KUZALISHA MBEGU YA MAHARAGE KIJITABU CHA KWANZA

Similar documents
Information for assessors (do not distribute this page to participants):

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI NA VITUNGUU TWAUMU (SWAUMU)

Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI

Uwepo, Athari na Udhibiti wa Sumu-Suvu Kwenye Vyakula vya

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees

pages/mkulima-mbunifu/

2 Usimamizi wa Rutuba ya Udongo Tanzania Organic Agriculture Movement

TIST HABARI MOTO MOTO

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu

Ni kwa nini mkulima awe maskini?

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Uzalishaji wa mboga na matunda ni muhimu kwa afya na kipato

Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana (SDSMV) Tanzania. Kiongozi Cha Mwezeshaji. Jaap Van Pol na Francesca Dalla Valle

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

4 WADUDU,MAGONJWA NA MAGUGU

MTI KWA MATUMIZI YA KILA AINA HDRA

PYRINEX. 1 Liter INSECTICIDE

Njia Bora za Ukusanyaji na Upimaji Maziwa

Njia bora za ukusanyaji na upimaji maziwa

Lishe na Ulaji Bora kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI

TIST HABARI MOTO MOTO. Benefits of Loan Repayment. Faida za ulipaji wa mikopo U OTESHAJI W A M ITI Y A M ATUNDA

Lishe na Ulaji Bora kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI VIDOKEZO MUHIMU KATIKA UNUNUZI NA USALAMA WA CHAKULA

Utunzaji, Uhifadhi na Usafirishaji Bora wa Maziwa

MBINU ZA IPM KWENYE KILIMO CHA KAHAWA

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Uzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza

Early Grade Reading Assessment for Kenya

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q

Teknolojia za Utayarishaji, Usindikaji na Matumizi ya Matunda na Mboga baada ya kuvuna

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA

Muhtasari wa taarifa ya warsha ya wataalamu juu ya mfumo wa habari kwa njia ya ramani (PGIS), Morogoro, Juni 30 - Julai 1, 2014

Bustani 10,000 Katika Afrika. Alberto Prina

Muongozo wa utatuzi. Kwa wasimamizi wa malaria RDTs 06/11/16. MALARIA Rapid Diagnostic Test

Vyote Unavyopaswa Kujua Kuhusu Viazi Vitamu

Wadudu na magonjwa ya mazao

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

Usindikaji bora wa maziwa

KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA

Mfumo na maelezo ya kina ya mpango wa kimataifa wa viwango vya chakula kwa wenye matatizo ya kumeza (IDDSI) Juni 2017

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

Mwongozo huu wa ufugaji kuku wa Asilia umezinduliwa rasmi leo tarehe 1 Agosti 2009 wakati wa sikukuu ya Wakulima Tanzania mjini Mbeya

CGAP Smallholder Household Survey in Tanzania / Utafiti wa kaya ndogondogo Tanzania

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza

Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira

Human Rights Are Universal And Yet...

TIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO

Vyote Unavyopaswa Kujua Kuhusu Viazi Vitamu

AMMA KWA AFRIKA RATIBA/ITIKADI. Ratiba Maalum ya Kutibu Magonjwa Maambukizi na Hususan Fikra Zinazoleta Pooza Mwili na Akili

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

Ufundishaji wa lugha nyingine

Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO. Training and Research Support Centre

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

UFUPISHO WA 35. Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji mazao: Clive James Chair, ISAAA Board of Directors

Njia za upimaji wa mpango wa kimataifa wa viwango vya chakula kwa wenye matatizo ya kumeza (IDDSI) VYAKULA VINYWAJI VYA KAWAIDA

International Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi

Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E)

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Jamii. ,,,^mm^mmm-<^^^^ illli MA RH-EREN.CE CENTRE

Siku ya kwanza. Mguso wa ngozi-kwa-ngozi (Ulezi wa kangaruu) Mtoto wako anaweza kuhisi mdundo wa moyo wako

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira

Upande 1.0 Bajeti yako

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Picha ni hati miliki ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Watoto(PCD), Imperial College London. Maelezo

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

Vyote Unavyopaswa Kujua Kuhusu Viazi Vitamu

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

Kijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia

muhtasari 37 brief 37 Kiwango cha kiutandawazi cha mazao ya kibiashara ya kibayoteki/ugeuzi jeni: 2007 Clive James Bordi ya wakurugenzi wa ISAAA

ONDOA MADINI YA RISASI KATIKA RANGI: LINDA AFYA YA WATOTO

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

MUONGOZO WA UTUNZAJI WA URITHI WA UTAMADUNI 1 SECURITY AT MUSEUMS

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

GENIUS CUP FINAL STANDART SEVEN

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017

Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

KISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA

Transcription:

KUZALISHA MBEGU YA MAHARAGE KIJITABU CHA KWANZA KIJITABU KWA WAZALISHAJI WADOGO WADOGO WA MBEGU YA MAHARAGE Kijitabu hiki kimetolewa na kituo cha kilimo kinachohusika na Maeneo ya kilimo katika sehemu za tropiki (CIAT). Mwandishi na Mhariri Soniia David Vielelezo na Bahizi Jovan KupanganaMfumo Fineline Pictures Kimetafsiriwa na Yona Mbwana Mshana M. Mwikari i

CIAT huhamasisha Mashirika na taasisi mbalimbali kutafsiri, na kutumia kijitabu hiki. Tafadhali tuma maelezo juu ya tafasiri ama uchapaji na utumiaji wa kijitabu hiki kwa: CIAT, P.O. Box 2704, Arusha, Tanzania. Fax: 255-27-2508557 Email: ciattz@habari.co.tz au CIAT, P.O. Box 6247, Kampala, Uganda. Fax: 256-41-567635 Email: ciatuga@imul.com Nakala za vielelezo zinaweza kupatikana kwa kutuma maombi kwa anwani hizi. Kunukuu: S. David 1998. Producing been seed: handbooks for smallscale been prdoucers. Handbook 1. Network on Bean Research in Africa, Occasional Publications Series, No. 29. CIAT, Kampala, Uganda. ii

WACHAPISHAJI Uhariri na uchapishwaji wa kijitabu hiki vimegharimiwa na Shirika lisilo la kiserikali la World Vision (WVT) pamoja na Idara ya Maendeleo ya Nchi za Nje ya Serikali ya Uingereza (DFID). Shrika lisilo la Kiserikali la Adventist Development and Relief Agency (ADRA T) ndilo lililogharimia tafsiri yote ya kijitabu hiki. WALIOTAFSIRI WAHARIRI Ni hawa wafutato: Yona Gabriel Mbwana Mwikari Mshana Walioshiriki kuhariri kijitabu hiki ni hawa wafutao: Andwerd Massam Hendry Mziray Matilda Mfoi Mwikari Mshana Sostenes Kweka Yona Gabriel Mbwana Ursula Hollenweger SHUKRANI Kituo cha Mawasiliano ya Kilimo, Kanda ya Kaskazini kinawashukuru wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine kutayarisha toleo la kijitabu hiki. Kituo kinawashukuru Shirika la Kimataifa la kuendeleza kilimo cha Maharage, CIAT hasa Dk. Soniia David na Dk. J.K.O Ampofo kwa kutoa idhini ya kutafsiri kijitabu hiki kutoka lugha ya Kiingereza kwenda Kiswahili na kutumia picha zilizomo. Shukrani zinatolewa pia kwa wataalam kutoka Tropical Pesticides Research Institute, (TPRI), Selian ARI, Arusha walioshikishwa katika kuhariri maneno ya kitaalamu. ADRA (T) na Wizara ya Kilimo inashukuriwa kwa kugharamia tafsiri ya toleo hili. Kituo kinatoa shukrani za pekee kwa Bi. Esther Makacha na Bi. Eva Ngallo kwa kutayarisha mfumo na kupiga chapa toleo hili. Shukrani zinatolewa pia kwa wengine wote walioshiriki kwa namna moja katika kuandaa kijitabu hiki. iii

