KATIKA UCHAGUZI MKUU HUU TUSIRUHUSU MAFISADI WALICHEZEE TAIFA

Similar documents
Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Human Rights Are Universal And Yet...

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

MIONGOZO MIWILI KUPAA NA KUTUNGULIWA KWA AZIMIO LA ARUSHA

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

K. M a r k s, F. E n g e l s

KIJARIDA JUU YA HAKI ZA RAIA KATIKA MFUMO JINAI

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

April 14, 2016 COUNTY ASSEMBLY DEBATES 52

NGUO MPYA ZA UKOLONI. Mikataba ya Ushirikiano wa Kiuchumi kati ya Umoja wa Ulaya na Afrika. Agosti 2017

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

Agano Lililofunikwa Kwa Damu

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.

Kuwafikia waliotengwa

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

PDF created with pdffactory trial version

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU 9 DESEMBA 2011.

Kamanda Boko Haram Mkristo-Prof. Ojobi

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

United Pentecostal Church June 2017

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

Waandishi: wa Toleo la 5. Scholastica Jullu Athanasia A. Soka Safina Hassan Mary Njau. Toleo la 5: 2008 ISBN

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT

Tanzania, sasa kondoo anayesubiri kuchinjwa

UNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

Adai kupigwa teke na mwalimu akienda kuswali Wanafunzi Wakristo wasimama kidete kumtetea

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,

Upatikanaji wa Silaha Ndogo ndogo na Hisia za Usalama nchini Kenya: Ukadiriaji

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.

ONYO LA MWISHO KWA DUNIA

Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College

Kutetea Haki za Binadamu

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Na Kituo cha Msaada wa Kisheria kwa Wanawake Toleola4

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

Roho Mtakatifu Ni Nini?

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

BUNGE LA TANZANIA MKUTANO WA NANE. Kikao cha Ishirini na Nane Tarehe 16 Julai, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Spika,

Transcription:

KATIKA UCHAGUZI MKUU HUU TUSIRUHUSU MAFISADI WALICHEZEE TAIFA Edward Lowasa ni balaa kwa Taifa! Democratic Party (DP) inatarajia kufikisha Mahakamani chama cha CCM pamoja na wanachama wake sita, Edward Lowasa na wengine, kwa mujibu wa Ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Tanzania, kwa kosa kubwa sana la kuvunja Katiba na Sheria za Nchi kwa kuanza kampeni ya Uchaguzi kabla ya wakati unaopasa kwa mujibu wa Sheria. 1. Tunao ushahidi mzito unaothibitisha kwamba Edward Lowasa na wenzake walianza kampeni ya urais ndani ya chama chao kabla ya wakati, na kwamba chama chao kiliwapa adhabu ya kutofanya siasa kwa miezi 12. Lakini safari hii Lowasa ameanza kampeni ya urais Arusha kwa mkutano mkubwa sana wa hadhara wa kampeni haramu na kumwaga rushwa ya kutisha! 2. Kama ni wadhamini alipaswa kuwapata katika ofisi za chama chake, katika mikoa nane (8) tu Tanganyika na mikoa miwili tu Unguja na Pemba, wadhamini 45 tu katika kila mkoa. Lakini Edward Lowasa amefanya mikutano nchi nzima, ya kuwaahidi maelfu ya wananchi katika kila mkutano wa hadhara, mambo atakayofanya kama wakimpa kura zao awe Rais! Hii ndiyo kampeni halisi, ambayo ni ukiukaji wa Katiba na Sheria za Nchi! Uchaguzi Mkuu unaendeshwa na Sheria, hivyo ni lazima Sheria ichukue mkondo wake dhidi yake kwa kuivunja. 3. Edward Lowasa amevunja Katiba ya Nchi na Sheria ya kiwango cha fedha kinachoruhusiwa kutumika katika shughuli halali za Uchaguzi, kiasi kwamba CCM na Taasisi zote za uchunguzi wa kifedha nchini, upelelezi wa Jinai na Usalama wa Taifa ni mlazima wanayo kazi muhimu sana ya kupata ukweli kuhusu haya mabilioni ya fedha yanayomwagwa nchini na fisadi Edward Lowasa, ameyapata wapi na kwa namna gani, kumehusika Money laundering au la, kama mapato ya mapesa hayo yote ni halali, na kama mapato hayo yote yalilipiwa kodi inayopasa kwa ajili ya Taifa. vs

