Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia

Similar documents
Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Mwabudu Yehova, Mfalme wa Umilele. Miaka 100 ya Utawala wa Ufalme Inakuhusuje? UKURASA WA 12 NYIMBO: 97, 101. Kufanya Maamuzi ya Hekima Ukiwa Kijana

"ATATOKEA MARA YA PILI, pasipo dhambi, kwa hao wamtazamiao kwa wokovu." Waebrania 9:28.

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

Theolojia Ujumla. Mike Taylor Semester Munguishi Bible College

GRACE COMMUNION INTERNATIONAL KANUNI YA IMANI

Ushindi ndani ya Kristo W. W. PRESCOTT

WEWE NI NANI? Toleo X Toleo Ukweli wa Injeli Toleo 23

B. Wanafunzi watapata ufahamu mkubwa wa kitabu hiki, na jinsi kinavyofundisha kuhusu kanisa.

United Pentecostal Church June 2017

MUNGU ANADHIHIRISHWA KUPITIA KWA YESU KRISTO.

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Kanuni. Muhimu za Kujifunza Biblia. Mchungaji Drue Freeman. Dan Hawkins & Joseph Brown. General Editors.

Kuiponya Picha Tuliyonayo Kuhusu Mungu

BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE

JE, YAWEZEKANA KUISHI BILA KUTENDA DHAMBI?

Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar

WAKOLOSAI MTAALA. B. Maoni: Tunapendekeza uwe na fafanuzi (commentary) yoyote yenye kushikilia mafundisho ya awali (conservative) katika Wakolosai.

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

WAFUNAJI WA NAFSI ABC By Vagn Rasmussen Translation by Lydia Madsen

Maisha Ya Mkristo Ni Nini?

Agano Lililofunikwa Kwa Damu

MUNGU ALIUMBA ULIMWENGU 1 WETU NA VYOTE VILIVYO HAI

Ndugu na dada zangu wapendwa,

walozaliwa, si kwa damu, wala mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, mbali kwa Mungu. Sisi sio tena binadamu wa kawaida tu kwa sababu sisi ni w

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

Nia Dhidi Ya Kristo Je Unamheshimu?

UKUFUNZI WENYE NGUVU MMOJA-KWA-MMOJA

IMANI NA MATENDO ELLEN G. WHITE

Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika

FORWARD BY DANIEL SZMIOT

Roho Mtakatifu Ni Nini?

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

MSAMAHA NA UPATANISHO

Uongozi Siri Na Larry Chkoreff. Version 1.2 Desemba 2010

MAHUBIRI TUNAYOWEZA KUONA

MAFUNDISHO YA UMISHENI

Kifo Na Mbingu. (Death And Heaven) Ellis P. Forsman. Kifo Na Mbingu (Death And Heaven) 1

Tazama Yuaja. Kuhusu Toleo Hili. Umuhimu wa Mafundisho ya Biblia. Nguvu katika neno la Mungu.

Human Rights Are Universal And Yet...

Inavyodaiwa na wanaochanganya Biblia. Ellis Forsman. Inavyodaiwa na Wanao changanya Biblia (Alleged Bible Contradictions) 1

Hakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn

Kiu Cha umtafuta Mungu

UTARATIBU WA KANISA. 2 Jambo la kwanza ninalotaka kusema ni kwamba mchungaji. 3 Sisi tunaamini katika Kanisa la kimitume, tukifundisha

VITAMBULISHO VITA NO DHA HIRI VYA KA NISA LA KWELI LA MUNGU ALIYE HAI

Tumaini Kwa Afrika. Thomas Schirrmacher. Hoja 66. Dibaji na Prof. Mchungaji Dk. Thomas K. Johnson. Thomas Schirrmacher Tumaini Kwa Afrika TASCM RVB

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Iliyoendelea sana. Kitabu cha mwanafunzi. Iliyoendelea sana

Aina Tatu Za Ibada. Ellis Forsman. Aina Tatu Za Ibada (Three Kinds Of worship) 1

Ndugu na dada zangu wapendwa,

PDF created with pdffactory trial version

NGUVU. Utangulizi. Yesu alisema,

Silaha Za Shetani. Ellis Forsman. Silaha Za Shetani (The Devices of Satan) 1

Kwa Nini Yesu Alikufa Msalabani?

Adhabu ya jino kwa jino na Musitakabali wa imani zetu

Watumishi Wa Kristo. Ellis P. Forsman. Watumishi Wa Kristo (Servants Of Christ) 1

Makasisi. Waingia Uislamu

Mafundisho Ya Msingi Wa Kikristo. Na Andrew Connally

Tafuteni Kwanza Ufalme Wa Mungu

UJASIRI WA YOHANA MBATIZAJI

Iliyoendelea sana. Kitengo cha 2. Kitabu cha mwanafunzi Iliyoendelea sana

RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI MWANDISHI: SALEH M. KYAMBO

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

UNABII WA BIBLIA. CBM Publishing 32 Blenheim Road, Far Cotton Northampton, England. NN4 8NW

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level

Sura ya 7 Kielelezo: Tumepatanishwa na Mungu na Wanadamu

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

Maisha Yaliyojaa Maombi

Kuwa Macho Na Mbwa Mwitu (Watch Out for Wolves)

Rahisi. Kitabu cha mwanafunzi. Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Rahisi

United Pentecostal Church April Kushangilia Kwa Sala

# 18 Uponyaji Kutokana na Kukataliwa

Uponyaji Wa Laana. (Kumb. 28:1-14).

Ufundishaji wa lugha nyingine

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Ndugu na dada zangu wapendwa,

maombi, kabla tu hatujalifungua Neno hili la Kiungu.

YEHOVA-YIRE 1. 2 Baba yetu wa Mbinguni, tunakikaribia Kiti Chako cha. 3 Tunakushukuru kwa kutuzuru jana jioni. Tunaomba

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa.

Jumuiya ya Waislamu Waahmadiyya Tanzania

Kifo Na Mbingu (Death And Heaven)

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Early Grade Reading Assessment for Kenya

ONYO LA MWISHO KWA DUNIA

MIAKA 500 YA MATENGENEZO YA KANISA NA USHUHUDA WETU Na Askofu Dr. Abednego Keshomshahara

KAMA MUNGU YU PAMOJA NASI, BASI YAKO WAPI MATENDO YAKE YA AJABU?