YALIYOMO UKURASA Shukrani vi Utangulizi vii Kwanini ubora wa mbegu ni muhimu?.... 1 Ni ipi mbegu bora? 2 Shughuli muhimu shambani 6 Kuchagua mbegu 7 Kuchagua eneo 8 Kutayarisha shamba 10 Kuboresha rutuba ya udongo 11 Kupanda 13 Kupalilia na kung oa 14 Kuthibiti wadudu 15 Kuvuna 17 Shughuli za kufanya baada ya kuvuna 18 Ukaushaji kwenye vitumba 18 Kupura maharage.... 21 Kukausha mbegu 23 Kupepeta na kuchambua 25 Kupima kiwango cha unyevu 27 Kupima uotaji wa mbegu 29 Kukinga 37 iv

Kuhifadhi 45 Muhtasari 51 Misamiati itumiwayo na wazalishaji wa mbegu 53 Viwango vya mbegu iliyoboreshwa na Kukubaliwa 55 Jaribio la kupima ubora wa mbegu 56 Maswali ya kawaida wanayouliza wakulima. 62 Michoro: Sehemu za mbegu 64 Zana ya kupuria mbegu 65 Zana ya kuchambulia mbegu 66 Chombo cha kuangalizia sampuli (Bambo) 67 Pipa la kuchanganyia mbegu na dawa. 68 Silo 69 v

SHUKRANI Fedha za kufanikisha toleo hili zimetolewa na Canadian International Development Agency (CIDA), kupitia World Vision Tanzania. Shukrani ziwaendee A. M. Masam, H. Mziray, M. Mfoi, M. M. Mshana, S. O. Kweka na Y. G. Mbwana, U. Hollenweger kwa kuhariri kijitabu hiki. Michango ya kitaalam iliyotolewa na watu binafsi, taasisi mbalimbali inashukuriwa sana. Taasisi ya utafiti wa kilimo ya Kawanda kule Uganda imechangia kwa kiasi kikubwa sana katika kubuni vifaa na mbinu za kuzalishia mbegu za maharage. Mwandishi anawapongeza sana mabwana Michael Odong; Cedric Mutyaba na Ulysses Acasio kwa msaada wao mkubwa. Ushauri wa kiufundi ulitolewa na bwana Martin Wamaniala na bwana Mark Wood wa mradi wa IDEA Kampala Uganda. Anna Szakaly alisaidia katika kuandika nakala ya awali na Christine Scyprinski alisaidia katika upangaji na kuchora vielelezo. Ushauri na mapendekezo muhimu ya kitaalam kuhusu agronomia na magonjwa ya maharage yametolewa na Charles Wortmann na Robbin Buruchara. Shukrani pia zinatolewa kwa Esther Makacha na Eva Ngallo kwa kuhazili kijitabu hiki. vi

UTANGULIZI Kijitabu hiki kimedhamiriwa kutumiwa na wakulma wadogo wadogo wazalishao mbegu ya maharage. Kimeandikwa kwa ajili ya wakulima wasio na ujuzi au Elimu na uzoefu katika uzalishaji mbegu ya maharage. Ili kuelewa vizuri baadhi ya mambo yaliyogusiwa katika kijitabu hiki waone watafiti, mashirika yasiyo ya kiserikali ama huduma za ugani (Extension). (CIAT, SARI, MAOF na NGOs). Kijitabu hiki kimetengenezwa kitumike pamoja na vitabu vingine viwili:- 1. Kudhibiti magonjwa na wadudu waharibifu katika mashamba ya mbegu ya maharage, na, 2. Establishing a bean seed business. vii

KUZALISHA MBEGU YA MAHARAGE Kwa nini ubora wa mbegu ni muhimu? Wakulima wengi wanafahamu kwamba sio maharage yote yanayozalishwa kila msimu yanayofaa kwa mbegu. Maharage yaliyovunjika au kupasuka yanaweza kufaa kwa kula; ila hayafai kwa mbegu. Mbegu ya maharage inunuliwayo madukani, sokoni au yatolewayo kama zawadi na wakulima wengine yanaweza pia kuwa yameharibiwa na wadudu, kuoza, kuvunjika au kuvunda. Maharage yaliyoharibika yakitumiwa kama mbegu, wakulima wanaweza wasipate mavuno mazuri. Hii ndiyo sababu wakulima huchagua mbegu BORA ya maharage ya kupanda.! UBORA wa mbegu ya maharage ni muhimu sana kwa sababu hutoa mavuno mengi. Mbegu bora 1 zinazalisha mavuno mengi

Mbegu mbovu. Haiwezi kustawi vizuri. Ni ipi mbegu bora? Mbegu bora ya maharage ni ile ambayo:-!"uwezo wake wa kuota ni wa kiwango cha juu.!"imekauka vizuri.!"ni safi: mbegu zote ni aina moja na zenye ukubwa mmoja.!"haina taka: Haikuchangamana na mawe au uchafu wowote ule.!"haikudhurika, kuvunjika haijasinyaa, haina kuvu, haikuharibiwa na wadudu.!"haikuoza.!"haikupoteza rangi yake. 2

Endapo unahitaji kuzalisha mbegu bora ya maharage ni sharti uhakikishe kuwa mbegu yako inatimiza ubora na viwango vifuatavyo:- Viwango kwa ajili ya mbegu bora ya maharage Asilimia ya uotaji 13-15 Mbegu zilizoharibika 0 Mbegu zilizooza 0 Mbegu zilizopekechwa 0 Mbegu zilizopoteza rangi 10% Uchafu (takataka) 0 Uotaji na usafi Asilimiayauotajihupimwakwakulinganishakatiyambeguzilizootana jumla ya mbegu ziliooteshwa. Maelekezo kuhusu uotaji yameelezwa katika ukurasa.. Kiwango cha chini cha uotaji 80% Kiwango cha juu unyevu 13 15% 3

! Endapo 80 kati ya 100 zimeota, asilimia ya kuota ni 80% 80 gawanya kwa 100 = 0.8 0.8 x 100% = 80% Mbegu bora ya maharage lazima iwe safi iliyotakata, yaani mbegu zote ziwe za aina moja na ukubwa mmoja. Isiwe na vyovyote kati ya hivi vifuatavyo:- Taka, mawe, mbegu zilizovunjika, zilizosinyaa, zenye kuvu, zilizooza, zilizopekechwa. Kiwango cha asilimia 10 cha mbegu zilizofifia rangi zinakubalika. Kupata asilimia ya mbegu zilizoharibika, gawanya idadi ya zilizoharibika na jumla ya mbegu zote kisha zidisha na 100.! Endapo mbegu 5 kati ya jumla ya mbegu 60 zimeharibika, basi asilimia 8% ni mbovu. 5 ikigawanywa na 60 = 0.083 0.083 x 100 = 8.3% 4

Kiwango cha unyevu Kuelewa kiwango cha unyevu ndani ya mbegu ya maharage ni vigumu sana na huhitaji uzoefu mkubwa. Njia mojawapo ya kupima kiwango cha unyevu ni kuliuma harage kwa meno ama kuliminya kwa vidole. Harage litakuwa gumu. Ikiwa ni laini lina unyevu mwingi. Kuumaaukuminyakwavidolehusaidiakupimakiwangochaunyevu. Madaraja ya mbegu Mbegu ya maharage hupangwa ili kuonyesha tofauti ya ubora. Ubora hupimwa kwa kiwango cha kuota, usafi, ukavu na isiyo na magonjwa. Mbegu zilizozalishwa na wazalishaji wajuzi kwa ajili ya kuuzwa kwa wakulima huitwa mbegu zilizothibitishwa. Wazalishaji wajuzi au watafiti wanaweza kuwa wa miradi ya mbegu. Maelezo yaliyotolewa katika kijitabu hiki ni kwa uzalishaji mbegu zilizoboreshwa. Mbegu zilizoboreshwa ni za daraja la chini zikilinganishwa na mbegu zilizothibitishwa ambazo huzalishwa katika mazingira ya mkulima. 5