Ni marufuku kabisa tena ni makufuru Edward Lowasa kuruhusiwa kugombea urais, kwa sababu amevunja Katiba ya Nchi na Sheria na Kanuni za Uchaguzi. Sifa mojawapo ya kustahili kugombea uongozi wa nchi yoyote ni maadili mema na uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na taratibu za Utawala wa Sheria 2 4. Edward Lowasa, kwa kujimilikisha maeneo nchi nzima kwa kutumia kifisadi Uwaziri wake wa Ardhi, ameliweka Taifa katika hatari kubwa ya mmwagiko wa damu baina ya wakulima na wafugaji, baada ya kueneza nchi nzima makundi ya ng ombe wake, na kusababisha mapigano makali ya mara kwa mara kila mahali nchini kati ya wafugaji wake na wakulima. Kwa sababu ya uovu huu hata katika kampeni yake haramu Lowasa ameshindwa kusema lolote juu ya kilimo, ingawa ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi yetu na ndiyo shughuli inayotunza uhai wa asilimia 95 ya wananchi! Kwa kuwaingilia wakulima katika ardhi yao, kuwaua ovyo, kuwaonea kiasi cha kufisha matumaini yao katika kilimo, kumeifanya kauli mbiu ya Kilimo kwanza kuwa porojo tu ya kisanii! 5. Edward Lowasa ni mwiko kabisa kupewa kugombea urais, kwa sababu siyo tu aliutumia kifisadi Uwaziri wa Ardhi akajitajirisha na kujipatia maeneo makubwa ya ardhi nchini kote, bali alitumia kifisadi zaidi uwaziri wa nchi katika ofisi ya Waziri Mkuu, katika uagizaji wa mashangingi ya Wabunge, mawaziri, wakuu wa Mikoa na Wilaya. 6. Edward Lowasa alikemewa mnamo mwaka 1995 na Mwalimu Nyerere anayeenziwa na CCM lama Baba yao, alipotaka kugombea urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, wala hakuweza kujitetea kwavile utapeli wote aliojitajirishia ulikuwa mezani. Leo baada ya mabiashara haramu mengi na kulipora sana Taifa kukiwa ni pamoja na utapeli wa kununua mvua Thailand na kuliibia Taifa mabilioni ya fedha kwa kutumia kampuni hewa ya RICHMOND, huyu ni fisadi-nyangumi. Ni mlemavu wa rushwa tu wa kununuliwa na mapesa machafu anayomwaga Lowasa, anayeweza kumruhusu fisadi Edward Lowasa agombee urais. Sifa za mtu wa kukugombea Urais zimeelezwa bayana na Mwenyezi Mungu katika Kumbukumbu la Torati 17:15-20, ambazo Edward Lowasa hana hata mojawapo! Lowasa awali alikemewa na Mwalimu Nyerere ambaye CCM wanamuenzi kama Baba yao, kuwa hafai kabisa kuwania urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, kama alivyomtangaza hata Reginald Mengi pale alipolazimika kujiuzulu Uwaziri Mkuu kwa ajili ya wizi kwa kampuni hewa ya Richmond, lakini leo akiwa fisadi la kutisha zaidi kuliko papa eti anataka urais! Si ajabu kwamba magabacholi yalioipora vibaya sana Nchi hii kama Sigh Setti na hata Nazir Karamagi wote wamo katika genge la Edward 3 Lowasa! Si ajabu hata fisadi Reginald Mengi leo kuungana na fisadi Lowasa yakizingatiwa machafu yake yeye mwenyewe, na kuhusika kwa Mengi na mauaji ya Chacha Wangwe, pamoja na mpango wa Chadema wa kumwua Mchungaji Mtikila, waraka feki wa kujaribu kuupotosha ukweli ukatangazwa kwa ITV yake. Katika uwaziri wake katika ofisi ya Waziri Mkuu, na katika Uwaziri wake wa Ardhi na Uwaziri Mkuu, Lowasa alifanya ufisadi ambao katika nchi kama China zenye uchungu na maslahi ya mataifa yao angekuwa wa kupigwa risasi hadharani, lakini katika nchi yetu anatafuta urais!