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

Oktoba-Desemba

Kiumbe Kipya Katika Kristo

Mabingwa kwa ajili ya tunda la Roho Mtakatifu. Ngumu. Ngumu. Kitabu cha mwanafunzi

wasiofaa. Naomba sana kila raia afanye bidii awezavyo kumkaribia Mwenyezi Mungu vile anavyoona inafaa, lakini asipitishe hukumu juu ya wengine.

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

Patanishwa, Hesabiwa Haki, Takaswa

H. M. Baagil, M. D. WAMY Studies on Islam

Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo

2 LILE NENO LILILONENWA

JE! MUNGU ANAMPA MWANAMKE HAKI YA KUTOA MIMBA IWAPO NI MHANGA WA UBAKAJI?

KWA NINI SISI SI MADHEHEBU?

Transcription:

34567 APRILI 15, 2013 Juni 3-9 Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia UKURASAWA 3 NYIMBO ZA KUTUMIWA: 114, 113 Juni 10-16 Jinufaishe na Uwanufaishe Wengine kwa KutumiaNenolaMungu UKURASAWA 18 NYIMBO ZA KUTUMIWA: 37, 92 Chapa Kubwa SEHEMU YA 1

34567 APRIL 15, 2013 Vol. 134, No. 8 Semimonthly SWAHILI MAKALA ZA FUNZO Pata Manufaa Kamili kwa Kusoma Biblia Jinufaishe na Uwanufaishe Wengine kwa Kutumia Neno la Mungu Paulo aliandika kwamba neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu. (Ebr. 4:12) Lakini nguvu hizo zitatunufaisha tu ikiwa tutajifunza na kufuata mafundisho ya Neno la Mungu lililoongozwa na roho takatifu. Makala hizi zinakazia njia nzuri ya kujifunza Biblia na zinaonyesha jinsi tunavyoweza kuruhusu hekima ya Mungu ituongoze katika huduma yetu na katika maisha yetu binafsi. Gazeti hili haliuzwi. Ni sehemu ya kazi ya elimu ya Bibliayaulimwengunipoteinayotegemezwakwamichango ya hiari. Isipokuwa iwe imeonyeshwa vingine, Maandiko yamenukuliwa kutoka katika Biblia Takatifu Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. The Watchtower (ISSN 0043-1087) is published semimonthly by Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.; L. Weaver, Jr., President; G. F. Simonis, Secretary-Treasurer; 25 Columbia Heights, Brooklyn, NY 11201-2483, and by Watch Tower Bible and Tract Society of South Africa NPC, 1 Robert Broom Drive East, Rangeview, Krugersdorp, 1739. 2013 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania. Haki zote zimehifadhiwa. Printed in South Africa.

Pata Manufaa Kamili kwakusomabiblia KwakwelinaipendasheriayaMungu. ROM. 7:22. TAFUTA MAMBO HAYA Utanufaikaje ukisoma kwa sauti ya chini? Unawezaje kujenga hazina ya Maandiko unayoweza kutumia kuwasaidia wengine? Kusoma Biblia kwa uangalifu kunakulindaje? KILA asubuhi ninamshukuru Yehova kwa kunisaidia kuielewa Biblia. Dada Mkristo aliyezeeka ambaye alisema maneno hayo ameisoma Biblia nzima zaidi ya mara 40, naye ameazimia kuendelea kuisoma. Dada mmoja mchanga aliandika kwamba kusoma Biblia kumemsaidia kumwona Yehova kuwa halisi. Kufanya hivyo kumemsaidia amkaribie zaidi Baba yake wa mbinguni. Alisema hivi: Sijawahi kamwe kuwa na shangwe kama hii maishani mwangu! 1-3. Tunapata faida gani tunaposoma Biblia na kutumia mafundisho yake? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 3

2 Mtume Petro alitutia moyo sote tukuze tamaa kwa ajili ya maziwa yasiyochanganywa kitu ambayo ni ya lile neno. (1 Pet. 2:2) Wale wanaotosheleza tamaa hiyo kwa kujifunza Biblia na kutumia mafundisho ya Biblia wana dhamiri safi na kusudi maishani. Wanasitawisha urafiki wa kudumu pamoja na wengine wanaompenda na kumtumikia Mungu wa kweli. Hizo zote ni sababu nzuri za kuipenda sheria ya Mungu. (Rom. 7:22) Hata hivyo, kuna faida nyingi zaidi.nizipibaadhiyafaidahizo? 3 Kadiri unavyojifunza mengi zaidi kumhusu Yehova na Mwana wake, ndivyo upendo wako kuwaelekea na kuelekea wanadamu wenzako utakavyozidi kukua. Kuwa na ujuzi sahihi wa Kimaandiko kutakusaidia kuona jinsi ambavyo hivi karibuni Mungu atawaokoa wanadamu watiifu kutoka katika mfumo huu unaoelekea mwisho wake. Una ujumbe mzuri wa habari njema wa kuwaambia watu katika huduma. Yehova atakubariki unapowafundisha wengine mambo uliyojifunza kupitia usomaji wako wa Neno la Mungu. 4 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

SOMA NA UTAFAKARI 4 Yehova hataki watumishi wake walisome Neno lake haraka-haraka. Alimwambia Yoshua wa nyakati za kale hivi: Kitabu hiki cha sheria kisiondoke katika kinywa chako, nawe ukisome kwa sauti ya chini mchana na usiku. (Yos. 1:8; Zab. 1:2) Je, agizo hilo linamaanisha kwamba utamke kwa sauti ya chini maneno yote unaposoma kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo? Hapana. Linamaanisha kwamba unapaswa kusoma kwa mwendo utakaokupa nafasi ya kutafakari. Kusoma Biblia kwa sauti ya chini, kutakusaidia kukazia fikira sehemu hususa zinazokufaa na kukutia moyo wakati huo. Unapopata masimulizi, mistari, au sehemu za aina hiyo, soma polepole, unaweza hata kutamka maneno hayo kimya-kimya unaposoma. Huenda ukaguswa moyo sana na wazo fulani la Kimaandiko. Kwa nini hilo ni muhimu? Kwa sababu kuelewa mashauri ya Mungu kutakuchochea sana kuyatumia. 4. Kuisoma Biblia kwa sauti ya chini kunamaanisha nini? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 5

