Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO. Training and Research Support Centre

Size: px
Start display at page:

Download "Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO. Training and Research Support Centre"

Transcription

1 Shangazi Stella Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO Training and Research Support Centre Zimbabwe

2

3 Shangazi Stella Kiongozi cha Mwezeshaji na Matumizi yake VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA MAHUSIANO Training and Research Support Centre, Zimbabwe

4 This Kiswahili version of Auntie Stella was adapted for an east African audience and produced in cooperation with the Tanzania German Programme to Support Health. TARSC would like to thank the German Technical Co-operation (GTZ) for the time, commitment and resources they put into the production of this version. For more information about TGPSH please see or contact the GTZ Country Office, Box 1519, Dar-es-Salaam, tel: , Thanks are also extended to the Prevention and Awareness in Secondary Schools of HIV/AIDS (PASHA) project of the Ministry of Education and Vocational Training, implemented by the Swiss Tropical Institute, and to TARSC-Tanzania (PO Box 93, Bagamoyo) for their supportive role in reviewing the translation. And to Mr M. Mwinyi (National Kiswahili Council) for polishing up the Kiswahili and Mr D. Chikoko for his creativity in producing some of the drawings in the translation. Tafsiri hii ya makala ya Shangazi Stella imetayarishwa na Mradi wa Afya unaoshirikisha serikali ya Ujerumani na Tanzania (Tanzanian German Programme to Support Health) Kituo cha Mafunzo na Utafiti (TARSC) kinashukuru Shirika la Kiufundi la Kijerumani (GTZ) kwa muda, kwa kujitoa kwa hali na mali katika kutayarisha makala hii. Kwa maelezo zaidi juu ya TGPSH, tafadhali rejea au wasiliana na Ofisi ya GTZ Tanzania S. L P Dar-es-Salaam, simu : , barua pepe: repro-gtz@africaonline.co.tz Shukrani pia ziwaendee Mradi wa Kuzuia maambukizo na kuongeza ufahamu juu ya Virusi vya UKIMWI katika Shule za Sekondari (PASHA) iliyopo katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kufadhiliwa na Taaasisi ya Uswisi ya nchi za Joto ( Swiss Tropical Institute) kwa msaada wao katika hatua za kumaliza hatua za mwisho za kutayarisha makala hii ikiwa ni pamoja na kufanya majaribio ya uelewa. Kwa Kituo cha Mafunzo na Utafiti- TARSC, kwa kuhakiki tafsiri hii. Anwani ya Ofisi ya Shirika ni P.O. Box 93. Bagamoyo, Bila kuwasahau Mr.M. Mwinyi wa Baraza la Kiswahili Tanzania kwa kuhakiki lugha iliyotumika na Mr. David Chikoko kwa uchoraji wa katuni na tafrsi kwenye baadhi ya katuni. Kituo cha Mafunzo na Utafiti- (TARSC) Zimbabwe ni shirika lisilo la kiuchumi ambalo limeandikishwa nchini Zimbabwe mwaka TARSC inatoa mafunzo, kufanya utafiti na kusaidia serikali pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali.tarsc ni kituo cha kujifunza na kuendeleza ujuzi kikizingatia katika kujenga ujuzi na mbinu za kusaidia kazi katika ngazi ya jamii, na uwajibikaji wa muda ili kuwajengea uwezo katika sekta binafsi na mashirika ya jamii. Tafadhali rejea mtandao wetu au wasiliana nasi kwenye anwani admin@tarsc.org kwa taarifa zaidi kuhusu Kituo hiki cha TARSC pia kuhusu njia na mbinu shirikishi za kufundishia na makala zinazohusu utafiti na miradi. Shangazi Stella: Vijana wanazungumza kuhusu ngono, maisha na mahusiano kimepigwa chapa na : Training and Research Support Centre (TARSC), PO Box CY 2720, Causeway Harare, Zimbabwe Simu: Fax: Barua pepe: admin@tarsc.org Tovuti: tarsc@mweb.co.zw, hati miliki Kituo cha Mafunzo na Utafiti / Barbara Kaim, Aprili 2005 TARSC na B. Kaim kwa pamoja wanamiliki yaliyomo kwenye makala hii. Wakati tunahimiza matumizi ya makala hii kwa mashirika yasiyo ya kiuchumi, tunawataka wote wanaopenda kutumia makala hii kutoa taarifa kwa TARSC na kuzingatia matakwa ya wamiliki ikiwa ni pamoja na kuonyesha shukrani na kuwa wamepata ruhusa kutoka kwa waandishi na pia kuwapatia nakala zitakazo tafsiriwa. ISBN:

5 YALIYOMO SEHEMU YA KWANZA: KIONGOZI CHA WAWEZESHAJI Shangazi Stella ni nini? Mada na kadi za Shangazi Stella Wajibu wa Mwezeshaji Mwongozo wa jumla kwa Wawezeshaji Kufanya kazi na vikundi Jinsi ya kutumia Shangazi Stella Mfano wa karatasi za kumbukumbu Kipindi cha msingi Vipindi vya majibu ya watu wawili, barua zao, na jinsi moja Vipindi vya mada Vipindi vya marudio Vidokezo kuhusu shughuli Changamoto kwa Mwezeshaji Mafunzo na msaada kwa Wawezeshaji Rasilimali za ziada SEHEMU YA PILI: MATUMIZI YA SHANGAZI STELLA Matumizi ya Shangazi Stella Kanuni za msingi za kuandika barua mpya na majibu Kuwahusisha vijana katika kuandika kadi mpya Kutoa majibu mazuri zaidi Mambo ya kujadiliana na kuyafanyia kazi Shukrani Jinsi ya kuwasiliana nasi

6 Wawezeshaji! Soma Kiongozi hiki kabla ya kuanza kutumia Shangazi Stella. Kinakueleza Shangazi Stella inahusu nini na kitakusaidia vipi kutumia kadi na kupanga programu zako. Sehemu Kuu ni: Wajibu wa Mwezeshaji (ukurasa wa 9) Jinsi ya kutumia Shangazi Stella (ukurasa wa 12) Sehemu mbili za Kiongozi hiki zimekusudiwa kwa ajili ya kusaidia upangaji: Matumizi ya Shangazi Stella(ukurasa wa 32) Mafunzo na msaada kwa wawezeshaji(ukurasa wa 28) Ni matarajio yetu kuwa Kiongozi hiki kitakuwa na manufaa kwako na kwamba vijana wote watakaotumia kadi za Shangazi Stella watakuwa na ari ya kufanya kazi kwa pamoja ili kuweka mazingira mazuri kwa ajili yao; Mazingira ambayo vijana watakuwa na uhusiano mzuri, watawajibika na watashiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii zao. 4

7 SEHEMU YA KWANZA Kiongozi cha mwezeshaji

8 SHANGAZI STELLA NI NINI? Nilitaka kipindi kisiwe rasmi, kwa hiyo nilichukua kadi na kwenda nazo uwanja wa mpira na kujifanya ninazisoma. Hii ilijenga udadisi kutoka kwa mtu binafsi mmoja au wawili ambao walinifuata na kuniomba kadi, na mimi niliwapa kadi hiyo ili wasome wenyewe. Jambo hili liliibua mjadala na kupandisha udadisi. Kadri muda ulivyoongezeka watu zaidi walikusanyika na kuanza kubishana. Kazi yangu ilikuwa kuwatolea jibu nikisisitiza kuwa limetoka kwa mtu mwenye uelewa mkubwa. Kwa ufupi kadi hizi husaidia sana. Mwalimu wa vijana Shangazi Stella: ni kifurushi chenye mchanganyiko wa taarifa za afya ya uzazi na jinsia kwa ajili ya vijana. Taarifa zilizomo zinawafaa vijana wenye umri wa miaka kati ya 12 na 19, walio shuleni na nje ya shule. Kilitayarishwa nchini Zimbabwe kwa ajili ya vijana wa nchi za Afrika ya kusini na mashariki, lakini vilevile kinaweza kutumika katika bara zima la Afrika na kimataifa Kifurushi kinatumia mfululizo wa kadi za maswali na majibu zinazofanana na barua zinazoandikwa katika safu za Shangazi femina kwenye magazeti, ukurasa ambao vijana husoma na kuuliza maswali ili kupata taarifa mbalimbali zinazohusu ujinsia. Kadi na visa vilivyomo katika kifurushi cha Shangazi Stella vinaelezea kwa upana masuala binafsi na ya kijamii ambayo yanaathiri maisha ya vijana, afya ya kijinsia na uhusiano (angalia orodha kamili ukurasa wa 8). Vijana wanapotumia Shangazi Stella kwa kawaida wanafanya kazi katika vikundi vidogo vya jinsi mchanganyiko au jinsi moja. Kikundi husoma barua kwenye kadi halafu huangalia maswali ya kuongozea na kujadili tatizo lililowasilishwa. Baada ya hapo husoma jibu la Shangazi Stella na kufanya shughuli husika kama igizo dhima na mchezo wa kuigiza, michezo, chemsha bongo, midahalo, usaili, miradi ya utafiti, vikundi vya msaada, kutunga nyimbo na hadithi, ramani na vielelezo. Washiriki wanaweza kutumia kadi katika njia nyingine pia - wengine hufanya kwa pamoja katika vikundi vidogo wengine katika kundi kubwa. Malengo ya Shangazi Stella ni pamoja na: Kuweka mazingira tulivu ambapo vijana wanaweza kujadili kwa uhuru bila kuogopa masuala yanayohusu miili yao, hisia na uhusiano, afya ya kijinsia na mienendo. Kuwapa taarifa sahihi zinazowahusu wao na mabadiliko ya miili yao Kuwasaidia vijana kupima mambo wanayoyachagua na kusaidiana jinsi ya kufanya na kuzingatia uamuzi wa busara. Kuwapa stadi za kupanga, kuwasiliana, kujadiliana, kuomba msaada, kusema bila woga kile wanachotaka na kuhitaji, kuwasiliana na asasi, familia, wenzi na marafiki. 6

9 Kuwahimiza vijana kutumia huduma za kiafya na kijamii na kuwajibika katika kuhakikisha kuwa asasi hizi zinakidhi mahitaji yao. Kwa kawaida vijana wanajua mahitaji yao ili wafurahi na kuwa na afya njema, na wakipata msaada sahihi, wanaweza kufanikiwa jambo hili. Mara chache sana Shangazi Stella huwaeleza vijana wafanye nini na kipi wasifanye. Badala yake huwasaidia kufikiri kwa kujikosoa kuhusu wenyewe na uhusiano yao na wana rika, familia na jamii. Vijana huulizwa jinsi wanavyoweza kufanya kazi pamoja, kushiriki katika maamuzi ambayo huathiri maisha yao na kufanya sauti zao zisikike. Kwa kufanya hivyo huhimizwa kufikiria dunia ambayo ni mzuri zaidi na wajibu gani wanaweza kufanya kutengeneza dunia ya hivyo. Barua za Shangazi Stella na njia ya ufundishaji vilitokana na utafiti na vijana wa Zimbabwe, huonyesha uzoefu wao, mahitaji na changamoto. Kadi zilifanyiwa majaribio katika nchi nyingine za Afrika ya kusini na mashariki ikiwa ni pamoja na Malawi, Afrika kusini Tanzania na Zambia. Kifurushi kina maswali 38 na kadi za majibu, Kiongozi na kadi mbili za taarifa moja ina orodha ya mada na ya pili huelezea maana ya maneno magumu. Kwa mara ya kwanza kifurushi cha Shangazi Stella kilitolewa kwa lugha ya Kiingereza mwaka 1997 na kupitiwa mwaka 2004/2005. Kadi zinapatikana katika lugha kadhaa za Afrika ikiwa ni pamoja na Kishona, Kindebele na toleo la Kireno linatayarishwa. Angalia tovuti ya TARSC kwa taarifa zaidi. Shangazi Stella katika Tovuti Shangazi Stella anapatikana katika tovuti na vilevile kwenye CD ROM. Toleo la tovuti limeandaliwa kwa ajili ya watumiaji wanaofanya peke yao au kwa watu wawili au vikundi vidogo wanaotumia kompyuta moja. Watumiaji huangalia kifurushi chote na kusoma kadi moja moja kwa kubofya katika viunganisho kwa jinsi wanavyo taka.. 7

10 KADI NA MADA ZA SHANGAZI STELLA 1 Je ninaweza kufanya naye mapenzi 2 Je, uume wangu ni mdogo sana? 3 Hivi ni lazima nifanye ngono na shemeji yangu? 4 Ninamhudumia mtu mwenye UKIMWI (MVIU) 5 Hivi sasa mimi ni mkuu wa kaya yangu 6 Ninataka kufanya ngono kama rafiki zangu 7 Niliambukizwa ugonjwa wa ngono, je, nimekuwa tasa? 8 Mwalimu wangu anataka kufanya ngono na mimi 9 Mpenzi wangu ni mjamzito 10 Nina ashiki kali 11 Ninapomlipia chakula cha mchana, je sistahili kufanya naye ngono? 12 Chunusi zimeota kwenye uume wangu 13 Ninahisi kuwa nimeambukizwa Virusi Vya UKIMWI (VVU) 14 Nina wasiwasi kuhusu saratani ya shingo ya kizazi 15 Nilibakwa 16 Je nifanye biashara ya ngono? 17 Ninapata ndoto nyevu 18 Dawa za kupunguza makali ya Virusi Vya UKIMWI (ARV) ni nini? 19 Anataka tufanye ngono 20 Hedhi yangu si ya kawaida 21 Je nimweleze kuwa nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI? 22 Je, bangi inaweza kuniondolea aibu? 23 Wazazi wangu hawanielewi 24 Je, nimweleze kuwa nina maambukizo ya magojwa ya ngono? 25 Nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI. Je nitakufa? 26 Je yawezekana nina mimba? 27 Mpenzi wangu anatarajia kuolewa 28 Mwalimu alimtia mimba rafiki yangu 29 Mume wangu si mwaminifu 30 Nina msongo wa mawazo 31 Mimba hii siitaki 32 Dini yangu inakataza matumizi ya kondomu. 33 Ninapata maumivu makali sana wakati wa hedhi 34 Buzi langu hunifanyia vituko 35 Ninashindwa kujisomea kwa sababu ya mapenzi 36 Mama yangu ana maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI na yuko wazi kusema 37 Je, nitazitibu vipi chunusi zangu? 38 Nina maambukizo ya Virusi vya UKIMWI na mimba 8

11 WAJIBU WA MWEZESHAJI Nilijihisi kijana na kujifunza mengi kutoka kwa vijana. Vijana wanajua mambo mengi kuliko ambavyo watu wazima wanavyodhani wanajua. Walinifanya nifikirie bila kutoa ushauri na kulikuwa hakuna msukumo mkubwa kwa sababu kwa kawaida mchakato hujiendesha wenyewe. Mwezeshaji Watu mbalimbali wanaweza kuwa wawezeshaji; kama vile, Vijana Waelimishaji Rika, Walimu, Wafanya kazi wa Afya au Wafanyakazi wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Wanasihi au Maafisa wa vijana katika Wakala wa Serikali na Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali. Kama mwezeshaji ni vizuri iwapo: Unafahamu mambo mengi kuhusu afya ya uzazi kwa vijana balehe na kujua wapi unaweza kupata nyenzo na taarifa za ziada. Unajisikia vizuri wakati wa kuzungumza na vijana kuhusu masuala yanayohusu ngono na uhusiano. Unaweza kuongoza bila ya kutawala na unaweza kuvisaidia vikundi kufanya shughuli kadhaa. Unafurahi kuwaacha vijana wafanye kazi katika vikundi vidogo vya majadiliano. Huhitaji kuwadhibiti au kuwasahihisha au kujua kila kitu wanachosema. Vijana wanakuamini na kukuheshimu kwa sababu unawaelewa na unataka kuwasaidia kuimarisha uhusiano kwa watu binafsi na jamii yao. Wajibu wenu katika vipindi vya Shangazi Stella ni muhimu. Kazi yenu kubwa ni kuandaa na kusimamia vipindi na kuwatia moyo washiriki katika kushirikiana mawazo; taarifa na maswali; kuzungumza kwa uhuru na kujifunza njia sahihi za kuchagua na kufanya maamuzi ya busara. Unataka wazungumze, watoe hoja na kucheka. Vile vile wacheze michezo, wafanye majaribio, waigize hali, waimbe na kueleza hadithi. Majibu ya matatizo hayatakiwi kutolewa na wewe bali na wao wenyewe. Wawezeshaji wengine wana uzoefu, hawahitaji mafunzo maalumu ya kufanya kazi na Shangazi Stella, ingawa kiongozi hiki bado kitakuwa na manufaa. Hata hivyo kama unaona kuna mafunzo ambayo yanaweza kukusaidia, jadili na shirika lako na angalia mapendekezo yaliyopo ukurasa wa 20,

12 MAELEKEZO YA UJUMLA KWA WAWEZESHAJI Tayarisha yale yote watakayo fanya vijana katika kila kipindi. Usijali iwapo itakubidi ubadilishe mambo wakati kipindi kinaendelea. Kubali mabadiliko. Weka mazingira kuwa ya kawaida ili kila mtu ajisikie huru kuzungumza. Usijali iwapo majadiliano yatakuwa moto na kelele nyingi kuwepo. Toa maelekezo yaliyo wazi na rahisi, na hakikisha kila mtu anaelewa cha kufanya. Watie moyo na heshimu mawazo ya kila mmoja usilazimishe maoni yako. Kila unalolisikia ni siri. Kamwe usitete kuhusu jambo lililosemwa na mtu wakati wa kipindi. Ukifanya hivyo hawatakuamini. Wakumbushe washiriki kuwaheshimu watu wengine katika kikundi, wasimcheke mtu akitoa wazo lake na yatakayozungumzwa ndani ya kikao ni siri. Kiongozi wa kikundi anatakiwa kusisitiza hili. Ruhusu kikundi kichague lugha wanayotaka kutumia. Wasiliana na mashirika mazuri, watu binafsi na viongozi wa jumuia katika eneo lako ambao unaona watakuwa na manufaa. Waeleze kuhusu programu yako na waombe msaada. Soma kadi kuona taarifa ipi inahitajika na washiriki unaowasilana nao wanachokihitaji Tafuta taarifa za ziada kuhusu mada zilizopo kwenye kadi kutoka wizarani, mashirika, intaneti (mtandao wa mawasiliano ya kimataifa wa ki kompyuta), vitabu, video au DVDs. Wasaidie washiriki kwa kuwapa mapendekezo kadhaa wanapofanya utafiti. Mambo gani humfanya Mwezeshaji awe mzuri? Lazima awe msiri. Lazima awe mtu anayewatia moyo wale wanaofanya vizuri. Asiwe mwenye hasira na ukitaka kuzungumza naye asiseme ana shughuli nyingi. Lazima awe mtu anayejali wengine. Lazima awe mtu ambaye anaelewa yanayowafika vijana. Lazima nijisikie salama ninapozungumza naye. Lazima awe mtu mvumilivu. Anatakiwa kuwa na moyo mzuri. Bonginkasi Bhayi 10

13 KUFANYA KAZI NA VIKUNDI Jambo ambalo Wawezeshaji waliliona kuwa lenye manufaa ni kujua tofauti kati ya jambo la kweli na maoni. Halafu waligundua kuwa wanahitaji kujua mambo yote ambayo ni ya kweli kuhusu VVU na magonjwa ya ngono, na ujana balehe, lakini kwamba kila mtu alikuwa na haki ya mawazo aliyoyatoa. Mkufunzi Walimu wetu wengi hawakuwaweka vijana katika vikundi vidogo ili kujadili kadi. Walipendelea kundi kubwa ambalo wangeweza kulidhibiti, ingawa kuna kipindi waliwagawa washiriki katika makundi ya wasichana na wavulana. Lakini, tulipokaa pamoja mwisho wa programu, niliona kulikuwa na matatizo mengi yaliyojitokeza, kama muda hautoshi, kila mtu kutaka kuongea kwa wakati mmoja, na wakati mwingine hakuna anayeongea. Matatizo haya yangetatuliwa kama wangetumia kundi dogo la watu 4 au 5. Mkufunzi Katika vipindi vingi vya Shangazi Stella, washiriki hufanya kazi katika vikundi vidogo. Kundi kubwa linaweza kutumika vile vile kutegemeana na hali halisi. Mwezeshaji anayo kazi tofauti katika kila sehemu. Vipindi vya vikundi vidogo Katika vipindi hivi, washiriki huangalia kadi katika vikundi vidogo mchanganyiko wavulana na wasichana na kila kikundi kinafanya peke yao. Katika vipindi hivi unatakiwa: Kuanzisha kila kitu, lakini waachie kwa muda waendelee. Ruhusu vikundi vifanye kazi kwa kasi yao. Gawa kadi mpya iwapo washiriki wamemaliza kadi waliyokuwa wanaitumia. Wahimize washiriki wakuone kwa ajili ya taarifa zilizo za kweli, wanapokuwa hawana uhakika wanatakiwa kufanya nini, au wanapoona neno gumu au wazo lililopo kwenye kadi. Usisikilize majadiliano yao, au kuuliza wamesema nini. Usitoe maoni yako. Vipindi vya kundi kubwa Andaa vipindi ambavyo kundi kubwa watafanya kazi kwa pamoja. Vinaweza kuwa vya kuelezea mada fulani au kupitia marudio ya vipindi vilivyopita ambapo watajadili athari za Shangazi Stella na kipindi cha shughuli maalum (Maelekezo yake yapo ukurasa wa 16-22) Tayarisha na kupanga vipindi kwa uangalifu, lakini uwe tayari kufanya marekebisho kutegemeana na muda unaotumika kwa kila shughuli. Ongoza majadiliano na shughuli zote zitakazofanyika. Hakikisha kuwa mambo yote ya kweli ambayo washiriki wanashirikishana ni sahihi. Sahihisha taarifa ambazo sio za kweli au potofu, na waeleze mahali ambapo wanaweza kupata taarifa zaidi. Weka muda maalum wa kufanya shughuli, lakini kumbuka kuwapa taarifa muda unapokaribia kwisha. Ikilazimu unaweza kubadilisha mpango wako wa kazi. 11

14 JINSI YA KUTUMIA SHANGAZI STELLA Shangazi Stella anaweza kutumika katika mazingira na hali tofauti, kwa mfano darasani, wakati wa mikutano ya vijana, klabu ya UKIMWI au michezo, vipindi vya unasihi au vipindi vya wazazi. Vipindi vinaweza kuwa vya dakika 40 (kawaida shuleni) au nusu siku. Kabla ya kuanza Soma kadi na shughuli zote ili uwe na uwezo wa kuelezea mtu yeyote atakaye hitaji msaada. Soma maelezo kuhusu aina tofauti za vipindi ukurasa wa Andaa programu, lakini kuwa tayari kuibadilisha kutegemeana na kile kinachotokea kwenye kipindi. Kuna mfano wa programu ya vipindi 12 ukurasa unaofuata. Unapoandaa mpango, angalia kadi zingine zinaweza kuwa hazifai kwa kundi ulilonalo kwa sababu ya mazingira ya mjini na kijijini. Tofauti ya utamaduni au nchi katika mazingira haya. Ruka mada hizo au jadili matatizo ambayo yanafanana na hayo yanayowakuta vijana katika eneo lenu. Angalia sehemu ya pili inayohusu kurekebisha Shangazi Stella kwa ajili ya mawazo zaidi. Soma kisanduku kinachoelezea usimamizi wa muda (jinsi ya kutumia muda vizuri) ili ikusaidie wakati wa kuandika mpango. Usimamizi mzuri wa muda Kupanga na kukubali mabadiliko, ni muhimu. Ni afadhali kufanya shughuli moja vizuri kwa kumhusisha kila mtu kuliko kufanya shughuli kadhaa kwa haraka hata kama sivyo ulivyopanga mwanzoni. Kadiri kundi linavyokuwa kubwa ndivyo mjadala utakavyochukua muda mrefu, kwa hiyo tumia vikundi vidogo katika vipindi vingi na baada ya hapo mnaweza kukaa pamoja katika kundi kubwa kujadili mada maalum na kutoa muhtasari, pamoja na kukagua taarifa (angalia maelezo ya vipindi vya mada na kupitia marudio ukurasa wa 17 22).Iwapo makundi mbalimbali yanafanya kazi katika muda tofauti haina shida ni vizuri tu. Kumbuka kuwa mambo ya kuyafanyia kazi mengine, shughuli zake zinaweza kufanywa wakati wa vipindi vinavyohusisha watu wengi. Unapofanya chemsha bongo, maigizo dhima na midahalo, punguza idadi ya shughuli katika kipindi na weka kikomo cha muda kwa kila hatua ya mchakato. Vikundi vinapofanya kazi, wakumbushe muda uliobaki mara zinapobaki dakika tano au zaidi. Jitahidi kubadilika na mazingira Unapopanga vipindi vyako, uwe na mambo mengine ya kuchagua, ili shughuli ikiisha mapema au ikichukua muda mrefu zaidi kuliko ulivyofikiria uwe umekwishajitayarisha. Katika vipindi vinavyohusisha watu wengi hakikisha kila mara unaacha dakika tano mwisho wa kipindi ili kutoa muhtasari wa yale waliyojifunza na ikilazimu amua mambo ambayo watu watafanya katika kipindi kijacho. Ni muhimu kumalizia kipindi vizuri usiharakishe kufunga. 12

15 MFANO WA PROGRAMU YENYE VIPINDI 12 VIPINDI 1 Kuanza (mwanzo) 2 Kipindi cha msingi 3 Kipindi cha msingi 4 Kipindi cha majibu kwa watu wawili 5 Kipindi cha msingi (au malizia majibu kwa watu wawili) 6 Kipindi cha marudio 7 Kipindi cha mada 8 Kipindi cha barua binafsi 9 Kipindi cha msingi 10 Kipindi cha mada 11 Kipindi cha mada 12 Kipindi cha marudio Kuanza Unahitaji bango kitita na kalamu Anza kuvunja ukimya kwa kutumia kichocheo chochote ili kila mtu ajisikie huru. Iwapo washiriki hawafahamiani fanya zoezi la kutambulishana Uliza kama kuna mtu ambaye husoma kwenye magazeti na wanazionaje (Femina, TAYOA Helpline, leta raha, nipashe jumapili) Waonyeshe kadi za maswali na majibu na waeleze jinsi watakavyozitumia Eleza kuwa, Mambo ya kujadiliana na Mambo ya kuyafanyia kazi ni muhimu kwa sababu ni kiungo kati ya hadithi za kwenye kadi na yale yanayotokea katika maisha yetu. Kipindi kipya kitaanza na taarifa ya shughuli au utafiti uliofanyika kipindi kilichopita Soma mada kadhaa na waonyeshe kadi iliyo na orodha ya mada Tayarisha taratibu (sheria) zitakazofuatwa na kikundi, kwa mfano: Hakuna ruhusa kumcheka mtu Kila mtu apate nafasi ya kuzungumza Hakuna ruhusa ya kusimulia hadithi ya mtu nje ya kipindi. Washiriki waziandike sheria na kuzibandika kwa kila kipindi Sisitiza kuwa hutawasikiliza majadiliano yao, lakini wanaweza kukuuliza swali au kuomba msaada iwapo watahitaji. Waonyeshe kadi ya Neno lile lina maana gani? na iache sehemu ya katikati kwa ajili ya washiriki kutumia. Waambie kuwa hata wewe pia unaweza kuwaeleza inapobidi. Washiriki wachague makundi wanayoyataka ya watu 4 mpaka 6. Kama atabaki mtu, awekwe kwenye kundi lolote. Waombe wachague jina la kikundi. Kila kikundi kitayarishe karatasi kwa ajili ya kumbukumbu. Karatasi ambalo wataorodhesha kadi ambazo wamemaliza kuzifanyia kazi. Vile vile weka kumbukumbu zako za kipindi kama inavyoonyesha kwenye mfano ukurasa wa 14. Waombe kila kikundi wachague kiongozi. Eleza kuwa kiongozi wa kikundi husaidia kikundi kufuata sheria, hujaza kumbukumbu za kikundi na huwakumbusha wana kikundi kutoa taarifa kuhusu Mambo ya kuyafanyia kazi wanayofanya kati ya vipindi. Panga makundi yakae kwa nafasi ili kundi moja lisisikie kinachozungumzwa katika kundi lingine. Waeleze kuwa wanaweza kuzungumza lugha yoyote wanayoipenda. Anza na kipindi cha msingi na endelea na njia nyingine za kutumia kadi mara kila mmoja anapokuwa ameelewa Shangazi Stella. 13

16 Kielelezo cha karatasi za kumbukumbu Kumbukumbu za vikundi za mwezeshaji Vikundi Kadi natarehe Shughuli Maoni ya kumaliza zilizofanyika Maoni haya yahusu njia zilizotumika vizuri, matatizo yaliyojitokeza, masuala utakayoyaangalia upya na utakayoyafanya tofauti safari ijayo Kumbukumbu Jina la kikundi Mahali Tarehe Kadi zilizokwisha Shughuli iliyofanyika Maoni na maswali Washiriki wanaweza kutoa maoni yao kuhusu vipindi ambayo yanaweza pia kukufaa wewe. Waandike maoni kwa kifupi; kwa mfano: Tumefurahia kipindi, au tunahitaji muda zaidi na kadhalika 14

17 KIPINDI CHA MAELEZO YA MSINGI Wanafunzi wa kidato cha kwanza walikuwa wanaona aibu sana, lakini wale wakubwa walikuwa wanauliza maswali mengi kwa sababu walikuwa na shauku ya kujua kila kitu, tofauti na vijana nje ya shule ambao tayari walikuwa wanafahamu baadhi ya mambo. Mwalimu wa vijana Njia kuu ni kufanya kazi katika vikundi vidogo, vyenye mchanganyiko wa jinsi. Kila kikundi kitasoma barua ya swali na kutumia maswali ya kuongozea yaliyoko kwenye Mambo ya kujadiliana ili kujadili tatizo. Baada ya hapo watasoma majibu ya Shangazi Stella na kufanya Mambo ya kuyafanyia kazi. Kati ya shughuli za Mambo ya kuyafanyia kazi, hufanywa wakati wa kipindi na zingine hufanywa nje ya kipindi na taarifa yake kutolewa katika kipindi kinachofuata. Mambo ya kuyafanyia kazi husaidia washiriki kufikiria zaidi ya hadithi inayojadiliwa ili kubaini jinsi suala hilo huathiri maisha yao na hatua za kuchukua kuhusiana na hilo Huchukua muda kati ya dakika 15 na saa moja kumaliza kadi, kutegemeana na wanavyovutiwa, na aina ya shughuli inayofanyika. Yafuatayo ni mapendekezo ya utaratibu wa kufuata: Toa kadi ya maswali kwa kila kikundi usijali mpangilio wa kadi. Njia moja wapo unayoweza kuitumia ni kuzichanganya. Kwa mfano ikiwa una makundi matano anza na 1, 9, 17, 25 na 32, ukifuatia na 2, 10,18,26, na 33. na kuendelea au vikundi vinaweza kuchagua kadi wanazotaka. Vikundi vifanye kazi kwa wakati wao, waje kwako kukuona iwapo wanahitaji kadi ya majibu au kadi mpya au kadi mpya ya maswali au kama wana maswali ya kuuliza. Dakika kumi kabla ya kipindi kuisha, omba vikundi vianze kujaza karatasi za kumbukumbu. Waorodheshe kadi zilizokwisha, kadi ambazo hazijaisha (wanaweza kuendelea nazo katika kipindi kijacho) na Mambo ya kuyafanyia kazi yoyote ambayo watahitaji kuyafanya kati ya vipindi. Kusanya karatasi zote za kumbukumbu, na ziweke pamoja katika kifurushi cha Shangazi Stella. Waulize kama wana swali lolote la jinsi ya kutumia kadi Katika vipindi vyote vinavyofuata mwombe mtu atundike karatasi la sheria au kanuni. Watafanya kazi katika vikundi vilevile (labda kama kuna sababu za msingi za kubadilisha vikundi) wakumbushe viongozi wa vikundi kuhakikisha vikundi vinafuata sheria. Baada ya hapo kila kikundi kichukue kadi za kumbukumbu na kadi zozote ambazo hazikumalizika. Waanze kipindi kipya kwa kuzungumzia kuhusu shughuli yoyote ya Mambo ya kuyafanyia kazi waliyoifanya kipindi kilichopita. 15

18 VIPINDI VYA MAJIBU KWA WATU WAWILI WAWILI, BARUA BINAFSI NA JINSI MOJA Zipo njia nyingi za kutumia kadi hizi. Njia hizi hufanya mpango uwe wa ufanisi zaidi na kukupa nafasi ya kuona kwamba kila mtu ana taarifa sahihi. Aina za vipindi zimeelezwa kama ifuatavyo: Vipindi vya majibu ya watu wawili wawili (vikundi vidogo) Washiriki huanzia kwenye vikundi vyao vya kawaida. Baadaye hugawanyika katika vikundi vya watu wawili wawili (au watatu). Kila kikundi husoma kadi ya swali na Mambo ya kujadiliana, na kuandika majibu pamoja, halafu hurudi kwenye kundi lao na kupeana nafasi ya kusoma maswali na majibu. Kila jibu lililotolewa hujadiliwa na baadaye kulinganisha na majibu ya Shangazi Stella na Mambo ya kuyafanyia kazi. Shughuli hii inaweza kuchukua zaidi ya kipindi kimoja. Vipindi vya barua binafsi (vikundi vidogo) Kila mshiriki huandika barua yake binafsi kwa Shangazi Stella kuhusu matatizo yake, ya marafiki au ndugu zake. Weka wazi kwamba hakuna mtu ambaye atajua nani ameandika barua ipi na kwamba hawatakiwi kuandika majina yao. Toa dakika za kuandika barua. Ambaye atamaliza mapema anaweza kuandika barua ya pili. Baada ya hapo kila mtu arudi kwenye kundi lake, akunje barua yake na kutumbukiza kwenye mfuko. Wakisha tulia kila mtu katika kikundi achukue barua moja kutoka kwenye mfuko na kusoma kwa sauti (zoezi hili lifanyike kwa zamu) kikundi kijadili majibu ya barua. Wakumbushe kuwa sheria walizojiwekea ni muhimu sana wakati huu. Hakikisha hakuna mtu anaemcheka mwenzake au kuchukia barua zao. Utahitaji zaidi ya kipindi kimoja kumaliza kazi hii. Vipindi vya jinsi moja (Vikundi vidogo) Washiriki wengi hufurahia kufanya kazi katika makundi mchanganyiko wa wasichana na wavulana, lakini katika kadi zingine wasichana wanaweza kupenda wawe peke yao na wavulana peke yao. Kwa kutumia orodha kamili ya mada zilizo kwenye kadi, wanaweza kuchagua kadi ambazo wangependa kujadiliana katika makundi ya jinsi moja na unaweza kueleza bayana kipindi ambacho watazitumia kadi hizo. Waombe waunde vikundi vipya vya jinsi moja, halafu endelea na kipindi cha msingi cha kawaida. Mwanzoni mwa kipindi kitakachofuata, katika vikundi vyao vya kawaida wanaweza kuwaeleza wenzao walichozungumza. Mapendekezo ya kadi kwa ajili ya vikundi vya jinsi moja (vinaweza kuwapo vingine pia) 2 Je uume wangu ni mdogo sana? 14 Nina wasiwasi kuhusu saratani ya mlango wa kizazi 17 Ninapata ndoto nyevu 20 Siku zangu za hedhi si za kawaida 16

19 VIPINDI VINAVYOHUSU MADA Vipindi vinavyohusu mada (vikundi vidogo na vikubwa) Katika vipindi vya kujadili mada kikundi kizima hujadili pamoja kuhusu mada maalum kwa kutumia kadi kadhaa zinazohusiana. Ukurasa unaofuata unaonyesha mada kumi zinazowezekana kuzifanyia kazi. Zingine zimegawanyika katika mada ndogo tofauti. Unaweza kufikiria nyingine pia. Unapochagua mada kuu na mada ndogo, waulize washiriki zinazowafaa zaidi. Kadi nyingi zinafaa kwa mada kadhaa na mada mara nyingi zinahusiana, kwa hiyo kipindi cha mada kwa kawaida hulenga katika mwelekeo maalum wa kadi Kabla ya kuanza : Chagua mada. Ni rahisi kushughulikia mada zikiwa sehemu ya mpango mkubwa, sio Shangazi Stella peke yake. Kwa hiyo ni vizuri kutafuta taarifa nyingine na shughuli mbalimbali za kutumia pamoja na kadi (angalia marejeo ya nyongeza katika ukurasa wa 30). Kumbuka kuwa zipo kadi ambazo kadi nzima inafaa kwa mada moja, wakati zingine unaweza kukuta shughuli moja tu ndiyo inafaa. Unapo panga programu chunguza hili. Zipo njia nyingi za kufanya vipindi vya kuelezea mada. Angalia njia zilizopo ukurasa wa 19 na 20 na chagua moja ambayo unataka kuitumia. Unaweza kuandaa njia yako mwenyewe baada ya kuufahamu mpango na kikundi chako vizuri. Panga kila sehemu ya kipindi na kadiria kila sehemu itachukua muda gani. Utahitaji kipindi kimoja au viwili kumaliza mada moja Amua shughuli za kufanya katika vikundi vidogo na zile za kufanya katika kikundi kubwa. Tafuta idadi ya vikundi utakavyohitaji. Panga kitu cha kufanya iwapo shughuli zitachukua muda zaidi au kidogo kuliko ulivyofikiria.. 17

20 Mapendekezo ya Mada Kuibadilisha jamii Kubadili mitazamo 15, 16, 21, 36 Kuchukua hatua 4, 15, 27, 28, 33 Kujenga ubia 5, 18, 19, 28, 33 9 Uhusiano kati ya familia, jamii, na vijana Uhusiano kati ya wazazi, watu wazima na vijana 3, 9, 23, 27, 36 Utumiaji wa huduma za kijamii na za afya. 4, 12, 13, 14, 18, 20 Kujenga mitandao ya misaada 3, 5, 8, 25 8 Kuzungumza waziwazi 1, 5, 13, 15, 22, 29 Shangazi Stella 1 Ukuaji Mabadiliko katika miili yetu 2, 10, 17, 20, 33, 37 Mabadiliko ya mihemko 22, 30, 35 Kujisikia vizuri 2, 6, 37 2 Ngono na uhusiano Mapenzi na ngono 1, 6, 11, 21, 29 Uhusiano wa kijinsia 3, 11, 15, 22, 29, 34 3 Ngono salama 1, 10, 21, 24, 26, 32 7 Kuishi na Virusi Vya UKIMWI na UKIMWI Kuishi na VVU na UKIMWI 13, 18, 21, 25, 38, Kukabiliana na athari za VVU/UKIMWI 4, 5, 36 6 Magonjwa ya ngono 7, 12, 24 4 Ngono ya kulazimishwa Shinikizo la kijamii na kiuchumi katika kufanya ngono 3, 11, 16, 19 Ubakaji na udhalilishaji 8, 15, 19, 28, 34 5 Mimba zisizotarajiwa 9, 26, 28, 31 18