SHUGHULI MUHIMU SHAMBANI Ukiisha amua kuanzisha biashara ya mbegu ya maharage (Angalia kijitabu Establishing a been business ) zipo hatua thabiti ambazo lazima zifuatwe ili kuzalisha mbegu za daraja bora zaidi. Sehemu hii inaelekeza unachotakiwa kufanya shambani, kuanzia kuchagua eneo hadi uvunaji wa zao la maharage. Sehemu inayohusu mambo baada ya uvunaji huelezea mambo yakufanya baada ya kuvuna, tangu kukausha hadi kuhifadhi. Zifuatazo ni hatua ambazo lazima zifuatwe katika kustawisha mbegu ya maharage. 1. Chagua aina za kuzalisha; 2. Chagua mbegu ya kupanda; 3. Chagua eneo utakapostawisha mbegu; 4. Andaa ardhi; 5. Panda mbegu 6. Palilia na kung oa mimea isiyotakiwa. 7. Dhibiti magonjwa na wadudu waharibifu 8. Vuna. 6

KUCHAGUA AINA Uchaguaji wa aina utakazozalisha ni jambo muhimu katika kuamua mafanikio ya biashara yako. Zalisha aina ambazo unafikiri zina soko la uhakika. Maelezo ya uchaguzi wa aina za kuzalisha yameelezwa katika kijitabu Establishing a been seed bussiness. Unaweza kuchagua kuzalisha mbegu ZILIZOBORESHWA (aina mpya zilizokuzwa na watafiti) au aina ya mbegu za asili (mbegu za asilia zinazopandwa na wakulima). KUCHAGUA MBEGU Panda mbegu safi ya maharage na iliyoboreshwa inayopatikana katika kituo cha utafiti au mradi wa mbegu wenye sifa ya kutoa mbegu bora kwani mbegu isiyo bora itatoa mazao hafifu. Kwa aina za kienyeji au asilia tafuta mbegu bora; kutoka kwa mkulima mwenye sifa ya ukulima bora. Kwa vile baadhi ya magonjwa ya maharage hujificha ndani ya mbegu na ugonjwa hauwezi kuonekana kwa macho, ni muhimu kubadili mara kwa mara mbegu unayopanda. Kuna aina kuu tano za magonjwa ya maharage yaliyofichika ndani ya mbegu: ukungu wa bakteria (common bacterial blighted) (common bean). 7

mosaic virus, anthracnose),. (Halo blight and ascochyta) kwa maelezo zaidi namna ya kuyatambua magonjwa haya, soma kitabu kiitwacho Magonjwa na wadudu waharibifu wa maharage. Endapo utaona mimea mingi shambani imeathiriwa na mojawapo ya magonjwa haya matano badilisha mbegu kila msimu mmoja au miwili ili kuhakikisha upatikanaji wa mazao yasiyo na magonjwa. KUCHAGUA ENEO Ili kupata maharage kwa wingi, chagua eneo lenye sifa ya kuzalisha maharage. Kwa mfano usipande kwenye miinuko mikali, ardhi inayotuamisha maji, udongo wa kichanga, udongo usio na kina, udongo wenye kwekwe sana. Angalia ishara zionyeshazo udongo wenye rutuba. Ardhi ya muinuko Ardhi yenye maji ya kutuama Magugu Mabaya kamakwekwe Udongowakichanga 8

Kwa vile magonjwa ya maharage hubakia kwenye udongo ni vyema mbegu zistawishwe kwa msimu mmoja au miwili tu katika eneo moja. Tumia mfumo wa kubadilisha mazao Katika kuchagua eneo, fikiria pia umbali toka shambani hadi utakapo hifadhi maharage. Ikiwa umbali ni mkubwa utapata usumbufu wa kusafirisha mavuno. Zingatia matatizo ya usafirishaji 9

KUTAYARISHA SHAMBA Ukiisha chagua eneo lako, tayarisha shamba lako mapema. Lima kwa kina. Endapo yapo majani au magugu mengi shambani, inakubidi ulime angalau mwezi mmoja kabla ya kupanda ili majani yaoze vizuri. Usipofanya hivyo, maharage yako yatachipua na rangi ya njano au kuota vibaya. Maandalizi mazuri ya shamba (Lima kwa kina) Uandalizi mbovu wa shamba (udongo usio na kina) 10

Ikiwezakana chunguza udongo wako. Chukua udongo sehemu tofauti tofauti katika shamba lako kwa kuchimba mashimo (matano) 5 kwa kila ekari moja yenye kina cha inchi 8. Chukua kiasi kidogo cha udongo toka kwa kila shimo na uuchanganye pamoja. Peleka sampuli hii kwenye kitengo cha utafiti. Matokeo yatakuonyesha ikiwa iko haja ya kutumia mbolea. KUBORESHA RUTUBA YA UDONGO Endapo itakubidi kuongeza mbolea, unaweza kuitandaza kwa mikono juu ya shamba kabla ya kulima. Kwa kila ekari moja weka kilogramu 40 za mbolea ya DAP (kilo 100 kwa kila Hekta) au kilo 40 za TSP pamoja na kilo 10 za Urea (kilo 100 pamoja na kilo 25 kwa Hekta) mazao yako yataongezeka na kuboreshwa. Shamba lililowekwa mbolea 11 Shamba lisilo na mbolea 11

Unaweza pia kutumia mbolea ya wanyama (Hasa mbolea ya kuku) au mboji ili kuboresha hali ya udongo. Kutumia mimea iitwayo MUCUNA na CANAVALIA pia huongeza uwezo wa udongo kuzalisha. Unaweza kupata mbegu za MUCUNA na CANAVALIA kutoka kwenye kituo cha utafiti wa kilimo (SARI) Afisa au mhusika wa ugani atakushauri mahali mbegu hizi zinapopatikana. Mmea wa mucuna upandwe kabla ya msimu na uachwe juu ya ardhi. Panda mbegu mbili za Mucuna au Canavalia katika shimo moja kwa upana wa sentimeta 60 (futi 2) kati ya mmea na mmea na sentiment 75 (futi 2.5) kati ya mstari na mstari. Kwa vile mimea hukua haraka na kufunika udongo mapema, ni vyema kupalilia majuma matatu baada ya kupanda. Ukiwa tayari kupanda maharage ya mbegu ng oa Mucuna na Canavalia na iache ikauke juu ya udongo. Unapopanda zao baada ya kupanda Mucuna au Canavalia hakuna haja ya kutifua udongo. Acha mimea mikavu ya Mucuna au Canavalia juu ya udongo wakati wa kupanda. 12

KUPANDA Ikiwa umeamua kupanda mbegu zilizokubalika kitaalam ya maharage, weka mbegu moja tu kwenye kila shimo. Endapo mbegu imepatikana toka kwa wakulima wengine ama maduka ya kawaida, panda mbegu 2 3 ndani ya kila shimo. Panda maharage katika miraba. Hii hurahisisha upaliliaji wa zao hilo. Inashauriwa kuacha nafasi ya sentimeta 50 kati ya mstari na mstari na sentimeta 15-20 kati ya mmea na mmea. Sm 50 Sm 15-20 Nafasi inayopendekezwa kati ya mimea na mistari Unapopanda aina mbali mbali za maharage, hakikisha kuacha nafasi ya meta 2 kati ya aina moja na nyingine. Hii huzuia hatari ya kuchangaya aina. Mita 2 Nafasi inayoshauriwa kati ya aina moja na aina nyingine 13