5 Unaweza kunufaika zaidi ukisoma kwa sauti ya chini vitabu vya Biblia usivyojua vizuri. Kwa mfano, wazia hali hizi tatu. Kwanza, fikiria ndugu kijana Mkristo ambaye amefikia unabii wa Hosea katika ratiba yake ya usomaji wa kibinafsi. Katika sura ya 4, anatua baada ya kusoma kwa sauti ya chini mstari wa 11 na wa 13. (Soma Hosea 4:11-13.) Kwa nini? Anakazia fikira mistari hiyo kwa sababu amekuwa akipambana na mikazo ya upotovu wa maadili shuleni. Anatafakari mistari hiyo na kuwaza hivi: Yehova anaona mambo mabaya ambayo watu wanafanya hata faraghani. Sitaki kumkasirisha. Ndugu huyo anaazimia kubaki safi kiadili mbele za Mungu. 6 Katika hali ya pili, dada Mkristo anasoma unabii wa Yoeli, naye anafika katika sura ya 2, mstari wa 13. (Soma Yoeli 2:13.) Anaposoma mstari huo kwa sauti ya chini, anatafakari jinsi anavyopaswa kumwiga 5-7. Toa mfano unaoonyesha jinsi kusoma Neno la Mungu kwa sauti ya chini kunavyoweza kukusaidia (a) kubaki safi kiadili; (b) kuwatendea wengine kwa subira na fadhili; (c) kumtegemea Yehova hata unapokabili hali ngumu. 6 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

Yehova, ambaye ni mwenye neema na rehema, ambayesimwepesiwahasirananimwingiwafadhilizenye upendo. Anaamua kujaribu kutosema maneno ya dhihaka na yenye hasira ambayo nyakati nyingine anatumia anapoongea na mume wake na wengine. 7 Katika hali ya tatu, mfikirie baba Mkristo aliyefutwa kazi ambaye ana wasiwasi kuhusu hali-njema ya mke na watoto wake. Katika Nahumu 1:7, anasoma kwa sauti ya chini kwamba Yehova hutambua wale wanaotafuta kimbilio kwake naye huwalinda kama ngome katika siku ya taabu. Wazo hilo linamfariji. Anahisi kwamba Yehova anamjali kwa upendo, naye anaacha kuhangaika kupita kiasi. Kisha anasoma kwa sauti ya chini mstari wa 15. (Soma Nahumu 1:15.) Ndugu yetu anaona kwamba anapohubiri habari njema chini ya hali ngumu, anaonyeshakwakwelikwambaanamwonayehovakuwangome yake. Ndugu yetu anapoendelea kutafuta kazi, anachochewa pia kuunga mkono mpango wa utumishiwashambanikatikatiyajuma. SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 7

8 Mambo hayo yenye manufaa yaliyotajwa yanatoka katika vitabu vya Biblia ambavyo huenda wengine wanaona havieleweki kwa urahisi. Unapochunguza vitabu vya Hosea, Yoeli, na Nahumu ukiwa na hamu ya kujifunza, utachochewa kusoma kwa sauti ya chini mistari mingine katika vitabu hivyo. Wazia faraja na hekima nyingi utakayopata kutokana na maandishi ya manabii hao! Namna gani vitabu vingine vya Biblia? Neno la Mungu ni kama mgodi uliojaa almasi. Chimba vizuri mgodi huo! Naam, soma Biblia nzima ukiwa na mradi wa kupata hazina, yaani, mwongozo wa Mungu na uhakikisho wake. JITAHIDI KUPATA UELEWAJI 9 Ingawa ni muhimu kusoma sehemu fulani ya Biblia kila siku, unataka pia kupata uelewaji na ufahamu. Kwa hiyo, tumia vizuri machapisho ya tengenezo la Yehova kwa kufanya utafiti kuhusu historia ya watu, maeneo, na matukio unayosoma. Au iki- 8. Eleza kwa ufupi hazina ya kiroho uliyopata katika usomaji wako wa Biblia. 9. Tunawezaje kuongeza uelewaji wetu kuhusu mapenzi ya Mungu? 8 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

wa hujui jinsi fundisho fulani la Biblia linavyoweza kukusaidia maishani, unaweza kumwomba msaada mzee wa kutaniko au Mkristo mwingine mkomavu. Ili kuonyesha umuhimu wa kuongeza uelewaji wetu, acheni tufikirie mfano wa Mkristo mmoja wa karne ya kwanza aliyejitahidi kufanya hivyo. Aliitwa Apolo. 10 Apolo alikuwa Mkristo Myahudi aliyekuwa na ujuzi mwingi sana wa Maandiko na aliyewaka roho. Kitabu cha Matendo kinasema hivi kumhusu: Akaanza kusema na kuyafundisha kwa usahihi mambo juu ya Yesu, lakini akiwa anaufahamu ubatizo wa Yohana tu. Bila kujua, Apolo alikuwa akifundisha uelewaji uliopitwa na wakati kuhusu ubatizo. Baada ya kumsikia akifundisha huko Efeso, Prisila na Akila, wenzi wa ndoa Wakristo walimfafanulia kwa usahihi zaidi njia ya Mungu. (Mdo. 18:24-26) Jambo hilo lilimsaidiaje Apolo? 11 Baada ya kuhubiri Efeso, Apolo alienda Akaya. 10, 11. (a) Apolo alisaidiwaje kufanya maendeleo akiwa mhudumu wa habari njema? (b) Tunaweza kujifunza nini kutokana na simulizi kumhusu Apolo? (Tazama sanduku lenye kichwa Je, Mafundisho Yako Yanapatana na Kweli za Hivi Karibuni? ) SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 9

