Kwa Kongamano Kuu 2016

Similar documents
Information for assessors (do not distribute this page to participants):

GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI

"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Agano Lililofunikwa Kwa Damu

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

United Pentecostal Church June 2017

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT

Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College

WEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23

MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.

walozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w

Ndugu na dada zangu wapendwa,

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

MELKISEDECK LEON SHINE. katoliki.ackyshine.com

UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?

Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia. Ellis Forsman. Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1

WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen

Ndugu na dada zangu wapendwa,

Kiu Cha umtafuta Mungu

Kifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1

IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE

Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

NGUVU. Utangulizi. Yesu alisema,

Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu?

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

UNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW

Kanuni. Muhimu za Kujifunza Biblia. Mchungaji Drue Freeman. Dan Hawkins & Joseph Brown. General Editors.

Roho Mtakatifu Ni Nini?

B. Wanafunzi watapata ufahamu mkubwa wa kitabu hiki, na jinsi kinavyofundisha kuhusu kanisa.

Kufunga Milango - Uponyaji Kutokana na Athari za Giza

Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia

BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE

UTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

United Pentecostal Church April Kushangilia Kwa Sala

MSAMAHA NA UPATANISHO

Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani?

Mwongozo wa Kanisa la Waadventista wa Sabato

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level

MWONGOZO WA NAMNA YA KUHAMASISHA MAOMBI YA MCHANA NA USIKU YA SIKU 10.

Tumaini Kwa Afrika. Thomas Schirrmacher. Hoja 66. Dibaji na Prof. Mchungaji Dk. Thomas K. Johnson. Thomas Schirrmacher Tumaini Kwa Afrika TASCM RVB

FORWARD BY DANIEL SZMIOT

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Oktoba-Desemba

RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO

Maisha Yaliyojaa Maombi

Watumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1

Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu

wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA

WAKOLOSAI MTAALA. B. Maoni: Tunapendekeza uwe na fafanuzi (commentary) yoyote yenye kushikilia mafundisho ya awali (conservative) katika Wakolosai.

Human Rights Are Universal And Yet...

Tazama Yuaja. Kuhusu Toleo Hili. Umuhimu wa Mafundisho ya Biblia. Nguvu katika neno la Mungu.

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi. Iliyoendelea sana

MAFUNDISHO YA UMISHENI

UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI

Sura ya 7 Kielelezo: Tumepatanishwa na Mungu na Wanadamu

Kifo Na Mbingu (Death And Heaven)

Mzabibu Na Matawi. (The Vine And The Branches) Ellis P. Forsman. Mzabibu Na Matawi (The Vine And The Branches) 1

KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU?

MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa.

Maisha Ya Mkristo Ni Nini?

Ndugu na dada zangu wapendwa,

ONYO LA MWISHO KWA DUNIA

Hakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn

VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu

Rahisi. Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Kitabu cha mwanafunzi. Rahisi

Uongozi Siri Na Larry Chkoreff. Version 1.2 Desemba 2010

Uponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14).

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu

JE! MUNGU ANAMPA MWANAMKE HAKI YA KUTOA MIMBA IWAPO NI MHANGA WA UBAKAJI?

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi

Patanishwa, Hesabiwa Haki, Takaswa

MASWALI NA MAJIBU JUU YA KITABU CHA MWANZO

KITABU CHA KUONGOZA FAMILIA

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

PDF created with pdffactory trial version

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

maombi, kabla tu hatujalifungua Neno hili la Kiungu.

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

YEHOVA-YIRE 1. 2 Baba yetu wa Mbinguni, tunakikaribia Kiti Chako cha. 3 Tunakushukuru kwa kutuzuru jana jioni. Tunaomba

Kiumbe Kipya Katika Kristo

Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu (Watch Out for Wolves)

Aina Tatu Za Ibada. Ellis Forsman. Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 1

Early Grade Reading Assessment for Kenya

Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele. Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? UKURASA WA 12 NYIMBO: 97, 101. Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana

# 18 Uponyaji Kutokana na Kukataliwa

Transcription:

The Upper Room za Kwa Kongamano Kuu 2016 Selected from The Upper Room Disciplines with Invited Writers

SIKU 60 ZA SALA Kwa Kongamano Kuu 2016 2016 na Upper Room Books. Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu ya kitabu hiki inaweza kutumiwa au kutolewa tena kwa njia yoyote ile bila idhini isipokuwa pale ambapo manukuu mafupi yaliyo katika makala au uhakiki muhimu. Kwa maelezo, andika: Upper Room Books, 1908 Grand Avenue, Nashville, TN 37212. Upper Room, Upper Room Books, na nembo za usanifu ni alama a biashara zinazomilikiwa na The Upper Room, Nashville, Tennessee. Haki zote zimehifadhiwa. Tovuti ya Upper Room Books: books.upperroom.org Cover design: Kielelezo cha Left Coast Design, Portland, Oregon Cover: Usanifu wa Tammy Smith Isipokuwa vinginevyo, manukuu ya maandiko matakatifu yanatolewa kwenye Biblia ya New Revised Standard Version, hakimiliki 1989 Baraza la Kitaifa la Makanisa ya Kristo nchini Marekani. Zinatumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa. Manukuu ya maandiko matakatifu yenye alamaap ni maneno mengine ya mwandishi. Manukuu ya maandiko matakatifu yenye alama (GNT) yanatoka Good News Translation katika Today s English Version Toleo la Pili Hakimiliki 1992 na Ameri- can Bible Society. Zinatumiwa kwa ruhusa. Manukuu ya maandiko matakatifu yenye alama kjv yametolewa kwenye King James Version. Manukuu ya maandiko matakatifu kutoka THE MESSAGE. Hakimiliki na Eugene H. Peterson 1993, 1994, 1995, 1996, 2000, 2001, 2002. Imetumiwa kwa idhini ya NavPress Publishing Group. The Upper Room inatoa idhini ya kutafsiri kijitabu katika lugha nyingine ili kukidhi mahitaji ya watu katika nchi nyinginezo. Chapisho ISBN: 978-0-8358-1560-4 Mobi ISBN: 978-0-8358-1558-1 Epub ISBN: 978-0-8358-1559-8 Taaluma za The Upper Room Katika kitabu hiki maarufu cha ibada, waandishi 53 kutoka asili, lugha, na tamaduni mbalimbali za Wakristo wanapima vina vya andiko takatifu. Kila wiki ina mada mpya kulingana na vifungu vya andiko takatifu vilivyoteuliwa kutoka Revised Com- mon Lectionary. Ili kuagiza Taaluma za The Upper Room, wasiliana na huduma kwa wateja kwa nambari 1-800-972-0433 This translation is provided by GCFA (General Council on Finance and Administration)

M HUTASARI WA MATUMIZI YA-KIKUNDI KIDOGO Huu hapa ni mpango rahisi wa mikutano ya kikundi kulingana na kusoma ibada hizi. Mtu mmoja anaweza kuigiza kama mshirikishi au jukumu linaweza kuzungushwa miongoni mwa wanachama wa kikundi. Unaweza kuwasha mshumaa mweupe wa Kristo ili kuashiria mwanzo wa muda wako pamoja. UFUNGUZI Mshirikishi: Tuje katika uwepo wa Mungu. Wengine: Bwana Yesu Kristo, asante kwa kuwa nasi. Tusaidie kusikia neno lako kwetu tunapozunguma pamoja. ANDIKO Mshirikishi anasoma andiko lililopendekezwa kwa siku hiyo. Baada ya kimya cha dakika moja au mbili, mshirikishi anauliza: Ulimsikia Mungu akisema nini katika kifungu hiki? Mwito huu unahitaji jibu gan? (Wanachama wanajibu kwa zamu ama wanavyoongozwa.) TAFAKARI Ni kifungu kipi cha andiko na tafakari kilikuwa na umuhimu kwako? Kwa nini? (Wanachama wanajibu kwa zamu ama wanavyoongozwa.) Ni hatua zipi ulizochochewa kuchukua kwa mujibu wa tafakari? (Wanachama wanajibu kwa zamu ama wanavyoongozwa.) Ni wapi ulipopata changamoto katika ufuasi wako? Ni vipi ulivyokabiliana na changamoto? (Wanachama wanajibu kwa zamu ama wanavyoongozwa.) KSALI PAMOJA Mshirikishi anasema: Kulingana na majadiliano ya leo, ni watu na hali gani unataka tuombee kwa sasa na wiki ijayo? Kisha mshirikishi au mtu mwengine wa kujitolea anaombea masuala yaliyotajwa. KONDOKA Mshirikishi anasema: Tuende kwa amani kumtumikia Mungu na jirani zetu katika mambo yote tunayoyafanya. Imetolewa kwenye mwongozo wa ibada ya kila siku The Upper Room, Januari Februari 2001. 2000 The Upper Room. Zinatumiwa kwa ruhusa. 3

Bwana,leo nipe mbingu mpya na dunia mpya. Nipe ajabu la mtoto ambaye kwa mara ya kwanza anafumbua macho yake ulimwenguni; furaha ya mtoto anayetambua Fahari yako katika kila kitu, katika kila kiumbe anachokumbana nacho, uhalisia wa utukufu Wako. Nipe furaha ya yule ambaye hatua zake ni mpya. Nipe furaha ya yule ambaye maisha yake ni kila siku mpya na isiyo na hatia na yenye tumaini, kila siku yenye msamaha. Michel Bouttier, katika Sala za Kijiji Changu Sala za Kijiji Changu na Michel Bouttier. Imetafsiriwa na Lamar Williamson. Hakimiliki 1994. Imetumiwa wa idhini ya Upper Room Books.

