MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

Similar documents
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

MALENGO YA MAENDELEO ENDELEVU

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Dodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Ripoti ya Mwaka ya Utekelezaji wa MKUKUTA 2006/07

TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

MWONGOZO WA MAANDALIZI YA MPANGO NA BAJETI KWA MWAKA 2017/18

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;

MKAKATI WA PILI WA TAIFA WA KUDHIBITI UKIMWI ( )

MAPENDEKEZO YA MTANDAO WA WANAWAKE NA KATIBA TANZANIA

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

Songa kwenye kilele cha upeo. Masuala ya Msingi na Ujuzi juu ya Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

NGUZO KUMI ZA KILIMO KWANZA

Kutetea Haki za Binadamu

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)

Kuuelewa Mchakato wa Bajeti Tanzania Mwongozo wa Asasi za Kiraia

Mradi wa Usimamizi Endelevu wa Rasilimali ya Madini Ukanda

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko

Nilikua na Ndoto ya Kumaliza Shule Changamoto za Elimu ya Sekondari Tanzania

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

AZAKI PIGA KURA UCHAGUZI MKUU TANZANIA OKTOBA. #TanzaniaTuitakayo OKTOBA 2015 ILANI YA UCHAGUZI YA AZAKI TANZANIA.

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

Mhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,

5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:

TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Human Rights Are Universal And Yet...

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

HAKI NA TARATIBU ZA AJIRA, KAZI NA HIFADHI YA JAMII

Taarifa Kuhusu Hali ya Uchumi wa Tanzania

In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO

TANZANIA TAARIFA YA MWISHO WA UTEKELEZAJI

JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO, MHESHIMIWA DKT. PHILIP I. MPANGO (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO

HUDUMA ZA AFYA KWA WOTE

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

Kuwafikia waliotengwa

Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI

Programu ya Uendelezaji Mifumo ya Maji Vijijini (PUMMV) katika Tanzania. Modeli wa Ukodishaji Mradi

3. Mheshimiwa Spika, 4. Mheshimiwa Spika,

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

RIPOTI YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI

Mwongozo wa Utekelezaji wa Njia za S5-UUE (KAIZEN)-UUU Tanzania

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

Mipango ya miradi katika udugu

Ripoti hii ni kwa heshima ya wale wanaharakati wengi wa Tanzania ambao ndio binafsi wanaopitia hali iliyoangaziwa, na vilevile wale walioyapoteza

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

UFUATILIAJI WA MIRADI NA TATHMINI

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...

Kimesanifiwa na:- E.D.Kissuu ECOMM TANZANIA S.L.P ,Dar es Salaam. Simu:

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu WEMA

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013

Pronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12

KIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI

Kufanya Uwekezaji kuwa wa Manufaa kwa Afrika: Jibu la Mbunge kuhusu Unyakuzi wa Ardhi

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA SABA. Kikao cha Thelathini na Tisa Tarehe 1 Juni, (Mkutano Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A

HOTUBA YA WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA MHESHIMIWA DKT

ORDER NO BACKGROUND

HISTORIA, MAENDELEO NA MABADILIKO YA KATIBA TANZANIA TANGU UHURU HADI MIAKA HAMSINI YA UHURU 9 DESEMBA 2011.

Transcription:

HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika Madai Crescent, 7 Ada Estate, Kitalu Na. 154 S.L.P. 7192 Dar es Salaam, Tanzania Simu: +255-22-2664890-2 Nukushi: +255-22-2664893 Barua pepe: information@thefoundation-tz.org Tovuti: www.thefoundation.or.tz Twitter: @FCSTZ

Ndugu msomaji, Hili ni chapisho maalum kabisa kwa ajili ya tukio muhimu sana kwa Foundation for Civil Society na sekta nzima ya asasi za kiraia (AZAKI) nchini mwetu. Linahusu maadhimisho ya miaka 15 tangu kuanzishwa kwa taasisi ya FCS. FCS pamoja na wadau wetu wote kuanzia AZAKI, Wadau wa Maendeleo, wawakilishi wa serikali, vyombo vya habari na wengineo tulisherehekea maadhimisho haya mwezi Novemba mwaka jana. Chapisho hili pamoja na kuwakumbusha kuhusu kazi tuliyofanya kwa muongo mmoja na nusu ya kujenga moja ya sekta madhubuti kabisa ya AZAKI barani Afrika kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, pia litakua kumbukumbu ya mambo yote muhimu yaliyosemwa na wadu wetu wakati wa maadhimisho hayo. Kwa Foundation, maadhimisho hayo yalikua kumbukumbu ya ahadi na juhudi ya kushirikiana na Wadau wa Maendeleo na Serikali na taasisi zake muhimu katika kujenga AZAKI. Kwa niaba ya asasi zote za kiraia na sekta nzima ya AZAKI nchini Tanzania, tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa wadau wetu wote kwa kushirikina nasi kwa miaka 15 kufikia sasa. Hivyo basi, hili chapisho linahusu matukio na hotuba muhimu za maadhimisho ya Miaka 15 ya FCS yaliyofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Wasemaji wengi kutoka kwenye sekta ya AZAKI, Sekta Binafsi, Serikalini na wanataaluma walishiriki mijadala mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo. UJUMBE WA MKURUGENZI MTENDAJI Miaka 15 ya kuwezesha sekta ya asasi za kiraia (AZAKI) nchini Tanzania Kama hukuhudhuria maadhimisho hayo, chapisho hili ni kwa ajili yako kwani limebeba mambo muhimu yaliyosemwa wakati wa sherehe hizo. Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru Wadau wa Maendeleo kwa kutufadhili na kutuwezesha kufanya kazi yetu kwa miaka 15 hii. Hii imetuwezesha kujutuma zaidi, kujitolea zaidi na kuwa wabunifu katika kutoa ruzuku na kujenga uwezo kwa AZAKI na hivyo kuwafikia wananchi wengi na jamii zao Tanzania Bara na Visiwani. Vilevile, napenda kutoa shukrani za kipekee sana kwa mdau wetu mkubwa kabisa Serikali na taasisi zake zote tunazofanya nazo kazi kwa kutuelekeza na kusimamia masuala ya kisera ya kazi yetu ya kuboresha maisha ya wananchi nchini. Tunakaribisha mashirikiano na ushauri wao katika utekelezaji wa kazi zetu na miradi ya AZAKI tunazowezesha nchini kote. Mwisho kabisa, napenda kushukuru wadau wote walioshiriki nasi wakati wa maadhimisho ya Miaka 15 ya FCS. Tunaahidi kushirikiana zaidi na wadau wote wakati tukiendelea na kazi yetu ya kujenga AZAKI nchini Tanzania. Asanteni sana! Francis Kiwanga Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society KWENYE TOLEO HILI Mchapishaji Foundation for Civil Society Mratibu Hamis Adam Tuma maoni kupitia: 7 Madai Crescent, Ada Estate, Kitalu No. 154, Kinondoni, Dar es Salaam Simu:+255-22-2664890-2 Nukushi: +255-22-2664893 Baruapepe: information@thefoundation-tz.org Tovuti: www.thefoundation.or.tz Kanusho: Maudhui haya ni maoni ya waandishi. Hayatoi msimamo rasmi wa Foundation for Civil Society au Wadau wa Maendeleo. Tahadhari imetumika kupitia taarifa zilizochapishwa, na zaidi ya makosa ya kawaida ya kibinadamu mchapishaji hatahusika na hasara yeyote itakayotokana na kutumia chapisho hili. 1 2 5 7 8 10 UJUMBE WA MKURUGENZI MTENDAJI NDOTO YETU HOTUBA YA MGENI RASMI UJUMBE WA WADAU WA MAENDELEO MAFANIKIO YA FCS AZAKI NA SEKTA BINAFSI 2 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society