Wakulima wengi hupendelea wazo la kilimo mseto. Hakikisha hufanyi hivyo katika shamba la mbegu ya maharage kwani hii husababisha utunzaji shambani wa zao hili kuwa mgumu na kuna hatari ya kuvuna kidogo. KUPALILIA NA KUNG OA Magugu hupunguza mavuno. Ndiyo sababu ni muhimu kupalilia angalau mara moja hadi mara mbili kila msimu. Palizi ya kwanza hufanyika kabla ya kwisha majuma 3 tangu kupanda. Palizi ya pili hutegemea ukuaji wa mmeanamaguguulivyo. Katikati ya kipindi cha majuma 5 tangu kupanda, kagua shamba lako kuona mimea yenye ugonjwa, kama ifuatavyo:- 1. Mara mimea iotapo toka ardhini, 2. Majuma mawili baada ya ukaguzi wa kwanza, 3. Mara maua ya mwanzo yanapotokea. Mimea ya maharage huathiriwa na magonjwa mengi. Inawezekana usitambue mengi ya maradhi hayo. Maelezo ya kina jinsi ya kuyatambua na namna ya kukagua shamba lako yamo katika kitabu cha Magonjwa na wadudu waharibifu wa maharage shambani. Endapo ni mimea michache tu inayoonyesha dalili za ugonjwa, iondoe ili ugonjwa usisambae kwa mimea yenye afya nzuri. Ng oa mimea migonjwa kisha ichome moto. 14

Ili kubakia na aina halisi ya maharage inabidi kung oa maharage yenye tofauti ya majani au umbo tofauti na yale halisi. Kwa mfano ng oa maharage yanayotambaa au majani na maua yenye umbo na rangi tofauti. KUDHIBITI WADUDU Wadudu waliozoeleka kuathiri mimea ya maharage ni kimamba, funza wa inzi wa maharage (Bean Stem Magot) vithiripi wa maua (flower thrips), mbawa kavu wa majani (Ootheca) na aina nyingine za wadudu zilazo vitumba na majani. Kitabu ( Magonjwa na wadudu waharibifu wa maharage shambani ) kinaelezea namna ya kutambua na kuwazuia wadudu. Kwa vile wadudu huweza kuathiri zao lote la mbegu, kagua shamba lako mara kwa mara kuona na kuua wadudu waharibifu. Kitabu hicho kinayo maelezo ya kina kwamba ufanyeje. Sio kila mdudu ni mharibidfu wa maharage. Kwa mfano nyuki hawadhuru zao la maharage. Buibui, sisimizi, siafu ni maadui wa asilia wa wadudu waharibifu. Madawa Wadudu waharibifu wanaweza kudhibitiwa kwa kutumia dawa. 15

Kimamba na vithiripi wa maua: tumia Dimethoate (Rogor) au sumithion kuua hawa wadudu waharibifu. Weka mililita 20 (vijiko 4 vya chai) kwa lita 15 za maji ndani ya bomba. La kupulizia dawa. Matoboa vitumba tumia Ambush au Bulldock dhidi ya wadudu hawa. Weka mililita 10 (vijiko 2 vya chai) kwa lita 15 za maji ndani ya bomba la kupulizia dawa. Wadudu walao majani. Hawa wana madhara kidogo. Labda kama watakula zaidi ya (theluthi 1/3) ya majani yote ya mmea. Ikiwa ni hivyo tumia kipimo kile kile uwekacho kwa matoboa vitumba. Funzawainziwamaharage. Endapo unalo tatizo la funza wa inzi wa maharage panda mbegu iliyochanganywa na dawa. Kijitabu kiitwacho Magonjwa na Wadudu Waharibifu wa Maharage Shambani kinayo maelezo yote kuhusu namna ya kudhibiti wadudu hawa. 16

KUVUNA Vuna maharage yaliyokomaa na kukauka. Mbegu zinazovunwa mapema mno hazizalishi mimea yenye Afya. Mmea uko tayari kuvunwa wakati vitumba vikishakauka. Usiache maharage kukaukia shambani baada ya kuyavuna kwa vile Yanaweza kuathiriwa na wadudu au wanyama. Maharage yaliyoachwa muda mrefu juani huwa makavu sana kwa kusafirishwa, na endapo yameachwa kwenye mvua, huwa na unyevu usiofaa kwa kusafishwa. Vuna mimea iliyokomaa Usichelewe kuvuna 17

SHUGHULI ZA KUFANYA BAADA YA KUVUNA Hatua hizi zifuatwe baada ya kuvuna: - 1. Kukausha maharage yakiwa kwenye vitumba. 2. Kupigapiga (kupura). 3. Kukausha maharage. 4. Kupepeta na kuchagua. 5. Kupima kiwango cha unyevu. 6. Kupima kiwango cha kuota. 7. Kukinga. 8. Kuhifadhi. KUKAUSHA KWENYE VITUMBA Kabla maharage hayajapurwa, sharti yakaushwe yakiwa kwenye vitumba. Ukiyapura mara tu baada ya kuvunwa unaweza kuathiri mbegu kwa sababu haijakauka vya kutosha. Pima kiwango cha unyevu ndani ya mbegu kabla ya kupura ukitumia meno yako au kuminya kwa vidole. Pia, kabla ya kukinga tumia jaribio la kutumia chumvi. Namna ya kutumia jaribio la kutumia chumvi limeelezewa katika ukurasa wa 27. 18

Usikaushe maharage ardhini. Kufanya hivyo kunaweza kuyachafua, kuongeza unyevu, au kuliwa na wanyama. Unaweza kukausha maharage juuyamkeka. Kukausha maharage kwenye mkeka Ni bora zaidi kukausha juu ya karatasi ya nailoni iliyowekwa juu ya kichanja. Kukausha juu ya kichanja 19

Chunga maharage yasiharibiwe na wanyama. Picha hii inaonyesha kwamba ni rahisi mtu kufunika endapo mvua itanyesha na ni rahisi kufukuza wanyama. Linda maharage yanapokaushwa Mara baada ya kuandaa mahali pa kukaushia maharage, fuata hatua zifuatazo:- 1. Ondoa magugu na vitumba ambavyo havikukomaa. 2. Sambaza vitumba kwenye kichanja, mkeka ama meza, ili kuruhusu mzunguko wa hewa na joto. 20

3. Kausha maharage juani kwa muda wa siku. 4. Pima maharage uone kama yamekauka vya kutosha. Kwa kupasua kitumba na kuuma kwa meno au kuminya kwa vidole. KUPURA MAHARAGE Ukishathibitisha kwamba maharage yamekauka vyakutosha unaweza kuyapura (kuyapigapiga). Kumbuka kwamba maharage yaliyokauka sana na yaliyo na unyevu sana yanaweza kuharibiwa wakati wa kupura. Ni muhimu kufanya yafuatayo unapopura. 1. Usivunje wala kudhuru; 2. Usichanganye mbegu na uchafu au makapi; 3. Usipoteze mbegu. 21

Kupura juu ya ardhi au kwenye gunia kunaweza kuharibu mbegu kwa urahisi. Mbegu zilizovunjika ama kupasuka hushambuliwa na wadudu na kwa urahisi na pia zinaweza zisiote. Kupura juu ya kifaa maalum (Threshing rack) husaidia mbegu zisidhurike kwa kuvunjika, kuchafuka au kusambaa ovyo. Mwanamke akipura juu ya kifaa maalum Kifaa hiki cha kupura hutengenezwa kwa vifaa vifuatavyo:-vipande vyembemba vya mbao, vilivyopangwa sawia kwenye fremu ikiwa na chekecheke upande wa chini kunasa na kuhifadhi mbegu zilizopurwa. Mbegu hizi hazitapakai kila mahali kwa vile huzuiwa na kuta za pembeni za fremu hii. Seremala yeyote anaweza kutengeneza kifaa hiki kama mchoro unavyoonyesha (ukurasa 65) 22

KUKAUSHA MBEGU Mbegu ikishapurwa, lazima ikaushwe mara ya pili. Kama kawaida ni vyema kuilinda mbegu isipatwe na mvua, wadudu, wanyama na uchafu. Mbegu iliyopurwa ikaushwe juu ya mikeka, makaratasi ya nailoni, makashayawavuaufremuzilizoinuka. 1. Sambaza mbegu ili kuruhusu hewa na jua kupenya kwa urahisi. 2. Geuza geuza mbegu ili zisiungue sana na jua. 23

