Banana Investments Ltd
|
|
- Jeremy Richard
- 5 years ago
- Views:
Transcription
1 Toleo la 21 Jarida litolewalo na; Banana Investments Ltd TOLEO NAMBA 21 HALIUZWI APRIL JUNE HALIUZWI
2 BODI YA WAHARIRI YALIYOMO Augustine Minja Mwenyekiti Gerald Lyimo Mjumbe Beatha Anthony Mhariri Mkuu Emanuel Nevava Mjumbe MAONI YA MHARIRI HABARI KUTOKA SINGIDA BANANA SPORTS CLUB YAJIPANGA UPYA KAMPUNI YABORESHA MASOKO SAFARI YANGU YA LOLIONDO KAMPUNI YASHIRIKI MEI MOSI BOHARI MPYA YAFUNGULIWA MOROGORO HABARI HUTOKA BOHARI YA DSM MPANGO WA KAMPUNI KUSAFISHA MAJI TAKA DONDOO MUHIMU ZA UNYAJI WA VILEO AJIRA MPYA NGUVU MPYA Y S MEN ARUSHA WAPOKEA UGENI KUTOKA GENEVA...07 SALAMU ZA MHARIRI Ni mara nyingine tena toleo la Mbiu ya Banana linatoka na kwa habari mbalimbali. Toleo hili tumeweka habari kutoka mikoa mbalimbali ambayo kampuni yetu inasambaza bidhaa zake. Hii ni kuonyesha kwamba kampuni inawajali wateja wake wote popote pale walipo. Tungependa sana kupokea makala kutoka kwa wateja wetu. Pia tunashauri kwamba makala hizo ziwe fupi na pia kwa namna moja au nyingine zihusiane na kampuni. Kwa wale wateja wetu ambao wataandika makala yao wazitume kwa kupitia magereva wetu wa Mauzo au wasambazaji. Pia unaweza kuleta hapa kiwandani na ukakabidhi mapokezi. Makala itakayochapishwa kwenye jarida mwandishi atalipwa kiasi cha shilingi 10,000/=. Tunatumia tena nafasi hii kuwakarisha katika kampuni ya Banana Investments Ltd watengenezaji na wasambazaji wa mvinyo halisi wa Ndizi. Kwa mawasiliano zaidi tumia namba za simu zilizopo ukurasa wa mwisho wa Jarida hili. WATU NA MATUKIO BI TECLA EDUARD, AFISA UGAVI APATA MWENZA Ilikua ni siku ya Alhamis tarehe 5/5/2011 yalisikika matatumbeta katika kijiji cha Oloirien, pale Bi Tecla akitokea nyumbani kwao kuelekea katika ukumbi wa kifahari wa Golden Rose ambapo wazazi wake alikua wamemuandalia tafrija kwa ajili ya kumuaga kwenda kuanza maisha ya kifamilia na Bw. Godbless Msuya wa Moshi. Baada ya sherehe hizo siku ya Jumamosi tarehe 7/5/2011 ilifanyika ibada ya ndoa takatifu katika kanisa la KKKT CKMC Moshi na kufuatiwa na sherehe zilizofanyika ukumbu wa chuo cha Ushirika hukohuko Moshi. Bwana harusi ni Afisa masoko wa TBL na Bibi harusi ni Afisa Ugavi wa Banana Investments Ltd. Beatha Anthony. 2 HALIUZWI
3 BANANA SPORTS CLUB YAJIPANGA UPYA KAMPUNI YADHAMIRIA KUBORESHA MASOKO Baada ya kimya kirefu sasa ile Club maarufu ya Banana imeanza kujipanga upya ili kuendeleza shughuli za michezo na utalii wa ndani na nje ya nchi. Ili kuhakikisha kuwa mipango yake yote inafanikiwa Club hiyo inatarajia kufanya uchaguzi wa viongozi katika ngazi za Mwenyekiti, Katibu, Mweka hazina na wajumbe wane. Viongozi hao wanatarajiwa kuwa wabunifu hasa kwa kuanzisha miradi itakayoongeza kipato cha Vlubu na kukusanya ada za wanachama kwa wakati. Pia Club hii inatarajia kuingia ubia na Club ya Genuine Sports Club iliyopo maeneo ya Kijenge Backdad kwaajili ya kufanya mazoezi ya viungo ya kunyanyua vyuma na Aerobics. Wanachama wanaombwa kuwa tayari kulipa ada zao za mwezi ili kuwezesha mipango yote hii. Adrian Anthony Katika kuhakikisha kwamba wateja wanapata huduma kwa wakati na kwa ubora wa hali ya juu, kampuni imesogeza huduma zake kwa karibu zaidi katika mikoa ya Kilimanjaro, Manyara na Dodoma. Hii ni pamoja na kuajiri wawakilishi wa masoko katika mikoa hiyo. Wawakilishi hao ambao wameanza kazi ya rasmi mwezi wa tano, 2011 pamoja na mambo mengine watasikiliza na kutatua matatizo mbalimbali ya wateja, watatoa fursa kwa wateja wapya watakaokua tayari kufanya biashara na kampuni yetu pia kuhakikisha kwamba bidhaa zetu zinafika kwa wateja kwa wakati unaotakiwa. Wawakilishi hao ni 1. MANYARA Patrice B. Menda - Namba ya simu DODOMA Denis Kessy- Namba ya simu KILIMANJARO Tumaini A Mungete Namba ya simu Kwa wateja wetu waliopo maeneo hayo