NDOTO YETU KUJENGA SEKTA YA ASASI ZA KIRAIA TANZANIA Na Dk. Stigmata Tenga, Rais wa Foundation for Civil Society Safari ya Foundation for Civil Society ilianza mwaka 2002 ambapo wadau mbalimbali ikiwemo serikali na Wadau wa Maendeleo (DPs) waliafiki ukosefu wa rasilimali katika kuwezesha asasi za kiraia na hivyo kukubaliana kutengeneza mazingira yatakayowezesha upatikanaji wa ruzuku na huduma za kujenga uwezo kwa asasi za kiraia (AZAKI). Tangu mwanzo mwa safari tumekumbana na changamoto na kujifunza mengi, lakini mafanikio ndio yamekuwa yakitusukuma kuendelea mbele zaidi. Wakati tunatimiza miaka 15 ya Foundation, tunajivunia kuweza kutoa ruzuku kwa miradi ya maendeleo ya AZAKI na pia kujenga uwezo wa AZAKI zaidi ya 5,000 zilizopo Tanzania Bara na Visiwani. Mpaka sasa, tumeweza kuwekeza kiasi cha Sh bil 200 katika lengo hili. Na cha kujivunia zaidi ni kwamba katika AZAKI tulizozifikia, nyingi ni zile ndogo ndogo za ngazi ya chini kabisa ya jamii yetu kwenye Wilaya na Kata mbalimbali. Kiasi hiki cha ruzuku, idadi ya AZAKI na miradi yao ya maendeleo tuliyofikia inatufanya kuwa kati miongoni mwa taasisi kubwa kabisa za utoaji ruzuku kujenga asasi za kiraia barani Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara. Hili ni jambo la kujivunia sana kwetu kuweza kutajwa kama kiungo muhimu katika ukuaji na maendeleo ya maelfu ya AZAKI katika jamii yetu. Tunajivunia sana kufanikiwa kuwezesha miradi ya maendeleo ya jamii iliyofikia Watanzania zaidi ya milioni 30. Miradi hii ni pamoja na ushiriki wa wananchi kwenye maamuzi ya michakato ya maendeleo, ufuatiliaji na usimamiaji wa maamuzi na utendaji wa watumishi wa umma, utawala bora na usalama wa kijamii. Takwimu zetu zinatufanya kuwa taasisi muwezeshaji mkubwa kabisa kwa asasi za kiraia nchini. Ni ukweli ulio wazi kabisa kuwa mafanikio yetu pamoja na maelfu ya AZAKI yamewezeswa kwa kiasi kikubwa sana na ruzuku na uwezeshaji kutoka kwa Wadau wetu wa Maendeleo. Kwa miaka 15 sasa, wametupa nguvu na uwezo kufanya kazi kubwa ya kujenga sekta ya asasi za kiraia nchini. Hivyo basi, nachukua nafasi hii kutoa shukrani za dhati kwa niaba ya AZAKI na mamilioni ya wananchi wa Tanzania waliofaidika na mashirikiano yetu na Wadau wa Maendeleo. Asanteni sana! Mwaka 2003, miezi 12 tu baada ya kuanzishwa, tuliwezesha AZAKI 32 kutokana na ruzuku tuliyopata kutoka kwa Wadau wa Maendeleo watatu (3) kwa kipindi hicho. Huo ni mwaka wetu wa kwanza kabisa. Lakini hivi sasa, baada ya miaka 15 na kufikia mamilioni ya wananchi na mamia ya jamii, Foundation inashirikiana na Wadau wa Maendeleo 10 kutoka nchi tofauti. Hawa ni pamoja na Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID), Shirika la Maendeleo la Norway (NORAD), Shirika la Maendeleo la Uswisi (SDC), Shirika la Maendeleo la Denmark (DANIDA), Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA), Shirika la Maendeleo la Kanada (CIDA), Ubalozi wa Uholanzi, Ubalozi wa Ufaransa na mashirika ya PATH, EQUIP na Trade Mark East Africa. Kwa upande mwingine, mashirikiano na ruzuku kutoka kwa Wadau wa Maendeleo yasingetoa matunda na mafanikio yetu kama tusingepata usaidizi, usimamizi na ushauri wa kisera kutoka kwa mdau wetu mkubwa kabisa, Serikali na taasisi zake zinazohusika na sekta ya asasi za kiraia nchini. Shukrani za kipekee kwa mamlaka za mikoa, wilaya na kata mbalimbali ambako AZAKI zetu zinatekeleza miradi ya maendeleo. Niwakumbushe tu kuwa Serikali ni Mdau wetu mkubwa kabisa na wa kimkakati kwa maendeleo ya AZAKI nchini. Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society 3