MAUDHUI MUHTASARI WA MATUMIZI YA-KIKUNDI KIDOGO / 3 KARIBU / 7 UTANGULIZI / 8 TAFAKARI KABLA YA KONGAMANO KUU Tangaza / 10 19 Ongoza / 20 29 Lea / 30 39 Tuma / 40 49 TAFAKARI KABLA YA KONGAMANO KUU Kama Tulivyoenda / 50, WARNER BROWN Nenda na Utangaze / 51, GREGORY V. PALMER Kuenda kwa Mamlaka / 52, CHRISTIAN ALSTED Unapoenda, Jifunze / 53, SALLY DYCK Kuenda kwa Ujasiri / 54, SUDA DEVADHAR Upendo na Upendo Pekee / 55, DEBORAH L. KIESEY Unapoenda, Waite Wote / 56, CYNTHIA FIERRO HARVEY Ili Tuwe Kitu Kimoja / 57, MARY ANN SWENSON Uovu Unaenda Pia / 58, JAMES SWANSON SR. Nenda kwa Kondoo Aliyepotea / 59, JOHN YAMBASU Nani Anakwenda Wapi? / 60, ELAINE J. W. STANOVSKY TAFAKARI BAADA YA KONGAMANO KUU / 61 KTUMIA KIDOLE UTATA KATIKA SALA / 70

Karibu Wpendwa kaka na dada wa familia ya Muungano wa Methodisti, Tunafahamu kuwa sala zetu ni muhimu, na kwa uhakika huo, ninawaalika katika safari ya sala ya siku 60 mnapojiandaa kwa Kongamano Kuu 2016. Viongozi wa kanisa, na wengine walio na haja hivi karibuni watakusanyika huko Portland kusikilizana, kutambua mapenzi ya Mungu kwa Kanisa la Muungano wa Methodisti, na kufanya maamuzi yatakayoongoza Muungano wa Wamethodisti kote ulimwenguni katika kutimiza lengo letu tulilopewa na Mungu. Wakati wewe na wao mnapopanga kufungua moyo na akili zenu kwa uongozi wa Mungu, tafakari hizi zinatoa desturi ya kijamii inayokusudiwa kulea roho wa umoja na ufuasi. Sali kwa uhakika kuwa wengine wanasali sala hiyo. Tafakari katika kijitabu hiki zinaanza wiki baada ya Pasaka, Alhamisi, Machi 31, na kuendelea hadi Jumapili, Mei 29. Zitakuongoza kwa siku arubaini kabla ya kikao cha ufunguzi, hadi siku kumi na moja za Kongamano Kuu, na katika siku tisa baada ya tukio kukamilika. Kila tafakari wakati wa Kongamano Kuu, Mei 10 20 (bila kujumuisha Mei 17), imeandikwa na askofu ambaye atahubiri siku hiyo hivyo unaweza kukumbana na maarifa kutoka kwa mtangazaji wa Neno la siku hiyo. Wafanyakazi wa The Upper Room walitoa chapisho hili kwa mwaliko wa Kamati ya Uabudu wa Tume Kuu ya Kongamano Kuu la 2016, na sisi hapa The Upper Room tunayo fahari kuaminiwa kwa kazi hii. Ninasubiri siku zetu sitini za sala pamoja. SARAH WILKE Mchapishaji, The Upper Room 7

Utangulizi Kitabu hiki cha Sala ya Siku 60 kinatumika kama jibu la ombi muhimu lililoandikwa katika andiko takatifu, Bwana, tufunze kusali. Tunakualika ujiunge na wajumbe, maaskofu, na viongozi wa Kongamano Kuu 2016 katika maandalizi yao ya kiroho kwa tukio, kupitia tukio, na siku za baadaye. Kila dhehebu la ndani katika kila sehemu ya ulimwengu linaweza kuomba na, na kuombea wajumbe 864 wa Kongamano Kuu. Kwa kutumia Intaneti na maandishi yanayopakulika, kila Muungano wa Methodisti utasoma andiko takatifu sawa, kuzingatia yaliyomo sawa, na kusali sala sawa kwa siku arubaini kabla ya Kongamano Kuu 2016 huko Portland, Oregon (Machi 31 hadi Mei 9), kila siku ya Kongamano Kuu (Mei 10 hadi 20); na siku tisa kufuatia tukio (Mei 21 hadi 29). Sote tunaweza kushiriki katika hali sawa ya andiko takatifu, neno, na Roho. Sala ni nguzo muhimu ya maisha na kazi ya Yesu na inasalia muhimu kwetu na kwa kanisa. Sala ilichukua nafasi muhimu katika kazi ambayo Mungu alianza kupitia John na Charles Wesley Uingereza ya karne ya kumi na nane. Huko Amerika ya Kaskazini, maisha ya Philip Otterbein, Jacob Albright, na Martin Boehm yote yanatoa ushahidi wa mafunzo ya John Wesley kuwa Mungu hafanyi chochote isipokuwa sala. Vuguvugu la Methodisiti lilipoenea hadi Karibea (1759), Sierra Leone (1792), Australia (1815), Afrika (1816), na Amerika Kusini (miaka ya 1830), sala ilitumika kama chanzo msingi cha mwelekeo na umuhimu wa kiroho. Barani Asia (1783) na Pasifiki (1822), hadithi ni ile ile. Tunaamini kuwa Mungu anataka kuongoza na kuboresha hatma ya Kanisa la Muungano wa Methodisti kupitia sala. Mwongozo huu wa sala utatumika kama mwongozo wa kila siku kwa wajumbe walioteuliwa wa Kongamano Kuu 2016. toa njia kwa wale waliopo kwenye Kongamano Kuu kuungana, kuzingirwa, na kusaidiwa kwa sala. shirikisha kila mwanamume, mwanamke, kijana, na mtoto wa Muungano wa Methodisti katika sala. Kila familia, kikundi kidogo, na kanisa la ndani kote ulimwenguni linawezsa kuomba na, na kuombea Kongamano hili Kuu. fungua njia mpya kwa ukuaji wa kiroho na imani katika madhehebu 8 Siku 60 za Sala

yote, kwa wanachama na marafiki wote kuungana katika sala kama mwili wa Kristo. anzisha mtandao wa sala ndani ya Kanisa la Muungano wa Methodisti ambao unaweza kusaidia maandalizi ya kiroho yanayohitajika kabla ya Kongamano Kuu, kuombeana kwa imani wakati wa siku za Kongamano, na kushiriki katika utekelezaji wa maamuzi yaliyofanywa kwenye Kongamano Kuu. Ni nini kitakachotendeka tunaposali pamoja? Hakuna anayejua kwa hakika. Hata hivyo, tunaamini kuwa mapenzi ya Mungu yatakuja kupitia sala na ufahamu. Kurasa zinazofuata zinatupa fursa ya kuungana katika sala ili mapenzi ya Mungu kutimizwa kwa njia ya Mungu na kwa wakati wa Mungu. Bwana, tufunze kusali. TOM ALBIN Mkuu wa Upper Room Chapel DENISE MCGUINESS Mkurugeni Mtendaji, Living Tree Services, P.S. Wenyeviti wa Timu ya Sala Siku 60 za Sala 9

Kwa hivyo, Nenda! ALHAMISI, MACHI 31 SOMA MATHAYO 28:19-20 Endelea! Ondoka hapa! Mhubiri mgeni alikuwa ameahidi kushiriki dua yake ya heri anayoipenda. Ni hitimisho lililoje la kushangaza la huduma ya uabudu rasmi! Ni hitimisho lililoje la kushangaza la huduma ya uabudu rasmi! Lakini Yesu ana utaalamu wa mahitimisho yanayoshangaza, na Mathayo anaidhihirisha katika Injili yake yote kuwa kumfuata Yesu si kwa wale wanaotaka imani iliyotulia. Lazima tuwe tayari kuenda! Leo, siku tano tu kabla ya kusherehekea muujiza wa Ufufuko, tunajitolea kwa kuenda na Yesu kama dhehebu. Kwa hivyo, nenda inasalia kuwa muhimu kwa dhamira yetu kama Kanisa la Muungano wa Methodisti, na tunayo fursa ya kujiahidi kikamilifu kwa dhamira hiyo tunapoanza safari yetu ya sala ya pamoja ya Kongamano Kuu. Je, mkutano huu utatimiza nini? Ni tofauti gani utakayoleta ulimwenguni? Ni vipi tukakavyosalia kweli kwa dhamira yetu? Huku muziki wa Pasaka ukiendelea kucheza masikioni mwangu, kwa hakika ninafahamu kuhusu nguvu isiyo kipimo, isiyofikirika ya Mungu na sala. Kwa hivyo, nenda pia ni muhimu kwa imani yangu kama mfuasi wa Yesu Kristo. Mara nyingi zaidi ninajaribu kuzingatia ufuasi kama kitu kingine kwenye orodha yangu ya mambo ya kufanya. Nenda huko nje, fanya mtu mmoja au wawili kuwa wafuasi, itie alama kwenye orodha yangu, na uende kwenye jukumu linalofuata! Katika kipindi chote cha uabudu kwenye Kongamano Kuu, tutachunguza jinsi Injili ya Mathayo inavyotambua kipengee cha ndani yake kwa mapambano ya muda mrefu kwenye safari yetu na Yesu. Hatujui tutakachokumbana nacho njiani. Lakini kuna habari njema: Yesu atakuwa nasi, na kanisa letu, na ulimwengu kwa safari nzima. Tuanze! Yesu, hatuna uhakika kule ambako safari hii itatufikisha, lakini tuko tayari kuenda na wewe. Amina. LAURA JAQUITH BARTLETT 10 Siku 60 za Sala