wawasiliane na hawa wawakilishi ili waweze kupata huduma kwa haraka zaidi. Emanuel Nevava NI M BAYA KWA KULINGANISHWA NA NINI HASA? Kuna mengi tusiyoyajua! Miongoni mwa wanafalsafa maarufu duniani ni Mgiriki Socrates. Kwa wale wanaosoma na kufuatilia maisha ya wanafalsafa wa kale hapa duniani, huenda watakuwa wanajua kuhusu ndoa ya mwanafalsafa huyu maarufu. Wanaofuatilia maisha ya wanafalsafa hao watakubaliana nami kuhusu mke wa Socrates. Watu au wenzake Socrates walipokuwa wanamuuliza kuhusu mke wake, wakitegemea kusikia akilalamika, kwa sababu mama huyu alikuwa na ghubu sana, hawakusikia malalamiko yoyote. Badala yake aliwauliza, mnataka kujua yukoje kwa kulinganisha na nini? Ni hivi, iwe ni kwa watu, maeneo, hali, matukio, na hata hisia zetu vyote hivyo havina maana yenye kulingana kwa watu wote. Vyote hivyo ni vizuri au vibaya kwa viwango kwa kutegemea tunavilinganisha na nini. Hebu tuchukue vikombe vya aina moja, kama kimoja kimebenduka, tunaweza kusema hakiko kamili. Ni rahisi kusema hivyo kwa sababu, tuna mahali pa kulinganisha, ambapo ni kwenye vile vikombe vingine vizima. Kwa binadamu hali ni tofauti kabisa, kwa sababu wote ni tofauti. Hebu fikiria kuhusu tukio fulani kwenye maisha yako. Lakini bado kuna swali, kwa kulinganisha na tukio lipi? Kila tukio linatokea mahali pake, muda wake na kwa sababu fulani ili maisha yaendelee kuwepo. Kwa nini kama ni hivyo udhani tukio fulani ni baya au zuri? Huu ubaya au uzuri ni kwa kulinganisha na tukio lipi wakati kila tukio lina mahali, muda,na sababu ya kutokea kwake? Tunaambiwa kwamba kila jambo ambalo linaingia kwenye mfumo wetu wa kufikiri ni vizuri au vema likawa limepimwa kwa mujibu wa tafsiri zetu ambazo hazipaswi kutuumiza. Unaona jambo ambalo linataka kukuumiza kihisia, ni kwa nini usijiulize kama jambo hilo ni baya, ni kwa kulinganisha na lipi? Kumbuka ni lazima kuwe na mahali ambapo tunasimama ili kupima uzuri au ubaya wa jambo kwa kulinganisha na mengine, ambayo kwa kawaida hayatarajiwi kubadilika. Kama yanabadilika, basi ni vigumu kusema kuwa ni mabaya au mazuri, kwani hatuna mahali pa kuyalinganisha. Kama vikombe vinavyofanana kabatini vingekuwa wakati mwingine kimoja kinakuwa kirefu kingine kifupi au kinabadilika rangi, tusingeweza kuvilinganisha pia. Binadamu kila mmoja ana haiba yake, kila mmoja ni yeye kwa tabia, mienendo na hata miili. Na, Peter Mapunda. 3 HALIUZWI
4 Toleo la 21 KAMPUNI YASHIRIKI MAONESHO SIKUU YA WAFANYAKAZI MEI MOSI Kampuni ya Banana Investments Ltd imekua ikishiriki maadhimisho ya sherehe za wafanyakazi za Mei Mosi kwa miaka mingi. Na kila mwaka huibuka na ushindi mnono. Mwaka huu vilevile kampuni imejinyakulia makombe mawili ikiwa ni pamoja na mashindano ya maandamano ya miguu na naonesho ya bidhaa kwenye maandamano ya magari. Magari ya Maonesho ya kampuni yakipita mbele ya mkuu wa Mkoa yakiwa yamepambwa vizuri. Maandamono ya Magari yakiongozwa na Pikipiki za kampuni Katika kuhakikisha kwamba wafanyakazi wanapongeza uongozi wa kampuni uliandaa tafrija fupi iliyofanyika katika ukumbi wa kampuni mara baada ya sherehe ya uwanjani. Karika tafrija hiyo ambayo ilijumuisha wafanyakazi tu, mkurugenzi mkuu alitoa hotuba fupi akiwashukuru wafanyakazi wote kwa moyo wao wa utendaji pamoja na kushiriki katika maonesho hayo. Pia aliahidi kuwa kampuni itaendelea kutoa huduma mbalimbali kwa wafanyakazi kwa uaminifu na kuomba pia wafanyakazi wonyeshe uzalendo na uaminifu katika kufanya kazi za kampuni. Pia aliwatakia sherehe njema ingawa na yeye pia alikuwepo mpaka mwisho wa tafrija. Mkurugenzi msaidizi akikabidhiwa ngao ya ushindi na mkuu wa Mkoa. Baada ya hotuba ya Mkurugenzi mtendaji wafanyakazi waliendelea kupata chakula na vinywaji na baadae lilipigwa disco la nguvu na Dj Rogaa. Sherehe iliisha salama na kila mfanyakazi kurejea nyumbani. Beatha Anthony Wafanyakazi wakiburudika na kinywaji na Muziki. 4 HALIUZWI