JE, MAFUNDISHO YAKO YANAPATANA NA KWELI ZA HIVI KARIBUNI? Ili tuwafundishe wengine ujuzi sahihi wa kweli ya Biblia, tunahitaji kuwa na uelewaji wa karibuni zaidi wa kweli hizo. Ukiwa na hilo akilini, ungejibuje maswali haya? ˇ Yesu alikuwa akirejelea nani alipozungumza kuhusu kizazi hiki katika Mathayo 24:34? Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 2010, ukurasa wa 10-11. ˇ Kutenganishwa kwa kondoo na mbuzi kunakotajwa katika Mathayo 25:32 kunatukia wakati gani? Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 1995, ukurasa wa 21-23. ˇ Kama inavyotajwa katika Luka 21:26, ni wakati gani watu watazimia kwa woga na tarajio la mambo yanayokuja juu ya dunia inayokaliwa? Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1994, ukurasa wa 19-20. Kwa kusoma Biblia kila siku na kuwa na funzo la kibinafsi lenye kina, tutaweza kuwasaidia wengine kutembea katika nuru inayozidi kuongezeka ambayo Yehova anatoa kupitia Neno lake lililoandikwa. Met. 4:18. Alipofika huko, akawasaidia sana wale waliokuwa wameamini kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu; kwa maana kwa juhudi nyingi alithibitisha kikamili hadharani kuwa Wayahudi ni wenye mako- 10 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

sa, huku akionyesha kwa Maandiko kwamba Yesu alikuwa ndiye Kristo. (Mdo. 18:27, 28) Kufikia wakati huo, Apolo aliweza kufafanua kwa usahihi maana ya ubatizo wa Kikristo. Akiwa na uelewaji ulioongezeka, Apolo aliwasaidia sana wapya kufanya maendeleo katika ibada ya kweli. Tunaweza kujifunza nini kutokana na simulizi hilo? Kama Apolo, tunajitahidi kuelewa mambo tunayosoma katika Biblia. Hata hivyo, mwamini mwenzetu mwenye uzoefu anapotupatia pendekezo la kutusaidia kufundisha kwa ustadi zaidi, tunapaswa kukubali msaada huo kwa unyenyekevu na shukrani. Tukifanya hivyo tutaboresha utumishi wetu mtakatifu. TUMIA MAMBO UNAYOJIFUNZA KUWASAIDIA WENGINE 12 Kama Prisila, Akila na Apolo, tunaweza kuwasaidia wengine. Unahisije wakati kitia-moyo chako kinapomsaidia mtu anayependezwa kushinda jambo linalomzuia kufanya maendeleo ya kiroho? Au 12, 13. Ukitumia mfano, eleza jinsi kutumia Maandiko kwa busara kunavyoweza kuwasaidia wanafunzi wa Biblia kufanya maendeleo. SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 11

ikiwa wewe ni mzee wa kutaniko, unahisije mwabudu mwenzako anapokushukuru kwa sababu ulimpa shauri la Kimaandiko lililomsaidia kukabili hali ngumu? Bila shaka, kutumia Neno la Mungu kuwasaidia wengine kuboresha maisha yao ni chanzo cha shangwe na uradhi. Ona jinsi unavyoweza kufanya hivyo. 13 Waisraeli wengi katika siku za Eliya waliyumbayumbakatiyaibadayakwelinayauwongo.shauri ambalo Eliya aliwapa watu hao linaweza kumsaidia mwanafunzi wa Biblia anayesita kufanya maendeleo ya kiroho. (Soma 1 Wafalme 18:21.) Fikiria hali nyingine: Ikiwa mtu anayependezwa anaogopa maoni ya marafiki au familia yake, unaweza kuimarisha azimio lake la kumwabudu Yehova kwa kuzungumza naye kuhusu kitabu cha Isaya 51:12, 13. Soma. 14 Ni wazi kwamba Biblia ina maneno mengi ya- Kwa kweli, hatutumii mashauri ya Biblia kuwalazimisha au kuwahukumu wengine. Tunapaswa kumtendea mwanafunzi wa Biblia kwa fadhili na subira kama Yehova anavyotutendea. Zab. 103:8. 14. Ni nini kitakachokusaidia kukumbuka maandiko ya Biblia unapohitaji kuwasaidia wengine? 12 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

nayoweza kuwatia moyo, kuwarekebisha, au kuwaimarisha wanaoisoma. Hata hivyo, huenda ukauliza, Ni nini kitakachonisaidia kukumbuka maandiko ninapoyahitaji? Soma Biblia na utafakari mawazo ya Mungu kila siku. Kwanjiahiyo,utajengahazinaya mawazo ya Mungu ambayo roho takatifu ya Yehova itakusaidia kuyakumbuka unapoyahitaji. Marko 13:11; soma Yohana 14:26. 15 Kama Mfalme Sulemani, sali ili Yehova akupe hekima itakayokusaidia kutimiza majukumu yako ya kitheokrasi. (2 Nya. 1:7-10) Kama manabii wa zamani, chunguza kwa bidii na utafute kwa uangalifu katika Neno la Mungu ujuzi sahihi kumhusu Yehova na mapenzi yake. (1 Pet. 1:10-12) Mtume Paulo alimhimiza Timotheo ajilishe maneno ya imani na ya fundisho zuri. (1 Tim. 4:6) Ukifanya hivyo, Namna gani ikiwa unakumbuka maneno makuu katika andiko lakini hukumbuki kitabu, sura, na mstari? Inaelekea kwamba utapata andiko hilo ukitafuta maneno hayo katika fahirisi iliyo kwenye kurasa za nyuma za Biblia, katika Watchtower Library, au katika konkodansi ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Kiingereza. 15. Ni nini kitakachokusaidia kuelewa Neno la Mungu kikamili zaidi? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 13

utakuwa tayari zaidi kuwasaidia wengine kiroho. Wakati huohuo, utajenga imani yako. ULINZI HAKIKA UNAOTEGEMEA NENO LA MUNGU 16 Wayahudi walioishi katika jiji la Beroya huko Makedonia walikuwa na desturi ya kuyachunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku. Paulo alipowahubiria Wayahudi hao habari njema, walilinganisha maneno yake na ujuzi waliokuwa nao wa Maandiko. Matokeo yakawa nini? Wengi wakasadiki kwamba alikuwa akifundisha kweli, nao wakawa waamini. (Mdo. 17:10-12) Hilo linaonyesha kwamba kuisoma Biblia kila siku humsaidia mtu kusitawisha imani yenye nguvu katika Yehova. Imani hiyo, yaani, tarajio lililohakikishwa la mambo yanayotumainiwa, ni muhimu sana ili tuokoke na kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu. Ebr. 11:1. 17 Paulo alikuwa na sababu nzuri alipoandika hivi: 16. (a) Kuyachunguza Maandiko kwa uangalifu kila siku kuliwanufaishaje Waberoya? (b) Kwa nini ni muhimu sana kwetu leo kusoma Biblia kila siku? 17, 18. (a) Imani yenye nguvu na upendo huulindaje moyo wa mfano wa Mkristo? (b) Tumaini linatulindaje dhidi ya hatari? 14 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