7. Edward Lowasa AFYA yake imempiga marufuku kugombea Urais! Kwa ajili ya kila ajira duniasni kote, moja ya mashart makuu ni lazima mwombaji awe na afya iliyo bora, ndiyo sababu ni lazima ajira ya kila mwombaji itegemee taarifa ya kitaalamu ya madaktari, inayothibitisha kwamba hana dosari kiafya. Sharti hili ni la lazima kwa sababu: a. Majukumu yote atakayopewa mwajiriwa atayatekeleza kikamilifu kwa kutumia viungo vya mwili wake, kwahiyo viungo vyake vyote ni lazima viwe katika hali iliyo imara kwa ajili ya kazi. b. Hata kama kwa uthibitisho wa kitaalamu wa madaktari mwajiriwa anazo akili nzuri kichwani mwake, akiwa na hitilafu katika viungo vingine vya mwili wake huathiri afya ya akili zake na uwezo wa utendaji wa akili zake. c. Kazi ya Rais ni ngumu sana, kwa sababu ni pamoja na kusimamia shughuli zote za maendeleo ya nchi nzima, na matatizo yote yanayowatokea wananchi wote kila walipo, na kusimamia utekelezaji wa majukumu yote ya watendaji wote katika Taifa, hivyo kwamba maamuzi sahihi yanatokana na afya bora yenye kuhakikisha uwezo unaopasa wa kiakili wakati wote d. Hitilafu katika afya hudhoofisha uwezo wa kifikira na kusababisha maamuzi mabovu, ambayo huleta athari mbaya sana kwa Taifa. Na udhaifu huo huathiri mpaka maadili na hata uzalendo wa huyo kiongozi mdhaifu. Kwa mfano akipatikana Rais anayeishi kwa matumaini, kwa hofu ya kupoteza uhai kabla hajaweka sawa mambo yake na ya familia na jamii yake atatumikia maslahi yake zaidi kuliko Taifa, tatizo hilo la afya likawa limelikosesha Taifa kipaumbele, na kuliangamiza kimaendeleo! e. Wanaowania kugombea urais ni lazima wachunguzwe kwa makini sana afya zao, kwa sababu kukifanyika makosa akatawazwa mwenye hitilafu za kiafya, atakwenda kuwa mzigo mzito sana kwa Taifa, hususan ugharamiaji wa utunzaji wa uhai wake ndani na nje ya nchi, kukosekana na umakini anaopasa kuwa nao kwa ajili ya dhamana kubwa aliyopewa n.k. Kutokana na AFYA yake kuwa dhaifu sana hata kwa kumwona kwa macho tu, kabla ya uchunguzi wa kitaalamu ni kwamba Edward Lowasa hawezi kabisa kugombea Urais. Kwani amekosa sifa muhimu sana ya afya bora, ambayo ni ya lazima kwa mtu yeyote anayestahili kupewa dhamana kubwa sana ya kuliongoza Taifa. Pengine hata kugombea urais kwenyewe anatafuta kutokana na hitilafu ya kiafya, iliyosababisha udhaifu katika kufanya maamuzi, hivyo amejikuta kwa bahati mbaya anagombea asichokiweza kabisa. Ni lazima wagombea wote wa Urais, wa Ubunge na hata wa Udiwani wachunguzwe kwa makini afya zao kabla ya kupewa kugombea, na hata kuchunguzwa tena katikati ya muhula wa utumishi wao, kama kweli tunalithamini na kuliheshimu Taifa. Sifa za urais ni wito au uhanga kwa ajili ya Nchi ambao ni zaidi ya maadili ya kizalendo, maono, vipawa na AFYA BORA. Ni dhana potofu sana kwamba sifa ya urais ni kushabikiwa na umati wa watu! Kwa sababu wengi hufuata mapesa na husombwa hata na magari ili umati wa kishabiki tu upatikane. Lakini kumpenda mtu huwa lazima kuwe na sababu, wakati ushabiki ni pepo mchafu au psychological deficiency.

