UCHANGANUZI WA NOMINO-MKOPO ZA KIGIRYAMA KUTOKA KIINGEREZA NANCY JUMWA NGOWA

Size: px
Start display at page:

Download "UCHANGANUZI WA NOMINO-MKOPO ZA KIGIRYAMA KUTOKA KIINGEREZA NANCY JUMWA NGOWA"

Transcription

1 UCHANGANUZI WA NOMINO-MKOPO ZA KIGIRYAMA KUTOKA KIINGEREZA NANCY JUMWA NGOWA TASNIFU ILIYOWASILISHWA ILI KUTIMIZA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMIFU YA CHUO KIKUU CHA PWANI. MEI, 2015

2 i UNGAMO Tasnifu hii ni kazi yangu mwenyewe na haijawahi kuwasilishwa katika Chuo Kikuu chochote kile ili kutimiza mahitaji ya shahada yoyote ile. Nancy Jumwa Ngowa Sahihi: Tarehe: Tunathibitisha kwamba kazi iliyowasilishwa katika tasnifu hii ya shahada ya Uzamifu ilifanywa na mtahiniwa chini ya usimamizi wetu. Hakuna sehemu ya tasnifu hii ambayo itatolewa kwa namna yoyote ile bila kibali kutoka kwa mwandishi na Chuo Kikuu cha Pwani. Wasimamizi: Prof. Rocha Chimerah: Chuo Kikuu cha Pwani Sahihi: Tarehe: Prof. Beja Karisa: Chuo Kikuu cha Pwani Sahihi: Tarehe:

3 ii TABARUKU Kwa wazazi wangu marehemu Karisa Chembe na Kahaso Chembe kwa kunipa msingi bora wa elimu na kwa wanangu Kuvuna na Mbodze kwa upendo wao mkuu.

4 iii SHUKRANI Kwanza kabisa, ninamshukuru Mwenyezi Mungukwa kunipa nguvu na bidii na kwa kweli ufanisi wa kazi hii ni dhihirisho la utukufu wake Mungu. Pia, ningependa kuwashukuru kwa dhati wasimamizi wanguprof. Rocha Chimerah na Prof. Beja Karisa kwa kunipa mwongozo mwema katika masomo ya Uzamifu. Kwa wasimamizi wangu ninasema asanteni sana. Nawashukuruwazazi wangu wapendwa marehemu Karisa Chembe na Kahaso Chembe kwa kunipa malezi bora na elimu. Pia nachukua nafasi hii kuwashukuru wanangu wapendwa Kuvuna na Mbodze kwa kunipa moyo katika kila hatua ya masomo haya ya Uzamifu. Kwa wananguhawa ninasema, nawapenda sana na Mungu awape ufanisi na maisha marefu duniani. Shukurani pia ziwaendee ndugu zangu Emmanuel, Dama, Anthony, Safari, Ngowa, Kazungu, Kadzo, Sadik, Katana, Furaha na Kahindi kwa kunishauri na kunihimiza kufanya bidii katika masomo yangu. Pia nawashukurumarafiri wapendwa;prof. Sheila Ryanga, Prof.Clara Momanyi, Susanne Mung aro, Patricia Mboghoh, Linet Mavu, Ruth Mole na Florence Bett kwa kunitia moyo katika kazi hii.

5 iv IKISIRI Utafiti huu umechanganua kimofofonolojia nomino-mkopo za lugha ya Kigiryama zinazotokana na lugha ya Kiingereza na kubainisha kanuni zinazoongoza michakato mahsusi. Madhumuni ya utafiti huu ni kutambulisha nomino-mkopo zinazotoka katika lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama katika shughuli za ukarabati na vifaa vya magari, pikipiki na baisikeli, kudhihirisha michakato ya kimofofonolojia ambayo inapitiwa na nomino-mkopo hizi na kubainisha kanuni za kimofofonolojia zinazodhibiti ukopaji wa nomino kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama. Nadharia ambayo iliongoza uchanganuzi huu ni Fonolojia Zalishi Asilia inayoangaziwa na Hooper (1976). Maeneo ya utafiti yaliyoteuliwa ni Bamba, Kaloleni, Kilifi, Malindi na Galana. Sampuli ya magareji yaliyoteuliwa ni yale yanayopatikana karibu na miji ya maeneo mahsusi. Data ya kimsingi ya utafiti ilikuwa nomino-mkopo za lugha ya Kigiryama zinazotokana na lugha ya Kiingereza. Nomino hizi zinazotokana na vifaa na shughuli mbalimbali za ukarabati zinazoendeshwa katika magereji ya magari, pikipiki na baiskeli. Data ilikusanywa kwa kutumia mbinu ya Uchunguzi Ushirikishi ambapo mtafiti alifanya kazi kama spannerboy kwa muda wa wiki moja katika kila gereji lililoteuliwa la makanika Wagiryama na kukusanya data ya nomino-mkopo za lugha ya Kigiryama kupitia mazungumzo na mahojiano yao. Mtafiti alikusanya data kwa kunakili nomino-mkopo moja kwa moja kutoka kwa wazungumzi wenyeji wa lugha ya Kigiryama. Ukusanyaji data pia ulihusisha kurekodi sauti za wazungumzaji ili kuweza kunasa matamshi mahsusi ya nomino-mkopo zilizokusanywa. Data ilichanganuliwa kwa kuzingatia hatua mahsusi. Kwanza nomino-mkopo zilipangwa katika makundi na kunukuliwa kifonetiki. Kisha mabadiliko ya sauti katika

6 v nomino-mkopo hizi yalitambuliwa na sauti mahsusi zinazobadilika kuweza kuthibitishwa. Baadaye ruwaza za mabadiliko ya fonimu zilitambuliwa na hatimaye kanuni zinazotawala michakato mahsusi ya kimofofonolojia ziliweza kuwekwa bayana. Maelezo, ufafanuzi, michoro na majedwali yalitumiwa katika utafiti huu. Tasnifu hii imepagwa katika sura tano. Sura ya kwanza inashughulikia utangulizi wa utafiti kwa kuzingatia misingi ya utafiti huu na kuweka bayana swala la utafiti, madhumuni ya utafiti, nadharia tete, upeo wa utafiti na natija ya utafiti. Katika sura ya pili, misingi ya nadharia ya utafiti huu pamoja na misingi ya kidhana imewekwa bayana. Sura ya tatu inaeleza utaratibu wa utafiti, eneo la utafiti, jumuia na uteuzi wa sampuli, vifaa vya kukusanyia data, utaratibu wa kukusanya data, jinsi data ilivyochanganuliwa, pamoja na kuonyesha uaminiki na maadili yaliyozingatiwa katika utafiti huu. Sura ya nne inashughulikia uchanganuzi wa data na matokeo ya utafiti na sura ya tano inatamatisha utafiti huu kwa kutoa hitimisho la utafiti huu na mapendekezo ya mada zingine zinazoweza kufanyiwa utafiti. Utafiti huu ni mchango muhim katika taaluma ya isimu linganishi kwa jinsi ambavyo unahusisha lugha mbili Kiingereza na Kigiryama. Zaidi ya hayo, utafiti huu unasaidia katika ufundishaji wa lugha ya pili kwa sababu vikwazo vya kifonolojia vya lugha hizi mbili vimewekwa bayana. Kwa jumla utafiti huu unachangia katika kuweka hai na kuendeleza lugha ya Kigiryama kwa sababu imeweza kupata ukwasi wa istilahi za kuweza kutumika katika uwanja wa kiteknolojia wa ukarabati wa magari, pikipiki na baiskeli. Kwa jumla utafiti huu ni mchango mpya katika tafiti za kiisimu za lugha ya Kigiryama na pia ni hazina kubwa katika uwanja wa Isimu za lugha za Kiafrika.

7 vi YALIYOMO Ungamo..i Tabaruku ii Shukrani...iii Ikisiri.iv Yaliyomo..vi Orodha ya vifupisho na alama...xii Orodha ya majedwali. xiii Orodha ya michoro.....xv SURA YA KWANZA: UTANGULIZI Usuli wa mada Swala la utafiti Madhumuni ya utafiti Nadharia tete Upeo wa utafiti Natija ya utafiti Maelezo ya istilahi

8 vii SURA YA PILI: MAPITIO YA MAANDISHI Kitangulizi Mapitio ya maandishi Maandishi katika vitabu kuhusu dhana ya ukopaji Maelezo katika majarida kuhusu ukopaji Tafiti katika tasnifu zinazohusu ukopaji Misingi ya nadharia Misingi ya kidhana Lugha ya Kigiryama Fonimu za lugha ya Kigiryama Mfumo wa vokali za Kigiryama Sifa za vokali za Kigiryama Mfumo wa konsonanti za Kigiryama Lugha ya Kiingereza Fonimu za lugha ya Kiingereza Vokali za Kiingereza Vokali sahili za Kiingereza Vokali Pacha za Kiingereza.50

9 viii Vokali utatu za Kiingereza Konsonanti za lugha ya Kiingereza SURA YA TATU: MBINU ZA UTAFITI Kitangulizi Utaratibu wa utafiti Jumuia na uteuzi wa sampuli Sampuli ya maeneo ya utafiti Sampuli ya magereji yaliyoteuliwa Nyanja zilizoshughulikiwa Aina ya maneno yaliyochunguzwa Watu waliohusishwa katika mazungumzo Mbinu ya ukusanyaji wa data Vifaa vya kukusanyia data Hatua za uchanganuzi wa data Matayarisho: kudondoa na kunukuu nomino-mkopo kifonetiki Kutambua mabadiliko ya sauti Kuthibitisha sauti mahsusi zinazobadilika Kutambua ruwaza za mabadiliko ya fonimu..62

10 ix Kubainisha kanuni za kimofofonolojia zinazotawala ukopaji Kutoa maelezo ya kanuni za kimofofonolojia Uaminiki na utegemewaji wa utafiti Maadili ya utafiti...66 SURA YA NNE: UWASILISHI NA UCHANGANUZI WA DATA Kitangulizi Dhana ya utohozi kama njia ya uundaji istilahi Mageuzi ya vokali Uchopekaji wa vokali Uchopekaji wa vokali /i/ Uchopekaji wa vokali / ͻ / Uchopekaji wa vokali /u/ Ufupishaji wa vokali Ufupishaji wa vokali / ɑ: / Ufupishaji wa vokali /i:/ Ufupishaji wa vokali /u:/ Ufupishaji wa vokali / ͻ / Ubadala wa vokali Ubadala wa vokali / / [a]...89

11 x Ubadala wa vokali / / [a] Ubadala wa vokali // / [a] ,3.4 Ubadala wa vokali //ı/ /ı/ Ubadala wa vokali / / [ ͻ] Ubadala wa vokali /eı / / / Ubadala wa vokali / / [u] Uimarikaji wa vokali Uimarikaji wa vokali /i/ kuwa konsonanti [j] Mageuzi ya konsonanti Udondoshaji wa konsonanti Udondoshaji wa /r/ Udondoshaji wa /k/ Udondoshaji wa /t/ Ubadala wa konsonanti Ubadala wa / / [ ] Kihitimisho.109 SURA YA TANO: HITIMISHO NA MAPENDEKEZO

12 xi 5.1 Kitangulizi Hitimisho Mapendekezo MAREJELEO VIAMBATISHO Orodha ya nomino mkopo zilizotumiwa Maneno mengine ya Kigiryama yaliyotumiwa katika ufafanuzi

13 xii ORODHA YA VIFUPISHO NA ALAMA FZA Fonolojia Zalishi Asilia SZA Sarufi Zalishi Asilia Kanuni F Kanuni ya Fonolojia Kanuni MF Kanuni ya Mofofonemiki # Mpaka wa neno Ø Kapa $ Mpaka wa silabi / / Uwakilishi wa fonimu [ ] Uwakilishi wa kifonetiki Mchakato Mazingira ya kifonetiki K Konsonanti V Vokali Mch. Mchoro Jedw. Jedwali

14 xiii ORODHA YA MAJEDWALI Jedw 2.1:Vokali za Kigiryama Jedw 2.2: Usawiri wa konsonanti za Kigiryama Jedw 2.3: Aina za konsonanti za Kigiryama Jedw 2.4: Konsonanti za nazali Jedw 2.5: Viyeyusho kama konsonanti Jedw 2.6: Usawiri wa vokali sahili za Kiingereza Jedw 2.7: Usawiri wa vokali pacha Jedw 2.8: Usawiri wa vokali utatu Jedw 2.9: Usawiri wa konsonanti za Kiingereza Jedw 4.1: Usawiri wa uchopekaji wa vokali /i/ katika konsonanti za mwanzo wa nomino Jedw 4.2: Usawiri wa uchopekaji wa vokali /i/ katika konsonanti za katikatiya nomino Jedw 4.3: Usawiri wa uchopekaji wa vokali /i/ katika konsonanti za tamati ya nomino Jedw 4.4: Uchopekaji wa vokali /i/ katika nafasi ya awali, katikati na tamati ya nomino Jedw 4.5: Uchopekaji wa vokali /i/ katika nafasi mbili za nomino Jedw 4.6: Uchopekaji wa vokali / ͻ / Jedw 4.7: Uchopekaji wa vokali /u/

