Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana (SDSMV) Tanzania. Kiongozi Cha Mwezeshaji. Jaap Van Pol na Francesca Dalla Valle

Similar documents
Information for assessors (do not distribute this page to participants):

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

KILIMO CHA VITUNGUU MAJI NA VITUNGUU TWAUMU (SWAUMU)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees

TIST HABARI MOTO MOTO

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

2 Usimamizi wa Rutuba ya Udongo Tanzania Organic Agriculture Movement

Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO. Training and Research Support Centre

4 WADUDU,MAGONJWA NA MAGUGU

Uhakika wa Mbegu kwa Uhakika wa Chakula MWONGOZO WA UZALISHAJI WA MBEGU ZA ASILI ZA MAHINDI

Mwongozo wa Mwezeshaji

Bustani 10,000 Katika Afrika. Alberto Prina

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

TIST HABARI MOTO MOTO. Benefits of Loan Repayment. Faida za ulipaji wa mikopo U OTESHAJI W A M ITI Y A M ATUNDA

KUZALISHA MBEGU YA MAHARAGE KIJITABU CHA KWANZA

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza

pages/mkulima-mbunifu/

Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo. Zanzibar, 7-10 Februari 2006

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

Ni kwa nini mkulima awe maskini?

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu

Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo

Muhtasari wa taarifa ya warsha ya wataalamu juu ya mfumo wa habari kwa njia ya ramani (PGIS), Morogoro, Juni 30 - Julai 1, 2014

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

TIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO

Uwepo, Athari na Udhibiti wa Sumu-Suvu Kwenye Vyakula vya

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo

Vyote Unavyopaswa Kujua Kuhusu Viazi Vitamu

Ufundishaji wa lugha nyingine

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira

Uzio wa pilipili unazuia tembo kuvamia mazao shambani! Jinsi ya kujenga na kudumisha uzio wa pilipili Tanzania

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Vyote Unavyopaswa Kujua Kuhusu Viazi Vitamu

Wadudu na magonjwa ya mazao

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

Lishe na Ulaji Bora kwa Watu Wanaoishi na Virusi vya UKIMWI

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

Muongozo wa utatuzi. Kwa wasimamizi wa malaria RDTs 06/11/16. MALARIA Rapid Diagnostic Test

Early Grade Reading Assessment for Kenya

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA

Uzalishaji wa mboga na matunda ni muhimu kwa afya na kipato

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Human Rights Are Universal And Yet...

Vyote Unavyopaswa Kujua Kuhusu Viazi Vitamu

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Kilimo cha kiekolojia cha Wakulima Wadogo Hufanikisha Haki za Mazingira

Makala ya Mshiriki wa Mafunzo

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Mfumo na maelezo ya kina ya mpango wa kimataifa wa viwango vya chakula kwa wenye matatizo ya kumeza (IDDSI) Juni 2017

Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health

MTI KWA MATUMIZI YA KILA AINA HDRA

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03

Namba ya moduli 3 Kuangalia sanaa

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

International Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo

MBINU ZA IPM KWENYE KILIMO CHA KAHAWA

KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

Utunzaji, Uhifadhi na Usafirishaji Bora wa Maziwa

Siku ya kwanza. Mguso wa ngozi-kwa-ngozi (Ulezi wa kangaruu) Mtoto wako anaweza kuhisi mdundo wa moyo wako

MAFUNZO YA AFYA YA UZAZI: Nyongeza ya Mtalaa Kwa vijana

Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E)

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Njia Bora za Ukusanyaji na Upimaji Maziwa

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

CGAP Smallholder Household Survey in Tanzania / Utafiti wa kaya ndogondogo Tanzania

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

UMRI WA MAKAMO NA KUKOMA KWA HEDHI

Kijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia

UFUPISHO WA 35. Hali ya kiulimwengu ya Tekinolojia ya kibiashara/ugeuzi jeni na uboreshaji mazao: Clive James Chair, ISAAA Board of Directors

Njia za upimaji wa mpango wa kimataifa wa viwango vya chakula kwa wenye matatizo ya kumeza (IDDSI) VYAKULA VINYWAJI VYA KAWAIDA

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue?

KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS

Transcription:

Programu kuhusu msaada wa sera kwa ajira vijijini na kazi yenye heshima kwa uhimizaji maisha sawa endelevu vijijini kulingana na mabadiliko ya tabia nchi Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana (SDSMV) Tanzania Kiongozi Cha Mwezeshaji Jaap Van Pol na Francesca Dalla Valle Kwa kushireikiana na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania (TFC) na Muungano wa Vyama vya Ushirika Zanzibar (CUZA). 1 Kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika na Wizara ya Kazi

Juzuu ya 1 Mtaala wa Mada za Kilimo za SDSMV 2

Yaliyomo Mada/zoezi Utangulizi wa ufundishaji 0.1. Zoezi: Kutambulishana na SDSMV Ukurasa 1 3 Mada za Kilimo A.1.1. Zoezi: Kujua shamba la kujifunzia na kufanya majaribio A.1.2. Zoezi: Sifa za shamba la Kilimo A.1.3. Zoezi: Jaribio la Utepe A.1.4. Zoezi: Kupanga shughuli zako za Kilimo A.1.5. Zoezi: Hatua za maisha ya mazao A.1.6. Zoezi: Kuandaa kalenda za mazao A.2.1. Zoezi: Kuchagua mbegu bora A.3.1. Zoezi: Jaribio la utoaji wa mbegu A.4.1. Zoezi: Kuandaa mpangilio wa shamba darasa A.4.2. Zoezi: Maandalizi ya Ardhi A.4.3. Zoezi: Kwa nini tunahitaji vitalu A.4.4. Zoezi: Kuandaa Kitalu A.5.1. Zoezi: Kuacha nafasi baina ya mimea A.6.2. Zoezi: Kuelewa mifumi ikolijoa ya shmamba A.6.1. Zoezi: Kuotesha mazao yanayostawi kwa IPM A.6.3. Zoezi: Desturi mbalimbali za kudhibiti visumbufu vya mimea A.6.4. Zoezi: Kanuni za Kiasili za Kudhibiti visumbufu vy mimea A.6.5. Zoezi: Kulinda mazao dhidi ya wadudu shambani shambani na taratibu za Udhibiti Husishi wa Visumbufu vya Mimea (IPM) 5 6 7 8 9 10 12 12 13 14 14 15 16 18 18 19 20 20 A.6.6. Zoezi: Kupata maarifa zaidi kuhusu wadudu na visumbufu vya mimea 3

vilivyochunguzwa katika shamba darasa A.6.7. Zoezi: Utayarishaji wa dawa kutoka mti wa mwarubaini kwa kudhibiti visumbufu A.6.8. Zoezi: Kuepuka madhara ya dawa na Kemikali za Kilimo A.7.1. Zoezi: Kutambulisha AESA. A.7.2. Zoezi: Ufuatiliaji wa mara kwa mara kwa Kutumia AESA. A.8.1. Zoezi: Palizi, Kwa nini, lini na namna ya kupalilia A.9.1. Zoezi: Upandikizaji wa miche (mboga za majani) A.10.1. Zoezi: Kuzitambua njia mbalimbali za umwagiliaji na unyevu kwenye udongo A.11.1. Zoezi: Urutubishaji wa Udongo A.11.2. Zoezi: Urutubishaji wa pili A.11.3. Zoezi: Udhibiti wa Rutuba ya Ardhi katika Kilimo Kisichotumia Mbolea za Kemikali A.11.4. Zoezi: Rundo la mboji ni nini na tunaweza kutumia vitu gani A.11.5. Zoezi: Kutayarisha Mboji A.11.6. Zoezi: Kuchagua, kugeuza na kutumia mboji A.12.1. Zoezi: Kulinda Shamba letu A.12.2. Zoezi: Kujenga uzio A.13.1. Zoezi: Wakati na namna ya Kuvuna A.14.1. Zoezi: Namna ya Kupunguza Hasara ya Mazao baada ya kuvuna A.14.2. Zoezi: Usindikaji/Uhifadhi wa vyakula A.14.3. Zoezi: Ghala/Stoo bora A.14.4. Zoezi: Kuuza bidhaa/mazao yetu Kiambatisho: Mtaala wa Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana (SDSMV) 21 21 22 23 25 27 27 29 30 31 31 32 32 34 35 35 36 36 37 38 39 41 4

Utangulizi wa Ufundishaji SDSMV Ufundishaji wa SDSMV Mwezeshaji anajaribu kutumia kwa ukamilifu kujifunza kwa (vijana) watu wazima kwa njia ya ugunduzi. Vijana watajifunza kadiri iwezekanavyo kwa vitendo, kufanya mazoezi ya kanuni zote za kilimo kwenye mashamba darasa yao, kugundua njia mbalimbali kwa kufanya majaribio, kuiga hali za maisha kwa njia ya igizo kifani au mchezo wa kuigiza, majadiliano katika vikundi vidogo vidogo na michezo na mbinu za kikundi. Kiwango chakukumbuka ni kama ifuatavyo 20% wakati wanaposikia 40% wakati wanapoona 80% wakati wanapogundua Uzoefu unaonyesha kuwa Unaposikia,unasahau Unapoona, unakumbuka Unapogundua unamiliki maishani Maana ya mwezeshaji Mtu anayeongoza na kuelekeza mchakato. Mtu anayehakikisha mtiririko unaofaa wa taarifa ndani ya kikundi ili washiriki washirikiane taarifa na kufikia uamuzi Kiongozi/msimamizi wa mchakato wa kujifunza kwa mbinu shirikishi. Anayesaidia katika kushirikiana taarifa kwa njia shirikishi 5

Jedwali: Tofauti kati ya kuwezesha na kufundisha Kuwezesha Kufundisha 1. Kunahusisha majadiliano Majadiliano kidogo 2. Ushiriki kwa ukamilifu Ushiriki mdogo 3. Kunahimiza mawazo yaliyopo na mapya Hutambulisha mawazo mapya tu 4. Mawasiliano miongoni mwa washiriki Mawasiliano kutoka kwa mwalimu 5. Kujifunza kusiko rasmi Kujifunza rasmi 6. Utoaji uamuzi wa pamoja Utoaji uamuzi kiasi 7. Kushirikiana mawazo Kuelekeza 8. Kuanzia chini kwenda juu Huanzia juu kwenda chini 9. Mtaala umetayarishwa kutokana na tathmini Mtaala umetayarishwa na wizara ya mahitaji 10. Vifaa vya kujifunza vinatokanana mshiriki Vifaa vya kujifunzia vinatokana na mwalimu K azi na Wajibu wa Mwezeshaji wa SDSMV Msaada mkubwa wa kiufundi Huongoza katika mchakato wa kujifunza Huwa kiungo cha mawasilianona watendaji wa nje na wataalamu Husaidia kikundi kufikia malengo yao Husaidia udhibiti wa migogoro Husaidia kuanzishwa kwa SDSMV mpya. Huelezamalengo na mchakato wa SDSMV Lazima asaidie uchaguzi na uchanganuzi Hufanya majadiliano yawe ya kusisimua Hudadisi ili kuwasaidia washiriki kufikia mahitimisho yanayofaa Husaidia kutanzua matukio ya kukandamiza mawazo na hisia za washiriki wengine. Husaidia washiriki kufikia mwafaka unaofaa Usimamizi wa muda Huwaheshimu washiriki wote na mawazo yao Huwasaidia washiriki kubainisha fursa na na uwezekano kwenye mazingira yao. Somo la SDSMV (saa 3 4). 1. Kuanza /kufungua (± dakika 5) 2. Muhtasari wa somo lililopita (± dakika 5) 3. Programu ya leo (± dakika 5) 6

4. Uchunguzi wa mfumo wa kilimo na Ikolojia (AESA) au mada ya maisha (± saa 1-2) 5. Mapumziko (± dakika 5) 6. Vichangamsho au group dynamics (± dakika 10) 7. Mada mahususi (kilimo au mada ya maisha ) (± dakika 50) 8. Muhtasari (± dakika 5) 9. Tathmini (± dakika 5) 10. Kufunga (± dakika 5) Mazoezi ya SDSMV Mazoezimbalimbali ya SDSMV yaliyochaguliwa yamekusanywa na kuwasilishwa kwenye kiongozi hiki kutokana na moduli za mwezeshaji wa SDSMV zilizotayarishwa na kuchapishwa na (ambazo hazijachapishwa) FAO. Mazoezi haya yamechaguliwa kutokana na mitaala ya SDSMV iliyotayarishwa wakati wa mafunzo ya wawezeshaji wa SDSMV yaliyofanyika Kibaha Conference Centre, Tanzania, mwezi Juni, 2011, angalia kiambatisho kwa ajili ya nakala za Mitaala ya SDSMV, mazoezi yamepangwa kulingana na mazoezi yanayohusu kilimo (Juzuu ya 1) na; mazoezi ya stadi za kazi na kutengeneza ajira (Juzuu ya 2) 7

Mada ndogo: Utangulizi wa SDSMV 0.1. Zoezi: Kutambulishana na SDSMV Muda: Karibu saa 2 Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea 1. Wakaribishe vijana wote na washiriki wengine waliohudhuria kwenye somo lakwanza la SDSMV 2. Jitambulishe pamoja na wawezeshaji wengine. Mwambie kila kijana ajitambulishe kwa kikundi (jina, umri, mahali wanakotoka) 3. Wagawe vijana katika vikundi vidogo vya watu watano au sita. Waambie vijana wajadili kile wanachotarajia kujifunza na kufanya wakati wa SDSMV na waandike matarajio yao kwenye karatasi kubwa. jadili kwa muhtasari matarajio waliyoorodhesha 4. Wasilisha mchezo wa vidoti tisa na waambie vikundi kama wanaweza kuunganisha vidoti vyote tisa kwa kutumia mistari minne iliyonyooka bila ya kuondoakalamu. Vipatie vikundi dakika 10 kufanya hivyo 5. Viulize vikundi vimefanya nini kutatua tatizo hili. Kamakikundi kimeweza kutatua tatizo, waambie waeleze ufumbuzi. Kama hakuna aliyepata ufumbuzi, kwanza jadili kwanini hakuna aliyepata jibu na halafu onyesha namna ya kufanya. 6. Waeleze vijana kuwa SDSMV itawasiaidia kwenda zaidi ya njia za kujifunza na kutafuta ufumbuzi zinazotumika. 7. Tambulisha moduli mbalimbali za mtaala wa SDSMV na eleza aina tofauti za shughuli wanazotarajiwa vijana wafanye wakati wa masomo ya SDSMV kwa mfano, shughuli kwenye shamba darasa, kujifunza kwa vitendo na majaribio, majadiliano na shughuli za vikundi vidogo, mchezo wa kuigiza na igizo dhima. 8

8. Waulize vijana ni aina gani ya sheria na kanuni ambazo SDSMV wafuate kujenga mazingira yenye mafanikio kwa vijana kufanya kazi na kujifunza pamoja. Orodhesha kwenye karatasi kubwa sheria na kanuni zote walizotaja - kwa mfano, kuwahi, kushiriki kwaukamilifu, kuheshimu mawazo ya kila mmoja, kumsikiliza kila mmoja, kuzungumza mmoja mmoja kwa zamu, kutopigana, 9. Ongeza kanuni na sheria zilizokosekana kwenye orodha. 10. Waulize vijana kama wako tayari kushiriki kwa ukamilifu katika masomo yote ya SDSMV, wako tayari kufanya kazi katika vikundi vidogo, kujifunza kwa vitendo na kuheshimu orodha ya sheria na kanuni za SDSMV zilizotayarishwa. 11. Toa muhtasari wa majadiliano. Maelezo kwa wawezeshaji Je, unatoka wapi? Je, umekuwa unaishi katika eneo hili kila mara? Je, unamfahamu kijana mwingine? Je, una jamaana ndugu katika kikundi cha vijana wanaoshiriki? Je, unasoma shule? Wakati wa SDSMV unataka kujifunza nini? Je, unapenda kujifunza zaidi kuhusu kilimo? Je, ungetaka kujifunza zaidi kuhusu aina gani za mazao au wanyama? Je, unataka kujifunza zaidi kuhusu afya, lishe au kuhusu uanzishaji wa biashara ndogondogo? Je, unapenda kujifunza kwa vitendo? Je, umezoea kufanya kazi katika vikundi? Je,kufanya kazi na kujifunza katika vikundi kuna maanagani? Je,unadhani nini muhimu wakati unapotakiwa kufanya kazi katika kikundi? Je, kuna majukumu ya aina gani unayotakiwakuyatimiza ili uweze kufanyakazi katika kikundi kwa mafanikio na ipasavyo? Je, ni kanuni na taratibu gani zinazotakiwa kuheshimiwa wakati wa kufanya kazi katika kikundi? 9

Mada za Kilimo 1. Mada ndogo: Kupanga katika kilimo Malengo: Kuelewa namna ya kuchagua mazaobora zaidi ya kupanda. Kuelewa namna ya kuanza kupanga shughuli za kilimo Wakati vijana wanapopanga shamba lao, ni lazima wafikirie kuhusu mambo mbalimbali kwa wakati mmoja. Je, wanataka kuzalisha nini, aina ya ardhi na udongo waliyonayo, aina ya mbegu na zana zilizopo kwa ajili yao, watakuwa namuda kiasi gani (na lini ) wa kuhudumia shamba lao, ni watu wengine gani watakaowasaidia shambani, n.k. A. 1.1. Zoezi. Kujua shamba la kujifunza na kufanya majaribio. Mada: Karibu saa 2 Vifaa: karatasi kubwa na kalamu za kuchorea Mahali muhimu katika mafunzoya SDSMV ni eneo la uwandani la kujifunza. Kwa kuwa kanuni muhimu ya SDSMV ni kujifunza kwa kufanya majaribio, mahali pa kujifunza ni pale ambapo washiriki watajifunza taratibu na stadi za usimamizi wa kilimo. Washiriki watagundua wenyewe njia bora zaidi ya kulima aina fulani ya mazao na kupambana na matatizoya mmomonyoko wa udongo au masuala mengine ya kilimo. Katika zoezi hili, vijana watatambulishwa malengo na shughuli za aina mbalimbali watakazofanya katika shamba darasa. 1. Anzisha mada ya shamba darasa. Waulize vijana kwanini SDSMV ina eneo la uwandani la kujifunzia na wanafikiri watafanya nini katika eneo la uwandani la kujifunzia wakati wavipindi vya SDSMV 2. Eleza kuwa shamba darasa litatumika kujifunza kuhusu taratibu bora na stadi za usimamizi wa kilimo kwa kufanya mazoezi kwa vitendo. Hakikisha kuwa wanaelewa uzalishaji wa kilimo si lengo kuu. 3. Waulize vijana kama wanaruhusiwa kufanya makosa katika shamba darasa yanayoweza kuathiri uzalishaji. Waeleze kuwa wanaruhusiwa kufanya makosa wakati wa kujifunza kwa kuwa kujifunza kunatokana na makosa na kuyaelewa ni njia bora ya kuwaongezea maarifa alimradi makosa hayo hayafanywi makusudi. 4. Nenda na vijana kwenye shamba darasa. Waulize wanapenda kupanda mazao gani na kwanini. 10

5. Eleza kuwa kwanza wanahitaji kuandaa mpango kuonyesha wanaopenda kupanda nini, wapi, lakini kwanamna gani katika shamba darasa na kuwa mpango ujumuishe majaribio madogo na mbinu mbalimbali zakilimo 6. Waulize washiriki kwa nini wanatakiwa kuingiza majaribio katika mpango 7. Eleza kuwa kuna njia nyingi za kulima mazao kulingana na hali ya shamba na ujuzi wa mkulima, kila mkulima anatakiwa kufuata njia bora zaidi ya kulima kulingana na hali yake. Njia bora zaidi kutekeleza hili ni kwakujaribu njia mbalimbali za katika maeneo madogo ya ardhi 8. Eleza kuwa katika wiki zijazo wataanza kupanga shughuli mbalimbali watakazotaka kufanya katika shamba darasa kwa kufanya mazoezi kadhaa. A.1.2. Zoezi : Sifa za shamba la Kilimo Muda: Karibu dakika 20 Vifaa : Shamba darasa, karatasi kubwa na kalamu za kuchorea Anzisha mada ya uchunguzi wa hali ya shambani. Waulize vijana kwanini wanafikiri ni muhimu kuchunguza hali ya shamba kabla ya kupanga mazao watakayopanda Waambie vijana wataje sifa zote muhimu za shamba la kilimo, ambazo mkulima anatakiwa kuzijua anapoanza kulima. Orodhesha sifa zote zilizotajwa kwenye karatasi kubwa. Iwapo unafikiri kuwa kuna kitu walichokisahau, kitaje na kujadili na vijana Sifa muhimu za shamba lakilimo Aina ya udongo (umbile: mwepesi mzito, muundo: ulioshikamana - kichanga, mbolea: nyingi kidogo) Kina chaudongo (kina kirefu cha kutosha kuwezesha ukuaji wa mizizi) Mteremko wa ardhi (hatari ya mmomonyoko, maji hutiririka, haufai kulima kwa kutumia mashine) Hali ya mtiririko wa maji (mabonde shambani, sehemu iliyo chini zaidi shambani) Kuwapo kwa vyanzo vya maji (kama kuna haja ya kumwagilia) 11

Mimea (je, kunamimea mingi? je, kunamajani?) Historia (kujua kilicholimwa katika shamba hilo siku za nyuma kunatoa habari kuhusu hali ya shamba) Mambo gani yanayofanyika katika mashamba jirani (nyasi, wadudunamagonjwa,mara nyingi huingia kutoka katika mashamba jirani) Toa muhtasari wa orodha ya sifa muhimu kwa ajili ya shamba darasa na waombe vijana wanakili orodha kwenye daftari zao. A.1.3. Kuchunguza Hali ya Udongo Majaribio rahisi yanayoweza kufanywa pamoja na vijana yametayarishwa kwa ajili ya kutambua umbile la udongo, muundo nahali ya aina mbalimbali ya udongo Muda: Saa 1 dakika 30 Vifaa na matayarisho: karatasi kubwa na kalamu za kuchorea 1. Anzisha mada ya kuchunguza hali ya udongo (umbile, muundo na aina za udongo na sifa zake) 2. Nenda na vijana kwenye shamba darasa halafu waulizevijanahao maana yaumbile namuundo wa udongo. Eleza maana ya rangi ya udongo, muundo wa udongona umbile la udongo 3. Chukua sampuli za udongo kutoka kwenye shamba darasa halafu waambie vijana waeleze rangi ya udongo na tunavyoweza kutambua umbile la sampuli ya udongo. 4. Waonyeshe vijana namna ya kutambua umbile la udongo kwa kutumia ribbon test (angalia hapo chini) 5. Waambie vijana wakusanye viganja vya udongo na warudie ribbon test 6. Toa muhtasariwa matokeo ya uchunguzi waliofanya kuhusu udongo na jadili matokeo yahaliya udongo uliyochunguzwa kwa ukuaji wa mazao 7. Toa muhtasari na hitimisha somo 12

Je, rangi ya udongo ina maana ganikwetu? Rangi nyeusi Udongo mweusi wa tabakala juu la ardhi, unaonyesha kiwango kikubwa cha mbolea, ikiwa na maana kwamba maji yanapenye kwa urahisi sana, virutubisho vingi na udongo wenye muundo mzuri. Rangi nyekundu - kahawia na rangi ya chungwa maji hutiririka na kupenye vizuri, mzunguko mzuri wa hewana maji. Kwa kuwa na maji ya kutosha ina maana rutuba pia ni ya kutosha. Hata hivyo tindikali (acidity) inaweza kuwa tatizo. Rangi ya manjano na buluu isiyokoza una matatizo la utiririshaji maji katika baadhi ya misimu (kufurika maji ) ambapo hewa hukosekana katika udongo, hasa wakati wa mvua. Rangi ya kijivu - huwa haupitishi maji vizuri, maji mengi na hakuna hewa ya kutosha. Chanzo: ABSA 1997 Jaribio la utoaji wa mbegu Vifaa Chupa ya maji Udongo kutoka tabaka na aina mbalimbali Uso laini wa kitu kigumu kamavile plywood au metali au kipande cha kadibodi Namna ya Kufunga (chanzo: FAO 2000b) Udongo lazima uwe na unyevunyevu ili kutambua umbile lake kwa kuugusa. Ongeza maji kidogo kidogo mpaka udongo uwe laini. Pitisha udongo kati ya kidole gumba na kidole cha shahada. Vunja chembechembe ngumu na ondoa mawe au mizizi yoyote itakayokuwemo. Utaweza kupata sifa ya mguso wa udongo: wenye chembechembe za mchanga huachana, wamfinyanzi hunata, udongo wa kitope/mchanga tope ni laini sana. Sokota vidole kati ya vidole gumba na na kidole cha shahada kutengeneza utepe. Kadiri utepe unavyokuwa mrefu ndivyo unavyoonyesha kuwa sampuli hiyo ina udongo mwingi wa mfinyanzi. Udongo wenye mchanga mwingi utaachana, udongo wenye udongo mwingi wa mfinyanzi unaweza kusokotwa kutengeneza utepe mzuri wenye urefu wa zaidi ya sentimita 5. Udongo wa kitope/mchangatope ni laini sana. Udongo tifutifu ni laini japo unanata na unahali ya 13

kichanga kidogo. Mwishowe baada ya kufanya mazoezi zaidi nitaweza kutathmini kwa usahihi aina ya udongo kwa kutumia mbinu hii. 1. Kama udongo una chembechembe za mchanga huwa unaachana (yaani haushikamani). Umbile la udongo ni mwepesi sana (mchanga mchanga) 2. Viringa udongo wa unyevunyevu kuwa gololi au mpira mdogo halafu bonyeza mpira huo kwakidole gumba na kuunda umbo la kikombe. Kama udongo huo hauwezi kuviringwa au kama kikombe kinamong onyoka, umbile la udongo ni. Mwepesi sana Kama mpira hauwezi kuviringwa lakini kikombe kinabaki na sura yake, endelea hatua ya 3. 3. Viringa bonge au mpira wa udongo kati ya viganja vyako, halafu kwenye kitu kigumu ili kuunda utepe mnene kama penseli wenye urefu wa shadi entimeta 20 25. Kama hakunautepeuliotengenezwa au ulikuwa mfupi zaidi, umbile la udongo ni.mwepesi (mchanga tifutifu) Kama utepe mrefu haukutengenezwa endeleahatua ya 4 4. Finyanga udongo kutengeneza utepe wa duara. Kama mduara huo utakuwa na nyufa umbile la udongo ni. Wastani (mfinyanzi mwepesi) Kama umefinyangwa mduara bila nyufa,na udongo unanata sana,umbile la udongo ni.. mzito (mfinyanzi mzito). A.1.4. Zoezi: Kupanga shughuli za kilimo Muda: Karibu saa 2 Vifaa: Karatasi ya chatipindu na kalamu ya kuchorea. Mkiwa shambani, waulize vijana maswali yafuatayo na orodhesha majibuyao kwenye chatipindu: Shamba darasa letu lina ukubwa gani? Wakati gani unafaa zaidi kulima mazao kwa kuangalia hali ya hewa na masoko? Ni mbinu za kilimo za aina gani zinazoweza kutumika kupanda mazao? Je, tutapanda namna gani mazao manne yaliyochaguliwa kwa shamba darasa? (moja kwa moja au kwanza kitalu na baadaye kupandikiza miche?) 14