8. Edward Lowasa ni msaliti wa Nchi yetu, kwa kulazimisha kwa ufisadi akisaidiwa na mwuaji mkuu dikteta Paul Kagame kuutwaa Urais wa Nchi yetu, ili tuwe koloni la Hima (Tutsi) empire. Ni taraja la dikteta Kagame kuwa wakimpa urais mtu wao Edward Lowasa, eti Bandari ya Dar es Salaam itakuwa yake, kwa ajili ya kusafirishia utajiri wa koloni lake la Congo (DRC), hila chafu ambayo Rais Kikwete aliipinga vikali kwa uzalendo wake, ikawa sababu mojawapo ya kuchukiwa na beberu huyo. Mwuaji Kagame ni jemadari wa Watusi wenye ile imani chafu sana, kwamba mungu wao aliumba Wabantu kwa ajili ya utumwa kwa Watusi, ila Watusi eti aliwaumba kuwa watawala wao! Imani hii ndiyo chimbuko la mkakati wa Watusi wa kuliteka eneo lote la Maziwa Makuu chini ya Hima au Tutsi empire, ambayo mkono wake umo katika Uchaguzi huu na mtu wao ni Edward Lowasa!. Lowasa anapigiwa debe kwa nguvu zote katika vijiwe vya Watusi nchini Rwanda, Burundi, Uganda na hapa nchini. Kagame anamiliki binafsi zaidi ya dola za Marekani Bilioni 2 anazolipora koloni lake la Congo, ndiyo sababu kampeni nzito ya urais wa Lowasa inayo mapesa ya kutisha! Miezi mitano iliyopita walimwagwa wanawake mia tatu Kigoma na Kagera, na wengi zaidi jijini Dar es Salaam, na kusambaa mikoani, wakimhubiri Lowasa kwamba ndiye anayefaa (kwa Watusi) kuwa Rais. Kampeni ya urais wa Lowasa inaendeshwa kila mahali na maajenti wa Hima empire waliopenyezwa au kununuliwa katika kila taasisi, vijiweni, makanisani na misikitini ambako Lowasa anamwaga rushwa ya kufuru, kutoka katika bahari yake ya pesa chafu. Ni Bi Janet mkewe Kagame aliyeleta mapesa mengi Kigoma akafikia Coast View Hotel, yaliyotumika kumpokonya Ubunge mzawa Dr. Walid Kaburu na kumpa raia wa Rwanda aitwaye Peter Serukamba mwenye ukoo na Kagame, ambaye safari hii amepangiwa na Kagame Ubunge wa Kigoma Kaskazini, kwa ajili ya udhibiti wa maeneo ya Manyovu na Kagunga, lango lake la utajiri wa Congo kuja Bandari ya Dar es Salaam, ambayo anatarajia kuitia mkononi kwa Urais wa mtu wao Edward Lowasa. Hii ni moja ya sababu za Kagame za kuweka rais wake yeye Burundi hata kwa mabavu. Saa ya ukombozi ni sasa! Wakati jasusi wa Kagame, Peter Serukamba anapiga kampeni ya nguvu sana ya Edward Lowasa, hatuushangai pia kumwona Ana Tibaijuka aliyepoteza Uwaziri wa Ardhi kwa kashfa ya Escrow Account, akipigania bila aibu urais wa chaguo la Watusi, Edward Lowasa! Kwani mwanamke huyu alitangulia kupewa na Museveni takrima ya ng ombe 100 akawaruhusu Kagame na Museveni kuingiza malaki ya ng ombe zao katika Hifadhi za Taifa letu Mkoani Kagera, pamoja na wanajeshi wao ambao walidhani ingekuwa rahisi kuliteka hilo eneo letu! Pamoja na mapesa ya Kagame, bahari ya mapesa ya urais wa Lowasa ni pamoja na mabilioni yanayotuhumiwa kutokana na ufisadi wa mamia ya mamilioni ya dola za Marekani yaliyoinyima Serikali yetu pamoja na Kampuni ya Vodacom mapato ya kutisha. Tunavitaka vyombo vyote vinavyohusika vichunguze taarifa hizi kwa msaada wa taasisi za nje kama FBI na Scotland Yard, ili ukora ukithibitika wafikishwe mbele ya Sheria mafisadi hawa wote! Fisadi Edward Lowasa, anasaidiwa na Mwajemi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Rostam Aziz, ambaye ameikomba nchi yetu Dola za Marekani 6 zaidi ya 550 milioni, zikiwa ni pamoja na mauzo ya hisa zake Vodacom, mapesa ya Taifa letu aliyojipatia kwa kutumia kampuni tata ya Dowans, na mapesa ya Taifa ya EPA aliyolitapeli Taifa kwa ukora wa kitumia kampuni hewa ya Kagoda Agriculture Ltd.