5 Toleo la 21 BOHARI MPYA YAFUNGULIWA MOROGORO Maendeleo ni hatua. Banana Investsments Ltd imepiga hatua moja kati ya hatua nyingi, ya kufungua bohari mjini Morogoro ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wateja wake. Bohari hii ipo maeneo ya Kihonda Magorofani Polyester Club mkabala na Carmel/Kanisa Katoliki. Fika ofisini au: Picha: Jengo ambalo linatumika kama bohari kabla ya marekebisho. Polyester Club Kihonda / / Simu: Wateja wa mkoa wa Morogoro na mikoa ya jirani sasa watahudumiwa vizuri kutokana na uwepo wa bohari RAHA: RAHISI: HALISI. BIDHAA BORA YA BANANA hii. Kampuni inakaribisha maoni, ushauri na mawainvestments LTD - ARUSHA kala maeneo ya Turiani, Kilosa, Ifakara, Morogoro vijijini, na Mahenge. Wasiliana na afisa masoko Michael Emanuel kwa maelezo zaidi. TANZIA HABARI KUTOKA SINGIDA Kampuni ya Banana Investments Ltd unasikitika kutangaza vifo vya wafanyakazi wawili wafuatao:- Baada ya kampuni kuanzisha utaratibu wa kutoa huduma mojakwa moja kwa wateja wake, sasa wananchi wa Mkoa wa Singida wanafurahia huduma hiyo kwani wanapata bidhaa yetu hususani Raha kwa bei nzuri inayo wawezesha kupata faida nono. Kampuni kwa kushirikiana na wasambazaji wake wanefanya upatikanaji wa kinywaji cha RAHA kuwepo na pia kuhakikisha kwamba bei yake inamuwezesha hata mwananchi ya kawaida kuweza kununua. Kampuni kupitia muwakilishi wake aliyeko mkoani Singida Ndg Frank Joseph Urio inakaribisha ushauri,maoni, kutoka kwa wateja mbalimbali katika kuboresha biashara yake kwa faida ya wateja na kampuni kwa ujumla. Mwakilishi wetu sasa anapatikana kwenye ofisi iliyoko eneo la Shule ya Msingi Mughanga chumba namba 23, Au wasiliana nae kwa simu namba , Frank Joseph Urio Bi. Editha Joachim alifariki tarehe na kuzikwa tarehe nyumbani kwake Moshono - Arusha. Bi Editha aliyekuwa anafanya kazi katika Idara ya Uzalishaji ameacha mtoto mmoja na wajukuu wawili. Mungu ailaze roho ya Marehemu Editha mahala pema peponi Amina. 5 Bw. Uhuru Kawiche alifariki tarehe na kuzikwa tarehe nyumbani kwake Marangu Mamba mkoa wa Kilimanjaro. Bw. Uhuru alikuwa anafanya kazi katika Idara ya Uzalishaji. Bw. Uhuru ameacha mke pamoja na watoto. Mungu ailaze roho ya Marehemu Uhuru mahala pema peponi Amina. BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE Joan Mrema HALIUZWI
6 DONDOO MUHIMU ZA UNYWAJI SALAMA WA KILEO ALCOHOL Kileo ni kitu chochote kinacholevya kilicho katika mfumo wa bia, mvinyo, ama spirits. Jamii yote duniani iwe Africa, Ulaya, Asia na hata Amerika, imekuwa na aina yake ya kileo kulingana na utamaduni wake. Wengi wameathirika kutokana na kutozingatia njia nzuri za unywaji salama. Umri wako unaruhusu? Kama una miaka chini ya miaka 18, USIJARIBU NA ACHA KILEO. Hapa chini ni dondoo muhimu kuhusu unywaji ulio salama: Daima zingatia chakula kwanza kabla ya kileo/ pombe. Watalamu wanashauri ule vyakula vyenye protini mfano nyama, samaki, jibini cheese kwa kuwa vyenyewe vinauwezo wa kupunguza kasi ya kileo kuingia katika mzunguko wa damu kukuepusha na madhara. Kubali kinywaji pale ukitakapo. Wengi wetu tumekuwa wataalamu wa ofa ya hapa na pale hata kama mtu umetoka hospitalini leo ukiambiwa ebwana karibu tule vitu, unavamia kileo. Je nafsi yako ipo tayari? Kumbuka nafsi yako ni muhimu sana kwenye maamuzi. Epa kileo kama unatumia Dawa. Kama unaumwa na unatumia dawa, acha kileo. Kama kuna umuhimu sana wa kunywa, omba ushauri kwa mtaalamu wa afya kwanza. Epa unywaji ukiwa na njaa na kwenye joto kali (juani). Wataalamu wanasema utapata kizunguzungu, udhaifu/legea, na kupoteza mood hali iitwayo hypoglycemia, Zingatia usalama wa maisha yako na wengine barabarani. Kama unajua utaendesha chombo cha moto (gari, pikipiki hata baiskeli) Uhalali wa kinywaji chenyewe; Kila