Waambie vijana katika vikundi vidogo vinne, kila kikundi kipatie mojawapo ya mazao manne yaliyochaguliwa na waambie watayarishe mpango utakaoonyesha mawazo ya hatua kwa hatua wanachopaswa kufanya ili kuzalisha zaohilo kwenye shamba darasa. Warejeshe washiriki pamoja na wape fursa wawasilishe mipango yao. Hitimisha somo kwa kuuliza maswali yafuatayo: Je,ilikuwa rahisi au vigumu kupanga mipango katika kikundi? Hatua gani za msingi tunahitaji kuzifuata ili kupanga mipango? Je, kupanga mipango ni wazo linalofaa? Kwa nini ndiyo na kwa nini hapana? A.1.5. Zoezi: Hatua za maisha ya mazao Muda: Saa 1 dakika 30 Vifaa na matayarisho: Karatasi ya chatipindu, kalamu za kuchorea na mifano ya mimea (mazao katika hatua mbalimbali iliyokusanywa na mwezeshaji kabla ya somo) 1. Waeleze washiriki mimea,kama kilivyo kiumbe kingine chochote kinachoishi, hupitia hatua mbalimbali 2. Waulize vijana wanafikiri zao moja linapitia hatua zipi mbalimbali za ukuaji,kwa mfano mahindi, ambayo wangependa kupanda kwenye shamba darasa? 3. Duria hatua ya 2 kwa zao moja au mawili ambayo vijana wangependa kuyapanda kwenye shamba darasa 4. Eleza hatua nne tofauti zinazotumika zaidi katika vitabu: hatua ya awali, hatua ya ukuaji wa mazao, hatua ya katikati ya msimu na hatua ya mwisho wa msimu. Fafanua hatua hizo mbalimbali na waonyeshe washiriki mifano ya hatua mbalimbali. 5. Waombe vijana wataje mahitaji ya mimea/mazaoili yaweze kukua kwa afya. Yaorodheshe kwenye karatasi kubwa na ikibidi ongeza vitu vilivyokosekana. 6. Jadiliana na vijana kuhusu mahitaji yaliyotajwa kwa kila mmea/zao moja hadi jingine 7. Wagawe vijana katika vikundi vidogo vidogo na waombe kila kikundi wachague zao moja na kujadili katika kikundi jinsi mahitaji mbalimbali ya mazao yanavyotofautiana kutoka hatua moja ya zao hadi nyingine.waambie kilakikundi waandike maelezo kwenye karatasi. 15

8. Waambie kila kikundi wawasilishe matokeo ya majadiliano yao 9. Toa muhtasari wa majadiliano. Maelezo kwa Mwezeshaji: Tumia maswali yafuatayo ya mwongozo Je, kuna hatua ambayo zao linahitaji maji kidogo? Je, kuna hatua ambayo zao haliwezi kustawi kwa maji kidogo? Je, kuna hatua za mazao ambapo mazao yanahitaji kuchukuliwa hatua maalumu za kuyalinda? Je, mahitaji ya mbolea yanatofautiana kutoka hatua moja ya zao hadi nyingine? Usuli: Kwa kawaida kipindi cha ukuaji wa mazao kimegawanyika katika hatua 4 za ukuaji (tazama mchoro hapa chini) 1. Hatua ya awali: hiki ni kipindi kuanzia wakati wakusia mbegu au kupandikiza, hadi mazao yanapofunika karibu asilimia 10 ya ardhi 2. Hatua ya ukuaji wa mazao: hiki ni kipindi cha kuanzia mwishoni mwa hatua ya awali nakuendelea hadi itakapofikia kufunika ardhi yote (ardhi inaweza kufunikwa 70-80%) 3. Hatua ya katikati ya msimu: kipindi hiki kinaanza mwishoni mwa hatua ya ukuaji wa mazao nakuendelea hadi kukomaa, kinajumuisha kutoa maua na kutoa punje 4. Hatua ya mwisho wa msimu: kipindi hiki kinaanza mwishoni mwa hatua ya katikati ya msimu na kuendelea hadi siku ya mwisho ya kuvuna; kinajumuisha kuvuna. 16

Crop Initial stage Crop development Mid-season Late season needs\stages Water ++ ++ +++ + Fertilizer ++ +++ +++ - Protection* ++++ +++ ++ + 17

A.1.6. Zoezi: Kuandaa Kalenda za Mazao Muda: Karibu saa 2 Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea Mwambie kijana ajitolee kueleza awamu mbalimbali za mzunguko wa maisha ya mimea. Chagua mojawapo ya mazao yaliyochaguliwa kwa ajili ya SDSMV (kwa mfano nyanya) namwambie kijana aeleze mzunguko wa maisha wa zao hili, hasa katika miezi ipi zao hili linalimwa, kupandwa na kuvunwa Onyesha kalenda tupu ya mazao kama hii iliyo hapa chini Nyanya Mwezi Shughuli za Kilimo Pembejeo/Vifaa gani vinahitajika Januari Februari Machi Aprili Mei Wagawe vijana katika vikundi vinne na kiambie kila kikundi kikamilishe kalenda ya mazao kwa zao walilopewa kushughulikia (nyanya, bamia,(ladies sugar), tango, boga) Wahimize washiriki kujaza jedwali kwa kutumia maswali kama vile:- Zao hili tunalipanda lini? Zaohili tunalivuna lini? Shughuli gani za kilimo zinafanyika katika kila awamu/hatua? 18

Wakusanye vikundi wote pamoja na waambie wawasilishe kazi yao ya kikundi. Hakikisha kuwa wamejumuisha shughuli muhimu zaidi (matayarisho ya shamba, utiaji mbolea wa kwanza, kupalilia, umwagiliaji maji, kupandikiza miche (nyanya), kupalilia mara ya pili, top dressing, IPM, kuvuna, baada ya kuvuna) na pembejeo/vifaa (mbegu (mboji) mbole, dawa za kuulia wadudu, wa mimea, zana za kilimo na kupalilia) A.2. Mada Ndogo: Uchaguzi wa mazao na mbegu Lengo: 1. Kuelewa umuhimu wa kuchagua mbegu bora Wakati wa SDSMV vijana watapanda aina nne za mazao (nyanya, tango, bamia na boga (boga)) ambayo hulimwana wakulimakatika kipindi hicho cha mwaka. Ni muhimu kwa kila zao kutumia mbegu bora. Ni muhimu kuelewa pia kwa nini tunapanda mboga na sifa za mbegu bora ni zipi A.2.1. Zoezi: Kuchagua mbegu bora Muda: Saa moja na dakika 30 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea 1. Wagawe vijana katika vikundi vidogo vidogo na waulize nini wanadhani nisifa za mbegu bora na waorodheshe sifa hizo kwenye karatasi kubwa 2. Waambie kila kikundi kiwasilishe orodha yao 19

3. Jadili orodha zilizowasilishwa na hitimisha zile sifa muhimu zaidi za mbegu bora (hutoa mazao mengi, hufaa zaidi kwamazingira na hali ya mahali (hali ya hewa), safi hazina virusi, n.k.) 4. Jadiliana na vijana kuhusu mahali watakapopata mbegu bora. A.3. Muda Mdogo: Kuelewa uwezo wa kutoa wa mbegu Lengo: kuelewa namna mbegu zinavyoota Vijana wanahitaji kujifunza kuwa mbegu zitakuwa tu kama kiini kina afya, wakati kinapokuwa na viini lishe vya kutosha na wakati kunapokuwa na maji na hewa ya oksijeni ya kutosha. A.3.1. Zoezi: Jaribio la uotaji wa mbegu Muda: Nusu siku nakaribu wiki moja ya ufuatiliji Vifaa: Karatasi laini (au njia nyingine mbadala kama vile majani au magomeya miti); mbegu zamazaombalimbali ya chakula/miti (mbegu za kutosha kwa kila kikundi cha vijana ) mifuko ya plastiki na maji safi 1. Wagawe vijana katika vikundi na waambie kila kikundi wahesabu mbegu 100 kutoka aina mbalimbali zambegu. 2. Waambie waandae matabaka mawili ya karatasi laini na kunyunyiza maji safi kwa makini hadi ziwe na unyevu zisilowe 3. Waambie vijana waweke mbegu 100 juu ya karatasi laini katika safu 10 zenye mbegu 10 (umbali kati ya mbegu na mbegu iwe karibu sm 2) 4. Waambie vijana wafunike mbegu na tabaka jingine la karatasi laini, nyunyuzia maji kwenye karatasi laini na zungushia karatasi laini lenye mbegu kwenye aina nyingine ya karatasi. 5. Waambie vijana waweke karatasi hiyo kwenye mfuko wa plastiki ili kutunza unyevu wa karatasi yenye mbegu (mbegu nyingi humea vizuri zaidi katika sehemu yenye giza, hivyo mfuko wa plastiki mweusi ni bora zaidi kutumiwa) 6. Waambie vijana waandike jina la kikundi kwenye mfuko, herufi ya bechi ya mbegu zilizomo ndani yake, na tarehe mbegu ziliposiwa. 7. Hakikisha kuwa unahifadhi mahali penye giza. 20

Kutegemea na zao, mchakato wa uotaji unaweza kuonekana baada ya siku 1, 2 au zaidi. Andika idadi ya mbegu zilizokwisha ota kwa kipindi hiki cha kwanza cha kuchunguza. Mara baada ya kuangalia na kuandika idadi (na kuondoa mbegu zilizoota ) zungushia tena karatasi laini na rudisha kwenye mfuko wa plastiki kwa ajili ya uchunguzi mwingine wa kila siku Wakati vijana wanapochunguza na kufuatilia mbegu waulize maswali yafuatayo: Imechukua muda gani kwa mbegukumea? Mbegu ngapi zimemea? Je, idadi ilikuwa ndogo au kubwa? Kwa nini ni muhimu kujua uwezo wa mbegu kumea? A.4. Mada Ndogo: Kuandaa shamba darasa Baada ya kuandaa mpango wa kuhusu kile watakacholima vijana kwenye shamba darasa lao itakubidi kuanza kuandaa shamba kwa ajili ya kilimo chenyewe A.4.1. Zoezi: Kuanda mpangilio wa shamba darasa. Vijana hawana budi kwanza kuamua kuhusu mpangilio wa shamba darasa ili kuelewa mahali pa kupanda na aina ya mazao Mada: Karibu saa 1 Vifaa : Chatipindu na kalamu za kuchorea 1. Nenda na vijana katika shamba darasa na waambie wakumbuke sifa zote za shamba darasa ambazo ni muhimu kwa kuandaa mpangilio wa shamba (mteremko, tofauti za rutuba ya udongo, njia ya kuingilia shamba, chanzocha maji n.k) 2. Waambie wanafunzi wabainishe maeneo mbalimbali ya shamba, mahali pa kitalu na njia zitakazojumuishwa kwenye mpangiliohuo Zingatia kwamba kila zao litapandwa kwenye eneo moja litakalolimwa kulingana na kanuni za IPM na wenyeji wanavyolima, ili mwishoni kuweza kuchunguza athari ya IPM. 21

3. Waambie vijana kwenye vikundi vyao vidogo waandae mipangilio ya shamba darasa zikiwemo sehemu zote, kitalu na njia. Waambie wazingatie mahali pa kupitishia maji na umwagiliaji shamba na mwelekeo wa matuta ya vitalu na safu/mistari 4. Waambie vikundi wawasilishe mipangilio yao na kuamua kuhusu mpangilio wa mwisho watakaotumia. A.4.2. Zoezi: Maandalizi ya Ardhi Kabla ya kupanda mbegu, ardhi haina budi kuandaliwa kwanza Muda: Karibu saa 1 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea Bungua bongo na vijana kuhusu kinachotakiwa kufanywa shambani kabla ya kuanza upandaji wa mbegu (kusafisha ardhi, kuondoa mabaki yote ya mimea, kusawazisha ardhi inapohitajiwa, kutumia mboji, kutifua na kuandaa vitalu vya mbegu). Jadili shughuli zote zilizotajwa, kwa nini lazima zifanywe na zifanywe namna gani. Panga shughuli mbalimbali kwa mfuatano unaofaa. Tayarisha mpango na vijana kuhusu lini kifanyike nini. Njia bora zaidi ya kueleza namna ya kufanya shughuli mbalimbali ni kwa kufanya kwa vitendo shughuli hizo na vijana. Kazi kubwa (kusafisha shamba na kulima na kutifua) lazima ifanywe na watu wazima. Mada Ndogo: Kuandaa kitalu na kupandikiza. Malengo: Kuelewa umuhimu wa vitalu Kujua namna ya kuandaa kitalu Kujua namna ya kupandikiza miche 22

Mazao mengi ambayo tunataka kuyapanda shambani, yanahitaji kupandwa kwenye vitalu kwanza, na kisha kuhamishiwa shambani baada ya wiki chache. Ni muhimu kwa washiriki kuelewa jinsi ya kuandaa kitalu, kupanda mbegu, kutunza miche na jinsi ya kuhamisha miche kwenda shamba darasa kwa wakati mwafaka. Hapa kuna baadhi ya mazoezi ya mfano ambayo unaweza kuhitaji kuyatumia. A.4.3. Zoezi: Kwanini tunahitaji vitalu? Muda: Karibu saa moja na dakika 30 Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea Waulize vijana maswali yafuatayo na andika majibu yao kwenye chatipindu Kwa nini wakulima mara nyingi hupanda mazao ya mbogamboga kwenye vitalu kwanza na baadaye kwenye shamba? Kutokana na majibu yako, unatakiwa kuandaa vipina wapi kitalu chako? Kisha wapeleke vijana mahali ambako umeamua kuandaa kitalu Waulize vijana maswali yafuatayo: Je, mbegu zilizosiwa kwenye kitalu zinahitaji kukingwa kutokana na vitu gani mbalimbali? Je, tutawezaje kutoa kinga inayotakiwa? Je, tunahitaji kutunza miche namna gani? Je, tutaandaa vipi vitalu ili visaidiae kukinga na kutunza vizuri miche? A.4.4. Zoezi: Kuandaa kitalu Muda: Karibu saa 2 Vifaa: Hakuna. Sasa vijana wataandaa kitalu kwa vitendo. Wapitishe katika hatua zifuatazo kwa kuzingatia kuwa kila mmoja anashiriki kwenye kazi hiyo. Kulingana na idadi ya vitalu mnavyoandaa, unawezakuwagawa washiriki katika vikundi vidogovidogo zaidi. 23

Sehemu ya 1.10 1. Tafuta udongo kwenye., vunja mabonge ya udongo naondoa mabaki ya mizizi na mashina ya majani 2. Tifua udongo na pandisha udongo toka pande zote ili kitalu kiwe kimeinuka na kuachaaaaa njia pande zote ili kuruhusu kupalilia bila kukanyaga juu yake. (upana wa mita ± 1) 3. Ongeza mbolea ya samadi/mboji na mchanga wa mtoni, changa vizuri. Mchanga unaweza kusaidia kulainisha udongo ili kuwe na mtiririko mzuri wa maji na kung oa mizizi ya miche kwa urahisi. 4. Sawazisha kitalu na ikibidi weka mipaka. Pasua mipaka kwa kutumia kijiti. 5. Sia mbegu (zilizowekwa dawa ya kukinga ikibidi) kwenye mistari kwa kina kilichopendekezwa. Acha nafasi ya kutosha kwa ajili ya ukuaji wa miche. 6. Funika mistari hiyo kwa udongo kidogo usiozidi mara 2-3 ya unene wa mbegu 7. Kama kuna tatizo la mchwa na konokono, tawanya majivu kwenye kitalu chote. 8. Tandaza majani, nyasi, mabua ya mpunga, mbolea ya samadi/mboji nakiasi fulani cha tabia za msituni kuzuia mbegu za udongo usisombwe na mvua kubwa nakuzuia magugu na kutunza unyegu wa udongo wakati wote 9. Ikibidi, jengea vivuli, kama paa dogo Sehemu ya 1.02. Mpangilio wa vitalu kupanga mbegu kujenga kivuli 24

MAMBO MUHIMU Kabla ya kuandaa kitalu Chagua mahali pazuri: Mahali panapofaa patakuwa sehemu ya karibu na shamba darasa (ili kitalu kitembelewe mara kwa mara nakutunzwa vizuri) yenye ardhi nzuri na yenye rutuba,karibu nachanzo cha maji kinachoaminika na ambapo maji hayatuami au kukusanyika. Epuka kuweka kitalu mahali ambapo mimea iliyopoya jamii moja na ile unayosia ina tatizo la wadudu waharibifu na magonjwa Safisha eneo: Ondoa visiki, mizizi na mawe katika eneo hilo. Majani na mabakimengine ya vitu visivyokuwa vya miti, yanaweza kutengenishwa na kufanywa mbolea ya mboji. Mpangilio wa vitalu: Ulalo, kamainawezekana vielekee (jua) mashariki kwenda magharibi, upana wa mita moja na nafasi kati ya kitalu na kitalu iwe nusu mita. A.5. Mada ndogo: Kupanda: Kuelewa umuhimu wa kuacha nafasi baina ya mimea Malengo: Kuelewa umuhimu wa kuacha nafasi baina ya mimea Kuelewa umuhimu wa uzazi wa mpango Ili kuotesha mazao yaliyostawi vizuri, kila mmea unahitaji kuwa nanafasi ya kutosha. Kuipa mimea nafasi ya kutosha ni sawa na kuupa kila mmea viini lishe na maji ya kutosha kutoka kwenye udongo uliyozunguka. Inakuwa rahisi vilevile kuondoa magugu na kupunguza mimea wakati utakapowadia. Wakati huo huo mkulima huwa anapenda kupanda mimea mingi kadiri iwezekanavyo. Ni muhimu kuelewa namna ya kupata mavuno mengi wakati huo huo kuhakikisha kuwa mazao yamestawi vizuri. Kuacha nafasibaina ya mimeani muhimu sana katika kuamua ni mazao gani ya kupanda na wakati gani wa kupanda mazao hayo. A.5.1. Zoezi: Kuacha nafasi baina ya mimea. Muda: Karibu saa 1 na dakika 30 Vifaa: Karatasi ya chatipindu na kalamu za kuchorea, tepu ya kupimia Andaa ziara ya kwendakwenye shambalenye mazao yaliyo komaa ili kila mtu aweze kuona nafasi baina ya mimea mbalimbali shambani hapo. 25

Wakati unapowasili shambani, waambie vijana waangalie nafasi kati ya mimeana wajaribu kufikiria jinsi ilivyopandwa (kwenye msatari, kwenye kitalu,bila mpangilio maalumu). Vijana mbalimbali wapime nafasi baina ya mimea ya mazao ya aina mbalimbali (nafasi baina ya mstari na baina ya kila mmea). Waambie waandike mambo waliyoona kwenye jedwali, wapange kulingana na mazao ya aina mbalimbali shambani. Waulize vijana maswali yafuatayo:- Je, wingi wa mazao una maana gani? Kwa nini ni muhimu kufuata nafasi fulani baina ya mimea au mbegu wakati wa kupanda mazao? Kuna faida au hasara gani kupanda mbegu kwenye mstari au bila mpangilio maalumu? Unafikiri kutatokea nini kwenye mimea kama itapandwa karibu karibu? Waeleze kwamba kupata wingi mzuri wa mimea, ni muhimu kupanda mbegu nyingi wakati wa msimu wa kupanda ili kuepuka baadhi ya mimea kutoota au mingine inaweza kufa ikiwa michanga kutokana na wadudu waharibifu au maginjwa. A.6. Mada Ngogo: Kupanda Mazao Yenye Afya Kupitia Kanuni za Udhibiti Husishi wa Wadudu Waharibifu (IPM) Utangulizi. Malengo: Kuelewa Kanuni Kuu za Udhibiti Husishi wa Wadudu Waharibifu wa Mimea Kuelewa maana ya mfumo wa kiikolojia Kuelewa umuhimu wa usafi na afya, mazingira shambani kama njia ya kukinga wqadudu waharibifu na maginjwa ya mimea Kupanda mazao yanayostawi ni ufunguo wa kilimo bora. Mazao yaliyostawi ni imara zaidi na yanawezakujilinda vizuri zaidi dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa. Njia mbalimbali ambazo tunatumia katika mashamba yetu zinaleta athari kwa ustawi wa mazao na zinaweza kutumika pia kudhibiti matatizo yoyote ya wadudu waharibifu. Kulima mazao yenye afya na yanayostawi ni kanuni ya kwanza ya Udhibiti Husishi wa Visumbufu vya Mimea (IPM). IPM inahusu wadudu waharibifu lakini ni zaidi ya udhibiti wa wadudu waharibifu. IPM si 26

kuhusu kuwaangamiza wadudu wote waharibifu. Baadhi ya wadudu waharibifu huhitajika kwa ajili ya kuwaondoa maadui shambani. IPM inahusu kuwapunguza wale wadudu waharibifu ambao husababisha uharibifu wa mazao na kuleta hasara. Mara nyingi IPM inaweza kulenga matumizi madogo ya dawa za kuulia wadudu waharibifu kadiri iwezekanavyo. Lakini msingi wa maamuzi ya udhibiti mzuri wa mazao ni kuelewa kwa ukamilifu mfumo wa ikolojia ya mazao, pamoja na yale ya wadudu waharibifu, maadui wao wa asili na mazingira ya mahali. Ufuatiliaji wa mazao ni hatua ya kwanza katika kuelewa mfumo wa ikolojia. Ifuatayo ni baadhi ya mifumo ya shughuli unayoweza kutumia kuanza kuwafundisha vijana Mada Maalumu ya Kilimo: Udhibiti Husishi wa Visumbufu vya Mimea. A.6.1. Zoezi: Kupanda mazao yanayostawi kwa kutumia IPM Muda: Saa 1 na dakika 30 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea Hatua: 1. Taja kanuni nne za Vdhibiti Husishi wa Visumbufu vya Mimea: Kupanda mazao yanayostawi Kuelewa na kuhifadhi wadudu wanaolinda Kutembelea shamba mara kwa mara Kuwa mtaalamu katika kusimamia mazao yako 2. Waulize vijana wanafikiri kila moja ya kanuni hizo ina maana gani. 3. Wagawe vijana katika vikundi na waambie kila kikundi waandike taratibu mbalimbali za usimamizi wa mazao ambazo wanafikiri zinaleta athari katika ustawi wa mazao 4. Mwambie mwakilishi mmoja kutoka katika kila kikundi awasilishe matokeo yao darasani. 27

