitolewa na Serikali ya Tanzania na kiasi cha shilingi 87, 663, 305,400/= zilitoka kwa wahisani mbalimbali, wakiwemo wahisani wanaochangia Mfuko wa Pamoja wa Afya (Health Basket Fund). Fedha hizo zimetumika kutekeleza miradi ifuatayo: - Ukarabati wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Wizara iliendelea kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (ADB) ili kukamilisha ukarabati mkubwa unaoendelea katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Ukarabati huu unaenda sambamba na ununuzi na ufungaji wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya Hospitali ya Taifa Muhimbili na hospitali za Manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni Kuendeleza ujenzi wa wodi ya watoto (Paediatric Ward Complex) Kuimarisha Hospitali Maalum na za Rufaa o Ukarabati wa majengo ya huduma ya wagonjwa wa nje, upasuaji, mfumo wa maji taka katika hospitali ya Meta mjini Mbeya, pamoja na ukarabati wa kijiji cha wagonjwa wa akili Isanga o Kutayarisha michoro kwa ajili ya ujenzi wa hosteli ya madaktari wanafunzi (Intern Doctors) na kukamilisha ujenzi wa chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali ya Rufaa Mbeya o Ununuzi wa vifaa vya tiba kwa ajili ya hospitali za rufaa na maalum o Serikali imeweza kutoa mchango wake wote kama ilivyopangwa katika Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) o Serikali iliweza kukarabati majengo ya vyuo vya mafunzo ya afya nchini o Serikali imeweza kumalizia kutoa mchango wake wote (counterpart fund) ili kununua vifaa vya Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili MOI o Udhibiti wa magonjwa ya kuambukiza 9

2.2 Sera na Mipango o Kukamilisha ujenzi wa jengo la ofisi za Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binaadamu (NIMR) Tukuyu o Kufanya ukarabati wa mifumo ya njia za umeme kwenye jengo la ofisi za Huduma za Mama na Mtoto Dar es Salaam o Kufanya ukarabati wa ofisi, mabweni na madarasa katika vyuo 33 vya afya vilivyo chini ya Wizara o Kuvipatia vituo vyote vya afya dawa na vifaa kwa ajili ya kukinga na kutibu magonjwa ya zinaa STIs o Kukomboa na kusambaza dawa za ugonjwa wa Kifua Kikuu na Ukoma. Serikali imetoa mchango wake (counterpart funds) kwenye mradi kwa ajili ya kudhibiti magonjwa haya o Kutayarisha na kusambaza vitabu vya Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji Huduma za Afya (MTUHA) nchi nzima. 2.2.1 Mabadiliko katika Sekta ya Afya (Health Sector Reforms) Wizara kwa mwaka 2004/2005 ilifanikiwa kuhamasisha na kutoa mafunzo kwa Halmashauri za Wilaya 92 Tanzania Bara na kuziwezesha kuandaa na kupitisha Sheria ndogo ya kuanzisha Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF). Halmashauri hizo hazijumuishi Halmashauri kwa Wilaya 8 ambazo ni mpya kwa kuwa Wizara bado inasubiri zipate mabaraza ya Madiwani, October 2005. Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) unaendelea kuwa mkombozi kwa wananchi wenye kipato cha chini kwa kutoa unafuu wa matibabu kwa wale wanaojiunga na mfuko huo kwa kuwahakikishia upatikanaji wa dawa, vifaa tiba na vifaa muhimu. Wilaya za Mbinga, Igunga, Singida, Iramba, Songea na Iringa zimeendelea kuwa mfano. Wizara kwa kushirikiana na TAMISEMI na Halmashauri imeweza kuandaa na kusaini Mikataba ya CHF inayolenga kuwa na mwongozo wa matumizi bora ya fedha za CHF. Wizara itatumia mikataba ya CHF kulipia tele kwa tele kwa Halmashauri 30 zilizochanga kwa awamu mbili, yaani mwezi Oktoba 2004 Wizara ililipa shilingi millioni 400 na Juni 2005 ililipa shilingi millioni 100. Wizara pia imehamasisha Halmashauri za Miji ya Moshi, Iringa, Mtwara na Jiji la Mwanza juu ya utaratibu wa kuchangia huduma za afya kabla ya kuugua kwa sekta isiyo rasmi katika maeneo ya mijini. Utaratibu huu unajulikana kwa jina la TIBA KWA KADI (TIKA). Mpango huu wa TIKA unafanana na CHF ya Halmashauri ya Wilaya na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ambapo kaya au watumishi wanachangia kabla ya kuugua na kupata matibabu ya mwaka mzima kwa kutumia KADI ya matibabu na hivyo kuzuia kutoa fedha taslimu ambazo zinaashiria mianya ya rushwa. Matarajio ya Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) Mwaka 2005/2006 Mwaka 2005/06 Wizara inatarajia kutekeleza yafuatayo: Kutoa mafunzo ya njia bora za kufanya makisio ya makusanyo Kuhamasisha kwa ufasaha na ufanisi Utunzaji na matumizi bora ya fedha za CHF 10

Kujenga msingi wa kudumu katika ngazi ya Kanda na Mikoa kwa kuvitumia vyuo vya kanda na kushauri Mikoa yote kuteua waratibu wa CHF wa Mikoa chini ya Kamati za uendeshaji huduma za afya za Mikoa, RHMT ili wawe kiungo kati ya Wizara, Kanda na Halmashauri Kushauri Halmashari nazo ziwe na waratibu wa CHF. Pia, Wizara imepanga kuhamasisha na kuziwezesha Halmashauri zote za Miji/Manispaa/Jiji kuanzisha mpango wa Tiba kwa Kadi (TIKA) kwa kutunga sheria ndogo za TIKA na kuidhinishwa katika ngazi ya Halmashauri. 2.2.2 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umeendelea kuimarisha shughuli zake na kuboresha huduma kwa wanachama wake. Mfuko huu sasa upo katika mwaka wake wa nne wa utekelezaji na sote tu mashahidi kuwa matatizo mengi ya awali yaliyotokana na uchanga wa Mfuko huu yamekuwa yakipatiwa ufumbuzi na kazi ya kuuboresha Mfuko huu inaendelea. Mwaka 2004/2005 Mfuko ulitekeleza yafuatayo:- Ulisajili wanachama wapya 6,321 na hivyo kuufanya Mfuko kufikisha jumla ya wanachama 248,829 ikilinganishwa na wanachama 242,508 waliokuwepo kipindi cha 2003/2004. Kati ya hao asilimia 56 ni wanaume na asilimia 44 ni wanawake. Juhudi zaidi za kusajili wanachama wapya zinaendelea kupitia ofisi za kanda pamoja na Makao Makuu ya Mfuko ili Watanzania wengi zaidi waendelee kunufaika na Mfuko huu Idadi ya wanaonufaika na mpango huu imeongezeka kutoka 1,115,537 kipindi cha mwaka 2003/2004 hadi kufikia 1,144,614 katika mwaka 2004/2005. Hii ni sawa na asilimia nne (4%) ya Watanzania wote. Kundi la wazee nalo lipo ambapo wazee wenye umri wa zaidi ya miaka 60 walioandikishwa na watoto wao kama wategemezi ni 468,148. Mfuko huu utaendelea kuangalia namna bora ya kuwajumuisha wazee wengi hasa kundi la wastaafu chini ya utaratibu huu Umetengeneza jumla ya vitambulisho 949,153 kutokana na fomu zilizopokelewa. Hii ni asilimia 83.1 ya lengo la kutengeneza vitambulisho 1,142,378 Mahudhurio katika vituo vya matibabu yameongezeka kutoka wastani wa wanachama 64,917 kwa mwezi katika mwaka 2003/2004 hadi kufikia wastani wa wanachama 98,825 kwa mwezi katika mwaka 2004/2005. Jumla ya mahudhurio (Total attendance) tangu mwaka 2001 hadi Januari 2005 ilikuwa 1,991,977. Kati ya waliotibiwa asilimia 62.5% ni walimu na asilimia 37% ni kundi la wanawake na watoto Aidha, jumla ya shilingi bilioni 7.35 zimekwishalipwa kwa watoa huduma wa Serikali na wale wa asasi zisizo za Serikali tangu utaratibu huu ulipoanza kutumika miaka minne iliyopita, ikiwa ni marejesho kwa huduma walizotoa kwa wanachama Jumla ya vituo 3,558 vya matibabu vilisajiliwa na Mfuko ili kuhudumia wanachama, ambapo asilimia 70 ya vituo hivi vipo vijijini. Kati ya vituo hivi vituo 519 vinamilikiwa na madhehebu ya dini na asasi zisizo za Serikali na maduka ya dawa ni 36 yanamilikiwa na wamiliki binafsi Umeweza kufanya tathmini ya uhai wa shughuli zake kwa kutumia wataalamu wake. Kwa upande wake Shirika la Kazi Duniani (ILO) limeipitia tathmini hiyo na kuridhika nayo. Utekelezaji wa tathmini hiyo utauwezesha uongozi wa mfuko kuboresha mafao mbalimbali pamoja na wigo wake, ikiwemo orodha ya madawa 11

Umekwishakamilisha mpango wake wa miaka 5 wa Strategic Corporate Plan unaoanza utekelezaji wake katika mwaka ujao wa fedha wa 2005/06. Mfuko utaweka kipaumbele vijijini katika mwaka wa kwanza wa utekelezaji wa mpango huo makini Umetoa elimu kwa wadau 96,414 wakiwemo viongozi wa vyama vya wafanyakazi, watoa huduma na vilevile kwa vyombo vya habari Umeimarisha ofisi zake saba za kanda kwa kuzipatia nyenzo, vifaa na madaraka zaidi. Katika kipindi hicho jumla ya watumishi 37 waliajiriwa katika Ofisi za Kanda, wengi wao wakiwa ni wakaguzi na hivyo kufanya Mfuko kuwa na watumishi 121 nchi nzima Ulifanya zoezi la sensa kwa wanachama wake pamoja na ukaguzi wa vituo vya matibabu. Zoezi hili lilifanyika katika kanda ya mashariki na kanda ya ziwa na linaendelea katika kanda nyingine. Lengo kuu la zoezi hili, ni kuhakiki taarifa muhimu za wanachama hususan upande wa vitambulisho na upatikanaji wa huduma za matibabu hasa vijijini. Tathmini imeonyesha mafanikio makubwa katika kulipatia ufumbuzi tatizo la vitambulisho, kuimarisha na kuboresha zaidi huduma kwa wanachama Umeweza kuimarisha shughuli zake kupitia teknolojia ya habari na mawasiliano ambapo shughuli nyingi sasa zinafanyika kupitia mfumo huo. Hii ni pamoja na kuziunganisha ofisi zote saba za kanda na Makao Makuu, kurahisisha uandaaji wa malipo kwa watoa huduma na mawasiliano ya haraka na wateja. Matarajio ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya mwaka 2005/2006 Mkakati utawekwa wa kutumia mbinu za soko ili kusajili waajiri wote wanaotakiwa kusajiliwa kisheria (k.m, Mashirika ya Umma na Taasisi za Umma) ikiwa ni katika kusajili wanachama wengi zaidi. Mfuko utaendelea na zoezi la sensa ya wanachama wake ili kutambua idadi yao, maeneo waishio na upatikanaji wa huduma za Afya katika maeneo husika. Zoezi hili pia linahusisha ujazaji wa fomu za uanachama kwa wanachama ambao walikuwa bado hawajajaza fomu za kujiandikisha na hivyo kutokuwa na vitambulisho. Zoezi hili limebaini kwamba asilimia kubwa ya wanachama wanaolalamikia kutokuwa na vitambulisho ukweli ni kuwa hawajajaza fomu za uanachama wala kuwasilisha picha. Mfuko umekwishaanza zoezi la ukaguzi wa watoa huduma wote kwa lengo la kuangalia huduma zitolewazo kwa wanachama, mazingira ya vituo, idadi ya wafanyakazi katika vituo, hali ya vifaa vya vipimo, tiba na vitendea kazi, majengo ya vituo, pamoja na mpangilio wa jinsi wagonjwa wa Mfuko wanavyohudumiwa. Lengo la zoezi la ukaguzi ni kuhakiki na kuboresha huduma za afya zitolewazo. Mfuko utaendelea na programu ya uelimishaji kwa kutumia mabango ambayo yanasambazwa katika maeneo ya vijijini ambako njia za mawasiliano ni hafifu. Mabango hayo yatachapisha ujumbe mbalimbali muhimu kuhusu Mfuko, kwa mfano, mafao yatolewayo na Mfuko, namna ya ujazaji wa fomu za uanachama, ujazaji wa fomu za madai, haki na wajibu wa Wanachama na Wadau wengine wa Mfuko. Programu maalum ya mafunzo kwa watoa huduma wa ngazi za vituo vya afya na zahanati ambako wanachama wengi wa Mfuko wanatibiwa itaendelea katika kipindi cha mwaka ujao wa fedha ili kujenga uwezo zaidi wa watoa huduma. 12

Mfuko unatarajia kuingia katika awamu ya mwisho ya zoezi la kufunga mitambo ya mfumo wa kompyuta na mifumo habari katika ofisi zote za Mfuko. Mifumo na mtandao huu wa teknolojia ya habari (TEKNOHAMA) unatarajiwa kuongeza uwezo wa kufanya mawasiliano na watoa huduma na kurahisha taratibu na mchakato wa ulipaji madai na hivyo kupunguza ucheleweshaji na kero zilizokuwepo hapo awali. Mfuko unatarajia kuwekeza zaidi katika eneo la utoaji wa huduma za Mfuko katika ofisi za kanda kwa vile uzoefu wa uendeshaji wa ofisi za kanda uliokwishapatikana katika kipindi cha miaka miwili iliyopita umebaini mahitaji zaidi ya watumishi na vitendea kazi. Mfuko umekusudia kuandaa na kuanza kutekeleza Mkakati maalum wa miaka mitano (2005-2009). Mkakati huu utaweka bayana na kuainisha maeneo ya msingi ambayo Mfuko utayapa kipaumbele katika kuhakikisha kuwa dira, dhamira na mipango ya Mfuko inatekelezwa kama ilivyopangwa. Mfuko unatarajia kufanya mapitio ya sera ya uwekezaji ya Mfuko, ili kuweza kuanzisha maeneo zaidi ya uwekezaji, mkakati unaolenga kuleta faida zaidi, pasipo kuwa na uwezekano mkubwa wa kupoteza fedha za wanachama. Ongezeko la akiba (Reserve) litauwezesha Mfuko kupanua uwigo wa mafao vikiwemo vipimo zaidi, miwani na muda mrefu zaidi wa kuhudumia wastaafu, ambavyo vitahitaji marekebisho ya sheria. Mfuko unakusudia kufanya marekebisho katika baadhi ya maeneo mfano, suala la mafao ambayo hayamo katika kitita cha mafao, (exclusions), wigo wa wanachama na uboreshaji wa mafao, ambavyo vinapendekezwa kuhamishiwa kutoka kwenye Sheria mama na kuwekwa katika Kanuni na Taratibu (Regulations), ili pindi vikihitaji kubadilishwa visiwe vinakuwa na mlolongo mrefu kama kurejeshwa Bungeni ambako huchukua muda mrefu. Lengo la marekebisho yote hayo ni kurekebisha mfumo wa utekelezaji na hivyo kuondoa kero mbalimbali zinazowasibu wanachama kwa vile baadhi ya malalamiko ya wanachama ni ya kweli lakini pamoja na dhamira ya Mfuko ya kuyashughulikia malalamiko hayo, sheria ya Mfuko bado hairuhusu maeneo hayo kujumuishwa. Lengo la baadaye la Mfuko ni kupanua uanachama ili kujumuisha wananchi wengi zaidi wakiwemo walio katika sekta ya ajira isiyo rasmi, ili kuboresha upatikanaji wa huduma bora ya Afya kwa wananchi wote. 2.2.3 Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya (MTUHA) Wizara imeendelea kutoa kipaumbele kwa upatikanaji wa takwimu katika sekta ya afya. Kumekuwapo na mikakati ya makusudi ili kuhakikisha kuwa takwimu zinazohitajika zinapatikana kwa ajili ya mipango, kutoa tathmini ya utoaji wa huduma za afya, kufuatilia utekelezaji wa mipango mbalimbali ya kisekta na kuboresha sera na miongozo mbalimbali ili kuhakikisha kwamba huduma zinatolewa katika ubora unaostahili. 13

Katika kufanikisha mipango ya upatikanaji wa takwimu mikakati ifuatayo imetekelezwa katika mifumo inayotumika kupata takwimu:- Mfumo wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya (MTUHA) umeendelea kuboreshwa katika ngazi ya Wilaya. Hii ni baada ya kuweka kompyuta na programu ya kuchambua takwimu hizo. Hii imesaidia kuongeza kasi ya upatiakanaji wa takwimu katika ngazi ya Wilaya, Mkoa na Taifa Takwimu zinazopatikana kupitia mfumo wa kufanya tafiti mbalimbali nao umeimarishwa zaidi. Mafunzo yametolewa kwa viongozi waliomo kwenye Kamati za Afya za uendeshaji wa huduma Wilayani na Mikoani. Lengo kuu la mafunzo hayo lililikuwa kuwapa uwezo wa kimbinu wa kuandaa miswada ya kukusanya takwimu zilizo sahihi, kufanya utafiti, kuchambua takwimu zitokananzo na tafiti na kutumia matokeo ya fafiti ili kuboresha huduma ngazi ya Wilaya na Jamii kwa ujumla Wizara imeendelea kuimarisha kitengo kinachoratibu takwimu za jamii ambazo zinakusanywa katika maeneo maalum hapa nchini. Takwimu hizi ndizo zinazotoa makadirio yanayoonyesha uzito wa matatizo ya magonjwa yanayoisibu jamii yetu Mfumo wa mawasiliano ya kompyuta katika Makao Makuu ya Wizara yamekamilika. Hii itaboresha upatikanaji wa takwimu katika idara, sehemu na vitengo mbalimbali kuwa na kasi zaidi. Mtandao wa kompyuta kupitia mfumo huo umeanza kufanya kazi na huduma nyinginezo zitaongezwa kulingana na mahitaji. Matarajio ya Mfuko wa Taarifa za Uendeshaji wa Huduma za Afya mwaka 2005/2006 Katika mwaka 2005/2006, Wizara inatarajia kuunganisha mfumo wa kompyuta uliopo makao Makuu ya Wizara na mifumo iliyopo mikoani na katika hospitali za mikoa na za rufaa. Lengo kuu ni kurahisisha ubadilishanaji wa taarifa mbalimbali zikiwemo takwimu za afya. Pia Wizara ipo mbioni kuanzisha tovuti yake kwa lengo la kuwapatia wananchi taarifa muhimu zinazohusu sekta ya afya. Pia, Wizara ipo mbioni kubadilisha nyenzo za kukusanya takwimu za afya za siku hadi siku. Mabadiliko hayo yanalenga kuhakikisha kuwa takwimu zinazokusanywa kutoka vituo vya kutolea tiba vinaingizwa kwenye kompyuta moja kwa moja badala ya kuandaa ripoti maalum inayopelekwa Wilayani kwa ajjili ya kuingizwa kwenye kompyuta Umuhimu wa takwimu kutoka katika jamii unazidi kuongezeka siku hadi siku. Kwa sababu hiyo mwaka 2005/2006 Wizara itaboresha huu mfumo ili vigezo vitakavyopatikana vitoe takwimu ya nchi nzima na sehemu muhimu za jamii. Lengo ni kupanua wigo wa maeneo ya kukusanya takwimu za aina hii. 2.3 Huduma za Kinga Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/2005 2.3.1 Udhibiti wa Magonjwa ya Kuambukiza Pamoja na juhudi kubwa zinazochukuliwa za kupambana na magonjwa, tatizo la magonjwa ya kuambukiza limeendelea kuwepo nchini. Katika kipindi cha Juni 2004 hadi Aprili 2005 kulikuwa na wagonjwa 3,462 wa kipindupindu na kati yao 93 walifariki ikilinganishwa na kipindi kama hicho 2003/2004 ambapo kulikuwa na wagonjwa 12,397 na vifo 217. Mikoa iliyoathirika zaidi na tatizo hili ni Dar es salaam, Morogoro, Tanga, Kigoma, Mbeya, Kagera, Arusha na Kilimanjaro. Ipo haja ya kuzingatia kanuni za afya bora ili kuondokana na ugonjwa huu unaotokana na uchafu. 14

Tatizo la watu kuumwa na mbwa au wanyama wanaohisiwa kuwa na kichaa cha mbwa limekuwa likiongezeka kila mwaka. Mwaka 2004 watu 15,528 waliumwa na mbwa au wanyama wanaohisiwa kuwa na kichaa cha mbwa na kati yao watu 98 waliugua ambapo 78 walifariki ikilinganishwa na mwaka 2003 ambapo watu 12,120 waliumwa na kati yao 56 waliugua ambapo 47 walifariki. Wizara inashughulikia kinga ya kichaa cha mbwa, pia iliendelea kuwasiliana na Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo, Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Wizara ya Maliasili na Utalii, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili kuandaa mkakati wa kukabiliana na tatizo la watu kuumwa na wanyama wanaohisiwa kuwa na ugonjwa wa kichaa cha mbwa. Kutokana na kuanzishwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, wananchi wa nchi zetu tatu wamekuwa na uhuru zaidi wa kutembeleana, kwa hiyo Wizara inashirikiana na Wizara husika za Kenya na Uganda katika kupanua wigo wa ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa ya milipuko hasa sehemu za mipakani. Udhibiti wa Magonjwa yanayoenezwa na Wadudu (Vectors and Vector Borne Diseases) Katika kipindi cha mwaka 2004/2005 Wizara ikishirikiana na Taasisi ya Viuatilifu ya Arusha (TPRI) imefanya utafiti ili kupata viuatilifu (acaricides) vinavyofaa kuangamiza papasi wanaoleta homa ya papasi na matokeo ya utafiti huu yatakapokamilika yatatolewa kwa wadau. Aidha, wananchi katika mikoa husika wameendelea kuhamasishwa juu ya ujenzi wa nyumba bora na usafi wa mazingira ikiwa ni pamoja na matumizi ya vitanda ili kujiweka mbali na mazalio ya papasi. Matarajio ya Udhibiti wa Magonjwa ya Kuambukiza mwaka 2005/2006 Ili kudhibiti magonjwa ya kuambukiza Wizara itaendelea kutoa mafunzo juu ya ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa kwa wataalam katika Wilaya 30. Wizara itaendelea na mapambano dhidi ya magonjwa yanayoenezwa na wadudu wanaoruka, wasioruka pamoja na wanyama (Vectors and vector borne diseases) kwa kufanya ufuatiliaji na usimamizi wa shughuli za udhibiti wa magonjwa hayo katika Wilaya 20. 2.3.2 Mpango wa Taifa wa kudhibiti Malaria Ugonjwa wa malaria bado ni tatizo kubwa hapa nchini na linahitaji jitihada za pamoja katika kukabiliana nalo. Katika kipindi cha 2004/2005, Wizara ilitekeleza majukumu mbalimbali katika kukabiliana na ugonjwa wa Malaria. Utekelezaji huo ulihusu:- kutoa mafunzo kwa wataalam mbalimbali wa afya kuhusu tiba sahihi, uhamasishaji juu ya utumiaji wa vyandarua vyenye viuatilifu hasa kwa mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka 5 utafiti wa usugu wa vimelea vya malaria utafiti juu ya tiba ya mseto utoaji wa tiba ya tahadhari kwa vipindi kwa mama wajawazito tahadhari za kudhibiti milipuko ya malaria katika wilaya zenye milipuko ya malaria na uimarishaji wa udhibiti wa malaria ngazi ya jamii. Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inaendelea na uhamasishaji wa jamii katika kutumia vyandarua vyenye viuatilifu. 15

Wizara pia ilizindua Mpango wa Taifa wa Hati Punguzo tarehe 22 Oktoba mwaka 2004, mpango ambao unawawezesha mama wajawazito na watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kupata vyandarua vyenye viuatilifu kwa bei nafuu. Kwa hivi sasa, mpango wa Taifa wa Hati Punguzo unatekelezwa katika mikoa ya Dar-es-salaam, Dodoma, Morogoro, Tanga, Pwani, Kilimanjaro na Arusha. Mpango huu utajumuisha mikoa yote ya Tanzania Bara ifikapo mwishoni mwa mwaka 2005. Kufikia mwezi Mei mwaka 2005, mpango huu umeonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji kwani mama wajawazito wapatao 100,000 wametumia Hati Punguzo kununulia vyandarua. Matarajio ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Malaria mwaka 2005/2006 Mwaka huu Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali iliadhimisha Siku ya Malaria Afrika iliyofanyika Kitaifa tarehe 25 Aprili, 2005 mkoani Singida. Kauli mbiu ya maadhimisho hayo ilikuwa Tushirikiane kwa pamoja tushinde Malaria. Kauli mbiu hii inakumbusha na kusisitiza umuhimu wa kuwashirikisha wadau wote katika Afya kupiga vita Malaria, hii ikiwa ni pamoja na jamii, Serikali kuu, Serikali za mitaa, wahisani mbalimbali, mashirika ya dini, watu binafsi nk. Pamoja na jitihada kubwa zinazofanyika ili kudhibiti ugonjwa wa Malaria nchini, kuna Wilaya 25 ambazo zipo katika hatari ya kupata milipuko ya ugonjwa wa malaria. Kwa hali hiyo, Wizara katika mwaka huu wa fedha imeandaa mikakati ya kuziweka wilaya zenye uwezekano wa kupata milipuko ya Malaria katika hali ya tahadhari ya kuweza kutabiri na kudhibiti milipuko hiyo. Wizara imeanza maandalizi ya kubadilisha matibabu ya Malaria kutoka dawa ya SP kwenda dawa ya mseto ya Artemether /Lumefantrine (ALU/Coartem). Maandalizi ya kubadili mwongozo wa matibabu, kuendesha mafunzo kwa watoa huduma za afya kuhusu tiba mpya na kuelimisha jamii yatafanyika. Matarajio ni kuanza kutumia dawa mseto ifikapo mwezi wa 8, mwaka 2006. 2.3.3 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma Mwaka 2004 kumekuwa na ongezeko la usajili wa wagonjwa wa Kifua Kikuu toka 64,665 mwaka 2003 hadi 65,644 mwaka 2004. Ongezeko hilo ni sawa na asilimia 1.5. Aidha, uponaji wa wagonjwa wa Kifua Kikuu pia umeongezeka kutoka asilimia 80.2 mwaka 2002 hadi asilimia 82.5 mwaka 2003. Ongezeko hili ni la asilimia 2.8. Vilevile, idadi ya wagonjwa wa Kifua Kikuu wasiomaliza matibabu kama ilivyoelekezwa na wahudumu imepungua kwa asilimia 0.5. Kwa upande wa ugonjwa wa Ukoma, wagonjwa wamepungua kutoka 5,771 mwaka 2003 hadi wagonjwa 5,602 mwaka 2004 ambalo ni punguzo la asilimia 3. Mafanikio haya yametokana na utekelezaji wa mikakati ya kudhibiti maradhi haya kwa kushirikisha jamii ambayo ni kuwatafuta, kuwatambua mapema na kutoa tiba kamilifu kwa wagonjwa chini ya usimamizi maalum unaoitwa Directly Observed Treatment Short Course (DOTS) kwa ajili ya Kifua Kikuu na Multi -Drug Therapy (MDT) kwa ajili ya Ukoma. 16

Katika kipindi cha Julai 2004 mpaka Juni 2005, Mpango wa Taifa wa Kifua Kikuu na Ukoma ulifanya ufuatiliaji wa watoto wa shule 1,048 waliobainika kuwa na uambukizo wa ugonjwa wa Kifua Kikuu katika mikoa ya Singida, Iringa, Mbeya, Kigoma na Kagera. Asilimia 48 ya watoto hao walipata uambukizo ndani ya kaya zao na jumla ya watoto 75 yaani asilimia 3 walikuwa tayari na ugonjwa wa Kifua Kikuu (active TB) na walipewa dawa za matibabu. Kampeni za kutokomeza ugonjwa wa Ukoma Duniani zilifanyika katika mikoa ya Kagera, Rukwa na Tabora ambako jumla ya wagonjwa wapya 836 waligunduliwa na kuanzishiwa tiba. Aidha, katika juhudi za kurekebisha ulemavu (prevention and rehabilitation of disabilities) unaotokana na Ukoma, watu walioathirika na Ukoma wenye ulemavu 175 walifanyiwa upasuaji wa aina mbalimbali na wengine 5,811 walipewa viatu maalum na watu 37 walipewa miguu bandia. Vile vile, madaktari bingwa wa upasuaji 5 walipewa mafunzo rejea juu ya upasuaji wa wagonjwa waliopata ulemavu kutokana na Ukoma. Katika kipindi cha 2004/2005, jamii iliendelea kuelimishwa kwa kutumia njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutoa matangazo kwa kutumia vyombo vya habari, kusambaza vipeperushi na mabango yenye ujumbe wa jinsi ya kutambua dalili, kujikinga na matibabu ya Kifua Kikuu na Ukoma. Aidha, dawa za kutosha za Kifua Kikuu na Ukoma ziliendelea kusambazwa katika mikoa, wilaya na vituo vyote vya matibabu. Dawa hizo zilitolewa kwa wagonjwa wote bila malipo. Matarajio ya Mpango wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma mwaka 2005/2006 Katika kipindi cha 2005/06 Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Kifua Kikuu na Ukoma utaendeleza kampeni za kutokomeza Ukoma katika mikoa ya Ruvuma, Morogoro na Tanga. Aidha, shughuli za kurekebisha rejesta za wagonjwa wa Ukoma zitaendelea sambamba na kampeni za kutokomeza Ukoma ili kufikia lengo la kimataifa ifikapo Desemba mwaka 2005. Mpango utaendelea kuimarisha huduma za pamoja za kudhibiti Kifua Kikuu na UKIMWI na zile za kudhibiti Kifua Kikuu sugu ili kisienee nchini. Aidha, uagizaji na usambazaji wa dawa za kutosha za Kifua Kikuu na Ukoma katika vituo vyote vya matibabu nchini utafanywa. Sambamba na hili, Mpango utaendelea kuelimisha jamii kwa kutumia vipeperushi, mabango na kutoa habari kwa njia ya luninga na radio jinsi ya kujikinga na maambukizi, kutambua mapema na taratibu za kufuata wakati wa matibabu ya magonjwa ya Kifua Kikuu na Ukoma. Wizara inategemea kuanzisha huduma kwa wagonjwa wenye Kifua Kikuu sugu (Multi Drug TB) katika hospitali ya Kibong oto iliyopo Wilayani Hai na kuanzisha mpango wa kutumia dawa za mseto zilizochanganywa pamoja (4 Fixed Dose Combinations) kutibu Kifua Kikuu katika Wilaya 6 za mwanzo za majaribio. Aidha, Wizara itaendelea na utekelezaji wa mpango wa pamoja wa kudhibiti uambukizo wa Kifua Kikuu na UKIMWI katika wilaya za Temeke, Korogwe na Iringa mjini. Bado jitihada za pamoja zinahitajika katika kuelimisha jamii kutambua dalili za Kifua Kikuu na Ukoma, kujitokeza kufanya uchunguzi na kuanza matibabu mapema ambayo hutolewa bila malipo katika vituo vya kutolea huduma za afya. 17