15 xiv Jedw 4.8: Ubadala wa vokali /ʌ/ [a] Jedw 4.9: Ubadala wa vokali / / [a] Jedw 4.10: Ubadala wa vokali / / [a] Jedw 4.11: Ubadala wa vokali /ı/ [i] Jedw 4.12: Ubadala wa vokali / / /ͻ/ Jedw 4.13: Ubadala wa vokali/eı/ / / Jedw 4.14: Ubadala wa vokali / / /u/ Jedw 4.15: Uimarikaji wa /i/ kuwa [j] Jedw 4.16: Ubadala wa konsonanti / / [ ]

16 xv ORODHA YA MICHORO Mch 2.1: Usawiri wa kidhana wa utafiti Mch 2.2: Usawiri wa sifa za vokali za Kigiryama Mch 3.1: Hatua za uchanganuzi wa data Mch 4.1: Usawiri wa mageuzi ya vokali /ʌ /, /ә /, / / kuwa [a]

17 1 SURA YA KWANZA UTANGULIZI 1.1 Usuli wa mada Kulingana na Kang (2008) ukopaji ni ile hali ya kuomba maneno kutoka lugha moja hadi nyingine. Utafiti huu unahusu uchanganuzi wa kimofofonolojia wa nomino mkopo kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama. Uchanganuzi huu umeweka bayana mageuzi ya kimofofonolojia ambayo nomino hizi za Kiingereza hupitia zinapoingizwa katika lugha ya Kigiryama. Kulingana na Langacker (1967), lugha husawiri mabadilika kila wakati. Mabadiliko haya yanatokana na hali ya lugha kuwa hai kila wakati. Hock (1991), Chimhundu (1983) na Chikanza (1986) wanakubaliana kwamba lugha ina sifa ya uhai na kutokana na sifa hii, lugha hudhihirisha mabadiliko kila wakati. Naye McMahon (1994) unaunga mkono kauli hii kwa kutetea kwamba mojawapo ya sababu za mabadiliko haya ya lugha ni kutokana na mgusano wa lugha. Mojawapo ya matokeo ya mgusano wa lugha ni ukopaji maneno. Ni dhahiri kwamba lugha hazina budi kukopa kutoka kwa lugha nyingine kwa sababu wazungumzi wa lugha hizi hutangamana kila wakati katika shughuli mbalimbali za maisha. Lugha ya Kiingereza ni lugha ambayo inahusika na maendeleo ya utamaduni wa kiteknolojia na hali hii inaifanya kuwa lugha ya fahari; hali ambayo inachangia ukopaji wa kiutamaduni na wa kileskia kama anavyoelezea Mwihaki (1998). Ukopaji wa kiutamaduni unahusu ukopaji wa istilahi zinazonasibishwa na vitu au shughuli mbalimbali za utamaduni wa lugha kopeshi. Istilahi zinazohusika huwa zina maana za kimsingi, hivyo basi ukopaji huu pia unaitwa ukopaji wa kileksia.

18 2 Kwa jumla, ukopaji huwa unahusu umbo la kimofofonimiki la neno husika na lenye dhana mpya lakini lenye muundo wa kifonolojia wa lugha kopaji. Hii ni kwa sababu maneno yanapoingizwa katika lugha nyingine huwa yanapitia mageuzi ya kimatamshi ili yaweze kukubaliana na kanuni za kifonolojia za lugha kopaji. Ukopaji huwa unaathiri lugha kopaji kifonolojia. Kwa upande mwingine, mofofonolojia ni mageuzi ya kifonimiki yanayopitiwa na fonimu zinazofuatana au kuambatana katika maneno kama inavyofafanuliwa na Hooper (1976). Utafiti huu unaafikiana na mawazo yanayotolewa na wataalamu mbalimbali. Kwanza kabisa lugha ya Kiingereza ilikuja na utamaduni wa kiteknolojia ambapo ulionekana wa kifahari na ilikuwa rahisi lugha za Kiafrika kukopa kama anavyoeleza Owino (2003). Zaidi ya hayo, kuna vitu mbalimbali ambavyo vilikuja na lugha ya Kiingereza na havikuwa katika mazingira ya Wagiryama kwa hivyo ikabidi Wagiryama wakope majina ya vitu hivyo kutoka lugha ya Kiingereza. Ni bayana kwamba ukopaji unategemea kiwango cha utangamano wa lugha mbili katika jamii mahsusi. Kulingana na Hagen (1950), Paradis na La Charite (1997), Paradis na La Charite (2008), Paradis na La Charite (2009), Hefferman (2007) na Friesner (2009), kiwango cha uhamisho wa maneno kutoka lugha kopeshi hadi lugha kopaji kinategemea uwili lugha uliopo katika jamii mahsusi. Kutokana na mawazo haya, ni wazi kwamba jamii ya Wagiryama imeweza kudhihirisha mazingira yenye rotuba nyingi ya ukopaji kwa sababu Wagiryama wanapata lugha ya Kiingereza moja kwa moja kutoka kwa mafunzo ya shule na maneno ya Kiingereza yanakopwa kwa urahisi katika lugha ya Kigiryama. Kwa upande mwingine, kulingana na Mwihaki (1998), Owino (2003), Kang (2008) na Evans (2011) wanafafanua kwamba ukopaji unahusisha mageuzi ya kifonolojia ya

19 3 maneno ili kuweza kuingizwa kikamilifu katika lugha kopaji. Ni muhimu kuzingatia kwamba maneno yanayokopwa sharti yazingatie masharti ya lugha kopaji ili yaingizwe na kukubalika katika lugha kopaji. 1.2 Swala la utafiti Utafiti huu ulihusu uchanganuzi wa kimofofonolojia wa nomino mkopo kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama. Kauli ya pamoja inaweza kutolewa kwamba, lugha zote huwa zinaongozwa na kanuni mahsusi. Utafiti huu unalenga lugha ya Kigiryama na lugha ya Kiingereza na unachunguza na kufafanua michakato ya kimofofonolojia ya nomino mkopo za lugha ya Kigiryama zenye asili ya lugha ya Kiingereza kwa kuweka bayana na kueleza kanuni zinazoongoza michakato hii. Kutokana na uchunguzi wa awali uliofanywa na mtafiti, uchanganuzi wa kimofofonolojia wa nomino mkopo za lugha ya Kigiryama na kanuni zinazoongoza michakato hii hazijawekwa bayana na kufafanuliwa kitaaluma. Hii inamaanisha kwamba kuna pengo la elimu ya kiisimu katika lugha ya Kigiryama na pengo hili ndilo lilimpatia mtafiti msukumo wa kuchunguza na kufafanua michakato hii muhimu ya kiisimu na kueleza kanuni mahsusi zinazohusika. 1.3 Madhumuni ya utafiti Utafiti uliongozwa na madhumuni mahsusi yafuatayo: i) Kutambulisha nomino-mkopo zinazotoka katika lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama katika shughuli za ukarabati na vifaa vya magari, pikipiki na baisikeli. ii) Kudhihirisha michakato ya kimofofonolojia ambayo inapitiwa na nomino-mkopo kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama.

20 4 iii) Kubainisha kanuni za kimofofonolojia zinazodhibiti ukopaji wa nomino kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama. 1.4 Nadharia tete Utafiti uliongozwa na nadharia tete zifuatazo: i) Lugha ya Kigiryama imekopa nomino zinazohusiana na shughuli na vifaa vya ukarabati wa magari, mapikipiki na baiskeli kutoka lugha ya Kiingereza. ii) Nomino za shughuli na vifaa vya ukarabati wa magari, mapikipiki na baiskeli zinazokopwa kutoka lugha za Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama hupitia michakato mahsusi ya kimofofonolojia. iii) Kuna kanuni za kimofofonolojia ambazo zinaongoza ukopaji wa nomino za shughuli na vifaa vya ukarabati wa magari, mapikipiki na baiskeli kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama. 1.5 Upeo wa utafiti Utafiti huu umejikita katika ukopaji wa nomino kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama kwa kuzingatia michakato ya kimofofonolojia ambayo nomino hizi hupitia katika mageuzi mahsusi. Lugha ya Kigiryama imekopa kutoka lugha zingine kama lugha ya Kiswahili na Kisanye. Utafiti huu hauhusishi maneno-mkopo kutoka lugha ya Kiswahili na Kisanye bali umejikita tu katika maneno ya lugha ya Kiingereza yanayokopwa hadi lugha ya Kigiryama. Ijapokuwa imewekwa bayana na watafiti kwamba baadhi ya maneno ya Kiingereza hayana asili ya Uingereza bali yamekopwa kutoka lugha zingine za Uropa kama anavyoeleza Langacker (1973), utafiti huu haunuii

21 5 kutafuta asili ya maneno haya ya Kiingereza bali umezingatia moja kwa moja jinsi nomino za Kiingereza zilivyokopwa hadi kuwa nomino za lugha ya Kigiryama. Inabainika kuwa maneno ya kukopwa hupitia mageuzi mbalimbali kama vile mnyambuliko wa maneno haya ya kukopwa na mageuzi kutoka kategoria ya neno moja hadi nyingine (mfano kutoka kategoria ya nomimo hadi kategoria ya kitenzi kama vile nomino ya Kiingereza #line# linavyogeuzwa hadi lugha ya Kigiryama na kuwa #lainisha# ambacho ni kitenzi). Hata hivyo eneo hili halijazingatiwa kwani utafiti huu umejikita tu katika mageuzi ya kimofofonolojia yanayohusu kategoria moja ya maneno ambayo ni nomino. Uchunguzi huu ni wa kisinkronia kwani data ilichukuliwa moja kwa moja kutoka kwa wazungumzi wenyeji wa lugha ya Kigiryama kama wanavyoitumia sasa. Nomino zinazohusishwa zinatoka katika taaluma ya Sayansi ya Ufundi katika viwanda vinavyojulikana kama Jua Kali. Viwanda hivi huhusika zaidi na shughuli za kutengeneza na kukarabati vifaa mbalimbali vinavyotokana na maendeleo ya kiteknolojia vikiwemo magari, mapikipiki, baiskeli, vyombo vya jikoni kama majiko, masahani, vikaango, masufuria na hata vifaa vya shambani kwa mfano majembe, mapanga, matangi ya maji na kadhalika. Ni bayana kwamba uwanja wa Jua kali ni mpana mno. Utafiti huu unajikita tu katika kuchunguza nomino-mkopo zinazohusiana na shughuli na vifaa vya ukarabati wa magari, pikipiki na baiskeli pekee. Ni bayana kwamba shughuli za ukarabati na vifaa vya magari, pikipiki na baiskeli na mambo yanayohusu kiteknolojia ambayo hayana asili yake miongoni mwa wazungumzi wa lugha ya Kigiryama bali yanatoka katika nchi za magharibi. Nomino zinazotokana na shughuli na vifaa vya ukarabati wa magari, mapikipiki na baiskeli ni mambo ya kigeni. Hivi ni kusema kuwa shughuli za ukarabati huu zinahusisha nomino

22 6 za Kiingereza. Nomino za shughuli za ukarabati na vifaa vya magari, pikipiki na baiskeli zinazotumika katika lugha ya Kiingereza ndizo zinazozingatiwa katika utafiti huu na kuona ni kwa jinsi gani fonimu za nomino hizi zinageuka ili kukubalika katika Fonolojia ya lugha ya Kigiryama wakati wa ukopaji. Utafiti huu unahusisha mazingira ya magereji ambapo shughuli za ufundi wa Juakali huwa zinafanyika. Magereji yanayohusishwa ni yale ambayo wafanyikazi wake ni Wagiryama ili iweze kudhihirika jinsi wanavyotamka nomino hizi kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama. Nomino za lugha ya Kiingereza zinazohusu shughuli mbalimbali za ukarabati wa magari, pikipiki na baisikeli. Vifaa vinavyohusika katika shughuli hizi huwa havipatikani katika lugha ya Kigiryama kwa hivyo Wagiryama hawana nomino zao za kuvitajia. Isitoshe, nomino hizi zinatamkwa kwa kutumia lugha ya Kiingereza, na sauti hizi ni ngeni kwa wazungumzi asili wa lugha ya Kigiryama. Tofauti ya matamshi kati ya lugha hizi mbili ndiyo inayoleta mabadiliko ya matamshi ya nomino mkopo za lugha ya Kigiryama. Wazungumzi wa lugha ya Kigiryama wametapakaa kwingi katika mkoa wa pwani ya Kenya. Maeneo ya Wagiryama yanayohusishwa katika utafiti huu ni Weruni (magereji ya sehemu za Kaloleni Giryama na Kilifi), Godoma (magereji ya sehemu za Bamba) na Galana (magereji ya sehemu za Malindi). Hii ni kwa sababu maeneo haya ndiyo yanahusishwa na wazungumzi asili wa lugha ya Kigiryama. Wagiryama wanaoishi katika miji mikubwa na kufanya kazi katika magereji ya magari, pikipiki na baiskeli hawakuhusishwa kwa sababu ya kule kutangamana kwao na watu lugha zingine kwa mfano lugha ya Kikamba, Kikikuyu, Kitaita, Kikisii na kadhalika kungeweza kutoa data isiyo sahihi na isiyoaminika kutokana na athari za lugha hizi.