21 Njia ya 1 Siku moja ya muhimu, ninaingia darasani, uso wangu ukiashiria mtu kuhisi kuna jambo. Ninasoma kadi moja kwa sauti na kuinua kichwa kuona macho ya wanafunzi wangu yanaitikiaje.kabla sijajua mwitikio wao, maswali yanaanza kunimiminikia. Hakuna shida, na mimi ninayarudisha kwa wanafunzi. Majibu yanatoka. Muda umefika wa kusoma majibu ya Shangazi Stella. Mtu wa kujitolea anachaguliwa. Ninawauliza iwapo wameridhika, wanajibu kuwa amemaliza yote. Nilisoma kadi nyingine, halafu nikawaacha hewani bila jibu. Siku ya pili yote yatakuwa yanajulikana. Shangazi Stella, umekuja kama ufunguo wa akili kwa vijana na asante kwa kuokoa siku zangu. Mwalimu wa vijana 1 Kusanya vifaa vya msingi utakavyohitaji na kuandaa kipindi kama ilivyoelezwa ukurasa wa 17 2 Kabla ya kuanza kipindi, eleza kwa kifupi masuala yanayohusiana na mada iliyochaguliwa ili kuonyesha mwelekeo na kueleza mawazo yoyote au maneno ambayo yanaweza kuwa hayajulikani au hayako wazi. Kwa mfano unaweza kutoa maana ya mawasiliano na ushirikiano 3 Mwanzoni mwa kipindi, washiriki wakifanya wawili wawili, waandike maswali yoyote yanayohusu mada hiyo. Andika maswali kwenye bango kitita na bandika mahali wakati kadi zinafanyiwa kazi. 4 Gawa washiriki katika makundi sawa na idadi ya kadi zilizopo zinazohusu mada hiyo (kadi 4 = vikundi 4) kila kikundi kipewe kadi moja. Baadaye wabadilishane kadi ili kila mtu apate nafasi ya kuzifanyia kazi kadi zote au karibu zote. Iwapo umeweka alama Mambo ya kuyafanyia kazi kwa ajili ya shughuli za kikundi kikubwa waombe waache shughuli hizo. 5 Kila mtu atakapokuwa amepitia karibu kadi zote waombe wakueleze mambo muhimu yaliyomo kwenye kadi. Yaandike kwenye bango kitita au karatasi kubwa. Baada ya hapo fanya shughuli zilizobakia kutoka kwenye kadi na shughuli zingine zozote ulizoainisha. Oanisha shughuli na mada zilizoorodheshwa na washiriki. 6 Mwisho rudi kwenye maswali yaliyotolewa na washiriki mwanzoni mwa kipindi. Je wanaweza kuyajibu sasa? Kama kutakuwa na masuala yaliyobaki, jadili mahali pa kuzipata taarifa wanazozihitaji iwapo huwezi kuwapatia jibu. (Unaweza kukuta masuala mengine yaliyobaki yanaangukia kwenye mada nyingine na hii itakupa uelekeo katika kuandaa kipindi cha mada inayofuata.) 7 Mwisho waulize wanataka kufanya nini ikiwa ni matokeo ya kujadiliana kuhusu mada hii, kama mtu binafsi katika uhusiano (na marafiki, familia, wenzi) na katika jamii? 8 Hatua hii ya mwisho ni muhimu sana, kwa hiyo hakikisha unaacha muda wa kutosha. 19

22 Njia ya 2 Fanya hatua ya 1, 2 na 4 kutoka katika njia ya kwanza Baada ya kila mtu kuona karibu kadi zote, uliza maswali haya Umejifunza nini kutokana na majadiliano yenu? Mawazo yaliyoko kwenye kadi yana manufaa gani katika maisha yenu? au maisha ya watu katika jamii yenu? Je, wapo watu au mashirika unayoyajua ambayo yanashughulikia masuala haya? Wanafanya nini? Ni mabadiliko gani ungependa kuyafanya katika maisha yenu na jamii kama matokeo ya kufanyia kazi mada hii? Unahitaji msaada na stadi zipi ili kufanya mabadiliko haya na utapataje? Baada ya hapo fanya shughuli ulizochagua. Njia ya 3 Fanya hatua ya 1 na 2 kutoka kwenye njia kwanza Kila kikundi kishughulikie kadi moja tofauti inayohusiana na mada (weka kikomo cha muda) halafu toa taarifa kwenye kikundi kikubwa kwa kujibu maswali haya: Ni tatizo au suala gani lililojitokeza kwenye kadi? Ni ushauri gani unauona kuwa ni mzuri sana sasa hivi kwa tatizo hilo? kwa nini? Kadi hii ina umuhimu gani katika maisha yenu, kama mtu binafsi, katika uhusiano na katika jamii yenu? Baada ya hapo fanya shughuli moja au zaidi zinazohusiana na mada kuu. Njia ya 4 Chagua mambo ya kuyafanyia kazi husika kutoka kwenye kadi yako kwa ajili ya kikundi kizima Karibu na mwisho waombe vijana wajadili maswali haya wawili wawili kwanza, halafu katika kikundi kizima Ni taarifa na stadi gani umezipata kutokana na kufanya shughuli hizi? Unataka kufanya nini ikiwa ni matokeo ya kuifanyia kazi mada hii kama mtu binafsi, katika uhusiano wako (na marafiki, familia, wenzi) na katika jamii? 20

23 VIPINDI VYA MARUDIO Vipindi vya marudio (katika vikundi vidogo na vikundi vikubwa) Katika kipindi cha marudio, washiriki hujadili yale ambayo wamejifunza mpaka kufikia sasa hivi na jinsi ambavyo yameathiri maisha yao. Vilevile wanaweza kuuliza maswali yoyote iwapo wanataka. Kipindi hiki husaidia kufanya tathmini ya jinsi mpango unavyoendelea na mambo ambayo washiriki wameyapata. Ni wazo zuri kufanya vipindi vya marudio kila baada ya vipindi vitano au sita, hususani iwapo umekuwa ukitumia vikundi vidogo. Wajibu wako ni kutoa taarifa zinazokosekana (au kuwaelekeza mahali wanapoweza kuzipata) na kusahihisha zisizo za kweli au ambazo zinaeleweka vibaya. Andika maswali yafuatayo ubaoni au kwenye bango kitita kabla ya kipindi. Maswali ya kuuliza katika vipindi vya marudio Ni kitu gani unafurahia zaidi na ni kitu gani hufurahii kuhusu kadi za Shangazi Stella? Ni mambo gani muhimu zaidi ambayo umejifunza au umefanya kutoka katika kadi ambazo umeziona? Una maswali yoyote kuhusu hadithi mlizojadiliana? Shughuli gani zilikuwa zenye manufaa katika Mambo ya kuyafanyia kazi? Je, kuna mabadiliko yoyote katika maisha yako, yaani hisia zako uhusiano, mtizamo au tabia kama matokeo ya kufanya mpango huu? Kama jibu ni ndio, ni mabadiliko gani? Kama kikundi au kwa kushirikiana na mashirika, mmefanya nini kubadili maisha yenu na mazingira? 21

24 Mara nyingi ni rahisi watu kujadili maswali haya katika vikundi vidogo kwanza hasa kama washiriki ni zaidi ya 15. Baada ya majadiliano watoe taarifa kwenye kikundi kikubwa kuhusu mawazo yao. Toa muhtasari wa maoni kufuatana na vipengele vifuatavyo: 1 Maudhui ya kadi Toa maoni kuhusu waliyojifunza na maswali yaliyoulizwa. 2 Mchakato wa Shangazi Stella Walichopenda na kile ambacho hawakupenda. 3 Matokeo kwa vitendo Mabadiliko yoyote au uamuzi uliofanyika katika maisha yao, familia na uhusianao katika jamii au nchi. Hakikisha unayaheshimu mawazo yao, hata kama yanaonekana kuwa sio sahihi au ya kijinga. Usimcheke mtu yeyote. Vilevile kumbuka kutofautisha kati ya jambo la ukweli na maoni. Maswali ya ziada ya kuchagua kwa ajili ya vipindi vya marudio vijavyo Uligundua nini katika sehemu hii ya Shangazi Stella? Kitu gani kilisaidia sana? Iwapo uliandika barua zako, je, kuna hadithi au maswali ambayo ungependa kushirikisha kikundi kizima? Umegundua nini kuhusu mawazo na uzoefu wa jinsi nyingine kutokana na kushughulikia kadi kwa pamoja? Shangazi Stella amekuathiri vipi katika namna unavyofikiri kuhusu wewe mwenyewe na mwili wako; uhusiano na wanarika wenzako na wenzi, uhusiano na familia yako na jamii? Je, Shangazi Stella amekubadilisha mwenendo wa maisha yako? Kwa vipi? Umejifunza nini kuhusu watu na mashirika ambayo hujaribu kutoa msaada kwa vijana katika jamii (ikiwa ni pamoja na programu za shule, kliniki, viongozi wa jamii, na huduma za majumbani? Je Shangazi Stella ameathiri mtazamo wako kwao? Umegundua njia zipi za kushirikiana ili kuleta mabadiliko? Ni mabadiliko gani ungependa kuyafanya hapo baadaye? Je umeanza kuhusika katika kufanya maamuzi ambayo yaanathiri maisha yako katika mashirika? Kwa vipi? 22

25 VIDOKEZO KUHUSU VITENDO Igizo dhima Washiriki huigiza hali iliyotolewa kama wenyewe au mtu mwingine. Kwa mfano msichana akijaribu kumshawishi mpenzi wake atumie kondomu, au mvulana akimshinikiza mpenzi wake wa kike kufanya ngono. Lengo ni kile kitakachotokea katika mazungumzo na jinsi inavyohusika na maisha halisi na sio jinsi watu wanavyoweza kuigiza vizuri. Watu wawili au watatu wanaweza kuigiza mbele ya wengine katika kikundi chote, au kila mtu anaweza kuigiza hali zinazofanana na kutoa taarifa baadaye kwenye kikundi Iwapo washiriki wanafanya kazi wenyewe katika vikundi vidogo, maswali yaliyoko kwenye kadi yatawaongoza kupitia igizo dhima. Hata hivyo iwapo ni kipindi cha kikundi kikubwa wewe utahusika zaidi. Mwisho wa igizo dhima, wasifu wote walioigiza na manufaa ya igizo dhima. Mara kwa mara waondoe waigizaji katika nafasi zao na kuwauliza: Umejisikiaje kushika nafasi hiyo? Wengine wameonyeshaje hisia zao? Jambo hili ni muhimu lifanyike hasa iwapo kuna mtu alikuwa akiigiza nafasi mbaya. Baada ya hapo, kila mtu ajadili: Kumetokea nini? Kwa nini? Je hili linaweza kutokea katika maisha halisi? Je waigizaji walifikia hitimisho zuri? Umejifunza taarifa na stadi zipi kutokana na igizo na ni msaada gani unahitaji ili kushughulikia hali kama hii? 23

26 Mchezo wa kuanza na kusimamisha Hili ni aina maalumu ya igizo dhima. Watu wachache katika kikundi wanaigiza na wengine kuangalia. Wale wanao angalia wanaweza kunyoosha mikono na kusimamisha igizo iwapo wanataka kuchukua nafasi ya yeyote, na kuigiza tofauti. Mwisho wa igizo usijadili nani ameigiza vizuri bali ni njia ipi ilikuwa nzuri katika kufanikisha madhumuni ya igizo dhima. Kwa mfano kuomba ushauri kutoka kwa mtu mzima. Maelezo ya kujadili Hizi ni sentensi ambazo washiriki wanaweka alama ya kweli/uongo au nakubali/sikubali. Washiriki huandika majibu yao binafsi kwanza, halafu wawili wawili au katika vikundi vidogo hujadili kila sentensi na kujaribu kufikia mwafaka hata kama hawana uhakika. Njia nyingine inayoweza kutumika katika kundi lote ni kuweka alama kwenye kona tatu za chumba kama, nakubali sikubali na sina uhakika. Soma sentensi moja baada ya nyingine. Halafu washiriki wapige kura kwa kusimama kwenye kona anayokubaliana nayo. Fanya majadiliano mafupi kuhusu ni kwa nini wamechagua hivyo lakini tumia muda mfupi ili wasichoke. Majaribio / chemsha bongo Majaribio yanatakiwa kuwa kiburudisho. Yasiwe kama yale ya shuleni yafanywe na watu wawili wawili au katika kikundi kidogo, au soma kwa sauti maswali na acha kila mtu binafsi aandike majibu na alama alizopata. Majadiliano ni kipengele muhimu katika majaribio haya kwa sababu majaribio mengine hulenga katika maoni kuliko mambo ya ukweli. Michoro na vielelezo Washiriki wanaweza kufanya haya katika karatasi, ubao, au kwenye mchanga. Sisitiza kuwa, hakuna haja ya kujua sana kuchora. Kinachotakiwa hapa ni kuonyesha mawazo yao. Tumia michoro kama mbadala wa kuandika. Kwa mfano Mti wa matatizo hulenga katika mada yoyote ukionyesha mizizi kama visababishi na matawi kama matokeo. Midahalo Chagua mada husika, ikiwezekana mada ambayo inaubishani sana miongoni mwa vijana. Chagua Mwenyekiti wa Mdahalo. Waombe wasemaji wawili wakujitolea wanaounga mkono na wawili wanaopinga wape muda wa kuandaa hoja zao ili kila mmoja ahusike. Panga muda kwa kila kitu, yaani maandalizi, hotuba na maswali. 24

27 Wakati mwingine vijana hujitolea kwa ujasiri kutoa ushuhuda wa kweli kuhusu maisha yao kwa sababu ya kutokuwa na aibu. Kulikuwa na msichana mmoja ambaye alifanya ngono na rafiki yake wa kiume kwa sababu alipewa zawadi, kama ilivyo kwenye kadi. Baada ya hapo alipata mimba na yule mvulana akamuacha. Aliwaeleza wenzake katika kikundi kwamba wasidanganyike na vitu vidogo vidogo kama zawadi ambazo zinaweza kuharibu maisha yao milele. Nilifurahi sana niliposikia ushuhuda kama huu na vile vile nilipata cha kujifunza. Mwalimu wa Vijana Mchezo wa kuigiza na hadithi Mchezo wa kuigiza na hadithi vinaweza kuandaliwa na kila kikundi na baadaye kuwasilisha kwenye kikundi kikubwa. Wape mada au hali (kwa mfano mimba katika umri mdogo, au kupima VVU) bila kutoa maelezo zaidi. Kitakachofuata baada ya mchezo wa kuigiza na hadithi ni majadiliano Acha muda wa kutosha kwa kila mtu kuwasilisha. Tumia vipindi viwili lakini vilevile weka kikomo cha muda. Mara kwa mara toa muhtasari wa taarifa na stadi walizojifunza wakati wa kipindi. Kualika wazungumzaji Jaribu kutafuta na kualika wazungumzaji ambao wana huruma kwa vijana na wanafahamu haki zao. kikundi kiandae maswali kuhusu mada hiyo mapema. Utafiti Vijana hujiamini zaidi kuuliza maswali na kutumia huduma iwapo watapata nafasi ya kutembelea maeneo yanayotoa huduma hizo kama vile kliniki. Waalike watoa huduma walioko katika eneo lako na mashirika kuwa sehemu ya mpango wa Shangazi Stella, ili wawe wa msaada na kupewa taarifa. Wahimize washiriki kuwasiliana na mashirika na watu binafsi wanaofaa. Wanapotoa taarifa ya utafiti na Kazi Maalum, toa muda wa kutosha. 25

28 CHANGAMOTO KWA WAWEZESHAJI Wakati mwingine ilikuwa vigumu sana kujadili kadi zingine. Nilijisikia vibaya sana kwa sababu nilikuwa ninaona aibu. Kama ingelikuwa sio mwenzi wangu nadhani ningetoka nje ya kipindi. Vijana nje ya shule walikuwa huru sana kuzungumza na hata kutumia maneno ya kihuni. Hata hivyo nilifurahi kusikia uzoefu wao katika maisha. Mwelimishaji wa Vijana Itakuwaje iwapo washiriki wanaelezana taarifa zisizosahihi? Hii inaweza kutokea katika vikundi vidogo ambako husikilizi wanachojadili. Ili kukabili hili, majibu ya Shangazi Stella hutoa taarifa sahihi na katika vipindi vya mada na marudio unawaze kuchunguza watu wanavyofikiria na kushughulikia matatizo yoyote. Vile vile hakikisha unatofautisha kati ya mambo ya kweli na maoni. Unaweza kusahihisha mambo ya kweli kwa kutumia majaribio ya uongo/ kweli (mfano namna VVU inavyoambukiza) au kwa kutoa makala za kusoma na baadaye vikundi kutoa taarifa. Lakini kwa upande wa maoni (kwa mfano kama tunatakiwa kufuata utamaduni) hakuna jibu lililosahihi, maoni ya kila mtu ni sawa, hata ya kwako pia. Jambo la muhimu ni kuwatia moyo vijana wajadili mawazo yao. Iwapo utazungumza maoni yako, weka wazi kuwa hawalazimiki kukubaliana na wewe. Itakuwaje iwapo nitafikiria kuwa ni makosa kuzungumzia mada fulani, au mada hizo zinanifanya nijisikie aibu? Watu wengi hujisikia aibu kujadili masuala ya Ujinsia. Hata hivyo tunahitaji kujaribu. Mwanzoni huwa vigumu lakini baadaye huwa rahisi. Maisha ya vijana yatakuwa hatarini iwapo hatutawapatia taarifa na stadi ili kuishi kwa usalama zaidi. Wanahitaji nafasi ya kujadili masuala muhimu na wakati mwingine masuala ya siri, kwa hiyo kuwa muwazi kwa sababu unaweza kufanya hivyo, na watie moyo wanapoona aibu. Ukimya husababisha kutoelewana na chuki. Uwazi unaweza kuleta mabadiliko na matendo ya kujenga. Labda inaweza kusaidia watu wakifanya kazi wawili wawili, mwanaume na mwanamke. Mwanaume afanye na mvulana; na mwanamke afanye na msichana, lakini wawe wanakutana mara kwa mara na kubadilishana mawazo. Itakuwaje iwapo mimi au washiriki hawakubaliani na majibu ya Shangazi Stella? Ni sawa, kwa vile hakuna jibu sahihi au lisilosahihi. (isipokuwa katika mambo ambayo ni ya kweli). Mara nyingi Mambo ya kuyafanyia kazi huuliza kikundi kinayaonaje mawazo ya Shangazi Stella. Jambo la muhimu ni kuwa, washiriki wajifunze kupima mawazo tofauti na kufanya uamuzi wa busara. Usijaribu kuwalazimisha maoni yako. Itakuwaje iwapo mmoja wapo wa washiriki atafadhaika sana? Mada nyingi zinahusu wasiwasi katika maisha ya watu, kwa hiyo jambo hili ni la kawaida. Iwapo mtu mmoja amefadhaika sana, wewe au mmoja wapo wa marafiki zake anaweza kumchukua mahali pa faragha na kumsikiliza kama anataka kuzungumza au kuwa naye tu. Wasiliana na mnasihi iwapo utamuhitaji. Kabla hujaanza shughuli watafute wanasihi 26

29 Waelimishaji wetu wa vijana walipendezewa jinsi Shangazi Stella alivyomfanya kila mtu azungumze na kubishana lakini waliogopa kelele. Walikuwa shuleni na wakati mwingine walipata wasiwasi walimu wengine wangesema nini kwa vile hawakuwa wanafundisha Shangazi Stella kama masomo mengine ya kawaida. Waliona majadiliano yenye kelele na hoja zenye kuvutia kama tatizo na faida kwa wakati mmoja. Labda, ili kutatua tatizo hili ni kufanya vipindi mahali nje ya Shule. Mkufunzi Changamoto kubwa kwa wawezeshaji wetu ilikuwa kujifunza kuacha yapite kama yalivyo, kuwaamini vijana waliofanya kazi nao, kujua lini awe mtaalamu na lini aruhusu kila mtu kuwa na maoni yake. Ni vigumu kukubali kuwa hutakiwi kuwadhibiti kila wakati na kwamba unaweza kuwaacha peke yao hususani wakati kila mtu anafanya kazi katika vikundi vidogo na kushughulikia matatizo wakati wa kutoa muhtasari mwishoni. Mkufunzi wazuri waliopo katika jamii. Hawa ni watu waliopata mafunzo ya kufanya kazi na vijana. Wanasihi wazuri huwasaidia watu kufanya uamuzi wenyewe na sio kuwapa ushauri. Itakuwaje washiriki wakiwa wanabishana sana? Hili sio tatizo, kumbuka Shangazi Stella anataka kila mtu azungumze. Iwapo unafanya na kikundi kikubwa na kila mtu anataka kuzungumza kwa wakati mmoja, wagawe katika vikundi vidogo ili kutoa nafasi kwa kila mtu kusikika. Kila kikundi wapatie fimbo ya kuzungumzia yule aliye na fimbo ndiye anayeruhusiwa kuongea na inatakiwa izunguke kwenye kikundi ili kila mtu apate nafasi. Fanya hili kama mchezo na waombe viongozi wa vikundi kuhakikisha inafanya kazi. Weka kikomo cha muda na hakikisha wanafikia hitimisho kabla muda haujaisha. Iwapo kelele zinaleta usumbufu kwa wengine, vitoe vikundi nje. Inakuwaje iwapo washiriki hawataki kuzungumza? Hii inaweza kutokea katika vipindi vinavyohusisha kikundi kikubwa. Kwanza hakikisha kila mtu anaelewa kazi ya kufanya. Je maswali ni magumu sana? Yarahisishe au usiwape. Iwapo wanaona aibu, ruhusu wafanye majadiliano katika vikundi vidogo na marafiki zao au watu waliozoeana, wanaweza kuwa watu wawili au watatu. Baada ya hapo waulize iwapo kuna mtu anataka kushirikisha mawazo yake na kikundi kikubwa. Iwapo mada haipendelewi, usihofu, iache na endelea na ile inayofuata. Itakuwaje iwapo muda hautoshi kufanya shughuli zote zilizopangwa kwa ajili ya kipindi hicho? Jambo hili mara nyingi hutokea katika vipindi vinavyo husisha kikundi kikubwa. Hili sio tatizo, unatakiwa kuwa tayari kufanya mabadiliko kutegemeana na kile ambacho washiriki wanafurahia na wanajihusisha nacho. Yafuatayo ni baadhi ya mapendekezo: Tumia vipindi zaidi kufanya mada moja Anza na shughuli iliyo muhimu zaidi Weka kipindi kimoja hususan kwa ajili ya shughuli zinazohusiana na kadi au mada maalum. Panga vipindi vinavyochukua muda mrefu. Angalia kwanza washiriki wangependa kufanya nini. Badilisha njia za uwezeshaji unapofanya mada. kwa mfano unaweza kuanza na jaribio. Angalia maelezo ya utumiaji mzuri wa muda ukurasa wa 12 kwa ajili ya mawazo zaidi. 27

30 MAFUNZO NA MSAADA KWA WAWEZESHAJI Wakati mwingine wawezeshaji huamini semi potofu. Kuna usemi mmoja unaosema ukimkamulia mtoto maziwa ya mama kwenye via vya uzazi hatakuwa malaya (kufanya mapenzi /ngono na watu wengi). Watu wengi hujifunza hili kutoka kwa bibi na wanaamini hivyo. Tunahitaji kuangalia taarifa tunazitoa wapi na jinsi tutakavyo weza kutambua zipi ni za kwelina zipi sio za kweli. Mkufunzi Wapo watu ambao wanasoma sayansi ambao bado wanaamini kwamba shahawa zimejaa protini, na kwamba unapofanya ngono, mwanamke huipata mwilini kupitia ukeni. Kwa hiyo wanasema ndio maana mwanamke hunenepa baada ya ndoa na mwanaume hukonda kwa sababu hupoteza shahawa. Mkufunzi Iwapo una uzoefu katika mafunzo shirikishi na unajua kuhusu masuala kadhaa ya afya ya uzazi kwa vijana au unaweza kupata taarifa hizo, utakuwa na uwezo wa kutumia Shangazi Stella bila ya mafunzo na taarifa ya ziada. Wengine watafaidi kutokana na mafunzo ambayo yameandaliwa vizuri. Ufuatao ni mwongozo wa nini wanafunzi wanatakiwa kufanya katika vipindi Fanya kadi za Shangazi Stella za vipindi vyote na shughuli zote zilizo ainishwa kama mshiriki wa kawaida. Jadili taarifa zinazohusu mada kuu zinazoeleza ukweli wa mambo (Tunahitaji kuondoa semi potofu zilizopo kwenye jamii yetu). Pata uzoefu wa kuendesha vipindi kwa kutumia njia shirikishi za kujifunza, na chunguza na kujadili faida na hasara ya kutumia njia hii. Pata nafasi ya kufanya mazoezi ya kuendesha majadiliano mwenyewe au wawili wawili. Kila mshiriki apate muda wa kupewa maoni na kuelekezwa. Jadili umuhimu wa kuwa msiri na elewa kuwa washiriki wanatakiwa kukuamini. Usengenyaji unaweza kusababisha mpango wote kuwa hatarini. Jenga stadi za msingi za uongozi na unasihi na tambua kuwa mnasihi mzuri huwasaidia watu kuwa na uwezo wa kufanya maamuzi wenyewe kuliko kuwaeleza wafanye nini. Mfano wa ratiba za mafunzo ya siku mbili au nne imetolewa katika ukurasa unaofuata lakini kila ratiba itategemea mahitaji maalum, muda, na rasilimali iliyopo. Iwapo wawezeshaji hawana uzoefu katika masuala ya afya ya vijana inapendekezwa yafanyike mafunzo ya muda mrefu zaidi. 28

31 Mfano wa muhtasari wa ratiba ya mafunzo Mpango wa mafunzo ya siku mbili au nne SIKU YA 1 Kipindi cha 1: Utangulizi Shughuli za utambulisho, matarajio na hofu, na sheria za mafunzo (taratibu / kanuni za mafunzo) Kipindi cha 2: Uwezeshaji shirikishi ni nini? Washiriki kupata uzoefu wa maigizo dhina. Sifa za mwezeshaji mzuri, umuhimu wa uwezeshaji shirikishi wakati wa kushughulikia masuala ya jinsia na uhusiano kwa vijana. Kipindi cha 3: Shangazi Stella ni nini? Vikundi vidogo hutumia kadi kwa dakika 45-60, na baada ya hapo kuelezea kwenye kikundi kikubwa walichojifunza, walichokipenda ambacho hawakukipenda au walichokiona kigumu. Baada ya hapo muandaaji hutambulisha kifurushi kizima na mbinu za kufundishia na kujifunzia. Kipindi cha 4: Kupitia tena kifurushi Vikundi vidogo kupitia kifurushi chote; yaani kadi na kiongozi chake. Baada ya hapo wanachagua kadi mbili au tatu kutoka kwenye orodha, wakilenga kadi ambazo zinaelezea mada ambazo aidha hawazijui, wanawasiwasi kuhusu kuwepo kwenye kifurushi au wanapendelea kuzitumia. Vikundi wazifanyie kazi na baadaye watoe taarifa kuhusu uwezo wa kutumia Shangazi Stella katika mazingira yao ya kazi. SIKU YA 2-3: taarifa za kiufundi (hiari) SIKU YA 4 Kuhusu VVU, UKIMWI na Afya ya uzazi kwa vijana; matumizi ya huduma za Afya na Kijamii; Vijana kama watetezi wa mabadiliko kadi za Shangazi Stella zinazotumika wakati wa kukazia hoja. Kipindi cha 1: Marudio ya majadiliano ya siku zilizopita Kipindi cha 2: Wajibu wa Wawezeshaji Katika vipindi vinavyohusisha vikundi vidogo na kikundi kikubwa. Thamani ya vipindi vya marudio, jinsi ya kuviongoza na lini vifanyike. Kipindi cha 3: Mambo ya kujadili na kuyafanyia kazi Tofauti zake, shughuli zinazotolewa. Waliojitolea kuwasilisha na kujadili. Kipindi cha 4: Vipindi vya mada Jadili kuhusu mada na njia mbalimbali za kuzitumia. Washiriki wafanye katika vikundi vidogo kutayarisha muhtasari wa vipindi vya mada. Kipindi cha 5: Changamoto kwa Wawezeshaji (hiari) Marudio ya maelezo katika Kiongozi wa Wawezeshaji. Watu wa kujitolea waendeshe kipindi cha Shangazi Stella katika kikundi kikubwa, wakihusika watu wawili au watatu kuigiza changamoto chache (Kwa mfano, ubishi wa hali ya juu, kutoa taarifa zisizo sahihi). Kikundi kufanya marudio ya mbinu za uwezeshaji. Kipindi cha 6: Kupanga mipango Kipindi kuhusu matumizi ya Shangazi Stella katika kazi zao. Angalia tena matarajio na hofu. Fanya muhtasari na kuhitimisha. 29

32 VITABU REJEA Kinga Elimu ya Afya kwa Ajili ya Kujikinga na UKIMWI, Kiongozi cha Mwezeshaji; Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Tanzania (Kinapatikana pia kwa lugha ya Kiingereza). UKIMWI na Magojwa ya Ngono Mwongozo wa Uelimishaji Rika Shule za Msingi; Mkuki Publishers, Darasa la 5, 6 na 7. Towards responsible sexuality (2nd edition) M. Sawaya, Mture Publishers, Dar es Salaam, Maswali waliyouliza Vijana na Majibu yake (1 9);. Kitabu hiki kimetengeneza pamoja na Vijana Repro GTZ Vinapatikana : Repro-gtz P.O.Box Dar es Salaam, barua pepe (reprogtz@africaonline.co.tz) Ni vitabu vya uwazi vikielezea mada mbalimbali zinazovutia vijana. School health education for prevention of HIV/AIDS and sexually transmitted infections, A training manual (2nd edition) Tanzania Ministry of Education and Vocational Training, Dar es Salaam, 2004, ISBN Choices: A guide for young people Kimeandikwa na Gill Gordon na kinapatikana kutoka Teaching Aids kwa bei nafuu. ( Iwapo unaweza kupata kitabu kimoja tu, kitabu hiki kinapendwa sana na vijana kinaelezea masuala mengi ambayo ni nyeti katika mtindo hai na chanya. Ni rahisi kukisoma, kina vitendo vingi vya kufanya na kinavutia ABC of all the questions we never dare to ask Kimechapishwa na kwela Books, Afrika kusini ( na Weaver Press Zimbabwe ( Kimetolewa kama maswali kutoka kwa vijana, pamoja na majibu ya moja kwa moja. Ni rahisi kukisoma, ni halisi, kinavutia na kinazo taarifa nyingi zenye manufaa. Sex education, health and advice for South African youth Kimechapishwa na Sached Books P O Box 396 Cape Town 8000 South Africa Kitabu hiki ni kitabu kinachovutia na ambacho na kina taarifa nyingi. Ni rahisi kukisoma na kina hadithi na maoni kutoka kwa vijana. Zipo vile vile picha za katuni na za kawaida. You, your life your dreams a book for adolescents Kimeandikwa na Caroline Watson na Ellen Brazier na kuchapishwa na Family Care International (Kenya na Straight Talk Foundation (Uganda) Barua pepe fcipubs@familycareintl.org. Ni kitabu kikubwa ambacho kimejazwa taarifa za thamani kuhusu masuala yanayohusiana na ukuaji. 30 You asked we answered! Answers to questions on HIV and AIDS asked by youth in Southern Africa Kinapatikana kutoka SAFAIDS katika info@safaids.org. Ni vitabu vitatu vilivyo na maswali na majibu kuhusu vipengele tofauti vya VVU na UKIMWI. Stepping Stones ACTIONAID : A training Package on HIV/AIDS, Communication and Relationship Skills Alice Welbourn, G. and A. Williams, Inaelezea njia shirikishi za kuendeleza au kuibua mijadala Kutoka. Filamu na kanda Zawadi ni mkanda wa lugha ya Kiswahili ambao unaeleza juu ya athari za mimba kwa mtu binafsi, familia na jamii katika umri mdogo haswa wakati ukiwa shuleni. Filamu hii ina mada sita kila mada dakika 30, inaweza kutumika katika kuibua mijadala mingi inayohusiana na athari za mimba za utotoni, mitazamo ya jamii na jinsi mila zinavyoweza kuchangia katika kuendeleza athari hizi. Inapatikana Repro-gtz P.O.Box Dar es Salaam, barua pepe (repro-gtz@africaonline.co.tz) Rama ni filamu ya saa moja na nusu ni mwendelezo ya filamu ya Zawadi. Inaonyesha zaidi mazingira hatarishi, nguvu za msukumo wa rika pamoja na athari za matumizi ya dawa za kulevya.inapatikana Repro-gtz P.O.Box Dar es Salaam, barua pepe (repro-gtz@africaonline.co.tz) Magonjwa ya zinaa na UKIMWI. Filamu ya dakika 30 ambayo inaonyesha bayana Magonjwa ya Zinaa, athari zake pamoja na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI pamoja na UKIMWI. Mkanda huu hupatikana katika ofisi za Waratibu Wa UKIMWI katika ngazi za Wilaya na Mkoani. Sogea Karibu na Mwongozo wake. Ina vipengele 6 ambavyo vinagusa ukuaji, uhusiano, mazingira hatarishi na stadi za maisha. Inapatikana Ubora wa Afya kwa Familia Duniani. S. L.P Dar es Salaam. Barua Pepe: (orawaafya@cats-net.com). (Pia kinapatikana pia kwa lugha ya Kiingereza na Kifaransa) Kimeandikwa na Alice Welbourn na kinapatikana TALK ( ) hiki ni kitabu kizuri sana cha mwongozo wa kufundishia kuhusu VVU na UKIMWI, stadi za mawasilano na uhusiano kwa wanawake na wanaume wa umri wowote. Usisahau! Katika kila nchi kuna mashirika ambayo yanaweza kutoa taarifa ya ziada kuhusu mada maalum kuhusiana na ujinsia, maisha na uhusiano wa vijana balehe.

33 SEHEMU YA PILI Utumiaji wa Shangazi Stella

34 MATUMIZI SHANGAZI STELLA TAARIFA MUHIMU KUHUSU HAKI MILIKI TARSC Zimbabwe wanayo haki miliki ya Shangazi Stella lakini tunaruhusu matumizi na marekebisho ya Shangazi Stella katika mradi wowote ambao sio wa biashara ambao madhumuni yake ni kuboresha afya ya uzazi ya watu. Hata hivyo tunaomba utaratibu ufuatao utumike. Wasiliana nasi kuhusu mradi wenu, tunaweza kusaidia Toa shukurani kwa ajili ya uandishi na haki miliki ya TARSC na Barbara Kaim na weka majina yetu, anwani na nembo mbele ya makala Tutumie nakala ya toleo lililorekebishwa. Endelea kutupatia taarifa kuhusu mradi wenu na maoni mtakayoyapata Kwa kufanya hivi wote tutapata faida kutokana na uzoefu. Kurekebisha Shangazi Stella maana yake ni kuibadili ili iendane na watu watakaoitumia, hali zao na mahitaji yao maalum. Kwa kweli, muundo, shughuli na mbinu za kujifunza na kufundishia zinaweza kubadilishwa na mtumiaji anaweza kurekebisha kifurushi moja kwa moja huku wakiendelea kutumia. Toleo hili la Shangazi Stella katika lugha ya Kiswahili kwa ajili ya matumizi katika nchi za Afrika Mashariki ni mfano halisi wa jinsi Shangazi Stella kinavyoweza kurekebishwa rasmi ili kionekane kinafaa kwa wahusika na katika maudhui. Marekebisho yoyote utakayochagua kufanya, kuna mambo mawili ambayo ni muhimu Hakikisha kuwa vijana na wawakilishi wa vikundi lengwa wanahusika katika kila hatua, na Hakikisha kuwa yeyote atakayehusika katika kufanya mabadiliko awe ameshiriki katika vipindi vya Shangazi Stella. Zipo aina mbalimbali za kufanya marekebisho. Baadhi zimeorodheshwa hapa chini: Kutafsiri Ili kutafsiri, ni vema kufanya katika timu ambayo itawahusisha vijana na waandishi mashuhuri waliopo. Katika kutafsiri unaweza kufanikisha kuondoa utamaduni ambao haukubaliki katika mazingira ya nchi. Kurekebisha utamaduni Shangazi Stella imeandaliwa katika mazingira ya tamaduni za Kishona na Kindebele nchini Zimbabwe. Katika toleo hili la Kiswahili majina ya wahusika yamebadilishwa. Vilevile kuna mabadiliko kidogo katika maudhui kulingana na hali halisi ya nchi za Afrika Mashariki. Watu wa dini mbalimbali na sehemu za mjini wana mahitaji tofauti. Kadi ya 27 Mpenzi wangu anatarajia kuolewa inaibua suala la kupangiwa mtu wa kuolewa naye, wakati mahari imelipwa na mchumba na familia yake. Katika mila na desturi zingine familia ya msichana ndio wanaotoa mahari. Kwa hiyo katika hali kama hii kadi mpya inaweza kuhitajika kuelezea tatizo tofauti linalojitokeza. Kurekebisha mada na masuala mengine Mada na masuala utakayoyashughulikia yatatofautiana. Kwa sababu ya hali halisi ya maambukizo ya Virusi vya UKIMWI katika nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika, Shangazi Stella kinalenga zaidi katika masuala yanayohusu Virusi vya UKIMWI 32

35 na UKIMWI. Katika jamii nyingine masuala mengine yanaweza kuwa na umuhimu zaidi. Kurekebisha kwa ajili ya kundi maalum la watu Unaweza kutumia Shangazi Stella na watu wenye umri mbalimbali, uzoefu, hofu na elimu. Hata vijana walio shuleni na wale walio nje ya shule ni tofauti. Mambo yote haya huathiri uhusiano wa kadi na jinsi ya kuzitumia. Mpango wa Shangazi Stella unaweza vilevile kurekebishwa kwa ajili ya wazazi, wafanya biashara ya ngono, wahudumu wa afya na wengine. Kurekebisha unapokuwa na muda mfupi Unaweza kuwa na kikundi kinachotaka kufanya kazi na Shangazi Stella lakini wana muda wa kufanya vipindi vichache. Itabidi wewe na kikundi mchague masuala muhimu au mada za kujadili. Angalia Shangazi Stella katika saa 6 hapo chini kama mfano mmoja. Kurekebisha kwa sababu ya matatizo mengine Unaweza kuwa unafanya kazi katika mazingira magumu yanayotokana na watu wengine. Usiruhusu matatizo yatakayotokana na kadi chache yatishie matumizi ya mpango nzima. Chagua kadi zinazohusika na zingine zote ziache. Shangazi Stella katika saa 6 Mradi wa afya ya uzazi kwa vijana, Regai Dzive Shiri, ambao upo manicaland, Zimbambwe ulitengeneza programu fupi ya Shangazi Stella kwa ajili ya wazazi. Programu ilikuwa ya vipindi viwili, kila kipindi kilichukua saa tatu, kipindi cha kwanza kilianza kwa shughuli za utambulisho, matarajio na hofu, na sheria za mafunzo. Baada ya hapo kadi na mada zilichaguliwa. Kipindi cha pili kiliishia na muhtasari wa yale waliyofanikisha, mpango wa kazi kwa ajili ya wakati ujao, na tathmini ya mikutano. Walichagua mada na kadi maalum zinazohusiana na wazazi wa vijana balehe na kuruhusu muda wa saa moja kwa ajili ya kuwasilisha kila mada. Mada zilizochaguliwa ni pamoja na: Ujana balehe kadi ya 17 na 30 Mawasiliano kadi ya 9 na 23 Magonjwa ya ngono kadi ya 7, 12, na 24 Uhusiano wa kijinsia na udhalilishaji wa watu wazima kadi ya 15 Uhusiano wa kijinsia na shinikizo rika kadi ya 1 33