2.3.4 Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho na Kudhibiti Ugonjwa wa Usubi Katika kipindi cha mwaka 2004/2005 Wizara imetekeleza azimio la kimataifa la kutokomeza upofu unaozuilika duniani ifikapo mwaka 2020 (Vision 2020 ) kwa kukamilisha na kuuzindua rasmi Mpango/Mkakati wa miaka mitano (2004-2008) wa Huduma za Macho Kitaifa. Mpango/Mkakati huu unatoa dira na mwelekeo wa Huduma za Macho katika jitihada za kudhibiti upofu ambao vyanzo vyake vikuu ni mtoto wa jicho, ukungu wa kioo cha jicho unaosababishwa na Trachoma, upungufu wa Vitamin A na Surua, presha ya macho, matatizo ya kuona yanayorekebishwa na lensi za miwani pamoja na Kisukari. Tanzania ni mojawapo ya mataifa ya kwanza kabisa kukamilisha Mpango Mkakati huu wa Kitaifa. Vilevile, katika kipindi hiki Wizara imeweza kutoa tiba ya ugonjwa wa Trachoma kwa kutumia dawa ya Zithromax kwa mtindo mpya unaoitwa District Wide Approach katika Wilaya 6 za Sikonge, Handeni, Dodoma vijijini, Tunduru, Magu na Ruangwa ambapo watu 1,186,913 walitibiwa ikiwa ni juhudi za kutokomeza ugonjwa wa Trachoma ulimwenguni ifikapo mwaka 2020. Wizara pia imeandaa Mpango Mkakati wa miaka mitano (2004-2008) wa kudhibiti Ugonjwa wa Trachoma ambao unatoa dira na mwelekeo wa kuzuia upofu unaosababishwa na ugonjwa wa Trachoma, ugonjwa ambao unakadiriwa kuathiri takriban wilaya 50 hapa nchini. Ili kuharakisha utokomezaji wa upofu utokanao na Trachoma, Shirika la Afya Duniani limetoa mwongozo mpya wa utoaji wa dawa ya Zithromax inayotumika kutibu na kuzuia Trachoma, dawa inayotolewa kwa msaada na kampuni ya Pfizer kupitia Shirika la Kimataifa la kudhibiti Trachoma (International Trachoma Initiative). Mwongozo huu ulipelekea kufanyika kwa utafiti wa awali ili kuweza kujua kiwango cha ugonjwa huu katika ngazi ya wilaya. Wizara kwa msaada wa shirika la Kimataifa la kudhibiti Trachoma imefanikiwa kukamilisha utafiti huo katika Wilaya thelathini zenye ugonjwa huu. Utafiti huu bado unaendelea katika Wilaya 20 zilizobakia. Tanzania ni nchi ya kwanza kufanya utafiti huu kulingana na mwongozo mpya na inachukuliwa kama nchi ya mfano kwa nchi nyingine ambazo zina tatizo la ugonjwa huu kulingana na mafanikio yaliyojitokeza. Matokeo ya awali ya utafiti huu yameonyesha kuwa wilaya 26 kati ya 30 zina ugonjwa huu kwa kiwango cha zaidi ya asilimia 10. Mpango wa Taifa wa kudhibiti ugonjwa wa Usubi uliweza kugawa dawa ya Mectizan katika vijiji 650 vilivyopo katika Wilaya 14 ambazo ni Ulanga, Kilombero, Kilosa, Songea, Mbinga, Tunduru, Ludewa, Rungwe, Kyela, Muheza, Mvomero, Morogoro, Korogwe, na Lushoto. Jumla ya wananchi 2,948,862 walipatiwa dawa hii katika kipindi cha mwaka 2004/2005. Wizara inatarajia kugawa dawa ya Mectizan kwa wananchi wapatao 3,000,000 katika kipindi hiki. Malengo ya Mpango wa Taifa wa Huduma za Macho na Kudhibiti ugonjwa wa Usubi mwaka 2005/2006 Katika kipindi cha 2005/2006 Wizara inatarajia kuongeza Wilaya 10 zaidi katika mpango wa kudhibiti ugonjwa wa Trachoma nchini kwa kutumia mtindo mpya wa District Wide- Approach. Jumla ya Wilaya 8 kati ya hizo zinatarajiwa kutolewa dawa ya Zithromax kwa wananchi wake. 18

Wilaya zitakazojumuishwa katika mpango huo ni Kongwa, Kilosa, Meatu, Iramba, Singida vijijini, Igunga, Simanjiro na Mkuranga ambapo watu wapatao 2,300,000 wanatarajiwa kupatiwa matibabu ya ugonjwa wa Trachoma. Wizara inatarajia pia kugawa dawa ya Mectizan kwa ajili ya tiba ya ugonjwa wa Usubi (mass treatment) kwa wananchi wapatao 3,000,000 katika vijiji 690 vilivyoko katika Wilaya 15 za Ulanga, Kilombero, Kilosa, Songea, Mbinga, Tunduru, Ludewa, Rungwe, Kyela, Muheza, Mvomero, Morogoro vijijini, Korogwe, Lushoto na Tunduru. 23.5 Huduma ya Elimu ya Afya Kwa Umma Kwa mwaka 2004/2005, kazi ya kuelimisha na kuhamasisha jamii ishiriki katika kutambua na kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya ki-afya yanayoisibu iliendelezwa. Aidha, Wizara inaendelea kukuza uwezo wa Kamati na Bodi za Afya za Wilaya ili ziweze kupanga, kutekeleza, kufuatilia na kutathmini huduma za Elimu ya Afya katika Jamii. Hii ni pamoja na kuwezesha Kamati na Bodi za Afya kubuni mikakati ya mawasiliano ya afya na kuandaa vielelezo vya afya vyenye uwezo wa kuleta mabadiliko yanayohitajika katika kuboresha afya ya jamii. Matarajio ya Huduma ya Elimu ya Afya kwa Umma mwaka 2005/2006 Katika kipindi cha 2005/2006, Kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma kitaendelea kushirikiana na wadau mbali mbali kuelimisha wananchi mbinu za kubadili tabia na mitindo ya maisha inayohatarisha afya zao. Aidha, Kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma kitaimarisha uratibu na kupanua wigo wa shughuli za utoaji Elimu ya Afya kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya habari vilivyopo katika jamii yetu, ikiwa ni pamoja na sanaa kwa maendeleo, ili kuweza kufikisha ujumbe wa afya kwa wananchi wengi. 2.3.6 Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto Katika kipindi cha 2004/2005, huduma maalum kwa wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano ziliendelea kutolewa bila malipo katika vituo vyote vya kutolea huduma vya Serikali. Huduma hizo ni pamoja na huduma kwa wanawake wajawazito, huduma za kujifungua, chanjo, matibabu kwa watoto wagonjwa wenye umri chini ya miaka 5 na uzazi wa mpango. Aidha, Wizara ilihakikisha upatikanaji na usambazaji wa dawa mbali mbali za uzazi wa mpango unafanyika nchini kwa kushirikiana na wahisani mbalimbali. Tathmini ya kina ya kutambua hali halisi ya uwezo wa vituo vyetu katika kukabiliana na dharura ya uzazi pamoja na rufaa imefanyika. Taarifa kamili itakuwa tayari Mwezi Julai 2005. Matokeo yatatumika katika kuimarisha mikakati iliyopo ya kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi ambapo wilaya zitakuwa ni watekelezaji wakuu. Aidha, tathimini ya kitaifa kuhusu hali halisi ya Afya ya Uzazi na Mtoto hapa nchini imefanyika (Tanzania Demographic Health Survey) kwa kushirikiana na National Bureau of Statistics. Matokeo ya awali yatapatikana mwezi Septemba 2005. Tathmini hii itatupatia takwimu ya hali halisi ya sasa ya vifo vya wanawake vinavyotokana na uzazi kitaifa. 19

Katika kipindi cha 2004/2005, watoa huduma na wakufunzi 130 walipata mafunzo rejea kuhusu uzazi wa mpango kutoka mikoa ya Dodoma, Kilimanjaro, Morogoro, Tanga, Lindi, Mbeya, Pwani na Mwanza. Pia, watoa huduma 100 kutoka mikoa ya Kilimanjaro, Dodoma, Tanga, Mtwara, Morogoro, Lindi, Mbeya, Mwanza na Pwani walipata mafunzo rejea ya utoaji huduma za wajawazito ikijumuisha matibabu ya tahadhari na kutoa kinga kwa wajawazito dhidi ya Malaria na upimaji wa ugonjwa wa Kaswende. Matarajio ya Huduma ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto mwaka 2005/2006 Wizara ya Afya itaendelea kuboresha huduma za afya ya uzazi, mama na mtoto bila malipo ikiwa ni huduma za matibabu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano, chanjo, uzazi wa mpango, huduma kwa wanawake wajawazito ambao watahudhuria kliniki na kujifungua katika vituo vya kutolea huduma vya Serikali. Aidha, Wizara itaendelea kununua na kusambaza dawa za uzazi wa mpango nchi nzima kwa kushirikiana na wahisani. Wizara imetenga fedha kiasi cha shilingi billion 6.8 kwa ajili ya manunuzi hayo na usambazaji. Wizara imepanga kutoa mafunzo mbalimbali katika maeneo ya uzazi wa mpango (100), uzazi salama (80), Afya ya uzazi kwa vijana (40) kutoka katika mikoa ya Kilimanjaro, Dodoma, Tanga, Mtwara, Morogoro, Lindi, Mbeya, Mwanza na Pwani. Ufuatiliaji na usimamizi wa masuala ya afya ya uzazi, mama na mtoto utafanyika katika mikoa saba hapa nchini. Uhakiki wa utumiaji wa dawa za uzazi wa mpango katika maghala ya MSD makao makuu na Kanda (6), pamoja na zile za baadhi ya Wilaya katika Kanda zote saba za Afya ya Uzazi na Mtoto utafanyika ili kuboresha utunzaji wa dawa husika. 2.3.7 Mkakati wa Kutibu Magonjwa ya Watoto kwa Uwiano (Intergrated Management of Childhood Illness-IMCI) Wizara ikishirikiana na wahisani iliendelea kutekeleza mkakati wa Udhibiti wa Magonjwa ya Watoto kwa Uwiano unaolenga kupunguza vifo vya watoto hasa vinavyotokana na Malaria, Kuharisha, Pneumonia, Surua na Utapiamlo. Katika kipindi cha 2004/2005, Wilaya 87 zimetekeleza mkakati wa IMCI. Jumla ya Wahudumu wa Afya 300 wamepata mafunzo kuhusu stadi za kumtibu mtoto. Wahudumu 40 kutoka hospitali 7 wamepata mafunzo juu ya huduma ya dharura na kuboresha huduma kwa mtoto aliyezidiwa. Aidha, jamii imeendelea kuelimishwa juu ya mienendo inayoboresha afya ya mtoto. Mienendo hii inakazia lishe kwa mtoto, Makuzi ya Mwili na Akili, pamoja na Uzuiaji wa Magonjwa ya Watoto. Mafunzo haya yametolewa hadi ngazi ya kaya katika Wilaya 13. Matarajio ya Udhibiti wa Magonjwa ya Watoto kwa Uwiano (IMCI) mwaka 2005/2006 Huduma za Afya na matibabu kwa watoto chini ya miaka mitano zitaendelea kuboreshwa katika ngazi zote. Wizara inatarajia kutoa mafunzo ya stadi za kutibu watoto kwa wahudumu wa afya na wakurufunzi 160. Mafunzo ya huduma ya dharura kwa wahudumu wa afya yatafanyika kwa wahudumu 30 na mafunzo ya wakurufunzi ngazi ya Taifa 50 na ngazi ya Wilaya 200 watapata mafunzo ya mienendo inayoboresha Afya ya Mtoto. 20

2.3.8 Mpango wa Taifa wa Chanjo Huduma za chanjo zimeendelea kutolewa nchi nzima kwa watoto wanaostahili kupata chanjo hizo kama juhudi za serikali za kupunguza vifo na magonjwa ya watoto yanayozuilika kwa chanjo. Magonjwa hayo ni Kifua Kikuu, Dondakoo, Kifaduro, Pepopunda, Polio, Surua na Homa ya ini. Viwango vya chanjo vimeendelea kuongezeka vikilinganishwa na viwango vya mwaka uliopita DPT HB3 kutoka 89% hadi 91%, Measles toka 90% hadi 93% Polio toka 92% hadi 93%, Kifua Kikuu kutoka 94% hadi 95%. Mafanikio haya yametokana na juhudi za serikali, jamii wadau mbalimbali pamoja na GAVI. Matarajio ya Mpango wa Taifa wa Chanjo mwaka 2005/2006 Katika kipindi cha mwaka 2005/2006, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na mikoa itaendelea kusimamia huduma za chanjo katika ngazi za Wilaya na itaendelea kutoa vitendea kazi na chanjo ili kuhakikisha watoto wote wanaostahili chanjo wanapata chanjo. Aidha, juhudi zitafanywa ili kutokomeza polio, kupunguza magonjwa ya surua, kufuta pepopunda kwa watoto wachanga na kupunguza vifo zitaendelea kuimarishwa. Wizara pia itaendelea kufanya tathmini ya magonjwa mengine yanayozuilika kwa chanjo ambazo hazijaanza kutumika hapa nchini. 2.3.9 Huduma za Afya Shuleni Katika mwaka 2004/2005 Wizara ilisambaza Kadi za kupimia Afya za wanafunzi katika Manispaa za IIala, Temeke na Kinondoni. Waratibu wapatao 150 kutoka ngazi ya mkoa na wilaya walipatiwa mafunzo juu ya Udhibiti wa Magonjwa ya Kichocho na Minyoo mingine. Aidha, utafiti kuhusu ugonjwa wa Kichocho katika shule za msingi umefanyika katika Wilaya zote nchini. Matarajio ya Huduma za Afya Shuleni mwaka 2005/2006 Katika mwaka 2005/2006, Wizara ya Afya inategemea kutoa mafunzo ya Huduma ya kwanza kwa Waratibu wa Afya Shuleni ngazi ya Wilaya, kuhamasisha Wilaya kuchangia katika kuchapisha kadi ya kupima afya za wanafunzi kwa shule za awali hadi sekondari. Utoaji wa dawa za Kichocho /Minyoo kwa wanafunzi pia utatekelezwa katika maeneo yaliyoathirika. 2.3.10 Afya ya Mazingira Katika mwaka 2004/2005, Wizara imeimarisha udhibiti wa taka za hospitali (Health care Waste Management) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa kuendesha mafunzo juu ya udhibiti taka za hospitali na ujenzi wa matanuru katika hospitali za Wilaya za Kilosa na Mahenge, Hospitali ya Ocean Road na Hospitali ya Rufaa ya Kibongoto. Aidha, Wizara imeboresha na kuinua hali ya Afya na Usafi wa Mazingira kwa kuendesha mashindano ya Afya na Usafi wa Mazingira nchini. Mashindano haya yalishirikisha Halmashauiri za Jiji la Mwanza, Manisipaa 12, Halmashauri za Miji 9 na Halmashauri 114 za Wilaya nchini. Ili kuinua kiwango cha usafi na ubora wa vyoo, kalibu (Moulds) za kutengenezea mabamba (slab) 560 zilitengenezwa na kusambazwa katika Wilaya za Rungwe, Bagamoyo, Kisarawe, Monduli na Mufindi pamoja na Mkoa wa Kigoma ili zitumike kujengea vyoo bora. 21

Aidha, Wizara iliandaa na kusambaza miongozo ya utekelezaji wa huduma za Afya ya Mazingira nchini Miongozo na mikakati iliyoandaliwa ni pamoja na:-. Mwongozo wa Mafunzo ya Mbinu Shirikishi Jamii katika kuboresha tabia za Afya na Usafi wa Mazingira Mwongozo wa Udhibiti wa Taka (Waste Management Policy Guideline) Mkakati wa Kitaifa wa Afya na Usafi wa Mazingira (National Environmental Health, Hygiene and Sanitation Strategy) mkakati huu unazingatia malengo ya kuondoa umaskini nchini pamoja na Malengo ya Maendeleo ya Milenia (Millenium Development Goals). Matarajio ya Afya ya Mazingira mwaka 2005/2006 Katika kipindi cha 2005/2006, Wizara ya Afya inakusudia kuanzisha Vijiji bora kwa kila Mkoa ambavyo vitakidhi mahitaji yote ya kiafya. Tunatarajia kuanza na Wilaya tano kwa kuchagua Kijiji kimoja kila Wilaya. Aidha, Wizara itaendelea kushirikiana na Wizara mbali mbali, jumuia za kimataifa, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali (NGOs) na jamii katika upangaji mipango mbinu shirikishi jamii ili kuboresha hali ya afya na usafi wa mazingira katika mikoa yote. Aidha, Wizara itaanza kutekeleza Mpango maalum wa Kudhibiti Taka za Hospitali (Health Care Waste Management) ili kudhibiti hali ya uambukizi wa maradhi kwa watoa huduma, wateja na jamii kwa jumla kwa vile mara nyingi taka zitokanazo na huduma za afya nchini zimekuwa zikionekana zikizagaa ovyo mahali zisipotakikana. Mpango huu utatekelezwa kwa muda wa miaka mitano 2005/06 2009/2010 katika mikoa yote. Mpango huu utaanza kwa kuzihusisha hospitali za Halmashauri zote za Wilaya, hospitali za mikoa na hospitali za rufaa nchini. Vilevile, itaratibu mapitio ya sheria ya Drainage and Sewerage Ordinance Cap 259 ya mwaka 1955 inayosimamia udhibiti wa maji taka nchini. Sheria hii ni ya zamani sana na imepitwa na wakati itapitiwa na kufanyiwa marekedisho yanayokidhi haja ya hali ilivyo kwa wakati huu. Katika kupima maendeleo ya Afya ya Mazingira Wizara itaendeleza mashindano ya Afya na Usafi wa Mazingira nchini, ambayo yataendelea kujumuisha halmashauri zote nchini (Jiji, Manisipaa, Mji na Wilaya). Lengo kuu la mashindano haya ni kushirikisha wananchi, sekta binafsi katika kuboresha hali ya usafi wa mazingira katika maeneo yao 2.3.11 Huduma za Afya Mipakani Katika kuhakikisha kuwa udhibiti wa magonjwa ya kuambukiza kutoka nje ya nchi unaimarika, Wizara imeboresha huduma za Afya Mipakani ambapo maafisa wa Afya wamepata mafunzo mbalimbali ikiwemo jinsi ya kupambana na majanga. Pia, vituo vimeimarishwa kwa kuongeza vitendea kazi na kuajiri wataalam wa afya katika vituo vya Afya. Katika mwaka huu wa fedha, zaidi ya tani 5,470,000 za vyakula zilikaguliwa ambapo tani 40,800 ziliharibiwa baada ya kuthibitika kuwa hazifai kwa matumizi ya binadamu. 22

Matarajio ya Huduma za Afya Mipakani mwaka 2005/2006 Wizara itaendelea kuhakikisha kuwa magonjwa ya kuambukiza ya kimataifa yanadhibitiwa kwa kufuata sheria za Afya za Kimataifa. Vituo vya mipakani vitapatiwa nyenzo na vitendea kazi vya kisasa ikiwemo usafiri. Pia, udhibiti wa uingizwaji wa vyakula, dawa na vipodozi visivyokidhi viwango vya Afya utaimarishwa kwa kushirikiana na wadau wengine kwa Halmashauri zote nchini 113. 2.3.12 Afya katika Sehemu za Kazi Kwa kuzingatia umuhimu wa Afya ya Wafanyakazi hususan maeneo ya viwanda, ujenzi na mashamba, Wizara imefanya uhamasishaji wa kamati za Halmashauri za Wilaya 48 juu ya uainishaji wa huduma za afya sehemu za kazi na huduma za afya ya msingi. Shughuli za usimamizi na ufuatiliaji wa afya sehemu za kazi zimefanyika katika Halmashauri 12. Aidha, mafunzo kwa wachimbaji wadogo wadogo 70 wa madini katika Mikoa ya Arusha na Mwanza yamefanyika. Matarajio ya Afya katika Sehemu za Kazi mwaka 2005/2006 Kwa kutambua umuhimu wa afya ya wafanyakazi mahali pa kazi, Wizara imeweka mikakati ya kuwafikia na kuwahamasisha wafanyakazi wote juu ya madhara yatokanayo na kazi ifikapo 2015. Aidha Wizara imeweka mikakati endelevu inayotilia mkazo juu ya uzuiaji wa maambukizi ya UKIMWI mahali pa kazi. Ili kufikia azma hii madaktari 118 wa Halmashauri za Wilaya watapatiwa mafunzo juu ya uboreshaji wa afya ya wafanyakazi sehemu za kazi. 2.3.13 Huduma za Afya Wilayani (District Health Services) Utekelezaji wa mabadiliko ya Sekta ya Afya ngazi ya Wilaya yalianza kutekelezwa kwa awamu tatu tofauti. Awamu ya kwanza ilikuwa kwa Halmashauri 37 kwa mwaka 2000, awamu ya pili 2002 Halmashauri 45 na awamu ya mwisho Halmashauri 31 na kufanya jumla ya Halmashauri za Wilaya, Jiji, Miji na Manispaa 113. Utekelezaji ulianza kwa kufundisha Halmashauri zote namna ya kuandaa Mipango Kambambe ya Afya ya Halmashauri (Comprehensive Council Health Plan) na kutayarisha taarifa za robo mwaka za utekelezaji zikihusu fedha na kazi halisi zilizotekelezwa (quarterly progress implementation reports technical and financial). Mpaka sasa Halmashauri zote zinaandaa, kutekeleza na kutoa taarifa ya utekelezaji wa mipango hii kama ilivyopangwa. Mabadiliko yamekwenda sambamba na uundaji wa taasisi na miundo ya kuwezesha jamii kushiriki katika uendeshaji, umiliki na usimamizi wa huduma za afya. Vyombo hivyo ni Bodi za Huduma za Afya za Halmashauri na Kamati za Vituo vya Tiba. (Council Health Service Boards and Health Facility Governing Committees). Aidha, mpaka sasa Halmashauri zote 113 zimehamasishwa na kuridhia uundaji wa Bodi za afya na Kamati za Vituo vya Tiba. Hati Rasmi pamoja na Sheria Ndogo ya Mfuko wa Afya ya Jamii zipo katika ngazi ya utekelezaji kwa kuwa zikitoka Wilayani zinapelekwa mikoani ili kupitiwa na kuandikiwa barua na kupelekwa kwa Waziri mwenye dhamana na Serikali za Mitaa. Mwisho Katiba na Sheria kuandikwa kama Sheria na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali. 23

Mpaka sasa kati ya Halmashauri 113 zilizohamasishwa ni Halmashauri 70 tu ambazo zimezindua Bodi za Huduma za afya na Kamati za vituo vya Tiba na zinafanyakazi. Wizara pia kwa mwaka jana ilibadilisha magari mapya 24 kwenye Halmshauri kwa ajili ya ufuatiliaji na usambazaji wa dawa na vifaa tiba na kinga kwenye vituo vya kutolea huduma. Matarajio ya Huduma za Afya Wilayani (District Health Services) mwaka 2005/2006 Mwaka 2005/06 Wizara itakamilisha uzinduzi wa Bodi za Afya katika Halmashauri 63 zilizobakia mara Sheria zao zitakapotangazwa kwenye Gazeti la Serikali. Sambamba na uzinduzi na uhamasishaji wa Bodi na Kamati za vituo vya Tiba, pia Halmashauri zitaendelea kuhamasishwa ili kuanzisha Mfuko wa Afya wa Jamii (Community Health Fund). Kwa vile hadi sasa Halmashauri za Wilaya 40 kati ya 113 zinatekeleza Mfuko wa Afya wa Jamii. Kwa kuwa Mfuko wa Afya wa Jamii unaendana na uzinduzi wa Bodi za Afya za Halmashauri inategemewa kwa mwaka wa 2005/06 kusaidia Halmashauri 73 zilizobakia ziwe zinatekeleza Mfuko huu. Wizara kwa mwaka 2005/06 itaendelea kutoa usimamizi wa kitaalam kwa Halmashauri juu ya uendeshaji wa huduma za afya katika ngazi ya Wilaya ili kuboresha huduma na kuendelea kubadilisha na kupeleka magari mapya 10 kwenye Halmashauri kwa ajili ya ufuatiliaji na usambazaji wa dawa na vifaa muhimu vya afya. Wizara itatoa mafunzo juu ya uainishaji wa MKUKUTA (NSGPR), Kitita cha Huduma Muhimu za Afya (NEPHI), Mpango wa Mabadiliko ya Afya wa miaka mitano (HSSP) na Mipango Kabambe ya Halmashauri CCHP). Aidha, mafunzo yatatolewa kwa timu za uandaaji Mipango ya Afya ya Halmashauri jinsi ya kutumia teknolojia ya kisasa ya kukotoa hesabu za bajeti za mipango ya Halmashauri (CCHP) kwa kulinganisha na mzigo wa magonjwa (Burden of Disease). 2.3.14 UKIMWI Katika kukabiliana na janga hili la UKIMWI nchini, Wizara ilitekeleza Mkakati wa Sekta ya Afya wa Kudhibiti UKIMWI 2003-2006, ambao ni pamoja na Huduma ya Damu Salama, kutoa Ushauri Nasaha, Kufuatilia Mwenendo wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI katika Jamii, pamoja na Huduma ya Magonjwa ya Ngono (Sexually Transmitted Infections STI). Mwaka 2004/05, kulikuwa na azma ya serikali ya kuanzisha mpango wa kitaifa wa kutoa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI. Mpango huu uliweza kununua dawa kwa kutumia fedha zilizotengwa na Serikali. Hadi sasa wagonjwa wapatao 4,200 wameanzishiwa dawa hizo katika vituo hivyo 32. Aidha, dawa zaidi zimeagizwa na zinategemewa kupokelewa hapa nchini kuanzia mwishoni wa mwezi April 2005. Dawa hizo zitatosha kuwaanzishia wagonjwa waliokusudiwa dawa wapatao 44,000. Aidha, katika kujenga uwezo wa hospitali wa kupima wagonjwa wa UKIMWI na kutambua hatua ya ugonjwa kwa lengo la kuanzisha matibabu, machine za Facs Count zinazopima viwango vya chembechembe za CD4 zipatazo 20 zimenunliwa na kusambazwa katika hospitali zote za rufaa na baadhi ya hospitali za mikoa. Mashine nyingine nane (8) zimeagizwa kwa ajili ya hospitali za mikoa iliyobakia. 24

Aidha, mafunzo kwa wataalam wa afya ambao watatoa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI kwa wagonjwa yametolewa kwa wataalam mbalimbali wa afya wapatao 492 kutoka vituo 96 vya kutolea huduma za Afya. Vituo hivyo 96 vinajumuisha hospitali zote za rufaa na mikoa, baadhi ya hospitali za Wilaya, hospitali za Mashirika ya dini na Watu Binafsi. Huduma za kutoa madawa ya kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI zitaendelezwa kwa awamu kulingana na uwezo wa kifedha wa Serikali. Nchi yetu ina idadi kubwa ya watu wanaaohitaji dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI. Idadi hiyo ambayo inakisiwa kufikia watu 500,000 ni kubwa sana kulinganisha na uwezo. Serikali itaendelea kuongeza idadi ya wagonjwa wanaopata huduma hii kwa awamu mpaka wote wafikiwe. Matarajio ya Mpango wa kukabiliana na Ugonjwa wa UKIMWI mwaka 2005/2006 Katika kuendelea kudhibiti ugonjwa wa UKIMWI na kutoa huduma kwa wale walioathirika na ugonjwa huu, Wizara mwaka 2005/2006 itaendelea kufuatilia mwenendo wa maambukizi ya virusi vya UKIMWI katika jamii kwa kufuatilia wajawazito katika kliniki 93 zilizopo kwenye mikoa 15 ya Tanzania Bara. Matokeo ya ufuatiliaji huu yatatoa picha kuhusu kuenea kwa virusi vya UKIMWI katika jamii na matokeo ya mikakati inayoendelea ya kudhibiti UKIMWI. Katika kipindi hiki, Wizara itakamilisha kuandaa utafiti wa kufuatilia usugu wa virusi vya UKIMWI kwa madawa yanayotumika hivi sasa kupunguza makali ya UKIMWI. Hivyo, ufuatiliaji wa usugu wa madawa ya kupunguza makali ya UKIMWI (HIV drug resistance threshold surveys) utaanzishwa katika mkoa wa Dar es Salaam ambapo dawa za kupunguza makali ya UKIMWI yalianza kutumika miaka kadhaa kabla ya serikali kuanza mpango wa kutoa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI kwa wagonjwa wa UKIMWI. Matokeo yake yatasaidia katika kugundua dawa ambazo tayari Virusi vya UKIMWI vimekwisha kuwa sugu nazo kiasi kwamba haziwezi kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI na hivyo kusaidia wataalam kutoa maelekezo ya dawa zinazofaa. Wizara itanunua na kusambaza dawa za kupunguza makali ya UKIMWI katika vituo 180 vilivyoteuliwa kutoa huduma hiyo kote nchini ili kuwafikia wagonjwa wapya 56,000 ili kufikia lengo jipya lililowekwa la kuwafikia wagonjwa 100,000 nchini kote ifikapo Juni 2006. Vituo vipya vitakavyohusishwa katika mpango huu ni pamoja na hospitali zote za Wilaya na hospitali za binafsi ziliopo kwenye mikoa ya pembezoni na mikoa iliyo na viwango vya maamukizi ya UKIMWI zaidi ya asilimia saba. Huduma za ushauri nasaha na upimaji wa hiari zitaendelea kutolewa katika vituo 521 vinavyotoa huduma ili kuweza kutoa ushauri nashaha kwa wagonjwa wote 100,000 watakaokuwa kwenye tiba ya dawa za UKIMWI. Aidha, tutahakikisha mafunzo kwa wataalam wa kutoa huduma za dawa za kupunguza makali ya UKIMWI katika kila kituo yatatolewa na angalau watalam wanne ambao wameshapatiwa mafunzo wanakuwepo katika vituo vya huduma. Wizara itaendelea kutoa huduma za Magonjwa ya Zinaa katika mikoa yote 21 pamoja na kuelimisha jamii kuhusu ugonjwa wa UKIMWI hususan kuacha kuwanyanyapaa wagonjwa wa UKIMWI na kuzingatia matumizi sahihi ya dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI. 25