3. Kausha mbegu kwenye jua kwa siku 1 hadi 3. 4. Jihadhari na zuia mbegu zisinyeshewe na mvua ama kuharibiwa na wanyama. 5. Pima maharage uone endapo yamekauka vya kutosha kwakuminyakwavidoleamakuumakwameno. 24

KUPEPETA NA KUCHAGUA Kupepeta kufanyike ili uchafu uondolewe pamoja na vumbi na takataka nyingine. Mwanamme akipepeta Baada ya kupepeta, okota maharage yote yaliyosinyaa, yaliyovunjika na mbegu za aina au rangi tofauti. Ukifanya kazi hii kwa kutumia mtambo wa kuchambulia mbegu, huifanya kazi kuwa rahisi. Mtambo huu una mashimo yanayoruhusu uchafu kutoka bila kuchanganyika na mbegu. Sehemu au kifaa cha kuchambulia hutengenezwa kwa mbao mbili zifanywazo kuwa kama mpare yenye waya na matrei ya kudaka mbegu. Hii nyenzo ya kuchambulia huwekwa juu ya meza na wachambuaji hufanya hiyo kazi wakiwa wameketi kuzunguka meza. 25

Kutumia nyenzo ya uchambuaji Kwa kutumia mtambo wa uchambuaji, mwaga mbegu zilizopepetwa na kukaushwa kwenye mpare. Mbegu hudondoka katika chekecheke. Mbegu ndogo na zilizovunjika, uchafu na takataka huondolewa kwa urahisi. Matundu tofauti tofauti kwenye chekecheke yanaweza kutumiwa kwa aina mbali mbali za mbegu na za ukubwa tofauti. Seremala wa kawaida anaweza kutengeneza mtambo wa Kuchambulia kwa kufuatisha mchoro uliopo ukurasa wa 66. 26

KUPIMA KIWANGO CHA UNYEVU Njia bora ya kutambua kiasi cha unyevu ndani ya mbegu ya maharage yaliyopurwa ni kwa kutumia chumvi. Utahitaji chupa safi moja, mfuniko wake, chumvi na mbegu za Chukua kiasi kidogo cha mbegu (kiganja kimoja kinatosha) toka katikati ya kila gunia la megu. Tumia kile kifaa maalum cha kutolea mbegu ndani ya gunia (Bambo) weka kila mbegu mahali tofauti. (Angalia ukurasa 67). Hatua za kufuata kupima unyevu kwa kutumia chumvi 1. Hakikisha kwamba chupa utumiayo ni safi na kavu. 27

2. Weka chumvi ndani ya chupa (Weka chumvi kujaza robo ya chupa) tumbukiza mbegu kiasi cha kujaza nusu chupa. Funika chupa kwa mfuniko. 3. Tikisa chupa vyema na acha mbegu zitulie kwa muda wa dakika kumi. 4. Endapo chumvi itagandamana kwenye kingo za chupa, basi mbegu hizo zina unyevu mwingi. Unyevu mwingi maanayakenikuwakiasicha unyevu kinachotakiwa kwa mbeguasilimia13 15 ambayo ndiyo kiasi kinachotakiwa kwa mbegu zilizoboreshwa. Kama chupa (kingo) zitabakia kavu na hakuna chumvi illiyogandamana, mbegu imekauka vizuri. 28

KUPIMA UOTAJI Baada ya kusafisha na kuchagua, ni lazima sampuli ya mbegu ifanyiwe majaribio ya uotaji. Matokeo ya jaribio yatawaelewesha wakulima kiasi cha mbegu watakachohitaji kupanda ili kupata mavuno mazuri. Kwa mfano endapo unafahamu kwamba asilimia 90 ya mbegu itaota, wakulima hawatahitaji kupanda mbegu zaidi kama ambavyo wangehitaji endapo ni asilimia 60 tu ya mbegu itaota. Mbegu inabidi zipimwe uotaji kabla hazijahifadhiwa. Endapo mbegu zimehifadhiwa kwa zaidi ya miezi mitano inabidi zipimwe tena kuona uotaji wake ni asilmia ngapi kabla ya kuziuza. Hatua za kufuata ili kufanya jaribio la uotaji. a. 1. Tayarisha sampuli ya kupimwa. a) Chukua sampuli za mbegu (kiganja hutosha) toka juu, katikati na chini ya kila gunia kwa kutumia kifaa maalum (Bambo). 29

b. b) Changanya vyema sampuli toka kwenye magunia yote ndani ya chombo. c. c) Chukua kilo moja ya mchanganyiko huu kisha changanya vizuri tena ndani ya chombo d. d) Halafu chukua mbegu 200za kwanza unazoziona. Usiokote kwa kuchagua; zihesabu ukianzia mwanzo mmoja wa kitita. Rudisha mbegu zilizobaki ndani ya magunia. 30

2. Panda mbegu Tenganisha sampuli ya hizi mbegu mia mbili zigawe mafungu mawili yanayolingana. Kila moja liwe na mbegu 100. Panda mbegu 100 kwa pamoja sehemu moja na mbegu 100 nyingine kwa pamoja sehemu nyingine kwa kufuata maelekezo yatuatayo:- Ni bora kufanya majaribio ndani ya vyombo viwili. Ni vizuri kutumia mchanga na kama huna mchanga tumia udongo. Weka udongo/mchanga safi wenye unyevu wa kina cha centimeta 10-12, usiugandamize ndani ya chombo. Weka mashimo ya kupandia mbegu sentimita 2 3 toka shimo hadi shimo kwa mistari ukitumia kijiti. Weka mbegu moja tu kwenye kila shimo. Kupanda mbegu kwenye udongo 31

Nguo au karatasi huweza pia kutumika badala ya udongo au mchanga. Lowanisha nguo au karatasi, weka mbegu juu yake kisha funika kwa kutumia kipande kingine cha nguo au karatasi iliyoloanishwa kwa maji. Kupanda mbegu kwenye nguo Baada ya kupanda, mwagilia maji na kagua kila siku ili kuona kwamba mchanga au udongo haukauki sana kuzuia mbegu kuota. Hakikisha kwamba chombo ulichotumia kina matundu kwa chini ili kuruhusu maji kutotuama. Mbegu lazima zianze kuota siku tatu hadi tano baada ya kupanda. Ni muhimu kuthibiti kiwango cha unyevu. Mbegu ziwe na unyevu ila zisiloane. Maji yakiwa mengi sana ama machache sana huweza kuzuia mbegu zisiote. Chombo kihifadhiwe ndani. Kama kimewekwa nje, hakikisha hakipigwi na jua wala kunyeshewa na mvua. 32

3. Ichunguze miche Siku nane (8) baada ya kupanda, chimba mche kwa uangalifu au uuchunguze uotavyo katika kitambaa au gazeti na igawanye makundi matatu:- a) Miche iliyostawi vizuri itakuwa na: Mizizi Shina Majani Ghala (cotyledons) (Ghala ihifadhiyo chakula upande wa ndani wa mbegu angalia picha hapa chini). Cotyledons b) Miche vilema: Itakuwa na mojawapo kati ya alama hizi: Hazina mzizi mkuu Hakuna majani Hakuna ghala Ghala zilizooza Mizizi dhaifu c) Mbegu zilizooza 33

Jaza aina hii ya jedwali likusaidie kuweka kumbukumbu zako: Jumla ya mbegu Miche mizuri Miche vilema Mbegu zilizooza Kundi 1 100 Kundi 2 100 Jumla 200 4. Pata asilimia ya zilozoota (a) Kwanza pata asilimia ya zilizoota kila kundi peke yake. Kwa vile umepanda mbegu mia moja kwa kila kundi, idadi ya mbegu nzuri ni sawa na asilimia ya uotaji wa miche katika kundi hilo. Endapo umepanda idadi tofauti ya mbegu itakulazimu kuhesabu upya i. Hesabu idadi ya miche mizuri. ii. Gawanya nambari hii kwa namba ya mbegu ulizopanda. iii. Zidisha nambari hii kwa 100. 34