Kwa kifupi, tunajivuia yafuatayo kwa miaka 15 ya kazi zetu: Uwezeshaji wa raia/wananchi kwenye masuala ya haki zao za kisheria Kupunguza ukatili wa kijinsia kupitia kampeni za kuhabarisha na kuelimisha jamii Kuwezesha masuala ya usalama na ulinzi wa mtoto Kuwezesha wanawake, hususan wa vijijini kuhusu masuala ya haki za ardhi Kuwezesha mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI Kuwezesha wanawake na vijana Kuwezesha ushiriki wa wananchi kwenye michakato ya maendeleo kama maamuzi, bajeti, ufuatiliaji wa matumizi ya rasilimali za umma, na uwajibikaji kwa jamii wa watumishi wa umma katika sekta muhimu kama elimu, maji na kilimo Kuwezesha wananchi kupata sauti na kutoa maoni yao katika masuala ya sera Kuwezesha masuala ya amani na utatuzi wa migogoro hususan katika medani ya siasa Kuwezesha masuala ya usaidizi kwa wazee katika upatikanaji wa huduma muhimu kama vile afya na lishe bora Tunaamini kwa dhati kwamba kinachotuunganisha sisi, AZAKI, Wadau wa Maendeleo na Serikali ni lengo la dhati la kuboresha maisha ya wananchi nchini. Na pia hatuvimilii ubadhirifu, ufujaji na matumizi mabaya ya ruzuku na rasilimali tunazotoa kwa AZAKI kwa ajili ya maendeleo ya raia kwani hatutawatendea haki wananchi wetu pamoja na wadau wetu wa maendeleo na walipa kodi wao. Napenda kuwakumbusha kwamba Foundation haivumilii ubadhirifu wa aina yeyote kwenye ruzuku tunazotoa. Kwa hili tutashirikiana na mamlaka husika za serikali ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) na Jeshi la Polisi. Mpaka sasa kuna kesi 10 za aina hii mahakamani. Kama taasisi, tumeendelea kujenga, kuboresha na kujenga mifumo yetu ya ndani ya ufuatiliaji ili kuhakikisha kuwa rasilimali na ruzuku zetu zinaelekezwa katika kuboresha maisha ya wananchi. Hii inahusisha pia usaidizi na ujenzi wa weledi kwa AZAKI zetu kwenye masuala ya utawala, fedha na usimamizi miradi. Foundation for Civil Society inafurahishwa na kasi na nia ya serikali kuboresha utendaji kwenye taasisi za umma, kuongeza uaminifu wa watumishi wake na juhudi za kupambana na rushwa. Tunaunga mkono juhudi za serikali kwani zinashabihiana na juhudi zetu za kuwezesha ufatiliaji wa matumizi ya rasilimai za umma na uwajibikaji katika sekta muhimu za maendeleo ya jamii. Tunamini kuwa juhudi hizi zitaongeza tija na ulinzi wa rasilimali za umma na hivyo kufaidisha wananchi wote kwa usawa. Kwa hili tunaipongeza Serikali. Hata hivyo, tunaiomba na kuikumbusha Serikali kutosahau kusimamia haki za msingi za wananchi wake. Hizi ni pamoja na uhuru wa habari, uhuru wa maoni na kujenga jamii yenye kuheshimu nafasi ya uraia katika juhudi zake za maendeleo. Kwa sasa kuna wasiwasi wa kuminywa kwa nafasi ya uraia na shughuli za asasi za kiraia katika Kata, Wilaya na Mikoa mbalimbali nchini. Kuna ripoti za wananchi kuhofia kutoa maoni kuhusu utendaji wa serikali na watumishi wake na kwa dhati kabisa tunaamini hii ni ishara mbaya kwenye ujenzi wa jamii huru ya kidemokrasia nchini Tanzania. Tunapenda sana kuipongeza na kuishukuru Serikali na taasisi zake kwa kusimamia maendeleo ya sekta ya asasi za kiraia nchini. Mfano mzuri ni zoezi la kuhakiki AZAKI na kuhimiza usimamizi madhubuti wa AZAKI kwa faida ya wananchi. Tunaona hili ni jambo muafaka kwa sasa katika kipindi ambacho mashirikiano yanakua madhubuti kati ya Serikali, AZAKI na Wadau wa Maendeleo katika kujenga moja kati ya sekta madhubuti ya asasi za kiraia. Kwa niaba ya AZAKI natoa shukrani kwa serikali. Mwisho, naenda kuzikumbusha AZAKI kuhusu changamoto ya kupungua kwa ufadhili na ruzuku kutoka kwa Wadau wa Maendeleo nchini Tanzania. Hii inatatiza miradi ya AZAKI sehemu mbalimbali nchini na pia kupunguza tija kwenye sekta. Kama mlivyosikia kwa msemaji mmoja, suluhisho kwa changamoto hii ipo kwenye mashirkiano na ubia kati ya AZAKI na Sekta Binafsi. Na kama alivyosema Mgeni Rasmi, hata Serikali inaunga mkono mashirikiano haya kwa mfumo wa Sekta za Umma na Binafsi (PPP) kwenye miradi ya maendeleo. 4 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society

(Kama ilivyowasilishwa na Mhe. Jenister Mhagama, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam, Tarehe 24 Novemba 2017) Sehemu ya Hotuba ya Mgeni Rasmi, Mh. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Tanzania Kwanza kabisa namshukuru Mungu kwa Baraka zake. Nawapongeza sana Foundation for Civil Society kwa kuadhimisha miaka 15 ya juhudi za kujenga sekta ya asasi za kiraia nchini. Tunafahamu nafasi, juhudi na matokeo ya Foundation kupitia taarifa za vyombo vya habari. Nipo hapa kutoa salamu za pongezi na shukrani kutoka serikalini kwa kazi na kujituma kwenu katika kuwahudumia Watanzania. Kama mlivyosikia kwa wasemaji waliotangulia, kupitia juhudi za Foundation tunaweza kuona umuhimu wa asasi za kiraia (AZAKI) kwenye michakato yetu ya maendeleo na uboreshaji wa maisha ya wananchi. Nimedokezwa hapa kuwa katika miaka 15 mmefanikiwa kufikia AZAKI 5,000 Tanzania Bara na Visiwani kwa ruzuku zenye thamani ya Shilingi za Kitanzania bilioni 200. Ruzuku hizi zimewezesha miradi kwenye utawala bora, ushiriki wa wananchi kwenye maendeleo, uwezeshaji kwa vijana na wanawake, pamoja na kuwezesha watu wenye ulemavu. Serikali inakiri kuwa uwezeshaji na ruzuku zenu kwa AZAKI zilizopo nchi nzima inasaidia sana juhudi zake za kupambana na umaskini na kuboresha maisha ya raia wake Bara na Visiwani. Tunaishukuru Foundation na wadau wake wote kwa juhudi hizi kwani zinaongeza uwezo wa kuwafikia wananchi wengi zaidi kupitia miradi ya maendeleo. Matokeo ya miaka 15 ya kazi za Foundation yanaweza kupimwa kwa ongezeko la ushiriki wa wananchi na ufuatiliaji wa masuala ya maendeleo katika maeneo yao. Haya ni pamoja na kuhoji mapato na matumizi ya pamoja na uwajibikaji katika watumishi na taasisi za umma. Hii inasaidia sana kwenye ufuatiliaji wa taasisi za umma. Vilevile, programu za mafunzo na kampeni za elimu kwa wananchi zimeongeza kwa kiasi kikubwa ushiriki wa raia kwenye kuhoji masuala ya bajeti, mipango, utendaji na matumizi bora ya rasilimali kwenye miradi ya maendeleo. Hii inaisaidia sana Serikali katika ufuatiliaji wa rasilimali za umma na kupunguza ubadhirifu na kupambana na rushwa katika miradi na taasisi za serikali. Kwa nafasi ya kipekee kabisa, napenda kuwapongeza Foundation kwa kusaidia na kuwezesha makundi maalum katika jamii wakiwemo walemavu, vijana, watoto, wanawake na wazee. Serikali inafurahishwa na juhudi zenu na matokeo yake kwa jamii. Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society 5