2.3.15 Mradi wa Uimarishaji Huduma Muhimu za Afya (MUHUMA) TEHIP Mradi wa Uimarishaji Huduma Muhimu za Afya (MUHUMA) umekuwa ukitekelezwa katika Wilaya mbili za Morogoro vijijini na Rufiji toka Mwaka 1997 mpaka mwaka 2004 ulipofikia kikomo kama mradi. Utafiti umeonyesha kuwa kasi ya vifo imepungua katika Wilaya zote mbili kwa asilimia zaidi ya 55% kwa watoto chini ya miaka mitano na asilimia 18% kwa watu wazima. Kupungua huku kumeziweka Wilaya hizo mbili kwenye matumaini ya kufikia moja ya malengo ya milenia ya Umoja wa Mataifa ya kupunguza kasi ya vifo miongoni mwa watoto chini ya miaka mitano kwa theluthi mbili ifikapo mwaka 2015. Kufuatana na matokeo haya, Wizara ya Afya ikishirikiana na wadau wengine imeanza mikakati ya kupata fedha za kueneza mbinu na nyenzo zilizobuniwa na kufanyiwa kazi katika Wilaya hizo mbili katika Wilaya zote nchini. Dhana ni kuwa endapo nchi nzima itatekeleza yaliyofanywa Morogoro na Rufiji basi kasi ya vifo vya watoto wadogo na wakubwa itapungua na hivyo Tanzania kuwa miongoni mwa nchi za mwanzo kutekeleza mpango huo. 2.4 Idara za Tiba Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/2005 2.4. 1 Huduma za Uchunguzi wa Magonjwa Mradi wa uimarishaji wa huduma za X-ray na Ultrasound ulikabidhiwa kwa Serikali kutoka kampuni ya Philips Medical Systems ya nchi ya Uholanzi ili tuweze kuuendeleza wenyewe. Makabidhiano hayo yalifanyika Jijini Mwanza katika hospitali ya Bugando tarehe 22 Februari 2005, ambapo Mheshimiwa Rais alikabidhiwa mashine kubwa na maalum ya Ultrasound kutoka kwa mwakilishi wa Kampuni hiyo yenye thamani ya takriban fedha ya kitanzania shilingi milioni 88. Mashine nyingine ilipelekwa Zanzibar katika hospitali ya Mnazi mmoja tarehe 14 Machi, 2005. Aidha, Wizara iliagizwa kusimamia ukarabati na kinga ya matengenezo ya mashine hizo baada ya mradi kwisha ifikapo mwishoni mwa mwaka 2005. Vilevile, Wizara imekamilisha taratibu zote za kupeleka Bungeni muswada wa sheria inayohusu usajili wa wanataaluma ya mionzi ili kuboresha huduma za mionzi. Kuhusu usimamizi na utekelezaji wa huduma za karakana zetu za Kanda, Wizara imeendelea kuziimarisha kwa kuzipatia vipuli, vifaa na nyenzo za utekelezaji wa matengenezo ya mashine hizo za kutolea huduma za Afya. Kuhusu uimarishaji wa maabara za hospitali ili ziweze kufuatilia wagonjwa wanaopatiwa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI, Wizara imekwishaweka mashine 20 za kupima CD4 katika hospitali zote za rufaa na mikoa 16. Mashine nyingine 8 za CD4 na dawa zake zimeshawasili kwa ajili ya mikoa iliyobaki na hospitali za manispaa za Dar es Salaam. Vilevile, mashine kwa ajili ya vipimo vingine (Clinical Chemistry and Haematology) kwa ajili ya hospitlai 10 za mikoa na 13 za Wilaya zimegizwa. Vipimo hivyo ni kwa ajili ya kufuatilia athari za ARV (Toxicity follow up) kwa wagonjwa wanaotumia. Kuhusu huduma ya damu salama, ujenzi wa vituo vya kanda vya upatikanaji wa damu (Zonal Blood Transfusion Centres- ZBTC) umekamilika katika Kanda za Ziwa, Kasikazini na Nyanda za juu Kusini. Kwa upande wa Kanda ya Mashariki, ujenzi umeshaanza Dar es Salaam na kanda ya Kusini ujenzi haujaanza. Mwongozo wa huduma za damu salama umekamilika. 26

Matarajio ya Huduma za Uchunguzi wa Magonjwa mwaka 2005/2006 Wizara itaingia mkataba na Kampuni ya Philips Medical Systems katika kuhakikisha kuwa, mashine za X-ray, Ultrasound na vifaa vingine chini ya mradi wa kuimarisha huduma za uchunguzi wa magonjwa nchini zinadumu kwa miaka mingi. Katika mkataba huo mafunzo maalum hasa yale ya mashine zenye teknolojia ya hali ya juu hususan X-ray na Ultrasound yatatolewa kwa watumiaji, makandarasi na mafundi wetu waliopo kwenye karakana za Kanda. Mkataba huu utakuwa wa miaka 5 kuanzia Januari 2006 hadi Desemba 2010. Wizara pia itaendelea kuvifanyia matengenezo ya mara kwa mara vifaa tiba kupitia karakana za kanda kwa maeneo yote yanayotoa huduma ya afya kuanzia zahanati hadi hospitali za rufaa, kwa utaratibu utakaopangwa kwa ajili ya utekelezaji wake kufuatana na mwongozo wa Wizara juu ya uboreshaji na matengenezo ya vifaa tiba vya hospitali nchini. Wizara inakusudia kupeleka Bungeni muswada wa sheria inayohusu taaluma ya mionzi nchini katika mwaka 2005/06. Pia Tanzania imepewa heshima na nchi za Afrika ya kuwa mwenyeji wa kongamano la wanataaluma ya Radiologia kutoka Afrika mnamo mwezi Septemba, 2005. Wizara itaendelea kuimarisha huduma za maabara kwa kuagiza mashine nyingine, na vifaa vya maabara kwa ajili ya kufuatilia wagonjwa wanaopatiwa dawa za kusaidia kupunguza makali ya UKIMWI. Aidha, baadhi ya maabara zitaboreshwa kwa kufanyiwa ukarabati ili kukidhi mahitaji ya utoaji wa huduma hizo. Kuhusu huduma ya damu salama, Wizara itakamilisha ujenzi wa Kanda ya Mashariki pamoja na kuanza mipango ya ujenzi wa Kanda za Kusini (Mtwara) na Kati (Dodoma). Wakati huo Kanda za Ziwa, Nyanda za Juu Kusini na Kaskazini zitaanza kazi ya ukusanyaji wa damu salama katika hospitali zetu kwa kushirikiana na Shirika la Msalaba Mwekundu Tanzania. 2.4.2 Huduma za Tiba Asili Mwaka 2002/2003 muswada wa Sheria ya Dawa, Tiba Asili na Tiba Mbadala, ulipitishwa na Bunge. Utekelezaji wa Sheria Namba 23 ya mwaka 2002 utaanza July 2005. Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala tayari limekwisha teuliwa na mamlaka husika kwa mujibu wa Sheria hiyo. Wizara ya Afya imeandaa Kanuni na Miongozo ya usajili wa Waganga wa Tiba Asili na Tiba Mbadala. Usajili wa vituo vya kutolea huduma za Tiba Asili na Tiba Mbadala; nidhamu na maadili kwa Waganga wa Tiba Asili na Tiba Mbadala; usimamizi na usajili wa bidhaa nyinginezo za Asili zinazotumika kwa ajili ya afya ya binadamu. Matarajio ya Huduma za Tiba Asili mwaka 2005/2006 Wizara itaendelea kuwaelimisha Waganga wa jadi na Wadau wa Tiba Asili na tiba mbadala ili kuielewa sheria ya tiba asili na tiba mbadala. Aidha, Wizara itaendelea na ufuatiliaji wa tiba asili na tiba mbadala likiwemo suala la utafiti. 27

2.4.3 Huduma za Afya ya Kinywa Katika mwaka 2004/2005, Wizara ya Afya imefunga vifaa vya Tiba ya Meno (Dental Units) katika Halmashauri za Wilaya zifuatazo: Mbarali, Karatu, Ngorongoro, Simanjiro, Kiomboi, Morogoro Vijijini, Morogoro Manispaa, Mbozi, Hanang, Sikonge, Mpanda, Mvomero, Bariadi, Bukombe, Kilombero, Liwale, Njombe, Ludewa, Sengerema, Geita, Ukerewe, Misungwi, Newala, Mwanga na Kwimba. Pia, vifaa vilifungwa katika hospitali zifuatazo: Iringa, Bombo, Mawenzi, Mt. Meru na KCMC. Aidha dawa na vifaa muhimu vya tiba ya meno vilinunuliwa kwa ajili ya matumizi ya hospitali za mikoa na kwa ajili ya mafunzo vyuoni. Matarajio ya Huduma za Afya ya Kinywa mwaka 2005/2006 Katika mwaka wa fedha 2005/2006 awamu ya pili ya ufungaji vifaa kwa kuzipatia kliniki za meno za Wilaya na Halmashauri viti (Dental Chairs), taa maalum (operating lights) na viti vya kukalia madaktari wa meno wanapofanya kazi (Operating Stools) utaanza. Wilaya/Halmashauri zitakazopatiwa vifaa hivyo ni:- Muheza, Korogwe, Chunya, Ileje, Mbeya Vijijini, Mbeya Manispaa, Mbarali, Rungwe, Kyela, Karatu, Ngorongoro, Simanjiro, Iramba, Morogoro Vijijini, Morogoro Manispaa, Mbozi, Hannang, Singida, Tabora, Sikonge, Mpanda, Musoma, Kigoma, Kilombero, Mvomero, Bariadi, Bukombe, Kishapu, Liwale, Njombe, Ludewa, Bukoba, Karagwe, Sengerema, Geita, Ukerewe, Misungwi, Newala, Mwanga, Kwimba, Dodoma Manispaa, Tarime, Bunda, Biharamulo, Tabora Manispaa, na Mbinga. Pia hospitali zifuatazo zitapatiwa vifaa hivyo; Kibosho, Mbeya Rufaa, Mawenzi, Mt. Meru, Bombo, Iringa, Dodoma, Mbeya Mkoa, Mirembe, Kilema, Bugando, Dareda, Ligula, Maweni, Singida na Bukoba. 2.4.4 Huduma za Afya ya Akili na Vita dhidi ya Dawa za Kulevya Mwaka 2004/2005, Wizara imeendelea kusimamia uboreshaji wa huduma za afya ya akili ngazi ya msingi. Shughuli hizo zinaendelezwa katika mikoa ya Dar es Salaam, Manyara, Mtwara na Mwanza. Toleo rasmi la kwanza la vitabu vya Huduma ya Afya ya Akili ngazi ya Msingi vimechapishwa nakala 4,500 na kusambazwa kulingana na utaratibu wa kutoa mafunzo katika kila Mkoa. Matarajio ya Huduma za Afya ya Akili mwaka 2005/2006 Kitengo kitaendelea na mipango ya kueneza huduma ya afya ya akili ngazi ya msingi kwa kushirikiana na wadau wa ndani na nje katika Mikoa ya Tanga, Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Mwanza kwa kushirikiana na MEHATA na CORDAID na Mkoani Mtwara kwa kushirikiana na shirika la Basic Needs. Mpango wa kutoa Mafunzo kwa watoa huduma ngazi ya msingi utaendelea katika Mikoa ya Dar es Salaam na Manyara. Pia, Wizara inategemea kukamilisha uchapishaji wa mwongozo wa Sera ya Afya ya Akili. 28

2.4.5 Huduma za Hospitali za Mashirika ya kujitolea, Makampuni na Watu Binafsi Katika mwaka 2004/2005, Hospitali mbili za Mashirika ya Dini (Karatu na Mugana) ziliombwa na Halmashauri za Wilaya ya Karatu na Bukoba Vijijini zitumike kama Hospitali Teule. Hospitali hizo tayari zimeanza kutumika kama hospitali Teule za Wilaya hizo. Ruzuku ilibakia kuwa TShs 30,000/= kwa kitanda kwa mwaka. Kulikuwa na ongezeko la vitanda 174 kwa ajili ya kupewa Ruzuku. Jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya vilivyosajiliwa mwaka 2004/2005 ni 53 ambavyo ni 73% kati ya 73 vilivyoombewa usajili. Matarajio ya Huduma za Hospitali za Mashirika ya kujitolea, Makampuni na Watu Binafsi mwaka 2005/2006 Wizara itaanza kutumia Service Agreement katika kufanya makubaliano kati ya Halmashauri za Wilaya na wamiliki wa hospitali za mashirika ya dini. Vile vile, Wizara itajadili maombi ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa kuhusu kutumia hospitali ya Tosamaganga kama hospitali Teule ya Wilaya hiyo. 2.4.6 Huduma ya Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba Mwaka 2004/05, kiasi cha Tshs. 35,175,356,000 zilitumika kununua dawa, vifaa na vifaa tiba kwa matumizi ya hospitali, Zahanati na Vituo vya Afya. Aidha, hospitali za Wilaya, Mikoa na Rufaa ziliendelea na utekelezaji wa uchangiaji wa gharama za dawa chini ya mfumo wa Capitalization of Hospital Pharmacies ambapo wananchi wanalipa nusu ya bei halisi ya dawa. Fedha kutokana na mauzo ya dawa ziliingizwa kwenye mfuko wa dawa (Drug Revolving Fund) kuwezesha hospitali hizo kununua dawa nyingine zilizohitajika. Mwaka 2004/2005, Zahanati mpya 526 na Vituo vya Aya 36 vilivyojengwa na Halmashauri na kwa nguvu za wananchi vilipewa masanduku ya dawa. Aidha, Zahanati 716 na vituo vya afya 88 katika Mikoa ya Kagera, Mara, Mwanza na Shinyanga vilianza kuagiza dawa na vifaa kwa kutumia mfumo wa Indent. Ili kurahisisha utoaji wa dawa na vifaa kwa mfumo huu, sehemu maalum imejengwa katika Bohari ya Mwanza kwa ajili ya kuhudumia Zahanati na Vituo vya Afya hivyo. Kutokana na hatua hiyo, Bohari ya Mwanza sasa imeondokana na mfumo wa usambazaji wa masanduku ya dawa. Wizara pia ilitoa mafunzo ya utekelezaji wa mfumo wa Indent kwa baadhi ya wajumbe wa Kamati za Uendeshaji wa Huduma za Afya katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Tanga. Wajumbe hawa watatoa mafunzo kwa watumishi katika Zahanati na Vituo vya Afya katika mikoa yao ili kuwezesha uagizaji wa dawa na vifaa kulingana na mahitaji na kwa kuzingatia mgao wa fedha na maradhi katika sehemu zao. Bohari ya Dawa iliendelea na usambazaji wa dawa na vifaa vya miradi misonge (vertical programmes) na vya misaada. Katika kipindi hicho, Bohari ya Dawa ilisambaza chanjo, dawa za kutibu Kifua Kikuu na Ukoma, Usubi, Uzazi wa Mpango, Matende, Ngirimaji na magonjwa ya mtegesheo kwa watu waishio na UKIMWI. 29

Matarajio ya Huduma ya Dawa, Vifaa na Vifaa Tiba mwaka 2005/2006 Katika mwaka wa fedha 2005/06, Wizara ya Afya imetengewa jumla ya Tshs. 32,320,996,556 kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vifaa na vifaa tiba kwa matumizi ya Zahanati, Vituo vya Afya na hospitali za Serikali na hospitali Teule kwa matumizi ya kawaida. Pia Serikali imetenga Tshs. 20,000,000,000 kwa ajili ya ununuzi na usambazaji wa dawa na vifaa tiba vya kupunguza makali ya UKIMWI. Wizara ya Afya kupitia Bohari ya Madawa, itasambaza dawa na vifaa katika Zahanati 3,500 na Vituo vya Afya 400. Kati ya hivyo, Zahanati 175 na Vituo vya Afya 25 vitakuwa vipya vilivyojengwa na Halmashauri na nguvu za wananchi. Aidha, katika kuboresha usambazaji wa dawa, vifaa na vifaa tiba, Wizara ya Afya itaendesha majaribio ya mfumo ujulikanao kama Integrated Logistics System katika mikoa ya Dodoma na Iringa. Mfumo huu utawezesha Zahanati, Vituo vya Afya na hospitali kuagiza dawa na vifaa vya kawaida na vile vya miradi na misaada chini ya mfumo mmoja. Mfumo huu unatarajiwa kuiwezesha Wizara kukusanya takwimu za mahitaji na matumizi halisi ya dawa, vifaa na vifaa tiba. 2.4.7 Huduma za kuzuia Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto Katika mwaka 2004/2005 wizara imesambaza huduma ya kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi kutoka kwa mama kwenda kwa mototo katika mikoa 9 zaidi ya Tanzania bara na kufanya huduma hii kupatikana katika hospitali zote za mikoa na 82 za Wilaya. Mikoa hiyo ni Lindi, Dodoma, Ruvuma, Rukwa, Kigoma, Mara, Shinyanga, Tanga na Singida. Vilevile, wizara inashirikiana na wadau mbalimbali ilikuweza kusambaza hudma hii katika hospitali na vituo vya kutolea huduma vinavyomilikiwa na mashirika ya dini. Wizara imeendelea na mpango wa kutoa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI kwa akinamama wajawazito, wazazi wenzao na watoto wao. Mpango huu ambao unaitwa MTCT Plus unaenda sambamba na mpango wa Taifa wa kutoa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI (ART programe) na hivyo umeanza kutekelezwa katika vituo 96 vilivyo katika mpango wa ART. Matarijio ya Huduma za kuzuia Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka kwa Mama kwenda kwa Mtoto mwaka 2005/2006 Katika mwaka 2005/2006 Wizara ya Afya imepanga kupanua huduma ya kuzuia maambukizi ya virusi vya UKIMWI kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT) katika wilaya 20 zaidi ambazo hazina huduma hiyo na kufanya jumla ya wilaya 102 kuwa na huduma hii. Vile vile, Wizara itaendelea kuimarisha huduma ya MTCT Plus ambayo imeanza kutolewa katika vituo vile 96 vilivyo katika mpango wa ART Programme. Lengo ni kuhakikisha akinamama wajawazito walioathirika na VVU na wenye vigezo vya kupata ART wapate huduma hiyo na wale ambao hawana vigezo wakisha jifungua waendelee kufuatiliwa na pindi watakapobainika kuwa wana vigezo wapatiwe huduma ya ART. 30

2.4.8 Huduma ya Matibabu Nje ya Nchi Wizara imefanya mazungumzo na wahisani kutoka nje ya nchi ili kuanzisha hapa nchini huduma ya tiba ya magonjwa ambayo kwa sasa yanatibiwa nje ya nchi. Wahisani hao ni Serikali ya Japan na Serikali ya Watu wa China. Mipango hii imelenga kulipunguzia Taifa gharama za tiba nje ya nchi pamoja na kuwapunguzia wagonjwa maumivu wakati wakingojea kwa muda mrefu kwenda kutibiwa nje ya nchi kutokana na upungufu wa fedha. Matarajio ya Huduma ya Matibabu Nje ya Nchi mwaka 2005/2006 Bajeti itaongezwa ili kuwezesha wagonjwa wengi zaidi kupelekwa kutibiwa nje ya nchi na kuendelea kutoa msaada kwa matibabu ya wagonjwa ambao badala ya kupelekwa kutibiwa nje ya nchi watatibiwa hapa nchini kwa vile wanashindwa kumudu gharama za matibabu hayo. Wizara itaendelea kushirikiana na mashirika na hospitali zinazoanzisha utoaji wa matibabu ambayo kwa sasa yanapatikana nje ya nchi, pamoja na Serikali ambazo zina mpango wa kusaidia nchi kuweza kutoa matibabu kama hayo. 2.5 Huduma ya Utawala na Watumishi 2.5.1 Idara ya Utawala Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/2005 Mwaka wa 2004/2005, Wizara ya Afya imeendelea kutekeleza Sera ya Menejimenti na Ajira katika Utumishi wa Umma ya Mwaka 1999, kwa kuajiri jumla ya Watumishi 148 wa kada mbalimbali za Afya. Aidha, katika kushughulikia maslahi na maendeleo ya watumishi ili kuimarisha utendaji kazi Wizara imewapandisha vyeo watumishi 6,587. Hili ni ongezeko la asilimia 65 ya lengo lililokuwa limewekwa la kuwapandisha vyeo watumishi 4,000. Watumishi wapatao 110 wa kada na ngazi tofauti walifanyiwa upekuzi (vetting) kwa madhumuni ya kuwawezesha kuelewa na kuzingatia misingi ya maadili mema katika utumishi wa Umma kwa mujibu wa Sheria, kanuni na taratibu zilizopo. Msisitizo mkubwa uliowekwa katika mafunzo hayo ulihusu suala zima la matumizi sahihi ya taarifa za Serikali na utii kwa Serikali. Aidha, Wizara iliendelea kutoa mafunzo ya jinsia kwa watumishi ili kuendelea kudumisha Utawala Bora ambapo jumla ya watumishi 744 walipatiwa mafunzo hayo. Pia Wizara ilitoa mafunzo kwa maafisa waandamizi na wa ngazi ya kati kuhusu misingi ya Utawala Bora na mapambano dhidi ya rushwa ili kuzuia matukio ya rushwa na kuziba mianya ya rushwa. Mafunzo haya yaliwahusisha Wakurugenzi wa Wizara ya Afya, Waganga Wakuu wa Mikoa, Waganga Wakuu wa Wilaya, Wakuu wa Vyuo vyote vya Afya nchini na Maafisa wengine. Jumla ya watumishi 1,169 walipatiwa mafunzo hayo. Sambamba na mapambano dhidi ya rushwa, Wizara ilichapisha vijarida 850 vya Mkataba wa Huduma kwa Mteja na kuvisambaza kwa wadau. Lengo lilikuwa kuwafahamisha wateja wetu kuhusu mahusiano yetu na majukumu yetu kwao pamoja na haki na wajibu wao. Mkataba huu unaelekeza pia namna mteja anavyoweza kutuma malalamiko/maoni kuhusu huduma zetu. 31

Matarajio ya Huduma za Utawala na Watumishi mwaka 2005/2006 Wizara ya Afya itaendelea kutoa kipaumbele katika kuimarisha na kuboresha maslahi, maendeleo na utendaji kazi (Capacity building) kwa watumishi wake ili kuimarisha na kuongeza utoaji wa huduma za afya kwa wananchi watakaohitaji huduma hiyo muhimu. Malengo haya yatafikiwa kwa kuajiri watumishi wapya ili kuziba mapengo yaliyopo na kuwapandisha vyeo watumishi waliopo kwa kuzingatia sifa, vigezo na ikama iliyoidhinishwa. Ili kwenda sambamba na mabadiliko yanayoendelea kufanyika katika Sekta ya Afya, Wizara imejiwekea mpango wa kutoa mafunzo ya Huduma kwa Mteja kwa watumishi wake wote (customer care and Public ethics).mafunzo haya yatawahusisha watumishi wapatao 3,336 kutoka Makao Makuu ya wizara, Hospitali tatu za Rufaa, Vyuo vya Afya 108 pamoja na Kanda 6 za mafunzo. Mafunzo hayo yataendeshwa kwa awamu tatu. Aidha, Wizara imejipangia kuanzisha teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Information Communication Technology) ili kuimarisha na kuongeza utoaji wa huduma bora ya upatikanaji na upashanaji wa habari kwa haraka zaidi. Wizara tayari imeanza utoaji wa mafunzo kwa watumishi wake na itaendelea na mafunzo hayo ili kuwawezesha kumudu matumizi ya teknolojia hiyo. Kwa kutambua umuhimu wa mashirikiano na Mashirika ya Kimataifa na kwa kuzingatia Sera ya Utandawazi, Wizara ya Afya itaendelea kushirikiana na Taasisi zote muhimu ili kwenda sambamba na maendeleo ya kisasa. Viongozi wa Wizara na watendaji wake wakuu watahudhuria mikutano muhimu ili kujadiliana na kutolea maamuzi muhimu ya kimaendeleo na kuchangia uzoefu wa nchi yetu katika masuala mbalimbali ambayo tumeonyesha kuyamudu. 2.6 Huduma ya Mafunzo ya Watumishi, Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/05 Katika kipindi cha mwaka 2004/2005 Wizara ilifanya yafuatayo: Wanafunzi 2,803 walihitimu katika vyuo mbalimbali vya afya hapa nchini katika fani za Uuguzi na Sayansi za Afya. Aidha, jumla ya wanafunzi 214 walihitimu mafunzo ya Madaktari Tiba, Wafamasia, Madaktari wa meno katika ngazi ya Shahada katika vyuo vya Muhimbili, KCMC na Hubert Kairuki Memorial University. Madaktari 136 walimaliza mafunzo ya internship na wanatarajia kupatiwa mafunzo ya kuwaandaa kufanya kazi (Inducton course) na kupangiwa vituo vya kazi sehemu mbalimbali nchini Wizara imegharamia mafunzo ya muda mrefu ya watumishi 257 nje na ndani ya nchi ambao wanatarajiwa kumaliza mafunzo yao mwaka huu Wizara imefanya mapitio kwa mitaala mitano katika vyuo vya Uguzi na Sayansi za Afya Jumla ya vyuo 17 viliweza kufanyiwa ukarabati ambao utaendelea katika mwaka ujao wa 2005/2006 katika baadhi ya vyuo Jumla ya vyuo 78 kati ya 93 vilivyokaguliwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) vilipata usajili wa baraza hilo Wizara kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) imeendelea kukagua vyuo vyote vinavyoendesha mafunzo katika fani ya Sayansi za Afya hapa nchini ili kupata usajili wa baraza hilo na kuviandaa kufikia hatua ya kupata ithibati (accreditation) 32

Wizara imetoa mafunzo kuhusu tiba ya kupunguza makali ya UKIMWI kwa watumishi 492 wakiwemo Madakatari, Wafamasia, Mafundi sanifu maabara, Wauguzi, watoa Ushauri nasaha na Wafauatiliaji wa wagonjwa majumbani (VCT counsellors and Home based care Providers). Vilevile, miongozo ya tiba ya ugonjwa wa UKIMWI na vijitabu vya kufundishia vilitengenezwa Watumishi katika hospitali 68 wakiwemo Madaktari wafawidhi wa hospitali, Wauguzi waandamizi na Wafamasia walipata mafunzo ya kujiendeleza kuhusu matumizi sahihi ya madawa Ukaguzi unaozingatia ubora wa viwango vya masomo, mafunzo ya vitendo na usafi wa mazingira ulifanyika katika vyuo 54 vilivyopo katika Kanda za Kaskazini, Mashariki, Kusini, Ziwa na Nyanda za juu Kusini Wizara imekamilisha miongozo ya mafunzo ya Timu za Usimamizi katika ngazi ya Mkoa, Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati na kuanza mafunzo hayo kwa timu za mikoa kwa awamu Wizara imeendesha mafunzo kwa timu za afya kwenye Sekretarieti za Mikoa. Lengo ni kuziimarisha timu hizi ziweze kuzisimamia na kuzisaidia Halmashauri za Wilaya kuboresha huduma wanazozitoa, matumizi ya rasilimali, utoaji taarifa na uzingatiaji wa viwango vya utoaji huduma. Katika mwaka huu timu za mikoa saba zilipatiwa mafunzo hayo. Kuhusu Mipango ya Watumishi mwaka 2004/2005 Wizara imefanya mambo yafuatayo:- Imeendesha utafiti wa matumizi ya wataalam wanaohitimu katika Taasisi ya Elimu ya Afya ya Msingi (Tracer study) Imeratibu vikao vya kamati ya wadau ya ufuatiliaji wa masuala ya maendeleo ya watumishi wa Sekta ya Afya Imetoa mafunzo na maelekezo juu ya mfumo wa utunzaji wa takwimu za watumishi utumiao mfumo wa kompyuta kwa wahusika wakuu wa utunzaji wa takwimu za watumishi katika ngazi za Wilaya 15 Imefanya mapitio ya Sera ya watumishi katika Sekta ya Afya na kukamilisha mapitio ya Ikama ya watumishi katika Vyuo vya Afya. 2.6.1 Matarajio ya Huduma ya Mafunzo ya Watumishi wa Afya mwaka 2005/2006 Mwaka 2005/2006 Wizara inatarajia kufanya yafuatayo; Wizara inatarajia kuvifanyia ukarabati vyuo vyake 27 ili kuviweka katika hali nzuri zaidi. Samabamba na hilo itaanzisha mafunzo ya Madaktari Wasaidizi katika kilichokuwa chuo cha Maafisa Tabibu Ifakara ambapo ukarabati mkubwa unaendelea hivi sasa Wizara itafanya utafiti ili kupata mahitaji halisi ya mafunzo yanayohitajika sehemu ya kazi (Training Needs Assesmnt) yenye lengo la kupata maeneo yanayohitajika kutilia mkazo mafunzo kwa watumishi, ili kuboresha utoaji huduma zinazotolewa kwa wananchi Wizara itaendesha mafunzo kwa timu za afya kwenye Sekretarieti za Mikoa. Lengo ni kuziimarisha timu hizi ziweze kuzisimamia na kuzisaidia Halmashauri za Wilaya kuboresha huduma wanazozitoa, matumizi ya rasilimali, utoaji taarifa na uzingatiaji wa viwango vya utoaji huduma. Katika mwaka 2005/2006 timu za mikoa 12 zitapatiwa mafunzo hayo Wizara itaendelea kufanya mapitio ya mitaala 4 ya Vyuo vya Sayansi ya Afya na uuguzi ili kuiboresha kulingana na mabadiliko yanayoendelea hivi sasa katika Sekta ya Afya 33