(b) Ukiisha panga kiwango cha uotaji cha kila kundi tofauti, lazima upate wastani wa kiwango cha uotaji. i. Ongeza asilimia ya kila kundi. ii. Gawanya nambari hii kwa namba ya makundi (batches) hapa makundi mawili (2 batches). Mfano: Katika mfano huu, upimaji wa uotaji umefanywa na mbegu 100 zilizopandwa katika makundi mawili. Jumla ya mbegu Miche Dhaifu Mbegu zilizooza Kundi 1 100 12 6 Kundi 2 100 9 5 Jumla 200 21 11 Kwa vile jumla ya mbegu zote ni 100: Kundi la kwanza lina asilimai 82% uotaji Kundi la pili lina asilimia 86% uotaji Ongeza asilimia: 82 + 86 = 168 Gawanya idadi hii kwa idadi ya makundi: 168 2 =84 35

Katika mfano huu, asilimia ya uotaji ni 84%. Zingatia: Mbegu inayoota chini ya asilimia 80% kamwe isiuzwe kwa matumizi ya mbegu Bali inaweza kuuzwa kwa chakula 36

KUKINGA/TIBA Madhumuni ya kutibu mbegu ya maharage ni ili kuilinda dhidi ya uharibifu wa wadudu, panya na Ukungu wakati inapohifadhiwa kwa muda mrefu. Mbegu iliyoharibiwa na Wadudu Mbegu inaweza kutibiwa/kukingwa ili kulilinda zao lisipatwe na ugonjwa au dhara ya wadudu wakatao shina la maharage. Soma maelezo katika kijitabu kiitwacho Magonjwa na wadudu waharibifu wa maharage shambani Ili kupata maelezo zaidi juu ya kukinga dhidi ya mdudu huyu akataye mashina ya maharage. Njia za Asilia za kutibu/kukinga dhidi ya uharibifu wakati wa kuhifadhi ghalani Njia hizi ni pamoja na: Kukausha juani mara kwa mara, kukinga kwa kupaka juisi ya ndizi au majivu, kutumia udongo wa mchwa, kuchanganya na pilipili au kuchanganya na majani ya Mkaratusi, majani au unga wa mwarubaini, changanya na unga na alizeti pori. 37

TIBA YA KEMIKALI Kemikali zinaweza kuwa na matokeo yanayotazamiwa zaidi kuliko njia za Asilia. Hata hivyo kemikali zina sumu, hivyo tahadhari kubwa ichukuliwe wakati zinapotumika. Muhimu Tumia dawa za kuua Wadudu baada ya Kuelimishwa juu ya Utumiaji wake. Tafadhali fuata Masharti kama ilivyo elekezwe kwenye mkebe wa dawa. Madawa ya kuua wadudu hupungua nguvu zake kadri zinavyokaa. Hivyo ikiwa dawa zimekuwa kabatini kwa muda mrefu kabla ya kununuliwa hazitakuwa na nguvu zinazohitajika kukinga. Kamwe usitumie kwa chakula mbegu ambazo zimewekewa Kemikali hata kama mbegu hizo zimekaa muda mrefu sana baada ya kuwekwa dawa. 38

Dawa (Kemikali) zilizopendekezwa kwa kukinga mbegu za Maharage ni pamoja na Actellic na Malathion. Katika kila uzito wa mbegu kilo 100, Gramu 200 za dawa ya kuua wadudu ichanganywe kwa wastani. Soma maeleyaliyoko kwenye kitini kilichoambatanishwa na dawa ili ufahamu vipimo sahihi. Ikibidi mwone bwanashamba. Ganda la kiberiti lililojaa kemikali linaujazo wa gramu 25. Kwa mfano kutibu kilo 100 za mbegu kwa ujazo wa Gramu 200 za kemikali, inakubidi upime maganda nane yaliyojaa kemikali. Kijaruba cha Kiberiti 39

Kuchanganya dawa kwa kutumia Sepeto Onyo! Tambua kwamba unapochanganya dawa za kemikali kwa kutumia sepeto au chombo, ni rahisi sana kwako kuvuta kemikali katika hewa jambo ambalo ni hatari kwa Afya yako. Kemikali ni sumu. Lazima unapozitumia uzitumie katika mahali penye hewa ya kutosha. Usivute sigara, wala usile chakula ama kunywa chochote mahali ambapo kazi hii inafanyika. 1. Mwaga mbegu yako mahali safi juu ya sakafu ama juu ya Karatasi ya Nailoni iliyohifadhiwa kwa ajili ya kazi hii tu. 40

2. Nyunyizia kiwango kilicho pendekezwa cha dawa ya kuua Wadudu. Sambaza kwa uwiano sahihi juu ya mbegu. 3. Kwa kutumia sepeto safi, au Jembe safi, Bakuli kubwa, ama debe la lita 20 lililokatwa, changanya taratibu rundo la mbegu hadi kila mbegu imepata kiasi cha kutosha cha dawa. Umalizapo, utaona hakuna mabakabaka ya dawa ambayo haikujichanganya vyema. 41

4. Hifadhi mbegu iliyowekwa dawa katika gunia na kuihifadhi mahali palipo safi, pakavu. 5. Osha mikono yako vizuri kwa maji unapomaliza kazi hii. Endapo utahifadhi mbegu yako zaidi ya miezi mitatu (3) itakubidi kuiwekea dawa tena. Tumia kiwango kile -kile cha kemikali ulichotumia awali na kufuata utaratibu uleule. Nawa mikono yako baada ya kuweka kemikali katika mbegu. 42

Kuweka dawa kwa kutumia pipa maalum Pipa la kuwekea dawa ni nyenzo rahisi ambayo ni pipa la chuma lililo himiliwa juu ya Kiunzi (fremu). Njia hii huruhusu kemikali kusambaa katika mbegu kwa uwiano mlinganifu na hivyo kuzuia athari ya kuvuta vumbi la kemikali wakati wa kukinga mbegu. Kutumia Pipa la kuchanganyia KutumiaPipalaKuchanganyiakemikali 1. Kabla ya kutumia pipa, hakikisha kwamba ni safi na liko katika hali nzuri, kamwe usitumie kitambaa chenye unyevu kwa sababu kinaweza kufanya pipa lishike kutu. Hakikisha kwamba umekaza bolt zote zilizolegea. 2. Mimina nusu ya mbegu ndani ya pipa. Kisha nyunyiza kiasi cha kemikali kinachotosha ndani ya hilo pipa. Kisha mimina ndani ya pipa nusu ya mbegu zilizokuwa zimebakia. 43

3. Ziba mdomo mdogo wa pipa kwa kukaza bolt kwa spana. Endapo nafasi wazi itabakia, funika mdomo kwa kuongezea kitambaa kabla ya kukaza bolti. 4. Zungusha pipa mara kumi na tano (15) ukiwa umesimama wima kandokando ya pipa. Subiri dakika tano zipite kabla ya kufungua mdomo wa pipa ili usidhurike kwa vumbi la kemikali Kumbuka kemikali ni sumu, hivyo usivute vumbi hilo. 5. Tandaza kipande kikubwa cha karatasi ya nailoni ama chombo kwenye mdomo wa pipa kisha fungua mlango na mimina mbegu iliyo na kemikali. Zungusha pipa ili kumwaga mbegu yote kutoka kwenye pipa. Ikiwa mbegu zimebakia ndani ya pipa tumia ufagio kuzitoa. Pipa la kuchanganyia mbegu lililo onyeshwa ukurasa wa 63 linao ujazo wa kilo 100 za mbegu. Utahitaji spana ili kufungua na kufunga mdomo mdogo wa pipa. Mchomeaji wa kawaida anaweza kukutengenezea pipa hilo kwa kufuatisha mchoro huo katika ukurasa 68. 44