A.6.2. Zoezi: Kuelewa mifumo ya ikolojia ya shamba Ili kukinga mazao dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa, vijana kwanza wanahitaji kuelewa mfumo wa ikolojia wa shamba darasa. Mfumo waikolojia ni mimea, wanyama na viumbe wadogo wote katika eneo fulani na namna wanavyoishi na kushirikiana na kutegemeana. Vijana watachunguza mfumo wa ikolojia wa shamba na nafasi ya wadudu wa asili katika kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa ya mimea. Mada: Saa 1 dakika 30 Vifaa na matayarisho: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea, mifuko ya plastiki, alkoholi na gundi. Hatua: 1. Anzisha mada ya kukinga mazao dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa 2. Waambie vijana wataje kanuni nne za IPM na kujadili kanuni hizo nne kuhusiana na kulinda mazao dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa ya mimea. 3. Waulize vijana wanafikiri mfumo wa ikolojia una maana gani. 4. Nenda na vijana kwenye shamba darasa na wagawe katika vikundi vidogo vidogo na waambie vikundi wakusanye aina mbalimbali za viumbe shambani (mfumo wa ikolojia) kadiri iwezekanavyo, ikiwemo mimea, mimea yenye magonjwa, wadudu, buibui, panya, nyoka n.k. 5. Waambie wanakikundi waende mahali penye kivuli. Miminia alkoholi kwenye mfuko waplastiki na uutikise ili wadudu na buibui wafe. 6. Jadili na tengenisha pamoja na vijana viumbe waliyokusanywa kulingana na kazi zao kwenye mfumo wa ikolojia. Waambie vijana wawapange katika matabaka mbalimbali; mimea chini, wala mimea katika tabaka la 2, maadui wa asili katika tabaka la 3, na waozeshaji katika tabaka la 4. Wagundishe kwenye karatasi. Kama hawana uhakika na kazi, wawekee kiumbe hicho lebo hawana uhakika 7. Waulize vijana kama mimea yote waliyoipata ni magugu. Kwanini ndiyo au kwanini hapana? Halafu waulize pia kama wadudu wote ni wadudu waharibifu. Kwa nini ndiyo au kwanini ni hapana? 8. Jadiliana na vijana namna maadui wa asili (walinzi) wanavyomsaidia mkulima katika kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa ya mimea shambani. 28

9. Toa muhtasari wa majadiliano na mambo mliyoyaona shambani. Maelezo kwa Mwezeshaji: Maswali ya Kuongoza. Je, wadudu wote ni wadudu waharibifu? Je, wadudu wote waharibifu waliyopo shambani husababisha matatizo? Je, tunahitaji maadui wa asili wangapi kudhibiti wadudu waharibifu? Je, mdudu mharibifu ni tatizo wakati wote wa hatua za ukuaji wake au wakati wa hatua moja au mbili tu? Je, nini hatua za ukuaji wa mmoja wa wadudu aliyechaguliwa? A.6.3. Zoezi: Desturi mbalimbali za kudhibiti visumbufu vya mimea Muda: Karibu saa 1 Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea Eleza kuwa kwa kutumia desturi mbalimbali za kilimo, mkulima anaweza kupunguza hatari ya mashambulizi ya wadudu waharibifu kwenye mazao yake. Waulize vijana kama wanaelewa baadhi ya desturi hizo. Ziorodheshe kwenye karatasi kubwa. Panga desturi hizo kwa makundi kulingana na zile za kiutamaduni, za kiutendaji na za kibiolojia na jaribu kukamilisha orodha pamoja na vijana Desturi za Kiutamaduni: Muda wa kulima/kupanda, kulima kwa kwa mzunguko wa mazao/kubadilisha mazao (crop rotation), kuchanganya mazao, kutumia mitego na kutandaza majani. Desturi za kiutendaji: Utumiaji jua/utashishaji, kupalilia, uondoaji wadudu waharibifu na/au mimea inayoambukiza Desturi za Kibiolojia: Wadudu wenye manufaa (adui wa asili) dawa za kuulia wadudu za viumbe (bio pesticides) na /au dawa za kunyunyizia mimea, mitego (pheromone traps). Jadiliana na vijana desturi zote zilizotajwa. 29

A.6.4. Zoezi : Desturi za kijadi za kudhibiti wadudu waaribifu wa mazao Matumizi ya dawa za kuulia wadudu waharibifu (vinatilifu) na kemikali yamezoeleka sana katika kipindi kilichopita cha miaka 30-40 kwenye nchi nyingi za tropiki na hasa kwakilimo cha biashara. Bado kuna maarifa mengi kuhusu namna ya kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa kwa kutumia dawa za mimeana mbinu za kijadi. Mara nyingi mbinu hizi wanazo wazee katika jamii Muda: Karibu saa 1 Vifaa: Mwenyeji mwenye maarifa ya kilimo. Mwalike( mzee) mtu kutoka kwenye jamii ambaye anafahamika kuwa ana maarifa mengi kuhusu matumizi ya dawa za mimea na mbinu za kijadi katika kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa katika kilimo. Waambie vijana watunge baadhi ya maswali katika vikundividogo vidogo na kumwuliza mwenyeji mwenye maarifa ya kilimo. Kama ikiwezekana kwa kushirikiana na mwenyeji huyo mwenye maarifa ya kilimo, kusanya baadhi ya mimea inayotumika na tayarisha dawa. A.6.5. Zoezi: Kulinda mazao dhidi ya wadudu na magonjwa katika shamba darasa (IPM) Muda: Karibu saa 2 Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea. 1. Waambie vijana wakae kwenye vikundi vyao vidogo vidogo na kugawa mazao yanayokuwa katika shamba darasa miongoni mwa vikundi vidogo, kwa mfano kila kikundi mazao mawili na kila zao lishughulikiwe na angalao vikundi viwili. Kila kikundi kichore safu mbili kwenye karatasi kubwa. 2. Kiambie kila kikundi kihorodheshe wadudu waharibifu na magonjwa ya mazao waliopangiwa kwa msingi wa walichochunguza katika shamba darasa wakati wa uchunguzi wa mfumo wa Ikolojia ya Kilimo (AESA) pamoja na kutokana na uzoefu katika safu ya kwanza 3. Kiambie kila kikundi kihorodheshe kwenye safu ya pili desturi za kulinda na kudhibiti wadudu waharibifu na magonjwa waliyotajiwa. 4. Kiambie kila kikundi kiwasilishe matokeo ya majadiliano yao ya kulinganisha mawasiliano yanayohusu wadudu waharibifu na magonjwa na desturi za kulinda za mazao hayo. 30

5. Jadili na kukubaliana kuhusu njia bora zaidi za kulinda wadudu waharibifu na magonjwa yaliyobainishwa kwa mazao mbalimbali yanayolimwa kwenye shamba darasa. 6. Kama bado kuna maswali yasiyohitaji kukatiwa shauri kuhusu baadhi ya wadudu waharibifu na magonjwa na namna ya kulinda, mwalike kwenye somo la SDSMV mkulima mwenyeji mwenye uzoefu na jadili maswali haya pamoja naye A.6.6. Zoezi: Kupata maarifa zaidi kuhusu wadudu waharibifu na magonjwa katika shamba darasa Kama matatizo au maswali yanayohusiana na kudhibiti baadhi ya magonjwa na wadudu katika shamba darasa hayawezi kutanzuliwa na vijana na mwezeshaji wa SDSMV, Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana, italazimika kuanzisha shughuli za ziada kupata taarifa inayotakiwa kutanzulia matatizo yaliyobainishwa. Njia ya a) Kumwalika mkulima mwenyeji mwenye uzoefu au mtaalamu (afisa kilimo wa ugani) kwenye somo la SDSMV na kuwapa fursa vijana kujadiliana naye matatizo hayo Njia ya b) Kama ufumbuzi unawezekana unafahamika, fanya jaribio dogo, kupima ufumbuzi mbalimbali. Kwa mfano, mimea michache au u 2 moja imetiwa dawa ya aina moja na mimea michache au m 2 moja imetiwa dawa nyingine. Njia ya c) Anzisha bustani ya wadudu Kwa maelezo zaidi kuhusu matumizi Kwa maelezo zaidi kuhusu matumizi na matayarisho ya bustani ya wadudu, tafadhali angalia kiambatisho cha 2 A.6.7.Zoezi : Kutayarisha dawa ya Mwarubaini kwa ajili ya kudhibiti wadudu waharibifu Mwarubaini ni dawa ya kuulia wadudu ya kiasili au ya mimea. Mwarubaini una uwezo mkubwa wa kudhibiti wadudu wa aina mbalimbali waharibifu. Ina kiwango kidogo sana cha sumu kwa binadamu na haiharibu mazingira. Miti ya mwarubaini inapatikana katika nchinyingi za tropiki hasa katika maeneo ya ukame. Sehemu nyingi za mmea huo zinaweza kutumika kwa utayarishaji wa dawa ya kudhibiti wadudu waharibifu lakini sehemu zinazotumika mara kwa mara ni mbegu na majani ya mti Njia raisi zaidi ya kueleza matayarisho ya dawa ya mwarubaini ni kwa kufanya kwa vitendo na watoto Muda: Karibu matayarisho ya saa 1, siku inayofuata, umaliziaji wa nusu saa. 31

Vifaa: Mbegu za mwarubaini, majani ya mwarubaini, kinu, kitambaa chepesina safi, ndoo, kipulizia dawa cha kubeba mgongoni 1. Kusanya mbegu za mwarubaini zilizoiva, hasa zile zilizoanguka kutoka mtini, menya maganda na zianike kivulini (ukaushaji kwa hewa). Kama ni lazima, hifadhi mbegu hizo kwenye magunia kwa matumizi ya baadaye. Inakadiriwa kwamba kilo 12 za mbegu za mwarubaini zisizomenywa zinatosha kutia dawa hekta 1 au eka 2.5 ya mazao yaliyoshambuliwa na wadudu waharibifu. Ili kupata uzito unaofaa wa dawa, gramu 50 za mbegu zisizomenywa hazina budi kulowekwa kwenye lita 1 ya maji. Mkulima anahitaji gramu 750 za mbegu za mwarubaini kama anataka kunyunyizia kwa klutumia kipuliza dawa cha kubeba mgongoni cha ujazo wa lita 15. 2. Weka kinuni kiasi kinachotakiwa cha mbegu za mwarubaini zisizomenywa na twanga mbegu kwa ukamilifu mpaka ziwe rojo. 3. Changanya rojo na maji na acha kwa usiku kucha 4. Itakapofika mchana, chuja maji ya mbegu kwa kitambaa safi na chepesi. Chujua/zimua mchanganyiko huo kwa uwiano wa 1:2 halafu nyunyizia mazao yaliyoshambuliwa na wadudu kwa kutumia kipulizia dawa cha kubeba mgongoni. 5. Changanya mabaki ya chembechembe ngumu za mbegu iliyochujwa na udongo wa kitalu ili kudhibiti wadudu wa kwenye udongo wa kitalu. Namna ya kutayarisha dawa ya majani ya mwarubaini. 1. Kusanya majani ya mwarubaini kabla mti haujaalika maua 2. Twanga kiasi cha kilo moja ya majani, changanya na maji kiasi cha gramu 100 (kiasi cha kiganja kilichojaa) cha pilipili hoho mbichi kwenye kinu. Pilipili hoho zinaongeza ufanisi wa dawa ya majani ya mwarubaini. 3. Loweka rojo la majani ya mwarubaini kwenye lita 5 za maji usiku kucha. 4. Chuja mchanganyiko kwa kitambaa safi na chepesi naongeza lita 1 ya sabuni ya maji. Sabuni ya maji itakuwa haina kiambata. 5. Chujua/zimua mchanganyiko huo kwa uwiano wa 1:2 kwa kunyunyizia moja kwa moja kwenye mazao ili kudhibiti wadudu. 32

A.6.8. Zoezi: Punguza matumizi ya kemikali za kilimo Wakulima wengi hutumia kemikali za kilimo katika urutubishaji na /au udhibiti wa wadudu waharibifu na magonjwa. Kemikali nyingi ni hatari sana na wakulima hawana budi kuzisambaza na kuzitumia kwa makini. Muda: Kiasi cha saa 2 Vifaa: Karatasi kubwana kalamu za kuchorea 1. Waambie vijana wataje aina mbalimbali za kemikali zinazotumiwa na wakulimakatika katika na waziorodheshe kwenye karatasi kubwa 2. Jadiliana na vijana hatari mbalimbali zilizopo katika kutumia kemikali hizi na namna mkulima anavyoweza kupunguza hatari. Orodhesha kwenye karatasi kubwa namna bora za kushughulikia kemikali hizo. 3. Waambie vijana wataje mifano ya ajali zilizotokea katika jamii zao na kiambie kikundi kimoja kifanye mchezo wa kugiza kuhusu mfano wa ajali 4. Jadili makosa yaliyofanywa katika kushughulikia kemikali kwenye mchezo wa kuigiza. Kaimbie kikundi kingine kiigize tena mchezo lakini safari hii huonyesha namna bora za kushughulikia 5. Hitimisha kuhusu namna bora za kushughulikia kemikali za kilimo Zingatia: Namna bora za kushughulikia kemikali za kilimo ni Chagua dawa za wadudu zilizo salama zaidi na tumia kiasi kidogo sana Tunza dawa za wadudu, kemikali za kulima na vifaa vya kupulizia dawa mahali salama na palipotengwa Andika majina/lebo kwenye dawa za wadudu na kemikali za kilimo (kwa kutumia Kiswahili) Weka njia salama za kushughulikia chupa na makopo ya dawa za wadudu na kemikali Kusanya taarifa za afya na usalama kwa mfano matumizi salama ya kemikali za kilimo na eneza taarifa hizo kwa jamii 33

A.7. Mada ndogo: Uchunguzi wa mfumo wa kilimo na ikolojia (AESA ) Zana ya ufuatiliaji na kufanya maamuzi katika kilimo Malengo: Kuelewa namna ya kuchanganua mara kwa mara jinsi mashamba yao yanavyoendelea Wakati wakupanga shughuli zaoza shamba, vijana hawana budi kujifunza kuchanganua hali ya mashamba yao kwanza kabla ya kufanya uamuzi kuhusu namna ya kusimamia mazao yao. AESA ni zana inayofaa kwa ajili ya kufanya shughuli hii, pamoja na kubadilishana maarifa. AESA inahusisha uchunguzi na uchanganuzi wa mara kwa mara wa mazao wakati wa hatua mbalimbali za ukuaji. Pia inahimiza kujifunza kwa kugundua. Vipengele vya msingi vya uchanganuzi ni:- Hakikisha mimea ina afya katika hatua mbalimbali za ukuaji wao Wadudu na wanyama wanaokula wenzao Hali ya udongo na maji Hali ya hewa A.7.1. Zoezi: Kutambulisha AESA MUDA: Karibu saa 2 VIFAA: Karatasi kubwa ya chatipindu, kalamu za kuchorea, tepu na shamba lenye mazao. 1. Eleza kwamba ni muhimu kuchunguza mazao mara kwa mara ili kuyatunza 2. Nenda na vijana kwenye shamba lenye zao maalumu, wagawe vujana katika vikundi vya vijana 6-7 na kila kikundi kiandae orodha ya mambo muhimu wanayotaka kuyaona kuhusu mazao. Wasaidie vijana kubaini mambo yafuatayo Idadi ya mimea iliyopo Idadi ya wadudu wanaoruka (wadudu waharibifu na wanyama wa asili wanaokula mazao), kwenye mimea na eneo la jirani Wadudu, wanyama wanaokula wenzao waliyopo kwenye eneo la udongo na kwenye mimea Mabaka, madoa na kuchujuka rangi kunakoonyesha kuwapo kwa magonjwa Madhara yanayosababishwa na wadudu na aina mbalimbali za magonjwa 34

Aina za nyasi,ukubwa na wingi ikilinganishwa na mazao Hali ya udongo Hali ya hewa siku hiyo (kwa mfano joto, mawingu kidogo, mvua, unyevunyevu/mavunde mavunde) 3. Chagua mmea wa mfano na waambie vijana wachunguze mambo yafuatayo Idadi ya majani Urefu wa mimea Sehemu za uzazi za mmea uliyochaguliwa Sifa nyingine zozote zitakazokusaidia kutoa uamuzi kuhusu mmea huo wiki zitakazofuata. 4. Waonyeshe vijana muundo watakao wasilishia data zao. Mfano umeonyeshwa hapa chini 5. Kwa kushirikiana kwa vikundi vyao, waambie vijana wajaribu kufanya AESA ya sehemu ya shamba 6. Waambie vijana wawasilishe kazi yao, na jadili tofauti zozote zilizojitokeza 7. Hitimisha somo kwa kuwauliza vijana, Je, AESA inawasaidiaje kufanya uamuzi? 35

Mfano wa Muundo wa Uwasilishaji wa Data - AESA AESA No. HALI YA HEWA Jina la kikundi Tarehe Taarifa ya ( jumla Aina ya mimea Je, umetumia mbolea(ya kemikali) Tarehe ya kupanda Wanyama walioonekan a Wadudu Muda wa kuchunguza (tarehe, saa n.k.) 36

Taarifa kuhusu udongo na maji Uchunguzi kuhusu mmea Upana wa jani Urefu wa mmea Wanyama wanaokula mazao wa asili Idadi ya majani Idadi ya vifuko vinavyoonekan a Magonjwa yaliyoonekana Uchunguzi wa jumla wa hali ya mmea na MAPENDEKEZO shamba 37

A.7.2. Zoezi: Ufuatiliaji wa Mara kwa Mara kwa kutumia AESA. AESA ilielezwa kwenye moduli iliyotangulia, lakini ni muhimu kukumbuka kuwa AESA inatakiwa kufanya mara kwa mara ili vijana waelewe kwa ukamilifu na kudhibiti ukuaji wa mazao yao. Alimradi mazao yako kwenye shamba darasa, washiriki wafanye AESA mara moja kila wiki. Muda: Wastani saa 2 Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea, tepu na kijiti 1. Endesha majadiliano ya kukumbuka na vijana kuhusu AESA 2. Nenda na vijana kwenye shamba darasa na wagawe katika vikundi vidogo vidogo 3. Panga eneo kwenye shamba darasa kwa kila kikundi kuchunguza ukubwa wa eneo lililochaguliwa au idadi ya mimea (kulingana na zao) 4. Viambie vikundi waandae orodha ya mambo muhimu waliyoona kuhusu ukuaji wa mazao 5. Waambie kila kikundi wajadili habari walizoandika na kupendekeza taratibu za udhibiti ili kutatua matatizo yoyote yatakayojitokeza. Kwa mfano, kama magugu mengi yameonekana, inawezekana kupendekeza palizi kama pendekezo la usimamizi 6. Toa muhtasari wa matokeo kwenye karatasi ambayo inaweza kutumika kama karatasi ya ufuatiliaji na kutunzia kumbukumbu: Michoro iwe rahisi na inayoonyesha hali/matokeo ya shamba. 7. Kila kikundi kidogo kiwasilishe matokeo yao. Hakikisha watu tofauti wanawasilisha matokeo kila wakati. 8. Jadili mawasiliano ya vikundi na njia za udhibiti zilizopendekezwa, na amueni pamoja kuhusu hatua gani zinatakiwa kuchukuliwa na nani watazichukua. Maelezo kwa Mwezeshaji: Maswali kwa ajili ya majadiliano katika hatua ya miche. Je, mimea imestawi vizuri (hatua ya miche)? Je, kwa jumla mazao yamestawi na yenye afya? Je, kuna hali ya majani kuwa njano? Kama ni hivyo ni kitu gani kinaweza kusababisha hali hiyo? Hali ya hewa ina athari gani katika ukuaji wa mimea? Je, unawaona aina gani ya wadudu waharibifu na wako wangapi? 38

Je, kuna mayai mengi ya wadudu rafiki? Je, uharibifu wa aina gani unafanywa na wadudu waharibifu katika hatua hii ya mazao? Je, kuna njia yoyote ya kuzuia wadudu hawa wasiongezeke? Je, hali ya wadudu waharibifu katika kashamba mengine kwenye eneo ikoje? Je, mashamba mengine yanaweza kuathiri shamba lako? Je, kuna aina gani ya maadui wa asili shambani? Je,wako wangapi? Unafikiri wanaweza kuwa wametoka wapi? Je, wanakula nini? Na walikuwa wanakila nini kabla hawajawa wadudu waharibifu? Je kuna wadudu ambao si waharibifu wala wadudu wa asili? Je, kuna wadudu waozeshaji ambao hula vitu vilivyokufa ndani ya udongo? Je, idadi ya wadudu waharibifu namaadui wa asili inaongezeka au kupungua ikilinganishwa na wiki zilizopita? Je, unatarajia kutatokea nini wiki ijayo? Je, kuna wadudu waharibifu maalumu wa kufuatilia kwa makini zaidi? Je,unafikiri kuna haja ya kutumia dawa ya kuulia wadudu waharibifu? Kama hapana,je kuna njia mbadala? Je, mimea imepata nafuu kutokana na uharibifu wa wadudu katika hatua iliyopita? Je, kuna ugonjwa wowote shambani? Unawezaje kudhibitiwa au kutibiwa? Je, mimea inakuwa kama ilivyotarajiwa (majani mangapi, kimo, n.k.) Je, kuna magugu kwa wingi? Ni wakati gani unafaa kufanya palizi? Je, kuna mpango gani waudhibiti kwa wiki ijayo? Je, uamuzi wa wiki iliyopita ullikuwa na ufanisi? 39

A.8.1. Zoezi: Palizi, Kwa nini, Wakati gani na namna gani Muda: Saa mbili Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea Zingatia: Shughuli hii ni lazima ifanywe kwenye shamba la karibu ambapo mazao tayari yanakuwa na magugu yamekuwa ni tatizo Hatua: 1. Wakiwa shambani, waambie vijana waketi katika mduara. Waulize wanafikiri mkulima atafanya nini kukinga mazao yasipatwe na magonjwa. Orodhesha mawazo yao yote 2. Himiza majadiliano kuhusu umuhimu wa kuzingatia usafi wamazingira katika shamba kupunguza hatari za wadudu waharibifu namagonjwa. Waambie vijana wataje shughuli nyingi ambazo mkulima anaweza kufanya kuweka usafi wa mazingira unaofaa shambani kwao. Orodhesha shughuli hizo (palizi, kuondoa magugu na sehemu za mimea zilizoathiriwa shambani) 3. Wagawe vijana katika vikundi vidogo vidogo na kiambie kila kikundi kichunguze sehemu moja ya shamba. Waulize vikundi kile kinachotakiwa kufanya 4. Jaribu kuhitimisha ni wakati gani mkulima anatakiwa aanze palizi na anatakiwa aondoshe nini na abakishe nini shambani. A.9.1. Zoezi: Kupandikiza miche (mboga za majani n.k.) Muda: Wastani wa saa 2 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea Upandikizaji huifanya mimea iwe minyonge. Kama upandikizaji haufanywi kwa makini, mimea haiwezi kukua vizuri. Kabla ya kwenda kwenye shamba darasa, waulize vijana maswali yafuatayo na orodhesha majibu yao kwenye chatipindu. Je, unadhani kupandikiza miche kuna hatua gani mbalimbali? Je, unafikiri ni mambo gani muhimu zaidi kufanya wakati unapopandikiza miche? Kwa nini unadhani ni muhimu kupandikiza miche jioni? Kwa nini unadhani mkulima lazima apandikize miche imara na si ile yenye afya ambayo imeambukizwa magonjwa? 40

Kwa nini ni muhimu kupandikiza miche ikifikia umri unaofaa, yaani si michanga sana wala si mikubwa sana? Je, unadhani mkulima atafanya nini kuipunguzia miche unyonge baada ya kupandikiza?(kutandaza nyasi na majani) Sasa unaweza kwenda na vijana kwenye shamba litakalopandikizwa miche inayotoka kwenye kitalu/vitalu. Waulize vijana maswali yafuatayo: Je,shamba limeandaliwa tayari kwa ajili ya kupandikiza miche? Kama ndiyo, kwanini unadhani liko tayari? Kama bado, unadhani kunahitajika kufanywa kitu gani ili kuanza kupandikiza miche? Sasa unaweza kuwaambia vijana washiriki katikakupandikiza miche. 1. Jadili hatua mbalimbali za kupandikiza miche 2. Mwagilia maji kitalu cha mbegu na onyesha namna ya kung oa miche kutoka kwenye kitalu 3. Waambie vijana wote wang oe miche mingi kutoaka kwenye kitalu 4. Onyesha namna ya kusafirisha miche mapaka shambani 5. Waambie vijana wakusnaye miche yote iliyong olewa kutoka kwenye kitalu na waipeleke shambani 6. Jadili na waonyeshe vijana namna ya kupandikiza miche kwenye shamba darasa 7. Waambie vijana wapandikize miche yote iliyobaki 8. Waambie vijana wamwagilie miche iliyipandikizwa Ukishamaliza, toa muhtasari wa hatua zote za kupandikiza miche. Taarifa ya msingi. Hatua za upandikizaji miche Vipengele muhimu 1. Kutayarisha shamba darasa Udongo uliolimwa na kutiwa mbolea vizuri, hakuna magugu 2. Kumwagilia kitalu chamnegu 3. Kung oa miche Jioni, chagua miche imara na yenye afya kwa ajili ya kupandikiza, bakisha udongo kwenye mizizi na uwe mwangalifu 41

usiharibi mizizi 4. Kusafirisha miche Muda mfupi,hakikisha kuwa imelowa na iwe kivulini. Miche iliyong olewa iondolewe kwenye udongo kwa muda mfupi tu (< saa moja). 5. Kupandikiza miche Jioni, kuwa mwangalifu usiharibu wala kupinda mizizi 6. Kumwagilia shamba darasa Mimea isikose maji baada ya kupandikizwa - isinyauke A.10. Mada ndogo: Umwagiliaji maji Malengo: Kuelewa maana ua umwagiliaji maji Kuelewa njia mbalimbali za umwagiliaji Kama ilivyotajwa hapo awali, kudhibiti maji shambani ni muhimu sana kwa ajili ya kulima mazao yanayostawi. Mvuainapokuwa kidogo sana, mhulima anatakiwa kutafuta njia ya kuyapatia mazao maji. Kuna njia mbalimbali za kumwagilia mazao. Ni muhimu kwa vijana kujua njia mbalimbali za umwagiliaji zinazotumika katika eneo hili. Pia wanahitaji kuelewa kuwa udongo unanyonya maji kwa haraka kiasi gani (kiasi cha udongo kupitisha maji)na kwa kiasi gani unavyoweza kuhifadhi maji (kiasi cha udongo kuhifadhi maji). Kwa kujua mambo haya mawili kutawasaidia kumwagilia mashamba yao kwa njia bora zaidi A.10.1. Zoezi: Kuelewa aina ya umwagiliaji na upitishaji maji Muda : Wastani wa saa2 Vifaa: Kiasi cha chupa 20 za maji ( lita 15 05), kisu kikali. Kilo 1ya udongo wa mchanga, kilo 1 ya udongo wa mfinyanzi na maji 42