Gabacholi Rostam Aziz alihusika hata katika kuua Shirika letu la Reli, na ndiye anayetuhumiwa kuleta vichwa 54 vya treni, kisha akavivushia Kenya, ili ikitimia ndoto ya urais wa Lowasa avirudishe, na waweze hata kujimilikisha Shirika lote la Reli. KAGAME NA HIMA EMPIRE NYUMA YA LOWASA Nchi yetu iliyokamiwa na Watusi wenye ile imani chafu sana, kwamba mungu wao aliumba Wabantu kwa ajili ya utumwa kwa Watusi, ila Watusi eti aliwaumba kuwa watawala wao! Imani hii ndiyo chimbuko la mkakati wa Watusi wa kuliteka eneo lote la Maziwa Makuu chini ya Hima au Tutsi empire, ambayo mkono wake umo katika Uchaguzi huu, watu wao wakiongozwa na Edward Lowasa! Mkakati wa Hima empire ulianza tangu tulipopata Uhuru. Mimi kwa kuwa niliujua undani wake Mungu aliniongoza kuupiga vita tangu ulipokuwa unajengwa misingi imara ubeberu huu. Sote tunajua jinsi huko Burundi na Rwanda Wahutu ambao ni asilimia 85% walivyokuwa watumwa wa Watusi ambao ni asilimia 14% tu, kwa zaidi ya miaka 400, hadi mapinduzi ya ukombozi wa Wahutu yaliyoongozwa na Gregory Kayibanda nchini Rwanda mwaka 1959. Watusi hawakuikimbia nchi yao ya Rwanda kwa ajili ya mateso, bali waliikimbia laana (abomination) ya kuwa sawa na Wahutu, na zaidi kuwa chini ya uongozi wa Wahutu wanaoamini kuwa ni watumwa wao! Ni kwa imani hii potofu kwamba genocide katika Maziwa Makuu ilianzia Burundi, baada ya mapinduzi ya Rwanda, mpaka Umoja wa Mataifa ukakiri kwamba maangamizi ya Wahutu yaliyokuwa yanafanywa na Watusi nchini Burundi ilikuwa genocide. Kwani Wahutu wanaume, wanawake na watoto wasio na silaha walikuwa wanaangamizwa kinyama na Watusi kwa malaki na maelfu! Kosa pekee la Wahutu lilikuwa uasi wa kudai usawa na Watusi! Hata uvamizi wa RPF nchini Rwanda tangu mwaka 1990 uliitwa ukombozi yaani kurejesha haki ya Watusi ya kuwatawala watumwa wao. 7 Kutokana na kutumiwa vibaya sana na Bill Clinton alipokuwa Rais wa Marekani na Tony Blair alipokuwa Waziri Mkuu wa Uingereza, Umoja wa Mataifa umefedheheka sana kwa kunyamazia genocide ya Burundi kwavile ni Wahutu waliokuwa wanaangamizwa na Watusi! Lakini Rwanda ambako Watusi nao waliuawa, ingawa RPF (Watusi) waliua Wahutu mara nne zaidi, liliitwa janga la dunia, na ukweli ukabadilishwa usomeke kwamba Wahutu au Interahamwe eti ndio wameangamiza Watusi 1.2 milioni!! Mungu ashukuriwe kwamba sasa Jumuiya ya Kimataifa inageukia ukweli, kwamba hiyo genocide ya Rwanda wauaji wa mamilioni ya watu ni RPF ikiongozwa na dikteta Paul Kagame, aliyeanza kwa kuwaua Marais wawili Wahutu, Habyarimana wa Rwanda na Cyprien Ntaryamira wa Burundi. Ulimwengu sasa unafunguka akili, kwamba kwavile ilipoanzishwa hiyo genocide nchini Rwanda na Kagame Aprili 1, 1994 idadi ya Watusi haikufika hata 400,000, hivyo kwamba katika hao 1,200,000 waliouawa ni dhahiri kwamba zaidi ya laki tisa walikuwa Wahutu, kwani hata Watusi si wote waliouawa, wengi wao walibaki hai baada ya genocide, ambayo hata wale Wahutu takriban 2,000,000 walioukimbizia uhai wao Congo, Kagame na RPF waliwafuata kule na kuwaangamiza wote!