Kufuatilia, kutathmini na kutoa ushauri juu ya hali ya watumishi katika Sekta ya Afya kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali Kuratibu vikao vya kamati ya Wadau ya kufuatialia masuala ya watumishi wa Sekta ya Afya Kundesha mafunzo na maelekezo ya mfumo wa utunzaji takwimu za watumishi kwa kutumia kompyuta katika ngazi za Wilaya kwa zile Wilaya ambazo hazijapata mafunzo haya Kuandaa mpango mkakati wa watumishi wa Sekta ya Afya Kuendeleza utafiti wa matumizi ya wahitimu wa chuo cha CEDHA utafiti (Tracer Study), wenye lengo la kuboresha matumizi sahihi ya wataalam wanaohitimu katika chuo hicho. 2.7 Ofisi ya Mganga Mkuu Kiongozi Utekelezaji wa Majukumu mwaka 2004/05 2.7.1 Huduma za Dharura na Maafa Katika Kipindi cha mwaka 2004/2005, kazi zifuatazo zilitekelezwa: Kuchapisha miongozo miwili ya utoaji wa Huduma za Dharura na Maafa yaani, Health Sector Guidelines and Protocol on Emergency and Disaster Management na Emergency Operation Plan (EOP) nakala 1,000 kila moja na kuzisambaza katika vituo vya kutolea huduma nchini Kutoa mafunzo ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa kwa watoa huduma ya afya katika Hospitali (First responders) ili kuongeza ufanisi katika kazi zao za kila siku Kutoa mafunzo maalum ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa kwa Kamati za Uendeshaji wa Huduma za Afya katika mikoa (RHMT), ili kuongeza ufanisi katika kusimamia kazi hiyo kwa watumishi katika hospitali Kufanya upembuzi yakinifu katika hospitali za Kilimanjaro, Tanga, Arusha na Mbeya ili kutoa ushauri wa maandalizi ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa, pindi yatokeapo. Matarajio ya Huduma za Dharura na Maafa mwaka 2005/2006 Katika kipindi cha mwaka 2005/2006, kitengo kinakusudia kufanya kazi zifuatazo: Kutembelea na kufanya ufuatiliaji (supportive supervision) katika Wilaya mbili (2) kwa kila mkoa, katika mikoa tisa ya Tanzania Bara kwa lengo la kufuatilia na kusimamia utoaji wa huduma za afya, ili kutoa ushauri na maelekezo ya kitaalam katika kuboresha huduma za afya hususani Dharura na Maafa Kutoa mafunzo maalum ya jinsi ya kukabiliana na dharura na maafa kwa wajumbe 40 wa Timu za Uendeshaji Huduma za Afya za Mikoa (RHMT), ili kuongeza ufanisi katika kusimamia utendaji wa kazi hiyo kwa watumishi katika hospitali zao Kutoa mafunzo maalum ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa kwa watumishi 36 wa hospitali za hapa nchini (First responders) ili kuongeza ufanisi katika kazi za Dharura na Maafa katika hospitali za hapa nchini Kuunda timu Maalum ya Kitaifa ya kukabiliana na Dharura na Maafa hapa nchini (National Rapid Response Team). Timu hii itapewa mafunzo maalum ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa nchini, ili kuongeza ufanisi katika kazi zao za kila siku 34

Watumishi wawili wa kitengo cha Dharura na Maafa watapata mafunzo maalum ya muda mfupi nje au ndani ya nchi ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa hapa nchini Mtumishi mmoja wa kitengo cha Dharura na Maafa atapata mafunzo ya Shahada katika fani ya Uuguzi katika moja ya vyuo hapa nchini, ili kuongeza ufanisi katika kazi zake za kila siku katika kukabiliana na Dharura na Maafa hapa nchini Kuendelea kufanya upembuzi yakinifu (Hazard Analysis and Vulnerability) ya jinsi ya kukabiliana na Dharura na Maafa nchini Kuimarisha kitengo kwa kununua vitendea kazi pamoja na samani kwa ajili ya ofisi. Vifaa hivyo ni pamoja na kompyuta, meza n.k kwa lengo la kuongeza ufanisi wa kazi za kitengo cha Dharura na Maafa. 2.7.2 Ukaguzi wa Huduma za Afya Mwaka 2004/2005, Wizara ilifanya kazi zifuatazo:- Kupanga na kuzindua mwongozo wa mfumo wa kimataifa wa ubora wa huduma za afya Kufanya mkutano na wadau kuhusu mwongozo wa kudhibiti na kuzuia maambukizo katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini Kuandaa viwango na viashiria vya utoaji bora wa huduma Kuandaa mwongozo wa kutathmini utendaji kazi kwa watumishi wa Afya Kuandaa mwongozo kwa watumishi wa afya wa kujitathmini wao wenyewe kiutendaji kuhusiana na ubora wa huduma za afya wanazozitoa Kuandaa mwongozo wa kutathmini utendaji kazi kwa watumishi wa Afya kuhusiana na ubora wa huduma za afya. Matarajio ya Ukaguzi wa Huduma za Afya mwaka 2005/2006 Kitengo cha Ukaguzi wa utoaji wa huduma za Afya nchini kinategemea kutekeleza kazi zifuatazo, mwaka 2005/2006: Kufanya usimamizi na ukaguzi katika Mikoa 8, Wilaya mbili kila mkoa Kufundisha wataalam wa Taifa (National Trainers of Trainers) kuwawezesha kufundisha watumishi wengine katika kudhibiti maambukizo (Infection Prevention and Control IPC) Kuendesha mafunzo juu ya udhibiti wa maambukizo (IPC), uboreshaji wa huduma za afya na mwongozo wa usimamizi na ukaguzi wa huduma za afya kwa Timu za Utendaji za Afya za Mikoa (Regional Health Management Teams) zote Kuandaa na kuchapisha muongozo wa udhibiti wa maambukizo kwa watumishi wa Zahanati na Vituo vya Afya (Infection Prevention and Control for Health Centers and Dispensaries) Kusambaza Mwongozo wa Kitaifa wa udhibiti wa maambukizo (National\Infection Prevention and Control Guidelines for Healthcare Services) na Mfumo wa Kitaifa wa Uboreshaji Huduma za Afya Tanzania (Tanzania Quality Improvement Framework). 2.7.3 Huduma za Uuguzi na Ukunga Mwaka 2004/2005, Wizara ilitoa kipaumbele katika utoaji wa huduma za Uuguzi kwa wagonjwa walioathirika na Virusi vya UKIMWI. Hii ni pamoja na kutayarisha miongozo ya utoaji wa huduma za uuguzi kwa wagonjwa hao katika vituo vya kutolea huduma, kufanya tathmini ya kazi ya kutoa ushauri nasaha inayofanywa na wauguzi. Hii ni kwa 35

kuzingatia kuwa, UKIMWI sasa ni tatizo kubwa mno katika vituo vyetu vya kutolea huduma bila kuwasahau watoa huduma wenyewe. Mafunzo ya uongozi wa wasimamizi wa huduma za Uuguzi na Ukunga yalitolewa kwa wasimamizi 16, ili kuwapa maarifa na stadi za usimamizi bora wa utowaji wa huduma katika vituo vya hospitali za mikoa na rufaa nchini. Matarajio ya Huduma za Uuguzi na Ukunga mwaka 2005/2006 Mwaka wa 2005/2006, kitengo kinatarajia kutekeleza kazi zifuatazo; Kuelimisha na kusambaza mwongozo wa utoaji wa huduma kwa watoa huduma kuhusu jinsi ya kujiepusha na kutoeneza maambukizi wakati wa kutoa huduma kwa walioathirika na UKIMWI nchini Kuandaa mkakati kabambe wa utoaji huduma za uuguzi na ukunga wa miaka mitatu 2005-2008, kwa kulingana na mkakati wa sera ya Wizara ya Afya ya kutoa huduna bora kwa kuzingatia MKUKUTA Kufanya usimamizi na ushauri wa kitaaluma wa utoaji wa huduma za Uuguzi na Ukunga katika mikoa minane ya Mwanza, Pwani, Kilimanjaro, Shinyanga, Kagera, Dodoma, Arusha na Mbeya. Kufuatilia kwa karibu watoa huduma hasa kwa kuzingatia malalamiko ya wananchi kuhusu lugha zisizofaa kwa kushirikiana na Baraza la Uuguzi na Ukunga Kutoa mafunzo kwa maafisa wa Kitengo juu ya uendeshaji na usimamizi wa utoaji wa huduma za Uuguzi na Ukunga ili kuinua viwango vya ubora wa huduma zitolewazo nchini Kuwawezasha kupata mafunzo maalum ya uendeshaji wa huduma za Uuguzi na Ukunga kwa maafisa wawili wa kitengo ndani na nje ya nchi, ili kuongeza ufanisi katika usimamiaji wa huduma za Uuguzi na Ukunga. 2.8 Uhasibu na Fedha 2.8.1 Ukusanyaji mapato kwa mwaka 2004/2005 Wizara ilikuwa na lengo la kukusanya jumla ya Tsh. 496,504,000/= kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato katika mwaka wa fedha wa 2004/05. Hadi kufikia tarehe 31 Machi, 2005, Wizara ilikuwa imekusanya jumla ya Tsh. 609,344,885.11 ambazo zimetokana na makato ya kodi za nyumba za Serikali na Mashirika ya Umma, malipo ya ununuzi wa vitabu vya maombi ya Zabuni za Wizara na marejesho ya masurufu. Wizara inategemea kukusanya kiasi cha Tshs 34,101,356.68 kati ya tarehe 1 Aprili, 2005 hadi 30 Juni, 2005. Kiasi halisi kinachotegemewa kukusanywa kitakuwa kimevuka lengo la mapato yaliyokadiriwa. Hali hii imetokana na kiasi kikubwa cha marejesho ya masurufu. Aidha, mapato haya hayajumuishi fedha zinazotokana na makusanyo ya kuchangia gharama za huduma za afya. Fedha za uchangiaji hutumika kwenye hospitali zinakokusanywa ili kuboresha huduma zitolewazo kwa wananchi, kulingana na Sera ya Uchangiaji. Matarajio ya Ukusanyaji mapato mwaka 2005/2006 Katika kipindi cha 2005/2006, Wizara ya Afya inatarajia kukusanya jumla ya Tshs 598,005,000.00. Mapato haya yatatokana na kodi za nyumba za Serikali na Mashirika ya Umma zinazochangiwa na wafanyakazi, marejesho ya masurufu ya fedha za Serikali na malipo ya kununua makabrasha ya Zabuni za Wizara. Kwa kuzingatia utaratibu uliopo, 36

mapato yanayotokana na makusanyo ya kuchangia gharama za huduma za afya hayajumuishwi katika makadirio haya. 2.8.2 Matumizi ya fedha za Kawaida mwaka 2004/2005 Mwaka wa fedha wa 2004/2005, Wizara ya Afya ilidhinishiwa jumla ya Tsh 195,800.00 kwa ajili yakugharamia utoaji wa huduma za afya. Kiasi cha Tsh 189.243,633,427.00 kati ya hizo zilitengwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ikijumuisha mishahara ya wafanyakazi wa Hospitali Teule (DDH), Hospitali ya Taifa Muhimbili, KCMC, Bugando na Taasisi zilizo chini ya Wizara. Kiasi kilichobaki cha Tsh. 6,642,499,373.00 kilitengwa kwa ajili ya mishahara ya watumishi wa Idara za Wizara ya Afya, Vyuuo vyote vinavyosimamiwa na Wizara na Hospitali za Kibong oto, Mbeya Rufaa na Mirembe. Makadirio ya matumizi ya Kawaida katika mwaka 2005/2006 Wizara ya Afya katika mwaka wa 2005/2006 inakadiria kutumia kiasi cha Tshs 180,305,853,900.00 kwa ajili ya matumzi ya kawaida. Katika mwaka 2004/2005 Wizara ilitengewa jumla ya Tsh 104,465,379,200.00 kwa ajili ya matumzi ya kawaida. Hivyo kuna ongezeko la Tsh 75,840,474,700.00 ikilinganishwa na mwaka 2004/2005. Kati ya fedha hizo zilizotengwa kiasi cha Tsh 6,406,945,600.00 zitatumika kulipa mishahara ya watumishiwa Wizara ya Afya makao makuu, Hospitali za Mbeya Rufaa, Mirembe na Kibong oto na Vyuo vyote vya mafunzo ya afya. Kiasi cha Tsh 173,898,908,300.00 kilichosalia kimetengwa kwa ajili ya Matumzi mengineyo (OC) kwa ajili ya kazi za Idara za Wizara ya Afya na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya. Kiasi hiki pia kinajumuisha mishahara ya Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya. Taasisi hizo ni pamoja na Taasisi ya Chakula na lishe (TFNC), Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Hospitali ya Taifa Muhimbili, Taasisi ya Mifupa (MOI), Taasisi ya Saratani Ocean Road, Hositali Teule (District Designated Hospitals DDH) na Hospitali za Mashirika ya kujitolea (Voluntary Agencies VA s). 2.8.3 Matumizi ya fedha za Miradi ya Maendeleo mwaka 2004/2005 Jumla ya Tsh 66,416,700.00 zilitengwa kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya hizo Serikali ya Tanzania ilitenga jumla ya Tsh 3,552,448,200.00 na Tshs 62,863,658,500.00 ni mchango wa Wahisani wanaosaidia Sekta ya Afya. Kiasi ambacho kilikuwa kimekwishatolewa na wahisani wa Mfuko wa Pamoja ni Tshs 40,680,869,900.00 na fedha zilizo nje ya Mfuko wa Pamoja ni Tshs 4,697,565,032.25. Fedha zote zilizotolewa na wahisani zikijumuishwa pamoja zinafanya jumla ya Tsh 48,930,883,132.25 ambayo ni sawa na asilimia 53.6 ya fedha zote zilizokisiwa kutolewa na Wahisani. Hadi tarehe 30 Aprili 2005, matumizi halisi kwa fedha zote za miradi ya maendeleo zikiwemo za Serikali pamoja na Wahisani ni Tsh 21,526,163,399.74. Makadirio ya Miradi ya Maendeleo mwaka 2005/2006 37

Katika mwaka wa fedha wa 2005/2006 Wizara ya Afya inakadiria kutumia jumla ya Tshs 90,862,748,400.00 kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizo shilingi 5,000,000,000.00 ni kutoka Serekali ya Tanzania na kiasi cha shilingi 85,862,748,400.00 ni kutoka Taasisi za Kimataifa zinazochangia Mfuko wa Pamoja wa Afya (Busket Fund) na wale walio nje ya mfuko. Fedha hizo zitatumika kutekeleza miradi ya maendeleo ifuatayo: Kuendeleza ukarabati wa Hospitali ya Taifa Muhimbili na hospitali za Jiji la Dar es Salaam Ukarabati wa wodi, maabara, chumba cha upasuaji na ujenzi wa hosteli ya madaktari walio katika mazoezi (Intern s doctors) katika hospitali ya Rufaa Mbeya Kuendeleza ukarabati wa wodi, nyumba za watumishi na jiko katika hospitali maalum ya Mirembe na Taasisi ya Isanga Ukarabati wa wodi 6 za wagonjwa wa nje, nyumba za watumishi na wodi za wagonjwa wa Kifua Kikuu na ununuzi wa vifaa kwa ajili ya hospitali maalum ya Kifua Kikuu ya Kibongoto Kuendeleza ujenzi wa wodi ya watoto katika hospitali ya Taifa Muhimbili Kuendeleza michango ya Serekali (counterpart funds) kwa ajili ya kuendeleza ukarabati wa majengo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, ujenzi wa hospitali maalum hapa Dar es Salaam itakayojengwa kwa kushirikiana na Serekali ya Tanzania na TOKUSHUKAI na ujenzi wa hospitali ya Kanda ya Kusini, Mtwara Kuendeleza ukamilishaji wa ujenzi wa maabara ya ubora (quality laboratory), Makao Makuu ya Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serekali pamoja na ununuzi wa vifaa na kemikali kwa ajili ya maabara mpya ya Mwanza ambayo imekamilika hivi karibuni Ukarabati wa vituo vya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu Amani, Gonja, Mwanza, Tukuyu na Dar es Salaam Ukarabati wa jengo la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya litakalotumika kama ofisi Kuendelea kukamilisha ukarabati wa vyuo vya afya 28 Kununua vifaa vya tiba kwa hospitali za Rufaa zote 6. 38

3.0 RIPOTI ZA TAASISI NA MAMLAKA ZILIZO CHINI YA WIZARA YA AFYA 3.1 Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC) Katika kipindi cha mwaka 2004/2005 Wizara ya Afya kupitia Taasisi yake ya Chakula na Lishe iliendelea kutoa ushauri wa kitaalam kwa Wilaya na kushirikiana na Taasisi na wadau mbali mbali katika kuboresha hali ya lishe ya jamii nchini. Katika juhudi za kudhibiti matatizo ya lishe, Taasisi iliendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuimarisha uwekaji wa madini joto kwenye chumvi katika Wilaya 25 zenye wazalishaji chumvi wadogo kwa kuhamasisha viongozi wa Wilaya 285. Aidha, Taasisi ilitoa mafunzo kwa wakaguzi wa chumvi (maafisa afya na maafisa madini) wapatao 451 na kuunda timu za wakufunzi wa wazalishaji wa chumvi katika suala la uwekaji madini joto kwenye chumvi. Zoezi hilo lilihusisha Wilaya za Mtwara, Lindi, Kilwa, Rufiji, Mkuranga, Temeke, Kinondoni, Bagamoyo, Dodoma, Manyoni, Singida, Iramba, Kigoma, Njombe na Mbozi. Wilaya nyingine ni Tanga, Pangani, Muheza, Korogwe, Same, Mwanga, Meatu, Babati, Hanang na Karatu. Juhudi zilielekezwa katika Wilaya hizo kutokana na hali halisi kuwa sehemu kubwa ya chumvi inayozalishwa hapa nchini inatokana na wazalishaji wadogo katika maeneo hayo. Aidha, takwimu zinaonyesha kwamba kati ya hao wazalishaji wadogo ni asilimia 30 tu ndio wamekuwa wakiweka madini joto kwenye chumvi. Katika kuhakikisha kwamba chumvi yote inayozalishwa nchini inawekwa madini joto, Taasisi ya Chakula na Lishe sambamba na kutoa mafunzo na uhamasishaji ilisambaza vifaa mbalimbali vya kuwekea madini joto kwenye chumvi kwa wazalishaji. Vifaa hivyo ni pamoja na kilo 5,000 za madini joto na pampu 4,650 za kunyunyuzia madini joto kwenye chumvi na jumla ya vichupa 93,750 vya kemikali ya kupima uwepo wa madini joto kwenye chumvi (Iodine test solution). Taasisi iliendelea kuratibu utoaji wa matone ya Vitamini A kwa watoto wa umri kati ya miezi sita hadi miaka mitano na vidonge vya kutibu minyoo ya tumboni kwa watoto wa umri kati ya mwaka mmoja hadi miaka mitano katika mikoa yote Tanzania bara. Katika zoezi lililofanyika Desemba 2004, asilimia 93 ya watoto waliolengwa walipata matone ya Vitamini A na asilimia 90 walipata vidonge vya kutibu minyoo. Katika juhudi za kuendeleza lishe na afya ya mtoto, mkakati wa kitaifa wa kusimamia Lishe na Afya ya Mtoto chini ya umri wa miaka mitano umeandaliwa na kuzinduliwa. Aidha, mpango wa utekelezaji wa mkakati huu wa miaka mitano 2005-2009 umeandaliwa. Mkakati na Mpango wa Utekelezaji unaainisha vipengele muhimu kuhusu uimarishaji wa lishe ya mtoto na pia majukumu ya wadau kutoka sekta mbalimbali ikiwemo sekta binafsi. Mkakati huu utawezesha wadau kuchangia kikamilifu katika kuendeleza lishe na afya ya mtoto hasa wakati huu wa janga la UKIMWI. 39

Taasisi pia iliandaa mwongozo wa kitaifa kuhusu lishe bora kwa wanaoishi na virusi vya UKIMWI. Jumla ya nakala 10,000 za mwongozo huo zilichapishwa na kusambazwa kwenye Wizara na taasisi husika, hospitali za rufaa, Mikoa na Wilaya, vyuo vya mafunzo na taasisi mbalimbali zinazoshughulika na tatizo la UKIMWI hapa nchini. Mpango wa Hospitali Rafiki wa Mama na Mtoto unaotekelezwa nchini toka mwaka 1992 unalenga katika kuboresha hali ya afya na lishe ya watoto wachanga. Chini ya mpango huu hospitali zinatakiwa kutekeleza na kuboresha Huduma za Afya na Uzazi kwa wanawake wajawazito na waliojifungua. Katika kufuatilia Hospitali Rafiki wa Mama na Mtoto, hospitali 17 katika Wilaya za Shinyanga, Kasulu, Ndanda, Nyakahanga, Rubya, Biharamulo, Mugana, Magu na Meatu ziliweza kufanikiwa kuwa rafiki wa Mama na Mtoto kwa vigezo vya kimataifa. Hii inafanya Tanzania kuwa na hospitali 68 ambazo ni Rafiki wa Mama na Mtoto. Matarajio ya Taasisi ya Chakula na Lishe mwaka 2005/2006 Katika kipindi cha mwaka 2005/2006, Taasisi itaendelea kuratibu shughuli za kitaifa za utoaji matone ya Vitamini A na vidonge vya kutibu minyoo kwa watoto walio na umri chini ya miaka mitano katika mikoa yote ya Tanzania bara. Wizara itaendelea kufuatilia na kutoa mafunzo na hamasa juu ya uwekaji wa madini joto kwenye chumvi ili kufikia lengo la asilimia 90 (au zaidi ya kaya zote nchini) linalopendekezwa na Shirika la Afya Duniani kwamba ziwe zinatumia chumvi yenye madini joto kutoka asilimia 84 ya hivi sasa. Taasisi pia itafanya utafiti kuhusu tatizo la upungufu wa damu kwa nchi nzima ili kuwa na takwimu sahihi za hali halisi ya tatizo hilo. Kupatikana kwa takwimu hizo kutasaidia katika kupanga mikakati na programu za kupunguza tatizo hili. Aidha, Taasisi itaandaa na kuchapisha vitabu zaidi kwa nia ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu lishe bora kwa wenye UKIMWI na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu lishe bora ili kuepukana na magonjwa sugu yenye uhusiano na ulaji usiofaa kama vile kisukari, magonjwa ya mfumo wa damu na moyo, saratani na mengineyo. Ili kuzidi kuendeleza afya na lishe ya mtoto, Taasisi itaratibu mapitio ya Sheria Na. 10 ya mwaka 1978 inayosimamia uingizaji na uuzaji wa vyakula vya watoto wachanga, ili kuingiza vipengele vinavyohusiana na ulishaji wa mtoto na janga la UKIMWI. Sheria hii inadhibiti ubora wa vyakula vinavyoingizwa nchini toka nje na vile ambavyo vinazalishwa katika nchi yetu. Taasisi pia itaendelea kutoa ushauri wa kitaalam kwa Wilaya ili ziweze kupanga na kutekeleza programu na miradi inayolenga kuboresha lishe na afya za wananchi. 3.2 Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Katika kipindi cha mwka 2004/2005, Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali iliweza kufanya yafuatayo; Kuendelea kutekeleza malengo yake ya kutoa huduma bora za kimaabara zinazohusu uchunguzi, ushauri wa kitaalam na utafiti katika nyanja za kemikali, vyakula, dawa, usalama wa mazingira na sayansi ya makosa ya jinai kwa wadau na wananchi kwa jumla Uchunguzi jumla ya sampuli 3,934 na kutoa matokeo katika muda wa siku 14 kama ilivyoainishwa katika Mkataba wa Huduma kwa Mteja. Kati ya sampuli zilizochunguzwa, asilimia 82 zilifikia viwango vinavyokubalika kitaifa na kimataifa kwa matumizi ya binadamu na usalama wa mazingira. Mafanikio hayo yametokana na 40

kununuliwa kwa mitambo ya kisasa na vifaa vya Maabara, wataalam kuongozewa ujuzi pamoja na kuzingatia maoni ya wateja Uchunguzi wa sampuli 4,213 za dawa za kulevya (mihadharati) kutoka Idara, Asasi na waathirika ili kuainisha aina za dawa husika na matokeo ya uchunguzi na kukabidhiwa kwa mamlaka husika. Matokeo ya uchunguzi huo yamesaidia kuharakisha usikilizaji wa kesi na utoaji haki mahakamani na ushauri kwa Asasi hususan hospitali katika kusaidia kutoa tiba sahihi kwa waathirika Kuendelea kutekeleza Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Kemikali zitumikazo Viwandani na Majumbani The Industrial and Consumer Chemicals (Management and Control) Act No. 3, 2003 ilioyoanza kutekelezwa Julai 2003, kwa lengo la kulinda afya za wananchi na mazingira Kutoa elimu kwa umma kupitia vyombo vya habari, magazeti na vipeperushi kuhusu kemikali zilizopigwa marufuku duniani kutokana na athari za kiafya na mazingira. Sheria hii imesaidia kuzuia uwezekano wa nchi yetu kuwa jalala la kemikali hatari zinazoathiri afya, kuchafua vyanzo vya maji na mazingira Imeshungulikia maombi 150 ya usajili wa kemikali kutoka kwa wadau Tanzania Bara na jumla ya vibali 365 vilitolewa kwa ajili ya uagizaji wa kemikali kutoka nje ya nchi Kununua, kufunga na kuzindua mtambo wa DNA ambao unachunguza vinasaba (genes vya urithi na ukoo) katika maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali. Matokeo ya uchunguzi wa sampuli kwa kutumia mtambo huu umesaidia vyombo vya dola na mamlaka nyingine mfano, katika masuala ya kusingiziwa, kuiba au kubadilishana watoto hospitalini na hivyo kuondoa kero za wananchi. Pia husaidia kutambua vinasaba vya magonjwa ya kurithi na tafiti mbalimbali zinazohusiana na vimelea vya magonjwa, mimea na ugunduzi wa dawa za tiba mbadala. Aidha kumbukumbu za wahalifu zitahifadhiwa kwa kutumia mtambo huo na zitasaidia kutambua wanaofanya makosa mara kwa mara kwa kutumia majina bandia Aidha, Maabara moja ya Kanda ya Ziwa Jijini Mwanza ilianzishwa ambayo imesaidia kuondoa kero ya kusafirisha sampuli na gharama kubwa inayohitajika kufika Dar es Salaam kufuatilia matokeo ya uchunguzi Kupeleka wafanyakazi 17 kwa mafunzo ya muda mfupi na mrefu katika fani mablimbali ndani na nje ya nchi kwa kuzingatia usawa wa jinsia na vipaumbele Kuzindua tovuti ya Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serikali (www.gcla.go.tz) katika kuimarisha mawasiliano kati ya Wakala, wadau na jamii kwa ujumla ili kwenda sambamba na utandawazi. Matarajio ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serekali kwa mwaka 2005/2006. Wakala inatarajia kufanya yafuatayo:- Kutumia kwa makini rasilimali watu, fedha na vifaa katika kutekeleza Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania Kuchunguza jumla ya sampuli 4,631 ambapo asilimia kubwa itatokana na usajili wa kemikali na kuanzishwa kwa Maabara ya Kanda ya Ziwa Jijini Mwanza Kupata wadau wengi wanaotarajia kujisajili kutokana na kuelimishwa kuhusu umuhimu wa sheria hii Kutangaza kwa kutumia vyombo vya habari na mawasiliano umuhimu wa mtambo wa vinasaba katika kufanya tafifi mbalimbali kwa nchi za Afrika zilizo Kusini mwa 41

Jangwa la Sahara na hatimaye kuongeza mapato ya Wakala kutokana na huduma zitakazotolewa Kukamilisha uchambuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi wa Maabara ya Kanda ya Kaskazini mjini Arusha Kuweka kipaumbele katika kuwasomesha wafanyakazi 19 katika maeneo yatakayosaidia kukuza uchumi na kupunguza umasikini wa kipato Kuendelea kujitangaza kupitia tovuti yake ili huduma zake zifahamike kote ulimwenguni. 3.3 Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Mamlaka hii ilianzishwa kwa sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi namba 1 ya mwaka 2003 ili kusimamia udhibiti wa ubora, usalama na ufanisi wa vyakula, dawa, dawa za mitishamba, vipodozi na vifaa tiba. Katika kipindi cha 2004/2005, Mamlaka imeandaa rasimu ya kanuni/sheria ndogo zifuatazo:- The Tanzania Food, Drugs and Cosmetics (Registration of pre-packed food) Regulations, 2004 The Tanzania Food, Drugs and Cosmetics (Cosmetics) Regulations, 2004 The Tanzania Food, Drugs and Cosmetics (Control of promotion of food) Regulations, 2004 na The Tanzania Food, Drugs, and Cosmetics (Control of drug promotion) Regulation, 2004. Aidha, mamlaka imeweza kuandaa miongozo ifuatayo:- Mwongozo wa namna ya kushughulikia maombi ya usajili wa dawa Mwongozo wa kutathmini maombi ya kutangaza bidhaa zinazodhibitiwa chini ya sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi ya mwaka 2003 Mwongozo wa kusajili vyakula nyongeza (food supplements). Jumla ya dawa 279 za binadamu, 12 za mifugo na 11 za vyakula zilisajiliwa. Mamlaka ilifanya kazi ya kutafuta taarifa za vyakula, vipodozi na dawa za miti shamba zinazozunguka sokoni bila kuthaminiwa na kusajiliwa kwa lengo la kutambua bidhaa hizo ili watengenezaji au waagizaji wake wahamasishwe kuleta maombi ya usajili. Jumla ya vyakula 5,066, vyakula nyongeza 126 na vipodozi 921 vilitolewa taarifa katika zoezi hilo. Vile vile, jumla ya maombi 17 ya kusajili dawa za mitishamba yalipokelewa na yanaendelea kufanyiwa tathmini. Katika kuhakikisha kwamba bidhaa zilizo katika soko la Tanzania ni bora na salama, Mamlaka imefanya uchunguzi wa kimaabara kwa jumla ya sampuli 767, sampuli 608 zilikidhi viwango na 159 hazikukidhi viwango. Bidhaa ambazo hazikukidhi viwango ziliondolewa sokoni na kwa zile zilizokuwa zinaombewa usajili, cheti cha kusajili hakikutolewa na hivyo kutoruhusiwa kuingizwa katika soko la Tanzania. Jumla ya aina 168 ya vipodozi vyenye viambato vyenye sumu vilipigwa marufuku. Mamlaka imefanya ukaguzi katika jumla ya maduka 630 ya dawa, 70 ya vipodozi na maduka 39 ya vyakula. Pia viwanda 183 vya ndani vya chakula na 72 (66 vya nje, na 6 vya ndani) vya dawa vilikaguliwa, na jumla ya maombi 3474 ya vibali vya kuingiza bidhaa nchini yalipokelewa. Vibali 1062 vya kuingiza vyakula kiasi cha tani 841,852.848 na vibali 2055 vya kuingiza dawa vilitolewa. 42