23 7 1.6 Natija ya utafiti Utafiti huu umesaidia katika kujua jinsi ukopaji wa nomino za lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama unavyofanyika. Utafiti huu pia umeweza kuweka bayana na kufafanua michakato ya kimofofonolojia na kanuni zinazoongoza ukopaji katika lugha ya Kigiryama na ujuzi huu ni machango mkubwa katika taaluma ya isimu za lugha za Kiafrika. Kwa upande mwingine, ni bayana kwamba uhusishi wa lugha mbili; Kiingereza na Kigiryama ni mchango muhimu katika taaluma ya Isimu Linganishi. Inadhihirishwa na wataalam Antilla (1972) na Anderson (1973) kwamba taratibu zinazohusu ukopaji katika lugha huipa lugha kopaji mtazamo mpya na muundo mpya na kuendeleza matumizi ya lugha hivyo basi lugha inaendelea kuishi. Mwihaki (1998) anasisitiza kuwa mabadiliko katika lugha huifanya lugha iweze kufahamika zaidi na kuendeleza lugha husika. Katika utafiti huu, mabadiliko yanayofanyika katika lugha ya Kigiryama kutokana na kukopwa yanaifanya lugha hii iwe hai na kuendelea kuishi na kufahamika zaidi ulimwenguni. Utafiti huu pia umesaidia katika uwanja wa isimu wa ujifunzaji wa lugha ya pili. Walimu na wataalum wa lugha ya pili watanufaika katika kushughulikia maswala ya upokeaji wa lugha ya pili na ujifunzaji wa lugha katika kiwango cha fonolojia. Zaidi ya hayo, utafiti huu umeweza kudhihirisha vikwazo vya kifonolojia katika ujifunzaji wa lugha ya pili. Kulingana na Witkins (1972), kuna vikwazo vya kifonolojia ambavyo hudhihirika katika ujifunzaji wa lugha ya pili. Ujuzi ambao umepatikana katika utafiti huu unasaidia katika kupunguza vikwazo hivi kwa jinsi ambavyo umeweka bayana na kufafanua kanuni zinazohusika katika ukopaji. Zaidi ya hayo, imekuwa wazi kwamba kwa sababu ya tofauti za kifonolojia na za kimuundo lugha

24 8 msomi wa lugha ya pili anaweza kutarajiwa kufanya makosa au makosa yanaweza kubashiriwa mapema kabla hayajatokea. Maelezo haya yanaelezwa waziwazi na James (1980). Utafiti huu pia umesaidia pakubwa katika nyanja ambazo haziwezi kuwekwa bayana na kufafanuliwa kikamilifu pasipo ukopaji. Kwa mfano, wasomi katika nyanja za kiakademia hukopa sana ili kuweza kujieleza kikamilifu katika nyanja zao. Hali hii inatokana na mataifa yaliyoendelea katika uvumbuzi wa sayansi na teknolojia yanapoibuka na istilahi ambazo ni geni katika mataifa mengine. Ili mataifa haya mengine yaweze kuenda sambamba na maendeleo hayo katika maswala ya kiteknolojia inabidi lugha za mataifa haya zikope istilahi hizi. Ukopaji huwa unazidi kunawirisha lugha kopaji. Mawazo haya yamefafanuliwa na Kennedy (1982). Hivyo basi lugha kopaji inapata utajiri wa istilahi na kuifanya iendelee katika maendeleo ya ulimwengu mzima. Ukopaji huu umeipa lugha ya Kigiryama istilahi za kutajia vifaa vya maelendeleo ya kiteknolojia. Pia hali hii imeongeza msamiati katika lugha ya Kigiryama. Kulingana na ruwaza ya Kenya ya 2030, mbali na kwamba inatambua sera ya taifa ya lugha kwamba lugha ya Kiingereza na Kiswahili ni lugha rasmi, imeweka pia hamasisho na mkazo katika uendelezaji wa lugha za kiasili nchini Kenya kwa kuhimiza zifanyiwe utafiti wa maswala mbalimbali ya Kiisimu, Fasihi na Utamaduni wa lugha hizi kuwekwa bayana na kufafanuliwa. Utafiti huu umeweka bayana maswala ya kiisimu ya lugha ya Kigiryama ambapo ni mchango mkubwa katika isimu ya lugha za Kenya na za Afrika kwa jumla. Pia lugha ya Kigiryama imekuwa na hazina ya data ya kiisimu ambapo ni jambo la thamani kwa lugha hii.

25 9 Pia kutokana na uchunguzi wa awali wa mtafiti, imebainika kwamba kuna tafiti chache sana za isimu ambazo zimefanywa kuhusu lugha za mwambao wa Pwani, hasa lugha za Kimijikenda. Utafiti huu umeweza kuongeza ujuzi wa kiisimu wa lugha za Kiafrika hasa lugha za Pwani ya Kenya. Utafiti huu pia ni muhimu kwa jinsi ambavyo unachangia katika kuipa lugha ya Kigiryama ukwasi wa istilahi hasa za kuelezea dhana ambazo ni ngeni. Ni bayana kwamba utafiti huu utachangia pakubwa katika uundaji wa kamusi ya lugha ya Kigiryama kwa jinsi ambavyo kuna hazina ya nomino-mkopo katika lugha ya Kigiryama iliyopatikana.

26 Maelezo ya istilahi Istilahi zifuatazo zimetumika katika tasnifu hii na zimefafanuliwa kama ifuatavyo: Ukopaji wa maneno ni hali ya lugha kuchukua maneno au utaratibu wa usemaji wa lugha nyingine na kutumia na hatimaye ukawa sehemu ya lugha hiyo. Fonimu ni kipashio kidogo kabisa katika mfumo wa sauti za lugha ambacho kina sifa pambanuzi za kuweza kukitofuatisha na vipashio vingine vya aina yake. Fonolojia ni tawi la isimu ambalo hushughulika na uchunguzi na uchanganuzi wa mfumo wa sauti za lugha mahsusi. Mofolojia ni taaluma ya isimu inayoshughulikia uchunguzi na uchanganuzi wa kanuni na mifumo inayohusu muundo wa mofimu mbalimbali ili kuunda maneno katika lugha. Mofofonolojia ni taaluma ya isimu inayohusu uchanganuzi na uainishaji wa vipengele vya kifonolojia vinavyoathiri maumbo ya mofimu. Ni taaluma ya isimu inayoshughulikia uhusiano uliopo baina ya Fonolojia na Mofolojia katika lugha. Mgusano ni hali ya lugha mbili au zaidi kuathiriana kutokana na kuishi pamoja kwa jamii mbili au zaidi zinazozungumza lugha mbili au zaidi. Mchakato na hali au kitendo kinachofanyika ambacho huleta mabadiliko katika vipashio vya lugha. Mageuzi ni utaratibu wa kiisimu wa kubadili maumbo kuwa maumbo mengine kwa kufuata kanuni maalum. Lugha kopeshi ni lugha ambayo maneno yanaazimwa na kuingizwa katika lugha nyingine. Lugha kopaji ni lugha ambayo inaazima maneno kutoka kwa lugha nyingine.

27 11 SURA YA PILI MAPITIO YA MAANDISHI 2.1 Kitangulizi Katika sehemu hii maandishi katika vitabu mbalimbali na majarida yanayotoa maelezo kuhusu dhana ya ukopaji yamezingatiwa na maelezo hayo kufafanuliwa ili kutoa mwangaza wa dhana ya ukopaji kwa jumla. Baadaye, tafiti za wataalam mbalimbali zinazohusu ukopaji na zenye uhusiano na mada hii ya utafiti zimechanganuliwa kwa kina kwa kuonyesha mlingano na utofauti uliopo pamoja na mchango wa tafiti hizo kwa utafiti huu. Zaidi ya hayo, misingi ya nadharia inayoongoza utafiti huu imejadiliwa ili kudhihirisha mwongozo faafu wa utafiti huu. Misingi ya kidhana pia imejadiliwa ili kuangazia hatua zilizofuatwa katika utafiti huu. 2.2 Mapitio ya maandishi Sehemu hii imepangwa kwa kuanzia kupitia mawazo mbalimbali yanayopatikana katika vitabu yanayohusu ukopaji kwa jumla, kutoa maelezo na mchango unaotokana na maandishi katika majarida kuhusu ukopaji na kisha kuzingatia tafiti mbalimbali zilizofanywa kuhusu ukopaji zinazopatikana katika tasnifu zenye uhusiano wa karibu na mada ya utafiti huu na zinazotoa mchango kwa utafiti huu. Mchango wa kazi hizi katika utafiti huu umetambuliwa kwa jinsi ambavyo umeweka nguzo na kuupa utafiti huu umantiki. Zaidi ya hayo, upekee wa utafiti huu pia umeweza kuonyeshwa Maandishi katika vitabu kuhusu dhana ya ukopaji Istilahi ya ukopaji imeweza kufafanuliwa na wasomi mbalimbali wa lugha. Kulingana na Tuki (2010), Ukopaji ni kuazima, kuchukua au kupokea kitu cha mtu mwingine. Katika muktadha wa lugha, ukopaji ni kuazima, kuchukua au kupokea maneno kutoka lugha nyingine. Naye Crystal (1987) anafafanua ukopaji kuwa ni kuingiza neno au

28 12 kipashio cha kiisimu cha lugha moja hadi lugha nyingine au lahaja moja hadi nyingine. Maneno yanayokopwa huitwa maneno mkopo. Nehru (1953) anasawiri kwamba ni rahisi kwa lugha fulani kuomba maneno kuliko kuunda maneno mapya magumu ili kuweza kutajia vitu vinavyoletwa na lugha ya mgusano. Ni bayana kwamba kuunda maneno mapya na kuyafanya yatumiwe na jamii ni jambo gumu na linalochukua muda mrefu. Katika utafiti huu, ni wazi kwamba lugha ya Kigiryama imeweza kuepukana na ugumu huu wa kuunda nomino mpya za shughuli na vifaa vya ukarabati wa magari, pikipiki na baiskeli na imekopa moja kwa moja nomino hizi kutoka lugha ya Kiingereza. Bynon (1977) anasema kuwa ukopaji ni uhamisho wa maneno ya kileksia kutoka lugha moja hadi nyingine. Maneno mkopo huwa mara nyingi ni istilahi zinazopatikana katika taaluma mbalimbali kama vile ya sayansi na tekinolojia, asasi za kidini, kijeshi na kadhalika. Kwa jumla, ukopaji ni kule kujaza pengo la kisemantiki ambalo halina istilahi yake katika lugha asili. Mawazo haya ni muhimu sana katika utafiti huu kwa sababu ni bayana kwamba ukopaji wa nomino za shughuli na vifaa vya ukarabati wa magari, pikipiki na baiskeli umetokana na sababu kwamba nomino hizi hazipatikani katika lugha kopaji kwa kuwa vifaa hivi ni vya kigeni vinavyohusu sayansi na tekinolojia. Kulingana na Eichhoff (1980) na Winter (1992), wanasema kwamba ukopaji wa kileksia ndio ni maarufu zaidi katika uwanja wa ukopaji na hutokea wakati ambapo lugha mbili zinakuwa na mgusano. Maneno ambayo yamehusishwa katika ukopaji wa utafiti huu ni ya kileksia ambayo ni nomino. Kuna sababu za lugha kukopa nomino kwa wingi kuliko kategoria nyingine ya maneno. Kulingana na Muysken (1994), ukopaji wa nomino unaletwa na hali ya kwamba nomino ndio maneno yanayobeba utamaduni wa

29 13 lugha mahsusi. Hivyo basi lugha inapohitaji kukopa kuhusu maswala ya utamaduni wa kigeni wa teknolojia katika lugha kopaji, lugha hii huzingatia ukopaji wa nomino kwani ndizo zinazobeba utamaduni ule. Zaidi ya hayo, Poplack (1988), anasisitiza kwamba nomino ndio kategoria ya maneno yanayopatikana katika ukopaji zaidi kwa sababu maneno haya ndiyo yanayobeba maudhui katika lugha. Naye Field (2002) anaongeza ufafanuzi kwa kusema kuwa nomino zina uwazi wa maana hivyo basi hukopwa kuliko maneno mengine yoyote. Kwa upande mwingine, maoni ya Moravcsiks (1978) ni kwamba ukopaji wa nomino ni kawaida ya lugha zinazotangamana na lugha hizi zinaweza kuendelea kuomba katika kategoria zingine za maneno iwapo tu kama zimekopa nomimo kwanza. Kwa hivyo ukopaji huanzia katika kategoria ya nomino halafu kategoria hizo nyingine zikafuata baadaye. Ni bayana kwamba kategoria ya nomino ndiyo yenye mantiki zaidi katika taaluma ya ukopaji na hii ndio sababu ya utafiti huu kujikita katika ukopaji wa nomino pekee. Vilevile, inabainika kwamba wakati mwingine lugha hukopa kwa sababu za kisiasa na kijamii za lugha inayohusika. Kulingana na Artlotto (1972), lugha mara nyingi hukopa maneno kutoka kwa lugha ambazo zinatoka katika jamii zinazoheshimika kisiasa na kijamii. Inaaminika kwamba jamii hizi zinazoheshimika huwa zina mawazo na dhana mpya ambazo zinaweza kuazima kwa lugha nyingine (lugha kopaji). Katika muktadha wa Wagiryama, inaaminika kwamba lugha ya Kiingereza ni ya kuheshimika kwa jinsi ambavyo ilikuja na usomi pamoja na mawazo na dhana mpya za vitu vya kiteknolojia ambavyo havikuwa vinapatikana katika mazingira yao. Kwa hivyo ni rahisi lugha ya Kigiryama kukopa kutoka kwa lugha ya Kiingereza ili iweze kutajia dhana mpya zisizopatikana katika lugha kopaji (Kigiryama).