36 KANUNI ZA MSINGI KATIKA KUANDIKA BARUA MPYA NA MAJIBU Tulisoma ile kadi ambayo kijana wa kiume anaeleza kuwa hawezi kuzungumza na wazazi wake ambao ni wagumu kumwelewa. Ninatamani ningesoma kadi hiyo wiki iliyopita. Nilikuwa nimeweka akiba ya pesa na nikazitumia kununua mashati ya shule ya kijana wangu. Nilifurahi sana nilipo yanunua, lakini alipoyaona, alinuna na kunisemesha kwa ukali, Kwa nini umenunua mashati? Kaptura zangu zote zimechanika na hazifai. Sasa nimesoma kadi, nimegundua kwamba nilitakiwa kuzungumza naye kabla ya kununua. Nilitakiwa nimwambie, Mwanangu ninazo pesa hizi, unahitaji sare ipi ya shule? Sasa ninajua, ni lazima niwasikilize watoto wangu na nizungumze nao na kufanya mambo kwa pamoja. Mama Lengo kuu Lengo lako kuu ni kuwatia moyo na kuwapa nguvu vijana na washiriki wengine. Kadi utakazo ziandika zinatakiwa ziwasaidie kujenga stadi zao za maisha, kutumia wanachokifahamu na kusaidiana katika kujikinga wenyewe na wale wanaowapenda. Lengo lingine ni kuwatia moyo wawasiliane na mashirika yanayotoa msaada na kutoa changamoto ya kipengele chochote ambacho kinaweza kuathiri jamii na utamaduni. Kanunu za msingi Zifuatazo ni kanuni za msingi ambazo unaweza kuzitumia wakati wa kurekebisha Shangazi Stella. Wahusishe vijana katika kurekebisha kadi. Wanaweza kuhusika katika kutoa hadithi halisi, kuchangia mawazo kuhusu majibu ya Shangazi Stella na kuzifanyia majaribio kadi kabla hazijaanza kutumika. Husisha mashirika mengine na viongozi wa jamiii katika utafiti na majaribio ya kadi Kuwa wazi kuhusu unachotaka kadi ifanikishe Lugha iwe rahisi na maelekezo yaeleweke vizuri na sauti isiyo rasmi Hakikisha hadithi ni halisi Kuwa mkweli, toa taarifa sahihi na sahihisha semi potofu na yale yanayoeleweka vibaya. Waongezee stadi zao za kufikia huduma, kuwasiliana, kupanga na kuweka mikakati. Wape vijana nafasi ya kutathmini hatari na kupima mema na mabaya ya mambo tofauti yanayotokana na utendaji, usihubiri kuhusu mambo wanayotakiwa kufanya. Watie moyo vijana wajiamini na kwamba wana uwezo wa kubadilika na kuweka malengo ya mahitaji yao katika maisha Watie moyo wafanye yale yanayoboresha afya ya jinsi na uhusiano Sifia tabia nzuri za kiafya Wasaidie waelewe yale ambayo wanaweza kubadili wenyewe na pale wanapohitaji msaada au kuwa sehemu ya watetezi wa mabadiliko. Waelimishe kuhusu unyanyapaa na ubaguzi dhidi ya wasichana, watu wanaoishi na VVU au UKIMWi, mashoga wasagaji na watu kutoka tamaduni zingine. 34

37 KUWAHUSISHA VIJANA KATIKA KUANDIKA KADI MPYA Unapokuwa tayari una mpango wa kurekebisha tayari unakuwa na mawazo kuhusu masuala yanayowaathiri vijana unaofanya nao kazi. Yachunguze mawazo yao kwa kutumia njia zifuatazo. Tumia kipindi kilichoelezwa kwenye ukurasa wa 16 ambapo washiriki wanaandika barua zao kwa Shangazi Stella. Kabla ya kuanza, waeleze kuwa barua zao zinawezakuonyesha wasiwasi na hofu zao pamoja na ndugu na marafiki. Baada ya hapo waombe kuwa barua zao utazitunza na hakikisha unatoa sababu ya kufanya hivyo. Waeleze kuwa barua zao hazina majina, kwa hiyo hatajulikana nani ameandika. Barua zitawasaidia vijana wenzao watakaokuwa katika hali zinazofanana na hizo. Fanya utafiti kwa vijana ambao ni walengwa. Utafiti wa mwanzo wa Shangazi Stella uliwahusisha wanafunzi walioko shuleni na wale walio nje ya shule nchini Zimbabwe. Tulitumia majadiliano na shughuli shirikishi nyingine kuchunguza mada mbalimbali zinazohusiana na maisha na hofu zao. Tumia mchakato huu kufafanua mausala maalumu ambayo yanawaathiri vijana na kutayarisha hadithi unazoweza kutumia katika barua. Waombe kikundi cha vijana kufanya majaribio ya kadi kabla ya kuanza kutumika kwa vijana wengine ili uweze kupata mawazo yao kuhusu lugha, uhalisi, uhusiano na moyo wa kupenda. Hatua hii ni muhimu sana. 35

38 KUTOA MAJIBU MAZURI ZAIDI Pata ushauri wa vijana Fikiria Shangazi Stella Tumia taarifa mpya Epuka kutoa hukumu Tia moyo wafanye vitendo Pata ushauri wa vijana kuhusu majibu ya Shangazi Stella. Tumia vipindi ambavyo majibu yanatolewa na watu wawili wawili kama ilivyoelezwa ukurasa wa 16, kwa kutumia barua zao wenyewe waombe tena ubaki na majibu waliyoyatoa. Katika kujibu maswali ni muhimu kumfikiria Shangazi Stella. Wakati wote Shangazi Stella yuko upande wa vijana wanaomwandikia. Halaumu vijana hata siku moja. Hutaka watafute wenyewe jinsi ya kufuata njia ambayo ni nzuri kwao. Ana huruma, hutia moyo, muwazi na hatoi hukumu, hutoa nafasi ya kuchagua na sio maelekezo. Anafahamu haki za vijana; yale yote waliyo na haki nayo, hata katika mazingira magumu. Huwaona kama watu binafsi na ni sehemu ya jamii inayoathiri maisha yao na ambayo wao wanaweza kusababisha mabadiliko. Tumia taarifa mpya kutoka kwa Wataalam, lakini rahisisha lugha. Epuka maneno ya kidaktari na mengine ya kitaalam, inapobidi eleza wazi yana maanisha nini. Wataalamu wanajua kila kitu kuhusu somo, washiriki wanahitaji mambo ya msingi tu. Mambo ya kuyafanyia kazi huongoza washiriki kupata taarifa za ziada. Vilevile unaweza kumwalika Mtaalamu kujibu maswali yao. Toa taarifa za kutosha lakini epuka kutoa mhadhara na hukumu. Kwa mfano, usiwaambie acha ngono, badala yake wape stadi za kuamua wenyewe. Wape mapendekezo chanya ya kuepuka kuliko vitendo hasi. Usitumie maneno kama lazima, unatakiwa ku Badala yake, sema ni muhimu ku. Au unahitaji ku Sisitiza matendo ya pamoja na ya mtu binafsi. Watie moyo vijana wajione kama sehemu ya jamii, kuwasiliana na vikundi vingine vya vijana na wengine wote wanaojishughulisha na huduma ya afya na kuona kwamba ni mambo gani ambayo wanaweza kufanya pamoja. Jibu swali Hakikisha unatoa majibu ya maswali katika barua. Watumiaji wanaposoma hadithi, husubiri kuelezwa majibu. Lakini vilevile shughulikia maswali yaliyoko kwenye Mambo ya kujadiliana. Mwanzoni kabisa hakikisha ujumbe umewafikia vizuri. Kwa mfano, watu wasifanye ngono iwapo hawataki au mnaweza kushirikiana kwa ajili ya mabadiliko. Usiegemee upande mmoja kuhusu utamaduni Watie moyo vijana kufanya tathmini ya tamaduni na mila. Epuka kuunga mkono au kushambulia vitendo ambavyo ni vya hatari. Ruhusa waamue wenyewe lililo zuri (na jinsi ya kulitunza) na lililobaya (na jinsi ya kulibadilisha) 36

39 MAMBO YA KUJADILIANA NA MAMBO YA KUYAFANYIA KAZI Tofauti yake ni nini? Mambo ya kujadiliana hutia moyo vijana kuijadili barua na masuala yanayohusika, kufikiria jinsi yanavyohusishwa na maisha yao na jamii, na kutathimini hatari wanazozifanya. Mambo ya kuyafanyia kazi huwasaidia washiriki kuunganisha hadithi iliyoko kwenye kadi na maisha yao halisi, ambako wanafanya kwa vitendo yale waliyoyajadili katika kikundi au binafsi. Vidokezo katika ukurasa wa vitakupa mawazo ya ziada. Maelekezo kwa ajili ya Mambo ya Kujadiliana na Kuyafanyia kazi Tumia maswali ambayo yanaruhusu mtu kujieleza na sio yale yanayoruhusu majibu ya ndio/hapana: Kwa mfano, una matatizo gani na wazazi wako? Usiseme Je una matatizo na wazazi wako? Yafanye masuala kuwa binafsi kwa kuuliza maswali kuhusu washiriki, rafiki zao na jamii yao kama ifuatavyo: Je, mambo haya hutokea mara nyingi katika eneo lenu? Kwa nini? Je, wewe au vijana unaowafahamu. Utajisikiaje ukiwa katika hali hiyo? Jambo gani baya lingetokea iwapo unge Lakini epuka maswali yoyote ambayo yanaweza kuwa binafsi zaidi, kufanya washiriki wajisikie vibaya au kuruhusu mtu yeyote kutambua watu binafsi wanaohusika. Ongezea maswali ambayo yanawatia moyo washiriki kutathmini matendo yao na ya jamii, huduma na mashirika yaliyopo, kuona nini hukidhi mahitaji yao na kitu gani kinaweza kuboreshwa. Kwa mfano upatikanaji wa taarifa za afya au kondomu (kadi ya 24) mtazamo wa wafanyakazi wa kliniki kwa vijana (kadi ya 12) Watie moyo kufanya tathmini ya taarifa na maadili gani waliyoyapata yanafaa na ni yapi hayafai. Kwa mfano kutathimini taarifa kuhusu ujana balehe na ujinsia (kadi ya 1 na 20) vitendo vya kiutamaduni na kuwaheshimu wazee (kadi ya 3). Wakati wa kutafuta utatuzi, wahimize kuchanganua mambo ambayo yanawezekana na kinachoweza kuzuia lisitokee au kufanya iwe rahisi. Watie moyo wafikie mabadiliko na kufikiri kwa kukosoa. Kwa mfano, kulinganisha jamii yao na dunia kamilifu ambayo hakuna ubakaji kabisa (kadi ya 15). Kupigana na unyanyapaa dhidi ya watu wanaishi na VVU (kadi ya 36) mtizamo kwa wanaouza ngono (kadi ya 16) kutengeneza mpango wa kazi kwa ajili ya mabadiliko (kadi ya 28 na 33) Tia moyo kufikiri kwa pamoja jinsi wanavyoweza kusaidiana na kuwasaidia wengine. Wasisitizie kutafuta mashirika ambayo wanaweza kufanya kazi pamoja ili kufanikisha maisha bora kwa vijana. 37

40 SHUKURANI Shukurani nyingi ziwafikie kila mtu binafsi na mashirika kutoka eneo lote la nchi na wa kimataifa ambao walishiriki katika kutengeneza toleo hili la Shangazi Stela, iwe katika utafiti, uandishi, warsha, taarifa, uchoraji, mashairi, majaribio ya mwanzo, mapitio ya kiufundi, mawazo, fedha na kuungwa mkono kwa hali. Kipekee tunapenda kuwashukuru wafanyakazi wa Kituo cha Mafunzo na Utafiti (TARSC) Zimbabwe na Kikundi cha Jamii cha Kazi juu ya Afya ( CWGH ) ambao bila wao utengenezaji wa makala hii usingewezekana. Tunawashukuru wote. Kimebuniwa na kutungwa na Waandishi Washauri wa Kiufundi Utafiti na kukijaribisha Mahariri, Usanifu na upangaji Vielelezo Barbara Kaim Barbara Kaim na Jane Nineham Dr Susan Laver, Dr.Rene Loewenson and Lois Lunga Caroline Mubaira Margo Bedingfield Anxious Katuruza na Mashet Ndlovu Utafiti na Majaribio ya mwanzo Vijana na Wawezeshaji kutoka mashirika yafuatayo walishiriki katika utafiti na majaribio ya Shangazi Stella Zimbabwe Malawi Africa Community Publishing and Development Trust, Matopos; Batsirai Group, Chinhoyi; Community working group on Health, Arcturus; Student Partnership Worldwide, Mutare; Youth for a Child in Christ, Bulawayo; ZimPATH/Belvedere Technical Teachers College, Harare; Youth Net and Counselling (YONECO); Zomba South Africa Ukukhula Projects, Kwa Zulu Natal and Mpumalanga Tanzania Zambia GTZ Tanzania, Student Partnership Worldwide Tanzania; Chezasalama, Dar es Salaam Family Health Trust, Lusaka Tafsiri ya Kiswahili Tafsiri hii ya Shanagazi Stella kwa lugha ya Kiswahili na toleo lake imetokana na jitihada za watu na taasisi tofauti hapa Tanzania. Tungependa kutoa shukrani za pekee kwa Mradi wa Afya wa ushirikiano wa Tanzania na Ujerumani (TGPSH), Shirika la Maendeleo ya Kiufundi la Kijerumani Tanzania (GTZ-Tanzania) na Kituo cha Mafunzo na Utafiti (TARSC)- Tanzania ambao wote walionyesha umakini na kujitolea ili kukamilisha makala hii ya Shangazi Stella kwa wazungumzaji wa lugha ya Kiswahili Africa ya Mashariki. Shukrani za pekee kwa: Walioratibu utayarishaji wa makala hii : Helen Prytherch, Akwillina Mlay wote wa TGPSH Tafsiri : Mrs Margaret Kilembe Uhakiki : Mr. Benedict Raymond Mangulu kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwajuma Masaigana wa TARSC- Tanzania, Irenei Kiria wa Youth Action Volunteers Upangaji na Ubunifu : Margo Bedingfield Wachoraji: Anxious Katuruza, Mashet Ndhlovu na David Chikoko Mrs Dorothea Coppard kutoka Mradi wa kuzuai na kuongeza ufahamu juu ya Maambukizo ya UKIMWI katika shule za sekondari (PASHA), Taasisi ya Uswisi ya nchi za Joto (STI). Agnes Kabigi kutoka Mradi ya Habari wa Afya na Mawasiliano wa Africa ya Mashariki (HIP) kwa kuunganisha makala ya Shangazi Stella katika mtandao wa Pia tunawashukuru wale wote ambao kwa namna moja au nyingine walishiriki lakini hatukuwataja. Our deepest thanks go to every individual and organisation from around the region and internationally who 38

41 ACKNOWLEDGEMENTS participated in the production of this version of Auntie Stella, whether in the form of research, writing, workshops, information, artwork, poetry, pilot testing, technical reviews, ideas, finances and moral support. In particular we would like to acknowledge the consistent and long-term institutional contributions of personnel at TARSC and CWGH, without whom the production of this material would not have been possible. We are grateful to you all. Created and developed by: Writers: Technical advisor: Research and pretesting: Editor, design and layout: Illustrators: Barbara Kaim Barbara Kaim and Jane Nineham Dr. Susan Laver Caroline Mubaira Margo Bedingfield Anxious Katuruza and Mashet Ndhlovu Research and Pretesting Youth and facilitators from the following organisations participated in the research and pretesting of Auntie Stella: Zimbabwe Malawi Africa Community Publishing and Development Trust, Matopos; Batsirai Group, Chinhoyi; Community Working Group on Health, Arcturus; Gays and Lesbians of Zimbabwe, Harare; Student Partnership Worldwide, Mutare; Youth for a Child in Christ, Bulawayo; The Centre, Harare; ZimPATH/Belvedere Technical Teachers College, Harare Youth Net and Counselling (YONECO), Zomba South Africa Ukukhula Projects, Kwa Zulu Natal and Mpumalanga Tanzania Zambia GTZ Tanzania/Chezasalama, Dar es Salaam Family Health Trust, Lusaka Kiswahili version The translation and production of this Kiswahili version of Auntie Stella was also a collective effort, involving many people and organisations in Tanzania. In particular, we would like to thank the Tanzania German Programme to Support Health, GTZ-Tanzania and TARSC-Tanzania all of whom showed steadfast commitment to making this version of Auntie Stella available to Kiswahili speakers in the east African region. In particular, we would like to thank: Coordinators of the Kiswahili version: Helen Prytherch, Akwilina Mlay and Joseph Matimbwi (TGPSH) Translator: Mrs Margaret Kilembe Reviewers: Mr M. Mwinyi of the National Kiswahili Council; Mr Benedict Raymond Mangulu from the Ministry of Education and Vocational Training; Mwajuma Masaigana of TARSC-Tanzania; Mr Irenei Kiria, Mr J. Kasenene: Youth Action Volunteers Design and layout: Margo Bedingfield Illustrators: Anxious Katuruza, Mashet Ndhlovu and D.Chikoko Mrs Dorothea Coppard from the Prevention and Awareneness of HIV/AIDS in Secondary Schools (PASHA) project, Swiss Tropical Institute Agnes Kabigi from the Health Information Project of the East African Development Communication Foundation for linking the web versions of Auntie Stella with And to all those who we may have inadvertently overlooked but to whom we are equally grateful. 39

42 TAFADHALI WASILIANA NASI Tafadhali wasiliana na sisi. Tunakaribisha maoni yoyote na maoni ambayo mnayo kuhusu kadi na kufurushi cha Shangazi Stella. Tunataka kusikia: Jinsi unavyoifanyia kazi. Jinsi vijana wanavyoitikia. Njia ulizotumia kurekebisha. Mambo unayoyapenda na usiyoyapenda. Jinsi tunavyoweza kuziboresha na ziwe za maana kwenu. Tumia anwani ifuatayo Auntie Stella Training and Research Support Centre (TARSC) P.O. Box CY 2720, Causeway, Harare, Zimbabwe Simu: Fax: Barua pepe: Tovuti:

43

44 Shangazi Stella Vijana wanazungumza maisha na uhusiano kuhusu ujinsia, Shangazi Stella:Vijana wanazungumza kuhusu ujinsia, maisha na uhusiano ni paketi ya utendaji ambayo imeandaliwa hususani kwa vijana wa shule na wale nje ya shule wenye miaka Kufuatia mtiririko wa barua 40 ambazo ziliandikwa kwa shangazi mwelewa vijana, vijana wanazungumzia mambo mengi ya kibinafsi na ya kijamii ambayo yanaathiri afya yao ya uzazi na uhusiano. Kila barua imeambatana na majibu na mambo mbalimbali ya kufanyia kazi kwa vikundi kutoka kwa shangazi Stella kuhusiana na mada husika ya maisha ya vijana. Pia kuna mwongozo ambao unawawezesha walimu na wawezeshaji. Mada zinazoongelewa ni: mabadiliko ya kimwili na hisia kwa vijana balehe, uhusiano na wazazi, vijana na jamii, shinikizo la kijamii na kiuchumi katika kufanya ngono, majukumu ya kijinsia, mimba zisizotarajiwa na magonjwa ya ngono, pamoja na mambo mbalimbali kuhusiana na VVU na UKIMWI. Shangazi Stella inavunja ukimya ambao umekuwa ukizizunguka mada za ujinsia na nyingine zinazofanana na hizo. Kupitia ukweli huu, vijana wanahamasika kikamilifu katika maamuzi ya maisha yao, wanashiriki katika jamii na wanafanya maamuzi sahihi kwa maisha yao ya baadae. Paketi hii ni tafsiri ya kiswahili ambayo imetokana na paketi ya Shangazi Stella ya lugha ya kingereza. Training and Research Support Centre Zimbabwe VIJANA WANAZUNGUMZA KUHUSU NGONO, MAISHA NA UHUSIANO Wakisaidiana na

45 MANENO HAYA YANA MAANA GANI? UKIMWI: Mgungo: Uraibu: Uraghibishi: ARVs: Ujasiri: Saratani: Seviksi: Uhimili: Msongo wa mawazo: Umwagaji: Udisaji: Ni kifupi cha Upungufu wa KInga MWIlini hali au hatua ambayo VVU hushambulia na kudhoofisha kinga ya mwili hivyo kuruhusu magonjwa mbalimbali kumshambulia mtu bila kikwazo chochote. Kuacha kabisa kufanya ngono,uamuzi wa hiari wa kutojihusisha na uhusiano wa kimapenzi wa aina yoyote, dawa za kulevya au kunywa pombe. Hali ya kuzoea ama kutawaliwa au kutegemea dawa za kulevya au pombe. Yaani huwezi kuishi bila ya kutumia Utetezi au Vitendo vya mtu binafsi au kikundi vilivyokusudia kuleta mabadiliko katika sera, mtizamo na matendo. Kifupi cha maneno Anti retrovirals. Dawa za kupunguza makali ya Virusi Vya UKIMWI na kwamba dawa hizi haziponyi. Zinatakiwa zitumike baada ya kufanyiwa vipimo na kupata ushauri kutoka kwa mtaalamu. Ujasiri, mtu kuwa na uwezo wa kutetea haki na imani yake. Ni ugonjwa unaobadili seli za mwili na kusababisha uvimbe. Saratani inaweza kuathiri matiti ya wanawake, shingo ya kizazi, tumbo au sehemu yoyote za mwili. Shingo ya kizazi / Sehemu ya ndani ya uke ambayo inatenganisha mfuko wa uzazi na uke. Ni wakati yai linaporutubishwa na mbegu ya kiume, na mwanamke kuwa mjamzito (Mimba) Hali ya kujisikia umenyong onyea, huzuni na kukosa raha kabisa. Wakati mwingine hata hamu ya kula hupotea Kukojoa manii yaani shahawa zenye mchanganyiko wa mbegu za kiume. Uume unapodinda- Mwanamume anapokuwa na ashiki, Uume husimama na kuwa mgumu Ngono na ya jinsia tofauti (heterosexual): Mahusiano ya kingono / kimapenzi kati ya jinsia tofauti yaani mwanamume na mwanamke. VVU: Wasenge: Wasagaji: Homoni: Uambukizo: Kujamiiana: Mahari/ Posa: Bangi: Punyeto: Hedhi: Ni kifupi cha Virusi Vya UKIMWI; Vimelea tegemezi vinavyo shambulia kinga ya mwili. Hawa ni wanaume au ambao hupenda kufanya ngono na wanaume wenzao jinsi moja. Ni wanawake wenye tabia ya kufanya ngono na wapenzi wa jinsi moja Ni vichocheo vilivyomo mwilini ambavyo hudhibiti mwili katika ukuaji. Hali ya kuingiliwa na vijidudu kama vile bakteria / virusi n.k vinavyosababisha maradhi mwilini. kufanya ngono au kufanya mapenzi. Pesa / ng ombe au mali yoyote ambazo hutolewa mwanaume kwa familia ya mwanamke kwa ajili ya kuoa Hii ni aina ya majani ambayo yakitumika hulevya. Ni kosa la jinai kutumia hapa Tanzania. Maneno mengine ni kama ganja, widi. Tendo la kujichua sehemu za via vya uzazi kwa ajili ya kujiridhisha mwenyewe kimapenzi. Kutokwa damu kwa mwanamke. Wengine husema kuingia mwezini, na wengine kuwa katika siku zao. Mzunguko wa hedhi: Ni kipindi kati ya hedhi moja na nyingine, mzunguko wa kwaida ni siku 28

46 MANENO HAYA YANA MAANA GANI? Njia ya dharura ya kuzuia mimba: Mchanganyiko wa vidonge vya uzazi wa mpango ambavyo vinaweza kuzuia mimba iwapo vitatumika ndani ya saa 72, baada ya kufanyika ngono isiyo salama. Ugonjwa nyemelezi /dandiaji: Ni ugonjwa ambayo Unahusishwa na UKIMWI kama TB, nimonia na vidonda mdomoni. Maambukizi haya yanaweza kuzuilika au kutibika. Kufikia kilele /Mshindo: mwili hufikia kiwango cha juu cha kuburudika kimapenzi wakati wa tendo la ngono Kokwa za mayai / Ovari: Vifuko viwili vilivyoko kila upande wa tumbo la uzazi la mwanamke. Kazi ya ovari ni kuhifadhi na kutunza mayai ambayo yakikutana na mbegu za kiume hutengeneza mtoto. Kupevuka: Mpako Papaniko: Uume: Kipindi yai linapokomaa na kutoka nje ya ovari. Kitendo hiki hutokea katikati ya mzunguko wa hedhi. Hiki ni kipindi ambacho mwanamke anaweza kupata ujauzito kwa urahisi Kipimo kinachotumika kuangalia dalili za mwanzo za saratani ya shingo ya kizazi. Kisehemu cha ngozi ya shingo ya kizazi hutolewa na kupimwa, kuangalia kuwepo kwa saratani. Sehemu mojawapo ya Via vya uzazi vya mwanamume Hadhari baada ya Hatari(PEP Post-Exposure Prophylaxis): Tiba ambayo hutolewa kwa mtu mara baada ya kugundulika kwamba anaweza kuwa amepata maambukizo ili kuzuia asipate maradhi baadae. Kama mtu yuko hatarini kupata VVU, tiba inatakiwa kuanza ndani ya masaa 72 baada kitendo. Tiba hii hutumika kwa mfano, kama ubakaji umetokea. Ufuska: Kahaba / Malaya: PMTCT: Mtu ambaye anafanya ngono na watu wengi, kwa kupenda mwenyewe. Mtu ambaye anafanya biashara ya ngono Mpango wa kuzuia mambukizo ya VIRUSI VYA UKIMWI kwenda kwa motto, wakati wa ujauzito,kujufungua na wakati wa kunyonyesha kwa kutumia dawa maalum. Mpango huu pia unamhusisha baba wa mtoto Ubalehe / Kuvunja ungo: kipindi cha mabadiliko kutoka utoto kwenda utu uzima Ubakaji: Ngono salama: Ngono salama zaidi: Kujiamini: Shahawa: Ni tendo la kumkamata, kutumia nguvu, cheo au mamlaka na kuzini na mtu bila bila ridhaa yake. Ngono ya kuaminiana wapenzi wawili ambao hawana maambukizo Kuzuia kupata magonjwa ya ngono na mimba kwa kutumia kondomu. Kujiamini katika utu wako, maadili na uwezo. Majimaji ambayo mwanamume hukojoa baada ya kufikia mshindo yanayochanganyika na mbegu za kiume. Udhalilishaji wa kijinsia: Mwanamume au mwanamke anapotumia nguvu ya aina yeyote kufanya ngono au kujiridhisha kimapenzi bila ya ridhaa ya mwenzake Shambulio la aibu: Ubakaji: Shambulio la aibu: Mwanamume au mwanamke anapomshika mtu kimapenzi bila ya ridhaa yake. Ni tendo la kumkamata, kutumia nguvu, cheo au mamlaka na kuzini na mtu bila bila ridhaa yake. Magonjwa ya Zinaa (STIs): Maambukizo ya magonjwa yatokanayo na tendo la ngono Uke: Via vya uzazi vya mwanamke Upimaji wa virusi vya UKIMWI: Upimaji VVU kwa hiari Bikira: Ndoto nyevu: Uterasi: Mwanamke au mwanamume ambaye hajawahi kufanya ngono Dalili za mvulana kukua na kuwa mtu mzima. Mfuko wa uzazi au mji wa mimba, hii ndiyo sehemu ambayo mtoto aliye tumboni anakua mpaka anapozaliwa

47 KADI NA MADA ZA SHANGAZI STELLA 1 Je ninaweza kufanya naye mapenzi 2 Je, uume wangu ni mdogo sana? 3 Hivi ni lazima nifanye ngono na shemeji yangu? 4 Ninamhudumia mtu mwenye UKIMWI (MVIU) 5 Hivi sasa mimi ni mkuu wa kaya yangu 6 Ninataka kufanya ngono kama rafiki zangu 7 Niliambukizwa ugonjwa wa ngono, je, nimekuwa tasa? 8 Mwalimu wangu anataka kufanya ngono na mimi 9 Mpenzi wangu ni mjamzito 10 Nina ashiki kali 11 Ninapomlipia chakula cha mchana, je sistahili kufanya naye ngono? 12 Chunusi zimeota kwenye uume wangu 13 Ninahisi kuwa nimeambukizwa Virusi Vya UKIMWI (VVU) 14 Nina wasiwasi kuhusu saratani ya shingo ya kizazi 15 Nilibakwa 16 Je nifanye biashara ya ngono? 17 Ninapata ndoto nyevu 18 Dawa za kupunguza makali ya Virusi Vya UKIMWI (ARV) ni nini? 19 Anataka tufanye ngono 20 Hedhi yangu si ya kawaida 21 Je nimweleze kuwa nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI? 22 Je, bangi inaweza kuniondolea aibu? 23 Wazazi wangu hawanielewi 24 Je, nimweleze kuwa nina maambukizo ya magojwa ya ngono? 25 Nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI. Je nitakufa? 26 Je yawezekana nina mimba? 27 Mpenzi wangu anatarajia kuolewa 28 Mwalimu alimtia mimba rafiki yangu 29 Mume wangu si mwaminifu 30 Nina msongo wa mawazo 31 Mimba hii siitaki 32 Dini yangu inakataza matumizi ya kondomu. 33 Ninapata maumivu makali sana wakati wa hedhi 34 Buzi langu hunifanyia vituko 35 Ninashindwa kujisomea kwa sababu ya mapenzi 36 Mama yangu ana maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI na yuko wazi kusema 37 Je, nitazitibu vipi chunusi zangu? 38 Nina maambukizo ya Virusi vya UKIMWI na mimba

48 MAPENDEKEZO YA MADA Kuibadilisha jamii Kubadili mitazamo 15, 16, 21, 36 Kuchukua hatua 4, 15, 27, 28, 33 Kujenga ubia 5, 18, 19, 28, 33 9 Uhusiano kati ya familia, jamii, na vijana Uhusiano kati ya wazazi, watu wazima na vijana 3, 9, 23, 27, 36 Utumiaji wa huduma za kijamii na za afya. 4, 12, 13, 14, 18, 20 Kujenga mitandao ya misaada 3, 5, 8, 25 8 Kuzungumza waziwazi 1, 5, 13, 15, 22, 29 Shangazi Stella 1 Ukuaji Mabadiliko katika miili yetu 2, 10, 17, 20, 33, 37 Mabadiliko ya mihemko 22, 30, 35 Kujisikia vizuri 2, 6, 37 2 Ngono na uhusiano Mapenzi na ngono 1, 6, 11, 21, 29 Uhusiano wa kijinsia 3, 11, 15, 22, 29, 34 3 Ngono salama 1, 10, 21, 24, 26, 32 7 Kuishi na Virusi Vya UKIMWI na UKIMWI Kuishi na VVU na UKIMWI 13, 18, 21, 25, 38, Kukabiliana na athari za VVU/UKIMWI 4, 5, 36 6 Magonjwa ya ngono 7, 12, 24 4 Ngono ya kulazimishwa Shinikizo la kijamii na kiuchumi katika kufanya ngono 3, 11, 16, 19 Ubakaji na udhalilishaji 8, 15, 19, 28, 34 5 Mimba zisizotarajiwa 9, 26, 28, 31

49 Shangazi Stella Vijana wanazungumza kuhusu ngono, maisha na uhusiano KADI ZA MASWALI

50 Je, ninaweza kufanya naye mapenzi? 1 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni Msichana mwenye Umri wa miaka 17. Ninampenda mvulana ambaye amenizidi umri kwa miaka miwili.tatizo langu ni kuwa, kila ninapokuwa naye anapenda nimridhishe kwa ngono. Huwa tunakumbatiana na kubusiana, jambo ambalo hunifurahisha sana, lakini simruhusu tufanye ngono. Kila tunapokutana naye huniambia kuwa atakuwa kipofu iwapo nitaendelea kumkatalia kufanya naye mapenzi. Marafiki zangu wa kike wameniambia kuwa iwapo ninataka kuendelea kuwa mpenzi wake itabidi nifanye naye ngono. Mimi vilevile ninaogopa nikimkatalia atafanya mapenzi na wasichana wengine, Je ninaweza kufanya naye mapenzi? Ameniambia kuwa, katika umri wetu kila mtu hufanya ngono. Zaituni Imechorwa na David Chikoko

51 MAMBO YA KUJADILIANA Je, wewe na marafiki zako mmewahi kujikuta katika mazingira kama ya Zaituni na mpenzi wake ambapo mmoja anataka kufanya ngono wakati mwingine hataki? Huwa mnafanya nini kuhusiana na suala hili? Waombe watu wawili katika kikundi chenu waigize mazungumzo kati ya Zaituni na rafiki yake wa kiume. Zaituni anampenda sana rafiki yake lakini hayupo tayari kufanya naye ngono. Rafiki yake anajaribu kumshawishi Zaituni wafanye ngono. Mwisho wa lgizo waulize waigizaji walivyojisikia wakati wa kuigiza. Je walifanikiwa kutatua tofauti zao? Iwapo hawakufikia makubaliano yoyote waombe warudi katika nafasi (za kawaida na si waigizaji) zao na wajaribu kutafuta jibu. Rafiki yake Zaituni amedai kuwa atakuwa kipofu iwapo atamkatiza asifikie kilele. Ana maana gani kusema atamkatiza asifikie kilele Ni mambo gani mengine wavulana husema yatawatokea iwapo: a Watakatishwa kufanya ngono baada ya kupata ashiki kutokana na kushikwa shikwa na kubusiana na b Hawatafanya ngono? Kati ya hayo yapi ya kweli? Je mambo hayo yanawahusu wasichana vilevile? Je, kuna mambo mengine ambayo watu wanaweza kufanya ili kuridhishana kimapenzi bila ya mvulana kumwingilia kimwili mpenzi wake? Je unaweza kushauri mambo haya yafanyike?

52 Je Uume wangu ni mdogo sana? 2 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni kijana ambaye ninakaribia kufikia umri wa miaka 14. Ninalo tatizo ambalo linanikera sana.tatizo lenyewe ni uume wangu kuwa mdogo sana. Ninawasiwasi kwa sababu haukui kama watu wengine ambao nimewaona na kwamba hii itaathiri maisha yangu ya baadaye nitakapoanza kufanya ngono. Tafadhali Shangazi niambie hivi ukubwa sahihi wa uume kwa mvulana mwenye umri wa miaka 14 ni upi? Jambo hili linanisononesha sana. Peter

53 MAMBO YA KUJADILIANA Kwa nini unafikiri wavulana wanapata hofu kuhusu ukubwa wa uume? Je, wasichana pia hujali ukubwa wa uume? Kwa nini ukubwa wa uume hutofautiana miongoni mwa wavulana? Ni kitu gani hufanya wengine kuwa na uume mkubwa na wengine mdogo: Umri wao? Maumbile ya mwili (iwapo ni wazito au wepesi, wanene au wembamba) Ukubwa wa uume wa baba au kaka zake? Iwapo wameanza wanafanya ngono au la? sababu nyingine? Je kuna ukubwa sahihi wa uume kwa mvulana mwenye umri wa miaka 14 kama Peter? Je unadhani ukubwa wa Uume huathiri namna ambavyo mwanaume atamridhisha mpenzi wake wakati wa kufanya ngono? Ni mambo gani mengine ya muhimu yanatakiwa yafanyike? Vijana balehe wa kiume na wa kike wanakuwa na wasiwasi gani kuhusiana na miili yao? Mkiwa katika vikundi vya wasichana peke yao na wavulana peke yao, chora picha ya mwili na onyesha sehemu ambazo wewe na rafiki zako mna wasiwasi nazo. Utamweleza nini mtu ambaye ana wasiwasi na sehemu za mwili wake, ili ajisikie vizuri zaidi? Toa mawazo yako na jaribu kuamua yapi ni mazuri zaidi na ni kwa nini unaona hivyo.

54 Hivi ni lazima nifanye ngono na shemeji yangu? 3 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 15 na ninaishi na dada yangu ambaye ameolewa. Shemeji yangu ni mchangamfu na anaheshimiwa sana na familia yetu. Mara nyingi amekuwa akinitania na kuzungumzia kuhusu unyago. Hivi karibuni aliniambia kuwa anataka ni kalale chumbani kwao na kwamba ni lazima nifanye hivyo kwa sababu huo ndio utamaduni wetu. Shangazi, hivi nifanye nini? Jambo hili ni sahihi kweli? Ninaogopa, inawezekana anataka kufanya ngono na mimi.wakati huohuo nina wasiwasi kwamba nikikataa atanifukuza nitoke nyumbani kwake. Patrisia

55 MAMBO YA KUJADILIANA Jadili unachokifahamu kuhusu Unyago. Je utamaduni kama huu upo katika jamii yenu? Mambo gani yanatakiwa kufanywa kuhusu utamaduni huu? Ni kitu gani hutokea hasa? Waheshimu wakubwa zako. Unadhani vijana wanatakiwa kuwaheshimu wakubwa zao wakati wote hata kama wakubwa zao wanawaambia wafanye mambo hatarishi yanayoweza kuwadhuru? Vijana wanaweza kupata msaada vipi katika mazingira kama haya? Ni ushauri gani utampa Patrisia? Ni nani anaweza kumsaidia? Waheshimu Vijana kama unataka wakuheshimu Imetokana na picha iliyochorwa na Chijema

56 Ninamhudumia mtu mwenye UKIMWI (MVIU) 4 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 15. Ninaogopa sana kuhusu UKIMWI. Miaka miwii iliyopita mke wa Mjomba alifariki na baadaye mjomba alikuja kuishi na sisi. Sasa hivi anaumwa sana na mama amenieleza kuwa anaumwa UKIMWI. Amekonda sana kiasi cha kutisha.yupo kitandani wakati wote. Sasa ninaogopa kuwa ninaweza kupata ugonjwa kwa sababu hana vyombo vyake vya kulia chakula wala choo cha kwake, na mara nyingi mimi humsaidia mama kumtunza.tafadhali niambie nifanye nini, kwa sababu nina wasiwasi kuwa iwapo nitakaa karibu naye na kuvuta hewa anayovuta nitapata ugonjwa wa UKIMWI. Eti Shangazi, niondoke? Petronila

57 MAMBO YA KUJADILIANA Je, unajua VVU vinavyoenea? Orodhesha jinsi wewe na watu wengine unadhani mnaweza kupata VVU. Pitia kwa makini orodha hiyo na kata yote ambayo siyo ya kweli. Hakikisha kuwa wewe na rafiki zako mnafahamu tofauti ya VVU na UKIMWI. Je, Petronila yuko sahihi kuogopa kuambukizwa UKIMWI na mjomba wake? Je kuna hatari sana, hatari kiasi, au hatari kidogo ya kupata maambukizi? Je, kuna mambo gani ambayo anatakiwa kufanya ili ajikinge asipate maambukizi? Je, marafiki na majirani zake Petronila wanatakiwa kufanya nini ili kumsaidia mjomba na familia yake? Iwapo kuna watu ambao wanaumwa UKIMWI katika jamii yako: a Ni nani anawatunza? b Wanapata matatizo gani na kwa nini? c Ni matatizo gani yaliyopo kwa watu wanaowatunza wagonjwa, na kwa nini? d Matatizo haya yanaweza kutatuliwaje?

58 Hivi sasa mimi ni mkuu wa kaya yangu 5 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 15 na ndiye kijana mkubwa katika familia. Baba yangu alituacha siku nyingi zilizopita na mama yangu alikufa kwa UKIMWI miezi michache ya nyuma. Ninao wadogo zangu wanne, wakike na wakiume ambao ninalazimika kuwatunza. Mama hakuandika wasia, kwa hiyo alipofariki, wajomba walitunyang anya mali zote.walituachia nyumba ndogo, nguo chache na masufuria machache.wakati mwingine mchungaji kutoka kanisani hutuletea chakula, na mimi mwenyewe huwasaidia akina mama kazi za shambani. Hata hivyo pesa hazitoshi. Mara nyingi ninakosa usingizi kwa sababu ya kuwa na wasiwasi ni kwa jinsi gani tutaishi na wadogo zangu.wapo watoto wengine wanabeba majukumu ya kulea familia kama mimi lakini huwa hatuzungumzii suala hili. Tafadhali Shangazi nisaidie, kwani tatizo hili linaniumiza usiku na mchana. Upendo

59 MAMBO YA KUJADILIANA Je, unawafahamu vijana wengine walio na matatizo kama haya? Hufanya nini katika kujikwamua wenyewe na familia zao? Hufanya nini katika kuyamudu maisha yao na; Nani anawasaidia? Kwa kawaida, ni mambo gani hutokea kwa watoto walio katika mazingira kama haya katika jamii yenu? Nani anaweza kuwasaidia? Wasia ni nini? Je, watu wazima huandika wasia katika jamii yenu? Ni kitu gani hutokea mtu akifa bila ya kuandika wasia? Watoto na vijana wanatakiwa kupata mahitaji gani ili waishi maisha yenye furaha na afya njema? Tayarisha Orodha ya mahitaji halafu weka maoni yako kwa mpangilio ukianzia na lile ambalo unadhani ni la muhimu zaidi. Utampa ushauri gani Upendo?