Mamlaka imefungua Ofisi za Kanda katika mikoa ya Mwanza na Arusha ili kusogeza huduma karibu na wananchi na mafunzo kuhusu sheria mpya katika Kanda za Kusini na Kaskazini yaliyofanyika kwa wadau 515. Katika kukabiliana na tatizo la ukiukwaji mkubwa wa sheria unaofanywa katika Maduka ya Dawa Baridi Mamlaka imeanzisha maduka 41 ya Dawa Muhimu (Accredited, Drug Dispensing Outlets ADDO) mkoani Ruvuma katika vijiji na miji midogo ikiwa ni nyongeza kwa maduka 110 yaliyokwisha funguliwa tangu mpango uanzishwe mnamo mwezi Agosti 2003. Tathmini ya mpango wa ADDO imefanyika na kuonyesha mafanikio makubwa katika kufikia malengo ya awali kuhusu mpango huo. Mwaka 2004/2005, kati ya matukio 42 ya madhara yaliyoshukiwa kutokana na matumizi ya dawa yametolewa taarifa kwa usahihi. Katika kushiriki vita dhidi ya UKIMWI Mamlaka imeendelea kuhakikisha kuwa dawa za kupunguza makali ya UKIMWI, zilizoingia nchini ni bora, salama na zina ufanisi uliofikia viwango vianvyotambulika. Katika kuelimisha wadau na kuboresha upashanaji habari, Mamlaka ilizindua tovuti yake mwaka 2004. Matarajio ya Mamlaka ya Chakula na Dawa mwaka 2005/2006 Mamlaka ya Chakula na Dawa inatarajia kutekeleza yafuatayo:- Kuendelea kusimamia ubora, usalama na ufanisi wa chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba n.k kwa kuimarisha mfumo wa usajili na ukaguzi ikiwa ni pamoja na ukaguzi wa viwanda vya nje na ndani, vituo vya mipakani na maeneo ya kufanyia biashara ya bidhaa hizo Kuimarisha maabara kuu na zile ndogo zinazohamishika zilizopo vituo vya mipakani na mkoani ili ziwe na uwezo wa kupima vipimo mbali mbali kwa kuzingatia viwango vinvayokubalika vya bidhaa zinazosimamiwa na Mamlaka kwa kutumia zana za kisasa Kuandaa miongozo na sheria ndogo ili kurahisisha utekelezaji wa Sheria Kuu, na kuboresha uelewa wa wadau Kuendelea kutoa mafunzo kwa watumishi ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi ikiwa ni pamoja na kuimarisha na kutoa vitendea kazi kwa kulingana na teknolojia mpya Mamlaka itaendelea kutoa elimu kwa wadau na wananchi wote kupitia vyombo vya habari na kupitia tovuti yake pamoja na kuendelea kutoa mafunzo mbalimbali Ofisi za Kanda zitaendelea kufunguliwa kwa kadri bajeti itakavyoruhusu. 3.4 Taasisi ya Utafiti wa Magojwa ya Binadamu (NIMR) Sheria ya Namba 23 ya mwaka 1979 inaitaka Taasisi kushughulikia masuala ya utafiti wa magonjwa ya binadamu. Mwaka 2004/2005, Taasisi ilishughulikia usimamizi, uratibu, udhibiti, uenezi, utangazaji wa matokeo na ukuzaji wa utafiti nchini. Magonjwa yaliyofanyiwa utafiti ni Malaria, Matende na Mabusha, Usubi, Kichocho, Minyoo ya Tumbo, Kuhara, Magonjwa ya Zinaa, Malale, Kifua Kikuu na UKIMWI. 43

Utafiti wa Malaria Katika kipindi cha 2004/2005 tafiti mbalimbali za Malaria zimetoa matokeo ambayo yanaonyesha kuwa usugu wa vimelea vya Malaria kwa dawa ya SP unakua na umefikia asilimia kumi na tano (15%). Hatua hii ya usugu iliyofikiwa inahitaji mabadiliko ya tiba dhidi ya Malaria itakayoweka viwango vipya vya dawa za kutibu Malaria na kuweka bayana mabadiliko ya sera ya tiba ya Malaria. Kiutafiti pendekezo linalotolewa kukabiliana na usugu huu ni matumizi ya dawa mchanganyiko (combination therapy). Taasisi inafuatilia kuona kama kuna uwezekano wa mbu kuwa na usugu kwa madawa yanayotumika katika vyandarua hapa nchini. Ufuatiliaji huo umefanyika katika wilaya za Muheza, Tanga, Korogwe, Lushoto, Babati, Arumeru, Magu, Tabora, Kyela, Moshi, Ifakara, Kinondoni na Pangani. Ugonjwa wa Usubi Uchunguzi juu ya nguvu za sumu ya kuulia mazalia ya wadudu wanaosababisha Usubi ulifanyika katika Wilaya za Rungwe na Kyela. Matokeo yalionyesha mafanikio mazuri kwa kuua wadudu hao kama ilivyotarajiwa. Mbinu hii itatumika kuongeza kasi ya Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Usubi. Utafiti wa Dawa Asilia Taasisi imefanya utafiti ili kutathmini kiwango cha dawa kinachopatikana katika mmea wa Artemisia Annua na pia kufanya utafiti katika ngazi ya kimaabara ya namna ya kutengeneza dawa itokanayo na mmea huo. Kutokana na utafiti huu, Taasisi imefanikiwa kupata mtiririko wa namna ya kutengeneza Artemisinin na baadaye kuibadilisha Artemisinin kuwa Dihydro-artemisinin, dawa inayofaa kwa kutibu Malaria. Aidha, kwa kushirikiana na kituo cha Munufu, Taasisi imeifanyia utafiti wa awali dawa ya Muhanse itumiwayo na wagonjwa wa UKIMWI na kuiona haina madhara ya kuhatarisha maisha ya mtumiaji pamoja na kwamba utafiti zaidi unahitajika. Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Matende Zoezi la Mapping kuangalia ukubwa wa tatizo la Matende limeonyesha kuwa Tanzania ina watu karibu milioni 30 ambao wapo katika hatari ya kupata ugonjwa wa Matende na Mabusha. Kati ya hao watu asilimia sita (6.6%) yaani milioni mbili tayari wameathirika na ugonjwa huu. Kimsingi asilimia 90% ya Wa-Tanzania wapo katika hatari ya kupata maambukizi ya ugonjwa wa Matende. Tathmini pia imegundua kwamba watu wenye vimelea vya ugonjwa wa Matende wapo katika Wilaya nchi isipokuwa Wilaya za Babati na Chunya Katika jitihada za kupambana na tatizo la Matende na Mabusha mwaka 2000 watu 38,000 waliopewa dawa katika kisiwa cha Mafia na mwaka 2001 watu 700,000 katika mkoa wa Pwani. Katika mwaka 2002 idadi ya Watanzania waliopewa dawa ilifikia milioni mbili laki nne baada ya kuongezeka mkoa wa Mtwara. Mwaka 2003 kumekuwapo na ongezeko la watu wapatao milioni mbili na laki nne waliopatiwa dawa na kuifanya idadi ya Wa-Tanzania waliopata tiba hiyo kuwa milioni nne na laki nne. Mwaka 2004 kulikuwa na ongezeko la watu laki tisa katika mkoa wa Tanga na hivyo kufanya watu walionufaika na mradi huu kuwa milioni tano. Mpango ulianza mwaka 2000 na umehusisha Wilaya 24. 44

Upasuaji wa Mabusha au mishipa ya kushuka unaendelea katika mkoa wa Pwani hususan katika hospitali ya Wilaya ya Mafia na hospitali ya Wilaya ya Kibaha. Idadi iliyofikiwa ya waliopasuliwa katika Mkoa wa Pwani ni 2,000. Aidha, Mpango ulishirikiana na Mpango wa kutokomeza Usubi katika zoezi la usambazaji na unyweshaji wa dawa ya Ivemectin katika Wilaya za Lushoto, Korogwe na Muheza. Hatua hii iliongeza ufanisi mkubwa kwani asilimia kubwa ya watu walikunywa dawa na hivyo kufanya mipango yote miwili kufanikiwa. Kituo cha Kuimarisha Mikakati Thabiti ya Kudhibiti Malaria (CEEMI) Ujenzi wa jengo la Kituo cha Kuimarisha Mikakati Thabiti ya Kudhibiti Malaria (CEEMI) ulikamilika na jengo kufunguliwa rasmi na Mhe. Naibu Waziri wa Afya Dk. Hussein Mwinyi (MB) Septemba 16, 2004. Jengo hili linatumika kwa ushirika na Mpango wa Taifa wa kuthibiti Malaria. Ushirika huu umerahisisha kujenga mahusiano ya karibu na kuleta ufanisi katika kupiga vita dhidi ya Malaria nchini. Matarajio ya Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu mwaka 2005/2006 Utafiti wa Malaria Taasisi inatarajia kufanya utafiti wa dawa mchanganyiko dhidi ya Malaria ili kuweza kutoa ushauri sahihi juu ya mchanganyiko huo wa dawa utakaoweza kukidhi haja na kupatikana kwa bei nafuu kwa jamii nzima ya Wa-tanzania. Aidha, Taasisi inatarajia kufanya majaribio ya madawa yatokanayo na miti shamba yanayoweza kuua au kufukuza mbu wa aina mbalimbali. Miti kadhaa imejaribiwa na ipo inayotia matumaini. Ugonjwa wa Usubi Utafiti utaendelea kwa lengo la kudhibiti usubi kwa njia ya kuua wadudu waambukizaji na kutathmini matokeo ya kazi hiyo katika kupunguza maambukizi ya Usubi. Pia, utafiti wa kupima kiwango cha Usubi katika jamii inayoishi kando kando ya mito inayonyunyiziwa dawa utafanyika. Utafiti wa Dawa Asilia Mwaka 2005/2006, Taasisi itafanya utafiti wa dawa za Malaria, viuatilifu kwa mbu na viluwiluwi wa mbu. Aidha, dawa nyingine zinazotumiwa na wagonjwa wa UKIMWI zitaendelea kufanyiwa utafiti kadiri nyenzo zitakavyoruhusu. Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Matende Inatarajiwa kuwa mpango huu utawafikia walengwa 2,800,000 katika Manispaa tatu za mkoa wa Dar-es-Salaam. Mikakati iliyowekwa ni pamoja na kuunda kamati mbalimbali za uhamasishaji (mabenki, wanahabari, asasi zisizo za kiserikali na Wizara mbalimbali) zitakazosaidia katika uhamasishaji wa zoezi la kunywa dawa za kinga dhidi ya Matende na Mabusha na kuwapatia wanafunzi wa shule vipeperushi vyenye kubeba ujumbe muhimu ili wavipeleke majumbani mwao. 3.5 Matatizo na Changamoto 45

Pamoja na mafanikio mengi yaliyopatikana bado kuna matatizo yanayoikabili Wizara. Matatizo hayo ni pamoja na:- Uhaba wa wataalam wa Afya katika ngazi zote Kuongezeka kwa uzito wa kazi katika hosptiali zote kutokana na ongezeko la wagonjwa wa UKIMWI Kuibuka kwa magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza Kupanda kwa gharama za ukomboaji, utunzaji na usambazaji wa vifaa na dawa kutoka MSD hadi mikoani na Wilayani Uchakavu wa majengo ya kutolea huduma za Afya nchini (majengo ya hosptiali na vyuo vya mafunzo ya afya) Kuendelea kwa maambukizi ya UKIMWI Vifo vya akinamama vianvyotokana na uzazi na vifo vya watoto wachanga bado ni vingi Uhaba wa vifaa muhimu vya hospitali na dawa Upungufu wa rasilimali za kutosheleza mahitaji muhimu ya kisekta unaotokana na msukumo wa Kitaifa na Kimataifa kwa mfano fedha kwa ajili ya UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria. 3.6 Maeneo yaliyopewa kipaumbele mwaka 2005/2006 Malengo ya Wizara yameelekezwa katika maeneo muhimu yaliyotajwa katika Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini Tanzania (MKUKUTA) na yale yaliyopo katika Malengo ya Milenia. Maeneo yaliyopewa kipaumbele katika bajeti ya matumzi ya kawaida na ya maendeleo katika bajeti ya 2005/2006 ni haya yafuatayo:- Kuhakikisha kuwa wafanyakazi wote walio chini ya Wizara ya afya wanalipwa mishahara na stahili zao Kuimarisha huduma za afya zitolewazo na hospitali za Rufaa, Mikoa, Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati na kuhakikisha upatikanaji wa dawa muhimu pamoja na vifaa vya kutolea huduma Kupunguza vifo vya watoto wachanga na vifo vya akinamama wajawazito Kuimarisha huduma za chanjo, lishe na huduma za mama na mtoto na kudhibiti Malaria, Kifua Kikuu na Ukoma Kutoa huduma kwa akinamama na kinababa baada ya umri wa uzazi (post Reproductive Age Services for Women and Men) Kutoa huduma kwa akinamama wanaoathirika kutokana na matatizo yanayotokana na uzazi (Vesicle Vaginal Fistula VVF) Kupambana na jana la ugonwja wa UKIMWI na hasa katika kuboresha huduma za kinga ili kupunguza maambukizi pamoja na ununuzi wa dawa za kupugnuza makali ya UKIMWI Kupambana na ugonjwa wa Ngirimaji, Matende na Usubi Kuendeleza na kuimarisha mabadiliko katika Sekta ya Afya ikiwa ni pamoja na kufanya mapitio eneo la msamaha katika uchangiaji wa huduma za afya Kuzipatia hospitali Teule (DDH) na Mashirika ya Kujitolea (VAs) rasilimali ili kuongeza uwezo wa kutoa huduma kwa wananchi katika sehemu zisizo na Vituo vya Afya vya umma 46

Kuimarisha huduma za afya za Halmashauri za Wilaya katika kuendesha huduma za afya kwa kutoa usafiri kwa ajili ya usimamizi, ufuatiliaji na usambazaji wa dawa na vifaa tiba Kuongeza wafanyakazi wenye ujuzi katika taaluma mbalimbali na kutoa mafunzo ya kitaalam ya watarajali (pre-service), wataalam wa afya na ya kujiendeleza katika kada zote za afya Kuinua ubora wa afya ya mazingira Kuendeleza utafiti wa magonjwa ya binafamu Kutoa mchango wa Serikali katika miradi yaote inayopewa fedha na wahisani mbalimbali Kukamilisha ujenzi na ukarbati unaoendelea wa majengo ya hospitali na ya vyuo vya kutolea mafunzo ya afya vilivyo chini ya Wizara ya Afya Kuendelea na ununuzi wa vifaa muhimu vya uchunguzi kwa hospitali za rufaa na maalum Kufanya uchunguzi wa vyakula, dawa, kemikali na vipodozi, kutoa ushauri wa kitaalam na kutambua vyanzo vya vifo kwa kufanya uchunguzi wa kisayansi (forensic science) Kusimamia na kudhibiti kemikali za viwandani na majumbani utakaotekelezwa na Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Ununuzi wa magari ya vyuo ambavyo havina magari kabisa Ujenzi wa hosteli ya madaktari wanafunzi hspitali ya Rufaa Mbeya, Ukarabati wa wodi za wagonjwa hospitali ya Mirembe na ujenzi wa majengo ya hospitali ya Kibong oto. 47

4.0 RIPOTI YA HUDUMA ZA AFYA MIKOA 4.1 Utangulizi Taarifa za huduma za afya nchini zinajumuisha zile zinazotoka Mikoani na Hospitali za Rufaa/Maalum ambazo zimekuwa zikitolewa katika vikao vya Waganga Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Hospitali za Rufaa/Maalum. Lengo la ripoti hizi ni kutoa/kuonyesha hali halisi katika utoaji wa huduma ya afya katika sehemu hizo. Taarifa hizi zinaonyesha hali ilivyo katika maeneo ya watumishi, huduma, na mapato zikiainisha mafanikio, matatizo, mikakati ya kuendeleza mafanikio na kutatua mataizo yanayojitokeza. Kwa miaka kadhaa, watendaji katika ngazi ya Mikoa na Hospitali za Rufaa walikusanya takwimu mbalimbali kila mwaka. Hata hivyo ukusanyaji wa takwimu hizi haukufuata mfumo mmoja na hivyo ilikuwa vigumu kufanya majumuisho ya kitaifa na kufanya mlinganisho. Hata hivyo watendaji wachache wameendelea kutuma ripoti ambazo hazifanani kimfumo. Ili kuwa na uwiano na uelewa wa pamoja katika kutoa huduma ya afya kwa kuzingatia Mabadiliko katika Sekta ya Afya, Idara ya Tiba ilipewa jukumu la kuratibu uandaaji wa mwongozo utakaotumika kuandaa ripoti. Mwongozo wa mfumo huu umezingatia takwimu muhimu zinazorahisisha ufuatiliaji wa utendaji kitaifa na mfumo wa uwasilishaji wa takwimu hizo bila kuathiri ukamilifu na ubora na takwimu hizo. 4.2 Mchanganuo wa Idadi ya watu katika Mikoa Tanzania bara ina idadi ya watu wapatao 34,718,009 kati ya hao akina mama wenye umri wa miaka 15-49 ni 34,718,009 (20%), watoto wa umri <1 1,621,461 (5%) na watoto wa umri <5 ni 6,645,101 (19%). Jedwali na. 1. Jedwali na 1: Mchanganuo wa Idadi ya watu katika Mkoa Mikoa Idadi ya Watu Mama Umri wa Miaka 15-49 Watoto Umri < 1 Watoto Umri < 5 Arusha 1,387,650 277,529 55,506 277,529 Dar es Salaam 2646921 430182 106974 446456 Dodoma 1777175 363426 71088 363426 Iringa 1524223 356565 60969 304885 Kagera 2146919 428933 89926 426244 Kilimanjaro 1430499 261160 46804 240032 Kigoma 1503989 59801 300798 305899 Lindi 825302 148554 24759 148554 Manyara 1128138 226527 42276 226527 Mara 1136393 286718 57545 286718 Mbeya 2425161 433009 84179 410415 Morogoro 1852504 369144 74098 370500 Mtwara 1174593 245889 44460 221739 Mwanza 3119237 601672 128206 601672 48

Pwani 928325 216272 28206 709247 Rukwa 1235046 245650 49739 25650 Ruvuma 1145467 481340 49495 481340 Singida 1170076 234017 46803 234017 Shinyanga 2975594 580469 116638 541488 Tabora 1479583 373915 74783 373916 Tanga 1705214 306930 68209 358094 Jumla Kitaifa 34,718,009 6,927,702 1,621,461 6,645,101 4.3 Mchanganuo wa hali ya Vifo vya Watoto na Akinamama wajawazito katika Mikoa Kasi ya vifo vya watoto umri wa chini ya mwaka mmoja kati ya vizazi hai 1,000 ilikuwa ya juu kwa mikoa ya Tanga (255), Pwani (153), Mtwara (126) na Kagera (106). (Mchoro na. 1). Mchoro 1: Kasi ya Vifo Vya Watoto Umri Chini ya Mwaka 1 Kasi ya vifo kati ya watoto 100 300.0 250.0 200.0 150.0 100.0 50.0 0.0 Tanga 255 153 126 106 90 Pwani Mtwara Kagera Morogoro 90 Shinyanga 74 Dar es Salaam 73 72 60 Iringa Lindi Mbeya Dodoma 56 40 Kilimanjaro 37 Mwanza 36 Arusha 36 Mara 16 Ruvuma 8 Manyara 78 Jumla Kitaifa, 2004 Mikoa Kuhusu kasi ya vifo vya watoto miaka 5+, kati ya vizazi hai 1000 mikoa iliyoongoza ni Rukwa (648), Tanga (487), Pwani (396), Mtwara (212), Kagera (167) na Morogoro (140). (Mchoro na. 2). 49

700.0 648 Mchoro 2: Kasi ya Vifo Vya Watoto Umri wa Miaka 5+ Kasi ya vifo kati ya watoto 100 600.0 500.0 400.0 300.0 200.0 100.0 487 396 212 167 142 140 100 79 70 51 43 41 41 29 27 27 21 14 6 137 0.0 Rukwa Tanga Pwani Mtwara Kagera Ruvuma Morogoro Dar es Salaam Mbeya Dodoma Mwanza Tabora Iringa Lindi Kilimanjaro Arusha Manyara Shinyanga Kigoma Mara Jumla Kitaifa, 2004 Mikoa Kuhusu vifo vya akinamama kwa sababu ya uzazi kasi kubwa ilikuwa kwa mikoa ya Morogoro (387), Manyara (328), Lindi (326), Kagera (266), Mbeya (265) na Tabora (261). (Mchoro na.3). 400 350 387 Mchoro 3: Kasi ya Vifo Vya Mama Wajawazito Katika Kila Mkoa 328 326 Kasi ya vifo 300 250 200 150 266 265 261 257 252 221 205 189 176 166 163 156 114 113 281 253 280 200 100 67 53 50 35 0 Morogoro Manyara Lindi Kagera Mbeya Tabora Mwanza Shinyanga Iringa Dodoma Mtwara Tanga Arusha Mara Ruvuma Kigoma Kilimanjaro Rukwa Pwani Dar es Salaam Jumla Kitaifa, 2001 Jumla Kitaifa, 2002 Jumla Kitaifa, 2003 Jumla Kitaifa, 2004 Mikoa 4.4 Mchanganuo wa Maeneo ya Kiutawala katika Mikoa Kiutawala Tanzania Bara kuna Tarafa 550, Vijiji 10,478, na Kaya 5,598,655. (Jedwali na 2). Jedwali na 2: Mchanganuo wa Maeneo ya Kiutawala katika Mikoa Mikoa Idadi ya Vijiji Idadi ya Kaya Idadi ya Tarafa Arusha 315 184443 22 Dar es Salaam 0 623939 10 Dodoma 496 382914 26 Iringa 720 357397 33 Kagera 556 393808 25 Kilimanjaro 492 249021 21 Kigoma 238 210263 19 50

Lindi 453 190761 28 Manyara 300 199860 52 Mara 444 259699 20 Mbeya 963 483387 27 Morogoro 817 141 30 Mtwara 232 170 35 Mwanza 715 368561 33 Pwani 417 81 25 Rukwa 436 222868 21 Ruvuma 514 238659 22 Singida 366 198589 21 Shinyanga 868 369598 27 Tabora 489 307503 20 Tanga 647 356993 33 Jumla Kitaifa 10478 55986655 550 4.5a: Uwiano wa Wataalam wa Afya na Idadi ya Watu Mikoa yenye uwiano mzuri wa Madaktari na idadi ya watu ni Arusha (1:38,545), Pwani (1: 42,196), Dar es Salaam (1:50,322) na Mara (1:58,120). Mikoa inayoongoza kwa kutokuwa na uwiano mzuri ni Rukwa na Mwanza (1:308,761 na 1:307,770). (Mchoro na. 4). Mchoro 4: Uwiano wa Daktari Mmoja na Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa Mkoa Rukwa Mwanza Shinyanga Iringa Dodoma Mbeya Manyara Tabora Morogoro Lindi Kilimanjaro Mtwara Kigoma Kagera Tan ga Ruvuma Mara Dar es Salaam Pwani Arusha Jumla Kitaifa, 2004 50,322 42,196 38,545 65,950 60,618 58,731 58,120 132,500 119,371 116,190 115,692 115,692 145,159 143,159 137,980 168,179 152,638 254,037 308,761 307,770 305,978-50,000 100,000 150,000 200,000 250,000 300,000 350,000 Idadi ya watu Kuhusu Madaktari Wasaidizi mikoa inayoongoza kwa kuwa na uwiano mzuri ni Mara (1:19,593), Arusha (1:22,381), Tanga (1:23,906) na Kilimanjaro (1:25,118). Mikoa inayoongoza kwa kutokuwa na uwiano mzuri ni Shinyanga (1:377,782), Pwani (1:197,552) na Mwanza (1:89,259). (Mchoro na. 5). 51

Mchoro 5: Uwiano wa Daktari Msaidizi Mmoja na Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa Mkoa Shinyanga Pwani Mwanza Kagera Tabora Manyara Dodoma Morogoro Mbeya Mtwara Kigoma Rukwa Dar es Salaam Lindi Ruvuma Iringa Kilimanjaro Tan ga Arusha Mara Jumla Kitaifa, 2004 26,741 25,118 23,906 22,381 19,593 38,595 35,419 34,816 30,121 47,513 44,235 44,235 65,951 57,264 57,264 53,690 51,458 67,145 89,259 197,552 377,782-50,000 100,000 150,000 200,000 250,000 300,000 350,000 400,000 Idadi ya watu Mikoa yenye uwiano mzuri wa Afisa Tabibu na idadi ya watu ni Tanga (1:5,715), Arusha (1: 5,930), Lindi (1:6,113) na Mara (1:6,210). Mikoa inayoongoza kwa kutokuwa na uwiano mzuri ni Pwani na Shinyanga (1:56,606 1:36,805). (Mchoro na. 6). Mchoro 6: Uwiano wa Afisa Tabibu (CO) Mmoja na Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa Mkoa Pwani Shinyanga Dar es Salaam Mtwara Kigoma Morogoro Mwanza Dodoma Rukwa Kagera Tabora Manyara Iringa Kilimanjaro Ruvuma Mbeya Mara Lindi Arusha Tan ga Jumla Kitaifa, 2004 12,966 12,966 12,029 11,565 10,989 10,647 9,956 8,103 8,103 7,293 7,093 7,076 6,913 6,210 6,113 5,930 5,715 13,307 23,056 36,805 56,606-10,000 20,000 30,000 40,000 50,000 60,000 Idadi ya watu Kuhusu Afisa Muuguzi mikoa inayoongoza kwa kuwa na uwiano mzuri ni Shinyanga (1:1226), Iringa (1:1,746), Ruvuma (1:1,932) na Arusha (1:2,234). Mikoa inayoongoza kwa kutokuwa na 52

uwiano mzuri ni Morogoro (1:12,561), Mbeya (1:12,462) na Dar ea Salaam (1:9,054). (Mchoro na. 7). Mchoro 7: Uwiano wa Afisa Muuguzo (NO & TN) Mmoja na Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa Mkoa Morogoro Mbeya Dar es Salaam Mtwara Kigoma Dodoma Kagera Mwanza Pwani Rukwa Mara Tabora Manyara Kilimanjaro Tan ga Lindi Arusha Ruvuma Iringa Shinyanga Jumla Kitaifa, 2004 3,642 3,609 3,609 3,504 2,921 2,723 2,234 1,932 1,746 1,226 5,428 5,221 4,761 4,491 5,349 9,054 8,796 8,796 8,265 12,561 12,462-2,000 4,000 6,000 8,000 10,000 12,000 14,000 Idadi ya watu 4.5b: Uwiano wa Wataalam wa Afya ya Kinywa (Dental) na Idadi ya Watu Mikoa ya Arusha na Dar es Salaam ndiyo yenye uwiano mzuri na wataalam wa Afya ya Kinywa wakati uwiano usio mzuri upo zaidi kwa mikoa ya Mwanza, Morogoro Mbeya na Tabora. (Jedwali na.3). Jedwali na 3: Uwiano wa Wataalam wa Afya ya Kinywa (Dental) na Idadi ya Watu Mikoa Madaktari wa Meno (DDS) Madaktari Wasaidizi wa Meno (ADO) Tabibu Meno (DTs) Fundi Sanifu Meno (DLTs) Arusha 1:277,530 1:231275 1:277,530 1:101724 Dar es Salaam 1:258,419 1:339309 1:256,591 1:658584 Dom 1:888,587 1:444,293 1:888,587 1:1,777,175 Iringa 1:508,075 1:381055 1:27,017 1:524223 Kagera 1:1,073,460 1:155794 1:450,566 1:14453 Kilimanjaro 1:1,376,702 1:286100 1:698,351 1:1376702 Kigoma 1:1,503,989 1:501,330 1:501330 0 Lindi 1:417,697 1:412,651 1:206,326 0 Manyara 1:128,138 1:64,079 42,713 0 Mara 1:1,136,393 1:284,098 1:568,196 1:1,136,393 Mbeya 1:277,547 1:119,004 1:156,542 1:299867 Morogoro 1:1,852,504 1:231,563 1:168,409 1:926252 Mtwara 1:174593 1:245,889 1:44,460 1:174593 Mwanza 1:3,119,237 1:445,606 1:445,606 1:1559619 Pwani 1:928,325 1:309,333 1:185,,665 0 Rukwa 1:1,235,046 1:617,523 1:617,523 1:1235046 Ruvuma 1:391542 1:293656 1:391542 1:1145467 Singida 1:1170076 1:1170078 1:39003 0 Shinyanga 1:2975594 1;991865 1;743899 0 Tabora 1:1,479,583 1:429477 1:428253 0 Tanga 1:424326 1:339460 1:242472 1:1697302 Jumla Kitaifa 4.5: Idadi ya Vituo vya kutolea Tiba na Umiliki wake 53

Zipo Zahanati 4,678 nchini ambapo 3,109 (66%) zinamilikiwa na Serikali, 737 (15%) Mashirika ya Dini, 739 (16%) Watu Binafsi na 135 (3%) Mashirika ya Umma (Mchoro na 8). Mchoro 8: Umiliki wa Zahanati Katika Tanzania Mashirika ya Umma 3% Binafsi 16% Mashirika ya Dini 15% Serikali 66% Mkoa wa Mwanza unaoongoza kwa kuwa na zahanati nyingi (336 ), ukifuatiwa na mikoa ya Kilimanjaro (332), Dar es Salaam (330), Mbeya (307) na Iringa (282). (Mchoro na 9). Mchoro 9: Jumla ya Zahanati ZoteKatika Kila Mkoa Mikoa Mwanz a Kilimanjaro DSM Mbeya Iringa Shinyanga Morogoro Dodoma Tan ga Kagera Tabora Kigoma Arusha Mara Rukwa Pwani Ruvuma Lindi Mtwara Singida Manyara 139 133 155 154 152 213 207 198 196 186 184 182 240 231 249 282 272 307 336 332 330 0 50 100 150 200 250 300 350 Idadi Vituo vya Afya 54