HATUA: Majadiliano ya Kikundi (Dakika 30) 1. Waulize vijana kama yuko anayefahamu umwagiliaji ni nini. Mara baada ya maana ya umwagiliaji kueleweka kwa kila mmoja,waulize vijana kwanini wanafikiria ni muhimu kumwagilia mimea wakati wa ukame. 2. Waulize vijana kama wanafahamu njia mbalimbali za umwagiliaji mazao shambani kwaonahalafu wabainishe njia zinazotumika na wakulima kwenye eneo/kijiji chao 3. Waulize vijana wanafikiri kuna umuhimu gani katika kumwagilia mazao yao na katika kuchagua njia inayofaa kumwagilia 4. Toa muhtasari wa matokeoya majadiliano: aina ya mazao, hatua ya mazao (kitalu au shambani), ukubwa wa shamba, mteremko na aina ya udongo 5. Pitia pamoja na vijana aina ya udongo uliyojadiliwa kwenye moduli iliyopita. Anza kueleza wazola sifa za udongo na namna zinavyoathiri kiwango cha upitishaji maji na uwezo ya kuhifadhi maji Kuonyesha na kufanya majaribio (saa 1 dakika 30) 1. Kata sehemu ya juu ya chupa (sehemu nyembemba) za chupa nnekwa kisu halafu toboa matundu sehemu ya kitako cha chupa mbili zamaji. Jaza udongo kwenye theluthi moja ya udongo kwenye chupa zenye matundu chupa moja udongo wa mchanga na chupa nyingine kiasi sawa cha udongo wa mfinyanzi. Tayarisha kiasi cha maji cha kutosha kwenye chupa nyingine (1/4 ya chupa) na weka alama kiwango cha maji. 2. Mwambie kijana mmoja aangalie saa. Mimina maji kwa uangalifu kwenye udongo uliyomo kwenye mojawapo ya chupa na anza kupima muda utakaochukua kwamaji kunywea kwenye udongo hadi kwenye chupa iliyowekwa chini ya udongo (inapoanza kudoda juu ya chupa na inapoacha kudoda) 3. Tayarisha kiasi sawa cha maji na mwambie klijana mwingine kufuatilia muda. Mimina maji kwa uangalifu juu ya udongo na kwenye chupa ya pili halafu pima muda utakaochukua kwa maji kunywea kwenye udongo 4. Jadili tofauti za muda uliotumika kwa maji kunywea katika aina mbalimbali za udongo (kiwango cha upitishaji maji) 5. Linganisha kiasi cha maji kilichoweza kunywea kwenye udongo na jadili kulitokea nini kwamaji yaliyobaki kwenye udongo(uwezo wakuhifadhi maji) 43

6. Wagawe vijana katika vikundi vya vijana watatu watatu au wanne na waambie warudie zoezi. Waambie kila kikundi kikusanye aina mbili tofauti za udongo karibu na wanapolutania kwa ajili ya SDSMV au kutumia kiasi sawa cha udongo kama uliotumiwa kwa zoezi. Wasaidie vijana wakati wa zoezi hilo na hakikisha kuchukua vipimo vyote vya majaribio Majadiliano ya Kikundi (Dakika 15) Jadili matokeo ya majadiliano kuhusiana na umwagiliaji. Udongo wenye uwezo mkubwa wa kuhifadhi maji unaweza kumwagiliwa mara chache zaidi ingawa kwa kutumia kiasi kikubwa cha maji. Kuhusu udongo wenye kiwango kikubwa cha upitishaji maji, maji yatatiririka haraka sana juu ya usawa wa bonde au mtaro kwa hiyo nilazima vijengwe kwamwinuko mkali. Toa muhtasari wa mambo yaliyoonekana katika jaribiona majadiliano. Maswali ya kuongoza majadiliano Tutajuaje kuwa tumemwagilia maji ya kutosgha? Je, tunatakiwa kumwagilia kila siku au mara moja kila baada ya siku mbili au tatu? Je, uwezo wa udongo kuhifadhi maji unaathari gani katika umwagiliaji Tutawezaje kukagua kama mmea/zao linahitaji kumwagiliwa? Je, ni dalili gani zinazoonyesha upungufu wa maji katika mmea/zao? Je, tutawezaje kutumia mteremko wa shamba kusambaza maji kwa usawa? Je,zao linahitaji kiasi gani cha maji kinacholingana kila siku? Mkulima afanyaje ili kupunguza mtiririko wa maji kwenye mtaro (umwagiliaji wa mtaro)? Kwa nini inatubidi kufikiria kuhusu mifereji ya kutoa maji mashambani vilevile tunapopanga umwagiliaji? 44

A.11.1. Zoezi: Urutubishaji Ardhi. Muda: Wastani wa saa 1 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea 1. Waulize vijana kama wanafahamu mbolea ni nini na kwa nini wakulima wengi wanatumia mbolea kwenye mazao yao. 2. Waambie vijana wataje aina mbalimbali za mbolea wanazozifahamu ambazo mkulima anaweza kutumia na waziorodheshe (mbolea za asili: mboji, samadi,mabakiya mimea nambolea za kemikali: urea, DAS, TSP, Potasium Kompaundi (NPK)). 3. Viambie vikundi vijadiliane kwa vikundi vidogo tofauti kati ya aina mbalimbali za mbolea, madhumuni yake na namna zinavyotakiwa kutumika. 4. Amua na vijana ni aina gani za mbolea zitumike kwenye shamba darasa na kiasi kinachotakiwa A.11.2. Zoezi: Utiaji mbolea wa mara ya pili Muda: Wastani wa saa moja Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea 1. Mazao mengi hayahitaji utiaji mbolea wa mara ya pili. Waulize vijana kwa nini wanafikiri kuwa wanahitaji (mbolea za naitrojeni zinachujisha au vukiza kwa urahisi udongo wa juu na kuhitaji kuongezwa baada ya miezi 2-3) 2. Jadili ni mazao gani katiya manne yaliyolimwa yanahitaji utiaji mbolea wa mara ya pili na zinahitajika mbolea za aina gani na zitumiwe lini (mazao ambayo hayajafikia hatua ya uzazi, baada ya miezi miwili,mbolea za naitrijeni, wiki chache kabla mazao hayajafikia hatua ya uzazi). Jadili njia bora zaidi ya kutia mbolea. Waambie vijana wafanye kwa vitendo shambani. 45

A.11.3. Zoezi: Ulindaji wa Rutuba ya udongo katika kilimo cha kutumia mbolea ya asili/kimaumbile Muda: Wastani wa dakika 20 Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea Katika kilimo cha kutumia mbolea ya asili/kimaumbile wakulima wanatumia njia mbalimbali za kutunza na kuboresha rutuba ya udongo wao Bungua bongo na wanafunzi kuhusu njia mbalimbali mkulima anazoweza kulinda rutuba ya ardhi yake (mbolea za kemikali, samadi kutoka kwa wanyama, matumizi ya mazao jamii ya kunde katika kilimo cha kubadili mazao ya mizizi mifupi na mirefu, kutumia mboji). Jadiliana na wanafunzi, iwapo mbolea za kemikali/chumvichumvi haziwezi kutumika, tutatumiaje ainanyingine za kilimo kwenye shamba darasa letu. Tumia matokeo ya majadiliano katika kupanga shughuli za shamba darasa Kutegemea mboji Mboji ni mbolea ya takataka zilizoozeshwa na bakteria na viumbe hai vingine aghalabu za kikaboni kwa kipindi fulani. Mboji ni nafuu na rahisi kwa kutengeneza. Aina mbalimbali za vitu vya kikaboni ambavyo mara nyingi vinaonekana kuwa ni takataka katika mashamba na nyumbani kama vile maganda ya mboga, maagugu, matunda, majani na takataka za jikoni vinaweza kutumika. Kutumia mboji kunaongeza rutuba ya udongo kwa uongezaji watija na mavuno shambani. Mkulima anaweza kutengeneza mboji yeye mwenyewe ili kuokoa fedha. Ni njia salama katika kilimo na hivyo kuhifadhi ardhi kwa vizazi vijavyo A.11.4. Zoezi: Je, kutengeneza mboji ni nini na tunaweza kutumia vitu gani? Muda: Wastani wa dakika 40 Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea. Ili kulinda rutuba ya udongo katika kilimo cha kutumia mbolea ya asili, mkulima anawezakutumia mboji anayoweza kuitengeneza yeye mwenyewe. Waulize vijana kama kuna mtu wanayemfahamu katika jamii yao anayetengeneza mboji. Kama wanamfahamu, waulize vijana iwapo wanajua mtu huyo anavyofanya. Eleza kwa muhtasari kutengeneza mboji ni nini na kwamba tunawezakutumia aina zote za vitu vya kikaboni vinavyoonekana kuwa ni takataka mashambani na nyumbani. Bungua bongo kuhusu aina mbalimbali za vitu vya kikaboni vilivyopo katika jamii vinavyoweza kutumika kwa kutengenezea mboji. 46

Waambie vijana wakusanye kwenye gunia kwa jumla moja takataka za kikaboni zilizoorodheshwa na kuzileta kwenye somo lijalo kwa ajili ya kutengeneza mboji A.11.5. Zoezi: Kutengeneza Mboji Muda: Wastani wa dakika 60 Vifaa: Ardhi, kasha, takataka za kikaboni, samadi, panga, sepeto, magunia, ndoo ya kumwagilia Eleza kuwa kuna njia mbalimbali za kutengeneza mboji. Mboji inawezakutengenezwa kwenye kasha, rundo, shimo, na kwenye rundo lililofukiwa kidogo (nusu mita), kutegemea hali ya mtiririko wa maji machafu mahali hapo. Jadiliana mfumo wa maji machafu na vijana na chagua namna ya kutayarisha mboji. Kama ni mboji ya shimo, mashimo matatu ya mboji yatachimbwa ubavuni kwa mfuatano. Mashimo hayo yatakuwa na kina cha sentimita 50, upana wa sentimita 150, na urefu kulingana na nafasi, kama inavyoonyeshwa kwenye Mchoro wa 1. Vitu vitakavyotumiwa, vinarundikwa kwa mpango maalumu kama ifuatavyo. 1. Tabia ya udongo wa mfinyanzi (a) inatandazwa chini ya shimo kuzuia upotevu wa maji yatakayomwagiliwa kwenye rundo 2. Tabaka ya matawi ya mti au mabua ya nafaka ya sentimita 15 (b) chini ya vitu vya kutengenezea mboji, husaidia kuzuia mmomonyoko 47

3. Tabaka ya vitu vya sentimita 15-30 (c ) kama vile mabaki ya mazao yaliyovunwa, nyasi, takataka za jikoni, n.k. huwa ndilo rundo kuu 4. Juu kuna samadi ya kina cha sentimeta 10 20 (d) ambayo hurutubisha mboji nakuharakisha kuoza 5. Katika hatua hii, umwagiliaji maji wa kutosha (lita 600-800 za maji kwa kila mita ya ujazo ya mboji) hufanywa. 6. Tabaka nyembamba ya udongo (e) huziba tabaka zilizotangulia ili kuhakikisha joto linabaki ndani 7. Rundo huongezeka kwa kurudia tabaka (c ), (d), umwagiliaji wa maji na tabaka (e) 8. Mwisho rundo linaezekwa tabaka la nyasi au mabua ya mimea sentimeta 20 (f) Rundo lililokamilika linaachwa lioze kwa siku 15 20 ambapo litageuzwa kutoka shimo 1 hadi la 2 ambapo litakaa kwa siku nyingine zaidi 15 20 kabla ya kugeuzwa na kuingizwakwenye shimo la 3. Mboji bora ya mwisho itakuwa tayari kutumiwa baadaya siku nyingine 15 20. Zingatia: Chomeka mti mrefu kwenye rundo tangu mwanzoili kuhakikisha hali joto. Kama mti una joto, inaonyesha kwamba mboji inaoza na ikiwa baridi inaonyesha kupungua kwa uozaji wa mboji. 48

A.11.6. Zoezi: Kukagua, Kugeuza na Kutumia Mboji. Vitu vyote vilivyotumika kutengenezea mboji ni lazima vioze kwa ukamilifu kabla ya kutumiwa shambani. Kwa hiyo vijana ni lazima wajifunze kukagua hali mara kwa mara. Watakagua kwa mti au kwa kuingiza mkono kwenye mboji. Kama vitu vya kutengenezea mboji vinaoza kwa ukamilifu, halijoto itakaribia 80 0 C. mti wakukagulia utakuwa na joto kali na mvuke kidogo utaonekana kwenye mti. Kama watakagua kwamkono, watumbukizemkono kwenye mboji kwa sekunde chache sana. Wakati halijoto inapoanza kupungua, (baada ya wiki mbili) mboji inahitaji kugeuzwa na kuchanganywa kwenye rundo jingine au shimo, na vitu ambavyo havijaoza kwa ukamilifu viwekwe katikati kadiri iwezekanavyo. Lazima igeuzwe mara mbili. Baada ya siku 45 60 mboji itakuwa tayari na inaweza kutumiwa shambani. Matumizi yake yataanza na ile mimea inayohitaji virutubisho vingi zaidi,mimea jamii ya kunde na hata mazao ya kwenye ardhi iliyorutubishwa kwa mboji msimu uliyopita, haihitaji mboji. Kiasi cha matumizi kitategemea aina ya mazao, hata hivyo kwa kawaida mboga za majani zinahitaji mboji kiasi cha kg/m 2 4-6. Mboji ni lazima ichanganywe kwenye udongo kabla ya kupanda mazao A.12. Mada ndogo: Kulinda shamba la Kilimo Malengo: Kuelewa umuhimu wa kulinda shamba la kilimo Kubainisha na kuorodhesha njia mbalimbali za kulinda mimea shambani Kueleza mbinu mbalimbali za kulinda shamba. Shamba darasa ni miongoni mwa sehemu muhimu za maisha ya vijana ambazo wanahitaji kulinda. Kuhakikisha kwamba, shamba darasa linalindwa ipasavyo, ni vizuri kwa vijana kushirikiana na jamii na kuomba msaada wao. Kama wakiridhishwa kuhusu umuhimu wa mradi, ulinzi wa shamba/bustani utafanikiwa. Matatizo kama ya kuingiliwa na wezi na wanyama yataepukwa kwa urahisi. Kama matatizo ya usalama yatatokea kuhusiana na shamba darasa/bustani ya SDSMV, omba kufanya mkutano na viongozi wa jamii kujadili tatizo hilo na kuomba kusaidiakushughulikia matatizo ya usalama. 49

A.12.1. Zoezi: Kulinda Shamba Letu Muda: Wastani wa saa 2 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea Mifano ya matatizo kwenye mashamba yasiyolindwa mbuzi huingia na kuharibu, na kula mazao ng'ombe huingia na kula kila kitu sungura huingia na kula saladi na kabichi changa panya huingia na kula mbegu za alizeti mavuno yanaweza kuibwa wakati wa usiku mazao hufa kutokana na ukame, wadudu au wadudu waharibifu 1. Endeshs majadiliano mafupi na vijana kupitia vipengele vyote walivyokwishapitia kabla kuhusu wanataka kuyalinda mashamba yao kutokana na nini? Ili kuwasaidia kukumbuka, unaweza kutaka kuuliza maswali yafuatayo Kwa nini inatubidi kulinda shamba letu? Kutatokea nini kama hatutalinda vizuri mashamba? Tutafanyaje kuboresha hali hii? 2. Wagawe vijana katika makundi manne. Waambie kila kikundi waandike au kuchora: Njia mbili za kulinda shamba dhidi ya wanyama wanaokula mimea. Njia moja ya kulinda dhidi ya ukame Njia mbili za kushughulikia wadudu waharibifu Njia mbili za kulinda dhidi ya wezi 3. Waambie watu wawili kutoka kila kikundi wawasilishe na kueleza hatua walizopanga kuchukua pamoja 50

A.12.2. Zoezi: Kujenga uzio na uzio zaidi. Muda: wastani wa saa 1 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea, karatasina penseli 1. Wapeleke vijana kwenye matembezi katika jamii na waambie wachague aina mbalimbali za uzio na maboma wanayoona 2. Waambie wawadadisi baadhi ya wakulima ambao wanakutana nao wakati wa matembezi yao. Baadhi ya maswali wanayoweza kuwauliza wakulima ni:- Kwa nini mlichagua aina hiyo ya uzio? Kuna faida na hasara gani za uzio mlionao? Vifaa gani mmetumia kujenga uzio wenu? Je, uliujengaje? Ilichukuwa muda gani kujenga? Je, umeridhika na uzio huo? Je, ungependelea kuwa na aina mbalimbali za uzio? Kwa nini au kwa nini hapana? 3. Baada ya matembezi na usaili, tafuta mahali penye kivuli kukaa na kufanya majadiliano ya jumla kuhusu wamejifunza nini. Wakati wa majadiliano, andaa mpango wa jinsi ya kupata vifaa ambavyo mtahitaji kwa ajili ya kujenga uzio na waambie vijana walete vifaa vya kujenga uzio kutoka nyumbani kwao kwa ajili ya somo linalofuata A.13. Mada ndogo: Kuvuna A.13.1. Zoezi: Wakati na mbinu za kuvuna Mazao mbalimbali katika shamba darasa yanahitaji kuvunwa siku chache kabla au wakati yamekwisha komaa kabisa, kutegemea aina ya mazao na matumizi ya mazao yaliyovunwa. Kila zao lina njia yake ya kuvuna. 51

Muda: Wastani wa dakika 30 Vifaa: Hakuna Waulize vijana kama wanajua namna ya kuvuna mazao mbalimbali yaliyolimwa kwenye shamba darasa. Je, wanawajua wakulima wowote wanaotumia mbinu mbalimbali na kwa nini wanavuna tofauti? Jadili namna ya kuvuna mazao mbalimbali kwenye shamba darasa. Waulize vijana ni wakati gani wa siku unaofaa zaidi kuvuna mahindi na mbogamboga Nyanya wakati mwingine zinavunwa zikiwa bado mbichi na wakati mwingine zikiiva. Jadili kwa nini na kwa nini ni muhimu kila mara kufikiria unachopanga kufanya na mavuno kuhusu lini na namna inavyokubidi kuvuna zao hilo. A.14. Baada ya Kuvuna A.14.1. Zoezi: Namna ya kupunguza hasara baada ya kuvuna. Mkulima bado anapoteza asilimia kubwa ya mazao yake kati ya kuvuna na utumiaji au kuvuna mazao yake. Kama mambo mengi ambayo mkulima anaweza kufanya kupunguza hasara ya baada ya kilimo, kuanzia wakati wa kuvuna, na kufuatiwa na usafirishaji kutoka shambani, uhifadhi na ufungashaji. Vijana watajadili mkulima anachotakiwa kufanya kupunguza hasara baada ya mavuno wakati wa shughuli mbalimbali za baada ya kuvuna. Lengo: Kujifunza kuhusu mkulima anapaswa kufanya nini kupunguza hasara baada ya kuvuna Muda: Wastani wa saa 1 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea Hatua: Kubungua bongo (Dakika 20) 1. Anza mada ya namna ya kupunguza hasara baada ya kuvuna. Waeleze vijana kuwa hasara baada ya kuvuna inaweza kugawanyika katika hasara ya kiasi (kg) na ubora. Aina mbili zote zinafanya hasara ya kiuchumi ya mazao. 52

2. Waulize vijana kuwa mkulima atafanya nini kupunguza hasara ya baada ya kuvuna. Andika hoja mbalimbali za hatua za uzingatiaji uliotajwa kwenye karatasi kubwa 3. Jadili hoja mbali za hatua atakazozingatia mkulima zilizotajwa na zipange kwenye shughuli mbalimbali za shughuli za baada ya kuvuna (kuvuna, usafirishaji wa mazao, uhifadhi, usafirishaji, ufungashaji na uuzaji) Majadiliano ya vikundi vidogo vidogo(dakika 40) 4. Wagawe vijana katika vikundi vidogo na kiambie kila kikundi kichague mojawapo ya mazao yanayolimwa katika eneo 5. Kwa zao walilolichagua, kiambie kila kikundi kijadili hoja za hatua za uzingatiaji ambazo mkulima hana budi kuchukua kwa shughuli mbalimbali za baada ya kuvuna ili kupunguza hasara ya mazao. Waambie kikundi watoe taarifa ya matokeo ya mazungumzo yao kwenye karatasi kubwa 6. Kiambie kila kikundi kiwasilishe matokeo ya majadiliano yao 7. Jadili mawasiliano mbalimbali 8. Toa muhtasari wa hoja za hatua za uzingatiaji ambazo mkulima hana budi kuchukua wakati wa shughuli mbalimbali za baada ya kuvuna ili kupunguza hasara ya mazao. Maelezo kwa Mwezeshaji: Swali lakuongoza Je, kufanyike nini kuhifadhi ubora wa mazao yaliyovunwa Taarifa ya Awali/Usuli: Hoja za kuzingatia wakati wa kuvuna kupunguza hasara baada ya kuvuna. Muda unaofaa wa kuvuna (mazao yasiive sana) Zuia kuharibika kwa mazao Kutenganisha mazao yaliyoathiriwa na yenye magonjwa. Matumizi ya aina safi ya kuvuna. Uvunaji wa rejareja unapunguza haja ya kuhifadhina hasara ya uhifadhi Punguza kuharibika kwa mazao wakati wa usafirishaji 53

A.14.1. Zoezi: Utayarishaji/Uhifadhi wa mazao Mazao mapya ya kilimo yaliyovunwa (aina ya mizizi, mbogamboga na/au matunda) mara nyingi yanaweza kusindikwa ili kuongeza muda wa kutunza/uhifadhi wa mazao. Kutegemea aina ya mazao, kunahitajika kusafishwa kwa maji, kukatwakatwa silesi, kuchemshwa, kukaushwa (kwa jua), kusagwa na/au kufungashwa kabla ya kuhifadhiwa mahali salama na pa kavu. Kwa wenyeji, njia mbalimbali za kusindika huwa zinafahamika. Vijana watajadili na kufanya kwa vitendo na mwezeshaji mwenyeji njia mbalimbali za kusindika mazao ya kilimo Muda: Saa 1 na dakika 30 Vifaa na matayarisho: Bainisha mwezeshaji mwenyeji anayefahamu usindikaji wa mazao ya kilimo ya chakula, mazao mapya, visu na sufuria. Majadiliano ya wote (Dakika 20) 1. Anza mada ya usindikaji/ na utunzaji wa chakula. Jadili na vijana madhumuni ya usindikaji/utunzaji wa chakula 2. Waulize vijana kama wanajua mifano mbalimbali ya utunzaji wa mazao ya kilimo (chakula) inayofanywa na watu katika eneo Vitendo (saa 1) 3. Mtambulishe mwezeshaji mwenyeji na mwombe aonyeshe na/au kufanya kwa vitendo na vijana baadhi ya desturi za wenyeji za utunzaji wa chakula 4. Jadili njia mbalimbali za utunzaji wa chakula na kuna mahitaji gani muhimu na maeneo yanayohitaji uzingativu maalumu katika utunzaji wa chakula (usafi, unyevunyevu na uhifadhi ghalani/ufungashaji) Majadiliano ya wote: (Dakika 10) Toa muhtasari wa somo A.14.3. Zoezi: Ghala bora Hasara inayotokana na uhifadhi ni tatizo kubwa. Wadudu waharibifu na magonjwa yanaweza kuharibu sehemu ya akiba kama mazao hayakuhifadhiwa mahali safi, pakavu na palipolindwa kwa ukamilifu. Vijana watajifunza aina mbalimbali za ghala za kuhifadhia zinazotumiwa katika eneo lao kuhifadhi aina mbalimbali za mazao ya kilimo 54

Lengo: Kujifunza kuhusu sifa muhimu za ghala bora Muda: Saa 1 dakika 30 Vifaa na matayarisho: Kabla ya somo bainisha idadi ya ghala zilizopo karibu na fanya mpango vijana waweze kuruhusiwa kuzitembelea Bungua bongo (Dakika 15) 1. Anza mada ya ghala bora 2. Waulize vijana masharti muhimu zaidi ya uhifadhi na maghala ya kuhifadhia ni yapi kwamazao ya kilimo kwa kipindi cha miezi kadhaa. Andika masharti hayo kwenye karatasi kubwa. Ongeza masharti yaliyoachwa kwenye orodha kama inahitajika 3. Jadili masharti ya uhifadhi Ziara (dakika 50) 4. Nenda na vijana kwenye ghala za kuhifadhia zilizopo karibu na jadili na vijana hali/masharti ya ghala hizo. Kama ikiwezekana zungumza na wamiliki na waulize faida na hasara za ghala zao. 5. Jadiliana na vijana ni ghala gani bora zaidi waliyoioana na kwa nini ni bora. Majadiliano ya wote: (dakika 15) 6. Toa muhtasari wa sifa muhimu za ghala ya kuhifadhia mazao 7. Jadili uwezekano wa kujenga ghala na SDSMV ya kuhifadhia mazao ya shamba darasa. Kama ikiwezekana andaa mpango wa kazi Maelezo kwa mwezeshaji: Maswali ya Kuongoza Ni kiasi gani cha mazao kinapotea wakati wa uvunaji, usafirishaji na uhifadhi wa mavuno? Je, kuna sababu gani kuu za hasara hiyo? Je, tutawezaje kupunguza hasara hii wakati wa uhifadhi wa mavuno? Je, tunawezaje kuzuia wadudu waharibifu na magonjwa visiingie kwenye ghala ya kuhifadhia? 55