30 14 Ni muhimu kutambua kwamba, wasomi wa lugha wengine wanakubaliana kwamba istilahi ya ukopaji inaenda na masharti. Kulingana na Hockett (1958) na Weinreich(1963) ukopaji unahitaji lugha chasili kuachilia muundo fulani na kuuazima kwa lugha kopaji kisha kuutarajia urudishwe na neno kopwa. Hivi ni kusema kuwa, lugha chasili huwa haipotezi kitu chochote katika ukopaji na zaidi huendelea kutumia neno kopwa bila kubadilisha muundo wake. Dhana hii ndiyo inafanya nomino za vifaa vya magari, pikipiki na baisikeli zilizokopwa kuhifadhi uasili muundo wake kileksia na kisemantiki. Kulingana na Apel na Muksken (1987), wanasema kwamba hali ya lugha kuomba maneno kutoka lugha nyingine ni ishara ya lugha kutangamana na lugha nyingine. Wazungumzi wa lugha tofauti wanapokutana huweza kutangamana na hali hii inaweza kufanya lugha moja kati yao ikope zaidi kuliko nyingine kama anavyoeleza Wardhugh (1987). Naye Hock (1986) anasema kwamba lugha huomba maneno kutoka kwa lugha nyingine ili jamii yake iwe na weledi zaidi katika nyanja za usomi, dini, siasa, sayansi na teknolojia. Utafiti huu umeegemea katika ukopaji wa nomino katika eneo la taaluma ya sayansi na teknolojia hasa katika uwanja wa ufundi wa Jua kali ili kuangazia ufahamu zaidi wa jamii katika uwanja huu. Ukopaji pia unategemea umantiki wa maana za maneno yanayokopwa na motisha ya ukopaji huo. Haya yanaangaziwa na waandishi mbalimbali kama Hockett (1958), Weinrich (1963), King (1969), langacker (1973) na Fromkin na Rodman (1988). Wataalamu hawa wanakubaliana kwamba ukopaji unaweza kufanyika katika nyanja au taaluma yoyote ile. Zaidi ya hayo, wanakubalina na wataalamu wengine kwamba ukopaji unatendeka zaidi katika kategoria ya nomino. Mawazo haya yanaafikiana na ya Bynon (1977)

31 15 anayesisitiza kwamba maneno mengi yanayokopwa huwa yanatokana na majina ya vitu na vifaa mbalimbali ambavyo vinafungamana na utamaduni wa lugha kopeshi. Kulingana na Fishman (1968), ukopaji ni njia ya kuingiza dhana fulani katika lugha nyingine ili kusimamia istilahi ambazo hazipo katika lugha kopaji. Mara nyingi wakopaji huzingatia tu matamshi wanayoyasikia katika lugha kopeshi na kuweza kuingiza matamshi haya katika lugha kopaji. Wakati mwingine matamshi yanaweza kutatizika na kukawa na tofauti za kimatamshi katika istilahi moja. Katika utafiti huu wa lugha ya Kigiryama, imebainika kwamba watu waliohusishwa kutoa data ni wale wanaotamka nomino mkopo kwa kuzingatia sauti za nomino hizo kama zinavyotamkwa katika lugha ya Kiingereza. Kwa upande mwingine, inabainika kwamba kuna waandishi wengine ambao wameingia kwa kina zaidi kuhusu dhana ya ukopaji kwa kuzingatia maswala ya kisarufi yanayoibuka wakati wa ukopaji wa maneno yanayohusika. Waandishi hawa ni Antilla (1972), Bynon (1977) na Hock (1986). Kwa kutumia mifano ya lugha za Uropa, waandishi hawa wamesawiri vipengele muhimu katika ukopaji ambavyo ni fonolojia, mofolojia na leksia. Waandishi hawa wanatambua kwamba wakati wa ukopaji, maswala ya kifonolojia, kimofolojia na kileksia ya lugha mbili (kopeshi na kopaji) sharti yazingatiwe. Maandishi haya yanatoa mchango wa mwangaza katika utafiti huu kuhusu kuhusisha mageuzi ya kifonolojia na kimofolojia ya maneno wakati wa ukopaji. Mchango huu unatekelezwa katika utafiti huu ambapo mageuzi ya kimofofonolojia (fonolojia na mofolojia) ya nomino mkopo za lugha ya Kigiryama yanashughulikiwa. Ni muhimu kutambua kwamba vipengele vyote vya ukopaji ni muhimu kwa kutegemea maneno yanayokopwa pamoja na hali za ukopaji wa maneno hayo. Hata hivyo, katika utafiti huu, msisitizo zaidi umewekwa katika mageuzi ya kifonolojia na kimofolojia ya

32 16 nomino zinazokopwa. Mageuzi ya kifonolojia yanalenga matamshi ya nomino mkopo. Hivi ni kusema kuwa mageuzi yanayopitiwa na nomino mkopo yanatakikana yaafiki matamshi yanayokubalika katika lugha kopaji. Kwa upande mwingine, maneno yanayokopwa sharti yaweze kuwa katika maumbo mahsusi yenye mantiki na maana inayokubalika katika lugha kopaji. Mofolojia ya maneno mkopo inahusishwa ambapo maumbo kamili yanayotokana na ukopaji yanachunguzwa na ukubalifu wake katika lugha kopaji kudhihirishwa. Kwa jumla, waandishi hawa wametoa mwanga katika dhana ya ukopaji kwa kuzingatia fonolojia na mofolojia wakati wa ukopaji. Uhusishaji wa fonolojia na mofolojia katika ukopaji ni mchango muhimu katika utafiti huu ambao umeegemea katika ukopaji wa kimofofonolojia wa nomino za lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kigiryama. Mawazo na maelezo yanayotolewa na waandishi hawa yamechangia katika kuujenga msingi wa utafiti huu na kuupa mwelekeo kwa kiasi kikubwa. Hata hivyo, tofauti ni kwamba maandishi haya yamejikita zaidi katika lugha za Uropa na mifano inayotolewa haitoi picha halisi ya jinsi mambo yalivyo katika lugha za Kibantu. Thomas (1991) alijadili na kudhihirisha kwamba ukopaji maneno kutoka lugha moja hadi nyingine unahusu mageuzi wa kifonolojia na kimofolojia. Anasisitiza kwamba ukopaji wa maneno kutoka lugha moja hadi nyingine kunahitaji utohozi wa maneno haya kifonolojia na kimofolojia ili kuleta ukubalifu katika lugha kopaji. Thomas (1991) anatambua kwamba maneno yanakopwa kwa kuzingatia utaratibu wa kifonolojia na kimofolojia wa lugha husika ili maneno mkopo yaweze kuafiki vigezo vya kifonolojia na kimofolojia vya lugha kopaji. Mawazo ya Thomas (1991) ni muhimu kwa utafiti huu kwa sababu maswala ambayo yameangaziwa katika utafiti huu ni mageuzi ya nomino mkopo kifonolojia na

33 17 kimofolojia. Nomino za lugha ya Kiingereza zimedhihirishwa jinsi zinavyogeuka kwa kupitia mageuzi ya kimofofonolojia na kukopwa kwa njia ya kukubalika kwa kuambatana na kanuni za kimofofonolojia za lugha ya Kigiryama. Tofauti ni kwamba, Thomas (1991) katika maelezo yake hajajikita na nadharia mahsusi inayoongoza utafiti na maelezo yake ilhali utafiti huu umehusisha nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia pamoja na kuhusisha lugha ya Kiingereza na Kigiryama. Dhana ya ukopaji pia imezingatiwa katika lugha ya Kikamba na Whiteley (1963). Kazi ya whitely (1963) imehusisha ufafanuzi wa michakato ya kimofofonolojia inayopitiwa na maneno wakati wa ukopaji. Kazi hii pia inaangazia vikwazo vya kitamaduni vinavyohusu utohozi wa kileksia. Kazi hii ni muhimu kwa jinsi ambavyo inazingatia utohozi wa maneno mkopo kimofofonolojia na ukubalifu wake katika lugha kopaji. Mchango wa kazi ya Whiteley (1963) ni kule kuzingatia ukopaji wa kimofofonolojia katika lugha ya Kikamba kama jinsi utafiti huu unavyozingatia ukopaji wa kimofofonolojia katika lugha ya Kigiryama. Hata hivyo, Whiteley (1963) ameshughulikia ukopaji katika lugha ya Kikamba ilhali utafiti huu umezingatia ukopaji katika lugha ya Kigiryama. Pia, kazi ya Whiteley (1963) ni maelezo ya ujumla zaidi na haijaonyesha kwa kina kanuni zinazotokana na michakato hii. Kazi zinazohusu maneno mkopo ya lugha ya Kiswahili zinaangaziwa na Johnson (1948), na Mbaabu (1985). Kazi hizi zinahusu ukopaji ambao umejikita katika motisha zinazipa lugha kukopa maneno hadi lugha nyingine na uhitaji wa maneno mkopo katika lugha kopaji. Ni muhimu kutambua kwamba lugha inapokopa huwa ina uhitaji wa maneno mkopo mahsusi katika taaluma husika. Hata hivyo, kazi hizi hazijazingatia michakato au vikwazo vinavyohusishwa katika ukopaji. Mchango zaidi wa maswala ya ukopaji yanapatikana katika majarida yaliyoandikwa na wataalam wa lugha kama ifuatavyo.

34 Maelezo katika majarida kuhusu ukopaji Maandishi katika majarida kadhaa yameshughulikia dhana ya ukopaji kwa kina. Katika majarida haya, wanaisimu wamedhihirisha kwamba maneno ya kukopwa huwa yanapitia mageuzi ili kuweza kuafiki kanuni za lugha kopaji. Kang (2008) anasisitiza kwamba mageuzi ambayo maneno yanayokopwa hupitia huwa ni ya kifonolojia, vipande sauti, sifa arudhi na kimofofonolojia. Kutokana na maelezo haya, data inayopatikana katika ukopaji wa maneno huweza kuweka bayana maswala muhimu katika uwanja wa usomi kuhusu kanuni za fonolojia asilia ya lugha kopaji kama inavyoelezwa na Holden (1976), Ahn na Iverson (2004), Kawahara (2008) na Wetzel (2009). Katika maelezo yake, Kang (2008) amedhihirisha kwamba katika ukopaji mageuzi muhimu yanadhibitiwa na kanuni mahsusi. Maelezo ya Kang (2008) kuhusu mageuzi ya kimofofonolojia katika ukopaji ni mchango muhimu katika utafiti huu kwa sababu mageuzi haya ndio kigezo kinachoongoza utafiti huu. Uhusishi wa fonolojia na mofolojia katika ukopaji ni kudhihirisha kwamba maneno mkopo yanapitia mifanyiko ya kifonolojia inayoathiri matamshi na maumbo ya maneno mahsusi. Matokeo ni kuwa na maneno mkopo yanayoafiki kanuni za fonolojia ya lugha kopaji. Mbali na mchango unaotolewa na Kang (2008) katika utafiti huu, ni muhimu kutambua kwamba anaelezea maswala mengine kama vipande sauti, na sifa arudhi ambayo hayajazingatiwa katika utafiti huu. Pia utafiti wake ni maelezo ya jumla zaidi na hajahusisha lugha mahsusi ilhali utafiti huu umehusisha lugha mahsusi ambao ni ukopaji katika lugha ya Kigiryama. Burenhult (2001) amezingatia ukopaji katika lugha ya Jahai. Katika utafiti wake, amedhihirisha kuwepo kwa ukopaji katika lugha hii na akadhibitisha kanuni mahsusi

35 19 zinazoongoza ukopaji huu. Burenhlt (2001) anaonyesha kwamba katika ukopaji maneno mkopo yanapitia mageuzi kabla ya kukubalika katika lugha kopaji. Baadhi ya mageuzi anayozungumzia ambayo yanapitiwa na maneno mkopo ni pamoja na utohozi wa kifonetiki, ubadilishaji wa kifonemiki, uundaji upya wa muundo wa silabi za maneno na uhamishaji wa mkazo. Mageuzi haya yanadhihirisha kwamba ukopaji wa maneno hautokei wenyewe bali unazingatia taratibu za mageuzi ya maumbo na kuibuka na maneno mkopo yenye mantiki na ukubalifu katika lugha kopaji. Maelezo ya Burenhult (2008) ni muhimu kwa utafiti huu kwa jinsi ambavyo ameonyesha ukopaji na michakato inayohusishwa ambapo ametoa mchango mkubwa katika utafiti huu kwa sababu michakato inayopitiwa na maneno mkopo wakati wa ukopaji ndicho kigezo cha utafiti huu. Michakato inayopitiwa na maneno mkopo na kanuni zinazobainishwa kutokana na michakato ya kimofofonolojia ndio hasa msingi wa utafiti huu. Hata hivyo utafiti huu unatofautiana na maelezo ya Burenhult (2008) kwa sababu mbali na kusawiri wa michakato ya kimofofonolojia, ameendelea zaidi kwa kuonyesha uhamishaji wa mkazo katika maneno- mkopo. Kipengele cha uhamisho wa mkazo katika nomino mkopo hakijazingatiwa katika utafiti huu. Kwa upande mwingine, Kadenge na Mabungu (2009) wameshughulikia ukopaji wa maneno kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kishona. Katika maelezo yao wameonyesha kwamba wazungumzi asilia wa lugha ya Kishona wanategemea michakato ya kifonolojia ikiwemo mabadiliko ya vipande sauti, uchopekaji na uundaji upya wa silabi katika maneno yanayokopwa ili maneno-mkopo haya yaweze kuafiki muundo wa kifonolojia wa lugha ya Kishona. Mchango mkubwa wa kazi ya Kadenge na Mabungu (2009) ni kule kushughulikia michakato ya kifonolojia ya ubadilishaji wa vipande sauti na uchopekaji wa fonimu katika maneno wakati wa ukopaji.