60 Ninataka kufanya ngono kama rafiki zangu 6 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 16. Ninasoma shule ya bweni na niko kidato cha tatu. Tatizo langu ni kwamba: Ninawafahamu wasichana wengi lakini ningependa nipate msichana mzuri ambaye tutafurahia mapenzi pamoja. Marafiki zangu wote hujigamba sana wanapozungumzia jinsi wanavyofanya ngono na wapenzi wao, na mimi ningependa kufanya hivyo. Ninaogopa kwa sababu umri wangu unaongezeka kuwa mkubwa kiasi cha kwamba, nitakapopata msichana atanicheka nikishindwa kufanya ngono vizuri. Ninafikiria kwenda kumuona Mganga wa kienyeji kwa ajili ya kupata dawa ya mapenzi, ili wasichana wanipende.tafadhali Shangazi, ninaomba ushauri wako. Maulid

61 MAMBO YA KUJADILIANA Kuna tofauti gani kati ya kupenda na ngono? Unadhani ni kweli rafiki zake Maulid wanafanya ngono? Iwapo sio kweli ni kwa nini wanajifanya kuwa wanafanya hivyo? Ni mafanikio gani ambayo wewe hujifanya kuwa umeyapata? Je kujifanya kunakusaidia au hakukusaidii wewe na rafiki zako? Kwa nini unafikiri wewe na rafiki zako mnatakiwa kuwa sawa, na kufanya mambo yanayofanana? Jambo hili linaweza kuwa na uzuri au hatari zipi? Umewahi kutokukubaliana na marafiki zako katika mambo wanayoyafanya? Je huwa unawaeleza kuwa hukubaliani nao au huwa unanyamaza? Je, Maulid aende kwa Mganga wa kienyeji? Ni ushauri gani mwingine ungeweza kumpatia Maulid? Haraka haraka haina baraka / subira yavuta kheri Usikimbilie katika kufanya mambo ama sivyo unaweza kuumia njiani au usifanikiwe kabisa Imechorwa na David Chikoko

62 Niliambukizwa ugonjwa wa ngono, je nimekuwa tasa? 7 Mpendwa Shangazi Stella Nilivunja uhusiano na rafiki yangu wa kiume miezi michache iliyopita kwa sababu niligundua alikuwa anafanya ngono na wasichana wengine.vilevile wiki iliyopita alikuja kunieleza kuwa ana maambukizo ya ugonjwa wa ngono na kwamba ninatakiwa nikapimwe iwapo na mimi nimepata maambukizo. Jana nilienda kliniki na baada ya kufanyiwa vipimo, muuguzi aliniambia nina maambukizo ya ugonjwa wa ngono. Alinieleza kuwa ni lazima nimeze vidonge vyote kwa sababu nisipofanya hivyo nitapata matatizo ya kutopata watoto hapo baadaye. Sasa, jambo hili linanitisha sana. Ningependa nizae watoto wengi nitakapo kuwa mkubwa na nitakapo kuwa nimempata mwanaume wa kweli. Hakika kweli nitakufa nitakapojua kwamba sitaweza kupata mimba maishani. Shangazi, hivi ni kweli? Unafikiri ninaweza kukosa watoto kabisa? Ninaomba uniambie. Mwanahamisi

63 MAMBO YA KUJADILIANA Je, ni kweli kwamba msichana au mvulana ambaye ana maambukizo ya magonjwa ya ngono yasipotibiwa kwa muda mrefu anaweza kuwa tasa? Ni mambo gani mengine yanaweza kusababisha utasa? Ni jambo gani litakupa hofu zaidi iwapo utagundua kuwa wewe ni tasa na hivyo huna uwezo wa kupata watoto? Unafikiri walio katika ndoa wanapokosa watoto, mara nyingi ni kwa sababu: Mwanaume ni tasa? Mwanamke ni tasa? Inawezekana mwanamume au mwanamke kuwa tasa? Unafikiri walio katika ndoa wanaweza kuwa na furaha bila watoto? Kwa nini? Je unafahamu njia yoyote ya kutibu utasa? Imechorwa na DavidChikoko

64 Mwalimu wangu anataka kufanya ngono na mimi 8 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 15, ninasoma kidato cha pili katika Shule ya bweni. Mwalimu wangu wa somo la sayansi alihamia shuleni kwetu mwaka huu. Mwaka jana tulikuwa hatuna mwalimu wa somo la sayansi; alipofika tu alijitolea kutufundisha vipindi vya ziada ili kufidia mada tulizozikosa. Siku moja baada ya kipindi hicho, mwalimu aliniomba nibaki ili nisaidie kuweka vizuri michoro. Marafiki zangu walipoondoka, alianza kunishika shika sehemu za siri na kuniambia ananipenda. Niliogopa lakini nilijisikia vibaya kumwambia aache. Sasa hivi sihudhurii vipindi vyake kwa sababu ninaogopa anaweza kurudia tena kunilazimisha kufanya ngono. Nimeanza kurudi nyuma katika masomo yangu, nifanyeje? Zawadi Imechorwa na David Chikoko

65 MAMBO YA KUJADILIANA Jambo kama hili limewahi kumtokea mtu yeyote unayemfahamu? Je huwapata wasichana tu au hata wavulana? Je, kulitokea nini kwa mwalimu? Je Zawadi Aache kuhofu, kwa vile sio muhimu? Anyamaze lakini aache kuhudhuria vipindi vya sayansi? Amweleze mtu mara moja: rafiki wa karibu, wazazi wake, mwalimu mwingine, au Mkuu wa shule? Amweleze kila mtu, ikiwa ni pamoja na polisi, na kuhakikisha mwalimu anafukuzwa kazi? Ajaribu kumshawishi mwalimu amuoe? Afanye mambo gani mengine? Zawadi anatakiwa kuchukua hatua gani iwapo mwalimu atarudia tena jambo hili? Imechorwa na David Chikoko

66 Mpenzi wangu ni mjamzito 9 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 17 na ninasoma kidato cha nne. Nina umri wa kutosha kuniwezesha kutongoza wasichana lakini bado ni mwanafunzi. Baba yangu aliwahi kunionya kuwa iwapo ataniona au atasikia uvumi kuwa ninajihusisha na msichana, hapo ndipo utakuwa mwisho wangu wa shule. Nilipofikia balehe nilianza kuvutiwa na wasichana na kusahau yale yote aliyonieleza baba. Nilianza kuwatongoza wasichana na nikafanya ngono na mmojawapo, sasa msichana huyu ameniambia ana mimba na anasema atakuja kuishi na mimi kama mke wangu. Bado sijamwambia baba jambo hili kwa sababu ninaogopa kupoteza nafasi yangu ya kusoma.tafadhali Shangazi Stella nisaidie katika jambo hili kwa sababu wasiwasi unazidi kila siku. Bakari Asiyesikia la Mkuu huvunjika guu Hata siku moja usidharau ushauri wa wazazi, kwani una maana sana katika maisha yetu.

67 MAMBO YA KUJADILIANA Kwa nini unafikiri Bakari hakusikiliza ushauri wa baba yake? Je, kwa kawaida vijana hufuata ushauri wa wazazi? Je, Bakari na Mpenzi wake wafanye nini? Angalia picha hapo chini, iliyochorwa na mwanafunzi mmoja. Unafikiri inawezakana kufurahia maisha na bado ukawajibika? Kwa vipi? Marafiki zangu wanasema ninatakiwa kufurahia ujana wangu na kufanya kila ninaloweza kwani mtu huishi mara moja tu. Kitabu cha Dini kinasema, ni lazima niwatii wazazi wangu na vile vile kufurahia ujana, lakini nikumbuke nitahukumiwa kwa matendo yangu yote. Wazazi wangu wananihimiza nisome kwa bidii na nisahau mambo mengine yote mpaka nitakapokuwa na elimu ya kutosha. Ninataka kufurahia maisha na bado niwajibike. Kwa nini inakuwa vigumu?

68 Nina ashiki kali 10 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 15 na ninasoma kidato cha pili.tatizo langu ni kwamba, kila ninapomwona msichana mzuri au ninapofikiria ngono, uume wangu hudinda na ninashindwa kujizuia, nami ninaogopa watu wanaweza kunigundua. Marafiki zangu wengine wananiambia nipige punyeto lakini wengine wanasema nikifanya hivyo nitakuwa kipofu au sitaweza kupata watoto.vilevile nina wasiwasi kwa sababu watu wa DINI wanasema ni dhambi na kwamba watu; wataadhibiwa wakifanya hivyo. Kwanza kabisa, je, ni vizuri kupiga punyeto? Nitafurahi sana iwapo utanieleza madhara yake kabla sijaanza kufanya hivyo. Nitashukuru sana kwa msaada wako. Simba Ahh! Nyie wasichana mnanipa shida sana! Nitazuia vipi hili lisitokee au ni jambo la kawaida? Kutoka shairi la Phellonu Dube

69 MAMBO YA KUJADILIANA Unafikiri mara nyingi wavulana wengi hudindisha uume wao wanapofikiria ngono? Iwapo kitendo hiki huwasononesha, wanatakiwa kufanya nini ili kuzuia uume wao kudinda? Nini maana ya kupiga punyeto? Iwapo mdogo wako wa kiume au wa kike atakuuliza swali kama hili, utampa maelezo gani? Kupiga punyeto kunaweza kuwasaidiaje vijana? JARIBIO: Kupiga Punyeto Kwa kila sentesi andika: kweli, sio kweli au sina uhakika. (Linganisha majibu yako na yale yaliyoko kwenye kadi ya majibu) 1 Punyeto huwafanya watu wapende kufanya ngono kila wakati. 2 Punyeto ni salama na ni njia ya kawaida ya kumaliza ashiki na kuutambua mwili wako. 3 Wavulana wanaopiga punyeto huharibu mbegu za kiume kwa hiyo hawawezi kutungisha mimba. 4 Punyeto inaweza kukufanya kipofu au kichaa. 5 Wasichana hawawezi kupiga punyeto. 6 Ukipiga punyeto, nywele zitaota kwenye mikono yako. 7 Ukipiga punyeto hutaweza kufanya ngono vizuri na mwenzi wako. Utampa Simba ushauri gani?

70 Ninapomlipia chakula cha mchana, Je sistahili kufanya naye ngono? 11 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana ninayesoma shule na ninataka kufanya ngono na rafiki yangu wa kike. Mara nyingi humnunulia chakula cha mchana, humlipia nauli yake ya basi na wakati mwingine humpa zawadi, lakini ananikatalia tusifanye ngono. Marafiki zangu wameniambia kuwa wasichana wengine wanakubali kufanya ngono. Kwa nini hakubali tufanye naye ngono ili kunishukuru kwa yote ninayomfanyia? Temba Imechorwa na David Chikoko

71 MAMBO YA KUJADILIANA WASICHANA: Unadhani ni lazima ufanye ngono na rafiki yako wa kiume kama amekupa zawadi au pesa? WAVULANA: Unategemea rafiki yako wa kike akubali mfanye naye ngono kwa sababu umemnunulia vitu? Unafikiri ni kwa nini rafiki yake Temba hukataa kufanya naye ngono? Ni ushauri gani ungeweza kumpa Temba? Na ni ushauri upi ungempa rafiki yake wa kike? Watu wengi husema kwamba mahitaji ya wavulana na wasichana katika mahusiano ni tofauti. Kwa mawazo yako, wavulana hutaka nini na wasichana hutaka nini? Wote mnakubaliana? Angalia picha ya hapo chini. Unauonaje wito wa Mawazo ya mapenzi? Andika wito wako kuhusu ngono, maisha na uhusiano.wito wa nani umepoa zaidi? Imechorwa na David Chikoko

72 Chunusi zimeota kwenye uume wangu 12 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 17.Tatizo langu ni kwamba chunusi zimeota kuzunguka kichwa cha uume wangu. Nilipokuwa kidato cha pili, mwalimu wetu alituambia kuwa huu ni ugonjwa unaoambukiza kwa njia ya ngono, na mtu akipata tatizo kama hili anaweza kuchanganyikiwa iwapo hatatibiwa. Hivi ni kweli? Huu ni ugonjwa gani na je unaweza kutibiwa? Ninaogopa kwenda hospitali, kwa sababu kila mtu anasema wauguzi ni wakali sana kwa vijana kama una ugonjwa kama huu. Jabu

73 MAMBO YA KUJADILIANA Unafikiri Jabu ana tatizo gani? Unadhani anaumwa ugonjwa unaoambukiza kwa njia ya ngono? Anatakiwa kupewa ushauri gani? JARIBIO: Magonjwa ya Ngono Je, sentesi hizi ni za kweli au sio kweli? (Linganisha majibu yako na yale yaliyo kwenye kadi ya majibu) 1 Huwezikupata ugonjwa wa ngono iwapo hujawahi kufanya ngono. 2 Unaweza kutibu magonjwa ya ngono kwa kufanya ngono na bikira. 3 Njia pekee ya kuzuia magonjwa ya ngono ni kutumia kondomu. 4 Magonjwa yote ya ngono husababisha maumivu makali sana wakati wa kukojoa mkojo. 5 Magonjwa ya ngono mengi yanaweza kutibika iwapo utatibiwa mapema. Kwa nini wahudumu wa afya wengine ni wakorofi kwa vijana wanaoumwa magonjwa ya ngono? Ni hatua gani zinazotakiwa kuchukuliwa kuhusu jambo hili?

74 Ninahisi kuwa nimeambukizwa Virusi Vya UKIMWI (VVU) 13 Mpendwa Shangazi Stella Mimi nina umri wa miaka 18 na rafiki yangu wa kiume ana miaka 20.Tumekuwa tukifanya ngono kwa muda wa miezi minne sasa. Mwanzoni tulikuwa tunatumia kondomu, lakini mpenzi wangu hakuzipenda. Baada ya miezi miwili aliniambia kuwa itabidi tuaminiane na tuache kutumia kondomu, kwa hiyo niliamua kutumia vidonge vya kuzuia mimba kwa sababu sikutaka kupata mimba. Sasa hivi nimegundua kwamba mmojawapo kati ya rafiki zake wa kike wa zamani anaumwa UKIMWI. Ninaogopa huyu rafiki yangu huenda naye anaumwa ugonjwa huu na anaweza kuwa ameniambukiza! Sijui nifanye nini. Nimesikia kwenye radio kuhusu kupima VVU, Lakini watu wanasema ukienda huko utaulizwa maswali mengi, tena magumu. Mara nyingine majibu wanayotoa sio sahihi na watu wengine wanaweza kujua majibu yangu. Siwezi kuzungumza na mpenzi wangu au mtu yeyote kuhusu jambo hili.vilevile sina uhakika kama ninataka kujua kama nina maambukizo ya VVU au sina. Nitafanya nini sasa? Shangazi, tafadhali nisaidie wakati wote huu nina wasiwasi sana. Flora

75 MAMBO YA KUJADILIANA Ni mara ngapi watu na wapenzi wao hufanya kama Flora, ambapo wanaanza kufanya ngono kwa kutumia kondomu na baadaye kuacha? Kwa nini wanafanya hivyo? Kuna hatari gani zinaweza kutokea? Sasa Flora afanye nini? Amweleze mpenzi wake ukweli kuhusu wasiwasi wake na kumshawishi warudie kutumia kondomu? Akapime VVU kwa siri halafu afanye uamuzi?. Amwambie mpenzi wake kwamba wote wakapime VVU? Aendelee kufanya ngono isiyosalama? Nini faida na hasara kwa kila chaguo? Unafahamu nini kuhusu kupima VVU. Mambo gani hutokea kwenye kituo cha kupimia VVU? Wafanyakazi wakoje? Majibu huchukua muda gani kutoka? Imechorwa na David Chikoko

76 Nina wasiwasi kuhusu saratani ya shingo ya kizazi 14 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 15. Nina wasiwasi sana na jambo moja ambalo nimewahi kulisikia. Shangazi yangu alisema kuwa jirani yake mmoja ni mgonjwa sana. Anaumwa saratani ya mlango wa kizazi, ugonjwa ambao unaweza kuua wanawake. Sijawahi kusikia kuhusu ugonjwa huu na nina wasiwasi kweli. Hivi watu wanapataje? Je, ni kweli kwamba mtu anaweza kufa akiugua ugonjwa huu? Shamsa

77 MAMBO YA KUJADILIANA Je, umewahi kusikia kuhusu saratani ya mlango wa kizazi? Je, Unafahamu saratani ya mlango wa kizazi husababishwa na nini? Je, Ugonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi ni wa kawaida nchini kwenu? Je, wanawake na wasichana wanatakiwa wafanye nini ili kuzuia wasipate ugonjwa huu? Je, saratani ya mlango wa kizazi inaweza kutibika?

78 Nilibakwa 15 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ninajisikia vibaya sana na wala sina mtu wa kuzungumza naye. Nilipokuwa mdogo mjomba alikuwa anatukumbatia vizuri na kutupatia zawadi. Lakini mwaka jana, nilipokuwa nimetimiza miaka 12 siku moja alinifuata porini nilipokuwa nimekwenda kuchota maji, na kunishika shika matiti na ndani ya sketi. Niliogopa lakini aliniambia kuwa iwe siri yetu ama sivyo wote tutakuwa matatani. Mwishoni mwa wiki hii mjomba alikuja kwenye mazishi ya ndugu yetu. Siku hiyo kila mtu alikuwa anakunywa pombe. Usiku nilipokuwa ninatoka chooni, alinishika kwa nguvu na kuniangusha chini na kunibaka. Kumbe alikuwa akinisubiri nje. Nilipata maumivu makali sana lakini nilipojaribu kulia alinipiga. Baadaye aliniambia lilikuwa kosa langu kwa sababu nilikuwa nimevaa sidiria ambayo ilimfanya apate ashiki. Tafadhali Shangazi nisaidie. Ninajisikia vibaya na ninajiona mchafu, kila mara ninazidi kukumbuka, na ninaogopa sana kuwaeleza wazazi wangu.wazazi watanikasirikia kwa sababu mjomba hutusaidia kutupatia chakula na pesa. Lakini, itakuwaje akirudia tena? Ninaogopa sana, Hivi nifanyeje? Sikudhani

79 MAMBO YA KUJADILIANA Kubakwa maana yake nini? Je, ni jambo la kawaida katika jamii yenu? Je, wanaobaka ni watu wa mbali au ni ndugu? Katika hadithi ya Sikudhani, nani alitakiwa kuwajibika kwa lililotokea? Kwa nini mjomba wake Sikudhani alifanya vile? Je, mwanamke au msichana anatakiwa kulaumiwa kwa sababu ya kabakwa? kwa mfano, kama amevaa nguo zinazo chochea ashiki. Andaa mdahalo kuhusu suala hili. Sikudhani anahitaji ushauri wa aina gani? Sikudhani anatakiwa afanye nini baada ya tukio hilo? Ungebakwa wewe ungefanya nini? (wajibu wavulana na wasichana) Je, Ungetoa taarifa polisi? Nini faida na hasara ya kutoa taarifa ya ubakaji? Mficha maradhi kifo kitamuumbua Kunyamaza kimya kunaweza kukuharibia maisha yako: kuzungumza yaliyo moyoni kunaweza kukuondolea matatizo yanayo kera na kusononesha

80 Je, nifanye biashara ya ngono? 16 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 19. Ninasoma kidato cha nne na ninategemea kufanya mitihani mwaka huu.wazazi wangu walifariki, nami ninaishi na bibi yangu. Nilikuwa ninalipiwa karo ya shule na mjomba ambaye naye amefariki mwaka jana. Sasa hivi sina mtu wa kunisaidia. Ninapenda sana nimalize shule na kufanya mitihani ili niweze kupata kazi, lakini siwezi kutafuta pesa kwa ajili ya karo, na gharama za mitihani nazo ni kubwa. Je, ni sahihi kufanya biashara ya ngono kwa sababu sina njia nyingine yoyote ya kuniwezesha kumaliza elimu yangu? Katika eneo hili wapo wanaume wengi ambao wako tayari kutoa pesa baada ya kufanya ngono na wasichana, lakini ninaogopa kufanya kazi hii. Rafiki yangu ambaye anafanya biashara hii aliniambia kuwa wakati mwingine wanaume hukataa kulipa pesa za kutosha, na kuna mwingine aliwahi kumpiga.tafadhali Shangazi nisaidie kutatua tatizo hili. Sikuzani

81 MAMBO YA KUJADILIANA Kaeni wawili wawili. Mmoja awe Sikuzani, mmoja awe ni mwanaume ambaye yupo tayari kutoa pesa baada ya kufanya naye ngono. (labda Sikuzani atake watumie kondomu lakini mwanaume akatae). a Fanya mazungumzo. b Baadaye, eleza kikundi yale yaliyozungumzwa. c Vilevile sema jinsi ulivyojisikia ulipokuwa unaigiza. d Mwisho, jadili yale yote uliyojifunza katika igizo hili. Chora chati ya mtiririko kama hii hapa chini kuonyesha faida na hasara ya kufanya biashara ya ngono, kwa mtu aliye katika mazingira kama ya Sikuzani. Je, thamani ya pesa inalingana na hatari ya kufanya jambo hilo? Faida (mazuri) Hasara (mabaya) Kusaidia Familia Kupata Pesa Kulipa karo ya Shule kupata kazi kupata mimba BIASHARA YA NGONO kupata VVU Hakuna mapenzi Wala heshima kuumizwa au kubakwa kuwa mgonjwa Sikuzani angelikuwa anaishi katika eneo lenu, angeweza kufanya nini ili kupata pesa au msaada wa kulipia ada ya shule na mitihani?

82 Ninapata ndoto nyevu 17 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 15. Ninalo tatizo ambalo ninaamini litakuwa rahisi kwako kulitafutia ufumbuzi. Sijawahi kufanya mapenzi na msichana lakini mara nyingi nikiamka usingizini hujikuta nimechafua shuka. Majimaji mazito yenye kunata hutoka uumeni. Jambo hili hunitokea hata kama siwazii ngono. Sasa nina wasiwasi mkubwa kwamba nitakapooa jambo hili linaweza kuathiri uhusiano wangu na mke wangu kwa vile hutokea mara tatu au nne kila wiki. Ninajisikia vibaya kwa sababu ya ndoto hizi lakini sijui ni kwa vipi ninaweza kuzuia. Je, mwili wangu una tatizo lolote? Na hili ni tatizo langu kwa vile ninaendelea kuota ndoto za namna hii? Edson

83 MAMBO YA KUJADILIANA Je, unafahamu kwamba jambo hili huwapata wavulana mara kwa mara? Je, unafikiri ni kitu gani husababisha ndoto nyevu? Je, unadhani ndoto hizi zina maanisha Edson ni mvulana wa kawaida? Edson anatakiwa aende hospitali? Edson lazima afanye ngono mapema iwezekanavyo kabla hajaugua? Je, Edson ataendelea kupata ndoto nyevu atakapokuwa ameoa au atakapoanza kufanya ngono? Itabidi kuondoa kabla mtu mwingine hajaona

84 Dawa za kupunguza makali ya Virusi Vya UKIMWI (ARV) ni nini? 18 Mpendwa Shangazi Stella Mimi nina umri wa miaka 19 na nina mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 3. Rafiki yangu wa kiume niliyezaa naye alikuwa mkubwa kwangu na aliniacha nilipopata mimba tu. Sasa hivi anaumwa sana, na ana UKIMWI. Mimi ninaishi kijijini na bibi yangu. Msimu wa mvua tunalima mahindi.vilevile tunafanya biashara ya kuuza samaki wakavu. Hata hivyo pesa hazitoshi. Afya yangu ni nzuri, Lakini mwaka jana nilianza kupungua uzito na mara nyingine kujisikia dhaifu na kuchoka. Miezi michache iliyopita Shangazi yangu alinipeleka kliniki ili nikapime kama nina maambukizo ya VVU. Huo ndio uliokuwa mwanzo wa kufahamu kwamba ninayo maambukizo ya VVU. Mama mmoja huko katika nyumba ya kufanyia ibada aliniambia kuwa zipo dawa za kupunguza makali ya VVU lakini ni ghali sana. Pamoja na hayo ningependa kupata dawa hizo.wasiwasi wangu mkubwa ni mtoto wangu. Nani atamtunza mimi nikifa? Bibi yangu ni mzee sana na wakati mwingine anakuwa mgonjwa. Ninataka kumuona mtoto wangu akienda shuleni na vilevile anakuwa na furaha. Tafadhali Shangazi naomba uniambie iwapo kuna mahali ambapo ninaweza kuzipata dawa hizi. Tedy

85 MAMBO YA KUJADILIANA Jadili yale yote mnayoyafahamu kuhusu dawa za kupunguza makali ya VVU (ARV) Kuna taarifa zozote kuhusu upatikanaji wa dawa hizo? Iwapo taarifa hazitoshi, unadhani ni kwa nini? Utafanya nini ili uweze kuzipata taarifa zaidi? Iwapo dawa za kupunguza makali ya VVU (ARV) hazipatikani,tedy anatakiwa kufanya nini zaidi ili afya yake iwe nzuri?, Imechorwa na David Chikoko DAWA ZA KUPUNGUZA MAKALI YA VVU HULETA MATUMAINI

86 Anataka tufanye ngono 19 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 15. Nimepanga chumba mjini karibu na shule yetu, na hapo ndipo ninapoishi.wazazi wangu wanafanya kazi kwenye mgodi kilomita 40 kutoka mjini. Mara nyingine wazazi wangu huchelewa kunitumia pesa kwa ajili ya kulipia chumba. Ikitokea hivyo mke wa mwenye nyumba hunifuata chumbani kwangu na kuniomba tufanye ngono. Ninaogopa kumkatalia kwani anaweza kunitoa nje ya chumba nami nitakuwa sina mahali pa kuishi. Mpaka sasa hivi nimejitahidi kutumia mbinu mbalimbali kumtoa nje ya chumba changu kabla ashiki haijampanda sana. Hali hii inazidi kuwa mbaya sasa, nami siwezi kumwambia mtu yeyote na sijui nifanye nini. Siku baba mwenye nyumba akimkuta chumbani kwangu nina uhakika atanilaumu sana. Oliva

87 MAMBO YA KUJADILIANA Unafikiri wavulana wanaweza kubakwa na wanawake au wanaume? Jamii ina mtazamo gani kwa wavulana waliobakwa? Kuna tofauti yoyote iwapo ni msichana amebakwa? Nini tofauti ya kubakwa na shambulio la aibu? Je Oliva anatakiwa amweleze nani kuhusu jambo hili? Ni hatua gani zaidi anapaswa kuzichukua? Je, wazazi wake wanaweza kumsaidiaje?

88 Hedhi yangu si ya kawaida 20 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 15, Nilivunja ungo nikiwa na umri wa miaka 13.Tatizo langu ni kwamba kwa kipindi cha miezi minne sasa sijapata hedhi. Mimi ni bikira na sijawahi kuwa na rafiki wa kiume. Je, nina tatizo lolote? Rafiki zangu wanasema mimi ni tasa. Hivi ni kweli? Tafadhali nisaidie kwa sababu ninaogopa huenda sitaweza kupata watoto. Paulina

89 MAMBO YA KUJADILIANA Je,Wasichana wote unaowafahamu wanapata hedhi kama kawaida? (yaani mara moja kwa mwezi) au kuna miezi mingine wanakosa? WASICHANA: WAVULANA: Eleza uzoefu wako katika kikundi. Eleza kila unachokifahamu. Jadili sababu zinazowafanya baadhi ya wasichana wawe na siku za hedhi zisizo za kawaida kama Paulina Je, unafikiri Paulina ni tasa kwa sababu hajaona siku zake? Kuna imani gani nyingine unazozifahamu zilizopo katika jamii zinazohusu wavulana, wasichana, ngono, mimba na mambo mengine yanayofanana na hayo? Tayarisha orodha ya imani potofu zilizopo katika jamii. Kwa mfano, ukiingia mwezini kila baada ya wiki mbili utazaa mapacha au mvulana akiota nywele usoni inamaanisha ameanza kufanya ngono. Kati ya hizo, ni zipi unakubaliana nazo na zipi ni imani potofu (yaani mambo ambayo watu wengi wanayaamini, lakini siyo ya kweli)

90 Je nimweleze kuwa nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI 21 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 19. Nilijitambua kuwa nina maambukizo ya VVU mwaka mmoja uliopita. Nilipoambiwa kwa mara ya kwanza nilipata mshituko, lakini baadaye nilimweleza dada yangu ambaye alinisaidia kumweleza mama.watu wengine hawajui hali yangu. Mimi siumwi na ninaendelea kufanya shughuli zangu za kushona nguo za kike. Hivi karibuni nilikutana na Tadei ambaye tunaimba naye kwaya. Ninampenda na yeye ananipenda. Lakini sasa ninaogopa kweli. Nisingependa kumwambia ninaishi na VVU kwa sababu hatanitaka niwe mpenzi wake. Vilevile anaweza kuwaeleza watu wengine. Matokeo yake nitakosa wateja wa kuja kushona nguo. Sina uhakika iwapo mtu kama mimi ninaweza kuwa na mpenzi. Kikundi kinachotoa msaada kwa wanaoishi na VVU hutoa maelezo kuwa tunaweza kufanya ngono ili mradi tutumie kondomu, lakini mimi bado ninaogopa. Kwani, si afadhali nisubiri niwe na mpenzi ambaye vilevile anaishi na VVU kwa vile atanielewa badala ya kunilaumu? Kwa hiyo maswali yangu ni haya: Je, nikubali Tadei awe mpenzi wangu? Iwapo nitakubali, Je lazima nimweleze kwamba nina maambukizo ya VVU kabla sijawa mpenzi wake? Tafadhali Shangazi naomba ushauri wako. Frida

91 MAMBO YA KUJADILIANA Je, unaweza kununua nguo alizoshona fundi iwapo unafahamu kuwa ana maambukizo ya VVU? Kwa nini? Je jibu lako linategemea taarifa sahihi ulizozipata? Kwa mawazo yako, ni vijana wangapi katika eneo lenu wanaanza kufanya ngono bila ya kujua hali ya maambukizo ya wapenzi wao? Iwapo Tadei hana maambukizo ya VVU Je, ni sahihi Frida kufanya naye ngono? Ni hatari gani zinazoweza kutokea?. Wanaweza kuzizuia vipi hatari hizo zisitokee? Ni wachache, kiasi, au wengi?. Ni wakati gani jambo hili ni hatari sana na ni wakati gani sio hatari sana? Je, inawezakana Tadei ana maambukizo ya VVU vilevile? Iwapo jibu ni ndio, anawashauri nini Tadei na Frida? Ni wakati gani Frida anaweza kumweleza Tadei kuwa ana maambukizo ya VVU? Asimweleze kabisa. Kabla ya kuanza kufanya naye ngono. Pale tu atakapo mwuliza. Watakapokuwa wanafahamiana zaidi. Pale tu watakapotaka kuzaa watoto. Toa sababu kwa kila jibu utakalo chagua. Katika kila jibu ulilo chagua fikiria mambo gani mazuri na mabaya yanaweza kutokea?

92 Je, bangi inaweza kuniondolea aibu? 22 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 16 na ninasoma kidato cha tatu. Ninalo tatizo kubwa, kwa sababu kila nikiwaona wasichana ninaona aibu. Rafiki zangu wananiambia kwamba iwapo nitavuta bangi nitajisikia jasiri na ninaweza kutongoza wasichana. Wenzangu wote wanao marafiki wa kike, na mimi ninajisikia nimepitwa na wakati na mpweke. Ninataka kuwa na rafiki wa kike lakini sitaki nivute bangi sasa nifanyeje? Philimoni

93 MAMBO YA KUJADILIANA Je, vijana wengi wana tatizo la aibu? Ni nani huona aibu zaidi, wavulana au wasichana? Je watu wengi unaowafahamu wanapenda kuwa na marafiki wa kike au wa kiume kwa sababu wengine wana marafiki? Je, hii ni sababu ya kutosha ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu? Je bangi inaweza kumsaidia Philimon? Kwa nini? Pombe na madawa ya kulevya Je? Ni ushauri gani Philimon apewe a Kuhusu jinsi ya kuondoa aibu? b Kuhusu kufanya urafiki na wasichana? c Kuhusu kuvuta bangi d Kuhusu kuwa na rafiki wa kike katika umri wake?

94 Wazazi wangu hawanielewi 23 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 18.Tatizo langu ni kwamba wazazi wangu wanaingilia sana maisha yangu. Kila mara wananichagulia nani awe rafiki yangu na kunionya nisifanye ngono kabla ya kufunga ndoa.wakati wote wanapenda kunieleza lipi nifanye na lipi nisifanye, lile ambalo sipendelei au kama nina tatizo lolote basi niwaeleze ili tuweze kujadiliana. Mjomba wangu anaishi mbali na sisi kwa hiyo sina mtu yeyote mkubwa kuliko mimi ambaye ninaweza kuomba ushauri. Nifanyeje? Daudi Jinsi ukuavyo ndivyo utakavyojua ukweli wa maisha.

95 MAMBO YA KUJADILIANA Je,Vijana wengi unaowafahamu huelewana vizuri na wazazi wao au hawaelewani? Na wewe je? Unaishije na wazazi wako? a Unajisikia huru kuzungumza nao? b Unapozungumza na wazazi wako, kuna ugumu gani unauona? c Ni nani kati ya baba na mama ambaye ukizungumza naye unajisikia huru? Je wazazi wako wanakutendea vipi? Je kuna sababu yoyote ya wao kufanya hivyo? Je wanawatendea tofauti wavulana na wasichana? Kama jibu ni ndio, kwa nini wanafanya hivyo? Ni ushauri gani ungeutoa kwa vijana kuhusu jinsi ya kuboresha mawasiliano na uhusiano na wazazi wao? Je, kuna watu wazima ambao unaweza kuzungumza nao kwa uhuru bila kuogopa? Ni akina nani? Ni kitu gani kinakufanya uwe huru kuongea nao?

96 Je, nimweleze kuwa nina maambukizo ya magonjwa ya ngono? 24 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni Mvulana mwenye umri wa miaka 17, na ninasoma shule. Ninaye rafiki yangu wa kike ambaye nilianza kufanya naye mapenzi miezi michache iliyopita. Likizo yangu iliyopita nilikwenda Dodoma kumsalimia mjomba wangu. Kule nilikutana na msichana mmoja nje ya bar.tulifanya ngono mara moja tu. Niliporudi nyumbani nilianza kuumwa ugonjwa ambao baadaye ilijulikana kuwa ni mmoja wapo wa magonjwa ya ngono. Katika kipindi cha Sayansi Mwalimu aliwahi kutuambia kuwa, mtu akipata magonjwa ya ngono ni vema kumtaarifu mwenzi wake.vilevile nimewahi kusoma mahali mambo haya, lakini kwa nini nimweleze mpenzi wangu?. Si atanichukia sana? Hivi hawezi kugundua wakati tunafanya ngono kuwa nina matatizo iwapo sitamwambia? Nisingependa kumpoteza mpenzi wangu. Ninaomba ushauri wako. Kizuri Kidumu

97 MAMBO YA KUJADILIANA Je, Kizuri Kidumu amweleze rafiki yake wa kike kuhusu maambukizo aliyoyapata? Kutatokea nini iwapo Kizuri Kidumu hatamweleza? Na akimweleza itakuwaje? Ungelikuwa mpenzi wa Kizuri Kidumu ungependa afanye nini? Utajisikiaje iwapo mpenzi wako atafanya mapenzi na msichana au mvulana mwingine? Je, utachukua hatua gani? Je,Vijana wengi unaowafahamu wanapata magonjwa ya ngono? Ni kitu gani kinasababisha? Je, inawezekana kuzuia? Je unaweza kumtambua mtu ambaye ana maambukizo ya magonjwa ya ngono? Ni dalili gani hujionyesha, kwa wanaume na wanawake?

98 Nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI. Je nitakufa? 25 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 18 na ninauza mboga sokoni. Nimepima VVU siku za hivi karibuni na nimekutwa nina maambukizo ya VVU. Mama yangu alifariki na sasa hivi ninaishi na Shangazi yangu. Baba aliachana na mama tukiwa wadogo. Ninaona aibu kumweleza Shangazi, rafiki zangu au mtu yeyote pale sokoni kwa sababu mara nyingi watu walio na UKIMWI hutaniwa.vilevile ninaogopa Shangazi atakasirika na kuhuzunika. Sikumbuki Mnasihi alieleza nini nilipokwenda kupima. Hivi ninatakiwa kufanya nini? Je kuna jambo lolote ambalo unaweza kunisaidia? Je, nile chakula maalum? Je, kuna vikundi vyovyote vya watu wanaoishi na VVU? Nilikuwa nimeanza kujifunza jinsi ya kutengeneza sabuni na stadi zingine, niendelee kujifunza au niache nisubiri kufa? Sijisikii kuumwa, lakini nina wasiwasi sana kiasi cha kushindwa kula au kulala vizuri. Ninajisikia kama ndio mwisho wa maisha yangu. Nilitaka niishi maisha ya kawaida, nimpate ninayempenda na tuzae watoto. Lakini sasa yote haya hayawezi kutokea. Je ni lazima niache kufanya ngono? Wakati mwingine ninafikiria bora kujiua kuliko kusubiri kufa kwa UKIMWI. Tafadhali Shangazi, nisaidie. Sina mtu mwingine yeyote ambaye ninaweza kumweleza mambo haya. Wema

99 MAMBO YA KUJADILIANA Nini tofauti kati ya VVU na UKIMWI. Je, watu wengi katika eneo lenu wanaishi na VVU au UKIMWI? Je wanaweza kuzungumza hali hiyo kwa uwazi? Kwa nini wanaweza au kwa nini hawawezi? Iwapo utagundua kuwa una maambukizo ya VVU. Ni kitu gani kitakuogopesha zaidi? Je,Wema asubiri kufa tu au yapo mambo ambayo anaweza kuyafanya ili kujikinga na kuwa na afya njema? Unaweza kujibu vipi swali lake la kuishi na VVU? Taja mambo yote ambayo watu husema kuhusu watu wanaoishi na VVU/UKIMWI. Gawa orodha hiyo katika makundi ambayo yanaunga mkono na ambayo yanakataa. Orodha ipi ni ndefu? Kwa nini imetokea hivyo?

100 Je yawezekana nina mimba? 26 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni Msichana mwenye umri wa miaka 16 na nimekuwa na uhusiano wa kimapenzi na mvulana kwa miezi minne sasa. Kila mara alikuwa akinitaka tufanye ngono lakini mimi nilimkatalia. Siku moja nilimkubalia. Hata hivyo sikufurahia. Hii ilitokea miezi miwili iliyopita na tangu hapo sijaona siku zangu (sijapata hedhi).tulifanya mara moja tu, bila kondomu. Rafiki zangu wanasema siwezi kupata mimba. Hivi ni kweli? Vilevile nimewahi kuwasikia wasichana wakizungumzia vidonge vya dharura vya kuzuia mimba iwapo umefanya ngono kwa makosa au umelazimishwa. Je, nimechelewa kuvitumia? Nisingependa kufanya jambo lolote la hatari.tafadhali nisaidie; Sijui la kufanya. Nyamboni

101 MAMBO YA KUJADILIANA Je unafahamu jinsi ya kuzuia mimba? Fanya jaribio hili ili kupima ufahamu wako. JARIBIO: Mimba Sentensi zipi ni za kweli na zipi ni sio za kweli (Linganisha majibu chini ya ukurasa huu) 1 Msichana hawezi kupata mimba siku ya kwanza atayofanya ngono. 2 Huwezi kupata mimba ukifanya ngono ukiwa umesimama. 3 Huwezi kupata mimba iwapo mwanaume atatoa uume kabla ya kukojoa manii. 4 Huwezi kupata mimba iwapo utasafisha uke au utakojoa mkojo mara baada ya ngono. 5 Msichana hawezi kupata mimba kabla ya kuvunja ungo. 6 Huwezi kupata mimba iwapo Mvulana ana umri chini ya miaka 15. Unafahamu nini kuhusu vidonge vya dharura vya kuzuia mimba, vinafanya nini na unaweza kuvipataje? Taja mambo ambayo wavulana husema ili kuwashawishi wasichana kufanya ngono. Kwa kila moja andika majibu yake. Fanya zoezi la kuzungumza nani anaweza kusema HAPANA ya kweli. Kitu gani kinaweza kukusaidia MAJIBU: Sentensi zote sio za kweli. Kama ulifikiri kuna ambayo ni ya kweli utahitaji kujikinga zaidi wewe mwenyewe au rafiki yako wa kike.