HIMA EMPIRE INAIVA Utawala wa Watutsi walioukusudia ukamate eneo lote la Maziwa Makuu na hata Kusini mwa Afrika kama mizimu na mikakati yao itafanikisha, umeshika kasi kubwa sasa, baada ya kumaliza kuiteka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, ambako Kagame alifanikiwa kumwua Rais Laurent Kabila na kumkabidhi nchi kijana wake Mnyarwanda aitwaye Hypolite Adrien Kanambe, aliyembandika jina bandia Joseph Kabila, na kumpa makamanda karibu wote wa juu wa Jeshi na watawala wote muhimu wa koloni lake hilo kutoka Rwanda. Ni Rwanda inayoitawala Congo! Baada ya kuikamata Congo na utajiri wake wote, Watusi sasa wana nguvu za kutisha za kiuchumi kwa kuipora nchi ya watu, na Kagame anao uwezo mkubwa sana wa kununua watu, kugharamia propaganda za kuudanganya ulimwengu, na hasa kuhusu damu ya mamilioni ya watu anayoimwaga usiku na mchana, na kuendesha mauaji ya wapinzani wake duniani kote, pamoja na Watutsi wenzake wote wanaopinga itikadi yake ya Tutsi Supremacy, wanaotetea usawa wa 8 binadamu wote na undugu wa kifamilia wa raia wote wa nchi yao, ambao kwa Kagame ni wasaliti na wahaini! Kagame amekuwa anaendesha mauaji ya kinyama katika nchi mbali mbali, kama vile Nchi Za Magharibi, Kenya alikowaua Sendashonga, Lizinde na wengine, Africa Kusini alikomwua hivi karibuni ndugu Kalegeya, na ambako amejaribu mara kadhaa kumwua Jenerali Kayumba Nyamwasa. Unyama wa Kagame uliliumiza sana Taifa letu, alipomwua mtaalamu wetu wa Sheria Profesa Jwani Mwaikusa, kwa kuutumia ubalozi wake. Ni Kagame aliyetishia hata kummaliza Rais wetu Jakaya Kikwete, alipotoa ushauri makini wa kidiplomasia AU, kwamba tatizo lake yeye Kagame la uhasama wa kiuaji na FDLR alimalize kwa amani kidiplomasia, kwa kukaa nao wayazungumze yaishe. Kagame akaropoka, I will hit him at the right time! (Nitampiga kwa wakati unaofaa) Katika kuimarisha ubeberu wake, Kagame alifanya uswahiba mkubwa sana na Rais Nkurunzinza wa Burundi, kwa lengo la kumfanya awe kibaraka wa kitumiwa ndani ya Tutsi empire yao. Lakini alipomtaka amtumie kummaliza Rais Kikwete akamkatalia, Kagame aliropoka kumng oa Nkurunziza madarakani, kwa ndoto ya kuikabidhi Burundi kwa Watusi wa itikadi kali tena, waliomwua kinyama hata marehemu Rais Melchior Ndadaye! Machafuko yote yanayoendelea Burundi yanatengenezwa Kigali na Paul Kagame. Hata maandamano ya Bujumbura yalijikita katika sehemu nne tu zenye Watusi wengi. Walalahoi wengi walishawishiwa kuandamana kwa motisha ya franca mpaka 50,000. Na wengi waliokubali ukimbizi walihubiriwa na manabii kutoka Kigali kwamba unakuja mmwagiko wa damu ambao haujawahi kutokea Burundi. Wengine wakadanganywa kuwa wakiwa ukimbizini watapelekwa uhamishoni Marekani na Canada. Lengo la maandamano na kuzalisha wakimbizi lilikuwa kuimarisha uzushi wa Kagame wa genocide, ili apate baraka za Jumuiya ya Kimataifa aendeshe maangamizi ya Wahutu Burundi, kwa kisingizio cha kukomesha hiyo genocide, kama alivyoteketeza mamilioni ya Wahutu wa Rwanda na Wakongo akalindwa na Bill Clinton na Tony Blair. Lakini safari hii Kagame ameshindwa kuipindua Burundi na kupachika mtawala wake yeye Pierre Buyoya, au Alexis Sinduhije, au Hussein Rajab aliyetuma makomando wake wakamtorosha kutoka gerezani Burundi na kumkimbizia Kigali, ili kuiweka Burundi katika Hima Empire.