36 20 Kadenge na Mabungu (2009) pia wamesisitiza kwamba michakato inayopitiwa na maneno- mkopo ni kutokana na dhima kuu ya lugha ya Kishona kuhifadhi muundo wa kifonolojia wa maneno- mkopo wakati wa ukopaji. Hata hivyo, imedhihirika kwamba maneno mengine ya Kiingereza yanapokopwa katika lugha ya Kishona yanakiuka mahitaji ya uhifadhi muundo wa lugha ya Kishona. Badala yake, maneno-mkopo yameonekana yanahifadhi muundo wa kifonolojia wa lugha chasili ambayo ni lugha ya Kiingereza. Uhifadhi muundo unahusu kuhifadhi mfuatano wa konsonanti na silabi funge; kinyume na sifa za lugha za Kibantu. Maelezo ya Kadenge na Mabungu (2009) ni mchango mkubwa kwa utafiti huu kwa jinsi ambavyo wanazingatia mageuzi ya kifonolojia ya ubadilishaji wa vokali na konsonanti na uchopekaji kwa dhima ya kuvunja mfuatano wa konsonanti na kwa kufanikisha mahitaji ya muundo wa silabi wazi wa lugha ya Kishona. Hata hivyo, tofauti wa kazi Kadenge na Mabungu (2009) ni kwamba maelezo yao ni ya kijumla na hawajahusisha nadharia ya kuongoza michakato inayohusika wakati wa ukopaji. Zaidi ya hayo, wamehusisha lugha ya Kiingereza na lugha ya Kishona ilhali utafiti huu umehusisha lugha ya Kiingereza na lugha ya Kigiryama. Kembo (1993) katika maandishi yake ameelezea jinsi maneno ya Kiingereza yanavyokopwa katika lugha ya Kidholuo kwa kuzingatia ufungamano wa vigezo vya kisarufi na kifonolojia vya maneno-mkopo yanayohusika. Kembo (1993) anazingatia ukopaji wa maneno ya Kidholuo kwa kuhusisha viwango viwili vya isimu; kiwango cha sarufi na kiwango cha fonolojia. Kembo (1993) ameangazia vipande sauti na vipamba sauti (sifa arudhi) katika ukopaji wa maneno ya Kingereza hadi Kidholuo. Zaidi ya hayo, Kembo (1993) anasisitiza kwamba ukopaji ni mmojawapo ya michakato ya kihalisia ya lugha. Anaendelea kwa kuelezea kwamba ukopaji unahusisha utohozi wa

37 21 maneno ya kigeni na kuyabadilisha ili yaweze kuingiliana na mahitaji kimuundo ya lugha kopaji. Maneno ya kukopwa hupitia usilimisho ili yaweze kutamkika vyema katika lugha kopaji. Kembo (1993) ametumia nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia katika kazi yake. Utafiti huu umepata mchango muhimu kutokana na kazi ya Kembo (1993) kwa jinsi ambavyo ameangazia ukopaji kwa kuzingatia mageuzi ya kifonolojia ya vipande sauti vya maneno husika. Pia ameonyesha kwamba mageuzi yanayohusika katika ukopaji ni katika harakati za usimilisho wa maneno- mkopo ili yaweze kuafiki matamshi ya lugha ya Kidholuo. Mawazo haya yameweza kusaidia utafiti huu wetu. Zaidi ya haya, Kembo (1993) ametumia nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia ambayo ndiyo iliyotumiwa katika utafiti huu. Hata hivyo, tofauti inaonekana pale ambapo Kembo (1993) anahusisha vipamba sauti katika utafiti wake ambavyo havijashughulikiwa katika utafiti huu. Pia, amezingatia lugha ya Kidholuo ilhali utafiti huu umezingatia lugha ya Kigiryama. Kulingana na Hyman (1970b), anajadili kwamba jukumu la ukopaji katika sarufi ni kwamba sauti huwa zinakopwa ili kukadiria matamshi ya maneno mkopo yanayohusika. Anasisitiza kwamba lugha huwa zinatafuta sauti za lugha kopaji zinazokaribiana na zile za lugha kopeshi ili kukadiria matamshi ya sauti zilizokopwa. Pia anaongezea kwamba sauti zinazokopwa hupitia vikwazo vya kifonolojia vinavyowekwa na lugha kopaji. Hyman (1970b) katika kazi yake anahusisha maneno-mkopo ya lugha ya Kiyakui yanayokopwa kutoka lugha ya Kihispaniola. Makala ya Hyman (1970b) yametoa mchango muhimu katika utafiti huu kwani yamejadili vikwazo vya kifonolojia vinavyopitiwa na sauti za lugha ya Kiyakui wakati wa ukopaji hadi katika lugha ya Kihispaniola. Vikwazo vya kifonolojia ndio michakato ya kifonolojia inayojadiliwa katika utafiti huu kwa hiyo mawazo ya Hyman yamekuza

38 22 utafiti huu. Hata hivyo, utofauti wake ni kuhusisha lugha ya Kihispaniola na Kiyakui ilhali utafiti huu unahusisha lugha ya Kigiryama na Kiingereza. Zaidi ya hayo, Hyman hajazingatia nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia kama utafiti huu ulivyofanya. Kwa upande mwingine, Kaye na Nykiel (1979), katika makala yao inayohusu sababu zinazofanya maneno-mkopo kusilimishwa katika mfumo wa lugha kopaji, wanadai kwamba maneno - mkopo hukopwa kwa kuzingatia vikwazo vya kifonolojia vya lugha Kopaji. Wanaongezea kwa kusema kuwa vikwazo pia vinawekwa katika kiwango cha uwakilishi wa kileksia. Wanasisitiza kwamba muundo wa ndani wa maneno yanayokopwa ambao haudhihiriki waziwazi ndio unachangia katika matokeo ya muundo wa maneno mkopo. Kaye na Nykiel (1979) wanafafanua mawazo haya kwa kutumia maneno mkopo yanayotokana na lugha ya Kiyoruba hadi Kinupe. Kazi ya Kaye na Nykiel (1979) inachangia utafiti huu kwa vile imeangazia maswala ya vikwazo vya kifonolojia katika ukopaji. Hata hivyo, tofauti ni kwamba, utafiti huu hauhusishi jinsi muundo ndani wa maneno yanayokopwa unavyoathiri muundo wa maneno-mkopo kama kazi ya Kaye na Nykiel (1979) inavyofanya. Pia waandishi hawa wanajadili maswala ya muundo katika ukopaji kwa kurejelea lugha ya Kiyoruba na ile ya Kinupe ilhali lugha zinazorejelewa katika utafiti huu ni Kiingereza na Kigiryama. Steinbergs (1985) katika makala yake ya fonolojia ya ukopaji katika lugha ya Kioshikwanyama, anajadili ule udhahania wa fonolojia ya ukopaji. Anatumia mifano ya sauti za nasali na konsonanti za lugha ya Kioshikwanyama na anaonyesha kwamba muundo wa nje unaoibuka na maneno-mkopo ni kutokana na matamshi ya haraka yanayohitajika wakati wa kutamka maneno hayo. Hata hivyo, anadhihirisha kwamba ukopaji unahusisha vikwazo vya muundo ndani wa maneno mkopo yanayohusika. Kazi ya Steinberg (1985) imechangia kwa kiasi utafiti huu kwa sababu imehusisha dhana ya

39 23 fonolojia ya ukopaji. Hata hivyo, utofauti wa kazi ya Steinberg (1985) ni jinsi anavyojadili muundo ndani wa maneno mkopo ilhali utafiti huu wetu unajadili michakato ya kimofofonolojia inayohusisha muundo nje wa nomino mkopo za Kigiryama zinazotokana na lugha ya Kiingereza. Kulingana na Hansford na Hansford (1989) na Katamba na Rottland (1987), ukopaji ni mchakato unaohusisha muundo nje wa maneno mkopo yanayohusishwa. Hawa wanatetea kwamba katika utohozi wa kifonolojia, muundo ndani wa maneno-mkopo hauhusishwi kamwe. Hansford na Hansford (1989) katika makala kuhusu manenomkopo ya lugha ya Kichimburung, wanaelezea kwamba sauti za maneno ya kukopwa huwa zinatafutiwa sauti zilizokaribiana kimatamshi katika lugha inayokopa ili ziweze kuingiliana vyema na fonolojia ya lugha kopaji. Kwa upande mwingine, Katamba na Rottland (1987) wanakubaliana na mawazo ya Hansford na Hansford (1989) katika makala yao ya ukopaji wa maneno ya Kiingereza hadi lugha ya Kiluganda. Katamba na Rottland (1987) katika kazi yao wameonyesha kuwa fonimu-mkopo za lugha ya Kiingereza hutafutiwa fonimu za Kiluganda zilizokaribiana kimatamshi wakati wa ukopaji. Zaidi ya hayo, Katamba na Rottland (1987) wanazingatia ukopaji wa silabi za Kiingereza katika lugha ya Kiluganda na kuonyesha kwamba konsonanti za vianzio vya maneno ya Kiluganda zinawekewa mipaka kuliko zile za maneno ya Kiingereza. Kwa hivyo katika ukopaji, silabi ina jukumu la kuwa kama kichungi cha kuchungia manenomkopo yanayoingia katika lugha ya Kiluganda. Makala ya Hansford na Hansford (1989) na Katamba na Rottland (1987) yamechangia pakubwa katika utafiti huu kwa sababu yamehusisha mageuzi ya muundo nje wa nomino-mkopo wakati wa ukopaji na kudhihirisha kwamba fonolojia ina dhima kubwa katika ukopaji wa maneno. Huu ni

40 24 mchango mkubwa katika utafiti huu wetu kwa sababu imedhihirika kwamba Fonolojia ya lugha ya Kiingereza na lugha ya Kigiryama zina dhima kubwa katika mchakato wa ukopaji. Hata hivyo, makala hizi zimehusisha silabi kama kichungi cha maneno-mkopo katika ukopaji ilhali utafiti huu haujahusisha silabi kama kichungi cha nomino mkopo. Kulingana na Singh (1980), katika makala yake ya Ukopaji wa maneno kutoka lugha ya Kiingereza hadi lugha ya Kihindi, anaonyesha kwamba jozi za konsonanti zinazopatikana katika vianzio vya maneno zinatengwa kwa mchakato wa uchopekaji. Hata hivyo jozi hizi za konsonanti zinapopatikana katikati ya maneno hazitengwi na zinaachwa hivyo. Singh (1980) anajadili kwamba jozi za konsonanti za katikati za maneno hazitengwi kwa sababu kila konsonanti katika jozi hizi huwa inapewa jukumu la kujisimamia kama silabi kamili katika lugha ya Kihindi. Makala ya Singh (1980) ina mchango muhimu katika utafiti huu kwa jinsi ambavyo inahusisha michakato ya kifonolojia kama uchopekaji ambao ni muhimu sana katika kutenganisha mfuatano wa konsonanti katika maneno yanayokopwa. Hata hivyo, makala ya Singh (1980) yanaonyesha kwamba uchopekaji hautokei katika konsonanti za katikati ya maneno na kwamba konsonanti hizi huweza kujisimamia kama silabi kamili; jambo ambalo haliwiani na utafiti huu. Mfuatano wa konsonanti katika lugha ya Kigiryama hauchukuliwi kuwa silabi moja bali sharti kuwe kuna vokali ili silabi inayoundwa iwe wazi. Kulingana na Kunene (1963) ambaye makala yake inashughulikia ukopaji wa maneno ya lugha ya Kiingereza hadi Kiafrikaana katika eneo la kusini mwa Sotho, anatambua kwamba lugha ya Kiafrikaana imeweza kukubali mfululizo wa konsonanti wa maneno ya Kiingereza katika maneno-mkopo ya Kiafrikaana. Mfululizo huu wa konsonanti umekubalika kuingizwa katika Fonolojia ya lugha ya Kiafrikaana wakati wa ukopaji

ATHARI ZA KIMOFOFONOLOJIA ZA KIOLUSUBA KATIKA MATUMIZI YA KISWAHILI SANIFU KAMA LUGHA YA PILI

ATHARI ZA KIMOFOFONOLOJIA ZA KIOLUSUBA KATIKA MATUMIZI YA KISWAHILI SANIFU KAMA LUGHA YA PILI ATHARI ZA KIMOFOFONOLOJIA ZA KIOLUSUBA KATIKA MATUMIZI YA KISWAHILI SANIFU KAMA LUGHA YA PILI MEROLYNE ACHIENG OTIENDE Tasnifu hii imewasilishwa kwa ajili ya kutosheleza baadhi ya mahitaji ya shahada ya

More information

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika

Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Kiswahili, utandawazi na umoja wa Afrika Stephen N. Kamau Abstract It is a fact that in the recent past, globalization has gradually taken shape in Africa and as such the continent has no choice but to

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2015 Citation 1. This Order may be cited

More information

DHANA NA MATKTIZO YA TAFSIRI:

DHANA NA MATKTIZO YA TAFSIRI: BCStf GFBMAEA COLLECT!*# DHANA NA MATKTIZO YA TAFSIRI: TATHMINI YA RISASI ZIANZAPO KUCHANUA. OMONDI L F. O S A N O Tasnifu hii imetolewa ili kutosheleza baadhi ya mahitaji ya shahada ya M.A. katika Chuo

More information

MIFANYIKO YA KIMOFOFONOLOJIA YA UKUZAJI NA UDUNISHAJI NOMINO ZA KIWANGA,KAKAMEGA, KENYA AGULL NICHOLAS OWINO

MIFANYIKO YA KIMOFOFONOLOJIA YA UKUZAJI NA UDUNISHAJI NOMINO ZA KIWANGA,KAKAMEGA, KENYA AGULL NICHOLAS OWINO MIFANYIKO YA KIMOFOFONOLOJIA YA UKUZAJI NA UDUNISHAJI NOMINO ZA KIWANGA,KAKAMEGA, KENYA AGULL NICHOLAS OWINO Tasnifu hii imewasilishwa kwa Halmashauri ya shahada za juu ili kutosheleza baadhi ya mahitaji

More information

ULINGANISHI WA KIISIMU KATI YA LAHAJA YA KIPEMBA NA KITUMBATU

ULINGANISHI WA KIISIMU KATI YA LAHAJA YA KIPEMBA NA KITUMBATU ULINGANISHI WA KIISIMU KATI YA LAHAJA YA KIPEMBA NA KITUMBATU BAKARI K. BAKARI TASNIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SHARTI LA SHAHADA YA UMAHIRI YA KISWAHILI (M.A KISWAHILI) i UTHIBITISHO Aliyetia

More information

UCHANGANUZI LINGANISHI WA SINTAKSIA YA SENTENSI SHARTI YA KISWAHILI SANIFU NA EKEGUSII CHUO KIKUU CHA NAIROBI

UCHANGANUZI LINGANISHI WA SINTAKSIA YA SENTENSI SHARTI YA KISWAHILI SANIFU NA EKEGUSII CHUO KIKUU CHA NAIROBI UCHANGANUZI LINGANISHI WA SINTAKSIA YA SENTENSI SHARTI YA KISWAHILI SANIFU NA EKEGUSII NA FRANCIS ONYONKA NYANDAGO CHUO KIKUU CHA NAIROBI TASNIFU HII IMETOLEWA KWA MADHUMUNI YA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI

More information

Information for assessors (do not distribute this page to participants):

Information for assessors (do not distribute this page to participants): R&P Cultural Orientation Model Assessment Written Version Swahili Information for assessors (do not distribute this page to participants): This written version of the Model Cultural Orientation (CO) Assessment

More information

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23)

GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER. (Made under Section 23) GOVERNMENT NOTICE No... PUBLISHED ON THE ELECTRICITY ACT, (CAP.131) ORDER (Made under Section 23) THE ELECTRICITY (STANDARDIZED SMALL POWER PROJECTS TARIFF) ORDER, 2016 citation 1. This Order may be cited

More information

CHUO KIKUU CHA NAIROBI

CHUO KIKUU CHA NAIROBI CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA KISWAHILI UCHUNGUZI WA SITIARI DHANIFU KATIKA METHALI ZA KISWAHILI - MTAZAMO WA NADHARIA YA UHUSIANO MISHECK NKANGA GAICHU C50/66914/2013 TASNIFU HII INAWASILISHWA KWA MINAJILI

More information

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya

Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya Nordic Journal of African Studies 9(2): 49-59 (2000) Usimulizi wa Riwaya ya Nyongo Mkalia Ini E. S. MOHOCHI University of Egerton, Kenya UTANGULIZI Tukichunguza hazina ya uhakiki uliofanywa katika taaluma

More information

MATUMIZI YA LUGHA KATIKA KANISA KATOLIKI: UCHANGANUZI WA UBADILISHAJI MSIMBO KATIKA MAHUBIRI

MATUMIZI YA LUGHA KATIKA KANISA KATOLIKI: UCHANGANUZI WA UBADILISHAJI MSIMBO KATIKA MAHUBIRI MATUMIZI YA LUGHA KATIKA KANISA KATOLIKI: UCHANGANUZI WA UBADILISHAJI MSIMBO KATIKA MAHUBIRI NA WAWERU TERESIA WANJIRU (SR) TASNIFU HII IMETOLEWA KWA MADHUMUNI YA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA

More information

MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012

MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012 MITAZAMO KUHUSU KISWAHILI MIONGONI MWA WAZUNGUMZAJI WA KIJALUO: KIFANI CHA SHULE ZA MSINGI KATIKA KAUNTI YA MIGORI. OWALA JAEL AKINYI C50/75493/2012 TASNIFU HII IMEWASILISHWA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI

More information

VITENDO USEMI NA ULINGANIFU WA MAANA KATIKA TAFSIRI: MIFANO KUTOKA TAFSIRI ZA KAZI MBILI TEULE ZA BARBARA KIMENYE

VITENDO USEMI NA ULINGANIFU WA MAANA KATIKA TAFSIRI: MIFANO KUTOKA TAFSIRI ZA KAZI MBILI TEULE ZA BARBARA KIMENYE VITENDO USEMI NA ULINGANIFU WA MAANA KATIKA TAFSIRI: MIFANO KUTOKA TAFSIRI ZA KAZI MBILI TEULE ZA BARBARA KIMENYE NAHASHON AKUNGAH NYANGERI Tasnifu hii imetolewa madhumuni ya kutosheleza baadhi ya mahitaji

More information

TASFIDA KAMA MKAKATI WA UPOLE: UWIANO WA TASFIDA ZA KISWAHILI NA EKEGUSII

TASFIDA KAMA MKAKATI WA UPOLE: UWIANO WA TASFIDA ZA KISWAHILI NA EKEGUSII TASFIDA KAMA MKAKATI WA UPOLE: UWIANO WA TASFIDA ZA KISWAHILI NA EKEGUSII NA FLORAH N. OMOSA C50/84117/2012 TASNIFU HII IMETOLEWA KWA MADHUMUNI YA KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJIYA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA

More information

ATHARI ZA KIISIMU ZA LAHAJA YA KIMAKUNDUCHI KATIKAKISWAHILI SANIFU KINACHOTUMIKA SHULENI MAKUNDUCHI ZANZIBAR

ATHARI ZA KIISIMU ZA LAHAJA YA KIMAKUNDUCHI KATIKAKISWAHILI SANIFU KINACHOTUMIKA SHULENI MAKUNDUCHI ZANZIBAR ATHARI ZA KIISIMU ZA LAHAJA YA KIMAKUNDUCHI KATIKAKISWAHILI SANIFU KINACHOTUMIKA SHULENI MAKUNDUCHI ZANZIBAR SALEH ABDELSALAM MOHAMMED SALEH TASINIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUKAMILISHA MASHARTI YA

More information

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E)

Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) 102/3 KISWAHILI KARATASI YA 3 Fasihi Julai/Agosti 2013 MUDA : SAA 2 ½ Hati ya kuhitimu kisomo Kenya (K.C.S.E) Kiswahili Karatasi 3 Julai/ Agosti Muda: Saa 2 ½ MAAGIZO: Andika jina lako na nambari yako

More information

Ufundishaji wa lugha nyingine

Ufundishaji wa lugha nyingine CHUO CHA ELIMU CHA KIMATAIFA OFISI YA ELIMU YA KIMATAIFA Ufundishaji wa lugha nyingine Na Elizabeth B. Bernhardt ELIMU MAZOEA KITABU NA. 20 1 Chuo cha Elimu cha Kimataifa (The International Academy of

More information

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania

KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 12(3): 296 309 (2003) KUSHUKA KWA HADHI YA LUGHA ZA JAMII NCHINI TANZANIA YOHANA P. MSANJILA University of Dar es Salaam, Tanzania ABSTRACT Lugha za jamii hapa nchini

More information

Evaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya

Evaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya Evaluation of Contextual Teaching of Kiswahili Proverbs in Secondary Schools in Kenya Oduori T. Wamubi Prof. Simala, K. Inyani Profesa Mshiriki Masinde Muliro University of Science and Technology Prof.

More information

CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA KISWAHILI MAMLAKA NA ITIKADI KATIKA NYIMBO TEULE ZA TAARAB

CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA KISWAHILI MAMLAKA NA ITIKADI KATIKA NYIMBO TEULE ZA TAARAB CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA KISWAHILI MAMLAKA NA ITIKADI KATIKA NYIMBO TEULE ZA TAARAB TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA CHUO KIKUU CHA NAIROBI NOVEMBA

More information

KUCHUNGUZA MCHOMOZO KATIKA FASIHI YA KISWAHILI: UTAFITI LINGANISHI WA USHAIRI KATIKA DIWANI YA USTADHI ANDANENGA

KUCHUNGUZA MCHOMOZO KATIKA FASIHI YA KISWAHILI: UTAFITI LINGANISHI WA USHAIRI KATIKA DIWANI YA USTADHI ANDANENGA KUCHUNGUZA MCHOMOZO KATIKA FASIHI YA KISWAHILI: UTAFITI LINGANISHI WA USHAIRI KATIKA DIWANI YA USTADHI ANDANENGA AUGUSTINO TENDWA TASNIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SHARTI PEKEE LA KUTUNUKIWA

More information

NAFASI YA MWANAMKE: JINSI INAVYOTETEWA KATIKA NYIMBO ZA TAARAB ZA ZANZIBAR ELIZABETH KANGOGO YEGO C50/68796/2011 IDARA YA ISIMU NA LUGHA

NAFASI YA MWANAMKE: JINSI INAVYOTETEWA KATIKA NYIMBO ZA TAARAB ZA ZANZIBAR ELIZABETH KANGOGO YEGO C50/68796/2011 IDARA YA ISIMU NA LUGHA NAFASI YA MWANAMKE: JINSI INAVYOTETEWA KATIKA NYIMBO ZA TAARAB ZA ZANZIBAR ELIZABETH KANGOGO YEGO C50/68796/2011 IDARA YA ISIMU NA LUGHA CHUO KIKUU CHA NAIROBI TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI

More information

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania

Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania Nordic Journal of African Studies 16(1): 18 29 (2007) Utumiaji Wa Kiswahili Na Lugha Za Jamii Kijinsia Nchini Tanzania Y.P. MSANJILA University of Dar-es-Salaam, Tanzania ABSTRACT This paper has attempted

More information

UHUSIANO WA MIKAKATI YA UFUNDISHAJI WA FASIHI YA WATOTO YA KISWAHILI NA UMILISI WA KUSOMA KATIKA SHULE ZA MSINGI, KASARANI, KAUNTI YA NAIROBI, KENYA

UHUSIANO WA MIKAKATI YA UFUNDISHAJI WA FASIHI YA WATOTO YA KISWAHILI NA UMILISI WA KUSOMA KATIKA SHULE ZA MSINGI, KASARANI, KAUNTI YA NAIROBI, KENYA UHUSIANO WA MIKAKATI YA UFUNDISHAJI WA FASIHI YA WATOTO YA KISWAHILI NA UMILISI WA KUSOMA KATIKA SHULE ZA MSINGI, KASARANI, KAUNTI YA NAIROBI, KENYA NA SELINA RHOBI CHACHA E55/23475/11 TASNIFU HII IMEWASILISHWA

More information

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI

LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI LUGHA YA KISWAHILI KATIKA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA ELIMU SHULE ZA SEKONDARI SIKOMBE YIZUKANJI YORADI TASNIFU YA KISWAHILI KWA MINAJILI YA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (MA. KISWAHILI) KITIVO CHA SANAA

More information

MADA MATUMIZI YA TAKRIRI NA SITIARI KATIKA UTENZI WA RASI LGHULI JUSTUS MAUNDU NDUMBU C50/65902/2011 CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA ISIMU NA LUGHA

MADA MATUMIZI YA TAKRIRI NA SITIARI KATIKA UTENZI WA RASI LGHULI JUSTUS MAUNDU NDUMBU C50/65902/2011 CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA ISIMU NA LUGHA MADA MATUMIZI YA TAKRIRI NA SITIARI KATIKA UTENZI WA RASI LGHULI NA JUSTUS MAUNDU NDUMBU C50/65902/2011 CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA ISIMU NA LUGHA TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI

More information

KUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA

KUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA KUCHUNGUZA MASUALA YA KISIASA KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: MFANO WA KUSADIKIKA NA KUFIKIRIKA BIBIANA MASSAWE AMBROSE TASINIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SHARTI PEKEE LA KUTUNUKIWA DIGRII

More information

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu

Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu The Human Rights Centre Uganda Azimio la Mkutano Mkuu 53/144 (8 Machi 1999) Azimio la Umoja wa Mataifa Kuhusu Watetezi wa Haki za Binadamu AZIMIO KUHUSU HAKI NA WAJIBU WA MTU BINAFSI, VIKUNDI NA JUMUIYA

More information

MATATIZO YA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA VYOMBO VYA HABARI: MIFANO KUTOKA KENYA 1 KITULA KINGE'I. 1. Utangulizi. AAP 64 (2000): Swahili Forum VII 45-56

MATATIZO YA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA VYOMBO VYA HABARI: MIFANO KUTOKA KENYA 1 KITULA KINGE'I. 1. Utangulizi. AAP 64 (2000): Swahili Forum VII 45-56 AAP 64 (2000): Swahili Forum VII 45-56 MATATIZO YA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA VYOMBO VYA HABARI: MIFANO KUTOKA KENYA 1 KITULA KINGE'I 1. Utangulizi Mwandishi mawufu wa fasihi bwani Afiika, Chinua Achebe