102 Mpenzi wangu anatarajia kuolewa 27 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni kijana balehe na ninampenda sana msichana ninayesoma naye anayeitwa Susan. Tunafanya bidii katika masomo yetu na tumeamua kuwa tukimaliza kidato cha nne tuoane.tatizo letu ni kwamba wazazi wake wamemtafutia mwanaume mwingine. Ingawa amewaeleza kwamba anataka kuolewa na mimi, wazazi wake wamekataa na kumwambia ni lazima afanye kama wanavyotaka wao. Tufanyeje? Iwapo ataendelea kukataa watamfukuza na kusema sio mtoto wao. Mwanaume wanayetaka aolewe naye ni mzee mwenye pesa. Ninadhani wazazi wake Susan wanataka aolewe naye kwa sababu ya pesa. Sasa hivi wanazungumzia kutoa mahari na kiasi gani atatakiwa kulipa. Hivi wazazi wanaruhusiwa kumlazimisha msichana kuolewa na mtu ambaye hamtaki? Tafadhali tunaomba utusaidie. Faraji

103 MAMBO YA KUJADILIANA Je, katika utamaduni wenu zipo ndoa za kupangiwa? Zinafanana na hii ya Susan, au ziko tofauti? Watu wengine hufikiri kwamba mahari huboresha uhusiano kati ya familia mbili husika, wengine husema wanawake wananyimwa haki zao na ni unyanyasaji, na wengine huamini kuwa imekuwa ni biashara ya aina yake.wewe unafikiriaje? Nini faida na hasara ya a Ndoa za kulazimishwa b Ndoa ambazo watu wanachagua nani amuoe au aolewe naye? Je, kuna njia zozote ambazo Faraji na Susan wanaweza kutumia ili Susan asiolewe na mwanaume ambaye hampendi? Jadili uchaguzi wao na washauri hatua nzuri zaidi ya kuchukua. Utajisikiaje iwapo wazazi wako watakuchagulia msichana wa kuoa au mume wa kuolewa naye? (Wajibu wavulana na wasichana)

104 Mwalimu alimtia mimba rafiki yangu 28 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni Msichana mwenye umri wa miaka 17. Ninategemea kufanya mitihani yangu ya kidato cha nne mwaka huu. Rafiki yangu mpendwa anayeitwa Upendo mwenye umri wa miaka 16, alifukuzwa shule mwezi uliopita. Upendo ninasoma naye darasa moja. Muhula uliopita, Mwalimu wetu wa hisabati alikuwa anamfundisha masomo ya ziada kwa sababu alikuwa anafanya vibaya katika somo hilo. Lakini baada ya kumfundisha vipindi kadhaa Mwalimu alimtongoza na kumwabia anampenda. Hakuweza kukataa kwa vile alikuwa Mwalimu wake na vilevile aliogopa angemlaumu. Matokeo yake alipata mimba na akafukuzwa Shule. Hata hivyo Mwalimu hajapewa adhabu yoyote. Mimi na marafiki zangu tunafikiria kuwa hii sio haki. Kwa nini Upendo ameadhibiwa peke yake? Kwa kweli, Mwalimu ndiye wa kulaumiwa.tutakuwa na mkutano wa kujadili nini cha kufanya.tunataka Mwalimu aadhibiwe.vilevile tunataka Upendo aruhusiwe kurudi shuleni ili afanye mtihani wa kidato cha nne. Sasa hivi tunafikiria kuandika barau ya malalamiko kwenye Bodi ya shule. Watu wengine wanafikiri hatuwezi kuingilia kati kwa sababu uongozi wa shule na wazazi ndio watakao amua Mwalimu afanywe nini. Lakini, itakuwaje iwapo hawatafanya lolote? Sisi tunaamini kwamba yale tunayoyafanya ni sahihi lakini wao wanasema sio kazi yetu. Shangazi, wewe unafikiriaje? Sikujua

105 MAMBO YA KUJADILIANA Unafikiri Sikujua na wenzake wako sahihi kwa jinsi walivyo hamaki na kukasirika kwa hali iliyojitokeza shuleni kwao? Kwa nini? Unauonaje mpango wao wa kuitisha mkutano? Unafikiri watafanikiwa? Kwa nini? Nini maana ya barua ya malalamiko? barua hiyo itamsaidiaje Upendo? Ni hatua gani huchukuliwa kwa mwanafunzi wa kike akipata mimba katika eneo lenu? Je, anaweza kuendelea na masomo? Je aliyempa mimba naye anapata matatizo yoyote?

106 Mume wangu si Mwaminifu 29 Mpendwa Shangazi Stella Niliolewa miaka miwili iliyopita nikiwa na umri wa miaka 19 na mume wangu wakati huo alikuwa na umri wa miaka 22.Tulipooana tulikuwa tunapendana sana na sasa tumejaliwa mtoto mmoja. Sijawahi kufanya ngono na mtu mwngine yeyote maishani mwangu. Isipokuwa mume wangu Tuli. Lakini miezi sita iliyopita alianza kurudi nyumbani akiwa amechelewa. Pamoja na kuwa alinieleza kuwa alikuwa anafanya kazi lakini ninauhakika ana mpenzi mwingine. Ninaogopa kweli UKIMWI, hivyo nilipata ujasiri wa kumweleza tutumie kondomu. Eh! Alichanganyikiwa na kuanza kunituhumu mimi kwa kutomwamini. Baada ya hapo niligundua kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke mmoja ambaye anaishi mtaa wa tatu kutoka kwetu. Mwishowe Tuli alikubali kuwa anaye mpenzi mwingine. Katika kulizungumzia suala hili alidai angemuacha kwani alikuwa ananipenda mimi sana. Nilipomwambia kuwa sitaweza kufanya ngono naye mpaka pale atakapopima VVU alikataa. Anasema hataki kabisa kusikia wala kujua. Jambo hili limekuwa likiendelea karibu mwezi sasa. Karibu nimfanye alale jikoni, alidai kuwa hakuna mtu anayeweza kumfanyia mume wake hivyo. Shangazi mimi nifanye nini? Bado ninampenda lakini ninaogopa kuambukizwa VVU. Tafadhali nisaidie labda sikutakiwa kuolewa nikiwa bado mdogo. Josephine

107 MAMBO YA KUJADILIANA Josephine aliolewa akiwa na umri wa miaka 19. Je watu katika jamii yenu huolewa katika umri huu au mapema zaidi? Kuna faida na hasara zipi za kuolewa ukiwa kijana? Ni kwa nini wanaume na wanawake hufanya ngono nje ya ndoa? Tayarisha orodha ya sababu na fikiria jibu la kila mojawapo. Katika nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika wanawake walio katika ndoa wako hatarini zaidi kupata maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI. Unafikiri ni kwanini? Je, jamii ina wajibu gani katika hili? Unafikiri Josephine anatakiwa afanye nini? Na Tuli ana wajibu gani? Usikate tamaa mambo mazuri hayataki haraka Imechorwa na David Chikoko

108 Nina msongo wa mawazo? 30 Mpendwa Shangazi Stella Mimi nina umri wa miaka 15. Nina tatizo moja ambalo linanifanya nisononeke sana. Kuna wakati ninapata msongo bila hata sababu za kueleweka. Rafiki zangu huwa na furaha wakati wote lakini mimi hujilazimisha na kujifanya nina raha. Jambo hili ni gumu lakini ninaelewa kuwa nisipowaigiza nitapoteza marafiki. Hivi nina matatizo gani? Tafadhali ninaomba unisaidie. Anna

109 MAMBO YA KUJADILIANA Je,Vijana wengi hujisikia kama Anna? Chora picha ya ngazi.weka sababu kuu zinazowafanya vijana wajisikie vibaya juu kabisa ya ngazi. Halafu weka sababu zingine kwa mpangilio ukielekea chini ya ngazi. Usisahau kusikitika bila sababu kama Anna. Madaktari wanasema kuwa vijana wanaweza kunyong onyea (kusikitika na kukata tamaa) bila sababu yoyote kwa sababu ya mabadiliko ya kikemikali ndani ya miili yao wakati wa ukuaji. Kwa mfano wasichana wanaweza kujisikia vibaya kabla ya kuona siku zao (kuingia mwezini). Ebu linganisha uzoefu wako halafu uone kama hili ni la ukweli. Je, inasadia mtu akifahamu kuwa hisia kama hizo ni za kawaida? Ukishirikisha tatizo, tatizo huwa nusu yake. Methali hii ina maanisha kuwa mtu anatakiwa kuzungumza kuhusu jambo linalomsumbua. Je unakubaliana na ushauri huu kwa ajili ya Anna na watu wengine kwa ujumla?. Anna anatakiwa afanye nini ili aweze kumudu hisia zake? Ni kitu gani kinakusaidia wewe unapojisikia una msongo wa mawazo?

110 Mimba hii, siitaki 31 Mpendwa Shangazi Stella Mimi nina umri wa miaka 16, ninasoma shule na ni mjamzito. Ninataka kujiua. Nimefanya ngono na mpenzi wangu mara chache tu na bado mimba imetokea. Nilipomweleza mpenzi wangu huyo alinijibu kuwa atajuaje kama ni yeye anayehusika. Hataki hata kuzungumza na mimi. Nikiwaeleza wazazi wangu watanifukuza. Mama yangu anajitahidi sana kumlipia ada ya shule kwa hiyo atakasirika sana kwa hili nililolifanya. Kwa kweli mimba hii siitaki na wala sitaki nikatishe masomo yangu. Nimefadhaika sana lakini siwezi kumweleza mtu yeyote. Njia pekee ninayoweza kufikiria ni kutafuta mtu anisaidie nitoe mimba. lakini pesa za kulipia sina.tafadhali nisaidie kutoa uamuzi. Prisila

111 MAMBO YA KUJADILIANA Taja mambo tofauti ambayo Prisila anaweza kufanya ukizingatia kuwa ni mjamzito. Baada ya hapo tengeneza mchoro kama ufuatao kuonyesha madhara yanayoweza kutokea mazuri na mabaya kwa kila moja na yajadili. Ungelikuwa Prisila ungefanya nini? Atapata tatizo la fedha Atampenda mtoto Matatizo ya kiuchumi MABAYA Atakuwa mama akiwa katika umri mdogo IWAPO ATAMLEA MTOTO MAZURI Mtoto hatakuwa amefanya kitendo kibaya cha kuua Prisila anafikiria kutoa mimba. Kuna hatari gani za kutoa mimba? Kwa nini unafikiri rafiki yake Prisila alikata mawasiliano? Unadhani anajisikiaje baada ya tukio hilo. Katika hali hii mvulana huyu na familia yake wanaweza kuchukua hatua gani? Prisila anaweza kutumia utaratibu gani ili kutoa taarifa hizi kwa wazazi wake ili waweze kukubaliana na hali iliyotokea.

112 Dini yangu inakataza matumizi ya Kondomu 32 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 18 na ninampenda kweli rafiki yangu wa kike.tumekuwa tukitoka pamoja kwa muda wa miezi kumi. Hatujawahi kufanya ngono, lakini huwa tunakumbatiana na kubusiana. Ninaelewa kuwa siku za karibuni huenda tutaanza kufanya ngono kwa vile wote tunataka. Sasa ninalo tatizo. Mimi ni mkristo na nimeokoka. Mchungaji wangu hueleza kuwa sio sahihi kutumia kondomu na watu wote wasitumie hata kama ni wanandoa. Anasema haitakiwi kufanya ngono kabla ya kuolewa. Mimi sikubaliani naye kwa sababu kwa vyovyote vile sisi tutaoana baadaye. Kabla sijaokoka nilikuwa nimefanya ngono na wasichana kadhaa. Ninaelewa ilikuwa ni makosa lakini sasa ninampenda sana msichana huyu na ninataka kumuonyesha kuwa ninampenda. Jambo lingine ni kuwa, pale kanisani kwetu watu wanasema kondomu zina matundu madogo sana ambayo hayawezi kuonekana kwa macho na huweza kupitisha VVU. Kwa hiyo haziwezi kumkinga mtu asipate maambukizo. Hii ni kweli? Tafadhali Shangazi Stella nisaidie. Nitafanya nini? Hosea

113 MAMBO YA KUJADILIANA Dini yako inakufundisha nini kuhusu ngono na uhusiano? Andika orodha yake. Je unakubaliana na kila kitu? Ni yapi ambayo hukubaliani nayo? Kwa nini? Hosea ana wasiwasi sana kama kondomu ni kinga kamili ya kuzuia VVU.Wewe unamshauri vipi? Mambo gani yanaweza kuwatokea Hosea na mpenzi wake iwapo watafanya ngono bila kutumia kinga. Ushauri gani utawapa Hosea na mpenzi wake?

114 Ninapata maumivu makali sana wakati wa hedhi 33 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 17. Kila ninapokuwa katika siku zangu za hedhi ninapata maumivu makali sana kiasi cha kushindwa kutembea na hivyo kutokwenda shuleni. Hujisikia kutapika na mara nyingine hujisikia mwili kuwa na joto au baridi. Jambo hili hutokea kila mwezi, kwa hiyo ninapokosa kufika shuleni marafiki zangu wanaelewa ni kwa nini sijaenda shule. Kwa sababu hiyo mimi hujisikia vibaya sana. Ninachukia sana ninapokuwa shuleni katika hali hii kwani hakuna sehemu ya kutupa pedi zilizotumika. Nikitupa chooni ninaogopa choo kitaziba. Ninaona aibu sana watu wanapojua kuwa mimi niko katika siku zangu za hedhi na kwamba watanicheka. Kwa hiyo Shangazi ninaomba unisaidie.wasiwasi wangu ni kwamba, ninakosa masomo sana kwa hiyo ninaweza kufanya vibaya katika mitihani yangu. Agnes Imetokana na picha ya Mkhululi Khumalo

115 MAMBO YA KUJADILIANA Je, kuna wasichana wengine ambao hukosa shule kwa sababu ya kuwa katika siku zake za hedhi? Kwa nini? Suala hili linaweza kuathiri namna gani elimu yao? Je,Agnes anatakiwa kuchuka hatua gani kuhusiana na maumivu anayoyapata wakati anapokuwa katika siku zake za hedhi? Elezea mambo yote unayoyafahamu ambayo unadhani yanaweza kumsaidia Agnes. Agnes na rafiki zake watafanya nini ili kuhakikisha kuwa kila mara ndoo au pipa la kutupia pedi zilizotumika lipo katika choo cha wasichana? Je, wewe (msichana au mvulana) au rafiki zako mmewahi kumcheka msichana ambaye yuko katika siku zake? Kwa nini? Unafikiri ni kwa nini Agness anajisikia vibaya watu wakijua kuwa yuko katika siku zake za hedhi? Hivi wasichana wengi hujisikia hivyo? Wewe na marafiki zako mnaionaje hali ya kuwa katika siku za hedhi:- kwamba ni uchafu na ni jambo la aibu ni jambo zuri na ni sehemu ya kwaida ya kuwa mwanamke au ni kitu kingine kabisa Je mitizamo hii inasaidia au ni mibaya kwa maisha yenu? Kama ni mibaya, unaweza kubadilisha vipi?

116 Buzi langu hunifanyia vituko 34 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 16. Niliacha kuendelea na masomo kwa sababu nilitaka kuwa mwana mitindo. Mpenzi wangu ni mfanya biashara na vile vile analo shamba kubwa. Nilikutana naye miezi mitatu iliyopita kwenye baa yake, ndipo aliponieleza kuwa ananipenda. Marafiki zangu walinishauri nikubali awe rafiki yangu kwa sababu ana pesa, gari na simu ya mkononi. Walisema mabuzi ni wazuri kwa sababu hutoa zawadi ya nguo na chakula kizuri kama nyama ya kuku. Tulipoanza, alikuwa ananipa zawadi na kuahidi angenisaidia katika ndoto yangu ya kuwa mwana mitindo. Aliwahi hata kumwajiri mdogo wangu katika shamba lake. Tulitumia gari lake kila tulipokwenda kutembea na wakati mwingine tulikaa hotelini. Siku hizi anataka ngono tu na kuondoka. Nikimwomba kitu chochote ananifokea na kuniita malaya. Wiki iliyopita nilimwomba tutumie kondomu kwa sababu ni salama lakini badala yake alikasirika na tulipofanya ngono aliniumiza sana. Alinieleza kuwa iwapo ninapenda zawadi basi niwe tayari kufanya naye ngono bila ya kondomu. Aliahidi kunitafutia dawa za kienyeji kama nitahitaji, lakini mimi ninaogopa. Mpaka sasa hivi hajazungumzia lolote kuhusu mimi kuwa mwana mitindo. Shangazi, mimi nifanyeje? Nilipompata nilijigamba sana kwa marafiki zangu ili waone wivu. Sasa watanicheka na kusema yuko wapi uliyekuwa unajidai naye iwapo nitaenda kuomba ushauri kwao. Huruma

117 MAMBO YA KUJADILIANA Mkiwa katika vikundi ya watu wawili, chora picha ya buzi na mpenzi wake. Ukipenda unaweza kuongezea kielelezo ili kufafanua zaidi kwa undani. Kila kikundi kielezee picha yake kwenye kikundi kikubwa. Kwa nini wanaume watu wazima hupenda kutafuta wasichana wadogo kama Huruma wawe wapenzi wao? Kwa nini wasichana balehe wanapenda kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mabuzi? Je zipo sababu ambazo ni nzuri na ambazo ni mbaya? Ni ushauri gani unaweza kuutoa kwa Huruma?

118 Ninashindwa kujisomea kwa sababu ya mapenzi 35 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 17. Ninaye rafiki wa kike shuleni kwetu ambaye ninampenda sana. Ninategemea kufanya mitihani ya Kidato cha nne mwaka huu na ningependa nifanye vizuri. Lakini sasa, ninampenda msichana huyu kiasi cha kwamba imeniathiri katika masomo yangu. Kila kitu nakiona ni shida tupu, hata kusoma vitabu, kwani kila mara ninakuwa ninamuwaza yeye. Kuna wakati niliamua niachane naye lakini nilishindwa kwa sababu hajanikosea kitu chochote. Sasa, nifanye nini? Tafadhali nisaidie Shangazi, nina wasiwasi sana ninaweza kushindwa mitihani yangu. Ninaomba ushauri. Jafari

119 MAMBO YA KUJADILIANA Je, unafikiri tatizo la Jafari ni la kawaida kwa vijana walioko shuleni? Je, umewahi kugundua kwamba mapenzi yaliwahi kukufanya upoteze hamu katika kitu kingine chochote? a Ilikuchukua muda gani? b Ulipata njia ya kudhibiti hali hiyo? c Mwisho wa yote kitu gani kilitokea? Ni ushauri gani unaweza kutoa kwa Jafari? Afanye nini iwapo anataka kuwa na mpenzi wake lakini bado afaulu mtihani wake? Soma shairi hili lililotungwa na Laura na Monica. Je umewahi kujisikia hivyo? MAPENZI NA KUJIFUNZA Mkono wangu umekwama siwezi kuandika kitu isipokuwa jina lako ndilo lenye maana. Kichwa kinasema jifunze. Moyo wangu unasema Paulo Yote ya muhimu yamekwenda nyuma ya ukuta wa moshi wa mapenzi yanayoungua yakitia wingu katika maisha yangu na Elimu yangu. Aisee! Mapenzi hayatanisaidia kupata kazi nzuri au kukwepa ubaya. Ni lazima nizinduke, niondoke kwenye utata huu. Laura Moyo and Monica Masukusa

120 Mama yangu ana maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI na yuko wazi kusema 36 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mvulana mwenye umri wa miaka 22. Mama yangu anaishi na VVU na yeye mwenyewe husema hivyo waziwazi. Yeye anafanya kazi katika shirika moja linaloshughulikia masuala ya UKIMWI. Mama husema hakuna haja ya kuona aibu kwa sababu ya VVU/UKIMWI. Yeye husema kwa nini nifiche? Tunaoishi na VVU tunahitaji upendo,kukubalika na kila mtu. Mama aliponiambia ana maambukizo ya VVU, mimi nilikuwa ninasoma darasa la nne. Mwanzoni niliogopa sana. Nilifikiri mama yangu angelikufa wakati wowote, lakini sasa hivi ninaelewa kuwa unaweza kuwa na maambukizo ya VVU na ukaishi kwa muda wa miaka mingi ukiwa na afya nzuri. Mama ameishi na VVU kwa muda wa miaka 12 sasa. Anajihudumia kwa kula chakula kizuri na kupumzika, kwa hiyo mara nyingi afya yake ni nzuri. Mama anasema tunatakiwa kuwa wawazi kuhusu VVU na UKIMWI na kuvunja uoga kwa kila mtu ili kila mtu aweze kuwahudumia vizuri wale wenye maambukizo. Mimi sikubaliani naye, watu wana mtazamo mbaya kuhusu UKIMWI kwa hiyo haina maana kuwaeleza. Ndugu wa karibu wanaweza kuelezwa lakini nao pia itabidi wasiseme kwa watu wengine yaani iwe siri. Jambo moja ambalo tunakubaliana ni kuwa, watoto lazima waelezwe kwa sababu, kwa vyoyote vile watajua tu. Ni muhimu wafahamu ukweli ili waweze kuzungumzia jambo hilo. Kwa hiyo Shangazi, wewe unalionaje jambo hili? Ninampenda sana mama yangu na ninajivunia kuwa naye. Lakini; nani kati yetu ni sahihi? Hamisi

121 MAMBO YA KUJADILIANA Unafikiri nini faida au hasara ya kuwaeleza watu kuwa una maambukizo ya VVU. Andika katika safu mbili. Kama ungegundua una maambukizo ya VVU / UKIMWI ungemweleza nani Mnasihi, Familia yako, Marafiki, Wafanya kazi wenzako au wengine kama akina nani? Ni nani usingemwambia kabisa? Kwa nini? Wazazi wako walipojaribu kukuficha kitu ulipokuwa ungali mdogo ulijisikiaje? Waeleze walio katika kikundi chako kuhusu hisia zako, na usieleze kuhusu siri yenyewe. Je unakubaliana na wazo la kuwa watoto waambiwe ukweli hata kama ni jambo la kuhuzunisha? Wazazi wanaweza kuwasaidiaje watoto wao kukubali kuwa wana maambukizo ya VVU? Jadili na wenzako halafu angalia uwezekano wa kupata taarifa zaidi kutoka katika shirika linaloshughulikia UKIMWI katika eneo lenu. Imechorwa na David Chikoko

122 Je nitazitibu vipi chunusi zangu? 37 Mpendwa Shangazi Stella Mimi nina umri wa miaka 15.Tatizo langu ni kwamba nina chunusi usoni kwangu ambazo zinaniuma sana ninaponawa uso. Hali hii ilinianza tangu nikiwa na umri wa miaka 14.Tangu hapo sijapata unafuu wowote Siku moja nilimwuliza Shangazi yangu kuhusu suala hili naye aliniambia kuwa ni dalili ya kubalehe. Hakujua namna ya kunitibu. Pamoja na kwamba nimejaribu kuwauliza watu wengi, mpaka sasa sijapata msaada wowote. Niliwahi kumwuliza muuguzi pale kliniki naye alinielekeza kuwa nioshe uso na sabuni ambayo sio kali na nimekuwa nikifanya hivyo. Kinachonishangaza mimi ni kwamba, badala ya chunusi kupungua, zinaongezeka, na kufanya uso wangu uchukize. Mara nyingine hujisikia kuwa mbaya sana kiasi cha kushindwa kutoka na marafiki zangu.tafadhali Shangazi nisaidie kuchagua losheni (mafuta) mazuri ya kupaka kabla sijaenda kwa Waganga wa kienyeji. Joan

123 MAMBO YA KUJADILIANA Je, Unafikiri chunusi za Joan zinatokana na nini? Ni kitu gani kinaweza kupunguza au kufanya chunusi zisiongezeke? a Kuna vyakula ambavyo ni vizuri au vibaya kwa ngozi yako? b Kuna vinywaji ambavyo ni vizuri au vibaya kwa ngozi yako? c Kuna sabuni au losheni ambazo ni nzuri au mbaya kwa ngozi yako? d Je una mengine ya kuongezea? Ni nani anaweza kusaidia katika hili, ni Daktari, Mtaalam wa mitishamba, Mganga wa kienyeji au Mtu mwingine yeyote? Imechorwa na David Chikoko

124 Nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI na mimba 38 Mpendwa Shangazi Stella Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 21. Nina mimba ya miezi sita. Mume wangu aliugua kwa muda mfupi na amefariki siku za karibuni. Sasa hivi ninaishi na wazazi wangu. Nilipo kwenda kliniki kupima mimba kwa mara ya kwanza Muuguzi aliniambia kuhusu mpango wa kupima VVU. Mimi nilikubali kupima. Nilipata majibu siku hiyo hiyo kuwa nilikuwa na maambukizo ya VVU; pamoja na kwamba nilikuwa sijawahi kuugua. Nilisikitika nilipopata majibu hayo, hasa kwa sababu ya mtoto. Nisingependa nimwambukize VVU. Muuguzi alinieleza kuwa wanaweza kunipa dawa inayoitwa Nevirapine kwa ajili ya kumsaidia mtoto asipate maambukizo.vile vile alizungumzia kuhusu kunyonyesha mtoto kwa muda mrefu. Sikuweza kuelewa kitu chochote alichoniambia kwa vile nilikuwa ninalia wakati wote. Sasa Shangazi, nifanye nini ili nimsaidie mtoto wangu? Je, atazaliwa akiwa mgonjwa? Mimi nina maambukizo ya VVU, Je ni salama kumnyonyesha mtoto? Rehema

125 MAMBO YA KUJADILIANA Je Rehema yuko sahihi kuwa na wasiwasi kuhusu mtoto? Kitu gani hutokea mama mjamzito anapokuwa na maambukizo ya VVU? Je maambukizi kwa mtoto hutokea wakati gani? Je, nini faida na hatari ya kumnyonyesha mtoto wakati una maambukizo ya VVU? Ungetoa ushauri gani kwa Rehema? Katika utamaduni wenu, nini mtazamo wa jamii kwa mama ambaye hamnyonyeshi mtoto? Watu wanatakiwa wafanye nini ili wabadili mtazamo hasa kwa wanawake ambao wanachagua kufanya hivi.

126

127 Shangazi Stella Vijana wanazungumza kuhusu ngono, maisha na uhusiano KADI ZA MAJIBU

128 Je ninaweza kufanya naye mapenzi? 1 Mpendwa Zaituni Ni vigumu sana watu wawili wanapokuwa na malengo tofauti lakini kama wahenga wasemavyo:- Subira yavuta heri / haraka haraka haina baraka.watu wengi huamua kutofanya ngono mpaka watakapokuwa wakubwa au watakapokuwa wameoa au kuolewa. Uamuzi wa namna hii una faida zake, ukiwa mkubwa unakuwa tayari kijinsia kuwa katika uhusiano wa kimapenzi. Vilevile unakuwa hauko katika hatari ya kupata maambukizo ya magonjwa ya ngono,vvu na mimba zisizotarajiwa. Kwa sasa hivi ni vizuri mkaishia kukumbatiana na kubusiana basi, na msiendelee zaidi ya hapo. Hii ni njia nzuri ya kuonyeshana kwamba mnapendana. Usihofu, wavulana na wasichana wanaweza kuishia katikati bila ya kupata madhara yoyote ya kiafya. Hata hivyo vijana wengi huamini kwamba watu wakianza kushikana shikana na kubusiana ni lazima waishie kufanya ngono. Kwa hiyo ni vizuri msikae peke yenu.waalike marafiki zenu mfurahi pamoja badala ya kuwa wawili tu mkikumbatiana na kubusiana. Mwisho, lazima vijana waamue lipi ni sahihi kwao bila ya kupata shinikizo kutoka kwa mtu mwingine. Mweleze mpenzi wako msimamo wako, kama anakupenda kweli, atakuelewa. Iwapo utaamua kufanya ngono baadaye, hakikisha mnatumia kondomu. Zungumzia suala hili na mpenzi wako mapema kwani ni vigumu kuelewana ukisubiri mpaka dakika za mwisho. Kumbuka, wasichana wanaweza kupata kondomu za kike na za kiume. Kila la kheri. Shangazi Stella

129 MAMBO YA KUFANYA Je, unafikiri inawezekana kukumbatiana na kubusiana halafu mnaishia hapo bila ya kufanya ngono? Kama siyo, wewe ungefanyaje? Ungelikuwa Zaituni ungeishia wapi ili ufurahie kuwa na mpenzi wako, lakini usifikie hatua ya kuhemka mpaka ufanye mambo ambayo usingependa kuyafanya? JARIBIO:Tupo tayari kufanya ngono? Fanya jaribio hili peke yako au na mpenzi wako. Jibu ndiyo, hapana au sijui. 1 Je, tunafahamiana vizuri na kuaminiana? 2 Je, sisi ni marafiki wazuri? 3 Je, tunaweza kuzungumzia ngono bila woga wowote na wapi tunataka kufikia? 4 Je, tumezungumzia na kukubaliana suala la jinsi ya kujikinga tusipate mimba, magonjwa ya ngono na VVU? 5 Je, tumejadiliana suala la kupima VVU kabla ya kuanza ngono? 6 Je, tumezungumzia tutafanya nini iwapo msichana atapata mimba? MAJIBU: Kama ulijibu hapana au sijui kwa swali lolote kati ya haya huenda wewe na mpenzi wako hamko tayari kufanya ngono. Huu ni uamuzi mzito Katika vikundi, andika sababu zinazosababisha vijana waanze kufanya ngono. Halafu orodhesha sababu zote zinazowafanya wengine wasubiri kufanya ngono mpaka wawe watu wazima. Ni sababu gani ungependa kuichagua na toa maelezo

130 Je Uume wangu ni mdogo sana? 2 Mpendwa Peter Usijali kwa sababu huna tatizo lolote. Uume huanza kukua wakati wa balehe, kipindi ambacho hutokea mvulana anapofikisha umri kati ya miaka 11 hadi 15. Hata hivyo wengine huanza mapema na wengine huchelewa. Ni jambo la kawaida vijana wa kiume kulinganisha ukubwa wa uume, lakini, kwa vile kila mtu hufikia kipindi cha balehe kwa wakati tofauti ni kawaida kabisa kwa wavulana wa umri ulio sawa kuwa na uume wenye ukubwa tofauti. Hata kama mwili umekua na kufikia mwisho, hakuna ukubwa wa uume ulio sahihi au ukubwa wa uume wa kawaida.watu wana ukubwa tofauti kwa hiyo hata ukubwa wa uume hutofautiana. Vilevile hakuna uhusiano wowote kati ya ukubwa wa uume na jinsi mtu anavyomfurahisha mpenzi wake wakati wa kufanya ngono. Siri ya mafanikio ni jinsi unavyoutumia uume wako na sehemu nyingine za mwili ili kumfanya mwenzi wako na wewe mwenyewe hujisikia vizuri. Kwa kawaida wanawake wanahitaji kushikwa shikwa na kubusiana kabla ya uume kuingizwa ndani ya uke kwa sababu wanawake huchelewa kupata ashiki, kuliko wanaume.vilevile watu hufurahia ngono iwapo wanafanya na mtu ambaye anajalia, na anajitahidi kugundua yale wanayoyapenda na yale wanayo yachukia. Ni rahisi sana kuwa na uhusiano wa namna hii unapokuwa umefikia umri mkubwa na uko tayari kuzungumzia kile unachokitaka. Shangazi Stella

131 MAMBO YA KUFANYA Ukubwa wa uume sio muhimu sana, katika uhusiano wenye furaha lakini ni nini hasa? (Fikiria haiba yako na jinsi matendo yako yalivyo, sio tu jinsi unavyoonekana). Andika jina lako juu ya karatasi na pitisha kwenye kikundi chako. Utakapopata karatasi la mwingine andika kila kinachokuvutia kuhusu wao. (kwa mfano tabasamu yako ni nzuri sana, ninapenda mabega yako yalivyo na nguvu, nywele zako ni nzuri sana). Unaweza kutia saini yako ukitaka. Karatasi lako litakapokurudia utakuwa umejua wenzako wanapenda nini kutoka kwako. Je kuna mtu yeyote katika jamii yako ambaye yuko tayari kukupatia ushauri unaofaa kuhusu masuala yanayohusu mwili wako, ngono na uhusiano kutoka ndani ya familia, shuleni, kliniki au kanisani? Jaribu kujadili na kuangalia, kati ya sehemu hizi wapi wana huruma na wanasaidia. Unayo haki ya kuuliza swali lolote na kupata jibu sahihi na msaada kwa vitendo. Iwapo hakuna taarifa na huduma za kutosha kwa ajili ya vijana katika eneo lenu utachukua hatua gani? Je kuna kituo chochote cha vijana karibu na kwenu au unaweza kuanzisha kimoja? Jadili na wenzako halafu chagua lile ambalo linawezekana kulitekeleza.

132 Hivi ni lazima nifanye ngono na shemeji yangu? 3 Mpendwa Patrisia Shemeji yako anadanganya kuhusu utamaduni. Katika mila na desturi za makabila mengi ya Tanzania siyo sahihi kulala au kufanya ngono na mume wa dada yako. Unayo haki ya kukataa. Huyo ana nia ya kukuharibia maisha. Mwombe Shangazi, rafiki wa familia au mtu mzima yeyote ambaye anaweza kukuhurumia akusaidie katika jambo hili. Ukipata msaada itakuwa rahisi kushughulikia jambo hili. Mweleze dada yako pia. Nchini Tanzania, mtu yeyote ambaye anafanya ngono na msichana au mvulana chini ya miaka 16 anafanya kosa la jinai. Mtu anayepatikana na kosa hili anaweza kufungwa. Kumlazimisha mtu wa umri wowote kufanya naye ngono ni kubaka.taarifa inatakiwa kupelekwa kituo cha polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe. Upo uwezekano mkubwa wa kupata mimba, maambukizo ya magonjwa ya ngono, ikiwa ni pamoja na VVU. Utamaduni wetu ni mzuri sana. Hutuweka pamoja kama familia na jamii moja. Watu hawatakiwi kutumia utamaduni wetu kama sababu ya kuwatendea watu wengine vibaya, hasa vijana. Shangazi Stella

133 MAMBO YA KUFANYA Zipo mila na desturi nchini Tanzania zinazowahusisha vijana na ngono. Kwa mfano unyago, kupima ubikira, kurithi wanawake na nyingine nyingi. Orodhesha za kwako nyingine. Baada ya kupata orodha hiyo, jadili na kuchagua ni zipi unazipenda na zipi huzipendi. Kwa mfano, ni zipi zinasaidia kuenea kwa VVU na ni zipi zinazuia kuenea kwa VVU? Je, mila na desturi katika utamaduni wenu zinamjali mtoto wa kiume na wa kike sawa? Ikiwa siyo, unajisikiaje kuhusu jambo hili. Unadhani unaweza kusaidiaje? Ni kwa namna gani unaweza kushirikiana na Viongozi wa jadi na Wazee kubadili mila na desturi ambazo zinawadhuru vijana siku hizi? Unadhani ni nani mwingine anaweza kusaidia? Kila jamii huathiriwa sio tu na utamaduni uliopo bali vilevile hata mambo mapya yanayokuja kutoka nje. Andika orodha inayoonyesha mambo ya kiutamaduni na mambo ya kisasa unayoyapenda zaidi. Je, unaweza kuchagua moja bora zaidi kutoka katika kila tamaduni ili yakupe mwongozo katika maisha yako?

134 Ninamhudumia mtu mwenye UKIMWI (MVIU) 4 Mpendwa Petronila Kwanza kabisa hakuna haja ya wewe kuondoka nyumbani kwa sababu huwezi kupata madhara yoyote. Kipindi hiki ambacho mjomba wako anaumwa anahitaji msaada wa kuwa na watu kwa karibu. Zipo njia kuu tatu ambazo mtu anaweza kupata maambukizo ya VVU: Ngono zembe na mtu aliye na maambukizo; kupitia damu iliyo na VVU ambayo mtu anaweza kuongezwa iwapo ana upungufu wa damu na anaumwa au sindano na nyembe ambazo hazikutasishwa, au kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa mimba, kujifungua au wakati wa kunyonyesha. Huwezi kuambukizwa VVU kwa kutumia sahani, taulo au choo pamoja na mgonjwa wa UKIMWI. Hata kulala naye chumba kimoja huwezi kupata maambukizo ya VVU. Hatari kidogo inaweza kuwepo iwapo mikono yako ina michubuko au vidonda na kukatokea mgusano wa moja kwa moja na damu au majimaji toka kwa mtu aliye na maambukizo ya VVU. Ili kujihakikishia usalama, unashauriwa kutumia glovu au mfuko wa nailoni wakati wa kusafisha kitu chochote chenye damu au maji maji yenye damu.wakati wote hakikisha unaosha mikono na mashuka machafu kwa kutumia maji na sabuni. Unaweza kutumia dawa yoyote ya kutolea madoa, kwa mfano JIK ukitaka. Kazi ya kumhudumia mgonjwa ni ngumu, kwa hiyo unahitaji uvumilivu na msaada.yapo mashirika na watu binafsi ambao hutoa msaada wa dawa na ushauri katika maeneo mengi.wanaweza kuzungumza na wewe kuhusu wasi wasi wako.wakati mwingine hutoa msaada wa chakula na ada ya shule. Kwa hiyo, kumbuka ya kuwa mjomba wako anahitaji msaada na kumhurumia. Usiogope. Shangazi Stella

135 MAMBO YA KUFANYA Katika familia nyingi, wanawake ndio wanaowajibika kutunza wagonjwa.wanaume na vijana wana wajibu gani? Kwa nini unafikiri kuna umuhimu wa kuwashirikisha? Tayarisha orodha ya mambo ambayo unaweza kuyafanya ili kuwasaidia wanaoumwa. Kwa mfano: Kusaidia kufanya usafi mahali wanapoishi, kuzungumza nao, kucheza na watoto au kuwasaidia katika kazi za shuleni, kutafuta kuni na kupika chakula. Tafuta mashirika,taasisi za Kidini au Kliniki zilizopo katika eneo lako ambazo zinatoa msaada kwa familia zinazohudumia watu wanaoishi na VVU/UKIMWI. Je, kuna ambazo zinatoa mafunzo ya huduma kwa wanaoishi na VVU majumbani? Je ungependa uyapate mafunzo hayo? Unaweza Ukaanzisha au ukajiunga katika kikundi cha vijana wanaowatunza watu wanaoishi na VVU kwa ajili ya kubadilishana mawazo, kuelezana mafanikio na kuondoa wasi wasi. Katika kikundi chako, eleza sababu zinazosababisha vijana wengi kupata maambukizi ya VVU. (zingatia mila na desturi, na matatizo mengine kama umasikini, kukosa kazi, huduma za hospitalini zisizo rafiki kwa vijana na mengineyo). a Kati ya matatizo haya ni yapi unaweza kuyapatia ufumbuzi?. b Kati ya matatizo haya ni yapi ambayo ni matatizo makubwa ambayo yanahitaji mashirika makubwa yenye uwezo kuchukua changamoto. c Je, vijana wanao wajibu wa kuyasaidia mashirika makubwa? Ni kwa namna gani unaweza kujikinga wewe na watu wengine wasipate maambukizo ya VVU.