kinywaji kina utaalamu wake unaokubalika kwa mnywaji kutoka kwa mamlaka husika. Tanzania tuna mamlaka inayoitwa TBS-hawa ni wataalamu wa viwango nchini na TFDA ni wataalamu wa vyakula na madawa. Kinywaji chako hakikisha kimeruhusiwa na kupewa nembo ya TBS kwa usalama wa afya yako Fahamu kiwango chako. Kama wewe ni mnywaji wa Raha kwa mfano, kwanini leo unywe Raha + bia + viroba? Ni hatari kuzidisha kiwango cha kileo. Kwa sababu huwezi kubaini kiasi ulichokunya kwa urahisi. Zingatia unywaji wa maji. Kama ulipata kileo kiwe kingi ama kidogo, shurti unywe maji mengi. Unywaji wa kileo husababisha upotevu wa maji mwilini kwa njia ya mkojo hivyo ukaribishaji wa mning inio hang over na kuumwa sana kichwa. Dawa yake ni maji Mwisho zingatia uchumi wako. Tunajua kuwa unapenda kunywa ila sasa uchumi wako unaruhusu? Kinywaji unachotaka kunywa unamudu kukinunua? Au unataka kunywa kwa mkopo, upigwe, au kupewa ofa daima huku familia yako ikidhalilika? Imeandikwa ma Michael Massawe - Deport Incharge Simu: / / michael@banana.co.tz Morogoro 6 HALIUZWI
7 Bw. Eliabu Joram Machine Operator Bw. Eliabu ana cheti cha Technician in Mechanical Engineering kutoka chuo cha Ufundi Arusha (ATC). Pia amehitimu kidato cha IV katika shule ya Iyunga Technical Secondary School. Ana uzoefu wa miaka 3 katika taasisi mbalimbali Bw. Marko Andongolile Machine Technician Bw. Marko ana Diploma ya Mechanical Engineering katika chuo cha Ufundi Arusha (ATC). Pia amehitimu kidato cha IV katika shule ya Ifunda Technical iliyopo Iringa. Ana uzoefu katika kazi hii kwa zaidi ya miaka 3 katika taasisi mbalimbali. AJIRA MPYA, NGUVU MPYA KAMPUNI YA BANANA Bw. Tumaini A. Mungete Marketing Development Supervisor (Kilimanjaro Region) Bw. Tumaini ana Stashahada ya Biashara na utawala katika chuo cha Biashara (CBE). Pia amehitimu kidato cha VI Kolila High School Moshi na kidato cha IV Highlands Secondary iliyoko Iringa. Ana uzoefu wa miaka 10 katika taasisi mbalimbali. Bw. Denis F. Kessy Marketing Development Supervisor (Dodoma Region) Bw. Denis ana Shahada ya juu ya biashara na mahesabu kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam. Pia amehitimu kidato cha VI Minaki High School na kidato cha IV Uru Seminary. Bw. Mohamed H. Luhindi Auditing Technician Bw. Mohamed ana cheti cha Accountancy Technician (ATEC II) kutoka National Board of Accountancy and Auditing (NBAA). Pia na Stashahada ya Elimu kutoka chuo cha Ualimu Dar es Salaam. Na amehitimu kidato cha VI katika shule ya Sekondari Union Islamic na kidato cha IV katika shule ya Same Sekondari. Bw. Patrice M. Melley Marketing Development Supervisor (Manyara region) Bw. Patrice ana cheti cha Biashara katika chuo cha Uchira Business College na cheti cha Auto mechanics grade two VETA Dar es Salaam. Pia amehitimu kidato cha IV Sarwatt Secondary School na anao uzoefu wa taasisi mbalimbali. miaka 10 katika Y S MEN ARUSHA WAPATA UGENI KUTOKA GENEVA Klabu ya kimataifa ya Y s Men imeendelea kujipatia umaarufu mjini Arusha kutokana na shuhuli zao ya kijamii wanazofanya kupitia wanachama wake waliopo mkoani hapo. Mnamo tarehe 12/04/2011 Klabu ya Y s Men Arusha walipata ugeni mkubwa kutoka makao makuu ya Taasisi hiyo iliyopo Geneva. Ugeni huo ulikua ni Mr Takao Nishimura ambae ni mtendaji mkuu wa taasisi hiyo. Pamoja na mambo mengine Mr Takao alitembelea kiwanda cha kuzalisha Net aina ya Olyset cha A to Z ambao wanatengeneza net zinazisambazwa na Y s Men hii ni kufanikisha project ya Y s Men ya kuzuia Malaria (Roll Back Malaria). Pia katika kuonyesha utendaji wake Mr Takao alishirikiana na wanachama wa Y s Men wa Arusha kupanda miti katika eneo la Mlima suye. Baadaye wanachama waliandaa chakula cha jioni katika mgahawa wa Albero uliopo barabara ya Haille Sillas na kubadilishana mawazo na mgeni huyo. Vilevile vijana hawakubaki