Mfano mzuri ni uwezeshaji katika kuanzisha majukwaa ya vijana kuanzia ngazi ya Kata mpaka Taifa ili kuwapa sauti na sehemu vijana ya kukutana, kujifunza na kubadilishana uzoefu wa masuala mbalimbali ya maendeleo. Ni imani yetu kuwa juhudi hizi zitajenga majukwaa ya vijana yasiyofata mirengo ya kisiasa na bali kuhusisha vijana wote. Napenda kusisitiza kuwa Serikali inathamini mchango wa Foundation na Wadau wa Maendeleo kujenga na kuwezesha AZAKI ili ziboreshe utoaji huduma kwa wananchi, haswa makundi maalumu kama walemavu. Tunaahidi kushirikiana nanyi. Serikali inakaribisha na kuthamini mashirikiano na ubia kutoka AZAKI zinazotumia vyema rasilimali na ruzuku za Foundation na Wadau wa Maendeleo katika kuboresha maisha ya Watanzania. Hata hivyo, hatutafumbia macho wale wanaotumia mgongo wa wananchi kujifaidisha na au ubadhirifu wa ruzuku za wananchi. Hawa mkono wa sheria unawasubiri na tunaionya Foundation kutojihusisha na asasi za aina hii. Mwisho, kwa niaba yangu na ya Serikali pia nawashukuru Wadau wa Maendeleo kwa uwezeshaji na misaada yao kwa Foundation na katika maeneo mengine kwenye michakato ya maendeleo nchini. Misaada yao ni rasilimali muhimu kwa AZAKI, lakini muhimu zaidi kwa jamii, kaya na wananchi wa Tanzania nzima. Ila, napenda kuwatahadharisha Foundation, AZAKI na sekta yenu kwa ujumla kutokuwa tegemezi wa wafadhili kwani ni hatari kwa shughuli zenu. Dunia inabadilika kwa kasi na kuwa tegemezi ni hatari. Ni wakati muafaka kwa Foundation na wadau wote wa AZAKI kutafuta njia mbadala za kupata rasilimali kuendesha shughuli zao. Njia mojawapo ni kushirikiana na Sekta Binafsi. Serikali inahimiza sana mashirikiano na ubia kwa mfumo wa Sekta za Umma na Binafsi (PPP). Hii italeta pamoja wadau katika lengo la pamoja la kuwahudumia wananchi. Napenda kutoa changamoto kwa Foundation kuhakikisha kuwa katika kila Wilaya nchini kuna taarifa toshelezi kuhusu AZAKI zilizopo, kazi zao na kuainisha maeneo au fursa za mashirikiano na Sekta Binafsi. Hii itawaleta pamoja wadau mbalimbali kuanza maongezi na majadiliano ya jinsi ya kushirikiana. Ni imani yangu kwa mashirikiano kupitia mfumo wa Sekta za Umma na Binafsi (PPP), AZAKI zitapata njia endelevu za kupata rasilimali za kuendesha miradi yao ya jamii. Ninashawishika kutamka kuwa mahusiano kati ya AZAKI na Serikali zetu zote, ile ya Muungano na ile ya Zanzibar, yapo madhubuti na kuna nafasi ya kuwa bora zaidi. Hii inahusisha pia Serikali za Mitaa (LGAs). Na pia Serikali inathamini ushiriki wenu kwenye zoezi la uhakiki wa AZAKI, kwa lilifanikiwa kwa kiwango kikubwa na kufikia asasi 3186. Kwa zile ambazo bado hazijafanya uhakiki, nawahimiza kufanya hivyo mapema kwa mamlaka husika. Kwa kumalizia, napenda kuwashukuru AZAKI kwa kutuwezesha kujipima utendaji wa serikali zetu mbili katika kuwahudumia wananchi. Tuna imani kuwa sekta yenu na wadau wote watakuwa na utamaduni wa kujitathmini ili kujua utendaji wao na pia kuwa kama mfano kwa sekta nyingine. Kuinyooshea kidole Serikali bila kujitathmini kama AZAKI hakutasaidia sana wananchi wetu. Sote tuna jukumu la kuboresha utawala bora kwa ajili ya jamii yetu. Ninyi pia mna jukumu la kujitathmini tija katika utendaji wenu. Mnatakiwa kujiuliza maswali magumu pia: Je, sisi ni waaminifu kwa Wadau wetu wa Maendeleo? Au kwa wananchi, jamii na Serikali? Je, mifumo yetu ya utendaji ni madhubuti na inashabihiana na kile tunachohimiza kwa wengine? Je, tuna uhuru na uwazi wa kutosha? Majibu ya maswali haya yatatupa tathmini ya tulipo na kuwa dira ya tunapoelekea. Napenda kurudia ujumbe wa Serikali kwa Foundation, AZAKI na sekta nzima ya asasi za kiraia, tunaona kazi yenu, tunathamini na kuunga mkono juhudi zenu. Lengo letu ni moja: kutumia jitihada zote kuboresha maisha ya Watanzania na kujenga jamii bora. 6 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society

