UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery school teachers), kwa ngazi ya cheti na diploma. Chuo hiki kimeanzishwa hapa nchini, ili kukidhi hitaji la upatikanaji wa walezi wa watoto na waalimu bora wa elimu ya awali wenye viwango na ubora unaokubalika kitaifa na kimataifa. ANUANI NA MANDHARI YA CHUO Chuo kimejengwa katika eneo tulivu na salama lililopo katika kijiji cha Mapinga, jirani na Daraja linalotenganisha Mkoa wa Dar es salam na Wilaya ya Bagamoyo. Aidha, chuo kina mazingira yaliyoandaliwa maalumu ili kumwezesha mwalimu mtarajiwa kupata ujuzi unaoendana na aina ya ujuzi anaoupata chuoni na kazi atakayoifanya mara baada ya kuhitimu mafunzo yake. KUTAMBULIKA KWA CHUO CHA IMTC International Montessori Teachers College (IMTC), tunatambuliwa na kushirikiana na Serikali jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha tunaandaa walezi wa watoto na walimu wa elimu ya awali wenye elimu, ujuzi na viwango vya kitaifa na kimataifa katika stadi za malezi na ufundishaji wa watoto. Pia, tunao usajili wa kudumu wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (National Council for Technical Education). Naomba yetu ya usajili ni NACTE No. REG/TLF/012. Usajili huo unatuwezesha kutoa mafunzo ya ngazi ya cheti na diploma kwa walezi na walimu wa elimu ya awali kuanzia ngazi ya NTA Level 4 hadi NTA Level 6. Pia, chuo hiki kimesajiliwa na kinashirikiana na Wizara ya afya na Ustawi wa jamii kutoa mafunzo ngazi ya cheti, kwa kozi ya huduma ya malezi ya watoto.
Kusajiliwa, kutambulika na kushirikiana na taasisi za Serikali zinazosimamia elimu na malezi ya watoto kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, kunamhakikishia mhitimu katika IMTC mambo makuu matatu kama ifuatavyo:- (a) Ubora wa elimu inayotolewa, (b) Uhakika wa nafasi ya ajira mara baada ya kuhitimu katika shule za Serikali au katika shule zinazomilikiwa na watu binafsi ama taasisi na mashirika, (c) Fursa na uhuru wa kujiendeleza kwenye chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali kwa ajili ya masomo ya digrii, nk. MIFUMO YA UFUNDISHAJI Tunao wakufunzi wa ngazi na viwango vya kimataifa, wanaotumia mbinu na stadi zinazomwezesha kila mwanachuo kujitambua, kujiamini na kujipatia ujuzi wa malezi na ufundishaji wa watoto wadogo. Aidha, ufundishaji wetu unazingatia nadharia na vitendo kama ifuatavyo:- (a) Mafunzo ya nadharia ya Darasani Ufundishaji wa nadharia unaambatana na utumiaji wa mifumbo mbalimbali ya teknolojia kama vile powerpoint, video na oudio. Aidha, walimu wanatumia mbinu shirikishi na mijadala ili kuhakikisha kila mwanafunzi anafikiwa, anajifunza na kufikia malengo. (b) Mafunzo kwa vitendo ya namna ya kutumia vifaa kufundisha watoto Tunalo darasa maalumu lenye vifaa mbalimbali, tunalolitumia kufundisha kwa vitendo. Lengo likiwa ni kumwezesha kila mwanafunzi kujua namna ya kutumia vifaa mbalimbali kulea na kufundisha watoto. Aidha, uwepo wa darasa hilo unatoa uhuru kwa mwanachuo kutumia muda wake wa ziada kufanya mazoezi kwa vitendo kadri anavyoweza ili kuhakikisha anatimiza malengo yake ya kujizoeza, kupata ujuzi na kufaulu vizuri majaribio ya kitaaluma. (c) Mafunzo kwa vitendo ya namna ya kutengeneza vifaa vya kufundishia watoto Chuo kinaendesha mafunzo kwa vitendo kwa kuwafundisha wanafunzi jinsi ya kutengeneza seti za vifaa mbalimbali vya