Mambo Msingi IJUMAA, APRILI 1 SOMA YEREMIA 31:10-14 Kipindi cha uhamisho huko Babeli pia huitwa utumwa wa Babeli. Watu wa Israeli walikuwa watumwa wa himaya yenye nguvu zaidi wakati wao. Kwao lazima hali ilionekana kukosa tumaini. Ilhali nabii Yeremia anatangaza nguvu ya Mungu itakayokomboa Israeli hata kutoka kwa mkuu huyo mwenye nguvu: Bwana amemwokoa Yakobo, na kumkomboa kutoka kwenye mikono yenye nguvu zaidi yake. Nguvu nyingi zinaweza kutufanya watumwa. Lakini hakuna aliye mkuu zaidi kuliko zamani. Dhidi ya mkuu yeyote, tunaweza kuasi. Lakini zamani tusiyoweza kubadilisha, inayofanya hisia zetu za kushindwa kuwa na nguvu zaidi. Miaka imepita, na hatuna nguvu ya kutendua tulichokifanya au hata kurejesha muda tuliopoteza tuliposhindwa kufanya tulichopaswa kufanya. Tunaweza kujaribu kutendua matokeo ya kale yetu na mara nyingi tunapaswa kufanya hivyo. Lakini kale yenyewe hatuwezi kuitendua. Ipo, kwa kudumu, na uwezo tusioweza tusioweza kukabilina nao. Licha ya jitihada zetu bora, hatuwezi kuitendua. Ni kuu zaid kuliko Wababeli walivyokuwa kwa Israeli. Kama tu Yakobo (Israeli) ilifungwa kwa mikono iliyokuwa na nguvu zaidi yake, hivyo ndivyo tulivyolemewa kwa uzito wa ya kale tusiyoweza kubadilisha. Lakini Mungu aliyemwokoa Yakobo kutoka kwenye mikono iliyokuwa na nguvu zaidi yake pia anaweza kutuokoa kutoka kwa chochote kinachotufunga haijalishi kina nguvu kiasi gani hata kutoka kwenye uzito wa mambo yaliyopita. Hiyo ndiyo maana na msamaha. Mungu hutuokoa kutoka kwenye dhambi yetu, kutoka kwenye aibu ya makosa yetu, kutoka kwenye uzito wa mambo yaliyopita. Hivyo, tunapokabiliana na kazi mpya, tunaweza kufanya hivyo kwa furaha sawa na ile iliyoonyeshwa katika maneno ya Yeremia. Yasome tena, na ufurahie naye! Mungu, tuondolee makosa na dhambi zetu zote. Tupe furaha ya wale wanaorejea kwako kutoka kwenye uhamisho wa dhambi na hatia. Amina. JUSTO L. GONZÁLEZ Siku 60 za Sala 11

Ukomavu wa Kiroho JUMAMOSI, APRILI 2 SOMA WAEBRANIA 5:7-9 Waandishi wa Injili wanatupa picha ya Yesu kwenye sala. Kutoka kwao tunajifunza kuwa alilia, akapiga kite katika roho, na kupambana na majaribu. Mwandishi wa Waebrania anaelezea kwa ujasiri vilio vya sauti na machozi ambavyo wakati mwingine viliandamana na sala za Yesu na utiifu aliojifunza kupitia mateso. Picha inayojitokeza inamtambua kama aliyejihusisha sana na maisha kwa viwango vyote na kama aliyekabiliana kwa ujasiri na wito wake. Rejeleo la siku za mwili wake linasisitiza hali ya mpito na udhaifu wa maisha ya mwanadamu. Bila shaka uchungu wa Gethsemani ulikuwa katika akili ya mwandishi. Katika bustani Yesu alijitolea, kwa njia ya uwakilishi na kujitoa mhanga, dhiki ya watu wote nyakati za uhitaji mkubwa. Alikabilina na woga wa kifo, akimwomba Mungu aondoe kikombe, lakini hatimaye akakubali mapenzi ya Mungu. Katika pambano hili hatari Yesu alijifunza utiifu kwa mapenzi ya Mungu kupitia mateso aliyostahimili. Ukomavu au ukamilifu katika sifa ya mwanadamu haujatulia lakini hukua kupitia makabiliano ya hali za maisha yanayoendelea kubalika. Luka 2:52 inasema kuwa Yesu akazidi kufanya maendeleo katika hekima na ukuzi wa kimwili akipata kibali kwa Mungu na wanadamu. Ukumbatiaji wa utata na majukumu ya maisha kwa moyo mmoja, pamoja na kuachia maslahi ya binafsi, kuliwezesha kuzungumza maisha yake kufanywa kuwa ya ukamilifu. Kuishi kila siku kwa kusikiliza sauti ya Mungu ndiyo njia ambayo tunatambua woga wetu, kusali dhiki yetu, na kukua kikamilifu kama wale walioumbwa kwa mfano wa Mungu. Zingatia sehemu ambazo Mungu anakuita ukue kupitia utiifu. ELIZABETH J. CANHAM 12 Siku 60 za Sala

Kipaji cha Imani JUMAPILI, APRILI 3 SOMA MATHAYO 14:22-33 Katika karne ya kumi na tisa, Johann Christoph Blum- hardt alihubiri katika kanisa dogo katika kijiji cha Ujerumani. Hakukuwa na chochote cha kipekee kuhusu kazi yake hamna, yaani, hadi wanandoa katika kanisa walipomwambia kuhusu matatizo waliyokuwa nayo na binti yao. Mhubiri Blumhardt alikutana nao ili kuomba na kumtembelea binti huyo. Mhubiri Blumhardt alitambua kuwa huenda anakabiliana na pepo kama wale aliokuwa amesoma katika Agano jipya. Ingawa ufadhili wa masomo wa historia muhimu wa Ujerumani ulikuwa ukijiandaa kuelezea pepo wa mbali katika ulimwengu wa sasa, hapa katik parokia ndogo ya Ujerumani, Blumhardt alitambua nguvu ya Yesu katika upungaji pepo. Kama ilivyo siku ya Yesu, habari njema za ukombozi kutoka kwenye nguvu za pepo zilianza kuenea haraka. Watu walikuja kuona kitu kipya kilichokuwa kikitendeka nguvu ambayo ilikuwa imetumiwa na huduma ya Mhubiri Blumhardt. Mungu alikuwa akifanya kitu kipya, na Mhubiri Blumhardt alikuwa akitaka kukiamini. Alianza kutambua kuwa watu wengi walikuja kwa sababu zisizofaa. Alianza kuambia wanaotafuta msisimko kuwa upungaji pepo haukuwa uponyaji lakini ishara ilikusudia kuwaelekeza watu kwenye ufalme wa Mungu. Muujiza wa Yesu wa kutembea juu ya maji unafuata mara moja ule wa kulisha watu elfu tano katika Injili ya Mathayo. Yesu anafahamu kile ambacho Mhubiri wa Blumhardt alijifunza karne kadhaa baadaye: Mara nyingi sisi huvitiwa sana na ishara za miujiza ya nguvu ya Mungu kuliko tulivyo katika vuguvugu la ufalme ambazo zinatuelekeza. Yesu anawaita wafuasi oligopistoi wenye imani ndogo. Anazunguza nasi sote. Ni jambo tofauti kuona nguvu ya Mungu na kujua kuwa ni halisi: na jambo jingine tofaut kabisa kumwamini Bwana anayeomba kila kitu, hata dhoruba inapoonyesha hasira kwako. Bwana Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, tupe imani ya kuamini maisha yetu yote vuguvugu la ufalme wako. Amina. JONATHAN WILSON-HARTGROVE Siku 60 za Sala 13