WANANCHI WANAYO NAFASI KWENYE MICHAKATO YA MAENDELEO YAO Na Mhe. Florence Tinguely Mattli, Balozi wa Uswisi nchini Tanzania Kwa niaba ya Wadau wa Maendeleo wenzangu Denmaki, Norway na Uingereza nina furaha na heshima kubwa kuwa hapa leo mkiadhimisha miaka 15 ya taasisi ya Foundation for Civil Society (FCS). Tunawapongeza sana! Tunasherehekea pamoja nanyi leo hii mchango mkubwa wa Foundation katika kujenga asasi za kiraia (AZAKI) na sekta nzima nchini Tanzania. Kwa kufanya hivi, mmechangia kwa kiwango kikubwa sana michakato ya maendeleo ya taifa lenu kwa muongo mmoja na nusu iliyopita. Taasisi ya Foundation ilianzishwa kama chombo muhimu cha kwezesha AZAKI, hususan zile ndogondogo nchini Tanzania. Kwa muda wote tangu kuanzishwa, mmekua kiungo na chachu ya maendeleo ya sekta ya AZAKI nchini, ambayo miaka 15 tu iliyopita asasi hii ilikua changa kabisa. Leo hii imekomaa. Vilevile, miongoni mwa malengo ya mwanzo, FCS ilitakiwa kujenga uwezo wa ushawishi wa AZAKI kwenye masuala muhimu ya maendeleo ya Tanzania katika kipindi ambacho hata masuala ya ushawishi yakiwa somo jipya kabisa kwa sekta ya AZAKI. Kulikua na asasi chache sana nchinni kipindi hicho. Leo hii, ni dhahiri kabisa mchango wenu kwa miaka 15 umewezesha uanzishwaji na ukuaji wa mtandao mkubwa kabisa wa AZAKI nchini! Leo hii tunapoadhimisha miaka 15 ya FCS, hatuiangalii taasisi hii kama mtoto mchanga, bali ni kijana mkubwa! Tanzania leo hii inajivunia kuwa na sekta madhubuti kabisa ya asasi za kiraia yenye ushiriki kamilifu katika michakato ya maendeleo ya nchi. Sisi kama wafadhili na wadau wa maendeleo, tumeridhishwa na ukomavu wenu kiasi tuliamua kujitoa kushiriki moja kwa moja kwenye ngazi za uongozi na kuwakabidhi Watanzania wenyewe kuongoza na kuendesha Foundation for Civil Society, ikiwemo Bodi yake. Hata hivyo, bado tunashirikiana na kuunga mkono jukumu la FCS kama taasisi mhimili ya kuwezesha AZAKI na sekta yao nchini Tanzania. Asasi za kiraia zinasaidia sana kuchagiza utoaji wa huduma bora kwa wananchi kwa kuwawezesha raia kusimamia haki na ushiriki wao katika michakato ya maendeleo. Kwa hivi mnashirki na kuunga mkono juhudi za taifa lenu za kujiletea maendeleo. Leo hii mnatakiwa kujivunia mafanikio ya kazi yenu. Ni ukweli usiopingika kuwa mtandao wa AZAKI mlizowezesha umesaidia sana kwenye ushiriki wa wananchi kwenye mapambano dhidi ya umaskini. Pia mmesaidia kujenga uwezo wa AZAKI na sekta yao na kuongeza ufanisi na uaminifu wake kwenye michakato ya maendeleo ya taifa. Mchango wenu umewezesha ushiriki wa makundi maalum kama vijana, wanawake na watu wenye ulemavu na kuhakikisha kuwa hakuna mtu anasahaulika kwenye maendeleo ya Taifa. Mwisho, niseme wazi tu kuwa Foundation for Civil Society ni mfumo mzuri sana wa kuratibu ruzuku za wafadhili. Mmesaidia sana kuleta ufanisi wa misaada yetu kwa AZAKI kwa kufikisha rasilimali kubwa kwa asasi nyingi sana ambazo sisi wenyewe tusingeweza kuwafikia. Tukiangalia mbele, FCS inakua kwa kasi. Kama ni binadamu ni muda mfupi tu ujao atatoka kwenye ujana na kuwa mtu mzima. Hii italeta fursa nyingi zaidi lakini pia na majukumu makubwa zaidi! Kama mhimili mkuu wa AZAKI, Foundation inahitaji kutathmini mchango na matokeo yake kwa mtandao wa asasi inazowezesha. Lengo ni kufanikiwa zaidi. Hii italazimisha kushirikiana zaidi na wananchi na serikali ili kuboresha maisha ya raia kupitia huduma bora zaidi kutokana na utawala bora na uwajibikaji kwa umma. Kama nchi wafadhili, tunaona na kuunga mkono ndoto kubwa na jitihada za Tanzania kujiletea maendeleo. Tunaamini kwa dhati kabisa, tena kutokana na uzoefu wa nchi zetu, kuwa kuwashirikisha wananchi na kuwapa nafasi ni ufunguo wa maendeleo kiuchumi na kijamii kwa taifa. AZAKI zina jukumu zito na muhimu kabisa katika hili na tunaamini ya kwamba Foundation for Civil Society leo hii ni mhimili muhimu sana na utawezesha ushiriki na mchango wa AZAKI na sekta ya asasi za kiraia kwenye michakato ya maendeleo ya Tanzania hivyo kutoa mchango mkubwa barani Afrika na duniani pia. Kwa mara nyingine tena, hongereni sana kwa yote mliyofanikisha kwa miaka 15! Hongera sana! Kwa niaba ya nchi wafadhili wenzangu tunawatakia mafanikio mengi zaidi! Tanzania inawahitaji sana! Na tunajivunia sana kuwashika mkono kwenye safari yenu hii ya mafanikio makubwa! Asanteni Sana! Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society 7