Kwa habari yetu sisi tulio wa mchana, na tutunze akili zetu na kuvaa bamba la kifuani la imani na upendo na lile tumaini la wokovu kama kofia ya chuma. (1 The. 5:8) Moyo wa askari-jeshi unahitaji kulindwa dhidi ya adui. Vivyo hivyo, moyo wa mfano wa Mkristo unahitaji kulindwa dhidi ya nguvu za dhambi. InakuwajemtumishiwaYehovaanapokuwanaimani yenye nguvu katika ahadi za Mungu na kumpenda Yehova na wanadamu wenzake? Mtumishi wa aina hiyo anavaa bamba la kifuani la kiroho lililo bora sana. Inaelekea kwamba hatafanya jambo lolote litakalomfanya apoteze kibali cha Mungu. 18 Paulo alitaja pia kofia ya chuma, yaani, tumaini la wokovu. Bila kulinda kichwa chake, askari-jeshi katika nyakati za Biblia angeuawa kwa urahisi vitani. Lakini akiwa na kofia nzuri ya chuma, angepigwa lakini hangeumizwa sana kichwani. Tunajenga tumaini letu katika matendo ya wokovu ya Yehova kwa kujifunza Neno lake. Tumaini lenye nguvu linatusaidia kuwapinga waasi-imani na maneno yao SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 15

matupu yaliyo kama kidonda kilichooza. (2 Tim. 2: 16-19) Tumaini letu litatuimarisha pia ili kuwapinga kabisa wale wanaotushawishi kufuata mwenendo unaoshutumiwa na Yehova. JAMBO MUHIMU ILI KUPATA WOKOVU 19 Kadiri ule mwisho unavyokaribia, ndivyo tunavyohitaji kulitegemea zaidi Neno la Yehova. Shauri tunalopata humo linatusaidia kurekebisha tabia mbaya na kudhibiti mielekeo yetu ya dhambi. Kupitia faraja na kitia-moyo cha Neno la Mungu, tutashinda majaribu ambayo Shetani na ulimwengu wake unatuletea. Tukifuata mwongozo ambao Yehova anatupatia katika Neno lake, tutabaki katika barabara ya uzima. 20 Kumbuka kwamba mapenzi ya Mungu ni kwamba watu wa namna zote waokolewe. Watumishi wa Yehova ni miongoni mwa watu hao wa namna zote. Pia, wanatia ndani wale ambao huenda tukawasaidia kupitia kazi yetu ya kuhubiri na kufundi- 19, 20. Kwa nini tunalithamini sana Neno la Mungu, na tunaonyeshaje kwamba tunalithamini? (Tazama sanduku lenye kichwa Yehova Hunipa Kile Tu Ninachohitaji. ) 16 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

YEHOVA HUNIPA KILE TU NINACHOHITAJI Dada mmoja kijana Mkristo aliandika hivi: Kati ya vikumbusho vyote vyenye upendo ambavyo Yehova hutupatia, kikumbusho cha kusoma Biblia kila siku kimenisaidia sana maishani mwangu. Nilianza kusoma Biblia mwaka wangu wa mwisho katika shule ya sekondari, na ilinichukua miaka miwili kuimaliza. Wakati huo, nilipata katika Neno la Yehova kila jambo nililohitaji ili kuamua jinsi nitakavyotumia maisha yangu. Sasa ninaisoma Biblia nzima kwa mara ya pili. Lakini ni kana kwamba ninasoma mambo mapya. Ninafurahia sana kuisoma tena Biblia kama tu nilivyofurahia nilipoisoma mara ya kwanza, na sasa ninaifurahia hata zaidi! Ninastaajabishwa na uwezo wa Yehova wa kunipa kile tu ninachohitaji. sha. Hata hivyo, ni lazima wote wanaotaka kupata wokovu wapate ujuzi sahihi wa kweli. (1 Tim. 2:4) Kwa hiyo, kuokoka siku hizi za mwisho kunategemea kusoma Biblia na kufuata maagizo yake yaliyoandikwa kwa mwongozo wa roho takatifu. Naam, tunaposoma Biblia kila siku tunaonyesha kwamba tunalithaminisananenolayehovalakwelilenyethamani. Yoh. 17:17. SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 17

Jinufaishe na Uwanufaishe Wengine kwa Kutumia Neno la Mungu Nimeyaona maagizo yote juu ya mambo yote kuwa ni sawa. ZA B. 119:128. UNGEJIBUJE? Unawezaje kutumia Maandiko kwa ustadi unapowafundisha wengine? Paulo alipotumia maneno kunyoosha mambo, alimaanisha nini? Ni kwa njia gani wazee na wazazi wanaweza kutia nidhamu katika uadilifu? WAZEE wanapofikiria ikiwa mwanafunzi wa Biblia anastahili kushiriki katika huduma ya shambani, wanajiuliza hivi: Je, maelezo yake yanaonyesha anaamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu lililoandikwa kwamwongozowarohotakatifu? Mtu anayetamani kuwa mhubiri wa Ufalme, na bila shaka watumi- Tazama kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 79. 1. Kwa nini tunapaswa kuwa na uhakika kabisa katika Neno la Mungu? 18 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