Kile Ambacho Imani Pekee Inaweza Kuona JUMATATU, APRILI 4 SOMA ZABURI 121 Nililala salama kama lami nyeusi na usiku unaonata kwa utulivu, mbali na sauti za magari na umbeya wa siku hadi niliposikia mgongo mkali kwenye zege. John, bawabu wetu wa zamu ya usiku, alikuwa amemwua nyoka mwenye sumu ambaye alikuwa amenyinyirika karibu na mlango wa mbele wa nyumbani kwetu nchini Ghana, Afrika Magharibi. Mimi na mke wangu, Safiyah, tulihudumu huko kama wamishionari. Marafiki walikuwa wametumbia, Mwajirini bawabu wa usiku ili alinde nyumba yenu ili mlale usiku. Waisraeli walimwamini Mungu kuwalinda, uaminifu usiopatikana kwa wafuasi wa miungu mingine. Katika aya ya 3-4 ya Zaburi 121, mtunga zaburi anatangaza kuwa Mungu wa Israeli hasinzii wala kulala. Kauli hii inalingana na jirani wa Israeli ambao kwa kawaida waliamini kuwa miungu yao ililala majira ya baridi kali na kuamka misimu ya ukuaji. Wakati fulani nilizuru hekalu la dini nyingine. Lilikuwa na wawakilishi halisi w miungu iliyoabudiwa hapo na upatu. Nilipouliza madhumuni ya upatu, kiongozi alijibu tunagonga upatu ili kuhakikisha kuwa miungu imeamka. Mtunga zaburi alitumia kila fursa kuthibitisha imani kwa Mungu wa Israeli. Mungu huyu aliumba mbinu na dunia. Mungu huyu halali. Mungu huyu alitupa kivuli kama hifadhi. Imani kuwa Mungu angewapa mahujaji kivuli ilionyesha imani yao kwa Mungu mkuu anayeweza kuwapa kivuli kujikinga jua mchana na mwezi usiku. Mtunga zaburi anaendelea kusema kuwa Mungu atatukinga dhidi ya maovu yote. Je wewe? Ni nini unachojivunia kuhusu Mungu? Ni sifa ipi kati ya sifa za Mungu unaiiga mwenyewe na wengine katika uabudu wa ushirika? Matamko yako kumhusu Mungu hukusaidia kuona maisha kwa macho yenye imani. Mungu, kwa kuwa husinzii wala kulala kamwe, niepushe na usiku wenye wasiwasi na asubuhi zenye woga. Amina. KWASI KENA 14 Siku 60 za Sala

Barabarani JUMANNE, APRILI 5 SOMA LUKA 24:33-35 Kifungu hiki kilianza kwa kutamausha na mfadhaiko wa wafuasi wa Yesu, haswa wale wawili wanaosafiri kuelekea Emau. Sasa tunasonga kwenye uthibitisho wa ufufuko wa Yesu na kushiriki kwa habari hiyo njema na wafuasi wa Yesu Kristo. Katika kifungu, tunaona maana ya dharura. Ingawa ilikuwa jioni, watu wawili walisafiri mwendo mrefu sana kurudi Yerusalemu kukutana na wafuasi kumi na mmoja. Kukutana kwao na Yesu aliyefufuka kulikuwa kukubwa zaidi hivi kwamba wasingesubiri hata saa moja. Kwa sababu ya furaha yao, umbali haukuwa tatizo kwao, na giza halikuwazuia. Dharura hii ya kushiriki habari njema ni msingi wa uinjilisti wetu na dhamira ya kanisa. Hakuna kinachoweza kutuzuia kushiriki hali ya ufahamu ya kukutana na Bwana wetu aliyefufuka. Wawili wanapowasili, wanapata wafuasi kumi na mmoja katika eneo moja. Pia wameshuhudia Kristo aliyefufuka: Bwana amefufuka, na amemtokea Simoni! Hatujui ikiwa Yesu alimtokea Simoni kabla ya watu wawili barabarani kuelekea Emau. Wakati wa kutokea si muhimu. Muhimu zaidi kwao ni uthibitisho wa ufufuko wa Yesu. Kwa kweli alikuwa ameaga dunia msalabani lakini alikuwa amefufuka kama alivyoahidi na kama maandiko matakatifu yalivyotabiri. Kushiriki hali yao ya kukutana na Kristo aliyefufuka barabarani wakielekea Emau unakuwa mtindo wa maisha ya kanisa, na hali ya ufahamu wakati wa kumega mkate inatoa maana zaidi ya Karamu ya Bwana katika maisha ya kanisa letu. Mungu wa ufufuko, tupe maana ya dharura ili kushiriki hali yetu ya Kristo anayeishi na watu wengine. Amina. JUNG YOUNG LEE Siku 60 za Sala 15

Tumaini la Ufufuko JUMATANO, APRILI 6 SOMA 1 PETERO 3:18-22 Kifungu hiki kinatumika kama msingi wa andiko la kauli katika Imani ya Mitume inyoungumzia Yesu kati ya kifo na ufufuko: Alishuka kuzimu. Mara nyingi jibu letu kwa kipengee hiki cha kakuni ya imani ni la mfadhaiko: Hili linaweza kumaanisha nini? Wakati mwingine kipengee hiki kinaachwa nje ya kanuni ya imani. Ilhali, kama maandishi kutoka kwa Petero wa Kwanza, kinatuonyesh sifa inayoshangaza ya tumaini letu kwa kusema kuwa vikwazo vyote vya upendo wa maisha kutoka kwa Mungu vinasambaratishwa msalabani. Kikwazo kilichosambaratishwa hapa ni kile ambacho kinatenganisha wazima na wafu, wale wanaoaga dunia bila tumaini na wale wanaoishi kwa tumaini. Kifungu kinazungumzia wale walioaga dunia katika mafuriko ambapo Mungu alitaka kutakasa dunia kwa kutiwa najisi kwa dhuluma na ukiukaji. Wale waliosombwa hawakuwa na tumaini la mabadiliko. Ilhali ni kwa ajili ya hawa, ambapo wote waliokuwa wameaga dunia, kwa wote walio chini ya hukumu ya haki ya Mungu, ambapo Kristo anatangaza kati ya kifo chake katika mwili na ufufuko wake. Kwa sababu ya kushuka kwake katika gereza la nafsi, tunathubutu kuwa na tumaini kwa wote wnaoonekana kutenganishwa na injili kupitia kifo au hukumu. Kwa kuwa si hata wala ghadhabu ya Mungu inayoweza kuzuia tangazo la neema ya tumaini kwa wote kuteemea kifo na ufufuko wa Kristo. Tumaini letu la ufufuko ni thabiti mno hivi kwamba hatuwezi kukata tamaa ya tumaini kwa yeyote, haijalishi umbali uliopo kati yake na Kristo; iwe ni katika maisha au kifo, Kristo amesogea karibu nao. Mungu, asante kwa tumaini katika Kristo. Amina. THEODORE W. JENNINGS 16 Siku 60 za Sala

Makao ALHAMISI, APRILI 7 SOMA WAFILIPI 3:17 4:1 Inamaanisha nini kuzungumza kuhusu nchi yetu kuwa mbinguni? Kwa sababu ya kuteseka na kuvunjika kwa maisha katika mwili, dhehebu la Unostiki liliamini kuwa maisha ya kawaida ulimwenguni kwetu ni maovu. Badala yake, wanachama wake walifikiri kuwa sisi wanadamu tulipaswa kuwa kiroho, kutojali kabisa ulimwengu halisi. Wengi wa Unostiki hawa walijitambua kuwa Wakristo. Walimwamini Yesu lakini sio mwili na damu ya Yesu. Badala yake, walifikiri kuwa Yesu alikuwa kama pepo aliyetumwa kutupa ujumbe wa wokovu wa yake aliyeishi nje ya uumbaji ili kutuleta karibu na ulimwengu wa kiroho. Kanisa la zamani lilipinga sana uwili huo uliokataa uzuri wa uumbaji wa Mungu na pia uhalisia wa Kufanyika kwa Mwili. Badala yake, mababu zetu Wakristo walithibitisha kuwa Mungu hakuwahi kukusudia ulimwengu wetu kuvunjika. Katika Waroma, Paulo anasisitiza kuwa uumbaji wenyewe unagumia katika aina ya utumwa unaotokana na dhambi ya mwanadamu. Mwisho wa nyakati, tutakapopokea mili ya ufufuko wetu, anasema, ulimwengu halisi pia uterejeshwa kwenye kusudi asili na upendo wa Mungu. Dunia hii iliyorejeshwa ni makao yetu. (Tazama Waroma 8:18-25.) Muundo ambao urejeshaji huu utachukua na wakati wake sio muhimu kwetu kujua, hata hivyo, uvumi kuuhusu unaweza kutukengeusha kutokan na kazi halisi ya upendo na maisha ya Wakristo. Hata hivyo, tunahitaji kukumbushwa kuhusu upendo na utunzaji wa Mungu kwa ulimwengu huu huu tunaoishi ndani. Mungu wa viumbe vyote, tufunze jinsi ya kujua ulimwengu wako kama ulivyokusudia uwe, na utusaidie kuupenda na kuishi ndani yake kama zawadi yako. Amina. ROBERTA C. BONDI Siku 60 za Sala 17

Siku ya Bwana IJUMAA, APRILI 8 SOMA LUKA 3:1-6 Luka anaanzisha hadithi ya Yohana Mbatizaji katika historia kwa kutusimulia aliyekuwa kiongozi wa nini wakati gani. Hii inajumuisha himaya ya Roma, gavana wa Roma ya Judea, mtawala wa Ituraea wa Galilaya na kaka yake aliyetawala sehemu za Siria. Inakamilika kwa mtawala anayejulikana kigodo wa Abilene, wilaya ya kaskazini magharibi ya Damaska, na wawili wa makuhani wakuu Yerusalemu. Kwa kusoma orodha mara ya kwanza kunaonekana kuwa utangulizi wa kuchosha wa huduma ya Yohana, iliyojaa majina yasiyojulikana ambayo ni magumu kutamka. Luka ana sababu nzuri kwa kuijumuisha, hata hivyo ile inayoenda moja kwa moja kwenye moyo wa Injili yake. Ikiwa tungalisambaza ramani ya ulimwengu katika siku za zamano na kuweka vibanio vyekundu katika maeneo ambayo watu wenye nguvu walitawala, tungalikuwa na turubai ambalo lingalianzia Yerusalemu hadi Roma. Ingalijumuisha Wayahudi, Washami, Wagiriki, na Waroma. Ingalijumuisha kiongozi wa jeshi mwenye mamlaka zaidi duniani, na pia viongozi wa dini wenye mamlaka zaidi katika Uyahudi na watu wote walioishi chini ya sheria yao. Luka anaonyesha kuwa hadithi anayokusudia kusimulia inahusu yote hapo juu. Si hadithi ya ndani kuhusu mwanakarama wa Kiyahudi aliyeanzisha dhehebu jipya la Uyahudi. Ni hadithi ya ulimwengu kuhusu mkwozi wa Mungu aliyekuja kuubadilisha ulimwengu. Luka ananukuu mstari wa mwisho wa unaabii wa Isya kama mada yake: Na mili yote itona wokovu wa Mungu. Kabla ya kanisa kuwepo, injili ilipewa watu wote. Leo hii kanisa lipo kwa wale wasiofaa. Ni kwa njia zipi unajaribu kummiliki Yesu? Unafikiri Yesu ni wa nani, na ni nini ambacho lazima watu wafanye ili awe wao? Jaribu kufanya alichokifanya Mungu: Mtoe Yesu bila malipo kwa ulimwengu mzima. BARBARA BROWN TAYLOR 18 Siku 60 za Sala