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA WA ELIMUMSINGI DARASA LA I NA LA II JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU SAYANSI TEKNOLOJIA NA UFUNDI MTAALA

More information

UJAGINA WA MWANAMKE KATIKA PANGO

UJAGINA WA MWANAMKE KATIKA PANGO UJAGINA WA MWANAMKE KATIKA PANGO NA MUNIU GEORGE GITHUCI C50/65581/2011 TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI KATIKA CHUO KIKUU CHA NAIROBI IDARA YA KISWAHILI NOVEMBER

More information

MAKALA: USHAIRI WA KISWAHILI KATIKA NJIA PANDA: KUTUMIA AU KUTOTUMIA METHALI

MAKALA: USHAIRI WA KISWAHILI KATIKA NJIA PANDA: KUTUMIA AU KUTOTUMIA METHALI MAKALA: USHAIRI WA KISWAHILI KATIKA NJIA PANDA: KUTUMIA AU KUTOTUMIA METHALI Na Joseph Nyehita Maitaria Mwanafunzi wa Ph.D Idara ya Kiswahili na Lugha za Kiafrika Chuo Kikuu cha Kenyatta Ikisiri Makala

More information

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti

Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Jifunze kusimamia pesa zako nchini Uskoti Mradi wa kujua kuhusu Pesa Aprili 2011 FLP - Swahili Mradi wa kujua kuhusu Pesa Ipindi vyetu vya maelezo vya bure, warsha na kozi hutoa fursa ya kujifunza kuhusu

More information

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania

Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Ufanisi katika Ufundishaji kwenye Shule za Msingi na Sekondari nchini Tanzania Desemba 2014 1 Shukurani Ripoti hii iliandikwa na Dk. Mkumbo. Ushauri wa kitaalamu ulitolewa na Elizabeth Missokia na Godfrey

More information

KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS

KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS KENYA NATIONAL EXAMINATION COUNCIL REVISION MOCK EXAMS 2016 TOP NATIONAL SCHOOLS ALLIANCE BOYS HIGH SCHOOL KISWAHILI KARATASI YA 2 SCHOOLS NET KENYA Osiligi House, Opposite KCB, Ground Floor Off Magadi

More information

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI

JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI JHSPH MAADILI YA KUFANYA UTAFITI WA MASUALA YA BINAADAMU MUONGOZO WA MAFUNZO YA UTAFITI Mwongozo huu utatumika kama njia ya kuwafunza watafiti watakaohusika na utafiti unaohusu binadamu. Muongozo huu utatumika

More information

KUCHUNGUZA UJINSIA NA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA METHALI ZA WAKURYA

KUCHUNGUZA UJINSIA NA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA METHALI ZA WAKURYA i KUCHUNGUZA UJINSIA NA MATUMIZI YA LUGHA KATIKA METHALI ZA WAKURYA TIMANYWA FELICIAN TASINIFU INAYOWAKILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SEHEMU YA SHARTI PEKEE LA KUTUNUKIWA SHAHADA YA UZAMILI (M.A. KISWAHILI)

More information

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI

MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA 2005 YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI MAKUBALIANO YA ULINZI NA UKUZAJI WA VIELELEZO VYA TAMADUNI ANUWAI Paris, 20 Oktoba 2005 Kongamano Kuu la Umoja wa Mataifa linalohusisha

More information

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza

Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Mwongozo wa Utamaduni Toleo la Kwanza Kubadilishana Tamaduni za Kijerumani na za Kitanzania Limeandaliwa na Anna Hoppenau, Johannes Hahn, Oliva Lyimo na Lisa Bendiek German-Tanzanian Partnership (DTP)

More information

UFASIHI SIMULIZI KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: Mifano kutoka Adili na Nduguze na Wasifu wa Siti Binti Saad. Khatib Khamis Saleh

UFASIHI SIMULIZI KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: Mifano kutoka Adili na Nduguze na Wasifu wa Siti Binti Saad. Khatib Khamis Saleh UFASIHI SIMULIZI KATIKA RIWAYA ZA SHAABAN ROBERT: Mifano kutoka Adili na Nduguze na Wasifu wa Siti Binti Saad Khatib Khamis Saleh Tasinifu ya Uzamili Katika Kiswahili Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Septemba,

More information

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada?

Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? Policy brief TZ.12/2010K Misamaha ya kodi Tanzania: Je, ni mikubwa sana na kutufanya tuwe tegemezi kwa misaada? 1. Utangulizi Kila mwaka Bunge la Tanzania hupitia na kuchanganua kwa makini bajeti ya Serikali.

More information

KISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA

KISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA KISWAHILI KARATASI YA 2 LUGHA Maagizo (a) Andika jina lako na namba yako katika nafasi ulizoachiwa hapo juu. (b) Tia sahihi yako na tarehe ya mtihani katika nafasi ulizoachiwa hapo juu. (c) Jibu maswali

More information

KUCHUNGUZA UFASIHI SIMULIZI UNAOJITOKEZA NDANI YA HADITHI ZA KUSADIKIKA NA ADILI NA NDUGUZE

KUCHUNGUZA UFASIHI SIMULIZI UNAOJITOKEZA NDANI YA HADITHI ZA KUSADIKIKA NA ADILI NA NDUGUZE KUCHUNGUZA UFASIHI SIMULIZI UNAOJITOKEZA NDANI YA HADITHI ZA KUSADIKIKA NA ADILI NA NDUGUZE MUHAMMED ALI SALIM TASINIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA SEHEMU YA MASHARTI YA KUTUNIKIWA SHAHADA YA

More information

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO

UTANGULIZI ANUANI NA MANDHARI YA CHUO UTANGULIZI International Montessori Teachers College (IMTC), ni chuo kilichoanzishwa hapa nchini Tanzania mwaka 2012 na kinatoa kozi ya kimataifa ya ualimu wa watoto wadogo (yaani child care and nursery

More information

FANI KATIKA NYIMBO TEULE ZA ANASTACIA MUKABWA MBURU JAMES MUNGAI TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA

FANI KATIKA NYIMBO TEULE ZA ANASTACIA MUKABWA MBURU JAMES MUNGAI TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA FANI KATIKA NYIMBO TEULE ZA ANASTACIA MUKABWA MBURU JAMES MUNGAI TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI YA MAHITAJI YA SHAHADA YA UZAMILI (M.A.) KATIKA IDARA YA KISWAHILI CHUO KIKUU CHA NAIROBI 2014

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level. SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 www.xtremepapers.com UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level *9257224991* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2013 Additional Materials: Answer Booklet/Paper

More information

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig

Huduma kwa wateja kupitia barua pepe na ujumbe mfupi Fig KITINI CHA JINSI YA KUTUMIA MFUMO WA SIMU YA KIGANJANI KATI YA BARAZA LA FAMASI NA WAMILIKI WA MADUKA NA WATAALAMU WA DAWA YALIYOMO UTANGULIZI... 3 SEHEMU YA KWANZA: MALIPO YA KUHUISHA VIBALI... 4 1.1

More information

V\ FANI KATIKA USHAIRI WA HASSAN MWALIMU MBEGA: UHAKIKI WA UPISHO WA UMALENGA NA DAFINA YA UMALENGA DONALD OMWOYO OSIEMO

V\ FANI KATIKA USHAIRI WA HASSAN MWALIMU MBEGA: UHAKIKI WA UPISHO WA UMALENGA NA DAFINA YA UMALENGA DONALD OMWOYO OSIEMO gftgff AROGAHA COLLECTION MADA: V\ FANI KATIKA USHAIRI WA HASSAN MWALIMU MBEGA: UHAKIKI WA UPISHO WA UMALENGA NA DAFINA YA UMALENGA NA: DONALD OMWOYO OSIEMO TASNIFU HII IMETOLEWA ILI KUTOSHELEZA BAADHI

More information

KUCHUNGUZA DHAMIRA ZA NYIMBO ZA UGANGA KATIKA JAMII ZA WASWAHILI WILAYA YA MKOANI KUSINI PEMBA

KUCHUNGUZA DHAMIRA ZA NYIMBO ZA UGANGA KATIKA JAMII ZA WASWAHILI WILAYA YA MKOANI KUSINI PEMBA KUCHUNGUZA DHAMIRA ZA NYIMBO ZA UGANGA KATIKA JAMII ZA WASWAHILI WILAYA YA MKOANI KUSINI PEMBA MUSSA YUSSUF ALI TASNIFU ILIYOWASILISHWA IKIWA NI SEHEMU YA MASHARTI YA KUPATIWA SHAHADA YA UZAMILI YA KISWAHILI

More information

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka

Ufunguo wa Kutaalamika Haraka 0 Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Ufunguo wa Kutaalamika Haraka Kijitabu Kielelezo; Nakala ya Bila Malipo Yaliyomo 1 Yaliyomo Utangulizi...04 Habari Fupi Kuhusu...08 Fumbo la Ulimwengu wa Ng ambo ya Pili...11

More information

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada

MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA PRO-ROUTES. Ombi kwa ajili ya fedha za umma wa mradi wa ziada Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Résumé non technique Version Swahili MKAKATI ATHARI YA MAZINGIRA NA KIJAMII YA KAZI YA

More information

NAFASI YA MUZIKI ULIOPENDWA KATIKA FASIID YA KISWAHILI PAMELA M. Y NGUGI. Inkisiri. M a kala. AAP 64 (2000): Swahili Forum VII

NAFASI YA MUZIKI ULIOPENDWA KATIKA FASIID YA KISWAHILI PAMELA M. Y NGUGI. Inkisiri. M a kala. AAP 64 (2000): Swahili Forum VII AAP 64 (2000): Swahili Forum VII 145-152 NAFASI YA MUZIKI ULIOPENDWA KATIKA FASIID YA KISWAHILI PAMELA M. Y NGUGI Inkisiri Nyimbo, kama tanzu ya fasihi yeyote ile zina majukumu mbalimbali ambayo hutekeleza

More information

Human Rights Are Universal And Yet...

Human Rights Are Universal And Yet... Human Rights Are Universal And Yet... Episode 05 Title : The right to education Author : Julien Adayé Editor : Aude Gensbittel Translator : Anne Thomas, Eric Ponda Proofreader: Pendo Paul Characters (sounds,

More information

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q

N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q N09/2/ABSWA/HP1/SWA/TZ0/XX/Q 88092387 SWAHILI B HIGHER LEVEL PAPER 1 SOUAHÉLI B NIVEAU SUPÉRIEUR ÉPREUVE 1 SUAHILI B NIVEL SUPERIOR PRUEBA 1 Tuesday 3 November 2009 (morning) Mardi 3 novembre 2009 (matin)

More information

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR

ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI KWA UCHUMI WA ZANZIBAR MUHTASARI WA RIPOTI YA YA MWISHO. JULY 2012 for Page i Muhtasari Utafiti huu wa athari za Mabadiliko ya Tabianchi kwa uchumi Zanzibar umetoa tathmini

More information

Hakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn

Hakimiliki na Jonathan Menn. Haki zote zimehifadhiwa TAFSIRI YA BIBLIA. Mwandishi. Jonathan M. Menn TAFSIRI YA BIBLIA Mwandishi Jonathan M. Menn B.A., University of Wisconsin-Madison, 1974 J.D., Cornell Law School, 1977 M.Div., Trinity Evangelical Divinity School, 2007 Equipping Church Leaders-East Africa

More information

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake

Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake Uongozi Bora Kitabu Cha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Wanawake UONGOZI BORA Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo. -Mshiriki katika Semina ya Mafunzo Uongozi Bora: Kitabu cha Mafunzo ya

More information

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA

TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF) KUHUSU HAKI ZA WATOTO KATIKA KATIBA MPYA Marekebisho ya 23 January 2013 YALIYOMO KURASA TAMKO LA JUKWAA LA HAKI ZA WATOTO (TCRF)... 0 KUHUSU HAKI ZA WATOTO... 0

More information

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi

Miradi na jamii. 3.1 Utangulizi 3.1 Utangulizi Miradi na jamii Lengo la sura hii ni mapitio ya mazingira pana ambayo chini ya ardhi kwa ajili ya maendeleo vijijini upatikanaji wa maji inafaa. majadiliano wakapanga meneja, au kiongozi

More information

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI

USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI USIMAMIZI MKUU WA UBORA WA MAHURUJI MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA WASTANI WANAOUZA BIDHAA NJE YA NCHI TOLEO LA PILI Geneva 2011 ii IKISIRI YA HUDUMA YA HABARI ZA BIASHARA ID=42653 2011 F-09.03

More information

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA)

UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Empowered lives. Resilient nations. UKUZAJI WA ASALI AFRICA (HONEY CARE AFRICA) Kenya Miradi ya Equator Wanafijiji na Maendeleo Himili ya Jamii MIRADI YA UNDP EQUATOR Kote duniani, jamiii zinazidi kubuni

More information

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013

Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 W N S E Muhtasari Ripoti ya Maendeleo ya Binadamu 2013 Kuinuka kwa Nchi za Kusini: Maendeleo ya Binadamu katika Ulimwengu Anuwai Empowered lives. Hati ya kunakili 2013 na Mradi wa Maendeleo ya Umoja wa

More information

Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi

Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Elimu Ina Umuhimu gani katika Jamii? Kuelekea Elimu Sahihi Gervas Zombwe 1 1. Utangulizi Katika mazingira ya kawaida kabisa ndani ya jamii yetu, Imezoeleka kusikia au kuona watu wakioanisha dhana ya elimu

More information

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org (

Haja Ya Dini. Author(s): Publisher(s): Translator(s): Category: Topic Tags: Featured Category: Published on Al-Islam.org ( Published on Al-Islam.org (https://www.al-islam.org) Home > Haja Ya Dini Haja Ya Dini Author(s): Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi [3] Publisher(s): Bilal Muslim Mission of Tanzania [4] Katika kijitabu

More information

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007

Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 Kufafanua Upya Elimu Bora Tanzania: Kutoka Zana za Dufundishia mpaka Uwezo wa Wanafunzi 1 Oktoba 2007 1. Utangulizi Changamoto kuu iliyopo kuhusiana na Elimu ya msingi nchini Tanzania kwa sasa ni namna

More information

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza

Mwongozo wa Familia wa Kujifunza Shule za umma za kata ya Fayette 1 Mwongozo wa Familia wa Kujifunza Muhtasari wa yale watoto wanastahili kufahamu na kuweza kufanya na njia za familia kuongeza masomo nyumbani. Tunaamini familia ni wenzetu.