nyuma kwani waliweza kutuma muwakilishi katika Mkutano wa Jimbo la Y s Men la kanda ya Africa, kusini Mashariki. iliyofanyika Kitwe, Zambia na pia walipokea ugeni kutoka Geneva ambae ni mtendaji mkuu Y s Youth Mami Hashikazi raia wa Japan. Katka Mkutano huu Tanzania iliwakilishwa na Willy Kwayu wa Club ya Arusha. Kutokana na changamoto zilizoonekana wakati wa mazungunzo na wakeni hao Club ya Y s Men Arusha pamoja na Y s Youth wamejipanga imara ili kuhakikisha wanatoa huduma kwa jamii kulingana na mungu alivyowajalia. Mr Takao akipanda mti katika maeneo ya Mlima Suye. Pia wanajipanga kuendesha mafunzo kuhusu TB na vilevile kufungua rasmi club ya Y s Youth ya Moshi. Kwa wale watakaopenda kujiunga wawaliliane na Rais wa Club hiyo ambae ni Miss Lucy Tesha Mob kwa upande wa vijana na Mr Shanell Kavishe Mob Na Beatha Anthon 7 HALIUZWI
8 Tunawakaribisha wafanyabiashara kujiunga na Kampuni yetu ya Banana Investments Ltd kusambaza kinywaji chetu kwenye mikoa ambayo RAHA haijafika. Hali ya sasa katika usambazaji wa mvinyo wa Raha upo kama unavyoonyesha hapo juu kwenye Ramani Makao Makuu Kiwanja Na. 311, Kitalu jj Oloirien Village, P. O. Box 10123, Arusha TANZANIA S i m u : , banana@banana.co.tz.banana.co.tz Dar es Salaam Depot Ubungo Kibangu, S. L. P , Dar es Salaam TANZANIA Simu: , darsales@banana.co.tz Morogoro Deport Kihonda Area Simu morosales@banana.co.tz Tanga Depot Barabara ya 4, S. L. P. 5150, Tanga TANZANIA Simu: tangasales@banana.co. tz 8 HALIUZWI
Information for assessors (do not distribute this page to participants):
R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited
More informationGOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)
GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited
More informationTIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees
TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST
More informationJifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti
Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013
www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper
More informationAzimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu
The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA
More informationTIST HABARI MOTO MOTO MAANDALIZI YA MWAKA 2000 Y2K PREPARATIONS SASA NI WAKATI WA KUANZA KUPANDA MBEGU ZAKO
TIST HABARI MOTO MOTO Tel. 026-2322246 P.O.BOX 53 MPWAPWA E-Mail tist@twiga.com 01 October 2000 Y2K PREPARATIONS Holes and Seedlings made ready for the year 2000 programme By Gayo Mhila The process of
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3
More informationUtangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu
Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu BLOOD PRESSURE UK Shinikizo la damu ndicho chanzo kikubwa cha ulemavu na vifo vya mapema kule Uingereza, kupitia kiharusi, mshtuko wa moyo na maradhi ya moyo.
More informationMATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza
1 Matumizi bora ya Facebook kwa Biashara MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA Kwa Wanaoanza For IT Services & Web Solutions Web: Email: info@dudumizi.com Phone: 0768816728 2 Matumizi bora ya Facebook kwa
More informationHOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE
HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI
More informationHuduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig
KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1
More informationHati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako
More informationElimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani
Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh
More informationSautiElimu. Sauti Yako Isikike
SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian
More informationHuman Rights Are Universal And Yet...