Je, tunawezaje kudhibiti/ kukagua ubora wa mazao yaliyohifadhiwa? Je, aina mbalimbali ya mazao ya kilimo yanaweza kuhifadhiwa ghalani kwa muda gani? (mapya, yasiyosindikwa) Je, mkulima atafanya nini kuongeza muda wa kuhifadhi mazao ya kilimo? Je, ni njia zipi zinazotumiwa zaidi katika eneo kutunza mazao ya kilimo? Taarifa ya Awali/Usuli: Sifa muhimu za ghala 2. Ghala bora haina budi kutunza mazao katika hali ya baridi na kavu. Lazima pia iweze kulinda mazao dhidi ya panya, ndege, wanyama wa shambani na wezi. Ghala nyingi ( isipokuwa baadhi ya ghala zenye ukuta imara za zege zinaweza kuzibwa) hazizuii kuingia kwa wadudu Ghala lazima ijengwe mahali pakavu, mbali na matawi ya miti, vinginevyo panya wanaweza kuruka kutoka kwenye matawi ya miti na kuingia ghalani. Ghala lazima liwe na paa linalomwaga maji ya mvua na lenye kivuli. Ghala hainabudi kuinuliwa juu ya usawa wa ardhi ili kuzuia maji yasinywee ghalani na kuzuia panya na wanyama wa shambani wasifikie mazao yaliyohifadhiwa. Kama zitatumiwa nguzo za miti/mbao kuinulia jengo la ghala ni lazima vikingwe dhidi ya mashambulizi ya mchwa, mara nyingi oili chafu ya magari hutumiwa kuipaka miti/mbao. Kinga dhidi ya panya lazima zifungwe kwenye miguu ya ghala kuzuia panya wasipande ghalani. Kinga dhidi ya panya zitafanya kazi tu kama ghala itainuliwa angalau mita moja kutoka ardhini na hakuna mimea au nguzo karibu na ghala zitakazowawezesha panya na panya buku kupanda. Ghala haina budi kujengwa angalau umbali wa mita 1 kutoka kwenye mgongo na miti. Paka na mbwa husaidia kuwafukuza panya 2. Chanzo: T., Namanda, S., Mwanga, R.O.M., Khisa, G., Kapinga, R. (2205) Manual for Sweetpotato Integrated Production and Pest Management Farmer Field Schools in sub-saharan Africa. International Potato Center, Kampala, Uganda 56

A.14.4. Zoezi: Kuuza Mazao Muda: Saa nyingi katika masaa mbalimbali Vifaa: Vifaa vinavyotakiwa kwa ufungashaji, utangazaji na usafiri wa mazao Hatua: 1. Kutegemea mikakati ya soko iliyotayarishwa, saidia vikundi mbalimbali matayarisho yao kwa ajili ya uuzaji wa mazao waliyovuna 2. Warahisishie vijana kuuza mazao yao. Waambie vijana watunze kumbukumbu zao vizuri na kiasi cha mazao walichouza, bei waliyopata, gharama walizotumia, muda waliotumia kutayarisha na kuuza mazao yao na faida waliyopata 3. Baada ya kuuza mazao yao, waambie vikundi wawasilishe matokeo yao ya shughuli za mauzo, wakieleza uzoefu wote waliopata, gharama na faida waliyopata 4. Jaribu kuhitimisha masomo muhimu zaidi waliyojifunza 57

Juzuu ya 2 Mtaala wa SDSMV Mada za Stadi za Maisha na Uanzishaji Shughuli 58

Yaliyomo: Mada/Zoezi uk Mazoezi ya Stadi za Maisha na Uanzishaji Shughuli J.1.1. Zoezi: Kupanga kwa ajili ya Baadaye J.2.1. Zoezi: Utunzaji Kumbukumbu J.3.1. Zoezi: Kutoa maamuzi J.4.1. Zoezi: Umuhimu wa Usafi bora J.4.2. Zoezi: Maandalizi Bora na Usafi wa Mtu J.5.1. Zoezi: Maji ni Uhai Ina maana gani? J.6.1. Zoezi: Desturi za Lishe Bora J.7.1. Zoezi: Utunzaji wa Kumbukumbu za Ushughulikiaji Mazao J.8.1. Zoezi: Mambo yanayolingana kuhusu kupanga biashara na kupanga katika kilimo J.9.1. Zoezi: Kuugua na kupata nafuu J.9.2. Zoezi: Magonjwa katika Maisha J.9.3. Zoezi: Jaribio la Kupiga Mpira wa VVU J.9.4. Zoezi: Mchezo wa Ugonjwa wa UKIMWI J.10.1. Zoezi: Je, Ajira kwa Watoto ni nini? J.10.2. Zoezi: Kutengeneza Sanamu Inayoishi J.10.3. Zoezi: Maigizo kuhusu Ajira J.10.4. Zoezi: Mgawanyo wa Kazi wa Kila siku wa Wavulana na Wasichana J.11.1. Zoezi: Haki za Ardhi ya Kijiji na Mali J.12.1. Zoezi: Kutayarisha Mkakati wa Kuuza Mazao ya Shamba Darasa J.12.2. Zoezi: Kumtembelea Mjasirianmali 2 2 3 4 4 5 7 8 8 8 10 11 11 13 14 17 18 23 26 26 59

J.12.3. Zoezi: P zote (Bidhaa,Mahali, Bei, Utangazaji, Watu na Mpango) J.12.4. Zoezi: Kuuza! Igizo Babu J.13.1. Zoezi: Kiuzwe Bei gani? J.13.2. Zoezi: Kutabiri Faida na Hasara J.14.1. Zoezi: Kubungua Bongo Wazola Biashara J.14.2. Zoezi: Uchambuzi wa Kina wa Mawazo ya Biashara J.14.3. Zoezi: Yanahitajika Kuunda Bidhaa au Huduma J.14.4. Zoezi: Zana za Utunzaji Hesabu za Biashara J.15.1. Zoezi: Gharama na Faida J.16.1. Zoezi: Kuweka Mtandao wa Utando wa Buibui Kujitayarisha kwa siku ya mahafali Mtaala wa SDSMV 27 29 33 36 37 41 43 46 52 57 60 61 60

Shughuli za Stadi za Maisha na Uzalishaji Shughuli J.1.1. Zoezi: Kupanga kwa ajili ya Baadaye Muda: Wastani wa saa 1 1. Wagawe vijana katika vikundi vya watu 8 au pungufu. 2. Kiambie kila kikundi kifikirie hadithi ( au hadithi iliyosimuliwa kwa wimbo) kuhusu umuhimu wa kupanga kwa ajili baadaye kwenye kilimona maisha. Mpango huo hauna budi kujumuisha maelezo mengi kuhusu watu, mahali, na hali zinazohusishwa. Wahimize watuamie kusema, kuimba na/au kuigiza kuwasilisha hadithi yao 3. Waambie kila kikundi kiwasilishe hadithi yao. Wahimize wasikilize hadithi nyingine kwa makini. 4. Waambie vijana watoe maoni kuhusu kila hadithi. Kwa mfano, je,ni halisi, je inafanya wajihisi namna gani? Ni mambo gani muhimu yaliyojitokeza? 5. Vijana wakimaliza kutoa mawazo yao, wahimize watafakari mawazo hayo kwa walichokiona. Baadhi ya maswali ya msaada ni:- Je, hadithi zimeonyesha nini kuhusu uhusiano kati ya watu katika jamii? Je, inaonyesha nini kuhusu mitazamo ya watu? Je zimeonyesha nini kuhusu changamoto kubwa zaidi zinazokabili jamii? Zingatia: Kama mbadala, wewe au mmoja wa vijana anaweza kuanza na sentensi mbili au tatu za kwanza za hadithi. Halafu mwombe mmoja apendekeze mistarimiwili au mitatu ifuatayo. Halafu mwambie mtu mwingine apendekeze mistari miwili au mitatu ifuatayo. Endelea kwa mtindo huo mpaka hadithi ifikie mwisho au imeeleza hoja muhimu mbalimbali 61

J.2.1. Utunzaji Kumbukumbu Muda: Wastani wa saa 1 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea 1. Jadili na vijana umuhimu wa kutunza kumbukumbu katika kuendesha biashara (kujua kama biashara inaingiza faida,ni mambo gani yanayohitajika, kuboreshwa siku zijazo, kulinganishambinu mbalimbali za kazi n.k.) 2. Eleza kuwa katika shamba darasa vijana watatakiwa kupanda mazao yao kama biashara na kwamba wanalinganisha pia desturi mbalimbali (IPM dhidi ya jodi). Kwa hiyo ni muhimu kwa vijana kutunza kumbukumbu za kila wanachofanya kwenye shamba darasa. 3. Waulize vujana ni ainagani ya kumbukumbu wanazotakiwa kutunza na waziorodheshe kwenye karatasi ya bango kitita (tarehe ya kupanda, kiasina bei ya mbegu, mbolea za kikaboni na dawa za kuulia wadudu (za viumbe) walizotumia tarehe za desturi zote, muda wa kazi, (saa) zana zinazohitajika, mavuno (kg), gharama za mauzo, fedha walizopata kwa mazao, n.k.) 4. Jadili kumbukumbu zilizoorotheshwa na kiambie kila kikundi kidogo kikamilishe orodha kwa mazo wanayoshughulikia. 5. Kiambie kila kikundi kiwasilishe orodha yao ya mwisho ya kumbukumbu itakayotunzwa na ongeza pale inapohitajika 6. Viarifu vikundi kwamba watatakiwa kuanza kutunza kumbukumbu kwa mashamba yanayowahusu kuanzia sasa na kuendelea mpaka wavune na kuuza mazao/mavuno yao 7. Viambie vikundi vitunze kumbukumbu katika daftari dogo moja na kuteua mtu mmoja wa kikundi chaokushughulikia daftari hilo la kumbukumbu. J.3.1.Zoezi: Kutoa maamuzi. Muda: Wastani wa saa 1 dakika 30 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea HATUA: 1. Wahadithie washiriki hadithi au elezea hali ambapo mtoto analazimika kufanya maamuzi (kwa mfano, mtoto anataka kucheza na rafiki zake, lakini mama yake anamtaka amsaidie kufanya 62

usafi wa nyumba; au mtoto mwingine ana wazazi ambao wamemweleza kuwa lazima awe mhasibu, lakini anataka kuwa dereva). 2. Waulize washiriki kuhusu maamuzi yote yanayoweza kufanywa katika hali yoyote na yaandike. 3. Wagawe washiriki katika vikundi vidogo vidogo (wavulana na wasichana). Waambie waandae mchezo wa kuigiza ambapo wataigiza mambo mawili makubwa: A. Mtoto ambaye anafuata matakwa ya wazazi wake; B. Mtoto ambaye anafuata ndoto zake mwenyewe. 4. Waambie kila kikundi kiiigize mchezo wao mbele ya wengine. 5. Warejeshe washiriki pamoja na waulize kuwa mambo hayo yana faida au hasara gani. Pia waulize walifanyaje maamuzi yao. 6. Waonyeshe washiriki dhana na awamu za mchakato wa kutoa maamuzi (onyesha namba kwenye ukurasa unaofuata). Waulize washiriki wanafikiri kila awamu ina maana gani: Pokea/chunguza habari Chambua habari Jaribio la kutumia njia mbalimbali Chunguza na chambua matokeo Fanya maamuzi (pasha/amua) DURU LA KUFANYA MAAMUZI 63

J.4. Mada Ndogo: Usafi J.4.1. Zoezi : Umuhimu wa Usafi Bora Muda: Saa Moja Vifaa: Hakuna HATUA: 1. Jadiliana na vijana umuhimu wa usafi. Waulize kama wanajua baadhi ya mifano ambayo watu kwenye jamii yao wanapata matatizo kutokana na desturi mbaya za afya. Waambie baadhi yao waeleze matukio/hadithi zao. 2. Kiambie kila kukindi kifanye mchezo wa kuigiza wa matukio/hadithi na kipatie kila kikundi dakika 10-15 za kujiandaa 3. Kiambie kila kikundi kionyeshe mchezo wake wa kuigiza kwa dakika 10-15. Baada ya kila igizo kwanza kiulize kikundi walitaka kuonyesha nini halafu vikundi vyote viombwe kutoa maoni yao 4. Toa muhtasari wa mafunzo waliyopata kutokana na maigizo mbalimbali J.4.2. Zoezi: Makuzi Bora na Usafi wa Mtu Muda: Saa 1 Vifaa: Hakuna HATUA: 5. Waambie vijana watayarishe onyesho kuhusu tabia mbaya na nzuri ta usafi wa mtu. Wanaweza kutumia vifaa halisi au kuigiza tabia hizo, kwa igizo bubu. 6. Waambie vijana wengine waeleze wameona nini na kwa nini desturi hiyo ilikuwa nzuri au mbaya 7. Waulize vijana kuhusu magonjwa /maradhi mahususi yanayoweza kuenezwa au kuzuiwa na desturi hizo, sababu kwa nini magonjwa hayo yanaweza kuenezwa na yanaweza kuenezwa kwa nini 64

8. Jadili kama desturi zinawezekana kufuatwa mara kwa mara, na kwa nini baadhi ya desturi mbaya zinaendelea kuwapo 9. Waulize vijana watafanya nini kufuata desturi nzuri wao wenyewe na kuwahimiza wengine nao wafanye hivyo J.5.1. Zoezi: Maji ni Uhai Ina maana gani? Lengo: Kuelewa umuhimu wa maji katika maisha yetu, na kuelewa umuhimu wa maji safi na salama kwa usafi wetu najinsi ya kusafisha maji 1. Muda: Saa 2 2. Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea, vitu kwa ajili ya kuandaa maji ya chumvina sukari (SRO) kwa ajili ya watu waliopungukiwa na maji mwilini kwa ugonjwa HATUA: 1. Utangulizi na kubungua bongo (dakika 5). Je, tunaweza kupata wapi maji? Maji ya juu ya ardhi, chini ya ardhi, hewani, ndani ya miili yetu 2. Wote: Eleza hadithi (dakika 10). Fikiria kuhusu hadithi fupi ya mtu ambaye anaugua kipindupindu au ugonjwa mwingine inayoonyesha jinsi watu wanavyoweza kuugua kama hawatumii maji safi na salama n.k. 3. (Wote: Majadiliano kuhusu hadithi. (Dakika 20). Kwa nini mtu anaugua? Kinatokea nini ikiwa watu wanakunywa maji yasiyo safina kula vyakula vilivyooshwa kwa maji machafu? Kitu ganikinasababisha ugonjwa? (kama vile, kuharisha) Kazi ya vikundi: (Dakika 30) Waambie wasichana na wavulana wachore njia mbalimbali ambazo tunaweza kupata na kuambukizwa vimelea vya magonjwa, (Angalia The Support List for Topics M 3.5, about Hygiene, Sanitation and Environment) See also the abstract of 2 nd support list in the following page. Waambie wajadili swali lifuatalo: Hatuwezi kuishi bila maji miilini mwetu.tutawezaje kuugua sana kutokana na kupoteza maji mwilini iwapo tutapata tatizo la kutapika na/ au kuharisha, n.k.? Uwasilishaji wa vikundi na majadiliano (Dakika 20) 65

Watu wanaweza kuugua kutokana na minyoo ya tumbini kutokana na kwenye mazingira ya uchafu Wakati mwingi, minyoo ya tumbo huingia kwenye kiungo kupitia mdomo, mikono michafu, maji yasiyochemshwa, na kutokuwa makini katika maandalizi ya chakula. Kuna watu ambao wanaweza kuwa na spishi mbili au tatu za minyoo kwenye matumbo yao kwa wakati mmoja. Minyoo hii hula kwenye damu yetu na chakula chetu. Inasababisha vidonda ndani ya utumbo na kuathiri afya yetu vibaya sana, kutufanya tuwe wadhaifu. Haituruhusu kukua kwa afya na kujifunza vizuri. Namna ya kuepuka minyoo ya tumbo 1. Nawa mikono yako kwa sabuni mara baada ya kutoka msalani (kumbadili vipi moto) na kabla ya kugusa chakula 2. Kunywa maji yaliyochemshwa au yaliyochujwa; 3. Osha tunda kabla ya kulila 4. Funika chakula kuepuka inzi; 5. Tumia choo kilichojengwa vizuri na kisafi. Jenga vyoo (na pia mashimo ya maji machafu na taka) angalau umbali wa mita 40 50 kutoka kwenye kima chabondeni 6. Kifanyie matengenezo kisima chako, kifunike na usikitumie kutupa taka na/au kuruhusu wanyama kunywa maji kwenye kisima 7. Osha viruri vyombo vyote kabla ya kujaza maji 66

Jinsi ya kuandaa maji ya chumvi na sukari (SRO) (Mchanganyiko huu unafaa sana kama unakabiliwa na ukosefu wa maji au kupoteza maji maji mwilini kutokana na ugonjwa ) Kama huwezi kupata mchanganyiko wa maji ya chumvi na sukari iliyokwisha andaliwa, tayarisha kama ifuatavyo : Lita 1 ya maji safi (yaliyochemshwa na kupoozwa) + chumvu ½ kijiko cha chai + sukari vijiko 8 vya chai Changanya vizuri na kunywa Mchanganyiko huu utakuwa na ladha yenye chumvi nyiingi kidogo zaidi ya machozi J.6. Mada Ngogo: Lishe Malengo: Kuelewa mambo muhimu kuhusu lishe bora Huu ni uhusiano wa ajabu kwa maisha unaohusianishwa na shughuli za kilimo ambazo vijana wamejifunza katika shamba darasa na darasani. Katika modul/somo hili, vijana wataanza kuelewa kuwa afya yao wenyewe ni muhimu zaidi kuliko afya ya mimea yao na kwamba njia moja bora zaidi kwao kuishi wenye afya na kwa kula vyakula bora vyenye afya J.6.1. Zoezi: Desturi za Lishe Bora Chakula na lishe ni muhimu katika kuweka miili yetu kuwa yenye afya. Watu wengi wanaugua kwa sababu miili yao haina uwezo wa kukabiliana na maradhi. Ukila aina sahihi ya vyakula vya kutosha, mwili 67

wako utakuwa imara na wenye afya. Kwa hiyo ni muhimu kwa vijana kuelewa aina mbalimbali za vyakula vyenye afya vinavyoweza kupatikana. Muda: Wastani wa saa 2 Vifaa: Chatipindu na Karatasi 1. Waeleze vijana kuwa mwili unahitaji aina mbalimbali za chakula kuufanya uwe na afya na imara. Uliza kama kuna kijana yeyote anayejua aina tatu tofauti za chakula. Kama hakuna waeleze kuwa chakula kimegawanyika katika makundi matatu. Vyakula vinavyoongeza nguvu kama vile wali/mchele, ndizi, viazi vitamu na vikuu, sukari ya miwa, mihogo, shelisheli, mafuta ya mawese, aina mbalimbali za mkate, na vinginevyo Vyakula vya kujenga mwili kama vile samaki, kuku, mayai, nyama, karanga, maharage, kabichi, maziwa ni baadhi tu Vyakula vya kulinda mwili kama vile machungwa, mananasi, tikitimaji, tufaa, papai, matembele, kisamvu, mafuta ya mbogamboga na nyanya Chakula kinamakundi sita ya virutubisho vinavyotufanya tuwe na afya. Vyakula vya wanga/kabohaidreti, mafuta, protini, madini, vitamin na maji. Tunaugua kama hatuli aina ya vyakula inayofaa 2. Waeleze vijana maana ya maneno yafuatayo: Mlo kamili: Wakati chakula na vinywaji vinatumiwa kila siku kwa uwiano sahihi. Aina moja isitumiwe kwa wingi na aina nyingine isiwe chache kuliko nyingine. Lishe wakati mtu anapokula vyakula vinavyolingana na mahitaji yamwili Vyakula vya kujenga mwili miili yetu inahitaji protini kwa ajili ya kujenga misuli. Protini inapatikana kwenye nyama, samaki, kuku, karanga, koroshona maharage Vyakula vinavyoongeza nguvu vyakula vinavyoipa nguvu miili yetu kwa kawaida ni vyakula vya wanga, vinavyojulikana kuwa kabohaidreti. Vyakula vya kulinda mwili matunda na mboga huipa miili yetu vitamin na madini muhimu kwa ajili ya kuifanya miili yetu kuwa imara. Vitamini zinasaidia miili yetu kukabiliana na vimelea vya ugonjwana vitu vinavyotufanya kuwa wagonjwa 3. Waambie vijana wataje aina za vyakula wanavyokula kila siku. Halafu waambie wavigawe vyakula hivyo katika makundi matatu ya chakula kwenye karatasi ya chatipindu. 4. Waulize vijana kama matokeo yanaelekea kuonyesha mlo kamili 68

5. Wagawe vijana katika makundi matatu Kundi la kuongeza nguvu Kundi la kujenga mwili na Kundi la kulinda mwili. Waambie kila kundi liorodheshe milo kamili miwili wanayamini kwamba ni milo kamili. 6. Kila kikundi kiwasilishe milo yake na kueleza kwa nini milo hiyo ni kamili J.7.1. Zoezi: Utunzaji wa Kumbukumbu za Ushughulikiaji mazao Muda: Wastani wa dakika 90 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea HATUA: 1. Waambie vikundi vine tofauti watayarishe mawasiliano ya maendeleo yaliyofanywa katika kuanzishwa mazao yanayohusika ambayo wanatakiwa kujumuisha shughuli mbili tofauti. Waambie wajitahidi kadiri iwezekanavyo kuelekeza mawasilisho yao kwenye kumbukumbu walizotunza (tarehe ya kupanda, ukubwa wa eneo, wingi wa mimea, n.k.). 2. Kiambie kila kikundi kiwasilishe 3. Jadiliana na vijana kuona kama kila kikundi kimeandika kumbukumbu zote zinazohitajika ili waweze kufuatilia maendeleo yaliyofanywa na kutambua tofauti kati ya ushughulikiaji wa aina mbili 4. Jadili umuhimu wa utunzaji bora wa kumbukumbu na matatizo yaliyokabiliwa na vikundi tofauti katika utunzaji wa kumbukumbu hizi 5. Toa muhtasari wa mahitimisho kuhusu umuhimu wa utunzaji wakumbukumbu nzuri na kinachohitajika kuboreshwa katika utunzaji wa kwa aina mbalimbali za mazo na ushughulikiaji 69

J.8.1. Zoezi: Mambo yanayolingana kuhusu kupanga biashara na kupanga katika kilimo Lengo: Kupitia baadhi ya hatua za mizunguko ya mazao katika kilimo na kulinganisha hatua hizi kwa jumla na mzunguko wa maisha ya biashara Muda: Saa 1 Vifaa na matayarisho: Chatipindu au ubao wenye michoro ya hatua tano za biashara kama zilivyoelezwa kwa muhtasari hapachini na baadhi ya mifano ya mimea (mazao) katika hauta mbalimbali Namna ya Kufanya Pitia kilichofundishwa kuhusu hatua za maisha ya mazao katika Moduli ya 2. Rudia kueleza kwamba vitu vyote vinavyoishi kama vile mazao hua vinapitia pia hatua mbalimbali katia maisha yake Waulize vijana wajaribu kukumbuka kwa nini ni muhimu kabla ya kuanza kulima mazao Fulani, kujifunzakuhusu hatua mbalimbali za ukuaji na maendeleo ya mimea (katika kila hatua,mahitaji ya mimea yanatofautiana na tunahitaji kuzingatia masharti sahihi ya ukuaji, kwa kuwa baadhi ya hatua za mimea/mazao zinahitaji majimengi au kidogo, mwanga wa jua, kulindwa dhidi ya wadudu waharibifu na magonjwa na /au magugu, zinahitaji urutubishaji/utiaji wa mbolea maalumu, na kadhalika) Pitia hatua nne tofauti za ukuaji wa mimea. Waambie vijana wakueleze tena mambo ambayo mimea/mazao yanahitaji kukua yenye afya na kustawi vizuri. Eleza tena kwa muhtasari kwamba kupanga katika kilimo kunaanza na uchaguzi wa mazao ya kupanda. Ni vipengele gani vitakavyoshawishi maamuzi yako kuhusu aina gani ya mazao ya kupanda. Eleza kwamba tunaweza kumlinganisha mkulima anayesimamia hatua kulima zao fulani na mzunguko wa biashara. Eleza kwamba,wakati wa kufikiria kuhusu biashara, tunaweza kuwa na hatua za mipango kama za kilimo. Eleza mifano halisi ya kuonyesha hatua tano ambazo biashara hupitia. Tumia picha au chora michoro rahisi kusaidia kufafanua maelezo yako. Mkulima anaanza kwa kufikiria kulima nini Tunafikiria kuhusu mawazo ya biashara Anaanza kuandaa shamba Tunapanga na kuandaa namna ya kuweka mawazo ya biashara katika utekelezaji (uliza ni vipengele gani vinavyoshawishi uamuzi kuhusu nini cha kupanga au 70

biashara gani ya kuuza) Anapanda mbegu na miche Tunazindua au kuuza biashara (inaweza kuwa polepole/hatua kwa hatua, kuliko kuwa uzinduzi mmoja mkubwa) Mimea ni lazima itunzwe Biashara inaanza kukua (ukuaji wa awali) na baadhi ya vitu vinahitajika ili kusaidia kukua Mazao yanavynwa (baadhi ya mbegu zinahifadhiwa kwa ajili ya mzunguko ujao wa mazao) Faida hupatikana lakini biashara ni lazima ikue na kupanuka zaidi. Baadhi ya faida huwekezwa kwenye kukuza zaidi biashara Waulize vijana ni mambo ganiyanayohitajika kusaidia mimea kukua, na ni mambo gani yanayohitajika kusaidia biashara kukua. Waambie vijana wachore hatua hizi. Onyesha picha/michoro waliyochora vijana Maelezo kwamwezeshaji Kutegemea kiwango cha vijana hao, unaweza kuwauliza mapendekezo zaidikama vile kinachohitajika kuikuza biashara (mkopo, faida, wateja,mwitikio, soko, stadi nzuri za mauzo ) Pia unaweza kueleza kwa muhtasari tofauti za kijinsia katika usimamizi wa mazao ni shughuli gani ambazo kwakawaida zinafanywa na wanawake/wasichana au wanaume/wavulana katika kutayarisha shamba na kupanda, palizi, kuvuna na kadhalika. Jaribu kuacha dhana ya mitazamo yoyote isiyotaka mabadiliko. Sisitiza kwamba, wanawake na wanaume, wasichana na wavulana, wote wanaweza kushirikishwa katika bishara. Marejeo: Imechukuliwa kutoka moduli ya 1.2, Zoezi la 4, ukurasa wa 49. Bauer, S. Finnegan, G & Haspels, N. (2004) GET Ahead for Women in Enterprise Training Package and Resource Kit. (ILO Bangkok) 71