MIAKA 15 YA FOUNDATION: UWEZESHAJI SEKTA YA ASASI ZA KIRAI NCHINI TANZANIA Na Francis Kiwanga Mkurugenzi Mkuu wa Foundation for Civil Society Kwa wale wasiofahamu, Foundation for Civil Society (FCS) ni shirika la Kitanzania lisilo la kibiashara lenye dhamana ya kujenga asasi za kiraia nchini kupitia ruzuku na huduma za kujenga uwezo wa kitaasisi kwa lengo la kuboresha ushiriki wa wananchi kwenye michakato ya maendeleo nchini. FCS ni taasisi huru inayoongozwa na Bodi na kwa kiasi kikubwa shughuli zake zinawezeshwa na Wadau wa Maendeleo (Development Partners) tangu mwaka 2002. Tunajivunia mchakato wetu wa kipekee kabisa hapa barani Afrika wa kuwezesha na kujenga asasi za kiraia. Hii ni taasisi ya Kitanzania kwa asilimia 100% na utendaji wetu umekua chachu kwa mashirika mengine barani hapa. Tunathamini kwa dhati mashirikiano na msaada kutoka serikalini katika maeneo ya sera, sheria na usimamiaji wa asasi za kiraia na sekta nzima. Hii imeweka mazingira chanya kwa FCS kukua na kufikia AZAKI na wananchi wengi Tanzania Bara na Visiwani; hususan juhudi za Rais John Pombe Magufuli na serikali yake katika kusafisha na kuboresha mfumo wa utawala na utoaji wa huduma muhimu kwa wananchi. Kutokana na juhudi hizi na mapambano dhidi ya ubadhirifu na rushwa, tunashuhudia matokeo mengi chanya kwenye uwezeshaiji wetu katika maeneno ya ufuatiliaji wa wazi wa matumizi ya rasilimali za umma, na uwajibikaji katika serikali za mitaa na taasisi za umma. Tunafanya kazi kwa karibu sana na wizara na taasisi husika na usimamizi na maendeleo ya asasi za kiraia na sekta nzima, mfano katika zoezi la hivi karibuni ka uhakiki wa uhalali wa asasi za kiraia nchini. FCS inaunga mkono hatua hii ya uhakiki ikiamini kuwa ililenga kusafisha sekta na kuongeza uaminifu na ufanisi wa sekta na watendaji wake na hivyo kuboresha mahusiano na mashirikiano baina ya asasi za kiraia na serikali. Pia, tunathamini na kushukuru kwa dhati kabisa mchango na uwezeshaji wa Wadau wa Maendeleo kwa Foundation mpaka hapa tulipofikia leo kama mwezeshaji mkubwa kabisa katika sekta ya asasi za kiraia nchini. Tunashukuru mchango wa wadau hawa kwa miaka 15 tuliyofanya kazi, wakiwemo Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID), Shirika la Maendeleo la Uswisi (SDC), Shirika la Maendeleo la Ireland (Irish Aid), Ubalozi wa Uholanzi nchini, Shirika la Maendeleo la Kanada (CIDA), Shirika la Maendeleo la Sweden (SIDA), Shirika la Maendeleo la Denmark (DANIDA), Shirika la Maendeleo la Norway (NORAD), na shirika la Comic Relief. Kutokana na uwezeshaji na mashirikiano na wadau wetu wa maendeleo, tumeweza kufanya kazi na kufikia jamii mbalimbali katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani. Kwa miaka hii 15, tumewezesha kupitia ruzuku na kujenga uweo wa asasi za kiraia (AZAKI) katika maeneo ya haki za binadamu na upatikanaji wa haki kwa jamii maskini, usawa wa kijinsia na haki za wanawake, haki za watu wenye ulemavu, haki za watoto na huduma kwa wazee. Pia tuligusa maeneo ya haki za wanawake kwenye masuala ya ardhi, watu wenye VVU na UKIMWI, utawala bora, ufatiliaji wa uwajibikaji katika sekta muhimu za huduma kwa umma, ujenzi wa demokrasia, amani na utatuzi wa migogoro. AZAKI tulizowezesha pia ziligusa uwezeshaji wa wanawake na vijana. Maendeleo endelevu ya AZAKI na sekta kwa ujumla Wadau wote wa AZAKI na sekta nzima ya asasi za kiraia nchini tunatakiwa kuona na kung amua mabadiliko makubwa yanayotokea duniani na kugusa shughuli zetu. Matukio mengi hapa barani na duniani yamekuwa yakigusa mahusiano na mashirikiano baina ya wadau wa maendeleo na nchi nyingi zikiwemo za Afrika. Hii imesababisha kuyumba kwa mashirika mengi katika sekta za kiraia duniani. Kwa sababu hii, kuna haja ya kuwa na mikakati madhubuti ya kupanua wigo wa njia tunazotumia kupata rasilimali za kuendesha shughuli za AZAKI badala ya kuwa tegemezi kwa njia moja tu. AZAKi zote zatakiwa kupitia upya mikakati yao ili kuongeza wigo wa upatikanaji wa rasilimali za kuendeshea shughuli zao. Kuna haja ya makusudi kabisa ya kuangalia njia mbadala za kupata mashirikiano mapya yatakayowezesha upatikanaji wa fedha kwa ajili ya shughuli zetu. Juhudi zetu pekee haziwezi kutosha. Tunahimiza AZAKI zetu kuanza kujenga utamaduni wa kutoa na kuhimiza utoaji kwenye jamii kwa ajili ya wenye uhitaji. Pia tunahimiza kuangalia fursa zilizopo kwenye mashirikiano baina ya AZAKI na sekta binafsi ambayo inahimizwa na kuungwa mkono kwa dhati na serikali kupitia mashirikiano ya Sekta za Umma na Binafsi (PPP). Huu ni wakati muafaka kwa AZAKI kutengeneza mikakati na mashirikiano mapya na sekta binafsi na mashirika ya ndani na ya nje ya nchi. Mashirikiano na Serikali za Mitaa na Mamlaka zake (TAMISEMI) Ili kuwa na miradi endelevu, AZAKI zinatakiwa kushirikiana na serikali za mitaa katika jamii tunazotekeleza shughuli zetu, hususan ile tunayowezesha. Katika kipindi chote cha miaka 15, tumekua tukisisitiza mashirikiano baina ya AZAKI na serikali za mitaa ili kufikia jamii nyingi. Tungependa kuona mashirikiano haya yanaenda mbele zaidi ili kuleta uendelevu wa shughuli za maendeleo ya jamii katika maeneo hayo. Katika kwenda mbele zaidi, tunahimiza mashirikiano ya AZAKI na serikali za mitaa kushirikiana kuanzia hatua za mwanzo kabisa za kuibua changamato za jamii na miradi ya kuzitatua ili itakapofadhiliwa na kuwezeshwa na FCS iweze kuwalenga wananchi na jamii moja kwa moja. Hii itakua moja ya mikakati ya kufanya miradi hii ya maendeleo ya AZAKI kuwa endelevu na kuwa mikononi mwa wananchi na jamii moja kwa moja. 8 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society