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,
More informationMAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY
HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika
More informationSERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH
Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017
More informationIn the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment
In the matter of an Application by the KIGOMA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (KUWASA) For a Tariff and Charges Adjustment Background 1. On 17 th May 2011 KUWASA submitted an application for
More informationUfunguo wa Kutaalamika Haraka
0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11
More informationSera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji
Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na
More informationTANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora
K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012
More informationMiradi na jamii. 3.1 Utangulizi
3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi
More informationMheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame M. Mbarawa (Mb.); Waheshimiwa Mawaziri na Wabunge wote mliohudhuria;
HOTUBA YA BALOZI MHANDISI JOHN W.H. KIJAZI, KATIBU MKUU KIONGOZI, WAKATI WA UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA WAHANDISI KWA MWAKA 2017, UKUMBI WA JAKAYA KIKWETE, DODOMA, SEPTEMBA 7, 2017 Mheshimiwa Waziri
More informationUTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO
UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery
More informationUnited Pentecostal Church June 2017
Kwa Nini Tusali? Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa "Chagua" Ladies Prayer International kwa Facebook United Pentecostal Church June 2017 Tuko na wafuasi Facebook katika Marekani, Hong Kong, Philippines,
More informationMwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara
Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo
More informationRIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI
International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa
More informationUtumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania
Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi
More informationMKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA
More informationRipoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara)
Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Ripoti Fupi ya Nchi kuhusu Kazi Zenye Staha TANZANIA (bara) Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2010 Toleo la kwanza 2010 Machapisho ya Ofisi
More informationMhashamu Askofu Jude Thaddaeus Ruwa ichi, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania; Mwadhama Policarp Kardinali Pengo,
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, KWENYE SHEREHE YA KUADHIMISHA MIAKA HAMSINI YA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA, TAREHE 08 JUNI 2008, MSIMBAZI CENTRE, DAR ES SALAAM Mhashamu
More informationUKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)
Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni
More informationJUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1
The Human Rights Centre Uganda JUA HAKI ZAKO, SEHEMU YA 1 AZIMIO LA KIMATAIFA JUU YA HAKI ZA KIBINADAMU SURA YA NNE YA KATIBA YA JAMHURI YA UGANDA YA 1995: MASIMULIZI YALIYOFASIRIWA KWA URAHISI NA KUFUPISHWA
More informationMwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza
Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)
More informationDeutsche Welle, Learning by Ear 2009 Seite 1 People Who Make A Difference Liberia: Anita Varney Health Facilitator, Fishtown/Liberia
Deutsche Welle, Learning by Ear 2009 Seite 1 Title: Anita Varney Health Facilitator, Fishtown/Liberia Author: Stefanie Duckstein, HA Afrika/ Nahost Editor: Christine Harjes Translator: Tony Dunham Sound
More informationORDER NO BACKGROUND
In the matter of an Application by the DAR ES SALAAM URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (DAWASA) For a Tariff Adjustment, Submitted on January 8 th, 2008 (TR-W-08-001) ORDER NO. 08-001 1.0 BACKGROUND
More informationHatari, Haki za Usalama katika Bahari 03
Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03 AEG swahili Bahari ya Aegean Brosha ya maelezo hii ni kwa watu wanaofikiria kuvuka bahari ya Aegean kati ya Ugiriki na Uturuki.Kuvuka kihramu ni uhalifu katika
More informationRoho Mtakatifu Ni Nini?
Roho Mtakatifu Ni Nini? kwa ajili ya mkutano. Mkutano huu utakuwa tofauti, kidogo na ile ya kawaida tunayokuwa nayo hapa. Kwa kawaida, kila wakati tunapokuja pamoja hapa, ni mkutano kwa wa kwa ajili ya
More informationUpande 1.0 Bajeti yako
Upande 1.0 Bajeti yako Bajeti (Budget) ni muhustari wa njisi wewe (na familia yako) mnavyopata na kutumia pesa. Inaunganisha pesa zinazoingia nyumbani kwako (Kipato/ income) na zile unazotumia (matumizi/expenses).
More informationATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR
ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini
More informationNewsletter. RC Arusha: I assure you my full support for Zone office. Motto: Fair Regulation for Positive IMPACT NOT FOR SALE SEPTEMBER 2017
NOT FOR SALE Newsletter SEPTEMBER 2017 ISSN 1821-7273 ISSUE NO. 019 RC Arusha: I assure you my full support for Zone office Motto: Fair Regulation for Positive IMPACT Previous issue: NOT FOR SALE Newsletter
More informationKubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania
Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA
More informationHati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E)
102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI/AGOSTI 2011 MUDA: 2 ½ Kiswahili Fasihi Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E) MAAGIZO Jibu maswali manne pekee Swali la kwanza ni lazima Maswali
More informationUNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level
UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level * 899145 4 672* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2010 Additional Materials: Answer Booklet/Paper READ
More informationKUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA
KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA Toleo la kwanza 2012 Mwandishi: USAID DELIVER PROJECT Wachangiaji: Gary Steele, John Snow, Inc. and Judith
More informationMukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika
Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi Ya Vikombe Vingi Vya Ushirika (A Summary Of Arguments For And Against Individual Communion Cups) Na J D Logan Communion Cups) 1 Mukhtasari Wa Mabishano Kwa Na Dhidi