136 Hivi sasa mimi ni mkuu wa Kaya Yangu 5 Mpendwa Upendo Ninakuonea huruma kwa kuwa mama yako hakuacha wasia. Kwa hakika angeacha wasia, maisha yako yasingekuwa magumu kiasi hicho. Ni aibu kwa Wajomba zako kuchukua mali za familia. Katika umri wako hutakiwi kushughulikia mambo haya peke yako. Katika kila jamii wapo watu binafsi na mashirika ambayo hutoa huduma kwa vijana ambao wamefiwa na wazazi wao. Jaribu kuwatafuta na kuomba msaada. Omba ushauri kutoka kwa Mchungaji / Sheikh wako. Zungumza na watu au mashirika yaliyopo katika eneo lenu hasa vikundi ambavyo hutoa msaada kwa familia ambazo zimeathirika na UKIMWI. Omba msaada kwa Wakuu wa shule,wauguzi,viongozi wa jadi na Maafisa wa serikali ngazi ya Wilaya. Usikate tamaa na wala usione aibu kuomba msaada kwa sababu vijana wote wanayo haki ya kuhudumiwa na kupata chakula, nguo, mahali pa kuishi, elimu na usalama wa maisha. Ni kweli vijana wengi wako katika hali kama hiyo ya kwako. Zungumza nao. Unayo mambo mengi ya kuwashirikisha, kwa mfano yanayohuzunisha, mapambano na yale ambayo unayashinda. Unaweza vilevile kubadilishana nao taarifa na maoni mbalimbali kuhusu matatizo yako. Panga shughuli ya pamoja, kama vile kuanzisha bustani. Omba msaada wa vitu mnavyohitaji kutoka serikalini au mashirika binafsi. Ukifanya shughuli katika kikundi utakuwa na nguvu na mafanikio zaidi kuliko kufanya peke yako. Ninakutakia kila la kheri wewe, kaka na dada zako. Shangazi Stella

137 MAMBO YA KUFANYA Watoto wanahitaji upendo, chakula, mahali pa kuishi, elimu na maisha ambayo yana usalama. Je, katika eneo lenu kuna vijana wengi ambao wana wazazi au hawana wazazi na hawapati huduma hizi? Je, wanaishije? Katika eneo lenu, watoto na vijana ambao wana matatizo kama ya kukosa upendo wanatakiwa waende wapi kuomba msaada?. Je, unadhani wanapata msaada wa kutosha? Kama sio, jamii ikiwa ni pamoja na wewe mnapaswa kufanya nini ili kurahisisha maisha yao? MCHEZO:Tengeneza mchezo wa kuigiza ambao utahusisha kikundi cha vijana yatima ambao wamealikwa kwenye mkutano wa Kamati ya Afya ya Wilaya au Kamati Shirikishi ya Kudhibiti UKIMWI ya Serikali za Mitaa kujadili msaada wanaouhitaji kutoka kwenye jamii. Amua watu wengine ambao wanatakiwa kuwepo kwenye mkutano, kama muuguzi, wawakilishi wa serikali, mtu mmoja kutoka shirika linalotoa huduma kwa watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi. Baada ya igizo, jadili maswali yafuatayo: a Mambo gani yalijitokeza katika mkutano? Je vijana walisikilizwa? Kwa nini? b Vijana watahakikishaje kwamba huduma za kiafya na kijamii zinalenga katika mahitaji na maoni yao? Ni msaada gani unahitajika ili mambo haya yafanyike na nani anaweza kuutoa?

138 Ninataka kufanya ngono kama rafiki zangu 6 Mpendwa Maulid Kwa hakika huhitaji dawa ya mapenzi ili mtu akupende. Ni raha iliyoje kupenda mtu, lakini huwezi kulazimisha itokee, hutokea tu. Katika umri wako, ni watu wachache ambao huanza kutafuta marafiki wa kike au wa kiume. Hata hivyo wengi huwa hawajihusishi mpaka baadaye sana. Hata inapotokea kuwa wanampenda mtu haimaanishi kwamba lazima wafanyenaye ngono. Usijali sana kuhusu maneno wanayosema marafiki zako. Kumbuka ya kuwa wengi wao hawasemi kweli. Mara nyingi vijana wengi hujisifu kuhusu uzoefu wao wa kufanya ngono, wakati ukweli ni kwamba hawajawahi kufanya hivyo.vilevile hakuna haja ya kufanya yale yote ambayo marafiki zako hufanya. Jaribu kufuata hisia zako au jiamini mwenyewe zaidi. Kwa hiyo basi, acha kuwa na wasiwasi bali furahia maisha yako ya peke yako mpaka utakapo mpata msichana umpendaye. Muda ukifika, ukosefu wa uzoefu hautakuwa na nafasi. Kwa sasa hivi ni vema ukalenga katika masomo yako. Tafuta mambo mengine unayoweza kufanya na jifunze kuwaheshimu na kuzungumza vizuri na wasichana bila ya kuwa na wasiwasi kuhusu mapenzi. Muda si mrefu mambo yatakuendea vizuri. Shangazi Stella

139 MAMBO YA KUFANYA Orodhesha mambo ambayo wewe huyafanya ili mradi ufanane na rafiki zako.amua kati ya hayo yapi ni mazuri na yapi ni hatari. Je ungependa kuacha kufanya yale ambayo ni ya hatari? Jadili na kundi lako jinsi ambavyo utafanya ili kuacha mambo hayo. Jipatie alama chini ya 10 kujipima mwenyewe kuhusu kujiamini. (kiasi gani unajiamini mwenyewe na uamuzi wako) Mwulize rafiki yako wa karibu iwapo anakubaliana na alama ulizojipatia. Iwapo alama yako ni ya chini unadhani ni kwa namna gani mnaweza kusaidiana ili kuwa jasiri. Iwapo alama ni ya juu, utakuwa na uhakika gani kuwa huwa unasikiliza maoni ya watu wengine? Eleza mambo mazuri yote yanayokuhusu wewe, ikiwa ni pamoja na ubora wako. (kwa mfano, mimi ni mkweli, nina huruma, ninaweza kutatua matatizo) na mengine mengi ambayo unaweza kufanya (ninaweza kucheza dansi vizuri, ninaweza kulima, mimi ni mchezaji bora, ninaweza kusimulia hadithi kwa watoto.) Weka orodha hii mahali peupe ili ukikumbuka jambo lingine uweze kuongezea. Je, ni jambo la kawaida kwa wavulana na wasichana unaowafahamu kuwa na uhusiano wa urafiki tu? Je ungependa hili litokee mara kwa mara? Kama hivyo ndivyo, kwa kutumia kundi mchanganyiko wa wavulana na wasichana fanya uamuzi wa kufanya shughuli mbili au tatu pamoja kwa wiki hii. Mwisho wa wiki jadili mliyojifunza kuhusu uhusiano wa kuwa marafiki.

140 Niliambukizwa ugonjwa wa ngono! Je, nimekuwa tasa? 7 Mpendwa Mwanahamisi Una bahati sana. Rafiki yako wa kiume asingekueleza kuhusu kuwa na maambukizo ya magonjwa ya ngono usingejua kuwa umepata maambukizi, Lakini kwa vile ulipata matibabu haraka sio rahisi kupata matatizo. Watu wengi hawana bahati kama ya kwako. Mara nyingi wanawake hawaonyeshi dalili zozote za maambukizi ya magonjwa ya ngono kwa muda mrefu na zaidi ya hapo huwa hawaelewi kama kuna tatizo lolote. Iwapo mtu hajatibu magonjwa ya ngono mapema, mirija iliyopo kwenye via vya uzazi inaweza kupata maambukizi na kuziba. Matokeo yake anaweza kushindwa kutunga au kutungisha mimba (kuwa tasa). Jinsi ambavyo mara kwa mara unapata maambukizi ya magonjwa ya ngono ndivyo ambavyo uwezekano wa kuwa tasa unavyokuwa mkubwa, na hatari ya kupata VVU inaongezeka. Kwa hiyo ni vema kutumia kondomu kila unapofanya ngono. Vilevile magonjwa ya ngono sio kisababishi pekee cha utasa. Matatizo mengine ya afya yanaweza kusababisha utasa. Wanandoa wanapokosa watoto ni vizuri wakaliona tatizo hilo kuwa ni lao wote na wakashirikiana kulitatua. Kliniki za Uzazi wa mpango zinaweza kusaidia katika hili. Jamii zetu mara nyingi humlaumu mwanamke inapotokea kwamba mtoto hapatikani. Lakini ukweli ni kwamba nusu ya wale wanaopata, tatizo hili husababishwa na wanaume. Watu ambao wana matatizo ya kupata watoto wanahitaji msaada na wala sio kukataliwa katika jamii. Ni matumaini yangu taarifa hii itakusaidia. Shangazi Stella

141 MAMBO YA KUFANYA Watu wanasemaje kuhusu wanaume ambao hawawezi kupata watoto? Na kwa wanawake Je? Tayarisha orodha mbili na linganisha iwapo hisia zinafanana au zinatofautiana. Ni nani ambaye anaonewa huruma zaidi? Unafikiri ni kwa nini? Jadili njia ambazo unaweza kuonyesha kuwa unawajali watu ambao ni tasa. Unaweza kuboresha vipi mtizamo wa jamii katika suala hili? Iwapo wewe na mwenzi wako mlipanga kuzaa watoto lakini imeshindikana. Je, mnaweza kufikiria kumchukua mtoto ambaye hana wazazi mkae naye na kumlea? kwa nini? Katika eneo lenu, watu wana hofu gani katika kulea mtoto ambaye amefiwa na wazazi wake na hasa yule aliye nje ya familia yako? Angalia kadi ya 13 na 25 kwa ajili ya taarifa za ziada kuhusu maambukizo ya magonjwa ya ngono?

142 Mwalimu wangu anataka kufanya ngono na mimi 8 Mpendwa Zawadi Upo sahihi kabisa kukataa matakwa ya Mwalimu ambayo hayafai kabisa.watu wengi watakubaliana na mimi kwamba Mwalimu huyu hafai kabisa kufundisha katika shule yoyote nchini baada ya kuonyesha tabia ya namna hii.tafadhali Zawadi, usiache kwenda kwenye vipindi vyake, lakini hakikisha unachukua hatua haraka kabla hajakudhuru. Udhalilishaji wa kijinsia ni makosa, mweleze rafiki yako, wazazi wako au mwalimu mwingine ili upate msaada. Iwapo unafikiri hakuna ambaye atakuamini, mweleze rafiki yako wa karibu na hakikisha kuwa Mwalimu atakapokuomba ubaki, rafiki yako naye anabaki. Mwalimu akisisitiza kuwa wewe unabaki peke yako hakikisha rafiki yako anabaki karibu na eneo hilo kiasi cha kusikia yanayozungumzwa. Iwapo Mwalimu atarudia tabia yake, piga kelele kwa nguvu na mwombe rafiki yako awe shahidi kwa yaliyotokea. Toa taarifa kwa Mkuu wa shule mara moja. Unatakiwa kuwataarifu polisi au shirika linalowasaidia watoto ambao wanatendewa vibaya, wanapigwa au wanadhalilishwa kijinsia. Shangazi Stella

143 MAMBO YA KUFANYA Iwapo Mwalimu au mtu yeyote mkubwa amekufanyia jambo lolote kama hili au amemfanyia rafiki yako, mweleze mtu anayeaminika, na toa taarifa kituo cha polisi mara moja. Katika nchi za Afrika, ya mashariki na kusini watoto na hata watu wazima wanaweza kupata msaada iwapo watapiga simu za dharura/hatari. Ni bure na hazina malipo yoyote. Unaweza kuwapata ukiwa mahali popote nchini.tafuta jina anuani, na namba ya simu ya msaada katika eneo lako. Piga simu au waandikie iwapo unahitaji msaada wa polisi, hospitali au moto.vilevile Waambie marafiki zako kuhusu yote haya. Mwalike Afisa wa Polisi au mtu yeyote kutoka shirika ambalo linashughulikia masuala ya vijana kuja shuleni kwenu kuzungumzia kuhusu ubakaji na aina nyingine za udhalilishaji wa kijinsia. HAPAAANA!

144 Mpenzi wangu ni mjamzito 9 Mpendwa Bakari Wakati mwingine watu hujifunza mambo magumu kutokana na makosa katika maisha.watu wote hufanya makosa.wengine makosa yao ni makubwa kuliko ya wengine. Njia nzuri zaidi ya kufanya iwapo mambo kama haya yakitokea ni kukubali tatizo na kutafuta njia ya kurekebisha tatizo hilo. Ingawa sasa hivi ushauri wa baba yako kuhusu suala hili unaweza kuwa umechelewa, ushauri wangu ni kwamba, kwanza zungumza na rafiki yako wa kike na amua kwa pamoja mngependa kufanya nini. Kuna wakati utatakiwa kuzungumza na shangazi yako au mjomba ambaye anaweza kumweleza baba yako. Vilevile utahitaji kuzungumza na wazazi wa msichana. Sifahamu wataitikia namna gani, lakini kumbuka mnawajibika wote kwa pamoja kwa mtoto. Usijidanganye kuwa tatizo hili ni la msichana wako peke yake. Ninategemea kuwa utaweza kumalizia elimu yako na kuwa mzazi mwenye kuwajibika. Vilevile ninategemea kuwa mtoto akikua mtatafuta njia ya kumsaidia kufanya uamuzi wa busara. Shangazi Stella

145 MAMBO YA KUFANYA Je, unawafahamu vijana ambao waliolewa au walizaa watoto wakati wakiwa bado wanasoma? Jambo hili liliwaathiri namna gani? IGIZO DHIMA: Katika vikundi vya watu wanne, igiza Usi na mjomba wake au shangazi wakiwaeleza wazazi yaliyotokea.watawaelezaje wazazi? Baba na Mama yake Usi wanasemaje na watachukua hatua gani? Ni ushauri gani wazazi wako hukupatia? Je huwa unazingatia ushauri wao? Iwapo huzingatii, ni kwa nini? Fikiria siku ulipofanya jambo moja ambalo ni la hatari sana. Kama vile kutoka na rafiki yako wa kike au kiume peke yako tena usiku, kunywa pombe sana au kufanya ngono bila kinga. a Kwa nini ulifanya hivyo? b Matokeo yake yalikuwa mazuri au mabaya? c Mambo gani mengine ungeweza kuyafanya? d Ni mara ngapi tabia inakuwa hatarishi?

146 Nina ashiki kali 10 Mpendwa Simba Usijali, hili ni jambo la kawaida kwa wanaume kuwa na ashiki, na uume kudinda mara kwa mara pindi wanapofikiria ngono. Njia rahisi na salama ya kutatua tatizo hili ni kupiga punyeto. Lakini inatakiwa ufanye mwenyewe tena kwa siri. Kupiga Punyeto ni kitendo cha kusugua via vyako vya uzazi ili ujisikie vizuri, ashiki ipande na mara ufikie mshindo. Kitendo hiki hufanya mawimbi ya minyweo katika via vya uzazi na mara nyingine katika mwili mzima. Mwanaume akifikia mshindo, shahawa hutoka kupitia kwenye uume. Mwanamke akifikia mshindo uke huvimba na kuwa na unyevunyevu mwingi. Wavulana na wasichana wote hufurahia kujishika shika. Wachumba au walio kwenye ndoa wakiamua kufanya ngono salama wanaweza kupiga punyeto. Punyeto haina madhara yoyote kiafya, kimwili na kiakili. Husaidia kuondoa msukumo wa kutaka kufanya ngono na ni njia nzuri ya kuchunguza mwili wako. Watu wa umri mbalimbali hupiga punyeto (walio katika ndoa au ambao bado). Ingawa kuna vikundi vya dini vinavyosema ni dhambi kupiga punyeto, wengine huacha kila mtu binafsi afanye uamuzi wake mwenyewe. Shangazi Stella

147 MAMBO YA KUFANYA MAJIBU: Jaribio la Punyeto Sentenzi zote sio za KWELI isipokuwa ya pili. Ni kitu gani kingine umewahi kusikia kuhusu punyeto? Eleza yaliyo chanya na hasi halafu chunguza yaliyo ya kweli Katika jamii yetu, watu wanamtazamo gani kuhusu punyeto? Kwa mfano, kama sehemu ya maisha ya kimapenzi ambayo ni ya kawaida na salama au kama jambo moja baya sana? Je, wasichana na wavulana wana mtizamo unaofanana? Watu huzungumzia suala hili kwa uwazi au ni siri? Iwapo unafikiri kuwa vijana wanatakiwa kuwa na mtazamo wa kichanya kuhusu punyeto, jadili jinsi unavyoweza kufanya hili litokee hivyo

148 Ninapomlipia chakula cha mchana, Je, sistahili kufanya naye ngono? 11 Mpendwa Temba Katika uhusiano, watu wanapokuwa na malengo tofauti hali huwa ngumu sana. Inaelekea kwako ngono ni muhimu zaidi ukilinganisha na jinsi rafiki yako wa kike anavyoiona. Hata hivyo ni wasichana wachache sana ambao huweka ngono mbele. Wasichana hawafurahii wanapoona wavulana wanataka kuwatumia kama chombo na kutoa zawadi na pesa kwa ajili ya ngono. Wavulana na hata wasichana wengi hupendelea kuzuia matatizo ambayo yanaweza kutokea kutokana na kufanya ngono wakiwa bado ni vijana. Hawapendi kuwa na hofu kuhusu mimba, magonjwa ya ngono na VVU. Kwa hiyo huamua kuchagua kuacha kabisa kufanya ngono mpaka watakapokuwa wakubwa. Ebu fikiria uhusiano mzuri. Je, uhusiano mzuri ni kufanya ngono tu au ungependa kuwa na rafiki wa kweli ambaye anakujali? Iwapo unataka urafiki na upendo wa namna hii unahitaji kufikiria yale unayoelezwa na mpenzi wako. Usimshinikize kufanya ngono, yeye hataki kufanya hivyo. Inawezekana watu wengine bado wanawafanyia wasichana mambo tofauti na wavulana. Mambo yanaenda yakibadilika sasa hivi. Wavulana na wasichana wanatendewa sawa. Ni mategemeo yangu hapo baadaye utakuwa na ujasiri wa kumwona mpenzi wako kama mwenzako na kwamba mtaishi pamoja kwa furaha na amani. Shangazi Stella

149 MAMBO YA KUFANYA Unayaonaje majibu ya Shangazi Stella? Unakubaliana na alichomweleza Temba? Iwapo hukubaliani naye, unatoa ushauri gani? WASICHANA: Taja mambo ambayo wavulana wanatakiwa kufanya na yale ambayo hawatakiwi kuwafanyia wasichana na kusema iwapo wanataka urafiki mzuri na wasichana. WAVULANA: Taja mambo ambayo wasichana wanatakiwa kufanya na yale ambayo hawatakiwi kuwafanyia wavulana na kusema iwapo wanataka urafiki mzuri na wavulana. Baada ya hapo tafuta kikundi cha jinsi tofauti. Badilishana orodha na zisome kwa makini. Kaa pamoja katika kikundi mchanganyiko na ulizana maswali ili kupata zaidi wengine wanafikiria nini Fanya mdahalo kuhusu moja wapo ya mada hizi. Msichana anatakiwa kufanya ngono na mpenzi wake iwapo amenunuliwa vitu Mapenzi bila ngono ni sawa na bustani ambayo haina maua. Je unakubaliana na hili? Sio sahihi kufanya ngono kabla ya kufunga ndoa

150 Chunusi zimeota kwenye uume wangu 12 Mpendwa Jabu Umefanya vizuri kuomba ushauri. chunusi zinapoota kwenye uume au kwenye via vya uzazi vya msichana zinaweza kuwa chunusi kama zile zinazotoka usoni, au zinaweza kuwa dalili za magonjwa ya ngono. Iwapo hujawahi kufanya ngono, kwa uhakika huna maambukizo ya magonjwa ya ngono. Hata hivyo kama siku za hivi karibuni umefanya ngono bila ya kutumia kondomu, chunusi hizo zinaweza kuwa dalili ya magonjwa ya ngono. Kwa mfano chunjua za kwenye uzazi, kaswende, pangusa au malengelenge. Inawezekana mwalimu wako wa kidato cha pili alikuwa anazungumzia kaswende, ugonjwa ambao usipotibiwa haraka unaweza kusababisha mtu kupata ugonjwa wa akili. Unatakiwa kufanyiwa uchunguzi haraka na kuanza matibabu mapema iwezekanavyo. Iwapo umepata maambukizi ya magonjwa ya ngono ni muhimu kumweleza mwenzi wako au wenzi iwapo unao wengi ili nao wapate matibabu, hususani wanawake wanaweza kuwa na maambukizo lakini wasionyeshe dalili zozote. Tafadhali nenda kliniki mapema. Magonjwa mengi ya ngono hutibika kiurahisi iwapo utawahi tiba. Nenda na rafiki yako au mtu mzima yeyote ambaye unamwamini ili akupe msaada iwapo unadhani wahudumu wa afya hawatakutendea haki au watakutania. Unayo haki ya kupewa huduma nzuri bila ya kunyanyaswa. Ninakutakia kila la kheri Shangazi Stella

151 MAMBO YA KUFANYA MAJIBU: Jaribio la magonjwa ya Ngono. Sentensi ya 1 na ya 5 ni za KWELI. Sentensi ya 2, 3 (vilevile kuacha ngono ni salama) na ya 4 (magonjwa ya ngono yana dalili tofauti, na wanawake mara nyingi hawaonyeshi dalili) SIO ZA KWELI. KAZI Mradi : Kwa kutumia vipeperushi vinavyotolewa na Wizara ya afya au taarifa zingine zozote kuhusu magonjwa ya ngono. Kila kikundi kitachagua aina moja ya magonjwa ya ngono na kuandaa kuzungumza na wengine. Toa taarifa zifuatazo kama zinapatikana Jina la ugonjwa ni nini? (la kawaida na lile la kitaalam) Dalili za ugonjwa huo ni zipi? (kwa wanaume na wanawake) Matibabu yake ni yapi? Jinsi gani ya kuzuia mtu asipate maambukizo hayo? Baada ya hapo, tayarisha maswali 10 yanahusu magonjwa ya ngono uliyojifunza. Majibu ya maswali yawekwe kwenye karatasi tofauti. Badilishana maswali na kikundi kingine, na jibu maswali yao. Baada ya hapo sahihisha majibu ya maswali uliyowapatia. Nani amepata alama za juu? Mwalike Muuguzi au Mfanyakazi wa idara ya afya aje kuzungumzia kuhusu magonjwa ya ngono na haki yako ya kupewa huduma. Chunguza vizuri mambo yanayotokea kijana anapokwenda hospitali akiwa na matatizo ya magonjwa ya ngono. Iwapo katika eneo lenu huduma za hospitali sio nzuri, ni hatua gani unaweza kuchukua ili kuboresha hali hiyo? Msaada utapata wapi?

152 Ninahisi kuwa nimeambukizwa Virusi Vya UKIMWI (VVU) 13 Mpendwa Flora Pole kwa kuwa katika hali hiyo uliyo nayo. Lakini ni vizuri kwamba unafikiria kwenda kupima VVU. Huu unaweza kuwa ni uamuzi wa kijasiri na busara ambao umewahi kuufanya katika maisha yako. Ni afadhali kujua kuliko kuishi kwa wasi wasi. Ukienda kupima VVU (kwa mfano kwenye vituo vya afya, hospitali za Wilaya, ANGAZA na pengine wanapotoa huduma hiyo) utawakuta wanasihi waliosomea ambao watazungumza na wewe kabla na baada ya kupima damu yako.watajibu maswali yako na watakusaidia jinsi ya kuyapokea majibu yako, kwa vyovyote vile yatakavyokuwa. Hutahitaji kuwaeleza jina lako, kila mtakalolizungumzia itakuwa siri. Muuguzi atatoa damu yako. Kwa kawaida majibu hutolewa siku hiyo hiyo. Kipimo kinaaminika, lakini kuna kipindi cha ficho. Iwapo ulipata maambukizi chini ya miezi mitatu iliyopita kipimo hakitaonyesha maambukizo, kwa hiyo majibu yakionyesha huna maambukizo, lakini wewe ulifanya ngono bila kinga katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita, itabidi upime tena baada ya miezi mitatu. Tafadhali mhimize mpenzi wako aende akapime VVU. Iwapo atakataa kupima na akakataa kutumia kondomu, utakuwa katika hali ngumu sana ya kufanya uamuzi. Iwapo utaonekana huna maambukizi ya VVU hakikisha unabaki katika hali hiyo ili usipate wasiwasi tena. Kila la kheri kwako na kwa mpenzi wako Shangazi Stella

153 MAMBO YA KUFANYA Iwapo Flora ataenda kupima VVU na kugundua kwamba hana maambukizo, ni ushauri gani utampa ili asipate maambukizi? Atahitaji msaada gani? Tayarisha orodha mbili a Eleza kwa nini watu hawataki kujua kama wana maambukizi ya VVU au hawana. b Eleza kwa nini ni muhimu kupima ili kujua kama una maambukizi ya VVU au huna? Orodha ipi ni ndefu? Ni ushauri gani unaweza kumpa mtu ambaye anafikiria kwenda kupima VVU? Chunguza sehemu ya jirani ambapo kuna huduma za kupima VVU kwa hiari. Uliza kama huduma ni ya kulipia au bure. Je, kuna kiwango cha umri wa watu kupima VVU? Je umewahi kufanya ngono bila kondomu? Iwapo umewahi kufanya hivyo fikiria kwenda kwenye kituo cha kupima VVU kwa hiari ili ukapime. Ni msaada gani unahitaji ili kupata ujasiri wa kufanya hivyo? Jaribu kusaidiana na wenzako pale inapowezekana. IGIZO DHIMA: Watu wawili waigize kama Flora na mpenzi wake. Igiza mazungumzo pale Flora anapomweleza mpenzi wake wasiwasi alionao na kumwomba waende wote wakapime kama wana maambukizo ya VVU. Kumetokea nini katika Igizo dhima? Iwapo mpenzi wake hakubaliani naye, jadili jinsi Flora anavyoweza kumshawishi vizuri zaidi. Angalia kadi ya 26 kwa taarifa zaidi inayohusu jinsi ya kuishi na VVU.

154 Nina wasiwasi kuhusu saratani ya shingo ya kizazi 14 Mpendwa Shamsa Hongera kwa kuuliza swali zuri. Saratani ya mlango wa kizazi huathiri mlango wa kizazi. Ugonjwa huu huwapata wanawake wengi nchini Tanzania lakini ni watu wachache sana wanaofahamu kuhusu ugonjwa huu. Saratani ya mlango wa kizazi inatibika kabisa iwapo utagundulika mapema na tiba kuanza mapema. Mwanamke yuko hatarini kupata saratani ya mlango wa kizazi iwapo: Alianza kufanya ngono akiwa na umri mdogo (miaka michache baada ya kuvunja ungo) Ana wapenzi wengi anaofanya nao ngono Mwenzi wake ana wapenzi wengi anaofanya nao ngono Amekuwa akiugua magonjwa ya ngono (Chunjua/vipele sehemu za via vya uzazi Ana maambukizi ya VVU au UKIMWI Umri wake ni zaidi ya miaka 35 Wapo wanawake ambao wanaumwa saratani ya mlango wa kizazi wakiwa na umri chini ya miaka 20. Fikiria mara mbili kabla hujaanza kufanya ngono ukiwa bado kijana na hakikisha unajitunza. Utakapoanza kufanya ngono hakikisha unafanya kipimo kinachoitwa Pap smear mara moja kwa mwaka, iwapo upo kwenye kundi la hatari ya juu na mara moja kila baada ya miaka mitatu iwapo haupo kwenye kundi la hatari. Kipimo hiki kinapatikana karibu katika hospitali zote nchini. Hakuna haja ya mwanamke kufa kwa saratani ya mlango wa kizazi iwapo itangundulika mapema. Shangazi Stella

155 MAMBO YA KUFANYA Umejifunza nini kuhusu saratani ya mlango wa kizazi? Zungumza na marafiki zako wa kike na hata ndugu zako. Waeleze kuhusu kipimo cha Pap smear Pitia barua ya Shangazi Stella. Je wewe na mwenzi wako mpo katika hatari ya kupata saratani ya mlango wa kizazi mtakapokuwa mmezeeka? Iwapo jibu ni ndio, Chunguza zaidi kuhusu saratani ya mlango wa kizazi na jinsi ya kupimwa. AIDHA Mwalike Muuguzi aje kuzungumza na wewe kuhusu saratani ya mlango wa kizazi. Aeleze saratani ya mlango wa kizazi ni nini, jinsi inavyoweza kugundulika na kutibiwa. AU Fanya utafiti kuhusu saratani ya mlango wa kizazi kwa kutembelea kliniki au maktaba.tayarisha taarifa fupi ili rafiki na ndugu zako wapate kufahamu Via vya uzazi vya ndani vya mwanamke Mrija wa falopio Uterasi (Mfuko wa kizazi) Ovari Sevikisi (mlango wa wa kizazi) Uke

156 Nilibakwa 15 Mpendwa Sikudhani Nimesikitika sana kusikia hadithi yako. Alichokufanyia mjomba wako ni kibaya sana. Sio kosa lako, yeye ndiye aliyefanya kosa na ni lazima aambiwe ili asirudie kufanya kosa hilo. Usiogope, lazima umweleze mtu mapema. Huwezi kuliweka jambo hili kama siri, mficha maradhi kifo humwumbua waeleze wazazi wako, ndugu mwingine, au mtu yeyote unayemwamini. Unahitaji mtu ambaye atakushauri na kukupa msaada. Mtu ambaye atakusaidia kukupeleka kituo cha polisi ili kupata msaada zaidi. Toa taarifa ya kubakwa mapema iwezekanavyo, ikiwezekana bila ya kuoga au kubadilisha nguo ili polisi waweze kuchukua ushahidi. Vilevile muombe Mhudumu wa afya akupe dawa ya kuzuia mimba (vidonge vya dharura vya kuzuia mimba). Hospitali zingine wanazo dawa za kuzuia maambukizi ya VVU, iwapo zitamezwa ndani ya siku tatu baada ya ubakaji kufanyika. Ubakaji sio kosa la yule aliyebakwa. Pamoja na hayo zipo njia ambazo wanawake wanaweza kujaribu kukwepa wasibakwe. Usitembee njiani peke yako ikibidi tembea kwa kujiamini na kwa haraka; katika umri wowote usizidishe kunywa pombe au kuvuta bangi; iwapo unampenda mvulana mweleze msimamo wako kabla ya kuanza kushikana shikana. Akikuvamia piga kelele kwa nguvu, mpige mateke, mng ate na meno, mpige kwa magoti kati ya miguu yake na jitahidi kukimbia. Sikudhani, ninategemea umepata msaada unaouhitaji. Shangazi Stella

157 MAMBO YA KUFANYA Kwa nini kuna ubakaji na vurugu nyingi dhidi ya wasichana na wanawake katika jamii yetu? Jadili. Kwa kila jibu litakalotolewa jiulize swali Lakini ni kwa nini? Ili kupata sababu kwa undani zinazosababisha ubakaji na udhalilishaji katika jamii yetu. Ubakaji na udhalilishaji katika jamii yenu Soma sentensi zifuatazo. Ni kwa vipi zinaelezea jamii yenu? Kwa kila sentensi andika kweli, sio kweli au sina uhakika. 1 Katika jamii yetu, wasichana na wanawake wanaweza kutembea salama popote pale, wakati wowote bila woga. 2 Ubakaji na udhalilishaji sio jambo la siri. Iwapo kijana ametoa taarifa ya kubakwa au kudhalilishwa, watu wazima huchukua hatua ya kuzuia lisitokee tena. Hakuna mtu ambaye humlaumu kijana kwa kubakwa. 3 Kijana akibakwa, huduma za matibabu na unasihi zipo kliniki na polisi hufanya wawezalo kumtafuta mkosaji na kumwadhibu. 4 Wavulana huamini na kuwaheshimu wasichana wanaposema HAPANA hawataki ngono. Hawafikirii kuwa wana haki ya kufanya ngono.wanajua, wanaweza kuhimili mhemko. Matokeo: Ni watu wachache kati yenu mtaweza kujibu (KWELI) kwa maswali yote hayo, mambo gani yanatakiwa yafanyike ili kuwepo na usalama, usiwepo ubakaji, vurugu na udhalilishaji katika jamii yenu? Chunguza zaidi kuhusu vidonge vya dharura kwa ajili ya kuzuia mimba na dawa ya kuzuia maambukizo ya VVU kwa watu waliobakwa. Uliza iwapo zinapatikana katika kliniki yenu. Kama hazipo, ni wapi unaweza kuzipata?

158 Je nifanye biashara ya ngono? 16 Mpendwa Tabu Hali uliyonayo ni ngumu, lakini kufanya ngono ili upate pesa kunaweza kukusababisha upate matatizo zaidi.wanaume wengi wanaolipia ngono hukataa kutumia kondomu, kwa hiyo, unaweza kujikuta una mimba au maambukizo ya VVU au vyote viwili. Vilevile inawezekana ukapigwa au kubakwa. Biashara ya ngono ni kosa la jinai nchini Tanzania ukipata matatizo polisi hawawezi kukusaidia badala yake unaweza kujikuta uko jela.tafadhali usifanye hivyo, utapata matatizo zaidi. Unachoweza kufanya ni kufikiria njia zingine zozote zinazoweza kukupatia pesa, au njia ya kumpata mtu au shirika la kukusaidia. Waombe watu wengi iwezekanavyo. Inaweza kuwa shuleni, Kanisani, au kwenye jamii, na endelea kuomba msaada Wizara ya Maendeleo ya vijana na michezo, hasa Idara ya Maendeleo ya Jamii wanaweza kukusaidia. Pamoja na Juhudi zako zote, ukikosa usikate tamaa, watu wengi humaliza shule wakiwa na umri mkubwa.vilevile zipo njia nyingine za kupata pesa. Pata stadi za kazi unazoweza kufanya usijali kama unalipwa au hulipwi. Chunguza miradi inayoendeshwa katika eneo lenu. Waombe kama unaweza kusaidia kazi yoyote.vilevile azima vitabu vya kusoma. Utakapoamua kufanya ngono fanya kwa sababu unampenda mpenzi wako na wala usifanye kwa sababu ya pesa. Hakikisha unajua kuhusu kondomu za kike na za kiume, vidonge vya uzazi wa mpango na njia nyingine ya kujikinga usipate mimba na magonjwa ya ngono vilevile. Kila la Kheri Shangazi Stella

159 MAMBO YA KUFANYA IGIZO DHIMA: Igiza watu wawili. Kila mmoja apate nafasi ya kuigiza nafasi ya kijana kama Simi ambaye anaomba ushauri kutoka kwa mzee anayeheshimika kuhusu jinsi anavyoweza kulipa karo yake ya shule. Baada ya igizo, eleza kwenye kikundi jinsi mlivyojisikia kuwa katika nafasi ya Simi. Ni mambo gani yalifanya kuomba msaada kuwe rahisi, na ni yapi yalikuwa ugumu? Ni ushauri gani unaweza kumpa mtu aliye na matatizo kama ya Simi? Tayarisha mdahalo utakaohusu mada zifuatazo: Wanawake wengi hujiingiza katika biashara ya ngono sio kwa sababu wanafurahia, bali ni kwa sababu wanahitaji pesa kwa ajili ya chakula na mavazi. Mara nyingi jamii huwalaumu wanaofanya biashara ya ngono kwa tabia yao lakini wanaume ambao hulipia huduma hiyo hawalaumiwi. Kwa nini unafikiri haya hutokea? Je ni sahihi? Iwapo sio sahihi, jamii inatakiwa kufanya nini kuhusu suala hili? Fanya utafiti na kutafuta sheria zinazohusu biashara ya ngono na vilevile zinazowahusu wateja wao nchini Tanzania na nchi nyingine. Je, watu wanaofanya biashara ya ngono wana haki na wanalindwa vipi katika nchi mbalimbali? Unafikiri mambo gani yanatakiwa yafanyike?