shi wote wa Mungu, ni lazima waamini jambo hilo. Kwa nini? Uhakika wetu katika Neno la Mungu na ustadi wetu wa kulitumia katika huduma utatuwezesha kuwasaidia wengine kumjua Yehova na kupata wokovu. 2 Mtume Paulo alikazia umuhimu wa Neno la Mungu alipomwandikia Timotheo hivi: Endelea katika mambo uliyojifunza na uliyoshawishiwa kuamini. Mambo aliyotaja Paulo ni kweli za Biblia zilizomchochea Timotheo kuamini habari njema. Kweli hizo zimetuchochea leo kwa njia hiyohiyo, na zinaendelea kutusaidia kuwa na hekima kwa ajili ya wokovu. (2 Tim. 3:14, 15) Kwa kawaida tunatumia maneno yafuatayo ya Paulo kuwaonyesha wengine kwamba Mungu ndiye chanzo cha Biblia, lakini huenda tukanufaika zaidi kibinafsi kutokana na maneno hayo yanayopatikana katika 2 Timotheo 3:16. (Soma.) Acheni tuchunguze kwa undani zaidi mstari huo. Kufanya hivyo kutatusaidia kuwa na 2. Kwa nini tunapaswa kuendelea katika mambo tuliyojifunza? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 19

uhakika zaidi kwamba mafundisho yote ya Yehova yako sawa. Zab. 119:128. LENYE FAIDA KWA KUFUNDISHA 3 Yesu aliliambia taifa la Israeli hivi: Ninatuma kwenu manabii na watu wenye hekima na wafundishaji wa watu wote. (Mt. 23:34) Yesu alikuwa akiongea kuhusu wanafunzi wake aliowafundisha kutumia Maandiko katika huduma yao. Katika Pentekoste ya 33 W.K., mtume Petro aliyekuwa mmoja wa wafundishaji hao wa watu wote, alihutubia umati wa watu huko Yerusalemu, na katika hotuba hiyo alinukuu sana Maandiko ya Kiebrania. Walipomsikia Petro akifafanua Maandiko hayo, wasikilizaji wengi walichomwa moyoni. Walitubu dhambi walizokuwa wamefanya. Watu elfu tatu hivi kati yao walitafuta msamaha wa Mungu na kuwa Wakristo. Mdo. 2: 37-41. 3-5. (a) Umati uliitikiaje hotuba ya Petro siku ya Pentekoste, na kwa nini? (b) Kwa nini watu wengi waliikubali kweli huko Thesalonike? (c) Leo, huenda watu wakavutiwa na nini katika huduma yetu? 20 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

4 Mtume Paulo aliyekuwa pia mfundishaji wa watu wote, alihubiri habari njema mpaka maeneo ya mbali nje ya Yerusalemu. Kwa mfano, katika jiji la Thesalonike huko Makedonia, aliongea na wale waliokuwa wakiabudu katika sinagogi. Kwa Sabato tatu, Paulo alijadiliana nao kwa kutumia Maandiko, akieleza na kuthibitisha kwa marejeo kwamba ilikuwa lazima Kristo ateseke na kufufuliwa kutoka kwa wafu. Matokeo yakawa nini? Baadhi yao [Wayahudi] wakawa waamini, na ndivyo na umati mkubwa kati ya Wagiriki. Mdo.17:1-4. 5 Watu wengi huvutiwa na jinsi watumishi wa Mungu wanavyotumia Biblia leo. Baada ya mwenye nyumba fulani nchini Uswisi kumsikiliza dada yetu akisoma andiko, alimuuliza hivi: Mnamwakilisha nani? Dada huyo akajibu: Sisi ni Mashahidi wa Yehova. Mwenye nyumba akasema: Nilipaswa kujua hivyo. Ni nani wengine wanaoweza kuja nyumbani kwangu kunisomea Biblia isipokuwa Mashahidi wa Yehova? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 21

6 Tunawezaje kuitumia Biblia kikamili zaidi tunapofundisha? Ikiwa una pendeleo la kufundisha kutaniko ukiwa jukwaani, taja maandiko hususa ya Biblia. Badala ya kueleza kwa maneno yako maandiko ya msingi au kusoma maandiko yaliyochapishwa kwenye karatasi au kuyasoma katika kifaa cha kielektroniki, fungua Biblia na usome maandiko hayo katika Biblia, na uwahimize wasikilizaji wafanye vivyo hivyo. Pia, chukua wakati wa kutosha kueleza maana ya maandiko hayo kwa njia inayowasaidia wasikilizaji kumkaribia Yehova zaidi. Badala ya kutumia mifano migumu na mambo yanayowachekesha tu wasikilizaji, tumia wakati kufafanua Neno la Mungu. 7 Tunahitaji kukumbuka nini tunapoongoza mafunzo ya Biblia? Tunapotumia machapisho yetu ya Kikristo, ni lazima tuwe waangalifu kutopuuza maandiko ya Biblia. Tunapaswa kumhimiza mwanafunzi asome maandiko yaliyoonyeshwa na kumsaidia kue- 6, 7. (a) Wale wanaofundisha kutaniko wanawezaje kuitumia Biblia vizuri? (b) Kwa nini ni muhimu sana kutumia Maandiko vizuri tunapoongoza mafunzo ya Biblia? 22 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

lewa maana ya maandiko hayo. Jinsi gani? Si kwa kutoa maelezo marefu kana kwamba tunatoa mfululizo wa hotuba, bali kwa kumtia moyo mwanafunzi ajieleze. Badala ya kumwambia mambo anayopaswa kuamini au kufanya, tunaweza kwa busara kumuuliza maswali yatakayomsaidia kufikia mkataa unaofaa. LENYEFAIDA...KWAKUKARIPIA 8 Mara nyingi, tunaona kukaripia ni kazi ya wazee Wakristo. Ni kweli kwamba waangalizi wana jukumu la kuwakaripia wenye mazoea ya kutenda dhambi. (1 Tim. 5:20; Tito 1:13) Lakini pia ni muhimu tujikaripie wenyewe. Paulo alikuwa mfano mzuri sana wa Mkristo aliyekuwa na dhamiri safi. (2 Tim. 1:3) Hata hivyo, aliandika hivi: Mimi naona ndani ya viungo vyangu sheria nyingine ikipigana na sheria ya akili yangu na kunichukua mateka kwa sheria ya dhambi. Tukichunguza muktadha wa maneno hayo, Yesu alipofundisha, mara nyingi aliuliza hivi: Mnaonaje? Kisha, alisubiri watoe jibu. Mt. 18:12; 21:28; 22:42. 8. Paulo alikuwa na pambano gani mwilini mwake? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 23