Kagame ameshindwa kumng oa Nkurunzinza, kwa sababu Warundi wanamkubali. Amewapa Wahutu karibu asilimia kubwa ya nafasi za elimu ya juu, amewapiga jeki kiuchumi, amewaingiza kwa wingi majeshini, ametoa kipaumbele kwa elimu na maendeleo ya watoto na wanawake, elimu ya bure Shule za msingi, huduma za bure za afya ya watoto chini ya miaka 5 na akina mama wazazi. Amewainua Wahutu kiuchumi mpaka soko lao Bujumbura likawa la kimataifa, kabla ya kuunguzwa na Watusi. Watu wote wa eneo la Maziwa Makuu wanaoijua hatari ya hawa Watutsi wa itikadi kali ya Tutsi supremacy na mkakati wao wa Hima empire wa kuifanya nchi yetu iwe koloni lao kama DRC, wanasimama pamoja na ndugu zao wa Burundi. Tunaieleza hatari ya Kagame ili aepukwe Edward Lowasa, anayemdhamini aje atumiwe kuitawala nchi yetu kama anavyomtumia Hypolite Adrien Kanambe (Joseph Kabila) Congo! UBEBERU WA KAGAME DHIDI YA NCHI YETU Hatari waliyoishinda Warundi inaikabili Nchi yetu! Kwani kama tulivyotangulia kusema, kutekwa Nchi yetu ili iwe koloni la Watusi kulianza tulipokuwa tunapata Uhuru wetu! Watusi walianza kupenyezwa kila sehemu nyeti ya utawala wa nchi yetu, hatimaye wakaweza kuikamata Nchi yetu na kututawala bila sisi kujijua, nchi yetu ikatumika kuwatawalisha Watusi Burundi, Uganda na Rwanda. Leo Taifa letu liko uchi kabisa mbele ya Watusi hasa wa Rwanda na Uganda. Ndiyo maana Kagame anadiriki kutudharau kama mataahira, kiasi cha kumtambia Rais wetu kwamba I will hit him at the right time, na kuwaimbisha wacheza ngoma wake kwamba Mwanaume ni Kagame, Kikwete ni nini? Akajigamba kwamba eti hatuwezi kushindana naye, kwa sababu eti anazo karata nyingi za kutumaliza ndani ya nchi yetu akitaka! Ndiyo, ana majasusi wake kila mahali, na viongozi wetu wengi amefanikiwa kuwapachika wanawake zake, yaani ni victims of sexual espionage! Kwa mfano, Seth Kamanzi tuliyemsomesha sana kuliko raia wetu, akawa mhadhiri Chuo cha Fedha IFM, akajipenyeza mpaka akawa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM, alipomaliza kazi aliyotumwa alitorokea kwao Rwanda na siri zetu zote, ambako sasa ni Seneta! Taifa letu likawasomesha Profesa Silas Lwakabamba akawa Dean wa Kitivo cha Uhandisi, na Dr. Albert Butare. Hawa wakawa wakuu wa miradi ya UNDP Arusha, lakini yalipopatikana mapesa mengi ya miradi mikubwa, wakafanya kila mbinu chafu na kuyakimbizia kwao Rwanda, ambako yalitumika kuanzisha Institute of Science and Technology! Leo Prof. Silas Lwakabamba ni Waziri wa Elimu kwao Rwanda, mwenye majukumu ya siri pia ya kushughulikia vibaraka wa Kagame katika nchi yetu, kama Edward Lowasa, kwa ajili ya Hima Empire, ambaye Watusi wanajivunia sana kama vile tayari ni Rais wa koloni lao! Mfano mchungu zaidi ni Lt. Colonel Celestine Seromba, aliyekuwa katika sehemu nyeti sana kwa usalama wa Taifa letu, kama Mkuu wa kitengo cha IT cha Jeshi la Ulinzi wa Nchi yetu, chenye siri zote za Jeshi letu pamoja na data zote za silaha zetu, mafunzo yetu na mikakati yote ya Ulinzi wetu tuliyo nayo, yaani nguvu zetu zote kama Taifa! Alipomaliza kazi aliyotumwa na mwuaji Paul Kagame alitoroka na siri hizo zote, na kupokelewa kwao Rwanda na dikteta Kagame kama shujaa, na kupandishwa cheo mara moja kuwa Colonel!