J.9.1. Zoezi: Kuugua na kupata nafuu Muda: Saa 2 Vifaa: Karatasi kubwa na kalamu za kuchorea Zingatia: Unaweza kutaka kumshirikisha katika somo hili mwunguzi au daktari mwenyeji wa mahali 1. Waulize vijana kama wanafahamu majina yoyote yamagonjwa ya binadamu yanayotokea katika eneolao 2. Waulize ugonjwa huo ulivyo wakati mtu anapokuwa anao 3. Andika kwenye chatipindu magonjwa yote waliyotaja Zingatia: Unawezakuongeza baadhi ya mapendekezo, kama vijana wametaja ugonjwa mmoja au mawili tu 4. Wagawe vijana katika vikundi na waambie wajadili maswali yafuatayo - Unapougua, unafanya nini ili kupata nafuu? - Je, unajua tiba yoyote kwa magonjwa uliyoyataja? - Je, unaelewa kuhusu VVU? - Je, unawezaje kukinga magonjwa yaliyotajwa? - Je, kliniki/zahanati/hospitali ya karibu iko wapi? - Je, unapougua, ni nani anayekutunza? 5. Vikusanye vikundi pamoja na kujadili Usisahau kutaja kwamba ni muhimu kujaribu kupata matibabu wakati unapokuwa mgonjwa, na tusijaribu kusubiri mpaka tuwe mahututi ndiyo tutafute msaada Onyesha uhusiano kati ya walichojifunza vijana kuhusu kudhibiti/kukinga maginjwa na wadudu waharibifu kwenye shamba darasa 72

J.9.2. Zoezi: Magonjwa katika maisha Muda: Wastani wa saa 1 dakika 30 Vifaa: Chatipinduna kalamu za kuchorea HATUA: 1. Waambie vijana wataje magonjwa yote yaliyopo kwenye jamii zao nakuorodhesha kwenye karatasi kubwa 2. Chagua magonjwa mawili yanayopatikana sana (kwamfano: malaria na kuharisha). Waambie vikundi wajadili dalili, vyanzo na namna ya kupunguza uwezekano wa kuambukizwa magonjwa hayo. Vikundiviwili vihusike na malaria navingine viwili kuharisha 3. Kiambie kila kikundi kiwasilishe na kujadili 4. Toa muhtasari wa dalili,vyanzo na njia zinazoweza kupunguza uwezekano wa kuambukiza magonjwa yaliyochaguliwa. Mada ndogo: Kuelewa na Kujilinda dhidi ya VVU/UKIMWI Malengo: Kuweza kueleza maana ya VVU na UKIMWI Kuweza kueleza namna VVU na UKIMWI vinavyoweza kuambukizwa na madhara yake. Kuorodhesha njia mbalimbali za kujilinda dhidi ya VVU na UKIMWI Ni muhimu kwa vijana kuelewa jinsi ya kujilinda kutokana na magonjwa, na hususani VVU/UKIMWI. VVU/UKIMWI ni moja ya mada tete, lakini ni muhimu kwa washiriki kuelewa ukweli kuhusu ugonjwa huu, na vilevile wapate ujuzi wanaohitaji ili kujilinda na kuepuka kuambukizwa. Zifuatazo ni shughuli kadhaa ambazo mnaweza kuzitumia kuwasaidia washiriki kuelewa VVU/UKIMWI. Ingawa si lazima shughuli zote zipitiwe katika moduli hii, ni bora kuziweka kwenye mlolongo wa namna zinavyowasilishwa. 73

J.9.3. Zoezi: Jaribio la mpira wa VVU Hii ni shughuli inayotumia nguvu ambayo inapitia kwa haraka habari zote za msingi kuhusu VVU na UKIMWI. Muda: Wastani wa saa 1 na dakika 30 Vifaa: Mpira, nafasi kubwa ya wazi (ikiwezekana nje), karatasi na kalamu za kuchorea. Hatua: 1. Waambie vijana wasimame katika duara. 2. Mshiriki wa kwanza amtupie mpira mshiriki mwingine. Mtu huyo anatakiwa kudaka mpira na kumrushia mtu mwingine na kuendelea. 3. Kama mtu atashindwa kumudu mpira (hawezi kudaka au kurusha mpira vizuri kwa mtu mwingine), lazima ajibu swali kuhusiana na VVU/UKIMWI (tazama maswali ya mfano hapo chini). Kama atajibu kwa usahihi, basi mchezo utaendelea. Kama hapana, basi mtu huyo atatoka kwenye mchezo. 4. Mchezo utaendelea hadi maswali yote yawe yameulizwa au mtu mmoja amebaki. 5. Baada ya mchezo kumalizika, kaa pamoja na washiriki na pitia kila swali tena. Eleza kila taarifa ya VVU/UKIMWI kwa makini na wahimize washiriki kuuliza maswali. 6. Waambie washiriki walinganishe kuenea na kuzuia VVU na kuenea na kuzuia magonjwa ya mazao na wanyama. 7. Wahimize washiriki kuchora kwenye karatasi au kurekodi kwa njia ya wimbo au mchezo kila moja ya taarifa kuhusu VVU/UKIMWI. Kama hawawezi kuchora au kurekodi mambo yote kutokana na muda kuwa mchache, wahimize kufanya mengi iwezekanavyo. Maswali ya Mchezo Kweli/Uongo: Unaweza kupata VVU mara ya kwanza unapofanya ngono. (Jibu: Kweli) UKIMWI ni kifupi cha nini? (Jibu: Upungufu wa Kinga Mwilini) Kweli/Si Kweli: Mara ukishapata VVU, utakuwa na VVU wakati wote. (Jibu: Kweli) Sehemu gani ya mwili inashambuliwa na VVU? (Jibu: Mfumo wa kinga) Kweli/Si Kweli: VVU unaweza kusambaa kwa kushikana mikono. (Jibu: Uongo) Ina maana gani kuwa mwaminifu? (Jibu: Kuwa na mwenza mmoja wa kufanya ngono) Kweli/Si Kweli: Mtu mwenye VVU anaweza kuishi muda mrefu kama atakula vizuri na kufanya mazoezi. (Jibu: Kweli) Muda huu unaitwaje, mara baada ya kupata maambukizi, wakati mtu anaweza kuwa na VVU lakini bado anaweza kupima na kuonekana hana ugonjwa? (Jibu: Kipindi cha Mpito) 74

Sehemu gani ya dunia imeathirika zaidi na VVU? (Jibu: Afrika) Njia ipi ni salama kwa 100% kujilinda kutokana na VVU? (Jibu: Kutofanya ngono, na kuwa makini kutochangia sindano, nyembe na vitu vingine vyenye ncha kali). Kweli/Uongo: Unaweza kujua kwa kumwangalia mtu ambaye ana VVU/UKIMWI. (Jibu: Uongo) Kweli/Uongo: Mbu wanaweza kueneza VVU. (Jibu: Uongo) Majimaji gani ya aina mbili kati ya sita ambayo yanaeneza VVU? (Jibu: Damu, manii, maji ya ukeni, usaha na maji ya uvimbe) Majimaji gani mengine ya aina mbili yanaweza kusambaza VVU? Kweli/Uongo: Kondomu hupunguza hatari ya kusambaza VVU. (Jibu: Kweli) Kweli/Si Kweli: Kina mama wenye VVU wanaweza kuwaambukiza VVU watoto wao. (Jibu: Kweli) VVU inasimama kwa ajili ya nini? (Jibu: Virusi Vya UKIMWI) Kweli/Si Kweli: VVU na UKIMWI ni kitu kimoja. (Jibu: Si Kweli. VVU ni virusi vinavyosababisha UKIMWI). Kweli/Si kweli: Ugonjwa wa kuambukiza kwa ngono, huongeza hatari ya mtu kupata VVU. (Jibu: Kweli) J.9.4. Zoezi: Mchezo wa kuenea kwa UKIMWI Muda: Wastani wa saa 1 na dakika 30 Vifaa: Eneo kubwa la wazi, karatasi ndogo, kalamu za kuchorea. Hatua: 1. Kwa kutumia kalamu ya kuchorea au kalamu, andika herufi A, H, C au N kwenye karatasi ndogo. (Kwa mfano, kama kuna wanafunzi 12 kwenye kikundi, wanafanya karatasi 3 za A, 3 za H, 3 za C na 6 za N.) Kunja karatasi ili kuficha herufi zisionekane. 2. Gawa karatasi moja kwa kila mshiriki na waambie WASIFUNGUE. Waelekeze wanafunzi kutembea na kushikana mikono na watu watatu tofauti. Wakumbuke wameshikana mikono na nani. 3. Waelekeze kila mmoja kurudi kwenye nafasi yake, wakae na kufungua karatasi zao. 4. Waambie wale ambao karatasi zao zimeandikwa H wasimame. Waambie kuwa wanafunzi hawa wana VVU. 5. Waambie kila mmoja aliyeshikana mikono na wanafunzi wenye VVU asimame waambie kila mmoja ambaye ameshikana mikono na hao waliosimama asimame. Fanya hivyo hadi wanafunzi wote wawe wamesimama. 75

6. Waambie washiriki ambao wenye A wakae. Wapongeze kwa kujizuia kufanya ngono na kujilinda kutokana na VVU/UKIMWI. 7. Waambie washiriki wenye karatasi zenye C wakae. Kama ni watu wazima, wapongeze kwa kuvaa kondomu na kujilinda. Kwa watoto, weka wazi kuwa hawawezi kupongezwa. 8. Waambie washiriki wenye N kuwa hawakuwa na VVU mwanzoni mwa mchezo. Hata hivyo, kama walishikana mikono na mtu ambaye ana karatasi yenye H, wameshaambukizwa. 9. Eleza kuwa katika shughuli hii, kushikana mikono ni ishara ya ngono. Sisitiza kuwa katika maisha halisi, kushikana mikono hakusababishi kuenea kwa VVU. Pia, kuwa makini kuhakikisha kuwa kikundi hakiwanyanyapai wanafunzi wenye karatasi zenye H. 10. Baada ya shughuli hii, ongoza majadiliano kwa kutumia maswali yafuatayo kama mwongozo: VVU vimeenea vipi miongoni mwa wanakikundi? Hii inafanana vipi na jinsi VVU vinavyoweza kusambazwa katika jamii? Ulijisikiaje kugundua kuwa ulikuwa na VVU? Unafikiri watu wanajisikiaje wanapojua kuwa wana VVU? Unajisikiaje kuambiwa kuwa ulikuwa huna VVU? Wanakikundi wangefanyaje ili kujilinda wasiweze kuambukizwa? 11. Waambie washiriki walinganishe jinsi VVU vinavyoenea na vinavyoweza kuzuiwa, ikilinganishwa na jinsi magonjwa ya mazao na mifugo yanavyoweza kuenea na yanavyoweza kuzuiwa. 12. Pitia na washiriki masuala kuhusu VVU na UKIMWI (kutoka jaribio la kupiga mpira la VVU/UKIMWI ). Jibu maswali yote. 13. Wahimize washiriki waonyeshe kwenye karatasi au rekodi kwa njia ya wimbo na ngoma mambo muhimu kuhusu VVU na UKIMWI J.10. Mada Ndogo: Kupunguza mazingira hatarishi ya VVU mchezo wa mawe ya kuvukia Malengo: Kuwasaidia kutofautisha kati ya ajira kwa watoto na kazi ambayo si mbaya kwao Kujenga uelewamiongoni mwa jamii kuhusu hali za watoto wanaolazimishwa kufanya kazi badala ya kwenda kusoma shule Kabla ya kuanza mazoezi haya, tafadhali soma maelezo kwa mwezeshaji wa sehemu hii. 76

J.10.1. Zoezi: Je, ajirakwa watoto ni nini? Muda: Saa 1 1 na dakika 30 Vifaa: Kabla ya kufanya zoezi hili, soma Maelezo kwa Mwezeshaji kuhusu ajira kwa watoto hapa chini Hatua: 1. Anza kwa kuuliza swali rahisi: mtoto ni nani? Fuatilia na katika umri gani unafikiri mtu si motto tena? Maelezo: Majibu yanayotofautiana yatatolewa (kwa mfano,wakati mtuanapopitia jando na unyago,anapo balehe au kuvunja ungo huoa au kuolewa,wanpoanza kufanya kazi,wanaondoka nyumbani,wanapokua yatima,wanapomaliza masomo) Itakua muhimu kuhusisha kwenye maana ya kisheria ya mtotot ili kuepuka utatizi.kwa kawaida mtoto anafafanuliwa kama mtu mwenye umri wa chini ya miaka 18. Ibara ya mapato ya umoja wa mataifa kuhusu haki za mtoto inaeleza kua mototo ni binadamu yeyote mwenye umri chini ya miaka 18,isipokua kama kwa mujibu wa sheria inayohusu motto,balehe au kuvunja ungo huanza na umri mdogo zaidi.angalia katiba ya nchi inavyoeleza 2. Fuatilia swali hili kwa kuuliza kama vijana wanafahamu kazi yoyote katika kilimo inayofanywa na watoto na kuwazuia kuhudhuria masomo au kuwachosha sana kiasi cha kushindwa kutimiza wajibuinavyopasa.wahimize washiriki wawe wazi zaid kuhusu muda na aina ya kazi(kwa mfano:palizi kila siku kwa muda mrefu,kuchunga mifugo kuanzia alfajiri mpaka jioni,kuwinga ndege siku nzima nyakati za masomo).andika shughuli mbalimbaliubaoni mua chatipindu. 3. Waambie washiriki wataje shughuli zinazofanywa na watoto zinazowafanya wachoke sana,wawe dhaifu au wagonjwa au zinazowasabisha wawe na majeraha(kwa mfano,wanaweza kuwa wananyunyizia dawa ya kuulia wadudu,kubeba mizigo mizito,au palizi kwa muda mrefu).orodhesha kazi hizo peke yake kwenye chaitpindu au ubaoni pia. 4. Halafu waambie vijana waeleze shughuli ambazo mara nyingi zinafanywa na watoto ambazo zinawafaa na wanajifunza stadimuhimu. Mfano inaweza kuwa ni kuwasaidia wazazi kuvuna.au palizi kw muda mfupi mwisho wa wiki au kujifunza shughuli kuhusu shamba/uwanja wa PROKA ADESUA orodhesha shughuli hizi pia. 5. Pitia orodha zote tatu tofauti na eleza kuwa kwa kawaida tunatumia neon ajira kwa watoto(au neon linalolingana linalotumika nchini)ueleze aina ya kazi zililozotajwa kwenye orodha mbili za kwanza.unaweza kutumia taarifa ya hapa nchini pia kama maelezo ya mwezeshaji ya 1. 77

Maelezo: Kusema kweli neon ajira kwa watoto linahusu kuwatumia watoto katika kazi na shughuli zisizokubalika na jamii na kiuadilifu. Kwa mfano inaweza kuwa ajira kwa watoto kama mtoto: Anafanyakazi muda wote badal a ya kua shuleni Anahusishwa kwenye kazi nyingi kwa muda mrefu. Anafanya kazi hadi usiku sana. Anafanya kazi katika hali na mazingira mabaya(hakuna chakula au maji au joto kali). Anafanya kazi kwa vitisho(kupigwa au kulazimishwa kufanya kazi). Anafanya kazi zaidi na malipo anapewa mtu mwingine. Kwa maelezo zaidi angalia.facilitators Notes 1: Basic Facts about Child Labour. 6. Anza majadiliano na watotoau walezi wao.tumia maswali yafuatayo kuchochea majadiliano: a) Kwa jumla wakati wa umri gani wenyeji wanafikiri kama ajira kwa watoto inajadiliwa? Je,inaweza kua wasichana au wavulana au wote? b) Je,ajira kwa watoto iko wapi? Ni sehemu gani ya nchi yetu au wilaya gani au miongini mwa makundi gani ya watu?. c) Je,wafanyakazi watoto wanalipwa? Je,wanaweza pia kufanya kazi bila malipo?. 7. Toa muhtasari na jaribu kuhakikisha kuwa imeeleweka vizuri kuwa ajira kwa watoto ni nini na ipi si ajira kwa watoto. 78

Maelezo kwwa wawezeshaji: Ajira kwa Watoto Watoto wanafanya kazi na shughuli nyingi tofauti.baadhi ya kazi hizo ni za kuchosha. Baadhi ni ngumu na zinahitaji bidii na na umakini nyingine ni hatari sana na si halali kiuadilifu. Si kazi zote zinazofanywa na watoto zitahesabiwa kwa kuwa ajira kwa watoto ambazo ni lazma zilengwe kutokomezwa. Ushiriki wa watoto au vijana wa umri mdogo katika kazi isiyodhuru afya yao na maendeleo na makuzi yake au isiyoingilia masomo,kwa kawaida inahesabiwa kuwa si mbaya.kazi hiyo inajumuisha shughuli kama kama vile: - Kuwasidia wazazi/walezi. - Kuasaidia biashara ya familia:au - kujipatia fedha za matumizi baada ya saa za masomo na wakati wa likizo za shule. Shughuli za namna hii zinachangia makuzi,maendeleo ya motto na ustawi wa familia zao. Shughuli hizi huwajengea watoto stadi na uzoefuna kusaidia kuwaandaa kuwa wazalishaji mali wakati wanapokuwa watu wazima. Neno ajira kwa watoto mara nyingi linafasiriwa: i. Kazi inayowanyima watoto utoto wao. ii. iii. iv. Uwezo wao. Hadhi yao; na Yenye madhara kwa ukuaji wa mwili na akili. Ni kazi ya hatari na yenye madhara kwa watotokiakili,kimwili,kijamii au kiuadilifu;na inaingilia masomo yao kwa: v. Kuwanyima fursa ya kuhudhuria masomo; vi. vii. Kuwalazimisha kuacha shule kabla ya kumaliza;au Kuwataka wajaribu kuchanganya mahudhurio ya shule na kazi nzito za muda mrefu. Ikiwa katika namna mbaya zaidi,ajira kwa watoto inahusishwa kufanywa mtumwa,kutenganishwa kutoka familia zao,kufanya kazi kutoka katika mazingira ya hatari zaidi 79

na ugonjwana/au kutelekezwa wajikimu wenyewe kwenye mitaa ya miji mikubwa-mara nyingi katika umri mdogo sana. Iwe ndiyo ama hapana aina mahususi ya kazi inaweza kuitwa ajira kwa watoto inategemea, - Umri wa mtoto, - Aina na muda wa kazi inayofanywa;na - mazingira yanayofanyiwa kazi. Jibu linalotofautiana kutoka nchi moja hadi nyingine,pamoja na miongoni mwa sekta za nda ni ya nchi 8. Viulize vikundi kama wanafikiri zifuatazo zitakua hali/mazingira ya ajira kwa mtoto au hapana. a) Mtoto wa umri wa miaka 12 anamtunza motto wa dada yake kwa muda wa saa mbili baada ya kutoka shule (hapana) b) Msichana mwenye umri wa miaka 9 anaham ia kwenye nyumba ya jamaa husaidia kazi za nyumbani,na haendi tena shule(ndiyo). c) Mtoto mwenye umri wa miaka 10 antumia siku nzima kufanya kazi shambani kila siku ya wiki(ndiyo) d) Mvulana mwenye umri wa miaka 13 anongozana na kaka yake kwanye safari ya kuvua kwa siku 2-3 wakati wa likizo(hapana,alimradi safari za kuvua haziingilii mara kwa mara mahudhurio ya shule). e) Mtoto mwenye umri wa miaka 15 aliyeajiriwa kunyunyizia aina zote za dawa za kuulia wadudu bila ya mavazi ya kujikinga na hana mahali pa karibu pa kunawa na kuoga(ndiyo) J.10.2. Zoezi: Kutengeneza sanamu inayoishi. Muda: Saa 1 Vifaa na matayarisho: Utakuwa umesoma maelezo kwa mwezeshaji kuhusu ajira kwa watoto mwisho wa mada ndogo. Hatua 1..Eleza kwa muhtasari baadhi ya vipengele vizuri vya kufanya kazi za kilimo kwa mfano kua nnje kwenye hewa safi;huchangia kwenye uhakika wa chakula;kuweza kuongeza thamani ya 80

ziada kwenye milo;huhisi mafanikio katika kulima mazao;kuwa karibu na maumbile kuliko kuishi mjini;hupata maarifa kuhusu kilimo 2.. Rudia maana ya ajira kwa watoto na isiyo ajira kwa watoto. 3. Tenga nafasi katikati ya chumba au tumia nafasi ya wazi nje. 4. Kila mwan afunzi lazma achague mwenzi. 5. waleze wanafunzi,wajipange kwa jozi,na kwamba mmoja wa wenzi atatakiwa aigize bvaadhi ya kazi za kilimo(kwa mfano,kunyunyiza dawa,kuinamisha mabega,kuinua mizigo mizito,kujikuna,kuvuna chini ya maji,kutembea masafa m arefu na wanyama),wakati mwenzi wake lazma aigize matokeo mabaya yanayowezokana ya shughuli hai (kwa mfano kukohoa,maumivu ya mgongo kujikata) 6. Zipatie jozi wastani wa dkika 10, kukubaliana kuhusu jambo la kuigiza. 7. Unda duara na waambiae wenzi hao,mmoja baada ya mwingine,kutengeneza sanaa zao katikati kwa ajili ya washiriki wengine. Sema ganda baada ya dakika chache,halafu waache jozi waeleze ni shughuli gani na matokeo mabaya wliyokua wakiigiza.jadili kama matokeo huenda yakatokeamara baada ya shughuli au baada ya kipindi kirefu. 8. Wape vijana fursa ya kuzungumzia kuhusu dalili za afya mbaya na majeraha.baadhi ya dalili ya afya mbaya inaweza isihusiane na kazi ya kilimo hata hivyo itabidi pia iorodheshwe.kwa mfano UKIMWI na VVU ;utapia mlo,mafua ya nguruwe n.k. Mwezeshaji anaweza kufafanua baadhi ya majeraha au taja majeraha mengine yanayohusiana.himiza majadiliano kuhusu uchunguzi wa familia kutoka kwenye zoezi. 9. Anzisha majadiliano kuhusu namna utakavyopunguza hatari katika kilimo. J.10.3. Zoezi: Maigizo kuhusu ajira kwa watoto Kwa kuigiza matukio na hali mbalimbali za ajira kwa watoto,washiriki wa SDSMV lazima waingie kwa wahusika wawaelewe na kujaribu kufuatisha hisia hisia zao.vijana wanaweza kutumia uzoefu wao wenyewe moja kwa moja hali na matukio ya vijana wenyewe ambayo yanaweza kusababisha makabiliano makali.maigizo yaliyomo kwenye zoezi hili yanaweza kufanywa kwa vijana wa SDSMV na mbele ya jamii pana wakiwemo walezi. Muda: Wastani wa saa 2 Vifaa na matayarisho: Andaa baadhi ya mpangilio wa matukio yanayoweza kuigizwa na watu wawili wawili au watatu yanayohusu motto anayetumiwa katika ajira kwa mtoto.katika kurasa zifuatazo kama mifano mine inayotolewa kwenye maboksi.mifano hii inaweza kubadilishwa au kutumika kilingana na hali ya mahali husika.kinyume chake,waambie vijana wabuni mpangilio wa matukio yao wenyewe. 81