Vipo vituo vya Afya 491 nchini, ambapo vituo 333 (67%) vinamilikiwa na Serikali, 113 (23%) Mashirika ya Dini, 10 (2%) Mashirika ya Umma na 37 (8%) Watu Binafsi. (Mchoro na. 10). Mchoro 10: Umiliki wa Vituo Vya Afya Mashirika ya Umma 2% Binafsi 8% Mashirika ya Dini 23% Serikali 67% Mkoa unayoongoza kwa kuwa na vituo vyingi vya afya ni Mkoa wa Mwanza ukifuatiwa na mikoa ya Iringa, Kilimanjaro na Morogoro. (Mchoro na 11). Mchoro 11: Idadi ya Vituo Vya Afya Katika kila Mkoa Mwanza Iringa 34 39 Kilimanjaro 32 Morogoro 31 Kagera 30 Arusha 29 Rukwa 28 Mbe ya 28 Shinyanga 27 Mkoa Tan ga DSM Ruvuma 21 23 25 Dodoma 21 Mara Kigoma 18 20 Pwani 17 Tabora 15 Singida 15 Lindi 15 Mtwara Manyara 11 14 0 5 10 15 20 25 30 35 40 Idadi Hospitali 55

Hospitali zipo 217, ambapo 86 (38%) zinamilikiwa na Serikali, 88 (39%) Mashirika ya Dini, 17 (7%) Mashirka ya Umma na 37 (16%) Watu Binafsi. (Mchoro na. 12). Mchoro 12: Umiliki wa Hospitali Katika Asilimia Tanzania Mashirika ya Umma 7% Binafsi 16% Serikali 38% Mashirika ya Dini 39% Mchoro na. 13 unaonyesha umiliki wa vituo vyote vya kutolea tiba Tanzania Bara 2004. Mchoro 13: Umiliki wa Vituo Vyote Vya Kutolea Tiba, Tanzania Mashirika ya Umma 3% Binafsi 15% Serikali 65% Mashirika ya Dini 17% 4.7: Idadi ya vitanda vya kulaza wagonjwa kwa kufuata Miliki ya Vituo vya kutolea tiba Vituo vya Afya 56

Uwezo wa vituo vya Afya kulaza wagonjwa nchini ni vitanda 10,184 na idadi ya vitanda vilivyopo ni 9,121 sawa na asilimia 86.8% ya uwezo wa kulaza. Kwa ujumla Mikoa ya Iringa, Tanga na Mwanza inaozongoza kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kulaza wagonjwa. Wakati Mikoa ya Manyara, Arusha na Dar es Salaam ina uwezo mdogo. Serikali inaongoza kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kulaza wagonjwa kwa (68.6%) ikifuatiwa na Mashirika ya Dini (30%), Watu Binafsi na (4.5%) Mashirika ya Umma (2%). (Jedwali na.4). Jedwali Na 4: Idadi ya Vitanda vya kulaza Wagonjwa kwa kufuata Miliki ya Vituo vya kutolea Tiba (Vituo vya Afya) Mikoa Idadi ya Vitanda Kwenye Vituo vya Huduma Jumla Serikali Mashirika ya Dini Mashirika ya Umma Binafsi Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Arusha 127 132 188 268 8 8 70 70 293 478 Dar es Salaam 126 84 100 100 0 15 40 50 216 249 Dodoma 422 373 80 97 0 0 30 22 490 492 Iringa 396 294 670 614 0 0 57 21 1123 929 Kagera 298 295 180 145 0 0 16 25 549 410 Kilimanjaro 405 453 33 58 0 5 18 53 356 569 Kigoma 237 294 147 223 15 0 15 0 414 217 Lindi 237 167 33 33 0 0 0 6 270 220 Manyara 70 137 30 78 0 0 0 0 60 215 Mara 260 201 100 104 25 14 50 50 435 369 Mbeya 504 414 173 157 0 0 3 29 760 547 Morogoro 390 297 50 30 52 29 30 0 406 362 Mtwara 245 255 115 110 0 0 0 0 360 365 Mwanza 777 497 96 96 0 0 35 35 858 177 Pwani 216 15 0 16 247 Rukwa 400 327 200 136 0 0 0 0 600 463 Ruvuma 548 524 415 630 0 0 0 0 963 1154 Singida 199 199 58 30 0 0 0 0 257 229 Shinyanga 490 377 50 0 0 0 0 0 552 437 Tabora 230 171 95 110 0 0 0 0 325 281 Tanga 660 497 237 201 0 0 13 13 897 711 Jumla Kitaifa 7021 6204 3050 3235 100 71 377 390 10184 9121 Hospitali Uwezo wa Hospitali nchini kulaza wagonjwa ni vitanda 25,710 na idadi ya vitanda vilivyopo ni 25,641 ikiwa na vitanda 69 zaidi. Serikali inaongoza kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kulaza wagonjwa (54.1%) ikifuatiwa na Mashirika ya Dini (39.9%), Watu Binafsi (4.8) na Mashirika ya Umma (1.5%). Mikoa yenye uwezo mkubwa ni Mwanza, Iringa na Dodoma na ile yenye uwezo mdogo ni Rukwa, Manyara na Kilimanjaro. (Jedwali na. 5). Jedwali Na 5: Idadi ya Vitanda vya kulaza Wagonjwa kwa kufuata Miliki ya Vituo vya kutolea Tiba (Hospitali) Mikoa Idadi ya Vitanda Kwenye Vituo vya Huduma Jumla Serikali Mashirika ya Dini Mashirika ya Umma Binafsi Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Uweazo Vilivyopo* Uwezo Vilivyopo* Arusha 701 642 649 618 30 30 12 12 1192 1302 Dar es Salaam 632 522 66 66 0 0 606 606 1184 1094 Dodoma 1463 1329 580 330 0 0 0 0 2043 1659 Iringa 925 745 990 961 150 40 235 85 2300 1831 Kagera 305 192 580 690 0 0 60 60 1487 1300 Kilimanjaro 542 873 320 1147 0 35 0 130 562 1735 Kigoma 549 549 227 227 0 0 0 0 776 776 Lindi 616 530 411 397 30 24 0 0 1057 951 Manyara 545 454 200 530 0 0 0 0 404 1004 Mara 769 769 285 262 0 0 0 0 1053 1031 Mbeya 590 450 899 901 0 0 40 30 1529 1381 Morogoro 520 527 778 790 135 135 73 73 1506 1525 Mtwara 1010 877 350 300 0 0 0 0 1360 1177 Mwanza 1087 854 1693 1693 0 0 20 20 2780 2508 Pwani 498 100 213 0 811 Rukwa 500 390 150 90 0 0 0 0 650 480 Ruvuma 325 665 645 1015 0 0 0 0 970 1679 Singida 630 444 995 912 0 0 0 0 1625 1356 Shinyanga 1038 838 250 188 0 0 88 88 1376 1104 Tabora 790 693 479 0 0 0 0 0 1269 1172 57

Tanga 948 559 542 520 0 0 65 65 1557 1444 Jumla Kitaifa 14160 13400 10444 10722 345 477 1199 1169 25710 25641 Mkoa wa Dar es Salaam una uwiano mbaya wa kitanda kimoja na idadi ya watu (1:1,686), ukifuatiwa na Kigoma (1:1,205), Rukwa (1:1186) na Kagera (1:1,177). Mikoa iliyo na uwiano mzuri ni Iringa (1:540), Shinyanga (1:437) na Singida (1:229). Kitaifa uwiano huo ni 1:928. (Mchoro na. 14). Mchoro 14: Uwiano wa Kitanda Kimoja kwa Idadi ya Watu Katika Kila Mkoa 1,800 1,686 1,600 1,400 1,200 1,205 1,186 1,177 1,154 1,091 1,070 Idadi ya Watu 1,000 800 974 929 851 837 787 759 729 724 673 598 928 600 540 400 437 200 229 - Dar es Salaam Kigoma Rukwa Kagera Tabora Ruvuma Mwanza Mbeya Mara Morogoro Manyara Pwani Mikoa Dodoma Tanga Mtwara Arusha Lindi Kilimanjaro Iringa Shinyanga Singida Jumla Kitaifa 4.8: Watumishi wa sekta ya Afya na Sehemu za Kazi Jumla ya watumishi waliopo kwenye sekta ya afya mikoani ni 31,952 ambapo 23,874 (74.7%) wameajiriwa Serikalini. Kwa ujumla Serikali ina upungufu wa watumishi 12,843 ikiwa ni 40.2%. (Jedwali na 6). Jedwali Na 6: Watumishi wa sekta ya Afya na Sehemu za Kazi Sehemu ya Kazi Watumishi Serekali Mashirika ya Dini Mashirika ya Umma Mashirika Binafsi Jumla Waliopo Pungufu Waliopo Pungufu Waliopo Pungufu Waliopo Pungufu Waliopo Pungufu 1 Medical Doctors 185 181 70 69 3 2 33 18 291 270 2 Specialist Doctors 43 74 22 29 5 2 17 2 87 107 3 Dental Surgeons 27 39 0 7 0 0 1 0 28 46 4 Specialist Dental Surgeons 8 14 0 5 0 0 1 0 9 19 5 Pharmacists 65 60 3 27 1 0 2 0 71 87 6 Chemists 12 22 0 2 1 0 3 3 16 27 7 Assistant Medical Officers 522 488 220 139 16 4 34 7 792 638 8 Assistant Dental Officers 338 178 19 46 2 1 13 8 372 233 9 Dental Therapists 307 115 29 49 13 2 15 10 364 176 10 Clinical Officer 2186 2128 420 635 49 7 116 25 2771 2795 11 Assistant Clinical Officers 998 417 119 22 1 0 18 6 1136 445 12 Nursing Officers 1466 519 980 275 32 22 43 6 2521 822 13 Nurse Tutors 506 348 60 19 47 10 10 0 623 377 14 Trained Nurses 688 805 294 252 7 0 11 2 1000 1059 15 Nurse Midwives 2225 1612 920 604 1 0 212 41 3358 2257 16 Public H. Nurse B 1492 2259 76 398 3 0 20 4 1591 2661 17 MCH Aides 1347 449 77 4 3 1 16 0 1443 454 18 Medical Laboratory Technicians 274 144 44 67 0 5 17 10 335 226 19 Radiographers 56 96 30 39 1 0 1 0 88 135 20 Dental Technicians 74 113 6 31 0 0 0 0 80 144 21 Optometry Technicians 19 83 11 26 0 0 0 0 30 109 22 Orthopaedic Technicians 8 46 7 13 0 0 0 0 15 59 23 Physiotherapists 49 84 14 26 1 0 1 0 65 110 58

24 Chemical Laboratory Technicians 12 31 2 5 0 1 0 0 14 37 25 Health Officers 676 358 12 24 3 2 8 0 699 384 26 Pharmac. Technicians 144 297 31 35 4 8 0 0 179 340 27 Medical Records Officers 135 232 65 84 0 1 4 14 204 331 28 Lauderers 176 199 84 51 4 0 2 4 266 254 29 Catering Officers 9 87 13 18 3 0 0 4 25 109 30 Health Secretaries 57 99 29 34 2 0 0 3 88 136 31 Wahudumu wa chumba cha maiti 111 87 35 43 6 2 28 3 180 135 32 All Others 1814 243 777 77 37 21 132 9 2760 350 33 Wahudumu Wauguzi 5961 449 1874 103 40 4 149 5 8024 561 34 Wahudumu Maabara 1221 118 211 22 6 0 27 1 1465 141 35 Wahudumu Meno 135 76 37 32 2 1 9 1 183 110 36 Wahudumu Pharmacy 97 82 36 40 2 1 12 2 147 125 37 Wahudumu X-ray 55 46 31 8 1 0 3 0 90 54 38 Accounts Assistant 53 67 48 33 0 0 7 3 108 103 39 Drivers 323 98 105 7 4 1 2 0 434 106 Jumla ya Watumishi Kitaifa 23874 12843 6811 3400 300 98 967 191 31952 16532 4.9a: Magari/Pikipiki Kuna jumla ya magari 733 ambapo asilimia 83.8 yanafanya kazi. Mikoa ya Mwanza na Mara inaongoza kwa kuwa na magari yanayofanya kazi (yote yanafanya kazi). Wakati Mikoa ya Rukwa na Iringa inaongoza kwa kuwa na magari mengi yasiofanya kazi asilimia 54 na 31. Kwa upande wa pikipiki Serikali ina pikipiki 433ambapo 90% ndizo zinazofanya kazi. Mikoa ya Kilimanjaro, Kigoma, Lindi na Rukwa pikipiki zote zinafanyakazi. Mkoa wa Iringa unaogoza kwa kuwa na pikipiki mbovu 35% ya pikipiki zote. (Jedwali na. 7). Jedwali na. 7: Magari/ Pikipiki Mikoa Hali ya Magari/Pikipiki Jumla Yanayofanya Kazi Yasiyofanya Kazi Magari Pikipiki Magari Pikipiki Magari Pikipiki Arusha 38 12 6 1 44 13 Dar es Salaam 29 22 2 1 31 23 Dodoma 24 24 7 2 31 26 Iringa 32 24 15 13 47 37 Kagera 25 14 3 2 28 16 Kilimanjaro 29 24 9 0 38 24 Kigoma 33 16 2 0 35 16 Lindi 30 15 8 0 38 15 Manyara 21 9 5 1 26 10 Mara 23 10 0 1 23 11 Mbeya 35 24 6 2 41 26 Morogoro 40 53 4 2 44 55 Mtwara 14 20 2 2 16 22 Mwanza 26 30 0 4 26 34 Pwani 32 0 2 34 0 Rukwa 23 4 27 0 50 8 Ruvuma 18 14 4 1 22 15 Singida 27 24 9 3 36 27 Shinyanga 35 22 4 0 39 22 Tabora 30 19 2 4 32 23 Tanga 47 10 5 0 52 10 Jumla Kitaifa 611 390 122 39 733 433 4.9b: Hadubini Kuna jumla ya hadubini 2,146 ambapo 80% zinafanya kazi. Mikoa yenye hadubini zinazofanya kazi kwa wingi ni Arusha na Dodoma. Mikoa yenye hadubini nyingi mbovu ni Rukwa na Lindi. (Jedwali na. 8). 59

Jedwali na. 8: Hadubini Mikoa Hali ya Hadubini Jumla Zinazofanya Kazi Zisizofanya Kazi Arusha 102 9 111 Dar es Salaam 75 16 91 Dodoma 64 6 70 Iringa 86 37 113 Kagera 176 27 203 Kilimanjaro 192 32 224 Kigoma 92 12 104 Lindi 30 15 54 Manyara 51 16 116 Mara 107 18 135 Mbeya 52 14 66 Morogoro 128 26 154 Mtwara 60 16 76 Mwanza 111 15 126 Pwani 45 12 57 Rukwa 23 21 44 Ruvuma 70 13 83 Singida 70 8 78 Shinyanga 63 16 79 Tabora 61 18 79 Tanga 67 16 83 Jumla Kitaifa 1,725 363 2146 4.9c: Mashine za X-ray Kuna jumla ya mashine za X-ray 244 mikoani ambapo 83% zinafanyakazi. Mikoa inayoongoza kwa kuwa na mashine nyingi za X-ray zinazofanya kazi ni Da es Salaam na Arusha wakati mikoa yenye X-ray chache zinazofanya kazi ni Dodoma na Rukwa. (Jedwali na. 9). Jedwali na. 9: Mashine za X-ray s Mikoa Hali ya X-ray Jumla Zinazofanya Kazi Zisizofanya Kazi Arusha 16 5 21 Dar es Salaam 28 2 30 Dodoma 4 2 6 Iringa 11 5 6 Kagera 10 0 10 Kilimanjaro 19 4 23 Kigoma 6 2 8 Lindi 10 4 14 Manyara 5 0 5 Mara 8 1 9 Mbeya 8 3 11 Morogoro 8 2 10 Mtwara 6 2 8 Mwanza 9 4 13 Pwani 7 1 8 Rukwa 5 3 8 Ruvuma 7 3 10 Singida 5 5 10 Shinyanga 9 0 9 Tabora 8 6 14 Tanga 11 11 Jumla Kitaifa 200 54 244 4.9d: Vifaa vya Utakasaji Kuna jumla ya mashine za utakasaji 3,116 mikoani ambapo 87% zinafanyakazi. Mikoa ya Rukwa, Lindi na Kigoma inaongoza kwa kuwa na mashine nyingi zisizofanyakazi. (Jedwali na. 10). 60

Jedwali na. 10: Vifaa vya Utakasaji Mikoa Hali ya Mashine za Utakasaji Jumla Zinazofanya Kazi Zisizofanya Kazi Arusha 34 17 51 Dar es Salaam 199 27 226 Dodoma 281 18 299 Iringa 72 2 74 Kagera 235 36 271 Kilimanjaro 382 52 434 Kigoma 11 5 16 Lindi 23 12 35 Manyara 24 5 29 Mara 14 0 14 Mbeya 520 83 613 Morogoro 300 20 320 Mtwara 96 4 100 Mwanza 84 24 108 Pwani 14 4 18 Rukwa 86 53 139 Ruvuma 15 5 20 Singida 24 26 50 Shinyanga 8 0 8 Tabora 18 14 32 Tanga 255 4 259 Jumla Kimkoa 2,695 411 3,116 4.9e: Vifaa vya Tiba ya Meno (Dental Unit and Chair) Jumla ya vifaa vya tiba ya meno ni 289 na vinavyofanyakazi ni 226 ambayo ni sawa na 78.7%. Mikoa ambayo ina vifaa vingi visivyofanya kazi ni Dar es Salaam (40%), Dodoma (40%) na Kilimanajro (35.7%). (Jedwali na. 11). Jedwali na. 11: Vifaa vya Tiba ya Meno (Dental Unit and Chair) Mikoa Hali ya Vifaa Jumla Vinavyofanya Kazi Visivyofanya Kazi Arusha 15 1 16 Dar es Salaam 15 10 25 Dodoma 9 6 15 Iringa 15 2 17 Kagera 7 1 8 Kilimanjaro 9 5 14 Kigoma 6 4 10 Lindi 6 4 10 Manyara 5 1 6 Mara 6 3 9 Mbeya 14 5 19 Morogoro 13 2 15 Mtwara 6 2 8 Mwanza 15 5 19 Pwani 14 4 18 Rukwa 4 0 4 Ruvuma 12 2 14 Singida 8 4 12 Shinyanga 10 1 11 Tabora 17 3 19 Tanga 20 0 20 Jumla Kitaifa 226 65 289 4.10 Magonjwa yanayotolewa Taarifa 61

Jumla ya wagonjwa 451,166 walitolewa taarifa kutoka Mikoa yote. Ugonjwa wa Dysentry uliongoza kwa kutolewa taarifa (22%) ukifuatiwa na Typhoid (17%), Meningitis (15%), Animal Bites (15%) na Measels (15%). (Mchoro na 15). Mchoro 15: Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Watu Wote, 2004 Yellow Fever 0% Acute Flaccid Paralysis Cholera 0% 2% Typhoid 17% Dysentery 22% Plague 0% Animal Bites 15% Meningitis 15% Measles 15% Louse Borne Typhus (Relapsing Fever) 14% Kwa watu wa umri chini ya miaka mitano magonjwa yaliyotolewa taarifa ni Dysentry (85%), Typoid (5%), Cholera (4%) na Measles (1%). (Mchoro na. 16). Mchoro 16: Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Umri Miaka < 5, 2004 Measles 1% Meningitis 3% Plague 0% Animal Bites 0% Typhoid 5% Acute Flaccid Paralysis 0% Yellow Fever 0% Cholera 4% Louse Borne Typhus (Relapsing Fever) 2% Dysentery 85% 62

Kwa walio na umri wa miaka 5 na zaidi magonjwa yaliyotolewa taarifa zaidi ni Typhoid (18%), Animal Bites (16%), Meningitis (16%), Measles (16%), Dysentery (16%) na Relapsing Fever (16%). (Mchoro na 17). Mchoro 17: Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Umri Miaka 5+, 2004 Yellow Fever Acute Flaccid Paralysis 0% 0% Cholera 2% Dys entery 16% Typhoid 18% Plague 0% Animal Bites 16% Louse Borne Typhus (Relapsing Fever) 16% Meningitis 16% Measles 16% Vifo vilivyotokana na magonjwa yanayotolewa taarifa kwa watu wote ni kama inavyoonyeshwa kwenye Mchoro na. 18. Mchoro 18: Vifo Vitokanavyo na Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Umri Kwa Watu Wote, 2004 Animal Bites 16% Typhoid 17% Acute Flaccid Paralysis Cholera 2% Dysentry 3% 10% Louse Borne Typhus (Relapsing Fever) 10% Plague 0% Measles 10% Neonatal Tetanus 16% Meningitis 16% 63

Kwa mwaka 2003 magonjwa yaliyoongoza kwa kutolewa taarifa yalikuwa Kuhara Damu (75%), Homa ya Matumbo (15%) na Kipindupindu (8%). (Mchoro na 19). Mchoro 19: Magonjwa Yaliyotolewa Taarifa Watu Wote, 2003 Kichaa cha mbwa 1% Kipindupindu 8% Tauni 0% Homa ya Matumbo 15% Uti wa Mgongo 1% Kuhara damu 75% 4.10 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa wa Nje (OPD) Katika magonjwa yaliyojitokeza kwa wagonjwa wa umri chini ya miaka 5 wa OPD ni Malaria (39.4%), ARI (16.5%), Pneumonia (9.6%) na Diarrhoea Disease (7.1%). (Mchoro na 20). 64

Mchoro 20: Magonjwa 10 Yaliyojitokeza Zaidi kwa Wagonjwa wa Nje Umri < ya Miaka 5, 2004 Malaria ARI 16.5 39.4 Aina ya Magonjwa Pneumonia Diarrhoeal Disease Intestinal Worms Eye Infections Skin Infections Anaemia Minor surgical Conditions Ear Infections 4.6 3.9 3.4 2.5 2.0 1.5 7.1 9.6 Ill Defined Symptoms (No diagnosis) 2.0 Other Diagnosis 7.6 0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0 35.0 40.0 Idadi Katika Asilimia Kwa wagonjwa wenye umri wa miaka 5 na zaidi magonjwa yaliyoongoza ni Malaria (48.4%), ARI (10.6%), Intestinal Worms ( 4.5%) na Pneumonia (4.5%). (Mchoro na. 21). Mchoro 21: Magonjwa 10 Yaliyojitokeza Zaidi kwa Wagonjwa wa Nje Umri Miaka 5+, 2004 Malaria ARI 10.6 48.4 Aina ya Magonjwa Intestinal Worms Pneumonia Diarrhoeal Disease Minor surgical Conditions Eye Infections Anaemia Urinary Tract Infections Non-infectious Gastro-intest Disease 4.5 2.8 2.3 2.0 1.9 1.1 4.5 4.5 Ill defined symptoms 2.8 Others Diagnosis 14.7 0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0 35.0 40.0 45.0 50.0 Idadi Katika Asilimia Kuhusu Ugonjwa wa Malaria, wagonjwa wa nje wenye umri chini ya miaka 5 waliokuja na tatizo la ugonjwa huu walikuwa wengi kwa mikoa ya Mwanza (10.8%), Morogoro (9.3%), Dar eas Salaam (8.2) na Mbeya (7.8%). Mikoa iliyokuwa na mahudhurio ya chini ni Iringa (1.5%), Manyara (2.1%), Kilimanjaro (3.4%) na Lindi (3.5%). (Mchoro na.22). 65

Mchoro 22: Wagonjwa Wa Nje wenye umri < miaka 5 Waliokuja na Tatizo la Malaria kwa kila mkoa, 2004 Mwanza 10.8 Morogoro 9.3 DSM 8.2 Mbeya 7.8 Tan ga 7.4 Kagera Dodoma 5.8 7.3 Mikoa Tabora Mtwara Kigoma 5.4 5.5 5.8 Pwani Mara Rukwa 3.8 3.7 5.0 Arusha Lindi Kilimanjaro Manyara Iringa 1.5 2.1 3.5 3.4 3.7 0.0 2.0 4.0 6.0 8.0 10.0 12.0 Idadi ya Wagonjwa Katika % Kwa wagonjwa wa nje wenye umri wa miaka 5 na zaidi waliokuja na tatizo la ugonjwa wa Malaria walikuwa wengi kwa mikoa ya Dar es Salaam (13.9%), Mwanza (11.9%), Tanga (8.5%) na Morogoro (7.6%). Mikoa iliyokuwa na mahudhurio ya chini kwa Malaria ni Rukwa (0.3%), Arusha (0.3%), Lindi (2.6%) na Manyara (3.0% ). (Mchoro na 23)). Mchoro 23: Wagonjwa wa Nje Umri Miaka 5+ Walikuja na Tatizo la Malaria Kwa Kila Mkoa,2004 DSM 13.9 Mwanza 11.9 Tan ga 8.5 Morogoro Pwani Kilimanjaro Mara 5.9 7.6 7.3 7.3 Mikoa Mbe ya Dodoma Kigoma Kagera 3.9 5.2 5.7 5.6 Iringa 3.8 Mtwara Tabora Manyara Lindi Arusha Rukwa 0.3 0.3 3.8 3.5 3.0 2.6 0.0 2.0 4.0 6.0 8.0 10.0 12.0 14.0 Idadi Katika Asilimia 4.10 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa Waliolazwa Magonjwa yaliyojitokeza kwa wagonjwa waliolazwa wenye umri chini ya miaka mitano, ni Malaria (31.2%), ARI (18.1%), Diarrhoeal Diseases (7.6%), Pneumonia (5.8%) na Aanemia (4.8%). (Mchoro na 24). 66

Mchoro 24: Magonjwa 10 Yaliyojitokeza Zaidi kwa Waliolazwa Umri < 5, 2004 Magonjwa Malaria- Uncomplicated Acute Respiratory Infections Malaria- Severe, Complicated Diarrhoeal Diseases Pneumonia Anaemia Intestinal Worms Respiratory Disease (Nyinginezo) Tuberculosis Epilepsy Ill Defined Symtoms, no Diagnosis Other Diagnosis 0.9 0.7 0.7 2.4 4.8 4.0 5.8 7.6 8.3 15.5 18.1 31.2 0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0 35.0 Idadi Katika Asilimia Kwa wagonjwa waliolazwa wa umri wa miaka 5 na zaidi magonjwa yaliyoongoza ni Uncomplicated Malaria (40.1%), ARI (12.3%) Severe and Complicated Malaria (11.6%) na Diarrhoea diseases (7.1%). (Mchoro na. 25). Mchoro 25:Magonjwa 10 Yaliyojitokeza Zaidi kwa Waliolazwa Umri 5+, 2004 Malaria- Uncomplicated 40.1 Acute Respiratory Infections 12.3 Malaria- Severe, Complicated 11.6 Diarrhoeal Diseases 7.1 Magonjwa Pneumonia Intestinal Worms Anaemia Tuberculosis 3.9 3.8 2.5 1.3 HIV/AIDS 1.0 Urinary tract Infections (UTI) 0.8 Other Diagnosis 14.9 Ill Defined Symptoms, no Diagnosis 0.9 0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0 35.0 40.0 45.0 Idadi Katika Asilimia Uncomplicated Malaria, Severe and Complicated Malaria, Anaemia pamoja na Pneumonia yaliongoza kati ya Magonjwa kumi yaliyosababisha vifo kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5. (Mchoro na. 26). 67

Mchoro 26: Magonjwa 10 Yaliyosababisha Vifo kwa Watoto Wenye Umri < ya Miaka 5, 2004 Magonjwa Malaria- Uncomplicated Malaria- Severe, Complicated Anaemia Pneumonia Diarrhoeal Diseases Respiratory Disease (Nyinginezo) Peri-natal Conditions HIV/AIDS Epilepsy Severe Protein Ernegy Malnut. Other Diagnosis Ill Defined Symtoms, no Diagnosis 1.1 4.6 3.9 3.0 2.8 2.3 2.2 7.1 11.8 13.1 23.2 24.9 0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 Idadi Katika Asilimia Kwa wagonjwa wa umri wa miaka 5 na zaidi vifo vyingi vilisababishwa na magonjwa ya Severe and Complicated Malaria (19.2%), HIV/AIDS (10.5%) na Uncomplicated Malaria (7.2%). (Mchoro na. 27). Mchoro 27: Magonjwa 10 Yaliyosababisha Vifo kwa Watu Wenye Umri Miaka 5+, 2004 Magonjwa Other Diagnosis Ill Defined Symptoms, no Diagnosis Malaria- Severe, Complicated HIV/AIDS Malaria- Uncomplicated Tu bercu l os i s Pneumonia Neoplasms Anaemia Thyroid Diseases Cardiac Failure Diarrhoeal Diseases 2.7 2.6 7.3 7.2 6.7 6.2 5.6 5.3 5.0 10.5 19.2 21.6 0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 Idadi Katika Asilimia 4.13 Taarifa ya Huduma Maalum Huduma maaalum zilijumuisha upasuaji, kufunga uzazi (sterilization), blood transfusion, X- rays na ushauri nasaha. (Jedwali 12). mkoa wa Dodoma ulikuwa na Major Surgeries chache 68

(904) kuliko mikoa yote wakati Mkoa wa Pwani ndio uliokuwa na Minor surgeries chache (1,134) kuliko yote. Sterilization kwa wanaume ilifanyika zaidi katika Mikoa ya Singida (7,260), Tabora (2,150), Kigoma (111) na Dar es Salaam (27). Mikoa ya Mtwara, Kilimanjaro na Manyara ilikuwa na Units chache zaidi za damu walizoongezewa wagonjwa kuliko mikoa mingine. Vilevile, mkoa wa Dodoma ulikuwa na idadi kidogo zaidi ya X-rays zilizopigwa wakati mikoa iliyopiga idadi kubwa ni Morogoro, Mwanza, Mbeya, Arusha na Iringa. Mikoa ya Kilimanjaro na Dodoma inatoa huduma kidogo zaidi za ushauri nasaha kuliko mingine. (Jedwali na 12). Jedwali na 12: Taarifa za Huduma Maalum Mikoa Major Surgeries Minor Surgeries Sterilization Blood Transfusions (Units) Idadi ya X- rays Counseling Services Wanaume Wanawake Arusha 4410 23435 7 779 1226 22499 11311 Dar es Salaam 4294 70848 27 5646 43079 18496 18496 Dodoma 904 3602 0 213 3018 3691 368 Iringa 5067 12538 0 1141 5650 21667 10891 Kagera 5096 14728 0 1027 6257 4097 6872 Kilimanjaro 3187 12271 7 2108 1633 8029 216 Kigoma 2925 19315 111 932 9197 4713 6822 Lindi 3867 3825 0 814 4925 5534 2189 Manyara 3418 11759 0 597 1996 4591 8891 Mara 3234 3873 0 1310 11496 11389 6424 Mbeya 4575 15275 3 924 4614 22609 23876 Morogoro 5876 13728 0 196 6495 36331 10002 Mtwara 1306 13465 0 416 1655 4566 603 Mwanza 5121 5965 7 1067 16847 25364 11057 Pwani 2336 1134 0 141 3055 6666 0 Rukwa 1395 3147 0 844 6252 8896 1959 Ruvuma 5661 12753 2 994 12078 17868 5676 Singida 17845 673 4720 2540 6110 7825 1110 Shinyanga 4717 13699 1 709 14654 15363 3606 Tabora 2077 7256 2150 3543 13937 8604 5490 Tanga 5169 9525 3 467 8428 9003 0 Jumla Kitaifa 764180 272814 7038 26408 182603 267801 135859 4.14 Aina ya X-ray zilizopigwa Kati ya Picha za X-ray zilizopigwa nyingi zilikuwa za Chest (37%), zikifuatiwa na Extremeties (33%), na Abdomen (15%). (Mchoro na. 28). 69