Lakini majasusi zaidi ya elfu kama huyu wamepenyezwa katika idara ya Usalama wa Taifa, Jeshini, Polisi, Uhamiaji, Vyuoni, katika Wizara zote nyeti za Serikali yetu, katika mashirika nyeti ya umma, katika makampuni mbali mbali, katika taasisi za kimataifa, makanisani na hata misikitini, achilia mbali majasusi wanawake wanaojifanya makahaba! Ndiyo maana Kagame ana jeuri chafu ya kumdharau Rais wetu, na hata kumpangia kummaliza eti wakati atakaoona yeye unafaa, kama vile Rais wetu anaishi kwa hisani ya mwuaji Paul Kagame! Saa ya ukombozi ni sasa! Ndiyo maana Kagame ameropoka kwa dharau sana juu ya mapungufu ya Jeshi letu, na kulikuza sana la kwake yeye kwa ajili ya ubeberu, na kujilimbikizia silaha mpaka puani, zikiwemo rada na makombora ya kisasa ya Scud yanayoweza kupiga Dar es Salaam moja kwa moja! Ingawa nduli Idd Amin alitudharau kuliko Kagame lakini tukampiga, na ingawa karata za Kagame zimeshindwa Burundi, tayari Watutsi kule Rwanda, Burundi na Uganda wana hakika ya kuitawala Nchi yetu kama vile Congo, kwa kutubandika Rais wao Edward Lowasa! Inafahamika juu ya wadhamini wa Lowasa wa Kigali, Kampala na Bujumbura, kwamba kwa ajili ya huyu mtu wao wamemwaga mapesa mengi, ya kuhakikisha kwamba wanamkabidhi nchi yetu atawale kwa ajili ya maslahi yao, yaani Hima empire. Watutsi kama Meja Jenerali Anatoly Kamazima aliyepenyezwa katika Jershi letu, kisha akapewa Taasisi nyeti ya TAKUKURU, komando wa Kagame Derick Kataraiha ambaye ni mpwae Prof Lwakabamba, ambaye ni afisa mikopo wa Benki yetu ya NMB, ni baadhi tu ya Wanyarwanda waliokuwa katika kampeni nzito ya urais wa Lowasa tangu mwaka 2011, mtandao huo wa Lowasa ukiwa na nguvu kubwa mno kifedha, kwani Kagame anaipora Congo kishenzi kwa malengo haya. Katika kufanikisha ndoto yao ya Hima empire, Watusi wameikamata Jumuiya ya Afrika Mashariki (E.A.C), viongozi wengi wakiwa majasusi wa Jeshi la Kagame, kama Katibu Mkuu Dr. Richard Sezibera ambaye ametumika kujaza askari wengi wa Kagame kama maafisa waandamizi, ambao ni mbali ya Martin Ngoga aliyeongoza genocide ya Kagame ya kuwamaliza Wahutu wa tabaka la juu kwa kutumia ICTR, ambaye sasa yumo katika Bunge la Afrika Mashariki. Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo imenyolewa na Watusi wa Hima Empire, Burundi inapambana isinyolewe, na sisi lazima tushikamane kama familia moja ya wahanga wa Nchi yetu katika mipaka ya ardhi yetu, na kupinga kwa sauti moja kwamba fisadi Edward Lowasa ni marufuku kugombea Urais wa Nchi yetu, kwa sababu mahali anapostahili ni JELA na kupata ukarabati wa afya yake..