Mafanikio ya FCS Katika kipindi cha miaka 15 Kufikia jamii nchi nzima: Katika miaka 15 ya FCS, tumeshatoa ruzuku za thamani ya Fedha za Kitanzania bilioni 200 tulizowezeshwa na Wadau wa Maendeleo na kufikia AZAKI zaidi ya 5,000 na wananchi milioni 30 Tanzania nzima. Ruzuku zetu zimewezesha miradi ya maendeleo katika jamii za mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani. Tunajivunia kuwa shirika mwezeshaji linalofikia jamii zote nchini na kiasi kikubwa cha ruzuku zetu kinalenga jamii za chini kabisa na vijijini. Uwezeshaji na ujenzi wa AZAKI: Tumeweka jitihada kubwa sana kujenga uwezo wa zaidi ya AZAKI 800 nchini kupitia ruzuku na kuwezesha mafunzo ya uboreshaji wa utendaji wa AZAKI na kuwafikia watendaji zaidi ya 280,000. Kuhimiza maboresho ya sera: FCS imetoa ruzuku 933 za thamani ya Shilingi za Kitanzania bilioni 30 kwa miradi ya AZAKI ya kuhimiza na kushinikiza maboresho ya sera mbali mbali, wakifikiwa wananchi milioni 10 nchi nzima. Juhudi hizi zimesaidia ushiriki wa wananchi/raia kwenye michakato ya maboresho na utungaji wa sera na sheria mbalimbali, zikiwemo Sera ya Taifa ya Ardhi, 1997; Sera ya Taifa ya Walemavu, 2004; Sera ya Taifa ya Wazee, 2003; Sera ya Taifa ya VVU na UKIMWI, 2001; na Sera ya Taifa ya Vijana, 2008. Ushirikishwaji wa makundi maalum: FCS imekumbuka makundi maalum kwa kutoa ruzuku zilizowezesha miradi ya kupigania haki za makundi hayo yanayosahaulika kwenye jamii. Mfano wazee zaidi ya 342,000 wasio na uwezo waliwezeshwa kupata huduma ya matibabu bila malipo. Pia zaidi ya wananchi 48,000 wenye ulemavu waliwezeshwa kupata huduma muhimu za jamii na kushirikishwa kwenye michakato muhimu ya maamuzi ya maendeleo. Kuhusu watu wenye ualbino, AZAKI zaidi ya 38 ziliwezeshwa kutekeleza miradi inayohusu usalama na kupinga mauaji na ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi. Usawa wa kijinsia: Foundation imechangia kwa kiwango kikubwa kwenye masuala ya usawa wa kijinsia na haki za wanawake. Mfano: Foundation imewezesha miradi iliyowezesha wahalifu zaidi ya 200 wa ukatili wa kingono na kijinsia dhidi ya wanawake kufikishwa mahakamani na kufanikiwa kuwaokoa wasichana zaidi ya 1,000 kutoka kwa mila potofu ikiwemo tohara. Uwajibikaji kwa umma: FCS imetoa ruzuku kwa asasi zaidi ya 730 za thamani ya Shilingi za Kitanzania bilioni 30 kuwezesha miradi ya utawala bora na uwajibikaji kwa umma, iliyofikia wananchi zaidi ya milioni 13 nchi nzima. Hii iliongeza uwazi na uwajibikaji kwenye matumizi ya rasilimali za umma na kuboresha utoaji huduma za jamii. Pia iliongeza kwa kiwango kikubwa ushiriki wa wananchi kwenye michakato ya utawala bora. Upatikanaji wa haki: FCS iliwezesha upatikanaji wa huduma za kisheria kwa wananchi zaidi ya 28,000 kupitia kliniki maalum za kisheria zinazotembea nchi nzima. Pia ilifadhili mafunzo kwa wasaidizi wa kisheria (paralegals) zaidi ya 121,000 na uanzishwaji wa vituo 133 vya msaada wa kisheria nchini ambavyo bado vinahudumia wananchi ikiwemo maeneo ya vijijini. Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society 9

ASASI ZA KIRAIA (AZAKI) ZAWEZAJE KUSHIRIKIANA NA SEKTA BINAFSI? Na Abid Malick, Mkurugenzi Mkazi, Taasisi ya Agha Khan Foundation Ili kuwa na mashirikiano yenye faida kwa pande mbili, asasi za kiraia (AZAKI) na Sekta Binafsi wanahitaji kuainisha maeneo muhimu ya ubia na ushirkiano wao. Ni lazima kuwe na malengo ya pamoja kati ya pande/sekta hizi mbili ambayo yatawafaidisha wote watakaposhirikiana. Kwa kifupi, asasi za kiraia mara nyingi zina jukumu la kufikia makundi maalum yanayosahaulika kwenye jamii na kuwapatia suluhisho kwenye changamoto nyingi za maisha yao. Kwa upande mwingine, Sekta Binafsi wao lengo lao ni kupata faida kwa kuangalia soko linahitaji nini na wao wakaleta suluhisho kwa huduma zao. Hapo ndio wao huingiza rasilimali zao. Hata havyo, jamii na hususan makundi maalum yaliyosahaulika hayawezi kutegemea nguvu za soko kuwapatia suluhisho la huduma zao muhimu. Na hapo ndio nafasi na mchango wa asasi za kiraia unakuja kuziba pengo lililoachwa na Sekta Binafsi. Kwa hiyo ukiniuliza, je, Sekta Binafsi inaweza kusaidia kutoa rasilimali na fedha kwa asasi za kiraia nchini Tanzania, nitakwambia NDIO, WANAWEZA! Pia, kwa upande mwingine sekta ya asasi za kiraia inaweza kabisa kusaidia ukuaji wa Sekta Binafsi. Tuchukue mfano wa kilimo. Asasi za kiraia zinaweza kuhamasisha wakulima wadogo kuboresha kilimo chao na hivyo kupata mavuno mengi ambayo wanunuzi wengi hutoka Sekta Binafsi. Kwa upande wa Sekta Binafsi, wanaweza kutumia utamaduni wa kurudisha kwa jamii (Corporate Social Responsibilities - CSR) ili kuweza kushirikiana na asasi za kiraia. Pande zote mbili zaweza kutafuta njia za kushirikiana na kufaidika na ubia wao. Kuna haja ya sekta hizi mbili kuangalia kila moja itafaidika vipi kwa kufanya ubia na mwenzake. Hii ndio hatua ya kwanza ya kuibua maeneo wanayoweza kushirikiana. Na mwisho wa siku, watakaofaidika zaidi hapa ni wananchi na jamii zao. 10 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society

UAMINIFU NA UWAJIBIKAJI HALI IKOJE KWA ASASI ZA KIRAIA (AZAKI)? Na Francis Uhadi, Meneja Programu, FCS Suala la uaminifu na uwajibikaji kwa asasi za kiraia (AZAKI) ni muhimu sana katika kuweka imani kwa Wadau wa Maendeleo, serikali na Sekta Binafsi. Lakini vilevile, ni muhimu zaidi katika kuweka imani kwa wadau wetu wakubwa wananchi na jamii. Kwa miaka 15 Foundation imefanya kazi kubwa sana kuweka misingi muhimu inayowezesha kufanya kazi zake bila kujali itikadi za kisiasa, rangi ama imani za kidini. Lengo letu kubwa ni kuwa na taasisi ambayo inawaleta pamoja Watanzania wote bila kujali imani, siasa au dini yao. Hata hivyo changamoto zipo kwenye sekta yetu. Ni ukweli ulio wazi kuwa kuna baadhi ya asasi za kiraia au watendaji wao wana uelekeo wa kufata itikadi au mrengo fulani wa kisiasa na wakati huohuo wanawahudumia wananchi kupitia asasi zao. Kiutendji, hali hii hudhoofisha uaminifu wao kwa wananchi na wadau wao katika sekta ya AZAKI. Katika hali kama hii ni vigumu kwa AZAKI hizo kuwa waadilifu na waaminifu kwa wadau wake wa ndani na nje pia. Na pia ni vigumu kutofungamana na upande wowote. Hii pamoja na ubadhirifu wa fedha na rasilimali nyingine za asasi, ukosefu wa uaminifu na hata kutokujituma kwa watendaji wake ni changamoto kubwa kwa baadhi ya AZAKI nchini. Changamoto hii pia ina angukia kwa Foundation for Civil Society kama mwezeshaji mkuu wa sekta ya asasi za kiraia nchini kwa sababu utendaji mbovu wa AZAKI hizi hudhoofisha juhudi za Foundation kukuza na kuboresha asasi hizi za jamii. Na ni ukweli ulio wazi kuwa changamoto na matatizo haya ya AZAKI humaanisha kuwa asasi hizi zinawaangusha wananchi ambao ndio wadau wakubwa wa miradi ya maendeleo ya AZAKI. Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society 11