Mambo yafuatayo hayana budi kusisitizwa - Jaribu kuepuka kadiri iwezekanavyo kuonyoesha taswira mbaya tu ya kazi za kilimo au uthikitisho kwamba kilimo ni kwa ajili ya vijana walioacha shule tu. - Hakikisha kwamba ujumbe katika igizo unazingatia maadili ya mahali kuhusu wajubu na kazi za watoto kuwasaidia wazazi. - Majadiliano yanye kuhoji ya kutosha hayanabudi kufanywa baada ya igizo.hii itampa fursa mwezeshaji na wale waliohusishwa kuibua masuala mapya.mara nyingi fanya majadiliano au midahalo na watazamaji baada ya igizo. Kisa cha 1: Dembe na Mjomba wake (waigizaji wawili). Dembe ameazimishwa na wazazi wake kuishi na kufanya kazi kwenye shamba la ndugu sehemu nyingine ya nchi Ndugu walimchukua na kwenda nae mbali.aliwahi kusikia majadiliano Fulani kati ya baba yake na mjomba wake kuhusu deni la fedha lakini hakuelewa Dembe hawafahamu vizuri ndugu hao, na anapewa kazi mara baada ya kufika. Kazi yake kuu ni kukata majani makavu ya migomba na mashina. Anatumia tawi dogo la mti lililopasuliwa kidogo na kisu kilichochomekwa kwenye mpasuko huo katika pembe mraba. Kutwa nzima anachuchumia na mti huo naa kujaribu kuvuta majani makavu ya juu ya mgomba hadi ubavuni mwa shina. Baada ya siku chache anakabiliwa na maumivu mgongo, kiuno, mabega na kujisikia mchovu sana kazi hii inachosha sana. Ameumwa sana na wadudu na hivyo kuwashwa. Wakati mwingine huwa anasaidia kukata na kubeba chakula cha mifugo. Anapokuwa shambani,hana maji ya kutosha. Anahofu kwamba maji yenyewe si safi na salama. Anafikiria sana kuwa mbali na kwao na kukosa masomo. Mara nyingi anafikiria namna ambavyo angependa kurudi shuleni, lakini anaogopa kuwa atakuwa nyuma kimasomo kama akiamua kurudi shule hivi karibuni. Siku moja Dembe anaamua kumwuliza mjomba wake shambani kuhusu matarajio yake ya baadaye o o Mhusika wa 1 anamwigiza Dembe akifanya kazi Mwigizaji 1 ni mjomba wake anayekuja kukagua kazi ya Dembe. Halafu Dembe anamwuliza mjomba wake kuhusu matarajio yake ya baadaye. 82

Kisa cha 2: Dando, Lumusi na Baba na mama yao (waigizaji wakuu wanne) Kaka (Danso) na dada (Lunusi) wafanyakazi katika shamba la wazazi wao kila siku baada ya kutoka shuleni. Wote wanafurahia kazi hiyona kila mara wanabadilishana hadithi kuhusu marafiki zao wa shuleni waliofanikiwa kufanya mashamba yao yawe na faida sana kwa kupanda mazao mbalimbali na kuwekeza kwenye vitu mbalimbali. Danso na Linusi mara nyingi wanashangaa kwa namna familia nyingine zinavyomudu. Danso na Linusi wana ndugu zao wanne wa kike na wakiume. Wazazi wao wanashughuli nyingi sana za kuhakikisha wanatimizamahitaji ya nyumbani. Baba yao haoni sababu ya Danso na Linusi kuendelea na masomo kwa kuwapo na shughuli za shamba za kutosha. Wanabishana na kujadiliana kwa pamoja kuhusu suala hili. Danso na Linusi wanajaribu kumshawishi baba yao kwamba lazima waendelee na masomo na kujaribu kumwambia mama yao asaidie kumshawishi baba yao. Lakini ni vigumu kubishana na baba yao. Kuna kazinyingi za kufanya na unahitajika msaada. Chakula ni haba na zaidi ya mahitaji ya kila siku, watoto hao wanatambua kuwa wanahitaji fedha pia kwa ajili ya shule Mwigizaji wa 1 ni Dando, Mwingine ni Linusi na wote wanajaribu kumshawishi baba yao (mwigizaji mwingine). Mtu mwingine anaweza kuwa ni mama, anayeona si rahisi kubishana na baba. Baadaye Danso anafikiria kwenda kufanya kazi kwenye shamba kubwa lililopo jirani ili apate fedha zitakazomwezesha kutimiza mahitaji yake ya shule bila ya kuwaomba wazazi wake. Linusi anafikiri kwamba kama Danso atafanya kazi hiyo, hatakuwa na muda tena wa kwenda shule. Linusi anajaribu kushauriana na Danso 83

Kisa cha 3: Pranab baba yake na Msimamizi (waigizaji wakuu watatu) Pranab,mvulana mwenye umri wa miaka 12 anafanya kazi pamoja na baba yake kama mfanyakazi anayelipwa mshahara. Leo wanawasili kwenye shamba linalomilikiwa na familia pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa ajira kamili na ajira ya muda. Mmiliki wa shamba amefika kijijini kwao juzi usiku akiwaambia kwamba anahitaji msaada shambani kwake. Pranab na baba yake walipakiwa kwenye gari la mmiliki wa shamba na kuteremshwa shambani Leo asubuhi shambani hapo dawa za kuulia wadudu zinachanganywa na zitatumika baadaye. Pranab amepewana kazi ya palizi na kuwinga ndege. Watoto huwa hawaruhusiwi kuchanganya dawa za kuulia wadudu kwa kuhofia kumwaga au kuifuja. Baba yake Pranab,ambaye hajui kusoma, anamsaidia mfanyakazi wa ajira kamili kushughulikia na kuchanganya dawa za kuulia wadudu. Pranab anamwona baba yake. Ingawa Pranab amesoma kidogo na anasikia dawahizi za kuulia wadudu zinaweza kuwa na hatari na kuona kuwa baba yake havai glovu. Anamjua mtu aliyetokwa na upele mwingi kutokana na kufanya kazi kwenye shamba hilo mwaka jana. Kusema kweli Pranab anakumbuka mawingu madogo au ukungu wa mvule hewani yaliyokuwa yakipeperushwa kuelekea alikokuwa akipalilia. Anakumbuka hisia ya kukosa hewa. Lakini baba yake Pranab yuko tayari kunyunyuzia/kupulizia dawa. Pranab anakwenda kule ambako baba yake na msimamizi wa wafanyakazi wanakofanyakazi. Pranab anajaribu kuzungumza polepole na baba yake kuhusu dawa za kuulia wadudu, lakini msimamizi wa wafanyakazi anasikia na yuko tayari kuwafukuza kazi kama hawaendeleina kazi... o Mwigizaji wa 1 ni Pranab anayepalilia na kuwinga ndege o Mwigizaji Mwingine ni Baba yake Pranab anayechanganya dawa za kuulia wadudu o Mwigizaji wa tatu ni msimamizi wa wafanyakazi aliyekasirishwa na uingiliaji kati wa Pranab. 84

Kisa cha 4. Miremba na bibi yake (waigizaji wakuu 2-4) Mama yake Miremba amefariki. Baba yake alikuwa mvuvi na alikuwa na watoto wengi. Watoto hawaendi shule kwa hiyo bibi yao aliamua kuwapeleka wakaishi kwa ndugu Miremba ana umri wa miaka 11 (mwigizaji 1). Hivi sasa anaishina familia yenye watoto watatu. Familia hiyo ina shamba dogo. Mkuu wa kaya anafanya kazi mahali fulani katika mji wa karibuni. Anamfanya akose raha. Mke wake ana genge dogo. Hana tatizo lakini Miremba anampa kazi nyingi sana. Kila siku Miremba anafagia nyumba, kuosha vyombo, anatumwa, kufua, kuteka majina kupika na kuandaa chakula. Miremba anatarajiwa pia kutunza miche na palizi, pia anakusanya makonokono na wadudu waharibifu Kaya ina ng ombe wawili na Miremba anatumia muda kulisha mifugo pia, kuwapeleka malishonina kuwatekea maji. Wakati mwingine anafanya kazi kwa saa 12 kwa siku, na haelekei kupumzika kutokana na kazi nyingi. Wakati mwingie anapopeleka ng ombe malishoni anazungumza na msichana (mwigizaji mwingine) anayeishi jirani ambaye pia ni mtumishi wa nyumbani. Mara nyingi wanajadiliana bei ya maziwa katika mji wa jirani. Msichana huyo alimwambia kuhusu utengenezaji wa kutokana na maziwa. Hivi karibuni Miremba amekuwa akisumbuliwa namaumivu ya kichwa na kusikia kizunguzungu na maumivu ya mgongo. Alijikata kidole kwa kisu kikali kwa bahati mbaya wakati alipokuwa akipika chakula na kidonda hicho bado hakijapona kwa ukamilifu. Kidonda kinauma sana wakati anapobeba vitu na wakati mwingine anapolima na kupalilia. Chakula na malazi ya Miremba ndiyo malipo yake kwa kazi zote anazofanya, na anajua kwamba kama hatakaa au analalamika, ataishia kuzurura mtaani. 85

Miremba hajarudi kwao tangu afike na hana uhakika kuwa amekaa hapo kwa muda gani. Leo bibi yake anakuja kumtembelea. Hajui atamwambia nini bibi yake. Je, amwambie kuhusu mkono wake? Kwa vyovyote vile bibi yake ataona. Je, amwambie kwamba kazi ni kubwa na nyingi? Bibi yake anawasili (mwigizajimwingine) o o o Igiza mazungumzo kati ya Miremba na msichana mwingine Igiza mazungumzo kati ya Miremba na bibi yake kama vile Unaweza pia kuongeza waigizaji wengine kama vile mwanamke anayemfanyiakazi Miremba na mume anayemkosesha raha Miremba Hatua: 1. Anza kwa kueleza dhana ya igizo waeleze kwamba watatarajiwa kuigiza hali inayoonyesha mtoto aliyekata tama kutokana na kazi. Soma mpangilio wa matukio kwa vikundi vya watoto na waeleze kwa makini matukio hayo.wapangie nafasi za kuigizza kuhakikisha kwamba kila mmoja anashiriki,bila kujali udogo wa nafasi hiyo,wateue waigizaji wengine kwa kila tukio (mwajiri,walezi wafanya kazi wengine na kadhalika). 2. Eleza kua wataigiza mchezo kwa vijana wenzao na walezi watakua watazamaji/hadhira.lazima waseme kwa sauti inayoeleweka na polepole.lazima watumie mbinu za msingi za drama/maigizo,kamakama vile kutokuwapa mgongo wazamaji/hadhira.lazima watie chumvi miondoko yote na vitendo. 3. Vipatie vikundi nusu saa au zaidi kwa ajili ya kuandaa igizo fupi kuhusu mpangilio wa matukio uliyowasomea.kama wakipenda waruhusu waendeleze zaidi maigizo hayo. 4. Vikundi vikishakua tayari kuigiza waalike watu wote wakiwemo walezi(pamoja na eneo litakalokua jukwaa).ttayarisha orodha ya mfuatano wa igizo.hakikisha kwamba vikundi vyote vinaangaliana wakati wa igizo.kwa igizo la kwanza unda mazingira yatakayowawezesha watu wengine kujua hali hiyo inahusu ninikwa kila igizo lipatie waigizaji wake. 5. Kila kikundi cha waigizaji lazima kipewe muda wa kati ya dakika 5 hadi 10 kuigiza.simamia muda Baada ya maigizo: 6. Ashiria mwisho wa maagizo na waambie watoto watoke kwenye uigizaji wao.washukuru waigizaji wote na waambie walivyojihisi kuhusu igizo. 86

7. Waombe maoni watazamaji waombe mawazo kuhusu wanachotakiwa kufanya watoto kwenye maigizo.waulize namna hali hiyo inayohusisiana na maisha ya watoto waliowazungumzia. 8. Ongoza majadiliano kuhusu kilichokua kinafanyika katika maigizo.toa muktasari wa hoja muhimu zilizotolewa. MAREJEO: Adapted from ILO-IPEC (2002) SCREAM Stop Child Labour Module entitled Role-play (Author: Nick Grisewood), and Activity Six Charades Game pp 43-44 Gender Equality and Child Labour, A participatory tool for facilitators. Amorim, A., Samouiller, S. Badrinath, S. & Murray, U. (2005) ILO/IPEC Geneva J.10.4 Zoezi mgawanyo wa kazi kila siku wa wavulana na wasichana. Katika zoezi hili,vijana wataanza kuelewa shughuli mbalimbali ambazo wanaume/wavulana na wanawake/wasichana hufanya.pia wataona jinsi mgawanyo wa kazi katika kaya nyingi unavyowaongezea wanawake na wasichana kazi nyingi zaidi za kufanya kwa ajili ya ustawi wa kaya.watajifunza zaidi athari iliyopo wakati watoto wanapotakiwa kuanza kufanya kazi za shamba au kaya na hawana nafasi tena ya kwenda shule. Muda: Wastani wa saa 1 na dakika 30. Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea. 1. Anza kueleza kuwa inafurahisha kuangalia mambo yanayotokea katika siku kwa wavulana na wasichana katika jamii wakati wanapofanya kazi au wanapokwenda shule. 2. Waonyeshe washiriki jinsi ya kuchora Saa ya kazi za kila siku(tazama mchoro hapo chini)kasha wakiwa katika vikundi vidogovidogo na vikundi mchangsnyiko(wavulana na wasichana),waambie kila kikundi wachore saa ya kazi za kila siku,moja kwa wavulana na nyingine kwa wasichana.lazima waeleze sifa za mvulana na msichana huyu( umri na aina ya kaya wanayoishi:lazima wabaki wakati mkuu wa kaya anapokua mzee,mwanamke,mwanaume au mtoto). 3. Vigawe vikundi,eleza kuwa nusu ya vikundi wachore saa kuonyesha mtu huyo(msichana au mvulana)anafanya ninoi anapokwenda shule katika siku ya msimu wa mvua na wengine watafanya hivyo kwa msichana na mvulana ambaye haendi shule na atatakiwa afanye kazi shambani au nyumbani msimu wa mvua.bila shaka mwezeshaji atasoma mifano miwli ifuatayo ya msichana na mvulana wakifanya kazi. 87

Kisa cha 1: Gyan. Gyian ni mvulana mwenye umri wa miaka 10 au 12,hana uhakika.amekua akifanya kazi kama mtumishi wa nyumbani na mchunga ng ombe kwa kipindi cha miaka miwili.kila siku anaanza kazi saa 12 asubuhi kwa kufagia nyumba,kujaza ndoo za maji kusafisha varanda na sakafu,kutayarisha chai,anasidia kupika na kuhakikisha kwamba watumishi sita mhadi saba watu wazima wamepata maji ya kuoga na chakula ifikapo saa 1:00 asubuhi,wanapoondoka kwenda kazini.halafu anchunga ng ombe.anafanya kazi nyingine ndogondogo mpaka saa 7.00 mchana na kwa kawaida hupata saa chache za kupumzika mchana.jioni,anafanya kazi ndogondogo mpaka mnamo saa 2.00 usiku ambapo kwa kawaidahumaliza. Gyan anlipwa kiasi cha us$2.70 kwa mwezi kwa kazi zote hizi.anawapa wazazi wake kiasi fulani cha fedha hizi na kutumia kiasi kilichobaki kwa ajili yake.kila siku yumo kazini kuanzia saa 12.00 asubuhi hadi saa 2.00 usiku,siku saba kwa juma.gyan hajasoma shule. Kisa cha 2: Pia Pia alianza kufanya kazi akiwa na umri wa miaka 11 na kuhama kutoka kwenye nyumba ya familia yao.mwajiri wake alimwahidi mama yake kwamba atamlea Pia na kumtendea vizuri.kuishi nyumbani kwa mwajiri ni anasa zaidi kuliko kule aliko kulia Pia,ambako ilikuwa nyumba ndogo ya udongo.hata hivyo,pia anatakiwa kufanya kaazi kwa saa 12 kila siku,na hapati muda wa kutosha wa kupumzika. Pia anaamka saa 11.00 alfajiri na kwenda kuleta maji kisimani kabla kaya hajaamka.halafu anatayarisha chai kwa kila mtu.inapofika saa 1.00 chai tayari kutokana na hali hiyo,shughuli kuu anazofanya Pia kila siku ni kuosha vyombo,kupika/kutayarisha vyakula vingine,kusafisha nyumba,kufua na kurekebisha nguo.anawalisha kuku,kukamua ng ombe maziwa na kupalilia bustani ya mboga.kupika na kuandaa chakula kunachukua muda mwingi na lazima kufanywe mara tatu kwa siku,kutegemea nani anafanya kazi na kula nyumbani siku hiyo. Pia anaosha vyombo na kwenda kuteka maji angalau mara tano kwa siku.kkisima hakiko mbali sana,lakini ndoo anzotumia ni nzito.pia kwa kawaida anafanya kazi katika bustani ya mboga mchana 88

wote kabla ya wakati wa kuanza kutayarisha chakula cha jioni.anapopalilia na kuwinga kuchakuro/kindh na sungura. Mshahara wake ni anapewa zawadi ndogondogo(kama vile nguo)na wakati mwingine,fedha kidogo,lakini hapewi fedha mara kwa mara.pia inabidi afanye kazi hata akiwa mgonjwa.pia,hana muda wa kwenda shule,lakini.kisirisiri anapenda kusoma. 4. Waambie wana kikundi wachore duara kubwa linalofanana na saa kwenye ardhi au kwenye karatasi.eleza kuwa duara linawakilisha saa inavyoonyesha saa 24 na kua vijana watawekea alama kila shughuli kwenye duara kulingana na wakati inapofanyika.kama kuna shughuli ambazo zinafnyika kwa wakati mmoja.kama malezi ya mtoto na kulima bustani,zitajwe kwa pamoja katika nafasi ya mudammoja.eleza kua itawabidi kutumia taswira kuwakulisha shughuli mbalimbali ili saa ieleweke kwa kila mtu. 5. Wape fursa kila kikundi kuwasilisha saa zao. 6. Waombe wana vikundi walinganishe siku ya mvulana na msichana,na aina za shughuli(kazi na mapumziko).masuala yafuatayo yatakusaidia katika kuwezesha majadiliano Muda umegawanyika vipi katika saa? Muda gani umetumika katika shughuli ambazo zinaingiza fedha? Muda gani unatumika kwa shughuli za uzalishaji wa chakula? Muda kiasi gani unatumika kwa ajili nya kazi za nyumbani na nani anafanya sehemu kubwa ya kazi hizi? Je,kuna shughuli zozoze za jamii zinazofanywa? Vipi kuhusu muda wa mapumziko? Je,kuna muda mkiasi gani kwa ajili ya kulala? Muda huu unabadilika kiasi gani katika misimu mbalimbali ya mwaka? Saa za wasichana na wavulana zinaweza kulinganishwa vipi?je,wanafanya mambo tofauti?wanatumia muda kiasi gani kwa kila shughuli? Je,ukubwa wa kazi zao utaathiri mahudhurio yao katika shamba,darasa na stadi za maisha kwa vijana? Tufanye nini ili kuhakikisha kuwa hata wasichana/wavulana wenye kazi nyingi zaidi wanaweza kushiriki shuleni na kwenye SDSMV? 89

MIFANO YA SAA SHUGHULI ZA KILA SIKU J.11. Haki za Ardhi na Mali. Haki za ardhi na mali masuala muhimu wakati mtu anapoanza kupanda mazao.mkulima anahitaji ardhi,zana za kilimo,ghala za kuhifadhia na nk.kuweza kuanza shughuli zao wenyewe za kilimo. Haki za Ardhi na mali huandaliwa kupitia kanuni na sheria.hasa kwa ardhi ya kilimo vijijini,sheria na kanuni za kimila bado zinatumika(hasa kwa ardhi ya kijiji).sheria na kanuni hizi za ardhi hutofautiana katika sehemu mbalimbaliza Tanzania.Kwahiyo kwa wakulima vijana kuelewa kwa ukamilifu kuhusu sheria na kanuni za mahali zinazohusu haki za ardhi na malinna,kwa maana hiyo,kuna kuna uwezekano gani kwao kupatiwa ardhi na kuweza kuanza shughuli zao za kilimo. 90

J.11.1.Haki za Ardhi ya kijiji na mali. Muda: Saa 1 na dakika 30 Vifaa matayarisho:chatipindu na kalamu za kuchorea,mwalike kiongozi wa jadi wa kijiji au ofisa wa kijiji anayehusika na haki na mali(kutoka kwenye ofisi ya mtendaji/kiongozi wa Jadi au ushirika). Htua: 1. Anza na mada ya haki za Ardhi na Mali.Waambie vijana wataje ardhi yote na mali vinavyihitajika kua dhamana ya shughuli ako mwenyewe za kilimo(ardhi,maji ya kumwagilia,zana,,usafirishaji,ghala za kuhifadhia nk).viorodheshe kwenye karatasi. 2. Waulize vijana wavyofikiri wataweza kufanya mpango wa kupata mali zote hizi zinazohitajika wakati watakapoanzisha shughuli zao wenyewe za kilimo. 3. Mtambulishe kiongozi wa jadi wa kijiji au ofisa wa kijiji na mwambie aeleze sheria za mahali hapo ni zipi kuhusiana na haki za Ardhi na mali zinazohusu vitu vilivyotajwa hapo na vijana. 4. Washawishi vijana wamuulize maswali kiongozi wa jadi wa kijiji au ofisa wa kijiji kuhusu namna gani,hasa vijana wenye dhamana ndogo/fedha,watakavyopata ardhi na mali vilivyoorodheshwa kwa ajili ya kuazishwa shughuli zao wenyewe za kilimo(kukodi,kupitia ndugu,kama kikundi nk). 5. Muulize kiongozi wa jadi wa kijiji au ofisa wa kijiji atawasaidiaje vijana wanoshiriki katika SDSMV kupata ardhi na mali inayohitajika kwa kuanzishwa shughuli zao wenyewe za kilimo. 6. Toa muhtasari wa mahitimisho ya majadiliano kuhusu haki za ardhi na mali. J.12. Mada ndogo: uuza mazao Vijana wanaoshiriki katika SDSMV watajifunza baadhi ya stadi za kazi kuuza kwa kuuza sehemu ya mazao kutoka kwenye shamba darasa lao.ili waweze kufanya hivyo,kwanza watatakiwa kujua watamuuzia mazao hayo nani na wapi,watauza kwa mashwrti gani,kwa bei gani n.k. 91

J.12.1.Zoezi: Kutayarisha mkakati wa kuuza mazao ya shamba darasa. Muda: Saa 2 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea Hatua: 7. Waarifu vijana kwamba wanatarajiwa kuuza sehemu ya mazao yao kutoka katika shamba darasa na kwamba wanatakiwa kutayarisha wakati wa kuuza 8. Waambie vijana waketi kwenye vikundi vyao vidogo na waorodheshe masuala yote muhimu wanayoweza kuyafikiria na kufanya uamuzi ni lini watauza sehemu ya mazao ya mavuno wanayoyamiliki katika shamba darasa 9. Waambie vikundi vidogo wawasilishe na kujadili orodha ya mwisho ya masuala muhimu yanayohusu kuuza mazao yao (watauza lini, wapi na watamuuzia nani, ubora unaotakiwa, ufungashaji unaotakiwa, usindikaji, bei n.k. 10. Waambie vijana warudi kwenye vikundi vyao na kushughulikia maelezo kwa kila suala linalohusu kuuza mazao ya mavuno wanayomiliki katika shamba darasa 11. Waambie kila kikundi kiwasilishe rasimu yao ya mkakati wa kuuza mazao yao J.12.2. Zoezi: Kumtembelea Mjasiriamali - Je, walifanyeje? Mjasiriamali aliyefanikiwa kiasi anakaribishwa kueleza amefanya nini hadi kufanikiwa kwenye biashara yake. Vijana wanahimizwa kuuliza baadhi ya maswali waliyotayarisha. Zoezi hili litawasaidia vijana wa SDSMV kubaini sifa na stadi anazotakiwa kuwa nazo kuwa mjasiriamali. Kuwaalika wajasiriamali wenyeji mara kwa mara kutasaidia kuorodhesha msaada kwa SDSMV kutoka katika jumuiya ya wafanyabiashara wenyeji Muda: Saa 3 Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea 92