Jangwa Litachanua Maua JUMAMOSI, APRILI 9 SOMA ISAYA 35:5-7 Wanasubiri. Watu wa jangwa. Wale wanaozidi maneno sahihi ya kusema. Zaidi ya uwezo wetu wa kukua kijani tena. Watu, maeneo, na hali zinakauka. Ni rahisi yaacha kwenye jangwa. Kinaonekana kuwa kitu kisichoaibisha sana kufanya. Haya hayasubiri mvua ya mwaka. Yamezoea marekebisho ya haraka ambayo yamekuja na kuenda pamoja na upepo wa wa kwanza mkali. Yanavumilia ahadi za wale wasiofahamu jangwa. Imekuwa rahisi kutarajia kuchoma mchanga badala ya maji na kufahamu kundi la mbweha. Uvumilivu wa machungu hauumii sana. Tumaini limekuwa hudhurungi na kukauka. Kisha Mungu anakuja. Hakuna anachogusa Mungu kinaweza kusalia vile vile. Si kijani cha ghafla. Ni unyunyizaji wa maji wa ndani, yanayopenya kiini cha kiumbe. Ni urejeshaji wa maji ya ardhini, sio kutiririk lakini kumiminika katika mkondo ili maisha yote yabadilishwe. Mizizi inaanza kuota hadi ndani kabisa. Uvumilivu wa machungu unageuka kuwa tumaini. Pindi tu tumaini linapoota, furaha inajitokeza. Nyika inaanza kuwa kijani hatua kwa hatua. Vidimbwi vya maji vinaonekana ambapo mchanga ulichoma nyayo zenye uchovu. Maji yanakimbia juu ya mawe yaliyojua upepo tu. Mbweha wanatafuta majangwa mengine. Macho ya vipofu yanaona. Wengine wanaanza kuona, lakini wote wanaona. Masikio ya viziwi yanazibuliwa. Wengine wanashika maji yanayokimbia, lakini wote wanasikia. Kiangazi cha muda mrefu cha roho kinaanza kuhisi, kuwa chochote anachogusa Mungu kinabadilika. Tumemsubiri Mungu, sio kutrajia kuonekana. Na Mungu amekuja. Mkuu wa jangwa, Mungu wa yasiyowezekana na kutotabirika, wa wakati. ninyunyizie maji, kulingana na mapenzi yako. Amina. RAY BUCKLEY Siku 60 za Sala 19

Utambuzi na Kuwa na Imani JUMAPILI, APRILI 1 0 SOMA MWANZO 12:1-9 Wakati Mungu anapomwita Abrahamu, Abrahamu anaenda. Abrahamu hasiti. Hashangai ikiwa anfanya jambo linalofaa. Hafikirii kuhusu gharama au hatari. Anachofanya ni kufuata amri ya Bwana bila kunung`unika wala kukataa. Maisha tunayoishi leo yanafanya kuwa vigumu kuiga mfano wa Abrahamu. Mahusiano ya ulimwengu wa mali yanatufunga kabisa. Kushughulika na kazi, familia zetu, kisha mahitaji mengi ya maisha ya kila siku, hatuwezi kufikiria kwa urahisi kuyaacha na kuenda eneo jipya kwa sababu Bwana ametuita kuenda huko. Majaribu yetu makubwa yanakuja kwa kutomtafuta Mungu wa kweli aliyejifanya mwili katika Yesu Kristo na ambaye mapenzi yake yasiyo na wakati na timilifu yanatufunga kila wakati. Badala yake tunamtafuta mungu mdogo, mungu ambaye hatawahi kutuomba kufanya chochote tusichotaka kufanya, kuacha chochote tusichotaka kuacha, au kuenda eneo ambalo hatutaki kuenda. Wakati wa kuanzisha Massachusetts Bay Colony, John Winthrop aliwaambia wanakondoo wake kuwa Mungu hajali kile unachomiliki lakini ikiwa, Mungu akibisha mlangoni petu na atuamuru tuache kile ambacho tunathamini sana kwa ajili ya Bwana, tutajibu. Tukitambua kuwa hatuwezi kuacha chochote, hutamfuati Kristo. Anaweza kuamuru tuache mali yanayothaminiwa au misimamo ya kisiasa inayothaminiwa au cheo kinachothaminiwa katika jamii yetu. Lakini kitu kimoja ambacho kila Mkristo anakifahamu kwa hakika ni kuwa hivi karibuni Bwana atabisha. Baba wa Mbinguni, nisaidie kuacha vitu vya ulimwengu huu, kusikiliza mwito wako ili kujitoa mhanga, na kuujibu kwa furaha na bila kuuza maswali. Amina. STEPHEN L. CARTER 20 Siku 60 za Sala

Tumeshafika? JUMATATU, APRILI 11 SOMA WAEFESO 2:1-7 Jinsi tunavyosema katika kanisa la Baptist nilipolelewa, nilioa nilipokuwa na miaka kumi na mmoja, miongo mitano iliyopita. Kipindi katika Shule ya Mfunzo ya Biblia kilikuwa kikiendelea. Jengo la kanisa letu lilikuwa hifadhi kwa zaidi ya njia moja. Muundo wa motofali mengi ilikuwa si tu sehemu ya kuwafunza watoto kuhusu Yesu; madarasa ya chini yalikuwa hifadhi bora mjini. Kusonga mbele hakukuwa kugumu. Kwa mtoto mchanga, lilikuwa jambo la maana sana, jambo ambalo lingalibadilish maisha yangu milele. Nilienda mbele kwa mwaliko na kumwambia mhubiri uamuzi wangu. Wokovu ni neno tunaloweza kuhusisha na ufufuo wa kiroho. Waefeso inaelezea shughuli ya Mungu ya kuokoa katika Kristo. Aya tatu za kwanza zinataja tunachookolewa kutoka kwacho: kifo kupitia dhambi, kufuata njia za ulimwengu, na kuwa watoto wa ghadhabu. Mwandishi haadhibu sana kama kutukumbusha kuhusu yaliyopita ili tuwe tayari kuthamini ujumuishwaji wetu katika hidhithi ya maisha ya Mungu ya wokovu wa sasa! Nilipokuwa na miaka kumi na mmoja, ahadi yangu ya kubadilisha maisha haikuhusu kubadilisha dhambi, zangu za zamani lakini kuhakikisha kuwa ilizua maswali mazito kuhusu jinsi ya kuwa Mkristo. Mara nyingi nilitaka kuacha kauli hiyo ya imani, lakini ahadi niliyokuwa nimetoa imeishia kunijenga. Haijawahi kunifanya kulegea, ingawa uelewa wangu wa kile inachomaanisha umebadilika kadri ninavyokomaa. Nimetambua utajiri wa huruma na ukarimu wa Mungu. Ninathamini kujitolea kwa Mungu kuchukua hatua kwa ajili ya manufaa na wokovu wangu. Niko hai pamoja na Kristo. Kwa ahadi hiyo, ninajaribu kila wakati kuwa na tumaini. Mungu, nisikie, nipe nguvu; niruhusu nikusikie. Amina. BILL DOCKERY Siku 60 za Sala 21