tutaelewa vizuri ni vita gani ambavyo Paulo alihitaji kupigana ili kudhibiti mwelekeo wake wa kufanya dhambi. Soma Waroma 7:21-25. 9 Paulo alijitahidi kuushinda udhaifu gani? Ingawa hakuutaja waziwazi, alimwandikia Timotheo kwamba mwanzoni, yeye alikuwa mtu mwenye dharau. (1 Tim. 1:13) Kabla ya kuwa Mkristo, Paulo aliwachukia sana Wakristo. Kuhusu hisia zake kuelekea wafuasi wa Kristo, aliungama hivi: Nilikuwa nimejawa na wazimu kupita kiasi juu yao. (Mdo. 26:11) Paulo alijifunza kudhibiti hasira yake, hata hivyo, huenda mara kwa mara alipambana ili kudhibiti maneno na hisia zake. (Mdo. 15:36-39) Ni nini kilichomsaidia kufaulu? 10 Alipowaandikia Wakristo waliokuwa Korintho, Paulo alieleza mbinu aliyotumia ili kujikaripia. (Soma 1 Wakorintho 9:26, 27.) Aliupiga udhaifu wake wa kibinadamu kwa ngumi za kiroho zilizoelekezwa vizuri. Inaelekea sana kwamba alitafuta ma- 9, 10. (a) Huenda Paulo alihitaji kupambana na udhaifu gani? (b) Inaelekea Paulo aliendelea kupigana jinsi gani na dhambi? 24 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

shauri katika Maandiko, akatoa dua ili Yehova amsaidie kuyatumia, kisha akajitahidi sana kuboresha utu wake. Tunaweza kufaidika kutokana na mfano wake kwa sababu tunapigana vita kama hivyo na mielekeo yetu ya kutokamilika. 11 Hatupaswi kamwe kutosheka tu na ibada yetu. Badala yake, tunahitaji kuendelea kujijaribu ili kuhakikisha kwamba kwa kweli tunatembea katika njia ya ile kweli. (2 Kor. 13:5) Tunaposoma maandiko kama vile Wakolosai 3:5-10, tunaweza kujiuliza hivi: Je, mimi ninajitahidi kabisa kuua mielekeo yangu ya dhambi, au je, ninadhoofika kiadili? Kituo kinachoonyesha mambo mapotovu kinapofunguka wakati ninapotumia Intaneti, je, mimi hukifunga mara moja au ninatafuta vituo vya Intaneti visivyofaa? Kutumia kibinafsi shauri la Neno la Mungu kwa njia hiyo Barua za Paulo zina mambo mengi yanayoweza kututia moyo kuishinda mielekeo ya dhambi. (Rom. 6:12; Gal. 5:16-18) Ni jambo linalopatana na akili kufikia mkataa wa kwamba yeye mwenyewe alitumia mashauri aliyowaandikia wengine. Rom. 2:21. 11. Tunawezaje kuendelea kujijaribu ili kuona ikiwa tunatembea katika njia ya ile kweli? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 25

kutatusaidia kukaa macho na kutunza akili zetu. 1 The. 5:6-8. LENYEFAIDA...KWA KUNYOOSHA MAMBO 12 Neno la Kigiriki linalotafsiriwa kunyoosha mambo linamaanisha kutengeneza vizuri, kusahihisha, kurekebisha, kurudisha katika hali nzuri. Nyakati nyingine, ni lazima tuchukue hatua ya kunyoosha mambo kati yetu na wengine ambao hawaelewi vizuri maneno au matendo yetu. Kwa mfano, viongozi wa dini ya Kiyahudi walilalamika kwamba Yesu aliwaonyesha fadhili wakusanya-kodi na watendadhambi. Yesu aliwaambia hivi: Watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali wenye kuugua ndio wanaomhitaji. Nendeni, basi, mkajifunze maana ya jambo hili, Ninataka rehema, wala si dhabihu. (Mt. 9:11-13) Kwa subira na fadhili, Yesu aliwafafanulia watu wote 12, 13. (a) Tunapaswa kuwa na kusudi gani tunaponyoosha mambo, na tunawezaje kuiga mfano wa Yesu tunapofanya hivyo? (b) Hatupaswi kutumia maneno ya aina gani tunaponyoosha mambo kati yetu na wengine? 26 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

maneno ya Mungu. Hivyo, watu wanyenyekevu walijifunzakwambayehovani Mungumwenyerehema na neema, si mwepesi wa hasira naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo na kweli. (Kut. 34:6) Kwa kuwa mwana wa Mungu alijitahidi kunyoosha mambo, wengi waliamini habari njema. 13 Mfano wa Yesu unatufunza jinsi tunavyopaswa kuwasaidia wengine. Mtu aliyekasirika anaweza kusema hivi kwa ukali: Ninataka kunyoosha jambo fulani kati yangu na wewe. Lakini njia hiyo ya kushughulikia mambo haipatani na andiko la 2 Timotheo 3:16. Andiko lote halitupi mamlaka ya kuwakemea wengine kwa hasira. Kama upanga unaochoma, mara nyingi kuwashutumu wengine vikali husababisha uchungu mwingi na kwa kawaida hakuleti faida yoyote. Met. 12:18. 14 Kwa hiyo, tunawezaje kuonyesha subira na fadhili tunaponyoosha mambo? Tuseme wenzi wa 14-16. (a) Wazee wanawezaje kunyoosha mambo kwa njia inayowasaidia wengine kutatua matatizo yao? (b) Kwa nini ni muhimu sana kunyoosha mambo kwa kutumia Maandiko unapolea watoto? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 27

ndoa wanaogombana mara kwa mara wanamwomba mzee Mkristo awasaidie. Mzee huyo atafanya nini? Bila kumuunga mkono yeyote kati yao, anaweza kuwasaidia akitumia kanuni za Biblia, labda kanuni zilizo katika sura ya 3 ya kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Mzee anapozungumza nao, wenzi hao wanaweza kuona shauri ambalo kila mmoja wao anapaswa kutumia kwa ukamili zaidi. Baadaye, itakuwa vizuri ikiwa mzee huyo atawauliza kuhusu hali ya familia yao na kuwapa msaada zaidi ikiwa unahitajika. 15 Wazazi wanawezaje kunyoosha mambo kwa njia inayowaimarisha kiroho watoto wao? Wazia kwamba unataka kumsaidia binti yako tineja kuepuka rafiki asiyefaa. Kwanza, unapaswa kujua mambo ya hakika kuhusu rafiki huyo. Kisha, ikiwa bado una wasiwasi, unaweza kuongea naye, labda ukitumia habari iliyo katika kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2. Baadaye, unaweza kutumia wakati zaidi pamoja naye. 28 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