kufundishia watoto. Vifaa hivyo ambavyo vina thamani ya zaidi ya milioni tano, mwanachuo uondoka navyo mara baada ya kuhitimu mafunzo ili aweze kujiajiri au kuvitumia mara anapokuwa ameajiriwa. Vifaa hivyo vyenye thamani ya zaidi ya milioni tano vimegawanyika katika makundi yafuatayo:- (i) (ii) (iii) (iv) (v) (vi) (vii) (viii) Vifaa vya kumjenga mtoto ili aweze kujitegemea katika maisha yake Vifaa vya kutafiti na kuchochea ukuaji wa milango ya fahamu ya mtoto Vifaa vya kumfundisha mtoto stazi za lugha na mawasilino Vifaa vya kumfundisha mtoto stadi za Hisabati Vifaa vya kumfundisha mtoto stadi za jiografia Vifaa vya kumfundisha mtoto stadi kuhusu mazingira Vifaa vya kumfundisha mtoto stadi za sayansi Vifaa vya kumfundisha mtoto asili na utamaduni (d) Mazoezi kwa vitendo shuleni Chuo kinamiliki na kuendesha shule ya awali ambayo uwawezesha wanachuo kujifunza kwa vitendo tabia, mienendo na malezi ya watoto. Pia, kwa kushirikiana na shule za awali washirika, chuo uwapangia wanachuo kufanya mafunzo ya mazoezi kwa vitendo chini ya uangalizi maalumu. Mazoezi hayo uwawezesha wanachuo kuimarisha ujuzi wao kwa vitendo kuhusu malezi ya watoto, mfumo wa ufundishaji wa watoto wadogo, utaratibu wa uendeshaji wa vituo vya kulea watoto na shule za awali, n.k. Utaratibu huu wa mazoezi kwa vitendo kwa wanachuo, pia ufungua milango ya uhakika wa fursa za ajira mara baada ya kuhitimu. Kwa
sababu waajiri na wamiliki wa shule upata fursa za kujua uwezo wa waajiriwa watarajiwa kabla ya kuingia katika soko la ajira. Pia, sifa na uwezo wa kila mwanachuo wa kumudu majukumu yake utambulika na kujulikana. UTARATIBU WA KUJIUNGA IMTC Mtu yeyote anayetaka kujiunga na International Montessori Teachers College (IMTC), anatakiwa kufika chuoni ili aweze:- (a) Kupata maelezo, kujionea na kujiridhisha (b) Kuchukua fomu ya maombi, kuijaza na kuirejesha kwa wakati (fomu inapatikana chuoni tu) (c) Kufanya mahojiano na majaribio ya kupima uwezo wa uelewa na mapenzi kwa watoto (d) Kukamilisha taratibu za kiutawala VIGEZO MUHIMU VINAVYOHITAJIKA Vigezo muhimu vinavyozingatiwa ili uchaguliwe kujiunga na International Montessori Teachers College (IMTC), ni:- (a) Kuwa mhitimu wa elimu ya sekondari, kidato cha nne au zaidi, (b) Mtu yeyote mwenye elimu ngazi ya cheti au zaidi (cheti kilichotolewa na taasisi au chuo kinachomilikiwa na Serikali au chuo kilichosajiliwa na kutambuliwa na Serikali), (c) Au mwenye cheti cha kuhitimu mafunzo ya malezi ya watoto kinachotolewa na Idara ya Ustawi wa Jamii, (d) Mwenye wito wa kulea na kufundisha watoto, (e) Kwa wanafunzi wa kigeni:-
Chuo chetu ni cha viwango vya kimataifa, hivyo kinatoa fursa kwa raia wa kigeni kujiunga na kozi zinazotolewa. Utaratibu wa kujiunga kwa raia wa kigeni umefafanuliwa katika kurasa za website yetu. Hata hivyo, ni muhimu pia kufahamu kwamba mhitimu katika chuo chetu anakuwa na misingi ya viwango, vigezo na uwezo wa kufanya kazi katika nyanja aliyoisomea popote duniani. KOZI ZITOLEWAZO Chuo kinatoa kozi za ualimu wa watoto wadogo kama ifuatavyo: 1. Diploma ya ualimu na malezi ya watoto Kozi hii ni ya muda wa miaka miwili (2), na ina masomo yafuatayo:- Child Development Teaching Methodology School Management Safety And First Aid Communication skills Education philosophy General knowledge Nutrition Mathematics Arts and raft Language- English and Kiswahili Leadership Health Civics Moja ya faida za kusoma kozi hii ni kuwezeshwa kuwa na ujuzi kamili wa kutengeneza vifaa vya kulea na kufundishia watoto. Pia mwanachuo akihitimu umilikishwa na kuruhusiwa kuondoka na vifaa vyote alivyovitengeneza wakati wa mafunzo. 2. Cheti cha ualimu na malezi ya watoto Kozi hii ni ya muda wa mwaka mmoja (1), na ina masomo yafuatayo:- Child Development