AZAKI NA CHANGAMOTO YA KUWAHUDUMIA Watu Wenye Ulemavu Na Fredrick Msigallah, Meneja wa Ushawishi na Mashirikiano, CCBRT Maendeleo-jumuishi kwa watu wenye ulemavu (disability inclusive development) hutokea pale jamii nzima, hususan watu wenye ulemavu wanapofaidika na michakato yote ya maendeleo ya Taifa. Ni hali inayotambua na kuthamini changamoto, weledi na mchango unaotokana na ulemavu kama sehemu ya maisha ya binadamu. Maendeleo-jumuishi kwa watu wenye ulemavu imejikita pia kwenye kupaza sauti na kukuza ushiriki wa makundi yanayosahaulika kwenye jamii. Pia ni mchakato unaohimiza usawa katika kupata na kufurahia haki zote kama raia kamilifu na kusimamia ushiriki wa watu wenye ulemavu kwenye maendeleo ya jamii yao. Ushiriki wa watu wenye ulemavu kwenye michakato ya maendeleo nchini una changamoto nyingi sana zikiwemo za kitaasisi, Za kitabia na hata za kimazingira na kimiundombinu. Za kitaasisi hubagua/hutenga watu wenye ulemavu kwenye mifumo yote muhimu ya kijamii mfano kwenye sheria, ajira, chaguzi, elimu na hata upatikanaji wa huduma za afya. Za kitabia ni kama vile chuki, ubaguzi na unyanyapaa ambazo zote kwa pamoja hufanya watu wenye ulemavu waonekane kama watu wasiojiweza, tegemezi, wasio waelewa na wagonjwa. Za kimazingira zinahusu zaidi miundombinu kwa walemavu katika maeneo ya huduma kama vile usafiri, mahospitalini, mashuleni, kwenye makazi, madukani, kwenye nyumba za ibada hata kwenye vyombo vya habari na upatikanaji wa habari kwa watu wenye ulemavu. Changamoto nyingi kwa watu wenye ulemavu ni za kimiundombinu. Lakini pia zipo nyingi za kimkakati mfano upatikanaji wa huduma muhimu kama vile afya, elimu na ushiriki kwenye maamuzi katika michakato ya maendeleo. Mfano mzuri hapa ni mtu mwenye ulemavu aliye kwenye kiti cha kusukuma/ magurudumu anaposindwa kushiriki na kupata huduma kikamilifu kwenye elimu, afya, fursa za kiuchumi, ushiriki kwenye siasa na uongozi, yote hii ni kwa sababu ya changamoto za ulemavu. Kwa takwimu za sasa, walemavu ni asilimia 9.3 ya jumla ya idadi watu wa Tanzania, kiwango ambacho kikipewa nafasi kinaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa katika michakato ya maendeleo ya Taifa. Ulemavu hupatikana kwa njia na katika hatua mbalimbali za maisha ya binadamu. Wengine hupata wakati wanazaliwa na wengine hupata baadae kutokana na sababu mbalimbali kama ajali au ugonjwa. Walemavu wanahitaji uangalizi tofauti kutokana na aina tofauti za ulemavu wao. Kwa hivyo ni muhimu sana kwa hatua zote za michakato ya maendeleo-jumuishi kufikiria changamoto za kila kundi la walemavu. Maendeleo-jumuishi ni jukumu la wadau wote kwenye jamii wakiwemo serikali, asasi za kiraia (AZAKI), Sekta Binafsi, Wadau wa Maendelo na watu wenye ulemavu wenyewe. Pamoja na changamoto zote zilizoainishwa, bado kunaa fursa na nafasi kubwa ya kuchangiza na kushurutisha ushiriki wa watu wenye ulemavu kwenye michakato ya maendeleo ya Taifa. Baadhi ya fursa hizi za kitaifa ni: Kuongeza uelewa kuhusu watu wenye ulemavu na haki zao Kusimamia vyema sheria na sera (za kitaifa na kimataifa) zinazosimamia haki za walemavu, mfano Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu wenye Ulemavu (United Nations Convention on the Rights of Persons with disabilities - UNCRPD), Maendeleo Endelevu (SDGs) na Sheria ya Walemavu ya 2010, Taarifa ya Dunia ya Walemavu (ya Benki ya Dunia na Shirika la Afya Duniani, 2011). Kuongeza ushawishi na utetezi kwa watu wenye ulemavu na haki zao kupitia asasi zao (Disabled Peoples Organisations - DPOs na Pro-Disability Organisations - PDOs). 12 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society

Uwezeshajwaji kutoka kwa Wadau wa Maendeleo kwa miradi inayolenga walemavu na haki zao. Msaada wa kiufundi na kitaaluma kuhusiana na ujumuishi wa walemavu kwenye michakato mbalimbali ya jamii. Baadhi ya fursa kupitia asasi za kiraia ni: (i) Ushawishi na utetezi kuhusu ushiriki madhubuti wa walemavu kwenye kupanga, kutekeleza na kusimamia mipango ya maendeleo. (ii) Kutenga rasilimali fedha na watu ili kutekeleza maendeleo-jumuishi kwa walemavu. (iii) Ushawishi na utetezi kuhusu usimamiaji wa sheria na sera kwa kuzingatia haki za walemavu. (iv) Ushawishi kuhusu maboresho ya sheria na sera za maendeleo ili kuzingatia haki za walemavu. (v) Kupanga na kutekeleza mikakati itakayoondoa vikwazo na changamoto kwa walemavu kushiriki kwenye michakato ya maendeleo. (vi) Tafiti kutoa taarifa na takwimu sahihi kwa ajili ya upangaji, utekelezaji na usimamiaji wa mipango ya maendeleo-jumuishi. Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society 13

Miaka 15 ya FCS Foundation for Civil Society yaadhimisha miaka 15 ya kuzijengea uwezo asasi za kiraia (AZAKI) Novemba 24, 2017 kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC) 14 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society

Madai Crescent, 7 Ada Estate, Kitalu Na. 154 S.L.P. 7192 Dar es Salaam, Tanzania Simu: +255-22-2664890-2 Nukushi: +255-22-2664893 Barua pepe: information@thefoundation-tz.org Tovuti: www.thefoundation.or.tz Twitter: @FCSTZ