More information5. Mheshimiwa Spika, Bunge lako Tukufu lilijadili kwa kina Miswada ifuatayo:
HOTUBA YA MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI WA KUTOA HOJA YA KUAHIRISHA MKUTANO WA KUMI NA MBILI WA BUNGE DODOMA TAREHE 29 AGOSTI 2008 UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, leo ni takriban
More informationKUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA
KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa
More informationKITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO
KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa
More informationMACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI
This booklet on Becoming a Parent was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at. MACHAGUO
More informationKIMAZINGIRA NA KIJAMII NA MPANGO WA UDHIBITI
Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized!. viromen-alsc:a.. Environmental & Social MRADI WA UMEME WA GESI YA * Assessment & Management
More informationJHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI
JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika
More informationMwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira
Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Moduli ya kwanza Uhamasishaji Jamii juu ya Afya ya Mazingira Kimechapishwa kutokana na Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Jeff Conant na Pam Fadem i COBIHESA
More informationTIST HABARI MOTO MOTO
TIST HABARI MOTO MOTO Tel. +255784-537720/+255717-062960/+255782-250947, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@tist.org May 2010 Cash Payments for Trees Clean Air Action has developed a way to pay the groups
More informationNdugu na dada zangu wapendwa,
UJUMBE WA URAIS WA KWANZA, MEI 2014 Na Rais Thomas S. Monson Upendo Asili ya Injili Hakika hatuwezi kumpenda Mungu kama hatuwapendi wasafiri wenzetu katika safari hii ya maisha duniani. ninafurahia mawazo
More informationInternational Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi
International Labour Office Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi 1 Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2007 Kimechapwa mara ya kwanza 2007 Machapisho ya Ofisi ya Shirika la
More informationBustani 10,000 Katika Afrika. Alberto Prina
Bustani 10,000 Katika Afrika Alberto Prina K i j i t a b u Timu ya wahariri: Abderrahmane Amajou, Typhaine Briand, Roba Bulga Jilo, Davide Dotta, Emanuele Dughera, Michela Lenta, Velia Lucidi, Irene Marocco,
More informationRipoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013
W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa
More informationIn the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment
In the matter of Application by the TANGA URBAN WATER SUPPLY AND SEWERAGE AUTHORITY (TANGA UWASA) For a Multi-Year Tariff Adjustment Background 1. On 4 th September, 2012, the Energy and Water Utilities
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JULAI 2001 Leo napenda nizungumze nanyi kuhusu umuhimu wa kuweka akiba, na umuhimu wa kulipa
More informationTAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU
TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya
More informationPronunciation: Mä-hret Zäläke Ndal-ka-tscho Molla Mare Gebre-gzabiär 1/12
Human Rights Are Universal And Yet... Episode 07 Title : The right to food drought and famine in Ethiopia Author : Tedla Getachew Editor : Aude Gensbittel, Pendo Paul Translator : Anne Thomas Proofreader:
More informationTIST HABARI MOTO MOTO. Benefits of Loan Repayment. Faida za ulipaji wa mikopo U OTESHAJI W A M ITI Y A M ATUNDA
TIST HABARI MOTO MOTO Tel. 026-2322246, P.O.BOX 53 MPWAPWA E-Mail tist@ twiga.com 01 June 2001 Benefits of Loan Repayment As the date of repayment nears, 15 June, groups are busy preparing crops, digging
More informationMAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI
MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha
More informationMWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI
MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality
More informationHOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA BENJAMIN WILLIAM MKAPA,KWA WANANCHI, 30 SEPTEMBA, 2001 Leo napenda nizungumze nanyi, kwa lugha nyepesi iwezekanavyo, juu ya mahusiano tunayowania
More informationUnited Pentecostal Church April Kushangilia Kwa Sala
Kushangilia Kwa Sala Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa Kushangilia Kwa Sala Na Wanda Fielder United Pentecostal Church April 2017 Kuwa alimfufua katika kanisa tangu kuzaliwa, daima aliamini Neno la
More informationUMRI WA MAKAMO NA KUKOMA KWA HEDHI
This booklet on menopause was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania.
More informationEllen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar
Ellen White, waasisi wa Kiadventista,na Sabato Lunar Ukristo leo unadhihirisha waumini karibu bilioni mbili katika maelfu ya madhehebu tofauti na tofauti na madhehebu. Kati ya hizi, zaidi ya 500 madhehebu
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAISI-TAMISEMI HALMASHAURI YA WILAYA BUMBULI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAISI-TAMISEMI HALMASHAURI YA WILAYA BUMBULI NAMBA ZA SIMU: Mkuu Wa Shule: 0784524029 / 0766805826. Makamu Mkuu Wa Shule: 0714356735 / 0767356735. SHULE YA SEKONDARI
More informationMSAMAHA NA UPATANISHO
Hakimiliki 2007-2017 na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa. MSAMAHA NA UPATANISHO na Jonathan M. Menn B.A., Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, 1974 J.D., Cornell Law School, 1977 M.Div., Trinity Evangelical
More informationusudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-
Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa
More informationKiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika
Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to
More informationTAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM)
TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 TAFSIRI RAHISI YA MPANGO WA MAENDELEO YA AFYA YA MSINGI (MMAM) 2007-2017 Kimetolewa na Sikika (Zamani YAV) S.L.P 12183 Dar Es Salaam
More informationMipango ya miradi katika udugu
Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi
More informationKuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo
Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo Mazoezi ya wenye umri wa miaka 11-14 Hivi Ndivyo Nilivyo kwa wenye umri wa miaka 11-14 Kuhusu Hivi Ndivyo Nilivyo Ikiwa
More informationJAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized
horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya
More informationYaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!