Matayarisho: Mtafute mtu kama mfugaji kuku, mfugaji wa wanyama au mkulima wa mazao atakayekuwa tayari kushirikiana uzoefu katika kuanza na kuendesha biashara. Zungumza na mgeni huyo mapema, hasa kama kuna vitu maalumu unavyotaka avitaje. Mjasiriamali mwenyeji hana budi kueleza namna alivyoanzisha biashara au shughuli yake kwa kiwango kidogo na kuanza kuiimarisha na kufanikiwa. Mweleze Mjasiliamali huyo kuwa madhumuni ya ziara ni kuonyesha stadi za sifa zinazohitajika kupata biashara yenye mafanikio Namna ya Kufanya: 1. Ukishamchagua na kuzungumza na Mjasiriamali anayefaa kutembelea shule, waambie vijana ni mjasiriamali ganina anafanya nini 2. Waambie vijana wafikirie baadhi ya maswali watakayomwuliza mgeni. Waambie wanze na maswali rahisi na baadaye maswali ya kina zaidi. Kwa mfano: Je, alipata wapi wazo? Je, ni nani alimsaidia? Je, alihitaji fedha za ziada kuanzisha biashara? Je, wateja wake ni kina nani? Je, kuna matatizo gani ya kuendesha biashara? Je,ilimbidi apitie mashaka gani? Je, jambo gani zuri kabisa na baya kuhusu kuendesha biashara yako mwenyewe 3. Kama mgeni huyo ni mwanamke, wahimize vijana kuuliza maswali kuhusu wanawake wanaoendesha biashara 4. Andika maswali muhimu kwenye chati au ukutani na jaribu kupanga mfuatano wa maswali ya vijana 5. Mara mgeni akifika, mtambulishe na eleza tena madhumuni ya ziara yake kwavijana 6. Mpe muda wa kutosha Mjasiriamali mgeni kushirikiana uzoefu wake na vijana bila taabu 7. Ruhusu muda wa kutosha kwa maswali kutoka kwaijana na andika hoja muhimu ubaoni ili yajadiliwe baadaye 8. Baada ya kumalizika masuala yote (au muda umekwisha) mshukuru mjasiriamali aliyetembelea 9. Baadaya mjasiriamali kuondoka, endesha majadiliano yasiyo rasmi. Waulize ni mambo gani aliyosema mjasiriamali ambayo yamewafurahisha sana vijana. Ni mambo gani aliyosema mjasiriamali waliyoona magumu kuyaelewa. Eleza msamiati wowote ambao waliuona mgumu kuuelewa. 93

10. Waulize vijana wamejifunza nini kuhusu namna mtu anavyoweza kuanzisha biashara yake mwenyewe au waambie vijana wataje mambo machache muhimu waliyojifunza kuhusu ujasiriamali. 11. Jadili baadhi ya sifa za mgeni zilizochangia mafanikio yake kama mfanyabiashara 12. Toa muhtasari wa majadiliano na hakikisha kuwa hoja muhimu zilizopo kwenye maelezo kwamwezeshaji (hapa chini ) zimeelezwa Maelezo kwa Mjasiriamali Ujasiriamali ni kitendo cha mtu kuanzisha biashara mpya. Ni uwezo wa kukuza biashara ndogo tangu mwanzo bila kitu kwa kuanza kubainisha na kupata rasilimali za kuzalisha bidhaa ambayo wateja wanahitaji na kununua. Ujasiriamali unamaanisha kuwa watu na mashirika wanazalisha bidhaa na hudumakwa kupata faida ya kiuchumi. Ujasiriamali unahitaji utamaduni wa biashara unafafanuliwa kuwa ni:- Seti ya mitazamo, maadili na imani vinavyofanyakazi ndaniya jamii mahususi au mazingira yanayoleta tabia ya kibiashara na matarajio ya kuelekea kujiamini 15 Mjasiriamali:- - Mtu anayeweza kubuni na kuanzisha biashara yake ndogo ndogo - Anabainisha bidhaa (mazao au mifugo) ya kuuza na watu watakaonunua bidhaa hiyo - Anapata vyanzo vya kupatia malighafi (chakula chamifugo,mbegu,dawa za kuulia wadudu n.k.) kuzalisha bidhaa na kutumia njia bora za uzalishaji ili kupata faida na kuendesha maisha mazuri Sifa za Mjasiriamalibora: - Ana uwezo wa kuwashawishi watu, teknolojia na mikakati inayofaa mahitaji ya soko - Anaweza kuchukua mashaka (kufanya uamuzi mzito bila hofu ya kushindwa) 94

- ana uwezo wa kupanga kushinda hali na mazingira magumu (kwa mfano, ukame, magonjwa na wadudu waharibifu wanapotokea, n.k) - Ni mtu mwenye nia na nidhamu, mwenye uwezo wa kutekeleza dira na mawazo - Ana uwezo wa kupanga mwelekeo wabaadaye (mtazamo wa siku zijazo) kuweza kuwa mjasiriamali, mtu ni lazima atathmini uwezo wake mwenyewe, kuafuta taarifa za ushauri, kutoa uamuzi, kupanga muda wake, kutekeleza wajibu uliokubaliwa, kuwasiliana na kufanya mapatano, kushughulika na watu wenye mamlaka na madaraka, kutanzua matatizo na kuamua migogoro, kutathmini utendaji wa mtu, na kumudu msongo na mhemko. Stadi nyingi zinazotakiwa kwa ajili ya biashara tayari zinafundishwa kwenye vipengele vingine vya mtaala wa SDSMV. Kwa mfano, mtaala unashughulika na kutanzua tatizo (kuhusu kilimo, udhibiti wa wadudu, mifugo, kilimo cha bustani), kupanga mipango ya baadaye na kufanya uamuzi kuhusu mbinu za msimamizi wa mazao kwamsingi wa majaribio ya kazi. Moduli nyingi zinahusikana kujistahi, kuwaheshimu wengine, na kadhalika. Unaweza kurejea moduli hizi kwa kujikumbusha, na kuhusisha 95

J.12.3. Zoezi: P zote (Bidhaa,Mahali, Bei, Utangazaji, Watu na Mpango) Zoezi hili linalokusudia kueleza kwa ukamilifu hadithi ya kuuza mazao yaliyozalishwa katika SDSMV kinahusisha kuelewa zaidi na si kulima mazao tu. Wanaweza kujua namna ya kulima zao Fulani, lakini wanatakiwa pia kufikiria namna ya kuuza bidhaa hizo. Zoezi hili linaeleza utaratibu unaofaa wa kufikiria namna ya kupata faida ambao watu wa biashara na masoko wanaita P 6 ( Bidhaa,Mahali, Bei, Utangazaji, Watu na Mpango) Muda : Saa 2 Vifaa na Matayarisho: Chora chati kama iliyopo hapa chini na P 6 za biashara na masoko. Kama kiwango cha kusoma, kuandika na kuhesabu ni kidogo, tumia picha kuwakilisha kila eneo P P P P 96

Inafanyaje kazi? 1. Wekeza vijana kuwa utawaambia hadithi kuhusu kufuga kuku.anza zoezi kwa kupitia mada ya kufuga kuku kutokea kwenye moduli za kilimo za SDSMV za kilimo.waulize wanafunzi wanachokumbuka.waulize maswali kama vile: Je,nini tofauti kati ya kuku wanaoachiwa kujitafutia chakula na wanaofugwa kwenye mabanda? Kwanini unawajengea mabanda kuku? Unahitaji vifaa gani kufuga kuku? Je,nini sifa za mvifaa vya kulishia na kunywea maji kuku? Unahakaikishaje kua mayai mengi zaidi yanaweza kukusanywa? Kwa nini vitulio vya kuku ni muhimu? Je,nini nsifa za kuku bora wa mayai ya vifaranga? Pia pitia njia za kuwakinga kuku na aina za magonjwa wanayopata.sisitiza namana kuku alivyomuhimu kwa lishe kwa nyama na mayai. 1. Onyesha chati ya P6 hapo juu na eleza maana ya kila neon kwa muhtasari (angalia maelezo ya wawezeshaji hapo chini.) Halafu soma hadiythi ifuatayo mara mbili kwa watoto.wakizingatia P6 wakati wanaposikiliza. Moja kati ya hadithi nyingi za kuku: Durah anakwenda mjini kumtembelea dada yake.dada yake anamwambia Durah kuwa anafuga na kuuza kuku anapata fedha kwa njia hiyo.durah anadhani hili ni wazo zuri sana.anarudi kijiji kwake na kuwaita wawili kati ya marafiki zake.marafiki hao waliwahi kuhudhuria SDSMV mwaka jana na wanakumbuka kusoma kuhusu maana ya kufuga kuku.durah anawaambia kuhusu haja ya kuku wengizaidi na anapendekeza kuwa wafa nye pamoja biashara hii.kila mmoja anakubali na wote wanachangia coin 20T.Siku inayofuata Durah na rafiki yake mmoja wanakwenda mjini kununua vifaranga 25 vyenye umri wa siku mmoja.kwahiyo ni lazima walale usiku mmoja mjini ili wapate vifaranga siku ya pili.wakati walipofika mjini hakukuwa na vifaranga vilivyobaki kutokanana na mahitaji kua makubwa kwa vifaranga vyenye umri chini wa siku moja.kwakua walilazimika kutumia fedha kununulia chakula na malazi,etamudu kununua vifaranga 15 tu siku ya pili. Baada ya kurudi kijijini wanabaini mkua wanahitaji pia chakula cha kuku.kaka take Durah 97

anaanza kujenga banda kwa ajili ya kuku,wakati,wakati Durah na rafiki yake wanakwenda kununua chakula cha kuku kutoka kwenye duka la kijiji.chakula hiki ni ghali na ubora wake ni mdogo,kwa sababu duka hilo haliwezi kumudu kununua chakula kipya kila wiki siku miliyofuata kuku watatu wamekufa kwenye kibanda kutokana na hali ya hewa ya joto na kwa sababu kaka yake hakumaliza kujenga paa la kuwalinda. Katika wiki chache zijazo,kikundi kinapeana zamu ya kuwahudumia kuku wao.kutokana na sababu mbalimbali (kupenya kwa mbwa kwenye uzio,ugonjwa unaowana baadhi ya kuku) walibaki kuku 7 tu kati ya 15.Hatimaye kuku wamekua wakubwa na kutoshwa kuuzwa.hata hivyo kijijini kwao,hakuna hata mtu anayetaka kuku,kwa sababu kila mmoja anao wa kwake.kutokana na kukosekana kuku kwa mahitaji wanaamua kuuza kuku kwenye soko la mjini. Sokono hapo,inaelekea kila mtu alikua akiuza kuku,wenye afya na wakubwa kuliko wa kwao.kusema kweli wanawake wanaanza kuona kuwa kuna aina nyingi za kuku wa kuuza sokoni.hatimaye walipofanikiwa kuuza kuku wao wadogo,wanabaini kwamba hawakupata faida yoyote kutokana na mtaji wao wa kuanzia.waliporudi nyumbani wajadili wamekosea nini. 2. Waulize vijana : Je,Durah na marafiki zake walipata wapi wazo la kuuza bidhaa yao (Eleza kuwa kuku ndiyo bidhaa yao). Kina nani walikua wateja wao (watu)? Je,walifikiria sana kuhusu bei ya kuku? Je,walifikiria ipasavyo kuhusu watakakouza bidhaa yao? (mahali) Je,walifikiria namana ya kuwavutia wateja (utangazaji)? Je,walikua na mpango wa jumloa kwenye biashara yao? (walioshorokishishwa) Je,watu hao walijitoa kiasi gani (Durah,marafiki wake na kaka yake)? Kwa jumla,unadhani Durah na marafiki zake wana soko kwa ajili ya kuku wao? Je,ulidhani bidhaa ndiyo inayofaa? 3. Eleza kuwa Durah na marafiki wake walitakiwa kutayarisha mkakati kuuza kuku wao? 4. Rudia kusoma hadithi hiyo na halafu waulize vijana watoe mapendekezo yao ku boresha mkabala wa kila hoja ya P 5. Hitimisha kwa kuwaambia vijana kua uuzaji wa kutafuta soko unahusu mahitaji ya wateja na kutosheleza mahitaji hayo kwa faida. Maelezo kwa mwezeshaji. 98

P6 hizi hazitabaki kuwa P kwa lugha nyingine ifuatayo ni taarifa ya chanzo/usuli kuhusu namna P6 zinavyochangia kwa mkakati wa mauzu/utafutaju soko. Bidhaa Fikiria kuhusu bidhaa au huduma: je, ni bidhaa bora? Je, inalingana na mahitaji ya wenyeji au wateja wanaotarajiwa? Je,wateja wanataka bidhaa ya namna gani? Bei: Je, ni bei nafuu kwa wateja? Je, bidhaa inauzwa kwa bei iliyopunguzwa ikilinganishwa na wengine wanaouza bidhaa ya namna hiyo? Je, bei itapungua kama itauzwa kwa wingi,au kwa wateja wanaotarajiwa? Je, inawezekana kupanga bei tofauti kwa wateja tofauti? Je, ni lazima ufanye hivyo? Utangazaji Je, watu wanajuaje kwamba bidhaa yako inauzwa? Je, bidhaa hiyo inatangazwa kwa usahihi? Je, kila mmoja anaweza kuiona bidhaa hiyo ikionyeshwa eneo la mauzo? Mahali: Je, bidhaa inauzwa wapi? Je, sehemu ya mauzo inafikika kwa urahisi? Je, unaweza kuwafikishia wateja bidhaa? je, ni wazo zuri? Je, mahali pa kuuzia panawavutia watu waliolengwa kununua? Watu: 99

Je, mfanyabiashara anahitaji stadi gani? Je, kuna uhusiano gani kati ya mfanyabiashara na washitiri wake? Je, ni mwenye tabasamu na mkarimu? Je, ni mtu maarufu katika eneo, kijiji au mji? Je, ana jina/sifa nzuri? Mpago: Je, nini mpango wa jumla kwa bidhaa ikiwemo kuitangaza na kuiuza? Marejeo : Story and notes come from pp 152-154 GET Ahead for Women in enterprise. Training Package and Resource Kit. Page 55. Also pp 26-27 Kane, K and the staff of Tototo Home Industries. Faidiki! Mombasa, Tototo Home Industries and World Education, Inc., 1990 100

J.12.4. Zoezi: Kuuza! Igizo Bubu Igizo bubu ni shughuli ya kuchekesha inayoweza kutumiwa kama kichangamsho katika ti ya somola muda mrefu au mfululizo wa masomo kuhusu ujasiriamaliau kabla ya kuanza shughuli nyingine. Igizo bubu kwa kawaida nimchezo wa kukisia ambapomtu mmoja au kikundi cha watu wanaigiza dhamira fulani. Mtu mmoja au wawili wanaigiza igizo babu na washiriki wengine lazima wakisiewanajaribu kuonyesha nini. Kanuni ya msingi ya igizo babu ni kwamba wanaofanya igizo hilo hawazungumzi. Sababu ya msingi ya kucheza igizo bubu kwenye zoezi hili na kuigiza njia mbalimbali za kutangaza na kuuza bidhaa. Zoezi linawezakufanywa mahali popote panapolenga shughuli za kiujasiriamali. Halina budi kusisitiza umuhimu wa kuuza stadi Mada: Saa moja mbili Vifaa na matayarisho: 1. Tayarisha orodha ya bidhaa zinazouzwa mahali hapo: aina zote za mbegu;makopa ya ndizi; ndizi vania,karanga, mahindi, mtama, viazi vitamu, kahawa, chai, kunde, uwele,mhogo, mpunga, pamba, alizeti, maharage ya soya, nyama ya ng ombe, au aina nyingine ya nyama; asali, uyoga,korosho, samaki wa kukausha, maua ya mapambo, mayai, kuku mbichi na kadhalika 2. Andaa mpangilio wa matukio yanayoweza kuigizwa kwa jozi yanayohusu kuuza bidhaa mbalimbali zinazofaa kwa hali ya mahali. Matukio hayohayana budi kuwa kati ya mteja na muuzaji. Tukio halina budi kuwa na maelezo machache ya shughuli ya kupanga na kuonyesha bidhaa, kuwavutia wateja na kuuza bidhaa. Andika matukiohayo au uwe tayari kuyaeleza kwa vijana wasiojua kusoma. Aina nyingine za matukio zinatayarishwa hapa chini lakini utawezakuandaa matukio yanayofaa zaidi wewe mwenyewe 101

- Mwigizaji A: Unaonyesha na kuuza maua ya mapambo. Unajaribu kumpata mteja aje aangalie jinsi yanavyovutia, kuyanusa na kuyanunua. Wewe ni mcheshi mwenye furaha na tabasamu sana. Unajaribu kumshawishi mtu aliyehuzunika anayepita kununua baadhi ya maua - Mwigizaji B: Una huzuni kwa sababu mama yako anaumwa. Hupendi kununua maua, ingawa muuzaji maua mwenye mvuto na furaha anakufuata wewe. Pengine maua yatamfurahisha mama yako? Lakini huna fedha za kutosha. - Mwigizaji A: Unauza mafagio yenye mpini mfupi uliyotengeneza mwenyewe unataka kuonyesha namna inavyofaa kwa kufagilia sakafu na ubora wake. Unamfuata mteja. Ana wasiwasi kuhusu ubora wa mafagio hayo - Mwigizaji B: Mtu mmoja anajaribu kukuuzia mafagio ya mkono. Una wasiwasi kwamba yanaweza kuvunjika. Hutaki kuumiza mgongo waako kwa kutumia fagio la mpini mfupi - Mwigizaji A Umetayarisha juisi ya matunda tamu na unaiuza sokoni. Unawezaje kuwavutia wateja katika eneo lako. Lazimauonyeshe kwamba ni kinywaji cha matunda na tunda zuri. Unataka kuonyesha namna ilivyo tamu. - Mwigizaji B Una kiu sana. Kuna genge lenye juisi inayouzwa. Huna uhakika kama juisi ni nzuri au hapana. Pia huna hakika kama imeongezwa maji mengi na kwamba maji yaliyoongezwa ni mazauri. Hatimaye unaiyona na kuipenda - Mwigizaji A : Una samaki wabichi (tilapia) kwa kuuza (mmoja mkubwa ba wawili wadogo ) na wanatukutika wakati wanapowatoa kwenye maji kuwaonyesha wateja. Unataka kumuuza samaki mkubwa lakini mteja anaelekea kutaka kuwanunua samaki wadogo kwa bei nafuu - Mwigizaji B: Unataka kuwanunua tilapia wadogo kwa bei sawa na mkubwa. Lazima upatane na mwuzaji. Mwuzaji anataka kuuza samaki mkubwa 102

- Mwigizaji A: Umebakiwa na kuuza kuku wawili wazuri. Kuku wako wamefugwa kwa kulishwa nafaka nzuri na vitamin, kwa hiyo wanaonekana wenye afya. Unataka kuwaarifu watu kuwa kuku wako ni wakubwa na kwamba kuku mmoja anaweza kulisha familia ya watu 10 - Mwigizaji B: Kuna mtu anauza kuku wakubwa. Huna hakika kama anaweza kununua kuku wakubwa. Je ni vizuri? - Mwigizaji A: Unauza mayai. Inabidi uwe mwangalifu yasijevunjika au kwamba wateja wasiyashike na kuyavunja. Unaamua kuyauza nyumba hadi nyumba. unagonga mlango mmoja na uso wenye tabasamu unajibu. Anataka kujua bei yake lakini yaelekea hana uelewa wa kununua mayai - Mwigizaji B: Uko nyumbani unafikiria kuku wako. Unasikia mlango unagongwa na kufunguka. Kuna mtu anayeuza mayai. Unajaribu kuyainua na kuyashika. Unataka kujua yanauzwa bei gani, hata kama hutaki kuyanunua Inafanyaje kazi? 1. Pasha kwa kuwaambia kila mmoja aorodheshe vitu vinavyouzwa sokoni. Rejea kwenye safari ya sokoni. 2. Kata mpangilio wa matukio uliyokwisha tayarisha kwa mchezo bubu. Wape vijana tukio la kuigiza pamoja na kueleza kwa makini mpangilio wa matukio kwa kila jozi. Wape vijana dakika 5 kutayarisha tukio na kuliendeleza zaidi. 3. Vijana wanapewa fursa ya kuigiza kibubu na kuigiza mpangilio wa matukio. Kila jozi ya waigizaji itapewa dakika 3 hadi tano kuigiza mchezo bubu wao. Wengine kikundini hawana budi kukisia nini kinachoendelea na wanauza nini. Wawezeshaji hawana budi kuwashawishi hadhira/watazamaji watoe mawazo. Lengo ni kuwawezesha vijana wengine kukisia nini kinachoendelea haraka iwezekanavyo na kukisia bidhaa inayouzwa 4. Unaweza kuanzisha aina ya shindano. Watangazie kwamba mshindi ni jozi ambayo igizo bubu lake inakisiwa haraka sana, au mtu ambaye mara nyingi anakuwa wa kwanza kukisia kwa usahihi igizo bubu na bidhaa. Unaweza pia kutoa alama kwa kila jozi kutegemea wameigiza vizuri kiasi gani mpangilio wa matukio. Mweeshaji anaweza kuweka alama za timu gani imekisia 103

idadi kubwa ya maigizo bubu kwa usahihi, nakutoa alama za ziada kwa timu iliyoigiza vizuri zaidi. Timu yenye idadi kubwa ya alama inashinda. 5. Baadaye huna budi kuongoza majadiliano kuhusu kuuza bidhaa na kuzitangaza Maelezo kwa Mwezeshaji Kama ilivyo kwa michezo mingi, sheria na mbinu za michezo zinatofautiana sana kutoka nchi moja hadi nyingine na wawezeshaji hawana budi kutumia muundo wowote wa maigizo bubu waliyoizoea zaidi. Wakati mwingine jozi zinahitaji msaada katika uigizaji wao, au vijana wote wanaweza kuhitaji vidokezo zaidi ili kukisia kile kinachoendelea, hasa kama igizo bubu ni gumu mno au vijana wanaoigiza si stadi wa kuigiza kuruhusu kusema na mchezo wa kuigiza kuliko igizo bubu Marejeo: Imechukuliwa kutoka Adapted from Activity Six Charades Game pp 43-44 Gender Equality and Child Labour, A participatory tool for facilitators. Murray, U., Amorim, A., Samouiller, S. Badrinath, S. (2005) ILO/IPEC Geneva Mada ndogo: Kupata Faida Kujifunza namna kukokotoa faida na hasara na kueleza umuhimu wa kutunza kumbukumbu, hakuna hata mtu mmoja atakayepata hasara kwenye shughuli ya biashara. Lazima tujue maana ya faida Faida = mapato ya mauzo kutoa gharama za kufanya mauzo hayo J.13.1. ZOEZI: Je, Kiuzwe Bei Gani? Muda: Saa moja Vifaa: Chatipindu na kalamu za kuchorea na andaa mifuko mitatu yenye mawe 10 kila mmoja. Inafanyaje kazi 1. Wagawe wanafunzi wa SDSMV katika makundi matatu. Kilaki kundimfuko wenye mawe 10 madogo. Waambie kwamba kila mfuko umenunuliwa kutoka mji wa jirani kwa senti 50. Waambie kwamba kila jiwe kusema kweli ni jiwe maalumu (jiwe la thamani) na kila moja litauzwa peke yake. Kiambie kila kikundi kiamue watauza kila jiwe kwa bei gani. Mawe yote kwenye mfuko lazima yawe bei moja. Wanapewa dakika 10 za kujadili na kuamua 104

2. Wakati huo huo, chora jedwali lifuatalo ubaoni Bei Mapato ya Mauzo Gharama Faida Kikundi la 1 Kikundi la 2 Kikundi cha 3 3. Waambie wanafunzi wa SDSMV tuchukulie kwamba kila kikundi kimeuza mawe yao yote. Waulize je, kila jiwe wameuza bei gani? Jaza majibu kwa kila kikundi na kujua namna hesabu zao ni sahihi. Je, hesabu zao ni sawa au tofauti? Kwa mfano kama kikundi kimoja kinauza jiwe kwa coin 5, kikundi kingine kwa coin 10 kila jiwe nakikundi cha tatu kwa coin 7 kila jiwe, cati iliyojazwa itakuwa kama hivi. Chati ya Mfano Bei Mapato ya Mauzo Gharama Faida Kikundi la 1 5 50 50 0 Kikundi la 2 10 100 50 50 Kikundi cha 3 7 70 50 20 4. Hakikisha kama kuna jibu lolote kutoka kwenye shamba linaloonyesha kwamba wanapata hasara. Kwa kikundi kinachotoza gharama kubwa zaidi kwa kila jiwe, waulize kama wanafikiri bei zao ni halisi 5. Unawezakutaka kufanya zoezi hili mara nyingine kwa kutumia mfano mwingine: Unaweza kufanya zoezi kuwa gumu zaidi, kwa mawe makubwa kuwa na bei tofauti ikilinganishwa na mawe madogo 105

6. Kama wanafunzi wa SDSMV wanaelekea kuwa tayari, unaweza kujadili gharama zaidi kuliko kuanzia coin 50 zilizotumika kununulia jiwe. Kwa mfano, waulize wanafunzi wa SDSMV kama wanafikiri kuwa watalazimika kulipa mahali (genge) sokoni kuuza mawe. Je watalipia kupata kupata nafasi sokoni? Je, watamlipa mtu kuwauzia mawe? Je, watafunga kila jiwe wanalouza? J.13.2. Zoezi: Kutabiri Faida na Hasara. Muda : Saa 1 Vifaa: Chatipindu na karatasi za kuchorea Inafanyaje kazi? 1. Soma hadithi ifuatayo au tunga hadithi inayofaa zaidi yenye majina tofauti na kadhalika. Kama wanafuzi wa SDSMV hawajui kusoma, kuandika na kuhesabu, tumia michoro/picha kwenye chati badala ya maeno Bashir, Gamba na Pili wanaishi pamoja katika kijiji kidogo katika eneo lenye joto na ukame. Wanataka kununua mbuzi. Walijadiliana wazo hilo pamoja na kufikiri kwamba kuna vichaka na mbuga za kutosha jirani kumlisha mbuzi. Walijadiliana wazo hilo pamoja na kufikiri kwamba kuna vichaka na mbuga za kutosha jirani kumlisha mbuzi. Wanafikiri kuwa maziwa ya mbuzi yana virutubisho vingi, na kama mambo yatakuwa mazuri yataweza hata kumwuza. Waliamua waweke akiba ili wanunue mbuzi atakaye gharimu coin 50 106