Mchoro 28: Aina ya X-Ray Zilizopigwa 2004 Abdomen 15% Others 4% Chest 37% Pelvic 3% Contrast Studies 1% Skull 3% Spine 4% Extremeties 33% 4.14 Huduma za Maabara Kuhusu Huduma za Maabara, vipimo vilivyoongoza kwa wingi ni vipimo vya Damu (B/S) (45%) vikifuatiwa na Wekundu wa Damu (Hb) (19%), Mkojo (13%) na Choo kikubwa (12%). (Mchoro na. 29). Mchoro 29: Mchanganuo wa Huduma za Maabara, 2004 Wingi wa Damu (Hb) 19% Kaswende 5% Sukari Kwenye Damu 2% Damu 45% Ngozi 0% Makohozi 4% Mkojo 13% Choo 12% 4.16 Matokeo ya Vipimo vya Maabara Kati ya Vipimo vilivyopimwa vilivyoongoza kwa wingi ni Blood Slides (5,890,174), zikifuatiwa na Hb (2,194,096) pamoja na vipimo vya mkojo 1,013,392. (Jedwali na. 13). 70

Jedwali 13: Matokeo ya Vipimo vya Maabara VIPIMO VYA DAMU B/S Jumla ya Vipimo 9263382 Positive Malaria 4350210 Positive Borellia 3461 Positive others 3731 VIPIMO VYA WEKUNDU WA DAMU (Hb) Jumla ya Vipimo 3194715 HB chini ya 7.0g/L (50%) 545734 VIPIMO VYA KASWENDE RPR/VORL Jumla ya Vipimo 544231 Positive syphilis 68892 VIPIMO VYA SUKARI KWENYE DAMU (B/Sugar) Jumla ya vipimo 344372 Juu ya 10mmo/L (180mg/L) 64192 VIPIMO VYA CHOO Jumla ya Vipimo 1508440 Positive kwa H/worms 117943 Positive kwa Ascaries 68202 Positive kwa E. Histolytica 37640 Positive Nyingine 68944 VIPIMO VYA MKOJO Jumla ya Vipimo 1766116 Positive kwa S. Haematobium 130723 Positive kwa H. Vaginalis 19685 Positive kwa Sugar 32159 VIPIMO VYA MAKOHOZI Jumla ya Vipimo 448715 Positive AFB 78504 VIPIMO VYA PROTEIN KWENYE DAMU Jumla ya Vipimo 140671 Positive Urea/Nitrogen 1301 4.17 Huduma za kliniki ya Meno Kung oa meno ndiyo tiba inayoongoza kwa asilimia 77 kati ya huduma za kinywa zinazotolewa. (Mchoro na. 30). Mchoro 30: Aina ya Tiba ya Meno Kuziba (Filling) 10% Tiba Nyinginezo 13% Kung oa (Extraction) 77% 4.18 Mahudhurio ya Kliniki kwa Mama Wajawazito Matarajio ya mahudhurio ya kliniki kwa mama wajawazito yalikuwa 1,536,131. Jumla ya waliohudhurio ni 1,310,004 ikiwa ni pungufu kwa asilimia 14.7 ya matarajio. (Jedwali na. 13). 71

Jedwali na 13: Mahudhurio ya Kliniki kwa Mama Wajawazito Mikoa Matarajio Mahudhurio kwa Mara ya Kwanza < wiki 20 Wiki 20+ Jumla ya Mahudhurio Arusha 55506 24641 27069 51710 Dar es Salaam 106943 52216 52628 104844 Dodoma 71046 40535 28509 69044 Iringa 4782 17392 27859 45251 Kagera 89923 37232 49691 86923 Kilimanjaro 48000 21977 22132 44109 Kigoma 59801 22831 35633 58464 Lindi 24759 17609 983 18592 Manyara 33245 12068 24333 36401 Mara 59183 28201 28364 56565 Mbeya 156329 36000 39864 75864 Morogoro 74468 39377 40160 79537 Mtwara 39074 20812 21168 41980 Mwanza 124537 61354 71826 133180 Pwani Rukwa 61748 16981 36960 53941 Ruvuma 46985 21372 22113 43485 Singida 45661 22104 26586 48690 Shinyanga 240507 39639 71655 121279 Tabora 123361 23342 52145 75487 Tanga 70273 27493 37201 64694 Jumla Kitaifa 1536131 583179 716879 1310040 4.18 Kiwango cha wajawazito waliojifungulia kliniki Mikoa ya Kagera, Ruvuma na Lindi iliongoza kwa asilimia kubwa ya wajawazito waliojifungulia kliniki. (Mchoro na. 31). Mchoro 31: Kiwango cha Wajawazito Waliofungulia Kliniki Kagera Ruvuma Lindi Tan ga 83.6 78.0 76.0 96.0 Arusha Iringa 66.9 75.0 Mbeya 63.1 Tabora Mara 61.0 60.3 Mikoa Mwanza Kigoma Dom Morogoro Shinyanga Singida Kilimanjaro 51.4 49.0 47.0 46.8 42.7 42.5 59.2 Rukwa Manyara 35.0 30.0 Mtwara Avarage 29.0 57.5 0.0 10.0 20.0 30.0 40.0 50.0 60.0 70.0 80.0 90.0 100.0 Kiwango Katika Asilimia 4.20 Huduma kwa Mama waliojifungua Jumla ya akinamama 976,858 walijifungulia katika vituo vya kutolea tiba. Asilimia 91.6 walijifungua kwa njia ya kawaida. (Mchoro na 32). 72

Mchoro 32: Taarifa za Kujifungua Wajawazito Katika Vituo Vya Kutolea Tiba Kupasuliwa(C/S) 4.9% Njia Nyinginezo 3.1% Vacuum 0.4% Kawaida 91.6% 4.21 Matatizo ya Akina mama wakati wa kujifungua Tatizo kubwa ambalo liliwapata akina mama wakati wa kujifungua lilikuwa ni kutokwa na damu nyingi baada ya kujifungua (PPH). (Jedwali na.14). Jedwali na 14: Matatizo ya Akina Mama wakati wa Kujifungua Mikoa Kutokwa Damu Nyingi Kondo la Nyuma Kubaki Kuchanika Msamba (3rd degree) Matatizo Mengine APH PPH Arusha 37 100 83 3 171 Dar es Salaam 89 4869 89 22 660 Dodoma 1 55 35 4 69 Iringa 7 97 51 22 99 Kagera 58 266 137 16 116 Kilimanjaro 62 168 51 7 159 Kigoma 107 235 139 14 48 Lindi 7 114 113 0 218 Manyara 28 189 141 8 107 Mara 0 78 97 0 100 Mbeya 11 214 113 7 138 Morogoro 160 126 72 11 1717 Mtwara 8 111 69 3 33 Mwanza 36 674 300 12 340 Pwani 100 33 2 116 53 Rukwa 2 18 59 5 26 Ruvuma 15 171 57 5 522 Singida 5 87 87 10 66 Shinyanga 23 248 127 2 421 Tabora 25 378 246 12 248 Tanga 0 144 110 3 256 Jumla Kitaifa 776 8288 2091 272 5501 4.22 Sababu za Vifo vya Mama Wajawazito 73

Sababu iliyoongoza mwaka 2004 kusababisha vifo vingi vya akinamama ni PPH (16%) ikifuatiwa na Puperial Sepsis (15%), Anaemia (12%), Eclampsia (10%) na Malaria (9%). (Mchoro na 34). Mchoro 34: Sababu zilizosababisha vifo vya akina mama waliojifungua mwaka 2004 Other Diagnosis 14% PPH 16% Obstructed Labour 4% Septicaemia 3% Puerperial Sepsis 15% APH 4% Ruptured Uterus 6% HIV/AIDS 8% Anaemia 12% Malaria 8% Eclampsia 10% Kwa mwaka 2003 vifo vingi vilisababishwa na PPH (34%), Anaemia (10%), Puperial sepsis (7%), na Eclampsia (7%). (Mchoro na. 35). Mchoro 35: Sababu zilizosababisha vifo vya akina mama waliojifungua mwaka 2003 HIV/AIDS 5% Abraptid Placenta 1% Others 19% Ruptured Uteraus 5% Chronic Infection 1% PPH 34% Unsafe Abotion 0% Malaria 5% Obstracted labour 2% Anaemia 10% APH 2% Relapsing Fever 0% Eclampsia 7% EPH gestrois 2% Puperal Sepsis 7% 4.23a Taarifa ya watoto waliozaliwa mmoja mmoja 74

Kati ya watoto waliozaliwa mmojammoja watoto 792,549 walizaliwa hai ambapo watoto 54,287 walikuwa na uzito < ya 2.5 kg.watoto 4,302 walifariki kabla na baada ya masaa 24. Watoto 13,549 walizaliwa wafu (Jedwali na 15). Jedwali na 15: Taarifa za Watoto Waliozaliwa Mmojammoja Mikoa Waliozaliwa Hai Uzito wa Waliozaliwa Hai Waliozaliwa Wafu Waliozaliwa Hai Kisha (Still Births) Wakafa Waliopimwa Idadi < 2.5 kg Macerated Fresh Saa < 24 Saa 24+ Arusha 25673 25673 1023 323 208 96 157 DSM 81280 81280 4417 869 433 191 227 Dom 36727 36301 639 151 101 49 19 Iringa 14578 45578 2555 573 383 171 135 Kagera 54481 40728 2534 444 276 104 61 Kilimanjaro 36494 31930 1335 205 238 193 136 Kigoma 54664 33781 2901 239 203 96 129 Lindi 18982 18399 1316 196 139 77 37 Manyara 15959 15524 999 224 132 82 85 Mara 29316 29266 250 135 147 33 58 Mbeya 37511 37067 2471 495 455 209 268 Morogoro 35600 35749 5104 530 396 171 260 Mtwara 27343 17819 1180 175 106 53 77 Mwanza 71959 69976 6398 1546 357 182 159 Pwani 25987 1785 247 159 29 28 Rukwa 33699 33699 1372 257 64 0 0 Ruvuma 37664 37664 4136 310 95 51 68 Singida 25138 20901 764 207 114 52 18 Shinyanga 53022 52946 1946 588 441 113 42 Tabora 46706 35832 9101 459 250 176 78 Tanga 29703 29436 2061 439 240 89 43 Jumla Kitaifa 792486 729549 54287 8612 4937 2217 2085 4.23b Taarifa ya Watoto waliozaliwa zaidi ya mmoja Kati ya watoto waliozaliwa zaidi ya mmoja, waliozaliwa hai walikuwa 120,225 ambapo watoto 753 walifariki kabla na baada ya masaa 24. Watoto waliozaliwa wafu ni 2,800. (Jedwali na. 16). Jedwali na. 16: Taarifa za watoto waliozaliwa zaidi ya mmoja Mikoa Waliozaliwa Hai Waliozaliwa Wafu (Still Births) Waliozaliwa Hai Kisha Wakafa (Still Births) Macerated Frsh Saa 24 Saa 24+ Arusha 870 27 37 15 15 Dar es Salaam 43285 222 109 32 1 Dodoma 547 15 14 6 10 Iringa 1073 29 26 34 20 Kagera 1852 20 34 15 10 Kilimanjaro 491 36 24 19 31 Kigoma 1894 19 16 19 24 Lindi 330 18 14 22 10 Manyara 453 11 12 21 5 Mara 177 15 21 5 2 Mbeya 8577 168 175 17 9 Morogoro 833 26 22 26 27 Mtwara 322 99 46 3 8 Mwanza 9061 226 87 58 23 Pwani 358 12 8 47 12 Rukwa 33711 322 127 0 0 Ruvuma 632 43 26 15 18 Singida 381 30 19 21 Shinyanga 1889 170 110 52 7 Tabora 12407 137 134 34 14 Tanga 1082 51 43 13 19 Jumla Kitaifa 120,225 1696 1104 474 279 4.24 Idadi ya watoto chini ya mwaka mmoja waliopata chanjo 75

Kuhusu chanjo ya BCG mikoa ya Lindi (121.3%), Mwanza (113.8%), Tanga (107%) iliongoza kwa viwango vikubwa kupita malengo. Mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, na Iringa ilikuwa na viwango vidogo (90.5 94%). (Mchoro na. 36). Mchoro 36: Kiwango cha Chanjo ya BCG 140.0 Kiwango Katika Asilimia 120.0 100.0 80.0 60.0 40.0 121.3 113.8 107.0 100.0 99.4 98.6 98.5 98.0 97.0 97.0 97.0 96.4 96.0 95.0 95.0 95.0 94.0 94.0 92.4 92.0 90.5 100.0 90.1 114.9 20.0 0.0 Lindi Mwanza Tanga Mbeya Kagera Rukwa Mara Dar es Salaam Kigoma Pwani Shinyanga Arusha Dodoma Morogoro Mtwara Mikoa na Taifa Tabora Iringa Singida Ruvuma Manyara Kilimanjaro Total 2001 Total 2002 Total 2003 Kwa chanjo ya DPT3 mkoa wa Kilimanjaro ulivuka lengo ambapo kiwango kilikuwa 109%, wakati mikoa ya Kigoma, Ruvuma, Tabora na Mtwara ilikuwa na viwango vya chini (79 83%). (Mchoro na. 37). Mchoro 37: Kiwango cha Chanjo ya DPT3 120.0 109.0 Kiwango Katika Asilimia 100.0 80.0 60.0 40.0 95.9 95.0 94.1 94.0 93.6 93.3 92.7 92.4 91.0 90.3 90.0 90.0 90.0 90.0 89.0 88.0 83.0 83.0 82.6 79.0 94.8 84.2 105.9 91.3 20.0 0.0 Kilimanjaro Mara Dodoma Mwanza Morogoro Lindi Pwani Kagera Arusha Manyara Dar es Salaam Mbeya Rukwa Shinyanga Singida Iringa Tanga Mikoa na Taifa Mtwara Tabora Ruvuma Kigoma Total 2001 Total 2002 Total 2003 Total 2004 76

Kwa chanjo ya Polio mikoa ya Kilimanjaro, Lindi na Mwanza iliongoza kwa kuvuka malengo kwa kuwa na viwango vikubwa (104 109.8%), wakati mikoa ya Mtwara, Tabora, Pwani na Kigoma ilikuwa na viwango vya chini (83 85.6%). (Mchoro na. 38). Mchoro 38: Kiwango cha Chanjo ya Polio3 120.0 100.0 109.8 106.7 104.0 97.1 96.9 95.0 94.0 93.8 93.0 92.2 92.0 92.0 91.0 90.6 89.1 88.0 88.0 85.6 85.6 85.0 83.0 88.0 108.5 93.1 Kiwango Katika Asilimia 80.0 60.0 40.0 49.0 20.0 0.0 Kilimanjaro Lindi Mwanza Ruvuma Mara Dodoma Tanga Kagera Morogoro Arusha Manyara Rukwa Shinyanga Dar es Salaam Mbeya Iringa Mikoa na Taifa Singgida Kigoma Pwani Tabora Mtwara Total 2001 Total 2002 Total 2003 Total 2004 Kuhusu chanjo ya Surua mikoa iliyoongoza kwa kuvuka malengo ni Lindi, Tanga, Mwanza na Kilimanjaro (109 116.8%), wakati mikoa iliyokuwa na viwango vidogo ni Mtwara, Tabora na Pwani (78.4 87.8%). (Mchoro na. 39). Mchoro 39: Kiwango cha Chanjo ya Surua 120.0 116.8 114.0 113.9 109.9 100.0 96.0 96.0 95.9 94.0 93.0 91.0 90.1 90.0 89.0 88.8 88.0 88.0 88.0 87.8 84.0 78.4 88.1 86.0 105.1 95.2 Kiwango Katika Asilimia 80.0 60.0 40.0 20.0 0.0 Lindi Tanga Mwanza Kilimanjaro DSM Rukwa Mara Dom Morogoro Singida Kagera Manyara Iringa Kigoma Arusha Mikoa na Taifa Mbeya Shinyanga Pwani Tabora Mtwara Total 2001 Total 2002 Total 2003 Total 2004 77

4.25 Chanjo ya TT2+ kwa akinamama wajawazito Mikoa ya Mwanza na Dar es Salaam iliongoza kwa Kiwango cha chanjo ya TT2+ kwa kuwa na viwango vikubwa (95.9 97.5) wakati mkoa uliokuwa na kiwango cha chini kabisa ni Pwani (26.1%). (Mchoro na. 40). Mchoro 40: Kiwango cha Chanjo ya TT2+ Kiwango Katika Asilimia 100.0 90.0 80.0 70.0 60.0 50.0 40.0 30.0 20.0 26.1 55.0 66.7 73.4 74.0 74.7 77.0 78.4 78.4 78.5 80.0 80.6 85.1 85.3 86.0 88.4 90.6 92.0 92.0 95.9 97.5 62.0 61.0 97.3 78.8 10.0 0.0 Pwani Tabora Kigoma Mbeya Manyara Rukwa Arusha Kilimanjaro Mtwara Ruvuma Morogoro Shinyanga Lindi Tanga Singida Iringa Kagera Dodoma Mara Dar ea Salaam Mwanza Total 2001 Total 2002 Total 2003 Total 2004 Mikoa na Taifa 4.26 Wateja wa uzazi wa mpango wanaoendelea na Huduma Mkoa wa Tanga unaongoza kwa kuwa na akina mama wengi wanaoendelea na uzazi wa mpango (60.5%) ukifuatiwa na Mbeya. Mikoa yenye viwango vya chini ni Kagera (15.4%) na Mtwara (16.6%). Kitaifa akinamama wanaoendelea na uzazi wa mpango ni 36.9%. (Mchoro na. 41). Mchoro 41: Mama Wanaoendelea na Uzazi wa Mpango Tan ga Mbeya Ruvuma 54.6 65.5 65.0 Dar ea Salaam Kilimanjaro Dodoma Iringa Arusha 48.0 44.0 43.0 42.0 53.7 Mikoa na Taifa Morogoro Singida Mara Tabora Pwani Mwanza 31.0 30.5 27.8 36.0 34.8 40.0 Lindi Manyara Kigoma 25.4 24.0 21.1 Shinyanga Mtwara Kagera Jumla Kitaifa,2004 18.6 16.6 15.4 36.9 0.0 10.0 20.0 30.0 40.0 50.0 60.0 70.0 Kiwango katika Asilimia 78

Mkoa wa Rukwa unaongoza kwa kuwa na wateja wengi wapya wa uzazi wa mpango (28%) ukifuatiwa na mikoa ya Mara na Dar es Salaam (22.8%) kila mkoa. Mikoa yenye kiwango cha chini kabisa ni Manyara (5.2%) na Shinyanga (7.4%). Kitaifa wateja wapya wa uzazi wa mpango ni (15.7%). (Mchoro na. 42). Mchoro na. 42: Kiwango cha Wateja Wapya wa Uzazi wa Mpango Rukwa Mara Dar ea Salaam 22.8 22.8 28.0 Dodoma Mtwara Tabora 18.0 20.0 22.0 Mikoa na Taifa Ruvuma Lindi Mbeya Tan ga Arusha Mwanza Singida Morogoro 17.4 17.1 15.6 14.4 14.0 13.4 13.0 13.0 Kigoma Kagera Kilimanjaro 10.6 10.1 12.3 Iringa 8.0 Shinyanga Manyara Jumla Kitaifa,2004 5.2 7.4 15.7 0.0 5.0 10.0 15.0 20.0 25.0 30.0 Kiwango katika silimia 4.27 Watoto waliopata matone ya Vitamin A Jumla ya watoto 2,277,173 wa umri wa miezi 6-11, walipata matone ya Vitamin A ambao ni asilimia 86.3 ya watoto wa umri huo. Mkoa wa Morogoro unaongoza kwa watoto wa umri wa miezi 6 11 waliopata matone ya Vitamini A (125%). Mkoa wa Manyara ulikuwa na kiwango cha chini (11%). Kitaifa asilimia 86.3 walipata matone ya Vitamin A. (Mchoro na.43). 79

Mchoro 43: Watoto Umri Miezi 6-11 Waliopata Matone ya Vitamin A Morogoro 125.0 Kigoma 123.2 Pwani 119.7 Mara 113.0 Tanga Mtwara 110.0 102.0 Mwanza Rukwa 97.6 96.3 Mikoa na Taifa Kilimanjaro Lindi Arusha Ruvuma Dodoma Mbeya 87.4 86.0 85.2 93.2 91.7 91.3 Tabora Dar es Salaam Shiinyanga Kagera Iringa Manyara 16.9 11.0 33.3 38.9 77.5 81.0 Jumla Kitaifa, 2004 86.3 0.0 20.0 40.0 60.0 80.0 100.0 120.0 140.0 Viwango Katika Asilimia Kwa watoto wa umri wa miaka 1 5 waliopata matone ya Vitamin A, kiwango cha Kitaifa kilikuwa ni 91.5%. Mkoa wa Mtwara uliongoza (125%) na Manyara ulikuwa wa mwisho (69%). (Mchoro na. 44). Mchoro 44: Watoto Umri Miaka 1-5 Waliopata Matone ya Vitamin A Mtwara 125.0 Tabora 108.0 Dodoma 100.0 Arusha 98.2 Kagera 98.1 Kigoma 96.3 Shinyanga 95.6 Mwanza Lindi 93.1 92.1 Pwani 90.9 Mikoa na Taifa Kilimanjaro Tanga Mara Ruvuma Dar es Salaam Morogoro Mbeya 89.0 89.0 88.5 88.3 85.0 78.9 90.4 Iringa 78.7 Rukwa 77.2 Manyara 69.0 Jumla Kitaifa, 2001 Jumla Kitaifa, 2002 Jumla Kitaifa, 2003 Jumla Kitaifa, 2004 26.0 87.0 92.0 91.5 0.0 20.0 40.0 60.0 80.0 100.0 120.0 140.0 Viwango Katika Asilimia 80

4.28 Kiwango cha Watoto wenye Utapiamlo Mkali Jumla ya watoto 71,536 kati ya 2,121,767 waliopimwa walikuwa na Utapiamlo mkali sawa na asilimia 3.8 ya kiwango Kitaifa. Mkoa wa Morogoro uliongoza kwa kiwango kikubwa cha watoto wenye utapiamlo mkali (13.5%). Mikoa ya Iringa na Dodoma imekuwa na viwango vya chini vya watoto wenye utapiamlo mkali (0.8% 0.9%). (Mchoro na. 45). Mchoro 45: Kiwango cha Utapiamlo Mkali 14.0 13.5 12.0 10.0 4.4 9.5 10.1 Asilimia 8.0 6.0 5.2 6.1 4.0 3.8 3.3 3.8 4.0 2.0 2.4 2.4 1.6 0.8 0.9 1.1 1.1 1.3 1.7 1.8 2.0 2.0 2.0 2.2 2.2 0.0 Jumla Kitaifa, 2004 Jumla Kitaifa, 2003 Jumla Kitaifa, 2002 Jumla Kitaifa, 2001 Iringa Dodoma Kagera Kilimanjaro Arusha Singda Mwanza Manyara Mara Mbeya Dar es Salaam Mikoa na Taifa Pwani Ruvuma Mtwara Tabora Kigoma Shinyanga Rukwa Lindi Tanga Morogoro 4.29 Kiwango cha Kaya zenye vyoo vinavyokubalika na maji toka vyanzo salama Kiwango cha Kaya zenye vyoo vinavyokubalika Kitaifa ni 64.8%. Mikoa iliyoongoza kwa kuwa na vyoo vinavyokubalika ni Shinyanga, Dar es Salaam na Iringa (80 84.4%). Mikoa iliyokuwa na viwango vya chini ni Tabora na Manyara (37 42%). (Mchoro na. 46). Mchoro 46: Kiwango cha Kaya Zenye Vyoo Vinavyokubalika Shinyanga 83.4 Dar es Salaam 80.8 Iringa 80.0 Tan ga 77.3 Dodoma 77.0 Arusha 76.2 Kiwango Katika Asilimia Ruvuma Mwanza Mbeya Singida Mtwara Morogoro Kigoma Lindi Pwani Rukwa 71.5 69.0 67.0 66.2 65.1 63.7 62.7 62.0 61.6 75.3 Kilimanjaro 55.8 Mara 54.0 Manyara 42.0 Tabora 37.0 Jumla Kitaifa 2001 Jumla Kitaifa, 2002 63.0 63.0 Jumla Kitaifa, 2003 65.0 Jumla Kitaifa, 2004 64.8 0.0 10.0 20.0 30.0 40.0 50.0 60.0 70.0 80.0 90.0 Mikoa na Taifa 81

Kuhusu Kaya zinazopata maji toka vyanzo salama, mikoa ya Dodoma, Rukwa na Arusha inaongoza kwa viwango vya juu (62.8 84.2%). Kitaifa 53% ya Kaya hupata maji toka vyanzo salama. Mikoa ya Kigoma, Mtwara na Manyara ina viwango vya chini (32.8 39%). (Mchoro na. 47). Mchoro 47: Kiwango cha Kaya Zenye Vyanzo Vya Maji Salaama Kagera 84.2 Dodoma 76.0 Rukwa 64.1 Arusha 62.8 Ruvuma 60.9 Pwani 60.0 Tan ga 59.0 Iringa 56.4 Kiwango Katika Asilimia Mwanza Mbe ya Lindi Mara Kilimanjaro Shinyanga Morogoro Tabora 39.2 39.0 43.1 43.0 47.4 54.3 54.0 53.0 Manyara 39.0 Mtwara 35.9 Singida Kigoma Jumla Kitaifa, 2001 Jumla Kitaifa, 2002 Jumla Kitaifa, 2003 Jumla Kitaifa, 2004 33.7 32.8 51.0 52.0 54.0 53.0 0.0 10.0 20.0 30.0 40.0 50.0 60.0 70.0 80.0 90.0 Mikoa na Taifa 4.30 Mapato na vyanzo vyake Mikoa mingi imetoa taarifa ya mapato na vyanzo vyake ikilinganishwa na miaka iliyopita. Kwa mwaka 2004 fedha nyingi zilikuwa za Serekali (OC 34% na PE 33%) zikifuatiwa na za Wahisani (Busket Fund) 23%. Mapato kutoka Halmashauri yalikuwa kidogo (1%). (Mchoro na. 48)). Mchoro 48: Vyanzo Mbalimbali vya Mapato, 2004 Vyanzo vingine 10% Cost Sharing 4% Fedha za Halmashauri 1% Community Health Fund 1% Capitalization 2% PE 34% Basket Funds 23% Miradi ya Maendeleo 2% OC 23% 82

Mkoa ulioongoza kwa mapato ulikuwa ni Morogoro ukifuatiwa na Iringa, Mwanza, Arusha na Mbeya. Mikoa iliyokuwa na mapato ya chini zaidi ni Dodoma, Mtwara, Kigoma, Ruvuma na Lindi. (Mchoro na. 49). Mchoro 49: Jumla ya Mapato Kwa Kila Mkoa, 2004 14,000,000,000 12,000,000,000 10,000,000,000 8,000,000,000 Tsh 6,000,000,000 4,000,000,000 2,000,000,000 - Dom Mtwara Kigoma Ruvuma Lindi Kagera Rukwa Tanga Kilima Shinyanga Mara Mikoa Pwani Tabora Manyara DSM Mbeya Arusha Mwanza Iringa Morogoro 4.31 Fedha zilizotumika Fedha nyingi zilizotumika ziliwiana na upatikanaji wake kutoka vyanzo mbalimbali ambapo matumizi makubwa yalikuwa kwa ajili ya PE (32.5%). (Mchoro na. 50). Mchoro 50: Vyanzo vya Fedha Zilizotumika, 2004 Fedha za Maendeleo 1.7% Fedha za Halmashauri 0.6% Vyanzo vingine 6.4% Cost Sharing 3.5% Community Health Fund 0.4% Capitalization 12.6% PE* 32.5% Basket Funds 21.3% OC 21.0% 83

Mkoa wa Morogoro umeongoza kwa kutumia fedha nyingi, ukifuatiwa na mikoa ya Iringa na Mwanza. Mikoa iliyotumia fedha kidogo zaidi ni Dodoma, Mwanza, Kigoma na Ruvuma. (Mchoro na 51). Mchoro 51: Kiasi cha Fedha kilichotumika, 2004 9,000,000,000 8,000,000,000 7,000,000,000 6,000,000,000 5,000,000,000 Tsh 4,000,000,000 3,000,000,000 2,000,000,000 1,000,000,000 - Kagera Mtwara Dodoma Rukwa Manyara Kilimanjaro Pwani Lindi Mikoa Tabora Mara Mwanza Arusha Mbeya Iringa Morogoro 84