KUHIFADHI Hifadhi vyema ili kuzuia kuharibika. Njia iliyo sahihi ni kuhakikisha kwamba unazitunza mbegu katika usafi na ziwe kavu. Mbegu ziwe kavu kabla ya kuwekwa kwenye magunia na kuhifadhiwa. Njia sahihi za kukausha hufanya mbegu zisiadhiriwe kwa urahisi na kuvu. Kiwango Cha unyevu kisizidi asilimia 13-15 %. Unapo fanya jaribio la kupima kiwango cha unyevu kwenye mbegu halafu chumvi ikanata kwenye chupa, basi, tambua ya kuwa kiwango cha unyevu ni kikubwa. Itabidi mbegu ikaushwe tena kabla ya kuhifadhiwa. Hakikisha kwamba chombo cha aina yoyote unachotumia kuhifadhia mbegu ni kisafi ambacho hakina viini vya wadudu. Osha vyombo kisha ondoa viini vya wadudu kwa kuvizamisha ndani ya maji ya moto yanayochemka kwa muda wa dakika tano. Loweka mifuko na vyombo ndani ya maji yanayo chemka kwamudawadakikatano. 45

Endapo utatumia mifuko ya nailoni kuua vijidudu, hakikisha kwamba haigusi kingo za sufuria au chungu isije ikaharibiwa na joto. Mifuko na vyombo vyote viwe vimekauka kabisa kabla ya kuhifadhia mbegu yoyote ndani yake. Kausha mifuko vizuri Ukiisha weka maharage katika mifuko au vyombo vingine, hifadhi mahali Safi na panapo ingiza hewa ya kutosha. Hakikisha kwamba ghala yako haivuji. Maji ya mvua yasiruhusiwe kuchuruzika katika kuta ndani ya ghala. Usiruhusu mvua kuvuja ndani ya ghala yako Ziba matundu yote ambapo wanyama waharibifu huweza kuingia 46

Funga mashimo yote na njia zote mahali ambapo Panya, wadudu, na maji yanaweza kuingia. Ziba nyufa zilizo ukutani, sakafuni na darini. Ili kuzuia panya katika eneo la kuhifadhi mbegu, weka mazingira hayo katika hali ya usafi.. Wanyama hawa hupendelea kula na kujificha katika mabaki ya vyakula na taka, hivyo basi ondoa mabaki ya vyakula na takataka toka katika maeneo yakuhifadhia mbegu. Ondoa uchafu na takataka zote. Fyeka majani kuzunguka eneo lenye ghala kwa vile Panya hawapendelei kuonekana mahali palipo wazi. Endapo ghala zako zimejengwa juu ya nguzo ni vyema kutengeneza vikinga panya ili usiruhusu panya kupanda ghalani. Vikinga panya 47

Unaweza kutengeneza vikinga Panya kutokana na kipande cha bati au kopo lililonyooshwa. Kunja na kutengeneza mfano wa pia lenye tundu katikati. Lizungushie Bati hilo katika nguzo na shikiza kwa misumari au waya. Vikinga panya Ua panya kwa kutumia mitego na sumu. Uwe mwangalifu unapotumia sumu. Kamwe usichanganye mbegu na sumu. Choma panya wote waliokufa. Zuia unyevu kwenye mbegu kwa kuweka mbao ama magogo chini ya mifuko ili mbegu zisigusane na sakafu wala ukuta. Magunia yenye mbegu yapangwe umbali wa meta moja kutoka ukutani. Mita 1 MBEGU YA MAHARAGE Mifuko juu ya magogo ama mbao. 48

Kamwe usihifadhi kwa kuchanganya mbegu mpya pamoja na mbegu za zamani, kwa sababu ikiwa mbegu za zamani zimeadhiriwa na wadudu na zilizo mpya zitaadhirika vile vile. Upangaji sahihi Upangaji mbaya Mbegu pia zinaweza kuhifadhiwa katika ghala la chuma ( Silo ). Silo zinaweza kutengenezwa za vipimo mbalimbali. Ukubwa ama udogo hutegemea kiwango cha uzalishaji mbegu. Mkulima akimimina mbegu zake ndani ya silo 49

Kwavile Silo hutengenezwa kwa kutumia chuma, mbegu huwa imekingwa dhidi ya athari za unyevu na wadudu. Mbegu zinaweza kumiminwa kwa urahisi ndani ya silo na nirahisi kuzitoa pia zinapohitajika. Fundi uchomaji vyuma wa kawaida anaweza kutengeneza silo ziwezazo kuwa na ujazo tofauti tofauti kwa kuigiza mchoro ulioko ukurasa 69 50

MUHTASARI Zipo hatua mbalimbali za kufuata ili kuzalisha mbegu bora. Mbegu bora 1. Ridhika na faida za mbegu bora: Ni bora kuliko mbegu ziuzwazo sokoni na madukani, kwa sababu zinaota kwa kiwango cha juu, zimekauka vyema, ni halisi, safi na hazina magonjwa na hazikuvunjika. 2. Hakikisha ubora wa zao lako la mbegu kwa kupanda mbegu safi. Mbegu zibadilishwe kila baada ya msimu 1 2 endapo mbegu zitaathiriwa na magonjwa yaliyofichika ndani ya mbegu. Pata mbegu toka mahali panapotegemewa. Panda mbegu safi tu Tunza zao lako vuzuri 3. Chagua ardhi yenye rutuba na tunza zao vizuri. Zao la mbegu hustawi vizuri katika udongo na ardhi iliyo tayarishwa mapema na udongo wenye kina kirefu. Tumia mbolea, vinyesi vya wanyama au mboji za mimea kama Mucuna na Canavalia hizi huongeza mavuno hivyo kuongeza faida zitokazo katika kuuza mbegu. Palilia zao mapema na kadri inavyohitajika ili kuboresha uvunaji. Maharagwe yaliyo kuwa wima vuna majani na vitumba vikiwa vimekauka. 51

4. Pandakatikamistari: Upandaji aina moja ya zao huzalisha mbegu zaidi na kupanda katika miraba hurahisisha palizi. 5. Zuia magonjwa na wadudu: Ondoa mimea yenye ugonjwa kutoka shambani na tumia kemikali kuzuia magonjwa na wadudu wanoaweza kuathiri zao lako la mbegu. 6. Kausha mbegu vizuri na pura bila kuvunja maharage: Ukaushapo zuia mbegu zisipatweunyevu na uchafu. Zuia uharibifu wa mbegu katika hatua zote. Zijaribu mbegu zako kuona kiwango cha unyevu na ubora wa kuota. 7. Tibu/kinga na kuhifadhi mbegu vizuri: Tibu mbegu kwa kemikali ili kuzikinga dhidi ya wadudu waharibifu shambani na katika kuhifadhi kisha weka katika ghala safi, mahali pakavu. Ukiishamudu hatua hizi unaweza kupanda zao lako la kwanza la mbegu za maharage. Kutokana na uzoefu utaboresha mbinu na ujuzi utaongezeka. Usisahau kusoma vitabu vingine viwili Kuzuia magonjwa na wadudu waharibifu wa maharage shambani na Establishing a bean seed business. 52

MANENO YATUMIWAYO NA WAZALISHA MBEGU NENO MAANA YAKE MAELEZO ZAIDI UKURASA MBEGU YA MAHARAGE MBEGU ILIYOTHIBITISHWA MBEGU BORA ZA MAHARAGE MBEGU BORA MBEGU ZA KIENYEJI ASILIMIA YA UOTAJI MBEGU (KIWANGO) Maharage yanayozalishwa hasa kwa ajili ya mbegu na sio kwa chakula. Mbegu iliyozalishwa kwa utaalam kwa kiwango kinachokidhi itoshelezayo mahitaji husika. Aina za mbegu zilizoboreshwa na watafiti. Aina hizi zinatoa mavuno na hustahimili magonjwa na athari za wadudu kuliko zile za wakulima. Mbegu iliyozalishwa kwa utaalam kutosheleza mahitaji yaliyochini ya viwango vya mbegu zilizothibitishwa. Mbegu za kienyeji zipandwazo na wakulima mahali kwa muda mrefu. Idadi ya mbegu zilizoota kuota kati ya mbegu mia moja zilizopandwa. 1-3 5 7 5,55 7 3,4,29-36 53