More information

Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E)

Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E) 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI/AGOSTI 2011 MUDA: 2 ½ Kiswahili Fasihi Hati ya Kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya.( K.C.S.E) MAAGIZO Jibu maswali manne pekee Swali la kwanza ni lazima Maswali

More information

ETIMOLOJIA YA MAJINA YA MAHALI YA KASKAZINI PEMBA KUWA UTAMBULISHO WA UTAMADUNI WA WAPEMBA

ETIMOLOJIA YA MAJINA YA MAHALI YA KASKAZINI PEMBA KUWA UTAMBULISHO WA UTAMADUNI WA WAPEMBA ETIMOLOJIA YA MAJINA YA MAHALI YA KASKAZINI PEMBA KUWA UTAMBULISHO WA UTAMADUNI WA WAPEMBA ZUWENA SULEIMAN ZUBEIR TASNIFU ILIYOWASILISHWA KWA AJILI YA KUTIMIZA BAADHI YA MASHARTI YA SHAHADA YA UZAMILI

More information

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu

Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu Utangulizi wa ugonjwa wa shinikizo la damu BLOOD PRESSURE UK Shinikizo la damu ndicho chanzo kikubwa cha ulemavu na vifo vya mapema kule Uingereza, kupitia kiharusi, mshtuko wa moyo na maradhi ya moyo.

More information

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi

Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Elimukombozi, Lugha na Upashanaji Habari nchini Tanzania, katika Muktadha wa Utandawazi Martha Qorro 1 1.0 Utangulizi Elimu ni suala la jamii ambalo mipango na taratibu zake zinahitaji kushirikisha wadau

More information

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized

JAMHURI YA KENYA. Mkakati wa Ushirikiano MUKHTASARI FY Public Disclosure Authorized. Public Disclosure Authorized horized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized Public Disclosure Authorized JAMHURI YA KENYA Mkakati wa Ushirikiano FY2014-2018 MUKHTASARI Mkakati wa Ushirikiano wa Jamhuri ya Kenya

More information

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level

UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level UNIVERSITY OF CAMBRIDGE INTERNATIONAL EXAMINATIONS General Certificate of Education Ordinary Level * 899145 4 672* SWAHILI 3162/01 Paper 1 May/June 2010 Additional Materials: Answer Booklet/Paper READ

More information

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA

Tora UTANGULIZI KWA TORA SOMO LA KWANZA SOMO LA KWANZA UTANGULIZI KWA TORA For videos, study guides and other resources, visit Third Millennium Ministries at thirdmill.org. 2014 nathird Millennium Ministries Haki zote zimehifadhiwa. Hakuna sehemu

More information

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani

Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere Rakesh Rajani HakiElimu: Mfululizo wa Mada za Uchambuzi Namba. 2003.4S Elimu ya Msingi inaelekea Upande Sahihi? Kufikiri na Nyerere 1 Rakesh

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA. Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo. TOLEO Na. JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA Ifahamu Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo TOLEO Na. 1, Desemba, 2012 Yaliyomo Orodha ya Vifupisho -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------3

More information

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA

KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA KAMATI ZA KUDHIBITI UKIMWI NCHINI TANZANIA NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? NI UFUMBUZI KATIKA KUSHIRIKISHA JAMII? Februari, 2013 Februari, 2013 SHUKURANI

More information

Mbinu za Ujenzi wa Wahusika na Usawiri wa Sifa Zao: Uhakiki wa Riwaya ya Dunia Uwanja Wa Fujo ya E. Kezilahabi

Mbinu za Ujenzi wa Wahusika na Usawiri wa Sifa Zao: Uhakiki wa Riwaya ya Dunia Uwanja Wa Fujo ya E. Kezilahabi 38 MULIKA NA. 34 Mbinu za Ujenzi wa Wahusika na Usawiri wa Sifa Zao: Uhakiki wa Riwaya ya Dunia Uwanja Wa Fujo ya E. Kezilahabi Leonard Flavian Ilomo Ikisiri Kipengele cha wahusika ni muhimu katika kuunda

More information

Shabaha ya Mazungumzo haya

Shabaha ya Mazungumzo haya Karibu Katika Mazungumzo Kuhusu Mchakato wa Uhamasishaji Maendeleo ya Kanisa na Jamii CCMP/UMOJA Shabaha ya Mazungumzo haya Kuwafahamisha viongozi wa makanisa kuhusu Mchakato wa CCMP ambao umekuwa ukitumika

More information

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA

KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUUNGANISHA VIZAZI KUPITIA RADIO MWONGOZO KUTOKA AFRIKA KWA WAANDAJI WA VIPINDI VYA RADIO WANAOFANYAKAZI NA WATOTO NA VIJANA KUWEZESHA Radio za kijamii Kutumia Tehama Mwongozo huu umeandaliwa ili kuvipa

More information

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH

SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Eneo La Huduma: Huduma Ya Ushirika Wa Biashara Kichwa: Sera Ya Mipango Ya Msaada Wa Kifedha SERA & TARATIBU YA YALE NEW HAVEN HEALTH Tarehe Kupitishwa: 09/20/2013 Tarehe Ya Ufanisi: 09/20/2013 1/1/2017

More information

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora

TANZANIA OSAKA ALUMNI. Kitabu cha Mbinu Bora K I T A B U C H A M B I N U B O R A C H A T O A U k u r a s a 1 TANZANIA OSAKA ALUMNI Kitabu cha Mbinu Bora Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa P.O. Box 1923, Dodoma. Novemba, 2012

More information

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA 2007 i WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAASISI YA ELIMU TANZANIA MTAALA WA ELIMU YA MSINGI TANZANIA

More information

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya

MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya Jina Nambari.. Shule... 102/3 KISWAHILI FASIHI KARATASI YA 3 JULAI / AGOSTI. 2007 MUDA: SAA 2 ½ MTIHANI WA MWIGO WILAYA YA BUTERE MUMIAS-2007 Hati ya kuhitimu Elimu ya Sekondari Kenya 102/3 KISWAHILI FASIHI

More information

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI

UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA MAREKANI UNACHOHITAJI KUJUA KUHUSU VIKWAZO VYA KULINDA MAISHA KATIKA USAIDIZI WA KIMATAIFA WA AFYA KWA MSAADA WA KIMATAIFA UNAOFADHILIWA NA 30 SEPTEMBA, 2017 UTANGULIZI Tarehe 23 Januari, 2017, Rais Donald Trump

More information

K. M a r k s, F. E n g e l s

K. M a r k s, F. E n g e l s W a (any a kazi wa nchi zote, unganeni! K. M a r k s, F. E n g e l s Maelezo ya chama cha kikomunist Idara ya Maendcleo Moscow Tafsiri hii ya "Maelezo ya Chama cha Kikomunist" inatokana na maandishi

More information

Kiinimacho cha mahali: kiambishi tamati cha mahali -ni. Ridder Samsom na Thilo C Schadeberg Chuo Kikuu cha Leiden

Kiinimacho cha mahali: kiambishi tamati cha mahali -ni. Ridder Samsom na Thilo C Schadeberg Chuo Kikuu cha Leiden AAP 37 (1994). 127-JJB Kiinimacho cha mahali: kiambishi tamati cha mahali -ni Ridder Samsom na Thilo C Schadeberg Chuo Kikuu cha Leiden The locative suffix -ni n this article we discuss two hypotheses

More information

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji

Sera ya Faragha. Upeo. Aina za Data na Mbinu za Ukusanyaji Sera ya Faragha Katika Sera hii ya Faragha ( Sera ), sisi, Qualcomm Incorporated na makampuni yetu tanzu (kwa pamoja sisi au yetu ), tunatoa maelezo kuhusu jinsi tunavyokusanya, kutumia, kuchakata, na

More information

Kutetea Haki za Binadamu

Kutetea Haki za Binadamu Kutetea Haki za Binadamu Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu Toleo la pili i Kutetea Haki za Binadamu: Kitabu cha Marejeo kwa watetezi wa Haki za Binadamu (Toleo la pili) 2012 East and

More information

Nadharia za Uhakiki kama Mchakato wa Kutaalamisha Usomaji wa Fasihi

Nadharia za Uhakiki kama Mchakato wa Kutaalamisha Usomaji wa Fasihi Journal of Linguistics and Language in Education Vol 8, Number 1 (2014): 37-48 Nadharia za Uhakiki kama Mchakato wa Kutaalamisha Usomaji wa Fasihi Richard M. Wafula * Ikisiri Utunzi na uhakiki wa fasihi

More information

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke-

usudi la Maisha Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na kupishana usiku na mchana, kuna kweli ishara kwa wenye akili, ambaye mkumbuke- Kusudi la Maisha hawatakuambia nini walihitimisha kupitia uchunguzi au hoja ya uchambuzi. Katika hali nyingi, hakika wao kukuambia nini mtu mwingine alisema... Au wao watakuambia nini kawaida kudhaniwa

More information

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU

TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TAARIFA FUPI KUHUSU SERA YA TAIFA YA ELIMU TANZANIA EDUCATION NETWORK / MTANDAO WA ELIMU TANZANIA () 1.0 USULI Tanzania, sawa na nchi nyingine, ilitia saini Malengo ya Maendeleo ya Milenia na Malengo ya

More information

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014-2019 JANUARI, 2014 Dibaji Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi

More information

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania

Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Kubadili Sheria Za Mbegu Na Ulinzi Wa Aina Za Mbegu Na Mimea Nchini Tanzania Athari Zake Kwa Mifumo Ya Mbegu Inayosimamiwa Na Wakulima Na Kwa Wakulima Wadogo April 2016 CONTENTS UTANGULIZI 3 MAELEZO YA

More information

Kiu Cha umtafuta Mungu

Kiu Cha umtafuta Mungu ZAIDI YA NAKALA MILLION 3 ZIMECHAPISHWA KATIKA LUGHA 59 KOTE DUNIANI K Kiu Cha umtafuta Mungu Huduma ya Daktari Richard A. Bennett ilianza katika mabaraza ya miji. Akiwa mwanafunzi chuoni, alikumbana na

More information

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)]

Azimio lililopitishwa na Mkutano Mkuu tarehe 18 Desemba 2013 [juu ya taarifa ya Kamati ya Tatu (A/68/456/Add.2)] This unofficial translation is provided by the International Service for Human Rights Umoja wa Mataifa A/AZI/68/ Ugaw Jumla Mkutano Mkuu 30 Januari 2014 Kikao cha Sitini na Nane Dondoo ya Ajenda 69(b)

More information

MARUDIO K.C.S.E KNEC KISWAHILI KARATASI 102/2 MASWALI NA USAHIHISHO

MARUDIO K.C.S.E KNEC KISWAHILI KARATASI 102/2 MASWALI NA USAHIHISHO 102 1B KISWAHILI KARATASI 1B OCT/ NOV 1995 2 ½ HOURS Jibu maswali yote MARUDIO K.C.S.E KNEC 1995 2010 KISWAHILI KARATASI 102/2 MASWALI NA USAHIHISHO 1. UFAHAMU Soma Makala yatuatayo kisha ujibu maswali

More information

UFAHAMU NAME INDEX SCHOOLDATE UFAHAMU

UFAHAMU NAME INDEX SCHOOLDATE UFAHAMU NAME INDEX SCHOOLDATE 1. 1995 1. UFAHAMU UFAHAMU Soma makala yafuatayo kisha ujibu maswali Ama kweli maisha ya vijana wa kisasa yanatofautiana na kuhitilafiana pakubwa na yale ya wazee wao. Sio katika

More information

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia

Kifaa Maalum cha Kutazamia Jua: Maelekezo ya kutumia : Maelekezo ya kutumia Kupatwa kamili kwa jua Jumatatu, 21 Agosti 2017 Agreement v1.4 Mar 2014 2014-2017 Eclipse2017.org, Eclipse2017.org, inc. inc. TERMS AND CONDITIONS FOR USE OF SOLAR VIEWER Please

More information

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio.

KUHUSU AFRODAD. Dira ya AFRODAD. Dhamira ya AFRODAD. AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. KUHUSU AFRODAD Dira ya AFRODAD AFRODAD inalenga mchakato sawa na endelevu wa maendeleo kuelekea Afrika yenye mafanikio. Dhamira ya AFRODAD Kupata sera zitakazorekebisha migogoro ya madeni ya Afrika kulingana

More information