5.0 RIPOTI ZA HOSPITALI ZA RUFAA 5.1 Utangulizi Hospitali ya Rufaa Bugando (BMC) Hospitali ya Rufaa Bugando (Bugando Medical Centre) iliyopo Jijini Mwanza inatoa huduma za kirufaa kwa Kanda ya Ziwa. Inaendeshwa kwa makubaliano ya uendeshaji wa pamoja kati ya Serikali na Kanisa chini ya Baraza la Maaskofu wa Kikatoliki Tanzania ikiwa na Bodi ya Wadhamini na Kamati ya Utendaji. Utekelezaji wa maboresho ya huduma za afya uliendelea katika Hospitali ya Bugando katika mwaka wa 2004. Maboresho hayo yalilenga Ukarabati, Utoaji mafunzo, Utoaji wa Dawa za Kupunguza Makali ya UKIMWI (ARVs). Ujenzi wa Kituo cha Kanda cha kuhifadhi Damu salama (Zonal Blood Bank) pamoja na Huduma ya Kutembelea Hospitali (Outreach Services) Hospitali hii imefanya ukarabati wa ghorofa 5 za Jengo Kuu la Hospitali kwenye maeneo yanayotumika kwa kutoa huduma kwa wagonjwa. Ukarabati huo uliojumuisha Wodi ya Wazazi na Chumba cha upasuaji wa Wazazi uligharimu Tshs.142,153,250/= kwa msaada kutoka Japan/Tanzania Food Counterpart Fund Mafunzo mahali pa kazi yalitolewa kwa wafanyakazi wa hospitali wa vitengo mbalimbali ili kuboresha huduma zinazotolewa. Aidha, wafanyakazi 45 walipelekwa kwenye mafunzo ya kujiendeleza vyuoni. Ili kuinua kiwango cha elimu kwa wafanyakazi wasio na elimu ya sekondari hospitali imeanzisha masomo ya sekondari kwa Wauguzi na watumishi wengine ili waweze kujipatia elimu hiyo kwenye sehemu yao ya kazi. Hospitali ya Rufaa ya Bugando ilianza kutoa Dawa za Kupunguza makali ya UKIMWI mwezi Oktoba 2004. Wananchi wengi wamejitokeza na zoezi linaendelea vizuri. Wagonjwa 1,000 wanahudhuria kliniki kati ya hao 300 ndio wapo kwenye matibabu ya dawa za kupunguza makali ya UKIMWI. Aidha, huduma za kuzuia maambukizi ya UKIMWI toka kwa mama kwenda kwa mtoto nazo zinaendelea kupanuka. Hospitali ya Rufaa ya Bugando imeendelea kukabiliwa na tatizo la upungufu mkubwa wa watumishi, hasa Madaktari. Kati ya jumla ya madaktari na madaktari bingwa 99 wanaotakiwa kuwepo, hospitali ina madaktari bingwa na madaktari wa kawaida 49 tu. Aidha, hospitali kwa sasa haina madaktari bingwa wa watoto na magonjwa ya akili. Hospitali ya Bugando imeanzisha mpango maalum kwa kuishirikiana na AMREF wa kupeleka madaktari bingwa kwenye hospitali za Mikoa ya Kagera, Kigoma, Shinyanga na Mwanza kila mwezi ili kutoa huduma za ubingwa. Katika eneo la hospitali pia vipo vyuo vya afya 6 na Chuo Kikuu Kishiriki cha Tiba chenye wanafunzi 35 (mwaka wa kwanza 25 na mwaka wa pili 10). Matarajio ya Hospitali ya Rufaa Bugando mwaka 2005/2006 Katika mwaka 2005/06 Hospitali ya Rufaa Bugando itaendelea na juhudi zake za kuboresha huduma kwa kuendelea na ukarabati wa jengo la hospitali, kuimarisha utoaji wa huduma kwa wagonjwa na kuendelea na juhudi za kutafuta Madaktari Bingwa na wa kawaida, hasa katika fani ambazo hazina wataalam hao na zenye upungufu mkubwa. 85

Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC) Hospitali hii ya rufaa inamilikiwa na shirika la Msamaria Mwema na inaendeshwa kwa kushirikiana na Serekali ya Tanzania. Mwaka 2004/05 hospitali ya KCMC ilikamilisha awamu ya kwanza ya upanuzi wa jengo la Idara ya Wagonjwa wa Dharura. Jengo hili pia linatumika kwa huduma za wagonjwa wa nje, vipimo vya ubongo, mionzi, Famasia, kutunza kumbukumbu za wagonjwa na huduma ya afya kazini. Pia Jengo la Bio-Techonolojia kwa ajili ya utafiti wa Malaria lilizinduliwa. Aidha hospitali imepokea vifaa vipya kwa ajili ya Kitengo cha Endoscopy vyenye thamani ya shilingi milioni 300 pamoja na kununua mashine ya kufulia. Katika kipindi hicho hospitali ilianza uzalishaji wa hewa ya oxygen na hivyo kuondokana na gharama za ununuzi wa hewa hiyo na ina uwezo wa kutoa huduma kwa hospitali za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Tanga kwa malipo. Hospitali ya KCMC ilifanya upasuaji wa kwanza wa wagonjwa wa moyo 13. Upasuaji huo ulifanywa na madaktari wa hospitali hiyo kwa kushirikiana na madaktari kutoka Florida Merekani. Mwaka 2004/05, mafunzo ya uganga yaliendelea kuongezeka katika Chuo Kikuu cha Tiba (KCMC College) kama ifuatavyo, mwaka wa kwanza wanafunzi 38, wa pili 27, wa tatu 24, wa nne 26 na wa tano 15. Pia kumekuwepo na ongezeka la madaktari wanaochukua mafunzo ya ubingwa hadi kufikia 87. Matarajio ya Hospitali ya KCMC mwaka 2005/2006 Mwaka 2005/06, hospitali ya KCMC inatarajia kuwapeleka madaktari wa upasuaji, nusu kaputi na wauguzi kwenye mafunzo ya muda mfupi ili kupata taaluma zaidi ya upasuaji wa moyo. Kwa kushirikiana na Harvad University Merekani, CIPRA/Duke University na London School of Hygiene and Tropical Medicine, hospitali itaendelea na utafiti wa magonjwa ya Malaria na UKIMWI. Hospitali itaimarisha huduma za wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kwa kuteua mratibu ambaye atahakikisha shughuli zote za mfuko zinaratibiwa. Aidha, itapanua huduma kwa wagonjwa wa UKIMWI kufuatia kukamilika kwa majengo ya wagonjwa wa nje. Aidha, Chuo Kikuu cha KCMC kinatarajia kuongeza nafasi za masomo ya udaktari ili kuongeza idadi yao hapa nchini kulingana na ufadhili wa Serekali. Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Hii ni hospitali pekee ya Taifa chini ya Wizara ya Afya yenye Bodi ya Wadhamini na shughuli zake kusimamiwa na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji. Majukumu ya hospitali hii ya rufaa ni pamoja na kutoa huduma za tiba za ngazi ya ubingwa (tertiary care ) na kufanya utafiti wa magonjwa. 86

Taarifa ya ujenzi na ukarabati wa majengo mbalimbali ulioanza mwaka 2003/2004 ni kama ifuatavyo: Ujenzi wa jengo la watoto bado unaendelea, awamu ya kwanza ya ghorofa tatu umeshakamilika kwa kiasi kikubwa. Sehemu zilizokamilika zimeshaanza kutumika kama maabara, chumba cha wagonjwa mahututi, vyumba vya upasuaji, wodi za wagonjwa n.k. Wizara inafuatilia kibali cha kuendelea na ujenzi kwa kutumia mkandarasi yule yule kutoka Central Tender Board Mradi unaofadhiliwa na Benki ya Africa unaendelea vizuri ambapo jengo la Sewahaji limeshakamilika na linatumika. Kazi imeanza kwenye jengo la Kibasila, jengo la upasuaji na X-ray. Jengo la upasuaji katika kitengo cha akina mama litakamilika mwezi Mei na kuanza kutumika mwezi Juni 2005. Majengo mengine yaliyopo kwenye hatua za mwisho kukamilika ni pamoja na Karakana ya matengenezo, banda la mashine za kuchomea taka, nyumba ya kuhifadhia maiti, vibanda vya vituo vya umeme pamoja na majenereta. Njia za maji safi, maji taka, umeme na barabara zipo kwenye hatua nzuri. Pamoja na ukarabati unaoendelea pia mashine 10 mpya za ufuaji, mashine moja ya kutakasa vifaa na mashine ya kuchomea taka hatari zimefungwa na zinafanya kazi. Mradi unaofadhiliwa na Abbott Laboratories unahusu kukarabati maabara kuu, ujenzi wa jengo jipya la mapokezi OPD na kuwekewa vifaa vipya vya kufanyia kazi pamoja na kujenga ukuta kuzunguka eneo lote la Muhimbili. Mradi huu unatagemewa kukamilika mwezi Mei 2005. Pamoja na hayo, mfadhili amegharamia ukarabati wa nyumba moja, jengo la usalama, paa la jengo la ufuaji, vifaa vya ulinzi kama radio call, mtandao wa mawasiliano, Computerization pamoja na ukarabati wa jengo la madaktari wanafunzi. Mategemeo ni kuwa, mwaka huu jengo la utawala litakarabatiwa, mtambo wa simu utawekwa na ujenzi wa jengo jipya la stoo ya kutunzia vifaa na madawa utaanza. Ujenzi wa jengo la ushauri nasaha umegharimiwa na Serikali ya Tanzania, JICA, na CDC. Jengo hili limeshakamilika na baadhi ya sehemu zimeanza kutumika. Matarajio ya Hospitali ya Rufaa Muhimbili mwaka 2005/2006 Mwaka 2005/06 Hospitali ya taifa Muhimbili itaimarisha huduma za tiba kwa wananchi ikiwa ni pamoja na wagonjwa wa UKIMWI kulingana na mpango wa Taifa wa kudhibiti UKIMWI kwa kushirikiana na Centre for Disease Control (CDC) Merekani, Columbia University na Abbott/Axios. Ujenzi wa Jengo la wodi ya watoto utakamilishwa na baadhi ya vifaa vinavyohitajika vitanunuliwa ili kuliwezesha jengo hilo kufanya kazi. Aidha, ukarabati wa jengo la Kibasila, upasuaji na X-ray utakamilika. Ukarabati wa majengo ya Mwaisela na Wazazi utaanza. Utengenezaji wa njia za maji safi, maji taka, umeme na barabara utaendelezwa. Ukarabati wa maabara kuu, ujenzi wa ukuta kuzunguka eneo la Muhimbili pamoja na jengo la mapokezi kwa msaada wa Abbott Laboratorie utakamilika. Pia hospitali inatarajia kuanza kutumia muundo mpya wa utumishi mwaka 2005/06. 87

Hospitali ya Rufaa Mbeya (MRH) Hospitali hii ni hospitali ya rufaa chini ya Wizara ya Afya kwa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini. Hospitali imegawanyika katika sehemu mbili, sehemu kuu ambayo ipo katikati ya mji wa Mbeya na kitengo cha magonjwa ya Akina Mama (obstetric and gynaecology) kilichopo eneo la Meta kilombeta 3 toka ilipo hospitali kuu. Pamoja na kutoa huduma za tiba za kirufaa, hushughulika na kufundisha wataalam mbalimbali wa afya na kufanya tafiti mbalimbali ili kubaini vyanzo vya matatizo. Hospitali ina Bodi ya Ushauri na inaendeshwa na Kamati ya Uongozi wa Hospitali. Mwaka wa fedha 2004/05 miradi ifuatayo ilitekelezwa:- Ujenzi wa wodi ya wagonjwa mahututi (ICU) ambayo inatarajia kugharimu Sh. 76,000,000/= Ujenzi wa uzio wa ukuta katika eneo la kijiji cha ukarabati wa wagonjwa wa akili Uyole, kazi hiyo itafanywa kwa gharama ya Sh. 78,203,140/= - Ununuzi wa mitambo ya nguvu za jua (Solar Heating System) kwa ajili ya hospitali ya Meta utagharimu Sh. 65,191,200 Michoro kwa ajili ya Ujenzi wa hosteli ya madaktari walio katika mazoezi na upanuzi wa jengo la maabara imekamilika na taratibu za kupata wakandarasi wa kufanya kazi hizo zinaendelea kufanywa Ununuzi wa samani kwa ajili ya wodi ya wagonjwa mahututi unatekelezwa kupitia MSD Ujenzi wa kituo cha mafunzo na matibabu ya wagonjwa wa UKIMWI na kufundishia wafanyakazi wa afya katika masuala ya kuwahudumia wagonjwa wa UKIMWI Ujenzi wa jengo kwa ajili ya utafiti wa chanjo ya ugonjwa wa UKIMWI yaani Vaccine Trial Center. Mradi huu umefadhiliwa na Serikali ya Ujerumani. Matarajio ya Hospitali ya Mbeya Rufaa mwaka 2005/2006 Mwaka 2005/06 Hospitali ya Rufaa Mbeya imepanga kufanya yafuatayo: Kukamilisha ukarabati wa wodi za hospitali kuu Kukamilisha ujenzi wa hosteli ya Intern doctors Upanuzi wa maabara ya hospitali Kuanza ujenzi wa kituo cha mafunzo, utafiti wa chanjo na matibabu ya ugonjwa wa UKIMWI Kuimarisha sehemu ya kuhifadhia kumbukumbu za wagonjwa Kuanza kutumia huduma kutoka sekta binafsi katika maeneo ya ulinzi, usafi wa nje na ufuaji nguo. 88

5.2 Ripoti ya Huduma zilizotolewa hospitali za Rufaa mwaka 2004 5.2.1 Mahudhurio ya Nje (OPD) Kwa mwaka 2004 mahudhurio ya nje (OPD) kwa kufuata umri yamekuwa ya idadi ndogo kwa Hospitali ya Bugando ikilinganishwa na hospitali nyingine (MNH, Mbeya Rufaa na KCMC). (Mchoro na. 1). Mchoro 1: Mahudhurio ya nje (OPD) kwa kufuata umri 600000 536175 500000 400000 336661 Idadi 300000 263223 195512 200000 100000 72510 40928 100221 6455 62658 69113 59675 30642 90317 0 Total Muhimbili KCMC Bugando Mbeya Hospital Miaka <5 Miaka 5+ Total Idara zilizoongoza kwa kupokea wagonjwa wengi wa OPD katika hospitali za Rufaa ni Emergency Medicine (17%) ikifuatiwa na Oplthalmology (11%), Obstretrics (10%) na General OPD (7%). (Mchoro na 2). Mchoro 2: Idara zilizoongoza kwa kupokea wagonjwa wengi wa nje (OPD) katika Hospitali za Rufaa 18 17 16 14 12 11 Wagonjwa % 10 8 6 4 2 10 7 6 6 5 4 4 4 4 3 3 3 2 2 2 0 Emergency Medicine Ophthalmology Obstetrics General OPD Main Physiotherapy General Surgery Dermatology Internal Medicine Mental Health (Psychiatry) Idara Oncology Ear Nose Throat (ENT) Orthopaedics Paediatrics TB Urology Neonatal Underfives 89

5.2.2 Wagonjwa Waliolazwa (IPD) Jedwali namba 1 linaonyesha mahudhurio ya ndani (IPD) likijumuisha idadi ya vitanda, wagonjwa waliolazwa, utumiaji wa vitanda, wastani wa mgonjwa kukaa hospitalini na kasi ya vifo kwa idara katika hospitali za rufaa mwaka 2004. Hospitali ya MNH haikutoa takwimu hizi. Jedwali na. 1: Hali ya wodi na vitanda katika hospitali zote za rufaa nchini Idadi ya Idadi ya waliolazwa kwa Average Days of Bed occupancy Uwiano(%) wa No. Wodi/Idara vitanda mwaka stay in Hospitals rate vifo kwa Idara 1 Internal Medicine 476 19338 9 63% 15% 2 Upasuaji 410 12700 16 77% 6% 3 Watoto 358 14767 7 53% 11% 4 Neonatal 191 12119 9 66% 18% 5 Orthopaedic 99 3407 7 77% 1% 6 Macho (Eye) 147 4432 16 42% 0% 7 ENT 47 2128 2 29% 1% 8 Dental 7 486 0 0% 0% 9 Psychiatry 152 2675 56 37% 2% 10 Wazazi (Obstetrics) 460 41333 3 72% 3% 11 Gynecology 161 8243 12 51% 3% 12 Urology 94 3082 4 30% 5% 13 Kifua kikuu (TB) 81 354 1 17% 16% 14 ICU 53 643 11 44% 31% 16 VVF 50 247 0 0% 0% 17 VIP Ward 11 107 0 1% 0% Jumla 2004 2,797 126,061 9 39% 113% 5.2.3 Magonjwa yaliyojitokeza kwa wingi kwa Mahudhurio ya Nje (OPD) Mchoro na 3 unaonyesha magonjwa yaliyojitokeza kwa wingi kwa mahudhurio ya nje (OPD) ni Malaria, Pneumonia, Diarrhoea Diseases, Anaemia, Hypertension na Dental Caries kwa hospitali za Bugando na Mbeya Rufaa. KCMC ni Malaria, ARI, UTI na Hypertension. Kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili magonjwa yaliyoongoza ni Dental caries, Anaemia, Hypertension, BPH, Disorders of the Ear na UTI. 90

Mchoro 3: Magonjw a yaliyojitokeza kw a w ingi kw a mahudhurio ya nje (OPD) katika Hospitali za Rufaa Mw aka 2004 45 40 35 30 Idadi % 25 20 15 10 5 0 Malaria Pneumonia ARI Diarrhoeal Diseases Hypertension UTI Ugonjwa Dental Caries Fractures Anaemia HIV/AIDS TB Bugando KCMC MNH Mbeya Kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, kwa mahudhurio ya OPD takwimu za magonjwa ya ARI na Diarrhoeal Diseases hazikupatikana wakati wa kuandaa hizi takwimu kutokana na baadhi ya kumbukumbu kutoonekana. 5.2.4 Magonjwa Kumi yaliyoongoza kwa Mahudhurio ya Nje (OPD) Magonjwa yaliyoongoza kwa mahudhurio ya nje (OPD) kwa hospitali za rufaa bado ni Malaria, Pneumonia, Anaemia, Kifua Kikuu, Intestinal Worms, na ARI. (Mchoro na. 4). Mchoro 4: Magonjwa yaliyoongoza kwa mahudhurio ya nje (OPD) 50 45 40 35 30 Idadi % 25 20 15 10 5 0 Malaria Pneumonia Anaemia Pulmonary Tuberculosis Intestinal Worms ARI Magonjwa Diarrheal Diseases Fractures UTI Refractive Error 91

5.2.5 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa wa Ndani (IPD) kwa ujumla Magonjwa yaliyojitokeza zaidi kwa wagonjwa wa ndani (IPD) kwa ujumla kwa hospitali zote ni Labour pains, Malaria, Pneumonia, Fractures, HIV/AIDS, Anaemia na Hypertension. (Mchoro na. 5). Mchoro 5: Magonjwa yaliyoongoza kwa wagonjwa wa ndani (IPD) 35 30 25 Idadi % 20 15 10 ` 5 0 Labour pains Malaria Pneumonia Fractures HIV/AIDS PTB Magonjwa Anaemia Hypertension Diabetes Mellitus Heart Failure Bugando KCMC Muhimbili Mbeya 5.2.6 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa waliolazwa Idara ya Internal Medicine Magonjwa yaliyojitokeza zaidi kwa wagonjwa waliolazwa Idara ya Internal Medicine ni Malaria, Pneumonia, HIV/AIDS, na Hypertension. (Mchoro na. 6). 7000 Mchoro 6: Magonjwa yaliyoongoza kwa kulazwa na vifo vingi idara ya Internal Medicine 6086 6000 5000 4000 idadi 3000 2447 2439 2000 1000 0 481 336 792 1404 154 1193 233 1039 110 985 161 785 100 772 131 741 134 Malaria Pneumonia HIV/AIDS Idadi Hypertension Vifo PTB Diarrhoea Diseases Magonjwa Diabetes Malignancies Anaemia CCF 92

5.2.7 Magonjwa yaliyojitokeza kwa Wagonjwa waliolazwa Wodi ya Upasuaji Magonjwa yaliyojitokeza zaidi kwa wagojwa waliolazwa wodi ya upasuaji ni Fractures Injuries excluding fractures, dislocation, sprains and strains, Intestinal Obstruction, Hernias, Peptic Ulcer, Abdominal Malignancy, na Chest Trauma. (Mchoro na. 7). Mchoro 7: Magonjwa yaliyojitokeza kw a w ingi na vifo w odi za upasuaji Fractures Injury excluding fractures, dislocation, sprains and strains Intestinal Obstruction Hernias Peptic Ulcer Disease Idadi Abdominal Malignancy Portal Hypertention BPH Head injury Goiter Foreign body in the ENT Malignacy of genital organs 0 100 200 300 400 500 600 700 800 900 1000 Magonjwa 5.2.8 Huduma za Upasuaji Wagonjwa Vifo Kwa hospitali zote za Rufaa vyumba vyote vya upasuaji ni Non dedicated na idadi ya upasuaji mkubwa na mdogo uliofanyika ni kama inavyoonekana katika Mchoro na. 8. Mchoro 8: Idadi ya vyumba vya upasuaji na aina ya upasuaji iliyofanyika 9000 8000 7285 8109 7000 6000 5151 5640 5000 idadi 4000 3000 2515 2000 1000 0 5 9 14 Idadi ya vyumba vya upasuaji Upasuaji Mkubwa 1437 529 629 Aina ya upasuaji Upasuaji Mdogo 1076 Jumla ya upasuaji Bugando KCMC Muhimbili Mbeya 93

Upasuaji mkubwa uliofanyika ulifanyika katika Idara za Obstetrics na Gynaecology (47%), Orthopedic (16%), General Surgery (14%) VVF/RVF (4%) na Opthalmology (2%). (Mchoro na. 9). Mchoro 9: Upasuaji Mkubwa uliofanyika Plasti Surgery 0% Neurology 0% Others 0% VVF/RVF 4% Ophthalmology 2% General Surgery 14% ENT 9% Paediatic Surgery 0% Orthopaedic 16% Urology 8% Obs and Gynnaecology 47% Upasuaji mdogo uliofanyika ulikuwa Evacuation (20%), EUA (18%), Incision and Biopsy (14%), Reduction and PoP (8%) na Excision (8%). (Mchoro na. 10). Mchoro 10: Upasuaji mdogo uliofanyika UWSD 5% Suprapubic Catheter 4% Bougnage 4% Oesophagascopy 2% Anal Dilation 1% Evacuation 20% Circumcision 4% Foreign Body Removal 6% Screw and Pin removal 6% EUA 18% Excision 8% Reduction and PoP 8% Insision and Biopsy 14% 94

5.2.9 Magonjwa ya Akina Mama (Gynaecology) Magonjwa yaliyoongoza kwa magonjwa ya akina mama ni Pelvic Inflammatory Disease, Infertility na Uterine Fibroid kwa hospitali za Bugando na Mbeya Rufaa. Magonjwa ya Uterine fibroid, Carcinoma of the Cervix na Infertility yalioongoza kwa Hospitali ya KCMC. Kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ni Malignant Neoplasm, Ectopic Pregnancy, Infertility na Pelvic Inflammatory Disease. (Mchoro na. 11). Mchoro 11: Magonjwa ya akina mama (gynaecology) 1600 1400 1200 1000 Idadi 800 600 400 200 0 Uterine Fibroid Infertility Adnexial Cyst Carcinoma of the Cervix Magonjwa Pelvic Inflammatory Disease Ovarian Tumors Genital Prolapse BUGANDO KCMC MNH MBEYA 5.2.10 Sababu za kulazwa Mama Wajawazito Sababu zilizoongoza katika kulazwa mama wajawazito ni Deliveries (89%), Abortions (6%), Malaria in Pregnancy (1%) na Ectopic Pregnancy (1%). (Mchoro na. 12). Mchoro 12: Sababu za kulazwa mama wajawazito Pelivic Inflamatory disease 3% Malaria in pregnancy 1% Hyperemesis gravidarum 0% Anaemia 0% Ectopic pregnancy 1% Abortions 6% Deliveries 89% Takwimu za Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa magonjwa ya Malaria in Pregnancy, Pelvic Inflammatory Disease, na Ectopic Pregnancy hazikupatikana kwa kukosekana kwa kumbukumbu wakati takwimu zinaandaliwa. 95

5.2.11 Kujifungua Mama Wajawazito Kuhusu kujifungua mama wajawazito zaidi ya asilimia 99 ya wale walioripotiwa walijifungulia hospitalini kwa hospitali zote. (Mchoro na. 13). Mchoro 13: Kujifungua Mama wajawazito BBAs 1% TBAs 0% Others (Taja) 0% Hospitali 99% Hospitali BBAs TBAs Others (Taja) 5.2.12 Aina ya kujifungua Mama Wajawazito Kuhusu aina ya kujifungua mama wajawazito, wengi wa akina mama walijifungua kwa njia ya kawaida Spontaneous Vaginal Delivery ikifuatiwa na upasuaji (Caesarian Section) na Vacuum Extraction (Mchoro na. 14). Mchoro 14: Aina ya kujifungua mama wajawazito Forceps delivery 0% Breech extraction 2% Destructive procedures 0% Others 0% Vacuum extraction 7% Caesarian section 24% Spontaneous vaginal delivery 67% Idadi ya akinamama waliojifungulia hospitali Bugando (5,451), KCMC (2,834), Muhimbili (11,530) na Mbeya (6,792) hailingani na idadi ya aina ya kujifungua kwa hospitali zote Bugando (6,989), KCMC (2,767), Muhimbili (11,414) na Mbeya (6,631). Hii ni kutokana na baadhi ya kumbukumbu kutopatikana. 96

5.2.13 Matokeo ya kujifungua Mama Wajawazito Matokeo ya kujifungua akina mama wajawazito ni kuwa, akina mama 18,470 walijifungua kawaida na watoto 24,782 walizaliwa hai. Watoto 5,790 walikuwa na matatizo (Macerated Still Birth, Fresh Still Birth, Pre-term Babies na Underweight 2.5 kg. (Mchoro na. 15). Mchoro 15: Matokeo ya kujifungua mama wajawazito 12000 10000 8000 Idadi 6000 4000 2000 0 Normal Deliveries Born Alive Macerated Still Birth Fresh Still Birth Pre-term Babies Under weight < 2.5 kg Ruptured Uterus Aina ya matokeo BUGANDO KCMC MNH MBEYA 5.2.14 Sababu za Vifo vya Mama Wajawazito Tatizo la vifo vya akinamama wajawazito katika hospitali za rufaa bado ni kubwa kwa vile katika kipindi cha mwaka 2004 pekee hospitali zimeripoti jumla ya akinamama 533 walifariki kutokana na matatizo ya uzazi. Septicaemia iliongoza kwa 17%, PPH 15%, Pneuomonia 11%, Eclampsia 10% na HIV/AIDS 5% kama inavyoonyeshwa katika Mchoro na. 16. Mchoro 16: Sababu za vifo mama wajawazito 18 17 16 15 14 12 11 10 10 Asilimia % 8 6 8 7 7 6 5 4 2 3 2 2 2 2 2 2 1 1 0 Septicaemia PPH Pneumonia Eclampsia Anaemia Obstructed Labour Malaria APH HIV/AIDS Pulmonary Oedema Meningitis Magonjwa Ruptured uterus Septic Abortion EPH Gestosis Puerperal Sepsis Unsafe Abortion Anaesthesis Accidents Others Kuhusu idadi ya vifo vya akina mama wajawazito, hospitali ya Bugando inaongoza kwa idadi kubwa. Sababu zilizoongoza kwa vifo vya akina mama wajawazito kwa hospitali zote ni Pneumonia, PPH, Malaria, Anaemia, Septecaemia pamoja na HIV/AIDS. 97

5.2.15 Sababu za kulazwa na vifo wodi za watoto Sababu zilizoongoza kwa kulazwa na vifo kwa watoto kwa hospitali zote ni Malaria, Pneumonia, Diarrhoea, Malnutrition, PTB na Prematurity (Mchoro na. 17). Takwimu kutoka hospitali ya Taifa Muhimbili hazina ripoti ya ugonjwa ya Diarrhoea kwa vile wagonjwa hawapo na wodi 17 iliyokuwa ikitumiwa kwa ajili hiyo inatumika kwa wagonjwa wengine. Mchoro 17: Sababu za kulazwa watoto wodi za watoto PTB 1% Dysentery 1% Septicaemia 2% Birth Asphyxia 3% Gastroenteritis 1% ARC 1% Pre maturity 3% Malaria 35% Malnutrition 11% Paediatric AIDS 3% Anaemia 13% Acute Watery Diarrhoea 12% Pneumonia 14% 5.2.16 Sababu ya Vifo vya Watoto wa umri chini ya mwaka mmoja Takwimu zilizokusanywa mwaka 2004 zinaonyesha kuwa sababu zilizoongoza kwa vifo vya watoto wa umri chini ya mwaka mmoja kwa hospitali zote ni:- Malaria, Pneumonia, Diarrhoea, Anaemia Pediatric AIDS na Malnutrition. Hospitali ya Taifa Muhimbili haikutoa takwimu kwa magonjwa ya Diarrhoea, Septicaemia, na Birth Asyphyxia kwa vile kumbukumbu hazikupatikana. (Mchoro na. 18). Mchoro 18: Vifo vya watoto chini ya mwaka mmoja 25 20 Asilimia % 15 10 5 0 Malaria Pneumonia Acute Watery Diarrhoea Anaemia Padiatric AIDS Malnutrition Pre maturity PTB Magonjwa Septicaemia Birth Asphyxia Gastroenteritis ARC Others (Taja) Congenital Abnormalities 98

5.2.17 Magonjwa ya Macho kwa waliolazwa Jumla ya wagonjwa 3079 walilazwa kwa magonjwa ya macho. Ugonjwa wa Cataract uliongoza kwa 70% ya wagonjwa wote ukifuatiwa na Trauma 12%, Trachoma 5%, Retinal/Optic disease 3% na mengine kama inavyoonyeshwa katika Mchoro na. 19. Mchoro 19; Waliolazwa magonjwa ya macho Trachoma 0% Glaucoma 5% Others 1% Retinal/Optic Disease 2% Corneal Ulcers 3% Corneal perforation 1% Uveitis 1% Endophthalmitis 1% Hyphaema 1% Orbital Cellulitis 1% Malignancy 2% Trauma 12% Cataract 70% 5.2.18 Magonjwa ya Akili kwa waliolazwa Jumla ya wagonjwa 1,095 waliripotiwa kulazwa kwa magonjwa ya akili na kati ya hao Non organic psyhcosis walikuwa 40%, Alcohol and Schizophrenia 29%, Manic depressive psychosis 23%, Drug abuse 17% na magonjwa mengine 4%. Hospitali ya KCMC haina wodi ya wagonjwa wa akili. (Mchoro na. 20). Mchoro 20: Magonjwa ya akili kwa waliolazwa Other Mental and behauvioral disorders 4% Other unspecified disorders of the nervous system 3% Mental deficiency 0% Schizophrenia 18% Alcohol and drugs abuse 10% Epilepsy 5% Organic brain syndrome 2% Acute psychosis 2% Non organic psycosis 25% Senile Psycosis 2% Manic depresive psychosis 14% Alcoholic psychosis 3% Psychoactive substance use disorders 10% Depression 2% 99