Kuitwa katika Agano na Mungu JUMANNE, APRILI 12 SOMA 2 SAMUELI 7:1-11, 16 Hata tukiwa na madhumuni yenye nia nzuri kwa kazi ya Mungu, ni vyema kufahamu kuwa lazima mapenzi ya Mungu yatawale. Uaminifu haumanishi tu kufanya mambo mazuri kwa ajili ya Mungu lakini kusikiliza ili kutambua kile ambacho Mungu angependa tukifanye. Mfalme Daudi anatamani sana kumfanyia Mungu jambo kubwa. Kwa kuongozwa na hisia yake ya furaha, Daudi anatmbua kuwa yeye binafsi anaishi katika nyumba ya mwerezi. Ikiwa hili linamfurahisha, kwa hakika nyumba bora kwa ajili ya safina itamfurahisha Mungu. Hili linaleta maana, sivyo? Lakini Mungu alitamani kumjengea Daudi (au nyumba ) ukoo wa kiroho. Kutoka kwenye urithi huu Mungu angalichagua muda na mzawa ambaye angalijenga hekalu. Muhimu zaidi, kutoka kwenye ukoo wa kiroho angetokea masiha. Ni mara ngapi katika maisha yetu tunawaza kile kitakachomfurahisha Mungu kulingana na hali zetu za wanadamu za furaha badala ya maarifa tunayopata kutoka kwenye maisha yetu ya kiroho? Tunapata maarifa ya kiroho kupitia uwazi wa kimaksudi kwa Mungu, kupitia kusikiliza na kutambua uwepo wa Mungu. Maarifa ya kiroho huandamana na uwazi na tarajio kwamba Mungu ana mapenzi na madhumuni, madhumuni tunayoweza kufahamu kupitia maisha yenye sala. Hata hivyo, neno la Mungu linamjia Daudi kupitia nabii Nathani, na Daudi anaweza kusikia. Watu wenye imani huishi kumfurahisha Mungu kupitia kuwepo kwao na vitendo vyao, kufahamu kuwa Mungu hufurahia katika kusikiliza kwa maombi sala zetu. Mungu, ninaomba mdundo wa kila siku ujumuishe wakati wa kuwepo nawe, kukujua vizuri zaidi, na kukupenda zaidi. Amina. NATHAN D. BAXTER 22 Siku 60 za Sala

Hekima, Tumaini, na Ahadi ya Mungu JUMATANO, APRILI 13 SOMA YOHANA 16:12-15 Hhatupokei maneno ya Mungu kwetu kila wakati. Yesu anajua kuwa wafuasi wake wengi watakuwa baharini bila umakini mkubwa, uhakika kutoka kwa Yesu kabla, kwa njia ya mwili, hajaondoka kwenye dunia hii. Kwa hivyo Yesu anawaambia, ningali na mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili kwa sasa. Roho wa ukweli ataapokuja, atawaongoza katika yote ya kweli. Wengi kufikia leo hii bado hawaelewi ukamilifu wa ahadi hiyo. Ulisikia lini Mkristo mcha Mungu akisema kitu kama hiki: Ninatamani Yesu asingalichukuliwa kutoka kwetu. Ninatamani angalikwepa kuondoka huko. Lakini kupaa kwa Yesu hakukuwa hasra kwetu; kulikuwa faida. Bwana katika kupaa kwake alipokea nguvu mpya. Wakati fulani alikuwa akiishi mbali kidogo; lakini sasa amefufuka, anapatikana kwa watu wote duniani saa zote mchana na usiku. Katika ufufuko wake alifikika kwa njia mpya. Aliyefufuka na kupaa hajazingirwa tena na vizuizi vya wakati na nafasi vinavyotuzuia sisi. Masuala ya kiroho kwetu hayatuchanganyi sana kama yalivyokuwa wakati wa kipindi cha siku arubaini kutoka Siku ya Pasaka hadi Siku ya Kupaa Mbinguni. Kutamani kuwa ungalirudisha nyuma saa kunanyima nguvu ya Roho Mtakatifu anayeweza kuwa nasi katika furaha yetu na huzuni zetu, nyakati za majaribu na nyakati za ushindi juu y dhambi. Hivyo, furahi na ushangilie, kwa kuwa Roho anatupa zaidi kuliko kile ambacho kupaa mbinguni kwa Bwana kungaliondoa kwetu. Hata zaidi, Roho yupo nasi na kuwa miongoni mwetu ahadi ambazo Yesu aliahidi wakati wa huduma yake ambazo tumesahau kwa kiasi kikubwa. Kile ambacho sisi na mababu zetu katika imani tusichokumbuka, Roho hutukumbusha. Roho Mtakatifu, njoo miongoni mwetu, tuhudumie sasa na milele. Amina. LAURENCE HULL STOOKEY Siku 60 za Sala 23

Kufanya Roho Mtakatifu Kuwa Mwili ALHAMISI, APRILI 14 SOMA LUKA 3:15-16 suala la ukomavu mdogo wa kiroho kujua kuwa mtu si Masihi. Hakuna N mtu katika kipindi chote cha mafunzo ya useminari aliwahi kunionya dhidi ya imani ya kuwa mwokozi. Badala yake, nilihimizwa kumwiga Yesu, kuwa mtumishi wa Mungu kwa watu. Katika miongo iliyofuata ya kufanya kazi na viongozi wa dini, wengi wao wakiwa wamechoka kwa kujaribu kutimiza matarajio ya wengine na yao binafsi au kuangamizwa kwa hitaji tupu la wanaparokia wao, nimetambua kuwa imani ya kuwa mwokozi, kwa watu wengi, haiwezi kutofautishwa na ahadi kwa Kristo. Yohana Mbatizaji alijua vyema. Ingawa alikuwa maarufu zaidi kuliko Yesu wakati wa maisha yake, Yohana hakuwahi kujaribiwa kwa tuzo maarufu au kwa maana yake isiyopingika ya mwito kwa kujifikiria binafsi kuwa masiha. Alikuwa na wajibu mkubwa kwa Mungu, lakini hakuwahi kupanga kutambua wajibu wake na ule wa Masiha. Martin Buber aliwahi kusema kuwa kuna kitu kisichoweza kulinganishwa kati ya kujifikiria kuwa masiha na kuwa masiha. Inawezekana kuwa wengi wetu hujipata wakifanya wajibu wa masiha kwa sababu hatujafia hitaji letu ili kuwa mtu mwingine. Inawezekana kuwa Yesu mweneyewe alikataa wajibu wa masiha ambao vizazi vya baadaye vilimpa. Majaribu yake katika nyika yanaonekana dhahiri kuwa kukataliwa kwa matumaini ya sasa ya masiha. Badala ya kujitambua na Mungu, alihusiana na Mungu. Aliupata mwito wake na kuufuata, kile ambacho vizazi vya baadaye vilimwita. Tunaweza kuhusiana na nguvu kama hizo za Mungu ndani yetu ambazo Yesu alihusiana nazo? Tunaweza kuwa vyombo vya uponyaji wa Mungu bila kujitambua binafsi na Mponyaji? Mungu, nifanye niwe mimi na kufanya kile tu ulichoniita nikifanye. Amina. WALTER WINK (1949 2012) 24 Siku 60 za Sala

Kumkaribisha Mungu IJUMAA, APRILI 15 SOMA YAKOBO 1:17-21 Swanadamu tunapaswa kufanya kilicho chema. Haiwezekani kuzua mjadala mkubwa kwa kauli hiyo. Lakini tunapaswa kuifanya vipi? Au kwa kugonga ndipo, kwa nini ni vigumu sana kwetu kufanya jambo jema? Kuwa wema? Tukiangalia karibu nasi, hatuhitaji kuangalia mbali kuona maisha yaliyoharibiwa, unyama, ufisadi, na uovu ni vitu vilivyo sehemu kubwa ya jamii yetu, kuanzia familia ndogo na mtaa hadi ngazi za taifa na kimataifa. Labda tumefasiri visivyo wajibu wetu katika kazi. Yakobo anatuambia kuwa matendo yote mema yana asili yake kwa Mungu. Hata Mungu alipouumba ulimwengu kwa neno moja: Mungu alisema... na ilikuwa, sasa katikati yetu neno la ukweli kutoka kwa Mungu linasababisha ulimwengu ulioanguka kuwa mzuri. Ikiwa mioyo yetu ina ukarimu kwa neno hilo la kweli, basi uzuri wenyewe wa Mungu unaanza kutuumba upya. Tunastahili kujiondoa yale yote yanayopinga neno zuri, kung`oa kwekwe ya hasira na utendaji dhambi kama mtunza bustani mzuri ambaye anatamani kutafuta nafasi ya mbegu nzuri. Mbegu nzuri ni neno la Mungu. Hatuwezi kujiundia wenyewe tafuta nafasi na ulikaribishe. Hiyo ni kazi ya kutosha. Tupe mioyo iliyo wazi kwako, Mungu, ili neno lako lipate makao ndani yetu. Amina. CATHERINE GUNSALUS GONZÁLEZ Siku 60 za Sala 25

Njoo, Roho Mtakatifu JUMAMOSI, APRILI 16 SOMA MATENDO 2:14-21 Petero, ambaye alikana kumjua Yesu, alikuwa jiwe ambalo Yesu alilijenga kanisa lake. Hapa anazungumza kwa mamlaka. Huku akiwa amezungukwa na mitume wake, anaangazia suala la umati. Hakuna miongoni mwao aliyelewa. Hawajawahi kuwa timamu zaidi. Anaripoti kuwa saa tatu kamili asubuhi hiyo Roho alining`inia juu yao kwa ndimi kama za moto, akawageuza kutoka ndani, na kuwafanya wajumbe wa Aliye Juu. Sio kwa maneno yake mwenyewe lakini kwa yale ya nabii Yoeli, Petero anafafanua kilichotendeka. Tusikilize unabii huu kana kwmba ni mara ya kwanza, na kugeuza matamko yake yafae. Tunaweza kuwa wachanga au wazee, mwanamume au mwanamke, mtumwa au huru, Wa taifa jingine au Myahudi na bado tuteuliwe na Mungu kama manabii wanaokataa kuridhishwa na hali iliyopo. Maisha kama tuyajuavyo hubadilika. Asili yenyewe inarekodi mwisho wa enzi na mwanzo wa enzi nyingine. Mabadiliko haya yatatusafirisha na Yesu kutoka kwenye uchungu katika bustani, kupitia kashfa ya msalaba, hadi utukufu wa asubuhi ya Pasaka. Damu, jasho, moto, moshi na ukungu hizi na ishara nyinginezo za misukosuko zinaashiria mabadiliko ambayo dunia na wakazi wake wanakaribia kupitia. Kwa ujio wa Roho, wokovu wetu uko karibu. Mitume wanapopokea mwanzo mpya kwa Roho Mtakatifu, vivyo hivyo lazima tuwe Wapentekoste, kuacha miradi yote ya wokovu wa binafsi na kumruhusu Mungu kuwa Mungu katika maisha yetu. Mkao wetu unakuwa moja ya unyenyekevu uliokithiri, tukipiga magoti mbele za Aliye Juu na kuliita jina la Mungu ndipo tunapoweza kujiondoa kwenye aina zote za kuabudu sanamu na kutoa ahadi kuu ya hisani. Njoo, Roho Mtakatifu, tumwagie kitulizo cha wokovu. Tupake mafuta ya furaha ili tuwe na ujasiri wa kutangaza kuwa Yesu Kristo ni Bwana. Amina. SUSAN MUTO 26 Siku 60 za Sala