160 Ninapata ndoto nyevu 17 Mpendwa Edson Ninasikitika kuwa unasumbuliwa na tatizo la ndoto nyevu. Usihofu huna matatizo yoyote na mwili wako wala hakuna sababu ya kujisikia vibaya. Ndoto nyevu ni dalili ya kukua kwako. Kwamba unabadilika kutoka utoto kwenda utu uzima. Hii huitwa kubalehe.wakati wa balehe mabadiliko hutokea katika mwili wako. Shahawa hutengenezwa na zinakuwa tayari kutoka nje, na mara nyingi hutoka kwa njia ya ndoto nyevu. Kuna wakati mwingine utaona uume umedinda unapoamka asubuhi. Hii haina maana ya kwamba umekuwa ukiota ndoto za mapenzi, ni dalili tu ya kwamba umeanza kubalehe. Ni jambo la kawaida kwa vijana kupata ndoto nyevu, ingawa wengine hundelea kupata hata wanapokuwa watu wazima. Kwa hiyo usiwe na hofu kuwa jambo hili litakuletea matatizo utakapooa. Ndoto nyevu unazozipata sasa hivi ni za kawaida. Wanaume wote hupitia kipindi hiki. Jaribu kumwuliza kaka yako au mjomba atakuthibitishia jambo hili. Shangazi Stella

161 MAMBO YA KUFANYA Malizia sentensi zifuatazo: a Ninapenda mabadiliko yanayotokea mwilini mwangu kila ninavyokua kwa sababu b Mabadiliko mengine siyapendi kwa sababu Washirikishe wenzako yale uliyoyasema katika kikundi Umejifunza nini katika zoezi hili? Kuna kitu chochote ungependa kufanya au kujua zaidi? Angalia uwezekano wa kufanya zoezi hili vizuri zaidi. Je una wasiwasi mwingine wowote kuhusu kitu ambacho ni cha kawaida? Zungumza na marafiki zako au mtu aliyekuzidi umri ambaye unamwamini Imechorwa na David Chikoko

162 Dawa za kupunguza makali ya Virusi Vya Ukimwi (ARV) ni nini? 18 Mpendwa Tedy Dawa za kupunguza makali ya VVU (ARVs) ni dawa ambazo zinaweza kuwasaidia watu ambao wana UKIMWI.VVU haviondoki lakini dawa husaidia visiendelee kuzaliana, hivyo kuruhusu kuongezeka kwa kinga ya mwili. Ni kweli dawa hizi ni ghali. Lakini bei sasa hivi zimepungua kidogo. Vilevile Serikali inatoa bure. Hata hivyo dawa hizi zina nguvu sana na hazieleweki vizuri, kwa kawaida watu huanza kuzitumia wanapokuwa wagonjwa sana. Kamwe usitumie dawa hizi bila ya kupima na kupata ushauri kutoka kwa daktari. Unatakiwa kujihakikishia kwamba unao uwezo wa kuzinunua kipindi chote cha maisha yako kwa sababu ni hatari kuanza kuzitumia halafu unaacha katikati na kurudia tena. Kumbuka vilevile kutumia dawa za kupunguza makali ya VVU sio njia pekee ya kuwa na afya.afya inaweza kurudia hali ya kawaida kwa kula chakula sahihi, kupata vitamini na kuishi kwa matumaini. Hii ni pamoja na kutibu magonjwa nyemelezi mapema. Dawa za kupunguza makali ya VVU hukufanya ujisikie vizuri zaidi lakini VVU vinakuwepo mwilini mwako, kwa hiyo unaweza kumwambukiza mtu mwingine au wewe mwenyewe kupata maambukizi mapya. Kumbuka, kila mara tumia kondomu unapofanya ngono au fanya ngono salama. Kama unatumia au hutumii dawa za kupunguza makali ya VVU, jaribu kuishi maisha ambayo sio hatarishi, utakuwa na miaka mingi ya kumtunza mtoto wako. Kila la kheri Shangazi Stella

163 MAMBO YA KUFANYA AIDHA: Tembelea kliniki na sehemu zingine ambazo hutoa msaada kwa watu wanaoishi na VVU na UKIMWI ili kujifunza zaidi kuhusu dawa na matibabu. AU Mwalike mtu mwenye ufahamu aje kuzungumza nanyi kuhusu dawa hizi. Chunguza zaidi kuhusu dawa za kupunguza makali ya VVU. Je, kila mtu anaweza kuzipata? Je zinatolewa bure au kuna gharama ya kulipia? Kama kuna gharama yoyote, ni kiasi gani? Vilevile chunguza uzuri na ugumu wa kutumia dawa hizo. Watu wanaotumia ARVs wanahitaji msaada gani? Na kutoka kwa nani? (Fikiria wajibu wa familia na marafiki, na vilevile aina ya huduma wanayoihitaji kutoka kwenye kliniki na taasisi zingine zilizoko kwenye jamii) Iwapo ARVs zinaweza kuokoa maisha ya mtu, unafikiri ni kwa nini hazipatikani kwa urahisi? Nchi kama ya Afrika Kusini, watu wa kawaida wamekuwa wakishirikiana kuishawishi serikali itoe dawa hizi kwa kila atakayezihitaji. Kuna vikundi gani katika jamii vinavyofanya kazi kwa pamoja kuhakikisha dawa zinapatikana na zinakuwa rahisi? Vinafanya kazi gani hasa? Nini wajibu wa vijana katika vikundi hivi? Angalia kadi ya 26 kwa taarifa zaidi kuhusu jinsi ya kuishi kwa matumaini na afya njema unapokuwa na VVU au UKIMWI

164 Anataka tufanye ngono 19 Mpendwa Oliva Iwapo mama mwenye nyumba anataka kufanya ngono na wewe, basi anakudhalilisha kijinsia. Hii huitwa shambulio la aibu na ni kosa la jinai. Ni lazima upate msaada na ujinasue kabla mambo hayajawa mabaya zaidi. Ninakubaliana na wewe kwamba ukilalamika kwa mume wake unaweza kupata matatizo. Kwa hiyo ninakushauri uwaeleze wazazi wako haraka na wakati huo huo tafuta mahali pengine pa kuishi. Nina uhakika wazazi wako wangependa uishi mahali ambapo pana usalama, kwa hiyo watahakikisha wanalipa kodi ya nyumba mapema. Iwapo atajaribu kurudia tena kabla hujahama mweleze moja kwa moja bila kumuonea haya aache kufanya hivyo. Akikulazimisha, kataa kabisa. Ni vigumu sana kuthibitisha kwamba mwanaume amedhalilishwa kijinsia na mwanamke, hasa kama hakuna dalili zozote za vurugu, hata hivyo mama mwenye nyumba anataka kukulazimisha ufanye ngono bila ya ridhaa yako, hii ni kinyume na haki zako. Tafadhali ondokana na hali hii mapema iwezekanayo. Shangazi Stella

165 MAMBO YA KUFANYA Haki za vijana katika uhusiano wa kimapenzi Soma orodha ya haki za kijana katika uhusiano wa kimapenzi na baadaye zungumzia maswali yanayofuata. 1 Mtu yeyote asikushike au kukufanya ufanye ngono wakati wewe mwenyewe hutaki 2 Inatakiwa iwe rahisi kupata dawa za kuzuia mimba na taarifa zinazohusu afya ya uzazi na ujana balehe 3 Wafanyakazi wote wanaofanyakazi sehemu kama za kliniki, kituo cha polisi wanatakiwa kuwa na taarifa za kutosha tena zilizo kamili, wenye uwezo wa kusaidia na huruma. 4 Kunatakiwa kuwepo huduma nzuri za upimaji, unasihi na matibabu ya VVU na UKIMWI, pia dawa zipatikane na kwa bei nafuu. 5 Wasichana wanaopata mimba wanayo haki ya kupata elimu 6 Iwapo una maambukizi ya VVU au UKIMWI mtu asikutendee tofauti na wengine au kikatili. 7 Kila mtu, awe mwanaume, mwanamke, kijana, mzee, mashuhuri, tajiri, mweusi, mweupe, mnene, mwembamba, shoga, mlemavu - anatakiwa kuheshimiwa. 8 Vijana wanayo haki ya kuandaa na kupata huduma nzuri za kiafya. Unaionaje orodha hii? Kuna kitu unaweza kuongezea au kuondoa? Je zote zinaweza kutumika kwa wavulana na wasichana? Toa alama chini ya 10 kwa jamii yako kuonyesha kiwango ambacho haki za vijana zinatekelezwa. Jipatie mwenyewe alama chini ya 10 kuonyesha kiwango ambacho unaheshimu haki za vijana wengine. Toa ahadi ya kuheshimu haki hizi kwa watu wengine na kupata msaada iwapo haki zako zinadhalilishwa.

166 Hedhi yangu si ya kawaida 20 Mpendwa Paulina Usihofu kwani hakuna sababu ya kufikiria kwamba hutaweza kupata watoto hapo baadaye. Ni jambo la kawaida kukosa hedhi katika miaka michache ya mwanzo baada ya kuvunja ungo.wasichana wengine hukosa hedhi kwa kipindi cha mwaka mzima baada ya kuvunja ungo. Baada ya muda utaona siku zako kama kawaida. Kuna vitu vingine ambavyo vinaweza kuathiri hedhi yako. Kwa mfano kama una wasiwasi, au umekonda sana au umekuwa mgonjwa kwa muda mrefu. Hata hivyo, kwa msichana ambaye amekuwa akifanya ngono, kutopata hedhi ni dalili kuu ya mimba. Zungumza na Muuguzi au Mhudumu wa afya, hususani kama hutaanza kuona tena siku zako baada ya mwaka mmoja. Jaribu kupata lishe bora ambayo ina matunda, mboga za majani na chakula chenye madini ya chuma kwa wingi kama vile njegere, mboga mboga, maharage, dengu, mayai, kuku samaki na aina nyingine za nyama, senene na kumbikumbi. Wewe na rafiki zako mnahitaji kupata taarifa kuhusu mabadiliko ya miili yenu. Panga kukutana na Mhudumu wa afya katika kliniki iliyokaribu ili upate maelezo kwa undani zaidi na maswali yako yatajibiwa. Au nenda kwenye kituo cha vijana na waombe taarifa zinazohusiana na suala hili. Shangazi Stella

167 MAMBO YA KUFANYA Paulina anaogopa kwamba yeye huenda ni tasa. Ninyi mna wasiwasi gani kuhusu miili yenu, ngono na kupata watoto? Jadili na wenzako kwenye kikundi uone watakusaidiaje. Iwapo mnataka kufanya kwa usiri ili asijulikane aliyeuliza swali, andika maswali yenu kwenye karatasi bila ya kuandika majina.weka makaratasi ndani ya mfuko halafu changanya. Baada ya hapo yatoe kwa majadiliano Iwapo hutapata msaada kutoka kwenye kikundi chako, utamwona nani kwa ushauri? Watu hupata taarifa kuhusu miili yao, ngono na uhusiano kutoka kwa watu na sehemu mbali mbali.wewe hupata wapi taarifa hizo? Taja jinsi unavyopata taarifa. Utafanya nini ili kutambua lililo la kweli na ambalo sio kweli? Chora picha ya kliniki rafiki kwa vijana ukionyesha kwa nini kliniki hiyo ni rafiki kwa vijana. Linganisha picha na kliniki unayoitembelea. Je unafikiri kliniki yenu huwatendea vijana kwa kuwaheshimu? Iwapo sio, wewe na wengine katika jamii mnaweza kufanya nini kwa pamoja ili kuifanya kliniki hiyo iwe rafiki zaidi kwa vijana?

168 Je nimweleze kuwa nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI? 21 Mpendwa Frida Jambo la muhimu, ninalotaka kusema ni kwamba, kuwa na maambukizo ya VVU hakuwezi kukufanya wewe uwe tofauti na vile ulivyokuwa mwanzo na hakuna mtu ambaye hutoa sheria za pekee kuhusu jambo lipi linaruhusiwa. Unastahili sawa kama watu wengine, yaani upendo, uhusiano, kuridhika kimapenzi, ndoa na watoto. Watu wengi wanaoishi na VVU wanao wenzi wao. Wakati mwingine wenzi wao nao wanaishi na VVU ingawa sio wote. Sio rahisi kumweleza Tadei kuwa una maambukizo ya VVU, lakini siku moja itabidi umweleze. Jaribu kumwelewa vizuri rafiki yako kabla hujafanya lolote. Kwa vyovyote utahitaji kujadili naye kuhusu VVU na matumizi ya kondomu kabla ya kuanza kufanya ngono naye. Iwapo atakataa kutumia kondomu au hatakubali wewe utumie kondomu ya kike au hatavumilia kufanya ngono salama, basi hakuna haja ya kufanya ngono hata kama yeye ni mzuri kiasi gani. Shangazi Stella

169 MAMBO YA KUFANYA Je unakubaliana na Shangazi Stella? Kwa nini? IGIZO DHIMA: Utahitaji watu wawili. Frida akimweleza Tadei kuwa ana maambukizo ya VVU, Baada ya Igizo waigizaji walieleze kundi jinsi walivyojisikia wakati wa mazungumzo. Sasa kila mtu ajadili maswali yafuatayo. a Mwisho ulikuwaje? Nani alitoa uamuzi? Waigizaji wote walipata shida? Je lilikuwa hitimisho zuri? Iwapo sio ungelifanya nini ili hitimisho liwe zuri zaidi? b Je Matokeo haya yanaweza kuwa ya kawaida kwa vijana unaowafahamu? c Iwapo Tadei ndiye angekuwa ana maambukizo ya VVU, na alitakiwa kumweleza Frida, mambo yangekuwa tofauti? Rudia igizo kwa kubadilishana nafasi ili kuona iwapo kuna mabadiliko na yanatokeaje. d Ni watu gani na mashirika gani ambayo yanaweza kuwasaidia watu walio katika hali hii.

170 Je, bangi inaweza kuniondolea aibu? 22 Mpendwa Philimoni Marafiki zako wanakushauri vibaya. Ingawa watu wengine husema bangi huwafanya waburudike, wengine huona inawafanya wachanganyikiwe na kuogopa. Ninaelewa kwamba unajisikia mpweke na kupitwa na wakati kwa sababu ya kukosa mpenzi lakini jambo zuri ni kuzungumza na wasichana kama marafiki tu. Uhusiano wa kimapenzi unaweza kutokea kutokana na urafiki. Anza kwa kumsalimia, toa tabasamu na kuzungumza mambo yanayohusu shule, hali ya hewa au kitu chochote. Kipimo cha kweli ni kuuliza watu wengine habari zao na kuwa na moyo wa kupenda maisha yao na matatizo yao.wasichana watathamini zaidi hili kuliko kujionyesha na kujigamba.vilevile kumbuka ya kuwa hakuna mtu anayekuangalia wewe ukifanya mambo ya kijinga.wenyewe tu wana wasiwasi mkubwa wa kufanya makosa. Huwezi hata siku moja kutatua matatizo yako kwa kutumia madawa ya kulevya kama bangi au pombe.wapo watu ambao hushindwa kujiheshimu wakiwa wamekunywa pombe, wakati mwingine hupigwa mawe, jambo ambalo husababisha matatizo na familia, marafiki na waajiri. Vilevile uvutaji bangi ni kosa la jinai unaweza kupata matatizo makubwa zaidi. Huhitaji dawa ya aina yoyote ili upendwe na watu wengine au upate ujasiri wa kufanya jambo lolote. Zipo njia nzuri zaidi za kupambana na aibu. Kila la kheri Shangazi Stella

171 MAMBO YA KUFANYA Taja aina zote za madawa ya kulevya unayoyafahamu na athari zake kwa watu wanaotumia. Ni yapi kati ya haya yana tabia ya kuuzoesha mwili vibaya? (yaani ukianza kutumia huwezi kuacha) Angalia orodha ya sababu zinazosababisha vijana kutumia madawa ya kulevya. Kati ya hizi ni zipi ambazo zinakuhusu wewe na rafiki zako. Ziweke kwa mpangilio kuanzia moja mpaka tano ukianzia na ile ambayo ni ya kawaida zaidi na kuishia na ile ambayo sio ya kawaida. Vijana hutumia madawa ya kulevya kwa sababu. Marafiki zao wanafanya hivyo Kukwepa matatizo ya maisha Wanataka kujiondoa kutoka katika hali yao ya kawaida Wanafikiri madawa yatawapa ujasiri Wamechoshwa na maisha Baada ya kujadili orodha hii, angalia iwapo upo katika hatari ya kutumia madawa ya kulevya.wewe na marafiki zako mnaweza kusaidianaje kuwa mbali na madawa ya kulevya. Nani mtu mwingine anaweza kuwasaidia? IGIZO DHIMA: Unahitaji msichana na mvulana. Mvulana mwenye aibu anamfuata msichana na kuanza kuzungumza naye. Baada ya dakika chache badilisha nafasi za waigizaji ili msichana aanze kuongea. Sasa jadili. a Ulijisikiaje kuanza mazungumzo na kuwa mtu mwingine? b Umejifunza nini kuhusu kuondokana na aibu na kutafuta marafiki?

172 Wazazi wangu hawanielewi 23 Mpendwa Daudi Si wewe peke yako.vijana wengi wanashindwa kuwasiliana vizuri na wazazi wao, hususani mambo yanayowahusu wao binafsi kama vile ngono na uhusiano.wazazi wanahitaji muda wa kuzoea mabadiliko yanayokutokea, kukuelewa na kukuamini kwa jinsi unavyouliza maswali na unavyojifunza na kukua. Jaribu kuelewa kuwa wazazi wako wanakujali na wana wasiwasi kuhusu wewe. Wanataka ukue kwa usalama, uwe na furaha na ufanikiwe katika maisha. Wanakumbuka wakiwa vijana wanapoona majaribu na hatari unazopambana nazo na jinsi ilivyo rahisi kufanya makosa. Maisha yamekuwa ya kutisha sana tangu wakiwa vijana, hasa kipindi hiki cha UKIMWI. Ndio maana wanakufuatilia sana. Kumbuka kwamba mara nyingi wanao ushauri mzuri wa kukupatia. Unaweza kuboresha uhusiano wako na wazazi. Jambo la kwanza, waonyeshe kuwa wanaweza kukuamini kwa kufuata sheria zao. Ukiona wanakuonea, zungumza nao na sikiliza wanapokushauri. Pili waombe wakupe maoni yao kuhusu tatizo lako ulilo nalo. Waeleze mategemeo yako ya maisha ili wakufahamu vizuri. Mwisho, siku zote zungumza na wazazi wako kwa upole na heshima, kamwe usikasirike au kuwafanyia fujo. Ukiona unapata hasira, ninakushauri uairishe mazungumzo mpaka wakati mwingine. Jaribu mara kadhaa kwa vile ina uzuri wake. Iwapo itashindikana, zungumza na mwalimu au rafiki wa familia. Shangazi Stella

173 MAMBO YA KUFANYA Orodhesha mambo unayoyapenda kuhusu wewe mwenyewe. Kwa mfano tabasamu nzuri, stadi za pekee ulizonazo au tabia maalum. Ulijifunza wapi yote haya? Je, inawezekana yametokana na familia yako? Je, zoezi hili linakufanya ujisikie vipi kuhusu mchango wa familia yako katika namna unavyofikiri na kuhisi? IGIZO DHIMA: Igiza wawili wawili. Chagua jambo la kawaida ambalo wazazi na vijana hutofautiana. Kila mtu apate nafasi ya kuigiza kama mzazi katika mabishano, na waeleze wenzako katika kikundi jinsi ulivyojisikia. Katika kikundi chenu, fikiria dunia ambayo wazazi na wazee hawatoi ushauri kabisa kwa vijana na watoto. Dunia ya namna hiyo itakuwaje? Wakilisha mawazo ya kikundi kwa kutumia mchoro, mchezo, wimbo au shairi. Weka miadi ya kuzungumza na mmoja au wazazi wote kuhusu jambo ambalo linakupa wasiwasi. Jaribisha utakayoyasema kwanza na kumbuka Shangazi Stella alivyosema kuwa unatakiwa kuwa mpole mwelewa na mwenye heshima.

174 Je, nimweleze kuwa nina 24 maambukizo ya magonjwa ya ngono? Mpendwa Kizuri kidumu Ukiamua kufanya ngono na mtu, maana yake kila mtu anawajibika kwa mwenzake. Unatakiwa usimuweke mpenzi wako katika hatari, kwa hiyo ni muhimu kumweleza mpenzi wako na kumkinga katika hatari ya kupata ugonjwa ambao ni hatari na ni wenye madhara makubwa, jambo lingine ni kwamba, iwapo ana maambukizi uwezekano wa kukuambukiza wewe ni mkubwa iwapo hatatibiwa. Magonjwa ya ngono yanatofautiana na kwa bahati mbaya dalili za magonjwa ya ngono mengi hazijionyeshi wazi. Wanawake wakipata mara nyingi hawaonyeshi dalili kwa muda mrefu. Kwa hiyo hakikisha wote mmetibiwa. Mwombe Muuguzi akupatie karatasi la kumtaarifu mpenzi wako kwa ajili ya mpenzi wako na (ikiwezekana kwa ajili ya mwanamke uliyekutana naye kwenye baa). Akipeleka karatasi hiyo kliniki atapata matibabu kama uliyopewa wewe bila ya kuulizwa maswali yoyote. Usichangie dawa na mpenzi wako. Hakikisha unakunywa dawa zote hata kama dalili zinakuwa zimeondoka. Wewe na mpenzi wako mnahitaji kujadili kuhusu kutumia kondomu kila mnapotaka kufanya ngono. Hii ni njia pekee ya kuzuia magonjwa ya ngono. Bakia na mpenzi mmoja, na kwa vile mlifanya ngono bila kinga anza kufikiria kuhusu kwenda kupima VVU. Kuhusu uhusiano, zungumzeni kwa uwazi misimamo yenu. Unataka nini kutoka kwa mwezio na yeye anataka nini. Uaminifu na kuaminiana ni mambo muhimu sana katika uhusiano. Ninawatakia kila la kheri nyie wote. Shangazi Stella

175 MAMBO YA KUFANYA IGIZO DHIMA : Utahitaji mvulana na msichana. Leo anaamua kumweleza mpenzi wake kwamba ana maambukizi ya magonjwa ya ngono. Mambo gani yanatokea? Kwa kuzingatia unayoyafahamu, kama ungekuwa leo ungewaeleza wapenzi wako kuwa una maambukizi ya magonjwa ya ngono? KAZI MRADI: Chora ramani ya eneo lenu ukionyesha sehemu zote unazozifahamu ambapo vijana wanaweza kupata kondomu. Kwa kila sehemu katika ramani yako onyesha majibu ya maswali haya a Je kondomu hutolewa bure au zinanunuliwa? b Ili uzipate unatakiwa uwe na umri gani? c Wasichana nao hupewa? d Je kondomu za kike hutolewa? e Je wanapowahudumia vijana ni wapole? Toa alama chini ya 10 kutegemea na majibu ya maswali haya Iwapo ramani yako inaonyesha kuwa vijana katika eneo lenu hawawezi kupata kondomu bure na kwa urahisi, utachukua hatua gani ili kuboresha hali hiyo? Ni shirika na watu gani binafsi wanaweza kukusaidia? Angalia kadi ya 7 na 13 kwa taarifa zaidi kuhusu magonjwa ya ngono.

176 Nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI. Je nitakufa? 25 Mpendwa Wema Majibu ya kuwa una maambukizo ya VVU si hukumu ya kifo. Kuna njia nyingi za kuzuia usiugue na kufikia hatua ya kufa mapema. Kwanza, unatakiwa kujitunza vizuri, kula chakula cha kawaida kinachopatikana katika eneo lenu, kulala usingizi wa kutosha na kufanya mazoezi, kuepuka vitu kama sukari na pombe, kutibu magonjwa nyemelezi mapema (haraka) na kutumia kondomu kila unapofanya ngono. Njia muhimu ya kujikinga na kuwa na afya nzuri ni kuishi kwa matumaini na kuwa na nia thabiti ya kuishi maisha mazuri. Jaribu kumtafuta mnasihi na kikundi kinachotoa msaada ili wakupe moyo wa kwenda kwenye kituo kinachopima VVU au shirika la afya la jamii. Vilevile wanaweza kuzungumza na Shangazi yako iwapo utaamua kuwaeleza. Watu wengi wanaogopa UKIMWI, wanaogopa kufa wakiwa peke yao, kupoteza marafiki, na kufanyiwa vibaya. Kwa kukutana na watu wengine wanaoishi na VVU husaidia sana kuondoa wasiwasi huu. Watu wengi wanaishi na VVU kwa kipindi cha miaka mingi na wana afya nzuri na wanafanikiwa katika maisha.wengi wana uhusiano wa kimapenzi na wengine huchagua kuzaa watoto. Unaweza kufanya yote haya ukipata ushauri na maelekezo.watu wengine wanaweza kukupatia matumaini, na historia zao zinaweza kukujenga, na wewe kuwasaidia watu wengine. Shangazi Stella

177 MAMBO YA KUFANYA Zungumza na watu ambao wako wazi kuhusu kuishi na VVU au UKIMWI.Waombe wakueleze kila kitu kinachowasaidia kuishi maisha yenye afya, kukubali hali na kwa matumaini. Kila mtu anahitaji taarifa hii kwa hiyo shirikiana na mashirika na vituo vya vijana kuwaeleza vijana wengine zaidi. Fanya utafiti mdogo wa kujua mtizamo wa watu kuhusu VVU/UKIMWI. Katika kipindi cha wiki moja sikiliza watu wanasema nini kuhusu watu wanaoishi na VVU na UKIMWI.Toa taarifa sahihi na ikiwa kuna wazo hasi lolote jaribu kueleza kwa utaratibu.toa taarifa na sema yale uliyojifunza. Ifikirie siku ambayo ulijisikia kukosa raha na kuwa mpweke na ukaweza kutatua tatizo hilo. Kitu gani kilikusaidia? Waeleze wenzako halafu jadili ni mambo gani kati ya hayo yanaweza kuwasaidia watu wanaoishi na VVU au UKIMWI. Angalia kadi ya 19, 22 na 40 kwa maswali mengine yanayoulizwa na watu wanaoishi na VVU.

178 Je, yawezekana nina mimba? 26 Mpendwa Nyamboni Ninasikitika kuwa upo katika hali hii ngumu. Ukweli ni kwamba unaweza kupata mimba siku ya kwanza utakayofanya ngono. Unahitaji kufanya kipimo cha mimba ili kujihakikishia kama unayo au huna. Unaweza kupima kliniki au unaweza kununua vifaa vya kupimia kutoka kwenye duka la madawa. Iwapo una mimba mweleze mpenzi wako na mtu mwingine wa karibu kwako. Tafadhali usijaribu kumdhuru mtoto au wewe mwenyewe. Zungumza na watu ambao wanaweza kukusaidia katika kufanya maamuzi ya jinsi ya kumtunza mtoto wako. Ninaelewa hili haliwezi kuwa rahisi lakini ninategemea familia na marafiki watakusaidia. Vidonge vya dharura vya kuzuia mimba hupatikana kliniki au kwenye maduka ya dawa. Huzuia mimba kutunga lakini iwapo tu vitamezwa ndani ya saa 72 baada ya kufanya ngono. Iwapo huna mimba, basi una bahati.wavulana wanaweza kukushinikiza kufanya ngono, lakini kama ulivyoona ngono haifurahishi iwapo hupendi au hunaraha unapofanya. Ikiwa unataka uendelee kuwa na mpenzi wako lakini msifanye ngono zungumza naye kuhusu jambo hilo. Unaweza kutoka naye kwa matembezi lakini msiwe peke yenu, na epuka kunywa pombe na madawa ya kulevya. Pombe na madawa ya kulevya hufanya mtu ashindwe kushikilia uamuzi aliokuwanao mwanzoni. Mwisho, napendekeza usubiri mpaka utakapokuwa mkubwa na unajua unataka nini kabla ya kufanya ngono. Watu wengi huamua kuacha mpaka watakapo olewa au kuoa. Huu ni uamuzi wako, vyovyote utakavyoamua unapofanya ngono hakikisha unakuwa salama kwa kutumia kondomu ya kiume au ya kike. Shangazi Stella

179 MAMBO YA KUFANYA IGIZO DHIMA Wafanye Wawili wawili (mvulana na msichana) mvulana anamtongoza msichana ambaye anamweleza kuwa anazo kondomu na anaweza kumsaidia kuivaa. Kitu gani kinatokea baada ya hapo? Rudia igizo lakini wabadilishane nafasi mvulana awe msichana na msichana awe mvulana. Je mambo yanafanana Jadili ni kwa nini wasichana na wavulana ambao wanaanza kufanya ngono wanatakiwa kubeba kondomu. JARIBIO: kondomu ya kike Sentensi zipi ni za kweli na zipi sio kweli? Angalia majibu mwisho wa ukurasa huu 1 Kondomu za kike huzuia mimba, magonjwa ya ngono na VVU kwa wanaume na wanawake. 2 Kondomu za kike ni ghali kuliko kondomu za kiume. 3 Kondomu za kike zinaweza kutoa kelele zinapotumika. Ili kuzuia kelele ivaliwe mapema (saa chache kabla ya kitendo). 4 Ni afadhali kutumia dawa ya kuulia mbegu za kiume pamoja na kondomu ya kike. Tunga wimbo au toa wito wa kuwatia moyo vijana kusubiri wasifanye ngono mpaka watakapokuwa watu wazima na kuwa na mpenzi mmoja, waimbie au waonyeshe wengine na kufanya uamuzi wa nani ana ushawishi zaidi. Angalia kadi ya 32 kwa taarifa zaidi kuhusu ufanye nini iwapo umepata mimba isiyaotarajiwa. JIBU: Sentensi zote ni za kweli.

180 Mpenzi wangu anatarajia kuolewa 27 Mpendwa Faraji Ninasikitika sana kuwa mpenzi wako yupo katika hali ngumu kama hiyo lakini nimefurahi kwamba upo tayari kumsaidia. Utaratibu wa mahari ni mzuri pale tu unapotumika vizuri na kwa usahihi. Mahari inapotolewa kwa sababu ya familia kutajirika haipendezi. Ni kinyume na haki za binadamu kwa mwanamke kulazimishwa kuolewa bila ya ridhaa yake. Zungumza na Susan ili ujue anataka umsaidie vipi. Kwa pamoja nyie wawili mnaweza kusaidiana kutatua tatizo hili. Wewe na Susan jaribu kuzungumza na ndugu zake Susan kuhusu kilicho bora kwake, kama wana huruma wanaweza kumsaidia wakati wa majadiliano na wazazi wake. Iwapo hakuna mabadiliko Susan anaweza kwenda kwenye shirika linaloshughulikia wanawake na kuomba msaada lakini hili lina matatizo yake. Itamaanisha Susan atakuwa anavunja uhusiano na familia yake. Huo ni uamuzi mkubwa kwake kwa hiyo jaribu kumpa msaada na usimuongezee shinikizo la ziada katika yale ambayo tayari anayo. Hali hii ni ngumu lakini ni matumaini yangu kuwa utapata msaada kutoka kwa mtu ndani ya familia ya mpenzi wako au kutoka kwenye jamii yenu. Shangazi Stella

181 MAMBO YA KUFANYA Wiki ijayo toa usaili kwa watu wazima na vijana. Waulize iwapo wazazi wana haki ya kuwachagulia watoto wao wachumba. Baada ya zoezi hili rudi na jadili yaliyojitokeza. Fikiria mifano mingine ambayo vijana na watu wazima wanakuwa na mawazo tofauti ya mambo yanayotakiwa kufanyika. Njia gani utaitumia kujadili tofauti hizo, kuelewa hoja za kila upande na kutatua tatizo kwa pamoja? Andaa kipindi ambapo utatumia kadi za Shangazi Stella katika kikundi chenye mchanganyiko wa vijana na watu wazima.waombe watu wazima kujadili sehemu ya mambo ya kujadiliana na kuyafanyia kazi. Baada ya hapo zungumzia maoni yako. Kuna tofauti yoyote? Je hii imesaidia kuondoa tofauti iliyopo kati ya makundi haya yenye umri tofauti?

182 Mwalimu alimtia mimba rafiki yangu 28 Mpendwa SIkujua Vizuri sana, mimi nimeufurahia uamuzi wako na wenzako unaosoma nao. Mtu anahitaji ujasiri kusimamia haki yake kwa bahati mbaya nimesikia taarifa kama hizi. Kumbuka kwamba pamoja na kwamba mnamsaidia Upendo, vilevile mnajaribu kubadilisha jinsi mfumo wa shule unavyoshughulikia walimu wanaowadhalilisha wanafunzi wao. Kazi hii si rahisi hata kidogo. Jaribu kuwapata watu wengi iwezekanavyo wa kuwapa nguvu na kutia saini kwenye lalamiko lenu, kama vile wanafunzi, walimu, wazazi, vijana na mashirika ya wanawake, na watu wengine ndani ya jamii hususani watu wanaoheshimiwa na wana ushawishi (kama viongozi wa kijamii, viongozi wa siasa na wafanya biashara). Peleka barua yenu kwenye magazeti ya taifa na binafsi ili watu na mashirika wajue mnachofanya. Jinsi watu wanaowaunga mkono watakavyo kuwa wengi ndivyo uwezekano mkubwa utakavyo kuwepo wa bodi ya shule kuwasikiliza. Jambo lingine, usihofu iwapo hatua hii haitafanikiwa, mabadiliko yoyote huja taratibu, usijisikie umeshindwa iwapo hutafanikiwa safari hii. Hatua yoyote ambayo hujaribu kubadili kitu kibaya hata kama ni ndogo tayari ni ushindi. Shangazi Stella

183 MAMBO YA KUFANYA Je, unalionaje jibu la Shangazi Stella? Unakubaliana na anayoyasema? Je, kuna matatizo yoyote katika shule yako au shirika au ndani ya jamii ambayo ungependa kuyabadilisha? Shirikiana kutengeneza mpango. Amua unachotaka kubadilisha na ni nani anaweza kusaidia. Andaa mkutano na tengeneza mpango wa kazi kama huu Tatizo Ufumbuzi Unaotakiwa Mkakati Rasilimali Mhusika Lini (Muda) Tatizo ni nini Mabadiliko gani unayataka? Tunatakiwa kufanya nini ili kufanikisha mabadiliko? Kwa mfano kufanya mikutano kuzungumza na watu ambao wanaweza kusaidia kuandaa barua ya malalamiko Tunahitaji nini (kama pesa watu na vifaa) Nani katika kundi ana wajibu gani kwa mfano Fadhili andaa mkutano Jefftengeneza mabango Linda pandika mabango Tarehe tuliyokubalia na kazi ifanyike na lini tunataka mambo yatokee

184 Mume wangu si mwaminifu 29 Mpendwa Josephine Mara nyingi kuolewa mapema huleta matatizo kwa sababu vijana wanabadilika na hawajui wanataka nini katika maisha. Lakini uelewe kuwa wanawake wengi siku hizi wako kama wewe, wanakataa kufanya ngono na waume zao bila ya kondomu.wengi wanasema hapana kwa wanaume kutokuwa waaminifu na hapana kwa kuogopa kupata VVU, kwa sababu ya hayo mambo ya kukosa uaminifu. Wewe ni jasiri kwa kuwa mkali kwa Tuli kwa ajili ya kujikinga mwenyewe na hususani kwa vile unaye mtoto wa kumfikiria pia. Unaweza kuchagua kutumia kondomu ya kike, lakini mambo haya hayawezi kuendelea hivi.wote wawili mnahitaji kupimwa VVU. Zungumza na Tuli kuhusu suala hili tena. Elewa kuhusu hofu yake. Kuna mtu yeyote ambaye anaweza kumtia moyo akapime? Iwapo hakuna, nenda kwenye kituo cha kupimia VVU kwa ushauri. Iwapo Tuli bado anakataa, itakubidi ufanye uamuzi mzito yaani kuhusu lipi ni muhimu kwako na ufanye nini baada ya hapo. Mweleze mume wako unachofikiria na angalia kama anataka kuokoa ndoa yenu. Ikiwa mnaishi pamoja hii ni nafasi nzuri ya kuzungumza kuhusu yale ambayo kila mmoja wenu anayahitaji katika ndoa yenu. Familia zenu au wanasihi wanaweza kuwasaidia. Kila la kheli kwenu wote. Shangazi Stella

185 MAMBO YA KUFANYA IGIZO DHIMA: Waigizaji wawili wajifanye kuwa mume na mke (hata kama ni wavulana wawili au wasichana wawili) Zungumzia aidha mke anataka mume atumie kondomu au anataka akapimwe VVU. Baada ya hapo waeleze wenzako katika kikundi kitu gani kimetokea. Wake na waume walijisikiaje? Umejifunza nini katika mazungumzo haya? Je, ni rahisi kwa msichana kumwomba mpenzi wake atumie kondomu au mwanamke kumwomba mume wake? Au ni sawa? Iwapo kuna tofauti kwa nini? Katika vikundi vyenu, chora mume na mke ambao wanaishi pamoja kwa furaha. Katika picha hiyo orodhesha mambo yote ambayo hufanya ndoa kuwa nzuri. Onesha picha kwa makundi mengine. Je, wote mlikuwa na mawazo sawa?

186 Nina msongo wa mawazo 30 Mpendwa Anna Kwa bahati mbaya, kuwa na huzuni ni sehemu ya kawaida ya maisha ya kila mtu.vijana wengi wana matatizo katika maisha kwa sababu ya umaskini na vurugu. Hata wale unaodhani wana maisha mazuri kuna wakati wanakosa raha. Kama kijana, mabadiliko hutokea katika mwili wako. Mabadiliko haya ni ya kibailojia, humfanya mtu abadilike hali kutoka kuwa na furaha na kuwa na huzuni halafu hali ya furaha kujirudia. Haya yote yanaweza kutokea ndani ya saa chache. Inawezekana wapo marafiki zako ambao wanajisikia kama wewe unavyojisikia. Waeleze kuhusu matatizo yako nao watajisikia huru kuzungumza na wewe. Wapo wasichana na wanawake ambao hujisikia kukosa raha kabla ya kuona siku zao (kuingia kwenye hedhi). Hii ni hali ambayo hujitokeza kabla ya kupata hedhi. Mwulize Mhudumu wa afya au mwanamke mtu mzima kuhusu tiba yake. Yapo mambo ambayo unaweza kuyafanya ili kushughulikia masononeko uliyonayo. Usijifanye, ni afadhali kuwashirikisha watu wengine hisia zako. Zungumza na marafiki zako na familia yako pia. Mazoezi yanaweza kukusaidia. Pumzika kwa kulala usingizi wa kutosha na kula chakula bora. Jaribu kujipumzisha na kufanya mambo yanayokufurahisha kama kuimba au kusoma vitabu.vilevile ikiwa unajisikia vibaya sana lia kwa sababu kulia kunaweza kukufanya ujisikie vizuri zaidi. Iwapo yote haya hayatakusaidia utahitaji msaada wa kitabibu na unasihi. Ninakutakia kila la kheri, umekuwa jasiri kwa kuuliza, nina uhakika hali hii ya kunyon gonyea na kukosa raha utaishughulikia kiujasiri. Shangazi Stella

187 MAMBO YA KUFANYA Katikati ya bango kitita chora picha ya mtu mwenye huzuni na kwa kumzunguka, orodhesha mambo yote ambayo yanaweza kumfanya ajisikie vizuri zaidi. Yale ambayo unadhani yatamsaidia zaidi yawe karibu na huyo mtu na mengine yawe mbali. Waeleze wenzako katika kundi kuhusu wakati wowote ulipojisikia mnyonge, umechanganyikiwa au kukasirishwa katika siku za karibuni. Sema kama kulikuwa na sababu ya kuwa na huzuni na jinsi ilivyopotea. Katika kila wiki, amua ni siku gani mtaambizana jinsi wiki ilivyokwenda na jinsi mnavyojisikia. Shughulikia jinsi mnavyoweza kusaidiana na wapi mnaweza kwenda kutafuta msaada (iwapo mnao utaratibu wa kukutana mara kwa mara anza na shughuli hii. Iwapo unafanya mazoezi chini ya mara tatu kwa wiki, kubaliana na marafiki zako kufanya jambo ambalo linakufanya ufurahi kama kutembea au kukimbia. Kutoa msaada kwa watu wengine ni njia mojawapo ya kumfanya mtu ajisikie vizuri. Amua shughuli mbili unazotaka kufanya (kwa mfano kujitolea kazi za kanisani au msikiti au kuwasaidia watoto wadogo wafanye kazi za nyumbani walizopewa shuleni). Tayarisha mpango wa kazi wa kufanyia shughuli hizi. Baada ya hapo jadili jinsi ulivyojisikia.

188 Mimba hii siitaki 31 Mpendwa Prisila Ninasikitika hili limetokea lakini wewe sio mtu wa kwanza.tafadhali ninakuomba usijidhuru wala kumdhuru mtoto wako. Zungumza na mtu unayemwamini katika familia yako au katika jamii yako. Mtu huyu anaweza kukusaidia kuwaambia wazazi wako.wazazi wanaweza kushituka au hata kukasirika wakisikia lakini baada ya hapo wanaweza kukusaidia. Unaweza kufanya kati ya mambo yafuatayo. Kaa na mtoto kwa msaada wa familia yako na ikiwezekana kutoka kwa mpenzi wako. Mtoto akikua unaweza kuendelea na masomo yako au mtu mmoja katika familia yako anaweza kupenda kumtunza mtoto wako wakati wewe unaendelea na shule. Toa mtoto kwa watu ambao wako tayari kumtunza. Kwa kutumia njia hii, mtu ambaye anamhitaji mtoto atapenda kumtunza mtoto.yapo mashirika ambayo yanaweza kukufanyia mpango huu. Tafadhali Prisila usitoe mimba, kutoa mimba ni kosa la jinai pia ni hatari sana kwa sababu kunaweza kusababisha utasa na kifo. Usiweke kitu chochote ukeni au kuruhusu mtu mwingine afanye hivyo.vilevile usifikirie kumtupa mtoto wako, ni kosa na itakufanya ujisikie vibaya na mwenye makosa wakati wote. Fikiria kwa uangalifu kabla ya kutenda. Ni matumaini yangu utapata msaada unaouhitaji kila la kheri. Shangazi Stella

189 MAMBO YA KUFANYA Nchini Tanzania utoaji mimba unaruhusiwa tu pale ambapo daktari ameshauri ili kuokoa maisha ya mama, ama sivyo ni kosa la jinai. Katika nchi nyingine, kwa mfano Afrika ya kusini wanawake wanaruhusiwa kutoa mimba iwapo mimba ina umri wa chini ya wiki 12. Unaonaje hili? Andaa mdahalo kuhusu mada hii IGIZO DHIMA: Watu watatu katika kikundi waigize ambapo mtu anaye msaidia Prisila anawaeleza wazazi wake kuhusu ujauzito wake. Mtu yeyote anayeangalia anaweza kusimamisha igizo wakati wowote, na kuchukua nafasi ya mtu yeyote anayeigiza na kufanya jambo lolote tofauti. Baada ya hapo jadili yote ambayo yanawezekana na yanaweza kumsaidia Prisila. Ni mashirika au vikundi gani vinavyotoa msaada unavyovifahamu katika eneo lako au sehemu nyingine ambavyo hutoa msaada na ushauri kwa wasichana kama Prisila ambao wana mimba zisizotakiwa? Yafanyie uchunguzi. Kati ya mashirika haya, yapo ambayo yanatetea utoaji mimba uhalalishwe katika nchi yako? Waombe waje kuzungumza nanyi kuhusu kazi wanazozifanya wao.