Yaliyomo Kuhusu kitabu hiki Kuhusu kitabu hiki.........................................................1 Unapojisikia vibaya.........................................................2 Unapoanza kuwa mzima
More informationUsimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya
Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma
More informationTANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko
TANZANIA MARKETS PAN Sera zinazoboresha masoko UPOTEVU WA MAZAO YA NAFAKA BAADA YA MAVUNO: CHANGAMOTO NA UBORESHAJI Usuli Kuna makubaliano ya jumla kwamba marekebisho ya sera zinazohusu sekta ya kilimo,
More informationDibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi
Dibaji ya Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Uongozi Mwaka wa nne wa utekelezaji wa Mpango wa Msaada wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDAP 2011-2016) nchini Tanzania ulikuwa na mafanikio makubwa lakini
More informationHaja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (
Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Haja Ya Dini Haja Ya Dini Author(s): Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi [3] Publisher(s): Bilal Muslim Mission of Tanzania [4] Katika kijitabu
More informationKAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA
KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI
More informationElimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi
Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau
More informationK. M a r k s, F. E n g e l s
W a (any a kazi wa nchi zote, unganeni! K. M a r k s, F. E n g e l s Maelezo ya chama cha kikomunist Idara ya Maendcleo Moscow Tafsiri hii ya "Maelezo ya Chama cha Kikomunist" inatokana na maandishi
More informationDodoma ambako kikao cha Bunge kinaendelea kuja kushiriki japo sehemu ya uzinduzi wa mkutano.
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO MHE. DKT. PHILIP I. MPANGO (MB) WAKATI WA UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIMATAIFA WA KUJADILI MATUMIZI YA TAKWIMU ZA UMASKINI NA NAMNA BORA YA KUPIMA HALI YA UMASKINI AFRIKA,
More informationMwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI
David M. Mwayafu, Richard Kimbowa, Kristy Graham Mwongozo wa Kutathimini mifumo ya Ugawanaji wa faida na Mapato Katika Miradi ya Jamii ya MKUHUMI Na: David M. Mwayafu, Richard Kimbowa (Uganda Coalition
More informationPDF created with pdffactory trial version
المملكة العربية السعودية وزارة التعليم العالي الجامعة الا سلامية بالمدينة المنورة عمادة البحث العلمي قسم الترجمة تعريف موجز بالا سلام بل( لغة السواحلية) ١ بسم االله الرحمن الرحیم MAELEZO KWA UFUPI KUHUSU
More informationJAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAMISEMI HALMASHAURI YA JIJI LA TANGA
SIMU NA: (027) 2642082 TANGA (OFISI) 0784 889 099 TANGA (NYUMBANI) Tovuti: www.tangaschool.sc.tz Barua pepe: tangaschool@yahoo.com JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAMISEMI HALMASHAURI YA
More informationBIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE
Toleo 10 BIBLICAL INSTRUCTION AND ENCOURAGEMENT FOR THE MAFUNDISHO YA BIBLIA NA HIMIZO KWA MISSION FIELD WORLDWIDE. KAZI YA KIMISHENI ULIMWENGUNI KOTE UBATIZO WA MUUMINI Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa
More informationHii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE. Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006
Hii ni Nakala ya Mtandao (Online Document) BUNGE LA TANZANIA MAJADILIANO YA BUNGE MKUTANO WA NNE Kikao cha Nane Tarehe 23 Juni, 2006 (Ulianza Ulianza Saa Tatu Asubuhi) D U A Spika (Mhe. Samuel J. Sitta)
More informationHOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT
HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA MHESHIMIWA DKT. WILLIAM AUGUSTAO MGIMWA (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAPENDEKEZO YA SERIKALI KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2013/2014 I. UTANGULIZI 1. Mheshimiwa
More informationKijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia
IDARA YA KUFIKIA HUDUMA ZA AFYA VERMONT Kijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia GreenMountainCare MIASHA YENYE AFYA BORA ZAIDI Jedwali la Yaliyomo Jedwali la Yaliyomo... 2 Karibu kwenye Programu ya
More informationTAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014
TAARIFA YA MWAKA YA UTENDAJI KAZI IDARA YA UTAWALA BORA 2013/2014 15 JULAI, 2014 1 YALIYOMO YALIYOMO... i MUHTASARI... ii SURA YA KWANZA... 1 1.0 UTANGULIZI... 1 1.1 Kuhusu Tume... 1 1.1.1 Dira ya Tume...
More information2
2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 29 30 31 32 33 34 35 36 37 CKRC VERBATIM REPORT OF CONSTITUENCY PUBLIC HEARINGS, KALOLENI CONSTITUTENCY, HELD AT MARIAKANI SECONDARY
More informationEWURA scoops the highest rank in Africa s regulatory dispensation
EWURA scoops the highest rank in Africa s regulatory dispensation Previous issue: EWURA to open three more zones this year From the Editor... 3 From the Desk of the Director General... 4 ZERA: We have
More informationSiku ya kwanza. Mguso wa ngozi-kwa-ngozi (Ulezi wa kangaruu) Mtoto wako anaweza kuhisi mdundo wa moyo wako
Siku ya kwanza Baada tu ya mtoto kuzaliwa ni wakati wa kufurahia, lakini pia ni wa kuchosha. Kujua vitu vichache kuhusu kunyonyesha hufanya siku ya kwanza kuwa rahisi kidogo. Baada ya kujifungua Wakati
More information