Pia, angalia mtazamo wake anaposhiriki katika utumishi wa shambani au tafrija ya familia. Ukionyesha subira na ukiwa mwenye fadhili, binti yako atatambua kwamba unampenda na kumjali. Inaelekea kwamba atachochewa kutumia shauri ulilompa na kuepuka madhara maishani. 16 Vivyo hivyo, tunaweza kuwatia moyo kwa subira na upendo walio na wasiwasi kuhusu afya yao, walioshuka moyo kwa sababu ya kufutwa kazi, au wale wanaotatanishwa na mafundisho fulani ya Kimaandiko. Kutumia Neno la Mungu kunyoosha mambo huwanufaisha sana watu wa Yehova. LENYEFAIDA...KWAKUTIA NIDHAMU KATIKA UADILIFU 17 Hakuna nidhamu inayoonekana kwa sasa kuwa yenye shangwe, bali ni yenye kuhuzunisha. Hata hivyo, baadaye kwa wale ambao wamezoezwa nayo hiyo huzaa tunda lenye kufanya amani, yaani, uadilifu. (Ebr. 12:11) Wakristo wengi ambao 17. Kwa nini tunapaswa kukubali na kuthamini nidhamu? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 29

sasa ni watu wazima wanakubali kwamba nidhamu waliyopewa na wazazi wao Wakristo iliwasaidia. Na kukubali nidhamu kutoka kwa Yehova inayotolewa na wazee Wakristo, hutusaidia kuendelea kutembea katika njia ya uzima. Met. 4:13. 18 Ustadi unahitajiwa ili kutoa nidhamu kwa njia inayofaa. Yehova aliwaambia Wakristo watoe nidhamu katika uadilifu. (2 Tim. 3:16) Hivyo, tunapaswa kutumia kanuni za Biblia tunapotoa nidhamu. Kanuni moja inapatikana katika Methali 18:13: Yeyote anapojibu jambo kabla ya kulisikia, huo ni upumbavu na aibu kwake. Kwa hiyo, wazee wanapohitaji kuzungumza na mtu aliyeshtakiwa kwamba amefanya dhambi nzito, ni lazima wachunguze kwa makini sana jambo hilo ili wajue mambo yote ya hakika. (Kum. 13:14) Ni kwa njia hiyo tu ndipo wanapoweza kutoa nidhamu katika uadilifu. 18, 19. (a) Kwa nini shauri la Methali 18:13 ni muhimu sana katika kutia nidhamu katika uadilifu? (b) Wazee wanapoonyesha upole na upendo wanaposhughulika na wakosaji, kwa kawaida matokeo huwa nini? 30 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 SEHEMU YA 1

19 Isitoshe, Neno la Mungu linawaagiza wazee Wakristo wawarekebishe wengine kwa upole. (Soma 2 Timotheo 2:24-26.) Ni kweli kwamba mtu anaweza kumletea Yehova suto na pia kuwaumiza wengine wasio na hatia. Lakini, mzee anapomshauri kwa hasira mtu huyo, hatamsaidia. Hata hivyo, wazee wanapoiga sifa ya fadhili za Mungu, wanaweza kumchochea mkosaji kutubu. Rom. 2:4. 20 Ili wazazi wawalee watoto wao katika nidhamu na mwongozo wa akilini wa Yehova, ni lazima wafuate kanuni za Biblia. (Efe. 6:4) Baba anapaswa kuepuka kumwadhibu mwana wake kwa kutegemea tu mambo anayoambiwa kuhusu tabia ya mtoto huyo. Hasira kali haipaswi kamwe kuonyeshwa katika familia ya Kikristo. Yehova ni mwenye upendo mwororo sana na mwenye rehema, na wale walio na daraka la kuwatia nidhamu watoto wanapaswa kujitahidi kuonyesha sifa hizo za upendo. Yak. 5:11. 20. Ni kanuni zipi ambazo wazazi wanapaswa kufuata wanapowatia nidhamu watoto wao? SEHEMU YA 1 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 31

ZAWADI YENYE THAMANI SANA TULIYOPEWA NA YEHOVA 21 Pindi moja, mwanamume aliyemwogopa Mungu alieleza sababu iliyomfanya aipende sheria ya Yehova. (Soma Zaburi 119:97-104.) Kwa kujifunza sheria hiyo, alipata hekima, ufahamu, na uelewaji. Kutii shauri la Mungu kulimsaidia kuepuka njia za uwongo zilizowaletea wengine maumivu ya moyo. Kujifunza Maandiko kulimpendeza na kumridhisha. Aliazimia kumtii Mungu ambaye maagizo yake yalimletea manufaa mengi maishani. 22 Je, unathamini sana kila Andiko? Maandiko yatakusaidia kuwa na imani kwamba Mungu atatimiza kusudi lake. Shauri lake lililoongozwa na roho hukulinda kutokana na madhara mabaya sana ya kuzoea kufanya dhambi. Unapoyafafanua kwa ustadi, unaweza kuwasaidia wengine kuipata na kuendelea kuifuata barabara inayoongoza kwenye uzima. Acheni tutumie kikamili kila Andiko tunapomtumikia Mungu wetu mwenye upendo na hekima yote, Yehova. 21, 22. Ni maneno gani katika Zaburi 119:97-104 yanayofunua vizuri jinsi unavyohisi kuhusu Neno la Yehova? 32 MNARA WA MLINZI APRILI 15, 2013 www.jw.org/sw wlp13 04/15-SW-1