NENO MUCUNA NA CANAVALIA KUNG OA MIMEA (ROGUING ) MAANA YAKE Mimea ipandwayo katika shamba na kisha kuchanganywa ardhini ili kuboresha/kurutubisha udongo. Kung oa mimea isiyotakiwa kwa sababu ya magonjwa au nyinginezo ili kuacha aina ya mimea inayotakiwa. MAELEZO ZAIDI UKURASA 12 14 54

VIWANGO VYA KUPIMA MBEGU ZILIZOTHIBITISHWA NA KUBORESHWA NENO Kutenganisha (Mita) Mbegu safi MBEGU ZILIZOBORESHWA 2 90% MBEGU ZILIZOTHIBITISHWA 5 99% Uotaji - kiwango cha chini. Kiwango cha ugonjwa (baada ya uhakiki wa mwisho). Unyevu Usafi. Zilizo nje ya viwango (kiwango cha juu). 80% Donda majani, baka bakteria, chulebuni, dalili katika majani tu. Kirusi cha maharage: hakuna 13% Haina maana 10/10,000 80% Hakuna 13% 99% 10/10,000 55

JARIBIO LA KUPIMA UBORA WA MBEGU Ili kuona tofauti kati ya mbegu bora mbalimbali, fanya jaribio lifuatalo:- 1. Chukua sampuli nne tofauti zenye mbegu (50 100) za aina moja. (i) Mbegu zilizochaguliwa kwa mtindo wa kawaida wa uchaguaji. (ii) Mbegu ambazo huchagui kabisa. 56

(iii) Mbegu mbovu ulizoziacha wakati wa kuchambua. (iv) Mbegu safi : Mbegu ulizopata toka kwa watafiti, mradi wa mbegu au mbegu ulizozalisha kwa kutumia utaratibu na njia zilizoelezwa katika kitabu hiki. 2. Chagua eneo lenye rutuba mahali ambapo maharage hayajawahi kuota kwa msimu mmoja au zaidi. 57

3. Panda sampuli zote nne (4) za mbegu tofauti tofauti katika mistari ama matuta. Kwa mfano, mbegu zilizochaguliwa zipandwe mistari miwili ya mwanzo, zisizochaguliwa mistari miwili baada ya hiyo, Mbegu mbovu mistari miwili inayofuata na Mbegu Safi miwili ifuatayo. Usisahau kuweka alama kila mstari ukionyesha aina ya mbegu iliyopandwa. Hakikisha kupanda aina zote nne za mbegu siku hiyo hiyo na andika tarehe uliyopandia. 58

4. Chunguza mimea katika hatua tofauti za ukuaji (i) (ii) (iii) (iv) Siku3 5baadayakupanda chunguza uotaji. Majani yaanzapo kutoka. Wakati wa kutoa maua, na Kabla tu ya kuvuna. 5. Katika kusaidia kuangalia jibu maswali yafuatayo kwa kila aina ya mbegu. 1. Uotaji Safi Iliyochaguliwa Isiyochaguliwa Mbovu a) Mbegu hizi ziliota siku ngapi baada ya kupandwa? b) Ni mbegu ngapi ulizopanda? c) Ni ngapi zilizoota? 59

Safi Iliyochaguliwa Isiyochaguliwa Mbovu 2. Ukuaji: a. Majani yalitokea baada ya siku ngapi tangu kupanda? b. Maua yalitokea baadayasiku ngapi? Safi Iliyochaguliwa Isiyochaguliwa Mbovu 3. Ugonjwa: a) Je, kuna mimea yenye ugonjwa? b) Ikiwa ndio mingapi? c) Ugonjwa unaonekanaje? 60

4. Mavuno: Safi Iliyochaguliwa Isiyochaguliwa Mbovu a) Kiasi gani cha mavuno? b) Kiasi gani ni mavuno mazuri? 5. Linganisha uotaji, ukuaji na dalili za ugonjwa. Safi Iliyochaguliwa Isiyochaguliwa Mbovu Ni mbegu zipi zilifanya vizuri? 61

MASWALI YA KAWAIDA WAULIZAYO WAKULIMA SWALI: Ikiwa nitaendelea kupanda maharage katika eneo hilo hilo kwa misimu zaidi ya miwili nini kitatokea? JIBU: Mazao yako yatapungua, kuna uwezekano wa kupata magonjwa na mizizi kuweza kushambuliwa na minyoo. SWALI: Kwa nini siruhusiwi kuchanganya mazao yangu shambani? JIBU: Itabidi uamue kama biashara yako itaruhusu upunguze mavuno. Kumbuka kuzalisha mbegu kibiashara unalenga kuongeza mavuno zaidi na kipato. SWALI: Je, na mimi naweza kupanda maharage yanayotambaa? JIBU: Ndio, endapo unafikiri soko lake lipo katika eneo lako, fuata hatua zote zilizoelekezwa kitabuni. Vuna vitumba vya maharage kadri mmea unavyokua SWALI: Je, inanibidi kutumia vifaa vyote vilivyopendekezwa kitabuni? JIBU: Vifaa vilivyotajwa katika kijitabu hiki vimebuniwa kurahisha uzalishaji wa mbegu bora. Hivyo unashauriwa uvitumie kwa vile vinatengenezwa na mafundi kijijini. 62

SWALI: Kutokana na uzoefu wangu, kuchemsha mifuko ya nailoni husabanisha ipasuke baada ya muda mfupi. Nifanyeje? JIBU: Inawezekana ikawa kweli, hata bila ya kuichemsha kwa muda inapasuka. Kwa sababu ushauri ni kuchemsha mifuko ili kuua wadudu, itabidi ufanye uchaguzi bora kulingana na mazingira yako. SWALI: Je, inawezekana kukawa na unyevu katika silo? JIBU: Hapana, labda kama silo haikuinuliwa vyakutosha toka ardhini; ama mbegu iliyohifadhiwa sio kavu vya kutosha. SWALI: Kijitabu kinaelezea kamwe usile mbegu zilizowekwa dawa hata kama zimekaa kwa muda mrefu. Sipendi na sitaki kutupa mbegu. Nifanyeje? JIBU: Ni jambo muhimu sana kutokula mbegu zilizowekwa dawa ili kuzuia madhara. Badala yake unaweza kuuza mbegu yako kwa bei pungufu ili mbegu yako inunuliwe na kwisha haraka au ihifadhi ghalani hadi hapo utakapo iuzayote, weka tena dawa kila baada ya miezi mitatu (3). Endapo inakuchukua muda mrefu kuuza aina ya mbegu, hii ni dalili kwamba unahitajika kufanya utafiti wa soko lako au kupanga vyema. Mauzo ya pole pole ni dalili ya uhaba wa soko au wanunuzi kwa aina fulani ya mbegu au bei yako iko juu zaidi. Unaweza kushusha bei yako, au kiwango cha uzalishaji wako ama uache kabisa kupanda aina hiyo ya mbegu isiyo na soko. 63

SEHEMU YA MBEGU YA HARAGE Jani Mzizi kimelea Ghala Ganda 64

Sehemu ya kupuria sm50 sm100 sm90 sm100 Chekecheke MTAMBO WA KUPURIA MBEGU 65

MTAMBO WA KUCHAMBULIA SAMPULI YA MBEGU 66

BAMBO 67

Mdomo PIPA LA KUCHANGANYIA DAWA NA MBEGU 68

SILO 69

Kijitabu hiki cha Wazalishaji Wadogo Wadogo wa Mbegu ya Maharage kimeandaliwa na Shirika la Kimataifa la Kuendeleza Maharage (CIAT) Kwa maelezo zaidi kuhusu kijitabu hiki wasiliana na: Pan African Coordinator, CIAT P.O. Box 6247, Kampala-Uganda Kimechapishwa na Tel: (256-41) 341402, 348020 Fax: (256-41) 347870 e-mail: qcprint@africaonline.co.ug