Kiongozi au Mtumishi? JUMAPILI, APRILI 17 SOMA MARKO 10:42-45 Kipindi kifupi kilichopita kuhusu utatanishi unaoonekana wa uongozi wa mtumishi. Tumepoteza thamani ya maneno na matendo ya Yesu yanayobainisha kwamba uongozi wa kweli unahusu kuwatumikia wengine, sio kuwatawala. Ilhli, kwa njia nyingi tumebadilisha mabadiliko ya Yesu kwa kukubali neno kiongozi mtumishi lakini kulirejesha tena kwa mitego ya nguvu na upendeleo. Sote tunafahamu cheo cha kuhani mkuu wa Roma, mtumishi wa watumishi wa Mungu. Huku tukiwatukuza makuhani wanyenyekevu kwa haki, ukweli ni kuwa cheo kina mamlaka na nguvu ambayo si tofauti sana na mamlaka ya nguvu ya kiongoi yeyote w siasa. Waprotestanti wanaweza kujihesabia haki kwa urahisi, kwa kutambua kwa kupinga fahari, nguvu, na upendeleo vilivyopew mtumishi wa watumishi wa Mungu. Lakini hatujafanya vivyo hivyo? Tumeepuka neno mtumishi wa watumishi wa Mungu, lakini tunawapa mamlaka na heshima kubwa viongozi wasimamizi kuliko wachungaji? Katika miduara ya Muungano wa Methodisti, maaskofu hawatwi tena kwa jina lakini kwa cheo. Na je, hatuthamini kutumikia makanisa tajiri kuliko makasina maskini? Kwa nini wachungaji wetu wengi bora wanatumwa kwenye makanisa makubwa kama zawadi ya kufanya vyema, badala ya makanisa yetu maskini zaidi ambapo wanaweza kusaidia kanisa kukua? Ikiwa kwa kweli tulithamini uongozi wa mtumishi, je, wachungaji wasingewania vyeo vijijini au mji wa ndani au makanisa maskini ambapo uongozi ungalikuwa wa kujitoa mhanga? Katika Marko 10 Yesu anabadilisha dhahiri cheo cha kijamii cha kiongozi kutoka sehemu ya mamlaka hadi sehemu ya huduma ya kujitoa mhanga, hata hadi sehemu anayoita utumwa. Kusulubiwa kwake kulizuia mabadiliko haya mbapo Mkuu aliteseka pamoja na aliye chini zaidi kwa ajili ya kumwokoa aliye chini. Sisi ni wafuasi wa Kristo. Ni vipi tunavyolinda dhidi ya hatari za fahari ya sehemu tunapochagua mahali tunapotaka kutumikia? MARJORIE HEWITT SUCHOCKI Siku 60 za Sala 27

Sehemu Mpya za Utiifu JUMATATU, APRILI 18 S O M Z A B U R I 5 1 : 6-1 2 Daktari bora haridhishwi kamwe kwa kuangalia tu dalili za ugonjwa. Anataka kujua ni nini kinachoendelea ndani ya mgonjwa na kugundua kinachosababisha dalili hizi. Utabibu wa kisasa umevumbua vifaa mbalimbali vya kuchunguza mambo yanayoendelea katika mwili wa binadamu. Hivyo, ulimwengu wa tiba hutumia uyoka (eksrei), vitambazaji vya aina tofauti, na laparaskopia kuelewa mambo yanayoendelea ndani ya mili yetu. Mungu, kama daktari mzuri, anataka kuchunguza ndani ya mioyo yetu. Kifaa pekee cha Mungu ni kichocheo cha kuanzisha kujitolea kwa mwanadamu kufungua moyo. Ndio kwa maana kitabu cha Ufunuo kinamwonyesha Yesu akisema, Nimesimama mlangoni, nikibisha; ukisikia sauti yangu na kuufungua mlango, nitaingia ndani yako (3:20). Mtunga zaburi anajitolea kuufungua mlango. Anajua kuwa Mungu anatamani ukweli ndani ya moyo wa kiumbe na hivyo anamwomba Mungu amfunze hekima katika wake. Tunapotuma ombi, Nisafishe, Mungu huja kutusafisha. Tunaposema tu, Nioshe, ndipo Mungu atakapokuja na kufanya hivyo. Tunapotamka tu, Jenga moyo safi ndani yangu, ndipo Mungu huja kuweka roho mpya na sahihi ndani yetu. Mungu anapotuita sehemu mpya za utiifu, Mungu anasubiri jibu letu, Ndiyo, Bwana. Uwepo wa Roho Mtakatifu kwetu unatuita daima kufuata njia ya Mungu. Tunaposema ndiyo kwa Roho, tunagundua kuwa furaha yetu inarejeshwa na roho ya kupenda inadumishwa ndani yetu. Zaburi hii haikamiliki kwa maombi ya maisha yaliyofanywa upya pekee; inakamilika kwa kumsifu Mungu na azimio la kuimba kwa sauti ukombozi wa Mungu. Tunaposema ndiyo kwa msamaha wa Mungu, tunaimba wokovu wa Mungu sio tu kupitia maneno bali kwa maisha yetu yote. Jenga ndani yangu moyo safi, Mungu, na uweke roho mpya na sahihi ndani yangu leo. Amina. M. THOMAS THANGARAJ 28 Siku 60 za Sala

Yule Tusiyemjua JUMANNE, APRILI 19 SOMA ZABURI 126:1-6 Kuishi kama Wakristo ni kuishi katika hali ya ndoto. Ndoto bora ni zile ambazo hatutaki kuziamsha. Ndani yake tunafurahia mchezo usiotelekezwa au tunapata kila kitu kwa ghafla kikiwa na maana au kufurahia sana kukumbatiwa na mpenzi. Kisha kengele inapolia katika giza la asubuhi yenye baridi kali, siku nyingine ya majukumu inaanza kutuamuru kutimiza matakwa, kutuweka katia majaribu ya kufumba macho na kujaribu kurefusha ndoto, ndoto tamu. Lakini majukumu yanatuandama, na tunaweka nyayo zetu kwenye sakafu baridi na kudetea hadi bafuni. Kwa dakika chache ndoto inasahaulika, na uhalisia kutukumba kwa matakwa, wasiwasi, na majukumu yake. Hata hivyo, kuishi kama Waktristo ni kuendelea kuishi ndoto bora zaidi: ndoto ya pumziko la sabato lisilokwisha, tunapoweza kuacha kazi zetu; ndoto ya maisha yanayoleta maana na pale yasipoleta maana, amani na uaminifu wa kuishi katika siri; ndoto ya maisha ya kuishi katika ukumbatiaji wa upendo daima. Ndoto hii ni muhimu sana hivi kwamba lazima tujitahidi kila wiki kwa uabudu, sala, kusoma andiko takatifu kuikumbika. Hizo zote ndizo maana za neema: mazoezi ya kutusaidia kukumbuka kuwa uhalisia wa mzigo- baadhi ya majukumu si halisi kama ilivyo ndoto. Kisha, kama mtunga zaburi, tunaweza kucheka kiasi kwa sababu ndoto ni furaha na kiasi kwetu binafsi kwa upumbavu wetu kwa kusahau ndoto haraka. Na haswa kwa sababu tunakumbushwa tena jinsi Mungu anapotushika, kila kitu kinageuzwa juu chini na ndani nje. Bwana, weka katika akili yangu ndoto, na uweke moyoni mwangu furaha ya kufahamu uhalisia wake. Amina. MARK GALLI Siku 60 za Sala 29