190 Dini yangu inakataza matumizi ya kondomu 32 Mpendwa Hosea Hongera kwa kutaka kujikinga wewe na mpenzi wako dhidi ya mimba zisizotakiwa VVU na magonjwa ya ngono. Mashirika mengi ya Dini yana watia moyo watu kuacha ngono mpaka watakapooa au kuolewa na wanahimiza watu wasitumie kondomu. Lakini watu wamebadilika katika Dini zote, wanaamini kuwa ni afadhali kutumia kondomu ili kuzuia maambukizi ya VVU. Wengine husema kufanya ngono nje ya ndoa ni dhambi, lakini ngono bila kondom, ukiwa unajua kuwa unamuweka mpenzi wako hatarini vilevile ni dhambi kwa sababu ni kinyume na amri kuu za Mungu Usiue. Iwapo wewe na mpenzi wako mtaamua kwa pamoja kufanya ngono, pima faida na hasara za kutumia kondomu. Faida za kiafya ziko wazi lakini itabidi ufikirie mtizamo wa Dini yako. Kuhusu swali lako rahisi, kondomu hazina matundu na wala VVU haviwezi kupenya. Kondomu zinaweza kuteleza na kutoka au kupasuka wakati wa tendo la ngono. Ndio maana kondomu sio salama kwa 100%. Lakini zikitumika vizuri, kwa usahihi na kila mara ngono inapofanyika, kondomu ni njia pekee nzuri ambayo inajulikana kwa kuzuia maambukizi ya VVU zaidi ya kuacha ngono au kuaminiana ambazo ni salama 100%. Iwapo umefanya ngono bila kondomu fikiria kuhusu kupima VVU Kabla ya kuanza ngono na mpenzi wako. Shangazi Stella

191 MAMBO YA KUFANYA Mwezi Machi 2004 Askofu Kevin Dowling wa Kanisa la Katoliki Dayosisi ya Rustenburg Nchini Afrika Kusini alisema Kuacha ngono kabla ya ndoa na uaminifu kwa mpenzi mmoja katika ndoa iliyo imara, kwa vyovyote vile hii ndiyo misingi ya kuishi vizuri na kuepuka maambukizi. Hata hivyo katika dunia ya sasa, Kanisa linatakiwa kuwapa nafasi waumini kuchagua, mojawapo ni matumizi ya kondomu, si kama njia ya kuzuia mimba bali kama njia ya kuzuia uambukizaji wa VVU, virusi ambavyo vimesababisha vifo duniani kote. Je unakubaliana na maelezo haya? Kwa nini? Fanya mdahalo kuhusu mada hii Unaweza kuwa na imani ya kidunia lakini bado ukawa na maoni yako tofauti kuhusu mambo yanayoathiri maisha yako na uhusiano na watu wengine. Zungumza na watu katika mashirika ya kidini yanayofanya kazi na familia na watu binafsi ambao wameathirika na VVU na UKIMWI wanasemaje kuhusu matumizi ya kondomu? Je katika eneo lenu kipo kikundi cha vijana wenye Dini tofauti au Dini moja ambao wanaweza kujadili na kushauriana kuhusu changamoto katika maisha yao? Kama hakuna, ni jinsi gani unaweza kuanzisha kikundi kama hicho? Na unaweza kushirikiana vipi na watu wengine ili kuwasaidia watu wenye shida katika jamii yenu?

192 Ninapata maumivu makali sana wakati wa hedhi 33 Mpendwa Agness Maumivu wakati wa hedhi ni jambo la kawaida. Ninasikitika kuwa wewe maumivu yako ni makali. Yapo mambo mengi unaweza kufanya ili kukusaidia. Sugua sehemu ya chini ya tumbo na kusukuma sehemu nyororo ya mkono kati ya dole gumba na kidole cha kwanza. Loweka kitambaa kizito ndani ya maji ya moto au tumia chupa maalumu ya maji ya moto na kuweka juu ya sehemu unayo sikia maumivu. Kunywa chai ya tangawizi au tumia dawa nyingine za kienyeji. Ukiweza fanya kazi zako za kila siku na jaribu kufanya mazoezi na kutembea. Kunywa dawa nyepesi za maumivu (kama asprini au paracetamol). Iwapo tatizo linaendelea mwombe Muuguzi au Mhudumu wa afya kuhusu dozi ya chini ya vidonge vya kuzuia mimba ambavyo vitadhibiti maumivu na kupunguza kiasi cha damu inayotoka. Ni salama kabisa kwa wasichana balehe. Usijisikie vibaya iwapo watu wanajua kwamba umepata hedhi. Ni sehemu ya kawaida ya kuwa msichana au mwanamke. Kwa nini usikae pamoja na rafiki zako wa kike na kumwomba Mwalimu wa kike awasaidie kutatua tatizo la vifaa shuleni? Unayo haki ya elimu, na iwapo suala hili hukulifanya wewe na wasichana wengine wakose masomo kila mwezi, wewe na shule mnatakiwa kushirikiana kutafuta ufumbuzi. Shangazi Stella

193 WASICHANA: Jaribu mojawapo ya ushauri wa Shangazi Stella. Iwapo unapata maumivu wakati wa hedhi.toa taarifa jinsi ushauri huo ulivyokusaidia. WAVULANA: Zungumza na dada zako au wasichana wa darasani kwenu. Chunguza zaidi kuhusu hedhi na washirikishe wasiwasi ulio nao. MAMBO YA KUFANYA Katika jamii kuna sehemu au hali ambazo ni rahisi kubadilisha kile ambacho hatukipendi, na sehemu nyingine ambazo hatuna jinsi ya kudhibiti au kujirekebisha kinachotokea.yasome Maputo hapa chini na uyagawe katika sehemu tatu Rahisi kubadili Inawezekana kubadili Ni vigumu sana kubadili shule Kikundi cha vijana Kliniki Sheria za kitaifa Klabu za michezo Sera za Elimu na ajila Klabu za akiba Mpenzi wa Kike/Kiume Kituo cha vijana Benki Kikundi cha waigizaji Kanisa Marafiki Kituo cha vijana Sasa chagua sehemu tatu au hali kutoka kwenye orodha ya rahisi kubadili, au inawezekana kubadili. Ungependa kubadili nini katika haya? Kwa kushirikiana na watu wengine mtafanya nini ili mabadiliko yatokee? Angalia mpango wa kazi mwisho wa kadi ya 29 na anza kutayarisha.

194 Buzi langu hunifanyia vituko 34 Mpendwa Huruma Ninasikitika kuwa mpenzi wako sio mtu mzuri tena kwako. Lakini mara nyingi haya hutokea kwa wanaume wazee na ambao wana pesa. Mabuzi hupenda wasichana wadogo kwa sababu ni wazuri na hawalalamiki.vilevile ni kwa sababu wanaamini kuwa wasichana hawa hawana maambukizi ya VVU. Lakini uhusiano hauna usawa, mwanaume anapochoka huanza kuvunja ahadi na kumfanyia vibaya msichana. Haya ndiyo yanayotokea kwako sasa hivi. Kufanya ngono bila ya kondomu ni hatari na mitishamba haiwezi kutibu VVU. Ingekuwa kweli Waganga wa kienyeji wangekuwa tajiri sana. Ukitumia miti shamba kwa ajili ya kutoa mimba ni hatari sana na unaweza usifanikiwe. Ni matumaini yangu utaamua kumuacha rafiki yako wa kiume. Uhusiano huu hauwezi kukufanya uwe na furaha. Jaribu kutafuta uhusiano ambayo una usawa na unaweza kusema unachotaka. Fikiria kuhusu maisha yako ya baadaye na jinsi ya kufanikisha ndoto zako ziwe za kweli. Ukijifunza stadi nyingine na kupata pesa unaweza kufanya kozi ya uana mitindo.wanamitindo wanahitaji elimu vilevile, na kwa kawaida wanakuwa na kazi nyingine. Kwa hiyo jaribu kutafuta shughuli nyingine ambayo unaweza kufanya ili uweze kuishi. Shangazi Stella

195 MAMBO YA KUFANYA Angalia nyuma kwenye mambo ya kujadiliana ili uone ni sababu gani ulizitoa kwa wasichana kupenda mabuzi. Kwa kila sababu tafuta njia ambayo wasichana wanaweza kupata haya bila ya kujihatarisha. Kwa mfano: Pesa na nguo nzuri wanaweza kupata. IGIZO DHIMA: Waigize Wawili wawili, igiza mazungumzo ya Nyarai anamweleza Godfrey kwamba hataki kumwona tena. Godfrey anachukua hatua gani? Baada ya hapo eleza kwenye kikundi chako kitu kilichotokea na jinsi kila mtu alivyojisikia mlipokuwa mnaigiza. Umejifunza nini kutokana na igizo? Watu wengine husema kuwa wanaume wazee wanaopenda wasichana wadogo huwadhalilisha wasichana na wanatakiwa kuadhibiwa na wengine hufikiri kuwa tatizo lipo kwa vijana wa kike ambao ni waroho na wanawafuata mabuzi ili wapate starehe. Wewe unaonaje? Wawili wawili au kwa kutumia vikundi vidogo, tayarisha wimbo kuonyesha mawazo yenu yanayohusu mabuzi. Panga muda wa kuimba katika kundi kubwa.

196 Ninashindwa kujisomea kwa sababu ya mapenzi 35 Mpendwa Jafari Mapenzi katika umri wa miaka 17 yanaweza kuwa ya kikweli kweli kama mapenzi katika umri wa miaka 27. Hata hivyo pamoja na kujisikia raha ya mapenzi unahitaji kuweka maisha mengine yaendelee kama kawaida. Kwa bahati nzuri mamilioni ya wapendanao wamegundua kwamba miezi michache ya kwanza ya kupenda sana inaweza kubadilika kuwa mapenzi ya undani na ya kutulia zaidi. Kwa hiyo si muda mrefu utaona ni rahisi kuzama katika kusoma vitabu. Hata hivyo, kutambua tatizo ni hatua moja kubwa katika kulitatua tatizo hilo. Zungumza na mpenzi wako kuhusu hisia zako na jadili jinsi mnavyoweza kuwa pamoja na mkaendelea na mafunzo yenu. Mnaweza kutenga muda wa kuonana au mnaweza kukubaliana kuwa mtakuwa mnaonana baada ya kumaliza kujifunza somo fulani. Au, Iwapo na yeye ana mitihani, mnaweza kujaribu kusoma pamoja. Ili mradi tu msome bila ya kushikana shikana. Iwapo uhusiano wenu ni mzuri hata kazi za kuchosha kama kupalilia zinaweza kuwaletea raha kama mkifanya kwa pamoja. Lolote utakalo amua wewe na rafiki yako wa kike mnaweza kuhimizana kufanya kazi za shule. Ndoto zenu za kimapenzi katika maisha na mengineyo zitakuwa na nafasi nzuri iwapo mtafaulu mitihani yenu. Shangazi Stella

197 MAMBO YA KUFANYA Tunga wimbo au shairi kuhusu mambo mazuri na mabaya ambayo unaweza kuyapata kwa sababu ya mapenzi. Soma au imba mbele ya wenzako katika kikundi. Je, wengi wenu mliona pande zote za mapenzi yaani mazuri na mabaya, au yote yalikuwa sawa? Mapenzi hufanya dunia izunguke lakini hayaweki mkate mezani Tunga vitendawili vyako vinavyohusu mapenzi. Ni vipi unavipenda zaidi? Katika kikundi cha watu wawili wawili tayarisha ratiba ya wiki. weka muda wa kujifunza au kufanya kazi, michezo au klabu, kusaidia familia, kusoma na muda wa kupumzika. Muda ambao unaweza kumuona mwenzi wako. Jaribu kuwa halisi. Wakati mwingine hisia zetu, za furaha au huzuni huonekana kama mto unaoenda kasi baada ya mvua nzito kunyesha na hatuwezi kusimama imara kwenye ardhi. Ikitokea hivi, ni kitu gani kitakufanya usimame imara zaidi ya kusali, kuzungumza na rafiki mzuri, kumsaidia mtu mwingine, au kucheza michezo? Waeleze wenzako kwenye kundi, na ahidi kusaidiana msaada utakapohitajika. Imechorwa na David Chikoko

198 Mama yangu ana maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI na yuko wazi kusema 36 Mpendwa Hamisi Siwezi kukupatia jibu kuhusu nani umweleze kuwa una maambukizo ya VVU au UKIMWI, ni uamuzi mzito na ni mkubwa. Kila mtu lazima afanye uamuzi wake mwenyewe. Wengine huamua kutomweleza mtu yeyote, wengine humwambia ndugu wa karibu au rafiki, wengine huwaeleza watu wengi na hufanya hivyo katika hatua tofauti. Lolote wanalochagua watu ni sawa tu. Watu wengi hujisikia kuwa na furaha wanapowashirikisha hisia zao watu wengine, kama mama yako ni jasiri mno kiasi cha kuongea hadharani. Na kwa yeyote anayeishi na VVU au UKIMWI kuwa na mnasihi wa kuzungumza naye au kikundi cha kutoa msaada ni muhimu sana. Hata hivyo, mpaka jamii itakapokuwa wazi kuhusu VVU, kuwaeleza watu una VVU kunaweza kuleta matatizo makubwa kama vile kupoteza kazi, marafiki au wapenzi au hata mahali pa kuishi.watu wanahitaji kupima faida dhidi ya hasara watakazozipata binafsi kabla ya kumweleza mtu yeyote kwamba wana maambukizo ya VVU. Iwapo ni mfanyakazi unahitaji kujua haki zako za kisheria kama mfanyakazi unayeishi na VVU. Kweli, ninakubaliana na wewe kuwa, kwa kawaida watoto huwa na furaha zaidi wanapojua ukweli hata kama unahuzunisha. Kwa hiyo, ninashukuru kwa kuwasaidia vijana wengi kuwa jasiri na wawazi. Hadithi yako na ya mama yako zitatoa matumaini kwa watu wengi. Shangazi Stella

199 MAMBO YA KUFANYA Unaonaje majibu ya Shangazi Stella? Eleza jinsi wewe na rafiki zako mnavyoweza kupambana na ubaguzi na unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na VVU au UKIMWI. (kwa mfano michezo ya kuigiza majaribio, midahalo hotuba za watu walio na VVU,Tshirts zilizoandikwa Nina Ukimwi au Rafiki yangu aliye na ukimwi bado ni rafiki yangu ). Chagua tatu ambazo ni nzuri zaidi kwa ajili ya kikundi chako na shughulikia jinsi mtakavyoendesha mawazo yenu IGIZO DHIMA: Katika kikundi chenu tengeneza mchezo ambapo watu wanazungumza kuhusu mtu ambaye ana UKIMWI.Wengi wao ni wabaya kuhusu mtu ambaye ana UKIMWI, lakini mtu mmoja anajadili kwa nguvu kujaribu kubadilisha mtizamo wao. Mwisho wake unakuwaje? Mwalike mtu mmoja kama Tausi na mama yake kuja na kuwazungumzia kuhusu matatizo ambayo wamekumbana nayo kutokana na mitazamo ya watu wengine kuhusu VVU na UKIMWI.Waulize ni kitu gani kimewasaidia katika kushughulikia mitazamo hiyo??

200 Je, nitazitibu vipi chunusi zangu? 37 Mpendwa Joan Inaelekea una matatizo ya chunusi za kawaida ambazo huwapata vijana balehe. Hizo ni dalili za kubalehe na vijana wengi hupitia hatua hiyo. Hata hivyo, hiyo haitakusaidia katika tatizo lililopo. Chunusi ni ngumu kutibika mara moja, lakini iwapo utafuata ushauri huu zinaweza kupungua au kutoweka kabisa. Kwanza kabisa, chakula unachokula ni muhimu. Kula matunda na mboga za majani za kutosha na tumia vyakula asilia kama vile mkate wa kumimina. Epuka kula vyakula visivyo na virutubisho kama pipi, biskuti, chakula chenye mafuta na vinywaji vyenye mapovu. Matunda au mahindi ya kuchoma au kuchemsha ni bora zaidi kuliko maandazi na keki. Pili kunywa maji mengi. Maji husaidia kusafisha mwili Tatu na ambalo ni muhimu ni kuupenda uso wako. Usipake losheni na krimu. Usikamue chunusi, nawa uso polepole na sabuni kwa kutumia maji ya uvuguvungu, na chua taratibu. Ukisugua uso wako taratibu kwa kutumia unga wa sembe na maji, ngozi huwa safi na hufanya iwe laini pia. Vijana wengine huhitaji msaada wa kitabibu, kama vile viuavijasumu kutoka kliniki au kwa daktari. Usifikirie kuhusu chunusi tu, kumbuka mambo mengi mazuri yanayohusu mwili wako. Usiache kutoka na marafiki zako, kwa sababu watu wengine huenda hawazioni chunusi hizo kama unavyofikiria. Kila la kheri Shangazi Stella

201 MAMBO YA KUFANYA Taja vitu vikuu ambavyo unakula.vigawe katika kundi la chakula kizuri na chakula kibaya (yaani chakula kisichokuwa na virutubisho). Angalia ni wakati gani unakula chakula kibaya na ni kwa vipi unaweza kula chakula kizuri mara nyingi zaidi? Chora picha yako mwenyewe.weka lebo ya mambo yote mazuri kuhusu mwili wako na mambo ambayo mwili unaweza kufanya. Kwa mfano, miguu yenye nguvu kwa ajili ya mpira wa miguu, macho makubwa ya kuangalia, masikio mazuri ya kusikilizia matatizo ya watu, meno meupe yanayovutia, mikono ya kutolea msaada kwa familia. Weka angalau lebo tano. Mwisho chora tabasamu kubwa kwenye uso wako. Imechorwa na David Chikoko

202 Nina maambukizo ya Virusi Vya UKIMWI na mimba 38 Mpendwa Rehema Hongera kwa kuwa jasiri kiasi cha kupima VVU. Sasa hivi unaweza kufanya mambo mengi ili kujitunza wewe mwenyewe na mtoto uliyebeba.watoto wengi wanaozaliwa na mama wenye maambukizo ya VVU hawapati maambukizi ya VVU. Watoto watatu kati ya kumi hupata maambukizo ya VVU. Maambukizi hutokea mtoto akiwa tumboni, wakati wa kuzaliwa na wakati wa kunyonyesha. Kwa bahati nzuri zipo njia nyingi za kupunguza hatari ya maambukizi kutokea. Kwanza, zipo dawa aina ya Nevirapine ambazo hutolewa bure kwa akina mama wajawazito wenye maambukizi. Dawa hizi hupatikana kliniki au hospitalini, husaidia watoto wasipate maambukizi wakati mama anapojifungua, na humkinga mtoto katika siku tatu za mwanzo.waulize kliniki kuhusu mpango wa kuzuia maambukizi ya mama kwa mtoto. Vilevile, aidha mlishe mtoto maziwa ya kopo au tafuta taarifa zote zinazohusu jinsi ya kunyonyesha salama kwa kumnyonyesha mtoto maziwa ya mama tu. (Yaani mtoto asipewe kitu kingine chochote isipokuwa maziwa ya mama ( hata maji asipewe) kwa kipindi cha miezi sita ya mwanzo. Mtoto akifikisha miezi sita unatakiwa kuacha kumnyonyesha kabisa na badala yake kumpa mtoto vyakula vingine. Vilevile msaidie mtoto kwa kujifunza na kuuliza ushauri kutoka kliniki. Kliniki watakueleza lini mtoto wako anaweza kupimwa VVU na njia nzuri ya kuhakikisha mtoto ana afya nzuri. Shangazi Stella

203 MAMBO YA KUFANYA IGIZO DHIMA: Mama mwenye VVU ameamua kumnyonyesha mtoto wake kwa kipindi cha miezi sita ya kwanza. Anahitajika kumweleza mama mkwe kwamba hawezi kumpa mtoto aina nyingine yoyote ya chakula au kinywaji. Unafikiri hili ni tatizo katika maisha halisi? Hatua gani zinaweza kuchukuliwa kuhusu suala hili? Taja faida na hasara ya kunyonyesha mtoto iwapo mama ana maambukizi ya VVU. Fanya hivyo hivyo iwapo mtoto atapewa maziwa ya kopo. Ungekuwa katika hali hii ungefanya nini? Unafikiri inakuwaje, ukiwa kama mama aliye na maambukizi ya VVU na una mtoto anayeugua? Chunguza kuhusu mipango yoyote katika jamii yako ya kuwasaidia wanawake walio katika mazingira haya. Je wanahitaji msaada zaidi? Utafanyaje ili kuwasaidia? Angalia kadi ya 26 kwa taarifa zaidi kuhusu jinsi ya kuishi kwa matumaini.

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper

More information

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) 102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako

More information

Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo. Zanzibar, 7-10 Februari 2006

Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo. Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Mazoezi yaliyofanyika wakati wa warsha kuhusu Elimu-Jumuishi kwa Vitendo Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Imechapishwa na: The Atlas Alliance Schweigaardsgt 12 SLP 9218 Grønland 0134 Oslo, Norway Simu: +47

More information

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza Shule za umma za kata ya Fayette 1 Mwongozo wa Familia wa Kujifunza Muhtasari wa yale watoto wanastahili kufahamu na kuweza kufanya na njia za familia kuongeza masomo nyumbani. Tunaamini familia ni wenzetu.

More information

Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo

Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo Kuwawezesha wasichana kwa kuboresha kujikubali na kujithamini Hivi Ndivyo Nilivyo Mazoezi ya wenye umri wa miaka 11-14 Hivi Ndivyo Nilivyo kwa wenye umri wa miaka 11-14 Kuhusu Hivi Ndivyo Nilivyo Ikiwa

More information

Mwongozo wa Mwezeshaji

Mwongozo wa Mwezeshaji JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Ushauri Nasaha na Upimaji wa VVU kwa Hiari Mwongozo wa Mwezeshaji Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Machi 2010 Kimetafsiriwa kutoka lugha

More information

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted

More information

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa

More information

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji!

Yaliyomo. Kuhusu kitabu hiki. Hautakuwa peke yako. Mfumo wa msaada ni wa manufaa sana wazazi wote wanahitaji! Yaliyomo Kuhusu kitabu hiki Kuhusu kitabu hiki.........................................................1 Unapojisikia vibaya.........................................................2 Unapoanza kuwa mzima

More information

Ufundishaji wa lugha nyingine

Ufundishaji wa lugha nyingine CHUO CHA ELIMU CHA KIMATAIFA OFISI YA ELIMU YA KIMATAIFA Ufundishaji wa lugha nyingine Na Elizabeth B. Bernhardt ELIMU MAZOEA KITABU NA. 20 1 Chuo cha Elimu cha Kimataifa (The International Academy of

More information

MAFUNZO YA AFYA YA UZAZI: Nyongeza ya Mtalaa Kwa vijana

MAFUNZO YA AFYA YA UZAZI: Nyongeza ya Mtalaa Kwa vijana MAFUNZO YA AFYA YA UZAZI: Nyongeza ya Mtalaa Kwa vijana Umeigwa kwa Mtindo wa Kenya a program of the International Youth Foundation The International Youth Foundation (IYF) invests in the extraordinary

More information

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA

More information

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017

More information

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika

More information

Human Rights Are Universal And Yet...

Human Rights Are Universal And Yet... Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,

More information

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako. Kitabu cha Vijana Balehe

Wewe Maisha Yako Ndoto Zako. Kitabu cha Vijana Balehe Wewe Maisha Yako Ndoto Zako Kitabu cha Vijana Balehe Wewe, Maisha Yako, Ndoto Zako: Kitabu cha Vijana Balehe Catherine Watson na Ellen Brazier Shukurani Kitabu cha Wewe, Maisha Yako, Ndoto Zako ni tafsiri

More information

Makala ya Mshiriki wa Mafunzo

Makala ya Mshiriki wa Mafunzo JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Ushauri Nasaha na Upimaji wa VVU kwa Hiari Makala ya Mshiriki wa Mafunzo Mpango wa Taifa wa Kudhibiti UKIMWI Machi 2010 Kimetafsiriwa kutoka

More information

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu BLOOD PRESSURE UK Shinikizo la damu ndicho chanzo kikubwa cha ulemavu na vifo vya mapema kule Uingereza, kupitia kiharusi, mshtuko wa moyo na maradhi ya moyo.

More information

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu

More information

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza

MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA. Kwa Wanaoanza 1 Matumizi bora ya Facebook kwa Biashara MATUMIZI YA FACEBOOK KWA BIASHARA Kwa Wanaoanza For IT Services & Web Solutions Web: Email: info@dudumizi.com Phone: 0768816728 2 Matumizi bora ya Facebook kwa

More information

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI

MACHAGUO YA UZAZI KUFIKIRIA KUWA MZAZI This booklet on Becoming a Parent was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at. MACHAGUO

More information

Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo

Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu. Nyenzo ya Mafunzo Mwongozo kwa familia zinazofanya kazi pamoja kwa maisha endelevu Nyenzo ya Mafunzo Vi Agroforestry Vi Agroforestry ni shirika la ushirikiano la maendeleo la Sweden, linalopambana dhidi ya umasikini na

More information

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited

More information

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue?

Tufundishane! Mwalimu Bora In this issue: Issue 6, December Do you want to be in our next issue? Tufundishane! Let s teach each other! This newsletter is published by The Foundation for Tomorrow and is meant to be a venue for teachers and schools to share and learn from each other s best practices.

More information

KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA

KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA KUWEZESHA MBINU ZA UZUIAJI MIMBA KATIKA SUHULA ZA AFYA: MASWALI 10 KWA VIKUNDI VYA JAMII KUZINGATIA Toleo la kwanza 2012 Mwandishi: USAID DELIVER PROJECT Wachangiaji: Gary Steele, John Snow, Inc. and Judith

More information

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi 3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi

More information

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited

More information

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)

More information

Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health

Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health Mwongozo wa Mafunzo Yaliyochanganywaya K4Health Wasiojua kusoma na kuandika katika karne ya 21 hawatakuwa wale wasiojua kusoma na kuandika lakini wale ambao hawawezi kujifunza, kutojifunza na kujifunza

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level * 899145 4 672* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2010 Additional Materials: Answer Booklet/Paper READ

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi

More information

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.

More information

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees

TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO. Kutunza miche yako. Take care of your seedlings. Take care of your trees TIST (TANGA) HABARI MOTO MOTO Tel. +255748-537720/632013, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@ tist.org April 2004 Take care of your seedlings This year, thousands of seedlings have been planted in the TIST

More information

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini...

Elimu Bora, lakini... C HakiElimu Elimu bora, lakini... Elimu Bora, lakini... Shukrani za dhati kwa wote waliotusaidia katika kutayarisha kijitabu hiki: Nsa Kaisi, Mshauri wa Rais, kwa mchango wake mkubwa wa mawazo Wafanyakazi wote wa HakiElimu 2003-2004 Many

More information

Namba ya moduli 3 Kuangalia sanaa

Namba ya moduli 3 Kuangalia sanaa Rasilimali za Msingi Mafunzo Ya Jamii Na Sanaa Namba ya moduli 3 Kuangalia sanaa Sehemu ya 1 Kuchunguza Kazi za Sanaa zionekanazo Sehemu ya 2 Kuandaa Shughuli za Sanaa kwa Vitendo- Sehemu ya 3 Kutumia

More information

Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana (SDSMV) Tanzania. Kiongozi Cha Mwezeshaji. Jaap Van Pol na Francesca Dalla Valle

Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana (SDSMV) Tanzania. Kiongozi Cha Mwezeshaji. Jaap Van Pol na Francesca Dalla Valle Programu kuhusu msaada wa sera kwa ajira vijijini na kazi yenye heshima kwa uhimizaji maisha sawa endelevu vijijini kulingana na mabadiliko ya tabia nchi Shamba Darasa na Stadi za Maisha kwa Vijana (SDSMV)

More information

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na

More information

SautiElimu. Sauti Yako Isikike

SautiElimu. Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike SautiElimu Sauti Yako Isikike Mtayarishaji : Godfrey Telli Mchangiaji : Robert Mihayo Mhariri : Rakesh Rajani Shukrani za dhati kwa timu ya waandaaji wa SautiElimu 1-10: Lilian

More information

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa

Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Child Abuse & Neglect 43(2015)8 21 Orodha Yaliyomo inapatikana katika ScienceDirect Unyanyasaji wa Watoto & Kutelekezwa Nakala ya Utafiti Mbinu za kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto kuanzia chini kwenda

More information

Early Grade Reading Assessment for Kenya

Early Grade Reading Assessment for Kenya EDDATA II Early Grade Reading Assessment for Kenya Baseline Instruments: Kiswahili and English EdData II Technical and Managerial Assistance, Task Number 4 Contract Number EHC-E-01-04-00004-00 Strategic

More information

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya

More information

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa.

Kocha Mkuu. mabingwa. itakuwa INASTAHILI. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa. itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa. Ili Kutoa mafunzo kwa wanafunzi wako kuwa mabingwa itakuwa ya kuumiza. Itachukua muda. Itahitaji moyo wa kujitoa. Mkuu Inahitaji dhabihu. Unahitaji kujisukuma hadi mwisho wako. Lakini nakupa ahadi hii,

More information

Kijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia

Kijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia IDARA YA KUFIKIA HUDUMA ZA AFYA VERMONT Kijitabu cha Maelezo cha Programu ya Famasia GreenMountainCare MIASHA YENYE AFYA BORA ZAIDI Jedwali la Yaliyomo Jedwali la Yaliyomo... 2 Karibu kwenye Programu ya

More information

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Desemba 2014 1 Shukurani Ripoti hii iliandikwa na Dk. Mkumbo. Ushauri wa kitaalamu ulitolewa na Elizabeth Missokia na Godfrey

More information

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya

More information

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh

More information

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery

More information

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE

HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE HOTUBA YA WAZIRI OFISI YA WAZIRI MKUU: KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU MHE. JENISTA MHAGAMA (MB), KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKU YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI DUNIANI DODOMA, 28 APRILI

More information

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau

More information

Kutetea Haki za Binadamu

Kutetea Haki za Binadamu Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and

More information

Kuwa na Ukimwi ni kama vile kutakiwa kuendelea kuuzima moto unaoniunguza bila kukoma.

Kuwa na Ukimwi ni kama vile kutakiwa kuendelea kuuzima moto unaoniunguza bila kukoma. This booklet on HIV/AIDS was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at VIRUSI VYA

More information

Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo

Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo Elimu-Jumuishi Kwa Vitendo Taarifa ya Warsha Kuhusu Elimu-Jumuishi Iliyofanyika Zanzibar, 7-10 Februari 2006 Kujifunza hakuna mwisho. Kazi ya vikundi imenipa fursa ya kujieleza bila kuhofia kuwa ningekosea.

More information

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump

More information

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI

RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI International Records Management Trust RIPOTI YA WARSHA KUHUSU HABARI KWA AJILI YA UWAJIBIKAJI ukumbi wa British Council Tanzania Auditorium Machi 27-28, 2000 Dar es Salaam, Tanzania warsha imeandaliwa

More information

Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira

Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Moduli ya kwanza Uhamasishaji Jamii juu ya Afya ya Mazingira Kimechapishwa kutokana na Mwongozo wa Jamii juu ya Afya ya Mazingira Jeff Conant na Pam Fadem i COBIHESA

More information

UMRI WA MAKAMO NA KUKOMA KWA HEDHI

UMRI WA MAKAMO NA KUKOMA KWA HEDHI This booklet on menopause was developed by the Tanzania Home Economics Association with support from Our Bodies Ourselves. Other booklets and more information on the project are available at http://www.ourbodiesourselves.org/tanzania.

More information

Siku ya kwanza. Mguso wa ngozi-kwa-ngozi (Ulezi wa kangaruu) Mtoto wako anaweza kuhisi mdundo wa moyo wako

Siku ya kwanza. Mguso wa ngozi-kwa-ngozi (Ulezi wa kangaruu) Mtoto wako anaweza kuhisi mdundo wa moyo wako Siku ya kwanza Baada tu ya mtoto kuzaliwa ni wakati wa kufurahia, lakini pia ni wa kuchosha. Kujua vitu vichache kuhusu kunyonyesha hufanya siku ya kwanza kuwa rahisi kidogo. Baada ya kujifungua Wakati

More information

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO

KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO KITEGO CHA MAREKEBISHO NA HAKI ZA MTOTO Mwaka 2009 Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha sheria mpya ya Mtoto ambayo ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha kuwa haki na ustawi wa

More information

Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E)

Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E) 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI/AGOSTI 2011 MUDA: 2 ½ Kiswahili Fasihi Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E) MAAGIZO Jibu maswali manne pekee Swali la kwanza ni lazima Maswali

More information

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara

Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Mwongozo kwa Lugha Rahisi wa Sera ya Maendeleo ya Ushirika na Sheria ya Vyama vya Ushirika Tanzania Bara Umetayarishwa na Shirikisho la Vyama vya Ushirika Tanzania kwa Kushirikiana na Idara ya Maendeleo

More information

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya

More information

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya Jina Nambari.. Shule... 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI / AGOSTI. 2007 MUDA: SAA 2 ½ MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya 102/3 KISWAHILI FASIHI

More information

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke- Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa

More information

TIST HABARI MOTO MOTO

TIST HABARI MOTO MOTO TIST HABARI MOTO MOTO Tel. +255784-537720/+255717-062960/+255782-250947, P.O.BOX 6049 MOROGORO E-Mail info@tist.org May 2010 Cash Payments for Trees Clean Air Action has developed a way to pay the groups

More information

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0

More information

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI

More information

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini

More information

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

More information

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia : Maelekezo ya kutumia Kupatwa kamili kwa jua Jumatatu, 21 Agosti 2017 Agreement v1.4 Mar 2014 2014-2017 Eclipse2017.org, Eclipse2017.org, inc. inc. TERMS AND CONDITIONS FOR USE OF SOLAR VIEWER Please

More information

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03

Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03 Hatari, Haki za Usalama katika Bahari 03 AEG swahili Bahari ya Aegean Brosha ya maelezo hii ni kwa watu wanaofikiria kuvuka bahari ya Aegean kati ya Ugiriki na Uturuki.Kuvuka kihramu ni uhalifu katika

More information

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka 0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11

More information

International Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi

International Labour Office. Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi International Labour Office Kazi za Ndani Zenye Madhara kwa Watoto: Kijitabu cha Maelezo Mafupi 1 Hakimiliki Shirika la Kazi Duniani 2007 Kimechapwa mara ya kwanza 2007 Machapisho ya Ofisi ya Shirika la

More information

Mipango ya miradi katika udugu

Mipango ya miradi katika udugu Partnerschaftlich Projekte planen Mipango ya miradi katika udugu 2 Dibaji... 3 Utangulizi... 4 I. Nafasi ya (Wajibu wa) Fedha katika Udugu: Mtazamo wa Ki-indonesi... 5 II. Namna UEM Inavyowezesha Miradi

More information

Shabaha ya Mazungumzo haya

Shabaha ya Mazungumzo haya Karibu Katika Mazungumzo Kuhusu Mchakato wa Uhamasishaji Maendeleo ya Kanisa na Jamii CCMP/UMOJA Shabaha ya Mazungumzo haya Kuwafahamisha viongozi wa makanisa kuhusu Mchakato wa CCMP ambao umekuwa ukitumika

More information

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY

MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY HABARI ISSN 1821-5335 Makala Maalum Miaka 15 ya Foundation for Civil Society MAADHIMISHO YA MIAKA 15 YA FOUNDATION FOR CIVIL SOCIETY Uwezeshaji wa moja ya sekta madhubuti za asasi za kiraia barani Afrika

More information

Palliative Care Toolkit

Palliative Care Toolkit KISWAHILI TRANSLATION INPATIENT CARE OUTPATIENT CLINIC HOME-BASED CARE DAY CARE SUPPORT HOSPITAL PALLIATIVE CARE TEAM Physical Psychological Spiritual Social Palliative Care Toolkit Improving care from

More information

Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi

Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Gervas Zombwe 1 1. Utangulizi Katika mazingira ya kawaida kabisa ndani ya jamii yetu, Imezoeleka kusikia au kuona watu wakioanisha dhana ya elimu

More information

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to

More information

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi

Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari Rakesh Rajani na George Omondi HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003. 6S Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) Muhtasari

More information

KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS

KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS ALLIANCE BOYS HIGH SCHOOL KISWAHILI KARATASI YA 2 SCHOOLS NET KENYA Osiligi House, Opposite KCB, Ground Floor Off Magadi

More information

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q 88092387 SWAHILI B HIGHER LEVEL PAPER 1 SOUAHÉLI B NIVEAU SUPÉRIEUR ÉPREUVE 1 SUAHILI B NIVEL SUPERIOR PRUEBA 1 Tuesday 3 November 2009 (morning) Mardi 3 novembre 2009 (matin)

More information

SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI KITABU CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO

SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI KITABU CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO KISWAHILI SANIFU KWA SHULE ZA SEKONDARI KITABU CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO KITABU CHA MWALIMU KIDATO CHA TANO YALIYOMO UTANGULIZI v MPANGILIO WA MASOMO YA KISWAHILI: KIDATO CHA TANO 1 FUNZO: Fasihi (Ukurasa

More information

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma

More information

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI SIKOMBE YIZUKANJI YORADI TASNIFU YA KISWAHILI KWA MINAJILI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (MA. KISWAHILI) KITIVO CHA SANAA

More information

Uzazi wa Mpango. Uzazi wa Mpango. Kulinganisha Ufanisi wa Njia za Uzazi wa Mpango. iwe na ufanisi zaidi. Zenye ufanisi.

Uzazi wa Mpango. Uzazi wa Mpango. Kulinganisha Ufanisi wa Njia za Uzazi wa Mpango. iwe na ufanisi zaidi. Zenye ufanisi. Uzazi wa Mpango MPANGO WA UZAZI WA W.H.O. MWONGOZO WA WATOA HUDUMA YA AFYA DUNIANI Kitabu hik nachukua nafasi ya kitabu cha Mambo ya Msingi katika Teknolojia ya Njia za Kuzuia Mimba SHIRIKA LA MISAADA

More information

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni

More information

MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012

MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012 MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012 TASNIFU HII IMEWASILISHWA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI

More information

Mwongozo wa Kitaifa wa Ujumbe wa Uzazi wa Mpango

Mwongozo wa Kitaifa wa Ujumbe wa Uzazi wa Mpango Mwongozo wa Kitaifa wa Ujumbe wa Uzazi wa Mpango Octoba 2013 1 w 2 Mwongozo wa Kitaifa wa Ujumbe wa Uzazi wa Mpango Octoba 2013 3 4 Yaliyomo Dibaji 7 Shukurani 8 Utangulizi 10-12 Faida za Uzazi wa mpango

More information

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia

Afya Bora, Utu na Kinga. Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Afya Bora, Utu na Kinga Ripoti ya Mashauriano ya Kiufundi 27-28 Aprili 2009, Hammamet, Tunisia Shukrani Ripoti

More information

Deutsche Welle, Learning by Ear 2009 Seite 1 People Who Make A Difference Liberia: Anita Varney Health Facilitator, Fishtown/Liberia

Deutsche Welle, Learning by Ear 2009 Seite 1 People Who Make A Difference Liberia: Anita Varney Health Facilitator, Fishtown/Liberia Deutsche Welle, Learning by Ear 2009 Seite 1 Title: Anita Varney Health Facilitator, Fishtown/Liberia Author: Stefanie Duckstein, HA Afrika/ Nahost Editor: Christine Harjes Translator: Tony Dunham Sound

More information

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI

MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 MWONGOZO WA UTUNGAJI WA SHERIA NDOGO NA USHIRIKI WA WANANCHI 2012 Kitabu hiki kimetayarishwa na Shirika la Equality for Growth (EfG) Equality

More information

United Pentecostal Church June 2017

United Pentecostal Church June 2017 Kwa Nini Tusali? Jarida la Maombi ya Wanawake Kimataifa "Chagua" Ladies Prayer International kwa Facebook United Pentecostal Church June 2017 Tuko na wafuasi Facebook katika Marekani, Hong Kong, Philippines,

More information

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA

More information

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012

More information

Evaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya

Evaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya Evaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya Oduori T. Wamubi Prof. Simala, K. Inyani Profesa Mshiriki Masinde Muliro University of Science and Technology Prof.

More information

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03

More information