Safety And First Aid Communication skills Education philosophy Montessori philosophy General knowledge Health & Nutrition Arts and raft Language- English and Kiswahili Civics Kozi hii haiambatani na utengenezaji wa vifaa vya kulea na kufundisha watoto. MFUMO WA KUPIMA UWEZO NA UELEWA - MITIHANI Mitihani ya kupima uelewa na ujuzi ni asilimia 100%. Asilimia hizi hupatikana kwa njia mbili, nazo ni jumla ya mazoezi na majaribio yote ya nadharia na vitendo ni 80% na mtihani wa mwisho wa mwaka ukamilisha alama 20% ili kutimia 100% UJUZI MWINGINE UNAOTOLEWA CHUONI Mafunzo ya ICT Chuo kinatoa mafunzo ya matumizi ya kompyuta bure kwa kila mwanachuo. Mafunzo haya yanalenga kumpa ujuzi wa ziada na kumwandaa mwanachuo kutumia ICT katika mfumo wa ufundishaji na kujifunza. Aidha, utaratibu huu unamwezesha mwanachuo kuwa ni mlezi na mwalimu anayekwenda kwa wakati kwa kuzingatia mifumo ya kisasa ya elimu, habari na mawasiliano. Pia, mfumo huu unatoa fursa kwa kila mwanachuo kutumia rasilimali hizo kutafuta taarifa mbalimbali zinazohusiana na masomo yake. Ujasiliamali na stadi za maisha Kwa kuzingatia mahitaji ya ajira na kujiajiri, chuo kinaendesha mafunzo maalumu yanayomjengea uwezo mwanachuo ili aweze kujiajiri mara baada ya kuhitimu. Utaratibu huu maalumu unamwezesha mwanachuo kujitambua,
kujiamini na kutumia fursa za ujuzi anaopewa ili kuwa chachu ya mabadiliko katika mfumo wa maisha yenye changamoto ya kukosekana kwa ajira. Aidha, mfumo wetu wa ufundishaji ni wa aina ya pekee na unazingatia mbinu ya elimu ya kujitegemea. Pia unamjenga na kumwezesha mwanachuo kuwa na ujuzi wa kutengeneza vifaa vya kufundishia ambavyo ni nyezo na mtaji wa kuweza kumudu kuanzisha kituo kwa ajili ya kutoa elimu ya awali kwa watoto. Vile vile mwanachuo anapewa mafunzo maalumu yanayomwezesha kutoa huduma ya ushauri nasaha kwa watoto na wazazi kuhusu ustawi na maendeleo ya watoto. Mafunzo ya upigaji picha kwa njia ya video Kila mwachuo anafundishwa ujuzi wa kutumia vifaa vya kisasa ili kuchukua na kuhifadhi kumbukumbu za watoto kwa njia ya picha, video na sauti. Utaratibu huu unazingatia ukweli kwamba, kila aliyefanikiwa hapa duniani amepitia katika mikono ya walezi na walimu walipo katika shule hasa za awali, ingawa kumbukumbu za walio wengi hazikuwekwa au kuhifadhiwa. Hivyo ili kukidhi hitaji hilo la kuweka kumbukumbu za watoto, chuo kimejenga studio za kisasa zenye vifaa vinavyotambulika kwa ubora ulimwenguni kwa lengo la kufanikisha utoaji wa ujuzi huo na kumwandaa mwanachuo kuweza kuchukua na kuhifadhi kumbukumbu za matukio muhimu ya watoto wanaopita mikononi mwake katika mchakato mzima wa malezi. Matuki hayo ni kama vile kumbukumbu za siku za kuzaliwa za watoto wa shule yake, kumbukumbu za mahafali, n.k Sanaa na ubunifu Moja ya misingi na aiba ya mlezi na mwalimu wa watoto wadogo, ni kuwa na vipaji vya ubunifu na sanaa. Ubunifu katika ufundishaji wa watoto unaoambatana na michezo na sanaa mbalimbali, urahisisha mfumo wa uamishaji wa maarifa na ujuzi kutoka kwa mwalimu kwenda kwa watoto. Hivyo, mkakati wa IMTC ni pamoja na kumwandaa mwanachuo kutumia michezo, sanaa na ubunifu katika kulea na kuwafundisha watoto. Lakini pia
unamjengea mwalimu na mlezi mtarajiwa uwezo wa stadi za kutambua vipaji vya watoto na mbinu za kuviendeleza. Huduma ya kwanza na usalama wa watoto Moja ya mafunzo yanatolewa katika mtaala wa masomo ni suala la ulinzi wa watoto, huduma ya kwanza na uokoaji. Mafunzo hayo humjengea mwanachuo stadi za tahadhari. Lakini pia umjengea uwezo wa kiufahamu wa hatua za kuchukua katika kukabiliana na ajali au majanga mbalimbali. ADA International Montessori Teachers College (IMTC), kwa kutambua mahitaji ya jamii kulingana na kipato cha Watanzania walio wengi, tumeweka utaratibu wa ulipaji wa ada unaozingatia uwezo wa kila mwanafunzi. Hivyo, ulipaji wa ada kidogo kidogo unajadiliwa na kuruhusiwa. HUDUMA NYINGINE MUHIMU ZINAZOTOLEWA NA CHUO Chuo kinamiliki hosteli nzuri yenye hadhi iliyojengwa katika mazingira ya chuo na huduma hii hutolewa bure kwa kila mwanachuo. Aidha, mazingira ya vyumba vya kulala ni mazuri na yenye vitanda na magodoro na huduma nyingine muhimu kama vile:- Maji safi na salama Umeme wa uhakika Ulinzi Viwanja vya michezo Chakula, nk.