Mteule Wa... JUMATANO, APRILI 20 SOMA 1 PETERO 2:2-10 Katika ulimwengu unaotangaza wengi wetu kukokuwa wema kabisa, inaweza kumaanisha nini kuamini kuwa kwa kweli sisi ni wateule, tunu, na wapendwa? Katika darasa la wanachama wapya tulizungumzia ubatizo: wakati huu mtakatifu ambapo tumetajwa kwa neema ya Mungu kwa nguvu kama hiyo haitatenduliwa. Fayette alikuwepo mwanamke anayeishi mitaani, akipambana na ugonjwa wa akili na lupasi. Alipenda sehemu kuhusu ubatizo na angaliuliza tena na tena, Na nikishabatizwa, mimi...? Baadaye tukajifunza kujibu, Mpendwa, mtoto tunu ya Mungu, na mrembo tazama. Ndiyo! angalisema, na kisha tungalirudi kwenye majadiliano yetu. Sikukuu ilifika. Fayette aliinana chini, akainuka akipaza sauti, na akalia, Na sasa mimi...? Na sote tukasema, Mpendwa, mtoto tunu ya Mungu, na mrembo tazama. Ndiyo! akapiga kelele huku akicheza karibu na ukumbi wa ushirika. Miezi miwili baadaye nilipigiwa simu. Fayette alikuwa amepigwa na kubakwa na alikuwa amelazwa kwenye hospitali ya kaunti. Kwa hivyo nikaenda. Niliweza kumwona kwa umbali, akitembea mbele na nyuma kwa kasi. Nilipofika mlangoni, nilisikia, Mimi ni mpendwa... Aligeuka, akaniona, na kusema, Mimi ni mpendwa, mtoto tunu ya Mungu, na... Kwa kujiangalia kwenye kioo nywele zikiwa zimesimama, damu na machozi vikidondoka usoni pake, nguo ikiwa imeraruka, mchafu, na vifungo bila mpangilio, alianza tena, Mimi ni mpendwa, mtoto tunu ya Mungu, na... Aliangalia kwenye kioo tena na kusema,... na Mungu bado ananitendea. Ukirudi kesho, nitakuwa mrembo zaidi nitakushangaza! Bwana, nibatize katika maji ya neema yako ili nikumbuke daima mimi ni nani na Yule ambaye mimi ni wake. Amina. JANET WOLF 30 Siku 60 za Sala

Zawadi za Ufuasi ALHAMISI, APRILI 21 SOMA HOSEA 11:1-11 Kusema kuwa Mungu anaumiza, Hosea anatupa dhana ya ajabu. Mungu Asiyeshindwa huhisi machungu. Mungu Msaniii Mchoraji, Mwandishi wa Ulimwengu, huhisi uchungu wa mwanadamu kukataa kuonyesha upendo, upendo unaomsaidia na kumponya mtoto. Mungu huumia, hatimaye, kwa sababu mtoto wa Mungu anaumia na kuvutia maumivi zaidi. Mtoto huvutia maumivi kwa kufuata miungu midogo inayoshawishi lakini inayodhuru. Ulafi, kama unavyoonekana kwa maafisa wa mashirika uliosababisha kuporomoka kwa uchumi wa 2008, ni moja ya miungu hiyo. Mwingine ni haki ya upendeleo, kama inavyotazamwa katika desturi ya sasa ya kutoa adhabu kuu kwa ubaguzi kwa wale wasiobahatika. Mtu kutokuwa tayari kusamehe hutumika kama mungu mwingine jambo linalosababisha hukumu ya Mungu. Tendo lolote la tamaa, linalotumikia miungu ambayo inawadhulumu wengine kwa kutimiza maslahi ya kibinafsi, linafanya kuwepo kwa hitaji ya Mungu. Hitaji gani? Tabia hizi za kuabudu miungu zinahitaji zawadi ya ghadhabu kutoka kwa Mungu. Hasira ya Mungu inatumika zaidi kuliko jibu la wivu wa mzazi aliyedharauliwa. Hasira iliyoonyeshwa wakati wa kutendea vibaya inanyanyua hadhi ya anayenyanyaswa na kutoa ilani kuwa uonevu hauwezi na hautakukubaliwa kimyakimya. Hasira ya Mungu inataka jibu la kutetea maumivu, jibu linalokomesha matendo yasiyo ya fadhili. Mungu anatamani upendo wetu, ili turidhiane na Mungu kwa kuwatendea wengine vizuri kwa upendo. Hosea anatukumbusha kuwa moyo wa Mungu huvunjika tunaposhindwa kupenda n kuw Mungu atazawidi kushindwa kwetu kwa jibu la hasira. Ni tishio. Ni ahadi! Cha kushangaza, hata licha ya ahadi ya hasira, Mungu bado anaturejesha nyumbani. Upendo wa ajabu kweli upendo wa kushukuru lakini sio wa kufanyiwa mzaha. Mungu wa upendo, tusaidie tupende kama unavyotaka na ulivyodhihirisha. Tunaomba kwa jina la Yesu. Amina. VANCE P. ROSS Siku 60 za Sala 31

Dhambi, Watenda dhambi, Wasio na dhambi. IJUMAA, APRILI 22 SOMA LUKA 15:3-10 Miezi kadhaa iliyopita katika uabudu, wakati wa kujiandaa kupokea Ushirika Mtakatifu, nilifahamu kwa uchungu kuhusu dhambi ya hivi majuzi. Sikuhisi kuwa tayari kuacha dhambi hiyo, na niliifahamu. Hivyo nilisali, Mungu, sistahili kupokea Komunyo asubuhi hii.... Haraka kama mwanga wa ghafla nilimsikia Mungu akisema moyoni mwangu, Oh? Na nyakati hizo nyingine zote ambazo umekuwa ukipokea? Nilistaajabu. Tunastahili? Kamwe. Tumekaribishwa? Daima. Hiyo ndiyo hali ya Mungu kukabiliana nsi. Kwa maneno ya Wesleyan, tunaita neema ya utangulizi wa ukaribisho wa kuwa tayari ya Mungu. Neema hii hutubeba kwa Mungu hata kabla hatujaamua kuanza safari. Ni Mungu anayetutongoza, kutupungia, kututafuta. Kwa kawaida Mungu haji katika maisha yetu kama mtaalam wa ubomoaji, kuporomosha majengo ya zamani kwa mlipuko mmoja wenye nguvu. Hilio huenda likawa rahisi kukwepa njia moja ya maisha pamoja na matatizo yake na mahusiano yaliyoharibika na kuanza upya. Lakini mara nyingi, Mungu hutubadilisha jinsi ambavyo kufungua madilirsha hubadilisha hewa chafu ndani ya nyumba kidogo kidogo kubadilisha kitu cha zamani na kitu kipya, chenye afya, kinachovutia zaidi. Na Mungu huendelea. Kama mchungaji aliye na wanyama walio tayari na wajinga, Mungu hutufuata katika mabonde yetu, kutuokoa ili baadaye tuweze kushirikiana katika mchakato wa kuokolewa. Tunaweza kujigamba kwa ujasiri wetu kuwa bora, lakini kuna swali msingi: Nini (nani) aliyetufanya kutoridhika na pale tulipokuwa? Mungu, mpenzi wetu mwaminifu. Na tunapoacha njia zinazotubomoa na kuchagua kitu kinachofaa, ni nani kiongozi wetu wa kushangilia mwenye furaha zaidi? Tena, Mungu. Mungu, kwa neema yako inayonitafuta hata wakati nisipotaka kupatikana, ninakushukuru. Amina. MARY LOU REDDING 32 Siku 60 za Sala

Wakati wa Uponyaji JUMAMOSI, APRILI 23 SOMA ZABURI 30 Kunayo kabla na baada kila mara. Mtunga zaburi anatuonyesha maisha na Mungu kati ya kabla hii na baada. Tunatoka kwenye ukataji tamaa hadi furaha, kutoka kwenye kujihisi kuwa mpweke, kuvunjwa moyo, na kusahauliwa hadi kuhisi kuinuliwa, kusaidiwa, na mwenye afya. Lazima tuwe makini ili tusifikirie hii kabla na baada ya maisha kama iliyosababishwa na Mungu kucheza nasi. Wala haitasaidia nafsi zetu kuona maisha kama mizunguko isiyo na mwisho wa kuendelea kuzunguka nyuma na mbele kwa mkanganyiko kati ya adhimu na ubovu. Njia zote mbili za kuona maisha zinaendelea kutujaribu. Mtunga zaburi anatuonyesha Mungu ambaye hutembea nasi kwa wakati, anayeridhika kuwa nasi katika kila wakati wa maisha. Kabla hujaamka leo hii Mungu alikuwepo nawe, akisubiri kuingia ndani yake nawe. Kabla hujakumabana na vitu vinavyoweza kukutamausha au kukuumiza au kukufanya kuvunjika moyo, Mungu yuko tayari kukuongoza siku nzima. Hata siku hii ikikuelekea kwenye makosa yasiyomfurahisha Mungu na kumwumiza jirani yako, Mungu hatakuwacha lakini atasubiri toba yako na kurudi kwako tena kwenye njia ya imani. Mungu ni Mungu wa tena na tena, ambaye anatamani kutuleta kwenye baada kila wakati: baada ya kuanguka, baada ya kutamausha, baada ya kuumiza. Hii ni njia ya Mungu, kutuondoa kutoka kwenye ishara za kifo hadi palipo uhai. Kwa hivyo, tuna unajisiri kwa kusifu kwetu na malalamiko yetu kwa Mungu, tukijua kuwa wakati wowote tunaishi na Mungu mwenye ubora wa kusikia. Wakati kati ya kabla na baada unaweza kuonekana kutakuwa na mwisho, lakini kutakuwepo na baada, kwa sababu Mungu ni mwaminifu. Bwana, nikumbushe katika nyakati zangu ngumu kwamba kulikuwa na kabla na ulikuwa nami wakati huo, na kutakuwepo na baada, kwa sababu uko nami hata sasa. Amina. WILLIE JAMES JENNINGS Siku 60 za Sala 33